Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
RAIS DKT MAGUFULI AWASHUKURU WATANZANIA
Asema hatasahau namna watanzania walivyoliombea Taifa
Ataka tuendelee na dua, kila mmoja kwa imani yake
RAIS Dkt. John Pombe Magufuli amewapongeza
waislam wote nchini kwa kumaliza mfungo wa
mwezi Mtukufu wa Ramadhani na anawashukuru
kwa namna walivyoshiriki kuliombea Taifa hasa
katika kipindi hiki cha kukabilia na ugonjwa wa
COVID-19.
Hayo yamesemwa leo (Jumapili, Mei 24, 2020) na
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wakati akizungumza
na waumini wa dini ya kiislam mara baada
ya kumaliza kuswali sala ya Eid El Fitri katika Msikiti
wa Gaddafi, jijini Dodoma. Pia Rais Dkt. Magufuli
amewashukuru waumini wa dini nyingine nchini
kwa kushiriki kikamilifu kwenye kuliombea Taifa.
“Leo hii tunamalizia dua ya kumshukru Mwenyezi
Mungu, jambo hili Mheshimiwa Rais anasema
hatasahau kwa viongozi wote wa dini kuwa
pamoja kuliombea Taifa. Pia Mheshimiwa Rais
amesema tuendelee na dua zetu, kila mmoja kwa
imani yake wakati wote ili Mwenyezi Mungu aendelee
kutuondoa katika janga hili ambalo limeleta
mtikisiko duniani kote.”
Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi
Watanzania wote kwa ujumla waendelee kushirikiana
katika kulifanya Taifa liwe la amani na utulivu
.
“Dini zetu zinatutaka kila mmoja aendelee
kuomba, nchi hii imekuwa na utulivu sana na
mfano duniani kwa nchi zinazotaka amani.”
“Tuendelee na tabia hii na vingozi wa dini
endeleeni kusisitiza suala la amani, Serikali
inawasisitiza muendelee na shughuli zenu, sisi
tutahakikisha tunaendelea kulinda amani, fanyeni
kazi, mkulima lima na kwa walio viwandani nao
waendelee kufanya kazi.”
Kadhalika, Waziri Mkuu amesema wananchi
wanatakiwa waendelee kuchukua tahadhari dhidi
ya ugonjwa wa COVID-19, ambapo amewasisitiza
wasiwe na hofu na waendelee kufanya kazi kwa
bidii.
Akizungumzia kuhusu hali ya ugonjwa wa
COVID-19 ilivyo kwa sasa nchini, Waziri Mkuu
amesema katika hospitali ya Amana yupo
mgonjwa mmoja, Mloganzila yupo mmoja,
Temeke hatuna mgonjwa aliyethibitishwa, Kairuki
hakuna mgonjwa, Rabiansia hakuna mgonjwa,
Regency hakuna mgonjwa, Aga Khan yuko
mgonjwa mmoja, Lulanzi Kibaha wapo wagonjwa
16 na Dodoma Mkonze mpaka leo asubuhi wapo
wagonjwa tatu.
Awali, Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Sheikh
Mustafa Rajab, amempongeza Rais Dkt Magufuli
Inaendelea Uk.2
1 JARIDA MAALUM