KILIMO NA HIFADHI BORA YA VITUNGUU - eRails
KILIMO NA HIFADHI BORA YA VITUNGUU - eRails
KILIMO NA HIFADHI BORA YA VITUNGUU - eRails
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>KILIMO</strong> <strong>NA</strong> <strong>HIFADHI</strong> <strong>BORA</strong> <strong>YA</strong> <strong>VITUNGUU</strong><br />
1. Utangulizi<br />
Vitunguu ni zao muhimu sana hapa Tanzania. Mikoa ya Arusha, Manyara, Iringa, Mbeya,<br />
Tanga, Singida na Kilimanjaro ni maarufu sana kwa kilimo cha vitunguu na ni zao la chakula na<br />
biashara kwa mkulima mdogo. Uzalishaji wa vitunguu bado ni mdogo (tani nne kwa hekta) na<br />
upotevu wa mazao baada ya kuvuna ni mkubwa (50 %– 80%) kutokana na hifadhi duni hivyo<br />
wakulima wanahitaji utaalamu wa kilimo bora na hifadhi ya vitunguu ili kuongeza uzalishaji na<br />
kipato.<br />
2.0 Uzalishaji wa vitunguu<br />
Zao la vitunguu linazalishwa kutokana na mbegu na miche inakuzwa kwenye kitalu kabla ya<br />
kupandikizawa shamban. Miche inakuwa na kuzaa vitunguu.Vitunguu vikikomaa, vinavunwa na<br />
kuhifadhiwa vikiwa katika hali ya kulala bwete. Katika hali hii vitunguu vinaweza kuhifadhiwa<br />
kwa muda mrefu aitha kwa ajili ya kuzalisha mbegu msimu unaofuata au kuuza.<br />
Wingi na ubora wa zao la vitunguu hutegemea; hali ya hewa, aina ya vitunguu, upatikanaji wa<br />
mbegu bora, kilimo bora, uangalifu wakati wa kuvuna, usafirishaji na hifadhi bora.<br />
2.1 Uzalishaji<br />
Hali ya hewa na maji<br />
Hali ya hewa na maji ni vipengele muhimu sana vya kuzingatia katika uzalishaji wa vitunguu.<br />
Vitunguu vinastawi vizuri katika hali ya ukavu kwa kutumia umwagiliaji. Maji mengi hasa<br />
wakati wa masika inasababisha magonjwa mengi hasa ukungu, vitunguu haviwezi kukomaa<br />
vizuri, hivyo kusababisha upotevu mkubwa wa mazao. Jua na hewa kavu ni muhimu sana wakati<br />
wa kukomaa na kuvuna vitunguu.<br />
Aina za vitunguu<br />
Aina bora za vitunguu ni pamoja na Mang’ola red, Red creole na Bombay Red. Hizi ni mbegu<br />
bora ambazo zinatoa mazao mengi kuanzia 40-60kgs kwa hekta ikiwa kilimo bora<br />
kitazingatiwa.Mkulima anaweza kuchagua mbegu kwa kuzingatia:-<br />
• mahitaji ya soko (vitunguu vyekundu hupendwa zaidi)<br />
• musimu wa kupanda<br />
• uwezo wa kuzaa mazao mengi<br />
• uwezo wa vitunguu kuhifadhiwa kwa muda mrefu.<br />
Mbegu bora<br />
Ubora wa mbegu ni muhimu sana, kwani ndiyo chanzo cha mazao bora. Mbegu bora inatoa<br />
miche yenye afya na kuzaa mazao mengi na bora. Mbegu za vitunguu inapoteza uoto wake upesi<br />
baada ya kuvunwa (mwaka1). Mbegu nzuri zina sifa zifuatazo:-<br />
• Uotaji zaidi ya 80%<br />
• Mbegu safi zisiyo na mchanganyhiko<br />
• Zimefungwa vizuri kwenye vyombo visivyopitisha hewa na unjevu.<br />
1
Hivyo mkulima anaponunua mbegu za vitunguu azingatie yafuatayo:<br />
• Chanzo cha mbegu<br />
