14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Nafsi - Vipaji Vya Asili - Kutoka 31:2-6<br />

Karama Za Kiroho-1 Kor. 12, Efe. 4:11, Rum. 12:6-8<br />

SURA YA KWANZA<br />

CHIMBUKO LA VIPAJI VYA ASILI NA<br />

KARAMA ZA KIROHO<br />

1. Jinsi Binadamu Alivyoumbwa Kwa Ajabu Na Kutisha<br />

Binadamu kwa asili ameumbwa kwa jinsi ya ajabu na<br />

kutisha kweli kweli. Haya si maneno yangu binafsi, bali ni maandiko<br />

ya mtunga Zaburi katika Biblia ambaye ndiye wa kwaza kufanya<br />

ugunduzi huu na kuandika kama ifuatavyo:<br />

“Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu<br />

na kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, na nafsi yangu yajua sana.”<br />

(Zab. 139:14)<br />

Vipaji Vya Asili Na Karama Za Kiroho Katika Maumbile Ya<br />

Binadamu<br />

Mwili - Milango 5 Ya Fahamu<br />

Roho<br />

1


Maandiko matakatifu yanayosimulia historia ya kuumbwa<br />

kwa binadamu kulivyokuwa kwa jinsi ya ajabu kama tunavyosoma<br />

hapa chini:<br />

“Mungu akasema, na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa<br />

sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na<br />

wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho<br />

juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano<br />

wa Mungu alimwumba mwanamume na mwanamke aliwaumba”<br />

(Mwa. 1:26-27)<br />

Hapa tunajifunza ya kwamba, binadamu aliumbwa akiwa<br />

tofauti kabisa na viumbe hai vingine vyote, kuanzia malaika,<br />

wanyama na vitu vingine vyote. Kisha tunajifunza binadamu<br />

ameumbwa kwa mfano na sura ya Mungu mwenyewe. Hii ndiyo<br />

ajabu na ya kutisha.<br />

Mfano wa Mungu na sura ya Mungu! Hapa haina maana<br />

ya kwamba Mungu aliumba Mungu mwingine mwenye kufanana<br />

naye. Mungu ni mmoja haumbwi wala kuumbika. Maandiko<br />

yanachomaanisha hapa ni kuwa Mungu katika uumbaji wake wa<br />

kiungu; aliamua kumuumba “kiumbe mtu” katika mfumo wenye<br />

kufanana naye kwa hekima na tabia ili aweze kumwakilisha Mungu<br />

katika utawala juu ya nchi na viumbe vyote vilivyomo.<br />

Maana Ya Mfano Wa Mungu Katika Binadamu<br />

Tumesoma maandiko yakisema, “... kwa mfano wa Mungu<br />

alimwumba mwanamume na mwanamke aliwaumba.” Ni nini<br />

maana hasa ya mfano wa Mungu na sura ya Mungu?<br />

Jina la kwanza la Mungu lililotumika katika Mwanzo wakati<br />

aliposema maneno haya, ni jina la Kiebrania la Elohim. Jina hili<br />

liko katika wingi wenye kumaanisha Mungu mmoja mwenye nafsi<br />

zaidi ya moja. Ni Mungu mmoja kwa sababu imeandikwa “Mungu<br />

akasema….” Lakini Mungu ana nafsi zaidi ya moja kwa kuwa<br />

maandiko yanasema “na tumfanye mtu kwa mfano wetu na sura<br />

yetu ...”.<br />

2


Haya maneno ya “mfano wetu” na “sura yetu” ndiyo yenye<br />

kuashiria Mungu mmoja lakini aliyejitambulisha katika nafsi zaidi ya<br />

moja. Kwa mukhtadha huu, Mungu aliamua kumuumba binadamu<br />

kwa mfano wake ambao ni “nafsi tatu” kama tunavyoshuhudia<br />

katika maandiko yafuatayo:<br />

“BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi,<br />

akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi.” (Mwa. 2:7)<br />

Maandiko tuliyosoma hapo juu yanadhihirisha mfumo<br />

wa utatu wa binadamu kimaumbile. Mavumbi ya ardhi ndiyo<br />

yalitengeneza mwili na “pumzi ya uhai” ni sehemu ya roho kutoka<br />

kwa Mungu mwenyewe aliyoipulizia ndani ya mwili; na kisha<br />

tunaona mtu anakuwa “nafsi hai”.<br />

Aidha, kila sehemu ya binadamu kuanzia mwili, nafsi na<br />

roho inavyo vitu vinavyoifanya kuwa sehemu kamili kiutendaji.<br />

Mathalan, mwili wa binadamu una kitu kinaitwa “milango ya<br />

maarifa” ambayo ni kuona, kusikia, kuonja, kugusa na kunusa.<br />

Milango hii hutenda kazi kupitia mfumo wa ubongo ambao ndiyo<br />

kama injini ya mwili.<br />

Nafsi ya mtu inavyo vitu vitatu ambavyo ni akili, hisia na<br />

utashi. Na roho nayo inavyo vitatu ambavyo ni “dhamiri”, “ushirika”<br />

na “utambuzi” ambavyo ndivyo Mungu huwasiliana na kuhusiana<br />

na binadamu katika roho.<br />

Uhai wa binadamu huonekana kupitia mwili. Nafsi ya<br />

binadamu ambayo ndiyo yenye akili na hisia na utashi ndiyo<br />

huufanya mwili kufanya mambo yenye kuonekana na wengine,<br />

kuazia kusema na kutenda kwake.<br />

Ukiutazama mchoro hapo juu utakuta jinsi ambavyo mduara<br />

mkubwa wa nje unawakilisha mwili. Mduara wa pili unawakilisha<br />

nafsi, na ule mduara mdogo wa katikati unawakilisha roho ya<br />

binadamu.<br />

3


Kwa mantiki hii, wakati ambapo “nafsi” ya mtu hujidhihirisha<br />

kupitia mwili; hali kadhalika na roho ya binadamu, ambayo ndiyo<br />

kiungo cha mawasiliano kati ya Mungu kiroho, utendaji wake<br />

unadhihirika kupitia nafsi.<br />

2. Tafsiri Ya Misamiati Ya Vipaji Na Karama<br />

Kipaji<br />

Kwa mujibu wa maandiko katika Biblia, kuna ushahidi<br />

wa kuwepo kwa <strong>vipaji</strong> vya asili ambavyo kusudi lake ni kufanya<br />

mambo ya kiufundi na kitaaluma lakini pasipo kupitia kwanza<br />

kwenye mafunzo na mfumo rasmi wa kielimu.<br />

Kipaji ni neno la Kiswahili ambalo Kamusi ya Kiswahili Sanifu<br />

imelitafsiri kuwa ni “kipawa”. Na neno “kipawa” limetafsiriwa<br />

kuwa ni “uwezo mtu aliozaliwa nao” ambao humwezesha kufanya<br />

jambo fulani vizuri.<br />

Hata hivyo, neno “kipaji” limetafsiriwa kwa lugha nyingine<br />

za kibiblia ambazo ni Kiebrania na kiyunani. Neno la Kiebrania<br />

lililotumika kutafsiri “kipaji” ni chokmah na limetajwa mara 149<br />

katika toleo la Kingereza la KJV.<br />

Tafsiri ya neno chokmah ni “hekima”. Katika Biblia kipaji<br />

cha asili kimetafsiriwa kwa neno “hekima” ambalo kwa lugha ya<br />

kiebrania limetumika neno chokmah na limetajwa mara 149 katika<br />

KJV. Maana ya neno chokmah ni: “fundi” wa silaha za kijeshi<br />

wakati wa vita; au “mbunifu” na mwerevu wa mitambo na vifaa<br />

vya ufundi; au stadi wa kazi za mikono.<br />

Kwa hiyo msamiati wa kibiblia wa neno kipaji ni hekima.<br />

Tunaweza kupata matumizi ya neno chokmah katika maandiko<br />

matakatifu yafuatayo:<br />

4


“Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa<br />

Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda; nami nimemjaza roho ya<br />

Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya<br />

kila aina, ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa<br />

fedha, na wa shaba, na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora<br />

miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.” (Kut. 31:2-5)<br />

“... ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa<br />

fedha, na wa shaba, Tena, tazama, nimemchagua, awe pamoja<br />

naye, huyo Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani;<br />

nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima,<br />

ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza” (Kut. 31:4-6)<br />

Katika maandiko haya kila mahali neno “hekima” kwa<br />

kiebrania ni chokmah likimaanisha <strong>vipaji</strong> mbali mbali kwa ajili<br />

ya ubunifu, ufundi na ustadi wa vifaa vya ujenzi na vyombo vya<br />

kutumia kwenye hema ya Mungu kukutana na wana wa Israeli.<br />

Tukiyachunguza maandiko ya Agano Jipya kwa lugha ya<br />

Kiyunani tunakutana na msamiati wa neno “Sophia” pia likiwa<br />

limetafsiriwa kuwa ni hekima ambalo linamaanisha <strong>vipaji</strong> vya asili.<br />

Neno sophia ambalo kwa Kiswahili ni hekima maana yake<br />

ni “uwezo mpana wa kujifunza na kushughulikia mambo mapya<br />

(full of intelligence); uwezo wa kutendea kazi maarifa na ufundi wa<br />

mambo mtambuka.” Neno sophia limetajwa mara 51 katika toleo<br />

la KJV kwenye Agano Jipya.<br />

Tunaweza kupata matumizi ya neno sophia kwenye<br />

maandiko matakatifu ya Agano Jipya ambayo ni haya yafuatayo:<br />

“Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima,<br />

na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.” (Luk. 2:40)<br />

“Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo,<br />

akimpendeza Mungu na wanadamu.” (Luk. 2:52)<br />

5


Neno hekima ambalo limetajwa kwa Yesu ni sophia<br />

likimaanisha <strong>vipaji</strong> vya asili. Yesu aliishi kwa muda wa miaka<br />

30 kabla ya kuanza huduma za kiroho ambapo alianza kutumia<br />

uwezo wa Roho Mtakatifu.<br />

Yesu Kristo tangu utoto hadi ujana wake alikuwa amejaa<br />

<strong>vipaji</strong> vya asili, ikiwemo kazi za ufundi seremala ambayo ilikuwa ni<br />

kazi ya Yusufu baba yake mlezi.<br />

Katika kitabu hiki, msamiati wa neno “kipaji cha asili” ndio<br />

utatumika ambao kwa mujibu wa Biblia ni hekima.<br />

Kipaji cha asili kinaitwa hivyo kwa sababu ya uwezo<br />

maalum wa asili unaomwezesha mtu kufanya jambo kwa viwango<br />

vya juu vya uzuri, ufundi na ubora pasipo kupitia mafunzo rasmi<br />

ya kitaaluma.<br />

Uwezo huu maalum wa asili ndio humfanya mtu kuonekana<br />

wa tofauti na watu wengine katika utendaji wa jambo fulani.<br />

Uwezo huu wa asili ambao ni wa kuzaliwa nao, ndio humfanya<br />

muhusika kujulikana au kuwa mtu maarufu katika jambo lile<br />

ambalo amekirimiwa kulijua na kulifanya kwa viwango vya ubora<br />

katika jamii.<br />

Kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika na wataalamu, kuna <strong>vipaji</strong><br />

vya asili kama saba ambavyo vimeorodheshwa kama ifuatavyo: 1.<br />

Ubunifu, 2. Uhusiano, 3. Lugha, 4. Hesabu, 5. Michezo, 6. Muziki,<br />

na 7. Picha.<br />

Japokuwa sio kila mtu huzaliwa na <strong>vipaji</strong> vyote saba,<br />

uchunguzi uliofanywa umebaini ya kwamba kila binadamu<br />

angalau huzaliwa na aina mojawapo ya kipaji kati ya <strong>vipaji</strong> hivi, na<br />

kama akipewa fursa ya kubaini na kuendeleza kipaji hicho, kuna<br />

uwezekano kwa kila mtu kuishi maisha bora kutokana na kipaji<br />

chake cha asili.<br />

6


Karama<br />

Kamusi ya Kiswahili Sanifu imetafsiri neno “karama” kuwa<br />

ni “kipawa anachokuwa nacho mtu kwa sababu ya kumwabudu<br />

sana Mungu, aghalabu humpa uwezo wa kuomba haja kwa<br />

Mwenyezi Mungu na kukubaliwa mara moja; ridhaa ya kupokelewa<br />

haja iombwayo”<br />

Kwa mujibu wa kamusi za Biblia, kabla ya kuchambua<br />

maana ya karama za kiroho, hatuna budi tupate kufahamu ya kuwa<br />

Biblia haitoi tafsiri na msamiati huu wa “karama za kiroho” lakini<br />

imetoa maelezo ya kina kuhusu asili yake na jinsi zinavyotenda<br />

kazi. Msamiati wa neno “karama” ndio umetafsiriwa kwa kiyunani<br />

kama “charismata” likiwa na maana ya “karama za neema” na<br />

likilenga “karama” au uwezo maalum kutoka kwa Mungu ambao<br />

hutolewa kwa waamini kupitia Roho Mtakatifu.<br />

Pia kuna tofauti kati ya “karama za kiroho” au “karama za<br />

Roho Mtakatifu na “kipawa cha Roho Mtakatifu”. Kuna aina nyingi<br />

za karama za kiroho, lakini Roho Mtakatifu ni mmoja tu. Kipawa<br />

cha Roho Mtakatifu hupokelewa baada ya mtu kumpokea Yesu<br />

Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wake na kuzaliwa upya kiroho.<br />

(Mdo. 2:38).<br />

Aidha, kuna mgawanyiko maalum wa “karama za kiroho”<br />

ambao ni “karama za Roho”, “ofisi za huduma”, na “karama<br />

za neema”. Wakati ambapo “karama za Roho” ni utendaji wa<br />

Roho Mtakatifu ndani ya mwamini kama ilivyoandikwa katika<br />

1 Wakorintho 12; pia ziko “ofisi za huduma” ambazo ni vipawa<br />

vya kiroho vya utendaji huduma tofauti kama zilivyotajwa katika<br />

Waefeso 4:11. Na pia kuna “karama za Neema” ambazo ni<br />

utendaji wa Mungu kwa ajili ya waamini kama ulivyoanishwa<br />

kwenye Warumi 12.<br />

Orodha ya “karama za Roho” zilizotajwa katika 1 Wakorintho<br />

12: ni kama ifuatayo:<br />

7


1. Neno la hekima<br />

2. Neno la maarifa<br />

3. Kupambanua roho<br />

4. Imani<br />

5. Karama za kuponya<br />

6. Matendo ya miujiza<br />

7. Unabii<br />

8. Kunena kwa lugha<br />

9. Tafsiri za lugha<br />

Hizi “karama za Roho” naweza kuzitafsiri kuwa ni “karama<br />

za udhihirisho” (Manifestational gifts). Maana yake zenyewe<br />

zinatenda kazi ya kudhihirisha utendaji wa Roho Mtakatifu ndani<br />

ya waamini ambao wamekirimiwa huduma na utumishi wa kiroho<br />

katika mwili wa Kristo.<br />

Orodha ya “ofisi za huduma” zilizotajwa katika Waefeso<br />

4:11: ni kama ifuatayo:<br />

1. Mitume<br />

2. Manabii<br />

3. Wainjilisti<br />

4. Wachungaji<br />

5. Waalimu<br />

Hizi zinaitwa “ofisi za huduma” ambazo nimeziita “karama<br />

za uwezesho” kwa sababu zinafanya kazi ya kuwakamilisha<br />

watakatifu ili kazi ya huduma itendeke. Ni karama za kuwezesha<br />

waamini kupata uzoefu wa kutumika katika kuujenga mwili wa<br />

Kristo.<br />

Orodha ya “karama za neema” zilizotajwa katika Warumi<br />

12 ni kama ifuatavyo:<br />

1. Uhamasishaji<br />

2. Utoaji<br />

8


3. Uongozi<br />

4. Rehema<br />

5. Unabii<br />

6. Huduma<br />

7. Ualimu<br />

Hizi ni “karama za neema” ambazo zinaitwa “karama za<br />

utumishi” (Serving Gifts). Mungu Baba huwagawia waamini<br />

karama za neema ili wapate kutumikiana wenyewe kwa wenyewe<br />

mara baada ya kukamilishwa na zile “karama za uwezo” ambazo<br />

ni “ofisi za huduma”.<br />

3. Tofauti Kati Ya Vipaji Vya Asili Na Karama Za Kiroho<br />

Kwanza kabisa ni muhimu kutambua mapema ya kwamba<br />

“<strong>vipaji</strong> vya asili” si “karama za kiroho”. Kwa kifupi ni kwamba, “kipaji<br />

cha asili” chimbuko lake ni kibaiolojia (natural and biological); na<br />

“karama za Roho” asili yake ni ya kiroho na ya kiungu (spiritual<br />

and supernatural).<br />

Jambo muhimu la pili ni kwamba, kila binadamu (mwamini<br />

na asiye mwamini) huzaliwa na <strong>vipaji</strong> vya asili lakini kimojawapo<br />

kati ya vingine ndicho hujitokeza zaidi na mhusika akajulikana<br />

kupitia kipaji hicho cha asili.<br />

Lakini si kila binadamu anayezaliwa kibaiolojia huzaliwa<br />

akiwa na “karama za kiroho”. Tumejifunza ya kwamba “karama za<br />

kiroho” ni kwa ajili ya “waamini peke yao”, na kwa ajili ya matumizi<br />

ya kiroho peke yake. Kwa hiyo, kipaji cha asili mtu huzaliwa nacho<br />

kwa mara ya kwanza, lakini “karama za kiroho” hupokelewa na<br />

mtu akiisha kuzaliwa mara ya pili kiroho.<br />

Jambo muhimu la tatu ni kwamba, “<strong>vipaji</strong> vya asili”<br />

huwanufaisha zaidi wenye kuzaliwa navyo ikiwa ni pamoja na<br />

kuwaneemesha kwa maslahi ya kibinafsi. Lakini “karama za<br />

9


kiroho” kusudi lake ni “kuwahudumia na kuwanufaisha wengine”<br />

ambao Mungu anapenda kuwasaidia kupitia uwezo wake wa<br />

kiungu (supernatural means).<br />

Jambo muhimu la nne, ni kwamba <strong>vipaji</strong> vya asili vinahitaji<br />

kuendelezwa kwa mafunzo na mazoezi; wakati ambapo “karama<br />

za kiroho” zenyewe hutenda kazi kulingana na kiwango cha ukuaji<br />

wa kiroho wa mwamini na uhusiano wa karibu wa kiroho kati yake<br />

na Mungu.<br />

Vipaji Vya Asili Hukaa Katika Nafsi Ya Mtu<br />

Katika uchambuzi wa utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya asili na karama<br />

za kiroho, tutaona ya kwamba, <strong>vipaji</strong> vya asili chimbuko lake ni<br />

katika nafsi ya binadamu, na chimbuko la “karama za kiroho”<br />

chimbuko lake ni katika roho ya binadamu.<br />

Hebu tupitie kwa ufupi kuhusu “<strong>vipaji</strong> vya asili” jinsi<br />

vinavyotenda kazi kutokea kwenye nafsi. Ndani ya nafsi ndimo<br />

mna vitu vikuu vitatu ambavyo ni akili, hisia na utashi. Kila “kipaji<br />

cha asili” kwa asili yake lazima “kitumie akili” ambayo ni sehemu<br />

ya nafsi, lazima “kiguse hisia” ambayo sehemu ya nafsi, na lazima<br />

kitokane na “utashi wa mtu’ ambao pia ni sehemu ya nafsi.<br />

• Ni rahisi kwako kuliko mengine na wengine<br />

• Hutumii nguvu nyingi kupita kawaida<br />

• Inaeleweka kwa urahisi<br />

• Unaona ni kawaida na unashangaa kwanini wengine hawawezi<br />

• Unafanya kwa ubora zaidi<br />

• Unafanya kwa furaha na shauku ya moyo<br />

Karama Za Kiroho Makao Yake Ni Katika Roho Ya Mtu<br />

Utendaji wa “karama za kiroho”, tofuati na “<strong>vipaji</strong> vya<br />

asili”, wenyewe chimbuko lake ni katika roho ya binadamu.<br />

Kama tulivyojifunza kwamba roho ya binadamu inatokana na vitu<br />

10


vitatu ambavyo ni dhamiri, ushirika na utambuzi. Kwa kuwa asili<br />

ya karama za kiroho ni “hali ya kiungu” (supernatural source) na<br />

hutenda kazi kutokea ndani ya roho yake.<br />

Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, tunajifunza ya kuwa<br />

Roho Mtakatifu ndiye mdhibiti mkuu wa karama na vipawa vya<br />

huduma za kiroho. Hatua ya kwanza kazi ya Roho Mtakatifu ni<br />

kumzaa mtu mara ya pili (Yoh. 3:3), na tunafundishwa hali hii ya<br />

kuzaliwa mara ya pili hufanyika ndani ya roho ya mtu (Yoh. 3:6).<br />

Baada ya Roho Mtakatifu kumzaa upya mtu katika roho<br />

yake, hatua ya pili ni kujaa ndani ya mtu na kufanya makao ya<br />

kudumu ndani roho ya binadamu. Na humo ndimo utendaji wa<br />

karama za Roho pamoja na vipawa vya huduma za kiroho hutokea<br />

na kudhihirika katika nafsi ya mtu.<br />

11


SURA YA PILI<br />

UCHAMBUZI WA VIPAJI VYA ASILI<br />

Utangulizi<br />

Kwa kuwa kipaji ni kitu cha asili ya kuzaliwa nacho, kila<br />

binadamu katika mfumo wa ubongo amesukwa kufikiri na kutenda<br />

kulingana na nguvu za fikra zilizowekwa ndani yake. Kwa hiyo<br />

katika kuchambua <strong>vipaji</strong> tunakwenda kupitia na kujifunza kuhusu<br />

uwezo wa asili alionao mwenye kipaji cha asili.<br />

Kimsingi, kipaji cha asili ndicho kinachomtofautisha mtu<br />

na watu wengine na ndio utambulisho wake kwa wengine katika<br />

jamii. Na hii inatokana na taarifa kutoka katika maandiko ya Bibilia<br />

pamoja na tafiti za kisayansi ambazo zinathibitisha ukweli huu.<br />

Ziko nadharia nyingi zinazofundisha habari ya <strong>vipaji</strong> vya<br />

asili, lakini katika sura hii, tunakwenda kufanya uchambuzi wa aina<br />

saba tu za <strong>vipaji</strong> vya asili ambavyo vimo ndani ya kila binadamu<br />

ukiwemo na wewe msomaji wa kitabu hiki.<br />

Katika kufanya uchambuzi kuhusu nguvu na uwezo alionao<br />

mwenye kipaji husika, pia tutachambua viashira vya ufanisi kwa<br />

kila kipaji. Viashiria vya ufanisi ni maeneo maalum ambayo kila<br />

kipaji huonesha upekee na umaalum wa ubora kupitia mwenye<br />

kipaji husika.<br />

Mwisho kabisa, uchambuzi wa <strong>vipaji</strong> vya asili utabainisha<br />

aina mbali mbali za fursa za kitaaluma ambazo mwenye kipaji<br />

anaweza kuzimudu kwa viwango vya ubora wake. Vipaji vya asili<br />

viko saba kama vilivyoorodheshwa hapa:<br />

12


1. Kipaji cha Ubunifu wa mawazo<br />

2. Kipaji cha Mahusiano<br />

3. Kipaji cha Lugha<br />

4. Kipaji cha Hesabu<br />

5. Kipaji cha Michezo<br />

6. Kipaji cha Muziki<br />

7. Kipaji cha Picha<br />

Kumbuka ya kwamba kila binadamu anapozaliwa viashiria<br />

vya mambo saba haya ya <strong>vipaji</strong> vya asili huwa vimo ndani yake.<br />

