Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Karama<br />
Kamusi ya Kiswahili Sanifu imetafsiri neno “karama” kuwa<br />
ni “kipawa anachokuwa nacho mtu kwa sababu ya kumwabudu<br />
sana Mungu, aghalabu humpa uwezo wa kuomba haja kwa<br />
Mwenyezi Mungu na kukubaliwa mara moja; ridhaa ya kupokelewa<br />
haja iombwayo”<br />
Kwa mujibu wa kamusi za Biblia, kabla ya kuchambua<br />
maana ya karama za kiroho, hatuna budi tupate kufahamu ya kuwa<br />
Biblia haitoi tafsiri na msamiati huu wa “karama za kiroho” lakini<br />
imetoa maelezo ya kina kuhusu asili yake na jinsi zinavyotenda<br />
kazi. Msamiati wa neno “karama” ndio umetafsiriwa kwa kiyunani<br />
kama “charismata” likiwa na maana ya “karama za neema” na<br />
likilenga “karama” au uwezo maalum kutoka kwa Mungu ambao<br />
hutolewa kwa waamini kupitia Roho Mtakatifu.<br />
Pia kuna tofauti kati ya “karama za kiroho” au “karama za<br />
Roho Mtakatifu na “kipawa cha Roho Mtakatifu”. Kuna aina nyingi<br />
za karama za kiroho, lakini Roho Mtakatifu ni mmoja tu. Kipawa<br />
cha Roho Mtakatifu hupokelewa baada ya mtu kumpokea Yesu<br />
Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wake na kuzaliwa upya kiroho.<br />
(Mdo. 2:38).<br />
Aidha, kuna mgawanyiko maalum wa “karama za kiroho”<br />
ambao ni “karama za Roho”, “ofisi za huduma”, na “karama<br />
za neema”. Wakati ambapo “karama za Roho” ni utendaji wa<br />
Roho Mtakatifu ndani ya mwamini kama ilivyoandikwa katika<br />
1 Wakorintho 12; pia ziko “ofisi za huduma” ambazo ni vipawa<br />
vya kiroho vya utendaji huduma tofauti kama zilivyotajwa katika<br />
Waefeso 4:11. Na pia kuna “karama za Neema” ambazo ni<br />
utendaji wa Mungu kwa ajili ya waamini kama ulivyoanishwa<br />
kwenye Warumi 12.<br />
Orodha ya “karama za Roho” zilizotajwa katika 1 Wakorintho<br />
12: ni kama ifuatayo:<br />
7