27.01.2015 Views

yaliyomo - The Foundation for Civil Society

yaliyomo - The Foundation for Civil Society

yaliyomo - The Foundation for Civil Society

SHOW MORE
SHOW LESS
  • No tags were found...

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

YALIYOMO<br />

UTANGULIZI .........................................................................................................................3<br />

1. MAELEZO YA FOUNDATION............................................................................................4<br />

1.1 Dira .........................................................................................................................4<br />

1.2 Lengo........................................................................................................................4<br />

1.3 Misingi......................................................................................................................4<br />

2. Maelezo ya maana ya maneno tunayotumia: Tunavyomaanisha katika<br />

maneno tunayotumia ...............................................................................................5<br />

3. Nani anaweza kuomba ruzuku...............................................................................6<br />

3.1 Matawi ya mashirika makubwa.................................................................................7<br />

3.2 Makundi yanayoshirikiana.........................................................................................7<br />

4. Programu ya ruzuku.................................................................................................7<br />

5. MAENEO YANAYOFADHILIWA NA FOUNDATION..........................................................8<br />

5.1. Ushiriki wa kutunga sera na kutekeleza (sera)............................................................8<br />

5.2 Kuimarisha utawala bora na haki za binadamu (utawala)...........................................9<br />

5.3 Kuimarishwa kwa Uwezo wa Asasi za Kiraia...........................................................10<br />

6. MAENEO AMBAYO HAYATAFADHILIWA NA FOUNDATION.........................................11<br />

7. Jinsi ya kutuma maombi ..........................................................................................12<br />

7.1 Nyaraka zinazotakiwa.............................................................................................12<br />

7.2 Matawi ya mashirika makubwa...............................................................................13<br />

7.3 Makundi yanayoshirikiana.......................................................................................13<br />

7.4 Ufadhili wa mradi mkubwa, wenye washirika wengi...............................................13<br />

8. WADHAMINI..................................................................................................................14<br />

8.1 Nani anastahili kuwa mdhamini wa maombi yako.................................................14<br />

8.2 Maoni ya wafadhili..................................................................................................15<br />

9. Mara ngapi waweza kutuma maombi.................................................................15<br />

9.1 Kama umeshawahi kupata fedha kutoka <strong>Foundation</strong> siku za nyuma........................15<br />

9.2 Utumaji wa maombi ya ruzuku...............................................................................15<br />

10. Nini kinatokea katika maombi yako.....................................................................15<br />

10.1 Vigezo vya tathmini.................................................................................................16<br />

10.2 Asasi yako..............................................................................................................16<br />

10.3 Mradi wako.............................................................................................................16<br />

10.4 Mambo yako ya kifedha..........................................................................................17


10.5 Kama maombi yako hayakufanikiwa (kukubaliwa)...................................................17<br />

11. Mwongozo wa bajeti...............................................................................................18<br />

11.1 Gharama za usafiri..................................................................................................18<br />

11.2 Malazi na gharama za chakula................................................................................18<br />

11.3 Kupitisha matumizi kwa kutumia risiti tu.................................................................19<br />

11.4 Malipo ya ushiriki....................................................................................................19<br />

11.5 Honoraria/Tunzo isiyodaiwa....................................................................................19<br />

11.6 Gharama za uendeshaji & utawala / Mishahara / Mtaji............................................19<br />

12. Uangalizi/ UFUATILIAJI..............................................................................................20<br />

13. Jinsi ya kujaza fomu za maombi ya ruzuku.......................................................20<br />

14. MASUALA unayostahili kuyajua.............................................................................25<br />

14.1 Maombi ya ruzuku..................................................................................................25<br />

14.2 Masharti ya ruzuku..................................................................................................25<br />

15. Viambatisho................................................................................................................26<br />

15.1 Kiambatisho 1: Wadhamini wa Ufadhili..................................................................26<br />

15.2 Kiambatisho II: Mpango wa Mafunzo .....................................................................27<br />

15.3 Kiambatisho III: Muundo wa Upangaji wa Bajeti.....................................................28<br />

15.4 Kiambatisho lV: Mpango wa Ufuatiliaji na Tathmini.................................................29


UTANGULIZI<br />

Tunawakushukuru kwa kuonyesha nia ya kushirikiana na <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong>. Kila kitu<br />

unachotaka kujua kuhusu ruzuku na namna ya kuomba kipo katika mwongozo huu. Tafadhali<br />

yasome maelezo haya kwa makini kabla ya kujaza fomu yako.<br />

Ndani ya mwongozo huuutapata maelezo juu ya nani anaweza kuomba ruzuku, nini tunakiangalia<br />

katika kufikiria maombi husika, namna ambavyo maombi yako yatashughulikiwa, na namna ya<br />

kujaza fomu ya maombi. Fomu za maombi zinapatikana katika lugha za Kiingereza na Kiswahili.<br />

Wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong> wanao wajibu wa kutoa ufafanuzi wa vipengele vya fomu ya maombi<br />

vinavyoleta utata na hali ya maombi yako kwa njia ya simu, nukushi, barua au barua pepe.<br />

Kama unataka kujadili swali lolote linalohusu fomu yako, tafadhali ipigie kwanza ofisi yetu ili iweze<br />

kupanga muda wa mkutano na mmoja wa wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong>. Nafasi za miadi zinapatikana<br />

Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 8:00 - 9:30 alasiri.<br />

Fomu za maombi zinapatikana kati ya Jumatatu hadi Ijumaa toka saa 2.30 asubuhi - 10.00 jioni.<br />

Kama huwezi kufika katika ofisi zetu kwa ajili ya kuchukua fomu za maombi unaweza kupiga simu,<br />

kuandika barua pepe au kutuandikia barua ya kawaida na tutakutumia kifurushi cha fomu. Pia fomu<br />

za maombi zinapatikana katika tovuti ya <strong>Foundation</strong> www.thefoundation-tz.org.<br />

<strong>Foundation</strong> utaipata kupitia<br />

<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong><br />

Haidery Plaza, Ghorofa ya tano,<br />

Mtaa wa Upanga/Kisutu,<br />

S.L.P 7192,<br />

Dar-es-Salaam,<br />

Tanzania.<br />

Simu: 022 - 2138530 / 2138531 / 2138532, 0754 - 005708<br />

Nukushi: 022 - 2138533.<br />

Barua pepe: in<strong>for</strong>mation@thefoundation-tz.org<br />

Tovuti: www.thefoundation-tz.org


1. NINI MAANA YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY<br />

<strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> (<strong>Foundation</strong>) ni asasi huru iliyoanzishwa Tanzania kama Kampuni<br />

isiyozalisha faida, inayofadhiliwa na wabia wa maendeleo wenye mawazo yanayofanana, na<br />

kuongozwa na Bodi iliyo huru.<br />

1.1 Dira<br />

Dira ya <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> ni ‘Tanzania ambayo wananchi wake wamewezeshwa kutambua haki zao<br />

na kushiriki katika michakato ya mabadiliko ambayo itaboresha hali zao za maisha.’<br />

1.2 Dhima<br />

Kuwawezesha wananchi kupitia utoaji wa ruzuku, kuwezesha kuundwa kwa mitandao na kuwezesha<br />

utamaduni wa kujifunza pasipo ukomo katika Sekta ya Asasi za Kiraia.<br />

1.3 Maadili ya Msingi<br />

<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> inaahidi kutekeleza maadili yafuatayo:<br />

Haki<br />

Tutafanya kila jitihada kuhakikisha kwamba huduma zetu haziwi za kibaguzi na kuzingatia<br />

misingi ya usawa kuwa ndio mwongozo wa kazi zetu.<br />

Uadilifu<br />

<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> na wafanyakazi wake watatenda na kuhubiri uadilifu, katika miundo yake<br />

yote, na katika shughuli zetu zote. Tutaendeleza sera ya ‘Kutovumilia Hata Kidogo’ aina zote<br />

za rushwa, za ndani na nje ya <strong>Foundation</strong>.<br />

Uweledi<br />

Tutaukuza na kuuendeleza utamaduni ambapo wale wote wanaokutana nasi watahudumiwa<br />

kwa uweledi, upole na heshima wakati wote. Tutajenga na kujivunia utamaduni wenye misingi<br />

ya ubora na ufanisi, na kuwawezesha wale wote wanaofanya kazi na <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> waige<br />

mfano huo katika shughuli zao zote.<br />

Uwazi na Uwajibikaji<br />

Tutakuwa wazi, hatutaficha na tutakuwa waaminifu. Tutawasilisha kwa uwazi yale yote<br />

tunayoyafanya kwa kuzingatia itifaki za kutunza siri. Tutawajibika kwa vitendo vyetu na kwa<br />

wale tunaowahudumia.<br />

Usawa wa Jinsia<br />

Tutajitahidi kuhakikisha kwamba masuala ya jinsia yanaingizwa kama ajenda rasmi katika<br />

shughuli zetu zote, na tutawasaidia wapokearuzuku na wabia wetu waone umuhimu wa<br />

kuzingatia jinsia.<br />

<strong>Foundation</strong> haina nia ya kuwa mwakilishi wa asasi za kiraia au kuzungumza kwa niaba yao, bali<br />

kujenga uwezo wa asasi hizo kwa kutumia utaratibu ulio ratibiwa vyema kukiwa na viwango vya<br />

juu vya uwajibikaji, uwazi, ubora na matokeo.


2. Maelezo ya maana ya maneno yaliyotumika<br />

Uwajibikaji<br />

Utetezi<br />

AZAKi<br />

Consortium<br />

Mjumbe<br />

Katiba<br />

Mali iliyowekwa wakfu<br />

(endowment)<br />

Usawa wa jinsia<br />

Utawala<br />

Rasilimali<br />

Mabadiliko/ matokeo<br />

ya muda mrefu<br />

Uchukuaji wa dhamana kwa matendo yanayofanyika katika utendaji wa<br />

shughuli stahiki.<br />

Mchakato wa kushawishi mabadiliko ya sera, utetezi unaweza kutumika<br />

kuelezea udhaifu wa sera, au mapungufu yaliyopo katika sera au sera<br />

ambazo zipo lakini hazifuatwi.<br />

Asasi zilizoundwa nje ya mfumo wa serikali ambazo huwezesha<br />

wananchi kueleza mawazo yao na kuyafanyia kazi kwa pamoja kufikia<br />

lengo lililokusudiwa. (Yaani Asasi za Kiraia).<br />

Ni muunganiko wa makundi tofauti ambayo yanashirikiana kufikia lengo<br />

ambalo ni moja.<br />

Mwanachama au mmoja wa wafaidika wanaowakilishwa na asasi au<br />

binafsi.<br />

Hati ya kisheria yenye vipengele vifuatavyo:<br />

- Jina la taasisi, madhumuni ya uwepo na malengo.<br />

- Maelezo ya kufikiwa kwa malengo.<br />

- Maelezo ya namna ya taasisi inavyoongozwa na kusimamiwa.<br />

- Maelezo ya jinsi watu wanavyojiunga katika taasisi.<br />

- Sahihi za viongozi na siku ya asasi kupitisha katiba.<br />

Kiasi cha fedha kinachotolewa kwa kampuni au asasi kwa lengo la<br />

kuzalisha fedha badala ya kutumia mara moja. Faida inayopatikana<br />

sehemu inatumika kuendeshea mhimili muhimu wa asasi husika na<br />

faida iliyobaki inagawiwa tena kutokana na sheria za ufadhili wa fedha<br />

ili kuhakikisha uongezekaji wa ukuaji kwa ajili ya riba zaidi na shughuli<br />

za baadaye za asasi husika.<br />

Ni pale ambapo mwanaume na mwanamke wanakuwa na nafasi sawa<br />

na kuelewa vizuri haki zao za binadamu na umuhimu katika kushiriki<br />

na kupata faida za maendeleo ya kitaifa, kisiasa, kiuchumi, kijamii na<br />

kitamaduni kwa kuzingatia haki za binadamu.<br />

Sheria na kanuni zinazotakiwa kufuatwa katika uendeshaji na utekelezaji,<br />

na ushirikiano wa nje wa asasi mbalimbali na serikali.<br />

Shughuli unazofanya ambazo zitaleta huduma zinazokusudiwa na mradi.<br />

Tofauti ya muda mrefu ambayo imechangiwa na mradi huo katika<br />

kuyabadili maisha ya watu.


