Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mamilioni ya makundi tete ya watu hutegemea<br />
mifugo kuendeshea maisha yao na kujikimu.<br />
Mifugo na mazao yake hugharimia mahitaji<br />
ya msingi ya kila siku na huwapatia fedha<br />
wakati wa shida.
Picha kwa hisani ya Anita Swarup Picha kwa hisani ya Steve Sloan<br />
Watu Bilioni moja wanaishi kwa kipato cha chini ya dola kwa siku<br />
Karibia milioni 700 ya watu hutegemea mifugo kuendesha maisha yao. Fedha inayopatikana kutokana na mauzo ya<br />
mifugo na mazao yake hugharamia elimu na huduma za afya. Wanyama hutoa samadi na hukokota zana za kilimo, hivyo<br />
kusaidia uzalishaji wa mazao, kutoa ajira na fursa za kibiashara. Mifugo husaidia majukumu muhimu ya kijamii na<br />
kiutamaduni kama vile utoaji wa mahari. Vifo vya wanyama kwa sababu ya magonjwa huathiri maisha ya wafugaji,<br />
familia na jamii ulimwenguni. Pale ambapo umaskini na mazingira havitoi njia nyingine, kuku, mbuzi, kondoo, ng’ombe<br />
na nguruwe humaanisha maisha, shule, mavazi, biashara, na chaguo la heshima na wito. Licha ya uhusiano wa karibu<br />
kati ya afya za wanyama wafugwao na afya za binadamu, kati ya wanyama wafugwao na maisha ya binadamu, ni 4% tu<br />
ya misaada ya kimataifa huelekezwa kwenye mahitaji ya kilimo kwenye nchi zinazoendelea.<br />
Dira na Dhamira ya GALVmed<br />
Dira<br />
> Kulinda wanyama, kuokoa maisha ya watu<br />
Dhamira<br />
> Kuletamaendeleo ya kudumu ya huduma ya<br />
utabibu wamifugo kwa wafugajimasikini katika nchi<br />
zinazoendelea<br />
> Kuendeleza, kuandikisha na kuzindua dawa 4 hadi<br />
6 za chanjo,madawa yamifugo au vifaa vya<br />
kuchunguzamagonjwa ifikapomwaka 2015 ili<br />
kukidhimahitaji ya wafugajimasikini<br />
> Kushirikiana namashirika wenza yaliyopo katika nchi<br />
zinazoendelea ili kuhakikisha utaratibu en delevu wa<br />
utoaji wa vifaa vipya kwa wafugaji masikini<br />
> Kutoa mfano bora na wenye mafanikio juu ya<br />
ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi na<br />
kuendelea kuongoza kiukanda, hivyo kuhakikisha<br />
utoaji wa vifaa vipya baada ya mwaka 2015<br />
Kuwa na shauku kubwa na kuzingatia utoaji wa vifaa vipya<br />
Si shirika tu bali ni utekelezaji wa kazi<br />
Utendaji kazi<br />
Kwa kushirikiana na uwanda mpana wa mashirika<br />
mengine, GALVmed (Global Alliance for Livestock<br />
Veterinary Medicines) inatengeneza chanjo, vifaa vya<br />
kuchunguza magonjwa na madawa ya mifugo,<br />
yanayopatikana kirahisi na kwa bei nafuu kwa<br />
mamilioni ya watu wanaotegemea mifugo.<br />
Kwa kuunga mkono Malengo ya Milenia, GALVmed<br />
inatafuta njia za kupambana na magonjwa yenye<br />
madhara makubwa na yale yaliyosahauliwa. Pale<br />
ambapo chanjo thabiti ipo, lakini upatikanaji wake ni<br />
mgumu, GALVmed na wabia wake hufanya kazi ya<br />
kuongeza uzalishaji na kushughulikia udhaifu katika njia<br />
za usambazaji. Hata hivyo, kwamagonjwamengine vifaa<br />
vipya vinahitajika. GALVmed inapokea na kutumia<br />
matokeo mazuri ya utafiti kutoka popote pale<br />
ulimwenguni na unaolenga uzalishaji na kutumika<br />
katika nchi zinazoendelea, pale inapobidi.<br />
1 Chanzo, Benki ya Dunia, 2007 Picha ya jalada la mbele, kwa hisani ya Getty Images
Changamoto za uwepo na upatikanaji wa huduma za afya za wanyama<br />
