12.12.2012 Views

KILIMO NA HIFADHI BORA YA VITUNGUU - eRails

KILIMO NA HIFADHI BORA YA VITUNGUU - eRails

KILIMO NA HIFADHI BORA YA VITUNGUU - eRails

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>KILIMO</strong> <strong>NA</strong> <strong>HIFADHI</strong> <strong>BORA</strong> <strong>YA</strong> <strong>VITUNGUU</strong><br />

1. Utangulizi<br />

Vitunguu ni zao muhimu sana hapa Tanzania. Mikoa ya Arusha, Manyara, Iringa, Mbeya,<br />

Tanga, Singida na Kilimanjaro ni maarufu sana kwa kilimo cha vitunguu na ni zao la chakula na<br />

biashara kwa mkulima mdogo. Uzalishaji wa vitunguu bado ni mdogo (tani nne kwa hekta) na<br />

upotevu wa mazao baada ya kuvuna ni mkubwa (50 %– 80%) kutokana na hifadhi duni hivyo<br />

wakulima wanahitaji utaalamu wa kilimo bora na hifadhi ya vitunguu ili kuongeza uzalishaji na<br />

kipato.<br />

2.0 Uzalishaji wa vitunguu<br />

Zao la vitunguu linazalishwa kutokana na mbegu na miche inakuzwa kwenye kitalu kabla ya<br />

kupandikizawa shamban. Miche inakuwa na kuzaa vitunguu.Vitunguu vikikomaa, vinavunwa na<br />

kuhifadhiwa vikiwa katika hali ya kulala bwete. Katika hali hii vitunguu vinaweza kuhifadhiwa<br />

kwa muda mrefu aitha kwa ajili ya kuzalisha mbegu msimu unaofuata au kuuza.<br />

Wingi na ubora wa zao la vitunguu hutegemea; hali ya hewa, aina ya vitunguu, upatikanaji wa<br />

mbegu bora, kilimo bora, uangalifu wakati wa kuvuna, usafirishaji na hifadhi bora.<br />

2.1 Uzalishaji<br />

Hali ya hewa na maji<br />

Hali ya hewa na maji ni vipengele muhimu sana vya kuzingatia katika uzalishaji wa vitunguu.<br />

Vitunguu vinastawi vizuri katika hali ya ukavu kwa kutumia umwagiliaji. Maji mengi hasa<br />

wakati wa masika inasababisha magonjwa mengi hasa ukungu, vitunguu haviwezi kukomaa<br />

vizuri, hivyo kusababisha upotevu mkubwa wa mazao. Jua na hewa kavu ni muhimu sana wakati<br />

wa kukomaa na kuvuna vitunguu.<br />

Aina za vitunguu<br />

Aina bora za vitunguu ni pamoja na Mang’ola red, Red creole na Bombay Red. Hizi ni mbegu<br />

bora ambazo zinatoa mazao mengi kuanzia 40-60kgs kwa hekta ikiwa kilimo bora<br />

kitazingatiwa.Mkulima anaweza kuchagua mbegu kwa kuzingatia:-<br />

• mahitaji ya soko (vitunguu vyekundu hupendwa zaidi)<br />

• musimu wa kupanda<br />

• uwezo wa kuzaa mazao mengi<br />

• uwezo wa vitunguu kuhifadhiwa kwa muda mrefu.<br />

Mbegu bora<br />

Ubora wa mbegu ni muhimu sana, kwani ndiyo chanzo cha mazao bora. Mbegu bora inatoa<br />

miche yenye afya na kuzaa mazao mengi na bora. Mbegu za vitunguu inapoteza uoto wake upesi<br />

baada ya kuvunwa (mwaka1). Mbegu nzuri zina sifa zifuatazo:-<br />

• Uotaji zaidi ya 80%<br />

• Mbegu safi zisiyo na mchanganyhiko<br />

• Zimefungwa vizuri kwenye vyombo visivyopitisha hewa na unjevu.<br />

1


Hivyo mkulima anaponunua mbegu za vitunguu azingatie yafuatayo:<br />

• Chanzo cha mbegu<br />

• Tarehe ya uzalishaji<br />

• Tarehe ya kuisha muda wake<br />

• Kifungashio cha mbegu.<br />

Inashauriwa mkulima asipande mbegu zenye umri zaidi ya mwaka mmoja<br />

Mbegu bora za vitunguu zinauzwa na makampuni binafsi kama: ALPHA Seed Co., Popvriend,<br />

