“Nguo za Utawa [Zifunikazo]” sehemu - Salah Allah
“Nguo za Utawa [Zifunikazo]” sehemu - Salah Allah
“Nguo za Utawa [Zifunikazo]” sehemu - Salah Allah
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>“Nguo</strong> <strong>za</strong> <strong>Utawa</strong> [<strong>Zifunikazo</strong>]<strong>”</strong> <strong>sehemu</strong><br />
ya pili<br />
BISMILA-HIR RAHMA-NIR RAHIM<br />
Asalamu Aleikum!<br />
Salamu katika jina lake Mwenyezi Mungu awekaye<br />
juu yetu vazi lifunikalo la ‘Haki’. Na ubarikiwe uwe na<br />
vazi hilo. Kurani Tukufu yatuambia… “Enyi<br />
wanaadamu! Hakika tumekuteremshieni nguo<br />
zifichazo tupu zenu na nguo <strong>za</strong> p ambo, na nguo <strong>za</strong><br />
utawa (yaani, kucha Mungu) ndizo bora. Hayo ni<br />
katika Ishara <strong>za</strong> (neema <strong>za</strong>) Mwenyezi Mungu ili<br />
wapate kukumbuka.<strong>”</strong><br />
Sura 7:026 Al Aaraf<br />
Kurani Tukufu inasema juu ya nguo zifunikazo <strong>za</strong> aina<br />
mbili… ya kwan<strong>za</strong> ni nguo zifunikazo<br />
zilizotengenezwa na wanadamu kuficha aibu yetu na<br />
utupu wetu… Hii ndiyo aina moja ya nguo zifunikazo<br />
au vazi. Walakini, nguo hizo hazitoshi katika hukumu<br />
ile. Kule tunahitaji vazi lifunikalo la aina nyingine lililo<br />
bora… Vazi lifunikalo la ‘haki’. Ni kwa vazi pekee<br />
lifunikalo la ‘haki’, yaani, hili la pili, ambalo sisi<br />
tutapewa, tutawe<strong>za</strong> kuingia katika ufalme wa<br />
Mbinguni.<br />
Kwa nini vazi hili la Haki ni la muhimu sana? Vazi hili<br />
la pili lifunikalo linaakisi tabia ya Mungu. Vazi hili la<br />
pili ni la mwisho, lakini ni bora. Lilipotezwa katika<br />
Bustani ya Edeni wa<strong>za</strong>zi wetu wale wa kwan<strong>za</strong><br />
walipoanguka kwa kuusikili<strong>za</strong> uongo wa Ibilisi. Ili<br />
kurudi katika ufalme wa Mungu ambao kutoka katika<br />
huo mwanadamu alianguka, anahitaji ‘haki’, ambayo<br />
ni kuishi maisha mema na kuwa<strong>za</strong> mawazo safi, kwa<br />
kifupi… “Dini ya Kweli.<strong>”</strong> Mwenyezi Mungu kwa<br />
fadhili <strong>za</strong>ke nyingi alikuwa amempa mtu yule wa<br />
kwan<strong>za</strong> na mkewe uthibitisho mwingi wa wema kwa<br />
kumpa yule mume na mkewe mahali kama pale<br />
papende<strong>za</strong>po katika ile Edeni ya Mungu. Kila mti<br />
ulio<strong>za</strong>a matunda ulikidhi mahitaji yao na yale yote<br />
ambayo yangefanya maisha yao kuwa ya furaha na<br />
yapende<strong>za</strong>yo walipewa. Hivyo upendo wa Mwenyezi<br />
Mungu ulionekana pande zote ukiwazunguka.<br />
Kwa upande mwingine, Ibilisi alikuwa hajawapa<br />
uthibitisho wo wote wa upendo wake kwao wala<br />
hakuwapa mahitaji yao, lakini maneno yake<br />
yalipokewa upesi na kusadikika kuliko lile Neno la<br />
Mwenyezi Mungu. Hivyo ndivyo, mume yule na<br />
mkewe waliokuwa watakatifu, walivyoanguka kutoka<br />
katika hali yao ya juu walipokula tunda lile<br />
lililokatazwa. Wakaipote<strong>za</strong> ile haki, yaani, lile vazi<br />
zuri lililowafunika walilokuwa wamepewa, walipoacha<br />
kumwamini Mungu.<br />
Haki ni kitu fulani kinachotokea ndani ya moyo wa<br />
muumini. Tangu anguko lile la mwanadamu, haki ni<br />
kitu fulani kisichowe<strong>za</strong> kutokea kwa juhudi <strong>za</strong><br />
kibinadamu. Hata wale wasioamini wanawe<strong>za</strong> kutoa<br />