Wanachama<br />

Isiyoendeshwa kwa<br />

Mabadiliko<br />

Matokeo ya awali<br />

Sera<br />

Mtandao wa usalama<br />

Mtaji jamii<br />

(Social capital)<br />

<strong>Foundation</strong><br />

Makundi yaliyo katika<br />

hali hatarishi<br />

Watu wanaohusika na asasi fulani. Asasi pia zinaweza kuwa<br />

wanachama.<br />

Fedha zinazopatikana na kuwekwa katika shughuli kwa ajili ya umma si<br />

kwa ajili ya mtu binafsi.<br />

Kitu ambacho kitaonyesha tofauti moja kwa moja katika utoaji huduma<br />

kwa watu na asasi, na mafanikio ambayo asasi itayapata.<br />

Mabadiliko ya moja kwa moja ambayo huduma yako itatoa kwa wale<br />

wanaofaidika na mradi.<br />

Sera ni muongozo, kanuni au maamuzi ambayo yanaziongoza au<br />

yanayoonyesha shughuli za watu au makundi ya watu. Sera zinaweza<br />

kuwepo katika maumbo na ukubwa wa aina zote, katika ngazi ya kijiji<br />

hadi mkoa, ngazi za kitaifa na kimataifa.<br />

Juhudi za jamii za kujihami na kujitoa kwa wale waliopo katika mazingira<br />

magumu miongoni mwao.<br />

Sheria na wajibu ulio ndani ya majukumu ya kijamii yanayowawezesha<br />

watu kufikia malengo yao binafsi na yale ya kijamii.<br />

<strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong>.<br />

Wale watu ambao wamebaguliwa kutokana na mazingira yao<br />

na wapo hatarini. Wanaweza kuwa wazee, watoto, wenye VVU/<br />

UKIMWI, wakimbizi yatima n.k.<br />

3. Nani anaweza kuomba ruzuku<br />

Tunakaribisha maombi kutoka kila pembe ya nchi yetu. Asasi yako inaweza kuomba ruzuku kutoka<br />

<strong>Foundation</strong> kama ni:<br />

• Asasi isiyo ya Kiserikali (NGO)<br />

• Asasi ya Kijamii (CBO)<br />

• Chama cha Kitaalamu<br />

• Chama cha Wafanyakazi<br />

• Chombo cha Habari <br />

• Chama cha Ushirika 2<br />

• Chama cha Kidini 3<br />

1 - 2 <strong>Foundation</strong> inaweza kutoa ruzuku kwa vyombo vya habari, vyama vya ushirika kama fedha zinazoombwa kwa ajili ya mradi hazichangii<br />

kuwapatia wao faida, kulipa madeni, kulipa gharama za uendeshaji, na mradi umelenga kuisaidia<br />

3 Kumbuka kuwa makanisa na misikiti sio sehemu ya asasi za kidini


Na kama:<br />

• Taasisi yako imesajiliwa Tanzania Bara au Visiwani.<br />

• Kama umeandikishwa kama chama kisichotengeneza faida.<br />

• Una katiba au kanuni za uendeshaji ambazo zinatambuliwa kisheria zikiwa zinaeleza wazi<br />

madhumuni ya asasi yako na namna ambavyo unaiendesha.<br />

• Asasi yako ina akaunti ya benki ambayo imekuwa na watia saini/sahihi zaidi ya mmoja.<br />

(i) <strong>Foundation</strong> inaweza kutoa ruzuku kwa vyombo vya habari vyama vya ushirika kama<br />

fedha zinazoombwa kwa ajili ya mradi hazichangii kuwapatia wao faida, kulipa madeni,<br />

kulipa gharama za uendeshaji, na mradi umelenga kuisaidia jamii.<br />

(ii) Taasisi ambazo zinajishughulisha na fedha kama kuweka na kukopa katika ngazi za vyama<br />

vya ushirika au wakopeshaji wadogo au wale ambao wanashughulika na uwezeshaji wa<br />

kifedha kwa lengo la uzalishaji watatakiwa kujieleza kwa undani zaidi kama watataka fedha<br />

kutoka <strong>Foundation</strong> kwa lengo la kufanya shughuli nyingine zaidi ya zile wanazozifanya.<br />

(iii) <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> haitoi ruzuku kwa AZAKi za kimataifa (INGOs).<br />

3.1 Matawi ya mashirika makubwa<br />

Asasi ambayo ni tawi la asasi kubwa inaweza kuomba ruzuku kama itaonyesha wazi kwamba<br />

inajiendesha bila kutegemea makao makuu yake.<br />

3.2 Makundi yanayoshirikiana (consortia)<br />

<strong>Foundation</strong> inashawishi asasi mbalimbali kufanya kazi kwa pamoja ili kutatua tatizo moja. Na kama<br />

asasi mbili au zaidi zitaomba ruzuku kwa pamoja zitachukuliwa kama kundi la asasi.<br />

4. Programu ya ruzuku<br />

Jedwali lifuatalo linaonyesha kiasi cha ruzuku kinachotolewa, tarehe ya mwisho ya kupokea maombi,<br />

na kipindi hadi utoaji wa ruzuku. Kuna aina nne za ruzuku ambazo zinatolewa na <strong>Foundation</strong>.<br />

Aina ya ruzuku na tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi<br />

Aina ya Ruzuku Kiwango<br />

cha juu<br />

kwa<br />

mwaka<br />

Muda wa<br />

juu wa<br />

ruzuku<br />

Muda wa<br />

mwisho wa<br />

kuomba<br />

Ruzuku Kubwa<br />

(SG)<br />

Ruzuku ya<br />

kiwango cha<br />

kati (MG)<br />

Ruzuku ndogo<br />

(RDG)<br />

Ruzuku ya<br />

Usajili (RDG)<br />

Shilingi<br />

Milioni<br />

125<br />

TZS<br />

Milioni 45<br />

Milioni<br />

7.5<br />

Laki mbili<br />

(200,000)<br />

Miaka 3 Machi 1<br />

Julai 1<br />

October 1<br />

Miaka 3 Machi 1<br />

Julai 1<br />

Oktoba 1<br />

Mara<br />

moja<br />

Mara<br />

moja<br />

Machi 1<br />

Julai 1<br />

Oktoba 1<br />

Machi 1<br />

Julai 1<br />

Oktoba 1<br />

Taarifa kwa<br />

walioleta<br />

fomu za<br />

maombi<br />

Kama ikipitishwa<br />

fedha hutolewa<br />

katika kipindi cha<br />

Wiki 16 Wiki 24<br />

Wiki 8 Wiki 16<br />

Wiki 8 Wiki 16<br />

Wiki 8 Wiki 16


Tunashauri uwasilishaji wa fomu za maombi mapema zaidi kabla ya tarehe wa mwisho<br />

Idadi ya maombi yanayoweza kushughulikiwa katika kila mkupuo mmoja ina kikomo kutokana na<br />

wingi wa mahitaji. Maombi yatapewa kipaumbele kulingana na yalivyowahi kufika kwa msingi wa<br />

“Kuwahi kufika, kuwahi kushughulikiwa”, na utapewa taarifa kama fomu yako haitashughulikiwa<br />

katika muda ambao umeombea.<br />

Waombaji wa ruzuku wanaruhusiwa kutuma maombi kupitia tovuti moja kwa moja LAKINI wanatakiwa<br />

kuhakikisha kwamba wanatuma pia fomu zilizotiwa saini na viambatanishi vya muhimu.<br />

Maombi yanayofika ofisini baada ya tarehe ya mwisho ya kuwasilisha kupita hayatashughulikiwa na<br />

yatarudishwa kwa muombaji.<br />

Ushiriki katika ufadhili wa pamoja<br />

<strong>Foundation</strong> ipo tayari kuchangia sehemu ya ufadhili kwenye mradi mkubwa ambao umefadhiliwa<br />

pia na wafadhili wengine. Unachotakiwa kufanya ni kuonyesha wazi ni sehemu gani <strong>Foundation</strong><br />

inaombwa kusaidia.<br />

5. MAENEO YANAYOFADHILIWA NA FOUNDATION<br />

<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> itafadhili maombi yote ambayo yamelenga kufanya shughuli<br />

mbalimbali kusaidia watu maskini na wenye mahitaji na hasa katika maeneo lengwa yafuatayo:<br />

5.1. Ushiriki katika utungaji wa sera na utekelezaji wake<br />

Sera inaweza kuelezwa kama kanuni ambazo kwazo serikali, vyama vya siasa, kampuni za biashara<br />

na asasi za kiraia, n.k. huongoza utekelezaji wa shughuli zake kwa umma au sheria katika utekelezaji<br />

wake. Kwa maneno mengine Sera ni mpango wa utendaji au maelezo ya nia na mawazo.<br />

Wajibu wa asasi za kiraia ni muhimu ili kuruhusu sauti za watu zisikike katika mchakato wa<br />

kutunga sera. <strong>Foundation</strong> inasaidia miradi na asasi ambazo zinaiwezesha jamii kujihusisha katika<br />

kutengeneza, kushirikiana na kutangaza sera; na ufuatiliaji na utekelezaji wa sera. <strong>Foundation</strong><br />

itatoa ruzuku kwa miradi na asasi ambazo zitaiwezesha jamii kujihusisha katika kutengeneza,<br />

kushirikiana na kuitangaza sera, pamoja na ufuatiliaji na utekelezaji wa sera. <strong>Foundation</strong> itafadhili<br />

miradi itakayowezesha sekta ya asasi za kiraia kuchangia katika kuimarisha uwezo wa wananchi<br />

kushiriki ipasavyo katika michakato ya sera ili waweze kuchangia katika jitihada za kupunguza<br />

umasikini. Miradi iliyoandikwa vyema yenye sifa zifuatazo itafikiriwa kupata ruzuku:<br />

• Ile yenye uwezekano wa kuongeza kuzingatiwa kwa sera, sheria na kanuni za maendeleo ya<br />

taifa,<br />

• Ile yenye uwezekano wa kupunguza vikwazo vya kisera, kisheria na usimamizi vinavyoathiri<br />

utoaji mzuri wa huduma,<br />

• Ile inayoweza kuchochea mabadiliko ya sera na utendaji ili kushughulikia mahitaji ya makundi<br />

yaliyo hatarini na pembezoni,<br />

• Ile inayoweza kuwahusisha na kushirikisha jamii, hususani wanawake, watoto, watu wenye<br />

ulemavu, masikini, makundi yaliyo hatarini na yaliyotengwa, katika kupanga vipaumbele kwa<br />

ajili ya kuunda sera katika ngazi zote.<br />

• Miradi ambayo inaweza kuongeza ufahamu wa wananchi kuhusu ubaguzi wa kijinsia, kutafsiri<br />

sera za jinsia na kuwezesha ushiriki wa wanawake na watu waliopo katika makundi mengine


ya waliotengwa, katika kupanga vipaumbele vya uundaji wa sera katika ngazi zote.<br />

• Miradi yenye uwezekano wa kuinua uelewa wa wananchi juu ya sera na athari zake katika<br />

maendeleo.<br />

• Miradi inayoweza kuongeza ushiriki wenye tija wa wananchi katika michakato ya sera (kutunga,<br />

kutekeleza na kufuatilia)<br />

• Miradi inayoweza kuchangia kuongezeka kwa rasilimali zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji<br />

wa sera maalumu.<br />

• Miradi inayoweza kuleta uraghibishi katika uwajibikaji na kujipanga vizuri kwa mikutano<br />

ya vijiji, kamati za maendeleo za kata na baraza kamili la madiwani la wilaya ili kuruhusu<br />

ushirikishwaji wa mwananchi na michakato ya sera ya mahali husika.<br />

• Miradi inayohakikishia kuzingatiwa kwa sera za kitaifa na kimataifa zinazoshughulikia mahitaji<br />

ya makundi maalumu.<br />

Mifano ya shughuli zilizopo chini ya ushiriki katika utungaji wa sera na utekelezaji wake ni pamoja na:<br />