• Tarehe ya uzalishaji<br />
• Tarehe ya kuisha muda wake<br />
• Kifungashio cha mbegu.<br />
Inashauriwa mkulima asipande mbegu zenye umri zaidi ya mwaka mmoja<br />
Mbegu bora za vitunguu zinauzwa na makampuni binafsi kama: ALPHA Seed Co., Popvriend,<br />
Rotian Seed, Kibo Seed, East African Seed Company nk. Wasambazaji wa mbegu ni pamoja na<br />
maduka ya TFA, na maduka ya bembejeo za kilimo katika maduka mbalimbali.<br />
Jinsi ya kuandaa kitalu na kuzalisha miche<br />
• Sehemu ya kitalu iwe wazi, mbali na kivuli na kiwe karibu na chanzo cha maji.<br />
• Tengeneza tuta la kubwa wa 1m x 2m . Urefu na idadi ya matuta hutegemea kiasi cha<br />
mbegu. Kiasi cha mbegu kwa hectare moja ni kilo 6 au 2 kg kwa eka.<br />
• Weka samadi iliyooza vizuri kiasi cha debe moja au mchanganyiko wa mbolea ya TSP na<br />
CAN (200gm) kwa uwiano wa 1:1 kwenye tuta changanya vizuri na udongo.<br />
• Sia mbegu kwenye mistari kwa nafasi ya 1 sm x 20 sm. Tawanya mbegu vizuri wakati<br />
wa kusia ili miche isisongamane.<br />
• Funika mbegu na weka matandazo ya nyasi kavu juu ya tuta na mwagiliwa maji. Udongo<br />
unatakiwa kuwa na unyevu kiasi mpaka mbegu ziote.<br />
• Nyasi ziondolewe mara tu mbegu zikiota (siku7-10 kutegemea hali ya hewa).<br />
• Miche itunzwe vizuri na kitalu kiwe katika hali ya usafi.<br />
• Miche imwagiliwe maji mpaka ifikie umri wa kupandikiza shambani (wiki 5-6)<br />
Matatizo ya miche kitaluni ni kama yafuatayo:<br />
Kuonza kwa mbegu, kunyauka kwa miche kabla na baada ya kuoto. Hali hii inasababishwa na<br />
ugonjwa wa ukungu “Kinyausi” .Dawa za ukungu kama Dithane M45 au Ridomil MZnk<br />
zinatumike kuzuia (changanya dawa na povu la sabuni ili dawa ijishike kwenye majani). Pia<br />
uangalifu uwepo wakati wa kumwagilia maji. Mwagilia maji wakati wa asubuhi au jioni. Epuka<br />
kumwagilia maji wakati wa jua kali kwani unjevunjevu hewani unaongeza na kusababisha<br />
vimelea vya magonjwa.<br />
Wadudu waharibifu ni pamoja na Chawa wekundu.ambao wanashambulia majani, Sota ambao<br />
hukata miche. Dawa za viwandani kama Thiodan , Selecron au Dusrban zinazuia na kudhibiti<br />
hwa wadudu.<br />
Baada ya wiki 5 au 6, kutegemeana na hali ya hewa miche itakuwa tayari kupandikiza<br />
shambani. Miche iimarishwe kwa kusitisha maji, wiki moja kabla ya kupandikiza.<br />
Kutayarisha shamba<br />
Shamba litayarishwe sehemu usiyokuwa na mwinuko, sehemu ya wazi ambayo haijalimwa<br />
vitunguu kwa muda wa miaka 2 -3. Shamba liwe karibu na chanzo cha maji kwa ajili ya<br />
umwagiliaji. Matuta 1m x 3m au majaruba ya 2mx 3m.yanafaa kwa kupanda miche. Matatu au<br />
majaruba yanarahisisha umwagiliaji, palizi na unyunyiziaji wa dawa.<br />
2
Kupandikiza miche shambani na matumizi ya mbolea<br />
Weka samadi debe 2 au mbolea ya TSP au DAP kwenye tuta au jaruba na kuchanganya na<br />