sadaka <strong>za</strong>o kwa maskini (<strong>za</strong>kat), na hilo ni jema sana,<br />
wanawe<strong>za</strong> kutenda matendo mengi ya huruma, lakini<br />
hayo yawe<strong>za</strong> kuwa ni mtindo wa haki kwa kuonekana<br />
nje na pasiwe na nia halisi kutoka moyoni iwe<strong>za</strong>yo<br />
kuwasukuma. Mengi hutendwa kwa madhumuni ya<br />
kujionesha kwa watu… ili watu waweze kukusifu kwa<br />
wema wako. Hii siyo haki. Hili lilikuwa tatizo huko<br />
nyuma katika siku <strong>za</strong>ke Isa [Yesu]. “Tena matendo<br />
yao [Wayahudi] yote huyatenda ili kuta<strong>za</strong>mwa na<br />
watu…<strong>”</strong> Injili Mathayo 23:5.<br />
Hata leo hii waumini wanawe<strong>za</strong> kusema sala<br />
zinazorudiwa mara nyingi, ambazo wamezikariri,<br />
mara tano kwa siku… walakini hilo linawe<strong>za</strong> kuwa<br />
tendo lifanyikalo bila kufikiri. Ni karibu sana sawa<br />
kama mashine… ni kama kumbukumbu<br />
iliyorekodiwa, unabonye<strong>za</strong> tu swichi, nawe unaisikia<br />
sala ile ile… je! hivi hayo ndiyo atakayo Mwenyezi<br />
Mungu? Yaani, sala zetu zilizorekodiwa? Bila shaka<br />
kuna jambo fulani lenye kina <strong>za</strong>idi litakiwalo, pengine<br />
sala zetu hazina budi kutoka ndani ya mioyo yetu.<br />
Mimi nimebahatika kuwa na watoto na wanapoongea<br />
nami kutoka moyoni mwao, nawe<strong>za</strong> kuyathamini sana<br />
wasemayo. Waniambiapo kwamba wananipenda,<br />
moyo wangu unasisimka. Lakini endapo<br />
wangerekodi upendo wao huo kwenye Sidi na kupiga<br />
ujumbe huo uliorekodiwa mara nyingi ili nisikilize,<br />
moyo wangu usingeguswa hata kidogo. Bila shaka<br />
kwa kiasi fulani huenda hilo likafanana na wakati ule<br />
tunapomkaribia Mungu. Maongezi yetu pamoja naye<br />
ni sharti yatoke ndani yetu na kusemwa kwa moyo<br />
wenye shukrani.<br />
Je, hivi kuna jambo fulani litokealo moyoni<br />
Mwenyezi Mungu anapotugusa ndani yetu?<br />
Haki ya kweli ni wakati ule matendo mema yatokapo<br />
ndani kabisa ya moyo wa mtu. Matendo kama vile…<br />
kukataa kulipi<strong>za</strong> kisasi na kumrudishia mtu fulani<br />
anapotukosea. Matendo kama kuwatendea mema<br />
maadui <strong>za</strong>ko, kuwa na huruma moyoni mwako…<br />
ukikataa kumwumi<strong>za</strong> mtu fulani aliyekuchuki<strong>za</strong> sana<br />
unapokuwa na uwezo kumdhuru. Kuwa na sala (dua)<br />
<strong>za</strong> faragha kwa ajili ya wale wanaokutesa. Ni Mungu<br />
peke yake awe<strong>za</strong>ye kutupa sisi haki ya jinsi hii. Kwa<br />
mwanadamu hilo haliwezekani. Ni <strong>za</strong>wadi kutoka<br />
Mbinguni kupitia yule aliyeteremshwa aitwaye Masihi<br />
Isa. Tunahitaji watu watakaoomba sana kuwa na<br />
utakatifu huu moyoni. Tena yaja ahadi hii kutoka kwa<br />
wakuu wale wa Zamani wa Mashariki, ambayo wewe<br />
wawe<strong>za</strong> kudai kama yako mwenyhewe.<br />
“Yeye humwomba Mungu, naye akamtakabalia;<br />
hata auone uso wake kwa furaha; Naye<br />
humrejezea mtu haki yake.<strong>”</strong><br />
Ayubu 33:26 Toleo la Kisasa la King James<br />
Mwenyezi Mungu ameahidi kureje<strong>za</strong> kile kilichopotea<br />
kule Edeni! Enyi rafiki <strong>za</strong>ngu, hizi ni habari njema<br />
zenye nguvu… ingawa sisi tumeanguka na kuwa na<br />
makosa, bado hatujaachwa. Twawe<strong>za</strong> kurejezewa<br />