Uvumbuzi<br />
Changamoto za<br />
kiufundi<br />
Uhaba wa taarifa<br />
kuhusu bidhaa<br />
zinazofaa<br />
Mipango<br />
iliyopotoka<br />
kimawazo<br />
Shughuli za GALVmed<br />
> Kutoa kipaumbele kwenye magonjwa yenye madhara makubwa yanayoathiri zaidi wafugaji maskini<br />
> Kuelewa vipingamizimuhimu vinavyojitokeza katika uvumbuzi wa vifaa vipya vinavyoweza kupunguza<br />
madhara yamagonjwa katika nchi zinazoendelea<br />
> Kubaini rasilimali na kuziba mapengo muhimu ya kiutaalam<br />
Kupanga na kusimamiamiradi ya kuendeleza afya yamifugo<br />
> Kupanga na kusimamiamiradi ya kuendeleza afya ya mifugo<br />
Sifa za GALVmed<br />
> Kulenga njia za kuwapatia vifaa vipya vinavyofaa watu wenye uwezo mdogo<br />
> Msimamo (kutimizamalengo, viwango)<br />
> Uwazi katika taratibu na utoaji maamuzi<br />
> Uongozi katika ushirikiano na utendaji kazi<br />
Ujuziwa GALVmed<br />
> Ujuzi wa hali ya juu wa kiufundi<br />
> Umahiri katika kutengeneza na kusajili madawa ya mifugo<br />
> Usimamizi wamiradi nambinu za kutoa ushauri<br />
> Ujuzi wa agenda za maendeleo<br />
> Ujuzi wa kuchangisha fedha<br />
> Kuanzisha Ushirikiano<br />
Maendeleo<br />
Ukosefu wa fedha<br />
kwa ajili ya utafiti<br />
wa masuala ya<br />
maendeleo<br />
Ubunifumbovu,<br />
usimamizi mbaya<br />
wa utafiti<br />
Usajili<br />
Uwepo wa taratibu<br />
nyingi za kisheria na<br />
zisizoeleweka<br />
Ukosefuwa utaratibu<br />
unaohakikisha<br />
viwango vya ubora<br />
Mamlaka tofauti za<br />
serikali<br />
GALVmed inavyoshughulikia changamoto hizi<br />
Uzalishaji<br />
Ukosefu wa mvuto<br />
wa kibiashara<br />
Mchakato wenye<br />
gharama kubwa<br />
Ukosefuwa<br />
utaratibuwa<br />
maendeleo<br />
Uendeshaji wa<br />
Kibiashara<br />
Ukosefuwa soko la<br />
mauzo<br />
Ukadiriaji mbaya wa<br />
mahitaji au matakwa<br />
Ukubwa wa vifurushi<br />
usio sahihi<br />
Ukosefu wa ufahamu<br />
au elimu juu ya<br />
matumizi sahihi<br />
Ugawaji<br />
endelevu<br />
Ugawaji usiokuwa na<br />
msimamo<br />
Vifaa vya magendo<br />
Ukosefuwa njia za<br />
kuzuia uigaji wa<br />
uvumbuzi<br />
Vifaa na utekelezaji<br />
usio bora<br />
Dhima yetu ni kuwezesha na kuongoza katika kukabiliana na changamoto hizi kwa kuwa na ubia ambao<br />
unamwezesha mfugaji maskini kuweza kupata huduma za afya kwa wanyama. GALVmed inashughulikia udhaifu<br />
katika mlolongo, kutoka kwenye uzalishaji wa bidhaa hadi kumfikia mnyama.<br />
>>
Picha kwa hisani ya Stuart Brown<br />
GALVmed ni nini?<br />
GALVmed ni shirikisho la kiulimwengu lisilo la<br />
kibiashara na ni la ubia wa sekta binafsi na sekta ya<br />
umma. Ina wanachama, wadau na washirika ambao<br />
ni pamoja na:<br />
Shirika la Chakula na Kilimo la UmojawaMataifa (FAO)<br />
Shirika la Afya yaWanyama Duniani (OIE)<br />
Umojawa Afrika (AU-IBAR)<br />
Umoja wa Ulaya<br />
Serikali za Nchi Zinazoendelea<br />
Kituo cha Utafiti wa Kilimo kwa ajili ya Maendeleo ya<br />
Kimataifa cha Ufaransa CIRAD<br />
Shirika la Kimataifa la Afya ya Wanyama (IFAH)<br />
Asasi za Kiraia kama vile FARM-Africa, Africare,<br />
VETAID, Mercy Corps, NESPOD na BAIF<br />
Wamaasai waishio Kaskazini mwa Tanzania waliiambia GALVmed<br />
Hakuna Chanjo ya<br />
Ndigana kali –<br />
Hakuna Ng’ombe.<br />
Hakuna ng’ombe –<br />
