14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Madhara Ya Pombe Mwilini<br />

Madhara ya kwanza ya pombe ni kuathiri mfumo wa<br />

ubongo ambao ndio asili ya nguvu ya <strong>vipaji</strong> vya asili. Baadhi ya<br />

athari za pombe katika ubongo ni kama zifuatazo:<br />

• Mishipa ya ubongo kupanuka kupita kawaida.<br />

• Ukosefu wa baadhi ya vitamin katika ubongo (mlevi hali mlo<br />

kamili)<br />

• Ukosefu wa vitamin B unaweza kusababisha matatizo ya akili<br />

katika ubongo<br />

• Kubadilika kitabia, kudhoofika kwa uwezo wa kufikiri, kupoteza<br />

kumbukumbu<br />

Athari kubwa zaidi za pombe katika ubongo ni eneo la<br />

mfumo wa neva. Wakati kisingizio cha matumizi ya pombe huwa<br />

ni kama kitulizo katika mfumo wa neva, badala yale pombe<br />

hutumika katika kuzikandamiza seli za neva katika ubongo kwa<br />

kuzifanya butu na kuuharibu uwezo wake wa kufanya kazi, hali<br />

ambayo hupelekea kusinzia, kuzimia na hata kifo.<br />

Madhara mengine ya pombe kwenye mfumo wa neva ni<br />

pamoja na haya yafuatayo:<br />

• Kudhoofisha uwezo wa kuona<br />

• Kubadilisha utambuzi wa muda na mahali<br />

• Kupoteza uwezo wa kusikia vizuri<br />

• Kupatwa na uzito katika kuitikia mambo<br />

• Kupoteza hisia ya harufu na ladha<br />

Kana kwamba hii haitoshi, madhara ya pombe hayaishii<br />

kuathiri ubongo na mfumo wa neva peke yake. Pombe huathiri<br />

kiungo kingine muhimu cha mwili ambacho ni moyo. Baadhi ya<br />

maeneo ambayo moyo huathiriwa na pombe ni pamoja na haya<br />

yafuatayo:<br />

67

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!