Ulu ul Azmi minna Rusulun Juzuu Al Thaniya
Al Mustakshif Abu Manal Danah Ulu ul Azmi minna Rusulun Juzuu Al Thaniya
Al Mustakshif Abu Manal Danah Ulu ul Azmi minna Rusulun Juzuu Al Thaniya
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
1
2
﴾
﴿أُوْلُواْ
الْعَزْمِ مِنَ
الر ُّسُلِ
الجزء ال ثن
تجميع وانتاج
المستكشف أبومنال دانا
UuLU AL A’AZMI MINA ALRRUSUL
AL JUZUI AL THANI
WENYE AZMA THABIT ZAIDI
MIONGONI MWA MITUME
SEHEMU YA PILI
KIMEKUSANYWA NA KUTAYARISHWA NA AL MUSTAKSHIF ABU MANAL DANAH
KIMECHAPISHWA NEW DELHI – INDIA.
MWAKA 1445 AL HIJRA – 2024 C.E
3
﴿ِسْ مِ ا ِ الرحمْ َنِ الرحِيمِ﴾
إن َّ الحَْمْدَ هللِ َِّ نحَْمَدُهُ ونَسْتَعِينُهُ وَنَسْتَغْفِرُهُ وَنَعُوذُ ابِ هلل َِّ ِمنْ شُرُورِ أَنْفُسِ نَا وَمِ ْن
سَيِّئَاتِ أَعْمَالِنَا، مَنْ يَهْدِهِ اهلل َُّ فَلاَ مُضِل َّ لَهُ وَمَنْ يُضْلِلْ فَلاَ هَادِيَ لَهُ وَأشْهَدُ
أنْ لاَ إِلَهَ إِلا َّ اهلل َُّ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ وَأشْهَدُ أن َّ محَُم َّدًا عَبْدُهُ وََر سُولُهُ
Inna Al-hamda Lillaahi nahmaduhu wanasta’eenahu wa nastaghfiruhu, wa
na’oodhu billaahi min shuroori anfusinaa wa min sayi’aati a’maalinaa. Man yahdih
Illaahu falaa mudhilla laahu wa man yudhlil falaa haadiya lahu. Wa ashhadu an laa
ilaaha ill-Allaahu wahdahu laa shareekallahu, wa ashhadu anna Muhammadan
‘Abduhu wa Rasooluhu.
Tafsir: Kwa jina la Allah, ambae anastahiki shukrani zote, tunaemuomba msaada na
msamaha wake. Tunajilinda kwa ulinzi wa Allah na kila maovu ya Nafsi zetu na
mambo mabaya yetu. Kwani kwa hakika mtu yeyote yule alieongozwa na Allah basi
hakuna atakaempotoa, na aliepotoshwa na Allah basi hakuna atakaemuongoa.
Nnashuhudia kua hakuna anaepaswa kuabudiwa isipokua Allah pekee asiekua na
mshirika, na nnashuhudia kua Muhammad (Salallahu A’layhi wa Salam) ni Mja wake
na ni Mtume wake.
يَقُولُ اللهُ عَز َّ وَجَ َّل
﴿َي ُّهَا ال َّذِينَ ءَامَنُواْ ات َّقُواْ اهلل ََّ حَق َّ تُقَاتِهِ وَلاَ تمَُوتُن َّ إِلا َّ وَأَنتُم م ُّسْلِمُونَ ﴾
Ya ayyuha alladhina amanoo ittaqoo Allaha haqqa tuqatihi wala tamootunna illa
waantum muslimoona (Surat Al Imran 3:102)
Tafsir: Enyi mlioamini! Muogopeni Allah (kwa kutekeleza maamrisho yake na
kuachana na makatazo yake) kama anavyostahiki kuogopewa. [Mtiini, mshukuruni
na daima mkumbukeni], na msife isipokua mkiwa katika hali ya kua ni Waislam.
4
﴿يَأَي ُّهَا الن َّاسُ ات َّقُواْ رَب َّكُمُ ال َّذِى خَلَقَكُمْ مِنْ ن َّفْسٍ وَحِ دَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا
وَبَث َّ مِنْهُمَا رِجَالاً كَثِيراً وَنِسَآءً وَات َّقُواْ اهلل ََّ ال َّذِى تَسَآءَلُونَ بِهِ وَالأَْرْ َح ا مَإِ َّنا هلل ََّ
﴾ كَا نَعَلَيْ ي ب كُمْرَقِ اً
Ya ayyuha alnnasu ittaqoo rabbakumu alladhi khalaqakum min Nafsin wahidatin
wakhalaqa minha zawjaha wabaththa minhuma rijalan kathiran wanisaan
waittaqoo Allaha alladhii tasaaloona bihi waal-arhama inna Allaha kana
AAalaykum raqeeban (Surat An Nisaa 4:1)
Tafsir: Enyi Watu! Mcheni Mola wenu aliekuumbeni kutokana na Nafsi moja (Adam),
na kutokana nae (Adam) akamuumba Mke wake (Hawwa), na kutokana nao (Adam
na Hawa) akawaumba Wanaume na Wanawake wengi na muogopeni Allah ambae
ana haki juu yenu, na msivunje udugu, kwani kwa Hakika Allah ni mwenye uangalifu
mkubwa juu yenu.
﴿َي ُّهَا ال َّذِينَ ءَامَنُواْ ات َّقُواْ اهلل ََّ وَقُولُواْ قَوْلاً سَدِيداً۞يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَلَكُ مْ وَيَغْفِ ْر
لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَن يُطِعِ اهلل ََّ وَرَسُولَهُ
فَقَدْ فَازَ فَوْزاً عَظِيماً ﴾
Ya ayyuha alladhina amanoo ittaqoo Allaha waqooloo qawlan sadeedan, Yuslih
lakum aAAmalakum wayaghfir lakum dhunoobakum waman yutiAAi Allaha
warasoolahu faqad faza fawzan AAadhiman (Al Ahzab 33:70-71)
Tafsir: Enyi Mlioamini! mcheni na muogopeni Allah, na (daima) semeni kauli za
ukweli ulionyooka, atakuongozeni kufanya mema na kukusameheni dhambi zenu. Na
kwa hakika yeyote yule ambae anaemtii Allah na Mtume wake (Salallahu A’layhi wa
Salam) basi atakua ni miongoni mwa waliofuzu kwa mafanikio makubwa sana.
Allahuma Ij’Aalna minna al faizin fawzan A’adhimah…Aamin
أَمَا بَعْدُ
5
قَالَ رَسُولِ اهلل َِّ صَل َّى اللهُ:فَإِن َّ أَصْدَقَ الحَْدِيثِ كِتَابُ اهلل َِّ، وَأَوْثََق الْعُرْي كَ لِمَ ةُ
الت َّقْوَى، وَخَيْرَ الْمِلَلِ مِل َّةُ إِبْرَاهِيمَ، وَخَيْرَ الس ُّنَنِ سُنَنُ محَُم َّدٍ صَل َّى اللهُ عَلَيْهِ
وَسَل َّمَ، وَأَشْرَفَ الحَْدِيثِ ذِكْرُ اهلل َِّ تَعَالىَ ، وَأَحْسَنَ الْقَصَصِ هَذَا الُْق رْآ ُن
Qala Rasul Allahi Salallahu A’alayhi wa Salam: fa'inn 'asdaqa alhadith kitab alllahi,
wa'awthaq al’aAuryi kalimat alttaqwaa, wakhayr almilal millat 'Ibrahima, wakhayr
alssunan sunan Muhammad Sala Allahu Alyhi wa Salam, wa'ashraf alhadith dhikr
allah taalaa, wa'ahsan alqasas hadha al Quran.
Amesema Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam kua: Kwa hakika hadith za kweli
kabisa ni za Kitabu cha Allah Subhanah wa Ta’ala, na kauli nzito ni kauli zenye
Taqwa, na Mila bora ni Milat Ibrahima, Na Sunna bora ni Sunna za Muhammad
(Sala Allahu Alyhi wa Salam) na Maneno Matukufu ni Dhikr Allah Ta’ala na Visa
bora ni hii Qur’an.
وَ يَقُولُ اللهُ عَز َّ وَجَ َّل
﴿وَبِٱلحَْقِّ أَنْزَلْنَاهُ وَبِٱلحَْقِّ نَزَلَ وَمَآ أَرْسَلْنَاكَ إِلا َّ مُبَشِّ راً وَنَذِيراً۞وَ قُرْآً فَرَقْنَاهُ لِتَقْرَأَهُ
عَلَى ٱلن َّاسِ ٰ عَلَى مُكْثٍ وَنَز َّلْنَاهُ تَنْزِيلاً۞قُلْ آمِنُواْ بِهِ أَوْ لاَ ۤ تُؤْمِنُواْ إِن َّ ٱل َّذِينَ أُوتُواْ
ٱلْعِلْمَ مِن قَبْلِهِ إِذَا ٰ يُتْلَى عَلَيْهِمْ يخَِر ُّونَ لِلأَذْقَانِ سُج َّداً۞وَيَ قُولُونَ سُبْحَانَ آ رَبّ نَ نِإ
كَانَ وَعْدُ رَبِّنَا لَمَفْعُولاً۞وَيخَِر ُّونَ لِلأَذْقَانِ يَبْكُونَ وَيَزِيدُهُمْ خُشُوعاً۞قُلِ ٱدْعُواْ
ِ
ٱهلل ََّ أَوِ ٱدْعُواْ ٱلر َّحمَْٰنَ أًَّ م َّا تَدْعُواْ فَلَهُ ٱلأَسمَْآءُ ٱلحُْسْنىَٰ وَلاَ تجَْهَرْ بِصَلاَتِكَ وَلاَ
تخَُا فِ ا تْهبَِ وَ ٱبْتَغِ بَينَْ ذٰلِكَ سَبِيلاً۞وَقُلِ ٱلحَْمْدُ هللِ َِّ ٱل َّذِى لمَْ يَت َّخِ ذْ وَلَداً وَلمَ يَكُ ْن
ل َّهُ شَرِيكٌ فىِ ٱلْمُلْكِ وَلمَْ يَكُنْ ل َّهُ وَليِ ٌّ م َّنَ ٱلذ ُّ لِّ وَكَبرِّْهُ تَكْبِيراً ﴾
6
Wabialhaqqi anzalnahu wabialhaqqi nazala wama arsalnaka illa mubashshiran
wanadheeran, Waqur-anan faraqnahu litaqraahu AAala alnnasi AAala mukthin
wanazzalnahu tanzeelan, Qul aminoo bihi aw la tu/minoo inna alladheena ootoo
alAAilma min qablihi idha yutla AAalayhim yakhirroona lil-adhqani sujjadan;
Wayaqooloona subhana rabbina in kana waAAdu rabbina lamafAAoolan;
Wayakhirroona lil-athqani yabkoona wayazeeduhum khushooAAan; Quli odAAoo
Allaha awi odAAoo alrrahmana ayyan ma tadAAoo falahu al-asmao alhusna wala
tajhar bisalatika wala tukhafit biha waibtaghi bayna dhalika sabeelan, Waquli
alhamdu lillahi alladhee lam yattakhidh waladan walam yakun lahu shareekun fee
almulki walam yakun lahu waliyyun mina aldhdhulli wakabbirhu takbeeran (Surat
Al Isra 17:105-111)
Tafsir: Na kwa haki tumeiteremsha chini (Hii Qur’an) na kwa haki imeshuka, na
tumekutuma wewe (Muhammad) si kwa chochote isipokua kwa ajili ya kuweka wazi
na kuonya. Na hii Qur’an ambayo tumeigawa (katika aya na sura tofauti) ili upate
kuisoma kwa watu kwa makusudio. Na tumeishusha hii (Qur’an) kwa vituo (tofauti).
Sema (Ewe Muhammad): ‘Iaminini au msiiamini. Kwani kwa hakika wale waliopewa
Ilm kabla yake (Ilm ya Ahl Al Kitab kina Abd Allah Ibn Salam, Salman Al Farsi n.k)’
waliposomewa, walianguka chini kwa nyuso zao kwa Unyenyekevu wa Kusjudu. Na
wakasema: ‘Utukufu ni wa Allah Pekee. Ahadi ya Mola wetu ni lazime iwe ni yenye
kutekelezwa’. Na wakaanguka kwa nyuso zao wakilia machozi na hii ilizidisha
Unyenyekevu wao. Sema (Ewe Muhammad) Muombeni Allah, au muombeni Ar
Rahmani, au kwa jina lolote (Katika Majina yake Matukufu), kwani kwake yeye ndio
kwenye umiliki wa Majina Matukufu, na Salini bila ya kufanya kelele au kwa sauti ya
chini, bali fuateni njia ya baina yake (hali hizo mbili). Na semeni, shukrani zote
anastahiki Allah ambae hana mtoto, na wala hana mshirika katika Ufalme wake, na
ni asiekua (na uhitaji wa) Msaidizi wala Mlinzi. Na Mkuzeni kwa Takbir.
ALLAHU AKBAR!
7
YALIYOMO
YALIYOMO ....................................................................................................... 7
VITABU VILIVYOTANGULIA VYA AL MUSTAKSHIF ABU MANAL
DANAH: ......................................................................................................... 13
UTANGULIZI ................................................................................................. 14
SURA YA KWANZA ........................................................................................ 20
MUONGOZO, MANUFAA, TIBA NA REHMA ZILIZOMO NDANI YA
QUR’AN. ........................................................................................................ 20
HIKMA NA BARAKA NDANI YA QUR’AN ..................................................... 28
MAFUMBO NA MITHALI ZILIZOMO NDANI YA QUR’AN. .......................... 35
AINA ZA KALIMAT (KAULI) NDANI YA QURÁN .......................................... 52
MANUFAA YA KUTAWANYIKA NA KUTEMBEA ARDHINI KULINGANA NA
QUR’AN. ........................................................................................................ 56
UMUHIMU WA HIJRA KATIKA ISLAM ......................................................... 66
MAUMBILE YA NYOYO ZA IBN ADAM: AL QALB, AL FUAD, AL LUBB, AL
SADR NA AN NAFS KATIKA QURÁN ............................................................ 74
AL QALB ........................................................................................................ 75
AL FUAD ........................................................................................................ 87
AL LUBB ........................................................................................................ 89
AL SADR......................................................................................................... 90
MAANA YA AQL, HIJR, HILM, NNUHA NA BALU. ....................................... 95
NAFS - MAUMBILE YAKE NA UHIBITI WAKE. .......................................... 101
NAFS AL AMMARAH BI ALSUI (NAFS SHAHWANIYYAH) ......................... 104
NAFS AL MULHIMAH ................................................................................. 105
NAFS AL LAWWAMAH. ............................................................................... 106
NAFS AL MUTMA’INAH .............................................................................. 107
NAFS RADHIYATAN .................................................................................... 111
NAFS MARDHIYAH. .................................................................................... 112
NAFS AL KAMILAH ..................................................................................... 112
8
KUSUDIO LA ALLAH SUBHANAH WA TA’ALA KUTUMA MITUME KWA
WAJA WAKE. ............................................................................................... 114
MITUME NA MANABII WALIOTAJWA KATIKA QURÁN. ........................... 124
MAANA YA MIUJIZA. .................................................................................. 137
SURA YA PILI............................................................................................... 146
HISTORIA YA MZEE IMRAN BABU YAKE NABII ISA IBN MARYAM BINT
IMRAN .......................................................................................................... 147
UHARAMU NA UTUKUFU WA DAMU KATIKA UISLAM. ......................... 149
ADHA YA DAMU YA KIMAUMBILE YA MWANAMKE................................ 179
KUKARIBIANA KIMAPENZI BAINA YA MKE NA MUME KATIKA
UISLAM ........................................................................................................ 185
KUZALIWA KWA MARYAM BINT IMRAN ................................................... 200
KAFFALA – ULEZI WA MARYAM BINT IMRAN. ........................................ 203
HAKI ZA YATIMA, MUNQATI NA LAQIT KATIKA UISLAM ...................... 210
AYAT AL QURSY - NYAKATI NA MATUKIO YA VIUMBE MBELE YA ALLAH
SUBHANAH WA TA'ALA .............................................................................. 247
SURAT AL MAA’UN – UMUHIMU WA KUJALI MAYATIMA, MASIKINI NA
SALA KATIKA DINI YA KIISLAM. ............................................................... 257
UMUHIMU WA UNYENYEKEVU KATIKA SALA NA DUA.......................... 300
KULELEWA KWA MARYAM BINT IMRAN NA NABII ZAKARIYAH ............ 364
KUZALIWA KWA NABII YAHYA IBN ZAKARIYAH ...................................... 373
SABABU YA KUSHUSHWA KWA SURAT MARYAM .................................... 383
HARFU MUQATTAA’AT NA KISA CHA NABII ISA. .................................... 389
MAANA NA FAIDA YA BIISMI ALLAHI ALRRAHMANI ALRRAHIM .......... 401
KAF – HA – YA – A’AYN – SAD ................................................................... 411
UJUMBE WA NAJRAN, THUMAMAH IBN UTHAL – UTHIBITSHO WA
WASIOKUA WAISLAM KURUHUSIKA KUINGIA MSIKITINI ..................... 419
MAUMBILE YA ISA IBN MARYAM NI MITHLI YA NABII ADAM. ............... 431
UTUKUFU WA KUTUNUKIWA UJA UZITO MARYAM BINT IMRAN ........ 441
KUZALIWA KWA NABII ISA IBN MARYAM ................................................ 463
9
KUZUNGUMZA KWA HOJA KWA ISA IBN MARYAM UTOTONI. .............. 470
HIJRA YA MARYAM BINT IMRAN NA NABII ISA BAINA YA MISRI NA
NASIRA......................................................................................................... 477
ANSARU ALLAH – AL HAWARIYINA .......................................................... 480
AL MAIDAH ................................................................................................. 488
UTHIBITISHO WA ISA IBN MARYAM KUA SI MUNGU. ............................ 497
KUPANDISHWA MBINGUNI KWA ISA IBN MARYAM NA KIFO CHA
MARYAM BINT IMRAN. ............................................................................... 503
ISA IBN MARYAM NA MARYAM MAJDALANIYAH ..................................... 512
WANAFUNZI WA NABII ISA IBN MARYAM KATIKA SURAT YASIN .......... 513
VITHIBITISHO VYA WANAZUONI JUU YA KUPANDISHWA JUU
MBINGUNI RUHI ALLAHI ISA IBN MARYAM WAKATI AKIWA HAI. ........ 521
TAQDIM WA TAAKHIR KATIKA QUR’AN .................................................. 527
ISA IBN MARYAM NA MAHDI, DAJJAL, JUJ WA MAJUUJ NA DHUL
QARNAYN. ................................................................................................... 532
KAULI ZA ISA IBN MARYAM A’LAYHI SALATU WA WASALAM
KATIKA AL RISALAT AL QUDSIYYAH. .................................................. 544
KAULI ZA NABII MUHAMMAD SALALLAHU ALYHI WA SALAM
KUHUSIANA NA NABII ISA ALAYHI SALAM. ............................................. 556
KAULI ZA ALLAH SUBHANAH WA TAALA JUU YA NABII ISA IBN
MARYAM. ..................................................................................................... 557
MAELEZO YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM
KUTOKA KATIKA YALE WALIORITHI MAYAHUDI NA WAKRISTO.......... 558
SURA YA TATU ............................................................................................ 561
IMAM AL ANBIYAI WAL ALMURSALINA MUHAMMAD SALALLAHU
A’LAYHI WA SALAM .................................................................................... 562
ASILI YA UARABU NA YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA
SALAM. ........................................................................................................ 563
NDOTO YA ABD UL MUTTALIB NA KISIMA CHA ZAMZAM ..................... 569
ABDULLAH IBN ABD UL MUTTALIB BABA YAKE RASUL ALLAH
SALALLAHU AAYHI WA SALAM ................................................................. 574
10
BARAKAH BINT THALABAH UMM AYMAN MAMA MLEZI WA RASUL
ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM .................................................. 579
AMINAH BINT WAHB MAMA MZAZI WA RASUL ALLAH SALALLAHU
ALAYHI WA SALAM ..................................................................................... 580
KIFO CHA ABDULLAH NA KUZALIWA KWA RASUL ALLAH SALALLAHU
ALAYHI WA SALAM. .................................................................................... 582
THUWAYBAH AL ASLAMIYAH MAMA MNYONYESHAJI WA PILI WA RASUL
ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM .................................................. 587
HALIMA BINT ABU DHUAYB AL SADIYA MAMA ALIEMNYONYESHA WA
RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM ...................................... 589
MIUJIZA YA UTOTONI MWA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA
SALAM WAKATI AKIWA KWA HALIMA BINT ABU DHUAYB .................... 591
INSHIRAH SADR YA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM. ... 595
TAFSIR YA SURAT AL INSHIRAH. .............................................................. 599
KIFO CHA AMINAH BINT WAHB MAMA YAKE RASUL ALLAH SALALLAHU
ALAYHI WA SALAM. .................................................................................... 608
USAFI WA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA USAFI WA
WAZEE WAKE. ............................................................................................. 611
RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA UMMU AYMAN
KATIKA NYUMBA YA ABU TALIB NA FATMA BINT ASAD ........................ 619
RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA HILF AL FUDUL ... 624
SAFARI YA KIBIASHARA YA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA
SALAM KATIKA ARDHI YA SHAM. ............................................................. 628
NDOA YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’ALAYHI WA SALAM NA
KHADIJA BINT KHUWAYLID RADHI ALLAHU ANHA. ............................. 637
MUHAMMAD AL AMIN SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA UJENZI WA
AL KAABAH. ................................................................................................ 641
RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA ALI IBN ABI TALIB 644
MAISHA YA UTUME WA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA
SALAM NA UPINZANI KUTOKA KWA WATU WAKE. ................................ 649
MAISHA YA DAR AL ARQAM NA HIJRA YA ABISINIYAH .......................... 668
DAMU YA KWANZA YA MASHAHIDI WA KIISLAM. .................................. 675
11
KUSILIMU KWA UMAR IBN AL KHATTAB RADHI ALLAHU ANHU ......... 689
KIFO CHA ABU TALIB NA KHADIJA BINT KHUWAYLID RADHI ALLAHU
ANHA ........................................................................................................... 696
SHAQQ AL QAMAR - MUUJIZA WA KUPASUKA KWA MWEZI................. 705
SIFA ZA UPEKEE WA KIMAUMBILE WA NABII MUHAMMAD SALALLAHU
ALAYHI WA SALAM: .................................................................................... 708
SAFARI YA ISRA NA MIRAJ. ........................................................................ 723
MAUMBILE YA BURAQ NA MIUJIZA YA SAFARI YA ISRA NA MIRAJ. ..... 734
MUSAB IBN UMARY BALOZI WA KWANZA WA UISLAM NA
MAKUBALIANO YA AQABAH. .................................................................... 747
DARJA ZA MASAHABA WA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA
SALAM. ........................................................................................................ 752
KUZALIWA KWA BAHR UL ILM ABDA ALLAH IBN ABBAS RADHI ALLAHU
ANHU. .......................................................................................................... 755
HIJRA YA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM ..................... 756
MUHAMMAD SALALLAHU ALAYHI WA SALAM, ALI IBN ABI TALIB NA
SUHAYB AL AL RUMI RADHI ALLAHU ANHUM NDANI YA ARDHI YA
QUBA ........................................................................................................... 769
MASJID TAQWA - MSIKITI WA MWANZO KUJENGWA NA RASUL ALLAH
SALALLAHU ALAYHI WA SALAM. .............................................................. 773
KUWASILI KWA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM KATIKA
MJI WA MADINAH AN NABI. ...................................................................... 777
MAKUBALIANO BAINA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM
NA WATU WA MADINAH ............................................................................ 784
KUWASILI KWA UMMU AYMAN KATIKA MJI WA MADINAH AN NABI. .. 787
RASUL ALLAH SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM NA MSAFARA WA
BIASHARA WA ABU SUFYAN ...................................................................... 791
YAWM AL FURQAN – SIKU YA VITA VYA BADR. ...................................... 797
KHALID IBN WALID NA VITA VYA UHUD, KHANDAK NA MUTAA. ........ 811
MAKUBALIANO YA SULHU AL HUDAYBIYYAH ........................................ 821
KUSILIMU KWA KHALID IBN WALID. ....................................................... 832
12
SAYFU ALLAH KHALID IBN WALID RADHI ALLAHU ANHU NA VITA VYA
MUTAH ........................................................................................................ 836
FAT-H MAKKIYAH - UFUNGUZI WA MJI WA MAKKAH. .......................... 838
WAKE WA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM. ........ 844
UMM AL MU’MININ SAWDAH BINT ZUMAH ........................................... 852
UMM AL MU’MININ AISHA BINT ABU BAKR AS SIDDIQ ........................ 853
UMM AL MU’MININ HAFSAH BINT UMAR IBN AL KHATTAB. ............... 855
UMM AL MU’MININ ZAYNAB BINT KUZAYMAH. .................................... 857
UMM AL MU’MININ RAYHANA BINT ZAYD ............................................. 859
UMM AL MU’MININ HIND UMMU SALAMAH. ........................................ 860
UMM AL MU’MININ MAYMUNA BINT HARITH IBN HAZAN AL
HILALIEH .................................................................................................... 862
UMM AL MU’MININ ZAYNAB BINT JAHSH. ............................................. 865
UMM AL MU’MININ RAMLA BINT ABU SUFYAN – UMMU HABIBA. ..... 867
UMM AL MU’MININ JUWAYRIYAH BINT HARITH. ................................... 870
UMM AL MU’MININ SAFIYYHA BINT HUYAY IBN AKHTTAB. ................ 871
UMM AL MU’MININ MARIA BINT SHAM. .................................................. 873
SURIYYAH NA MILK AL YAMIN KATIKA UISLAM ..................................... 875
MFUMO WA UTUMWA NA MATEKA WA VITA KATIKA UISLAM. ............ 880
AAL, AHL, ZAWJ NA QAWWAM KATIKA UISLAM. .................................... 888
WANAWAKE WALIO JIPENDEKEZESHA KINDOA NA WALIOCHIKA WA
NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM. .......................... 907
MAVAZI YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM. ...... 912
HIJA YA KUAGA YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA
SALAM. ........................................................................................................ 914
KHUTBA YA KUAGA YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA
SALAM. ........................................................................................................ 920
KIFO CHA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM. ........ 923
MAUTI, BARZAKH NA KABURI KATIKA AYA NA HADITH ....................... 942
13
KUHIFADHIWA NA KURAHISISHWA KWA QUR’AN. ............................... 980
MARUDIO YA VITABU VILIVYOTUMIKA KATIKA KITABU
HIKI: ....................................................................................................... 998
MARUDIO YA MITANDAO ILIVYOTUMIKA KATIKA KITABU
HIKI......................................................................................................... 999
VITABU VILIVYOTANGULIA VYA AL MUSTAKSHIF ABU MANAL DANAH:
1- IJTIHAD NA TAQLID HISTORIA YA UISLAM: MAIMAMU NA MADHHAB
YAO KATIKA UISLAM - TOLEO LA KWANZA - MWAKA - 1435 AL HIJRA
(2014).
2- IJTIHAD NA TAQLID HISTORIA YA UISLAM: MAIMAMU NA MADHHAB
YAO KATIKA UISLAM - TOLEO LA PILI - MWAKA - 1437 AL HIJRA
(2016).
3- IJTIHAD NA TAQLID HISTORIA YA UISLAM: MAIMAMU NA MADHHAB
YAO KATIKA UISLAM - TOLEO LA TATU - MWAKA 1439 AL HIJRA
(2018).
4-TAFSIR SURAT YUSUF – AHSAN AL QASAS - MWAKA 1441 AL HIJRA
(2020).
5-ULU UL AZMI MINNA RUSULUN JUZUU AL AWWAL – WENYE AZMA
THABIT MIONGONI MWA MITUME JUZUU YA KWANZA – MWAKA 1443
AL HIJRA(2022)
14
UTANGULIZI
﴿لَقَدْ كَ انَ فىِ قَصَصِ هِ مْ عِبْ رَةٌ لأُوْ لىِ
ٱلأَلْبَابِ مَا كَانَ حَدِيثاً يُفْتَرَ ٰى وَلَٰكِن
ّ كُل شَيْءٍ وَهُدًى وَرَحمَْةً لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ ﴾
تَصْدِيقَ ٱل َّذِى بَينَْ يَدَيْهِ وَتَفْصِيلَ ِ
Laqad kana fee qasasihim AAibratun li-olee al-albabi ma kana hadeethan yuftara
walakin tasdeeqa alladhee bayna yadayhi watafseela kulli shay-in wahudan
warahmatan liqawmin yu/minoona (Surat Yusuf 12:111)
Tafsir: Kwa Hakika katika Visa vyao, kuna mafunzo kwa watu wenye kufahamu,
Haikua (hii Quran) Hadith ya kughushi, bali ni Usadikisho wa Vitabu (Zabur,
Tawrat, Injil n.k vilivyopo vya Allah) wenye maelezo ya kina juu ya kila kitu na
Muongozo na Rehma kwa Ummah wa Walioamini.
﴿ٱلحَْمْدُ هللِ َِّ رَبِّ ٱلْعَالَمِينَ ﴾
Alhamd Lillah Rabbi Al Aálamin!
Awali namshukuru Allah Subhanahu wa Ta’ala na kumuombea Rehma na Amani M-
bora na Mtukufu wa viumbe, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam.
Pili namshukuru Allah Subhanahu wa Ta’ala kwa kutujaalia kua ni wenye kuingizwa
kwenye Rehma zake kwa kujaaliwa kupata Muongozo wake na hivyo kua ni wenye
kumuamini yeye na Mtume wake Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam, na kwa
kunineemesha neema hii yenye manufaa na kisha kuniwezesha kua ni mwenye uwezo
wa kujaribu kuandika kwa mara nyengine tena. Namuomba Allah Subhanahu wa Ta’ala
atunufaishe kwa yale mambo yenye manufaa ndani ya kitabu hiki na pia yale
15
yaliyokuwemo katika maisha yetu na pia atuepushe na yale yasiyokua na manufaa
nasi..Aamiin.
Tunapoiangalia Qurán ambayo ni kitabu kitukufu cha Allah Subhanah wa Ta’ala basi
tunaona kua ndani yake imezungumzia mambo mengi sana yenye manufaa katika maisha
ya Ibn Adam, ikiwemo maamrisho, makatazo na pia visa kadhaa ndani yake, na pale
iliposhuka na kuelezea baadhi ya visa vya Manabii na Mitume basi ilikua na ujumbe wa
kumpa nguvu, utulivu na kumliwaza mpokeaji wake ambae ni Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam na vile vile Waislam wote kwa ujumla na hivyo tuweze
kutafakkar na kua na ustahmilivu na subra katika mitihani tutayo kumbana nayo katika
kipindi cha mpito cha uhai wa hapa Ulimwenguni kwa ujumla, ambapo hatukuletwa kwa
ajili ya kucheza, kwani tumeletwa kwa ajili ya kumuabudu Mola wetu na kua katika
mapigano dhidi ya Iblis na pia dhidi ya Matamani ya Nafsi zetu.
Kwani ukweli ni kua katika kipindi cha karne yetu tunayoishi basi Waislam wengi
wamekua ni wenye kuishi kimazoea badala ya kua ni wenye kuishi kulingana na Ilm ya
dini yao kwa kutumia njia na mifano iliyoainishwa ndani ya Quran na Sunnah, na
Waislam hivyo kua katika hali na mazingira yanayosikitisha Kidini, Kielimu, Kiafya,
Kiufahamu, Kimamlaka, Kiuchumi, n.k na hivyo ni kuonekana kua ni dhalili na wenye
kukosa subra, ustahmilivu mkubwa pale inapokosekana msaada wenye manufaa kwao
katika kutatua matatizo yao ambayo mengi hua ni yenye kutokana na mapambo ya
kidunia kiasi ya kua wanafikia kuitumia Dini yao kwa ajili ya manufaa yao ya kidunia na
hivyo kua ni wenye kukaribia kuingia katika ile hali ambayo imeelezewa na aya ifuatayo:
﴿وَمِنَ الن َّاسِ مَن يَعْبُدُ الل َّهَ ٰ عَلَى حَرْ فٍ ۖ فَإِنْ أَصَابَهُ خَيْرٌ اطْمَأَن َّ بِهِ ۖ وَإِنْ
أَصَابَتْهُفِ ْنَةٌ انقَلَبَ ٰ عَلَى وَجْهِهِ ا خَسِ ل َر د ُّ ن ْيَا وَالآْ خِ رَةَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الخُْسْرَ انُ
الْمُبِينُ ﴾
Wamina alnnasi man yaAAbudu Allaha AAala harfin fa-in asabahu khayrun
itmaanna bihi wa-in asabat-hu fitnatun inqalaba AAala wajhihi khasira alddunya
waal-akhirata Dhalika huwa alkhusranu almubeenu.(Surat Al Hajj 22:11)
Tafsir: Na miongoni mwa watu ni wale ambao Wanamuabudu Allah wakiwa
Ukingoni, hivyo kama akifikwa na Mema basi hua ni mwenye kuridhia, lakini
akifikwa na Mitihani basi hua ni mwenye kugeuza uso wake (hua na shaka na hivyo
hua ni mwenye kukosa Imani na Mola wake) hula hasara hapa Duniani na Akhera.
Huko hua ni kula hasara sana kuliko wazi.
16
Ama kuhusiana na ayah hii basi anasema Jarra Allah, Sultan Al Balagha Imam Abu Al
Qasim Al Zamakhshari kua: ‘Neno ‘Harfin’ lililotumika katika ayah hii linamaanisha
hali ya mtu ambae hayupo katikati ya dini, yaani yupo pembeni kabisa kama vile
mtu anaeenda vitani kisha akakaa kwenye mstari wa nyuma kabisa huku akisubiri
watu wakishinda basi akimbilie ngawira na wakishindwa basi awe ni wa mwanzo
kukimbia’
Yaani hawa ni watu ambao Imani zao zimekua dhaifu na ingawa wanamuabudu Allah
Subhnah wa Ta’ala lakini hata hivyo hawana Imani thabit katika nyoyo zao kwani Nuru
ya Dini yao katika nyoyo zao ni dhaifu kiasi ya kua akipata mtihani mdogo tu basi
anaweza kua ni mwenye kuangukia katika hali mbaya ya kuiuza dini yake na hivyo kua
ni miongoni mwa wenye sifa ya unafiq.
Allah Subhanah wa Ta’ala ni mwenye kuwapima waja wake kwa kuwapa mitihani katika
mazingira tofauti kama alivyotuonesha kupitia katika viza vilivyomo ndani ya Qur’an
hivyo unapofuatilia njia na mifano iliyomo ndani ya Qurán basi unaona kua ingawa
Qurán imezungumzia visa vingi katika sura zake mbali mbali ambapo hapo hapo hakuna
kujirudia rudia kwa visa hivyo wala kupingana kwa visa hivyo katika kuvielezea kwake,
lakini kuelezewa kwa visa hivyo kamwe hakukuwa ni kwa ajili ya kutuelezea historia au
kutuburudisha kwa hadith zake tu, bali ni kwa ajili ya kutoa mifano yenye mafunzo na
pia yenye maonyo kwa kutuonesha namna Allah Subhanah wa Taála anavyowapenda,
anavyowahurumia na kuwajali waja wake wanaomtii kumshukuru na namna
anavyowaonya kabla ya kuwaadhibu wale wenye kumuasi na kumkufuru na ndio maana
akawa ni mwenye kutuhimiza kumtii kwa kutuambia:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ ٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ م َّا قَد َّمَتْ لِغَدٍ وَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ إِن َّ ٱهلل ََّ
خَبِيرٌ بمَِا تَعْمَلُونَ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo ittaqoo Allaha waltandhur nafsun ma qaddamat
lighadin waittaqoo Allaha inna Allaha khabeerun bima taAAmaloona (Surat Al
Hashr 59:18)
Tafsir: Enyi Mlioamini! Muogopeni Allah na tekelezeni majukumu yenu juu yake. Na
kila mmoja wenu aangalie ni nini Nafsi yake imetanguliza kwa ajili ya kesho. Na
Muogopeni Allah. Kwani Kwa Hakika Allah ni mwenye habari juu ya kila
mnachokifanya.
17
Hivyo mbali ya kua Allah Subhanah wa Taála ni mwenye kutuonya na kutuhimiza
kutekeleza majukumu yetu juu yake kupitia katika kitabu chake kitukufu lakini pia ni
mwenye kutuongoza ndani yake kama alivyosema:
بِكُل
ّ
﴿وَمَا كَانَ ٱهلل َُّ لِيُضِل َّ قَوْماً بَعْدَ إِذْ هَدَاهُمْ حَتى َّ ٰ يُبَينِّ َ لهَُم م َّا يَت َّقُونَ إِن َّ ٱهلل ََّ ِ
شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴾
Wama kana Allahu liyudhilla qawman baAAda idh hadahum hatta yubayyina
lahum ma yattaqoona inna Allaha bikulli shay-in AAaleemun (Surat At Tawba
9:115)
Tafsir: Na si juu ya Allah kuwapotosha watu baada ya kuwaongoza hadi
akawabainishia ni jambo gani la kujiepusha nalo. Hakika Allah ni mwenye kujua juu
ya kila kitu.
Anasema Imam Ibn Al Mundhir Al Nishapuri kua: ‘Ilikua ni kawaida ya Sahaba Abd
Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu, kuwasomesha darsa Wanafunzi wake katika
kila siku ya Alkhamis na kisha baada ya kumaliza darsa basi hua ni mweye kusema:
‘Yeyote yule miongoni mwenu anaetaka kua Mwanazuoni basi na aombe dua juu
ya hilo. Na asiombe chochote baada ya hilo kwa sababu Mwanazuoni na
MWanafunzi wako sawa kimalipo. Enyi watu mimi sikhofu kua nyie mtaulizwa juu
ya kile ambacho Allah Subhanah wa Taála amekuwekeeni wazi juu yenu, kwani
amesema: ‘Wama kana Allahu liyudhilla qawman baAAda idh hadahum hatta
yubayyina lahum ma yattaqoona inna Allaha bikulli shay-in AAaleemun’ yaani, Na si
juu ya Allah kuwapotosha watu baada ya kuwaongoza hadi akawabainishia ni
jambo gani la kujiepusha nalo. Hakika Allah ni mwenye kujua juu ya kila kitu.’ ’
Hivyo ni wajibu wetu kuachana na kuepukana na kuishi kimazoea na badala yake
tujitahid kushikamana na njia na mifano iliyomo ndani ya Qur’an, na Sunnah za Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam na pia kushikamana na ufafanuzi wa Wanazuoni wa
skuli za Madhhab na mitazamo yao juu ya Vitu viwili hivyo ambavyo ndio vyanzo vya
Hukmu na Sharia vinavyotuongoza kidini katika njia iliyonyooka na hivyo kua ni wenye
kudumu katika njia ya uongofu.
Mpangilio wa Kitabu hiki kimegawika katika sura mbili ambapo katika Sura ya Kwanza
inazungumzia juu umuhimu wa kuisoma, kuifahamu na kuizingatia Qur’an kwa kina ili
kuweza kua ni wenye kunufaika na Mafunzo, Hikma na Busara zilizomo ndani yake na
nimeyaelezea haya kabla ya kuingia katika Sura ya Pili ambamo ndani yake ndio mna
18
Visa vya Manabii na Mtume Watano Waliokua na Azma kubwa zaidi katika Maisha yao
na kujaribu kufafanua historia zao, mitihani yao, subra na ustahmilivu wao uliotokana na
kua na Nuru ya Iman kwa Mola wao katika Vifua, Nyoyo na Nafsi zao na kua na
misimamo imara na hivyo kua ni mifano bora kwetu kutokana na yaliyomo ndani yake.
Na ingawa Mitume hao wako watano ambao ni Nabii Nuh Alayhi Salam, Nabii Ibrahim
Alayhi Salam Nabii Musa Alayhi Salam, Nabii Isa Ibn Mayram Alayhi Salam na
Muhammad Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, lakini hata hivyo katika kitabu cha
Juzuu ya kwanza sikuweza kuwaeleza Mitume hao wote, kwani nimewaelezea Mitume
watatu tu ambao ni Nabii Nuh Alayhi Salam, Nabii Ibrahim Alayhi Salam Nabii Musa
Alayhi Salam.
Na hii ni kwa sababu ya kua kama ningewaelezea wote kwa pamoja katika kitabu kimoja
basi Kitabu kingekua kikubwa sana yaani kingekaribia kurasa 2000, hivyo nimeona bora
nikigawe mara mbili kwa kutoa juzuu ya kwanza ili kurahisisha usomaji, na uzingatiaji
wa ujumbe uliomo ndani yake kwanza, na Alhamd lillah Allah Subhanah wa Ta’ala
ameniwezesha kutoa Juzuu ya pili ambayo ndani yake nimemuelezea Nabii Isa Ibn
Maryam Alayhi Salam na Nabii Muhammad Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
hivyo namshukuru Allah Subhanah wa Ta’ala kwa kuniwezeshe kutekeleza ahadi yangu
hii.
Hivyo kama tukizingatia mafunzo yaliyomo ndani yake basi tutakua ni wenye kunufaika
na mengi sana hususan katika wakati huu wa mitihani ndani ya Uhai wetu, kwani
kitatuongezea Imani kwenye Nafsi na Nyoyo zetu na kutupa Muongozo stahiki katika
kupigana vita dhidi ya uadui wa ndani kutoka katika Nafsi zetu na uadui wa nje
unaotokana na Shaytan na wafuasi wake wanaotuzunguka katika mazingira yetu kwani
anasema Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
﴿ٱهلل َُّ نَز َّلَ أَحْسَنَ ٱلحَْدِيثِ كِتَاابً م ُّتَ شَاهبِ اً م َّثَانىِ َ تَقْشَعِر ُّ مِنْهُ جُ لُودُ ٱل َّذِينَ يخَْشَوْنَ
رَب َّهُمْ ثمُ َّ تَلِينُ جُلُودُهُمْ وَقُلُوبُهُمْ إِلىَٰ ذِكْرِ ٱهلل َِّ ذٰلِكَ هُدَى ٱهلل َِّ يَهْدِى بِهِ مَن
يَشَآءُ وَمَن يُضْلِلِ ٱهلل َُّ فَمَا لَهُ مِنْ هَادٍ ﴾
Allahu nazzala ahsana alhadeethi kitaban mutashabihan mathaniya taqshaAAirru
minhu juloodu alladheena yakhshawna rabbahum thumma taleenu julooduhum
waquloobuhum ila dhikri Allahi dhalika huda Allahi yahdee bihi man yashao
waman yudlili Allahu fama lahu min hadin (Surat Az Zumar 39:23)
19
Tafsir: Allahu ameshusha hadithi bora kabisa, Kitabu (Quran) chenye sehemu ndani
yake zinazofanana kwa wema na usahih. Ngozi za wale wenye kuomuogopa Allah
zinatetemeka (Wanapoisikia Qurán). Na kisha Nyoyo zao na ngozi zao hulainika
kutokana na kumkumbuka Mola wao. Huo ni Uongofu wa Allah. Ambae humuongoza
amtakae na anaepotoshwa na Allah basi hakuna atakaemuongoza.
Namuomba Allah Subhanah wa Ta’ala awe ni mwenye kunifanikishia malengo yangu
ya kufikisha ujumbe katika kuvielezea Visa vya Ulu ul Azmin Minna Rusul Juzuu ya
Kwanza na hii ya Pili na kuinufaisha Nafsi yangu na kuwanufaisha Waislam wengine
wote kwa ujumla kutokana na Mafunzo, Hikma, Busara na Miongozo inayopatikana
ndani yake kulingana na Aya za Quran Tukufu, Sunnah na Hadith za Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na pia kulingana na Mitizamo ya Wanazuoni tofauti
waliotumia mda wao na Ilm yao katika kuelezea namna walivyofaham juu ya visa vya
Mitume hao husika na hivyo kua ni wenye kutunufaisha nasi. Na muomba Allah
Subahanh wa Ta’ala awalipe kwa jitihada zao na awazidishie ziada katika amali zao.
Na vile vile namuomba Allah Subhanah wa Ta’ala anisamehe kwa makosa na kasoro
zitakazojitokeza katika jitihada yangu hii kwani ukamilifu ni wake yeye tu, na ni yeye
pekee ndie mwenye kuijua nia yangu katika utekelezaji wa haya nnayoyafanya.
Amiin ya Rabb!
20
SURA YA KWANZA
MUONGOZO, MANUFAA, TIBA NA REHMA ZILIZOMO NDANI YA QUR’AN.
Bila ya shaka katika aya za Qur’an nilizoanza nazo ndani ya kitabu hiki na nyenginezo
nyingi zilizomo ndani ya Qura’an tumeona kua Allah Subhanah wa Taála ametuwekea
wazi kua ndani ya kitabu chake mna muongozo wa kina wa kila kitu katika maisha yetu,
ikiwemo pia Muongozo dhidi ya matatizo mbali mbali ya kidunia na kiakhera, lakini hata
hivyo kamwe hatutoweza kuikimbia hali ya matatizo tuliyokua nayo wakati bado tukiwa
ni wenye kuutupa ufunguo unaofungua mlango wa utatuzi wa matatizo hayo, ufunguo
ambao si mwengine bali ni Qurán yenyewe ambayo ndani yake hamna Muongozo tu,
lakini pia mna Kinga, Rehma na Tiba pia ya maradhi tofauti kuanzia ya Kimwili,
Kinyoyo, Kinafsi, Kiroho n.k kama inavyoweka wazi aya ifuatayo:
﴿وَنُنَزِّلُ مِنَ ٱلْقُرْآنِ مَا هُوَ شِ فَآءٌ وَرَحمَْةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ وَلاَ يَزِيدُ ٱلظ َّالِمِينَ إَلا َّ
خَ سَاراً ﴾
Wanunazzilu mina alqur-ani ma huwa shifaon warahmatun lilmu/mineena wala
yazeedu aldhdhalimeena illa khasaran (Surat Al Isra 17:82)
Tafsir: Na tumeiteremsha hii Qur’an ndani yake mkiwa na Tiba na Rehma kwa
Walioamini, lakini kwa Madhalimu haiwanufaishi na chochote isipokua Hasara.
Naam aya imetumia neno Shifaun ambalo ni lenye kutokana na neno Shafa. Na kwa
kilugha basi neno Shafa hua ni lenye kumaanisha Kuponya, Kutibu, Kurudisha Afya,
Kuridhisha, Kurudisha katika hali yake ya Asili au ya Kimaumbile, na ndio maana wenye
Lugha yao hua wanasema: ‘Shaf’ahu aAn Al Mas-alati’ kumaanisha kua
Amemuondolea Mashaka na kumridhisha Nafsi yake juu ya Jambo fulani.
Anasema Sultan al Mutakallimin Mujaddid ud Din Imam Abu Abd Allah Muhammad
Ibn Umar Ibn Al Husayn Al Taymi Al Bakri Al Tabaristan Fakhr Ad Din Al Razi Al
Shafii kuhusiana na ayah hii kua: ‘Quran ni Tiba ya Kitabia, Kijamii, Kiroho na
Kiafya pia. Na bila ya shaka baadhi ya Aya zake zimebainika kua ni Tibba ya
Maradhi tofauti ya Kimwili’
21
Ama kwa upande mmoja basi Hujjat Ul Islami Mujaddid Ad Din Imam Abu Hamid Ibn
Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii anatuambia
kua miongoni mwa manufaa yanayohitajika kupatikana katika Quran basi ni kujua darja
za usomaji wake katika hali tofauti kwa kusema kua: ‘Amesema Amir ul Muuminina
Ali Ibn Abi Talib kua: ‘Yeyote yule atakaesoma Qur’an wakati akiwa amesimama
kwenye Sala basi anapata thawabu 100 kwa kila herufi moja ya Qur’an, na
atakaesoma Qur’an wakati akiwa amekaa kitako ndani ya Sala basi hua ni mwenye
kupata thawabu 50 kwa kila herufi, yeyote yule atakaesoma Qur’an nje ya Sala
akiwa katika hali ya kua na udhu basi hua anapata thawabu 25 kwa kila herufi, na
kwa kila atakaesoma Qur’an bila ya udhu kutokana na kua ni mwenye kuihifadhi
Moyoni mwake basi atapata thawabu 10 kwa kila herufi’
Na kwa Upande mwengine basi Hujjat ul Islami Mujadid Ad Din Imam Abu Hamid
Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii basi
anatuwekea wazi namna ya kunufaika na Muongozo, Tiba na Rehma zilizomo ndani ya
Qur’an kwa kutubainishia umuhimu wa kuzifaham siri za ndani na za nje zinazotakiwa
kupatikana katika kisomo cha Qur’an ambazo ni:
1 – Unapoanza kusoma basi inatakiwa uhisi ukubwa na uwezo wa mwenye maneno
hayo ambae ni Allah Subhanah wa Ta’ala. Na athari hio unaweza kuihisi ndani ya
Moyo wako pale unapoanza kuhisi ukubwa wa Arshi na Mamlaka yake Duniani na
Mbinguni na kila kilichomo ndani yake wakiwemo viumbe vyake, Ibn Adam,
Majini, Wanyama, na Miti. Unatakiwa ukumbuke kua Muumbaji wa vitu vyote
hivyo ni Mmoja, na Vitu vyote hivyo vimo ndani ya mamlaka yake na uwezo wake.
Kuhisi Neema zake na Rehma zake basi kunakupelekea kua ni mwenye kutaka
kuzisoma aya zake na kuona ndani yake Sifa zake, Majina yake, Uzuri wake, Ilm
yake na Hikma zake.
Faham kua kama ilivyokua Qur’an inawezekana kuguswa na wale waliotoharika –
na hivyo kua ni iliyofichikana kwa wasiokua tohara – kwa kimaana na kisiri basi
ndio hivyo hivyo inavyofichikana kutokana na Nyoyo zisizokua Nadhifu.
2 – Unatakiwa utafakkar na kuzingatia maana yake wakati unapokua unaisoma
kama ukitaka kua ni miongoni mwa watu wenye kuisoma Qur’an. Unatakiwa
urudie kila ulichokisoma kwa ulimi wako wakati akili yako ilipokuwa haipo kwenye
kisomo cha aya husika. Kwani haitakiwi kuhesabu kisomo ambacho hakina
mazingatio ndani yake kua ni sehemu ya kufanya amali njema. Kwa sababu ubora
wa kisomo cha Qur’an hua ni katika kuzidisha mazingatio yake. Amesema Sayyidna
Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kua: ‘Hakuna Ubora katika Amali njema pale
inapokua hakuna ufahamu juu ya Amali hio, na pia katika kisomo kisichokua na
Mazingatio.’
22
3 – Unatakiwa uwe ni mwenye kuvuna Matunda ya Ilm kutoka katika Matawi yake
na kuyatafutia kutoka katika asili yake zinakopatikana, huku ukiwa ni mwenye
kutafakkar. Usitafute Kinga kutoka katika sehemu ambayo unatafutia hazina, na
usitafute Hazina katika sehemu ambayo unatafutia Miski na harufu yake nzuri,
kwani katika kila Tunda basi hua lina tawi lake na kila hazina ina chanzo chake.
Jambo hili hua linarahisika pale unapojua kua kuna aina za aya za Quran
kulingana na kusudio la ujumbe wake kwa mfano:-
A - Aya ambazo zinazomzungumzia Allah Subhanah wa Ta’ala, Sifa zake na
Vitendo vyake. Hivyo tafuta ndani ya haya Ilm ya kujua Ukubwa na Ufalme wa
Allah Subhanah wa Ta’ala.
B – Aya ambazo zinazungumzia Muongozo wa njia iliyonyooka: Hivyo tafuta ndani
ya haya Ilm ya Rehma zake, Neema zake na Hikma zake.
C – Aya ambazo hua ni zenye kuzungumzia Maangamizo: Hivyo tafuta ndani yake
Ilm ya Uwezo, Ujabari na Utukufu wake Allah Subhanah wa Ta’ala.
D – Aya ambazo hua ni zenye kuzungumzia Maish ya Mitume: hivyo tafuta ndani
yake Ilm ya Huruma na Ukarim wake, Baraka, Neema na Misaada yake kwa waja
wake.
Hivyo kwa kila kusudio basi tafuta manufaa yaliyomo ndani yake kwa kadiri
inavyowezekana.
4 – Inakubidi ujilinde na kila kitu kinachozuia ufahamu wako kwa sababu kitu
hicho hua ndio pazia linalokuzuia kufaham kama alivyosema Allah Subhanah wa
Ta’ala:
﴿إِ َّ جَعَلْنَا عَلَى ٰ قُلُوهبِِمْ أَكِن َّةً أَن يَفْقَهُوهُ وَفىِ آذَاِِمْ وَقْراً وَ إِن تَدْعُهُمْ إِلىَٰ ٱلهُْدَىٰ
فَلَنْ يَهْتَدُو ۤ اْ إِذاً أَبَداً ﴾
Inna jaAAalna AAala quloobihim akinnatan an yafqahoohu wafee adhanihim
waqran wa-in tadAAuhum ila alhuda falan yahtadoo idhan Abadan (Surat Al Kahf
18:57)
Tafsir: Na kwa hakika sisi tumejaalia katika nyoyo zao mapazia ili wasiifahamu
(Quran), na katika masikio yao uziwi. Na hata kama wewe ukiwaita katika uongofu
basi hawatoongoka Abadan.
23
Faham kua mtu mwenye ufahamu unaomtafuta Mola wake hua unapewa mitihani
ya aina mbili: Aidha hua unakua na mtihani wa kua na shaka na kukanusha ambao
hua ni wenye kuwajaribu wale ambao ni wenye Imani dhaifu. Au hua na mtihani
wa pazia linalojaa matamanio ya Moyo ambalo hua ni lile linalomfunika yule Mtu
mwenye kuiendekeza Dunia.
Ama kuhusiana na Mja ambae ni mwenye Iman na hivyo hua ni mwenye kua na
umakini katika Njia ya Mola wake, basi nao hua na Mapazia ya aina mbili. Ambapo
la kwanza ni vishawishi vya wasi wasi vinavompelekea kutofikiria hata juu ya kutia
katika Ibada husika, kwa mfano jee mwanzo wake ulikuaje Ibada hii, au bado niko
katika Ikhlas?, n.k. Aina ya pili ya vishawishi vya wasi wasi ni vile ambayo hua
vinakutoa katika umakini wa kutamka kwa usahih, na hivyo hukupelekea kua na
wasi wasi na kurudia tena kauli husika katika Ibada. Jambo hili hutokea ndani ya
Sala na nje ya Sala pia.
Jee itakuaje siri za Ufalme wa Allah Subhanah wa Ta’ala zipatikane na Moyo ambao
umakini wae upo katika kuhisi ni namna gani Midomo inafunga na kufunguka na
ni vipi Ulimi na Taya zinafanya kazi na hewa inapitaje baina yake?
Aina ya pili ya pazia linalokuwepo kwa Mja mwenye Imani ni pale mtu anapokua
hajui maana ya ndani ya kina cha aya za Qur’an. Kwani hali hii huuzuia ufaham
wake, kwani Allah Subhanah wa Ta’ala amemuamrisha Mja wake kua ni mwenye
kumuamini kulingana na hali ya vigezo tofauti ambavyo hua vipi katika ufahamu
wa juu juu na ufaham wa kina zaidi kama mfupa na nyama nyama iliyomo ndani
ya Mfupa kwa mfano: Allah Subhanah wa Ta’ala amewataka waja wake wawe ni
mwenye kuamini kua ni anaweza kuonekana, lakini hata hivyo kuonekana hua
kuna aina mbili ambazo ni:
Kama mtu atakua anaamini kua kumuona Allah Subhanah wa Ta’ala ni sawa na
kuoa kwa kutumia macho kama tunavyoona Ibn Adam Ulimwenguni basi
anategemea kujua nini juu ya siri ya Allah Subhanah wa Ta’ala pale aliposema:
﴿وَلَم َّا جَآءَ مُوسَى ٰ لِمِيقَاتِنَا وَكَل َّمَهُ رَب ُّهُ قَالَ رَبِّ أَرِنيِ ۤ أَنظُرْ إِلَيْكَ قَالَ لَن تَرَانىِ
وَلَٰكِنِ انْظُرْ إِلىَ الجَْبَلِ فَإِنِ اسْتَقَر َّ مَكَانَهُ فَسَوْفَ تَرَانىِ فَلَ َّما ٰ تجََل َّى رَب ُّهُ لِلْجَبَِل
ٰ موسَى صَعِقاً فَلَم َّآ أَفَاقَ قَالَ سُبْحَانَكَ تُبْتُ إِلَيْكَ وَأََْ أَو َّلُ جَعَلَهُ دَكّاً وَخَ َّر
ٱلْمُؤْمِنِينَ ﴾
24
Walamma jaa moosa limeeqatina wakallamahu rabbuhu qala rabbi arinee andhur
ilayka qala lan taranee walakini ondhur ila aljabali fa-ini istaqarra makanahu
fasawfa taranee falamma tajalla rabbuhu liljabali jaAAalahu dakkan wakharra
moosa saAAiqan falamma afaqa qala subhanaka tubtu ilayka waana awwalu
almu/mineena (Surat Al Araf 7:143)
Tafsir: Na kisha akaja Musa katika eneo na mda maalum tuliompangia na
akazugungumza na Mola wake, (Nabii Musa)akasema : ‘Ewe Mola wangu Nioneshe
nipate Nikuone’ Allah Subhanah wa Ta’ala akasema: ‘Huwezi kuniona, lakini
angalia Mlima, kama utabakia katika sehemu yake. Basi nawe utaweza utaniona’
Kisha alipouonesha Utukufu wake Mola wake kwa Mlima, akaujaalia kua ni wenye
kupukutika na kua vumbi. Na akaanguka nakupoteza faham Musa. Kisha
alipozindukana akasema: ‘Utukufu ni wako, Mimi Natubu kwako na hakika mimi ni
wa awali miongoni mwa Walioamini’
Na jee mtu huyo atafaham vipi kua haiwezekani kumuona kwa macho kama
tunavyoona katika Ulimwengu huu kwani jicho la kutizamia Ulimwengu hua
haliwezi kuona kila kitu, kila sehemu na kila upande, na jee atafaham vipi maana
ya maana ya maneno ya Allah Subhanah wa Ta’ala pale aliposema:
﴿لا َّ تُدْرِكُهُ ٱلأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ ٱلأَبْصَارَ وَهُوَ ٱلل َّطِيفُ ٱلخَْبِيرُ ﴾
La tudrikuhu al-absaru wahuwa yudriku al-absara wahuwa allateefu alkhabeeru
(Surat 6:103)
Tafsir: Hakuna Mtizamo utakaoweza kumuona yeye, lakini Mtizamo wake yeye huona
kila kitu. Kwani kwa hakika yeye ni Mpole na mwenye kujua kila kitu.
Aya ambayo inaenda sambamba na kauli yake isemayo:
﴿وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ َّضِرَةٌ۞ إِلىَٰ رَهبَِّا َظِرَةٌ ﴾
Wujoohun yawma-dhin nadhiratun, Ila rabbiha nadhiratun (Surat Al Qiyamah
75:22-23)
Tafsir: Baadhi ya Nyuso siku hio zitang’ara, kutokana na kumuangalia Mola wao.
25
5 – Hutakiwi kua ni mwenye kufuatilia juu ya kupata Nuru ya Qur’an tu, lakini pia
unatakiwa upate hisia na athari zinazotakiwa kupatikana katika kuisoma Qur’an.
Hivyo usiisome aya bila ya kua si mwenye kujipamba na sifa zake. Kutokana na
kua na hali hio basi utakua ni mwenye kufaham na kuhisi athari ya kila aya
unayoisoma, kiasi ya kua rehma na usamehevu unapotajwa basi unakua unahisi
utulivu na furaha, na inapotajwa adhabu basi unahisi maumivu na khofu, kutokana
na kutajwa kwa Allah Subhanah wa Ta’ala, na Ukubwa wake na Sifa zake basi wewe
hua ni mwenye kuinamisha kichwa chako kutokana na Unyenyekevu unaouhisi
ndani ya mwili wako, kama vile mtu ambae unaetoweka kutokana na kumuona
Mola wako. Na wanapotajwa Makafiri na Utukufu wa Allah Subhanah wa Ta’ala
wa kua mbali sana na sifa ya kua na Mke na Mtoto basi wewe hua ni mwenye
kuinamisha kichwa chako na kupunguza sauti yako kama vile mtu anaejificha
kutokana na kuona haya isiyokua na kifani.
Athari hizi huonekana wazi kwenye viungo vya mwili wako kama vile kutokwa na
kilio kwa huzuni, kutokwa na jasho kwenye paji la uso kwa kuona aibu mbele ya
Mola wako, kutetemeka kwa furaha ya kuuona Utukufu wa Allah Subhanah wa
Ta’ala na kujisikia raha ndani ya viungo vyako, ulimi wako na sauti unapoona
habari njema ndani ya maneno yake Allah Subhanah wa Ta’ala na kua na khofu
unapoona ndani yake habari zenye kuonya. Kama ikiwa ni mwenye kufanikiwa kua
na hali ya hisia kama hivyo basi utakua ni mwenye kufanikiwa kupata Baraka za
Qur’an.
Kwa upande mwengine basi Shifaa na Rehma za Qur’an sio kua zinapatikana kutokana
na kuisoma na kuifanyia kazi tu lakini pia hua zinapatikana kwa kuisikiliza Qur’an
yenyewe pale inapokua inasomwa na ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala akasema
katika Qur’an:
﴿وَإِذَا قُرِ ئَ ٱلْقُرْآنُ فَٱسْتَمِعُواْ لَهُ وَأَنصِتُواْ لَعَل َّكُمْ تُرْحمَُونَ ﴾
Wa-idha quri-a alqur-anu faistamiAAoo lahu waansitoo laAAallakum turhamoona
(Surat At Aaraf 7:204)
Tafsir: Kwa hivyo inaposomwa Quran isikilizeni, na mkae kimya kwa umakini ili
mpate kua ni wenye kurehemewa.
Abd Allah Ibn Masoud Radhi Allahu Anhu, anasema kuhusiana na ayah hii kua:
‘Inaposomwa Quran basi mnatakiwa mkae kimya huku mkiisikiliza kwa umakini
na kuitafakkari.’
26
Mtizamo wa Sahaba Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu ni mtizamo ambao
haujaachana na mtizamo wa Hujjat ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali. Hivyo tuiangalie ayah hii kulingana na mtizamo mwengine
ambao unatuthibitishia athari ya Qur’an katika miili yetu pale unapotulia na kuisikiliza,
na ili kufaham vizuri zaidi basi kwanza inabidi tufahamu kuhusiana na mawimbi ya
umeme yanayosambaza hisia za mawasiliano katika Ubongo wa miili yetu.
Katika kusafirisha hisia mbali mbali ndani ya miili yetu basi Ubongo hua unazalisha
nguvu ya mawimbi ya umeme ambayo nayo yamegawika katika aina nne. Aina ya
kwanza ni ilie inayoitwa Beta, aina hii huzalishwa pale mtu anapokua yuko katika hali
ya pirika pirika za kazi au jambo ambalo linahitaji umakini sana katika utekelezaji wake,
mawimbi haya hua na kasi ya mizunguko 15-40 kwa sekunde kulingana na namna
Ubongo unavyofanya kazi kwa ari katika wakati huo.
Aina ya pili ni ile iitwayo Alpha ambayo hua ni yenye kuzalishwa baada ya mtu husika
kumaliza jambo lililokua likimshughulisha akili yake, na hivyo kua kwenye hali ya
mapumziko ya ubongo na mwili, mawimbi haya ya Alpha hua yanatofautiana na Beta
kutokana na kua ni ya utulivu na hivyo hua ni yenye kasi ya mizunguko 9-14 kwa
sekunde, hali hii hua anayo pia mtu ambae amekaa na kutafakkari kitu kwa utulivu, au
akiwa anatembea taratibu kwa ajili ya kupata hewa nzuri na hivyo hua ni mwenye
kuridhika.
Aina ya tatu ya mawimbi hua ni ile inayoitwa Theta ambayo hua na kasi ya mzunguko
wa kati kwani hua na mizunguko 5-8 kwa sekunde, hali hii hua nayo yule ambae
ameshamaliza kazi, ameshapoa na kutulia na hivyo anakua ni mwenye kufikiria au
kukumbuka mambo mazuri mazuri yaliyopita au atakayoyapata baada ya yale
aliyoyafanya.
Aina ya mwisho ambayo ni aina ya nne ya mawimbi hua inaitwa Delta ambayo hua na
kasi ya mzunguko mdogo zaidi kwani hua na mizunnguko 1-4 kwa sekunde, na hali hii
hua nayo mtu pale anapokua anasinzia hadi anapoingia katika hali ya usingizi na kulala
fofofo!
Hivyo Mtu unaposikia Qur’an, ukanyamaza na kuisikiliza kwa umakini basi mzunguko
wa mawimbi ya Ubongo wako hua ni wenye kutoka katika hali iliyokuwepo na kuingia
katika hali ya Alpha ambayo ni ya kua mwenye kuridhika Kimwili, Kinafsi, Kiufaham
na Kiakili. Na hivyo kukupelekea kua na Muongezeko wa Imani ya Kiroho, ongezeko la
Uwezo wa Nguvu ya Kinga ya mwili, na ongezeko la uzalishaji wa seli mbali mbali za
mwili na hivyo kua ni tiba kwa Maradhi ya Saratani, huzidisha nguvu ya Akili katika
sehemu ya Ufahamu na kuhifadhi, Huimarisha mishipa ya Moyo na sambamba na hayo
27
basi usikilizaji wa Qur’an hukupunguzia Hisia za Khofu, Mshtuko, Wasi wasi, Uzito wa
mkusanyiko wa mawazo na hukupa utulivu wa kiakili kukupunguzia uvamizi wa maradhi
yanayotokana na mshtuko wa Moyo na mzunguko wa damu na utulivu wa kimwili pia
kwa ujumla kwani hata wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji basi hua ni wenye kupona
haraka maumivu yao pale wanapokua wanasikiliza Qur’an mara kwa mara.
Kwa upande mwengine basi tunaona kua Allah Subhanah wa Ta’ala anatuthibitishia
haya tena pale aliposema:
﴿ٱل َّذِينَ آمَنُواْ وَتَطْمَئِن ُّ قُلُوبُهُمْ بِذِكْرِ ٱهلل َِّ أَلاَ بِذِكْرِ ٱهلل َِّ تَطْمَئِن ُّ ٱلْقُلُوبُ ﴾
Alladheena amanoo watatma-innu quloobuhum bidhikri Allahi ala bidhikri Allahi
tatma-innu alquloobu (Surat Ar Rad 13:28)
Tafsir: Wale walioamini na wakazipatia utulivu Nyoyo zao kutokana na kumkumbuka
Allah. Kwani kwa hakika ni katika kumkumbuka Alla ndiko kunakoupa Nyoyo
utulivu.
Ambapo anasema Imam Abu Muhammad Abd Allah Al Tustari kua: ‘Katika kufanya
(dhikr) huku ukiwa na (ʿilm) basi hua unapata utulivu (sukūn), na katika kufanya
Dhikr kwa Ufahamu (ʿaql) basi hua kunakuletea Utulivu mkubwa (ṭutmaʾīna).
Katika kufanya Dhikr huku ukiwa na (ʿilm) basi hua kunakuletea mapumziko ya
utulivu (sukūn), na Katika Kufanya Dhikr kwa ufahamu (ʿaql) Basi hua kuna
Utulivu mkubwa (ṭutmaʾīna) ’
Allah Subhanah wa Ta’ala anatuambia haya kwa sababu ni maumbile ya Nafsi za Ibn
Adam kua kila Nafsi zinapofikiria ya mapambo ya Kidunia, basi hua ni yenye kutaka
kuikimbilia na kujitumbukiza ndani yake na kutaka chengine zaid ya kile ambacho
kishaingia ndani yake. Lakini unapokua unamfikirira Allah Subhanah wa Ta’ala ambae
ndie Muumba basi hua hakuna kitu chengine chochote bora zaidi yake, hivyo kwako
wewe hua hakuna unachohitaji kwani kwake yeye kuna kila unachokihitaji na zaidi ya
utakachokihitaji kutoka kwake. Na hivyo hukupelekea kuyakimbia yasiyofaa na
kutokukukaribisha karibu yake, jambo hili hukupelekea kujawa na Imani na ari zaidi ya
kutekeleza maamrisho yake na kua ni mwenye kumtegemea yeye tu katika kila jambo
lako, na huo hua ni muongozo tosha kwa moyo na Nafsi yako, kama inavyosema aya
ifuatayo juu ya hayo.
28
﴿َٰي ُّهَا ٱلن َّاسُ قَدْ جَآءَتْكُمْ م َّوْعِظَةٌ مِّن ر َّبِّكُمْ وَشِ فَآءٌ لِّمَا فىِ ٱلص ُّدُورِ وَهُدًى
وَرَحمَْةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ ﴾
Ya ayyuha alnnasu qad jaatkum mawAAidhatun min rabbikum washifaon lima fee
alssudoori wahudan warahmatun lilmu/mineena (Surat Yunus 10:57)
Tafsir: Enyi Watu! Kwa hakika yamekujieni Mawaidha kutoka kwa Mola wenu na
Tiba kwa ajili ya Vifua (Nyoyo) vyenu, na Muongozo kwa Walioamini.
Bila ya shaka tunapozungumzia Muongozo kwa Waumini wanaoishi katika hali ya
maisha ya Kiislam basi hatuwezi kukamilisha bila ya kugusia Hikma na Baraka
zinazopatikana ndani ya Muongozo huo kutoka kwa Mola wetu tuliobainishiwa ndani ya
kitabu kitukufu cha Qurán.
HIKMA NA BARAKA NDANI YA QUR’AN
Neno Hikma limetokana na asili ya neno Hakama ambalo kwa lugha ya Kiarabu hua ni
lenye kumaanisha Kuzuia, Kudhibiti, Kuamrisha, kua na Mamlaka, Kuhukumu, kua na
Hikma au Busara, kua na Uadilifu na kua na l’lm. Neno Hikma pia kimaana ndani yake
hua linajumuuisha tabia njema na kila sifa zilizo njema.
Tunapoiangalia Qurán basi tunaona pia kua ina sifa ya kua ni Uhkimat, yaani yenye
Kulindwa na Kudhibitiwa kutokana na Upotovu, na hivyo hua ni yenye kuweka bayana
kila lenye manufaa na kuweka bayana kila lisilokua na manufaa kwa kila Ibn Adam tena
bila ya kua na shaka yeyote ndani yake kutokana na asili yake. Kwani anasema Allah
Subhanah wa Taála kua;
﴿ بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ ۞ حم ۤ ۞ وَٱلْكِتَابِ ٱلْمُبِينِ۞ إِ َّ جَعَلْ نَاهُ قُرْآً عَرَبِيّاً
ل َّعَل َّكُمْ تَعْقِلُونَ۞ وَإِن َّهُ فيِ ۤ أُمِّ ٱلْكِتَابِ لَدَيْنَا لَعَلِي ٌّ حَكِيمٌ ﴾
29
Bismi Allahi alRrahmani alRraheemi; Ha-meem, Waalkitabi almubeeni, Inna
jaAAalnahu qur-anan AAarabiyyan laAAallakum taAAqiloona, Wa-innahu fee
ommi alkitabi ladayna laAAaliyyun hakeemun (Surat Az Zukhruf 43:1-4)
Tafsir: Kwa jina la Allah mwingi wa Rehma na mwingi wa Huruma; Ha Mim. Na
(Naapa) kwa kitabu chenye kubainisha. Kwa hakika tumekijaalia Qurán kua katika
Lugha ya Kiarabu ili mpate kuzingatia. Na kwa Hakika hii (Quran) imo ndani ya
kitabu Mama mbele yetu, ni Kitukufu kilichojaa Hikma.
Anasema Imam Abu Al Qasim Al Zamakhshari kua: ‘Qurán kimeitwa Umm ul Kitab
yaani Kitabu Mama kwa sababu hiki ni Kitabu ambacho ndio kilichotoa vitabu
vyote vya Mitume waliotangulia hapo kabla. Hivyo vitabu vyote vilivyotangulia
vimetokana na Kitabu Mama Qurán - Umm ul Kitab’
Umm ul Kitab si kitabu ambacho kilichojaa Hikma tu lakini pia ni kitabu ambacho
kimejaa Baraka ndani yake na juu ya hili basi linabainishwa na Qurán yenyewe pale
iliposema:
﴿وَهَٰذَا كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ مُبَارَكٌ م ُّصَدِّقُ ٱل َّذِى بَينَْ يَدَيْهِ وَلِتُنذِرَ أُم َّ ٱلْقُرَىٰ وَمَنْ
حَوْلهََا وَٱل َّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِٱلآخِ رَةِ يُؤْمِنُونَ بِهِ وَهُمْ عَلَى ٰ صَلاَهتِِمْ يحَُ افِظُونَ ﴾
Wahadha kitabun anzalnahu mubarakun musaddiqu alladhee bayna yadayhi
walitundhira omma alqura waman hawlaha waalladheena yu/minoona bialakhirati
yu/minoona bihi wahum AAala salatihim yuhafidhoona (Surat Al AnAam
6:92)
Tafsir: Na hiki ni Kitabu (Qurán) ambacho kimeshushwa kikiwa kimejaa Baraka,
kuthibitisha vilivyotangulia kabla yake, ili upate kuuonya mji Mama (wa Makkah) na
iliyo pembeni yake, Wale ambao wanaamini juu ya Akhera wanaiamini (Qurán) na
wale ambao juu ya Sala zao wanahifadhi.
Neno Baraka kwa Lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kuongezeka, Kukua na pia
humaanisha Furaha. Neno Barakah linatokana na neno linalomaanisha sehemu ya mbele
ya Ngamia ambae amekaa chini na kuididimiza miguu ndani ya mchanga bila ya kutaka
kuondoka sehemu hio, na pia humaanisha msimamo thabiti wa mtu au kitu bila ya kurudi
nyuma kama vile anavyokua mtu shujaa anapobakia peke yake katika uwanja wa vita
30
dhidi ya maadui wote hivyo huamua kupigana hadi mwisho bila ya kukimbia mapigano,
Kua na msimamo, Kuishi, Kupewa heshima.
Hivyo Baraka hua ni muendelezo au muongezeko wa milele wa jema kutoka kwa Allah
Subhanah wa Taála wenye faida ndani yake ambalo hua halionekani kupungua kwake
bali hua linaonekana katika kuongezeka kwake bila ya kujua chanzo cha muendelezo au
muengezeko huo. Kwa mfano pale mtu anapotoa Sadaka na hivyo Baraka huingia katika
mali yake na kuonekana kwa muongezeko wa wingi wa Mali hio.
Anasema Allamah Abu Qasim Ibn Husein Ibn Mufadal Ibn Muhammad Raghib Al
Isfahani kua: ‘Baraka hua ni tofauti na Neema ambayo hua inamaanisha kitu au
jambo fulani maalum liwe kidogo au kikubwa kingi, na hua ni neema pale mtu
aliepewa anapokua na akili na ufahamu.’ Allah Subhanah wa Ta’ala amesema
katika Qurán:
﴿وَآاتَكُم مِّن ِ كُل مَا سَأَلْتُمُوهُ وَإِن تَعُد ُّواْ نِعْمَةَ ٱهلل َِّ لاَ تحُْصُوهَا إِن َّ ٱلإنْسَانَ
لَظَلُومٌ كَ ف َّارٌ ﴾
ّ
Waatakum min kulli ma saaltumoohu wa-in taAAuddoo niAAmata Allahi la
tuhsooha inna al-insana ladhaloomun kaffarun (Surat Ibrahim 14:34)
Tafsir: Na amekupeni nyinyi kila mlichotaka, na kama mkitaka kuzihesabu Neema za
Allah basi kamwe hamtoweza kuzihesabu. Kwa Hakika Mtu ni mwenye kujidhulumu
na mwenye kukufuru.
Hivyo tunapozungumzia kuhusiana na Allah, basi hua inazungumziwa kwa ujumla, na
kwa umoja kumaanisha: ‘Misaada na Fadhila zake Allah Subhanah wa Ta’ala'
anayoitoa kwa Waja wake. Na hua inajumuisha dalili zake, malipo yake, manufaisho
yake kwa Viumbe wake, Neema zake, Rehma zake, n.k.
Neno Barakah pia hua ni lenye kumaanisha al Ziyadah yaani Ziada, al Sa’adah yaani
Furaha, Al Du’a yaani Dua. Al Manfaáh yaani Manufaa, Al Baqah yaani Kinachobaki
Milele, Al Taqdis yaani Kitu kitukufu. Kwa hivyo Allah Subhanahu wa Taála anapotia
Barakah ndani ya kitu basi hata kama mwanzoni kitu hicho kilikua si chochote, lakini
baada ya kutiwa Barakah basi kitu hicho huanza kubadilika wingi, thamani yake,
31
manufaa yake na hata uzuri wake hupelekea kuzidisha idadi ya wingi wake. Barakah
kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala hua inakuja kutoka katika upande usiotegemewa
wala kufikirika na haihitaji wingi wa kitu.
Ama tunapozungumzia Barakah ndani ya Qurán kama ilivyoelezewa katika aya
tuliyoanza nayo ya Surat Al An Aam 6:92 na pia katika aya ifuatayo:-
﴿وَهَٰذَا كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ مُبَارَكٌ فَٱت َّبِعُوهُ وَٱت َّقُواْ لَعَل َّكُمْ تُرْحمَُ ونَ ﴾
Wahadha kitabun anzalnahu mubarakun faittabiAAoohu waittaqoo laAAallakum
turhamoona (Surat Al AnAam 6:155)
Tafsir: Na hiki ni Kitabu (Qurán) ambacho kimeshushwa kikiwa kimejaa Baraka,
hivyo kifuateni na kuweni na Taqwa, ili muwe ni wenye kupata rehma.
Basi tunaona kua anasema Mujaddid ud Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Maana
ya Kitabun Mubarakan hua linamaanisha Kitabu chenye Rehma na Neema za Milele
kwa sababu hua ni chenye kuusia mema, malipo mengi zaidi na msamaha mkubwa
sana, na hapo hapo hua ni chenye kuonya kwa wanaomuasi Allah Subhanah wa
Ta’ala kwa kufanya Dhambi na Maovu’.
Ama kwa upande wa Imam Abu Al Thana’ Shihab ad-Dīn Sayyid Maḥmūd Ibn ‘Abd
Allāh Al Ḥusaynī Al Alusi Al Baghdadi basi yeye anasema kua: ‘Maana ya Kitabun
Mubarakan hua kunamaanisha Kitabu kilichojaaliwa kua na baraka nyingi ndani
yake, kwani kinajumuisha manufaa ya hapa Duniani na manufaa ya kesho Akhera
na kuweka wazi Ilm ya mambo ya sasa na yaliyotangulia’ (Ruh al-Ma'ani fi Tafsir al-
Qurán Al 'Adhim wa Sab'a Al Mathani)
Qurán imetumia aya zaidi ya 10 zenye kuzungumzia juu ya Baraka za Allah Subhanah
wa Taála katika vitu na mambo mbali mbali muhimu kwa Waislam kwa mfano: Mji wa
Makkah kama sehemu yenye nyumba ya awali ya kufanyia Ibada katika Surat Al Imran
3:96, Mji wa Jerusalem ulipotajwa Masjid Al Aqsa katika Surat Al Isra 17:1, Jangwa la
Sinai ambalo ni lenye Mlima Tur sehemu ambayo Allah Subhanhah wa Ta’ala
aliyozungumza na Nabii Musa, Ardhi ya Mji wa Sham sehemu ambayo waliozaliwa na
pia kuishi Mitume wengi zaidi katika Surat Al Anbiyah 21:71, Usiku wa Barakah
ulioshushwa Qurán katika Surat Ad Dukhan 44:3 na Surat Al Qadr.
32
Mti wa Mzaitun pia umetajwa kua na sifa ya kua Mubaraka katika Surat An Nur 24:35
ambapo matunda yake yanatoa mafuta ambayo hua ni yenye kutoa Nuru kali ya aina ya
Infra Red isiyoonekana kwa macho ya kawaida ya Ibn Adam lakini huweza kuonekana
kwa kutumia darubini maalum si hapa ulimwenguni tu lakini pia Nuru yake huweza
kuonekana hata kutoka katika kituo cha uchunguzi wa kisayansi cha angani. Mitume nao
pia ni miongoni mwa waliopewa sifa ya kua Mubaraka kama Nabii Nuh alipotajwa katika
Surat Hud 11:48, Nabii Ibrahim na Nabii Is-haq kama walivyotajwa katika Surat Saffat
37:113, Nabii Isa Ibn Maryam katika Surat Maryam 19:31. n.k
Neno Barakah ndio lililotoa neno Mubarik ambalo hua ni Isim fa'il yaani ni sifa ya
mweye kutoa Barakah ambae ni Allah Subhanah Allahu wa Taála pekee na ndio maana
Allah Subhanah wa Taála akawa na sifa ya kua na Tabarak ambayo ipo katika hali ya Al
Taqdis yaani ya Utukufu wa Kutoa Barakah pale aliposema katika Qurán:
ّ كُل شَيْءٍ
﴿ بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ ۞تَبَارَكَ ٱل َّذِى بِيَدِهِ ٱلْمُلْكُ وَهُوَ ٰ عَلَى ِ
قَدِيرٌ ﴾
Biismi Allahi AlRrahmani AlRrahim; Tabaraka alladhee biyadihi almulku wahuwa
AAala kulli shay-in qadeerun (Surat Al Mulk 67:1-2)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma na Mwingi wa Huruma; Ametukuka yule
ambae ndani ya mikono yake kuna Mamlaka, na ni yeye ambae ni mwenye uwezo wa
juu ya kila kitu.
Neno Tabaraka limetajwa ndani ya Qurán mara 9, ambapo aya zilizotaja na kutumia sifa
hii zimemsifia yule ambae tu ni pekee anaestahiki kua na sifa hio ya Al Mutabarik pekee,
ambae anatuwekea wazi juu ya hilo pale aliposema katika aya nyengine iliyotumia neno
Tabarakah Allahu ambayo inasema:
﴿إِن َّ رَب َّكُمُ ٱهلل َُّ ٱل َّذِى خَلَقَ ٱلسَمَاوَاتِ وَٱلأَرْضَ فىِ سِ ت َّةِ أَ َّمٍ ثمُ َّ ٱسْتَوَىٰ عَلَ ى
ٱلْعَرْشِ يُغْشِ ى ٱلْل َّيْلَ ٱلن َّهَارَ يَطْلُبُهُ حَثِيثاً وَٱلش َّمْسَ وَٱلْقَمَرَ وَٱلن ُّجُومَ مُسَخ َّرَا ٍت
أبَِمْرِهِ أَلاَ لَهُ ٱلخَْلْقُ وَٱلأَمْرُ تَبَارَكَ ٱهلل َُّ رَب ُّ ٱلْعَالَمِينَ ﴾
33
Inna rabbakumu Allahu alladhee khalaqa alssamawati waal-ardha fee sittati
ayyamin thumma istawa AAala alAAarshi yughshee allayla alnnahara yatlubuhu
hatheethan waalshshamsa waalqamara waalnnujooma musakhkharatin bi-amrihi
ala lahu alkhalqu waal-amru tabaraka Allahu rabbu alAAalameena (Surat Al Araf
7:54)
Tafsir: Hakika Mola wako ni Allah ambae yeye ndie alieumba Mbingu na Ardhi kwa
siku sita kisha akasimama juu ya Arshi, ni yeye ambae anauleta usiku kwa kuufunika
mchana kwa utaratibu usiosita, na Jua, na Mwezi, na Nyota zikiwa chini ya amri yake,
kwa hakika ni vyake viumbe na amri. Utukufu ni wake Allah Mola wa Ulimwengu.
Katika aya tuliyoianisha hapo juu ya Surat Al Araf 7:54 tunaona kua Allah Subhanah wa
Tabarak anatuwekea wazi kua Utukufu ni wake yeye tu kwani yeye ndie alietuumba sisi
viumbe na kila kitu kinachotuzunguka ulimwenguni na kuainisha Utukufu wake kwa kua
ndie mwenye Mamlaka ya kila kitu Mbiguni na Ardhini na kua ni yeye tu ndie aijuae
Siku ya Malipo na kutuhakikishia kua kwake yeye ndio marejeo yetu kama anavyosema
katika aya inayofuatia:
﴿وَتَبَارَكَ ٱل َّذِى لَهُ مُلْكُ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَعِندَهُ عِلْمُ ٱلس َّاعَةِ
وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴾
Watabaraka alladhee lahu mulku alssamawati waal-Ardhi wama baynahuma
waAAindahu AAilmu alssaAAati wa-ilayhi turjaAAoona (Surat Az Zukhruf 43:85)
Tafsir: Na Utukufu ni wa yule ambae mwenye mamlaka ya Mbiguni na Ardhini na
kila kilichomo baina yake, na yeye ndie mwenye kujua saa ya kiama na kwake yeye
ndio marudio yenu.
Hivyo ayah hii ya Surat Az Zukhruf 43:85 iko wazi kua ni jambo lisilokua na shaka kua
mwisho wetu Ibn Adam ni kufika tulikotoka yaani kwa Mola wetu lakini wakati bado
tupo safarini hapa ulimwenguni ndani ya Mamlaka yake kuelekea kwa Mola wetu basi
tunaweza kunufaika baada ya kufuata Muongozo wake na hivyo kupata Baraka na
Fadhila nyingi sana na za aina tofauti kutoka kwake Allah Subhanah wa Taála kama
inavyosema aya ifuatayo:
34
﴿َ أَي ُّهَا ٱل َّذِينَ ۤ آمَنُو اْ إِ ن تَت َّقُواْ ٱهلل ََّ يجَْعَل ل َّكُمْ فُرْقَاً وَيُكَفِّرْ عَنكُمْ ا سَيِّئَ تِكُمْ
وَيَغْفِرْ لَكُمْ وَٱهلل َُّ ذُو ٱلْفَضْلِ ٱلْعَظِيمِ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo in tattaqoo Allaha yajAAal lakum furqanan
wayukaffir AAankum sayyi-atikum wayaghfir lakum waAllahu dhoo alfadhli
alAAaDheemi (Surat Al Anfal 8:29)
Tafsir: Enye Mlioamini! Kama mtamcha Allah basi atakujaalie Furqan na
kukufutieni Madhambi yenu na atakusameheni, na kwa hakika Allah ndie mmiliki
wa fadhila Kubwa.
Tunapoitafakkar ayah hii basi tunaona kua ayah imetumia neno Furqan ambalo maana
yake hua ni Muongozo unaotofautisha baina ya jema na ovu, na bila ya shaka neno hili
hua linafasirika vizuri zaidi pale tunapoiangalia maana ya aya ifuatayo ya Surat Al
Furqan:
﴿تَبَارَكَ ٱل َّذِى نَز َّلَ ٱلْفُرْقَانَ عَلَى ٰ عَبْدِهِ لِيَكُونَ لِلْعَالَمِينَ نَذِيراً ﴾
Tabaraka alladhee nazzala alfurqana AAala AAabdihi liyakoona lilAAalameena
nadheeran (Surat Al Furqan 25:1)
Tafsir: Ametukuka yule ambae ameishusha Furqan (Qurán) kwa mja wake ili awe ni
muonyaji kwa viumbe.
Naam, neno Furqan linatokana na neno Faraqa ambalo kwa kiarabu hua linamaanisha
Kubagua, Kutofautisha, Kuamua au Kugawa, hivyo Furqan hua ni Uthibitisho, Hoja au
kitu kinachotofautisha baina ya Jema na Ovu, Nuru na Kiza, n.k.
Hivyo Qurán imepewa jina la sifa ya Furqan kwa sababu Quran ni yenye muongozo
wenye kubainisha na kutofautisha baina jema na ovu kwa kutumia njia tofauti za
kubainisha mambo kwa moja kwa moja, kwa mafumbo na njia ya mithali za aina tofauti
zenye mafunzo ndani yake.
35
MAFUMBO NA MITHALI ZILIZOMO NDANI YA QUR’AN.
Neno Mathala kwa kiarabu hua ni lenye kumaanisha Mithili ya kitu, Mfano, Mfanano,
Mfananisho, Sawasawa na kitu fulani, Muwakilisho, Msemo, Mithali n.k na baadhi ya
wakati neno hili hua linatumika kumaanisha Hoja!
Tunapoiangalia Qurán basi tunaona kua imetumia neno Mathala katika hali mbali mbali
mara 114 katika kutoa mafunzo yake ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala ameamua
kutumia pia njia za mithali au mifano ili sisi walengwa wenye kupewa ujumbe huo tupate
kutafakkar, kuzingatia na kufahamu kwa kina zaid mafunzo yanayotakiwa kupatikana
kutoka ndani ya kile kinachoelezewa juu yake kama anavyotueleza Allah Subhanah wa
Taála pale aliposema:
﴿وَلَقَدْ صَر َّفْنَا فىِ هَٰذَا ٱلْقُرْآنِ لِلن َّاسِ مِن ِ كُل مَثَلٍ وَكَانَ ٱلإِنْسَانُ أَكْثَرَ شَيْ ءٍ
ّ
جَدَلاً۞
وَمَا مَنَعَ ٱلن َّاسَ أَن يُؤْمِنُو ۤ اْ إِذْ جَآءَهُمُ ٱلهُْدَىٰ وَيَسْتَغْفِرُواْ رَب َّهُمْ إِلا َّ أَن
أتَْتِيَهُمْ سُن َّةُ ٱلأَو َّلِينَ أَوْ َْتِيَهُمُ ٱلْعَذَابُ قُبُلاً ﴾
Walaqad sarrafna fee hadha alqur-ani lilnnasi min kulli mathalin wakana al-insanu
akthara shay-in jadalan; Wama manaAAa alnnasa an yu/minoo idh jaahumu
alhuda wayastaghfiroo rabbahum illa an ta/tiyahum sunnatu al-awwaleena aw
ya/tiyahumu alAAadhabu qubulan (Surat Al Kahf 18:54-55)
Tafsir: Na kwa hakika tumeelezea ndani ya hii Qur’an kila aina ya mithali kwa ajili
ya Watu. Lakini mtu hua ni mwenye kupenda kuliko (kiumbe) yeyote kujadili. Na
hakuna kinachowazuia watu kutokana na kutoamini wakati uongofu umewafikia na
kuomba msamaha kwa Mola wao. Isipokua ni kua na hali ya kufuata njia za watu
waliotangulia au wapewe adhabu itakayokabiliana nao uso kwa uso.
Bila ya shaka Ibn Adam ni kiumbe mwenye kupenda kujadili juu ya kila kitu kuliko
kiumbe mwengine yeyote yule wa Allah Subhanah wa Ta’ala, na hivyo hua si wenye
urahisi wa kujifunza kutokana na wanayoambiwa na mifano wanayoelezewa, na hivyo
hua ni wenye kuishi kwa kufuata mazoea ya wazee wao na waliowatangulia kabla yao,
kiasi ya kua kwa wengi wao inakua vigumu kwao kufumbuka macho kutokana na mazoea
hayo mpaka uwafikie ujumbe wenye kuonya na baadhi ya wakati hadi watu iwashukie
36
adhabu ya Mola wao juu yao. Allah Subhanah wa Ta’ala anaendelea kutumithilishia
mifano kwa kutuambia kua:
﴿وَلَقَدْ ضَرَبْنَا لِلن َّاسِ فىِ هَٰذَا ٱلْقُرْآنِ مِن ِ كُل مَ ثَلٍ ل َّعَل َّهُمْ يَتَذَك َّ رُونَ۞ قُرْآً عَرَبِيّاً
غَيْرَ ذِى عِوَجٍ ل َّعَل َّهُمْ يَت َّقُونَ ﴾
ّ
Walaqad dharabna lilnnasi fee hadha alqur-ani min kulli mathalin laAAallahum
yatadhakkaroona; Qur-anan AAarabiyyan ghayra dhii AAiwajin laAAallahum
yattaqoona (Surat Az Zumar 39:27-28)
Tafsir: Na kwa hakika tumepiga kwa ajili ya watu ndani ya hii Qurán mithali za kila
aina ili (Watu) wawe ni wenye Kukumbuka. Qurán ya Kiarabu ambayo haina ubaya
wowote ndani yake ili wapate kua ni wacha Mungu.
Ingawa aya ya Surat Al Kahf 18:54 imetumia neno Sarafna ambalo hua ni lenye
kumaanisha Kuweka, kuelezea lakini ayah inayofuatia baada ya hio ambayo ni ya Surat
Zumar 39:27 na aya nyenginezo nyingi ambazo zimetumika katika njia ya kufunza kwa
kutoa Mithali hua zimetumia neno Dharaba ambalo kwa lugha ya Kiswahili hua
linamaanisha Dharuba. Hivyo Allah Subhana wa Taála ametumia neno Dharaba kwa
sababu kwa lugha ya Kiarabu neno Dharaba hua linamaanisha Kupiga kitu kwa nguvu
hadi kikatoa sauti, Kuponesha, Kutaja, Kufananisha, Kutafuta njia, Kufunga safari,
Kupigania kitu kwa ajili ya kupata faida au manufaa.
Hivyo aya zimetumia neno Dharaba kwa sababu zinatutaka tupiganie manufaa yaliyomo
ndani ya mithali hizo kama tukiwa hatujalala kiakili, na kama tumelala kiakili basi aya
zinatutaka tuzindukane kama vile watu waliopigwa dharuba yaani kibao usoni na hivyo
kua ni wenye umakini wa kuzingatia mithali tunazopigiwa na Mola wetu alietuumba
ambae ndie anaetujua maumbile yetu ndani nje.
Ndio maana ikawa mbali ya kua Qurán ni kitabu kilichaojaa Baraka lakini pia ni kitabu
ambacho tumeshushiwa Waislam kupitia kwa Rasul Allahi Salallahu A’layhi wa Salam
ili kitupe muongozo kwa ajili ya kumkumbuka Mola wetu na hivyo kutuwezesha kufuzu
katika maisha yetu ya hapa Duniani na ya kesho Akhera, hivyo hali hii ya kuletewa
muongozo kutoka kwa Muumba kwa ajili yetu ili tuufuate na kua na Ucha Mungu ni
fadhila kubwa sana kwa kila mmoja miongoni mwetu ambae atauamini na kuufuata
muongozo huo, kwani Allah Subhanah wa Taála alieuleta muongozo huo na kumpa kila
amtakae anatuambia katika Qurán kwa kusema:
37
﴿ذٰ لِكَ فَضْلُ ٱهلل َِّ يُؤْتِيهِ مَن يَشَآءُ وَٱهلل َُّ ذُو ٱلْفَضْ لِ ٱلْعَظِيمِ ﴾
Dhalika fadhlu Allahi yu/teehi man yashao waAllahu dhoo alfadhli alAAadheemi
(Surat Al Jumuah 61:4)
Tafsir: Hio ni Fadhila ya Allah ambayo humpa amtakae, ama kwa hakika Allah ni
mwenye fadhila kubwa sana.
Hivyo tusipotafakkar na kutoizingatia Qurán basi hatutonufaika na fadhila hizo zilizo
bora na tutakua kama watu waliotangulia kabla yetu waliotajwa katika aya inayofuata
baada ya hio ambayo nayo inasema kwa kumithilisha kua:
ُ
﴿مَثَلُ ٱل َّذِينَ حمُِّلُواْ ٱلت َّوْرَاةَ ثمُ َّ لمَْ يحَْمِلُوهَا كَمَثَلِ ٱلحِْمَارِ يحَْمِلُ أَسْفَاراً بِئْسَ مَثَل
ٱلْقَوْمِ ٱل َّذِينَ كَذ َّبُواْ آبَِتِ ٱهلل َِّ وَٱهلل َُّ لاَ يَهْدِى ٱلْقَوْمَ ٱلظ َّالِمِينَ ﴾
Mathalu alladheena hummiloo alttawrata thumma lam yahmilooha kamathali
alhimari yahmilu asfaran bi/sa mathalu alqawmi alladheena kadhdhaboo bi-ayati
Allahi waAllahu la yahdee alqawma aldhdhalimeena (Surat Al Jumuah 62:5)
Tafsir: Mithili ya wale ambao wale waliopewa (Majukumu ya) Tawrat, lakini hapo
hapo wakashindwa kuyabeba (Majukumu hayo kwa kutekeleza amri zilizomo ndani
yake) hua ni kama mithili ya Punda aliebeba shehena za vitabu, Ni m-baya sana mfano
wa wale ambao wamekadhibisha aya za Allah na kwa hakika Allah hawaongozi watu
madhalimu.
Naam, hapa tunaona kua aya imetumia maneno Kamathali alhimari yahmilu asfaran –
Kama mithili ya Punda aliebeba Asfara, ambapo neno Asfara ni neno linalotokana na
neno Sifr la Kiarabu ambalo limetokana na neno Safara ambalo mbali ya kua hua
linamaanisha Safari lakini pa hua linamaanisha Kufagia, Kutawanyika, Kutembea,
Kufunua, Kupambazuka, Kuweka wazi kwa Maandishi yaani kwenye Kitabu na hivyo
neno Asfara lililotumika hapa hua linamaanisha Vitabu vikubwa vyenye kufunua macho
na ufahamu wa mtu kutokana na yaliyomo ndani yake kama ikiwa mtu huyo atavisoma,
atazingatia na kutafakkari yaliyomo ndani yake.
Na Alhamd Lillah sisi Waislam tumejaaliwa kua ni miongoni mwa waliochaguliwa
kupata fadhila bora kutoka kwa Allah Subhanah wa Taála hivyo tusipotafakkar na
kuzingatia Qurán basi hatutokua sawa na Punda tu aliebeba mzigo wa vitabu vyenye
38
thamani kubwa lakini asiejua thamani iliyomo ndani ya uzuito wa mzigo wake, bali
tutakua pia ni sawa na wale watu ambao wanaelezewa katika aya ya mithali ifuatayo:
﴿أُوْ لَٰئِكَ ٱل َّذِينَ ٱشْتَرُواْ ٱلض َّلاَلَةَ بِٱلهُْدَىٰ فَمَا رَبحَِتْ تجَِّارَتُهُمْ وَمَا كَانُواْ
مُهْتَدِينَ۞مَثَلُهُمْ كَمَثَلِ ٱل َّذِى ٱسْتَوْقَدَ َراً فَلَم َّآ أَضَاءَتْ مَا حَوْلَهُ ذَهَبَ ٱهلل َُّ
بِنُورِهِمْ وَتَرَكَهُمْ فىِ ظُلُمَاتٍ لا َّ يُبْصِرُونَ ﴾
Ola-ika alladheena ishtarawoo aldhdhalalata bialhuda fama rabihat tijaratuhum
wama kanoo muhtadeena, Mathaluhum kamathali alladhee istawqada naran
falamma adhaat ma hawlahu dhahaba Allahu binoorihim watarakahum
fee dhulumatin la yubsiroona (Surat Al Baqara 2:16-17)
Tafsir: Hawa ni wale watu ambao, wameununua upotovu kwa bei ya uongovu, hivyo
biashara yao imekua haina faida, na hawakuongozwa. Mithili yao watu hao ni mithili
ya wale ambao wamewasha moto, kisha ukawamurikia katika maeneo yao, na kisha
Allah akauchuchukua mwangaza wao nao wakawa ni waliobakia katika kiza.
Yaani mithili yetu itakua sawa na watu ambao wamewekewa wazi uongofu lakini badala
ya kuutafakkar na kuufanyia kazi basi wao wakaachana nao hivyo kuendelea kupotoka
kwa kutokua na Shukrani, Yaqini na Ikhlas katika mambo yao, na hivyo kua ingawa
wamepata Nuru ya muangaza baada ya kua gizani, lakini kwa kutoujali muangaza huo
basi muangaza huo ukazimika na kutoweka kwani kila mtu unapokua na Shukran, Yaqini
na Ikhlasi kwa Mola wako basi ndivyo Nuru ya muangaza inavyozidi kuongezeka katika
Moyo wako, na unapokua na shaka na wasi wasi basi ndivyo inavyozidi kufifia nuru ya
muangaza huo na hivyo hutoweza kuongoka na hutoweza kua huru kutokana na
Matamanio ya Nafsi yako na upotovu wa Iblis.
Qurán inayaweka wazi haya pale Allah Subhnah wa Taála alipotoa mithali husika katika
aya ifuatayo:
﴿ضَرَبَ ٱهلل َُّ مَثَلاً عَبْداً مم َّْلُوكاً لا َّ يَقْدِرُ عَلَى ٰ شَيْءٍ وَمَن ر َّزَقْنَاهُ مِن َّا رِزْقاً حَسَناً
فَهُوَ يُنْفِقُ مِنْهُ سِ رّاً وَجَهْراً هَلْ يَسْتَوُونَ ٱلحَْمْ دُ هللِ َِّ بَلْ أَكْثَرُهُ ْم
لاَ
يَعْلَمُونَ۞وَضَرَبَ ٱهلل َُّ مَثَلاً ر َّجُلَينِْ أَحَدُهمَُآ أَبْكَمُ لاَ يَقْدِرُ عَلَى ٰ شَيْءٍ وَهُوَ َكل ٌّ
39
عَلَى ٰ مَوْلاهُ أَيْنَمَا يُوَجّ ِ هه ُّ لاَ َْتِ بخَِيرٍْ هَلْ يَسْتَوِى هُوَ وَمَن َْمُرُ بِٱلْعَ دْ لِ وَهُوَ
عَلَى ٰ صِرَاطٍ م ُّسْتَقِيمٍ ﴾
Dharaba Allahu mathalan AAabdan mamlookan la yaqdiru AAala shay-in waman
razaqnahu minna rizqan hasanan fahuwa yunfiqu minhu sirran wajahran hal
yastawoona alhamdu lillahi bal aktharuhum la yaAAlamoona, Wadharaba Allahu
mathalan rajulayni ahaduhuma abkamu la yaqdiru AAala shay-in wahuwa kallun
AAala mawlahu aynama yuwajjihhu la ya/ti bikhayrin hal yastawee huwa waman
ya/muru bialAAadli wahuwa AAala siratin mustaqeemin (Surat An Nahl 16:75-76)
Tafsir: Anakupigieni Allah mfano wa Mja ambae anamilikiwa na (Mja) mwenzake, na
hivyo akawa hana uwezo wowote, na Mtu mwengine ambae tumemjaalia riski nyingi
kutoka kwetu na hivyo akawa anatumia kwa siri na kwa uwazi, jee watakua sawa watu
hawa? Shukrani zote anastahiki Allah, lakini wengi wao hawajui. Na Allah anatoa
mfano wa watu wawili, ambapo mmoja wao ni bubu ambae hana uwezo wowote, na
hivyo kua ni mzigo kwa bwana wake, kwa kila upande amuelekezao hua hana faida
yeyote juu yake. Jee huyu hua ni sawa na yule anaeamrisha mema wakati mwenyewe
akiwa katika njia iliyonyooka.
Hayo ni maneno ya Muumba wa kila kitu na ndie pia alietuumba sisi na ndie anaetumiliki
na hivyo anatupa mithali zilizowazi kua bila ya shaka kitu ambacho kinamilikiwa na
hakina mamlaka yeyote basi hakiwezi pia kua na maamuzi yeyote isipokua kutekeleza
maamrisho ya Mmiliki na hivyo kuthibitisha kua Mwenye Mamlaka ya kila kitu
ulimwenguni ni Allah Subhanah wa Ta’ala na yeye pekee ndie anaestahiki Kuabudiwa
na Kushukuriwa kwani yeye ndie Muumba. Na juu ya hili basi kila mtu mwenye akili na
kutafakari hua ni mwenye kujua kua kuna tofauti baina ya Muumba na Kiumbe, pia baina
ya Mwenye uwezo na Asiekua na uwezo, Mwenye Nguvu na asiekua na nguvu, hivyo ni
ujinga ulio wazi pale inapokua Mtu hawezi kuona tofauti baina ya vitu viwili hivyo.
Kwa kua Allah Subhanah wa Ta’ala yeye ndie Muumba na Mmiliki wa kila kitu
Ulimwenguni iwe kikubwa au kidogo basi anawawekea wazi waja wake, kua yeye haoni
shida kututolea mifano hata kama ya mdudu Mbu, na zaid ya Mbu kiukubwa na pia zaidi
ya mbu kiudogo pia, pale aliposema katika Qurán:
40
﴿إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يَسْتَحْىِ أَن يَضْرِبَ مَثَلاً م َّا بَعُوضَةً فَمَا فَوْقَهَا فَأَم َّا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ
فَيَعْلَمُونَ أَن َّهُ ٱلحَْق ُّ مِن ر َّهبِِّمْ وَأَم َّا ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ فَيَقُولُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱهلل َُّ هبَِ ٰذَا مَثَلاً
يُضِ ل ُّ بِهِ كَثِيراً وَيَهْ دِى بِهِ كَثِيراً وَمَا يُضِل ُّ بِهِ إِلا َّ ٱلْفَاسِ قِينَ ﴾
Inna Allaha la yastahyee an yadhriba mathalan ma baAAoodhatan fama fawqaha
faamma alladheena amanoo fayaAAlamoona annahu alhaqqu min rabbihim
waamma alladheena kafaroo fayaqooloona madha arada Allahu bihadha mathalan
yudhillu bihi katheeran wayahdee bihi katheeran wama yudhillu bihi illa
alfasiqeena (Surat Al Baqara 2:26)
Tafsir: Hakika Allah haoni haya kukupigieni mifano hata ya Mdudu Mbu au juu yake
zaidi wakati unapokua uko juu (mfano wa ukubwa wa huyo mbu). Ama wale wenye
kuamini, basi wanajua kua ni ukweli kutoka kwa Mola wao, ama kwa wale wasioamini
basi husema: ‘Ah Allah amekusudia nini juu ya mfano huu.’ Kutokana na mfano huo
basi huwapotosha wengi na kuwaongoza wengi. Na huwapotosha wale tu ambao ni
wenye kumuasi.
Naam, anasema Sultan al Mutakallimin Mujaddid ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi
kua: Allah Subhanah wa Taála haoni haya kutoa mfano wa kile alichokiumba, lakini
hapo hapo hua ni mwenye kuona haya juu ya kutojibu dua ya maombi ya mja wake
aliemuomba kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: Allah
Subhanah wa Taála ni Hai na ni Mkarimu, kiasi ya kua anaona Haya kua mja wake
amenyanyua juu mikono yake kwa ajili ya kumuomba dua kisha yeye asimjibu dua
hio.
Katika kufafanua sehemu ya pili ya aya hii basi Sultan Al Balagha Imam Abu Al Qasim
Al Zamakhshari kua: Upotoshwaji hapa umenasibishwa na Allah Subhanah wa Taála
kwa sababu yeye ndie mwenye kutoa Mithali ambazo ndani yake hua kuna
muongozo kwa watu. Hivyo kwa wale watakaoufuata basi watakua ni wenye
kuongoka kutokana nao na wale watakaoukataa basi watapotoka. Anasema Malik
Ibn Dinar kua Siku moja alimtembelea mfungwa ambae alikua amefungwa
kutokana na kua na madeni mengi, na hivyo mtu huyo akamwambia Malik Ibn
Dinar kua: Hebu angalia namna tulivyofungiwa na kudhulumiwa haki zetu. Hivyo
Malik Ibn Dinar, akaangalia juu, na kuona kua kuna mkoba unaning’inia.
41
Hivyo nae akauliza: Jee ule ni mkoba wa nani? Ambapo yule mfungwa akajibu kwa
kusema: Ni wangu mie. Hapo Malik Ibn Dinar akaushusha mkoba ule chini ili
kuangalia mna nini ndani yake, na akaona kua mna Kuku na Halua, Hapo Malik
Ibn Dinar akasema: Ama hiki ndio kilichokufungisha. Yaani kuendekeza
matamanio ya Dunia na ya Nafsi.
Kwa upande mwengine basi, tunaona kua ayah hii ya mithali ya mdudu Mbu imetumia
neno BaAAoodhatan ambalo maana yake hua ni Mbu lakini mwishoni mwa jina hilo
kuna harfu Ta ambayo ni yenye kuonesha kua Mbu huyu si mbu yeyote yule, bali
ni Mbu jike kwani aya pia imetumia neno fawqaha yaani juu zaidi yake mbu jike.
Tunaweza kujiiuliza kwa nini labda Allah Subhanah wa Taála akatumia mfano wa
Mdudu mdogo huyu huku akibainisha kua haoni haya kummithilisha, kwa mtizamo wa
ghafla basi tunaweza kusema kua labda kutokana na uwezo wake Mbu jike wa kumdhuru
Ibn Adam na baadhi ya wakati kuweza kumsababishia hata kifo, kwani Mbu jike ndie
anaenyonya damu na kuitumia kwa ajili ya Mayai yao.
Lakini huo ni mtizamo wa juu juu tu, kwani mdudu Mbu ingawa ni mdogo kiumbo lakini
ana Miujiza mikubwa zaid inayostaajabisha. Kwani miongoni mwa sifa zao ni pamoja
na:
1-Kuna aina 2700 za Mbu.
2-Uzito wa Mbu hua ni baina 2-2.5 Milligram.
3-Mbu Jike katika uhai wake anaweza akanyonya lita milioni za Damu.
4- Mbu Dume huishi kwa muda wa siku 10-20 lakini Mbu Jike huishi kwa mda wa
siku 10-100.
5-Katika siku za kungára Mwezi basi Mbu huongezeka kwa mara 500 zaidi.
6-Mbawa za Mbu hua ni zenye kupiga mara 500 kwa kila sekunde moja.
7-Mbu ndio wadudu wanaoongoza kwa kuusababisha vifo Ulimwenguni.
8-Mbu hua wanapendelea damu ya watoto zaidi kuliko ya Watu wazima.
9-Mbu wanachukia mafuta ya ndimu kwa sababu hua yanawaumiza miguu yao.
10-Mbu anaweza akamfuatilia Mtu anaemtaka kumnyonya damu yake kwa umbali
wa futi 18.
11-Mbu wana Nyoyo tatu ambazo hufanya kazi sambamba.
12- Mbu wana Macho zaidi ya 100 kwenye kichwa chao.
13-Mbu wana Meno 48 katika midomo yao.
14-Mbu wana mbawa 3.
15-Mbu wana Sindano 6 katika pua zao, na kila Sindano ina kazi yake maalum.
16-Mbu wanaona kwa kutumia mionzi ya X-Ray na hivyo huweza kuona na
kuitaofautisha ngozi ya Ibn Adam na vitu venyine katika kiza.
17-Mbu wanauwezo wa kupima aina ya Damu wanayoihitaji kwa sababu hua
wanapenda zaidi damu ya Group O, na hua hawapendi damu ya Group A.
18-Mbu wanaweza kusikia harufu ya Ibn Adam kutoka umbali wa futi 100.
42
19-Mbu huwa wananyonya damu za viumbe wengine lakini hupendelea zaidi damu
ya Ibn Adam kwa sababu hua ni rahisi kuwanyonya, na hua wanaweza kugundua
harufu ya hewa ya Carbon Dioxide tunayoitoa mwilini ambayo hua imechanganyika
na Lacti Acid, Octenol, Uric Acid na Fatty Acid na hivyo hua wanajua kua kuna Ibn
Adam katika maeneo ya karibu.
20-Mbu hua wana chanjo ya ganzi ya kuondoa maumivu ambayo humpiga mtu
wanaetaka kumyonya damu mara tu wanapotua juu ya ngozi ya mtu ili mtu huyo
asihisi maumivu ya kutobolewa na kuingizwa sindano ya mbu na kisha kunyonywa
damu huyo.
21-Mbu hua wana pampu ambayo huwaongezea kasi ya kunyonya damu nyingi
zaidi pale wanapoifungua na kuanza kunyonya damu wanayoitaka.
Hio ni baadhi tu ya Miujiza mikubwa ya Mithali ya Mdudu Mbu, na bila ya shaka Qurán
haikutumia Mithali ya mdudu Mbu tu bali pia imetumia mithali ya Mdudu Nzi pale
iliposema katika aya ifuatayo:
﴿َٰي ُّهَا ٱلن َّاسُ ضُرِبَ مَثَلٌ فَٱسْتَمِعُواْ لَهُ إِن َّ ٱل َّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِ ٱهلل َِّ لَن يخَْ لُقُواْ
ذُابَابً وَلَوِ ٱجْتَمَعُواْ لَهُ وَإِن يَسْلُبْهُمُ ٱلذ ُّابَ بُ شَيْئاً لا َّ يَسْتَنقِذُوهُ مِنْهُ ضَعُفَ
ٱلط َّالِبُ وَٱلْمَطْلُوبُ ﴾
Ya ayyuha alnnasu dhuriba mathalun faistamiAAoo lahu inna alladheena
tadAAoona min dooni Allahi lan yakhluqoo dhubaban walawi ijtamaAAoo lahu wain
yaslubuhumu aldhdhubabu shay-an la yastanqidhoohu minhu dhaAAufa
alttalibu waalmatloobu (Surat al Hajj 22:73)
Tafsir: Enyi watu! Mnapigiwa mfano, hivyo usikilizeni kwa makini: Wale ambao
mnawaomba badala ya Allah, hawawezi kuumba hata Mdudu Nzi, hata kama
wakijikusanya pamoja kwa lengo hilo, na kama huyo Nzi akipokonya kitu kutoka
kwao, basi kamwe hawatokua na uwezo wa kumnyang’anya, wako dhaifu sana
waombaji na wanaoomba.
Hii ni mithali ambayo ndani yake Allah Subhanah wa Ta’ala anawapigia wale watu
wasiomuamini, mfano wa mdudu Nzi, mdudu ambae ni mdogo, asie na thamani,
asiependezesha sehemu anayotua kwa sababu hua ni sehemu yenye uchafu, na hata kama
haina uchafu basi Nzi akitua katika sehemu basi huwacha uchafu pale anapoondoka
katika sehemu husika, na pia huchukua kitu katika sehemu husika kiasi ya kua hakuna
Ibn Adam anaeweza kuona kwa macho yake kile alichokiwacha mdudu huyo wala
43
alichochukua mdudu huyo na hivyo hua haiwezekani kumpokonya alichochukua, kwa
sababu Nzi anapotaka kuchukua kitu fulani basi hutoa maji yenye kemikali ambayo
hukilainisha kitu hicho na kisha yeye hunyonya kilichomo ndani ya kitu husika na
kuondoka nacho kile cha ndani tu na hivyo hubakisha bua tupu yaani kile
kinachoonekana kwa mizamo wa nje na hivyo hua haonekani ni nini alichokichukua,
hivyo hua hakuna na uwezekano wa kupokonyeka kile alichokichukua.
Hapa haina haja ya kuzungumzia wingi wa wadudu Nzi, kwani kiaina tu basi kuna aina
90,000 za mdudu Nzi, ambao hua wanazaana kila baada ya wiki 2 huku kila Nzi jike hua
ni mwenye kutaga mayai 100. Na pia haina haja kuainisha juu ya maumbile ya Mbawa
zake mdudu Nzi ambapo kimaumbile hua zina hali ya upekee, ya kua na uwezo wa
kudhuru na uwezo wa kutibu.
Ambapo anasema Mujaddid ud Din Imam Shah Waliyu Allah Al Dahlawi katika Hujjat
Allah Al Baligha kua: Allah Subhanah wa Ta’ala anaweka wazi Hikma na Busara
zake katika kumuumba kwake Mdudu Nzi kua kila mdudu mwenye sumu basi hua
ni mwenye kujaaliwa kua na dawa ya kuondoa sumu hio kwa ajili ya kuulinda na
kuendeleza uhai wa mdudu huyo.
Ama kwa upande wa Shaykh al Akbar Imam Muhyi ad Din Abu Bakr Ibn Al Arabi basi
yeye anasema kua: Nzi mara zote hua ni mwenye kuliweka juu bawa lake lenye dawa
ili lisiguse kile kitu chenye umaji maji alichotulia juu yake, ili aweze kutumia Ubawa
huo kwa ajili ya kurukia anapotaka kuondoka kwa haraka katika sehemu hio, na
hii pia ni miongoni mwa Maumbile aliyojaaliwa kua nayo kutoka kwa Muumba,
ambapo sifa hii pia wanayo Sisimizi, Nyuki na Ndege wa aina ya Hud Hud. (Imam
al-Tahawi, Sharh Mushkil (8:343-344) Imam al-Khattabi, Ma`alim al-Sunan (4:459))
Ama hizi mithali za mdudu Nzi, Mbu na mithali nyenginezo zinathibitisha kua Allah
Subhanah wa Taála ndie Nuru ya kila kitu ulimwenguni yaani ni mwenye kuweka wazi
kile ambacho kilichokua hakijulikani na viumbe wake kama anavyosema yeye
mwenyeye katika aya ifuatayo:
﴿ٱهلل َُّ نُورُ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ مَثَلُ نُورِهِ كَمِشْكَ واةٍ فِيهَا مِصْبَاحٌ ٱلْ مِ صْبَاحُ فىِ
زُجَاجَةٍ ٱلز ُّجَاجَةُ كَأَن َّهَا كَوْكَبٌ دُرِّي ٌّ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ م ُّبَارَكَةٍ زَيْتُونَةٍ لا َّ شَرْقِي َّةٍ وَلاَ
غَرْبِي َّةٍ يَكَادُ زَيْتُهَا يُضِي ۤ ءُ وَلَوْ لمَْ تمَْسَسْهُ َرٌ ن ُّورٌ عَلَى ٰ نُورٍ يَهْدِى ٱهلل َُّ لِنُورِهِمَن
ّ بِكُل شَيْءٍ عَلَيِمٌ ﴾
يَشَ آءُ وَيَضْرِبُ ٱهلل َُّ ٱلأَمْثَالَ لِلن َّاسِ وَٱهلل َُّ ِ
44
Allahu nooru alssamawati waal-Ardhi mathalu noorihi kamishkatin feeha
misbahun almisbahu fee zujajatin alzzujajatu kaannaha kawkabun durriyyun
yooqadu min shajaratin mubarakatin zaytoonatin la sharqiyyatin wala
gharbiyyatin yakadu zaytuha yudee-o walaw lam tamsas-hu narun noorun AAala
noorin yahdee Allahu linoorihi man yashao wayadribu Allahu al-amthala lilnnasi
waAllahu bikulli shay-in AAaleemun.(Surat Al-Noor 24:35).
Tafsir: Allah ni Nuru ya Mbingu na Ardhi, mithli ya Nuru yake ni kama Mishkat
(Mishkat ni sehemu kama kidirisha ambacho hujengwa maalum kwa ajili ya kuwekea
taa ukutani na hivyo kufanya muangaza wa taa hiyo uwe mkubwa zaid pale taa
inapokua ndani ya kidirisha hicho kuliko taa hiyo ikikaa katika sehemu iliyo wazi), na
ndani yake mna taa, na taa hiyo imo ndani ya kioo. Kioo ambacho kinang’ara kama
nyota ya Durriyun (aina ya nyota yenye kung’ara sana kama Lulu), (taa) ambayo
imewashwa kutokana na mti mtakatifu wa Mzaituni usio wa Mashariki wala
Magharibi, ambao mafuta yake hutoa mwangaza bila ya kuguswa (kuwashwa) na
moto wowote. Nuru juu ya Nuru! Allah humuongoza katika mwangaza wake yeyote
yule amtakae. Na Allah anaweka wazi mifano kwa Bani Adam, Na hakika Allah ni
mwenye kujua kila kitu.
Hapa tunaona kua aya hii imetumia kiunganishi ‘ka’ kinachotafsirika kwa lugha ya
Kiswahili kama ‘kama’ ambacho hujulikana kama Kaf at tashbih ambayo inayoleta
maana ya kushabihisha kitu kimoja kua kinafanana tu na kitu chengine lakini hata hivyo,
kitu hicho si kitu chenyewe kilichokusudiwa. Kutumika kwa Kaf at Tashbih katika aya
hii kunaonesha kutokuwepo uwezekano wa kuelezea sifa za Majina ya Allah Subhanah
wa Ta’ala hata kupitia kwa njia za kufananisha kwani yeye mwenyewe anasema kua:
﴿لَيْسَ كَ مِ ثْلِهِ شَ ىْ ءٌ﴾
Laysa kamithlihi shay-un (Surat Ash Shuraa 42:11)
Tafsir: Hakuna kitu chenye mithli yake.
Na vile vile akasema:
﴿وَلمَْ يَكُ نْ ل َّهُ كُ فُواً أَحَ دٌ ﴾
Walam yakun lahu kufuwan ahadun (Surat Al Ikhlas 112:4)
Tafsir: Hakuna anaefanana nae.
45
Hivyo ufananisho huu wa Sifa ya ‘Nuru ya Allah’ hauwezi kuonesha ukweli halisi
ulivyo, bali ufafanisho huu umetumika ili kufafanua kimaana kutokana na ufahamu wa
walengwa waliokusudiwa, kwa sababu ukweli halisi wa ‘Nur ya Allah’ ni ukweli ambao
hauwezi kufikirika kwa hali yeyote ya kiumbe yeyote yule na wala hauwezi kuelezeka
kwa lugha ya kiumbe chochote.
Hujjat ul Islami Mujaddid ud Din Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali katika kuielezea maana ya Al Nur anasema kua: Al Nur ni yule
anaeonekana kutokana na kuvifanya vitu vyote vionekane, kwani kila kitu
kinachoonekana chenyewe na kusababisha vitu vyengine vionekane hua kinaitwa
Nuru. Tukiangalia kwa mtazamo wa kua kila kilichokuwepo hupingana na
kisichokuwepo, basi kile kinachoonekana hakiwezi kulinganishwa na kitu chengine
isipokua tu na kile kilichokuwepo. Kwani hakuna kiza kilichokua cheusi zaidi
kuliko kile kiza cha kitu kisichokuwepo.
Kile kilichokua huru kutokana na giza la kutokuwepo, na kua na uwezekano wa
kutokuwepo, na huondoa kila kitu kutoka katika kiza cha kutokuwepo na
kukiingiza katika udhihirisho wa kuwepo, basi hua kinastahiki kuitwa Nuru.
Kuwepo ni Nuru iliyohuru isiyotegemea kitu inayomurika kila kitu kutokana na
asili ya Nuru yake Allah Subhanah wa Ta’ala, kwani Allah Subhanah wa Ta’ala ni
Nuru ya Mbingu na Ardhi. Na kama ilivyokua hakuna hata muale mmoja wa
muangaza wa Jua ambo huonesha kua hio ndio chanzo cha muangaza wa Jua hilo,
basi vile vile hakuna hata chembe moja ya kitu kutoka katika vitu vilivyomo ndani
ya Mbingu na Ardhi, ambacho hakimpelekei mtu kukosa uhakika wa kutokana na
uwezekano wa kuwepo kwake bila ya kuhitaji kuwepo kwa yule aliesababisha
kuwepo kwa kitu hicho.
Hivyo kutokana na Nuru, hususan Nuru ya Allah, basi kila kitu hua kiko wazi, chenye
kuonekana, chenye kufahamika na hivyo kua ni chenye uhakika na chenye kua na yakini.
Ama kwa upande mwengine basi anasema Hasan Al Basr kua: ‘Mithali ya Nuru ya
Qurán ni Misbah (Taa). Misbah ambayo Sirajan (Moto au Muangaza) yake ni
Maarifah (Maarifa ya kuokoka Kinafsi) na Fatil (Utambi) yake ni Faraidh (FArdhi
za Dini) ambao Dhuhn (Mafuta) yake ni Ikhlas na Nuru yake (Ya Kiroho) ni ya
Ittisal (Kufikia Darja inayotakiwa kufikiwa). Hivyo kila Ikhlas ikizidi kiusafi basi
mwangaza wa Taa ndio hua unazidi Zaidi. Na kila fArdhi za dini zinapozidi basi
ndio unapopatikana uhakika (Haqiqa) na ndivyo Nuru inavyozidi.’
Allah Subhanah wa Taála anatupigia mifano myengine juu ya wale watu ambao
hawatomuamini yeye na hivyo kua ni wenye kumshirikisha kua ni wasiojua udhaifu
mkubwa sana wa kile wanachokiamini na kuona kua kinawanufaisha kwa kusema:
46
﴿مَثَلُ ٱل َّذِينَ ٱتخ ََّذُواْ مِن دُونِ ٱهلل َِّ أَوْلِيَآءَ كَمَثَلِ ٱلْعَنكَبُوتِ ٱتخ ََّذَ تْ بَيْتاً وَإِ َّن
أَوْهَنَ ٱلْبُيُوتِ لَبَيْتُ ٱلْعَنكَبُوتِ لَوْ كَانُواْ يَعْلَمُونَ ﴾
Mathalu alladheena ittahadhoo min dooni Allahi awliyaa kamathali alAAankabooti
ittakhadhat baytan wa-inna awhana albuyooti labaytu alAAankabooti law kanoo
yaAAlamoona (Surat Al Anqabut 29:41)
Tafsir: Mithili ya wale ambao wanaoichukua Miungu myengine zaidi ya Allah, hua ni
mithli ya Buibui ambae hujijengea nyumba. Lakini kwa hakika! Hakuna nyumba
dhaifu kama nyumba ya Buibui, lau kama wao wangejua.
Katika aya hii ya Surat Al Anqabut ambayo ndio aya iliyotoa jina la Sura hii, basi tunaona
kua Allah Subhanah wa Taála anatutolea mfano wa Al Anqabut yaani mdudu Buibui
ambae anaelezewa Nyumba yake anayoijenga na kuishi kwa kutumia uzi laini wa Hariri
ambao anautoa ndani ya mdomo wake tena kwa wingi sana kiasi ya kua anaweza
akajenga nyumba baina ya miti miwili kwa kuurusha uzi huo kwa umbali mita 25 kutoka
upande mmoja hadi mwengine bila ya kuonekana kwa dalili ya kuishiwa kwa uzi wake
huo wa Hariri wala kuanguka chini kwa uzi huo kwani hunyooka kama waya katika
kutembea kwake kutoka upande mmoja kuelekea upande mwengine.
Uzi wa Buibui ni uzi wenye kutokana na Protein ambayo inatokana na madini ya Carbon,
Hydrogen, Oxygen na Nitrogen zinazozalishwa kwa wingi sana na mwili wake, na hadi
hii leo Wanasayansi na utaalamu wao wote bado hawajapata jibu juu ya uwezo wa Buibui
katika kuzalisha kwa wingi uzi huo bila ya kuishiwa na madini hayo hususan
ukilinganisha na ukubwa wa mwili wa mdudu Buibui.
Tunapoiangalia aya hii basi tunaona kua imetumia neno ‘Ittakhadha’ ambalo kwa kiarabu
hua ni lenye kumaanisha: Afanyae Kitu, Mwenye kuchukulia Kitu au Mwenye Kitu.
Lakini sasa neno Ittakhadha lililotumika hapa mwishoni mwake limeishia na harfu
‘ta’ na hivyo limekua katika hali ya Ittahadhat ambayo ni yenye kumaanisha jinsia
ya Kike.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala hapa anatuwekea wazi kua Buibui anaejenga nyumba
hua ni Buibui jike, na hivyo ni Buibui jike ndie anaedumu katika nyumba husika na wala
si Buibui dume. Jambo ambalo limethibitishwa pia na Wanasayansi wa Kijerumani
mnamo mwaka 1984 pale walipochapisha matokeo ya uchunguzi wao huo katika gazeti
la Cosmos Magazine la Ujerumani ambao umethibitisha hivyo. Hii ni kuthibitisha
miongoni mwa Miujiza mingi ya Qurán.
47
Ni maumbile ya Mdudu Buibui kua na uwezo wa kuzalisha uzi huu wa kujengea nyumba
yake ambapo nyumba hio hua na nyuzi aina tano tofauti, kuna nyuzi pana ambazo ndio
hua msingi wa nyumba na ndio anazotumia yeye katika kuzunguka na kuisimamia
nyumba hio, ingawa uzi huu ambao ndio msingi wa nyumba yake hua ni mpana lakini
upana wake haufiki hata upana wa milimita moja, Buibui pia hua anazalisha Uzi maalum
kwa ajili ya kuhifadhia Mayai yake, Uzi maalum kwa ajili ya kujilinda, na Uzi maalum
kwa ajili ya Kuhifadhia chakula chake na wadudu anaowakamata, na pia huzalisha uzi
mwengine ambao ni mwembemba zaidi kwa ajili ya hujenga ukuta ambao hua pia kama
mtego kwa ajili ya maadui zake na hapo hapo kwa ajili ya wadudu ambao hua ndio
chakula chake, na hivyo Buibui hua ni mwenye kusubiri katikati ya nyumba yake hado
pale nyuzi nyembamba zinapotetemeka na hivyo hujua kua upande fulani kuna mdudu
ameshaganda tayari, hivyo Buibui kwa kutumia nyuzi nene basi huelekea upande
uliotokea mtetemeko huo kwa kutumia nyuzi nene na kutembea hadi katika sehemu
aliyoganda mdudu kwenye mtego wake.
Kwa kimaumbile nyuzi zote hizi za aina mbili ingawa ni laini na nyembamba ambapo
nyuzi zenye uzito wa gramu 320 hua na uwezo wa kuzungushwa dunia nzima kutoka
pande moja hadi nyengine, lakini ni nyuzi ambazo hazina mfano wake katika uimara
wake, kwani nyuzi hizi hua na umadhubuti wa mara 100 zaidi ukilinganishwa na
umadhubuti wa uzi wa chuma cha pua ambacho ni chuma kigumu zaidi, mbali ya kua
Uzi wa Buibui ni madhubuti lakini pia uzi huo hua na uwezo wa kuvutika kwa mara nne
zaidi ya urefu wake wa kimaumbile bila ya kukatika na ukikusanywa pamoja hua na
ugumu mkubwa sana kwa mara 10 zaidi ya materiali ya Kevla ambayo hutumika kwa
ajili ya kutengenezea mavazi ya Bullet Proof yaani yanayovaliwa ili kuzuia risasi isitokee
upande wa pili na hivyo kuzuia zisiingie mwilini mwa Ibn Adam.
Si hivyo tu bali pia uzi huu wa Buibui hua ni wenye kujivuta na kupunguza urefu wake
kwa 50% unaponyeshewa na mvua na pia una uwezo wa kupitisha nguvu za mawasiliano
ya umeme haraka na kwa wingi zaidi kuliko kitu chochote kile kwani hata waya wa shaba
ambao ndio unaotumika kusafirishia umeme majumbani hua haufikii uwezo wa uzi wa
Buibui. Mbali ya kua na sifa zote hizo na nyenginezo lakini hapo hapo Allah Subhanah
wa Ta’ala anasema kua:
﴿وَإِن َّ أَوْهَنَ ٱلْبُيُوتِ لَبَيْتُ ٱلْعَنكَبُوتِ لَوْ كَانُواْ يَعْلَمُونَ ﴾
Wa-inna awhana albuyooti labaytu alAAankabooti law kanoo yaAAlamoona (Surat
Al Anqabut 29:41)
Tafsir: Lakini kwa hakika! Hakuna nyumba dhaifu kama nyumba ya Buibui, lau kama
wao wangejua.
48
Kua hii ni nyumba ambayo mbali ya kua ni nyumba iliyojengwa kwa nyuzi zenye
umadhubuti wa hali ya juu kwa mdudu Buibui mwenyewe na wadudu wengine ambao
hua ndio chakula chake, lakini hapo hapo basi tunaona kua hakuna nyumba iliyo dhaifu
ndani na nje kama ilivyo nyumba ya Buibui, kwani mbali ya kua kwa nje inaweza
kuvunjwa na kuteketezwa mara moja na wale wenye uwezo zaidi ya Buibui na haiwezi
kumzuia Buibui huyo na madhara ya mvua wala ya jua kama tunavyojua lakini pia kwa
ndani ya nyumba hio basi hua na mazingira ya kutoishika kwa Buibui dume ambae yeye
kufariki kwake hutokea mara tu baada ya kumnyatia taratibu na kumuingilia Buibui jike
ambapo Buibui jike nae humgeuza Buibui dume huyo kua ni chakula chake huku wakiwa
katika hali ya kuingiliana. Jambo hili humpelekea Buibui jike kupata mayai ya akiba zaidi
kutoka kwa Buibui dume.
Na kwa baadhi ya Buibui basi pia Buibui jike hua ni mwenye kufariki mda mfupi tu mara
baada ya mayai kutoa watoto kwani watoto hao humgeuza mama kua ndio chakula chao
na ndio maana Buibui hutaga mayai takriban 3000 kwa mkupuo mmoja.
Bila ya shaka Allah Subhanah wa Ta’ala anatupigia mithali ili tupate kutafakkar ambako
nako kutatupelekea kufaham maana na makusudio ya mithali hizo kama alivyosema:
﴿وَتِلْكَ ٱلأَمْثَالُ نَضْرِبُهَا لِلن َّاسِ وَمَا يَعْقِلُهَآ إِلا َّ ٱلْعَالِمُونَ ﴾
Watilka al-amthalu nadhribuha lilnnasi wama yaAAqiluha illa alAAalimoona
(Surat Al Anqabut 29:43)
Tafsir: Na tunaipiga mifano hii kwa watu, lakini hakuna atakaefahamu isipokua wale
wenye kujua.
Allah Subhana wa Ta’ala anamalizia kuweka wazi juu ya aina mbali mbali za mifano na
mithali kwa ajili ya kuwanufaisha viumbe wake kwa kusema:
﴿وَلَقَدْ ضَرَبْنَا لِلن َّاسِ فىِ هَٰذَا ٱلْقُرْآنِ مِن ِ كُل مَثَلٍ وَلَئِن جِ ئْتَهُمْ آبِيَةٍ ل َّيَقُولَ َّن
ٱل َّذِينَ ۤ كَفَرُواْ إِنْ أَنتُمْ إِلا َّ مُبْطِلُونَ ﴾
ّ
Walaqad dharabna lilnnasi fee hadha alqur-ani min kulli mathalin wala-in ji/tahum
bi-ayatin layaqoolanna alladheena kafaroo in antum illa mubtiloona (Surat Ar Rum
30:58)
49
Tafsir: Na bila ya shaka, tumeipiga kwa ajili ya watu ndani ya hii Quran kila mifano,
lakini kama ukiwaletea wao vithibitisho basi wasioamini watasema kua: Hakika nyinyi
hamkua isipokua ni wenye kujishughulisha na mambo ya kipuuzi.
Hivyo bila ya shaka mifano na mithali hizo wamepigiwa Ibn Adam ili watumie akili zao
wapate kujiokoa na adhabu za Mola wao, kwani wasipotafakkar basi watakua ni watu
waliopotoka na wataingia Motoni, na hua si sawa watu Motoni na watu wa Peponi, kwani
watu wa Peponi hua si watu waliopotoka bali hua ni watu waliofuzu. Allah
anatukumbusha haya na kutuwekea wazi, thamani, uzito na umuhimu wa Qurán kwa
kutuambia:
﴿لاَ يَسْتَوِي ۤ أَصْحَابُ ٱلن َّارِ وَأَصْحَابُ ٱلجَْن َّةِ أَصْحَابُ ٱلجَْن َّةِ هُمُ ٱلْفَآئِزُونَ۞ لَ وْ
أَنزَلْنَا هَٰذَا ٱلْقُرْآنَ عَلَى ٰ جَبَلٍ ل َّرَأَيْتَهُ خَاشِ عاً م ُّتَصَدِّعاً مِّنْ خَشْيَةِ ٱهلل َِّ وَتِلْكَ
ٱلأَمْثَالُ نَضْرِبُهَا لِلن َّاسِ لَعَل َّهُمْ يَتَفَك َّرُونَ۞ هُوَ ٱهلل َُّ ٱل َّذِى لاَ إِ لَٰهَ إِلا َّ هُوَ عَالمُِ
ٱلْغَيْبِ وَٱلش َّهَادَ ةِ هُوَ ٱلر َّحمَْٰنُ ٱلر َّحِ يمُ هُوَ ٱهلل َُّ ۞ ٱل َّذِى لاَ إِلَٰهَ إِلا َّ هُ وَ ٱلْمَلِكُ
ٱلْقُد ُّوسُ ٱلس َّلاَمُ ٱلْمُؤْمِنُ ٱلْمُهَيْمِنُ ٱلْعَزِيزُ ٱلجَْب َّارُ ٱلْمُتَكَبرُِّ سُبْحَانَ ٱهلل َِّ عَم َّا
يُشْرِكُونَ۞ هُوَ ٱهلل َُّ ٱلخَْالِقُ ٱلْبَارِ ئُ ٱلْمُ صَوِّرُ لَهُ ٱلأَسمَْآءُ ٱلحُْسْنىَٰ يُسَبِّحُ ا لَهَُم فىِ
ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلحَْكِيمُ ﴾
La yastawee as-habu alnnari waas-habu aljannati as-habu aljannati humu alfaizoona;Law
anzalna hadha alqur-ana AAala jabalin laraaytahu khashiAAan
mutasaddiAAan min khashyati Allahi watilka al-amthalu nadribuha lilnnasi
laAAallahum yatafakkaroona; Huwa Allahu alladhee la ilaha illa huwa AAalimu
alghaybi waalshshahadati huwa alrrahmanu alrraheemu; Huwa Allahu alladhee la
ilaha illa huwa almaliku alquddoosu alssalamu almu/minu almuhayminu
alAAazeezu aljabbaru almutakabbiru subhana Allahi AAamma yushrikoona;
Huwa Allahu alkhaliqu albari-o almusawwiru lahu al-asmao alhusna yusabbihu
lahu ma fee alssamawati waal-Ardhi wahuwa alAAazeezu alhakeemu; (Surat Al
Hashr 59:20-24)
50
Tafsir: Hawako sawa watu wa Motoni na Watu wa Peponi, kwani Watu wa Peponi
watakua ni waliofuzu. Lau kama tungeishusha hii Qurán kwa ajili ya Majabali, basi
kwa hakika ungeona namna Majabali yanavyonyenyekea na kumomonyoka kutokana
na kumuogopa Allah. Na hizi ni Mithali ambazo tunawapigia watu ili watafakkari!
Hakika yeye ni Allah ambae hakuna Mungu isipokua yeye. Mjuzi wa yasiyoonekana
na yanayoonekana. Yeye ni mwingi wa Rehma na Huruma. Yeye ni Allah ambae
hakuna Mungu isipokua yeye, yeye ndie Mfalme, Mtukufu, Asiekua na Kasoro,
Mwenye kuwahakikishia Usalama viumbe wake, Msimamizi wa Amani ya viumbe
wake wote, Muangalizi wa vitendo vya Viumbe wote, Mwenye uwezo Mkubwa sana wa
kulipa kwa kuadhibu kwa adhabu kali kabisa, Mwenye Uwezo Mkubwa wa kusimamia
mambo ya viumbe na kuwaweka chini ya khiari yake kama atakavyo, Mwenye Ukubwa
wa pekee usiokua na Kifani katika kila kitu. Utukufu ni wake yeye Allah ambae hana
mshirika. Yeye ni Allah ambae ndie Muumbaji, Muanzishaji wa kila kitu bila ya
kuhitajika kuwepo kwa kitu chengine katika kuanzisha kwake huko, Mwenye Kuumba
kwa namna na aina ya vitu atakavyo, kwake yeye ndio kwenye Umiliki wa Majina
Yenye Sifa Bora ambae anatukuzwa na kila kilichomo Mbinguni na kilichomo
Ardhini, na ni Mwenye Uwezo wa kila kitu na mwenye Hikma katika kila kitu
akifanyacho.
Baaada ya kutuwekea wazi hayo basi Allah Subhanah wa Taála anatupa mithali nyengine
hapo hapo kutuwekea wazi kua Viumbe walioumbwa na kupewa ukubwa wa mara 1000
zaidi yetu, yaani Milima basi hua inafahamu jukumu lake mbele ya Mola wake kiasi ya
kua kama ingeshushiwa Qurán basi bila ya shaka ingetetemeka na kububujika kutokana
na kua na khofu kwa Mola wake, lakini Ibn Adam asietumia akili yake na kutafakkar juu
ya Qurán basi basi hua ni mjinga mwenye kuipuuza na kutokua na khofu yeyote mbele
ya Mola wake kutokana na ujinga wake na kutojua majukumu yake.
Hivyo, basi Allah Subhanah wa Ta’ala anatoa mithali na visa ndani ya Qurán ili angalau
tupate kujifunza pale tutakapozingatia na kutilia maanani visa, mifano na mithali hizo na
ni kutokana na kutafakkar na kuzingatia kwake basi ndio tunapopata uongofu kwa
kufuata njia sahih tunazoelekezwa ndani yake na kuachana na njia potovu tunazokatazwa
kuzifuata kulingana na mifano hai tunayooneshwa kupitia katika njia zilizomo ndani ya
Kitabu chake Qurán na Sunnah za Nabii wake Muhammad Salallahu Aálayhi wa Salam
ikiwemo Mithali zinazoainisha kanuni za mawasiliano ya kauli kama isemavyo aya
ifuatayo:
﴿أَلمَْ تَرَ كَ يْفَ ضَرَبَ ٱهلل َُّ مَثَلاً كَ لِمَ ةًطَيِّبَةًكَشََجر أ ةٍطَيِّبَةٍ َ صْلُهَ ا اثَبِتٌ وَفَرْعُهَا فىِ
ٱلس َّمَآءِ ۞ يُثَبِّتُ ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ بِٱلْقَوْلِ ٱلث َّابِتِ فىِ ٱلحَْيَاةِ ٱلد ُّنْيَا وَفىِ ٱ لآ خِ رَةِ
51
وَيُضِل ُّ ٱهلل َُّ ٱلظ َّالِمِينَ وَيَفْعَلُ ٱهلل َُّ مَا يَشَآءُ۞ وَمَثلُ كَ لِ َمةٍ َخبِيثَةٍ كَشَجَرَةٍ خَبِيثٍَة
ٱجْتُث َّتْ مِن فَوْقِ ٱلأَرْضِ مَا لهََا مِن قَرَارٍ ﴾
Alam tara kayfa dharaba Allahu mathalan kalimatan tayyibatan kashajaratin
tayyibatin asluha thabitun wafarAAuha fee alssama/-I, Tu/tee okulaha kulla heenin
bi-idhni rabbiha wayadribu Allahu al-amthala lilnnasi laAAallahum
yatadhakkaroona, Wamathalu kalimatin khabeethatin kashajaratin khabeethatin
ijtuththat min fawqi al-Ardhi ma laha min qararin (Surat Ibrahim 14:24-26)
Tafsir: Jee hujaona namna Allah anavyopiga mifano, kauli nzuri hua ni kama mti
ambao asili yake (mizizi yake) iko thabit (imekomaa ardhini) na umechipua kuelekea
juu angani, huzaa matunda kila msimu kwa idhini ya Mola wake, na Allah anatoa
mifano kwa watu ili wapate kukumbuka. Na mithili ya kauli mbovu hua ni sawa na
mti uliong’oka na kua juu ya Ardhi ukiwa hauna uimara.
Bila ya shaka mfano wa Mti usiokua na mizizi Imara au mti ambao upo juu juu hua ni
mti usiokua na faida yeyote kwani hautoweza kutoa matunda, huu ni mfano mzuri ambao
pia unatuonesha kua amali za mtu asiekua ni mwenye kuamini basi hua hazina faida
kwake isipokua hapa hapa Duniani kwani Akhera hua hana malipo yeyote isipokua
hasara.
Anasema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alienda kwa Masahaba akawakuta wanazungumzia juu ya Kalimatan
Tayyibatan ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Kalimatan
Tayyibatan ni kama Muumini ambae mizizi yake, imezama ardhini na Matawi yake
yako Mbinguni.’ Yaani amali zake hua zinanyanyuliwa Mbinguni na zinakubaliwa
Hivyo hii mithali ambayo Allah Subhanah wa Taála amemithilisha kwa Waumini
na Makafiri.
Na akasema Kalimatan Tayyibatan hua ni kauli za kweli zenye Ikhlasi ndani yake,
hua ni Shajaratin Tayyibatin yaani kama Mtende ambao mizizi yake ni madhubuti
ardhini na majani yake yamefikika Mbiguni. Vile vile ndivyo ilivyo amali za
Muumini ambazo zimepatikana kutokana na kuthibitisha kwa Kalimat at Tawhid
ambayo ni mzizi madhubuti wenye matawi yake Mbinguni yaani amali zake
zimenyanyuliwa juu Mbinguni na ni zenye kukubaliwa, isipokua labda ziwe ni
zenye kasoro (Ihdath) ndani yake.
52
Lakini hata hivyo Mzizi wa amali zake katika kumpwekesha Mola wake
hauondolewi, hivyo hii inakua kama vile ambavyo upepo unapovuma na
kuyumbisha majani ya Mtende tu, huku mizizi yake ikiwa madhubuti ardhini.
Na amezimithilisha kauli za Mtu asieamini na Shajara al Khabitha kwa kusema kua:
‘Wamathalu kalimatin khabeethatin kashajaratin khabeethatin’ kumaanisha mti wa
aina ya Hanzal (Matikiti ya Jangwani yasiyolika) ambao hakuna mti wenye ladha
mbaya sana kama huo, kwani hauna mizizi chini yake. Kama vile ilivyokua Kufr na
Unafiq ambao haustahmiliwi kesho Akhera. Hivyo katika hazina ya Allah
Subhanah wa Taála hakuna hazina nzito kama Kalimat Tawhid!’
AINA ZA KALIMAT (KAULI) NDANI YA QURÁN
Neno Kalimatan ni neno lililotokana na neno Kalama ambalo kwa Lugha ya Kiarabu hua
linamaanisha Kutoa Kauli, Kuzungumza, Kusema, Kuelezea kwa maneno, Kutoa
Mtizamo juu ya jambo Fulani, Kutoa habari au Amri, Ahadi, Kuwasilisha Ujumbe na pia
humaanisha Mtizamo au mawazo ambayo yamo ndani ya Ufahamu lakini bado
haujatamkwa.
Hivyo Qurán inatutolea mithali ya kauli njema kwa kutufunza pia umuhimu wa kanuni
za mawasiliano ya kufikisha ujumbe baina ya Mitume na watu wanaowapelekea ujumbe
katika jamii zao, Viongozi, Watawala, Wenye I’lm na wasiokua na I’lm, wafuasi wao na
wapinzani wao na kadhalika, kwa sababu kanuni za mawasiliano ya kufikisha ujumbe
kwa wahusika ni sehemu ya Iman na Ihsan ya dini ya Kiislam.
Kwani anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Al Islam
(Uislam) ni Hukm, Al Iman ni Wasl (Kuiwasilisha kwa Allah Subhanah wa Taa’la)
na Ihsan ni Thawab (Malipo). Hivyo Uislam ni Iqrar (kuthibitisha) ambako hua ni
kwenye kuonekana, lakini Iman hua haionekani, wakati Ihsan hua ni Taábud
(Ufanyaji Ibada)’
Hivyo ingawa neno Kalimah hua ni lenye kumaanisha pia Qawl (Kauli) lakini pia hapo
hapo hua linatofautiana kimaana pale tunapoona kua neno Kalimah hua linamaanisha pia
Mtizamo ambao umo ndani ya ufahamu wa Ibn Adam lakini haujatamkwa na ulimi, wala
kuoneshwa kwa njia yeyote ya ishara na hivyo hua ni mtizamo ambao haujaingia katika
hali ya Qawl.
53
Neno Qawl hua ni lenye kutokana na neno Qulu ambalo kwa kilugha hua linamaanisha
Kutoa kauli, Kusema, Kuzungumza, Kutamka, Kuelezea, Kuhadithia, Kunukuu na hua
pia linatumika katika kuainisha kitu au tukio halisi linalotokea bila ya kusikika sauti ya
maneno, kwa mfano pale mtu anaposema: ‘Qalat laha al aynayn samaAna wa ta’Atan’
yaani: ‘Yalimwambia yeye macho yangu nimesikia na nitatii’. Au pale wanaposema:
‘Imta'a ala hawdhu wa qala qatni’, yaani: ‘Lilijaa Hodhi hadi likasema imetosha’.
Neno Qala ndio lililotoa neno Qawlan ambalo humaanisha kutoa Kauli, Kusema,
Kuashiria au Kuelezea kwa kutumia njia ya kutoa sauti kama inavyosema aya ifuatayo
ambayo inakataza utumiaji wa kauli mbovu zisizokua na maana na hususan inapokua ni
kwa kupaza sauti, pale iliposema:
﴿م َّا يَفْعَلُ ٱهلل َُّ بِعَذَابِكُمْ إِن شَكَرْتمُْ وَآمَنْتُمْ وَكَانَ ٱهلل َُّ شَاكِراً عَلِيماً ۞ لا َّ يحُِ ُّب
ٱهلل َُّ ٱلجَْهْرَ بِٱلس ُّو ۤ ءِ مِنَ ٱلْقَوْلِ إِلا َّ مَن ظُلِمَ وَكَانَ ٱهلل َُّ سمَِيعاً عَلِيماً ﴾
Ma yafAAalu Allahu biAAadhabikum in shakartum waamantum wakana Allahu
shakiran AAaleeman, La yuhibbu Allahu aljahra bialssoo-i mina alqawli illa
man dhulima wakana Allahu sameeAAan AAaleeman (Surat An Nisaa 4:147-148)
Tafsir: Kwa nini Allah Subhanah wa Taála akuadhibuni nyinyi wakati Mmemshukuru
na Kumuamini. Na hakua Allah isipokua ni mwingi wa Kukubali, kuridhia na
kuthamini na Mwenye kujua kila kitu. Hapendi Allah uovu unaowekwa wazi kwa njia
ya kauli ya kupaza sauti, isipokua kwa yule aliedhulumiwa. Na hakika Allah ni mwingi
wa kusikia na mwingi wa ujuzi.
Naam aya mbili hizi zimetumia neno Shakartum na neno Jahara ambapo Hali ya
kuonesha Shukrani mbele ya Allah Subhanah wa Taála ni katika kumjua kwake na
Rehma zake ndani ya Nyoyo zetu, na kuthibitisha kwa njia ya Kauli na katika vitendo
vyetu. Sasa tunapozungumzia neno Shakartum ambalo ni lenye kutokana na Jina la Sifa
Tukufu ya Allah Subhanah wa Taála ambalo ni Shakir ambalo hua linamaanisha Mwingi
wa kukubali, kuridhia na kuthamini yale anayofanyiwa na Waja wake wanaompenda,
yaani hapa tunazungumzia kulingana na uhusiano baina ya Muumba kwa Kiumbe wake.
Ama tunapozungumzia kuhusiana na Kiumbe kwa Mja wake basi neno Shakir hua
linamaanisha Kukubali na kushukuru Rehma za Muumba juuu yake.
Hivyo aya inayofuatia ambayo ndio imetumia neno Jahara ambalo hua linamaanisha
kusema kwa Kupaza Sauti. Hivyo Allah Subhanah wa Taála anaweka wazi kua
54
hakubaliani na kauli mbovu zinazotolewa kwa kupaza sauti na Wanafiq, lakini hata hivyo
baadhi ya wakati mtu anapopandishiwa sauti basi inaruhusika kurudisha majibu ya kauli
hizo, hivyo aya hii inaweka wazi kua Allah Subhanah wa Taála anachukia Kauli mbovu.
Ambapo Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al
Qurtubi basi yeye anasema juu ya maana ya ayah hii ni kua: ‘Hapa kwanza inabidi
tuiangalie hali ya sharti la Illa yaani ‘Isipokua’, kisha ndio tunaangalia maana ya
aya yote kwa ujumla na hivyo kuona kua Ni mwenye kufanya Dhulma tu ndie
ambae hua ni mwenye kupaza sauti katika uovu.’
Allah Subhanah wa Taála anahoji kuhusiana na utumiaji bora wa mawasiliano ya kauli
katika Surat Fusilat kua:
﴿وَمَنْ أَحْسَنُ قَوْلاً ممِّ َّن دَعَآ إِلىَ ٱهلل َِّ وَعَمِلَ صَ ا لحِاً وَقَا لَ إِن َّنىِ مِ نَٱ لْمُسْلِمِينَ ﴾
Waman ahsanu qawlan mimman daAAa ila Allahi waAAamila salihan waqala
innanee mina almuslimeena (Surat Fusilat 41:33)
Tafsir: Na ni nani mwenye kauli bora, zaidi ya yule anaewaita watu kwa Allah, na
akafanya mema na akasema: Hakika mimi ni Miongoni mwa Waisalam.
Katika kuilezea ayah hii basi anasema Hasan Al Basri kua: ‘Huyu hua ni mtu
anaependwa na Allah Subhanah wa Taála, ni mtu aliechaguliwa, na ndie
anaependwa na Allah Subhanah wa Taála zaid ya watu wote hapa duniani, kwani
yeye hua ni mwenye kuitikia wito wa Allah Subhanah wa Taála, na hivyo hua ni
mwenye kufanya mema na kusema kua: ‘Mimi ni miongoni mwa Waislam’ huyu
hua ndie Khalifa wa Allah hapa Ulimwenguni.’
Ama kwa upande wa Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari basi yeye
anasema kua: ‘Alie bora kwa Kauli ni yule ambae, anaewaongoza watu kumuelekea
Mola wao. Ibada zake na Sunna zake, na mwenye kujilinda juu ya makatazo ya
Mola wake, na anaeongoza katika Idama (Msisitizo) na Istiqama (Msimamo Thabit)
mbele ya Allah, na hivyo hua ni mwenye msimamo kutokana na khofu ya Khatma
yake. Na hua ni mwenye kua katika Tariqat al Wusta (Njia ya kati na kati), na kua
katika Jadda Mustaqima (Njia ilinyooka) ambayo ila atakaeifuta basi atakua
Salama, ambayo ni njia itakayompelekea kila atakae kua mbali nayo na kujawa na
Nadama (Majuto)’
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari ametumia neno Tariqat Wusta
yaani Njia ya Msimamo wa Kati na Kati, kwani Ummah wa Kiislam unajulikana kwa
55
kua na sifa ya Ummatan Wasatan yaani Ummah wenye kufuata misimamo ya kati kati
bila ya kua ni wenye Ghuluw yaani kuvuka mipaka kwa kua na misimamo mikali katika
mambo yao na bila ya kua ni wenye Tafrit yaani kuvuka mipaka kwa kudharau mambo
yao.
