08.06.2013 Views

“Nguo za Utawa [Zifunikazo]” sehemu - Salah Allah

“Nguo za Utawa [Zifunikazo]” sehemu - Salah Allah

“Nguo za Utawa [Zifunikazo]” sehemu - Salah Allah

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>“Nguo</strong> <strong>za</strong> <strong>Utawa</strong> [<strong>Zifunikazo</strong>]<strong>”</strong> <strong>sehemu</strong><br />

ya pili<br />

BISMILA-HIR RAHMA-NIR RAHIM<br />

Asalamu Aleikum!<br />

Salamu katika jina lake Mwenyezi Mungu awekaye<br />

juu yetu vazi lifunikalo la ‘Haki’. Na ubarikiwe uwe na<br />

vazi hilo. Kurani Tukufu yatuambia… “Enyi<br />

wanaadamu! Hakika tumekuteremshieni nguo<br />

zifichazo tupu zenu na nguo <strong>za</strong> p ambo, na nguo <strong>za</strong><br />

utawa (yaani, kucha Mungu) ndizo bora. Hayo ni<br />

katika Ishara <strong>za</strong> (neema <strong>za</strong>) Mwenyezi Mungu ili<br />

wapate kukumbuka.<strong>”</strong><br />

Sura 7:026 Al Aaraf<br />

Kurani Tukufu inasema juu ya nguo zifunikazo <strong>za</strong> aina<br />

mbili… ya kwan<strong>za</strong> ni nguo zifunikazo<br />

zilizotengenezwa na wanadamu kuficha aibu yetu na<br />

utupu wetu… Hii ndiyo aina moja ya nguo zifunikazo<br />

au vazi. Walakini, nguo hizo hazitoshi katika hukumu<br />

ile. Kule tunahitaji vazi lifunikalo la aina nyingine lililo<br />

bora… Vazi lifunikalo la ‘haki’. Ni kwa vazi pekee<br />

lifunikalo la ‘haki’, yaani, hili la pili, ambalo sisi<br />

tutapewa, tutawe<strong>za</strong> kuingia katika ufalme wa<br />

Mbinguni.<br />

Kwa nini vazi hili la Haki ni la muhimu sana? Vazi hili<br />

la pili lifunikalo linaakisi tabia ya Mungu. Vazi hili la<br />

pili ni la mwisho, lakini ni bora. Lilipotezwa katika<br />

Bustani ya Edeni wa<strong>za</strong>zi wetu wale wa kwan<strong>za</strong><br />

walipoanguka kwa kuusikili<strong>za</strong> uongo wa Ibilisi. Ili<br />

kurudi katika ufalme wa Mungu ambao kutoka katika<br />

huo mwanadamu alianguka, anahitaji ‘haki’, ambayo<br />

ni kuishi maisha mema na kuwa<strong>za</strong> mawazo safi, kwa<br />

kifupi… “Dini ya Kweli.<strong>”</strong> Mwenyezi Mungu kwa<br />

fadhili <strong>za</strong>ke nyingi alikuwa amempa mtu yule wa<br />

kwan<strong>za</strong> na mkewe uthibitisho mwingi wa wema kwa<br />

kumpa yule mume na mkewe mahali kama pale<br />

papende<strong>za</strong>po katika ile Edeni ya Mungu. Kila mti<br />

ulio<strong>za</strong>a matunda ulikidhi mahitaji yao na yale yote<br />

ambayo yangefanya maisha yao kuwa ya furaha na<br />

yapende<strong>za</strong>yo walipewa. Hivyo upendo wa Mwenyezi<br />

Mungu ulionekana pande zote ukiwazunguka.<br />

Kwa upande mwingine, Ibilisi alikuwa hajawapa<br />

uthibitisho wo wote wa upendo wake kwao wala<br />

hakuwapa mahitaji yao, lakini maneno yake<br />

yalipokewa upesi na kusadikika kuliko lile Neno la<br />

Mwenyezi Mungu. Hivyo ndivyo, mume yule na<br />

mkewe waliokuwa watakatifu, walivyoanguka kutoka<br />

katika hali yao ya juu walipokula tunda lile<br />

lililokatazwa. Wakaipote<strong>za</strong> ile haki, yaani, lile vazi<br />

zuri lililowafunika walilokuwa wamepewa, walipoacha<br />

kumwamini Mungu.<br />

Haki ni kitu fulani kinachotokea ndani ya moyo wa<br />

muumini. Tangu anguko lile la mwanadamu, haki ni<br />

kitu fulani kisichowe<strong>za</strong> kutokea kwa juhudi <strong>za</strong><br />