udongo. Mbolea kiasi cha mifuko 2 TSP au DAP kwa hekta au ¾ mfuko kwa eka moja<br />
inashauriwa. Chagua miche yenye afya, majani na mizizi ya ipunguzwe ili kurahisisha upandaji.<br />
Panda miche kwenye mistari kwa nafasi ya sm 20 toka mstari hadi mstari, na miche hadi mche<br />
kwa nafasi ya sm 8 au sm 10. Tumia kijiti au kitu chochote chenye ncha kuchimba vijishimo<br />
vya kupandia miche. Mwagilia maji ya kutosha kila siku hasa sehemu zenye jua kali. Mbolea ya<br />
kukuzia CAN kiasi cha mifuko 2 kwa hekta au ¾ mfuko kwa eka moja iwekwe wiki mbili baada<br />
ya kupandikiza miche. Matumizi ya mbolea ya CAN yanataka uangalifu sana. Mbolea ikizidi<br />
hufanya mimea kuwa teketeke, shingo ya vitunguu kuwa nene, kuchelewesha kukoma na<br />
kupunguza mazao na ubora wa vitunguu. Pia kuoza kwa vitunguu ghalani kunaongezeka<br />
Kuzuia magugu<br />
Miche ya vitungguu, huota taratibu sana, hivyo miezi ya mwanzoni, miche husongwa sana na<br />
magugu. Palizi mbili mpaka tatu zinashauriwa na zinatosha kuweka shamba safi. Matumizi ya<br />
dawa za magugu ni madogo lakini dawa zinazoshauriwa ni pamoja na Alachlor na Oxyflourfen<br />
(Goal 2E). Hizi dawa ni nzuri kwani zina uwezo wa kuua magugu aina mbalimbali. Dawa<br />
inapuliziwa wiki mbili mpaka tatu baada ya kupandikiza miche shambani. Palizi baada ya<br />
kutumia dawa ya magugu ni muhimu ili kuondoa magugu sugu na pia kutifulia vitunguu.<br />
Wakati wa palizi, vitunguu na mizizi iliyowazi ifunikwe kwa udongo ili kuzuia jua lisiunguze<br />
mizizi au kubabua vitunguu.<br />
2.2 Magonjwa na wadudu waharibifu<br />
Vitunguu vinashambuliwa na magonjwa na wadudu mbalimbali na kusababisha upungufu na<br />
ubora wa mazao. Ili kudhibiti tatizo kwanza shamba likaguliwe mara kwa mara kuona dalili za<br />
mashambulizi. Endapo kuna dalili za mashambulizi, chukua hatua za kuzuia kabla uharibifu<br />
mkubwa haujatokea.<br />
2.2.1 Magonjwa<br />
a) Baka zambarau (Puple Blotch)<br />
Ungonjwa huu unasababishwa na kuvu (fangasi). Chanzo kikubwa cha ugonjwa ni mbegu zenye<br />
ugonjwa. Pia ugonjwa unajitokeza wakati kuna ukungu na unyevunyegu mwingi hewani has<br />
wakati wa masika. Kiasi cha 60-80 % ya mazao yanaweza kupotea kama ugonjwa<br />
hautadhibitiwa. Dalili za ugonjwa ni:-<br />
• kujitokeza madoa meupe yaliyodidimia kwenye majani na kwenye mashina ya mbegu<br />
• rangi ya zambarau kuwepo katikati ya doa jeupe.<br />
• majani kuanguka<br />
• mashina ya mbegu kuanguka kabla ya mbegu kutengenezwa<br />
Njia za kudhibiti:-<br />
• kupanda mbegu safi<br />
3
• kupanda vitunguu kwa kutumia mzunguko wa mazao<br />
• kuteketeza msalii ya vitunguu baada ya kuvuna<br />
• kupulizia dawa zilizopendekezwa kama Dithane M45 na Ridomil MZ. Dawa hizi<br />
zinachanganywa na povu la sabuni ili zijishike kwenye majani.<br />
b) Ubwiri vinyoya (Downy Mildew)<br />