Rotian Seed, Kibo Seed, East African Seed Company nk. Wasambazaji wa mbegu ni pamoja na<br />

maduka ya TFA, na maduka ya bembejeo za kilimo katika maduka mbalimbali.<br />

Jinsi ya kuandaa kitalu na kuzalisha miche<br />

• Sehemu ya kitalu iwe wazi, mbali na kivuli na kiwe karibu na chanzo cha maji.<br />

• Tengeneza tuta la kubwa wa 1m x 2m . Urefu na idadi ya matuta hutegemea kiasi cha<br />

mbegu. Kiasi cha mbegu kwa hectare moja ni kilo 6 au 2 kg kwa eka.<br />

• Weka samadi iliyooza vizuri kiasi cha debe moja au mchanganyiko wa mbolea ya TSP na<br />

CAN (200gm) kwa uwiano wa 1:1 kwenye tuta changanya vizuri na udongo.<br />

• Sia mbegu kwenye mistari kwa nafasi ya 1 sm x 20 sm. Tawanya mbegu vizuri wakati<br />

wa kusia ili miche isisongamane.<br />

• Funika mbegu na weka matandazo ya nyasi kavu juu ya tuta na mwagiliwa maji. Udongo<br />

unatakiwa kuwa na unyevu kiasi mpaka mbegu ziote.<br />

• Nyasi ziondolewe mara tu mbegu zikiota (siku7-10 kutegemea hali ya hewa).<br />

• Miche itunzwe vizuri na kitalu kiwe katika hali ya usafi.<br />

• Miche imwagiliwe maji mpaka ifikie umri wa kupandikiza shambani (wiki 5-6)<br />

Matatizo ya miche kitaluni ni kama yafuatayo:<br />

Kuonza kwa mbegu, kunyauka kwa miche kabla na baada ya kuoto. Hali hii inasababishwa na<br />

ugonjwa wa ukungu “Kinyausi” .Dawa za ukungu kama Dithane M45 au Ridomil MZnk<br />

zinatumike kuzuia (changanya dawa na povu la sabuni ili dawa ijishike kwenye majani). Pia<br />

uangalifu uwepo wakati wa kumwagilia maji. Mwagilia maji wakati wa asubuhi au jioni. Epuka<br />

kumwagilia maji wakati wa jua kali kwani unjevunjevu hewani unaongeza na kusababisha<br />

vimelea vya magonjwa.<br />

Wadudu waharibifu ni pamoja na Chawa wekundu.ambao wanashambulia majani, Sota ambao<br />

hukata miche. Dawa za viwandani kama Thiodan , Selecron au Dusrban zinazuia na kudhibiti<br />

hwa wadudu.<br />

Baada ya wiki 5 au 6, kutegemeana na hali ya hewa miche itakuwa tayari kupandikiza<br />

shambani. Miche iimarishwe kwa kusitisha maji, wiki moja kabla ya kupandikiza.<br />

Kutayarisha shamba<br />

Shamba litayarishwe sehemu usiyokuwa na mwinuko, sehemu ya wazi ambayo haijalimwa<br />

vitunguu kwa muda wa miaka 2 -3. Shamba liwe karibu na chanzo cha maji kwa ajili ya<br />

umwagiliaji. Matuta 1m x 3m au majaruba ya 2mx 3m.yanafaa kwa kupanda miche. Matatu au<br />

majaruba yanarahisisha umwagiliaji, palizi na unyunyiziaji wa dawa.<br />

2


Kupandikiza miche shambani na matumizi ya mbolea<br />

Weka samadi debe 2 au mbolea ya TSP au DAP kwenye tuta au jaruba na kuchanganya na<br />

udongo. Mbolea kiasi cha mifuko 2 TSP au DAP kwa hekta au ¾ mfuko kwa eka moja<br />

inashauriwa. Chagua miche yenye afya, majani na mizizi ya ipunguzwe ili kurahisisha upandaji.<br />