• Ufuatiliaji wa miradi shirikishi ya kupunguza umasikini, ambayo inalinganisha na kutofautisha<br />

habari juu ya umasikini na kuzisambaza eneo pana<br />

• Kupanga mipango ndani ya jamii juu ya jinsi mabadiliko ya sera fulani yanavyoathiri maisha<br />

yao na jinsi watakavyoitikia<br />

• Ushiriki wa jamii katika kupanga vipaumbele kwa ajili ya sera za kitaifa<br />

• Kuinua ufahamu wa umma juu ya masuala ya sera<br />

5.2 Kuimarisha utawala bora na haki za kiraia<br />

Azaki ni vyombo muhimu vya kuhakikisha kwamba taasisi za umma zinafanya kazi katika mazingira<br />

ya uwazi na kwamba watu wanaelewa kuhusu haki zao. <strong>Foundation</strong> husaidia asasi zote ambazo<br />

zinaamsha uelewa wa watu kuhusu haki zao na majukumu ya serikali, kuimarisha ushirikiano kati<br />

ya asasi zinazofanya kazi katika masuala ya haki za binadamu katika ngazi za chini na kitaifa na<br />

kuongeza upatikanaji wa haki kwa wananchi wote wa Tanzania.<br />

Utawala bora unaweza kufafanuliwa kama ifuatavyo:<br />

• Kuheshimu kikamilifu haki za binadamu,<br />

• Jamii inayothamini wajibu na majukumu yake ya kiraia,<br />

• Utawala wa sheria,<br />

• Ushiriki athirifu,<br />

• Ubia unaohusisha watendaji wengi pamoja na wingi wa vyama vya siasa<br />

• Uwazi<br />

• Michakato inayowajibika ndani na baina ya taasisi<br />

• Sekta za umma, binafsi na asasi za kiraia zilizo na ufanisi na zenye kutimiza majukumu yao,<br />

• Uhalali, upatikanaji wa maarifa, habari na elimu,<br />

• Uwezeshaji wa watu kisiasa, usawa, uendelevu, misimamo na maadili ambayo inajenga<br />

kuwajibika, mshikamano na kuvumiliana.<br />

<strong>Foundation</strong> itatoa ruzuku kwa miradi ambayo itawezesha taasisi za serikali, umma na binafsi kuwa<br />

wazi zaidi, kuwajibika na kuheshimu utawala wa sheria na haki za binadamu. Mahususi, <strong>Foundation</strong><br />

itafadhili miradi ambayo itahakikisha wananchi wanafahamu haki na wajibu wao, waweze kudai<br />

uwajibikaji kutoka katika rasilimali za umma na hivyo miradi itakuwa na athari chanya katika<br />

maeneo yafuatayo:<br />

• Kuongezeka kwa uwezo wa wananchi, wake kwa waume, kupata habari juu ya shughuli za


Mamlaka za Serikali za Mitaa ambazo zinagusa jamii (katika eneo lile),<br />

• Kuongezeka kwa uwajibikaji wa kijamii kwa mamlaka husika za umma na binafsi,<br />

• Kuongezeka kwa ushiriki wa watu katika mikutano ya kijiji au serikali za mitaa,<br />

• Kuhakikisha kwamba rasilimali za umma na vitegauchumi vinasambazwa kwa usawa na kwa<br />

ufanisi na kusimamimiwa katika ngazi za vijiji na mitaa,<br />

• Kuhakikisha panakuwepo na sheria na kanuni zinazotosheleza ambazo zinadhamini<br />

kuheshimiwa kwa haki za binadamu<br />

• Kuhakikisha kwamba mipango na bajeti za taifa na wilaya zinajumuisha na kushughulikia<br />

mahitaji ya makundi maalumu<br />

• Kuongezeka kwa idadi ya watu wanaoripoti kuridhishwa na mfumo wa sheria<br />

• Kuongezeka kwa ushiriki wa wananchi katika programu za elimu ya uraia na mpiga kura<br />

• Kuimarisha uwajibikaji kati ya wananchi na viongozi wao waliowachagua, kama vile Madiwani<br />

na Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.<br />

Mifano ya shughuli chini ya Utawala Bora na Uwajibikaji ni pamoja na:<br />

• Mikutano ya hadhara juu ya sera za taifa<br />

• Vipindi vya radio juu ya masuala ya utawala bora kama vile rushwa<br />

• Michezo ya kuigiza shirikishi inayoamsha uelewa wa haki za binadamu<br />

• Mafunzo ya viongozi wa asasi za kiraia na serikali za mitaa juu ya mabadiliko katika wajibu<br />

na majukumu chini ya maboresho ya serikali za mitaa.<br />

5.3 Kuimarishwa kwa Uwezo wa Asasi za Kiraia<br />

Nia ya <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> ni kuhakikisha kwamba Asasi za Kiraia zinakuwa nguzo<br />

imara ya kuleta mabadiliko; kufanikisha malengo yake yaliyokusudiwa na inatekeleza wajibu wake<br />

wa utetezi kwa vipaumbele vya maendeleo. Tunapenda kuona sekta ya asasi za kiraia yenye ari,<br />

ubunifu, inayotimiza majukumu yake, endelevu na inayowajibika; ambayo inachangia kikamilifu<br />

katika kuleta mabadiliko ya kudumu katika maendeleo nchini Tanzania. Tunaelekeza nguvu zetu<br />

katika maendeleo ya asasi moja moja na mitandao. Lengo la itikadi hii ni kuzifanya asasi za kiraia<br />

zionekane na ziweze kutekeleza kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii yaliyo chanya.<br />

Kama sehemu ya uimarishaji wa uwezo wa asasi za kiraia, <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> itahakikisha uwepo wa<br />

muunganisho miongoni mwa asasi za kiraia katika kupeana habari na kujifunza, na kuwezesha<br />

utetezi imara uweze kufanyika. Wakati huo huo, asasi moja moja zinahitaji kukua ili ziweze kufanya<br />

utetezi ulio na tija.<br />

Mahususi <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> itafadhili maombi ambayo yanachangia katika mambo yafuatayo:<br />

• Kuboresha uwezo wa utawala, usimamizi na utendaji wa AZAKi na mitandao nchini<br />

Tanzania<br />

• Kuongezeka kwa uwiano wa AZAKi zenye mifumo imara ya usimamizi wa fedha yenye vyanzo<br />

vya fedha vinavyotosheleza na endelevu,<br />

• Kuongezeka kwa kuunganisha mitandao miongoni mwa AZAKi ili kuhakikisha upatikanaji rahisi<br />

na kupeana habari, na kuwa na sauti ya pamoja katika masuala mbalimbali ya maendeleo,<br />

• Kuongezeka kwa uwezo wa AZAKi katika kuwa na utaalamu maalumu wa sekta mbalimbali<br />

na kutumia mbinu za uweledi katika masuala ya maendeleo,<br />

• Kuboreka kwa AZAKi katika kujiingiza kwenye masuala ya sera.<br />

• Kuboreka kwa uwezo wa AZAKi katika kuandika mapendekezo ya miradi<br />

• Kuongezeka kwa uwazi, kujihusisha, ushiriki na uwajibikaji kwa walengwa wao<br />

10


• Kuongezeka kwa hadhi ya kisheria ya asasi moja moja na mitandao.<br />

Mifano ya shughuli zilizopo chini ya Uimarishaji wa Asasi za Kiraia ni pamoja na:<br />

• Kuimarisha mitandao<br />

• Kujenga uwezo<br />

• Kuunda na kusaidia mitandao ya wilaya<br />

• Mafunzo ya stadi katika uchambuzi wa sera na utetezi kwa ajili ya wafanyakazi<br />

Katika maeneo yote hapo juu, kuwahusisha masikini na makundi maalumu ni muhimu. Ubunifu<br />

unahimizwa sana. <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> inapendelea miradi ambayo inatumia mbinu za kuwafikia watu<br />

wengi zaidi, k.m. kutumia vyombo vya habari kuhakikisha idadi kubwa ya wananchi inalengwa na<br />

miradi inayofadhiliwa.<br />

6. MAENEO AMBAYO HAYATAFADHILIWA NA FOUNDATION<br />

<strong>Foundation</strong> inaweza kutoa ruzuku kwa asasi ambazo zimeanzishwa si kwa nia ya kupata faida au<br />

kwa ufupi hazizalishi kwa nia ya kupata faida. Hata kama mradi ulioombea si wa faida, hutakuwa na<br />

nafasi ya kupata ruzuku kama katiba yako haionyeshi wazi kwamba asasi yako kimeanzishwa kwa<br />

ajili ya huduma na wala si kwa kutengeneza faida. Kama unadhani kwamba asasi yako itakabiliwa<br />

na sharti kama hili tafadhali pata ushauri kutoka kwetu kabla hujaandika maombi ya ruzuku.<br />

<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> haitatoa ruzuku kwa hili/haya yafuatayo:<br />

• Fedha za kutunisha mfuko<br />

& msaada wa masomo au<br />

utaalamu<br />

• Mradi au shughuli ambazo<br />

zipo nje ya Tanzania<br />

• Mradi au shughuli ambazo<br />

tayari zimemalizika<br />

• Miradi ambayo inatoa<br />

ruzuku kwa taasisi nyingine<br />

• Bakshishi kwa ajili ya<br />

wafanyakazi wa asasi<br />

• Miradi inayozalisha faida<br />

/ shughuli za ukopeshaji<br />

fedha<br />

• Maombi ya ruzuku kutoka kwa wataalamu<br />

wa kuchangisha fedha au washauri ambao<br />

wanajitegemeza kwa niaba ya asasi<br />

• Watu binafsi<br />

• Vyama vya siasa<br />

• Mradi ambao unapendelea dini fulani<br />

• Sekta binafsi (Labda iwe chama<br />

kisichotengeneza faida)<br />

• Asasi ambazo zina madeni makubwa<br />

• Warsha, vingivevyo ziwe katika mpango<br />

mkubwa wa shughuli ambazo zimeungana<br />

zinaeleza kwa uwazi matokeo yake<br />

• Gharama ambazo hazikutarajiwa<br />

• Utoaji wa huduma za kijamii<br />

ZINGATIA: Taasisi zote ambazo huendesha shughuli za utoaji mikopo kama vyama vya kuweka<br />

na kukopa, taasisi za kifedha zinazotoa mikopo hata ile midogo au wale ambao biashara ya fedha<br />

ndio mhimili wao mkubwa wanatakiwa kuwasilisha mchakato ambao umeweka wazi na wenye<br />

ushawishi mkubwa kuhusu mradi wao kama watataka kushughulikia masuala nje na utaratibu wao<br />

wa kawaida wa biashara ya fedha. <strong>Foundation</strong> haitatoa fedha kwa ajili ya kukopesha watu binafsi<br />

au makundi.<br />

11


7. Jinsi ya kutuma maombi<br />

Tafadhali hakikisha kwamba unapata fomu halisi zinazohusiana na ruzuku yako au umeweza<br />

kupata kielelezo cha maombi kwa mahitaji yako. Vyote tunavyotaka kujua kutoka kwako vipo<br />

katika Mwongozo huu wa maombi ya ruzuku. Tafadhali hakikisha kwamba umejaza nafasi zote<br />

unazopaswa kujazwa katika fomu. Fomu ambazo hazijakamilika hazitashughulikiwa na zitarejeshwa<br />

kwako mwenyewe.<br />

Unatakiwa kutumia fomu au muundo ulioelekezwa na <strong>Foundation</strong> iwe katika mfumo wa nakala ya<br />

karatasi au ya kwenye kompyuta. Fomu zote zinatakiwa kuwasilishwa ama kwa uasili wake kama<br />

ni nakala ngumu (ya kwenye karatasi) au kutumia fomu iliyopo katika mtandao wa <strong>Foundation</strong>.<br />

Kumbuka kuwa wote wale watakaojaza fomu kwa kutumia njia ya mtandao, ni lazima pia kupeleka<br />

fomu zilizotiwa saini katika nakala ngumu pamoja na nyaraka nyingine zinazotakiwa kuambatana<br />

nazo.<br />

Kama utaona kwamba hakuna nafasi ya kutosha katika fomu yako ya maombi, tafadhali usitumie<br />

zaidi ya karatasi mbili za ziada kukamilisha majibu ya maswali. Karatasi zaidi zinaweza kutumika<br />

katika mapendekezo ya bajeti na mipango ya mafunzo kama ni lazima.<br />

7.1 Nyaraka zinazotakiwa<br />

Ili maombi yako yaweze kufikiriwa tunahitaji nyaraka zifuatazo:<br />

(i) Nakala mbili za fomu zako zikiwa zimekamilishwa,<br />

(ii) Nakala mbili za cheti cha usajili wa asasi,<br />

(iii) Nakala mbili za hati za kisheria zinazohusu asasi yako,<br />

(iv) Nakala mbili za taarifa za kibenki zinazoelezea mwenendo wa akaunti yako angalau kwa<br />

kipindi cha miezi sita iliyopita. Moja inatakiwa kuwa halisi ikiwa na muhuri na saini ya<br />

benki,<br />

(v) Nakala mbili za maelezo yaliyoandikwa na bodi ya wadhamini au miniti ya mkutano<br />

inayoonyesha kwamba wamepitisha fomu hiyo unayoiwakilisha <strong>Foundation</strong> na wamekubaliana<br />

na mradi,<br />

(vi) Majina ya wadhamini wawili ambao wanaweza kuzungumza kuhusu asasi yako kwa<br />

kujiamini,<br />

(vii) Majina mawili ya Wadhamini wa ufadhili wa zamani katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita<br />

na namna ya kuwapata (anuani) hasa kwa Ruzuku ya Kati na Ruzuku Kubwa. Kielezo cha<br />

wafadhili kinaambatanishwa hapa kama Kiambatanisho 1,<br />

(viii) Nakala mbili za taarifa ya fedha ya mwaka wa karibuni (kama una maombi ya Ruzuku ya Kati<br />

ya shilingi zinazofikia milioni 35),<br />

(ix) Nakala mbili za taarifa ya fedha iliyokaguliwa na kupewa cheti cha ripoti safi kwa miradi<br />

ambayo inachukua miaka mingi (Kama unaomba zaidi ya shilingi milioni 35).<br />

(x) Kama maombi yako yana kipengele cha mafunzo, unatakiwa pia kuleta:<br />

Nakala mbili za mpango wa mafunzo. Mpango wa mafunzo hayo ni lazima uelezwe kwa<br />

kina malengo ya mafunzo, kundi linalohusika, vigezo vilivyotumika kuwapata washiriki wa<br />

mafunzo, wasifu wa walimu na mchanganuo wa mafunzo yenyewe, vitu ambavyo vitafundishwa<br />

kwa washiriki. Kielezo cha mpango wa mafunzo/Kongamano kimeambatanishwa hapa kama<br />

