08.06.2013 Views

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe (Mathayo 24:32-<br />

35).<br />

Yesu hakutaka wanafunzi Wake wanaswe bila kufahamu – na hilo ndilo jambo la<br />

msingi katika Mafundisho ya pale Mlima wa Mizeituni. Wangejua kwamba “yuko<br />

malangoni” baada ya kuona “mambo hayo yote” – dhiki duniani kote, kurudi nyuma kwa<br />

watu, kutokea kwa manabii na makristo wa uongo, tangazo la mpingakristo kwamba ni<br />

Mungu, na kutiwa giza jua na mwezi pamoja na kuanguka kwa nyota, wakati karibu na<br />

kurudi Kwake.<br />

Ila, baada tu ya kuwaambia kuhusu ishara zitakazotangulia kuja Kwake kwa miaka<br />

michache, au miezi au siku, aliwaambia sasa wakati hasa wa kurudi Kwake ungebakia<br />

kuwa siri.<br />

Walakini kwa habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika<br />

walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake (Mathayo 24:36).<br />

Mara nyingi andiko hili linatajwa kinyume cha mantiki yake! Kwa kawaida linatajwa<br />

ili kuunga mkono dhana kwamba hatuna habari Yesu atarudi lini, kwa sababu anaweza<br />

kurudi wakati wowote na kunyakua kanisa. Lakini katika mantiki yake, Yesu<br />

hakumaanisha hicho. Alikuwa ndiyo kamaliza kuhakikisha kwamba wanafunzi Wake<br />

wangekuwa tayari kwa ajili ya kurudi Kwake kwa kuwaambia ishara nyingi ambazo<br />

zingetokea muda mfupi tu kabla ya kurudi Kwake. Sasa anachowaambia ni kwamba, siku<br />

hasa na saa havitafunuliwa kwao. Tena, Yesu hasemi juu ya kuja Kwake mara ya kwanza<br />

kabla ya kipindi cha Dhiki ya miaka saba kuanza, wakati ambapo kanisa lingenyakuliwa,<br />

bali kuhusu kurudi Kwake wakati wa mwisho au karibia mwisho wa Dhiki. Hilo halina<br />

matatizo ukitazama mantiki vizuri.<br />

Je, Kurudi Kwake Hakujulikani Kabisa?<br />

Hoja ambayo mara nyingi hutumika dhidi ya Unyakuo kutokea karibu au wakati wa<br />

mwisho wa Dhiki ni kwamba kurudi kwa namna hiyo kusingekuwa kitu kisichojulikana<br />

kama Yesu alivyodaiwa kusema, kwa sababu kurudi kwa namna hiyo kungetazamiwa<br />

kwa matukio ya Dhiki. Lazima kuwe na Unyakuo kabla ya dhiki, la sivyo waamini<br />

wasingehitaji kuwa tayari na kukaa macho kama Maandiko yasemavyo wanapaswa<br />

kuwa, maana watajua ni miaka saba au zaidi kabla ya Yesu kurudi.<br />

Ila, hoja hii inapingwa na ukweli kwamba lengo kuu la Mafundisho ya Yesu pale<br />

Mlima wa Mizeituni lilikuwa ni kuhakikisha kwamba wanafunzi Wake wawe tayari kwa<br />

ajili ya kurudi Kwake wakati au karibu na mwisho wa Dhiki, naye aliwafunulia ishara<br />

nyingi tu ambazo zingetangulia kuja Kwake. Mbona Mafundisho ya Mlimani yamejaa<br />

mashauri mengi sana kwamba watu wawe tayari na kuwa macho, ingawa Yesu alijua<br />

kwamba kurudi Kwake kuko mbele miaka mingi sana baada ya kusema maneno hayo?<br />

Bila shaka ni kwa sababu Yesu aliamini kwamba Wakristo wanahitaji kuwa tayari na<br />

kuwa macho hata ingawa kurudi Kwake bado kuko miaka mingi mbele. Mitume ambao<br />

hayo yote yatafanyika katika kizazi kimoja, au pengine kwamba taifa la Wakristo (au Wayahudi basi)<br />

lisingepita mpaka mambo hayo yote yatimie.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!