Panda miche kwenye mistari kwa nafasi ya sm 20 toka mstari hadi mstari, na miche hadi mche<br />

kwa nafasi ya sm 8 au sm 10. Tumia kijiti au kitu chochote chenye ncha kuchimba vijishimo<br />

vya kupandia miche. Mwagilia maji ya kutosha kila siku hasa sehemu zenye jua kali. Mbolea ya<br />

kukuzia CAN kiasi cha mifuko 2 kwa hekta au ¾ mfuko kwa eka moja iwekwe wiki mbili baada<br />

ya kupandikiza miche. Matumizi ya mbolea ya CAN yanataka uangalifu sana. Mbolea ikizidi<br />

hufanya mimea kuwa teketeke, shingo ya vitunguu kuwa nene, kuchelewesha kukoma na<br />

kupunguza mazao na ubora wa vitunguu. Pia kuoza kwa vitunguu ghalani kunaongezeka<br />

Kuzuia magugu<br />

Miche ya vitungguu, huota taratibu sana, hivyo miezi ya mwanzoni, miche husongwa sana na<br />

magugu. Palizi mbili mpaka tatu zinashauriwa na zinatosha kuweka shamba safi. Matumizi ya<br />

dawa za magugu ni madogo lakini dawa zinazoshauriwa ni pamoja na Alachlor na Oxyflourfen<br />

(Goal 2E). Hizi dawa ni nzuri kwani zina uwezo wa kuua magugu aina mbalimbali. Dawa<br />

inapuliziwa wiki mbili mpaka tatu baada ya kupandikiza miche shambani. Palizi baada ya<br />

kutumia dawa ya magugu ni muhimu ili kuondoa magugu sugu na pia kutifulia vitunguu.<br />

Wakati wa palizi, vitunguu na mizizi iliyowazi ifunikwe kwa udongo ili kuzuia jua lisiunguze<br />

mizizi au kubabua vitunguu.<br />

2.2 Magonjwa na wadudu waharibifu<br />

Vitunguu vinashambuliwa na magonjwa na wadudu mbalimbali na kusababisha upungufu na<br />

ubora wa mazao. Ili kudhibiti tatizo kwanza shamba likaguliwe mara kwa mara kuona dalili za<br />

mashambulizi. Endapo kuna dalili za mashambulizi, chukua hatua za kuzuia kabla uharibifu<br />

mkubwa haujatokea.<br />

2.2.1 Magonjwa<br />

a) Baka zambarau (Puple Blotch)<br />

Ungonjwa huu unasababishwa na kuvu (fangasi). Chanzo kikubwa cha ugonjwa ni mbegu zenye<br />

ugonjwa. Pia ugonjwa unajitokeza wakati kuna ukungu na unyevunyegu mwingi hewani has<br />

wakati wa masika. Kiasi cha 60-80 % ya mazao yanaweza kupotea kama ugonjwa<br />

hautadhibitiwa. Dalili za ugonjwa ni:-<br />

• kujitokeza madoa meupe yaliyodidimia kwenye majani na kwenye mashina ya mbegu<br />

