Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Nafsi - Vipaji Vya Asili - Kutoka 31:2-6<br />
Karama Za Kiroho-1 Kor. 12, Efe. 4:11, Rum. 12:6-8<br />
SURA YA KWANZA<br />
CHIMBUKO LA VIPAJI VYA ASILI NA<br />
KARAMA ZA KIROHO<br />
1. Jinsi Binadamu Alivyoumbwa Kwa Ajabu Na Kutisha<br />
Binadamu kwa asili ameumbwa kwa jinsi ya ajabu na<br />
kutisha kweli kweli. Haya si maneno yangu binafsi, bali ni maandiko<br />
ya mtunga Zaburi katika Biblia ambaye ndiye wa kwaza kufanya<br />
ugunduzi huu na kuandika kama ifuatavyo:<br />
“Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu<br />
na kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, na nafsi yangu yajua sana.”<br />
(Zab. 139:14)<br />
Vipaji Vya Asili Na Karama Za Kiroho Katika Maumbile Ya<br />
Binadamu<br />
Mwili - Milango 5 Ya Fahamu<br />
Roho<br />
1
Maandiko matakatifu yanayosimulia historia ya kuumbwa<br />
kwa binadamu kulivyokuwa kwa jinsi ya ajabu kama tunavyosoma<br />
hapa chini:<br />
“Mungu akasema, na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa<br />
sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na<br />
wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho<br />
juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano<br />
wa Mungu alimwumba mwanamume na mwanamke aliwaumba”<br />
(Mwa. 1:26-27)<br />
Hapa tunajifunza ya kwamba, binadamu aliumbwa akiwa<br />
tofauti kabisa na viumbe hai vingine vyote, kuanzia malaika,<br />
wanyama na vitu vingine vyote. Kisha tunajifunza binadamu<br />
ameumbwa kwa mfano na sura ya Mungu mwenyewe. Hii ndiyo<br />
ajabu na ya kutisha.<br />
Mfano wa Mungu na sura ya Mungu! Hapa haina maana<br />
ya kwamba Mungu aliumba Mungu mwingine mwenye kufanana<br />
naye. Mungu ni mmoja haumbwi wala kuumbika. Maandiko<br />
yanachomaanisha hapa ni kuwa Mungu katika uumbaji wake wa<br />
kiungu; aliamua kumuumba “kiumbe mtu” katika mfumo wenye<br />
kufanana naye kwa hekima na tabia ili aweze kumwakilisha Mungu<br />
katika utawala juu ya nchi na viumbe vyote vilivyomo.<br />
Maana Ya Mfano Wa Mungu Katika Binadamu<br />
Tumesoma maandiko yakisema, “... kwa mfano wa Mungu<br />
alimwumba mwanamume na mwanamke aliwaumba.” Ni nini<br />
maana hasa ya mfano wa Mungu na sura ya Mungu?<br />
Jina la kwanza la Mungu lililotumika katika Mwanzo wakati<br />
aliposema maneno haya, ni jina la Kiebrania la Elohim. Jina hili<br />
liko katika wingi wenye kumaanisha Mungu mmoja mwenye nafsi<br />
zaidi ya moja. Ni Mungu mmoja kwa sababu imeandikwa “Mungu<br />
akasema….” Lakini Mungu ana nafsi zaidi ya moja kwa kuwa<br />
maandiko yanasema “na tumfanye mtu kwa mfano wetu na sura<br />
yetu ...”.<br />
2
Haya maneno ya “mfano wetu” na “sura yetu” ndiyo yenye<br />
kuashiria Mungu mmoja lakini aliyejitambulisha katika nafsi zaidi ya<br />
moja. Kwa mukhtadha huu, Mungu aliamua kumuumba binadamu<br />
kwa mfano wake ambao ni “nafsi tatu” kama tunavyoshuhudia<br />
katika maandiko yafuatayo:<br />
“BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi,<br />
akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi.” (Mwa. 2:7)<br />
Maandiko tuliyosoma hapo juu yanadhihirisha mfumo<br />
wa utatu wa binadamu kimaumbile. Mavumbi ya ardhi ndiyo<br />
yalitengeneza mwili na “pumzi ya uhai” ni sehemu ya roho kutoka<br />
kwa Mungu mwenyewe aliyoipulizia ndani ya mwili; na kisha<br />
tunaona mtu anakuwa “nafsi hai”.<br />
Aidha, kila sehemu ya binadamu kuanzia mwili, nafsi na<br />
roho inavyo vitu vinavyoifanya kuwa sehemu kamili kiutendaji.<br />
Mathalan, mwili wa binadamu una kitu kinaitwa “milango ya<br />
maarifa” ambayo ni kuona, kusikia, kuonja, kugusa na kunusa.<br />
Milango hii hutenda kazi kupitia mfumo wa ubongo ambao ndiyo<br />
kama injini ya mwili.<br />
Nafsi ya mtu inavyo vitu vitatu ambavyo ni akili, hisia na<br />
utashi. Na roho nayo inavyo vitatu ambavyo ni “dhamiri”, “ushirika”<br />
na “utambuzi” ambavyo ndivyo Mungu huwasiliana na kuhusiana<br />
na binadamu katika roho.<br />
Uhai wa binadamu huonekana kupitia mwili. Nafsi ya<br />
binadamu ambayo ndiyo yenye akili na hisia na utashi ndiyo<br />
huufanya mwili kufanya mambo yenye kuonekana na wengine,<br />
kuazia kusema na kutenda kwake.<br />
Ukiutazama mchoro hapo juu utakuta jinsi ambavyo mduara<br />
mkubwa wa nje unawakilisha mwili. Mduara wa pili unawakilisha<br />
nafsi, na ule mduara mdogo wa katikati unawakilisha roho ya<br />
binadamu.<br />
3
Kwa mantiki hii, wakati ambapo “nafsi” ya mtu hujidhihirisha<br />
kupitia mwili; hali kadhalika na roho ya binadamu, ambayo ndiyo<br />
kiungo cha mawasiliano kati ya Mungu kiroho, utendaji wake<br />
unadhihirika kupitia nafsi.<br />
2. Tafsiri Ya Misamiati Ya Vipaji Na Karama<br />
Kipaji<br />
Kwa mujibu wa maandiko katika Biblia, kuna ushahidi<br />
wa kuwepo kwa <strong>vipaji</strong> vya asili ambavyo kusudi lake ni kufanya<br />
mambo ya kiufundi na kitaaluma lakini pasipo kupitia kwanza<br />
kwenye mafunzo na mfumo rasmi wa kielimu.<br />
Kipaji ni neno la Kiswahili ambalo Kamusi ya Kiswahili Sanifu<br />
imelitafsiri kuwa ni “kipawa”. Na neno “kipawa” limetafsiriwa<br />
kuwa ni “uwezo mtu aliozaliwa nao” ambao humwezesha kufanya<br />
jambo fulani vizuri.<br />
Hata hivyo, neno “kipaji” limetafsiriwa kwa lugha nyingine<br />
za kibiblia ambazo ni Kiebrania na kiyunani. Neno la Kiebrania<br />
lililotumika kutafsiri “kipaji” ni chokmah na limetajwa mara 149<br />
katika toleo la Kingereza la KJV.<br />
Tafsiri ya neno chokmah ni “hekima”. Katika Biblia kipaji<br />
cha asili kimetafsiriwa kwa neno “hekima” ambalo kwa lugha ya<br />
kiebrania limetumika neno chokmah na limetajwa mara 149 katika<br />
KJV. Maana ya neno chokmah ni: “fundi” wa silaha za kijeshi<br />
wakati wa vita; au “mbunifu” na mwerevu wa mitambo na vifaa<br />
vya ufundi; au stadi wa kazi za mikono.<br />
Kwa hiyo msamiati wa kibiblia wa neno kipaji ni hekima.<br />
Tunaweza kupata matumizi ya neno chokmah katika maandiko<br />
matakatifu yafuatayo:<br />
4
“Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa<br />
Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda; nami nimemjaza roho ya<br />
Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya<br />
kila aina, ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa<br />
fedha, na wa shaba, na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora<br />
miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.” (Kut. 31:2-5)<br />
“... ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa<br />
fedha, na wa shaba, Tena, tazama, nimemchagua, awe pamoja<br />
naye, huyo Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani;<br />
nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima,<br />
ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza” (Kut. 31:4-6)<br />
Katika maandiko haya kila mahali neno “hekima” kwa<br />
kiebrania ni chokmah likimaanisha <strong>vipaji</strong> mbali mbali kwa ajili<br />
ya ubunifu, ufundi na ustadi wa vifaa vya ujenzi na vyombo vya<br />
kutumia kwenye hema ya Mungu kukutana na wana wa Israeli.<br />
Tukiyachunguza maandiko ya Agano Jipya kwa lugha ya<br />
Kiyunani tunakutana na msamiati wa neno “Sophia” pia likiwa<br />
limetafsiriwa kuwa ni hekima ambalo linamaanisha <strong>vipaji</strong> vya asili.<br />
Neno sophia ambalo kwa Kiswahili ni hekima maana yake<br />
ni “uwezo mpana wa kujifunza na kushughulikia mambo mapya<br />
(full of intelligence); uwezo wa kutendea kazi maarifa na ufundi wa<br />
mambo mtambuka.” Neno sophia limetajwa mara 51 katika toleo<br />
la KJV kwenye Agano Jipya.<br />
Tunaweza kupata matumizi ya neno sophia kwenye<br />
maandiko matakatifu ya Agano Jipya ambayo ni haya yafuatayo:<br />
“Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima,<br />
na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.” (Luk. 2:40)<br />
“Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo,<br />
akimpendeza Mungu na wanadamu.” (Luk. 2:52)<br />
5
Neno hekima ambalo limetajwa kwa Yesu ni sophia<br />
likimaanisha <strong>vipaji</strong> vya asili. Yesu aliishi kwa muda wa miaka<br />
30 kabla ya kuanza huduma za kiroho ambapo alianza kutumia<br />
uwezo wa Roho Mtakatifu.<br />
Yesu Kristo tangu utoto hadi ujana wake alikuwa amejaa<br />
<strong>vipaji</strong> vya asili, ikiwemo kazi za ufundi seremala ambayo ilikuwa ni<br />
kazi ya Yusufu baba yake mlezi.<br />
Katika kitabu hiki, msamiati wa neno “kipaji cha asili” ndio<br />
utatumika ambao kwa mujibu wa Biblia ni hekima.<br />
Kipaji cha asili kinaitwa hivyo kwa sababu ya uwezo<br />
maalum wa asili unaomwezesha mtu kufanya jambo kwa viwango<br />
vya juu vya uzuri, ufundi na ubora pasipo kupitia mafunzo rasmi<br />
ya kitaaluma.<br />
Uwezo huu maalum wa asili ndio humfanya mtu kuonekana<br />
wa tofauti na watu wengine katika utendaji wa jambo fulani.<br />
Uwezo huu wa asili ambao ni wa kuzaliwa nao, ndio humfanya<br />
muhusika kujulikana au kuwa mtu maarufu katika jambo lile<br />
ambalo amekirimiwa kulijua na kulifanya kwa viwango vya ubora<br />
katika jamii.<br />
Kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika na wataalamu, kuna <strong>vipaji</strong><br />
vya asili kama saba ambavyo vimeorodheshwa kama ifuatavyo: 1.<br />
Ubunifu, 2. Uhusiano, 3. Lugha, 4. Hesabu, 5. Michezo, 6. Muziki,<br />
na 7. Picha.<br />
Japokuwa sio kila mtu huzaliwa na <strong>vipaji</strong> vyote saba,<br />
uchunguzi uliofanywa umebaini ya kwamba kila binadamu<br />
angalau huzaliwa na aina mojawapo ya kipaji kati ya <strong>vipaji</strong> hivi, na<br />
kama akipewa fursa ya kubaini na kuendeleza kipaji hicho, kuna<br />
uwezekano kwa kila mtu kuishi maisha bora kutokana na kipaji<br />
chake cha asili.<br />
6
Karama<br />
Kamusi ya Kiswahili Sanifu imetafsiri neno “karama” kuwa<br />
ni “kipawa anachokuwa nacho mtu kwa sababu ya kumwabudu<br />
sana Mungu, aghalabu humpa uwezo wa kuomba haja kwa<br />
Mwenyezi Mungu na kukubaliwa mara moja; ridhaa ya kupokelewa<br />
haja iombwayo”<br />
Kwa mujibu wa kamusi za Biblia, kabla ya kuchambua<br />
maana ya karama za kiroho, hatuna budi tupate kufahamu ya kuwa<br />
Biblia haitoi tafsiri na msamiati huu wa “karama za kiroho” lakini<br />
imetoa maelezo ya kina kuhusu asili yake na jinsi zinavyotenda<br />
kazi. Msamiati wa neno “karama” ndio umetafsiriwa kwa kiyunani<br />
kama “charismata” likiwa na maana ya “karama za neema” na<br />
likilenga “karama” au uwezo maalum kutoka kwa Mungu ambao<br />
hutolewa kwa waamini kupitia Roho Mtakatifu.<br />
Pia kuna tofauti kati ya “karama za kiroho” au “karama za<br />
Roho Mtakatifu na “kipawa cha Roho Mtakatifu”. Kuna aina nyingi<br />
za karama za kiroho, lakini Roho Mtakatifu ni mmoja tu. Kipawa<br />
cha Roho Mtakatifu hupokelewa baada ya mtu kumpokea Yesu<br />
Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wake na kuzaliwa upya kiroho.<br />
(Mdo. 2:38).<br />
Aidha, kuna mgawanyiko maalum wa “karama za kiroho”<br />
ambao ni “karama za Roho”, “ofisi za huduma”, na “karama<br />
za neema”. Wakati ambapo “karama za Roho” ni utendaji wa<br />
Roho Mtakatifu ndani ya mwamini kama ilivyoandikwa katika<br />
1 Wakorintho 12; pia ziko “ofisi za huduma” ambazo ni vipawa<br />
vya kiroho vya utendaji huduma tofauti kama zilivyotajwa katika<br />
Waefeso 4:11. Na pia kuna “karama za Neema” ambazo ni<br />
utendaji wa Mungu kwa ajili ya waamini kama ulivyoanishwa<br />
kwenye Warumi 12.<br />
Orodha ya “karama za Roho” zilizotajwa katika 1 Wakorintho<br />
12: ni kama ifuatayo:<br />
7
1. Neno la hekima<br />
2. Neno la maarifa<br />
3. Kupambanua roho<br />
4. Imani<br />
5. Karama za kuponya<br />
6. Matendo ya miujiza<br />
7. Unabii<br />
8. Kunena kwa lugha<br />
9. Tafsiri za lugha<br />
Hizi “karama za Roho” naweza kuzitafsiri kuwa ni “karama<br />
za udhihirisho” (Manifestational gifts). Maana yake zenyewe<br />
zinatenda kazi ya kudhihirisha utendaji wa Roho Mtakatifu ndani<br />
ya waamini ambao wamekirimiwa huduma na utumishi wa kiroho<br />
katika mwili wa Kristo.<br />
Orodha ya “ofisi za huduma” zilizotajwa katika Waefeso<br />
4:11: ni kama ifuatayo:<br />
1. Mitume<br />
2. Manabii<br />
3. Wainjilisti<br />
4. Wachungaji<br />
5. Waalimu<br />
Hizi zinaitwa “ofisi za huduma” ambazo nimeziita “karama<br />
za uwezesho” kwa sababu zinafanya kazi ya kuwakamilisha<br />
watakatifu ili kazi ya huduma itendeke. Ni karama za kuwezesha<br />
waamini kupata uzoefu wa kutumika katika kuujenga mwili wa<br />
Kristo.<br />
Orodha ya “karama za neema” zilizotajwa katika Warumi<br />
12 ni kama ifuatavyo:<br />
1. Uhamasishaji<br />
2. Utoaji<br />
8
3. Uongozi<br />
4. Rehema<br />
5. Unabii<br />
6. Huduma<br />
7. Ualimu<br />
Hizi ni “karama za neema” ambazo zinaitwa “karama za<br />
utumishi” (Serving Gifts). Mungu Baba huwagawia waamini<br />
karama za neema ili wapate kutumikiana wenyewe kwa wenyewe<br />
mara baada ya kukamilishwa na zile “karama za uwezo” ambazo<br />
ni “ofisi za huduma”.<br />
3. Tofauti Kati Ya Vipaji Vya Asili Na Karama Za Kiroho<br />
Kwanza kabisa ni muhimu kutambua mapema ya kwamba<br />
“<strong>vipaji</strong> vya asili” si “karama za kiroho”. Kwa kifupi ni kwamba, “kipaji<br />
cha asili” chimbuko lake ni kibaiolojia (natural and biological); na<br />
“karama za Roho” asili yake ni ya kiroho na ya kiungu (spiritual<br />
and supernatural).<br />
Jambo muhimu la pili ni kwamba, kila binadamu (mwamini<br />
na asiye mwamini) huzaliwa na <strong>vipaji</strong> vya asili lakini kimojawapo<br />
kati ya vingine ndicho hujitokeza zaidi na mhusika akajulikana<br />
kupitia kipaji hicho cha asili.<br />
Lakini si kila binadamu anayezaliwa kibaiolojia huzaliwa<br />
akiwa na “karama za kiroho”. Tumejifunza ya kwamba “karama za<br />
kiroho” ni kwa ajili ya “waamini peke yao”, na kwa ajili ya matumizi<br />
ya kiroho peke yake. Kwa hiyo, kipaji cha asili mtu huzaliwa nacho<br />
kwa mara ya kwanza, lakini “karama za kiroho” hupokelewa na<br />
mtu akiisha kuzaliwa mara ya pili kiroho.<br />
Jambo muhimu la tatu ni kwamba, “<strong>vipaji</strong> vya asili”<br />
huwanufaisha zaidi wenye kuzaliwa navyo ikiwa ni pamoja na<br />
kuwaneemesha kwa maslahi ya kibinafsi. Lakini “karama za<br />
9
kiroho” kusudi lake ni “kuwahudumia na kuwanufaisha wengine”<br />
ambao Mungu anapenda kuwasaidia kupitia uwezo wake wa<br />
kiungu (supernatural means).<br />
Jambo muhimu la nne, ni kwamba <strong>vipaji</strong> vya asili vinahitaji<br />
kuendelezwa kwa mafunzo na mazoezi; wakati ambapo “karama<br />
za kiroho” zenyewe hutenda kazi kulingana na kiwango cha ukuaji<br />
wa kiroho wa mwamini na uhusiano wa karibu wa kiroho kati yake<br />
na Mungu.<br />
Vipaji Vya Asili Hukaa Katika Nafsi Ya Mtu<br />
Katika uchambuzi wa utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya asili na karama<br />
za kiroho, tutaona ya kwamba, <strong>vipaji</strong> vya asili chimbuko lake ni<br />
katika nafsi ya binadamu, na chimbuko la “karama za kiroho”<br />
chimbuko lake ni katika roho ya binadamu.<br />
Hebu tupitie kwa ufupi kuhusu “<strong>vipaji</strong> vya asili” jinsi<br />
vinavyotenda kazi kutokea kwenye nafsi. Ndani ya nafsi ndimo<br />
mna vitu vikuu vitatu ambavyo ni akili, hisia na utashi. Kila “kipaji<br />
cha asili” kwa asili yake lazima “kitumie akili” ambayo ni sehemu<br />
ya nafsi, lazima “kiguse hisia” ambayo sehemu ya nafsi, na lazima<br />
kitokane na “utashi wa mtu’ ambao pia ni sehemu ya nafsi.<br />
• Ni rahisi kwako kuliko mengine na wengine<br />
• Hutumii nguvu nyingi kupita kawaida<br />
• Inaeleweka kwa urahisi<br />
• Unaona ni kawaida na unashangaa kwanini wengine hawawezi<br />
• Unafanya kwa ubora zaidi<br />
• Unafanya kwa furaha na shauku ya moyo<br />
Karama Za Kiroho Makao Yake Ni Katika Roho Ya Mtu<br />
Utendaji wa “karama za kiroho”, tofuati na “<strong>vipaji</strong> vya<br />
asili”, wenyewe chimbuko lake ni katika roho ya binadamu.<br />
Kama tulivyojifunza kwamba roho ya binadamu inatokana na vitu<br />
10
vitatu ambavyo ni dhamiri, ushirika na utambuzi. Kwa kuwa asili<br />
ya karama za kiroho ni “hali ya kiungu” (supernatural source) na<br />
hutenda kazi kutokea ndani ya roho yake.<br />
Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, tunajifunza ya kuwa<br />
Roho Mtakatifu ndiye mdhibiti mkuu wa karama na vipawa vya<br />
huduma za kiroho. Hatua ya kwanza kazi ya Roho Mtakatifu ni<br />
kumzaa mtu mara ya pili (Yoh. 3:3), na tunafundishwa hali hii ya<br />
kuzaliwa mara ya pili hufanyika ndani ya roho ya mtu (Yoh. 3:6).<br />
Baada ya Roho Mtakatifu kumzaa upya mtu katika roho<br />
yake, hatua ya pili ni kujaa ndani ya mtu na kufanya makao ya<br />
kudumu ndani roho ya binadamu. Na humo ndimo utendaji wa<br />
karama za Roho pamoja na vipawa vya huduma za kiroho hutokea<br />
na kudhihirika katika nafsi ya mtu.<br />
11
SURA YA PILI<br />
UCHAMBUZI WA VIPAJI VYA ASILI<br />
Utangulizi<br />
Kwa kuwa kipaji ni kitu cha asili ya kuzaliwa nacho, kila<br />
binadamu katika mfumo wa ubongo amesukwa kufikiri na kutenda<br />
kulingana na nguvu za fikra zilizowekwa ndani yake. Kwa hiyo<br />
katika kuchambua <strong>vipaji</strong> tunakwenda kupitia na kujifunza kuhusu<br />
uwezo wa asili alionao mwenye kipaji cha asili.<br />
Kimsingi, kipaji cha asili ndicho kinachomtofautisha mtu<br />
na watu wengine na ndio utambulisho wake kwa wengine katika<br />
jamii. Na hii inatokana na taarifa kutoka katika maandiko ya Bibilia<br />
pamoja na tafiti za kisayansi ambazo zinathibitisha ukweli huu.<br />
Ziko nadharia nyingi zinazofundisha habari ya <strong>vipaji</strong> vya<br />
asili, lakini katika sura hii, tunakwenda kufanya uchambuzi wa aina<br />
saba tu za <strong>vipaji</strong> vya asili ambavyo vimo ndani ya kila binadamu<br />