Hakuna Wamaasai<br />
Taasisi za utafiti na za elimu za nchi zilioendelea na<br />
zinazoendelea, ikiwa ni pamoja na Taasisi ya Kimataifa<br />
ya Utafiti wa Mifugo (ILRI), Chuo cha Mifugo cha<br />
Onderstepoort (OVI); Watengenezajiwa chanjo za<br />
wanyama, Vifaa vya Kibiologia vya Onderstepoort<br />
(OBP); Taasisi ya Taifa UtabibuwaMifugo, Ethiopia<br />
(NVI); Taasisi ya Taifa ya Utibabu wa Mifugo Botswana<br />
(BVI); Learned Society, Chama cha Wataalamu wa<br />
Mifugo Uingereza; Chuo cha UtafitiMifugo cha Tamil<br />
Nadu, Taasisi ya Utafiti ya Moredun (MRI), pamojab na<br />
washiriki binafsi kamamashirika ya afya ya wanyama:<br />
Pfizer,Merial, Intervet, CEVA Animal Health; kampuni<br />
za uchunguzi wa magonjwa, IDEXX na Indian<br />
Immunologicals Limited.<br />
GALVmed haiwezi kutatua matatizo yote peke yake, ila<br />
ni mojawapo ya sululisho. Mwanzoni GALVmed ilianza<br />
shughuli zake Novemba 2005, na kuanzia Septemba<br />
2008 ilianza kukuza muundo wake pamoja na utendaji<br />
wake wa kazi. Baada ya hapo, imefanya juhudi kubwa<br />
za kuongeza zanaa zake kwa kusudi maalumu ya<br />
kuendeleza uchunguzi wa magonjwa, dawa za chanjo<br />
na madawa ya kukabili magonjwa ya mifugo.
Picha kwa hisani ya Anita Swarup<br />
GALVmed inatiliamkazomagonjwamuhimu<br />
ambayo yanahusiana zaidi na utaratibu wa<br />
kupunguza umasikini na kuboresha ustawi wa<br />
maisha katika maeneo yaliolengwa. Magonjwa<br />
haya yamegawanywa katika makunde manne:<br />
magonjwa ya ng’ombe, ya wanyama wadogo<br />
wanaocheua, nguruwe na ndege, ijapokuwa<br />
kuna magonjwa yanayoathiri makundi yote. Vifo<br />
vya wanyama vinavyosababishwa na magonjwa<br />
vinawaacha wafugaji wengi wawe katika hali<br />
mbaya, kwa hiyo dawa za chanjo na matibabu ni<br />
muhimu katika uchumi wao na zinachangia<br />
kudumisha afya za wafugaji na familia zao.<br />
Marry, Kiongozi wa Chama cha Wanawake Kijiji cha Mairowa,<br />
Longido, Tanzania<br />
Magonjwa yanayotiliwa mkazo na GALVmed<br />
Kwa sababu ya dawa ya<br />
chanjo, Nimefanikiwa kupata<br />
ndamawengi ambao<br />
ninawauza na kuweza kulipa<br />
ada ya shule. Ninaweza<br />
kutenga pesa za ada ya shule<br />
kwa sababu ninajua kwamba<br />
Ndama wana afya nzuri<br />
Ng’ombe<br />
Ndingana kali<br />
Ugonjwa wa Homa ya Mapafu ya Ng’ombe<br />
Ugonjwa wa Hemorrhagic Septicaemia<br />
Ugonjwa wa Nagana<br />
Wanyama wadogo wanaocheua<br />
Virusi vyamaradhi vinavyoambukizambuzi na<br />
kondoo<br />
Ugonjwa wa Homa ya Mapafu ya Mbuzi<br />
Kondoo & Mbuzi<br />
Ndui ya kondoo na mbuzi<br />
Nguruwe<br />
Ugonjwa waminyoo ya nguruwe<br />
Ugonjwa wa homa ya nguruwe<br />
Homa yamafua ya nguruwe<br />
Ndege<br />
Ugonjwa wa Mdondo wa Kuku<br />
Mafua Makali ya Ndege<br />
Magonjwa yanayoathiri makundi yote<br />
Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa<br />
>>
Picha kwa hisani ya Steve Sloan<br />
Kutafuta Ufumbuzi wa Matatizo<br />
Magonjwa ya kipaumbele ambayo GALVmed na wabia<br />
wake wanayashughulikia ni:<br />
Ndingana kali (East Coast Fever) Ndigana inaua kadiri<br />
ya ng’ombe milioni moja kila mwaka Afrika, ingawa<br />
chanjo yake ambayo hutengenezwa na Taasisi ya<br />
Kimataifa ya Utafiti wa Mifugo iliyopo Nairobi imekuwepo<br />
tangu mwaka 1970. Hivi sasa, chanjo hiyo haipatikani<br />