• rangi ya zambarau kuwepo katikati ya doa jeupe.<br />

• majani kuanguka<br />

• mashina ya mbegu kuanguka kabla ya mbegu kutengenezwa<br />

Njia za kudhibiti:-<br />

• kupanda mbegu safi<br />

3


• kupanda vitunguu kwa kutumia mzunguko wa mazao<br />

• kuteketeza msalii ya vitunguu baada ya kuvuna<br />

• kupulizia dawa zilizopendekezwa kama Dithane M45 na Ridomil MZ. Dawa hizi<br />

zinachanganywa na povu la sabuni ili zijishike kwenye majani.<br />

b) Ubwiri vinyoya (Downy Mildew)<br />

Ugonjwa huu unasababishwa na kuvu (fangasi) na kuenezwa na mbegu, hewa na masalia ya<br />

vitunguu. Unajitokeza wakati kuna unyevunyevu mwingi hewani hasa wakati wa masika na<br />

dalili zake ni kama zifuatazo:-<br />

• madoa yenye umbo la yai, rangi ya njano iliyofifia hujitokeza kwenye majani makukuu<br />

na kusambaa mpaka kwenye majani machanga.<br />

• baada ya siku chache madoa ya njano yanafunikwa na ukungu wa rangi ya kijivu.<br />

• majani yanasinyaa na kufa kuanzia kwenye ncha.<br />

• shina la mbegu huzungukwa na vidonda na kusababisha kichwa cha mbegu kuanguka.<br />

Njia za kudhibiti ugonjwa ni kama zifuatavyo:-<br />

• kupanda mbegu safi<br />

• kupanda vitunguu kufuata mzunguko wa mazao<br />

• kupulizia dawa za ukungu kama dithane m45 na ridomil mz.<br />

• kuweka shamba safi<br />

• kuteketeza mabaki ya vitunguu<br />

• kumwagiliaji maji nyakati za asubuhi au jioni<br />

c) Kinyausi (Damping – off)<br />

Ugonjwa huu unasababishwa na fangasi na kuenezwa na udongo, mbegu na masalia ya mazao.<br />

Ugonjwa huu unasababisha mbegu kuoza kabla ya kuota na kunjauka kwa miche baada ya kuota.<br />

Ugonjwa unajitokeza hasa kitaluni ikiwa hali ya hewa ina unyevunyevu na udongo una maji<br />

maji.<br />

Njia za kudhibiti ni kama zifuatazo:-<br />

• mbegu ziwe safi na ziwekwe dawa ya thiram<br />

• kutumia mzunguko wa mazao<br />

• kusia mbegu kwa nafasi za kutosha<br />

• kuepukana na kubananisha miche kitaluni<br />

• kuepukanana na kumwagilia maji wakati wa jua kali au wakati kuna ukungu<br />

d) Virusi njano vya vitunguu (Onion yellow Dwarf virus)<br />

• Ugonjwa huu unasababishwa na virusi na kuenezwa na wadudu aina ya vidukari (wadudu<br />

mafuta). Dalili za ugonjwa ni:-<br />

• mistari ya rangi ya manjano kwenye majani.<br />

• kujikunja kwa majani<br />

• majani kugeuka rangi ya manjano na kuanguka<br />

• mimea mzima kudumaa, kujikunja na kufa.<br />

Njia za kudhibiti ugonjwa huu ni:-<br />

• kutumia mbegu safi<br />

• kuweka shamba katika hali ya usafi<br />

4


• kuzuia wadudu kwa kupulizia dawa kama selecron, actellic, dursban nk.<br />

2.2.2 Wadudu<br />

Wadudu wanaosababisha uharibifu mkubwa kwenye vitunguu ni chawa wekundu (thrips) na sota<br />

(cutworms). Wadudu wengine ni pamoja na utitiri wekundu (red spider mites) na vipekecha<br />

majani (leaf miner)<br />

a. Wadudu chawa (thrips)<br />

Uharibifu uletwao na wadudu chawa, unatofautiana msimu mmoja na mwingine kutegemeana na<br />

hali ya hewa. Mvua kidogo pamoja na joto kali unasababisha mlipuko wa wadudu.<br />

Wanshambulia majani kwa kukwaruakwarua na kunyonya maji hivyo kusababisha majani kuwa<br />

na rangi ya fedha/siliver na baadaye majani yanakauka. Upungufu mkubwa wa mazao unatokea.<br />