ukiwemo na wewe msomaji wa kitabu hiki.<br />
Katika kufanya uchambuzi kuhusu nguvu na uwezo alionao<br />
mwenye kipaji husika, pia tutachambua viashira vya ufanisi kwa<br />
kila kipaji. Viashiria vya ufanisi ni maeneo maalum ambayo kila<br />
kipaji huonesha upekee na umaalum wa ubora kupitia mwenye<br />
kipaji husika.<br />
Mwisho kabisa, uchambuzi wa <strong>vipaji</strong> vya asili utabainisha<br />
aina mbali mbali za fursa za kitaaluma ambazo mwenye kipaji<br />
anaweza kuzimudu kwa viwango vya ubora wake. Vipaji vya asili<br />
viko saba kama vilivyoorodheshwa hapa:<br />
12
1. Kipaji cha Ubunifu wa mawazo<br />
2. Kipaji cha Mahusiano<br />
3. Kipaji cha Lugha<br />
4. Kipaji cha Hesabu<br />
5. Kipaji cha Michezo<br />
6. Kipaji cha Muziki<br />
7. Kipaji cha Picha<br />
Kumbuka ya kwamba kila binadamu anapozaliwa viashiria<br />
vya mambo saba haya ya <strong>vipaji</strong> vya asili huwa vimo ndani yake.<br />
Lakini kuna kipaji kimojawapo ambacho hujitokeza na kuonekana<br />
zaidi kuliko vingine na hicho ndicho hutafsiriwa kuwa kipaji cha<br />
mhusika.<br />
Kwa hiyo, tunakwenda kupitia kwanza nguvu za kimaumbile<br />
za kila kipaji, pili, tunachambua viashiria vya ufanisi wa kila kipaji,<br />
na tatu, tunaorodhesha aina ya fursa za kitaaluma zinazoambatana<br />
na <strong>vipaji</strong> vya asili kwa wahusika.<br />
13
UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />
UBUNIFU<br />
14
Kipaji cha ubunifu kwa lugha ya Kiingereza ni Intrapersonal<br />
Intelligence ambacho kimebeba uwezo maalum wa kubuni<br />
mambo mapya.<br />
Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Ubunifu<br />
Mwenye kipaji hiki ni mtu ambaye ana uwezo mkubwa<br />
katika kufikiri, kupata na kukusanya mawazo pamoja.<br />
Kimaumbile katika mfumo wake wa ubongo seli za<br />
fahamu zimesukwa katika hali ya fikra zenye kina, kukusanya<br />
mawazo pamoja, kufanya maamuzi yenye mwelekeo, uwezo wa<br />
kuchambua katika hali ya uhuru wa hiari.<br />
Mwenye kipaji cha ubunifu pia anao uwezo mkubwa wa<br />
kujitathmini na kujifahamu kibinafsi kuanzia mawazo, hisia na<br />
utambuzi wa ndani.<br />
Kana kwamba hii haitoshi, mwenye kipaji cha ubunifu<br />
ana uwezo mkubwa wa kuiongoza tabia binafsi, kujua nguvu na<br />
udhaifu binafsi, kubuni fikira mpya, kupanga shughuli na kutatua<br />
matatizo.<br />
Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Ubunifu<br />
Kila mwenye kipaji cha ubunifu atajulikana na kutambulika<br />
kwenye maeneo yake ya ufanisi unatokana na nguvu za kipaji<br />
chake. Baadhi ya maeneo ya ufanisi wa kipaji cha ubunifu ni<br />
pamoja na:<br />
• Utambuzi wa viwango vya hisia binafsi<br />
• Uwezo wa kujitawala na kufanyia kazi mawazo na hisia binafsi<br />
• Njia nyepesi za kueleza mawazo binafsi<br />
• Hamasa ya kubaini na kutekeleza malengo<br />
• Ufanisi wa kazi uwapo huru mwenyewe na peke yako<br />
15
• Udadisi wa kujua maana ya maisha<br />
• Uwezo wa kujitawala kibinafsi wakati wa kujifunza<br />
• Kutamani sana kupata uzoefu wa ndani ya nafsi<br />
• Uwezeshaji na uhamasishaji wengine<br />
• Kufurahia kufikiri mikakati, kuandika makala na kupenda<br />
mikakati ya kujitathimini binafsi<br />
• Kujua ukomo wa mipaka ya uwezo wako<br />
• Uwezo wa kuchambua, kubaini na kutathmini mambo/<br />
mazingira<br />
Fursa Za Kitaaluma<br />
Kipaji cha ubunifu kina fursa nyingi za kitaaluma iwapo<br />
mwenye kipaji hiki atajaliwa kujitambua mapema na kukinoa kwa<br />
ajili ya matumizi yenye tija. Baadhi ya fursa ambazo mwenye kipaji<br />
cha ubunifu anaweza kuzimudu kwa ufanisi mkubwa ni pamoja na<br />
kuwa:<br />
• Jaji<br />
• Mshauri<br />
• Wakili<br />
• Mkufunzi<br />
• Mwanasheria<br />
• Mtaalamu wa matibabu<br />
• Mwanandishi wa riwaya<br />
• Muuguzi wa magonjwa ya akili<br />
• Mwana falsafa<br />
• Mtaalamu wa hisabati<br />
• Kiongozi<br />
16
UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />
UHUSIANO<br />
17
Kipaji cha uhusiano kwa lugha ya Kiingereza ni Interpersonal<br />
Intelligence ambacho kimebeba uwezo maalum wa kutengeneza<br />
na kudumisha mahusiano.<br />
Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Uhusiano<br />
Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha uhusiano, katika<br />
mfumo wa ubongo wake anazo seli za neva zenye kumwezesha<br />
kutengeneza mawasiliano na wengine. Anao uwezo mkubwa wa<br />
mwingiliano wa kijamii, usikivu, ushirikishaji, kujenga mahusiano,<br />
utoaji na uwezo wa kuelewa na kufanya kazi vizuri na watu.<br />
Mtu mwenye kipaji cha uhusiano ni mwepesi na mwenye<br />
ukaribu wa kuchukuliana na watu na ushiriki wa kihisia wa mambo<br />
wanayopitia. Hii ni pamoja na uwezo wa kutawala, kusuluhisha,<br />
kuhamasisha, kuongoza, kuelekeza na kushauri wengine.<br />
Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Uhusiano<br />
Mwenye kipaji cha uhusiano hutambulika kwa viashiria vya<br />
uhusiano ambavyo ni pamoja na:<br />
• Nguvu za kuongoza<br />
• Ufanisi katika kujenga mtandao na wengine<br />
• Uwezo wa kujadiliana, kujenga hoja za utetezi na mzuri katika<br />
usuluhishi<br />
• Uwezo wa kuongea na kupangilia mambo<br />
• Kufurahia kuwa mlezi wa <strong>vipaji</strong> vya wengine<br />
• Uwezo wa kutanguliza wengine<br />
• Uwezo wa kuhisi na kutambua hisia, hulka, tabia na matarajio<br />
ya wengine<br />
• Uwezo wa kushawishi wengine<br />
• Ufanisi katika kufanya kazi na kundi, juhudi za pamoja katika<br />
kikundi na utendaji wa pamoja<br />
• Uwezo wa kuunganisha watu wakawa wamoja<br />
• Uwezo wa kujenga mahusiano ya kijamii ya kudumu<br />
18
Fursa Za Kitaaluma<br />
Kipaji cha uhusiano kina fursa nyingi za kitaaluma ambazo<br />
mhusika anaweza kuonesha ufanisi wa kitaaluma. Baadhi ya fursa<br />
za kitaaluma ni pamoja na hizi zifuatazo:<br />
• Mwanasiasa<br />
• Kiongozi wa dini<br />
• Muuzaji<br />
• Mkufunzi<br />
• Mshauri<br />
• Mtaalamu wa sayansi ya jamii<br />
• Msemaji/Mtalaamu wa lugha<br />
• Mtaalamu wa kijamii<br />
• Mtaalamu wa saiklojia<br />
• Afisa mahusiano<br />
• Mkurugenzi wa rasilimali watu<br />
• Meneja<br />
• Mhamasishaji<br />
19
UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />
LUGHA<br />
20
Kipaji cha lugha kwa lugha ya Kiingereza ni Linguistic<br />
Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum wa umahili katika<br />
lugha.<br />
Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Lugha<br />
Kimauimbile mtu mwenye kipaji cha lugha, katika mfumo<br />
wa ubongo wake anazo seli za neva zinazojenga umahili wa lugha<br />
na umakini wa maana za maneno, sauti, mahadhi pamoja na<br />
matumizi tofauti ya lugha mbali mbali.<br />
Uwezo wa kufikiri kwa njia ya maneno na kutumia maneno<br />
kwa ufasaha katika kuongea na kuandika.<br />
Pia mwenye kipaji cha lugha huwa ni mwepesi wa kujifunza<br />
mifumo na miundo ya lugha na matumizi yake.<br />
Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Lugha<br />
• Huhitaji kujieleza kibinafsi kwa kuandika au kutumia maneno<br />
mengi<br />
• Hupenda kulumbana, kuhoji, kuburudisha na kuelekeza<br />
• Hupenda kuandika, kucheza na maneno, kusoma na kusimulia<br />
visa na hadithi<br />
• Huwa na kiwango kizuri cha elimu ya jumla<br />
• Huuliza maswali mengi<br />
• Hupenda kuongoza/kushiriki katika mijadala<br />
• Hupendelea mbao za kuandikia, vifaa vya kutunza maneno, na<br />
vifaa vya kunakili maneno<br />
• Utamkaji vizuri wa maneno<br />
• Kujifunza lugha kwa urahisi<br />
• Huwa na kumbukumbu nzuri ya majina, tarehe, na majina ya<br />
maeneo<br />
21
Fursa Za Kitaaluma<br />
• Mhariri<br />
• Mwandishi wa hotuba<br />
• Mtunga mashairi<br />
• Mwandishi wa riwaya<br />
• Mwanasiasa<br />
• Mtunza hakimiliki<br />
• Msemaji/Mtaalamu wa lugha<br />
• Mwandishi wa michezo ya kuigiza<br />
• Mwanasheria/Wakili<br />
• Mwandishi wa habari<br />
• Mkufunzi<br />
22
UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />
HESABU<br />
23
Kipaji cha hesabu kwa lugha ya Kiingereza ni Logic/<br />
Mathematical Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum wa<br />
kuchanganua matatizo ya kinadharia kwa kutumia mahesabu.<br />
Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Hesabu<br />
Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha hesabu, katika mfumo<br />
wa ubongo wake anazo seli za neva zinazojenga uwezo wa kufikiri<br />
na kuchambua mambo kisayansi; uwezo wa kuelewa kanuni na<br />
mifumo na michanganuo ya kimahesabu.<br />
Viashiria Vya Kipaji Cha Hesabu<br />
• Uwezo wa nidhamu ya ndani katika kufikiri<br />
• Uwezo wa kuhesabu na kuthibisha majibu ya hesabu<br />
• Uwezo wa kufikiria sana mambo<br />
• Shauku ya kujua nini kinafuata mbeleni<br />
• Kupenda kutafakari mambo kimahesabu<br />
• Kupenda kubuni nadharia zinazoonesha jinsi kufanya mambo<br />
• Hupenda kuthibitisha usahihi wa kitu kabla ya kukitumia<br />
• Kuonesha uwezo wa kutambua na kutatua matatizo<br />
Fursa Za Kitaaluma<br />
• Mwanasayansi<br />
• Daktari wa tiba<br />
• Mwanahisabati<br />
• Meneja wa mradi<br />
• Mhasibu<br />
• Mkutubi wa chuo kikuu<br />
• Mhandisi<br />
• Mtafiti<br />
• Mtaalamu wa programu za kompyuta<br />
• Mtaalamu wa tiba ya mifuba<br />
• Mtaalamu wa benki<br />
• Mwanasheria<br />
• Mpelelezi<br />
• Mwindaji wanyama<br />
• Mfanyabiashara/mjasiriamali<br />
24
UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />
MICHEZO<br />
25
Kipaji cha michezo kwa lugha ya Kiingereza ni Kinesthetic<br />
Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum wa ufundi wa<br />
kutumia viungo vya mwili na miondoko; na uwezo kumudu vitu au<br />
mambo yanayokuzunguka.<br />
Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Michezo<br />
Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha michezo, katika<br />
mfumo wa ubongo wake anazo seli za neva ufundi wa miondoko,<br />
kugeuza maungo ya mwili, na mizunguko hususani kucheza mpira<br />
wa miguu, riadha, kubiringika juu ya kiti bila kuumia, kujigeuza<br />
mwili pasipo maumivu;<br />
Hali kadhalika mwenye kipaji cha michezo ana ufundi wa<br />
asili wa kutumia viungo vya mwili na miondoko; na uwezo wa<br />
kumudu vitu au mambo yanayokuzunguka; Wenye <strong>vipaji</strong> vya<br />
michezo ni watu walioumbwa kujifunza na kufikia viwango vya<br />
ubora wa <strong>vipaji</strong> kwa njia ya michezo.<br />
Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Michezo<br />
• Uwezo mzuri wa kujikusanya kimwili<br />
• Mwepesi kuwahi muda na kufanya kwa wakati<br />
• Hukabiliana na matatizo kwa nguvu za mwili<br />
• Kupenda kunyoosha viungo vya mwili na mazoezi<br />
• Kupenda michezo ya kuigiza<br />
• Kupenda kucheza ngoma/muziki<br />
• Hufikiri wakati wa miondoko<br />
• Hupenda kuchonga vinyago na burudani<br />
• Kubuni vitu vipya vya kimichezo<br />
Fursa Za Kitaaluma<br />
• Mwigizaji<br />
• Mwanariadha<br />
• Mcheza mziki<br />
26
• Mvumbuzi<br />
• Sonara<br />
• Mchongaji<br />
• Mwanasanaa<br />
• Dreva wa mashindano ya magari<br />
• Mtaalamu wa tiba maungo<br />
27
UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />
MUZIKI<br />
28
Kipaji cha muziki kwa lugha ya Kiingereza ni Musical<br />
Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum wa kutumia sehemu<br />
ya ubongo iitwayo sular ambayo imejaa fikira za muziki na hutumia<br />
utambuzi wa ndani wa kufahamu mambo yasiyo dhahiri.<br />
Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Muziki<br />
Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha muziki, katika mfumo<br />
wa ubongo wake anazo seli za neva zenye uwezo wa kuimba<br />
au kupiga vyombo vya muziki, uwezo wa kutambua mahadhi na<br />
kupambanua mambo yasiyo dhahiri kupitia muziki. Pia mwenye<br />
kipaji cha muziki ana uwezo wa kuwasoma watu kwa kusikiliza<br />
sauti zao na lugha kupitia maungo ya mwili, na sio kwa kusikiliza<br />
maneno peke yake.<br />
Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Muziki<br />
• Utambuzi wa ndani wa kuhisi wakati mambo ni mazuri au<br />
mabaya<br />
• Hafanyi mambo mpaka amejisikia yuko sahihi<br />
• Hawezi kujieleza lakini ana hisia za kutambua ni nani wa<br />
kuaminiwa na ambaye sio<br />
• Yuko makini na hisia kali na mazingira na kujisikia au kutojisikia<br />
raha katika maeneo fulani<br />
• Hutafuta kusikiliza sauti, huvutiwa na muziki, na hupenda<br />
kutunga nyimbo/muziki<br />
• Uwezo wa kuimba vizuri kwa vina na mjuzi wa kupiga vyombo<br />
• Kutunza muda katika kuimba<br />
• Uwezo wa kusikiliza na kukosoa muziki<br />
• Ukusanyaji wa nyimbo, ala na muziki<br />
• Hupenda kuchezesha miguu, vidole au kalamu anapofanya<br />
kazi au kusikiliza jambo<br />
29
Fursa Za Kitaaluma<br />
• Mwongozaji<br />
• Mtunga ala<br />
• Mtunzi wa nyimbo<br />
• Mhandisi wa muziki<br />
• Mtaalamu wa kinanda<br />
• Msimamizi wa disko<br />
• Mwalimu wa Muziki<br />
• Mtaalamu wa nyimbo za ala<br />
• Mchezaji wa jukwaani<br />
• Mchezaji muziki<br />
• Mwanamuziki<br />
Mwimbaji<br />
• Mhadisi wa uzalishaji muziki<br />
• Msemaji wa shughuli au mshehereshaji (MC)<br />
30
UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />
PICHA<br />
31
Kipaji cha picha kwa lugha ya Kiingereza ni Visual/Spatial<br />
Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum kupokea kutoka<br />
ulimwengu wa picha/maumbo na kuyachora, hadi kutoa kitu halisi<br />
kwa mfano wa picha kutoka akilini.<br />
Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Picha<br />
Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha picha katika mfumo<br />
wa ubongo wake anazo seli za neva za kutazama rangi, mwanga,<br />
umbo na vina vya vitu; ikiwa ni pamoja na kufumba macho na<br />
kutafakari, kuona mambo ambayo hayaonekani kwa macho ya<br />
asili; uwezo wa kukitoa kitu kwenye nafsi ya ndani (non-conscious)<br />
hadi kwenye akili (consciousness).<br />
Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Picha<br />
• Hufikiri katika mfumo wa picha na kutafsiri michoro/picha kwa<br />
urahisi<br />
• Uwezo wa kupokea mawazo kwa njia ya maumbo na kuyachora<br />
mawazo hayo katika mfumo wa picha<br />
• Uwezo wa kukumbuka sura lakini husahau majina<br />
• Huweza kuvusha mawazo huku akiendelea kusikiliza<br />
Fursa Za Kitaaluma<br />
• Mchongaji<br />
• Mwanamazingira<br />
• Kiongozi<br />
• Mtendaji mkuu<br />
• Mbunifu wa michoro<br />
• Mhandisi<br />
• Mwandishi wa Sheria<br />
• Nahodha<br />
• Mtaalamu wa video<br />
• Mpiga picha<br />
32
• Mpaka rangi<br />
• Mwendeshaji<br />
• Mtaalamu wa mikakati ya vita<br />
• Msanifu wa majengo<br />
• Rubani<br />
33
Njia Za Kutambua Kipaji Chako<br />
Utangulizi<br />
Kujitathmini na kutambua una kipaji gani cha asili si kazi<br />
nyepesi. Si tukio la mara moja bali ni mchakato. Na mchakato<br />
wenyewe unategemea mambo mengi kuanzia umri wako,<br />
mazingira unamoishi na kukulia kimalezi; aina ya watu walio karibu<br />
na wewe mfano wazazi au walezi na jamaa wa karibu; kama ni<br />
mwanafunzi ni aina gani ya shule, chuo na masomo unayochukua.<br />
Yote haya ni mazingira ambayo yana mchango mkubwa kwako<br />
katika kufanikisha au kutokufanisha zoezi la kujitathmini na<br />
kutambua kipaji chako.<br />
Hata hivyo, kwa kuwa kipaji cha asili ni hali ya kuzaliwa<br />
nayo, uchunguzi unaonesha kwamba mpaka mtu anapofikia umri<br />
wa miaka 14 tayari anaweza kujitathmini na kubaini kipaji chake.<br />
Kama mtu hakupatwa majanga ya kuathiri afya yake, uwezo wa<br />
<strong>vipaji</strong> ndani yake huendelea kuwemo ndani kama atadhamiria<br />
kujitathmini kwa kutafuta kujua anaweza nini ili kujipanga kupata<br />
elimu itakayomsaidia kunoa kipaji chake.<br />
Uwezo wa kuzaliwa nao hauwezi kuathiriwa na upungufu<br />
wa elimu au uzoefu, japokuwa elimu na uzoefu vinaweza kutumika<br />
kuboresha uwezo wa kipaji cha asili alichonacho mtu.<br />
Kila mtu amezaliwa na uwezo pekee na maalum ambao<br />
humfanya kuwa tofauti na wengine katika jamii. Yafuatayo ni<br />
baadhi ya mambo machache ya kukusaidia kutambua una <strong>vipaji</strong><br />
au kipaji gani:<br />
1. Kitu Gani Kilicho Kushughulisha Sana Utotoni?<br />
Kama wewe ni mtu mzima tayari, hasa kuanzia miaka 30<br />
na kuendelea, hebu tumia muda kama dakika mbili kujikumbusha<br />
enzi zako za furaha kuanzia shule ya msingi. Ni jambo gani<br />
34
ambapo ushiriki wako ulikuwa unapata furaha sana kiasi kwamba<br />
unapokumbuka unasisimka mpaka leo. Na jambo gani hasa<br />
lililochukulia muda mwingi na hata kukufanya ukorofishane na<br />
wazazi au walimu au watoto wenzako wakati kumbe hilo ndilo<br />
ulilokuwa ukilifurahia sana?<br />
Pengine ulikuwa unahamasika kushiriki mashindano<br />
katika michezo kama mpira wa miguu au riadha. Marafiki zako<br />
walikufurahia sana ukiwa katika timu yao wakitarajia watashinda<br />
kwa sababu yako. Na wewe uliifurahia sana hali hiyo. Pengine<br />
ulikuwa unapendelea sana kuimba kwaya au mashairi au ngoma,<br />
na hata kuwa kiongozi wa kwaya au kutunga na kufundisha<br />
nyimbo au mashairi. Pengine ulikuwa unapenda sana michezo ya<br />
kuigiza na kila mara ulikuwa nyota katika michezo uliyoshiriki.<br />
Hapa ni muhimu kutofautisha kupenda kitu kwa sababu kina<br />
umaarufu, na kuwa na uwezo wa kufanya kitu hicho kwa viwango<br />
vya ubora bila kutumia nguvu nyingi kama wengine. Maana watu<br />
wengi wanapenda mambo ambayo wanaona yamewafanya<br />
wengine kuwa maarufu na wao wanatafuta umaarufu kwa kuiga<br />
lakini hawana uwezo wa kufanya mambo hayo kwa viwango vya<br />
ubora. Kumbuka “kupenda sana” ni tofauti na “kuweza sana.”<br />
Kwa hiyo, katika kutafakari enzi zako za utotoni, hebu<br />
fuatilia ni jambo gani ambalo limeendelea kushika nafsi yako<br />