Lakini kuna kipaji kimojawapo ambacho hujitokeza na kuonekana<br />

zaidi kuliko vingine na hicho ndicho hutafsiriwa kuwa kipaji cha<br />

mhusika.<br />

Kwa hiyo, tunakwenda kupitia kwanza nguvu za kimaumbile<br />

za kila kipaji, pili, tunachambua viashiria vya ufanisi wa kila kipaji,<br />

na tatu, tunaorodhesha aina ya fursa za kitaaluma zinazoambatana<br />

na <strong>vipaji</strong> vya asili kwa wahusika.<br />

13


UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />

UBUNIFU<br />

14


Kipaji cha ubunifu kwa lugha ya Kiingereza ni Intrapersonal<br />

Intelligence ambacho kimebeba uwezo maalum wa kubuni<br />

mambo mapya.<br />

Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Ubunifu<br />

Mwenye kipaji hiki ni mtu ambaye ana uwezo mkubwa<br />

katika kufikiri, kupata na kukusanya mawazo pamoja.<br />

Kimaumbile katika mfumo wake wa ubongo seli za<br />

fahamu zimesukwa katika hali ya fikra zenye kina, kukusanya<br />

mawazo pamoja, kufanya maamuzi yenye mwelekeo, uwezo wa<br />

kuchambua katika hali ya uhuru wa hiari.<br />

Mwenye kipaji cha ubunifu pia anao uwezo mkubwa wa<br />

kujitathmini na kujifahamu kibinafsi kuanzia mawazo, hisia na<br />

utambuzi wa ndani.<br />

Kana kwamba hii haitoshi, mwenye kipaji cha ubunifu<br />

ana uwezo mkubwa wa kuiongoza tabia binafsi, kujua nguvu na<br />

udhaifu binafsi, kubuni fikira mpya, kupanga shughuli na kutatua<br />

matatizo.<br />

Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Ubunifu<br />

Kila mwenye kipaji cha ubunifu atajulikana na kutambulika<br />

kwenye maeneo yake ya ufanisi unatokana na nguvu za kipaji<br />

chake. Baadhi ya maeneo ya ufanisi wa kipaji cha ubunifu ni<br />

pamoja na:<br />

• Utambuzi wa viwango vya hisia binafsi<br />

• Uwezo wa kujitawala na kufanyia kazi mawazo na hisia binafsi<br />

• Njia nyepesi za kueleza mawazo binafsi<br />

• Hamasa ya kubaini na kutekeleza malengo<br />

• Ufanisi wa kazi uwapo huru mwenyewe na peke yako<br />

15


• Udadisi wa kujua maana ya maisha<br />

• Uwezo wa kujitawala kibinafsi wakati wa kujifunza<br />

• Kutamani sana kupata uzoefu wa ndani ya nafsi<br />

• Uwezeshaji na uhamasishaji wengine<br />

• Kufurahia kufikiri mikakati, kuandika makala na kupenda<br />

mikakati ya kujitathimini binafsi<br />

• Kujua ukomo wa mipaka ya uwezo wako<br />

• Uwezo wa kuchambua, kubaini na kutathmini mambo/<br />

mazingira<br />

Fursa Za Kitaaluma<br />

Kipaji cha ubunifu kina fursa nyingi za kitaaluma iwapo<br />

mwenye kipaji hiki atajaliwa kujitambua mapema na kukinoa kwa<br />

ajili ya matumizi yenye tija. Baadhi ya fursa ambazo mwenye kipaji<br />

cha ubunifu anaweza kuzimudu kwa ufanisi mkubwa ni pamoja na<br />

kuwa:<br />

• Jaji<br />

• Mshauri<br />

• Wakili<br />

• Mkufunzi<br />

• Mwanasheria<br />

• Mtaalamu wa matibabu<br />

• Mwanandishi wa riwaya<br />

• Muuguzi wa magonjwa ya akili<br />

• Mwana falsafa<br />

• Mtaalamu wa hisabati<br />

• Kiongozi<br />

16


UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />

UHUSIANO<br />

17


Kipaji cha uhusiano kwa lugha ya Kiingereza ni Interpersonal<br />

Intelligence ambacho kimebeba uwezo maalum wa kutengeneza<br />

na kudumisha mahusiano.<br />

Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Uhusiano<br />

Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha uhusiano, katika<br />

mfumo wa ubongo wake anazo seli za neva zenye kumwezesha<br />

kutengeneza mawasiliano na wengine. Anao uwezo mkubwa wa<br />

mwingiliano wa kijamii, usikivu, ushirikishaji, kujenga mahusiano,<br />

utoaji na uwezo wa kuelewa na kufanya kazi vizuri na watu.<br />

Mtu mwenye kipaji cha uhusiano ni mwepesi na mwenye<br />

ukaribu wa kuchukuliana na watu na ushiriki wa kihisia wa mambo<br />

wanayopitia. Hii ni pamoja na uwezo wa kutawala, kusuluhisha,<br />

kuhamasisha, kuongoza, kuelekeza na kushauri wengine.<br />

Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Uhusiano<br />

Mwenye kipaji cha uhusiano hutambulika kwa viashiria vya<br />

uhusiano ambavyo ni pamoja na:<br />

• Nguvu za kuongoza<br />

• Ufanisi katika kujenga mtandao na wengine<br />

• Uwezo wa kujadiliana, kujenga hoja za utetezi na mzuri katika<br />

usuluhishi<br />

• Uwezo wa kuongea na kupangilia mambo<br />

• Kufurahia kuwa mlezi wa <strong>vipaji</strong> vya wengine<br />

• Uwezo wa kutanguliza wengine<br />

• Uwezo wa kuhisi na kutambua hisia, hulka, tabia na matarajio<br />

ya wengine<br />

• Uwezo wa kushawishi wengine<br />

• Ufanisi katika kufanya kazi na kundi, juhudi za pamoja katika<br />

kikundi na utendaji wa pamoja<br />

• Uwezo wa kuunganisha watu wakawa wamoja<br />

• Uwezo wa kujenga mahusiano ya kijamii ya kudumu<br />

18


Fursa Za Kitaaluma<br />

Kipaji cha uhusiano kina fursa nyingi za kitaaluma ambazo<br />

mhusika anaweza kuonesha ufanisi wa kitaaluma. Baadhi ya fursa<br />

za kitaaluma ni pamoja na hizi zifuatazo:<br />

• Mwanasiasa<br />

• Kiongozi wa dini<br />

• Muuzaji<br />

• Mkufunzi<br />

• Mshauri<br />

• Mtaalamu wa sayansi ya jamii<br />

• Msemaji/Mtalaamu wa lugha<br />

• Mtaalamu wa kijamii<br />

• Mtaalamu wa saiklojia<br />

• Afisa mahusiano<br />

• Mkurugenzi wa rasilimali watu<br />

• Meneja<br />

• Mhamasishaji<br />

19


UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />

LUGHA<br />

20


Kipaji cha lugha kwa lugha ya Kiingereza ni Linguistic<br />

Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum wa umahili katika<br />

lugha.<br />

Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Lugha<br />

Kimauimbile mtu mwenye kipaji cha lugha, katika mfumo<br />

wa ubongo wake anazo seli za neva zinazojenga umahili wa lugha<br />

na umakini wa maana za maneno, sauti, mahadhi pamoja na<br />

matumizi tofauti ya lugha mbali mbali.<br />

Uwezo wa kufikiri kwa njia ya maneno na kutumia maneno<br />

kwa ufasaha katika kuongea na kuandika.<br />

Pia mwenye kipaji cha lugha huwa ni mwepesi wa kujifunza<br />

mifumo na miundo ya lugha na matumizi yake.<br />

Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Lugha<br />

• Huhitaji kujieleza kibinafsi kwa kuandika au kutumia maneno<br />

mengi<br />

• Hupenda kulumbana, kuhoji, kuburudisha na kuelekeza<br />

• Hupenda kuandika, kucheza na maneno, kusoma na kusimulia<br />

visa na hadithi<br />

• Huwa na kiwango kizuri cha elimu ya jumla<br />

• Huuliza maswali mengi<br />

• Hupenda kuongoza/kushiriki katika mijadala<br />

• Hupendelea mbao za kuandikia, vifaa vya kutunza maneno, na<br />

vifaa vya kunakili maneno<br />

• Utamkaji vizuri wa maneno<br />

• Kujifunza lugha kwa urahisi<br />

• Huwa na kumbukumbu nzuri ya majina, tarehe, na majina ya<br />

maeneo<br />

21


Fursa Za Kitaaluma<br />

• Mhariri<br />

• Mwandishi wa hotuba<br />

• Mtunga mashairi<br />

• Mwandishi wa riwaya<br />

• Mwanasiasa<br />

• Mtunza hakimiliki<br />

• Msemaji/Mtaalamu wa lugha<br />

• Mwandishi wa michezo ya kuigiza<br />

• Mwanasheria/Wakili<br />

• Mwandishi wa habari<br />

• Mkufunzi<br />

22


UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />

HESABU<br />

23


Kipaji cha hesabu kwa lugha ya Kiingereza ni Logic/<br />

Mathematical Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum wa<br />

kuchanganua matatizo ya kinadharia kwa kutumia mahesabu.<br />

Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Hesabu<br />

Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha hesabu, katika mfumo<br />

wa ubongo wake anazo seli za neva zinazojenga uwezo wa kufikiri<br />

na kuchambua mambo kisayansi; uwezo wa kuelewa kanuni na<br />

mifumo na michanganuo ya kimahesabu.<br />

Viashiria Vya Kipaji Cha Hesabu<br />

• Uwezo wa nidhamu ya ndani katika kufikiri<br />

• Uwezo wa kuhesabu na kuthibisha majibu ya hesabu<br />

• Uwezo wa kufikiria sana mambo<br />

• Shauku ya kujua nini kinafuata mbeleni<br />

• Kupenda kutafakari mambo kimahesabu<br />

• Kupenda kubuni nadharia zinazoonesha jinsi kufanya mambo<br />

• Hupenda kuthibitisha usahihi wa kitu kabla ya kukitumia<br />

• Kuonesha uwezo wa kutambua na kutatua matatizo<br />

Fursa Za Kitaaluma<br />

• Mwanasayansi<br />

• Daktari wa tiba<br />

• Mwanahisabati<br />

• Meneja wa mradi<br />

• Mhasibu<br />

• Mkutubi wa chuo kikuu<br />

• Mhandisi<br />

• Mtafiti<br />

• Mtaalamu wa programu za kompyuta<br />

• Mtaalamu wa tiba ya mifuba<br />

• Mtaalamu wa benki<br />

• Mwanasheria<br />

• Mpelelezi<br />

• Mwindaji wanyama<br />

• Mfanyabiashara/mjasiriamali<br />

24


UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />

MICHEZO<br />

25


Kipaji cha michezo kwa lugha ya Kiingereza ni Kinesthetic<br />

Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum wa ufundi wa<br />

kutumia viungo vya mwili na miondoko; na uwezo kumudu vitu au<br />

mambo yanayokuzunguka.<br />

Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Michezo<br />

Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha michezo, katika<br />

mfumo wa ubongo wake anazo seli za neva ufundi wa miondoko,<br />

kugeuza maungo ya mwili, na mizunguko hususani kucheza mpira<br />

wa miguu, riadha, kubiringika juu ya kiti bila kuumia, kujigeuza<br />

mwili pasipo maumivu;<br />

Hali kadhalika mwenye kipaji cha michezo ana ufundi wa<br />

asili wa kutumia viungo vya mwili na miondoko; na uwezo wa<br />

kumudu vitu au mambo yanayokuzunguka; Wenye <strong>vipaji</strong> vya<br />

michezo ni watu walioumbwa kujifunza na kufikia viwango vya<br />

ubora wa <strong>vipaji</strong> kwa njia ya michezo.<br />

Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Michezo<br />

• Uwezo mzuri wa kujikusanya kimwili<br />

• Mwepesi kuwahi muda na kufanya kwa wakati<br />

• Hukabiliana na matatizo kwa nguvu za mwili<br />

• Kupenda kunyoosha viungo vya mwili na mazoezi<br />

• Kupenda michezo ya kuigiza<br />

• Kupenda kucheza ngoma/muziki<br />

• Hufikiri wakati wa miondoko<br />

• Hupenda kuchonga vinyago na burudani<br />

• Kubuni vitu vipya vya kimichezo<br />

Fursa Za Kitaaluma<br />

• Mwigizaji<br />

• Mwanariadha<br />

• Mcheza mziki<br />

26


• Mvumbuzi<br />

• Sonara<br />

• Mchongaji<br />

• Mwanasanaa<br />

• Dreva wa mashindano ya magari<br />

• Mtaalamu wa tiba maungo<br />

27


UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />

MUZIKI<br />

28


Kipaji cha muziki kwa lugha ya Kiingereza ni Musical<br />

Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum wa kutumia sehemu<br />

ya ubongo iitwayo sular ambayo imejaa fikira za muziki na hutumia<br />

utambuzi wa ndani wa kufahamu mambo yasiyo dhahiri.<br />

Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Muziki<br />

Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha muziki, katika mfumo<br />

wa ubongo wake anazo seli za neva zenye uwezo wa kuimba<br />

au kupiga vyombo vya muziki, uwezo wa kutambua mahadhi na<br />

kupambanua mambo yasiyo dhahiri kupitia muziki. Pia mwenye<br />

kipaji cha muziki ana uwezo wa kuwasoma watu kwa kusikiliza<br />

sauti zao na lugha kupitia maungo ya mwili, na sio kwa kusikiliza<br />

maneno peke yake.<br />

Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Muziki<br />

• Utambuzi wa ndani wa kuhisi wakati mambo ni mazuri au<br />

mabaya<br />

• Hafanyi mambo mpaka amejisikia yuko sahihi<br />

• Hawezi kujieleza lakini ana hisia za kutambua ni nani wa<br />

kuaminiwa na ambaye sio<br />

• Yuko makini na hisia kali na mazingira na kujisikia au kutojisikia<br />

raha katika maeneo fulani<br />

• Hutafuta kusikiliza sauti, huvutiwa na muziki, na hupenda<br />

kutunga nyimbo/muziki<br />

• Uwezo wa kuimba vizuri kwa vina na mjuzi wa kupiga vyombo<br />

• Kutunza muda katika kuimba<br />

• Uwezo wa kusikiliza na kukosoa muziki<br />

• Ukusanyaji wa nyimbo, ala na muziki<br />

• Hupenda kuchezesha miguu, vidole au kalamu anapofanya<br />

kazi au kusikiliza jambo<br />

29


Fursa Za Kitaaluma<br />

• Mwongozaji<br />

• Mtunga ala<br />

• Mtunzi wa nyimbo<br />

• Mhandisi wa muziki<br />

• Mtaalamu wa kinanda<br />

• Msimamizi wa disko<br />

• Mwalimu wa Muziki<br />

• Mtaalamu wa nyimbo za ala<br />

• Mchezaji wa jukwaani<br />

• Mchezaji muziki<br />

• Mwanamuziki<br />

Mwimbaji<br />

• Mhadisi wa uzalishaji muziki<br />

• Msemaji wa shughuli au mshehereshaji (MC)<br />

30


UCHAMBUZI WA KIPAJI CHA<br />

PICHA<br />

31


Kipaji cha picha kwa lugha ya Kiingereza ni Visual/Spatial<br />

Thinking ambacho kimebeba uwezo maalum kupokea kutoka<br />

ulimwengu wa picha/maumbo na kuyachora, hadi kutoa kitu halisi<br />

kwa mfano wa picha kutoka akilini.<br />

Nguvu Za Asili Za Kipaji Cha Picha<br />

Kimauimbile, mtu mwenye kipaji cha picha katika mfumo<br />

wa ubongo wake anazo seli za neva za kutazama rangi, mwanga,<br />

umbo na vina vya vitu; ikiwa ni pamoja na kufumba macho na<br />

kutafakari, kuona mambo ambayo hayaonekani kwa macho ya<br />

asili; uwezo wa kukitoa kitu kwenye nafsi ya ndani (non-conscious)<br />

hadi kwenye akili (consciousness).<br />

Viashiria Vya Ufanisi Wa Kipaji Cha Picha<br />

• Hufikiri katika mfumo wa picha na kutafsiri michoro/picha kwa<br />

urahisi<br />

• Uwezo wa kupokea mawazo kwa njia ya maumbo na kuyachora<br />

mawazo hayo katika mfumo wa picha<br />

• Uwezo wa kukumbuka sura lakini husahau majina<br />

• Huweza kuvusha mawazo huku akiendelea kusikiliza<br />

Fursa Za Kitaaluma<br />

• Mchongaji<br />

• Mwanamazingira<br />

• Kiongozi<br />

• Mtendaji mkuu<br />

• Mbunifu wa michoro<br />

• Mhandisi<br />

• Mwandishi wa Sheria<br />

• Nahodha<br />

• Mtaalamu wa video<br />

• Mpiga picha<br />

32


• Mpaka rangi<br />

• Mwendeshaji<br />

• Mtaalamu wa mikakati ya vita<br />

• Msanifu wa majengo<br />

• Rubani<br />

33


Njia Za Kutambua Kipaji Chako<br />

Utangulizi<br />

Kujitathmini na kutambua una kipaji gani cha asili si kazi<br />

nyepesi. Si tukio la mara moja bali ni mchakato. Na mchakato<br />

wenyewe unategemea mambo mengi kuanzia umri wako,<br />

mazingira unamoishi na kukulia kimalezi; aina ya watu walio karibu<br />

na wewe mfano wazazi au walezi na jamaa wa karibu; kama ni<br />

mwanafunzi ni aina gani ya shule, chuo na masomo unayochukua.<br />

Yote haya ni mazingira ambayo yana mchango mkubwa kwako<br />

katika kufanikisha au kutokufanisha zoezi la kujitathmini na<br />

kutambua kipaji chako.<br />

Hata hivyo, kwa kuwa kipaji cha asili ni hali ya kuzaliwa<br />

nayo, uchunguzi unaonesha kwamba mpaka mtu anapofikia umri<br />

wa miaka 14 tayari anaweza kujitathmini na kubaini kipaji chake.<br />

Kama mtu hakupatwa majanga ya kuathiri afya yake, uwezo wa<br />

<strong>vipaji</strong> ndani yake huendelea kuwemo ndani kama atadhamiria<br />

kujitathmini kwa kutafuta kujua anaweza nini ili kujipanga kupata<br />

elimu itakayomsaidia kunoa kipaji chake.<br />

Uwezo wa kuzaliwa nao hauwezi kuathiriwa na upungufu<br />

wa elimu au uzoefu, japokuwa elimu na uzoefu vinaweza kutumika<br />

kuboresha uwezo wa kipaji cha asili alichonacho mtu.<br />

Kila mtu amezaliwa na uwezo pekee na maalum ambao<br />

humfanya kuwa tofauti na wengine katika jamii. Yafuatayo ni<br />

baadhi ya mambo machache ya kukusaidia kutambua una <strong>vipaji</strong><br />

au kipaji gani:<br />

1. Kitu Gani Kilicho Kushughulisha Sana Utotoni?<br />

Kama wewe ni mtu mzima tayari, hasa kuanzia miaka 30<br />

na kuendelea, hebu tumia muda kama dakika mbili kujikumbusha<br />

enzi zako za furaha kuanzia shule ya msingi. Ni jambo gani<br />

34


ambapo ushiriki wako ulikuwa unapata furaha sana kiasi kwamba<br />

unapokumbuka unasisimka mpaka leo. Na jambo gani hasa<br />

lililochukulia muda mwingi na hata kukufanya ukorofishane na<br />

wazazi au walimu au watoto wenzako wakati kumbe hilo ndilo<br />

ulilokuwa ukilifurahia sana?<br />

Pengine ulikuwa unahamasika kushiriki mashindano<br />

katika michezo kama mpira wa miguu au riadha. Marafiki zako<br />

walikufurahia sana ukiwa katika timu yao wakitarajia watashinda<br />

kwa sababu yako. Na wewe uliifurahia sana hali hiyo. Pengine<br />

ulikuwa unapendelea sana kuimba kwaya au mashairi au ngoma,<br />

na hata kuwa kiongozi wa kwaya au kutunga na kufundisha<br />

nyimbo au mashairi. Pengine ulikuwa unapenda sana michezo ya<br />

kuigiza na kila mara ulikuwa nyota katika michezo uliyoshiriki.<br />

Hapa ni muhimu kutofautisha kupenda kitu kwa sababu kina<br />

umaarufu, na kuwa na uwezo wa kufanya kitu hicho kwa viwango<br />

vya ubora bila kutumia nguvu nyingi kama wengine. Maana watu<br />

wengi wanapenda mambo ambayo wanaona yamewafanya<br />

wengine kuwa maarufu na wao wanatafuta umaarufu kwa kuiga<br />

lakini hawana uwezo wa kufanya mambo hayo kwa viwango vya<br />

ubora. Kumbuka “kupenda sana” ni tofauti na “kuweza sana.”<br />

Kwa hiyo, katika kutafakari enzi zako za utotoni, hebu<br />

fuatilia ni jambo gani ambalo limeendelea kushika nafsi yako<br />

mpaka wakati huu wa ukubwani.<br />

Bado unapenda kushiriki mashindano ingawa hivi sasa<br />

ushindani wako umeuelekeza labda kwenye biashara mpya, bado<br />

unaweza kuwa unapendelea kufanya mambo magumu magumu,<br />

na miradi ya kimkakati japokuwa sasa unaifanyia kwenye<br />

makampuni ya ushauri.<br />

Mpaka hivi sasa, <strong>vipaji</strong> vya asili hujidhihirisha kupitia<br />

mambo tunayopenda sana na tunajikuta tuna uwezo nayo kuliko<br />

mengine.<br />

35


Mara nyingi msukumo wa kupenda au kuchagua kufanya<br />

mambo fulani ambayo unayamudu vizuri kuliko wengine hutokana<br />

na nguvu za <strong>vipaji</strong> vya asili vilivyomo katika nafsi zetu.<br />

2. Jambo Gani Unalipenda Sana?<br />

Swali hili ni kwa kila mtu. Jambo gani unalipenda sana.<br />

Tafadhali zingatia, kupenda kunakotajwa hapa ni mvuto wa hisia<br />

za ndani za kutamani kufanya jambo fulani hata kama hutapata<br />

malipo yoyote. Tena wakati mwingine wewe ndio uko tayari kulipia<br />

gharama za kufanya jambo unalolipenda sana badala ya wewe<br />

kulipwa.<br />

Haya tuseme leo ni jumamosi ambapo si siku ya kazi. Una<br />

muda ambao ni huru wa kufanya jambo unalolipenda. Pengine<br />

ni kupiga gitaa au kinanda au kuandika riwaya au jambo jingine<br />

lolote (lakini isiwe kutazama tv na tamthilia).<br />

Hili jambo ambalo umeamua kulifanya, kila mara<br />

unapolifanya, linakuvuta kweli kweli. Akili zote, mwili na hisia na<br />

utambuzi wa ndani vinajikuta vikilifanya kwa ukamilifu na kwa<br />

kunogewa hasa. Unazama katika kufanya jambo hilo mpaka<br />

unasahau ni saa ngapi, na hata unasahu muda wa kula.<br />

Haya, fikiria kazi unayoifanya katika siku za kawaida za<br />

kazi, kama ungeifanya katika msukumo na mvuto na mzamo<br />

kama ulivyozama kwenye jambo hili la Jumamosi huru, ufanisi<br />

wako ungelikuwaje kazini?<br />

Nakwambia watu wengi wanafanya kazi kwa sababu ya<br />

malipo ya mshahara lakini sio kwamba wanafanya kwa msukumo<br />

wa <strong>vipaji</strong> vya asili. Ndiyo maana kufanya kazi ambazo haziendani<br />