Kiambatanisho II,<br />

(xi) Kwa asasi ambazo hazikusajiliwa kama asasi za kiraia chini ya Sheria ya Asasi Zisizo za<br />

12


Kiserikali (NGO Act) kuwa na Hati ya Kukubalika (Certificate of Compliance) kutoka kwa<br />

msajili wa NGOs itasaidia zaidi.<br />

Zingatia: Kama asasi hazitafikia masharti yanayostahiki hazitafikiriwa.<br />

7.2 Matawi ya mashirika makubwa<br />

Kama AZAKi yako ni tawi la asasi kubwa ni lazima utoe:<br />

• Nakala mbili za taarifa kutoka makao makuu kwamba wanajua mradi huo na wanakubaliana<br />

na fomu za maombi ya ruzuku unayopeleka <strong>Foundation</strong>.<br />

Pia lazima uwe katika nafasi ya kuthibitisha kwamba tawi lako lina haya yafuatayo:<br />

• Kamati ya menejimenti inayojitegemea,<br />

• Ina akaunti ya Benki,<br />

• Ina hesabu za kila mwaka,<br />

• Ina kauli juu ya mapato na matumizi yake.<br />

Zingatia: Kama ruzuku itapitishwa itachukua miezi 4 kutoka mwisho wa tarehe ya maombi hadi<br />

kupatikana kwa fedha. Unatakiwa kuhakikisha kwamba mpango wako wa utekelezaji hauanzi katika<br />

kipindi cha miezi minne tangu umepeleka maombi yako.<br />

7.3 Makundi yanayoshirikiana (Consortia )<br />

Kama mpo AZAKi tofauti lakini mnaomba ruzuku kama kundi linaloshirikiana ambalo linatambulika<br />

na kusajiliwa kisheria na lina katiba inayojitegemea iliyotengenezwa na wanachama wake, maombi<br />

ya ruzuku yataangaliwa kama maombi ya taasisi nyingine zinazotaka ufadhili.<br />

Lakini kama unaomba kwa niaba ya kundi ambalo halikusajiliwa kisheria lakini lina wanachama<br />

wanaotaka kufanyakazi pamoja kufikia lengo fulani lazima kufanya yafuatayo:<br />

• Lazima asasi moja ichaguliwe kama kiongozi ili kufanya kazi kwa niaba ya wenzake<br />

wanaohusika na mpango mzima;<br />

• Jaza fomu kwa ajili ya kundi lote (Hii ifanywe na AZAKi inayoongoza);<br />

• Mkubaliane kwamba ruzuku hiyo italipwa kwa asasi kiongozi ambayo itawajibika kutekeleza<br />

masharti ya ruzuku;<br />

• Ni lazima kuwasilisha maelezo ya AZAKi nyingine kuonyesha kukubaliana na fomu hiyo.<br />

Mkitaka ruzuku kama kundi (consortia) ni lazima ueleze wazi nafasi ya kila kundi katika utekelezaji<br />

wa mradi husika.<br />

ZINGATIA: Kundi linaweza kupeleka maombi mara moja tu kwa muda husika. Lakini wanachama<br />

wa kundi wanaweza kuomba ruzuku kwa miradi mingine ambayo haihusiki na mradi ulioombewa<br />

ruzuku kwa kupitia kundi walilopo. Na katika hili waombaji ni lazima waeleze wazi kabisa tofauti<br />

za maombi yao kutoka katika maombi ya kikundi( consortia)<br />

7.4 Ufadhili wa mradi mkubwa wenye washirika wengi<br />

Kama utaomba ufadhili kwa mradi mkubwa wenye wafadhili wengi ni lazima utoe uthibitisho<br />

ufuatao:<br />

• Nakala mbili za barua za kuthibitisha ufadhili kutoka kwa washiriki wote wa mradi husika.<br />

Barua hizo zieleze wazi kabisa kiwango cha fedha ambazo zinatolewa na wafadhili hao,<br />

13


muda ambao fedha zitawakilishwa na fedha hizo zitafanya nini katika mradi husika. Ni lazima<br />

ueleze wazi shughulia ambayo unataka ifadhiliwe na <strong>Foundation</strong>.<br />

Kumbuka<br />

Tafadhali hakikisha kwamba unaambatanisha nakala mbili kwa kila hati unayowasilisha ambayo<br />

inatakiwa kuambatana na maombi yako. Pia kumbuka kuandika jina la asasi yako na anuani juu<br />

ya kila hati inayoambatana na fomu za maombi. Hii itatusaidia kuhakikisha kwamba nyaraka<br />

husika zote zipo pamoja na maombi ya ufadhili.<br />

8. WADHAMINI<br />

Tutakuwa tunawasiliana na wadhamini na wafadhili wengine ambao umetujulisha katika maombi<br />

yako ya ruzuku.<br />

Ndio kusema unapotupatia anuani ya wafadhili wako wa sasa na waliotangulia na namba yako ya<br />

utambulisho tuliyokupa hakikisha haya yafuatayo yapo sahihi:<br />

• Taarifa zilizomo zipo sahihi,<br />

• Wahusika wameambiwa juu ya maombi yako,<br />

• Wahusika wanaweza kupatikana kwa njia ya simu ili kusaidia kujibu baadhi ya maswali kutoka<br />

<strong>Foundation</strong> katika kipindi cha wiki tatu tangu kuwasilisha kwako kwa fomu za maombi. Kama<br />

mhusika hawezi kupatikana kwa simu hakikisha kwamba unatoa anuani yake ya posta na<br />

anuani ya barua pepe, na kuwasilisha maombi yako mapema zaidi.<br />

Maombi yote ya ruzuku lazima yawe na wadhamini wawili.<br />

8.1 Nani anastahili kuwa mdhamini wa maombi yako<br />

Mdhamini lazima awe mtu mkweli ambaye unamfikiria kuwa mwaminifu na mtu ambaye anaaminika<br />

na maamuzi yake yanaweza kuaminika. Hao wawili lazima wawe wanajua asasi yako si chini ya<br />

mwaka mmoja na wawe na uwezo wa kubadilishana mawazo juu ya uwezo na uzoefu wa asasi<br />

husika. Ni lazima wawe wanaelewa vyema shughuli za asasi yako, menejimenti na fedha.<br />

Wadhamini hawapaswi kuwa:<br />

• Watu wa familia yako, ndugu au marafiki au yoyote ndani ya asasi,<br />

• Kiongozi wa asasi yako au alikuwa mfanyakazi wa zamani au wa sasa,<br />

• Mtu ambaye kwa sasa unashirikiana naye katika shughuli za asasi au zako,<br />

• Watu ambao unaweza kuwahusisha baadaye na shughuli za mradi unaouombea fedha.<br />

Tafadhali hakikisha kwamba wadhamini wako wanayotaarifa ya wewe kuwaweka katika fomu za<br />

kuomba ruzuku <strong>Foundation</strong> na kwamba utawatumia kama wadhamini na waambie mradi ambao<br />

umeuombea ruzuku.<br />

ANGALIA: Ni lazima ueleze wazi uhusiano ulionao na wadhamini husika katika maombi yako.<br />

Tunatarajia kwamba utatumia nafasi yako vyema ya kuchagua wadhamini wako. Kama wadhamini<br />

wataonekana hawafai basi maombi yako hayatafikiriwa.<br />

14


8.2 Maoni ya wafadhili<br />

Wafadhili ni wale ambao walishawahi kukupatia ruzuku katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.<br />

Orodhesha wafadhili wote bila kujali kama tutawauliza au la. Ni vyema kuorodhesha wafadhili<br />

wako wote wa zamani katika fomu ya kuombea ruzuku. Kama mtu unayemfahamu katika Asasi<br />

iliyowafadhili amebadilishwa, tafadhali elezea hili na itakuwa ni vema kama utatueleza nafasi hiyo<br />

kwa sasa imeshikwa na nani na jina lake kama inawezekana.<br />

Kielelezo cha wadhamini wafadhili kimeambatanishwa na kutambulishwa kama kiambatanisho I.<br />

Inatakiwa kueleweka mapema kwamba waombaji wa ruzuku watatakiwa kutengeneza muhtasari<br />

wa ufadhili ambao ulitolewa na wadhamini hao na kuelezea mabadiliko ambayo yamepatikana<br />

katika jumuiya ikiwa ni matokeo ya utekelezaji wa mradi huo hivi karibuni.<br />

9. Mara ngapi waweza kutuma maombi<br />

AZAKi hairuhusiwi kuomba ufadhili zaidi ya mmoja katika kipindi kimoja. Kama utapeleka maombi<br />

zaidi ya moja katika kila programu, maombi yote yatakataliwa. Inatakiwa utambue kwamba AZAKi<br />

inaweza kupokea ruzuku ya aina moja tu kwa kipindi kutoka <strong>Foundation</strong>.<br />

AZAKi yoyote ile ambayo imepeleka ombi lake la ufadhili la aina yoyote ile inashauriwa kusubiri<br />

majibu kutoka <strong>Foundation</strong> kwa ombi lake la kwanza kabla ya kutuma maombi mengine. Hii itasaidia<br />

kuona kwamba mambo yote yaliyoelezwa yanashughulikiwa inavyostahili.<br />

9.1 Kama umeshawahi kupata fedha kutoka <strong>Foundation</strong> siku za nyuma<br />

Ombi lako la zamani ni lazima liwe limeshughulikiwa na kufungwa rasmi kabla ya ombi jipya<br />

kufikiriwa.Tathmini ya mradi wako ni lazima iwe imefanywa na <strong>Foundation</strong> kabla ya kuanza kufikiria<br />

ombi jipya.<br />

Utatakiwa kuonyesha matokeo ya mradi wa kwanza, kuelezea mafanikio, mambo ambayo mmejifunza<br />

kutoka katika ruzuku yako ya kwanza, kutafakari uzoefu uliopatikana kutokana na utekelezaji wa<br />

mradi na kuelezea kwanini unataka kuendelea na mradi huo au kuupanua zaidi .<br />

9.2 Utumaji wa maombi ya ruzuku<br />

Mara tu utakapokuwa umekamilisha kujaza maombi yako ya ruzuku na kuambatanisha na hati<br />

zinazostahili unatakiwa kutuma maombi yako hayo kwa anuani ambayo imeonyeshwa ndani ya<br />

kitabu hiki. Maombi hayo yanatakiwa kufika katika ofisi za <strong>Foundation</strong> kabla ya muda wa mwisho<br />

wa kupokea maombi kutimia. Maombi pia yanaweza kuwasilishwa kwa kutumia tovuti kwa kutumia<br />

anuani ya barua pepe iliyomo ndani ya mwongozo huu.<br />

10. Nini kinatokea katika maombi yako<br />

Mara tu utakapowasilisha maombi yako ya ruzuku utapatiwa namba ya rejea ambayo ni namba<br />

ya utambulisho ikiwa ni kama kutambua kuwasilishwa kwa maombi yako ya ruzuku. Tafadhali<br />

usipige simu au kuulizia maombi yako mpaka siku uliyoambiwa kuulizia. Tafadhali tupatie muda wa<br />

kuangalia maombi yako kwa mujibu wa mwongozo huu kabla hatujakupa jibu.<br />

15


Kila maombi hupitia hatua kadhaa za kuangaliwa kabla ya kufikiwa kwa maamuzi. Uteuzi wa<br />

asasi zinazostahili kupata ruzuku hufanywa na manejimenti ya <strong>Foundation</strong>. Matokeo ya uteuzi huo<br />

huwasilishwa kwa bodi ya wakurugenzi ya <strong>Foundation</strong>.<br />

Matokeo hayo yatawasilishwa kwa wadau walioomba kwa njia ya barua, tovuti na magazeti.<br />