Kwani Waislam ni wenye kutumia kauli nzuri, Allah Subhanah wa Ta’ala
anatuthibitishia kua walioamuamini yeye na wakawa wanafanya mema watakua ni wenye
kulipwa Pepo kwani wao ndio wale ambao walioongozwa kutokana na kauli njema kwa
kusema:
﴿إِن َّ اهلل َّ يُدْخِ لُ ال َّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الص َّ الحَِاتِ جَن َّاتٍ تجَْرِي مِنْ تحَْتِهَا
يحَُل َّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِنْ ذَهَبٍ وَلُؤْلُؤًا وَلِبَاسُهُمْ فِيهَا حَرِيرٌ
الط َّيِّبِ مِنَ الْقَوْلِ وَهُدُوا إِلىَ صِرَاطِ الحَْمِيدِ﴾
وَهُدُوا إِلىَ
الأَْنْهَاُر
۞
Inna Allaha yudkhilu alladheena amanoo waAAamiloo alssalihati jannatin tajree
min tahtiha al-anharu yuhallawna feeha min asawira min dhahabin walu/lu-an
walibasuhum feeha hareerun; Wahudoo ila alttayyibi mina alqawli wahudoo ila
sirati alhameedi (Surat Al Hajj 22:23-24)
Tafsir: Hakika Allah atawaingiza wale waliomuamini na wakafanya mambo mema
katika Bustani (Peponi) ambazo chini yake kuna mito ambamo watapambwa ndani
yake kwa makoja ya Dhahabu na Lulu na nguo zao zitakua za Hariri. Na
Wameongozwa kutokana na (utumiaji) bora miongoni mwa kauli na wakaongozwa
katika njia iliyonyooka.
Hivo ni baadhi tu ya mifano ya umuhimu wa kauli nzuri, iliyotajwa katika Qurán, lakini
tukifuatilia kwa makini basi tunaona kua Qurán imetumia asili ya neno Qulu katika hali
tofauti mara 1726 ikiwemo pale ilipotilia mkazo umuhimu wa kutovuka mipaka katika
mawasiliano baina yetu kwa njia ya kauli na kututaka kua na misimamo bora ya kati na
kati hata katika mazungumzo yetu na hivyo kuzijumuisha kauli tofauti katika aina 6 za
kauli bora ambazo ni:-
1. Qawlan Sadida
2. Qawlan Baligha
3. Qawlan Ma'rufan
4. Qalan Karima
5. Qawlan Layyina
56
6. Qawlan Maysura.
Katika kipindi ambacho Waislam tumezungukwa na mitihani katika kila upande ambayo
inayotupelekea kuhitaji kuthibitisha zaidi Imani na kumtegemea zaidi Allah Subhanah
wa Ta’ala katika maisha yetu na hivyo kuwa na uwezo wa kujilinda na madhara ya
viumbe na mitihani katika mazingira yetu na pia katika mazingira ya waliotangulia kabla
yetu, basi Qur’an haikutufunza namna ya kua na kauli nzuri tu bali pia Qur’an
imetuamrisha pia kujifunza kwa vitendo kwa kutumia njia ya kutembea katika maeneo
mbali mbali ardhini, kwani amesema Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
﴿وَمِنْ آَتِهِ أَنْ خَلَقَكُمْ مِّن تُ رَابٍ ثمُ َّ إِذَآ أَنتُمْ بَشَرٌ تَنتَشِ رُونَ ﴾
Wamin ayatihi an khalaqakum min turabin thumma idha antum basharun
tantashiroona (Surat Rum 30:20)
Tafsir: Na Miongoni mwa Dalili mwake ni kua amekuumbeni nyie kutokana na
Udongo kisha mkawa katika Maumbo ya Watu Mliotawanyika na kutembea.
MANUFAA YA KUTAWANYIKA NA KUTEMBEA ARDHINI
KULINGANA NA QUR’AN.
Ni jambo lililowazi kua bila ya shaka Qurán imebeba kila aina ya ujumbe wenye manufaa
kwa ajili yetu ndani yake, na miongoni mwa mambo hayo yenye manufaa ni namna ya
kutembea ardhini kwa ajili ya kuzingatia hali na maumbile ya vitu mbali mbali vilivyomo
ndani yake na ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala akatutaka kutokua na Kibr katika
wakati wetu hapa Ulimwenguni kwani kufanya hivyo hakutotunufaisha wala
hakutotupelekea kuzingatia malengo ya kuumbwa kwetu na vinavyotuzunguka katika
mazingira yetu kama zinavyosema aya:
﴿وَلاَ تمَْشِ فىِ ٱلأَرْضِ مَرَ حاً إِن َّكَ لَن تخَْرِقَ ٱلأَرْضَ وَلَن تَبْلُغَ ٱلجِْبَالَ طُولاً ﴾
Wala tamshi fee al-Ardhi marahan innaka lan takhriqa al-ardha walan tablugha
aljibala toolan (Surat Al Isra 17:37)
57
Tafsir: Na msitembee juu ya Ardhi kwa madaha, kwani kwa hakika kamwe hamtoweza
kudidimia ndani ya ardhi, na wala hamtoufikia urefu wa milima.
Tunapoiangalia aya hii basi tunaona inatuonesha kua Ibn Adam tunatakiwa kua
wanyenyekevu na kamwe hatutakiwi kuishi maisha ya kujiona kwa kutembea kwa
madaha, kudunda au kwa ubabe kwani kufanya kwetu hivyo hakuto ipelekea Ardhi kua
ni yenye kutoboka na sisi kudidimia ndani yake na wala hakutopelekea kua warefu kiasi
ya kuufikia urefu wa milima, kwani kuna wengi waliokuja kabla yetu ambao nao walikua
wakijiona na kua na Kibr, lakini hata hivyo nao wakawa ni wenye kuacha kila kitu
Duniani kama walivyokikuta.
Na haya pia ndio maneno ambayo Luqman Al Hakim alitumia kumuusia Mtoto wake
kama inavyoelezewa katika Surat Luqman na aya zifuatazo:
﴿وَلاَ تُصَعِّ رْ خَد َّكَ لِلن َّاسِ وَلاَ تمَْشِ فىِ ٱلأَرْضِ مَرَحاً إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يحُِب ُّ كُل َّ مخُْ تَالٍ
فَخُورٍ۞ وَٱقْصِدْ فىِ مَشْيِكَ وَٱغْضُضْ مِن صَوْتِكَ إِن َّ أَنكَرَ ٱلأَصْوَاتِ لَصَوْتُ
ٱلحَْمِيرِ ﴾
Wala tusaAAAAir khaddaka lilnnasi wala tamshi fee al-ardhi marahan inna Allaha
la yuhibbu kulla mukhtalin fakhoorin, Waiqsid fee mashyika waoghdud min
sawtika inna ankara al-aswati lasawtu alhameeri (Surat Luqman 31:18-19)
Tafsir: Na usigeuze uso wako kwa kujiona, na wala usitembee kwa madaha. Kwani
kwa hakika Allah hawapendi wenye kujivuna kwa fakhari. Na usiwe ni mwenye
haraka katika kutembea kwako, na punguza sauti yako, kwani sauti kubwa
inayochukiza ni sauti ya Punda.
Hivyo kabla ya mtu kua na Kibr na hivyo kutembea kwa madaha kutokana na uzuri wako,
mamlaka yako, mali zako, Ilm yako n.k basi inabidi kutafakkar ni nini kilichowafika wale
waliotangulia kabla yetu na hii ndio miongoni mwa sababu ambazo Allah Subhanah wa
Ta’ala akatuhimiza kutembea ardhini kwa unyenyekevu ili kupata kuona na kuzingatia
mazingira ya Ulimwengu katika aya takriban 14 ambazo zimetumia neno Nadhara.
Neno Nadhara kwa Lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kuona, Kuangalia, Kutizama
kwa kituo, Mtizamo, Kuchunguza, Kufikiria, Kusubiri, Kusubiri ili upate kuona au
kuthibitisha, Kufuatilia kwa umakini kwa kutumia macho, Kutafuta, Kuzingatia na pia
humaanisha Kutafakkar. Wenye Lugha yao hua wanasema Nadharat FiiHi yaani Angalia
Uone!
58
Neno Nadhara ndio lililotoa neno Undhuru ambalo ni lenye kumaanisha Angalia
Uzingatie, Ili kufahamu zaidi basi na tuangalie mfano unaofafanua wazi maana ya neno
Undhuru katika ifuatayo ambayo imetumia neno Undhurna:
﴿َأَي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ لاَ تَقُولُواْ رَاعِنَا وَقُولُواْ ٱنْظُرَْ وَٱسمَْعُواْ وَ لِلكَافِرِينَ عَذَابٌ
أَلِيمٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo la taqooloo raAAina waqooloo undhurna
waismaAAoo walilkafireena AAadhabun aleemun (Surat Al Baqara 2:104)
Tafsir: Enyi Mlioamini! Msiseme (Kumwambia Rasul Allah Salallahu A’layhi wa
Salam) Raina semeni Undhurna na Sikilizeni! Na kwa Waliokufuru ni juu yao
Adhabu kali.
Ambapo tunaona kua anasema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Waarabu
walikua wakipenda kutumia neno Raina (lenye kumaanisha kua Tuangalie), hivyo
Mayahudi waliposikia Waarabu wakitumia neno hilo pamoja na Rasul Allah
Salallahu A’layhi wa Salam, basi nao wakalipenda, kwa sababu neno Raina hua ni
lenye kumaanisha matusi kwa lugha ya Kiyahudi, (Ambapo kwa Lugha ya Kiarabu
pia hua linamaanisha Mchungaji wa Wanyama wetu, na pia Mtu Mjinga na Laghai)
Hivyo Mayahudi wakasema: ‘Zamani tulikua tukimtukana Muhammad kisiri siri,
hivyo sasa hivi tunaweza kumtukana wazi wazi kwa kutumia hili neno Raina
ambalo limo katika Lugha yao.
Hivyo wakawa wanakuja mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
kusema: ‘Ya! Muhammad Raina!’ kisha wanaanza kucheka! Siku moja walipokuja
akawepo Sa’ad Ibn Ubadah Radhi Allahu Anhu ambae ni miongoni mwa Ansari
mwenye kujua maana ya neno Raina kama walivyokua wakikusudia Mayahudi.
Hivyo Sa’ad Ibn Ubaidah Radhi Allahu Anhu akawaambia: ‘Enyi Maadui wa Allah!
Allah akulaanini nyie. Hakika mimi nnaapa kwa yule ambae ndani ya Mamlaka
yake imo Roho ya Muhammad Rasul Allah Salallahu Alyhi wa Salam. Kua kama
nikimsikia mtu yeyote yule anatumia tena neno hilo, basi Wa Allahi nitamkata
kichwa chake!’
Mayahudi hao nao wakapinga na kusema: ‘Lakini jee nyinyi hamtumii neno hilo?’
hivyo basi baada ya majibishano hayo ndio Allah Subhanah wa Taála akashusha
aya hio.’’
59
Hivyo neno Raina lina maana zenye utata ndani yake kwani hua halina maana ya
kutizama kwa ulazima wa kuona tu pekee. Lakini neno Undhurna maana yake ni kua:
‘Tuangalie kwa kituo ili Utuone au Tusubiri’, na ukweli ni kua kutokana na kua na
maana hio ya Kuangalia au Kutizama kwa ajili ya Kuona kwa kituo na mazingatio kwa
ajili ya kupata mafundisho na manufaa yaliyomo ndani ya kinachoangaliwa, basi Qurán
imetilia mkazo Kuangalia kwa ajili ya Kuona na Kutafakkar katika aya nyingi ndani yake
na kwa kuzungumzia mambo mengi ndani yake na hivyo kuzijumuisha pamoja aina tatu
muhimu za Safari kwa ajili ya Kuona ambazo ni:
Aina ya kwanza: Ni ile iliyoainishwa katika aya ambazo zimezungumzia Safari lakini
hazikutumia neno Undhuru, na hizi ni zile aya ambazo zinazungungmzia habari na Visa
vya Mitume na Manabii wakiwemo Nabii Nuh, Nabii Ibrahim, Nabii Musa, Dhul
Qarnayn, Al Khidhr, Nabii Yaqub, Nabii Yusuf, Nabii Sulaiman, Malqia Bilqis, Nabii
Yunus, Maryam Bint Imran, Nabii Isa, As-hab Al Kahf, Uzayr n.k.
Ambapo ndani yake zimewazungumzia watu wema hawa ambao ni miongoni mwa
mifano ya kuigwa mbele yetu. Haina haja kwetu sisi kuzianisha aya hizi kwa sababu
tutazizungumzia baadhi yake katika kurasa za mbele za kitabu wakati tukielezea maisha
ya Ulu ul Azmi Minna Rusul ambayo ndio mada kuu ya Kitabu chetu.
Aina ya Pili: Ni ile iliyoainishwa katika aya ambazo zinatuamrisha sisi kutembea ardhini
kwa malengo na makusudio ya kujifunza mambo mbali mbali tangu kuanzia kwa Viumbe
vya Ulimwenguni, Uwezo na Maajabu yao ya hadi kufikia katika kuona Uwezo Mkubwa
na Maajabu ya Muumba wa Ulimwengu wote na kila kitu kilichomo ndani yake. Aya hizi
hua zina malengo ya kututanua kiakili na kututayarisha kiufahamu na kutufunza juu ya
namna ya kukabiliana na mitihani na mambo mengine yaliyo mbele yetu kwa kua na
subra na ustahamilivu kama vile walivyokua wale waliotangulia kabla yetu ambao ni
miongoni mwa Waliomuamini Allah Subhanah wa Taála na pia miongoni mwa wale
ambao hawakumuamini, kwa mfano katika Surat Al Imran pale aliposema:
﴿قَدْ خَلَتْ مِنْ قَبْلِكُمْ سُنَنٌ فَسِ يرُواْ فىِ ٱلأَرْضِ فَٱنْظُرُواْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ
ٱلْمُكَذِّبِينَ ﴾
Qad khalat min qablikum sunanun faseeroo fee al-Ardhi faondhuroo kayfa kana
AAaqibatu almukadhdhibeena (Al Imran 3:137)
60
Tafsir: Kwa hakika yamewafika mengi waliokuja kabla yenu (Walioamini na
Wasioamini), hivyo tembeeni katika Ardhi ili mpate kuona ni upi ulikua mwisho wa
wale waliokadhibisha.
Na mfano wa aya zinazohimiza kusafiri ili kupata vithibitisho juu ya Ukubwa wa Allah
na Uwezo wake katika Kuumba kwake ni pamoja ile isemayo:
﴿قُلْ سِ يرُواْ فىِ ٱلأَرْضِ فَٱنظُرُواْ كَيْفَ بَدَأَ ٱلخَْلْقَ ثمُ َّ ٱهلل َُّ يُنشِ ئُ ٱلن َّشْأَةَ ٱلآخِ رَةَ إِ َّن
ّ ل شَ يْ ءٍ قَدِيرٌ ﴾
ٱهلل ََّ ٰ عَلَى كُ ِ
Qul seeroo fee al-Ardhi faondhuroo kayfa badaa alkhalqa thumma Allahu yunshio
alnnash-ata al-akhirata inna Allaha AAala kulli shay-in qadeerun (Al-Ankabut
29:20)
Tafsir: Sema: Tembeeni katika Ardhi na mpate kuona (namna Allah) alivyoanzisha
Uumbaji wake, na kisha Allah atawafufua viumbe kesho Akhera. Kwa Hakika Allah
ni muweza juu ya kila kitu.
Bia ya shaka Allah Subhanah wa Ta’ala hamuamrishi tu kila Ibn Adam kutembea ili
apate kujifunza kwa kuona lakini pia anatutilia mkazo zaidi sisi Waislam, tuliomuamini
juu ya jambo hilo. Aya inayofuatia pia ni miongoni mwa mifano mwa aya hizo.
﴿قُلْ سِ يرُواْ فىِ ٱلأَرْضِ فَٱنْظُرُواْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ ٱل َّذِينَ مِن قَبْلُ كَانَ أَكْثَرُهُمْ
م ُّشْرِكِينَ ﴾
Qul seeroo fee al-ardi faondhuroo kayfa kana AAaqibatu alladheena min qablu
kana aktharuhum mushrikeena (Ar-Rum 30:42.)
Tafsir: Sema (Ewe Muhammad): Tembeeni katika Ardhi na mpate kuona ni upi ulikua
mwisho wa wale waliokuja kabla yenu. Walikua wengi wao ni Washirikina.
Aina ya Tatu: Ni ile iliyoainishwa katika aya ambazo zinawahoji wale ambao
hawatembei ardhini wakaona yaliyowafika wale walikuja kabla yao, ama kwa ujumla
basi aya za kundi hili la tatu zinawashutumu wale ambao hawakumuamini Allah
61
Subhanah wa Ta’ala, Mitume wake na vitabu vyake na hivyo kua ni wenye kupingana
na maamrisho ya Mola wao kutokana na ujinga wao kwa mfano pale Qurán iliposema:
﴿أَوَلمَْ يَسِ يروُاْ فىِ ٱلأَرْضِ فَيَنظُرُواْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ ٱل َّذِينَ كَانُواْ مِن قَبْلِهِمْ كَانُواْ
هُمْ أَشَد َّ مِنْهُمْ قُو َّةً وَآاثَراً فىِ ٱلأَ رْضِ فَأَخَذَهُمُ ٱهلل َُّ بِذُنُوهبِِمْ وَمَا كَانَ لهَُ م مِّنَ ٱهلل َِّ
مِن وَاقٍ ﴾
Awa lam yaseeroo fee al-ardhdhi fayandhuroo kayfa kana AAaqibatu alladheena
kanoo min qablihim kanoo hum ashadda minhum quwwatan waatharan fee al-
Ardhi faakhadhahumu Allahu bidhunoobihim wama kana lahum mina Allahi min
waqin (Surat Ghafir 40:21)
Tafsir: Jee hawakutembea juu ya Ardhi na wakaona, yalivyokua mabaki ya
waliotangulia kabla yao? Walikua na wingi wa kinguvu na kiathari walizoacha
ardhini zaidi yao. Lakini akawapa adhabu Allah kwa dhambi zao na hawakua na wa
kuwasaidia dhidi ya Allah.
Na vile vile ikasema tena katika Sura hio hio:
﴿أَفَلَمْ يَسِ يرُواْ فىِ ٱلأَرْضِ فَيَنظُرُواْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ ٱل َّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۤ كَانُواْ أَكْ ثَرَ
﴾
ن ِم ْ هُ مْ وَأَشَد َّ قُو َّةً وَآاثَراً فىِ ٱلأَرْضِ فَمَآ أَغْنىَٰ عَنْهُم م َّا كَانُواْ يَكْسِ بُونَ
Afalam yaseeroo fee al-Ardhi fayandhuroo kayfa kana AAaqibatu alladheena min
qablihim kanoo akthara minhum waashadda quwwatan waatharan fee al-Ardhi
fama aghna AAanhum ma kanoo yaksiboona (Surat Ghafir 40:82)
Tafsir: Jee hawakutembea juu ya Ardhi na wakaona, yalivyokua mabaki ya
waliotangulia kabla yao? Walikua wengi zaid yao na wenye uwezo mkubwa kinguvu,
na katika athari zao walizoacha katika ardhi, lakini hata hivyo kila kitu chao
walichokua nacho hakikua ni chenye kuwasaidia.
Hapa wale wasioamini wanatakiwa kutafakkar yale mambo ambayo yaliwafika watu
waliotangulia kabla yao ambao wao walikua ni wakubwa kimaumbile na kinguvu pia
kiasi ya kua athari zao walizoacha hadi hii leo bado zipo na zimekua ni miongoni mwa
62
maajabu ya Dunia, kwa mfano: Piramidi za Misri, Makasri, Ngome na Majumba
waliyoyajenga kwa kuchonga Milima ya mawe nchini Afghanistan, Iran, Iraq, Syria,
Jordan, Yemen n.k kwa kutumia utaalamu na zana ambazo hadi hii leo bado Wanasayansi
wa karne yetu hawajajua ni zana gani za karne hizo zinazochonga mawe kama zana za
karne yetu, kiasi ya kua ukiona athari zake basi lazima utastaajabu, kutokana na ukubwa
na umadhubuti wa Matofali, Mawe na Urefu wa Nguzo na Minara waliyojenga
kimpangilio kulingana na mpangilio wa nyota na sayari za angani, ambapo uzuri wa
Nakshi na mapambo yake baadhi miongoni mwa Majengo hayo hua ni kama yenye
kuonekana kama yamechongwa kwa kutumia mashine maalum za katika kipindi chetu
cha wakati wa maendeleo kutokana na unadhifu wake.
Lakini hata hivyo Ukubwa wao, Nguvu zao, Maarifah yao, Ujuzi wao, Utaalamu wao,
Mali zao, Majumba yao, Mafanikio ya athari zao walizokua nazo na kubakia hadi hii leo
basi vyote hivyo havikuwasaidia kitu, kwani kumsahau kwao Mola wao na kuenda
kinyume na maamrisho yake ndiko kulikosababisha kushushiwa adhabu kwao kupata
maangamizo yao kama inavyosema aya inayofuatia ya Surat Muhammad 47:10 ambayo
pia ni miongoni mwa mifano ya aya za Fayandhuru:-
﴿أَفَلَمْ يَسِ يرُواْ فىِ ٱلأَرْ ضِ فَيَنظُرُواْ كَ يْفَ كَ انَ عَاقِبَةُ ٱل َّذِينَ مِ ن قَبْلِهِمْ دَم َّرَ ٱهلل َُّ
عَلَيْهِمْ وَلِلْكَافِرِينَ أَمْثَالهَُا﴾
Afalam yaseeroo fee al-ardi fayandhuroo kayfa kana AAaqibatu alladheena min
qablihim dammara Allahu AAalayhim walilkafireena amthaluha (Surat Muhammad
47:10)
Tafsir: Jee hawajatemea ardhini, na hivyo wakaona ni upi ulivyokua mwisho wa wale
ambao waliotangulia kabla yao (Waliokua wakifanya maovu) hakika aliwashushia
Allah juu yao maangamizo, na kwa makafiri yatawakuta mithili yake.
Ingawa Allah Subhanah wa Ta’ala anawataka Ibn Adam katika aya hizo za Safari zenye
malengo ya kujifunza lakini wale wajinga wasiojua miongoni mwetu wamekua katika
mstari wa mbele katika jitihada za kufuta athari za watu hawa waliotangulia kabla yetu
na ambao tumetakiwa kujifuza kutoka kwao tena kupitia katika aya zilizowazi kama
tunavyoona katika mifano ya aya hizo.
Inasikitisha kuona kua Watu wanaojiita Waislam tena walioamini kua wanavamia
miji ya Zamani ya Kihistoria na kisha kuvunja na kubomoa Majengo na Athari
mbali mbali za Kihistoria zilizozungumziwa kwenye Qurán, hususan katika Ardhi
ya Mashariki ya Kati kwani Miskiti mingi ya Kihistoria za watu Watukufu, kama
63
Mawalii, Masahaba, Maimamu n.k imeripuliwa kwa mabomu kwa mfano Masjid
Khalid Ibn Walid wa Mjini Homs nchini Syria, Mji wa Palmira, nchini Iraq mji wa
Nimrudh, nchini Libya mji wa Cyrene uliojengwa na Warumi miaka 630 kabla ya
Nabii Isa, nchini Yemen katika mji wa Barqaish, nchini Afghanistan, Lebanon,
Palestina, Miskiti na Maktaba za Mji wa Timbuktu, nchini Mali n.k
Watu hawa wasiojua hua wanatumia kisingizio cha ile hadith ya Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam isiemayo kua: ‘Msifunge safari kwa malengo ya kutembelea Miskiti
isipokua katika Misikiti Mitatu, Misikiti huu (Masjid An Nabbawi wa Madinah ),
Masjid Al Haram wa Makkah na Masjid Al Aqsa’(Sahih Bukharin a Muslim)
Huku ni kutofaham maana halisi ya Hadhith hio kwani anasema Al Hafidh Imam Zayn
Ad Din Abd Rahim Al Iraqi kua: ‘Miongoni mwa maana nzuri iliyobebwa na Hadith
hii, ni kukatazwa kwa malengo ya kutembelea Miskiti husika. Lakini, kutembea
kwa malengo ya Kutafuta I’lm, Kumtembelea Mtu Mtakatifu, Rafiki au Jamaa, au
kwa Malengo ya kufanya Biashara, Kuuburudisha Moyo, Kujizidishia Iman n.k
basi inaruhusiwa kwani hayo hayajajumuishwa ndani ya Hadith hii, na hili
linafafanulika vizuri zaidi na Hadith nyengine ya Abu Said Al Khudri ambae
anasema kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua : ‘Hairuhusiki
kwa mtu, kutembelea Miskiti kwa malengo ya Kusali ndani ya Msikiti huo, isipokua
kwa ajili ya Miskiti mitatu: Masjid Al Haram (Makkah), Masjid Al Aqsa na Misikiti
wangu huu (Masjid An Nabbawi wa Madinah ),’’’’((Musnad Imam Ahamd, Musannaf
Ibn Shaybah) Al Hashiyah Minhaj Al Tulab – Imam Al Jamal Shaykh Sulaiman Ibn
Mansur)
Na akasema Mujaddid Ad Din Imam Taj Ad Din Al Subki kua: ‘Hakuna sehemu juu ya
mgongo wa Ardhi ambayo iliyokua haina Utukufu wake, kwa ajili ya mtu
kutembelea sehemu hio kutokana na Utukufu husika, isipokua sehemu hizi (Masjid
Al Haram, Masjid Al Aqsa na Masjid An Nabbawi wa Madinah ). Na nnaposema
Utukufu wa sehemu husika, basi hua nnakusudia juu ya ule Utukufu uliothibitishwa
na Sharia za Kiislam. Ambapo Mtu hatakiwi kutembelea sehemu kwa ajili ya
Utukufu wa Sehemu hio husika, bali kwa sababu ya kutafuta I’lm, kwa kutembea,
au kwa sababu nyengine yeyote ile inayokubalika Kisharia. Wale ambao
wanaopinga juu ya hilo basi hua ni wenye kukosea katika Imani yao, kwani
kutembelea Msikiti husika hua kunatokana kwa ajili ya wale waliomo ndani ya
Msikiti husika, na si kwa ajili ya Msikiti husika. Hivyo Hadithi hii imepinga
kutembelea Miskiti kama Miskiti isipokua kwa ajili ya Miskiti Mitatu hio husika.
Lakini kufunga safari kwa sababu ya kumtembelea Mtu, au kwa sababu ya
kutafuta I’lm, basi hua si kwa sababu ya Msikiti huo, bali hua ni kwa ajili ya wale
waliomo kwenye Msikiti huo) (Hashiyah Minhaj Al Tulab – Imam Al Jamal Shaykh
Sulaiman Ibn Mansur)
64
Tumalizie sehemu hii kwa kuangalia aya ya Fayandhuru inayofuata ambayo kutokana
na ujumbe wake basi tunaona kua, Allah Subhanah wa Ta’ala anatuainishia tena
umuhimu wa kutembea pia kwa ajili ya kuona na kufahamu madhara yaliyowafika wale
waliokua ni wenye kupingana na Ujumbe wa Mitume wake kwani kupinga kwa watu hao
baada ya kuwekewa vithibitisho vilivyowazi hakukua na faida yeyote kwao wao na
badala yake ilikua ni kujitia maangamizo na hivyo kua ni wenye kujidhulumu wao
wenyewe, kama inavyoweka wazi aya ifuatayo:
﴿أَوَلمَْ يَسيرُواْ فىِ ٱلأَرْضِ فَيَنظُرُواْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ ٱل َّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ كَانُ و ۤ اْأَشَد َّ
مِنْهُمْ قُو َّةً وَأَاثَرُواْ ٱلأَرْضَ وَعَمَرُوهَآ أَكْثَرَ ممِ َّا عَمَرُوهَا وَجَآءَتْهُمْ رُسُلُهُم بِٱلْبَيِّنَاتِ
فَمَا كَانَ ٱهلل َُّ لِيَظْلِمَهُمْ وَلَٰكِن كَ انُو ۤ اْ أَنفُسَ هُمْ يَظْلِمُونَ ﴾
Awa lam yaseeroo fee al-Ardhi fayandhuroo kayfa kana AAaqibatu alladheena min
qablihim kanoo ashadda minhum quwwatan waatharoo al-ardha waAAamarooha
akthara mimma AAamarooha wajaat-hum rusuluhum bialbayyinati fama kana
Allahu liyadhlimahum walakin kanoo anfusahum yadhlimoona (Surat Rum 30:9)
Tafsir: Jee hawatembei ardhini na kuona mwisho wa wale ambao waliotangulia kabla
yao, walikua wakubwa zaidi yao kinguvu, na wakawacha athari zao katika ardhi, na
wakaijaza Ardhi kuliko walivyofanya hawa, na wakaja kwao wao Mitume wenye
vitibitisho vilivyowazi. Hakika Allah hakuwadhulumu, bali wao ndio waliokua
wakijidhulumu.
Hakika watu hao waliotangulia walikua ni kama sisi yaani wenye Nyoyo, Macho na
Masikio na kadhalika lakini hata hivyo wao walikua ni miongoni mwa waliojidhulumu
kutokana na kutumia sivyo neema za viungo vyao hivyo muhimu walivyopewa na Mola
wao aya inayofuatia inaweka wazi juu ya jambo hilo.
﴿أَفَلَمْ يَسِ يرُواْ فىِ ٱلأَرْضِ فَتَكُونَ لهَُمْ قُلُوبٌ يَعْ قِلُونَ هبَِآ أَوْ آذَانٌ يَسْمَعُونَ هبَِا
فَإِن َّهَا لاَ تَعْمَى ٱلأَبْصَارُ وَلَٰكِن تَعْمَى ٰ ٱلْقُلُوبُ ٱل َّتىِ فىِ ٱلص ُّدُورِ ﴾
Afalam yaseeroo fee al-Ardhi fatakoona lahum quloobun yaAAqiloona biha
aw adhanun yasmaAAoona biha fa-innaha la taAAma al-absaru walakin taAAma
alquloobu allatee fee alssudoori (Surat Al Hajj 22:46)
65
Tafsir: Jee hawakutembea wao juu ya ardhi? Hawakua wao na nyoyo ambazo ni za
kufahamu na masikio ya kusikilizia? Kwa hakika sio macho yao yanayokua na upofu
wa kutoona bali ni nyoyo ndani ya vifua vyao ndio vilivyokua na upofu.
Moyo wa Ibn Adam unafahamu kulingana na mitizamo ya aina mbili aina ya kwanza ni
ya kuona kwa mtizamo wa ndani ya Moyo ambao ni kwa kupitia kwa njia ya hisia za
kuhisi kwa Moyo na mtizamo wa pili ni mtizamo wa kuona kwa mtizamo wa nje ya
Moyo, hivyo kutembea na kuona kwa mitizamo yote miwili hii, hua kuna manufaa zaid
kwani hupelekea kuuelimisha na kuupumzisha Moyo, Ufahamu na Akili ya Ibn Adam
kama anavyosema Mujaddid ad Din Imam Muhammad Idris al Shafii katika kitabu chake
cha Al Diwan kua:
Uache Mji wako kwa ajili ya kutafuta
Darja kwa kuelimika
Na Safiri. Kwani katika kusafiri kuna
faida Tano.
Kuiwepesishia Mzigo Nafsi na kujitafutia
Maisha yako.
Na I’lmu na Adabu na Marafiki bora.
Kama ikisemwa kua kusafiri ni Madhila
na Ugumu wa mambo.
Na urefu wa kuvuka Majangwa, ugumu
na matatizo.
Basi Kifo ni bora kwa Mtu kuliko
kubakia sehemu moja.
Katika Manyanyaso baina ya Usaliti na
Husda.
تغرب عن الأوطان في طلب العلى
وسافر ففي الأسفار خمس فوائد
تفريج هم واكتساب معيشةٍ
وعلمٍ وآدابٍ وصحبة ماجد
فإن قيل في الأسفار ذل ومحنة
وقطع الفيافي وارتكاب الشدائد
فموت الفتى خير له من قيامه
بدار هوان بين واش وحاسد
Naam neno Undhur basi limetumika pia tena katika Quran pale iliposema:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ ٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ م َّا قَد َّمَتْ لِغَدٍ وَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ إِن َّ ٱهلل ََّ
خَبِيرٌ بمَِا تَعْمَلُونَ ﴾
66
Ya ayyuha alladheena amanoo ittaqoo Allaha waltandhur nafsun ma qaddamat
lighadin waittaqoo Allaha inna Allaha khabeerun bima taAAmaloona (Surat Al
Hashir 59:18)
Tafsir: Enyi Mlioamini, Muogopeni Mola wenu, na Nafsi ijichunguze juu ya kile
ilichokitanguliza kesho, na Mcheni Allah kwani kwa hakika Allah ana habari juu ya
kila mnachokifanya.
Aya inatuwekea wazi kua Ulimwengu tulionao unawakilisha siku ya leo katika Uhai wetu
na Ulimwengu wa Akhera unawakilishwa a siku ya kesho ambayo kwa hakika itakuwepo
kwa kila mmoja miongoni mwetu. Hivyo bila ya shaka kuna umuhimu wa kuziangalia
Nyoyo zetu na kufanya safari ndani yake kama anavyosema Mawlana Jalal Ad Din Al
Rumi kua: ‘Safari hukurudishia nguvu ya mwili, na mapenzi ndani ya Moyo wako.
Hivyo hata kama ikiwa huwezi kusafiri kuelekea kokote basi fanya safari ndani ya
sehemu za Moyo wako’
Hivyo amri ya Undhur imetumika kututaka Ibn Adam kutumia ipasavyo viungo vya miili
yetu yaani Miguu, Ufahamu wa Akili, Macho na mtizamo na ufahamu wa Moyo katika
kutafakkar na kuondoka kutoka katika hatua moja ya maisha duni ya kiimani na kuingia
katika hatua nyengine iliyobora zaid kiimani na hivyo kua ni wenye kupata ridhaa ya
Allah Subhanah wa Ta’ala kwa sababu hua ni wenye kufanya Hijra.
UMUHIMU WA HIJRA KATIKA ISLAM
Neno HIJRA linatokana na neno HAJARA la Kiarabu ambalo hua ni lenye kumaanisha
Kunyangánya kutoka kwa, Kupokonya kutoa kwa, Kuficha, Kudhibiti, Kukataza au
Kuzuia kuingia katika sehemu fulani, kuweka Kizingiti, Kusahaulika, Kuachana na kitu.
Neno Hajara ndio ililotoa neno Hijrun ambalo maana yake hua ni Kitu chochote
kilichokatazwa kufanywa, Ufahamu wa Ibn Adam, na pia likatoa neno Hajar ambalo
maana yake hua ni Jiwe, hivyo Jiwe limeitwa Hajar kwa sababu ya kutokana na kua na
maumbile ya Ugumu wenye kujidhibiti sana.
Neno Hajara ndio lilotoa neno Hijra ambalo pia hua ni lenye kumaanisha kuhama kutoka
katika sehemu moja isiyokubalika, au isiyowezekana kubakia na kuelekea katika sehemu
nyengine, ambapo hali hiyo ya kuhama hua inagawika katika sehemu mbili.
67
Ambapo kwanza ni kuhama kwa watu au mtu kutoka sehemu moja kwa ajili ya kuihami
nafsi yake au dini yake kuelekea sehemu nyengine yenye usalama zaid na aina hii ya
Hijra inazungumziwa na Allah Subhanah wa Taála ndani ya Qurán pale aliposema:
﴿وَمَن يُهَاجِ رْ فىِ سَبِيلِ اهلل َِّ يجَِدْ فىِ ٱلأَرْضِ مُرَاغَماً كَثِيراً وَسَعَةً وَمَن يخَْرُجْ مِن
بَيْتِهِ مُهَاجِ راً إِلىَ ٱهلل َِّ وَرَسُولِهِ ثمُ َّ يُدْرِكْهُ ٱلْمَوْتُ فَقَدْ وَقَعَ أَجْرُهُ عَلىَ ٱهلل َِّ وَكَانَ ٱهلل َُّ
غَفُوراً ر َّحِ يماً ﴾
Waman yuhajir fee sabeeli Allahi yajid fee al-Ardhi muraghaman katheeran
wasaAAatan waman yakhruj min baytihi muhajiran ila Allahi warasoolihi thumma
yudrik-hu almawtu faqad waqaAAa ajruhu AAala Allahi wakana Allahu ghafooran
raheeman (Surat An Nisaa 4:100)
Tafsir: Na yule ambae atakaehama kwa ajili ya Allah Subhanah wa Taála, basi atakuta
katika Ardhi sehemu nyingi sana za kuishi. Na yeyote yule atakaehama kutoka katika
nyumba kuhmia kwa Allah na Mtume wake na kifo kikamkuta basi atayakuta Malipo
yake yapo kwa Allah. Na kwa hakika Allah ni mwingi wa usamehevu na mwingi wa
Rehma.
Neno Hijra halikutumika katika Qurán kumaanisha kuhama kwa ajili ya kujinusuru
kutoka katika Ardhi moja kuelekea katika Ardhi nyengine tu lakini limetumika kuhama
kwa ajili ya kusimamia haki baina ya Mke Muadilifu na Mume Muadilifu pale Allah
Subhanah wa Ta’ala aliposema katika aya ifuatayo:
﴿ٱلرِّجَالُ قَو َّامُونَ عَلَى ٱلنِّسَآءِ بمَِا فَض َّلَ ٱهلل َُّ بَعْضَهُمْ عَلَى ٰ بَعْضٍ وَبمَِآ أَنْفَقُ واْ مِنْ
أَمْ وَالهِِمْ فَٱل َّ صالحَِاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بمَِا حَفِظَ ٱهلل َُّ وَٱللا َّتِى تخََافُو َن
نُشُوزَهُن َّ فَعِظُوهُن َّ وَٱهْجُرُوهُن َّ فىِ ٱلْمَضَاجِ عِ وَٱضْرِبُوهُن َّ فَإِنْ أَطَعْنَكُمْ فَلاَ تَ بْغُواْ
عَلَيْهِ ن َّ سَبِيلاً إِن َّ ٱهلل ََّ كَ انَ عَلِيّاً كَ بِير اً ﴾
Alrrijalu qawwamoona AAala alnnisa-i bima faddala Allahu baAAdahum AAala
baAAdin wabima anfaqoo min amwalihim faalssalihatu qanitatun hafidhatun
lilghaybi bima hafidha Allahu waallatee takhafoona nushoozahunna
faAAidhoohunna waohjuroohunna fee almadajiAAi waidriboohunna fa-in
68
ataAAnakum fala tabghoo AAalayhinna sabeelan inna Allaha kana AAaliyyan
kabeeran(Surat An Nisaa 4:34)
Tafsir: Wanaume ni Qawwamoona (wasimamizi) juu ya Wanawake kwa sababu Allah
amewafadhili baadhi yao (Wanaume) juu ya baadhi yao (Wanawake) kutokana na kile
wanachokichuma na kukitumia juu yao. Hivyo Wanawake wema ni watiifu (kwa Mola
wao na kwa Waume zao wenye kuwasimamia) na hujilinda wanapokua Waume zao
hawapo kile walivyoamrishwa na Allah kujilinda. Ama kwa Wanawake ambao
mnaona kua wanafanya maovu, basi waonyeni (kwanza), (kisha kama hawakusikia
basi) Fanyeni Hijra kutoka katika vitanda vyao, (Na kama hio haijasaidia basi)
wapigeni kidogo, lakini kama wakirudi katika utiifu wenu, basi msitafute njia za
kuwakera. Kwa hakika Allah ni alie Juu zaidi ya Kila kitu na ni Mkubwa sana.
Hapa tunaona kua kwanza aya imetumia neno Qawwam kwa kilugha hua linamaanisha
kusimamia au kuhudumia kitu kwa muda mrefu, hivyo tunapozungumzia kifamilia basi
neno hili hua linajumuisha jukumu la kusimamia kimwili, kimahitaji, kiheshima na
kimajukumu kwa upande wa kidunia na kiakhera.
Hivyo maana ya neno Qawwam hua kamwe haimaanishi kama vile wanavyofikiria watu
wengi kua maana yake ni kudhibiti, kuweka chini yake au chini ya mamlaka yake, kwani
kufikiria hivyo basi hua ni sawa na walivyokua wakifanya jamii za watu wa Jahiliyyah.
Katika kuielezea maana ya aya hii, basi Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakkalimin Imam
Al Ghazali Al Thani Imam Fakhr al Din Al Razi anasema kua sehemu ya aya hii ya Surat
An Nisaa 4:34 ambayo ni: ‘Alrrijalu qawwamoona AAala alnnisa-i (Wanaume ni
wasimamizi wa Wanawake) ina uhusiano na sehemu ya aya nyengine kabla yake
isemayo:
﴿وَلاَ تَتَمَن َّوْاْ مَا
فَض َّلَ ٱهلل َُّ بِهِ بَعْضَكُمْ عَلَىٰ بَعْ ٍض ﴾
Wala tatamannaw ma fadhala Allahu bihi baAAdhakum AAala baAAdhin’ (Surat
An Nisaa 4:32)
Tafsir: Na wala msitamani kile ambacho Allah amewafadhili baadhi yenu kuliko
wengine.
Imam Fakhr Ad Din Al Razi anaendelea kwa kusema: Aya ambayo tulisema kua
ilishushwa kwa sababu baadhi ya Wanawake walitoa kauli kuhusiana na Allah
kuwapendelea Wanaume katika Urithi. Hivyo Allah ameweka wazi katika ayah hii
kua amewafadhili tu Wanaume juu ya Wanawake kwa sababu Wanaume ni
Wasimamizi wa Wanawake. Kwani ingawa wote Mke na Mume wanafaidika na
matunda na haki zinazotokana na kua pamoja, basi Allah amemuamrisha
69
Mwanamme kumlipa Mwanamke sehemu ya ndoa yao, na kumhudumia katika
mahitaji ya kila siku, hivyo ongezeko la upande mmoja hukabiliana na ongezeko la
upande wa pili – na hivyo hua kama vile hamna pendeleo baina yao. Jambo hili
linaweka wazi mpangilio wa namna zilivyopangika aya.’
Hivyo darja ya Qawwam aliyokua nayo mwanamme kwa familia yake hua ni kuilinda,
kuisimania na kuwahudumia A’al, Ahl, Zawj au familia yake katika hali ya kiuadilifu, na
hapa msimamizi husika hua anatakiwa kuitumia fadhila hiyo aliyopewa na Allah
Subhanah wa Ta’ala, kwa kua na umakini, huruma, busara na subra katika kutekeleza
majukumu hayo, kwani vyenginevyo itakua ni kuenda kinyume na matakwa ya mfadhili
na mtoaji wa majukumu hayo na hivyo Mwanamme husika hupoteza haki ya kua na Darja
hiyo ya Qawwam.
Kwa upande wa pili basi tunaona kua Ayah hii ya Surat al Nisaa 4:34 imetumia pia neno
Hijra kwa kuwapa amri Wanaume wenye sifa ya Qawwam kwa wake zao kufanya Hijra
katika vitanda vya wake zao, pale inapokua Waume hao hawatekelezewi haki zao na
Wake zao wasiokua na utiifu kwao. Hivyo ayah hii inawapa haki Wanaume wenye sifa
ya Qawwam kuwapa adhabu Wake zao hao kwa kuwafanyia Hijra.
Ama juu ya Hijra hii basi kuna mitizamo tofauti kwani kuna wasemao kua Hijra hii
iliyomaanishwa hapa ni Hijra ya kutowaingilia Wanawake kwa muda fulani hadi
watakapojirekebisha. Na pia kuna wasemao kua Hijra hii inaamanisha kua wanaweza
kuwaingilia lakini wajizuie na kuwasemesha, na pia kuwapa mgongo wakati wa kulala
kama ikiwa watalala katika kitanda kimoja. Hizo ni miongoni mwa aina za Hijra
zilizotajwa ndani ya Qurán na ambazo Waislam tunatakiwa kuzifanya kwa kutumia
kiwiliwili katika kipindi cha uhai wetu hapa Ulimwenguni.
Ama tunapozungumzia Hijra ya pili basi hua ni ile ya kuhama kutoka katika hali moja
kuenda katika hali nyengine pia, lakini aina hii ya Hijra hufanywa kwa kutumia njia za
Kiroho, Kinafsi, Kiakili na Kifikra kama vile ambavyo Allah Subhanah wa Taála
alipomwambia Rasul Allah Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kua awe na Subra
na anayofanyiwa na Makafiri huku akiwa ni mwenye kuachana nao na kutoshirikiana nao
kwa ukarimu na katika hali nzuri pale aliposema katika Surat Al Muzzamil:-
﴿وَٱصْبرِْ عَلَى ٰ مَا يَقُولُونَ وَٱهْجُرْهُمْ هَجْراً جمَِيلاً ﴾
Waisbir AAala ma yaqooloona waohjurhum hajran jameelan (Surat Al Muzzamil
73:10)
Tafsir: Na kua na Subra (Ewe Muhammad) juu ya kile wanachokisema, na achana
nao kwa muachano mwema.
70
Hivyo Hijra hii ya aina ya pili yaani ya Kinafsi na Kiroho ni Hijra ambayo inajumuisha
pia kuhama kutoka katika hali ya kiza cha maasi na kuingia katika hali nyengine iliyo
bora zaidi ambayo ni hali ya kuingia katika Nuru, Muangaza na kua na Utiifu kwa Allah
Subhanah wa Taála na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Hijra ya aina hii ni Hijra ambayo inahimizwa na kutiliwa mkazo zaid kufanywa kwa kila
mmoja miongoni mwetu katika Dini ya Kiislam. Kwani hii hua ni hali ya kujidhibiti na
matamanio ya Nafsi dhidi ya kuiendekeza Dunia na hivyo kuzirudisha Nafsi katika
kumuelekea na kumtii Allah Subhanah wa Taála na Mtume wake Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam.
Umuhimu wa aina hii ya Hijra katika maisha yetu unathibitishwa na malengo ya
Muumba wetu kutuletea Qur’an ili iwe ndio muongozo wa kila kitu katika Maisha yetu
na hivyo kutakiwa kuifanyia kazi kama ipasavyo Qurán bila ya kuihama, kwani kuihama
Qurán hua ni kuenda kinyume na Imani ya Dini ya Kiislam na hivyo tutakua na masuali
ya kujibu mbele ya Mola wetu kama inavyosema Surat Al Furqan:
﴿وَقَالَ ٱلر َّسُولُ يٰرَبِّ إِن َّ قَوْمِى ٱتخ ََّذُواْ هَٰذَا ٱلْقُرْآنَ مَهْجُوراً ﴾
Waqala alrrasoolu ya rabbi inna qawmee ittakhadhoo hadha alqur-ana
mahjooran (Surat Al Furqan 25:30)
Tafsir: Na atasema Rasul, Ya Rabbi! Hakika kaumu yangu wameichukulia hii Qurán
kua ni Mahame.
Tunapozungumzia hali ya Qur-ána Mahjuran basi ingawa tunaona kua aya
inawazungumzia watu wa Kabila la Quraysh ambao ndio waliokua wakilalamikiwa
katika ayah hii kua hawakuiamini na waliichukulia Qurán kua ni kama hekaya za kale na
mashairi yasiyokua na maana yeyote. Lakini pia ayah hii inavizungumzia vizazi
vilivyofuatia baadae vikiwemo vizazi vilivyokuja kabla yetu, vizazi vyetu na vizazi
vitakavyokuja baada yetu. Vizazi hivyo ingawa ni vizazi vya Kiislam lakini hua
vimeifanya Qurán kua Mahjuran yaani iliyohamwa kwa njia nyingi sana ikiwemo,
Kutoisoma kabisa, Kuisoma lakini bila ya Kuitafakkar na Kuifaham, Kutochukua jitihada
yeyote ile ya kutaka kuifaham, Kutosimamia maamrisho yake, hukmu zake na Sharia
zilizomo ndani yake, Kutoitilia maanani n.k
Ukweli ni kua Waislam hatutakiwi kua ni wenye kuifanya Qurán kua Mahjuran bali
tunatakiwa Dunia ndio tuifanye kua ni Mahjuran, hivyo tunapaswa kufanya Hijra kutoka
kwenye matamanio ya Dunia na kuhamia ndani ya Qurán na kua ni wenye kufanikiwa
kwa kurudi kwa Mola wetu huku tukiwa ni wenye kufuzu kwa kua na Nyoyo zisizokua
na madoa ndani yake kwani Moyo ndio Msingi wa Mja kumjua Mola wake na hivyo ni
kiungo ambacho kinatakiwa kua kisafi na salama ndani nje na ndio maana Waislam
71
tukawa ni wenye kutiliwa mkazo wa kufanya Hijra ya kuachana na maasi na kurudi chini
ya utiifu wa Allah Subhanah wa Taála.
Kwani Anasema Allah Subhanah wa Taála kua:
﴿بَلَى ٰ مَنْ أَسْ لَمَ وَجْهَهُ هلل َِّ وَهُوَ محُْسِ نٌ فَلَهُ أَجْرُهُ عِندَ رَبِّهِ وَلاَ خَوْفٌ عَلَ يْهِمْ وَلاَ
هُمْ يحَْزَنُونَ ﴾
Bala man aslama wajhahu lillahi wahuwa muhsinun falahu ajruhu AAinda rabbihi
wala khawfun AAalayhim wala hum yahzanoon (Surat Al Baqar 2:112)
Tafsir: Bali yeyote yule ambae atausalimisha uso wake kwa Allah, akiwa ni mwenye
kufanya mema, basi malipo yake yapo kwa Mola wake na haina haja kwake kua na
khofu wala kua na huzuni.
Bila ya shaka aya iko wazi kua yeyote yule ambae atausalimisha uso wake na akajitolea
kwa ajili ya Mola wake pekee, na akajisafisha a kutokua na uchafu wa dhambi, akawa
Mcha Mungu, akawa ni mwenye I’lm ya kujua kila anachokifanya katika Ibada zake basi
hua ni mwenye kufanya mema katika mambo yake, basi hawatakua na khofu ya kua ni
wenye kufanyiwa Hajar (Kuachwa, au kusahaulika) na Mola wao kwani kwa hakika
Malipo yao watayakuta kwa Mola wao.
Ayah hii pia imetumia neno Wajh yaani Uso kwa sababu uso ndio sehemu muhimu ya
mwili wa Ibn Adam inayoonekana wazi na ndio inayomtambulisha mtu husika mbele ya
watu wengine na hivyo basi katika Lugha ya Kiarabu neno Wajh hua linawakilisha
muonekano wa mwili mzima wa Ibn Adam, na limetumika mara nyingi sana katika
Qurán kumaanisha kiwiliwili cha Ibn Adam.
Ayah hii pia imetumia neno Muhsin (Mwenye kuufanya Mema kwa kumtii Mola wale)
ambalo hua ni lenye kutokana na neno la Kiarabu Ihsan ambalo Kisharia maana yake hua
ni Kumuabudu Allah kama unamuona, na kama humuoni basi yeye anakuona, hivyo mtu
mwenye sifa ya Muhsin hua ni mtu ambae tayari ameshafanya Hijra ya kurudi kwa Mola
wake na hivyo katika kila analolifanya basi hua anamuona Mola wake na hivyo hua
hatakiwi kua na khofu ya kufanyiwa Hajar na Mola wake bali hua na ukaribu zaidi na
Mola wake kwa sababu mtu anapomkaribia Mola wake kwa hatua moja basi Allah
Subhanah wa Taála humkaribia mtu huyo kwa hatua mbili zaid, sasa katika hali kama
hii basi mtu huyu hua ni mwenye kufanya kila anachokifanya kwa Ihsan na hivyo hua ni
Muhsin katika matendo yake na hua ni Muhsin katika hali yake ya Kimaumbile kutokana
na jitihada zake kwa ajili ya Mola wake zinazotokana na muonekano wa nje wa viungo
vya mwili wake unaojumuishwa na Moyo wake na viungo vyengine vya ndani ya mwili
wake.
72
Mujaddid ad Din, Sultan al Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi anaifafanua maana
ya Muhsin iliyotumika katika ayah hii kwa ile hadith isemayo kua:
”إِنم ََّا الأَْعْمَالُ ابِلنِّي َّاتِ “
Innama al aAmal bi alniyyati
Tafsir: Uhakika wa Amal hutegemea na nia yake.
Kwa kutuambia kua: Nia hua ni kitu ambacho kinatoka ndani ya kina cha Moyo
kutokana na Ikhlas iliyomo katika tendo jema husika, bila ya kuamua kua na
maamuzi juu ya tendo husika. Kwani siku zote mtu alieshiba kamwe hawezi
kuamua tu na kusema kua sasa hivi nna njaa, na akawa na njaa katika wakati
huo huo kama alivyoamua huku akiwa ameshiba, jambo hili hua haliwezekani,
bali mtu huyu humbidi kutafuta njia ya kukitamani chakula kutoka ndani ya
Moyo wake, na njia hio hujulikana kama Nia Sahih ambayo haipatikani hadi
pale mtu huyu atakapoweza kuuthibitishia Moyo wake na Ufahamu wake.
Hivyo Nia ya Muhsin hutokana na kujua na kufahamu malipo yanayotokana na
kitendo husika, huku kukijumuishwa I’lm iliyokuwemo katika kina cha Moyo
kua Allah Subhanah wa Taála ni mwenye uwezo juu ya kila kitu, na hivyo ndie
mwenye uwezo wa kutoa zawadi au kuadhibu na hakuna mwengine anaeweza
kufanya hivyo isipokua yeye. Kila Uthibitisho huu unapokua mkubwa na kua na
nguvu zaidi katika Nafsi na Moyo wa mtu husika kutokana na I’lm ya kujua
hayo basi ndivyo inavyozidi usafi wa Nia ya mtu husika.
Ama kwa upande wa Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Ibn Muhammad Ibn Muhammad
Al Ghazali basi yeye anasema kuhusiana mambo muhimu yanayohitajika katika
kufanikisha Amali njema za Muhsin ni kua:
1- Kua na Moyo Msafi katika kutekeleza Amali husika.
2- Kua na Ikhlas katika kutekeleza Amali husika.
3- Kuuhudhurisha Moyo na Ufahamu katika kutekeleza wa Amali husika.
4- Kua na Unyenyekevu mbele ya Allah Subhanah wa Taála.
5- Kua na Khofu mbele ya Allah Subhanah wa Taála.
6- Kua na Mapenzi Juu ya Allah Subhanah wa Taála.
7- Kua ni mwenye kuona Haya mbele ya Allah Subhanah wa Taála
8- Kua na Matumaini na kua ni mwenye kumuamini Allah Subhanah wa
Taála.
Ambapo mambo manane hayo hua yanafafanulika kwa kujumuishwa katika hali
zifuatazo:
73
1- Kua na Moyo Msafi na Ikhlas.
2- Kuuhudhurisha Moyo na Ufahamu katika kutekeleza Amali husika.
3- Kua na Unyenyekevu mbele ya Allah Subhanah wa Taála.
4- Kua na Khofu na Mapenzi mbele ya Allah Subhanah wa Taála.
5- Kuaona Haya, kua na Matumaini na Kua ni mwenye Kumtegemea Allah
Subhanah wa Taála baada ya kumaliza Amali husika.
Hujjat Islami Imam Abu Hamid Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali
anayafafanua majumuisho hayo kwa kusema kua:
1- Kua na Moyo Msafi na Ikhlas – Hii ni hali ambayo inajumuisha kuusafisha Moyo
kutokana na kua na Maradhi ya Nafsi na kua na Tabia Mbovu, katika hali pia Moyo
inabidi usafishwe na hivyo usiwe na nia au malengo yeyote ya kufanya jema kwa
ajili ya yeyote au chochote isipokua iwe kwa ajili ya Allah Subhanah wa Taála pekee
na hivyo Moyo wa Mtu husika hautakiwi kua na kitu chochote ndani yake isipokua
Muumba wa Moyo huo ambae ni Allah Subhanah wa Taála. Kiasi ya kua athari ya
Ikhlas ndani ya amali zake hua ni yenye kuonekana kuanzia kwenye Moyo wake na
hivyo hua ni zenye kuthibitishika katika kiwiliwili chake katika utekelezaji wa Amali
njema hizo. Ambapo hali ya juu kabisa ya kua na Moyo Msafi na Ikhlasi katika
matendo ya Mja hufikika pale inapokua Mja anafanya mambo mema kwa ajili ya
Mapenzi kwa Mola wake bila ya kutegemea Malipo kutoka kwake wala kua na khofu
au kutaka kuokoka kutokana na adhabu za Mola wake.
2- Kuuhudhurisha Moyo na Ufahamu katika kutekeleza Amali husika – Hii hua ni
ile hali ambayo inajumuisha ufanyaji wa amali njema huku Moyo na ufahamu ukiwa
unaenda sambamba na kauli na vitendo vya Mtu husika. Ambapo hapa hua
tunazungumzia mfumo mzima wa Ufahamu wa mtu katika kujua umuhimu wa jambo
analilofanya huku akiwa ni mwenye kumkumbuka Mola wake kimawazo, kikauli na
kivitendo katika kila hatua ya utekelezaji wa Amali husika.
3- Kua na Unyenyekevu mbele ya Allah Subhanah wa Taála – Hali hii inajumuisha
hali ya Kumnyenyekea, Kumtukuza, Kumkuza, Kumsifu Mola wako.
4- Kua na Khofu na Mapenzi mbele ya Allah Subhanah wa Taála – Hali hii
inajumuisha Al Taqwa (Taqwa), Al Khawf (Khofu) na Al Mahabbah (Mapenzi) kwa
Allah Subhanah wa Taála katika utekelezaji wa Amali husika. Na haya yote hua
yanategemeana na Ilm ya Mja juu ya Uwezo, Ukubwa, Malipo, Adhabu za Mola
wake wake na Wingi wa kasoro zake Mja huyo na wingi wa dhambi zake mbele ya
Mola wake. Kila mtu anaopokua anajua juu ya mambo haya basi ndio Khofu na
Mapenzi yanavyozidi kuongezeka kwa Mola wake.
74
5- Kuona Haya, kua na Matumaini na Kua ni mwenye Kumtegemea Allah
Subhanah wa Taála baada ya kumaliza Amali husika – Hali hii hua inajumuisha
Al Raja (Matumaini) na Tawakkul (kumtegemea Allah Subhanah wa Taála tu katika
kila kitu) baada ya kumaliza kutekeleza Amali husika. Kwani Mja anatakiwa kua ni
mwenye kuona haya kutokana na kua na kasoro nyingi katika Matendo yake na hivyo
anatakiwa kua na khofu ya kutokukubaliwa kwa Amali zake njema, lakini hapo hapo
anatakiwa kua ni mwenye kumtegemea Allah Subhanah wa Taála na kua na
matumaini kua atamkubalia amali njema zake hizo.
Ili kufahamu juu ya Hijra inayompelekea Mja kua na sifa ya Muhsin, basi na tuangalie
Maumbile ya Moyo ambacho ni kiungo kinachohusika moja kwa moja na utayarishaji
wa uthibitisho wa mtu husika kufanya Hijra kutoka katika hali ya kua ni mtu wa kawaida
na kuingia kuingia katika hali hio ya Muhsin, kwani tofauti na tunavyodhani sisi mimi na
wewe kua Moyo ni Moyo yaani ni Al Qalb, lakini tunapoiangalia Qurán basi tunaona
kua Moyo ni kiungo muhimu kilichogawika katika hali nne za darja tofauti kulingana na
mazingira ya Maumbile yake kama zilivyotajwa na Allah Subhanah wa Taála ndani ya
Qurán ambazo ni Al Qalb, Al Fuad, Al Lub na Al Sadr.
MAUMBILE YA NYOYO ZA IBN ADAM: AL QALB, AL FUAD, AL
LUBB, AL SADR NA AN NAFS KATIKA QURÁN
Maamrisho yote ya Dini ya Kiislam na Hukmu zake yamewekwa na Allah Subhnaha wa
Taála kwa ajili ya kusimamia Maslahi ya kila kiumbe kilichopo Ulimwenguni, lakini
Maslahi hayo huwezi kuyaona hadi pale utakapoisoma Dini ya Kiislam na kuifaham kwa
kutumia ufahamu wa Moyo na hapo ndipo utakapohisi athari zake ndani ya mwili wako
na pia ndipo utakapopata mantiki ya maamrisho hayo kama isemavyo aya ifuatayo ya
Surat Az Zumar ambao tushaiangalia katika Utangulizi:
﴿ٱهلل َُّ نَز َّلَ أَحْسَنَ ٱلحَْدِيثِ كِتَاابً م ُّتَشَاهبِ اً م َّثَانىِ َ تَقْشَعِر ُّ مِنْهُ جُلُودُ ٱل َّذِينَ يخَْشَوْنَ
رَب َّهُمْ ثمُ َّ تَلِينُ جُلُودُهُمْ وَقُلُوبُهُمْ إِلىَٰ ذِكْرِ ٱهلل َِّ ٰذلِكَ هُدَى ٱهلل َِّ يَهْدِى بِهِ مَن
يَشَآءُ وَمَن يُضْلِلِ ٱهلل َُّ فَمَا لَهُ مِنْ هَادٍ ﴾
Allahu nazzala ahsana alhadeethi kitaban mutashabihan mathaniya taqshaAAirru
minhu juloodu alladheena yakhshawna rabbahum thumma taleenu julooduhum
75
waquloobuhum ila dhikri Allahi dhalika huda Allahi yahdee bihi man yashao
waman yudhlili Allahu fama lahu min hadin (Surat Az Zumar 39:23)
Tafsir: Allahu ameshusha hadithi bora kabisa, Kitabu (Quran) chenye sehemu ndani
yake zinazofanana kwa wema na usahih. Ngozi za wale wenye kuomuogopa Allah
zinatetemeka (Wanapoisikia Qurán). Na kisha Nyoyo zao na ngozi zao hulainika
kutokana na kumkumbuka Mola wao. Huo ni Uongofu wa Allah. Ambae humuongoza
amtakae na anaepotoshwa na Allah basi hakuna atakaemuongoza.
Naam aya zimesema hivyo kwa sababu Moyo una maumbile ya kua ni kiungo kikamilifu
kinachojitegemea na hivyo kua na ufahamu wake na maamuzi yake yasiyotegemeana na
kiuongo chochote mwilini, na ndio maana Allah Subhanaha wa Taála akawa
ameuzungumzia Moyo katika hali tofauti na mara nyingi sana katika kitabu chake
kitukufu cha Qurán, hivyo na tuanze kwa kuangalia maana na matumizi ya neno Qalb
kama lilivyotumiwa katika Qur’an.
AL QALB
Neno Qalaba kwa Kiarabu hua ni lenye kumaanisha Kugeuka, Kugeuza kitu Juu Chini
au Mbele Nyuma au Ndani Nje, Kubadilisha, Kubadilika Hali au Muelekeo,
Kubadilishana Mmoja baada ya Mwengine. Neno Qalaba ndio lililotoa neno Qulub
ambalo maana yake hua ni Moyo, na tunapoiangalia Qurán basi tunaona kua imetumia
neno Qalaba mara 168 katika hali tofauti ikiwemo katika hali ya neno Qulubu ambalo
ndio lililotumika katika aya ya Surat Al Araf pale Allah Subhanah wa Ta’ala aliposema:
ن َّ ﴿وَلَقَدْذَرَأَْلجَِه مَكَثِير اًمِّنَ ٱلجِْنِّ وَٱلإِنْسِ لهَُمْ قُلُوبٌ لا َّ يَفْقَهُونَ هبَِ ا وَلهَُمْ أَعْينُ ٌ
لا َّ يُبْصِرُونَ هبَِا وَلهَُمْ آذَانٌ لا َّ يَسْمَعُونَ هبَِآ أُوْلَٰئِكَ كَٱلأَنْعَامِ بَلْ هُمْ أَضَل ُّ أُوْلَٰئِ كَ
هُمُ ٱلْغَافِلُونَ ﴾
Walaqad dhara/na lijahannama kathiiran mina aljinni waal-insi lahum quloobun
la yafqahoona biha walahum aAAyunun la yubsiroona biha walahum adhanun la
yasmaAAoona biha ola-ika kaal-anAAami bal hum adhallu ola-ika humu
alghafiloona (Surat Al Araf 7:179)
76
Tafsir: Na kwa hakika tumewaumba kwa ajili ya Jahannam wengi miongoni mwa
Majini na Watu. Wana nyoyo ambazo hawafahamu kutokana nazo, wana macho
ambayo hawaoni kutokana nayo, na wana masikio lakini hawasikii. Wao wako kama
Ngo’mbe lakini wao wamedhalilika zaidi, kwani hawa ndio wale ambao wamekubwa
na Mghafiliko.
Naam tunapoiangalia aya hii basi tunaona kua imetumia maneno yasemayo Walaqad
Dhara/na Li Jahannama yaani Na kwa hakika Tumewaumba kwa ajili ya Jahannam na
neno kwa ajili ya Jahannam limeunganishwa na harfu Laam. Ambayo ni Laam tofauti na
ile Laam ya LiyaAAbuduuni iliyotumika katika aya ifuatayo:
﴿وَمَا خَلَقْتُ ٱلجِْن َّ وَٱلإِنسَ إِلا َّ لِيَعْبُدُونِ ﴾
Wama khalaqtu aljinna waal-insa illa liyaAAbudooni (Surat Adh Dhariyyat 51:56)
Tafsir: Sikuwaumba Majini na Ibn Adam isipokua kwa ajili ya kuniabudu mimi tu.!
Kwani Laam iliyotumika katika aya Surat Adh Dhurriyat 51:56 yaani Laam ya
LiyaAabuduuni hua inajulikana kama Laam Al Ghaayah yaani Laam inayoweka wazi
Kusudio la Kitu Fulani na Laam iliyotumika katika aya yetu ya Surat Al Aaraf 7:179
ambayo ni Laam ya Li Jahannama inajulikana kama Laam al Aqibah yaani Laam
inayoweka wazi kinachobakia baada ya tukio fulani.
Na ijapokua Wanazuoni wengi wanasema kua Laam zote mbili katika aya hizi ni Laam
Al Ghayah, lakini Laam ya LiyaAabuduuni hua pia inahesabika kua ni Laam al Tashrii
yaani Lam ya Kisharia wakati Laam ya Li Jahannama inahesabika kua ni Laam Al
Takwini yaani Laam ya Mfumo wa Kimaumbile.
Hivyo basi Laam iliotumika katika Li Jahannama ambayo ni Laam al Aqibah na hapo
hapo ikawa ni Lam Al Takwin imetumika ili kuweka wazi kua kutokana na Maumbile
yao viumbe viwili hivi yaani Ibn Adam na Majini basi wengi wataghafilika na
watashindwa kujizuia na matamanio ya Nafsi zao na hivyo kushindwa kwao kuzitumia
ipasavyo neema za Viungo hivyo walivyopewa na Mola wao ambavyo ni Macho,
Masikio na Nyoyo zao basi kutapelekea kutokea tukio la kuingizwa Motoni kwa wengi
miongoni mwao kutokana na makosa ya kutovitumia ipasavyo viungo hivyo kwa
kutokana na kughafilika, na ingawa kughafilika ni sehemu ya Maumbile ya Ibn Adam,
lakini hata hivyo hakuna Kughafilika kubaya kama kughafilika juu ya Mola Wako
aliekuumba!…Allahuma ajirna minna Naar!..Aamiin!
77
Hivyo tuungalie maumbile ya Al Qalb kulingana na mtizamo wa Kisayansi ili tupate
kujua kwani nini Allah Subhanah wa Ta’ala akasema:
﴿لهَُمْ قُلُوبٌ لا َّ يَفْقَهُونَ هبَِا﴾
Lahum quloobun la yafqahoona biha – Wana Nyoyo Lakini hawafahamu kutokana
na Nyoyo hizo!
Mara nyingi sana Allah Subhanah wa Ta’ala katika Qurán amekinasibisha kiungo cha
Moyo na Kuona, Kufaham na Kutafakkari pia kwa sababu kimaumbile Moyo ni kiungo
cha mwili ambacho kinajitegemea kwa kua na ufaham wenye nguvu ya upekee katika
mwili mzima wa Ibn Adam. Ufahamu wa Moyo wa Ibn Adam hua unafanya kazi zake
kimaumbile kwa kuishirikisha mifumo mikuu minne ya usafirishaji wa nguvu za hisia za
mwili wa Ibn Adam ambazo ni:
1- Mfumo wa Usambazaji wa hisia za sehemu tofauti za mwili.
2- Mfumo wa Viasili vinavyodhibiti maumbile ya ufanyaji kazi wa mwili
vinavyozalishwa na Moyo.
3- Mfumo wa Usambazaji Kemikali kupitia katika mapigo ya Moyo na
usambazaji Damu.
4- Mfumo wa Uzalishaji Nguvu za Kimaumbile za mwili za ufanyaji kazi wa
viungo vya Ibn Adam na nguvu za Mawimbi ya Mvutano wa Umeme wa
Sumaku za ndani ya Mwili na nje ya Mwili.
Kimaumbile Moyo wa Ibn Adam hua na uwezo wa kuzalisha nguvu za umeme zenye
asili ya mawimbi ya sumaku zenye nguvu mara 5000 zaid na nguvu kama hizo
zinazozalishwa na Ubongo wa Ibn Adam, nguvu hizo ambazo pia huweza kuhisika hata
nje ya mwili wa Ibn Adam kwa takriban umbali wa mita 3 hua na uwezo wa kusambaza
na kupokea na kuwasiliana na hisia mbali mbali kutoka katika ubongo wa mtu husika na
sehemu nyengine za mwili mzima wa mtu huyo na wakati huo hua na uwezo wa
kuwasiliana na nguvu zinazozalishwa na watu wengine zaidi ya wanane waliopo karibu
nae na hivyo hua na uwezo wa kuwaathiri watu hao walio karibu nawe kihisia.
Nguvu hizi zinazozalishwa na Moyo pia huweza kuwasiliana kihisia na kuathiri nguvu
za mvutano wa mawimbi ya umeme ya viumbe wengine waliokuwepo karibu yake mtu
ikiwemo Wanyama na Viumbe wengine wasioonekana wa Ulimwengu wa Al Ghayb. Na
ndio maana baadhi wakati mtu anaweza akakaa peke yake na ghafla akahisi kama mwili
unamsisimka, kwa sababu nguvu hizi za kimaumbile za Moyo hua na uwezo wa kuhisi
kutokea kuwepo kwa Viumbe wengine wasioonekana kama vile Majini ambao wao
78
Maumbile yao yana asili za nguvu hizi. Na ni kutokana na athari ya nguvu hizi ndio
Viumbe Majini hua na uwezo wa aidha kuwadhibiti Ibn Adam au kuwaogopa na
kuwakimbia Ibn Adam.
Moyo wa Ibn Adam una nyuroni 40000 ambazo kwa pamoja hua zinaunda kitu
kinachoitwa Akili ya Moyo, ambayo hua ni yenye uwezo wa kukumbuka kwa muda fupi
na kwa mda mrefu, kujifunza na kufanya maamuzi yake wenyewe bila kuitegemea akili
na hivyo hua na uwezo wa kuyadhibiti mapigo ya Moyo, athari ya Ufahamu wa Moyo
hua na uwezo wa kuubadilisha hata mtizamo wa ufahamu wa akili kihisia na kimaamuzi
katika mambo mbali mbali.
Kila Moyo unapopiga basi hua ni wenye kuzalisha nguvu za mawimbi ya umeme wa
sumaku na hivyo kusababisha athari mbali mbali za Moyo ikiwemo kuona kwa mtizamo
wa Jicho la Moyo, kuhisi kwa hisia za Moyo, ambapo hisia zote hizi zinapotokea ndani
ya Moyo hua zina athari kubwa zaidi ndani ya mwili wa Ibn Adam na zinazotofautiana
sana na zile zenye kutokea moja kwa moja kupitia katika akili ya Ibn Adam, ambapo
mawasiliano kutoka kwenye Moyo kuelekea kwenye Akili hua ni maradufu zaidi yana
umuhimu zaidi kwa ufanyaji kazi wa Mwili kuliko mawasliano ya kutoka kwenye Akili
kuelekea kwenye Moyo.
Hii inaonekana wazi pale Moyo unapobadilika hali yake kulingana na hisia na vitendo
tofauti vinavyosababishwa na ufaham wa akili na hivyo kuufanya Mwili wa Ibn Adam
kua dhaifu na kuishiwa nguvu, kwa mfano Ibn Adam anapokua na hasira, wasiwasi
mkubwa, mawazo mengi au khofu basi hali ya mapigo ya Moyo hubadilika na hivyo
hufanya mawasiliano na akili ambayo nayo baada ya kupata mawasiliano hayo basi hua
ni yenye kujua kua kuna hisia ambazo sio nzuri kwenye Moyo na mwili mzima kwa
ujumla na hivyo kusababisha akili kupungukiwa na uwezo wake wa kufanya kazi kwa
umakini na kufikiria ipasavyo.
Na hivyo kila Ibn Adam akiwa na hali kama hio mara kwa mara basi Moyo wake
hudhooofika, jambo ambalo hupelekea na viungo vyengine muhimu vya mwili
kudhoofika ikiwemo, Mafigo, Ini, Mapafu n.k na kusababisha madhara makubwa sana
mwilini ikiwemo mshtuko wa Moyo.
Mbali ya kua ni Moyo hua ni wenye nguvu za umeme zenye asili ya mawimbi ya sumaku
lakini pia hua ni wenye kusababisha uzalishwaji wa kemikali ambazo husababisha hisia
nzuri kwa Ibn Adam zikiwemo zile zinazojulikana kama Dopamine,Oxytocin,
Endorphines, Seratonin, n.k ambazo hua na jukumu la kukamilisha sifa ya maumbile ya
asili ya kila mtu yanayotokana na maana ya neno Al Ins. Neno Al Ins linatokana na neno
Anisa ambalo maana yake hua ni kua na Mazoea, Kupenda, Kua na Umoja kijamii, au
Kushikamana pamoja.
79
Hivyo Mtu ameitwa Insan kwa Lugha ya Kiarabu kwa sababu neno hilo hua linamaanisha
Kiumbe ambae Maumbile ya mwili wake yana sifa ya kuzalisha kemikali za Dopamine
na Oxytocin zinazosimamia hisia za Mapenzi, Matamanio, Mshikamano, Kusaidiana,
Kuhurumiana, n.k baina ya Mke na Mume, Baba na Mama, Kaka na Dada, Ndugu na
Familia, n.k kulingana na uhusiano wa hali ya hisia hizo zinazosababishwa kuzalishwa
kutokana na nguvu na uwezo wa Moyo na pia Ubongo wa Ibn Adam.
Kwani tunapozungumzia Oxytocin basi hua tunazungumzia kemikali ambazo kimaarufu
hua zinajulikana kama kemikali za ‘Mapenzi na Uaminifu’ na huzalishwa ndani ya miili
yetu baada ya kupatikana hisia zinazotokana na ufanyaji kazi wa viungo vya hisia za
Mwili za Kuona, Kusikia Sauti, Kuhisi Harufu au Kugusana na hivyo hutupelekea kua
na hali ya kujisikia kua na Raha, Upendo, Utulivu, Usalama, Amani pale tunapokua
karibu na wale tunaowapenda na hivyo kutuzidishia hisia za kutotaka kukosana au
kuachana na watu hao na kuwapenda, kuwajali, kuwafanyia ukarimu na kuwaonea
huruma.
Kemikali za Oxytocin pia hua ndizo zinazosimamia jukumu la kuvitayarisha viungo vya
mwili wa Mwanamme na Mwanamke katika kuingiliana kimwili, kwa ajili ya kuendeleza
vizazi na pia kwa ajili ya kuupa utulivu na kuupumzisha mwili kwa kuupa hisia za Raha
inayotokana na kitendo cha kuingiliana kimwili, ambayo hutegemeana na wingi wa
uzalishwaji wa Oxytocin kwani kila zinavyozidi kuzalishwa kwa wingi zaidi katika
wakati wa tendo hilo basi ndio inavyozidi kupatikana hisia za Raha ambayo haina mfano
wake katika tendo hilo kama anavyoelezea Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Imam Abu
Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali pale aliposema kua:
‘Raha ya mda mfupi inayopatikana katika kuingiliana kimwili basi hua ni Raha
ambayo kamwe haiwezi kufananishwa na Raha nyengine, na kama ingekua ni yenye
kudumu basi ingekua ni moja kati ya dalili ya moja kati ya Raha za Milele
tulizoahidiwa Peponi’
Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali anatufafanulia zaidi pale aliposema: ‘Hikma ya Allah Subhanah wa
Ta’ala na Rehma zake zinaonekana pale unapoangalia katika kuweka Matamanio ya aina
aina mbili katika Maisha yetu. Matamanio ya kwanza ni ya muonekano wa kimaisha wa nje
pale mtu anapokua anaendeleza kizazi chake kupitia kwa watoto wake. Na muonekano wa
pili ni wa muonekano wa kimaisha ya ndani unaohusiana na maisha ya baadae kesho
Akhera. Kwani raha ya kuingiliana kimwili hua si yenye kudumu katika ulimwengu huu na
ni lazima iwe ni ya mda mfupi, na yenye kikomo kwa kumalizika mara tu baada ya kuihisi
raha hio kiasi ya kua humpelekea Ibn Adam kua na hamu ya kutaka raha hio iwe ni yenye
kudumu, na hivyo hii humfanya Ibn Adam kua ni mwenye kudumu katika Mema kiibada
ambayo yatampelekea kupata Raha kama hizo milele.’
80
Allah Subhanah wa Ta’ala anaelezea Miujiza ya ufanyaji kazi wa Oxytocin katika
maumbile yetu ambazo kuzalishwa kwake kunasababishwa na Moyo na Ubongo na
kutusababishia kua na hali ya Upendo na Utulivu baina yetu katika maisha yetu
aliposema:
﴿وَمِنْ آَتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِ كُمْ أَزْوَاجاً لِّتَسْكُنُو ۤ اْ إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُ م
م َّوَد َّةً وَرَحمَْةً إِن َّ فىِ ذٰلِ كََ لآَتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَك َّرُونَ ﴾
Wamin ayatihi an khalaqa lakum min anfusikum azwajan litaskunoo ilayha
wajaAAala baynakum mawaddatan warahmatan inna fee Dhalika laayatin
liqawmin yatafakkaroona (Surat Rum 30:21)
Tafsir: Na miongoni mwa alama zake ni kukuumbieni wake kwa ajili yenu kutoka
miongoni mwenu, ili mpate utulivu pamoja nao, na akakuwekeeni baina yenu mapenzi
na rehma. Kwa hakika katika hili kuna dalili kwa wale wenye kutafakkar.
Aya inatuwekea wazi kua: ‘Miongoni mwa Dalili za Utukufu, Uwezo na Rehma
kubwa za Allah Subhanah wa Ta’ala juu yetu ni kutujaalia Ibn Adam kua wa aina
moja lakini hapo hapo kua ni wenye maumbile mawili tofauti baina yetu kwani
kuna umbo la kijinsia ya Kiume na jinsia ya Kike, ambapo mbali ya kua kuna
utofauti wa Muonekano mzuri na wa kuvutia wa Umbo la nje baina ya jinsia mbili
hizo lakini pia kuna utofauti wa maumbile ya ndani ya miili katika mifumo ya
kiufanyaji kazi, kuanzia katika mfumo wa Hisia, Ufaham, Akili, Uzazi n.k.
Tofauti zote hizo za kimaumbile ni kwa ajili ya kutufanya kua ni wenye kuendana,
kuvaana, kutegemeana katika kutimiziana mahitaji ya kimwili na hivyo kua ni
wenye kupata utulivu wa nafsi zetu unaopatikana kutoka ndani ya uhusiano
unaokubalika kisharia na Allah Subhanah wa Ta’ala baina ya jinsia mbili hizo za
Kiume na Kike kwa ajili ya kuendeleza kizazi na pia kuistarehesha miili yetu na
akili zetu na hivyo ndani ya uhusiano huo kupatikana Furaha, Mapenzi, Huruma
na kutakiana mema baina ya Mume na Mke.’
Kwa upande mwengine basi, kemikali za Oxytocin zinapozalishwa na kuachiwa ndani ya
mwili wa Mwanamke basi hua pia ni zenye kuzidisha mtetemeko wa kizazi cha
mwanamke na hivyo kurahisisha manii ya Mwanamme kulifikia yai la Mwanamke na pia
hua ni zenye kuutayarisha mwili wa Mwanamke pale anapotaka kujifungua na kupelekea
kutanuka kwa njia ya Uzazi pale Mtoto anapotaka kuzaliwa na pia ndio zenye
kusababisha utayarishaji wa Maziwa baada ya mtoto kuzaliwa na kua tayari kwa ajili ya
kunyonya maziwa.
81
Ama kwa upande wa Dopamine basi inapozalishwa hua ni yenye kutupelekea kua na
hamu, ari maamuzi ya kutekeleza na kutimiza mahitaji yetu kijamii na matamanio yetu
kimaumbile na kihisia na hivyo hua inajulikana pia kama kemikali inayochangia
kuchochea kupatikana kwa hisia za kujisikia raha na hivyo kutupeleka kutaka kuongeza
bidii zaidi juu ya jambo lililotupa raha au manufaa na hivyo kua ni wenye kuridhika
kutokana na kutimiza malengo, mahitaji na matamanio yetu. Dopamine pia hua na
jukumu la kuhifadhi kumbukumbu ndani ya Ubongo, kusababisha umakini wa mtu katika
jambo husika, n.k
Hivyo basi Dopamine na Oxytocin hua ni zenye kufanya kazi pamoja sambamba ili
kuimarisha mshikamno wa uhusiano baina ya Mume na Mke, Kifamilia na Kijamii, n.k
kiasi ya kua Dopamine inapokosekana au inapokua imezalishwa kidogo basi hata kama
Oxytocin itazalishwe kwa wingi peke yake haitowezi kusababisha mshikamano huo
unaotakiwa kupatikana ili kua na ukaribu baina yetu na pia inapokosekana Oxytocin basi
Dopamine peke yake haiwezi kusababisha mshikamano huo.
Kwa upande wa Seratonin basi hua ni zenye kumfanya mtu kuuona Umuhimu na thamani
yake katika jamii au familia husika, hivyo Seratonin inapokua haijazalishwa mwilini basi
mtu husika hua ni mweye kujisikia mpweke na mwenye huzuni, mfano mtu
unaposhukuriwa baada ya kufanya jambo fulani basi shukrani hio husababishia
uzalishwaji wa Seratonin katika mwili na kumfanya mhusika awe ni mwenye kuridhika
kuona kua ni mwenye thamani na kukubalika, kwa sababu shukrani hua ni hali ya hisia
ya Moyo kuonesha kukubali thamani ya jambo jema ulilofanyiwa kutoka ndani ya moyo
wa mtu uliemfanyia wema huo.
Hivyo ushirikiano baina ya kemikali hizi za Oxytocin, Dopamine, Seratonin n.k ambazo
kuzalishwa kwake kunategemeana na mfumo wa ufanyaji kazi wa Moyo basi ndio
unaopelekea kuwepo kwa maingiliano ya watu na mshikamano katika Kifamilia na
Kijamii na hivyo huwapelekea watu unapowakosea kusema: ‘Ah unanitia uchungu ndani
ya Moyo!’ au unapowaambia maneno Qawlan Sadida basi husema ‘Maneno yako
yananigusa ndani ya Moyo!’ au ‘Hakika Mimi nampenda fulani kwa Moyo wangu wote’
n.k.
Hivyo ukweli ni kua Ibn Adam hua anautaja Moyo pale anapoathiriwa sana na kitu fulani
na hii ni kwa sababu kama kuhisi basi kabla ya kuhisi kwa ufahamu wa akili na Ubongo
basi kiungo kinachohisi kwanza hua ni Moyo, yaani hali ya hisia husika huanzia kwenye
Macho, au Masikio ambayo hupeleka habari kwenye Ubongo ambapo Ubongo nao
hutuma habari kwenye Moyo kisha Moyo hutoa maamuzi sahih juu ya jambo husika kwa
aidha kuzidisha kasi au kuyawacha katika hali yake ya kawaida mapigo ya Moyo na
sambamba hapo hapo Moyo hutoa habari zinazopelekea kuzalisha kemikali na
zinazosababisha mwili wa Ibn Adam kuchukua hatua stahiki kwa ajili ya jambo husika,
iwe kulia, kucheka, kupenda, kuchukia, kupigana, kukimbia, n.k.
82
Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi anasema kua: ‘Al Qalb na Fuad
vinahifadhiwa ndani ya Sadr, hivyo Fuad inajumuisha Moyo mzima ambao
unajumuisha mishipa ya damu. Hivyo Qalb hua ni sehemu ambayo ndio kiti cha
hisia mbali mbali za upendo, chuki, hasira, ufahamu, n.k.’
Kwa upande mwengine basi tunaona kua Al Qalb yaani Moyo pia hua ni wenye uwezo
wa kuhifadhi hisia hizo na kukumbuka ndani yake tena kwa mda mrefu pia kama vile
ilivyokua kwa upande wa Ubongo, Na ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala
akatuelezea katika aya ifuatayo kwa kutuambia kua:
﴿ٱ ل َّ ذِي نَآ مَنُواْ وَتَطْمَئِن ُّ قُلُوبُهُمْ بِذِكْرِ ٱهلل َِّ أَلاَ بِذِكْرِ ٱهلل َِّ تَطْمَئِن ُّ ٱلْقُلُ وبُ ﴾
Alladheena amanoo watatma-innu quloobuhum bidhikri Allahi ala bidhikri Allahi
tatma-innu alquloobu (Surat Ar Rad 13:28)
Tafsir: Wale wenye kuamini, na ambao nyoyo zao zinapata utulivu kutokana na
kumkumbuka Allah. Kwani ni katika kumkumbuka Allah ndio Nyoyo hupata utulivu.
Aya hii imekiambatanisha kiungo cha Moyo wa Ibn Adam na Hisia za Kufaham na
Kukumbuka kwani, imetumia maneno mawili ambayo ni Al Qalb liliopo katika hali ya
wingi ambalo ni Qulubu na kisha ikatumia neno Dhikri lenye kumaanisha Kukumbuka,
Kuhifadhi au kuweka kwenye Ufahamu, Kuonya, Kusifu, Kutukuza n.k hivyo aya
inaweka wazi Maumbile ya hali ya Utulivu unaopatikana ndani ya Moyo na Ufahamu
wake kutokana na Moyo husika kua na kumbukumbu ya kumkumbuka Allah Subhanah
wa Ta’ala. Na ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala akasema tena kumwambia Mtume
wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua:
﴿إِن َّ فىِ ذٰلِ كََ لآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم م ُّؤْمِنِينَ۞ وَإِن َّ رَب َّكَ لهَُوَ ٱلْعَزِ يزُ ٱلر َّحِ يمُ۞
وَإِن َّهُ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلْعَالَمِينَ۞
نَزَلَ بِهِ ٱلر ُّوحُ ٱلأَمِينُ۞
عَلَى ٰ قَْلبِكَ لِتَكُونَ مِ َن
ٱلْمُنْذِرِينَ۞ بِلِسَانٍ عَرَبيِ ّ ٍ م ُّبِينٍ۞ وَإِن َّهُ لَفِى زُبُرِ ٱلأَو َّلِينَ ﴾
Wa-inna rabbaka lahuwa alAAazeezu alrraheemu, Wa-innahu latanzeelu rabbi
alAAalameena; Nazala bihi alrroohu al-ameenu; AAala qalbika litakoona mina
almundhireena; Bilisanin AAarabiyyin mubeenin; Wa-innahu lafee zuburi alawwaleena;
(Surat Shu-ara 26: 191-196)
83
Tafsir: Na kwa hakika Mola wako ni Mwenye uwezo Mkubwa na ni Mwingi wa Rehma,
Na ka hakika hii (Qur’an)ni teremsho kutoka kwa Mola wa Ulimwengu wote.
Imeteremshwa kupitia kwa Ruhi Al Amiin (Malaika Jibril), Kwenye Moyo wako (Ewe
Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) Ili uwe ni mwenye kuonya. Kupitia katika
Lugha ya Kiarabu iliyowazi kabisa. Na Hii (Qur’an) imo ndani ya maandiko
(Zaburi, Tawrat na Injil) yaliyotangulia.
Hivyo kutajwa kwa Moyo katika ayah hii kua Qur’an imeteremshwa na kua ni kama
iliyogongwa muhuri kwenye Moyo wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ili isitoke,
kunatilia mkazo umuhimu wa kiungo hicho cha Al Qalb katika kuhifadhi kumbukumbu
kwake, kiasi ya kua aya imetoa kipaumbele zaidi kwa Ufahamu wa Moyo kuliko kwa
Ufahamu wa Ubongo na Akili.
Wanasayansi wamethibitisha haya ya kua Moyo unahifadhi kumbukumbu pale
walipofanya upasuaji wa upandikizaji wa Moyo uliofanyika mnamo mwaka 1988 nchini
Marekani kwa mgonjwa wa Moyo aitwae Claire ambae alipandikizwa Moyo na kisha
baadae aliandika kitabu Mabadilio ya Moyo ambacho ndani yake anaelezea yaliyomkuta
baada ya upandikizwaji wake huo wa Moyo kua alianza kupenda kunywa vilevi na
vyakula visivyokua na lishe na mambo mengine mengi ambayo yanayopendwa kufanya
na vijana walio tofauti na rika lake, kwani yeye alikua ni mtu mzima anaekaribia miaka
45-50 hivyo alikua hapendi kuyafanya mambo ya ujana ambayo keshayapita tayari kabla
ya kufanyiwa upadikizaji huo wa Moyo, yaani alibadilika tabia zake zote. Na kufikia
wakati ikawa anaota wazi wazi kua ana uhusiano wa kimapenzi na kijana mdogo kwake
kiumri wa Kiume aitwae Timothy. Claire alikua akihisi hisia za mapenzi makubwa sana
juu ya kijana huyu ambae hata hivyo alikua hamjui wala hajawahi kumuona katika
maisha yake, kwani yeye alikua akimuona ndotoni tu.
Hivyo Claire akaamua kufanya uchunguzi ambapo akagundua kua Moyo wake
aliopandikizwa ulikua ni wa Mtu aliekwisha fariki ambae alikua akijulikana kwa jina la
Timothy. Alipofuatilia kwa kina na kukutana na wazazi wa Timothy basi alithibitisha
kua kijana huyo ndie aliekua akimuona ndotoni pale alipooneshwa picha ya Timothy na
wazee wake, na wazee nao wakathibitisha kua Timothy ambae alifarikia akiwa na umri
wa miaka 18 alikua ni mwenye kupenda vilevi na vyakula vyote ambavyo Claire alikua
havipendi lakini akaanza kuvipenda baada ya kupandikizwa Moyo wa Timothy.
Mfano mwengine ni wa Mwanamme aitwae Graham wa Marekani pia ambae nae baada
ya kupandikizwa Moyo wa mtu mwengine basi akaanza kua na hisia za mapenzi na
Mwanamke aitwae Cheryl ambae alikua ni Mjane wa Mtu ambae alifariki baada ya kujiua
kwa kujipiga risasi na hivyo Moyo wake ukapandikizwa kwa Graham ambae alikua na
matatizo ya Moyo wake. Baada ya kupandikizwa na kutoka hospitali basi Graham
akamuoa Cheryl, ndoa ambayo ilidumu kwa miaka 12 kisha baada ya hapo, Graham
84
akajiua kwa kujipiga risasi kama alivyofanya yule mume wa mwanzo wa Cheryl ambae
Moyo wake ulipandikizwa kwa Graham.
Vile vile kuna mfano wa Professor wa Marekani aitwae Benjamin ambae nae alikua na
matatizo ya Moyo na mara tu baada ya kubadilishwa Moyo wake nakufanyiwa
upandikizwaji basi akawa ni mweye kuota ndoto zenye kutisha, kwani alikua anaota kua
anapigwa na Radi ambayo inamuunguza na kufikia kuuhisi ujuoto wa moto wake.
Professor Benjamin hakumwambia mtu yeyote juu ya ndoto hii isipokua Mke wake,
ambae nao akamuelezea Mke wa alietolewa Moyo huo baada ya kufariki kwake, na hivyo
Mke huyo akashtuka na akathibitisha kua mume wake alipigwa na Radi na baada ya
kupigwa na radi hio basi alifariki hapo hapo.
Ingawa huo ni mtizamo wa Kisayansi juu ya moyo na Maumbile yake tunapozungumzia
kuhusiana na Maumbile ya Moyo, lakini tunaporudi katika mtizamo wa I’lm ya Dini ya
Kiislam kupitia katika aya za Qurán basi tunaona kua: Mujaddid ad Din Hujjat ul Islami
Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhmmad Al Ghazali katika Ihya
Ulum Ad Din kua: ‘Al Qalb una sifa ya Latifah (Ni wenye uwezo na Sifa ya Kuona na
Kufaham mambo ambayo hayako wazi) na Rabbaniyyah (Utukufu wa Kimungu) na
Kiroho na ndio asili ya Ibn Adam. Al Qalb katika mwili wa Ibn Adam hua ni kiungo
kinachofaham, kinachotafakkari, kinachozingatia, kinachozungumziwa pale
unapozungumza na mtu, ndicho kinachoadhibu, ndicho kinacholaumu na ndio
kinachobeba Majukumu yote ya Ibn Adam. Al Qalb ni kama Mfalme wa mwili na
viungo vyengine ni kama Askari na wasaidizi’
Imam al Ghazali anaendelea kusema kua: ‘Heshima na Utukufu wa Ibn Adam, ambao
unawapita Viumbe wote walioumbwa na Allah Subhanah wa Taála unatokana na
Kumjua Allah Subhanah wa Taála, Al Qalb ni ndio unaojumuisha Ubora, Ukamilifu
na Uzuri wa Ibn Adam katika Ulimwengu huu na Malipo yake yatakayokuwepo
katika Ulimwengu unaofuatia. Ibn Adam Amejaaliwa kufaham na Kupata I’lm hii
kupitia kwa Moyo wake tu, na wala si kwa kutumia Viungo vyengine vyote
vilivyabakia. Kwani ni Moyo ndio unaomjua Allah, Unaofanya kazi kwa ajili ya
Allah, Unaojitahidi kwa ajili ya Allah, Unaomkaribia Allah, na kuweka wazi kile
inachokiona mbele ya Allah. Na viungo vyake vyote vya Ibn Adam vilivyobakia hua
ni wafuasi, watumwa na vifaa ambavyo Moyo huvitumia na kuviajiri.
Kwani ni Moyo unaokubaliwa na Allah ndio unaokua uko huru dhidi ya kila kitu
isipokua Allah Subhanah wa Taála, Moyo huwekewa pazia usimuone Allah
Subhnaha wa Taála pale Moyo huo unapokua umejaa kila kitu zaidi ya Allah, Al
Qalb ni ule ambao Mtu akiujua Moyo wake basi hua ni mwenye kuijua Nafsi yake
na akiijua Nafsi yake basi hua ni alimjua Mola Wake. Moyo ndio ule ambao Mtu
asipoujua Moyo wake, basi hatoijua Nafsi yake na hivyo hatomjua Mola wake.
85
Hivyo I’lm ya kuyajua maumbile ya Moyo na sifa zake ndio mzizi wa Dini na ndio
msingi wa njia ya yule mwenye kutamfuta Mola wake.’
Wenye kua na Ilm hio ya kumjua Mola wao ndio wale wanaoelezewa katika Aya
ifuatayo:
﴿م َّنْ خَشِ ىَ ٱلر َّحمَْٰنَ بِٱلْغَيْبِ وَجَآءَ بِقَلْ بٍم ُّنِي بٍ ۞ ٱدْخُلُوهَا بِسَلاَ مٍ ذٰ لِكَ يَوْمُ
ٱلخُُلُودِ ﴾
Man khashiya alrrahmana bialghaybi wajaa biqalbin muneebin; Odkhulooha
bisalamin dhalika yawmu alkhuloodi (Surat Qaf 50:33-34)
Tafsir: Yule ambae anamuogopa mwingi wa Rehma katika Ulmwengu wa Ghayb, na
akaja na Moyo wenye kujirudia katika kufaya Toba. Wataambiwa: ‘Ingia ndani yake
kwa usalama, kwani hiya ni maisha ya Milele’
Watu hawa hua ni wenye kumuogopa Mola wao, wanapokua faragha hapa Duniani na
wanapokua mbele za watu pia, kabla ya hata hawajawa mbele ya Mola wao kesho
Akhera, ambapo hua wanamuogopa Mola wao kutokana na Rehma zake zaidi ya kitu
chochote, kiasi ya kua mbali ya kua ni mwenye kumjua Mola wake kutokana na Rehma
zake lakini hata hivyo hua si mwenye kufanya dhambi. Bila ya Shaka katika haya kuna
mafunzo mengi kwa kila mwenye Moyo wenye kutaka kuzingatia na hivyo ndivyo yenye
kusema aya ifuatayo:
﴿إِن َّ فىِ ذٰ لِكَ لَذِكْرَىٰ لِمَن كَانَ لَهُ قَلْبٌ أَوْ أَلْقَى ٱلس َّمْعَ وَهُوَ شَهِيدٌ ﴾
Inna fee dhalika ladhikra liman kana lahu qalbun aw alqa alssamAAa wahuwa
shaheedun (Surat Qaf 50:37)
Tafsir: Kwa Hakika katika haya kuna ukumbusho kwa yule mwenye Moyo na akatoa
sikio lake kwa kusikiliza huku akiwa ni mwenye kushuhudia.
86
Kulingana na ufafanuzi huo basi ndio tunaona uzito na umuhimu wa majukumu ya Al
Qalb yaani Moyo pale Qurán ilipokua ikizungumzia siku ya Malipo siku ambayo
hakitomfaa kitu chake isipokua Qalbin Saliimin kwa kusema:
﴿يَوْمَ لاَ يَنفَعُ مَالٌ وَلاَ بَنُونَ۞ إِلا َّ مَنْ أَتَى ٱهلل ََّ بِقَلْبٍ سَلِيم﴾
Yawma la yanfaAAu malun wala banoona; Illa man ata Allaha biqalbin saleemin
(Surat Ash Shuara 26:88-89)
Tafsir: Katika siku ambayo haitomfaa mtu Mali wala watoto wake, Isipokua yule
atakaempa Allah Moyo ulio Salama.
Ama kuhusiana na aya hii basi anasema Sultan Al Balagha Imam Al Zamakhshari na pia
Sultan Al Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua, Qalbin Saliimin maana yake:
Hua ni Moyo ambao uko Salima yaani umejiweka huru na Kumshirikisha Allah
Subhanah wa Ta’ala na hivyo ukawa Aslama yaani na ukawa Salama, na ukawa
Salama yaani ukapata Usalama kutokana na Nyoyo za viumbe wengine, na Moyo
huo uka Istaslama yaani ukajisalimisha kwa Allah.’
Ama kwa upande wa Allamah Raghib Al Isfahani basi yeye anasema kua: Al Qalb hua
na maana ya Kugeuza kitu juu chini, au kukizungusha kitu, kama vile ambavyo
mtu unavyoigeuza Nguo, au unapogeukia upande mwengine tofauti na ule
ulioelekea. Hivyo maana yake hujumuisha hali ya kugeuka geuka, na ndio maana
Qurán inatumia neno Inqalib kumaanisha wale watu ambao wamegeuza muelekeo
wao, au waliokimbia kutoka katika uwanja wa vita, au hutumika kama jina
kumaanisha kitendo cha kupindua, na pia hutumika kumaanisha kwa mtu kurudi
tena kwa Allah Subhanah wa Ta’ala yaani baada ya kufariki kwa mtu huyo.
Allamah Raghib Al Isfahani anaendelea kufafanua kwa kusema kua: Jina hili la Al Qalb
hutumiwa kumaanisha Moyo wa Ibn Adam kwa sababu ya kua na maumbile ya
kugeuka geuka kila mara, au kama tunavyosema kua mtu yupo katika hali ya
mabadiliko ya Moyo pale anapokua anabadilika kihisia, kimtizamo, kimaamuzi.
Neno lenyewe Al Qalb, hua pia linajumuisha Nafsi, I’lm, Ushujaa, n.k.
Lakini hata hivyo Al Qalb hua si sawa na Ufahamu, bali Al Qalb mara nyingi hua
unajumuishwa na Ufahamu kama vile ambavyo unavyojumuishwa Mto wa maji
87
usiotembea, wakati ukweli ni kua ni Maji ya Mto ndio yanayotembea, lakini
kutembea huko hua kunajumuishwa na Mto kwa sababu Mto ndio wenye Maji.
Allah Subhanah wa Ta’ala ametumia maneno Nuqallibu af-ida pale aliposema:
﴿وَنُقَلِّبُ أَفْئِدَتَهُ مْ وَأَبْصَارَهُمْ كَ مَ ا لمَْ يُؤْ مِ نُواْ بِهِ أَو َّلَ مَر َّةٍ وَنَذَ رُهُمْ فىِ طُغْيَاِِمْ
يَعْمَهُونَ ﴾
Wanuqallibu af-idatahum waabsarahum kama lam yu/minoo bihi awwala
marratin wanadharuhum fee tughyanihim yaAAmahoona (Surat Al Anaam 6:110)
Tafsir: Na tutazigeuza Nyoyo zao na Macho yao (mbali na uongofu), kwani wamekataa
kuukubali kwa mara ya kwanza, na tutawaachia katika kupita kwao wakiwa na upofu.
Hivyo hapa Allah Subhanah wa Ta’ala ametumia neno Nuqallibu Af-ida ambapo
kutokana na mtizamo mwengine basi hua tunaona kua jina jengine la Moyo hua ni Fuad.
AL FUAD
Neno Fuad linatokana na neno Fa’ada ambalo kwa Kiarabu hua linamaanisha Kuumizwa
Moyoni, Kupigwa Moyoni, Kuumwa na Moyo. Mbali ya kua neno Fa’ada limetoa neno
Fu’ad lakini pia neno hili ndio pia lililotoa neno Af’idah ambalo humaanisha Moyo au
Ufahamu.
Allamah Al-Raghib Al Isfahani anasema kua Al Fuad hua moja kwa moja linamaanisha
Qalb, likiwa na utofauti wa kua Moyo unaitwa Fuad kwa sababu ya kua pia na Maumbile
ya kua ni wenye kua na hisia ya kuripuka moto, kwani Fuad linatokana na kuoka Moto
nyama kwenye jiko au mkaa yaani juu ya Moto uwakao, kama mishikaki ambapo nyama
hio baada ya kuiva hua ni yenye kuitwa Faiid. Hivyo Moyo huitwa Fuad kwa ajili ya
kuainisha kwa kiasi gani mripuko wa Moyo wa mtu hua na uwezo wa kuathiri mambo
mengi katika maisha yake Ibn Adam.
88
Wakati Moto unapowaka ripuripu basi hua ni sawa na Moyo unapojaa jazba na hivyo
ndani yake hua na hisia za kutokua na utulivu na kuongezeka kwa mapigo yake na
hamasa, hali hii inawekwa wazi katika aya ya Qurán iliyotumia majina yote mawili ya
Moyo ambayo ni Qalb na Fuad pale Allah Subhanah wa Ta’ala anapotuelezea kisa cha
Nabii Musa baada ya Nabii Musa kutumbukizwa mtoni na kuokotwa na Asia bint
Muzahim Mke wa Fir’awn na kukabidhiwa mama yake Nabii Musa ili amnyonyeshe,
kwa kusema:
﴿وَأَصْبَحَ فُؤَادُ أُمِّ مُوسَى ٰ فَارِغاً إِن كَادَتْ لَتُبْدِى بِهِ لَوْلا ۤ أَن ر َّبَطْنَا عَلَى ٰ قَلْبِهَ ا
لِتَكُونَ مِنَ ٱلْمُ ؤْمِنِينَ ﴾
Waasbaha fu-adu ommi moosa farighan in kadat latubdee bihi lawla an rabatna
AAala qalbiha litakoona mina almu/mineena (Surat Al Qasas 28:10)
Tafsir: Na ukawa mtupu (usiokua na mawazo yeyote isipokua mawazo juu ya Musa)
Moyo wa Mama yake Musa. Kiasi ya kua alikua tayari kuiweka wazi Siri yake (kua
Musa ni Mtoto wake) kama si sisi kuuthibitishia Moyo wake (kwa Iman), ili apate kua
ni miongoni mwa Walioamini.
Al Fuad pia hua unaitwa ni ufuniko wa hisia ulio juu ya Al Qalb, na hivyo kumaanisha
kua Al Qalb uko ndani zaidi na una umaalum zaidi kuliko sehemu ya juu ya Al Fuad.
Ingawa huu ni mtizamo wa Kilugha tu, lakini Wanazuoni wa U’lum ul Qurán wanasema
kua Al Fuad hua ni sehemu inayopatikana ndani zaidi ya Moyo kuliko Al Qalb kwani hio
ndio sehemu ambayo Nuru ya I’lm ya kumjua Allah Subhanah wa Taála huanzia na ndio
maana Allah Subhanah wa Taála akasema katika Qurán kua:
﴿وَلاَ تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ إِن َّ ٱلس َّمْعَ وَٱلْبَصَرَ وَٱلْفُؤَادَ كُل ُّ أُولٰئِكَ كَانَ عَ نْهُ
مَسْ ؤُولاً ﴾
Wala taqfu ma laysa laka bihi AAilmun inna alssamAAa waalbasara waalfu-ada
kullu ola-ika kana AAanhu mas-oolan (Surat Al Isra 17:36)
89
Tafsir: Na Msifuate kile ambacho hamkijui. Kwani bila ya shaka ya Macho, Masikio
na Nyoyo kila kimoja juu yake mtaulizwa.
Hivyo kwa kua Al Fuad ndio sehemu inayoanzia hisia mbali mbali ikiwemo Nuru ya Ilm
ya kumjua Allah Subhanah wa Taála huanzia basi bila ya shaka ndio tutakayoulizwa juu
ya namna tulivyoutumia, na hivyo hatutoulizwa juu ya Al Qalb, Al Sadr wala Al Lubb.
AL LUBB
Neno Al Lubb linatokana na neno la Kiarabu Labba ambalo hua ni lenye kumaanisha
Kujaaliwa kua na ufahamu wa kina, Moyo wenye huruma. Neno Labba ndio lililotoa pia
neno Albabun ambalo hua na maana ya Moyo, Sehemu ya kati kati ya kitu, Kiini au
Ufahamu wa Kitu, Sehemu ya kitu isiyokua na Doa wala Dosari yeyote, Moyo wa Ibn
Adam au wa Tunda kama vile Moyo wa Nanasi au Fenesi.
Hivyo neno Lubb ambalo wingi wake hua Albaab ambalo humaanisha ufahamu msafi
usiokua na dosari, Al Lubb pia humaanisha aina ya ufahamu ambao ni wenye kuona kitu
kwa kina au kwa mtizamo wa ndani kabisa ya Moyo. Na ukweli ni kua sehemu ya Al
Lubb ndio inayokaa Nuru ya Allah Subhanah wa Taála ndani ya Moyo wa Ibn Adam,
ambapo Ibn Adam mwenye Moyo wenye Nuru hio basi hua ni mtu asiekua na mapenzi
ya kitu chochote ndani ya Moyo wake isipokua mapenzi ya Allah Subhanah wa Ta’ala
pekee na hivyo hua na darja ya juu kabisa miongoni mwa Viumbe kiasi ya kua Viumbe
wote hua chini yake, wakiwemo Majini na Malaika.
Hivyo kila Lubb hua ni Ufahamu lakini si kila Ufahamu hufikia darja au uwezo wa
kufahamu wa Lubb na ndio maana Allah Subhanah wa Taála akasema katika Quran kua:
﴿يُؤّتِى الحِْكْمَةَ مَن يَشَآءُ وَمَن يُؤْتَ الحِْكْمَةَ فَقَدْ أُوتِىَ خَيرْ اً كَثِيراً وَمَا يَ ذ َّك َّرُ إِلا َّ
أُوْ لُواْ ٱلأَلْبَابِ ﴾
Yu/tee alhikmata man yashao waman yu/ta alhikmata faqad ootiya khayran
katheeran wama yadhdhakkaru illa oloo al-albabi (Surat Al Baqara 2:269)
90
Tafsir: Humpa hikma yule amtakae, na yule anaepewa hikma nae, basi kwa hakika
hua ni mwenye kupewa Kheri nyingi sana, na hawatokumbuka isipokua Ulu Albaab.
Kutokana na kua na maana hiyo basi ndio maana Allah Subhanah wa Taála akatumia
neno Ulu al Baab mara kadhaa katika Qurán ili kuweka wazi wale Waumini ambao wana
ufahamu mkubwa wa Kiakili, Kihisia na Kiimani, na hivyo kua ni wenye kujua, kuona
na kuhisi alama za Allah Subhanah wa Ta’ala na katika kila kitu na katika kila jambo.
Sehemu ya hali ya Moyo ya Al Lubb hua ni sehemu ambayo ina utulivu wa hali ya juu na
hivyo hua haina miripuko kama ya Al Fuad wala uwepezi wa Al Qalb na pia ni tofauti na
Al Sadr.
AL SADR
Neno Sadara kwa Kiarabu hua ni lenye kumaanisha Kurudi, Kuendelea Mbele, Kupita,
Kutokea, Kufikia, au Kupiga Kifua. Neno Sadara ndio lililotoa neno Sadrun ambalo
humaanisha Kifua, Sehemu ya juu ya mwili, Ufaham, Moyo. Na pia likatoa neno Sudur
ambalo maana yake hua ni Nyoyo au Vifua.
﴿َٰي ُّهَا ٱلن َّاسُ قَدْ جَآءَتْكُمْ م َّوْعِظَةٌ مِّن ر َّبِّكُمْ وَشِ فَآءٌ لِّمَ ا فىِ ٱلص ُّدُورِ وَهُدً ى
وَرَحمَْةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ ﴾
Ya ayyuha alnnasu qad jaatkum mawAAidhatun min rabbikum washifaon lima fee
alssudoori wahudan warahmatun lilmu/mineena (Surat Yunus 10:57)
Tafsir: Enyi Watu! Hakika yamekujieni Mawaidha kutoka kwa Mola wenu, na ponyo
kwa yaliyomo ndani ya vifua vyenu. Muongozo na Rehma kwa Waumini.
Allah Subhanah wa Ta’ala anapozungumzia kuhusiana na Al Sadr basi hua anamaanisha
Moyo kuanzia nje yake hadi ndani kwenye kiini chake yaani Al Sadr hua unajumuisha
Ufahamu na Nguvu za uwezo wa Moyo katika kubeba hisia mbali mbali na kama
tunavyoona katika mfano wa aya iliyo hapo juu. Na ndio maana pale Allah Subhana wa
Ta’ala alipozungumzia kisa cha Nabii Musa katika Qurán basi anatuambia kua:
91
﴿قَالَ
رَبِّ ٱشْرَحْ لىِ صَدْرِي﴾
Qala rabbi ishrah lee sadree (Surat Ta-Ha 20:25)
Tafsir: Akasema (Musa) Ewe Mola wangu nifunulie Moyo wangu kwa ajili yangu.
Aya inatuwekea wazi kua baada ya Nabii Musa kufahamu kua anataka kubebeshwa
mzigo mkubwa na mzito wa kueneza ujumbe wa Mola wake basi akajua kua atahitaji kua
na kifua kikubwa chenye ustahmilivu wa kubeba siri na kudhibiti hisia tofauti ikiwemo
hasira, huruma n.k yaani Al Sadr hua ni kama Sanduku ambalo ndani yake mna vitu
vilivyofichwa na pia kupingana na vishawishi vinavyotokana na minong’onezo ya
Shaytani kama vile iliyotumika katika aya ifuatayo:
﴿ٱل َّذِى يُوَسْوِسُ فىِ صُدُورِ ٱلن َّاسِ ﴾
Alladhee yuwaswisu fee sudoori alnnasi (Surat Nas 114:5)
Tafsir: Yule ambae anaenong’oneza ndani ya Nyoyo za Watu.
Shaytan kamwe hawezi kuinong’oneza Qulub bali hua ni mwenye kuinong’oneza Al
Sadr, kwa sababu Allah Subhanah wa Taála ameuumba Al Qalb kua ni kitu kitukufu na
kisafi kabisa, yaani hapa tunaona kua mfano wa Al Qalb kua kama sanduku lenye hazina
ndani yake, lakini pia ni kama Ngome ambayo huwezi kuifikia hadi kwa kupitia katika
njia za viungo vyengine vya Mwili kama Macho, Masikio, Ulimi n.k ambazo ni miongoni
tu mwa Neema nyingi zisizohesabika za Allah Subhanah wa Taála juu yetu ambazo mara
nyingi tunakumbushwa katika Qur’an ikiwemo katika aya ifuatayo:
﴿وَٱذْكُرُواْ نِعْمَةَ ٱهلل َِّ عَلَيْكُمْ وَمِيثَاقَهُ ٱل َّذِى وَاثَقَكُم بِهِ إِذْ قُلْتُمْ سمَِعْنَا وَأَطَعْ نَا
وَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ إِن َّ ٱهلل ََّ عَلِيمٌ بِذَاتِ ٱلص ُّدُورِ ﴾
Waodhkuroo niAAmata Allahi AAalaykum wameethaqahu alladhee wathaqakum
bihi idh qultum samiAAna waataAAna waittaqoo Allaha inna Allaha AAaleemun
bidhati alssudoori (Surat Al Maidah 5:7)
92
Tafsir: Na kumbukeni Neema za Allah juu yenu, na makubaliano yake ambayo
mlikubaliana nae, pale mliposema: Tumesikia na Tunatii. Na Mcheni Allah kwani
kwa hakika Allah ni mwenye kujua yaliyomo ndani ya vifua.
Hivyo kutokana na Rehma zake Allah Subhanah wa Taa’la juu yetu basi hakumjaalia
Iblis kua ni mwenye uwezo wa kuingia ndani ya Qulub zetu, bali amemjaalia kua na
uwezo wa kuingia ndani ya Sudur, na hivyo ni sisi Ibn Adam kutokana na ujinga, kutojali
na kukosa shukrani kwa Mola wetu basi ndio tunajiachia na hivyo kumpa nafasi Iblis
kuingia ndani ya Qulub zetu kwa kupitia kwenye Sudur na kujaribu kutupotosha kwa
kupingana na Makubaliano tuliyokubaliana na Mola wetu, hili ni kosa ambalo kila mmoja
wetu ataenda kuulizwa juu yake kwani Allah Subhanah wa Taála anatuambia kua:
﴿إِن تَكْفُرُواْ فَإِن َّ ٱهلل ََّ غَنيِ ٌّ عَ نكُمْ وَلاَ يَرْضَى ٰ لِعِبَادِهِ ٱلْكُفْرَ وَإِن تَشْ كُرُواْ يَرْضَهُ
لَكُمْ وَلاَ تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ ثمُ َّ إِلىَٰ رَبِّكُمْ م َّرْجِ عُكُمْ فَيُنَبِّئُكُمْ بمَِا كُنتُمْ تَعْمَلُو َن
إِن َّهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ ٱلص ُّدُورِ ﴾
In takfuroo fa-inna Allaha ghaniyyun AAankum wala yardha liAAibadihi alkufra
wa-in tashkuroo yardhahu lakum wala taziru waziratun wizra okhra thumma ila
rabbikum marjiAAukum fayunabbi-okum bima kuntum taAAmaloona innahu
AAaleemun bidhati alssudoori (Surat Az Zumar 39:7)
Tafsir: Na kama mkikufuru, basi kwa hakika Allah si mwenye kuhitaji kitu kutoka
kwenu, na haridhii kufuru kutoka kwa Waja wake, na kama mkimshukuru basi
atakuridhieni. Hakuna mwenye mzigo atakaebeba mzigo wa mwenzake. Hivyo kwa
Mola wenu ndio marejeo yenu ambapo atakuambieni mliyokua mkiyafanya. Kwani
yeye ni mwenye kujua yale yaliyomo ndani ya Sudur.
Hivyo Moyo ndio wenye uuwezo wa kuchagua baina ya jema na ovu, jambo lililo sahih
na lisilo sahih kwa sababu kiungo hicho ndio makao makuu ya ufahamu wa Ibn Adam.
Hujjat ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali anasema kua: ‘Ingawa Moyo, Akili, Roho na Nafsi hua ni vitu
vyenye maana tofauti, lakini viungo hivi vyote kwa pamoja ndivyo vinavyowakilisha
kile ambacho kinachojulikana kama Viungo muhimu visivyoonekana vyenye uwezo
mkubwa wa Ibn Adam aliopewa na Allah Subhanah wa Ta’ala, kwani hivi ndivyo
vinavyoyapadisha darja Maumbile ya Ibn Adam na kumtofautisha yeye na Viumbe
wengine’.
93
Na ndio maana kukawa kuna makubaliano ya Ijmaa juu ya utukufu, ukubwa na darja ya
Amali zinazofanywa na Moyo hua ziko juu zaidi kulingana na zile zinazofanywa na
kiwiliwili. Hivyo kuna umuhimu wa Ibn Adam kujisalimisha kwa Allah Subhanah wa
Taála kwa kutumia Nyoyo zao, Kumuamini Mola wao kwa kutumia Akili zao na kufanya
Ibada kwa kutumia Miili yao.
Anasema Imam Mahammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Fahamu kua Allah
Subhanah wa Taála alipotaka kuiweka wazi Ilm ya kujulikana kwake basi aliiweka
Ilm hio ndani ya Aql, kisha akaweka sharti kua hakuna Ibn Adam yeyote
atakaeweza kuifikia Ilm hio kwa njia yeyote ile isipokua kwa njia ya kutumia Aql,
Hivyo mtu yeyote yule alienyimwa Aql basi hua pia ni alienyiwa Ilm. Na kua na Aql
basi ni kua na Husn Al Nadhar (Hikma) mtazamo bora ya kujidhibiti juu ya kila
unachokifanya kwa ajili yako na kwa ajili ya Mola wako.’
Na kwa mtizamo huo basi tunaona kua Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al
Tustari anatufafanulia kua maumbile ya ndani ya Ibn Adam yanajumuisha hali ya
Kimaumbile ya Nafsi, Al Qalb, Aql na Al Ruh kama alivyosema katika maana ya aya
ifuatayo:
﴿فَٱلْمُلْقِيَاتِ ذِكْ راً ﴾
Faalmulqiyati Dhikran (Surat Al Mursalat 77:05)
Tafsir: Na kwa Malaika Wanaoshusha Ukumbusho.
Ambapo ayah inazungumzia Ujumbe wa Qurán na kwa mtizamo wa Imam Abu
Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari basi tunaona anasema kua: Hii Qurán ni
Wahy, unaopita katika njia ya Ilham, ambayo inajumuisha Nafs Al Ruh, Aql na Qalb
na kuwekwa juu ya Nafsi ya Maumbile. Na hii hua ndio njia ya Dhikr al Khafiy
(Ukumbusho uliyofichikana).
Kwaini Allah Subhanah wa Ta’ala amesema katika Qur’an kua:
﴿فَمَن يُرِدِ ٱهلل َُّ أَن يَهْدِيَهُ يَشْرَحْ صَدْرَهُ لِلإِسْلاَمِ وَمَن يُرِدْ أَن يُضِل َّهُ يجَْعَلْ صَ دْرَهُ
ضَيِّقاً حَرَجاً كَأَنم ََّا يَص َّع َّدُ فىِ ٱلس َّمَآءِ كَذٰ لِكَ يجَْعَلُ ٱهلل َُّ ٱلرِّجْسَ عَ لَى ٱل َّذِينَ لاَ
يُؤْمِنُونَ ﴾
94
Faman yuridi Allahu an yahdiyahu yashrah sadrahu lil-islami waman yurid an
yudhillahu yajAAal sadrahu dhayyiqan harajan kaannama yassaAAAAadu fee
alssama-i kadhalika yajAAalu Allahu alrrijsa AAala alladheena la yu/minoona
(Surat Al An Aam 6:125)
Tafsir: Ama kwa yule ambae Allah hutaka kumuogoza basi humfungulia kifua chake
kwa ajili ya Uislam, na kwa yule ambae hutaka kumdhalilisha basi humfungia kifua
chake na kua ni chenye kubana kama kwamba ni mwenye kupanda juu kuelekea
Angani. Hivyo ndivyo Allah anavyotoa adhabu kwa wale ambao hawakuamini.
Anasema Imam Muhammad Ibn Jarir Al Tabari Al Shafii kuhusiana na aya hii kua Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliulizwa: ‘Jee Moyo hufunguka vipi kwa ajili ya
Uislam?’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu: ‘Ni Nuru ya Allah
Subhanah wa Ta’ala ndio inayoingizwa ndani ya Nyoyo za Ibn Adam, hivyo Moyo
hua ni wenye kutulia na kufunguka.’
Na ingawa aya imetumia neno Harajan ambalo hua ni lenye kumanisha: Kubana kwa
matawi ya mti kiasi ya kua sehemu ya matawi hayo yaliyobanana haiwezi kufikika
na mtu wala na mnyama, lakini kwa upande wa Sayyidna Umar Ibn Al Khattab Radhi
Allahu Anhu alipoambiwa juu ya maana hiyo na mabedui ambao wao ni wataalamu
wakubwa wa lugha ya Kiarabu, basi Sayyidna Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu
akasema: ‘Huo hua ni Mfano wa Nyoyo za Wanafiq, kwani kamwe hakuna jema
linaloweza kuingia ndani ya Nyoyo zao.’
Na anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala ametofautisha baina ya Murid (Mja anaemtafuta Mola wake)
na Murad (Mja anaetafutwa na Mola wake) ijapokua Waja wawili hawa wote ni
kutoka kwake yeye mwenyewe Allah Subhanah wa Ta’ala. Lakini yeye Allah
Subhanah wa Ta’ala ni mwenye kutofautisha baina ya Khusus (Wenye sifa hususan
maalum) na Umum (Wenye sifa ya Ujumla) na hivyo kawatofautisha wale Murad
(wanaotafutwa na Allah Subhanah wa Ta’ala) katika ayah hii na nyenginezo’
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari anaendelea kutufafanulia kwa
kusema kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala hua ni mwenye kuziangalia Nyoyo, zote
kwani nyoyo hua ziko mbele yake, hivyo anapoona Moyo fulani una unyenyekevu
juu yake basi huujalia jema atakalo juu yake Moyo huo, Kisha baada ya hapo
hufuata Nyoyo zenye kubadilika haraka na kurudi kwake yeye Allah Subhanah wa
Ta’ala. Hizo ni aina mbili za Nyoyo anazozijaalia mema.’
Na kisha Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari akasema: ‘Kila wakati
Allah anapouangalia Moyo na akauona kua ni wenye kua na hamu ya Ulimwengu
huu, basi huuchukia Moyo huo na kuchukia kwake huko, hua kunajionesha kupitia
95
katika kuuwachia Moyo huo pamoja na Nafsi ya Mtu huyo. Kwani Moyo
haumilikiwi na yeyote isipokua Allah Subhanah wa Ta’ala, na hivyo hautakiwi
kumtii yeyote isipokua Allah Subhanah wa Ta’ala. Hivyo kama ukiwa unaujali
Moyo wako basi Mfanye Mola wako awe ndie msiri wako.’
Hivyo kama vile ambavyo Quran ilivyotumia maneno Qalb, Fuad, Lubb na Sadr
kumaanisha Moyo basi pia tunapoiangalia neno Aql yaani Akili basi tunaona kua Qurán
imeitaja sehemu ya kiungo hiki katika hali tofauti lakini kimaana kuenda sambamba na
hali za Hijr, Hilm, Nuha na Balu.
MAANA YA AQL, HIJR, HILM, NNUHA NA BALU.
Neno Aql linatokana na neno Aqala la Kiarabu ambalo hua ni lenye kumaanisha.
Kufunga, Kuzuia, Kua na Busara, Kufahamu, Kulipia Fidya Mtu fulani. Kupanda juu ya
Kilele cha Mlima na pia hua ni lenye kumaanisha Kutumuia Ufahamu au Akili.
Ingawa kuna tofauti kimaandishi na kimatamshi lakini Quran ilipozungumzia Ufahamu
basi imetumia maneno kadhaa yenye kuenda sambamba kimaana na neno Aql, miongoni
mwao ikiwemo neno Naha ambalo hua ni lenye kumaanisha Kujizuia au Kufaham,
ambapo tunaona kua hali nyengine ya neno hili ni ile hali ya Nuhyatun ambayo hua ni
yenye kumaanisha kile kinachomzuia Ibn Adam kutovuka mipaka na kutofanya mambo
yasiyoingia akilini. Neno Nuha limetumika katika Qurán pale iliposema:
﴿أَفَلَمْ يَهْدِ لهَُمْ كَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُمْ مِّنَ ٱلْقُرُونِ يمَْشُونَ فىِ مَسَاكِنِهِمْ إِن َّ فىِ ذٰ لِ كَ
لآَ َتٍ لأُِ وْ لىِ ٱ ل ن ُّ هَ ٰ ى ﴾
Afalam yahdi lahum kam ahlakna qablahum mina alqurooni yamshoona fee
masakinihim inna fee dhalika laayatin li-olee alnnuha (Surat Ta-Ha 20:128)
Tafsir: Jee si Muongozo kwao wao (Kujua) kua tumeviangamiza vizazi vingapi kabla
yao. Ambavyo wao wanatembea juu ya makazi yao? Hakika katika haya kuna mafunzo
kwa waliopewa Nnuha (Ufaham).
96
Quran imetumia pia neno Ahlam ambalo linatokana na neno Halama lenye kumaanisha
Ndoto, Muono na pia hua linamaanisha Ustahmilivu. Neno Ahlam hua pia linamaanisha
Kupea Kiufaham na maana hii inaonekana wazi pale Allah Subhanah wa Ta’ala ilipohoji
juu ya Makafiri kua na ufahamu wa kutafakkari, kutokana na kukanusha kwao lakini
hapo hapo kua na ufahamu tu si hoja bali hoja ni kua na ufahamu uliopea kwani huo ndio
ambao unamsababisha mtu kua na uwezo wa Kutafakari kwa kina na ndio maana Allah
Subhanah wa Ta’ala akauliza:
﴿أَمْ أتَْمُرُهُمْ أَحْ لاَمُهُمْ هبَِٰذَ آ أَمْ هُمْ قَوْ مٌ طَاغُونَ ﴾
Am ta/muruhum ahlamuhum bihadha am hum qawmun taghoona (Surat AT Tur
52:32)
Tafsir: Jee Ahlamuhum (Ufahamu wao) ndio unawaamrisha (kukuzulia ewe
Muhammad) au wao ni watu wanaopenda kuvuka mipaka?
Hivyo bila ya shaka ni kua ufahamu wao watu hao ambao ni Makafiri unaonesha kua
umepea lakini hata hivyo wanafanya hivyo kwa sababu ya kua na Kibri tu kutokana na
maumbile ya baadhi ya Ibn Adam wanapoona kua katika hali ya kua ni wenye
kujitosheleza ambayo hua ni sawa na ile hali inayoelezewa na aya ifuatayo:
﴿ كَلا َّ إِن َّ ٱلإِنسَانَ لَيَطْغَى ٰ ۞ أَن ر َّآهُ ٱسْتَغْنىَٰ ﴾
Kalla inna al-insana layatgha; An raahu istaghna (Surat Al Alaq 96:6-7)
Tafsir: Hakika Ibn Adam hua ni mwenye kuvuka mipaka. Anapojiona kua
anajitosheleza.
Ama kuhusiana na jambo hili la kutotumia Ahlam kutokana na kua na Kibri basi mwisho
wake hua majuto katika siku ya Malipo kama inavyoweka wazi hivyo Quran kwa
kusema:
﴿وَقَالُواْ لَوْ كُن َّا نَسْمَعُ أَوْ نَعْقِلُ مَا كُ ن َّا فيِۤ أَصْ حَ ابِ ٱلس َّ عِيرِ ﴾
Waqaloo law kunna nasmaAAu aw naAAqilu ma kunna fee as-habi alssaAAeeri
(Surat Al Mulk 67:10)
97
Tafsir: Na wao watasema: ‘Lau kama tungesikiliza au tungetumia akili zetu, basi
kamwe tusingekua ni miongoni mwa watu wa Motoni’
Mbali ya kua Neno Hajara ambalo ndio asili ya neno Hijra, lenye kumaanisha Kuhama
na ndio maana ambayo wengi sana ni wenye kuijua kutokana na tukio la Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kuhama kutoka katika Mji wa Makkah na kuhamia katika Mji
wa Madinah ambapo ndani ya tukio hili basi mna mafunzo mengi ikiwemo lile la
Umuhimu wa Nia katika kila Jambo analolifanya Muislam, kwani amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua:
‘Ama kwa hakika Amali Hutegemeana na Nia, na Kwa Hakika Kila mtu atalipwa
Kulingana na Nia yake, Hivyo yeyote Yule aliefanyq Hijra kwa Ajili ya Kidunia au
kwa ajili ya Mwanamke Basi Hijra yake hua ni kwa Ajili ya alichokifanyia
Hijra’(Sahih Bukhari)
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliyasema maneno ya Hadith hii kwa
ajili ya kuainisha Umuhimu wa Nia katika Kila Jambo. Na tunapoangalia hadith basi
tunaona kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anazungumzia Hijra kisha ndani
yake akainisha aina za Nia na Madhumuni ya Hijra.
Kwani katika Wakati huo, na hadi katika wakati wa leo pia Kuna watu hua ni wenye
Kufanya Hijra kwa ajili ya Dini yao, na kuna wanaofanya Hijra kwa ajili ya Dunia yao.
Na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kuhusiana na Wanawake kwa sababu
kuna Watu walifanya Hijra ya kutoka Makkah kuelekea katika Mji wa Madinah si kwa
sababu ya Dini yao wala si kwa sababu ya Mola wao na Mtume wake basi kwa sababu
tu ya Kusikia kua katika Mji wa Madinah kuna Wanawake wazuri zaid kuliko Wanawake
wa Makkah.
Ambapo kwa upande mwengine basi anasema Imam Maaruf Al Kharki kua: ‘Kila
kinapotokea Kitendo kinachofanywa na Ibn Adam basi hua ni chenye kutokana na
Nia Ndani yake, Hivyo Kama Nia ni Sahih basi na Kitendo hua Sahih. Na kama Nia
si Sahih basi na Kitendo hia si Sahih
Ambapo Nia Sahih juu ya Kitendo Sahih hua katika hali 3 zifuatazo;
1-Kama ikiwa Nia juu ya Kitendo Husika hua ni yenye kutokana na Kumuogopa
Allah Subhanah wa Ta'ala. Basi Kitendo hicho hua ni sawa na kufanya Ibada kwa
Mja huyo mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala.
98
2-Kama ikiwa Nia Juu ya Kitendo Hua ni yenye kutokana na Kuikimbilia Pepo ya
Allah Subhanah wa Ta'ala. Basi Kitendo hicho hua ni sawa na kufanya Biashara
kwa Mja huyo mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala. kwa ajili ya Akhera yake.
3-Kama ikiwa Nia juu ya Kitendo hicho hua ni yenye kutokana na Kuona aibu kwa
Mja Mbele ya Mola wake, na hivyo hua ni kutekeleza Wajibu wake na kuonesha
Shukrani kwa Mja huyo mbele ya Mola wake. Basi Kitendo hicho hua ni sawa na
Ibada ya Mtu mwenye Kujikomboa na Kutaka kujitafutia Uhuru unaotokana na
kua na uzito wa Majukumu yake mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Naam, Inasikitisha kuona kua wengi wetu pia leo hii hua tunafanya Ibada zetu nyingi
huku tukiwa na nia ya hali ya 3 yaani kwa sababu tu ya kujipunguzia Uzito wa
Majukumu.
Yaani kwa Mfano: Watu Wanafanya Ibada fulani kwa sababu tu ya Kumrishwa Na
Muumba kufanya Ibada hio, bila kutilia maanani kua kufanya kwao Ibada husika mbali
ya kua ni Jukumu lao lakini hua ni kwa ajili ya Manufaa yao wao wenyewe.
Na hivyo hatufanyi Vitendo kwa ajili ya Nia ya Aina ya kwanza yaani kwa Ikhlasi au
kwa ajili ya Nia ya Aina ya pili yaani kujitolea kufanya Bishara na Allah Subhanah wa
Ta’ala kwa ajili ya kuwekeza katika Akhera yetu, na hivyo kutokua ni wenye kufanya
Ibada kwa Kutumia Hisia na Ufaham juu ya kile tunachokifanya, na hii ndio maana
nyengine ya Hijr.
Kwani pia neno Hajara ndio asili ya neno Hijrun ambalo maana yake hua ni Kua na hisia
na Ufaham, mfano wa matumizi wa maana hii ni katika aya ifuatayo:
﴿هَلْ فىِ ذٰ لِكَ قَسَمٌ لِّذِى حِ جْرٍ ﴾
Hal fee dhalika qasamun lidhee hijrin (Surat Al Fajr 89:5)
Tafsir: Hakika katika hayo mna vithibitisho kwa wale wenye Hijrin (Ufahamu).
Na tumalizie kwa kuangalia neno Balun ambalo nalo ni linaloenda sambamba kimaana
na neno Aql neno hili limetumika katika Qurán kumaanisha Moyo, Akili, Ufahamu, Nia
au Hali ya Ufahamu, Mawazo, Mtizamo au Jambo muhimu sana, miongoni mwa aya
zilizotumia neno hili ni pamoja na:
99
﴿وَقَالَ ٱلْمَلِكُ ٱئْتُونىِ بِهِ فَلَم َّا جَآءَهُ ٱلر َّسُولُ قَالَ ٱرْجِ عْ إِلىَٰ رَبِّكَ فَاسْأَلْهُ مَا ابَ لُ
ٱلنِّسْوَةِ ٱللا َّتِى قَط َّعْنَ أَيْدِيَهُن َّ إِن َّ رَبىِّ بِكَيْدِهِن َّ عَلِيمٌ ﴾
Waqala almaliku i/toonee bihi falamma jaahu alrrasoolu qala irjiAA ila rabbika
fais-alhu ma balu alnniswati allatee qattaAAna aydiyahunna inna rabbee
bikaydihinna AAaleemun (Surat Yusuf 12:50).
Tafsir: Na akasema Mfalme: ‘Mleteni mbele yangu’. Lakini Wajumbe hao walipofika
mbele yake (Yusuf) basi akasema: ‘Rudini kwa bwana wenu na mmuulize: ‘Ni ipi hali
ya ufahamu wao wale Wanawake waliojikata viganja vyao?’ Hakika Mola wangu ni
mwenye kujua juu ya hila zao’
Ambapo aya hio Nabii Yusuf anauliza juu ya hali ya Akili, Ufahamu, Mawazo au
Mtizamo wa wale Wanawake waliompelekea yeye kua ni mwenye kuenda Jela bila ya
kua na makosa. Jee wametafakkar na kuona kua wao ndio wenye makosa? Jee Ufahamu
wao utakubali kua wao ndio wenye makosa? n.k.
Na mfano mwengine ni pale Firáwn alipomwambia Nabii Musa kama inavyoelezewa:
﴿قَالَ فَمَا ابَلُ ٱلْقُرُونِ ٱلأُولىَٰ ﴾
Qala fama balu alqurooni al-oola (Surat Ta-Ha 20:51)
Tafsir: Akasema (Firáwn): ‘Jee ni ni hali yao wale waliotangulia kabla yetu?’
Yaani Fir’awn anamhoji Nabii Musa kua kama kweli kuna Mungu, alieumba kila kitu na
kukipa muongozo, kwa nini watu hao basi hawakumuabudu Mola wao? Ufahamu wao
na akili zao ilikuaje ukawakoseshea uongofu? Jee walikua hawana Akili na Ufahamu?
Ina maana wameangamia au vipi?
Hivyo ukweli ni kua Qurán inazungumzia mambo mengi sana ambayo bila ya kufuatilia
basi hua ni yenye kuonekana kua ni ya kawaida, na ni pale tu tutakapoyafuatilia, na
kuyatafakkari basi ndipo tutakaponufaika na kupata Baraka zilizomo ndani yake, kwani
vyenginevyo basi tutakua ni miongoni mwa walioingia katika hali ya Sakara.
100
Neno Sakara kwa lugha ya Kiarabu kwa upande mmoja hua ni lenye maana sawa na neno
Aql ambayo ni Kuzuia, Kufunga, Kudhibiti, Kua katika hali ya kujilinda, n.k. Lakini kwa
upande mwengine wa kimaana basi neno Sakara hua ni lenye kupingana kimaana na neno
Aql, kwani tumeona kua Aql hua inamanisha kua na Akili, Kua na Ufahamu na pia kua
ni mweye Kutumia Akili wakati neno Sakara huani lenye kukanusha mtu kua na Ufaham,
yaani kua katika hali ya Kua ni kizingiti baina ya mtu na Ufahamu wake, Raha kubwa
sana au Maumivu Makali sana yanayotoa Akili, Kutokua na Ufahamu, Kutokua na Akili,
Kulaaniwa kiakili au Kulewa.
Anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Sakara hua ni
kitu chochote kile ambacho kinachoilevya Nafsi ya Ibn Adam hapa Duniani na
hivyo kumpelekea Ibn Adam huyo kua ni mwenye kuisahau Akhera yake’
Ndio maana Allah Subhanah wa Taála akatuzindua ili tusimsahau yeye na tusiisahau siku
ya mwisho ya Ulimwengu tunaoishi ambayo watu wataonekana kama wamelewa lakini
hawajalewa kama inavyosema aya ifuatayo:
ُ
﴿َٰي ُّهَا ٱلن َّاسُ ٱت َّقُواْ رَب َّكُمْ إِن َّ زَلْزَلَةَ ٱلس َّاعَةِ شَيْءٌ عَظِيمٌ ۞ يَ وْمَ تَرَوْنَهَا تَذْهَل
كُل ُّ مُرْضِ عَةٍ عَم َّ آ أَرْضَعَتْ وَتَضَعُ كُل ُّ ذَاتِ حمَْلٍ حمَْلَهَا وَتَرَى ٱلن َّاسَ سُ َك ارَ ٰى
وَمَا هُم بِسُكَارَىٰ وَلَٰكِن َّ عَذَابَ ٱهلل َِّ شَدِيدٌ ﴾
Ya ayyuha alnnasu ittaqoo rabbakum inna zalzalata alssaAAati shay-on
AAadheemun; Yawma tarawnaha tadhhalu kullu murdhiAAatin AAamma ardaAAat
watadaAAu kullu dhati hamlin hamlaha watara alnnasa sukara wama hum bisukara
walakinna AAathaba Allahi shadeedun (Surat Al Hajj 22:1-2)
Tafsir: Enye Watu! Mcheni Mola wenu! Kwani Mtetemeko wa Ardhi wa Saa (Ya
Kiama) ni kitu kibaya sana. Katika Siku hio mtaona kila Mama anaenyonyesha
atamsahau Mtoto wake anaemnyonyesha, na mwenye Mimba ataiangusha (Itatoka
kwa Hamkani) Mimba yake, na Utawaona watu wakiwa katika hali ya kua ni Sukara
(Waliolewa), lakini hakuna atakaekua ni Sakara (kalewa), na kwa hakika Adhabu ya
Allah ni kali sana.
Naam aya inazungumzia hali itakavyokua katika saa ya mwisho ya Ulimwengu ambayo
itakuja kabla ya Siku ya Kufufuliwa, na ndio maana ikazungumzia juu ya kutoka kwa
Mimba kutokana na hamkani na tafrani zake siku hio, kwani hii ni siku ambayo
Ulimwengu utabadilika Maumbile yake na hivyo Jua litachomoza kutoka katika upande
101
wa Magharibi, Mfumo wa Nguvu wa Sayari utakwisha nguvu zake za Mvutano kutokana
na amri ya Mola wake alieuumba na hivyo kua ni wenye kusimama kwa ghafla moja.
Sayari, Nyota na Mwezi zitakosa muelekeo na kuanza kupukutika na hivyo Dunia
itashindwa kutulia kwenye mhimili wake nayo pia itakua ni yenye kutetemeka katika hali
nzito, yenye kasi kubwa isiyokua ya kawaida, na hivyo basi huenda baadhi ya Sayari na
vipande vyake vikaangukia Duniani. Hii ni hali ya hatari sana kwa Ibn Adam na ukweli
ni kua ni hali isiyoelezeka wala kufahamika kiufaham kwa ufahamu wa Ibn Adam kwani
hua ni yenye kuonesha kuwepo kwa Muumba na uwezo wake ambae ni Allah Subhanah
wa Taa’la.
Anasema Imam Musa Ibn Jafar Al Sadiq kua: ‘Lam Yakhaf Allaha Man Lam Yaaqil
Aani Allah – Yeyote yule asiemuogopa Allah Basi Hana Akili au Ufahamu juu ya
Allah.’
Kwa kumalizia juu ya hali za Maumbile na hali za Nyoyo na Akili na Ufahamu wa
Viungo hivyo basi na tuangalie hali hizo kulingana na mtizamo wa Imam Abu Abd Allah
Muhammad Ibn Ali Ibn Hasan Ibn Bashir Al Hakim Al Tirmidhi ambae yeye anasema
katika kitabu chake cha Bayan al Farq Bayn Al Sadr al Al Qalb wa Al Fuad wa Al Lubb
kua:
AL SADR – Ndio Sehemu inayokaa Nuru ya Uislam na pia hujulikana kama Nafs Al
Ammarah.
AL QALB – Ndio Sehemu inayokaa Nuru ya Iman na pia hujulikana kama Nafs Al
Mulhimah.
AL FUAD – Ndio Sehemu inayokaa Nuru ya Maarifah na pia hujulikana kama Nafs Al
Lawwamah.
AL LUBB - Ndio Sehemu inayokaa Nuru ya Tawhid na pia hujulikana kama Nafs Al
Mutma’inah.
Huo ni mtizamo wa Imam Al Hakim Al Tirmidhi, hivyo ili kuifahamu zaid basi na
tufafanue hizi aina nne za Nafsi zilizonasibishwa na hali nne za Nyoyo, ambapo tunaona
kua Neno Nafsi limetokana na neno Nafasa ambalo kwa lugha ya Kiarabu hua na maana
ya Kitu chenye Thamani, Katika kuomba, Kuliwaza, Kufurahisha.
NAFS - MAUMBILE YAKE NA UHIBITI WAKE.
Neno Nafs linatoka na neno Nafasa ambao kwa lugha ya Kiarabu hua ni lenye
kumaanisha Kitu Adimu na chenye Thamani Kubwa sana, kiasi ni hasara kubwa sana
102
kukitupa au kukipoteza na kama ukikipoteza basi bila ya shaka pengo lake hua kamwe
haliwezi kuzibika. Neno Nafasa hua pia ni lenye Kumaanisha Kuliwaza, Kuchangamsha
au Omba.
Subhana Allah! Bila ya shaka lugha ya Kiarabu ni lugha yenye kujitosheleza tena sana,
kwani tuunapoangalia maana ya neno Nafasa ambalo ndio lililotoa neno Nafsi basi neno
hilo moja tu kimaana limebeba Uzito mkubwa sana wa maana ya Nafsi kwa kina na
kutuonesha kua Nafsi ni kitu chenye Thamani kubwa sana na kilicho adimu sana kiasi ya
kua ukikipoteza basi hua umekula hasara kubwa sana na kamwe hutoweza kuliziba pengo
lake.
Neno Nafasa ndio lililotoa neno Nafsun ambalo maana yake hua ni Nafsi, Roho, Uhai,
Mtu alie hai, Ufahamu, Hisia za ndani za matamanio. Na pia neno Nasafa limetoa neno
Nafsi ambalo nalo pia maana yake hua ni Mimi mwenyewe Binafsi, Kitu chenyewe,
Damu, Kanuni za Msingi, Nia au Makusudio, Matamanio, Moyo, n,k
Nafsi hua ni kitu ambacho kimo ndani ya Miili ya Viumbe lakini hakionekani wala
hakikamatiki isipokua kwa Allah Subhanah wa Ta’ala ambae ndie alietuumba. Hivyo
ingawa Nafsi haikamatiki wala haionekani lakini kimaumbile Nafsi hua inadhibitika na
kiumbe husika mwenye Nafsi hio kwani hua inajumuisha hali ya uhusiano wa ufanyaji
kazi wa hisia zote kamilifu za mwili wa kiumbe kwa kutumia Ufaham, Akili, Moyo na
Ubongo, n.k. Na ndio maana akatuusia Allah Subhanah wa Ta’ala kwa kusema kua:
﴿وَٱذْكُر ر َّب َّكَ فىِ نَفْسِ كَ تَضَر ُّعاً وَخِ يفَةً وَدُونَ ٱلجَْهْرِ مِنَ ٱلْقَوْلِ بِٱلْغُدُوِّ
وَٱلآصَالِ وَلاَ تَكُنْ مِّنَ ٱلْغَافِلِينَ ﴾
Waodhkur rabbaka fee nafsika tadharruAAan wakheefatan wadoona aljahri mina
alqawli bialghuduwwi waal-asali wala takun mina alghafileena (Surat Al Isra 7:205)
Tafsir: Na Mkumbuke Mola wako katika Nafsi yako, kwa Unyenyekevu na kwa Khofu,
bila ya kupaza sauti Asubuhi na Jioni na Usiwe miongoni mwa wenye kughafilika.
Na kisha akatoa onyo juu ya watakaoshindwa kuzidhibiti Nafsi zao, na kuwaahidi wale
watakao weza kuzidhibiti Nafsi zao kwa kusema:
103
﴿فَأَم َّا مَن طَغَى ٰ ۞ وَآثَرَ ٱلحَْيَاةَ ٱلد ُّنْيَا ۞ فَإِن َّ ٱلجَْحِ يمَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ ۞ وَ أَم َّا مَنْ
خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ وَنَهَى ٱلن َّفْسَ عَنِ ٱلهَْوَىٰ ۞ فَإِن َّ ٱلجَْن َّةَ هِ ىَ ٱلْمَ أْوَىٰ ﴾
Faamma man tagha; Waathara alhayata alddunya; Fa-inna aljaheema hiya
alma/wa; Waama man khafa maqama rabbihi wanaha alnnafsa AAani alhawa; Fainna
aljannata hiya alma/wa (Surat An Naziat 79:37-41)
Tafsir: Ama kwa yule atakaevuka mipaka. Na akawa ni mwenye kupendelea Maisha
ya Dunia, Basi kwa Hakika Motoni ndio yatakapokua makazi yake. Ama kwa yule
atakae kua ni mwenye kua na khofu ya kusimama mbele ya Mola wake na akaizuia
Nafsi yake na Matamanio, Basi kwenye Bustani (Peponi) ndio yatakayokua makazi
yake.
Ili kufahamu zaidi juu ya udhibiti wa Nafsi na hali zake basi na tuangalie mtizamo wa
Sultan al Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi ambae anatufafanualia kwa kusema
kua: Kimaumbile Nafsi hua ni kitu kimoja, lakini ni chenye hali nyingi
zinazotofautiana. Nafsi inapokua katika hali yake husika ya juu kabisa basi hua
katika hali ambayo ni yenye kusimamia hali yake hio na kuizidishia nguvu kwa
kuzidisha mwamko wake wa kuendelea kua katika hali husika.
Ama kwa upande wa Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad
Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii basi yeye anatuambia kua:
Kimaumbile Nafsi zimegawika katika aina mbili:-
1- Al Nufus Al Sahiha – Yaani Nafsi zenye Afya yake ya kimaumbile na hivyo hua
ni zenye kupeka Wahy na Ilham. Aina hii ya nafsi hua ni zenye kuonesha Miujiza
kwa sababu hua hazishuguliki na matamanio ya Kidunia. Hizi Hua ni Nafsi za
Maitume na Manabii ambao wao hua ni Madaktari wa Nafsi.
2- Al Nufus Al Maridha – Yaani Nafsi zenye maradhi ambazo nazo hua katika darja
tatu zifuatazo:
a) Nafsi zenye Maradhi kutokana na Matamanio ya Kidunia, lakini hua ni zenye
kutibika na kurudi katika hali yake ya kiafya ya kimaumbile kupitia katika
njia ya Kutafuta I’lm, Kutafakkar na Kuzingatia.
104
b) Nasi zenye Maradhi kutokana na hamu na ushawishi wa kuyakumbatia
Matamanio ya Kidunia na hivyo nafsi hizi hua ni zenye kua na Nuru. Ambayo
hua inaisaidida kuipigania Nafsi hii katika maisha yake yote ili kuirudisha
katika hali yake ya afya ya kimaumbile kwa kupitia katika njia ya I’lm
ambayo hua ni yenye kuyaangamiza Maradhi yaliyoikumba Nafsi hio bila
ya kutegemea.
c) Nafsi zenye Maradhi kutokana na kuharibika kwa hali ya kimaumbile ya nafsi
hio. Nafsi hii hua katika hali ambayo haiwezekani kutibika wala
kurekebishika na kurudi katika hali yake ya kimaumbile.
Wanazuoni wanasema kua Nafsi ziko katika hali 7 tofauti, ambazo ni Nafs al Ammara,
Nafs Al Lawwamah, Nafs Al Mulhimah, Nafs Al Mutma’inah, Nafs ar Radhiyah, Nafs Al
Mardhiyah na Nafs al Kamilah, ambapo kulingana na mtizamo wa Imam Al Hakim Al
Tirmidhi basi zinafafanulika kulingana na mifano ya aya zilizotaja hali za Nafsi ambazo
ni:
NAFS AL AMMARAH BI ALSUI (NAFS SHAHWANIYYAH)
Nafs Al Ammarah bi al Sui au Nafs Shahwaniyya (Nafsi ya Matamanio) hali ya Nafsi
ambayo inanasibishwa na hali ya sehemu ya hali ya Moyo inayokaa Nuru ya Uislam
yaani Al Sadr. Hali hii ya Nafsi hua ni yenye kumuelekeza Ibn Adam katika kufanya
maovu, hali hii inawekwa wazi katika Qurán pale ilipozungumzia juu ya kisa cha Nabii
Yusuf ambae alisema:
﴿وَمَآ أُبَرِّئُ نَفْسِ ي ۤ إِن َّ ٱلن َّفْسَ لَأَم َّارَةٌ بِٱلس ُّو ۤ ءِ إِلا َّ مَا رَحِ مَ رَبيّ ِ ۤ إِن َّ رَبىِّ غَ فُورٌ
ر َّحِ يمٌ ﴾
Wama obarri-o nafsee inna alnnafsa laammaratun bialssoo-i illa ma rahima rabbee
inna rabbee ghafoorun raheemun (Surat Yusuf 12:53)
Tafsir: Nami Siiwachi huru Nafsi yangu, kwani kwa Hakika Nafsi ni yenye kuamrisha
kufanya maovu isipokua pale Mola wangu anapoingiza Rehma zake, Hakika Mola
wangu ni mwingi wa usamehevu na ni mwingi wa Rehma.
105
Nafsi inapokua katika hali ya Ammara bi Su yaani kuamrisha kufanya Maovu basi hua ni
yenye kuelemea zaidi na kuzama katika matamanio ya kidunia na ndio maana kwa
upande mwengine ikawa inaitwa Nafs Shahwaniyyah hivyo hakuna mwenye uwezo wa
kuiokoa Nafsi hio kutokana na Maovu yake isipokua kutokana na msaada wa Allah
Subhanah wa Taála alieiumba Nafsi hio, kama vile anavyosema Allah Subhanah wa
Ta’ala katika Qurán kua:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ لاَ تَت َّبِعُواْ خُطُوَاتِ ٱلش َّيْطَانِ وَمَن يَت َّبِعْ خُطُوَاتِ ٱلش َّيْطَ انِ
فَإِن َّهُ َْمُرُ بِٱلْفَحْشَآءِ وَٱلْمُنْكَرِ وَلَوْلاَ فَضْلُ ٱهلل َِّ عَلَيْكُمْ وَرَحمَْتُهُ مَا َز كَا مِنكُمْ مِّ ْن
أَحَدٍ أَبَداً وَلَٰكِن َّ ٱهلل ََّ يُزَكِّى مَن يَشَآءُ وَٱهلل َُّ سمَِيعٌ عَلِيمٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo la tattabiAAoo khutuwati alshshaytani waman
yattabiAA khutuwati alshshaytani fa-innahu ya/muru bialfahsha-i waalmunkari
walawla fadhlu Allahi AAalaykum warahmatuhu ma zaka minkum min ahadin
abadan walakinna Allaha yuzakkee man yashao waAllahu sameeAAun AAaleemun
(Surat Nur 24:21)
Tafsir: Enyi mlioamini! Msifute hatua za Shaytan, na yeyote yule atakaefuata hatua
za Shaytan, basi (Shaytan) hua anamuamrisha kufanya maovu na kuasi. Na kama si
fadhila za Allah juu yenu na Rehma zake juu yenu, basi hakuna miongoni mwenu
ambae angelikua msafi asiekua na dhambi. Lakini Allah humsafisha amtakae na kwa
hakika yeye ni mwenye kuona na kujua.
Bila ya shaka Nafsi hii ya Al Ammarah bi al su hua ni Nafsi ambayo haina hali ya
kutafakkari, yenye ubiNafsi, na hivyo hua ni yenye kuendekeza Shahawa (Matamanio
yake) na kufanya mambo kwa kutumia nguvu bila ya kufikiria matokeo yake ya baadae,
na ikiachiwa bila ya kupata msaada wa Allah Subhanah wa Taála alieiumba basi hua ni
Nafsi yenye kuelekea katika mahala pabaya na hivyo hua ni yenye kujiangamiza kwa
kufuata muongozo wa Shaytani kutokana na kukosa muongozo wa Muumba ambao ni
muongozo wa Dini ya Kiislam, hali hii ya Nafsi hua ni tofauti na Nafsi Al Mulhima.
NAFS AL MULHIMAH
106
Nafs Al Mulhima hali ya Nafsi ambayo inanasibishwa na hali ya sehemu ya Moyo
inayokaa Nuru ya Iman yaani Al Qalb, hii hua ni hali ya Nafsi ambayo inapata Ilham
yaani Muongozo wa Kimaumbile kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala alieiumba Nafsi
hio. Aina hii ya Nafsi imetajwa katika aya ifuatayo:
﴿وَنَفْسٍ وَمَا سَو َّاهَا۞فَأَلهَْمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا﴾
WaNafsin wama sawwaha, Faalhamaha fujooraha wataqwaha (Surat Ash Shams
91:7-8)
Tafsir: Naapa kwa Nafsi, Na kwa yule alieweka sawa kikamilifu. Kisha akaionesha ni
kipi kilicho kiovu juu yake na ni kipi kilicho sahih juu yake.
Nafs Al Mulhima hua ni Nafsi ambayo imekamilika kwa kua na Nuru ya Iman ya Dini ya
Allah Subhanah wa Ta’ala katika kumpwekesha kwake na hua ni yenye Maumbile ya
kutafakkar na kujua kua jambo fulani ni ovu na jambo fulani ni sahih, na hivyo hua ni
wenye kudumu katika kumtii Mola wake, na kuonesha shukran, ukarimu, upole, huruma,
unyenyekevu n.k na hii ni kutokana na Nafsi hio kua ni yenye kua na hisia za ndani kwa
ndani zenye ujumbe wa kuitia ari Nafsi hio kufanya Mema na kuiongoza katika njia iliyo
sahih, aina hii ya Nafsi hua ni tofauti na Nafs Al Lawwamah.
NAFS AL LAWWAMAH.