na <strong>vipaji</strong> vya asili hakuleti ufanisi mkubwa na maendeleo yake ni<br />

duni.<br />

36


Lakini kama mtu akifanya kazi ambayo inaendana na kipaji<br />

chake, hataangalia saa ya kumaliza kazi bali anavutwa kufanikisha<br />

kazi ile ifikie viwango vya ubora stahiki na hiyo ndiyo inayomfanya<br />

ajitume kufanya vema kuliko wengine.<br />

Pasipo kujali mazingira uliyomo hivi sasa, na mambo<br />

unayoyafanya kwa sababu ya desturi tu, hebu tafakari ni jambo<br />

gani ambalo una msukumo wa ndani unaokushuhudia kuwa<br />

ukilifanya utalimudu vizuri bila kutumia nguvu nyingi na utafanya<br />

kwa viwango vya ubora tofauti na wengine?<br />

Inawezekana jambo hilo ni tofauti kabisa na shughuli<br />

unayoifanya hivi sasa ambayo pengine ndiyo inayokupatia riziki.<br />

Au pengine bado ni mwanafunzi lakini masomo unayochukua<br />

hayaendani na jambo lile unalolitamani sana kulifanya na ukipewa<br />

fursa utalimudu vizuri kuliko hata masomo unayochukua hivi sasa.<br />

Kama unahusika katika eneo hili, ujue kwamba unakabiliwa<br />

na changamoto ya mgongano wa kimaslahi kati ya kipaji cha asili<br />

na mambo unayoyafanya hivi sasa yanayokupatia riziki au msaada<br />

wa kimaisha. Unahitaji hekima ya Mungu katika kuyaweka kwenye<br />

mizania sawa.<br />

Ushauri wangu hapa ni kwamba wakati wa muda wako wa<br />

ziada ambapo hauko kazini au masomoni, wakati umekamilisha<br />

majukumu yako ya kila siku kwa mujibu wa mkataba, tumia<br />

muda wa ziada katika kufanyia mazoezi hilo jambo ambalo una<br />

msukumo nalo.<br />

Kama ni mwanafunzi omba ushauri kwa wazazi/walezi na<br />

walimu kuhusu msukumo uliomo ndani yako na jinsi unavyofikiria<br />

kama ungepewa fursa ya kufanya jambo hilo ungetimiza ndoto<br />

yako kuhusu hatma yako.<br />

Kama ni mfanyakazi uliyeajiriwa au mjasiliamali<br />

unayejitegemea, hakikisha unajipanga vizuri kuhusu jinsi<br />

37


utakavyolianza jambo hilo pasipo kuingiliana na mambo yako<br />

yanayokuwezesha kupata riziki au msaada wa mahitaji yako ya<br />

sasa. Tafuta ushauri na pengine anza taratibu kwa muda wa ziada.<br />

Inategemea ni jambo gani na kama linawezekana kwa<br />

muda wa ziada. Lakini ujue kwamba kama jambo hilo linakunyima<br />

usingizi na linakukereketa kila mara, huenda kipaji chako cha asili<br />

kimebebwa kwenye jambo hilo.<br />

3. Wengine Wanasemaje Juu Yako?<br />

Njia nyingine ya kutambua una kipaji gani cha asili ni maoni<br />

ya wengine walio karibu na wewe. Ni muhimu kusikiliza kwa makini<br />

vile wengine walio karibu na wewe wanavyokutafsiri vile ulivyo.<br />

Kwa kuwa kipaji cha asili kazi yake ni kuhudumia wengine<br />

katika jambo lile ulilopewa uwezo kulifanya kwa viwango vya<br />

ubora kuliko wengine, lazima wahusika watasema habari zako<br />

kuhusu uwezo wako.<br />

Hebu tafakari ni jambo gani ambalo watu huja kwako<br />

kutafuta msaada wako, au kukuomba utoe huduma kwao kwa<br />

jambo hilo.<br />

Maoni ya wengi kuhusu jambo unalolimudu vizuri ni<br />

sehemu ya ushahidi kwamba una kipaji cha asili katika jambo<br />

hilo. Na hasa ikiwa watu wako tayari kukulipa kwa ajili ya jambo<br />

hilo. Sio kwamba wanakupenda wewe bali wanapenda kipaji<br />

chako. Wanakihitaji katika kuboresha mambo yao ambayo wewe<br />

ni mmoja wa waboreshaji wao.<br />

4. Jambo Gani Unaliweza Kwa Urahisi?<br />

Kimsingi hakuna jambo jepesi hata kama ni dogo. Lakini<br />

kwa muktadha wa mada hii, kati ya mambo ambayo ni magumu<br />

kwa wengine, huenda kuna jambo ambalo kwako ni jepesi kwako<br />

38


na halikupi shida wala kukuhenyesha kama wengine.<br />

Mara nyingi mambo ambayo ni rahisi sasa kwako, sio<br />

kwamba ni rahisi bali wewe umejaliwa uwezo maalum wa<br />

kuyamudu ndiyo maana yanakuwa mepesi kwako. Katika hayo<br />

mepesi, ambayo yanawatoa jasho wengine, huenda ndipo kipaji<br />

chako cha asili kilipolalia.<br />

Matumizi Mabaya Ya Vipaji Vya Asili<br />

Katika harakati za kutafuta na kufanya mambo kwa<br />

muktadha wa <strong>vipaji</strong> vya asili, yako mambo ambayo hayatakiwi<br />

kutafsiriwa kuwa ni <strong>vipaji</strong> vya asili. Japokuwa wahusika wanaweza<br />

kulazimisha na kushinikiza ya kwamba wanatumia <strong>vipaji</strong> vya asili<br />

kufanya mambo hayo, ukweli unabakia kwamba <strong>vipaji</strong> vya asili<br />

vinatambuliwa kwa nguvu na viashiria vyake vya ufanisi. Baadhi<br />

ya mambo ambayo si <strong>vipaji</strong> vya asili ni haya yafuatayo:<br />

1. Tamaa Ya Umaarufu Wa Kutajirika Haraka<br />

Kuna watu wenye tamaa ya kutafuta utajiri wa haraka na<br />

huwa tayari kuupata kwa haraka pasipo kufuata taratibu halali za<br />

kuupata utajiri huo. Kundi hili hutafuta “umaarufu” kama njia ya<br />

mkato ya kujipatia utajiri wa haraka.<br />

Wako tayari kuwania fursa za umaarufu kama uongozi wa<br />

kisiasa au huduma za kikanisa kwa sababu tu huko ndiko kuna<br />

majukwaa ya kuwafikia watu wengi.<br />

Misukumo ya jinsi hii haiwezi kutafsiriwa kuwa ni “<strong>vipaji</strong> vya<br />

asili” kwa sababu wahusika pamoja na kutumia nguvu kubwa za<br />

kujinadi ili wapate kukubalika, bado hushindwa kuonesha viwango<br />

vya utendaji bora katika nafasi walizozivamia tu kwa tamaa zao<br />

wenyewe.<br />

39


Mwenye kipaji cha asili katika uongozi uwe wa kisiasa au<br />

kikanisa, hatumii nguvu kubwa kujinadi wala hatumii hila na ujanja<br />

wa kujitangaza kwa vyeo akidhani vyeo ndio umaarufu. Mwenye<br />

kipaji hujikuta akiwa maarufu kutokana na ushawishi alionao wa<br />

kusikilizwa na kufuatwa na wengi kwa sababu ya mvuto wa kipaji<br />

uliomo ndani yake.<br />

2. Wivu Wa Kuharibu Mafanikio Ya Wengine<br />

Kuna kundi jingine la watu wenye wivu wa kutokufurahia<br />

mafanikio ya watu wengine. Kundi hili hujiona kwa kuwa lenyewe<br />

bado halijafanikiwa, basi hakuna haki kwa wengine kufanikiwa,<br />

na kama wakifanikiwa basi mafanikio yao kwa mtazamo wao<br />

wanayahesabu si halali.<br />

Katika msukumo wa wivu, watu hawa hujikuta wakitumia<br />

kila njia za kuzuia, kukwamisha, na hata kuharibu mafanikio<br />

ya watu wengine, na wanatafsiri kuwa hivyo ndivyo <strong>vipaji</strong> vyao<br />

vya asili! Hakuna <strong>vipaji</strong> vya kupambana na kuweka vikwazo vya<br />

kuharibu mafanikio ya wengine.<br />

Mwenye kipaji cha asili, hasumbuliwi na wivu dhidi ya<br />

mafanikio ya wengine. Badala yake hufurahia na kusifia mafanikio<br />

ya wengine na hata kujifunza mbinu za kufanikiwa kama wao ikiwa<br />

atapewa fursa hiyo. Mwenye kipaji anaweza kutumia kipaji chake<br />

kufanikisha mambo ya wengine ili mradi tu apate uzoefu kabla ya<br />

kuanza kufanya mambo yake mwenyewe.<br />

3. Wizi Wa Mawazo Ya Wengine<br />

Kundi jingine la kujihadhari nalo ni lile la wenye tamaa ya<br />

kuiba mawazo ya wengine kwa kudhani watakuwa maarufu kama<br />

wenye maono waliyodokoa bila ridhaa ya wahusika. Kundi hili<br />

linajulkana kama “copy cats”.<br />

40


Tamaa hii inafanana kidogo na ile ya kutafuta umaarufu<br />

kwa sababu ya utajiri wa haraka haraka. Ila tamaa ya jinsi hii<br />

hujikita katika kutafuta kupeleleza na kudokoa au kuiba mawazo<br />

ya wale wanaoonekana kufanikiwa ili na wao wafanikiwe kama<br />

wale wenye maono halisi.<br />

Kwa kiasi fulani wanaweza kufanikiwa ila hawafikii viwango<br />

vya ubora wa maono yale waliyoiba kwa wengine. Kuiba mawazo<br />

ya wengine sio kipaji cha asili. Huu ni wizi wa kawaida hata kama<br />

hakuna ushahidi wa kukamatwa kwa wenye tabia hizi.<br />

Ngazi Za Ukuaji Na Utendaji Wa Vipaji Vya Asili<br />

Utangulizi<br />

Baada ya kuchambua aina za <strong>vipaji</strong> vya asili na jinsi<br />

vinavyotenda kazi, sasa tunakuja kwenye ngazi au hatua za<br />

kutenda kazi kuanzia umri mdogo mpaka uzeeni.<br />

Tumejifunza katika sura ya kwanza ya kuwa <strong>vipaji</strong> vya<br />

asili ni <strong>vipaji</strong> vya kuzaliwa navyo kibaiolojia na kisaikolojia. Hii<br />

ikimaanisha ya kwamba <strong>vipaji</strong> huanza tangu mtu anapotungwa<br />

mimba katika tumbo la mama yake.<br />

Jambo jingine la kujikumbusha ni kwamba kila binadamu<br />

huumbwa na kipaji cha asili ambacho ndicho humtofautisha<br />

na binadamu wengine katika jamii. Hivyo ndivyo Mungu<br />

alivyomkusudia kila binadamu atakayezaliwa na kuishi duniani.<br />

Tunasoma ngazi za ukuaji wa kipaji cha mtu katika maandiko<br />

yafuatayo:<br />

“Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, zaeni,<br />

mkaongezeke, mkaijaze nchi na kuitiisha; mkatawale...” (Mwa.1:28)<br />

41


Katika maandiko haya tunakuta maneno muhimu yafuatayo:<br />

“zaeni”, “mkaongezeke”, “mkaijaze nchi”na “kuitiisha”. Katika<br />

maneno haya tunapata kuziona ngazi za utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani<br />

ya mtu katika mtiririko wa ngazi ya “ubunifu”, ngazi ya “uzalishaji”,<br />

ngazi ya “usimamizi” na ngazi ya “urithishaji”:<br />

1. Ngazi Ya Ubunifu<br />

Wengi hulitafsiri neno hili kwa maana moja tu “wana ndoa<br />

kuzaa watoto”! Lakini neno hili “zaeni” lina maana kubwa zaidi<br />

“kuzaa watoto”. Neno “zaeni” linabeba maana nzito ya “ubunifu<br />

wa mawazo mapya”. Kuzaa kunaanzia katika wazo kwanza. Ngazi<br />

ya kuzaa ni ngazi ya ubunifu wa mawazo ambayo wengi huyaita<br />

“maono mapya”.<br />

Wanandoa wanapoanza maisha, hatua yao ya kwanza ni<br />

ya “ubunifu wa mawazo mapya” ya jinsi wanavyotaka kuendesha<br />

maisha yao ya ndoa, kila mwanandoa akitimiza wajibu wake katika<br />

sehemu yake. Kuzaa watoto huanza katika ngazi ya ubunifu wa<br />

kuona umuhimu wa kuwa na watoto na jinsi ya kuwalea mpaka<br />

watakapokuwa watu wazima kama wao.<br />

Hatua ya kwanza ambapo kipaji ndani ya mtu kinapoanza<br />

kutenda kazi katika ubongo wake. Umri unaokadiriwa kwa kipaji<br />

kuanza ubunifu katika ngazi ya mawazo ni miaka 12-25.<br />

Muda huu ndipo mtoto anapokuwa katika mabadiliko<br />

makubwa ya kibaiolojia na kisaikolojia. Ndipo wakati anapokuwa<br />

na mawazo ya ubishi mwingi na kuhoji mambo mengi na wakati<br />

mwingine hata kujiamulia mambo kulingana na anavyowaza akilini<br />

mwake.<br />

Huu ndio wakati wa mafunzo ya kunoa <strong>vipaji</strong> unapotakiwa.<br />

Wakati anapokuwa shuleni ndio wakati ambapo waalimu na<br />

waangalizi wanatakiwa kumsoma mtoto ana kipaji gani. Na<br />

sio kumsoma tu bali kuanza kumwandaa kisaikolojia mtoto<br />

42


ajitambue na kujiandaa kwa ajili ya kutumikia kipaji chake wakati<br />

atakapohitimu masomo yake.<br />

Hapa ndipo mifumo yetu ya elimu katika nchi za kiafrika<br />

ilipodhoofishwa na wakoloni waliotawala mataifa ya kiafrika. Kwa<br />

ujanja walituandalia mifumo ya elimu kwa nia ya kutufanya vibarua<br />

katika mashamba na miradi yao, na sio kwa ajili ya kuwaandaa<br />

watoto wa kiafrika wagundue na kunoa <strong>vipaji</strong> vyao ili wakihitimu<br />

waweze kujitegemea kupitia <strong>vipaji</strong> vyao vya asili.<br />

Kwa bahati mbaya, mpaka hivi sasa bado mifumo ya “elimu<br />

tegemezi” inaendelea kutumika; na ndiyo chimbuko la “dhana ya<br />

kuajiriwa”. Badala ya mhitimu kuwa na mtazamo wa “kujitegemea”<br />

kwa yeye kubuni kazi zake za ustadi na kutoa huduma za kulipwa<br />

kulingana na thamani ya viwango vya ubora; yeye anataka “nafasi<br />

ya kuajiriwa”.<br />

Naomba ieleweke kwamba si makosa wala si dhambi<br />

kuajiriwa. Mantiki hapa ni kwamba nafasi za ajira katika serikali<br />

na taasisi za umma ambazo ni haki ya kila mhitimu ni chache<br />

kuliko idadi ya wahitimu. Na hata sekta binafsi ina vigezo vyake<br />

vya kuajiri ikiwa ni pamoja na malipo ya chini ili kutengeneza faida<br />

kubwa. Hii ndiyo changamoto ya kutegemea ajira peke yake.<br />

Kama nilivyokwisha kusema tangu awali, kila mtoto<br />

ambaye ni binadamu kamili, mwenye afya njema na akili timamu,<br />

anacho kipaji cha asili ndani yake cha kumwezesha kuishi maisha<br />

ya kujitegemea pindi atakapokuwa mtu mzima.<br />

Lakini basi, katika ngazi hii ya ubunifu, ndipo mtoto<br />

anapotumia uwezo wake wa kufikiri kuelekea aina ya kipaji chake<br />

alichoumbiwa tangu tumboni mwa mama yake.<br />

43


2. Ngazi Ya Uzalishaji<br />

Neno la pili katika ngazi za utendaji wa <strong>vipaji</strong> lilikuwa ni<br />

“mkaongezeke”. Neno hili ndilo linatuleta katika ngazi ya pili ya<br />

“uzalishaji”. Katika ngazi hii, mtoto ameondoka katika ngazi ya<br />

utoto wa kuwa tegemezi anaanza kuyatendea kazi mawazo yake<br />

mapya ambayo tayari amekwisha kuyajaribu na kupata mwelekeo<br />

wa ni nini anatakiwa kuwekeza nguvu zake zote katika uzalishaji<br />

wa kile ambacho ni kipaji chake cha asili.<br />

Katika ngazi ya uzalishaji, muhusika anatarajiwa kuwa<br />

amefikia umri wa miaka 25 na ataendelea katika nguvu za kuzalisha<br />

mpaka miaka 45.<br />

Hii inaitwa ngazi ya uzalishaji kwa sababu ndio wakati<br />

kwa mwenye kipaji anapokuwa amewekeza nguvu zake katika<br />

vipaumbele vya mambo ambayo alikwisha kuyajaribu yakaonesha<br />

mafanikio, au yakadhihirisha uwezo alio nao wa kufikia viwango<br />

vyake vya ubora. Na ndio wakati ambapo kipaji chake kinaanza<br />

kumpatia mhusika matunda au malipo stahiki. Ndio wakati wa<br />

kufanya mikataba ya malipo au kuendesha huduma za kujitegemea<br />

na kutengeneza ajira kwa wengine.<br />

3. Ngazi Ya Usimamizi<br />

Usimamizi ni ngazi ya tatu katika kukuza na kutendea kazi<br />

<strong>vipaji</strong> vya asili. Usimamizi unaotamkwa hapa ni uzoefu unaofikia<br />

hekima na busara ya kuanza kuweka akiba na kutunza mali na<br />

fedha zilizokwisha kupatikana kutokana na uzalishaji mzito<br />

uliotangulia katika ile hatua ya pili.<br />

Umri wenyewe ambao ni kuanzia miaka 45 hadi kufikia<br />

miaka 55 ndipo akili za wenye <strong>vipaji</strong> hupata msukumo wa kutunza<br />

kile kinachozalishwa kupitia <strong>vipaji</strong> na taaluma zao huku wakihisi<br />

nguvu za mwili zinaanza kupungua.<br />

44


Aidha, hii ndiyo hatua ambayo wenye <strong>vipaji</strong> wenye hekima<br />

wanapoanza kupunguza majukumu na kukaimisha au kunaibisha<br />

kwa wale wanaotarajia kuwarithisha majukumu ya kiuchumi na<br />

kiuongozi.<br />

Na ndio wakati huu ambapo kizazi kipya cha umri wa miaka<br />

25 kinapojaribiwa katika kubeba baadhi ya majukumu ili kunoa<br />

<strong>vipaji</strong> vyao vya asili katika uzalishaji na uongozi pia.<br />

Mwasisi aliyekuwa ndiye Mtendaji Mkuu wa kampuni<br />

au taasisi ya huduma hupunguza majukumu na kuyagawa kwa<br />

walioko chini yake ambao anawaandaa kushika hatamu badala<br />

yake.<br />

Lile neno “kutiisha” katika Biblia kwa kiingereza linaitwa<br />

“replenish” likimaanisha kujaza tena, au kuziba utupu uliokuwepo<br />

mahali. Katika usimamizi wa <strong>vipaji</strong>, kutiisha ni kuongeza nguvu<br />

mahali ambapo nguvu zilianza kupungua katika uzalishaji. Ni<br />

kuongeza nguvu katika usimamizi wa vilivyokwisha kuzalishwa ili<br />

vidumu na kuendelea kusaidia kizazi kinachoinukia.<br />

4. Ngazi Ya Urithishaji<br />

Urithishaji ndio hatua ya nne na ya mwisho katika kukuza<br />

na kutendea kazi <strong>vipaji</strong> vya asili. Nitaelezea kwa kina kipengele<br />

hiki katika Sura ya Nne kwa sababu kinawahusu zaidi warithishaji<br />

kuliko warithishwaji.<br />

Hata hivyo, kwa muktadha wa hatua za ukuaji na utendaji<br />

wa <strong>vipaji</strong> vya asili, hatua hii ndiyo ya juu na mwisho kwa wote<br />