10.1 Vigezo vya tathmini<br />

<strong>Foundation</strong> huangalia kila ombi kwa kutazama vipengele ambavyo tayari vimewekwa katika kufikia<br />

kuamua AZAKi fulani kupewa ruzuku. Kama sehemu ya mchakato wa kupitia maombi unaweza<br />

kuletewa ombi la kutoa maelezo ya ziada. Lakini pamoja na kuulizwa maswali ya ziada na<br />

wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong> kamwe usifikiri kwamba nafasi yako ya kupewa ruzuku imeongezeka<br />

kutokana na maswali hayo.<br />

Kama asasi yako inastahili kuomba ruzuku, tambua kwamba maombi yako yataangaliwa kwa<br />

kuzingatia vigezo vifuatavyo:<br />

10.2 Asasi yako<br />

Vigezo hivi vinatusaidia kuangalia muundo na menejimenti ya asasi yenu. Tunahitaji kuwa na<br />

uhakika na:<br />

• Kuwa asasi yako ina muundo wa kiutawala ambao ni thabiti na unaowajibika,<br />

• Kwamba unaweza kabisa kupangilia fedha za asasi na kuzidhibiti,<br />

• Kwamba asasi yako ina njia za wazi kabisa za kupanga na kuendesha shughuli zake,<br />

• Shughuli za asasi ziko wazi kwa wote na inakazania kutoa haki sawa kwa kila mtu,<br />

• Kwamba asasi yako inaonyesha wazi kwamba ina uzoefu na utaalamu wa kufanya shughuli<br />

iliyosababisha uwepo wake,<br />

• Kwamba asasi yako ina mahusiano na asasi nyingine zenye malengo kama yako,<br />

• Kwamba asasi yako inajiendesha kwa kulingana na misingi ya <strong>Foundation</strong>,<br />

10.3 Mradi wako<br />

Vipengele vilivyotajwa hapa chini vinasaidia kutathmini mapendekezo ya mradi wako. Hivyo<br />

tunahitaji kuwa na uhakika na:<br />

• Kwamba tatizo lililoainishwa katika mradi unaoombewa ruzuku kuwa ni kweli ni hitaji kuu la<br />

kundi lililolengwa (wafaidika au jamii husika),<br />

• Kwamba mradi uliouibua umepangwa vilivyo na una wafanyakazi wanaostahiki,<br />

• Kusudio la mradi wako linaonyesha wazi kabisa haja iliyopo,<br />

• Mpango wako unaweza kufuatiliwa kwa urahisi kwa kutumia taarifa za awali zilizopo na<br />

kwamba inapimika kwa kutumia viashiria vilivyo madhubuti,<br />

• Mchanganyiko wa shughuli zinazolengwa kufanyika kama zinaweza kuleta mabadiliko ya<br />

msingi yaliyoainishwa na kutarajiwa (matokeo ya awali na mabadiliko),<br />

• Mradi wako unachangia kufikia dira, lengo la <strong>Foundation</strong> na angalau na moja kati ya maeneo<br />

makuu ya <strong>Foundation</strong>.<br />

16


Matokeo na mabadiliko yatakayoletwa na mradi wako sharti yawe:<br />

Maalumu - Je Matokeo & mabadiliko yana mwelekeo maalum<br />

Yanayopimika<br />

Yanatekelezeka<br />

Sahihi<br />

Muda maalumu<br />

Endelevu<br />

- Je mabadiliko unayoyataka yanaweza kuangaliwa kwa kuona hali halisi<br />

iliyopo sasa<br />

- Je mabadilkiko yanawezekana katika muda uliopo<br />

- Je matokeo & mabadiliko vinafanana na wazo la mradi ulioombewa ufadhili<br />

Je yanawiana na mapendekezo yako ya washiriki uliowapendekeza<br />

- Je unaweza kutambua muda ambao utaona matokeo & mabadiliko<br />

- je matokeo & mabadiliko yataendelea kuonekana hata baada ya mradi<br />

kumalizika<br />

10.4 Mambo yako ya kifedha<br />

Vigezo vifuatavyo vinatusaidia sisi kutambua namna unavyodhibiti fedha zako. Tunahitaji kuwa na<br />

uhakika na:<br />

• Kwamba asasi yako inaendeshwa vyema kifedha na inahitaji kupewa ruzuku,<br />

• Akaunti ya benki ya asasi yenu ina waweka sahihi zaidi ya mmoja.<br />

Mapendekezo ya bajeti ya mradi wako yawe kama ifuatavyo:<br />

Ya kina:<br />

Kila shughuli lazima ioneshe gharama zake kwa kina. Shughuli zote<br />

zilizoorodheshwa katika fomu yako ya maombi lazima ziwe zinaeleza<br />

bajeti kwa undani zaidi .Ni lazima katika maelezo yako utoe kwa<br />

muhtasari kidogo shughuli husika (Itafanyika wapi na kwa namna gani,<br />

lini itafanyika, watu wangapi watashiriki katika shughuli hiyo), na kueleza<br />

gharama yake kwa undani zaidi.<br />

Za kweli:<br />

Sahihi:<br />

Yanayostahiki:<br />

Thamani ya fedha:<br />

Mifumo ya fedha:<br />

kwamba mahitaji yaliyoorodheshwa katika bajeti ni ya gharama za kweli<br />

na yanatosheleza.<br />

Vifaa husika vinaakisi bei halisi na vimejumlishwa kwa usahihi<br />

Kwamba bajeti iliyopangwa ndiyo inayostahiki kwa asasi husika kwa<br />

kuzingatia ukubwa wa asasi na uzoefu wake<br />

Kama bajeti imezingatia gharama na inakidhi. Maombi ambayo<br />

yataonyesha matokeo mazuri na makubwa kwa gharama ndogo<br />

yataangaliwa kwa makini zaidi na kupewa kipaumbele.<br />

<strong>Foundation</strong> inatarajia kupata maombi kutoka kwa AZAKi zenye mfumo<br />

bora wa menejimenti na fedha na hivyo kuwa na rekodi za mapato na<br />

matumizi na kwa njia hiyo kudhibiti fedha.<br />

Kielelezo cha bajeti kimo ndani ya Mwongozo huu kama kiambatanisho III<br />

17


10.5 Kama maombi yako hayakupita<br />

Kama <strong>Foundation</strong> inaamua kwamba haitatoa ruzuku kwa asasi yako basi utapatiwa taarifa kwa njia<br />

ya posta wiki nane baada ya kupita kwa muda wa mwisho wa kuwasilisha maombi katika kipindi<br />

husika. Utapata barua inayokueleza wazi kwa nini <strong>Foundation</strong> imeshindwa kukubaliana na ombi<br />

lako la kutaka ruzuku. Ni vyema kama utaisoma barua hiyo kwa uangalifu unaostahili.<br />

Kama mtaamua kutuma maombi tena kwa <strong>Foundation</strong> kwa mradi huo huo itawapasa kujaza tena<br />

fomu mpya na kuhakikisha mambo yote yaliyoelekezwa katika barua mnayatekeleza.<br />

11. Mwongozo wa bajeti<br />

Unatakiwa kuwasilisha bajeti katika muundo ambao ni wazi na rahisi kuelewa kwa mujibu wa<br />

maelekezo ambayo yapo katika mwongozo huu (Angalia muundo katika kiambatanisho III). Bajeti<br />

yako ni lazima ionyeshe wazi kwamba kiasi kilichoombwa kwa ajili ya mradi husika kimezingatiwa.<br />

Wakati unatengeneza bajeti, kuwa na uhakika na kitu ambacho umepanga kukifanya, namna<br />

utakavyofanya na kiasi gani cha fedha kinachotakiwa kwa mradi husika.<br />

<strong>Foundation</strong> haitakaa kuzungumza nawe kuhusiana na kilichomo au kiasi kilichopo katika bajeti<br />

yako au <strong>yaliyomo</strong> ndani mwake ambayo yamewasilishwa katika barua yako ya maombi. Hivyo ni<br />

muhimu sana kuwasilisha bajeti yenye kila kitu, sahihi na inayoonyesha dhahiri thamani ya fedha.<br />

Tengeneza bajeti kwa kuzingatia gharama halisi na kuwa na wastani katika maombi .Ni vyema katika<br />

hili ukatambua kwamba si lazima kupata kiasi cha fedha cha kiwango cha juu ambacho kipo.<br />

Maombi yako hayatafikiriwa iwapo bajeti yako haikutoa taarifa za kina na haioani na maelekezo na<br />

viwango vilivyotolewa katika mwongozo wa bajeti.<br />

11.1 Gharama za usafiri<br />

Safari zote lazima zifanywe katika hali ya kuzingatia unafuu wa njia ya usafiri na uiweke bajeti hiyo<br />

kama ni lazima watu wasafiri kwa umbali mrefu kushiriki katika shughuli za mradi.<br />

11.2 Malazi na gharama ya chakula<br />

Gharama zote za malazi na chakula ni lazima zithibitishwe kwa kutumia risiti katika taarifa ya<br />

matumizi ya fedha ya robo mwaka. <strong>Foundation</strong> haitapitisha bajeti ya matumizi bila kuwa na risiti<br />

halali za matumizi ya fedha. Tunahimiza asasi husika kulipa gharama hizi moja kwa moja badala ya<br />

kuwalipa washiriki.<br />

Ufuatao ni mwongozo unaostahili kutumika kwa ajili ya malazi na chakula:<br />

Eneo Malazi Posho ya kujikimu<br />

Majiji, Zanzibar, Dodoma, Bagamoyo Mjini 32,000 13,000<br />

Manispaa 22,000 13,000<br />

Mikoa na miji mikuu ya wilaya 11,000 9,000<br />

Maeneo mengine yote 5,000 6,000<br />

18


11.3 Kupitisha matumizi kwa kutumia risiti peke yake<br />

Wakati unandaa bajeti yako, tafadhali kumbuka kwamba tumekupatia mwongozo wa kiwango cha<br />

juu ambacho kinaweza kutumika kwa ajili ya usafiri, malazi na posho ya kujikimu.<br />

Gharama zote za usafiri, malazi na posho ya kujikimu ni lazima kulipwa kwa wale ambao wanatoka<br />

nje ya mji unakofanyika mradi husika (kwa wale washiriki ambao hawaishi katika eneo ambalo<br />

zinafanyika shughuli husika). Washiriki ambao ni wakazi wa eneo ambako ndiko mradi unakofanyika<br />

hawaruhusiwi kupewa malipo haya.<br />

11.4 Malipo ya ushiriki<br />

Hairuhusiwi kulipa malipo ya ushiriki kama motisha (posho za vikao) kwa ajili ya kushiriki katika<br />

warsha au mikutano mingine.<br />

11.5 Bakshishi (Honoraria)<br />

Bakshishi (Honoraria) inaweza kulipwa kwa mtu wa nje ambaye ametoa au amefanya kazi fulani<br />

ya huduma katika mradi. Chagua watu wako wa kukuendeshea mambo kwa kuzingatia bajeti yako<br />

na njia mbadala ya kupunguza gharama za matumizi. Honoraria kamwe isilipwe kwa wafanyakazi<br />

wenye mshahara katika AZAKi yako. Zingatia kwamba kama honoraria zako, posho ya kujikimu na<br />

malazi yapo juu maombi yako yanaweza kukataliwa.<br />

11.6 Gharama za uendeshaji & utawala / Mishahara<br />

Unaweza kabisa kubajeti sehemu fulani ya fedha zako kwa ajili ya kujiendesha na hii isizidi asilimia<br />