kibinadamu. Hata wale wasioamini wanawe<strong>za</strong> kutoa<br />

sadaka <strong>za</strong>o kwa maskini (<strong>za</strong>kat), na hilo ni jema sana,<br />

wanawe<strong>za</strong> kutenda matendo mengi ya huruma, lakini<br />

hayo yawe<strong>za</strong> kuwa ni mtindo wa haki kwa kuonekana<br />

nje na pasiwe na nia halisi kutoka moyoni iwe<strong>za</strong>yo<br />

kuwasukuma. Mengi hutendwa kwa madhumuni ya<br />

kujionesha kwa watu… ili watu waweze kukusifu kwa<br />

wema wako. Hii siyo haki. Hili lilikuwa tatizo huko<br />

nyuma katika siku <strong>za</strong>ke Isa [Yesu]. “Tena matendo<br />

yao [Wayahudi] yote huyatenda ili kuta<strong>za</strong>mwa na<br />

watu…<strong>”</strong> Injili Mathayo 23:5.<br />

Hata leo hii waumini wanawe<strong>za</strong> kusema sala<br />

zinazorudiwa mara nyingi, ambazo wamezikariri,<br />

mara tano kwa siku… walakini hilo linawe<strong>za</strong> kuwa<br />

tendo lifanyikalo bila kufikiri. Ni karibu sana sawa<br />

kama mashine… ni kama kumbukumbu<br />

iliyorekodiwa, unabonye<strong>za</strong> tu swichi, nawe unaisikia<br />

sala ile ile… je! hivi hayo ndiyo atakayo Mwenyezi<br />

Mungu? Yaani, sala zetu zilizorekodiwa? Bila shaka<br />

kuna jambo fulani lenye kina <strong>za</strong>idi litakiwalo, pengine<br />

sala zetu hazina budi kutoka ndani ya mioyo yetu.<br />

Mimi nimebahatika kuwa na watoto na wanapoongea<br />

nami kutoka moyoni mwao, nawe<strong>za</strong> kuyathamini sana<br />

wasemayo. Waniambiapo kwamba wananipenda,<br />

moyo wangu unasisimka. Lakini endapo<br />

wangerekodi upendo wao huo kwenye Sidi na kupiga<br />

ujumbe huo uliorekodiwa mara nyingi ili nisikilize,<br />

moyo wangu usingeguswa hata kidogo. Bila shaka<br />

kwa kiasi fulani huenda hilo likafanana na wakati ule<br />

tunapomkaribia Mungu. Maongezi yetu pamoja naye<br />

ni sharti yatoke ndani yetu na kusemwa kwa moyo<br />

wenye shukrani.<br />

Je, hivi kuna jambo fulani litokealo moyoni<br />

Mwenyezi Mungu anapotugusa ndani yetu?<br />

Haki ya kweli ni wakati ule matendo mema yatokapo<br />

ndani kabisa ya moyo wa mtu. Matendo kama vile…<br />

kukataa kulipi<strong>za</strong> kisasi na kumrudishia mtu fulani<br />

anapotukosea. Matendo kama kuwatendea mema<br />

maadui <strong>za</strong>ko, kuwa na huruma moyoni mwako…<br />

ukikataa kumwumi<strong>za</strong> mtu fulani aliyekuchuki<strong>za</strong> sana<br />