Njia ya kudhibiti hawa wadudu ni:-<br />

• kuweka shamba katika hali ya usafi<br />

• kuondoa magugu shambani na yanayozunguka shamba la vitunguu<br />

• kupulizia dawa ya wadudu kama karate, selecron, dursban, actellic.<br />

b. Sota (Cutworms)<br />

Sota au viwavi wa nondo wanasababisha uharibifu mkubwa. Viwavi wanakata mashina ya miche<br />

michanga sehemu ya chini ya shina juu ya ardhi. Sota wanapendelea kula wakati wa usiku na<br />

mchana kujificha kwenye ardhi karibu sana na sehemu waliokata shina. Uharibifu huu<br />

unapunguza sana idadi ya mimea shambani na kuleta upungufu wa mazao.<br />

Wadudu hawa wanadhibitiwa kwa kupulizia dawa kama; Karate Dursban na Actellic na kuweka<br />

shamba katika hali ya usafi.<br />

c. Utitiri wekundu (Red spider mites)<br />

Hawa ni wadudu wadogo sana, ambao wanajificha upande wa chini wa majani. Wanafyonza<br />

maji maji kwenye majani na kusababisha majani kuwa na rangi nyeupe. Wadudu hawa<br />

wanatengeneza utando mweupe kuzunguka majani na mashina. Mmea unashindwa kutengeneza<br />

chakula na baadaye inakufa.<br />

Njia ya kudhibiti:<br />

• kupulizia dawa za wadudu Karate na Selecron.<br />

• kuteketeza masalia ya mazao<br />

• kutumia mzunguko wa mazao<br />

d. Vipekecha majani (leaf miner)<br />

Hawa ni aina ya inzi wadogo, ambao viwavi wake wanashambulia majani, kwa kupekecha na<br />

kutengeneza mitandao wa mitaro kwenye majani. Viwavi wanashambulia majani na<br />

kusababisha majani kukauka. Upungufu mkubwa wa mazao hutokea.<br />

Njia ya dhibiti:<br />

• kupulizia dawa ya wadudu kama karate Selecron na Dursban<br />

• kuteketeza masalia ya mazao<br />

• kutumia mzunguko wa mazao<br />

3.0 Kuvuna na hifadhi ya vitunguu<br />

Kabla ya kuvuna vitunguu kagua shamba ili kuhakikisha kuwa vitunguu vimekomaa.<br />

5


Dalili ya vitunguu kukomaa ni:-<br />

• majani kunyauka na kuanza kukauka<br />

• asilimia 75 -100% kuangusha shingo na majani kukauka.<br />

3.1 Kuvuna<br />

Vitunguu vinavunwa kwa mikono. Mimea inangolewa au kuchimbuliwa kwa kutumia rato<br />

(jembe uma). Baada ya kuvuna vitunguu vinaweza kuachwa shambani vikiwa vimefunikwa na<br />

majani kukinga jua kali kwa muda wa siku mbili au tatu kutegemeana na hali ya hewa. Lengo ni<br />

kuimarisha ngozi ya vitunguu na kufanya michubuko na majeraha madogo madogo yanayotokea<br />

wakati wa kuvuna kuwa magumu na kutengeneza mokovu ambayo yanazuia vimelea vya<br />

magonjwa kuingia ndani. Pia kupunguza unyevu kwenye majani na mashina na kuruhusu<br />

sehemu ya chini ya shingo kufunga. Ikiwa usalama ni mdogo, vitunguu vinachambuliwa na<br />

kukatwa majani na mizizi na kuanikwa sehemu nyingine.<br />

3.2 Kuchambua<br />

• Tenga vitunguu vilivyooza, kuchubuka na kupasuka. Vitunguu vizuri vikaushwe peke<br />

yake.<br />

• Iwapo vitunguu vitahifadhiwa kwa kuninginiza kwenye chaga, basi shingo zisikatwe, bali<br />

zisukwe na kufungwa pamoja, na kuninginizwa<br />

3.3 Kukausha<br />

Hatua hii ni muhimu ili kupunguza unyevu, kufanya vitunguu viwe vigumu na kuwa katika hali<br />

