18.04.2013 Views

galvmed brochure

galvmed brochure

galvmed brochure

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mamilioni ya makundi tete ya watu hutegemea<br />

mifugo kuendeshea maisha yao na kujikimu.<br />

Mifugo na mazao yake hugharimia mahitaji<br />

ya msingi ya kila siku na huwapatia fedha<br />

wakati wa shida.


Picha kwa hisani ya Anita Swarup Picha kwa hisani ya Steve Sloan<br />

Watu Bilioni moja wanaishi kwa kipato cha chini ya dola kwa siku<br />

Karibia milioni 700 ya watu hutegemea mifugo kuendesha maisha yao. Fedha inayopatikana kutokana na mauzo ya<br />

mifugo na mazao yake hugharamia elimu na huduma za afya. Wanyama hutoa samadi na hukokota zana za kilimo, hivyo<br />

kusaidia uzalishaji wa mazao, kutoa ajira na fursa za kibiashara. Mifugo husaidia majukumu muhimu ya kijamii na<br />

kiutamaduni kama vile utoaji wa mahari. Vifo vya wanyama kwa sababu ya magonjwa huathiri maisha ya wafugaji,<br />

familia na jamii ulimwenguni. Pale ambapo umaskini na mazingira havitoi njia nyingine, kuku, mbuzi, kondoo, ng’ombe<br />

na nguruwe humaanisha maisha, shule, mavazi, biashara, na chaguo la heshima na wito. Licha ya uhusiano wa karibu<br />

kati ya afya za wanyama wafugwao na afya za binadamu, kati ya wanyama wafugwao na maisha ya binadamu, ni 4% tu<br />

ya misaada ya kimataifa huelekezwa kwenye mahitaji ya kilimo kwenye nchi zinazoendelea.<br />

Dira na Dhamira ya GALVmed<br />

Dira<br />

> Kulinda wanyama, kuokoa maisha ya watu<br />

Dhamira<br />

> Kuletamaendeleo ya kudumu ya huduma ya<br />

utabibu wamifugo kwa wafugajimasikini katika nchi<br />

zinazoendelea<br />

> Kuendeleza, kuandikisha na kuzindua dawa 4 hadi<br />

6 za chanjo,madawa yamifugo au vifaa vya<br />

kuchunguzamagonjwa ifikapomwaka 2015 ili<br />

kukidhimahitaji ya wafugajimasikini<br />

> Kushirikiana namashirika wenza yaliyopo katika nchi<br />

zinazoendelea ili kuhakikisha utaratibu en delevu wa<br />

utoaji wa vifaa vipya kwa wafugaji masikini<br />

> Kutoa mfano bora na wenye mafanikio juu ya<br />

ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi na<br />

kuendelea kuongoza kiukanda, hivyo kuhakikisha<br />

utoaji wa vifaa vipya baada ya mwaka 2015<br />

Kuwa na shauku kubwa na kuzingatia utoaji wa vifaa vipya<br />

Si shirika tu bali ni utekelezaji wa kazi<br />

Utendaji kazi<br />

Kwa kushirikiana na uwanda mpana wa mashirika<br />

mengine, GALVmed (Global Alliance for Livestock<br />

Veterinary Medicines) inatengeneza chanjo, vifaa vya<br />

kuchunguza magonjwa na madawa ya mifugo,<br />

yanayopatikana kirahisi na kwa bei nafuu kwa<br />

mamilioni ya watu wanaotegemea mifugo.<br />

Kwa kuunga mkono Malengo ya Milenia, GALVmed<br />

inatafuta njia za kupambana na magonjwa yenye<br />

madhara makubwa na yale yaliyosahauliwa. Pale<br />

ambapo chanjo thabiti ipo, lakini upatikanaji wake ni<br />

mgumu, GALVmed na wabia wake hufanya kazi ya<br />

kuongeza uzalishaji na kushughulikia udhaifu katika njia<br />

za usambazaji. Hata hivyo, kwamagonjwamengine vifaa<br />

vipya vinahitajika. GALVmed inapokea na kutumia<br />

matokeo mazuri ya utafiti kutoka popote pale<br />

ulimwenguni na unaolenga uzalishaji na kutumika<br />

katika nchi zinazoendelea, pale inapobidi.<br />

1 Chanzo, Benki ya Dunia, 2007 Picha ya jalada la mbele, kwa hisani ya Getty Images


Changamoto za uwepo na upatikanaji wa huduma za afya za wanyama<br />

Uvumbuzi<br />

Changamoto za<br />

kiufundi<br />

Uhaba wa taarifa<br />

kuhusu bidhaa<br />

zinazofaa<br />

Mipango<br />

iliyopotoka<br />

kimawazo<br />

Shughuli za GALVmed<br />

> Kutoa kipaumbele kwenye magonjwa yenye madhara makubwa yanayoathiri zaidi wafugaji maskini<br />