Ugonjwa huu unasababishwa na kuvu (fangasi) na kuenezwa na mbegu, hewa na masalia ya<br />
vitunguu. Unajitokeza wakati kuna unyevunyevu mwingi hewani hasa wakati wa masika na<br />
dalili zake ni kama zifuatazo:-<br />
• madoa yenye umbo la yai, rangi ya njano iliyofifia hujitokeza kwenye majani makukuu<br />
na kusambaa mpaka kwenye majani machanga.<br />
• baada ya siku chache madoa ya njano yanafunikwa na ukungu wa rangi ya kijivu.<br />
• majani yanasinyaa na kufa kuanzia kwenye ncha.<br />
• shina la mbegu huzungukwa na vidonda na kusababisha kichwa cha mbegu kuanguka.<br />
Njia za kudhibiti ugonjwa ni kama zifuatavyo:-<br />
• kupanda mbegu safi<br />
• kupanda vitunguu kufuata mzunguko wa mazao<br />
• kupulizia dawa za ukungu kama dithane m45 na ridomil mz.<br />
• kuweka shamba safi<br />
• kuteketeza mabaki ya vitunguu<br />
• kumwagiliaji maji nyakati za asubuhi au jioni<br />
c) Kinyausi (Damping – off)<br />
Ugonjwa huu unasababishwa na fangasi na kuenezwa na udongo, mbegu na masalia ya mazao.<br />
Ugonjwa huu unasababisha mbegu kuoza kabla ya kuota na kunjauka kwa miche baada ya kuota.<br />
Ugonjwa unajitokeza hasa kitaluni ikiwa hali ya hewa ina unyevunyevu na udongo una maji<br />
maji.<br />
Njia za kudhibiti ni kama zifuatazo:-<br />
• mbegu ziwe safi na ziwekwe dawa ya thiram<br />
• kutumia mzunguko wa mazao<br />
• kusia mbegu kwa nafasi za kutosha<br />
• kuepukana na kubananisha miche kitaluni<br />
• kuepukanana na kumwagilia maji wakati wa jua kali au wakati kuna ukungu<br />
d) Virusi njano vya vitunguu (Onion yellow Dwarf virus)<br />
• Ugonjwa huu unasababishwa na virusi na kuenezwa na wadudu aina ya vidukari (wadudu<br />
mafuta). Dalili za ugonjwa ni:-<br />
• mistari ya rangi ya manjano kwenye majani.<br />
• kujikunja kwa majani<br />
• majani kugeuka rangi ya manjano na kuanguka<br />
• mimea mzima kudumaa, kujikunja na kufa.<br />
Njia za kudhibiti ugonjwa huu ni:-<br />
• kutumia mbegu safi<br />
• kuweka shamba katika hali ya usafi<br />
4
• kuzuia wadudu kwa kupulizia dawa kama selecron, actellic, dursban nk.<br />
2.2.2 Wadudu<br />
Wadudu wanaosababisha uharibifu mkubwa kwenye vitunguu ni chawa wekundu (thrips) na sota<br />
(cutworms). Wadudu wengine ni pamoja na utitiri wekundu (red spider mites) na vipekecha<br />
majani (leaf miner)<br />
a. Wadudu chawa (thrips)<br />
Uharibifu uletwao na wadudu chawa, unatofautiana msimu mmoja na mwingine kutegemeana na<br />
hali ya hewa. Mvua kidogo pamoja na joto kali unasababisha mlipuko wa wadudu.<br />
Wanshambulia majani kwa kukwaruakwarua na kunyonya maji hivyo kusababisha majani kuwa<br />
na rangi ya fedha/siliver na baadaye majani yanakauka. Upungufu mkubwa wa mazao unatokea.<br />
Njia ya kudhibiti hawa wadudu ni:-<br />
• kuweka shamba katika hali ya usafi<br />
• kuondoa magugu shambani na yanayozunguka shamba la vitunguu<br />