kirahisi na idadi ya mwisho ya dawa ilitegenezwamwaka<br />
1996. Tiba ya ugonjwa huu imetimizamafanikio ya tiba<br />
kwa asilimia 98% nchini Tanzania, na kwa kushirikiana<br />
na ILRI, GALVmed inafanya mpango wa kuweza<br />
kurahisisha upatikanaji wa chanjo kwa bei rahisimara tu<br />
itakaposajiliwa. Usajili unahitaji msimamo thabiti wa<br />
majaribio ili kuhakikisha usalama wa dawa na<br />
kuhakikisha uwezekano wa kufanya biashara na<br />
kuanzisha mtandao wa ununuzi na kutoa huduma ili<br />
kuwapatia kipato watu waliopo katika nchi<br />
zinazoendelea. Mpaka sasa GALVmed imefanikiwa<br />
kusajili dawa ya chanjo nchini Kenya, Tanzania na<br />
Malawi.<br />
Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever)<br />
ni ugonjwa unaoambukizwa na mbu na unaua binadamu<br />
pamoja na wanyama. Kwa sababu huwa inatokea kila<br />
baada yamiaka 5 hadi 7, wafugaji wenyemapatomadogo<br />
wanasita kuchanjamifugo dhidi ya ugonjwa huu. Kama<br />
wafugaji wakichanganya chanjo dhidi ya ugonjwa huu na<br />
chanjo zamagonjwamengine kama vile Ugonjwa wa<br />
Mapele ngozi au Ndui ya Kondoo/Mbuzi, wafugaji<br />
watapatamafanikiomakubwa.<br />
Ugonjwawa Mdondo wa Kuku (Newcastle Disease)<br />
inaua kadiri ya asilimia 100% ya kuku,mabata. Katika<br />
bara la Afrika tu,milioni 589 ya kuku wako katika hatari<br />
ya kuambukizwa na ugonjwa huo ambao unaweza<br />
Kimani Merendei, Tanzania<br />
Dawa ya chanjo dhidi ya<br />
Ndigana Kali inanipa amani.<br />
Maisha yangu yamezidi kuwa<br />
mazuri. Nataka watoto wangu<br />
wapate kazi mjini auwawe na<br />
ng’ombe au mashamba ya<br />
kisasa.<br />
kuambukiza kuku ambao nimuhimu kwamaisha ya<br />
mamilioni ya wananchi wenye uwezomdogo. Chanjo<br />
dhidi ya ugonjwa huu unapatikana kwa wafugaji<br />
wanaofanya biashara, lakini ukubwa wa kifurushi na<br />
mahitaji ya frigi inakuwa ngumu kwa wafugajimasikini<br />
kupata dawa hizi za chanjo. GALVmed inashirikiana na<br />
washiriki wenza katikambinu za kukabilimasuala haya.<br />
Ugonjwa wa minyoo ya nguruwe (Porcine Cysticercsis)<br />
ni ugonjwa ulionea Afrika, Amerika ya Kusini na Asia.<br />
Nguruwe walioambukizwa inabidi wauzwe kwa bei<br />
rahisi au inabidi wauwawe. Ugonjwa huu pia unaweza<br />
kuathiri binadamu na kusababisha uvimbe katika<br />
ubongo wa binadamu, na inasemekana ugonjwa huu<br />
unasababisha vifo 50,000 kwamwaka katika nchi<br />
zinazoendelea, na pia husababisha kati ya asilimia<br />
20 – 50% ya ugonjwa wa kifafa duniani ambao huwa<br />
unajitokeza baada yamuda, na kuletamadharamakubwa<br />
katikamaisha ya watu. GALVmed na washiriki wenza<br />
wanafanya jitihada za kuhakikisha kwamba dawa za<br />
chanjo na madawa yanayohitajika dhidi ya ugonjwa huu<br />
wa nguruwe, hii ikiwa ni njiamojawapo ya kupunguza<br />
hatari ya kumuambukiza binadamu.<br />
GALVmed pia imeanza kujishughulisha namagonjwa<br />
mengine, kama vile Ugonjwa wa Homa yaMapafu ya<br />
Ng’ombe ambao ni ugonjwa wamlipuko usiokuwa na<br />
mpaka na huletamadharamakubwa Afrika; Ugonjwa wa<br />
Homa yaMapafu yaMbuzi ni ugonjwa unaoweza kuua<br />
kati ya asilimia 60 – 100% yambuzi walioambukizwa, na<br />
Virusi vyamaradhi vinavyoambukizambuzi na kondoo ni<br />
ugonjwa unaothiri uchumi na ulianza kujitokeza<br />
mwanzoni wamwaka 1980.