> Kuelewa vipingamizimuhimu vinavyojitokeza katika uvumbuzi wa vifaa vipya vinavyoweza kupunguza<br />

madhara yamagonjwa katika nchi zinazoendelea<br />

> Kubaini rasilimali na kuziba mapengo muhimu ya kiutaalam<br />

Kupanga na kusimamiamiradi ya kuendeleza afya yamifugo<br />

> Kupanga na kusimamiamiradi ya kuendeleza afya ya mifugo<br />

Sifa za GALVmed<br />

> Kulenga njia za kuwapatia vifaa vipya vinavyofaa watu wenye uwezo mdogo<br />

> Msimamo (kutimizamalengo, viwango)<br />

> Uwazi katika taratibu na utoaji maamuzi<br />

> Uongozi katika ushirikiano na utendaji kazi<br />

Ujuziwa GALVmed<br />

> Ujuzi wa hali ya juu wa kiufundi<br />

> Umahiri katika kutengeneza na kusajili madawa ya mifugo<br />

> Usimamizi wamiradi nambinu za kutoa ushauri<br />

> Ujuzi wa agenda za maendeleo<br />

> Ujuzi wa kuchangisha fedha<br />

> Kuanzisha Ushirikiano<br />

Maendeleo<br />

Ukosefu wa fedha<br />

kwa ajili ya utafiti<br />

wa masuala ya<br />

maendeleo<br />

Ubunifumbovu,<br />

usimamizi mbaya<br />

wa utafiti<br />

Usajili<br />

Uwepo wa taratibu<br />

nyingi za kisheria na<br />

zisizoeleweka<br />

Ukosefuwa utaratibu<br />

unaohakikisha<br />

viwango vya ubora<br />

Mamlaka tofauti za<br />

serikali<br />

GALVmed inavyoshughulikia changamoto hizi<br />

Uzalishaji<br />

Ukosefu wa mvuto<br />

wa kibiashara<br />

Mchakato wenye<br />

gharama kubwa<br />

Ukosefuwa<br />

utaratibuwa<br />

maendeleo<br />

Uendeshaji wa<br />

Kibiashara<br />

Ukosefuwa soko la<br />

mauzo<br />

Ukadiriaji mbaya wa<br />

mahitaji au matakwa<br />

Ukubwa wa vifurushi<br />

usio sahihi<br />

Ukosefu wa ufahamu<br />

au elimu juu ya<br />

matumizi sahihi<br />

Ugawaji<br />

endelevu<br />

Ugawaji usiokuwa na<br />

msimamo<br />

Vifaa vya magendo<br />

Ukosefuwa njia za<br />

kuzuia uigaji wa<br />

uvumbuzi<br />

Vifaa na utekelezaji<br />

usio bora<br />

Dhima yetu ni kuwezesha na kuongoza katika kukabiliana na changamoto hizi kwa kuwa na ubia ambao<br />

unamwezesha mfugaji maskini kuweza kupata huduma za afya kwa wanyama. GALVmed inashughulikia udhaifu<br />