• kupulizia dawa ya wadudu kama karate, selecron, dursban, actellic.<br />
b. Sota (Cutworms)<br />
Sota au viwavi wa nondo wanasababisha uharibifu mkubwa. Viwavi wanakata mashina ya miche<br />
michanga sehemu ya chini ya shina juu ya ardhi. Sota wanapendelea kula wakati wa usiku na<br />
mchana kujificha kwenye ardhi karibu sana na sehemu waliokata shina. Uharibifu huu<br />
unapunguza sana idadi ya mimea shambani na kuleta upungufu wa mazao.<br />
Wadudu hawa wanadhibitiwa kwa kupulizia dawa kama; Karate Dursban na Actellic na kuweka<br />
shamba katika hali ya usafi.<br />
c. Utitiri wekundu (Red spider mites)<br />
Hawa ni wadudu wadogo sana, ambao wanajificha upande wa chini wa majani. Wanafyonza<br />
maji maji kwenye majani na kusababisha majani kuwa na rangi nyeupe. Wadudu hawa<br />
wanatengeneza utando mweupe kuzunguka majani na mashina. Mmea unashindwa kutengeneza<br />
chakula na baadaye inakufa.<br />
Njia ya kudhibiti:<br />
• kupulizia dawa za wadudu Karate na Selecron.<br />
• kuteketeza masalia ya mazao<br />
• kutumia mzunguko wa mazao<br />
d. Vipekecha majani (leaf miner)<br />
Hawa ni aina ya inzi wadogo, ambao viwavi wake wanashambulia majani, kwa kupekecha na<br />
kutengeneza mitandao wa mitaro kwenye majani. Viwavi wanashambulia majani na<br />
kusababisha majani kukauka. Upungufu mkubwa wa mazao hutokea.<br />
Njia ya dhibiti:<br />
• kupulizia dawa ya wadudu kama karate Selecron na Dursban<br />
• kuteketeza masalia ya mazao<br />
• kutumia mzunguko wa mazao<br />
3.0 Kuvuna na hifadhi ya vitunguu<br />
Kabla ya kuvuna vitunguu kagua shamba ili kuhakikisha kuwa vitunguu vimekomaa.<br />
5
Dalili ya vitunguu kukomaa ni:-<br />
• majani kunyauka na kuanza kukauka<br />
• asilimia 75 -100% kuangusha shingo na majani kukauka.<br />
3.1 Kuvuna<br />
Vitunguu vinavunwa kwa mikono. Mimea inangolewa au kuchimbuliwa kwa kutumia rato<br />
(jembe uma). Baada ya kuvuna vitunguu vinaweza kuachwa shambani vikiwa vimefunikwa na<br />
majani kukinga jua kali kwa muda wa siku mbili au tatu kutegemeana na hali ya hewa. Lengo ni<br />
kuimarisha ngozi ya vitunguu na kufanya michubuko na majeraha madogo madogo yanayotokea<br />
wakati wa kuvuna kuwa magumu na kutengeneza mokovu ambayo yanazuia vimelea vya<br />
magonjwa kuingia ndani. Pia kupunguza unyevu kwenye majani na mashina na kuruhusu<br />
sehemu ya chini ya shingo kufunga. Ikiwa usalama ni mdogo, vitunguu vinachambuliwa na<br />
kukatwa majani na mizizi na kuanikwa sehemu nyingine.<br />
3.2 Kuchambua<br />
• Tenga vitunguu vilivyooza, kuchubuka na kupasuka. Vitunguu vizuri vikaushwe peke<br />
yake.<br />
• Iwapo vitunguu vitahifadhiwa kwa kuninginiza kwenye chaga, basi shingo zisikatwe, bali<br />
zisukwe na kufungwa pamoja, na kuninginizwa<br />
3.3 Kukausha<br />
Hatua hii ni muhimu ili kupunguza unyevu, kufanya vitunguu viwe vigumu na kuwa katika hali<br />
