yaliyomo - The Foundation for Civil Society
yaliyomo - The Foundation for Civil Society
yaliyomo - The Foundation for Civil Society
- No tags were found...
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
YALIYOMO<br />
UTANGULIZI .........................................................................................................................3<br />
1. MAELEZO YA FOUNDATION............................................................................................4<br />
1.1 Dira .........................................................................................................................4<br />
1.2 Lengo........................................................................................................................4<br />
1.3 Misingi......................................................................................................................4<br />
2. Maelezo ya maana ya maneno tunayotumia: Tunavyomaanisha katika<br />
maneno tunayotumia ...............................................................................................5<br />
3. Nani anaweza kuomba ruzuku...............................................................................6<br />
3.1 Matawi ya mashirika makubwa.................................................................................7<br />
3.2 Makundi yanayoshirikiana.........................................................................................7<br />
4. Programu ya ruzuku.................................................................................................7<br />
5. MAENEO YANAYOFADHILIWA NA FOUNDATION..........................................................8<br />
5.1. Ushiriki wa kutunga sera na kutekeleza (sera)............................................................8<br />
5.2 Kuimarisha utawala bora na haki za binadamu (utawala)...........................................9<br />
5.3 Kuimarishwa kwa Uwezo wa Asasi za Kiraia...........................................................10<br />
6. MAENEO AMBAYO HAYATAFADHILIWA NA FOUNDATION.........................................11<br />
7. Jinsi ya kutuma maombi ..........................................................................................12<br />
7.1 Nyaraka zinazotakiwa.............................................................................................12<br />
7.2 Matawi ya mashirika makubwa...............................................................................13<br />
7.3 Makundi yanayoshirikiana.......................................................................................13<br />
7.4 Ufadhili wa mradi mkubwa, wenye washirika wengi...............................................13<br />
8. WADHAMINI..................................................................................................................14<br />
8.1 Nani anastahili kuwa mdhamini wa maombi yako.................................................14<br />
8.2 Maoni ya wafadhili..................................................................................................15<br />
9. Mara ngapi waweza kutuma maombi.................................................................15<br />
9.1 Kama umeshawahi kupata fedha kutoka <strong>Foundation</strong> siku za nyuma........................15<br />
9.2 Utumaji wa maombi ya ruzuku...............................................................................15<br />
10. Nini kinatokea katika maombi yako.....................................................................15<br />
10.1 Vigezo vya tathmini.................................................................................................16<br />
10.2 Asasi yako..............................................................................................................16<br />
10.3 Mradi wako.............................................................................................................16<br />
10.4 Mambo yako ya kifedha..........................................................................................17
10.5 Kama maombi yako hayakufanikiwa (kukubaliwa)...................................................17<br />
11. Mwongozo wa bajeti...............................................................................................18<br />
11.1 Gharama za usafiri..................................................................................................18<br />
11.2 Malazi na gharama za chakula................................................................................18<br />
11.3 Kupitisha matumizi kwa kutumia risiti tu.................................................................19<br />
11.4 Malipo ya ushiriki....................................................................................................19<br />
11.5 Honoraria/Tunzo isiyodaiwa....................................................................................19<br />
11.6 Gharama za uendeshaji & utawala / Mishahara / Mtaji............................................19<br />
12. Uangalizi/ UFUATILIAJI..............................................................................................20<br />
13. Jinsi ya kujaza fomu za maombi ya ruzuku.......................................................20<br />
14. MASUALA unayostahili kuyajua.............................................................................25<br />
14.1 Maombi ya ruzuku..................................................................................................25<br />
14.2 Masharti ya ruzuku..................................................................................................25<br />
15. Viambatisho................................................................................................................26<br />
15.1 Kiambatisho 1: Wadhamini wa Ufadhili..................................................................26<br />
15.2 Kiambatisho II: Mpango wa Mafunzo .....................................................................27<br />
15.3 Kiambatisho III: Muundo wa Upangaji wa Bajeti.....................................................28<br />
15.4 Kiambatisho lV: Mpango wa Ufuatiliaji na Tathmini.................................................29
UTANGULIZI<br />
Tunawakushukuru kwa kuonyesha nia ya kushirikiana na <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong>. Kila kitu<br />
unachotaka kujua kuhusu ruzuku na namna ya kuomba kipo katika mwongozo huu. Tafadhali<br />
yasome maelezo haya kwa makini kabla ya kujaza fomu yako.<br />
Ndani ya mwongozo huuutapata maelezo juu ya nani anaweza kuomba ruzuku, nini tunakiangalia<br />
katika kufikiria maombi husika, namna ambavyo maombi yako yatashughulikiwa, na namna ya<br />
kujaza fomu ya maombi. Fomu za maombi zinapatikana katika lugha za Kiingereza na Kiswahili.<br />
Wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong> wanao wajibu wa kutoa ufafanuzi wa vipengele vya fomu ya maombi<br />
vinavyoleta utata na hali ya maombi yako kwa njia ya simu, nukushi, barua au barua pepe.<br />
Kama unataka kujadili swali lolote linalohusu fomu yako, tafadhali ipigie kwanza ofisi yetu ili iweze<br />
kupanga muda wa mkutano na mmoja wa wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong>. Nafasi za miadi zinapatikana<br />
Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 8:00 - 9:30 alasiri.<br />
Fomu za maombi zinapatikana kati ya Jumatatu hadi Ijumaa toka saa 2.30 asubuhi - 10.00 jioni.<br />
Kama huwezi kufika katika ofisi zetu kwa ajili ya kuchukua fomu za maombi unaweza kupiga simu,<br />
kuandika barua pepe au kutuandikia barua ya kawaida na tutakutumia kifurushi cha fomu. Pia fomu<br />
za maombi zinapatikana katika tovuti ya <strong>Foundation</strong> www.thefoundation-tz.org.<br />
<strong>Foundation</strong> utaipata kupitia<br />
<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong><br />
Haidery Plaza, Ghorofa ya tano,<br />
Mtaa wa Upanga/Kisutu,<br />
S.L.P 7192,<br />
Dar-es-Salaam,<br />
Tanzania.<br />
Simu: 022 - 2138530 / 2138531 / 2138532, 0754 - 005708<br />
Nukushi: 022 - 2138533.<br />
Barua pepe: in<strong>for</strong>mation@thefoundation-tz.org<br />
Tovuti: www.thefoundation-tz.org
1. NINI MAANA YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY<br />
<strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> (<strong>Foundation</strong>) ni asasi huru iliyoanzishwa Tanzania kama Kampuni<br />
isiyozalisha faida, inayofadhiliwa na wabia wa maendeleo wenye mawazo yanayofanana, na<br />
kuongozwa na Bodi iliyo huru.<br />
1.1 Dira<br />
Dira ya <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> ni ‘Tanzania ambayo wananchi wake wamewezeshwa kutambua haki zao<br />
na kushiriki katika michakato ya mabadiliko ambayo itaboresha hali zao za maisha.’<br />
1.2 Dhima<br />
Kuwawezesha wananchi kupitia utoaji wa ruzuku, kuwezesha kuundwa kwa mitandao na kuwezesha<br />
utamaduni wa kujifunza pasipo ukomo katika Sekta ya Asasi za Kiraia.<br />
1.3 Maadili ya Msingi<br />
<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> inaahidi kutekeleza maadili yafuatayo:<br />
Haki<br />
Tutafanya kila jitihada kuhakikisha kwamba huduma zetu haziwi za kibaguzi na kuzingatia<br />
misingi ya usawa kuwa ndio mwongozo wa kazi zetu.<br />
Uadilifu<br />
<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> na wafanyakazi wake watatenda na kuhubiri uadilifu, katika miundo yake<br />
yote, na katika shughuli zetu zote. Tutaendeleza sera ya ‘Kutovumilia Hata Kidogo’ aina zote<br />
za rushwa, za ndani na nje ya <strong>Foundation</strong>.<br />
Uweledi<br />
Tutaukuza na kuuendeleza utamaduni ambapo wale wote wanaokutana nasi watahudumiwa<br />
kwa uweledi, upole na heshima wakati wote. Tutajenga na kujivunia utamaduni wenye misingi<br />
ya ubora na ufanisi, na kuwawezesha wale wote wanaofanya kazi na <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> waige<br />
mfano huo katika shughuli zao zote.<br />
Uwazi na Uwajibikaji<br />
Tutakuwa wazi, hatutaficha na tutakuwa waaminifu. Tutawasilisha kwa uwazi yale yote<br />
tunayoyafanya kwa kuzingatia itifaki za kutunza siri. Tutawajibika kwa vitendo vyetu na kwa<br />
wale tunaowahudumia.<br />
Usawa wa Jinsia<br />
Tutajitahidi kuhakikisha kwamba masuala ya jinsia yanaingizwa kama ajenda rasmi katika<br />
shughuli zetu zote, na tutawasaidia wapokearuzuku na wabia wetu waone umuhimu wa<br />
kuzingatia jinsia.<br />
<strong>Foundation</strong> haina nia ya kuwa mwakilishi wa asasi za kiraia au kuzungumza kwa niaba yao, bali<br />
kujenga uwezo wa asasi hizo kwa kutumia utaratibu ulio ratibiwa vyema kukiwa na viwango vya<br />
juu vya uwajibikaji, uwazi, ubora na matokeo.
2. Maelezo ya maana ya maneno yaliyotumika<br />
Uwajibikaji<br />
Utetezi<br />
AZAKi<br />
Consortium<br />
Mjumbe<br />
Katiba<br />
Mali iliyowekwa wakfu<br />
(endowment)<br />
Usawa wa jinsia<br />
Utawala<br />
Rasilimali<br />
Mabadiliko/ matokeo<br />
ya muda mrefu<br />
Uchukuaji wa dhamana kwa matendo yanayofanyika katika utendaji wa<br />
shughuli stahiki.<br />
Mchakato wa kushawishi mabadiliko ya sera, utetezi unaweza kutumika<br />
kuelezea udhaifu wa sera, au mapungufu yaliyopo katika sera au sera<br />
ambazo zipo lakini hazifuatwi.<br />
Asasi zilizoundwa nje ya mfumo wa serikali ambazo huwezesha<br />
wananchi kueleza mawazo yao na kuyafanyia kazi kwa pamoja kufikia<br />
lengo lililokusudiwa. (Yaani Asasi za Kiraia).<br />
Ni muunganiko wa makundi tofauti ambayo yanashirikiana kufikia lengo<br />
ambalo ni moja.<br />
Mwanachama au mmoja wa wafaidika wanaowakilishwa na asasi au<br />
binafsi.<br />
Hati ya kisheria yenye vipengele vifuatavyo:<br />
- Jina la taasisi, madhumuni ya uwepo na malengo.<br />
- Maelezo ya kufikiwa kwa malengo.<br />
- Maelezo ya namna ya taasisi inavyoongozwa na kusimamiwa.<br />
- Maelezo ya jinsi watu wanavyojiunga katika taasisi.<br />
- Sahihi za viongozi na siku ya asasi kupitisha katiba.<br />
Kiasi cha fedha kinachotolewa kwa kampuni au asasi kwa lengo la<br />
kuzalisha fedha badala ya kutumia mara moja. Faida inayopatikana<br />
sehemu inatumika kuendeshea mhimili muhimu wa asasi husika na<br />
faida iliyobaki inagawiwa tena kutokana na sheria za ufadhili wa fedha<br />
ili kuhakikisha uongezekaji wa ukuaji kwa ajili ya riba zaidi na shughuli<br />
za baadaye za asasi husika.<br />
Ni pale ambapo mwanaume na mwanamke wanakuwa na nafasi sawa<br />
na kuelewa vizuri haki zao za binadamu na umuhimu katika kushiriki<br />
na kupata faida za maendeleo ya kitaifa, kisiasa, kiuchumi, kijamii na<br />
kitamaduni kwa kuzingatia haki za binadamu.<br />
Sheria na kanuni zinazotakiwa kufuatwa katika uendeshaji na utekelezaji,<br />
na ushirikiano wa nje wa asasi mbalimbali na serikali.<br />
Shughuli unazofanya ambazo zitaleta huduma zinazokusudiwa na mradi.<br />
Tofauti ya muda mrefu ambayo imechangiwa na mradi huo katika<br />
kuyabadili maisha ya watu.