mpaka wakati huu wa ukubwani.<br />
Bado unapenda kushiriki mashindano ingawa hivi sasa<br />
ushindani wako umeuelekeza labda kwenye biashara mpya, bado<br />
unaweza kuwa unapendelea kufanya mambo magumu magumu,<br />
na miradi ya kimkakati japokuwa sasa unaifanyia kwenye<br />
makampuni ya ushauri.<br />
Mpaka hivi sasa, <strong>vipaji</strong> vya asili hujidhihirisha kupitia<br />
mambo tunayopenda sana na tunajikuta tuna uwezo nayo kuliko<br />
mengine.<br />
35
Mara nyingi msukumo wa kupenda au kuchagua kufanya<br />
mambo fulani ambayo unayamudu vizuri kuliko wengine hutokana<br />
na nguvu za <strong>vipaji</strong> vya asili vilivyomo katika nafsi zetu.<br />
2. Jambo Gani Unalipenda Sana?<br />
Swali hili ni kwa kila mtu. Jambo gani unalipenda sana.<br />
Tafadhali zingatia, kupenda kunakotajwa hapa ni mvuto wa hisia<br />
za ndani za kutamani kufanya jambo fulani hata kama hutapata<br />
malipo yoyote. Tena wakati mwingine wewe ndio uko tayari kulipia<br />
gharama za kufanya jambo unalolipenda sana badala ya wewe<br />
kulipwa.<br />
Haya tuseme leo ni jumamosi ambapo si siku ya kazi. Una<br />
muda ambao ni huru wa kufanya jambo unalolipenda. Pengine<br />
ni kupiga gitaa au kinanda au kuandika riwaya au jambo jingine<br />
lolote (lakini isiwe kutazama tv na tamthilia).<br />
Hili jambo ambalo umeamua kulifanya, kila mara<br />
unapolifanya, linakuvuta kweli kweli. Akili zote, mwili na hisia na<br />
utambuzi wa ndani vinajikuta vikilifanya kwa ukamilifu na kwa<br />
kunogewa hasa. Unazama katika kufanya jambo hilo mpaka<br />
unasahau ni saa ngapi, na hata unasahu muda wa kula.<br />
Haya, fikiria kazi unayoifanya katika siku za kawaida za<br />
kazi, kama ungeifanya katika msukumo na mvuto na mzamo<br />
kama ulivyozama kwenye jambo hili la Jumamosi huru, ufanisi<br />
wako ungelikuwaje kazini?<br />
Nakwambia watu wengi wanafanya kazi kwa sababu ya<br />
malipo ya mshahara lakini sio kwamba wanafanya kwa msukumo<br />
wa <strong>vipaji</strong> vya asili. Ndiyo maana kufanya kazi ambazo haziendani<br />
na <strong>vipaji</strong> vya asili hakuleti ufanisi mkubwa na maendeleo yake ni<br />
duni.<br />
36
Lakini kama mtu akifanya kazi ambayo inaendana na kipaji<br />
chake, hataangalia saa ya kumaliza kazi bali anavutwa kufanikisha<br />
kazi ile ifikie viwango vya ubora stahiki na hiyo ndiyo inayomfanya<br />
ajitume kufanya vema kuliko wengine.<br />
Pasipo kujali mazingira uliyomo hivi sasa, na mambo<br />
unayoyafanya kwa sababu ya desturi tu, hebu tafakari ni jambo<br />
gani ambalo una msukumo wa ndani unaokushuhudia kuwa<br />
ukilifanya utalimudu vizuri bila kutumia nguvu nyingi na utafanya<br />
kwa viwango vya ubora tofauti na wengine?<br />
Inawezekana jambo hilo ni tofauti kabisa na shughuli<br />
unayoifanya hivi sasa ambayo pengine ndiyo inayokupatia riziki.<br />
Au pengine bado ni mwanafunzi lakini masomo unayochukua<br />
hayaendani na jambo lile unalolitamani sana kulifanya na ukipewa<br />
fursa utalimudu vizuri kuliko hata masomo unayochukua hivi sasa.<br />
Kama unahusika katika eneo hili, ujue kwamba unakabiliwa<br />
na changamoto ya mgongano wa kimaslahi kati ya kipaji cha asili<br />
na mambo unayoyafanya hivi sasa yanayokupatia riziki au msaada<br />
wa kimaisha. Unahitaji hekima ya Mungu katika kuyaweka kwenye<br />
mizania sawa.<br />
Ushauri wangu hapa ni kwamba wakati wa muda wako wa<br />
ziada ambapo hauko kazini au masomoni, wakati umekamilisha<br />
majukumu yako ya kila siku kwa mujibu wa mkataba, tumia<br />
muda wa ziada katika kufanyia mazoezi hilo jambo ambalo una<br />
msukumo nalo.<br />
Kama ni mwanafunzi omba ushauri kwa wazazi/walezi na<br />
walimu kuhusu msukumo uliomo ndani yako na jinsi unavyofikiria<br />
kama ungepewa fursa ya kufanya jambo hilo ungetimiza ndoto<br />
yako kuhusu hatma yako.<br />
Kama ni mfanyakazi uliyeajiriwa au mjasiliamali<br />
unayejitegemea, hakikisha unajipanga vizuri kuhusu jinsi<br />
37
utakavyolianza jambo hilo pasipo kuingiliana na mambo yako<br />
yanayokuwezesha kupata riziki au msaada wa mahitaji yako ya<br />
sasa. Tafuta ushauri na pengine anza taratibu kwa muda wa ziada.<br />
Inategemea ni jambo gani na kama linawezekana kwa<br />
muda wa ziada. Lakini ujue kwamba kama jambo hilo linakunyima<br />
usingizi na linakukereketa kila mara, huenda kipaji chako cha asili<br />
kimebebwa kwenye jambo hilo.<br />
3. Wengine Wanasemaje Juu Yako?<br />
Njia nyingine ya kutambua una kipaji gani cha asili ni maoni<br />
ya wengine walio karibu na wewe. Ni muhimu kusikiliza kwa makini<br />
vile wengine walio karibu na wewe wanavyokutafsiri vile ulivyo.<br />
Kwa kuwa kipaji cha asili kazi yake ni kuhudumia wengine<br />
katika jambo lile ulilopewa uwezo kulifanya kwa viwango vya<br />
ubora kuliko wengine, lazima wahusika watasema habari zako<br />
kuhusu uwezo wako.<br />
Hebu tafakari ni jambo gani ambalo watu huja kwako<br />
kutafuta msaada wako, au kukuomba utoe huduma kwao kwa<br />
jambo hilo.<br />
Maoni ya wengi kuhusu jambo unalolimudu vizuri ni<br />
sehemu ya ushahidi kwamba una kipaji cha asili katika jambo<br />
hilo. Na hasa ikiwa watu wako tayari kukulipa kwa ajili ya jambo<br />
hilo. Sio kwamba wanakupenda wewe bali wanapenda kipaji<br />
chako. Wanakihitaji katika kuboresha mambo yao ambayo wewe<br />
ni mmoja wa waboreshaji wao.<br />
4. Jambo Gani Unaliweza Kwa Urahisi?<br />
Kimsingi hakuna jambo jepesi hata kama ni dogo. Lakini<br />
kwa muktadha wa mada hii, kati ya mambo ambayo ni magumu<br />
kwa wengine, huenda kuna jambo ambalo kwako ni jepesi kwako<br />
38
na halikupi shida wala kukuhenyesha kama wengine.<br />
Mara nyingi mambo ambayo ni rahisi sasa kwako, sio<br />
kwamba ni rahisi bali wewe umejaliwa uwezo maalum wa<br />
kuyamudu ndiyo maana yanakuwa mepesi kwako. Katika hayo<br />
mepesi, ambayo yanawatoa jasho wengine, huenda ndipo kipaji<br />
chako cha asili kilipolalia.<br />
Matumizi Mabaya Ya Vipaji Vya Asili<br />
Katika harakati za kutafuta na kufanya mambo kwa<br />
muktadha wa <strong>vipaji</strong> vya asili, yako mambo ambayo hayatakiwi<br />
kutafsiriwa kuwa ni <strong>vipaji</strong> vya asili. Japokuwa wahusika wanaweza<br />
kulazimisha na kushinikiza ya kwamba wanatumia <strong>vipaji</strong> vya asili<br />
kufanya mambo hayo, ukweli unabakia kwamba <strong>vipaji</strong> vya asili<br />
vinatambuliwa kwa nguvu na viashiria vyake vya ufanisi. Baadhi<br />
ya mambo ambayo si <strong>vipaji</strong> vya asili ni haya yafuatayo:<br />
1. Tamaa Ya Umaarufu Wa Kutajirika Haraka<br />
Kuna watu wenye tamaa ya kutafuta utajiri wa haraka na<br />
huwa tayari kuupata kwa haraka pasipo kufuata taratibu halali za<br />
kuupata utajiri huo. Kundi hili hutafuta “umaarufu” kama njia ya<br />
mkato ya kujipatia utajiri wa haraka.<br />
Wako tayari kuwania fursa za umaarufu kama uongozi wa<br />
kisiasa au huduma za kikanisa kwa sababu tu huko ndiko kuna<br />
majukwaa ya kuwafikia watu wengi.<br />
Misukumo ya jinsi hii haiwezi kutafsiriwa kuwa ni “<strong>vipaji</strong> vya<br />
asili” kwa sababu wahusika pamoja na kutumia nguvu kubwa za<br />
kujinadi ili wapate kukubalika, bado hushindwa kuonesha viwango<br />
vya utendaji bora katika nafasi walizozivamia tu kwa tamaa zao<br />
wenyewe.<br />
39
Mwenye kipaji cha asili katika uongozi uwe wa kisiasa au<br />
kikanisa, hatumii nguvu kubwa kujinadi wala hatumii hila na ujanja<br />
wa kujitangaza kwa vyeo akidhani vyeo ndio umaarufu. Mwenye<br />
kipaji hujikuta akiwa maarufu kutokana na ushawishi alionao wa<br />
kusikilizwa na kufuatwa na wengi kwa sababu ya mvuto wa kipaji<br />
uliomo ndani yake.<br />
2. Wivu Wa Kuharibu Mafanikio Ya Wengine<br />
Kuna kundi jingine la watu wenye wivu wa kutokufurahia<br />
mafanikio ya watu wengine. Kundi hili hujiona kwa kuwa lenyewe<br />
bado halijafanikiwa, basi hakuna haki kwa wengine kufanikiwa,<br />
na kama wakifanikiwa basi mafanikio yao kwa mtazamo wao<br />
wanayahesabu si halali.<br />
Katika msukumo wa wivu, watu hawa hujikuta wakitumia<br />
kila njia za kuzuia, kukwamisha, na hata kuharibu mafanikio<br />
ya watu wengine, na wanatafsiri kuwa hivyo ndivyo <strong>vipaji</strong> vyao<br />
vya asili! Hakuna <strong>vipaji</strong> vya kupambana na kuweka vikwazo vya<br />
kuharibu mafanikio ya wengine.<br />
Mwenye kipaji cha asili, hasumbuliwi na wivu dhidi ya<br />
mafanikio ya wengine. Badala yake hufurahia na kusifia mafanikio<br />
ya wengine na hata kujifunza mbinu za kufanikiwa kama wao ikiwa<br />
atapewa fursa hiyo. Mwenye kipaji anaweza kutumia kipaji chake<br />
kufanikisha mambo ya wengine ili mradi tu apate uzoefu kabla ya<br />
kuanza kufanya mambo yake mwenyewe.<br />
3. Wizi Wa Mawazo Ya Wengine<br />
Kundi jingine la kujihadhari nalo ni lile la wenye tamaa ya<br />
kuiba mawazo ya wengine kwa kudhani watakuwa maarufu kama<br />
wenye maono waliyodokoa bila ridhaa ya wahusika. Kundi hili<br />
linajulkana kama “copy cats”.<br />
40
Tamaa hii inafanana kidogo na ile ya kutafuta umaarufu<br />
kwa sababu ya utajiri wa haraka haraka. Ila tamaa ya jinsi hii<br />
hujikita katika kutafuta kupeleleza na kudokoa au kuiba mawazo<br />
ya wale wanaoonekana kufanikiwa ili na wao wafanikiwe kama<br />
wale wenye maono halisi.<br />
Kwa kiasi fulani wanaweza kufanikiwa ila hawafikii viwango<br />
vya ubora wa maono yale waliyoiba kwa wengine. Kuiba mawazo<br />
ya wengine sio kipaji cha asili. Huu ni wizi wa kawaida hata kama<br />
hakuna ushahidi wa kukamatwa kwa wenye tabia hizi.<br />
Ngazi Za Ukuaji Na Utendaji Wa Vipaji Vya Asili<br />
Utangulizi<br />
Baada ya kuchambua aina za <strong>vipaji</strong> vya asili na jinsi<br />
vinavyotenda kazi, sasa tunakuja kwenye ngazi au hatua za<br />
kutenda kazi kuanzia umri mdogo mpaka uzeeni.<br />
Tumejifunza katika sura ya kwanza ya kuwa <strong>vipaji</strong> vya<br />
asili ni <strong>vipaji</strong> vya kuzaliwa navyo kibaiolojia na kisaikolojia. Hii<br />
ikimaanisha ya kwamba <strong>vipaji</strong> huanza tangu mtu anapotungwa<br />
mimba katika tumbo la mama yake.<br />
Jambo jingine la kujikumbusha ni kwamba kila binadamu<br />
huumbwa na kipaji cha asili ambacho ndicho humtofautisha<br />
na binadamu wengine katika jamii. Hivyo ndivyo Mungu<br />
alivyomkusudia kila binadamu atakayezaliwa na kuishi duniani.<br />
Tunasoma ngazi za ukuaji wa kipaji cha mtu katika maandiko<br />
yafuatayo:<br />
“Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, zaeni,<br />
mkaongezeke, mkaijaze nchi na kuitiisha; mkatawale...” (Mwa.1:28)<br />
41
Katika maandiko haya tunakuta maneno muhimu yafuatayo:<br />
“zaeni”, “mkaongezeke”, “mkaijaze nchi”na “kuitiisha”. Katika<br />
maneno haya tunapata kuziona ngazi za utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani<br />
ya mtu katika mtiririko wa ngazi ya “ubunifu”, ngazi ya “uzalishaji”,<br />
ngazi ya “usimamizi” na ngazi ya “urithishaji”:<br />
1. Ngazi Ya Ubunifu<br />
Wengi hulitafsiri neno hili kwa maana moja tu “wana ndoa<br />
kuzaa watoto”! Lakini neno hili “zaeni” lina maana kubwa zaidi<br />
“kuzaa watoto”. Neno “zaeni” linabeba maana nzito ya “ubunifu<br />
wa mawazo mapya”. Kuzaa kunaanzia katika wazo kwanza. Ngazi<br />
ya kuzaa ni ngazi ya ubunifu wa mawazo ambayo wengi huyaita<br />
“maono mapya”.<br />
Wanandoa wanapoanza maisha, hatua yao ya kwanza ni<br />
ya “ubunifu wa mawazo mapya” ya jinsi wanavyotaka kuendesha<br />
maisha yao ya ndoa, kila mwanandoa akitimiza wajibu wake katika<br />
sehemu yake. Kuzaa watoto huanza katika ngazi ya ubunifu wa<br />
kuona umuhimu wa kuwa na watoto na jinsi ya kuwalea mpaka<br />
watakapokuwa watu wazima kama wao.<br />
Hatua ya kwanza ambapo kipaji ndani ya mtu kinapoanza<br />
kutenda kazi katika ubongo wake. Umri unaokadiriwa kwa kipaji<br />
kuanza ubunifu katika ngazi ya mawazo ni miaka 12-25.<br />
Muda huu ndipo mtoto anapokuwa katika mabadiliko<br />
makubwa ya kibaiolojia na kisaikolojia. Ndipo wakati anapokuwa<br />
na mawazo ya ubishi mwingi na kuhoji mambo mengi na wakati<br />
mwingine hata kujiamulia mambo kulingana na anavyowaza akilini<br />
mwake.<br />
Huu ndio wakati wa mafunzo ya kunoa <strong>vipaji</strong> unapotakiwa.<br />
Wakati anapokuwa shuleni ndio wakati ambapo waalimu na<br />
waangalizi wanatakiwa kumsoma mtoto ana kipaji gani. Na<br />
sio kumsoma tu bali kuanza kumwandaa kisaikolojia mtoto<br />
42
ajitambue na kujiandaa kwa ajili ya kutumikia kipaji chake wakati<br />
atakapohitimu masomo yake.<br />
Hapa ndipo mifumo yetu ya elimu katika nchi za kiafrika<br />
ilipodhoofishwa na wakoloni waliotawala mataifa ya kiafrika. Kwa<br />
ujanja walituandalia mifumo ya elimu kwa nia ya kutufanya vibarua<br />
katika mashamba na miradi yao, na sio kwa ajili ya kuwaandaa<br />
watoto wa kiafrika wagundue na kunoa <strong>vipaji</strong> vyao ili wakihitimu<br />
waweze kujitegemea kupitia <strong>vipaji</strong> vyao vya asili.<br />
Kwa bahati mbaya, mpaka hivi sasa bado mifumo ya “elimu<br />
tegemezi” inaendelea kutumika; na ndiyo chimbuko la “dhana ya<br />
kuajiriwa”. Badala ya mhitimu kuwa na mtazamo wa “kujitegemea”<br />
kwa yeye kubuni kazi zake za ustadi na kutoa huduma za kulipwa<br />
kulingana na thamani ya viwango vya ubora; yeye anataka “nafasi<br />
ya kuajiriwa”.<br />
Naomba ieleweke kwamba si makosa wala si dhambi<br />
kuajiriwa. Mantiki hapa ni kwamba nafasi za ajira katika serikali<br />
na taasisi za umma ambazo ni haki ya kila mhitimu ni chache<br />
kuliko idadi ya wahitimu. Na hata sekta binafsi ina vigezo vyake<br />
vya kuajiri ikiwa ni pamoja na malipo ya chini ili kutengeneza faida<br />
kubwa. Hii ndiyo changamoto ya kutegemea ajira peke yake.<br />
Kama nilivyokwisha kusema tangu awali, kila mtoto<br />
ambaye ni binadamu kamili, mwenye afya njema na akili timamu,<br />
anacho kipaji cha asili ndani yake cha kumwezesha kuishi maisha<br />
ya kujitegemea pindi atakapokuwa mtu mzima.<br />
Lakini basi, katika ngazi hii ya ubunifu, ndipo mtoto<br />
anapotumia uwezo wake wa kufikiri kuelekea aina ya kipaji chake<br />
alichoumbiwa tangu tumboni mwa mama yake.<br />
43
2. Ngazi Ya Uzalishaji<br />
Neno la pili katika ngazi za utendaji wa <strong>vipaji</strong> lilikuwa ni<br />
“mkaongezeke”. Neno hili ndilo linatuleta katika ngazi ya pili ya<br />
“uzalishaji”. Katika ngazi hii, mtoto ameondoka katika ngazi ya<br />
utoto wa kuwa tegemezi anaanza kuyatendea kazi mawazo yake<br />
mapya ambayo tayari amekwisha kuyajaribu na kupata mwelekeo<br />
wa ni nini anatakiwa kuwekeza nguvu zake zote katika uzalishaji<br />
wa kile ambacho ni kipaji chake cha asili.<br />
Katika ngazi ya uzalishaji, muhusika anatarajiwa kuwa<br />
amefikia umri wa miaka 25 na ataendelea katika nguvu za kuzalisha<br />
mpaka miaka 45.<br />
Hii inaitwa ngazi ya uzalishaji kwa sababu ndio wakati<br />
kwa mwenye kipaji anapokuwa amewekeza nguvu zake katika<br />
vipaumbele vya mambo ambayo alikwisha kuyajaribu yakaonesha<br />
mafanikio, au yakadhihirisha uwezo alio nao wa kufikia viwango<br />
vyake vya ubora. Na ndio wakati ambapo kipaji chake kinaanza<br />
kumpatia mhusika matunda au malipo stahiki. Ndio wakati wa<br />
kufanya mikataba ya malipo au kuendesha huduma za kujitegemea<br />
na kutengeneza ajira kwa wengine.<br />
3. Ngazi Ya Usimamizi<br />
Usimamizi ni ngazi ya tatu katika kukuza na kutendea kazi<br />
<strong>vipaji</strong> vya asili. Usimamizi unaotamkwa hapa ni uzoefu unaofikia<br />
hekima na busara ya kuanza kuweka akiba na kutunza mali na<br />
fedha zilizokwisha kupatikana kutokana na uzalishaji mzito<br />
uliotangulia katika ile hatua ya pili.<br />
Umri wenyewe ambao ni kuanzia miaka 45 hadi kufikia<br />
miaka 55 ndipo akili za wenye <strong>vipaji</strong> hupata msukumo wa kutunza<br />
kile kinachozalishwa kupitia <strong>vipaji</strong> na taaluma zao huku wakihisi<br />
nguvu za mwili zinaanza kupungua.<br />
44
Aidha, hii ndiyo hatua ambayo wenye <strong>vipaji</strong> wenye hekima<br />
wanapoanza kupunguza majukumu na kukaimisha au kunaibisha<br />
kwa wale wanaotarajia kuwarithisha majukumu ya kiuchumi na<br />
kiuongozi.<br />
Na ndio wakati huu ambapo kizazi kipya cha umri wa miaka<br />
25 kinapojaribiwa katika kubeba baadhi ya majukumu ili kunoa<br />
<strong>vipaji</strong> vyao vya asili katika uzalishaji na uongozi pia.<br />
Mwasisi aliyekuwa ndiye Mtendaji Mkuu wa kampuni<br />
au taasisi ya huduma hupunguza majukumu na kuyagawa kwa<br />
walioko chini yake ambao anawaandaa kushika hatamu badala<br />
yake.<br />
Lile neno “kutiisha” katika Biblia kwa kiingereza linaitwa<br />
“replenish” likimaanisha kujaza tena, au kuziba utupu uliokuwepo<br />
mahali. Katika usimamizi wa <strong>vipaji</strong>, kutiisha ni kuongeza nguvu<br />
mahali ambapo nguvu zilianza kupungua katika uzalishaji. Ni<br />
kuongeza nguvu katika usimamizi wa vilivyokwisha kuzalishwa ili<br />
vidumu na kuendelea kusaidia kizazi kinachoinukia.<br />
4. Ngazi Ya Urithishaji<br />
Urithishaji ndio hatua ya nne na ya mwisho katika kukuza<br />
na kutendea kazi <strong>vipaji</strong> vya asili. Nitaelezea kwa kina kipengele<br />
hiki katika Sura ya Nne kwa sababu kinawahusu zaidi warithishaji<br />
kuliko warithishwaji.<br />
Hata hivyo, kwa muktadha wa hatua za ukuaji na utendaji<br />
wa <strong>vipaji</strong> vya asili, hatua hii ndiyo ya juu na mwisho kwa wote<br />
wenye umri kuanzia miaka 55-65. Hiki ndicho kizazi kinachotakiwa<br />
kustaafu na kukabidhi majukumu ya uzalishaji na uongozi kwa<br />
kizazi kipya.<br />
Lakini ni muhimu kutambua kuwa kukabidhi sio kususa au<br />
kukimbia majukumu ghafla, eti kwa sababu ya uzee. Kukabidhi<br />
45
lazima kuwe ni mchakato wa taratibu na wenye kukabidhi<br />