ya kulala bwete.Vitunguu vinaweza kukaushwa kwa kuninginiza kwenye chaga zilizopangwa<br />
mfano wa dari ndani ya banda au kutandaza kwenye kichanja chenye kuruhusu mzunguko wa<br />
hewa pande zote, chini ya kivuli sehemu kavu. Epuka kukausha vitunguu chini kwenye aridhini<br />
na hasa sehemu zenye jua kali. Jua linababusha vitunguu na kusababisha uharibifu. Ukaushaji<br />
huchukua muda wa siku 7 au zaidi kutegemeana na hali ya hewa.<br />
3.4 Kupanga madaraja<br />
Vitunguu vinachambuliwa tena baada ya kukausha ili kuondoa vitunguu vyote vyenye ugonjwa<br />
au dalili za ugonjwa, vilivyoota na kutoa mizizi na vyenye shingo nene. Vitunguu vinapangwa<br />
kwenye madaraja mbalimbali kufuata ukubwa, umbo au rangi. Hii inawezesha kuapta soko zuri<br />
na kuepukana na upotevu mkubwa wakati wa kuhifadhi.<br />
3.5 Kufungasha na kuweka vitambulisho<br />
Vifungashio vinavyopatikana ni mifuko ya nyavu vyenye uwezo wa ujazo wa kilo 20 au<br />
magunia ya katani. Mifuko ya nyavu ina ujazo mdogo na pia inarahisisha ubebaji. Magunia ya<br />
katani yanatumika lakini yanaficha vitunguu visionekane pia vinachukua mzigo mzito na kuleta<br />
usumbufu wakati wa kupakia na kupakua.<br />
Vitambulisho vinawekwa kwenye vifungashio ili kusaidia wasafirishaji kujua mzigo ulikotoka<br />
na pia kutangaza bidhaa inayohusika kwenye masoko ya nje na ndani.<br />
Kwa soko la nje vitambulisho vinatakiwa na habari zifuatazo:<br />
• Jina la bidhaa mf. Vitunguu Mango’la Red<br />
• Uzito kamili mf. 20 kg<br />
• Jina na anwani ya mkulima au kikundi, jina na anwani ya msafirishaji<br />
6
• Jina la kijiji wilaya, Mkoa na nchi mf. Igurusi, Mbarali, Mbeya, Tanzania<br />
• Grade 1<br />
Kwa soko la ndani vitambulisho vinakuwa na habari zifuatazo:<br />
• Jina la bidhaa.mf.vitunguu Mango,la Red<br />
• Uzito kamili mf. 20 kg<br />
• Jina la mkulima au kikundi na anwani John Geda au Jitegemee, Box 200, Mbarali<br />
Mbeya<br />
• Jina na anwani ya msambazaji mf:Mr. Saidi Mbaga Box 670, Mbeya<br />
3.6 Kusafirishaji<br />
Uangalifu wakati wa kupakia, kusafirisha na kupakua ni muhimu ili kuepukana na uharibifu na<br />
upotevu wa vitunguu. Mara nyingi vitunguu vinaharibika kutokana na ujazo kupita kiasi kwenye<br />
vifungashio na vyombo vya usafiri, pia kutokana na upakiaji na mpangilio mbaya, ambao<br />
unasababisha ugandamizaji na kubonyea kwa vitunguu. Wakati wa usafirishaji yafuatayo<br />
yazingatiwe:-<br />
• kutumia vyombo vya usafiri vinavyofaa hasa magari yenye nafasi ya kutosha na yenye<br />
kupitisha hewa<br />
• kupanga mifuko katika tabaka zenye safu zisizodi tatu<br />
• mifuko isitupwe wakati wa kupakia na kupakua<br />
• vitunguu visichanganywe na mazao mengine.<br />
3.7 Kuhifadhi<br />
Vitunguu vinahifadhiwa kwenye maghala bora kama kribu au mabanda ambayo yanaruhusu<br />
