21.06.2013 Views

HOTUBA ILIYOTOLEWA NA PROFESA

HOTUBA ILIYOTOLEWA NA PROFESA

HOTUBA ILIYOTOLEWA NA PROFESA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>HOTUBA</strong> <strong>ILIYOTOLEWA</strong> <strong>NA</strong><br />

PROF. JOHN HABWE WA CHUO KIKUU CHA<br />

<strong>NA</strong>IROBI KATIKA SIKU YA MWISHO WA<br />

MWAKA KATIKA SHULE YA UPILI YA<br />

TAREHE 12- APRILI 2013<br />

Utangulizi<br />

MAUTUMA<br />

KAUNTI YA LUGARI<br />

Wageni waalikwa, walimu, halmashauri ya shule ya<br />

Mautuma, wazazi, wanafunzi, mabibi na mabwana. Nina<br />

furaha isiyo kifani kupata fursa hii ya kuzungumza nanyi<br />

katika siku hii muhimu ya muktano wa mwaka. Furaha<br />

yangu inatokana na umaarufu wa shule hii, nafasi yake<br />

katika kaunti ya Lugari nzima na taifa la Kenya kwa jumla.<br />

Na kwamba shule hii ndiyo tegemeo letu la siku za usoni<br />

Ninapopata fursa ya kuzungumzia suala la elimu kama leo<br />

ninapata ugumu fulani kwa sababu ya wepesi wa suala<br />

lenyewe na kwa wakati huo mmoja ugumu wa suala hilo .<br />

Maswali hunijia akilini mara moja.


1) Je, elimu bado ni muhimu katika wakati huu?<br />

2) Je, ni kweli mtoto anaweza kuasi elimu na mambo<br />

yakamwendea sawa?<br />

3) Je, kijana asipopata elimu atashughulika na nini na vipi?<br />

4) Je,jamii ingali na nia ya kujitolea mhanga kufanya lolote<br />

almradi kusomesha vijana?<br />

5) Je, kesho ya msichana katika juhudi hizi ni ipi?<br />

6) Je, elimu bado imefungwa kwenye suala la kazi?<br />

Tunapowazia maswali haya kwa makini ndipo tunapopata<br />

changamoto kubwa ya kushughulika na juhudi ya kutafuta<br />

elimu kutwa kucha. Lakini safari hii ya kutafuta elumu ina<br />

matatizo na changamoto zake chungu nzima. Ni kama njia<br />

ndefu inayoelekea mgodini kuliko na almasi, dhahabu na<br />

fedha lakini yenye mikosi, majukumu na wakati mwingine<br />

hata kuvunja moyo.Lazima niseme elimu na sawa na<br />

JUHUDI. Pia elimu ni kitu ambacho kimejikita kwenye<br />

neno UTEUZI. Ni kitu cha hiari lakini ambacho kina<br />

fanaka ukikiteua mradi uwe na subira na uvumilivu.<br />

Mwanafunzi lazima aweze kuhiari kusoma na mzazi awe<br />

na hiari kumsomesha mwanawe.Ikiwa wana hiyo hiari<br />

lazima waweze kutafakari na kutekeleza mambo yafuatayo:


