Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Maandiko yametuhakikishia kwamba uvivu husababisha<br />
umaskini. Mtu asipofanya kazi kwa makusudi hatapata mapato<br />
na hivyo kuishia kuwa maskini.<br />
Kuwa mzigo kwa wengine<br />
Mwathirika wa tabia sugu ya uvivu kwa kuwa hana kipato,<br />
lakini bado ana mahitaji ya lazima ya kula, kunywa, kuvaa, malazi<br />
na mengine, haya yote huwatwika watu wengine wabebe mzigo<br />
huo.<br />
“Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa<br />
mavuno ataomba, hana kitu.” (Mit. 20:4)<br />
Kwa sababu shida za mvivu haziishi, leo ana shida hii<br />
kesho ana shida ile na asiposaidiwa atalaumu na kulalamika<br />
kana kwamba ni haki yake kusaidiwa wakati si mlemavu. Hii<br />
husababisha kero kwa wale walio karibu naye.<br />
Kupoteza Fursa Matumizi Ya Vipaji<br />
Mwathirika wa tabia ya uvivu hushindwa kutumia kipaji<br />
chake kila anapopewa fursa ya kuzalisha. Yesu alitoa mfano wa<br />
talanta ambapo tajiri aliwapa watumwa wake talanta za kuzalisha.<br />
Mmoja kati yao aliyepewa talanta moja kwa sababu ya uvivu wake<br />
alishindwa kuzalisha lakini akaja na visingizio kama ifuatavyo:<br />
“… Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana,<br />
nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda,<br />
wakusanya usipotawanya; basi nikaogopa, nikaenda nikaificha<br />
talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako. Bwana wake<br />
akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua<br />
ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; basi,<br />
ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija<br />
ningalipata iliyo yangu na faida yake. Basi, mnyang’anyeni talanta<br />
hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. Kwa maana kila mwenye<br />
kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile<br />
65