Wanachama<br />
Isiyoendeshwa kwa<br />
Mabadiliko<br />
Matokeo ya awali<br />
Sera<br />
Mtandao wa usalama<br />
Mtaji jamii<br />
(Social capital)<br />
<strong>Foundation</strong><br />
Makundi yaliyo katika<br />
hali hatarishi<br />
Watu wanaohusika na asasi fulani. Asasi pia zinaweza kuwa<br />
wanachama.<br />
Fedha zinazopatikana na kuwekwa katika shughuli kwa ajili ya umma si<br />
kwa ajili ya mtu binafsi.<br />
Kitu ambacho kitaonyesha tofauti moja kwa moja katika utoaji huduma<br />
kwa watu na asasi, na mafanikio ambayo asasi itayapata.<br />
Mabadiliko ya moja kwa moja ambayo huduma yako itatoa kwa wale<br />
wanaofaidika na mradi.<br />
Sera ni muongozo, kanuni au maamuzi ambayo yanaziongoza au<br />
yanayoonyesha shughuli za watu au makundi ya watu. Sera zinaweza<br />
kuwepo katika maumbo na ukubwa wa aina zote, katika ngazi ya kijiji<br />
hadi mkoa, ngazi za kitaifa na kimataifa.<br />
Juhudi za jamii za kujihami na kujitoa kwa wale waliopo katika mazingira<br />
magumu miongoni mwao.<br />
Sheria na wajibu ulio ndani ya majukumu ya kijamii yanayowawezesha<br />
watu kufikia malengo yao binafsi na yale ya kijamii.<br />
<strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong>.<br />
Wale watu ambao wamebaguliwa kutokana na mazingira yao<br />
na wapo hatarini. Wanaweza kuwa wazee, watoto, wenye VVU/<br />
UKIMWI, wakimbizi yatima n.k.<br />
3. Nani anaweza kuomba ruzuku<br />
Tunakaribisha maombi kutoka kila pembe ya nchi yetu. Asasi yako inaweza kuomba ruzuku kutoka<br />
<strong>Foundation</strong> kama ni:<br />
• Asasi isiyo ya Kiserikali (NGO)<br />
• Asasi ya Kijamii (CBO)<br />
• Chama cha Kitaalamu<br />
• Chama cha Wafanyakazi<br />
• Chombo cha Habari <br />
• Chama cha Ushirika 2<br />
• Chama cha Kidini 3<br />
1 - 2 <strong>Foundation</strong> inaweza kutoa ruzuku kwa vyombo vya habari, vyama vya ushirika kama fedha zinazoombwa kwa ajili ya mradi hazichangii<br />
kuwapatia wao faida, kulipa madeni, kulipa gharama za uendeshaji, na mradi umelenga kuisaidia<br />
3 Kumbuka kuwa makanisa na misikiti sio sehemu ya asasi za kidini
Na kama:<br />
• Taasisi yako imesajiliwa Tanzania Bara au Visiwani.<br />
• Kama umeandikishwa kama chama kisichotengeneza faida.<br />
• Una katiba au kanuni za uendeshaji ambazo zinatambuliwa kisheria zikiwa zinaeleza wazi<br />
madhumuni ya asasi yako na namna ambavyo unaiendesha.<br />
• Asasi yako ina akaunti ya benki ambayo imekuwa na watia saini/sahihi zaidi ya mmoja.<br />
(i) <strong>Foundation</strong> inaweza kutoa ruzuku kwa vyombo vya habari vyama vya ushirika kama<br />
fedha zinazoombwa kwa ajili ya mradi hazichangii kuwapatia wao faida, kulipa madeni,<br />
kulipa gharama za uendeshaji, na mradi umelenga kuisaidia jamii.<br />
(ii) Taasisi ambazo zinajishughulisha na fedha kama kuweka na kukopa katika ngazi za vyama<br />
vya ushirika au wakopeshaji wadogo au wale ambao wanashughulika na uwezeshaji wa<br />
kifedha kwa lengo la uzalishaji watatakiwa kujieleza kwa undani zaidi kama watataka fedha<br />
kutoka <strong>Foundation</strong> kwa lengo la kufanya shughuli nyingine zaidi ya zile wanazozifanya.<br />
(iii) <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> haitoi ruzuku kwa AZAKi za kimataifa (INGOs).<br />
3.1 Matawi ya mashirika makubwa<br />
Asasi ambayo ni tawi la asasi kubwa inaweza kuomba ruzuku kama itaonyesha wazi kwamba<br />
inajiendesha bila kutegemea makao makuu yake.<br />
3.2 Makundi yanayoshirikiana (consortia)<br />
<strong>Foundation</strong> inashawishi asasi mbalimbali kufanya kazi kwa pamoja ili kutatua tatizo moja. Na kama<br />
asasi mbili au zaidi zitaomba ruzuku kwa pamoja zitachukuliwa kama kundi la asasi.<br />
4. Programu ya ruzuku<br />
Jedwali lifuatalo linaonyesha kiasi cha ruzuku kinachotolewa, tarehe ya mwisho ya kupokea maombi,<br />
na kipindi hadi utoaji wa ruzuku. Kuna aina nne za ruzuku ambazo zinatolewa na <strong>Foundation</strong>.<br />
Aina ya ruzuku na tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi<br />
Aina ya Ruzuku Kiwango<br />
cha juu<br />
kwa<br />
mwaka<br />
Muda wa<br />
juu wa<br />
ruzuku<br />
Muda wa<br />
mwisho wa<br />
kuomba<br />
Ruzuku Kubwa<br />
(SG)<br />
Ruzuku ya<br />
kiwango cha<br />
kati (MG)<br />
Ruzuku ndogo<br />
(RDG)<br />
Ruzuku ya<br />
Usajili (RDG)<br />
Shilingi<br />
Milioni<br />
125<br />
TZS<br />
Milioni 45<br />
Milioni<br />
7.5<br />
Laki mbili<br />
(200,000)<br />
Miaka 3 Machi 1<br />
Julai 1<br />
October 1<br />
Miaka 3 Machi 1<br />
Julai 1<br />
Oktoba 1<br />
Mara<br />
moja<br />
Mara<br />
moja<br />
Machi 1<br />
Julai 1<br />
Oktoba 1<br />
Machi 1<br />
Julai 1<br />
Oktoba 1<br />
Taarifa kwa<br />
walioleta<br />
fomu za<br />
maombi<br />
Kama ikipitishwa<br />
fedha hutolewa<br />
katika kipindi cha<br />
Wiki 16 Wiki 24<br />
Wiki 8 Wiki 16<br />
Wiki 8 Wiki 16<br />
Wiki 8 Wiki 16
Tunashauri uwasilishaji wa fomu za maombi mapema zaidi kabla ya tarehe wa mwisho<br />
Idadi ya maombi yanayoweza kushughulikiwa katika kila mkupuo mmoja ina kikomo kutokana na<br />
wingi wa mahitaji. Maombi yatapewa kipaumbele kulingana na yalivyowahi kufika kwa msingi wa<br />
“Kuwahi kufika, kuwahi kushughulikiwa”, na utapewa taarifa kama fomu yako haitashughulikiwa<br />
katika muda ambao umeombea.<br />
Waombaji wa ruzuku wanaruhusiwa kutuma maombi kupitia tovuti moja kwa moja LAKINI wanatakiwa<br />
kuhakikisha kwamba wanatuma pia fomu zilizotiwa saini na viambatanishi vya muhimu.<br />
Maombi yanayofika ofisini baada ya tarehe ya mwisho ya kuwasilisha kupita hayatashughulikiwa na<br />
yatarudishwa kwa muombaji.<br />
Ushiriki katika ufadhili wa pamoja<br />
<strong>Foundation</strong> ipo tayari kuchangia sehemu ya ufadhili kwenye mradi mkubwa ambao umefadhiliwa<br />
pia na wafadhili wengine. Unachotakiwa kufanya ni kuonyesha wazi ni sehemu gani <strong>Foundation</strong><br />
inaombwa kusaidia.<br />
5. MAENEO YANAYOFADHILIWA NA FOUNDATION<br />
<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> itafadhili maombi yote ambayo yamelenga kufanya shughuli<br />
mbalimbali kusaidia watu maskini na wenye mahitaji na hasa katika maeneo lengwa yafuatayo:<br />
5.1. Ushiriki katika utungaji wa sera na utekelezaji wake<br />
Sera inaweza kuelezwa kama kanuni ambazo kwazo serikali, vyama vya siasa, kampuni za biashara<br />
na asasi za kiraia, n.k. huongoza utekelezaji wa shughuli zake kwa umma au sheria katika utekelezaji<br />
wake. Kwa maneno mengine Sera ni mpango wa utendaji au maelezo ya nia na mawazo.<br />
Wajibu wa asasi za kiraia ni muhimu ili kuruhusu sauti za watu zisikike katika mchakato wa<br />
kutunga sera. <strong>Foundation</strong> inasaidia miradi na asasi ambazo zinaiwezesha jamii kujihusisha katika<br />
kutengeneza, kushirikiana na kutangaza sera; na ufuatiliaji na utekelezaji wa sera. <strong>Foundation</strong><br />
itatoa ruzuku kwa miradi na asasi ambazo zitaiwezesha jamii kujihusisha katika kutengeneza,<br />
kushirikiana na kuitangaza sera, pamoja na ufuatiliaji na utekelezaji wa sera. <strong>Foundation</strong> itafadhili<br />
miradi itakayowezesha sekta ya asasi za kiraia kuchangia katika kuimarisha uwezo wa wananchi<br />
kushiriki ipasavyo katika michakato ya sera ili waweze kuchangia katika jitihada za kupunguza<br />
umasikini. Miradi iliyoandikwa vyema yenye sifa zifuatazo itafikiriwa kupata ruzuku:<br />
• Ile yenye uwezekano wa kuongeza kuzingatiwa kwa sera, sheria na kanuni za maendeleo ya<br />
taifa,<br />
• Ile yenye uwezekano wa kupunguza vikwazo vya kisera, kisheria na usimamizi vinavyoathiri<br />
utoaji mzuri wa huduma,<br />
• Ile inayoweza kuchochea mabadiliko ya sera na utendaji ili kushughulikia mahitaji ya makundi<br />
yaliyo hatarini na pembezoni,<br />
• Ile inayoweza kuwahusisha na kushirikisha jamii, hususani wanawake, watoto, watu wenye<br />
ulemavu, masikini, makundi yaliyo hatarini na yaliyotengwa, katika kupanga vipaumbele kwa<br />
ajili ya kuunda sera katika ngazi zote.<br />
• Miradi ambayo inaweza kuongeza ufahamu wa wananchi kuhusu ubaguzi wa kijinsia, kutafsiri<br />
sera za jinsia na kuwezesha ushiriki wa wanawake na watu waliopo katika makundi mengine
ya waliotengwa, katika kupanga vipaumbele vya uundaji wa sera katika ngazi zote.<br />
• Miradi yenye uwezekano wa kuinua uelewa wa wananchi juu ya sera na athari zake katika<br />
maendeleo.<br />
• Miradi inayoweza kuongeza ushiriki wenye tija wa wananchi katika michakato ya sera (kutunga,<br />
kutekeleza na kufuatilia)<br />
• Miradi inayoweza kuchangia kuongezeka kwa rasilimali zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji<br />
wa sera maalumu.<br />
• Miradi inayoweza kuleta uraghibishi katika uwajibikaji na kujipanga vizuri kwa mikutano<br />
ya vijiji, kamati za maendeleo za kata na baraza kamili la madiwani la wilaya ili kuruhusu<br />
ushirikishwaji wa mwananchi na michakato ya sera ya mahali husika.<br />
• Miradi inayohakikishia kuzingatiwa kwa sera za kitaifa na kimataifa zinazoshughulikia mahitaji<br />
ya makundi maalumu.<br />
Mifano ya shughuli zilizopo chini ya ushiriki katika utungaji wa sera na utekelezaji wake ni pamoja na:<br />
• Ufuatiliaji wa miradi shirikishi ya kupunguza umasikini, ambayo inalinganisha na kutofautisha<br />
habari juu ya umasikini na kuzisambaza eneo pana<br />
• Kupanga mipango ndani ya jamii juu ya jinsi mabadiliko ya sera fulani yanavyoathiri maisha<br />
yao na jinsi watakavyoitikia<br />
• Ushiriki wa jamii katika kupanga vipaumbele kwa ajili ya sera za kitaifa<br />
• Kuinua ufahamu wa umma juu ya masuala ya sera<br />