hewa na paa kuezekwa kwa manyasi ili kupunguza joto.<br />
Hifadhi kwenye kribu<br />
Kribu inajengwa kwa fito au mianzi na kuinuliwa juu mita moja toka usawa wa aridhi. Upana<br />
wa kribu uwe kati ya sm 60 na 150 ili kuruhusu upepo kupita kwa urahisi. Upepo unaondoa<br />
unyevu na joto kwenye vitunguu. Kribu igawanywe sehemu mbili zenye kina cha sm 60 kila<br />
moja na kutenganishwa na uwazi was m 30, ili kuruhusu mzunguko wa hewa. Wakati wa<br />
kutengeneza kribu yaafutayo yazingatiwe:-<br />
• Kribu ijengwe kwenye sehemu yenye upepo<br />
• Kribu iezekwe kwa nyasi ili kudhibiti joto na jua<br />
• Miguu ya kribi iwekwe vizuizi vya panya.<br />
• Weka vutunguu tabaka mbili na kina cha vitunguu kisizidi sm 60<br />
Hifadhi kwa kuninginiza vitunguu kwenye banda<br />
Hili ni banda lenye uwazi mkubwa, lenye upana usiozidi mita tano, na urefu toka chini hadi<br />
juu usizidi mita 2½. Banda linajengwa kwa miti, fito, mbao au mianzi na vitunguu<br />
vinahifadhiwa kwa kuninginiza kwenye fremu za fito ndani ya banda. Safu za vitunguu<br />
hupangwa kufuata urefu wa banda na kimo cha banda. Urefu wa banda huelekezw a kwenye<br />
mkondo wa upepo ili kuruhusu upepo kuingia na kutoka. Banda liezekwe kwa nyasi ili<br />
kudhibiti joto na jua. Kribu au banda vinahifadhi vitunguu vizuri kwa muda wa miezi sita<br />
bila kuharibika.<br />
7
3. 8. Upotevu wa vitunguu ghalani<br />
Vitunguu vingi hupotea wakati wa kuhifadhi kwa sababu ya:-<br />
• Kuoza<br />
• Kuota (toa majani na mizizi)<br />
• Kupoteza uzito<br />
3.8.1. Kuoza<br />
Kuoza kwa vitunguu vikiwa ghalani kunasababishwa na vimeliea vya fangasi au bacteia. Joto<br />
pamoja na unyevunyevu ndani ya ghala, kunasababisha kuzaliana na kuongezeka kwa vimelea<br />
vya magonjwa<br />
Kudhibiti:<br />
• Weka ghala katika hali ya usafi, kausha vizuri na chambua vitunguu ili kabla ya<br />
kuhifadhi.<br />
a ) Muozo Kitako (Bottom rot or basal rot)<br />
Vimelea vya aina ya fungus vinavyoishi kwenye udongo, vinashambulia sehemu ya chini ya<br />
vitunguu. Vimelea vinapenya kwenye sehemu zenye michubuko, inayotokea wakati wa palizi,<br />
kuvuna au kusafirishwa. Vitunguu vinaoza na baadaye vinakauka na kusinyaa. Njia zifuatazo<br />
zinadhibiti:-<br />
• mzunguko wa mazao<br />
• kuchambuaji mzuri kabla ya kuhifadhi<br />
• kuepuka michubuko wakati wa palizi na kuvuna<br />
b) Ukungu mweusi (Black mould).<br />
Ugonjwa huu unaletwa na vimelea vya fangasi, vinavyoishi kwenye udongo. Vimelea<br />
vinazaliana katikati ya maganda na ukungu mweusi kama poda unaonekana. Baadaye maganda<br />
yanasinyaa na kuvunjika.<br />
Kudhibiti<br />
• kutumia mzunguko wa mazao<br />
• kukagua ghala mara kwa mara na kuondoa vitunguu vilivyooza<br />
• kuweka ghala katika hali ya usafi.<br />
• Kuondoa masalia ya vitunguu na kuchoma moto.<br />
c) Kuoza shingo (Neck rot)<br />