tabia ya Mwenyezi Mungu! Yeye ni mwema kwa<br />
wasio na shukrani. Anawajali makafiri, akiwapa jua<br />
na mvua, vidonda vyao anaviponya… Wasio na<br />
shukrani wanacho chakula, mavazi na mahali pa<br />
kulala. Mwenyezi Mungu hutoa wokovu kwa wasio<br />
haki. Atatufunika tena na vazi lake la Haki. Je,<br />
twayasadiki hayo? Hii maana yake ni kuwa na “dini<br />
ya kweli<strong>”</strong> si ule mfano wake tu, bali yenyewe hasa.<br />
Kitu fulani cha kweli kitokacho moyoni na kuonekana<br />
katika maisha ya kila siku! Hilo likitokea, basi, mfumo<br />
wa dua zetu huwa tofauti kabisa. Hatuwi tena na dua<br />
zilizorekodiwa ambazo twazisema kwa sauti ya chini<br />
na kuharakisha kana kwamba tunatimi<strong>za</strong> wajibu<br />
fulani, lakini itikio litokalo moyoni huonesha Mwenyezi<br />
Mungu alivyo wa maana kwetu. Rafiki <strong>za</strong>ngu, je!<br />
hayo ndiyo mnayotamani moyoni mwenu? Mwawe<strong>za</strong><br />
kuwa nayo na yatatolewa kwenu bure! Yote haya<br />
hupitia <strong>za</strong>wadi ya ‘Mwana Mwenye Haki’
aliyeteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Sura<br />
19:10 Maryam.<br />
Hii ndiyo hali ya kila mtu… “Kwa maana najua ya<br />
kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu,<br />
halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali<br />
kutenda lililo jema sipati.<strong>”</strong> Warumi 7:18<br />
Lakini kama Ibrahimu sisi twawe<strong>za</strong> kuziamini ahadi…<br />
“[Ibrahimu] akamwamini BWANA, naye akamhesabia<br />
jambo hili kuwa haki.<strong>”</strong> Taurati Mwanzo 15:6<br />
Bila kujali kasoro walizo nazo watu wa Mungu, Kristo<br />
hawapi kisogo watu wake anaowajali. Anao uwezo<br />
wa kuyabadilisha mavazi yao. Anaondoa mavazi<br />
machafu [uchoyo wote na dhambi], anaweka juu ya<br />
wale wanaotubu na kumwamini vazi lake mwenyewe<br />
la Haki, na kuandika msamaha mbele ya majina yao<br />
katika kumbukumbu <strong>za</strong> mbinguni. Anawakiri mbele<br />
ya ulimwengu wa mbinguni. Ibilisi, adui yao,<br />
anadhihirishwa kuwa ni mshitaki wao na<br />
mdanganyaji. Mwenyezi Mungu atatenda haki kwa<br />
wateule wake. Mungu wetu asema…<br />
"Mvueni [huyo mwenye dhambi] nguo hizi zenye<br />
uchafu. Kisha akamwambia yeye, Ta<strong>za</strong>ma,<br />
nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika<br />
mavazi ya thamani nyingi …<strong>”</strong> Zekaria 3:4,5.<br />
Hata hivyo, Mungu atakufunika wewe na <strong>”</strong>vazi la<br />
haki.<strong>”</strong> Isaya 61:10.<br />
Kumbuka kwamba vazi hili la haki ni ishara itokayo<br />
kwa Mwenyezi Mungu… “Na nguo <strong>za</strong> utawa (yaani<br />
kucha Mungu) ndizo bora. Hayo ni katika Ishara <strong>za</strong><br />
(neema <strong>za</strong>) Mwenyezi Mungu…<strong>”</strong> Sura 7:026 Al Aaraf<br />
Hakika vazi hili au kifuniko hiki cha Mwenyezi Mungu<br />
ni ile Haki yake Kristo, yaani, tabia yake mwenyewe<br />
isiyo na waa, ambalo kwa imani hutolewa kwa wote<br />
wanaompokea yeye kama Mwokozi wao kila mmoja<br />
binafsi.<br />
Lile vazi jeupe la utakatifu lilivaliwa na wa<strong>za</strong>zi wetu<br />
wa kwan<strong>za</strong> walipowekwa na Mungu katika Edeni<br />
takatifu. Waliishi kikamilifu kulingana na mapenzi<br />
yake Mungu. Nuru nzuri ambayo mwanga wake<br />