5.2 Kuimarisha utawala bora na haki za kiraia<br />
Azaki ni vyombo muhimu vya kuhakikisha kwamba taasisi za umma zinafanya kazi katika mazingira<br />
ya uwazi na kwamba watu wanaelewa kuhusu haki zao. <strong>Foundation</strong> husaidia asasi zote ambazo<br />
zinaamsha uelewa wa watu kuhusu haki zao na majukumu ya serikali, kuimarisha ushirikiano kati<br />
ya asasi zinazofanya kazi katika masuala ya haki za binadamu katika ngazi za chini na kitaifa na<br />
kuongeza upatikanaji wa haki kwa wananchi wote wa Tanzania.<br />
Utawala bora unaweza kufafanuliwa kama ifuatavyo:<br />
• Kuheshimu kikamilifu haki za binadamu,<br />
• Jamii inayothamini wajibu na majukumu yake ya kiraia,<br />
• Utawala wa sheria,<br />
• Ushiriki athirifu,<br />
• Ubia unaohusisha watendaji wengi pamoja na wingi wa vyama vya siasa<br />
• Uwazi<br />
• Michakato inayowajibika ndani na baina ya taasisi<br />
• Sekta za umma, binafsi na asasi za kiraia zilizo na ufanisi na zenye kutimiza majukumu yao,<br />
• Uhalali, upatikanaji wa maarifa, habari na elimu,<br />
• Uwezeshaji wa watu kisiasa, usawa, uendelevu, misimamo na maadili ambayo inajenga<br />
kuwajibika, mshikamano na kuvumiliana.<br />
<strong>Foundation</strong> itatoa ruzuku kwa miradi ambayo itawezesha taasisi za serikali, umma na binafsi kuwa<br />
wazi zaidi, kuwajibika na kuheshimu utawala wa sheria na haki za binadamu. Mahususi, <strong>Foundation</strong><br />
itafadhili miradi ambayo itahakikisha wananchi wanafahamu haki na wajibu wao, waweze kudai<br />
uwajibikaji kutoka katika rasilimali za umma na hivyo miradi itakuwa na athari chanya katika<br />
maeneo yafuatayo:<br />
• Kuongezeka kwa uwezo wa wananchi, wake kwa waume, kupata habari juu ya shughuli za
Mamlaka za Serikali za Mitaa ambazo zinagusa jamii (katika eneo lile),<br />
• Kuongezeka kwa uwajibikaji wa kijamii kwa mamlaka husika za umma na binafsi,<br />
• Kuongezeka kwa ushiriki wa watu katika mikutano ya kijiji au serikali za mitaa,<br />
• Kuhakikisha kwamba rasilimali za umma na vitegauchumi vinasambazwa kwa usawa na kwa<br />
ufanisi na kusimamimiwa katika ngazi za vijiji na mitaa,<br />
• Kuhakikisha panakuwepo na sheria na kanuni zinazotosheleza ambazo zinadhamini<br />
kuheshimiwa kwa haki za binadamu<br />
• Kuhakikisha kwamba mipango na bajeti za taifa na wilaya zinajumuisha na kushughulikia<br />
mahitaji ya makundi maalumu<br />
• Kuongezeka kwa idadi ya watu wanaoripoti kuridhishwa na mfumo wa sheria<br />
• Kuongezeka kwa ushiriki wa wananchi katika programu za elimu ya uraia na mpiga kura<br />
• Kuimarisha uwajibikaji kati ya wananchi na viongozi wao waliowachagua, kama vile Madiwani<br />
na Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.<br />
Mifano ya shughuli chini ya Utawala Bora na Uwajibikaji ni pamoja na:<br />
• Mikutano ya hadhara juu ya sera za taifa<br />
• Vipindi vya radio juu ya masuala ya utawala bora kama vile rushwa<br />
• Michezo ya kuigiza shirikishi inayoamsha uelewa wa haki za binadamu<br />
• Mafunzo ya viongozi wa asasi za kiraia na serikali za mitaa juu ya mabadiliko katika wajibu<br />
na majukumu chini ya maboresho ya serikali za mitaa.<br />
5.3 Kuimarishwa kwa Uwezo wa Asasi za Kiraia<br />
Nia ya <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> ni kuhakikisha kwamba Asasi za Kiraia zinakuwa nguzo<br />
imara ya kuleta mabadiliko; kufanikisha malengo yake yaliyokusudiwa na inatekeleza wajibu wake<br />
wa utetezi kwa vipaumbele vya maendeleo. Tunapenda kuona sekta ya asasi za kiraia yenye ari,<br />
ubunifu, inayotimiza majukumu yake, endelevu na inayowajibika; ambayo inachangia kikamilifu<br />
katika kuleta mabadiliko ya kudumu katika maendeleo nchini Tanzania. Tunaelekeza nguvu zetu<br />
katika maendeleo ya asasi moja moja na mitandao. Lengo la itikadi hii ni kuzifanya asasi za kiraia<br />
zionekane na ziweze kutekeleza kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii yaliyo chanya.<br />
Kama sehemu ya uimarishaji wa uwezo wa asasi za kiraia, <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> itahakikisha uwepo wa<br />
muunganisho miongoni mwa asasi za kiraia katika kupeana habari na kujifunza, na kuwezesha<br />
utetezi imara uweze kufanyika. Wakati huo huo, asasi moja moja zinahitaji kukua ili ziweze kufanya<br />
utetezi ulio na tija.<br />
Mahususi <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> itafadhili maombi ambayo yanachangia katika mambo yafuatayo:<br />
• Kuboresha uwezo wa utawala, usimamizi na utendaji wa AZAKi na mitandao nchini<br />
Tanzania<br />
• Kuongezeka kwa uwiano wa AZAKi zenye mifumo imara ya usimamizi wa fedha yenye vyanzo<br />
vya fedha vinavyotosheleza na endelevu,<br />
• Kuongezeka kwa kuunganisha mitandao miongoni mwa AZAKi ili kuhakikisha upatikanaji rahisi<br />
na kupeana habari, na kuwa na sauti ya pamoja katika masuala mbalimbali ya maendeleo,<br />
• Kuongezeka kwa uwezo wa AZAKi katika kuwa na utaalamu maalumu wa sekta mbalimbali<br />
na kutumia mbinu za uweledi katika masuala ya maendeleo,<br />
• Kuboreka kwa AZAKi katika kujiingiza kwenye masuala ya sera.<br />
• Kuboreka kwa uwezo wa AZAKi katika kuandika mapendekezo ya miradi<br />
• Kuongezeka kwa uwazi, kujihusisha, ushiriki na uwajibikaji kwa walengwa wao<br />
10
• Kuongezeka kwa hadhi ya kisheria ya asasi moja moja na mitandao.<br />
Mifano ya shughuli zilizopo chini ya Uimarishaji wa Asasi za Kiraia ni pamoja na:<br />
• Kuimarisha mitandao<br />
• Kujenga uwezo<br />
• Kuunda na kusaidia mitandao ya wilaya<br />
• Mafunzo ya stadi katika uchambuzi wa sera na utetezi kwa ajili ya wafanyakazi<br />
Katika maeneo yote hapo juu, kuwahusisha masikini na makundi maalumu ni muhimu. Ubunifu<br />
unahimizwa sana. <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> inapendelea miradi ambayo inatumia mbinu za kuwafikia watu<br />
wengi zaidi, k.m. kutumia vyombo vya habari kuhakikisha idadi kubwa ya wananchi inalengwa na<br />
miradi inayofadhiliwa.<br />
6. MAENEO AMBAYO HAYATAFADHILIWA NA FOUNDATION<br />
<strong>Foundation</strong> inaweza kutoa ruzuku kwa asasi ambazo zimeanzishwa si kwa nia ya kupata faida au<br />
kwa ufupi hazizalishi kwa nia ya kupata faida. Hata kama mradi ulioombea si wa faida, hutakuwa na<br />
nafasi ya kupata ruzuku kama katiba yako haionyeshi wazi kwamba asasi yako kimeanzishwa kwa<br />
ajili ya huduma na wala si kwa kutengeneza faida. Kama unadhani kwamba asasi yako itakabiliwa<br />
na sharti kama hili tafadhali pata ushauri kutoka kwetu kabla hujaandika maombi ya ruzuku.<br />
<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> haitatoa ruzuku kwa hili/haya yafuatayo:<br />
• Fedha za kutunisha mfuko<br />
& msaada wa masomo au<br />
utaalamu<br />
• Mradi au shughuli ambazo<br />
zipo nje ya Tanzania<br />
• Mradi au shughuli ambazo<br />
tayari zimemalizika<br />
• Miradi ambayo inatoa<br />
ruzuku kwa taasisi nyingine<br />
• Bakshishi kwa ajili ya<br />
wafanyakazi wa asasi<br />
• Miradi inayozalisha faida<br />
/ shughuli za ukopeshaji<br />
fedha<br />
• Maombi ya ruzuku kutoka kwa wataalamu<br />
wa kuchangisha fedha au washauri ambao<br />
wanajitegemeza kwa niaba ya asasi<br />
• Watu binafsi<br />
• Vyama vya siasa<br />
• Mradi ambao unapendelea dini fulani<br />
• Sekta binafsi (Labda iwe chama<br />
kisichotengeneza faida)<br />
• Asasi ambazo zina madeni makubwa<br />
• Warsha, vingivevyo ziwe katika mpango<br />
mkubwa wa shughuli ambazo zimeungana<br />
zinaeleza kwa uwazi matokeo yake<br />
• Gharama ambazo hazikutarajiwa<br />
• Utoaji wa huduma za kijamii<br />
ZINGATIA: Taasisi zote ambazo huendesha shughuli za utoaji mikopo kama vyama vya kuweka<br />
na kukopa, taasisi za kifedha zinazotoa mikopo hata ile midogo au wale ambao biashara ya fedha<br />
ndio mhimili wao mkubwa wanatakiwa kuwasilisha mchakato ambao umeweka wazi na wenye<br />
ushawishi mkubwa kuhusu mradi wao kama watataka kushughulikia masuala nje na utaratibu wao<br />
wa kawaida wa biashara ya fedha. <strong>Foundation</strong> haitatoa fedha kwa ajili ya kukopesha watu binafsi<br />
au makundi.<br />
11
7. Jinsi ya kutuma maombi<br />
Tafadhali hakikisha kwamba unapata fomu halisi zinazohusiana na ruzuku yako au umeweza<br />
kupata kielelezo cha maombi kwa mahitaji yako. Vyote tunavyotaka kujua kutoka kwako vipo<br />
katika Mwongozo huu wa maombi ya ruzuku. Tafadhali hakikisha kwamba umejaza nafasi zote<br />
unazopaswa kujazwa katika fomu. Fomu ambazo hazijakamilika hazitashughulikiwa na zitarejeshwa<br />
kwako mwenyewe.<br />
Unatakiwa kutumia fomu au muundo ulioelekezwa na <strong>Foundation</strong> iwe katika mfumo wa nakala ya<br />
karatasi au ya kwenye kompyuta. Fomu zote zinatakiwa kuwasilishwa ama kwa uasili wake kama<br />
ni nakala ngumu (ya kwenye karatasi) au kutumia fomu iliyopo katika mtandao wa <strong>Foundation</strong>.<br />
Kumbuka kuwa wote wale watakaojaza fomu kwa kutumia njia ya mtandao, ni lazima pia kupeleka<br />
fomu zilizotiwa saini katika nakala ngumu pamoja na nyaraka nyingine zinazotakiwa kuambatana<br />
nazo.<br />
Kama utaona kwamba hakuna nafasi ya kutosha katika fomu yako ya maombi, tafadhali usitumie<br />
zaidi ya karatasi mbili za ziada kukamilisha majibu ya maswali. Karatasi zaidi zinaweza kutumika<br />
katika mapendekezo ya bajeti na mipango ya mafunzo kama ni lazima.<br />
7.1 Nyaraka zinazotakiwa<br />
Ili maombi yako yaweze kufikiriwa tunahitaji nyaraka zifuatazo:<br />
(i) Nakala mbili za fomu zako zikiwa zimekamilishwa,<br />
(ii) Nakala mbili za cheti cha usajili wa asasi,<br />
(iii) Nakala mbili za hati za kisheria zinazohusu asasi yako,<br />
