14.02.2018 Views

vipaji_pages1-100

hugggugu

hugggugu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

“Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo; miongoni mwa<br />

walao nyama kwa pupa; kwa maana mlevi na mlafi huingia<br />

umaskini, na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.” (Mit. 23:20-<br />

21)<br />

Baadhi ya athari za kiuchumi zitokanazo na pombe ni kama<br />

hizi zifuatavyo:<br />

• Kudhoofika kwa viwango vya ubunifu wa mipango endelevu<br />

ya kiuchumi<br />

• Kudhoofika kwa uwezo wa kufanya kazi<br />

• Utoro makazini<br />

• Kupoteza ajira<br />

• Kufilisika kibiashara/kimiradi<br />

• Kukumbwa na umaskini wa kujitakia kibinafsi, familia na jamii<br />

kwa jumla<br />

Athari Za Kijamii<br />

• Kudhoofisha uwajibikaji wa mtu kama mwanandoa au kama<br />

mzazi<br />

• Kusababisha ugomvi katika familia<br />

• Kukaa nje ya familia kwa muda mrefu<br />

• Kutelekeza familia na kuwasababishia wasiwasi, mashaka na<br />

msongo wa mawazo<br />

• Kuchochea vitendo vya zinaa ambavyo hueneza maambukizo<br />

ya VVU<br />

• Malezi duni kwa watoto<br />

Tabia Sugu Ya Zinaa<br />

Msamiati wa neno “zinaa” unajumuisha matumizi ya<br />

maneno mawili maarufu kama “uasherati” na “Uzinzi”. Tafsiri<br />

rasmi ya neno uasherati maana yake ni “tendo la kujamiiana<br />

linalofanywa na mtu/watu ambao hawajaoa wala kuolewa kwa<br />

mujibu wa sheria”. Na tafsiri rasmi ya neno uzinzi maana yake<br />

69

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!