wenye umri kuanzia miaka 55-65. Hiki ndicho kizazi kinachotakiwa<br />

kustaafu na kukabidhi majukumu ya uzalishaji na uongozi kwa<br />

kizazi kipya.<br />

Lakini ni muhimu kutambua kuwa kukabidhi sio kususa au<br />

kukimbia majukumu ghafla, eti kwa sababu ya uzee. Kukabidhi<br />

45


lazima kuwe ni mchakato wa taratibu na wenye kukabidhi<br />

wanabaki kutoa ushauri elekezi kwa waliowarithisha.<br />

46


SURA TA TATU<br />

CHANGAMOTO ZINAZOATHIRI VIPAJI<br />

VYA ASILI<br />

Utangulizi<br />

Baada ya kujifunza utajiri mkubwa uliomo katika <strong>vipaji</strong><br />

vya asili na michakato ya kuvikuza, maswali makubwa yanakuja<br />

akilini na kuhoji kama kweli kila binadamu huzaliwa na kipaji cha<br />

kumwinua na kumfanikisha kwa viwango vya ubora wa hali ya<br />

juu, je, kwanini sasa hatuvioni <strong>vipaji</strong> hivi vikifanya kazi kwa kila<br />

mtu katika jamii? Kwanini ni watu wachache sana ambao ndio<br />

wanatokea kuwa maarufu kupitia <strong>vipaji</strong> vya asili?<br />

Katika kusaidia kupatikana kwa majibu ya maswali haya<br />

na mengine yenye kufanana na haya, ndiyo maana sura hii<br />

imeandaliwa ili kufanya uchambuzi makini kuhusu changamoto<br />

zenye kuathiri <strong>vipaji</strong> vya asili, tukianza na kipengele cha vikwazo<br />

vya maendeleo ya <strong>vipaji</strong> na karama.<br />

Changamoto maana yake ni mambo yanayojitokeza<br />

kinyume na maendeleo ya mtu. Hata hivyo, changamoto ni<br />

sehemu ya maisha ya kila mtu na ndiyo maana maisha hutafsiriwa<br />

kuwa ni “mapambano” dhidi ya “changamoto”.<br />

Sasa tunapokuja katika suala la <strong>vipaji</strong>, napo zipo changamoto<br />

ambazo kusudi lake kama sio kuharibu kabisa, basi ni kudhoofisha<br />

utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya wahusika. Kwa hiyo ndiyo maana ni<br />

vema kuzifahamu, na kisha kupata mbinu za kupambana nazo<br />

kikamilifu. Changamoto zenyewe zimegawanyika katika sehemu<br />

kuu mbili.<br />

47


Sehemu ya kwanza ni “changamoto za nje” kwa maana<br />

ya mambo hasi yanayomzunguka kila mtu ili kudhoofisha kipaji<br />

chake. Pili, ni “changamoto za ndani” ambazo ni mambo hasi<br />

ya ndani yanayomwathiri kila mtu binafsi kitabia. Hebu tuanze<br />

kuchambua baadhi ya hizo changamoto za nje.<br />

Changamoto Za Nje<br />

Katika ulimwengu tunamoishi tumezungukwa na mambo hasi<br />

mengi yaliyoko kinyume nasi ambayo ni lazima tupambane<br />

nayo ikiwa kweli tunataka kuendeleza <strong>vipaji</strong> vyetu kama Mungu<br />

alivyotukusudia. Baadhi ya mambo hayo ni pamoja na:<br />

1. Marafiki Wabaya<br />

Binadamu ameumbwa na hulka ya ushirika na binadamu<br />

wengine. Katika hulka hizo, kuna binadamu wanakuwa na ushirika<br />

wa karibu zaidi kuliko binadamu wengine. Na ndipo msamiati wa<br />

neno urafiki unapoanzia. Katika harakati za kutambua na kukuza<br />

<strong>vipaji</strong> mbali mbali lazima kuwepo kwa ushirikiano na watu wengine<br />

hususan wenye <strong>vipaji</strong> vinavyoshabihiana. Ni katika harakati za<br />

kutafuta kukuza na kutumia kukuza <strong>vipaji</strong> ndipo mtu hujenga<br />

ukaribu na watu wapya ambao huwa marafiki.<br />

Tafsiri Ya Marafiki Wabaya<br />

Tafsiri ya msamiati wa neno rafiki maana yake ni “mtu<br />

anayependana na kuaminiana na mwingine; sahibu, mwandani,<br />

bui, somo, na mbasi.” Maneno muhimu ya tafsiri ya urafiki ni<br />

“kupendana” na “kuaminiana.”<br />

Lakini kwa muktadha wa kipengele hiki, ni muhimu<br />

kufahamu kuna “marafiki wema” na “marafiki wabaya.” Kuwa na<br />

marafiki wabaya maana yake ni “kupendana na kuaminiana na<br />

marafiki wabaya”<br />

48


Aina Za Marafiki Wabaya<br />

Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, “marafiki wabaya”<br />

wamegawanyika katika makundi mbali mbali ambayo ni kama<br />

haya yafuatayo:<br />

“Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki;<br />

wala hakusimama katika njia ya wakosaji; wala hakuketi barazani<br />

pa wenye mizaha. Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na<br />

sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti<br />

uliopandwa kandokando ya vijito vya maji, uzaao matunda yake kwa<br />

majira yake, wala jani lake halikauki; na kila alitendalo litafanikiwa.<br />

Sivyo walivyo wasio haki; hao ni kama makapi yapeperushwayo<br />

na upepo. Kwa hiyo, wasio haki hawatasimama hukumuni, wala<br />

wakosaji katika kusanyiko la wenye haki. Kwa kuwa BWANA<br />

anaijua njia ya wenye haki, bali njia ya wasio haki itapotea.” (Zab.<br />

1:3-6)<br />

Katika maandiko haya tunasoma kuhusu “shauri la wasio<br />

haki”, “njia ya wakosaji” na “baraza la wenye mizaha”. Kupitia<br />

maneno haya ndipo tunayapata makundi ya aina tatu ya “marafiki<br />

wabaya”.<br />

Kundi la kwanza la marafiki wabaya ni “wasio haki” ambao<br />

tafsiri yake ni “watu waovu au wahalifu”. Na maana ya “kutokwenda<br />

katika shauri la wasio haki” maana yake ni kutokupokea na<br />

kutendea kazi “ushauri wa waovu au wahalifu.”<br />

Kundi la pili la “marafiki wabaya” ni “wakosaji” ambao<br />

tafsiri yake ni watu “watenda dhambi” au “wasio na maadili ya<br />

kimungu”. Makatazo ya “kutokusimama katika njia ya wakosaji”<br />

tafsiri yake ni “kujitenga na vitendo vya dhambi za hao “watenda<br />

dhambi”.<br />

Kundi la tatu la “marafiki wabaya” ni la watu “wenye<br />

mizaha” ambao maana yake ni “watu wenye maneno ya dhihaka,<br />

49


kejeli, na dharau, dhidi ya itikadi za watu wengine”. Maandiko<br />

yanamkataza mchaji Mungu kutojumuika na makundi ya watu<br />

wenye “kudhihaki” na “kukejeli” itikadi za wengine.<br />

Athari Za Marafiki Wabaya<br />

Muktadha wa “marafiki wabaya” unalenga watu wenye<br />

tabia mbaya wanapokuwa na ushawishi wa kuvutia kwa “watu<br />

wema” hata wakajenga urafiki baina yao. Biblia ndiyo imeandika<br />

habari za kutahadharisha “watu wema” kujihadhari katika kujenga<br />

ushirika wa kirafiki na watu wabaya ambao huathiri vibaya tabia<br />

njema:<br />

“Msidanganyike; mazungumuzo mabaya huharibu tabia<br />

njema.” (1 Kor. 15:33)<br />

“Do not be deceived: [a] Bad company corrupts good<br />

morals.”<br />

Maandiko haya hapo juu yanashuhudia jinsi ambavyo<br />

marafiki wabaya wanavyoweza kuathiri tabia njema za wachaji<br />

Mungu.<br />

Marafiki wabaya sio tu hauthiri tabia njema za watu wema,<br />

lakini pia huathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya asili vya watu wema.<br />

Pale mtu mwenye kutaka kunoa kipaji chake anaposhirikiana na<br />

marafiki wabaya, urafiki huo husababisha kukwamisha juhudi za<br />

kutumia kipaji chake kwa viwango vyake vya ubora, maana hata<br />

yeye huharibika.<br />

Kutokana na kuwa na marafiki wabaya, kuna <strong>vipaji</strong> vingi<br />

vimeathiriwa kwa sababu ya wahusika nao kuharibika kitabia.<br />

2. Imani za uchawi na ushirikina<br />

Uchawi na ushirikina ni changamoto inayoongoza katika<br />

kudhoofisha utendaji bora wa <strong>vipaji</strong> vya asili. Tafsiri ya ‘uchawi’<br />

50


maana yake ni ufundi wa kutumia dawa au vitabu maalum vya<br />

uganga ili kuleta madhara kwa viumbe; na maana nyingine ni<br />

‘vifaa vinavyotumika katika shughuli za kurogea’.<br />

Utafiti uliofanyika umeonesha dhahiri ya kwamba imani za<br />

uchawi na ushirikina ni kikwazo kikubwa sana kwa maendeleo ya<br />

<strong>vipaji</strong> vya asili. Pamoja na kwamba Biblia imekataza watu kushiriki<br />

katika vitendo vya uchawi na ushirikina, lakini bado vitendo<br />

hivyo vimekuwa vikiongoza katika kuvuta watu wengi wakidhani<br />

wanakwenda kupata nguvu za kunoa <strong>vipaji</strong> kumbe wanajikuta<br />

wanapokea nguvu za kukwamisha na kuharibu <strong>vipaji</strong> vyao. Ndiyo<br />

maana maandiko matakatifu yalikataza na kupiga marufuku<br />

ushiriki wa vitendo vya uchawi na ushirikina kama ilivyoandikwa<br />

hapa chini:<br />

“Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti<br />

yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu<br />

atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,<br />

wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye<br />

pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. Kwa maana mtu<br />

atendaye hayo ni chukizo kwa BWANA; kisha ni kwa sababu ya<br />

hayo BWANA, Mungu wako, anawafukuza mbele yako”(Kumb.<br />

18:10-12)<br />

Ni miaka miwili iliyopita tangu Tanzania ilipotangazwa<br />

kushika nafasi ya kwanza kwa umahiri wa kuamini katika uchawi<br />

kimataifa. Mojawapo ya taasisi zilizoitangaza Tanzania kwamba<br />

imekithiri kwa mambo ya uchawi ni Pew Research lenye makao<br />

yake Washington DC nchini Marekani.<br />

Kwa mujibu wa taarifa zake inasadikiwa kwamba miongoni<br />

mwa nchi 19 za kusini mwa Jangwa la Sahara zilizofanyiwa<br />

utafiti, Tanzania iliongoza kwa kuwa na idadi ya watanzania 93%<br />

wanaoamini katika uchawi na ushirikina.<br />

51


Aidha, inasadikiwa pia ya kuwa vitendo vya uchawi<br />

vinavyoongoza Tanzania ni pamoja na juju, utoaji wa kafara kwa<br />

mizimu kwa ajili ya bahati za kupata vyeo, utajiri na umaarufu<br />

katika michezo na muziki.<br />

Sasa basi, katika mazingira kama haya, tunaweza kuona<br />

jinsi ushirikina na uchawi vinavyodhoofisha <strong>vipaji</strong> vya asili kwa<br />

sababu ya wahusika kutegemea ndumba badala ya kutambua na<br />

kunoa <strong>vipaji</strong> vijiendeshe vyenyewe.<br />

3. Mifumo Butu Ya Elimu<br />

Mifumo butu ya elimu ni “mitaala ya elimu isiyolenga kunoa<br />

<strong>vipaji</strong> vya wanafunzi.” Pamoja na kwamba elimu inayotolewa<br />

kweli inawapatia wanafunzi maarifa ya kawaida ya kujua kusoma<br />

na kuandika pamoja na ujuzi katika masomo mengineyo;<br />

changamoto kubwa ni pale ambapo wahitimu wengi hawana<br />

uwezo wa kujitegemea kiuchumi pasipo fursa ya ajira.<br />

Wakati kipaji kinamjengea mtoto uwezo wa kubuni na<br />

ustadi wa kazi atakayoimiliki mwenyewe; elimu bado ni butu<br />

kwa kuwa haimwezeshi mtoto kutambua na kunoa kipaji chake<br />

ambacho akihitimu kitamwezesha kujitegemea moja kwa moja.<br />

Elimu ya sasa inamfanya mwanafunzi akihitimu awazie<br />

kutafuta ajira peke yake, badala ya kubuni na kusimamia kazi<br />

yake mwenyewe. Ndiyo maana changamoto ya ukosefu wa ajira<br />

itaendelea kuwepo kwa muda mrefu kwa sababu uzalishaji wa<br />

wahitimu hauendani na fursa za ajira zilizopo katika jamii.<br />

Ufumbuzi kamili wa tatizo la ukosefu wa ajira ni lazima<br />

uanzie kwenye mitaala ya elimu ambayo italenga kuibua na kunoa<br />

<strong>vipaji</strong> vya watoto ili wanapohitimu wanakuwa na ujuzi kubuni kazi<br />

zao wenyewe na kujitegemea kiuchumi badala ya kutegemea<br />

ajira.<br />

52


Athari Za Utandawazi Dhidi Ya Vipaji Vya Asili<br />

Tafsiri Ya Utandawazi<br />

“Mfumo wa uhusiano wa kimataifa katika nyanja mbali mbali<br />

kama vile biashara, uchumi au siasa uliowezeshwa na maendeleo<br />

ya teknolojia ya habari yanayofanya mataifa kuwasiliana kwa<br />

urahisi.” (Kamusi Ya Kiswahili Sanifu).<br />

Nguvu Za Mitandao Ya Kijamii<br />

Miaka ya hivi karibu, mitandao ya kijamii imekuwa na<br />

ushawishi mkubwa kiulimwengu kwa kiasi ambacho kasi yake ni<br />

tishio kwa maadili ya kizazi kipya. Katika mwaka 2017 kiwango<br />

cha ushawishi wa mitandao ya kijamii kimepanda kwa viwango<br />

vifuatavyo:<br />

• Facebook hivi sasa ina watumiaji zaidi ya milioni 900<br />

• 50% ya ulimwengu mzima iko chini ya umri wa miaka 50<br />

• 96% ya umri kuanzia miaka 18-35 wako ni watumiaji wa<br />

mitandao ya kijamii<br />

• Kama facebook ingekuwa ni nchi, ingeshika nafasi ya tatu kwa<br />

ukubwa ulimwenguni<br />

• Mtumiaji wa kawaida wa facebook ana marafiki 130<br />

• Youtube ni ya pili kwa mtandao mkubwa ulimwenguni<br />

• Twitter nayo immeshafikia watumiani milioni 500<br />

• Kama Twitter ingelikuwa ni nchi ingekuwa ya 12 kwa ukubwa<br />

duniani. Kuna watu 750 wanao-twiti kila nukta.<br />

• Kuna wenye kurasa (blogs) zaidi ya milioni 200<br />

• Kuna kurasa mpya mlioni 3 zinazofunguliwa kwenye internet<br />

kila mwezi<br />

• Kuna picha milioni 5 zinazorushwa kwenye instagram kila siku<br />

• Watu zaidi ya bilioni 6.9 wamekwisha kutazama Youtube<br />

channel<br />

53


Matokeo Chanya Ya Matumizi Ya Mitandao Ya Kijamii<br />

Kama ilivyo kawaida ya vuguvugu jipya linaloibuka katika<br />

jamii linakuwa na matokeo ya aina zote mbili. Kuna matokeo<br />

chanya na pia kuna matokeo hasi. Hebu tuangalie matokeo<br />

chanya ya matumizi ya mitandao ya kijamii:<br />

• Husaidia kujenga mitandao ya kibiashara na huduma za<br />

kijamii. Matangazo ya biashara kupitia redio, televisheni na<br />

magazeti yana gharama kubwa. Lakini kupitia mitandao ya<br />

kijamii matangazo yanawafikia wateja wengi kwa gharama<br />

nafuu sana na wakati mwingine bure.<br />

• Mitandao ya kijamii imetoa fursa kwa wenye <strong>vipaji</strong> na taaluma<br />

mbali mbali kuwasiliana na kupeana taarifa na wateja wao<br />

kuliko ilivyokuwa huko nyuma.<br />

• Mitandao ya kijamii imeondoa vikwavyo vya mawasiliano ya<br />

moja kwa moja. Wanafunzi wanawasiliana na wataalamu na<br />

kubadilisha taarifa muhimu.<br />

• Mitandao ya kijamii imeunganisha watu kimawasiliano na<br />

kuwezeshana katika kutimiza malengo kuanzia ngazi ya<br />

kifamilia, kitaifa na kimataifa (dunia nzima imekuwa kijiji<br />

kimoja).<br />

• Kuna soko pana zaidi. Unaweza kuuza bidhaa nyingi zaidi na<br />

kupata faida, na hata kutengeneza ajira.<br />

• Walaji nao hunufaika. Ushindani hufanya bidhaa kuwa na bei<br />

za chini, na upatikanaji haraka wa bidhaa mpya.<br />

Matokeo Hasi Ya Matumizi Ya Mitandao Ya Kijamii<br />

• Inashika Nafsi Kama Ulevi Sugu.<br />

• Kutumia muda mwingi zaidi kwenye mitandao ya kijamii na<br />

kushindwa kufanya mambo mengine yenye tija.<br />

• Inadhoofisha Mahusiano Ya Ana Kwa Ana<br />

• Inadhoofisha motisha wa kuhusiana na watu moja kwa moja,<br />

na hasa kwa vijana na wanafunzi.<br />

• Wanakuwa tegemezi kwenye teknolojia na internet zaidi kuliko<br />

54


kujifunza kwa akili ili kupata ujuzi wa maisha ya kila siku.<br />

• Jumbe Za Vitisho Na Udhalilishaji (Cyberbullying)<br />

• Shirika moja lijulikanalo kama Enough is Enough, lilifanya utafiti<br />

na kugundua kwamba 95% vijana wanaotumia mitandao ya<br />

kijamii wameshuhudia mawasiliano ya vitisho na udhalilisha na<br />

33% yao ni waathirika wa mawasliano hayo<br />

• Watoto Huathirika Vibaya Zaidi Na Mitandao Ya Kijamii<br />

Wasipodhibitiwa<br />

• Hii ni kwa sababu kwenye mitandao hii zinarushwa picha<br />

mbaya za ugomvi na picha za uchi ambazo huwaathiri<br />

kisaikolojia watoto na vijana. Baadaye husababisha watoto na<br />

vijana kujihusisha na vitendo vya uhalifu na ngono haramu.<br />

• Kichocheo Cha Mkengeuko Wa Maadili Mema<br />

• Maambukizi ya mkengeuko wa maadili ya kimaani na<br />

kiutamaduni kwa sababu ya mwingiliano wa walioharibika<br />

kitabia, waliojaa tamaa ya kupata faida kubwa bila kujali<br />

maadili mema katika nchi husika.<br />

Changamoto Za Ndani<br />

Katika utangulizi wa sehemu hii tumepata tafsiri kuhusu<br />

changamoto za ndani kuwa ni mambo hasi ya ndani yanayomwathiri<br />

kila mtu binafsi kitabia. Katika uchambuzi wa changamoto za<br />

ndani tunakwenda kutumia msamiati mpya ambao unaitwa “tabia<br />

sugu”. Msamiati huu unalenga kuchambua tabia sugu zenye<br />

kuathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya mhusika.<br />

Tafsiri Ya Misamiati Ya Tabia Sugu<br />

Sasa tumefikia kipengele ambacho hasa ndio kikwazo<br />

sugu chenye kuathiri <strong>vipaji</strong> vya asili katika jamii. Labda nianze na<br />

uchambuzi wa misamiati. Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili<br />