wanabaki kutoa ushauri elekezi kwa waliowarithisha.<br />
46
SURA TA TATU<br />
CHANGAMOTO ZINAZOATHIRI VIPAJI<br />
VYA ASILI<br />
Utangulizi<br />
Baada ya kujifunza utajiri mkubwa uliomo katika <strong>vipaji</strong><br />
vya asili na michakato ya kuvikuza, maswali makubwa yanakuja<br />
akilini na kuhoji kama kweli kila binadamu huzaliwa na kipaji cha<br />
kumwinua na kumfanikisha kwa viwango vya ubora wa hali ya<br />
juu, je, kwanini sasa hatuvioni <strong>vipaji</strong> hivi vikifanya kazi kwa kila<br />
mtu katika jamii? Kwanini ni watu wachache sana ambao ndio<br />
wanatokea kuwa maarufu kupitia <strong>vipaji</strong> vya asili?<br />
Katika kusaidia kupatikana kwa majibu ya maswali haya<br />
na mengine yenye kufanana na haya, ndiyo maana sura hii<br />
imeandaliwa ili kufanya uchambuzi makini kuhusu changamoto<br />
zenye kuathiri <strong>vipaji</strong> vya asili, tukianza na kipengele cha vikwazo<br />
vya maendeleo ya <strong>vipaji</strong> na karama.<br />
Changamoto maana yake ni mambo yanayojitokeza<br />
kinyume na maendeleo ya mtu. Hata hivyo, changamoto ni<br />
sehemu ya maisha ya kila mtu na ndiyo maana maisha hutafsiriwa<br />
kuwa ni “mapambano” dhidi ya “changamoto”.<br />
Sasa tunapokuja katika suala la <strong>vipaji</strong>, napo zipo changamoto<br />
ambazo kusudi lake kama sio kuharibu kabisa, basi ni kudhoofisha<br />
utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya wahusika. Kwa hiyo ndiyo maana ni<br />
vema kuzifahamu, na kisha kupata mbinu za kupambana nazo<br />
kikamilifu. Changamoto zenyewe zimegawanyika katika sehemu<br />
kuu mbili.<br />
47
Sehemu ya kwanza ni “changamoto za nje” kwa maana<br />
ya mambo hasi yanayomzunguka kila mtu ili kudhoofisha kipaji<br />
chake. Pili, ni “changamoto za ndani” ambazo ni mambo hasi<br />
ya ndani yanayomwathiri kila mtu binafsi kitabia. Hebu tuanze<br />
kuchambua baadhi ya hizo changamoto za nje.<br />
Changamoto Za Nje<br />
Katika ulimwengu tunamoishi tumezungukwa na mambo hasi<br />
mengi yaliyoko kinyume nasi ambayo ni lazima tupambane<br />
nayo ikiwa kweli tunataka kuendeleza <strong>vipaji</strong> vyetu kama Mungu<br />
alivyotukusudia. Baadhi ya mambo hayo ni pamoja na:<br />
1. Marafiki Wabaya<br />
Binadamu ameumbwa na hulka ya ushirika na binadamu<br />
wengine. Katika hulka hizo, kuna binadamu wanakuwa na ushirika<br />
wa karibu zaidi kuliko binadamu wengine. Na ndipo msamiati wa<br />
neno urafiki unapoanzia. Katika harakati za kutambua na kukuza<br />
<strong>vipaji</strong> mbali mbali lazima kuwepo kwa ushirikiano na watu wengine<br />
hususan wenye <strong>vipaji</strong> vinavyoshabihiana. Ni katika harakati za<br />
kutafuta kukuza na kutumia kukuza <strong>vipaji</strong> ndipo mtu hujenga<br />
ukaribu na watu wapya ambao huwa marafiki.<br />
Tafsiri Ya Marafiki Wabaya<br />
Tafsiri ya msamiati wa neno rafiki maana yake ni “mtu<br />
anayependana na kuaminiana na mwingine; sahibu, mwandani,<br />
bui, somo, na mbasi.” Maneno muhimu ya tafsiri ya urafiki ni<br />
“kupendana” na “kuaminiana.”<br />
Lakini kwa muktadha wa kipengele hiki, ni muhimu<br />
kufahamu kuna “marafiki wema” na “marafiki wabaya.” Kuwa na<br />
marafiki wabaya maana yake ni “kupendana na kuaminiana na<br />
marafiki wabaya”<br />
48
Aina Za Marafiki Wabaya<br />
Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, “marafiki wabaya”<br />
wamegawanyika katika makundi mbali mbali ambayo ni kama<br />
haya yafuatayo:<br />
“Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki;<br />
wala hakusimama katika njia ya wakosaji; wala hakuketi barazani<br />
pa wenye mizaha. Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na<br />
sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti<br />
uliopandwa kandokando ya vijito vya maji, uzaao matunda yake kwa<br />
majira yake, wala jani lake halikauki; na kila alitendalo litafanikiwa.<br />
Sivyo walivyo wasio haki; hao ni kama makapi yapeperushwayo<br />
na upepo. Kwa hiyo, wasio haki hawatasimama hukumuni, wala<br />
wakosaji katika kusanyiko la wenye haki. Kwa kuwa BWANA<br />
anaijua njia ya wenye haki, bali njia ya wasio haki itapotea.” (Zab.<br />
1:3-6)<br />
Katika maandiko haya tunasoma kuhusu “shauri la wasio<br />
haki”, “njia ya wakosaji” na “baraza la wenye mizaha”. Kupitia<br />
maneno haya ndipo tunayapata makundi ya aina tatu ya “marafiki<br />
wabaya”.<br />
Kundi la kwanza la marafiki wabaya ni “wasio haki” ambao<br />
tafsiri yake ni “watu waovu au wahalifu”. Na maana ya “kutokwenda<br />
katika shauri la wasio haki” maana yake ni kutokupokea na<br />
kutendea kazi “ushauri wa waovu au wahalifu.”<br />
Kundi la pili la “marafiki wabaya” ni “wakosaji” ambao<br />
tafsiri yake ni watu “watenda dhambi” au “wasio na maadili ya<br />
kimungu”. Makatazo ya “kutokusimama katika njia ya wakosaji”<br />
tafsiri yake ni “kujitenga na vitendo vya dhambi za hao “watenda<br />
dhambi”.<br />
Kundi la tatu la “marafiki wabaya” ni la watu “wenye<br />
mizaha” ambao maana yake ni “watu wenye maneno ya dhihaka,<br />
49
kejeli, na dharau, dhidi ya itikadi za watu wengine”. Maandiko<br />
yanamkataza mchaji Mungu kutojumuika na makundi ya watu<br />
wenye “kudhihaki” na “kukejeli” itikadi za wengine.<br />
Athari Za Marafiki Wabaya<br />
Muktadha wa “marafiki wabaya” unalenga watu wenye<br />
tabia mbaya wanapokuwa na ushawishi wa kuvutia kwa “watu<br />
wema” hata wakajenga urafiki baina yao. Biblia ndiyo imeandika<br />
habari za kutahadharisha “watu wema” kujihadhari katika kujenga<br />
ushirika wa kirafiki na watu wabaya ambao huathiri vibaya tabia<br />
njema:<br />
“Msidanganyike; mazungumuzo mabaya huharibu tabia<br />
njema.” (1 Kor. 15:33)<br />
“Do not be deceived: [a] Bad company corrupts good<br />
morals.”<br />
Maandiko haya hapo juu yanashuhudia jinsi ambavyo<br />
marafiki wabaya wanavyoweza kuathiri tabia njema za wachaji<br />
Mungu.<br />
Marafiki wabaya sio tu hauthiri tabia njema za watu wema,<br />
lakini pia huathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya asili vya watu wema.<br />
Pale mtu mwenye kutaka kunoa kipaji chake anaposhirikiana na<br />
marafiki wabaya, urafiki huo husababisha kukwamisha juhudi za<br />
kutumia kipaji chake kwa viwango vyake vya ubora, maana hata<br />
yeye huharibika.<br />
Kutokana na kuwa na marafiki wabaya, kuna <strong>vipaji</strong> vingi<br />
vimeathiriwa kwa sababu ya wahusika nao kuharibika kitabia.<br />
2. Imani za uchawi na ushirikina<br />
Uchawi na ushirikina ni changamoto inayoongoza katika<br />
kudhoofisha utendaji bora wa <strong>vipaji</strong> vya asili. Tafsiri ya ‘uchawi’<br />
50
maana yake ni ufundi wa kutumia dawa au vitabu maalum vya<br />
uganga ili kuleta madhara kwa viumbe; na maana nyingine ni<br />
‘vifaa vinavyotumika katika shughuli za kurogea’.<br />
Utafiti uliofanyika umeonesha dhahiri ya kwamba imani za<br />
uchawi na ushirikina ni kikwazo kikubwa sana kwa maendeleo ya<br />
<strong>vipaji</strong> vya asili. Pamoja na kwamba Biblia imekataza watu kushiriki<br />
katika vitendo vya uchawi na ushirikina, lakini bado vitendo<br />
hivyo vimekuwa vikiongoza katika kuvuta watu wengi wakidhani<br />
wanakwenda kupata nguvu za kunoa <strong>vipaji</strong> kumbe wanajikuta<br />
wanapokea nguvu za kukwamisha na kuharibu <strong>vipaji</strong> vyao. Ndiyo<br />
maana maandiko matakatifu yalikataza na kupiga marufuku<br />
ushiriki wa vitendo vya uchawi na ushirikina kama ilivyoandikwa<br />
hapa chini:<br />
“Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti<br />
yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu<br />
atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,<br />
wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye<br />
pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. Kwa maana mtu<br />
atendaye hayo ni chukizo kwa BWANA; kisha ni kwa sababu ya<br />
hayo BWANA, Mungu wako, anawafukuza mbele yako”(Kumb.<br />
18:10-12)<br />
Ni miaka miwili iliyopita tangu Tanzania ilipotangazwa<br />
kushika nafasi ya kwanza kwa umahiri wa kuamini katika uchawi<br />
kimataifa. Mojawapo ya taasisi zilizoitangaza Tanzania kwamba<br />
imekithiri kwa mambo ya uchawi ni Pew Research lenye makao<br />
yake Washington DC nchini Marekani.<br />
Kwa mujibu wa taarifa zake inasadikiwa kwamba miongoni<br />
mwa nchi 19 za kusini mwa Jangwa la Sahara zilizofanyiwa<br />
utafiti, Tanzania iliongoza kwa kuwa na idadi ya watanzania 93%<br />
wanaoamini katika uchawi na ushirikina.<br />
51
Aidha, inasadikiwa pia ya kuwa vitendo vya uchawi<br />
vinavyoongoza Tanzania ni pamoja na juju, utoaji wa kafara kwa<br />
mizimu kwa ajili ya bahati za kupata vyeo, utajiri na umaarufu<br />
katika michezo na muziki.<br />
Sasa basi, katika mazingira kama haya, tunaweza kuona<br />
jinsi ushirikina na uchawi vinavyodhoofisha <strong>vipaji</strong> vya asili kwa<br />
sababu ya wahusika kutegemea ndumba badala ya kutambua na<br />
kunoa <strong>vipaji</strong> vijiendeshe vyenyewe.<br />
3. Mifumo Butu Ya Elimu<br />
Mifumo butu ya elimu ni “mitaala ya elimu isiyolenga kunoa<br />
<strong>vipaji</strong> vya wanafunzi.” Pamoja na kwamba elimu inayotolewa<br />
kweli inawapatia wanafunzi maarifa ya kawaida ya kujua kusoma<br />
na kuandika pamoja na ujuzi katika masomo mengineyo;<br />
changamoto kubwa ni pale ambapo wahitimu wengi hawana<br />
uwezo wa kujitegemea kiuchumi pasipo fursa ya ajira.<br />
Wakati kipaji kinamjengea mtoto uwezo wa kubuni na<br />
ustadi wa kazi atakayoimiliki mwenyewe; elimu bado ni butu<br />
kwa kuwa haimwezeshi mtoto kutambua na kunoa kipaji chake<br />
ambacho akihitimu kitamwezesha kujitegemea moja kwa moja.<br />
Elimu ya sasa inamfanya mwanafunzi akihitimu awazie<br />
kutafuta ajira peke yake, badala ya kubuni na kusimamia kazi<br />
yake mwenyewe. Ndiyo maana changamoto ya ukosefu wa ajira<br />
itaendelea kuwepo kwa muda mrefu kwa sababu uzalishaji wa<br />
wahitimu hauendani na fursa za ajira zilizopo katika jamii.<br />
Ufumbuzi kamili wa tatizo la ukosefu wa ajira ni lazima<br />
uanzie kwenye mitaala ya elimu ambayo italenga kuibua na kunoa<br />
<strong>vipaji</strong> vya watoto ili wanapohitimu wanakuwa na ujuzi kubuni kazi<br />
zao wenyewe na kujitegemea kiuchumi badala ya kutegemea<br />
ajira.<br />
52
Athari Za Utandawazi Dhidi Ya Vipaji Vya Asili<br />
Tafsiri Ya Utandawazi<br />
“Mfumo wa uhusiano wa kimataifa katika nyanja mbali mbali<br />
kama vile biashara, uchumi au siasa uliowezeshwa na maendeleo<br />
ya teknolojia ya habari yanayofanya mataifa kuwasiliana kwa<br />
urahisi.” (Kamusi Ya Kiswahili Sanifu).<br />
Nguvu Za Mitandao Ya Kijamii<br />
Miaka ya hivi karibu, mitandao ya kijamii imekuwa na<br />
ushawishi mkubwa kiulimwengu kwa kiasi ambacho kasi yake ni<br />
tishio kwa maadili ya kizazi kipya. Katika mwaka 2017 kiwango<br />
cha ushawishi wa mitandao ya kijamii kimepanda kwa viwango<br />
vifuatavyo:<br />
• Facebook hivi sasa ina watumiaji zaidi ya milioni 900<br />
• 50% ya ulimwengu mzima iko chini ya umri wa miaka 50<br />
• 96% ya umri kuanzia miaka 18-35 wako ni watumiaji wa<br />
mitandao ya kijamii<br />
• Kama facebook ingekuwa ni nchi, ingeshika nafasi ya tatu kwa<br />
ukubwa ulimwenguni<br />
• Mtumiaji wa kawaida wa facebook ana marafiki 130<br />
• Youtube ni ya pili kwa mtandao mkubwa ulimwenguni<br />
• Twitter nayo immeshafikia watumiani milioni 500<br />
• Kama Twitter ingelikuwa ni nchi ingekuwa ya 12 kwa ukubwa<br />
duniani. Kuna watu 750 wanao-twiti kila nukta.<br />
• Kuna wenye kurasa (blogs) zaidi ya milioni 200<br />
• Kuna kurasa mpya mlioni 3 zinazofunguliwa kwenye internet<br />
kila mwezi<br />
• Kuna picha milioni 5 zinazorushwa kwenye instagram kila siku<br />
• Watu zaidi ya bilioni 6.9 wamekwisha kutazama Youtube<br />
channel<br />
53
Matokeo Chanya Ya Matumizi Ya Mitandao Ya Kijamii<br />
Kama ilivyo kawaida ya vuguvugu jipya linaloibuka katika<br />
jamii linakuwa na matokeo ya aina zote mbili. Kuna matokeo<br />
chanya na pia kuna matokeo hasi. Hebu tuangalie matokeo<br />
chanya ya matumizi ya mitandao ya kijamii:<br />
• Husaidia kujenga mitandao ya kibiashara na huduma za<br />
kijamii. Matangazo ya biashara kupitia redio, televisheni na<br />
magazeti yana gharama kubwa. Lakini kupitia mitandao ya<br />
kijamii matangazo yanawafikia wateja wengi kwa gharama<br />
nafuu sana na wakati mwingine bure.<br />
• Mitandao ya kijamii imetoa fursa kwa wenye <strong>vipaji</strong> na taaluma<br />
mbali mbali kuwasiliana na kupeana taarifa na wateja wao<br />
kuliko ilivyokuwa huko nyuma.<br />
• Mitandao ya kijamii imeondoa vikwavyo vya mawasiliano ya<br />
moja kwa moja. Wanafunzi wanawasiliana na wataalamu na<br />
kubadilisha taarifa muhimu.<br />
• Mitandao ya kijamii imeunganisha watu kimawasiliano na<br />
kuwezeshana katika kutimiza malengo kuanzia ngazi ya<br />
kifamilia, kitaifa na kimataifa (dunia nzima imekuwa kijiji<br />
kimoja).<br />
• Kuna soko pana zaidi. Unaweza kuuza bidhaa nyingi zaidi na<br />
kupata faida, na hata kutengeneza ajira.<br />
• Walaji nao hunufaika. Ushindani hufanya bidhaa kuwa na bei<br />
za chini, na upatikanaji haraka wa bidhaa mpya.<br />
Matokeo Hasi Ya Matumizi Ya Mitandao Ya Kijamii<br />
• Inashika Nafsi Kama Ulevi Sugu.<br />
• Kutumia muda mwingi zaidi kwenye mitandao ya kijamii na<br />
kushindwa kufanya mambo mengine yenye tija.<br />
• Inadhoofisha Mahusiano Ya Ana Kwa Ana<br />
• Inadhoofisha motisha wa kuhusiana na watu moja kwa moja,<br />
na hasa kwa vijana na wanafunzi.<br />
• Wanakuwa tegemezi kwenye teknolojia na internet zaidi kuliko<br />
54
kujifunza kwa akili ili kupata ujuzi wa maisha ya kila siku.<br />
• Jumbe Za Vitisho Na Udhalilishaji (Cyberbullying)<br />
• Shirika moja lijulikanalo kama Enough is Enough, lilifanya utafiti<br />
na kugundua kwamba 95% vijana wanaotumia mitandao ya<br />
kijamii wameshuhudia mawasiliano ya vitisho na udhalilisha na<br />
33% yao ni waathirika wa mawasliano hayo<br />
• Watoto Huathirika Vibaya Zaidi Na Mitandao Ya Kijamii<br />
Wasipodhibitiwa<br />
• Hii ni kwa sababu kwenye mitandao hii zinarushwa picha<br />
mbaya za ugomvi na picha za uchi ambazo huwaathiri<br />
kisaikolojia watoto na vijana. Baadaye husababisha watoto na<br />
vijana kujihusisha na vitendo vya uhalifu na ngono haramu.<br />
• Kichocheo Cha Mkengeuko Wa Maadili Mema<br />
• Maambukizi ya mkengeuko wa maadili ya kimaani na<br />
kiutamaduni kwa sababu ya mwingiliano wa walioharibika<br />
kitabia, waliojaa tamaa ya kupata faida kubwa bila kujali<br />
maadili mema katika nchi husika.<br />
Changamoto Za Ndani<br />
Katika utangulizi wa sehemu hii tumepata tafsiri kuhusu<br />
changamoto za ndani kuwa ni mambo hasi ya ndani yanayomwathiri<br />
kila mtu binafsi kitabia. Katika uchambuzi wa changamoto za<br />
ndani tunakwenda kutumia msamiati mpya ambao unaitwa “tabia<br />
sugu”. Msamiati huu unalenga kuchambua tabia sugu zenye<br />
kuathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya mhusika.<br />
Tafsiri Ya Misamiati Ya Tabia Sugu<br />
Sasa tumefikia kipengele ambacho hasa ndio kikwazo<br />
sugu chenye kuathiri <strong>vipaji</strong> vya asili katika jamii. Labda nianze na<br />
uchambuzi wa misamiati. Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili<br />
Sanifu, neno “tabia” limetafsiriwa kuwa ni: “mazoea yatokanayo<br />
na kurudiarudia hali, mwenendo au matendo”<br />
55
Kamusi ya Kiswahili Sanifu imelitafsiri neno “sugu”<br />
kuwa ni “hali isiyoweza kuondolewa kwa urahisi”. Usemi “tabia<br />
sugu” haumo katika kamusi kama msamiati; isipokuwa mimi<br />
nimeyaunganisha maneno mawili, “tabia” na “sugu” na kupata<br />
usemi maalum wa “tabia sugu”.<br />
Kwa hiyo kama ukiunganisha tafsiri za maneno “tabia” na<br />
“sugu” unapata maana ya usemi wetu wa “tabia sugu”ambao tafsiri<br />
yake ni: “mazoea yatokanayo na kurudiarudia hali, mwenendo au<br />
matendo isiyoweza kuondolewa kwa urahisi”.<br />
Maeneo Ya Uharibifu Wa Tabia Sugu<br />
Uharibifu Wa Kitabia<br />
Sehemu ya kwanza ya madhara ya tabia sugu ni uharibifu<br />
wa kitabia unaolenga kuharibu “utu”, “ubinadamu” na “uungwana”<br />
katika maisha ya mwathirika. Pengine ni vizuri tukaangalia<br />
misamiati ya maneno haya ya “utu”, “ubinadamu” na “uungwana”<br />
ili tujue maana zake:<br />
Neno “utu” limetafsiriwa kuwa ni: “hali ya kuwa na tabia<br />
zinazolingana na hadhi ya mtu”. Neno “ubindamu” limetafsiriwa<br />
kuwa ni: “hali ya utambuzi wa jinsi ya kutekeleza wajibu juu ya<br />
maisha katika jamii”. Neno “uungwana” limetafsiriwa kuwa ni:<br />
“mtu mwenye adabu na tabia zinazokubalika katika jamii”.<br />
Baada ya kupata tafsiri ya misamiati hapo juu tunaweza<br />
kuona kwamba madhara mabaya ya “tabia sugu” kwa mhusika<br />
ni: kumharibia (utu); ambao ni hadhi yake kama mtu; kumharibia<br />
(ubinadamu wake) ambao ni hali ya utambuzi wa kutekeleza<br />
wajibu wake kwa jamii; kumharibia (uungwana) ambao ni<br />
adabu na kumfanya kutokukubalika kitabia katika jamii. Haya<br />
ndiyo madhara ya “tabia sugu” ambayo kimsingi, ndiyo yenye<br />
kukwamisha utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya walio navyo, na kukwama<br />
kufikia viwango vya mafanikio kulinganana <strong>vipaji</strong> vyao.<br />
56
Hata hivyo, ashukuriwe Mungu kupitia Bwana Yesu Kristo<br />
ambaye kwa neema yake ametoa ufumbuzi wa kupambana na<br />
kukomesha madhara ya tabia sugu, ikiwa masharti na kanuni<br />
zitazingatiwa:<br />
“Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani,<br />
ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa TABIA YA UUNGU<br />
mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa” (1<br />
Pet. 1:4)<br />