(iv) Nakala mbili za taarifa za kibenki zinazoelezea mwenendo wa akaunti yako angalau kwa<br />
kipindi cha miezi sita iliyopita. Moja inatakiwa kuwa halisi ikiwa na muhuri na saini ya<br />
benki,<br />
(v) Nakala mbili za maelezo yaliyoandikwa na bodi ya wadhamini au miniti ya mkutano<br />
inayoonyesha kwamba wamepitisha fomu hiyo unayoiwakilisha <strong>Foundation</strong> na wamekubaliana<br />
na mradi,<br />
(vi) Majina ya wadhamini wawili ambao wanaweza kuzungumza kuhusu asasi yako kwa<br />
kujiamini,<br />
(vii) Majina mawili ya Wadhamini wa ufadhili wa zamani katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita<br />
na namna ya kuwapata (anuani) hasa kwa Ruzuku ya Kati na Ruzuku Kubwa. Kielezo cha<br />
wafadhili kinaambatanishwa hapa kama Kiambatanisho 1,<br />
(viii) Nakala mbili za taarifa ya fedha ya mwaka wa karibuni (kama una maombi ya Ruzuku ya Kati<br />
ya shilingi zinazofikia milioni 35),<br />
(ix) Nakala mbili za taarifa ya fedha iliyokaguliwa na kupewa cheti cha ripoti safi kwa miradi<br />
ambayo inachukua miaka mingi (Kama unaomba zaidi ya shilingi milioni 35).<br />
(x) Kama maombi yako yana kipengele cha mafunzo, unatakiwa pia kuleta:<br />
Nakala mbili za mpango wa mafunzo. Mpango wa mafunzo hayo ni lazima uelezwe kwa<br />
kina malengo ya mafunzo, kundi linalohusika, vigezo vilivyotumika kuwapata washiriki wa<br />
mafunzo, wasifu wa walimu na mchanganuo wa mafunzo yenyewe, vitu ambavyo vitafundishwa<br />
kwa washiriki. Kielezo cha mpango wa mafunzo/Kongamano kimeambatanishwa hapa kama<br />
Kiambatanisho II,<br />
(xi) Kwa asasi ambazo hazikusajiliwa kama asasi za kiraia chini ya Sheria ya Asasi Zisizo za<br />
12
Kiserikali (NGO Act) kuwa na Hati ya Kukubalika (Certificate of Compliance) kutoka kwa<br />
msajili wa NGOs itasaidia zaidi.<br />
Zingatia: Kama asasi hazitafikia masharti yanayostahiki hazitafikiriwa.<br />
7.2 Matawi ya mashirika makubwa<br />
Kama AZAKi yako ni tawi la asasi kubwa ni lazima utoe:<br />
• Nakala mbili za taarifa kutoka makao makuu kwamba wanajua mradi huo na wanakubaliana<br />
na fomu za maombi ya ruzuku unayopeleka <strong>Foundation</strong>.<br />
Pia lazima uwe katika nafasi ya kuthibitisha kwamba tawi lako lina haya yafuatayo:<br />
• Kamati ya menejimenti inayojitegemea,<br />
• Ina akaunti ya Benki,<br />
• Ina hesabu za kila mwaka,<br />
• Ina kauli juu ya mapato na matumizi yake.<br />
Zingatia: Kama ruzuku itapitishwa itachukua miezi 4 kutoka mwisho wa tarehe ya maombi hadi<br />
kupatikana kwa fedha. Unatakiwa kuhakikisha kwamba mpango wako wa utekelezaji hauanzi katika<br />
kipindi cha miezi minne tangu umepeleka maombi yako.<br />
7.3 Makundi yanayoshirikiana (Consortia )<br />
Kama mpo AZAKi tofauti lakini mnaomba ruzuku kama kundi linaloshirikiana ambalo linatambulika<br />
na kusajiliwa kisheria na lina katiba inayojitegemea iliyotengenezwa na wanachama wake, maombi<br />
ya ruzuku yataangaliwa kama maombi ya taasisi nyingine zinazotaka ufadhili.<br />
Lakini kama unaomba kwa niaba ya kundi ambalo halikusajiliwa kisheria lakini lina wanachama<br />
wanaotaka kufanyakazi pamoja kufikia lengo fulani lazima kufanya yafuatayo:<br />
• Lazima asasi moja ichaguliwe kama kiongozi ili kufanya kazi kwa niaba ya wenzake<br />
wanaohusika na mpango mzima;<br />
• Jaza fomu kwa ajili ya kundi lote (Hii ifanywe na AZAKi inayoongoza);<br />
• Mkubaliane kwamba ruzuku hiyo italipwa kwa asasi kiongozi ambayo itawajibika kutekeleza<br />
masharti ya ruzuku;<br />
• Ni lazima kuwasilisha maelezo ya AZAKi nyingine kuonyesha kukubaliana na fomu hiyo.<br />
Mkitaka ruzuku kama kundi (consortia) ni lazima ueleze wazi nafasi ya kila kundi katika utekelezaji<br />
wa mradi husika.<br />
ZINGATIA: Kundi linaweza kupeleka maombi mara moja tu kwa muda husika. Lakini wanachama<br />
wa kundi wanaweza kuomba ruzuku kwa miradi mingine ambayo haihusiki na mradi ulioombewa<br />
ruzuku kwa kupitia kundi walilopo. Na katika hili waombaji ni lazima waeleze wazi kabisa tofauti<br />
za maombi yao kutoka katika maombi ya kikundi( consortia)<br />
7.4 Ufadhili wa mradi mkubwa wenye washirika wengi<br />
Kama utaomba ufadhili kwa mradi mkubwa wenye wafadhili wengi ni lazima utoe uthibitisho<br />
ufuatao:<br />
• Nakala mbili za barua za kuthibitisha ufadhili kutoka kwa washiriki wote wa mradi husika.<br />
Barua hizo zieleze wazi kabisa kiwango cha fedha ambazo zinatolewa na wafadhili hao,<br />
13
muda ambao fedha zitawakilishwa na fedha hizo zitafanya nini katika mradi husika. Ni lazima<br />
ueleze wazi shughulia ambayo unataka ifadhiliwe na <strong>Foundation</strong>.<br />
Kumbuka<br />
Tafadhali hakikisha kwamba unaambatanisha nakala mbili kwa kila hati unayowasilisha ambayo<br />
inatakiwa kuambatana na maombi yako. Pia kumbuka kuandika jina la asasi yako na anuani juu<br />
ya kila hati inayoambatana na fomu za maombi. Hii itatusaidia kuhakikisha kwamba nyaraka<br />
husika zote zipo pamoja na maombi ya ufadhili.<br />
8. WADHAMINI<br />
Tutakuwa tunawasiliana na wadhamini na wafadhili wengine ambao umetujulisha katika maombi<br />
yako ya ruzuku.<br />
Ndio kusema unapotupatia anuani ya wafadhili wako wa sasa na waliotangulia na namba yako ya<br />
utambulisho tuliyokupa hakikisha haya yafuatayo yapo sahihi:<br />
• Taarifa zilizomo zipo sahihi,<br />
• Wahusika wameambiwa juu ya maombi yako,<br />
• Wahusika wanaweza kupatikana kwa njia ya simu ili kusaidia kujibu baadhi ya maswali kutoka<br />
<strong>Foundation</strong> katika kipindi cha wiki tatu tangu kuwasilisha kwako kwa fomu za maombi. Kama<br />
mhusika hawezi kupatikana kwa simu hakikisha kwamba unatoa anuani yake ya posta na<br />
anuani ya barua pepe, na kuwasilisha maombi yako mapema zaidi.<br />
Maombi yote ya ruzuku lazima yawe na wadhamini wawili.<br />
8.1 Nani anastahili kuwa mdhamini wa maombi yako<br />
Mdhamini lazima awe mtu mkweli ambaye unamfikiria kuwa mwaminifu na mtu ambaye anaaminika<br />
na maamuzi yake yanaweza kuaminika. Hao wawili lazima wawe wanajua asasi yako si chini ya<br />
mwaka mmoja na wawe na uwezo wa kubadilishana mawazo juu ya uwezo na uzoefu wa asasi<br />
husika. Ni lazima wawe wanaelewa vyema shughuli za asasi yako, menejimenti na fedha.<br />
Wadhamini hawapaswi kuwa:<br />
• Watu wa familia yako, ndugu au marafiki au yoyote ndani ya asasi,<br />
• Kiongozi wa asasi yako au alikuwa mfanyakazi wa zamani au wa sasa,<br />
• Mtu ambaye kwa sasa unashirikiana naye katika shughuli za asasi au zako,<br />
• Watu ambao unaweza kuwahusisha baadaye na shughuli za mradi unaouombea fedha.<br />
Tafadhali hakikisha kwamba wadhamini wako wanayotaarifa ya wewe kuwaweka katika fomu za<br />
kuomba ruzuku <strong>Foundation</strong> na kwamba utawatumia kama wadhamini na waambie mradi ambao<br />
umeuombea ruzuku.<br />
ANGALIA: Ni lazima ueleze wazi uhusiano ulionao na wadhamini husika katika maombi yako.<br />
Tunatarajia kwamba utatumia nafasi yako vyema ya kuchagua wadhamini wako. Kama wadhamini<br />
wataonekana hawafai basi maombi yako hayatafikiriwa.<br />
14
8.2 Maoni ya wafadhili<br />
Wafadhili ni wale ambao walishawahi kukupatia ruzuku katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.<br />
Orodhesha wafadhili wote bila kujali kama tutawauliza au la. Ni vyema kuorodhesha wafadhili<br />
wako wote wa zamani katika fomu ya kuombea ruzuku. Kama mtu unayemfahamu katika Asasi<br />
iliyowafadhili amebadilishwa, tafadhali elezea hili na itakuwa ni vema kama utatueleza nafasi hiyo<br />
kwa sasa imeshikwa na nani na jina lake kama inawezekana.<br />
Kielelezo cha wadhamini wafadhili kimeambatanishwa na kutambulishwa kama kiambatanisho I.<br />
Inatakiwa kueleweka mapema kwamba waombaji wa ruzuku watatakiwa kutengeneza muhtasari<br />
wa ufadhili ambao ulitolewa na wadhamini hao na kuelezea mabadiliko ambayo yamepatikana<br />
katika jumuiya ikiwa ni matokeo ya utekelezaji wa mradi huo hivi karibuni.<br />
9. Mara ngapi waweza kutuma maombi<br />
AZAKi hairuhusiwi kuomba ufadhili zaidi ya mmoja katika kipindi kimoja. Kama utapeleka maombi<br />
zaidi ya moja katika kila programu, maombi yote yatakataliwa. Inatakiwa utambue kwamba AZAKi<br />
inaweza kupokea ruzuku ya aina moja tu kwa kipindi kutoka <strong>Foundation</strong>.<br />
AZAKi yoyote ile ambayo imepeleka ombi lake la ufadhili la aina yoyote ile inashauriwa kusubiri<br />
majibu kutoka <strong>Foundation</strong> kwa ombi lake la kwanza kabla ya kutuma maombi mengine. Hii itasaidia<br />
kuona kwamba mambo yote yaliyoelezwa yanashughulikiwa inavyostahili.<br />
9.1 Kama umeshawahi kupata fedha kutoka <strong>Foundation</strong> siku za nyuma<br />
Ombi lako la zamani ni lazima liwe limeshughulikiwa na kufungwa rasmi kabla ya ombi jipya<br />
kufikiriwa.Tathmini ya mradi wako ni lazima iwe imefanywa na <strong>Foundation</strong> kabla ya kuanza kufikiria<br />
ombi jipya.<br />
Utatakiwa kuonyesha matokeo ya mradi wa kwanza, kuelezea mafanikio, mambo ambayo mmejifunza<br />
kutoka katika ruzuku yako ya kwanza, kutafakari uzoefu uliopatikana kutokana na utekelezaji wa<br />
mradi na kuelezea kwanini unataka kuendelea na mradi huo au kuupanua zaidi .<br />
9.2 Utumaji wa maombi ya ruzuku<br />
Mara tu utakapokuwa umekamilisha kujaza maombi yako ya ruzuku na kuambatanisha na hati<br />
zinazostahili unatakiwa kutuma maombi yako hayo kwa anuani ambayo imeonyeshwa ndani ya<br />
kitabu hiki. Maombi hayo yanatakiwa kufika katika ofisi za <strong>Foundation</strong> kabla ya muda wa mwisho<br />
wa kupokea maombi kutimia. Maombi pia yanaweza kuwasilishwa kwa kutumia tovuti kwa kutumia<br />