ya kulala bwete.Vitunguu vinaweza kukaushwa kwa kuninginiza kwenye chaga zilizopangwa<br />

mfano wa dari ndani ya banda au kutandaza kwenye kichanja chenye kuruhusu mzunguko wa<br />

hewa pande zote, chini ya kivuli sehemu kavu. Epuka kukausha vitunguu chini kwenye aridhini<br />

na hasa sehemu zenye jua kali. Jua linababusha vitunguu na kusababisha uharibifu. Ukaushaji<br />

huchukua muda wa siku 7 au zaidi kutegemeana na hali ya hewa.<br />

3.4 Kupanga madaraja<br />

Vitunguu vinachambuliwa tena baada ya kukausha ili kuondoa vitunguu vyote vyenye ugonjwa<br />

au dalili za ugonjwa, vilivyoota na kutoa mizizi na vyenye shingo nene. Vitunguu vinapangwa<br />

kwenye madaraja mbalimbali kufuata ukubwa, umbo au rangi. Hii inawezesha kuapta soko zuri<br />

na kuepukana na upotevu mkubwa wakati wa kuhifadhi.<br />

3.5 Kufungasha na kuweka vitambulisho<br />

Vifungashio vinavyopatikana ni mifuko ya nyavu vyenye uwezo wa ujazo wa kilo 20 au<br />

magunia ya katani. Mifuko ya nyavu ina ujazo mdogo na pia inarahisisha ubebaji. Magunia ya<br />

katani yanatumika lakini yanaficha vitunguu visionekane pia vinachukua mzigo mzito na kuleta<br />

usumbufu wakati wa kupakia na kupakua.<br />

Vitambulisho vinawekwa kwenye vifungashio ili kusaidia wasafirishaji kujua mzigo ulikotoka<br />

na pia kutangaza bidhaa inayohusika kwenye masoko ya nje na ndani.<br />

Kwa soko la nje vitambulisho vinatakiwa na habari zifuatazo:<br />

• Jina la bidhaa mf. Vitunguu Mango’la Red<br />

• Uzito kamili mf. 20 kg<br />

• Jina na anwani ya mkulima au kikundi, jina na anwani ya msafirishaji<br />

6


• Jina la kijiji wilaya, Mkoa na nchi mf. Igurusi, Mbarali, Mbeya, Tanzania<br />

• Grade 1<br />

Kwa soko la ndani vitambulisho vinakuwa na habari zifuatazo:<br />

• Jina la bidhaa.mf.vitunguu Mango,la Red<br />

• Uzito kamili mf. 20 kg<br />

• Jina la mkulima au kikundi na anwani John Geda au Jitegemee, Box 200, Mbarali<br />

Mbeya<br />

• Jina na anwani ya msambazaji mf:Mr. Saidi Mbaga Box 670, Mbeya<br />

3.6 Kusafirishaji<br />

Uangalifu wakati wa kupakia, kusafirisha na kupakua ni muhimu ili kuepukana na uharibifu na<br />

upotevu wa vitunguu. Mara nyingi vitunguu vinaharibika kutokana na ujazo kupita kiasi kwenye<br />

vifungashio na vyombo vya usafiri, pia kutokana na upakiaji na mpangilio mbaya, ambao<br />

unasababisha ugandamizaji na kubonyea kwa vitunguu. Wakati wa usafirishaji yafuatayo<br />

yazingatiwe:-<br />

• kutumia vyombo vya usafiri vinavyofaa hasa magari yenye nafasi ya kutosha na yenye<br />

kupitisha hewa<br />

• kupanga mifuko katika tabaka zenye safu zisizodi tatu<br />

• mifuko isitupwe wakati wa kupakia na kupakua<br />

• vitunguu visichanganywe na mazao mengine.<br />

3.7 Kuhifadhi<br />

Vitunguu vinahifadhiwa kwenye maghala bora kama kribu au mabanda ambayo yanaruhusu<br />

