Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
“Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo; miongoni mwa<br />
walao nyama kwa pupa; kwa maana mlevi na mlafi huingia<br />
umaskini, na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.” (Mit. 23:20-<br />
21)<br />
Baadhi ya athari za kiuchumi zitokanazo na pombe ni kama<br />
hizi zifuatavyo:<br />
• Kudhoofika kwa viwango vya ubunifu wa mipango endelevu<br />
ya kiuchumi<br />
• Kudhoofika kwa uwezo wa kufanya kazi<br />
• Utoro makazini<br />
• Kupoteza ajira<br />
• Kufilisika kibiashara/kimiradi<br />
• Kukumbwa na umaskini wa kujitakia kibinafsi, familia na jamii<br />
kwa jumla<br />
Athari Za Kijamii<br />
• Kudhoofisha uwajibikaji wa mtu kama mwanandoa au kama<br />
mzazi<br />
• Kusababisha ugomvi katika familia<br />
• Kukaa nje ya familia kwa muda mrefu<br />
• Kutelekeza familia na kuwasababishia wasiwasi, mashaka na<br />
msongo wa mawazo<br />
• Kuchochea vitendo vya zinaa ambavyo hueneza maambukizo<br />
ya VVU<br />
• Malezi duni kwa watoto<br />
Tabia Sugu Ya Zinaa<br />
Msamiati wa neno “zinaa” unajumuisha matumizi ya<br />
maneno mawili maarufu kama “uasherati” na “Uzinzi”. Tafsiri<br />
rasmi ya neno uasherati maana yake ni “tendo la kujamiiana<br />
linalofanywa na mtu/watu ambao hawajaoa wala kuolewa kwa<br />
mujibu wa sheria”. Na tafsiri rasmi ya neno uzinzi maana yake<br />
69