You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Madhara Ya Pombe Mwilini<br />
Madhara ya kwanza ya pombe ni kuathiri mfumo wa<br />
ubongo ambao ndio asili ya nguvu ya <strong>vipaji</strong> vya asili. Baadhi ya<br />
athari za pombe katika ubongo ni kama zifuatazo:<br />
• Mishipa ya ubongo kupanuka kupita kawaida.<br />
• Ukosefu wa baadhi ya vitamin katika ubongo (mlevi hali mlo<br />
kamili)<br />
• Ukosefu wa vitamin B unaweza kusababisha matatizo ya akili<br />
katika ubongo<br />
• Kubadilika kitabia, kudhoofika kwa uwezo wa kufikiri, kupoteza<br />
kumbukumbu<br />
Athari kubwa zaidi za pombe katika ubongo ni eneo la<br />
mfumo wa neva. Wakati kisingizio cha matumizi ya pombe huwa<br />
ni kama kitulizo katika mfumo wa neva, badala yale pombe<br />
hutumika katika kuzikandamiza seli za neva katika ubongo kwa<br />
kuzifanya butu na kuuharibu uwezo wake wa kufanya kazi, hali<br />
ambayo hupelekea kusinzia, kuzimia na hata kifo.<br />
Madhara mengine ya pombe kwenye mfumo wa neva ni<br />
pamoja na haya yafuatayo:<br />
• Kudhoofisha uwezo wa kuona<br />
• Kubadilisha utambuzi wa muda na mahali<br />
• Kupoteza uwezo wa kusikia vizuri<br />
• Kupatwa na uzito katika kuitikia mambo<br />
• Kupoteza hisia ya harufu na ladha<br />
Kana kwamba hii haitoshi, madhara ya pombe hayaishii<br />
kuathiri ubongo na mfumo wa neva peke yake. Pombe huathiri<br />
kiungo kingine muhimu cha mwili ambacho ni moyo. Baadhi ya<br />
maeneo ambayo moyo huathiriwa na pombe ni pamoja na haya<br />
yafuatayo:<br />
67