hewa na paa kuezekwa kwa manyasi ili kupunguza joto.<br />

Hifadhi kwenye kribu<br />

Kribu inajengwa kwa fito au mianzi na kuinuliwa juu mita moja toka usawa wa aridhi. Upana<br />

wa kribu uwe kati ya sm 60 na 150 ili kuruhusu upepo kupita kwa urahisi. Upepo unaondoa<br />

unyevu na joto kwenye vitunguu. Kribu igawanywe sehemu mbili zenye kina cha sm 60 kila<br />

moja na kutenganishwa na uwazi was m 30, ili kuruhusu mzunguko wa hewa. Wakati wa<br />

kutengeneza kribu yaafutayo yazingatiwe:-<br />

• Kribu ijengwe kwenye sehemu yenye upepo<br />

• Kribu iezekwe kwa nyasi ili kudhibiti joto na jua<br />

• Miguu ya kribi iwekwe vizuizi vya panya.<br />

• Weka vutunguu tabaka mbili na kina cha vitunguu kisizidi sm 60<br />

Hifadhi kwa kuninginiza vitunguu kwenye banda<br />

Hili ni banda lenye uwazi mkubwa, lenye upana usiozidi mita tano, na urefu toka chini hadi<br />

juu usizidi mita 2½. Banda linajengwa kwa miti, fito, mbao au mianzi na vitunguu<br />

vinahifadhiwa kwa kuninginiza kwenye fremu za fito ndani ya banda. Safu za vitunguu<br />

hupangwa kufuata urefu wa banda na kimo cha banda. Urefu wa banda huelekezw a kwenye<br />

mkondo wa upepo ili kuruhusu upepo kuingia na kutoka. Banda liezekwe kwa nyasi ili<br />

kudhibiti joto na jua. Kribu au banda vinahifadhi vitunguu vizuri kwa muda wa miezi sita<br />

bila kuharibika.<br />

7


3. 8. Upotevu wa vitunguu ghalani<br />

Vitunguu vingi hupotea wakati wa kuhifadhi kwa sababu ya:-<br />

• Kuoza<br />

• Kuota (toa majani na mizizi)<br />

• Kupoteza uzito<br />

3.8.1. Kuoza<br />

Kuoza kwa vitunguu vikiwa ghalani kunasababishwa na vimeliea vya fangasi au bacteia. Joto<br />

pamoja na unyevunyevu ndani ya ghala, kunasababisha kuzaliana na kuongezeka kwa vimelea<br />

vya magonjwa<br />

Kudhibiti:<br />

• Weka ghala katika hali ya usafi, kausha vizuri na chambua vitunguu ili kabla ya<br />

kuhifadhi.<br />

a ) Muozo Kitako (Bottom rot or basal rot)<br />

Vimelea vya aina ya fungus vinavyoishi kwenye udongo, vinashambulia sehemu ya chini ya<br />

vitunguu. Vimelea vinapenya kwenye sehemu zenye michubuko, inayotokea wakati wa palizi,<br />

kuvuna au kusafirishwa. Vitunguu vinaoza na baadaye vinakauka na kusinyaa. Njia zifuatazo<br />

zinadhibiti:-<br />

• mzunguko wa mazao<br />

• kuchambuaji mzuri kabla ya kuhifadhi<br />

• kuepuka michubuko wakati wa palizi na kuvuna<br />

b) Ukungu mweusi (Black mould).<br />

Ugonjwa huu unaletwa na vimelea vya fangasi, vinavyoishi kwenye udongo. Vimelea<br />

vinazaliana katikati ya maganda na ukungu mweusi kama poda unaonekana. Baadaye maganda<br />

yanasinyaa na kuvunjika.<br />

Kudhibiti<br />

• kutumia mzunguko wa mazao<br />

• kukagua ghala mara kwa mara na kuondoa vitunguu vilivyooza<br />

• kuweka ghala katika hali ya usafi.<br />

• Kuondoa masalia ya vitunguu na kuchoma moto.<br />

c) Kuoza shingo (Neck rot)<br />

Vimelea vya fangasi vinashambulia vitunguu vikiwa shambani kabla ya kuvuna. Ugonjwa<br />