Nafs Al Lawwamah hali ya Nafsi ambayo inanasibishwa na hali ya sehemu ya Moyo
inayokaa Nuru ya Maarifah yaani Al Fuad. Hali ya Nafsi ambayo ni yenye kujua kasoro
zake za kimaumbile hivyo hua ni yenye kujilaumu laumu, na imetajwa katika ile aya
isemayo:
﴿وَلاَ أُقْسِ مُ بِٱلن َّفْسِ ٱلل َّو َّامَةِ ﴾
Wala oqsimu bialnNafsi allawwamati (Surat Al Qiyama 75:2)
107
Tafsir: Na nnaapa kwa Nafsi yenye Lawama.
Nafs Al Lawwamah hua ni Nafsi ambayo ina maarifa na hivyo inafanya mambo kwa
kujua na kisha inajiangalia na kujilaumu, na hivyo kuipelekea mtu husika kujihisi ana
makosa, hujuta, hujisikia aibu na kuhisi bora hata asingefanya hayo aliyoyafanya na
hivyo kuamua kutorudia tena makosa husika, Mtu husika hua yuko katika Mapigano na
Nafsi yake kiasi ya kua baadhi ya wakati Nafsi inamshinda na kufanya Madhambi na
baadhi ya wakati hua anafanikiwa kuidhibiti Nafsi yake na kujizuia na kufanya
Madhambi.
Nafsi al Lawwamah hua ni Nafsi yenye Sifa za mtu Kujijua, Kua na khofu na Kutamani
kufanya mema, kuzisaidia Nafsi Nyengine, na hivyo kila hatua anayopiga mtu katika
kufanya mema huonekana ni hatua kubwa zaidi kuliko ile hatua aliyokua nayo mtu hapo
kabla na hivyo hua katika hali ya hatari ya kuingia kwenye Unafiq, kwani hali ya Nafsi
hii humfanya mtu ajione kua anajua, ameshafanya mema mengi sana na hivyo anastahiki
heshima kutoka kwa watu wengine wasiojua. Na hivyo hua na hali ambayo haiko salama
dhidi ya vishawishi vya Iblis, tofauti na Nafs al Mutma’inah.
NAFS AL MUTMA’INAH
Nafs Al Mutma’inah hali ya Nafsi ambayo inanasibishwa na hali ya sehemu ya Moyo
inayokaa Nuru ya Tawhid yaani Al Lubb. Neno Mutma’ina linatokana na neno
Tamana ambalo kwa kiarabu hua ni lenye kumaanisha Kupumzika, Kutulia, Tegemea,
Kuweka kitu kwa Utulivu au kwa Ukimya, Kutuliza kwa Kiakili, KiNafsi na Kiroho.
Hali ya Nafsi hii hua imeegemea na kuelekea kwenye mambo ya Kiroho na uhalisia wake
wa Kimaumbile na hivyo hua na utulivu wa hali ya juu kabisa, Nafsi inapofikia katika
hali hii basi hua na sifa ya kutofanya makosa, kutokua na upotovu na hua ni yenye
kufanikiwa Duniani na Akhera hivyo hua ni yenye kupata utulivu, raha na furaha
kutokana na kumjua na kua na ukaribu na Mola wake. Allah Subhanah wa Ta’ala
anazitaja sifa za Nafsi za aina hii ya Nafsi kwa kusema kua:
﴿َٰي َّتُهَا ٱلن َّفْسُ ٱلْمُطْمَئِن َّةُ ﴾
Ya ayyatuha alnnafsu almutma-innatu (Surat Al Fajr 89:27)
Tafsir: Wataambiwa: Enyi nyinyi wenye Nafsi zenye utulivu.
108
Anasema Sultan al Mutakallimin Mujaddid ud Din Imam Al Ghazali Al Thani Imam
Fakhr ad Din Al Razi kuhusiana na Nafs Al Mutma’inah kua: ‘Ni Nafsi za watu wenye
I’lm ya Kumjua Mola wao na hua na Utiifu kwa Mola wao na hivyo kua na utulivu
na kuridhika. Na Jee ni kwa namna gani Nafsi hua ni yenye kupata Utulivu?
Nafsi hupata utulivu kutokana na njia mbili zifuatazo, ambapo njia ya kwanza ni
kupitia katika Moyo Kumkumbuka Alieuumba kama inavyoelezewa katika ile aya
isemayo:
﴿ٱل َّذِينَ آمَنُواْ وَتَطْمَئِن ُّ قُلُوبُهُمْ بِذِكْرِ ٱهلل َِّ أَلاَ بِذِكْرِ ٱهلل َِّ تَطْمَئِن ُّ ٱلْقُلُوبُ ﴾
Alladheena amanoo watatma-innu quloobuhum bidhikri Allahi ala bidhikri Allahi
tatma-innu alquloobu (Surat Ar Rad 13:28)
Tafsir: Wale wenye kuamini, na ambao nyoyo zao zinapata utulivu kutokana na
kumkumbuka Allah. Kwani ni katika kumkumbuka Allah ndio Nyoyo hupata utulivu.
Njia ya pili ni kupitia katika kutafakkar ipasavyo, yaani wakati Ibn Adam mwenye
ufahamu anapo uangalia ulimwengu basi hua ni mwenye kuona kua mahitaji yake
yamefungamana na njia fulani ya uhakika ambayo kwa kutumia njia hizo basi hua
ni mwenye kupata mahitaji yake. Lakini hata hivyo kila anapoangalia asili ya
mshikamano wa njia hizo basi hua pia ni mwenye kuona kua njia hizo zenyewe, pia
hua ni zenye kutegemea njia nyengine au sababu nyengine.
Na kila anapoendelea kufuatilia zaidi basi ndivyo anavyozidi kuona kua njia hizo
zimeshikamana na njia nyengine, hivyo hivyo hadi kufikia mwisho wake hua ni
mwenye kulifikia sababisho la kila kitu kilichopo au Wajib al Wujud (Wajibu wa
Kuwepo) yaani Allah Subhanah wa Ta’ala. Na hivyo husimamia hapo kwa sababu
ya kua mfuatiliaji hua ni mtu mwenye Yaqini basi hua hakuna haja kwake
kufuatilia zaidi baada ya kumfikia yule ambae hakuna kitu chochote
kisichowezekana kwake, hali hii huleta utulivu ndani ya Nafsi ya mhusika.
Hali hii inatuwekea wazi kua mtu yeyote yule ambae atapendelea kua na I’lm juu
ya Kidunia kuliko I’lm ya Kiakhera basi mtu huyu hua ni mtu asiekua na utulivu,
hali ambayo hua ni tofauti na ya yule ataependelea kua na I’lm ya Kiakhera zaidi
kuliko I’lm ya Kidunia ambae yeye hua na Nafsi yenye utulivu.
Katika kuielezea Nafs al Mutma’inah basi tumegusia Wajib Al Wujud hivyo kabla ya
kuendelea zaid basi kidogo tufafanue nini maana ya Wajib al Wujud, ambapo ukweli ni
kua ni vigumu kuelezea maana ya Wujud kwa kimaana kama inavyomaanishwa na Lugha
ya Kiarabu lakini tutajaribu kufafanua ili tufahamu japo kwa juu kuhusiana na Wujud
109
kama inavyotokana na neno Mawjud kwani kulingana na mtizamo wa Aqidat al Wujud
yaani Imani ya Sifa ya Kuwepo imegawika katika sehemu tatu:-
WAJIB AL WUJUD yaani hali ya Wajibu wa Kuwepo, hali ambayo hua inaelezea na
kuthibitisha Wajibu wa Kuwepo kwake Allah Subhanah wa Taála ambae ndie Muumba
wa kila kitu. Ambapo kuwepo kwake hua kupo bila kutegemea kitu chengine chochote,
na kuwepo kwake hua ni Wajibu kwa ajili ya vitu vyengine vyote vilivyokuwepo ili
viwepo. Hali hii pia hujulikana kama Wahdat al Wujud au Upekee wa kuwepo kwake
bila ya kua na Mshirika.
Na tunapozungumzia sifa hii ya upekee ya Wajib Al Wujub ya Wajibu wa Kuwepo kwake
Allah Subhanah wa Ta’ala basi hua pia tunazungumzia Kutaka kwake, kwani kutokana
na hali ya viumbe wake kua ni wenye hali na mambo maalum, yaani mazingira yao,
maumbile yao, ukubwa wao, wakati wao, n.k basi hali hio ya kutaka kwake inatuonesha
kua ni mwenye Kua na Maamuzi na kufanya maamuzi hua kunaendana na Matakwa. Vile
vile hua pia tunazungumzia I’lm yake, kwani maamuzi hayo hua hayatokani na kutojua
bali hua yanatokana na kujua, na pia tunazugumzia Uwezo wake, kwani asiekua na
uwezo basi kamwe hua hawezi kufanya kitu chochote hususan tunapozungumzia kufanya
kitu bila kutegemea kitu chengine chochote.
Na bila ya shaka sifa zote hizi tatu yaani Kutaka Kwake, Ilm yake na Uwezo wake
haziwezi kuwepo bila ya kuwepo kwa Sifa ya Kua Hai kwake, ambako nako kunaenda
sambamba na Kua na Upekee na Kutokua na Mshirika, kwani kutokua na upekee kwake
na kua na Mshirika basi hua ni kwenye kupelekea kuwepo kwa mapingano na mvutano
katika mpangilio wa Viumbe vyake kwani kuwepo Maumbaji zaidi ya Mmoja basi
hupelekea upinzani baina ya Waumbaji na matokeo yake hakutokua na Kiumbe chochote
kama anavyosema mwenye Allah Subhanah wa Ta’ala katika Qurán:
﴿لَوْ كَانَ فِيهِمَآ آلهَِةٌ إِلا َّ ٱهلل َُّ لَفَسَدَاتَ فَسُبْحَانَ ٱهلل َِّ رَبِّ ٱلْعَرْشِ عَم َّا يَصِفُو نَ ﴾
Law kana feehima alihatun illa Allahu lafasadata fasubhana Allahi rabbi alAAarshi
AAamma yasifoona (Surat Al Anbiyah 21:22)
Tafsir: Lau Kama ndani yake (Mbinguni na Ardhini) ingekua kuna na Miungu zaidi
ya Allah, basi vyote (Mbingu na Ardhi) vingekua vishafisidika (vishaangamia),
Utukufu ni wake Allah pekee, Mola wa Arshi, yuko mbali na wanavyomsifia.
Yaani kama ingekua kuna mshirika wake Allah Subhanah wa Taála basi bila ya shaka
ingekua kuna mvutano baina yao, kwani aidha wangekua wana nguvu moja au wana
nguvu tofauti kwani kama mmoja angakua dhaifu basi ingebidi kwa kuadiwa ni mwenye
110
nguvu, na kama wote wangekua na nguvu sawia basi mmoja angataka inyeshe mvua
mwengine angekataa, mwengine angeamua Duniani uingie usiku na mwengine angetaka
uchelewe kuingia, kwani fahali wawili hawakai zizi moja.
Na akathibitisha Allah Subhanah wa Taála jua ya Wahdat ul Wujud kwa hoja kusema
kua,
﴿مَا ٱتخ ََّذَ ٱهلل َُّ مِن وَلَدٍ وَمَا كَانَ مَعَهُ مِنْ إِلَهٍ إِذاً ل َّذَهَبَ كُل ُّ إِلَٰهٍ بمَِا خَلَقَ وَلَعَلاَ
بَعْضُهُمْ عَلَى ٰ بَعْضٍ سُبْحَانَ ٱهلل َِّ عَم َّا يَصِفُونَ ﴾
Ma ittakhadha Allahu min waladin wama kana maAAahu min ilahin idhan
ladhahaba kullu ilahin bima khalaqa walaAAala baAAdhuhum AAala baAAdhin
subhana Allahi AAamma yasifoona (Surat Al Muuminun 23:91)
Tafsir: Kamwe hakua Allah ni mwenye mtoto na kamwe hakukua na Mungu
mwengine zaidi yake, (Kama angekua na Washirika) basi kila Mungu angechukua
alichokiumba, na baadhi yao wangejaribu kuwazidi nguvu wengine. Utukufu ni wake
Allah pekee, alie mbali na wanavyomsifia.
Na pia akatoa hoja nyengine tena Allah Subhanah wa Taála juu ya Wahdat ul Wujud kwa
kusema:
﴿قُلْ ل َّوْ كَ انَ مَعَهُ آلهَِةٌ كَمَا يَقُولُونَ إِذاً لا َّبْتَغَوْاْ إِلىَٰ ذِى ٱلْعَرْشِ سَبِيلاً ﴾
Qul law kana maAAahu alihatun kama yaqooloona idhan laibtaghaw ila dhee
alAAarshi sabeelan (Surat Al Isra 17:42)
Tafsir: Waambie (Hao Makafikri): ‘Kama kungekua kuna Miungu wengine pamoja
nae kama wanavyosema wao, basi bila ya shaka (Miungu hao) wangetafuta njia ya
kua karibu na Mola wa Arshi Tukufu’
Ama kwa upande mwengine basi tunaona kua Umoja wa kuwepo kwa Muumba mmoja
unaonekana wazi pale tunapoona kua Maumbile ya Ulimwengu yalivyo, ambapo tunaona
kua kanuni za kisayansi zinaonesha kua Duniani kuna nguvu za kimaumbile za kifizkia
ambazo zinaenda sambamba bila kuzidiana ambazo ni nguvu za kifizikia zilizo dhaifu,
nguvu za kifizikia zilizo imara, nguvu za umeme za sumaku (Electromagnetic Forces)
na nguvu za kuvuta chini ardhini (Gravitational Forces). Bila ya kuwepo kwa nguvu hizi
111
sambamba basi ingakua vigumu kuata mawasiliano ya anga za nje. Hivyo kuwepo kwa
umoja huu wa nguvu za kimaumbile unathibitisha Wahdat ul Wujud.
MUMKIN AL WUJUD yaani hali ya Uwezekano wa Kuwepo, hali ambayo hua
inaelezea na kuthibitisha Uwezekano wa Kuwepo kwa Viumbe walioumbwa ambao
wanaweza wakawa wapo na pia wanaweza wakawa hawapo. Viumbe hawa Walioumbwa
hua hawana uhuru wa kuwepo na hivyo basi kuwepo kwao hua hakuna ulazima. Allah
Subhanah wa Taála amewajaalia kua wapo kutokana na Kutaka kwake, Uwezo wake,
Nguvu zake, I’lm yake na kama angetaka basi bila ya shaka viumbe hivyo
visingekuwepo. Kwani Viumbe hua vipo kutokana na Allah Subhanah wa Taála kutaka
kua viwepo yaani viumbe kuwepo kwa viumbe hivyo kunategemea kuwepo kwake yeye
ambae kuwepo kwake yeye hakutegemei kuwepo kwa kitu chengine.
MUSTAHIL AL WUJUD yaani hali ya Kutowezekana Kuwepo, ambako kunajumisha
kuwepo kwa ushiriki wa Majina, Sifa na Vitendo vya Allah Subhanah wa Ta’ala jambo
ambalo haliwezekani si kulingana na mtizamo wa Maandiko tu bali pia kulingana na
Ufahamu na Mantiq.
Sultan al Mutakallimin Mujaddid ud Din Imam Fakhr ad Din Al Razi anaendelea
kutuelezea kuhusiana na Nafs Al Mutma’inah kua Hivyo watu wenye hali ya Nafsi ya
Al Mutma’inah (Yaani Nafsi iliyotulia baada ya kutafakkar na kufuatilia hadi
wakalifikia sababisho la kitu yaani Wajib Al Wujub na hivyo kua na ukaribu na Mola
wao) basi wao ndio ambao watakaoambiwa katika wakati watakapo ondoka hapa
Duniani kua:
﴾
﴿َٰي َّتُهَا ٱلن َّفْسُ ٱلْمُطْمَئِن َّةُ ۞ ٱرْجِ عِى إِلىَٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً م َّرْضِي َّةً
Ya ayyatuha alnnafsu almutma-innatu IrjiAAee ila rabbiki radhiyatan
mardhiyyatan (Surat Al Fajr 89:27-28)
Tafsir: Enyi wenye Nyoyo zenye utulivu! Rejeeni kwa Mola wenu huku mkiwa
Mmeridhika na Mola wenu na huku mkiwa ni Mmeridhiwa na Mola wenu.
Hivyo Allah Subhanah wa Taála anazitaja Nasf al Mutma’inah katika Surat Al Fajr
89:27-28 huku akiziainisha kua ni zenye sifa mbili kuu ambazo ni Radhiyatan na
Mardhiyah ambapo ndani yake ndio tunapata Nafs Radhiyatan na Nafs Mardhiyatan:
NAFS RADHIYATAN
112
Hii ni hali ya Nafsi ambayo ipo katika Mutma’ínah yaani katika hali ya utulivu na
kuridhia hukmu za Allah Subhanah wa Taála juu yake kiasi ya kua hakuna kitu ambacho
kinazifurahisha Nafsi hizi isipokua kua na Maridhia na majaaliwa ya Mola wake, hivyo
mtu mwenye Nafsi ya aina hii hua anajua kua majaliwa ya Mola wake juu yake
yanatokana na kile kilichoridhiwa na kufurahiwa na Mola wake.
NAFS MARDHIYAH.
Hali hii ya Nafsi ambayo ipo pia katika hali ya Mutma’inah hua ni hali ambayo ina Amani
kutokana na kutofanya dhambi, hii hua ni Nafsi ambayo haina matamanio ya Dhambi,
kwani Matamanio yake ni ya halali tu, hivyo Nafsi za watu hawa hua hazina sifa ya
kutofanya dhambi tu lakini pia hazitamani kufanya mambo maovu, kwani wao hutamani
yale tu ambayo Allah Subhanah wa Taála ameyaridhia na hivyo kua ni wenye kuachana
na yale ambayo Allah Subhanah wa Ta’ala hakuyaridhia.
NAFS AL KAMILAH
Hii hua ni hali ya Nafsi ambayo pia hua inajulikana kama Nafs Al Nuraniyyah yaani Nafsi
yenye Nuru au Nafsi Al Muhhibah yaani Nafsi ya mwenye Kupenda au ya Urafiki wa
Karibu sana ambayo hua haipo katika hali ya Mutma’ainah tu bali pia hua ipo katika
Darja ya Ubora yaani Maqam al Ihsan na hii hua ni darja ambayo iko juu kabisa ya darja
zote, kwani mwenye Nafsi hii hua ni mwenye kufikia katika Darja ya ukaribu wa ambao
unajulikana kama qaba qawsayni aw adna yaani baina ya mipinde miwili au karibu zaid,
nyuma ya Nyayo za Rasul Allah Sallalahu Alayhi wa Salam. Hizi ni Nafsi za watu ambao
wameelezewa katika aya ifuatayo:
﴿أَي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ مَن يَرْتَد َّ مِنكُمْ عَن دِينِهِ فَسَوْفَ َْتِى ٱهلل َُّ بِقَوْمٍ يحُِب ُّهُمْ
وَيحُِب ُّونَهُ أَذِل َّةٍ عَلَى ٱلْمُؤْمِنِينَ أَعِز َّةٍ عَلَى ٱلْكَافِرِينَ يجَُاهِدُونَ فىِ سَبِيلِ ٱهلل َِّ وَلاَ
يخََافُونَ لَوْمَةَ لا ۤ ئِمٍ ذٰلِكَ فَضْلُ ٱهلل َِّ يُؤْتِيهِ مَن يَشَآءُ وَٱهلل َُّ وَاسِ عٌ عَلِيمٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo man yartadhdha minkum AAan deenihi fasawfa
ya/tee Allahu biqawmin yuhibbuhum wayuhibboonahu adhillatin AAala
113
almu/mineena aAAizzatin AAala alkafireena yujahidoona fee sabeeli Allahi wala
yakhafoona lawmata la-imin dhalika fadhlu Allahi yu/teehi man yashao waAllahu
wasiAAun AAaleemun(Surat Al Maidah 5:54)
Tafsir: Enye Mlioamini! Yeyote yule atakaerudi nyuma miongoni mwenu kutoka
katika Dini hii, basi Allah atawaleta watu ambao atawapenda nao watawapenda, Nao
watakua wanyenyekevu kwa wale walioamini,na wakali kwa waliokufuru, watapigana
kwa ajili ya Allah na kamwe hawatoogopa lawama kutoka kwa wanaolaumu. Hii nio
fadhila ya Allah nae humpa amtakae miongoni mwa waja zake. Hakika Allah ni
mwenye kuwatosheleza Waja wake na ni mwenye kujua kila kitu.
Na pia pale alipoelezea tena Allah Subhanah wa Taála kwa kumwambia Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam awaambie waja wake kua:
﴿قُلْ إِن كُنتُمْ تحُِب ُّونَ ٱهلل ََّ فَٱت َّبِعُونىِ يحُْبِبْكُمُ ٱهلل َُّ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَٱهلل َُّ غَفُورٌ
ر َّحِ يمٌ ﴾
Qul in kuntum tuhibboona Allaha faittabiAAoonee yuhbibkumu Allahu wayaghfir
lakum Dhunoobakum waAllahu ghafoorun raheemun (Surat Al Imran 3:31)
Tafsir: Sema kama kweli mnampenda Allah basi nifuateni mimi na Allah
atakupendeni na atakusameheni dhambi zenu. Hakika Allah ni mwingi wa usamehevu
na ni mwingi wa Rehma.
Hivyo hii ni hali ya darja ya kua na ukamilifu wa kua ni Mtumwa wa Allah Subhanah wa
Ta’ala kwa kupitia katika ukamilifu wa kufuata mafunzo ya Rasul Allah Salalahu Alayhi
wa Salam, hivyo yule ambae amejaaliwa kuifikia darja hii hua ni mwenye kujaaliwa
kujua mapenzi kamilifu juu ya Allah Subhanah wa Ta’ala na Rasul Allah Salallahu
A’lahi wa Salam kwani hua wenye kujua kwa yakini kusudio la kuumbwa kwao.
Hivyo kutokana na kuwepo kwa utofauti wa Kimaumbile wa Nafsi za Ibn Adam basi
ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala ambae ndie Muumba akaamua kutuma Mitume
na Manabii kwa waja wake wenye kusudio maalum.
114
KUSUDIO LA ALLAH SUBHANAH WA TA’ALA KUTUMA MITUME
KWA WAJA WAKE.
Ili kujua nia na kusudio la Allah Subhanah wa Ta’ala kutuma Mitume kwa waja wake
kila baada ya muda fulani ulimwenguni basi kwanza inabidi tukumbuke kua Allah
Subhanah wa Taála amewaumba Ibn Adam kua ndio watawala wa Ulimwenguni na
alipotuumba alituumba katika umbo lililo bora kabisa kuliko viumbe wote kama
anavyosema katika aya ifuatayo:
﴿لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلإِنسَانَ فيِ ۤ أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ ﴾
Laqad khalaqna al-insana fee ahsani taqweemin (Surat At Tin 95:5)
Tafsir: Kwa hakika tumemuumba mtu katika Taqwiim bora kabisa.
Naam aya hii ya Surat At Tin 95:5 ni miongoni mwa aya ambazo zinanukuliwa sana na
Waislam ulimwenguni lakini ni wachache wenye kuijua maana halisi ya ayah hii, kwa
sababu wengi sana hua wanazungumzia ubora wa muonekano wa nje wa mwili wa Ibn
Adam, lakini ukweli ni kua aya inaweka wazi ubora uliokamilia usiokua na kasoro wa
mwili wa Ibn Adam, ubora ambao unajumuisha mfumo mzima wa ufanyaji kazi
kikamilifu wa umbo la nje la mwili wa Ibn Adam ukishirikiana na ufanyaji kazi wa
mifumo yote kamilifu ya ndani ya mwili wa Ibn Adam ambayo inajumuisha Mfumo wa
Ubongo na Ufahamu wake, Mfumo wa hisia wa Uti wa mgongo na hisia zake tofauti
ikiwemo hisia za njaa, joto, baridi, matamanio, mapenzi, furaha, huzuni, maumivu n.k
Ubora huo unajumuisha pia mfumo kamilifu wa mzunguko wa Damu ndani ya Moyo na
ufahamu wake. Tunapozungumzia Moyo basi hua tunazungumzia kiungo ambacho ni
chenye ufahamu mkubwa na wa kina unaojitegemea kinguvu na kiuwezo kama
tulivyoona hapo kabla ambavyo vyote hivyo ni tofauti na uwezo wa ufahamu wa akili na
ufaham wa viumbe wengine kama Malaika na Majini.
Hivyo kamwe hatukukamilishwa kwa kujaaliwa kua na maumbile bora labda kwa ajili
ya kumhudumikia kwa kumtafutia riski au kumfanyia jambo lolote lile Muumba wetu
ambae ni Allah Subhanah wa Taála kwani yeye ni Muumba hivyo ni mwenye
kujitosheleza juu ya kila kitu na ni mwenye kua na uwezo wa kuwatosheleza viumbe
wake wote aliowaumba, hivyo Ibn Adam tumeumbwa kwa maumbile bora ili tupate
kutafakkar na kumjua, kumuabudu, kumshukuru na kumnyenyekea Allah Subhanah wa
Taála kama alivyotuwekea wazi kwenye Qurán kwa kusema:
115
﴿وَمَا خَلَقْتُ ٱلجِْن َّ وَٱلإِنسَ إِلا َّ لِيَعْبُدُونِ۞ مَآ أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَآ أُرِيدُ أَن
يُطْعِمُونِ ﴾
Wama khalaqtu aljinna waal-insa illa liyaAAbudooni, Ma oreedu minhum min
rizqin wama oreedu an yutAAimooni (Surat Adh Dhariyyat 51:56-57)
Tafsir: Sikuwaumba Majini na Ibn Adam isipokua kwa ajili ya kuniabudu mimi tu.!
Sitaki kutoka kwao Riziki wala sitaki wanipe chakula.
Anasema Allamah Abu Qasim Ibn Husein Ibn Mufadhal Ibn Muhammad Raghib Al
Isfahani kuhusiana na neno LiyaA’Abuduuni lililotumika katika aya hii kua: ‘Ubudiyya –
Utumwa hua ni kuuonesha unyenyekevu. Na Ibada hua ni kutilia mkazo, kwani
Ibada ndio mpaka wa unyenyekevu, na hakuna anaestahiki unyenyekevu au
kuabudiwa isipokua yule ambae ni mwenye uwezo wa kujaalia kila kitu ambae ndie
anaestahiki kuabudiwa ambae ni Allah Subhnahah wa Ta’ala na ndio maana
akasema:
﴿وَقَضَى ٰ رَب ُّكَ أَلا َّ
ۤ تَعْبُدُواْ إِلا َّ إِ َّهُ ﴾
Waqadha rabbuka alla taAAbudoo illa iyyahu (Surat Al Isra 17:23)
Tafsir: Na Mola wako amejaalia kua usimuabudu yeyote isipokua yeye’
Ama tunapozungumzia kuhusiana na LiyaA’Abuduuni basi hua kuna Ibada za aina mbili:
1. Unyenyekevu wa Ulazima – Ambao hua ni hali inayojumuisha kila kitu cha Mja
kinachohusiana na Muumbaji kutokana na kutokua na kitu na hivyo kua na uhitaji wa
Mja kwa Muumba ambae ni Allah Subhanah wa Taála.
2. Unyenyekevu wa Khiari – Ambao hua ni hali inayojumuisha hali moja kati ya mambo
ya matatu yafuatayo:
116
a) Unyenyekevu wa yule mtu ambae hayuko huru (yaani ni mtumwa alie chini ya
mtu mwengine, iwe kiutumwa, kiutumwa wa kileo ambao hua ni wa kikazi au
kifungo)
b) Unyenyekevu wa yule mtu ambae yuko huru lakini hua ni anaemtumikia Allah
Subhanah wa Taála (Ambalo ndio kusudio la uhalisia wa kila Kiumbe)
c) Unyenyekevu wa yule mtu ambae yuko huru lakini hua ni mwenye kumtumikia
Allah Subhanah wa Taála katika kuabudu na kihuduma, yaani anaemtumikia Allah
Subhanah wa Ta’ala kwa Ikhlasi na hivyo utumwa wake ni katika uhai wa Maisha
haya na kila kinachohusiana nayo. [Imam Raghib Al Isfahani, Mufradat Alfadh Al
Qurán, 542]
Hivyo Allah Subhanah wa Taála anatuwekea wazi kua hakutuumba sisi Ibn Adam na
Majini isipokua kwa ajili ya Kumuabudu na kumnyenyekea yeye peke yake, kwa sababu
yeye ndie Mola wetu alietuumba na kuendelea kutulea tangu tulikotoka, hapa tulipofikia
na hadi tutakapoelekea katika mwisho wetu kwa kutujaalia afya, nguvu, uwezo, rizki,
familia na kadhalika kwa kila mmoja miongoni mwetu kabla ya kuufikia mwisho wetu
ambao hakuna anaeujua miongoni mwetu isipokua yeye Mola wetu kama alivyosema
katika aya ifuatayo:
﴿وَهللِ َِّ غَيْبُ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَمَآ أَمْرُ ٱلس َّاعَةِ إِلا َّ كَلَمْحِ ٱلْبَصَرِ أَوْ هُوَ
أَقْرَبُ إِن َّ ٱهلل ََّ ٰ عَلَى ِ كُل شَيْءٍ قَدِيرٌ۞ وَٱهلل َُّ أَخْرَجَكُم مِّن بُطُونِ أُم َّهَاتِكُمْ لاَ
تَعْلَمُونَ شَيْئاً وَجَعَلَ لَكُمُ ٱلْس َّمْعَ وَٱلأَبْصَارَ وَٱلأَفْئِدَةَ لَ عَل َّكُ مْ تَشْكُرُونَ ﴾
ّ
Walillahi ghaybu alssamawati waal-Ardhi wama amru alssaAAati illa kalamhi
albasari aw huwa aqrabu inna Allaha AAala kulli shay-in qadeerun; WaAllahu
akhrajakum min butooni ommahatikum la taAAlamoona shay-an wajaAAala
lakumu alssamAAa waal-absara waal-af-idata laAAallakum tashkuroona (Surat An
Nahl 16:77-78)
Tafsir: Na kwa Allah ndiko kwenye umiliki wa Ulimwengu usioonekana wa Mbiguni
na ardhini, na amri juu ya wakati si chochote bali ni kama kupepesa kwa jicho au
karibu zaidi. Kwa hakika Allah ni mwenye uwezo juu ya kila kitu. Na Allah ndie
117
aliekutoeni katika matumbo ya uzazi wa mama zenu wakati nyinyi mkiwa hamjui kitu,
na akakupeni Masikio, Macho na Moyo ili mpate kua ni wenye kushukuru.
Tunapozungumzia juu ya Ibada ya kumuabudu Allah Subhanah wa Taála katika Dini ya
Uislam basi hua hatuzungumzii tu Kusali, Kufunga kutoa Zakkah na Sadaka bali hua
tunazungumzia utekelezaji wa Majukumu yote tuliyoamrishwa na Allah Subhanah wa
Taála katika wakati wa uhai wetu wote tunapokua hapa Ulimwenguni, tangu kuingia
kwetu hadi kutoka kwetu, kwani sisi tumekuja hapa Duniani kwa ajili ya Mola wetu na
hivyo kua katika hali ya mapigano ya kutafuta mafanikio yetu ya baadae dhidi ya
vichochezi vya Iblis na Nafsi zetu zitakazopelekea kuachana na lengo la kuumbwa kwetu,
hivyo hatukuja Duniani kwa ajili ya mchezo jambo ambalo linawekwa wazi na aya
zifuatazo:
﴿لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلإِنسَانَ فىِ كَبَدٍ ۞ أَيحَْسَبُ أَن ل َّن يَقْ دِرَ عَلَيْهِ أَحَ دٌ ﴾
Laqad khalaqna al-insana fee kabadin, Ayahsabu an lan yaqdira AAalayhi ahadun
(Surat Al Balad 90:5-6)
Tafsir: Kwa hakika tumemuumba Ibn Adam katika hali ya Harakati na Mapigano, Jee
anajihesabu kua hakuna mwenye kuweza kumdhibiti juu yake?
Aya zinatuwekea wazi kua Ibn Adam ameumbwa kwa ajili ya kua katika hali ya
mapigano yenye kudumu na kuendelea katika kipindi cha uhai wake wote, harakati na
mapigano ambayo yanaanzia tangu kutafutwa kwake na Wazee wake, hadi kupatikana
kwake anapozaliwa, anapokua kwake, anapoidhibiti Nafsi yake na hadi katika wakati wa
kutolewa Roho yake, yeye yupo katika hali ya harakati na mapigano ambayo yanatakiwa
yampelekee kua na unyenyekevu juu ya Mola wake ambae ni Allah Subhanah wa Ta’ala,
Lakini wapi kila anavyokua na kupata afya, uwezo, mali na kadhalika basi ndio kwanza
anapozidi kujiona kua hakuna kama yeye. Hivyo jee kweli anafikiria kua hakuna
atakaemdhibiti? Suali hili linatiliwa mkazo kwa kuulizwa tena katika aya ifuatayo pale
Qurán iliposema:
﴿أَيحَْسَ بُ ٱلإِ نسَانُ أَن يُتْ رَكَ سُدً ى﴾
Ayahsabu al-insanu an yutraka sudan (Surat Al Qiyama 75:36)
Tafsir: Hivi anajihesabu mtu kua ataachwa bila kuhukumiwa?
118
Hivi jee kweli inawezekana kiumbe Ibn Adam kiachiwe tu bila ya kudhibitiwa na
Muumba wake juu ya majukumu yake kwa Mola wake na kwa viumbe wenzake? Bila ya
kuamrishwa kua lipi alifanye na kukatazwa lipi asilifanye na jee anafikiria kua
hatohesabiwa na kuhukumiwa kwa kila analolifanya hapa Ulimwenguni? Na kama
anafikiria hivyo basi huyu ni kiumbe ambae hakumuamini Mola wake kwani anaamini
kua Allah Subhanah wa Ta’ala alieumba kila kitu hana habari na kila kiumbe chake na
wala hajui kitu chochote juu yake, jambo ambalo haliingii akilini.
Kwani Allah Subhnah wa Ta’ala ambae ndie alieiumba Dunia na kuipamba kwa ajili ya
Waja wake ili wasipate shida katika mazingira yao na hapo hapo wasighafilike juu yake
basi anasema katika Qur’an kua:
﴿زُيِّنَ لِل َّذِينَ كَ فَ رُواْ ٱلحَْيَاةُ ٱلد ُّنْيَا وَيَسْخَرُونَ مِنَ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ وَٱل َّذِينَ ٱت َّ قَواْ فَوْقَهُمْ
يَوْمَ ٱلْقِيَامَةِ وَٱهلل َُّ يَرْزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيرِْ حِ سَابٍ ۞كَانَ ٱلن َّاسُ أُم َّةً وَاحِ دَةً فَبَعَ َث
ٱهلل َُّ ٱلن َّبِيِّينَ مُبَشِّ رِينَ وَمُنذِرِينَ وَأَنزَلَ مَعَهُمُ ٱلْكِتَابَ بِٱلحَْقِّ لِيَحْكُمَ بَينَْ ٱلن َّاسِ فِيمَا
ٱخْتَلَفُواْ فِيهِ وَمَا ٱخْتَلَفَ فِيهِ إِلا َّ ٱل َّذِينَ أُوتُوهُ مِن بَعْدِ مَا جَآءَتْهُمُ ٱلْبَيِّنَاتُ بَغْياً
بَيْنَهُمْ فَهَدَى ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ لِمَا ٱخْتَلَفُواْفِي هِمِ نَٱ لحَْقِّ ِإبذْنِهِ وَٱهلل َُّ يَهْدِى مَن
يَشَآءُ إِلىَٰ صِرَاطٍ م ُّسْتَقِيمٍ ﴾
Zuyyina lilladheena kafaroo alhayatu alddunya wayaskharoona mina alladheena
amanoo waalladheena ittaqaw fawqahum yawma alqiyamati waAllahu yarzuqu
man yashao bighayri hisabin; Kana alnnasu ommatan wahidatan fabaAAatha
Allahu alnnabiyyeena mubashshireena wamundhireena waanzala maAAahumu
alkitaba bialhaqqi liyahkuma bayna alnnasi feema ikhtalafoo feehi wama ikhtalafa
feehi illa alladheena ootoohu min baAAdi ma jaat-humu albayyinatu baghyan
baynahum fahada Allahu alladheena amanoo lima ikhtalafoo feehi mina alhaqqi biidhnihi
waAllahu yahdee man yashao ila siratin mustaqeemin(Surat Al Baqara
2:212-213)
Tafsir: Yamependezeshewa kwa waliokufuru Maisha ya Duniani na hivyo huwafanyia
maskhara walioamini, na wale wanaomcha (wanaotii maamrisho ya Allah Subhnaha
wa Ta’ala na kukaa mbali na makatazo yake), watakua juu yao katika siku ya Kiama,
Na Allah humruzuku amtakae bila ya kiasi. Walikua watu ni umma mmoja kisha Allah
119
akawatumia Manabii wenye Kubainisha na Kuusia, na pamoja nao akawatumia
Maandiko kwa haki ili watoe hukumu baina ya Watu katika mambo waliyotofautiana,
na hawakuhitilafiana navyo (Vitabu hivyo) isipokua wale waliokwishapewa baada ya
kubainishiwa kutokana na chuki baina yao, kisha akawaongoza Allah wale
walioamini kutokana na kile walichohitilafiana kuwaelekeza katika haki kutokana na
Idhini yake. Na kwa hakika Allah humuongoza amtakae katika njia iliyonyooka.
Kutokana na maneno ya aya hio basi ndio maana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akawa ni mwenye kupenda kuisoma dua ifuatayo katika wakati wa usiku anaposali Salat
Dhuha.
(الل َّهُم َّ رَب َّ جِ بْرَائِيلَ وَمِيكَائِيلَ وَإِسْرَافِيلَ، فَاطِرَ ال َّسمَوَاتِ وَالأَرْضِ ، عَالمَِ الْغَيْ ِب
وَالش َّهَادَةِ، أَنْتَ تحَْكُمُ بَينَْ عِبَادِكَ فِيمَا كَانُوا فِيهِ يخَْتَلِفُونَ، اهْدِنيِ لِمَا اخْتُلِ َف
فِيهِ مِنَ الحَْقِّ إبِ ذْنِكَ ، إِن َّكَ تَهْدِي مَنْ تَشَاءُ إِلىَ صِرَاطٍ مُسْتَقِيمٍ)
(Allahumma Rabb Jibrail wa Mikail waI'iisrafila, fatir alssamawat wal'ardhi,
aA’alim alghayb walshshahadati, 'ant tahkum bayn aIibadik fima kanuu fih
yakhtalifuna, ahdini lima akhtulif fih min alhaqq bi'idhnika, 'innak tahdi man
tasha' 'iilaa sirat mustaqimin)
Tafsir: Ya Allah Rabbi wa Jibril, na Mikail na Israfil, Muanzilishi wa Mbingu na
Ardhi, Mwenye kujua yaliyofichikana na yaliyowazi, hakika wewe ni mwenye
kuhukumu baina ya waja wako juu ya kile walichokhitilafiana, niongoze kutokana na
kile walichohitilafiana niwe katika Haki kwa idhini yako, kwa hakika wewe ni mwenye
kuwaongoza uwatakao katika njia iliyonyooka.
Hii ni Dua muhimu sana ambayo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua
akimuomba Allah Subhanah wa Ta’ala ambae ni mola wa Malaika Jibril, Mikail na Israfil
kwa ajili ya uongofu wa Hapa Duniani na kesho Akhera, kwani hakuna usalama katika
siku ya malipo kesho Akhera hadi uwe ni mwenye kujihakikishia kua upo kwenye njia
iliyonyooka ambayo ndio njia ya waliofuzu kama anavyosema Allah Subhanah wa
Ta’ala:
120
﴿إِن َّ اهلل َّ يُدْخِ لُ ال َّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الص َّ الحَِاتِ جَن َّاتٍ تجَْرِي مِنْ تحَْتِهَا
يحَُل َّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِنْ ذَهَبٍ وَلُؤْلُؤًا وَلِبَاسُهُمْ فِيهَا حَرِيرٌ
الط َّيِّبِ مِنَ الْقَوْلِ وَهُدُوا إِلىَ صِرَاطِ الحَْمِيدِ﴾
الأَْنْهَاُر
۞ وَهُدُوا إَِلى
Inna Allaha yudkhilu alladheena amanoo waAAamiloo alssalihati jannatin tajree
min tahtiha al-anharu yuhallawna feeha min asawira min dhahabin walu/lu-an
walibasuhum feeha hareerun; Wahudoo ila alttayyibi mina alqawli wahudoo ila
sirati alhameedi (Surat Al Hajj 22:23-24)
Tafsir: Hakika Allah atawaingiza wale waliomuamini na wakafanya mambo mema
katika Bustani (Peponi) ambazo chini yake kuna kuna mito ambamo watapambwa
ndani yake kwa makoja ya Dhahabu na Lulu na nguo zao zitakua za Hariri. Na
Wameongozwa kutokana na (kutumia) bora miongoni mwa kauli (Dhikr Allah, Lâ
ilâha ill-Allâh, Alhamdu lillâh, Kusoma Qur’an, Kuamrishana Mema n.k) na
wakaongozwa katika njia iliyonyooka.
Hivyo bila ya shaka Allah Subhanah wa Ta’ala ambae ametujaalia mahitaji yetu yote
hapa Ulimwenguni ni mwenye kujua na kuona kila kitu juu yetu hivyo ni wajibu wetu
kumuamini na kumtii na kufahamu kua bila ya shaka baadae kuna kuhesabiwa amali zetu
na ambapo kwa watakaoamini na kujichunga basi watakua ni miongoni mwa waliofuzu
na wale wasioamini na kucheza basi watakua ni miongoni mwa waliokula hasara kwani
mwisho wake watafikia mahali pabaya sana kama inavyosema Qurán:
﴿يُثَبِّتُ ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ بِٱلْقَوْ لِ ٱلث َّابِتِ فىِ ٱلحَْيَاةِ ٱلد ُّنْيَا وَفىِ ٱلآخِ رَةِ وَيُضِل ُّ ٱهلل َُّ
ٱلظ َّالِمِينَ وَيَفْعَلُ ٱهلل َُّ مَا يَشَآءُ ۞أَلمَْ تَرَ إِلىَ ٱل َّذِينَ بَد َّلُواْ نِعْمَةَ ٱهلل َِّ كُ فْ راً وَأَحَ ل ُّواْ
قَوْمَهُمْ دَارَ ٱلْبَوَارِ۞جَ هَ ن َّمَ يَصْ لَْونَهَ ا وَبِئْسَ ٱلْقَرَارُ۞وَجَعَلُواْ هللِ َِّ أَنَدا د اًلِّيُ ضِل ُّواْ عَن
سَبِيلِهِ قُلْ تمََت َّعُواْ فَإِن َّ مَصِيرَكُمْ إِلىَ ٱلن َّارِ۞قُل لِّعِبَادِىَ ٱل َّ ِذينَ آمَنُواْ يُقِيمُواْ ٱلص َّلاَةَ
وَيُنْفِقُواْ ممِ َّا رَزَقْنَاهُمْ سِ رّاً وَعَلانِيَةً مِّن قَبْلِ
أَن َْتِىَ يَوْمٌ لا َّ بَيْعٌ فِيهِ وَلاَ
خِ لاَلٌ ۞ٱهلل َُّ ٱل َّذِى خَلَقَ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضَ وَأَنزَلَ مِنَ ٱلس َّمَآءِ مَآءً فَأَخْرَجَ بِِه
121
مِنَ ٱلث َّمَرَاتِ رِزْقاً ل َّكُمْ وَسَخ َّرَ لَكُمُ ٱلْفُلْكَ لِتَجْرِىَ فىِ ٱلْبَحْرِ أبَِمْرِهِ وَسَخ َّرَ لَ ُكُم
ٱلأَنْهَارَ۞ وَسَخ َّر لَكُمُ ٱلش َّمْسَ وَٱلْقَمَرَ دَآئِبَينِْ وَسَخ َّرَ لَكُمُ ٱلْل َّيْل
َ
ٱ ل ن َو َّ هَا رَ ۞وَآاتَكُم مِّن ِ كُل مَا سَأَلْتُمُوهُ وَإِن تَعُد ُّواْ نِعْمَةَ ٱهلل َِّ لاَ تحُْصُوهَا إِ َّن
ٱلإنْسَانَ لَظَلُومٌ كَف َّارٌ ﴾
Yuthabbitu Allahu alladheena amanoo bialqawli alththabiti fee alhayati alddunya
wafee al-akhirati wayudhillu Allahu aldhdhalimeena wayafAAalu Allahu ma
yasha/o; Alam tara ila alladheena baddaloo niAAmata Allahi kufran waahalloo
qawmahum dara albawari; Jahannama yaslawnaha wabi/sa alqararu;
WajaAAaloo lillahi andadan liyudhilloo AAan sabeelihi qul tamattaAAoo fa-inna
maseerakum ila alnnari, Qul liAAibadiya alladheena amanoo yuqeemoo alssalata
wayunfiqoo mimma razaqnahum sirran waAAalaniyatan min qabli an ya/tiya
yawmun la bayAAun feehi wala khilalun; Allahu alladhee khalaqa alssamawati
waal-ardha waanzala mina alssama-i maan faakhraja bihi mina alththamarati
rizqan lakum wasakhkhara lakumu alfulka litajriya fee albahri bi-amrihi
wasakhkhara lakumu al-anhara; Wasakhkhara lakumu alshshamsa waalqamara
da-ibayni wasakhkhara lakumu allayla waalnnahara; Waatakum min kulli ma
saaltumoohu wa-in taAAuddoo niAAmata Allahi la tuhsooha inna al-insana
ladhaloomun kaffarun (Surat Ibrahim 14:27-34)
Tafsir: Allah atawapa msimamo wenye kauli thabit wale wanaomuamini hapa Duniani
na Akhera, na Allah atawapotosha wale wenye kujidhulumu na Allah hufanya kile
akitakacho. Jee hujawaona wale ambao wamebadilisha Neema za Allah kua ni Kufuru
na kuwasababishia watu wao kukaa katika sehemu ya maangamizo? Jahannama ndio
utakaowaunguza! Na kwa hakika ni sehemu mbaya sana kukaa ndani yake, na
wanajaalia Miungu myengine dhidi ya Allah ili kuwapotosha watu kutokana na
muongozo wake, Waambie: Kuleni Raha!kwani kwa hakika mtakapofikia mwisho
wenu ni Motoni. Waambie (Ewe Muhammad) waja wangu walioamini! Kua
wasimamishe Sala, na watoe kutokana na kile tulichowaruzuku kwa siri na kwa
dhahir, kabla ya kuwasili siku ambayo itakua hakuna kupatana wala kupendeleana.
Allah ni yule ambae alieumba Mbigu na Ardhi na akashusha maji kutoka mbiguni,
na kutokana nayo akatoa matunda kua ni rizki kwa ajili yenu, na akazifanya Meli kua
kwa ajili ya matumizi yenu, ili muweze kuelea (kusafiri) juu ya Bahari kutokana na
amri yake na Mito kua kwa ajili yenu. Na akalifanya Jua na Mwezi kua daima ni yenye
kupita katika njia zake kwa ajili yenu, na akajaalia Mchana na Usiku kua ni kwa ajili
yenu. Na akakupeni kila kitu mlichohitaji. Na kama mtazihesabu Neema za Allah juu
ّ
122
yenu, basi kamwe hamtoweza kuzihesabu. Ama kwa Hakika Mtu ni mwenye
kujidhulumu na ni mwenye kukufuru
Allah Akbar! Wa Alhamd lillah! wa La Illah Ila Allah! Allah Subhanah wa Ta’ala ambae
ndie Mola wa Ulimwengu wote na kila kilichomo ndani yake, anatuwekea wazi namna
anavyotupenda sana waja wake na hivyo bila ya shaka yeye ni mwenye kutuonea huruma
kutokana na udhaifu wa Nafsi zetu na matamanio ya Ulimwengu huu wa mpito na
kututahadharisha juu ya siku ya Malipo siku ambayo itakua hakuna kupatana wala
kupendeleana.
Naam, kutokana na Ukarimu wake juu yetu kwa kutujaalia kila aina ya Neema
tunazozihitaji basi pia akatujaalia kutumwagia Rehma zake juu yetu Ibn Adam, kwa
kutupa nafasi ya kuomba msamaha wake kwa kila atakaeamua kurudi kwake, na pia kwa
kutuma Mitume kwa kila baada ya mda ili kutukumbusha waja wake juu yake, Mitume
hao ni kutoka miongoni mwa watu wa jamii husika ili watoe muongozo, maonyo na
kuwausia watu juu yake pale watu hao wanapopotoka kutokana na njia iliyosahih ya
kuelekea kwake kabla ya yeye kuamua kuwashushia wanaopotoka adhabu kali isiyoweza
kustahmilika kutokana na maumbile yetu Ibn Adam, kama inavyosema Qurán katika aya
zifuatazo.
﴿م َّنِ ٱهْتَدَىٰ فَإِنم ََّا يَهْتَدِ ى لِنَفْسِ هِ وَمَن ضَل َّ فَإِنم ََّا يَضِل ُّ عَلَيْهَا وَلاَ تَ زِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ
أُخْرَىٰ وَمَا كُن َّا مُعَذِّبِينَ حَتى َّ ٰ نَبْعَثَ رَسُولاً ۞ وَإِذَآ أَرَدَْ أَن ن ُّهْ لِكَ قَرْيَةً أَمَرَْ
مُتْرَفِيهَا فَفَسَقُواْ فِيهَا فَحَق َّ عَلَيْهَا ٱلْقَوْلُ فَدَم َّرَْهَا تَدْمِيراً ﴾
Mani ihtada fa-innama yahtadee linafsihi waman dhalla fa-innama yadhillu
AAalayha wala taziru waziratun wizra okhra wama kunna muAAadhdhibeena
hatta nabAAatha rasoolan, Wa-idha aradna an nuhlika qaryatan amarna
mutrafeeha fafasaqoo feeha fahaqqa AAalayha alqawlu fadammarnaha tadmeeran
(Surat Al Isra 17:15-16)
Tafsir: Ama kwa yule atakeongoka basi hua ni mwenye kuiongoa Nafsi yake, na
mwenye kupotoka basi hua ni mwenye kuipotosha Nafsi yake, na hakuna mbebaji
atakaebeba mzigo wa mwenzake. Na sisi kamwe hatuadhibu hadi inapokua tayari
tumeshatuma Mjumbe (kuonya). Na tunapoamua kuuangamiza Mji basi hua
tunatuma amri kwanza (kwa watu husika kua wamtii Allah Subhanah wa Taála) kwa
baadhi miongoni mwao ambao wamepewa vizuri katika uhai huu. Na kisha wakavuka
mipaka kutokana na kupewa huko, basi hapo ndio kauli (ya adhabu) inawahalalikia
123
juu yao. Na kisha baada ya hapo ndio tunauangamiza (Mji au Ummah husika) kabisa
kabisa.
Anasema Sultan al Mutakallimin Mujaddid ud Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi juu ya
ayah hii kua: ‘Wakati Allah Subhanah wa Taála anapotaka kuuangamiza mji
kutokana na dhambi za watu wake, basi hua haharakishi katika kuungamiza mji
husika kwa sababu ya kuwepo kwa madhambi hayo, bali huwaamrisha wenye
uwezo miongoni mwa watu hao kuachana na dhambi husika, kwani wenye uwezo
wanapofanya dhambi hizo wao basi wale wasiokua na uwezo nao huwafuata katika
hayo. Hivyo wanapo kataa kuachana na dhambi husika basi ndio huadhibiwa kwa
adhabu husika, na wamelengwa wenye uwezo kwa sababu wao ndio ambao
wanatakiwa zaid kumshukuru Allah Subhanah wa Taála kwa kuwapendelea kwa
neema alizowajaalia. Hivyo baada ya onyo la kwanza basi huwapa nafasi watu hao
kwa kuwaonya tena mara kadhaa, na wakiendelea kudumu katika dhambi hizo basi
na Adhabu husika huwashukia watu hao.’
Mbali ya kua Allah Subhanah wa Ta’ala anatuambia katika Qurán kua hashushi adhabu
hadi atume Mitume wake kuonya ili wawaonye watu na kuwarudisha watu katika njia
moja ya haki ya kimaumbile ya kumpwekesha Allah Subhanah wa Taála lakini pia hapo
hapo, inatuwekea wazi kua kila Ummah wa wakati husika ulikua ni wenye kutumia
Hukmu na njia tofauti zilizokua zikiendana na Nyakati husika, kwa mfano tunapoiangalia
kitabu cha Zabur cha Nabii Daud basi tunaona kua mbali ya kua kilikua kinabashiria
mambo yatakayotokea katika miaka ya baadae lakini pia kilikua ni kitabu kilichokua
hakina Sharia wala Hukmu ndani yake, lakini kilikua kinazungumzia mambo ya Halali
na Haram tu basi ndani yake.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala katuwekea wazi kua Qurán ndio kitabu kilichokuja
kubatilisha vitabu vyote vya Mitume wengine vilivyokuja kabla yake na hivyo
kumwambia Mtume wake Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam kua Qurán ndio
chenye kauli ya mwisho na chenye uthibitisho juu ya vitabu vyote walivyopewa Mitume
waliotangulia kabla yake, na yaliyoteremshwa ndani ya Qurán ndio yanayotakiwa
kufuatwa badala yake kwa kusema:
﴿وَأَنزَلْنَآ إِلَيْكَ ٱلْكِتَابَ بِٱلحَْقِّ مُصَدِّقاً لِّمَا بَينَْ يَدَيْهِ مِنَ ٱلْكِتَابِ وَمُهَيْمِناً عَ لَيْهِ
ٍ
ّ
فَٱحْكُم بَيْنَهُم بمَِآ أَنزَلَ ٱهلل َُّ وَلاَ تَت َّبِعْ أَهْوَآءَهُمْ عَم َّا جَآءَكَ مِنَ ٱلحَْقِّ لِكُل جَعَلْنَا
124
مِنكُمْ شِ رْعَةً وَمِنْهَاجاً وَلَوْ شَآءَ ٱهلل َُّ لجََعَلَكُمْ أُم َّةً وَاحِ دَةً وَلَٰكِن لِّيَبْلُوَكُمْ فىِ مَآ
آاتَكُم فَاسْتَبِقُوا الخَيْرَاتِ إِلىَٰ اللهِ مَرْجِ عُكُمْ جمَِيعاً فَيُنَبِّئُكُم بمَِا كُنتُمْ فِيهِ تخَْتَلِفُونَ ﴾
Waanzalna ilayka alkitaba bialhaqqi musaddiqan lima bayna yadayhi mina
alkitabi wamuhayminan AAalayhi faohkum baynahum bima anzala Allahu wala
tattabiAA ahwaahum AAamma jaaka mina alhaqqi likullin jaAAalna minkum
shirAAatan waminhajan walaw shaa Allahu lajaAAalakum ommatan wahidatan
walakin liyabluwakum feema atakum faistabiqoo alkhayrati ila Allahi
marjiAAukum jameeAAan fayunabbi-okum bima kuntum feehi takhtalifoona
(Surat Al Maidah 5:48)
Tafsir: Na kwako wewe tumetuma Kitabu kwa Haki na Ukweli, kuthibitisha vitabu
vilivyotangulia kabla yake na chenye uongofu na uthibitisho zaidi juu yake. Hivyo toa
hukumu baina yao kutokana na alivyoteremsha Allah, na kamwe usifuate matamanio
yao, yatakayokutoa katika Haki iliyokujia wewe. Kwa kila mmoja miongoni mwenu
amebainishiwa Sharia na njia iliyowazi. Kama Allah angelitaka basi angekujaalieni
nyie kua Ummah mmoja. Lakini (mipango yake) ni kukujaribuni nyinyi juu ya kile
alichokujaalieni, hivyo jitahidini kwa kukimbilia katika kufanya mema. Marejeo ya
kila mmoja wenu ni kwa Allah. Ni yeye ndie ambae atakaekuonesheni ukweli juu ya
kile mnachohitilafiana.
Ama kuhusiana na aya hii basi anasema Qatadah kua; ‘Ingawa watu wa Mataifa yote
ya hapo awali yalikua yakifuata Dini Moja inayompwekesha Allah Subhanah wa
Ta’ala pekee, lakini wote walikua na Shariah tofauti’. Hapa sasa umefika wakati wa
kuwaangalia Mitume na Manabii hao waliotangulia na kutajwa katika Qurán.
MITUME NA MANABII WALIOTAJWA KATIKA QURÁN.
Kwa lugha ya kiarabu neno ‘Nabi’ lina maana ya habari au ripoti. Hivyo mtu huitwa
‘Nabi’ (Nabii) kwa sababu hua anatoa habari kuhusiana na Mola wake na pia hua
anapokea habari kutoka kwa Mola wake kupitia kwa Malaika Jibril. Kwa kishariah
neno ‘Nabi’ yaani Nabii, humaanisha mtu alie na sifa ya ubora ambayo
amehamasishwa kwa kupitia njia za Wahy kufanya vitendo vyake bila ya
125
kuamrishwa kuwafikishia watu wengine ujumbe wa Wahy huo na hivyo mtu huyo
huutekeleza ujumbe huo yeye mwenyewe binafsi.
Na ‘Rasul’ (Mtume) humaanisha mtu alie na sifa ya ubora ambayo amehamasishwa
kwa kupitia njia za Wahy kufanya vitendo vyake na kuamrishwa kuueneza na
kuwafikishia watu wengine ujumbe wa wahy huo. Hivyo kila Rasul (Mtume) hua ni
lazima kua Nabi (Nabii) lakini si lazima kwa kila Nabi (Nabii) kua ni Rasul (Mtume).
Katika kulifafanua zaidi hili basi na tuangalie mtizamo wa Imam Jaffar As Sadiq ambae
yeye anasema kua: Manabii wamegawika katika makundi manne:
1 - Nabii ambae hua anapokea Wahy na Ilham lakini hua hana jukumu la kueneza
ujumbe ulio ndani ya Wahy au Ilham husika kwa watu wengine.
2 - Nabii ambae hua anaona na kusikia ujumbe anaoletewa katika wakati ambao
akiwa macho wazi yaani hajalala na hayuko usingizini au katika wakati macho
yakiwa ameyafunga yaani akiwa usingizini lakini nae pia hua hana jukumu la
kueneza ujumbe huo kwa watu wengine.
3 - Nabii ambae hua ni Nabii Al Mursal ambae yeye hua anapokea ujumbe na
kuamrishwa kuutanaza ujumbe husika kwa baadhi ya watu tu.
4 - Nabii ambae hua ni hua anapokea Wahy na kutumwa kuueneza ujumbe huo kwa
watu wote kwa ujumla.
Anasema Hujjat ul Islami Mujaddid ud Din Imam Abu Hamid Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali kua: Kama ilivyokua kwa viumbe Ibn Adam kutofautishwa
na wanyama wengine kwa wao Ibn Adam kupewa Nafsi yenye Ufahamu, basi ndio
hivyo hivyo walivyotofautishwa Ibn Adam wengine na Mitume na Manabii kwani
Nafsi na Roho za Mitume na Manabii hutofautiana na za watu wa kawaida kwa
sababu wao hua ni waliopewa Uongofu na Ufahamu wenye kuongoka zaidi tofauti
na watu wengine, kwani Uongofu wao huwaongoza katika njia ya Allah Subhanah
wa Taála. Kama vile ilivyokua mwendo wa kutembea wa Ibn Adam kua ni tofauti
na ni Miujiza kwa Wanyama wengine basi ndio hivyo hivyo inavyokua kwa miendo
ya Mitume kuelekea kwa Mola wao kwani miendo yao hua ni tofauti na ni Miujiza
kwa Ibn Adam wengine.
Hivyo kushushiwa kwa Mitume na Manabii kwa watu hua ni Rehma kubwa sana kutoka
kwa Allah Subhanah wa Ta’ala. Tukiangalia historia ya Ulimwengu tunaona kua
ustaarabu Ulimwenguni ulianzia katika maeneo ya Mashariki ya kati baina ya nchi za
Misri, Syria, Iraq na Uarabuni, na hii ni kwa sababu maeneo hayo ndio maeneo ambayo
126
yalikua na idadi kubwa ya jamii za watu katika kipindi cha mwanzoni mwa maisha ya
Ulimwenguni kuliko maeneo mengine, hivyo idadi hiyo kubwa ya jamii za watu
waliokua wakiishi katika maeneo hayo kulipelekea kutumiwa kwa Mitume na Manabii
wengi katika maeneo hayo.
Mitume na Manabii hao walikua na miongoni mwa wenye sifa kuu zifuatazo:
1. Mitume na Manabii walitoka miongoni mwa Bani Adam, hawakutoka miongoni
mwa Majini au Malaika.
2. Mitume na Manabii walikua na sifa za uaminifu, ukweli, kutokufanya dhambi.
Hua hivi ili madai yao yakubaliwe na kupandishwa darja ya juu.
3. Mitume na Manabii walikua na sifa za kua na ufahamu uliokamilia, uhakika na
uongofu.
4. Mitume na Manabii walikua ni lazima wafikishe kwa watu wao ujumbe wote wa
Wahyi walioamriwa kuufikisha, hawakuficha kitu chochote.
5. Mitume na Manabii walikua ni Wanaume.
Ama kuhusiana na sifa ya tano, basi kuna kutofautiana kuhusiana na mtizamo wa
waliopewa Unabii kua ni Wanaume tu, kwani kwa tizamo wa Wanazuoni wanaofuata
mitizamo ya Aqida ya Maturidi basi wao wanaosema kua waliopewa Utume walikua ni
Wanaume tu.
Ama kwa upande wa Wanazuoni wanaofuata mtizamo wa Aqida ya Ashari basi wao
wanasema kua miongoni mwa waliopewa Unabii walikuemo pia Wanawake.
Kwa upande wa wafuasi wa Maturidi ambao ndio wanaosema kua waliopewa Unabii
walikua ni wanaume tu, basi wao wanasimamia katika uthibitisho wa aya ambayo
imetumia neno “Rijalan”, ambapo kwa mtizamo wao basi ni kua neno hilo hua
linamaaisha kua ni Mwanamme, aya hio ni ile isemayo kua:
﴿وَمَآ أَرْسَلْنَا قَبْلَكَ إِلا َّ رِجَالاً ن ُّوحِ ى إِلَيْهِمْ فَاسْئَلُواْ أَهْلَ الذِّكْرِ إِن كُنتُمْ لاَ
تَعْلَمُونَ﴾
127
Wama arsalna qablaka illa rijalan noohee ilayhim fais-aloo ahla aldhdhikri in
kuntum la taAAlamoona. (Surat al-Anbiya 21:7)
Tafsir: Na hatukutuma kabla yako Rijalan yeyote isipokua watu ambao
tuliwahamasisha, hivyo uliza wenye kujua ikiwa wewe hujui.
Lakini hata hivyo miongoni mwa Wanazuoni wenye I’lm ya Tafsir ambao ni wafuasi wa
Aqida ya Ashari wanasema katika kutafsiri aya hii kua neno 'Rijalan’, lililotumika hapa
linajumuisha Wanaume na Wanawake, hivyo miongoni mwa Manabii pia wapo Manabii
wanawake. Miongoni mwa Wanazuoni wenye mtizamo huo ni pamoja na Imam Abu
Hasan Al Ashari, Imam Fakhr Ad Din Al Razi (Katika Al Durr Al Mukhtari), Imam Al
Suyuti (Katika kitabu chake cha Al Ashbah wal Nazair), Imam Kamal al Humam (katika
kitabu cha Husun al Uswah), Imam Ibn Hazm, Imam Al Mubarkafuri (katika kitabu cha
Tuhfat al Awhathi) n.k.
Wanazuoni hao wanasimamia katika hoja ya vithibitisho ambavyo miongoni mwao ni
pamoja na pale Allah Subhanahu wa Ta’ala aliposema kuhusiana na Yuhanz ambae ni
mama yake Nabii Musa kua: ‘Na tukamshushia Wahyi mama yake Musa’, katika Surat
Al Qasas isemayo:
﴿وَأَوْحَيْ نَآ إِلىَٰ أُمِّ مُوسَ ى ٰ أَنْ أَرْضِ عِيهِ فَإِذَا خِ فْ تِ عَلَيْهِ فَأَلْقِيهِ فىِ ٱليَمِّ وَلاَ تخََاِفى
وَلاَ تحَْزَنيِۤ إِ َّ رَآد ُّوهُ إِلَيْكِ وَجَاعِلُوهُ مِنَ
ٱلْمُرْسَلِ َين ﴾
Waawhayna ila Ummi Moosa an ardhiAAeehi fa-idha khifti AAalayhi faalqeehi fee
alyammi wala takhafee wala tahzanee inna raddoohu ilayki wajaAAiloohu mina
almursaleena (Surat Al Qasas 28:7)
Tafsir: Na tukamshushia Wahyi mama yake Musa (kumwambia): ‘Mnyonyeshe
(Musa), lakini ikiwa utakhofia juu yake, basi mtie mtoni na wala usiwe na khofu yeyote
wala huzuni. Kwani kwa hakika sisi tutamrudisha kwako wewe na tutamfanya kua ni
miongoni mwa Mitume yetu’.
Na uthibitisho uliomo katika Surat Maryam, pale Allah Subhanahu wa Ta’ala aliposema:
128
﴿وَٱذْكُرْ فىِ ٱلْكِتَابِ مَرْيمََ إِذِ ٱنتَبَذَتْ مِ نْ أَهْ لِهَ ا مَكَ اً شَ رْقِياً ۞ فَٱتخ ََّذَ ْت مِن
دُوِِم حِ جَاابً فَأَرْسَلْنَآ إِلَيْهَآ رُوحَنَا فَتَمَث َّلَ لهََا بَشَراً سَوًِّ ۞ قَالَ ْت إِنيّ
بِٱلر َّحمَْٰنِ مِ نكَ إِن كُ نتَ تَقِيّاً ۞ قَالَ إِنم ََّآ أََْ رَسُولُ رَبِّكِ لاًّهَبَ لَكِ م غُلَ اًزَكِيّاً ﴾
ِۤ أَعُوذُ
Waodhkur fee alkitabi maryama idhi intabadhat min ahliha makanan sharqiyyan;
Faittakhadhat min doonihim hijaban faarsalna ilayha roohana fatamaththala laha
basharan sawiyyan; Qalat innee aAAoodhu bialrrahmani minka in kunta taqiyyan;
Qala innama ana rasoolu rabbiki li-ahaba laki ghulaman zakiyyan (Surat Maryam
19:16-19)
Tafsir: Na ametajwa katika kitabu, Maryam, wakati alipojitenga kutokana na familia
yake katika sehemu inayoelekea upande wa Mashariki; Akaweka pazia kabla yao,
kisha tukamtumia Ruhi (Malaika) wetu alietokea mbele yake katika umbo la mtu
aliejaa heshima; Nae akasema: ‘Hakika mimi ninajilinda kwako na kwa Mwingi wa
Rehma, ikiwa unamuogopa Allah’; Nae (Malaika) akasema: ‘Mimi ni mjumbe kutoka
kwa Mola wako, (kukubashiria kua) utapata mtoto alie mwema’.
Kwani Allah Subhanahu wa Ta’ala alimchagua Maryam bint Imran na akamuamrisha
Malaika Jibril Alayhi Salaam kumshushia Wahyi wa kumbashiria habari njema kama
inavyofafanuliwa zaidi katika Surat Al Imran kwa kusema:
﴿وَإِذْ قَالَتِ
ٱلْمَلاَئِكَةُ يمَٰرْيمَُ إِن َّ ٱهلل ََّ ٱصْطَفَاكِ وَطَه َّرَكِ وَٱصْطَفَاكِ عَلَى ٰ نِسَآِء
ٱلْعَالَمِينَ ﴾
Wa-idh qalati almala-ikatu ya Maryamu inna Allaha istafaki watahharaki
waistafaki AAala nisa-i alAAalameena (Surat Al Imran 3:42)
Tafsir: Na (kumbuka) wakati Malaika aliposema: ‘Ewe Maryam! Kwa Hakika Allah
amekuchagua wewe na kukutakasa, na kukuchagua kua juu zaid ya Wanawake wote
wa Ulimwenguni’.
Na vile vile pale Allah Subhanahu wa Ta’ala alipomjumuisha Maryam bint Imran ambae
ni Mama yake Nabii Isa katika hali ambayo amewajumuisha Manabii wengine kwa
kusema katika Surat Al Imran:
129
﴿إِن َّ ٱهلل ََّ ٰ ٱصْطَفَى آدَمَ وَنُوحاً وَآلَ إِبْرَاهِيمَ وَآلَ عِمْرَانَ عَلَى ٱلْعَالَمِينَ ﴾
Inna Allaha istafa adama wanoohan waala ibraheema waala AAimrana AAala
alAAalameena (Surat Al Imran 3:33)
Tafsir: Hakika Allah amemchagua Adam, Nuh, familia ya Ibrahim na familia ya
Imran kua juu ya Alamin (Majini na Bani Adam wa wakati huo).
Na pia katika Surat Maryam pale Allah Subhanahu wa Ta’ala aliposema:
﴿أُولَٰئِكَ ٱل َّذِينَ أَنْعَمَ ٱهلل َُّ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلن َّبِيِّينَْ مِن ذُرِّي َّةِ ءادَمَ وَممِ َّنْ حمََلْنَا مَعَ نُو ٍح
وَمِن ذُرِّي َّةِ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْرَائِيلَ وَممِ َّنْ هَدَيْنَا وَٱجْتَبَيْنَآ إِذَا تُتْلَى ٰ عَلَيْهِمْ آَتُ ٱلر َّحمَْٰ ِن
خَ ر ُّو اْ سُج َّداً وَبُكِيّاً ﴾
Ula-ika alladhina anAAama Allahu AAalayhim mina alnnabiyyeena
min dhurriyyati adama wamimman hamalna maAAa noohin wamin dhurriyyati
ibraheema wa-isra-eela wamimman hadayna waijtabayna idha tutla AAalayhim
ayatu alrrahmani kharroo sujjadan wabukiyyan (Surat Maryam 19:58)
Tafsir: Wao ni wale ambao Allah amewaneemesha kutoka katika miongoni mwa
Mitume, kutoka katika kizazi cha Adam, na wale tuliowachukua pamoja na Nuh, na
miongoni mwa kizazi cha Ibrahim na Israel na miongoni mwa wale tuliowaongoza na
kuwachagua. Wakati aya za mwenye wingi wa Rehma zinaposomwa, husujudu na
kulia.
Ambapo miongoni mwa kizazi cha Adam ni Idris, na miongoni mwa wale tuliowachukua
pamoja na Nabii Nuh katika Safina ni kizazi cha wazee waliomtoa Nabii Ibrahim, na
miongoni mwa kizazi cha Ibrahim ni Is-haq, Yaqub na Ismai’l na miongoni mwa Bani
Israel ni Mama yake Musa, Musa, Harun, Zakariyah, Yahya, Maryam na Isa Ibn Maryam.
Wanazuoni wanasema kua katika wanawake hao pia yumo Hawa mke wa Nabii Adam,
na vile vile Sarah aliekua mke wa Nabii Ibrahim, kama ilivyoelezewa katika Qurán kwa
kutumia njia ya kauli ya Sarah pale alipozungumza na Malaika walipokuja kumtembelea
Nabii Ibrahim na yeye akiwepo na kuwabashiriwa mtoto kama inavyoelezewa katika aya
ifuatayo:
130
﴿قَالَتْ يٰوَيْلَتَا ءَأَلِدُ وَأََْ عَجُوزٌ وَهَذَا بَعْلِى شَيْخًا إِن َّ هَذَا لَشَىْءٌ عَجِ يبٌ ۞
ۤ قَالُو اْ أَتَعْجَ بِينَ مِ نْ أَمْ رِ ٱهلل َِّ رَحمَْةُ ٱهلل َِّ وَبَرَكَاتُهُ عَلَيْكُمْ أَهْلَ ٱلْبَيْ ِت إِن َّهُ حمَِيدٌ مج َِّيٌد ﴾
Qalat ya waylata aalidu waana AAajoozun wahadha baAAlee shaykhan inna hadha
lashay-on Aaajeebun; Qaloo ataAAjabeena min amri Allahi rahmatu Allahi
wabarakatuhu AAalaykum ahla albayti innahu hameedun majeedun (Surat Hud
11:72-73)
Tafsir: Akasema (kwa kushangaa) ‘Ole wangu! Nitapata mtoto wakati mimi ni
kikongwe, na huyu hapa mume wangu ni kizee’. Nao (Malaika) wakasema: ‘Unaona
ajabu juu ya yale aliyoyakadiria Allah? Rehma za Allah na Baraka zake ziwe juu yenu,
Enyi familia ya Ibrahim. Hakika yeye (Allah) Mwenye kustahiki sifa zote na mwenye
Kushinda.’
Na pia habari hiyo kuelezewa kwa njia ya kuonesha picha ya vitendo katika Surat Adh
Dhuriyyat:
﴿فَأَقْبَلَتِ ٱمْرَأَتُهُ فىِ صَر َّةٍ فَصَك َّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ ۞ قَالُواْقَا لُواْ
كَذٰ لِكِ قَالَ رَب ُّكِ إِن َّهُ هُوَ ٱلحَْكِيمُ ٱلْعَلِيُم
﴾
Faaqbalati imraatuhu fee sarratin fasakkat wajhaha waqalat AAajoozun
Aaaqeemun; Qaloo kadhaliki qala rabbuki innahu huwa alhakeemu alAAaleemu
(Surat Adh Dhuriyyat 51:29-30)
Tafsir: Kisha Mke wake (Sarah) akakabiliana nao, na akajipiga vibao usoni na
kusema: ‘Kikongwe alie Mgumba!’. Nao (Malaika) wakasema: ‘Kadhalika hivyo
ndivyo asemavyo Mola wako. Hakika yeye ni mwingi wa Hikma, na ni Mjuzi wa kila
kitu.’
Na miongoni mwa Wanawake hao pia ni pamoja na Asiyah Bint Muzahim aliekua mke
wa Fir’awn, kutokana na kua ni mfano bora miongoni mwa wenye kuamini kama
isemavyo Qurán:
131
﴿وَضَرَبَ ٱهلل َُّ مَثَلاً لِّل َّذِينَ آمَنُواْ ٱمْرَأَةَ فِرْعَوْنَ إِذْ قَالَتْ رَبِّ ٱبْنِ لىِ عِنَدكَ بَيْتاً ِفى
ٱلجَْن َّةِ وَنجَِّنىِ مِن فِرْعَوْنَ وَعَمَلِهِ وَنجَِّنىِ مِنَ ٱلْقَوْمِ ٱلظ َّالِمِينَ ﴾
Wadharaba Allahu mathalan lilladheena amanoo imraata firAAawna idh qalat
rabbi ibni lee AAindaka baytan fee aljannati wanajjinee min firAAawna
waAAamalihi wanajjinee mina alqawmi aldhdhalimeena. (Surat At Tahrim 66:11)
Tafsir: Na Allah anatoa mfano kwa wale walioamini: Mke wa Fir’awn, pale
aliposema: ‘Mola wangu! Nijengee mimi nyumba kwako wewe Peponi, na uniokoe
kutokana na Fir’awn na amali zake, niokoe kutokana na watu madhalimu’
Ambapo aya inayofuatia baada ya hiyo inamsifia tena Maryam Bint Imran kwa kusema:
﴿وَمَرْيمََ ٱبْنَةَ عِمْرَانَ ٱل َّتيِ ۤ أَحْصَنَتْ فَرْجَهَا فَنَفَخْنَا فِ يهِ مِن ر ُّ وحِنَا وَ صَد َّ قَتْ
بِكَلِمَاتِ رَب َّهَا وَكُتُبِهِ وَكَانَتْ مِنَ ٱلْقَانِتِينَ ﴾
Wamaryama ibnata AAimrana allatee ahsanat farjaha fanafakhna feehi min
roohina wasaddaqat bikalimati rabbiha wakutubihi wakanat mina alqaniteena
(Surat At Tahrim 66:12)
Tafsir: Na Maryam Bint Imran ambae alijihifadhi sehemu zake za Siri. Kisha
tukampulizia Roho kutoka kwetu, na akathibitisha Kauli ya Mola wake na Vitabu
vyake, na alikua ni miongoni mwa wenye Kumcha Mungu.
Hivyo kutokana na vithibitisho vyao hivyo tunaona kua Wanawake pia kama Wanaume
hua na sifa na uwezo wa kua miongoni mwa wenye kupokea Wahyi na hivyo hua kuna
uwezekano wa kua Manabii na vile vile kua ni miongoni mwa mifano bora inayofaa
kuigwa, ingawa hawakutajwa kua na Unabii kwa majina, kwani Allah Subhanahu wa
Ta’ala anasema kua kuna Mitume aliowataja majina na kuhadithia visa vyao katika
Qurán na vile vile pia kuna Mitume na Manabii ambao hakuwatajwa kwa majina katika
Qurán, kama inavyoelezea aya ifuatayo:
132
﴿إِ َّ أَوْحَيْنَآ إِلَيْكَ كَمَآ أَوْحَيْنَآ إِلىَ نُوحٍ وَٱلن َّبِيِّينَ مِن بَعْدِهِ وَأَوْ َحيْنَآ إِلىَٰ إِبْرَهِيَم
وَإِسمَْعِيلَ وَإْسْحَقَ وَيَعْقُوبَ وَالأَْسْبَا ِط وَعِيسَ ٰ ى وَأَي ُّوبَ وَيُونُسَ وَ َهرُونَ وَسُلَيْمَ َن
وَءَاتَيْنَا دَاوُودَ زَبُوراً ۞ وَرُسُلاً قَدْ قَصَصْنَهُمْ عَلَيْكَ مِن قَبْلُ وَرُسُلاً لم َّْ نَْقصُصْهُ ْم
عَلَيْكَ وَكَل َّمَ اهلل َُّ مُوسَى تَكْلِيماً ۞ ر ُّسُلاً م ُّبَشِّ رِينَ وَمُنذِرِينَ لِئَلا َّ يَكُونَ لِلن َّا ِس
عَلَى ٱهلل َِّ حُج َّةٌ بَعْدَ الر ُّسُلِ وَكَا َن ٱهلل َُّ عَزِيزاً حَكِيماً﴾
Inna awhayna ilayka kama awhayna ila noohin waalnnabiyyeena min baAAdihi
waawhayna ila ibraheema wa-ismaAAeela wa-ishaqa wayaAAqooba waal-asbati
waAAeesa waayyooba wayoonusa waharoona wasulaymana waatayna dawooda
zabooran; Warusulan qad qasasnahum AAalayka min qablu warusulan lam
naqsus-hum AAalayka wakallama Allahu moosa takleeman; Rusulan
mubashshireena wamundhireena li-alla yakoona lilnnasi AAala Allahi hujjatun
baAAda alrrusuli wakana Allahu AAazeezan hakeeman (Surat An Nisaa 4:163-165)
Tafsir: Hakika tumekushushia Wahyi wewe kama vile tulivyomshushia Nuh na
Manabii waliofuata baada yake. Na pia tulimshushia Wahyi Ibrahim, Isma`il, Ishaq,
Ya`qub, na Al-Asbat (kizazi cha watoto 12 wa Nabii Ya`qub) `Isa, Ayyub, Yunus,
Harun, na Sulayman; na Daud tukampa Zabur. Na Mitume ambayo tumekutajia wewe
kabla, na Mitume ambayo hatukukutajia, na Musa aliezungumza moja kwa moja na
Allah. Mitume kama wabebaji ujumbe mwema na maonyo pia, ili watu wawe hawana
kisingizio baada ya (kutumiwa) Mitume. Hakika Allah ni mwenye uwezo na ni mwingi
wa Hikma.
Na vile vile akasema tena Allah Subhanah wa Taála:
﴿وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلاً مِّن قَبْلِكَ مِنْهُم م َّن قَصَصْنَا عَلَيْكَ وَمِنْ ُهمْ م َّن لم َّْ نَقْصُ ْص
قُضِى
عَلَيْكَ وَمَا كَانَ لِرَسُولٍ أَن َْتِىَ آبِيَةٍ إِلا َّ إبِِذْنِ ٱهلل َِّ فَإِذَا جَآءَ أَمْرُ ٱهلل َِّ َ
بِٱلحَْقِّ وَخَسِ رَ هُنَالِكَ ٱلْمُبْطِلُونَ ﴾
133
Walaqad arsalna rusulan min qablika minhum man qasasna AAalayka waminhum
man lam naqsus AAalayka wama kana lirasoolin an ya/tiya bi-ayatin illa bi-ithni
Allahi fa-itha jaa amru Allahi qudhiya bialhaqqi wakhasira hunalika almubtiloona
(Surat Al Ghafir 40:78)
Tafsir: Na kwa hakika sisi tulituma Mitume kabla yako (Ewe Muhammad), ambapo
baadhi yao tumekuhadithia juu yao na baadhi yao hatukuhadithia juu yao, na
haikuwahi kutokea kwa Mtume yeyote yule kupewa aya zetu isipokua kwa idhini ya
Allah, Hivyo inapokuja amri ya Allah basi jambo hilo litaamuliwa kwa haki na
wataofuata vyenginevyo watakua ni waliopotea.
Ama kwa upande mwengine basi Abu Dhar Radhi Allahu Anhu anasema kuhusiana na
idadi ya Mitume na Manabii katika hadith ifuatayo ambayo ni ndefu kidogo lakini yenye
mafunzo mengi ndani yake kua: ‘Siku moja niliingia Msikitini nikamkuta Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akiwa amekaa peke yake. Hivyo nikamuuliza: ‘Ya Rasul
Allah (Salallahu Alayhi wa Salam) Niambie kuhusiana na Ibada ya Sala ambazo
umetuamrisha?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Sala ni Ibada bora. Hivyo Sali kwa
wingi zaid kwa kadiri utakavyoweza’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee Ibada ipi ni Bora zaid?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Kumuamini Allah na kupigana
Jihad kwa ajili yake.’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee ni yupi Mumuumini bora?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Muumini bora ni yule alie m-bora
katika tabia zake’
Abu Dhar akauliza; ‘Jee ni Muumini yupi aliekua salama?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Muumini alie salama ni yule ambae
Waislamu wenzake watakua salama kutokana na ulimi wake’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee Ni yupi Muhajirina (Mhamiaji) bora?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Mhamiaji bora ni yule alie yahama
maovu yake’
134
Abu Dhar akauliza: ‘Jee ni Sala ipi ndio Bora?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Sala bora ni ile yenye Kisimamo
Kirefu’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee ni Funga ipi ndio Bora?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Funga bora ni Funga za FArdhi
ambazo zinazolipwa kikamilifu. Kwani Allah hutoa Malipo makubwa zaid’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee Kafara ipi ndio bora zaidi?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Ya yule aliechinja na kuimwaga
damu kwa mikono yake’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee Kuachia huru kuopi ndio bora zaid?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Mtumwa alie ghali kuliko wote na
alie m-bora kwa watu wake’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee Sadaka ipi ndio bora zaidi?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Yenye jitihada za asiekua na kitu
na yenye kutolewa kwa siri kwa mwenye shida’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee ni ipi aya yenye uzito zaidi uliyowahi kushushiwa?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Ayat Al Kursiy’ kisha Rasul Allah
Salallahu Aályhi wa Salam akaongezea kwa kusema: ‘Abu Dhar! Mbingu 7 si chochote
mbele ya Ayat Kursy bali ni kama chembe ya mchanga katika sehemu ya Ardhi na
Kursy si chochote mbele ya Arshi bali ni chembe ya mchanga katika sehemu ya
ardhi’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee Kuna Mitume Mingapi?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Manabii 124000’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee ni wangapi miongoni mwao walikua ni Mitume?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Mitume 313, wengi sana na
wazuri sana’
135
Abu Dhar akauliza: ‘Jee ni Nabii gani wa Mwanzo?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Nabii Adam’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee nae alikua ni Mtume pia?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Naam, Allah alimuumba kwa
mikono yake, kisha akampulizia Roho yake, na akamuweka sawasawa’, kisha Rasul
Allah Salallahu A’layhi wa Salam akaongezea kwa kusema: ‘Abu Dhar! Wanne
miongoni mwao walikua ni Wasyria: Adam, Shith, Idris ambae ndie wa kwanza
kuandika kwa Kalamu na Nuh. Wanne miongoni mwao walikua ni Waarabu: Hud,
Shuayb, Salih na Mtume wako (Rasul Allah Salallahu Aályhi wa Salam). Ya Abu
Dhar! Mtume wa Mwanzo miongoni mwa Bani Israil ni Musa na wa Mwisho ni Isa,
Mtume wa Mwanzo ni Adam na wa Mwisho ni Muhammad.’
Abu Dhar akauliza: ‘Ya Rasul Allah! Jee Allah ameshusha vitabu vingapi?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Vitabu 104: Kwa Shith 50, kwa
Idris 30, kwa Ibrahim 10, kwa Musa 10 kabla ya kumshushia Tawrat, na kisha
akashusha Tawrat, Zabur, Injil na Furqan.’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee mlikua mna nini katika Suhufi Ibrahima?’ (Maandiko ya
Nabii Ibrahim)
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Visa vyenye mafunzo na Wasia
kama vile: ‘Enyi Wenye Kibr! Wafalme wenye kufanya dhulma, sikukuchagueni
nyie mjikusanyie mali, nimekuchagueni ili msimamie matatizo ya wenye
kudhulumiwa, mimi mwenyewe sikatai maombi ya mwenye kudhulumiwa, hata
kama aliefanyiwa dhulma huyo atakua ni mtu asieniamini’ na ‘Mtu mwenye akili
huugawa mda wake katika sehemu zifuatazo: Sehemu moja kwa ajili ya
kuwasiliana na Mola wake ambapo ndani yake atachukua sehemu ya amali zake,
Sehemu nyengine kwa ajili ya kutafakari uumbaji wa Allah Subhanah wa Taála, na
sehemu nyengine kwa ajili ya kujitafutia riski yake. Na mtu mwenye akili
hajishughulishi isipokua katika mambo matatu: Matayarisho kwa ajili ya Akhera
yake, Kufanya kazi kwa kujitafutia Riski yake na Kufurahia kile ambacho
hakijaharamishwa. Na mtu mwenye Ufahamu humbidi kuutumia vyema mda wake
kwa kujishughulisha na mambo yanayomhusu, kuulinda ulimi wake, kwani kila
anaegundua kua kauli zake ni sawa na vitendo vyake basi hatozungumza isipokua
mazungumzo yaliyo muhimu na kua na maana’’
Abu Dhar akauliza: ‘Na jee ni nini kilichoandikwa ndani ya Suhufi Musa?’(Maandiko
ya Nabii Musa)
136
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Ibar (Maneno yenye kuonya) kama
vile: ‘Inashangaza kwa yule mtu ambae ana uhakika wa kifo lakini akawa ni
mwenye kuzikimbilia anasa’’
Abu Dhar akauliza: ‘Jee na sisi tunayo maneno kama hayo katika kitabu chetu?’
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Naam!’ Kisha Rasul Allah Salallahu
A’layhi wa Salam akasoma aya zifuatazo:
﴿قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَك َّى ٰ ۞ وَذَكَرَ ٱسْمَ رَبِّهِ فَصَل َّى ٰ ۞ بَلْ تُؤْثِرُونَ ٱلحَْ يَاةَ ٱلد ُّنْيَا۞
وَٱلآخِ رَةُ خَيْرٌ وَأَبْقَى ٰ ۞ إِن َّ هَٰذَا لَفِى ٱلص ُّحُفِ ٱلأُولىَٰ۞ صُحُفِ إِبْرَ اهِيمَ
وَمُوسَى ٰ ﴾
Qad aflaha man tazakka; Wadhakara isma rabbihi fasalla; Bal tu/thiroona
alhayata alddunya; Waal-akhiratu khayrun waabqa; Inna hadha lafee alssuhufi aloola;
Suhufi ibraheema wamoosa(Surat Al Aála 87:14-19)
Tafsir: Ama kwa hakika amefuzu yule anaejitakasa, Na akalikumbuka jina la Mola
wake na kisha akasali. Lakini nyinyi mnakumbatia maisha ya Dunia. Ijapokua maisha
ya akhera ni bora na yenye kudumu zaidi. Hakika haya yametajwa katika Suhufi
zilizotangulia, Suhufi za Ibrahim na Musa.(Al Anwaa wa Al Taksim Al Hafidh Imam
Abu Hatim Abd Rahman Muhammad Ibn Idris Al Razi Ibn Hibban Al Basti)
Ama kuhusiana na aya hizi 5 za Surat Al Aála, basi anasema Ikrimah Mawla Abd Allah
Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Qad aflaha man tazakka – Kwa hakika amefuzu
yule aliejitakasa, ambapo aliefuzu kwa kujitakasa ni yule ambae ni mwenye
kumpwekesha Allah Subhanah wa Taála tu.’
Na akasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua kua: ‘Wadhakara isma
rabbihi – ‘Na akilikumbuka jina la Mola wake’ - hua kunamaanisha ukamilifu
unaopatikana ndani ya Nafsi ya mtu kutokana na kumjua Allah Subhanah wa
Taála. Na neno fasalla ‘Na kisha akasali’ basi linamaanisha Ukamilifu wa Mwili na
viungo vyake katika kumtii Mola wake’
Ama kuhusiana na ‘Bal tu/thiroona alhayata alddunya; Waal-akhiratu khayrun
waabqa’- basi amesema Muhaqiq Al Faqih Imam Shihab Ad Din Abu Abbas Ahmad
Ibn Muhammad Ibn Ali Ibn Hajar Al Haytami Al Makki Al Shafii kua: Amesema
137
Abu Musa Al Ashari kua amesema Rasul Allahi Salalahu A’layhi wa Salam kua:
‘Yeyote yule anaeipenda Dunia hii basi ataidhuru Akhera yake, na yeyote yule
anaeipenda Akhera yake basi ataidhuru Dunia hii, hivyo mnatakiwa muipendelee
Akhera yenu ambayo ni ya kudumu dhidi ya Dunia hii ambayo ni ya mpito.’
Na akasema Malik Ibn Dinar kua: ‘Kama ingekua Dunia hii ni Dhahabu lakini ni
yenye kupita na kutoweka na Akhera ni Tambara bovu lenye kudumu, basi Akhera
inatakiwa ipewe kipaumbele zaidi, Jee hali itakuaje pale ambapo Dunia hii ni
Tambara bovu la mpito na Akhera ni Dhahabu ya Milele?’
Na juu ya ‘Inna hadha lafee alssuhufi al-oola; Suhufi ibraheema wamoosa’ - Basi
anasema Imam Al Shanqiti kua: ‘Maneno haya yanaonesha kua Ibar – Maonyo ni
maunganisho yanayounganisha Vitabu na Maandiko yaliyopita katika mnyororo
mmoja’
Baada ya ufafanuzi huo kuhusiana na maana, sifa na tofauti baina ya Mitume na Manabii
basi na tuangalie kuhusiana na dalili na alama za Mitume wa Allah Subhanahu wa Ta’ala
ambazo hujulikana pia kama Miujiza.
MAANA YA MIUJIZA.
Miujiza hua ni maajabu ya Allah Subhanahu wa Ta’ala ambayo hua yanavunja Sharia’h
za kawaida za kimaumbile kupitia katika njia au mikono ya Mitume wake, ili kuthibitisha
Uaminifu na Ukweli wa Mitume wake. Muujiza unaweza kua katika njia ya kauli kama
vile Qurán au kwa njia ya vitendo.
‘Allamah Muhammad Sarfaraz Khan Safdar anasema kua: ‘Kilugha neno Mu’jizat hua
linatokana na neno ‘Ajz (Ajizi, au kutokua na uwezo), ambalo ni kinyume na neno
Qudrah (uwezo), na ‘ta’ [ambayo ni tāʼ marbūṭah kwa kilugha na huashiria kua ni
herufi ya mwisho katika neno na hutamkwa kwa kuhemewa ‘-a’ bila ya ‘t’, kihistori
herufi hii ilikua ikitamkwa kama ‘ha’ na ndio maana ‘ta marbutah hua inaonekana
kama ‘ha’] iliyoko mwishoni mwa neno hilo hua inaonesha msisitizo. Neno Mu‘jizat
hua ni sifa kama lilivyo neno Ayah (Alama, Dalili), n.k. Ni Allah Subhanahu wa
Ta’ala ambae hutengeneza ‘Ajz (Ajizi) ndani ya Mu‘jizat na hivyo kiukweli ni kua
huwaondolea uwezo wale wanaopinga. Mu’jizat hua unatoka kwa Allah Subhanahu
138
wa Ta’ala pekee, lakini hupitia katika mikono ya Mtume. Mtume hua hana uwezo
juu ya Miujiza yake. (Hidayat al-Murtab Ila Tariq al-Sawab fi Tahqiq al-Mu’jizat)
Mujaddid ud Din Imam Al Ghazali anasema kuhusiana na Miujiza kua: ‘Sababu
inayofanya Mu‘jizat kua inadhihirisha ukweli wa Mitume, ni kua katika kila kitu
ambacho Bani Adam hawezi kukifanya au hawezi kutoa mfano wake basi hua ni
lazima kimefanywa na Allah. Kila jambo hili linapohusishwa na changamoto za
Mtume, basi hua kama Allah Subhanahu wa Ta’ala anathibitisha kwa kusema,
‘Hakika wewe ni wa Kweli.’’(Ihya ‘Ulum al-Din)
Mujaddid ud Din Imam Fakhr Al Din Razi anasema kuhusiana na Miujiza kua,
‘Kutokana na aya nyingi kua zinazounga mkono ukweli tuliouzungumzia basi
tunaona kua, wakati Allah Subhanahu wa Ta’ala alipozungumzia kuhusiana na
Makafiri kua walitaka Miujiza mingi mikubwa mikubwa (Al Mu’jizat Al Qakhirah)
kutoka kwake yeye, Allah Subhanahu wa Ta’ala alisema katika maelezo yake:
﴿وَقَالُواْ لَن ن ُّؤْمِنَ لَكَ حَتى َّٰ تَفْجُرَ لَنَا مِنَ الأَْرْضِ يَنْبُوعًا ۞ أَوْ تَكُ ونَ لَكَ جَ ن َّةٌ
مِّن نخ َِّيلٍ وَعِنَبٍ فَتُفَجِّ رَ الأَْنْهَرَ خِ لَلَهَا تَفْجِ يرًا ۞ أَوْ تُسْ قِ َط ٱلس َّمَآءَكَمَا
زَعَمْتَ عَلَيْنَا كِسَفًا أَوْ أتَْتِىَ بِٱهلل َِّ وَٱلْمَ لائِكَ ۤ ِة أَوْ يَكُونَ لَكَ بَيْتٌ مِّن
زُخْرُفٍ أَْو تَرْقَ ٰ ى فىِ الس َّمَآءِ وَلَن ن ُّؤْمِنَ لِرُقِيِّكَ حَتى َّ تُنَزِّلَ عَلَيْنَا كِتَاًاب ن َّقْرَءُهُ قُ ْل
قَبِيلاً ۞
سُبْحَنَ رَبىِّ هَلْ كُنتُ إَلا َّ بَشَرًا ر َّسُولاً﴾
Waqaloo lan nu/mina laka hatta tafjura lana mina al-Ardhi yanbooAAan; Aw
takoona laka jannatun min nakheelin waAAinabin fatufajjira al-anhara khilalaha
tafjeeran; Aw tusqita alssamaa kama zaAAamta AAalayna kisafan aw ta/tiya
biAllahi waalmala-ikati qabeelan; Aw yakoona laka baytun min zukhrufin aw tarqa
fee alssama-i walan nu/mina liruqiyyika hatta tunazzila AAalayna kitaban
naqraohu qul subhana rabbee hal kuntu illa basharan rasoolan. (Surat Al Isra 17:90-
93)
Tafsir: Na wao husema: ‘Hatutokuamini hadi pale utakaposababisha maji kutoka
ardhini kwa nguvu kwa ajili yetu; Au wewe una bustani ya Mitende na Mizabibu, na
usababishe maji kutoka kwa nguvu baina yao kwa wingi; Au usababishe Mbingu
kutuangukia vipande vipande kama ulivyojidai, au utuletee Allah na Malaika wake
mbele yetu uso kwa uso; Au una nyumba ya Zukhruf (iliyopambwa kwa Dhahabu) au
139
upae juu mbiguni, na hata hivyo hatutokuamini katika kupaa kwako hadi pale
utakaposhuka na kitabu ambacho tutakisoma’. Sema: Ametukuka Mola wangu! Mimi
sikua yeyote isipokua ni Bashar (mtu), alietumwa kama Rasul.
‘Yaani kwa maneno mengine, Bani Adam kua kiumbe chenye sifa za Utume,
kunamaanisha kua amekamilika katika vitendo vyake na kauli zake, na anaweza
kuwatibu Bani Adam wengine ambao waliokua hawana sifa mbili hizo; lakini si
lazima kua kutokana na kua na sifa hii (ya Utume) basi akawa na uwezo wa
kukutoleeni mambo [Mu’jizat] ambayo nyinyi mnamtaka akutoleeni’. (Matalib
‘Aliyyah, Mawlana Shibli Nu’mani)
Miujiza hua na sifa zifuatazo:
1. Hutokana kwa Allah Subhanah wa Ta’ala.
2. Huvunja Sharia’h za kawaida za kimaumbile katika kutokea kwake.
3. Hua na hali isioweza kuelezeka.
4. Hupitia kwa Mtume husika ili kuthibitisha Utume huo.
5. Hua inayoendana na madai yanayodaiwa.
6. Hua haipingani na madai yanayodaiwa.
7. Hua haizidishi wala haipunguzi kiasi cha madai husika.
A’llamah ‘Abd Al Rahman Ibn Khaldun anasema kuhusiana na Miujiza kua, ‘Miongoni
mwa alama za Mitume ni kufanya Miujiza ambayo huthibitisha ukweli wao.
Miujiza hua ni vitendo ambavyo mithili yake hua kamwe haiwezekani kufanywa na
Bani Adam. Na ndio maana ikaitwa Miujiza (Mu’jizat). Kwani hua haimo ndani ya
uwezo wa Bani Adam bali imo nje ya uwezo wao. Kuna utofauti wa mitazamo
kuhusiana na namna gani inavyotokea na namna gani huthibitisha ukweli wa
Mitume. Wachunguzi wa mitizamo ya kidini (Mutakallimun) wamesimamia katika
misingi ya Imani ya kua, Miujiza hua ni mambo ambayo hutokea kwa kutaka, na
hivyo husema kua Miujiza hutokea kutokana na uwezo wa Allah Subhanah wa
Ta’ala, na si kupitia katika vitendo vya Mitume wake. Mu’tazila wao wana mtizamo
wa kua vitendo vyote vya Bani Adam hutokana na Bani Adam mwenyewe, lakini
hata hivyo Miujiza hua haimo katika aina hizo za vitendo vinavyofanywa na watu.
Kulingana na Skuli za Madhhab yote, nafasi ya Mitume katika kufanya Miujiza hua
ndani ya mipaka ya ‘Changamoto zinazoendelea’ (Tahaddi) ambayo yeye huitoa
kutokana na amri ya Allah. Yaani Mtume hutumia Miujiza kabla ya kutokea
kwake, kama kithibitisho cha ukweli wa madai yake. Hivyo wao hua wanachukua
nafasi ya maelezo ya wazi kutoka kwa Allah kudhihirisha kua Mtume fulani ni wa
Kweli’.(Al Muqaddimah)
Ingawa Qurán haikuwataja Mitume wote lakini imetaja na kuhadithia visa na Hadith za
baadhi ya Mitume, ambao idadi yao ni 25 tu, na imefanya hivyo kwa sababu ndani ya
140
visa na Hadith hizo kuna mafunzo na mifano bora ya kuigwa katika uhai wa kila Bani
Adam, kama vile vile anavyosema mwenyewe Allah Subhanah wa Taála:
﴿وَكُلاًّ ن َّقُص ُّ عَلَيْكَ مِنْ أَنْبَاءِ ٱلر ُّسُ ِل مَا نُثَبِّتُ بِهِ فُؤَادَكَ وَجَآءََك
وَمَوْعِظَةٌ وَذِكْرَىٰ لِلْمُؤْمِنِ َين ﴾
ِفى هَٰذِهِٱ لحَْ ُّق
Wakullan naqussu AAalayka min anba-i alrrusuli ma nuthabbitu bihi fu-adaka
wajaaka fee hadhihi alhaqqu wamawAAidhatun wadhikra lilmu/mineena (Surat
Hud 11:120)
Tafsir: Na vyote tunavyokuhadithia kuhusiana na habari za Mitume ni kwa ajili ya
kuupa nguvu moyo wako kutokana navyo. Na ndani yake hii (Qurán) umekujia ukweli
na pia mawaidha na ukumbusho kwa walioamini.
Sababu nyengine za kutajwa kwa visa vya Mitume na Manabii hao 25 ndani ya Qurán
hua ni pamoja na kuudhibitishia ukweli wa utukufu wa Utume na kazi ya aliyeshushiwa
Qurán hiyo ambae ni Mtume wa Mwisho Muhammad Rasul Allah Salallahu A’layhi wa
Salam, kuthaminisha thamani ya Ummah wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam dhidi ya Úmma za watu wa Manabii na Mitume waliotangulia, kuzihuisha njia za
Maisha ya Mitume na Manabii hao walizokua wakipita ili ziendelee kuwepo, kufahamika
na kufuatwa kwa milele.
Tunapoiangalia Qurán basi tunaona kua imewataja Mitume mbali mbali na tofauti
kulingana na mazingira yao waliyokabiliana na mitihani mbali mbali. Kwa mfano
tunapoiangalia Surat Al An Aam basi tunaona kua imetaja Mitume ambao
imewatafautisha kwa kua na sifa zifuatazo:
Nabii Nuh Alayhi Salatu wa Salam basi yeye ametajwa kua ni Nabii na Mtume wa
mwanzo kupingana na Jamii ya watu wanaoabudu Masanamu.
Nabii Is-haq na Nabii Yaqub Alayhim Salatu Salam basi wao wametajwa kua ndio
waanzilishi wa watu wa Bani Israil.
Nabii Daud na Nabii Sulayman Alayhim Salam wote wawili wametajwa kwa
kutofautishwa na Mitume wengine kwa kua na sifa ya Utume, Mali na Utawala wa
Mamlaka ya Kifalme.
141
Nabii Ayub na Nabii Yusuf Alayhim Salam wametajwa kwa kutofautishwa kwa
kujaribiwa kwa Mitihani na Ustahmilivu wao.
Nabii Musa na Nabii Harun Alayhim Salam wao wametajwa kwa kutofautishwa
kwa kua na uwezo na nguvu za kudhoofisha nguvu za Utawala wenye Nguvu kubwa
sana Kimamlaka.
Nabii Zakariyah, Nabii Yaqub, Nabii Isa Ibn Maryam na Nabii Ilyas Alayhim Salam
basi wao wametajwa kwa kutofautishwa kwa kua ni mfano wa kuigwa katika Ucha
Mungu, Ilm yao ya Kiroho na Kujitolea Muhanga.
Na vile vile tunapoangalia kwa upande wa Shaykh Al Akbar Imam Muhammad Ibn Ali
Ibn Muhammad Abu Bakr Muhyi Al Din Ibn Al Arabi Al Hatimi Al Ta’i Al Andalusi Al
Mursi Al Dimashqi ambae yeye ni mtaalamu wa I’lm Tasawwuf basi tunaona kua yeye
amewataja Mitume, Manabii na watu wengine Watukufu waliotajwa katika Qurán na
Hadith na kuwaainisha kulingana na aina za Hikma za ujumbe wa Allah Subhanah wa
Ta’ala zinazopatikana katika kuhadithiwa habari zao na hivyo tunaona kua:-
1. NABII ADAM – HIKMAH ILAHIYYAH – Hikma ya Uungu.
2. SHITH – HIKMAH NAFTHIYYAH – Hikma ya Matarajio.
3. NABII IDRIS – HIKMAH QUDUSIYYAH– Hikma ya Utukufu.
4. NABII NUH – HIKMAH SUBUHIYYAH – Hikma ya Kupandisha Darja.
5. NABII SALIH – HIKMAH FATIHIYYAH – Hikma ya Ufunguzi wa Kila Jambo.
6. NABII HUD - HIKMAN AHADIYYAH – Hikma ya Umoja wa kutokua na
Mshirika
7. NABII IBRAHIM – HIKMAH MUHAYMIYYAH – Hikma ya Upendo.
8. NABII LUT – HIKMAH MALIKIYYA – Hikma ya Uwezo wa Kiutawala.
9. NABII ISMAIL – HIKMAH ALIYYAH – Hikma ya Kujisalimisha.
10. NABII IS-HAQ – HIKMAH HAQQIYAH – Hikma ya Ukweli.
11. NABII YAQUB – HIKMAH RUHIYYAH – Hikma ya Kiroho.
12. NABII YUSUF – HIKMAH NURIYYAH – Hikma ya Nuru.
13. NABII SHUAYB – HIKMAH QALBIYAH – Hikma ya Kimoyo.
14. NABII UZAYR - HIKMAH QADARIYYAH – Hikma ya Makadirio.
15. NABII DAUD – HIKMAH WUJUDIYAH – Hikma ya Kua Hai.
16. NABII SULAYMAN – HIKMAH RAHMANIYYAH – Hikma ya Rehma.
17. NABII YUNUS – HIKMAH NAFASIYYAH – Hikma ya Sehem ya Kuvuta Hewa.
18. NABII AYYUB – HIKMAH GHAYBIYYAH – Hikma ya Ghayb.
19. NABII ILYAS – HIKMAH INASIYYAH – Hikmah ya Ukaribu
20. NABII MUSA – HIKMAH ULUWIYYAH – Hikma ya Mafanikio.
21. NABII HARUN – HIKMAH IMAMIYYAH – Hikma ya Uongozi
22. LUQMAN AL HAKIM – HIKMAH IHSANIYYAH – Hikma ya Tabia Njema.
142
23. NABII ZAKARIYYAH – HIKMAH MALIKIYYAH – Hikma ya Mamlaka.
24. NABII YAHYA – HIKMAH JALALIYYAH – Hikma ya Sifa Njema.
25. NABII ISA – HIKMAH NUBUWIYYAH – Hikma ya Unabii.
26. KHALID IBN SINAN – HIKMAH AS SAMADIYYAH – Hikma ya Kila kitu
kurudi Kwake.
27. NABII MUHAMMAD SALALLAHU ALAYHI WA SALAM – HIKMAH
FARDIYAH – Hikma ya Umoja wa Upekee
Ambapo anasema Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
﴿وَمَآ أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن ر َّسُولٍ إِلا َّ نُوحِ ي ۤ إِلَيْهِ أَن َّهُ لا ۤ إِلَٰهَ إِلا َّ أََْ فَٱعْبُدُونِ ﴾
Wama arsalna min qablika min rasoolin illa noohee ilayhi annahu la ilaha illa ana
faoAAbudooni (Surat Al Anbiyah 21:25)
Tafsir: Na sisi hatukutuma kabla yako (Ewe Muhammad) Mitume isipokua
tuliwashushia ujumbe kua Hakuna anaestahiki kuabudiwa ila mimi hivyo Niabuduni.
Kwa upande wa Imam Baddiuzzamman Said Nursi basi yeye anasema kua miongoni
mwa sababu ambazo zinamepelekea kuwepo kwa takriri au kurudiwa kwa Visa Vya
Manabii na Mitume katika sura tofauti za Quran hua kunatokana na kuonesha Miujiza
yake Allah Subhanah wa Ta’ala ambayo ni yenye malengo makuu yafuatayo:
1-Kuelezea sehemu za visa ambazo zimetajwa katika sehemu nyengine maalumu
kulingana na mazingira maalum, na hivyo ingawa hiii hua si Takriri lakini
huonekana kua kama ni Takriri kwa sababu ya mazingira ya muonekano wake.
2-Kuweka wazi ufasaha na uwazi wa aya za Qur’an, kwani katika baadhi ya sehemu
kisa husika hua kimetajwa kwenye sura husika kwa aya chache lakini katika baadhi
ya sura kimetajwa kwa kina na kwa aya nyingi.
3-Kuweka wazi uthibitisho wa Utume wa Rasul Allah Sallahu A’layhi wa Salam,
kubainisha kuwepo kwake Mungu mmoja tu ambae ni Allah Subhanah wa Ta’ala,
kutoa mafunzo ya kua Allah Subhanah wa Ta’ala ana uwezo juu ya kila kitu
ikiwemo kuwaadhibu wanaomuasi, kuwaonya wasiomuamini kwa kuwawekea wazi
yaliyowafika wale waliotangulia kabla yao. Kiasi ya kua kila Takrir iliyotumka basi
hua imetumika kwa ajili mazingira husika na katika wakati husika ili kufikisha
ujumbe husika.
143
4-Kumliwaza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na pia kuwaliwaza Waislam
ambao walikua wanakumbana na matatizo na mitihani mingi sana katika kipindi
hiki cha mwanzoni mwa Uislam, kwa mfano tunapoangalia kisa cha Nabii Musa na
Nabii Ibrahim basi tunaona kua vilikua vinarudiwa kwa sababu ya kuwaonesha
Waislam waliokua kwenye mitihani dhidi ya Makafiri kua lazima mwanzoni
wanaowaamini Mitume hao hua wanapata misukosuko lakini baadae hua kuna
uongofu na uokovu kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala.
Na pia kwa upande mwengine tunapoangalia mifano ya kuangamizwa kwa jamii za
Watu wa Nabii Lut na Fir’awn kutokana na Uasi wao basi hua kunaonesha kua
haina haja na wala haitakiwi kwa Ibn Adam kua ni wenye kufanya dhambi dhidi
ya viumbe wenzao, dhidi ya Mola wao na hawatakiwi kumuuasi Mola wao.
5-Kuwapa Moyo Waumini kujidhibiti dhidi ya adui wao mkubwa ambae ni Shaytan
na dhidi ya Uadui wa Nafsi zao, na kuwawekea wazi malipo watakayoyapata pale
watakapofanikiwa kujidhibiti na maadui zao hao, na hapo hapo kuwavunja Moyo
wasiwe ni wenye kudumu katika dhambi.
6-Kuwafundisha Waumini Dua na namna ya kumkumbuka Mola wao, kufuata
Maamrisho yake, kumpwekesha na kuwasisitizia kua wao ni viumbe na watumwa
wa Allah Subhanah wa Ta’ala. Na hivyo kuwaonesha Malengo na Makusudio ya
kuumbwa kwao na kuumbwa kwa Ulimwengu wanaoishi ndani yake ambao nao
una kila kitu wanachokihitaji katika maisha yao hapa Ulimwenguni.
7-Kuwaponya watu wa kila aina kuanzia wenye ufahamu wa hali ya juu na wenye
ufaham mdogo, wenye Taqwa na waliopotoka, wenye kuikimbilia Akhera yao na
wenye kuikumbatia Dunia yao.
Lakini hata hivyo si kila mtu hua ni mwenye bahati ya kusioma Qur’an yote,
ambayo ni ponyo na ni dawa kwa kila mtu. Kwa hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala
aambae ndie mwenye kuweka Lulu, Hikma na Busara katika kila kitu akifanyacho
ndani yake, na ndie ambae mwingi wa Rehma na Huruma kwa waja wake basi
akaamua kuweka ndani yake Sura ambazo ni zenye kubeba malengo makuu ya
Qur’an. Kiasi ya kua kila sura imekua kama ni Qur’an ndogo na hivyo kua ni zenye
kumrahisishia kila mtu kunufaika nayo, ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala
akasema katika Qur’an
﴿وَلَقَدْ يَس َّرَْ ٱلْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن م ُّد َّكِرٍ ﴾
144
Walaqad yassarna alqur-ana lildhdhikri fahal min muddakirin (Surat Al Qamar
54:17)
Tafsir: Na kwa Hakika (kutokana na kuishusha katika Lugha ya Ibn Adam)
Tumeifanya Qur’an iwe ni rahisi kwa ukumbusho. Lakini jee ni nani mwenye
kuufuata ukumbusho huo?
8-Imeelezewa katika hadithi na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: Kila
aya ina kina cha maana kuna Muhkamat na Mutashabihat, yaani maana iliyowazi
na maana ya ndani ambayo inaweza kufahamika na wenye kujua tu. Hii hua ni
kama kina cha mzunguko wa kimaana, na kila kina cha mzunguko wa kimaana
umegawika sehemu nne kimaelezo, kialama, kimatawi na kiainisho. Kwa mtizamo
mwengine basi kila aya ya Qur’an ina matabaka ya kimaana, na mambo mengi
ndani yake, ikiwemo Hukmu, Manufaa na ainisho kwa malengo maalum. Hivyo
kutokana na sababu hio basi ndio maana kisa kimezungumziwa katika sehemu
moja na kisha kikazungumziwa katika seheu nyengine, ambapo katika sura moja
kimeelezewa kwa sababu fulani na katika sura nyengine kwa sababu tofauti.
Kutokana na hali hii basi hua hakuna takrir katika Qur’an, yaani hii ni kama vile
yalivyofanana macho na masikio ya watu, lakini ukweli ni kua yote yapo tofauti.
9-Kama ilivyokua mwili wa Ibn Adam unavyohitaji mahitaji tofauti ambapo baadhi
ya mahitaji hayo hua yanahitajiika kila mara kama uvutaji wa hewa kwa mfano,
na baadhi ya mahitaji huhitajika baada ya mda fulani kama kula, kunywa maji n.k
na baadhi hua ni yenye kuhitajika kila baada ya wiki, mwezi au mwaka mara moja
kama vile matumizi ya dawa. Na hivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa mahitaji ya kiroho
kwa upande wa Ibn Adam kila mmoja hua na njia zake za kufanya Dhikr Allah,
kuna kila wakati wasema wasemao Allah! Allah, kuna wasemao Biismi Allahi kuna
wasemao La Illah Ila Allah kila baada ya saa n.k kutokana na kuwepo kwa hali hii
basi Qur’an pia imekua na takrir ndani yake kwa kutokana na kuhitajika kwake
na umuhimu wake.
Kulingana makusudio hayo na mengineyo mengi ambayo hatukuyataja basi
tunaona kua ingawa ndani ya Qur’an kuna takrir za mara kadhaa lakini hata hivyo
kujirudia huko basi kamwe hakukua ni kwenye kusababisha kukosekana kwa
mvuto wa Qur’an kama vile ambavyo yaliyo maneno au mazungumzo ya Watu,
lakini kwa upande wa Qur’an hali imekua ni kinyume chake, kwani kila ukiisoma
basi ndio hamu yya kuizoma zaidi ndivyo inavyozidi kukua na kuongezeka, vile vile
Qur’an ni Nuru ya kila Muumini katika kila wakati wa maisha yake yote hapa
Ulimwenguni na imekua hivyo kwa karne na karne, na imekua ikisomwa tena na
tena katika sala zao, na imerahisishwa kwa watoto kuihifadhi, Qur’an ni tamu kama
145
maji ya Zam Zam kwa mtu alie katika wakati wa kukata roho. Na haya yote
yanaonesha miujiza ya Qur’an iliyopo katika kila hali.
Baada ya kuangalia takrir katika Qur’an ambazo zimetumika katika kuelezea visa vya
Mitume tofauti ambapo ingawa Mitume na Manabii wote wanatoka kwa Allah Subhanah
wa Ta’ala kwa ajili ya kuja kueneza ujumbe wake Muumba na kuwaongoza watu katika
njia iliyosahih, na hivyo kukumbana na mitihani mingi sana kutoka kwa watu
wanaowausia juu ya ujumbe huo lakini baadhi miongoni mwao walikua na sifa ya darja
ya juu zaidi kuliko wengine na hii ni kulingana na mitihani waliyoipata na namna
walivyokabiliana na mitihani hio, na hivyo basi kutoka na kua na sifa hizo basi Mitume
hawa walikua wakijulikana kama Ulu al A’zmi mina al Rusul.
146
SURA YA PILI
عيسى ابن
االله روحي مريم
147
HISTORIA YA MZEE IMRAN BABU YAKE NABII ISA IBN MARYAM
BINT IMRAN
Tunapozungumzia Kisa cha Nabii Isa Ibn Maryam Alayhi Salam, basi hua hatuwezi
kukikamilisha kisa hicho bila ya kugusia ndani yake kisa cha Mzee Imran, Maryam Bint
Imran, Nabii Zakarriyah na Nabii Yahya na hivyo moja kwa moja tunatua katika aya za
mwanzoni zilizozungumzia kisa cha Mzee Imran katika Surat ya tatu iliyomo ndani ya
Qur’an ambayo imetumia jina lake Mzee Imran ambayo ni Surat Al Imran.
Ambao neno Al Imran ni lenye kutokana na neno Amara ambalo hua linamaanisha Kuishi
Ndani yake, Kutengeneza kitu kilichoharibika, Kujenga, Kufanya ziara Takatifu na pia
humaanisha Kujaza watu au Wakaazi katika sehemu fulani ya Ardhi.
Neno Amara ndio ia lililotoa neno Umrun ambalo hua linamaanisha Umri, Kuishi kwa
Mda mrefu, au Utu Uzima, na likatoa neno Umrah yaani Ibada ya Hija Ndogo na pia
likatoa neno Maamur ambalo hua inamaanisha Sehemu inayotembelewa na viumbe
wengi mara kwa mara.
Neno Amara ndio pia lililotoa jina la Imran ambalo ni moja kati ya Majina ya watu
Wawili watukufu waliotajwa ndani yake Qur’an yaani Mzee Imran ambae ni Baba yake
Nabii Musa alieishi miaka 1400 kabla ya kuzaliwa Mzee Imran wa pili ambae ni Baba
yake Bi Maryam Bint Imran ambae ndie Mama yake Nabii Isa Ibn Maryam Bint Imran
na hivyo Mzee Imran huyu kua ni Babu yake Nabii Isa.
Ambapo kwa mara ya kwanza Mzee Imran Babu yake Nabii Isa ambae alikua ni Mkuu
wa Makuhani wa Jerusalem alitajwa katika Qur’an pale Allah Subhanah wa Ta’ala
aliposema:
﴿إِن َّ ٱهلل ََّ ٱصْطَفَى ٰ آدَمَ وَنُوحاً وَآلَ إِبْرَاهِيمَ وَآلَ عِمْرَانَ عَلَى ٱلْعَالَمِينَ۞ ذُ رِّي َّةً
بَعْضُهَا مِنْ بَعْضٍ وَٱهلل َُّ سمَِيعٌ عَلِيمٌ ۞ إِذْ قَالَتِ ٱمْرَأَةُ عِمْرَانَ رَبِّ إِنىّ ِ نَذَرْتُ
لَكَ مَا فىِ بَطْنىِ محَُر َّراً فَتَقَب َّلْ مِنىِّ إِن َّكَ أَنتَ ٱلس َّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ ﴾
Inna Allaha istafa adama wanoohan waala ibraheema waala AAimrana AAala
alAAalameena; Dhurriyyatan baAAdhuha min baAAdhin waAllahu sameeAAun
148
AAaleemun; Idh qalati imraatu AAimrana rabbi innee nadhartu laka ma fee batnee
muharraran fataqabbal minnee innaka anta alssameeAAu alAAaleemu (Surat Al
Imran 3:33-35)
Tafsir: Hakika Allah amempandisha (Darja) Adam na Nuh na Ibrahim na Imran juu
zaidi ya Walimwengu wengine, Vizazi vya baadhi miongoni mwa baadhi yao, Na
kumbuka aliposema Mke wa Imran: ‘Ewe Mola Wangu, hakika mimi nimeweka
Nadhiri kua Mtoto wangu aliemo tumboni mwangu nimemtolea kwa ajili ya
kukutumikia wewe, hivyo nikubalie kwani kwa hakika wewe ni mwingi wa kusikia na
ni mwingi wa kujua juu ya kila kitu.’
Anasema Imam Muhammad Ibn Is-haq kua: ‘Imraat ul Imran alikua akijulikana kwa
jina la Hannah Bint Faqudh, na Imran mwenyewe alikua ni chifu wa watu wa Bani
Israil na akijulikana kwa jina la Imran Ibn Sahim Ibn Amur Ibn Mishan Ibn Hizqil
Ibn Ahraf Ibn Buam Ibn Azaziyah Ibn Amasiyah Ibn Nawus Ibn Nutha Ibn Barid
Ibn Yahushafat Ibn Radim Ibn Ababa Ibn RajiAm Ibn Sulayman Ibn Daud Alayhi
Salatu wa Salam.
Ambapo Nabii Zakariyah na Mzee Imran walikua ni watu wawili waliowaoa
Mabinti wawili wa kike wa Mzee Faqudh ambao ni Hannah Bint Faqudh na Isha
Bint Faqudh. Hivyo Nabii Zakariyah alimuoa Isha Bint Faqudh ambae ndie mama
yake Nabii Yahya na Mzee Imran alimuoa Hanah Bint Faqudh ambae ndie Mama
yake Maryam Bint Imran.’
Ambapo Hannah hakuwa na uwezo wa kupata Mtoto hadi pale alipokua Mtu mzima na
kufikia hali ya kutokua na matumaini ya kupata hata ujauzito, na kama zinavyosema aya
kua familia yao ilikua ni yenye kupandishwa Darja maalum na Allah Subhana wa Ta’ala,
ambapo siku moja wakati Hannah alipokua amekaa chini ya Mti basi alimuona ndege
kiwa anamlisha kinda wake chakula, na tukio hili likamtia simanzi kwani akakumbuka
kama hata ndege wanakua na watoto wao, basi inakuaje yeye hadi anafikia umri huo na
mumewe Imran hajajaaliwa kupata mtoto?
Lakini anasema Imam Abd Rahman Muhammad Ibn Al Husayn Ibn Muhammad Ibn
Musa Ibn Khalid Ibn Salim Ibn Rahawiyah Al Sulami Al Nishapuri Al Shafii kua: ‘Yule
ambae hana Subra juu ya kile alichojaaliwa na Mola wake juu yake, basi hatokua
na Subra juu ya kupata Uongofu kutoka kwa Mola wake.’ Hivyo bila ya shaka kwa
Upande wa Mzee Imran na Bi Hanah Bint Faqudh hawakua ni wenye kuvunjika Moyo
na majaaliwa ya Mola wao juu yao.
Na hivyo Hannah Bint Faqudh akasema baada ya tukio la kumuona ndege huyo maneno
yafuatayo: ‘Ya Allah. Hakika mimi naweka Nadhiri kwako kua kama utanijaalia
kua ni mwenye kupata Mtoto wa kiume, basi nitamtoa Mtoto huyo kwa ajili yako,
149
na hivyo atakua ni mwenye kujitolea kufanya huduma za kuyatumikia Madhabahu
yako, kama sehemu ya kuonesha shukurani zangu juu yako.’
Hivyo baada ya kuweka Nadhiri hio basi Allah Subhanah wa Ta’ala akamjaalia Mzee
Imran na Hannah Bint Faqudh kua ni wenye kupata mtoto, lakini bila ya kujua kua mtoto
huyo ni alikua ni Mwanamke, na wo walitaka Mtoto wa Kiume kwa sababu katika kipindi
hicho ilikua ni kawaid wa Wacha Mungu kuwateu watoto wao wa kiume wanapozaliwa
kua ni kwa ajili ya kumtumikia Mola wao kwa kuhudumia Madhabahuni ambayo ni
sehemu ya kutolea Kafara iliyopo ndani ya Majumba ya Ibada ya watu wa Bani Israil.
Hivyo watoto hao wa kiume hua wanakaa ndani ya Majumba hayo na kuhudumia Usafi
na usimamizi wa ndani ya Majengo hayo hadi pale watakapofikia umri wa miaka 15, na
kisha baada ya hapo hua ni wenye kua na hiari ya aidha kubakia ndani ya majengo hayo
na kua Watawa au kutoka nje na kuenda kuishi maisha yao ya kawaida, na jukumu hili
lilikua ni kwa ajili ya watoto wa kiume tu, halikuweza kua ni jukumu la watoto wa kike
kwa sababu ya maumbile yao Wanawake na sharia zao wafuasi wa Dini ya Kiyahudi kwa
wakati huo na mpaka hii leo kutokana na kua Wanawake hua ni wenye Maumbile ya
kutokwa na Damu ya Hedhi kwa kila mwezi na pia kutokwa na Damu ya Nifasi baada ya
kujifungua na kupata Mtoto.
UHARAMU NA UTUKUFU WA DAMU KATIKA UISLAM.
Tunapozungumzia kuhusiana na Damu basi hua tunazungumzia kitu ambacho ni kitukufu
katika Dini ya Kikristo, Kiyahudi, Kikristo, Kipagani n.k ambacho hua kinawakilisha
Roho au Uhai wa Kiumbe. Kwani Damu ndio kiungo pekee muhimu kilichomo ndani ya
Mwili wa Kiumbe ambacho kinajumuisha Mfumo mzima unaojitegemea ambao upo
katika maumbile ya mtiririko wenye wingi wa lita 5 kwa upande wa Ibn Adam.
Mfumo wa Damu hua ni wenye kufanya kazi ya kuisaidia mifumo myengine muhimu ya
ufanyaji kazi ya ndani ya mwili katika kusimamia utekelezaji wa majukumu yake mbali
mbali ndani yake, hivyo bila ya kua na Damu basi kiumbe husika hua hana uwezo wa
Kuishi Ulimwenguni. Kwa sababu Damu hua inategemewa na takriban na kila mfumo
wa mwili wa kiumbe husika ndani ya mwili ikiwemo mfumo wa chakula ambao ni wenye
kusafirisha, kuchuja, kutawanya na kuhifadhi vitu muhimu vinavyohitajika na mwili
vilivyomo ndani ya chakula husika na kisha kukitoa nje ya mwili kila kile kisichohitajika
ndani ya mwili husika.
150
Damu husaidia pia mfumo wa kusafirisha na kuisambaza Hewa safi inayoingia ndani ya
mwili kuanzia kwenye mapafu ambapo huinyonya na kisha kuisambaza katika kila
kiungo kinachohitajika ndani ya mwili, wakati ikiwa katika hli ya usafi na kisha huitoa
nje ya mwili hewa chafu, kwani ikibakia ndani yake basi hua ni yenye kusababisha
madhara katika mwili wa mtu husika.
Damu hua ndio kiungo ambacho mfumo wake hua na kazi ya kusafirisha na kuzalisha
kemikali (hormones) mbali mbali za hisia, ulinzi na ukuaji wa mwili wa Kiumbe na pia
husafirisha vitamins, glucose, aminoacids, madini mbalimbali virutubisho vyenginevyo,
na kisha hapo hapo Mfumo wa Damu hua ndio unaosimamia kutoa nje ya mwili kila kitu
kisichohitajika ndani ya mwili baada ya kuchujwa kwake.
Na pia Damu hua ndio inayosimamia mfumo wa kudhibiti hali ya joto ndani ya Mwili
kulingana na hali ya mabadiliko ya mazingira husika yaliyopo nje ya mwili wa kiumbe
husika, na pia kulingana na mabadiliko ya hali ya kimaumbile ya ndani ya mwili husika.
Kwani mwili unapokua umezidiwa na joto basi Mfumo wa Damu huifanya mishipa ya
Damu kua ni yenye kutanuka na kupanda juu karibu na ngozi na kuifanya sehemu ya juu
ya mwili yaani ngozi kua ni yenye kuachia na kutoa nje Joto la ndani ya mwili.
Na inapokua mwili umepungukiwa na joto na kuhisi baridi basi Mfumo wa Damu
huifanya mishipa ya Damu kua ni yenye kubana na kuingia ndani zaidi na hapo huanza
kutokea vipele pele vidogo dogo vingi kwenye ngozi huku nywele za ngozi hua ni zenye
kusimama, ambapo tukio hili hua ni lenye kuifanya misuli ya ndani ya mwili kua ni yenye
kubana na kutetemeka na kuufanya mwili kua ni wenye kuzalisha joto zaidi na huku
mishipa hio ya Damu iliyobana na kuzama zaidi hua ni yenye kuhifadhi joto lisitoke nje
ya mwili na hivyo lisipungue ndani ya mwili.
Ambapo kwa upande mwengine basi Mfumo wa Damu ndio unaozalisha Mfumo wa
Kinga ya mwili dhidi ya maradhi ya ndani ya mwili na nje ya mwili, na hili linaonekana
wazi pale mtu anapokua anaumwa basi joto la mwili hupanda kutokana na kua Mfumo
wa Damu hua ni wenye kuongeza ufanyaji kazi wake na hivyo hua ni wenye kuzalisha
zaidi Seli nyeupe za Damu ambazo hua zinajulikana kama Leukocytes kwa ajili ya
kuulinda mwili na kupigana na kila kinachoonekana kua ni chenye kutaka kusababisha
madhara kwa mwili.
Ambapo kwa upande wa nje ya mwili unapopata jeraha, kisha kuanza kutokwa na Damu
basi mfumo wa Damu pia hua ni wenye kushirikiana na Protein ili kusimamia uzuiaji wa
utokaji wa Damu hio ili isipotee kwa kuigandisha na kuikausha sehemu ya juu ya nje ya
mwili iliyojeruhiwa.
151
Kutokana na umuhimu huo basi wa Damu kwa mwili wa Kiumbe kua ni sawa na Uhai
wa kiumbe husika ambao hua unaanzia kutokana nayo kama alivyoelezea mwenyewe
Muumba kwenye Qur’an pale aliposema:
﴿خَلَقَ ٱلإِنسَانَ مِنْ عَلَقٍ ﴾
Khalaqa al-insana min AAalaqin(Surat Al Aala 96:2)
Tafsir: Aliemuumba Mtu kutokana na Aa’alaqin.
Ambapo neno Aa’alaqin linatokana na neno Aliqa ambalo hua linamaanisha, Kushikama,
Kunata, Kuganda. Kung’ang’ania na pia hua linamaanisha Kitu chenye Thamani na
hivyo kisichotakikana Kuachiwa au Kuachika.
Hivyo neno Aa’alaqin hua linamaanisha Maumbile ya kitu kilichoshikamana kama
Damu, Manii ya Mwanamme au Mayai ya Uzazi wa Mwanamke na pia humaanisha
Mshikamano wa Kimapenzi. Na ndio maana Wanazuoni wakalitafsiri neno A’alaqin kua
ni Mshikamano wa pande au tone la Damu, na hii ni kwa sababu Aa’alaqin kua ni Kitu
ambacho kinategemea Uhai wake kutokana na kushikama na Damu na Kuinyonya Damu
ambayo hua ni Chakula chake.
Kwani pia hata mwanzoni mwa Uhai wa Ibn Adam baada ya kukutana kwa Mayai ya
Uzazi ya Baba na Mama na kushikamana, basi mshikamano huo wakati ukiwa ndani ya
Fuko la Uzazi la Mama huanza kukua na katika hali ya maumbile ya kama kipande cha
Damu ambacho nacho hua kinakua kutokana na kutegemea Damu ya Mama kwa
kushikamana na sehemu ya Fuko la Uzazi la Mama.
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anazielezea hatua zaidi za maumbile hayo ndani ya
Qur’an kwa kutuambia kua:
﴿وَلَقَدْ خَلَقْنَا ٱلإِنْسَانَ مِ ن سُلاَلَةٍ مِّن طِينٍ ۞ ثمُ َّ جَعَلْنَاهُ نُطْفَةً فىِ قَرَارٍ
ِعظَاماً
م َّكِينٍ۞ثمُ َّ خَلَقْنَا ٱلن ُّطْفَةَ عَلَقَةً فَخَلَقْنَا ٱلْعَلَقَةَ مُضْغَةً فَخَلَقْنَا ٱلْمُضْغَةَ
فَكَسَوَْ ٱلْعِظَامَ لحَْماً ثمُ َّ أَنشَأَْهُ خَلْقاً آخَرَ فَتَبَارَكَ ٱهلل َُّ أَحْ سَنُ ٱلخَْالِقِينَ ﴾
Walaqad khalaqna al-insana min sulalatin min teenin; Thumma jaAAalnahu
nutfatan fee qararin makeenin; Thumma khalaqna alnnutfata AAalaqatan
fakhalaqna alAAalaqata Mudghatan fakhalaqna almudghata AAidhaman
152
fakasawna alAAidhama lahman thumma ansha/nahu khalqan akhara fatabaraka
Allahu ahsanu alkhaliqeena (Surat Al Muuminun 23:12-14)
Tafsir: Na kwa hakika tumemuumba Mtu kutokana na Udongo wa Mfinyanzi, Kisha
tukamjaalia kua katika Nutfah (Mchanganyiko wa maji ya uzazi ya Mwanamme na
Mwanamke) na tukayahifadhi ndani Hifadhio Maalum (Fuko la Uzazi la Mama). Na
kisha tukaumba kutokana na Nutfatan katika Aa’alaqatin (Pande la Damu) na kisha
tukalifanya pande la Damu kua ni pande laini laini la Nyama, na tukafanya kutokana
na pande laini laini la Nyama kuwepo na Mifupa laini, na kisha tukaivisha Mifupa
kwa Nyama na kisha tukaumba kutokana nayo kua kiumbeca mwisho(Ibn Adam).
Hivyo Utukufu ni wa Allah tu ambae ndie mbora wa Kuumba.
Na baada ya kutuwekea wazi maumbile hayo basi katika sehemu nyengine Allah
Subhanah wa Ta’ala anahoji na kufafanua tena kua:
﴿بِ سْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ ۞ هَلْ أَتَى ٰ عَلَى ٱلإِنسَانِ حِ ينٌ مِّنَ ٱلد َّهْرِ لمَْ يَ كُن شَيْئاً
م َّذْكُوراً ۞ إِ َّ خَلَقْنَا ٱلإِنسَانَ مِن ن ُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ ن َّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَاهُ سمَِيعاً بَ صِ يراً ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Hal ata AAala al-insani heenun mina alddahri
lam yakun shay-an madhkooran; Inna khalaqna al-insana min nutfatin amshajin
nabtaleehi fajaAAalnahu sameeAAan baseeran; (Surat Al Insan 76:1-3)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma na Mwingi wa Huruma;Hivi Jee hakua
Mtu katika kipindi wakati akiwa si kitu chochote kinachoweza kuzunguzmiwa?Kwani
kwa hakika tumemuumba Mtu kutokana na Nutfah kwa ajili ya kumjaribu na hivyo
tukamfanya kua ni mwenye kusikia na kuona.
Hivyo tunapoziangalia aya basi tunaona kua zinazungumzia kuhusiana na hatua za
maumbile ya Ibn Adam yaani Mtoto anaezaliwa na Mtu kua ni kuanzia kwenye Nutfah,
kisha Aa’alaqin na kisha Mudghah. Ambapo amesema Abd Allah Ibn Masud Radhi
Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Maumbile
ya Mkusanyiko wa kila mmoja wenu unakusanyika ndani ya Fuko la Uzazi wa
Mama yake ndani ya siku 40, na kisha hua Aalaqah kwa siku 40, na kisha hua
Mudghah kwa kwa siku 40. Na kisha Malaika hua anatumwa kwa ajili ya
kumuandikia mambo manne: Riziki yake, Uhai wake; Amali zake na Kama atakua
mwema au Muovu, nakisha hupuliziwa Roho yake’’(Bukhari na Muslim)
Na ndio maana akasema Mujaddid Ad Din Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid
Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali kua: ‘Hairuhusiki kuitoa
153
Mimba kwa sababu kuitoa Mimba hua ni sawa na Kuua, hususan Mimba hio
inapopita umri wa siku 120, kwani kufanya hivyo hua ni kuitoa Roho iliyokwisha
ingizwa ndani ya mwili wake na mwili wake hua ni wenye kujitegemea’
Kwani hatua ya kwanza ya Mtoto hua ni pale Manii yanapoingia Ndani ya Fuko la
Uzazi na kuchanganyika na Maji ya Uzazi ya Mama na hivyo hua tayari ni yenye
kujitayarisha kwa ajili ya Uhai, hivyo ni kusababishia madhara hua ni haram
ambapo dhambi za kuitoa Nutfah katika umri wa siku 40 hua ni ndogo kuliko
dhambi za kuitoa Aalaqah inapokua baina ya siku 40-80 ambazo hua ni ndogo
kuliko dhambi za kuitoa Mudgha ambazo hua ni baina ya umri wa siku 80-120.’
Na ndio maana pia Mwanamke Mjamzito anapofanya kosa linalostahiki kuadhibiwa
adhabu ya Kifo basi kwa sharia za Kiislam hua hahukumiwi hadi pale atakapojifungua
na kisha kua ni mwenye kumyonyesha Mtoto wake kwa muda wa kunyonyesha ambao
ni miaka miwili.
Kwani inapofikia umri wa siku 120 basi hua tayari ni Dhambi za Kudhulumu Nafsi ya
Mtu na hivyo Kutoa Mimba kwa kipindi hiki hua hakuruhusiki isipokua kwa sababu
inayokubalika Kisharia kwa mfano pale inapokua Mimba inahatarisha Afya na Uhai wa
Mama Mjamzito.
Ambapo kwa upande wa Al Muhaqqiq Imam Ibn Hajar Al Haytami basi yeye anasema
katika Tuhfah Al Muhtaj kua: ‘Ni haram kuitoa Mimba pale wakati ambapo Nutfah
imeshakua tayari imeshafanya Istiqrar (katika siku za 40 za mwanzo)’ na kwa
Upande wa Shaykh Ul Islami Imam Shams Ad Din Al Ramli basi yeye anasema katika
Nihayat Al Muhtaj kua: ‘Inaruhusika kuitoa pale inapokua haijafikia siku 120 yaani
kabla ya kupuliziwa Roho kwa Mimba hio.’ Ambao huu pia ndio mtizamo wa
Madhhab Imam Abu Hanifa
Ambapo kwa upande wa Imam Abu Qasim Ibn Juzay Al Qalbi Al Maliki basi yeye
anasema kua: ‘Pale inapokua Fuko la Uzazi limeshikamana na Manii basi hua
hairuhusiki kuingia baina yake na kukatisha muendeleo wake, na mbaya zaidi pale
inapokua tayari Mimba tayari imeshaanza kua pande la nyama, na mbaya zaidi
pale inapokua tayari imeshapuliziwa Roho yake kwani hii hua ni Kuua Nafsi
kulingana na Makubaliano ya Ijmaa.’ Na huu pia ndio Mtizamo wa Madhhab ya Imam
Ahmad Ibn Hanbal
Ambapo anasema Abu Hurayrah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wanawake wawili wa kabila
la Hudhayl walipigana, ambapo mmoja wapo akachukua Jiwe akampiga
mwenzake, na hivyo akamuuma Mtoto aliemo ndani ya Tumbo lake. Hivyo kesi hii
ikapelekwa mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi Alayhi wa Salam ambae akaamua
kua aliempiga mwenzake alipe Ghurra.’
154
Ambapo Ghura maana yake hua ni Malipo ya fidia yanayolipwa na Mtu ambae
amesababisha madhara kuharibika kwa Mimba ya Mtu. Ambapo Ghura hua inatakiwa
kulipwa ndani ya mwaka mmoja kwa wale waliodhurika kutokana na madhara hayo
wakati wakiwa ni wenye haki ya kurithi kutoka kwa Kiumbe kilichomo ndani ya Mimba
iliyoharibika, isipokua yule aliesababisha Madhara ya kutoka Mimba hio labda tuseme
Mama mwenyewe au Baba n.k basi hua hawezi kurithi na badala yake atalipa Ghura
ambayo hua ni malipo ya kutoa Ngamia watano ambayo hua ni sehemu moja kati ya 20
za Diya yaani fidya ya kumwaga damu bila ya kukusudia.
Kwani kwa upande wa Uislam ikawa hairuhusiki kuimwaga Damu ya Ibn Adam bila ya
sababu inayokubalika kisharia, kama vile ambavyo Allah Subhanah wa Ta’ala
alivyowaamrisha watu wa Bani Israil hapo kabla kwa kusema:
﴿مِنْ أَجْلِ ذٰلِكَ كَتَبْنَا عَلَى ٰ بَنيِ ۤ إِسْرَائِيلَ أَن َّهُ مَن قَتَلَ نَفْساً بِغَيرِْ نَفْسٍ أَوْ فَ سَادٍ
فىِ ٱلأَرْضِ فَكَأَنم ََّا قَتَلَ ٱلن َّاسَ جمَِيعاً وَمَنْ أَحْيَاهَا فَكَأَنم ََّا أَحْ يَا الن َّاسَ جمَِيعاً وَلَقَ ْد
جَآءَتْهُمْ رُسُلُنَا بِٱلّبَيِّنَاتِ ثمُ َّ إِن َّ كَثِيراً مِّنْهُمْ بَعْدَ ذٰلِكَ فىِ ٱلأَرْضِ لَمُسْرِفُونَ ﴾
Min ajli dhalika katabna AAala banee isra-eela annahu man qatala nafsan bighayri
nafsin aw fasadin fee al-ardhi fakaannama qatala alnnasa jameeAAan waman
ahyaha fakaannama ahya alnnasa jameeAAan walaqad jaat-hum rusuluna
bialbayyinati thumma inna katheeran minhum baAAda dhalika fee al-ardhi
lamusrifoona (Surat Al Maidah 5:32)
Tafsir: Kutokana na hilo basi tumewaamrisha watu wa Bani Israil kua kwa yeyote yule
atakaeiua Nafsi (ya Mtu) bila ya (sababu ya kuuliwa) Nafsi ya mtu mwengine, au
kufanya ufisadi Ardhini basi ni kama alieua Watu wote kwa pamoja. Na atakae
ihuisha Nafsi basi ni sawa na aliewahuisha watu wote kwa ujumla. Na kwa hakika
walikuja kwao wao Mitume wetu wakiwa na Vithibitisho vilivyo wazi, lakini wengi wao
baada yake waliendelea kufanya Israfu ardhini.
Na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akakataza pia kumwaga Damu ya Mtu aliemuamini
Allah Subhanah wa Ta’ala kama ilivyosema aya:
155
﴿وَمَن يَقْتُلْ مُؤْمِناً م ُّتَعَمِّداً فَجَزَآؤُهُ جَهَن َّمُ خَالِداً فِيهَا وَغَضِبَ ٱهلل َُّ عَلَيْهِ وَلَعَنَهُ
وَأَعَد َّ لَهُ عَذَاابً عَظِيماً ﴾
Waman yaqtul mu/minan mutaAAammidan fajazaohu jahannamu khalidan feeha
waghadhiba Allahu AAalayhi walaAAanahu waaAAadda lahu AAadhaban
AAadhiman (Surat Al Maidah 4:93)
Tafsir: Na yeyote yule atakaemuua Muumini kwa makusudi, basi malipo yake ni
Jahanama atakapokaa milele, na Adhabu na Laana za Allah zitakua juu yake, na
ametayarishiwa kwa ajili yake Adhabu kali sana.
Hivyo ingawa Damu ya Ibn Adam hua hairuhusiki kumwagwa kutokana na Utukufu
wake lakini hata hivyo kwa upande mwengine basi pia hairuhusiki kuiuza Damu wala
kuinunua kama inavyofanywa kwenye Mahospitali mbali mbali leo hii Duniani.
Na hii ni kutokana na kauli ya Abu Juhayfa Radhi Allahu Anhu ambae alimnunua
Mtumwa ambae kazi yake ilikua ni kufanya Hijama na kisha akaamrisha kua vifaa vyake
vya kufanyia Hijama vivunjwe, alipoulizwa ni kwa sababu gani akaamrisha hivyo basi
alisema kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ameharamisha bei ya
Damu’(Sahih Bukhari)
Ambapo kutokana na hadithi hii basi Mujaddid Ad Din Shaykh ul Islami Al Hafidh Imam
Shihab Ad Din Ahmad Ibn Hajjar Al Asqalani basi amesema kua: ‘Kinachomaanishwa
hapa katika hadithi hii ni kua Ni Haram kuuza Damu kama vile ambavyo ilivyokua
Haram kuuza Nyama ya Mnyama aliekufa na Nyama ya Nguruwe na ni Haram
kuuza na kununua Damu kulingana na makubaliano ya Wanazuoni.’(Fat-h Al Barr)
Na Mujtahid Imam Abu Bakr Muhammad Ibn Ibrahim Ibn Al Mundhir Al Nishapuri basi
yeye anasema kua: ‘Kuuza Damu hua ni Haram na hivyo Makubaliano ya kuuziana
Damu hua hayajuzu kutokana na maneno ya aya isemayo:
﴿قُل لا َّ أَجِ دُ فىِ مَآ أُوْحِ ىَ إِلىَ َّ محَُر َّماً عَلَى ٰ طَاعِمٍ يَطْعَمُهُ إِلا َّ أَن يَكُونَ مَ يْ تَةً أَوْ
دَماً م َّسْفُوحاً أَوْ لحَْمَ خِ نزِيرٍ فَإِن َّهُ رِجْسٌ أَوْ فِسْقاً أُهِل َّ لِغَيرِْ ٱهلل َِّ بِهِ فَمَنِ ٱضْطُ َّر
غَيْرَ ابَغٍ وَلاَ عَادٍ فَإِن َّ رَب َّكَ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
156
Qul la ajidu feema oohiya ilayya muharraman AAala taAAimin yatAAamuhu illa
an yakoona maytatan aw daman masfoohan aw lahma khinzeerin fa-innahu rijsun
aw fisqan ohilla lighayri Allahi bihi famani idhturra ghayra baghin wala AAadin
fa-inna rabbaka ghafoorun raheemun(Surat Al AnaAm 6:145)
Tafsir: Sema (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam): ‘Sikuona katika
nilivyoshushiwa wahyi chochote kile kilichoharamishiwa kuliwa na mtu mwenye
kutamani kula isipokua itakapokua ni Maiti au ni Damu yenye kutiririka au Nyama
ya Nguruwe, kwani kwa hakika huo ni uchafu au ni kufanya uovu kwa kuchinja si
kwa ajili ya Allah, lakini atakaelazimika bila ya kua na hiari ya kufanya uasi na
kuvuka mipaka basi kwa hakika Mola wako ni mwingi wa Kusamehe na ni mwingi wa
Huruma.’
Ambapo aya imetumia neno Daman masfoohan yaani Damu iliyokua Masfuha. Na neno
Masfuuha limetokana na neno Safaha ambalo hua linamaanisha Kumwaga, Kutiririka au
Kumiminika.
Neno Safaha ndio pia lililotoa neno Musafihun ambalo hua linamaanisha Mtu
anaemmwagia mwenzake manii au anaemwagiwa manii nje ya ndoa yaani anaefanya
Usharati au Uzinifu.
Ambapo kwa upande wa Imam Muhamamd Yusuf Al Atfayyesh basi yeye anasema kua:
‘Neno Safaha hua linamaanisha Mchanganyiko wa kua na Ufahamu Dhaifu na
kutumia kitu katika njia za uovu.’
Na si Damu tu bali kila kiungo cha Ibn Adam hua hairuhusiki kukiuza wala kukinunua
kutokana na Utukufu wa Mwili wa Ibn Adam kama alivyosema Allah Subhanah wa
Taala kua:
﴿وَلَقَدْ كَ ر َّمْ نَا بَنىِ ءَادَمَ﴾
Walaqad karramna banee adama (Surat Al Israa, 17:70)
Tafsir: Na kwa hakika tumemkirimu Bani Adam.
Lakini hata hivyo hapa pia inabidi tufahamu kua ingawa hairuhusi kuuza wala kununua
viungo vya mwili vya Ibn Adam au Damu ya Ibn Adam lakini inaruhusika kufidia kwa
kutoa kiasi cha malipo na kumpa mtu anaehitajika Damu yake iongezewe kwa mtu
mwengine, kutokana na kua mtu huyo mwenye Damu hio ya ziada ni mwenye kukataa
kutoa Damu hio kwa ajili ya Ibn Adam mwenzake hadi pale atakapota malipo hayo, na
157
hivyo hua una dharura isiyikua na khiaria mabyo ndio iliyoelezewa na sehemu ya aya
isemayo:
﴿فَمَنِ ٱضْطُر َّ غَيْرَ ابَغٍ وَلاَ عَادٍ فَإِن َّ رَب َّكَ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Famani idhturra ghayra baghin wala AAadin fa-inna rabbaka ghafoorun
raheemun(Surat Al AnaAm 6:145)
Tafsir: Lakini atakaelazimika bila ya kua na hiari ya kufanya uasi na kuvuka mipaka
basi kwa hakika Mola wako ni mwingi wa Kusamehe na ni mwingi wa Huruma.’
Na hivyo basi kutokana na hali ya malipo hayo basi mtu anaetoa malipo kwa ajili ya
Damu hio hua hana kosa na hapati dhambi kutokana na kulipia huko, ila mwenye
kupokea malipo hayo kwa ajili ya Damu hio basi hua ni mwenye kujibadilishia malipo
ya jambo jema kwa kupata malipo ya jambo ovu.
Naam hio ni kuhusiana na Damu ya Ibn Adam, ama tunapozungumzia kuhusiana na
Damu ya mnyama ambae ni halali kuliwa basi hua inakubalika kumwagwa Damu yake
pale inapokua kufanya hivyo hua ni kwa ajili ya kutoa kafara kwa ajili ya Allah Subhanah
wa Ta’ala
Imam Khalil Ibn Is-haq Al Jundi Al Maliki anatubainishia Hikma ya kuruhusiwa kwa Ibn
Adam kuchinja Wanyama kwa kusema kua: ‘Wakati Allah alipowakirimu Ibn Adam
kwa ufaham, basi aliwafanya Wanyama wengine kua ni wenye kuruhusiwa kua
chakula chake kwa ajili ya kuwaimarishia Miili yao Ibn Adam, kubainisha
Makadirio yake Muumba kupitia katika njia ya Nyama yao na kuwaonesha Ibn
Adam kua anawajali kwa kuwaweka wao juu zaidi yao Wanyama hao.’
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anasema katika Qur’an kua:
﴿وَٱلْبُدْنَ جَعَلْنَاهَا لَكُمْ مِّن شَعَائِرِ ٱهلل َِّ لَكُمْ فِيهَا خَيْرٌ فَٱذْكُرُواْ ٱسْمَ ٱهلل َِّ عَلَيْ هَا
صَوَآف َّ فَإِذَا وَجَبَتْ جُنُوبُهَا
فَكُلُواْ مِنْهَا وَأَطْعِمُواْ ٱلْقَانِعَ وَٱلْمُعْتَر َّ كَ ٰذلِ َك
سَخ َّرَْهَا لَكُمْ لَعَل َّكُمْ تَشْكُرُونَ۞لَن يَنَالَ ٱهلل ََّ لحُُومُهَا وَلاَ دِمَآؤُهَا وَلَٰ ِكن يَنَالُهُ
158
ٱلت َّقْوَىٰ مِنكُمْ كَذٰ لِكَ سَخ َّرَهَا لَكُمْ لِتُكَبرُِّواْ ٱهلل ََّ عَلَى ٰ مَا هَدَاكُ مْ وَبَشِّ رِ
ٱلْمُحْسِ نِينَ ﴾
Waalbudna jaAAalnaha lakum min shaAAa-iri Allahi lakum feeha khayrun
faodhkuroo isma Allahi AAalayha sawaffa fa-idha wajabat junoobuha fakuloo
minha waatAAimoo alqaniAAa waalmuAAtarra kadhalika sakhkharnaha lakum
laAAallakum tashkuroona; Lan yanala Allaha luhoomuha wala dimaoha walakin
yanaluhu alttaqwa minkum kadhalika sakhkharaha lakum litukabbiroo Allaha
AAala ma hadakum wabashshiri almuhsineena (Surat Al Hajj 22:36-37)
Tafsir: Na Wanyama wa Kuchinja (Ngombe, Ngamia n.k) tumewajaalia wao kwa ajili
yenu kua alama ya Allah, ndani yake mna kheri nyingi. Hivyo tajeni Jina la Allah juu
yao wanapokua kwenye safu (kwa ajili ya kuchinjwa), kisha wanapoanguka (baada ya
kuchinjwa) kuleni kutokana nao na walisheni kutokana nayo Masikini wenye kuomba
na wasioomba. Hivyo tumewafanya kua chini yenu ili mpate kushukuru. Na si Nyama
yao wala Damu yao inayomfikia yeye (Allah Subhanah wa Ta’ala) bali ni Taqwa
kutoka kwenu ndio inayomfikia. Hivyo tumewafanya kua chini yenu ili mpate
kumkuza Allah, kutokana na Uongozi wake juu yenu, na (Ewe Muhammad) wape
habari njema wenye kufanya mema.
Ambapo aya zimetumia neno Budna lenye kutokana na neno Badan ambalo hua
linamaanisha, Kunona, Kua na Mwili Mkubwa, Kua na Mwili bila ya Roho. Neno Badan
ndio lililotoa neno Budun ambalo hua linamaanisha Mnyama wa Kuchinja au wa
Kutolewa Kafara. Ambapo ingawa neno Badan na neno Jism hua ni yenye kufanana
kimaana lakini hapo hapo neno Jism hua linamaanisha Mwili au Kiwiliwili lakini pale
kinapozungumziwa kuhusiana na hali ya muonekano wake na rangi yake, wakati neno
Badan hua linatumika pale inapozungumziwa kuhusiana na mkubwa wa kiumri.
Na ikatumia neno Sawaffa ambalo ni lenye kutokana na neno Saffa ambalo humaanisha
Safu, Kupanga Mstari au kwa mpangilio, hivyo baadhi ya Wanazuoni hua ni wenye
kulisoma neno hili katika hali ya Saafinah ambalo hua linamaanisha pia Hali ya kutembea
kwa miguu, au Kujifunga wenyewe na hivyo kumfanya Ngamia kua ni mwenye
kusimama kwa miguu mitatu, na hivyo kua ni mwenye kuchinjwa wakati akiwa
amesimama katika hali hio na kuangukia upande mmoja kutokana na kushindwa kujizuia
baada ya kutokwa na damu nyingi sana.
Ambapo neno Saafinah pia ndio lile lililotumika katika ya zinazoelezea kisa cha Nabii
Sulayman pale alipokua akiangalia Farasi wazuri sana waliokua wakipitishwa mbele
159
yake wenye kuvutia kutokana na muonekano wao na madaha yao ya kusimama kwa
miguu mitatu kama ilivyosema aya:
﴿إِذْ عُرِضَ عَلَيْهِ بِٱلْعَشِ ىِّ ٱلص َّافِنَاتُ ٱلجِْيَادُ ﴾
Idh AAuridha AAalayhi bialAAashiyyi alssafinatu aljiyadu (Surat Sad 38:31)
Tafsir: Wakati walipooneshwa mbele yake katika wakati wa Alasiri, Farasi bora
wanaopendeza.
Ambapo kwa upande mwengine basi anasema Imam Muhammad Ibn Jarir At Tabari kua
‘Kuna baadhi ya Wanazuoni ambao wamelifaham neno Sawaaf kua linamaanisha
na sawa ya ile maana ya neno Khaalis yaani Ikhlasi.’