Picha kwa hisani ya Meritxell Donadeu Picha kwa hisani ya WRENmedia<br />
Mtizamo wa Biashara wa GALVmed<br />
Ukweli<br />
Bilioni 1.1 yawatuwanaishi kwa pato la chini ya dola 1<br />
kwa siku<br />
(Bill & Melinda Gates Foundation)<br />
Karibu bilioni 2.5 yawatuwanaishi kwa pato la chini ya<br />
dola 2 kwa siku<br />
(Bill & Melinda Gates Foundation)<br />
Bilioni 1.02 yawatu hawana chakula cha kutosha – idadi<br />
hii ni zaidi yawananchiwanaoishi Amerika, Kanada<br />
pamoja na Jumuia ya Ulaya<br />
(FAO 19 June 2009)<br />
Licha yaMalengo yaMaendeleo yaMilenia, idadi ya watu<br />
wasio na lishe bora duniani imeongezeka na<br />
kufikiamilioni 75mwaka 2007 namwaka 2008 kufikia<br />
milioni 40, na sababu kubwa ni ongezeko la bei ya<br />
chakula<br />
(FAO 9 Dec 2008)<br />
Kati yawatotomilioni 9.7, asilimia 53%yawatoto<br />
wanakufa kwa kosefuwa lishe bora katika nchi<br />
zinazoendelea kilamwaka – mtotommoja kila sekunde 6<br />
(FAO 2004)<br />
Ni asilimia 4%tu yamsaadawa kimataifa ndiyo<br />
inatumika katika shughuli za kilimo duniani<br />
(World Bank, 2007).<br />
Malengo muhimu<br />
> Uongozi<br />
> Mtizamo<br />
> Mikakati<br />
> Ushirikiano<br />
> Utaratibu waMaendeleo<br />
> Kutafuta njiampya<br />
> Usimamizi + Ukadiriaji<br />
Lengo la 1<br />
Kuandaa nyenzo za kufanya maamuzi kwa kuzingatia<br />
takwimu juu ya athari za kiuchumi na kijamii na<br />
uelewa wa masoko<br />
Lengo la 2<br />
Kutengeneza chanjo dhidi ya magonjwa 6 ya<br />
wanyama ambazo ni muhimu katika kupunguza<br />
umasikini na maisha ya watu<br />
Lengo la 3<br />
Kushughulikia Utumiaji, Upatikanaji, Ugawaji<br />
mlolongo wenye faida na kuelezea juu ya maendeleo<br />
endelevu<br />
Lengo la 4<br />
Kurahisishamawasiliano + mtandao katika ngazi zote<br />
ili kuwe na uwezo wa kufuatiliamabadiliko yamipango<br />
na utekelezaji
Wasiliana na GALVmed:<br />
Ofisi ya Uingereza:<br />
Doherty Building, Pentlands Science Park, Bush Loan, Edinburgh EH26 0PZ, UK<br />
Simu: +44 (0)131 445 6264<br />
Nukushi: +44 (0)131 445 6222<br />
Barua peper: info@<strong>galvmed</strong>.org<br />
Ofisi ya Afrika:<br />
Ghorofa ya Kwanza, Tawi la Magharibi, A.K.D. House II, Fairgrounds, Kitalu No. 54478,<br />
Gaborone – Botswana, S.L.P. 45108, Gaborone<br />
Simu: +267 3121 202/203/209<br />
Barua pepe: info@<strong>galvmed</strong>.org<br />
www.<strong>galvmed</strong>.org<br />
Kwa sasa inafadhiliwa na:<br />
GALVmed imesajiliwa kama shirikisho la kiulimwengu la kimsaada na lisilo la kibiashara linalohusisha ubia wa sekta ya umma, sekta binafsi na serikali.<br />
Imesajiliwa Scotland kama shirika la msaada SC039197 Imesajiliwa kama shirika la msaada England na Wales: 1115606<br />
Jina la usajili: Global Alliance for Livestock and Veterinary Medicines<br />
Imesajiliwa England na Wales Na. 5393391, kwa ukomo wa udhamini<br />
Ofisi ya usajili: Maclay Murray & Spens, One London Wall, London EC2Y 5AB, UA