08.06.2013 Views

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

Mchungaji Afanyaye Watu Kuwa Wanafunzi Sura Ya Ishirini Na Tisa ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

linatufanya tuseme kwamba wamenyakuliwa, hawajauawa – ni waaminio<br />

waliokombolewa kutoka katika dhiki ile kuu.<br />

Ni sahihi kudhani kwamba Unyakuo utatokea wakati fulani mara tu baada ya matukio<br />

hayo ya mbinguni yanayotajwa katika Ufunuo 6:12 na 13, kwa sababu yanafanana na<br />

yale aliyosema Yesu katika Mathayo 24:29-31. Ila, hatuna ishara iliyo dhahiri kuhusu<br />

wakati wa kutokea hayo mambo yanayotajwa katika Ufunuo 6:12 na 13, katika kipindi<br />

cha dhiki ya miaka saba. Kama matukio yanayotajwa katika Ufunuo 6:1-13 yanafuatana,<br />

na kama Unyakuo unatokea mara tu baada ya 6:13, hilo linatuongoza kuamini kwamba<br />

Unyakuo hautatokea mpaka baada ya kufunuliwa kwa mpingakristo (ona 6:1, 2), na vita<br />

ya dunia nzima (ona 6:3-4), njaa (ona 6:5, 6), kufa kwa robo ya watu wa duniani kwa<br />

vita, njaa, magonjwa na wanyama wakali (ona Ufunuo 6:7-8), na wafia dini wengi<br />

kupatikana (ona Ufunuo 6:9-11). Hakika matukio hayo yote yanayotajwa yanaweza<br />

kutokea kabla ya kumalizika kipindi cha Dhiki cha miaka saba, lakini pia yanaweza kuwa<br />

ndiyo yatakayotokea katika kipindi chote cha miaka saba cha dhiki, na Unyakuo kuwa<br />

mwisho kabisa.<br />

Wazo la Unyakuo kutokea kabla ya mwisho wa miaka saba ya dhiki linaongezewa<br />

uzito na kweli kwamba Kitabu cha Ufunuo kinaeleza juu ya makundi mawili ya hukumu<br />

saba, baada ya Ufunuo sura ya 8, kama ifuatavyo: “hukumu za baragumu” na “hukumu<br />

za vitasa”. Hizi za vitasa zinasemekana ndiyo mwisho wa ghadhabu ya Mungu (ona<br />

15:1). Lakini, kabla ya hukumu hizo za vitasa kuanza, Yohana anawaona “wale wenye<br />

kushinda, watokao kwa yule mnyama na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake,<br />

wamesimama kandokando ya hiyo bahari ya kioo” (15:2). Hawa watakatifu washindi<br />

yawezekana walinyakuliwa. Lakini tena, yawezekana walifia imani yao. Maandiko<br />

hayaelezi. Tena, hatujui kama mambo ya 15:2 yana uhusiano wowote na maelezo ya<br />

mambo yanayotajwa hapo.<br />

Kweli nyingine inayopatikana katika Ufunuo, yenye kuweza kuongezea uzito kwenye<br />

wazo la Unyakuo kutokea kabla ya mwisho wa miaka saba, ni hili: Wakati wa “hukumu<br />

ya baragumu” ya tano katika Ufunuo 9:1-12, tunaambiwa kwamba nzige wenye kuuma<br />

wataruhusiwa kuwadhuru wale tu “wasiokuwa na muhuri ya Mungu kwenye vipaji vya<br />

nyuso zao” (9:4). <strong>Watu</strong> pekee tunaoambiwa watakuwa na muhuri ni Waisraeli mia na<br />

arobaini na nne elfu (144,000) tu (ona Ufunuo 7:3-8). Basi inaonekana kwamba waamini<br />

wengine wote itabidi wanyakuliwe kabla ya baragumu hiyo ya tano ya hukumu;<br />

vinginevyo, hawataepuka nguvu za hao nzige waumao. Tena, kwa sababu nzige hao<br />

watawaumiza watu kwa miezi mitano (9:5, 10), inadhaniwa kwamba ni lazima Unyakuo<br />

utokee miezi mitano kabla ya kumalizika kwa miaka ile saba ya Dhiki.<br />

Kuna jinsi ya kufafanua hoja hizo. Pengine kuna wengine waliotiwa muhuru ambao<br />

hawatajwi katika kitabu cha Ufunuo. Vyovyote vile, kama hili linathibitisha kwamba<br />

Unyakuo utatokea kabla ya hukumu yabaragumu ya tano, pia linaonyesha kwamba kuna<br />

kundi moja la waamini ambao hawatanyakuliwa kabla ya kuachiwa kwa hao nzige<br />

waumao – wale Waisraeli mia na arobaini na nne elfu (144,000) waliotiwa muhuri. Ila,<br />

watakuwa na alama ya kuwalinda wasipatikane na ghadhabu ya Mungu, itakayokuwa<br />

inatolewa kwa njia ya nzige hao waumao.<br />

Tuhitimishe. Cha kusema ni kwamba bila shaka Unyakuo utatokea karibu na mwisho<br />

au mwishoni kabisa mwa ile miaka saba ya Dhiki. Waamini wasihofu kuhusu ghadhabu<br />

ya Mungu, lakini pia wawe tayari kwa ajili ya mateso makali na hata kufa kwa ajili ya<br />

imani yao.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!