Ambapo kwa upande wa Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari basi yeye
anasema kuhusiana na maneno yasemayo kua: ‘Fa-idha wajabat junoobuha yaani na
kisha wanapoanguka’ kua Neno Wajabat hua ni sawa na neno Saqata ambalo
humaanisha Kuanguka, ambapo kwa upande wa Zayd Ibn Aslam Radhi Allahu Anhu
anasema kua: ‘Wanapoanguka na Kufa’ na hii ni kwa sababu Mnyama anaechinjwa
hua hairuhusiki kukatwa sehemu ya mwili wake, kunyonyolewa, kuchunwa ngozi n.k
bali hua inaruhusika kufanyiwa hivyo pale anapokua ameshachinjwa na hayuko hai.
Kwani katika kipindi cha wakati wa Uhai wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi
watu wa Madinah walikua na tabia ambayo inaelezewa na Abu Waqiy Radhi Allahu Anhu
kwa kusema kua: ‘Kabla ya kuja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika Mji
wa Madinah ilikua ni kawaida kwa watu kukata Nundu ya Ngamia na Mkia wa
Kondoo hivyo Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam akaema kua: ‘Chochote kile
kitakachokatwa kutokana na Mnyama wakati akiwa hai basi hua Maiti (isiyofaa
kuliwa).’(Imam At Tirmidhii)
Na kwa upande wa Imam Abu Maali Al Juwayni Al Haramayn ambae ni mwalimu wake
Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali basi yeye
anasema katka Kitabu chake cha Nihayat Al Matlab kua mpaka kuikata sehemu ya
Samaki aliekua mzima baada ya kuvuliwa kwake basi hua haifai kwa sababu hii hua ni
sehemu ya kumuadhibu kiumbe huyo, lakini hua haimharamishi Samaki huyo na wala
haiiharamishi sehemu yake hio kutokana na kuliwa.
Na amesema Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alitangazia katika mji wa Makkah katika mwaka ambao Mji wa Makkah
ulitekwa na Waislam kua: ‘Kwa Hakika Allah na Mtume wake ameharamisha
160
uuzwaji wa Pombe, Maiti, Nguruwe na Masanamu’ Hivyo mtu mmoja akauliza:
‘Ya Rasul Allah! Vipi kuhusiana na Mafuta ya Mnyama aliekua Maiti? Kwani
yalikua yanatumika kwa ajili ya kupakaza kwenye Majahazi. Kuzipaka Ngozi na
watu walikua wakitumia kwa ajili ya kuwashia Taa zao.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Mafuta hayo pia ni Haram. Kwani
Allah aliwalaani Mayahudi, kwani kwa hakika (Nyama ya Mnyama aliekufa) Maiti
iliharamishwa juu yao, na kisha wao wakaigeuza katika hali nyengine (kwa
kuichanganyana vitu vyengine) wanaiuza na kupata faida kutokana nayo.’(Bukhari
na Muslim)’
Ambapo hadithi hii inatubainishia uthibitisho wa kua hairuhusiki kukificha kitu
kilichokua haramu na kisha kukichanganya na kitu kilichokua halali au kukigeuza jina
na kisha kukiuza baada ya kukipendezesha, kwani hii hua pia ni sawa na vile zilivyosema
aya zifuatazo:
﴿إِنم ََّا حَر َّمَ عَلَيْكُمُ ٱلْمَيْتَةَ وَٱلْد َّمَ وَلحَْمَ ٱلخَْنْزِيرِ وَمَآ أُهِل َّ لِغَيرِْ ٱهلل َِّ بِهِ فَمَنِ ٱضْطُ َّر
غَيْرَ ابَ غٍ وَلاَ عَادٍ فَإِن َّ ٱهلل ََّ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ۞ وَ ت لاَ َ قُولُواْلَِما تَصِ فُ أَ لْسِ نَتُكُمُ ٱلْكَذِ َب
هَٰذَا حَلاَلٌ وَ هَٰذَا حَرَامٌ لِّتَفْتَرُواْ ٰ عَلَى ٱهلل َِّ ٱلْكَذِبَ إِن َّ ٱل َّذِينَ يَفْتَرُونَ ٰ عَلَى ٱهلل َِّ
ٱلْكَذِبَ لاَ يُفْلِحُونَ ﴾
Innama harrama AAalaykumu almaytata waalddama walahma alkhinzeeri wama
ohilla lighayri Allahi bihi famani idturra ghayra baghin wala AAadin fa-inna
Allaha ghafoorun raheemun; Wala taqooloo lima tasifu alsinatukumu alkadhiba
hadha halalun wahadha haramun litaftaroo AAala Allahi alkadhiba inna
alladheena yaftaroona AAala Allahi alkadhiba la yuflihoona(Surat AnNaml 16:115-
116)
Tafsir: Hakika (Allah Subhanah wa Taala) amekuharamishieni juu yenu Maiti na
Damu na Nyama ya Nguruwe na kilichochinjwa ambacho si kwa ajili ya Allah, lakini
kama (mtu) atalazimika bila ya kua na khiari wala kuvuka mipaka basi hakuna kosa
juu yake. Kwani kwa hakika Allah ni miwingi wa Kusamehe na ni mwingi wa Huruma.
Na wala msiseme kuhusiana na ndimi zenu zenye kukadhibisha kua hiki ni halali na
hiki ni haramu kuzusha dhidi ya Allah Uongo, hakika wale wanaozua Uongo dhidi ya
Allah hawatofuzu.
161
Imam Burhan Ad Din Abu Hassana Ali Ibn Ab Bakar Ibn Abd Jalil Al Farghani Al-
Marghinani Al Hanafi kua: ‘Malengo ya Kuharamishwa baadhi ya Vyakula hua ni
kutokana na umuhimu wa kuilinda heshima ya Mwili wa Ibn Adam kwa kuuzuia
kutokana na kudhalilika kunakotokana na kula vyakula vilivyoharamishwa’, yaani
makatazo hayo hua ni yenye kukatazwa kutokana na madhara ya vitu hivyo kwa mwili
wa Ibn Adam na pia utumiaji wa vyakula vilivyoharamishwa hua ndio sababu kuu
inayompelekea Ibn Adam kua ni mwenye kufanya maasi, na hivyo anapokua anajidhibiti
basi humpelekea mtu husika kua ni mwenye kupendelea kufanya mema zaidi.
Hivyo vile vyakula vilivyoharamishwa vimeharamishwa kwa sababu ya madhara yake
na vilivyohalalishwa vimehalalishwa kutokana na faida zake na kuamrishwa kugawiana
na wengine pia wasiokua na uwezo navyo wapewe ili nao wanufaike navyo kama
ilivyoamrishwa kwenye aya zetu za Surat Al Hajj 22:36-37 ambazo ndani yake mna
maneno yasemayo;
﴿فَكُلُواْ مِنْ هَ ا وَأَطْعِ مُواْ ٱلْقَانِعَ وَٱلْمُعْتَر َّ ﴾
Fakuloo minha waatAAimoo alqaniAAa waalmuAAtarra (Surat Al Hajj 22:36)
Tafsir Hivyo kuleni kutokana nao na walisheni kutokana nayo Masikini wenye
kuomba na wasioomba.’
Ambapo maana ya maneno haya na amrisho liliomo ndani yake basi ndio msingi uliotoa
Hukmu ya Fiqh kua Nyama ya Mnyama anaechinjwa inatakiwa igaiwe katika sehemu
tatu ambapo sehemu moja hua ni kwa ajili ya Mchinjaji, sehemu ya pili kwa ajili ya Watu
wa karibu au Marafiki na sehemu ya tatu ni kwa ajili ya Masikini.
Na anasema Hujjat Ul Islami Mujaddid Ad Din Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad
Ibn Muhammad Al Ghazali kua; ‘Allah Subhanah wa Taala amewataka Viumbe wake
kufuata maamrisho yake na hivyo kua ni wenye kula kile ambacho ni kisafi, kizuri,
kikamilifu chenye kunufaisha na chenye ladha tamu’ ambapo sifa zote hizi
zimejumuishwa kwenye neno Tayyib kama ilivyoelezewa kwenye aya ifuatayo:
﴿قُلْ مَنْ حَر َّمَ زِينَةَ ٱهلل َِّ ٱل َّتيِ ۤ أَخْرَجَ لِعِبَادِهِ وَالْط َّيِّبَاتِ مِنَ ٱلرِّزْقِ قُلْ هِىَ لِل َّ ذِينَ
آ مَنُو اْفىِٱ لحَْيَا ةِٱلد ُّنْيَا خَالِصَةً يَوْمَ ٱلْقِيَامَةِ كَذٰ لِكَ نُفَصِّلُ ٱلآَتِ لِقَوْمٍ يَ عْلَمُونَ
162
۞قُلْ إِنم ََّا حَر َّمَ رَبىَِّ ٱلْفَوَاحِ شَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ وَٱلإِثمَْ وَٱلْبَغْىَ بِغَيرِْ ٱلحَْ قِّ وَأَن
تُشْرِكُواْ بِٱهلل َِّ مَا لمَْ يُنَزِّلْ بِ هِ سُلْطَاً وَأَن تَقُولُواْ عَلَى ٱهلل َِّ مَا لاَ تَ عْلَمُونَ ﴾
Qul man harrama zeenata Allahi allatee akhraja liAAibadihi waalttayyibati mina
alrrizqi qul hiya lilladheena amanoo fee alhayati alddunya khalisatan yawma
alqiyamati kadhalika nufassilu al-ayati liqawmin yaAAlamoona; Qul innama
harrama rabbiya alfawahisha ma dhahara minha wama batana waal-ithma
waalbaghya bighayri alhaqqi waan tushrikoo biAllahi ma lam yunazzil bihi
sultanan waan taqooloo AAala Allahi ma la taAAlamoona (Surat Al A’raf 7:32-33)
Tafsir: Sema (Ewe Muhammad): ‘Ni nani alieharamisha Vizuri vya Allah, ambavyo
amevitoa kwa ajili ya Viumbe wake na (Tayyibati) vizuri na visafi miongoni mwa riziki
zake’ Sema: ‘Hivi ni wa ajili ya wale walioamini katika maisha ya Dunia hii, lakini ni
kwa ajili yao tu katika siku ya Malipo.’ Hivyo ndivyo tunavyoelezea dalili zetu kwa
wale wenye kufaham. Sema: ‘Hakika aliyoyaharamisha Mola wangu ni mambo
machafu iwe ya dhahiri au ya siri, dhambi na kuvuka mipaka dhidi ya Ukweli au Haki
na kumshirikisha Allah kwa kile ambacho hakukipa mamlaka yake. Na kusema
kuhusiana na Allah juu ya mambo msiyoyajua.’’
Hapa tunaona kua aya zimetumia neno Tayyiba ambalo ni lenye kutokana na neno Tabba
ambalo hua ni lenye kumaanisha Kua Vizuri, Kupendeza, Kukubalika, Kuhalalika, Kua
na Usafi, Kufurahisha, Kuvutia kwa utamu.n.k
Hivyo basi tunapozungumzia kuhusiana na Tayyibati mina al Rizqi basi ndani yake
mnaingia kila kitu ambacho si kizuri na kinavutia, kisafi na kitamu tu lakini pia ndani
yake mnaingia kila chenye manufaa na mwili wa Ibn Adam, kukitumia bila ya kua na
kibri au kufanya israfu au kikimbilia baada ya kukikosa, kwani amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Yeyote yule mwenye chembe ya Kibri ndani ya
Moyo wake basi hatoinga Peponi.’
Mmoja kati ya Masahaba akauliza: ‘Ya Rasul Allah! Kama mtu anapenda Nguo zake
na Viatu vyake viwe vizuri ’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Kwa
hakika Allah ni Mzuri na hivyo anapenda vilivyo vizuri. Kibri hua ni kusimama
dhidi ya Haki na Ukweli na kuwaangalia watu kwa chini.’
Na akasema tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Allah anapomjaalia Mja
wake fadhila zake basi hua ni mwenye kupenda kuona uzuri wa athari yake neema
hio juu ya mja huyo.’(Imam At Tirmidhii)
163
Hata hivyo kwa upande mwegine basi Mtu kua na vitu vizuri hua hakumaanishi kua ndio
mtu huyo anao ukaribu na Allah Subhanah wa Ta’ala na ndio maana Umar Ibn Al
Khattab Radhi Allahu Anhu akawa ni mwenye kusema kua: ‘Tungekula Vyakula vizuri
lakini Qur’an imesema:
﴿وَيَوْمَ يُعْرَضُ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ عَلَى ٱلن َّارِ أَذْهَبْتُمْ طَيِّبَاتِكُمْ فىِ حَيَاتِكُمُ ٱلد ُّنْيَ ا
وَٱسْتَمْتَعْتُمْ هبَِا فَٱلْيَوْمَ تجُْزَوْنَ عَذَابَ ٱلهُْونِ بمَِا كُنتُمْ تَسْتَكْبرُِونَ فىِ ٱلأَرْضِ بِغَيرِْ
ٱلحَْقِّ وَبمَِا كُ نتُمْ تَفْ سُقُ ونَ ﴾
Wayawma yuAAradhu alladheena kafaroo AAala alnnari athhabtum tayyibatikum
fee hayatikumu alddunya waistamtaAAtum biha faalyawma tujzawna AAathaba
alhooni bima kuntum tastakbiroona fee al-ardhi bighayri alhaqqi wabima kuntum
tafsuqoona(Surat Al Ahqaf 46:20)
Tafsir: Na katika siku ambayo wale waliokufuru watadhihirishiwa Moto (na
kuambiwa) Nyinyi mlipewa vitu vizuri katika maisha yenu ya Duniani na mkastarehe
kutokana navyo. Hivyo leo mtalipwa kwa Adhabu yenye kunyanyasisha kwa sababu
mlikua na Kibri katika ardhi bila ya kua na haki yeyote na kutokana na kua ni waasi
na wenye kufanya maovu.
Na kwa upande wa Hasan Al Basr basi yeye amesema kuhusiana na wale ambao ni wenye
kuyakimbilia mazuri ya Dunia ili wayapate hata kwa kutumia njia za haramu kua: ‘Allah
Subhnaha wa Ta’ala alipomtuma Mtume wake aliemchagua, ambae hakua ni
mwenye kufunga Mlango wake. Hakutafuta Mlinzi kwa ajili yake, hakua ni mwenye
kufanya dhulma, alikua ni mwenye kukaa chini ardhini, na alikua akila chakula
chake akiwa katika hali hio ya kukaa kitako chini, aliekua akiramba vidole vyake
baada ya kulaa kwake, hakua akivaa nguo za hariri, aliekua akipanda Punda na
kukubali Mtumwa wake kua ni abiria mwenzake juu ya Punda wake. Na alikua
akisema: ‘Yeyote yule mwenye kuachana na Sunnah zangu hua si wa miongoni
mwangu’’
Hasan Al Basr anaendelea kusema kua: ‘Na Sasa hivi tuna watu ambao wameachana
na Sunnah zake, hawa ni wale wapotovu ambao ni wenye kula Riba na kula vitu
vyengine vilivyoharamishwa, wajinga, na walionekana kua ni wajinga na
kuchukiwa na Mola wao, wanaamini kua hakuna ubaya katika kila chakula bora
164
wanachokimbilia kukitia mikononi mwao, wakayapamba majumba yao kwa
mapambo bora kabisa huku wakidai kusoma aya isemayo kua:
﴿قُلْ مَنْ حَر َّمَ زِينَةَ ٱهلل َِّ ٱل َّتيِ ۤ أَخْرَجَ لِعِبَادِهِ وَالْط َّيِّبَاتِ مِنَ ٱلرِّ زْقِ ﴾
Qul man harrama zeenata Allahi allatee akhraja liAAibadihi waalttayyibati mina
alrrizqi (Surat Al A’raf 7:32)
Tafsir: Sema (Ewe Muhammad): ‘Ni nani alieharamisha Vizuri vya Allah, ambavyo
amevitoa kwa ajili ya Viumbe wake na (Tayyibati) vizuri na visafi miongoni mwa riziki
zake’
Hasan Al Basr anaendelea kusema kua: ‘Watu hawa hawajui kua Vitu hivyo ni kwa
ajili ya Marafiki wa Shaytan’
Naam..hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala ametujaalia vilivyo vizuri na kuwaweka chini
yetu wanyama wa chakula kwa ajili ya kua ni miongoni mwa vyakula vyetu vilivyo halali
yetu ambavyo hata hivyo inabidi vipatikane kwa njia ya uhalali na kisha ndio tupate
kuonesha shukrani kwake kwa kupitia njia ya kutoa kafara ya kumwaga damu ya
Wanyama hao kwa ajili yake yeye Muumba na hivyo basi hua hairuhusiki kula nyama ya
Mnyama aliechinjwa isipokua awe ni aliechinjwa kulingana na sharia za Kiislam,
ambayo inaanzia kwa mnyama huyo kutajiwa jina la Allah Subhana wa Ta’ala juu yake
katika wakati wa kuchinjwa. Kama inavyosema aya:
﴿فَكُلُواْ ممِ َّا ذُكِرَ ٱسْمُ ٱهلل َِّ عَلَيْهِ إِن كُنتُمْ آبَِتِهِ مُؤْمِنِينَ ﴾
Fakuloo mimma dhukira ismu Allahi AAalayhi in kuntum bi-ayatihi mu/mineena
(Surat Al Anaam 6:118)
Tafsir: Na Kuleni kile ambacho kimetajiwa Jina la Allah juu yake kama kweli nyinyi
ni wenye kuamini aya zetu.
Ambapo amesema Jundub Ibn Sufyan Al Bajali Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mara moja
sisi tulichinja Wanyama kua Kafara pamoja na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, hivyo baadhi ya Watu wakachinja kabla ya Sala ya Iddi, na baada ya Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kumaliza kusali, basi akaona kua wamechinja
kabla ya sala hivyo akasema: ‘Yeyote yule aliechinja Mnyama kabla ya Sala basi na
achinje tena badala yake na wale ambao hawakuchinja mpaka baada ya kumaliza
kusali basi na wchinje kwa kutaja jina la Allah’’(Sahih Bukhari)
165
Kwani nyama ambayo haikuchinjwa kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala hua ni sawa
na Maiti, ambayo ni Nyama iliyoharamishiwa kuliwa kama ilivyosema aya zenye
kubainisha vilivyoharamishwa kuliwa kwa kusema:
﴿حُرِّمَتْ عَلَيْكُمُ ٱلْمَيْتَةُ وَٱلْد َّمُ وَلحَْمُ ٱلخِْنْزِيرِ وَمَآ أُهِل َّ لِغَيرِْ ٱهلل َِّ بِهِ وَٱلْمُنْخَنِقَةُ
وَٱلْمَوْقُوذَةُ وَٱلْمُتَرَدِّيَةُ وَٱلن َّطِيحَةُ وَمَآ أَكَلَ ٱلس َّبُعُ إِلا َّ مَا ذَك َّيْتُمْ وَمَا ذُبِحَ عَلَى
ٱلن ُّصُبِ وَأَنْ تَسْتَقْسِ مُواْ بِٱلأَزْلاَمِ ذٰلِكُمْ فِسْقٌ ٱلْيَوْمَ يَئِسَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ مِن دِينِكُ ْم
فَلاَ تخَْشَوْهُمْ وَٱخْشَوْنِ ٱلْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتمَْمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتىِ
وَرَضِيتُ لَكُمُ ٱلأِسْلاَمَ دِيناً فَمَنِ ٱضْطُر َّ فىِ مخَْمَصَةٍ غَيْرَ مُتَجَانِفٍ لإِثمٍْ فَإِن َّ ٱهلل ََّ
غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Hurrimat AAalaykumu almaytatu waalddamu walahmu alkhinzeeri wama ohilla
lighayri Allahi bihi waalmunkhaniqatu waalmawqoodhatu waalmutaraddiyatu
waalnnateehatu wama akala alssabuAAu illa ma dhakkaytum wama dhubiha
AAala alnnusubi waan tastaqsimoo bial-azlami dhalikum fisqun alyawma ya-isa
alladheena kafaroo min deenikum fala takhshawhum waikhshawni alyawma
akmaltu lakum deenakum waatmamtu AAalaykum niAAmatee waradheetu
lakumu al-islama deenan famani idhturra fee makhmasatin ghayra mutajanifin liithmin
fa-inna Allaha ghafoorun raheemun(Surat Al Maidah 5:3)
Tafsir: Mmeharamishiwa juu yenu Maiti na Damu na nyama ya Nguruwe na kile
ambacho kimechinjwa si kwa ajili ya Allah, na kilichonyongwa au kupigwa kwa
kipigo cha nguvu, au kwa kuangukia Kichwa, au kwa Kutobolewa na Pembe za
Mnyama mwengine, na kile kilichobakia baada ya kuliwa na Wanyama wengine
isipokua kama mtawahi kukichinja (kabla hakijafa). Na kile ambacho kimechinjwa
kwa kutolewa kafara kwenye Madhabahu ya Masanam. Na pia kutumia mishare
kwa ajili ya kutafuta bahati au kutoa maamuzi, yote hayo ni Uasi. Leo hii
Wasioamini wote wameishiwa na matumaini juu ya Dini yenu, hivyo msiwe na
khofu nao, bali kuweni na khofu nami. Leo hii nimeikamilisha Dini yenu,
nimekamilisha fadhila zangu juu yenu na nimeuchagua Uislam kua ndio Dini yenu.
Lakini kwa yule ambae atakumbana na Njaa kali (basi anaweza kula hivyo
166
vilivyokatazwa), bila ya (kua ni mwenye) kuelemea kwenye dhambi, na kwa hakika
Allah ni mwingi wa Kusamehe na ni mwingi wa Rehma.
Ambapo iliposhuka aya hii basi Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu basi alilia sana
kutokana na kujua kua umewadia mda wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kuondoka Duniani kwani ameshatimiza wajibu wake wa kufikisha ujumbe wake kutoka
kwa Mola wake kwa ajili ya viumbe wake. Na bila ya shaka hili lilikua sahih kwa sababu
mara baada ya kushuka aya hii basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliishi kwa
mda wa siku 81 tu.
Ama kuhusiana na hukmu ya katazo hili liliomo ndani ya aya hii basi anasema Imam
Aḥmad Ibn Mūsá Ibn Marduwayh kua: ‘Suday Ibn Ajalan Radhi Allahu Anhu ambae
pia ni marufu kama Abu Umamah alichaguliwa na Rasul Allah Salallahu A’layhi
wa Salam akawausie watu wake kuhusiana na ujumbe wa Imani ya Dini Kiislam,
na wakati alipokua akiwausia juu ya ujumbe huo basi watu hao wakamletea Sahani
iliyojaa Damu ambayo ilikua imepikwa, nao watu hao wakamkaribisha. Lakini
akawaambia kua yeye ameharamishiwa kula chakula hicho na akawasomea aya hii.
Na kisha akaendelea kuwausia kuhusiana na ujumbe wa Dini ya Kiislam. Lakini
nao wakakataa, na kisha akawaomba maji kwani alikua ana kiu kubwa sana, lakini
nao wakakataa kumpa maji hayo na kumwambia kua bora wamwachie afe kwa kiu
kuliko kumpa maji. Abu Umamah anasema kua: ‘Mimi nilikua na kitambaa,
nikajifunika kichwa na kulala kutokana na joto kali. Wakati nikiwa nimelala akaja
mtu huku akiwa amebeba bakuli zuri sana ambalo uzuri wake hakuna anaeweza
kuufikiria, ambalo ndani yake mlikua mna kinywaji kitamu sana kisichoweza
kufikirika utamu wake. Akanipa kinywaji hicho nami nikanywa, na kutokana
nacho basi mimi nikaamka. Na Wa Allahi sikuona kiu tena! Na wala sikukihitaji
tena kile kitambaa baada ya kunywa kinywaji hicho.
Kisha nikawasikia wale watu wakiwa wanasema: ‘Angalieni, huyu mtu alikuja
kwenu kutoka katika jamii ya watu wa Milimani, lakini hamkumpa hata kinywaji’
hivyo wakanipa mie kinywaji cha Maziwa yaliyochanganywa na Maji, lakini nami
nikawaambia kua: ‘Hakika mimi sihitaji kinywaji chenu tena kwani Allah
amenipatia kinywaji. Na nikawaonesha tumbo langu, na watu wote hao wakaingia
katika Uislam. ’’ (Imam Ibn Abi Hatim, Imam Ibn Marduwayh, na Imam Al Hakim)
Ambapo aya zinaamrisha kuchinja na kumwaga Damu ambayo ni haram kuliwa kama
ilivyokatazwa na Allah Subhanah wa Ta’ala na ndio maana ikaamrishwa kuchinja kabla
ya kumla Mnyama kwa sababu Mnyama anapochinjwa kwa kukatwa Mishipa yake
mikuu ya Damu na bomba ya hewa basi Damu yote iliyomo ndani ya mwili wake hua ni
yenye kutoka kwa kutiririka kwa pamoja bila ya kubakia ndani ya mishipa ya damu
167
iliyomo ndani mwili wa Mnyama husika kutokana na kua Damu hua ni yenye
kusukumwa na Moyo.
Na ndio maana ikawa haitakiwi kumchinja mnyama kwa kumtenganisha kichwa na
kiwiliwili katika wakati wa kuchinja, bali kichwa kinatakiwa kutenganishwa na
kiwiliwili mara baada ya kumalizika kutoka kwa Damu ndani ya Mwili wa Mnyama, kwa
sababu kikitengenishwa kichwa mbali na kiwiliwili basi utokaji wa Damu
unaosababishwa na mapigo ya Moyo hua ni wenye kusita, na kisha Damu ya mnyama
hubakia ndani ya Nyama jambo ambalo hupelekea Nyama hio kua ni yenye kuweza
kuharibika mapema sana, na pia kua ni yenye kusababisha madhara kwa mlaji.
Ambapo hali hua tofauti wakati anapopigwa na kitu kizito au kunyongwa kwani katika
tukio hilo basi damu ya Mnyama husika, hua si yenye kutoka ndani ya mwili wake na
badala yake hua ni yenye kubakia ndani ya Mwili huo na kufanya mapande na kugandana
na nyama ya mnyama husika na hivyo kusababisha Nyama hio pia kua isiyoruhusika
kuliwa.
Na amesema Shaykh ul Islami Imam Muhammad Ibn Ahmad Ibn Zakariyah Al Ansari
kua amesema: ‘Muhyi Ad Din Abu Zakarriyah Sharaf An Nawawi kua: ‘Baadhi ya
Wanazuoni wamesema kua Hikma ya kutakiwa kuchinja hua ni Anhar Al Dam
yaani kuimwaga Damu yote na kutofautisha Uhalali wa Nyama na Mafuta na kile
kilichoharamishwa kwa Mnyama aliekufa kutokana na kubakiwa na Damu ndani
ya miili yao’(Asna Matalib)
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi
kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala ameharamisha Nyama ya mnyama alieuliwa kwa
kunyonga au kwa kupigwa kwa kipigo cha dharuba kwa sababu ya kukosekana
Umuhimu wa kutoka na kumwagika kwa damu ya mnyama husika.’
Na Imam Abu Bakar Ahmad Ibn Ali Al Razi Al Jassas akasema kua: ‘Mtizamo wa Abd
Allah Ibn Umar Radhi Allahu Anhu kuhusiana na Mnyama alieuliwa kwa kipigwa
silaha ya aina ya Banduqah (ambayo hua ni silaha kama jiwe, dongo la Duara au
chuma cha Duara), hua haruhusiki kuliwa’
Kwani amesema Imam Ahmad Ibn Hanbal kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Msile mlichokipiga kwa Banduqah isipokua kama itakua
mliwahi kukichinja.’’ na huo ni mtizamo wa Imam Al Shafii, Imam Abu Hanifa na pia
Imam Malik.
Na amesema pia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kurusha Mawe
hakutomuua anaewindwa na wala hakutomuua Adui lakini kunaweza kuvunja
meno, au kutofoa Jicho.’(Sahih Imam Bukhari)
168
Na akasema Abd Allah Ibn Abbs Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam amekataza Sharita ya Shaytani. Ambayo ni Mnyama aliechinjwa kwa
kukatwa wazi huku Mshipa ya Damu ikiwa haijachinjwa na kisha akaachiwa kua
afe’(Sunnan Abu Daud)
Ambapo Adi Ibn Abi Hatim Radhi Allahu Anhu alimwambia Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Ya Rasul Allah! Hakika mimi hua nnawinda kwa kutumia
Upinde ambao hauna manyoya nyuma yake jee Nyama yake ni halali?’ Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Unaweza ukala nyama yake kama ikiwa Ncha
ya Upinde imemtaboa, kwani aliepigwa na kuuliwa kwa ujiti wa upinde usiokua na
ncha hua ni mawqudha(aliegongwa mpaka akafa) hivyo msimle’(Bukhari na Muslim)
Na amesema Abaya Ibn Rafa’a Ibn Rafth Ibn Khadij kua: ‘Sisi tulikua na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam katika maeneo ya Dhul-Hulaifa, na hivyo watu walikua
na njaa na walikua wameteka Ngamia na Kondoo. Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam alikua Nyuma ya Watu, ambao walikua wakihangaikia kuchinja Wanyama
na kuwatia kwenye vyombo na kuwapika. Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akaamrisha vyombo viachiwe na akaanza kugawa wanyama waliotekwa,
kuhusiana na Kondoo kumi kua sawa na Ngamia mmoja. Hapo Ngamia mmoja
akakimbia, na watu wakaanza kumkimbilia mpaka wakachoka. Katika wakati huo
kulikua na Farasi kidogo. Hivyo mtu mmoja akachukua Upinde na akampiga nao
Ngamia huyo na Allah akamsimamisha Ngamia huyo kutokana na Upinde huo.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Baadhi ya Wanyama hawa hua
ni kama Wanyama wa Mwituni, hivyo wakiwa hawadhibitiki basi wafanyieni kama
hivi (kwa kuwapiga upinde) kabla ya kuwagawanya Wanyama hao kwa Jeshi basi
Babu yangu akasema: ‘Tunaweza tukakutana na maadui baadae na hatutokua na
Visu, jee tunaweza kuwachinja Wanyama kwa kutumia Ncha za Mipinde?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Tumieni chochote kile kitakacho
sababisha kumwagika kwa damu, na kisha mleni Mnyama kama akiwa ametajiwa
Jina la Allah juu yake. Msimchinje Mnyama kwa Meno au kwa Kucha, na
nitakuambieni kwanini, kwa sababu Meno hua ni Mifupa (haiwezi kukata vizuri)
na Kucha zinatumiwa na Wahabeshi (na hivyo msiwaige kwani ni Makafiri)’’(Sahih
Bukhari)
Mbali ya kua aya hii imezungumzia kuhusiana na aina ya Nyama iliyoharamishwa kuliwa
na umuhimu wa kumwagwa Damu ya Mnyama husika lakini pia imezungumzia
kuhusiana na Azlami ambalo ni neno lililotokana na neno Zalama lenye kumaanisha
Kuzunguka zunguka, Kutembea, Kutoa zawadi ambayo ni ndogo sana, Kukata kitu na
kukifanya kua butu.
169
Na hivyo neno Azlami hua linamanisha Upinde ambao umekatwa hauna ncha wala
manyoya hivyo kua hauna mbele wala nyuma, ambao hua ni wenye kutumiwa na watu
waliokua wakiangalia na kubashiri kua kama mambo yatakua ama la, yana kheri ama la
n.k ambapo watu walipokua wanashaka juu ya jambo basi walikua wakienda kwenye
Majumba yao ya Ibada ambapo ndani yake hua kuna sehemu ambayo imewekwa Mipinde
hio, ambayo imeandikwa maneno yasemayo Naam, La, Mungu karidhia, Mungu
hakuridhia n.k
Hivya mtu huyo mwenye shaka juu ya jambo lake basi huenda kwenye mipinde yenye
kujibu kuhusiana na jambo husika kwa mfano kilimo, biashara, ndoa, vita, safari n.k na
akiingiza mkono kwenye sehemu iliyowekwa mipinde hio na akitoa ulioandikwa kua
Mungu ameridhia basi hua ni mwenye kufanya jambo hilo, na kama akitoa ambao
umeandikwa Mungu hakuridhia basi huachana na jambo hilo, n.k
Ambapo Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al
Qurtubi kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua amekubaliana na Fa’al
hua hakuhusiani na njia za kubashiria. Kwani Fa’al hua ni kuangalia kutokana na
neno jema ambalo mtu analisikia pale anapokua anaumwa, kwa mfano: ‘Ya Salim
ambalo humaanisha ‘Ewe uliesalimika na kua mzima na mwenye Afya’ na hivyo
mtu hua ni mwenye kuangalia kutokana na kusikia hali yake kutokana na
kuambiwa kua ni mwenye afya na hivyo hua ni mwenye matumaini ya kupona
haraka.
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakukubaliana kuhusiana na
kuangalia kuhusiana na hali ya ubaya wa kitu hali ambayo hua inajulikana kama
Tiyara ambayo hua ni kuangalia kutokana na Ndege anaeruka au Mwanamke
anaepita, n,k. Kwani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua ni mwenye
kupenda kushikamana na matumaini na kuangalia jambo kulingana na mtizamo
wa muonekano mzuri wa jambo husika na wala si kulingana na mtizamo wa
muonekano mbaya wa jambo husika.’
Ambapo anasema Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alikua akitufundisha sisi kufanya Istikhara katika kila jambo,
kama vile alivyokua akitufundisha Qur’an kwani alikua akisema: ‘Wakati mmoja
wenu anapokua na nia ya kufanya jambo, basi na asali Rakaa 2 zisizokua za Fardhi
na kisha aseme maneno ya Dua (ifuatayo):
170
الل َّهُم َّ إنيِّ أَسْ تَخِ يرُكَ بِعِلْمِ كَ , وَأَسْتَقْ دِرُكَ بِقُدْ رَتِكَ , وَأَسْ أَلُكَ مِ نْ فَضْ لِكَ الْعَظِيِم
فَإِن َّكَ تَقْدِرُ وَلا أَقْدِرُ, وَتَعْلَمُ وَلا أَعْلَمُ, وَأَنْتَ عَلامُ الْغُيُوبِ , الل َّهُ م َّ إنْ كُ نْ َت
تَعْلَمُ أَن َّ هَذَا الأَمْرَ (هنا تسمي حاجتك) خَيْرٌ ليِ فيِ دِينيِ وَمَعَاشِ ي وَعَاقِبَةِ
أَمْرِي أَوْ قَالَ : عَاجِ لِ أَمْرِي وَآجِ لِهِ, فَاقْدُرْهُ ليِ وَيَسِّرْهُ ليِ ثمُ َّ ابَرِكْ ليِ فِيهِ, الل َّهُ َّم
وَإِ نْكُنْ ت تَ َ عْلَمُ أَن َّ هَذَا الأَمْرَ (هنا تسمي حاجتك) شَر ٌّ ليِ فيِ دِينيِ وَمَعَاشِ ي
وَعَاقِبَةِ أَمْرِي أَوْ قَالَ : عَاجِ لِ أَمْرِي وَآجِ لِهِ, فَاصْرِفْهُ عَنيِّ وَاصْرِفْنيِ عَنْهُ وَاقْدُرْ ليِ
الخَْيْرَ حَيْثُ كَانَ ثمُ َّ ارْضِنيِ بِهِ
‘Ya Allah, hakika mimi natafuta msaada wako kwa kupitia katika Ilm yako,
natafuta msaada wako kupitia katika uwezo wako, natafuta msaada wako kupitia
katika fadhila zako, kwani kwa hakika wewe ni mwenye kujua kile nisichokijua
mimi, ni mwenye kujua yaliyofichikana, Ya Allah kama unajua juu ya jambo hili
(Hapa unataja jambo lako) lina kheri kwangu, kwa dini yangu na mwisho wa khatma
yangu, basi nipe uwezo nalo na unirahisishie juu yake, na tia baraka ndani yake.
Lakini kama unajua kua jambo hili (Hapa unataja jambo lako) halina wema juu
yangu na kwa dini yangu na kwa riziki yangu na mwisho wangu basi niepushe nalo
jambo hili na nipe uwezo juu ya lile lililo bora nami, kutoka kokote kule
litakalokuwepo na nitie ridhaa juu yake.’’
Aya pia imezungumzia kuhusiana na kuruhusika kuliwa vilivyoharamu pale inapokua
kuna ulazima wa kufanya hivyo kwani aliulizwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam:
‘Jee ni wakati gani vile vilivyo haramu vinaweza kua halali?’ Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akajibu: ‘Pale inapokua huna chakula cha Mchana, na ukakosa cha
Jioni, na ikawa huwezi kupata hata mboga za Majani basi unaweza kula.’
Na anasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hakika Allah anapenda
anaporuhusu kitu basi kikubalike kama vile anavyochukia kuasiwa’ (Sahih Ibn
Hibban)
Ambapo ili mtu awe ni mwenye kuruhusika kula kisichoruhusiwa basi inabidi awe katika
mazingira ya hali zifuatazo;
171
1-Mtu huyo lazima awe katika hali isiyokua ni ya kupata msaada na hivyo inambidi
ale kwa sababu hana njia nyengine ya kufanya ya kuokoa maisha yake na ya
wanaomtegemea.
2-Mtu huyo lazima awe hana nia ya kuvunja sharia za Allah Subhanah wa Ta’ala
kutokana na kula kwake huko kwani anfanya hivyo kwa sababu hana njia nyengine.
3-Mtu inapombidi kula chakula ambacho hakiruhusiwi kula basi hatakiwi kula
chakula hicho mpaka akashiba yaani anatakiwa ale kidogo tu kwa ajili ya
kupunguza njaa tu.
Hivyo ingawa Damu imeharamishwa lakini kwa upande mwengine basi tunaona kua sio
Damu yote iliyoharamishwa kwani amesema Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu Anhu
kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu A’layi wa Salam kua: ‘Aina mbili za Maiti
zimehalalishwa juu yangu ambazo ni Samaki na Nzige, na aina mbili za Damu
zimehalalishwa juu yangu ambazo ni Ini na Wengu.’(Mishkat Al Anwar)
Hivyo tunapozungumzia kuhusiana na Uhalali wa umwagaji wa damu ya mnyama
anaechinjwa kukubalika kuliwa hua ni kufanya Ibada ya kuonesha Shukran mbele ya
Allah Subhanah wa Ta’ala kwa ajili ya kutujaalia Nyama ya mnyama huyo kua ni
chakula chetu basi tunaona kua Wanazuoni wanakubaliana kua ili mnyama huyo awe
halali kuliwa na Muislam basi inabidi kuwepo na utekelezwaji wa Masharti muhimu
matano yafuatayo:
1-Tasmiyah – yaani kutajwa kwa Jina la Allah Subhnah wa Ta’ala katika wakati wa
kuchinjwa kwa Mnyama huyo.
2-Kumsalia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
3-Kumuelekeza Kibla Mnyama huyo wakati wa Kumchinja.
4-Takbir – yaani kusema Allahu Akbar.
5-Kuomba Dua ya kukubaliwa kwa Ibada hio ya kuchinja.
(Imam Shihab Ad Din Ahmad Ibn Husein Ibn Ahmad Abu Shujaa Al Isfahani katika Ghayat
At-Taqrib Fi Fiqh Al Shafii)
Ambapo ingawa tunapozungumzia kuhusiana na Tasmiyah basi tunaona hii ni kutokana na
uthibitisho wa ile aya isemayo:
﴿فَكُلُواْ ممِ َّا ذُكِرَ ٱسْمُ ٱهلل َِّ عَلَيْهِ إِن كُ نتُمْ آبِ َ تِهِ مُؤْ مِ نِينَ ﴾
Fakuloo mimma dhukira ismu Allahi AAalayhi in kuntum bi-ayatihi mu/mineena
(Surat Al Anaam 6:118)
172
Tafsir: Na Kuleni kile ambacho kimetajiwa Jina la Allah juu yake kama kweli nyinyi
ni wenye kuamini aya zetu.
Na pia kutokana na pale aliposema tena Allah Subhnah wa Ta’ala kua:
﴿وَلاَ أتَْكُلُواْ ممِ َّا لمَْ يُذْكَرِ ٱسْمُ ٱهلل َِّ عَلَيْهِ وَإِن َّهُ لَفِسْقٌ وَإِن َّ ٱلش َّيَاطِينَ لَيُوحُ ونَ إِلىَۤ
أَوْ لِيَآئِهِ مْ لِيُجَ ادِلُوكُ مْ وَ إِنْ أَطَعْتُمُوهُمْ إِ ن َّكُمْ لَمُشْ رِكُونَ ﴾
Wala ta/kuloo mimma lam yudhkari ismu Allahi AAalayhi wa-innahu lafisqun wainna
alshshayateena layoohoona ila awliya-ihim liyujadilookum wa-in
ataAAtumoohum innakum lamushrikoona (6:121)
Tafsir: Na wala msile kile ambacho hakikutajiwa Jina lake juu yake, kwani ni Dhambi
na uasi na kwa hakika Shaytani huwanongo’neza marafiki zake kukugombanisheni
na kama mkiwatii basi mtakua ni washirikina.
Ambapo Wanzuoni wanasema kua asili ya kushushwa kwa aya hizi zenye amrisho hili
basi ni kutokana na kua kuna baadhi ya Wauza Nyama wa Makkah, waliposilimu walikua
wakishukiwa na Waislam kua walipokua wakichinja basi walikua wakitaja majina ya
Miungu yao ya zamani ndani ya Nyoyo zao. Hivyo Waislam wakasita kununua Nyama
katika Maduka yao ya kuuzia Nyama.
Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akashusha aya iamrishayo kutamkwa kwa jina la
Allah katika kuchinja, na hivyo amrisho hili kua ni sharti litakalowapelekea wenye
Maduka hayo ya Nyama wasiwe ni wenye kutaja jina la Miungu wengine. Na hata kama
Wauza maduka hao wa Nyama au wachinjaji hao wakiwa si Waislam lakini wakataja jina
la Allah Subhanah wa Ta’ala katika kuchinja kwao.
Kwani kwa upande wa Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, Imam
Mujahid Ibn Sulayman, Ikrimah Mawla Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, Imam
Abd Rahman Al Suddi na wengineo basi wanasema kua aya ya Surat Al Maidah 5:5
imebainisha kua Nyama iliyochinjwa na Mayahudi na Wakristo hua ni halali kwa
Waislam pale iliposema:
173
﴿ٱلْيَوْمَ أُحِ ل َّ لَكُمُ ٱلط َّيِّ بَاتُ وَطَعَامُ ٱل َّذِينَ أُوتُواْ ٱلْكِتَابَ حِ ل ٌّ ل َّكُمْ وَطَعَامُكُمْ حِ ل ٌّ
له َُّمْ وَٱلْمُحْصَنَاتُ مِنَ ٱلْمُؤْمِنَاتِ وَٱلْمُحْصَنَاتُ مِنَ ٱل َّذِينَ أُوتُواْ ٱلْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ
إِذَآ آتَيْتُمُوهُن َّ أُجُورَهُن َّ محُْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِ ينَ وَلاَ مُت َّخِ ذِ ي ۤ أَ ْخدَانٍ وَمَن يَكْفُْر
بِٱلإِيمَانِ فَقَدْ حَبِطَ عَمَلُهُ وَهُوَ فىِ ٱلآخِ رَةِ مِنَ ٱلخَْاسِ رِينَ ﴾
Alyawma ohilla lakumu alttayyibatu wataAAamu alladheena ootoo alkitaba hillun
lakum wataAAamukum hillun lahum waalmuhsanatu mina almu/minati
waalmuhsanatu mina alladheena ootoo alkitaba min qablikum idha
ataytumoohunna ojoorahunna muhsineena ghayra musafiheena wala
muttakhidhee akhdanin waman yakfur bial-eemani faqad habita AAamaluhu
wahuwa fee al-akhirati mina alkhasireena (Surat Al Maidah 5:5)
Tafsir: Leo mmehalalishiwa kila kilicho kizuri na kisafi, na chakula chao (watu wa)
Ahl al Kitab ni halali kwenu na chakula chenu ni halali kwao, kama vile (ilivyokua
halali kwenu) Wanawake wasafi walioamini na Wanawake wasafi wa watu wa Ahl al
Kitab wa kabla yenu, pale mtakapowapa ujira (mahari) wao mkiwa ni wenye kutafuta
usafi na wala si wenye kuendekeza matamanio na wala mkiwa hamkuwachukua kua
ni wapenzi wa siri na atakaeikufuru imani, basi amali zake hua zimepotea na katika
akhera atakua ni miongoni mwa waliokula hasara.
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din, Sultan Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi
kuhusiana na aya hii kua: ‘Ili kuifaham aya hii (Surat Al Maidah 5:5) basi inabidi
uangalie aya iliyofuatia kabla ya aya hii (Surat Al Maidah 5:3) ambayo imesemwa
ndani yake:
﴿ٱلْيَوْمَ يَئِسَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ مِن دِينِكُمْ فَلاَ تخَْشَوْهُمْ وَٱخْشَوْنِ ٱلْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُ مْ
دِينَكُمْ وَأَتمَْمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتىِ وَرَضِيتُ لَكُمُ ٱلأِسْلاَمَ دِيناً فَمَنِ ٱضْطُر َّ فىِ مخََْمصَةٍ
غَيْرَ مُتَجَانِفٍ لإِثمٍْ فَإِن َّ ٱهلل ََّ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Alyawma ya-isa alladheena kafaroo min deenikum fala takhshawhum waikhshawni
alyawma akmaltu lakum deenakum waatmamtu AAalaykum niAAmatee
174
waradheetu lakumu al-islama deenan famani idhturra fee makhmasatin ghayra
mutajanifin li-ithmin fa-inna Allaha ghafoorun raheemun(Surat Al Maidah 5:3)
Tafsir: Leo hii Wasioamini wote wameishiwa na matumaini juu ya Dini yenu, hivyo
msiwe na khofu nao, bali kuweni na khofu nami. Leo hii nimeikamilisha Dini yenu,
nimekamilisha fadhila zangu juu yenu na nimeuchagua Uislam kua ndio Dini yenu.
Lakini kwa yule ambae atakumbana na Njaa kali (basi anaweza kula hivyo
vilivyokatazwa), bila ya (kua ni mwenye) kuelemea kwenye dhambi, na kwa hakika
Allah ni mwingi wa Kusamehe na ni mwingi wa Rehma.
Hivyo Mujaddid Ad Din, Sultan Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi anamalizia
kwa kusema kua : ‘Ambapo fadhila zilizozungumziwa hapa ni juu ya Dini na kila
kitu kinachohusiana na Dini, na hivyo basi Allah Subhanah wa Ta’ala
anatubainishia kua pia ametukamilishia fadhila za kila kitu tunachokihitaji’
Na kwa upande wa Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari basi yeye anasema
kua: ‘Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu basi yeye alisema kua: ‘Msile vile
ambavyo vilivyochinjwa na Banu Taghrib kwani mimi nnaamini kua wao
hawakuchukua chochote kutokana na Ukristo isipokua Kulewa.’
Na kulingana na mtizamo wa Abu Darda Radhi Allahu Anhu, Ubaidah Ibn Samit Radhi
Allahu Anhu, Imam An Nakhai, Imam Sufyan Ath Thawry, Imam Abu Hanifa, Imam
Malik n.k basi ni kua Nyama iliyochinjwa na watu wa Ahl al Kitab hua ni Haram pale
inapokua hawakutaja jina la Allah Subhanah wa Ta’ala katika wakati wa kuchinja kwao.
Lakini pia kwa upande mwengine basi pia kuna ile hadith isemayo kua: ‘Amesema Aisha
Radhi Allahu Anha kua: ‘Kuna watu walikuja kwa Rasul Allah Salallau A’layhi wa
Salam ambao walisema kua: ‘Ya Rasul Allah (Salallahu Alayhi wa Salam) kuna
watu miongoni mwa Waarabu, ambao walitupa sisi Nyama ambayo hatujui kama
waliitamkia Jina la Allah juu yake ama la.’ Rasul Allah Salallau A’layhi wa Salam
akasema: ‘Itamkieni Jina la Allah Kisha ileni.’’’(Sahih Bukhari na Muslim, Imam Taqiy
ud Din Al Hisni Al Husayni katika Kifayat Al-Akhyar)
Hivyo tunapozungumzia kuhusiana na suali la Tasmiyah katika kuchinja na kumwaga Damu
ya Mnyama kwa njia za Kiislam basi tunaona kua kuna hali tano zifuatazo:
1-Kichinjo cha aliesema Tasmiyyah, ambae Dhabiha yake ni halali wa Makubaliano ya
Ijmaa.
2- Kichinjo cha aliesahau Tasmiyyah ambae Dhabiha yake ni Halali kulingana na Mtizamo
wa Madhhab ya Imam Al Shafii, Hanafi na Madhhab ya Imam Malik.
3-Kichinjo cha yule ambae hakusahau Tasmiyyah lakini kwa hakufanya Makusudi.
175
Ambapo kwa upande wa Madhhab ya Imam Al Shafii, basi anasema Mujaddid al Din Imam
Muhammad Idris Al Safii kua: ‘Wakati Muislam anapomwachia Mbwa wake au Ndege
wake aliefundishwa kuwinda, basi mimi hua nnapendelea (Tasmiyah Mustahab) kua
alitamke jina la Allah Subhanah wa Ta’ala. Lakini hata kama akisahau kulitamka na
kisha Mnyama wake huyo akamuua Mnyama anaewindwa basi anaweza kumla. Na hii
ni kwa sababu hata mtu akisahau kulitaja jina la Allah wakati anapochinja basi hua
anaruhusika kumla Mnyama huyo, kwa sababu Muislam hua ni mwenye kuchinja kwa
ajili ya Allah, hivyo hata akisahau kutaja jina la Allah basi hamna tatizo na hivyo basi
Mnyama alieuliwa na muwindaji Muislam kwa kutumia Mnyama wake hua sawa na
mauaji yanayofanywa kwa kuchinja kwa mkono’(Kitab Al Umm)
Kisha Mujaddid Ad Din Imam Muhammad Idris Al Shafii akamalizia kwa kusema: ‘Kama
ikiwa Muislam amesahau kutaja jina la Allah basi Mnyama wake aliechinja
anaruhusika kuliwa, lakini kama akiwa amewacha kulitaja kwa makusudi basi kichinjo
hicho hua hakifai kuliwa.’
Ambapo kwa upande mwengine basi kutokana na kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alisema katika Hadithi tuliyoiangalia kua ‘Itamkieni Jina la Allah Kisha ileni.’ na Imam
Al Shafii amesema kua Tasmiyyah ni Mustahab basi anasema Imam Abu Hasan Ali Ibn
Muhammad Ibn Habib Al Mawardi Al Shafii: ‘Ash Shafii amesema kua: ‘Wakati
Muislam anapomwachia Mbwa wake aliefundishwa kuwinda, basi mimi hua
nnapendelea (Tasmiyah Mustahab) kua alitamke jina la Allah Subhanah wa Ta’ala.
Lakini hata kama akisahau kulitamka na kisha Mnyama wake huyo akamuua Mnyama
anaewindwa basi hamna tatizo juu yake, na hii ni kwa sababu kutaka jina la Allah kwa
mnyama anaewindwa au anaechinjwa ni Sunna na wala si Wajib, na hivyo kama mtu
akiwa hakulitaja kwa makusudi au kwa kusahau basi Kichinjo chake ni Halali, na huu
ndio mtizamo wa Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu na Abu Hurayra Radhi
Allahu Anhu, na miongoni mwa Wanafiqh wa Mwanzoni wenye Mtizamo huu pia ni
Ataa na Malik’(Al Hawi Al Kabir Fii Madhhab Al Imam Al Shafii)
Ambapo kwa upande wa Shaykh ul Islami Imam Abu Zakarriyah Sharraf An Nawawi basi
anasema kua : ‘Tasmiyyah ni Mustahab katika kuchinja au katika kutumia kifyatulio
katika wakati wa Kuwinda, au katika wakati wa kumtuma Mbwa au kama yeye. Na
kama Tasmiyyah ikiachwa kwa makusudi au kwa kusahauliwa basi Dhabiha inakua
Halali na kama ikiachwa kwa makusudi basi inakua ni Makruh, na huo ndio mtizamo
sahih wa Madhhab ukiwa na hali ya Makruh inayopendekezwa (Tanzih) bila ya kua na
Makruh ya kuharamishwa (Tahrim)’
Na akasema tena Shaykh ul Islami Imam Abu Zakarriyah Sharraf An Nawawi kua: ‘Katika
Madhhab yetu kufanya Tasmiyyah hua ni Sunnah katika kila jambo, hivyo kama
ikisahauliwa au ikiachwa kwa makusudi basi kichinjo hua halali na hakuna kosa juu
yake.’
176
Ambapo kwa upande wa Imam Muhammad Ibn Ahmad Al Khatib Ash Shirbini basi yeye
anasema: ‘Na Tasmiyyah si Wajibu, na mtu kama akiiwacha kwa makusudi au kwa
kusahau basi (Kichinjo) hua ni Halali’(Al Mughni Al Muhtaj)
4 - Kichinjo cha yule ambae hakuitaja Tasmiyyah kutokana na kuona kua haina maana
wala uzito wowote (Istikhaf).
Hapa inabidi tujue kuhusiana na maana ya neno Istikhfaf ambalo maana yake hua ni ile
inayotokana na neno Khaffa ambao hua linamaanisha Kua na Ufaham Mdogo, Kutokua na
Uzito, Kuchukulia Jambo kua ni Jepesi na pia humaanisha Kudharau jambo kwa wepesi wake.
Ambapo neno Istikhfaf hua linaenda sambamba kimaana na neno Istihza ambalo hua
linatokan na neno Hazza ambalo hua linamaanisha Kukichukulia kitu kwa wepesi, Kutokipa
kitu Uzito na Kutokitilia maanani na pia humaanisha Kufanya Mzaha.
Hivyo kwa upande wa Madhhab ya Imam Al Shafii basi neno Istikhfaf na neno Istihza hua
yanatumika sambamba kimaana kumaanisha kukichukulia kitu kwa wepesi, yaani kama vile
ambavyo Shaykh ul Islami Imam Shams Ad Din Al Ramli aliposema kua: ‘Imam An
Nawawi anasema katika Minhaj yake kua: ‘Kuritadi hua kunamaanisha kukata
mawasiliano na Uislam kwa nia, kwa kauli au kwa kitendo cha kukufuru, bila kuangalia
kama mtu alisema kauli ya kukufuru kwa Istahzai, au kutokana na Ukaidi wake tu au
kutokana na kuamini’ yaani kama vile mtu anapoambiwa kua Kata Kucha zako, nae
akajibu kua: ‘Sitokata Kucha hata kama ni Sunnah’’
Hivyo mfano huu hua ni sawa na mchinjaji atakaposema: ‘Sitosema Tasmiyyah japo kua ni
Sunnah’ na hivyo mtu atakaefanya hivyo basi basi atakua ni mwenye kosa la kufanya Istihzai
ambayo pia ni Istikhfaf na hivyo hali yake hua ni sawa na ni mwenye kufanya Kufr kutokana
na kulichukulia jambo hili kwa wepesi na kua ni la mzahaha na lisilokua na uzito wala maana
na hivyo basi kichinjo chake hicho hua si Halali ni Haramu na hakiruhusii kuliwa.
5- Kichinjo cha yule ambae ndie kawaida yake kutoitaja Tasmiyyah (Tahawun)
Neno Tahawun linatokana na neno Tawahin ambalo maana yake hua ni Kinu cha kusagia
Nafaka ambacho kua kinasaga kutokana na Mzunguko wake wa kijirudia rudia, hivyo neno
Tawahun hua maana yake hua ni mtu mwenye kawaida ya kutofanya kitu fulani mara kwa
mara kwa kurudia kutofanya kila wakati.
Hivyo tunapozungumzia Muislam ambae hua ni mwenye kawaida ya Kuchinja bila ya
kufanya Tasmiyyah ambapo hii hukmu yake kwa upande wa Madhab ya Imam Al Shafii
basi hua inaruhusika kula kichinjo chake, kama vile ambavyo ilivyoelezewa katika hali
ya tatu ya kichinjo kulingana na uthibitisho wa hadith ya Mama Aisha Radhi Allahu
Anha.
Huo ni mtizamo wa Madhhab ya Imam Al Shafii kuhusiana na kuchinja ambapo kwa
upande mwengine basi tunaona kua Wanazuoni wa Baraza la Wanazuoni wa Fiqh wa
177
Islamic Fiqh Assembly of the Organization Of Islamic Conference basi wao
wamekubaliana kuhusiana na mtizamo wa Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi
Allahu Anhu, Imam Mujahid Ibn Sulayman, Ikrimah Mawla Abd Allah Ibn Abbas, Imam
Abd Rahman Al Suddi ambao wasema kua aya ya Surat Al Maidah 5:5 imebainisha kua
Nyama iliyochinjwa na Mayahudi na Wakristo hua ni halali kwa Waislam pale iliposema:
﴿ٱلْيَوْمَ أُحِ ل َّ لَكُمُ ٱلط َّيِّبَاتُ وَطَعَامُ ٱل َّذِينَ أُوتُواْ ٱلْكِتَابَ حِ ل ٌّ ل َّكُمْ وَطَعَامُكُمْ حِ ل ٌّ
له َُّمْ وَٱلْمُحْ صَنَاتُ مِنَ ٱلْمُؤْمِنَاتِ وَٱلْمُحْصَنَاتُ مِنَ ٱل َّذِينَ أُوتُواْ ٱلْكِتَابَ مِن قَْبلِكُ ْم
إِذَآ آتَيْتُمُوهُن َّ أُجُورَهُن َّ محُْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِ ينَ وَلاَ مُت َّخِ ذِي ۤ أَخْدَانٍ وَمَن يَكْفُرْ
بِٱلإِيمَانِ فَقَدْ حَبِطَ عَمَلُهُ وَهُوَ فىِ ٱلآخِ رَةِ مِ نَ ٱلخَْاسِ رِينَ ﴾
Alyawma ohilla lakumu alttayyibatu wataAAamu alladheena ootoo alkitaba hillun
lakum wataAAamukum hillun lahum waalmuhsanatu mina almu/minati
waalmuhsanatu mina alladheena ootoo alkitaba min qablikum idha
ataytumoohunna ojoorahunna muhsineena ghayra musafiheena wala
muttakhidhee akhdanin waman yakfur bial-eemani faqad habita AAamaluhu
wahuwa fee al-akhirati mina alkhasireena (Surat Al Maidah 5:5)
Tafsir: Leo mmehalalishiwa kila kilicho kizuri na kisafi, na chakula chao (watu wa)
Ahl al Kitab ni halali kwenu na chakula chenu ni halali kwao, kama vile (ilivyokua
halali kwenu) Wanawake wasafi walioamini na Wanawake wasafi wa watu wa Ahl al
Kitab wa kabla yenu, pale mtakapowapa ujira (mahari) wao mkiwa ni wenye kutafuta
usafi na wala si wenye kuendekeza matamanio na wala mkiwa hamkuwachukua kua
ni wapenzi wa siri na atakaeikufuru imani, basi amali zake hua zimepotea na katika
akhera atakua ni miongoni mwa waliokula hasara.
Na pia kulingana na hadith tuliyoiangalia isemayo kua: ‘Amesema Aisha Radhi Allahu
Anha kua: ‘Kuna watu walikuja kwa Rasul Allah Salallau A’layhi wa Salam ambao
walisema kua: ‘Ya Rasul Allah (Salallahu Alayhi wa Salam) kuna watu miongoni
mwa Waarabu, ambao walitupa sisi Nyama ambayo hatujui kama waliitamkia Jina
la Allah juu yake ama la.’ Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema:
‘Itamkieni Jina la Allah Kisha ileni.’’’(Sahih Bukhari na Muslim.)(Imam Taqiy-ud-Din
Al-Hisni Al-Husayni katika Kifayat Al-Akhyar)
Hivyo basi Wanazuoni hao wa Baraza la Wanafiqh la Islamic Fiqh Assembly of the
Organization Of Islamic Conference wamesema katika kikao chao cha 95 (Resolution no
178
95) kua: ‘Inaruhusika Kwa Mgeni wa Kiislam au Muislam anaeishi kwenye Nchi
isiyokua ya Kiislam kula Nyama za Wanyama waliochinjwa na Watu wa Ahl Al
Kitab pale inapokua Wanyama hao ni Halali kuliwa. Hivyo Waislam wanatakiwa
kuhakikisha kua Nyama hio haijachanganyika na vitu ambavyo ni
vilivyoharamishwa katika Uislam, na kuchinjwa kwenyewe pia kuwe kumefanyika
kwa njia za Kiislam’
Hii ni pale inapokua kuna uwezo wa kufuatilia kuhusiana na uchinjaji, lakini inapokua ni
vigumu kuhusiana na kujua kwake basi hali ya uchinjaji hua inachukuliwa kua ni yenye
utata juu yake, kwani haijulikani kua ulikua wa kihalali ama la. Na kutokana na kutokua
na uhakika huo basi, inabidi ihesabiwe kua ulikua ni wa Kihalali…Wallahu Aaalam!
Hio ni kuhusiana na Damu ya Ibn Adam na Damu ya Wanyama wa chakula, hivyo na
tuangalie kuhusiana na Damu ya kimaumble ya Mwanamke ambayo ndio sababu ya
Imraat Imran yaani Hannah Bint Faqudh kua ni wenye kusema kama ilivyosema aya:
﴿إِذْ قَالَتِ ٱمْرَأَةُ عِمْرَانَ رَبِّ إِنىّ ِ نَذَرْتُ لَكَ مَا فىِ بَطْنىِ محَُر َّراً فَتَقَب َّلْ مِنىِّ إِ ن َّكَ
أَنتَ ٱلس َّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ ﴾
Idh qalati imraatu AAimrana rabbi innee nadhartu laka ma fee batnee muharraran
fataqabbal minnee innaka anta alssameeAAu alAAaleemu (Surat Al Imran 3:35)
Tafsir: Na kumbuka aliposema Mke wa Imran: ‘Ewe Mola Wangu, hakika mimi
nimeweka Nadhiri kua Mtoto wangu aliemo tumboni mwangu nimemtolea kwa ajili
ya kukutumikia wewe, hivyo nikubalie kwani kwa hakika wewe ni mwingi wa kusikia
na ni mwingi wa kujua juu ya kila kitu.’
Tunapoiangalia aya yetu hii basi tunaona kua Imraat Imran amedhamiria kumfanya
mtoto wake awe Muharraran. Ambapo neno Muharraran ni neno linalotokana na neno
Harra ambalo hua linamaanisha Kua Huru, Mtu alie huru, Mtu ambae yuko huru
kutokana na Utumwa na hivyo hua ni mwenye kumtumika Allah Subhanah wa Taa’ala
tu. Hivyo neno Muharrarah linamaanisha kua Mtu alie huru kutokana na mambo ya
kidunia kwani ni mtu aliejitolea kwa Ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala peke yake.
Kwa maana hio basi mtoto aliekua akimtaka Imraat Al Imran alikua anatakiwa asiwe ni
mtoto mwenye kua na Adha.
179
ADHA YA DAMU YA KIMAUMBILE YA MWANAMKE.
Anasema Imam Ahmad Ibn Hanbal kua: ‘Amesema Anas Ibn Malik Radhi Allahu
Anhu kua: Mayahudi walikua wakijitenga na Wanawake zao katika kipindi cha
wakati wa siku zao za Mwezi, kiasi ya kua walikua wakikata hataa kukaka nao
pamoja kwenye Meza zao katika wakati wa kula, hivyo Maansari nao wakaathirika
na jambo hilo na wao pia wakaanza kufanya hivyo hivyo kwa wake zao. Hivyo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaulizwa kuhusiana na jambo hilo na hivyo Allah
Subhana wa Ta’la akamshushia Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam aya hii
ambayo inasema:
﴿وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ ٱلْمَحِ يضِ قُلْ هُوَ أَذًى فَٱعْتَزِلُواْ ٱلنِّسَآءَ فىِ ٱلْمَحِ يضِ وَلاَ
تَقْرَبُوهُن َّ حَتى َّ ٰ يَطْهُرْنَ فَإِذَا تَطَه َّرْنَ فَأْتُوهُن َّ مِنْ حَيْثُ أََمرَكُمُ ٱهلل َُّ إِن َّ ٱهلل ََّ يحُِ ُّب
ٱلت َّو َّابِينَ وَيحُِب ُّ ٱلْمُتَطَهِّرِينَ ﴾
Wayas-aloonaka AAani almaheedhi qul huwa adhan faiAAtaziloo alnnisaa fee
almaheedhi wala taqraboohunna hatta yat-hurna fa-idha tatahharna fa/toohunna
min haythu amarakumu Allahu inna Allaha yuhibbu alttawwabeena wayuhibbu
almutatahhireena (Surat Al Baqara 2:222)
Tafsir: ‘Na wanakuuliza kuhusiana na Hedhi waambie kua: ‘Ni Adha, hivyo kaeni
mbali na Wanawake wanapokua katika Hedhi na msiwakaribie mpaka wawe tohara.
Na kisha watakapojitoharisha basi waingilieni katika sehemu aliyokuamrisheni Allah,
kwani kwa hakika Allah anawapenda wenye kufanya toba na wenye kujitoharisha.’’
Hii ni miongoni mwa aya 2 ambazo zimetumia neno Mahiidh ambalo ni lenye kutokana
na neno Hadhat ambalo hua linamaanisha Kua katika Njia yake, Kua katika Siku zake,
Kua katika Hedhi, Kutoka Damu kwenye Fuko la Uzazi, hivyo neno Mahiidh hua
linamanisha Wakati wa Kutoka Damu, Sehemu ya Kutoka Damu.
Ambapo Shaykh Al Akbar Imam Muhyi Ad Din Abu Bakar Ibn Arabi amesema kua:
‘Kuna aina nane za majina ya Mwanamke mwenye Hedhi ambayo ni Haidh, Aarik,
Farik, Tamis, Daris, Kabir, Dhahik na Tamith.’
180
Na pia ikatumia neno Adha ambalo hua linamaanisha Kuudhi, Kuumiza, Kuharibika,
Kunyanyasika, Kudhuru, Kusababisha Maumivu ya Mwili na pia humaanisha
Kusababisha maumivu ya Kihisia.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala ametumia neno Adha katika aya hii kwa sababu kama
linavyoonesha maana yake neno hilo katika mitizamo tofauti basi ndio hali anayokua
nayo Mwanamke wakati akiwa kwenye Hedhi na hii ni kwa sababu kama tulivyosema
hapo kabla kuhusiana na Moyo wa Ibn Adam kua ni wenye kusababisha uzalishwaji wa
kemikali mbali mbali ikiwemo zile ambazo husababisha hisia nzuri kwa Ibn Adam
ambazo zinazojulikana kama Dopamine, Oxytocin, Endorphines, Seratonin,n.k ambazo
hua na jukumu la kukamilisha sifa ya maumbile ya asili ya kila mtu yanayotokana na
maana ya neno Al Ins. Neno Al Ins linatokana na neno Anisa ambalo maana yake hua ni
kua na Mazoea, Kupenda, Kua na Umoja kijamii, au Kushikamana pamoja.
Hivyo kila Kemikali hizi zikizalishwa kwa wingi basi Mwili wa Ibn Adam husika hua na
hisia za kujisikia vizuri zaidi, raha zaidi, kua na furaha zaidi na pia kutaka kua karibu na
Ibn Adam wenzake zaidi. Na kila zikipungua ndani ya mwili basi hali ya Ibn Adam
husika hua na hali ya kinyume chake, yaani mtu hua ni mwenye kutaka kua peke yake,
hua mnyonge, mwenye huzuni, mwenye kukerea kirahisi, asiekua na furaha n.k.
Na tunapozungumzia wakati wa Mahiidh kama ilivyotajwa kwenye aya yaani katika
kipindi hiki cha wakati wa Hedhi basi Maumbile ya mwili wa Mwanamke hua ni yenye
kupunguza uzalishwaji wa kemikali za Estrogen. Progesteron na Serotonin na hivyo
kemikali hizi zinapokua zimepungua ndani ya mzunguko wa Damu basi mwili wa
Mwanamke husika hua na mabadiliko ya kihisia yanayosababishwa hisia maumivu ya
kuumwa na Kichwa, Mgongo, Tumbo, Kutopata Usingizi vizuri, Maumivu ya Maziwa
kutokana na kua ni yenye kuvimba, n.k hali ambayo humpelekea mwanamke husika kua
ni mwenye kukosa raha na utulivu wa kihisia na kimwili.
Katika aya hii basi Allah Subhnah wa Ta’ala anatubainishia kwa kusema Huwa adhan
yaani ‘Ni Adha’ Na hivyo moja kwa moja kutuonesha kua anatutahadharisha kua Hiki
ni kitu ambacho kina madhara ndani yake na hivyo kua ni mwenye kututayarisha na
amrisho litakalofutia baada ya tahadhari hio ambalo linasema faiAAtaziloo alnnisaa fee
almaheedhi wala taqraboohunna hatta yat-hurna yaani ‘Hivyo kaeni mbali na
Wanawake wanapokua katika Hedhi na msiwakaribie kwa kuwaingilia mpaka wawe
tohara.’
Na katika amrisho hili basi tunaona kua ndani yake mna katazo lenye neno La Taqrabu
ambalo ni lenye kutokana na neno Qaraba ambalo hua linamaanisha Kukaribia, Kufikia
Karibu, Kua na Ukaribu katika Uhusiano au Katika Mahusiano iwe ya Udugu, ya Urafiki
au ya Kimapenzi.
181
Ambapo neno Qaraba ndio lililotoa neno Qurban ambalo humaanisha Mnyama
anaemwagwa Damu yake kwa kuchinjwa kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala kwa
ajili ya Kuutafuta Ukaribu wa Allah Subhanah wa Ta’ala.
Hivyo basi katazo ili halimaanishhi kua Waislam Wanaume wanatakiwa Kujitenga na
kukaa mbali na Wake zao, au Waislam wanawake wanataiwa wakae mbali na Waume
zao, kwani maana ya La Taqrab inayotumika hapa ni ile yenye maana ya kua
‘Msiwakaribie Kiuhuisano wa Kimapenzi wa Kuingiliana Kimwili’
Na ndio maana baada ya kushushwa aya hii basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasema: ‘Kila kitu kinaruhusika isipokua kuwaingilia tu.’ Hivyo Mayahudi
waliposikia kuhusiana na aya hii basi wakasema: ‘Hakika hii ni tofauti na kila kitu
kuhusiana na vile tunavyofanya sisi’
Baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kusema hivyo basi Usayd Ibn Hudayr
Radhi Allahu Anhu na Abbad Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu basi wakamuuliza Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kwa kusema kua: ‘Kama ikiwa Mayahudi wamesema hivyo
(kua wanajitenga na wake zao wanapokua katika siku zao na hawakai nao hata katika
chumba kimoja), hivi kwanini na sisi tusiruhusiwe kuwaingilia Wanawake wetu ili
kuwachochea zaidi na kuwatia wazimu zaidi? (Kua sisi tuko tofauti na nao)’
Waliposema maneno hayo basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikasirika sana
kiasi ya kua walidhani kua huenda akaamua kuwaadhibu. Hivyo hapo hapo wakatoka nje
na kisha wakarudi kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kumletea zawadi ya
Maziwa ili kumpunguzia hasira zake, na kisha wakaondoka tena. Na walipoondoka basi
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akatuma watu wakawaite Usayd na Abbad Radhi
Allahu Anhum na kisha akakaa na kunywa nao Maziwa hayo ili wasidhani kua
amewakasirikia.
Ambapo tunaporudi katika katazo hili basi pia tunaona kua limewataka Wanaume
kutokua na uhusiano wa kimpenzi na Wake zao wanaokua katika Hedhi kwa sababu ya
Madhara yake lakini halikusema ni nani anaedhurika na hivyo halimaanishi kua ni
Wanaume tu ndio wanaodhurika na Mahiidh au ni Wanawake tu, bali hii inamaanisha
kua Madhara haya yanawadhuru wote pale watakapokaribiana kwa kuingiliana kimwili
katika wakati huo.
Na ili tufahamiane vizuri basi bora na tuangalie kile kinachotokea katika mwili wa
Mwanamke katika wakati huo, ambae kimaumbile hua na Mifuko ya Mayai ya uzazi
inayojumuisha sehemu ya juu ya viungo vya Uzazi vya Mwanamke. Mifuko hii ya mayai
ya Uzazi ambayo iko miwili hua imeunganishwa kwa mrija au njia zilizo juu ya Mfuko
wa Uzazi, kwa kulia kwake na kwa kushoto kwake hua ni yenye kutoa Yai kila mwezi
mara moja ambako kunasababishwa na Kemikali zinazozalishwa na sehemu ya Ubongo
182
inayosimamia mfumo wa Uthibiti wa Kemikali mbali mbali za Mwilini ambao unaitwa
Pituitary Gland ambazo huzitaarifu Kemikali zilizopo juu ya Mifuko ya Mayai ziitwazo
Estrogen na Progesteron ambazo huzalishwa zaidi katika kipindi kwa Yai la Uzazi kwa
ajili ya kufanya mandalizi ya kuachia yai la Uzazi kuanzia siku 13-15 baada ya mzunguko
wa Hedhi iliyotangulia hapo kabla.
Hivyo Yai hilo linapoachiwa hua linaanza safari yake kupitia kwenye mirija ya Usafiri
wa Yai la Uzazi kuelekea kwenye Mfuko wa Uzazi kwa ajili ya matayarisho ya kuandaa
mazingira ya kulea mtoto, kwani kama yai hilo likikutana na yai la Uzazi la Mwanamme
basi Mfuko wa Uzazi hulipokea na kuligandanisha na Ukuta mpya maalum wa Mfuko
wa Uzazi wa Mwanamke ambao nao pia hua umeandaliwa baada ya kuongezeka
uzalishwaji wa kemikali za Estrogen ambazo hujenga Ukuta mpya huo na Progesteron
ambazo huuimrisha Ukuta kwa ajili ya matayarisho ya kumlea na kumkuza mtoto ndani
ya mfuko wa Uzazi.
Hivyo katika wakati huu ukuta huo wa Mfuko wa Uzazi wa Mwanamke hua na maumbile
ya kua na ukuta kama ukungu laini wa Damu iliyotolewa na mishipa ya Damu ya ukuta
wa Fuko la Uzazi ambayo ni nyepesi na isiyoweza kuganda ambayo kwa kawaida wingi
wake hua hauzidi vijiko vitatu, na hua na idadi ndogo ya kemikali za Protein, Chuma,
Prothromin, Thrombin na Fibrinogen, na hivyo hua tofauti na damu ya kawaida kwani
hii Damu hua ni maalum kwa ajili ya kusimamia jukumu la kulikuza yai la uzazi la
Mwanamke lililokutanishwa na yai la Mwanamme kwa ajili ya kupatikana mtoto.
Ambapo ili yai la Uzazi la Mwanamme likutane na yai la Uzazi la Uzazi la Mwanamke
wakati linapomwagwa ndani ya sehemu za Uzazi za Mwanamke basi inabidi Mayai ya
Mwanamme husika yawe na wingi usiopungua mayai milioni 15 hadi milioni 250 kwa
mililita moja ya kila mmwagiko mmoja wa Manii na hua na kasi ya kuogelea isiyopungua
micrometer 25 kwa sekunde moja.
Na hii ni kwa sababu ndani ya Mfumo wa njia ya Uzazi ya Mwanamke hua kuna kemikali
zenye acid ambazo kazi yake ni kusimamia ulinzi na uimarishaji wa mfumo huo wa
Mwanamke ili Viungo vya Uzazi vya Mwanamke visidhurike. Hivyo Mwanamme
anapomwaga mayai yake, basi hali hua kama majeshi ya upande wa Mwanamme na
upande wa Upande wa Mwanammke yamekutana na kukabiliana kwa mapigano
uwanjani, yaani Mayai ya Mwanamme yanatakiwa kulikimbilia Yai moja la
Mwanammke lililotolewa kwenye mfuko wa Mayai ambalo linakimbilia kuja kwenye
Mfuko wa Uzazi.
Hivyo katika mapigano hayo, kemikali za acid za ulinzi wa sehemu ya Uzazi wa
Mwanamke ambazo kimaumbile hua na mtizamo wa kua kila kitu kinaingia kutoka nje
ya mwili wake hua kina madhara na hivyo hakitakiwi kifike kwenye Mfuko wa Uzazi wa
Mwanamke na inabidi kizuiwe kisisababishe madhara, basi hua zinapingana na Mayai ya
183
Uzazi wa Mwanamme ambayo mbali ya wingi wake lakini linatakiwa yai litakalowahi
mwanzo tu kuingia kwenye yai la Uzazi la Mwanamke. Hivyo mamilioni kati ya
mamilioni hayo ya mayai ya Mwanamme hua ni yenye kubakia njiani kutokana na
kutofanikiwa kwake, kwani ni mwenye nguvu tu na afya ndie atakaeufikia Mfuko wa
Uzazi wa Mwanamke na ndie atakaelifikia yai la Uzazi la Mwanamke.
Na akilifikia tu basi kwa usalama wake hua ni mwenye kuingiza kichwa chake ndani,
kisha mkia wake hukatika na yai hilo la kike hutengeneza ukuta ili lisiingie ndani yake
yai jengine la Uzazi la Mwanamme, na kama yakiwahi kuingia mawili kwa pamoja basi
yai hilo la uzazi la Mwanamke hua ni lenye kubeba watoto pacha, n.k. Na kama mayai
ya Mwanamme yakiwa kidogo yaani tunazungumzia chini ya milioni 15 kwa kila
umwagaji mmoja au hayana nguvu na kasi basi hua inamaanisha kua Mwanamme husika
hana uwezo wa kupata mtoto.
Tunapoangalia matukio haya ya maumbile ya mfumo wa Uzazi wa Mwanamme na
Mwanamke na purukushani zinazotokea ndani ya Miili yao wakati wa kutafuta Mtoto
basi ndio tunaona maana halisi ya maneno ya ile aya isemayo:
﴿لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلإِنسَانَ فىِ كَبَدٍ ﴾
Laqad khalaqna al-insana fee kabadin (Surat Al Balad 90:4)
Tafsir: Kwa Hakika Tumemuumba Mtu katika Kabad
Ambapo ingawa kwa upande wa Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu, Abd Allah
Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, Imam Mujahid Ibn Sulayman na Ikrimah Mawla Abd
Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi tunaona kua wao wanasema: ‘Neno Kabad
linamaanisha Kusimama sawia, yaani tofuti na wanyama wengine wasioweza
kusimama sawia.’
Lakini pia neno Kabad hua linamaanisha Kujeruhi kwenye Ini, Kumuumiza Mtu mpaka
akasikia Maumivu makali sana, Kukusudia Kitu, Kukumbana na Matatizo, Mapigano,
Purukushani, Kukutana na Kikwazo au Kizingiti, Kua katikati ya mapigano n.k.
Na hivyo basi kwa mtizamo huo hua unaamaanisha kua Mtu ameumbwa akiwa katika
hali ya mapigano tangu katika kutafutwa kwake Mtoto mpaka kupatikana kwake, kukaa
ndani ya fuko la uzazi la mama yake, kutoka ndani ya tumbo la mama yake, kulelewa
kwake mpaka kukua kwake, mpaka kufa kwake hua yuko katika hali ya kupiga hatua
moja hadi nyengine kutoka katika mapigano mbali mbali maishani mwake ikiwemo
mapigano ya kujidhibiti na matamanio ya Nafsi yake.
184
Hivyo Damu ya Hedhi hua ni yenye kumtoka Mwanamke pale inapokua Mfuko wake wa
Mayai ya Uzazi umeachia Yai la kila mwezi ambalo halikuweza kukutana na Yai la Uzazi
la Mwanamme na hivyo Yai hilo hua haliwezi kugandanishwa na Ukuta wa Mfuko wa
Uzazi na hivyo Ukuta wake huo laini wa Ukungu wa Damu uliotayarishwa kwa ajili ya
kulihudumia Yai la Uzazi, Na hivyo mfumo wa Yai la Uzazi huanza kupunguza uzalishaji
wa Kemikali Estrogen za kuukuza Ukuta huo na kupunguza uzalishaji wa kemikali za
Progesterone za kuuimarisha ukuta huo kunakopelekea kubana na kukaza kwa Mishipa
midogo midogo ya Damu ya Ukuta wa Uzazi ambako nako kunakosababisha maumivu
ya tumbo na kushuka kwa joto la Mwili wa Mwanamke husika na kupungua kwa kasi ya
mapigo ya Moyo na kasi ya mzunguko wa Damu.
Na kutokana na matukio haya ya kimwili yanayojumuisha kupunguzwa kwa uzalishaji
wa kemikali zinazouimarisha ukuta huo wa Damu basi ukuta huo hukosa uimara wake
na kidogo kidogo ukuta huo huanza kuporomoka, na kuweka wazi kua hakuna ujauzito,
hivyo na hivyo Ukuta wa Damu na Yai na Maji maji mengine yaliyoandaliwa kwa ajili
ya kuulinda Ujauzito, na hivyo kua vitu vyote hivyo vilivyoandaliwa kwa ajili ya uja
uzito hua havihitajiki tena Mwilini na hivyo inabidi vitoke nje.
Hivyo Damu zilizojumuisha ukuta huo unaoporomoka pamoja na sehemu ya Yai la Uzazi
la Mwanamke ambalo halikufanikiwa kutungwa na Yai la kiume kwa wakati huo huanza
kutoka nje ya Mwili na kujulikana kama Damu ya Hedhi.
Hivyo hii hua ni sehemu ya kimaumbile ya namna Mfumo wa Uzazi wa Mwanamke
unavyojitayarisha kwa ajili ya kuendeleza kizazi, na inapokua hakuna mafanikio hayo
basi Mfumo huo hua ni wenye kujisafisha wenyewe kimaumbile, kwa ajili ya
matayarisho ya kutoa yai jengine la Uzazi katika mwezi unaofuatia na kutayarisha ukuta
mwengine mpya kwa ajili ya kulea yai hilo jipya la Uzazi la Mwanamke husika kama
litakutana na yai la Uzazi la Mwanamme.
Subhnah Allah w Allahu Akbar! Ukiyaangalia haya na kuyatafakar basi ndio unaona
maana ya ile aya isemayo:
﴿لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلإِنسَانَ فيِ ۤ أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ ﴾
Laqad khalaqna al-insana fee ahsani taqweemin (Surat At Tin 95:5)
Tafsir: Kwa hakika tumemuumba mtu katika Taqwiim bora kabisa.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala amesema kua ‘Huwa Adhan aiAAtaziloo alnnisaa fee
almaheedhi wala taqraboohunna hatta yat-hurna yaani ‘Hio ni Adha Hivyo kaeni
185
mbali na Wanawake wanapokua katika Hedhi na msiwakaribie kwa kuwaingilia
mpaka wawe tohara.’
Kwa sababu ya kua hali iko wazi kama tulivyoelezea kua mabadiliko haya ya kimaumbile
hua yanasababisha kukosekana kwa utulivu wa kihisia na utulivu wa kimwili kwa
Mwanamke na kwa baadhi ya Wanawake hua wanapungukiwa na Nguvu pia, na ndio
maana Allah Subhnah wa Ta’ala akawaamrisha kua wasifunge wala wasisali wanapokua
katika Hedhi.
Hivyo tunapoangalia kuhusiana na kukaribiana kimapenzi baina ya Mume na Mke katika
hali ya kawaida bila ya kugusia suali la wakati wa Hedhi basi bila ya shaka ili Mume na
Mke waridhishane kimapenzi basi kwanza lazima kuwe na utulivu baina yao, na
inapotokea kua mmoja wao kua hana utulivu, au hajapata utulivu katika wakati wa
kujitayarisha na tendo la kuingiliana, basi hua ni kinyume na maamrisho ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam.
KUKARIBIANA KIMAPENZI BAINA YA MKE NA MUME KATIKA
UISLAM
Amesema Allah Subhanah wa Ta’ala kua
﴿هُن َّ لِبَاسٌ ل َّكُمْ وَأَنتُمْ لِبَاسٌ له َُّن َّ﴾
Hunna libasun lakum waantum libasun lahunna (Surat Al Baqara 2:187)
Tafsir : Wao (Wake zenu) ni Lîbas kwenu na nyie (Waume zao) ni Lîbas kwao.
Neno Lîbas kwa kiarabu lina maana ya Stara, Hifadhi, Nguo au Vazi, na kama
inavyojulikana kazi ya vazi kua ni kuvaliwa ili kuulinda na kuuhifadhi mwili wa Bani
Adam na athari za nje kama vile jua, baridi, mvua n.k, kusitiri sehemu za siri ambazo ni
aibu kuzionesha, kuupendezesha mwili n,k basi ndio vile vile, wanavyositiriana na
kuheshimiana na kulindana Mume na Mke kutokana na matamanio ya nje yaliyokatazwa.
Na hivyo hali ya Libasi inatakiwa kua ndio iwe hali inayowapelekea Mume na Mke kua
ni wenye kusaidiana katika kupendezeshana na kuridhishana pale wanapokua pamoja na
katika kutaka kutimiza matamanio ya kukaribiana kimapenzi baina yao katika njia
inayoruhusika kisharia ambayo ni bila ya kuudhiana, kudhuriana wala kukirihishana,
186
kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kila mchezo anaocheza
Mtu hua hauna maana isipokua Kutunga Shabaha kwa upinde, Kumfundisha
Farasi na Kucheza na Mke wake’(Imam Ibn Majah)
Na amesema Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Mtu hatakiwi atimize haja yake (ya kumuingilia mke wake)
kutoka kwa mke wake kama (anavyofanya) Mnyama bali baina yao kuwe na
kuchezeana kwa mabusu na maneno’’(Imam Al Daylami)
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ameusia hivi kwa sababu inakua ni
Adha na Maumivu kwa viungo vya siri vya Mwanamke kukaribiwa na kuingiliwa bila
ya kutayarishwa kwa sababu Allah Subhanah wa Ta’ala katika kukamilisha Uzuri wa
mwili wa Mwanamke basi amemjaalia Mwanamke kemikali maalum ziitwazo Bartholin
Glands ambazo hua na kazi ya kuzirowanisha sehemu za Siri za Mwanamke kwani
Mwanamke anapotayarishwa basi mwili wake huanza kuzalisha Madini ya Nitric Oxide
ambayo hua na kazi ya kuongeza Mzunguko wa damu katika sehemu mbali mbali za
mwili ikiwemo katika sehemu za siri za Mwanamke.
Na hivyo muongezeko huo wa Nitric Oxide hua ni wenye kuzifanya sehemu hizo kua ni
zenye kuzisababishia Bartholin Glands kuzirowanisha sehemu hizo huku ukuta wa ndani
wa sehemu hizo ukiwa ni wenye kuongezeka ukubwa wake kwa kuelekea ndani ya Mwili
wake, na kukisukuma kizazi ndani zaidi ya mwili ili kutosheleza eneo la kupokea na
kuzivaa Sehemu za Siri za Mwanamme, na hapo hapo kutosababisha adha, maumivu na
madhara kwa Mfuko wa Uzazi wa Mwanamke.
Na hivyo inapotokea hali hio Mwanamke hua na hisia ya kuhisi kile kinachotokea ndani
ya Mwili wake katika sehemu ya ndani ya sehemu ya Siri kwani hua kama na hali kama
ya kuhisi kua ndani yae ana kama ukuta wa pango au uwazi fulani ambao hua inabidi
ujazwe kitu au kuzibwa na hivyo Mwanamke hua na hamu ya kutotaka kitu chochote
isipokua ya kutaka Nikah yaani kuzivaa sehemu za siri za Mwanamme na hapo basi ndio
hua inaruhusika kumuingilia na hivyo kupatikana kwa hisia za raha na starehe ambayo
haiwezekani kupatikana kama ikiwa kuna Adha na Maumivu hivyo ili kusiwe na adha na
maumivu kwa Mwanamke basi ni lazima kwanza atayarishwe.
Ambapo Imam Muhamad Ibn Muhammad Murtada Al Zabidi katika Ufafanuzi wa Ihya
Ulum Ad Din ya Hujjat Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammd Ibn
Muhammad Al Ghazali katika mlango wa ndoa ambapo amesema kua ‘Kuingiliana
Kimapenzi baina ya Mume na Mke kunatakiwa kuanze na maneno laini laini na
Kubusiana’ basi Imam Al Zabidi anasema kua: ‘Kubusu haimaanishi kua Mume
ayabusu Mashavu na Midomo tu bali pia anatakiwa ayapapase Maziwa na Chuchu
187
na kila sehemu ya mwili wa Mke wake’(Idhaf Al Sada Al Muttaqin Bi Sharah Ihya
'Ulum al-Din )
Na ndio maana akasema Allama Muhammad Abd Rauf Al Munawi kua : ‘Kupapasana,
kuchezeana na Kubusiana kwa mapenzi kabla ya kuingiliana (Baina ya Mume na
Mke) ni Sunnah Muakkadah, na ni Makruh kufanya vyenginevyo’(Faidh al-Qadir)
Hivyo bila ya kuwepo kwa matayarisho basi aidha haitowezekana kutokea kwa tendo
hilo au itawezekana lakini hakutokua na utekelezwaji wa haki na usawa baina ya watu
wawili hao katika tendo hilo, kwani mmoja hua amemvunjia haki yake mwenziwe na
hivyo hii hua ni sawa na ubakaji yaani Nikah bil Ikrah yaani Kuingilia kwa Chuki.
Ambapo neno Nikah basi ndio lile lilitumika katika ile aya isemayo:
﴿ٱلز َّانىِ لاَ يَنكِحُ إِلا َّ زَانِيَةً أَوْ مُشْرِكَةً وَٱلز َّانِيَةُ لاَ يَنكِحُهَآ إِلا َّ زَانٍ أَوْ مُشْرِكٌ
وَحُرِّمَ ذٰلِكَ عَلَى ٱلْمُؤْمِنِينَ ﴾
Alzzanee la yankihu illa zaniyatan aw mushrikatan waalzzaniyatu la yankihuha illa
zanin aw mushrikun wahurrima dhalika AAala almu/mineena(Surat Nur 24:3)
Tafsir: Mzinifu wa Kiume hamuingilii isispokua Mzinifu wa Kike au Mshirikini wa
Kike na Mzinifu wa Kike Haingiliwi ila na Mzinifu wa Kiume au Mshirkina wa Kiume
na hili limeharamishwa kwa Waumini.
Ambapo ayah hii imetumie aneno Nikah ambalo hua linamanisha Kufunga Kitu kwa
Kamba, kwa Kufuli au kwa Kukiziba kwa Kuingiza kitu chengine kwenye uwazi wake,
Kuunganisha, na pia hua linamaanisha Kuoa.
Hivyo wengi hua wanaitafsiri ayah hii kua Mzinifu wa Kiume hua kamwe hamuoi
isipokua Mzinifu wa Kike au Mshirikina na Mzinifu wa Kike Haolewi isipokua na
Mzinifu mwenzake wa Kiume au Mshirikina, na hili limeharamishwa kwa Waumini,
hivyo kwa upande mmoja hii hua si Tafsir sahih kwa sababu kuna Wanaume ambao
walikua wazinifu na baadae wakaoa Wanawake ambao ni wasafi, na pia kuna Wanawake
ambao walikua wazinifu baadae wakatulia kutokana na Kuolewa na Wasiokua wazinifu
waliowapenda, na kama tunavyojua kua Qur’an haisemi uongo, hivyo kama tukiitafsiri
kua watu hawa hawaoani isipokua wenyewe kwa wenyewe basi itakua inamanisha kua
hata huyu mwanamke Msafi alieolewa na Mtu aliekua Mzinifu hapo kabla basi nae
huenda akawa ni Mzinifu au na huyu Mwanamme pia baadae akawa Mzinifu. Jambo
ambalo si sahih.
188
Hivyo mbali ya kua Nikah ni neno linalotumika kumaanisha Kuoa, lakini pia hua
linamanisha Kuingilia na ndio maana Ubakaji au Kumuingilia Mwanamke kwa Nguvu
hua kunaitwa Nikah bil Ikrah yaani ni Kuingilia kwa kukirihisha au kwa chuki yaani bila
ya ridhaa ambayo hua pia ni sawa na Hirabah yaani yaani Kuchukua kitu kwa Nguvu au
kwa njia ya vitisho vya kutumia nguvu.
Kwani anasema Mujaddid Ad Din Imam Muhammad Idris Al Shafii kua: ‘Kama ikiwa
Mtu ana Mke mmoja au Suria ambae hua anamuingilia, basi anatakiwa kua ni
mwenye kumugopa Allah, na hivyo asimsababishie Madhara katika wakati wa
kumuingilia.’ (Kitab Al Umm)
Ambapo Imam Abu Sharaf Zakariyyah An Nawawi anasema kua: ‘Kama haiwezekani
kwa Mume kumuingilia Mke wake bila ya kumsababishia Madhara basi hua
haikubaliki kumuingilia’(Sharh Muhadhdhab)
Na ingawa kuna baadhi wanaweza wakatumia kisingizio cha Hadith ikiwemo ile ya Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam isemayo: ‘Nnaapa kwa yule ambae Maisha yangu
yapo Mikononi mwake kua: ‘Hakuna Mume anaemwita Mke wake kwa ajili ya
Kuingiliana Kimwili na Mwanamke akamkataa isipokua Allah Hua ni mwenye kua
na Ghadhabu nae (Mke) hadi Mume atakaporidhika nae’(Sahih Muslim)’
Ambapo ingawa hadith hii inamaanisha kua hairuhusiki kwa Mke kumkatalia Mumewe
anapomwita Kitandani kwa ajili ya Kukaribiana nae na kuingiliana kimwili, lakini pia
anasema Imam Abu Sharaf Zakariyyah An Nawawi kua: ‘Hadithi hii inamaanisha kua
ni Haram kwa Mke kumkatalia Mume wake pale anapomtaka bila ya kuwepo
sababu inayokubalika kisharia, na Hedhi haiwezi kukubalika kua ni sababu
inayokubalika kisharia kwa sababu Mume anayo haki ya Kustarehe nae wakati
akiwa na nguo zake mke huyo’
Lakini hata hivyo kama tukiiangalia hadithi hii kwa makini basi tunaoona kua Hadith hii
ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam imesema kua: ‘Allah Hua ni mwenye kua
na Ghadhabu nae (Mke) hadi Mume atakaporidhika nae’ hivyo maneno haya
yanamaanisha kua inapotokea hali kama hii basi Mume anatakiwa ajidhibiti, na awe na
Subra, au amsamehe Mkewe kwa sababu kama ingekua sio hivyo basi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam angesema badala yake kua ‘Mume anayo haki ya
Kumuingilia mke wake huyo kwa Nguvu’ na kama hivyo ni sahihi basi Rasul Allah
Salallau Alayhi wa Salam anayo haki ya kusema hivyo na Allah Subhanah wa Ta’ala
anao uwezo wa kudhihirisha hilo na hadithi haikusema hivyo na haikudhihirishwa hivyo
na wala na aya hazikusema hivyo.
Hivyo mbali ya kua hairuhusikia kumuingilia mke wakati anapokua katika siku zake au
anapokua katika siku za Nifasi lakini pia Mke anayo haki ya kukataa kuingiliwa na
189
Mumewe kwas sababu zinazokubalika Kisharia, kwa mfano Anaumwa, au Mumewe
anamnyanyasa na hivyo Mke kutokua na raha wakati anapokua karibu ya Mumewe, au
anamchukia na hawezi kua nae pamoja, au hua anamdhuru katika kumuingilia kwake, au
mwanamke amechoka na yuko taabani, au hayuko katika hali ya kujisikia kuingiliana
kimwili na hivyo Mwili wake hauwezi kutayarishika kwa ajili ya kuingiliwa na hivyo
kumuingilia huko huweza kusababisha madhara kwa mwili wake.
Kwani amesema Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
﴿لاَ يُكَلِّفُ ٱهلل َُّ نَفْساً إِلا َّ وُسْعَهَا﴾
La yukallifu Allahu nafsan illa wusAAaha(Surah Al Baqarah, 2:286)
Tafsir: Haikalifishi Allah Nafsi isipokua juu ya kile kilichomo ndani ya mipaka yake
Nafsi hio.
Hivyo Wanaume wa Kiislam wanatakiwa wajue kua Wake zao sio mashine za kufanyia
Mapenzi kwamba unaweza kumuingilia katika kwa matamanio ya nafsi yake katika
wakati uutakao na vyoyote atakavyo bila ya kujali hali yake ya kimaumbile aliyokua nayo
Mke katika wakati huo kwa sababu na wao ni Watu ambao wametokana nasi, kama
zinavyosema aya:
﴿وَمِ نْ آَ تِهِ أَنْ خَ لَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِ كُمْ أَزْوَاجاً لِّتَسْكُنُو ۤ اْ إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْ نَكُم
م َّوَد َّةً وَرَحمَْةً إِن َّ فىِ ذٰلِ كََ لآَتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَك َّرُونَ ﴾
Wamin ayatihi an khalaqa lakum min anfusikum azwajan litaskunoo ilayha
wajaAAala baynakum mawaddatan warahmatan inna fee Dhalika laayatin
liqawmin yatafakkaroona (Surat Rum 30:21)
Tafsir: Na miongoni mwa alama zake ni kukuumbieni wake kwa ajili yenu kutoka
miongoni mwenu, ili mpate utulivu pamoja nao, na akakuwekeeni baina yenu mapenzi
na rehma. Kwa hakika katika hili kuna dalili kwa wale wenye kutafakkar.
Hivyo basi Wanawake nao wanachoka na wanahisia za kimaumbile kwani ni Ibn Adam
na wala si viumbe Majini labda ambao wanastahmili kwa mda mrefu na kua na nguvu na
uwezo zaidi ya Ibn Adam, na ndio maana akasema Mujaddid Ad Din Imam Muhammad
190
Idris Al Shafii kua: ‘Ama kuhusiana na Kuingiliana basi ni jambo linalohusiana na
starehe na hivyo mtu hatakiwi kulazimishwa’(Kitab Al Umm)
Na Uislam ni Dini ya Uadilifu na Haki hivyo ni yenye kusimamia haki za Wanawake na
Wanaume hususan katika Ndoa na miongoni mwa mifano ya haya ni ile hadith ya Abd
Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu inayomuelezea Mke wa Thabit Ibn Qays Radhi
Allahu Anhu aitwae Jamila, ambapo tunapomzungumzia Thabit Ibn Qays basi hua ni yule
Sahaba ambae iliposhuka ile aya isemayo:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ لاَ ۤ تَرْفَعُواْ أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ ٱلن َّبىِ ِّ وَلاَ تجَْهَرُواْ لَهُ ٱ بِ لْقَ وْ لِ
كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن تحَْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لاَ تَشْعُرُونَ ﴾
Ya ayyuha allatheena amanoo la tarfaAAoo aswatakum fawqa sawti alnnabiyyi wala
tajharoo lahu bialqawli kajahri baAAdhikum libaAAdhin an tahbata aAAmalukum
waantum la tashAAuroona (Surat Al Hujurat 49:2)
Tafsir: Enyi Mlioamini Msinyanyue Sauti zenu juu ya sauti ya Nabii (Muhammad
Sallahu Alayhi wa Salam) na wala msizungume nae kama mnavyozungumza
miongoni mwenu, ili amali zenu zisije zikawa ni za bure wakati nyinyi mkiwa hamjui.
Basi Thabit Ibn Qays Radhi Allahu Anhu akasema kua: ‘Mimi ndie nilietajwa kwenye
Ayah hii, kwani nanyanyua sauti yangu mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, hivyo amali zangu zote zimekua ni za bure, nami nimekua ni mtu wa Motoni’
hivyo akabakia nyumbani kwake na hakutoka huku akimuomba Msamaha Allah
Subhanah wa Ta’ala na kulia machozi, Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipopata
habari hii basi akamtuma mtu kumuliza Thabit Ibn Qays Radhi Allahu Anhu kwanini
akawa katika hali hio?
Ambapo Thabit Ibn Qays Radhi Allahu Anhu akaanza kuelezea dhmabi zake moja baada
ya moja, na kasha kasemakua: ‘Hakika nnakhofia mimi kua nitakua ni miongoni mwa
watu ambao amefutiwa mema yake yote’ hapo Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam
akamwambia Thabit Ibn Qays Radhi Allahu Anhu kua: ‘La Takhaf, kwani kwa hakika
wewe ni mtu mwenye kuendesha maisha yako katika njia yenye kusifika, na utakua
shahidi hapo baadae na Allah Subhanah wa Ta’ala atakuingiza Peponi.’
Hivyo anasema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mke wa Thabit Ibn
Qays Ibn Shammas, Jamilah ambae ni dada yake Abdulla Ibn Ubbay, alikuja kwa
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kusema: ‘Ya Rasul Allah Salallahu Alayhi
191
wa Salam Hakika mimi sina lalamiko baya dhidi ya Thabit Ibn Qays kuhusiana na
Dini yake wala Tabia zake, lakini sasa sitaki mimi kufanya jambo la Kikafiri wakati
nikiwa Muislam’’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuuliza Jamilah: ‘Hivi Jee
utamrudishia Bustani yake?’ kwani Mahari yake yalikua ni hio Bustani aliyopewa,
hivyo nae akasema: ‘Naam’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akamuamrisha Thabit Ibn Qays kwa kusema kua: ‘Chukua Bustani yako na kisha
mpe Talaka moja.’(Fath al-Bari.)
Ambapo kwa upande mwengine basi siku moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alikua amekaa na Al Ababs Ibn Abd Ul Muttalib Radhi Allahu Anhu na hivyo akasema:
‘Ya Al Abbas, hivi Jee haistaajabishi namna Mugheeth anavyompenda Barirah na
namna Barirah anavyomchukia Mugheeth?’
Ambapo Barirah ambae alikua ni Mtumwa aliolewa na Mugheeth ambapo wote wawili
walikua ni Watumwa, hivyo Aisha Radhi Allahu Anha akamnunua Barirah na kisha
akamuachia Huru, na Kiislam Mwanamke aliekua Huru hua hawezi kuolewa na
Mwanamme ambae ni Mtumwa, hivyo Barirah akawa na haki ya hiari ya kuamua kubakia
na Mughith au kuachana nae. Na ingawa Mughith alikua akimpenda sana Barirah kiasi
ya kua kila Mtu katika Mji wa Madinah alikua anajua juu ya Mapenzi hayo Makubwa
sana ya Upande mmoja, lakni hata hivyo kutokana na haki aliyokua nayo Barirah basi
nae akaamua kuitumia haki yake hio ya hiari na akataka kuachana na Mughith.
Ambapo kama alivyosema Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam kumwambia Ami yake
Al Abbas Ibn Abd Ul Muttalib Radhi Allahu Anhu kua ‘Ya Al Abbas, hivi Jee
haistaajabishi namna Mugheeth anavyompenda Barirah na namna Barirah
anavyomchukia Mugheeth?’ kwani kila mtu pia katika Mji wa Madinah alikua akijua
Barirah alikua hampendi Mughith. Hivyo Barirah alipopata uhuru wake basi akasema:
‘Alhamd Lillah, hakika mimi nimeshachoka na ndoa hii na nimepata nafasi ya
kutoka ndani yake, hivyo natoka’
Baada ya Barirah kuamua kutoka ndani ya Ndoa hio basi Mughith akawa anapita huku
akilia kwa huzuni na kulalamika na kumuomba kila mtu anaehisi kua atamsaidia katika
kumuusia Barirah ili arudi kwenye ndoa yake lakini jitihada zake hizo hazikufua dafu,
kwani Barirah alikua hataki hata kumtizama Mughith wala kuzungumza nae. Hivyo
Mughith akaamua kuenda kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kumuomba
amsaidie kumrudisha Barirah katika maisha yake ya ndoa pamoja nae.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuonea huruma Mughith na hivyo akamwita
Barirah na kumwambia bora arudi kwa Mughith kwani anampenda sana, na anaumia na
kuhuzinika Moyo wake kwa ajili yake, ambapo Barirah akamwambia Rasul Allah
192
Salallahu Alayhi wa Salam: ‘Hivi Jee unaniamrisha au unamuombea’ Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akajibua: ‘Namuombea’ hivyo Barirah akajibu: ‘Kwa hali
hio basi mimi simtaki.’ Na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakuweza
kumlazimisha Barirah kurudi kwenye ndoa yake na Mughith.
Hivyo tunapozungumzia kuhusiana na mshikamano wa Uhusiano wa Mapenzi basi
lazima kuwe na maelewano yenye kushikamanisha Nyoyo zinazopendana na hivyo
inapotokea hali hio ya mshikamano kama huo basi hua hakuna kitu
kitakachopelekea kuvunjika kwa mshikamano huo, isipokua kile kitakachokua ni
chenye nguvu zaidi ya mshikamano huo, hivyo kama ikiwa mshikamano huo kua ni
wenye kutokana na sababu ya kitu fulani au malengo fulani basi mshikamano huo
wa hisia hizo za mapenzi nao hua ni wenye kutoweka pale sababu ya hio
inapotoweka au malengo hayo yasipofikiwa.
Kwani amesema Aisha Radhi Allahu Anha kua: ‘kulikua kuna Mwanamke mmoja
ambae alikua akienda kwa Quraysh na kuwachekesha, na alikuja Madinah pia na
kukaa kwa Mwanamke mmoja na akawa pia anawachekesha Watu’ hivyo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akauliza: ‘Hivi jee Fulani bint Fulani anakaa na
nani?’ ambapo Aisha Radhi Allahu Anha akasema: ‘Anakaa pamoja na Fulani Bint
Fulani ambae ndie anaewachekesha watu’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Nafsi ziko kama Askari
walioshikamana, wale wanaoafikiana nao basi ndio hua pamoja nao na wale
wasiofikiana nao basi hawawezi kua pamoja nao’(Musnad Imam Ahmad Ibn Hanbal)
Na ndio maana akasema Allah Subhanah wa Ta’ala ndani ya Qur’an kua:
﴿ٱلخَْبِيثَاتُ لِلْخَبِيثِينَ وَٱلخَْبِيثُونَ لِلْخَبِيثَاتِ وَٱلط َّيِّبَاتُ ٱ لِلط َّيِّبِينَ ل َو ط َّيِّبُو نَ لِلْط َّيِّبَا تِ
أُوْلَٰئِكَ مُبَر َّءُونَ ممِ َّا يَقُولُونَ لهَُم م َّغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَ رِيمٌ ﴾
Alkhabeethatu lilkhabeetheena waalkhabeethoona lilkhabeethati waalttayyibatu
lilttayyibeena waalttayyiboona lilttayyibati ola-ika mubarraoona mimma
yaqooloona lahum maghfiratun warizqun kareemun(Surat Nur 24:26)
Tafsir: Mabaya hua ni kwa Watu wabaya, na Watu wabaya hua ni wenye kua na
Mabaya, Mazuri hua ni kwa Watu wazuri na Watu wazuri hua ni wenye Mazuri, kwani
193
wao (Wazuri) hua hawana makosa katika Mabaya wayasemayo kwani hua ni wenye
kusamehewa, na hupata Malipo yaliyo bora.
Ambapo baadhi ya Wafasiri wametafsiri aya kwa kusema kua Wanawake wabaya hua
ni kwa Wanaume wabaya, na Wanaume Wabaya hua ni kwa Wanawake Wabaya,
Na aya imetumia maneno Alkhabeethatu lilkhabeetheena waalkhabeethoona
lilkhabeethati ambayo yametokana na nenno Khabutha ambalo hua ni lenye kumaanisha
Kutokua na Rutba Au Kutokua na Faida, Kua Mbaya, Kua Ovu, kutokua na Thamani,
Kua na Uchafu wa maneno au vitendo.
Hivyo Waislam tunatakiwa kua wasafi na wenye sifa nzuri katika mahusiano yetu kwa
ujumla na wala tusiwe ni wenye kuudhiana, kukirihishana na kulazimishana na
kusababishiana madhara iwe kwa maneno au kwa vitendo baina ya Ibn Adam kwa
Ujumla, na kutokana namaamrisho hayo basi ndio maana tukaambiwa kua tusiwakaribie
Wanawake kwa kutaka kuwaingilia kimapenzi wakati wanapokua kwenye Mahiidh hadi
watakapokua tohara yaani wasafi.
Kwani mbali ya kua Mwanamke kua katika kiindi hiki hua na mabadiliko ya Mfumo wa
kihisia za kimaumbile na kimwili kwa kujisikia hali ya uchovu na kutokua na nguvu za
mwili kama kawaida yake na kuhisi maumivu katika sehemu tofauti za mwili wake
kulingana na maumbile ya Mwanamke husika, na hivyo tendo hili kua ni Adha kwake
lakini pia kwa upande wa Kiafya basi tendo hili hua ni lenye kuwadhuru wote
Mwanamme na Mwanamke yaani aliekatatazwa asikaribie kimapenzi na aliekatazwa
kukaribiwa kimapenzi.
Na hii ni kwa sababu katika wakati huu ukuta wa Mfuko wa Uzazi hua katika hali ya
udhaifu na usiokua na ulinzi Imara na hivyo huweza kusababisha madhara makubwa sana
kwa upande wa Mfuko huo, kwa Mayai ya Uzazi wa Mwanamke, Mirija ya Uzazi wa
Mwanamke na huweza kusababisha kutowezekana kupatikana kwa uja uzito wa
Mwanamke au pia kusababisha ujauzito wa aina ya Ectopic yaani mimba kutunga nje ya
mfuko wa Uzazi, ambapo aidha huweza kutunga kwenye Mirija ya Uzazi, kwenye Mayai
ya Uzazi, n.k na hivyo kusababisha utokwaji wa damu nyingi sana na pia husababisha
matatizo mkubwa ikiwemo yatakayosababisha kutolewa Kizazi, na pia maradhi mengine
mbali mbali ya maambukizi ikiwemo maradhi ya Mkojo, Kibofu cha Mkojo, Mafigo, n.k
Na kwa upande wa Mwanamme basi kumkaribia Mwanamke katika wakati wa Hedhi
humplekea Mwanamme kutoweza kuingiliana nae Mwanamke kwa sababu ya hali ya
Damu inayotoka, na hata kama ataweza basi pia Damu hio huweza kumsababishia
maradhi kwenye sehemu zake za siri na kwenye njia ya Mkojo na kwenye Mfumo wa
Mayai ya Uzazi ya Kiume.
194
Ambapo amesema Imam Al Qaffal Al Shashi amesema kua: ‘Aya imetumia neno Wa
La Taqrabuhuna ambapo neno La Taqrab linamaanisha Usifanye kitu lakini
ukisema La Tuqrib basi hua inamaanisha Usikaribie, hivyo hii inamaanisha kua:
‘Msiwaingilie Wanawake zenu’’
Hivyo bila ya shaka Allah Subhanah wa Ta’ala ambae ni Muumba ni mwenye kujua kitu
na kutokana na kujua kwake kutokana na hikma zake basi ndio maana akakataza
kuwakaribia kwa kuwaingilia kimwili tu Wanawake katika siku hizo, na vyengine vyote
inaruhusika, kula nao, kukaa nao, kuwakumbatia, kuwabusu na kustarehe na kila sehemu
ya mwili wake isipokua baina ya Kitovu na Magoti. Kwani amesema Aisha Radhi Allahu
Anha kua: ‘Wakati mimi nilipokua niko kwenye siku zangu, nilikua namchana
Nywele zake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na alikua akiniegemea kwenye
mapaja yangu huku akiwa anasoma Qur’an.
Na Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al
Qurtubi amesema kua :‘Amesema Ibrahim Ibn Masruq kua: ‘Mimi nilimuuliza
Aisha: ‘Jee ni kipi kilicho halali yangu juu ya mke wangu anapokua yuko kwenye
Hedhi?’Aisha akajibu: ‘Kila kitu isipokua sehemu zake za Siri.’’
Hivyo kuna makubaliano ya Wanazuoni juu ya jambo hili ni kwamba atakaeenda
kinyume na amrisho hili basi hua ni mwenye kufanya dhambi na ingawa hatakiwi kutoa
fidya au kupewa adhabu yeyote lakini hua ni wajibu wake kufanya toba kwa Mola wake.
Kwa upande mwengine pia tunaona kua Allah Subhanah wa Ta’ala anatuwekea wazi kua
hairuhusiki kuwaingilia Wanawake wanapokua wenye Hedhi pale alipomalizia kwenye
aya hio kwa kusema:
﴿فَإِذَا تَطَه َّرْنَ فَأْتُوهُن َّ مِنْ حَيْثُ أَمَرَكُمُ ٱهلل َُّ إِن َّ ٱهلل ََّ يحُِب ُّ ٱلت َّو َّابِينَ وَيحُِ ُّب
ٱ لْمُتَطَهِّري نَ ﴾
Fa-idha tatahharna fa/toohunna min haythu amarakumu Allahu inna Allaha
yuhibbu alttawwabeena wayuhibbu almutatahhireena (Surat Al Baqara 2:222)
Tafsir: ‘Na kisha watakapojitoharisha basi waingilieni katika sehemu
aliyokuamrisheni Allah, kwani kwa hakika Allah anawapenda wenye kufanya toba na
wenye kujitoharisha.’
195
Ambapo aya hii imetanguliza masharti mawili ya kutumizwa kabla ya kufikia hatua ya
kuwaingilia Wanawake waliokua na Hedhi ambayo ni kwanza Wamalize siku zao, pili
Wajitoharishe.
Ambapo kuhusiana na umuhimu wa kujitoharisha basi amesema Allah Subhanah wa
Ta’ala kua:
﴿إِذْ يُغَشِّ يكُمُ ٱلن ُّعَاسَ أَمَنَةً مِّنْهُ وَيُنَزِّلُ عَلَيْكُم مِّنَ ٱلس َّمَآءِ مَآءً لِّيُطَهِّرَكُمْ بِهِ وَيُذْهِبَ
عَنكُمْ رِجْزَ ٱلش َّيْطَانِ وَلِيَرْبِطَ عَلَى ٰ قُلُوبِكُمْ وَيُثَبِّتَ بِهِ ٱلأَقْدَامَ ﴾
Idh yughashsheekumu alnnuAAasa amanatan minhu wayunazzilu AAalaykum
mina alssama-i maan liyutahhirakum bihi wayuthhiba AAankum rijza alshshaytani
waliyarbita AAala quloobikum wayuthabbita bihi al-aqdama (Surat Al Anfal 8:11)
Tafsir: Kumbuka wakati alipokufunikeni kwa usingizi kua kama ulinzi kutoka kwake,
na akajaalia Maji kumwagika kutoka Mbinguni kwa ajili ya kukusafisheni na
kukuondeleeni athari za uchafu wa Shaytan na kukutieni nguvu nyoyo zenu na
kuithibitishia uimara miguu yenu.
Ambapo neno Rijz hua linamaanisha Uchafu, Uchafuzi wa kugusana au kuingiliana kwa
kitu kilichokua kichafu kuchanganyika na kilichokua kisafi.
Na ikatumia neno Shaytan ambalo mbali ya kua ni lenye kumaanisha Kuasi, Kua mbali
kutokana na Rehma za Allah, Kiumbe kilichomuasi Allah Subhanah wa Ta’ala, Kiumbe
mwenye Kutoutaka na hivyo kua ni mwenye kuukimbia Ukweli, na pia humaanisha
Uovu.
Hivyo Kujitoharisha kwa kutumia Maji hua ni sehemu ya kujiondolea na kujisafisha
kutokana na madhara ya athari mchafuko unaotokana na nguvu za mionzi isiyoonekana
katika mazingira tunayoishi katika maisha yetu pamoja na viumbe wengine
wanaoonekana na wasioonekana, kwani kimaumbile kila kiumbe hai Duniani hua ni
chenye kuzalisha, kuathiri na pia kuathirika na mawimbi ya mionzi ya nguvu za mvutano
wa Sumaku miongoni mwetu.
Na haya tunaweza kuyaona na kuyajua pale tunapochunguza na kuuangalia mfano mmoja
tu ambao ni wa Mfumo wa Moyo wa Ibn Adam ambao hua unafanya kazi zake
kimaumbile kwa kuishirikisha mifumo mikuu minne ya usafirishaji wa nguvu za hisia za
mwili wa Ibn Adam ambazo ni:
196
1- Mfumo wa Usambazaji wa hisia za sehemu tofauti za mwili.
2- Mfumo wa Viasili vinavyodhibiti maumbile ya ufanyaji kazi wa mwili
vinavyozalishwa na Moyo.
3- Mfumo wa Usambazaji Kemikali kupitia katika mapigo ya Moyo na
usambazaji Damu.
4- Mfumo wa Uzalishaji Nguvu za Kimaumbile za mwili za ufanyaji kazi wa
viungo vya Ibn Adam na nguvu za Mawimbi ya Mvutano wa Umeme wa
Sumaku za ndani ya Mwili na nje ya Mwili.
Kimaumbile Moyo wa Ibn Adam hua unazalisha nguvu za umeme zenye asili ya
mawimbi ya sumaku zenye nguvu mara 5000 zaid na nguvu kama hizo zinazozalishwa
na Ubongo wa Ibn Adam, kwani Ubongo nao katika kufanya kazi kwake basi hua
unazalisha pia nguvu za mawimbi ya sumaku, ambapo nguvu za mfumo wa Moyo
huweza kuhisika hata nje ya mwili wa Ibn Adam kwa takriban umbali wa mita 3 hua na
uwezo wa kusambaza na kupokea na kuwasiliana na hisia mbali mbali kutoka katika
ubongo wa mtu husika na sehemu nyengine za mwili mzima wa mtu huyo na wakati huo
hua na uwezo wa kuwasiliana na nguvu zinazozalishwa na watu wengine zaidi ya wanane
waliopo karibu nae na hivyo hua na uwezo wa kuwaathiri watu hao walio karibu nawe
kihisia.
Moyo wa Ibn Adam una nyuroni 40000 ambazo kwa pamoja hua zinaunda kitu
kinachoitwa Akili ya Moyo, ambayo hua ni yenye uwezo wa kukumbuka kwa muda fupi
na kwa mda mrefu, kujifunza na kufanya maamuzi yake wenyewe bila kuitegemea akili
na hivyo hua na uwezo wa kuyadhibiti mapigo ya Moyo, athari ya Ufahamu wa Moyo
hua na uwezo wa kuubadilisha hata mtizamo wa ufahamu wa akili kihisia na kimaamuzi
katika mambo mbali mbali.
Kila Moyo unapopiga basi hua ni wenye kuzalisha nguvu za mawimbi ya umeme wa
sumaku na hivyo kusababisha athari mbali mbali za Moyo ikiwemo kuona kwa mtizamo
wa Jicho la Moyo, kuhisi kwa hisia za Moyo, ambapo hisia zote hizi zinapotokea ndani
ya Moyo hua zina athari kubwa zaidi ndani ya mwili wa Ibn Adam na zinazotofautiana
sana na zile zenye kutokea moja kwa moja kupitia katika akili ya Ibn Adam, ambapo
mawasiliano kutoka kwenye Moyo kuelekea kwenye Akili hua ni maradufu zaidi yana
umuhimu zaidi kwa ufanyaji kazi wa Mwili kuliko mawasiliano ya kutoka kwenye Akili
kuelekea kwenye Moyo.
Nguvu hizi zinazozalishwa na Moyo pia huweza kuwasiliana kihisia na kuathiri nguvu
za mvutano wa mawimbi ya umeme ya viumbe wengine waliokuwepo karibu yetu
ikiwemo Wanyama na Viumbe wengine wasioonekana wa Ulimwengu wa Al Ghayb. Na
ndio maana baadhi wakati mtu anaweza akakaa peke yake na ghafla akahisi kama mwili
unamsisimka, kwa sababu nguvu hizi za kimaumbile za Moyo hua na uwezo wa kuhisi
197
kutokea kuwepo kwa Viumbe wengine wasioonekana kama vile Majini ambao wao
Maumbile yao yana asili za nguvu hizi.
Na ni kutokana na athari ya nguvu hizi ndio Viumbe Majini hua na uwezo wa aidha
kuwadhibiti Ibn Adam au kuwaogopa na kuwakimbia Ibn Adam. Kwani tunazalisha
nguvu za Mawimbi ya Umeme ambazo ni zenye maumbile kama ya viumbe Majini
ambao sisi Ibn Adam kamwe hua hatuwezi kuwaona kwa sababu wao hawana maumbo
bali wako katika Hali kama ya mionzi ya Xray, ya Ultra Sound, ya Simu, ya Radio, ya
Tv n,k na hivyo hua pia na uwezo wa kimaumbile wa kuingia ndani ya Miili yetu Katika
Nyoyo, Ufaham, Mishipa ya Damu, Ubongo n,k bila ya sisi kuhisi kama vile ambavyo
inaweza kuingia ndani ya Miili yetu mionzi ya Xray, Ultra Sound.n.k.
Kwa hivyo kujitoharisha kwa Maji hua kunapelekea Ibn Adam kua msafi na kujiondolea
mchafuko wa athari mbali mbali zenye madhara ya Kiroho, Kimwili na Kihisia za mionzi
isiyoonekana inayotuzunguka kwenye mazingira yetu ikiwemo athari za maingiliano ya
nguvu za kimaumbile baina ya viumbe mbali mbali ikiwemo Majini katika Miili yetu na
pia kwa kuizima nguvu ya Mionzi ya viumbe Shaytani wanaotaka kutudhibiti kwa
kutokea ndani ya Miili yetu kimaumbile.
Ampapo anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua : ‘Maneno
yasemayo Min haythu amara kumullah yana maana nyingi nyingi na maana
iliyoelezewa hapa inamaanisha kua Mtu anaweza kumuingilia Mke wake kwa
kulala, kwa kusimama, kwa juu kwa chini, kwa kukaa, katika sehemu
iliyoamrishwa na Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Ambapo Allah Subhanah wa Taala anatubainishia wazi baada ya aya hio kwa kusema
kuhusiana na Wake zetu kwa kutumia neno Haratha ambalo ni lenye kumaanisha
Kulima, Kupanda Mbegu, Kuotesha Kitu, Kukata Kitu, Kuvuna, Kutifua Ardhi kwa ajili
ya kuotesha Mbegu au Mimea, Kukisoma kitu kwa undani zadi, Bustani, Mazao, Shamba
na pia humaanisha Mke.
Allah Subhanah wa Ta’ala amesema katika aya iliyotumia neno Harthun:
﴿نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ ل َّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنى َّٰ شِ ئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنْفُسِ كُمْ وَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَٱعْلَمُو ۤ اْ
أَن َّكُمْ م ُّلاَقُوهُ وَبَشِّ رِ ٱلْمُ ؤْ مِ نِينَ ﴾
198
Nisaokum harthun lakum fa/too harthakum anna shi/tum waqaddimoo lianfusikum
waittaqoo Allaha waiAAlamoo annakum mulaqoohu wabashshiri
almu/mineena (Surat Al Baqara 2:223)
Tafsir: Wake zenu ni Mashamba yenu, hivyo yaendeeni Mashamba yenu mtakavyo na
tangulizeni (kufanya mema) kwa ajili ya Nafsi zenu na muogopeni Allah, na jueni kua
mtakutana nae na Wabashirie (habari Njema) Waumini.
Tunapoiangalia aya hii katika kutumia kwake neno Harthun basi tunona kua inamaanisha
kua Mume hua ni Mkulima, Mke hua ni Shamba. Manii Hua ni Mbegu na Mtoto
anaepatikana kutokana na mchanganyiko wa Makadirio na Majaaliwa ya Allah Subhanah
wa Ta’ala na Jitihada za Mkulima katika kulihudumia Shamba lake hua ndio Matunda
yanayotokana na Shamba hilo.
Ambapo anasema Imam Bukhari kua amesema Nafi’i Mawal Ibn Umar Radhi Allahu
Anhu kua: ‘Wakati Ibn Umar alipokua akiisoma Surat Al Baqara alipoifikia aya hii
basi aliniuliza: ‘Jee unajua aya hii ilishushwa kwa sababau gani?’ nami nikasema :
‘La’ Hivyo nae akasema: ‘Ilishushwa kuhusiana na kadha na kadha kadha’ kisha
Imam Bukhari akaendelea kusema: ‘Amesema Abd Samad kutoka kwa Baba yake
kutoka kwa Ayyub kutoka kwa Nafi’i kua Ibn Umar amesema kua Aya hii
inamaanisha vyovyote vile mnavyotaka’ ’
Ambapo Imam Abu Daud amesema kua Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu
amesema kua: ‘Ibn Umar kuna kitu hakufaham. Kwani kulikua na kabila fulani la
Ansari ambao walikua ni Makafiri, na kuna kabila la Mayahudi ambao walikua ni
watu wa Ahl al Kitab, na wao Maansari walidhani kua Mayahudi walikua wako juu
zaidi kiilm. Hivyo wakawa wanawaiga Mayahudi katika wanayoyafanya.
Wakawaamrisha wasiwaingilie wake zao isipokua kwa upande mmoja (yaani
wanapokua wamelala chali) kwa sababu hii ndio njia ambayo inawafunika zaidi
Wanawake. Hivyo watu hawa wa Ansari wakawaiga kufanya hivyo Mayahudi.’
‘Wakati Maquraysh walikua wamezoea kuwavua nguo zote Wanawake wao na
kustarehe nao wakiwa chali na wakiwa kifudifudi. Hivyo wakati Muhajjiruna
walipokuja katika Mji wa Madinah na kuoa Mwanamke wa Kiansari basi Mtu
alikua anamuingilia katika hali hio na Mwanamke hakupenda na akamwambia:
‘Sisi tunaingiliwa kwa upande mmoja tu hivyo fanya hivyo au achana na mimi’
Habari hii ikaenea katika Mji wa Madinah na kumfikia Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam, hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akaishusha aya hii ‘Nisaokum
harthun lakum fa/too harthakum anna shi/tum’’ yaani ‘Wake zenu ni Mashamba
yenu, hivyo yaendeeni Mashamba yenu mtakavyo’ Kumaanisha kua Wake zenu ni
199
mashamba yenu Waingilieni wakiwa wamelala chali au wakiwa kifudifudi kwa
kupitia sehemu ambayo anayozaliwa mtoto’
Kwani amesema Khuzaymah Ibn Thabit Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul
Allahu Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Allah haoni haya sana kusema Ukweli’
mara tatu, kisha akasema: ‘Msiwaingilie Wanawake kwenye tupu zao za
Nyuma.’’(Imam Ibn Majah)
Imam Abu Hasan Ali Ibn Muhammad Ibn Habib Al Mawardi Al Shafii anasema
kuhusiana na Hadithi hii ambayo ni Mutawattir yaani iliyonukuliwa na Masahaba wengi
sana kiasi ya kua inakua vigumu Masahaba hao kukubaliana kusema Uongo kua: ‘Hii ni
kwa sababu ya kua kuna Makubaliano ya Masahaba juu ya hili, kwani imenukuliwa
na Ali Ibn Abi Talib, Abd Allah Ibn Abbas, Abd Allah Ibn Masud na Abu Dardaa
Radhi Allahu Anhum.’(Kitab Al Hawi Al Kabir Fi Fiqh Madhhab Shafii)
Ambapo wengine miogoni mwa Masahaba walionukuu hadithi hii ni pamoja na Sayyidna
Ali Ibn Abi Talib, Abu Darda, Abd Allah Ibn Amr Al As, na Abu Hurayrah Radhi Allahu
Anhum. Na huo pia ndio mtizamo wa Imam Said Ibn Musayyib, Abu Bakr Ibn Abd
Rahman, Mujahid Ibn Sulayman, Ikrimah Mawla Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu
Anhu, Imam Muhammad Idris Al Shafii, Imam Ibn Al Mundhiri Al Nishapuri.
Ama baada ya hapo Allah Subhanah wa Taala anatupa ukumbusho kwa kutuambia kua
mbali ya kuturuhusu kustarehe na wake zetu lakini tusimsahau yeye hata tunapokua
kwenye kilele cha starehe hizo kwa kusema:
﴿وَقَدِّمُواْ لأَنْفُسِ كُمْ وَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَٱعْلَمُو ۤ اْ أَن َّكُمْ م ُّلاَقُوهُ وَبَشِّ رِ ٱلْمُؤْمِنِينَ ﴾
Waqaddimoo li-anfusikum Waittaqoo Allaha waiAAlamoo annakum mulaqoohu
wabashshiri almu/mineena (Surat Al Baqara 2:223)
Tafsir: Na tangulizeni (kufanya mema) kwa ajili ya Nafsi zenu na muogopeni Allah,
na jueni kua mtakutana nae na Wabashirie (habari njema) Waumini.
Hivyo tunapoangalia kuhusiana na kwa upande wa Maisha ya wafuasi wa Dini ya
Uyahudi basi hua kuna mtizamo tofauti kuhusiana na Damu, kwani kwa upande wao ni
kitu kitukufu na ndio maana hata nyama zao wanazochinja ambazo ingawa huchinjwa
kama wanavyochinja Waislam lakini baada ya kuchinjwa inabidi Nyama hio itiwe
Chumvi na ikaushwe Damu yote na kisha ndio inaweza kuitwa Kosha ambayo ndio aina
ya Nyama wanayoruhusika kuitumia kwa ajili ya kula..
200
Ambapo kwa upande wa Wanawake na Hedhi na maumivu na Maradhi yanayotokana na
damu ya Hedhi, basi kwao wao ilikua katika wakati kama huo ambao Mwanamke
anapoingia kwenye siku zake basi hua kuna hali inayojulikana kama Niddah ambayo hua
inamaanisha Utenganishwaji au Utolewaji ambao hua ni kutangenishwa na familia zao
kwa mda wa siku 7 ambazo Wanawake hao huchukulikwa na kuwekwa kwenye Jengo
maalum lililojengwa kwa ajili yao.
Ndani ya Jengo hilo ambalo linajulikana kama Jumba la wasiokua tohara hua
hawaruhusiwi kutoka kurudi majumbani mwao mpaka zipite siku 7, katika kipindi hiki
wanapokua kwenye Jengo hilo hua hawaruhusiwi kujipamba ambapo baada ya siku hizo
basi hua tayari wameshakua Tohara moja kwa moja bila ya kujitoharisha kwa kukoga au
kwa kutayamam pale inapokua hakuna maji kama ilivyo kwa upande wa Uislam, na
ingawa hua wanaruhusiwa kurudi Majumbani mwao, lakini hua hawaruhusiwi kuingia
kwenye Majumba ya Ibada hadi pale watakapopeleka ndege wawili kwa Kasisi wao kwa
ajili ya kutoa Kafara ambayo baada ya kuchinjwa kwake basi ndio inahesabika kua
wanaweza kuingia kwenye Majumba ya Ibada na kua mbele ya Mungu wao.
Kutokana na mazingira hayo basi ndio maana Hannah Bint Faqudh alikua akitegemea
kua Mtoto wake atakua ni wa kiume ili maisha yake yote mtoto huyo yawe ndani ya
Mahekalu ya Kuabudia, kwani kama akiwa mwanamke basi lengo lake hilo halitoweza
kufanikiwa kwani kuna kipindi Mtoto huyo itabidi awe ni mwenye ulazima wa kutolewa
kutoka kwenye Jumba la Ibada na kutengwa kutokana na Niddah.
KUZALIWA KWA MARYAM BINT IMRAN
Hivyo baada ya kunadhiria kwake huko Hannah Bint Faqudh basi akaendelea na uja uzito
wake, ambapo kati kati ya uja uzito huo basi Allah Subhnah wa Taala ambapo mtihani
Hannah Bint Faqudh ambao ni wa kondokewa na Mumewe yaani Mzee Imran ambae
alifariki Dunia, na hivyo Hannah akawa na huzuni kwani Mtoto huyo atakua ni mwenye
kukua bila ya baba yake.
Baada ya kupita Mtihani huo basi Allah Subhana wa Ta’ala akamjaalia kua ni mwenye
kujifungua baada ya mda wake kufika ambapo mara tu baada ya kujifungua basi Hannah
Bint Faqudh akaona kua mtoto aliejifungua alikua ni Mwanamke badala ya Mwanamme
aliemtegemea kumpata kwa ajili ya kutimiza nadhiri yake aliyoiweka na hivyo akaomba
radhi kwa Mola wake kama inavyobainisha aya:
201
﴿فَلَم َّا وَضَعَتْهَا قَالَتْ رَبِّ ِ إِنىّ وَضَعْتُهَآ ٰ أُنْثَى وَٱهلل َُّ أَعْلَمُ بمَِا وَضَعَتْ ٱ وَلَيْس ل ذ َّكَرُ
ٰ كَٱلأُنْثَى ِ وَإِنىّ سمَ َّيْتُهَا مَرْيمََ ِ وِإِنىّ أُعِيذُهَا بِكَ وَذُرِّي َّ تَهَا مِنَ ٱلش َّيْطَانِ ٱلر َّجِ يمِ ﴾
َ
Falamma wadhaAAat-ha qalat rabbi innee wadaAAtuha ontha waAllahu aAAlamu
bima wadaAAat walaysa aldhdhakaru kaalontha wa-innee sammaytuha maryama
wa-innee oAAeedhuha bika wadhurriyyataha mina alshshaytani alrrajeemi(Surat
Al Imran 3:36)
Tafsir: Kisha alipomzaa akasema: ‘Ewe Mola wangu hakika mimi nimejifungua Mtoto
Mwanamke.’ Na Allah ni mwenye kujua zaidi juu ya kile alichojifungua: ‘Na
Mwanamme sio kama Mwanamke na kwa hakika mimi nimemwita Maryam. Na kwa
hakika nnaomba hifadhi yake kutoka kwako na kizazi chake kutokana na Shaytan
aliefukuzwa’
Amesema Abu Hurayra kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua :
‘Bila ya kumjumuisha Maryam na Mtoto wake basi hakuna Ibn Adam ambae
amezaliwa bila ya kuguswa na Shaytan katika wakati wa kuzaliwa, na ambae halii
kutokana na kuguswa na Shaytan’’
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi
kwa lugha yao basi neno Maryam maana yake hua ni Mja au Mtumwa au Mwenye
Kuabudu na hivyo basi Hanah Bint Faqudh anaweka wazi kuhusiana na kutimiza nadhiri
yake kupitia kwa Mtoto huyu kwa kuanzia na jina lake ‘Maryam’ hata kama ni
Mwanamke.
Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi anaendelea
kutuambia kua aya hii inatafsirika katika hali mbili ambazo ni kua kwanza, kama itakua
tutaisoma aya hii kwa kusema: ‘WaAllahu aAAlamu bima wadaAAatu yaani Na Allah
ni mwenye kujua zaidi ju ya ile lichojifungua’ basi maneno yasemayo ‘Walaysa
aldhdhakaru kaalontha’ yatakua yanamanisha kua ni maneno aliyoyasema Hannah Bint
Faqudh yaani Imraat Al Imran.
Na hivyo basi hapa itakua Hannah Bint Faqudh hamaanishi kua kwake yeye basi bora
angepata Mtoto wa Kiume, bali alikua akimaanisha kua: ‘Hakika mimi nilitaka mtoto
wa Kiume lakini Allah Subhanah wa Ta’ala amenijaalia mimi Mtoto wa Kike, na
Mtoto wa kiume ambae niliemtaka hawezi kua kama mtoto huyu wa kike ambae
alienijaalia Allah Subhnah wa Ta’ala, kwani hata huyu pia ni bora’ na hii ni kwa
sababu Hannah Bint Faqudh alikua ni mwenye kuujua uwezo wa Mola wake juu yake
202
ambae ni mwenye kujua ni kipi bora kwa ajili yake, na hivyo hua ni mwenye kujaaliwa
na Mola wake kile kilichobora zaidi kwake,
Ambapo kama kama itakua tutaisoma aya hii kwa kusema: ‘WaAllahu aAAlamu bima
wadaAAat yaani Na Allah ni mwenye kujua zaidi ju ya kile alichojifungua’ basi
maneno yasemayo ‘Walaysa aldhdhakaru kaalontha’ yatakua yanamaanisha kua ni
maneno aliyoyasema Allah Subhanah wa Ta’ala.
Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala kua ni mwenye kumjibu Hannah Bint Faqudh kwa
kumaanisha kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala ni mwenye kujua ni kipi bora zaidi
kuhusiana na mtoto huyu wa kike aliezaliwa ambapo hapo baadae Maryam na
Mtoto wake wa kiume watakua ni wenye kuanza kua ni Muijiza kwa Ulimwengu
huu’ ambapo hata hivyo Hannah Bint Faqudh alikua hajui juu ya hilo kwani mtizamo
wake yeye ni wa kiumbe Ibn Adam ambao umejaa muonekano wa mazingira ya ufahamu
wa kimaumbile ya Ibn Adam na ndio maana akawa ni mwenye kuomba samahani kwa
Mola wake, kutokana na kuona kua malengo yake aliyonadhiria yatakua hayafanikiwi
kutokana na kutokujua kua Binti huyo ni bora zaidi kuliko mtoto mwengine yeyote yule
ambae angempata badala yake.
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anatuambia kuhusiana na kilichofuatia baada ya hapo
kwa kusema katika aya ifuatayo baada ya hio kua:
﴿فَتَقَب َّلَهَا رَب ُّهَا بِقَبُولٍ حَسَنٍ وَأَنبَتَهَا نَبَااتً حَسَناً وَكَف َّلَهَا زَكَرِ َّ كُل َّمَ ا دَخَلَ عَلَيْهَا
زَكَرِ َّ ٱلْمِحْرَابَ وَجَدَ عِندَهَا رِزْقاً قَالَ يمَٰرْيمَُ أَنى َّٰ لَكِ هَٰذَا قَالَتْ هُوَ مِنْ عِندِ ٱهلل َِّ
إنًّ ٱهللًَّ يَرْزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيرِْ حِ سَابٍ ﴾
Fataqabbalaha rabbuha biqaboolin hasanin waanbataha nabatan hasanan
wakaffalaha zakariyya kullama dakhala AAalayha zakariyya almihraba wajada
AAindaha rizqan qala ya maryamu anna laki hadha qalat huwa min AAindi Allahi
inna Allaha yarzuqu man yashao bighayri hisabin(Surat Al Imran 3:37)
Tafsir: Hivyo akamkubalia Mola wake kwa mkubalio ulio bora. Na akamfanya akuwe
katika makuzi mazuri na kumuweka chini ya usimamizi wa Zakarriyah. Hivyo kila
akiingia kwenye Mihrab (kumuangalia) alikua akimkuta na Riziki yake, hivyo
akasema: ‘Ewe Maryam, Umepata wapi yote haya?’ akasema (Maryam): ‘Hivyo ni
kutoka kwa Allah’ kwani kwa hakika Allah humruzuku amtakae bila ya hesabu
203
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamkubalia Hannah Bint Faqudhi maombi yake hayo
kwa mkubalio ulio bora kabisa na Maryam akawa ni mwenye Uzuri wa kimaumbile na
ubora wa kipekee usiokua na kuzidi ukubwa wa kitu chochote wake wala wa kupungua
kwenye mwili alikua ni mwenye kuvutia kuliko wote katika Wanawake wa wakati wake.
Uzuri wake huo ulikua ni wenye kuonekana dhahiri tangu wakati alipozaliwa kiasi ya
kua mtu alivutiwa nae na alipopelekwa kwa Makuhani kwa ajili ya kuombewa basi
walipomuona kila mtu ambae aliekua na uhusiano na Mzee Imran alikua anataka kua
ndio awe mlezi wake Mtoto huyo. Na Makuhani wakataka wamlee wao kwani ni mtoto
wa Mzee Imran ambae ndie aliekua Kiongozi wao Makuhani hao.
Hivyo Nabii Zakariyah ambae ni Mume wa Isha Bint Faqudh ambae ni Mama yake
Mdogo Maryam akasema kua yeye anastahiki kua ndie mlezi zaidi kwa sababu Mke wake
ni Mama yake mdogo Maryam.
KAFFALA – ULEZI WA MARYAM BINT IMRAN.
Hivyo jamii ya watu hao ikaamua kua wakarushe kalamu zao Mtoni na hivyo Kalamu ya
yule ambae haitozama kwenye maji ya Mto huo basi ndie atakaekua na Bahati ya kumlea
Mtoto huyo. Hivyo wakaondoka watu 19 pamoja na Nabii Zakariyyah hadi katika Mto
Jordan, na kisha wakachukua Kalamu zao ambazo ndio walizokua wakiandikia Tawrat,
na walipofika kwenye Mto huo basi wakazirusha Mtoni moja baada ya nyengine. Na hii
ni kutokana na kama ilivyolezewa katika aya ifuatayo ambayo Allah Subhnah wa Ta’ala
anamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kusema:
﴿ذٰلِكَ مِنْ أَنْبَآءِ ٱلْغَيْبِ نُوحِ يهِ إِلَيكَ وَمَا كُنْتَ لَدَيْهِمْ إِذْ يُلْقُونَ أَقْلاَمَهُمْ أَي ُّهُمْ
يَكْ فُلُ مَرْيمََ وَمَا كُ نْتَ لَدَ يْهِ مْ إِذْ يخَْتَصِ مُونَ ﴾
Dhalika min anba-i alghaybi nooheehi ilayka wama kunta ladayhim idh yulqoona
aqlamahum ayyuhum yakfulu Maryama wama kunta ladayhim idh yakhtasimoona
(Surat Al Imran 3:44)
Tafsir: Haya ni katika habari za Ghayb tunakushushia juu yako, na wewe hukua mbele
yao waliporusha Kalamu zao (kuamua) ni yupi amtunze Maryam na hukua mbele yao
walipokua wakihasimiana.
204
Ambapo aya hii inatuonesha kuruhusika kufanya Bahati Nasibu ya aina hii ambayo ni
Bahati Nasibu ya Qurah (kupiga Kura), hivyo hapa haikusudiwi kua ile ya Kamari, kwani
kuna Bahati Nasibu ya Kamari na kuna Bahati Nasibu ya Bahati Nasibu yaani ya Qurah
ambapo Mujaddid Ad Din Shaykh Ul Islami Imam Ibn Hajar Al Asqallani na pia Imam
Abu Hasan Ali Ibn Muhammad Ibn Habib Al Mawardi Al Shafii wanaelezea Bahati
Nasibu ya Qurah ambayo ndio inayokubalika kisharia kwa kusema kua: ‘Bahati Nasibu
(Qurah) iliyokua ikifanywa ilikua kuna majina yanaandikwa kwenye vitu na kisha,
huitwa Mtu ambae ni Mgeni achague, na yule aliechaguliwa jina lake basi hua ndie
alieshinda na ndie atakaechaguliwa. ’
Na pia akasema Shaykh Islami Imam Abu Abd Allah Badr Ad Din Muhammad Ibn Abd
Allah Ibn Bahadir Al Zarkashi Al Shafii.: ‘Vyovyote vile itakafanywa (Qurah) Bahati
Nasibu basi hua inakubalika.’
Na kwa kua tumezungumzia Bahati Nasibu inayokubalika na Bahati Nasibu
isiyokubalika ambayo ni ya Kamari basi tuwekeane wazi zaidi kuhusiana na tofauti yake,
ambapo ‘Bahati Nasibu ya Kamari hua ni ile ya Watu kua wanatoa Kitu au
Wanalipia au Wanatuma Ujumbe wa Simu, na hivyo kua ni wenye kulipia asilimia
fulani inayokatwa kwenye simu zao kutokana na Ujumbe huo kwa ajili ya
kujumuishwa kwenye Mchuano wa Kuchaguliwa, ambapo kwa upande wa ujumbe
wa Simu hua zawadi haitolewi mpaka ifikie idadi fulani ya ujumbe uliotumwa
ambao utafikisha malengo ya kiasi cha pesa kinachotakikana kwa ajili ya kutoa
zawadi husika na hivyo kutokana na hali basi hili hua ndio jambo ambalo
lisilokubalika kisharia, kwani hua ni aina ya Kamari.’
Hivyo Mayahudi hawa akiwemo mzee Imran wakafanya Bahati Nasibu hio, na anasema
Imam Abd Rahman Al Suddi kua: ‘Ziliporushwa Kalamu hizo basi Kalamu ya
Zakariyyah ikaibuka juu a kusimama wima kama vile iliyorushwa kwenye Tope na
kisha ikaganda, huku Kalamu nyengine zote zikiwa ni zenye kuchukuliwa na
mkondo wa maji ya mto huo.’ hivyo Nabii Zakarriyah akawa ni mwenye kushinda
mashindano hayo na kua ni mwenye kubeba jukumu la kua ndie Mlezi wa Maryam Bint
Imran.
Na ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala akasema: ‘Waanbataha nabatan hasanan
wakaffalaha zakariyya kullama dakhala AAalayha Zakariyya yaani Na akamfanya
akuwe katika makuzi mazuri na kumuweka chini ya usimamizi wa Zakarriyah’
Ambapo aya imetumia neno Nabata ambalo mara nyingi hua linatumika
inapozungumziwa Miti na Mimea mbali mbali inayoota Ardhini kwani neno hili hua
linamaanisha Kuchipua, Kuota, Kukua, Kutoa Majani au Kunawiri bila ya kuonekana
athari ya kile chakula chake inachokula Mimea hio ambacho ni chenye kutokana na
Hewa, Maji na Udongo.
205
Ambapo tunapozungumzia Mtoto wa Ibn Adam basi hua inamaanisha Kukua katika
Mazingira yanayotokana na kuhudumiwa juu ya kila kitu, na hii ndio hali aliyokua nayo
Maryam kwani alikua na kila kitu ambacho anakihitajia ijapokua kitu hicho hakipatikani
kwenye maeneo ya ardhi hio au hayapatikani kwa sababu ya kua si msimu wake wa
kupatikana kitu hicho.
Na pia ikatumia neno Kaffala lenye kumaanisha Kulea Mtoto ambae si wa kuzaa yaani
wa Mtu mwengine, Kujali, Kusimamia, Kutunza, Kudhamini au Kuchunga ambapo neno
Kaffala ndio lililotoa neno Dhul Kifl ambalo ni jina lenye kumaanisha Mtu mwenye kua
na sehemu kubwa sana ya I’lm ambae amejitolea kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala
tu pekee.
Hivyo aya haikutumia asili ya neno Rabba lenye kumaanisha kua Mlezi ambae pia ni
Mzazi, kua Bwana kua Mmiliki, Bosi, Kutawala, Kumiliki, Kusimamia kwa kulea kutoka
hatua moja mpaka kuingia kwenye hatua nyengine, Kutunza, n.k. Neno Rabba ndio
lililotoa neno Rabb ambalo hua linamaanisha Muumba, Mtawala, Mfalme wa Kila kitu
cha Kimaumbile, Mwanzilishi na Msimamizi wa kila kitu tangu mwanzo hadi mwisho,
na hivyo kutubainishia kua Ibn Adam ni Kiumbe ameumbwa katika hatua zisizokua na
mipaka kimaendeleo.
Hivyo aya imetumia neno Kaffala kwa sababu neno hili kimaana hua pia linawakilisha
Kumuondolea Mzigo au Uzito mtu ambae ni mwenye kuhitaji kuwekwa chini ya
Uangalizi, Udhamini na uhifadhi na yule mwenye kubeba jukumu la Uangalizi huo
kisharia ambae hua ni Kafil juu ya yule mwenye kuhitaji kusimamiwa, kutokana na kua
ni mwenye sifa ya kua ni Yatima.
Ambapo miongoni mwa haki anazostahiki kuzisimamia Kafil basi ni lazima kwake
yeye ahakikishe kua anasmami majukumu yafuatayo:
Malezi Mazuri Kulingana na Imani ya Dini ya Kiislam: Ni wajibu wake Kafil
kuhakikisha kua anamsimamia na kumlea na kumtunza Yatima kulingana na malezi
yanayotokana na Mafunzo ya Kiislam kulingana na Maamrisho ya Qur’an na Hadith za
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuhusiana na malezi ya Mtoto.
Kwani tunapozungumzia Malezi Mazuri Kulingana na Dini ya Kiislam juu ya Mayatima
basi ili yakamilike Malezi hayo Ndani yake inabidi kuwe na Miongoni mwa Hali
zifuatazo ambazo hua ni Jukumu la Mlezi:
1-Kila Mlezi mwenye kubeba Jukumu la Kulea Mtoto ambae ni Yatima basi
anatakiwa Ahakikishe kua Anamlea Mtoto Husika katika Malezi ya Kiislam kama
ilivyoamrishwa na Allah Subhanah wa Ta'ala na Mtume wake Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam Hivyo Mtoto Huyo anatakiwa amsimamie katika kumtekelezea
206
Mahitaji yake muhimu kama ya Chakula, Malazi, Mavazi, Usimamizi wa Mirathi
yake n.k
2-Anaebeba Jukumu la Kulea Mayatima basi hua ni Wajibu wake kuhakikisha kua
Watoto au Mtoto wanapata haki yao ya Kupata Elimu ya Dini ya Kiislam kwa ajili
ya Dunia yao na Kwa Ajili ya Akhera yao, na pia ahakikishe kua Yatima au
Mayatima hao Wanapata Elimu ya Kidunia kwa ajili ya kuendeleza na Kuboresha
Maisha yao Duniani hapo baadae.
3-Mwenye Kubeba Jukumu la Kulea Watoto Mayatima au Yatima anatakiwa
ahakikishe kua Watoto au Mtoto Wanaishi katika Mazingira yaliyojaa Imani,
Upendo, Huruma na Tabia Njema Ndani yake Ili watoto hao wasije wakaharibika
kutokana na kurithi tabia zisizokua za Kiislam kutokana na kutofunzwa Akhlaki
na maadili ya Kiislam na hivyo, kua na Mitizamo mikali ya Dini yake au Kutokua
na Iman ya Dini yake, ma hivyo kukosa kua ni mwenye Huruma na Upendo kwa
Watoto wenzake na viumbe wengine katika maisha yake.
4-Wenye kulea Watoto Mayatima au Yatima hawatakiwi kubeba uzito wa Mzigo
wa zaidi ya Uwezo wao kama vile ilivyo kwa wengi miongoni mwa baadhi ya Watu
kiasi ya kua Matokeo yake Watu kuanza kutumia kisingizio cha Watoto hao na
kuanzisha Usumbufu na maaudhi kwa wenzake kutokana na kuwatumia watoto
hao kua ni chanzo cha kuingizia mapato kwa Kuomba Omba ovyo hapa na pale, wa
ajili ya kuwatekelezea mahitaji yao.
Kwa Sababu mbali ya Kua Uislam Umekataza Kuomba, kulingana na Aya na pia
Kulingana na Hadith za Rasul Allah A'alayhi wa Salam kwa Sababu katika Kuomba
Omba hua wanawasababishia Dhambi Waislam wenzao wanaowaomba. Na hii pia ni
kwa Sababu si kila mwenye Kutoa basi hua ni mwenye kutoa kwa Nia na Moyo Msafi,
kwani kuna wanaotoa kwa kinyongo, kuna wanaotoa kwa Unafiq, kuna wanaotoa kwa
kujikalifisha, kuna wanaotoa kwa kujionesha n.k.
Ambapo amesema Qabisah Ibn Mukharik Al Hilali Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi
nilingia kwenye Deni kwa ajili ya kupatanisha watu wawili na hivyo nikaenda kwa
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kumuomba msaada kutokana na deni hilo,
hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kua: ‘Subiri pamoja nasi
mpaka tuletewe Zakkah na kisha nitaamrisha upewe kitu chochote’ kisha Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaema: ‘Ewe Qabisah! Fahamu kua kuomba
Msaada hakuruhusiki isipokua katika hali tatu zifuatazo:
‘Kwa Mtu ambae ameingia kwenye Deni kwa sababu ya kupatanisha pande mbili,
kwani huyu anaruhusika kuomba mpaka amalize deni hilo, na kisha ajizuie
kuomba;
207
Kisha yule mtu ambae aliefikwa na Msiba ambao umemuangamizia Mali yake yote,
huyu hua anaruhusika kuomba hadi pale atakapokaa sawa;
Na kisha yule ambae ni Masikini sana, na hivyo watu watatu wenye Busara
miongoni mwa watu wake, wakathibitisha kua amefikwa na Umasikini na
anastahiki kuomba hivyo hapa hua anaruhusika kuomba msaada hadi pale
atakapotokana na hali hio.’
‘Hivyo Vyenginevyo zaidi ya hali hizi basi Mtu haruhusiwi kuomba, Ewe Qabisah!
Ni Haram kuomba Msaada, na anaeomba kisha akawa ni mwenye kula kutokana
na alichoomba basi hua anakula Haram’(Sahih Muslim, Musnad Imam Ahmad, Sunan
An Nasai, Sunan Abu Daud.)
Akasema tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hairuhusiki kumpa
Sadaka mtu ambae ni Mwenye uwezo au kwa yule ambae ni mwenye Nguvu na
Afya’(Imam At Tirmidhii)
Na siku moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimpa Umar Ibn Al Khattab Radhi
Allahu Anhu zawadi, hivyo Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akasema
kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Ya Rasul Allah bora mpe
mtu mwengine mwenye shida nayo zaidi yangu
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Yule ambae anaeomba
wengine kwa ajili ya kujiongezea Mali yeye mwenyewe basi hua ni sawa na
anaeomba Makaa ya Moto (wa Jahannam) hivyo mwache mwenye kuomba aombe
kidogo au zaidi: ‘Chukua, kisha kaa nayo au igawe kama Sadaka, na chochote kile
kitakachokuja kwako katika hali kama hii bila ya wewe kua ni mwenye Tamaa au
Kuomba basi pokea lakini kitakapokuja katika hali ya mazingira mengine basi
usikikimbilie kwa kukitamania’’(Sahih Muslim)
Na ndio maana akasema Imam Nur Al Din Abu Al Diya `Ali Ibn Al Shabramilisi Al Shafii
kua: ‘Kama Mtu Mmoja atampa Mtu fulani Sadaqa yake kwa kudhania kua Mtu huyo
ni fulani, na kisha akagundua kua mtu huyo sie aliemdhania basi Mtu alietoa Sadaka
anaruhusika kuichukua mwenyewe sadaka yake hio.’ (Hashiyyat Al Shabramilisi ala
Nehayat al-Muhtajj)
Ambapo kitu kinachotolewa katika Njia kama hizi hua hakina Barka ndani yake kwa
anaetoa na pia kwa anaepokea na Bila ya Shaka unapopokea kitu kama hiki basi unaweza
ukawasababishia matatizo mbalimbali wle unaowalea ikiwemo ya Udhaifu wa Kiimani
wale unaowalea.