anuani ya barua pepe iliyomo ndani ya mwongozo huu.<br />
10. Nini kinatokea katika maombi yako<br />
Mara tu utakapowasilisha maombi yako ya ruzuku utapatiwa namba ya rejea ambayo ni namba<br />
ya utambulisho ikiwa ni kama kutambua kuwasilishwa kwa maombi yako ya ruzuku. Tafadhali<br />
usipige simu au kuulizia maombi yako mpaka siku uliyoambiwa kuulizia. Tafadhali tupatie muda wa<br />
kuangalia maombi yako kwa mujibu wa mwongozo huu kabla hatujakupa jibu.<br />
15
Kila maombi hupitia hatua kadhaa za kuangaliwa kabla ya kufikiwa kwa maamuzi. Uteuzi wa<br />
asasi zinazostahili kupata ruzuku hufanywa na manejimenti ya <strong>Foundation</strong>. Matokeo ya uteuzi huo<br />
huwasilishwa kwa bodi ya wakurugenzi ya <strong>Foundation</strong>.<br />
Matokeo hayo yatawasilishwa kwa wadau walioomba kwa njia ya barua, tovuti na magazeti.<br />
10.1 Vigezo vya tathmini<br />
<strong>Foundation</strong> huangalia kila ombi kwa kutazama vipengele ambavyo tayari vimewekwa katika kufikia<br />
kuamua AZAKi fulani kupewa ruzuku. Kama sehemu ya mchakato wa kupitia maombi unaweza<br />
kuletewa ombi la kutoa maelezo ya ziada. Lakini pamoja na kuulizwa maswali ya ziada na<br />
wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong> kamwe usifikiri kwamba nafasi yako ya kupewa ruzuku imeongezeka<br />
kutokana na maswali hayo.<br />
Kama asasi yako inastahili kuomba ruzuku, tambua kwamba maombi yako yataangaliwa kwa<br />
kuzingatia vigezo vifuatavyo:<br />
10.2 Asasi yako<br />
Vigezo hivi vinatusaidia kuangalia muundo na menejimenti ya asasi yenu. Tunahitaji kuwa na<br />
uhakika na:<br />
• Kuwa asasi yako ina muundo wa kiutawala ambao ni thabiti na unaowajibika,<br />
• Kwamba unaweza kabisa kupangilia fedha za asasi na kuzidhibiti,<br />
• Kwamba asasi yako ina njia za wazi kabisa za kupanga na kuendesha shughuli zake,<br />
• Shughuli za asasi ziko wazi kwa wote na inakazania kutoa haki sawa kwa kila mtu,<br />
• Kwamba asasi yako inaonyesha wazi kwamba ina uzoefu na utaalamu wa kufanya shughuli<br />
iliyosababisha uwepo wake,<br />
• Kwamba asasi yako ina mahusiano na asasi nyingine zenye malengo kama yako,<br />
• Kwamba asasi yako inajiendesha kwa kulingana na misingi ya <strong>Foundation</strong>,<br />
10.3 Mradi wako<br />
Vipengele vilivyotajwa hapa chini vinasaidia kutathmini mapendekezo ya mradi wako. Hivyo<br />
tunahitaji kuwa na uhakika na:<br />
• Kwamba tatizo lililoainishwa katika mradi unaoombewa ruzuku kuwa ni kweli ni hitaji kuu la<br />
kundi lililolengwa (wafaidika au jamii husika),<br />
• Kwamba mradi uliouibua umepangwa vilivyo na una wafanyakazi wanaostahiki,<br />
• Kusudio la mradi wako linaonyesha wazi kabisa haja iliyopo,<br />
• Mpango wako unaweza kufuatiliwa kwa urahisi kwa kutumia taarifa za awali zilizopo na<br />
kwamba inapimika kwa kutumia viashiria vilivyo madhubuti,<br />
• Mchanganyiko wa shughuli zinazolengwa kufanyika kama zinaweza kuleta mabadiliko ya<br />
msingi yaliyoainishwa na kutarajiwa (matokeo ya awali na mabadiliko),<br />
• Mradi wako unachangia kufikia dira, lengo la <strong>Foundation</strong> na angalau na moja kati ya maeneo<br />
makuu ya <strong>Foundation</strong>.<br />
16
Matokeo na mabadiliko yatakayoletwa na mradi wako sharti yawe:<br />
Maalumu - Je Matokeo & mabadiliko yana mwelekeo maalum<br />
Yanayopimika<br />
Yanatekelezeka<br />
Sahihi<br />
Muda maalumu<br />
Endelevu<br />
- Je mabadiliko unayoyataka yanaweza kuangaliwa kwa kuona hali halisi<br />
iliyopo sasa<br />
- Je mabadilkiko yanawezekana katika muda uliopo<br />
- Je matokeo & mabadiliko vinafanana na wazo la mradi ulioombewa ufadhili<br />
Je yanawiana na mapendekezo yako ya washiriki uliowapendekeza<br />
- Je unaweza kutambua muda ambao utaona matokeo & mabadiliko<br />
- je matokeo & mabadiliko yataendelea kuonekana hata baada ya mradi<br />
kumalizika<br />
10.4 Mambo yako ya kifedha<br />
Vigezo vifuatavyo vinatusaidia sisi kutambua namna unavyodhibiti fedha zako. Tunahitaji kuwa na<br />
uhakika na:<br />
• Kwamba asasi yako inaendeshwa vyema kifedha na inahitaji kupewa ruzuku,<br />
• Akaunti ya benki ya asasi yenu ina waweka sahihi zaidi ya mmoja.<br />
Mapendekezo ya bajeti ya mradi wako yawe kama ifuatavyo:<br />
Ya kina:<br />
Kila shughuli lazima ioneshe gharama zake kwa kina. Shughuli zote<br />
zilizoorodheshwa katika fomu yako ya maombi lazima ziwe zinaeleza<br />
bajeti kwa undani zaidi .Ni lazima katika maelezo yako utoe kwa<br />
muhtasari kidogo shughuli husika (Itafanyika wapi na kwa namna gani,<br />
lini itafanyika, watu wangapi watashiriki katika shughuli hiyo), na kueleza<br />
gharama yake kwa undani zaidi.<br />
Za kweli:<br />
Sahihi:<br />
Yanayostahiki:<br />
Thamani ya fedha:<br />
Mifumo ya fedha:<br />
kwamba mahitaji yaliyoorodheshwa katika bajeti ni ya gharama za kweli<br />
na yanatosheleza.<br />
Vifaa husika vinaakisi bei halisi na vimejumlishwa kwa usahihi<br />
Kwamba bajeti iliyopangwa ndiyo inayostahiki kwa asasi husika kwa<br />
kuzingatia ukubwa wa asasi na uzoefu wake<br />
Kama bajeti imezingatia gharama na inakidhi. Maombi ambayo<br />
yataonyesha matokeo mazuri na makubwa kwa gharama ndogo<br />
yataangaliwa kwa makini zaidi na kupewa kipaumbele.<br />
<strong>Foundation</strong> inatarajia kupata maombi kutoka kwa AZAKi zenye mfumo<br />
bora wa menejimenti na fedha na hivyo kuwa na rekodi za mapato na<br />
matumizi na kwa njia hiyo kudhibiti fedha.<br />
Kielelezo cha bajeti kimo ndani ya Mwongozo huu kama kiambatanisho III<br />
17
10.5 Kama maombi yako hayakupita<br />
Kama <strong>Foundation</strong> inaamua kwamba haitatoa ruzuku kwa asasi yako basi utapatiwa taarifa kwa njia<br />
ya posta wiki nane baada ya kupita kwa muda wa mwisho wa kuwasilisha maombi katika kipindi<br />
husika. Utapata barua inayokueleza wazi kwa nini <strong>Foundation</strong> imeshindwa kukubaliana na ombi<br />
lako la kutaka ruzuku. Ni vyema kama utaisoma barua hiyo kwa uangalifu unaostahili.<br />
Kama mtaamua kutuma maombi tena kwa <strong>Foundation</strong> kwa mradi huo huo itawapasa kujaza tena<br />
fomu mpya na kuhakikisha mambo yote yaliyoelekezwa katika barua mnayatekeleza.<br />
11. Mwongozo wa bajeti<br />
Unatakiwa kuwasilisha bajeti katika muundo ambao ni wazi na rahisi kuelewa kwa mujibu wa<br />
maelekezo ambayo yapo katika mwongozo huu (Angalia muundo katika kiambatanisho III). Bajeti<br />
yako ni lazima ionyeshe wazi kwamba kiasi kilichoombwa kwa ajili ya mradi husika kimezingatiwa.<br />
Wakati unatengeneza bajeti, kuwa na uhakika na kitu ambacho umepanga kukifanya, namna<br />
utakavyofanya na kiasi gani cha fedha kinachotakiwa kwa mradi husika.<br />
<strong>Foundation</strong> haitakaa kuzungumza nawe kuhusiana na kilichomo au kiasi kilichopo katika bajeti<br />
yako au <strong>yaliyomo</strong> ndani mwake ambayo yamewasilishwa katika barua yako ya maombi. Hivyo ni<br />
muhimu sana kuwasilisha bajeti yenye kila kitu, sahihi na inayoonyesha dhahiri thamani ya fedha.<br />
Tengeneza bajeti kwa kuzingatia gharama halisi na kuwa na wastani katika maombi .Ni vyema katika<br />
hili ukatambua kwamba si lazima kupata kiasi cha fedha cha kiwango cha juu ambacho kipo.<br />
Maombi yako hayatafikiriwa iwapo bajeti yako haikutoa taarifa za kina na haioani na maelekezo na<br />
viwango vilivyotolewa katika mwongozo wa bajeti.<br />
11.1 Gharama za usafiri<br />
Safari zote lazima zifanywe katika hali ya kuzingatia unafuu wa njia ya usafiri na uiweke bajeti hiyo<br />
kama ni lazima watu wasafiri kwa umbali mrefu kushiriki katika shughuli za mradi.<br />
11.2 Malazi na gharama ya chakula<br />
Gharama zote za malazi na chakula ni lazima zithibitishwe kwa kutumia risiti katika taarifa ya<br />
matumizi ya fedha ya robo mwaka. <strong>Foundation</strong> haitapitisha bajeti ya matumizi bila kuwa na risiti<br />
halali za matumizi ya fedha. Tunahimiza asasi husika kulipa gharama hizi moja kwa moja badala ya<br />
kuwalipa washiriki.<br />
Ufuatao ni mwongozo unaostahili kutumika kwa ajili ya malazi na chakula:<br />
Eneo Malazi Posho ya kujikimu<br />
Majiji, Zanzibar, Dodoma, Bagamoyo Mjini 32,000 13,000<br />
Manispaa 22,000 13,000<br />
Mikoa na miji mikuu ya wilaya 11,000 9,000<br />
Maeneo mengine yote 5,000 6,000<br />
18
11.3 Kupitisha matumizi kwa kutumia risiti peke yake<br />
Wakati unandaa bajeti yako, tafadhali kumbuka kwamba tumekupatia mwongozo wa kiwango cha<br />
juu ambacho kinaweza kutumika kwa ajili ya usafiri, malazi na posho ya kujikimu.<br />
Gharama zote za usafiri, malazi na posho ya kujikimu ni lazima kulipwa kwa wale ambao wanatoka<br />
nje ya mji unakofanyika mradi husika (kwa wale washiriki ambao hawaishi katika eneo ambalo<br />
zinafanyika shughuli husika). Washiriki ambao ni wakazi wa eneo ambako ndiko mradi unakofanyika<br />
hawaruhusiwi kupewa malipo haya.<br />
11.4 Malipo ya ushiriki<br />
Hairuhusiwi kulipa malipo ya ushiriki kama motisha (posho za vikao) kwa ajili ya kushiriki katika<br />
warsha au mikutano mingine.<br />
11.5 Bakshishi (Honoraria)<br />
Bakshishi (Honoraria) inaweza kulipwa kwa mtu wa nje ambaye ametoa au amefanya kazi fulani<br />
ya huduma katika mradi. Chagua watu wako wa kukuendeshea mambo kwa kuzingatia bajeti yako<br />
na njia mbadala ya kupunguza gharama za matumizi. Honoraria kamwe isilipwe kwa wafanyakazi<br />
wenye mshahara katika AZAKi yako. Zingatia kwamba kama honoraria zako, posho ya kujikimu na<br />
malazi yapo juu maombi yako yanaweza kukataliwa.<br />
11.6 Gharama za uendeshaji & utawala / Mishahara<br />