Vimelea vya fangasi vinashambulia vitunguu vikiwa shambani kabla ya kuvuna. Ugonjwa<br />
hauonekani mpaka vitunguu vikomae, vivunwe, vikaushwe na kuhifadhiwa ghalani, ndipo<br />
ugonjwa hujitokeza. Ugonjwa unasababisha kuoza kwa vitunguu. Maganda ya vitunguu<br />
yanalainika kuanzia shingoni na nyama ya kitunguu huwa na sura ya maji maji. Vitunguu<br />
vilivyooza vinyauka na kusinyaa.<br />
Kudhibiti;<br />
• kukausha vitunguu vizuri kabla ya kuhifadhi<br />
• kuchoma na kuharibu masalia ya vitunguu shambani na ghalani.<br />
d) Muozo laini (Bacterial soft rot)<br />
8
Ugonjwa unasababishwa na vimelea vya bacteria. Dalili kubwa ya ugonjwa huu ni kulainika<br />
kwa vitunguu na kutoa harufu mbaya. Ukiminya kitunguu maji yenye harufu mbaya yanatoka<br />
kwenye shingo. Muozo laini unatokea wakati hali ya hewa ikiwa na unyevunyevu na jotoi. Pia<br />
vitunguu vyenye shingo nene ambavyo havijakauka vizuri ni sehemu nzuri sana ya vimelea<br />
kuzaliana.<br />
Kudhibiti :<br />
• Ukaushaji wa haraka na wa uhakika baada ya kuvuna unapunguza sana ugonjwa huu<br />
3.8.2 Kuota na kupoteza uzito wa vitunguu<br />
Vitunguu vinakuwa katika hali ya kulala bwete bila kuota kwa zaidi ya miezi sita ikiwa hali ya<br />
hewa ghalani ni nzuri. Unyevunyevu mwingi ghalani ni adui mkubwa wa vitunguu<br />
vilivyohifadhiwa kwani inasababisha kuota kwa majani na mizizi. Pia hewa ikiwa kavu sana<br />
vitunguu hupoteza maji upesi na kusinyaa. Kuongezaka kwa joto na unyevunyevu ndani ya ghala<br />
kutokana na mzunguko mbaya wa hewa, uchafu ghalani, ukaushaji na uchambuaji mbaya<br />
vinasababisha uharibifu kubwa wa vitunguu ghalani<br />
Kudhibiti ;<br />
• ghala liwe safi pia liwe na uwezo wa kupitisha hewa kavu na ubaridi wa kutosha.<br />
• ghala lijengwe sehemu yenye upepo na kuruhusu mzunguko mzuri wa hewa.<br />
• vifungashio vya vitunguu vipangwe vizuri ili kuruhusu hewa kupita juu na chini.<br />
• vitunguu ndani ya kribu/ghala vijazwe kina cha sentimeta 30-50.<br />
• vitunguu vichambuliwe vizuri kabla ya kuhifadhi.<br />
• vitunguu ghalani vikaguliwe mara kwa mara ili kuondoa vitunguu vilivyoharibika<br />
4.0 Uuzaji wa vitunguu<br />
Watu wa aina mabalimabali wanahusika na ununuzi na uuzaji wa vitunguu wakiwa ni pamoja na:<br />
wakulima, wachuuzi, wafanya biashara ndogondogo, wauza jumla, wauza rejareja, wasafirishaji<br />
na madalali. Ili koboresha uuzaji na kipato ni muhimu kuzingatia yafuatayo:<br />
• Kuboresha ujazo kwa kufuata vipimo vinavyokubalika (kufuta lumbesa<br />
• Kupeana habari za masoko na bei.<br />
• Kuboresha usafirishaji kwa kutumia vikundi.<br />
• Kuwepo na mtiririko wa kuuza vitungu mwaka mzima, kwa kuboresha hifadhi ikiwa<br />
ni pamoja na maghala.<br />
• Kutathimini na kuzingatia ubora wa vitunguu.<br />
• Kutathimini na kuboresha ufungashaji na usafirishaji<br />
.<br />
9