208
Hivyo kama vile ambavyo Riziki yako inavyotakiwa iwe ya halali na isiwe iliyopatikana
kutoka kwa mtu ambae amekupa kwa kinyongo, kwa shingo upande, bila kuridhia au bila
ya Moyo Msafi na Nia safi n.k
Ambapo amesema Abu Kabshah Al Anmari Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alisema kua: ‘Nnaapa juu ya vitu vitatu ambavyo
nakutakeni nyinyi myahifadhi maneno yangu juu yake kua: ‘Sadaqah inayotolewa
katika Mali hua haipunguzi Mali husika, Mtu anaepatwa na Mitihani na akawa na
Subra juu yake, basi Allah Subhanah wa Ta’ala humpa Uwezo (na kumpandisha
Darja) na Mtu anaeanza Kuomba kua Allah Subhanah wa Ta’ala atamsababishia
mtu huyo kua na umasikini.’’’(Imam At Tirmidhi)
Ambapo tunapoangalia kuhusiana na Upande wa Fiqh basi kuna hali tatu tofauti
kuhusiana na Maumbile ya Kuomba, ambazo ni:
1- Hairuhusiki Kuomba: Kua imekatazwa kwa mtu kua ni mwenye kuwaomba watu na
huu ni mtizamo wa wengi miongoni mwa Wanazuoni, ambapo miongoni mwao ni
pamoja na Imam Muhammad Idris Al Shafii, Imam Ahmad Ibn Hanbal, Imam Abd Al
Barr Al Maliki, Imam Al Qurtubi, Imam Al Sannani, Imam Al Sarkhasi, Imam Al Kasani,
Imam Al Razi, Imam Al Shibrini, Imam Ibn Qudamah n.k ambapo kwa upande wa
Madhhab ya Imam Abu Hanifa basi wanasema kua : ‘Hairuhusiki kumpa mtu
anaeomba Msikitini’
Kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kuomba Pesa hua si
sawa na Mtu anaeomba Makaa ya Motoni’(Sahh Muslim) na pia akasema kua:
‘Kuomba ni Jambo baya sana wenye Uso wa Mtu isipokua pale mtu anapokua
anaemuomba ni Mtawala wake au ni kitu cha muhimu sana’(Imam At Tirmidhi)
Ambapo kwa upande wa Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Al Ghazali kua:
‘Tunapozungumzia kuhusiana na kuomba basi kua tunaona hua ni kulalamika kwa
kubainisha Umasikini wa Muombaji kua amepungukiwa na Rehma za Allah
Subhnah wa Ta’ala. Na pia huonesha kua na unyenyekevu kwa mwengine zadi ya
Allah Subhnah wa Ta’ala wakati Waumini wanatakiwa wawe wanyenyekevu kwa
Allah Subhanah wa Ta’ala tu na mara nyingi hua inasababisha kero kwa
anaeombwa, na hii ni kwa ababu labda hua hawataki kutoa na hivyo hua ni wenye
kutoa kwa ajili ya kujionesha au kwa njia ya kuona aibu au kwa njia ya Unafiq. Au
huwabidi kutoa ili wasionekane kua ni Mabakhili. Hivyo kuomba kumekatazwa
kwa anaepokea’
Na wa Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye anasema kua: ‘Ingawa hairuhusiki
kuomba, lakini hua inakubalia pale inapokua anaeomba hua hajidhalilishi mbele
209
ya anaemuomba na hamsababishii kero yule anaemuomba, kwani ikiwa ni hivyo
basi hairuhusiki kabisa.’
Ambapo Imam An Nawawi amesema kuhusiana na Hadith hi kua: ‘Kuomba
kumekatazwa kwa sababu vyenginevyo basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
asingehimiza kuachana nako kuomba’
2- Ni Makruh Kuomba: Hujjat ul Islami Imam Mujaddid Ad Din Abu Hamid
Muhammad Al Ghazali anasema kua: ‘Ni Makruh kuomba ndani ya Msikiti lakini sio
Sadaqa isipokua pale inapokua Imam anatoa Khutba, na hii hua inakatazwa kwa
sababu wale wanaoomba hua wanafanya lile lililokatazwa na hawatakiwi kusaidiwa
kufanya hivyo.
Ambapo kwa upande wa Imam Zakariyah Al Ansari basi yeye anasema kua: ‘Kuomba
Msikitini haipendekezwi na hua inakirihisha na kuwapa wanaoomba hua kuna
malipo na hakukirihishi bali kuna katazwa, kama alivyosema Imam Al Shafii kua:
‘Kumuomba mtu kwa Jina la Allah au kwa ajili ya Allah kunakirihisha, yaani kwa
mfano kusema; ‘Nakuomba kwa jina la Allah, au Nakuomba kwa ajili ya Allah’ na
hivyo kuwapa watu kama hao wanaosema hivyo hua haipendekezwi’’
3- Inaruhusika Kuomba: Wengi miongoni mwa Wanazuoni wanakubaliana kua
kuomba kwa yule ambae atafanya hivyo kwa ajili ya kutatua matatizo yanayotokana na
kula hasara ya kupoteza Mali au Roho kwa kufiwa au kwa kutakiwa kulipa pesa za fidiya,
au kwa ajili ya kutatua ugomvi baina ya pande mbili, basi hua wanaruhusika kuomba
hadi pale watakapofanikiwa kutatua matatizo yao kama ilivyoelezewa kwenye hadith ya
Qabisah.
Hivyo kutokana na hali hii inayobainisha Ubaya wa kuomba basi Mtu unatakiwa uwe
makini zaid pale unapokua Una jukumu la Kuwalea watoto Mayatima kwani ukifanya
sivyo na kuanza kuomba basi badala ya Kupata Thawabu ya kulea Mayatima basi hua
unapata Dhambi badala yake.
Kwa Upande Mwengine pia ndani yake Jukumu hili pia hua pia inaingia ile hali ya Mtu
Kulea Mtoto wa Ndugu yake, au Baba yake Mdogo au Mama yake mdogo n.k Pale
inapokua Mzee wa Mtoto huyo hana Uwezo wa Kumhudumia Mtoto huyo, na Hivyo Mtu
husika anaechukua Jukumu la Ulezi huamua Kubeba jukumu hilo kwa ajili ya Kumsaidia
Ngugu yake huyo Ulezi wa Watoto wake kutokana na yeye kua na uwezo zaidi yake. Na
ndio maana jana nikasema Kua Mtu asiekua na Uwezo wa Kulea Mayatima basi hatakiwi
Kuikalifisha Nafsi yake kwa kubeba Jukumu asiloliweza kwani atakua anapata dhambi
badala yake.
210
Hivyo asiekua na Uwezo anaruhusika Kulea Yatima Lakini wa Jamaa yake pale inapokua
hakuna Njia nyengine ya kufanya yaani hakuna Mtu mwengine zaid yake na hivyo yeye
atapata Malipo zaid kutoka kwa Mola wake. Kutokana na Kua huo ni Mtihani kwake
ambao inabidi awe na Subra nao kwa Upande mwengine basi Mtu mwenye uwezo
anaruhusika Kubeba Jukumu la Kulea Mtoto iwe ni mwenye Uhusiano nae kama Jamaa
yake ama la.
Hata Kama Mzee wa Mtoto huyo atakua Bado yuko hai au wako hai, Lakini itakua Bora
zaid pale atakapomlea Mtoto ambae Mzee wa Mtoto huyo aliekua hai lakini hana Uwezo
wa Kiuchumi wa Kumlea Mtoto huyo.
Ambapo Jukumu hilo la Kumlea Mtoto huyo hua ni sawa na Uzito wa Jukumu la kumlea
Yatima, Laqit na Munqati, Kwani humbidi kumtekelezea Haki zake zote kama
tulivyoeleza hapo kabla na tunapoangalia Mfano mzuri wa jambo hili basi tunauona
katika tukio alilolifanya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika kipindi cha Uhai
wake kabla ya Kupata Utume wake pale alipoamua kumsaidia ulezi Ami yake yaani Abu
Talib Radhi Allahu Anhu kwa kuamua kumlea Ali Ibn Abu Talib Radhi Allahu Anhu
kama tutakavyoona hapo baadae kwenye kitabu hiki.
HAKI ZA YATIMA, MUNQATI NA LAQIT KATIKA UISLAM
Neno Yatima linatokana na neno Yatama ambalo hua linamanisha Kua Yatima, Kua bila
ya Baba katika wakati ambao mtu hajafikia umri wa miaka 15, Kua bila ya Mama kwa
Mnyama, na kwa upande wa Mwanamke hua ni Yatima pale anapokua hana Mume
kutokana na kua hajafikia Umri wa Kuolewa au Mjane wa Kufiwa na Mumewe au wa
Kuachwa, Kua peke yake, Kufifia, na pia humaanisha kua Mchovu.
Ambapo Imam Raghib Isfahani basi yeye anasema kua: ‘Yatima hua ni Kitu au Mtu
ambae yuko peke yake, alietengwa na hana mtu yeyote. Kwa mfano Durra Al Yatima
hua linamaanisha Lulu kubwa sana iliyoghali na isiyokua na mpinzani kwa
thamani. Na hivyo neno Yatima hua linamaanisha pia Kitu chenye thamani kubwa
zaidi ukilinganisha na vyenzake, Mtu aliewapita wenzake katika mambo
mbalimbali, Mtoto asiekua na Baba hua anaitwa Yatima na Mtoto asiekua na Mama
hua anaitwa Munqati (yaani Mtu aliekatiwa Mama yake)’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala katika ya hii anatuonesha umuhimu na utukufu wa
Yatima ambae hapa anawakilishwa na mtoto wa kike aitwae Maryam Bint Imran ambae
amefiwa na Baba yake, kama vile aliyoelezea kwenye Surat Adh Dhuha kuhusiana na
211
Yatima ambae si mwengine yeyote isipokua Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam
kwa kusema:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٰ ٱلر َّحِ يمِ۞وَٱلض ُّحَى ٱ ۞َو ل ل َّيْ لِإِذَا سَ جَ ٰ ى ۞مَا وَد َّ عَكَ رَب ُّكَ وَمَا
قَلَى ٰ ۞وَلَلآخِ رَةُ خَيْرٌ ل َّكَ مِنَ ٱلأُولىَٰ۞وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَب ُّ َك
فَتَرْضَى ٰ ۞أَلمَْ يجَِ دْ َك
يَتِيماً فَآوَىٰ ۞وَوَجَدَكَ ضَآلاًّ فَهَدَىٰ ۞وَوَجَدَكَ عَآئِلاً فَأَغْنىَٰ ۞فَأَم َّا ٱلْيَتِيمَ فَلاَ
تَقْهَرْ ۞وَأَم َّا ٱلس َّآئِلَ فَلاَ تَنْهَرْ ۞وَأَم َّا بِنِعْمَ ةِ رَبِّكَ فَحَ دِّثْ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi, Waaldhdhuha; Waallayli idha saja, Ma
waddaAAaka rabbuka wama qala; Walal-akhiratu khayrun laka mina al-oola;
Walasawfa yuAAteeka rabbuka fatardha; Alam yajidka yateeman faawa;
Wawajadaka dhallan fahada; Wawajadaka AAa-ilan faaghna; Faamma alyateema
fala taqhar; Waamma alssa-ila fala tanhar; Waamma biniAAmati rabbika
fahaddith(Surat Adh Dhuha 93:1-13)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma Mwingi wa Huruma. Naapa kwa wakati
wa Dhuha (baina ya Asubuhi na kabla ya Adhuhuri) Na Kwa Usiku unapoingia na
kutulia. Hajakuacha Mola wako wala hajakuchukia; Na kwa hakika yatakayokuja ni
bora kwako kuliko ya Awali yaliyotangulia. Na kwa hakika uwezo kamilifu atakupa
Mola wako na Utaridhika. Jee hakukuona wewe kua ni Yatima akakupa makazi? Na
hakukona wewe kua umepotea akakuongoza? Jee hakukuona wewe huna kitu
akakutajirisha? Hivyo na Yatima usimdidimize. Na mwenye kuomba usimfukuze. Na
kuhusiana na Neema za Mola wako zihadithie.
Ambapo katika Sura hii basi Allah Subhanah wa Ta’ala anaanza na:
ٰ ﴿وَٱلض ُّحَى ٱ ۞َو ل ل َّيْ لِإِذَا سَ جَ ٰ ى ﴾
Waaldhdudha; Waallayli idha saja (Surat Adh Dhuha 93:1-3)
Tafsir: Naapa kwa wakati wa Dhuha (baina ya Asubuhi na kabla ya Adhuhuri) Na
Kwa Usiku unapoingia na kutulia.
212
Ambapo neno Dhuha ni lenye kutokana na neno Dhahiya lenye kumaanisha Kupigwa na
Nuru ya Mionzi ya Jua, Kudhurika kutokana na Mionzi ya Jua, Kufunuliwa au Kuachiwa
wazi, Kuonekana wazi na Jicho au na Ufaham. Hivyo neno Dhuha linamaanisha Wakati
au Mda unaofuatia mara tu bada ya kuchomoza Jua, Mwangaza Kamili wa Jua, sehemu
ya siku ambayo tayari Jua lishapanda na liko juu.
Na neno Saja hua linamaanisha Kua na Utulivu, Kua Kimya, Kutulia, Kufunikwa,
Kutandazwa kwa kugubikwa na kiza.
Na hivyo basi maneno ya aya 2 hizi yanatubainishia Kiapo cha Allah Subhnah wa Ta’ala
anachokiapia kutokana na Maumbile ya Wakati na umuhimu wa Wakati katika kuwepo
kwake, kwani wakati wa kitu hua ni kulingana na hali ya kuwepo kwake kitu hicho
kulingana na matukio na hali ya mabadiliko ya kitu na ndio maana Shaykh Al Akbar
Muhyi Ad Din Imam Abu Bakr Ibn Arabi Al Maliki Al Qurtubi akasema kua: ‘Wakati
wa kitu hua ni katika kuwepo kwake’.
Hivyo tunapoangalia hali ya mabadiliko ya wakati Uhai wa Ibn Adam hua kama wakati
wa siku mwanzo wake huanzia Asubuhi na mwisho wake hua Usiku, na aya imeainisha
wakati na kubainisha matukio na mabadiliko ya hali ya kimaumbile yanayotokea baina
ya Asubuhi na kabla ya Mchana na Usiku unapoingia na Kiza kinapotanda na kinapotulia,
na hivyo kuwapa viumbe wa Allah Subhanah wa Ta’ala wakati wa kupata utulivu wa
kujipumzisha baada ya matukio ya harakati za kujitafutia Riziki Mchana kutwa.
Na kwa kua Sura hii inamzungumzia Rasul Allahu Salallahu Alayhi wa Salam basi
inatuonesha kua Allah Subhanah wa Ta’ala ameapa kwa wakati kuthibitisha na
kusisitizia umuhimu wa wakati kuainisha mabadiliko ya kimaumbile ya Rasul Allahu
Salallahu Alayhi wa Salam kwa kuanzia na wakati wa Dhuha na hivyo kuwakilisha
kipindi cha wakati wa pirika pirika za maisha ya Utotoni wa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam na kisha ikamalizia na wakati Usiku unapoingia na kutulia kuwakilisha wakati
wa baadae wa Rasul Allah Salallahu A’alayi wa Salam utakavyokua hapa Duniani na
Kesho Akhera, na haya yote yanawekwa wazi na aya zilizomo ndani yake Sura hii
ambapo aya zinendelea kwa kusema:
﴿مَا وَد َّعَكَ رَب ُّكَ وَمَا قَلَى ٰ ﴾
Ma waddaAAaka rabbuka wama qala (Surat Adh Dhuha 93:3)
Tafsir: Hajakuacha Mola wako wala hajakuchukia;
213
Ambapo sababu ya kushushwa kwake inaelezewa na hadith ya Jundub Ibn Sufyan Radhi
Allahu Anhu ambae anasema:
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua anaumwa na hivyo hakua ni mwenye
Kusali Qiyam Al Layl kwa siku 2-3. Kutokana na hali hio basi kuna Mwanamke
alikuja kwake na kumwambia: ‘Muhammad, natumai kua Shaytan wako
amekuacha na kukukimbia, kwa sababu sijamuona mimi karibu yako kwa siku 2-
3 hivi.’(Sahih Muslim)
Na kwa upande wa Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari basi yeye anasema
kua huyu hakua ni Mwanamke yeyote yule isipokua alikua ni Arwa Bint Harb ambae ni
maarufu kama Ummu Jamil ambae ni dada yake Abu Sufyan Radhi Allahu Anhu na ni
mke wa Abu Lahab ambae ni Ami yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Ambapo kwa upande wa Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakkalimin Imam Fakhr Ad Din
Al Razi basi yeye anahoji kwa kusema kua: ‘Hivi jee ilikua kuna umuhimu wa Allah
Subhanah wa Ta’ala kusema kua hamchukii Rasul Allah Salallahu Alahyi wa
Salam?’ kisha Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakkalimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi
anajibu hoja hio kwa kusema: ‘Bila ya shaka La! bali hii ni kutokana na tuhuma
zilizoshutumiwa hivyo imebidi ibainishwe, yaani hii ni kama vile ambavyo mtu
anapoambiwa kua Mfalme anamchukia, hivyo Mfalme anapotaka kulipinga hilo
basi humwambia mtu huyo kua; ‘Hakika mimi sikuchukii wewe wala si sikupendi,
na hivyo karibuni nitakupa darja ambayo itakuridhisha kutokana na kua pamoja
nami.’’
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anamuahidi Mtume wake Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kwa kumwambia kua:
﴿وَلَلآخِ رَةُ خَيْرٌ ل َّكَ مِنَ ٱلأُولىَٰ ﴾
Walal-akhiratu khayrun laka mina al-oola (Surat Ad Dhuha 93:4)
Tafsir: Na kwa hakika yatakayokuja hapo baadae ni bora kwako kuliko ya yale ya
Awali yaliyotangulia hapo kabla.
Na hivyo kuainisha umuhimu wa kua na Subra na kutokata tamaa juu ya kile
anachokitaka ambapo bila ya shaka hii pia ni kwa sababu Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam mwenyewe alikua ni mwenye kupendelea yajayo kesho Akhera ambayo ni
yenye kudumu milele ukilinganisha na ya leo ya mpito ya Kidunia, kwani siku moja
alikua amelala kwenye Jamvi, na kutumia bega lake na mkono wake kua ndio mto wake
214
hivyo aliponyanyuka basi bega lake likawa limefanya alama ya jamvi hilo alilolalia na
akawa anajisugua sugua ili alama hio iondoke.
Hivyo Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu akamwambia Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kama atawaruhusu basi watamtengenezea tandiko laini, na hivyo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Mimi niifanye nini Dunia hii? Wakati
mfano wangu kwa Dunia hii ni sawa na mpanda Farasi alie safarini katika siku ya
joto kali kisha akafika chini ya mti na kukuta kivuli na hivyo akaamua kupumzika,
na kisha akaondoka kwenye sehemu hio na akaenda zake. ’
Kwani amesema Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
﴿زُيِّنَ لِل َّذِينَ كَفَرُواْ ٱلحَْيَاةُ ٱلد ُّنْيَا وَيَسْخَرُونَ مِنَ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ وَٱل َّذِينَ ٱت َّقَواْ فَ وْقَهُمْ
يَوْمَ ٱلْقِيَامَةِ وَٱهلل َُّ يَرْزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيرِْ حِ سَابٍ ﴾
Zuyyina lilladheena kafaroo alhayatu alddunya wayaskharoona mina alladheena
amanoo waalladheena ittaqaw fawqahum yawma alqiyamati waAllahu yarzuqu
man yashao bighayri hisabin (Surat Al Baqara 2:212)
Tafsir: Yamependezeshwa kwa waliokufuru maisha ya Dunia na yamedharaulishwa
kwa wenye Kuamini, na kwa wale watakao kua na Taqwa basi watakua juu yao katika
Siku ya Malipo, na Allah ni mwenye kumruzuku amtakae bila ya hesabu.
Naam..hiki ni kigongo katika Vigongo Vinavyoumiza wale wenye Akili na kutafakkari,
hivyo kama hujakihisi basi Jipekue ndani ya Moyo wako ili ujijue Imani, Akili na
Ufaham wako umeenda Wapi?
Kwani tunatakiwa tutanabahi ili tufahamu kua Ingawa kweli Sisi tunajihesabu kua ni
Waislam lakini jee Tunapoiangalia Dunia hii tunaionaje? Inatuvutia na Kupendeza
kwenye Macho na Nyoyo zetu au Inadharaulika na kuonekana kua ni Dhihaka kwenye
Macho na Nyoyo zetu?
Ambapo kulingana na Aya basi tunaona kua: Hata waliotangulia walijiona kua Wamefika
hapa Duniani, walikua na Mamlaka makubwa na yenye Nguvu, walikua na Ulinzi
Mkubwa, Majumba Makubwa na Magari ya Kifahari n.k Lakini waliondoka na kuacha
kila kitu hapa hapo Duniani
215
Naam.. Hio ndio Hali ya Wasiojua kua Wakati wao uliopita na waliokua nao si chochote
kwani yote yaliyotokea ndani yake hayana thamani, yenye Thamani ni yale Yajayo katika
Wakati utakaokuja.
Kwani alisema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Ni kawaida ya Ibn Adam
kua ni mwenye kusema: Mali zangu Mali zangu, Lakini Jee Hivi Kuna Mali yako
gani zaidi ya ile ambayo tayari Umeshaila na Kuimaliza? zaidi ya ile ambayo tayari
Umeshaivaa na Imeshachakaa? zaidi ya ile ambayo Umeshaitumia na
Imeshamalizika? Hivyo Kilochobakia hakitakua chako kitakua wengine pale wewe
utakapokua hupo(Sahih Muslim)
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anamthibitishia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuhusiana na kutimizwa kwa ahadi hio kwa
kumwambia kua:
﴿وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَب ُّكَ فَتَرْضَى ٰ ﴾
Walasawfa yuAAteeka rabbuka fatardha.(Surat Adh Dhuha 93:5)
Tafsir: Na kwa hakika uwezo kamilifu atakupa Mola wako na kisha Utaridhika
Kwani neno Sawfa ni lenye kutokana na neno Safa ambalo hua linamaanisha Kua na
Harufu, Kua na Subira, Kuakhirisha, Kumpa mtu uwezo kamilifu wa kufanya atakavyo.
Hivyo neno Sawfa hua linamaanisha Ahadi yenye uhakika kamilifu itakayotekelezwa
hapo baadae.
Ambapo Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi yeye anasema
kuhusiana na aya hii kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alioneshwa Hazina
zote ambazo watafunuliwa watu wa Ummah wake baada yake. Jambo hili
lilimfurahisha sana, kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akamshushia Aya hii na
akamjengea makasri 1000 Peponi, ambao kila moja likiwa na Mke na wafanya kazi
watakaomfaa yeye.’(Imam At Tabari)
Ama kwa upande wa Bab Al Ilm Amir u Muuminin Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu
basi yeye anasema kua: ‘Hii inamaanisha atapewa Uombezi autakao juu ya Ummah
wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa namna atakavyoridhia’ Bab Al Ilm
Amir u Muuminin Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu alisema pia kua: ‘Watu wa Iraq
walikua wakiichukulia kua aya ya Surat Az Zumar isemayo:’
216
﴿قُلْ يٰعِبَادِىَ ٱل َّذِينَ أَسْ رَفُواْ عَلَى ٰ أَنفُسِ هِ مْ لاَ تَقْنَطُواْ مِن ر َّحمَْةِ ٱهلل َِّ إِن َّ ٱهلل ََّ يَغْفِرُ
ٱلذ ُّنُوبَ جمَِيعاً إِن َّهُ هُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلر َّحِ يمُ ﴾
Qul ya AAibadiya alladheena asrafoo AAala anfusihim la taqnatoo min rahmati
Allahi inna Allaha yaghfiru aldhdhunooba jameeAAan innahu huwa alghafooru
alrraheemu(Surat Az Zumar 39:53)
Tafsir: ‘Sema: ‘Enyi Waja wangu ambao mliovuka mipaka dhidi ya Nafsi zenu (Kwa
kufanya maasi), msikate tamaa na Rehma za Allah kwani kwa hakika Allah
anasamehe Dhambi zote kwani kwa hakika yeye ni mwingi wa Kusamehe na ni mwingi
wa Rehma’’
Kua ndio tegemeo lao kubwa, lakini sisi Watu wa Ahl Al Bayt tunaamini kua aya
iliyobeba matumaini yote ni ile isemayo: Walasawfa yuAAteeka rabbuka fatardha -
Na kwa hakika uwezo kamilifu atakupa Mola wako na kisha Utaridhika’
Kwani Mbali ya Kua Amir ul Muuminin Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu amesema
kuhusiana na aya hii ya 6 kua inabashiria kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
Atapewa Nafasi Kamilifu ya kuuombea Ummah wake katika siku ya Malipo pale
atakapokua katika Mahal Al Shufaa.
Lakini pia kwa upande mwengine basi anasema Imam Abu Muhammad Abd Allah Sahl
Al Tustari kua: ‘Aya Hii inamaanisha Kua Allah Subhanah wa Ta'ala amemridhia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Hivyo katika Siku ya Malipo atampa pia
Darja ya Kipekee ambayo ni ya kua katika sehemu inayojulikana kama Mahal Al
Shafaa katika Darja ya Maqaman Mahmudan’
Kwani Maqaman Mahmudan hua inamaanisha Sehemu Tukufu kuliko zote kufikika kwa
Ibn Adam ambayo hakuna atakaeweza kuifikia isipokua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kwani sehemu ya Daraja hio hua ni katika Upande wa Kulia wa Arshi ya Allah
Subhanah wa Ta'ala.
Ambapo neno Maqaman hua ni lenye Kutokana na neno Qama ambalo hua linamaanisha
Kusimama, Kunyanyuka, Kutulia tuli katika hali ya kusimama, Kustahmili, Kunyanyuka
kwa heshima.
Hivyo Neno Maqam hua linamaanisha Kukaa au Kusimama Katika sehemu fulani au
katika Darja fulani.
217
Na Neno Mahmuda hua ni lenye kutokana na neno Hamida ambalo humaanisha Kusifu,
Kutukuza, Kushukuru kutokana na sifa na Darja ya Anaeshukuriwa.
Neno Hamida ndio lilolotoa Hamd ambalo hua ni lenye kutumika kwa Ajili ya Allah
Subhanah wa Ta'ala katika kuonesha Shukran, Utukufu na Unyenyekevu Kuelezea
Upekee anaostahiki Kushukuriwa Allah Subhanah wa Ta'ala.
Hivyo neno Mahmuda hua linamaanisha Mwenye kusifika kwa Sifa Nzuri na
Kuheshimika. Na neno Mahmud ndio lililotoa Jina Muhammad ambalo ni la Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam lenye kumaanisha Mwenye Sifa Nzuri na Heshima Kubwa.
Ambapo amesema Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kuhusiana na
Maqaman Mahmudan kua: ‘Ni Darja ambayo atapewa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam katika siku ya Malipo, ambayo hii ni siku ambayo Watu watakua kama
walivyozaliwa bila ya nguo wala viatu, huku wakiwa wanasubiri kuhesabiwa Amali
zao. Halafu baada ya kusubiri baada ya mda mrefu, basi Rasul Allah Salallahu Alayi
wa Salam ataruhusiwa kuwaombea watu wake, hii sehemu atakayosimama
kuwaombea watu wake ndio inajulikana kama Maqaman Mahmuda’
Hivyo basi kwa maana hio basi aya hii pia hua inamaanisha kua Allah Subhanah wa
Ta'ala anamwambia Mtume wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kile
nilichokutayarishia Ewe Muhammad ni bora kuliko ulichonacho sasa hivi Unabii
wako na Utume wako, kwani mimi nimekutayarishia Mahal Al Shafaa na Maqaman
Mahmudan’
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anamkumbusha juu ya yale yaliyopita juu yake Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kumwambia kwa njia ya kumhoji na kumthibitishia
hali aliyokua nayo ya Uyatima katika wakati huo wa utotoni mwake na namna Allah
Subhanah wa Ta’ala alivyomsaidia kwa kusema:
﴿أَلمَْ يجَِدْكَ يَتِيماً فَآوَىٰ ﴾
Alam yajidka yateeman faawa; (Surat Adh Dhuha 93:6)
Tafsir: Jee hakukuona wewe kua ni Yatima akakupa makazi?
Ambapo katika kuhoji kwake basi Allah Subhanah wa Ta’ala ametumia neno Yajid
linalotokana na neno Jada ambalo hua linamaanisha Kuona kile kilichopotea, Kupata
Kitu kilichopotea, Kupata Kitu au Kuona. na pia akatumia neno Awa ambalo hua
218
linamaanisha Kuwajibisha au kusababisha kupata sehemu ya Makazi salama na yenye
utulivu, Kutulia, Kustaafu au Kupumzika, Kupata au kupewa Ukaribisho wenye utulivu.
Na hivyo Aya kua ni yenye kumuwekea wazi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alikua chini ya Uangalizi wa Mola wake katika kila hatua ya Maisha yake kuanzia katika
kipindi ambacho alipofiwa na Baba yake kabla ya kuzaliwa kwake an hivyo kua ni
Yatima, na akalelewa na Mama yake chini ya usimamizi wa Babu yake na kisha kufiwa
na Mama yake alipokua na umri wa miaka 6 na alipofiwa na Babu yake huyo alipokua
na umri wa miaka 8 na hivyo akalelewa na Ami yake, na pia pale alipofariki watu wa
Makkah walipotaka kumuua na Allah Subhanah wa Ta’ala akampa Awa katika Mji wa
Madinah .
Na hivyo pia aya ni kutuwekea wazi umuhimu wa Mayatima kua ni wenye kustahiki
kupata Awa yaani Kupewa sehemu ya Makazi, Kupewa sehemu ya kukaribishwa kuishi
ili apate utulivu asijihisi mnyonge au yuko peke yake au anaonewa kwa sababu mzee
wake hayuko n.k. kama tunapoona katika mfano wa hadith ifuatayo:
Anasema Mujaddid Ad Din Al Hafidh Imam Shihab ad Din Imam Ibn Hajar Al Asqalani
kua: ‘Siku moja baada ya Salat al Idd basi Rasul Allahi Salallahu Alayi wa Salam
alikutana na Mtoto (Zuhayr Al Saghir) ambae alikua amevaa nguo mbovu mbovu,
huku akiwa amekaa peke yake analia, wakati watoto wengine wakiwa wanacheza
kwa furaha. Hivyo Rasul Allah Sallallahu Aalayhi wa Salam akamkaribia Mtoto
huyo na kumwambia: ‘Mbona umekaa peke yako huku ukiwa unalia? Kwa nini
huendi kucheza na wenzako?’
Yule Mtoto ambae alikua hajui kua Mtu anaezungumza nae kua ni Rasul Allah
Saalallahu Alayhi wa Salam huku akiwa na kilio cha kwikwi akasema: ‘Oh..Sayyid,
hakika mimi Baba yangu amefariki, na Mama yangu ameolewa tena na Mume
mwengine, ambapo Baba yangu wa Kambo amenifukuza Nyumbani kwake, hivyo
nna njaa, sina nguo wala makazi, na leo hii nnaona wenzangu wakiwa na Wazee
wao jambo ambalo imenikumbushia Baba yangu ndio maana nikawa nnalia’
Baada ya kusikia maneno hayo ya Zuhayr Al Saghir basi Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akatokwa na machozi na kumkumbatia Mtoto huyo na kisha
akabusu kichwa chake na kumwambia: ‘Ewe Mtoto Mdogo, usiwe na huzuni kwani
unaweza kuniita mimi kua ni Baba yako, na Aisha ni Mama Yako, Ali kama Ami
yako, Hasan na Husein kama ndugu zako na Fatma kama Dada yako.’
Hapo uso wa Zuhayr Al Saghir ukang’ara kwa Nuru ya furaha, kutokana na kua
tayari ni mwenye kuingizwa kwenye familia ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam. Akachukuliwa hadi nyumbani kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akamvisha Nguo nzuri na wakala pamoja nae, kisha Zuhayr Al Saghir akatoka na
219
kuenda kucheza na watoto wenzake ambao walishangaa kumuona katika kama hali
hio.
Hivyo nao wakamuuliza: ‘Hapo kabla ulikua unalia na sasa hivi umekua na furaha,
kwanini?’ Zuhayr Al Saghir akajibu: ‘Hapo kabla nilikua nna njaa, lakini sasa hivi
nimeshiba, na nilikua Yatima lakini sasa hivi nna Baba kwani Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam ndie Baba yangu, Aisha ni Mama yangu, Ali ni Ami yangu, Fatma
ni Dada yangu na Hasan na Husein ni ndugu zangu’’ (Asbab Al Wurud - Fat-h Al
Barr)
Naam..hivyo kisha baada ya aya hio ya Surat Adh Dhuha 93:7 basi Allah Subhanah wa
Ta’ala anamhoji tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa njia ya kumthibitishia:
﴿وَوَجَدَكَ ضَآلاًّ فَهَدَىٰ ﴾
Wawajadaka dhallan fahada (Surat Adh Dhuha 93:7)
Tafsir: Na jee hakukona wewe kua umepotea akakuongoza?
Ambapo hii ni aya ambayo imetumia neno Dhallan ambalo lina maana kadhaa pia
ikiwemo Kua katika Giza, Kupotea, Kutoweka, Kusahau, Kupotoka, Kuchukuliwa akili
kutokana na mawazo ya kitu fulani, Kupenda kitu na kukifikiria sana.
Na hii ni hali ambayo ilikua kama vile ambavyo alivyokua Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kabla ya kupewa Utume na Mola wake kama inavyoeleza aya ifuatayo:
﴿وَكَذٰ لِكَ أَوْحَيْنَآ إِلَيْكَ رُوحاً مِّنْ أَمْرَِ مَا كُنتَ تَدْرِى مَا ٱلْكِتَابُ وَلاَ ٱلإِيمَانُ
وَلَٰكِن جَعَلْنَاهُ نُوراً ن َّهْدِى بِهِ مَن ن َّشَآءُ مِنْ عِبَادَِ وَإِن َّكَ لَتَهْدِ ۤ ي إِلىَٰ صِرَا ٍط
م ُّسْتَقِيمٍ۞صِرَاطِ ٱهلل َِّ ٱل َّذِى لَهُ مَا فىِ ٱلس َّمَاوَاتِ وَمَا فىِ ٱلأَرْضِ أَلاَ إِلىَ ٱهلل َِّ تَ صِيرُ
ٱلأُمُورُ ﴾
Wakadhalika awhayna ilayka roohan min amrina ma kunta tadree ma alkitabu
wala al-eemanu walakin jaAAalnahu nooran nahdee bihi man nashao min
AAibadina wa-innaka latahdee ila siratin mustaqeemin; Sirati Allahi alladhee lahu
220
ma fee alssamawati wama fee al-ardhi ala ila Allahi taseeru al-omooru (Surat Ash
Shura 42:52)
Tafsir: Na kadhalika tumekushushia wewe Ruhan (Wahy au Rehma) kutoka katika
Maamrisho yetu, wakati wewe ulikua hujui ni nini Kitabu wala Imani, lakini sisi
tukaijaalia hii (Qur’an kua) Nuru ambayo kutokana nayo tunamuongoza tumtakae
miongoni mwa waja wetu. Na kwa hakika wewe (Muhammad Salallahu Alayhi wa
Salam) unaongoza (Watu) katika njia iliyonyooka. Njia ya Allah ambae kwake yeye
kuna umiliki wa kila kilichomo Mbinguni na Ardhini. Na kwa hakika kila kitu mwisho
wake kinaenda kwa Allah.
Neno Dhallan kwa upande mwengine hua pia linamaanisha Mti ambao uliokua uko peke
yake Jangwani. Kwani anasema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi kua: ‘Waarabu walikua wakikuta Mti uko peke yake
katika sehemu ya ardhi basi walikua wakiuita Dhallan na alikua wakiutumia kua
kama ni alama katika njia za safari zao.’
Hivyo kutokana na maana hii basi Allah Subhanah wa Ta’ala alimuita Rasul Allah
Salallahi Alayhi wa Salam Dhallan kwa sababu Rasul Allah Salallahi Alayhi wa Salam
alikua ni mtu ambae katika jamii yake alikua yuko peke yake kivyake vyake katika
kuutafuta ukweli kuhusiana na Mola wake, na alimchagua kua Kiongozi wa Watu na
hivyo yeye kua ni Alama inayoongoza watu njia sahih.
Ambapo tunapolitumia neno Dhallan kwa kumaanisha Kupenda kitu na kukifikiria sana
basi tunaona kua aya inamanisha kua: ‘Jee hatukukuona sisi kua unapenda sana
Uongofu nasi tukakuongoza?’
Ambapo kwa upande wa Shayh ul Islami Imam Muhammad Tahir Ibn Ashur basi yeye
anasema kua: ‘Dhallan hua ni hali ambayo Mtu hua anajihisi kua amepotea na
amechanganyikiwa kiasi ya kua hajui afuate njia gani’
Na kwa upande wa Jarrah Allah Sultan Al Balagha Imam Abu Qasim Al Zamakhshari
kua: ‘Inasemekana kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua pamoja na
watu wake kwa mda wa miaka 40, hivyo kama ikiwa hii inamaanisha kua yeye
hakua ni mwenye kujua kuhusiana na Ilm iliyoshushwa hapo awali katika vitabu
vilivyotangulia basi itakua ni sahih.
Lakini kama itakua inamaanisha kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua
amepotoka na anafuata njia za wazee wake, basi maana hii itakua sio sahih. Na hii
ni kwa sababu Allah Subhanah wa Ta’ala kua ni mwenye kuwaongoza Mitume wake
wote na kuwalinda kutokana na kuabudu Masanam kabla ya hata kuwapa Utume’
221
Na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anaendelea kwa kumhoji tena Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwa njia ya kumthibitishia:
﴿وَوَجَدَكَ عَآئِلاً فَأَغْنىَٰ ﴾
Wawajadaka AAa-ilan faaghna (Surat Ad Dhuha 93:8)
Tafsir: Na Jee hakukuona wewe huna kitu akakutajirisha?
Ambapo neno Ailan ni lenye kutokana na neno Ala ambalo hua linamaanisha Kuyumba,
Kugeuka, Kudharau, Kufanya Dhulma, Kufanya Kosa, Kumpa Mtu wakati Mgumu, Kua
na Shida, Kua na Familia kubwa, Kuihudumia Familia, Kumlisha Mtu Masikini.
Ambapo neno Aailan limetumika tena katika ile aya maarufu sana ya Surat An Nisaa
ambayo ni yenye kukataza kua na zaidi ya wake wanne, tunaona kua iliposhuka kukataza
Waislam kua na zaidi ya wake wanne haikukataza kua na Suria bali ilikua ikikhiyarisha
kwa wale watakaokosa kua na uadilifu basi waoe mke mmoja au wabakie na ‘Milk al
Yamin’ (Kilichomo ndani ya umiliki wa kisharia wa mkono wa kulia) yaani wale
wanaomilikiwa baada ya kutekwa vitani au baada ya kua ni miongoni mwa
wanaomilikiwa katika hali ya Utumwa katika wakati huo, hivyo aya hii imesema kua:
ٰ ٱلْيَتَامَى فَٱنكِحُواْ مَا طَابَ لَكُمْ مِّنَ ٱلنِّسَآءِ مَثْنىَٰ
﴿وَإِنْ خِ فْتُمْ أَلا َّ تُقْسِ طُواْ فىِ
ٰذلِكَ أَدْ نىَٰ
وَثُلاَثَ وَرُابَعَ فَإِنْ خِ فْتُمْ أَلا َّ تَعْدِلُواْ فَوَاحِ دَةً أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيمَْانُكُمْ
﴾ أَلا َّ تَعُولُواْ
Wa-in khiftum alla tuqsitoo fee alyatama fainkihoo ma taba lakum mina alnnisa-i
mathna wathulatha warubaAAa fa-in khiftum alla taAAdiloo fawahidatan aw ma
malakat aymanukum dhalika adna alla taAAooloo. (Surat An-Nisaa’ 4:3).
Tafsir: Na ikiwa mnakhofu kua hamtoweza kuwafanyia haki mayatima, basi oeni
Wanawake wengine mnaowataka, wawili, au watatu, au wanne; lakini ikiwa
mnakhofu kua hamtoweza kuwafanyia uadilifu basi oeni mmoja tu, au wale
mnaowamiliki mikononi mwenu (Mliowateka vitani na Watumwa). Kufanya hivyo hua
ni kukaribia kujilinda kutokana na kutokua waadilifu.
222
Na hivyo basi kwa upande mwengine maneno dhalika adna alla taAAooloo mbali ya
kua hua yanatafsirika Kufanya hivyo hua ni kukaribia kujilinda kutokana na kutokua
waadilifu. Lakini pia hua yanatafsirika kua: Kufanya hivyo hua ni njia bora ya
kujilinda kutokana na kufanya Dhulma. Na vile vile hua pia yanatafsirika kua:
Kufanya hivyo hua ni njia bora ya kujilinda kutokana na kua na familia kubwa.
Na ndio maana ikawa kuna baadhi ya Wanazuoni wakawa wameitafisiri aya hii isemayo:
﴿وَوَجَدَكَ عَآئِلاً فَأَغْنىَٰ ﴾
Wawajadaka AAa-ilan faaghna (Surat Ad Dhuha 93:8)
Tafsir: Na Jee hakukuona wewe huna kitu akakutajirisha?
Ambapo hali inayozungumziwa hapa ni hali ya Umasikini aliyokua nayo kabla ya
kuingizwa Bi Khadija Bint Khuwaylid Radhi Allahu Anha ndani ya maisha yake na Allah
Subhanah wa Ta’ala na hivyo kumtajirisha Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam, kua
maneno haya pia yanamaanisha pia kua: ‘Jee Hatukukuona wewe ukiwa na familia
kubwa kuihudumia hivyo tukakusaidia kukuongezea baraka?’ na pia: ‘Jee
hatukukuona wewe kua unashida ya Kiroho, Kinafsi kutokana na kutojua ufanye nini
kuhusiana na wayafanyayo watu wako kwa ujahili wao nasi tukakusaidia
kukuongezea Ilm?’
Neno Aailan limetumika tena katika aya ifuatayo pale iliposema:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُو ۤ اْ إِنم ََّا ٱلْمُشْرِكُونَ نجََسٌ فَلاَ يَقْرَبُواْ ٱلْمَسْجِ دَ ٱلحَْرَامَ بَ عْدَ عَامِهِمْ
هَٰذَا وَإِنْ خِ فْتُمْ عَيْلَةً فَسَوْفَ يُغْنِيكُمُ ٱهلل َُّ مِن فَضْلِهِ إِن شَآءَ إِن َّ ٱهلل ََّ عَلِيمٌ حَ كِيمٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo innama almushrikoona najasun fala yaqraboo
almasjida alharama baAAda AAamihim hadha wa-in khiftum AAaylatan fasawfa
yughneekumu Allahu min fadhlihi in shaa inna Allaha AAaleemun hakeemun(Surat
At Tawba 9:28)
Tafsir: Enyi Mlioamini, hakika ya Washirikina ni Najisi hivyo msiwaruhusu
kuukaribia Masjid Al Haram baada ya mwaka huu na kama mtakua mnaukhofia
223
Umasikini, basi Allah atakutajirisheni kutokana na fadhila zake akitaka, Hakika Allah
ni mwenye kujua kila kitu na ni mwenye Hikma nyingi sana.
Hivyo maneno wa-in khiftum AAaylatan yanamaanisha Na kama mtakua mnaukhofia
Umasikini. Ambapo amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hakika ya
Utajiri hua ni Utajiri wa Moyo, Na Umasikini hua ni Umasikini wa Moyo.’ Na akasema
tena: ‘Mtu Tajiri hua si yule ambae mwenye Mali nyingi bali ni yule mwenye Moyo
ulioridhika’
Kisha baada ya Allah Subhanah wa Ta’ala kutoa hoja na vithibitisho vyote hivyo vya
yale matukio muhimu sana na mabadiliko yaliyotokea hapo kabla ndani baina ya wakati
wa uhai wake Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam na yatakayotokea baadae kama
alivyoanza mwenyewe Allah Subhanah wa Ta’ala na Waaldhdudha; Waallayli idha
saja yaani Naapa kwa wakati wa Dhuha (baina ya Asubuhi na kabla ya Adhuhuri) Na
Kwa Usiku unapoingia na kutulia.
Na hivyo kutubainishia umuhimu wa wakati kulingana na hali ya matukio na hali ya
mabadiliko ya kitu basi Allah Subhanah wa Ta’ala anamuusia Mtume wake Salallahu
Alayhi wa Salam kuhusiana na Mayatima kama vile ambavyo alivyokua Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam chini ya usimamizi wa Allah Subhanah wa Ta’ala kwa
kusema kua:
﴿فَأَم َّا ٱلْيَتِيمَ فَلاَ تَقْهَرْ ﴾
Faamma alyateema fala taqhar .(Surat Adh Dhuha 93:8)
Tafsir: Hivyo na Yatima usimdidimize
Ambapo neno Taqhar linatokana na neno Qahara lenye kumaanisha Kukandamiza,
Kuvunjia Haki, Kudidimiza, Kufanyia au Kuenda kinyume na matakwa, Kudhibiti,
Kuzidi kinguvu, Kua Juu Ya kitu, Kua Katili , Kua mshindi dhidi ya mwengine.
Na hivyo aya kua ni yenye kutuwekea wazi kutowanyanyasa Mayatima, na kutuamrisha
kuwafanyia wema na kua wakarimu nao, ambapo anasema Abu Ummamah Radhi Allahu
Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Yoyote yule atakae
mpapasa kichwa Yatima kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala basi atapata
thawabu kwa kila Nywele utakaokua chini ya Mkono wake, na mimi na mtu huyo
atakaemhurumia Yatima basi tutakua kama hivi (kisha Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akabana kidole chake cha kati na cha shahada na kuwaonesha
Masahaba zake) Peponi’’
224
Na kutokana na Hadith hii basi Abd Alla Ibn Umar Radhi Allahu Anhu akawa kila siku
akikutana na Yatima basi humpapasa kichwa chake na kumpa kitu chochote kizuri
alichokua nacho.
Na pia anasema Al Hasan kua: ‘Kila wakati ilipokua Abd Allah Ibn Umar Radhi
Allahu Anhu anakula basi alikua anawaita Mayatima wote wa Mtaa wake, kiasi ya
kua siku moja wakati anajitayarisha kula basi akamwambia Mtumwa wake kua
amuitie Mayatima wote wa mtaani, ambapo Yatima mmoja akakosekana kwani
alikua hayupo. Hivyo Mayatima waliokuwepo wakakaa na Abd Allah Ibn Umar
Radhi Allahu Anhu na wakaanza kula’
‘Na kila siku baada ya kula basi Abd Allah Ubn Umar Radhi Allahu Anhu alikua
akipewa Sharbati tamu sana aliyokua akiipenda. Hivyo katika siku hio Abd Allah
Ibn Umar Radhi Allahu Anhu akala na Mayatima wake chakula chote hadi
wakamaliza. Kisha baada ya kumaliza Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu Anhu
akachukua Bilauri akawa anataka kunywa Sharbati yake na mara akatokea yule
Yatima ambae alikua akitafutwa na akawa haonekani Hivyo Abd Allah Ibn Umar
Radhi Allahu Anhu alipomuona Yatima huyo basi akarudisha chini bilauri hio ya
Sharbati na kisha Akampa Yatima huyo huku akimwambia: ‘Kunywa hii kisha
mimi ndio nitajua kua sikukufanyia Taqhar.’
Na Allah Subhanah wa Ta'ala ameusia kuhusiana na Mayatima na Kutonyanyaswa kwa
sababu si tu kuwanyanyasa na kuwakandamiza hua ni sawa kukadhibisha Dini kama
tulivyoona kwenye Surat Al MaAu'n.
Lakini Kutowanyanyasa Mayatima hua ni sawa na kua na Taqwa na Kumpenda Allah
Subhanah wa Ta'ala na Mtume wake Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo hua ni sifa ya
Watu wa Peponi, Kwani mongoni mwa Watu wa Peponi ni wale watu ambao Allah
Subhanah wa Ta'ala amewataja kwenye Qur'an kwa kusema:
﴿إِن َّ ٱلأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُوراً۞عَيْناً يَشْرَبُ هبَِ ا عِبَادُ ٱهلل َِّ
يُفَجِّ رُونَهَا تَفْجِ يراً۞يُوفُونَ بِٱلن َّذْرِ وَيخََافُونَ يَوْماً كَانَ شَر ُّهُ مُسْتَطِير اً ﴾
Inna al-abrara yashraboona min ka/sin kana mizajuha kafooran; AAaynan
yashrabu biha AAibadu Allahi yufajjiroonaha tafjeeran; Yoofoona bialnnadhri
wayakhafoona yawman kana sharruhu mustateeran; (Surat Al Insan 76:5-7)
225
Tafsir: Hakika ya Waja Wema Watakunywa Kutoka kwenye Gilasizenye Maji kutoka
Katika Mto wa Peponi wa Kafuran. (Kafura ni) Chemchem Watakazokunywa
Kutokana nazo Waja wa Allah na Kuyasababishia Maji hayo Matamu Kutoka kwa
Kufoka kwa wingi bila ya kua na upungufu wala mwisho wake. Hao ndio Wale Ambao
waliotekeleza Nadhiri na Ahadi zao Na wakawa na Khofu na Siku Ambayo Itakua
Shari yake ni Iliyoenea na Kutapakaa.
Ambapo aya zinatubainishia kua Miongoni mwa watu wenye Sifa za kua ni Waja Wema,
basi ni wale wenye Sifa za kua ni wenye kutekeleza Nadhiri na Ahadi zao, kutokana na
kumuogopa Allah Subhanah wa Ta'ala na kuiogopa Siku ya Malipo siku ambayo Ubaya
au Shari yake itakua ni Kubwa na nzito kuliko Kheri yake
Kwani hii ni siku ya Malipo ambayo Watu watakimbiana Baba atamkimbia Mama na
Watoto wake, Mama atawakimbia Watoto wake, Ndugu atawakimbia Ndugu zake na kila
anaekimbia wenzake basi na yeye hua anatafutwa na kufukuziwa na hao anaowakimbia,
kwani kila mtu anataka kuiokoa Nafsi yake, kutokana na kujua kua yule anaemkimbia
ndie aliekua na jukumu la kumsimamia lakini hakumsimamia kwa hivyo atamkimbilia ili
amlaumu na kumdai kua ampunguzie Uzito wa Madhambi yake kwa kutotekeleza
majukumu yake Juu yake katika kumsimamia kwake.
Hivyo bila ya shaka siku hio, shari yake itakua ni Mustatiiran yaani itaenea kila shemu
na kwa kila mtu kama nuksi au laana fulani na hivyo kila mmoja atakua anaona tafrani
kutokana na uzito wa Mashakil yake..Ya Allah tustiri na Mitihani ya Siku hio ambayo
Sharruhu Mustatiiran..Amiin
Kwani ingawa hali itakua hivyo kwa wengi lakini kwa wachache haitokua hivyo na
wachache hao ni wale ambao Waja wema wenye sifa ya kua ni Abrar, wenye sifa ya kua
ni wenye Kutimiza Ahadi zao, Nadhiri zao, wenye sifa ya kutumia kwa kutoa Neema
walizoneemeshwa na Mola wao, mbali ya kua wanazipenda Neema hizo, lakini
wakadhihirisha Mapenzi yao kwa Mola wao kwa kuzitoa Neema hizo kwa ajili ya Mola
wao kwa kuwasaidia Masikini, Mayatima na Asir yaani Wasiokua huru.
﴿وَيُطْعِمُونَ ٱلط َّعَامَ عَلَى ٰ حُبِّهِ مِسْكِيناً وَيَتِيماً وَأَسِ يراً ﴾
WayutAAimona alttaAAama AAala hubbihi miskeenan wayateeman waaseeran
(Surat Al Insan 76:8)
Tafsir: Na Wakawa ni Wenye Kuwalisha Chakula kwa kutokana na mapenzi ya
Kumpenda kwao Allah Subhanah wa Ta’ala, kwa kuwasaidia Masikini Mayatima na
Mateka.
226
Kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Sadaqa Bora hua ni ile
ambayo unayoitumia wakati ukiwa na Afya Njema, Wakati ukiwa unaipenda Mali
Yako na Huku Ukiwa Unakhofia Umasikini’
Ambapo Jarah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari anasema kua: ‘Ndani ya maana
ya neno Asir yaani Wafungwa, Mateka au wasiokua huru basi wanaingia pia wale
ambao wamefungika kwa Matatizo ikiwemo wenye Madeni.’
Kwani Allah Subhanah wa Ta'ala anaendelea kutueleza kuhusiana na hao wanaosaidia
Masikini, Mayatima na Wenye Matatizo ya kutokua huru kwa kuwapa msaada kwa
Ikhlasi kua hua ni sawa na wenye kusema:
﴿إِنم ََّا نُطْعِمُكُمْ لِوَجْهِ ٱهلل َِّ لاَ نُرِيدُ مِنكُمْ جَزَآءً وَلاَ شُكُوراً۞فَوَقَ اهُمُ ٱهلل َُّ شَر َّ ذٰلِكَ
ٱلْيَومِ وَلَق َّاهُمْ نَضْرَةً وَسُرُوراً۞وَجَزَاهُمْ بمَِا صَبَرُواْ جَن َّةً وَحَرِيراً ﴾
Innama nutAAimukum liwajhi Allahi la nureedu minkum jazaan wala shukooran;
Inna nakhafu min rabbina yawman AAaboosan qamtareeran; Fawaqahumu
Allahu sharra dhalika alyawmi walaqqahum nadhratan wasurooran(Surat Al Insan
76:9-11)
Tafsir: (Wanasema) ‘Hakika ya kukusaidieni kwetu ni kutokana na kutaka hesabu
kwa Allah, kwani sisi hatutaki Kutoka kwenu Malipo wala Shukurani; Kwani kwa
hakika sisi tunakhofia kutoka kwa Mola wetu siku ambayo ni nzito itakayozifanya
Nyuso kua na muonekano mbaya kabisa’; Hivyo Allah atawaokoa Watu hao na shari
ya Siku hio na kuwapa Muonekano wenye Nuru na furaha( katika siku hio)
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anamuusia tena Mtume wake Salallahu Alayhi wa
Salam kuhusiana na kuwajali Masikini wasiokua na kitu, kama vile ambavyo alivyokua
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kabla ya kumuoa bi Khadija Radhi Allahu Anha
kwa kusema kua:
﴿وَأَم َّا ٱلس َّآئِلَ فَلاَ تَنْهَرْ ﴾
Waamma alssa-ila fala tanhar; (Surat Adh Dhuha 93:10)
Tafsir: Na mwenye kuomba usimfukuze.
227
Ambapo neno Tanhar limetokana na neno Nahara ambalo hua linamaanisha
Kusababisha Mchirizi, au Njia ya Maji au Mkondo wa Maji kupita katika nja yake.
Kutiririka bila matatizo, Kukukemea, Kufukuza, Kukasirikia na pia humaanisha Kufanya
kitu katika wakati wa Mchana.
Na mbali ya kua wengi wanaitumia aya hii kwa ajili ya watu wanaoomba kuhusiana na
rizki zao, lakini aya pia aya hii inawazungumzia wale ambao ni wenye kuomba kuhusiana
na yale wasiyoyajua kuhusiana na Ilm ya Dini yao, kwani amesema Allah Subhanah wa
Ta’ala kua:
﴿إِن َّ ٱل َّذِينَ يَكْتُمُونَ مَآ أَنزَلْنَا مِنَ ٱلْبَيِّنَاتِ وَٱلهُْدَىٰ مِن بَعْدِ مَا بَي َّن َّاهُ لِلن َّاسِ فىِ
ٱلْكِتَابِ أُولَٰئِكَ يَلعَنُهُمُ ٱهلل َُّ وَيَلْعَنُهُمُ ٱللا َّعِنُونَ۞إِلا َّ ٱل َّذِينَ َاتبُواْ وَأَصْ لَحُواْ وَبَي َّنُواْ
فَأُوْلَ ئِ كَأَتُوبُ عَلَيْهِمْ وَأََ الت َّو َّابُ الر َّحِ يمُ ﴾
Inna alladheena yaktumoona ma anzalna mina albayyinati waalhuda min baAAdi
ma bayyannahu lilnnasi fee alkitabi ola-ika yalAAanuhumu Allahu
wayalAAanuhumu allaAAinoona; Illa alladheena taboo waaslahoo wabayyanoo
faola-ika atoobu AAalayhim waana alttawwabu alrraheemu (Surat Al Baqara 2:159-
160)
Tafsir: Hakika ya wale ambao wamekaa kimya kuhusiana na walichoshushiwa
kutokana na ubainisho na uongofu baada ya kua tumewawekea wazi ndani ya kitabu
basi hao wamelaaniwa na Allah na wamelaaniwa na wenye kulaani. Isipokua wale
ambao watatubu na wakafanya mema na wakabainisha (kile walichokificha), hivyo
hawa ndio nitakaowakubalia toba zao na kwa hakika mimi ni mwingi wa kusamehe
na ni mwingi wa huruma.
Na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Yeyote yule atakaeulizwa kuhusiana
na Mada na llm na yeye akawa anajua kuhusiana nayo kisha akaificha basi katika
Siku ya Malipo atafungwa hatamu ya Moto mdomoni mwake.
Na ndio maana Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu akasema kua: ‘Kama hii ingekua sio
aya ya Qur’an basi nisingenukuu hadithi yeyote’
Na akasema Imam Abu Hanifa kua: ‘Anapokujia Mtu mwenye kuomba kutaka kujua
kuhusiana na Ilm ya Dini yake basi Mtu huyu unatakiwa umpokee kwa
kumtandikia Zulia la Dhahabu chini ya miguu yake.’
228
Ambapo hata hivyo basi sio kila aina ya Ilm unakua ni mwenye kuitoa kwa sababu ya
kua unayo, kwani baadhi ya wakati unaweza ukasababisha madhara kwa wasiofaham na
kwa baadhi wanaweza wakawa hawakuamini, kama alivyosema Abd Allah Ibn Masud
Radhi Allahu Anhu kua: ‘Haiwezekani kua usitoe Ilm kwa wale wasiopea kilm na
kiufaham miongoni mwao isipokua watakua na shaka juu yake’
Na akasema Ali Ibn Abi Talib Radhi Allah Anhu kua: ‘Zungumza Na watu kulingana
na Uwezo wa Ufaham wao, au unataka Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume wake
Salallahu Alayhi wa Salam wakanushwe?’
Ambapo tunapozungumzia kuhusiana na upande wa wanaoomba Riziki basi Imam
Ibrahim An Nakhai amesema kua: ‘Waombaji ni wafanyakazi wa Posta wa Akhera,
ambao hua wanakuja kwenye Mlango wako na kusema: ‘Hivi Jee kuna kitu
chochote kile ambacho unataka kukituma Akhera?’’
Ambapo kwa upande mwengine basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua
akiwapa vitu watu wanaoomba kwa ustaarabu na pia alikua akiwapa wale wanaoomba
kwa kukirihisha, kwani alikua akisema kua: ‘Wamenifanya mimi nichague baina ya
kutoa vitu vizuri na baina ya kua bakhili kwa kutumia maneno yanayokirihisha,
wakati mimi si bakhili.’
Na Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al
Qurtubi amesema kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua:
Wapeni Msikini japo kidogo pale wanapoomba, au waondoeni kwa maneno mazuri,
kwa sababu inawezekana Masikini huyo akawa ni Malaika wa Allah Subhanah wa
Ta’ala amekuja kukujaribuni namna mnavyotumia neema mlizoneemeshwa na
Allah Subhanah wa Ta’ala’
Na akasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Yeyote yule atakeotoa kwa
ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala kitu atakachoombwa basi Allah Subhanah wa
Ta’ala atamuandikia Thawabu 70 kwa alichotoa’ na pia akasema kua ‘Mtu
atakaeomba kwa kusema kua anaomba kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala basi
hua amelaaniwa. Na mtu atakaemkatalia mtu anaeomba kwa kusema kua anaomba
kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala basi hua amelaaniwa pia, kwani mtu huyo
atakua amefanya Uovu’ kwani: ‘Ni Pepo tu pekee ndio inayoombwa kwa ajili ya
Allah Subhanah Wa Ta’ala’(Fatawa Al Hindi)
Ambapo maneno haya ya Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam yanamaanisha
kua: Haitakiwi kua Mtu aombe kitu kwa kuapa kwanza kwa jina la Allah Subhanah
wa Ta’ala au kwa kutumia kisingizio cha jina la Allah Subhana wa Ta’ala kua
anaomba kitu Fulani kutokana na shida aliyokua nayo, na mtu atakaemkatalia mtu
huyo mwenye kuomba kwa anjia hio hua amelaaniwa kwa sababu hua ni mwenye
229
kukataa kufanya jambo la kutoa msaada kwa ajili ya Allah Subhana wa Ta’ala
wakati anao uwezo wa kusaidia.
Kwani amesema Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hakika Malaika Jibril amenishushia mimi kwenye
Moyo wangu kua, hakuna Nafsi itakayokufa hadi pale itakapokua Nafsi hio
imemaliza Riziki yake iliyopangiwa, hivyo muogopeni Allah na tafuteni Riziki zenu
kwa njia njema, kama ikiwa Riziki imekawia basi basi msiitafute kwa kutumia njia
zitakazopelekea kumuasi Allah, kwa sababu Riziki kutoka kwa Allah hua kamwe
haiwezekani kupatikana kwa njia yeyote ya kumuasi kwake.’’(Al Targhib wa Al
Tarhib)
Na ingawa kuna vithibitisho hivyo lakini hata hivyo inabidi tujue kua Waombaji hawa
waliokusudiwa hapa sio wale ambao wanapita katika Maduka kila Ijumaa kwa ajili ya
kuomba, au wanapita katika kila mlango kwa ajili ya kuomba, au wanaosimama
mabarabarani kwa ajili ya kuomba, kwani hawa sio waliokusudiwa hapa kwa sababu ni
masikini kwa sababu unakuta mtu kijana na nguvu zake anapita akiomba, na kuna
wengine wanawake wari hawana kazi yeyote isipokua kuomba yaani imekua ndio ajira
yao ya kujitafutia maisha.
Ambapo amesema Abu Dardaa Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alyhi wa Salam kua: ‘Bila ya Shaka Riziki ya Mtu hua ni yenye kumfuata
Mtu kama vile ambavyo Kifo kinavyomfuata Mtu husika’’ (Al Targhib wa Al Tarhib)
Na akasema Abu Said Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallah Alyhi
wa Salam kua: ‘Hata kama mtu atakua ni mwenye kuikimbia Riziki yake basi Riziki
yake hio itamkuta tu kama vile kitakavyomkuta Kifo chake’’(Al Targhib wa Al
Tarhib)
Na akasema Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alipata Tende, ambapo akatokea Masikini akamuomba na akampa Tende
hio huku akisema kwa kumwambia: ‘Angalia kwani kama hii hukuifuata basi
ingekufuata wewe’’
Hivyo tunapozungumzia kuhusiana na Waombaji yaani wenye shida kutokana na
kutokua na uwezo, basi Qur’an imewalezea kwa kutumia maneno mawili ambayo ni
Fuqara na Masaakin ambayo ingawa ni tofauti lakini hata hivyo hua yanaingiliana
kimaana.
Kwani neno Fuqara hua ni lenye kutokana na neno Faqura ambalo hua linaaamansha
Mtu Aliekua Maskini, Mtu Mwenye Shida Kubwa na Nyingi sana. Hivyo neno Fuqara
hua linatumika kumaanisha Mtu ambae anawategemea watu wengine kwa ajili ya
230
mahitajio yake ya kimaisha kutokana na sababu mbali mbali za kimaumbile ikiwemo
Uzee, Ulemavu au kutokana na mitihani mbali mbali ya kimaisha, na ndio maana neno
Faqira hua pia linamaanisha Kuzidiwa na Mithani ambayo huweza kumpelekea Mtu
kuhisi uzito wa maumivu ya Mtihani huo ndani ya Uti wa Mgongo, na neno Faqiratun
hua linamaanisha Mtihani wa Kuvunjika Mgongo.
Ambapo kwa upande wa neno Masakin hua linatokana na neno Sakana ambalo hua
linamaanisha Kutulia, Kukaa Kimya, Kusimama tulii. Hivyo neno Masakin hua
linamaanisha Mnyenyekevu, Mtulivu, Masikini, Mtu anaestahiki kusaidiwa kutokana na
Udhaifu au Unyenyekevu wake.
Neno Sakana ndio pia lililotoa neno Sikin yaani Kisu ambacho Kimeitwa hivyo kwa
sababu Kisu ndio chanzo cha Kukifanya Kiumbe Kitulie baada ya Kuchinjwa kwake.
Ambapo kwa upande wa Imam Muhyi Ad Din Imam Abu Zakarriyah Yahyah Sharaf An
Nawawi basi yeye anasema kua: ‘Maneno haya mawili Fukara na Masakin hua yana
maana moja yanapokua yametumika katika sehemu tofauti, lakini yanapotumika
katika sehemu moja hua yana maana tofauti.’
Na Wanazuoni wametofautiana katika maana ya maneno haya mawili kutokana na
yalivyotumika hapa kwani kwa upande wa Wanazuoni wa Madhhab ya Imam
Muhammad Idris Al Shafii na wafuasi wa Madhhab ya Imam Ahmad Ibn Hanbal basi
wao wanasema kua: ‘Fukara hua ni tu mwenye shida zaidi kuliko Masikini na hii ni
kutokana na mpangilio wa maneno haya yaliyotajwa kwenye aya hii, kwani
mwanzo ametajwa Fukara na kisha baadae ndio akatajwa Masikini.’
Na kwa upande wa Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Abu Hanifa na Madhhab ya Imam
Malik Ibn Anas basi wao wanasema kua: ‘Maskini ndie mwenye shida zaidi kuliko
Fukara.’
Kwa kumalizia kuhusiana na Fukara na Masikini basi tunaona kua:
Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Abu Hanifa basi wao wanafafanua maana mbili hizi
kwa kusema: ‘Masikini hua ni mtu ambae hana kitu kabisa. Fukara hua ni mtu
ambae anacho kitu kidogo ambacho hata hivyo hakimtoshi kwa mahitaji yake ya
kila siku.’
Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Malik Ibn Anas basi wao wanafafanua maana mbili
hizi kwa kusema: ‘Masikini hua ni mtu ambae hana kitu kabisa na hivyo hua
anaomba watu msaada. Fukara hua hana kitu hata kidogo lakini hata hivyo haombi
kwa watu.’
231
Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Muhammad Idris Al Shafii basi wao wanafafanua
maana mbili hizi kwa kusema: ‘Fukara hua ni mtu ambae hana kitu kabisa. Maskini
hua ni mtu ambae anacho kitu kidogo ambacho hata hivyo hakimtoshi kwa mahitaji
yake ya kila siku.’
Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Ahmad Ibn Hanbal basi wao wanafafanua maana mbili
hizi kwa kusema: ‘Fukara hua ni mtu ambae hana hata kitu kitachomtosheleza hata
nusu ya mahitaji yake. Maskini hua ni mtu ambae anacho kitu kidogo ambacho ni
zaidi ya nusu ya mahitaji yake na hivyo hua hakimtoshi kwa mahitaji yake ya kila
siku.’
Naam, tunarudi kwenye aya yetu ya mwisho ya Surat Adh Dhuha ambapo tunaona kua
Allah Subhanah wa Taa’ala baada ya kumtolea hoja na vithibitisho Mtume wake
Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam na kumuuisia basi anamwambia
﴿وَأَم َّا بِنِعْمَ ةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ ﴾
Waamma biniAAmati rabbika fahaddith .(Surat Adh Dhuha 93:11)
Tafsir: Na kuhusiana na Neema za Mola wako zihadithie.
Anasema Abu Al Ahwas kua amesema Baba yake kua: ‘Mimi nilikua nimekaa na Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam na akaniona kua nimevaa nguo chakavu, hivyo
akaaniuliza: ‘Hivi Jee wewe huna pesa?’ nami nikasema: ‘Nnazo nyingi tu’ Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaniambia : ‘Wakati Allah Subhanah wa Ta’ala
anapokujaalia kitu basi wacha athari yake ionekane juu yako.’’(Imam Abu Abd Allah
Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi)
Na amesema Imam Muhammad Ibn Jarir At Tabari kua: ‘Tangu enzi za zamani sisi
tumesikia kutoka kwa Waislam kua moja kati ya njia ya Kumshukuru Allah
Subhanah wa Ta’ala ni kutangazia Neema hizo.’
Ambapo siku moja Imam Abu Firas Abd Allah Ibn Ghalib Al Huddani Al Basri alisema
kumwambia rafiki yake: ‘Alhamd lillah Hakika mimi nimesali sana na nimesoma
sana Qur’an pia’ hivyo Rafiki yake huyo akasema: ‘Hivi inakuaje mpaka mtu kama
wewe anakua anasema kama hivyo?’ hivyo Abu Firas Abd Allah Ibn Ghalib Al
Huddani Al Basri akasema: ‘Bila ya Shaka kwani Allah Subhanah wa Ta’ala
amesema:’ Waamma biniAAmati rabbika fahaddith’
232
Ambapo anasema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al
Ansari Al Qurtubi kua: ‘Kusema Allahu Akbar baada ya kusoma Surat Adh Dhuha ni
Sunnah na hii ni kwa sababu amesema Imam Muhammad Idris Al Shafii kua:
‘Inapendekezwa baada ya kusoma Sura hii basi Mtu na aseme Allahu Akbar!’na
kuna wasemao kua inapendekezwa kusema: ‘Allahu Akbar, La ilaha illa Allahu, Allahu
Akbar.’
Na amesema Imam Ibn Muflih Al Hanbali kua: ‘Imam Ahmad anachukulia kua ni
jambo lenye kupendekezwa kusema Takbir kuanzia baada ya mwisho wa Surat Adh
Dhuha mpaka mwishoni mwa kila Sura za mwishoni wa Qur’an. Na hii imetajwa
na Ibn Tamim na wengineo, na hii ni namna walivyokua wakisoma watu wa
Makkah ambapo Imam Ul Qiraah Abu Hasan Muhammad Ibn Ahmad Al Bazzi
amenukuku kutoka kwa Ibn Kathir ambae nae amenukuu kutoka kwa Mujahid
ambae nae amenukuu kutoka kwa Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu ambae
nae amenukuu kutoka kwa Ubbay Ibn Qaab Radhi Allahu Anhu ambae nae
amenukuu kutoka kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ’ na pia kuhusiana na
jambo hili basi amesema Imam Abu Abdullâh Muḥammad Ibn Abdullah Al Hakim
katika Mustadrak Al Hakim na Imam Abū Muḥammad Al Ḥusayn Ibn Masʻūd Ibn
Muḥammad Al Farrā' Al Baghawi pia.
Ambapo kwa upande mwengine tunapoiangalia Qur’an basi tunaona kua inaelezea visa
vya Mitume ambao waliokua pia na sifa ya Laqit. Ambapo neno Laqit linatokana na neno
Laqatta ambalo hua linamaanisha Kitu Kilichookotwa, Kitu kilichokusanywa baada ya
kuanguka, Kitu kilichochukuliwa, Mabaki ya Punje za Nafaka na pia humaanisha Kitu
ambacho hakitakiwi na hivyo kimetupwa na mtu mmoja na kuokotwa na mwengine.
Na tunapochunguza hali ya Laqit ndani ya Qur’an basi hua tunaoneshwa mfano wa kisa
cha Nabii Yusuf na Nabi Musa ambapo kwa Nabii Yusuf alitupwa na kuigizwa Kisimani
kutokana na Wivu wa kina Al Asbati yaani Kaka zake Nabii Yusuf na kisha akaokotwa
na kutolewa Kisimani na hivyo tukio hili kua ni sehemu ya maandalizi ya kuja kubebea
jukumu lake alilotayarishiwa na Mola wake. Na kutupwa Nabii Musa ambae alitupwa
Mtoni na Mama yake kutokana na maamrisho ya Mola wake ili kumuokoa kutokana na
mitihini ya mazingira yake na pia kumuingiza katika njia ya kukulia katika mazingira
yatakayorahisisha jukumu lake atakalopewa na Mola wake pia, kama ilivyosema aya:
233
﴿إِذْ أَوْحَيْنَآ إِلىَٰ أُمِّكَ مَا يُوحَى ٰ ۞أَنِ ٱقْذِفِيهِ فىِ ٱلت َّابُوتِ فَٱقْذِفِيهِ فىِ ٱلْيَمِّ فَلْيُلْقِهِ
ٱلْيَم ُّ بِٱلس َّاحِ لِ َْخُذْهُ عَدُو ٌّ لىِّ وَعَدُو ٌّ ل َّهُ وَأَلْقَيْتُ عَلَيْكَ محََب َّةً مِّنىِّ وَلِ تُصْنَعَ عَلَىٰ
عَيْنيِ ۤ ﴾
Idh awhayna ila ommika ma yooha, Ani iqdhifeehi fee alttabooti faiqdhifeehi fee
alyammi falyulqihi alyammu bialssahili ya/khudhhu AAaduwwun lee
waAAaduwwun lahu waalqaytu AAalayka mahabbatan minnee walitusnaAAa
AAala AAaynee (Surat Al Ta-Ha 20:38-39)
Tafsir: Tulipomshushia Wahyi Mama yako juu yako juu ya tuliyomshushia,
tukamwambia Mtie ndani ya Tabut na kisha kitie ndani ya Mto, kisha Mto
utakichukua mpaka ukingoni, na atachukuliwa na adui yangu na adui yake. Na
nitakupamba kwa mapenzi kutoka kwangu, ili uwe ni mwenye kulelewa kutoka chini
ya uangalizi wangu.
Hii ni mifano ya hali ya Mitume walipokua Laqit walipokua wadogo ambapo
tunapozungumzia hali ya kua Laqit kwa Mtoto wa kawaida basi hua ni hali ambayo hatari
zaidi kuliko hali ya kua Yatima kwa sababu Yatima hua ni Mtoto ambae hana Baba lakini
anae Mama au ndugu na jamaa hivyo kama hakumtaka huyu basi atamtaka yule, wakati
hali ya Laqit hua ni hali ya Mtoto ambae hatakiwi kutokana na Mzee wake mtoto huyo
kua ni mwenye khofu ya umasikini kutokana na kutokua na kitu au kutokana na kuogopa
kutengwa kwa Uzinifu na hivyo humuacha na kumtupa mtoto katika sehemu bila ya
kumjali, na kutokana na hali kama hii basi Laqit anapokua Mchanga na kutupwa hua
hana Jina wala Nasaba tofauti na Yatima ambae hua na Nasaba.
Hivyo katika Surat Adh Dhuha basi Allah Subhanah wa Ta’ala anatufunza kwa
kutuonesha ndani yake Qur’an mifano hai ya kuwajali na kuwalea na kuwahudumia
Mayatima na Laqit kwa kutumia njia ya kufanya Kafala neno ambalo ni lenye maana
pana kama yalivyo maneno mengine Lugha ya Kiarabu na Allah Subhanah wa Ta’ala
amelitumia neno Kafala mara kadhaa ikiwemo pale aliposema:
﴿م َّن يَشْفَعْ شَفَاعَةً حَسَنَةً يَكُنْ ل َّهُ نَصِيبٌ مِّنْهَا وَمَن يَشْفَعْ شَفَاعَةً سَيِّئَةً يَ كُنْ
ّ ل شَ يْ ءٍ م ُّقِيتاً ﴾
ل َّهُ كِفْ لٌ م َّنْ هَ ا وَكَ انَ ٱهلل َُّ ٰ عَلَى كُ ِ
234
Man yashfaAA shafaAAatan hasanatan yakun lahu naseebun minha waman
yashfaAA shafaAAatan sayyi-atan yakun lahu kiflun minha wakana Allahu AAala
kulli shay-in muqeetan (Surat An Nisaa 4:85)
Tafsir: Na yeyote yule atakaeingilia jambo kwa nia nzuri basi atalipwa Malipo
yanayonasibiana kutokana nalo, na yeyote atakaieingila jambo kwa nia mbovu basi
(yakun lahu kiflun) atabeba jukumu litokanalo. Na Allah ni mwenye uwezo juu ya kila
kitu.
Na kisha akasema tena pale alipozungumzia kuhusiana na kesi aliyoletewa Nabii Daud
kua:
﴿إِن َّ هَذَآ أَخِ ى لَهُ تِسْعٌ وَتِسْعُونَ نَعْجَةً وَلىَِ نَعْجَةٌ وَاحِ دَةٌ فَقَالَ أَكْفِلْنِيهَا
وَعَز َّنىِ فىِ ٱلخِْطَابِ ﴾
Inna hadha akhee lahu tisAAun watisAAoona naAAjatan waliya naAAjatun
wahidatun faqala akfilneeha waAAazzanee fee alkhitabi (Surat Sad 38:23)
Tafsir: (Alipoambiwa Nabii Daud) Hakika huyu Kaka yangu ana Kondoo tisini na
tisa, wakati mimi ninae mmoja tu, na anasema: ‘Akfilniiha –Nipe nimlee, na amenizidi
kwa maneno’
Na pale alipoinasibisha Kafala na Rehma kwa kusema:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ ٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَآمِنُواْ بِرَسُولِهِ يُؤْتِكُمْ كِفْلَينِْ مِن ر َّحمَْتِهِ وَ يجَْعَل ل َّكُمْ
نُوراً تمَْشُونَ بِهِ وَيَغْفِرْ لَكُمْ وَٱهلل َُّ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo ittaqoo Allaha waaminoo birasoolihi yu/tikum
kiflayni min rahmatihi wayajAAal lakum nooran tamshoona bihi wayaghfir lakum
waAllahu ghafoorun raheemun (Surat Al Hadid 57:28)
Tafsir: Enyi Mlioamini (Nabii Musa na Nabii Isa) Muogopeni Allah na Muaminini
Mtume wake, nae atakupeni Kiflayni min Rahmatihi (Atakutunzeni Mara Mbili
kutokana na Rehma zake) na atakupeni Nuru ambayo mtatembelea (katika njia
iliyonyooka) na atakusameheni na Allah ni Mwingi wa Kusamehe na Mwingi wa
Rehma.
235
Ambapo amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kuna watu wa aina
tatu ambao ndio watakaopata Malipo mara mbili:
1-Yule Mtu ambae anamiliki Mtumwa, akamsomesha, akamfundisha tabia njema
na kisha akamuachia huru na kisha akamuoa basi atalipwa mara mbili.
2-Yule Muumini ambae alikua ni wa Ahl Al Kitab, na akawa ni Muumini wa kale
na akamuamini Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi atalipwa mara mbili.’
3-Na yule Mtumwa ambae ni mwenye kusimamia haki za Allah na akawa ni
Muaminifu kwa mwenye mali pia basi atalipwa mara mbili.’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Baina ya Wakati wenu na
wakati wa waliotangulia kabla yenu kuna Sala ya Asr na Maghrib, na mfano wenu
kulinganisha na mfano na Mayahudi na Wakristo basi hua ni sawa na Mtu ambae
amewaajiri Wafanyakazi na kusema; ‘Jee ni nani atakaefanya kazi kwa ajili yangu
kwa nusu siku kwa malipo ya siku kamili?’
Mayahudi wakafanya kazi kwa nusu siku kwa malipo ya siku nzima. Kisha Allah
Subhnah wa Ta’ala akauliza: ‘Jee ni nani atakaefanya kazi kuanzia Adhuhuri hadi
Al Asr kwa malipo ya siku nzima’ Hivyo Wakristo wakafanya kazi kuanzia
Adhuhuri hadi Al Asr.’ Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akasema:‘Jee ni nani
atakaefanya kazi kwa ajili kuanzia Al Asr mpaka Maghrib kwa malipo ya siku mbili
zaidi yake?’
‘Hivyo enyi Waislam nyinyi ndio mtakaofanya kazi baina ya Al Asr na Maghribi
kwa malipo ya siku mbili, na bila ya shaka mtalipwa mara mbili zaidi.’ Hivyo
Mayahudi na Wakristo wakakasirika na kusema: ‘Jee itakuaje sisi tufanye kazi na
kulipwa kwa chini zaidi?’ Allah Subhanah wa Ta’ala akauliza: ‘Jee mimi
nimekudhulumuni haki yenu?’ nao wakajibu : ‘La!’ Allah Subhanah wa Ta’ala
akasema: ‘Hizi ni fadhila zangu namfadhili nimtakae’(Imam Ibn Hibban)
Ambapo kutokana na hadithi hii basi na nyenginezo Wanazuoni wa Madhhab ya Imam
Abu Hanifa wamependekeza kua wakati baina ya sala ya Al Asr na Maghrib uwe mfupi
kuliko mda wa baina ya sala ya Adhuhuri na Al Asr, na hivyo Sala ya Al Asr hua
wanaichelewesha.
Hivyo Allah Subhnah wa Ta’ala anatutambulisha kisa cha Maryam Bint Imran kua kama
ni mfano wa Kaffala ili kutuelezea kuhusiana na umuhimu wa kuwajali Mayatima na sifa
anayostahiki kua nayo Kafil yaani mtu mwenye jukumu la kuwasimamia Mayatima,
ambapo katika kisa hiki basi umechaguliwa mfano wa Nabii Zakarriyah na Isha Bint
Faqudh, kwani amesema Allah Subhanahh wa Ta’ala ktika Qur’an kua:
236
﴿وَٱبْتَلُواْ ٰ ٱلْيَتَامَى حَتى َّ ٰ إِذَا بَلَغُواْ النِّكَا حَ فَإِنْ آنَسْتُمْ مِّنْهُمْ رُشْ داً فَٱدْفَعُواْ إِلَيْهِمْ
أَمْوَالهَُمْ وَلاَ أتَْكُلُوهَآ إِسْرَافاً وَبِدَاراً أَن يَكْبَرُواْ وَمَن كَانَ غَنِيّاً فَلْيَسْتَعْفِفْ ن وَمَ
كَانَ فَقِيراً فَلْيَأْكُلْ بِٱلْمَعْرُوفِ فَإِذَا دَفَعْتُمْ إِلَيْهِمْ أَمْوَ الهَُمْ فَأَشْهِدُواْ عَلَيْهِمْ وَكَفَ ٰ ى
يباً ﴾ بِٱهلل َِّ حَسِ
Waibtaloo alyatama hatta idha balaghoo alnnikaha fa-in anastum minhum rushdan
faidfaAAoo ilayhim amwalahum wala ta/kulooha israfan wabidaran an yakbaroo
waman kana ghaniyyan falyastaAAfif waman kana faqeeran falya/kul
bialmaAAroofi fa-idha dafaAAtum ilayhim amwalahum faashhidoo AAalayhim
wakafa biAllahi haseeban (Surat An Nisaa 4:6)
Tafsir: Na wajaribuni (Kiakili na ufaham wao) Mayatima hadi wawe wamebaleghe na
kufikia umri wa kuoa, na mkiwaona wana ufaham mzuri, basi wapeni mali zao, na
wala msizitumie kwa Israfu kutokana na kua na khofu kua watakua wakubwa. Na
kama ikiwa mmoja miongoni mwenu ni Tajiri basi asichukue malipo. lakini kama
akiwa Fukara basi na wacha na achukue kinachostahiki, na kisha mtakapowakabidhi
Mali zao basi kuwe na shahidi juu yao na kwa hakika anatosheleza Allah Kuchukua
Mahesabu.
Ambapo aya imetumia neno Bala ambalo linamaanisha Kujaribu, Kufanyia Mtihani iwe
kwa ajili ya Kupandisha Darja au kwa Kuadhirisha, Kuthibitisha, Kusimama. Kufadhili,
Hivyo aya inatubainishia kua kwa kila mwenye kufanya Kaffal yaani kulea basi baada ya
kufika mda wa kumalizika kipindi cha kulelewa Mayatima yaani wamesha baleghe basi
wanatakiwa kujaribiwa ufaham wao kuangaliwa kama wanao uwezo wa kusimamia Mali
zao, ambapo kwa upande wa Imam Abu Hanifa na Imam Malik basi mtizamo wao
kuhusiana na Umri stahiki kwa mtoto kua tayari ameshakua mkubwa hua ni miaka 17 wa
Mwanamke na miaka 18 wa Mwanamme.
Ambapo kwa Wanafunzi wa Imam Abu Hanifa ambao ni Wanazuoni wa Madhhab ya
Hanafi kma Imam Muhammad Abu Yusuf basi yeye anaendana sambamba na mtizamo
wa Imam Al Shafii na Imam Ahmad Ibn Hanbal kuhusiana na suali hili kwani wao
wanasema kua Umri wa mtoto kua Mkubwa ni miaka 15 bila ya kutofautisha baina ya
Mwanamme na Mwanamke.
237
Na hii ni kutokana na hadith isemayo: ‘Amesema Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu
Anhu kua: ‘Mimi nilipendekeza kwa Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam kua
niende kupigana katika vita vya Uhud nilipokua na umri miaka 14, lakini
hakuniruhusu. Hivyo nikapendekeza kwake tena niende kwenye vita vya Khandak
nilipokua na umri wa miaka 15 na akaniruhusu’(Sahih Muslim)
Na anasema Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari kua: ‘Kwa upande wa
Imam Abu Hanifa basi kama Mtoto huyo itabidi akabidhiwe Mali zake bila ya
kujali kua kama ataweza kuisimamia ama la pale anapotimia umri wa miaka 25,
lakini Wanafunzi wake wametofautiana nae, kwa kusema kua kama Mtoto huyo
atakua bado hajaonesha kua amekua kiakili basi hastahiki kupewa jukumu la
kusimamia Mali zake.’
Ambapo kwa upande wa Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye
anasema kua: ‘Mtizamo wa kua kama Mtoto huyo atakua bado hajaonesha kua
amekua kiakili basi hastahiki kupewa jukumu la kusimamia Mali zake, basi ndio
pia Mtizamo wa Imam Al Shafii’
Hapa kuna baadhi wanaweza wakajiuliza hivi kwa nini Wanafunzi wa Imam Abu Hanifa
wakabadilisha Mtizamo na kuenda kinyume na Mtizamo wa Imam wao mkuu? Ambapo
jibu la suali hili kwa kirefu linapatikana katika kitabu changu cha Ijihad na Taqlid
Historia ya Wanazuoni na Madhhab yao katika Uislam, ambacho kinapatikana
mtandaoni kwa bure kama sadaqa. hivyo hapa tutazungumzia kwa juu juu tu ili kwa wale
ambao hawajakipata basi nao wanufaike.
Hivyo hii ni kwa sababu Imam Al Shafii alisoma kwa Imam Malik na kwa MWanafunzi
mkuu wa Imam Abu Hanifa kisha na yeye akamsomesha Imam Hanbal.
Sasa katika wakati wa kipindi cha uhai wake Imam Al Shafii basi kukatokea Mvutano
wa Kifiqh baina ya Madhhab ya Imam Abu Hanifa na Madhhab ya Imam Malik wakati
Maimamu wao hao wakuu wameshafariki na Imam Al Shafii akaombwa Autatue mzozo
huo.
Hivyo Imam Al Shafii akautatua kwa kuyatoa kasoro Madhhab hayo mawili kwa
kuziainisha Tofauti zao kwenye Vitabu viwili tofauti kimoja ni Ikhtilafi Al Maliki na
chengine ni Ikhtilafi Al Iraqiyyin (Hanafi). Kisha akaandika kitabu chake yeye na
kufafanua njia sahih ya kufuatwa katika Fiqh kiitwacho Al Risala. Na kutokana na
kuaandika Al Risala basi ndio Imam Al Shafii akawa anajulikana kama ni Baba wa Usul
Fiqh
238
Na Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Maliki na Imam Abu Hanifa wakivipitia vitabu
vyao walivyoandikiwa na Imam Al Shafii na kisha wakakipitia kitabu cha Imam Al Shafii
cha Al Risala na wakakubaliana na Mtizamo wa Imam Al Shafii.
Kwa hivyo sasa hapa ndio ikatokea Mitizamo miwli kwa Madhhab haya mawili kwani
kwa upande wa Madhhab ya Hanafi basi kuna mitizamo ya kabla ya kuja kwa Imam Al
Shafii ambayo ndiyo Mitizamo ya Imam Abu Hanifa Mwenyewe. Na kwa Madhhab ya
Imam Malik pia kuna Mitizamo wa kabla ya kuja Imam Al Shafii ambao ndio Mitizamo
ya Imam Malik mwenyewe.
Sasa unaposikia kua katika Madhhab kuna mitizamo miwili basi mmoja ni wa zamani
usiokua na Nguvu na wa pili ni mtizamo mpya yaani baada ya kuja Imam Al Shafii ambao
ni wenye Nguvu zaidi. Kwa mfano kama tulivyoona kwenye mfano wa upande wa
Madhhab ya Imam Abu Hanifa na Imam Malik kuhusiana na umri wa Kukabidhiwa mali
zake Yatima.
Hivyo inabidi tusijichanganye Kama vile ambavyo kwa mfano wanavyojichanganya
watu wasiojua pale wanaposikia kua katika Madhhab ya Imam Abu Hanifa na Madhhab
ya Imam Malik kuna mitizamo miwili ya kuhusiana na Muandamo wa mwezi. Ambapo
wa kwanza ni wa zamani na usiokua na nguvu ambao ni kabla ya kuja Imam Al Shafii ni
kua Mwezi Mmoja kwa Dunia nzima.
Halafu kuna mtizamo wa pili ambao ni Mpya ambao ndio unaokubalika ambao ni wenye
nguvu ambao ni wa baada ya kuja Imam Al Shafii na kuwakosoa na kuwaonesha kasoro
zao nao wakakubali ambao ni kua Kila sehemu na Muandamo wa mwezi wake.
Na ndio maana ukasikia kua kuna makubaliano ya Wanazuoni kuhusiana na Muandamo
wa kila Machweo na Muandamo wake kwa sababu Wanazuoni wa Madhhab mengine
wamekubaliana juu yake baada ya kuthibitishiwa na Mujaddid Ad Din Imam Muhammad
Idris Al Shafii.
Ila sasa ili kuyafaham haya inabidi usome historia za Maimamu hawa Uwafaham
Ipasavyo na Madhhab yao uyafaham ipasavyo na njia wanazotumia katika kutoa hukmu
zao katika Qur'an, Hadith, Sunna na Qiyas au Makisio na uzifaham ipasavyo.
Kisha ndio utajua kua hata Kiakili haifai kufuata Mtizamo ambao ni wa zamani na
usiokua na nguvu. Kwani ingawa ukweli ni kua zamani Qur'an ilikua inaandikwa
kwenye Ngozi kwenye Magome, na hata hadith pia zilikua zimeandikwa katika sehemu
tofauti lakini ukaja mtizamo mpya na Masahaba wakakubaliana kua ikusanywe pamoja
kwenye Mas-haf moja na Hadith zikusanywe pamoja na hivyo leo hii kila mtu anafuata
Mtizamo huo mpya kwani ndio unaokubalika zaidi na ndio unaonufaisha zaid.
239
Lakini ingawa watu hukubaliana kua hata nguo, Vyakula Matibabu, simu n.k za zamani
hazikubaliki, Lakini inashangaza kuona kua kuhusiana na Muandamo wa mwezi watu
bado wameng'ang'ania Mtizamo wa Zamani na usiokubalika wa kua Dunia Si Mviringo
bali ni Mraba.
Na bila ya shaka kuna baadhi wanaweza wakajiuliza ilikuaje mpaka Imam Al Shafii
akaweza kuwathibitishia Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Abu Hanifa kwa mfano, kwa
sababu Wanafunzi wa Imam Abu Hanifa ambao nia Imam Abu Yusuf na Imam Ash
Shaybani ni walimu wa Imam Al Shafii.
Sasa inakujae mpaka Walimu anakubali kua kweli sisi hapa tumekosea? Na sio hao tu
hata Imam Malik mwenyewe kuna wakati katika uhai wake alikubali mbele ya Imam Al
Shafii kua kweli hapa nimekosea na wewe uko sahih, na hili tunaliona pale wakati Imam
Al Shafii akiwa bado mdogo akisoma kwa Imam Malik.
Ambapo siku moja Al Shafi’i alikua amekaa chini ya miguu ya Imam Malik
akisomeshwa, alikuja mtu na kumwambia Imam Malik: ‘Hakika mimi nimeshamuacha
mke wangu jee nifanye nini?’
Imam Malik akamuuliza jee ilikuaje? Yule mtu akajibu: ‘Mimi kazi yangu ni kuuza
ndege, hivyo dukani kwangu alikuja mnunuzi akataka kumnunua ndege aina ya
Kasuku, alipofika akaniuliza kama yule Kasuku analia ama la, nami nikamuapia
kua kama halii basi mke wangu awe ameachika, kwani yule Kasuku alikua akilia,
hivyo yule mnunuzi akamnunua yule Kasuku lakini baada ya siku kadhaa
alimrudisha na kusema kua yule kanga halii.’
Imam Malik akajibu, ‘Hakika umeshamuacha mke wako, hivyo usimkaribie’. Al
Shafi’i akaingilia kati na kusema: ‘Subiri kwanza nikuulize. ‘Jee, baina ya kulia na
kunyamaza kwa kanga wako kupi ni kukubwa zaidi?’’
Yule muuzaji akajibu, ‘Kulia kwake ni kukubwa zaidi kuliko kunyamaza kwake’.
Al Shafi’i akajibu ‘Basi mkeo hajaachika’.
Hapo Imam Malik akaingilia kwa kusema ‘Ya Al Shafi’i unajuaje?’.
Al Shafi’i akajibu ‘Kwa sababu ulinidadithia kua kutoka kwa Al Zuhri, kutoka kwa
Abu Salam Ibn Abd al Rahman, kutoka kwa Umm Salama ambae amesema kua
Fatma bint Qayis alisema ‘Ya Rasul Allah! Abu Jahm na Muawiyah wote wawili
wameniposa’
240
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salaam akajibu ‘Muawiyah hana pesa, na Abu
Jahm hatui mzigo chini kutoka kwenye bega lake (kwa Safari), akiwa na maana:
Hali yao ya kila mara; Kwa Waarabu hutumia hali ya kila mara kutokana na
utokeaji wa mara kwa mara kwa kitu au jambo. Hivyo kwa kua Kasuku wake
alikua akilia hapo kabla kwa mda mrefu kulingana mda alionunuliwa ambao alikua
ni mwenye kunyamaza. Hivyo basi hii inamaanisha Kasuku wake huy bwana
analia’.
Imam Malik akaridhika na kumwambia Al Shafi’i ‘Naam uko Sahih!’.
Na ndio nikasema kua inabidi uwasome hawa Wanazuoni uwajue ndani nje na kisha ndio
utafaham, kua katika Moja kati ya Jambo ambalo Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Abu
Hanifa na Imam Malik walikua wanakosea katika mifumo yao ya Fiqh ilikua ni katika
Hadith au kauli ambayo ni ya Mtu mmoja.
Hii inaitwa Habar Al Wahid, kwani wao walikua hawaitumii ipasavyo, na bila ya shaka
Fatwa ya Mwezi ya Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua kila sehemu
na Muandamo wake pale yeye alipokua anakaa Makkah na kuukataa Muandamo wa Syria
kwa sababu Matlai yao ni tofauti, ni moja kati ya Habar Al Wahid yaani habari au kauli
ya Mtu mmoja.
Lakini sasa alipokuja Imam Muhammad Idris Al Shafii akawaambia kua Hii Habar al
Wahid ni Habari ambayo inastahiki kutumiwa kua pia kama chanzo cha kutolea Hukmu
za Sharia za Kiislam.
Kama mfano wa habari Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua kila sehemu na
Muandamo wake pale yeye alipokua anakaa Makkah na kuukataa Muandamo wa Syria
kwa sababu Matlai yaani Machweo yao ya Jua ni tofauti, na kisha akasema kua ‘Hivi
ndivyo alivyotufundisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.’
Hivyo kauli hii ya Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu ni moja kati ya Habar Al
Wahid yaani habari au kauli ya Mtu mmoja ambayo inakubalika kutoa Humu ya Kisharia.
Hivyo Imam Muhammad Idris Al Shafii akawaambia kua Hii Habar al Wahid ni Habari
ambayo inastahiki kutumiwa kua pia kama chanzo cha kutolea Hukmu za Sharia za
Kiislam kwa sababu Masahaba walikua wanaitumia na ilikua inakubalika kwao wao.
Kisha Imam Al Shafii akasema kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kua: Allah Subhanah wa Ta’ala humnawirisha yule Mja ambae amesikia maneno
yangu kisha akayakumbuka, akayahifadhi na kisha akayasogeza mbele zaidi kwa
wengine.’
241
Imam Al Shafii anaendelea kusema kua: ‘Inawezekana Mtu huyo anaeyasogeza mbele
akawa ana Ilm ya Fiqh lakini akawa ni Mwanafiqh, na anaweza akawaa ni
Mwanafiqh lakini akayasogeza mbele zaidi maneno hayo kwa wanaojua zaid yake.
Na Moyo wa Muislamu kamwe hauwezi kua na kinyongo kwa watu wa aina tatu’
1-Mwenye Ikhlasi katika kumtumikia Allah Subhanah wa Ta’ala.
2-Mkweli na Muamninifu kwa Waislam.
3-Mwenye Kuthibitisha katika jamii kua yeye anasimamia Maslahi ya Waislamu
na Kuwakinga na Upotovu.
Kisha Imam Muhammad Idris Al Shafii akatoa Mfano wa matumizi ya Habar Al Wahid
kwa kusema kua: ‘Abu Talha Radhi Allahu Anhu na wenzake waliivunja Mitungi
yao yote ya Pombe baada ya kuambiwa na Mtu kua Kuna aya imeshuka
inayoharamisha Pombe.’
Hivyo Abu Talha Radhi Allahu Anhu na wenzake hawakuhoji kweli au Uongo, imeshuka
jana au leo, bali wao waliposikia tu basi hapo hapo wakavunja Mitungi yao yote na
kumwaga Pombe iliyomo ndani yake yote.
Kisha akatoa na mfano mwengine ambao ni ule unaohusiana na iliposhuka aya ya 144 ya
Surat Al Baqara iliyoamrisha kua Sasa hivi Waislam wasikielekee Kibla cha Bayt ul
Maqdis bali waelekee Kibla cha Makkah pale iliposema:
﴿قَدْ نَرَىٰ تَقَل ُّبَ وَجْهِكَ فىِ ٱلس َّمَآءِ فَلَنُوَلِّيَن َّكَ قِبْلَةً تَرْضَاهَا فَوَلِّ وَجْهَكَ شَطَْر
ٱلْمَسْجِ دِ ٱلحَْرَامِ وَحَيْثُ مَا كُنْتُمْ فَوَل ُّواْ وُجُوِهَكُمْ شَطْرَهُ وَإِن َّ ٱل َّذِينَ أُ وتُواْ ٱلْكِتَا َب
لَيَعْلَمُونَ أَن َّهُ ٱلحَْق ُّ مِن ر َّهبِِّمْ وَمَا ٱهلل َُّ بِغَافِلٍ عَم َّا يَعْمَلُونَ ﴾
Qad nara taqalluba wajhika fee alssama-i falanuwalliyannaka qiblatan tardhaha
fawalli wajhaka shatra almasjidi alharami wahaythu ma kuntum fawalloo
wujoohakum shatrahu wa-inna alladheena ootoo alkitaba layaAAlamoona annahu
alhaqqu min rabbihim wama Allahu bighafilin AAamma yaAAmaloona (Al-
Baqarah 2:144)
Tafsir : ‘Kwa hakika! Tumeona muelekeo wa uso wako kuelekea Mbinguni, Hakika
tutakuelekeza katika Qiblah ambacho kitakuridhisha. Hivyo geuzia uso wako kuelekea
Al Masjid Al Haram. Na kokote kule mliko basi geuzeni Nyuso zenu katika muelekeo
242
huo. Kwa hakika wale waliopewa Kitabu wanajua kua (kugeuzia kwenu muelekeo
kuelekea Al Kaabah) Haki kutoka kwa Mola wao na Allah hakughafilika na
wanayoyafanya.’
Ambapo ya hii ilishuka katika mwezi 15 Shaaban ya mwaka wa pili Al Hijra wakati wa
Sala ya Dhuhr hivyo Masahaba wakasali na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
katika Msikiti wake, na wakiwa hawakuelekea katika Kibla cha Jerusalem katika Masjid
Al Aqsa kama ilivyokua kawaida yao hapo kabla, bali walisali huku wakiwa wameelekea
katika Kibla kipya cha Makkah kilichoamrishwa kwenye aya hii, kisha baada ya sala
mmoja kati ya Watu wa ukoo wa Banu Salama akawa anarudi nyumbani akapita kwenye
Masjid Al Quba akawakuta Waislam wanasali sala ya Al Asr wakiwa wameeleka Bayt al
Maqdis.
Hivyo Muislam huyo kutoka katika ukoo wa Banu Salama akanadia Msikitini humo kwa
kusema kua: ‘Imeshuka aya inayosema kua Kibla cha Waislam sasa hivi ni kuelekea
katika Al Kaabah Mjini Makkah’ Na hapo hapo Masahaba waliomo kwenye Sala hio
wakageukia Katika Upande wa Mji wa Makkah, huku wengine walikua katika Kurukuu.
Ambapo huu ndio Msikiti pekee ambao ndani yake ilisaliwa Sala ambayo nusu yake watu
waliianza kuisali huku wakiwa wameelekea kibla cha Jerusalem na nusu yake
wakaimalizia huku watu wake wakiwa wamelekea kibla cha Makkah, na ndio maana
ukawa unaitwa Masjid Qiblatayn.
Tafakkar! Kwani Masahaba hawa hawakukata Sala, wala hawakuuliza kasema nani
kuhusiana na habari hio? Na kama jee ni kweli au ni Uongo? Kwani mtu aliesema
hawakumuona wao wamesikia sauti tu inawataarifu juu ya habari al wahid hio, wakati
wakiwa ndani ya Sala.
Nadhani japo kidogo itakua tumefahamiana kuhusiana na kwanini ikawa kuna tofauti
kwenye Madhhab haya Mawili ya Imam Abu Hanifa na Imam Malik ya mitizamo ya
Fiqh ya zamani na Mipya katika kesi kama hizi za umri Yatima kukabidhiwa mali yake,
Mwandamo wa mwezi, Itiqaf, n.k Hivyo Wanazuoni waliofuatia wa Madhhab hayo
wakakubaliana kufuata Mitizamo mipya.
Hivyo baada ya Surat An Nisaa 4:6 kuzungumzia kuhusiana na Ukabidhiwaji wa Mali
zao Mayatima basi ikakataza utumiwaji wa mali za Mayatima kwa israfu ambapo Imam
Muhammad Al Shafii anasema kua: ‘Mtu yeyote yule anaesimamia mali ya Yatima
basi anaweza kuchukua kutokana nayo kua kama sehemu ya malipo yake, na hua
hain hja ya kuzirudisha’ Ambapo pia ndio mtizamo wa Imam Hasan Al Basr, Imam
Ibrahim An Nakhai, Imam Ibn Attiyah na hii ni kutokana na uthibitisho wa ile hadithi
ambayo inasema: ‘Kuna mtu alimwambia Rasul Allah Salallahu Alayi wa Salam kua:
Hakika mimi sina njia ya kujipatia Riziki, lakini nina Yatima chini ya usimamizi
243
wangu’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Unaweza kutumia mali
yake Yatima lakini bila ya kufanya Israfu, au kuutumia msingi wenyewe na wala
usiokoe mali yako kutokana na kutumia mali yake’(Sahih Ibn Majah, Imam Ibn
Marduwayh, Imam An Nasai, Imam Ahmad, Imam Ibn Hibban na Imam Abu Daud.)
Ambapo kwa upande wa Amir ul Muuminin Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu
basi yeye alisema: ‘Mimi hua naichukulia Mali ya Bayt ul Maal kama
ninavyoichukulia mali ya Yatima, wakati ninapokua na kitu basi hua najitenga
nayo, na ninapokua sina kitu basi hua nnachukua kama mkopo, na kisha
ninapopata hua narudisha’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anatuelezea visa hivi vya watoto wenye sifa za
Uyatima na Laqit ndani ya Qur’an kupitia kwa watu Watukufu na wenye darja kubwa
sana mbele yake na juu yetu ambao ni Mitume na Manabii kwa ajili ya kutufundisha
umuhimu wa kuwajali katika kuwalea na kuwahudumia ili watoto hao wakulie katika
hali na mazingira bora yatakayowaongoza katika maisha yao hapa Duniani na kesho
Akhera, kutokana na muongozo wa malezi ya mlezi husika, kwani kufanya hivyo hua ni
kuonesha kua na Subra na Ucha Mungu na malipo yake mbele ya Allah Subhanah wa
Ta’ala ni makubwa sana kama zinavyosema aya:
﴿إِن َّ ٱلأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُوراً۞عَيْناً يَشْرَبُ هبَِ ا عِبَادُ ٱهلل َِّ
يُفَجِّ رُونَهَا تَفْجِ يراً۞يُوفُونَ بِٱلن َّذْرِ وَيخََافُونَ يَوْماً كَانَ شَر ُّهُ ُمسْتَطِيراً۞وَيُطْعِمُوَن
ٱلط َّعَامَ ٰ عَلَى حُبِّهِ مِسْكِيناً وَيَتِيماً وَأَسِ ا يراً۞ إِنم ََّ نُطْعِمُ كُمْلِوَ جْهِٱ هلل َِّ لاَ نُرِيدُ مِنكُ ْم
َك
جَزَآءً وَلاَ شُكُوراً۞إِ َّ نخََافُ مِن ر َّبِّنَا يَوْماً عَبُوساً قَمْطَرِيراً۞فََوقَاهُمُ ٱهلل َُّ شَر َّ ذٰلِ
ٱلْيَومِ وَلَق َّاهُمْ نَضْرَةً وَسُرُوراً۞وَجَزَاهُمْ بمَِا صَبَرُواْ جَن َّةً وَحَرِيراً ﴾
Inna al-abrara yashraboona min ka/sin kana mizajuha kafooran; AAaynan
yashrabu biha AAibadu Allahi yufajjiroonaha tafjeeran; Yoofoona bialnnadhri
wayakhafoona yawman kana sharruhu mustateeran; WayutAAimona alttaAAama
AAala hubbihi miskeenan wayateeman waaseeran; Innama nutAAimukum liwajhi
Allahi la nureedu minkum jazaan wala shukooran; Inna nakhafu min rabbina
yawman AAaboosan qamtareeran; Fawaqahumu Allahu sharra dhalika alyawmi
walaqqahum nadratan wasurooran; Wajazahum bima sabaroo jannatan
wahareeran (Surat Al Insan 76:8-12)
244
Tafsir: Hakika ya Wacha Mungu, watakunywa kutoka kwenye Gilasi Kafuran (Kinyaji
kinachotokana na Chemchem ya Peponi),Chemchem ambayo watakunywa Waja wa
Allah na kuisababisha kufoka kwa wingi zaidi, hawa ni wale waliotimiza Nadhiri zao
na wanaoiogopa siku ambayo Shari yake itaenea, Ni wanaotoa Chakula mbali ya kua
ni wenye kukipenda, kwa Masikini, Na Mayatima na Mateka; (Wakiwaambia
kua)’Hakika sisi tunakulisheni nyinyi kwa kutaka Malipo ya Allah tu, hatutaki Mlipo
kutoka kwenu waa shukurani. Kwani sisi tunaogopa kutoka kwa Mola wetu ile siku
Ngumu na Nzito ambyo itazifanya Nyuso ziwe ni zenye kukunjana; Hivyo Allah
amewaokoa wao kutokana na shari ya siku hio na kuwapa muonekano mzuri wa
furaha, Na Malipo yo kutokana na Subira yao itakua ni Pepo na Nguo za Hariri.’
Aya inatuwekea wazi kua Watu wenye Taqwa na Waja wema hua ni wale ambao ni
wenye Huruma na Ukarimu na wenye kuamini kua kufanya kwao hivyo hua ni kwa ajili
ya Akhera yao kwani watahurumwa na kukirimiwa na Mola wao kesho Akhera, kutokana
na huruma na ukarimu wao kama vile wao walivyofanyiwa ukarimu na Mola wao hapa
Ulimwenguni, na ndio maaana akasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua:
‘Peponi Kuna Mlango unaoitwa Furaha, ambao hawatoingia ndani yake isipokua
wale waliokua wakiwafurahisha Watoto’ (Imam Ad Daylami)
Amesema Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam: ‘Hakuna yeyote yule mwenye
kuwahudumia Mayatima basi atakua pamoja nami Peponi kama hivi – Huku
akionesha vidole vyake viwili cha shahada na cha kati vikiwa pamoja’ (Imam
Bukhari)
Hivyo Muislam yeyote yule atakaeendana kinyume na mtizamo huu na hivyo kua si
mwenye kuwajali Mayatima basi atakua ni miongoni mwa watu wenye sifa ya kua ni
Wanafiq.
Ambapo alisema Hasan Al Basr kua: ‘Hakuna anaeuogopa Unafiq isipokua yule Mtu
ambae ni Alieamini kweli, na hakuna anaejihisi kua amesalimika na Unafiq
isipokua yule ambae ni Mnafiq na Hakuna asieuogopa Unafiq isipokua Mtu huyo
hua ni Mnafiq.’
Ambapo Hasan Al Basr alisema hivi kwa sababu ya kua Unafiq ni Sifa ambayo haifai
kua nayo Muislam. Kwani Sifa ya Unafiq ni Sifa ambayo inachukiza mbele ya Allah
Subhanah wa Ta'ala na Mtume wake Salallahu Alayhi wa Salam kutokana na kua
Madhara yake ni Makubwa kuliko Madhara ya Mtu alie Kafiri. Na hii inawekwa wazi na
ile aya ambayo inasema;
245
﴿وَمِنَ ٱلن َّاسِ مَن يَقُولُ آمَن َّا بِٱهلل َِّ وَبِٱلْيَوْمِ ٱلآخِ رِ وَمَا هُم بمُِؤْمِنِينَ۞يخَُ ادِعُونَ ٱهلل ََّ
وَٱل َّذِينَ آمَنُوا وَمَا يخَْدَعُونَ إِلا َّ أَنْفُسَهُم وَمَا يَشْعُرُونَ۞فىِ قُلُوهبِِم م َّرَضٌ فَزَادَهُمُ ٱهلل َُّ
ِض
مَرَضاً وَلهَُم عَذَ ابٌ أَلِيمٌ بمَِا كَانُوا يَكْذِبُونَ۞وَإِذَا قِيلَ لهَُمْ لاَ تُفْسِ دُو اْ فىِ ٱلأَرْ
ۤ قَالُو اْ إِنم ََّا نحَْنُ مُصْلِحُونَ۞أَلا إِن َّهُمْ هُمُ ۤ ٱلْمُفْسِ دُونَ وَلَٰكِن لا َّ يَشْعُرُونَ ﴾
Wamina alnnasi man yaqoolu amanna biAllahi wabialyawmi al-akhiri wama hum
bimu/mineena, YukhadiAAoona Allaha waalladheena amanoo wama
yakhdaAAoona illa anfusahum wama yashAAuroona; Fee quloobihim maradhun
fazadahumu Allahu maradhan walahum AAadhabun aleemun bima kanoo
yakdhiboona; Wa-idha qeela lahum la tufsidoo fee al-ardi qaloo innama nahnu
muslihoona(Surat Al Baqara 2:8-11)
Tafsir: Na Miongoni mwa Watu kuna wale wasemao kua Wamemuamini Allah na
Siku ya Mwisho lakini hawakuamini wanadhani kua Wanamhadaa Allah na
Walioamini na Lakini Hawamhadai yeyote Isipokua Nafsi zao lakini wao Hawalioni
hilo kwani Ndani ya Nyoyo zao Wana Maradhi na Kisha Allah Akawaongezea
Maradhi Na Juu yao kuna Adhabu kali sana kutokana na Wanayoyakadhibisha
Wanapoambiwa Msifanye Ufisadi kwenye Ardhi hua Wanasema kua kwa Hakika Sisi
ni wenye Kutafuta Usuluhisho.
Hizi ni miongoni mwa aya za Mwanzoni mwanzoni mwa Surat Al Baqara, Sura ambayo
kwanza imeanza kufunguliwa kwa kuwazungumzia Waumini walioamini na Sifa zao
kama vile ambavyo imemalizia kufungwa kwa aya zake za Mwisho katika kuelezea Sifa
za Waumini pia na hivyo kuonesha na kusisitizia Umuhimu wa Kuamini Nguzo 6 za
Imani ya Dini ya Kiislam.
Ambapo kutokana na Kua na Sifa hio basi hata Sahaba Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu
Anhu aliusia kua: Katika wakati atakapofariki na Kuzikwa basi katika Upande wa
Kichwani kwake asomewe Kichwa cha Surat Al Baqara yaani aya 5 za Mwanzo za
Surat Al Baqara (2:1-5) na Miguuni mwake asomewe Kifungio cha Surat Al Baqara
yaani aya mbili za Mwishoni za Surat Al Baqara (2:285-286)
Hivyo katika Aya hizi za Surat Al Baqara 2:8-11 basi Allah Subhanah wa Ta'ala
anawazungumzia Wanafiq na Ubaya wao Kua ni Wenye Kufanya Hadaa kwa Maneno
yao, yaani ni wenye Kusema Uongo lakini hawajui kua Kufanya kwao Hadaa huko hua
ni Kujihadaa Nafsi zao, ambazo zina Maradhi ambayo wanayaendekeza na hivyo Allah
246
Subhanah wa Ta'ala akawazidishia Maradhi zaid ili apate kuwachoma vizuri kesho
Akhera kutokana na Unafiq wao kama zinavyosema aya:
﴿وَمَن يُشَاقِقِ ٱلر َّسُولَ مِن بَعْدِ مَا تَبَين ََّ لَهُ ٱلهُْدَىٰ وَيَت َّبِعْ غَيْرَ سَبِيلِ ٱلْمُؤْمِنِ
نُوَلِّهِ مَا َّ ٰ تَوَلى وَنُصْلِهِ جَهَن َّمَ وَسَآءَتْ مَصِيراً ﴾
َين
Waman yushaqiqi alrrasoola min baAAdi ma tabayyana lahu alhuda wayattabiAA
ghayra sabeeli almu/mineena nuwallihi ma tawalla wanuslihi jahannama wasaat
maseeran (Surat An-Nisa 4:115)
Tafsir : Na yeyote yule akayebisha na kumpinga Mtume, baada ya kua ameoneshwa
wazi njia iliyonyooka, na akafuata njia nyengine isiyokua ya walioamini,
Tutamuelekeza katika njia aliyochagua, na tutamchoma motoni - na huo hua ni
mwisho mbaya sana’
Na hii ni kwa sababu Miongoni mwa Sifa zao watu hao Wanafiq basi hua ni wenye
Kufanya Ufisadi Ardhini au Kusababisha Madhara katika Uislam. Lakini wanapoambiwa
kua hivyo wafanyavyo kua sivyo kwani hua wanaharibu badala ya kutengeneza basi wao
hua hawakosi Kisingizio kwa kusema kua Hivyo wafanyavyo wao hua si Kuharibu, si
Kusababisha Ufa katika Uislam bali ni Kujenga Uislam. Na bila ya shaka katika hili wako
wengi Sana, na wanaingia Waliokuwemo na wasiokuwemo kutokana na Watu kutojua
kwao na kupenda kufuata Mkumbo.
Kwani ndani yake ndio unakuta Waislam wenye Sifa ya Unafiq ambao wanawafanyia
Ufisadi Waislam wenzao katika Ardhi za Kiislam kama Yemen, Syria, Falestina,
Aghanistan, Iraq n.k kwa kuwasababshia mapigano na kusaidia uasi katka ardhi za
Waslam wenzao kwa manufaa yao ya kidunia na hivyo kuua Waislam wasiokua na hatia
na kusababisha madhara makubwa sana katika jamii za Kislam.
Na kisingizio chao? Wanasema Innama Nahnu Muslihoona na ambapo suluhisho lao
wao hua ni kuwaweka wale wanaoendana na Mitazamo yao na kusimamia maslahi yao,
ya kidunia ya kutaka kudumu zaidi madarakani, na hivyo ua ni wenye utafuta wafusi
wengi kwa kutumia njia za kuwashawishi watu wafuate mitizamo yao na hivyo kuanzisha
aina nyengine ya Unafiq wa kuwagawa Waislam katika jamii zao, kwa kutengeneza
makundi ya wale Waislam ambao wanaojitenga na wenzao katika Miandamo ya Mwezi
ya ardhi zao wanazoishi kwa ajli ya kuwafuta wao na kuwaimarishia mamlaka na itiqadi
zao.
247
Na hivyo kutokana nao basi takriban katika kila ardhi za Waislam sasa hivi kuna makundi
ya wanaofuata Muandamo wa mwezi wa Saudia na kuna wafuatao Muandamo wa nchini
mwao, hivyo kutokana na kuwepo kwa Unafiq katika Jamii za Kiislam basi ndani ya kila
nchi ambayo watu wanasali sala zao katika wakati mmoja basi kuna Ramadhani mbili na
sikukuu nne tofauti, na hao wanaofuata Muandamo ambao si wa ardhi zao basi nao wao
wanasema pia Innama Nahnu Muslihoona yaani Kwa Hakika sisi ni Wenye Kutafuta
Suluhisho.
Kutokana na kutofahamu kwao basi watu hawa hua hawajui kuhusiana na Maumbile ya
Matokeo na Nyakati baina ya Viumbe na Muumba, na hivyo hawajui ukubwa wa uwezo
wa Allah Subhanah wa Ta’ala na kwa sababu labda hawajaifaham maana ya Ayat al
Kursy.
AYAT AL QURSY - NYAKATI NA MATUKIO YA VIUMBE MBELE YA
ALLAH SUBHANAH WA TA'ALA
Ayat Al Qursy ambayo ilishuka katika mji wa Madinah na mbali ya kua Ayat al Kursiy
kua inajulikana kama Ayat Al Arshi lakini hua pia inajulikana kwa majina yafuatayo:
1-Sayyidat Ayi Al Qur’an.
2-Al Ruqqyat.
3-Ayyati Al Haris.
4-Wa Al Muhsanati.
5-Wa Al Junnati.
6-Wa Al Waqqiyati.
7-Wa Al Kafiyyati.
8-Wa Al Sharifati.
9-Wa Al Aadhimati.
10-Wa Ashraf Ayati.
11-Wa Aadham Ayati.
12-WatudaAai fii al Tawrati Ayyati Allah.
Hivyo tunapozungumzia Ayat Al Kursiy basi hua tunazungumzia kuhusiana na maneno
Matukufu ya Allah Subhanah wa Ta’ala yaliyomo katika aya tukufu kuliko zote ambayo
ni yenye kusema kua:
﴿ٱهلل َُّ لاَ إِلَٰهَ إِلا َّ هُوَ ٱلحَْى ُّ ٱلْقَي ُّومُ لاَ أتَْخُذُهُ سِ نَةٌ وَلاَ نَوْمٌ ل َّهُ مَا فىِ ٱلس َّمَاوَاتِ
وَمَا فىِ ٱلأَرْضِ مَن ذَا ٱل َّذِى يَشْفَعُ عِنْدَهُ إِلا َّ إبِِذْنِهِ يَعْلَمُ مَا بَينَْ أَيْدِيهِمْ وَمَا
248
خَلْفَهُمْ وَلاَ يحُِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلا َّ بمَِا شَآءَ وَسِ عَ كُرْسِ ي ُّهُ ٱلس َّمَاوَاتِ
وَٱلأَرْضَ وَلاَ يَؤُودُهُ حِ فْظُهُمَا وَهُوَ ٱلْعَلِى ُّ ٱلْعَظِيمُ ﴾
Allahu la ilaha illa huwa alhayyu alqayyoomu la ta/khudhuhu sinatun wala
nawmun lahu ma fee alssamawati wama fee al-ardhi man dha alladhee yashfaAAu
AAindahu illa bi-idhnihi yaAAlamu ma bayna aydeehim wama khalfahum wala
yuheetoona bishay-in min AAilmihi illa bima shaa wasiAAa kursiyyuhu
alssamawati waal-ardha wala yaooduhu hifdhuhuma wahuwa alAAaliyyu
alAAadheemu (Aya Al Qursy - Surat Al Baqara 2:255)
Tafsir: Allah! La ilaha illa Huwa Hakuna anaestahiki Kuabudiwa Isipokua Yeye (Yeye
Allah Subhanah wa Ta'ala) Ni Mwenye Uhai wa Milele na ndie Mwenye Kujisimamia
juu ya Kila kitu na ndie Msimamizi juu ya Kila kitu (Yeye ndie ambae) Haimpitii Hali
ya Kusinzia wala ya Kulala Usingizi Kwake yeye Ndio kwenye Umiliki wa Kila
Kilichomo Mbinguni na Ardhini Jee Ni Nani yule Ambae atakaeweza Kuingilia
Mambo yake (Allah Subhanah wa Ta'ala) Bila ya Idhini yake? (Allah Subhnah wa
Ta'ala) Kwani yeye (Allah Subhanah wa Ta'ala) Ni mwenye Kujua juu ya kila kitu
Kabla ya kutokea kwake na Baada ya Kutokea kwake na Hakuna atakaekua na
Chochote kutokana na Ilm yake Isipokua kwa kile akitakacho (kijulikane) Na Arshi
yake (Ukubwa wake) Imeenea Mbinguni na Ardhini na wala hachoki katika
kuvihifadhi na kuvisimamia vitu (Vilivyomo ndani yake Mbinguni na Ardhini) Na
Yeye ndie Aliejuu Kidarja na Kiutukufu hakuna alie zaidi yake
Hii ni Aya ambayo ndani yake inabeba ujumbe Mzito sana, kwani inaelezea mambo
mengi ambayo wengi hatuyajui kutokana na Ufinyu wa Ufaham wetu. Na aya inathamani
na manufaa Makubwa Sana ambayo pia wengi wetu hatuyajui na hatuyathamini, kwa
sababu ni kawaida ya yule asiekijua kitu basi kua ndie asiekithamini.
Hivyo basi tunafahamishana ili angalau tupate kuyajua baadhi ya Mambo hayo, kwani
hatuwezi kuelezana yote, kwa sababu tukitaka kuelezana yote basi hatuwezi kuyamaliza
yote leo hii ambapo Miongoni mwa Mambo tusiyoyajua sisi Waislam wa leo Kuhusiana
na Aya hii basi ni Sifa Tukufu na Majina Matukufu ya Allah Subhanah wa Ta'ala.
Na hivyo tunashindwa Kufaham na Kuelewa Ukubwa wa Uwezo wa juu ya kila kitu wa
Allah Subhanah wa Ta'ala kama ilivyobainisha Ayat Al Kursiyu. Na Ukweli ni kua Hili
sio Jambo Dogo la Kulidharau au la kutokukumbushana kwa sababu linaweza
kumpelekea Mtu kua ni Mnafiq na kila mtu anajua sehemu ya Mnafiq baada ya Kufariki
kwake na kesho Akhera kama zinavyoonesha Aya na Hadith.
249
Na kutokana na kutojua Uwezo na Ukubwa wa Allah Subhanah wa Ta'ala na Maana ya
maneno ya Ayat Al Kursiyyu basi ndio maana unakuta watu wanaulizana Kuhusiana
kwanini baadhi ya Matukio Muhimu ya Kiislam yawe yatofautiane kiwakati Duniani na
hivyo Wasiojua kua ni wenye Kutaka kua lazima yawe ni yenye kutokea katika hali ya
Umoja Duniani kote, Ambapo hapa tunachukulia mfano wa Usiku wa Laylat Al Qadr,
Funga ya Arafa, Idd, n.k
Ambapo Mara nyingi watu wanashindwa kufaham kua Moja kati ya Sifa za Allah
Subhanah wa Ta'ala ni Al Hakim yaani ni Mwingi wa Hikma, pia ni Al Aadil yaani ni
Mwingi wa Uadilifu. Na Tunapozungumzia kuhusiana na sifa za Hikma na Uadilifu basi
ndani yake ndio tunaona kua Allah Subhanah wa Ta'ala hua ni Mwenye Kufanya kila
kitu chake kwa Hikma zake na kukisimamia kwa Uadilifu wake. Hivyo hua ni Mwenye
Kumlipa Mja wake kwa Uadilifu kulingana na Amali yake
Kwani tunapoiangalia Aya Al Kursiy basi tunaona hizi sifa 2 za Al Hayyu Al Qayyum,
ambayo ni sifa zinatupa Majibu ya Masuali yetu yote haya wanayoulizana wale wasiojua.
Kwa Sababu tunapozungumzia Al Hayy kwa Ufaham wa Kibinadam basi hua
inamaanisha kua Ni Mwenye Kuishi Milele, na tunapozungumzia Kuishi basi hua
tunazungumzia kuwepo kwa kitu husika, na tunapozungumzia kuhusu Milele basi hua
tunazungumzia hali ya Kitu kua katika Kutokua na Mwanzo wala mwisho na kutokana
na kutokua na Mwanzo wala mwisho basi kitu hicho hua katika kila sehemu kipo na kila
wakati kipo.
Hivyo tunapozungumzia kuhusiana na Sifa hii ya Allah Subhanah wa Ta'ala basi hua
inatubainishia kua kwake yeye hua Hakuna Mipaka ya kuwepo kwake na pia hakuna
mipaka ya kutokuwepo kwake katika ila sehemu na katika kila wakati.
Yaani alikuwepo, yupo na atakuwepo kwa Mda wote na Katika sehemu yeyote kabla ya
kuwepo kwake sehemu hio na baada ya kuwepo kwake sehemu hio na hii ni kwa Sababu
yeye ndie Muumba
Kwani kwa Kiumbe Jambo hili hua haliwezekani kwa sababu kiumbe hua na mipaka ya
Wakati wa kuwepo kwake ambao hua ni hali inayolingana na mazingira yake na tukio la
kuwepo kwake katika sehemu husika.
Kwani Sifa ya pili ya Jina Tukufu la Allah Subhanah wa Ta'ala liliopo ndani ya aya hii
baada ya Sifa ya Al Hayyu, basi ni sifa ya Al Qayyum. Ambapo hii ni Sifa ambayo yenye
Kumaanisha kua yeye Allah Subhanah Wa Ta'ala ni Mwenye Kujisimamia kila Kitu juu
yake, ambapo sifa hii hua inaenda Sambamba na sifa ya Al Ghaniyuu.
250
Yaani ni Tajiri mwenye kila kitu na asiehitaji kitu chochote kutoka kwa yeyote, ambapo
hapo hapo katika kua na Utajiri wake huo basi kwake yeye hakipungui kitu chochote
katika Kutoa kwake kwa ajili ya kuwapa Viumbe wake. Hivyo kwa upande mwengine
hii hua ni sawa na hali ya Sifa Al Qayyum kwani katika Kusimamia kwake juu ya viumbe
wake basi hua ni mwenye Kusimamia kwa Ukamilifu kila kitu alichokiumba tangu
kuanzia kabla ya kuwepo kwake kitu hicho mpaka kutokea kwake na pia baada ya
kutoweka kwake kitu hicho Hapa Duniani na kesho Akhera pia.
Na hii yote ni kwa sababu ya hii sifa ya Al Hayyu yaani Mwenye Kuishi Milele. Hivyo
Kwa Kuangalia kwa juu juu maana ya Sifa za Majina Matukufu haya mawili tu, ya hii
Ayat Al Qur'siy basi hua tunaona wazi kua, Allah Subhanah wa Ta'ala anaweza wa
Kumsimamia Kila Kiumbe wake katika Kila kitu chake na katika sehemu na mazingira
yake na katika kuwepo kwake kiumbe huyo.
Kwani kila Mtu mwenye Kuamini basi anajua kua, unapokua Unasali Basi hua
umesimama Mbele ya Allah Subhanah wa Ta'ala. Ambapo kutokana na Sifa ya Al Hayyu
Al Qayyum yaani ya Kua na Uhai wa Milele na kua ni Mwenye Kusimamia kila kitu basi
Allah Subhanah wa Ta'ala hua mbele ya kila Mtu na anamsimamia na kumuangalia
katika Sala yake yote iwe Mtu huyo Anasali Chumbani kwake, Ukumbini kwake,
Msikitini, Jela, kwenye Ndege, kwenye Boti n.k
Na hii ni kwa Kila Mtu na ni kwa kila wakati na kwa sehemu Duniani na Mbinguni kwa
upande wa kila Malaika. Hivyo Basi hii haimaanishi kua Kama Mtu anafanya Ibada
Nyumbani kwake basi hua hayuko Mbele ya Mola wake na hivyo pia hua hayuko mbele
ya Usimamizi wake
Hivyo hali hii huwepo pia pale tunapozungumzia kuhusiana na Funga ya Arafah, Usiku
wa Laylat al Qadr, Ramadhan, Idd, Ashura, n.k basi haimaanishi kua kwa sababu ya
kutokea matukio hayo Mtukufu katika Muda ambao ni tofauti na wakati ni tofauti na siku
ni tofauti kutokana na utofauti wa Muandamo wa Mwezi ambao umesababishwa
kutokana na Hikma zake Allah Subhanah wa Ta'ala ambae ni mwingi wa Hikma kua
isiwezekane kwa Mtu kulipwa Malipo ya Ibada alizofanya katika Siku husika na Mahala
husika kulingana na Mazingira yake husika.
Kwa Sababu asiekua na Uwezo wa Kusimamia Hali hio hua Ni Kiumbe, lakini si
Muumba wa Kila ambae ni Allah Subhanah wa Ta'ala ambae yuko mbali Sana tena Sana,
tena Sana na Sifa za Viumbe wake, kwani yeye Allah Subhanah wa Ta'ala ni mwenye
uwezo wa Kusimamia kila kitu kwa Ukamilifu na kwa Uadilifu katika kila wakati na kila
sehemu kulingana na Maumbile ya Ulimwengu na kila kitu kilichomo ndani yake ambae
yeye ndie alieviumba na kuviumbia mazingira yake husika kutokana na Hikma zake
kulingana na Maslahi ya Viumbe wake.
251
Hivyo kutokana na Sifa zake mbili hizi tu, Tukufu basi Allah Subhanah wa Ta'ala anao
uwezo wa Kusimamia Kikamilifu na Kiuadilifu kila kitu cha Viumbe wake katika kila
sehemu kulingana na wakati wake Viumbe hao na kulingana na Mazingira yao viumbe
hao Ardhini na Mbinguni.
Na Ndani yake Usimamizi huo, ikiwemo pia Ibada husika za Waja wake kulingana na
wakati wao na sehemu zao, hivyo hii haimaanishi kua aliefanya Ibada husika
inayotegemeana na nyakati za Muandamo wa Mwezi kwa kufuata Muandamo wa sehemu
aliyokuwepo kua hayuko sahih na atakosa Malipo sahih kutokana na kua ametofautiana
na waliofanya Ibada husika wa Saudia labda tukuchukulie mfano kwa waliokesha kwa
kufuata nyakati za Usiku wa Laylat Ul Qadr au kwa Mahujaj waliokuwepo kwenye Siku
ya Arafah na hivyo kua ni wenye kuangaliwa kwa Jicho la Rehma na Allah Subhnah wa
Ta’ala kutokana na sehemu na mazingira yao hapo kabla ya kufunga yeye jana yake.
La, Kwani kutokana na kua Allah Subhanah wa Ta'ala ni mwenye sifa ya Al Hayyu Al
Qayyum, basi bila ya shaka kwa Hikma zake na Uadilifu wake huwaangalia pia kwa jicho
la Rehma wale waliokesha au waliofunga siku ya pili yake kulingana na Wakati wao na
hali Mazingira yao kua ni yenye kutofautiana na mazingia ya sehemu nyengine kiasi ya
kua kwao wao haiwezekani iwe siku hio ndio siku ya Arafa, au Laylat al Qadr kwani
haya yanayotokana na Hikma zake katika Kuumba kwake na Kukadiria kwake kwa
Rehma zake, Maslahi na manufaa ya Viumbe wake.
Hivyo Siku husika au tukio husika iwe la Funga ya Arafa, Laylat ul Qadir n.k hua ni
Moja Mbele ya Allah Subhanah wa Ta'ala tu, na hii ni kutokana na kua yeye ni Al Hayyu
al Qayyum
Lakini kwa upande wa Viumbe hutofautiana na hii ni kulingana na Mazingira yao na
Maumbile yao hapa Ulimwenguni, kwani viumbe hua wana mipaka ya kisehemu na ya
kinyakati katika kuishi kwao ambayo hua hawawezi kuivuka kutokana na maumbile yao
na Maumbile ya Ulimwengu wao, kwa namna walivyoumbiwa na Mola wao ambae ni Al
Hayyu al Qayyum.
Ambae anao uwezo pia wa kuwajaalia viumbe wake hao kua wote wawe na Usiku mmoja
na Mchana mmoja na Muandamo mmoja Ulimwengu mzima lakini hakufanya hivyo
kutokana na Hikma zake na pia kulingana na Maslahi ya Viumbe wake ndani ya
Ulimwengu wake.
Hivyo kwa wasiojua na kutofaham haya kutokana na udogo wa ufaham wao na kutotaka
kujua zaidi kwao basi wao huona kua kufnya kwao hivyo wafanyavyo kua ni wenye
kutafuta Suluhisho la kutaka Umoja wa Uislam wa Kidunia tena kwa kuanzia na
kuwatimizia haki zao wale Waislam ambao wako mbali nao kimasafa kwanza, badala ya
kuanza kulitafuta suluhisho hilo kwa kuanzia Majumbani mwao kwenye familia zao,
252
kisha kwa majirani zao, kisha katika mitaa yao, kisha katika miji yao, na kisha ndio
unawatafuta wale wa kuwatekelezea haki zao wa Kimataifa.
Kwani hivi ndivyo ambavyo alivyoamrisha Allah Subhanah wa Ta’ala pale alipoweka
mpangilio maalum wenye kusimamia malengo ya kuboresha maslahi ya Umoja wa
Kiislam kwa utekelezaji wa haki za wanaostahiki upewa kipaumbele kwanza katika
kufanyiwa wema na ukarimu kama alivyoanisha katika aya ifuatayo:
﴿وَٱعْبُدُواْ ٱهلل ََّ وَلاَ تُشْرِكُواْ بِهِ شَيْئاً وَبِٱلْوَالِدَيْنِ إِحْسَاً وَبِذِى ٱلْقُرْبىَٰ وَٱلْيَتَامَ ٰ ى
وَٱلْمَسَاكِينِ وَٱلجَْارِ ذِى ٱلْقُرْبىَٰ وَٱلجَْارِ ٱلجُْنُبِ
َوٱبْنِ ٱلس َّبِيِل
وَٱلص َّاحِ بِ بِٱلجَنْبِ
وَمَا مَلَكَتْ أَيمَْانُكُمْ إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يحُِب ُّ مَن كَانَ مخُْتَالاً فَخُوراً ﴾
WaoAAbudoo Allaha wala tushrikoo bihi shay-an wabialwalidayni ihsanan
wabidhee alqurba waalyatama waalmasakeeni waaljari dhee alqurba waaljari
aljunubi waalssahibi bialjanbi waibni alssabeeli wama malakat aymanukum inna
Allaha la yuhibbu man kana mukhtalan fakhooran (Surat An Nisaa 4:36)
Tafsir: Na muabudu Allah na wala usimshirikishe, na wafanyie wema Wazazi wako,
na Ndugu zako, na Mayatima na Masikini, na Jirani yako wa Karibu kiudugu na jirani
yako wa Mbali, na Rafiki yako wa Karibu, na Msafiri na Mtumwa wanaomilikiwa na
Mikono yenu. Kwani kwa hakika Allah hawapendi wenye kujiona na kua na Ufakhari.
Ambao aya hii kwanza Allah Subhanah wa Ta’ala ameanza kwa kuainisha kua haki ya
kwanza ya kusimamiwa ni ya Allah Subhanah wa Ta’ala, kisha inakuja haki ya Wazee
kisha ndugu zako ndani ya familia yako na kisha, kisha haki ya Mayatima na kisha ya
Masikini, na kisha haki ya Majirani wa karibu na wa mbali na wasafiri na watumwa.
Hivyo inakuaje Mtu unajiita Muislam halafu katika wakati wa kutekeleza haki ya Allah
Subhanh wa Ta’ala kwa mfano ya Kufunga mwezi wa Ramadhani basi wewe baada ya
kufuata mpangilio wa aya hii kwa kuanza kutekeleza haki ya Wazee wako na Ndugu
zako, na Mjirani zako basi wewe unaanza moja kwa moja na kutekeleza haki ya watu
mbao uko nao kwa umbali wa maelfu ya kilomita?
Kisha mtu unakula mwezi wa Ramadhani na kujigamba na kujiona na kujisifu kua wewe
huwezi kufuata Muandamo wa mwezi wa eneo ulilokuwepo pamoja watu wa jamii yako
ambao unaosali nao Sala tano pamoja na hivyo kushindwa kujumuika nao katika kufunga
au kufungua na kujumuika katika kusheherekea sikukuu moja ya Kiislam kwani lazima
usheherekee kivyako na kisha hua unaona fakhari kufanya hivyo.
253
Wakati hapo hapo aya hii imemalizia kwa kusema: ‘Innah Allaha la yuhibbu man kana
mukhtalan fakhooran’ yaani Kwani kwa hakika Allah hawapendi wenye kujiona na
kua na Ufakhari.
Inasikitisha kua watu hawa kwa ujinga wao basi hawajui kua katika kufanya kwao hivyo,
yaani kufuata Muandamo wa mwezi wa sehemu tofauti na jamii yao huku wakiwa
wanaona fakhari basi, kwa upande mmoja hua ni wenye kukosa Subra, kuwavunjia haki
zao watu wao katika jamii yao na kwa upande wa pili hua ni wenye kusababisha
kuvunjka kwa umoja wa Kiislam katika jamii husika ambapo hili hua ni jambo ambalo
hua ni lenye kufanywa na wale watu wenye sifa zenye malengo ya Unafiq ambayo ni
kuuvunja nguvu Uislam, na hivyo wewe kua ni mwenye kuyatekeleza malengo hayo na
kukupeleka kua ni miongoni mwa Wanafiq.
Na ndio maana aliusia Harith Al Muhasibi kwa kusema kua: ‘Ni hasara kwetu kama
ikiwa tutapoteza vitu vitatu ambavyo ni Muonekano Mzuri wa Sura zetu
unaojumuisha kua na heshima, Kauli nzuri zinazojumuisha na Uaminifu na Umoja
wa Kindugu wenye Nguvu Unaojumuisha Kutosalitiana’
Na tumeona mara kadhaa kua baada ya Allah Subhanah wa Ta’ala kuhimiza usimamiwaji
wa haki zake basi hua ni sambamba mwenye kusisistiza kusimamiwa kwa haki za wazee,
na pia kuna aya hadithi kadhaa zinazohimiza usimamiaji wa haki ndugu, Mke, Mume,
Watoto na familia wa ujumla na pia ziko zinazozungumzia haki za majirani zako ambapo
miongoni mwao ni pamoja na zile ambazo zinasema:
Amasema Salman Ibn Amr Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Kutumia kwa ajili ya Maskini hua ni Sadaqa, lakini kutumia
kwa ajili ya Masikini ambae ni wa karibu yako hua ni sadaka ya mara mbili zaid,
ambapo Sadaka ya aina ya kwanza hua ni kwa kutokana na kuunganisha udugu na
Sadaqa ya pili hua ni kutokana na kile ulichokituma ambacho ni sadaqa ya kawaida
(Imam At Tirmidhii)
Ama kuhusiana na haki ya Jirani basi Amesema Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam
kua: ‘Migogoro ya kwanza itakayo hukumiwa katika siku ya Malipo basi ni ile
migogoro ya haki baina ya Mtu na Jirani yake.’ ambapo Ummu ul Muuminin Aisha
Radhi Allahu Anha alimuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam: ‘Ya Rasul Allah!
Wakati mimi nnao Majirani wawili, jee ni Jirani yupi anaestahiki kupewa zawadi?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Yule Jirani ambae uko karibu nae
zaidi.’(Sahih Muslim)
Na amesema Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Jibril aliendelea kuniusia mimi kuhusiana na kua
254
na uhusiano mzuri na Jirani hadi nikafikiria kua mwishowe huenda
akawajumuisha katika mirathi’(Sahih Bukhari)’
Ambapo anasema Miqdad Ibn Aswad Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam aliwauliza Masahaba zake kwa kusema: ‘Hivi mnafikiriaje
kuhusiana na Zinaa’ Ambapo Masahaba wakasema: ‘Bila ya shaka ni Dhambi
iliyokatazwa na Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume wake Salallahu Alayhi wa
Salam na itakayobakia kua hivyo hadi katika Siku ya Malipo’ Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akasema: ‘Basi ni bora kwa Mtu awe ni mwenye Kuzini na
wanawake 10 kuliko kuzini na mke wa jirani yake’
Kisha akawauliza tena Masahaba zake: ‘Jee mnafikiriaje kuhusiana na Wizi?’’
Masahaba wakasema ; ‘Bila ya shaka ni Dhambi iliyokatazwa na Allah Subhanah
wa Ta’ala na Mtume wake Salallahu Alayhi wa Salam na itakayobakia kua hivyo
hadi katika Siku ya Malipo’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Basi ni
bora kwa Mtu kuiba kwenye nyumba 10 kuliko kuiba kwenye Nyumba ya Jirani
yake’(Imam Ahmad)
Na ukweli ni kua Mfano wa Unafiq wa aina kama hii uko katika hali nyingi sana ambazo
wasiojua hua hawazioni na hata wakivishwa Miwani basi bado Mtu atakua haoni kwa
sababu Allah Subhanah wa Ta'ala tayari ameshaweka wazi kama tulivyoona kwenye aya
tulizoziangalia
Kwani wengi wetu hua wanadhani kua Unafiq hua ni ule ulioainishwa kwenye Hadith ya
Abd Allah Ibn Amr Radhi Allahu Anhu ambayo inasema: ‘Sifa nne akiwa nazo mtu
basi Mtu huyo hua ni Mnafiq, na yeyote yule atakae kua nayo japo moja kati ya
hizo basi hua na maumbile ya Unafiq hado atakapochana nayo ambazo ni:
Akiaminiwa basi husaliti, Akisema basi hudanganya, Akitoa ahadi hua hatekelezi
na Akipigana au Kugombana basi huvuka mipaka.’(Sahi Bukhari)
Lakini unafiq hua uko katika aina mbili ambazo ni Unafiq wa Maneno na Vitendo na
Unafiq wa Imani, ambapo ingawa Unafiq wa Amali na maneno hua haumtoi mtu kutoka
kwenye Imani ya Dini ya Kiislam lakini maneno na vitendo vyake vinapozidi kua na
Unafiq basi wingi wake huo huweza kumpelekea Mtu kuingia kwenye Unafiq wa Imani
na hivyo kumungamiza mtu husika.
Kwani Ubaya wa Unafiq na Madhara yake yanapokosa Tiba kutokana na Mnafiq kuona
kua yeye yuko Sahih basi hua ni Mwenye kusababisha Madhara Makubwa zaid kwa
Kuambukiza Maradhi hayo mpaka kwenye Kizazi chake na hivyo kupelekea
kuidhoofisha na kuiharibu kwa kuidhuru Jamii husika ya Kiislam.
255
Na kwa kua Watu hawa hua ni waliomo ndani ya Jamii husika ya Kiislam basi ni wale
wenye Ilm na kujua tu ndio wanaowajua kua hawa ni Wanafiq. Kwani hata Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alisema: Tahadharini na Moyo wa Muumini Mwenye
Kujua. Naam..bila ya Shaka Kwani wenye kujua hua ni wenye Kuona kwa Jicho la
Mtizamo wa Moyo!
Na ndio maana ingawa mimi si mwenye kujua lakini hua Namuomba Allah
Subhanah wa Ta'ala Aniepushe na Ujinga wa Kutojua zaidi na pia na ujinga wa
kutofuata wenye kujua na hivyo kua ni mwenye kufuata wasiojua badala yake. Kwa
sababu hakuna ujinga Mkubwa zaidi kuliko kua na Ujinga wa kutojua na kisha
hapo hapo ukawa pia ni mwenye kufuata wale Wajinga Wasiojua na kisha pia kua
Hujui kua unawaofuata ni wale Wajinga wasiojua.
Kwani unapokua katika hali kama hii halafu ukawa unajiita kua ni Muislam basi hali
yako inakua kama vile alivyosema Allah Subhanah wa Ta'ala katika aya zenye
Kumithilisha ambazo zinasema;
﴿مَثَلُهُمْ كَمَثَلِ ٱل َّذِى ٱسْتَوْقَدَ َراً فَلَم َّآ أَضَاءَتْ مَا حَوْلَهُ ذَهَبَ ٱهلل َُّ بِنُورِهِمْ
وَتَرَكَهُمْ فىِ ظُلُمَاتٍ لا َّ يُبْصِرُونَ۞صُم ٌّ بُكْمٌ عُمْيٌ فَهُمْ لاَ يَرْجِ عُونَ ﴾
Mathaluhum kamathali alladhee istawqada naran falamma adhaat ma
hawlahu dhahaba Allahu binoorihim watarakahum fee dhulumatin la yubsiroona;
Summun bukmun AAumyun fahum la yarjiAAoona(Surat Al Baqara 2:17-18)
Tafsir: Mithili yao Watu hao ni Kama Mithali ya Wale Ambao waliowasha Moto (Ili
wapate Muangaza wa kuona njia) Na Kisha Moto Unapowaka kuwaangazia Basi
Anaichukua Allah Nuru yao Na Kisha Huwawacha Kwenye Giza Na Huku wakiwa Si
wenye Kuona (Hivyo watu jao hua) Ni Viziwi, Mabubu na Vipofu Wala Hawarudi
(kwenye Njia iliyokua Sahih)
Nadhani aya ziko wazi kua hali ya Wanafiq hua ni wenye Kujiona kua wako sahih katika
Mambo yao na husema kua Wanajenga Uislam kumbe hua wanauvunja badala yake na
wanapoambiwa kua Wanafuata wasiojua basi hali yao hua ni:
Summun - Viziwi - Yaani Hua Wabishi hawakusikii wala hawakusikilizi hata
uwasomeshe vipi.
256
Bukmun - Mabubu Yaani Watapigwa na Mshangao na kukushangaa wewe Badala
yake kama vile anavyokua Bubu ambae hawezi kusoma Midomo yako unaposema
na Wala hawezi kusoma Alama za Vitendo vyako hivyo hakujibu kua amekubali
kua Kakosea.
Aumyun - Vipofu Yaani Hawaoni Ukweli wa Unayowaonesha.
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala pia anawaelezea katika aya isemayo:
﴿وَإِذَا رَأَيْتَهُمْ تُعْجِ بُكَ أَجْسَامُهُمْ وَإِن يَقُولُواْ تَسْمَعْ لِقَوْلهِِمْ كَأَن َّهُمْ خُشُبٌ
م ُّسَن َّدَةٌ يحَْسَبُونَ كُل َّ صَيْحَةٍ عَلَيْهِمْ هُمُ ٱلْعَدُو ُّ فَٱحْذَرْهُمْ قَاتَلَ هُ مُ ٱهلل َُّ أَ َّنى
﴾
يُؤْفَكُونَ
Wa-idha raaytahum tuAAjibuka ajsamuhum wa-in yaqooloo tasmaAA liqawlihim
kaannahum khushubun musannadatun yahsaboona kulla sayhatin AAalayhim
humu alAAaduwwu faihdharhum qatalahumu Allahu anna yu/fakoona (Surat Al
Munafiqun 63:4)
Tafsir: Na kama ukiwaangalia basi miili yao inakuvutia, na wanapozungumza basi
utasikiliza maneno yao, wao ni kama mapande ya Mbao yaliyoenegemzwa ukutani,
wanadhani kua kila kilio ni dhidi yao. Wao ndio Maadui hivyo tahadhari nao, Laana
ya Allah juu yao, wamepotea sana.
Naam kwani Wanafiq hua hawana ufaham, wanavutia kimuonekano, na kimaneno lakini
kiakili hua hawana maana yeyote kama mbao ambazo zimeegemezwa ukutani zikiwa
zinaharibika
Kwani hio ni kwa juu juu tu kuhusiana na Madhara ya Unafiq wa Wanafiq Dhidi ya
Uislam Waislam, Unafiq wa Wanafiq dhidi ya Waislam Wenzao, katika kuvunja Umoja
wa Waislam, Kuwakandamiza Waislam, Kuwadhulumu Waislam n.k
Kwani Amesema tena Hasan Al Basr kua: ‘Muislam hubakia kua ni Muislam pale
anapokua anajiusia Nafsi yake na kuendelea kujichunga kwa kujihesabia Kasoro
zilizomo ndani ya Nafsi yake’
Na akasema Imam Yusuf Ibn Asbati kua: ‘Unyenyekevu Ni kumuona na Kumfikiria
Ibn Adam mwenzako kua ni mbora zaidi yako mbele ya Mola wako’
257
SURAT AL MAA’UN – UMUHIMU WA KUJALI MAYATIMA,
MASIKINI NA SALA KATIKA DINI YA KIISLAM.
Allah Subhanah wa Taa’la anatuambia kuhusiana na yule Mtu asiefanya vile alivyofanya
Nabii Zakarriyah pamoja na Makuhani wenzake katika kukimbilia kuchukua majukumu
ya ulezi wa Mtoto Yatima basi hua ni sawa na wale wenye kukadhibisha siku ya Malipo
ambapo ndani yake kuna Makafiri na pia kuna wanaojiita kua ni Waislam lakini
hawatekelezi majukumu yao Kiislam, na hivyo kua ni hua ni wenye sifa za Unafiq.
Na ili kuangalia hayo na kuweza kuyafaham vizuri basi moja kwa moja na tuingie
kwenye Surat Al Maaun ambayo ni Moja kati ya Sura ndogo miongoni mwa Sura ndogo
za Qur'an, kwani ina aya 8 tu, tukiijumuisha ndani yake na Biismi Allahi Rahmani Rahim.
Hivyo kama tunavyoiona Udogo wake lakini hii ni Sura ambayo ina Ujumbe Mzito sana
ndani yake. Kwani ni Sura ambayo inazungumzia Sifa za wale ambao ni Wenye
Kuikanusha Dini ya Kiislam. Ambapo kwanza inabidi tujue kua tunapozungumzia
kuhusiana na hali ya Kukadhibisha na Kukikubali kitu basi hua ni hali mbili tofauti
zinazopingana kimaana.
Ambapo hali ya kwanza hua ni hali ya Kukikubali Kitu, na hii hua ni hali ya Kuthibitisha
Hali ya kitu, iwe katika kuwepo kwake au katika kuonekana kwake kua kitu hicho kweli
kipo na kama kina manufaa ama la. Na mara nyingi ili kitu kikubalike basi hubidi
kionekane Uzuri wake au Manufaa yake.
Ambapo kukithibitisha kitu hua ni kazi rahisi sana kuliko kazi ya Kukadhibisha kitu
ambayo ndio hali ya pili yenye maana ya Kutokikubali kitu, na hivyo hua ni hali ya
kinyume ya hali ya kwanza ya Kukikubali kitu. Ama tunapozungumzia Ugumu wa
Kukikadhibisha Kitu basi mara nyingi hua ni kazi kubwa zaid, kwani ili ukikadhibishe
kitu basi hukubidi kwanza uthibitishe hicho kitu kama kipo au hakipo.
Na baada ya kuthibitisha kua kipo basi inabidi utafute kasoro zake, na ili ujue kasoro ya
kitu basi inakubidi Uingie ndani ya hicho kitu ukifaham ndani nje kisha ndio unaweza
ukakitoa kasoro zake kulingana na Ufaham wako. Ambapo hapo hapo ndani ya kitu
husika basi wewe unaetafuta kasoro basi huenda ukagundua kasoro kulingana na
Mtizamo wako, lakini kumbe kulingana na Mtizamo wa aliekitengeneza kitu hicho basi
hio unayoiona wewe kua ni kasoro juu ya kitu hicho, basi hua ndio Ubora wa kitu hicho
ambao huwezi kuujua mpaka akufafanulie yule aliekitengeneza kitu hicho, kisha na
wewe uwe tayari kukubaliana na Mtizamo wake.
258
Hivyo tunapoiangalia Surat Al Maaun basi tunaona kua Allah Subhanah wa Ta'ala ambae
ndie alieanzisha Dini ya Uislam ambayo ni Njia ya Mfumo wa Maisha ambayo inatakiwa
kufuatwa na Viumbe wa Allah Subhanah wa Ta'ala katika kuishi kwao hapa
Ulimwenguni kwa ajili ya manufaa yao hapa Duniani na Akhera na kwa manufaa ya
Viumbe wengine hapa Ulimwenguni. Basi tunaona Kua Allah Subhanah wa Ta'ala
Anautetea Mfumo wake huo aliouweka kwa ajili ya Viumbe wake hapa Duniani kua ni
Mfumo bora ambao hautakiwi kukadhibishwa.
Na hivyo basi Mfumo huo ambao ni wa Njia ya Maisha ya Kiislam hua hauwezi
kukadhibishwa isipokua na Watu wa Aina Mbili.
Ambapo wa kwanza ni Makafiri yaani wanaomkadhibisha kabisa Allah Subhanah wa
Ta'ala na kisha wa pili ni Wanafiq Ambao wao ni wenye Kuwadanganya Ibn Adam
wenzao na pia Kuzidanganya Nafsi zao kua Wameamini lakini kumbe ni wenye
Kukadhibisha Kutoka ndani ya Imani ya Dini ya Kiislam.
Kwani Surat Al Maun inaweka wazi Ubaya wa Wanafiq kwa kuwanasibisha na wale
ambao ni wenye Kuikadhibisha/Kuipinga Dini ya Allah Subhanah wa Ta'ala, na Ubaya
zaidi ni kua Ukabidhishaji huo unatoka Ndani ya Nafsi za Wafuasi wa Dini ya Kiislam.
kama zilivyobainisha aya zifuatazo zilizobainisha sifa 6 za wale wenye kukadhibisha
Dini na Siku ya Malipo ambapo sifa 2 kati yake ni za wale wasiowajali Mayatima na
Maskini, na sifa 4 zilizobakia ni za Waislam wa Kuchovya ambapo aya zinasema:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞أَرَأَيْتَ ٱل َّذِى يُكَ ذِّبُ بِٱلدِّينِ۞فَ ذٰ لِكَ ٱل َّذِى يَدُع ُّ
ٱ لْيَتِي مَ ۞وَلاَ يحَُض ُّ ٰ عَلَى طَعَامِ ف ٱلْمِسْكِينِ۞ َوَيْلٌ لِّلْمُ صَلِّ ينَ ۞ ٱل َّذِينَ هُمْ عَن
صَلاَهتِِمْ سَ اهُونَ۞ ٱل َّذِينَ هُمْ يُرَآءُونَ ۞ وَيمَْنَعُونَ ٱلْمَاعُونَ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Araayta alladhee yukadhdhibu bialddeeni;
Fadhalika alladhee yaduAAAAu alyateema; Wala yahudhdhu AAala taAAami
almiskeeni; Fawaylun lilmusalleena; Alladheena hum AAan salatihim sahoona;
Alladheena hum yuraoona; WayamnaAAoona almaAAoona (Surat Al Maun 107:1-
7)
Tafsir: Kwa Jina La Allah Mwingi wa Rehma Mwingi wa Huruma, Hivi Jee
Umemuona wewe yule ambae anakadhibisha Dini? Huyu ni yule ambae ni mwenye
kumfukuza Yatima; Na kisha yule ambae hahimizi kulisha Masikini; Na Kisha Ole
Wao wale Wenye Kusali. Wale Ambao juu ya Sala zao Sahuna (Wanazidharau na
259
kuzichelewesha kwa kutosali katika wakati wake). Wale wenye kufanya Mema ili
waonekane, na Wenye kukataa Maaun (Kutoa japo kitu kidogo).