Unaweza kabisa kubajeti sehemu fulani ya fedha zako kwa ajili ya kujiendesha na hii isizidi asilimia<br />
30 ya fedha zilizoombwa kutoka <strong>Foundation</strong>. Hii ni sawasawa na kutoa msaada katika gharama<br />
za uendeshaji na inatakiwa kuendesha gharama zote za msingi za kuendeshea AZAKi (kama vile<br />
gharama ya pango, vifaa vya ofisi, mishahara, gharama za magari, muda wa wafanyakazi wa utawala,<br />
na huduma za azaki ambazo haziko mahsusi kwa ajili ya mradi). Bajeti yako isiongeze gharama za<br />
huduma za kiutawala kwa zaidi ya asilimia 30. Kwa wale ambao wataomba chini ya asilimia hizo<br />
wataangaliwa vyema kwani inaonekana wao wanatambua thamani ya fedha.<br />
Kumbuka<br />
Ukiwa unakamilisha fomu yako ya maombi tafadhali kumbuka:<br />
• Jaza maombi ya ruzuku kwa kuzingatia uzoefu wa AZAKi na mipango yake.<br />
• Tunaangalia kwa makini sana juu ya mawazo yako na si maneno tu unayotumia katika<br />
fomu yako ya maombi ya ruzuku. Kama tutahisi kwamba maombi yako ya mradi<br />
yameandaliwa na mtaalamu wa masuala ya utunishaji mfuko, huenda tukakutoa kwani<br />
hustahili.<br />
• Unatakiwa kutupatia taarifa za kweli na takwimu zinazounga mkono ombi lako.<br />
• Unatakiwa kuwa na uhakika juu ya mradi wako na kitu unachoweza kufanikiwa.<br />
• Andaa bajeti yako kwa kuzingatia gharama halisi kwa kutumia mwongozo uliopewa.<br />
Usiweke bei ya juu ya vifaa au kupandisha gharama.<br />
• Usiambatanishe na taarifa za ziada ambazo hazikuombwa.<br />
• Zingatia maelekezo uliyopewa katika Mwongozo huu na maelezo ya mwongozo<br />
kwenye fomu yako kwa ukamilifu.<br />
19
12. Ufuatiliaji<br />
Miradi yote ambayo imepewa ufadhili na <strong>Foundation</strong> itafuatiliwa na kukaguliwa kila mara. Unatarajiwa<br />
kuwasilisha kwa <strong>Foundation</strong> taarifa za robo mwaka za fedha na nadharia ya mwenendo wa mradi kama<br />
makubaliano ya mkataba yanavyodai. Ukaguzi huo utafanyika katika shughuli ambazo zimekubaliwa<br />
na katika taarifa zao za robo mwaka za maendeleo ya mradi na ripoti za fedha. Mpango wa kuripoti<br />
na muundo wake vitatolewa kwako mara tu baada ya kutia saini mkataba huo. Kielelezo cha mpango<br />
wa ufuatiliaji wa mradi kipo humu kwenye mwongozo kama Kiambatanisho IV.<br />
13. Namna ya kujaza fomu za maombi ya ruzuku<br />
Kipengele hiki kina maelekezo yanayohusu jinsi ya kujaza fomu za maombi. Lengo la sehemu hii<br />
ni kusaidia waombaji kuwa na elimu ya kutosha kuhusu maelekezo yanayotakiwa katika ujazaji wa<br />
fomu. Ni matumaini yetu kwamba waombaji wataona eneo hili kuwa na msaada mkubwa kwao.<br />
Tutashukuru kama waombaji watatutumia maoni au taarifa zao za mrejesho ambazo zitatusaidia<br />
kuboresha zaidi huduma zetu katika sekta ya AZAKi za Tanzania.<br />
Fomu za kuombea ruzuku zina sehemu nne kama ifuatavyo:<br />
• Sehemu ya 1: Taarifa ya mradi,<br />
• Sehemu ya 2: Muundo wa uendeshaji,<br />
• Sehemu ya 3: Angalia kama maombi yako yamejazwa vyema na kukamilika,<br />
• Sehemu ya 4: Kipengele cha makubaliano.<br />
Sehemu ya 1: Taarifa ya mradi<br />
1.1. Jina la Mradi: Muombaji hapa anatakiwa kuandika jina la mradi. (kwa mfano: Mradi wa<br />
udhibiti wa VVU na UKIMWI).<br />
1.2. Maeneo yanayofadhiliwa<br />
Hapa mwombaji anatakiwa kuonyesha ni eneo lipi kati ya maeneo yanafodhaliwa na<br />
<strong>Foundation</strong> ambapo mradi wake anauombea. Yaani mradi wake unaangukia katika wazo gani<br />
linaloshughulikiwa na <strong>Foundation</strong>.<br />
1.3. Lengo kuu la mradi: katika kipengele hiki muombaji anatakiwa kuandika taarifa kwa ufupi<br />
juu ya mafanikio ya mradi huo kwa upana wake, yaani mafanikio ya mradi katika ngazi za<br />
maendeleo ya kitaifa na ya kisekta (Mathalani, Kuboresha hali ya kiafya kwa wananchi wa<br />
wilaya XXX kwa kufanikiwa kushawishi wananchi kukabiliana na matatizo ya UKIMWI kwa<br />
namna endelevu zaidi).<br />
1.4. Muhtasari wa mradi: Toa maelezo ya kwa ufupi juu ya y mradi unalenga kufanikisha nini<br />
katika kipindi chote cha utekelezaji wake kwa walengwa wa eneo husika.<br />
Kwa mfano: Mradi utahakikisha unakuwa endelevu katika kukabiliana na tatizo la VVU na<br />
UKIMWI na magonjwa ya zinaa kupitia mpango wa CBHC, Uhamasishaji na ushiriki wa jamii<br />
(Community mobilization and participation), BCCI, Kuishauri jamii (Community Counseling),<br />
Msaada kwa Vijana( support <strong>for</strong> Youths) PLWHA na kushawishi upimaji hiari na ushauri nasaha.<br />
20
Pia mradi utaangalia athari za malaria kama ugonjwa nyemelezi ambao huharakisha vifo vya<br />
wagonjwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI au kuongeza mzigo kwa familia zilizoathirika<br />
na ugonjwa wa UKIMWI. Shughuli za mradi zitatekelezwa kwa ushirikiano wa karibu kati ya<br />
serikali ya Tanzania (kama: MOH na MOEC) Wilaya na serikali za vijiji na NACP. Utekelezaji<br />
wa mradi utasimamiwa na wizara ya Afya (MOH) kupitia mpango wake wa Kuzuia na Kudhibiti<br />
VVU/UKIMWI/Magonjwa ya zinaa MTP III) na NACP.<br />
Lengo kuu la kimaendeleo: Ni kuboresha afya za wakazi wa wilaya XXX kwa kuwashawishi<br />
kuwa na mpango endelevu wa kukabiliana na UKIMWI. Masuala makuu yatakayoangaliwa:<br />
Kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI; kuhudumia na kuwasaidia wananchi wanaoishi<br />
na viurusi vya UKIMWI; Kuhudumia na kuwasaidia watoto yatima na wale wanaoishi katika<br />
mazingira magumu na kuwa na mtandao wa elimu na utetezi kuhusu VVU/UKIMWI.<br />
1.5. Maelezo ya tatizo linalohitaji ufumbuzi kupitia mradi huu - Nini hasa kinakushawishi uone<br />
kuwa mradi huu unahitajika (Toa amelezo ya kitu ambacho kinatakiwa kubadilishwa kwa<br />
kundi husika kwa kutekeleza mradi huo).<br />
(Kwa mfano: Kwa mujibu wa ripoti ya National AIDS Control Program (NACP) asilimia 90<br />
ya wananchi wanaelewa kuhusu ukimwi. Ukweli huu hata hivyo unagongana na kasi ya<br />
maambukizi, inayosababisha kuwepo kwa idadi kubwa inayotisha ya wagonjwa wengi wa<br />
ukimwi. Janga hili limesambaa kwa kasi katika maeneo ya vijijini na mwaka 1997, zaidi ya<br />
asilimia 10 ya wanawake waliokuwa wakihudhuria kliniki za uzazi katika baadhi ya maeneo<br />
ya vijijini walibainika kuwa na virusi vya ukimwi.<br />
Idadi ya wagonjwa wa ukimwi kama ilivyoripotiwa na NACP kwa upande wa Tanzania<br />
Bara ilipanda kutoka 25,503 mwishoni mwa mwaka 1990 kufikia 88,667 mwaka 1996. Kiasi<br />
cha aislimia 80 ya waliokutwa na ugonjwa ni wale wenye umri wa miaka 20-44. Tanzania<br />
ni nchi iliyo kusini mwa Jangwa la Sahara ambayo imeathiriwa vibaya na janga hili ikiwa na<br />
wastani wa maambukizo ya asilimia 10 kwa watu wazima. Utafiti zaidi wa Tanzania National<br />
AIDS Control Program (NACP) Tanzania Bara unaonyesha kupanda kwa wagonjwa kutoka<br />
25,503 mwishoni mwa miaka ya 1990 kufikia 88,667mwaka 199. Kulikuwa na wagonjwa<br />
14,112wa ukimwi kwa mwaka 2001 na hivyo kusababisha idadi ya wagonjwa kufikia 144498<br />
toka 1983. Na zaidi ya asilimia 80 ya watu waliokutwa na ugonjwa huo ni watu wa umri wa<br />
miaka 20 – 44. Kuna wastani wa watu 2229770 wenye ukimwi ambao umri wao ni kuanzia<br />
miaka 15 na kuendelea. Magonjwa ya kuambukiza kwa njia ya zinaa (STIs) yaliyoripotiwa<br />
mwaka2001 yalikuwa 211291 na 149222 kwa mwaka 2000 na 39385 mwaka 1999 (Taarifa<br />
ya VVU/UKIMWI STI surveillance report NACP 2002). Kutokana na hali hiyo Wizara ya afya<br />
nchini Tanzania imebuni mkakati wa kukabiliana na hali hiyo unaoitwa (MTP – III) ukiainisha<br />
harakati mbalimbali zinazofanywa na taifa kukabiliana na ugonjwa huo kwa kuzingatia<br />
takwimu za mwaka 1998 hadi 2002).<br />
Itambulike wazi kuwa maandiko mazuri ya kauli ya tatizo lazima yawe na mambo yafuatayo:<br />
• Kueleza kwa uwazi kabisa hali ambayo inastahili kubadilishwa kwa utekelezaji wa mradi<br />
kwa kuzingatia ukweli wa mambo ulivyo,<br />
• Itaonyesha kwa wazi kabisa nani na nini kimeathirika,<br />
• Kuhalalisha uwepo wa tatizo,<br />
21
• Kuelezea tatizo ambalo linalhusiana na nia ya kuanzishwa kwa asasi,<br />
• Kuelezea ukubwa wa tatizo katika jamii husika.<br />
1.6. Muda wa mradi: Muda wa utekelezaji wa mradi. (Mfano: Mradi huu utatekelezwa kwa miezi<br />
24).<br />
1.7. Katika kipengele hiki muombaji anatakiwa kuonyesha kiwango cha fedha anachohitaji kutoka<br />
<strong>Foundation</strong> (kwa mfano. Sh. 249,000/=).<br />
1.8. Maelezo yanatakiwa kutolewa kama ufadhili unaoombwa ni wa kushirikiana yaani kama<br />
<strong>Foundation</strong> inatakiwa kugharamia sehemu tu ya ruzuku.<br />
1.9. Uchanganuzi wa Bao la Mantiki (Logical Framework Analysis).<br />
Lengo mahususi la mradi:<br />
Hapa muombaji anatakiwa kuandika matokeo anayoyatarajia katika mradi wake yaani faida yake<br />
kwa maendeleo ya wananchi, muda wa mradi utakapokuwa umekwisha. Wananchi watakuwa<br />
wamefaidi nini. Kumbuka kwamba vipengele vyote vya mradi vitachangia matokeo hayo.<br />
Viashiria vya mabadiliko:<br />
Hapa mwombaji anatakiwa kutoa maelezo mwishoni mwa mradi kuonesha kuwa mafanikio<br />
yamepatikana na manufaa yake ni endelevu.<br />
Matokeo ya awali:<br />
Hapa mwombaji anatakiwa kuandika matokeo ya moja kwa moja yatakayotolewa (bidhaa na<br />
huduma za mradi) ambazo zaidi zipo chini ya usimamizi wa menejimenti.<br />
Viashiria vya matokeo:<br />
Viashiria katika kiwango matokeo hupima kiasi na ubora wa matokeo na muda wa ufikishaji kwa<br />
wahusika. Kanuni hizi hutumika pia wakati wa kuuangalia mradi na pia kuufanyia tathmini.<br />
Shughuli<br />
Hapa muombaji anatakiwa kuwasilisha kazi zitakazofanywa katika utekelezaji wa mradi na hivyo<br />