unapokuwa na uwezo kumdhuru. Kuwa na sala (dua)<br />

<strong>za</strong> faragha kwa ajili ya wale wanaokutesa. Ni Mungu<br />

peke yake awe<strong>za</strong>ye kutupa sisi haki ya jinsi hii. Kwa<br />

mwanadamu hilo haliwezekani. Ni <strong>za</strong>wadi kutoka<br />

Mbinguni kupitia yule aliyeteremshwa aitwaye Masihi<br />

Isa. Tunahitaji watu watakaoomba sana kuwa na<br />

utakatifu huu moyoni. Tena yaja ahadi hii kutoka kwa<br />

wakuu wale wa Zamani wa Mashariki, ambayo wewe<br />

wawe<strong>za</strong> kudai kama yako mwenyhewe.<br />

“Yeye humwomba Mungu, naye akamtakabalia;<br />

hata auone uso wake kwa furaha; Naye<br />

humrejezea mtu haki yake.<strong>”</strong><br />

Ayubu 33:26 Toleo la Kisasa la King James<br />

Mwenyezi Mungu ameahidi kureje<strong>za</strong> kile kilichopotea<br />

kule Edeni! Enyi rafiki <strong>za</strong>ngu, hizi ni habari njema<br />

zenye nguvu… ingawa sisi tumeanguka na kuwa na<br />

makosa, bado hatujaachwa. Twawe<strong>za</strong> kurejezewa<br />

tabia ya Mwenyezi Mungu! Yeye ni mwema kwa<br />

wasio na shukrani. Anawajali makafiri, akiwapa jua<br />

na mvua, vidonda vyao anaviponya… Wasio na<br />

shukrani wanacho chakula, mavazi na mahali pa<br />

kulala. Mwenyezi Mungu hutoa wokovu kwa wasio<br />

haki. Atatufunika tena na vazi lake la Haki. Je,<br />

twayasadiki hayo? Hii maana yake ni kuwa na “dini<br />

ya kweli<strong>”</strong> si ule mfano wake tu, bali yenyewe hasa.<br />

Kitu fulani cha kweli kitokacho moyoni na kuonekana<br />

katika maisha ya kila siku! Hilo likitokea, basi, mfumo<br />

wa dua zetu huwa tofauti kabisa. Hatuwi tena na dua<br />

zilizorekodiwa ambazo twazisema kwa sauti ya chini<br />

na kuharakisha kana kwamba tunatimi<strong>za</strong> wajibu<br />

fulani, lakini itikio litokalo moyoni huonesha Mwenyezi<br />

Mungu alivyo wa maana kwetu. Rafiki <strong>za</strong>ngu, je!<br />

hayo ndiyo mnayotamani moyoni mwenu? Mwawe<strong>za</strong><br />

kuwa nayo na yatatolewa kwenu bure! Yote haya<br />

hupitia <strong>za</strong>wadi ya ‘Mwana Mwenye Haki’


aliyeteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Sura<br />

19:10 Maryam.<br />

Hii ndiyo hali ya kila mtu… “Kwa maana najua ya<br />

kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu,<br />

halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali<br />

kutenda lililo jema sipati.<strong>”</strong> Warumi 7:18<br />

Lakini kama Ibrahimu sisi twawe<strong>za</strong> kuziamini ahadi…<br />

“[Ibrahimu] akamwamini BWANA, naye akamhesabia<br />

jambo hili kuwa haki.<strong>”</strong> Taurati Mwanzo 15:6<br />

Bila kujali kasoro walizo nazo watu wa Mungu, Kristo<br />

hawapi kisogo watu wake anaowajali. Anao uwezo<br />

wa kuyabadilisha mavazi yao. Anaondoa mavazi<br />

machafu [uchoyo wote na dhambi], anaweka juu ya<br />

wale wanaotubu na kumwamini vazi lake mwenyewe<br />

la Haki, na kuandika msamaha mbele ya majina yao<br />

katika kumbukumbu <strong>za</strong> mbinguni. Anawakiri mbele<br />

ya ulimwengu wa mbinguni. Ibilisi, adui yao,<br />

anadhihirishwa kuwa ni mshitaki wao na<br />

mdanganyaji. Mwenyezi Mungu atatenda haki kwa<br />

wateule wake. Mungu wetu asema…<br />

"Mvueni [huyo mwenye dhambi] nguo hizi zenye<br />

uchafu. Kisha akamwambia yeye, Ta<strong>za</strong>ma,<br />

nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika<br />

mavazi ya thamani nyingi …<strong>”</strong> Zekaria 3:4,5.<br />

Hata hivyo, Mungu atakufunika wewe na <strong>”</strong>vazi la<br />

haki.<strong>”</strong> Isaya 61:10.<br />

Kumbuka kwamba vazi hili la haki ni ishara itokayo<br />

kwa Mwenyezi Mungu… “Na nguo <strong>za</strong> utawa (yaani<br />

kucha Mungu) ndizo bora. Hayo ni katika Ishara <strong>za</strong><br />

(neema <strong>za</strong>) Mwenyezi Mungu…<strong>”</strong> Sura 7:026 Al Aaraf<br />