30 ya fedha zilizoombwa kutoka <strong>Foundation</strong>. Hii ni sawasawa na kutoa msaada katika gharama<br />

za uendeshaji na inatakiwa kuendesha gharama zote za msingi za kuendeshea AZAKi (kama vile<br />

gharama ya pango, vifaa vya ofisi, mishahara, gharama za magari, muda wa wafanyakazi wa utawala,<br />

na huduma za azaki ambazo haziko mahsusi kwa ajili ya mradi). Bajeti yako isiongeze gharama za<br />

huduma za kiutawala kwa zaidi ya asilimia 30. Kwa wale ambao wataomba chini ya asilimia hizo<br />

wataangaliwa vyema kwani inaonekana wao wanatambua thamani ya fedha.<br />

Kumbuka<br />

Ukiwa unakamilisha fomu yako ya maombi tafadhali kumbuka:<br />

• Jaza maombi ya ruzuku kwa kuzingatia uzoefu wa AZAKi na mipango yake.<br />

• Tunaangalia kwa makini sana juu ya mawazo yako na si maneno tu unayotumia katika<br />

fomu yako ya maombi ya ruzuku. Kama tutahisi kwamba maombi yako ya mradi<br />

yameandaliwa na mtaalamu wa masuala ya utunishaji mfuko, huenda tukakutoa kwani<br />

hustahili.<br />

• Unatakiwa kutupatia taarifa za kweli na takwimu zinazounga mkono ombi lako.<br />

• Unatakiwa kuwa na uhakika juu ya mradi wako na kitu unachoweza kufanikiwa.<br />

• Andaa bajeti yako kwa kuzingatia gharama halisi kwa kutumia mwongozo uliopewa.<br />

Usiweke bei ya juu ya vifaa au kupandisha gharama.<br />

• Usiambatanishe na taarifa za ziada ambazo hazikuombwa.<br />

• Zingatia maelekezo uliyopewa katika Mwongozo huu na maelezo ya mwongozo<br />

kwenye fomu yako kwa ukamilifu.<br />

19


12. Ufuatiliaji<br />

Miradi yote ambayo imepewa ufadhili na <strong>Foundation</strong> itafuatiliwa na kukaguliwa kila mara. Unatarajiwa<br />

kuwasilisha kwa <strong>Foundation</strong> taarifa za robo mwaka za fedha na nadharia ya mwenendo wa mradi kama<br />

makubaliano ya mkataba yanavyodai. Ukaguzi huo utafanyika katika shughuli ambazo zimekubaliwa<br />

na katika taarifa zao za robo mwaka za maendeleo ya mradi na ripoti za fedha. Mpango wa kuripoti<br />

na muundo wake vitatolewa kwako mara tu baada ya kutia saini mkataba huo. Kielelezo cha mpango<br />

wa ufuatiliaji wa mradi kipo humu kwenye mwongozo kama Kiambatanisho IV.<br />

13. Namna ya kujaza fomu za maombi ya ruzuku<br />

Kipengele hiki kina maelekezo yanayohusu jinsi ya kujaza fomu za maombi. Lengo la sehemu hii<br />

ni kusaidia waombaji kuwa na elimu ya kutosha kuhusu maelekezo yanayotakiwa katika ujazaji wa<br />

fomu. Ni matumaini yetu kwamba waombaji wataona eneo hili kuwa na msaada mkubwa kwao.<br />

Tutashukuru kama waombaji watatutumia maoni au taarifa zao za mrejesho ambazo zitatusaidia<br />

kuboresha zaidi huduma zetu katika sekta ya AZAKi za Tanzania.<br />

Fomu za kuombea ruzuku zina sehemu nne kama ifuatavyo:<br />

• Sehemu ya 1: Taarifa ya mradi,<br />

• Sehemu ya 2: Muundo wa uendeshaji,<br />

• Sehemu ya 3: Angalia kama maombi yako yamejazwa vyema na kukamilika,<br />

• Sehemu ya 4: Kipengele cha makubaliano.<br />

Sehemu ya 1: Taarifa ya mradi<br />

1.1. Jina la Mradi: Muombaji hapa anatakiwa kuandika jina la mradi. (kwa mfano: Mradi wa<br />

udhibiti wa VVU na UKIMWI).<br />

1.2. Maeneo yanayofadhiliwa<br />

Hapa mwombaji anatakiwa kuonyesha ni eneo lipi kati ya maeneo yanafodhaliwa na<br />

<strong>Foundation</strong> ambapo mradi wake anauombea. Yaani mradi wake unaangukia katika wazo gani<br />

linaloshughulikiwa na <strong>Foundation</strong>.<br />

1.3. Lengo kuu la mradi: katika kipengele hiki muombaji anatakiwa kuandika taarifa kwa ufupi<br />

juu ya mafanikio ya mradi huo kwa upana wake, yaani mafanikio ya mradi katika ngazi za<br />

maendeleo ya kitaifa na ya kisekta (Mathalani, Kuboresha hali ya kiafya kwa wananchi wa<br />

wilaya XXX kwa kufanikiwa kushawishi wananchi kukabiliana na matatizo ya UKIMWI kwa<br />

namna endelevu zaidi).<br />

1.4. Muhtasari wa mradi: Toa maelezo ya kwa ufupi juu ya y mradi unalenga kufanikisha nini<br />

katika kipindi chote cha utekelezaji wake kwa walengwa wa eneo husika.<br />

Kwa mfano: Mradi utahakikisha unakuwa endelevu katika kukabiliana na tatizo la VVU na<br />

UKIMWI na magonjwa ya zinaa kupitia mpango wa CBHC, Uhamasishaji na ushiriki wa jamii<br />

(Community mobilization and participation), BCCI, Kuishauri jamii (Community Counseling),<br />

Msaada kwa Vijana( support <strong>for</strong> Youths) PLWHA na kushawishi upimaji hiari na ushauri nasaha.<br />

20


Pia mradi utaangalia athari za malaria kama ugonjwa nyemelezi ambao huharakisha vifo vya<br />

wagonjwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI au kuongeza mzigo kwa familia zilizoathirika<br />

na ugonjwa wa UKIMWI. Shughuli za mradi zitatekelezwa kwa ushirikiano wa karibu kati ya<br />

serikali ya Tanzania (kama: MOH na MOEC) Wilaya na serikali za vijiji na NACP. Utekelezaji<br />

wa mradi utasimamiwa na wizara ya Afya (MOH) kupitia mpango wake wa Kuzuia na Kudhibiti<br />

VVU/UKIMWI/Magonjwa ya zinaa MTP III) na NACP.<br />

Lengo kuu la kimaendeleo: Ni kuboresha afya za wakazi wa wilaya XXX kwa kuwashawishi<br />

kuwa na mpango endelevu wa kukabiliana na UKIMWI. Masuala makuu yatakayoangaliwa:<br />

Kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI; kuhudumia na kuwasaidia wananchi wanaoishi<br />

na viurusi vya UKIMWI; Kuhudumia na kuwasaidia watoto yatima na wale wanaoishi katika<br />

mazingira magumu na kuwa na mtandao wa elimu na utetezi kuhusu VVU/UKIMWI.<br />

1.5. Maelezo ya tatizo linalohitaji ufumbuzi kupitia mradi huu - Nini hasa kinakushawishi uone<br />

kuwa mradi huu unahitajika (Toa amelezo ya kitu ambacho kinatakiwa kubadilishwa kwa<br />

kundi husika kwa kutekeleza mradi huo).<br />

(Kwa mfano: Kwa mujibu wa ripoti ya National AIDS Control Program (NACP) asilimia 90<br />

ya wananchi wanaelewa kuhusu ukimwi. Ukweli huu hata hivyo unagongana na kasi ya<br />

maambukizi, inayosababisha kuwepo kwa idadi kubwa inayotisha ya wagonjwa wengi wa<br />

ukimwi. Janga hili limesambaa kwa kasi katika maeneo ya vijijini na mwaka 1997, zaidi ya<br />

asilimia 10 ya wanawake waliokuwa wakihudhuria kliniki za uzazi katika baadhi ya maeneo<br />

ya vijijini walibainika kuwa na virusi vya ukimwi.<br />

Idadi ya wagonjwa wa ukimwi kama ilivyoripotiwa na NACP kwa upande wa Tanzania<br />

Bara ilipanda kutoka 25,503 mwishoni mwa mwaka 1990 kufikia 88,667 mwaka 1996. Kiasi<br />

cha aislimia 80 ya waliokutwa na ugonjwa ni wale wenye umri wa miaka 20-44. Tanzania<br />

ni nchi iliyo kusini mwa Jangwa la Sahara ambayo imeathiriwa vibaya na janga hili ikiwa na<br />

wastani wa maambukizo ya asilimia 10 kwa watu wazima. Utafiti zaidi wa Tanzania National<br />

AIDS Control Program (NACP) Tanzania Bara unaonyesha kupanda kwa wagonjwa kutoka<br />

25,503 mwishoni mwa miaka ya 1990 kufikia 88,667mwaka 199. Kulikuwa na wagonjwa<br />

14,112wa ukimwi kwa mwaka 2001 na hivyo kusababisha idadi ya wagonjwa kufikia 144498<br />

toka 1983. Na zaidi ya asilimia 80 ya watu waliokutwa na ugonjwa huo ni watu wa umri wa<br />

miaka 20 – 44. Kuna wastani wa watu 2229770 wenye ukimwi ambao umri wao ni kuanzia<br />

miaka 15 na kuendelea. Magonjwa ya kuambukiza kwa njia ya zinaa (STIs) yaliyoripotiwa<br />

mwaka2001 yalikuwa 211291 na 149222 kwa mwaka 2000 na 39385 mwaka 1999 (Taarifa<br />

ya VVU/UKIMWI STI surveillance report NACP 2002). Kutokana na hali hiyo Wizara ya afya<br />

nchini Tanzania imebuni mkakati wa kukabiliana na hali hiyo unaoitwa (MTP – III) ukiainisha<br />

harakati mbalimbali zinazofanywa na taifa kukabiliana na ugonjwa huo kwa kuzingatia<br />

takwimu za mwaka 1998 hadi 2002).<br />

Itambulike wazi kuwa maandiko mazuri ya kauli ya tatizo lazima yawe na mambo yafuatayo:<br />

• Kueleza kwa uwazi kabisa hali ambayo inastahili kubadilishwa kwa utekelezaji wa mradi<br />

kwa kuzingatia ukweli wa mambo ulivyo,<br />

• Itaonyesha kwa wazi kabisa nani na nini kimeathirika,<br />

• Kuhalalisha uwepo wa tatizo,<br />

21


• Kuelezea tatizo ambalo linalhusiana na nia ya kuanzishwa kwa asasi,<br />

• Kuelezea ukubwa wa tatizo katika jamii husika.<br />

1.6. Muda wa mradi: Muda wa utekelezaji wa mradi. (Mfano: Mradi huu utatekelezwa kwa miezi<br />

24).<br />

1.7. Katika kipengele hiki muombaji anatakiwa kuonyesha kiwango cha fedha anachohitaji kutoka<br />

<strong>Foundation</strong> (kwa mfano. Sh. 249,000/=).<br />

1.8. Maelezo yanatakiwa kutolewa kama ufadhili unaoombwa ni wa kushirikiana yaani kama<br />

<strong>Foundation</strong> inatakiwa kugharamia sehemu tu ya ruzuku.<br />

1.9. Uchanganuzi wa Bao la Mantiki (Logical Framework Analysis).<br />

Lengo mahususi la mradi:<br />

Hapa muombaji anatakiwa kuandika matokeo anayoyatarajia katika mradi wake yaani faida yake<br />

kwa maendeleo ya wananchi, muda wa mradi utakapokuwa umekwisha. Wananchi watakuwa<br />

wamefaidi nini. Kumbuka kwamba vipengele vyote vya mradi vitachangia matokeo hayo.<br />

Viashiria vya mabadiliko:<br />

Hapa mwombaji anatakiwa kutoa maelezo mwishoni mwa mradi kuonesha kuwa mafanikio<br />

yamepatikana na manufaa yake ni endelevu.<br />

Matokeo ya awali:<br />

Hapa mwombaji anatakiwa kuandika matokeo ya moja kwa moja yatakayotolewa (bidhaa na<br />

huduma za mradi) ambazo zaidi zipo chini ya usimamizi wa menejimenti.<br />

Viashiria vya matokeo:<br />

Viashiria katika kiwango matokeo hupima kiasi na ubora wa matokeo na muda wa ufikishaji kwa<br />

wahusika. Kanuni hizi hutumika pia wakati wa kuuangalia mradi na pia kuufanyia tathmini.<br />