kuleta matokeo.<br />
22
Mpangilio wa namna ya kufanya kazi<br />
Matokeo Viashiria vya matokeo Nguvu inayotolewa<br />
kwa kila tokeo<br />
Kupunguza<br />
maambukizo<br />
ya UKIMWI<br />
kupitia mpango<br />
endelevu wa<br />
afya ya msingi<br />
ya jamii,<br />
msaada wa<br />
kijamii, na<br />
mabadiliko ya<br />
kitabia ifikapo<br />
Desemba 2009<br />
• Mfumo wa<br />
kubadilishana<br />
taarifa za UKIMWI<br />
inaanza kufanya<br />
kazi ifikapo.<br />
Desemba 2009<br />
• Wengi wa vijana<br />
wanaanza kufanya<br />
ngono salama<br />
katika wilaya X<br />
ifikapo Desemba<br />
2009.<br />
Wananchi 40 kuwa<br />
wameshafunzwa<br />
masuala ya PRA ifikapo<br />
Desemba 08.<br />
Shughuli za kufanya kwa kila<br />
tokeo<br />
• Kutambua wanavijiji 40 ili<br />
kufundwa ifikapo Oktoba<br />
07.<br />
• Kuwezesha mafunzo ya<br />
PRA kwa jamii lengwa 40<br />
ifikapo Januari 08.<br />
• Kuandaa taarifa ya mafunzo<br />
Februari 08.<br />
Wanajamii 40<br />
waliofunzwa wanaanza<br />
shughuli za PRA katika<br />
vijiji 21 kwenye wilaya<br />
X ifikapo desemba 9.<br />
• Kuwezesha ufuatiliaji na<br />
tathmini baada ya mafunzo<br />
Desemba 08.<br />
Kuwa na wanavijiji<br />
wa kujitolea 30<br />
waliofunzwa VVU/<br />
UKIMWI na BCCI<br />
ifikapo Desemba 08.<br />
• Kutambua watu<br />
wa kujitolea 30 ili<br />
wafundishwe ifikapo Machi<br />
08.<br />
• Kuwezesha mafunzo ya<br />
HIV/AIDS na BCCI kwa<br />
watu 30 waliotambulika<br />
katika vijiji ifikapo April 08.<br />
• Kuandaa taarifa ya mafunzo<br />
ifikapo Mei 08.<br />
• Kuwezesha ufuatiliaji na<br />
tathmini baada ya mafunzo<br />
ifikapo Oktoba 08.<br />
Waelimisha rika 40<br />
wakitoa elimu ya VVU/<br />
UKIMWI kwa warika<br />
21 katika vijiji 21 vya<br />
wilaya X ifikapo Dec.<br />
09.<br />
• Kuwazuru waelimisha rika<br />
katika kila robo mwaka.<br />
23
1.10. Mpango wa ufuatiliaji wa Matokeo (Mfano)<br />
Matokeo Viashiria Zilikotoka takwimu Muda wa<br />
kukusanya data<br />
Kupunguza kiwango cha<br />
maambukizi ya VVU kwa<br />
kupitia mpango wa afya ya<br />
msingi, msaada wa kijamii<br />
na mabadiliko ya kitabia<br />
kufikia Desemba 2009.<br />
Kuwepo kwa<br />
mfumo wa<br />
kubadilishana<br />
taarifa za<br />
ukimwi kufikia<br />
mwaka 2009.<br />
• Kumbukumbu ya<br />
mahudhurio kituo cha<br />
taarifa.<br />
• Mchanganuo wa taarifa<br />
za makundi lengwa.<br />
• Taarifa za tathmini.<br />
• Kila mwezi.<br />
• Kwa miezi<br />
mitatu (kila<br />
robo mwaka).<br />
• Kwa mwaka.<br />
1.11. Walengwa: Idadi na mahali walipo<br />
Taja idadi binafsi ya watu waliofaidika na mradi, vijiji, wilaya na mikoa<br />
Sehemu ya 2: Maelezo ya Asasi (Shirika)<br />
2.1. Jina la asasi: Jaza jina kama lilivyo katika katiba na usajili.<br />
2.2. Jina ambalo unalitumia (Tofauti na lile la 2:1): Utajaza nafasi hii kama jina unalotumia tofauti<br />
na lile la 2:1 hasa kama ni kifupisho.<br />
2.3. Usajili: Hapa unatakiwa kuhakikisha kwamba unatoa taarifa zote za asasi ikiwemo aina ya<br />
usajili, tarehe ya usajili na anuani.<br />
2.4. Kama unaomba kama sehemu ya ubia au muungano wa asasi: Tafadhali orodhesha majina ya<br />
AZAKi nyingine mnazoshirikiana au mtakazoshirikiana katika mradi huo. Na kama ni zaidi ya<br />
sita basi tengeneza kiambatanisho mwishoni mwa ukurasa.<br />
2.5. Mtu atakayekuwa anawasiliana na <strong>Foundation</strong>: Jaza jina la mhusika, nafasi yake na anuani za<br />
mawasiliano atakazofanya baina yake na <strong>Foundation</strong> kwa niaba ya asasi.<br />
2.6. Viongozi na wafanyakazi: Orodhesha majina ya viongozi wa asasi yako na nyadhifa walizonazo.<br />
Wanaweza kuwa Bodi ya wadhamini, Kamati ya usimamizi, au bodi ya wakurugenzi.<br />
2.7. Taarifa za kina za Akaunti ya benki: Mwombaji anatakiwa kutoa taarifa za akaunti ya benki<br />
kama: Jina la akaunti, namba ya akaunti, aina ya akaunti, Jina kamili la benki iliyopo akaunti<br />
hiyo, tawi lake, anuani ya tawi na majina ya watia saini na nyadhifa zao katika asasi.<br />
2.8. Wadhamini huru: Wadhamini hawa wanatakiwa kuwa wakweli na ambao maamuzi yao si rahisi<br />
kuyumbishwa au kupingwa na ni watu wenye heshima zao. Aidha, wanatakiwa wawe wamejua<br />
asasi husika kwa mwaka mzima na wenye uwezo wa kuelezea asasi husika kiuwezo na kiuzoefu.<br />
Wanatakiwa kuijua vyema asasi husika hasa shughuli zake, menejimenti na masuala ya kifedha.<br />
KUMBUKA: Unatakiwa kueleza wazi uhusiano wako na wadhamini na <strong>Foundation</strong> inatarajia<br />
kwamba utatumia busara zako vyema katika kumchagua mdhamini. Kama Mdhamini<br />
ataonekana hafai maombi yako hayatafikiriwa.<br />
Sehemu ya 3: Kifungu cha makubaliano<br />
Hiki kinatakiwa kujazwa na mwenyekiti, Katibu au mweka hazina lakini hawatastahili kuwa watu<br />
ambao wanawasiliana moja kwa moja na <strong>Foundation</strong>.<br />
Sehemu ya 4: Angalia kama maombi yako yamekamilika<br />
Waomba ruzuku wanashauriwa kutumia maelekezo yaliyopo katika mwongozo kuhakikisha<br />
kwamba wanafanyakazi ya kujaza fomu za maombi kwa unadhifu, uhakika. Unatakiwa kujaza kila<br />
kisanduku kabla ya kuwasilisha maombi.<br />
24
14. Masuala unayotakiwa kuyajua<br />
Tafadhali soma masuala yafuatayo kwa uangalifu zaidi. Ni sharti kwa kila mtu ambaye anataka<br />
ruzuku kutoka <strong>Foundation</strong> akayasoma, kuyaelewa na kuyakubali:<br />
14.1 Maombi ya Ruzuku<br />
(i) Mwongozo huu na fomu za maombi zinatolewa bure.<br />
(ii) Kwamba taarifa zilizomo katika mwongozo huu na fomu za maombi zinaweza kubadilika<br />
kila inapobidi. Tuna haki ya kubadili kipengele chochote katika sera zetu, kanuni na<br />
vigezo vya mchakato.<br />
(iii) Fomu ya maombi ya ruzuku inaweza isiwe na taarifa zote zinazohitajika kuamua maombi<br />
gani yanaweza kupewa ruzuku. Tunaweza kutaka taarifa zaidi kutoka kwako kuthibitisha<br />
maombi yako. Pia tutataka taarifa kutoka mtu wa tatu kama vile wadhamini wako na<br />
wafadhili wa sasa ulionao.<br />
(iv) Maombi yanafanywa kwa matakwa ya mwombaji. Kutokana na hilo hatuwezi kushtakiwa<br />
kwa hasara, uharibifu au gharama zinazotokana na mchakato mzima wa kuomba ruzuku,<br />
kukataliwa kwa ruzuku au kushughulikia maombi yako.<br />
(v) Uamuzi wa kutoa ruzuku bado ni haki ya Menejimenti ya <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong>,<br />
na maamuzi yake ni ya mwisho na hayakatiwi rufaa.<br />
(vi) Iwapo viongozi, Menejimenti au wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong> watamjua mtu kati ya wale<br />
walioomba ruzuku, wanatakiwa kutangaza mgongano wa maslahi na kujiondoa katika<br />
kushughulikia shauri linalomhusu mtu huyo.<br />
(vii) Maombi yako yatatupwa kama itabainika kwamba umedanganya au kutoa taarifa ambazo si<br />
sahihi wakati wa mchakato wa kuomba ruzuku au kufungiwa baada ya kupokea ruzuku.<br />
14.2 Masharti ya ruzuku<br />
a. Wakati muda wa ruzuku umekwisha, hakuna ulazima wa aina yoyote kwa <strong>Foundation</strong><br />
kutoa ruzuku tena kwa mradi husika.<br />
b. Fedha hazitatolewa mpaka asasi husika inatiliana saini mkataba na <strong>Foundation</strong> ambao<br />
utaeleza wazi masharti ya fedha ya ruzuku.<br />
c. Kama asasi haitafuata makubalino wakati wa utekelezaji basi ruzuku hiyo inaweza<br />
kuondolewa, kusimamishwa au kufutwa muda wowote.<br />
d. Tunaweza kutumia jina la asasi yako na mradi husika katika kujitambulisha kwa umma<br />
na kazi zake na taarifa ya mradi wako na jina lake itakuwa ni kitu cha wazi kwa umma<br />
na kitatangazwa. Hata hivyo huna ruksa ya kutumia jina au alama ya <strong>Foundation</strong> kwa<br />
manufaa yako au ya asasi yako bila kibali cha maandishi kutoka kwa <strong>Foundation</strong>.<br />
e. Maombi yote ya ruzuku ambayo yatakuwa yamepitishwa yatatangazwa katika magazeti<br />
ya kitaifa kama sehemu ya sera za uwazi za <strong>Foundation</strong>.<br />
f. <strong>Foundation</strong> itahakikisha inaipa taarifa serikali juu ya ruzuku zote ilizotoa kitaifa na ngazi<br />
ya chini. Wote waliopokea ruzuku wanatarajiwa kutoa taarifa ya ruzuku zao kwa serikali<br />
za mitaa kwa maandishi.<br />
g. Mradi wako utaangaliwa na kukaguliwa na wafanyakazi wa <strong>Foundation</strong>, washauri wake<br />
na wafadhili wake. Wale wanaopewa ruzuku wanatarajiwa kuweka kumbukumbu za<br />
fedha zikiwemo vocha za matumizi kwa ruzuku zote wanazopewa.<br />
h. Wapokea ruzuku wa <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> inawalazimu kuzingatia Kanuni za Maadili za<br />
Mashirika Yasiyo ya Serikali (NGOs)zilizoambatishwa na mwongozo huu.<br />
25
15. Viambatisho<br />
15.1 Kiambatanisho 1 Wadhamini wa ufadhili<br />
Jina la asasi ...........................................................................................................................................<br />
Jina la Mfadhili Mtu wa kuwasiliana<br />
naye<br />
Taarifa za anuani ya<br />
madhamini kama<br />
simu, sanduku la<br />
posta anuani ya<br />
barua pepe<br />
kiasi cha fedha<br />
kilichowahi kutolewa<br />
naye<br />
jina la Mradi siku ya kuanza na<br />
kumalizika<br />
Zingatia: Kwa wale walioomba ruzuku ya Kati watatakiwa kujaza taarifa za wafadhili kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita<br />
26
15.2 Kimabatanisho cha II: Mpango wa mafunzo<br />
Malengo ya<br />
mafunzo/<br />
Warsha<br />
Dondoo za mada<br />
zitakazozungumziwa<br />
Mbinu za<br />
ufundishaji<br />
zitakazotumika<br />
Kundi lililolengwa Vigezo vilivyotumika<br />
kupata washiriki<br />
Elimu iliyotolewa<br />
itakavyoweza kusambazwa<br />
kwa makundi mbalimbali<br />
27