katika mlolongo, kutoka kwenye uzalishaji wa bidhaa hadi kumfikia mnyama.<br />

>>


Picha kwa hisani ya Stuart Brown<br />

GALVmed ni nini?<br />

GALVmed ni shirikisho la kiulimwengu lisilo la<br />

kibiashara na ni la ubia wa sekta binafsi na sekta ya<br />

umma. Ina wanachama, wadau na washirika ambao<br />

ni pamoja na:<br />

Shirika la Chakula na Kilimo la UmojawaMataifa (FAO)<br />

Shirika la Afya yaWanyama Duniani (OIE)<br />

Umojawa Afrika (AU-IBAR)<br />

Umoja wa Ulaya<br />

Serikali za Nchi Zinazoendelea<br />

Kituo cha Utafiti wa Kilimo kwa ajili ya Maendeleo ya<br />

Kimataifa cha Ufaransa CIRAD<br />

Shirika la Kimataifa la Afya ya Wanyama (IFAH)<br />

Asasi za Kiraia kama vile FARM-Africa, Africare,<br />

VETAID, Mercy Corps, NESPOD na BAIF<br />

Wamaasai waishio Kaskazini mwa Tanzania waliiambia GALVmed<br />

Hakuna Chanjo ya<br />

Ndigana kali –<br />

Hakuna Ng’ombe.<br />

Hakuna ng’ombe –<br />

Hakuna Wamaasai<br />

Taasisi za utafiti na za elimu za nchi zilioendelea na<br />

zinazoendelea, ikiwa ni pamoja na Taasisi ya Kimataifa<br />

ya Utafiti wa Mifugo (ILRI), Chuo cha Mifugo cha<br />

Onderstepoort (OVI); Watengenezajiwa chanjo za<br />

wanyama, Vifaa vya Kibiologia vya Onderstepoort<br />

(OBP); Taasisi ya Taifa UtabibuwaMifugo, Ethiopia<br />

(NVI); Taasisi ya Taifa ya Utibabu wa Mifugo Botswana<br />

(BVI); Learned Society, Chama cha Wataalamu wa<br />

Mifugo Uingereza; Chuo cha UtafitiMifugo cha Tamil<br />

Nadu, Taasisi ya Utafiti ya Moredun (MRI), pamojab na<br />

washiriki binafsi kamamashirika ya afya ya wanyama:<br />

Pfizer,Merial, Intervet, CEVA Animal Health; kampuni<br />

za uchunguzi wa magonjwa, IDEXX na Indian<br />

Immunologicals Limited.<br />

GALVmed haiwezi kutatua matatizo yote peke yake, ila<br />

ni mojawapo ya sululisho. Mwanzoni GALVmed ilianza<br />

shughuli zake Novemba 2005, na kuanzia Septemba<br />

2008 ilianza kukuza muundo wake pamoja na utendaji<br />

wake wa kazi. Baada ya hapo, imefanya juhudi kubwa<br />

za kuongeza zanaa zake kwa kusudi maalumu ya<br />

kuendeleza uchunguzi wa magonjwa, dawa za chanjo<br />

na madawa ya kukabili magonjwa ya mifugo.