Sanifu, neno “tabia” limetafsiriwa kuwa ni: “mazoea yatokanayo<br />

na kurudiarudia hali, mwenendo au matendo”<br />

55


Kamusi ya Kiswahili Sanifu imelitafsiri neno “sugu”<br />

kuwa ni “hali isiyoweza kuondolewa kwa urahisi”. Usemi “tabia<br />

sugu” haumo katika kamusi kama msamiati; isipokuwa mimi<br />

nimeyaunganisha maneno mawili, “tabia” na “sugu” na kupata<br />

usemi maalum wa “tabia sugu”.<br />

Kwa hiyo kama ukiunganisha tafsiri za maneno “tabia” na<br />

“sugu” unapata maana ya usemi wetu wa “tabia sugu”ambao tafsiri<br />

yake ni: “mazoea yatokanayo na kurudiarudia hali, mwenendo au<br />

matendo isiyoweza kuondolewa kwa urahisi”.<br />

Maeneo Ya Uharibifu Wa Tabia Sugu<br />

Uharibifu Wa Kitabia<br />

Sehemu ya kwanza ya madhara ya tabia sugu ni uharibifu<br />

wa kitabia unaolenga kuharibu “utu”, “ubinadamu” na “uungwana”<br />

katika maisha ya mwathirika. Pengine ni vizuri tukaangalia<br />

misamiati ya maneno haya ya “utu”, “ubinadamu” na “uungwana”<br />

ili tujue maana zake:<br />

Neno “utu” limetafsiriwa kuwa ni: “hali ya kuwa na tabia<br />

zinazolingana na hadhi ya mtu”. Neno “ubindamu” limetafsiriwa<br />

kuwa ni: “hali ya utambuzi wa jinsi ya kutekeleza wajibu juu ya<br />

maisha katika jamii”. Neno “uungwana” limetafsiriwa kuwa ni:<br />

“mtu mwenye adabu na tabia zinazokubalika katika jamii”.<br />

Baada ya kupata tafsiri ya misamiati hapo juu tunaweza<br />

kuona kwamba madhara mabaya ya “tabia sugu” kwa mhusika<br />

ni: kumharibia (utu); ambao ni hadhi yake kama mtu; kumharibia<br />

(ubinadamu wake) ambao ni hali ya utambuzi wa kutekeleza<br />

wajibu wake kwa jamii; kumharibia (uungwana) ambao ni<br />

adabu na kumfanya kutokukubalika kitabia katika jamii. Haya<br />

ndiyo madhara ya “tabia sugu” ambayo kimsingi, ndiyo yenye<br />

kukwamisha utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya walio navyo, na kukwama<br />

kufikia viwango vya mafanikio kulinganana <strong>vipaji</strong> vyao.<br />

56


Hata hivyo, ashukuriwe Mungu kupitia Bwana Yesu Kristo<br />

ambaye kwa neema yake ametoa ufumbuzi wa kupambana na<br />

kukomesha madhara ya tabia sugu, ikiwa masharti na kanuni<br />

zitazingatiwa:<br />

“Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani,<br />

ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa TABIA YA UUNGU<br />

mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa” (1<br />

Pet. 1:4)<br />

Mungu ameahidi, kupitia Yesu Kristo, waathirika wa tabia<br />

sugu, wanaweza kubadilika, na kunusurika na uharibifu wa dunia<br />

hii unaosababishwa na tamaa na kwa kubadilika kitabia na kuwa<br />

wachaji Mungu na raia wema katika jamii.<br />

Uharibifu Wa Kiafya<br />

Kudhoofisha mishipa inayosafirisha damu moyoni, uharibu<br />

wa mfumo wa neva, ambao huanzia katika kudhoofisha uwezo<br />

wa kufikiri na hatimaye kuishia kuwa zezeta; saratani ya damu;<br />

shinikizo la damu na maradhi ya moyo; maradhi ya mtoto wa<br />

jicho; saratani ya mlango wa kizazi; saratani ya figo; saratani ya<br />

kongosho; saratani ya tumbo; maradhi ya uasherati na zinaa na<br />

VVU/UKIMWI.<br />

Uharibifu Wa Kifamilia<br />

Uharibifu wa kifamilia utokanao na tabia sugu ni pamoja<br />

na: Migororo sugu katika ndoa; ugumba na utasa (utoaji mimba/<br />

madawa ya kuzuia mimba); wanandoa kutelekezana/kuvunjika<br />

kwa ndoa; malezi mabovu kwa watoto; ongezeko la watoto wa<br />

mitaani.<br />

57


Uharibifu Wa Kiuchumi<br />

Uharibifu wa kiuchumi utokanao na tabia sugu ni pamoja<br />

na: Ufukara katika familia; udhaifu katika ubunifu wa mipango<br />

endelevu ya kiuchumi; rasilimali asilia kuwanufaisha wageni badala<br />

ya wenyeji; uharibifu wa mazingira; wenyeji kuwa watumwa wa<br />

wageni katika nchi yao wenyewe.<br />

Aina 5 Za Tabia Sugu Zenye Kuharibu Vipaji<br />

1. Tabia Ya Kunung’unika Na Kuhukumu<br />

Kunung’unika ni hali ya “kusema kwa sauti ya chini, aghalabu<br />

peke yako; kusema kwa kulalamika kwa sababu yakutokuridhika<br />

na jambo.”<br />

Kuhukumu ni hali ya “kuhesabia wengine makosa pasipo<br />

ushahidi” “kusema makosa ya wengine pasipo ridhaa yao na kwa<br />

nia ya kuwadhalilisha”.<br />

Mtu mlalamishi na mgung’unikaji na mwenye kuhukumu<br />

wengine huwa ni mwathirika wa mtazamo hasi dhidi ya wengine.<br />

Ni mtu aliyejawa na mawazo mabaya ya kutafuta makosa ili apate<br />

kukosoa na kuhukumu kwa nia ya kuona wahusika wanapatwa na<br />

mabaya kama adhabu ya makosa yao.<br />

Je, Unapenda kukosoa na kutoa lawama dhidi ya wengine?<br />

Unasukumwa kutafuta makosa katika kila jambo au kwa kila mtu?<br />

Huwa unaona ugumu au uzito wa kuona jambo jema pasipo kuona<br />

makosa? Unajiona huru kukosoa na kulaumu wengine hadharani<br />

pasipo kujali hisia zao wala heshima zao? Kama majibu ya maswali<br />

haya kwako ni “ndiyo” maana yake wewe ni mwathirika wa fikra<br />

na mtazamo hasi wa kulaumu na kuhukumu wengine.<br />

58


Angalizo<br />

Si kila kukosoa ni mtazamo hasi. Wala kuona makosa<br />

na kuyasema kwa nia ya kusahihisha sio vibaya. Muktadha<br />

wa kipengele hiki ni kwa wale walioathiriwa na “tabia sugu ya<br />

kulalamika na kuhukumu wengine”.<br />

Mtu ambaye hajaathiriwa na tabia sugu ya kulalamika<br />

na kuhukumu wengine anapoona makosa huchukua hatua za<br />

kumwendea mkosaji na kumwelimisha kwa nia njema na lugha<br />

ya upole, tena baada ya kumsikiliza kwanza na kupata uhakika<br />

kutoka kwa muhusika.<br />

Lakini mwathirika wa tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu<br />

wengine, hata kama analalamikia mambo ya kweli, huwa hatumii<br />

njia ya kuelimisha bali lugha ya kudhalilisha hadharani kwa kuanika<br />

makosa ya wengine. Tatizo huwa sio “kuona makosa” bali “njia ya<br />

kushughukilia makosa yenyewe”<br />

Mtu ambaye ni mwathirika wa “tabia sugu ya kulalamika<br />

na kuhukumu wengine” anaweza hata kujitetea ya kwamba ana<br />

mzigo wa kuwasaidia wale anaowakosoa wajirekebishe; lakini<br />

lugha inayotumika katika kukosoa ni ya kuudhi, kuumiza hisia,<br />

kudhalilisha, na kuwavunjia heshima wengine hadharani, wale<br />

anaodai kuwakosoa.<br />

Dalili Kuu Za Tabia Ya Kulalamika Na Kuhukumu Wengine<br />

Ulalamishi<br />

Mlalamishi ni mtu mwenye hulka ya kutokuridhika<br />

na mambo ya wengine. Hata pale mambo yakifanyika vizuri<br />

walalamishi hawana shukrani wala pongezi kwa wengine. Lakini<br />

likitokea dosari au udhaifu wao wataukomalia huo utafikiri hakuna<br />

jambo jema kwa wale wanaolalamikiwa.<br />

59


“Ndugu msinung’unukiane, msije mkahukumiwa. Angalieni,<br />

mwamuzi amesimama mlangoni.” (Yak. 5:9)<br />

“Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala<br />

mashindano, mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama,<br />

wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi<br />

kilichopotoka’ ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga<br />

katika ulimwengu.” (Flp. 2:14-15)<br />

Tabia ya kuhukumu wengine<br />

Mwenye lawama za hukumu ni mtu aliyeathiriwa na<br />

mtazamo hasi wa kuhukumu wengine kwa dhana pasipo ushahidi<br />

kamili. Mwepesi wa kulaumu bila hata kusikia upande wa pili<br />

unasemaje kuhusu jambo husika. Hujiamini sana kwamba ana<br />

ujuzi wa kugundua makosa ya wengine lakini yeye mwenyewe<br />

haoni makosa yake mwenyewe.<br />

“Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona<br />

huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.” (Yak. 2:13)<br />

Usengenyaji<br />

Msengenyaji ni yule mwenye kufunua mambo binafsi ya siri<br />

za wengine kwa nia ya kuwadhalilisha na kuwavunjia heshima zao<br />

mbele za wengine. Msengenyaji hujifanya kuwa na taarifa nyeti za<br />

mambo ya watu lakini mwenyewe hayuko tayari kujulikana kama<br />

ndiye chanzo cha taarifa hizo.<br />

“Tena pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizungukazunguka<br />

nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni<br />

wachongezi na wadadisi wakinena maneno yasiyowapasa.”<br />

(1 Tim. 5:13)<br />

60


Udhalilishaji<br />

Mdhalilishaji ni mtu anayezua mambo ya uongo kwa nia ya<br />

kuharibu heshima na hadhi za wengine hadharani. Mdhalilishaji<br />

huzalisha kashfa ili kuharibu maisha ya wengine.<br />

“Basi wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na<br />

husuda na masingizio yote.” (1 Pet. 2:1)<br />

Madhara Ya Kulalamika Na Kuhukumu Wengine<br />

Hudhoofisha Ubunifu Wa Kipaji<br />

Mwathirika wa mtazamo hasi wa kulalamika na kuhukumu<br />

hukiathiri kipaji chake cha asili kwa kudhoofisha uwezo wake wa<br />

asili wa kubuni mambo mapya. Kumbuka ya kwamba utendaji wa<br />

kipaji unategemea nguvu za ubunifu wa mambo mapya. Na nguvu<br />

za ubunifu hutokana na mawazo chanya.<br />

Kimaumbile “mawazo hasi” hayawezi kutenda kazi kwa<br />

wakati mmoja na “mawazo chanya”. Kila kimoja kinafanya kazi<br />

kwa wakati wake kinapokuwa kimepewa nafasi ya kwanza. Kwa<br />

hiyo, “mawazo hasi” huamsha “hisia hasi” ambazo huwa kikwazo<br />

cha utendaji wa mawazo chanya. Wakati mwathirika wa mtazamo<br />

hasi hutumia mawazo hasi na kughubikwa na hisia hasi; hali hiyo<br />

huzuia upande wa pili wa mawazo chanya na hisia chanya kufanya<br />

kazi kwa wakati mmoja.<br />

Changamoto iliyopo hapa ni kwamba, muda wote ambapo<br />

mawazo hasi, na hisia hasi vinatenda kazi ndani ya mwathirika,<br />

kipaji chake kinakuwa kimefungiwa ule uwezo wake wa kutenda<br />

kazi yenye tija kwa muhusika. Kwa hiyo, muda mwingi unaopotea<br />

kwenye kulalamika na kuhukumu wengine, mambo yake<br />

mwenyewe husimama au kukwama.<br />

61


Huharibu Mahusiano Na Wengine<br />

Mara nyingi, mwathirika wa “tabia sugu ya kulalamika na<br />

kuhukumu wengine” huwa hana marafiki wengi. Na hata akiwapata<br />

hawadumu pamoja naye kwa muda mrefu. Hata wale wachache<br />

anaobaki nao hugombana nao mara kwa mara. Tena baadhi ya<br />

hao marafiki wachache nao pia huwa ni waathirika wa tabia sugu<br />

hiyo hiyo ya kulalamika na kuhukumu wengine kama yeye.<br />

Katika mazingira ya kuwa na marafiki wachache, au<br />

kukimbiwa na marafiki, hali hii husababisha <strong>vipaji</strong> vya mwathirika<br />

kutokuwafikia na kuwahudumia walengwa wa <strong>vipaji</strong> vyake. Maana<br />

mwathirika wa “tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu wengine”<br />

anaweza kuwa na kipaji kizuri sana lakini kimeathiriwa na hulka<br />

yake. Kila anapokitumia kinakuwa kama chakula kitamu lakini<br />

chenye pilipili kupita kiasi. Kila anayekula lazima pua zitalowa kwa<br />

mafua na macho kutoka machozi mengi.<br />

Kwenda Kinyume Na Makatazo Ya Yesu Kristo<br />

Yesu Kristo mwenyewe pamoja na kwamba alikuwa<br />

mkali katika kukosoa mitazamo hasi ya jamii ya Mafarisayo<br />

na Masadukayo; bado alipiga marufuku kwa wanafunzi wake<br />

kuendekeza tabia ya kulalamika na kuhukumu wengine:<br />

“Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi<br />

hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.” (Luk. 6:37)<br />

Makatazo ya Yesu kuhusu tabia ya kulaumu na kuhukumu<br />

kunadhirisha matokeo ya tabia hiyo kuwa inaambatana na<br />

malipizo yake. Unapomlaumu na kumhukumu mtu mwingine na<br />

kumsababishia maumivu pamoja na madhara, maana yake wewe<br />

pia tarajia kupatwa na lawama na hukumu zitakazokusababishia<br />

maumivu na madhara kama ulivyowafanyia wengine. Hii ni kanuni<br />

ya kiroho na inafanya kazi chini ya udhibiti wa Mungu mwenyewe.<br />

62


Kana kwamba hii haikutosha, Yesu alitoa sababu ya msingi<br />

ya kutokulaumu na kuhukumu wengine kwa sababu mwenye<br />

kufanya hivyo kwa wengine pengine ana makosa kama wao au<br />

zaidi ya hao anaowakosoa.<br />

“Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi. Kwa kuwa<br />

hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile<br />

mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa. Basi mbona wakitazama<br />

kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani<br />

ya jicho lako mwenyewe huiangalii. Au utamwambiaje nduguyo,<br />

niache nitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani<br />

ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe itoe kwanza ile boriti<br />

katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile<br />

kibanzi katika jicho la ndugu yako.” (Mat. 7:1-5)<br />

Katika maandiko haya, Yesu anaonesha udhaifu wa tabia<br />

ya kuhukumu wengine pasipo kujitathmini binafsi kama hatuna<br />

makosa yale yale au yenye kufanana na ya wale tunaowahukumu.<br />

Aidha, Yesu anatafsiri kuwa ni unafiki mtupu kuwa na tabia ya<br />

kulalamika na kulaumu wengine wakati mhusika naye ana<br />

madhambi yake mwenyewe.<br />

Na kisha Yesu akaagiza kwamba badala ya kutumia<br />

nguvu kubwa kutuhumu na kuhukumu wengine, tumia fursa hiyo<br />

kujichunguza na kujirekebisha kwanza kisha ndipo utakuwa na<br />

uzoefu wa kukosoa wengine.<br />

Tena kuna mahali pengine ambapo Yesu alitoa mwongozo<br />

pale ambapo kunatokea kutokuelewana au kukoseana ambapo<br />

hatua stahiki ni kukutana wahusika peke yao na kujaribu<br />

kusuluhishana. Na pale inaposhindikana basi kesi hiyo iwasilishwe<br />

kwenye ngazi ya juu, hatua kwa hatua mpaka muafaka upatikane.<br />

63


Tabia Sugu Ya Uvivu<br />

Uvivu ni hali ya “kutokutaka kufanya kazi” au hali ya<br />

“ulegevu katika kazi”, au “utepetevu” na “ulegevu”. Tabia sugu ya<br />

uvivu ni mojawapo ya changamoto zinazokiandama kizazi kipya.<br />

Kuna ushahidi wa kutosha kwamba vijana wengi hawapendi<br />

kufanya kazi za nguvu au wakifanya basi hufanya kwa ulegevu.<br />

Kwa mujibu wa Biblia tunajifunza ya kwamba mtu mvivu mikono<br />

yake hukataa kufanya kazi:<br />

“Matakwa ya mtu mvivu humfisha kwa maana mikono yake<br />

hukataa kufanya kazi.” (Mit. 21:25).<br />

Kwa kifupi, mtu mvivu hukataa kufanya kazi (Mit.12:27);<br />

hataki kulima wakati wa baridi (Mit. 20:4); hupenda sana uzingizi<br />

(Mit. 6:9); huwa na njaa (Mit.19:15); kazi yake ni kuomba omba<br />

misaada (Mit.20:4).<br />

Kwa dalili hizi, kazi ya kunoa kipaji nayo ni ngumu kwa<br />

mwathirika wa tabia sugu ya uvivu. Mojawapo ya sifa ya utendaji<br />

wa kipaji ni kufanya kazi kwa ustadi na viwango vya ubora.<br />

Mwathirika wa uvivu sio kwamba hawezi bali pia hataki kutoka<br />

jasho. Anataka mafanikio ya haraka bila jasho.<br />

Madhara Ya Tabia Sugu Ya Uvivu<br />

Umaskini Wa Kipato<br />

Madhara makubwa yampatayo mwathirika wa tabia sugu<br />

ya uvivu ni umaskini wa kipato. Tumekwisha kuthibitisha ukweli<br />

huu kupitia maandiko matakatifu na baadhi yake ni haya yafuatayo:<br />

“Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini; bali<br />

mkono wake aliye na bidii hutajirisha.” (Mit. 10:4)<br />

64


Maandiko yametuhakikishia kwamba uvivu husababisha<br />

umaskini. Mtu asipofanya kazi kwa makusudi hatapata mapato<br />

na hivyo kuishia kuwa maskini.<br />

Kuwa mzigo kwa wengine<br />

Mwathirika wa tabia sugu ya uvivu kwa kuwa hana kipato,<br />

lakini bado ana mahitaji ya lazima ya kula, kunywa, kuvaa, malazi<br />

na mengine, haya yote huwatwika watu wengine wabebe mzigo<br />

huo.<br />

“Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa<br />

mavuno ataomba, hana kitu.” (Mit. 20:4)<br />

Kwa sababu shida za mvivu haziishi, leo ana shida hii<br />

kesho ana shida ile na asiposaidiwa atalaumu na kulalamika<br />

kana kwamba ni haki yake kusaidiwa wakati si mlemavu. Hii<br />

husababisha kero kwa wale walio karibu naye.<br />

Kupoteza Fursa Matumizi Ya Vipaji<br />

Mwathirika wa tabia ya uvivu hushindwa kutumia kipaji<br />

chake kila anapopewa fursa ya kuzalisha. Yesu alitoa mfano wa<br />

talanta ambapo tajiri aliwapa watumwa wake talanta za kuzalisha.<br />

Mmoja kati yao aliyepewa talanta moja kwa sababu ya uvivu wake<br />

alishindwa kuzalisha lakini akaja na visingizio kama ifuatavyo:<br />

“… Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana,<br />

nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda,<br />

wakusanya usipotawanya; basi nikaogopa, nikaenda nikaificha<br />

talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako. Bwana wake<br />

akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua<br />

ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; basi,<br />

ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija<br />

ningalipata iliyo yangu na faida yake. Basi, mnyang’anyeni talanta<br />

hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. Kwa maana kila mwenye<br />

kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile<br />

65


alicho nacho atanyang’anywa.” (Mat. 25:24-29)<br />

Katika maandiko haya tunasoma maneno haya “… Wewe<br />

mtumwa mbaya na mlegevu.” Unaona? Anatajwa moja kwa<br />

moja ya kuwa kilichomfanya akashindwa kutumia kipaji chake ni<br />

ulegevu wake mwenyewe na madhara yake ni kunyang’anywa<br />

hata hicho alichokuwa nacho.<br />

Tabia Sugu Ya Ulevi Na Madawa Ya Kulevya<br />

Miaka 3,000 iliyopita kabla ya elimu ya sayansi kuwepo,<br />

manabii walitoa maonyo kuhusu matumizi ya pombe wakisema<br />

athari zake ni pamoja na kuharibu fahamu za wanadamu:<br />

“Uzinzi na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu.”<br />

(Hos. 4:11)<br />

Maandiko haya yanathibitisha kwamba pombe ina athari<br />

kubwa kwa kipaji cha binadamu kwa kuwa inadhoofisha uwezo<br />

wa kufikiri. Kwa mantiki hii divai mpya inajumuisha kila kitu<br />

kinacholewesha ikiwemo uvutaji wa bangi; matumizi ya dawa za<br />

kulevya unaojumuisha unga wa kubugia, kunusa, au uchomaji<br />

sindano.<br />

Maandiko matakatifu, kama jina lake lilivyo, yameandika<br />

waziwazi ya kwamba ndani ya pombe mna sumu inayoharibu<br />

tabia ya mtu na kumwondolea ubinadamu wake na kufanya awe<br />

kama hayawani:<br />

“Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali<br />

mjazwe Roho.” (Efe.5:18)<br />

Neno “ufisadi” katika maandiko haya linamaanisha “uchafu<br />

uliokithiri”. Huu si uchafu wa mwili bali vitendo haramu visivyo vya<br />

kimaadili. Ndiyo maana nimeorodhesha ulevi kuwa ni “tabia sugu”<br />

inayoharibu utendaji wa <strong>vipaji</strong> ndani ya binadamu.<br />

66


Madhara Ya Pombe Mwilini<br />

Madhara ya kwanza ya pombe ni kuathiri mfumo wa<br />

ubongo ambao ndio asili ya nguvu ya <strong>vipaji</strong> vya asili. Baadhi ya<br />

athari za pombe katika ubongo ni kama zifuatazo:<br />

• Mishipa ya ubongo kupanuka kupita kawaida.<br />

• Ukosefu wa baadhi ya vitamin katika ubongo (mlevi hali mlo<br />

kamili)<br />

• Ukosefu wa vitamin B unaweza kusababisha matatizo ya akili<br />

katika ubongo<br />

• Kubadilika kitabia, kudhoofika kwa uwezo wa kufikiri, kupoteza<br />

kumbukumbu<br />

Athari kubwa zaidi za pombe katika ubongo ni eneo la<br />

mfumo wa neva. Wakati kisingizio cha matumizi ya pombe huwa<br />

ni kama kitulizo katika mfumo wa neva, badala yale pombe<br />

hutumika katika kuzikandamiza seli za neva katika ubongo kwa<br />

kuzifanya butu na kuuharibu uwezo wake wa kufanya kazi, hali<br />

ambayo hupelekea kusinzia, kuzimia na hata kifo.<br />

Madhara mengine ya pombe kwenye mfumo wa neva ni<br />

pamoja na haya yafuatayo:<br />

• Kudhoofisha uwezo wa kuona<br />

• Kubadilisha utambuzi wa muda na mahali<br />

• Kupoteza uwezo wa kusikia vizuri<br />

• Kupatwa na uzito katika kuitikia mambo<br />

• Kupoteza hisia ya harufu na ladha<br />

Kana kwamba hii haitoshi, madhara ya pombe hayaishii<br />

kuathiri ubongo na mfumo wa neva peke yake. Pombe huathiri<br />

kiungo kingine muhimu cha mwili ambacho ni moyo. Baadhi ya<br />

maeneo ambayo moyo huathiriwa na pombe ni pamoja na haya<br />

yafuatayo:<br />

67


• Moyo huathirika kwa ukosefu wa baadhi ya vitamini.<br />

• Mapigo ya moyo hudhoofika<br />

• Kupanuka kwa moyo<br />

• Ongezeko la shinikizo la damu<br />

• Huzuia uzalishaji wa seli nyekundu na nyeupe za damu<br />

• Hatari za ugonjwa wa moyo na kiharusi<br />

Viungo vingine ambavyo huathiriwa na pombe ni ini ambapo<br />

seli za ini huharibika na kudhoofisha utendaji wa ini (Cirrhosis).<br />

Imebainika ya kwamba theluthi mbili za wagonjwa wa Cirrhosis<br />

Uingereza husababishwa na pombe.<br />

Pombe pi huathiri tumbo kwa kusababisha maumivu na<br />

vidonda vya tumbo pamoja na matatizo katika mfumo wa usagaji<br />

chakula. Madhara mengine ya pombe ni dhidi ya ngozi ambapo<br />

mishipa ya damu hupanuka na ngozi kujaa damu nyingi, na pia<br />

pombe husababisha mwili kuwa na joto kubwa na rangi ya ngozi<br />

hubadilika.<br />

Eneo la mwisho lakini lenye athari kubwa zitokanazo na<br />

pombe ni katika mfumo wa uzazi. Pombe husababisha kudhoofika<br />

kwa mfumo wa uzazi katika maeneo yafuatayo:<br />

• Kudhoofika kwa nguvu za kiume<br />

• Kwa wanawake katika ujauzito kizazi huathirika<br />

• Kuzaliwa kwa watoto njiti<br />

• kudhoofisha uwezo wa akili wa mtoto<br />

• Mtoto kurithi tabia ya ulevi<br />

• Viungo vya uzazi kudhoofika na kusababisha ugumba<br />

• Kwa wanawake hatari ya kupata saratani ya matiti<br />

Athari Za Kiuchumi<br />

Pombe haikomei katika kuathiri afya bali husababisha hata athari<br />

za kiuchumi. Kwa mujibu wa maandiko ya Biblia tunaonywa<br />

kuhusu ulafi na ulevi kama ifuatavyo:<br />

68


“Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo; miongoni mwa<br />

walao nyama kwa pupa; kwa maana mlevi na mlafi huingia<br />

umaskini, na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.” (Mit. 23:20-<br />