ulififia, yaani, nuru ya Mungu iliwazunguka, mume<br />
yule na mkewe, ambao walikuwa watakatifu. Vazi hili<br />
la nuru lilikuwa ishara ya mavazi yao ya kiroho ya<br />
utakatifu wao wenye asili ya mbinguni.. Laiti kama<br />
wangalidumu kuwa wanyofu kwa Mungu lingeendelea<br />
daima kuwafunika. Walakini dhambi ilipoingia,<br />
walikata kiungo chao kilichowaunganisha na Mungu,<br />
na ile nuru iliyokuwa imewazunguka ikaondoka.<br />
Wakiwa uchi na wakiona aibu, walijaribu kushona<br />
majani ya mtini kujifunika ili yawe badala ya mavazi<br />
yale ya mbinguni.<br />
Hakuna cho chote awe<strong>za</strong>cho kubuni mwanadamu<br />
kiwe<strong>za</strong>cho kuchukua mahali pa vazi lake la utakatifu<br />
lililopotea. Ni vazi lile tu lifunikalo ambalo Kristo<br />
mwenyewe ametoa lawe<strong>za</strong> kutufanya sisi tufae<br />
kuonekana mbele <strong>za</strong>ke Mungu. Vazi hili lifunikalo,<br />
yaani, vazi la haki yake, Kristo ataliweka juu ya kila<br />
mtu atubuye na kuamini. “Nakupa shauri,<strong>”</strong> anasema,<br />
“ununue kwangu… mavazi meupe upate kuvaa, aibu<br />
ya uchi wako isionekanwe.<strong>”</strong> Ufunuo 3:18. Anasema,<br />
“ununue<strong>”</strong>, yaani, litakugharimu kila kitu ili kulipata,<br />
lakini lenyewe linatolewa bure.<br />
Vazi hili, lililofumwa katika kiwanda cha mbinguni,<br />
ndani yake halina hata uzi mmoja uliobuniwa na<br />
mwanadamu. Katika ubinadamu wake Kristo alikuwa<br />
na tabia kamilifu, na tabia hii anajitolea kutugawia<br />
sisi. “Matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama<br />
nguo iliyotiwa unajisi.<strong>”</strong> Isaya 64:6<br />
Kila kitu tuwe<strong>za</strong>cho kufanya sisi wenyewe<br />
kimechafuliwa na dhambi. Lakini Mwana wa Mungu<br />
“alidhihirishwa ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo<br />
ndani yake.<strong>”</strong> Dhambi inafafanuliwa kuwa ni “uvunjaji<br />
wa sheria.<strong>”</strong> 1 Yohana 3:5,4.<br />
Haki yake Kristo haitafunika dhambi moja<br />
inayopendwa sana moyoni.<br />
Ni kile tu kipatanacho na kanuni <strong>za</strong> sheria ya Mungu<br />
kitakachosimama hukumuni.<br />
Hapo baadaye hapatakuwapo na nafasi nyingine ya<br />
kujitayarisha kwa umilele. Ni katika maisha haya<br />
tunatakiwa kuvaa vazi la haki yake Kristo. Hii ndiyo<br />
nafasi pekee kwetu ya kujenga tabia kwa ajili ya<br />
makao yale aliyowaandalia wale wanaozishika amri<br />
<strong>za</strong>ke. Siku <strong>za</strong> muda wetu wa kujaribiwa [kupimwa]<br />
zinaharakisha sana kuisha. Mwisho ule u karibu.<br />
“Heri akeshaye, na kuyatun<strong>za</strong> mavazi yake, asiende<br />
uchi hata watu wakaione aibu yake.<strong>”</strong> Ufunuo 16:15.<br />
Wapendwa rafiki <strong>za</strong>ngu, hatuna muda wa kuchelewachelewa<br />
na kulipuuzia somo hili muhimu. Sasa ndio<br />
wakati wa kusali na kusihi kwa dhati ili Mwenyezi<br />
Mungu atupe sisi mbaraka huo. Msifanye kosa,<br />
kukosa hapa ni kukosa umilele. Mwenyezi Mungu na<br />
atupe ishara yake… yaani, Vazi la Haki.<br />
Kwa maelezo <strong>za</strong>idi juu ya somo hili na mengineyo,<br />
tafadhali tembelea tovuti yetu chini. Maswali yako au<br />
maoni yako yanakaribishwa sana!<br />
www.salallah.com<br />
“Vazi la Haki<strong>”</strong><br />
Sehemu ya Pili<br />
Sura 7:26<br />
Al Aaraf<br />
R.M. Harnisch<br />
Mfululizo na.33