Picha kwa hisani ya Anita Swarup<br />

GALVmed inatiliamkazomagonjwamuhimu<br />

ambayo yanahusiana zaidi na utaratibu wa<br />

kupunguza umasikini na kuboresha ustawi wa<br />

maisha katika maeneo yaliolengwa. Magonjwa<br />

haya yamegawanywa katika makunde manne:<br />

magonjwa ya ng’ombe, ya wanyama wadogo<br />

wanaocheua, nguruwe na ndege, ijapokuwa<br />

kuna magonjwa yanayoathiri makundi yote. Vifo<br />

vya wanyama vinavyosababishwa na magonjwa<br />

vinawaacha wafugaji wengi wawe katika hali<br />

mbaya, kwa hiyo dawa za chanjo na matibabu ni<br />

muhimu katika uchumi wao na zinachangia<br />

kudumisha afya za wafugaji na familia zao.<br />

Marry, Kiongozi wa Chama cha Wanawake Kijiji cha Mairowa,<br />

Longido, Tanzania<br />

Magonjwa yanayotiliwa mkazo na GALVmed<br />

Kwa sababu ya dawa ya<br />

chanjo, Nimefanikiwa kupata<br />

ndamawengi ambao<br />

ninawauza na kuweza kulipa<br />

ada ya shule. Ninaweza<br />

kutenga pesa za ada ya shule<br />

kwa sababu ninajua kwamba<br />

Ndama wana afya nzuri<br />

Ng’ombe<br />

Ndingana kali<br />

Ugonjwa wa Homa ya Mapafu ya Ng’ombe<br />

Ugonjwa wa Hemorrhagic Septicaemia<br />

Ugonjwa wa Nagana<br />

Wanyama wadogo wanaocheua<br />

Virusi vyamaradhi vinavyoambukizambuzi na<br />

kondoo<br />

Ugonjwa wa Homa ya Mapafu ya Mbuzi<br />

Kondoo & Mbuzi<br />

Ndui ya kondoo na mbuzi<br />

Nguruwe<br />

Ugonjwa waminyoo ya nguruwe<br />

Ugonjwa wa homa ya nguruwe<br />

Homa yamafua ya nguruwe<br />

Ndege<br />

Ugonjwa wa Mdondo wa Kuku<br />

Mafua Makali ya Ndege<br />

Magonjwa yanayoathiri makundi yote<br />

Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa<br />

>>


Picha kwa hisani ya Steve Sloan<br />

Kutafuta Ufumbuzi wa Matatizo<br />

Magonjwa ya kipaumbele ambayo GALVmed na wabia<br />

wake wanayashughulikia ni:<br />

Ndingana kali (East Coast Fever) Ndigana inaua kadiri<br />

ya ng’ombe milioni moja kila mwaka Afrika, ingawa<br />

chanjo yake ambayo hutengenezwa na Taasisi ya<br />

Kimataifa ya Utafiti wa Mifugo iliyopo Nairobi imekuwepo<br />

tangu mwaka 1970. Hivi sasa, chanjo hiyo haipatikani<br />

kirahisi na idadi ya mwisho ya dawa ilitegenezwamwaka<br />

1996. Tiba ya ugonjwa huu imetimizamafanikio ya tiba<br />

kwa asilimia 98% nchini Tanzania, na kwa kushirikiana<br />

na ILRI, GALVmed inafanya mpango wa kuweza<br />

kurahisisha upatikanaji wa chanjo kwa bei rahisimara tu<br />

itakaposajiliwa. Usajili unahitaji msimamo thabiti wa<br />

majaribio ili kuhakikisha usalama wa dawa na<br />

kuhakikisha uwezekano wa kufanya biashara na<br />

kuanzisha mtandao wa ununuzi na kutoa huduma ili<br />

kuwapatia kipato watu waliopo katika nchi<br />

zinazoendelea. Mpaka sasa GALVmed imefanikiwa<br />

kusajili dawa ya chanjo nchini Kenya, Tanzania na<br />

Malawi.<br />

Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever)<br />

ni ugonjwa unaoambukizwa na mbu na unaua binadamu<br />

pamoja na wanyama. Kwa sababu huwa inatokea kila<br />

baada yamiaka 5 hadi 7, wafugaji wenyemapatomadogo<br />

wanasita kuchanjamifugo dhidi ya ugonjwa huu. Kama<br />

wafugaji wakichanganya chanjo dhidi ya ugonjwa huu na<br />

chanjo zamagonjwamengine kama vile Ugonjwa wa<br />

Mapele ngozi au Ndui ya Kondoo/Mbuzi, wafugaji<br />

watapatamafanikiomakubwa.<br />

Ugonjwawa Mdondo wa Kuku (Newcastle Disease)<br />

inaua kadiri ya asilimia 100% ya kuku,mabata. Katika<br />

bara la Afrika tu,milioni 589 ya kuku wako katika hatari<br />

ya kuambukizwa na ugonjwa huo ambao unaweza<br />

Kimani Merendei, Tanzania<br />

Dawa ya chanjo dhidi ya<br />

Ndigana Kali inanipa amani.<br />

Maisha yangu yamezidi kuwa<br />

mazuri. Nataka watoto wangu<br />

wapate kazi mjini auwawe na<br />

ng’ombe au mashamba ya<br />

kisasa.<br />

kuambukiza kuku ambao nimuhimu kwamaisha ya<br />

mamilioni ya wananchi wenye uwezomdogo. Chanjo<br />

dhidi ya ugonjwa huu unapatikana kwa wafugaji<br />

wanaofanya biashara, lakini ukubwa wa kifurushi na<br />

mahitaji ya frigi inakuwa ngumu kwa wafugajimasikini<br />

kupata dawa hizi za chanjo. GALVmed inashirikiana na<br />

washiriki wenza katikambinu za kukabilimasuala haya.<br />

Ugonjwa wa minyoo ya nguruwe (Porcine Cysticercsis)<br />

ni ugonjwa ulionea Afrika, Amerika ya Kusini na Asia.<br />

Nguruwe walioambukizwa inabidi wauzwe kwa bei<br />

rahisi au inabidi wauwawe. Ugonjwa huu pia unaweza<br />

kuathiri binadamu na kusababisha uvimbe katika<br />

ubongo wa binadamu, na inasemekana ugonjwa huu<br />

unasababisha vifo 50,000 kwamwaka katika nchi<br />

zinazoendelea, na pia husababisha kati ya asilimia<br />

20 – 50% ya ugonjwa wa kifafa duniani ambao huwa<br />

unajitokeza baada yamuda, na kuletamadharamakubwa<br />

katikamaisha ya watu. GALVmed na washiriki wenza<br />

wanafanya jitihada za kuhakikisha kwamba dawa za<br />

chanjo na madawa yanayohitajika dhidi ya ugonjwa huu<br />

wa nguruwe, hii ikiwa ni njiamojawapo ya kupunguza<br />

hatari ya kumuambukiza binadamu.<br />

GALVmed pia imeanza kujishughulisha namagonjwa<br />

mengine, kama vile Ugonjwa wa Homa yaMapafu ya<br />

Ng’ombe ambao ni ugonjwa wamlipuko usiokuwa na<br />

mpaka na huletamadharamakubwa Afrika; Ugonjwa wa<br />

Homa yaMapafu yaMbuzi ni ugonjwa unaoweza kuua<br />

kati ya asilimia 60 – 100% yambuzi walioambukizwa, na<br />

Virusi vyamaradhi vinavyoambukizambuzi na kondoo ni<br />

ugonjwa unaothiri uchumi na ulianza kujitokeza<br />

mwanzoni wamwaka 1980.


