26.05.2020 Views

JARIDA MAALUM OFISI YA WAZIRI MKUU

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

RAIS DKT MAGUFULI AWASHUKURU WATANZANIA

Asema hatasahau namna watanzania walivyoliombea Taifa

Ataka tuendelee na dua, kila mmoja kwa imani yake

RAIS Dkt. John Pombe Magufuli amewapongeza

waislam wote nchini kwa kumaliza mfungo wa

mwezi Mtukufu wa Ramadhani na anawashukuru

kwa namna walivyoshiriki kuliombea Taifa hasa

katika kipindi hiki cha kukabilia na ugonjwa wa

COVID-19.

Hayo yamesemwa leo (Jumapili, Mei 24, 2020) na

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wakati akizungumza

na waumini wa dini ya kiislam mara baada

ya kumaliza kuswali sala ya Eid El Fitri katika Msikiti

wa Gaddafi, jijini Dodoma. Pia Rais Dkt. Magufuli

amewashukuru waumini wa dini nyingine nchini

kwa kushiriki kikamilifu kwenye kuliombea Taifa.

“Leo hii tunamalizia dua ya kumshukru Mwenyezi

Mungu, jambo hili Mheshimiwa Rais anasema

hatasahau kwa viongozi wote wa dini kuwa

pamoja kuliombea Taifa. Pia Mheshimiwa Rais

amesema tuendelee na dua zetu, kila mmoja kwa

imani yake wakati wote ili Mwenyezi Mungu aendelee

kutuondoa katika janga hili ambalo limeleta

mtikisiko duniani kote.”

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi

Watanzania wote kwa ujumla waendelee kushirikiana

katika kulifanya Taifa liwe la amani na utulivu

.

“Dini zetu zinatutaka kila mmoja aendelee

kuomba, nchi hii imekuwa na utulivu sana na

mfano duniani kwa nchi zinazotaka amani.”

“Tuendelee na tabia hii na vingozi wa dini

endeleeni kusisitiza suala la amani, Serikali

inawasisitiza muendelee na shughuli zenu, sisi

tutahakikisha tunaendelea kulinda amani, fanyeni

kazi, mkulima lima na kwa walio viwandani nao

waendelee kufanya kazi.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema wananchi

wanatakiwa waendelee kuchukua tahadhari dhidi

ya ugonjwa wa COVID-19, ambapo amewasisitiza

wasiwe na hofu na waendelee kufanya kazi kwa

bidii.

Akizungumzia kuhusu hali ya ugonjwa wa

COVID-19 ilivyo kwa sasa nchini, Waziri Mkuu

amesema katika hospitali ya Amana yupo

mgonjwa mmoja, Mloganzila yupo mmoja,

Temeke hatuna mgonjwa aliyethibitishwa, Kairuki

hakuna mgonjwa, Rabiansia hakuna mgonjwa,

Regency hakuna mgonjwa, Aga Khan yuko

mgonjwa mmoja, Lulanzi Kibaha wapo wagonjwa

16 na Dodoma Mkonze mpaka leo asubuhi wapo

wagonjwa tatu.

Awali, Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Sheikh

Mustafa Rajab, amempongeza Rais Dkt Magufuli

Inaendelea Uk.2

1 JARIDA MAALUM

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!