Mungu ameahidi, kupitia Yesu Kristo, waathirika wa tabia<br />
sugu, wanaweza kubadilika, na kunusurika na uharibifu wa dunia<br />
hii unaosababishwa na tamaa na kwa kubadilika kitabia na kuwa<br />
wachaji Mungu na raia wema katika jamii.<br />
Uharibifu Wa Kiafya<br />
Kudhoofisha mishipa inayosafirisha damu moyoni, uharibu<br />
wa mfumo wa neva, ambao huanzia katika kudhoofisha uwezo<br />
wa kufikiri na hatimaye kuishia kuwa zezeta; saratani ya damu;<br />
shinikizo la damu na maradhi ya moyo; maradhi ya mtoto wa<br />
jicho; saratani ya mlango wa kizazi; saratani ya figo; saratani ya<br />
kongosho; saratani ya tumbo; maradhi ya uasherati na zinaa na<br />
VVU/UKIMWI.<br />
Uharibifu Wa Kifamilia<br />
Uharibifu wa kifamilia utokanao na tabia sugu ni pamoja<br />
na: Migororo sugu katika ndoa; ugumba na utasa (utoaji mimba/<br />
madawa ya kuzuia mimba); wanandoa kutelekezana/kuvunjika<br />
kwa ndoa; malezi mabovu kwa watoto; ongezeko la watoto wa<br />
mitaani.<br />
57
Uharibifu Wa Kiuchumi<br />
Uharibifu wa kiuchumi utokanao na tabia sugu ni pamoja<br />
na: Ufukara katika familia; udhaifu katika ubunifu wa mipango<br />
endelevu ya kiuchumi; rasilimali asilia kuwanufaisha wageni badala<br />
ya wenyeji; uharibifu wa mazingira; wenyeji kuwa watumwa wa<br />
wageni katika nchi yao wenyewe.<br />
Aina 5 Za Tabia Sugu Zenye Kuharibu Vipaji<br />
1. Tabia Ya Kunung’unika Na Kuhukumu<br />
Kunung’unika ni hali ya “kusema kwa sauti ya chini, aghalabu<br />
peke yako; kusema kwa kulalamika kwa sababu yakutokuridhika<br />
na jambo.”<br />
Kuhukumu ni hali ya “kuhesabia wengine makosa pasipo<br />
ushahidi” “kusema makosa ya wengine pasipo ridhaa yao na kwa<br />
nia ya kuwadhalilisha”.<br />
Mtu mlalamishi na mgung’unikaji na mwenye kuhukumu<br />
wengine huwa ni mwathirika wa mtazamo hasi dhidi ya wengine.<br />
Ni mtu aliyejawa na mawazo mabaya ya kutafuta makosa ili apate<br />
kukosoa na kuhukumu kwa nia ya kuona wahusika wanapatwa na<br />
mabaya kama adhabu ya makosa yao.<br />
Je, Unapenda kukosoa na kutoa lawama dhidi ya wengine?<br />
Unasukumwa kutafuta makosa katika kila jambo au kwa kila mtu?<br />
Huwa unaona ugumu au uzito wa kuona jambo jema pasipo kuona<br />
makosa? Unajiona huru kukosoa na kulaumu wengine hadharani<br />
pasipo kujali hisia zao wala heshima zao? Kama majibu ya maswali<br />
haya kwako ni “ndiyo” maana yake wewe ni mwathirika wa fikra<br />
na mtazamo hasi wa kulaumu na kuhukumu wengine.<br />
58
Angalizo<br />
Si kila kukosoa ni mtazamo hasi. Wala kuona makosa<br />
na kuyasema kwa nia ya kusahihisha sio vibaya. Muktadha<br />
wa kipengele hiki ni kwa wale walioathiriwa na “tabia sugu ya<br />
kulalamika na kuhukumu wengine”.<br />
Mtu ambaye hajaathiriwa na tabia sugu ya kulalamika<br />
na kuhukumu wengine anapoona makosa huchukua hatua za<br />
kumwendea mkosaji na kumwelimisha kwa nia njema na lugha<br />
ya upole, tena baada ya kumsikiliza kwanza na kupata uhakika<br />
kutoka kwa muhusika.<br />
Lakini mwathirika wa tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu<br />
wengine, hata kama analalamikia mambo ya kweli, huwa hatumii<br />
njia ya kuelimisha bali lugha ya kudhalilisha hadharani kwa kuanika<br />
makosa ya wengine. Tatizo huwa sio “kuona makosa” bali “njia ya<br />
kushughukilia makosa yenyewe”<br />
Mtu ambaye ni mwathirika wa “tabia sugu ya kulalamika<br />
na kuhukumu wengine” anaweza hata kujitetea ya kwamba ana<br />
mzigo wa kuwasaidia wale anaowakosoa wajirekebishe; lakini<br />
lugha inayotumika katika kukosoa ni ya kuudhi, kuumiza hisia,<br />
kudhalilisha, na kuwavunjia heshima wengine hadharani, wale<br />
anaodai kuwakosoa.<br />
Dalili Kuu Za Tabia Ya Kulalamika Na Kuhukumu Wengine<br />
Ulalamishi<br />
Mlalamishi ni mtu mwenye hulka ya kutokuridhika<br />
na mambo ya wengine. Hata pale mambo yakifanyika vizuri<br />
walalamishi hawana shukrani wala pongezi kwa wengine. Lakini<br />
likitokea dosari au udhaifu wao wataukomalia huo utafikiri hakuna<br />
jambo jema kwa wale wanaolalamikiwa.<br />
59
“Ndugu msinung’unukiane, msije mkahukumiwa. Angalieni,<br />
mwamuzi amesimama mlangoni.” (Yak. 5:9)<br />
“Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala<br />
mashindano, mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama,<br />
wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi<br />
kilichopotoka’ ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga<br />
katika ulimwengu.” (Flp. 2:14-15)<br />
Tabia ya kuhukumu wengine<br />
Mwenye lawama za hukumu ni mtu aliyeathiriwa na<br />
mtazamo hasi wa kuhukumu wengine kwa dhana pasipo ushahidi<br />
kamili. Mwepesi wa kulaumu bila hata kusikia upande wa pili<br />
unasemaje kuhusu jambo husika. Hujiamini sana kwamba ana<br />
ujuzi wa kugundua makosa ya wengine lakini yeye mwenyewe<br />
haoni makosa yake mwenyewe.<br />
“Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona<br />
huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.” (Yak. 2:13)<br />
Usengenyaji<br />
Msengenyaji ni yule mwenye kufunua mambo binafsi ya siri<br />
za wengine kwa nia ya kuwadhalilisha na kuwavunjia heshima zao<br />
mbele za wengine. Msengenyaji hujifanya kuwa na taarifa nyeti za<br />
mambo ya watu lakini mwenyewe hayuko tayari kujulikana kama<br />
ndiye chanzo cha taarifa hizo.<br />
“Tena pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizungukazunguka<br />
nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni<br />
wachongezi na wadadisi wakinena maneno yasiyowapasa.”<br />
(1 Tim. 5:13)<br />
60
Udhalilishaji<br />
Mdhalilishaji ni mtu anayezua mambo ya uongo kwa nia ya<br />
kuharibu heshima na hadhi za wengine hadharani. Mdhalilishaji<br />
huzalisha kashfa ili kuharibu maisha ya wengine.<br />
“Basi wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na<br />
husuda na masingizio yote.” (1 Pet. 2:1)<br />
Madhara Ya Kulalamika Na Kuhukumu Wengine<br />
Hudhoofisha Ubunifu Wa Kipaji<br />
Mwathirika wa mtazamo hasi wa kulalamika na kuhukumu<br />
hukiathiri kipaji chake cha asili kwa kudhoofisha uwezo wake wa<br />
asili wa kubuni mambo mapya. Kumbuka ya kwamba utendaji wa<br />
kipaji unategemea nguvu za ubunifu wa mambo mapya. Na nguvu<br />
za ubunifu hutokana na mawazo chanya.<br />
Kimaumbile “mawazo hasi” hayawezi kutenda kazi kwa<br />
wakati mmoja na “mawazo chanya”. Kila kimoja kinafanya kazi<br />
kwa wakati wake kinapokuwa kimepewa nafasi ya kwanza. Kwa<br />
hiyo, “mawazo hasi” huamsha “hisia hasi” ambazo huwa kikwazo<br />
cha utendaji wa mawazo chanya. Wakati mwathirika wa mtazamo<br />
hasi hutumia mawazo hasi na kughubikwa na hisia hasi; hali hiyo<br />
huzuia upande wa pili wa mawazo chanya na hisia chanya kufanya<br />
kazi kwa wakati mmoja.<br />
Changamoto iliyopo hapa ni kwamba, muda wote ambapo<br />
mawazo hasi, na hisia hasi vinatenda kazi ndani ya mwathirika,<br />
kipaji chake kinakuwa kimefungiwa ule uwezo wake wa kutenda<br />
kazi yenye tija kwa muhusika. Kwa hiyo, muda mwingi unaopotea<br />
kwenye kulalamika na kuhukumu wengine, mambo yake<br />
mwenyewe husimama au kukwama.<br />
61
Huharibu Mahusiano Na Wengine<br />
Mara nyingi, mwathirika wa “tabia sugu ya kulalamika na<br />
kuhukumu wengine” huwa hana marafiki wengi. Na hata akiwapata<br />
hawadumu pamoja naye kwa muda mrefu. Hata wale wachache<br />
anaobaki nao hugombana nao mara kwa mara. Tena baadhi ya<br />
hao marafiki wachache nao pia huwa ni waathirika wa tabia sugu<br />
hiyo hiyo ya kulalamika na kuhukumu wengine kama yeye.<br />
Katika mazingira ya kuwa na marafiki wachache, au<br />
kukimbiwa na marafiki, hali hii husababisha <strong>vipaji</strong> vya mwathirika<br />
kutokuwafikia na kuwahudumia walengwa wa <strong>vipaji</strong> vyake. Maana<br />
mwathirika wa “tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu wengine”<br />
anaweza kuwa na kipaji kizuri sana lakini kimeathiriwa na hulka<br />
yake. Kila anapokitumia kinakuwa kama chakula kitamu lakini<br />
chenye pilipili kupita kiasi. Kila anayekula lazima pua zitalowa kwa<br />
mafua na macho kutoka machozi mengi.<br />
Kwenda Kinyume Na Makatazo Ya Yesu Kristo<br />
Yesu Kristo mwenyewe pamoja na kwamba alikuwa<br />
mkali katika kukosoa mitazamo hasi ya jamii ya Mafarisayo<br />
na Masadukayo; bado alipiga marufuku kwa wanafunzi wake<br />
kuendekeza tabia ya kulalamika na kuhukumu wengine:<br />
“Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi<br />
hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.” (Luk. 6:37)<br />
Makatazo ya Yesu kuhusu tabia ya kulaumu na kuhukumu<br />
kunadhirisha matokeo ya tabia hiyo kuwa inaambatana na<br />
malipizo yake. Unapomlaumu na kumhukumu mtu mwingine na<br />
kumsababishia maumivu pamoja na madhara, maana yake wewe<br />
pia tarajia kupatwa na lawama na hukumu zitakazokusababishia<br />
maumivu na madhara kama ulivyowafanyia wengine. Hii ni kanuni<br />
ya kiroho na inafanya kazi chini ya udhibiti wa Mungu mwenyewe.<br />
62
Kana kwamba hii haikutosha, Yesu alitoa sababu ya msingi<br />
ya kutokulaumu na kuhukumu wengine kwa sababu mwenye<br />
kufanya hivyo kwa wengine pengine ana makosa kama wao au<br />
zaidi ya hao anaowakosoa.<br />
“Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi. Kwa kuwa<br />
hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile<br />
mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa. Basi mbona wakitazama<br />
kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani<br />
ya jicho lako mwenyewe huiangalii. Au utamwambiaje nduguyo,<br />
niache nitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani<br />
ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe itoe kwanza ile boriti<br />
katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile<br />
kibanzi katika jicho la ndugu yako.” (Mat. 7:1-5)<br />
Katika maandiko haya, Yesu anaonesha udhaifu wa tabia<br />
ya kuhukumu wengine pasipo kujitathmini binafsi kama hatuna<br />
makosa yale yale au yenye kufanana na ya wale tunaowahukumu.<br />
Aidha, Yesu anatafsiri kuwa ni unafiki mtupu kuwa na tabia ya<br />
kulalamika na kulaumu wengine wakati mhusika naye ana<br />
madhambi yake mwenyewe.<br />
Na kisha Yesu akaagiza kwamba badala ya kutumia<br />
nguvu kubwa kutuhumu na kuhukumu wengine, tumia fursa hiyo<br />
kujichunguza na kujirekebisha kwanza kisha ndipo utakuwa na<br />
uzoefu wa kukosoa wengine.<br />
Tena kuna mahali pengine ambapo Yesu alitoa mwongozo<br />
pale ambapo kunatokea kutokuelewana au kukoseana ambapo<br />
hatua stahiki ni kukutana wahusika peke yao na kujaribu<br />
kusuluhishana. Na pale inaposhindikana basi kesi hiyo iwasilishwe<br />
kwenye ngazi ya juu, hatua kwa hatua mpaka muafaka upatikane.<br />
63
Tabia Sugu Ya Uvivu<br />
Uvivu ni hali ya “kutokutaka kufanya kazi” au hali ya<br />
“ulegevu katika kazi”, au “utepetevu” na “ulegevu”. Tabia sugu ya<br />
uvivu ni mojawapo ya changamoto zinazokiandama kizazi kipya.<br />
Kuna ushahidi wa kutosha kwamba vijana wengi hawapendi<br />
kufanya kazi za nguvu au wakifanya basi hufanya kwa ulegevu.<br />
Kwa mujibu wa Biblia tunajifunza ya kwamba mtu mvivu mikono<br />
yake hukataa kufanya kazi:<br />
“Matakwa ya mtu mvivu humfisha kwa maana mikono yake<br />
hukataa kufanya kazi.” (Mit. 21:25).<br />
Kwa kifupi, mtu mvivu hukataa kufanya kazi (Mit.12:27);<br />
hataki kulima wakati wa baridi (Mit. 20:4); hupenda sana uzingizi<br />
(Mit. 6:9); huwa na njaa (Mit.19:15); kazi yake ni kuomba omba<br />
misaada (Mit.20:4).<br />
Kwa dalili hizi, kazi ya kunoa kipaji nayo ni ngumu kwa<br />
mwathirika wa tabia sugu ya uvivu. Mojawapo ya sifa ya utendaji<br />
wa kipaji ni kufanya kazi kwa ustadi na viwango vya ubora.<br />
Mwathirika wa uvivu sio kwamba hawezi bali pia hataki kutoka<br />
jasho. Anataka mafanikio ya haraka bila jasho.<br />
Madhara Ya Tabia Sugu Ya Uvivu<br />
Umaskini Wa Kipato<br />
Madhara makubwa yampatayo mwathirika wa tabia sugu<br />
ya uvivu ni umaskini wa kipato. Tumekwisha kuthibitisha ukweli<br />
huu kupitia maandiko matakatifu na baadhi yake ni haya yafuatayo:<br />
“Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini; bali<br />
mkono wake aliye na bidii hutajirisha.” (Mit. 10:4)<br />
64
Maandiko yametuhakikishia kwamba uvivu husababisha<br />
umaskini. Mtu asipofanya kazi kwa makusudi hatapata mapato<br />
na hivyo kuishia kuwa maskini.<br />
Kuwa mzigo kwa wengine<br />
Mwathirika wa tabia sugu ya uvivu kwa kuwa hana kipato,<br />
lakini bado ana mahitaji ya lazima ya kula, kunywa, kuvaa, malazi<br />
na mengine, haya yote huwatwika watu wengine wabebe mzigo<br />
huo.<br />
“Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa<br />
mavuno ataomba, hana kitu.” (Mit. 20:4)<br />
Kwa sababu shida za mvivu haziishi, leo ana shida hii<br />
kesho ana shida ile na asiposaidiwa atalaumu na kulalamika<br />
kana kwamba ni haki yake kusaidiwa wakati si mlemavu. Hii<br />
husababisha kero kwa wale walio karibu naye.<br />
Kupoteza Fursa Matumizi Ya Vipaji<br />
Mwathirika wa tabia ya uvivu hushindwa kutumia kipaji<br />
chake kila anapopewa fursa ya kuzalisha. Yesu alitoa mfano wa<br />
talanta ambapo tajiri aliwapa watumwa wake talanta za kuzalisha.<br />
Mmoja kati yao aliyepewa talanta moja kwa sababu ya uvivu wake<br />
alishindwa kuzalisha lakini akaja na visingizio kama ifuatavyo:<br />
“… Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana,<br />
nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda,<br />
wakusanya usipotawanya; basi nikaogopa, nikaenda nikaificha<br />
talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako. Bwana wake<br />
akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua<br />
ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; basi,<br />
ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija<br />
ningalipata iliyo yangu na faida yake. Basi, mnyang’anyeni talanta<br />
hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. Kwa maana kila mwenye<br />
kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile<br />
65
alicho nacho atanyang’anywa.” (Mat. 25:24-29)<br />
Katika maandiko haya tunasoma maneno haya “… Wewe<br />
mtumwa mbaya na mlegevu.” Unaona? Anatajwa moja kwa<br />
moja ya kuwa kilichomfanya akashindwa kutumia kipaji chake ni<br />
ulegevu wake mwenyewe na madhara yake ni kunyang’anywa<br />
hata hicho alichokuwa nacho.<br />
Tabia Sugu Ya Ulevi Na Madawa Ya Kulevya<br />
Miaka 3,000 iliyopita kabla ya elimu ya sayansi kuwepo,<br />
manabii walitoa maonyo kuhusu matumizi ya pombe wakisema<br />
athari zake ni pamoja na kuharibu fahamu za wanadamu:<br />
“Uzinzi na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu.”<br />
(Hos. 4:11)<br />
Maandiko haya yanathibitisha kwamba pombe ina athari<br />
kubwa kwa kipaji cha binadamu kwa kuwa inadhoofisha uwezo<br />
wa kufikiri. Kwa mantiki hii divai mpya inajumuisha kila kitu<br />
kinacholewesha ikiwemo uvutaji wa bangi; matumizi ya dawa za<br />
kulevya unaojumuisha unga wa kubugia, kunusa, au uchomaji<br />
sindano.<br />
Maandiko matakatifu, kama jina lake lilivyo, yameandika<br />
waziwazi ya kwamba ndani ya pombe mna sumu inayoharibu<br />
tabia ya mtu na kumwondolea ubinadamu wake na kufanya awe<br />
kama hayawani:<br />
“Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali<br />
mjazwe Roho.” (Efe.5:18)<br />
Neno “ufisadi” katika maandiko haya linamaanisha “uchafu<br />
uliokithiri”. Huu si uchafu wa mwili bali vitendo haramu visivyo vya<br />
kimaadili. Ndiyo maana nimeorodhesha ulevi kuwa ni “tabia sugu”<br />
inayoharibu utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya binadamu.<br />
66
Madhara Ya Pombe Mwilini<br />
Madhara ya kwanza ya pombe ni kuathiri mfumo wa<br />
ubongo ambao ndio asili ya nguvu ya <strong>vipaji</strong> vya asili. Baadhi ya<br />
athari za pombe katika ubongo ni kama zifuatazo:<br />
• Mishipa ya ubongo kupanuka kupita kawaida.<br />
• Ukosefu wa baadhi ya vitamin katika ubongo (mlevi hali mlo<br />
kamili)<br />
• Ukosefu wa vitamin B unaweza kusababisha matatizo ya akili<br />
katika ubongo<br />
• Kubadilika kitabia, kudhoofika kwa uwezo wa kufikiri, kupoteza<br />
kumbukumbu<br />
Athari kubwa zaidi za pombe katika ubongo ni eneo la<br />
mfumo wa neva. Wakati kisingizio cha matumizi ya pombe huwa<br />
ni kama kitulizo katika mfumo wa neva, badala yale pombe<br />
hutumika katika kuzikandamiza seli za neva katika ubongo kwa<br />
kuzifanya butu na kuuharibu uwezo wake wa kufanya kazi, hali<br />
ambayo hupelekea kusinzia, kuzimia na hata kifo.<br />
Madhara mengine ya pombe kwenye mfumo wa neva ni<br />
pamoja na haya yafuatayo:<br />
• Kudhoofisha uwezo wa kuona<br />
• Kubadilisha utambuzi wa muda na mahali<br />
• Kupoteza uwezo wa kusikia vizuri<br />
• Kupatwa na uzito katika kuitikia mambo<br />
• Kupoteza hisia ya harufu na ladha<br />
Kana kwamba hii haitoshi, madhara ya pombe hayaishii<br />
kuathiri ubongo na mfumo wa neva peke yake. Pombe huathiri<br />
kiungo kingine muhimu cha mwili ambacho ni moyo. Baadhi ya<br />
maeneo ambayo moyo huathiriwa na pombe ni pamoja na haya<br />
yafuatayo:<br />
67
• Moyo huathirika kwa ukosefu wa baadhi ya vitamini.<br />
• Mapigo ya moyo hudhoofika<br />
• Kupanuka kwa moyo<br />
• Ongezeko la shinikizo la damu<br />
• Huzuia uzalishaji wa seli nyekundu na nyeupe za damu<br />
• Hatari za ugonjwa wa moyo na kiharusi<br />
Viungo vingine ambavyo huathiriwa na pombe ni ini ambapo<br />
seli za ini huharibika na kudhoofisha utendaji wa ini (Cirrhosis).<br />
Imebainika ya kwamba theluthi mbili za wagonjwa wa Cirrhosis<br />
Uingereza husababishwa na pombe.<br />
Pombe pi huathiri tumbo kwa kusababisha maumivu na<br />
vidonda vya tumbo pamoja na matatizo katika mfumo wa usagaji<br />