21)<br />

Baadhi ya athari za kiuchumi zitokanazo na pombe ni kama<br />

hizi zifuatavyo:<br />

• Kudhoofika kwa viwango vya ubunifu wa mipango endelevu<br />

ya kiuchumi<br />

• Kudhoofika kwa uwezo wa kufanya kazi<br />

• Utoro makazini<br />

• Kupoteza ajira<br />

• Kufilisika kibiashara/kimiradi<br />

• Kukumbwa na umaskini wa kujitakia kibinafsi, familia na jamii<br />

kwa jumla<br />

Athari Za Kijamii<br />

• Kudhoofisha uwajibikaji wa mtu kama mwanandoa au kama<br />

mzazi<br />

• Kusababisha ugomvi katika familia<br />

• Kukaa nje ya familia kwa muda mrefu<br />

• Kutelekeza familia na kuwasababishia wasiwasi, mashaka na<br />

msongo wa mawazo<br />

• Kuchochea vitendo vya zinaa ambavyo hueneza maambukizo<br />

ya VVU<br />

• Malezi duni kwa watoto<br />

Tabia Sugu Ya Zinaa<br />

Msamiati wa neno “zinaa” unajumuisha matumizi ya<br />

maneno mawili maarufu kama “uasherati” na “Uzinzi”. Tafsiri<br />

rasmi ya neno uasherati maana yake ni “tendo la kujamiiana<br />

linalofanywa na mtu/watu ambao hawajaoa wala kuolewa kwa<br />

mujibu wa sheria”. Na tafsiri rasmi ya neno uzinzi maana yake<br />

69


ni: “mwanandoa anapojamiiana na mtu/watu wengine nje ya<br />

mwanandoa mwenziwe”.<br />

Kwa mujibu wa maandiko ya Biblia, tendo la ndoa linatakiwa<br />

kufanywa na mwanamume na mwanamke ambao wameamua<br />

kufunga ndoa ili kuishi pamoja kwa maisha yao yote mpaka kifo.<br />

Mtu ambaye hajafunga ndoa halali haruhusiwi kujamiiana mpaka<br />

atakapofikia umri na muda wa kufunga ndoa rasmi.<br />

Mojawapo ya amri kumi maarufu katika Biblia ni pamoja<br />

na “usizini” (Kut. 20:14). Zinaa ni miongoni mwa tabia sugu zenye<br />

kuharibu utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya wanadamu na ndiyo maana<br />

imekatazwa kimaadili.<br />

Madhara Ya Tabia Sugu Ya Zinaa Kimaadili<br />

Mojawapo ya athari za tabia sugu ya zinaa ni “kupungukiwa na<br />

akili”:<br />

“Uzinzi na divai mpya huondoa fahamu za wanadamu.”<br />

(Hosea 4:11)<br />

Biblia inaposema zinaa inaondoa “fahamu za wanadamu”,<br />

maana yake inalenga uharibifu wa kitabia wenye kuathiri utendaji<br />

wa <strong>vipaji</strong> vya asili. Mtu akiisha kujiingiza katika vitendo vya<br />

zinaa, tayari fahamu zake au fikira zake zinaathirika na kupoteza<br />

mwelekeo wa kimaadili na hivyo kudhoofisha utendaji bora wa<br />

<strong>vipaji</strong> vyake. Maandiko mengine yamerejea kusisitiza ya kwamba<br />

mwenye kufanya zinaa tayari ana matatizo ya kiakili:<br />

“Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo<br />

litakalomwangamiza nafsi yake.” (Mit. 6:32)<br />

Hapa tunasoma habari kuhusu zinaa inavyozuzua akili za<br />

mtu mpaka anajiingiza kwenye mazingira ya kuhatarisha uhai<br />

wake lakini hata hajali. Kumbuka wakati huo maandiko haya<br />

70


yalipoandikwa, hukumu ya zinaa ilikuwa ni mtu “kupigwa mawe<br />

mpaka kufa” (Law. 20:10). Kwa hiyo, mtu akiisha kuonja zinaa<br />

humponza kiasi cha kujitoa mhanga kupigwa mawe hadi kufa<br />

kama atafumaniwa.<br />

Kufuatia athari mbaya za kimaadili zinazotokana na<br />

tabia sugu ya zinaa, maandiko yametoa mwongozo wa kila mtu<br />

kujiepusha nayo kwa kadiri iwezekanavyo kama ilivyoandikwa<br />

hapa chini:<br />

“Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje<br />

ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda juu ya mwili wake<br />

mwenyewe.” (1 Kor. 6:18)<br />

Vichocheo Vya Zinaa<br />

Pamoja na makatazo ya vitendo vya zinaa bado<br />

kumekuwepo mmomonyoko wa kimaadili wenye kusababisha<br />

kukithiri kwa vitendo hivyo katika jamii. Baadhi ya vichocheo vya<br />

zinaa ni pamoja na:<br />

• Tamaa za ujanani<br />

• Mila na desturi zisizoheshimu ndoa ya mke na mume mmoja<br />

• Ngoma na miziki inayohamasisha vitendo vya ngono<br />

• Picha za ngono katika magazeti, luninga, video na tovuti<br />

• Mavazi yasiyo ya staha<br />

• Ulevi na madawa ya kulevya<br />

• Umaskini<br />

Athari Za Nyingine Za Tabia Sugu Ya Zinaa<br />

• Zinaa huleta unajisi unaomtenga mtu na Mungu kiroho<br />

• Zinaa huathiri utu kwa kuvunja hadhi ya mtu binafsi<br />

• Zinaa hivunjia taasisi ya ndoa heshima yake mbele za jamii<br />

• Zinaa husababisha kuzaliwa watoto nje ya ndoa na kukosa<br />

malezi bora<br />

71


• Zinaa huharibu akili na uwezo wa kufikiri mambo ya maana<br />

• Zinaa husababisha umaskini kwa matumizi ya anasa zisizo na<br />

udhibiti<br />

• Zinaa husababisha uhasama/chuki/uadui mpaka mauaji<br />

• Zinaa husababisha migogoro na kusambaratisha familia<br />

• Zinaa hueneza maambukizo ya maradhi ya zinaa na VVU<br />

Tabia Sugu Ya Chuki Na Hasira<br />

Tabia ya chuki na hasira imetokea kuwa miongoni mwa<br />

tabia sugu ambazo zinaathiri <strong>vipaji</strong> vya asili kwa sababu waathirika<br />

wengi ni vijana, tena ambao ndio nguvu kazi ya taifa. Kimaumbile<br />

kila binadamu ana “hisia hasi” za chuki na hasira. Lakini hisia<br />

hizi zinatakiwa kudhibitiwa ili kudumisha mahusiano mema ya<br />

kifamilia na kijamii. Pale ambapo mtu anashindwa kudhibiti chuki<br />

na hasira matokeo yake atajikuta amesababisha madhara yenye<br />

kuathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya asili, kwa yeye mwenyewe na kwa<br />

jamii inayomzunguka pia.<br />

Tafsiri Ya Misamiati Ya Chuki Na Hasira.<br />

Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu, neno “chuki”<br />

limetafsiriwa kuwa ni: “ tabia ya kutopenda watu au hali ya kuwa<br />

na roho mbaya, au kinyongo.” Neno hasira limetafsiriwa kuwa ni:<br />

“ ghadhabu au hamaki au fundo.”<br />

Hapa nitoe angalizo ya kwamba, hii “tabia sugu ya chuki<br />

na hasira”, inatofautiana na ile “tabia sugu ya kulalamika na<br />

kuhukumu” ambayo tayari tumejifunza habari zake. Mtu mmoja<br />

anaweza kuwa na tabia sugu zote mbili, lakini sio lazima aliye na<br />

tabia moja kati ya hizi awe na tabia ya pili.<br />

Kuna watu wameathiriwa na “tabia sugu ya chuki na hasira”<br />

lakini hawana hulka ya “tabia sugu ya kulalamika na kuhukumu”<br />

wengine hadharani. Waathirika wa “chuki na hasira” wanaweza<br />

kuchukua hatua kali za kulipa visasi pasipo kupiga kelele hata<br />

kidogo.<br />

72


Wakati huo huo, watu wenye “tabia sugu ya kulalamika<br />

na kuhukumu wengine” huwa ni chanzo kikuu cha kuwachochea<br />

watu walioathiriwa na “tabia sugu ya chuki na hasira” ambao<br />

huhamaki na kutafuta kulipiza visasi dhidi ya mahasimu wao.<br />

Vyanzo Vya Hasira Na Chuki<br />

Hisia hasi za chuki na hasira zina vyanzo viwili tofauti.<br />

Kuna vyanzo vya nje ambavyo ni maumivu ya nafsi yatokanayo<br />

na kunenewa au kutendewa mabaya; au uchungu wa kukosa<br />

huduma na haki stahili kutoka kwenye mamlaka husika.<br />

Chanzo cha pili ambacho ni kutoka ndani kinajumuisha hisia<br />

ya ndani ambayo ni ama aibu ya moyoni itokanayo na kushindwa<br />

au kutokufanikiwa katika jambo mbele za watu, au kusutwa<br />

na dhamiri kwa sababu ya makosa au dhambi zilizofanywa na<br />

hazijasuluhishwa bado.<br />

“BWANA akamwambiaKaini, kwanini una ghadhabu?<br />

Kwanini uso wako umekunjamana?Kama ukitenda vema hutapata<br />

kibali?Usipotenda vema dhambi iko inakuotea mlangoni, nayo<br />

inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.” (Mwa. 4:6-7)<br />

Athari Za Hasira Na Hamaki<br />

Pamoja na kwamba mwenye hasira na chuki anaweza<br />

kujihesabia haki kutokana na sababu anazoziona kuwa ni halali<br />

kwake; pasipo kujitambua kumbe anajisababishia athari yeye<br />

mwenyewe ambazo baadhi yake ni kama hizi zifuatazo:<br />

Kudhoofisha Kazi Za Kimaendeleo<br />

Mwenye chuki na hasira hujikuta hajali muda na kuchelewa<br />

kufika kwenye shughuli za kimaendeleo na kazini kwa sababu<br />

ameshuka moyo wa kufanya kazi. Wengine hujiingiza kwenye<br />

vitendo vya ulevi, kula kupita kiasi, kuwa tegemezi kwa wengine,<br />

73


na ulemavu wa kihisia.<br />

Madhara Ya Kiafya<br />

• Hasira hupandisha mwendo wa moyo kutoka kiasi cha 80<br />

mpaka 180 hata zaidi kwa dakika<br />

• Shinikizo la damu nalo kupanda kutoka 120 kwa 80 kwenda<br />

220 kwa 130 au zaidi<br />

• Kasi ya kupumua huongezeka ili kuingiza hewa safi mwilini<br />

• Mlipuko wa nguvu husababisha kushuka kwa sukari kiasi mtu<br />

huweza hata kutetemeka<br />

• Mwili hutoa kemikali za kugandisha damu kana kwamba kuna<br />

ajali imetokea mwilini hali ambayo mgando wa damu huenda<br />

moyoni au katika ubongo<br />

• Mwenye hasira hukabiliwa na hatari ya mlipuko wa moyo au<br />

ugonjwa wa kiharusi<br />

• Hasira sugu husababisha mfadhaiko na msongo wa mambo<br />

ambavyo hupelekea vidonda vya tumbo<br />

• Hasira sugu hudhoofisha mfumo wa kinga na kusababisha<br />

pumu, maradhi ya ngozi, ugonjwa wa baridi yabisi.<br />

Mchakato Wa Kudhibiti Changamoto Zenye Kudhoofisha<br />

Vipaji<br />

Baada ya kuzipitia baadhi ya changamoto zilizoanishwa<br />

katika sura hii, sasa ni wakati muafaka wa kutafuta kujua mbinu za<br />

kupambana na kuudhibiti huu udhoofishaji wa <strong>vipaji</strong>. Tumezipitia<br />

changamoto za nje ambazo ni marafiki wabaya, imani za uchawi<br />

na ushirikina, mifumo butu ya elimu, na athari za utandawazi<br />

kupitia mitando ya kijamii. Pili, tumepitia changamoto za ndani<br />

kupitia “tabia sugu zenye kuathiri utendaji wa <strong>vipaji</strong> kutokea ndani<br />

ya wahusika.<br />

Suala zima la kudhibiti changamoto hizi haliwezi kuwa<br />

tukio la mara moja tu. Lazima liwe katika mfumo wa kimchakato.<br />

Madhara yaliyopo hayakujitokeza siku moja bali yalichukua muda<br />

74


mrefu. Hali kadhalika na mchakato wa kuyadhibiti kunahitaji<br />

muda ili tuweze kuona matokeo. Hakuna njia ya mkato katika<br />

kurekebisha mambo yaliyojisokota kwa muda mrefu.<br />

Zifuatazo ni ngazi makini za kufanya matengenezo ya<br />

madhara yaliyokwisha kufanyika na mbinu za kujikinga ili athari<br />

zisiendelee kujitokeza tena huko mbeleni:<br />

1. Kumrudia Mungu Muumbaji Wetu<br />

Tumejifunza habari za <strong>vipaji</strong> na karama kwamba ni vitu<br />

vinavyotoka kwa Mungu aliyemwumba binadamu kwa mfano<br />

wake na sura yake. Aidha tumejifunza pia ya kwamba, Mungu<br />

ndiye anayejua kusudi la kuwepo kwako na pia ndiye mwenye<br />

kujua mwanzo na mwisho wa kila binadamu hapa duniani.<br />

Kwa hiyo, tunapotafuta kufanya matengenezo ya kitabia na<br />

kunoa <strong>vipaji</strong> vilivyomo ndani yetu, lazima kwanza tumrudie Mungu<br />

na kujenga uhusiano wa kiroho pamoja naye. Uzuri ni kwamba<br />

sio sisi tunayemrudia Mungu kwa juhudi zetu wenyewe, bali yeye<br />

mwenyewe alikwisha kututafuta na kutuonesha njia ya kumrudia<br />

bila gharama yoyote. Katika kumrudia Mungu tunaanza na hatua<br />

ya kwanza inayojulikana kama toba.<br />

Tafsiri Ya Toba<br />

Biblia imeandika kuhusu toba ikitumia maneno ya<br />

Kiebrania na Kiyunani. Kwa Kiebrania neno lililotumika kuhusu<br />

toba ni nocham. Maana yake ni kuugulia, kuomboleza, kujuta<br />

na kuacha kutenda dhambi na kugeuka na kurejea kwa Mungu.<br />

Kwa Kiyunani neno lililotumika kuhusu toba ni metanoia. Maana<br />

yake ni kubadilia nia na kuachana na kusudi la kuendeleza jambo,<br />

kugeuka nyuma na kurudi ulikotoka.<br />

75


Kwa muktadha wa maneno nocham na metanoia, yote<br />

yanatoa maana ya mtu kujutia hali yake ya dhambi, kuamua<br />

kubadili nia na mtazamo wake kuhusu dhambi zake, na kugeuka<br />

nyuma kisha kurejea katika uhusiano wa kiroho na Mungu.<br />

Watu wengi huchanganya maana ya maneno “toba” na<br />

“ungamo” wakidhani ni kitu kile kile. Ukweli ni kwamba “kutubu” ni<br />

tofauti na “kuungama” tu. Kuungama ni “kukubali na kukiri ukweli<br />

wa makosa yaliyofanywa.” Lakini “kutubu” ni “kujutia na kubadili<br />

nia” kwa “kuachana na mwenendo wa dhambi na kumgeukia<br />

Mungu” ili kuishi maisha tofauti na yaliyopita.<br />

Agizo La Toba<br />

Mungu amekwisha kutoa agizo maalum kwa watu wote<br />

ambao ni waathirika wa tabia sugu zilizotajwa katika sura hii<br />

wapate kutubu kwake kama ilivyoandikwa:<br />

“Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni;<br />

bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu. Kwa<br />

maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki,<br />

kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa<br />

mambo haya kwa kumfufua katika wafu.” (Mdo. 17:30-31)<br />

Maandiko haya yaliandikwa kwa ajili ya kuwataka watu wote<br />

waliokuwa ni waathirika na imani za uchawi na ushirikina pamoja<br />

na tabia sugu wabadili nia zao na kumrudia Mungu Muumbaji wao<br />

na kujiweka salama wasiagukie kwenye maangamizi yaliyokuwa<br />

yakiwakabili.<br />

Mchakato wa kufanya matengenezo dhidi ya madhara ya<br />

changamoto zenye kuathiri <strong>vipaji</strong> na karama unatakiwa kuanza na<br />

toba kwa mujibu wa maandiko tuliyosoma. Uzuri wa maandiko<br />

haya ni kwamba Mungu yuko tayari kuachilia makosa yaliyokwisha<br />

kufanyika kwa kujifanya kama hayajui kwa sababu yalifanyika<br />

kutokana na kutokujua.<br />

76


Faida Za Toba<br />

Kutoka Katika Mitego Ya Ibilisi<br />

Shetani ndiye chimbuko kuu la changamoto zote za nje na<br />

za ndani ambazo zinadhoofisha utendaji wa <strong>vipaji</strong> vya wanadamu.<br />

Kufanya toba ya kweli ndio mlango wa kutoka katika mtego wa<br />

Ibilisi ambao aliutumia kuwanasa wengi katika vifungo vya dhambi<br />

na tabia sugu:<br />

“akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama<br />

ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli; wapate<br />

tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao<br />

wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake.” (2 Tim. 2:25-26)<br />

Maandiko haya yanataja habari za “kupata tena fahamu”<br />

ambazo hapo awali ziliharibiwa na tabia sugu za ulevi na zinaa.<br />

Pili, tunasoma habari za “kutoka katika mtego wa Ibilisi” ambao ni<br />

vishawishi au vitisho vyenye kuwafanya waathirika kuzama katika<br />

maisha ya imani za uchawi na ushirikina.<br />

Katika kufanya toba ya kweli tunasoma kuna kufumbuliwa<br />

macho ya kiroho na kutambua kuwa uko gizani na kuamua<br />

kuigeukia nuru:<br />

“uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na<br />

kuigeukia nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea<br />

Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni<br />

mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.” (Mdo. 26:18)<br />

Maandiko haya yanataja pia habari za “kuziacha nguvu za<br />

shetani” ambazo zinasababishwa na imani za uchawi na ushirika<br />

pamoja na vifungo vya tabia sugu zlizokwisha kutajwa katika sura<br />

hii.<br />

77


Kuzaliwa Upya<br />

Faida ya pili ya kufanya toba ya kweli ni muujiza wa<br />

mabadiliko ya ndani ya kiroho ambayo hufanywa na Mungu<br />

mwenyewe kwa kumtumia Roho wake Mtakatifu:<br />

“si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali<br />

kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa<br />

upya na Roho Mtakatifu” (Tit. 3:5)<br />

Itakumbukwa ya kwamba maana ya tabia sugu ni<br />

“mazoea yatokanayo na kurudiarudia hali isiyoweza kuondolewa<br />

kwa urahisi”. Katika hatua ya kufanya toba, pasipo kutumia<br />

nguvu za kibinadamu za kujibadilisha kitabia, kuna rehema za<br />

Mungu zinazomshukia mwenye kutubu na kuihuisha roho yake<br />

kupata nguvu za mabadiliko ya kiroho. Mabadiliko haya ndiyo<br />

yanajulikana kuwa ni “kuzaliwa kwa pili” na “kufanywa upya” na<br />

Roho Mtakatifu.<br />

2. Kupokea Nguvu Za Kiungu Za Kudhibiti Tabia Sugu<br />

Baada ya kufanya toba ya kweli na kupata mabadiliko ya<br />

ndani ya kiroho; hatua inayofuata ni kupokea nguvu za kiungu<br />

za kudhibiti tabia sugu ambazo ni “mazoea yatokanayo na<br />

kurudiarudia hali isiyoweza kuondolewa kwa urahisi” Maandiko<br />

yafuatayo yanatuthibitishia uhakika wa kudhibiti tabia sugu kama<br />

ifuatavyo:<br />

“Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote<br />

imefunuliwa, nayo yatufundisha kutaa ubaya na tamaa za kidunia;<br />

tupate kuishi kwa kiasi, haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa<br />

sasa.” (Tit. 2:11)<br />

Maandiko hayo hapo juu yanatujulisha jinsi ambavyo<br />

Mungu amekwisha kutoa neema ya kuwaokoa wanadamu wote,<br />

kama wakiamua kutubu kwa dhati na kumrudia yeye. Na neema<br />

78


hii inafanya kazi ya kutufundisha jinsi ya kukataa ubaya na tamaa<br />

za kidunia ambazo zinadhoofisha utendaji wa <strong>vipaji</strong> na karama<br />

ndani yetu. Katika maandiko mengine tunajulishwa kukirimiwa<br />

ahadi kubwa za thamani za kutuwezesha kupokea tabia za uungu<br />

ambazo huweza kudhibiti tabia sugu:<br />

“Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani,<br />

ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washiriki wa tabia ya Uungu,<br />

mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.” (<br />

2 Pet. 1:4)<br />

3. Kuutafuta Kwanza Ufalme Wa Mungu Na Haki Yake<br />

Changamoto kubwa ya binadamu hapa duniani ni kutafuta<br />

maisha kwa kila njia, ziwe halali au haramu. Kipaumbele chake ni<br />

kufanikiwa katika kujipatia na kujilimbikizia mali nyingi. Hata hivyo,<br />

mambo ni tofauti kwa mtu aliyekwisha kumrudia Mungu kwa<br />

njia ya toba. Baada ya kuchukua hatua za kiroho zilizotangulia,<br />

kinachofuata ni kupanga upya vipaumbele vya maisha:<br />

“Msisumbuke, basi, mkisema, tule nini? Au Tunywe nini?<br />

Au tuvae nini? Kwa maana hayo yote mataifa huyatafuta; kwa<br />

sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hao<br />

yote. Bali utafute kwanza ufalme wake na haki yake; na hayo yote<br />

mtazidishiwa.” (Mat.6:32-33)<br />

Maandiko haya yametafsiriwa kinyume na maana yake<br />

kwa nadharia zinazokataza watu kufanya kazi eti badala yake<br />

wategemee sala peke yake kwa kuwa Mungu anajua mahitaji yao.<br />

Dhana ya kutokufanya kazi na kutegemea kuishi kwa miujiza peke<br />

yake sio muktadha wa maandiko haya.<br />

Kile Yesu alichomaanisha hapa ni wanafunzi wake kubadili<br />

mtazamo kuhusu maisha na kuweka upya vipaumbele kwa kigezo<br />

cha kutanguliza ufalme wa Mungu. Yesu hakukataza kufanya kazi,<br />

alitoa mwongozo wa kufanikiwa kupitia vipaumbele na Mungu<br />

79


akiwa ndiye kipaumbele cha kwanza.<br />

Wakati watu wasiomcha Mungu wanaabudu mali za duniani<br />

hii lakini hawana ushirika na Mungu aliyewaumba; wanafunzi<br />

wa Yesu waliagizwa kumtafuta na kumtanguliza Mungu kwanza<br />

katika kutafuta kwao ili kufanikiwa kwao chimbuko lake liwe ni<br />

Mungu badala ya shetani.<br />

Kutafuta kwanza ufalme wa Mungu ni kumtafuta Mungu<br />

akufunulie na kukudhihirishia kusudi lake katika maisha yako.<br />

Na atafanya hivyo kwa kuanza kuibua <strong>vipaji</strong> vyako, na karama za<br />