hauonekani mpaka vitunguu vikomae, vivunwe, vikaushwe na kuhifadhiwa ghalani, ndipo<br />

ugonjwa hujitokeza. Ugonjwa unasababisha kuoza kwa vitunguu. Maganda ya vitunguu<br />

yanalainika kuanzia shingoni na nyama ya kitunguu huwa na sura ya maji maji. Vitunguu<br />

vilivyooza vinyauka na kusinyaa.<br />

Kudhibiti;<br />

• kukausha vitunguu vizuri kabla ya kuhifadhi<br />

• kuchoma na kuharibu masalia ya vitunguu shambani na ghalani.<br />

d) Muozo laini (Bacterial soft rot)<br />

8


Ugonjwa unasababishwa na vimelea vya bacteria. Dalili kubwa ya ugonjwa huu ni kulainika<br />

kwa vitunguu na kutoa harufu mbaya. Ukiminya kitunguu maji yenye harufu mbaya yanatoka<br />

kwenye shingo. Muozo laini unatokea wakati hali ya hewa ikiwa na unyevunyevu na jotoi. Pia<br />

vitunguu vyenye shingo nene ambavyo havijakauka vizuri ni sehemu nzuri sana ya vimelea<br />

kuzaliana.<br />

Kudhibiti :<br />

• Ukaushaji wa haraka na wa uhakika baada ya kuvuna unapunguza sana ugonjwa huu<br />

3.8.2 Kuota na kupoteza uzito wa vitunguu<br />

Vitunguu vinakuwa katika hali ya kulala bwete bila kuota kwa zaidi ya miezi sita ikiwa hali ya<br />

hewa ghalani ni nzuri. Unyevunyevu mwingi ghalani ni adui mkubwa wa vitunguu<br />

vilivyohifadhiwa kwani inasababisha kuota kwa majani na mizizi. Pia hewa ikiwa kavu sana<br />

vitunguu hupoteza maji upesi na kusinyaa. Kuongezaka kwa joto na unyevunyevu ndani ya ghala<br />

kutokana na mzunguko mbaya wa hewa, uchafu ghalani, ukaushaji na uchambuaji mbaya<br />

vinasababisha uharibifu kubwa wa vitunguu ghalani<br />

Kudhibiti ;<br />

• ghala liwe safi pia liwe na uwezo wa kupitisha hewa kavu na ubaridi wa kutosha.<br />

• ghala lijengwe sehemu yenye upepo na kuruhusu mzunguko mzuri wa hewa.<br />

• vifungashio vya vitunguu vipangwe vizuri ili kuruhusu hewa kupita juu na chini.<br />

• vitunguu ndani ya kribu/ghala vijazwe kina cha sentimeta 30-50.<br />

• vitunguu vichambuliwe vizuri kabla ya kuhifadhi.<br />

• vitunguu ghalani vikaguliwe mara kwa mara ili kuondoa vitunguu vilivyoharibika<br />

4.0 Uuzaji wa vitunguu<br />

Watu wa aina mabalimabali wanahusika na ununuzi na uuzaji wa vitunguu wakiwa ni pamoja na:<br />

wakulima, wachuuzi, wafanya biashara ndogondogo, wauza jumla, wauza rejareja, wasafirishaji<br />

na madalali. Ili koboresha uuzaji na kipato ni muhimu kuzingatia yafuatayo:<br />

• Kuboresha ujazo kwa kufuata vipimo vinavyokubalika (kufuta lumbesa<br />

• Kupeana habari za masoko na bei.<br />

• Kuboresha usafirishaji kwa kutumia vikundi.<br />

• Kuwepo na mtiririko wa kuuza vitungu mwaka mzima, kwa kuboresha hifadhi ikiwa<br />

ni pamoja na maghala.<br />

• Kutathimini na kuzingatia ubora wa vitunguu.<br />

• Kutathimini na kuboresha ufungashaji na usafirishaji<br />

.<br />

9

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!