Tunapoiangalia aya ya kwanza ya Sura hii basi tunaona kua iko katika hali ya kuhoji kwa
kutumia neno Araayta ambalo ni lenye kutokana na neno Raa ambalo hua ni lenye
kumaanisha Kuona, Kufikiria, Kua na Mtizamo au Kudhania.
Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala ametumia nneno Araayta hapa wa ajili ya kututaka
tuwe makini na kile anachotaka kutuonesha au kutubainishia kwenye aya zinazofuatia
baada ya hio, ambapo mwishoni mwa aya hii basi Allah Subhanah wa Ta’ala anatuwekea
wazi kua hilo jambo analotaka kutubanishia basi lina madhara makubwa sana ambayo
yanaweza kumpelekea Mtu kupoteza Imani yake.
Ili kufaham uzito wa kauli hii basi na tuchukulie mfano wa kua Kuna watu wamekaa
chini ya Mti halafu akaja mtu na kuja kusimama kwa mbali kidogo mbele yao, kisha mtu
huyo ambae anaona kila kitu chao watu hao basi akawaambia: ‘Hivi jee mmemuona
huyo Nyoka hapo alie juu yenu?’
Hivyo jee hali itakuaje kwa watu waliokuwepo chini ya Mti huo? Naam..hivyo hali hii
basi inatuonesha namna hali inavyotakiwa iwe kwa kila Muumini mwenye kuoneshwa
na kutakiwa kuyaangalia na kukaa mbali nayo yale ambayo yanayotakiwa kujihadhari
nayo na aya hii.
Halafu pia imetuma Neno Dana ambao kwa Lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Dini,
Kukubali Imani ya Dini, Kuamini Iman ya Dini, Kutumikia, Kuhukumu au Kuhudumia.
Neno Dana pia hua ni Jina la Mtoto wa Kike ambalo hua linamaanisha Lulu Kubwa Sana.
Ambapo neno Dana pia limetoa neno Dayn ambalo hua linamaanisha Deni au Mkopo.
Na pia neno Dana ndio lililotoa Neno Dinun ambalo humaanisha Malpo, Mamlaka,
Usimamizi, Shariah, Hukumu ya Kidini, Ushindi na pia hua linamaanisha Utiifu.
Hivyo tunapoiangalia maana ya neno Dana kimatumizi basi hua inategemea na sehemu
na sehemu kwa mfano katika ile hadith isemayo:
Alisema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Al Dinu Nasihat’ yaani Dini ni
Nasiha au kunasihiana. Hivyo Masahaba wakamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salaam : ‘Juu ya nini?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Juu ya Allah
Subhanah wa Ta’ala, na Kitabu chake na Mtume wake na juu ya viongozi wa Dini
ya Kiislam na Juu ya Waislam wa Kawaida.’ (Sahih Muslim)
260
Na neno Dana pia hutumika katika Kumaanisha Kitendo Chochote Kile iwe Kizuri au
Kibaya. Na hii ndio maana iliyotumika kwenye ile Hadith ambayo ni Mursal, yaani
Hadith ambayo imenukuliwa na Tabiina kutoka kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam bila ya kupitia kwa Sahaba ambayo inasema kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua Wema hauharibiki, Dhambi haisahauliki, Deni halifi
hivyo kua kama utakavyo kwani Kama Tadiinu Tudan’ ambapo maneno Kama
Tadiinu Tudani hua yanamaanisha kua Kama utakavyofanya basi nawe ndivyo
utakavyofanyiwa.
Hivyo ingawa wengi miongoni mwa Wafasiri hapa hua wanatafsiri kwa kusema kua:
Araayta alladhee yukadhdhibu bialddeeni hua inamanisha Hivi jee umemuona yule
ambae ni mwenye kuikadhibisha Siku ya Malipo?
Lakini pia kwa kua Neno Al Diin lililotumika hapa linatokana na neno Dana ambalo
maana yake ni kama tulivyoifafanua hapo awali tunapozungumzia Mtu anaeikadhibisha
Dini ya Kiislam hua pia ni mwenye kukadhibisha Siku ya Malipo, na anaekadhibisha
siku ya Malipo basi hua pia ni mwenye Kuikadhibisha Imani ya Dini ya Kiislam
Hivyo basi kimaana tafsiri hizi mbili hua zimetokana na neno moja na hivyo pia
zinaendana sambamba kimaana ambapo kwa upande wa wengi sana waliotafsiri neno Al
Diin katika aya hii kua Ni siku ya Malipo basi wao wamechukua Mtizamo wa Bahr Ul
Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu.
Na sio kama mimi sikubaliani na tafsiri hio, La. Bali nimetafsiri hivyo kama
walivyotafsiri wengine wachache kwa sababu hua napenda Watu wajue na Mitizamo
tofauti. Kwani alisema Imam Abu Hanifa kua Mwenye kujua Mitizamo tofauti na sababu
zake basi ndie mwenye kujua vizuri zaid.
Naam..hivyo tunapoangalia aya yetu hii ya kwanza ya Surat Al Maaun basi tunaona kua
hapa Allah Subhana wa Ta'ala anamwambia Mtume wake Salallahu Alayhi wa Salam.
Na hapo hapo anatuambia sisi Waislam mimi na wewe Ili tupate kutafakkar kuhusiana
na jambo tunalouliziwa na Mola wetu ambalo ni:
Araayta alladhee yukadhdhibu bialddeeni; - Hivi Jee Unamjua yule ambae Ndie
anaekadhibisha Dini (Ya Kiislam au Kuwepo kwa Siku ya Malipo)?
Bila ya shaka hili si suali dogo, bali ni suali kubwa na zito sana na hivyo basi Allah
Subhanah wa Ta'ala anatutanabahisha Umuhimu wa kutafakkari Suali hili na hivyo
kututaka kua tunaposikia maneno yake haya basi tunatakiwa tuache kila kitu
tunachofanya na kuondoa kila kitu katika Ufaham wetu, ili tupate kujua ni nani hao
wenye Sifa ambayo ni yenye kuenda Kinyume na Maamrisho yake ambayo ndio Nguzo
ya Imani ya Dini ya Kiislam.
261
Na hapo hapo kututaka sisi mimi na wewe Kukaa mbali na wenye Sifa hizo zenye
kuangamiza ikiwemo ile ya kutowajali Mayatima na Masikini ambazo tumeshaziangalia
hapo kabla na ndio sababu ya kuitafsiri Surah hii ya Al Maun,
Hivyo miongoni mwa Watu wanaokadhibisha Dini na Siku ya Malipo basi ni wale wenye
Kuwafukuza na kutowajali Mayatima na Masikini kama zilivyosema aya:
﴿فَذٰ لِ كَ ٱل َّذِى يَدُع ُّ ٱلْيَتِيمَ ﴾
Fadhalika alladhee yaduAAAAu alyateema; (Surat Al Maun 107:2)
Tafsir: Huyu ni yule ambae ni mwenye kumfukuza Yatima;
Ambapo tunaona kua aya hii imetumia neno Da’Aa ambalo hua linamaanisha Kusukuma.
Kufukuza, Kutumia Nguvu katika kupingana na Kitu. Allah Subhanah wa Ta’ala
ameitumia tena neno hili pale aliposema katika ya zifuatazo:
ف َوَيْ ي لٌ َوْمَئِذٍلِّلْمُ كَ ذِّبِ ينَ ۞ٱل َّذِينَ هُمْ فىِ خَوْضٍ يَلْعَبُونَ۞يَ وْمَ يُدَع ُّونَ إِلىَٰ َرِ
جَ هَ ن َّمَ دَ عًّا﴾
﴿
Fawaylun yawma-idhin lilmukadhdhibeena; Alladheena hum fee khawdhin
yalAAaboona; Yawma yudaAAAAoona ila nari jahannama daAAAAan(Surat At
Tur 52:11-13)
Tafsir: Ole wao katika Siku hio wale wanaokadhibisha; Ambao wanajiingiza kwenye
kucheza mambo ya Kiupuuzi. Hio ni siku ambayo watakaposukumwa kwa nguvu
kwenye Moto kwa Msukumo mbaya sana.
Hivyo hili ni neno tofauti kimaana na lile neno Da’a ambao hua linamaanisha Dua, Kuita,
Kuomba, Kukaribisha, Kusali, Kuomba Dua, Kulia kwa ajili ya Kutaka kitu, kama vile
lilivyotumika katika aya ifuatayo:
﴿وَقَالَ رَب ُّكُمْ ٱدْعُونيِ ۤ أَسْتَجِ بْ لَكُمْ إِن َّ ٱل َّذِينَ يَسْتَكْبرُِونَ عَنْ عِبَادَتِى
سَيَدْخُلُونَ جَهَن َّمَ دَاخِ رِينَ ﴾
262
Waqala rabbukumu odAAoonee astajib lakum inna alladheena yastakbiroona
AAan AAibadatee sayadkhuloona jahannama dakhireena (Surat Ghafir 40:60)
Tafsir: Na amesema Mola wenu: ‘Niombeni Nitakujibuni. Kwani kwa hakika wale
wanaozifanyia Kibri Ibada zangu, wataingia Motoni kwa Muadhirisho.’
Hivyo maneno Fadhalika alladhee yaduAAAAu alyateema basi hua yanamaanisha ‘Huyo
ni yule ambae ni mwenye kumfukuza Yatima’ yaani baada ya kumuita Yatima kwa upole
na kumuonea Huruma basi hua ni mwenye kumfukuza, kutotaka kua karibu nae au kua
na ukaribu nae kutokana na kutomuonea huruma, kwani yeye hua hajali hali ya Mtoto
huyo kua ni mwenye kuhitaji Msaada, Ukarimu, Upendo na Huruma kwani hua ni
mwenye udhaifu kutokana na kua hana wazee kama vile ilivyokua kwa watoto wengine
ambao ni wenye kutetewa haki zao, kusimamiwa mambo yao, kutunzwa na kuhudumiwa
na wazee wao katika kila hitajio lao.
Na kutokana na kua Uislam ni Dini ya Uadilifu, Ukarimu. Upendo, Upole na hivyo kua
ni yenye kusimamia Maslahi ya Viumbe hapa Duniani kulingana Maamrisho na Sharia
za mwenyewe Muumba wa Dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, basi yeyote yule
atakaemfukuza Yatima hua ni mwenye Kukadhibisha Dini.
Kama ilivyosema Aya ya Mwanzo kushuka ambayo inayowazungumzia watu hao kwa
kuwabainishia Allah Subhanah wa Ta’ala anawaona kwani anaangalia na kuona kila kitu
kwa urahisi mkubwa sana na kwa umakini mkubwa sana na kuona kila kitu juu yao,
katika aya zilizotumia neno Rasada ambalo hua linamaanisha Kukaa Kwa Kuangalia kitu
kwa umakini mkubwa sana ndani nje bila ya kukosa kuona chochote juu ya kitu hicho
kinachoangaliwa, na hivyo kua na uwezo wa kukivamia na kukifanya vyovyote kitu
hicho kinachoangaliwa;
Ambapo hizi si aya nyengine bali ni zile ambazo anasema Imam Muqatil Ibn Sulayman
kuhusiana nazo kua: ‘Aya zilishushwa kuzungumzia Khalaf Ibn Ummayah ambae
alikua akimlea Yatima aitwae Qudamah Ibn Maz'un’ pale aya ziliposema:
﴿إِن َّ رَب َّكَ لَبِٱلْمِرْصَادِ۞فَأَم َّا ٱلإِنسَانُ إِذَا مَا ٱبْتَلاَهُ رَب ُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَع َّمَهُ فَيَقُولُ ِ رَبيّ ۤ
أَكْ رَمَنِ۞وَأَم َّآ إِذَا مَا ٱبْتَلاَهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبيّ ِۤ أَهَ انَنِ۞كَلا َّ بَل لا َّ تُكْرِمُونَ
ٱ لْيَتِي مَ﴾
263
Inna rabbaka labialmirsadi; Faamma al-insanu idha ma ibtalahu rabbuhu
faakramahu wanaAAAAamahu fayaqoolu rabbee akramani; Waamma idha ma
ibtalahu faqadara AAalayhi rizqahu fayaqoolu rabbee ahanani; Kalla bal la
tukrimoona alyateema. (Surat Al Fajr 89:14-17)
Tafsir: Kwa hakika Mola wako ni mwenye kuwaangalia kwa uangalifu mkubwa sana,
ama kuhusiana na Mtu pale anapojaribiwa na Mola wake, kwa kumkirimu na
kumneemesha, basi hua ni mwenye kusema: ‘Mola wangu amenikirimu’ Lakini
anapomjaribu kwa kumbania riziki yake, basi hua ni mwenye kusema: ‘Mola wangu
amenidhalilisha’ (Wataambiwa) La Bali Nyinyi Mlikua Hamuwakirimu Mayatima.
Na hivyo aya kua ni zenye Kuonya kuhusiana na Kutowajali Mayatima, kuwavunjia Haki
zao na kuzitumia sivyo Mali zao. Na pia kutowarudishia Mali zao baada ya kufikia Mda
wao wa kurudushiwa Mali hizo.
Ambapo amesema Allah Subhanah wa Ta'ala katika Surat An Nisaa kua:
﴿إِن َّ ٱل َّذِينَ َْكُلُونَ أَمْوَالَ ٱلْيَتَامَى ٰ ظُلْماً إِنم ََّا َْكُلُونَ فىِ بُطُوِِمْ َراً وَسَيَصْلَ وْنَ
سَعِيراً ﴾
Inna alladheena ya/kuloona amwala alyatama dhulman innama ya/kuloona fee
butoonihim naran wasayaslawna saAAeeran (Surat An Nisaa 4:10)
Tafsir: Kwa Hakika Wale ambao wanaokula Mali za Mayatima kwa Dhulma basi kwa
Hakika Wanakula Ndani ya Matumbo yao Moto na Watachomwa kwenye Moto Mkali
Sana.
Kwani tunapoiangalia Aya yetu hii basi tunaona kua ni Miongoni mwa Aya ambazo
zinawazungumzia wale Watu ambao ni wenye Kulea Mayatima na hivyo kua pia ni
Wenye kusimamia Mali walizorithi Mayatima hao kutoka kwa Wazee wao waliofariki.
Ambapo Msimamizi au Mtunzi au Mlezi wa Yatima husika hua pia na Jukumu la
kuisimamia Mali hio ya Mirathi kama vile ambavyo walivyoachiwa kuwasimamia
Mayatima hao. Hivyo basi kama vile ambavyo Uislam unavyoamrisha Kuwasimamia
Mayatima Kiuadilifu basi ndio hivyo hivyo unavyotakiwa usimamizi juu ya Mali zao.
264
Ambapo amesema Abu Said Al Khudri Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wakati Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alipoenda katika Safari ya Miraj basi alikutana na Watu
ambao Wana Midomo Mirefu kama ya Ngamia
Na inaposemwa kua ni Midomo mirefu basi haimaanishwi kua ni Umbo la Mdomo
linalojumuisha na Mifupa Ya Kidevu na Meno yake, La. bali hua inamaanishwa Nyama
Mbili ziliopo kwenye Milango ya Midomo yetu, ambazo umuhimu wake hautokani na
kua n kw ajili ya kunyonyea ziwa la Mama tu tunapokua wadogo lakini pia zina aina
tofauti za umuhimu wa kimaumbile.
Kwani katika Viungo vya Mwili wa Ibn Adam ambavyo ni vyenye Hisia kali sana basi
ni Nyama hizi mbili za Midomo. Kwani Nyama mbili hizi za Midomo ni miongoni mwa
Nyama ambazo laini za Ibn Adam kwa sababu ni Nyama za Ndani ya Mwili zilizoumbwa
na Allah Subhanah wa Ta’ala kua ziwe Nje kwa sababu ya matumizi yake kwa mwili wa
Ibn Adam na pia hapo kua ni pambo la wake, na hivyo zina Viunganishi vya vyanzo vya
hisia Milioni Moja vinavyosafirisha hisia moja kwa Moja kwenye Ubongo.
Na wingi wa Hisia zake unaonekana pale unapompapasa Mtu taratibu katika sehemu hizo
kwa kidole kikavu juu yake, wakati nyama hizo zina ukavu basi mtu huyo lazima
Atajiramba Midomo yake. Kutokana na kua ni viungo vyenye hisia kali sana basi
Midomo pia hua na kazi ya kurekebisha joto la mwili kwa kulipunguza na kulitoa nje au
kulihifadhi zaid pale inapohitajika na ndio maana ikawa unapoona baridi basi mtu hua
unabana midomo yako, na pia ndio mana Watu wanaoishi kwenye nchi za Baridi yaani
Wazungu wakawa na maumbile ya Midomo myembamba kwa ajili ya kuhifadhi zaidi
Joto la mwili wao katika kipindi cha baridi kali, na watu wenye kuishi kwenye ardhi za
nchi Joto hua na maumbile ya kua na Midomo minene.
Na kutokana na kua ni kiungo chenye Hisia Kali sana cha Mwili wako, basi ndio maana
ikawa mtu katika kuonesha wingi wa hisia za Mapenzi yako na pia kupokea wingi wa
Hisia hizo basi hua Kiungo hicho hua kinatumia kwa ajili ya kusafirisha na kuwasilisha
Hisia za Mapenzi kwa njia ya Kunyonya au Kubusu iwe Mkono, Paji la Uso, Pua, Shavu,
Mdomo Mwengine, Shingo, Ziwa n.k
Kwani pia kuwasilisha hisia kwa kiungo cha Mdomo hua kuna athari kubwa na nyingi
zaid tofauti na viungo vyengine. Kwa upande mwengine wa mfano mzuri wa kuhisi wingi
wa hisia hizo basi fikiria pale unapokua unakula chakula kisha ukakosea na ukajitafuna
tu Mdomo kwa Bahati mbaya au ukaungua kutokana na umoto wa chakula, hua inakuaje
hali yako.
Na si hivyo tu, ingawa kila Mtu ana maumbile yake Nyama hizo lakini pia Allah
Subhanah wa Ta'ala amejaalia Kila Ibn Adam kua na Alama za peke yake za Midomo
265
yake, yaani kama vile ambavyo kila Mtu ana alama zake peke yake za Vidole vyake basi
na Lips pia zina alama ya peke yake.
Naam..Hivyo Abu said Al Khudri Radhi Allahu Anhu anatuambia katika Hadith hio kua:
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliona katika Safari yake ya Miraj kua
Kuna Watu wana Nyama za Midomo Mirefu kama ya Ngamia, na Wanavutwa
kutokana nazo
Na kisha Wakawa Wanalishwa Mawe ya Moto ambayo Yanaingizwa Midomoni
Mwao na Kutokea kwenye Tupu zao za Nyuma’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipomuuliza Malaika Jibril: ‘Jee ni Kina nani
hao?’
Basi Malaika Jibril akajibu: ‘Hao ni wale watu ambao ni wenye Kula Mali za Yatima’
Ambapo Ukali wa Adhabu yake basi kidoogo hua unaweza kuonekana pale Mtu
unapokula Pili pili kali sana, ambazo kimaumbile hua zina kemikali inayojulikana kama
Capsaicin ambayo hua iko katika hali ya mafuta mafuta yanayokaa kwenye Moyo wa
pilipili na sehemu ya nje ya Kokwa za pilipili, ambapo unapozigusa hizo basi hupelekea
nyama au ngozi yako kua na hisia ya kuzidi kwa joto katika sehemu uliyoigusisha katika
mwili wako, na hivyo sehemu hio ya mwili wako hua ni yenye kua na hisia za kuwaka
moto.
Moto ambao huupelekea Moyo wako kuzidisha mapigo yake na hivyo kuzalisha kemikali
nyenginezo mwilini mwako ikiwemo kemikali za Endorphins ambazo hua ni zenye kazi
ya kupunguza hisia za maumivu ndani ya Mwili wako, na hivyo kemikali hizi pia hua na
kazi ya kukufanya uhisi hisia za raha ya aina fulani ambayo ndio inayowafanya
wanaopenda Pilipili kuona chakula kua hakina Ladha bila ya kula na pilipili, ambapo wa
upande mwengine basi kemkali za Endorphins hua pia ni zenye kuhusika pia kukupa
hisia za raha inayopatikana katika wakati wa kuingiliana kimwili.
Na tunapozungumzia Kemikali hizi za Capsaicin basi ukali wake hua haupungui isipokua
kwa kutumia Maziwa ya baridi, na mbali ya kemikali ya Capsaicin lakini pia Pilipili hua
zina Vitamin C, Vitamin K, Vitamin B, Vitamin A, Madini ya Shaba na Potassium
ambazo husaidia katika kuujenga Mwili na kuulinda na maradhi mbali mbali.
Hivyo hapa hatuzungumzii mfano wa ukali wa Moto wa Duniani, bali tunazungumzia
mfano wa Ukali wa Maumivu ya kawaida tu ya joto la Pilipili, inapokuwashia Moto
Mdomoni au unapochukua kisha ukajipaka katika sehemu za Siri au katika sehemu
yeyote utakayojigusa Mwilini basi hali yake hua ni ya tafrani, isiyokua na kifani, Sasa
Jee hali yako itakuaje wakati umeshavutwa Nyama zenye hisia kali sana za Mdomo wako
266
Kisha Unalishwa Mawe Ya Moto yanaingia ndani ya Tumbo lako, yanautokotesha
Utumbo wako mpaka unachemka halafu inabidi Uyatoe Mawe hayo ambayo bado
yamoto.
Na hio ndio maana ya kua: Wanaokula Mali ya Yatima hua hawali chochote isipokua
Wanakula Mawe ya Moto, na hivyo ndivyo watakavyolishwa katika Siku ya Malipo
na Ndivyo watakavyoyatoa ndani ya Matumbo yao na kuyala tena na kuyatoa tena
kwa mfululizo..Allah atustiri na Adhabu kama hizo.
Kwani kwa upande mwengine basi anasema Imam Abd Rahman Al Suddi kua: ‘Mtu
yeyote yule anaekula Mali ya Yatima, Basi katika Siku ya Malipo atafufuliwa huku
akiwa anatokwa na Moto Mdomoni, Puani na Masikioni, Kiasi ya Kua Watu
watajua kua huyu alikua ni Mtu aliekua akila Mali ya Yatima.’
Na inaposemwa kua Mtu atatoka Moto basi haimaanishi kua hali yake itakua kama
Dragon au Mvuta sigara yaani hahisi Madhara ya Moshi wa sigara. La.
Bali hua inamaanisha kua Mtu anaungua mdomo kama alienyweshwa Uji uliotoka moja
kwa moja jikoni, lakini sasa hapa hali ni mbaya zaidi kwani, inakua katika kila sehemu
ya kiungo chake kinatoka Moto, Mdomoni, Machoni, Masikioni, Puani na kwenye
sehemu zake za Siri anaungua na kuwiva lakini Nyama za sehemu zake hizo zinaota tena
na tena na kuungua tena na tena. Yaani haya ni Maumivu yasiyosita wala kua na
Mwisho...Allah atustiri
Naam hio ndio maana ya aya yetu hio ya kwanza ya Surat An Nisaa 4:10 juu ya Adhabu
za Watakaokula Mali za Yatima kwani hua ni Dhulma Kubwa tena Sana, kwani Allah
Subhanah wa Ta'ala ametuwekea wazi katika aya ya Surat An Nisaa 4:10, kuhusiana na
adhabu ya kila anaekula Mali ya Yatima kua ni Mwenye Kujijazia Mawe ya Moto
Tumboni mwake, na kama tulivyoona pia kwenye Hadith.
Kwani sijui mimi na wewe tumehisi nini baada ya Kuifaham aya hio, kwa sababu Ingawa
Masahaba walikua wanawapenda Mayatima kutokana na Kuona Mfano Bora Wa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam namna alivyokua hakuwajali Mayatima.
Lakini iliposhuka Aya hii basi Masahaba waliingiwa na Khofu kutokana na Imani yao na
Taqwa mbele ya Allah Subhanah wa Ta'ala kiasi ya kua ilifikia hali Hata Chakula
alichopakuliwa Yatima basi wakawa wana hiyari wasikile hata kama Yatima huyo
ameshakula au ameshiba. Na hii ni kutokana na kuogopa Kuvutwa Midomo yao na
Kujazwa Mawe Moto ndani ya Matumbo yao.
Na Ndio Wenye Kujua hua Wanalia wanaposoma baadhi ya Aya kutokana kuhisi Uzito
wa Aya ndani ya Nyoyo zao.
267
Na hii ni kulingana na Mtu na Mtu kwani kuna wanaolizwa na aya za Adhabu na kuna
wanaolizwa na aya zinazosuta Nafsi, n.k Hivyo kama mimi na wewe tunasoma Qur'an
halafu hakuna hata aya moja ambayo inayoweza kutuliza na kutokwa na Machozi, basi
inabidi tujijue kua tuna kasoro tena kubwa sana.
Yaani aidha tuna Udhaifu wa kiimani na hivyo tuna Unafiq kwani hatujali na wala
hatugusiwa na maana ya Maneno hayo Matukufu, Au tunasoma Qur'an lakini hatujui
maana yake na hivyo haituathiri inavyotakiwa ituathiri, Hivyo tujiangalie kisha tujaribu
kutafuta Utatuzi wa Kasoro hizo.
Hivyo baada ya aya hio ya Surat An Nisaa 4:10 basi kama tulivyosema kua Masahaba
waliathiriwa na aya ifuatayo:
كَيْل
﴿وَلاَ تَقْ رَبُواْ مَالَ ٱلْيَتِيمِ إِلا َّ بِٱل َّتىِ هِ ىَ أَحْ سَ نُ حَ تى َّ ٰ يَبْ لُغَ أَشُد َّ هُ وَأَوْ فُواْ ٱلْ َ
َولَوْ بِٱلْقِسْطِ لاَ نُكَلِّفُ نَفْساً إِلا َّ وُسْعَهَا وَإِذَا قُلْتُمْ فَٱعْدِلُواْ كَ انَ ذَا قُرْبىَٰ
وَٱلْمِيزَانَ
وَبِعَهْ دِ ٱهلل َِّ أَوْ فُواْ ذٰ لِكُ مْ وَص َّاكُ مْ بِهِ لَعَل َّكُمْ تَذَك َّ رُونَ ﴾
Wala taqraboo mala alyateemi illa biallatee hiya ahsanu hatta yablugha ashuddahu
waawfoo alkayla waalmeezana bialqisti la nukallifu nafsan illa wusAAaha wa-idha
qultum faiAAdiloo walaw kana dha qurba wabiAAahdi Allahi awfoo dhalikum
wassakum bihi laAAallakum tadhakkaroona(Surat Al Anaam 6:152)
Tafsir: Na Wala Usiikaribie Mali ya Yatima isipokua Kwa ajili ya Kuiboresha, hadi
pale atakapofikia umri wa kua mkubwa. Na toeni kwa ukamilifu na pimeni kwa
uadilifu, sisi hatuikalifishi Nafsi isipokua kwa uwezo wake. Na mnaposema basi
kuweni na uadilifu hata kama ikiwa anaehusika ni mtu wa karibu yenu. Na timizeni
ahadi kwa Mola wenu, hii anakuamrisheni ili mpate kukumbuka.
Ambapo anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kuhusiana nayo
kua: ‘Watu waliosadiki, hua ni wenye kusema katika hali nne, Hua wanazungumza
maneno kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala, kwa Kupitia katika Ujumbe wa
Allah Subhanah wa Ta’ala, kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala au Maneno
ambayo yanaendana na Maneno ya Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Ambapo kuna watu pia ambao huzungumza na Nafsi zao na kwa ajili ya Nafsi zao,
na hivyo hawa hua ni waliohifadhiwa kutokana na kuzungumza kauli sizo. Na kuna
watu ambao hua wanazungumzia watu wengine na hivyo hua ni wenye kuzisahau
268
Nafsi zao, hivyo hua ni wenye kuzusha na kua ni wenye kupotoka. Na upotofu hua
ni ule waliouzusha.
Hivyo achaneni na Mazungumzo kwa ajili ya kutafuta Ilm. Na mzungumze yale tu
ambayo ni Muhimu. Na hivyo utakua ni mwenye kuhifadhika kutokana na
madhambi ya mazungumzo. Na hivyo aya inatuamrisha kuhusiana na Uadlifu wa
maneno kua Usiseme hadi pale itakapokua unaogopa kua kama hukusema basi
utapata dhambi’
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari anaendelea kutuambia kua:
‘Yeyote yule Mwenye kua na dhana basi hatokua na Yaqini, na yeyote yule
atakaezungumzia jambo lisilomhusu basi huondokewa na Imani. Na yeyote yule
anaejihusisha na jambo jengine lolote lile lisilokua ni kwa ajili ya Mola wake basi
huondokewa na Ucha Mungu, na anaeondokwa na vitu vitatu hivi basi hua ni
mwenye kuangamia, kwani atahesabiwa kua ni miongoni mwa maadui wa Allah
Subhanah wa Ta’ala.’
Na kisha baada ya hapo basi Allah Subhanah wa Ta’ala akamalizia kwa kusema:
﴿وَأَن َّ هَٰذَا صِرَاطِى مُسْتَقِيماً فَٱت َّبِعُوهُ وَلاَ تَت َّبِعُواْ ٱلس ُّبُلَ فَتَفَر َّقَ بِكُمْ عَ ن سَبِي لِهِ
ذٰلِكُمْ وَص َّاكُمْ بِهِ لَعَل َّكُمْ تَت َّقُونَ ﴾
Waanna hadha siratee mustaqeeman faittabiAAoohu wala tattabiAAoo alssubula
fatafarraqa bikum AAan sabeelihi dhalikum wassakum bihi laAAallakum
tattaqoona(Surat Al Anaam 6:153)
Tafsir: Na kwa hakika hii ndio Njia Sahih, hivyo ifuateni na wala msifuate nyengine
kwani zitakufarakisheni kutoka katika njia yake, anakuamrisheni hivyo ili mpate kua
Wacha Mungu.
Ambapo anasema Imam Muhammad Ibn Jarir At Tabari kua: ‘Amesema Abd Allah Ibn
Masud Radhi Allahu Anhu kua: ‘Siku moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alichora Mstari Ardhini na kisha akasema: ‘Hii ndo njia ya Allah’ kisha akachora
mistari myengine kushoto kwake na kulia kwake kisha akasema: ‘Hizi ni njia
ambazo mbeleni mwake amekaa Shaytani akiwavutia watu ndani ya muelekeo
wake’ na kisha akasoma aya hii (ya Surat Al Anaam 6:153)’
269
Na kwa upande mwengine basi amesema Ardab Ibn Sarriyah Radhi Allahu Anhu kua:
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alituusia sana sisi kiasi ya kua machozi yalijaa
kwenye Macho yetu na Nyoyo zetu zikailinika, hivyo tukasema: ‘Ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam hakika huu ni ujumbe ambao unajaza macho yetu, hivi
jee ungependa kutuusia zaid?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hakika mmi nimekuachieni
Weupe ambao Kiza chake hua ni kama Mchana wake, hivyo hakuna atakaeteleza
isipokua yule ambae atakaejiangamiza mwenyewe. Hivyo yeyote yule atakeishi
baada yangu. Atashuhudia tofauti nyingi. Ambapo ni juu yenu itakua kuhusiana na
Sunnah zangu, na Sunnah za Makhalifa wangu waongofu na ni juu yenu utiifu wenu
hata kama (Kiongozi wenu) atakua ni Mhabeshi Mwenye pua iliyolala, shikamaneni
na haya hata kwa kutumia meno yenu. Kwani Muumini hua kama Ngamia
aliefungwa hatamu hua anaenda kokote kule anakoongozwa.’’(Imam At Tirmidhi)
Ambapo anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Fuateni
Sunnah na njia za Watu wema waliotangulia. Kwani mimi nna khofu kua utafika
wakati ambao Watu watakua wanachukia kuambiwa kua wamfuate Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam katika kila Jambo, hivyo watu wataachana na wale
wanaowausia juu ya hilo na watawaadhirisha.’
Na hivyo sasa Masahaba ndio wakaona kua amrisho hili liliomo kwenye aya hizi za
(Surat Al Anaam 6:152) sasa limekua lina balaa zaid, kwani hata kusogelea Tusiisogelee!
Hivyo anasema Imam Ahmad Ibn Musa Ibn Marduwayh kua: ‘Baada ya tukio hili basi
Kuna Sahaba alimfuata Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kumsikitikia kwa
kumwambia: ‘Ya Rasul Allah! Hakika mimi sina njia ya kujipatia Riziki yangu.
Lakini sasa nnae Yatima nnaemlea’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia Mtu huyo kua: ‘Unaweza
Kutumia Mali ya Yatima lakini bila ya Kuifuja wala kuifanyia Israfu, kwa
kutoutumia Msingi wake na wala Kujikusanyia Mali kutokana na Msingi wa Mali
yake hio.’
Ambapo Maneno haya ya Imam Ibn Marduwayh ni yenye kutokana na Hadith Sahih
ambayo imo pia kwenye Musnad Imam Ahmad, Sunnan Imam Abu Daud, Sunan An
Nasai, Sunnan Ibn Majah na Sahih Ibn Hiban.
Ambapo tunapoangalia maana ya Hadith hii basi ndani yake tunakutana na maana
inayoendana sambamba na Mtizamo wa Amir ul Muuminin Umar Ibn Al Khattab Radhi
Allahu Anhu, Atah Ibn Abi Rabbah, Ikrimah Mawla Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu
Anhu, Ibrahim An Nakhai, na pia ndio Mtizamo wa Hasan Al Basr na wa Mujaddid Ad
Din Imam Muhammad Idris Al Shafii pia kua: ‘Mtu ambae ni Masikini na kisha akawa
270
anamhudumia Yatima ambae ana Mali aliyorithi kutoka kwa Mzee wake, basi Mtu
hua haruhusiki kutumia Mali hio isipokua tu kiasi ya kile ambacho ni kidogo
ambacho anaweza kukitumia kwa ajili ya kua kama ni Ujira wake tu, na hivyo hiki
kidogo anachochukua kua kama Ujira wake basi hua hana ulazima kukirudisha.’
Ambapo kwa upande wa Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, Umm ul
Muuminin Aisha Radhi Allahu Anha, Imam Amr Ibn Al Shabi, Imam Abu Aliyah basi
wao wanasema kua:
Kinachoruhusika Kutumiwa na Kafil yaani Mtu anaemsimamia Yatima kutokana
na Mali yake basi hua ni vitu vile ambavyo ni Muhimu kwa ajili ya Matumizi ya
Nyumbani, kwa Mfano Vyakula, Matunda, Mboga Mboga, Maziwa na vitu kama
hivyo, hivyo Mtu hua anaruhusiwa kuvitumia lakini sio kwa Fujo wala kwa Israfu,
atumie kwa kiasi chake Nyumbani kwake, kua kama ni Malipo yake kutokana na
Kulea kwake
Lakini kuna vitu vya Thamani kama Dhahabu, Fedha, Almasi, Pesa Nyingi n.k basi
hua hairuhusiki kuchukua isipokua labda kama ukiwa na nia ya kua hicho
unachochukua kua unakichukua kua kama ni Mkopo na hivyo baadae
Utakirudisha.
Kwani Allah Subhanah wa Ta'ala pia amesema katika Surat An Nisaa kua:
﴿وَٱبْتَلُواْ ٰ ٱلْيَتَامَى حَتى َّ ٰ إِذَا بَلَغُواْ النِّكَاحَ فَإِنْ آنَسْتُمْ مِّنْهُمْ رُشْداً فَٱدْفَ عُواْ إِلَيْهِمْ
أَمْوَالهَُمْ وَلاَ أتَْكُلُوهَآ إِسْرَافاً وَبِدَاراً أَن يَكْبَرُواْ وَمَن كَانَ غَنِيّاً فَلْيَسْتَعْفِفْ ن وَمَ
كَانَ فَقِيراً فَلْيَأْكُلْ بِٱلْمَعْرُوفِ فَإِ ذَا دَفَعْتُمْ إِلَيْهِمْ أَمْوَالهَُمْ فَأَشْهِ دُواْ عَلَيْهِمْ وَكَفَ ٰ ى
يباً ﴾ بِٱهلل َِّ حَسِ
Waibtaloo alyatama hatta idha balaghoo alnnikaha fa-in anastum minhum rushdan
faidfaAAoo ilayhim amwalahum wala ta/kulooha israfan wabidaran an yakbaroo
waman kana ghaniyyan falyastaAAfif waman kana faqeeran falya/kul
bialmaAAroofi fa-idha dafaAAtum ilayhim amwalahum faashhidoo AAalayhim
wakafa biAllahi haseeban (Surat An Nisaa 4:6)
Tafsir: Na wajaribuni (Kiakili na ufaham wao) Mayatima hadi wawe wamebaleghe na
kufikia umri wa kuoa, na mkiwaona wana ufaham mzuri, basi wapeni mali zao, na
271
wala msizitumie kwa Israfu kutokana na kua na khofu kua watakua wakubwa. Na
kama ikiwa mmoja miongoni mwenu ni Tajiri basi asichukue malipo. lakini kama
akiwa Fukara basi na wacha na achukue kinachostahiki, na kisha mtakapowakabidhi
Mali zao basi kuwe na shahidi juu yao na kwa hakika anatosheleza Allah Kuchukua
Mahesabu.
Kwa upande mwengine basi pia inabidi tujue unapokua na Imani basi kwako wewe kua
tahadhari hua ni bora zaid, na ndio maana kwa Upande wa Sayyidna Umar Ibn Al Khattab
Radhi Allahu Anhu basi yeye alikua akisema:
‘Hakika Mimi hua naichukulia Mali ya Ummah kua ni sawa na Mali ya Yatima,
yaani pale nnapokua na kitu basi hua siigusi Mali hio na nnapokua sina kitu na na
shida sana basi hua nnachukua kua kama Mkopo, na hivyo nikipata basi hua
nnarudisha’
Na hii ni kutokana na wasia wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae alimuusia
Abu Dhar Radhi Allahu Anhu kwa kumwambia: ‘Ewe Abu Dhar! Hakika mimi nauona
Udhaifu wako ndani yako, hivyo napendelea kwa ajili yako kile ambacho
nnakipendelea kwa ajili ya Nafsi yangu, Kua kamwe usikubali kua kiongozi baina
ya watu wawili na wala usikubali kuisimamia Mali ya Yatima.’(Sahih Muslim)
Kwani ili uifaham maana ya Hadith hii basi inabidi kwanza Umjue Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam na Sifa zake ambapo Allah Subhanah wa Ta'ala amemsifia kua ni
Kiumbe bora na ni mwenye Rehma na Huruma kwa Walimwengu pale aliposema katika
Qur'an:
﴿وَمَآ أَرْسَلْنَاكَ إِلا َّ رَحمَْةً لِّلْعَالَمِينَ ﴾
Wama arsalnaka illa rahmatan lilAAalameena(Surat Al Anbiyah 21:107)
Tafsir: Na Hatukukutuma wewe isipokua kua ni Rehma kwa Ulimwengu.
Na pia pale ilipothibitisha Qur'an kwa kusema:
﴿لَقَدْ جَآءَكُمْ رَسُولٌ مِّنْ أَنفُسِ كُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِت ُّمْ حَرِيصٌ عَلَيْكُمْ بِٱلْمُؤْمِنِ ينَ
رَءُوفٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
272
Laqad jaakum rasoolun min anfusikum AAazeezun AAalayhi ma AAanittum
hareesun AAalaykum bialmu/mineena raoofun raheemun(Surat At Tawba 9:128)
Tafsir: Kwa Hakika Amekuja Kwenu Mtume Kutokana na Miongoni mwa Nafsi zenu
(yaani si katika Maumbile yeyote yale isipokua katika Maumbile ya Kiibinadam kama
mlivyo nyinyi) Mna thamani kubwa sana ya Kimapenzi kwake yeye, Hataki Mdhurike
au Muwe na Ugumu wa Mambo yenu. Kwani Anajali sana Juu yenu kwa Waumini ni
Mwenye Kuwaonea Huruma na Mwingi wa Rehma.
Hivyo hizi ni aya mbili ambazo zinazomuelezea Rasul Allah Salallahu Alayhu wa Salam
kwa Kifupi lakini hapo hapo kwa Mapana Makubwa Sana.
Na hapa sitaki kushuka katika kufafanua kwa sababu nikishuka tutachukua Mda mrefu
kwani Mada yake inahitaji Kitabu Kizima, Ila kwa ufafanuzi mfupi tu basi katika wakati
wa Kukusanywa Qur'an basi Sayyidna Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu alikua
haikubali aya ya Qur'an mpaka apate Uthibitisho wa Mashahidi walioihifadhi aya hio
tena Mashahidi hao wawe Masahaba wacha Mungu na wenye Ilm kweli.
Lakini aliposomewa aya hii basi hakutaka hata shahidi bali aliikubali Moja kwa Moja
kwani alisema kua: ‘Aya hii ya Surat at Tawba ni aya inayomuelezea Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kama alivyo.’ hivyo hapa tunaona kua Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam ambae ni mwenye sifa ya kua ni mwenye Rehma kwa
Waumini basi anamuusia Sahaba wake kua asikubali Kusimamia Mali ya Yatima.
Hapa kwanza nataka tufahamiane kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
hakumuusia Sahaba wake huyo ambae ni Abu Dhar Radhi Allahu Anhu kua Asilee
Yatima bali alimuusia kua asikubali kusimamia Mali ya Yatima. Ambapo hivi ni vitu
viwili tofauti na bila ya shaka Kulea Yatima hua ni Kazi rahisi zaid na ni Jukumu Jepesi
zaidi kuliko Kusimamia Mali ya Yatima
Kwani baada ya Kumjua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi tunatakiwa pia
tumjue Sahaba Abu Dhar Al Ghifari Radhi Allahu Anhu. Ambapo kwa juu juu basi Abu
Dhar Al Ghifari Radhi Allahu Anhu alikua ni Mtu wa 5 Kuingia katika Dini ya Uislam.
Halafu alikua ni Miongoni mwa Masahaba ambao wana Ucha Mungu na Muaminifu
mkubwa Sana.
Kiasi ya Kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisema kua: ‘Mbingu hazijawahi
kumfunika chini yake Mtu Muaminifu Kama Abu Dhar’ (Imam At Tirmidhi)
Na Abu Dhar Al Ghifari Radhi Allahu Anhu alikua ni Mtu wa mwanzo kabisa Miongoni
mwa Waislam kua ni mwenye Kutumia salam ya Asalaam Alaykum
273
Hivyo mimi na wewe leo hii tukisema Salaam Alaykum, basi na Abu Dhar Al Ghifari
Radhi Allahu Anhu nae anapata sehemu ya Thawabu zake kutokana na kua sisi ni wenye
kumuiga yeye kutokana na maamkizi hayo kwani yeye ndie wa Mwanzo, na kulingana
na Hadith basi atakaeanzisha Jambo jema basi kila likifanywa na Yeye hua anapata
Thawabu zake bila ya kumpunguzia Mfanyaji.
Na anaeanzisha ovu pia anapata dhambi za kila afanyae Ovu hilo. Sasa Fikiria kil
Ukisema Asalaam Alaykum basi wewe una thawabu 10 na Abu Dhar Radhi Allahu Anhu
anapata 10. Na hii tangu Mwanzo wa Uislam mpaka leo..Jee tunazungumzia Salam
ngapi? Zenye Thawabu 10, 10,10 mara ngapi?
Naam..hio pia ni kwa ufupi kuhusiana na Abu Dhar Radhi Allahu Anhu. Hivyo
tukiiangalia Hadith hii ya Wasia kuhusiana na Mali ya Yatima basi tunaona kua wasia
huo unatoka kwa M-bora wa Viumbe, Mwenye Rehma na Huruma kwa Ulimwengu na
Wauamini, unaelekea kwa Mtu ambae hakuna Muaminifu zaidi yake chini ya Mbingu
ambae anaambiwa na M-bora wa viumbe kua hakika yeye pia anaweza akafeli Mtihani
wa Mali ya Yatima.
Ya Allah!...Hivi Kama itakua Abu Dhar Radhi Allahu Anhu ambae hakuna anaemfikia
kwa Uaminifu anaambiwa kua asikubali Kusimamia Mali ya Yatima kutokana na
Ukubwa wa Jukumu la Mali hio na Uzito wa Mitihani yake, Jee hali itakuaje kwangu
mimi na wewe?
Na kisha akasema tena Allah Subhanah wa Ta'ala:
كَيْل
﴿وَلاَ تَقْ رَبُواْ مَالَ ٱلْيَتِيمِ إِلا َّ بِٱل َّتىِ هِ ىَ أَحْ سَ نُ حَ تى َّ ٰ يَبْ لُغَ أَشُد َّ هُ وَأَوْ فُواْ ٱلْ َ
وَٱلْمِيزَانَ بِٱلْقِسْطِ لاَ نُكَلِّفُ نَفْساً إِلا َّ وُسْعَهَا وَإِذَا قُلْتُمْ فَٱعْدِلُواْ وَلَوْ كَ انَ ذَا قُرْبىَٰ
وَبِعَهْ دِ ٱهلل َِّ أَوْ فُواْ ذٰ لِكُ مْ وَص َّاكُ مْ بِهِ لَعَل َّكُمْ تَذَك َّ رُونَ ﴾
Wala taqraboo mala alyateemi illa biallatee hiya ahsanu hatta yablugha ashuddahu
waawfoo alkayla waalmeezana bialqisti la nukallifu nafsan illa wusAAaha wa-itha
qultum faiAAdiloo walaw kana dha qurba wabiAAahdi Allahi awfoo thalikum
wassakum bihi laAAallakum tadhakkaroona(Surat Al Anaam 6:152)
Tafsir: Na Wala Usiikaribie Mali ya Yatima isipokua Kwa ajili ya Kuiboresha , hadi
pale atakapofikia umri wa kua mkubwa. Na toeni kwa ukamilifu na pimeni kwa
uadilifu, sisi hatuikalifishi Nafsi isipokua kwa uwezo wake. Na mnaposema basi
274
kuweni na uadilifu hata kama kiwa anaehusika ni mtu wa karibu yenu. Na timizeni
ahadi kwa Mola wenu, hii anakuusieni ili mpate kukumbuka.
Kwani anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wakati Allah
Subhanah wa Ta'ala aliposhusha aya hizi Mbili basi Kila Mtu miongoni mwa
Masahaba aliekua na Yatima alijitenga na Yatima aliekua nae Watu wakawa
Wanakula na Kunywa Tofauti na Mayatima wao, na Baadhi walikua hawali
Chakula alichopikiwa Yatima wake, hadi akile Mwenyewe Yatima huyo, na baadhi
ya Wakati hufikia Chakula cha Yatima husika Kuharibia kutokana na kutoliwa
(Imam An Nasai)
Naam..hivyo ndivyo Walivyokua Masahaba wakishikamana na Maamrisho ya Allah
Subhanah wa Ta'ala. ‘Ambapo Hali hii iliendelea mpaka sasa Masahaba Wakaona
huu ushakua Mtihani mkubwa Sana, kwa sababu wao wamefaham kua Yatima
akiwekewa Chakula basi kisiliwe mpaka aje kula mwenyewe.’
Hivyo Wakamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam juu ya Uzito wa
Maneno ya Aya hizi Juu yao.’
Na baada ya Kulalamika huko basi Allah Subhanah wa Ta'ala akawashushia Amrisho
lenye ufafanuzi ndani yake kupitia kwa Mtume wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam katika aya iliyotumia neno Salaha tulilolifafanua maana yake hapo kabla ambalo
liko katika hali ya Islahun pale Allah Subhanah wa Ta'ala aliposema katika Qur'an kua:
﴿وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ ٱلْيَتَامَى ٰ قُلْ إِصْلاَحٌ له َُّمْ خَيْرٌ وَإِنْ تخَُالِطُوهُمْ فَإِخْوَانُكُمْ وَٱهلل َُّ
يَعْلَمُ ٱلْمُفْسِ دَ مِنَ ٱلْمُصْلِحِ وَلَوْ شَآءَ ٱهلل َُّ لأَعْنَتَكُمْ إِن َّ ٱهلل ََّ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾
Wayas-aloonaka AAani alyatama qul islahun lahum khayrun wa-in tukhalitoohum
fa-ikhwanukum waAllahu yaAAlamu almufsida mina almuslihi walaw shaa Allahu
laaAAnatakum inna Allaha AAazeezun hakeemun(Surat Al Baqra 2:220)
Tafsir: Na Wanakuuliza (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) Kuhusiana na
Yatima: ‘Waambie (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) kua Islahun (Kua
Na Wema na Uadilifu) Juu ya Mali zao ni Bora na Kama Mkichanganyika nao (katika
mambo yenu) Basi wao Ni Ndugu zenu na Allah Ni Mwenye Kumjua Fisadi Na
Mwenye Islahi (Mwenye wema na Uadilifu) Na Kama angetaka Allah Basi
angekuwekeeni Ugumu hakika Allah ni Mwenye Uwezo Mkubwa Sana na ni Mwenye
Hikma Kubwa sana.
275
Neno Salaha kwa Lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kua Sahih, Kua Mzuri, Kua
Muadilifu na pia umaanisha Suluhu. Neno Salaha ndio lililotoa Neno Islah ambalo hua
linamaanisha Kuweka Kitu Sawa, Kuboresha Kitu, Kukifanya Kitu Kiwe Kizuri.
Na pia likatoa neno Salih ambalo ni Jina la Nabii wa Allah Subhanah wa Ta'ala
alietumiwa watu wa Thamud ambalo hua linamanisha Mtu Mwema. Na pia ndio lililotoa
neno Muslihuna yaani Watu wenye Kufanya Mema, au wenye Kusuluhisha mambo.
Ambapo aya inatuwekea wazi kuhusiana na kuwafanyia Wema juu ya mali zao, kama
ilivyokua ni jukumu la kila mtu kua anatakiwa kua na Uadilifu katika usimamizi wa Mali
yake basi ndio hivyo hivyo anavyotakiwa kua na uadilifu juu ya Mali ya Yatima.
Yaani kama itakua matumizi ya Mali hio itakua ni kwa ajili ya mambo sio, yaani
mambo ya maasi na kufanya israfu basi matumizi hayo hua hayaruhusiki.
Na kama ikiwa matumizi hayo ni kwa ajili ya mambo mema na kutafuta ridhaa ya
Allah Subhanah wa Ta’ala na katika kutekeleza wajibu wa Kidini juu ya Mali hio
au juu ya Yatima hao, kwa mfano kuitolea Zakkah Mali hio unapowadia mda wake,
basi utumiaji huo wa Mali hio hua ni wa Wajibu pia na kufanya hivyo hua ni
kusimamia na kuwatekeleza Mayatima hao haki yao juu ya Mali yao.
Na inapokua matumizi hayo yatakua hayana ulazima lakini haitoathiri Mali yao
kwa mfano kutoa Sadaka kutokana nayo basi inaruhusika, lakini kama ikiwa utoaji
huo wa Sadaka utaathiri Mali ya Mayatima hao kutokana nayo basi haitoruhusika
kuitolea Sadaka mali hio, kwani kufanya hivyo itakua ni sawa na kuwavunjia haki
yao Mayatima hao.
Na katika kututilia msisitizo wa kutoruhusika kufanya Dhulma na kuwavunjia haki
Mayatima na Mali zao katika Uislam basi ndio Allah Subhanah wa Ta’ala ndio
akashusha aya isemayo:
﴿وَلاَ تَقْرَبُواْ مَالَ ٱلْيَتِيمِ إِلا َّ بِٱل َّتىِ هِىَ أَحْسَنُ حَتى َّ ٰ يَبْلُغَ أَشُد َّهُ وَأَوْفُواْ ابِ لْعَهْدِ إِ َّن
ٱلْعَهْ دَ كَ انَ مَسْ ؤُولاً ﴾
Wala taqraboo mala alyateemi illa biallatee hiya ahsanu hatta yablugha ashuddahu
waawfoo bialAAahdi inna alAAahda kana mas-oolan (Surat Al Isra 17:34)
276
Tafsir: Na wala usiikaribie Mali ya Yatima isipokua kwa ajili ya kuiboresha, hadi pale
watakapofikia umri mkubwa wa kubaleghe, na tekelezeni ahadi kwani kwa hakika juu
ya ahadi Mtaulizwa
Kwani hapo zamani hali ilikua kama anavyosema Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas
Radhi Allahu Anhu kua:
Hapo zamani Katika Zama za Kijahiliya Watu walikua hawawapi Mali zao Watoto
wadogo wa Kike na wa Kiume, hivyo Siku Moja kuna Ansar aliekua akiitwa Aus
Ibn Thabit Radhi Allahu Anhu ambae alifariki Dunia. Na kuacha Watoto wawili wa
Kike na Mmoja wa Kiume.
Hivyo baada ya kufariki Aus Radhi Allahu Anhu basi, wakatokea Watoto wa Kiume
wa Baba mdogo Aus Radhi Allahu Anhu na kisha wakachukua Mali zake zote
alizowacha ambazo ni za Urithi wa watoto wake. Hivyo Mke wake Aus akawaambia
Watoto hao wa Kiume wa Baba yake Mdogo Aus Radhi Allahu Anhu kua:
Kama Mnachukua Mali zote basi bora waoeni Mabinti zake ambao nao pia
Wanaasili ya Damu moja nanyi, lakini nao wakakataa
Hivyo mke huyo wa Aus Radhi Allahi Anhu akakimbilia kwa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kushtaki, Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaita
Watu hao wawili ambao ni watoto wa Kiume wa Baba mdogo wa Aus na
kuwaambia: ‘Msichukue Mali ya Mayatima kwani nimepokea Wahy kua watoto
wote wa Kike na Kiume wa Mfiwa hua wanapewa urithi wao’ (Imam Al Sabuni katika
Tafsir Ayat al Ahkami Al Quran)
Hivyo katika enzi za Ujahiliya Watu hawakua tu wakiwanyang'anya Mayatima Urithi
wao kama kwenye Mfano tuliouangalia wa Kifo cha Aus Ibn Thabit Radhi Allahu Anhu.
lakini pia Watu walikua wakichukua Mali za Mayatima na kuzibadilisha na zao wao au
kwa kuzichanganya na Mali zao wao, na kisha baadae huwapa Mayatima zile mali zenye
thamani ya chini zaidi ya Mali zao. Kwa Mfano Watu walikua wakichukua Kondoo
walionona wa Mayatima na kisha huwarudishia Mayatima hao Kondoo wagonjwa au
waliokonda badala yake.
Hivyo kutokana na Matukio kama haya basi Allah Subhanah wa Ta'ala akashusha ile aya
isemayo:
277
﴿وَآتُواْ ٱلْيَتَامَى ٰ أَمْوَالهَُمْ وَلاَ تَتَبَد َّلُواْ ٱلخَْبِيثَ بِٱلط َّيِّبِ وَلاَ أتَْكُلُو ۤ اْ أَمْوَالهَُ مْ إِلىَٰ
أَمْ وَالِكُمْ إِن َّهُ كَ انَ حُ وابً كَ بِيراً ﴾
Waatoo alyatama amwalahum wala tatabaddaloo alkhabeetha bialttayyibi wala
ta/kuloo amwalahum ila amwalikum innahu kana hooban kabeeran (Surat An Nisaa
4:2)
Tafsir: Na Wapeni Mayatima Mali zao Na Wala Msizibadilishe (Mali zenu nyie) Mbaya
kwa Nzuri (Zao wao)Na Wala Msile Mali zao kwa (kuzijumuisha) na Mali zenu Kwani
Kwa Hakika Kufanya Hivyo ni Dhambi Kubwa sana.
Hii ni ay ambayo imetumia neno Huban ambalo ni tofauti kimaana na neno Hubban
kwani Neno Hubban ni lenye kutokana na neno Hubb ambalo hua linamaansiha Mapenzi,
Upendo au Kitu ambacho kinavutia na kupendezesha. Ambapo neno Huban lililotumika
kwenye aya hii katikati lina harfu waw na hivyo kua ni lenye kumaanisha Kuvuka
Mipaka, Kufanya Dhambi, Kufanya Jambo lisilofaa, Kufanya Uhalifu au Kufanya
Maangamizi.
Ambapo anasema Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Katika
Wakati ambao Sahaba Abu Ayub Al Ansari Radhi Allahu Anhu alipokua anataka
Kumtaliki Mke wake, aitwae Umm Ayub Radhi Allahu Anha hivyo Abu Ayub Al
Ansari alienda kuomba Ushauri kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, kama
amuwache Mke wake huyo ama la.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia Abu Ayub Al Ansari
Radhi Allahu Anhu kua: ‘Ama kwa hakika kwako wewe kumuacha Umm Ayoub
basi itakua ni Huuban Kabiran’Ambapo Abu Ayub Al Ansari Radhi Allahu Anhu
alipoambiwa hivyo basi akaachana na Mawazo hayo ya kuachana na Mke wake
huyo.
Hivyo kulingana na Kauli hii ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi maneno
Huuban Kabiran haikumaanisha kua Kumuacha Umm Ayub Radhi Allahu Anha yatakua
Mapenzi makubwa sana kwani kama mtu ana mapenzi Makubwa sana na Mke wake basi
hua hataki Kumuacha.
Hivyo hapa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akimaanisha kama ilivyokua
ikimaanisha Aya kua Kufanya hivyo hua ni Kosa Kubwa Sana.
278
Na hivyo kwa maana hio basi Aya inatuwekea wazi kua Kula Mali ya Yatima au
Kumbadilishia Mali yake Nzuri na Kumpa Mbovu basi hua Ni Kosa La Dhambi Kubwa
linaangamiza. Kama tulivyoona katika aya tuliyoiangalia juzi ya Surat An Nisaa 4:10
tulipozungumzia Kuhusiana na Mdomo na Kujaza Matumbo Moto.
Na pia kama alivyoonya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kusema katika
hadith kua: Jiepusheni na Mambo Saba yenye Kuangamiza ambayo ni:
1-Kumshirikisha Allah Subhanah wa Ta'ala.
2-Kufanya Uchawi.
3-Kuua Mtu bila ya Sababu inayokubalika Kishariah.
4-Kula Riba.
5 –Kula Mali Ya Yatima.
6-Kukimbia kutoka kwenye Uwanja wa Vita vya Jihad kwa Ajili ya Allah Subhanah
wa Ta'ala.
7-Kuwasingizia Uchafu Wanawake ambao ni Wasafi.
(Imam Al Bukhari)
Hivyo kuhusiana Mayatima basi ukweli ni kua kila mmoja anatakiwa awe na ufahamu
juu Haki zao. Kwani kutofaham juu ya haki zao hua ni Ujinga wa Kutojua Dini yako na
kukufanya wewe kua na Uyatima wa Kutokua na Ilm ya Dini yako.
Kwani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisema kuwaambia Masahaba zake kua:
‘Yatima hua si Mtu ambae Hana Baba wala Mama Bali Yatima hua ni Mtu Ambae
Ni Mjinga asiekua na Ilm’(Imam Ibn Majah)
Na katika hili basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anatuwekea wazi kua Mtu
aisekua na Ilm hua ni mwenye Ugumu wa Maisha yake kutokana na Ujinga Wake. Kwani
Ilm humsaidia na kumrahisishia Mtu Maisha yake hapa Duniani na Kesho Akhera kama
vile Yatima anavyosaidiwa na Mzee wake.
Kwani unapokua huna Ilm basi unaweza pia ukawa ni miongoni mwa wanaokadhibisha
Dini kutokana na ujinga wao ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anaendelea kutuelezea
aina nyengine ya Watu hao wanaokadhibisha Dini kwa kuwaambatanisha pamoja na
wasiowakirimu Mayatima pale aliposema:
279
﴿كَلا َّ بَل لا َّ تُكْرِمُونَ ٱلْيَتِيمَ۞وَلاَ تحََاض ُّونَ عَلَى ٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ ﴾
Kalla bal la tukrimoona alyateema; Wala tahadhdhoona AAala taAAami
almiskeeni (Surat Al Fajr 89:17-18)
Tafsir: (Wataambiwa) La Bali Nyinyi Mlikua Hamuwakirimu Mayatima. Wala
hamkuwa ni wenye kuamrisha kuwapa chakula Maskini.
Ambapo katika Surat Al Maun basi alisema:
﴿وَلاَ يحَُض ُّ عَلَى ٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ ﴾
Wala yahudhdhu AAala taAAami almiskeeni; (Surat Al Maun 107:3)
Tafsir: Na kisha yule ambae hahimizi kulisha Masikini.
Aya mbili hizi zimetumia asili ya Neno Hudhdhu ambalo hua linamaanisha Kuhimiza,
Kutia Ari au Mwaamko au Kuchochea au Kuamrisha.
Kama tuko makini na kutafakkari basi itakua tunaona kua Aya mbili hizi, kwa kua ni za
Mwanzoni kushuka katika Kipindi cha Mwanzoni mwa Utume basi ingawa hazikua ni
zenye Kukemea sana juu ya Makosa hayo Mawili ya Kutowakirimu Mayatima na
Masikini, kwani zilikua zinaweka wazi tu kua haya ni Mambo Mabaya sana.
Hivyo tunapoziangalia aya hizi za Surat Al Maun, basi tunaona kua kimaana zunaenda
sambamba na aya tulizoziangalia za Surat Al Fajr, lakini hata hivyo aya hizi zinatofauti
kimaana.
Kwani aya hizi za Surat Al Maun zimekuja na Tangazo zito sana tena lenye Onyo la kua
kwa Kila anaejihesabu kua Ameamini lakini akawa anafanya Makatazo yaliyomo Ndani
ya Tangazo hilo, basi Moja kwa Moja Mtu huyo atakua ni Mwenye Kuikadhibisha Dini,
mwenye Kuikadhibisha Siku ya Malipo.
Na Hivyo hata kama anasali basi mbele ya Waislam wenzake Muislam huyo atakua ni
mwenye Kusimamisha Nguzo za Dini ya Kiislam lakini ndani ya Moyo wake hua ni
mwenye kuvunja Nguzo ya Imani ya Dini ya Kiislam.
280
Ili kufahamu vizuri hapa basi na tuchukulie Mfano kwamba Mtu anaumwa na Malaria,
kisha Labda akaambiwa na Daktari kua Dawa yake ni kua amalize dozi ya Vidonge
Viwili vya dawa kwa siku tatu.
Hivyo Mtu huyo akawa hakuamini kua Dawa hio itamsaidia, na hivyo akawa ni mwenye
kuchukua hizo dawa alizopewa kisha badala ya kula Vidonge viwili basi yeye akameza
vidonge vya siku moja tu. Hivyo bila ya Shaka Mtu huyo hatoweza kupona kwa sababu
amevunja Nguzo moja ya Imani ya Kumuamini Daktari wake. Sasa Homa ikimzidi sijui
atamlaumu nani, kwa kukosa kwake Imani.
Ambapo tunapozungumzia Kuikadhibisha Dini kulikotajwa kwenye Aya hii ni
kutoaamini na hivyo kutokukubaliana na kile kilichoamrishwa na Allah Subhanah wa
Ta'ala. Sasa hii hua ni hali ya Muislam kua ni Mnafiq kama tutaitafsiri aya hii kwa
kutumia maana ya Kukadhibisha Dini, yaani sehemu ya Dini kua anaiamini lakini
sehemu nyengine haiamini.
Ama kama tutaitafsiri aya hii kwa maana ya kusema kua ni mwenye Kuikadhibisha siku
ya Malipo. Basi bila ya shaka, hapo ndani yake wanaingia pia wale ambao si Waislam
pia, kwani Muislam hua anaamini Siku ya Malipo lakini asiemuamini Allah Subhanah
wa Ta'ala basi hua haamini juu ya siku ya Malipo.
Ambapo hii sifa ya Kutohimizana kuwaonea huruma na kuwasadia Masikini kwa Pesa,
Chakula, Nguo n.k Imewekwa wazi kabisa kua ni sifa ya yule Mtu ambae si Mwenye
kumuamini Allah Subhanah wa Ta'ala pale alivyosema Allah Subhanah wa Ta'ala katika
Surat Al Haqqah kua Mwenye Uwezo wa Kuwasaidia Masikini kisha akawa
hajawasaidia basi katika Siku ya Malipo atakua ni mwenye kusema:
﴿يٰلَيْتَهَا كَانَتِ ٱلْقَاضِيَةَ۞مَآ أَغْنىَٰ عَنىِّ مَالِيَهْ۞ه َّ لَكَ عَنىِّ سُلْطَ انِيَهْ ﴾
Ya laytaha kanati alqadhiyatu; Ma aghna AAannee maliyah; Halaka AAannee
sultaniyah(Surat Al Haqqah 69:27-29)
Tafsir: Ya Laiti (Bora Kifo) kingekua Ndio Mwisho wangu; Haukunifaa Utajiri wa
Mali yangu; Yamekimbia kutoka kwangu Mamlaka yangu
Yaani Mtu Ataomba asingefufuliwa baada ya Kufariki kwake, kwani haumfai Utajiri
wake wala Mamlaka yake, na baada ya kuonesha kwao Majuto hayo katika siku hio basi
Allah Subhanah wa Ta'ala atawaambia Malaika wa Motoni ambao Ukubwa wao na
Nguvu zao basi hakuna hata kiumbe mmoja anaeweza kupingana nao.
281
Kwani hawa uwezo wao ni pamoja na Kuwasimamia Majini ambao, Ukubwa wao zaidi
ya Mlima wa Kilimanjaro, sasa hao ni Majini na Miili yao na watadhibitiwa kama
Vifaranga vidogo vidogo, jee hali itakuaje kwa Ibn Adam anaekadhibisha Dini na hivyo
Kumuasi Mola wake, itakuaje hali yake siku hio ambayo Allah Subhanah wa Ta'ala
anatoa Amri kuwaamrisha Malaika hao Dhidi ya Kila Kiumbe aliemuasi kwa kusema:
﴿خُذُوهُ فَغُل ُّوهُ۞ثمُ َّ ٱلجَْحِ يمَ صَل ُّوهُ۞ثمُ َّ فىِ سِ لْسِ لَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعاً
فَاسْ لُكُوهُ ﴾
Khudhoohu faghulloohu; Thumma aljaheema salloohu; Thumma fee
silsilatin dharAAuha sabAAoona dhiraAAan faoslukoohu (Surat Al Haqqa 69:33-
35)
Tafsir: Mkamateni Kisha Mfungeni Minyororo, Kisha Ndani ya Moto Mkali Sana
Mtupeni, Kisha Mfungeni Kwa Mnyororo Wenye Urefu wa Dhiraa Sabiini;
Kwani wengi Hua ni wenye kupenda kurushiana vipande vya picha za filamu za Kwenye
Whatsapp ambazo zinaonesha namna Watu Wanaojionesha wanavyowachoma kwenye
Moto kwa kuwafanya Mshikaki Kuku, Mbuzi, Kondoo, Ngo'ombe, n.k Huku akiwa
anazungushwa zungushwa, na anapowiva Mnyama huyo basi Nyama yake hua laini sana
na hivyo kua ni tamu nzuri kwa ajili ya kuliwa.
Hivyo kila mmoja anatakiwa afahamu kua kama atakua ni Mwenye Kumuasi Mola wake
basi haya maneno tunayokumbushana katika aya hizi yanamaanisha kua Mtu huyo katika
siku ya Malipo nae atakua kama inavyochomwa Mishikaki ya nyama za Wanyama hao.
Ambapo Wanazuoni wanasema kua Hii Minyororo inayozungumziwa ambayo Mtu
Muasi atafungwa nayo siku hio yenye Ukubwa wa Dhiraa 70 basi Kwanza utaingizwa
Puani kwenye tundu ya kwanza na kutokea Mdomoni. Kisha unaingizwa kwenye tundu
ya pili ya Pua na kutokea kwenye njia ya haja kubwa, kisha unatumbukizwa ndani ya
shimo la Moto wa Jahannam, kisha kama anavyogeuzwa Kuku au Kondoo basi na yeye
ndivyo atakavyogeuzwa.
Ila sasa Ubaya ni Kua Hawa Wanyama tunaowachoma sisi Wanakua washachinjwa na
hawana Uhai, lakini sisi tukimuasi Allah Subhanah wa Ta'ala basi tutafanywa Mishkaki
huku tukiwa hai…Ya Allah, Tustiri na Adhabu ya Moto huo..Allahuma Aaamiin
282
Kwani Allah Subhanah wa Ta'ala anajua kua Watu watajiuliza kwanini Watapewa
Adhabu hio, hivyo ili watu wasiulize basi yeye anaweka wazi kwa kusema kua huyo
atakaefanywa hivyo ni yule ambae:
﴿إِن َّهُ كَانَ لاَ يُؤْمِنُ بِٱهلل َِّ ٱلْعَظِيمِ۞وَلاَ يحَُض ُّ عَلَى ٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ ﴾
Innahu kana la yu/minu biAllahi alAAadheemi; Wala yahudhdhu AAala taAAami
almiskeeni; (Surat Al Haqqa 69:34-35)
Tafsir: Hakika huyu Hakua ni Mwenye Kuamini Juu ya Allah Subhanah wa Ta'ala
Mwenye Utukufu Na Hakua ni mwenye Kuhimiza Kuwalisha Masikini.
Kwani Muislam anaponeemeshwa Neema ya Mali na Allah Subhnah wa Ta’ala basi hua
anatakiwa aitumie ipasavyo kwa ajili ya kumridhisha Allah Subhnah wa Ta’ala kwa
kuwasaidia watu wengine katika Jamii yake, kwani Mali hio aliyopewa hakuipata
kutokana na jitihada zake bali ameipata kutokana na majaaliwa ya Mola wake ambae
ndie Mmiliki wa kila kilichomo Mbinguni na Ardhini.
Ambapo siku moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliwahoji Masahaba zake kwa
kusema: ‘Hivi jee ni nani miongoni mwenu ambae Mali atakazowaachia waarithi
wake anazipenda zaidi kuliko Mali zake?’ Masahaba wakasema: ‘Hakika sisi
tunazipenda zaidi Mali zetu’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema
kuwaambia Masahaba zake kwa kusoma aya ifuatayo:
﴿وَمَا لَكُمْ أَلا َّ تُنفِقُ واْ فىِ سَبِيلِ ٱهلل َِّ وَهللِ َِّ مِيرَاثُ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ لاَ يَ سْتَوِى
مِنكُم م َّنْ أَنفَقَ مِن قَبْلِ ٱلْفَتْحِ وَقَاتَلَ أُوْلَٰئِكَ أَعْظَمُ دَرَجَةً مِّنَ ٱل َّذِينَ أَنفَقُواْ مِن
بَعْدُ وَقَاتَلُواْ وَكُلاًّ وَعَدَ ٱهلل َُّ ٱلحُْسْنىَٰ وَٱهلل َُّ بمَِا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴾
Wama lakum alla tunfiqoo fee sabeeli Allahi walillahi meerathu alssamawati waalardhi
la yastawee minkum man anfaqa min qabli alfathi waqatala ola-ika
aAAdhamu darajatan mina alladheena anfaqoo min baAAdu waqataloo wakullan
waAAada Allahu alhusna waAllahu bima taAAmaloona khabeerun (Surat Al Hadid
57:10)
283
Tafsir: Inakuaje mpaka nyinyi hamtoi kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala? Wakati
kwa Allah ndiko kwenye umiliki wa mirathi ya Mbinguni na Ardhini. Hawako sawa
miongoni mwenu wale ambao ni wenye kutoa na wenye kupigana kwa ajili ya Allah
kabla ya Ushindi. Kwani hawa wako juu zaidi kidarja kuliko wale waliotoa na kisha
kupigana baada yake. Lakini kwa wote basi Allah ameahidi malipo mema na Allah ni
mwenye kujua juu ya kila mnachokifanya.
Yaani Aya inawahoji walioneemeshwa mali kwa ajili ya kuzisimamia kwa mda mfupi
katika maisha yao hapa Duniani na mwenye Utajiri wa Milele na wa kutohitajia kitu
chochote ambae si mwengine isipokua ni Allah Subhanah wa Ta’ala kua kwanini
hawatumii neema hio ya mali na kisha wakanufaishwa zaidi na yule aliewapa mali hio
kwa kulipwa Pepo kutokana na kutumia kwao kwa ajili yake hapa Ulimwenguni?
Na pia aya hii inazungumzia tofauti baina ya Darja ya Masahaba waliotumia Mali zao
kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala na waliopigana kwa ajili ya Allah Subhanah wa
Ta’ala kabla ya Kutekwa kwa Mji wa Makkah na Waislam na Darja ya Masahaba
waliotumia Mali zao kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala na waliopigana kwa Ajili ya
Allah Subhanah wa Ta’ala baada ya kutekwa kwa Mji wa Makkah na Waislam.
Ambapo neno Sadaqah hua ni lenye kumaanisha Kua mkweli, kua Muaminifu, Kusema
Ukweli, Kuthibitisha Ukweli, Kuamini, Kusadiki, Kua na Imani, na pia Kutoa kitu kwa
ajli ya Kusidia. Hivyo kutubainishia kua ni wale tu wenye kumuamini Allah Subhnaha
wa Ta’ala na kua ni wenye Taqwa na kuamini juu ya siku malipo na kuhesabiwa ndio
wenye Kutoa Sadaqah.
Na kutokana na kumuamini Mola wao na kuamini juu ya hayo basi hua ni wenye kutoa
miongoni mwa vile vinavyostahiki kutolewa kulingana na maamrisho yake Allah
Subhnah wa Ta’ala kwa kujali uzuri na ubora wa anachotoa kama alivyosema katika aya
ifuatayo:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُو ۤ اْ أَنْفِقُواْ مِن طَيِّبَاتِ مَا كَسَبْتُمْ وَممِ َّآ أَخْرَجْنَا لَكُم مِّنَ ٱلأَرْضِ
وَلاَ تَيَم َّمُواْ ٱلخَْبِيثَ مِنْهُ تُنْفِقُونَ وَلَسْتُمْ آبِخِ ذِيهِ إِلا َّ أَن تُغْ مِ ضُواْ فِيهِ وَٱعْلَمُ و ۤ اْ أَ َّن
ٱهلل ََّ غَنيِ ٌّ حمَِيدٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo anfiqoo min tayyibati ma kasabtum wamimma
akhrajna lakum mina al-ardhi wala tayammamoo alkhabeetha minhu tunfiqoona
walastum bi-akhidheehi illa an tughmidoo feehi waiAAlamoo anna Allaha
ghaniyyun hameedun (Surat Al Baqara 2:267)
284
Tafsir: Enyi mlioamini, toeni (Sadaqa) kutokana na kile mlichokichuma kwa halali na
kutokana na vile tulivyovizalisha kwa ajili yenu kutoka ardhini. Na wala msitoe kile
ambacho ni kibaya wakati nyinyi wenyewe hamtokubali kukipokea isipokua (labda
mtapokea) mkiwa mmefumba macho. Na Allah ni Tajiri anaejitosheleza na mwenye
kustahiki kusifiwa.
Na si kwa kujaalia Ubora na Uzuri tu lakini kutoa kulingana na uwezo wake mtu, bila
kujali kingi, kikubwa au kidogo kwani mtoaji hua ametoa kwa ajili ya kutafuta radhi za
Allah Subhanah wa Ta’ala ambae si mwenye kudharau kilichotolewa kabla ya kuangalia
Nia ya alietoa kisha ndio kuangalia kilichotolewa kama alivyosema katika aya ifuatayo:
﴿ٱل َّذِينَ يَلْمِزُونَ ٱلْمُط َّوِّعِينَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ فىِ الص َّدَقَاتِ وَال َّذِينَ لاَ يجَِدُونَ إِلا َّ
جُهْدَهُمْ فَيَسْخَرُونَ مِنْهُمْ سَخِ رَ ٱهلل َُّ مِنْهُمْ وَلهَُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴾
Alladheena yalmizoona almuttawwiAAeena mina almu/mineena fee alssadaqati
waalladheena la yajidoona illa juhdahum fayaskharoona minhum sakhira Allahu
minhum walahum AAadhabun aleemun (Surat At Tawba 9:79)
Tafsir: Ama wale ambao ni wenye kuzikejeli Sadaqa zilizotolewa na Waumini na wale
wasioweza kutoa isipokua kwa ikhlasi, basi Allah atawaadhirisha na kuwakejeli
nawatapata Adhabu kali sana
Ambapo anasema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Aya hii ilishuka pale
baada ya Abd Rahman Ibn Awf alipotoa Waqiah 40 za Dhahabu (Kumpa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kama Sadaqah yake kwa Uislam) na Sahaba
mwengine akatoa sehemu ndogo ya punje za Nafaka. Hivyo Wanafiq wakasema:
‘Wa Allahi Abd Rahman hakukusudia kufanya chochote isipokua kufanya Riya
katika kutoa kwake, na kuhusiana na yule mwengine basi Allah Subhanah wa Ta’ala
hana haja ya kimchango chake kidogo’’
Ambapo mtizamo mwengine ni ule usemao kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam aliitisha mchango wa Sadaqa, hivyo akatokea Mtu mweusi mwenye
muonekano usiopendeza akiwa na Ngamia wake mzuri sana na kumtoa Sadaqa.
Hivyo mmoja kati ya Wanafiq akasema: ‘Hakika Ngamia wake ni Mzuri kuliko
yeye mwenyewe’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamsikia na
akasema: ‘La, Bali yeye ni Mbora zaidi ya Ngamia wake na ni mbora zaidi yenu.’’
285
Ambapo amesema Abu Hurayrah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah
Alayhi wa Salam kua: ‘Kama mmoja wenu atatoa Sadaqa yenye ukubwa wa Kokwa
moja ya Tende kutokana na kichumo chake cha halali basi Allah Subhanah wa
Ta’ala huipokea kwa mkono wake wa kulia. Na kisha huyakuzisha malipo yake
kama vile mmoja wenu anavyomlea mtoto wa Farasi wake, hadi malipo hayo
yakawa makubwa sana kama Mlima’’(Imam Bukhari)
Kwani amesema pia Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
﴿آمِنُواْ بِٱهلل َِّ وَ رَسُولِهِ وَأَنفِقُواْ ممِ َّا جَعَلَكُم م ُّسْتَخْلَفِينَ فِيهِ فَٱل َّذِينَ آمَ نُواْ مِنكُمْ
وَأَنفَقُواْ لهَُمْ أَجْ رٌ كَ بِيرٌ ﴾
Aminoo biAllahi warasoolihi waanfiqoo mimma jaAAalakum mustakhlafeena feehi
faalladheena amanoo minkum waanfaqoo lahum ajrun kabeerun (Surat Al Hadid
57:7)
Tafsir: Aminini Allah (Subhanah wa Ta’ala) na Mtume wake (Salallahu Alayhi wa
Salam) na tumieni kutokana na kile tulichokujaalieni kua na Ukhalifa juu yake. Na
kwa wale walioamini miongoni mwenu na wakatumia tulichowapa basi watakua na
Malipo makubwa sana.
Hivyo ili tunufaike zaidi basi inabidi tujue ni Masikini gani ambao tusipohimizana
kuwalisha na kuwasaidia basi tutakua na masuali mazito ya kujibu, kwa sababu kwa
upande mmoja basi hali iko kama tunavyoona kua Uislam unakataza kuomba, hivyo jee
hawa Masikini wanaozungumziwa hapa ni Masikini wa aina gani?
Hivyo jibu la suali hili tunalipata pale tunapoangalia maneno ya Imam Abu Jafar
Muhammad Ibn Jarir At Tabari ambae anatuambia kua : ‘Amesema Abu Hurayra Radhi
Allahu Anhu kua : ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Masikini
wa kweli hua si yule ambae anaenda na kuwaomba watu kwa ajili ya Tende moja
mbili, au kwa kula chakula cha tonge moja au mbili, bali ni yule ambae anaeona
haya kuomba, soma kama unataka aya isemayo:
286
﴿لِلْفُقَرَآءِ ٱل َّذِينَ أُحصِرُواْ فىِ سَبِيلِ ٱهلل َِّ لاَ يَسْتَطِيعُونَ ضَرْابً فىِ ٱلأَرْضِ يحَْ سَبُهُمُ
ٱلجَْاهِلُ أَغْنِيَآءَ مِنَ ٱلت َّعَف ُّفِ تَعْرِفُهُم بِسِ يمَاهُمْ لاَ يَسْأَلُونَ ٱلن َّاسَ إِلحَْافاً وَمَا
تُنفِقُواْ مِنْ خَيرٍْ فَإِن َّ ٱهلل ََّ بِهِ عَلِيمٌ ﴾
Lilfuqara-i alladheena ohsiroo fee sabeeli Allahi la yastateeAAoona dharban fee alardhi
yahsabuhumu aljahilu aghniyaa mina alttaAAaffufi taAArifuhum
biseemahum la yas-aloona alnnasa ilhafan wama tunfiqoo min khayrin fa-inna
Allaha bihi AAaleemun (Surat Al Baqara 2:273)
Tafsir: (Sadaka hua ni) Kwa Mafukara ambao wamezuilika kwa ajili ya kujitolea kwa
ajili ya Allah, na hawawezi kutembea Ardhini (kwa ajili ya kufanya kazi au biashara),
na wale wasiowajua huwadhania kua ni Matajiri kutokana na kujiheshimu kwao.
Unaweza kuwajua kutokana na alama yao, hua hawawaombi watu kwa kukera, na
chochote kile mtakachotumia kwa ajili ya kheri basi Allah anajua juu yake’
Katika aya hii Allah Subhanah wa Ta'ala anatubainishia kua Wanaostahiki kupewa
Sadaqa kua ni wale ambao ni wenye sifa ya kua ni ‘Uhsiruu fii Sabli Allahi’ yaani
Wamezuilika kwa ajili ya kujitolea Katika Njia ya Allah.
Na tunapozungumzia kuhusiana na ‘Uhsiruu fii Sabli Allahi’ basi hua ni yenye
kuwaelezea wale Watu wenye Kuzuilika kutokana na kufanya Kazi zao za Kujitafutia
Maisha kwa sababu ya kua ni wenye Kujitolea kwa ajili ya Kupigania Njia ya Allah
Subhanah wa Ta'ala na hivyo basi tunapoyaangalia Maneno haya basi tunaona kua Ndani
yake wanaingia Wale watu ambao hua ni wenye kuacha yao na kisha wakawa ni wenye
kujitolea kwa Ajili ya Allah Subhanah wa Ta'ala.
Ambapo tunapowazungumzia watu wa aina hii basi wengi wetu hua ni wenye
kuwasahau, kwani hawa hua si wengine isipokua ni wale Maimamu wa Miskitini,
Wahudumu wa Miskitini, Walimu wa Madrasa wanao wanaowasomesha Watoto wa
Kiislam Dini yao, Wanafunzi wanotafuta Ilm ya Dni ya Kiislam, Waislam waliojitolea
kwa Ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala, na kisha wakawa na hali mbaya ya Maisha n.k
Hivi jee leo hii Wazee wangapi wanawalipia ipasavyo watoto wao Madrasa na hivyo
katika Kulipa kwao Ipasavyo kua ni wenye Kuwafikishia Sadaqa yao stahiki Walimu wa
Madrasa kutokana na kujitolea kwao kwa ajili ya Allah, Kama ilivyosema Aya?
287
Au Jee ni Waislam Wangapi katika Kutoa Kwao Misaada na Sadaqa hua
Wanawakumbuka Walimu wa Madrasa? Au ni Waislam wangapi katika Kutoa kwao
Misaada na Sadaqa hua wanawakumbuka Maimamu wa Miskiti wanaowasalisha, au
Waadhini, au Wahudumu wa Miskitini, n.k?
Kwani hawa wote wanajumuishia katika watu waliotajwa kwenye aya hii kua wanatakwa
wapewe kipaumbele katika kupewa Sadaqa kwa sababu ni mongoni mwa walio katika
hali ya Uhsiruu Fii Sabili Allah.
Na kisha kwa upande mwengine basi tunaona kua katika aya yetu hii kua Allah Subhanah
wa Ta'ala anatubainishia kua Wanaostahiki Sadaqa ni wale ambao ni wenye sifa ya kua
ni AlttaAAaffufi.
Ambapo neno alttaAAaffufi hua ni lenye kutokana na neno A'affa lenye kumaanisha
Kujizuia, Kujihifadhi, Kujidhibiti kutokana na kile ambacho kimekatazwa, Kujizuia na
kile ambacho ni Haram. Ambapo Neno TaA'affuf hua linamaanisha Kua na Heshima,
Kuona Haya au Kujizuia.
Na ili tufaham vizuri zaid kuhusiana na maana ya Neno hili na hivyo Kufaham sifa za
Masikini Stahiki kama ilivyozungumzia Aya basi na tuangalie mifano ifuatayo ambapo
mfano wa kwanza ni ule wa aya ambayo inasema:
﴿وَلْيَسْتَعْفِفِ ٱل َّذِينَ لاَ يجَِدُونَ نِكَاحاً حَتى َّ ٰ يُغْنِيَهُمُ ٱهلل َُّ مِن فَضْلِهِ وَٱل َّذِينَ يَبْتَغُونَ
الْكِتَابَ ممِ َّا مَلَكَ تْ أَيمَْانُكُمْ فَكَ اتِبُوهُمْ إِنْ عَلِمُتُمْ فِيهِمْ خَيرْ اً وَآتُوُهمْ مِّن م َّالِ ٱهلل َِّ
ٱل َّذِي ۤ آاتَكُمْ وَلاَ تُكْرِهُواْ فَتَيَاتِكُمْ عَلَى ٱلْبِغَآءِ إِنْ أَرَدْنَ تحََص ُّناً لِّتَبْتَغُواْ عَرَضَ ٱلحَْيَاِة
ٱلد ُّنْيَا وَمَن يُكْرِههُن َّ فِإِن َّ ٱهلل ََّ مِن بَعْدِ إِ كْ رَاهِهِن َّ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
WalyastaAAfifi alladheena la yajidoona nikahan hatta yughniyahumu Allahu min
fadlihi waalladheena yabtaghoona alkitaba mimma malakat aymanukum
fakatiboohum in AAalimtum feehim khayran waatoohum min mali Allahi alladhee
atakum wala tukrihoo fatayatikum AAala albigha-i in aradna tahassunan
litabtaghoo AAarada alhayati alddunya waman yukrihhunna fa-inna Allaha min
baAAdi ikrahihinna ghafoorun raheemun(Surat An Nur 24:33)
Tafsir: WalyastaAAfifi (Na Wajizuie Kwa Kujihifadhi na Yaliyokatazwa) Wale Ambao
hawana Uwezo (Wa Kifedha) Kwa ajili ya Kuoa hadi Pale Watakapowezeshwa na
288
Allah kutokana na Fadhila zake (Neema zake) Na miongoni mwa mnaowamiliki
wakitaka kuandikiwa mkataba wa uhuru wao, waandikieni hivyo, ikiwa mnawajua
kua ni waaminifu. Na wapeni baadhi ya mali zenu zinazotokana na utajiri wa Allah
aliokupeni juu yenu. Na msiwalazimishe kufanya ukahaba, ikiwa wanataka usafi, ili
mpate kunufaika kidunia. Lakini ikiwa mmoja wenu atawalizimisha (kufanya
ukahaba), basi baada ya kulazimishwa huko, Allah ni mwenye kusamehe na ni mwingi
wa rehma (Atawasamehe wanawake hao kutokana na kulazimishwa kwao kufanya
dhambi hiyo).
Kwani hii ni aya ambayo inafafanuliwa na ile Hadith ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam isemayo kua: ‘Ndoa ni sehemu ya Sunnah yangu, yeyote yule asietekeleza
Sunnah yangu basi hua si Miongoni mwangu. Hivyo Oaneni kwani kwa Hakika
mimi nitajisifia wingi wenu kiidadi mbele ya Ummah Nyengine. Hivyo kila mwenye
uwezo na Aoe na asiekua na Uwezo basi na Afunge, kwani funga humzuilia Hamu
yake’(Imam Ibn Majah)
Na akasema tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kuna watu wa aina tatu
ambao msaada juu yao hua wenye kusaidia kusimamia jukumu la Allah. Kumsaidia
yule anaetaka kuoa, kumlipia Mtumwa ili awe huru na Kumlipia Mtu anaepigania
kwa ajili ya njia ya Allah’(Imam Ibn Majah, Imam At Tirmidhii)
Nadhani tumefahamiana maana ya aya yetu kulingana na Ufafanuzi wa Hadith hii na
tunapoangalia mfano wa pili wa aya iliyotumia neno A’affa basi tunakutana na ule wa
mfano wa aya ya Tabbaruj ambayo inasema:
﴿وَٱلْقَوَاعِدُ مِنَ ٱلنِّسَآءِ ٱل َّلاَتِى لاَ يَرْجُونَ نِكَاحاً فَلَيْسَ عَلَيْهِن َّ جُنَاحٌ أَن يَضَعْنَ
ثِيَابَهُن َّ غَيْرَ مُتَبَرِّجَاتِ بِزِينَةٍ وَأَن يَسْتَعْفِفْنَ خَيْرٌ له َُّن َّ وَٱهلل َُّ سمَِيعٌ عِلِيمٌ ﴾
WaalqawaAAidu mina alnnisa-i allatee la yarjoona nikahan falaysa AAalayhinna
junahun an yadaAAna thiyabahunna ghayra mutabarrijatin bizeenatin waan
yastaAAfifna khayrun lahunna waAllahu sameeAAun AAaleemun(Surat An Nur
24:60)
Tafsir: Na Kwa wale (Wazee waliopitiliza Umri wa Kutokua na Matamanio ya
Kuingiliana) Miongoni mwa Wanawake ambao Hawategemei Kurudi Katika Maisha
ya Ndoa basi Hua Hakuna Makosa Juu yao kama Wakiwacha Nguo zao bila ya
Kutoonesha Mapambo yao lakini kama YastaAaffifna (watajizuia na Kuihifadhi) basi
hua ni kheri kwao, Na Allah ni Mwingi wa Kusikikia na Mwingi wa Kujua
289
Ambapo aya hii ya Surat An Nur 24:60 inabainisha kua kwa Wanawake ambao washakua
Wazee na hawavutii tena Miili yao na hawana Matamanio ya Kimwili na hivyo hawana
haja wala hamu ya kutaka kuolewa tena basi wanaruhusika kutojihifadhi, kwa kuvaa
nguo za kawaida tu bila ya kujitanda, ila kama Wanawake hao YastaAAfifna (watajizuia
na Kuihifadhi) basi hua ni bora kwao, na kwa hakika Allah Subhanah wa Ta’ala ni
mwingi wa kusikia na kujua.
Yaani Hili ni Onyo kua Wanawake wasichukue Kisingizio cha Kua anajiona kua
ameshakoma Hedhi Labda na hivyo hataki Kuolewa akasema kua hana hata hamu ya
Matamanio ya Kimwili lakini Hapo hapo Mwili wake Unavutia Wazee wenzake au vijana
pia wanaopenda Wazee na hivyo Mwanamke huyo akauwacha wazi Makusudi Mwili
wake huo bila ya kujistiri ipasavyo ili kuonesha Uzuri wa Maumbile Uonekane wazi.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta'ala katika Onyo hili basi anaweka wazi kua yeye ni
mwenye kusikia yanayosemwa na Nyoyo za kila Kiumbe wakiwemo Wanawake hao na
mimi na wewe pia.
Hivyo anajua Nia yako ni ipi, na hata kama Mwanamke akiwa hana nia hio ya kujionesha
lakini pia hapo hapo tumesema kua kuna wazee wa Kiume ambao wanapenda Wazee
wenzao, na pia kuna Vijana ambao wanavutiwa na Wanawake wazee kwani hua
wanasema kua Ng’ombe hazeeki Maini. Na ndio maana Allah Subhanah wa Ta'ala
akasema kua Kama Wanawake hao watajiheshimu na kujihifadhi basi ni kheri kwao.
Hivyo hii ni mifano ya maana ya neno AlttaAAaffufi. Lililotumika kwenye ya 273 ya
Surat Al Baqara inayoelezea aina za watu Masikini wenye kustahiki kupewa Sadaqah,
kwani hawa hua ni wenye kujiheshimu, wenye kukinai na wenye kuridhika na Majaaliwa
ya Mola wao juu yao na hivyo hua ndio wenye kujua maana ya ile aya isemayo:
﴿وَأَن َّهُ هُ وَ أَغْنىَٰ وَأَقْنىَٰ ﴾
Waannahu huwa aghna waaqna(Surat An Najm 53:48)
Tafsir: Na kwa hakika ni yeye (Allah Subhanah wa Ta’ala) ndie mwenye kutoa kingi
kinachotosheleza (kinachotajirisha) na kidogo kinachokinaisha.
Naam bila ya shaka, kwani ukijua maana ya maneno ya aya hii na kuyatafakkari basi
utakua ni Mtu mwenye Kutosheka na pale Allah Subhanah wa Ta'ala anapokumwagia
Rehma na Neema zake kwa wingi, na hivyo utakua ni mwenye kuonesha Shukrani kwa
kuzitumia ipasavyo neema hizo katika njia ya Kukunufaisha wewe na Viumbe wenzako
290
Na hapa ndani yake haiingia Mali tu au pesa, bali pia ndani yake inaingia Afya, Cheo,
Madaraka, Mamlaka, Umoja katika jamii yako ya Kiislam n.k. Naam..hio ni katika hali
ya Aghna yaani ya Kutajirishwa au Kutoshelezwa na Neema kutoka kwa Mola wako.
Ambapo tunapoangalia kwa upande wa Aqna basi hua ni Kukinai yaani pale unapopewa
Kitu kiasi chako, au kidogo zaidi ya mahitaji yako, na kisha ukawa na mtizamo wa kua
kwako wewe ni muhimu kupata hicho ulichopata kuliko kukosa kabisa kwani angalau ya
kua wewe umepata hicho kidogo kwani kuna wengine hawakupata. Na katika kukinai pia
ndani yake mnaingia kila Rehma na Neema ya kila kitu ulichopewa na Mola wako, na
hivyo kua ni mwenye kuridhika na Mjaaliwa yake juu yako kwa ni yeye ndie mwenye
kujua kilicho bora kwako, hivyo kua na Subra kwako na kushukuru basi hua ni bora
kwako
Hivyo hii ndio hali waliyokua nayo watu Masikini waliozungumziwa kwenye aya yetu
ya Surat Al Baqara 2:273, Hua ni wenye sifa ya AlttaAaffuf ya Kujizuia na kua na Subra
kwani wanajua kua vyovyote vile itakavyokua basi wao wamekinai kwani kutokana na
makadirio ya Allah Subhnah wa Ta’ala hio ni kheri kwao.
Kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Watu wa Peponi ni wa
aina tatu:
1-Mtu mwenye Mamlaka na akawa Muadilifu, na mwenye kutoa Sadaqah na
Muongofu.
2-Mu mwenye huruma na Moyo Mlaini kwa Ndugu zake na Waislam wenzake.
3-Mtu aliekua msafi na asieomba Msaada ingawa ana watoto wengi’(Imam Muslim)
Kwani anasema Abu Said Al Khudri Radhi Allahu Anhu kua: ‘Safari Moja sisi tulikua
tuna hali mbaya sana. Hivyo kuna Mtu akaniambia kua nikaonane na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kumuomba msaada
Hivyo Nami nikafuata Ushauri huo na kutoka hadi kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam lakini nilipofika tu kwake basi nikamsikia anasema kua: ‘Mtu yeyote yule
atakaefanya TaAaffuf kujizuia kutokana na Kuomba basi Allah Subhanah wa
Ta'ala atamuokoa Mtu huyo kutokana na Kuomba, Mtu yeyote yule atakaemuomba
Allah Subhanah wa Ta'ala riziki kutoka kwake, basi Allah Subhanah wa Ta'ala
atamruzuku Mtu huyo. Lakini Hata Hivyo Mtu akituomba basi tusimkatalie
Kumpa pale inapokua tunao Uwezo wa Kumsaidia.’
Abu Said Al Khudhri Radhi Allahu Anhu anaendelea kusema kua Hivyo Nami
nikaiambia Nafsi yangu kua: ‘Kwanini mimi nisifanye TaAaffuf (Kujizuia Kuomba),
291
na hivyo Allah Subhanah wa Ta'ala akanijaalia Mimi kupata Uokovu wa Kua si
miongoni mwa wenye Kuomba?
Hivyo nami nikarudi Nyumbani na tangu siku hio basi nikaiahidi Nafsi yangu kua:
‘Hakika mimi sitomuomba Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa chochote
Kile hadi utakapofika Mwisho wetu hata kama Dunia itatuangukia juu yetu au
itatuzamisha ndani yake, Isipokua kwa yule atakaenusuriwa na Allah Subhanah wa
Ta'ala miongoni mwetu.’
Naam, ndani ya tukio hili tunatakiwa tuzingatie namna Masahaba walivyokua Wakiishi
na kufuata Maamrisho ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika kufanya
Ta'aAaffuf, yaani kujizuia kutokana na waliyokatazwa na Allah Subhanah wa Ta'ala na
pia na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Kwani anasema Mujaddid Ad Din, Sultan Al Mutakallimin Imam Al Mushaqiqin, Imam
Al Ghazali Al Thani Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Al Husayn Ibn Umar Fakhr
Ad Din Al Razi kuhusiana na aya hii ya 273 ya Surat Al Baqara kua:
‘Aya inatubainishia kua Masikini hawa waliotajwa hapa ni huwezi kuwajua
kutokana na Muonekano wao bali utaweza kuwajua kutokana na Roho na Nyoyo
zao, kwani kama vile ambavyo haiwezekani kuonekana kwa Khofu ya Mwili wa
Mnyama wa Mwituni pale anapokua katika hali ya kua ni mwenye kumuona Simba
na kumuogopa.
Na hii ni kwa sababu sio Wanyama wengi ambao tayari wameshawahi kukumbana
na Nguvu na purukushani za Simba anapovamia. Hivyo ndivyo pia inavyokua hali
ya Watu hawa, ambao huweza kujulikana kutokana na Utulivu wa Nyoyo na Roho
zao ambayo hua ni katika hali ya Upekee wa Kimaumbile ambao ndio
zinazowadhihirisha sifa zao.’
Kwani Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi anaendelea kutubainishia kwa njia
ya kuhoji kua: Kama imeshawekwa wazi kua hali yao ya Al TaaAaffuf - yaani ya
Kujizuia Kuomba ndio Alama yao basi inakua inamaanisha nini kua Hawawaombi
watu kwa njia ya Kukera?
Naam..kwa sababu kuna watu wasiokua na TaAaffuf hua wanaomba kama Ruba yaani
akikuganda kwa ajili ya kukuomba basi hakuganduki mpaka umpe sadaka yake, yeye
hafikirii kua labda na wewe hua una matatizo yako, la, kwani hua ana ubinafsi wa
kujifikiria yeye tu kiasi ya kua Ukimuona tu au ukiona simu yake basi unaanza kusema
Astaghfir Allah!. Kwa sababu unakua unajua kua sasa hivi nafikwa na Mtihani ambao ili
kuuepuka basi inabidi niseme Uongo, au nafikwa na Mtihani huu kwa sababu ya
Madhambi yangu..nk.
292
Na hii ndio hali ambayo Waislam hatutakiwi kua nayo, yaani ya Mtu kua anaomba mpaka
anawakera wale anaowaomba, na hivyo kujipatisha dhambi za bure Muombaji na pia
kumsababishia dhambi mwenye kutoa Msaada, kwa sababu tayari mtu keshakua anatoa
kwa kusikitika inamaana kua yeye hapati thawabu kwa kutoa kwake na wewe unapata
dhambi kwa kumsababishia Udhia mwenzako.
Kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Watu wa aina tatu
hatozungumza nao Allah Subhanah wa Ta’ala katika siku ya Malipo, wala
hatowaangalia na wala hatowasafisha:
1-Wenye Kibri
2-Wenye kutoa Sadaqa huku wakiwa ni wenye kulalamika na kukumbushia juu ya
ukarimu wao.
3-Wale wanaouza bidhaa na kuapa uongo’(Imam At Tirmidhii)
Hivyo Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi anaendelea kutupa Majibu ya suali
lake ambalo wengi huenda walijiuliza kua. ‘Kama Aya imesema kua wanajizuia
Kuomba, sasa inakuaje kua hapo hapo inasema Hawaombi kwa kukera?’
Ambapo jibu la suali hili ni kua: ‘Kinachoelezewa hapa hua sio Sifa yao watu hao kua
ni wenye kuomba kwani Tayari aya imeshasema kua Watu hawa wanafanya
TaaAaffuf yaani Wanajizuia na Kuomba. Hivyo basi haya Maneno yasemayo kua
Hawawaombi watu kwa kukera yanawalenga wale Wanaoomba kua hawatakiwi
kuomba hadi kufikia hali ya kua ni wenye Kukera.’
Mujaddid Ad Din Fakhr Ad Din Al Razi anaendelea kutufafanualia kwa kusema kua:
‘Yaani hapa hali inakua kama vile ambavyo Mtu umekaa kwako, kisha wakaingia
watu wawili, Ambapo mmoja wao akiwa ni Mtu Mwema na mwengine ni Mtu
Muovu, kisha wewe ukawa ni mwenye kumsifu yule Mtu Mwema kwa kusema kua:
‘Mashaa Allah, Una sifa nzuri zilizo Njema sana’
Na kisha hapo hapo ukamwambia na yule Mtu Muovu kwa kusema: ‘Lakini na
wewe pia si Muovu’ Ambapo katika kusema kwako huko kumwambia Mtu huyo
Muovu kua na yeye si Muovu, basi hua kunamaanisha kua Mtu huyo ni Muovu.’
Na amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Allah Subhanah wa Ta'ala
hapendezewi na Mambo Matatu:
1-Mazungumzo yasiyokua na Maana.
293
2-Kufanya Israfu katika Mali.
3-Kuomba Omba watu kwa Kukera’ (Imam Muhammad Ibn Jariri At Tabari)
Ambapo anasema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Abd Allah Al Hakim al
Nishapuri kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, Alipohimiza kutoa Sadaqa
basi mmoja kati ya Masahaba akasema: ‘Ya Rasul Allah Mimi nna Dinar Moja!
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hio Itumie kwa ajili ya Nafsi
yako’
Kisha Mtu huyo akasema: ‘Na Nikiwa nna moja zaidi?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Itumie kwa ajili ya Mke wako’
Mtu Huyo akasema: ‘Na Kama nikiwa na Moja zaidi?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Itumie kwa ajili ya Watoto wako’
Kisha Mtu huyo akasema: ‘Na kama nikiwa na moja zaid?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hio sasa unajua vizuri ni nani
anaestahiki zaidi’
Naam..hivyo aya inatuonesha kua Kila utakachokua nacho na kukitumia basi Allah
Subhanah wa Ta'ala anajua juu yake, na anajua juu ya nia yako. Ambapo hadithi hii
inatuonesha ni nani anaestahiki kupata sadaqa yako kutoka kwako kulingana na Uwezo
wako.
Na Ndio Maana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia Sahaba wake huyu
kua kwanza aanze na Nafsi yake, Kisha kwa ajili ya Mkewe, kisha kwa ajili ya Watoto
wako, kisha ndio utoe Sadaqa kwa watu wengine. Na hivyo sio Unatoa sadaka
kuwasaidia Omba omba ili watu wakuone halafu Watoto wako Nyumbani wanalia Njaa.
Hii inakua ni Dhambi badala ya Thawabu Au Unatoa halafu Ukaombe ili Utoe tena, Au
huna kisha unapewa kisha nawe Unatoa ili upewe tena. Hii pia hua haifai
Kwani amesema tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Sadaqah bora ni ile
inayotumiwa kutokana na ziada, mkono wa Juu (Unaotoa) ni bora kuliko wa chini
(Unaopokea) na anza (kwa kumpa) yule mwenye familia kubwa zaidi’ (Imam
Bukhari)
294
Na katika Hadith nyengine pia basi amesema Abdallah Ibn Jabir Radhi Allahu Anhu kua:
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua amekaa na Masahaba zake mara
akaja mmoja miongoni mwa Masahaba huku akiwa na Kipande cha Dhahabu,
kama yai na kisha akasema: ‘Ya Rasul Allah Pokea hiki kua ni kama Sadaqa yangu,
na nnaapa kua sina kitu chengine Hapa Duniani zaidi ya hii Dhahabu.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akageukia upande wa pili. Ambapo Sahaba
huyo akamfuata upande huo aliogeukia, hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akageukia tena Upande Mwengine.
Sahaba huyo akamfuata Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika upande huo
huo tena, Huku akimpa Dhahabu hio.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaichukua Dhahabu hio halafu akaitupa
huku akisema: ‘Mtu anakuja kwangu mimi akiwa na kile tu anachokimiliki na
kutaka kukitoa Sadaqa halafu baada ya kukitoa anakaa chini na Kuanza Kua
Omba Omba..Sadaka Inatakiwa itoke kwenye Kilicho cha ziada!’ (Imam Muhammad
Ibn Jarir At Tabari)
Ambapo kwa upande mwengine basi ingawa haipendekezwi kuwapa Sadaqa watu
wasiokua na sifa stahiki ya kusaidiwa lakini hapo hapo, kama itakua kutoa sadaqa huko
kutasaidia kubadilisha aina za hali za watu hao basi hua inakubalika kwa mfano kama
inavyowekwa wazi na hadithi ifuatayo:
‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kuna mtu alisema kua:
‘Nitatoa Sadaqah’ hivyo siku ya pili akatoka na kumpa Sadaqah Mwizi, na watu
wakasema, : ‘Amempa Sadaqah Mwizi’ hivyo mtu huyo akasema: ‘Ya Allah,
Alhamd lillah kua nimempa Sadaqah Mwizi.’
Na siku ya pili usiku akampa pesa Mwanamke mzinzi na watu wakasema, :
‘Amempa Sadaqah Mzinzi’ hivyo mtu huyo akasema: ‘Ya Allah, Alhamd lillah kua
nimempa Sadaqah Mzinzi.’ na siku ya tatu asubuhi akampa pesa Tajiri na watu
wakasema : ‘Amempa Sadaqah Tajiri’ hivyo mtu huyo akasema: ‘Ya Allah,
Alhamd lillah kua nimempa Sadaqah Mwizi, Mzinzi na Tajiri.’
Hivyo akaambiwa: ‘Ama kuhusiana na Sadaqah aliyopewa Mwizi, basi labda
itamfanya asiibe, Ama Sadaqah aliyopewa Mzinifu basi Labda itamfanya Asizini
na aliyopewa Tajiri basi labda itamfanya awe ni mwenye kuingiwa na ari na hivyo
kutoa kutokana na kile alichoneemeshwa na Allah.’’(Sahih Bukhari na Sahih Muslim)
Hivyo baada ya Allah Subhanah wa Ta’ala kuwazungumzia wale wasiohimizana kutoa
na kuwasadia Masikini katika aya 3 za mwanzo za Sura hii ya Al Maun na kuwajumuisha
295
kua ni miongoni mwa wanaokadhibisha Dini basi Allah Subhnah wa Ta’ala anaendelea
kwa kujumuisha ndani yake kwa kuwazungumzia Wanafiq ambao ni wale wenye sifa ya
Aaan Salatihim Sahun kama zinavyosema aya;
ف َوَيْلٌ لِّلْمُ ﴿ صَلِّ ينَ ۞ ٱل َّذِينَ هُمْ عَن صَلاَهتِِمْ سَاهُونَ ﴾
Fawaylun lilmusalleena; Alladheena hum AAan salatihim sahoona; (Surat Al Maun
107:4-5)
Tafsir: Na Kisha Ole Wao wale Wenye Kusali. Wale Ambao juu ya Sala zao Sahuna
(Wanazidharau na kuzichelewesha kwa kutosali katika wakati wake).
Ambapo aya hizi zimewajumuisha watu waliomo kwenye makundi yafuatayo:
Wale wasiosali Kabisa.
Wale wanaosali lakini si ndani ya wakati wake Sala hio bali ni nje ya wakati wa
Sala.
Wale wanaosali lakini hawasimamishi Nguzo za Sala.
Wale ambao hawana Kushuu ndani ya Sala.
Ambapo kulingana na mtizamo wa Sa’ad Ibn Abi Waqqas Radhi Allahu Anhu basi yeye
anasema kua: ‘Kilichokusudiwa hapa si kukosekana kwa Khushuu bali ni kulingana
na kudharau wakati wa Sala mpaka unapokua umepita.’
Na kwa upande wa Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, basi anasema
kua: ‘Hii inahusiana na Kutosali kabisa, jambo ambalo lilikua linafanywa na
Wanafiq, yaani walikua wanasali wanapokua pamoja na watu lakini wanapokua
peke yao hua hawasali’
Na kwa upande wa Imam Mujahid Ibn Sulayman, Imam Qatadah Al Sadusi, na Jabir Ibn
Zayd basi wao wanasema kua: ‘Hii inahusiana na wale ambao ni wenye kuzidharau
Sala zao kwa kusali pale tu wanapopenda kusali na wasipotaka basi hua hawasali’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amewazungumzia wale ambao ni wenye
kuzidharau Sala zao kua ni Wanafiq ambao wamezungumziwa na aya ifuatayo:
296
﴿إِن َّ ٱلْمُنَافِقِينَ يخَُادِعُونَ ٱهلل ََّ وَهُوَ خَادِعُهُمْ وَإِذَا قَامُو ۤ اْ إِلىَ ٱلص َّلاَةِ قَامُواْ كُسَالىَٰ
يُرَآءُونَ ٱلن َّاسَ وَلاَ يَذْكُرُونَ ٱهلل ََّ إِلا َّ قَلِيلاً ﴾
Inna almunafiqeena yukhadiAAoona Allaha wahuwa khadiAAuhum wa-idha
qamoo ila alssalati qamoo kusala yuraoona alnnasa wala yadhkuroona Allaha illa
qaleelan(Surat An Nisaa 4:142)
Tafsir: Na kwa hakika Wanafiq wanataka kumfanyia hadaa Allah, lakini Allah ndie
anaewahada wao. Na wanaposimama kusali hua wanasimama kwa uvivu ili
waonekane na watu, na hawamkumbuki Allah (Ndani ya Sala zao) isipokua kidogo tu.
Ambapo amesema Anas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Hio ni Sala ya Mnafiq, hua ni mwenye kusubiri hadi Jua
linapotua baina ya ncha mbili za pembe za Shaytan, halafu ndio haraka sana
hukimbilia kudonoa ardhini mara nne na hivyo hua ni mwenye kumkumbuka
Allah kwa mda mfupi sana’(Sahih Muslim)
Ambapo amesema Ata’ Ibn Dinar kua: ‘Alhamd lillah kua Allah Subhanah wa Ta’ala
amesema katika aya hizi kua ‘Wale ambao ni wenye kua na dharau ndani ya Sala
zao, bali amesema: ‘Wale wenye kudharau Sala zao’ kwani hakuna hata mmoja
miongoni mwetu ambae si mwenye kukosa au kupungukiwa na umakini kwenye
Sala.’
Na Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari amesema kua: ‘Hali hii hua
inaonekana na wengi sana miongoni mwa wale ambao ni wenye kujidai kua wao ni
Waislam (lakini huku Nyoyo zao zikiwa zimezongwa na Matamanio ya kidunia),
Unapokua pamoja nao basi utaona kua hawana wanachokizungumzia isipokua
Dunia yao, na hivyo hua hawamkumbki Allah Subhanah waTa’ala isipokua kidogo
tu.’
Ambapo Allah Subhana wa Ta’ala amezungumzia tena kuhusiana na Unafiq wa wale
wanaosali kwa kusema tena katika Qur’an:
﴿وَمَا مَنَعَهُمْ أَن تُقْبَلَ مِنْهُمْ نَفَقَاتُهُمْ إِلا َّ أَن َّهُ مْ كَ فَ رُواْ بِٱهلل َِّ وَبِ رَسُولِهِ وَلاَ َْتُونَ
ٱلص َّلواَةَ إِلا َّ وَهُمْ كُسَالىَٰ وَلاَ يُنفِقُونَ إِلا َّ وَهُمْ كَارِهُونَ ﴾
297
Wama manaAAahum an tuqbala minhum nafaqatuhum illa annahum kafaroo
biAllahi wabirasoolihi wala ya/toona alssalata illa wahum kusala wala yunfiqoona
illa wahum karihoona(Surat At Tawba 9:54)
Tafsir: Na kitu gani kinachosababisha kisikubaliwe kile wanachokitoa wao isipokua
ni kua wao hawakumuamini Allah na Mtume wake (Salallahu Alayhi wa Salam). Na
hawaji kusali isipokua wanakua katika hali ya uvivu, na hawatoi kitu isipokua wakiwa
katika hali ya kukirihishwa.
Tunapoziangalia aya hizi basi tunaona kua katika kuelezea sala za Wanafiq hao
wanapokua wanasali basi aya mbili hizi zote zimetumia neno Kusala ambalo hua
linamaanisha Kua Mvivu, Kuregea, kutokua na Umakini, kua Mzito, Kua na Ajizi.
Ambapo hii hua ni sifa mbaya sana yenye madhara makubwa kwa Muislam kua Kaslan
basi amesema Malik Ibn Anas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallau Alayhi wa
Salam alikua akiomba Dua kwa kusema: ‘Allahumma inni a'udhu bika minal-'ajzi,
wal-kasali, wal-jubni, wal-hirami, wa a'udhu bika min 'adhabil-qabr wa a'udhu bika
min fitnat al-mahya wal-mamat’’ yaani Ya Allah hakika mimi natafuta hifadi yko
kutokana na Kua na Ajizi, Kua Kaslan (Mvivu), kutokana na kua Mwoga na kua
na Uzee, kutokana na Adhabu ya Kaburi na kutokana na Mitihani ya Maisha na
Mauti’(Sahih Bukari)
Na ndio maana kwa upande wa Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari akasema
kua: ‘Aya imetumia neno Kusala ambalo wingi wake hua ni Kaslan yaani watu
ambao ni Wavivu, na hivyo basi Muumini wa kweli hatakiwi kua ni mwenye kusema
kua alikua ni Kaslan kuhusiana na mambo mema ya kheri ambayo hakuyafanya.’
Na kwa upande wa Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye anasema
kuhusiana na maana ya aya hizi kua: ‘Hawa ni wale watu ambao hua ni wenye kusali
katika Sala za Jamaa wanapokua mbele za watu lakini wanapokua peke yao hua
hawasali, na hivyo kutuwekea wazi kua, vitendo vya Ibada inatakiwa viwe ni vyenye
kutoka kwenye Nyoyo na hapo ndio vitamridhisha Allah Subhanah wa Ta’ala. Na
hivyo kama havikufanywa kutokana na ndani ya Nyoyo basi hua havina manufaa
yeyote, bali hua ni vyenye kua na madhara badala yake.’
Ambapo amesema Abu Qatadah Radhi Allahu Anhu amesema kua : ‘Amesema Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hakuna Mwizi mbaya kuliko yule anaejiibia
kutoka kwenye Sala zake.’ Abu Qatadah Radhi Allahu Anhu akauliza: ‘Itakuaje Mtu
ajiibie kutoka kwenye Sala zake?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema
kua: ‘Kwa kutorukuu na kusjudu ipasavyo’(Mustadrak Al Hakiim)
298
Kwa upande wa Hudhayfah Ibn Al Yaman Radhi Allahu Anhu basi yeye alisema kua:
‘Jihadharini na Khushuu ya Mnafiq’ na alipoulizwa: ‘Ndio nini Khushuu ya
Mnafiq?’ basi Hudhaifah Ibn Al Yaman Radhi Allahu Anhu alisema: ‘Wakati Kiwili
wili kinapokua na Khushuu lakini Moyo ukiwa hauna Khushuuu. ’
Hudhayfah Ibn Al Yaman Radhi Allahu Anhu alisema pia kua ‘Kitu cha Mwanzo
ambacho kitaondoka kwenye kwenye Dini yenu hii ni Khushuu, na kitu cha Mwisho
ambacho mtakipoteza kwenye Dini yenu ni Sala, ambapo mtamuona Mtu anasali
lakini akiwa hana jema ndani yake na kisha itafikia wakati mtakua mnaingia
Misikitini na hamto muona hata mtu mmoja wenye Khushuu ndani yake.’
Na Abu Abd Allah Al Ashari Radhi Allahu Anhu amesema kua : ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam Mtu anaesali bila ya kurukuu na kusjudu ipasavyo hua
ni sawa mtu mwenye njaa sana. Kisha akala kokwa moja au mbili za Tende. Hua
hamsaidii kitu kabisaa’(Imam At Tabarani)
Kwani Sala ndio Msingi wa Jengo la Dini ya Kiislam, hivyo kama Ukiwa na Umakini
katika Kuusimamia Ujenzi wa Msingi huo na ukawa Imara basi hata ujengewe Ghorofa
ngapi za Mitihani Juu yake basi bado Uislam wako Utakua Imara. Na pia ndivyo
utakavyokua Imara Uislam wa wale waliochini yako kama utawasimamia katika Sala
zao.
Na hii ni kutokana na ile aya ya Surat Al Ankabuut ambayo inasema:
﴿ٱتْلُ مَا أُوْحِ ىَ إِلَيْكَ مِنَ ٱلْكِتَابِ وَأَقِمِ ٱلص َّلواَةَ إِن َّ ٱلص َّلواَةَ تَنْهَى ٰ عَنِ ٱلْفَحْشَآءِ
وَٱلْمُنْكَرِ وَلَذِكْرُ ٱهلل َِّ أَكْبَرُ وَٱهلل َُّ يَعْلَمُ مَا تَصْنَعُونَ ﴾
Otlu ma oohiya ilayka mina alkitabi waaqimi alssalata inna alssalata tanha AAani
alfahsha-i waalmunkari waladhikru Allahi akbaru waAllahu yaAAlamu ma
tasnaAAoona (Surat Al Anqabut 29:45)
Tafsir: Wasomee (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) Kile tulichokushushia
kutoka ndani ya Kitabu, Na simamisha Sala, kwani kwa hakia Sala Inazuia ufanyaji
Dhambi za Matamanio na Maasi ya Kufr, na kumkumbuka llah ni kukubwa kimalipo
na Allah ni mwenye kujua juu ya Mnayoyafanya.
Hivyo bila ya shaka kama Msingi wa Jumba la Imani ya Kiislam kwa upande wa Sala
zako ukiwa Mbovu basi bila ya shaka Nyumba ya Imani yako itakua ni yenye
299
Kuporomoka, na hivyo kuna hatari ya kuangukia kwenye Unafiq na pia kwenye kua ni
Miongoni mwa wenye Kukadhibisha Dini na Siku ya Malipo na hivyo bila ya shaka
Hutakua na Mwisho Mwema.
Kutokana na aya hizi na hadith basi ndio tunaona umuhimu wa kutoona Uvivu katika
kufanya Ibada na pia kutuonesha umuhimu wa kua na Unyenyekevu kwenye Ibada kwani
kutokana nao Unyenyekevu huo yaani Khushuu ndio hupatikana mafanikio ya Dunia na
Akhera kama anavyosema Hasan Al Basr pale alipousia:
‘Tafuteni Utamu unaopatikana katika Mambo matatu. Jambo la kwanza ni utamu
wa ndani ya Sala, Utamu wa Kufanya Dhikr Allah na Utamu wa Kusoma Qur’an,
kwani Utamu wake vitu hivi hupatikana ndani yake, na ukiupata ndani yake basi
fahamu kua Mlango wa Peponi uko wazi kwa ajili yako, na kama ukiukosa basi
Mlango wa Peponi umefungwa kwa ajili yako.’
Ambapo katika hadith nyengine basi tunaona kua amesema Abu Said Al Khudhri Radhi
Allahu Anhu kua kuhusiana na kua na umakini na unyenyekevu ndani ya Sala kua:
‘Wakati mmoja wenu anapoenda miayo ndani ya Sala, basi na ajizuie kwa kadri
atakavyoweza, ili shaytan asiingie ndani ya mdomo wake’(Sahih Muslim)
Na akasema tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Sala Tano ambazo Allah
Subhanah wa Ta’ala amezifaridhisha, basi kila atakaetia udhu ipasavyo kwa ajili
yake na kisha akasali kwa wakati wake, na akarukuu kikamilifu huku akiwa na
unyenyekevu, basi imeahidiwa na Allah Subhanah wa Ta’ala kua atasamehewa,
lakini kwa yeyote yule ambae hatofanya hivvyo basi hua hakuna ahadi hio kwa ajili
yake yaani kama Allah akitaka atamsamehe na kama akitaka atamuadhibu’(Sunan
Abu Daud)
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anaendelea kutuambia katika Hadith nyengine
kuhusiana na kudharau Sala kwa kusema: ‘Hakika Mja anaweza kusali na kisha
akawa hakupata chochote kutokana nayo Sala hio isipokua sehemu ya 10 ya Sala
hio, au 9 au 8 au 7, au 6 au 5 au Robo au Nusu’(Musnad Imam Ahmad)
Ambapo amesema Hasan Al Basr kua: ‘Kama itakua huijali Sala yako, basi utakua
unajali nini zaidi yake? Kwa sababu kila unapokua unaijali Sala yako basi ndio
unavyojaaliwa kuyarekebisha maisha yako, hivi jee hamjasikia kua Sala
imeambatanishwa na Mafanikio? Pale inaponadiwa ‘Hayya aAala Al Salah Hayya
Aala al Falah!’ yaani ‘Njooni katika Sala, Njooni katika Mafanikio’ hivi jee
Utamuombaje Allah Subhanah wa Ta’ala akupe Mafanikio wakati hutimizi wajibu
wako kwake?’
300
Hivyo ili nasi tupate mafanikio kwenye Sala na Dua zetu kama alivyojaaliwa mafanikio
ya dua zao Hannah Bint Faqudh na Nabii Zakarriyah basi na tuangalie umuhimu wa
kujaribu kua na Unyenyekevyu kwenye Ibada.
UMUHIMU WA UNYENYEKEVU KATIKA SALA NA DUA
Anasema Mujaddid Ad Din Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali kua: ‘Hivi Jee ni watu wangapi ambao hua ni wenye
kuwaheshimu Wafalme na kuogopa Mamlaka yao ingawa hawahitaji kitu
chochote kutoka kwao? Lakini hata hivi kwa upande wa Allah Subhanah wa
Ta’ala bsi hua ni wajibu kwa Mja kua ni mwenye kutegemea malipo kutoka kwake
kutokana na kumtukuza kwake na kumuomba kwake kwenye Sala, kama vile
ambavyo Mja huyo hua anakhofu kutokana na Adhabu yake Allah Subhanah wa
Ta’ala kutokana na makosa yake Mja huyo.’
Hivyo ili mtu afahamu maana ya yale ayasemayo ndani ya Sala wakati anapokua ndani
ya sala basi hua ni wajibu wake mtu huyo kujifunza na kujikumbusha maana ya maneno
hayo ya ndani ya Sala na hivyo awe ni mwenye kujilinda na kila kitu ambacho ni chenye
kumpelekea kumuondolea Unyenyekevu ndani yake, kwani kila mja anapokua ni
mwenye kufaham kwa kina maana ya maneno yaliyomo ndani ya Sala basi ndio
anavyojua zaidi kuhusiana na maana ya Sala na jukumu la Sala yake juu yake.
Kwa kuanzia na kujua ni nini maana ya neno Sala ambapo tunapoangalia maana ya neno
Sala basi hua tunaona kua ni lenye kutokana na Mzizi wa herufi Sad-Lam-Waw ambalo
hua ni lenye kumaanisha Kuumia au kua na maumivu katika sehemu ya Chini ya
Mgongo, Kuifanya Sehemu ya Kati ya Mgongo kua ni yenye kupinda kwa kuingia ndani
na pia humaanisha Kusali au Kuomba Dua.
Baada ya kujua maana hio basi hua ndio utaona namna gani unatakiwa uwe muonekano
wa mwili wako katika kila hatua ya kitendo chako unapokua ndani ya Sala. Kwani
hutakiwi kua ni mwenye Kusimama, na Kurukuu, na Kusjudu na Kukaa kama Mtu ambae
ni mwenye Mamlaka Makubwa na Kujiona, na wala hutakiwi vitendo vyako vionekane
kama vya Mtu ambae kama alieonewa au aliechoka na yuko taabani hajiwezi, bali
unatakiwa uwe ni mwenye muonekano wa Mtumwa ambae anampenda sana na
kumheshimu na Kumti mmiliki wake kutokana na Ukarimu na Huruma ya Mmiliki wake
huyo alie mbele yake.
301
Ambapo hapa Mtumwa hua ni wewe unaesali na Mmiliki hua ni Allah Subhanah wa
Ta’ala ambae ndie yuko mbele yako, Hivyo unaposimama basi Nyoosha Mgongo wako
na Mwili wako mzima uwe umenyooka, huku Uso wako ukiwa unaangalia chini mbele
yako katika sehemu unayosujudia huku miguu yako ikiwa umeitanua kwa nyanda moja
baina yake, hivyo usiitanue kama mtu anaetaka kucheza Sumo wala usiibane kama askari
alieambiwa akaze miguu.
Unapoingia kwenye Sala na Kusema ‘Allahu Akbar’ na unaponyanyua mikono hadi
usawa wa Mabega, na kisha unapoifunga mikono yako Kifuani mkono wa kulia juu ya
mkono wa kushoto chini ya Moyo wako hua unamaanisha kua umeirembea kwa mikono
yako Dunia yote na kila kitu chake kutoka ndani ya mwili wako na kisha kuujaza Moyo
wako, Roho yako, Nafsi yako na Ufahamu wako umakini na yakini kua uo mbele ya Mola
wako kwa ajili ya Maombi yako.
Unapo rukuu na kushika Magoti yako basi pia nyoosha mgongo wako sawasawa kiasi ya
kua kama itawekwa gilasi ya Maji juu ya Mgongo wako basi itakaa bila ya kuanguka
yaani usiupinde mgongo wako ukatokeza juu kama Upinde, na hakikisha Miguu yako
imenyooka sawasawa sawa bila ya kupinda kwenye sehemu za magoti yako, huku
mikono yako ikiwa imeshika magoti yako na vidole vyako vikiwa vimetanuka.
Ukisjudu pia usiupinde Mgongo bali nyoosha Mgongo wako ukae sawasawa kiasi ya kua
kama mtu atakuwekea gilasi ya maji maji kwenye uti wako wa mgongo basi gilasi ya
maji hayo haitoanguka kutoka mgongoni mwako.
Unaposjudu basi kwanza ni magoti yako ndio yanayotakiwa kua yaguse ardhi, kabla ya
mikono yako na kisha mikono na kisha ndio paji la uso huku ukihakikisha kua paji lako
la uso na pua yako vinagusa sehemu unayosjudia huku miguu magoti na viganja vya
mikono tu vikiwa vimegusa chini, hivyo mikono usiilaze chini yote kama anavyoilaza
paka au mbwa wakati anapolala, na wala usikunje ngumi wakati wa kusjudu bali kunjua
huku ukiwa umevibana vidole vyako na hapo hapo mikono yako usiitanue sana kama
ndege anaetaka kuruka na hivyo kua ni mwenye kuwakera wenzako kutokana na
kutanuka kwa mikono yako, bali iweke mikono yako katika mtanuko wa kiasi ikiwa
sawa na mabega yako, huku ukihakikisha kua vidole vya miguu yako pia vikiwa
vimeelekea Kibla.
Hivyo hapa kuna utofauti wa namna vinayotakiwa kukaa vidole vya mikono katika
wakati wa Kurukuu ambapo hua inakubidi kuviachanisha na katika wakati wa kusujudu
unatakiwa kuvibana.
Unapokaa Attahiyyat basi pia nyoosha mgongo na wala usiupinde mpaka ukafanya
kibyongo na tumbo likaingia ndani kama unavyopindika Upinde unapovutwa kwa ajili
ya kuachia Mshale uliomo ndani yake, na wala usiupinde Ubavu wako mpaka ukawa
302
unamuegemea mwenzako kiasi ya kua kama akiondoka basi huendaa ukaanguka
kutokana na kushidwa kujizuia kwako kutokana na kumuegemea.
Huku mguu wako wa Kushoto ukiwa umeukalia na wa Kulia ukiwa umebakia kama
ulivyokua katika wakati wa Kusjudu. Na ni Suna kusali huku ukiwa miguu chini bila ya
soksi wala khuf.
Hii ni hali unayotakiwa kua nayo Mtu katika muonekano wa vitendo vya viungo vya
kiwiliwili chako, ambapo mbali ya kua na hali hio, lakini kiufaham, kiakili kinafsi na
kimoyo ili mtu uwe na unyenyekevu ndani ya Sala yako basi unatakiwa uwe katika hali
zifuatazo:
Hudhur Al Qalb - Kuuhudhurisha Moyo ndani ya Sala. Yaani kuufanya Moyo wako
uwe huru kutokana na kila kitu isipokua kile ambacho uko katika kutaka kukifanya
katika wakati huo, yaani Ibada ya Sala yako. Hivyo ili uweze kuhudhurisha Moyo wako
kwenye Sala basi hua inakubidi kufuta kila kitu unachokifikria katika ufaham wako
katika wakati huo kabla ya kuinga kwenye Takbir ya ufunguzi wa kuingia Ndani Sala.
Al Tafahhum – Kufaham kila kitendo unachofanya na kila neno unalosema ndani
ya Ibada ya Sala. Kwani kufahamu maana ya kila kitendo na maana ya kila neno hua
ni kwenye kuhudhurisha pia Moyo katika kurahisisha Kufaham kila hatua ya Sala kama
inavyotakiwa, kwani hii ndio ambayo inayokufanya uwe na uwezo wa kuachana na kila
Ovu.
Al Taadhim – Utukuzaji wa Allah Subhanah wa Ta’ala ambae unasimama mbele
yake katika wakati wa Ibada yako. Hili ni jambo muhimu sana katika Sala yako,
Kwani hata kama ukiwa umehudhurisha Moyo wako kwenye Sala na pia unafahamu
kila unachokifanya ndani yake basi kamwe huwezi kupata hali ya unyenyekevu kama
ikiwa hukua ni mwenye kuhisi Ukubwa na Utukufu wa yule ambae umesimama mbele
yake na hivyo hutokua na hali inayotakikana kupatikana kutokana na kua ni mwenye
kumkumbuka Mola wako kwa kuona na kuhisi kua yuko mbele yako.
Al Haibah – Heshima ya hali ya juu inayotokana na kuvutiwa kwa kujawa
Mapenzi na Utiifu wa Hali ya Juu. Hii hua ni hali ambayo hua inapatikana baada ya
kufanya Taadhim, kwani hua ni hali ya heshima inayotakana na kua na Mapenzi na
Unyenyekevu uliojaa Taqwa kutokana na kujua ukubwa na uwezo wa Allah Subhanah
wa Ta’ala.
Al Rajaa – Matumaini yaani kua na Matumaini ya kupata malipo Mema kutokana
na kutekeleza Ibada yako hio ya Kumkumbuka na kumtukuza Allah Subhanah wa
Ta’ala ndani yake.
303
Al Haya – Kuona Haya yaani kukubali na kujiona kua wewe kama kiumbe basi una
kasoro nyingi na kubwa sana kutokana na Udhaifu wako mbele ya Mola wako
aliekuumba ambae kwa wakati huo yuko mbele yako.
Ambapo anasema Hudhayfah Ibn Al Yaman Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi nilisali
pamoja na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika usiku mmoja, kisomo
chake kilikua kirefu na alipokua akisoma aya yenye Tasbih basi alikua akisema
Subhana Allah na alipokua akisoma aya inayouliza Suali basi huuliza Suali,
anaposoma aya inayoomba ulinzi kutoka kwa Allah basi nae huomba Ulinzi kwa
Allah Subhanah wa Ta’ala’(Sahih Muslim)
Na akasema tena Hudhayfah Ibn Al Yaman Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi nilisali
pamoja na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika usiku mmoja, alipokua
akisoma aya yenye kutaja Rehma basi alikua akiomba Rehma za Allah Subhanah
wa Ta’ala na alipokua akisoma aya inayotaja Adhabu za Allah Subhanah wa
Ta’ala basi huomba msamaha, anaposoma aya inayoomba ulinzi kutoka kwa
Allah basi nae huomba Ulinzi kwa Allah Subhanah wa Ta’ala na anaposoma Aya
zinazomuelezea Allah Subhanah wa Ta’ala husema Subhaan Allah’(Taadim Qadr
Al Salah)
Ambapo katika hadith nyengine basi amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kua: ‘Wakati Imam anaposema Aamiin basi na nyinyi itikieni Aamiin kwani kila
anaeitikia Aamiin na kisha ikaendana sambamba na Amiin ya Malaika basi mtu
huyo hua ni mwenye kusamehewa Dhambi zake zote zilizopita (Imam Bukhari)’
Tunapoangalia mfano wa wenye kua na unyenyekevu ndani ya Sala basi miongoni mwao
hua ni mfano wa Sahaba wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aitwae Abbad Ibn
Bishr Radhi Allahu Anhu ambae siku moja wakati Jeshi la Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam lilipokua katika bonde la kuelekea katika maeneo ya Najd basi Rasul Allahu
Salallahu Alayhi wa Salam aliamua kupiga kambi katika eneo moja ambalo aliliona kua
linafaa kwa ajili ya kambi hio, na hivyo akawauliza Masahaba jee nani atakua Mlinzi wa
kambi katika usiku wa siku hio.
Ambapo Abbad Ibn Bishr na Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu ambao ni marafiki na
ni ndugu wa Uislam uliotokana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kumkutanisha
Ansar Abbad Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu na kumkabidhi Amar Ibn Yasir Radhi Allahu
Anhu ambae alikua ni Muhajjirina alipohamia Madinah basi wao wakaamua kua ndio
wataolinda kambi kwa usiku wa siku hio.
Hivyo Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu akalala katika sehemu ya kwanza ya usiku huo
ili baadae aamke kisha ampishe Abbad Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu ili nae alale huku
304
yeye akiendelea na kusimamia ulinzi. Baada ya Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu
kulala basi Abbad Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu akatia udhu wake na kisha akaanza kusali
Qiyam Al Layl na baada ya kumaliza kusoma Surat al Fatiha basi akatiririka na Surat Al
Kahf ambayo ina aya 110.
Wakati yuko katikati ya Sura hio huku akiwa amezama kwenye Utamu wa Ladha ya
kisomo chake na Utulivu wa Sala yake wakati akiwa mbele ya Mola wake, basi mara
hapo hapo bila ya kujijua akajikuta kua yuko pia mbele ya ya Adui yake miongoni mwa
maadui wa Uislam ambae alikua amejificha kwenye moja kati ya Majabali ya Bonde hilo
na hivyo Adui huyo akachomoa Upinde wake na kuanza kutunga Shabaha yake kwenye
mwili wa Abbad Ibn Bishar Radhi Allahu Anhu ambae alikua ndani ya Sala yake mbele
ya Mola wake.
Kwa hivyo ghafla Abbad Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu akashtukia Mshale wa Upinde
umezama kwenye mwili wake, ambapo kwa hali ya kawaida basi kwa kila Ibn Adam
anaefikwa na tukio kama hili basi lazima awe ni mwenye kuhisi maumivu yake, lakini
hata hivyo Abbad Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu hakua ni mwenye kuhisi Maumivu ayo
kutokana na namna alivyozama kwenye ladha ya Utamu wa Ibada yake huku akiendelea
na kisomo chake, na mara akisikia akasikia mshindo wa mshale wa pili ukizama katika
sehemu nyengine ya Mwili wake, na wakati anamalizia Kisomo chake mara akahisi
muingio wa mshale wa tatu kwenye nyama ya mwili wake.
Abbad Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu akamalizia kisomo chake kisha akaichomoa Mishale
hio mitatu, kisha akaelekea kwenye rukuu na kisha akanyanyuka na kisha akaelekea
kwenye Sijda aksjudu sijda ya kwanza akakaa kitako na kisha alipoelekea kwenye sijda
ya pili nguvu zikamuishia akaanguka n kumuta rafiki yake Ammar Ibn Yasir Radhi
Allahu Anhu, na kumwambia: ‘Amka uendelee na Ulinzi kwani kwa hakika mimi
nimeshambuliwa na kujeruhiwa.’
Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu akaamka na alipomuona ndugu yake huyo akiwa
katika hali kama hio ya kua ni mwenye kuanguka huku akitokawa na damu tele basi
alishtuka na kumuuliza ndugu yake huyo kwa kusema: ‘Subhana Allah! Kwanini
hukuniamsha mara tu wakati ulipopigwa mshale wa kwanza?’
Abbad Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Kwa sababu siku hisi kutokana na kua
nilikua niko katikati ya kisomo cha Surat Al Kahf na utamu wake ukanizidi ndani
ya Moyo wangu kiasi ya kua nilishindwa kukikatisha Kisomo hicho. Na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam pia aliniamrisha kua niihifadhi kwenye Moyo Sura hio,
hivyo kwangu mimi Kifo ni bora kuliko kukikatisha kisomo cha Sura hio’
Kwa upande mwengine basi baada ya kufariki Amir ul Muuminin Abu Baqr As Siddiq
Radhi Allahu Anhu basi Amir Ul Muuminina Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu
305
basi alimuuliza Asma Bint Uways Radhi Allahu Anha ambae ni Mkewe Abu Baqr As
Sadiq Radhi Allahu Anhu kwa kusema: ‘Hivi Jee Abu Baqr alikua akifanya Ibada
katika hali gani anapokua nyumbani?’
Asma Bint Uways Radhi Allahu Anha akajibu: ‘Alikua akitia Udhu katika wakati wa
Sala ya Tahajjud, na kisha huanza kusali, na alipokua akisoma Qur’an ndani yake
basi alikua akilia, na wakati wa Kusjudu alikua akilia, na alipokua akiomba Dua
pia alikua akilia’ baada ya kusikia sifa hizo basi Amir Ul Muuminina Umar Ibn Al
Khattab Radhi Allahu Anhu nae akaanza kulia.
Ambapo kwa upande wa Amir ul Muuminin Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu basi
ilikua kila ukiingia wakati wa Sala alikua akionekana kua ni mtu mwenye khofu na uso
wake hubadilika rangi, na alipoulizwa kwanini hali yake imekua hivyo basi alisema: ‘Wa
Allahi, umefika wakati tuliojiaminisha kuibeba Amana’ na kisha husoma aya
ifuatayo:
﴿ إِ َّعَرَ ضْنَا الأَْمَانَةَ عَلَى ٱلس َّمَاوَا ِت وَٱلأَرْضِ وَٱلجِْبَاِل فَأبَينَْ أَن يحَْمِلْنَهَا
وَأَشْ فَقْ نَ مِنْ هَ ا وَحمََلَهَ ا ٱلإِنْسَا ُن إِن َّهُ كَ انَ ظَلُوماً جَ هُ ولاً ﴾
Inna AAaradhna al-amanata AAala alssamawati waal-ardhi waaljibali faabayna an
yahmilnaha waashfaqna minha wahamalaha al-insanu innahu kana dhaluuman
jahuulan; (Al Ahzab 33:72)
Tafsir: Kwa hakika tuliipa Amana, Mbingu na Ardhi na Milima lakini vikaikataa
kuichukua; kwa sababu ya kuogopa: lakini Mtu akaichukua: Hakika alikua ni
mwenye kujidhulumu na ni mjinga;
Ambapo ili tuifaham vizuri zaidi maana aya hii basi ni vizuri kuanza na aya zilizotangulia
kabla yake ambazo zinasema:
﴿َي ُّهَا ال َّذِينَ ءَامَنُواْ ات َّقُواْ اهلل ََّ وَقُولُواْ قَوْلاً سَدِيداً ۞يُ صْلِ حْلَكُ مْ أَعْمَلَكُ مْ َويَغْفِْر
لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَن يُطِعِ اهلل ََّ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزاً عَظِيماً۞ إِ َّ عَرَضْنَا الأَْمَانَةَ
عَلَى ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَٱلجِْبَاِل فَأبَينَْ أَن يحَْمِلْنَهَا وَأَشْفَقْنَ مِنْهَا وَحمََلَهَا
ٱلإِنْسَانُ
إِن َّهُ كَانَ ظَلُوماً جَ هُولاً ﴾
306
Ya ayyuha alladhina amanoo ittaqoo Allaha waqooloo qawlan sadeedan, Yuslih
lakum aAAmalakum wayaghfir lakum dhunoobakum waman yutiAAi Allaha
warasoolahu faqad faza fawzan AAadhiman; Inna AAaradhna al-amanata AAala
alssamawati waal-ardhi waaljibali faabayna an yahmilnaha waashfaqna minha
wahamalaha al-insanu innahu kana dhaluuman jahuulan. (Al Ahzab 33:70-71)
Tafsir: Enyi Mlioamini! mcheni na muogopeni Allah, na (daima) semeni kauli za
ukweli ulionyooka, atakuongozeni kufanya mema na kukusameheni dhambi zenu. Na
kwa hakika yeyote yule ambae anaemtii Allah na Mtume wake (Salallahu A’layhi wa
Salam) basi atakua ni miongoni mwa waliofuzu. Kwa hakika tuliipa Amana, Mbingu
na Ardhi na Milima lakini vikaikataa kuichukua; kwa sababu ya kuogopa: lakini Mtu
akaichukua: Hakika alikua ni mwenye kujidhulumu na ni mjinga.
Ambapo kutokana na aya hizi basi tunaona kua ingawa wengi wetu miongoni mwa
wasiojua hua ni wenye kuona kua kipimo cha Mafaniko ya Mtu hapa Duniani kua ni kua
mwenye kumiliki Mali au Mamlaka, lakini hata hivyo ukweli ni kua hicho sio kipimo
sahihi kwani hiki kilichotajwa hapa kwenye aya hii yaani cha Kua na Taqwa na
kumogopa Allah Subhanah wa Ta’ala ndio kipimo pekee kinachoonesha Mafanikio ya
Mtu, na sio hapa Duniani tu bali pia na Akhera.
Na ndio maana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawa ni mwenye kupendelea
sana katika Khutba zake Kuanza na aya nne za Taqwa ambapo ndani yake mna aya za
70-71 za Surat Al Ahzab kwa mpangilio ufuatao:
﴿َي ُّهَا ال َّذِينَ ءَامَنُواْ
ات َّقُواْ اهلل ََّ حَق َّ تُقَاتِهِ وَلاَ تمَُوتُن َّ إِلا َّ وَأَنتُم م ُّسْلِمُو َن ﴾
Ya ayyuha alladhina amanoo ittaqoo Allaha haqqa tuqatihi wala tamootunna illa
waantum muslimoona (Surat Al Imran 3:102)
Tafsir: Enyi mlioamini! Muogopeni Allah (kwa kutekeleza maamrisho yake na
kuachana na makatazo yake) kama anavyostahiki kuogopewa. [Mtiini, mshukuruni
na daima mkumbukeni], na msife isipokua mkiwa katika hali ya kua ni Waislam.
Ambapo tunapoziangalia aya hizi zinazozungumzia kuhusiana na umuhimu wa Taqwa
basi tunaona kua Allah Subhana wa Ta’ala amesema ndani yake kwa kuanza na Ya
Ayyuha Alladhina Amanoo yaani Enyi Mlioamini kisha akasema kwa kumalizia pamoja
nayo Ittaqoo Allaha yaani Muogopeni Allah na katika aya nyengine ya Surat An Nisaa
4:1 ambayo ni miongoni mwao aya 4 hizo basi amesema Ya Ayyuha Al Nassu yaani
Enyi Watu kisha akasema kwa kumalizia pamoja nayo Ittaqoo Rabbakumu yaani
Muogopeni Mungu wenu. Kama tutakavyoona katika kufafanua hapo mbele.
307
Ambapo anasema Imam Abu Muhamamd Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘‘Ittaqoo
Rabbakumu’ yaani ‘Muogopeni Mungu’ wenu wanaambiwa wale ambao ni wenye
Kutaka kuchuma Malipo kwani wao hua ni wenye kutafuta Neema na Rehma na
hivyo watu hawa hua wanatafuta kitu kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala’
‘Na ‘Ya Ayyuha Alladhina Amanoo Ittaqoo Allaha yaani Enyi Mlioamini Allah’ hua
wanaambiwa wale ambao ni wenye Kumjua Allah Subhanah wa Ta’ala kwani wao
hua ni wenye kutaka kuipata Siri ya Allah Subahanh wa Ta’ala na hivyo wao hua
ni wenye kutafuta njia ya Kumpata mwenyewe Allah Subhanah wa Ta’ala’
Hivyo kua na Taqwa hua kuko katika hali tatu. Ambapo kwanza hua ni katika
Kuuogopa Moto wa Allah Subhanah wa Ta’ala ambao umetayarishwa kwa ajili ya
Makafiri na hivyo kwa Walioamini hua ni wenye kuepukana nao kwa kua na Subra
na kujizuia kutokana na Maovu na kumtii Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume
wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo hua ni wenye kuingizwa
kwenye za Allah Subhanah wa Ta’ala na kupata Ridhaa ya Mola wao kama
zinavyosema Aya:
﴿وَٱت َّقُواْ ٱلن َّارَ ٱل َّتيِ ۤ أُعِد َّتْ لِلْكَافِرِينَ۞وَأَطِيعُواْ ٱهلل ََّ وَٱلر َّسُولَ لَعَ ل َّكُمْ
تُرْحمَُونَ۞وَسَارِعُو ۤ اْ إِلىَٰ مَغْفِرَةٍ مِّنْ ر َّبِّكُمْ وَجَن َّةٍ عَرْضُهَا ٱلس َّمَاوَاتُ وَٱلأَرْضُ أُعِد َّتْ
لِلْمُت َّقِينَ ﴾
Waittaqoo alnnara allatee oAAiddat lilkafireena; WaateeAAoo Allaha
waalrrasoola laAAallakum turhamoona; WasariAAoo ila maghfiratin min
rabbikum wajannatin AAardhuha alssamawatu waal-ardhu oAAiddat
lilmuttaqeena(Surat Al Imran 3:131)
Tafsir: ‘Na uogopeni Moto ambao umetayarishwa kwa ajili ya Makifiri. Na mtiini
Allah na Mtume wake ili mpate kuingizwa kwenye Rehma; Na kimbilieni katika
Usamehevu wa Mola wenu na kwa ajili ya Pepo ambayo upana wake ni kama ilivyo
Mbingu na Ardhi ambayo imetayarishwa kwa ajili ya wenye Taqwa’
Pili hua ni katika Kumcha Allah Subhanah wa Ta’ala na hivyo Mja hua ni mwenye
kuonesha Shukran kwa Neema na Rehma za Allah Subhanah wa Ta’ala juu yake.
Na Tatu hua ni katika kumcha Allah Subhanah wa Ta’ala kwa kutomshirikisha,
bila ya kutegemea Malipo kutoka kwake.
308
Ambapo hali ya Kwanza ya Kumcha Allah Subhanah wa Ta’ala hua ni hali ya Watu
waliokua ni wa Chini miongoni mwa waja wake, hali ya Pili hua ni hali ya waliokua
Kati na kati na hali ya Tatu hua ni ya waliokua Juu yaani Waliotangulia na hawa
wenye hali ya Tatu ndio wale waliotajwa kwenye aya ifuatayo:
﴿وَلْتَكُنْ مِّنْكُمْ أُم َّةٌ يَدْ عُونَ إِلىَ ٱلخَْيرِْ وَ َْمُرُونَ بِٱلْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ ٱلْمُنْكَرِ
وَأُوْ لَٰئِكَ هُمُ ٱلْمُفْ لِحُونَ ﴾
Waltakun minkum ommatun yadAAoona ila alkhayri waya/muroona
bialmaAAroofi wayanhawna AAani almunkari waola-ika humu almuflihoona
(Surat Al Imran 3:104)
Tafsir: Na kuweni miongoni mwenu na kundi la Watu ambao watakua ni wenye
kuwaita watu kwenye Kheri kwa Kuamrisha Mema na Kukataza Mabaya, na hawa
ndio wale watakaokua wamefuzu.
Kwani Hawa ni watu ambao wanasimama kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala
tu. Hawa hua hawarudi nyuma wala hawazuiliki kutokana na kusimamia na
kuamrisha maamrisho ya Mola wao na kuyakataza makatazo yake na hua
hawamtegemei yeyote katika jambo lolote, kwani hua ni wenye kuona kasoro zao
na udhaifu wa Nafsi zao na hivyo wanatumia uhai wa Maisha yao kwa ajili ya
kutafuta Ridhaa ya Mola wao.
Na hivyo hua Wanafanya Matendo yao kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala,
wanausia juu ya Dini ya Allah Subhanah wa Ta’ala na ni wenye kuwaita Viumbe
warudi kwa Allah Subhanah wa Ta’ala, hivyo biashara yao imewanufaisha na
hawajutii juu ya makubaliano yao na Mola wao.
Hawa hua ni wale watu ambao hua wamesimama kwenye Yakini na hivyo wamekua
huru kutokana na Hiari zao na Uwezo wao na wameachana na Matamanio ya Nafsi
zao, wanamjua Allah Subhanah wa Ta’ala na wanamtegemea na kumuomba na
kujitahidi kwa ajili ya Mola wao tu.
Wao hua kamwe hawafikirii kuhusiana na Mitizamo ya watu juu yao, kwani
kwenye Nyoyo zao wana urafiki na Mola wao, kwenye Macho yao wanaona Ufunuo
wa Nafsi zao na hivyo hua ni wenye kukiona kila kitu kama kilivyo katika Maumbile
ya uhakika wake. Kwani wakati wengine hua wanaangalia Maumbile kwa mtizamo
wa Viumbe basi wao hua wanaangalia Maumbile kwa Mtizamo wa alieumba. Hawa
ndio waliochaguliwa na Allah Subhanah wa Ta’ala na kuainishwa kwa alama ya
Ufalme wake.
309
Ingawa kwa kimaumbile Mja hua anatamani kitu chengine na Muumba hua
anataka kitu chengine, lakini hapo hapo wote kwa pamoja hua wanataka kitu
kimoja na hii ni kutokana na makubaliano yao baina yao. Na hii ndio maana ya ile
kauli isemayo kua: ‘Pale Mja anapojali kuhusiana na anayoyajali Mola wake basi
Allah Subhanah wa Ta’ala humuondolea khofu kuhusu Dunia na Akhera yake’
Hivyo Umoja hua ni kumuangalia yule alie Mmoja tu na kujua kua yeye ni Mmoja
tu pekee, na hivyo kila kitu hua kinatoka katika sehemu Moja ambayo ni ya
kutokana nae na Makadirio yote hua ni kutokana nae.
Ama kuhusiana na Kutofautiana na Shariah, basi hua kuna aina mbili. Ambapo
aina ya kwanza hua ni katika Kanuni za Sharia na aina ya pili hua katika Matawi
ya Sharia.
Ambapo kutofautiana kuhusiana na Kanuni basi hua ni kubaya sana na ni hatari
sana, na hii ni kwa sababu hapa hua kuna hali ya pande mbili tu, kuna hali ya
upande ulio Sahih na hali ya upande usiokua Sahih na ndio maana Allah Subhanah
wa Ta’ala akabainisha njia ya upande uliokua Sahih na kusema:
﴿وَأَن َّ هَٰذَا صِرَاطِى مُسْتَقِيماً فَٱت َّبِعُوهُ وَلاَ تَت َّبِعُواْ ٱلس ُّبُلَ فَتَفَر َّقَ بِكُمْ عَ ن سَبِي لِهِ
ذٰلِكُمْ وَص َّاكُمْ بِهِ لَعَل َّكُمْ تَت َّقُونَ ﴾
Waana Hadha siratee mustaqeeman faittabiAAoohu wala tattabiAAoo alssubula
fatafarraqa bikum AAan sabeelihi dhalikum wassakum bihi laAAallakum
tattaqoona (Surat Al Anaam 6:153)
Tafsir: Na hii ndio njia yangu iliyonyooka hivyo ifuateni na wala msifuate njia
nyengine kwani zitakupotosheni kutokana na njia yake, na hivyo ndivyo anavyo
kuamrisheni ili mpate kua wacha Mungu.
Ama kuhusiana na hali ya pili ya kutofautiana kwenye Matawi ya Sharia basi hua
ni sawa na kua na makundi mawili tofauti ambayo hua ni yenye kuelekea Safari
moja yenye lengo moja lakini kila mmoja akachukua njia yake na kuifuata, hivyo
ingawa watu hawa hua ni wenye kufuata njia tofauti lakini mwisho wake hua ni
wenye kukutana kwenye lengo moja kuu la safari yao, hivyo kutofautiana huku hua
kuna Rehma pia ndani yake, na hii ndio maana ya yale maneno yasemayo kwenye
aya ifuatayo:
310
﴿وَجَاهِدُوا فىِ ٱهلل َِّ حَق َّ جِ هَادِهِ هُوَ ٱجْتَبَاكُمْ وَمَا جَعَلَ عَلَيْكمْ فىِ ٱلدِّينِ مِنْ
حَرَجٍ ﴾
Wajahidoo fee Allahi haqqa jihadihi huwa ijtabakum wama jaAAala AAalaykum
fee alddeeni min harajin (Surat Al Hajj 22:78)
Tafsir: Na jitahidi kupigania kwa ajili ya Allah kwa haki kama inavyostahiki kupigania
kwani amekuchagueni na hakukujaaleni katika Dini kua na ugumu.
Na pia pale aliposema:
﴿يُرِيدُ ٱهلل َُّ بِكُمُ ٱلْيُسْرَ وَلاَ يُرِيدُ بِكُمُ ٱلْعُسْرَ ﴾
Yureedu Allahu bikumu alyusra wala yureedu bikumu alAAusra (Surat Al Baqra
2:185)
Tafsir: Allah anakutakieni urahisi na hataki kukufanyeni Ugumu.
Kisha Rasu Allah Salallahu Alayhi wa Salam hufuatia kwa aya ifuatayo:
﴿يَأَي ُّهَا الن َّاسُ ات َّقُواْ رَب َّكُمُ ال َّذِى خَلَقَكُمْ مِنْ ن َّفْسٍ وَحِ دَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا َزوْجَهَا
وَبَث َّ مِنْهُمَا رِجَالاً كَثِيراً وَنِسَآءً وَات َّقُواْ اهلل ََّ ال َّذِى تَسَآءَلُونَ بِهِ وَالأَْرْحَامَ إِن َّ اهلل ََّ
﴾ كَا نَعَلَيْ ي ب كُمْرَقِ اً
Ya ayyuha alnnasu ittaqoo rabbakumu alladhi khalaqakum min Nafsin wahidatin
wakhalaqa minha zawjaha wabaththa minhuma rijalan kathiran wanisaan
waittaqoo Allaha alladhii tasaaloona bihi waal-arhama inna Allaha kana
AAalaykum raqeeban (Surat An Nisaa 4:1)
Tafsiri: Enyi Watu! Mcheni Mola wenu aliekuumbeni kutokana na Nafsi moja
(Adam), na kutokana nae (Adam) akamuumba mke wake (Hawwa), na kutokana nao
(Adam na Hawa) akawaumba Wanaume na Wanawake wengi na muogopeni Allah
311
ambae ana haki juu yenu, na msivunje udugu, kwani kwa Hakika Allah ni mwenye
uangalifu mkubwa juu yenu.