Roho ili utendaji wako utokane na nguvu alizowekeza ndani yako.<br />

Kuweza kufanikisha zoezi hili unahitaji mshauri wa kiroho<br />

mwenye uzoefu na maisha ya ukuzaji <strong>vipaji</strong> kwa mujibu wa maadili<br />

ya kibibilia.<br />

Lakini, hatua hizi tatu ukizipa uzito unaostahili, tayari<br />

utakuwa umefanikiwa kupata ujuzi na uwezo wa kupambana na<br />

changamoto zenye kudhoofisha <strong>vipaji</strong> na kuzishinda. Inaweza<br />

kuonekana ni ngumu lakini sio kwamba haiwezekani kabisa.<br />

Ni uamuzi wako binafsi kama unataka mabadiliko chanya ya<br />

kutambua na kuchochea <strong>vipaji</strong> vyako.<br />

80


SURA YA NNE<br />

Utangulizi<br />

WAJIBU KWA KIZAZI CHA SASA<br />

KURITHISHA KIZAZI KIPYA<br />

Kitabu hiki hakitakuwa na msaada kwa msomaji kama<br />

hakutakuwepo na uchambuzi makini unaohusu wajibu kwa kizazi<br />

cha sasa, kizazi cha wazee, kutambua wajibu mkuu wa kurithisha<br />

majukumu ya kijamii, kiuchumi na kiuongozi kwa kizazi kipya.<br />

Kizazi kilichopo hivi sasa kimefikia mahali kilipo hivi sasa<br />

kwa sababu kizazi cha zamani, kilichotangulia kiliacha misingi<br />

ambayo kiliirithisha kwa kizazi kinachomaliza muda wake sasa.<br />

Kwa bahati mbaya, nadharia ya uritishaji imeanza<br />

kupoteza umuhimu wake kwa jamii kiasi kwamba kizazi kipya<br />

hakina matumaini wala mwelekeo wa kule kinakojiandaa<br />

kuelekea. Muktadha wa kitabu hiki ni kukihimiza kizazi cha sasa<br />

kinachomaliza muda wake kutimiza wajibu wake wa kurithisha<br />

kizazi kipya majukumu ya msingi kwa mustakabari wa taifa.<br />

Makundi muhimu yenye wajibu wa kusimamia mchakato<br />

wa urithishaji kwa kizazi kipya unaanzia na “wazazi” au “walezi”<br />

katika ngazi ya familia. Ngazi ya familia ndio kitovu cha malezi<br />

kuanzia mtoto anapozaliwa, kukua hadi anapofikia umri wa<br />

kujitegemea kama mtu mzima.<br />

Kundi la pili ambalo linahusika katika wajibu wa kurithisha<br />

kizazi kipya ni kanisa. Natumia msamiati kanisa kwa maana ya<br />

taasisi inayosimamia kueneza na kurithisha maadili ya kiimani<br />

kwa wafuasi wake. Wakati familia ni mlezi mkuu wa maisha ya<br />

81


mtoto kijamii, kanisa ni mlezi mkuu kimaadili. Kundi la tatu lenye<br />

wajibu mkuu katika kurithisha kizazi kipya ni serikali na vyombo<br />

vyake vya dola na taasisi zake za umma.<br />

Katika sura hii tunakwenda kupitia mtiririko wa kihistoria<br />

kuhusu nadharia ya urithishaji, sababu za msingi wa urithishaji,<br />

hatua za urithishaji, vitu muhimu vya kurithisha na visivyofaa<br />

kurithishwa kizazi kipya. Tutapitia pia ukweli kuhusu ukomo wa<br />

umri wa kuishi wa kizazi kilichopo pamoja na ukomo wa nadharia<br />

za uchumi na uongozi. Kisha tutahitimisha na uchambuzi kuhusu<br />

hitaji kuu la viongozi wa kizazi kipya pamoja na mchakato wa<br />

kuandaa uongozi wa kizazi kipya.<br />

Historia Ya Nadharia Ya Urithishaji<br />

Nadharia ya urithishaji yaweza kuonekana kama kitu kipya<br />

kwa baadhi ya watu katika jamii. Kihistoria, nadharia ya urithishaji<br />

chimbuko lake ni taasisi ya ndoa ambayo ni “muungano wa<br />

mwanamume na mwanamke walioamua kuishi pamoja maisha<br />

yao yote“. Baada ya mwanamume na mwanamke kuoana na<br />

kuzaa watoto, wahusika hupanda daraja na kuitwa baba na mama<br />

au wazazi. Ni katika ngazi hii tunapata jina familia.<br />

Katika ngazi ya familia maisha na shughuli za uzalishaji<br />

na utunzaji wa familia yakiwemo malezi ya watoto hufanyika na<br />

kustawi katika jamii. Kilele cha malezi ya wazazi kwa watoto, ni<br />

pale ambapo watoto wamekuwa watu wazima na kufikia daraja<br />

la kuanzisha taasisi mpya za ndoa na kuanza kuishi maisha yao<br />

wenyewe.<br />

Kama ni binti huagwa na wazazi kwa zawadi na hatarajiwi<br />

kurejea kwao na kuwa sehemu ya familia ile tena. Na kwa upande<br />

wa mtoto wa kiume, huwezeshwa katika kuandaa mahali pake<br />

maalum, nyumba au chumba atakapoishi na mkewe; kulipiwa<br />

mahari, na kufanyiwa sherehe ya arusi.<br />

82


Kuanzia wakati huo, bwana arusi hutambuliwa kuwa mtu<br />

mzima anayestahili kuendesha maisha mapya ya taasisi ya ndoa<br />

yake, na anatarajiwa kuacha kabisa kuwa tegemezi kwa wazazi<br />

kama alivyokuwa kijana asiye na ndoa.<br />

Kwa baadhi ya makabila au mataifa mengine, nadharia ya<br />

urithishaji, huanza kutekelezwa na wazazi katika hatua ya kuozesha<br />

au kufungisha ndoa za watoto wao. Lakini kwa makabila mengine<br />

hatua ya urithishaji hufanyika wakati baba wa familia amefariki<br />

dunia. Baada ya kuhitimisha msiba wake, ndipo wanafamilia<br />

wakisaidiana na ukoo hutekeleza nadharia ya kurithisha mali za<br />

marehemu kwa mjane na watoto wote pasipo kujali wana ndoa au<br />

hawana ndoa.<br />

Sababu Za Msingi Wa Urithishaji<br />

Ukomo Wa Umri Wa Kuishi<br />

Biblia imetabiri ukomo wa umri wa kuishi ni miaka 70 mpaka<br />

80. Dalili za kizazi kinachomaliza muda wake kimekadiriwa watu<br />

kuanzia miaka 50 na kuendelea. Ukomo wa umri wa kutumikia<br />

serikali na taasisi za umma ni miaka 60.<br />

Kwa hiyo, watu wote wenye umri wa kuanzia miaka 50 na<br />

kuendelea, popote walipo, kwa mambo yoyote wanayofanya,<br />

mojawapo ya mipango muhimu kwetu ni kujiandaa kuachia<br />

majukumu tuliyo nayo na kuyarithisha kwa kizazi kinachoinukia<br />

hivi sasa.<br />

Umri wa kizazi kinachotakiwa kurithishwa ni kuanzia miaka<br />

18 mpaka 49. Kipindi cha kurithisha kinahitaji maandalizi yasiyozidi<br />

miaka 10 kwa watu waliofikisha miaka 50.<br />

Kwa hiyo tunalazimika kurithisha kwa sababu ya ukomo<br />

wa umri wa kuishi ambao hatuna udhibiti nao. Kwa bahati<br />

mbaya baadhi yetu tunaogopa kurithisha mapema kwa hofu<br />

83


ya kupinduliwa au kupoteza umaarufu tuliojijengea katika jamii.<br />

Lakini tusipotumia muda muafaka tutamaliza vibaya na kuacha<br />

migogoro ya kifamilia na kijamii nyuma yetu.<br />

Wana-rika wenzangu, tusiposhituka na kuanza maandalizi<br />

ya urithishaji wa uchumi na uongozi hivi sasa, muda hautungoji.<br />

Miaka 10 iliyoko mbele yetu inakimbia mbio za kasi, kufumba na<br />

kufumbua tutajikuta iko mbele yetu.<br />

Uzalishaji na usimamizi ni mambo yanayotegemea nguvu<br />

na akili. Kwa kadiri umri unavyoongezeka ndivyo na nguvu za<br />

uzalishaji na akili za kufanya maamuzi hubadilka. Kwa lugha<br />

nyingine kasi ya kufanya mambo hupungua na uzito katika kufanya<br />

maamuzi nao huongezeka.<br />

Kwenye suala la uchumi ambapo ulimwengu unabadilika<br />

kila kukicha, mambo mapya yanazaliwa na elimu inaongezeka<br />

kwa kasi, wakati jamii ya wazee bado iko katika enzi zao. Bahati<br />

mbaya kasi na hamu ya kujifunza mambo mapya kwa wazee<br />

huzidi kupungua. Hizi ndizo dalili zinazoashiria kwamba, wakati<br />

wa kurithisha wengine wenye uwezo na nguvu umekaribia.<br />

Kuendeleza Jina<br />

Maendeleo ya kiuchumi na kijamii hufanywa na watu, kila<br />

mtu mmoja mmoja, na kwa ushirikiano wa kimakundi. Mojawapo<br />

ya hamasa za kimaisha, ni mtu kutoa mchango wa kimaendeleo<br />

ambao utakumbukwa baada ya kuondoka kwake duniani. Hii<br />

ndiyo inaitwa “kuacha jina”. Kuna mambo ambayo baadhi ya<br />

wazee waliotutangulia walifanya enzi za ujana wao, na sisi<br />

tumeyakuta, tumeyarithi, na tunawakumbuka kwa ajili ya mambo<br />

hayo. Wenyewe wamekufa, lakini mambo yao bado yako hai,<br />

na hivyo majina yao yanaendelea kutajwa japokuwa wenyewe<br />

hawapo tena.<br />

84


Kuendeleza Kizazi<br />

Sababu nyingine muhimu sana ni kukiwezesha kiuchumi<br />

na kiuongozi kizazi kipya cha watoto waliozaliwa na kulelewa<br />

katika mazingira ya kifamilia, kitaasisi na kitaifa. Sababu ya<br />

kwanza ya kurithisha tulisema ni kigezo cha ukomo wa muda<br />

wa kuishi. Sababu hii ndiyo inapaswa kuchochea moyo wa<br />

kizazi kinachomaliza muda wake kufanya maandalizi mapema ya<br />

kukabidhi majukumu ya kiuchumi na kuiongozi kwa kizazi kipya.<br />

Katika ngazi ya familia, ni fahari ya wazazi pale ambapo<br />

watoto wao waliowazaa wanapofikia umri wa kutaka kujitegemea<br />

kimaisha.<br />

Vijana wa kiume wanapofikia umri wa kuoa huhimizwa na<br />

wazazi na kufundishwa, na hata kusaidiwa jinsi ya kujenga misingi<br />

ya kujitegemea kama kuwa na shughuli maalum ya uzalisha wa<br />

kujipatia kipato binafsi, kujenga nyumba, kuwa na samani za<br />

ndani n.k.<br />

Kwa upande wa vijana wa kike, wanapofikia umri wa<br />

kuolewa huandaliwa rasmi jinsi ya kuishi katika ndoa na kutunza<br />

familia zao mpya baada ya kuolewa.<br />

Kuendeleza Maono Ya Kitaasisi<br />

Changamoto katika urithishaji ziko kwenye ngazi ya<br />

kitaasisi na kitaifa. Katika ngazi ya kitaasisi, kuna jamii ya watu<br />

waitwao “waasisi”. Hawa ni waanzilishi wa mawazo ya awali<br />

ya kuanzishwa kwa taasisi husika na kwa njia hiyo wamekuwa<br />

viongozi wake tangu ngazi ya uchanga mpaka hapo ambapo<br />

taasisi hizo zimekomaa kiutendaji. Ninaposema taasisi nina<br />

maana ya vyama vya hiari, au madhehebu ya dini, au vikundi vya<br />

kijamii ambavyo vimesajiliwa kwa mujibu wa sheria.<br />

85


Katika ngazi ya kitaasisi, (tofuati na serikali na taasisi za<br />

kiserikali, ambazo utumishi wake una ukomo kwa mujibu wa sheria)<br />

baadhi ya taasisi binafsi hazina utamaduni wa kisheria wa ukomo<br />

wa utumishi. Katika ngazi hii, mara nyingi wale waitwao “waasisi”<br />

kwa maana ya walioanzisha taasisi au huduma hizo huwa wazito<br />

sana kuachia madaraka ya uongozi kwa vijana wao. Kuacha<br />

utumishi katika ngazi ya kitaasisi hushinikizwa na maaradhi, au<br />

kifo; au shinikizo la uasi ndani ya taasisi ambao matokeo yake<br />

husababisha mifarakano na matengano ya kitaasisi.<br />

Kuendeleza Kizazi Cha Kijaamii Kitaifa<br />

Katika ngazi hii, urithishaji unategemea mfumo wa utawala<br />

na uzoefu katika zoezi ya kuachia madaraka. Kwa upande wa<br />

Tanzania, kisiasa tuna sifa njema katika Bara la Afrika kwa kuwa<br />

na utamaduni wa watawala wa kitaifa kuachia madaraka mara<br />

baada ya kufikia ukomo wa muda wao.<br />

Hata hivyo, changamoto iliyopo katika ngazi hii, ni pale<br />

ambapo wale wanaomaliza muda wao wa utumishi wa umma<br />

kupewa mikataba maalum na kuendelea kutumika. Utetezi<br />

unaotumika katika kulinda utaratibu huu ni kuwepo kwa baadhi<br />

ya nafasi za utumishi ambazo bado hazina watu wenye ujuzi na<br />

uzoefu; na hivyo wastaafu husika wakaonekana bado wanahitajika<br />

kutumika katika ngazi husika.<br />

Pamoja na utetezi huu, pia kumekuwepo na upande<br />

mwingine wenye malalamiko dhidi ya utaratibu huu kwamba<br />

unawanyima haki wengine waliostahili kushika nafasi za wastaafu<br />

kwa mujibu wa sheria.<br />

86


Ngazi Muhimu Za Urithishaji<br />

Urithishaji Wa Ngazi Ya Kifamilia<br />

Katika ngazi hii, ni wazazi ndio hurithisha watoto mali<br />

walizochuma katika familia. Kama tulivyokwisha kupitia kihistoria<br />

kuhusu urithishaji katika ngazi ya familia, hapa ni muhimu<br />

tuzingatie kwamba jamii ya kizazi chetu kwa sehemu kubwa<br />

imepoteza utamaduni wa kurithisha majukumu na raslimali kwa<br />

kizazi kinachoinukia.<br />

Ushahidi ni kuongezeka kwa migogoro na kesi za mirathi<br />

zilizojaa mahakamani siku hizi. Badala ya walezi kifamilia<br />

kusimamia mchakato wa urithishaji kwa watoto wa marehemu<br />

au wale wanaostahili kurithishwa, wao ndio wanateka mali hizo<br />

na kuzitapanya kwa sababu za kibinafsi na watoto wanaanza<br />

kuhangaika.<br />

Kupotea kwa utamaduni wa kurithisha pia kumechangiwa<br />

kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya kimaendeleo na kijamii<br />

ambapo familia zimetawanyika mijini na vijijini. Lakini pia ukosefu<br />

wa wazazi kuandika wosia mapema kuhusu mgawanyo wa mali<br />

kwa familia.<br />

Jambo linalosikitisha zaidi katika udhaifu wa kutokurithisha<br />

ni pale ambapo wazazi huishia kuzaa watoto lakini hawana<br />

mpango maalum wa kutunza urithi kwa ajili ya watoto. Badala<br />

yake wazazi wanafanya kazi ya kuchuma na kutafuta bila kuweka<br />

akiba kwa ajili ya watoto.<br />

Kuna ongezeko la kuparaganyika kwa familia kunakotokana<br />

na mmomonyoko wa maadili katika jamii. Hii imezalisha familia za<br />

aina tofauti ambazo watoto wanaozaliwa au kulelewa ndani yake<br />

wanakosa mwelekeo wa kimaadili na hivyo kupotoka kitabia.<br />

87


Kuparaganyika kwa familia nyingi kumezalisha changamoto<br />

kubwa nyingine ya ongezeko la kizazi kinachoitwa kwa jina maarufu<br />

kama “watoto wa mitaani”. Hawa ni watoto ambao baadhi yao<br />

hawana wazazi au walezi na wamekosa malezi ya kifamilia na ndio<br />

maana wameishia mitaani. Hiki nacho ni kizazi ambacho badala<br />

ya kurithishwa msingi wa kimaendeleo wanaishia kurithi umaskini<br />

na maisha ya uhalifu.<br />

Si lengo la kitabu hiki kuzungumuzia matatizo ya kifamilia,<br />

ila haya yanatajwa kama viashiria vya familia kushindwa kutimiza<br />

wajibu wake wa kurithisha kizazi kipya. Wito makini wa ujumbe<br />

wa kitabu hiki kwa kila familia yenye mtoto au watoto, wawe wa<br />

kuwazaa au kuwalea, ni kurejea katika utamaduni wa kijamii wa<br />

kurithisha majukumu na rasilimali kwa watoto pindi wanapofikia<br />

umri wa kujitegemea na kuwa watu wazima.<br />

Urithishaji Wa Ngazi Ya Kitaasisi<br />

Uritishaji wa kitaasisi ni urithishaji wa mali na madaraka ya<br />

kusimamia taasisi husika. Taasisi hapa tunajumuisha makampuni<br />

binafsi, vikundi vya uzalishaji, na vikundi vinginevyo ambavyo<br />

madhumuni yake ni uzalishaji na wanahisa kugawana mapato<br />

kwa mujibu wa makubaliano ya kisheria.<br />

Katika ngazi hii ya urithishaji wa kitaasisi, viongozi waasisi<br />

ndio wenye wajibu wa kurithisha madaraka ya usimamizi wa<br />

taasisi. Japokuwa jambo la kurithisha uongozi litaelezwa kwa<br />

kina katika vipengele vinavyofuata, hapa ni muhimu kuzingatia<br />

mapema ya kuwa kila mwasisi na mtendaji mkuu wa kampuni ya<br />

kifamilia au kijamii atie akilini mwake kuwa ni muhimu kumwandaa<br />

mrithi wake wakati bado ana nguvu.<br />

Mwasisi asisubiri wakati amezeeka ndipo akabidhi<br />

majukumu. Kurithisha majukumu ya uongozi na utawala katika<br />

mambo ya uzalishaji sio kama kurithisha mali za marehemu.<br />

Unahitaji muda wa kutosha wa kuachilia baadhi ya majukumu<br />

88


kwa watoto au warithi ambao wanapata uzoefu wakati mwasisi<br />

bado yuko hai.<br />

Urithishaji Kwa Kizazi Cha Kitaifa<br />

Ngazi ya urithishaji kwa kizazi cha kitaifa ni hatua ya<br />

juu kabisa katika jamii. Hapa tunazungumuzia ngazi ya kitaifa.<br />

Taifa kama Tanzania ambalo mna makabila zaidi ya 120<br />

yanayounganishwa na utaifa wenye sifa ya uraia mmoja.<br />

Tanzania kama taifa, linayo jamii ya watu waliozaliwa kwa<br />

wakati mmoja wa historia, ambao kwa lugha nyingine huitwa rika<br />

moja. Hawa ndio huitwa kizazi cha kitaifa. Lakini tunapo itathmini<br />

Tanzania kijamii tunakuta kuna mgawanyiko wa sehemu mbili za<br />

vizazi vya kitaifa; kuna kizazi cha watoto, na pili, kuna kizazi cha<br />

watu wazima.<br />

Kizazi cha watoto kinatambuliwa kwa umri kuanzia mwaka<br />

mmoja (1) mpaka miaka kumi na saba (17). Watu wote katika umri<br />

huu hawaruhusiwi kufanya maamuzi huru kama watu wazima.<br />

Wahusika wanahesabiwa kuwa chini ya uangalizi wa kifamilia<br />

na malezi ya kitaifa. Ishara iliyo wazi zaidi ni kuwa hawaruhusiwi<br />

kupiga kura kwenye uchaguzi wa uongozi wa kitaifa.<br />

Kizazi cha watu wazima ni kuanzia umri wa miaka kumi<br />

na nane (18) mpaka sitini (60). Hiki ndicho kizazi chenye idhini ya<br />

kufanya maamuzi na kuwajibika kisheria. Wahusika wanaruhusiwa<br />

kupiga kura na kuwania madaraka ya uongozi katika ngazi mbali<br />

mbali za utumishi wa umma kitaifa.<br />

Katika ngazi ya kizazi cha kitaifa, wenye wajibu wa<br />

kurithisha ni wazee ambao wamefikia umri wa kustaafu kwa<br />

mujibu wa sheria. Hiki ndicho kigezo muhimu cha Urithishaji wa<br />

kizazi. Wazee wanapostaafu huwaachia majukumu ya uzalishaji<br />

na usimamizi vijana ambao wamechukua nafasi zao.<br />

89


Vitu Muhimu Vya Kurithisha<br />

Elimu Na Ujuzi<br />

Zamani za wahenga wetu, urithi ulihusu mali zilizoachwa<br />

na marehemu tu. Na hii ndiyo asili ya neno Urithi. Mali au vitu<br />

vinavyoachwa na marehemu na kupewa mtu fulani wa ukoo<br />

husika. Lakini siku hizi mambo yamekwisha kubadilika. Urithi wa<br />

kwanza na wa kudumu ni elimu na ujuzi.<br />

Kama tulivyokwisha kusoma sehemu uliyotangulia ya kuwa<br />

wajibu wa kurithisha elimu na ujuzi unaanzia katika ngazi ya familia,<br />

halafu unakuja kwenye taasisi na kisha ngazi ya kitaifa. Isitoshe,<br />

ni haki ya kibinadamu kwa kila mtu kupata elimu ili kujiendeleza<br />

kiujuzi.<br />

Kwa kuwa kitabu hiki kinahusu <strong>vipaji</strong> vya asili, huko mbeleni<br />