chakula. Madhara mengine ya pombe ni dhidi ya ngozi ambapo<br />
mishipa ya damu hupanuka na ngozi kujaa damu nyingi, na pia<br />
pombe husababisha mwili kuwa na joto kubwa na rangi ya ngozi<br />
hubadilika.<br />
Eneo la mwisho lakini lenye athari kubwa zitokanazo na<br />
pombe ni katika mfumo wa uzazi. Pombe husababisha kudhoofika<br />
kwa mfumo wa uzazi katika maeneo yafuatayo:<br />
• Kudhoofika kwa nguvu za kiume<br />
• Kwa wanawake katika ujauzito kizazi huathirika<br />
• Kuzaliwa kwa watoto njiti<br />
• kudhoofisha uwezo wa akili wa mtoto<br />
• Mtoto kurithi tabia ya ulevi<br />
• Viungo vya uzazi kudhoofika na kusababisha ugumba<br />
• Kwa wanawake hatari ya kupata saratani ya matiti<br />
Athari Za Kiuchumi<br />
Pombe haikomei katika kuathiri afya bali husababisha hata athari<br />
za kiuchumi. Kwa mujibu wa maandiko ya Biblia tunaonywa<br />
kuhusu ulafi na ulevi kama ifuatavyo:<br />
68
“Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo; miongoni mwa<br />
walao nyama kwa pupa; kwa maana mlevi na mlafi huingia<br />
umaskini, na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.” (Mit. 23:20-<br />
21)<br />
Baadhi ya athari za kiuchumi zitokanazo na pombe ni kama<br />
hizi zifuatavyo:<br />
• Kudhoofika kwa viwango vya ubunifu wa mipango endelevu<br />
ya kiuchumi<br />
• Kudhoofika kwa uwezo wa kufanya kazi<br />
• Utoro makazini<br />
• Kupoteza ajira<br />
• Kufilisika kibiashara/kimiradi<br />
• Kukumbwa na umaskini wa kujitakia kibinafsi, familia na jamii<br />
kwa jumla<br />
Athari Za Kijamii<br />
• Kudhoofisha uwajibikaji wa mtu kama mwanandoa au kama<br />
mzazi<br />
• Kusababisha ugomvi katika familia<br />
• Kukaa nje ya familia kwa muda mrefu<br />
• Kutelekeza familia na kuwasababishia wasiwasi, mashaka na<br />
msongo wa mawazo<br />
• Kuchochea vitendo vya zinaa ambavyo hueneza maambukizo<br />
ya VVU<br />
• Malezi duni kwa watoto<br />
Tabia Sugu Ya Zinaa<br />
Msamiati wa neno “zinaa” unajumuisha matumizi ya<br />
maneno mawili maarufu kama “uasherati” na “Uzinzi”. Tafsiri<br />
rasmi ya neno uasherati maana yake ni “tendo la kujamiiana<br />
linalofanywa na mtu/watu ambao hawajaoa wala kuolewa kwa<br />
mujibu wa sheria”. Na tafsiri rasmi ya neno uzinzi maana yake<br />
69
ni: “mwanandoa anapojamiiana na mtu/watu wengine nje ya<br />
mwanandoa mwenziwe”.<br />
Kwa mujibu wa maandiko ya Biblia, tendo la ndoa linatakiwa<br />
kufanywa na mwanamume na mwanamke ambao wameamua<br />
kufunga ndoa ili kuishi pamoja kwa maisha yao yote mpaka kifo.<br />
Mtu ambaye hajafunga ndoa halali haruhusiwi kujamiiana mpaka<br />
atakapofikia umri na muda wa kufunga ndoa rasmi.<br />
Mojawapo ya amri kumi maarufu katika Biblia ni pamoja<br />
na “usizini” (Kut. 20:14). Zinaa ni miongoni mwa tabia sugu zenye<br />
kuharibu utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya wanadamu na ndiyo maana<br />
imekatazwa kimaadili.<br />
Madhara Ya Tabia Sugu Ya Zinaa Kimaadili<br />
Mojawapo ya athari za tabia sugu ya zinaa ni “kupungukiwa na<br />
akili”:<br />
“Uzinzi na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu.”<br />
(Hosea 4:11)<br />
Biblia inaposema zinaa inaondoa “fahamu za wanadamu”,<br />
maana yake inalenga uharibifu wa kitabia wenye kuathiri utendaji<br />
wa <strong>vipaji</strong> vya asili. Mtu akiisha kujiingiza katika vitendo vya<br />
zinaa, tayari fahamu zake au fikira zake zinaathirika na kupoteza<br />
mwelekeo wa kimaadili na hivyo kudhoofisha utendaji bora wa<br />
<strong>vipaji</strong> vyake. Maandiko mengine yamerejea kusisitiza ya kwamba<br />
mwenye kufanya zinaa tayari ana matatizo ya kiakili:<br />
“Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo<br />
litakalomwangamiza nafsi yake.” (Mit. 6:32)<br />
Hapa tunasoma habari kuhusu zinaa inavyozuzua akili za<br />
mtu mpaka anajiingiza kwenye mazingira ya kuhatarisha uhai<br />
wake lakini hata hajali. Kumbuka wakati huo maandiko haya<br />
70
yalipoandikwa, hukumu ya zinaa ilikuwa ni mtu “kupigwa mawe<br />
mpaka kufa” (Law. 20:10). Kwa hiyo, mtu akiisha kuonja zinaa<br />
humponza kiasi cha kujitoa mhanga kupigwa mawe hadi kufa<br />
kama atafumaniwa.<br />
Kufuatia athari mbaya za kimaadili zinazotokana na<br />
tabia sugu ya zinaa, maandiko yametoa mwongozo wa kila mtu<br />
kujiepusha nayo kwa kadiri iwezekanavyo kama ilivyoandikwa<br />
hapa chini:<br />
“Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje<br />
ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda juu ya mwili wake<br />
mwenyewe.” (1 Kor. 6:18)<br />
Vichocheo Vya Zinaa<br />
Pamoja na makatazo ya vitendo vya zinaa bado<br />
kumekuwepo mmomonyoko wa kimaadili wenye kusababisha<br />
kukithiri kwa vitendo hivyo katika jamii. Baadhi ya vichocheo vya<br />
zinaa ni pamoja na:<br />
• Tamaa za ujanani<br />
• Mila na desturi zisizoheshimu ndoa ya mke na mume mmoja<br />
• Ngoma na miziki inayohamasisha vitendo vya ngono<br />
• Picha za ngono katika magazeti, luninga, video na tovuti<br />
• Mavazi yasiyo ya staha<br />
• Ulevi na madawa ya kulevya<br />
• Umaskini<br />
Athari Za Nyingine Za Tabia Sugu Ya Zinaa<br />
• Zinaa huleta unajisi unaomtenga mtu na Mungu kiroho<br />
• Zinaa huathiri utu kwa kuvunja hadhi ya mtu binafsi<br />
• Zinaa hivunjia taasisi ya ndoa heshima yake mbele za jamii<br />
• Zinaa husababisha kuzaliwa watoto nje ya ndoa na kukosa<br />
malezi bora<br />
71
• Zinaa huharibu akili na uwezo wa kufikiri mambo ya maana<br />
• Zinaa husababisha umaskini kwa matumizi ya anasa zisizo na<br />
udhibiti<br />
• Zinaa husababisha uhasama/chuki/uadui mpaka mauaji<br />
• Zinaa husababisha migogoro na kusambaratisha familia<br />
• Zinaa hueneza maambukizo ya maradhi ya zinaa na VVU<br />
Tabia Sugu Ya Chuki Na Hasira<br />
Tabia ya chuki na hasira imetokea kuwa miongoni mwa<br />
tabia sugu ambazo zinaathiri <strong>vipaji</strong> vya asili kwa sababu waathirika<br />
wengi ni vijana, tena ambao ndio nguvu kazi ya taifa. Kimaumbile<br />
kila binadamu ana “hisia hasi” za chuki na hasira. Lakini hisia<br />
hizi zinatakiwa kudhibitiwa ili kudumisha mahusiano mema ya<br />
kifamilia na kijamii. Pale ambapo mtu anashindwa kudhibiti chuki<br />
na hasira matokeo yake atajikuta amesababisha madhara yenye<br />
kuathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya asili, kwa yeye mwenyewe na kwa<br />
jamii inayomzunguka pia.<br />
Tafsiri Ya Misamiati Ya Chuki Na Hasira.<br />
Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu, neno “chuki”<br />
limetafsiriwa kuwa ni: “ tabia ya kutopenda watu au hali ya kuwa<br />
na roho mbaya, au kinyongo.” Neno hasira limetafsiriwa kuwa ni:<br />
“ ghadhabu au hamaki au fundo.”<br />
Hapa nitoe angalizo ya kwamba, hii “tabia sugu ya chuki<br />
na hasira”, inatofautiana na ile “tabia sugu ya kulalamika na<br />
kuhukumu” ambayo tayari tumejifunza habari zake. Mtu mmoja<br />
anaweza kuwa na tabia sugu zote mbili, lakini sio lazima aliye na<br />
tabia moja kati ya hizi awe na tabia ya pili.<br />
Kuna watu wameathiriwa na “tabia sugu ya chuki na hasira”<br />
lakini hawana hulka ya “tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu”<br />
wengine hadharani. Waathirika wa “chuki na hasira” wanaweza<br />
kuchukua hatua kali za kulipa visasi pasipo kupiga kelele hata<br />
kidogo.<br />
72
Wakati huo huo, watu wenye “tabia sugu ya kulalamika<br />
na kuhukumu wengine” huwa ni chanzo kikuu cha kuwachochea<br />
watu walioathiriwa na “tabia sugu ya chuki na hasira” ambao<br />
huhamaki na kutafuta kulipiza visasi dhidi ya mahasimu wao.<br />
Vyanzo Vya Hasira Na Chuki<br />
Hisia hasi za chuki na hasira zina vyanzo viwili tofauti.<br />
Kuna vyanzo vya nje ambavyo ni maumivu ya nafsi yatokanayo<br />
na kunenewa au kutendewa mabaya; au uchungu wa kukosa<br />
huduma na haki stahili kutoka kwenye mamlaka husika.<br />
Chanzo cha pili ambacho ni kutoka ndani kinajumuisha hisia<br />
ya ndani ambayo ni ama aibu ya moyoni itokanayo na kushindwa<br />
au kutokufanikiwa katika jambo mbele za watu, au kusutwa<br />
na dhamiri kwa sababu ya makosa au dhambi zilizofanywa na<br />
hazijasuluhishwa bado.<br />
“BWANA akamwambiaKaini, kwanini una ghadhabu?<br />
Kwanini uso wako umekunjamana?Kama ukitenda vema hutapata<br />
kibali?Usipotenda vema dhambi iko inakuotea mlangoni, nayo<br />
inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.” (Mwa. 4:6-7)<br />
Athari Za Hasira Na Hamaki<br />
Pamoja na kwamba mwenye hasira na chuki anaweza<br />
kujihesabia haki kutokana na sababu anazoziona kuwa ni halali<br />
kwake; pasipo kujitambua kumbe anajisababishia athari yeye<br />
mwenyewe ambazo baadhi yake ni kama hizi zifuatazo:<br />
Kudhoofisha Kazi Za Kimaendeleo<br />
Mwenye chuki na hasira hujikuta hajali muda na kuchelewa<br />
kufika kwenye shughuli za kimaendeleo na kazini kwa sababu<br />
ameshuka moyo wa kufanya kazi. Wengine hujiingiza kwenye<br />
vitendo vya ulevi, kula kupita kiasi, kuwa tegemezi kwa wengine,<br />
73
na ulemavu wa kihisia.<br />
Madhara Ya Kiafya<br />
• Hasira hupandisha mwendo wa moyo kutoka kiasi cha 80<br />
mpaka 180 hata zaidi kwa dakika<br />
• Shinikizo la damu nalo kupanda kutoka 120 kwa 80 kwenda<br />
220 kwa 130 au zaidi<br />
• Kasi ya kupumua huongezeka ili kuingiza hewa safi mwilini<br />
• Mlipuko wa nguvu husababisha kushuka kwa sukari kiasi mtu<br />
huweza hata kutetemeka<br />
• Mwili hutoa kemikali za kugandisha damu kana kwamba kuna<br />
ajali imetokea mwilini hali ambayo mgando wa damu huenda<br />
moyoni au katika ubongo<br />
• Mwenye hasira hukabiliwa na hatari ya mlipuko wa moyo au<br />
ugonjwa wa kiharusi<br />
• Hasira sugu husababisha mfadhaiko na msongo wa mambo<br />
ambavyo hupelekea vidonda vya tumbo<br />
• Hasira sugu hudhoofisha mfumo wa kinga na kusababisha<br />
pumu, maradhi ya ngozi, ugonjwa wa baridi yabisi.<br />
Mchakato Wa Kudhibiti Changamoto Zenye Kudhoofisha<br />
Vipaji<br />
Baada ya kuzipitia baadhi ya changamoto zilizoanishwa<br />
katika sura hii, sasa ni wakati muafaka wa kutafuta kujua mbinu za<br />
kupambana na kuudhibiti huu udhoofishaji wa <strong>vipaji</strong>. Tumezipitia<br />
changamoto za nje ambazo ni marafiki wabaya, imani za uchawi<br />
na ushirikina, mifumo butu ya elimu, na athari za utandawazi<br />
kupitia mitando ya kijamii. Pili, tumepitia changamoto za ndani<br />
kupitia “tabia sugu zenye kuathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> kutokea ndani<br />
ya wahusika.<br />
Suala zima la kudhibiti changamoto hizi haliwezi kuwa<br />
tukio la mara moja tu. Lazima liwe katika mfumo wa kimchakato.<br />
Madhara yaliyopo hayakujitokeza siku moja bali yalichukua muda<br />
74
mrefu. Hali kadhalika na mchakato wa kuyadhibiti kunahitaji<br />
muda ili tuweze kuona matokeo. Hakuna njia ya mkato katika<br />
kurekebisha mambo yaliyojisokota kwa muda mrefu.<br />
Zifuatazo ni ngazi makini za kufanya matengenezo ya<br />
madhara yaliyokwisha kufanyika na mbinu za kujikinga ili athari<br />
zisiendelee kujitokeza tena huko mbeleni:<br />
1. Kumrudia Mungu Muumbaji Wetu<br />
Tumejifunza habari za <strong>vipaji</strong> na karama kwamba ni vitu<br />
vinavyotoka kwa Mungu aliyemwumba binadamu kwa mfano<br />
wake na sura yake. Aidha tumejifunza pia ya kwamba, Mungu<br />
ndiye anayejua kusudi la kuwepo kwako na pia ndiye mwenye<br />
kujua mwanzo na mwisho wa kila binadamu hapa duniani.<br />
Kwa hiyo, tunapotafuta kufanya matengenezo ya kitabia na<br />
kunoa <strong>vipaji</strong> vilivyomo ndani yetu, lazima kwanza tumrudie Mungu<br />
na kujenga uhusiano wa kiroho pamoja naye. Uzuri ni kwamba<br />
sio sisi tunayemrudia Mungu kwa juhudi zetu wenyewe, bali yeye<br />
mwenyewe alikwisha kututafuta na kutuonesha njia ya kumrudia<br />
bila gharama yoyote. Katika kumrudia Mungu tunaanza na hatua<br />
ya kwanza inayojulikana kama toba.<br />
Tafsiri Ya Toba<br />
Biblia imeandika kuhusu toba ikitumia maneno ya<br />
Kiebrania na Kiyunani. Kwa Kiebrania neno lililotumika kuhusu<br />
toba ni nocham. Maana yake ni kuugulia, kuomboleza, kujuta<br />
na kuacha kutenda dhambi na kugeuka na kurejea kwa Mungu.<br />
Kwa Kiyunani neno lililotumika kuhusu toba ni metanoia. Maana<br />
yake ni kubadilia nia na kuachana na kusudi la kuendeleza jambo,<br />
kugeuka nyuma na kurudi ulikotoka.<br />
75
Kwa muktadha wa maneno nocham na metanoia, yote<br />
yanatoa maana ya mtu kujutia hali yake ya dhambi, kuamua<br />
kubadili nia na mtazamo wake kuhusu dhambi zake, na kugeuka<br />
nyuma kisha kurejea katika uhusiano wa kiroho na Mungu.<br />
Watu wengi huchanganya maana ya maneno “toba” na<br />
“ungamo” wakidhani ni kitu kile kile. Ukweli ni kwamba “kutubu” ni<br />
tofauti na “kuungama” tu. Kuungama ni “kukubali na kukiri ukweli<br />
wa makosa yaliyofanywa.” Lakini “kutubu” ni “kujutia na kubadili<br />
nia” kwa “kuachana na mwenendo wa dhambi na kumgeukia<br />
Mungu” ili kuishi maisha tofauti na yaliyopita.<br />
Agizo La Toba<br />
Mungu amekwisha kutoa agizo maalum kwa watu wote<br />
ambao ni waathirika wa tabia sugu zilizotajwa katika sura hii<br />
wapate kutubu kwake kama ilivyoandikwa:<br />
“Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni;<br />
bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu. Kwa<br />
maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki,<br />
kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa<br />
mambo haya kwa kumfufua katika wafu.” (Mdo. 17:30-31)<br />
Maandiko haya yaliandikwa kwa ajili ya kuwataka watu wote<br />
waliokuwa ni waathirika na imani za uchawi na ushirikina pamoja<br />
na tabia sugu wabadili nia zao na kumrudia Mungu Muumbaji wao<br />
na kujiweka salama wasiagukie kwenye maangamizi yaliyokuwa<br />
yakiwakabili.<br />
Mchakato wa kufanya matengenezo dhidi ya madhara ya<br />
changamoto zenye kuathiri <strong>vipaji</strong> na karama unatakiwa kuanza na<br />
toba kwa mujibu wa maandiko tuliyosoma. Uzuri wa maandiko<br />
haya ni kwamba Mungu yuko tayari kuachilia makosa yaliyokwisha<br />
kufanyika kwa kujifanya kama hayajui kwa sababu yalifanyika<br />
kutokana na kutokujua.<br />
76
Faida Za Toba<br />
Kutoka Katika Mitego Ya Ibilisi<br />
Shetani ndiye chimbuko kuu la changamoto zote za nje na<br />
za ndani ambazo zinadhoofisha utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya wanadamu.<br />
Kufanya toba ya kweli ndio mlango wa kutoka katika mtego wa<br />
Ibilisi ambao aliutumia kuwanasa wengi katika vifungo vya dhambi<br />
na tabia sugu:<br />
“akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama<br />
ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli; wapate<br />
tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao<br />
wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake.” (2 Tim. 2:25-26)<br />
Maandiko haya yanataja habari za “kupata tena fahamu”<br />
ambazo hapo awali ziliharibiwa na tabia sugu za ulevi na zinaa.<br />
Pili, tunasoma habari za “kutoka katika mtego wa Ibilisi” ambao ni<br />
vishawishi au vitisho vyenye kuwafanya waathirika kuzama katika<br />
maisha ya imani za uchawi na ushirikina.<br />
Katika kufanya toba ya kweli tunasoma kuna kufumbuliwa<br />
macho ya kiroho na kutambua kuwa uko gizani na kuamua<br />
kuigeukia nuru:<br />
“uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na<br />
kuigeukia nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea<br />
Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni<br />
mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.” (Mdo. 26:18)<br />
Maandiko haya yanataja pia habari za “kuziacha nguvu za<br />
shetani” ambazo zinasababishwa na imani za uchawi na ushirika<br />
pamoja na vifungo vya tabia sugu zlizokwisha kutajwa katika sura<br />
hii.<br />
77
Kuzaliwa Upya<br />
Faida ya pili ya kufanya toba ya kweli ni muujiza wa<br />
mabadiliko ya ndani ya kiroho ambayo hufanywa na Mungu<br />
mwenyewe kwa kumtumia Roho wake Mtakatifu:<br />
“si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali<br />
kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa<br />
upya na Roho Mtakatifu” (Tit. 3:5)<br />
Itakumbukwa ya kwamba maana ya tabia sugu ni<br />
“mazoea yatokanayo na kurudiarudia hali isiyoweza kuondolewa<br />
kwa urahisi”. Katika hatua ya kufanya toba, pasipo kutumia<br />
nguvu za kibinadamu za kujibadilisha kitabia, kuna rehema za<br />
Mungu zinazomshukia mwenye kutubu na kuihuisha roho yake<br />
kupata nguvu za mabadiliko ya kiroho. Mabadiliko haya ndiyo<br />
yanajulikana kuwa ni “kuzaliwa kwa pili” na “kufanywa upya” na<br />
Roho Mtakatifu.<br />
2. Kupokea Nguvu Za Kiungu Za Kudhibiti Tabia Sugu<br />
Baada ya kufanya toba ya kweli na kupata mabadiliko ya<br />
ndani ya kiroho; hatua inayofuata ni kupokea nguvu za kiungu<br />
za kudhibiti tabia sugu ambazo ni “mazoea yatokanayo na<br />
kurudiarudia hali isiyoweza kuondolewa kwa urahisi” Maandiko<br />
yafuatayo yanatuthibitishia uhakika wa kudhibiti tabia sugu kama<br />
ifuatavyo:<br />
“Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote<br />
imefunuliwa, nayo yatufundisha kutaa ubaya na tamaa za kidunia;<br />
tupate kuishi kwa kiasi, haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa<br />
sasa.” (Tit. 2:11)<br />
Maandiko hayo hapo juu yanatujulisha jinsi ambavyo<br />
Mungu amekwisha kutoa neema ya kuwaokoa wanadamu wote,<br />
kama wakiamua kutubu kwa dhati na kumrudia yeye. Na neema<br />
78
hii inafanya kazi ya kutufundisha jinsi ya kukataa ubaya na tamaa<br />
za kidunia ambazo zinadhoofisha utendaji wa <strong>vipaji</strong> na karama<br />
ndani yetu. Katika maandiko mengine tunajulishwa kukirimiwa<br />
ahadi kubwa za thamani za kutuwezesha kupokea tabia za uungu<br />
ambazo huweza kudhibiti tabia sugu:<br />
“Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani,<br />
ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washiriki wa tabia ya Uungu,<br />
mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.” (<br />
2 Pet. 1:4)<br />
3. Kuutafuta Kwanza Ufalme Wa Mungu Na Haki Yake<br />
Changamoto kubwa ya binadamu hapa duniani ni kutafuta<br />
maisha kwa kila njia, ziwe halali au haramu. Kipaumbele chake ni<br />
kufanikiwa katika kujipatia na kujilimbikizia mali nyingi. Hata hivyo,<br />
mambo ni tofauti kwa mtu aliyekwisha kumrudia Mungu kwa<br />
njia ya toba. Baada ya kuchukua hatua za kiroho zilizotangulia,<br />
kinachofuata ni kupanga upya vipaumbele vya maisha:<br />
“Msisumbuke, basi, mkisema, tule nini? Au Tunywe nini?<br />
Au tuvae nini? Kwa maana hayo yote mataifa huyatafuta; kwa<br />
sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hao<br />
yote. Bali utafute kwanza ufalme wake na haki yake; na hayo yote<br />
mtazidishiwa.” (Mat.6:32-33)<br />
Maandiko haya yametafsiriwa kinyume na maana yake<br />
kwa nadharia zinazokataza watu kufanya kazi eti badala yake<br />
wategemee sala peke yake kwa kuwa Mungu anajua mahitaji yao.<br />
Dhana ya kutokufanya kazi na kutegemea kuishi kwa miujiza peke<br />
yake sio muktadha wa maandiko haya.<br />
Kile Yesu alichomaanisha hapa ni wanafunzi wake kubadili<br />
mtazamo kuhusu maisha na kuweka upya vipaumbele kwa kigezo<br />
cha kutanguliza ufalme wa Mungu. Yesu hakukataza kufanya kazi,<br />
alitoa mwongozo wa kufanikiwa kupitia vipaumbele na Mungu<br />
79
akiwa ndiye kipaumbele cha kwanza.<br />
Wakati watu wasiomcha Mungu wanaabudu mali za duniani<br />
hii lakini hawana ushirika na Mungu aliyewaumba; wanafunzi<br />
wa Yesu waliagizwa kumtafuta na kumtanguliza Mungu kwanza<br />
katika kutafuta kwao ili kufanikiwa kwao chimbuko lake liwe ni<br />
Mungu badala ya shetani.<br />
Kutafuta kwanza ufalme wa Mungu ni kumtafuta Mungu<br />
akufunulie na kukudhihirishia kusudi lake katika maisha yako.<br />
Na atafanya hivyo kwa kuanza kuibua <strong>vipaji</strong> vyako, na karama za<br />
Roho ili utendaji wako utokane na nguvu alizowekeza ndani yako.<br />
Kuweza kufanikisha zoezi hili unahitaji mshauri wa kiroho<br />
mwenye uzoefu na maisha ya ukuzaji <strong>vipaji</strong> kwa mujibu wa maadili<br />
ya kibibilia.<br />
Lakini, hatua hizi tatu ukizipa uzito unaostahili, tayari<br />
utakuwa umefanikiwa kupata ujuzi na uwezo wa kupambana na<br />
changamoto zenye kudhoofisha <strong>vipaji</strong> na kuzishinda. Inaweza<br />
kuonekana ni ngumu lakini sio kwamba haiwezekani kabisa.<br />
Ni uamuzi wako binafsi kama unataka mabadiliko chanya ya<br />
kutambua na kuchochea <strong>vipaji</strong> vyako.<br />
80
SURA YA NNE<br />
Utangulizi<br />
WAJIBU KWA KIZAZI CHA SASA<br />
KURITHISHA KIZAZI KIPYA<br />
Kitabu hiki hakitakuwa na msaada kwa msomaji kama<br />
hakutakuwepo na uchambuzi makini unaohusu wajibu kwa kizazi<br />
cha sasa, kizazi cha wazee, kutambua wajibu mkuu wa kurithisha<br />
majukumu ya kijamii, kiuchumi na kiuongozi kwa kizazi kipya.<br />
Kizazi kilichopo hivi sasa kimefikia mahali kilipo hivi sasa<br />
kwa sababu kizazi cha zamani, kilichotangulia kiliacha misingi<br />
ambayo kiliirithisha kwa kizazi kinachomaliza muda wake sasa.<br />
Kwa bahati mbaya, nadharia ya uritishaji imeanza<br />
kupoteza umuhimu wake kwa jamii kiasi kwamba kizazi kipya<br />
hakina matumaini wala mwelekeo wa kule kinakojiandaa<br />
kuelekea. Muktadha wa kitabu hiki ni kukihimiza kizazi cha sasa<br />
kinachomaliza muda wake kutimiza wajibu wake wa kurithisha<br />
kizazi kipya majukumu ya msingi kwa mustakabari wa taifa.<br />
Makundi muhimu yenye wajibu wa kusimamia mchakato<br />
wa urithishaji kwa kizazi kipya unaanzia na “wazazi” au “walezi”<br />
katika ngazi ya familia. Ngazi ya familia ndio kitovu cha malezi<br />
kuanzia mtoto anapozaliwa, kukua hadi anapofikia umri wa<br />
kujitegemea kama mtu mzima.<br />
Kundi la pili ambalo linahusika katika wajibu wa kurithisha<br />
kizazi kipya ni kanisa. Natumia msamiati kanisa kwa maana ya<br />
taasisi inayosimamia kueneza na kurithisha maadili ya kiimani<br />
kwa wafuasi wake. Wakati familia ni mlezi mkuu wa maisha ya<br />
81
mtoto kijamii, kanisa ni mlezi mkuu kimaadili. Kundi la tatu lenye<br />
wajibu mkuu katika kurithisha kizazi kipya ni serikali na vyombo<br />
vyake vya dola na taasisi zake za umma.<br />
Katika sura hii tunakwenda kupitia mtiririko wa kihistoria<br />
kuhusu nadharia ya urithishaji, sababu za msingi wa urithishaji,<br />
hatua za urithishaji, vitu muhimu vya kurithisha na visivyofaa<br />
kurithishwa kizazi kipya. Tutapitia pia ukweli kuhusu ukomo wa<br />
umri wa kuishi wa kizazi kilichopo pamoja na ukomo wa nadharia<br />
za uchumi na uongozi. Kisha tutahitimisha na uchambuzi kuhusu<br />
hitaji kuu la viongozi wa kizazi kipya pamoja na mchakato wa<br />
kuandaa uongozi wa kizazi kipya.<br />
Historia Ya Nadharia Ya Urithishaji<br />
Nadharia ya urithishaji yaweza kuonekana kama kitu kipya<br />
kwa baadhi ya watu katika jamii. Kihistoria, nadharia ya urithishaji<br />
chimbuko lake ni taasisi ya ndoa ambayo ni “muungano wa<br />
mwanamume na mwanamke walioamua kuishi pamoja maisha<br />
yao yote“. Baada ya mwanamume na mwanamke kuoana na<br />
kuzaa watoto, wahusika hupanda daraja na kuitwa baba na mama<br />
au wazazi. Ni katika ngazi hii tunapata jina familia.<br />
Katika ngazi ya familia maisha na shughuli za uzalishaji<br />
na utunzaji wa familia yakiwemo malezi ya watoto hufanyika na<br />
kustawi katika jamii. Kilele cha malezi ya wazazi kwa watoto, ni<br />
pale ambapo watoto wamekuwa watu wazima na kufikia daraja<br />
la kuanzisha taasisi mpya za ndoa na kuanza kuishi maisha yao<br />
wenyewe.<br />
Kama ni binti huagwa na wazazi kwa zawadi na hatarajiwi<br />
kurejea kwao na kuwa sehemu ya familia ile tena. Na kwa upande<br />
wa mtoto wa kiume, huwezeshwa katika kuandaa mahali pake<br />
maalum, nyumba au chumba atakapoishi na mkewe; kulipiwa<br />
mahari, na kufanyiwa sherehe ya arusi.<br />
82
Kuanzia wakati huo, bwana arusi hutambuliwa kuwa mtu<br />
mzima anayestahili kuendesha maisha mapya ya taasisi ya ndoa<br />
yake, na anatarajiwa kuacha kabisa kuwa tegemezi kwa wazazi<br />
kama alivyokuwa kijana asiye na ndoa.<br />
Kwa baadhi ya makabila au mataifa mengine, nadharia ya<br />
urithishaji, huanza kutekelezwa na wazazi katika hatua ya kuozesha<br />
au kufungisha ndoa za watoto wao. Lakini kwa makabila mengine<br />
hatua ya urithishaji hufanyika wakati baba wa familia amefariki<br />
dunia. Baada ya kuhitimisha msiba wake, ndipo wanafamilia<br />
wakisaidiana na ukoo hutekeleza nadharia ya kurithisha mali za<br />
marehemu kwa mjane na watoto wote pasipo kujali wana ndoa au<br />
hawana ndoa.<br />
Sababu Za Msingi Wa Urithishaji<br />
Ukomo Wa Umri Wa Kuishi<br />
Biblia imetabiri ukomo wa umri wa kuishi ni miaka 70 mpaka<br />
80. Dalili za kizazi kinachomaliza muda wake kimekadiriwa watu<br />
kuanzia miaka 50 na kuendelea. Ukomo wa umri wa kutumikia<br />
serikali na taasisi za umma ni miaka 60.<br />
Kwa hiyo, watu wote wenye umri wa kuanzia miaka 50 na<br />
kuendelea, popote walipo, kwa mambo yoyote wanayofanya,<br />
mojawapo ya mipango muhimu kwetu ni kujiandaa kuachia<br />
majukumu tuliyo nayo na kuyarithisha kwa kizazi kinachoinukia<br />
hivi sasa.<br />
Umri wa kizazi kinachotakiwa kurithishwa ni kuanzia miaka<br />
18 mpaka 49. Kipindi cha kurithisha kinahitaji maandalizi yasiyozidi<br />
miaka 10 kwa watu waliofikisha miaka 50.<br />
Kwa hiyo tunalazimika kurithisha kwa sababu ya ukomo<br />
wa umri wa kuishi ambao hatuna udhibiti nao. Kwa bahati<br />
mbaya baadhi yetu tunaogopa kurithisha mapema kwa hofu<br />
83
ya kupinduliwa au kupoteza umaarufu tuliojijengea katika jamii.<br />
Lakini tusipotumia muda muafaka tutamaliza vibaya na kuacha<br />
migogoro ya kifamilia na kijamii nyuma yetu.<br />
Wana-rika wenzangu, tusiposhituka na kuanza maandalizi<br />
ya urithishaji wa uchumi na uongozi hivi sasa, muda hautungoji.<br />
Miaka 10 iliyoko mbele yetu inakimbia mbio za kasi, kufumba na<br />
kufumbua tutajikuta iko mbele yetu.<br />
Uzalishaji na usimamizi ni mambo yanayotegemea nguvu<br />
na akili. Kwa kadiri umri unavyoongezeka ndivyo na nguvu za<br />
uzalishaji na akili za kufanya maamuzi hubadilka. Kwa lugha<br />
nyingine kasi ya kufanya mambo hupungua na uzito katika kufanya<br />
maamuzi nao huongezeka.<br />
Kwenye suala la uchumi ambapo ulimwengu unabadilika<br />
kila kukicha, mambo mapya yanazaliwa na elimu inaongezeka<br />
kwa kasi, wakati jamii ya wazee bado iko katika enzi zao. Bahati<br />
mbaya kasi na hamu ya kujifunza mambo mapya kwa wazee<br />
huzidi kupungua. Hizi ndizo dalili zinazoashiria kwamba, wakati<br />
wa kurithisha wengine wenye uwezo na nguvu umekaribia.<br />
Kuendeleza Jina<br />
Maendeleo ya kiuchumi na kijamii hufanywa na watu, kila<br />
mtu mmoja mmoja, na kwa ushirikiano wa kimakundi. Mojawapo<br />
ya hamasa za kimaisha, ni mtu kutoa mchango wa kimaendeleo<br />
ambao utakumbukwa baada ya kuondoka kwake duniani. Hii<br />
ndiyo inaitwa “kuacha jina”. Kuna mambo ambayo baadhi ya<br />
wazee waliotutangulia walifanya enzi za ujana wao, na sisi<br />
tumeyakuta, tumeyarithi, na tunawakumbuka kwa ajili ya mambo<br />
hayo. Wenyewe wamekufa, lakini mambo yao bado yako hai,<br />
na hivyo majina yao yanaendelea kutajwa japokuwa wenyewe<br />
hawapo tena.<br />
84
Kuendeleza Kizazi<br />
Sababu nyingine muhimu sana ni kukiwezesha kiuchumi<br />
na kiuongozi kizazi kipya cha watoto waliozaliwa na kulelewa<br />
katika mazingira ya kifamilia, kitaasisi na kitaifa. Sababu ya<br />
kwanza ya kurithisha tulisema ni kigezo cha ukomo wa muda<br />
wa kuishi. Sababu hii ndiyo inapaswa kuchochea moyo wa<br />
kizazi kinachomaliza muda wake kufanya maandalizi mapema ya<br />
kukabidhi majukumu ya kiuchumi na kuiongozi kwa kizazi kipya.<br />
Katika ngazi ya familia, ni fahari ya wazazi pale ambapo<br />
watoto wao waliowazaa wanapofikia umri wa kutaka kujitegemea<br />
kimaisha.<br />
Vijana wa kiume wanapofikia umri wa kuoa huhimizwa na<br />
wazazi na kufundishwa, na hata kusaidiwa jinsi ya kujenga misingi<br />
ya kujitegemea kama kuwa na shughuli maalum ya uzalisha wa<br />
kujipatia kipato binafsi, kujenga nyumba, kuwa na samani za<br />
ndani n.k.<br />
Kwa upande wa vijana wa kike, wanapofikia umri wa<br />
kuolewa huandaliwa rasmi jinsi ya kuishi katika ndoa na kutunza<br />
familia zao mpya baada ya kuolewa.<br />
Kuendeleza Maono Ya Kitaasisi<br />
Changamoto katika urithishaji ziko kwenye ngazi ya<br />
kitaasisi na kitaifa. Katika ngazi ya kitaasisi, kuna jamii ya watu<br />
waitwao “waasisi”. Hawa ni waanzilishi wa mawazo ya awali<br />
ya kuanzishwa kwa taasisi husika na kwa njia hiyo wamekuwa<br />
viongozi wake tangu ngazi ya uchanga mpaka hapo ambapo<br />
taasisi hizo zimekomaa kiutendaji. Ninaposema taasisi nina<br />
maana ya vyama vya hiari, au madhehebu ya dini, au vikundi vya<br />
kijamii ambavyo vimesajiliwa kwa mujibu wa sheria.<br />
85
Katika ngazi ya kitaasisi, (tofuati na serikali na taasisi za<br />
kiserikali, ambazo utumishi wake una ukomo kwa mujibu wa sheria)<br />
baadhi ya taasisi binafsi hazina utamaduni wa kisheria wa ukomo<br />
wa utumishi. Katika ngazi hii, mara nyingi wale waitwao “waasisi”<br />
kwa maana ya walioanzisha taasisi au huduma hizo huwa wazito<br />
sana kuachia madaraka ya uongozi kwa vijana wao. Kuacha<br />
utumishi katika ngazi ya kitaasisi hushinikizwa na maaradhi, au<br />
kifo; au shinikizo la uasi ndani ya taasisi ambao matokeo yake<br />
husababisha mifarakano na matengano ya kitaasisi.<br />
Kuendeleza Kizazi Cha Kijaamii Kitaifa<br />
Katika ngazi hii, urithishaji unategemea mfumo wa utawala<br />
na uzoefu katika zoezi ya kuachia madaraka. Kwa upande wa<br />
Tanzania, kisiasa tuna sifa njema katika Bara la Afrika kwa kuwa<br />
na utamaduni wa watawala wa kitaifa kuachia madaraka mara<br />
baada ya kufikia ukomo wa muda wao.<br />
Hata hivyo, changamoto iliyopo katika ngazi hii, ni pale<br />
ambapo wale wanaomaliza muda wao wa utumishi wa umma<br />
kupewa mikataba maalum na kuendelea kutumika. Utetezi<br />
unaotumika katika kulinda utaratibu huu ni kuwepo kwa baadhi<br />
ya nafasi za utumishi ambazo bado hazina watu wenye ujuzi na<br />
uzoefu; na hivyo wastaafu husika wakaonekana bado wanahitajika<br />
kutumika katika ngazi husika.<br />
Pamoja na utetezi huu, pia kumekuwepo na upande<br />
mwingine wenye malalamiko dhidi ya utaratibu huu kwamba<br />
unawanyima haki wengine waliostahili kushika nafasi za wastaafu<br />
kwa mujibu wa sheria.<br />
86
Ngazi Muhimu Za Urithishaji<br />
Urithishaji Wa Ngazi Ya Kifamilia<br />
Katika ngazi hii, ni wazazi ndio hurithisha watoto mali<br />
walizochuma katika familia. Kama tulivyokwisha kupitia kihistoria<br />
kuhusu urithishaji katika ngazi ya familia, hapa ni muhimu<br />
tuzingatie kwamba jamii ya kizazi chetu kwa sehemu kubwa<br />
imepoteza utamaduni wa kurithisha majukumu na raslimali kwa<br />
kizazi kinachoinukia.<br />
Ushahidi ni kuongezeka kwa migogoro na kesi za mirathi<br />
zilizojaa mahakamani siku hizi. Badala ya walezi kifamilia<br />
kusimamia mchakato wa urithishaji kwa watoto wa marehemu<br />
au wale wanaostahili kurithishwa, wao ndio wanateka mali hizo<br />
na kuzitapanya kwa sababu za kibinafsi na watoto wanaanza<br />
kuhangaika.<br />
Kupotea kwa utamaduni wa kurithisha pia kumechangiwa<br />
kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya kimaendeleo na kijamii<br />
ambapo familia zimetawanyika mijini na vijijini. Lakini pia ukosefu<br />
wa wazazi kuandika wosia mapema kuhusu mgawanyo wa mali<br />
kwa familia.<br />
Jambo linalosikitisha zaidi katika udhaifu wa kutokurithisha<br />
ni pale ambapo wazazi huishia kuzaa watoto lakini hawana<br />
mpango maalum wa kutunza urithi kwa ajili ya watoto. Badala<br />
yake wazazi wanafanya kazi ya kuchuma na kutafuta bila kuweka<br />
akiba kwa ajili ya watoto.<br />
Kuna ongezeko la kuparaganyika kwa familia kunakotokana<br />
na mmomonyoko wa maadili katika jamii. Hii imezalisha familia za<br />
aina tofauti ambazo watoto wanaozaliwa au kulelewa ndani yake<br />
wanakosa mwelekeo wa kimaadili na hivyo kupotoka kitabia.<br />
87
Kuparaganyika kwa familia nyingi kumezalisha changamoto<br />
kubwa nyingine ya ongezeko la kizazi kinachoitwa kwa jina maarufu<br />
kama “watoto wa mitaani”. Hawa ni watoto ambao baadhi yao<br />
hawana wazazi au walezi na wamekosa malezi ya kifamilia na ndio<br />
maana wameishia mitaani. Hiki nacho ni kizazi ambacho badala<br />
ya kurithishwa msingi wa kimaendeleo wanaishia kurithi umaskini<br />
na maisha ya uhalifu.<br />
Si lengo la kitabu hiki kuzungumuzia matatizo ya kifamilia,<br />
ila haya yanatajwa kama viashiria vya familia kushindwa kutimiza<br />
wajibu wake wa kurithisha kizazi kipya. Wito makini wa ujumbe<br />
wa kitabu hiki kwa kila familia yenye mtoto au watoto, wawe wa<br />
kuwazaa au kuwalea, ni kurejea katika utamaduni wa kijamii wa<br />
kurithisha majukumu na rasilimali kwa watoto pindi wanapofikia<br />
umri wa kujitegemea na kuwa watu wazima.<br />
Urithishaji Wa Ngazi Ya Kitaasisi<br />
Uritishaji wa kitaasisi ni urithishaji wa mali na madaraka ya<br />
kusimamia taasisi husika. Taasisi hapa tunajumuisha makampuni<br />
binafsi, vikundi vya uzalishaji, na vikundi vinginevyo ambavyo<br />
madhumuni yake ni uzalishaji na wanahisa kugawana mapato<br />
kwa mujibu wa makubaliano ya kisheria.<br />
Katika ngazi hii ya urithishaji wa kitaasisi, viongozi waasisi<br />
ndio wenye wajibu wa kurithisha madaraka ya usimamizi wa<br />
taasisi. Japokuwa jambo la kurithisha uongozi litaelezwa kwa<br />
kina katika vipengele vinavyofuata, hapa ni muhimu kuzingatia<br />
mapema ya kuwa kila mwasisi na mtendaji mkuu wa kampuni ya<br />
kifamilia au kijamii atie akilini mwake kuwa ni muhimu kumwandaa<br />
mrithi wake wakati bado ana nguvu.<br />
Mwasisi asisubiri wakati amezeeka ndipo akabidhi<br />
majukumu. Kurithisha majukumu ya uongozi na utawala katika<br />
mambo ya uzalishaji sio kama kurithisha mali za marehemu.<br />
Unahitaji muda wa kutosha wa kuachilia baadhi ya majukumu<br />
88
kwa watoto au warithi ambao wanapata uzoefu wakati mwasisi<br />
bado yuko hai.<br />
Urithishaji Kwa Kizazi Cha Kitaifa<br />
Ngazi ya urithishaji kwa kizazi cha kitaifa ni hatua ya<br />
juu kabisa katika jamii. Hapa tunazungumuzia ngazi ya kitaifa.<br />
Taifa kama Tanzania ambalo mna makabila zaidi ya 120<br />
yanayounganishwa na utaifa wenye sifa ya uraia mmoja.<br />
Tanzania kama taifa, linayo jamii ya watu waliozaliwa kwa<br />
wakati mmoja wa historia, ambao kwa lugha nyingine huitwa rika<br />
moja. Hawa ndio huitwa kizazi cha kitaifa. Lakini tunapo itathmini<br />
Tanzania kijamii tunakuta kuna mgawanyiko wa sehemu mbili za<br />
vizazi vya kitaifa; kuna kizazi cha watoto, na pili, kuna kizazi cha<br />
watu wazima.<br />
Kizazi cha watoto kinatambuliwa kwa umri kuanzia mwaka<br />
mmoja (1) mpaka miaka kumi na saba (17). Watu wote katika umri<br />
huu hawaruhusiwi kufanya maamuzi huru kama watu wazima.<br />
Wahusika wanahesabiwa kuwa chini ya uangalizi wa kifamilia<br />
na malezi ya kitaifa. Ishara iliyo wazi zaidi ni kuwa hawaruhusiwi<br />
kupiga kura kwenye uchaguzi wa uongozi wa kitaifa.<br />
Kizazi cha watu wazima ni kuanzia umri wa miaka kumi<br />
na nane (18) mpaka sitini (60). Hiki ndicho kizazi chenye idhini ya<br />
kufanya maamuzi na kuwajibika kisheria. Wahusika wanaruhusiwa<br />
kupiga kura na kuwania madaraka ya uongozi katika ngazi mbali<br />
mbali za utumishi wa umma kitaifa.<br />