Hivyo: ‘‘Ittaqoo Rabbakumu’ yaani ‘Muogopeni Mola wenu’ wanaambiwa wale watu
wa kawaida ambao Ucha Mungu wao hua unatokana na kua ni wenye kuziona
Neema na Rehma za Allah Subhanah w a Ta’ala na msukumo wao hutokana na
kutumia Neema na Rehma hizo kwa Miili yao kwa ajili ya kumtumkia Mola wao’
‘Na ‘Ya Ayyuha Alladhina Amanoo Ittaqoo Allaha yaani Enyi Mlioamini Muogopeni
Allah’ hua wanaambiwa wale ambao ni wenye Kumjua na kumjali Allah Subhanah
wa Ta’ala na hivyo Ucha Mungu wa hua unatokana na kua ni wenye Kumuangalia
Allah Subhanah wa Ta’ala na malengo yao hua ni kupatikana kwa utulivu ndani ya
Nyoyo zao kutokana na Kumshuhudia Mola wao’
Ambapo amrisho hili la kumuogopa Allah Subhanah wa Ta’ala hua ni kwa ajili ya
Waja kulifanya kua ndio ngao yao ya kujizuia wasifikiwe na Makatazo ya Mola
wao. Ambao kwanza hua ni mwenye kutafuta Ulinzi katika kifungo cha Tawhid na
kuepukana na Shirk.
Pili hua ni kutafuta Ulinzi katika Utiifu na kukaa mbali na njia ya Uasi.
Tatu hua ni kutafuta Ulinzi kwa Tahadhari na kuyakimbia yenye kua na shaka
ndani yake.
Hivyo yeyote yule atakaepanda Ngazi hizi za Kumcha Allah Subhanah wa Ta’ala
basi ataufikia Uokovu, na asiepanda Ngazi hizo basi atakua amekula hasara kama
zinavyofafanua aya pale ziliposema:
﴿وَيُنَجِّ ى ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ ٱت َّقَوْاْ بمَِفَازَهتِِمْ لاَ يمََس ُّهُمُ ۤ ٱلس ُّو ءُ وَلاَ هُمْ يحَْزَنُونَ۞ٱ هلل ََُّخا لِ قُ
ِ كُل شَيْءٍ وَهُوَ ٰ عَلَى كُل وَكِيلٌ۞ل َّهُ مَقَالِيدُ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَٱل َّ ذِيَن
ّ شَيْءٍ
ِ
كَ فَرُواْ بِآَ تِ ٱهلل َِّ أُوْ لَٰئِكَ هُ مُ ٱلخَْاسِ رُونَ ﴾
ّ
Wayunajjee Allahu alladheena ittaqaw bimafazatihim la yamassuhumu alssoo-o
wala hum yahzanoona; Allahu khaliqu kulli shay-in wahuwa AAala kulli shay-in
wakeelun; Lahu maqaleedu alssamawati waal-ardhi waalladheena kafaroo bi-ayati
Allahi ola-ika humu alkhasiroona. (Surat Az Zumar 39:61-63)
312
Tafsir: Na atawaokoa Allah wale ambao wenye Taqwa kwenye sehemu zao za
waliofuzu, na hawatoguswa na Ovu na wala hawatokua na Huzuni. Allah ndio
Muumba wa kila kitu na yeye ndie Msimamizi wa kila kitu. Kwake yeye ndiko kwenye
funguo za Mbingu na Ardhi na wale waliozikufuru aya za Allah wao ndio watakaokula
hasara.
Na pia pale ziliposema tena aya katika Surat At Talaq:
﴿وَمَن يَت َّقِ ٱهلل ََّ يجَْعَل ل َّهُ مخَْرَجاً۞وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لاَ يحَْتَسِ بُ وَ مَن يَتَوَك َّلْ عَلَى
ّ لِكُل شَيْءٍ قَدْراً ﴾
ٱهلل َِّ فَهُوَ حَسْبُهُ إِن َّ ٱهلل ََّ ابَلِغُ أَمْرِهِ قَدْ جَعَلَ ٱهلل َُّ ِ
Waman yattaqi Allaha yajAAal lahu makhrajan; Wayarzuqhu min haythu la
yahtasibu waman yatawakkal AAala Allahi fahuwa hasbuhu inna Allaha balighu
amrihi qad jaAAala Allahu likulli shay-in qadran (Surat At Talaq 65:2-3)
Tafsir: Na atakae Muogopa na kutekeleza Majukumu ya Allah juu yake basi (Allah
Subhanah wa Ta’ala) atamjaalia njia ya kutoka katika kila tatizo. Na atamruzuku
kupitia katika njia ambazo hatozitegemea, na atakaemtegemea Allah (Subhanah wa
Ta’ala) basi atamtosheleza, hakika Allah atamfanikishia Jambo lake. Kwani kwa
hakika Allah amejaalia makadirio juu ya kila kitu.
Kwani baada ya aya hio ya Surat An Nisaa 4:1 basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam ndio hua anamalizia na aya ya Tatu ya Taqwa ambayo hua ni iliyobeba Qawlan
Sadida yaani Kauli Iliyonyooka ambayo inasema.
﴿َي ُّهَا ال َّذِينَ ءَامَنُواْ ات َّقُواْ اهلل ََّ وَقُولُواْ قَوْلاً سَدِيداً ۞يُ صْلِ حْلَكُ مْ أَعْمَلَكُ مْ وَيَغْفِ ْر
لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَن يُطِعِ اهلل ََّ وَرَسُولَهُ
فَقَدْ فَازَ فَوْزاً عَظِيماً ﴾
Ya ayyuha alladhina amanoo ittaqoo Allaha waqooloo qawlan sadeedan, Yuslih
lakum aAAmalakum wayaghfir lakum dhunoobakum waman yutiAAi Allaha
warasoolahu faqad faza fawzan AAadhiman (Al Ahzab 33:70-71)
Tafsir: Enyi Mlioamini! mcheni na muogopeni Allah, na (daima) semeni kauli za
ukweli ulionyooka, atakuongozeni kufanya mema na kukusameheni dhambi zenu. Na
313
kwa hakika yeyote yule ambae anaemtii Allah na Mtume wake (Salallahu A’layhi wa
Salam) basi atakua ni miongoni mwa waliofuzu kwa darja kubwa sana.
Ambapo tunapoziangalia Aya zote hizi na mpangilio wake basi tunaona kua
zinazungumzia kuhusiana na kutilia mkazo Taqwa na hivyo ndani yake zimetaja neno
Taqwa mara 4.
Ambapo aya hii inatubainishia kua Kufuzu kwa Walioamini hapa Duniani na Akhera
hakupimwi kulingana na Mamlaka uliyokua nayo, Pesa ulizokua nazo, Mali ulizokua
Nazo, Uzuri uliokua Nao, Nguvu ulizokua nazo, Umaarufu uliokua nao n.k kwani
ukipimwa kulingana na vipimo hivyo basi utakua Dhaluman Jahulan katika Kipimo cha
Kufuzu kwako na hivyo ili usiwe Dhaluman Jahulan basi hua Kipimo kinachotumika
hua ni kutokana na Taqwa yako Mbele ya Mola wako.
Hivyo hii ni Aya ambayo Imefunika Kila Kitu katika aya hizi 4 ambazo hua zinajulikana
kama Aya za Taqwa kwani zimezungumzia kuhusiana na Taqwa ndani yake mara 4.
Ambapo kwa upande wa Hujjat ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad
Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii basi yeye anasema kua:
‘Qur'an ina Aya 741 ambazo zina Sifa Ya Kua ni Lulu za Qur'an kwani ni Aya
zinazomuonesha Ibn Adam Njia Sahih ya Kuifuata katika Maisha yake
Na pia Qur'an ina aya 763 ambazo zina sifa ya Kua ni Mataji ya Hazina za Qur'an
kwani hua zinazungumzia kuhusiana na Sifa za Allah Subhanah wa Ta'ala.’
Na miongoni mwa Lulu 741 za Qur'an basi 4 kati yao ni aya hizi za Taqwa ambazo pia
hua ni aya za Tawhid
Ambapo anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Qawlan
Sadida hua ni maneno ya Tawhid ambayo ndio msingi wa Dini ya Kiislam na Ndio
Nguzo kubwa ya Kujisalimisha na kuingia ndani yake. Mwanzo wa Ilm za Dini yote
ni Tawhid. Msingi wa kujua kila kitu ni Tawhid. Ukuta baina ya Imani na Kufr ni
Tawhid, Tofauti baina ya Rafiki na Adui ni Tawhid, Kidhibiti cha baina ya Mbingu
7 na Ardhi 7 ni kupitia katika Tawhid. Nuru ya Viumbe vya Ulimwengu wa Dhahir
na Ulimwengu wa Al Ghayb ni Tawhid na hali ya Maumbile ya Ulimwengu mzima
wa Al Dhadhir na wa Al Ghayb unatokana na Nuru ya Tawhid. Na Lulu ya Mwanzo
ya Irfan ni Tawhid na mwanzo wa Kujua baada ya Kuitafuta Hakika ni Tawhid’
‘Hivyo unapoiweka Tawhid katika sehemu yake basi mtazamo wako hua ni wenye
kuchukua na kupata Muonekano wa Uongufu, Ulimi wako huanza kua ni Hazina
ya Hikma na Busara, Usikivu wako hua ni Chaza yenye Lulu ya Amanah na
314
Uaminifu. Moyo wako hua ni sehemu kuu ya Kutafakkar na Kuzingatia na Nafsi
yako hua ni sehemu ambayo Matamanio huweka Soji lake tayari kwa ajili ya
kupandwa na kudhibitiwa.’
‘Tawhid hua ni nauli ya kuingia Peponi na Tawhid hua ni yenye kutosheleza kua ni
Ibada, kwani Tawhid hua ni Bei ya kuingia Peponi na inatosheleza kila kila kitu
katika matendo yote ya Ibada. Tawhid hua si kumpwekesha Allah Subhanah wa
Ta’ala peke yake bali Tawhid hua ni kujihesabu kua wewe uwe ni mmoja tu ambae
ni kwa ajili yake Allah Subhanah wa Ta’ala’
Anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Wakati Allah
Subhanah wa Ta’ala anapompa mtu mafanikio katika kuweza kufanya mema basi,
hii hua ni Dalili kua Mtu huyo kua ni mwenye kusamehewa na Allah Subhanah wa
Ta’ala’
Hivyo hali ya kua na Taqwa hua inaenda sambamba na kua na Uwezo wa kusimamia
jukumu la Amanah na hivyo pia kua na mafanikio. Neno Amanah linatokana na mzizi wa
herufi za kiarabu Alif-Mim-Nun, ambalo maana yake ni kua katika hali ya amani,
usalama, ulinzi, uaminifu na kua na imani na kitu. Usalama na amani wa sehemu fulani
huweza hupatikana kutokana na ulinzi na uaminifu wa yule anaeyatawala mazingira
hayo. Hivyo tunapozungumzia maana ya Amanah Kiislamu basi hua tunazungumzia kitu
kinachotegemeana na Khalifah anaetawala Ulimwenguni ambae ni Bani Adam.
Tukiangalia kwa undani zaid basi tunaona kua neno Amanah limetumika katika Qur’an
kutoa maana yenye kina kirefu zaidi. Kwani inaelezea kuhusiana na haki ya Bani Adam
na majukumu yake dhidi ya Bani Adam wenzake, mazingira yake na pia viumbe vyengine
vyote vilivyoumba na Allah Subhanahu wa Ta’ala. Kila kitu alichojaaliwa kupewa au
kuamrishwa kiumbe Bani Adam afanye, hata kama ikiwa ni kwa manufaa yake, basi hua
ni Amanah na hivyo huhitajiwa kuchungwa na kutumiwa kulingana na Sharia’h za yule
aliempa Amanah hiyo ambae ni Allah Subhanah wa Ta’ala. Kwani ni wajib unapopewa
Amanah aidha kuirudisha kama ilivyokua, kwa aliekupa ama kuitumia kulingana na
matakwa au muongozo wa aliekupa Amanah hiyo.
Ambapo amesema Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kuuliwa katika njia ya Allah Subhanah wa
Ta’ala hua ni kwenye kufuta Dhambi zote isipokua dhambi za Amanah, kwani mtu
mwenye kupewa Amana na kisha akawa hakujiaminisha, basi ataletwa katika siku
ya Malipo, na kuambiwa ikabidhishe amana kama ulivyopewa.
Nae atasema: ‘Ya Rabb Dunia haipo tena’ ataambiwa: ‘Ikabidhishe Amanah’ nae
atasema tena: ‘Ya Rabbi Dunia haipo tena (nitaikabidhisha vipi mie?)’ hapo
wataambiwa Malaika: ‘Muingizeni katika Hawwiyah (Moto Mkali sana)!’ hivyo
315
Mtu huyo atachukuliwa na kutupwa kwenye Moto wa Jahannam. Kisha atazama
hadi chini ya kina cha chini cha mwisho kabisa cha Moto huo.
Na chini yake huko ndani ya Hawwiyah ataikuta Amana yake hio, na kisha ataibeba
na kuiweka juu ya mabega yake. Na kuja nayo juu hadi kwenye kingo za Moto huo
na kutaka kutoka nayo, lakini atateleza na itamponyoka na kutumbukia tena hadi
chini ya kina cha Moto huo, na tukio hili litakua ni lenye kujirudia Milele.’
Ambapo kuhusiana na mtizamo wa Fiqh juu ya Amanah tunazopeana Ibn Adam basi
Wanazuoni wametofautiana kuhusiana nazo pale inapokua mtu aliekabidhiwa Amanah
husika ikawa imempotea mbali ya kua alikua akisimamia ipasavyo, kwani kwa upande
wa Wanazuoni wa Madhhab ya Imam Al Shafii basi wanasema kua itabidi Mtu huyo
aliekabidhiwa aitafute nyengine kisha aikabidhi kwa aliemkabidhi au alipe fidya
kulingana na matakwa ya mwenye Amanah, ambapo kwa Upande wa Madhhab ya Imam
Abu Hanifa basi wao wanasema kua haina haja kukabidhi nyengine wakati ile ikiwa
imepotea kwa bahati mbaya.
Na amesema Zayd Ibn Wahab kua : ‘Hudhayfah alituambia sisi kua: ‘Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alituambia sisi kuhusiana na mambo mawili ambapo
mimi nimeliona moja likiwa tayari limeshatokea, huku nikiwa nasubiri na la pili
litokee’
Kwani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisema: ‘Amanah (Uaminifu)
imeshushwa ndani ya mizizi ya Nyoyo za Watu. Na kisha watu hao wakajifunza
Qur’an na wakajifunza Sunnah’ na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akatuambia kuhusiana na namna itakavyo ondolewa Amanah kwa kusema: ‘Mtu
atakua ni mwenye kusinzia na Uaminifu wake utaondolewa kutoka kwenye Moyo
wake na hivyo athari yake itakua kama kovu ndogo yenye rangi ya kiza kiza na
kisha atasinzia tena na itaondolewa tena na athari yake kua kama suguru gumu
linaouathiri mkono wa mtu kutokana na kufanya kazi ngumu za sulubu. Au kama
cheche ya Moto ambao hua mnaizima kwa kuipiga piga na kuikanyaga kwa miguu.
Na hivyo mtamuona mtu huyo kua ni mfano wa kuigwa, ingawa hakuna kitu chenye
thamani ndani yake mtu huyo, na kisha watu watakua wanahudumiana lakini
hakuna hata mmoja mwenye kujali kua na uaminifu kiasi ya kua watu watakua
wanasema kuhusiana na atakaekua na Uaminifu kua: ‘Kuna mtu miongoni mwa
watu fulani ambae ni Muaminifu’ na itasemwa kuhusiana na mtu kua: ‘Ni Mtu
Hodari sana, Ni Mtu Mwenye akili sana, ni Mtu mzuri sana.’ Lakini Mtu huyo
hatokua na Iman ndani ya Moyo wake hata Chembe.’
Kwani pia mara kadhaa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amekua akisema katika
Khutba zake kua: ‘Hakuna Imani kwa mtu ambae si Muaminifu Kiamana na hakuna
Dini kwa yule ambae asietimiza Ahadi.’
316
Kutokana na aya ya 72 ya Surat Al Ahzab tunaona kua Allah Subhanahu wa Ta’ala
aliikabidhi Amanah kwa viumbe vyengine ikiwemo Mbingu, Milima na Ardhi lakini
viumbe hivyo vikaikataa Amanah hiyo kutokana na uzito wake na hivyo kuogopa kua
baadae vitashindwa kuitekeleza.
Anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kuhusiana na kukataa Mbingu,
Ardhi na Milima juu ya amanah hio kua: ‘Kukataa kwao huko hakui sawa na kukataa
kwa Ibilis, kwa sababu kukataa kwa Ibilisi kulikua ni kukataa kutii amri, lakini
kukataa Kulikotajwa hapa kunatokana na khiyari kwani vitu hivi viliulizwa
kwanza kabla ya kutakiwa kubeba Amanah, Na pili kukata kwa Ibilisi unatokana
na Kiburi lakini kukataa kwa vtu hivi kunatokana na Unyeneyekevu.’
Lakini hata hivyo Amanah hiyo alipopewa Bani Adam, yeye akaipokea kwa mikono
miwili. Hivyo kulingana na Mtizamo huu wa Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu
Anhu basi tunaona kua Amanah inayozungumziwa hapa si nyegine isipokua ni Sala.
Lakini kwa upande wa Ubay Ibn Qaab Radhi Allahu Anhu basi yeye anasema kua: ‘Kila
kitu ulichojaliwa na Mola wao ni Amanah hata Uchi wa Mwanamke kwake yeye
Mwanamke hua ni Amanah.’
Na kwa upande wa Abd Allah Ibn Amr Ibn Al Aas Radhi Allahu Anhu basi yeye amesema
kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala alipomuumba Mwanamme basi alimwambia
kuhusiana na Uchi wake kua ni Amanah na hivyo asiutumie isipokua kwa njia za
Halali.’
Na Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu basi yeye anasema kua: ‘Amanah
iliyokusudiwa hapa hua ni Mali na kila kitu ambacho ulichoneemeshwa na Allah
Subhanah wa Ta’ala hua ni Amanah na ulichoamrishwa Kiislam pia.’
Ambapo kwa upande wa Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, Imam
Qatadah Al Sadusi na Imam Said Ibn Jubayr basi wao wanasema kua: ‘Amanah
iliyokusudiwa hapa hua ni majukumu ya Maamrisho ya Allah Subhanah wa Ta’ala
juu yetu na Makatazo yaliyomo ndani ya mipaka aliyoiweka ndani yake.’
Ambapo tukimuangalia Imam Abu AMuhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari basi
yeye anasema kua: ‘Amanah hua ni utiifu juu ya Allah Subhanah wa Ta’ala katika
kutekeleza Maamrisho yake ya Fardhi aliyoyaamrisha kupita katika njia ya Dini
yake.’
Na Kwa Upande wa Imam Abu Qasim Al Qushayri basi yeye anasema kua: ‘Amanah
hua ni kusimamia na kutumiza kile ambacho ni wajib kulingana na kanuni za Fiqh,
317
na pia hua tunaweza kusema kua ni Imani ya Kumpwekesha Allah Subhanah wa
Ta’ala na kujilinda kwa ajili ya kutovuka nje ya mipaka yake aliyoiweka ndani ya
maamrisho yake’
Swali la kujiuliza ni kua Jee ilikuaje Bani Adam akaikubalia Amanah ambayo viumbe
vyengine waliikataa?
Tukiangalia Tafsir ya Imam Ibn Kathir basi tunaona inasema kua, Wakati Allah
Subhanahu wa Ta’ala alipovipa Amanah viumbe vyake yaani Mbingu, kisha Ardhi
na kisha Milima ilikua si katika hali ya kuvilazimisha viumbe hivyo kubeba jukuma
la Amanah hiyo, bali ilikua ni katika hali ya hiari na hivyo alivipa pia uamuzi wa
kuchagua, kwani hali hiyo ulikua katika hali ya kuulizwa: ‘Jee mtakua tayari
kuyatekeleza masharti ya Amanah hii kutoka kwetu ili mpate malipo yake?’, viumbe
vyote hivyo vikauliza: ‘Malipo gani hayo?’, na wakaambiwa : ‘Ikiwa mtaweza
kutekeleza masharti ya Amanah hii, kutokana na juhudi zenu zote, mtaliwa malipo
bora, hususan kupata ukaribu zaid mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala, lakini
ikiwa hamtoweza kutekeleza masharti yake, basi mtapata adhabu kali sana.’
Hivyo baada ya kusikia masharti ya amana hiyo viumbe vyote hivyo vikubwa vikajibu
kwa kusema: ‘Mola wetu, hata sasa hivi sisi tuko chini ya amri yako, lakini sasa hivi
(kutokana na kupewa uamuzi wa kuchagua) tunajisikia kua tuko dhaifu sana
kuubeba mzigo huo mzito na hatutoweza kutekeleza masharti yake, ama kuhusiana
na malipo sisi hatuyataki, na kuhusiana na adhabu hatuwezi kuistahmilia.’
Tukiangalia kwa upande wa Tafsir ya Imam Al Qurtubi, tunaona kua, baada ya viumbe
vitatu hivyo yaani Mbingu, Ardhi na Milima kupewa Amanah hiyo na kuikataa, basi
Allah Subhanah wa Ta’ala akamuambia kiumbe Insan au mtu: ‘Tumeipa Amanah yetu
kwa Mbigu, Ardhi na Milima lakini ikaweka wazi kutoweza kwao kubeba jukumu
zito la Amanah hiyo, Jee vipi wewe utaibeba Amanah hii ukijua uzito wa majukumu
yake?’, Mtu akauliza, ‘Ya Rabbi ni majukumu gani hayo’, na majibu yakawa: ‘Kama
ikiwa utafanikiwa kutekeleza majukumu ya Amanah hiyo kadri uwezavyo (yaani
kua mtiifu kadri utakavyoweza) utalipwa (kwa kuupata ukaribu wa Allah na
fadhila zake juu yako na pia kuishi milele Peponi) na kama ukishindwa kutekeleza
majukumu ya Amanah hiyo basi utaadhibiwa’. Hivyo Adam (akiwa na hamu kubwa
sana ya kupata kua na ukaribu na Allah na pia ridhaa yake) akakubaliana na
majukumu hayo na hivyo kuibeba Amanah hiyo.
Ni jambo lililowazi hapa kua, tukio la kupewa Amanah lilitokea kabla ya tukio la
ahadi, yaani lile tukio la kuulizwa kwa watu wote : ‘Jee mimi si Mola wenu?’, kwani
swali hilo la ahadi lililoulizwa hapo linatokana na kukubaliana kubeba Amanah na
318
kutekeleza majukumu yake. Kwani ili kua Khalifah ardhini, basi kitu cha muhimu
na cha lazima ni uwezo wa kulibeba jukumu la Amanah.
Kama ilivyokwisha kadiriwa na Allah Subhanah wa Ta’ala, kua Allah Subhanahu
wa Ta’ala alikua ameshaamua kumteua Adam kama Khalifah wake katika ardhi na
ukhalifa huu huweza kukabidhiwa yule atakaeweza kubeba jukumu la kutii
maamrisho ya muumbaji – kwa sababu lengo la ukhalifa ni kua hukmu na Sharia’h
za Allah Subhanahu wa Ta’ala zitumike ardhini na hivyo viumbe vya Allah
Subhanahu wa Ta’ala vishawishiwe kutekeleza hukmu na Sharia’h hizo. Kutokana
na utofauti wa viumbe Adam akakubali kubeba jukumu la Amanah hiyo – ijapokua
alikua akifahamu kua kuna uwezekano wa kutokea kwa baadhi ya watu miongoni
mwa viumbe hivyo, kutokua na uwezo kubeba Amanah hiyo. (Mazhari na Bayan ul
Qur’an)
Ambapo kuhusiana na tukio la ahadi linalozungumziwa hapa ni lile lililotajwa kwenye
aya isemayo:
﴿وَإِذْ أَخَذَ رَب ُّكَ مِن بَنيِ ۤ آدَمَ مِن ظُهُورِهِمْ ذُرِّي َّتَهُمْ وَأَشْهَدَهُمْ عَلَى ٰ أَنفُسِ هِمْ
أَلَسْتُ بِرَبِّكُمْ قَالُواْ بَلَى ٰ شَهِدَْ أَن تَقُولُواْ يَوْمَ ٱلْقِيَامَةِ إِ َّ كُن َّا عَنْ هَٰذَا
غَافِلِينَ۞أَوْ تَقُولُو ۤ اْ إِنم ََّآ
أَشْرَكَ آابَؤَُ مِن قَبْلُ وَكُن َّا ذُرِّي َّةً مِّن بَعْدِهِمْ أَفَتُهْلِكُنَا بمَِا
فَعَلَ ٱلْمُبْطِلُونَ۞وَكَذٰ لِكَ نُفَصِّلُ ٱلآَتِ وَلَعَل َّهُمْ يَرْجِ عُونَ ﴾
Wa-idh akhadha rabbuka min banee adama min dhuhoorihim dhurriyyatahum
waashhadahum AAala anfusihim alastu birabbikum qaloo bala shahidna an
taqooloo yawma alqiyamati inna kunna AAan hadha ghafileena; Aw taqooloo
innama ashraka abaona min qablu wakunna dhurriyyatan min baAAdihim
afatuhlikuna bima faAAala almubtiloona; Wakadhalika nufassilu al-ayati
walaAAallahum yarjiAAoona (Surat Al Araf 7:172-173)
Tafsir: Na Kumbuka pale Alipochukua Mola wako Kutoka kwa Ibn Adam kutoka
kwenye Migongo yao Vizazi vyao Na Kuwashuhudisha kwa Nafsi zao (Kwa
Kuwauliza): ‘Jee Mimi Sie Mola wenu?’ Wakasema : ‘Naam!’ Tunashuhudia; hivyo
Msije mkasema katika siku ya Malipo kua : ‘Sisi hatukua na habari juu ya hili’ au
Msije mkasema: ‘Waliokushirikisha ni Wazee wetu waliotangulia kabla yetu na sisi ni
vizazi vyao tu vilivyofuata baada yao. Hivyo utatuangamizaje sisi kutokana na
319
waliyofanya wabatilishaji?’ na hivyo ndivyo tunavyofafanua Aya zetu ili wapate
Kurudi (kwa Mola wao)
Neno Dhahara kwa Kilugha hua linamaanisha Dhahiri, Kutokea, Kuonekana,
Kutofautika, Kufunguka, Kuchomoza, Kuweka wazi, Kudhihirisha, Kujua, Kupanda
Kushinda na pia humaanisha Kudharau.
Neno Dhahara ndio lililotoa neno Adhuhuri ambalo Humaanisha wakati ambao Jua
lishachomoza na lishaupita katika Usawa wa Kichwa. Na pia neno Dhahara hua
linamaanisha Mgongo au Kumuumiza Mtu Mgongoni.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta'ala pia hakutuficha bali ametuwekea wazi kuhusiana na
tukio hilo na hii ni kwa sababu tukio hili lilitokea wakati sisi tukiwa katika hali ya
Vinasaba ndani ya Migongo ya wazee wetu na wao ndani ya migongo ya wazee wao
ndani ya mapazia ya Ulimwengu usioonekana maelfu ya miaka na miaka ndani yake.
Ambapo Anasema Jarrah Allah Imam Abu Qasim al Zamakhshari kua: Tukio hili la
Kiapo lilitokea katika hali ya Kiroho, pale tulipotakiwa na Allah Subhanah wa
Ta'ala kua Tuwe na Tukawa.
Na anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kuhusiana na aya hii
kua: Allah Subhanah wa Ta'ala aliwachukua Mitume na Manabii wote kutoka
kwenye Sehemu za Siri za Adam. Kisha akatoa katika kila Mtume na Nabii kizazi
cha Ummah wake vikiwa katika hali ya Uqul (Akili). Kisha akachukua Ahadi
kutoka kwa Mitume kwanza kama alivyosema katika aya ifuatayo:
﴿وَإِذْ أَخَذَْ مِنَ ٱلن َّبِيِّينَْ مِيثَاقَهُمْ وَمِنْكَ وَمِن ن ُّوحٍ وَإِبْرَاهِيمَ وَمُوسَى ٰ وَعِيسَى ٱبْ ِن
مَرْيمََ وَأَخَذَْ مِنْهُمْ مِّيثَاقاً غَلِيظاً﴾
Wa-idh akhadhna mina alnnabiyyeena meethaqahum waminka wamin Nuuhin wa-
Ibraheema waMuusa waAAeesa ibni Maryama waakhadhna minhum meethaqan
ghaleedhan (Surat Al Ahzab 33:7)
Tafsir: Na Kumbuka tulipochukua kutoka kwa Manabii Ahadi zao Kutoka kwako (Ewe
Muhammad) na kwa Nuh na kwa Ibrahim na kwa Musa na kwa Isa Ibn Maryam Na
Tumechukua kutoka kwao Ahadi nzito sana.
320
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari anaendelea kutuambia kua:
‘Ahadi walioitoa Mitume hawa ni kua Watafikisha Ujumbe wa Allah Subhanah wa
Ta'ala kuhusiana na Maamrisho Yake na Makatazo yake, Kisha baada ya Mitume
hio kutoa ahadi hio basi Allah Subhanah wa Ta'ala akavikusanya Vizazi vyote vya
Ibn Adam kuanzia mwanzo hadi mwisho wake kisha akawauliza Ibn Adam hivi jee
mimi sie Mola wenu?
Ibn Adam wakaitikia kua Ndie, ambapo huu ulikua ni Mtihani Juu ya Ibn Adam
na baada ya Kujibu Suali hilo na hivyo kua ni wenye Kuoa si mtihani huo basi
wakarudishwa ndani ya sehemu za Siri za Adam. Na ndio maana akawatuma kwa
ajili ya Kuwaongoa kwa kuwakumbusha Makubaliano yao Ibn Adam kwake yeye
Na ni kwake yeye Allah Subhanah wa Ta'ala kwenye Ilm ya kujua kuhusiana na
siku ya tukio hilo la Ahadi Na pia ni kwake yeye ndiko kwenye Ilm ya kujua ni nani
atakubaliana nayo ahadi hio na kuitimiza na ni nani atakaeikataa na kuikadhibisha
hakitofika Kiama hadi pale itakapokua tayari kila Mtu aliekubali na kuthibitisha
ahadi hio kua ni mwenye Kuishi Duniani’
Naam Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari aliulizwa kuhusiana na
Utiifu na Uovu mbele ya Allah Subhanah wa Ta'ala, ambapo nae akajibu kwa kusema
kua: ‘Ama kwa hakika miongoni mwa Dalili za Uovu hua ni Kukataa Utukufu wake
Allah Subhanah wa Ta'ala. Na katika Dalili za Utiifu hua ni Kutanuka kwa Kifua
na Moyo na kujaa Nuru ya Imani, na hivyo Moyo wako hua ni wenye kujazwa na
ulinzi wa kufanya Utiifu na mafanikio ya kuachana na Dunia.’
Kwani kuhusiana na Uovu na Utiifu wa mtu Mbele ya Allah Subhanah wa Ta'ala basi:
Amesema Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: Makadirio ya Maumbile ya Mtu hua ni Kuwekwa
ndani ya tumbo la Uzazi la Mama yake kwa siku 40. Kisha hua ni katika pande la
Damu kwa siku hizo hizo, na kisha hua katika pande la Nyama katika Siku hizo
hizo. Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala huamrisha kuandikwa kwa Amali, Riziki,
Kifo na Utiifu au Uasi wa Mtu huyo, Kisha Mtu huyo Hupuliziwa Roho yake.’
‘Hivyo Miongoni mwenu kuna mtu ambae atafanya Mema mpaka atafikia dhiraa
moja kukaribia kuingia Peponi halafu kile kilichokadiriwa kimfike kitatokea na
kuamua matokeo yake na ataanza kufanya Maovu ya watu wa Motoni. Na
Miongoni mwenu kuna mtu atafanya maovu mpaka itabakia dhiraa moja tu baina
yake na Moto na kisha kilichokadiriwa juu yake kitatokea na ataanza kufanya
Mema.’(Sahih Bukhari)
321
Hii ni hadith inayomaanisha kua Mbali ya kua Ibn Adam walikubali kua Allah Subhanah
wa Ta'ala ndio Mola wao na hivyo Watakua watiifu kwake, lakini hapo hapo kuna watu
wataenda Motoni na wengine wataenda Peponi.
Na hii ni kulingana na Amali zake Mtu husika kua ataenda Peponi kutokana na kutaka
kwake Mtu huyo kuenda Peponi kwa kufuata Maamrisho ya Mola wake. Na atakae enda
Motoni ataenda Motoni kutokana na Makosa yake. Kwani ndani ya Maumbile ya Uhai
wa kila Ibn Adam basi kuna kitu kinaitwa Qadar na kuna Kuna Kitu kinaitwa Qadha.
Ambapo tunaopozungumzia Qadha basi hua ni ile hi ambayo Allah Subhanah wa Ta'ala
ameibanisha katika Aya isemayo:
﴿بَدِيعُ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَإِذَا ٰ قَضَى أَمْراً فَإِنم ََّا يَقُولُ لَهُ كُنْ فَيَكُونُ ﴾
BadeeAAu alssamawati waal-ardhi wa-idha qadha amran fa-innama yaqoolu lahu
kun fayakoonu.(Surat Al Baqara 2:117)
Tafsir: Muumbaji wa Mbingu na Ardhi, anapotaka kitu kiwe, hukiambia kua na hua.
Ambapo Mujaddid Ad Din, Shaykh ul Islami Al Hafidh Imam Shihab Ad Din Ibn Hajar
Al Asqallani anasema kuhusiana na aya hii kua: ‘Qadhaa hua inahusiana na Makadirio
ya Ujumla kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta'ala ya Milele.’
‘Na Qadar hua inahusiana na Maelezo juu ya Qadha na Utekelezaji wake katika
Maisha ya Mtu husika katika Wakati husika.’
Naam..kutokana na Maana hio basi hua tunaona maana ya maneno ya Hadith yetu
isemayo kua tayari kuna Makadirio ya Mtu mwema na Muovu hua yanamaanisha kua
Allah Subhanah wa Ta'ala ni mwenye kujua Mwanzo wa kitu kama kua kwake katika
kukua kwake na mwisho wake kutokana na Ilm yake.
Na hii ni kwa sababu Kitakachompeleka Mtu Peponi au Motoni hua ni Matendo yake
ambayo hua yanabainishwa na Ilm ya Allah Subhanah wa Ta'ala juu ya mtu husika kwa
kutumia njia ya Qadar.
Ambapo neno Qadar hua linamaanisha Makadirio, Ilm, Ufaham, Kipimo kikamilifu,
Uwezo, Makisio, Maamuzi, Sharia, Mpangilio, Mandalizi. n.k
Ambapo amesema Allah Subhanah wa Ta'ala katika Qur'an kua:
322
﴿بَدِيعُ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَإِذَا ٰ قَضَى أَمْراً فَإِنم ََّا يَقُولُ لَهُ كُنْ فَيَكُونُ ﴾
BadeeAAu alssamawati waal-ardhi wa-idha qadha amran fa-innama yaqoolu lahu
kun fayakoonu.(Surat Al Baqara 2:117)
Tafsir: Muumbaji wa Mbingu na Ardhi, anapotaka kitu kiwe, hukiambia kua na hua.
Kwani Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu katika kipindi cha Utawala wake
katika wakati alipokua wakienda katika Vita vya Siffin na Jeshi lake basi aliulizwa: ‘Ya
Amir ul Muuminin! Jee hii kuenda kwetu kwenye Vita hivi kunatokana na Qadha
na Qadar ya Allah Subhanah wa Ta'ala?
Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akajibu: ‘Naam! hakika mimi nnaapa
kwa Allah Subhanah wa Ta'ala ambae ndie aliejaalia Miti na Majani yaote na
akavipa Uhai Viumbe vyake, kua Katika kila kitu basi ndani yake hua mna Qadha
na Qadar ya Allah Subhanah wa Ta'ala’
Ambapo aliemuuliza suali Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akasema:
‘Kama ni Hivyo, basi itakua kila tunachikifanya hua tunakifanyia kazi bure’
Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akasema: ‘La sio hivyo! Kwani Allah
Subhanah wa Ta'ala hua anakulipa wakati ukielekea kupigana kwa ajili yake na pia
hukulipa wakati unaporudi baada ya kupigana, na hii ni kwa sababu hakuna
aliekulazimisha kufanya hivyo bali umefanya hivyo kutokana na hiari yako
mwenyewe.’
Hivyo Sayyidna Ali Radhi Allahu Anhu akaulizwa tena: ‘Hivi Sio Qadar na Qadha ndio
inayotuongoza sisi kufanya haya tunayofanya?
Amir ul Muuminin Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu Akasema: ‘La! Hivi
wewe unafikiria kua Qadha imekuganda wewe na Qadar imeshikamanishwa na
wewe? Sio hivyo, Kwani kama ingekua kama hivyo basi ingekua hakuna Malipo ya
Thawabu wala Malipo ya Adhabu, na ingekua hakuna haja ya Pepo wala vitisho
vya Jahannam, wala Sharia wala Makatazo. Hivyo Allah Subhanah wa Ta'ala
asingewaaadhibu wale wanaofanya dhambi na wala asingewasifu wale wanaofanya
mema. Hivyo Wale wanaofanya Mema wangekua hawastahiki kusifiwa kwani ni
sawa na wale wanaofanya Maovu. Na wanaofanya Maovu wangekua haina haja juu
yao Kulaaniwa kwani ni sawa na wanaofanya Mema’
323
‘Hivyo Maneno hayo ya wanaosema kua kila tunalofanya linatokana na sisi
kuongozwa na Qadha na Qadar hua ni Maneno ya Wasioamini, yaani wapiganaji
wa Jeshi la Shaytani, Wanafiq na wasiouona Ukweli. Hao ni Walioangamia na ni
wenye kuabudu Moto walio katika Ummah huu. Kwani Allah Subhanah wa Ta'ala
amewapa Watu Maamrisho kutokana na kua ni mwenye kuwapa Uhuru wa
kuchagua’
‘Na amekataza Mambo kwa ajili ya kuwataka wakae nayo mbali mambo hayo.
Amekifanya kila kitu kua na Urahisi katika Maamrisho yake, na wala
hakuwalazimisha watu kumuasi kwa kutumia nguvu wala uwezo wake juu yao. Na
wala hakuwatuma Mitume bure bure tu!, Hakuiumba Ardhi na Mbingu na kila
kilichomo ndani yake kwa kucheza bure bure’
‘Hivyo Mawazo ya mtu kama huyo anaefikiria hivyo hua ni Mawazo ya Mtu
asieamini, hawaoni hata aibu na Moto wa Jahannam uwe juu yao. ‘
Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akaulizwa tena: ‘Haya hebu Tuambie
Jee Qadha na Qadar hua zinatuongoza kwenye nini?’
Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Qadha na Qadar ni Matakwa
na Makadirio ya Allah kama alivyosema katika Qur'an:
ٰ ﴿وَقَضَى رَب ُّكَ أَلا َّ ۤ تَعْبُدُو اْ إِلا َّ إِ َّهُ وَبِٱلْوَالِدَيْنِ إِحْسَاً ي إِم َّا َ بْلُغَن َّ عِندَكَ ٱلْكِبَرَ
أَحَدُهمَُا أَوْ كِلاَهمَُا فَلاَ تَقُل له َُّمَآ أُفٍّ وَلاَ تَنْهَرْهمَُا وَقُل له َُّمَا قَوْلاً كَرِيماً ﴾
Waqadha rabbuka alla taAAbudoo illa iyyahu wabialwalidayni ihsanan imma
yablughanna AAindaka alkibara ahaduhuma aw kilahuma fala taqul lahuma offin
wala tanharhuma waqul lahuma qawlan kareeman (Surat Al Isra 17:23)
Tafsir: Na Ametaka Mola wako Kua Usimuabudu Yeyote isipokua yeye, na kuwafanyia
wema Wazee wawili na kama mmoja wao au wote wawili kati yao ama wa akiwa wazee,
basi usiwaambie hata uf! Na wala usiwakripie na zungumz nao kwa Kauli zenye
Ukarimu. (Surat Al Isra 17:23)
Naam..aliemuuliza Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akasema: Ya Amir ul
Muuminin Hakika wewe ni Mtu ambae mtu anaweza kutegemea Radhi za Allah
Subhanah wa Ta'ala kupitia kwa kutii Maamrisho yako, kwani kwa hakika
324
umetubainishia jambo ambalo linawachanganya wengi katika Dini yetu, hivyo
Allah Subhanah wa Ta'ala akulipe kwa hayo.
Hivyo ili tufaham zaid basi inabidi tuingie kwenye Fani ya Ilm ambayo inajulikana kama
Ilm Al Kalam ambapo ndani yake tunakutana na Kanuni inayosema kua: ‘Ilm ya Kitu
husika hua juu ya kile kinachojulikana’ hivyo kutokana nayo basi bila ya shaka Allah
Subhanah wa Ta'ala hua ni Mwenye Kujua ni nani Miongoni mwetu Ibn Adam ataenda
Motoni na ni nani ataenda Peponi.
Yaani tuchukulie mfano wa vile sisi tunavyojua kua kipindi hiki cha mwezi huu Sala ya
Alfajir hua inaingia saa ngapi na ya Magharibi inaingia saa ngapi na hivyo hua tunajua
kua ikifika saa kumi na nusu jioni basi Magharibi hua haijaingia na saa kumi Usiku basi
Alfajiri bado haijaingia. Hivyo hata Ukiamka na Ukiadhini wewe saa tisa Usiku basi
huwezi kusali Alfajiri wala kusalisha Sala ya Alfajiri kwa sababu mda wa Sala ya Alfajiri
haujafika. Hivyo hii hua ni hali ya Qadha kwa sababu Allah Subhanah wa Ta'ala ametaka
iwe hivyo.
Lakini sasa tunapozungumzia kuhusiana na Qadar yaani Makadirio basi hua kuna aina
ya hali mbili:
Ambapo hali ya kwanza hua ni kuhusiana na yale mambo ambayo yako nje ya
uwezo wa Kiumbe na hivyo kiumbe hua hana hiari nayo. Kwa mfano Siku, Wakati,
wa Kuzaliwa kwake, Wazee wake, Ndugu zake, Nchi atakayozaliwa, Siku na wakati
wa Kifo chake n.k
Hivyo hii hua ni kama kwa upande wa Sala Kiumbe unakua huna hiari, kwani
ukifika wakati wake basi huwezi kuuzuia usiingie, na ukitoka wakati wake basi
huwezi kuurudisha.
Ambapo hali ya pili ya Qadar hua ni Katika yale ambayo ingawa ni Jukumu lake
Kiumbe lakini anakua na hiari juu yake kutekeleza ama la.
Hivyo na hapa tuchukulie tena Mfano wa Sala, Kua Tayari Mda wa Kusali Maghribi
umeshaingia hivyo ni Jukumu lako kusali na hivyo kua na sifa ya Kaslan (Kuona Uvivu)
au Saahun (Kudharau) hua ni Hiari yako. Na kutokana na hii Hiari basi ndio maana Allah
Subhanah wa Ta'ala akatuwekea Malaika Kiraman Katibin wawili Raqib na Atid kwa
ajili ya kutuandikia kwenye Vitabu vyetu kuhusiana na Qadar yaani Makadirio yaliyomo
ndani ya uwezo wa Hiari yetu Kimatendo.
Hivyo kama ukitekeleza Jukumu lako ipasavyo basi Malaika wataandika ipasavyo na
utalipwa na Mola wako ipasavyo. Na kama hukutekeleza Jukumu lako na ukadharau na
325
kuona Uvivu basi bila ya Shaka Utaandikiwa Ipasavyo na Utaadhibiwa na Mola wako
ipasavyo.
Ambapo kwa upande mwengine basi tunapoangalia hadith nyengine ya Qadha na Qadar
katika kitabu cha Sahih Muslim basi tunaona kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
aliwaambia Masahaba zake kua : ‘Hakuna hata mmoja Miongoni mwenu isipokua
Allah Subhanah wa Ta'ala anajua iko wapi Nafasi yake Mtu huyo katika Pepo au
Motoni’
Masahaba wakauliza: ‘Ya Rasul Allah! Hivyo Jee kwanini basi sisi tunafanya Mema?
Kwanini tusitegemee hali hio?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu: ‘La Endeleeni kufanya Mema kwani
kila mmoja kati yenu atajikuta kua kwake yeye inakua rahisi kufanya mambo hayo’
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salama akasoma Aya zifuatazo:
﴿إِن َّ سَعْيَكُمْ لَشَتى َّ ٰ ۞فَأَم َّا مَ نْ أَعْ ٰ طَى َو ٱت َّقَ ٰ ى۞ وَ صَد َّ قَ بِٱ لحُْسْ نىَٰ ۞فَسَنُيَسِّ رُهُ
لِلْيُسْرَىٰ ۞وَأَم َّا مَن بخَِلَ وَٱسْتَغْنىَٰ ۞وَكَذ َّبَ بِٱلحُْسْنىَٰ ۞فَسَنُيَسِّ رُهُ لِلْعُسْرَىٰ ﴾
Inna saAAyakum lashatta; Faamma man aAAta waittaqa; Wasaddaqa bialhusna;
Fasanuyassiruhu lilyusra; Waamma man bakhila waistaghna; Wakadhdhaba
bialhusna; Fasanuyassiruhu lilAAusra(Surat Al Layl 92:5-10)
Tafsir: Jitihada zenu katika Matendo yenu yametofautiana (Kimalengo na
kimakusudio), Hivyo kwa Yule atakaetoa (Sadaqa) na Kutekeleza Wajibu wake kwa
Allah; Na Akaamini Katika mema hayo; Basi sisi Tutamrahisishia Njia ya Kufanya
mema hayo; Na Atakae kua Bakhili na Kujiona kua Anajitosheleza; Na
Akakadhibisha Juu ya Mema hayo; Basi Tutamrahisishia Njia hio ya kufanya Maovu
hayo.
Hivyo tujitahid kutekeleza Majukumu yetu katika Kumtii Mola wetu na Kufanya Mema,
na kisha bila ya shaka Allah Subhanah wa Ta'ala ataturahisishia Njia ya Kufanya Mema
zaidi, kwani kufanya kwetu mema na kuachana na makatazo yake hua kunaonesha kua
tuna Adabu na Utiifu mbele ya Mola wetu.
326
Kwani anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Kwa
hakika miongoni mwa dalili ya kupotoka hua ni kukataa Ufalme wake Allah
Subhanah wa Ta’ala. Na kwa hakika miongoni mwa dalili za Utulivu na furaha ya
Moyo hua ni kutanuka kwa Moyo wako kutokana na kujaa Imani na hivyo kua ni
mwenye kujaaliwa utajiri wa Moyo wako, na kupata hifadhi ya kua na Utiifu kwa
Mola wako na Kuachana na Ulimwengu (Zuhd).
Kwani yeyote yule atakaejaaliwa kua na Adabu baina yake na Mola wake basi hua
ni mwenye kujaaliwa kusafishwa Moyo wake na hivyo hua ni mwenye furaha na
utulivu, na hakuna kitu chengine chochote kizuri kama kua na Adabu mbele ya
Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari anatuambia kua: ‘Ni jambo la
kawaida pale Watu wanapokabidhiana Amana basi hua ni wenye kuweka Alama
ya muhuri juu ya amana hio, na wanapoitaka kuichukua wenyewe amanah hio
basi hukagua alama ya muhuri huo, na hivyo kama alama hio ko kama ilivyokua
katika wakati wa makabidhiano basi aliekabidhiwa hua ni mwenye kupongezwa
kutokana na uaminifu wake.
Hivyo nawe umekabidhiwa Amanah pale Allah Subhnah wa Ta’ala alipokuuliza:
‘Jee mimi sie Mola wako?’ na kutokana na suali hilo basi ikawa umepigwa muhuri
kwa kuitikia kwako pale uliposema: ‘Naam bila ya shaka na wewe Ndie Mola
wangu’
Na unapofika mwisho wa Uhai wako hapa Duniani basi utapelekewa kwenye
Makazi ya Vumbi na Malaika atakuja na kukuuliza: ‘Hivi Jee ni Nani Mola
wako?’ Suali hili hua ni katika hali ya kuangalia Muhuri wako upo au haupo.’
‘Hivyo ewe Ibn Adam, Muhuri umewekwa kuanzia tangu juu ya kichwa chako
hadi kwenye Miguu yako. Huo haukua Muhuri wowote isipokua Muhuri wa
Mapenzi (Mihr) ya Mola wako juu yako. Kuonesha kua Wewe ni wake Allah
Subhanah wa Ta’ala na yeye ni kwa ajili yako’
Kwani Milima haikua na uwezo wa ya kuweza kubeba uzito wa Amanah hii, na
wala Ardhi pia, hivi jee hamjaona namna Allah Subhanah wa Ta’ala
alivyothibitisha katika Qur’an pale aliposema:
327
﴿لَوْ أَنزَلْنَا هَٰذَ ا ٱلْقُرْآنَ عَلَى ٰ جَبَلٍ ل َّرَأَيْتَهُ خَاشِ عاً م ُّتَصَدِّعاً مِّنْ خَشْيَةِ ٱهلل َِّ وَتِلْكَ
ٱلأَمْثَالُ نَضْرِبُهَا لِلن َّاسِ لَعَل َّهُمْ يَتَفَك َّرُونَ ﴾
Law anzalna hadha alqur-ana AAala jabalin laraaytahu khashiAAan
mutasaddiAAan min khashyati Allahi watilka al-amthalu nadhribuha lilnnasi
laAAallahum yatafakkaroona (Surat Hashr 59:21)
Tafsir: Lau Kama tungeishusha Qur’an juu ya Jabali basi kwa hakika ungeliona
linavyonyenyekea na kububujika kutokana na kumuogopa Allah Subhanah wa
Ta’ala. Na hio ni Mifano tunayowapigia watu ili wapate kutafakkari.
Hivi Jee mmemuona Malaika, ambae Mabawa yake akiyatanua Upana wake hua
yanauweka upeo wa Macho mawili Chini yake, lakini hata hivyo huyo Malaika nae
hana uwezo wa kuibeba Amanah hio, halafu fikiria kua Maskini Ibn Adam ambae
ngozi yake imetandazwa juu ya Mifupa yake, kama Mpiganaji Shupavu asiekua
na Woga na kunywa Mvinyo wa Mitihani kutoka ndani ya Gilasi la rafiki wa
Karibu, na hivyo kua haathiriki na mabadiliko yeyote yanayomtokea juu yake.
Jee unajua kwa nini? Kwa sababu yeye Ibn Adam ni Mmiliki wa Moyo, na Moyo
ndio wenye kubeba kile itu ambacho Mwili hauwezi kubeba yaani Nuru ya Allah
Subhanah wa Ta’ala. Hivyo wakati Adam aliechaguliwa, ambae ni mwenye
Maajabu ya Viumbe vyote na upekee wa Matamanio yake alipooona basi alipoona
kua Mbingu na Ardhi zimekataa kubeba Amanah hio basi yeye akatoka mbele
kama Ibn Adam na kuchukua jukumu la kubeba Amanah hio na kusema kua:
‘Hakika viumbe hawa wameangalia juu ya uzito wa jukumu la Amanah na hivyo
wakakataa, lakini mimi nimeangalia Ukarimu wa Mwenye Kuweka Dhamana na
ndio maana nikaichukua.’
Ambapo hapa Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari anamaanisha kua:
‘Jukumu la Kuibeba Amanah hio halichukuliwi na kubebwa kutokana Nguvu bali
hubebwa kutokana na hisia za Ari na Msukumo wa Kimaumbile wa Nafsi.’
Kwani amesema Allah Subhanah wa Ta’ala kuhusiana na Maumbile ya Nafsi na
Msukumo wake kua kama zinavyosema aya:
328
﴿وَنَفْسٍ وَمَا سَو َّاهَا۞فَأَلهَْمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا۞قَدْ أَفْلَحَ مَن زَ ك َّاهَا۞وَقَدْ
خَابَ مَن دَس َّاهَا﴾
Wanafsin wama sawwaha; Faalhamaha fujooraha wataqwaha; Qad aflaha man
zakkaha ; Waqad khaba man dassaha (Surat ash Shams 91:7-10)
Tafsir: Nnaapa Kwa Nafsi na kwa yule (Mwenyewe Allah Subhanah wa Ta’ala)
alieiweka sawa kiukamilifu, na Kisha akaionesha kwa kuitia Msukumo juu ya kile
kilichokua sicho juu yake na kilichokua ndicho juu yake. Kwa hakika Amefuzu
atakaeitakasa (Nafsi yake) na kwa hakika ameangamia yule atakaeiendekeza.
Ambao tunaona kua zetu zimetumia neno Lahama ambalo hua ni lenye kumaanisha
Kumeza Kitu, Kumeza Funda la Maji au la Chakula, ambapo neno Lahama ndio lililotoa
neno Ilham ambalo hua linamaanisha Maumbile ya Kiumbe Hisia za Unyama ndani
yake, Hali ya Kiumbe Kua na Ukaribu Mkubwa na wa haraka wenye Msukumo kutoka
kwa Muumba yaani Allah Subhanah wa Ta’ala, na pia humaanisha Ujumbe kutoka kwa
Muumba yaani Allah Subhanah wa Ta’ala.
Na ikatumia pia neno Fajara ambalo hua ni lenye kumaanisha Kumwagia Maji, Kuvunja,
Kuchimba, Kuchimbia, Kufuata upande mwengine usiotakiwa, Kusababisha kuenea na
Kumwagika na pia humaanisha Kufurika na kumwagika.
Ambapo neno Fajara ndio lililotoa neno Fajrun ambalo hua linamaanisha Kuvunjka kwa
Usiku na Kuingi kwa Asubuhi. Na pia likatoa neno Fujjar ambalo hua linamaanisha
Uovu, Utovu wa Nidhamu au Kufanya Makosa.
Na pa katua neno Waqaya ambalo hua ni lenye kumaanisha Kulinda, Kuhifadhi,
Kukiweka kitu chini ya Ulinzi ili kisidhurike na uovu au Madhara, kua Salama, Kua na
Ngao na pia humaanisha Kusamamia Jukumu. Ambapo neno Waqaya ndio liliotoa neno
Taqwa ambalo humaanisha Kujilinda, Kukaa mbali na Maovu, Kusimamia Jukumu, na
pia humaanisha Kujizuia
Na hivyo basi maneno Faalhamaha fujooraha wataqwaha hua yanamaanisha kua Moja
kati ya sifa za Ukamilifu wa Kimaumble wa Nafsi uliojaaliwa na Allah Subhanah wa
Ta’ala basi ni kua imepewa Ukaribu mkubwa sana na wa haraka wenye Msukumo
kutoka kwa Allah Subhnah wa Ta’ala wa kuoneshwa njia isiyokua sahih na hivyo ya
329
kuachana nayo na pia kuoneshwa Jukumu lake ambalo hua ni lenye kusimamia na
kuihifadhi Nafsi isidhurike kwa kufanya Makosa.
Hivyo yule atakaeisafisha na kuisimamia Nafsi hio na ikawa ni yenye kufuata njia yake
ya kimaumbile na hivyo kutofuata upande usiotakiwa basi atakua amefuzu, na yeyote
yule atakaeiendekeza na kushindwa kuisimamia basi atakua amepotoka na hua ni
miongoni mwa walioangamia.
Na ndio maana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawa ni mwenye kupenda
kuomba Dua isemayo: ‘Ya Rabb, Ipe Nafsi Taqwa yake, kwani kwa hakika wewe
ndie Msimamizi wake na Ndie Mmiliki wake, Na Isafishe kwani wewe ni M-bora
Miongoni mwa wenye Kusafisha.’
Kwani kila Ibn Adam atakuja kuulizwa juu ya Nafsi yake kama zinavyosema aya:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ ٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ م َّا قَد َّمَتْ لِغَدٍ وَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ إِن َّ ٱهلل ََّ
خَبِيرٌ بمَِا تَعْمَلُونَ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo ittaqoo Allaha waltandhur nafsun ma qaddamat
lighadin waittaqoo Allaha inna Allaha khabeerun bima taAAmaloona (Surat Al
Hashir 59:18)
Tafsir: Enyi Mlioamini Mcheni Allah na kila mmoja aiangalie Nafsi yake imetanguliza
nini (kwa Mola wake) na Mtiini Allah, kwani kwa hakika Allah ni mwenye kua na
habari juu ya kila mnachokifanya.
Ambapo katika Aya hii basi Allah Subhanah wa Ta’ala anatoa onyo kuhusiana na siku
ya Malipo kua kila mmoja atakuja kuulizwa kuhusiana na mambo matatu ambayo ni
kuhusiana na: Juu ya yale anayodaiwa na Nafsi yake; Anayodaiwa kulingana na
Anayoyajua baina yake na Mola wake, na yale anayodaiwa juu ya Ufaham wake.
Na ndio maana akasema Hasan Al Basr kua: ‘Ibn Adam anapofariki basi Ibn Adam
wenzake huulizana juu ya Ibn Adam huyo aliefariki kwa kusema: ‘Jee amewacha
Nini?’ ambapo kwa upande wa Malaika basi wao hua ni wenye kuulizana juu ya
Ibn Adam huyo aliefariki kwa kusem kua: ‘Jeea ametanguliza nini’’
Hivyo ni jukumu la kila Muumini kua ni mwenye kujitahidi kua ni mwenye kutekeleza
maamrisho ya Allah Subhanah wa Ta’ala na kufanya mema kwa ajili ya kutanguliza kwa
Mola wake na wakati huohuo sambamba akiwa ni mwenye kusimamia jukumu lake la
330
Amanah aliyokubali kuichukua kutoka kwa Mola wake, ambapo inabidi awe hivyo ili
aweze kua miongoni mwa wenye kuthibitisha juu ya kukubali kwake kubeba jukumu la
Aamana hio na hivyo kua pia ni mwenye kuisimamia na kutimiza Ahadi hio aliyoitoa
mbele ya Mola wake na kushuhudia kama zinavyothibitisha aya pale ziliposema:
﴿َوٱ ل َّ ذِي نَهُمِْ لأَمَا َ هتِ ِمْوَ عَهْ دِ هِمْرَا عُو نَ ۞وَال َّ ذِينَ هُمْ بِشَهَادَاهتِِم قَائِ مُونَ ﴾
Waalladheena hum li-amanatihim waAAahdihim raAAoona; Waalladheena hum
bishahadatihim qa-imoona (Surat Al Maarij 70:32-33)
Tafsir: Na wale ambao juu ya Amana zao na Ahadi zao wametimiza, Na wale ambao
Shahada zao wamezisimamisha.
Ambapo wenye kuzisimamisha shahada hua ni wale ambao hawakumshirikisha Allah
Subhanah wa Ta’ala baada ya kushuhudia na hivyo hawatokua ni wale ambao
wametajwa mwishoni mwa maneno ya aya yetu yasemayo:
﴿إِن َّهُ كَانَ ظَلُوماً جَهُولاً﴾
Innahu kana dhaluuman jahuulan – Kwa hakika alikua ni mwenye kujidhulumu na
mjinga.
Ambapo neno Dhaluma maana yake ni kua aliejidhulumu Nafsi yake na neno Jahula
linamaanisha kutokujua matokeo yake, na kutokana na maneno haya basi kwa ujumla
inaonekana kua Mtu analaumiwa kua ni mjinga kwa kujidhulumu kutokana na kukubali
kubeba Amanah kubwa yenye jukumu zito ambayo inazidi uwezo wake.
Lakini kutokana na maelezo yaliyowazi kutoka katika Qur’an, basi tunaona kua hivi
sivyo ilivyokusudiwa kwa sababu neno ‘Mtu’ linamaanisha Adam au Bani Adam wote.
Sasa Adam yeye kama Nabii, basi ana ulinzi wa Allah wa kutofanya dhambi. Hivyo
mzigo wa jukumu alioubeba aliubeba kihalali na kiuhakika, na matokeo yake ndio
akapewa cheo cha kua Khalifah wa Allah na akatumwa ardhini.
Adam alifanywa kua kiumbe cha kusujudiwa na Malaika, hivyo na Akhera pia, makazi
yake yatakua yapo juu kuliko hata yale ya Malaika. Na ikiwa neno ‘Mtu’ linamanisha
Bani Adam, basi katika mtizamo huu pia kuna Maelfu ya Mitume watukufu na Mamilioni
ya watu wema wa Allah (Awliya Allah) hata Malaika huwaiga - wale waliokubalika
kutokana na mambo yao katika maisha kiasi ya kua waliweza kuidhibiti na kuibeba
331
Amanah hiyo ya Allah. Kutokana na msingi huu uliowekwa na roho za watu wema kama
hawa ambao walipata haki ya kihalali na kiasili ya kubeba amana hiyo nzito kiasi ya kua
Qur’an yenyewe imetangazia kua Bani Adam ni kiumbe bora kuliko viumbe wote pale
iliposema:
Walaqad karramna banee adama (Surat Al Israa, 17:70)
Tafsir: Na kwa hakika tumemkirimu Bani Adam.
﴿وَلَقَدْ كَ ر َّمْ نَا بَنىِ ءَادَ مَ﴾
Aya hii inaonesha kua Adam hana makosa na vile vile Bani Adam hawana makosa pia.
Hivyo Mufassirin, wanaotafsiri wamesema kua meneno haya ‘Kwa hakika alikua ni
mwenye kujidhulumu na mjinga’, hayana maana ya kutoa lawama, au kulaumu, bali yapo
katika hali ya kuelezea hali ya tukio miongoni mwa wengi kati ya Bani Adam. Kiasi ya
kua, ikiwa hali ya wengi miongoni mwa Bani Adam wakajidhihirisha kua ni Dhaluman
(waliojidhulumu) na Jahulan (wajinga wasiojua matokeo ya mwisho) basi hua ni
walioshindwa kutekeleza haki na matakwa ya Amanah hiyo na wataingia katika hasara
kubwa. Bani Adam hua wanasifika hivyo kwa sababu hivi ndivyo hali halisi ilivyo kwa
idadi kubwa sana miongoni mwao.
Hivyo maana ya aya hiyo ni kua, kwa sababu Bani Adam amekubali kubeba jukumu la
Amanah hiyo, basi matokeo yake yamewagawa Bani Adam katika makundi mawili:
Kundi la kwanza ni la wasioamini, wanafiq na wengineo ambao wanapinga na pia
kuenda kinyume na maamrisho ya Allah Subhanah wa Ta’ala na hivyo wakawa ni
miongoni mwa waliolipoteza jukumu la Amana hiyo na matokeo yake ni kua
watapata adhabu kali baadae, hawa ndio ambao waliojidhulumu kutokana na
ujinga wao.
Kundi la pili ni wale walioamini na wakatekeleza maamrisho ya Allah Subhanah wa
Ta’ala, matokeo ya watu hawa ni kuingizwa katika Rehma na Usamehevu wa Allah
Subhanahu wa Ta’ala, hawa ndio watakaokua miongoni mwa waliofuzu.
Na hivi ndivyo ilivyotafsiriwa maana ya maneno Dhaluman na Jahula na wengi
miongoni mwa wafasiri – Kua maneno haya hayawajumuishi Bani Adam wote kwa
ujumla kua wana sifa hiyo. Bali inawazungumzia wale walioshindwa kutekeleza
majukumu ya Amanah waliyopewa na matokeo yake basi ni kama inavyosema aya
inayofuatia baada ya hio kua:
332
لِّيُعَذِّبَ ٱهلل َُّ ٱلْمُنَافِقِينَ وَٱلْمُنَافِقَاتِ وَٱلْمُشْرِكِينَ وَٱلْمُشْرِكَاتِ وَيَتُوبَ ٱهلل َُّ عَلَى
ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَاتِ وَكَانَ ٱهلل َُّ غَفُوراً ر َّحِ يماً ﴾
LiyuAAadhdhiba Allahu almunafiqeena waalmunafiqati waalmushrikeena
waalmushrikati wayatooba Allahu AAala almu/mineena waalmu/minati wakana
Allahu ghafooran raheeman (Al Ahzab 33: 73)
Tafsir: Hivyo Allah atawaadhibu Wanafiq wa kiume na wanafiq wa kike na Al
Mushrikûn (wanaume na wanawake wanaomshirikisha). Na Allah atawasamehe
Waumini wa kweli wa kiume na wa kike. Na hakika Allah ni mwingi wa Usamehevu
na ni mwingi wa Rehma.
Na kwa upande wa Imam Zayn Al Abidiin Ali Ibn Husayn Ibn Ali Ibn Abi Talib Radhi
Allahu Anhu ambae alikua anapenda sana kusali, kiasi ya kua anaweza akabakia katika
kusjudu kwa saa nzima. Hivyo siku moja alikua Nyumbani kwake, Nyumba yake ikawa
inawaka Moto, na yeye alikua kwenye Sijda. Watu wakatoka ndani ya Nyumba hio huku
wakinadia Moto! Moto!
Wakatoka watu wote na vitu vyao, na walipofika nje wakajiona kua wako peke yao bila
ya kuwepo Imam Zayn al Abidin Radhi Allahu Anhu. Watu hao wakanza kuulizana yuko
wap na wakajawa na khofu, wasiwasi na huzuni kubwa sana.
Lakini baada ya mda Moto ukaisha na kuzimika, watu wakaingia ndani na kumkuta Imam
Zayn Al Abidin bado akiwa kwenye Sijda huku akiwa hajadhurika hata kidogo kutokana
na Moto huo hivyo wakamsubiri mpaka alipomaliza Kusali na alipomaliza basi
wakamuuliza:‘Ya Zain Al Abidin hivi hukusikia wewe watu walipokua wakinadia
Moto Moto!?’
Imam Zayn Al Abidin akasema: ‘Bila ya shaka nilisikia lakini sasa akili yangu yote
ikakimbilia kufikiria kwenye Moto wa Jahannam badala ya kukimbilia kufikiria
Moto wa Duniani, hivyo khofu yangu ikazama kwenye moto wa Akhera kwani ndio
mkali zaidi, ikanibidi nibakie kwenye Sijda kumuomba Mola wangu aniepushe na
Moto wa Jahannam.’
Na anasema Imam Husayn Al Karabisi ambae ni mWanafunzi wa Imam Muhammad
Idris Al Shafii kua: ‘Imam Al Shafii alikua akisali katika sehemu ya robo tatu ya
Usiku na alikua akisoma aya zaidi ya 50, na wakati mwengine zaidi ya aya 100. Na
katika kisomo chake alikua katika kila aya ya Rehma akiomba Rehma kwa Mola
wake, na katika kila aya ya Adhabu alikua akiomba Maghfira baada yake, na hivyo
kua ni mwenye kujumuisha pamoja ndani ya sala yake Matumaini yake juu ya Mola
wake na Khofu yake juu ya Mola wake. ’
﴿
333
Ambapo kwa upande wa Imam Malik Ibn Anas muanzilishi wa Madhhab ya Imam Malik
basi yeye alikua katika wakati wa Sala zake basi kila akisoma Surat Takathur akifika
katika aya ya mwisho isemayo:
﴿ثمُ َّ لَتُسْأَلُن َّ يَوْمَئِذٍ عَنِ ٱلن َّعِيمِ ﴾
Thumma latus-alunna yawma-idhin AAani alnnaAAeemi (Surat Takathur 102:8)
Tafsir: Na kisha Mtaulizwa katika siku hio kuhusiana na Neema Mlizopewa.
Basi Imam Malik alikua anairudia aya hii na kuirudia huku akilia sana kutokana na
kuguswa na maana ya maneno aya hii. Na vile vile kwa upande wa Imam Sufyan Ath
Thawry yeye alikua pia na hali kama hii ya kurudia na kuirudia rudia aya huku akilia
wakati anaposali pale anapofikia katika aya ya ya 5 ya Surat Al Fatiha isemayo:
﴿إِ َّ كَ نَعْبُدُ وإِ َّ كَ نَسْتَعِينُ ﴾
Iyyaka naAAbudu wa-iyyaka nastaAAeenu(Surat Al Fatiha 01:05)
Tafsir: Hakika wewe tu ndie tunaekuabudu na ni wewe tu ndie tunaekuomba
Msaada.
Na alipoulizwa kwanini hua ni mwenye kuiruda rudia aya hii huku akilia basi Imam
Sufyan Ath Thawry alisema: ‘Kwa sababu sisi tunasema kua tunamuadudu Allah
Subhanah wa Ta’ala na kumtegemea lakini ukweli ni kua sisi hua tunategemea
Dinari na Dirham.’
Na alisema Said Ibn Muadh kua: ‘Hakika mimi nna sifa tatu ambazo hua nna hamu
sana kushikamana nazo mda wote, na hapo nitakua mzuri sana. Wakati wa kusali
hua sifikirii kitu chochote isipokua Sala nnayoisali, nikisikia hadith yeyote kutoka
kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi hua sina shaka nayo na
nnapohudhuria kwenye Maziko basi hua sifikirii chochote isipokua Maziko hayo
na kile kinachotakiwa ndani yake.’
Hivyo tunapozungumzia kuhusiana na Khushuu au unyenyekevu basi hua ni kitu
muhimu sana kuwemo ndani ya Sala, kwani bila ya kua nayo khushuu ndani yake basi
tutakua hatujatofautiana na Wanafiq ambao wao juu ya Sala zao wana hali ya Sahuun
na Kaslan, na ndio maana katika kujaribu kujitofautisha na hali yao basi ikawa
inapendekezwa kujitenga na kila kitu ambacho kitapelekea kukuondolea umakini wako
kwenye Ibada ya Sala kama alivyosema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam pale
334
alipoingia kwenye Jengo la Al Kaabah na kusali rakaa mbili, lakini kabla ya kusali basi
aliona kua pembeni kuna pembe mbili za Kondoo.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam baada ya kumaliza kusali Sala yake basi
alimwambia Uthman Al Hajabi kua: ‘Nilisahau kukwambia kua uzifunike hizo
pembe mbili, kwa sababu haitakwi ndani ya Nyumba kua na kitu ambacho
kitamshughulisha mtu mwenye kufanya Ibada.’(Imam Abu Daud)
Na ndio maana pia akasema Imam Abu Sulayman Hamd Ibn Muhammad Al Khattabi
Al Shafii kua: ‘Ama kuhusiana na kusali nyuma ya watu ambao watakua
wanazungumza, basi kwa upande wa Imam Al Shafii na Imam Ahmad Ibn Hanbal
basi wao wanasema kua ni Makruuh, na pia kua mazungumzo yao hayo hua
yanamshughulisha mfanyaji Ibada.’
Na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliwaambia Masahaba zake kua: ‘Hakika
nyinyi nyote mnapokua mnasali basi hua mnazungumza na Mola wenu, hivyo
msishughulishane na msinyanyue sauti zenu mnapokua mnasoma au ndani ya
Sala’(Musnad Imam Ahmad)
Ambapo katika wakati wetu huu wa leo ndani yake watu wenye kua na sifa ya Sahuuna
na Kaslan basi hua wanaingia pia wale watu ambao hua wanaingia Misikiti huku
wakiwa na simu zao, bila ya kuzizima au bila kuondoa mlio wa sauti na kuziweka
kimya, hivyo hii pia hua ni miongoni mwa aina ya Unafiq.
Na nnasema hivi kwa sababu Muislam huyo hua hajali yuko katika sehemu gani, kwani
kuingia kwake Msikitini hua ni kutokana na mazoea tu, yaani kama vile ambavyo Mtu
ambae hua ni mwenye mazoea ya kila siku kuenda katika majengo ya kufanyia mazoezi
na hivyo ukifika mda hua anaenda kuinama na kuinuka na kujinyoosha kwa dakika
kadhaa na kisha anatoka.
Na hivyo kutokana na kuendekeza Matamanio na Mapambo ya Kidunia basi Muislam
huyu hua ni mwenye kuyakumbatia na kuingia nayo matamanio yake na mapambo yake
Msikitini wakati akiwa mbele ya Mola wake, na matokeo yake Matamanio hayo na
mapambo ya Dunia yaliyomo ndani ya Mfuko wake wa Kanzu au wa Suaruali yanaanza
kumwita kwa mlio wa simu uwe wa mziki au mwengineo wakati yeye akiwa
anamsujudia Mola wake, na hivyo baada ya kuitwa huko na simu yake hio basi akili
yake hua kwa haraka sana ni yenye kuruka kutoka kwenye Sala na faham za kua yuko
mbele ya Mola wake na kuhamia kwenye Mapambo ya kidunia yaliyomo mfukoni
mwake.
335
Hapo hapo Muislam huyo hua ni tayari ni mwenye kuonyesha Dharau mbele ya Mola
wake, kujitoa kwenye Khushuu ya Sala yake na pia kuwatoa kwenye Khushuu za Sala
zao wenzake anaosali nao pamoja na kuwashughulisha kwa kuendekeza kuyakumbtaia
matamanio ya Dunia yake.
Hivyo inatakiwa kila mmoja wetu kujua kua unapokua unasali hua si kua upo mbele ya
Hakimu ambae haoni wewe umetia nini mfukoni mwako au unafikria nini ndani ya
Moyo wako, bali hua uko mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala ambae ni mwenye kuona
kusikia na kujua kila kitu juu yako na juu ya viumbe vyote na vitu vyengine vyote
vilivyokuzunguza katika mazingira yako na hivyo basi kama hukuzima sala yako hua
unakua ni miongoni mwa wenye kumvunjia heshima na kumuonesha dharau Mola wako
na hivyo kua ni miongoni mwa Fawaylun lil Mussalina alladhiina hum Aan Salatihim
Sahuuna na pia miongoni mwa Waidha Kamu Salati Qamu Kusala na kwa maana hio
hua hua ni mwenye kusali huku ikimilaani Sala yake hio.
Na kuhusiana na wale wenye sifa ya Alladheena hum yuraoona ambao ni wenye kufanya
Riya. Kwani wenye kufanya Riya hua ni tofauti ni wenye kufanya Unafiq, na tofauti yao
ni kua Mnafiq hua hana imani kabisa na hivyo hua ni mwenye kuficha hali ya kutoamini
kwake kwa kujionesha kufanya Ibada, ambapo kwa upande wa Mwenye kufanya Riya
basi yeye hua ni Mwenye kuamini na mwenye kufanya Mema lakini hua ni mwenye
kuyaonesha kwa watu mema yake hayo ayafanyayo.
Na bila ya shaka ni wale wenye Ikhlasi tu ndio wenye kujua kuhusiana mna Kujionesha,
wengineo wote hua hawajui na hivyo hua wanaona ni jambo la kawaida tu kufanya mema
kisha wakawa wanasifiwa nao wakwa ni wenye kujisikia raha kutokana na kusifiwa
kwao.
Na ndio maana Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari akwa ni mwenye
kuusia kwa kusema kua: ‘Tafuteni Ikhlasi ya matendo yenu kuanzia ndani kutoka
katika Nia yenu kwani ni pale tu unapokua na Ikhlasi ya kwenye nia ndio hua ni
mwenye kujua kuhisiana na Riya’
Na akasema tena Imam Abu Muhamamd Sahl Abd Allah Al Tustari kua: ‘Mja hatoonja
ladha ya Imani hadi pale atakapoachana na mambo yafuatayo: Yaliyokua Haram
kwake,Yaliyokua na Shaka, Ujinga, Vyenye Kulevya na Kujionesha. Na kisha
akawa n mwenye kushikamana na mambo yafuatayo: Kua na Ilm, Kua na usahihi
katika Matendo mema yake, Kua na Moyo Safi, Kua na Ulimi wenye Hikma, Kua
na Tabia Njema kwa watu na kua na Ikhlasi kwa Mola wake hua hajioni kwani hua
anajua Kasoro zake. ’
‘Na kwa hakika yule mwenye Kufanya Toba basi hua ni mwenye kukaa mbali na
Dhambi na hua ni Mtifu kwa Mola wake, Kwani yule mwenye Utiifu kwa Mola
336
wake hua si mwenye haja ya Kujionesha kwani hua daima yuko katika
Kumkumbuka Mola wake, na mwenye kumkumbuka Mola wake’
Kwani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliwauliza Masahaba zake kwa kusema
kua: ‘Hivi Jee nikuambieni ni kipi ambacho mimi nna kikhofia zaidi ya Masih
Dajjal?’
Masahaba Wakauliza: ‘Ni kitu gani hicho Ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hakika Mimi nnakhofia zaidi Shirk
Iliyofichikana, Ambayo ni ya kumuona Mtu akiwa Anasimama kwa ajili ya Kusali
lkisha anaipamba Sala yake kwa ajili ya wengine Ili waione’ (Sunnan Ibn Majah)
Kwani tunappzungumzia kuhusiana na Kujionesha katika Ibada kua ni Kwenye
Kumaanisha Kukadhibisha Dini na Siku ya Malipo na hivyo kua na Sifa ya Unafiq basi
hua haimaanishi katika Sala tu bali pia na katika Ibada nyenginezo kama vile alivyosema
Allah Subhanah wa Ta'ala katika Qur'an:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ لاَ تُبْطِلُواْ صَدَقَاتِكُم بِٱلْمَنِّ وَٱلأَذَىٰ كَٱل َّذِى يُنْفِقُ مَالَهُ رِ آئَ ءَ
ٱلن َّاسِ وَلاَ يُؤْمِنُ بِٱهلل َِّ وَٱلْيَوْمِ ٱلآخِ رِ فَمَثَلُهُ كَمَثَلِ صَفْوَانٍ عَلَيْهِ تُرَابٌ فَأَصَابَهُ وَابِ ٌل
فَتَرَكَهُ صَلْداً لا َّ يَقْدِرُونَ ٰ عَلَى شَيْءٍ ممِّ َّا كَسَبُواْ وَٱهلل َُّ لاَ يَهْدِى ٱلْقَوْمَ ٱلْكَافِرِينَ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo la tubtiloo sadaqatikum bialmanni waal-adha
kaalladhee yunfiqu malahu ri-aa alnnasi wala yu/minu biAllahi waalyawmi alakhiri
famathaluhu kamathali safwanin AAalayhi turabun faasabahu wabilun
fatarakahu saldan la yaqdiroona AAala shay-in mimma kasaboo waAllahu la
yahdee alqawma alkafireena (Surat Al Baqara 2:264)
Tafsir: Enyi Wale ambao Mlioamini msitoe Sadaqa Zenu Kwa Kukumbusha juu ya
kutoa Kwenu au Kwa Kufanya Adha Kama yule Ambae anatumia mali yake Ili
Aonekane na Watu Huku akiwa Hamuamini Allah Na Siku ya Malipo Kwani Mfano
wake hua kama mfano wa Jiwe Gumu ambalo Juu yake Kuna Vumbi Likanyeshewa
Mvua Kubwa Sana Na kisha ikaliwacha Likiwa Wazi na Tupu Hawawezi Kufanya
chochote Juu ya kile walichokichuma na Allah Hawaongozi watu Makafiri.
Kwani tunapoiangalia Aya hii basi bila ya shaka tunaona kua ni Aya inayoenda
Sambamba kimaana na Aya ya kwanza ya Sura yetu isemayo Araayta Alladhii
Yukadhdhibu BiAlddin yaani Jee Uemuona Yule ambae ni Mwenye kukadhibisha Dini?
337
Kwani nayo pia baada ya kuainisha Kasoro za Wenye Kutoa na kisha Kujionesha na
Kusimbulia kwa Maneno kua wao Wametoa na Kukumbusha Namna walivyosaidia na
kusimbulia, kua Hawana kitu na hivyo hua ni Sawa Na Waliokadhibisha Dini na Siku ya
Malipo na hivyo Hawakumuanini Allah Subhanah wa Ta'ala na siku ya Malipo.
Ambapo Watu hawa hua Hawana Kitu na Allah Subhanah wa Ta'ala anatutolea Mfano
wa Kua Katika Kutoa kwao basi hali yao hua Kama Jiwe la Gumu na Kubwa kama Mlima
wa Safwa lililovaa Koti la Vumbi Kubwa halafu Jiwe hilo likanyeshewa Mvua Kubwa
Sana.
Ambapo katika kiweka wazi maana halisi ya aya hii basi Allah Subhanah wa Ta’ala neno
Wabilun ambalo ni lenye kutokana na neno Wabala ambalo hua linamaanisha Mvua
Kubwa Sana na yenye Matone Makubwa na Mazito sana ya Maji kiasi ya kua kama
yakikupiga basi hua yanaweza kukusababishia Madhara. Na hivyo aya kua ni yenye
kuweka wazi kua Jiwe hilo mbali ya ukubwa wake na maumbile yake ya kua na mapango
na michongoko lakini likishukiwa Wabilun basi hua ni lenye Kuvuliwa Koti lake lote la
Vumbi liliopo Juu yake na katika kila Michongoko na mapango yake na hivyo kua tupu
kiasi ya kua hata uzito wake hupungua, yaani hivyo ndivyo pia Unavyopungua Uzito wa
Kile unachokitoa baada ya Kusimbulia na Kujionesha.
Ambapo kwa upande mwengine ambao ni kulingana na Mtizamo wa Imam Muhammad
Ibn Jarir At Tabari basi yeye anasema kuhusiana na Aya hii kua:
Amesema Amr Ibn Hurayth kua: ‘Kuna Mtu alienda katika Vita Vya Jihad, na kisha
hakua ni Mwenye Kufanya Dhambi yeyoye Ndani yake lakini akawa ni mwenye
Kurudi Vitani huku akiwa hana Malipo yeyote mbele ya Mola wake’
Hivyo Amr Ibn Hurayth akaulizwa: ‘Itakuaje Hali hio?’
Amr Ibn Hurayth akasema: ‘Hii hua ni Hali ya Muislam ambae Alienda katika Vita
vilivyoamrishwa na Allah Subhanah wa Ta'ala na kisha alipofika Vitani akawa ni
mwenye Kumlaumu Kiongozi wake kwa kusema: ‘Hakika Mimi sitoenda Tena nae
Vitani Kiongozi huyu!’
Huyu hua ni Mtu ambae Hua hana Kitu katika Malipo ya Waliopigana Jihadi, na huyu
ndie yule ambae Allah Subhanah wa Ta'ala anamzungumzia kwa kusema: Enyi Wale
ambao Mlioamini msitoe Sadaqa Zenu Kwa Kukumbusha juu ya kutoa Kwenu au Kwa
Kufanya Adha Kama yule Ambae anatumia mali yake Ili Aonekane na Watu Huku
akiwa Hamuamini Allah Na Siku ya Malipo
Ya Allah! Huu ni Mtihani mkubwa Sana kwani Ukiangalia Ndani yake aya hii basi hua
Wanaingia pia Wale Ambao Wasiofuata Mitizamo ya Viongozi wao wa Dini Katika
338
Jamii zao Kiibada na Kuwakosoa na kisha badala yake Wakawa wanawafuata Kiibada
Viongozi wa Nchi Nyengine walio Mbali kabisa na Jamii zao kwa mfano kuhusiana na
Miandamo ya Mwezi. Na hii ni kwa Sababu Tunapozungumzia Riya na Kujiona na
Kujionesha katika Ibada basi tunazungumzia Bahari pana sana yenye kina kirefu sana.
‘Kwani Hakuna Mwenye Kujua kuhusiana Ujinga isipokua yule ambae ni Mwenye
Kua na Ilm.’
Ambapo anasema Shufay Ibn MaAati ambae alikua ni Tabiina amesema kua: ‘Siku Moja
Mimi Niliingia katika Mji wa Madinah na nikamuona Mtu ambae alikua
amezungukwa na watu Hivyo nikauliza Huyu Ndie Nani?’
Nami nikaambiwa kua: ‘Huyu ndie Abu Hurayra’
Hivyo baada ya kusikia Jina lake basi nami nikamsogelea Mtu huyo na kumsogelea
hadi nikamfikia katika wakati ambao watu walikua wameshapungua. Nami
nikamwambia: ‘Nakuomba kwa Al Haqq na najua kua Unasema Ukweli, hivyo
tafadhali niambie Jambo ambalo umelisikia Moja kwa Moja kutoka kwa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu akaniambia
mimi kua: Bila ya Shaka nitakuambia wewe kile ambacho mimi nimekisia Moja
kwa Moja kutoka kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na nikakifaham
ipasavyo’.
Lakini sasa kabla ya kuniambia kitu hicho basi Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu
akazimia.
Kisha baada ya Mda akapata ufaham na kizidukana na kisha kuniambia:
‘Nitakuambia Jambo ambalo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliniambia
mimi Nyumbani kwake wakati ilipokua hakuna mtu yeyote ndani ya Nyumba yake’
Kisha Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu akazimia tena, na kisha akapata faham na
kuzindukana, kisha akasema: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ameniambia
kua: Allah Subhanah wa Ta'ala atawafufua Watu katika siku ya Malipo na
kuwakusanya na atakuja kuwahukumu. Na kila mtu atakua amepiga Magoti’
Subhana Allah! Ya Allah!
Kwani hapa ndio Unaona kwanini Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu akawa ni
mwenye Kuzimia kwa Khofu ya Ujumbe uliomo kwenye Manano aliyoyasema
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, ambapo Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu
anaendelea kwa kusema: ‘Mtu wa Mwanzo kuitwa atakua ni Mtu alieisoma Qur'an
na Mtu aliepigana Jihadi na kuupata Ushahidi na Tajiri aliepewa Mali na Allah
Subhanah wa Ta'ala.’
339
Na Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala atamuuliza Mwanazuoni wa Qur'an kwa
kusema: ‘Hivi Jee Mimi sikukufundisha wewe kile ambacho nilikishusha kwa
Mtume wangu.’
Ambapo Mwanazuoni huyo atasema: ‘Naam..Bila ya Shaka Ndio ewe Mola wangu.’
Allah Subhanah wa Ta'ala atauliza: ‘Hivyo Jee ulitumia vipi Ilm Uliyojifunza?’
Mwanazuoni huyo atasema: ‘Nilitumia usiku wangu na Mchana katika Kuisoma’
Allah Subhanah wa Ta'ala atasema: ‘La Hakika wewe Unasema Uongo!’
Na Malaika nao watasema: ‘Hakika wewe Unasema Uongo! ’
Allah Subhanah wa Ta'ala atasema: ‘Kwani wewe Ulifanya hivyo kutokana na
kutamani kua Watu waseme kua fulani ni Mwanazuoni na Watu wamesema Juu ya
hilo kuhusiana nawe’
Kisha ataitwa Mtu aliepewa Mali na kuulizwa: ‘Hivi Jee Mimi sikukuneemesha
wewe kwa Mali kiasi hukua na haja ya Kumuomba yeyoye?’
Aliepewa Mali atasema: ‘Naam..Bila ya Shaka Ulinineemsha ewe Mola wangu’
Allah Subhanah wa Ta'ala atauliza: ‘Hivi Jee Ulitumiaje Mali hio?’
Aliepewa Mali atasema: ‘Hakika Mimi niliitumia kwa ajili ya Kuunga Udugu, Kwa
kuitumia kwa ajili ya Ndugu na Jamaa zangu na Nikatoa Zakkah na Sadaqa.’
Allah Subhanah wa Ta'ala atasema: Hakika wewe Ni mwenye Kusema Uongo
Na Malaika watasema: ‘Hakika Umesema Uongo!’
Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala atasema: ‘Wewe Uliitumia kwa sababu ya Kua na
hamu ya Kuonekana kua ni Mkarimu Na hivyo watu wakusifie, na Wamekusifia
Juu yako’
Kisha Ataulizwa Mpiganaji Jihadi aliefariki na Kupata Ushahidi: ‘Hivi wewe
Ilikuaje Mpaka Ukauliwa?’
Mpiganaji huyo atasema: ‘Ewe Mola wangu Uliamrisha kua watu wapigane Jihadi
kwa ajili yako, hivyo na mimi nimepigana na kuuliwa kwa ajili yako.’
340
Allah Subhanah wa Ta'ala atasema: Hakika wewe Unasema Uongo
Na Malaika watasema Hakika wewe Umesema Uongo!
Allah Subhanah wa Ta'ala atasema: ‘Hakika wewe Ulipigana na Kuuawa kwa
Sababu ulikua unataka watu waseme kua wewe ni Shujaa mahiri sana, na Watu
wamesema hilo kuhusiana nawe’
Kwani Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu anaendelea kusema kua: ‘Hapa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akanipiga Goti langu na kisha akasema: 'Hawa
ndio watakaokua Watu wa Mwanzo Kutumbukizwa Motoni kua kama kuni za
Moto huo’
Hivyo kila mmoja wetu anatakiwa azingatie kua hii hali ya inayohusiana na hawa watu
watatu hawa waliotajwa kwenye Hadithi hii ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam,
basi itamkuta pia kila Mmoja wetu, kwani tutaulizwa katika Kila Jambo letu tulifanya
kwa ajili gani?
Na kama hatutokua na Ikhlasi katika nia basi sote tutakua ni Miongoni mwa Alladhiina
Hum YuraaUna - Wenye Kujionesha katika Amali zao kwani amesema Allah Subhanah
wa Ta’ala kua:
﴿مَن كَانَ يُرِيدُ ٱلحَْيَاةَ ٱلد ُّنْيَا وَزِينَتَهَا نُوَفِّ إِلَيْهِمْ أَعْمَالهَُمْ فِيهَا وَهُمْ فِيهَا لاَ
يُبْخَسُونَ۞أُوْلَٰئِكَ ٱل َّذِينَ لَيْسَ لهَُمْ فىِ ٱلآخِ رَةِ إِلا َّ ٱلن َّارُ وَحَبِطَ مَا صَنَعُواْ فِ يهَا
وَابَ طِلٌ م َّا كَ انُواْ يَعْمَ لُونَ ﴾
Man kana yureedu alhayata alddunya wazeenataha nuwaffi ilayhim aAAmalahum
feeha wahum feeha la yubkhasoona; Ola-ika alladheena laysa lahum fee al-akhirati
illa alnnaru wahabita ma sanaAAoo feeha wabatilun ma kanoo yaAAmaloona
(Surat Hud 11:15)
Tafsir: Yeyote yule anaetaka Maisha ya Kidunia na Mapambo yake tutamlipa malipo
ya amali zake ndani yake kikamilifu bila ya kumpunguzia. Hao ni wale ambao hawana
sehemu yao Akhera isipokua Moto na ni bure matendo yayo waliyoyafanya ndan yake
(Duniani na ni batili waliyokua wakiyafanya.
Kwani anasema Mujaddid Ad Din, Shaykh Ul Islami Muhyi Ad Din Imam Abu Zakarriyah
Sharaf An Nawawi kua:
341
Kujionesha hua kuko katika aina Mbili, Ambazo aina zote huzifanya Amali kua
hazina thamani
Aina ya Kwanza hua ni Kufanya Ibada kwa ajili ya kupata ukaribu na Allah
Subhanah wa Ta'ala huku ukiwa ni Mwenye Kutegemea Kusifiwa na Watu
Aina ya Pili hua ni Kufanya Ibada kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta'ala ili kupata
Kusifiwa na Watu.
Kisha Imam An Nawawi anaendelea kutuambia kua: ‘Hakuna Mtu anaeweza
Kuifahamu Riya na kuyafaham Maumbile yake kwa Namna yalivyofichikana,
Isipokua kwa yule Mtu ambae ni Mwenye kuitafuta Ikhlasi, kwani Mtu huyo hua
ni mwenye Kujitahidi Kuufaham Uhalisia wa Kujionesha ili aweze kua ni Mwenye
Kujua Uhalisia wa Ikhlas.’
Ambapo kwa upande wa Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari basi yeye
anasema kua: ‘Hakuna Kitu Kigumu kwa Nafsi kama Ikhlasi na hii ni kwa sababu
Nafsi yenye Matamanio hua haiwezi kua na Ikhlasi.’
‘Na hii pia ni kwa sababu hisia za Nafsi kupenda Riya au Kujionesha hua zina
Nguvu kubwa sana kiasi ya kua huweza Kupenya ndani ya Imani imani ya Mtu.’
‘Ambapo ndani ya Imani ya Mtu hua ndio kwenye Chanzo cha Ibada za Fardhi,
hivyo basi Imani ya Mtu huweza kughilibika na kua ni ya Unafiq kutokana na
Kujionesha.’
‘Na hii huonekana wazi pale Mtu anapokua kwa Muonekano wa nje anaonekana
hana kasoro kutokana na Mtizamo wa kila mtu juu yake, lakini sasa hua ni Allah
Subhanah wa Ta'ala pekee ndie Mwenye kujua Mtizamo wa Ndani wa Mtu huyo na
mtizamo huo wa ndani ya Moyo wake unapokua tofauti na Mtizamo wa nje basi
Mtu huyo Tayari hua ni Mwenye Kufanya Riya au Kujionesha na hivyo hua ni
Mnafiq.’
‘Hivyo Basi Kitendo cha Mtu yeyote yule kitakachofanywa na kikawa ni tofauti na
Mtizamo wa Moyo wake basi hua ni kitendo cha Kujionesha kwa sababu ya
kutokana na Athari ya Watu wengine Juu yako basi hua ni Shirk.’
Kwani ili tuijue zaid Ikhlasi ili tuweze kukimbia Kujionesha basi na tumuangalie Imam
Abu Qasim Al Junayd ambae yeye anatuambia kua: ‘Ikhlasi hua ni Kitendo ambacho
ndani yake hakitafutwi kitu chochote isipokua kutafutwa Ukaribu wa Allah
Subhanah wa Ta'ala popote pale kitakapofanyika Kitendo hicho.’
342
Siku moja Amir ul Muuminin Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu alimkuta Sahaba
Muadh Ibn Jabal Radhi Allahu Anhu akiwa amekaa kwenye Kaburi la Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam huku akiwa analia, Sayyidna Umar Radhi Allahu Anhu
akamuuliza Muadh Ibn Jabal Radhi Allahu Anhu: ‘Ya Muadh mbona Umekaa hapo
huku ukawa unalia?’
Ambapo Muadh Ibn Jabal Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Hakika mimi simlilii Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam bali nnalia kutokana na kukumbuka Maneno yake
ambayo aliniambia alipokua katika sehemu hii hii kua hata sehemu Ndogo tu ya
Kujionesha hua ni Shirk’
‘Na hivyo wale watu watakao kua na Taqwa basi watakua na thamani kubwa sana
mbele ya Allah Subhanah wa Ta'ala ambao watakua:
Watakapokua hawapo katika sehemi basi Watatafutwa. Watakapo kua wapo
katika sehemu basi Hawatojulikana kama ndio wao. Hao ndio Taa za Ilm na
Viongozi wa Uongofu.’
Ambapo alisema Hasan Al Basr kua : ‘Hakika mimi nimeishi na Masahaba 70
waliopigana Vita vya Badr na kama Leo Hii Watafufuka basi Kama Nyinyi
Mtawaona Wanavyoishi basi Mtawaona kua ni Wenda Wazimu kutokana na Khofu
yao Juu ya Allah Subhanah wa Ta'ala’
‘Na Wao wakikuoneni Nyinyi Leo hii Mnavyoishi basi watasema kua Nyinyi
Hamkumuamini Allah Subhanah wa Ta'ala na hawatokujueni isipokua kwa
Kukuoneni Kibla Chenu katika Wakati mnaposali.’
Na bila ya shaka ingawamaneno haya ya Hasan Al Basr aliyazungumza kuwaambia watu
wa Jamii yake ndani ya Miaka 100 ya kwanza ya Uislam, lakini maana yake natgusua
tena sana hadi sisi leo hii. Hivyo ili kufaham zaid maana aliyokua akiikusudia Hasan Al
Basr basi hakuna mifano mizuri kuliko ile inayoonesha namna watu Wema waliotangulia
Kabla yetu walivyokua Wakiichukulia maana ya aya tunayoinglaia yasemayo Alladhiina
hum Yuraauuna - Wale ambao ni wenye Kujionesha Katika Amali zao.
Na hivyo kua ni wenye Kuogopa sana na Kuikimbia hali ya YuraaAuna kwani mfano wa
Kwanza tunakutana na Mfano wa Imam Sufyan Ath Thawry ambae yeye alikua akiingia
kwenye Mtaa na kisha akaona Mbele yake kuna watu wanaomjua, basi alikua
akibadilisha Njia, kwa Sababu ya Kuogopa kua huenda Watu hao wataanza kuoneshana
kua huyu ndio Imam Sufyan Ath Thawry Mcha Mungu Mkubwa sana.
343
Na hivyo Sufyan Ath Thawry alikua akiogopa kua huenda Kuoneshana kwao huko
kuhusiana nae huenda kukamfanya Ajisikie na Kujiona na hivyo kuhesabiwa na Mola
wake kua yeye ni Miongoni mwa wenye Kujiona katika Amali zao.
Mfano wa Pili tunachukua Mfano wa Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad
Din Imam Al Shafii Al Thani Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii ambae Darja yake kwa leo basi hakuna
anaemfikia kwani ni sawa na Mitume wa Bani Israil, kitabu chake cha Ihya Ulum Ad Din
tu kinathibitisha ukubwa wa Ilm yake na Darja yake kwani ni Imamu ambae anakubalika
na Kunukuliwa na Madhhab yote ya Kiislam ya Hanafi, Malik, Shafii, Hanbal, Ibadhi na
Shia pia, na ili kuyajua haya basi inabidi umsome na umjue kwa kumfanyia utafiti wa
kina.
Ambapo katika wakati wa kipindi cha Uhai wake basi alipofikia Umri wa miaka 40 alikua
tayari vitabu vyake vinasomwa kwenye Ulimwengu mzima wa Kiislam, hii ilikua ni hali
ambayo kwake yeye ilikua ni ya Mtihani kwani alikua kama Mfalme kwa namna watu
wanavyomkubali, hivyo akaingiwa na khofu kutokana na kuona huenda hli ho
ikabatalisha amali zake njema Mbele ya Mola wake, hivyo akaamua kujitolea kwa ajili
ya Mola wake kwan ialihisi kua md wake wote alikua akiwatumikia Waislam kwa
kuwanufaisha kwa Ilm Yake bila ya kumuangala Mola wake.
Hivyo Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani
Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al
Shafii akamua kuhama kutoka kwenye Mji wake wa Baghdad hivyo akaiweka familia
yake chini ya Usimamizi wa Kaka yake ambae ni Imam Ahmad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Ghazali na kumkabidhi fedha za matumizi yao kwa mda atakaokua hayupo
pamoja nao.
Kisha Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani
Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al
Shafii akaaga na kuondoka na kutembelea sehemu mbali mbali za Ardhi za Kiislam bila
ya kujulikana kua yeye ni nani, wala kujitambulisha na alikua akifikia katika Mji basi
alikua akifikia Miskitini na kua ni mfanyaji usafi wa Msikiti anaoufikia na kila siku
husafisha kuanzia ndani, nje mpaka vyooni, na alikua hakai mda mrefu katika Mji
anaofikia kwani kuna baadhi ya Miskiti ilikua inasomeshwa darsa kupita katika Vitabu
vyake, hali hii ilikua ikimfanya kujihisi kua huenda akaanza kujiskia ndani ya Nafsi yake
na kumkosesha Unyenyekevu mbele ya Mola wake.
Katika safari zake Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii
Al Thani Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al
Tusi Al Shafii alihama kutoka katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa wa Damascus wa Banu
344
Ummayad baada kua ni mfanyaji Usafi wa Msikiti huo, kisha jioni moja wakati Darsa
inaendelea basi Imam Mkuu wa Msikiti huo anaesomesha Darsa aliulizwa Suali kisha
nae kajibu kwa kusema kua Kuna mitizamo tafauti juu ya hili ambapo kwa mfano Hujjat
ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Al Ghazali amesema kuhusiana na suali kua..
Ambao Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani
Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al
Shafii hapo hapo akanyanyuka na kuondoka na kuhama katika Msikiti huo kutokana na
kua na Khofu ya kua asije akaingia na hali ya kujiona kua ananukuliwa na Imam huyo
kwenye darsa hio, ambapo ili ujue ukubwa wa Ilm ya Imam huyo wa Msikiti huo aliekua
akimnukuu Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani
Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al
Shafii basi pia inabidi ujue kua tuapozungumzia Msikiti wa Banu Ummayad ambao ni
Msikiti Mkuu wa Ijumaa wa Damascus nchini Syria basi hua tunazungumzia Msikiti
ambao ndani yake umetoa na unatoa Wanazuoni wakubwa na darsa zake zinasomeshwa
na Maimamu wakubwa wa fani za Ilm mbali mbali za Dini ya Kiislam, kwani hata Imam
na Nawawi ametoka kwenye Msikiti huo na pia amesomesha kwenye Msikiti huo.
Vile vile katika wakati wake huo ambapo ulikua ni wa kipindi cha muda wa Miaka 10
ambayo mwisho wake alimalizia katika Masjid Aqsa na ndimo alimoandika kitabu chake
cha Ihya Ulum Ad Din, basi Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam
Al Shafii Al Thani Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al
Ghazali Al Tusi Al Shafii alifikia safari moja katika Msikiti ambao aliendelea kufanya
Usafi kama kawaida yake, ambapo siku moja wakati akiwa amelala kwa kujipumzisha
ndani ya Msikiti huo, huku Maimamu wa Msiiti huo wakiwa wanaendelea kusomesha
Darsa, basi akaja Mtu na kuwauliza suali Maimamu hao, huku yeye akisikia suali hilo
ambapo nao wakashindwa kutoa jawabu la suali hilo.
Hivyo wakati alieuiza suali aliposhindwa kupata jibu na akuamua kutoka Msikitini basi
akapitia karibu na sehemu aliyokua amejinyoosha Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az
Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad
Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii huku akiwa na muonekano unaosikitisha
kwenye Uso wake kutokana na kutopata ufumbuzi wa sual lake hilo. Hivyo Hujjat ul
Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani Imam Abu Hamid
Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii akamuita mtu
huyo na kumpa jibu la suali lake hilo.
Ambapo Mtu huyo akaanza kucheka kwa sauti na kusema: ‘Unafikiria kua mimi sikujui
wewe? Wewe si mfagiaji tu na mpigaji deki wa Msikiti huu, hivyo inakuaje inajidai
unajua jibu lake wakati wale pale unaowaona ni Maimamu wa Msikiti huu
wameshindwaa kutoa jibu lake, hivi jee unafikiria nitaweza kukuamini mimi?’
345
Baada ya kusema hivyo basi wale Maimamu walioulizwa suali basi wakaja karibu kutaka
kujua imekuaje mpaka yule mtu akawa anasema hivyo? Na walipofika na kumuuiza Mtu
huyo imekuaje basi yule Mtu akasema: ‘Kuhusiana na lile suali nililokuulizeni na
mkashindwa kulijibu basi huyu mfanya usafi hapa Msikitini amesema kua jibu lake
ni kadhaa wa kadhaa’ hivyo wale Maimamu wakaangaliana na kutafakari kisha
wakatabasamu na kusema: ‘Naam…huyu bwana itakua yuko sahih kuhusiana na
suali lako hili..Sahih’
Kisha wakamgeukia Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii
Al Thani Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al
Tusi Al Shafii huku wakiwa wamejwa na mshangao na kumuuliza: ‘Ah! Hivi wewe
umejuaje juu ya jibu lake? kwani wewe ni nani? Mbona una Ilm kubwa kiasi
hicho?’.
Ambapo hapo hapo bila ya kujibu Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din
Imam Al Shafii Al Thani Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad
Al Ghazali Al Tusi Al Shafii basi akanyanyuka kisha kisha kaenda kuchukua vitu vyake
na kuhama kutoka katika Mji wenye Msikitini huo, kwa khofu ya kutotaka kujulikana
kua yeye ni nani ili asiipe Nafsi yake nafasi ya kua ni yenye kumkosesha Unyenyekevu
kutokana na kua ni mwenye kujiona.
Naam...ukiangalia Mifano hii basi unaona uhalisi wa maneno ya Imam Hasan Al Basr
kua sisi leo hii mtu akifanya hivyo basi ataonekana ni Mwenda wazimu...lakini watu
hawa walikua wakipigana Vita na Matamanio ya Nafsi zao ili zisiweze kua na hisia za
Kujiona na hivyo kua na Ikhlasi katika Ibada zao.
Kwani mfano mwengine ni ule wa Imam Yahya Ibn Muadh ambae yeye alikua akienda
Katika Ibada ya Hija basi alikua akienda peke yake na kivyake vyake.
Alipoulizwa kwanini hakuondoka na Misafara ya Mahujaji wakienda Makka katka Ibada
ya Hijjah basi alisema kua: ‘Kuondoka na Msafara wa Mahujaji kwangu mimi hua
si chochote isipokua ni Kujionesha katika Ibada’ Na sio yeye tu bali pia Imam Abu
Ubayd alikua akisema hivyo hivyo.
Naam hivyo ndivyo watu waliotangulia kabla yetu walivyokua wakiogopa Riya au
Kujionesha katika Kila kitu chao.
Hivyo Jee Kama watu hawa watafufuliwa leo hii na kisha wakatuona mimi na wewe
tunaojiita kua ni Waislam na namna tunavyoishi watasema Tumeamini kweli?
346
Wakati kila mtu anataka ajulikane kua yeye anafuata Saudia, au anajua zaidi leo amesali
Msikiti fulani au amaeenda Umra Makkah au Kuhiji na Selfie na Video kwenye Insta,
Facebook na whatsapp n.k tunatuma
Kwani Jee na sisi mimi na wewe leo hii tukiwaona watu kama hawa hatutosema kua ni
Wendawazimu au Wanajifanya wacha Mungu Sana kwa namna wanavyomuogopa Allah
Subhanah wa Ta'ala na kuikimbia Riya na kupigana vita na Matamanio ya Nafsi zao kwa
nguvu zao zote ili wawe na Ikhlasi katika Ibada zao?
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi
kua; ‘Kuna mtu alimwambia mwenzake ambae alikua amekaa kwa mda mrefu
katika kusjudu, hivyo akamwambia baada ya Kusali kua: ‘Ingekuwa Vizuri zaidi
kama Sijda yako hiyo ungeifanya Nyumbani kwako.’ Na hii ni kwa sababu Riya hua
vigumu kuonekana na mtu aifanye kwani hua ni sawa na Sisimizi mweusi aliepo
kwenye Jiwe Jeusi tena katika Usiku wa kiza.’
Anasema Imam Jamal Al Islam Abu Qasim Ibn Hawarin Ibn Abd Al Malik Ibn Talha Al
Qushayri kua: ‘Kwa miaka mingi kulikua kuna Shaykh ambae alikua kila siku
anawahi kwenye Safu ya mbele katika Msikiti ambao alikua akisali kila siku. Siku
moja akapatwa na dharura na hivyo akachelewa kuenda Msikitini na ikambidi asali
katika Safu ya Nyuma kabisa. Kisha baada ya siku hio akawa hakuonekana tena
Msikitini hapo’
Ambapo baada ya mda alipoonekana njiani na akaulizwa kwanini siku hizi
haonekani Msikitini basi Shaykh huyo akajibu kwa kusema kua: ‘Siku zote mimi
nilikua nikisali kwenye Safu ya Mbele, kwa takriban mwaka mzima na nilikua
nahisi kua nilikua nna ikhlasi katika kusali kwangu huko. Lakini katika siku
ambayo nilichelewa kusali, basi niliona aibu kua huenda kuna mtu ataniona nikiwa
nasali katika safu ya nyuma.’
‘Kutokana na tukio hili na kuhisi kwangu huko basi nikajua kua katika kusali
kwangu kote basi mimi sikua na Ikhlasi ndani ya Sala zangu nilizosali Msikitini,
kwani nilikua na khofu juu ya namna watakavyonifikiria Waislam wenzangu, hivyo
nikaamua bora niwe nasali Nyumbani.’
Na ndio maana kwa upande wa Hujjat ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn
Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali katika Fatwa zake basi akasema : ‘Kama ikiwa
Mtu atakua anaona kua anaposali peke yake hua anakua na unyenyekevu zaidi basi
kwa mtu kama huyo hua ni bora kwake kusali peke yake nyumbani kwake.’
Mujaddid Ad Din Shaykh ul Islam Imam Abu Zakarryah Sharaf An Nawawi anasema kua:
‘Ni vigumu sana kwa Mtu kua ni Mwenye uwezo wa kuijua Riya, na kuyajua
347
maumbile ya uficho wake, hivyo ili mtu uwe ni mwenye kua na uwezo wa kujiua
Riya basi inabidi kwanza ujue uhalisi wa Ikhlasi’(Bustani Al Arifin.)
Ambapo amaesema Imam Abu Qasim Al Junayd kua: ‘Ikhlasi hua ni kitendo ambacho
ndani yake hakitafutwi kitu chochote isipokua Ukaribu wa Allah Subhanah wa
Ta’ala Popote pale kitakapofanyika kitendo hicho.’
Ambapo alisema Imam Abu Yazid Al Bistami kua: ‘Hakika mimi nilikua mhunzi wa
Nafsi yangu kwa Muda wa miaka 12, ambapo baada ya miaka mitano nikakiona
kioo cha Moyo wangu, na kisha baada ya mwaka nikaanza kuuchunguza Moyo na
Nafsi yangu, na nikaanza kuona ufuniko kwenye Moyo wangu, hivyo nikatumia
miaka 12 kuukata ufuniko huo, halafu ghafla nikaona ufuniko juu ya Nafsi yangu
na hivyo nikatuma miaka 5 kuukata na kisha baada ya hapo ndio nikapata Ufunuo,
na baada ya hapo ikawa nikiwangalia viumbe basi hua nawaona kua ni wafu (yaani
hawawezi kumnufaisha wala kumdhuru, hawawezi kumpungizia wala
kumuongezea chochote) na hivyo nikaanza kumkuzisha Mola wangu mara nne zaid.
’
Na akasema Imam Abu Said Al Kharaz kua: ‘Ikhlasi haiwezi kua Ikhlasi isipokua pale
inapokua na Usadikisho na Subra ndani yake, na Subra haiwezi kua ni Subra
sipokua pale inapokua na Ikhlasi na Usadikisho ndani yake na Usadikisho hauwezi
kua Usadikisho isipokua pale utakapokua na Ikhlasi na Subra ndani yake.’
Na akasema tena Imam Abu Qasim Al Junayd kua: ‘Mtu mwenye kufanya Ibada kwa
Ikhlasi hua ni mwenye kubadilisha Ufanyaji wa Ibada zake mara 40 kwa siku,
ambapo Mtu mwenye Unafiq hua ni mwenye kudumu na hali yake hio hio kwa
Miaka 40 ’ yaani Mtu huyo huyo hua si mwenye kuridhika na namna ya kufanya Amali
hio hio moja katika hali moja tu kila siku, bali hua ni mwenye kutafuta njia ya kuboresha
Amali zake katika kila hali, ambapo katika hili ndio tunaona umuhimu wa kutafuta Ilm
yaani mtu hutakiwi kua ni mwenye kutosheka na I’lm uliyokua nayo tu kama walivyo
wengi miongoni mwa Waislam wa leo, bali unatakiwa uwe ni mwenye kutafuta Ilm zaid
na kutafakkari zaidi ili kuboresha amali zako kwa Ikhlasi.
Kwani anasema Allah Subhanah wa Ta’ala katika Qur’an kua:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞تَنزِيلُ ٱلْكِتَابِ مِنَ ٱهلل َِّ ٱلْعَزِيزِ ٱلحَْكِيمِ۞إِ َّ أَنزَلْنَآ إِلَيْكَ
ٱلْكِتَابَ بِٱلحَْقِّ فَٱعْبُدِ ٱهلل ََّ مخُْلِصاً ل َّهُ ٱلدِّينِ۞أَلاَ هللِ َِّ ٱلدِّي ُن ٱلخَْالِصُ وَٱل َّذِينَ ٱتخ ََّذُواْ
348
مِن دُونِهِ أَوْلِيَآءَ مَا نَعْبُدُهُمْ إِلا َّ لِيُقَرِّبُوَ إِلىَ ٱهلل َِّ زُلْفَى ۤ إِن َّ ٱهلل ََّ يحَْكُمُ بَيْنَهُمْ فىِ مَا
هُمْ فِيهِ يخَْتَلِفُونَ إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يَهْدِى مَنْ هُوَ كَاذِبٌ كَف َّارٌ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi;Tanzeelu alkitabi mina Allahi alAAazeezi
alhakeemi; Inna anzalna ilayka alkitaba bialhaqqi faoAAbudi Allaha mukhlisan
lahu alddeena; Ala lillahi alddeenu alkhalisu waalladheena ittakhadhoo min
doonihi awliyaa ma naAAbuduhum illa liyuqarriboona ila Allahi zulfa inna Allaha
yahkumu baynahum fee ma hum feehi yakhtalifoona inna Allaha la yahdee man
huwa kadhibun kaffarun (Surat Az Zumar 39:1-3)
Tafsir: Kwa Jina La Allah mwingi wa Rehma Mwingi wa Huruma. Teremsho la Kitabu
(Qur’an) ni kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala mwingi wa Utukufu mwingi wa
Hikma. Kwa hakika tumekushushia wewe (Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam)
kwa Haki. Hivyo Muabudu Allah pekee kwa Ikhlasi kwa ajili ya Dini yake (bila ya
kujionesha wala kumshirikisha). Kwani kwa hakika Dini ni kwake yeye Allah tu pekee.
Na wale ambao ni weye kuchukua zaidi yake Wasaidizi na (kisha wakasema): ‘Sisi
hatuwaabudu isipokua kwa ajili ya kutukaribisha karibu ya Allah’ basi kwa hakika
Allah atahukumu baina yao juu ya yale waliyokhtilafiana. Kwa hakika Allah
hawaongozi wale ambao ni wenye kukadhibisha na Makafiri.
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua tunapozungumzia
kuhusiana na neno kwa Haki basi hua linamaanisha hali mbili ambapo maana ya kwanza
ni kua Kitabu kinachozungumziwa hapa yaani Qur’an kimeshushwa huku kikiwa ni
chenye kubeba Ukweli ndani yake. Na maana ya pili ni kua. Kitabu hicho kimeshushwa
kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala kwani hakuna uwezekano wowote wa kua
kimeandikwa na Ibn Adam.
Kwani Imam Hasan Al Basr alikua na Rafiki yake aitwae Farazdaq. Na Farazdaq alikua
na Mke ambae pia alikua akimjua Hasan Al Basr. Hivyo ikatokea kipindi ambacho
Mkewe Farazdaq alikua anaumwa sana kiasi ya kua alikua akijua kua hatoweza kupona
kutokana na Maradhi hayo, hivyo akausia kua atakapofariki basi Imam wa Kuongoza
Sala ya Maiti juu yake awe ni Hasan Al Basr. Hivyo Mke huyu wa Farazdaq hakuchukua
mda mrefu isipokua alifariki Dunia na hivyo ulipowadia wakati wa kusaliwa basi Imam
Hasan Al Basr akaambiwa kuhusiana na namna alivyousia Maiti huyo kabla ya kufariki
kwake.
Hivyo Hasan Al Basr akaongoza Sala ya Maiti ya Mke huyo wa Rafiki yake kisha
akamuombea Dua na wakaenda Kumzika Makaburini kama kawaida. Baada ya kuzika
349
basi Hasan Al Basr akamuuliza Farazdaq: ‘Hivi Jee umejitayarisha vipi kwa ajili ya
Siku hii?’
Farazdaq akajibu: ‘Nimetayarishia Kauli ya Shahada’
Imam Hasan Al Basr akasema: ‘Bila ya Shaka Shahada ndio Nguzo Kuu ya Hema
lakini Jee vipi kuhusiana na Kamba za Hema?’
Kwani anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kuhusiana na Kauli hii
ya Imam Hasan Al Basr kua:
Katika Kila hema linalojengwa basi hua linahitaji Nguzo na Kamba ya Kuzuilia Turubali
la Hema husika na kisha Hema ndio litasimama hivyo Shahada hua ni Nguzo na Amali
njema hua ndio Kamba
Naam..hivyo kwa Muislam Mbali ya kua ni Mwenye kutakiwa kua ni mwenye kutamka
Shahada lakini pia Ili Uislam wake Usimame na uwe katika hali ya Msimamo Thabit
basi Muislam huyo hua ni Menye Kuhitajika Kufanya Mema kwa Kumtii kwa Ikhalsi
Mola wake aliemuumba.
Ambapo aya hizi za Surat Az Zumar 39:1-3 zinatuwekea wazi kua:
Ibn Adam anatakiwa amuabudu Allah Subhanah wa Ta’ala peke yake tena kwa
Ihklasi.
Ibn Adam anatakiwa asifuate Dini Nyengine yeyote isipokua Dini Ya Kiislam kwani
hio ndio Dini ya Allah Subhanah wa Ta’ala na ambayo yeye Muumba ameamrisha
kua ndio ifuatwe
Ibn Adam asifanye Amali njema yeyote bila ya kua na Ikhlasi ndani yake yaani
Amali hio isiwe kwa ajili ya mwengine yeyote isipokua ni kwa ajili ya Allah
Subhanah wa Ta’ala.
Kwani Vyengine Atakua ni Miongoni mwa wenye Kujionesha na hivyo kua ni Miongoni
mwa Alladhiina hum YuraAuna yaani ni mwenye kujionesha na hivyo Ibn Adam huyo
atakua ni sawa na Alitayarisha Kujenga Hema huku akiwa na Turubali na Nguzo tu, bila
ya kua na Kamba ya Kushikamanisha Turubali hilo na Nguzo hio.
Na hivyo katika Siku ya Malipo Mtu atakua na Mlima wa Amali Njema, lakini Allah
Subhanah wa Ta'ala atamwambia kuhusiana na amali zake hizo kua:
350
Hakika wewe Ulisali katika siku fulani kwa sababu tu ya kuambiwa kua Umesali lakini
mimi Ndio Mola wako ambae hakuna mwengine zaid yake Ulifunga siku fulani kwa
sababu ya fulani lakini mimi ndie Mola wako hakuna mwengine zaid yangu, Ulitoa
Sadaqa kwa sababu ya Kuonekana,n.k
Na kisha Mlima wake huo wa Amali zake njema zote alizofanya Utaporomoka kama
vile ambavyo unavyoona inavyopangwa Chungu ya Machungwa na kisha ikaanza
kuondolewa Chungwa moja baada ya moja kuanzia Chini ya chungu hio ya Machungwa
Na hivyo atakua hana pa kujihifadhi kwani Amejenga Hema bila ya kua na Kamba na
hivyo Hema limepeperuka na atajuta badala yake kwani akiangalia anaona Adhabu Kali
inamsubiri huku aliyoyategemea yote yametoweka
Amesema Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Kinyongo hakitouvamia Moyo wa yule Muislam ambae
atakaethibitisha kua na mambo matatu yafuatayo: Ikhlasi mbele ya Allah
Subhanah wa Ta’ala katika vitendo vyake, Kutoa Ushauri wa kweli kwa wenye
Madaraka na Kushikamana na Waislam katika jamii yake.’’(Imam At Tirmidhii)
Ambapo amesema Imam Dhu Nun Al Misri kua: ‘Ikhlasi hua ni yenye kukamilika pale
inapokua Mtu una usadikisho ndani yake na ni mwenye subira ndani yake. Na
Usadikisho hukamilika pale inapokua kuna Ikhlasi na Udumisho ndani yake. Na
hua kuna alama tatu za mtu mwenye Iklasi: Kwanza Mtu hua ni mwenye kuona
kua kusifiwa kwake na kulaumiwa kwake kutoka kwa Ibn Adam wenzake kua ni
sawasawa. Pili mtu huondokewa na hisia za kua ni mwenye kufanya Mema pale
anapokua anafanya Mema hayo. Tatu hua ni mwenye kusahau na kutojali
kuhusiana na Malipo kutokana na anayoyafanya.
Na hivyo Ikhlasi hua ni siri baina ya Mja na Mola wake, kwani hata Malaika hua
hawajui kitu chochote kutokana nayo, na hivyo hua hawawezi kuandika kwenye
daftari la Matendo ya Mja wanaemuandikia.’
Ambapo kwa upande wa Abu Uthman Al Maghribi basi yeye anasema kua: ‘Ikhlasi hua
ni hali ambayo Nafsi hua hajisikii raha kua nayo. Hii hua ni Ikhlasi ya wale watu
ambao ni wa kawaida. Ama kuhusiana na Ihlasi ya watu waliochaguliwa na Allah
Subhanah wa Ta’ala basi hua inawajia si kwa hutokana na kutaka kwao, bali
mambo mema yao hua ni yenye kutokana na Ikhlasi yao lakini hua hawana habari
nayo na wala hawayahesabu kua ni mema, hio ndio Ikhlasi ya waliochaguliwa’
Ambapo kwa upande wa Imam Al Ruwaym basi yeye amesema kua: ‘Ikhlasi katika
Mema hua ni kua Mtu anafanya Mema bila ya kutaka Malipo hapa Dunani wala
351
kesho Akhera na wala hataki kukirimiwa na Malaika wawili Munkar na Nakir wa
Kaburini.’
Na anasema Mmoja kati ya Wanafunzi wa Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah
Al Tustari kua: ‘Ijumaa Moja mimi nilienda kwa Imam Sahl Al Tustari mda Mfupi
kabla ya kuanza Sala ya Ijumaa na nilipofika baada ya kugonga Mlango wake na
Kuitikiwa basi nikaingia ndani lakini ghafla nikashtuka na kusita, hapo hapo
mlangoni kwani mbele yangu niliona kua kuna Nyoka.
Lakini hata hivyo Imam Al Tustari ambae alikua ukimbini kwake akaniambia:
‘Ingia ndani Usiwe na Khofu, kwani hakuna Ibn Adam atakaepanda Darja yake
Kiimani kama atakua anaogopa Viumbe wenzake hapa Ardhini’
Hivyo nami taratibu nikaingia ndani, nikamsalimia, nae akanishika Mkono na
kuniuliza: ‘Leo ni Ijumaa, hivi jee Unataka kwenda Msikitini pamoja Nami?’
Hivyo nami nikajibu: ‘Nataka lakini sasa tatizo ni kua tumeshachelewa kwani
kutoka hapa tulipo hadi katika Msikiti wa Ijumaa basi ni safari ya Siku nzima
nzima hivyo hatutowahi Sala ya Ijumaa’
Imam Al Tustari akatabasam na kisha akaubana Mkono wangu, na kufumba na
kufumbua mimi nae tukawa tuko mbele ya Msikiti wa Ijumaa. Hivyo tukaingia
ndani Msikitini na kisha tukasali Sala ya Ijumaa pamoja na watu wengine. Kisha
baada ya Ibada ya Sala ya Ijumaa tukatoka nje mimi na Imam Al Tustari ambae
akasimama na kisha akwa anawaangalia watu waliokua wakitoka Msikitini baada
ya Sala ya Ijumaa hio kisha akaniambia: ‘Ma-shaa Allah! Msikiti una Watu wengi
Sana wanaosimamia La Ilaha Illa Allah, lakini inasikitisha kuona kua Ndani yake
Miongoni mwa hawa wanaotoka basi ni Wawili watatu tu ndio wenye Ikhalsi, kwani
takribn wengine wote ni wenye Kujionesha’
Naam huyo ni Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari ambae ni Miongoni
mwa Mawalii wa Allah Subhanah wa Ta'ala. Ambae alizaliwa mwaka mmoja kabla ya
kufariki Imam Muhammad Idris Al Shafii, yaani mnamo mwaka 203 Al Hijra na alisoma
pamoja na Imam wa Hadith Imam Abu Daud na alikua pamoja na Dhu Nun Al Misri.
Ambapo Imam Adh Dhahabi alisema kuhusiana na Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd
Allah Al Tustari kua: ‘Imam Al Tustari alikua ni Shaykh Al Arifin yaani Shaykh wa
wenye Kujua.’
Ambapo alisema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Mtu
yeyote yule atakaemfumbia Jicho Allah Subhanah wa Ta'ala kwa sekunde Moja tu,
basi kamwe Mtu huyo hatokua ni Miongoni mwa Walioongoka’
352
Naam..sijui jama tumeifaham kauli hii ama la, lakini kama hatujaifaham basi inabidi
tufaham kua Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari anamaanisha kua:
Ibn Adam hutakiwi kumfumbia jicho lako Mola wako hata kwa sekunde moja
kwani kufanya hivyo hua kunamaanisha kua ni Kumsahau Mola wako na kujidai
kua kama hayuko na hivyo ukawa unafanya yako, kwani ukifanya hivyo basi hua
inamaanisha kua tayari umeshapotea njia na hivyo sasa unaanza kutokwa na
Ikhlasi na kuanza kufanya Mambo yako kwa ajili ya Viumbe wenzako badala ya
Mola wako.
Hivyo kutokana na Mtizamo na ufafanuzi huu wa Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd
Allah Al Tustari basi tunaona kua Unapokua Unafaham maana ya Tawhid au
Kumpwekesha Allah Subhanah wa Ta'ala bila ya kumshirikisha basi hua kunakufanya
wewe usiwe ni mwenye Kujionesha, kwa sababu unakua unajua kua wengine wote
hawastahiki Kile ambacho anastahiki Mola wako kutoka kwako.
Hivyo hapa inabidi rutafakkari na kuulizana tena kua kama ikiwa Imam Abu Muhammad
Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari alisema kuhusiana na Watu walioishi katika Mwaka wa
Karne ya 2-3 ya Kiislam kua Wengi ni wenye Kusema La Ilaha Illa Allah, lakini hawana
Ikhlasi na Badala yake ni wenye Kujionesha Hivi Jee itakuaje hali yetu leo hii sisi mimi
na wewe?
Kwani alisema Imam Ali Ibn Sahl kua: ‘Mtu unapokimbilia kufanya Mema basi hua
ni dalili ya kupata Kasi kutoka kwa Mola wako. Unapojizuia Kufanya Maovu basi
hii hua ni Dalili ya kua ni Mwenye Tahadhari. Unapokua Unahifadhi Siri za Moyo
wako na Mioyo ya wengine basii hii hua ni dalili ya Kupata Ufunuo, na Unapokua
unajionesha basi hua Unathibitisha Ujinga wako. Na yeyote yule asiesimamisha
vizuri msingi wa Jitihada zake katika kujiboresha Kiimani basi kamwe hatofikia
Malengo stahiki yanayotakiwa kufikiwa Kiimani’
Na Imam Sufyan At Thawri alimuandia barua rafiki yae aliekua akiishi Syria aitwae
Abbad Ibn Abbad Al Khawwas Al Arsufi na kumwambia: ‘Faham kua uko katika
waati ambao Masahaba wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam walikua
hawataki kukutana nao, na wao walikua na I’lm ambayo sisi leo hii hatuna kwani
wao walikua na vyanzo vya llm ambavyo sisi hatuna. Hivyo itakuaje hali yetu sisi
kuufikia wakati huu huku tukiwa hatuna Ilm kubwa kiasi hicho? Hatuna Subra?
Hatuna wasaidizi katika kufahamishana lipi Jema, lipi Ovu miongoni mwa watu na
Duniani kwa ujumla? Hivyo chukua lile lililo sahih ushikamane nalo.
Na nami nakuusia wewe kubakia kutokua na Umaarufu, kwani huu ni wakati wa
kubakia katika hali ya kutojulikana na kutojionesha, kwani wacha Mungu hua ni
wenye kuogopa kujionesha, na kua ni wenye kutegemea kupata Ikhlasi katika Ibada
zao, Na usijichanganye na watu, kwani ilikua watu wakikutana hua ni wenye
353
kunufaishana katika akhera yao lakini leo hii hakuna hali hio katika kukusanyika
kwa watu. Hivyo ni bora zaid kutojichanganya nao.’
Na kwa upande mwengine basi kuhusiana na maneno yasemayo:
﴿ٱل َّذِينَ هُمْ يُرَآءُونَ ﴾
Alladheena hum yuraoona (Surat Al Maun 107:6)
Tafsir: Wale wenye kufanya Mema ili waonekane.
Hapa inabidi tufahamu kua aya hii haiendani kinyume na ile aya ambayo tuliyoiangalia
hapo kaba ya Surat Adh Dhuha ambayo inasema:
﴿وَأَم َّا بِنِعْمَ ةِ رَبِّكَ فَحَ دِّثْ ﴾
Waamma biniAAmati rabbika fahaddith.(Surat Adh Dhuha 93:11)
Tafsir: Na kuhusiana na Neema za Mola wako zihadithie.
Ambapo kuhusiana na maana ya maneno haya basi kwanza tumuangalie tena Thabit Ibn
Qays Radhi Allahu Anhu alikua ni Muandishi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na hivyo alikua ni mtu mwenye kupenda kuonekana kua amependeza kila wakati, na
hivyo iliposhushwa ile aya isemayo:
﴿وَلاَ تُصَعِّرْ خَد َّكَ لِلن َّاسِ وَلاَ تمَْشِ فىِ ٱلأَرْضِ مَرَحاً إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يحُِب ُّ كُل َّ مخُْتَالٍ
فَخُورٍ ﴾
Wala tusaAAAAir khaddaka lilnnasi wala tamshi fee al-ardhi marahan inna Allaha
la yuhibbu kulla mukhtalin fakhoorin, (Surat Luqman 31:18)
Tafsir: Na usigeuze uso wako kwa kujiona, na wala usitembee kwa madaha. Kwani
kwa hakika Allah hawapendi wenye kujivuna kwa fakhari.
Basi Thabit bin Qays Shammas Radhi Allahu Anhu hakutoka nje akawa ni mwenye kukaa
ndani kwake tu na kulia kwani alihisi kua ayah hii inamzungumzia yeye katika wakati
anapotoka hukua akiwa amevaa mavazi yake mazuri na ya kupendeza, lakini sasa
354
akaanza kuona kua kupendeza kwake imekua kunamuonesha kua ni mwenye kujiona na
kua na fakhari
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipoipata habari hii ya Thabit bin Qays
Shammas Radhi Allahu Anhu basi akatuma mtu ili akaulizwe kwanini amekua akijifungia
ndani na kulia tu na kufaya Istighfar?, na hivyo Thabit bin Qays Shammas Radhi Allahu
Anhu akajibu: ‘Hakika mimi napenda nikitoka niwe nimevaa nguo Nzuri’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hakika wewe sie ulietajwa
kwenye Ayah hii, kwani wewe ni mwenye kuishi Maisha mazuri na utaendelea
kuishi Maisha vizuri, na Allah Subhanah wa Ta’ala atakuingiza Peponi.’
Na hata Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akiwashauri watu wake wanaotoka
kwenye kufikisha ujumbe wa Dini ya Kiislam mbele ya Makafiri kua ni wenye kuvalia
nguo nzuri ili kuuwakilisha Uislam katika hali hali ya ubora wake.
Hivyo inaruhusika kuonesha Neema ulizojaliwa kupewa na Mola wako bila ya kua na
kibr au kujiona pia baadhi ya mambo katika kufanya Ibada za fardhi kwa ajili ya kuwatia
ari Waislam wawe ni wenye kufanya mema kama inavyosema aya ifuatayo:
﴿إِن تُبْدُواْ ٱلص َّدَقَاتِ فَنِعِم َّا هِىَ وَإِن تخُْفُوهَا وَتُؤْتُوهَا ٱلْفُقَرَآءَ فَهُوَ خَيْرٌ ل َّكُ مْ
وَيُكَفِّرُ عَنكُم مِّن سَيِّئَاتِكُمْ وَٱهلل َُّ بمَِا تَعْمَلُو نَ خَبِيرٌ ﴾
In tubdoo alssadaqati faniAAimma hiya wa-in tukhfooha watu/tooha alfuqaraa
fahuwa khayrun lakum wayukaffiru AAankum min sayyi-atikum waAllahu bima
taAAmaloona khabeerun(Surat Al Baqara 2:271)
Tafsir: Na kama Mkizidhihirisha Sadaka zenu (katika kutoa kwenu) basi ni bora,
Lakini kama mkifanya siri na kuwapa Masikini basi hua ni Kheri kwenu. Na Allah
atakusameheni katika madhambi yenu, na Allah ni mwenye kujua juu ya yale
mnayoyafanya.
Ambapo hapa aya imetumia neno FaniAaimma linalotokana na neno Naa’ama ambalo
hua linamaanisha Neema, Kuishia Maisha yasiyokua na Shida, Kua na Raha katika
Maisha, Kutokua na Mashakil. Neno Naa’ama linapoongezewa harfu Mim mbele yake
hua linatoa neno NaA’amma ambalo linamaanisha kuvumishi cha sifa ya Kua na hali ya
Ubora.
355
Na pia imetumia neno Khayrun linalotokana na neno Khara ambalo hua linamaanisha
Kupata Utajiri, Kustawi au Kunawiri Kimaisha, Kua Bora, Kua Na Kheri na Manufaa
na Faida zaidi, Kua katika hali nzuri inayopendelewa zaidi, Inayokubalika zaidi. Neno
Khara ndio lililotoa neno Khayran ambalo hua linamaanisha Ucha Mungu zaidi.
Hivyo basi ingawa maneno haya Naama na neno Khara yanafanana kimaana lakini neno
Khayrun linamaanisha kua ni Kitu bora zaid, na hivyo aya inatuthibitishia kua Kutoa
Sadaqa dhahiri mbele za watu ni Bora pale inapokua Mtu anafanya hivyo kwa Ikhlasi
yaani bila ya kua na nia ya kujionesha mbele za watu lakini hata hivyo mtu anapokua ni
mwenye Kutoa kwa Faragha au kisirisiri hua ni kufanya Ucha Mungu zaidi na hivyo
kunapendekezwa zaidi.
Naam..hivi jee tumeziona namna aya mbili hizi ambazo zimo ndani ya Sura Moja ambayo
ni Surat Al Baqara 2:164 na 2:171 namna zilivyokaa na namna zinavyosema?
Kwani ndani yake mpangilio wa aya hizi na mada inayozungumziwa ndani yake na
maana ya aya zinavyosema kwa kuanzia na aya ya 164:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ لاَ تُبْطِلُواْ صَدَقَاتِكُم بِٱلْمَنِّ وَٱلأَذَىٰ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo la tubtiloo sadaqatikum bialmanni waal-adha (Surat
Al Baqara 2:264)
Tafsir: Enyi Wale ambao Mlioamini msitoe Sadaqa Zenu Kwa Kukumbusha juu ya
kutoa Kwenu au Kwa Kufanya Adha.
Na aya ya 2:171 ambayo inasema:
﴿إِن تُبْدُواْ ٱلص َّدَقَاتِ فَنِعِم َّا هِىَ وَإِن تخُْفُوهَا وَتُؤْتُوهَا ٱلْفُقَرَآءَ فَهُ وَ خَيْرٌ ل َّكُمْ ﴾
In tubdoo alssadaqati faniAAimma hiya wa-in tukhfooha watu/tooha alfuqaraa
fahuwa khayrun lakum (Surat Al Baqara 2:271)
Tafsir: Na kama Mkizidhihirisha Sadaka zenu (katika kutoa kwenu) basi ni Bora zaid,
Lakini kama mkifanya siri na kuwapa Masikini basi hua ni Ucha Mungu zaidi.
Basi tunaona kua Allah Subhanah wa Ta'ala anabainisha hikma zake ktika aina mbili za
Ufanyajji wema kwa Ujumla ambazo ni:
356
1-Ufanyaji wa Wema unaofanywa na Mtu na kisha Kutoa Maneno ya Kujisifu na
Kukumbusha Wema au Msaada Uliofanya na Mtu husika na Kusimbulia. Ambao
hua si wa Ikhlasi bali ni wenye kua na Kibri na Kujionesha ndani yake na hivyo
haufai na hua ni Makosa kufanya hivyo kwani hua Unajifutia Malipo ya Mema
yako yote uliyoyafanya.
2-Ufanyaji Wema unaofanywa na Mtu Kwa Ikhalsi Hadharani na bila ya Kujiona
au Kusimbulia ambao hua ni Bora, na pia wa Siri siri ambao hua ni Uchamungu.
Huu hua ni Ufanyaji wema Unaohimizwa na Kupendekezwa kwani una Malipo
Makubwa.
Naam..kwa maana hio basi Muislam Unatakiwa uwe katika hali moja tu katika kila kitu
chako, yaani hali ya Kua ni Mwenye kumkumbuka Mola wako kutokana na neema zake
alikupendelea na kukujaalia wewe zaid ya wengine.
Hivyo Ukitoa Msaada, Kumfanyia Mtu wema au Ukifanya wema basi hutakiwi Uhesabu
Fadhila unazowafanyia Wengine labda kua Mimi Nimekufanyia wewe hiki na hiki, au
Nimekusaidia hili na Lile, au Kama sio Mimi basi asingejua Kitu au asingekua Vile au
Nishasomesha Sana, Nishafanya Dhikr Sana n.k
Kwani ukishasema hivyo basi unakua tayari Unasimbulia na Kujionesha na kua ni
Mwenye Adha pia kwa viumbe wenzako na kwa Mola wako. Na hivyo unaporomosha
Amali njema zako na kujifisidi na kujidhulumu Nafsi yako bila ya Kujijua.
Kama vile alivyoambiwa Abu Dhar Radhi Allahu Anhu pale alipomuuliza Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Ya Rasul Allah! Jee ipi Sadaqa ni bora zaid?’Rasul
Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Kumpa Sadaqa Mtu mwenye kuhitaji
kisirisiri na kumsaidia Mtu anaejitahidi kutafuta Riziki yake.’’
Ambapo anasema Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Itakapokua mtu anasali kikamilifu anapokua
hadharani na akafanya hivyo hivyo anapokua faragha, basi Allah Subhanah wa
Ta’ala hua ni mwenye kusema: ‘Kwa hakika huyu ndio Mja wangu wa
Kweli’’’(Mishkat Masabih)
Hapa vile vile inabidi tufahamiane pia kua tunapozungumzia kuhusiana na wale wenye
sifa ya Alladheena hum yuraoona yaani ambao ni wenye kufanya Riya. Basi ndani yake
hawaingii wale ambao ni wenye hali ya Mtu kujisikia hisia za Raha ndani ya Nafsi yake
kutokana na Kufanya Mema kwani hali hii ya hisia hizi hua si miongoni mwa Riya kwani
hii hua ni hali ya hisia ambayo mtu husika anakua anaipata pale anapokua anafanya
Jambo jema husika ambayo hua ni Ibada kwa ajili ya Mola wake tu.
357
Na hivyo Moyo wake hua umefunguka na kutanuka na Akili na Ufahamu wake hua
umezama ndani ya Ibada hio na hivyo hua ni mwenye kujihisi kua yuko yeye na Allah
Subhanah wa Ta’ala wake katika wakati huo, na hisia hizi humpa Mtu husika hisia ya
kama kuna Mto unaotiririsha hisia za Raha na Utulivu ndani ya Moyo wake na Mwili
wake, na hii ndio maana ya ile aya inayosema:
﴿ٱل َّذِينَ آمَنُواْ وَتَطْمَئِن ُّ قُلُوبُهُمْ بِذِكْرِ ٱهلل َِّ أَلاَ بِذِكْرِ ٱهلل َِّ تَطْمَئِن ُّ ٱلْقُلُوبُ ﴾
Alladheena amanoo watatma-innu quloobuhum bidhikri Allahi ala bidhikri Allahi
tatma-innu alquloobu(Surat Ar Rad 13:28)
Tafsir: Wale walioamini na Nyoyo zao zikapata utulivu kutokana na Kumkumbuka
Allah, Kwani katika Kumkumbuka Allah Hupatika Utulivu wa Nyoyo.
Na anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kuhusiana na aya hii
kua: ‘Katika kumkumbuka Allah Subhanah wa Ta’ala kwa kutumia Ilm basi hua
kunapatikana (Sukun) Utulivu ndani yake, na katika kumkumbuka Allah
Subhanah wa Ta’ala kwa kutumia Ufahamu basi hua kunapatikana (Tutma’inina)
utulivu ndani yake’
Hivyo Mja yeyote yule anaesema kua anafanya Dhikr basi hua anaingia katika moja kati
ya hali mbili zifuatazo: Kuna wale ambao Wanaomuogopa Allah Subhanah wa Ta’ala
kikweli na hivyo hua hawaondokewi na hali hio, hivyo hawa hua ndio wanoihisi hali
ya Mapenzi makubwa na uzito wa hisia hizo ndani ya Nyoyo zao, hawa hua ndio
wanaofanya Dhikr Allah na ndio wanaoishi kwa ajili ya Mola wao, Akhera yao, Ilm
na Sunnah.
Halafu kuna wale ambao wanaosema kua wanahisi uzito wa hisia hizo, furaha na
raha katika kila hali. Hawa hua ndio wenye kuishi kwa ajili ya Ibilisi, Dunia hii,
Ujinga na Bidaa, hawa ndio watu wabaya zaidi.
Kwani siku moja Hasan Ibn Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu aliambiwa: ‘Watu
wanasema kua wewe ni mwenye kujiona’ ambapo nae akajibu: ‘Hakika mimi si
mwenye kujiona bali ni mwenye kujiheshimu na kuijua thamani yangu, kwani hii
hali niliyokua nayo mimi inahusiana na kujiheshimu kunakoenda sambamba na
unyenyekevu na kujitosheleza ambako hakuathiriki kutokana na Umasikini’
Ambapo anasema Jarrah Allah Imam Al Zamakhshari kua: ‘Kuna tofauti baina ya
kujiona na kujiheshimu, ambapo ni wale wenye kua na Ilm hua ni wenye kuweza
kutofautisha baina ya sifa ya kujiona na sifa ya kujiheshimu Nafsi yako.’
358
Na kwa upande wa Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye anasema
kua: ‘Kujiheshimu na Kujithamini hua si sawa na Kujiona na Kua na Kibr, kwani
kujiheshimu hua ni Wajibu wa Muumini ambae hua hatakiwi kuidharau thamani
yake.
Wakati Kujiona hua kunatokana na Mtu kutoijua thamani yake na huku
Kujiheshimu hua kunatokana na Mtu kua ni mwenye kuijua Thamani yake, hivyo
hali ya kujiheshimu hua inakaribiana kimaana na Kujiona isipokua hua
zinatofautiana kiuhalisia.’
Ama kuhusiana na maneno yasemayo WayamnaAAoona almaAAoona
﴿وَيمَْنَعُونَ ٱلْمَاعُونَ ﴾
WayamnaAAoona almaAAoona(Surat Al Maun 107:7)
Tafsir: Na Wenye kukataa Maaun (Kutoa japo kitu kidogo).
Basi neno MaAun hua linamaaanisha Kusafiri masafa marefu kwa kasi kubwa sana.
Mtiririko wa Maji, Kutoa Kitu kirahisi, Kutoa Sadaka, Zaka, Kua na Ukarim wa kusaidia
au kutoa vitu vidogo vidogo vyenye maana kimatumizi kama Sindano, Uzi, Chumvi,
Kibiriti n.k kwa ajili ya kuwapa Majirani wanapokua na shida navyo.
Ambapo kwa upande wa Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi yeye
anaema kua: ‘MaAun ni vitu vidogo vidogo vinavyotumika Nyumbani’ ambapo kwa
upande wa Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu basi yeye anasema kua: ‘MaAun
ni Vitu vidogo vidogo ambavyo watu huazimana kama Nyundo, Ndoo, mkoba, n.k’
Imam Bukhari basi yeye anasema kua neno hili linamaanisha Ma’ruf Kullun yaani Kila
Jambo Jema, na baadhi ya Wanazuoni wametafsiri manemo haya WayamnaAAoona
almaAAoona kua ni yenye kumaanisha kua: Watu hawa ni wenye kukataa kutoa
Zaka.
Hivyo aya zinatuonesha kua baada ya kuzungumzia Ubakhili wa Kiibada yaani katika
Sala basi aya zinazungumzia kuhusiana na Ubakhili wa Mali kwa kuwataja wale ambao
ni ‘WayamnaAAoona almaAAoona’ yaani Na Wenye kukataa Maaun (Kutoa japo kitu
kidogo) kwani kama ikiwa mtu anashindwa kutoa vitu ambavyo havina thamani juu yake
basi atategemewaje katika kutoa vitu vyenginenyo, kama Sadaka, Zakah, n.k?
359
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimwambia Bibi Aisha Radhi Allahu Anha kua:
‘Ewe Aisha Hakika Allah Subhanah wa Ta'ala ni Mpole na Mkarimu na ni mwenye
Kupenda Upole na Ukarimu hivyo hua ni Mwenye Kulipa kwa Ukarimu Kile
ambacho hakitolewi kwa Ugumu na hua Halipi chengine zaid yake’(Sahih Muslim)
Na akasema tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Yeyote yule
atakaemrahisishia Muislam mwenzake matatizo yake ya Kidunia, basi Allah
Subhanah wa Ta'ala atamuokoa Mtu huyo kutokana na matatizo yake ya Kiakhera.
Yeyote yule atakaemsaidia Muislam Mwenzake kulipa Deni lake ambalo hawezi
kulilipa basi Allah Subhanah wa Ta'ala atamrahisishia Matatizo yake hapa Duniani
na Kesho Akhera Yeyote yule atakaeficha Siri za za Muislam Mwenzake basi Allah
Subhanah wa Ta'ala atamfichia Siri zake kesho Akhera’(Sahih Muslim)
Ambapo Siku moja Aisha Radhi Allahu Anha Alimuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kuhusiana na vitu ambavyo havitakiwi kukataliwa, Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akasema: ‘Maji, Moto na Chumvi.’ Hivyo Aisha Radhi Allahu Anha
akasema: ‘Kwa hakika tunafahamu kuhusiana na umuhimu wa Watu kua ni wenye
kuhitaji Maji, lakini jee ni vipi kuhusiana na Moto na Chumvi.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Mtu anaetoa Moto atapata malipo
ya kutoa Sadaqa kwa kila kitakachopikwa na na Moto huo, na mtu anaegawa
Chumvi atalipwa kua ametoa Sadaka katika kila chakula kitakachopikiwa na
kutiwa ladha na Chumvi hio. Na mtu anaempa Muumini maji funda moja katika
sehemu ambayo haina matatizo ya Maji basi hua ni sawa na mtu aliemuachia huru
Mtumwa. Na mtu atakaempa funda moja la Maji Muumini katika sehemu ambayo
haina maji basi hua ni sawa na alieokoa Uhai wa Mtu.’(Al Mishkat)
Hadith inatuonesha kua kumpa Muislam mwenye kiu Funda moja la Maji katika sehemu
isiyokua na Maji basi hua ni Sawa na Kumuachia Huru Mtumwa ambacho ni tu kidogo
sana. Lakini Jee tunajua Thamani ya Kuamchia Huru Mtumwa?
Naam Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kama Muislam
akimuachia Huru Mtumwa basi Allah Subhanah wa Ta'ala atamuokoa Muislam
huyo na Moto kwa kila sehemu yake ya Mwili kutokana na Kuuokoa Mwili wa
Mtumwa huyo kutokana na Utumwa’ (Sahih Al Bukhari)
Ambapo kuhusiana na kumpa maji mtu katika sehemu ambayo Maji hakuna kua ni sawa
na kumpa uhai mtu basi amesema pia Allah Subhanah wa Ta’ala kuhusiana na kumpa
Uhai mtu mmoj kua ni:
360
﴿مِنْ أَجْلِ ذٰلِكَ كَتَبْنَا ٰ عَلَى بَنيِ ۤ إِسْرَائِيلَ أَن َّهُ مَن قَتَلَ نَفْساً بِغَيرِْ نَفْسٍ أَوْ فَ سَادٍ
فىِ ٱلأَرْضِ فَكَأَنم ََّا قَتَلَ ٱلن َّاسَ جمَِيعاً وَمَنْ أَحْيَاهَا فَكَأَنم ََّا أَحْ يَا الن َّاسَ جمَِيعاً وَلَقَ ْد
جَآءَتْهُمْ رُسُلُنَا بِٱلّبَيِّنَاتِ ثمُ َّ إِن َّ كَثِيراً مِّنْهُمْ بَعْدَ ذٰلِكَ فىِ ٱلأَرْضِ لَمُسْرِفُونَ ﴾
Min ajli dhalika katabna AAala banee isra-eela annahu man qatala nafsan bighayri
nafsin aw fasadin fee al-ardhi fakaannama qatala alnnasa jameeAAan waman
ahyaha fakaannama ahya alnnasa jameeAAan walaqad jaat-hum rusuluna
bialbayyinati thumma inna katheeran minhum baAAda dhalika fee al-ardni
lamusrifoona (Surat Al Maidah 5:32)
Tafsir: Kutokana na hayo tuliyowaamrisha watu wa Bani Israil basi ni kua kama Mtu
akiiua Nafsi moja bila ya kulipiza kisasi cha Kuua basi hua ni sawa na alieua
Ulimwengu Mzima na Mtu yeyote atakaokoa uhai wa Mtu mmoja basi hua ni sawa na
alieokoa Uhai wa watu wa Dunia nzima. Na kwa hakika walikuja kwao wao Mitume
wetu na mabainisho yetu, lakini hakika wengi miongoni mwao baada yake wakawa ni
wenye kuendelea kufanya israfu.
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Mtu alieamini (Allah Subhanah
wa Ta'ala) hua ni Mkarimu, kwani hakuna Jema kwa yule Mtu ambae Si Mkarimu
wala si Mwenye Urafiki’ (Musnad Imam Ahmad)
Na akasema tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Ukarimu hauwezi
kuonekana katika kitu chochote isipokua Utaongeza Uzuri wa Kitu hicho. Na
Hauwezi kukosekana katika Kitu chochote isipokua Utakitia Dosari kitu hicho
kutokana na kukosekana kwake’(Imam Muslim)
Siku Moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliwauliza Masahaba zake kwa
kusema: ‘Hivi Jee nikuambieni juu ya yule Mtu ambae ataharamishiwa na Moto?’
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam mwenyewe akajibu kwa kusema kua: ‘Ni
yule Mtu ambae anakaribika, Mkarimu na mwenye Misimamo ya kati na
kati’(Imam At Tirmidhii)
Kwani amesema Aisha Radhi Allahu Anha kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam aliomba Dua kuwaombea Watu wa Ummah wake kwa kusema: ‘Ya Allah!
Yeyote yule atakaekua na huruma juu ya Ummah wangu basi mimi nakuomba
wewe kua uwe na Huruma juu yake Mtu huyo, na yeyote yule atakaekosa huruma
361
juu ya Ummah wangu basi mmi nakuomba wewe umfanyie ugumu katika mambo
mambo yake.’’ (Musnad Imam Ahmad)
Naam, Allah Subhanah wa Ta’ala anafananisha hali ya mtu asiemjali Yatima ambae hua
pia ni Maskini kua ni sawa na mtu ambae anakadhibisha kuwepo kwa siku ya Malipo, na
kuamini kuwepo kwa siku ya Malipo hua ni sehemu ya Nguzo za Imani ya Dini ya
Kiislamu, na kwa maana hiyo basi mtu anaemfukuza na asiemjali Yatima basi hua ni
sawa na mtu ambae amevunja Nguzo ya Imani ya Dini yake na hivyo kua si Muislam, na
hata kama alikua ni Muislam basi atakuja kujuta katika siku ya Malipo pale atakapopewa
kitabu chake kwa mkono wa kushoto kama zinavyosema aya:
﴿وَأَم َّا مَنْ أُوتِىَ كِتَابَهُ بِشِ مَالِهِ فَيَقُولُ يٰلَيْتَنىِ لمَْ أُوتَ كِتَابِيَهْ۞وَ لمَْ أَدْ رِ مَا
حِ سَابِيَهْ۞يٰلَيْتَهَا كَانَ ِت
ٱلْقَاضِيَةَ۞مَآ أَغْنىَٰ عَنىِّ مَالِيَهْ۞ه َّلَكَ عَنىِّ سُلْطَانِيَهْ۞
ِذرَاعاً فَاسْ لُكُوهُ۞
خُذُوهُ فَغُل ُّوهُ۞ثمُ َّ ٱلجَْحِ يمَ صَل ُّوهُ۞ثمُ َّ فىِ سِ لْسِ لَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ
إِن َّهُ كَانَ لاَ يُؤْمِنُ بِٱهلل َِّ ٱلْعَظِيمِ۞وَلاَ يحَُض ُّ عَلَى ٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِ ينِ ﴾
Waamma man ootiya kitabahu bishimalihi fayaqoolu ya laytanee lam oota
kitabiyah; Walam adri ma hisabiyah; Ya laytaha kanati alqadhiyatu; Ma aghna
AAannee maliyah ; Halaka AAannee sultaniyah, Khudhoohu faghulloohu;
Thumma aljaheema salloohu; Thumma fee silsilatin dharAAuha
sabAAoona dhiraAAan faoslukoohu; Innahu kana la yu/minu biAllahi
alAAadheemi; Wala yahuddu AAala taAAami almiskeeni (Surat Al Haaqah 69:25-
34)
Tafsir: Na ama yule atakepewa Kitabu Chake kwa Mkono wa Kushoto basi atasema:
‘Natamani bora nisingepewa hesabu yangu’; Na kamwe nisingejua ikoje Hesabu
yangu; Ya Laiti! huu(bora) ungekua ndio mwisho wangu’. ‘Mali zangu hazikunifaa
kitu’, ‘Yako wapi Mamlaka yangu?; (Itaamrishwa)’Mkamateni na Mfungeni’; ‘Kisha
Mtupeni Ndani ya Moto Mkali sana’; ‘Kisha Mfungeni kwa minyororo ambayo
ukubwa wake ni dhiraa 70’; ‘Kwani kwa hakika alikua Hamuamini Allah Mtukufu’;
‘Na hakua ni mwenye kuhimiza kuwalisha Maskini’
Hivyo Allah Subhaanah wa Ta’ala anatuonesha umuhimu wa kuwajali Mayatima na
kutufunza namna ya kutekeleza majukumu ya kuwalea na kuwasimamia Mayatima
kupitia katika kisa hiki cha Maryama Bint Imran pale alipolelewa na Nabii Zakariyyah
kua ni sehemu ya Kufanya wema, na kua ni sehemu ya kutekelezea Mamrisho ya Allah
362
Subhnah wa Ta’ala na hivyo kua ni sehemu ya kutokadhicshisha Dini na Kuwepo kwa
siku ya Malipo na hivyo kutokua na sehemu ya Unafiq ndani ya Moyo wako.