Picha kwa hisani ya Meritxell Donadeu Picha kwa hisani ya WRENmedia<br />

Mtizamo wa Biashara wa GALVmed<br />

Ukweli<br />

Bilioni 1.1 yawatuwanaishi kwa pato la chini ya dola 1<br />

kwa siku<br />

(Bill & Melinda Gates Foundation)<br />

Karibu bilioni 2.5 yawatuwanaishi kwa pato la chini ya<br />

dola 2 kwa siku<br />

(Bill & Melinda Gates Foundation)<br />

Bilioni 1.02 yawatu hawana chakula cha kutosha – idadi<br />

hii ni zaidi yawananchiwanaoishi Amerika, Kanada<br />

pamoja na Jumuia ya Ulaya<br />

(FAO 19 June 2009)<br />

Licha yaMalengo yaMaendeleo yaMilenia, idadi ya watu<br />

wasio na lishe bora duniani imeongezeka na<br />

kufikiamilioni 75mwaka 2007 namwaka 2008 kufikia<br />

milioni 40, na sababu kubwa ni ongezeko la bei ya<br />

chakula<br />

(FAO 9 Dec 2008)<br />

Kati yawatotomilioni 9.7, asilimia 53%yawatoto<br />

wanakufa kwa kosefuwa lishe bora katika nchi<br />

zinazoendelea kilamwaka – mtotommoja kila sekunde 6<br />

(FAO 2004)<br />

Ni asilimia 4%tu yamsaadawa kimataifa ndiyo<br />

inatumika katika shughuli za kilimo duniani<br />

(World Bank, 2007).<br />

Malengo muhimu<br />

> Uongozi<br />

> Mtizamo<br />

> Mikakati<br />

> Ushirikiano<br />

> Utaratibu waMaendeleo<br />

> Kutafuta njiampya<br />

> Usimamizi + Ukadiriaji<br />

Lengo la 1<br />

Kuandaa nyenzo za kufanya maamuzi kwa kuzingatia<br />

takwimu juu ya athari za kiuchumi na kijamii na<br />

uelewa wa masoko<br />

Lengo la 2<br />

Kutengeneza chanjo dhidi ya magonjwa 6 ya<br />

wanyama ambazo ni muhimu katika kupunguza<br />

umasikini na maisha ya watu<br />

Lengo la 3<br />

Kushughulikia Utumiaji, Upatikanaji, Ugawaji<br />

mlolongo wenye faida na kuelezea juu ya maendeleo<br />

endelevu<br />

Lengo la 4<br />

Kurahisishamawasiliano + mtandao katika ngazi zote<br />

ili kuwe na uwezo wa kufuatiliamabadiliko yamipango<br />

na utekelezaji


Wasiliana na GALVmed:<br />

Ofisi ya Uingereza:<br />

Doherty Building, Pentlands Science Park, Bush Loan, Edinburgh EH26 0PZ, UK<br />

Simu: +44 (0)131 445 6264<br />

Nukushi: +44 (0)131 445 6222<br />

Barua peper: info@<strong>galvmed</strong>.org<br />

Ofisi ya Afrika:<br />

Ghorofa ya Kwanza, Tawi la Magharibi, A.K.D. House II, Fairgrounds, Kitalu No. 54478,<br />

Gaborone – Botswana, S.L.P. 45108, Gaborone<br />

Simu: +267 3121 202/203/209<br />

Barua pepe: info@<strong>galvmed</strong>.org<br />

www.<strong>galvmed</strong>.org<br />

Kwa sasa inafadhiliwa na:<br />

GALVmed imesajiliwa kama shirikisho la kiulimwengu la kimsaada na lisilo la kibiashara linalohusisha ubia wa sekta ya umma, sekta binafsi na serikali.<br />

Imesajiliwa Scotland kama shirika la msaada SC039197 Imesajiliwa kama shirika la msaada England na Wales: 1115606<br />

Jina la usajili: Global Alliance for Livestock and Veterinary Medicines<br />

Imesajiliwa England na Wales Na. 5393391, kwa ukomo wa udhamini<br />

Ofisi ya usajili: Maclay Murray & Spens, One London Wall, London EC2Y 5AB, UA

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!