26.05.2020 Views

JARIDA MAALUM OFISI YA WAZIRI MKUU

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

JARIDA MAALUM

Toleo la 2 Mei, 2020

Ofisi ya Waziri Mkuu

1

ASANTENI

RAIS Dkt. John Pombe Magufuli

amewapongeza waislam wote nchini

kwa kumaliza mfungo wa mwezi

Mtukufu wa Ramadhani na

anawashukuru kwa namna walivyoshiriki

kuliombea Taifa....

-

2

UTOAJI MICHE YA CHIKICHI BURE

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa,

amesema upandaji wa zao la

michikichi utaanza rasmi

Oktoba mwaka huu.....

JARIDA LA MTANDAONI


RAIS DKT MAGUFULI AWASHUKURU WATANZANIA

Asema hatasahau namna watanzania walivyoliombea Taifa

Ataka tuendelee na dua, kila mmoja kwa imani yake

RAIS Dkt. John Pombe Magufuli amewapongeza

waislam wote nchini kwa kumaliza mfungo wa

mwezi Mtukufu wa Ramadhani na anawashukuru

kwa namna walivyoshiriki kuliombea Taifa hasa

katika kipindi hiki cha kukabilia na ugonjwa wa

COVID-19.

Hayo yamesemwa leo (Jumapili, Mei 24, 2020) na

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wakati akizungumza

na waumini wa dini ya kiislam mara baada

ya kumaliza kuswali sala ya Eid El Fitri katika Msikiti

wa Gaddafi, jijini Dodoma. Pia Rais Dkt. Magufuli

amewashukuru waumini wa dini nyingine nchini

kwa kushiriki kikamilifu kwenye kuliombea Taifa.

“Leo hii tunamalizia dua ya kumshukru Mwenyezi

Mungu, jambo hili Mheshimiwa Rais anasema

hatasahau kwa viongozi wote wa dini kuwa

pamoja kuliombea Taifa. Pia Mheshimiwa Rais

amesema tuendelee na dua zetu, kila mmoja kwa

imani yake wakati wote ili Mwenyezi Mungu aendelee

kutuondoa katika janga hili ambalo limeleta

mtikisiko duniani kote.”

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi

Watanzania wote kwa ujumla waendelee kushirikiana

katika kulifanya Taifa liwe la amani na utulivu

.

“Dini zetu zinatutaka kila mmoja aendelee

kuomba, nchi hii imekuwa na utulivu sana na

mfano duniani kwa nchi zinazotaka amani.”

“Tuendelee na tabia hii na vingozi wa dini

endeleeni kusisitiza suala la amani, Serikali

inawasisitiza muendelee na shughuli zenu, sisi

tutahakikisha tunaendelea kulinda amani, fanyeni

kazi, mkulima lima na kwa walio viwandani nao

waendelee kufanya kazi.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema wananchi

wanatakiwa waendelee kuchukua tahadhari dhidi

ya ugonjwa wa COVID-19, ambapo amewasisitiza

wasiwe na hofu na waendelee kufanya kazi kwa

bidii.

Akizungumzia kuhusu hali ya ugonjwa wa

COVID-19 ilivyo kwa sasa nchini, Waziri Mkuu

amesema katika hospitali ya Amana yupo

mgonjwa mmoja, Mloganzila yupo mmoja,

Temeke hatuna mgonjwa aliyethibitishwa, Kairuki

hakuna mgonjwa, Rabiansia hakuna mgonjwa,

Regency hakuna mgonjwa, Aga Khan yuko

mgonjwa mmoja, Lulanzi Kibaha wapo wagonjwa

16 na Dodoma Mkonze mpaka leo asubuhi wapo

wagonjwa tatu.

Awali, Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Sheikh

Mustafa Rajab, amempongeza Rais Dkt Magufuli

Inaendelea Uk.2

1 JARIDA MAALUM


kwa kuwapa Watanzania moyo wa kishujaa na

ujasiri katika kukailiana na ugonjwa wa COVID-19

kwa kuwataka wamwombe Mwenyezi Mungu ili

aliepushe Taifa na janga hilo, wakati Mataifa na

viongozi wengine duniani yakikumbwa na taharuki.

“Hakuna mkombozi zaidi ya Mwenyezi Mungu,

shida zetu, matatizo yetu na hata tukijaribiwa kwa

maradhi au mtihani wa aina yoyote Mwenyezi

Mungu anatupa ushujaa wa kukabiliana nao. Hofu

ya maradhi ni kifo hivyo tusiwe na hofu tumtegemee

Mwenyezi Mungu kama Rais wetu anavyotusisitiza.”

2

Amesema wananchi hawana sababu ya kuwa na

hofu kwani tayari Rais Dkt. Magufuli alitangaza

siku tatu kwa ajili ya kumuomba Mwenyezi

Mungu aliepushe Taifa na corona na viongozi wa

dini zote waliitikia wito na waliongoza maombi

ambayo yamejibiwa na sasa huo ugonjwa umepungua

nchini.

