08.06.2013 Views

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Hapa tena, kitu ambacho Yesu anajali ni kwamba wanafunzi Wake wawe tayari kwa<br />

ajili ya kurudi Kwake. Hicho ndicho kilisababisha yote aliyosema kabla ya hapa na baada<br />

ya hapa, katika mafundisho <strong>Ya</strong>ke. Maonyo <strong>Ya</strong>ke mwengi kwamba wawe tayari na<br />

wakeshe si kwamba ni kwa kuwa kurudi Kwake kutakuwa kwa kushtukiza, bali ni ishara<br />

ya jinsi ambavyo itakuwa vigumu kwa sababu ya upinzani wa wakati wenyewe,<br />

kuendelea kuwa macho na kuwa tayari. Basi, wale wanaotarajia Unyakuo kabla ya Dhiki,<br />

wakati wowote, wanaodhani kwamba wako tayari kuliko Wakristo wengine, wanaweza<br />

wasiwe tayari kwa uhalisi kabisa, kwa kile kinachokuja. Kama hawatazamii dhiki yoyote<br />

na wajikute katikati ya mateso ya dunia nzima, wakati wa utawala wa mpingakristo,<br />

jaribu la kuanguka linaweza kuwazidi nguvu. Afadhali kuwa tayari kwa kile<br />

kinachofundishwa na Maandiko kwamba kitatokea.<br />

Halafu tena – kama ungemwuliza Petro, <strong>Ya</strong>kobo au Yohana kwamba walitazamia<br />

kumwona lini Yesu akirudi, wangekwambia kuhusu ishara hizo zote ambzo Yesu<br />

aliwaambia zingetokea, kabla ya kurudi Kwake. Wasingetazamia kumwona kabla ya<br />

kipindi cha dhiki, au kutokea kwa mpingakristo.<br />

Mwivi Usiku<br />

Ona kwamba hata mfano wa Yesu wa “mwivi usiku” uko katika mantiki ya Yeye<br />

kudhihirisha ishara nyingi ambazo zingewasaidia wanafunzi Wake wasinaswe ghafula<br />

kwa kurudi Kwake. Basi, mfano huo hauwezi kutumiwa kisahihi kuonyesha kwamba<br />

hakuna mtu anayeweza kuwa na wazo lolote kuhusu Yesu anarudi lini.<br />

Paulo na Petro walitumia mfano wa Yesu wa “mwivi usiku” walipokuwa wanaandika<br />

kuhusu “siku ya Bwana” (ona 1Wathes. 5:2-4; 2Petro 3:10). Waliamini huo mfano<br />

ulikuwa na maana kwa habari ya Yesu kurudi kwa ghadhabu wakati wa au mwisho wa<br />

Dhiki ya miaka saba. Ila, Paulo aliwaambia hivi wasomaji wake: “Bali ninyi, ndugu,<br />

hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi” (1Wathes. 5:4). Yeye alitafsiri kwa<br />

usahihi mfano wa Yesu, akitambua kwamba wale walio macho na makini kuona zile<br />

ishara, na wenye kumfuata Yesu kwa utiifu, hawakuwa gizani mpaka kuja kwa Kristo<br />

kuwapate kwa ghafula. Kwa watu namna hiyo, Yesu asingekuja kama mwivi usiku. Ni<br />

wale walio gizani tu ndiyo wangeshtushwa – na ndivyo Yesu alivyofundisha. (Ona vile<br />

vile matumizi ya Yesu ya maneno “mwivi usiku” katika Ufunuo 3:3 na 16:15. Hapo<br />

anatumia maneno hayo kusema juu ya kuja Kwake kwenye vita ya Har-magedoni.)<br />

Kuanzia hapa na kuendelea katika Mafundisho <strong>Ya</strong>ke ya pale Mlima wa Mizeituni,<br />

Yesu alirudia kuwaonya wanafunzi Wake kuwa tayari kwa ajili ya kurudi Kwake. Hapo<br />

hapo akawaambia pia jinsi ya kuwa tayari, aliposema mifano kuhusu mtumwa asiyekuwa<br />

mwaminifu, kuhusu wanawali kumi, na kuhusu talanta, na baadaye akatabiri hukumu ya<br />

kondoo na mbuzi (yote inafaa kusomwa). Katika hiyo mifano yote, aliwaonya kwamba<br />

jehanamu ilikuwa inawasubiri wale wote wasiokuwa tayari kwa ajili ya kurudi Kwake<br />

(ona Mathayo 24:50, 51; 25:30, 41-46). Njia ya kuwa tayari ni kupatikana ukifanya<br />

mapenzi ya Mungu, wakati Yesu atakaporudi. 10<br />

10 Ni dhahiri kwamba uwezekano wa wanafunzi wa Yesu kutokuwa tayari wakati wa kurudi Kwake<br />

ulikuwepo, maana aliwaonya sana kuhusu hilo. Kama aliwaambia kwamba adhabu ni hukumu ya milele<br />

kwa kutokuwa tayari kwa sababu ya dhambi, basi ilikuwa inawezekana kwao kupoteza wokovu kwa<br />

sababu ya dhambi. Hili linapaswa kutupa angalizo juu ya umuhimu wa utakatifu, na tutambue kwamba ni

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!