14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

“Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa<br />

Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda; nami nimemjaza roho ya<br />

Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya<br />

kila aina, ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa<br />

fedha, na wa shaba, na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora<br />

miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.” (Kut. 31:2-5)<br />

“... ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa<br />

fedha, na wa shaba, Tena, tazama, nimemchagua, awe pamoja<br />

naye, huyo Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani;<br />

nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima,<br />

ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza” (Kut. 31:4-6)<br />

Katika maandiko haya kila mahali neno “hekima” kwa<br />

kiebrania ni chokmah likimaanisha <strong>vipaji</strong> mbali mbali kwa ajili<br />

ya ubunifu, ufundi na ustadi wa vifaa vya ujenzi na vyombo vya<br />

kutumia kwenye hema ya Mungu kukutana na wana wa Israeli.<br />

Tukiyachunguza maandiko ya Agano Jipya kwa lugha ya<br />

Kiyunani tunakutana na msamiati wa neno “Sophia” pia likiwa<br />

limetafsiriwa kuwa ni hekima ambalo linamaanisha <strong>vipaji</strong> vya asili.<br />

Neno sophia ambalo kwa Kiswahili ni hekima maana yake<br />

ni “uwezo mpana wa kujifunza na kushughulikia mambo mapya<br />

(full of intelligence); uwezo wa kutendea kazi maarifa na ufundi wa<br />

mambo mtambuka.” Neno sophia limetajwa mara 51 katika toleo<br />

la KJV kwenye Agano Jipya.<br />

Tunaweza kupata matumizi ya neno sophia kwenye<br />

maandiko matakatifu ya Agano Jipya ambayo ni haya yafuatayo:<br />

“Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima,<br />

na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.” (Luk. 2:40)<br />

“Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo,<br />

akimpendeza Mungu na wanadamu.” (Luk. 2:52)<br />

5

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!