Shughuli<br />

Hapa muombaji anatakiwa kuwasilisha kazi zitakazofanywa katika utekelezaji wa mradi na hivyo<br />

kuleta matokeo.<br />

22


Mpangilio wa namna ya kufanya kazi<br />

Matokeo Viashiria vya matokeo Nguvu inayotolewa<br />

kwa kila tokeo<br />

Kupunguza<br />

maambukizo<br />

ya UKIMWI<br />

kupitia mpango<br />

endelevu wa<br />

afya ya msingi<br />

ya jamii,<br />

msaada wa<br />

kijamii, na<br />

mabadiliko ya<br />

kitabia ifikapo<br />

Desemba 2009<br />

• Mfumo wa<br />

kubadilishana<br />

taarifa za UKIMWI<br />

inaanza kufanya<br />

kazi ifikapo.<br />

Desemba 2009<br />

• Wengi wa vijana<br />

wanaanza kufanya<br />

ngono salama<br />

katika wilaya X<br />

ifikapo Desemba<br />

2009.<br />

Wananchi 40 kuwa<br />

wameshafunzwa<br />

masuala ya PRA ifikapo<br />

Desemba 08.<br />

Shughuli za kufanya kwa kila<br />

tokeo<br />

• Kutambua wanavijiji 40 ili<br />

kufundwa ifikapo Oktoba<br />

07.<br />

• Kuwezesha mafunzo ya<br />

PRA kwa jamii lengwa 40<br />

ifikapo Januari 08.<br />

• Kuandaa taarifa ya mafunzo<br />

Februari 08.<br />

Wanajamii 40<br />

waliofunzwa wanaanza<br />

shughuli za PRA katika<br />

vijiji 21 kwenye wilaya<br />

X ifikapo desemba 9.<br />

• Kuwezesha ufuatiliaji na<br />

tathmini baada ya mafunzo<br />

Desemba 08.<br />

Kuwa na wanavijiji<br />

wa kujitolea 30<br />

waliofunzwa VVU/<br />

UKIMWI na BCCI<br />

ifikapo Desemba 08.<br />

• Kutambua watu<br />

wa kujitolea 30 ili<br />

wafundishwe ifikapo Machi<br />

08.<br />

• Kuwezesha mafunzo ya<br />

HIV/AIDS na BCCI kwa<br />

watu 30 waliotambulika<br />

katika vijiji ifikapo April 08.<br />

• Kuandaa taarifa ya mafunzo<br />

ifikapo Mei 08.<br />

• Kuwezesha ufuatiliaji na<br />

tathmini baada ya mafunzo<br />

ifikapo Oktoba 08.<br />

Waelimisha rika 40<br />

wakitoa elimu ya VVU/<br />

UKIMWI kwa warika<br />

21 katika vijiji 21 vya<br />

wilaya X ifikapo Dec.<br />

09.<br />

• Kuwazuru waelimisha rika<br />

katika kila robo mwaka.<br />

23


1.10. Mpango wa ufuatiliaji wa Matokeo (Mfano)<br />

Matokeo Viashiria Zilikotoka takwimu Muda wa<br />

kukusanya data<br />

Kupunguza kiwango cha<br />

maambukizi ya VVU kwa<br />

kupitia mpango wa afya ya<br />

msingi, msaada wa kijamii<br />

na mabadiliko ya kitabia<br />

kufikia Desemba 2009.<br />

Kuwepo kwa<br />

mfumo wa<br />

kubadilishana<br />

taarifa za<br />

ukimwi kufikia<br />

mwaka 2009.<br />

• Kumbukumbu ya<br />

mahudhurio kituo cha<br />

taarifa.<br />

• Mchanganuo wa taarifa<br />

za makundi lengwa.<br />

• Taarifa za tathmini.<br />

• Kila mwezi.<br />

• Kwa miezi<br />

mitatu (kila<br />

robo mwaka).<br />

• Kwa mwaka.<br />

1.11. Walengwa: Idadi na mahali walipo<br />

Taja idadi binafsi ya watu waliofaidika na mradi, vijiji, wilaya na mikoa<br />

Sehemu ya 2: Maelezo ya Asasi (Shirika)<br />

2.1. Jina la asasi: Jaza jina kama lilivyo katika katiba na usajili.<br />

2.2. Jina ambalo unalitumia (Tofauti na lile la 2:1): Utajaza nafasi hii kama jina unalotumia tofauti<br />

na lile la 2:1 hasa kama ni kifupisho.<br />

2.3. Usajili: Hapa unatakiwa kuhakikisha kwamba unatoa taarifa zote za asasi ikiwemo aina ya<br />

usajili, tarehe ya usajili na anuani.<br />

2.4. Kama unaomba kama sehemu ya ubia au muungano wa asasi: Tafadhali orodhesha majina ya<br />

AZAKi nyingine mnazoshirikiana au mtakazoshirikiana katika mradi huo. Na kama ni zaidi ya<br />

sita basi tengeneza kiambatanisho mwishoni mwa ukurasa.<br />

2.5. Mtu atakayekuwa anawasiliana na <strong>Foundation</strong>: Jaza jina la mhusika, nafasi yake na anuani za<br />

mawasiliano atakazofanya baina yake na <strong>Foundation</strong> kwa niaba ya asasi.<br />

2.6. Viongozi na wafanyakazi: Orodhesha majina ya viongozi wa asasi yako na nyadhifa walizonazo.<br />

Wanaweza kuwa Bodi ya wadhamini, Kamati ya usimamizi, au bodi ya wakurugenzi.<br />

2.7. Taarifa za kina za Akaunti ya benki: Mwombaji anatakiwa kutoa taarifa za akaunti ya benki<br />

kama: Jina la akaunti, namba ya akaunti, aina ya akaunti, Jina kamili la benki iliyopo akaunti<br />

hiyo, tawi lake, anuani ya tawi na majina ya watia saini na nyadhifa zao katika asasi.<br />

2.8. Wadhamini huru: Wadhamini hawa wanatakiwa kuwa wakweli na ambao maamuzi yao si rahisi<br />

kuyumbishwa au kupingwa na ni watu wenye heshima zao. Aidha, wanatakiwa wawe wamejua<br />

asasi husika kwa mwaka mzima na wenye uwezo wa kuelezea asasi husika kiuwezo na kiuzoefu.<br />

Wanatakiwa kuijua vyema asasi husika hasa shughuli zake, menejimenti na masuala ya kifedha.<br />

KUMBUKA: Unatakiwa kueleza wazi uhusiano wako na wadhamini na <strong>Foundation</strong> inatarajia<br />

kwamba utatumia busara zako vyema katika kumchagua mdhamini. Kama Mdhamini<br />

ataonekana hafai maombi yako hayatafikiriwa.<br />

Sehemu ya 3: Kifungu cha makubaliano<br />

Hiki kinatakiwa kujazwa na mwenyekiti, Katibu au mweka hazina lakini hawatastahili kuwa watu<br />

ambao wanawasiliana moja kwa moja na <strong>Foundation</strong>.<br />

Sehemu ya 4: Angalia kama maombi yako yamekamilika<br />

Waomba ruzuku wanashauriwa kutumia maelekezo yaliyopo katika mwongozo kuhakikisha<br />

kwamba wanafanyakazi ya kujaza fomu za maombi kwa unadhifu, uhakika. Unatakiwa kujaza kila<br />

kisanduku kabla ya kuwasilisha maombi.<br />

24


14. Masuala unayotakiwa kuyajua<br />

Tafadhali soma masuala yafuatayo kwa uangalifu zaidi. Ni sharti kwa kila mtu ambaye anataka<br />

ruzuku kutoka <strong>Foundation</strong> akayasoma, kuyaelewa na kuyakubali:<br />

14.1 Maombi ya Ruzuku<br />

(i) Mwongozo huu na fomu za maombi zinatolewa bure.<br />

(ii) Kwamba taarifa zilizomo katika mwongozo huu na fomu za maombi zinaweza kubadilika<br />

kila inapobidi. Tuna haki ya kubadili kipengele chochote katika sera zetu, kanuni na<br />

vigezo vya mchakato.<br />

(iii) Fomu ya maombi ya ruzuku inaweza isiwe na taarifa zote zinazohitajika kuamua maombi<br />

gani yanaweza kupewa ruzuku. Tunaweza kutaka taarifa zaidi kutoka kwako kuthibitisha<br />

maombi yako. Pia tutataka taarifa kutoka mtu wa tatu kama vile wadhamini wako na<br />

wafadhili wa sasa ulionao.<br />

(iv) Maombi yanafanywa kwa matakwa ya mwombaji. Kutokana na hilo hatuwezi kushtakiwa<br />

kwa hasara, uharibifu au gharama zinazotokana na mchakato mzima wa kuomba ruzuku,<br />

kukataliwa kwa ruzuku au kushughulikia maombi yako.<br />

(v) Uamuzi wa kutoa ruzuku bado ni haki ya Menejimenti ya <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong>,<br />

na maamuzi yake ni ya mwisho na hayakatiwi rufaa.<br />

(vi) Iwapo viongozi, Menejimenti au wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong> watamjua mtu kati ya wale<br />

walioomba ruzuku, wanatakiwa kutangaza mgongano wa maslahi na kujiondoa katika<br />

kushughulikia shauri linalomhusu mtu huyo.<br />

(vii) Maombi yako yatatupwa kama itabainika kwamba umedanganya au kutoa taarifa ambazo si<br />

sahihi wakati wa mchakato wa kuomba ruzuku au kufungiwa baada ya kupokea ruzuku.<br />

14.2 Masharti ya ruzuku<br />

a. Wakati muda wa ruzuku umekwisha, hakuna ulazima wa aina yoyote kwa <strong>Foundation</strong><br />

kutoa ruzuku tena kwa mradi husika.<br />

b. Fedha hazitatolewa mpaka asasi husika inatiliana saini mkataba na <strong>Foundation</strong> ambao<br />

utaeleza wazi masharti ya fedha ya ruzuku.<br />

c. Kama asasi haitafuata makubalino wakati wa utekelezaji basi ruzuku hiyo inaweza<br />

kuondolewa, kusimamishwa au kufutwa muda wowote.<br />

d. Tunaweza kutumia jina la asasi yako na mradi husika katika kujitambulisha kwa umma<br />

na kazi zake na taarifa ya mradi wako na jina lake itakuwa ni kitu cha wazi kwa umma<br />

na kitatangazwa. Hata hivyo huna ruksa ya kutumia jina au alama ya <strong>Foundation</strong> kwa<br />

manufaa yako au ya asasi yako bila kibali cha maandishi kutoka kwa <strong>Foundation</strong>.<br />

e. Maombi yote ya ruzuku ambayo yatakuwa yamepitishwa yatatangazwa katika magazeti<br />

ya kitaifa kama sehemu ya sera za uwazi za <strong>Foundation</strong>.<br />

f. <strong>Foundation</strong> itahakikisha inaipa taarifa serikali juu ya ruzuku zote ilizotoa kitaifa na ngazi<br />

ya chini. Wote waliopokea ruzuku wanatarajiwa kutoa taarifa ya ruzuku zao kwa serikali<br />

za mitaa kwa maandishi.<br />

g. Mradi wako utaangaliwa na kukaguliwa na wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong>, washauri wake<br />

na wafadhili wake. Wale wanaopewa ruzuku wanatarajiwa kuweka kumbukumbu za<br />

fedha zikiwemo vocha za matumizi kwa ruzuku zote wanazopewa.<br />

h. Wapokea ruzuku wa <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> inawalazimu kuzingatia Kanuni za Maadili za<br />

Mashirika Yasiyo ya Serikali (NGOs)zilizoambatishwa na mwongozo huu.<br />

25


15. Viambatisho<br />

15.1 Kiambatanisho 1 Wadhamini wa ufadhili<br />

Jina la asasi ...........................................................................................................................................<br />

Jina la Mfadhili Mtu wa kuwasiliana<br />

naye<br />

Taarifa za anuani ya<br />

madhamini kama<br />

simu, sanduku la<br />

posta anuani ya<br />

barua pepe<br />

kiasi cha fedha<br />

kilichowahi kutolewa<br />

naye<br />

jina la Mradi siku ya kuanza na<br />

kumalizika<br />

Zingatia: Kwa wale walioomba ruzuku ya Kati watatakiwa kujaza taarifa za wafadhili kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita<br />