nitaweka bayana ni aina gani ya elimu na ujuzi vinavyotakiwa<br />

kurithishwa kama njia ya kuinua na kunoa <strong>vipaji</strong>.<br />

Rasilimali<br />

Msamiati wa neno rasilimali umetafsiriwa kuwa ni “jumla<br />

ya mali aliyonayo mtu au nchi.” Kama nilivyotangulia kudokeza<br />

hapa juu kwamba, rasilimali ndio urithi unaofahamika tangu enzi<br />

za wahenga na hata sasa bado umeendelea kuwepo.<br />

Hapa inabidi tuzingatie kwamba rasilimali ni mali<br />

iliyozalishwa na kumilikiwa na familia. Ni wajibu wa kila familia<br />

kufanya kazi kwa bidii, kuchuma mali na kuzimiliki kifamilia.<br />

Tufahamu kwamba kiasi cha rasilimali ilichonacho familia ndicho<br />

kinachoweza kurithishwa kwa watoto wanapokuwa watu wazima.<br />

Ngazi ya pili ya kurithisha rasilimali ni ngazi ya kitaifa.<br />

Hapa nikiwa na maana ya serikali ya nchi kuhakikisha kila raia<br />

anatengenezewa mazingira ya kumwezesha kuzalisha na kumiliki<br />

90


asilimali kwa njia halali na kwa mujibu wa sheria.<br />

Aidha, ni kuhakikisha rasilimali za asili katika nchi zinalindwa<br />

kwa matumizi ya sasa na vizazi vijavyo; na Kipaumbele katika<br />

matumizi ya rasilimali za asili kiwe ni kuwawezesha raia kuwa na<br />

haki ya umiliki wake kisheria.<br />

Uongozi<br />

Tumekwisha kujifunza kwamba uongozi ni mojawapo ya<br />

sehemu ya <strong>vipaji</strong> vya asili. Kimsingi, kipaji hakiwezi kurithishwa<br />

toka mtu kwenda mtu mwingine. Muktadha wa “uongozi wa<br />

kurithisha” ni ile nafasi au madaraka ya usimamizi na utawala, iwe<br />

ni katika taasisi na makampuni binafsi, au katika serikali na taasisi<br />

zake za umma.<br />

Kwa mantiki hii, uongozi nao ni kitu maalum ambacho<br />

kinatakiwa kurithishwa. Japokuwa si kila mtu anaweza kurithishwa<br />

uongozi, lakini uongozi kama nadharia na mfumo lazima urithishwe<br />

ili kuweza kusimamia masuala ya uchumi na huduma za kijamii<br />

kwa raia wa nchi husika.<br />

Njia za urithishaji wa uongozi hazianzi na kugawa vyeo vya<br />

utawala bila kuzingatia uwezo wa kuongoza. Njia za kurithisha<br />

uongozi lazima ziwe na vigezo vilivyo wazi na makini tena kwa<br />

mujibu wa sheria na taratibu rasmi, ili warithishwe watu wenye<br />

uwezo wa kuongoza. Kama nilivyotangulia kudokeza kabla, ni<br />

kwamba nitachambua kwa kina suala la urithithishaji wa uongozi<br />

huko mbeleni katika sura hii.<br />

Vitu Visivyofaa Kurithishwa Kizazi Kipya<br />

Ujinga<br />

Kuna usemi uliozoeleka usemao: “Kama unaona elimu<br />

ni ghali, basi jaribu ujinga”. Kizazi cha utawala kilichopo hivi<br />

91


sasa kinaweza kuona kwamba kuwekeza katika “elimu na ujuzi”<br />

ni gharama kubwa, na kutafuta unafuu na urahisi ili kukwepa<br />

kugharimia viwango bora vya elimu na ujuzi. Kumbe katika<br />

kushusha “viwango vya ubora” tayari tumechagua kurithisha<br />

“viwango duni vya elimu” kwa kizazi kinachoinukia ambacho<br />

hakitaweza kumudu ushindani wa kimataifa katika uzalishaji.<br />

Sio siri hivi sasa kuona kwamba watoto na vijana wetu<br />

wamesongwa katika mazingira magumu ya kimfumo wa huduma<br />

za elimu kwa sababu mbali mbali. Baadhi ya sababu za watoto na<br />

vijana wetu kukosa kupata elimu bora ni pamoja na: i) uhaba wa<br />

nafasi za kuendelea na elimu ya juu katika mfumo wa elimu yetu.<br />

ii) udhaifu wa mitaala isiyokidhi viwango vya ubora wa elimu ya<br />

kimataifa. iii) Vitendo vya uchakachuaji wa mitihani kunakotokana<br />

na kukithiri kwa rushwa katika taasisi zinazosimamia mitihani. iv)<br />

Walimu kukosa motisha katika utoaji wa elimu kwa wanafunzi.<br />

Kwa kadiri ambavyo idadi kubwa ya watoto na vijana<br />

wengine wanavyoishia katika viwango vya chini vya elimu;<br />

hiyo ndiyo dalili iliyo waziwazi kwamba kizazi chetu tuliopo hivi<br />

sasa tumeamua kurithisha ujinga kwa kizazi kijacho. Kimsingi,<br />

tumekuwa tukifanya zoezi la kurithisha ujinga na kizazi kinachokuja<br />

kitatukumbuka kwa urithi wa ujinga tuliokiachia.<br />

Mabadiliko yoyote ya kimfumo hayaji kwa miujiza. Yanakuja<br />

kwa utashi na uamuzi wa nguvu. Lazima tuutumie utashi wetu<br />

na kufanya uamuzi wa kukataa kuendelea kurithisha ujinga kwa<br />

watoto na vijana wetu. Uwezo na nguvu tunazo, kinachokosekana<br />

ni nia ya dhati. Lazima tukatae kurithisha ujinga kwa watoto na<br />

vijana wetu.<br />

Umaskini<br />

Kuna mtu mmoja maarufu sana anayeongoza kwa utajiri<br />

hapa duniani anaitwa Bill Gates. Miaka ya hivi karibuni alitoa kauli<br />

ambayo imezua mjadala mpaka hivi sasa, lakini ina ushawishi<br />

92


mkubwa kiasi ambacho hakuna ambaye amefaulu kuipinga na<br />

akashinda. Alisema hivi:“kama umezaliwa katika familia masikini<br />

sio kosa lako; lakini ukifa maskini hilo ni kosa lako mwenyewe”.<br />

Kwa kauli hii ni rahisi sana Bill Gates kutafsiriwa kuwa<br />

amejikinai kwa kuwahukumu watu wanaokufa maskini kwamba<br />

hayo ni makosa yao. Lakini baada ya kuutafakari kwa makini<br />

usemi wake nilipata kumwelewa kwa sehemu kile alichokuwa<br />

amemaanisha.<br />

Bila shaka alikuwa anatoa ujumbe kwamba mtu<br />

anapozaliwa katika familia ambayo ni maskini sio kosa lake kwa<br />

sababu sio yeye aliyechangia wala kufanya maamuzi ya kimaisha<br />

hata kusababisha umaskini alioukuta. Kwa maneno mengine mtu<br />

hajichagulii azaliwe katika familia ya namna gani, bali hujikuta<br />

amezaliwa katika familia husika.<br />

Lakini iwapo muhusika aliyezaliwa katika familia maskini<br />

anapokuwa mtu mzima ana uhuru wa kufanya maamuzi ya mwisho<br />

kuhusu maisha yake. Na hii ni pamoja na kutafuta fursa nyingi<br />

zilizopo mbele yake na kuanza kuzitumia kwa uzalishaji, kwa nia<br />

ya kubadili maisha yake ya umaskini wa kuzaliwa na kuitwa jina<br />

tofauti katika jamii.<br />

Neno Umaskini limetafsiriwa na Kamusi ya Kiswahili Sanifu<br />

kuwa ni “hali ya kukosa mali; ufukara, uhitaji, na ukata”. Najua<br />

kwamba kuna nadharia na dhana nyingi kwa habari ya umaskini,<br />

hususan huu wa kipato. Aidha kumekuwepo na itikadi zenye<br />

kutetea umaskini kama janga linalowapata watu pasipo wenyewe<br />

kutaka au kuusababisha. Kwa utafiti wangu naweza kutafsiri<br />

sababu za umaskini katika sehemu zifuatazo:<br />

Ulemavu:<br />

Ulemavu wa viungo vya mwili au akili ambao mlemavu<br />

hawezi kufanya shughuli halali ya kujipatia kipato. Ulemavu wa<br />

93


jinsi hii, ni hali ambayo iko nje ya uwezo na uamuzi wa mhusika,<br />

na hivyo analazimika kuishi kwa kutegemea fadhila za binadamu<br />

ambao si walemavu katika jamii.<br />

Majanga Ya Kimazingira:<br />

Majanga ya kimazingira ni kama vile mafuriko, matetemeko<br />

au vita vya kiraia. Haya ni matukio ambayo huharibu rasilimali za<br />

watu na kupoteza muda wa jamii kufanya kazi za uzalishaji mpaka<br />

mazingira yarejee katika hali inayoruhusu uzalishaji.<br />

Katika mazingira kama haya waathirika hujikuta hawana rasilimali<br />

wala kipato cha kuwawezesha kukidhi mahitaji yao, isipokuwa nao<br />

wanaishi kwa fadhila za binadamu wengine ambao hawajakumbwa<br />

na majanga ya kimazingira.<br />

Uvivu Na Anasa:<br />

Tafsiri ya uvivu ni “hali ya kutotaka kufanya kazi; hali ya<br />

ulegevu katika kazi; utepetevu na ulegevu.” Ikiwa mtu mzima,<br />

ambaye si mlemavu, si mgonjwa, si mzee kikongwe; halafu mtu<br />

mwenyewe anaishi kwenye mazingira yenye fursa za uzalishaji<br />

mali (ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha, ustawi wa mimea na<br />

malisho ya mifugo), halafu mtu huyo katikati ya mazingira hayo<br />

bado hana shughuli maalum inayompatia kipato; basi tena, huyo<br />

mtu sifa yake ni moja tu, ni mvivu.<br />

Kutokufanya kazi; au kuwa mlegevu katika kazi,<br />

husababisha ukosefu wa kipato na matokeo yake ni umasikini wa<br />

kipato na rasilimali. Huu ndio umaskini ambao Bill Gates alisema,<br />

“mtu akifa katika umaskini wa jinsi hii ni makosa ya mhusika’.<br />

Tafsiri ya anasa ni “mambo au hali ya starehe na raha<br />

nyingi; au kitu chenye thamani kubwa ambacho sio muhimu.”<br />

Unaona? Haya ni maisha ambayo watu wanatumia rasilimali zao<br />

kwa mambo yasiyo na tija iwe ni katika familia au katika jamii.<br />

94


Uvivu hupelekea ukosefu wa kipato wakati anasa ni matumizi<br />

yasiyo na muhimu na kupita kiasi. Jambo lenye kushangaza na<br />

kusikitisha ni pale ambapo mtu asiye na kipato cha uhakika na<br />

akapata msaada wa kumwezesha kujikwamua katika umaskini,<br />

lakini anaamua kuutumia msaada ule kwenye anasa za ulevi,<br />

ulaji na kununua vitu vya thamani kubwa kuliko mahitaji yake ya<br />

muhimu.<br />

Matumizi ya anasa matokeo yake ni umaskini. Umaskini<br />

ambao haukupaswa kuwepo kabisa, lakini unamkumba mtu<br />

kwa sababu sio kwamba hakupata bali alipata akatumia vibaya,<br />

kwa anasa. Kumbuka kwamba matumizi ya anasa ni kuzalisha<br />

umaskini.<br />

Huu ndio umaskini ambao Bill Gates alisema, “mtu akifa<br />

katika umaskini wa jinsi hii ni makosa ya mhusika”. Umaskini wa<br />

namna hii unaweza kuzuilika kwa utashi na sio kwa misaada.<br />

Tunaweza kuukataa umaskini huu usiendelee kuanzia katika ngazi<br />

ya familia, ngazi ya kitaasisi na ngazi ya kitaifa.<br />

Hitaji Kuu La Viongozi Wa Kizazi Kipya<br />

Ni lazima tukubali kwamba hivi sasa, kwa sababu ya<br />

mmomonyoko wa maadili ya kimani; hata sifa na kanuni za<br />

kuwapata viongozi wenye uwezo stahili navyo vimechakachuliwa<br />

kabisa. Tumejikuta tuko katika mazingira ya kuwa na “bora<br />

viongozi” badala ya “viongozi bora”. Kwa mtindo huu kamwe<br />

hatuwezi kutarajia kwamba “uongozi wa kizazi kinachoinukia”<br />

utakuwa bora iwapo hatukuamua kwa makusudi kurejea<br />

katika kuweka “viongozi bora” ili wawe mwongozo kwa kikazi<br />

kinachoinukia.<br />

Kama ambavyo, kitaifa tuko kwenye mchakato wa<br />

mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kimifumo; bila shaka suala<br />

la uongozi nalo ni lazima lipewe kipaumbele ndani ya katiba,<br />

angalau kwa kuweka sifa na vigezo makini vyenye kuliwezesha<br />

95


taifa kuwapata viongozi bora. Sisi ambao ni kizazi kinachomaliza<br />

muda wake ni lazima tufumbe macho na kuacha kuangalia aina<br />

ya viongozi waliopo sasa hivi kuwa ndio kigezo cha viongozi wa<br />

kizazi kinachoinukia. Tuamue kukinusuru kizazi kipya kwa kuweka<br />

vigezo vya kuwapata viongozi bora, hususan, viongozi wenye<br />

<strong>vipaji</strong> vya uongozi na kuwanoa mapema ili wapate uzoefu wa<br />

kuongoza kizazi chao kinachoinukia.<br />

Kwa uzoefu wangu binafsi, pamoja na tafiti mbali mbali<br />

zilizofanyika kwa habari ya “aina ya viongozi bora”, kuna ushahidi<br />

kamili kwamba suala la “uongozi bora” linatakiwa kuzingatia<br />

mambo makuu matatu yafuatayo:<br />

1. Kipaji<br />

2. Uzoefu<br />

3. Uadilifu<br />

Kipaji kinawakilisha uwezo wa kuongoza kwa ushawishi<br />

wa nguvu za hoja na hekima ya kufanya maamuzi yenye kuleta<br />

ufumbuzi badala ya kusababisha matatizo makubwa zaidi. Kipaji<br />

cha uongozi kinahitaji mazoezi maalum ili kipate kunolewa kwa njia<br />

mbali mbali ambapo ndipo kigezo cha “uzoefu” kinachukua nafasi<br />

yake. Kimsingi kipaji cha uongozi hujidhihirisha chenyewe ndani<br />

ya mtu na wala hakuhitajiki kazi za “kupiga ramli za kindumba ili<br />

kukitambua”.<br />

Kipaji cha uongozi kikidhihirika ndani ya wahusika, lazima<br />

jamii iwe na mfumo wa kuwawezesha kufanya mazoezi ya<br />

kuongoza ili kigezo cha uzoefu nacho kichukue mkondo wake.<br />

Suala la uadilifu ni matunda ya maadili ya kiimani ambayo ndiyo<br />

mazingira wahusika wamefundwa na kukulia tangu ngazi ya<br />

familia, na imani kwa Mungu na huu ndio msingi wa kuwafanya<br />

kukamilisha sifa za kiuongozi.<br />

Tunapotaka kurithisha maono kwa kizazi kipya, tukija<br />

kwenye suala la uongozi, kipaji, uzoefu na uadilifu ni vitu<br />

96


vinavyotakiwa kuwa mwongozo kwa wanoaji na warithishaji<br />

maono kwa kizazi kipya.<br />

Kwa kuwa shina la uongozi mbovu linatokana na<br />

mmomonyoko wa maadili ya kiimani katika jamii; bila shaka hapa<br />

ndipo mahali pa kuanzia kufanya maandalizi ya viongozi bora.<br />

Kuweka mkazo wa maadili ya kiimani, maadili ya kitaaluma na<br />

maadili ya uongozi.<br />

Malezi ya kimaadili ya kiimani huanzia nyumbani katika<br />

familia. Ni wakati muafaka kwa kanisa kuandaa mipango<br />

ya mafunzo ya kimaadili kwa wazazi ili yawasaidie kuwalea<br />

watoto wao kimaadili. Bila shaka, wazazi wenyewe nao lazima<br />

wanatambua kwamba wajibu wa kulea watoto kimaadili unaanzia<br />

kwao kama wazazi katika kuyashika maadili yenyewe ili wawe<br />

mfano kwa watoto wao.<br />

Wakati huo huo, juhudi zielekezwe katika kuandaa<br />

mitaala ya maadili kwa wanafunzi mashuleni na vyuoni ambapo<br />

watoto watafundishwa somo la maadili, huku kanisa likisimamia<br />

majukumu ya maadili ya kiimani.<br />

Ili tuweze kuona matokeo mazuri lazima tuanze na watoto<br />

na vijana wa kizazi kipya ambao muda si mrefu watakuwa<br />

wanakabiliwa na changamoto za uongozi wa kizazi kinachomaliza<br />

muda wake duniani. Katika vizazi vilivyopita, kila taifa ambalo<br />

liliweka kipaumbele kwa malezi ya kimaadili, limetoa viongozi<br />

bora ambao wameweka rekodi ya uongozi katika historia na<br />

wanakumbukwa mpaka hivi leo.<br />

Mchakato Wa Kuandaa Uongozi Wa Kizazi Kipya<br />

Kama nilivyotangulia kusema hapa juu kuwa suala la<br />

uongozi linahusiana na kipaji, hapa nataka kusisitiza kwamba,<br />

lazima kuwepo kwa mchakato mahsusi wa kuvibaini <strong>vipaji</strong> vya<br />

uongozi.<br />

97


Kuvibaini Vipawa Vya Uongozi<br />

Ziko nadharia za aina nyingi katika kushughulikia maandalizi<br />

ya viongozi. Nadharia moja inadai kwamba uongozi ni kipawa na<br />

hivyo hakuhitajiki mafunzo ya kitaaluma ya kuandaa kiongozi.<br />

Nadharia ya pili inadai kwamba, uongozi ni taaluma ya kawaida<br />

ambayo kila mtu anatakiwa kupitia mafunzo ili apate ujuzi wa<br />

kuongoza kwa mujibu wa taaluma yenyewe.<br />

Binafsi nimekwisha kuonesha msimamo kwamba, uongozi<br />

ni kipawa. Lakini ili kuweza kubaini kipawa cha uongozi lazima<br />

uwepo mkakati mahususi wenye kutafuta na kugundua kila<br />

mwenye nacho. Kama nilivyokwisha kusema hapo awali, malezi<br />

ya kimaadili kwa vijana wa kizazi kipya lazima yaende sambamba<br />

na kuvibaini vipawa vya uongozi kwa ajili ya kuvitambua na<br />

kutengenezea mazingira ya kutumika kwa wakati muafaka.<br />

Mafunzo Ya Kunoa Vipawa Vya Uongozi<br />

Baada ya kuvibaini vipawa vya uongozi, hatua inayofuata ni<br />

kuandaa mafunzo maalum ya kuvinoa kwa ajili ya matumizi yenye<br />

ufanisi unaozingatia viwango vya ubora. Kuvitambua vipawa<br />

na kuanza kuvitumia bila mafunzo ni kusababisha vituko katika<br />

uongozi. Kipawa kinahitaji kunolewa ili kuweza kuleta matokeo<br />

yanayotarajiwa.<br />

Ile nadharia kwamba kila mtu anaweza kujifunza taaluma<br />

ya uongozi na akaweza kuongoza hata kama hana kipawa, bado<br />

ina upungufu. Tunao viongozi wengine waliopata mafunzo ya<br />

uongozi na wakapewa uongozi lakina wamekuwa si wabunifu,<br />

wala hawana ushawishi kwa wale wanaowaongoza. Lakini<br />

mwenye kipawa cha uongozi akipata mafunzo; ni sawa na upanga<br />

kunolewa ili kuboresha makali yake wakati wa kutumika.<br />

98


Majaribio Ya Uongozi<br />

Baada ya kuvinoa vipawa kimafunzo, ndipo unafika sasa<br />

wakati muafaka wa kuvifanyia majaribio ya uongozi. Kuvifanyia<br />

vipawa majaribio ya uongozi ni pamoja na kuwapa fursa wenye<br />

vipawa kushika nafasi za uongozi kuanzia ngazi za chini na huku<br />

wakitathminiwa jinsi wanavyodhihirisha uwezo na sifa zao kabla<br />

hawajaanza kuonja madaraka makubwa na ya juu katika ngazi za<br />

uongozi.<br />

Mbinu mbali mbali za kufanya majaribio ya uongozi ni<br />

pamoja na kuunda vyama na jumuiya mbali mbali zitakazotoa<br />

fursa za uongozi ili wale wanaojaribiwa wapewe uongozi na kisha<br />

wakionekana wameiva waanze kupewa nafasi zile za kiutendaji<br />

zisizotakiwa kufanya majaribio.<br />

99


Vyanzo Vya Rejea Vilivyotumika<br />

1. Biblia Takatifu<br />

2. BlueBibleLetter.or<br />

3. King James Version Bible<br />

4. Amplified Bible (AMP)<br />

5. Kamusi ya Kiswahili Sanifu<br />

6. https://www.wikipedia.org/<br />

7. The Gift in You (7 Pillars of Thinking designed to discover your<br />

Gift) Dr. Caroline Leaf<br />

8. drleaf.com/blog/perfectly-you-online-program-introduction<br />

9. The Seven Pillars of Thinking with the Copeland’s and Dr.<br />

Caroline Leaf<br />

10. www.biblestudytools.com/kjv<br />

WAPO Mission International Makao Makuu<br />

Mbezi Beach, Barabara Ya Bagamoyo, Jogoo, Dar-es-Salaam<br />

Tovuti: www.wapo.or.tz<br />

S.L.P. 6178 Dar-es-Salaam, Tanzania<br />

<strong>100</strong>

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!