Hakika vazi hili au kifuniko hiki cha Mwenyezi Mungu<br />

ni ile Haki yake Kristo, yaani, tabia yake mwenyewe<br />

isiyo na waa, ambalo kwa imani hutolewa kwa wote<br />

wanaompokea yeye kama Mwokozi wao kila mmoja<br />

binafsi.<br />

Lile vazi jeupe la utakatifu lilivaliwa na wa<strong>za</strong>zi wetu<br />

wa kwan<strong>za</strong> walipowekwa na Mungu katika Edeni<br />

takatifu. Waliishi kikamilifu kulingana na mapenzi<br />

yake Mungu. Nuru nzuri ambayo mwanga wake<br />

ulififia, yaani, nuru ya Mungu iliwazunguka, mume<br />

yule na mkewe, ambao walikuwa watakatifu. Vazi hili<br />

la nuru lilikuwa ishara ya mavazi yao ya kiroho ya<br />

utakatifu wao wenye asili ya mbinguni.. Laiti kama<br />

wangalidumu kuwa wanyofu kwa Mungu lingeendelea<br />

daima kuwafunika. Walakini dhambi ilipoingia,<br />

walikata kiungo chao kilichowaunganisha na Mungu,<br />

na ile nuru iliyokuwa imewazunguka ikaondoka.<br />

Wakiwa uchi na wakiona aibu, walijaribu kushona<br />

majani ya mtini kujifunika ili yawe badala ya mavazi<br />

yale ya mbinguni.<br />

Hakuna cho chote awe<strong>za</strong>cho kubuni mwanadamu<br />

kiwe<strong>za</strong>cho kuchukua mahali pa vazi lake la utakatifu<br />

lililopotea. Ni vazi lile tu lifunikalo ambalo Kristo<br />

mwenyewe ametoa lawe<strong>za</strong> kutufanya sisi tufae<br />

kuonekana mbele <strong>za</strong>ke Mungu. Vazi hili lifunikalo,<br />

yaani, vazi la haki yake, Kristo ataliweka juu ya kila<br />

mtu atubuye na kuamini. “Nakupa shauri,<strong>”</strong> anasema,<br />

“ununue kwangu… mavazi meupe upate kuvaa, aibu<br />

ya uchi wako isionekanwe.<strong>”</strong> Ufunuo 3:18. Anasema,<br />

“ununue<strong>”</strong>, yaani, litakugharimu kila kitu ili kulipata,<br />

lakini lenyewe linatolewa bure.<br />

Vazi hili, lililofumwa katika kiwanda cha mbinguni,<br />

ndani yake halina hata uzi mmoja uliobuniwa na<br />

mwanadamu. Katika ubinadamu wake Kristo alikuwa<br />

na tabia kamilifu, na tabia hii anajitolea kutugawia<br />

sisi. “Matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama<br />

nguo iliyotiwa unajisi.<strong>”</strong> Isaya 64:6<br />

Kila kitu tuwe<strong>za</strong>cho kufanya sisi wenyewe<br />

kimechafuliwa na dhambi. Lakini Mwana wa Mungu<br />

“alidhihirishwa ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo<br />

ndani yake.<strong>”</strong> Dhambi inafafanuliwa kuwa ni “uvunjaji<br />

wa sheria.<strong>”</strong> 1 Yohana 3:5,4.<br />

Haki yake Kristo haitafunika dhambi moja<br />

inayopendwa sana moyoni.<br />

Ni kile tu kipatanacho na kanuni <strong>za</strong> sheria ya Mungu<br />

kitakachosimama hukumuni.<br />

Hapo baadaye hapatakuwapo na nafasi nyingine ya<br />

kujitayarisha kwa umilele. Ni katika maisha haya<br />

tunatakiwa kuvaa vazi la haki yake Kristo. Hii ndiyo<br />

nafasi pekee kwetu ya kujenga tabia kwa ajili ya<br />

makao yale aliyowaandalia wale wanaozishika amri<br />

<strong>za</strong>ke. Siku <strong>za</strong> muda wetu wa kujaribiwa [kupimwa]<br />

zinaharakisha sana kuisha. Mwisho ule u karibu.<br />

“Heri akeshaye, na kuyatun<strong>za</strong> mavazi yake, asiende<br />

uchi hata watu wakaione aibu yake.<strong>”</strong> Ufunuo 16:15.<br />

Wapendwa rafiki <strong>za</strong>ngu, hatuna muda wa kuchelewachelewa<br />

na kulipuuzia somo hili muhimu. Sasa ndio<br />

wakati wa kusali na kusihi kwa dhati ili Mwenyezi<br />

Mungu atupe sisi mbaraka huo. Msifanye kosa,<br />

kukosa hapa ni kukosa umilele. Mwenyezi Mungu na<br />

atupe ishara yake… yaani, Vazi la Haki.<br />

Kwa maelezo <strong>za</strong>idi juu ya somo hili na mengineyo,<br />

tafadhali tembelea tovuti yetu chini. Maswali yako au<br />

maoni yako yanakaribishwa sana!<br />

www.salallah.com<br />

“Vazi la Haki<strong>”</strong><br />

Sehemu ya Pili<br />

Sura 7:26<br />

Al Aaraf<br />

R.M. Harnisch<br />

Mfululizo na.33

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!