Sheikh Rajab aliongeza kuwa baada ya Mwenyezi

Mungu kukubali dua hizo na Rais, Dkt. Magufuli,

kutenga siku tatu za kumshukuru Mwenyezi

Mungu ambazo zinaisha leo, wananchi hawana

budi waendelee kumshukuru na kamwe wasishiriki

kwenye kufanya maasi. “Tuwe ni watu wenye

kushukuru neema tunazojaaliwa na Mwenyezi

Mungu na kamwe tusiwe wenye kuzikufuru

JARIDA MAALUM


MAJALIWA: TUTATOA MICHE YA CHIKICHI BURE KWA WANANCHI

Asema lengo ni kuhakikisha nchi inakuwa na utoshelevu wa mafuta

Upandaji kuanza rasmi Oktoba

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa, amesema upandaji wa zao la michikichi utaanza

rasmi Oktoba mwaka huu na kama kuna mtu mmoja mmoja au kikundi wanataka

kulima chikichi, waandae mashamba yao na miche ya awali watapewa bure.

“Serikal imedhamiria tulime zao hili kwa wingi na

tuwasaidie wakulima kwani tunatumia pesa

nyingi sana kununua mafuta ya mawese kutoka

nje. Tukilima kwa wingi tutajitosheleza na hatutaagiza

mafuta kutoka nje.”

Waziri Mkuu amesema kwa sasa Tanzania haitaagiza

mbegu za michikichi kutoka sehemu yoyote

duniani na badala yake itazalisha mbegu zake

yenyewe. “Tayari tuna miche milioni 1.8 na wataalamu

wetu wanaendelea kuzalisha.”

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumamosi, Mei

23, 2020) baada ya kukagua kitalu cha miche ya

michikichi cha Halmashauri ya Kigoma Ujiji

pamoja na kitalu cha JKT Bulombora akiwa katika

ziara ya kikazi mkoani Kigoma.

Vile vile, Waziri Mkuu amemwagiza Mkuu wa

Mkoa wa Kigoma Brigedia Mstaafu, Emmanuel

Maganga, ahakikishe JKT Bulombora wanapewa

ardhi waliyoomba kwa ajili ya kupanua kilimo cha

michikichi.

“Michikichi Kigoma ndio uchumi, tunataka wakulima

wengi walime zao hili na Kigoma ndio chanzo

cha zao la michikichi, Kigoma ndio iliyotoa chikichi

kwenda nchi nyingine.”

Amesema Ilani ya CCM ya 2015-2020 imeelekeza

kuwa kufufuliwa kwa zao hilo na Serikali imetekeleza

hilo kwa kuanzia Kigoma na kisha

yatafuatia maeneo mengine ya nchi.

Inaendelea Uk.4

3

JARIDA MAALUM


Waziri Mkuu amesema kwa sasa Tanzania haitaagiza

mbegu za michikichi kutoka sehemu yoyote

duniani na badala yake itazalisha mbegu zake

yenyewe. “Tayari tuna miche milioni 1.8 na wataalamu

wetu wanaendelea kuzalisha.”

“Michikichi Kigoma ndio

uchumi, tunataka wakulima

wengi walime zao hili na

Kigoma ndio chanzo cha zao la

michikichi, Kigoma ndio iliyotoa

chikichi kwenda nchi

nyingine.”

Amesema Ilani ya CCM ya 2015-2020 imeelekeza

kuwa kufufuliwa kwa zao hilo na Serikali imetekeleza

hilo kwa kuanzia Kigoma na kisha

yatafuatia maeneo mengine ya nchi.

Waziri Mkuu amesema awali kituo cha utafiti wa

zao hilo kilikuwa jijini Dar es Salaam, Serikali

ikaona haiwezekani na kuamua kukihamishia

Kihuinga, mkoani Kigoma.

Amesema wataalam walihamishiwa Kihinga na

tayari wameshazalisha zaidi ya miche milioni 1.8 na

kazi iliyobaki ni kuwapa wananchi ili waweze

kupanda kwenye mashamba yao.

Pia, Waziri Mkuu amewaagiza Maafisa Kilimo

wawasaidie wakulima kulima zao hilo kitaalamu

pamoja na wale wenye michikichi ya zamani jinsi

ya kuitoa na kupanda michikichi hizi mpya,

Waziri Mkuu amewasisitiza wananchi wajiwekee

utaratibu wa kupalilia mashamba yao ili michikichi

iweze kustawi na wahakikishe hawachomi

moto mapori kwani utaharibu michikichi yao.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewataka Wananchi

nchini kote waendelee kuchukua tahadhari juu ya

ugonjwa wa COVID-19 na wafuate masharti ya

wataamu. Hata hivyo amesema idadi ya wagonjwa

wa COVID-19 imepungua sana nchini.

Naye, Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Omar

Mgumba, amesema anamshukuru Waziri Mkuu

kwa maelekezo yake ya kuagiza miche ya michikichi

igawiwe bure kwa wananchi. “Tumetumia sh.

bilioni 10.8 kwa ajili ya zoezi hili, na hizi ni jitihada

za Rais, Dkt. John Pombe Magufuli.”

4 JARIDA MAALUM


KATIBU MKUU

Ofisi ya Waziri Mkuu

2 Mtaa wa Relini, S.L.P 980

40480 Dodoma,

Baruapepe: ps@pmo.go.tz, Simu:+255262322480

Fax:+255262324534, Tovuti: www.pmo.go.tz

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!