a) Nidhamu na maadili<br />

Ulimwengu una maendeleo makubwa. Maendeleo haya<br />

yamelifanya gumu zaidi suala la nidhamu na maadili<br />

ambalo tayari lilikuwa gumu hapo awali. Mtandao umeleta<br />

mawasiliano ya haraka miongoni mwa vijana. Licha ya<br />

manufaa yake kuna madhara yake pia. Suala la madawa ya<br />

kulevya limekuwa sugu hapa nchini Kenya linaathiri vijana<br />

wetu- wake kwa waume.<br />

Wanafunzi wetu wengi wamejipata katika vita hivi vya<br />

kijamii ambapo maadili yanamomonyoka kwa wepesi wa<br />

ajabu.Ningependa kuwauliza swali. Je,wanafunzi<br />

wanaweza kupita mtihani bila kuwa na maadili mema?<br />

Haiwezekani! Kupita mitihani kunakwenda moja kwa moja<br />

na maadili mema na nidhamu sio shuleni tu bali nyumbani<br />

pia. Sio sasa tu bali hata katika maisha ya baadaye. Walimu<br />

wamekabiliwa na shida kubwa ya kupambana na<br />

wanafunzi wasio na maadili mema ili kuwafanya waache<br />

ili wasiweze kuwaambukiza wanafunzi wengine kusumba<br />

ya kiburi, usodai, udanganyifu, dharau , ulevi, nk. Lakini<br />

changamoto na shida kubwa ya walimu hasa wale walio<br />

katika idara ya ushauri shuleni ni kwamba, wazazi


wametekeleza jukumu lao la kawaida katika kuinua hali ya<br />

maadili ya watoto wao. Licha ya kutotekeleza jukumu hili<br />

wazazi pia wanaudhika watoto wao wakirekebishwa. Kazi<br />

ya wazazi imekuwa ni kuwatendekeza watoto wao kwa<br />

kuwaita “ Mummy” na “Daddy” na kudhani ati watoto wao<br />

ni watu wazima.<br />

b) Kuhimili Mwalimu<br />

Walimu wengi wanataka wanafunzi wapite mitihani yao.<br />

Lakini wanakosa nyenzo za kimsingi za kuwasaidia<br />

kutekeleza kazi hii. Tunaweza kuuliza Je, inawezekana<br />

mwalimu kusomesha Jumamosi bila chai au bila chakula<br />

cha mchana?<br />

Hapana! Haiwezekani! Taasisi nyingi zimeamua kumsaidia<br />

mwalimu. Jinsi mbili ni muhimu katika kumhimili<br />

mwalimu. Kwanza kwa kumheshimu. Pili kwa kumpa<br />

usaidizi autakao. Na usaidizi huu ni muhimu zaidi ikiwa<br />

wanafunzi anaoshughulika nao ni wale watakao msaada<br />

zaidi “ slow learners” maarufu katika Kiingereza. Ninajua<br />

wazazi wana mizigo mingi lakini ningependa<br />

kuwakumbusha kuwa huu pia ni mzigo mwingine<br />

unaotaka muushughulikie. Japo sasa ni mzito katika siku<br />

za baadaye utakuwa mzito zaidi. Afadhali kumwelimisha


mwanao badala ya kumkimu na kumsaidia yeye na familia<br />

yake uzimani wakati ambapo utakuwa huna nguvu au<br />

uwezo.<br />

c) Suala la Karo<br />

Karo ndio msingi wa shule yoyote. Ningependa<br />

kuwahimiza wazazi muilipe mapema iwezekanavyo ili<br />

watoto wenu watunzwe vyema. Bila karo shule haiwezi<br />

kutekeleza majukumu yake ya kimsingi kama vile kununua<br />

chakula, kujenga na na kukarabati sehemu ambazo huwa<br />

zimeharibika . Moja katika sifa za shule ambazo hupita<br />

katika mitihani ni ulipaji wa mapema wa karo ili shule<br />

ipange mikakati na mambo yake mengine mapema ya<br />

kujiendesha. Hatungependa hali ambapo mkuu wa shule<br />

badala ya kufundisha, kusimamia shule shughuli yake<br />

nyingine iwe kuzunguka katika madeni na wadeni ili<br />

kukopa maziwa, mkate, nyama ili kuendesha shule hali na<br />

wazazi nyinyi mmekaa raha mustarehe. Ninajua uchumi<br />

wetu umemwelemea mzazi na kumwia mzito lakini ombi<br />

hili nalitoa kama rafiki yenu na pia kama mzazi<br />

mwenzenu.


d) Kutambua vipawa vya watoto wetu<br />

Wazazi wenzangu ningewaomba muwasaidie watoto wenu<br />

kutambua vipawa vyao. Nyinyi ndio mnaokaa nao kuliko<br />

hata walimu wala msiwalazimishe watoto wenu kufanya<br />

mambo hawataki. Ikiwa watoto wenu wana utashi na<br />

hajana na mambo fulani wasaidieni kuyapata. Msilazimishe<br />

watoto wenu kuwa wahandisi kama wanataka kuwa<br />

walimu. Wala msiwalazimeshe kusomea udaktari kama<br />

wanataka kuwa marubani. Pia msiwalazimishe kuwa<br />

mameneja ikiwa watakachokuwa ni wanamuziki. Acheni<br />

wafanye kazi waitakayo. Lakini muhimu kwanza ni<br />

kuwapa msingi wa elimu kwa kulipa karo mapema na<br />

kuwasaidia katika kitu wanachokitaka kutegemea uwezo<br />

wenu.<br />

e) Kuwasikiliza na kuwa na wakati nao.<br />

Wazazi wengi mimi nikiwa mmoja wao hawana muda na<br />

watoto wao. Hii ni kwa sababu ya pilkapilka za kazi na<br />

shughuli nyingine za maisha .Wazazi wengi hawajui tabia<br />

za watoto wao hata wanapoingilia madawa ya kulevya<br />

hushtuka. Kwa mfano, kuna wazazi wasiojua kama Watoto<br />

wao wako kidato cha pili au tatu. Hii ndiyo sababu mzazi


anapoelezwa mwanawe anafanya jambo fulani anasema<br />

kuwa mwanawe hawezi kufanya hivyo hali inayopelekea<br />

ugumu katika kumsaidia na kumrekebisha. Tutengeni<br />

muda na wanaetu ili wapate kusoma na kufaulu maishani.<br />

Wasaalam,<br />

Prof. Hamu Habwe

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!