15.3 Kiambatanisho III: Muundo wa upangaji wa Bajeti<br />
JINA LA ASASI:…………………………………………………………………………….<br />
S/No Shughuli zinazohusika na vinavyotakiwa Gharama<br />
ya<br />
mkataba<br />
1.0 Maandalizi ya Mradi Waratibu 4, 2 kila<br />
Wilaya … Siku 3<br />
Gharama<br />
za Jumla<br />
QTR 1<br />
Gharama za<br />
Jumla QTR 2<br />
Gharama za<br />
Jumla QTR 3<br />
Gharama<br />
za Jumla<br />
QTR 4<br />
Mwaka<br />
wa 1<br />
Jumla<br />
Mwaka<br />
wa 2<br />
Jumla<br />
Mwaka<br />
wa 3<br />
Jumla<br />
1.1 Nauli Waratibu 2 @ 10,000/= 20,000 20,000 0 0 0 20,000<br />
1.2 Nauli Waratibu 2 @ 12,000/= 24,000 24,000 0 0 0 24,000<br />
1.3 Posho kujikimu Waratibu 4 @ 11,000/= X Siku<br />
2<br />
1.4 Kuchapa barua ya mwaliko nakala 1 X<br />
1,000/=<br />
1.5 Kuchapa barua ya taarifa ya mafunzo nakala 1<br />
X 1,000/=<br />
1.6 Kuchapa barua ya mwaliko kwa viongozi<br />
serikali nakala 1 X 1,000/=<br />
1.7 Kurudufu (kutoa nakala) barua za kuhudhuria<br />
mafunzo nakala 220 @ 50/=<br />
1.8 Kudurufu barua za taarifa ya mafunzo<br />
Wawezeshaji nakala 4 X 50/=<br />
1.9 Kudurufu barua ya mwaliko Viongozi wa<br />
Serikali 4 X 50/=<br />
88,000 88,000 0 0 0 88,000<br />
1,000 1,000 0 0 0 1,000<br />
1,000 1,000 0 0 0 1,000<br />
1,000 1,000 0 0 0 1,000<br />
11,000 11,000 0 0 0 11,000<br />
200 200 0 0 0 200<br />
200 200 0 0 0 200<br />
1.10 Bahasha Pcs 228 @ 50/= 11,400 11,400 0 0 0 11,400<br />
1.11 stempu kutuma barua Pcs 228 X 400//= 91,200 91,200 0 0 0 91,200<br />
Jumla ndogo Na.1 249,000 249,000 0 0 0 249,000<br />
(Katika mstari wa 1.0, 2.0, 3.0 na nyingine katika kolamu ya Shughuli na pembejeo (Activity and Inputs) inaonyesha masuala mbayo yanatakiwa kufanyiwa kazi kwa ujumla wake bila kuacha,<br />
inatakiwa ionyeshe nini kinatakiwa kufanywa, wapi, kw amuda gani na kwa ajili ya nani. Kutoka mstari wa 1.1 kuelekea chini katika kolam ya Shughuli na pembejeo (Activity and Inputs)<br />
,kunaonyesha na kutengeneza hesabu ya gharama za jumla kwa kila pembejeo inayotakiwa; Inatakiwa ionyeshe wazi, idadi ya namba na gharama kwa kila pembejeo inatakiwa kwa ajili ya<br />
kukamilisha Shughuli. Gharama halisi kwa kila kimoja inatakiwa ionyeshe kama Jumla ya thamani ya mkataba (Total Contract Value). Kwa gharama za jumla za Ruzuku ndogo ya QTR 1<br />
inatakiwa iwe sawa na Jumla ya thamani ya mkataba ( Total Contract Value) , kwa miradi yenye miaka mingi na wafadhili wengi, makadirio ya wastani kwa kila mwaka lazima yaonyeshwe<br />
chini ya kila mwaka 1, 2 na 3. na katika kila mwaka wa uendeshaji gharama zinatakiwa kugawanywa katika robo kwa kutegemea ni wakati gani shughuli hiyo itafanyika). Tunashauri bajeti<br />
itengenezwe wakati mipango ya kazi imeshaandaliwa.<br />
28
15.4 Kiambatanisho lV: Mpango wa ufuatiliaji na tathmini<br />
Mabadiliko Maelezo ya lengo<br />
viashiria vinavyoweza kutathminiwa (Idadi<br />
ya viashiria kwa kila tokeo visizidi viwili (2])<br />
Matokeo<br />
Shughuli<br />
Mabadiliko<br />
Matokeo<br />
Shughuli<br />
Chanzo cha taarifa<br />
(Data Source)<br />
Namna ya<br />
ukusanyaji wa<br />
takwimu<br />
Muda wa<br />
kukusanya<br />
takwimu hizo<br />
29
15.5 Sera ya ‘Kutovumilia Rushwa Hata Kidogo’:<br />
<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> inaendesha sera ya ‘Kutovumilia Rushwa Hata Kidogo’ kwa aina<br />
zote za rushwa, ndani ya the <strong>Foundation</strong> na huduma zake, pia nje pamoja na wale wote ambao the<br />
<strong>Foundation</strong> inaweza kuwa na mahusiano ya aina yoyote. Mfanyakazi yeyote wa the <strong>Foundation</strong><br />
atakayepatikana na hatia, kufuatia uchunguzi wa kina wa vitendo visivyofaa vya rushwa, atachukuliwa<br />
hatua kali chini ya taratibu za kinidhamu za <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong>.<br />
Pale ambapo mwananchi yeyote atakuwa na sababu za kumtilia shaka mtu yeyote anayehusiana na the<br />
<strong>Foundation</strong>, basi anatakiwa awasiliane na Mkurugenzi Mtendaji, akimwamini kabisa, na kumuarifu<br />
juu ya masuala hayo mapema iwezekanavyo, kwa maandishi ikiwezekana, au kwa njia nyingine<br />
zilizopo, akitoa ushahidi kadri awezavyo kusaidia madai yake mara tu atakapo tahadharishwa au<br />
kufuatwa moja kwa moja.<br />
Mkurugenzi Mtendaji atahakikisha kwamba jambo hili linachunguzwa kwa siri na kwa unyeti wake<br />
ndani ya taratibu za the <strong>Foundation</strong> za malalamiko na kuhakikisha kutobainika kwa mlalamikaji,<br />
ili kumlinda asiwekwe katika hatari. Mlalamikaji hatabaguliwa kwa aina yoyote ile kutokana na<br />
kuwasilisha malalamiko ya kweli.<br />
Baada ya hapo the <strong>Foundation</strong> itaendesha uchunguzi wa kina, ambao matokeo yake yatarejeshwa<br />
kwa mlalamikaji yakiwa na maamuzi yaliyo kamili na yanayostahili.<br />
Ikumbukwe kwamba uchunguzi wowote na matokeo yoyote yatazingatia sera ya malalamiko na<br />
taratibu za the <strong>Foundation</strong>, hususani ikizingatia misingi ya haki na Sheria za Tanzania. Kwa taarifa<br />
zaidi ya jinsi ya kuwasilisha malalamiko rejea Sera ya the <strong>Foundation</strong> ya Kushughulikia Malalamiko<br />
(15.6), ambayo pia hupatikana katika tovuti yetu, www.thefoundation-tz.org<br />
15.6 Sera ya Kushughulikia Malalamiko<br />
<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> <strong>for</strong> <strong>Civil</strong> <strong>Society</strong> ina maadili 5 ya msingi, ambayo ni haki, uadilifu, uweledi, uwazi<br />
na uwajibikaji, na usawa wa kijinsia. Katika misingi ya maadili haya, the <strong>Foundation</strong> inadhamiria<br />
kutoa fursa kwa wanaopokea huduma zetu kutoa malalamiko kwenye masuala ya rushwa, tabia,<br />
taratibu na kufanya maamuzi. Hivyo basi, the <strong>Foundation</strong> imetayarisha Sera hii ya Kushughulikia<br />
Malalamiko ili itumike na wadau wetu wote. Lazima ieleweke kwamba Sera ya Kushughulikia<br />
Malalamiko hairuhusu kwa namna yoyote ile ukataji wa rufaa kwa maamuzi yaliyofanywa na<br />
the <strong>Foundation</strong>. Maamuzi kuhusu ruzuku yaliyofanywa na the <strong>Foundation</strong> ni ya mwisho, lakini<br />
malalamiko dhidi ya maamuzi yataisaidia the <strong>Foundation</strong> kuboresha maamuzi/huduma zake za<br />
baadaye. <strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> itashughulikia malalamiko yote katika njia iliyo ya haki, bila upendeleo,<br />
uwazi na kwa muda unaofaa.<br />
<strong>The</strong> <strong>Foundation</strong> inakusudia kufanya yafuatayo:<br />
• Kushughulikia malalamiko kwa uzito wake na kwa ufanisi<br />
• Kutatua malalamiko haraka pale inapowezekana<br />
• Kujifunza kutokana na malalamiko na kuchukua hatua za kuboresha huduma zetu<br />
• Kumsaidia na kumlinda mlalamikaji<br />
Unatakiwa ufanye nini unapokuwa na malamiko<br />
Unapotaka kuwasilisha malalamiko kuhusu the <strong>Foundation</strong>, ruzuku iliyotolewa na the <strong>Foundation</strong> au<br />
30
kuhusu mfanyakazi wa the <strong>Foundation</strong>, au Mjumbe wa Bodi, unaweza kufanya hivyo kwa maandishi,<br />
kwa kutumia nukushi, barua pepe (malalamiko@thefoundation-tz.org), kwa simu au kwa kuja wewe<br />
mwenyewe. Wale wanaopenda kuja kutoa malalamiko yao wenyewe watahitaji wapangiwe muda.<br />
Iwapo malalamiko yako utayatuma kwa kuandika barua, nukushi au barua pepe, tafadhali onyesha<br />
namba yako ya simu, iwapo jibu la awali kwa kutumia simu litafaa. Iwapo unatuma kwa baruapepe,<br />
tafadhali onyesha iwapo unahitaji majibu kwa barua pepe, kama sivyo, tafadhali toa anuani<br />
kamili ya posta. Tutakuomba uweke malalamiko yako katika maandishi, iwapo umewasiliana nasi<br />
kwa mdomo. Tutaweza kukupatia msaada kwa hili iwapo ni lazima. Kwa mara ya kwanza wasilisha<br />
malalamiko yako moja kwa moja kwa Mkurugenzi Mtendaji wa the <strong>Foundation</strong> au iwapo inastahili<br />
na katika mazingira yasiyo ya kawaida, kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi.<br />
Utapokea uthibitisho kutoka kwetu kwamba malalamiko yako yamepokelewa. Iwapo hutapokea<br />
uthibitisho ndani ya siku saba za kazi za kuwasilisha malalamiko yako, tafadhali wasiliana na<br />
Mkurugenzi Mtendaji moja kwa moja.<br />
Nini kinafuata baada ya hapo<br />
Baada ya kupokea malalamiko yako, tutalenga kujibu mara moja, na mara zote ndani ya siku 14.<br />
Iwapo hili haliwezekani, tutaeleza kwa nini na kukujulisha itachukua muda gani.<br />
Iwapo hujafurahia majibu ya awali unayopata, wasiliana na Mkurugenzi Mtendaji tena na utafute<br />
ufafanuzi. Kufuatia jibu la pili, iwapo bado hujaridhika, unashauriwa kumuandikia Mwenyekiti wa<br />
Bodi ya Wakurugenzi.<br />
Iwapo bado hujafurahishwa na matendo ya the <strong>Foundation</strong>, unaweza kumuomba Mwenyekiti wa<br />
Bodi apeleke malalamiko yako kwa Waamuzi huru wachunguze malalamiko yako jinsi ambavyo<br />
yalivyoshughulikiwa.<br />
Usiri<br />
Kwa ujumla walalamikaji wanahimizwa na the <strong>Foundation</strong> watamke majina yao na jinsi ya kuwapata,<br />
wanapowasilisha malalamiko. Kwa kufanya hivyo wanahakikishiwa viwango vya juu kabisa vya<br />
usiri na Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti wa Bodi. Hata hivyo, katika mazingira yasiyo ya<br />
kawaida, mlalamikaji anaweza kuamua kutoonyesha jina lake au maelezo ya jinsi ya kumpata na<br />
anaweza kuwasilisha malalamiko yasiyo na jina. Hata hivyo, walalamikaji watambue kwamba<br />
ushirikiano wa moja kwa moja na walalamikaji unawezesha kwa kiwango kikubwa kushughulika, na<br />
kuirahisishia the <strong>Foundation</strong> kuchukua hatua za kutosha, za haki na endelevu ili kutatua mapungufu<br />
yanayohusika.<br />
31