26


15.2 Kimabatanisho cha II: Mpango wa mafunzo<br />

Malengo ya<br />

mafunzo/<br />

Warsha<br />

Dondoo za mada<br />

zitakazozungumziwa<br />

Mbinu za<br />

ufundishaji<br />

zitakazotumika<br />

Kundi lililolengwa Vigezo vilivyotumika<br />

kupata washiriki<br />

Elimu iliyotolewa<br />

itakavyoweza kusambazwa<br />

kwa makundi mbalimbali<br />

27


15.3 Kiambatanisho III: Muundo wa upangaji wa Bajeti<br />

JINA LA ASASI:…………………………………………………………………………….<br />

S/No Shughuli zinazohusika na vinavyotakiwa Gharama<br />

ya<br />

mkataba<br />

1.0 Maandalizi ya Mradi Waratibu 4, 2 kila<br />

Wilaya … Siku 3<br />

Gharama<br />

za Jumla<br />

QTR 1<br />

Gharama za<br />

Jumla QTR 2<br />

Gharama za<br />

Jumla QTR 3<br />

Gharama<br />

za Jumla<br />

QTR 4<br />

Mwaka<br />

wa 1<br />

Jumla<br />

Mwaka<br />

wa 2<br />

Jumla<br />

Mwaka<br />

wa 3<br />

Jumla<br />

1.1 Nauli Waratibu 2 @ 10,000/= 20,000 20,000 0 0 0 20,000<br />

1.2 Nauli Waratibu 2 @ 12,000/= 24,000 24,000 0 0 0 24,000<br />

1.3 Posho kujikimu Waratibu 4 @ 11,000/= X Siku<br />

2<br />

1.4 Kuchapa barua ya mwaliko nakala 1 X<br />

1,000/=<br />

1.5 Kuchapa barua ya taarifa ya mafunzo nakala 1<br />

X 1,000/=<br />

1.6 Kuchapa barua ya mwaliko kwa viongozi<br />

serikali nakala 1 X 1,000/=<br />

1.7 Kurudufu (kutoa nakala) barua za kuhudhuria<br />

mafunzo nakala 220 @ 50/=<br />

1.8 Kudurufu barua za taarifa ya mafunzo<br />

Wawezeshaji nakala 4 X 50/=<br />

1.9 Kudurufu barua ya mwaliko Viongozi wa<br />

Serikali 4 X 50/=<br />

88,000 88,000 0 0 0 88,000<br />

1,000 1,000 0 0 0 1,000<br />

1,000 1,000 0 0 0 1,000<br />

1,000 1,000 0 0 0 1,000<br />

11,000 11,000 0 0 0 11,000<br />

200 200 0 0 0 200<br />

200 200 0 0 0 200<br />

1.10 Bahasha Pcs 228 @ 50/= 11,400 11,400 0 0 0 11,400<br />

1.11 stempu kutuma barua Pcs 228 X 400//= 91,200 91,200 0 0 0 91,200<br />

Jumla ndogo Na.1 249,000 249,000 0 0 0 249,000<br />

(Katika mstari wa 1.0, 2.0, 3.0 na nyingine katika kolamu ya Shughuli na pembejeo (Activity and Inputs) inaonyesha masuala mbayo yanatakiwa kufanyiwa kazi kwa ujumla wake bila kuacha,<br />

inatakiwa ionyeshe nini kinatakiwa kufanywa, wapi, kw amuda gani na kwa ajili ya nani. Kutoka mstari wa 1.1 kuelekea chini katika kolam ya Shughuli na pembejeo (Activity and Inputs)<br />

,kunaonyesha na kutengeneza hesabu ya gharama za jumla kwa kila pembejeo inayotakiwa; Inatakiwa ionyeshe wazi, idadi ya namba na gharama kwa kila pembejeo inatakiwa kwa ajili ya<br />

kukamilisha Shughuli. Gharama halisi kwa kila kimoja inatakiwa ionyeshe kama Jumla ya thamani ya mkataba (Total Contract Value). Kwa gharama za jumla za Ruzuku ndogo ya QTR 1<br />

inatakiwa iwe sawa na Jumla ya thamani ya mkataba ( Total Contract Value) , kwa miradi yenye miaka mingi na wafadhili wengi, makadirio ya wastani kwa kila mwaka lazima yaonyeshwe<br />

chini ya kila mwaka 1, 2 na 3. na katika kila mwaka wa uendeshaji gharama zinatakiwa kugawanywa katika robo kwa kutegemea ni wakati gani shughuli hiyo itafanyika). Tunashauri bajeti<br />

itengenezwe wakati mipango ya kazi imeshaandaliwa.<br />

28


15.4 Kiambatanisho lV: Mpango wa ufuatiliaji na tathmini<br />

Mabadiliko Maelezo ya lengo<br />

viashiria vinavyoweza kutathminiwa (Idadi<br />

ya viashiria kwa kila tokeo visizidi viwili (2])<br />

Matokeo<br />

Shughuli<br />

Mabadiliko<br />

Matokeo<br />

Shughuli<br />

Chanzo cha taarifa<br />

(Data Source)<br />

Namna ya<br />

ukusanyaji wa<br />

takwimu<br />

Muda wa<br />

kukusanya<br />

takwimu hizo<br />

29


15.5 Sera ya ‘Kutovumilia Rushwa Hata Kidogo’:<br />

<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> inaendesha sera ya ‘Kutovumilia Rushwa Hata Kidogo’ kwa aina<br />

zote za rushwa, ndani ya the <strong>Foundation</strong> na huduma zake, pia nje pamoja na wale wote ambao the<br />

<strong>Foundation</strong> inaweza kuwa na mahusiano ya aina yoyote. Mfanyakazi yeyote wa the <strong>Foundation</strong><br />

atakayepatikana na hatia, kufuatia uchunguzi wa kina wa vitendo visivyofaa vya rushwa, atachukuliwa<br />

hatua kali chini ya taratibu za kinidhamu za <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong>.<br />

Pale ambapo mwananchi yeyote atakuwa na sababu za kumtilia shaka mtu yeyote anayehusiana na the<br />

<strong>Foundation</strong>, basi anatakiwa awasiliane na Mkurugenzi Mtendaji, akimwamini kabisa, na kumuarifu<br />

juu ya masuala hayo mapema iwezekanavyo, kwa maandishi ikiwezekana, au kwa njia nyingine<br />

zilizopo, akitoa ushahidi kadri awezavyo kusaidia madai yake mara tu atakapo tahadharishwa au<br />

kufuatwa moja kwa moja.<br />

Mkurugenzi Mtendaji atahakikisha kwamba jambo hili linachunguzwa kwa siri na kwa unyeti wake<br />

ndani ya taratibu za the <strong>Foundation</strong> za malalamiko na kuhakikisha kutobainika kwa mlalamikaji,<br />

ili kumlinda asiwekwe katika hatari. Mlalamikaji hatabaguliwa kwa aina yoyote ile kutokana na<br />

kuwasilisha malalamiko ya kweli.<br />

Baada ya hapo the <strong>Foundation</strong> itaendesha uchunguzi wa kina, ambao matokeo yake yatarejeshwa<br />

kwa mlalamikaji yakiwa na maamuzi yaliyo kamili na yanayostahili.<br />

Ikumbukwe kwamba uchunguzi wowote na matokeo yoyote yatazingatia sera ya malalamiko na<br />

taratibu za the <strong>Foundation</strong>, hususani ikizingatia misingi ya haki na Sheria za Tanzania. Kwa taarifa<br />

zaidi ya jinsi ya kuwasilisha malalamiko rejea Sera ya the <strong>Foundation</strong> ya Kushughulikia Malalamiko<br />

(15.6), ambayo pia hupatikana katika tovuti yetu, www.thefoundation-tz.org<br />

15.6 Sera ya Kushughulikia Malalamiko<br />

<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> ina maadili 5 ya msingi, ambayo ni haki, uadilifu, uweledi, uwazi<br />

na uwajibikaji, na usawa wa kijinsia. Katika misingi ya maadili haya, the <strong>Foundation</strong> inadhamiria<br />

kutoa fursa kwa wanaopokea huduma zetu kutoa malalamiko kwenye masuala ya rushwa, tabia,<br />

taratibu na kufanya maamuzi. Hivyo basi, the <strong>Foundation</strong> imetayarisha Sera hii ya Kushughulikia<br />

Malalamiko ili itumike na wadau wetu wote. Lazima ieleweke kwamba Sera ya Kushughulikia<br />

Malalamiko hairuhusu kwa namna yoyote ile ukataji wa rufaa kwa maamuzi yaliyofanywa na<br />

the <strong>Foundation</strong>. Maamuzi kuhusu ruzuku yaliyofanywa na the <strong>Foundation</strong> ni ya mwisho, lakini<br />

malalamiko dhidi ya maamuzi yataisaidia the <strong>Foundation</strong> kuboresha maamuzi/huduma zake za<br />

baadaye. <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> itashughulikia malalamiko yote katika njia iliyo ya haki, bila upendeleo,<br />

uwazi na kwa muda unaofaa.<br />

<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> inakusudia kufanya yafuatayo:<br />

• Kushughulikia malalamiko kwa uzito wake na kwa ufanisi<br />

• Kutatua malalamiko haraka pale inapowezekana<br />

• Kujifunza kutokana na malalamiko na kuchukua hatua za kuboresha huduma zetu<br />

• Kumsaidia na kumlinda mlalamikaji<br />

Unatakiwa ufanye nini unapokuwa na malamiko<br />

Unapotaka kuwasilisha malalamiko kuhusu the <strong>Foundation</strong>, ruzuku iliyotolewa na the <strong>Foundation</strong> au<br />

30


kuhusu mfanyakazi wa the <strong>Foundation</strong>, au Mjumbe wa Bodi, unaweza kufanya hivyo kwa maandishi,<br />

kwa kutumia nukushi, barua pepe (malalamiko@thefoundation-tz.org), kwa simu au kwa kuja wewe<br />

mwenyewe. Wale wanaopenda kuja kutoa malalamiko yao wenyewe watahitaji wapangiwe muda.<br />

Iwapo malalamiko yako utayatuma kwa kuandika barua, nukushi au barua pepe, tafadhali onyesha<br />

namba yako ya simu, iwapo jibu la awali kwa kutumia simu litafaa. Iwapo unatuma kwa baruapepe,<br />

tafadhali onyesha iwapo unahitaji majibu kwa barua pepe, kama sivyo, tafadhali toa anuani<br />

kamili ya posta. Tutakuomba uweke malalamiko yako katika maandishi, iwapo umewasiliana nasi<br />

kwa mdomo. Tutaweza kukupatia msaada kwa hili iwapo ni lazima. Kwa mara ya kwanza wasilisha<br />

malalamiko yako moja kwa moja kwa Mkurugenzi Mtendaji wa the <strong>Foundation</strong> au iwapo inastahili<br />

na katika mazingira yasiyo ya kawaida, kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi.<br />

Utapokea uthibitisho kutoka kwetu kwamba malalamiko yako yamepokelewa. Iwapo hutapokea<br />

uthibitisho ndani ya siku saba za kazi za kuwasilisha malalamiko yako, tafadhali wasiliana na<br />

Mkurugenzi Mtendaji moja kwa moja.<br />

Nini kinafuata baada ya hapo<br />

Baada ya kupokea malalamiko yako, tutalenga kujibu mara moja, na mara zote ndani ya siku 14.<br />

Iwapo hili haliwezekani, tutaeleza kwa nini na kukujulisha itachukua muda gani.<br />

Iwapo hujafurahia majibu ya awali unayopata, wasiliana na Mkurugenzi Mtendaji tena na utafute<br />

ufafanuzi. Kufuatia jibu la pili, iwapo bado hujaridhika, unashauriwa kumuandikia Mwenyekiti wa<br />

Bodi ya Wakurugenzi.<br />

Iwapo bado hujafurahishwa na matendo ya the <strong>Foundation</strong>, unaweza kumuomba Mwenyekiti wa<br />

Bodi apeleke malalamiko yako kwa Waamuzi huru wachunguze malalamiko yako jinsi ambavyo<br />

yalivyoshughulikiwa.<br />

Usiri<br />

Kwa ujumla walalamikaji wanahimizwa na the <strong>Foundation</strong> watamke majina yao na jinsi ya kuwapata,<br />

wanapowasilisha malalamiko. Kwa kufanya hivyo wanahakikishiwa viwango vya juu kabisa vya<br />

usiri na Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti wa Bodi. Hata hivyo, katika mazingira yasiyo ya<br />

kawaida, mlalamikaji anaweza kuamua kutoonyesha jina lake au maelezo ya jinsi ya kumpata na<br />

anaweza kuwasilisha malalamiko yasiyo na jina. Hata hivyo, walalamikaji watambue kwamba<br />

ushirikiano wa moja kwa moja na walalamikaji unawezesha kwa kiwango kikubwa kushughulika, na<br />

kuirahisishia the <strong>Foundation</strong> kuchukua hatua za kutosha, za haki na endelevu ili kutatua mapungufu<br />

yanayohusika.<br />

31

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!