Katika ngazi ya kizazi cha kitaifa, wenye wajibu wa<br />
kurithisha ni wazee ambao wamefikia umri wa kustaafu kwa<br />
mujibu wa sheria. Hiki ndicho kigezo muhimu cha Urithishaji wa<br />
kizazi. Wazee wanapostaafu huwaachia majukumu ya uzalishaji<br />
na usimamizi vijana ambao wamechukua nafasi zao.<br />
89
Vitu Muhimu Vya Kurithisha<br />
Elimu Na Ujuzi<br />
Zamani za wahenga wetu, urithi ulihusu mali zilizoachwa<br />
na marehemu tu. Na hii ndiyo asili ya neno Urithi. Mali au vitu<br />
vinavyoachwa na marehemu na kupewa mtu fulani wa ukoo<br />
husika. Lakini siku hizi mambo yamekwisha kubadilika. Urithi wa<br />
kwanza na wa kudumu ni elimu na ujuzi.<br />
Kama tulivyokwisha kusoma sehemu uliyotangulia ya kuwa<br />
wajibu wa kurithisha elimu na ujuzi unaanzia katika ngazi ya familia,<br />
halafu unakuja kwenye taasisi na kisha ngazi ya kitaifa. Isitoshe,<br />
ni haki ya kibinadamu kwa kila mtu kupata elimu ili kujiendeleza<br />
kiujuzi.<br />
Kwa kuwa kitabu hiki kinahusu <strong>vipaji</strong> vya asili, huko mbeleni<br />
nitaweka bayana ni aina gani ya elimu na ujuzi vinavyotakiwa<br />
kurithishwa kama njia ya kuinua na kunoa <strong>vipaji</strong>.<br />
Rasilimali<br />
Msamiati wa neno rasilimali umetafsiriwa kuwa ni “jumla<br />
ya mali aliyonayo mtu au nchi.” Kama nilivyotangulia kudokeza<br />
hapa juu kwamba, rasilimali ndio urithi unaofahamika tangu enzi<br />
za wahenga na hata sasa bado umeendelea kuwepo.<br />
Hapa inabidi tuzingatie kwamba rasilimali ni mali<br />
iliyozalishwa na kumilikiwa na familia. Ni wajibu wa kila familia<br />
kufanya kazi kwa bidii, kuchuma mali na kuzimiliki kifamilia.<br />
Tufahamu kwamba kiasi cha rasilimali ilichonacho familia ndicho<br />
kinachoweza kurithishwa kwa watoto wanapokuwa watu wazima.<br />
Ngazi ya pili ya kurithisha rasilimali ni ngazi ya kitaifa.<br />
Hapa nikiwa na maana ya serikali ya nchi kuhakikisha kila raia<br />
anatengenezewa mazingira ya kumwezesha kuzalisha na kumiliki<br />
90
asilimali kwa njia halali na kwa mujibu wa sheria.<br />
Aidha, ni kuhakikisha rasilimali za asili katika nchi zinalindwa<br />
kwa matumizi ya sasa na vizazi vijavyo; na Kipaumbele katika<br />
matumizi ya rasilimali za asili kiwe ni kuwawezesha raia kuwa na<br />
haki ya umiliki wake kisheria.<br />
Uongozi<br />
Tumekwisha kujifunza kwamba uongozi ni mojawapo ya<br />
sehemu ya <strong>vipaji</strong> vya asili. Kimsingi, kipaji hakiwezi kurithishwa<br />
toka mtu kwenda mtu mwingine. Muktadha wa “uongozi wa<br />
kurithisha” ni ile nafasi au madaraka ya usimamizi na utawala, iwe<br />
ni katika taasisi na makampuni binafsi, au katika serikali na taasisi<br />
zake za umma.<br />
Kwa mantiki hii, uongozi nao ni kitu maalum ambacho<br />
kinatakiwa kurithishwa. Japokuwa si kila mtu anaweza kurithishwa<br />
uongozi, lakini uongozi kama nadharia na mfumo lazima urithishwe<br />
ili kuweza kusimamia masuala ya uchumi na huduma za kijamii<br />
kwa raia wa nchi husika.<br />
Njia za urithishaji wa uongozi hazianzi na kugawa vyeo vya<br />
utawala bila kuzingatia uwezo wa kuongoza. Njia za kurithisha<br />
uongozi lazima ziwe na vigezo vilivyo wazi na makini tena kwa<br />
mujibu wa sheria na taratibu rasmi, ili warithishwe watu wenye<br />
uwezo wa kuongoza. Kama nilivyotangulia kudokeza kabla, ni<br />
kwamba nitachambua kwa kina suala la urithithishaji wa uongozi<br />
huko mbeleni katika sura hii.<br />
Vitu Visivyofaa Kurithishwa Kizazi Kipya<br />
Ujinga<br />
Kuna usemi uliozoeleka usemao: “Kama unaona elimu<br />
ni ghali, basi jaribu ujinga”. Kizazi cha utawala kilichopo hivi<br />
91
sasa kinaweza kuona kwamba kuwekeza katika “elimu na ujuzi”<br />
ni gharama kubwa, na kutafuta unafuu na urahisi ili kukwepa<br />
kugharimia viwango bora vya elimu na ujuzi. Kumbe katika<br />
kushusha “viwango vya ubora” tayari tumechagua kurithisha<br />
“viwango duni vya elimu” kwa kizazi kinachoinukia ambacho<br />
hakitaweza kumudu ushindani wa kimataifa katika uzalishaji.<br />
Sio siri hivi sasa kuona kwamba watoto na vijana wetu<br />
wamesongwa katika mazingira magumu ya kimfumo wa huduma<br />
za elimu kwa sababu mbali mbali. Baadhi ya sababu za watoto na<br />
vijana wetu kukosa kupata elimu bora ni pamoja na: i) uhaba wa<br />
nafasi za kuendelea na elimu ya juu katika mfumo wa elimu yetu.<br />
ii) udhaifu wa mitaala isiyokidhi viwango vya ubora wa elimu ya<br />
kimataifa. iii) Vitendo vya uchakachuaji wa mitihani kunakotokana<br />
na kukithiri kwa rushwa katika taasisi zinazosimamia mitihani. iv)<br />
Walimu kukosa motisha katika utoaji wa elimu kwa wanafunzi.<br />
Kwa kadiri ambavyo idadi kubwa ya watoto na vijana<br />
wengine wanavyoishia katika viwango vya chini vya elimu;<br />
hiyo ndiyo dalili iliyo waziwazi kwamba kizazi chetu tuliopo hivi<br />
sasa tumeamua kurithisha ujinga kwa kizazi kijacho. Kimsingi,<br />
tumekuwa tukifanya zoezi la kurithisha ujinga na kizazi kinachokuja<br />
kitatukumbuka kwa urithi wa ujinga tuliokiachia.<br />
Mabadiliko yoyote ya kimfumo hayaji kwa miujiza. Yanakuja<br />
kwa utashi na uamuzi wa nguvu. Lazima tuutumie utashi wetu<br />
na kufanya uamuzi wa kukataa kuendelea kurithisha ujinga kwa<br />
watoto na vijana wetu. Uwezo na nguvu tunazo, kinachokosekana<br />
ni nia ya dhati. Lazima tukatae kurithisha ujinga kwa watoto na<br />
vijana wetu.<br />
Umaskini<br />
Kuna mtu mmoja maarufu sana anayeongoza kwa utajiri<br />
hapa duniani anaitwa Bill Gates. Miaka ya hivi karibuni alitoa kauli<br />
ambayo imezua mjadala mpaka hivi sasa, lakini ina ushawishi<br />
92
mkubwa kiasi ambacho hakuna ambaye amefaulu kuipinga na<br />
akashinda. Alisema hivi:“kama umezaliwa katika familia masikini<br />
sio kosa lako; lakini ukifa maskini hilo ni kosa lako mwenyewe”.<br />
Kwa kauli hii ni rahisi sana Bill Gates kutafsiriwa kuwa<br />
amejikinai kwa kuwahukumu watu wanaokufa maskini kwamba<br />
hayo ni makosa yao. Lakini baada ya kuutafakari kwa makini<br />
usemi wake nilipata kumwelewa kwa sehemu kile alichokuwa<br />
amemaanisha.<br />
Bila shaka alikuwa anatoa ujumbe kwamba mtu<br />
anapozaliwa katika familia ambayo ni maskini sio kosa lake kwa<br />
sababu sio yeye aliyechangia wala kufanya maamuzi ya kimaisha<br />
hata kusababisha umaskini alioukuta. Kwa maneno mengine mtu<br />
hajichagulii azaliwe katika familia ya namna gani, bali hujikuta<br />
amezaliwa katika familia husika.<br />
Lakini iwapo muhusika aliyezaliwa katika familia maskini<br />
anapokuwa mtu mzima ana uhuru wa kufanya maamuzi ya mwisho<br />
kuhusu maisha yake. Na hii ni pamoja na kutafuta fursa nyingi<br />
zilizopo mbele yake na kuanza kuzitumia kwa uzalishaji, kwa nia<br />
ya kubadili maisha yake ya umaskini wa kuzaliwa na kuitwa jina<br />
tofauti katika jamii.<br />
Neno Umaskini limetafsiriwa na Kamusi ya Kiswahili Sanifu<br />
kuwa ni “hali ya kukosa mali; ufukara, uhitaji, na ukata”. Najua<br />
kwamba kuna nadharia na dhana nyingi kwa habari ya umaskini,<br />
hususan huu wa kipato. Aidha kumekuwepo na itikadi zenye<br />
kutetea umaskini kama janga linalowapata watu pasipo wenyewe<br />
kutaka au kuusababisha. Kwa utafiti wangu naweza kutafsiri<br />
sababu za umaskini katika sehemu zifuatazo:<br />
Ulemavu:<br />
Ulemavu wa viungo vya mwili au akili ambao mlemavu<br />
hawezi kufanya shughuli halali ya kujipatia kipato. Ulemavu wa<br />
93
jinsi hii, ni hali ambayo iko nje ya uwezo na uamuzi wa mhusika,<br />
na hivyo analazimika kuishi kwa kutegemea fadhila za binadamu<br />
ambao si walemavu katika jamii.<br />
Majanga Ya Kimazingira:<br />
Majanga ya kimazingira ni kama vile mafuriko, matetemeko<br />
au vita vya kiraia. Haya ni matukio ambayo huharibu rasilimali za<br />
watu na kupoteza muda wa jamii kufanya kazi za uzalishaji mpaka<br />
mazingira yarejee katika hali inayoruhusu uzalishaji.<br />
Katika mazingira kama haya waathirika hujikuta hawana rasilimali<br />
wala kipato cha kuwawezesha kukidhi mahitaji yao, isipokuwa nao<br />
wanaishi kwa fadhila za binadamu wengine ambao hawajakumbwa<br />
na majanga ya kimazingira.<br />
Uvivu Na Anasa:<br />
Tafsiri ya uvivu ni “hali ya kutotaka kufanya kazi; hali ya<br />
ulegevu katika kazi; utepetevu na ulegevu.” Ikiwa mtu mzima,<br />
ambaye si mlemavu, si mgonjwa, si mzee kikongwe; halafu mtu<br />
mwenyewe anaishi kwenye mazingira yenye fursa za uzalishaji<br />
mali (ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha, ustawi wa mimea na<br />
malisho ya mifugo), halafu mtu huyo katikati ya mazingira hayo<br />
bado hana shughuli maalum inayompatia kipato; basi tena, huyo<br />
mtu sifa yake ni moja tu, ni mvivu.<br />
Kutokufanya kazi; au kuwa mlegevu katika kazi,<br />
husababisha ukosefu wa kipato na matokeo yake ni umasikini wa<br />
kipato na rasilimali. Huu ndio umaskini ambao Bill Gates alisema,<br />
“mtu akifa katika umaskini wa jinsi hii ni makosa ya mhusika’.<br />
Tafsiri ya anasa ni “mambo au hali ya starehe na raha<br />
nyingi; au kitu chenye thamani kubwa ambacho sio muhimu.”<br />
Unaona? Haya ni maisha ambayo watu wanatumia rasilimali zao<br />
kwa mambo yasiyo na tija iwe ni katika familia au katika jamii.<br />
94
Uvivu hupelekea ukosefu wa kipato wakati anasa ni matumizi<br />
yasiyo na muhimu na kupita kiasi. Jambo lenye kushangaza na<br />
kusikitisha ni pale ambapo mtu asiye na kipato cha uhakika na<br />
akapata msaada wa kumwezesha kujikwamua katika umaskini,<br />
lakini anaamua kuutumia msaada ule kwenye anasa za ulevi,<br />
ulaji na kununua vitu vya thamani kubwa kuliko mahitaji yake ya<br />
muhimu.<br />
Matumizi ya anasa matokeo yake ni umaskini. Umaskini<br />
ambao haukupaswa kuwepo kabisa, lakini unamkumba mtu<br />
kwa sababu sio kwamba hakupata bali alipata akatumia vibaya,<br />
kwa anasa. Kumbuka kwamba matumizi ya anasa ni kuzalisha<br />
umaskini.<br />
Huu ndio umaskini ambao Bill Gates alisema, “mtu akifa<br />
katika umaskini wa jinsi hii ni makosa ya mhusika”. Umaskini wa<br />
namna hii unaweza kuzuilika kwa utashi na sio kwa misaada.<br />
Tunaweza kuukataa umaskini huu usiendelee kuanzia katika ngazi<br />
ya familia, ngazi ya kitaasisi na ngazi ya kitaifa.<br />
Hitaji Kuu La Viongozi Wa Kizazi Kipya<br />
Ni lazima tukubali kwamba hivi sasa, kwa sababu ya<br />
mmomonyoko wa maadili ya kimani; hata sifa na kanuni za<br />
kuwapata viongozi wenye uwezo stahili navyo vimechakachuliwa<br />
kabisa. Tumejikuta tuko katika mazingira ya kuwa na “bora<br />
viongozi” badala ya “viongozi bora”. Kwa mtindo huu kamwe<br />
hatuwezi kutarajia kwamba “uongozi wa kizazi kinachoinukia”<br />
utakuwa bora iwapo hatukuamua kwa makusudi kurejea<br />
katika kuweka “viongozi bora” ili wawe mwongozo kwa kikazi<br />
kinachoinukia.<br />
Kama ambavyo, kitaifa tuko kwenye mchakato wa<br />
mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kimifumo; bila shaka suala<br />
la uongozi nalo ni lazima lipewe kipaumbele ndani ya katiba,<br />
angalau kwa kuweka sifa na vigezo makini vyenye kuliwezesha<br />
95
taifa kuwapata viongozi bora. Sisi ambao ni kizazi kinachomaliza<br />
muda wake ni lazima tufumbe macho na kuacha kuangalia aina<br />
ya viongozi waliopo sasa hivi kuwa ndio kigezo cha viongozi wa<br />
kizazi kinachoinukia. Tuamue kukinusuru kizazi kipya kwa kuweka<br />
vigezo vya kuwapata viongozi bora, hususan, viongozi wenye<br />
<strong>vipaji</strong> vya uongozi na kuwanoa mapema ili wapate uzoefu wa<br />
kuongoza kizazi chao kinachoinukia.<br />
Kwa uzoefu wangu binafsi, pamoja na tafiti mbali mbali<br />
zilizofanyika kwa habari ya “aina ya viongozi bora”, kuna ushahidi<br />
kamili kwamba suala la “uongozi bora” linatakiwa kuzingatia<br />
mambo makuu matatu yafuatayo:<br />
1. Kipaji<br />
2. Uzoefu<br />
3. Uadilifu<br />
Kipaji kinawakilisha uwezo wa kuongoza kwa ushawishi<br />
wa nguvu za hoja na hekima ya kufanya maamuzi yenye kuleta<br />
ufumbuzi badala ya kusababisha matatizo makubwa zaidi. Kipaji<br />
cha uongozi kinahitaji mazoezi maalum ili kipate kunolewa kwa njia<br />
mbali mbali ambapo ndipo kigezo cha “uzoefu” kinachukua nafasi<br />
yake. Kimsingi kipaji cha uongozi hujidhihirisha chenyewe ndani<br />
ya mtu na wala hakuhitajiki kazi za “kupiga ramli za kindumba ili<br />
kukitambua”.<br />
Kipaji cha uongozi kikidhihirika ndani ya wahusika, lazima<br />
jamii iwe na mfumo wa kuwawezesha kufanya mazoezi ya<br />
kuongoza ili kigezo cha uzoefu nacho kichukue mkondo wake.<br />
Suala la uadilifu ni matunda ya maadili ya kiimani ambayo ndiyo<br />
mazingira wahusika wamefundwa na kukulia tangu ngazi ya<br />
familia, na imani kwa Mungu na huu ndio msingi wa kuwafanya<br />
kukamilisha sifa za kiuongozi.<br />
Tunapotaka kurithisha maono kwa kizazi kipya, tukija<br />
kwenye suala la uongozi, kipaji, uzoefu na uadilifu ni vitu<br />
96
vinavyotakiwa kuwa mwongozo kwa wanoaji na warithishaji<br />
maono kwa kizazi kipya.<br />
Kwa kuwa shina la uongozi mbovu linatokana na<br />
mmomonyoko wa maadili ya kiimani katika jamii; bila shaka hapa<br />
ndipo mahali pa kuanzia kufanya maandalizi ya viongozi bora.<br />
Kuweka mkazo wa maadili ya kiimani, maadili ya kitaaluma na<br />
maadili ya uongozi.<br />
Malezi ya kimaadili ya kiimani huanzia nyumbani katika<br />
familia. Ni wakati muafaka kwa kanisa kuandaa mipango<br />
ya mafunzo ya kimaadili kwa wazazi ili yawasaidie kuwalea<br />
watoto wao kimaadili. Bila shaka, wazazi wenyewe nao lazima<br />
wanatambua kwamba wajibu wa kulea watoto kimaadili unaanzia<br />
kwao kama wazazi katika kuyashika maadili yenyewe ili wawe<br />
mfano kwa watoto wao.<br />
Wakati huo huo, juhudi zielekezwe katika kuandaa<br />
mitaala ya maadili kwa wanafunzi mashuleni na vyuoni ambapo<br />
watoto watafundishwa somo la maadili, huku kanisa likisimamia<br />
majukumu ya maadili ya kiimani.<br />
Ili tuweze kuona matokeo mazuri lazima tuanze na watoto<br />
na vijana wa kizazi kipya ambao muda si mrefu watakuwa<br />
wanakabiliwa na changamoto za uongozi wa kizazi kinachomaliza<br />
muda wake duniani. Katika vizazi vilivyopita, kila taifa ambalo<br />
liliweka kipaumbele kwa malezi ya kimaadili, limetoa viongozi<br />
bora ambao wameweka rekodi ya uongozi katika historia na<br />
wanakumbukwa mpaka hivi leo.<br />
Mchakato Wa Kuandaa Uongozi Wa Kizazi Kipya<br />
Kama nilivyotangulia kusema hapa juu kuwa suala la<br />
uongozi linahusiana na kipaji, hapa nataka kusisitiza kwamba,<br />
lazima kuwepo kwa mchakato mahsusi wa kuvibaini <strong>vipaji</strong> vya<br />
uongozi.<br />
97
Kuvibaini Vipawa Vya Uongozi<br />
Ziko nadharia za aina nyingi katika kushughulikia maandalizi<br />
ya viongozi. Nadharia moja inadai kwamba uongozi ni kipawa na<br />
hivyo hakuhitajiki mafunzo ya kitaaluma ya kuandaa kiongozi.<br />
Nadharia ya pili inadai kwamba, uongozi ni taaluma ya kawaida<br />
ambayo kila mtu anatakiwa kupitia mafunzo ili apate ujuzi wa<br />
kuongoza kwa mujibu wa taaluma yenyewe.<br />
Binafsi nimekwisha kuonesha msimamo kwamba, uongozi<br />
ni kipawa. Lakini ili kuweza kubaini kipawa cha uongozi lazima<br />
uwepo mkakati mahususi wenye kutafuta na kugundua kila<br />
mwenye nacho. Kama nilivyokwisha kusema hapo awali, malezi<br />
ya kimaadili kwa vijana wa kizazi kipya lazima yaende sambamba<br />
na kuvibaini vipawa vya uongozi kwa ajili ya kuvitambua na<br />
kutengenezea mazingira ya kutumika kwa wakati muafaka.<br />
Mafunzo Ya Kunoa Vipawa Vya Uongozi<br />
Baada ya kuvibaini vipawa vya uongozi, hatua inayofuata ni<br />
kuandaa mafunzo maalum ya kuvinoa kwa ajili ya matumizi yenye<br />
ufanisi unaozingatia viwango vya ubora. Kuvitambua vipawa<br />
na kuanza kuvitumia bila mafunzo ni kusababisha vituko katika<br />
uongozi. Kipawa kinahitaji kunolewa ili kuweza kuleta matokeo<br />
yanayotarajiwa.<br />
Ile nadharia kwamba kila mtu anaweza kujifunza taaluma<br />
ya uongozi na akaweza kuongoza hata kama hana kipawa, bado<br />
ina upungufu. Tunao viongozi wengine waliopata mafunzo ya<br />
uongozi na wakapewa uongozi lakina wamekuwa si wabunifu,<br />
wala hawana ushawishi kwa wale wanaowaongoza. Lakini<br />
mwenye kipawa cha uongozi akipata mafunzo; ni sawa na upanga<br />
kunolewa ili kuboresha makali yake wakati wa kutumika.<br />
98
Majaribio Ya Uongozi<br />
Baada ya kuvinoa vipawa kimafunzo, ndipo unafika sasa<br />
wakati muafaka wa kuvifanyia majaribio ya uongozi. Kuvifanyia<br />
vipawa majaribio ya uongozi ni pamoja na kuwapa fursa wenye<br />
vipawa kushika nafasi za uongozi kuanzia ngazi za chini na huku<br />
wakitathminiwa jinsi wanavyodhihirisha uwezo na sifa zao kabla<br />
hawajaanza kuonja madaraka makubwa na ya juu katika ngazi za<br />
uongozi.<br />
Mbinu mbali mbali za kufanya majaribio ya uongozi ni<br />
pamoja na kuunda vyama na jumuiya mbali mbali zitakazotoa<br />
fursa za uongozi ili wale wanaojaribiwa wapewe uongozi na kisha<br />
wakionekana wameiva waanze kupewa nafasi zile za kiutendaji<br />
zisizotakiwa kufanya majaribio.<br />
99
Vyanzo Vya Rejea Vilivyotumika<br />
1. Biblia Takatifu<br />
2. BlueBibleLetter.or<br />
3. King James Version Bible<br />
4. Amplified Bible (AMP)<br />
5. Kamusi ya Kiswahili Sanifu<br />
6. https://www.wikipedia.org/<br />
7. The Gift in You (7 Pillars of Thinking designed to discover your<br />
Gift) Dr. Caroline Leaf<br />
8. drleaf.com/blog/perfectly-you-online-program-introduction<br />
9. The Seven Pillars of Thinking with the Copeland’s and Dr.<br />
Caroline Leaf<br />
10. www.biblestudytools.com/kjv<br />
WAPO Mission International Makao Makuu<br />
Mbezi Beach, Barabara Ya Bagamoyo, Jogoo, Dar-es-Salaam<br />
Tovuti: www.wapo.or.tz<br />
S.L.P. 6178 Dar-es-Salaam, Tanzania<br />
<strong>100</strong>