Na mtu unapokua huna Unafiq ndani ya Moyo wako, na hivyo kua ni mwenye Ikhlas
katika kila jambo lako basi Allah Subhanah wa Ta’ala hua ni mwenye kukujaalia Kiflayni
kutoka katika Rehma zake kama alivyosema katika Qur’an:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ ٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَآمِنُواْ بِرَسُولِهِ يُؤْتِكُمْ كِفْلَينِْ مِن ر َّحمَْتِهِ وَ يجَْعَل ل َّكُمْ
نُوراً تمَْشُ ونَ بِهِ وَيَغْفِرْ لَكُمْ وَٱهلل َُّ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo ittaqoo Allaha waaminoo birasoolihi yu/tikum
kiflayni min rahmatihi wayajAAal lakum nooran tamshoona bihi wayaghfir lakum
waAllahu ghafoorun raheemun(Surat Al Hadid 57:28)
Tafsir: Enyi Mlioamini Muogopeni Allah na Muaminini Mtume wake, nae atakupeni
Kiflayni min Rahmatihi (Atakutunzeni Mara Mbili kutokana na Rehma zake) na
atakupeni Nuru ambayo mtatembelea (katika njia iliyonyooka) na atakusameheni na
Allah ni Mwingi wa Kusamehe na Mwingi wa Rehma.
Kwa sababu Allah Subhanah wa Ta’ala ni mwenye kuona na kujua kila kilichomo ndani
ya Nyoyo za Waja wake kabla yake na baada yake na hivyo pia ni mwenye kujua ni kipi
kile anachostahiki Mja wake na matokeo yake baada ya kukipata kwake na hivyo ndio
mana akasema kua atamppa yule anaemtii Kiflayni min Rahmatihi, kama alivyopewa
Hana Bint Faqudh alipoomba ajaaliwe Mtoto wa Kiume, lakini badala yake akajaaliwa
Mtoto bora wa kike ambae nae akatoa mtoto bora wa Kiume hivyo hapa kuna Rehma
mbili kubwa ambazo ziliambatana sambamba zilizotokana na Maombi ya Hannah Bint
Faqudh kutokana na kua na Usafi wa Nafsi na Moyo wake katika kuomba kwake katika
wakati wa tukio au haja husika.
Kwani amesema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Dua bora
ambayo hua ni rahisi kujibiwa hua ni ile dua iliyoombwa kwenye wakati wake’
Ambapo anasema Imam Jamal Islam Abu Qasim Abd Al Karim Ibn Hawazin Al
Qushayri kuhusiana na Uombaji wa Dua kua: ‘Faida ya Kuomba Dua ni katika
kubainisha shida yako ijulikane mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala, na hivyo hua
si kumfanya Allah Subhanah wa Ta’ala kufanya atakavyo juu yako. ’
363
Imam Jamal Islam Abu Qasim Abd Al Karim Ibn Hawazin Al Qushayri anaendelea
kutuambia kua: ‘Dua ya Mtu wa Kawaida Hua inabainishwa kwa maneno yake. Dua
ya Wacha Mungu hua inabainishwa na Vitendo vyake na Dua ya Mawalii wa Allah
Subhanah wa Ta’ala hua inabainishwa na hali yake aliyokua nayo.’ Na ‘Dua Bora
ni ile inayoombwa katika wakati wa Huzuni.’
Siku moja Nabii Musa katika kuishi kwake alikutana na mtu ambae alikua akiomba Dua
kwa unyenyekevu sana, hivyo Nabii Musa akasema kumwambia Allah Subhanah wa
Ta’ala kua: ‘Ya Allah, Hakika kama Shida yake ingekua imo ndani ya mikono yangu
mie basi ningemtekelezea’
Hivyo Allah Subhnah wa Ta’ala akamwambia Nabii Musa kua: ‘Ewe Musa Hakika
mim ni mwenye huruma zaidi yako juu yake. Na ingawa yeye ananiomba mimi
lakini Moyo wake uko pamoja na Kondoo wake, hivyo mimi hua simjibu Mja ambae
Moyo wake Unafikiria kitu chengine zaidi yangu.’
Hivyo Nabii Musa kamfuata mtu huyo na kumwambia alivyosema Allah Subhanah wa
Ta’ala kisha mtu huyo akamgeuzia Allah Subhnah wa Ta’ala Moyo we wote na
akajibiwa Dua yake.
Na Imam Jafar As Sadiq aliulizwa siku moja na Wanafunzi wake kwa kuambiwa: ‘Hivi
kwa nini sisi hu ni wenye kuomba Dua lakini Dua zetu hazikubaliwi?’ Imam Jafar
As Sadiq akajibu: ‘Kwa sababu hua Mnamuomba yule ambae hamna Ilm Juu yake.’
Ambapo kwa upande mwengine basi Imam Yahya Ibn Said Al Qattani alimuona Allah
Subhanah wa Ta’ala ndotoni katika usingizi wake na hivyo akamwambia: ‘Ya Rabb,
mimi nimekua nikikuomba sana lakini sijaona kujibiwa maombi yangu.’ Hivyo
Allah Subhanah wa Ta’ala akamwambia Imam Al Qattani kua: ‘Ewe Mja wangu
Yahya, hii ni kwa sababu mimi napenda kusikia sauti yako.’
Na pia kwa upande wa Imam Al Wasiti aliombwa aombe Dua ambapo nae akasema:
‘Hakika mimi nna khofu ya kua kama nikiomba Dua basi Allah Subhanah wa Ta’ala
atasema: ‘Kama ikiwa utaniomba kile kitu ambacho nimeshakukadiria basi itakua
umenitilia shaka, na kama ikiwa umeniomba kitu ambacho sikukukadiria basi
itakua hukunitukuza kama inavyostahiki, lakini kama utaridhika basi kwa mda
muwafaka nitakupa kila nilichokukadiria’’
Na akasema Imam Muhammad Ibn Khuzaymah kua: ‘Mimi nilikua katika Mji wa Al
Iskandriyah (Alexandria, Misri) wakati Ahmad Ibn Hanbal alipofariki, na nikawa
nimejawa na Huzuni sana. Hivyo usiku nilipolala nikamuona Ahmad Ibn Hanbal
akiwa anacheza cheza, hivyo nikamuuliza Ahmad Ibn Hanbal. ‘Ewe Abu Abd
364
Allah! Hivi hivyo unavyofanya ndio nini?’ Nae akajibu: ‘Hii ndio hali ya Mja
anaekua Peponi’
‘Nami nikamuuliza: ‘Allah amekufanya nini?’ Ahmad Ibn Hanbal akasema:
‘Amenisamehe makosa yangu yote na amenivisha Taji kichwani mwangu na kunipa
vitu vya dhahabu na kuniambia kua: ‘Hakika hii ni kutokana na wewe kua ni
mwenye kusema kua Qur’an ni Maneno yangu’
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akasema: ‘Ewe Ahmad Ibn Hanbal hebu niombee
kama vile ambavyo alivyokufundisha Sufyan Ath Thawry ulipokua Duniani’
Ahmad Ibn Hanbal akasema: ‘Ya Rabb, Ewe Mola wa kila kitu, kutokana na uwezo
wako juu ya kila kitu nakuomba unisamehe juu ya kila kitu na usiniulize chochote
kile juu ya kila kitu’ hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akasema: ‘Ewe Ahmad ingia
Peponi’ hivyo nami nikaingia.
KULELEWA KWA MARYAM BINT IMRAN NA NABII ZAKARIYAH
Anasema Imam Muhammad Ibn Is-haq kua: ‘Amesema Allah Subhanah wa Ta’ala
kua:
﴿وَأَنبَتَهَا نَبَااتً حَسَناً وَكَف َّلَهَا زَكَرِ َّ كُل َّمَا دَخَلَ عَلَيْهَا زَكَرِ َّ ٱلْمِحْرَابَ وَجَدَ
عِندَهَا رِزْقاً قَالَ يمَٰرْيمَُ أَنى َّٰ لَكِ هَٰذَا قَالَتْ هُوَ مِنْ عِندِ ٱهلل َِّ إنًّ ٱهللًَّ يَرْزُقُ مَن
يَشَآءُ بِغَيرِْ حِ سَابٍ ﴾
Waanbataha nabatan hasanan wakaffalaha zakariyya kullama dakhala AAalayha
zakariyya almihraba wajada AAindaha rizqan qala ya maryamu anna laki hadha
qalat huwa min AAindi Allahi inna Allaha yarzuqu man yashao bighayri
hisabin(Surat Al Imran 3:37)
Tafsir: Na akamfanya akuwe katika makuzi mazuri na kumuweka chini ya usimamizi
wa Zakarriyah. Hivyo kila akiingia kwenye Mihrab (Kumuangalia na kumpelekea
Mataji yake) alikua akimkuta na Riziki yake, hivyo akasema: ‘Ewe Maryam, Umepata
wapi yote haya?’ akasema (Maryam): ‘Hivyo ni kutoka kwa Allah’ kwani kwa hakika
Allah humruzuku amtakae bila ya hesabu.
365
Hivyo Nabii Zakarriyah akamchukua Mtoto huyo na kumteua Isha Bint Faqudh
ambae ni Mama yake Nabii Yahya kua ndie Mlezi wa Mayam Bint Imran na
kumsimamia juu ya kila kitu, kisha alipokua mkubwa basi Nabii Zakarriyah
akamjengea Maryam Bint Imran Mihrab yaani Chumba maalum cha Kuishi na
kufanyia Ibada kwa ajili yake katika upande wa Mashariki na kuweka mlango
wake juu hivyo mtu hawezi kuingia ndani yake mpaka atumie ngazi, na kila siku
alikua akimpelekea mahitaji yake, chakula, kinywaji na mafuta ya kujipaka, na
kisha huondoka na kumuacha huku akiwa ni mwenye kuufunga mlango huo kwa
kufuli na ufunguo huondoka nao.
Kama zinavyosema Aya kuhusiana na sehemu hio ya Masharii kua:
﴿وَٱذْكُرْ فىِ ٱلْكِتَابِ مَرْيمََ إِذِ ٱنتَبَذَتْ
مِ نْ أَهْ لِهَ ا مَكَ اً شَ رْقِياً﴾
Waodhkur fee alkitabi maryama idhi intabadhat min ahliha makanan sharqiyyan
(Surat Maryam 19:16)
Tafsir: Na ametajwa katika kitabu, Maryam, wakati alipojitenga kutokana na familia
yake katika sehemu inayoelekea upande wa Mashariki.
Ambapo neno Mihrab linatokana na neno Haraba amblo hua linamaanisha Kuharibu
Kitu, Kukifanya Kitu kua hakifai na Hakina Maana, ambapo neno hili ndio lililotoa neno
Harb ambalo hua linaamaanisha Vita au Mapigano, na hivyo Mihrab hua ni sehemu ya
pembeni ya ndani ya Nyumba au chumba ambacho mtu hua anakaa ndani yake peke yake
kwa ajili ya kua na Mola wake na hivyo kua ni mwenye kupigana vita na Iblisi kwa ajili
ya Nafsi yake na Mola wake.
Hivyo Nabii Zakrriyah ambae alikua pia ni mwenye kazi ya Useremala basi alikua kila
siku alikua akienda kwenye Mihrab hio kumuangalia Maryam Bint Imran na Nabii
Zakarriyah alikua akimkuta tayari Maryam Bint Imran ana chakula ndani ya Mihrab hio,
ambacho hua ni mchanganyiko wa kila aina ya Vyakula vizuri na vitamu, kiasi ya kua
kuna baadhi ya vyakula vya msimu basi vilikua vinakutikana ndani ya Mihrabu hio
anayoishi Maryam Bint Imran hata kabla ya msimu wake kufika kwa mfano vyakula vya
wakati wa kiangazi vilikua vinapatikana katika wakati wa Masika na vya wakati wa Vuli
vinapatikana katika wakati wa Kipupwe na kuna vyengine vilikua ni kutoka sehemu za
mbali ambavyo ingawa mimea yake ilikua haioti katika maeneo ya Jerusalem lakini
chumbani kwake Maryam Bint Imran vilikua vinapatikana.
Jambo hili lilimshangaza sana Nabii Zakarriyah hivyo akamuuliza Maryam Bint Imran
kama zinavyosema aya:
366
﴿قَالَ يمَٰرْيمَُ أَنى َّٰ لَكِ هَٰذَا قَالَتْ هُوَ مِنْ عِندِ ٱهلل َِّ إنًّ ٱهللًَّ يَرْزُقُ مَن يَ شَآءُ بِغَيرِْ
حِ سَابٍ ﴾
Qala ya maryamu anna laki hadha qalat huwa min AAindi Allahi inna Allaha
yarzuqu man yashao bighayri hisabin(Surat Al Imran 3:37)
Tafsir: Hivyo akasema (Nabii Zakrriya kwa kuuliza): ‘Ewe Maryam, Umepata wapi
yote haya?’ akasema (Maryam): ‘Hivyo ni kutoka kwa Allah’ kwani kwa hakika Allah
humruzuku amtakae bila ya hesabu.
Ama kuhusiana na tukio hili basi anasema Jafar Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua:
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua anakaa kwa mda wa siku kadhaa
bila ya kua na chakula hadi inafikia wakati inakua taabu juu yake, hivyo alikua
akienda kwa nyumbani kwa Wake zake na ilikua hakuna kitu chochote ndani yake.
Hivyo akaenda kwa Fatma na kumwambia: ‘Ewe Binti yangu Kipenzi, jee unacho
chakula chochote kile? Kwa sababu mimi nnaona njaa’ Fatma akajibu: ‘Wa Allahi
naapa kwa Baba yangu na kwa Mama yangu, Sina Chakula.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipoondoka, basi mara Mfanyakazi wa
Fatma akaleta Bakuli ambalo ndani yake mlikua na Vipande vya Mikate viwili na
Nyama kidogo, hivyo Fatma akalipokea Bakuli hilo na kisha akalifunika na
kusema: ‘Naomba kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anirahisishie mimi
na familia yangu kupitia hili’ kwani wote walikua ni wenye shida ya chakula.
Hivyo Fatma akawatuma Hasan na Husein kwa Babu yao, na mara Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akaja kwa Fatma na alipofika basi: ‘Naapa kwa ajili
yako, kwa Baba yangu, kwa Mama yangu kua Allah Subhanah wa Ta’ala
ametuletea kitu ambacho nami nimekihifadhi kwa ajili yako’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akachukua Bakuli hilo na kulifunua. Subhana
Allah! Bakuli hilo lilikua limejaa Mikate na Nyama. Na hapo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akamuona Fatma kua ni mwenye muonekano wa
mshangao mkubwa sana, nae Fatma akajua kua ni Miujiza ya Allah Subhanah wa
Ta’ala hivyo akamshukuru na kumtukuza Allah Subhanah wa Ta’ala na kumsalia
Mtume wake Salallahu Alayhi wa Salam’
367
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akauliza: ‘Vimetokea wapi hivi ewe Binti
yangu?’ na Fatma akajibu:
﴿هُوَ مِنْ عِندِ ٱهلل َِّ إنًّ ٱهللًَّ يَرْزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيرِْ حِ سَابٍ ﴾
Huwa min AAindi Allahi inna Allaha yarzuqu man yashao bighayri hisabin (Surat
Al Imran 3:37)
Tafsir: ‘Hivyo ni kutoka kwa Allah’ kwani kwa hakika Allah humruzuku amtakae bila
ya hesabu’
Na hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Sifa zote anastahiki Allah
Subhanah wa Ta’ala ambae amekufanya wewe kua ni sawa na Mwanamke wa Watu
wa Bani Israil, kwani nae pale alipopewa Riziki yake na alipoulizwa kuhusiana nayo
basi alijibu:
﴿هُوَ مِنْ عِندِ ٱهلل َِّ إنًّ ٱهللًَّ يَرْزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيرِْ حِ سَابٍ ﴾
Huwa min AAindi Allahi inna Allaha yarzuqu man yashao bighayri hisabin(Surat
Al Imran 3:37)
Tafsir: Hivyo ni kutoka kwa Allah’ kwani kwa hakika Allah humruzuku amtakae bila
ya hesabu’
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaita watu wote ndani ya nyumba
hio Fatma, Hasan, Husein na wake zake wote Rasul Allahu Alayhi wa Salam wakala
mpaka wakashiba, huku bakuli hilo likiwa limebakia kama lilivyokua hapo awali,
Fatma akaamrisha kua sehemu nyengine iliyobakia wagaiwe Majirani zake wote.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala alitia baraka yake kwenye bakuli lenye Mikate
miwili na Nyama kidogo na kua ni bakuli lenye Mikate na Nyama ya kushiba kila
mtu.
Hali ya Maryam Bint Imran kulelewa na Nabii Zakariyah iliendelea kwa mda hadi
ikafikia wakati Nabii Zakaria akawa ni Mtu Mzima sana. Hivyo akawaambia Makuhani
wa Bani Israil kua. Hakika mimi tayari nimeshakua Mtu mzima sana kua ni mwenye
kumsimmia Maryam Bint Imran, hivyo jee ni nani miongoni mwenu atakaeweza
kunisadia jukumu langu hili?
368
Hivyo watu hao wakakubaliana kua kuna Mtu mmoja miongoni mwa watu wa Bani Israil
ambae anaitwa Yusuf Ibn Yaqqub Ibn Mathan Ibn Amur Ibn Mishan Ibn Hizqil Ibn
Ahraf Ibn Buam Ibn Azaziyah Ibn Amasiyah Ibn Nawus Ibn Nutha Ibn Barid Ibn
Yahushafat Ibn Radim Ibn Ababa Ibn RajiAm Ibn Sulayman Ibn Daud ambae ni Mcha
Mungu na yeye alikua ni Fundi Seremala na alikua ni Ibn Ami yake Maryam Bint Imran
na hivyo anastahiki kutokana na kua na sifa na vigezo kua ndie Al Kaffal wa Maryam
Bint Imran.
Hivyo Maryam Bint Imran akawa chini ya uangalizi wa Yusuf Ibn Yaqqub na baada ya
mda kupita basi Nabii Zakarriyah akaona kua miaka inaenda kwani katika kipindi hiki
alikua tayari ana umri wa miaka 300 na yeye hana ndugu wala jamaa wala mtoto, kwani
jamaa zake aliokua nao kwa wakati huo walikua ni Isha ambae Mke wake na Maryam
Bint Imran tu, hivyo akaamua kumuomba Mola wake ili apate Mtoto mwema ambae
atakaeweza kuendeleza kizazi chake, na kumrithisha majukumu yake hivyo akasema
kama zinavyosema aya:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞ك ۤ هيع ۤ ص ۤ ۞ ذِكْرُ رَحمَْةِ رَبِّكَ عَبْدَهُ زَكَرِ َّ ۞إِذْ َدَىٰ رَب َّهُ
نِدَآءً خَفِيّاً۞قَالَ رَبِّ إِنى َّ وَهَنَ ٱلْعَظْمُ مِنىِّ وَٱشْتَعَلَ ٱلر َّأْسُ شَيْباً وَلمَْ أَكُنْ بِدُعَآئِ َك
رَبِّ شَقِيّاً۞وَإِنىّ ِ خِ فْتُ ٱلْمَوَالىَِ مِن وَرَآئِى وَكَانَتِ ٱمْرَأَتِى عَاقِراً فَهَبْ لىِ مِن
ل َّدُنْكَ وَلِيّاً۞يَرِثُنىِ وَيَرِثُ مِنْ آلِ يَعْقُوبَ وَٱجْعَلْهُ رَبِّ رَضِيّاً ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Kaf-ha-ya-AAayn-sad;Dhikru rahmati
rabbika AAabdahu Zakariyya; Idh nada rabbahu nidaan khafiyyan; Qala rabbi
innee wahana alAAadhmu minnee waishtaAAala alrra/su shayban walam akun
biduAAa-ika rabbi shaqiyyan; Wa-innee khiftu almawaliya min wara-ee wakanati
imraatee AAaqiran fahab lee min ladunka waliyyan; Yarithunee wayarithu min ali
yaAAqooba waijAAalhu rabbi radhiyyan.(Surat Maryam 19:1-6)
Tafsir: Kwa Jina Allah Mwingi wa Rehma Mwingi wa Huruma. Kaf-Ha-Ya-Aayn-Sad;
Zinatajwa Rehma za Mola wako kwa Mja wake Zakarriyah. Alimpomnadia Mola wake
mnadio wa Siri. Aliposema: ‘Ewe Mola wangu hakika mimi mifupa yangu imekua
myepesi kwangu na Mvi zimeenea kwenye kichwa changu, na kamwe sikua kwenye
Dua zangu kwako ewe Mola wangu kua ni mwenye kuvunjika Moyo, Na nnakhofia
jama zangu baada yangu kwani mke wangu ni Tasa, Hivyo nipe mimi kutoka kwako
Msaidizi, ambae atanirithi mimi na atarithi kutoka katika familia ya Yaqub na mjaalie
Ewe Mola wangu kua ni mwenye kuridhiwa nae.’
369
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Kuna sababu
nyingi ambazo zinaweza kuelezewa kwanini Nabii Zakariyyah akaomba Dua kwa
Siri, kwa mfano labda alikua akiomba Dua katika wakati wa Usiku Mkubwa Sana
na hivyo hakutaka kuwakera watu wengine, au kwa sababu kuomba dua kwa sauti
ndogo hua ni sehemu ya kuonesha Ikhlasi, au kwa sababu alikua na khofu kua watu
watamsikia na kuanza kumsimanga kwa kutafuta mtoto wakati akiwa na umri
mkubwa, n.k’
Ambapo katika kuomba kwake Nabii Zakarriyah basi Qur’an inatuonesha namna ya
kuomba Dua kua Kwanza unatakiwa ukubali udhaifu wako kwa kuutaja mbele ya Mola
wako ili kuonesha kukubali na kuthibitisha uwezo wake na ukubwa wake na kua
unathamini rehma na neema zake juu yako na hivyo unahitaji kutoka kwake.
Na katika kuomba kwake basi tunaona kua Nabii Zakarriyah ametumia neno Waliyyan
ambalo hua linatokana na neno Waliya ambao hua lina maana nyingi ikiwemo Karibu,
Fuata, Karibia. Neno Waliya ndio lililotoa neno Walin ambalo humaanish Mlinzi, Rafiki
Msaidizi, Rafiki Anaelinda au Kutetea, na pia hua linamaanisha Mrithi au Msimamizi na
pia hua linamaanisha Ibn Ami, Baba Mdogo, Baba Mkubwa n.k
Ambapo kwa upande mwengine basi Allah Subhanah wa Ta’ala anatuelezea ni Waliyyan
gani ambae Nabii Zakarriyah alikua akimtaka pale alipoelezea tukio hili katika Surat Al
Imran pale aliposema:
﴿هُنَالِكَ دَعَا زَكَرِ َّ رَ ب َّهُ قَالَ رَبِّ هَبْ لىِ مِنْل َّدُنْ كَذُرِّي َّةًطَيِّبَةً إِن َّكَ سمَِيعُ ٱلد ُّعَآءِ ﴾
Hunalika daAAa zakariyya rabbahu qala rabbi hab lee min ladunka dhurriyyatan
tayyibatan innaka sameeAAu aldduAAa/-I (Surat Al Imran 3:38)
Tafsir: Wakati kiwa huo Zakariyyah akamuomba Mola wake (na) Kusema: ‘Ewe Mola
Wangu nipe mimi kutoka kwako Kizazi Kizuri kwani kwa hakika wewe ni mwenye
kusikia Dua’
Na hivyo kumaanisha kua Nabii Zakarriyah alikua anataka ajaaliwe Mtoto wa Kiume
kutoka kwa Mola wake, ambae ataendeleza majukumu yake na ya Babu yake ambae ni
Nabii Yaqub, kwani watu wa Bani Israil wote asili yao ni kutoka kwa Nabii Yaqub ambae
yeye nie Mtu wa kwanza kua ni mwenye kuitwa Israil kutokana na kua alikimbia kutoka
kwao baada ya kutishiwa kuuliwa na Kaka yae, na hivyo kawa ni mwenye kutembea
Usiku usiku na mchana kua ni mwenye kujificha. Hivyo kutokana na kutembea kwake
usiku basi ndio kawa na sifa ya kua ni mwenye Sara bil Layl – Israil.
370
Anasema Jarrah Allah Sultan Al Balagha Imam Abu Qasim Al Zamakhshari kuhusiana
na maneno ya Surat Maryam 19:6 yasemyo kua kua: ‘Nabii Zakkariyah amesema:
‘Yarithunee wayarithu min ali yaAAqooba waijAAalhu rabbi radhiyyan’ yaani ‘ambae
atanirithi mimi na atarithi kutoka katika familia ya Yaqub na mjaalie Ewe Mola
wangu kua ni mwenye kuridhiwa nae’, hivyo Nabii Zakarriyah alisisitiza kwa
kusema min ali YaAaquuba kwa sababu si kila aliekuwemo kwenye kizazi cha Nabii
Yaqub alikua ni Nabii na hivyo kua ni mwenye Ilm ambayo inastahiki kurithiwa’
Aya pia zinatuthibitishia umuhimu wa uomba kupata watoto wema kwani ndio chanzo
cha kupata manufaa hapa Duniani na kesho Akhera. Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala
akamwambia Nabii Zakarriyah kwa kusema kama zisemavyo aya:
﴿فَنَادَتْهُ ٱلْمَلا ۤ ئِكَةُ وَهُوَ قَ ائِمٌ يُصَلِّى فىِ ٱلْمِحْرَابِ أَن َّ اهلل ََّ يُبَشِّ رُكَ بِ يَحْيَى ٰ مُصَدِّقاً
بِكَلِمَةٍ مِّنَ ٱهلل َِّ وَسَيِّداً وَحَصُوراً وَنَبِيّاً مِّنَ ٱلص َّالحِِينَ ﴾
Fanadat-hu alMala-ikatu wahuwa qa-imun yusallee fee almihrabi anna Allaha
yubashshiruka bi Yahya musaddiqan bikalimatin mina Allahi wasayyidan
wahasooran wanabiyyan mina alssaliheena; (Surat Al Imran 3:39-41)
Tafsir: Na kisha Malaika wakanadia huku yeye akiwa amesimama akisali katika
Mihrabu: (wakasema)‘Hakika Allah anakubashiria (Mtoto) Yahya kuthibitisha Kauli
kutoka kwa Allah (Nabii Isa), na mja mwema mwenye cheo, na msafi asiekua na
dhambi na Nabii na Miongoni mwa Waja wema’
Hapa tunaona kua katika kumsifu kwake Yahya basi Allah Subhanah wa Ta’ala kua
atakua ni mwenye kuthibisha Unabii wa Nabii Isa, na pia Nabii Yahya ni mwenye sifa
ya kua ni mwenye Darja, Cheo cha Unabii na ni Miongoni mwa waja wema wenye sifa
ya kua ni Hasur, ambapo aya ametumia neno Hasur ambalo ni lenye kutokana na neno
Hasara au Hasira ambalo hua linamaanisha Kuzuia, Kubana au Kufungwa.
Neno Hasara ndio lililotoa neno Hasir ambalo hua linamanisha Jela, Kifungoni au
Gerezani. Hivyo neno Hasur lililotumika hapa linamaanisha kua ni Msafi ambae
haendekezi matamanio ya kutaka Wanawake.
Na kutokana na aya hii basi tunaona kua baadhi ya Wanazuoni wanasema kutooa
kama mtu unaweza kujizuia basi ni bora na inaruhusika, yaani hii inakua kama hali
ya Shaykh ul Islami Muhyi Ad Din Imam Abu Zakarriya Sharraf An Nawawi ambae
ni miongoni mwa Maimamu ambao hawakuoa na ndani yake anaingia pia Imam
371
Bukhari, Imam Abu Qasim Al Zamakhshari, Imam Muhammad Ibn Jarir At Tabari,
Imam Abd Allah Ibn Abi Najih, Imam Bishr Ibn Harith Al Hafi, Imam Abu Sad Al
Sam’ani, Imam Mulla Ali Al Qari, Shaykh Ibn Taymiyah. nk
Ambapo amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Enyi Vijana,
yeyote yule mwenye uwezo basi na aoe kwani kufanya hivyo hua ni sehemu ya
kuinamish mtizamo wa macho na kulinda kwa usafi, ama kwa wale wasiokua
na uwezo basi na wafunge kwa sababu funga hua inaangamiza Matamanio.’
Na akasema tena Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam kua: ‘Mambo manne
yalikua ni Sunna za Mitume, Kuona haya, Kujitia Mfuta Mazuri, Kusugua
Meno na Kuoa.’(Imam At Tirmidhii)
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anasema tena katika Qur’an kua:
﴿وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلاً مِّن قَبْلِكَ وَجَعَلْنَا لهَُمْ أَزْوَاجاً وَذُرِّي َّةً وَمَا كَانَ لِ رَسُولٍ أَن
ّ لِكُل أَجَلٍ كِتَابٌ ﴾
َْتِىَ آبِيَةٍ إِلا َّ إبِِذْنِ ٱهلل َِّ ِ
Walaqad arsalna rusulan min qablika wajaAAalna lahum azwajan wadhurriyyatan
wama kana lirasoolin an ya/tiya bi-ayatin illa bi-idhni Allahi likulli ajalin kitabun
(Surat Rad 13:38)
Tafsir: Na Kwa Hakika tumetuma Mitume kabla yako na tukawajalia kua ni wenye
kuoa na kupata watoto na haikua kwa Mitume kuleta uthibitisho isipokua kwa Idhni
ya Allah. Kwani kwa kila kitu kimeandikiwa kwenye Kitabu.
Hivyo Nabii Zakarriyah akasema:
﴿قَالَ رَبِّ أَنى َّٰ يَكُونُ لىِ غُلاَمٌ وَقَدْ بَلَغَنىِ ٱلْكِبَرُ وَٱمْرَأَتِى عَاقِرٌ قَالَ كَذٰ لِكَ ٱهلل َُّ
يَفْعَلُ مَا يَشَآءُ۞قَالَ رَبِّ ٱجْعَلْ لىِّ ۤ آيَةً قَالَ آيَتُكَ أَلا َّ تُكَلِّمَ ٱلن َّاسَ ثَلاَثَةَ أَ َّمٍ إِلا َّ
رَمْزاً وَٱذْكُرْ ر َّب َّكَ ير كَثِ ٱ اًوَسَبِّحْ بِ ى لْعَِش َوٱ لإِبَْكا رِ ﴾
372
Qala rabbi anna yakoonu lee ghulamun waqad balaghaniya alkibaru waimraatee
AAaqirun qala kadhalika Allahu yafAAalu ma yasha/o; Qala rabbi ijAAal lee
ayatan qala ayatuka alla tukallima alnnasa thalathata ayyamin illa ramzan
waodhkur rabbaka katheeran wasabbih bialAAashiyyi waal-ibkari; (Surat Al Imran
3:40-41)
Tafsir: Akasema (Nabii Zakarriyah): ‘Ewe Mola wangu jee nitapataje Mtoto wakati
mimi tayari ni Mzee na mke wangu ni Tasa?’ Allah Akasema: ‘Kadhalika Allah
hufanya vile atakavyo’ Akasema (Nabii Zakarriyah): ‘Ewe Mola wangu nijalie dalili’:
Akaambwa Dalili yako hua hutozungumza na watu kwa siku 3 isipokua kwa kutumia
alama za mikono. Na mkumbuke Mola wako kwa wingi na mtukuze mchana na
asubuhi.
Ambapo aya zinatuonesha kua kulingana na maneno ya Nabii Zakarriyah, basi hakua ni
mwenye kua na shaka juu ya kukubaliwa kwa maombi yake bali alikua yuko katika hali
ya kuhoji kutokana na kutaka kupata muongozo wa kujua njia gani atumie? Wakati Mke
wake ni Tasa na yeye ni Mzee, au itabidi afanye kama alivyofanya Nabii Ibrahim kuoa
Mwanamke mwengine kijana? Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamhakikishia kwa
kumwambia kua atakavyo Allah Subhanaha wa Ta’ala basi ndivyo itavyokua yaani
atapata mtoto katika umri aliokua nao, bila ya kurudishiwa yeye ujana na bila ya kuhitaji
kuoa mke mwengine kijana.
Ambapo kuna badhi ya Wafasiri wanasema kua Nabii Zakarriyah aliuliza hivi kwa
sababu ilichukua mda wa takriban miaka 20 baina ya kuomba kwake Dua na kupokea
majibu ya Dua yake hiyo. Na kuna wasemao kua hoja hii alitoa kwa ajili ya kumtaka
Allah Subhnah wa Ta’ala amfafanulie vizuri zaidi kuhusiana na tukio hili.
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anambainishia Nabii Zakarriyah kua kwake yeye ni
mwenye uwezo juu ya kila kitu, kwani hata Nabii Zakarriyah aliumbwa kutokana na kua
tone la manii ambalo halina thamani yeyote kama isemavyo aya:
﴿قَالَ كَذٰ لِكَ قَالَ رَب ُّكَ هُوَ عَلَى َّ هَينٌِّ وَقَدْ خَلَقْتُكَ مِن قَبْلُ وَلمَْ تَكُ شَيْئاً ﴾
Qala kadhalika qala rabbuka huwa AAalayya hayyinun waqad khalaqtuka min
qablu walam taku shay-an;(Surat Maryam 19:9)
Tafsir: Kadhalika hivyo ndivyo asemavyo Mola wako: ‘Ni rahisi kwangu mie. Kwani
kwa hakika nimekuumba wewe hapo kabla wakati ulikua si chochote.’
373
Kisha Nabii Zakarriyah akaomba aoneshwe dalili ya kutokea kwa jambo hilo, ambapo
akambiwa kua hatokua na uwezo wa kuzungumza na watu kwa mda wa siku tatu ijapokua
hatokua na tatizo lolote, kama zinavyobainisha aya:
﴿قَالَ رَبِّ ٱجْعَل ليِ ۤ آيَةً قَالَ آيَتُكَ أَلا َّ تُكَلِّمَ ٱلن َّاسَ ثَلاَثَ لَيَالٍ سَوًِّ۞فَ خَرَجَ
عَلَى ٰ قَوْمِهِ مِنَ ٱلْمِحْرَابِ فَأَوْحَى ٰ إِلَيْهِمْ أَن سَبِّحُواْ بُكْرَةً وَعَشِ يّاً ﴾
Qala rabbi ijAAal lee ayatan qala ayatuka alla tukallima alnnasa thalatha layalin
sawiyyan; Fakharaja AAala qawmihi mina almihrabi faawha ilayhim an sabbihoo
bukratan waAAashiyyan(Surat Maryam 19:10-11)
Tafsir: Akasema (Zakarriyah) ‘Nijaalie Dalili.’ (Allah Subhanah wa Ta’ala)Akasema:
‘Dalili yako ni kua hutozungumza na Watu kwa Usiku Mitatu huku ukiwa mzima
ulietimia’. Akatoka kwa watu wake kutokea kwenye Mihrabu akawaambia kwa
kutumia alama za mikono kumtukuza Allah Asubuhi na Jioni.
Naam hii ni miongoni mwa Aya ambazo zinathibitisha kuruhusika kutumika kwa Alama
za mikono na ishara katika Sharia za Dini ya Kiislam, kwani hii pia hua ni kama vile
ambavyo alivyofanya Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam pale alipomuuliza
Mtumwa kuhusiana na kama anamjua yeye Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ni
nani? Ambapo Mwanamke huyo akamuoneshea Kidole Rasul Allah Salallahu Alyhi wa
Salam na kisha akaoneshea kidole hicho Mbinguni. Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam akasema kua: ‘Huyu Ni Muislam’
Na pia katika hadithi nyengine pale alipomuuliza Mtumwa huyo: Jee unajua Allah
Subhanah wa Ta’ala yuko wapi? Ambapo Mtumwa huyo akaonesha Kidole Juu
Mbinguni.
Hivyo Nabi Zakarriyah akatoka nje ya Mihrabu ambapo watu hao hua wanamsubiri kwa
ajili ya kumsabihi Allah Subhanah wa Ta’ala na kisha akawasalisha lakini akawa hawezi
kutoa sauti, hivyo akawa nazungumza nao na kuwafahamisha na kuwasalisha kwa
kutumia alama za mikono, kwani hio ndio ilivyokua dalili ya kujaaliwa kupata mtoto
aliemuomba ambae ni yule aitwae Yahya.
KUZALIWA KWA NABII YAHYA IBN ZAKARIYAH
374
﴿يٰزَكَرِ َّ إِ َّ نُبَشِّ رُكَ بِغُلاَمٍ ٱسمُْهُ يحَْيىَٰ لمَْ نجَْعَل ل َّهُ مِن قَبْلُ سمَِيّاً ﴾
Ya zakariyya inna nubashshiruka bighulamin ismuhu yahya lam najAAal lahu min
qablu samiyyan (Surat Maryam 19:7)
Tafsir: Akasema Allah Subhanah wa Ta’ala kua: ‘Ewe Zakarriyah hakika sisi
tunakubashiria wewe Kijana jina lake Yahya ambalo hatukumjaalia yeyote hapo
kabla’
Ambapo kwa upande wa Imam Qatadah Al Sadusi basi yeye anasema kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala hakuwahi kumpa Mtu yeyote yule jina hili isipokua Nabii
Yahya, hata kama ikiwa Ibn Adam aliwahi kufanya hivyo.’
Na kwa upane wa Bahar Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu anhu basi yeye
anasema kua: ‘Hakuna Mwanamke aliekua katika hali ya Uzee na Utasa wa Isha kua
atapata mtoto kama huyo’
Na kwa upande wa Imam Mujahid Ibn Sulayman basi yeye anasema kua: ‘Maana ya
Samiyya iliyokusudiwa hapa hua ni sawa na ile ambayo hua inamaanisha kama
linavyomaanisha neno Shabiha ambalo maana yake hua ni kushabihiana kama vile
lilivyotumika katika aya ifuatayo:’
﴿ر َّب ُّ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا فَٱعْبُدْهُ وَٱصْطَبرِْ لِعِبَادَتِهِ هَلْ تَعْلَمُ لَهُ
سمَِيّاً ﴾
Rabbu alssamawati waal-ardhi wama baynahuma faoAAbudhu waistabir
liAAibadatihi hal taAAlamu lahu samiyyan (Surat Maryam 19:65)
Tafsir: Mola wa Mbingu na Ardhi na kila kilichomo ndani yake, hivyo muabuduni na
dumuni katika kumuabudu jee mnamjua nani mwenye sifa kama yeye?
Hivyo Isha akashika Mimba na kua na ujauzito wa Mtoto huyo ambae aliekua akijulikana
kwa jina la Yahya, ambapo mtoto huyo alipozaliwa alikua ni Mwema na Mcha Mungu
sana kwani tangu utotoni alikua akimuabudu Mola wake na kuwapita watu wazima
waliokua wakubwa zake, na pia alikua ni mwenye kuwausia watu wake kuhusiana na
Mola wake yeye pamoja na Baba yake yaani Nabii Zakariyah.
Ambapo anasema Allah Subhanah wa Ta’ala kuhusiana nae kua:
375
﴿يٰيَحْيىَٰ خُذِ ٱلْكِتَابَ بِقُو َّةٍ وَآتَيْنَاهُ ٱلحُْكْمَ صَبِيّاً۞وَحَنَاً مِّ ن ل َّدُ َّ وَزَكَوٰةً وَكَانَ
تَقِيّاً۞وَبَرّاً بِوَالِدَيْهِ وَلمَْ يَكُن جَب َّاراً عَصِيّاً۞وَسَلاَمٌ عَلَيْهِ يَوْ مَ وُلِدَ وَيَوْمَ يمَُوتُ وَيَوْمَ
يُبْعَثُ حَياً ﴾
Ya yahya khudhi alkitaba biquwwatin waataynahu alhukma sabiyyan; Wahananan
min ladunna wazakatan wakana taqiyyan; Wabarran biwalidayhi walam yakun
jabbaran AAasiyyan; Wasalamun AAalayhi yawma wulida wayawma yamootu
wayawma yubAAathu hayyan.(Surat Maryam 19:12-15)
Tafsir: Ewe Yahya shikamana na Kitabu (Taurat) kwa nguvu na tukampa Hikma
wakati akiwa mtoto mdogo, Na tukamfanya kua ni mwenye Huruma na akawa Msafi
na Mwema. Na akawa Mtiifu kwa wazee wake na wala hakua Jabari na mwenye kuasi
kwa Mola wake. Na salamu iwe juu yake katika Siku Aliyozaliwa, katika Siku
Atakayokufa na katika Siku Atakayofufuliwa.
Hivyo mtoto huyo ambae ni Nabii Yahya alikua ni Mja mwema tangu katika kipindi cha
utotoni mwake, na kua nimiongoni mwa Manabii ambao walipewa Unabii Utotoni na
kua mtiifu kwa Mola wake na kwa Wazee wake, na kuingizwa kwenye usalama na Allah
Subhanah wa Ta’ala katika siku ya kuzaliwa wake, siku ya kufa kwake na katika siku ya
Kufufuliwa kwake.
Anasema Imam Sufyan Ibn Uyayna kua: ‘Maneno yanayoainisha siku hizi tatu katika
aya hii yanamaanisha siku tatu ambazo Ibn Adam anakua na khofu na wasiwasi
sana ambazo ni Siku ya Kuzaliwa, Siku ya Kufa na Siku ya Kufufuliwa.’
Siku moja Nabii Yahya alimuomba Allah Subhanah wa Ta’ala : ‘Ya Allah hakika mimi
nilikua nataka unioneshe Ibilisi akiwa katika maumbile yake kama alivyoumbwa
na nataka anijibu masuali yangu yote nitakayomuuliza bila ya kunificha kitu
chochote.’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamwambia Ibilis: ‘Nenda kwa Mja wangu Yahya
Ibn Zakarriyah katika hali ya maumbile kama ulivyoshuka kwa mara ya kwanza
kutoka Mbinguni kuelekea Ardhini, na usimfiche juu ya kitu chochote kile
atakachokuuliza.’
Hivyo Ibilisi akaenda kwa Nabii Yahya akiwa kama alivyokua wakati aliposhuka kutoka
Mbinguni kwa mara ya kwanza, na alipofika kwa Nabii Yahya akajitambulisha kwa
376
kusema: ‘Ewe Nabbiyu Allah Yahya hakika mimi ni Ibilisi, Mola wangu amenituma
nije kwako kama nilivyoshuka mara ya kwanza kutoka Mbinguni.’ Nabii Yahya
akamuangalia Ibilis na akamuona kua na maumbile yenye kutisha huku akiwa na ndege
ndege wadogo wanamzunguka juu kichwani mwake, na katika sehemu zake za Siri kuna
vijumba vijumba vya ndege hao, na kwenye mguu wake kuna vikuba vya fedha.
Na hivyo Nabii Yahya akamuuliza Iblisi: ‘Hivi kwanini una videge vinavyoruka ruka
juu ya kichwa chako?’ Ibilisi akasema: ‘Kwa kuwatumia wao hua nnaziteka nyara
akili za Ibn Adam’Nabii Yahya akasema: ‘Na hivyo vikuku kwenye mguu?’ Ibilisi
akajibu: ‘Hua nnavipiga piga hivi kwa ajili ya watu hadi Ibn Adam hao waimbe na
kucheza mziki.’
Nabii Yahya akamuuliza Iblisi:‘Jee ni katika wakati gani hua unawadhibiti Ibn
Adam?’ Ibilisi akasema: ‘Pale anapokua ameshiba’ Nabii Yahya akamuuliza Iblisi:
‘Hivi jee umeona kitu chochote kile kwangu ambacho hakiridhishi ndani ya Nafsi
yangu?’ Ibilisi akasema: ‘La, Sijaona’ Nabii Yahya akauliza: ‘Hata mara moja?’
Ibilisi akasema: ‘Naam ilitokea mara moja pale ilipotokea, ulipokua umefunga na
kisha ukawa umeshiba baada ya kula sana iftari, ambapo katika usiku wa siku hio
hukuweza kuuhuisha usiku wako ama ilivyo kawaida yako.’
Hivyo Nabii Yahya akasema: ‘Basi Bila ya shaka sitokula tena Mpaka nikashiba’ Na
Ibilisi nae akasema: ‘Hakika nami, sitomwambia ukweli Ibn Adam tena’
Nabii Yahya alikua ni Mtu ambae anaependwa na kukubalika sana miongoni mwa Watu
wa Bani Israil, na katika wakati wa kipindi cha wakati huo kulikua na Mfalme ambae
alimuoa mjane mmoja ambae alikua na binti yake mdogo, hivyo binti huyo alipokua
mkubwa alikua mzuri sana na hivyo Mfalme huyu akataka kumuoa binti huyo huku
akiwa sambamba na Mama yake lakini akawa haijulikani uhalali wa Ndoa hio.
Ambapo anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Nabii Isa
Bint Maryam alimtuma Nabii Yahya Ibn Zakarriyah akiwa na miongoni mwa
Wanafunzi wake 12, kuwafundisha watu wa Bani Israil, na miongoni mwa mambo
aliyowakataza ilikua ni kutooana ndugu, hivyo Mfalme akawa anataka kumuoa na
hivyo Mfalme akawa anamtimizia matakwa yake yote’
Hivyo mama wa binti huyo akamwambia Mfalme huyo inabidi atafutwe Nabii Yahya
auliziwe juu yake. Nabii Yahya alipoitwa akasema kua Ndoa hio haikubaliki kisharia,
wakati Makuhani wao walisema kua inakubalika kutokana na kua na hofu juu ya Mfalme
huyo. Mfalme huyo akakasirika na kusema kua Nabii Yahya hataki Mfalme amuoe Bint
huyo, na binti nae akasema kua haiwezekani kwake kuolewa na Mfalme hadi
377
atakapouliwa Nabii Yahya na Baba yake, yaani Nabii Zakarriyah. Hivyo Mfalme
akaamua kutekeleza matakwa hayo.
Nabii Yahya akakamatwa na kisha akauliwa kwa kukatwa Kichwa, ambapo sehemu
iliyodondokea Damu yake basi ilikua ikichemka kama yanavyochemka maji ya Moto.
Na kila sehemu hio ikifukiwa basi bado damu inachemka tena kwa wingi zaidi.
Kwa upande wa Nabii Zakarriyah alipopata habari hio na kujua kua na yeye pia
anatafutwa basi akakimbia, na wakati anakimbia akakutana na Mti ambao akauombea
mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala kua mtu huo ufunguke ili aingie na patae nusra ndani
yake, ivyo mti ukafunguka na Nabii Zakariyyah akainga ndani yake.
Watu waliokua wakimtafuta Nabii Zakarriyah wakashindwa kumjua wapi alipojificha,
hivyo akatokea Iblisi na kuwaambia kua amemuona Nabi Zakariyyah wakati alipoingia
kwenye mtu huo. Na hata hivyo watu wa Bani Israil hawakuweza kumuamini Ibilisi
lakini nae akawathibitishia kwa kuwaonesha kipande cha Kilemba cha Nabii Zakarriyah
ambacho kilikua kimetokeza nje ya Mti huo.
Hivyo watu wa Bani Israil wakaamua kuukata mti huo, katikati kwa msumeno wakati
Nabii Zakarriyah akiwa ndani yake. Walipokua wanaukata wakamkuta Nabii Zakarriyah
ndani yake lakini nao hawakusita bali waliendelea kuukata na kumata pamoja nao Nabii
Zakarriyah aliekua ndani yake, Nabii Zakarriyah akaanza kulia huku akitaka kunadia
kumuomba msaada Mola wake. Lakini mara akatokea Malaika Jibril na kumwambia
Nabii Zakariyyah kua: ‘Ewe Zakarriyah Mola wako anakuambia kua, Kua na Subra
kwani ukilia na kuomba msaada basi matabaka 7 ya Ardhi yataangamia kwa ajili
yako, hivyo bora kaa kimya tulia na kua na ustahmilivu’
Hivyo Allah Subhanh wa Ta’ala akaamua kuwapa Adhabu kwa kuwatumia watu wa Bani
Israil Jeshi la watu ambao watawaangushia Mamlaka yao na kuwafanya Watumwa.
Hivyo sambamba katika wakati wa kipindi hiki katika ardhi ya Iraq kulikua kuna Mfalme
ambae alikua anaitwa Sennercherib na Jemedari wake Mkuu alikua akijulikana kwa jina
la Nebuchadnezer.
Hivyo Mfalme Sennerceherib akamuamrisha Nebuchadnezar atayarishe Jeshi ili
akawavamie watu wa Bani Israil, hivyo walipofika katika Mji wa Jerusalem wakakuta
Mji Umezungushiwa Ukuta Mkubwa sana na wakashindwa kuuvamia mji huo hivyo
wakaweka kambi nje, ambapo walikaa kwa masiku kadhaa bila ya mafanikio na
wakaamua kua waondoke na jeshi lao na kurudi Iraq.
Na walipokua wanajitayarisha kuondoka akatokea Bibi Kizee mmja wa Bani Israil na
kuwauliza: ‘Hivi yuko wapi kongozi wa Jeshi Hili?’ Bibi huyo akapelekwa kwa
Nebuchadnezer na alipofika basi akasema: ‘Hakika mimi nimesikia kua mnataka
378
kuondoka kabla ya kuuteka mji huu’ hivyo Nebuchadnezer akasema: ‘Naam..kwa
sababu tumeshakaa kwa mda mrefu na hatuwezi kuuteka kutokana na huu ukuta
na Wanajeshi wangu wameshaishiwa na subira na pia mahitaji yetu yanamalizika
hivyo hatuna njia isipokua kuondoka bila kufanikisha Lengo letu.’
Yule Bibi akasema: ‘Hakika mimi nilikua nafikiria hivi jee kama nikikuambieni
jambo la kufanya cha kufanya na mkafanikiwa kuingia ndani ya Mji huu, mtaahidi
kunipa kile nikitakacho? Na kisha mtamuua ninaetaka auliwe? Na mtamuachia
huru nitakaetaka aachiwe?’
Nebuchadnezar akasema: ‘Naam, tunaahidi kufanya kama utakavyo kama
ukitusaidia’ Yule Bibi akasema: ‘Sawa, hivyo utakapoamka asubuhi, basi ligawe
Jeshi lako katika makundi manne aambpo kila kundi litakaa katika upande mmoja
wa Mji. Halafu nyanyueni mikono na mseme: ‘Ya Allah hakika wewe ni mwenye
kujua juu ya kila kitu, hivyo tuongoze kwa yule aliemuua Yahya Ibn Zakarriyah’
na wakishasema hivyo basi ukuta huu mnauona mkubwa na Imara utaanguka chini
mara moja’
Hivyo ilipowasili Asubuhi basi Nebuchadnezer akaligawa Jeshi lake katika makundi
manne, kisha akaliamrisha lifanye kama vile alivyoambiwa na yule Bibi na hapo hapo
Ukuta huo ukaanguka, na jeshi lake inakinga ndani ya Mji huo kutoka katika pande nne
tofauti, walipofika ndani basi yule bibi akamwambia Nebuchadnezer: ‘Wachinje watu
wa Bani Israil juu ya sehemu hii mmoja baada ya mwengine mpaka nikwambie
basi’
Hivyo katika sehemu hio wakachinjwa Watu wa Bani Israil mmoja baada ya mwengine
mpaka wakafikia watu 70000. Na hapo sehemu hio ikasita kuchemka, yule Bibi akasema:
‘Basi imetosha kwani akichinjwa Nabii wa Allah, basi Allah hua haridhiki hadi pale
itakapokua yule aliemchinja Nabii huyo na kila ya yule aliefurahia jambo hilo
achinjwe pia.’ Na kisha baada ya hapo wakalivunja Jengo la Asahraa liliomo ndani ya
Ardhi ya Al Quds na akawateka watu wa Bani Israil na kufanya Watumwa
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anaelezea namna Mayahudi walivyokua wakiwaua
Mitume waliotumiwa kwa kusema:
379
﴿وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَى ٰ ٱلْكِتَابَ وَقَف َّيْنَا مِن بَعْدِهِ بِٱلر ُّسُلِ وَآتَيْنَا عِيسَى ٱبْنَ مَرْ يمََ
ٱ ب لْ أ َيِّنَا َ تَِو ي َّدَْهُ بِرُو حِ
ٱلْقُدُسِ أَفَكُل َّمَا جَآءَكُمْ رَسُولٌ بمَِالاَتَهْوَىٰ أَنُْفسُكُمْ ٱسْتَكْبَرْتمُْ
فَفَرِيقاً كَذ َّبْتُمْ وَفَرِيقاً تَقْتُلُونَ ﴾
Walaqad atayna moosa alkitaba waqaffayna min baAAdihi bialrrusuli waatayna
AAeesa ibna Maryama albayyinati waayyadnahu biroohi alqudusi afakullama
jaakum rasoolun bima la tahwa anfusukumu istakbartum fafareeqan
kadhdhabtum wafareeqan taqtuloona (Surat Al Baqara 2:87)
Tafsir: Na kwa hakika tulimpa Musa Kitabu na baada yake tukatuma Mitume wengine,
na tukampa Isa Ibn Maryam vithitibitisho vilivyokua wazi na takamthibishia kwa Ruhi
Al Qudus (Malika Jibril) hivi jee kila wakija Mitume na kile ambacho hakiendani na
Matamanio ya Nafsi zenu Mtafanya Kibri? Na mkawakadhibisha baadhi yao na
mkawaua baadhi yao.
Ambapo amesema Abu Ubaidah Ibn Jarrah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Watu wa Bani Israil waliua kwa kila siku
Mitume 43 na Wacha Mungu 170 ambao walikua wanawaamrisha kufanya mema.’’
Na akasema tena Allah Subhanah wa Ta’ala katika Qur’an kua:
﴿فَبِمَا نَقْضِهِمْ م َّيثَاقَهُمْ وَكُفْرِهِم آبََ تِ ٱهلل َِّ وَقَتْلِهِمُ ٱلأَنْبِيَآءَ بِغَيرِْ حَقٍّ وَقَوْلهِِمْ
قُلُوبُنَا غُلْفٌ بَلْ طَبَعَ ٱهلل َُّ عَلَيْهَا بِكُفْرِهِمْ فَلاَ يُؤْمِنُونَ إِلا َّ قَلِيلاً ﴾
Fabima naqdihim meethaqahum wakufrihim bi-ayati Allahi waqatlihimu alanbiyaa
bighayri haqqin waqawlihim quloobuna ghulfun bal tabaAAa Allahu
AAalayha bikufrihim fala yu/minoona illa qaleelan (Surat An Nisaa 4:155)
Tafsir: Na kutokana na kuvunja kwao Miadi yao na kuzikufuru aya za Allah, na katika
kuwaua Mitume bila ya haki, na kutokana na kusema kwao: ‘Nyoyo zetu zimefunikwa
(Hatukifaham wanachokisema Mitume), La bali Allah ameweka muhuri kwenye
nyoyo zao kutokana na kukufuru kwao, kwani hawakuamini isipokua kidoogo tu’
380
Ambapo wanasema Wanazuoni wamesema kua Allah Subhanah wa Ta’ala aliwajaalia
watu hawa wa Bani Israil kua ni wenye kufikwa na Mitihani na hivyo waliuawa watu
70000 badala yake kutokana na kumuua Nabii Zakarriyah na watu 70000 kutokana na
kumuua Nabii Yahya.
Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kutakua na Hijra baada ya
Hijra, hivyo watu bora Duniani ni wale ambao wakaishi katika Ardhi ya Hijra ya
Nabii Ibrahim’(Mustadrak Al Hakim)
Na amesema Al Azdi Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alitutuma sisi tukatafute Ngawira kwa miguu, lakini hatukupata kitu Hivyo
tukarudi ambapo nae aliona namna tulivyokua tumechoka kutokana na
muonekano wa Nyuso zetu
Hivyo akasimama na kisha akasema: Ya Allah Usiwaachie peke yao kwa Ajili yangu
pale nitakapokua Dhaifu kwa ajili yao Usiwaachie peke yao kwa ajili yao pale
watakapokua Dhaifu kwa ajili ya Watu wao, pale watakapozuiliwa Mema kwa ajili
yao
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaweka Mkono juu ya kichwa
changu na kusema: Ewe Ibn Hawalah! Kama ukiona Ukhalifa umeingia kwenye Al
Quds, halafu ikafuatia Mitetemeko ya Ardhi, kisha Mitihani, na mambo mengi
Makubwa yakafuatia, basi Wakati uliobakia utakua karibu kwa watu kuliko huu
mkono wangu kwenye Kichwa chako’ (Mustadrak Al Hakim)
Na amesema Imam Abu Muhammad Al Hasan Ibn Hibat Allah Ibn Abd Allah Ibn Asakir
kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: Hili jambo (la Ukhalifa)
litafuata baada yangu hapa Madinah , kisha katika Ardhi ya Sham, Kisha Hijaz,
Kisha Iraq, Kisha Mjini (Istanbul) Kisha Bayt ul Maqdis hivyo likifika Baytu ul
Maqdis basi itakua limefikia sehemu yake hivyo hakuna watu watakaoliondoa
kutoka katika Mji wao ambao watalipata tena jambo hilo.’
Naam..Ama kuhusiana na Hadithi hizi zote zinazungumzia kuhusiana na Ukhalifa wa
Kiislam katika Ardhi husika, na Historia inaonesha kua sehemu zote zilizotajwa katika
Hadith juu ya Ukhalifa wa Kiislam kua ni tayari Ukhalifa ushawahi kutawaliwa..isipokua
Bayt ul Maqdis yaani Jerusalem.
Kwani amesema Allah Subhanah wa Ta'ala katika Surat Al Isra kua:
381
﴿وَقَضَيْنَآ إِلىَٰ بَنىِ إِسْرَائِيلَ فىِ ٱلْكِتَابِ لَتُفْسِ دُن َّ فىِ ٱلأَرْضِ مَر َّتَينِْوَلَ ت َعْلُ ن َّ عُلُوّاً
كَبِيراً۞فَإِذَا جَآءَ وَعْدُ أُولاهمَُا بَعَثْنَا عَلَيْكُمْ عِبَاداً ل َّنَآ أُوْلىِ أبَْسٍ شَدِيدٍ فَجَاسُواْ
خِ لاَلَ ٱلدَِّرِ وَكَانَ وَعْداً م َّفْعُولاً ﴾
Waqadhayna ila banee isra-eela fee alkitabi latufsidunna fee al-ardhi marratayni
walataAAlunna AAuluwwan kabeeran; Fa-idha jaa waAAdu oolahuma
baAAathna AAalaykum AAibadan lana olee ba/sin shadeedin fajasoo khilala
alddiyari wakana waAAdan mafAAoolan(Surat Al Isra 17:3-4)
Tafsir: Na Tumewatakia Bani Israil katika Kitabu kua Mtafanya Ufisadi Ardhini mara
mbili na mtakua madhalimu na wenye Kibri kikubwa sana kisha Itapokamilika Ahadi
ya kwanza baina yake tutatuma Dhidi yenu waja wetu wenye nguvu kubwa (wa Kivita)
Wataingia Mpaka Ndani kabisa ya Majumba yenu na Ilikua ni Ahadi iliyotimizwa.
Ambapo anasema Imam Said Ibn Jubayr kuhusiana na aya hizi kua: ‘Aya hizi
zinazungumzia tukio lililowakuta Watu wa Banii Israil walipotawala na kuja juu
sana kisha Wakavamiwa na Nebuchadnezer. Ambae aliangamiza kila kitu chao
Bani Israil katika Mji wa Jerusalem na kisha akawaua baadhi yao na waliobakia
akawachukua na kuenda Nao katika Ardhi ya Babylon na kuwafanya Watumwa
wa utawala wake kwa mda wa miaka 70. Na kisha baada ya miaka 70, Utawala wa
Uajemi Ukauvamia Utawala wa Nebuchadnezer na Kuuangusha, na kisha
ukawaachia Huru watu wa Bani Israil nao wakarudi tena Jerusalem.’
Naam..Allah Subhanah wa Ta'ala anaendelea kuliezea tukio kwa kusema katika Surat Al
Isra kua:
﴿ثمُ َّ رَدَدْ َ لَكُ مُ ٱلْكَ ر َّةَ عَلَيْهِ مْ وَأَمْ دَ دْ َ كُ م أبَِمْ وَالٍ وَ بَنِينَ وَجَ عَلْنَاكُ مْ أَكْثَرَ نَفِير اً۞إِنْ
أَحْسَنْتُمْ أَحْسَنْتُمْ لأَِنْفُسِ كُمْ وَإِنْ أَسَأْتمُْ فَلَهَا فَإِذَا جَآءَ وَعْدُ ٱلآخِ رَةِ لِيَسُوءُواْ
وُجُوهَكُمْ وَلِيَدْ خُ لُواْ ٱلْمَسْجِ دَ كَمَا دَخَلُوهُ أَو َّلَ مَر َّةٍ وَلِيُتَبرُِّواْ مَا عَلَوْاْ تَتْبِ يراً ﴾
Thumma radadna lakumu alkarrata AAalayhim waamdadnakum bi-amwalin
wabaneena wajaAAalnakum akthara nafeeran; In ahsantum ahsantum li-
382
anfusikum wa-in asa/tum falaha fa-idha jaa waAAdu al-akhirati liyasoo-oo
wujoohakum waliyadkhuloo almasjida kama dakhaloohu awwala marratin
waliyutabbiroo ma AAalaw tatbeeran(Surat Al Israa 17:6-7)
Tafsir: Na Kisha tukakurudushieni nyie ushindi juu yao watu hao (wa Nebuchadnezer)
Na Tukakusaidieni kwa Mali na Watoto Na tukakujaalieni Uwezo mkubwa wa
Kunguvu (Nasi tukasema) Kama Mtakua Wema basi Mtakua wema kwa ajili ya Nafsi
zenu Na Kama Mkiasi basi ni kwa hio (Nafsi yenu pia) Na Kisha Itakapokuja Ahadi
ya Pili Kuzihuzunisha Nyuso zenu (Kwa tutakalokuleteeni) Na Kuingia (Maadui zenu)
Msikitini (Al Quds) Kama walipoingia mara ya kwanza na kukuangamizeni kwa
Muangamizo mkubwa utokanao na mikono yao.
Kwani aya mbili hizi zinazungumzia kuhusiana na tukio kubwa litakalotokea baada ya
Watu wa Bani Israil ambalo ni la pili baada ya lile lililowakuta kutoka kwa Mfalme
Nebuchadnezer, ambapo baada yake walirudi tena Jerusalem na juu ya hili basi tunaona
kua kuna mitizamo tofauti, kwani ukweli ni kua kabla na baada ya tukio la
Nebuchadnezer na Mayahudi kurudi Jerusalem basi Mayahudi waliasi tena mara kadhaa,
na wakaletewa Mitume na Manabii Kadhaa.
Ambapo mara ya moja wapo ni wakati wa Miaka 170 kabla kipindi cha Nabii Zakarriyah,
Nabii Yahya na Nabii Isa, basi akatokea Mfalme wa Uturuki, akawavamia na kuwaua na
kuwateka waliobakia. Na kisha baada ya hapo watu wa Bani Israil waliookoka baada ya
kukimbia wakarudi Jerusalem na wakavamiwa na Utawala wa Roman Empire.
Na pia katika kipindi cha Miaka minane kabla ya kuzaliwa Nabii Isa Alayhi Salam, na
kisha miaka ya baadae Watu wa Bani Israil wakaasi dhidi ya Utawala wa Roman Empire,
ambapo katika Uasi huo basi Watu wa Bani Israil wakashambiliwa na kuuliwa tena na
kutekwa. Hivyo kutokana na Uasi wao kwa Mola wao basi Allah Subhanah wa Ta'ala
amewaahidi kua Watarudi Jerusalem, ambapo Watapigwa tena kwa pigo kubwa zaidi.
Na tumeona Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika hadith alisema kua Ukhalifa
Utaingia Jerusalem kisha ndio kitafuata Kiama. Hivyo bila ya shaka, kuna pigo kubwa
zaid ambalo linawasubiri Mayahudi, ambalo litapelekea kuwepo kwa Ukhalifa wa
Kiislam katika ardhi ya Jerusalem, na kwa kua hatujafika huko, basi na turudi katika kisa
chetu ambacho ndani yake kinamjumuisha kwa pamoja, Nabii Zakarriyah, Nabii Yahya,
Maryam Bint Imran na kuzaliwa kwa Nabii Isa Ibn Maryam kama ilivyozungumziwa
ndani ya Surat Maryam.
383
SABABU YA KUSHUSHWA KWA SURAT MARYAM
Tunapozungumzia kisa cha Nabii Isa Ibn Maryam basi hua tunazungumza kisa ambacho
kwa upande mmoja Allah Subhanah wa Ta’ala amekizungumzia ndani ya Kitabu chake
Kitukufu kwa ajili ya kumtia Moyo zaid na kumfunza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam na Masahaba zake juu ya yale yaliyotokea kwa Mitume waliofuatia kabla ya kuja
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ili awe ni mwenye kua na subra na ustahmilivu
zaidi kutokana na madhila makubwa anayofanyiwa yeye na wafuasi wake wa Dini ya
Kiislam katika ardhi ya Makkah kutokana na Chuki dhidi yao kutoka kwa watu wa Kabila
la Quraysh.
Kwani kwanza watu wa Quraysh walianza kuwaadhibu wale Masahaba ambao walikua
ni dhaifu miongoni mwa waliokua wakiamini Imani ya Dini ya Kislam, kwa kuwaadhibu
Wanawake wake kwanza kwa mfano kuna Mwanamke ambae alikua akijulikana kwa jina
la Zimmira Radhi Allahu Anha ambae walimtesa sana, na kuna aitwae Al Nahdiya au
Hakima Bint Habib ibn Kuwayb, Radhi Allahu Anha ambae walimpiga mpaka akopeteza
Nuru ya Macho yake, bila ya shaka hatuwezi kumsahau Sumayyah Bint Khayat Radhi
Allahu Anha ambae ndie mtu wa kwanza kupata ushahidi baada ya kua ni Muislam wa
kwanza kuuliwa kutokana na Imani yake.
Halafu wakahamia kwa Watoto ambao ni vijana kama Musab Ibn Umayr Radhi Allahu
Anhu ambae likua ni Sahaba kijana mwenye kuvutia kuliko vijana wote wa Kiume wa
mji wa Makkah, kwani kila Mwanamke wa Mji wa Makkah alikua anatamani kuolewa
nae, na hii pia ni kutokana na kua Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu alikua na wazee
ambao ni matajiri sana na walikua wanaompenda sana, na hivyo alikua anavaa vizuri na
kupendeza kuliko watu wote katika mji wa Makkah.
Lakini aliposilimu tu na kuamua kuingia kwenye Dini ya Kiislam basi mambo yake
mazuri yote haya yalitoweka, kwani alifungiwa ndani kwa mda wa miaka mitatu na
kuzuiliwa asitoke nje kwani akitoka basi ataonana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, na alipoachiwa na kuonekana kua hana muelekeo wa kuachana na Iman ya Dini
ya Kiislam basi alipokonywa kila kitu chake, na akawa ni mwenye kuonekana kama
Omba omba anaevaa matambara mabovu badala yake, lakini hata hivyo haya yote
hayakumfanya Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu kua ni mwenye kuachana na Imani
yake hio mpya kwani hali ilikua ni kinyume chake. Na matokeo yake Musab Ibn Umayr
Radhi Allahu Anhu akawa ndie Balozi wa kwanza wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam katika Mji wa Madinah na alifanikiwa kuupata ushahidi katika Vita vya Badr.
384
Na alikuwemo pia Talha Ibn Ubayd Allah Radhi Allahu Anhu ambae alikua ni mwenye
Umri wa miaka 15, pale alipoingia kwenye Uislam ambapo mama yake alikua akimfunga
kamba na kutembea nae sokoni kama mbuzi huku akimtukana, na Makafiri wakimpiga
na kumlaani ni nzima.
Alikuwemo pia Imran Ibn Husein Radhi Allahu Anhu ambae alificha tukio la kusilimu
kwake, na hivyo siku moja Baba yake Imran akaenda katika Dar Al Arqam ambayo ni
Nyumba ya Arqam Ibn Abi Arqam Radhi Allahu Anhu ambae ni Sahaba mdogo kijana
wa umri wa miaka 14 ambae aliirithi kutoka kwa Baba yake, Nyumba hii ilikuwepo
katika upande wa Kaskazini chini ya Kilima cha Safa ambamo ndani yake walikua
wakikutana Masahaba pamoja na Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam kwa siri
kusomeshana Qur’an.
Na hivyo mzee Husein alipoingia ndani basi Masahaba walimficha Imran kwa kumkalia
ili asionekane na Baba yake kisha akaja kudhuriwa lakini badala yake Mzee Husein
alipoingia ndani basi alienda moja kwa moja kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na akasilimu, na baada ya kusilimu basi Imran akatoka chini ya miguu ya Masahaba
waliokua wamemkalia na akamkimbilia Baba yake na kukumbatia kwa furaha na
mapenzi yake juu ya Baba yake, huku yeye na Masahaba waliobakia wakilia kwa wingi
wa Imani na hisia zilizowaja Nyoyoni mwao baina yao.
Ambapo kwa upande wa pili kisa hiki kiliteremshwa na kuzungumziwa ndani ya Qur’an
kwa ajili ya kua ni kama Silaha na Kinga kwa ajili ya Waislam dhidi ya Maadui zao hao.
Kwani kisa hii kilikua ndio Silaha na kinga pekee ambayo iliwafanya Waislam wawe
washindi dhidi ya Makafiri wa Makkah pale walipozidiwa na hivyo kuamua kukimbilia
uhamishoni katika ardhi ya Uhabeshi, hivyo bila ya shaka Allah Subhanah wa Ta’ala
ambae ndie m-bora wa kupanga na kukadiria, aliamua kukishusha kisa hiki kabla ya
kufanyika kwa Hijra hio mnamo mwishoni mwa mwaka wa 4 baada ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kushushiwa Utume.
Hivyo mwanzoni mwa mwaka wa 5 wa Utume, basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akawaambia Masahaba zake kua wahamie Uhabeshi, kwani ndani ya Ardhi hio
kuna ‘An Najash’ yaani ‘Mfalme’ ambae anajulikana kwa jina la An Najash Ashama Ibn
Abjar ambae ni Muadilifu na hakuna anaepata madhara kutokana nae kama
wanavyoelezewa miongnoni mwa Ahl Al Kitab wenye sifa ya Uadilifu pale iliposema
Qur’an katika aya ifuatayo:
385
﴿وَمِنْ أَهْلِ ٱلْكِتَابِ مَنْ إِنْ أتَْمَنْهُ بِقِنْطَارٍ يُؤَدِّهِ إِلَيْكَ وَمِنْهُمْ م َّ نْ إِن أتَْمَنْهُ بِدِينَارٍ
لا َّ يُؤَدِّهِ إِلَيْكَ إِلا َّ مَا دُمْتَ عَلَيْهِ قَآئِماً ذٰلِكَ أبَِن َّهُمْ قَالُواْ لَيْسَ عَلَيْنَا فىِ ٱلأُمّ يَِّين ِ
سَبِيلٌ وَيَقُولُونَ عَلَى اهلل َِّ ٱلْكَذِبَ وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴾
Wamin ahli alkitabi man in ta/manhu biqintarin yu-addihi ilayka waminhum man
in ta/manhu bideenarin la yu-addihi ilayka illa ma dumta AAalayhi qa-iman thalika
bi-annahum qaloo laysa AAalayna fee al-ommiyyeena sabeelun wayaqooloona
AAala Allahi alkadhiba wahum yaAAlamoona (Surat Al Imran 3:75)
Tafsir: Na miongoni mwa watu wa Ahl ul Kitab kuna yule ambae hata kama
akiaminiwa Qantri (Mali nyingi sana) basi atakurudishia mwenyewe, na miongoni
mwao ni yule ambae ukimuamini Dinari moja basi hatokurudishia, isipokua pale
inapokua unamdai kwa mfululizo, na hii ni kwa sababu wamesema: ‘Hakuna tatizo
kwetu sisi kusaliti na kuchukua mali ya wasiojua’ na wanasema kuhusiana na Allah
uongo na wanajua juu ya hilo.
Hivyo Masahaba 10 Wanaume na Masahaba wa 4 Wanawake wakahamia kisiri siri,
ambao ni Sad Ibn Abi Waqqas, Jahsh Ibn Riyab, Abd Allah Ibn Jahsh, Jafar Ibn Ab Talib,
Uthman Ibin Affan na mkewe Ruqayyah Bint Rasul llah Salallahu Alayhi wa Salam, Abu
Hudhayfah Ibn Utbah na Mkewe Sahla Bint Suhayl Zubayr Ibn Awwam, Musab Ibn
Umair, Abd Rahman Ibn Awf, Abu Salama Abd Allah Ibn Al Asad na mkewe Ummu
Salamah Hind Bint Abi Umayyah, Uthman Ibn Mazun, Amr Ibn Rabiah, Laylat Bint
Asmah Radhi Allahu Anhum.
Masahaba hawa walisafiri kwa kutumia Jahazi kutoka katika mji wa Shuaiba na kufikia
katika mji wa Adulis, na ingawa leo hii hua liko katika ardhi ya maeneo ya Eritrea lakini
katika wakati huo eneo hilo lote lilikua linajulikana kama Abissiniyah yaani Ethiopia. Na
kisha baada ya hapo ukafuatia msafara wa Masahaba 83 ambao ni Wanaume na
Masahaba 18 ambao ni Wanawake wakahamia pia.
Ambapo anasema Ummu Salamah Radhi Allahu Anha kua: ‘Wakati sisi tulipohamia
katika Ardhi ya Uhabeshi, basi tuliishi na miongoni mwa Majirani bora ambae ni
An Najashi, tulitekeleza Ibada zetu kwa usalama na amani, tulimuabudu Allah
Subhanah wa Ta’ala bila ya kubughudhiwa na hatukuwahi kusikia tu chochote kile
ambacho hatukikipenda. Hivyo habari hizi zilipowafikia watu wa Quraysh basi
wakaazana kupanga njama zao dhidi yetu.’
386
Yaani watu wa Kabila la Quraysh la Makkah waliamua kuwatuma Wajumbe maalum
wawili ambao ni vijana mahiri kwa kua na sifa ya kujadiliana na kushawishi kidiplomasia
hawa hawakua vijana wowote isipokua walikua ni Amr Ibn Al Aas ambae mbali ya kua
ni mwenye hikma na busara sana miongoni mwa Vijana wa Quraysh lakini pia alikua ni
Kijana Mpiganaji mahiri sana, ambapo pamoja nae akatumwa Abd Allah Ibn Abi Rabii
ambae pia alikua ni mfanya biashara maarufu anaejulikana mpaka Abissiniyah.
Wajumbe wawili hawa walipewa jukumu la kuwatumia zawadi wajumbe wa Baraza la
washauri la An Najash kwa ajili tu ya kumshauri An Najash awarudishe Waislam hao
katika Mji wa Makkah, hivyo Amr Ibn Al Aas akamwambia An Najash kua: ‘Kwa
hakika katika Ardhi yako kuna watu waliotoka kwetu ambao wameasi na
wamewakimbia watu wao, baada ya kuachana na Imani ya wazee wao na wamekuja
kuishi katika ardhi yako na kuendeleza Imani ya Dini yao mpya, lakini hawakuingia
kwenye Dini yako, hivyo tungependa uturuhusu kuwarudisha kwetu katika familia
zao kwani kuna watu wao ambao wanasikitika na kuhuzunika kutokana na
kuondoka kwao.’
Baada ya Amr Ibn Al Aas kumalizia kuelezea kuhusiana na matakwa ya watu wa
Quraysh, mbele ya An Najash na baraza lake la Washauri, basi washauri hao
wakamuunga mkono Amr Ibn Al Aas, kua kama hali ya watu hao ni hali ya waasi
waliosababisha machafuko katika ardhi yao, na wamekimbia na kukimbilia Abissiniya
basi bila ya shaka inabidi watu hao warudishwe kwao, ili wasije wakaleta machafuko
kutokana na Imani ya Dini yao hiyo mpya ambayo pia ni tofauti na Imani ya Dini ya
Utawala wa An Najash, lakini hata hivyo kwa upande wa An Najash kutokana na Uadilifu
wake basi mara tu baaada ya kusikiliza hoja hizo basi akasema: ‘La, kamwe sitoweza
kuwaruhusu watu hawa ambao ni Majirani zangu kwa watu wawili hawa, hata
kama watu hai watakua wanampango ya siri dhidi ya Utawala wangu, hadi pale
nitakapowata na kuzungumza nao na kusikiliza kuhusiana na majibu yao kutokana
na hoja na shutuma zenu. Na hakika ni wajibu wangu mimi kua na uhusiano mzuri
nao kwani nao wana uhusiano mzuri nami.’
Na kisha baada ya hapo An Najash akaamrisha kua Waislam hao waletwe mbele yake,
kwa ajili ya kufanya mahojiano nao. Masahaba hao wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam walipopata habari ya wito huo basi basi wakakaa na kuulizana namna ya kujibu
suali hilo la na Najash, kwa kusema: ‘Hivi jee sisi tutamwambia nini sisi An Najash?’
na hivyo wakakubaliana kua watamchagua kijana Mdogo ambae nae pia ni mahiri kwa
ufahamu wa Lugha na mwenye kujaa Hikma na Busara katika kuzungumza kwake.
Huyu hakua kijana mwengine yeyote isipokua alikua ni ingawa Jafar Ibn Abi Talib Radhi
Allahu Anhu alikua ni Ibn Ami wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam lakini
pia alikua ni miongoni mwa Masahaba watano waliotoka katika ukoo wa Banu Hashim
waliofanana sana kisura na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ambapo
387
miongoni mwa waliofanana nae pia wakiwemo Hasan Ibn Ali Ibn Abi Talib (mjukuu wa
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam), Abu Sufyan Ibn Al Harith, As Sayb Ibn
Ubayd (Babu wa babu yake Imam Muhammad Idris Al Shafi’i) na Qutham Ibn Al Abbas
Radhi Allahu Anhum.
Hivyo Masahaba wakamchagua Jafar Radhi Allahu Anhu ambae babu yake ndie
aliekabiliana na Jeshi la Abraha katika mwaka wa Tembo pale Abraha ambae ndie
aliekua Gavana wa Yemen anaemuwakilisha Mtawala wa Abissiniya hapo kabla
alipotaka kulivunja Al Kaabah, na akaangamizwa na Allah Subhanah wa Ta’ala, ambapo
kujitambulisha kwake Jafar mbele ya An Najash basi kutambanishia An Najash kua
anazungumza na nani, hivyo Jafar atasema ukweli kama ulivyo kwa kusema: ‘Bila ya
shaka tutamwambia kama alivyotuamrisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
bila ya kujali kitakachofuata baada ya hapo.’
Na hivyo walipowasili kwa An Najash basi wakamkuta An Najasha akiwa na Makasisi
wake na Vitabu vyao pamoja na Wajumbe wa Baraza lake la Washauri, ambapo nae
baada ya kuwakaribisha basi akawauliza Masahaba hao kwa kusema: ‘Nimesikia kua
nyinyi mna Dini mpya ambayo ni tofauti na Dini ya asili ya watu wenu, hivyo nilikua
nataka kujua hivi jee hii dini yenu ni Dini gani, na kwanini kutokana nayo mkawa
mmewaasi wazee wenu? Na hapo hapo mkawa hampo kwenye ufuasi wa Dini yetu’
Hivyo anasema Umm Salamah Radhi Allahu Anha kua: ‘Mzungumzaji wetu alikua ni
Jafar Ibn Abu Talib ambae alisema: ‘Ewe Mfalme, sisi tulikua ni watu wajinga,
tuliokua tukiishi kama wanyama wa mwituni, mwenye nguvu miongoni mwetu
aliishi kwa kuwatumia wasiokua na nguvu. Tulikua hatuna sheria yeyote, na tulikua
hatuna mamlaka isipokua wenye nguvu dhidi ya wasiokua na nguvu. Tulikua
tukiabudu masanamu yaliyotengenezwa kutokana na udongo au miti, na hatukujua
ni nini maana ya heshima wala nini maana ya Utu.
Halafu Mungu akatushushia Rehma zake, akatutumia Mtume kutoka miongoni
mwetu, ambae anafahamika kutokana na ukweli wake na uaminifu wake, tabia
zake ni mfano wa kuingwa miongoni mwetu, na ni mwenye kutoka katika ukoo bora
miongoni mwa Waarabu. Akatuita katika kumuabudu Mungu mmoja, na
akatukataza kuyaabudia Masanamu, akatuamrisha kusema ukweli, kuwalinda
wasiokua na nguvu, Masikini, Wanyonge, Wajane na Mayatima.
Ametuamrisha kuwaheshimu Wanawake na kua tusiwasingizie mambo ya uongo.
Wengi miongoni mwa watu wetu bado ni wenye kua na Miungu mingi na
wanachukia maamuzi yetu ya kujiunga na Imani mpya ambayo inayoitwa Uislam.
Hivyo wameanza kututeketeza, na ni katika kukimbia mauaji yao ndio tukafuata
usalama katika Ufalme wako.’
388
Maneno haya yalikua ni yenye sifa ya Qawlan Sadidah na hivyo ujumbe wake ulifika
ndipo na kama unavyotakwa ufike na kuacha athari inayotakiwa ndani ya Moyo wa An
Najash na kumbakisha akiwa ni mwenye fikira na hisia kubwa sana An Najash, hivyo
akasema kumwambia Jafar Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kua: ‘Hivi Jee unao
uthibitisho wowote ule kutoka kwenye Kitabu cha huyo Mtume wenu?’ ambapo
Jafar Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akajibu: ‘Naam!’ An Najash akasema: ‘Nisomee’
Hivyo Jafar Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kuanza kumsomea An Najash Surat
Maryam, kuanzia mwanzo wake hadi katika aya ya 34, kama tutakavyoona katika Tafsir
yake na hivyo kutokana na kusikiliza kwake kisomo cha Jafar Ibn Abi Talib Radhi Allahu
Anhu na maana ya tafsir yake basi kulimpelekea An Najash kutokwa na machozi, hadi
Ndevu zake zikaroa kwa machozi, na Makasisi wa An Najash nao wakajaza vitabu vyao
machozi, kutokana na Aya hizo, kisha An Najsha akasema: ‘Naapa kwa jina la Mungu
kua Hiki Kitabu chenu na Kitabu cha Musa vimetokana na Chanzo kimoja, Wa
Allahi mimi sitokuslimisheni bali nitakubakisheni kwenye ardhi yangu na
sitokusalitini na sitokurudisheni mkateswe na maadui zenu.’
Umm Salamah Radhi Allahu Anha anaendelea kusema kua: ‘Baada ya Amr Ibn Al Aas
kuondoka na Abd Allah Ibn Rabiah kuondoka mbele ya An Najash basi Amr Ibn
Al As akasema: ‘Wa Allahi nnaapa mimi kua kesho nitawakilisha maelezo ambayo
yataung’oa Mzizi wa Kila kitu katika maisha yao’ ambapo Abd Allah Ibn Rabia Radhi
Allahu Anhu akasema: ‘Haina haja kwa sababu hata hivyo hawa watu wetu wana
haki za Nasaba ya Kifamilia Nasi, hata kama ikiwa wamepingana nasi’ hivyo Amr
Ibn Al Aas akasema: ‘Wa Allahi nitamjuulisha An Najash kua Hawa Waislam
wanasema kua Isa Ibn Maryam ni Mja.’
Hivyo Siku ya pili yake Asubuhi Amr Ibn Al Aas akamwambia An Najash kua: ‘Ewe
An Najash hakika hawa watu wanasema sivyo kuhusiana na Isa Ibn Maryam, hivyo
hebu waite uwaulize upate kujua Jee wanasemaje juu yake?’ naam, maneno haya
yalimshtua An Najash, kwa sababu alikua ameshawakubalia Waislam na kuwaahidi
usalama watakapokua katika ardhi yake, lakini sasa kama inakuwa wanasema sivyo
kuhusiana na Isa Ibn Maryam basi itabidi asiwaonee huruma kwani hata watu wake
hawatoweza kumfaham na watasababisha machafuko na hivyo nae atapata upinzani
mkubwa sana, hivyo akaamrisha kua Waislam hao waitwe tena mbele yake.
Waislam walipoitwa basi wakulizwa: ‘Hivi Jee Dini yenu inasemaje nyie kuhusiana
na Isa Ibn Maryam’
Hivyo Jafar Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Hakika sisi tunasema kile
ambacho amekisema Mtume wetu kutokana na Kitabu alichokuja nacho ambacho
kinasema kua: ‘Isa Ibn Maryam ni Mja wa Allah, Ni Mtume wake, Ni Ruhi ambae
389
ameumbwa na yeye, Ni Kauli yake ambayo imepitia kwa Maryam Bint Imran,
ambae ni Bikira’
Baada ya kusikia hivyo basi An Najash akainama na kuchora mstari chini kwa
fimbo yake kisha na kisha akasema: ‘Isa Ibn Maryam hakuvuka juu ya kile
mnachokisema hata kwa upana wa mstari wa fimbo hii.’ Kisha akawageukia
Waislam na kuwaambia: ‘Wallahi Naapa kua mko huru kuabudu mtakavyo katika
ardhi yangu, na yeyote yule atakae kubughudhini basi atapata adhabu kali juu yake
na pia atalipa fidya ya dhahabu juu ya yeyote yule atakaembughudhi miongoni
mwenu’
Ummu Salamah Radhi Allahu Anha anaendelea kusema kua: ‘Hivyo Amr Ibn Al Aas
na Abd Allah Ibn Rabiah wakaondoka huku wakiwa wameadhirika sana, huku sisi
tukiwa tumebakia na kuishi katika makazi mazuri pamoja na jirani yetu An
Najash.’
Naam..hivyo hio ndio sababu na malengo ya kushushwa Surat Maryam ambayo ni yenye
98 ambazo takriban zote ni zenye kumalizikia na harkah ya Fat-ha tein na hivyo kuifanya
kua ni miongoni mwa Sura ambazo zina mpangilio mzuri sana na wa kuvutia sana
kimtiririko katika kuisoma kwake.
Ambapo anasema Ummu ul Muuminina Aisha, Abd Allah Ibn Zubayr, Bahr ul Ilm Abd
Allah Abbas Radhi Allahu Anhum kua: ‘Surat Maryam ni Sura iliyoshuswa katika Mji
wa Makkah’ na Imam Muqatil Ibn Sulayman amesema kua: ‘Surat Maryam yote
Imeshushwa Makah isipokua Aya yake 58 ya Sijda ndio iliyoshushwa katika Mji
wa Madinah ’ na Kwa upande wa Imam Al Suyuti basi yeye amesema kua : ‘Surat
Maryam yote imeshushwa Makkah isipokua Aya yake 58 na aya ya 71 ndio
zimeshushwa Madinah ’
HARFU MUQATTAA’AT NA KISA CHA NABII ISA.
Neno MuqattaA’at ni neno lililotokana na neno Qata’a ambalo kwa Lugha ya Kiarabu
hua linamaanisha Kukata, Kutengenisha, Kugawa, Kutofautisha. Hivyo Harfu
MuqattaA’at hua inamaanisha herufi za Lugha ya Kiarabu ambazo zinapoandikwa na
zinaposomwa hua zinasomwa kwa kutengenishwa kwa mfano herufi Kaf Ha Ya Aain
Saad ambalo ndio neno la mwanzo baada ya aya ya ufunguzi ya Biismi Allahi Rahmani
Rahim wa Surat Maryam ambayo ni Sura ya 19 iliyomo ndani ya Qur’an, na herufi hizi
kwa baadhi pia hua wanaziita kua ni Huruf al Mutafarriqa yaani Herufi zilizotenganika.
390
Ambapo ingawa kuna Wanazuoni wasemao kua neno كٓھیعٓصٓ Kaf Ha Ya Aain Saad ni
miongoni mwa yale maneno yanayojumuishwa katika Harfu MuqattaA’at (Harfu
zilizokatwa au zilizofupishwa) ambazo hua hakuna anaejua maana yake isipokua
mwenyewe Allah Subhanah wa Taála.
Lakini kwa upande wa Mujaddid ad Din Sultan Al Mutakallimin Imam Fakhr Ad Din Al
Razi amesema kua: ‘Haiwezekani kua Allah Subhanah wa Taála, aingize kitu ndani
ya Kitabu chake Qur’an ambacho sisi hatutokifaham maana yake. Na kwa sababu
yeye Allah Subhanah wa Taála ndie alietuamrisha sisi kukitafakkar kitabu chake
kwa lengo la kutupa uongofu kutokana nacho. Hivyo basi lengo hili la kuitafakkari
Qur’an halitoweza kufikiwa kama ikiwa hatutoifaham maana yake, kwani lengo
hili huweza kufikiwa pale tu baada ya kufaham maana yake. (Mafatih al Ghayb,
Tafsir al Kabir)
Baadhi ya wenye kujua wamesema kua Harfu hizo MuqaattaAt zinamaanisha:
.الله Mimi) au neno Allah ,أنا) Inayowakilisha neno Anā :(ا) Alif
Hā :(ه) Inayowakilisha neno Al-Hādī ,الھادي) Muongozi) Inayowakilisha neno Huwa
.(Yeyeھو)
Ḥā :(ح) Inayowakilisha neno Al-Ḥamīd ,الحمید) Kushukuriwa).
Ṭā :(ط) Inayowakilisha neno (Ewe).
یقین Inayowakilisha neno (Ewe) au Yaqin :(ي) Yā
Kāf :(ك) Inayowakilisha neno Al-Kāfī ,كافي) Anaetosheleza).
(التف Herufi ya pili katika Neno Allah) au (Latif ,الله) Inayowakilisha neno Allāh :(ل) Lām
Mīm :(م) Inayowakilisha neno Al-ʿAlīm ,العلیم) Herufi ya mwisho ya neno Alim) au
inayowakilisha neno Al-Majīd ,المجید) Mshindi).
Nūn :(ن) Inayowakilisha neno Al-Qalam (Inayowakilisha neno "Kalamu au Peni") au
) نر (Nur
Sīn :(س) Inayowakilisha neno As-Samī' ,السمیع) Mwenye Kusikia).
A’in :(ع) Inayowakilisha neno Al-ʿAlīm ,العلیم) Mwenye Kujua).
Ṣād :(ص) Inayowakilisha neno As-Ṣādiq ,الصادق) Mkweli).
Qāf :(ق) Inayowakilisha neno Al-Qādir ,القادر) Mwenye Kukadiria).
.(رائي / رأى / رؤیا / یرى / بصی رKuona Inayowakilisha neno Al Raa (Mwenye :(ر) Rā
Qurán ina Surah 29 zilizoanzia na Huruf MuqattaA’at ambapo 3 kati yao zina herufi
1, 9 kati yao zina herufi 2, 13 kati yao ina herufi 3, 2 kati yao zina herufi 4 na 2 zina
herufi 5, Sura hizo ni:
Nambari Namba ya Surah Jina la Sura Huruf-a-MuqattaA’at
1 38 Surat Saad صٓ Saad
391
2 50 Surat Qaaf قٓ Qaaf
3 68 Surat Al Qalam نٓ Nun
4 40 Surat Al Ghafir حمٓ Ha Mim
5 41 Surat Al Fusilaat حمٓ Ha Mim
6 43 Surat Az Zukhruf حمٓ Ha Mim
7 44 Surat Ad Dukhan حمٓ Ha Mim
8 45 Surat Al Jathiyyah حمٓ Ha Mim
9 46 Surat Al Ahqaaf حمٓ Ha Mim
10 20 Surat Ta-Ha طھ Ta-Ha
11 27 Surat An Naml طسٓ Ta Sin
12 36 Sura Yasin یسٓ Ya-Sin
13 10 Surat Yunus الر Alif Lam Ra
14 11 Surat Hud الر Alif Lam Ra
15 12 Surat Yusuf الر Alif Lam Ra
16 14 Surat Ibrahim الر Alif Lam Ra
17 15 Surat Al Hijr الر Alif Lam Ra
19 29 Surat Al Anqabut المٓ Alif Lam Mim
20 30 Surat Ar Rum المٓ Alif Lam Mim
21 31 Surat Luqman المٓ Alif Lam Mim
22 32 Surat As Sajda المٓ Alif Lam Mim
23 2 Surat Al Baqara الم Alif Lam Mim
24 3 Surat Al Imran الم Alif Lam Mim
18 26 Surat Ash Shuara طسۤ مۤ Taa Sin Mim
25 28 Surat Al Qasas طسٓمٓ Taa Sin Mim
26 7 Surat Al Araf المٓصٓ Alif Lam Mim Sad
27 13 Surat Rad المٓر Alif Lam Mim Ra
28 19 Surat Maryam كٓھیعٓصٓ Kaf Ha Ya Aain Saad
29 42 Surat Ash Shuraa حمٓ عٓسٓقٓ Ha Mim Aain Sin Kaf
Tunapoangalia Harfu MuqattaAat kulingana na mitizamo ya Wanazuoni wenye Ilm ya
Tasawwuf katika Fani ya Ruhaniyya basi wao wanasema kua Harfu hizo ambazo ni zipo
mwanzo mwa sura 19 tulizoziangalia hapo juu kua zimezigawa harfu za lugha ya Kiarabu
nusu kwa nusu, kwani hizo zinaitwa Al Huruf Al Nuranniyah (Yaani Herufi zenye sifa
ya kua na Nuru) ambazo ziko 14. Na Herufi zilizobakia hua zinaitwa Al Huruf al
Dhalamiyyah ambazo nazo zimegawika sehemu mbili.
Sehemu ya kwanza ni yenye herufi 7 zenye sifa ya darja ya juu na sehemu ya pili ni zenye
darja ya chini. Herufi hizi hua zina athari yake kinguvu, ambapo katika Surat Al Fatiha
tunaona ina herufi zote hizo herufi 7 zenye darja ya chini ambazo hujulikana kama
Sawaqit al Fatihah.
392
Herufi hizo ni zenye kunasibishwa na Majina Matukufu ya Allah Subhanah wa Taála na
hivyo kua ni zenye kufanyiwa Dhikr kila moja katika siku yake kwa mpangilio ufuatao:
-’Faف Al Fardan lenye kumaanisha Mwenye Upekee. Ambalo ni jina la Dhikr ya siku
ya Jumaatatu.
Jimج – Al Jabbar lenye kumaanisha Mwenye Nguvu na Ujabari wa kipekee ambalo ni
jina la Dhikr ya siku ya Jumanne.
Shinش – Al Shahid lenye kumaanisha Mwenye Kushuhudia kila kitu ambalo ni jina la
Dhikr ya siku ya Jumatano.
-’Thaث Al Thabit lenye kumaanisha Mwenye Uthabiti wa Kipekee ambalo ni jina la
Dhikr ya siku ya Alkhamis.
Dha – Al Dhahir lenye kumaanisha Mwenye Kuonekana dhahir kwa dalili zake ظ
ambalo ni jina la Dhikr ya siku ya Ijumaa.
Kha’ – Al Khabbir lenye kumaanisha Mwenye Habari juu ya Kila kitu ambalo ni jina خ
la Dhikr ya siku ya Jumamosi.
Zay – Al Zakiy lenye kumaanisha Mwenye Utukufu wa Juu kabisa ambalo ni jina la ز
Dhikr ya siku ya Jumapili.
Ama kwa upande wa Dhu Nun Al Misri basi yeye anasema kua: ‘Majina Matukufu ya
Allah Subhanah wa Ta’ala, ni mharakisho wa dua ambayo ikiombwa kupitia katika
Majina hayo basi Dua hio hua ni yenye Kujibiwa Haraka. Na ndani yake mna
Herufi 7 na katika Ummu ul Kitaab yaani Surah Al Fatiha ambayo ni Sura yenye
Aya 7 basi herufi zote za Kiarabu zimo katika aya isipokua ث Tha’ (500), ج Jim (3),
’ (80) Fa’ ف (900), Dha’ ظ (300), Shin ش (7), Zal ز (600), Kha’ خ
Ama katika kitabu cha Manbah Usul Al Hikma basi Imam Al Sanusi mara kadhaa
amekua akitumia herufi hizo katika Dua zake kwa kuanzia na neno Wa Bi Haqqi ث Tha’
. (80) Fa’ ف (900), Dha’ ظ (300), Shin ش (7), Zal ز (600), Kha’ خ (3), Jim ج (500),
Kwa upande wa Shaykh Al Akbar Imam Abu Bakr Ibn Al Arabi basi yeye anasema kua:
‘Inabidi Mjue Harfu Muqataa’at zote, zilizoanza mwanzoni mwa Sura za Qur’an ni
majina ya Malaika na nimezitaja katika baadhi ya matukio, ambapo kamwe
haijawahi kutokea kwangu kuzitumia bila ya kutokea Malaika ambae alinielezea
mie juu ya Jambo nisilolijua. Kwa kifupi hawa ni Walimu wangu. Hivyo nikiita
moja kati ya Harfu hizo basi hua ni sawa na kumuita mmoja kati ya Malaika ambae
nae hutokea na kunisaidia kama ninavyohitaji’
Ambapo:
Harfu Siku yake Msimamizi wake Jina Maalum
Kha (600)خ
Jumapili Rawfa’il Khabirخبیر
393
Shin (300)ش
Jumatatu Jibril Shakirشاكر (7) Zal ز
Jumanne Samsama’il Zakiyزكي 900)Dhal)ظ Jumatano Mika’il
Dhahirظاھر Tha (500)ث
Alkhamis Sirfaya’il Thabitثابت 3)Jim)ج Ijumaa ‘Anya’il
Jabbarجبار Fa (80)ف
Jumamosi ‘Azra’il Fatirفاطر Shaykh Al Akbar Imam Abu Bakr Ibn Al Arabi anaendelea kutuambia katika Al-Durr al
Maknūnfī 'Ilm al-Ḥurūf, kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala alimfundisha Nabii wake
Adam Jina tukufu kuliko yote. Kisha baada ya hapo Nabii Adam akamfundisha
mtoto wake Seth ambae nae akamfundisha Nabii Idrisa Alayhi Salaam. Nabii Idrisa
Alayhi Salaam alikua ni mwenye kupokea vitabu 30 kutoka kwa Allah Subhanah
wa Ta’ala na akapewa I’lm ya herufi, na siri za Hikma, Nambari na mambo
mengineyo, na yeye ndie aliyekua ni wa mwanzo kuandika kwa kutumia Kalamu.
Nabii Idrisa aliandika kitabu kiitwacho Kanzu Al Asrar (Hazina ya Siri), ambacho
Thabit Ibn Qurta Al Harani ameandika kukielezea juu yake. Na mimi nilipokutana
nae Nabii Idrisa baada ya kupata ufunuo, basi nikamuuliza, ufunuo zaidi juu yake
ambapo nae akasema: ‘Ufunuo huu ni ile ambayo iliyohifadhiwa nje ya Kitabu
kwani myengine yote iliyobakia imefichika na imefungwa ndani yake. Kisha
akanifunulia baadhi ya Siri zisizojulikana ambazo hakuna mtu mwenye kuzijua juu
yake. Ilm hii ya Herufi baadae ikarithiwa na watu 40 tu wa Haramisa wa Misri’’
Kwani baadhi wanaweza kujiuliza kwa nini kila nikiandika herufi basi hua ninaandika
nambari mbele yake kwa mfano ’Thaث (500), ج Jim (3), خ Kha’ (600), ز Zal (7), Shinش
’Faف (80) n.k, kwani hii ni kulingana na mtizamo wa Ilm (900), Dha’ ظ (300),
Ruhaniyyah ambapo harfu hizi zimepewa thamani ya uzito wa kiidadi kama ifuatavyo.
الف 1 ب 2 ج 3 د 4 ه 5 و 6 ز 7 ح 8 ط 9 ى 10 ک 20 ل 30 م 40 ن 50 س 60 ع 70 ف 80
ص 90 ق 100 ر 200 ش 300 ت 400 ث 500 خ 600 ف 700 ض 800 ظ 900 غ 1000.
Na wenye Ilm Ruhaniyyah hua wanatumia uthibitisho wa kua kila kitu kina idadi yake
kinambari kutokana na ile aya ambayo inasema:
﴿لِّيَعْلَمَ أَن قَدْ أَبْلَغُواْ رِسَ الاَتِ رَهبِِّمْ وَأَحَ اطَ بمَِا لَدَ يْهِ مْ وَأَحْ صَى ٰ كُ ل َّ شَ يْ ءٍ
عَدَداً ﴾
LiyaAAlama an qad ablaghoo risalati rabbihim waahata bima ladayhim waahsa
kulla shay-in AAadadan (Surat Al Jinn 72:28)
394
Tafsir: Na huwalinda (Mitume) hadi ahakikishe kua wamefikisha ujumbe wa Mola
wao. Na yeye (Allah) amekizunguka na amekilinda kila kitu katika idadi.
‘Ambapo aya imetumia neno Ahata lenye kutokana na neno Ha-Ta linalomaanisha
Kuangalia, Kulinda, Kuzunguka, Kugubika, au Kujua kitu kwa Undani, na pia
ikatumia neno Ahsa ambalo linalotokana na neno Ha-Ssa ambalo hua ni lenye
kumaanisha Kupiga Changarawe au Kijiwe kimoja kimoja, Kuhesabu kwa
Umakini, Kutia Nambari, Kuhesabu Kiidadi, Kujua au Kufahamu Idadi ya Kitu’.
Ama kwa upande mwengine basi Imam Muhammad Ibn Is-haq amesema kua amesema
Imam Muhammad Ibn Saib Al Kalbi kua amesema Abu Salih, kua amesema Jabir Ibn
Abd Allah Ibn Riyab: Abu Yasir Ibn Akhtab, pamoja na baadhi ya Mayahudi
walipita mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae nae alikua akisoma
Surat Al Fatiha, kisha akasoma Alif Lam Miim, Dhalika Al Kitab La Rayba Fihi
Hudda lil Mutaqqin.
Hivyo (Abu Yasir Ibn Akhtab) akamfuata ndugu yake Huyayy Ibn Akhtab ambae
alikua amekaa na Mayahudi wenzake na kuwaambia: ‘Wallahi! Nimemsikia
Muhammad akisoma kile alichoteremshiwa, Alif Lam Miim, Dhalika Al Kitab La
Rayba Fihi Hudda lil Mutaqqin.’ Huyayy akamuuliza: ‘Umemsikia akisoma maneno
hayo?’ Abu Yasir akajibu; ‘Naam!’ Hivyo Mayahudi hao wakaondoka wote kwa
pamoja hadi kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kumuuliza: ‘Jee Jibril
amekuteremshia maneno yasemayo Alif Lam Miim, Dhalika Al Kitab La Rayba Fihi
Hudda lil Mutaqqin?’ Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Naam.’
Mayahudi wakasema: ‘Allah ameleta Mitume kabla yako, lakini sisi kamwe
hatujawahi kusikia miongoni mwao ambae ametaarifiwa juu ya mda wa Mamlaka
isipokua wewe. Na mda wa uhai watakaoishi watu wa Ummah wako kwani, Alif ni
1, Lam ni 30, Mim ni 40, na hio jumla yake ni 71. Hivyo hio ni miaka 71, sasa jee
tunataka kumfuata Mtume ambae Mamlaka yake mwisho wake ni Miaka 71 na
uhai wa Watu wake mwisho wao ni miaka 71?’
Kisha wakamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam: ‘Ya Muhammad Jee
kuna jambo jengine uliloshushiwa zaidi linalofanana na hili?’ Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akasema: ‘Naam.’ Mayahudi wakauliza: ‘Jee ni lipi?’ Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Alif Lam Mim Sad.’ Mayahudi wakasema:
‘Hio ni zaidi, kwani Alif ni 1, Lam ni 30, Mim ni 40, Sad ni 90 hivyo hapa
inamaanisha miaka 161.’
Mayahudi wakauliza: ‘Ya Muhammad jee kuna jengine zaid?’ Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Naam. Alif Lam Ra.’ Mayahudi wakasema:
‘Alif ni 1, Lam ni 30 na Ra ni 200. Hio hua ni miaka 231’.
395
Wakauliza tena: ‘Ya Muhammad jee kuna jengine zaid?’ Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akasema: ‘Alif, Lam, Mim, Ra’. Mayahudi wakasema: ‘Alif ni 1,
Lam ni 30, Mim ni 40 na Ra ni 200. Hio ni miaka 271.’
Kisha Mayahudi hao wakaondoka na kusema: ‘Ya Muhammad hakika sisi
tumechanganyikiwa juu ya mambo yako haya, kwani hatujui juu ya mda wa
Mamlaka yaliopewa Ummah wako kama utakua ni mrefu ama la.’
Mayahudi hao wakaambiana: ‘Twende zetuni’ kisha wakaondoka kwa pamoja
huku Huyay akimwambia Abu Yasir pamoja na Rabbi wao kua: ‘Na ni nani
atakaeweza kujua kwani huenda miaka hio yote 71, 61, 100, 231, na 271 hua ni 734
ni kwa ajili ya Ummah wa Muhammad, na bado kuna myengine ambayo
hayakuhesabiwa.’(Tarikh Imam Bukhari, Durr al Manthur na katika Al Itiqan Fi Ulumu
Ul Qur’an Imam Al Suyuti, Tafsir Imam Ibn Kathir Maktabah Qurtubah Al Qahira.)
Kwa upande wa Suhayli basi yeye anasema: ‘Inaonekana kua jumla ya idadi ya herufi
MuqataaAt zote zilizorudiwa ndio Urefu wa Mamlaka ya Ummah huu.’
Ama kwa upande wa Imam Abu Al Khayr Shams Al Din Muhammad Ibn Muhammad
Ibn Muhammad Ibn Ali Ibn Yusuf Al Jazari Al Shafii basi yeye anasema katika ushairi
wake wa Al I’lm Hukm Al Qiraat kua:
والبیت ھو أبیاتھا قاف وزاي في العدد....من یحسن التجوید یظفر بالرشد
وقاف في العدد = 100 و زاي = 7
آي عدد الآبیات 107 بیت والله أعلم
‘Na Nyumba yake ni Nyumba za Qaf na Zay katika Idadi..Na anaekiboresha kisomo
chake cha Tajwid kwa kutumia muongozo wa Jaffar,
Na Qaf kiidadi ni 100 na Zay 7 hivyo idadi ya nyumba yake ni 107.
Na Allah ni mwenye kujua zaid (Mandhumat Al Muqaddimat, Imam Ibn Al Jazari)
Vile vile tunapoangalia miongoni mwa Wanazuoni katika kuitafsiri Surat Ar Rum basi
anasema Imam Abu Shamah Shihab Ad Din Abd Rahman Ibn Ismail Ibn Ibrahim Ibn
Uthman Ibn Abi Baqr Ibn Ibrahim Ibn Muhammad Al Maqdisi kua: Alisema Imam Abu
Al Hakam Abd Salam Ibn Abd Al Rahman Ibn Mohammad Ibn Barrajan katika
kuitafsiri Surat Ar Rum:
396
﴿ال ۤ م۞ ٱ غُلِبَ تِ ل ُّرو مُ ﴾
ۤ
Alif, Laam, Miim, Ghulibati Alrum (Surat 30:1-2)
Tafsir: Alif Laam Miim; Warumi wameshindwa.
Kua: ‘Jerusalem itakua chini ya Mamlaka ya Utawala wa Roman Empire hadi
katika mwaka 583 Al Hijr kwani katika mwaka huo ndio watakaposhindwa na
kupinduliwa. Na Jerusalem itakua chini ya Mikono ya Uislam hadi mwisho wa
Dunia. Na hii ni kulingana na idadi iliyomo ndani aya hii’. Na hivyo ndivyo
ilivyotokea. (Tarikh Al Khulafa, Imam Al Suyuti, Al Itiqan Fi Ulumu Ul Qur’an Imam Al
Suyuti)
Tafakkar! Kwani Imam Ibn Barrajani alichukua idadi ya neno Ghulibat yaani
watashindwa ambalo kiidadi ni 1432 na hivyo wenye kushindwa hua ni wenye kula
hasara hivyo akatoa neno Al Rum ambalo kiidadi ni 277, hivyo akapata jawabu ya 1155
kisha akajumlisha na nambari ya Sura ambayo ni 3 na kisha akajumlisha na nambari ya
aya ambayo ni 2 akapata jawabu ya mwaka 1187 Christian Era.
Ingawa hio ni mitizamo mbali mbali pale tunapozungumzia harfu Al MuqattaAat kupitia
katika Ilm ya Ruhaniyya lakini pia kuna mtizamo wa pili nao una ufafanuzi tofauti juu
yake, ufafanuzi huo unawekwa wazi na mfano ufuatao: Katika kipindi cha Utawala wa
Khalifa Al Mutawakkil ambae alikua ni mtawala wa Mamlaka ya Al Abbas, basi
aliandikwa barua na Mtawala wa Rumi ambayo ilikua inasema: ‘Hakika mimi
nimesikia kua katika kitabu cha Dini yenu mna Sura ambayo ina herufi zote
isipokua herufi 7 (Sawaqit al-Fatiha: ث Tha’ (500), ج Jim (3), خ Kha’ (600), ز Zal
’Faف (80)) ndani yake. Na kama Surah hii ikisomwa (900), Dha’ ظ (300), Shinش (7),
basi humpatia Pepo yule aisomae. Hivyo mimi nilikua nataka kujua ni Sura gani
hio na kwa nini herufi hizi hazimo ndani yake’
Suali la barua hii lilimchanganya sana Khalifa Abu Al Faḍhl Jaʽfar ibn Muḥammad Al
Muʽtaṣim Billāh maarufu kama Al Mutawakkil, hivyo ikambidi kumtafuta Imam Ali An
Naqi ambae alikua akiishi katika Ardhi ya mjini Samara. Imam Ali An Naqi alipoulizwa
juu ya suali hilo basi akajibu: ‘Sura hio ni Surat Al Fatiha, na herufi hizo hazimo
ndani yake kwa sababu kila moja kati ya Sawaqit hizo zinawakilisha maneno yenye
maana maangamizo katika kauli ya Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Khalifa al Mutawakkil akamuuliza Imam Ali An Naqi juu ya herufi 7 za Sawaqit, ambapo
Imam Ali An Naqi nae akajibu: ‘Herufi ya kwanza ni herufi Thaث ambayo
397
inawakilisha maangamizo yaani Thubur, herufi ya pili ni ج Jim ambayo
inawakilisha Moto wa Jahannam yaani Jahim. Herufi ya tatu ni خ Kha ambayo
inawakilisha Ubaya yaani Khubth au Hasara yaani Khusr. Herufi ya nne ni ز Zal
ambayo inawakilisha Zaqqum ambao ni mti wa Motoni ambao Matunda yake ni
yenye sumu na machungu yasiyokua na mfano wake. Herufi ya tano ni ش Shin
ambayo inawakilisha Shaqawa. Herufi ya sita ni ظ Dhal ambayo inawakilisha
Dhulma na herufi ya saba ni ف Fe ambayo inawakilisha Afat yaani Mitihani na
maangamizo kwa ujumla.’
Kwa upande wa wataalamu wa Lugha wanasema kua kila herufi ya Kiarabu hua ina
maana pekee inayojitegemea kwa mfano: Herufi Alif inapokua peke yake inatumika
kuuliza Suali, herufi Mim inawakilisha kuuliza juu ya kitu au Mtu na pia humaanisha
wingi katika kiwakilishi, Herufi Lam huwakilisha Kukataa, n.k hivyo basi kulingana na
mtizamo huo hua tunaona kua Neno Alif Lam Mim hua linamaanisha hali ya Mahojiano,
Kupinga au Kuuliza masuali, yaani kupinga baadhi ya mambo na kuafikiana baina ya
mambo yanayopingana. Sultan Al Mutakallimi Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al
Razi anasema pia kua: ‘Waarabu walikua wakitumia herufi 'ع' kumaanisha Pesa,
herufi 'غ' kumaanisha Mawingu, herufi 'ن' kumaanisha Samaki, n.k’
Katika kuunga mkono maana hizo basi tuangalie mifano ifuatayo ambapo tunapoangalia
moja kati ya mashairi ya Walid Ibn Uqba Ibn Abu Mua’yit basi tunaona kua anasema:
Qultu Laha Qifiy faqalat Qaf.
قلت لھا قفي فقالت قاف
Tafsir: ‘Nilimwambia yeye (Mwanamke): ‘Kaa Kidogo’, nae akajibu: ‘Qaf. Ambapo
herufi ya mwisho ambayo ni Qaf imetumika kuwakilisha neno: Waqaftu ambaloوقفت
maana yake ni Kusimama. Mfano mwengine ni ule wa Imam Abu Abd Allah
Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi ambae anatoa mfano
kwa kusema kua Waarabu hua wanasema:
كف لنا السیف شا
Qafa Lana al Sayf Shin yaani: ‘Unatutosha sisi Upanga kua Sha’ ambapo Herufi Shin
imetumika kumaanisha neno Shafii. Na wengine hua wanasema kua inamaanisha neno
Shahidan’
Kwa upande wa Imam Abu Talib Al Makki basi yeye anasema kua: ‘Sayyidna Ali Ibn
Abi Talib Karamah Allahu Wajh alikua akiomba dua kwa kwa maneno yasemayo:
‘Ya Kaf, Ha, Ayn, Sad, hakika mimi nakuomba kupitia kwako uninusuru na Dhambi
398
zenye kuangamiza, kuondokewa na Baraka, kuondokewa na mvua, au kuzidiwa na
Maadui zangu. Ya Allah! Tulinde dhidi ya Nafsi zetu.’’ Ambapo harfu Kaf
inawakilisha Jina la Allah Subhanah wa Ta’ala la Al Kafi, Ha ni Al Hadi, Ya ni Al Yaqin,
A’ayn ni Al A’lim na Sad ni Al Ssadiq.
Ama tunapomuangalia Imam Tahir Ibn Ashur katika kuitafsiri Surat Yasin basi amesema
kua neno Ya Sin ambazo ni Harfu mbili za Ye na Sin hua linamaanisha Ya Sayyid yaani
Ewe Bwana (wa Mitume).
Ambapo Imam Hamid Al Din Abu Hasan Ahmad Ibn Abd Allah Al Kirmani basi yeye
anasema kuhusiana na Surat Ta-Ha kua: ‘Ta-Ha maana yake ni Mwezi Mweupe kwani
Harfu Ta ina uzito wa idadi ya 9 na harfu Ha ina thamani ina uzito wa idadi ya 5 na
ukijzijumlisha kwa pamoja unapata 14 kumaanisha mwezi 14 muandamo.’(Al
Gharaib)
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari ambae yeye anatuambia kua: ‘Kila
Kitabu ambacho Allah Subhanah wa Ta’ala alikishusha basi kina mfumo wa siri
ndani yake, na mfumo wa siri wa Qur’an umo katika herufi ambazo ndio ufunguzi
wa Sura husika, kwa sababu Herufi hizo ndizo ni Majina na Sifa zake. Kama
anavyosema Alif Lam Mim (2:1, 3:1, 29:1 na 31:1), au Sad (38:1) au Alif Lam Ra
(10:01, 11:1,) n,k. basi harfu hizi zinapojumuishwa pamoja, zinatoa jina Tukufu la
Allah Subhanah wa Ta’ala. Kwa mfano Alif, Lam, Ra, Ha, Mim na Nun basi hua
tunapata jina la Al Rahman. Ambapo kwa Abda Allah Ibn Abbas na Dahhaq Ibn
Muzahim basi wao wamesema kua Alif Lam Min hua inamaanisha: ‘Mimi ni Allah
na Nnajua’.
Ambapo kwa Upande wa Ali Ibn Abi Talib Karama Allahi Wajh basi yeye anasema kua:
‘Haya ni Majina ambayo, yapo katika hali ya herufi zilizotawanyika. Lakini kama
ikichukuliwa herufi moja kutoka katika kundi kila kwa mpangilio wa kua ni tofauti
na herufi iliyokaribu yake herufi hio, na zikakusanywa pamoja kiidadi basi hua ni
zenye kuunda jina la mwingi wa Rehma. Hivyo kama ikiwa jina hili litajulikana na
kisha likatumiwa katika maombi ya Dua basi litakua ni jina lenye Nguvu sana kiasi
ya kua Dua ya muombaji kwa kupita jina hilo itakua ni yenye kukubaliwa.’’
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari anaendelea kutufafanulia kwa
kutuambia kua: ‘Nimepokea Hadith kutoka kwa Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu
Anhu ambae anasema kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala ameapa kua kitabu chake
hiki, alichomshushia Nabii Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam, ni kitabu
ambacho kipo chini ya uangalizi wake. Hivyo akasema: ‘Alif Lam Mim. Hiki ni
Kitabu..ambapo Alif hua inamanisha Allah, Lam inamaanisha Jibril na Mim hua
inamaanisha Muhammad, hivyo basi hapa inaonesha kua Allah Subhanah wa
399
Ta’ala, amekula kiapo kwa ajili yake yeye mwenyewe, na kwa ajili ya Malaika wake
Jibril, na kwa ajili ya Nabii wake Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam.’’’
Tumalizie kwa kuangalia upande wa Imam Jafar As Sadiq kupitia kwa Sufyan Ath
Thawry ambae anasema kua: ‘Mimi nilimuuliza Imam Jafar As Sadiq: ‘Ya Ibn Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam, jee ni nini maana maneno ya Allah Subhanah wa
Ta’ala katika kusema kwake Alif, Lam, Miim na Alif, Lam, Miim, Saad na Aliif, Lam,
Ra na Aliif, Lam, Miim, Ra na Kaf, Ha, Ya, Ayn, Saad na Ta, Ha na Ta, Siin na Ta,
Siin, Miim na Ya, Siin na Saad na Ha, Miim na Ha, Miim, `Ayn, Siin, Qaaf and Qaaf
na Niin’’
Imam Jafar As Saddiq akajibu: ‘Ama kuhusiana na Alif-Lam-Mim iliyo mwanzoni
mwa Surat Al Baqara basi hua inamaanisha Mimi ni Allah Mfalme na Alif-Lam-
Miim iliyo mwanzoni mwa Surat Al Imran basi hua yenye kumaanisha Mimi ni Allah
Mtukufu na Alif-Lam-Miim-Saad humaanisha Mimi ni Allah Muamuzi wa Kila kitu
na Mkweli. Alif-Lam-Ra hua inamaanisha Mimi ni Allah Mwenye Wingi wa
Usamahevu. Maana ya Alif-Lam-Miim-Ra hua inamanisha Mimi ni Allah Mwenye
Kuhuisha, Mwenye Kufisha, Mwenye Kutoa Rizki. Maana ya Kaf-Ha-Ya-Ayn-Sad
hua ni Mimi Mwenye Kutosheleza, Mwenye Kuongoza, Mwenye Kuhifadhi,
Mwenye Ilm, Mwenye katika Ahadi zake.
Ama kuhusiana na Ta-Ha basi hili ni jina miongoni mwa Majina ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam. Na hua linamaanisha Ewe Mwenye Kuutafuta ukweli
na Kuongoza katika njia ya Ukweli. Hatujakuteremshia Qur'an ili usifanikiwe
katika njia yako, bali tumekuteremshia kwa sababu ya kukuboreshea Hali yako.
Ama juu ya maana ya Ta-Sin basi maana yake hua ni Mimi ndie Mwenye Madai ya
Kutekelezewa na ndie Mwenye Kusikia Kila Kitu. Ama kuhusiana na Ta-Sin-Miim
basi hua inamaanisha Mimi Ndie mwenye Madai, mwenye Kuona Kila Kitu, ndio
wa Mwanzo na Ndie wa Mwisho.
Ama kuhusiana na Yasin basi nalo pia ni jina la Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam na hua linamaanisha Ewe Mwenye Kusikiliza Uteremsho wetu na Qur'an
iliyojaa Hikma, Kwa Hakika wewe ni Mjumbe Wetu Katika Njia Iliyonyooka. Ama
kuhusiana na Saad basi ni Chemchem inayotiririka kutoka chini ya Arshi ya Allah
Subhanah wa Ta'ala na ndio kutokana na maji ya Chemchem hii basi ndio rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam alitilia Udhu wake pale alipopelekewa juu
Mbinguni katika Usiku wa Miraj. Na ndio Chemchem ambayo Malaika Jibril
huenda kujitumbukiza kila siku, kisha hutoka na kujikunuta Maji yote yaliyomo
kwenye mbawa zake. Na hakuna hata tone moja linalopukutika kutokana na maji
hayo kutoka kwenye mbawa zake isipokua Allah Subhanah wa Ta'ala hua ni
mwenye kuumba Malaika ambae hua ni mwenye kumtukuza na kumisfu Allah
Subhanah wa Ta'ala kwa mda wote mpaka siku ya Malipo.
400
Ama kuhusiana na Ha-Mim basi hua inamaanisha Mwenye Kustahiki Kusifiwa na
Kutukuzwa. na Ha-Miim-Ayn-Sin-Qaf basi hua linamaanisha Mstahmilivu,
Mwenye Kulipa Malipo Bora kwa Wafanyao Mema, Mwenye Kujua Kila kitu,
Mwenye Kusikia Kila Kitu, Mwenye Uwezo wa Kila Kitu na mwenye Nguvu Juu ya
Kila kitu. Na Qaf hua inamaanisha Mlima ambao ni wenye Kuizunguka na
Kuifunika Dunia na kupitia katika Mlima huu ndio Allah Subhanah wa Ta'ala
akaitandaza Dunia kwa ajili ya Ibn Adam kuishi ndani yake. Ama Kuhusiana na
Nun basi huu ni Mto wa Peponi ambao Allah Subhanaha wa Ta'ala aliuambia
ujikusanye na uwe mgumu na akatoa Kalamu na Wino kutokana nao, kisha
akaiambia Kalamu hio: 'Andika!' nayo ikaandika kwenye Al Lawh Al Mahfudh kila
kitu kilichotokea na kitakachotokea hadi siku ya Malipo. Na Kalamu hio ni yenye
Nuru ya Allah Subhnaha wa Ta'ala na Lawh ni yenye Nuru ya Allah Subhanah wa
Ta'ala.'
Sufyan Ath Thawry akamwambia Imam Jafar As Sadiq: 'Ewe Ibn Rasul Allah! Hebu
Nielezee juu kikamilifu juu ya Amri ya Lawh na Kalamu na Wino wake na
nifundishe kile ambacho Allah Subhanah wa Ta'ala amekufundisha.' Imam Jafar
As Sadiq akasema: 'Ewe Ath Thawry, kwa hakika kama wewe usingekua mtu
anaestahiki kujibiwa basi mimi nisingekujibu. Hivyo fahamu kua Nun ni Malaika
anaeielekeza Kalamu, na Kalamu ni Malaika anaeielekeza Al Lawh, na Al Lawh ni
Malaika anaemuelekeza Malaika Israfil na Israfil anamuelekeza Mikail na Mikail
anamuelekeza Jibril na Jibril anawaelekeza Mitume wote Sala na Salamu ziwe Juu
yao' Sufyan Ath Thawry anasema kua, kisha Imam Jafar As Sadiq akaniambia:
'Haya nenda zako ewe Ath Thawry kwani hakuna kizingiti juu yako kutokana na
Ilm niliyokuachia kwako'’
Tunaporudi kwa Sultan Al Mutakallimi Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi
Al Shafii, na pia Imam Abu Jafar Muhammad Ibn Jarir at Tabari Al Shafii basi tunaona
kua wanasema pia kua: 'Harfu MuqataA'at zilikua pia ni zenye umuhimu wa kutaka
kuwaonesha Makafiri wa Mji wa Makkah utofauti na maajabu ya Qur'an na hivyo
iwavutie, kwani wao walikua ni wenye kuapa kua kamwe hawatosikiliza Qur'an.
Hivyo basi Maajabu ya Harfu hizi yaliwafanya wawe na hamu ya kutaka kujua
kuhusiana na Qur'an ambayo tayari walikua hawako tayari kuisikiliza.'
Na ndio maana pia akasema Sultan Al Balagha Imam Abu Al Qasim Al Zamakhshari na
Imam Nasir Ad Din Al Baydawi kua: 'Malengo ya Harfu MuqataA'at ni kuwawekea
wazi Makafiri kua Qur'an ina herufi ambazo na wao pia hua ni wenye kuzitumia
katika Lugha yao lakini hata hivyo wakawa ni wenye kushindwa kutoa mithili ya
sura moja tu ambayo itafanana na japo moja kati ya Sura 114 za zilizomo ndani ya
Qur'an'
401
Hivyo kwa njia moja au nyengine basi hua haishangazi kwanini Wanazuoni wakawa
wana mitizamo tofuati juu ya herufi hizi kwa sababu Qur'an tukufu ina aya Mutashabihat
ambazo hua ni zenye maana nyingi ndani yake na hii hua ni yenye kuweka wazi Ukubwa
usiokua na mwisho wa I'lm ya alieteremsha Qur'an ambae ni Allah Subhanah wa Ta'ala.
Hivyo basi ni jambo la kawaida kwa Harfu Muqata'Aat kua ni zenye siri ndani yake na
pia kua na maana tofauti kulingana na mitizamo wa Wanazuoni tofauti juu yake.
Hivyo kabla ya kuingia katika Surat Maryam basi na tuangalie maana ya Biismi Allahi
Al Rahmani Al Rahim:
MAANA NA FAIDA YA BIISMI ALLAHI ALRRAHMANI ALRRAHIM
﴿بِسْمِ اهلل َِّ الر َّحمَْنِ
الر َّحِ يمِ﴾
Biismi Allahi AlRahmani AlRahiim.
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma Mwingi wa Huruma.
Hii ni aya ya mwanzo ya Qur’an na pia ni Utangulizi na Ufunguzi wa kila kitu
kinachofanywa na kila Mtu aliemuamini Allah Subhanah wa Ta’ala. Anasema Mujaddid
Ad Din Sultan Al Mutakallimin Imam Al Mushakikin Shaykh ul Islami Imam Fakhr Ad
Din Al Razi kuhusiana na ayah hii kua: ‘Harfu Ba iliyopo mwanzoni mwa ayah hii hua
inamaanisha Ilsaq (kiunganishi) ‘Kwa’ ambacho kinaunganisha uanzaji wa kitendo
na jina la Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Neno Allah kwa lugha ya Kiarabu hua ni lenye kumaanisha Jina Tukufu ambalo ni la
Muumba wa Kila kitu, kilichomo kwenye Ulimwengu unaoonekana na usioonekana,
ambae ni Mmiliki wa kila kitu Mbinguni na Ardhini, ambae ndie mmiliki wa Sifa nzuri
zote na Majina Matukufu yote. Hivyo Majina yote Matukufu ya Allah Subhanah wa
Ta’ala na sifa zake Tukufu ambazo kwa ufahamu wa Ibn Adam hua haziwezi
kufafanulika kikamilifu na ipasavyo kama inavyobidi kuelezewa zilizotajwa ndani ya
Qur’an ni yenye kuweka wazi maana ya jina la Allah Subhanah wa Ta’ala kulingana na
Ufahamu wa Ibn Adam.
Anasema Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din, Zuhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani
Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al
Shafii kua: 'Allah ni Jina la yule ambae yupo hai, ambae ni mwenye sifa za kua ni
402
Muumba na Mlezi juu ya kila kitu alichokiumba. Yeye ni mwenye upekee pale
tunapozungumzia usahihi wa kuwepo kwake, na bila ya shaka hakuka kitu
chengine chochote kile kilichokuwepo ambacho kinaweza kupewa sifa stahiki ya
kuwepo kwake kitu hicho kutokana na utukufu wa kuwepo kwake. Kwani kile
ambacho inabidi kiwepo kulingana na sifa ya kutoweka kwake, kwani kila
kinachokuwepo basi lazima kitoweke. Iipokua kuwepo kwake Allah Subhanah wa
Ta'ala.'
Inabidi ujue kua Jina hili ‘Allah’ ni Jina Kubwa na Tukufu kuliko yote katika ya
Majina 99 ya Allah Subhanah wa Ta'ala, kwa sababu jina hili ndilo linalojumuisha
sifa zote za Allah Subhanah wa Ta'ala. Kwani kila jina lake moja hua na maana
moja, kama Alimu, Qawiyum, Qayyum n.k lakini jina hili la 'Allah' ni jina maalum
la Allah Subhanah wa Ta'ala. Hakuna mwenye kutumia jina la Allah isipokua Allah
mwenyewe. Iwe kwa njia ya moja kwa moja au kwa njia nyengine, wakati majina
mengine kama Al Qadir, Al Alim, ArRahman n,k yanaweza kutumika kwa njia
nyengine. Lakini jina la Allah halitumiki kwa yeyote yule isipokua yeye na ndio
maana likawa ndio jina Tukufu kuliko yote.'
Imam Jamal Islam Abu Qasim Abd Al Karim Ibn Hawazin Al Qushayri basi anasema
kua: 'Kilugha harfu Ba katika Neno Biismi Allahi hua kinawakilisha kiunganishi
yaani Bi-llah humaanisha Kupitia kwa Allah Subhanah wa Ta'ala. Ambapo mambo
mapya hua ni yenye kubainishika na kupitia kwake yeye basi viumbe vilivyoumbwa
huwepo. Na hua kamwe hamna katika viumbe vipya vilivyoumbwa (hadith
makhluq) au mshikamano wa matukio yanayotokea sambamba (Hasl Mansuq), au
kutokana na kitu kinachoonekana au kinacho hisika kihisia kwa athari zake, n.k.
Au kitu chochote kutokana na jiwe au udongo au majani au miti au alama
zinazobakia ardhini (Rasm) au mabaki yaliyosimama (Talal) au hukmu yeyote au
sababu ambayo inayoonekana kuwepo kwake.
Ambapo hua haviwezi kuwepo isipokua kwa kuwepo mwenye Hakika ya kuwepo.
Na Hakika hio hua ni katika Mamlaka yake. Ambayo Mwanzo wake hua ni kutoka
kwake na Mwisho wake hua ni kurudi kwake. Kupitia kwake yeye basi yule
anaetangazia Tawhid Allah basi hua ni mwenye kupata na anaepinga hua ni
mwenye kukosa Iman. Kupitia kwake yeye basi yule anaekubali hua ni mwenye
kujua na kupitia kwake basi yule mwenye kuasi hua ni asiejua na kubakia nyuma.
Allah Subhanah wa Ta’ala amesema ‘Biismi Allahi’ hakusema ‘Bi Allahi’. Na
kulingana na mitizamo ya baadhi ya watu basi husema kua hii ni njia yakutafuta
Baraka kupitia katika kumtaja jina lake. Na kulingana na wengine basi basi hua ni
kutokana na tofauti ya maneno haya ‘Biismi Allahi’ na Kiapo ‘Bi Allahi’. Na
kulingana na baadhi ya Wanazuoni basi pia tunaona kua wanasema kua ni kwa
sababu ya ‘Ism’ jina basi ndio kitu hua ni chenye kinaitwa ‘Musamma’.
403
Ama kulingana na mtizamo wa watu wenye Ilm ya Ruhaniyyat ya Kiroho ya ‘Irfan’
basi ili kupata usafi wa Moyo kutokana na mshikamano na kuikomboa Nafsi
kutokana na vikwazo ili neno ‘Allah’ lipate kuingia ndani ya moyo uliokua msafi na
nafsi iliyosafika.
Baada ya kuitaja ayah hii, basi baadhi ya watu hua wanakumbushwa kutokana na
harfu ‘Ba’ ambayo ni yenye kutokana na Wema au Ukarimu (Birr) na Mawalii
wake na harfu ‘Sin’ ni kutokana na Siri ‘Sirr’ baina yake na wale aliowachagua na
kutokana na harfu ‘Mim’ kutokana na neno Rehma zake ‘Manna’ kwa waja wake
wenye Uwalii (Ahl Al Walaya). Ambao hua wanajua kua kutokana na Rehma zake
basi hua wenye kujua Siri zake, na kutokana na Rehma zake juu yao hua ni wenye
kutekeleza maamrisho yake, na kutokana nae Allah Subhanah wa Ta’ala basi hua
ni wenye kujua uwezo wake.
Na kwa upande mwengine basi kuna wasemao kua: kutokana na kusikia Biismi
Allahi hua ni wenye kukumbushwa kutokana na harfu ‘Ba’ inayotokana na neno
Wema au Ukarimu (Baraa) ya Allah Subhanah wa Ta’ala na harfu ‘Sin’ kutokana
na neno Salama na kutokua na kasoro na harfu ‘Mim’ inayotokana na neno
Utukufu wake Mkubwa (Majid) katika Utukufu wa kuelezewa kwake. Wengine hua
ni wenye kukumbushwa kutokana na harfu ‘Ba’ kutokana na Uzuri wake wenye
Upekee (Baha) na harfu ‘Sin’ kutokana na neno Kung’ara kwa Nuru yake (Sana),
na harfu ‘Mim’ kutokana na Mamlaka yake ‘Mulk’.
Ama kwa upande wa Imam Abd Razak Al Kashani basi yeye anasema kua: ‘Kupitia
katika kutojidhihirisha, basi yule alie na hali ya Al Wahid (Upekee) basi hujionesha
kupitia katika hali ya Al Wahidiyyah (Umoja). Hivyo hapa hali ya Al Ayan Al
Thabitah (Utibitisho) ambayo hua ni utambulisho kwa Ulimwengu kujionesha
katika hali hii. Uthibitisho huu huendelea kujionesha katika sifa za kiumbaji.
Kutokana na kutokea na hali hio ya kujionesha basi, hali hio ya Al Tajalli Al
Shuhudiyy (kujidhihirisha wazi na kushuhudiwa) hupelekea kutokea maumbile ya
jina yaani Asmaiyyah.
Katika hali kama hii basi jina na sifa za Muumba hua ni zenye kuonekana wazi.
Hivyo basi jina hili la Allah hua ni jina ambalo huonesha sifa za Muumba, na jina
lake tukufu la Allah hua linaitwa Al Asm al Adhim. Kwa hivyo jina hili la Allah hua
ni jina la mwanzo katika majina yake yote, na hivyo hivyo ndivyo hali inavyokua
kwa sifa zake zote tukufu, kwani jina la Allah linajumuisha majina yake yote
Matukufu na sifa zake zote tukufu.
Jina la Allah hua linayaunganisha pamoja majina yake yote matukufu na sifa zake
zote tukufu, na hivyo Hadhrat Ilahiyyah (hudhihirisha sifa ya Uumbaji) hua inakua
inakaa juu ya Majina yake yote Matukufu
404
Ama kwa upande wa Shaykh Al Akbar Imam Ibn Arabi basi yeye anasema kua: ‘Jina la
Allah hua linawakilisha hali ya kuwepo kwake Muumbaji kupitia katika njia ya
Hikma na Busara, kwa mfano: Jina la Muumba (Al Asm Al Alam) hua linatokana
na vitu vilivyopewa majina. Kwa hivyo basi jina la Muumba hua linaashiria Tanzih
(Kutokuwepo Muingiliano) baina ya muumbaji na viumbe. Na jina la Muumba
hubainisha Ithbat (Uthibitisho) ya maumbile ya Sifa Tukufu. Hata hivyo hali ya yule
aliepo hua hairuhusu kugawanyika kiidadi kwa sababu Muumbaji ni Qiyam al Adad
(Alie mmoja Kiidadi). Majina ya muumbaji hua ni yenye cheo cha kuthibitisha sifa
tukufu, kwa mfano Al Alim (Mwenye kujua juu ya kila kitu), Al Qadir (Mwenye
uwezo wa kukadiria juu ya kila kitu) Al Murid (Mwenye uwezo wa Kutaka kila
kitu), Al Samiu (Mwenye Kusikia kila kitu) Al Basir (Mwenye Kuona Kila kitu),
n.k.’
Anasema Allaamah Abu Bishr Ibn Amr Ibn Uthman Ibn Qanbar Al Basr maarufu kama
Al Sibawayh anasema kua: ‘Herufi Alif na Lam yaani Al ambazo haziwezi
kutenganishwa peke yake mwanzoni mwa jina la Allah basi hua ni Muuganiko wa
Jina hilo na wala halitokani na Neno au Jina lolote. Kwani Jina Allah kamwe
haliwezi kua ni kifupi cha Al-Ilah kama wanavyodhani baadhi ya watu. Hivyo Jina
la Allah ni Jina kamili la Muumba na hivyo halina ushabihiano na Jina jengine
lolote la lugha yeyote. Hivyo basi Jina la Allah halitakiwi kutafsiriwa kwa lugha
yeyote bali linatakiwa kubakia katika hali yake ya asili kama lilivyo yaani Allah!’
Ama kwa upande wa Imam Nasir Ad Din Al Baydawi anasema kua: ‘Muongozo huu
wa kuanza na kila kitu na Biismi Allahi unamfunza Muumini kutafuta Baraka
kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala katika kila jambo lake katika maisha yake.’
Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakallimin Imam Al Mushakiqin Shaykh ul Islami Imam
Al Ghazali Al Thani Imam Fakhr Ad Din Al Razi kuhusiana na ayah hii kua: ‘Biismi
Allahi hua inamfunza Muislam kuomba msaada kwa Allah Subhanah wa Ta’ala
kupitia katika Neema na Baraka zake katika kila kitu chake na hivyo hua ni yenye
kumfanya Muislam kuanza kila kitu chake na Dhikr Allah. Na ndio maana katika
kufanya kila kitu chako basi kuisoma ayah hii hua inapendekezwa na hua na hali
ya Mandub katika Sharia za Fiqh’
Katika kufafanua zaid maana aliyoinisha Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakallimin Imam
Al Mushakiqin Shaykh ul Islami Imam Al Ghazali Al Thani Imam Fakhr Ad Din Al Razi
anaielezea hali ya Biismi Allah kulingana na Sharia za Fiqh na matumizi yake kwa
kusema kua:
1) Biismi Allah hua ni Fardhi: kuitamka pale Muislam anapotaka kuchinja mnyama
kwa ajili ya kula au anaporusha Upinde, Mshale, Risasi wakati wa kuwinda au
anapomuachia Mnyama wa kuwindia katika wakati wa kuwinda.
405
Na pia ni Fardhi kwa Mtizamo wa Madhhab ya Imam Muhammad Idris Al Shafii
kuisoma katika Sala unaposoma Surat Al Fatiha au Mwanzoni mwa Sura nyengine
yeyote isipokua Surat At Tawba ile kwa sababu Biismi Allah hua ni Moja kati ya aya ya
mwanzo katika kila Sura isipokua Surat At Tawba. Na kuisoma kwa Biismi Allahi kwa
Sala za Kutoa Sauti hua ni Wajib kwa kila Sura isipokua Surat At Tawba au unapoanza
katikati ya Sura. Kusoma Biismi Allahi kwa Sauti hua kunaulainisha Moyo wa Msomaji.
Kwani anasema Imam Abu Zakariyyah Sharaf An Nawawi kua: ‘Mtu anaetaka kusoma
basi asome Biismi Allah Rahmani Rahim mwanzoni mwa kila Sura isipokua Surat
Baraa’ah (At Tawba), kwa sababu wengi miongoni mwa Wanazuoni wamesema kua
hii ni aya popote pale itakapoandikwa ndani ya Mus-haf. Na imeandikwa mwanzoni
mwa kila Sura isipokua katika Surat At Tawbah. Hivyo kama atasoma mwanzoni
mwa kila Sura isipokua Surat At Tawba basi hua na uhakika kua amesoma Qur’an
nzima au Sura nzima. Na kama atakua hakusoma Biismi Allah basi atakua
ameiacha sehemu ya Qur’an na hii ni kutokana na mtizamo wa wengi miongoni
mwa Wanazuoni’
2) Biismi Allah hua ni Sunnah kuitamka wakati wa kusoma Surat Al Fatiha katika Sala
kulingana na mtizamo wa Madhab ya Hanafi ambao ni mtizamo wa Imam Abu Hanifa,
Imam Ibn Al Hammam na Imam Al Halabi.
3) Biismi Allah hua si Mustahab wala si Sunnah na wala si Makruh kuitamka katika
wakati wa kusoma Surat Al Fatiha katika Sala kulingana na Mtizamo wa Imam Abu
Yusuf.
4) Biismi Allah hua ni Makruh kuitamka katika wakati kuisoma Surat At Tawba
ambayo haina Biismi Allahi mwanzoni mwake, ila kwa Mtizamo wa Imam Al Ramli basi
hua ni Sunnah kuitamka unapoanza kati kati ya Sura hio ama kwa upande wa Mujaddid
Ad Din Al Hafidh Imam Shihab ad Din Imam Ibn Hajar Al Asqalani basi hua ni Sunnah
kuisoma mwanzoni mwa Surat Tawbah na ni Makruh kuisoma wakati unapoanza kati
kati ya Surat At Tawba.
Na pia hua ni Makruh kuitamka katika wakati wa kufanya mambo ambayo yana shaka
ndani yake kwa mfano kama kuvuta sigara.
5) Biismi Allah hua ni Mubah kuitamka wakati wa kuanza kutembea, kukaa kitako au
kusimama.
6) Biismi Allah hua ni Haram Kuitamka katika wakati wa kufanya mambo ya Haram,
Kuitamka wakati unapokua na Janaba, Unapokua na Hedhi au Nifasi pale unapokua na
nia ya kuisoma aya za Qur’an isipokua haiwi haram pale inapokua unafanya hivyo kwa
sababu yua kutabarruk au kwa ajili ya kufanya Dhikr.
406
Ama kwa upande wa Shaykh Muhammad Al Amin Ash Shanqeeti basi yeye anasema
kua: ‘Wanazuoni wametofautiana juu juu ya Biismi Allahi kua ni aya mwanzoni
mwa kila Sura au ni aya mwanzoni wa Surat Al Fatiha tu au ni aya kamili
inayojitegemea kama aya nyengine ama la.
Ama kulingana na aya isemayo:
﴿إِن َّهُ مِن سُلَيْمَانَ وَإِن َّهُ بِسْمِ ٱهلل َِّ ٱلر َّحمَْٰنِ ٱلر َّحِ يمِ ﴾
Innahu min Sulaymana wa-innahu bismi Allahi alrrahmani alrraheemi(Surat An
Naml 27:30)
Tafsir: Hii ni kutoka kwa Sulayman na hakika inasema Biismi Allahi Rahmani Rahim
Basi bila ya shaka hii ni moja kati ya aya za Qur’an na hii ni kulingana na
makubaliano ya Ijmaa. Ama kuhusiana na Surat Baraat (At Tawbah) Basi Biismi
Allahi sio miongoni mwa aya za Sura hio, lakini kuna kutofautiana kuhusiana na
hayo mambo mengine, kwani baadhi ya Wanazuoni wa Usul wamesema kua Biismi
Allahi si miongoni mwa Aya za Qur’an na baadhi wamesema kua ni miongoni mwa
Aya ya Surat Al Fatiha tu. Na pia wako wanaosema kua Biismi Allahi ni Aya
Mwanzoni mwa kila Sura, na huu ni Mtizamo wa Imam Muhammad Idris Al Shafii.
Baada ya kuangalia mitizamo hio basi tunaona kua kuna umuhimu mkubwa sana kua
unapoanza kufanya kitu chako na kauli ya Biismi Allahi katika kila jambo lako jema na
linaloruhusika Kisharia hua pia ni mwenye kuonesha Shukrani kwa Mola wako kutokana
na kukujaalia Neema zake zisizohesabika kutoka kwake, katika uhai wako hapa
Ulimwenguni na hivyo hua ni mwenye kuukubali uwezo mkubwa wa Mola wako juu ya
kila kitu alichokujaalia, huku yeye akiwa si mhitaji wa kitu chochote kutoka kwako.
Kwa maana hiyo basi Muislam anapokua ni mwenye kuzoea kuanza kufanya jambo kila
jambo lake kwa Biismi Allahi basi hua ni mwenye kujichunga sana, katika mambo yake,
na hivyo hua si mwenye kutaka kuingiza mambo yasiyofaa ndani ya jambo hilo, au
mambo ya haram na hivyo kumharibia jambo lake hilo, kwani kusema Biismi Allahi hua
kunamkumbusha Muislam kua anaanza kufanya jambo ambalo lake hilo ambalo litapita
katika njia za halali na hivyo kupata Baraka na Neema zaidi kutokana na kua limo ndani
ya Maamrisho ya Mola wake na pia kwa kua hua haliendani kinyume na maamrisho ya
Mola wake.
Na ndio maana akasema Al Ghawth Al Adham Al Qutb Muhyi Ad Din Shaykh Abd Al
Qadir Al Jilani kua:
407
‘Biismi Allah hua ni Hazina ya wale Ambao ni wenye kukumbuka.
Biismi Allah hua ni Muhimu sana na ni ulinzi wenye nguvu kwa walio dhaifu.
Biismi Allah hua ni Nuru kwa wenye kupenda na ni furaha kwa wenye kua na hamu.
Biismi Allah hua ni Liwazo kwa maumbile ya Nafsi zetu.
Biismi Allah hua ni Ukombozi wa Miili yetu.
Biismi Allah hua ni Nuru inayong’arisha vifua vyetu.
Biismi Allah hua ni Mfumo wa kanuni unaoendesha kila jambo katika maisha yetu.
Biismi Allah hua ni Taji la kila mwenye kujiamini.
Biismi Allah hua ni Taa ya wenye kufikia malengo yao.
Biismi Allah hua ni Maridhio ya mahitajio ya mwenye kuhitaji.
Biismi Allah hua ni Jina la yule ambae anaempandisha darja mja mmoja na
kumshusha darja Mja mwengine.
Biismi Allah hua ni Jina la yule ambae anaeuhifadhi Moto wa Jahannam kwa ajili
ya kuwachoma maadui zake kama malipo yao na anauhifadhi Uzuri wa Pepo kwa
ajili ya miadi ya Marafiki zake.
Biismi Allah hua ni Jina la Yule ambae yuko peke yake asiekua na Mshirika.
Biismi Allah hua ni Jina la Mwenye kuishai milele bila ya kua na Mwisho.
Biismi Allah hua ni Jina la yule ambae mwenye uwezo wa Upekee bila ya kuhitaji
usaidizi.
Biismi Allah hua ni Dua ambayo hua ni utangulizi wa kila Sura katika Qur’an.’
Naam, tunapoangalia kwa upande wa I’lm Ruhaniyyat basi wanasema Wanazuoni wenye
I’lm hio kua: ‘Kuna Majina 3000 ya Allah Subhanah wa Ta’ala. Ambapo kati ya hayo
basi Majina 1000 ni yenye kujulikana na Malaika pekee, Majina 1000 mengine
pekee yanajulikana na Manabii, Majina 300 yametajwa kwenye Tawrat, Majina
300 yametajwa kwenye Injeel, Majina 300 Yametajwa kwenye Zabur na Majina 99
yametajwa kwenye Qur’an Tukufu. Hivyo Majina yote hua ni 2999. Jina moja
lililobakia linajulikana na Allah Subhanah wa Ta’ala ambae amemjuulisha Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam juu ya Jina hilo na limo katika Biismi Allahi Ar
Rahmani Rahim. Hivyo mwenye kuisoma aya hio basi hua ni sawa na mwenye
kupata malipo ya aliesoma majina hayo 3000’
Baada ya kuangalia maana na matumizi ya Jina la Allah kwa kifupi kulingana na
mitizamo ya wanazuoni mbali mbali basin a tuangalie maana ya jina la pili liliomo katika
Biismi Allahi Rahmani Rahim ambalo ni Rahman na Rahim, ambayo ni majina
yanayotokana na mzizi mmoja wa neno Rahima ambalo hua ni lenye kumaanisha
Kupenda, Kua na Upole, Kua na Huruma, Kua na Ukarimu, kua na Wema, Kua na
Rehema.
Na kama kawaida tunapozungumzia Sifa za Majina Matukufu ya Allah Subhanah wa
Taa’ala kimaana basi hua tunajaribu tu kuelezea kulingana na mtizamo wa ufahamu wa
Ibn Adam, kwani ukweli ni kua kama anavyosema Mujaddid Ad Din Hujjat Ul Islami
408
Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali kua kwa
vyovyote vile tutakavyojaribu kuelezea maana ya Majina Matukufu ya Allah Subhanah
wa Ta’ala basi kamwe hatutoweza kuelezea maana yake kikamilifu kama inavyostahiki,
yaani tuchukulie mfano wa hili neno Rahman ambalo limetumika kwenye aya ifuatayo:
﴿قُلِ ٱدْعُواْ ٱهلل ََّ أَوِ ٱدْعُواْ ٱلر َّحمَْٰنَ أًَّ م َّا تَدْعُواْ فَلَهُ ٱلأَسمَْآءُ ٱلحُْسْنىَٰ ﴾
Quli odAAoo Allaha awi odAAoo alrrahmana ayyan ma tadAAoo falahu al-asmao
alhusna (Surat Al Isra 17:110)
Tafsir: Sema (Ewe Muhammad): Muombe Allah au Muombe Mwingi wa Rehma,
vyovyote vile utakavyomuomba kwani kwake yeye ndiko kwenye Umiliki wa Majina
Matukufu.
Naam, ayah hii ya Surat Al Israa inaweka wazi umuhimu wa kumuomba Allah Subhanah
wa Ta’ala kwa kutumia Majina yake Matukufu ambapo Jina la Al Rahman linamaanisha
Yule ambae ni mwenye Rehma nyingi sana kupita kiasi na hivyo kutokua na mfano wake
katika Rehma zake, kwani yeye si mwenye kua na Rehma pekee tu bali pia hua ni
mwenye kusababisha Rehma zake kuwafikia wale awatakao miongoni mwa waja wake
waliomuamini kama inavyosema aya ifuatayo:
﴿هُوَ ٱل َّذِى يُصَلِّى عَلَيْكُمْ وَمَلاَئِكَتُهُ لِيُخْرِجَكُمْ مِّنَ ٱلظ ُّلُمَاتِ إِلىَ ٱلن ُّورِ وَكَانَ
بِٱلْمُؤْمِنِينَ رَحِ يماً ﴾
Huwa alladhee yusallee AAalaykum wamala-ikatuhu liyukhrijakum mina
aldhdhulumati ila alnnoori wakana bialmu/mineena raheeman (Surat Al Ahzab
33:43)
Tafsir: Ni yeye ambae ndie mwenye kukusalia na Malaika wake, ili akutoe kutoka
katika kiza na kukuingiza katika Nuru. Na ni yeye ambae kwa Waumini ni Mwingi wa
Rehma.
Kulingana na aya hizi basi tunaona kua Ar Rahman maana yake ni mwenye sifa ya kua
na Rehma na Ar Rahim maana yake hua ni kutoa Rehma. Na kulingana na mtizamo wa
Shaykh Al Akbar Imam Muhyidiin Ibn Al Arabi basi yeye anasema kua kuna: ‘Neno Ar
Rahma lina athari mbili ambapo ya kwanza ni Athar bi al Dhat na Athar bi al Sual.
409
Na tunapozungumzia Athar bi al Dhat basi hua tunazungumzia athari inayotokana
na bainisho la Rehma za Allah Subhanah wa Ta’ala kupitia katika sifa za Rehma
hizo. Kwani kimaumbile basi viumbe vyote vilivyopo hua ni vyenye kuanisha sifa
ya kuwepo kwa Rehma zake. Ama kwa mtizamo mwengine basi tunapozungumzia
Athar bi al Sual basi hua tunazungumzia athari ya Rehma ilivyogaiwa kwa viumbe.
Hususan kwa viumbe Ibn Adam ambao wao hua ni wenye kupewa Rehma
kulingana na jithada zao, kwa mfano pale wanapoomba kama inavyosema aya
ifuatayo: ’
﴿إِن َّهُ كَانَ فَرِيقٌ مِّنْ عِبَادِى يَقُولُونَ رَب َّنَآ آمَن َّا فَٱغْفِرْ لَنَا وَٱرْحمَْنَا وَأَنتَ خَيْرُ
ٱلر َّاحمِِينَ ﴾
Innahu kana fareequn min AAibadee yaqooloona rabbana amanna faighfir lana
wairhamna waanta khayru alrrahimeena (Surat Al Muuminun 23:109)
Tafsir: ‘Bila ya shaka walikua ni miongoni mwa Makundi ya Waja wangu ambao
walikua wakisema: ‘Ewe Mola wetu! Hakika sisi tumekuamini, Hivyo tusamehe, na
utuingize katika Rehma zako, kwani kwa hakika wewe ni m-bora wa wenye kua na
Rehma.’
Yaani kutokana na jitihada hizo za kumuomba Mola wao basi Allah Subhanah wa Ta’ala
hua ni mweye kuwaingiza watu hao kwenye Rehma zake, kwani watu hao hua
wanajulikama kama Ahl al Hadhrah yaani watu ambao wameingia kwenye hadhara ya
Mola wao.
Sultan Al Mutakkalimin Mujaddid Ad Din Imam Al Ghazali Al Thani Imam Fakhr Ad
Din Al Razi kua: ‘Katika Biismi Allahi’ kuna harfu 19, ambazo ni sawa na idadi ya
Malaika wa Jahannam ambao ni 19 hivyo kila unaposema Biismi Allahi basi unakua
na matumaini ya kuvuka kizuizi cha adhabu ya kila mmoja kati ya Malaika hao 19
wa Moto.’ (Na huo pia ndio mtizamo wa Mujaddid Ad Din Shaykh ul Islami Al Hafidh
Imam Ibn Hajar Al Asqalani katika kitabu chake Al Majmaa Al Muasisi na pia Imam Abu
Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi katika Ahkam
Al Quran na Mujaddid Ad Din Imam Abd Rahman Al Suyuti katika Al Durr al Mandhur)
Tunaingia katika maana ya Biismi Allahi Ar Rahmani Al Rahim ambapo tunaona kua
Hujjat Al Islami Mujaddid Ad Din Az Zuhruf ad Din Imam Abu Hamid Muhammad Ibn
Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali anasema kua: ‘Katika ayah hii basi tunaona
kua ndani yake mmejumuishwa Ilm yote inayohusiana na Sifa za Majina Matukufu
za Allah Subhanah wa Ta’ala, na Ilm ya Sifa za Ar Rahmani Ar Rahim
410
zimejumuishwa kwani hizi ni Sifa ambazo zimezipita Sifa zote Tukufu Kiuwezo na
Kiilm. Na Sifa mbili hizi hua ni zenye kuleta hali ya hisia nzuri na zinazovutia
tofauti na nyengine ambazo hua zinaamsha Ghadhabu au Khofu.’
Ama kulingana na mtizamo wa Shaykh Al Akbar Imam Ibn Arabi basi tunaona kua yeye
anasema kua: ‘Jina la Al Rahman hua ni Sifa yenye kujumuisha ukubwa kamilifu wa
Hikma zake kuhusiana na Ulimwengu mzima kulingana na mapokezi ya mwanzoni
mwa yule alie wa mwanzo. Al Rahim hua ni Sifa inayojumuisha ukubwa kamilifu
kimaana kwa ajili ya Ibn Adam kuhusiana na Mwishoni mwa yule alie wa mwisho.
Na hii ni kwa sababu wanasema wenye kujua kua: Ya Rahman hua ni kwa ajili ya
Dunia na Akhera na Ya Rahim hua ni kwa ajili ya Akhera. Hii inamaanisha
kuunyanyua Ukamilifu wa Ibn Adam na kuwakirimu kwa hali zote za ki ujumla na
kimahsusi kwa kila mmoja, na ni kudhihirisha Sifa ya Allah.’
Ama kwa upande wa Imam Nasir Ad Din Al Khayr Abd Allah Ibn Umar Al Baydawi
anasema kua: ‘Maneno haya mawili Al Rahmani Al Rahim hua yanathibtisha
thamani ya mubalagha (kutoa maana yenye uzito mkubwa wa kitu) kuhusiana na
Rehma. Kwani sifa ya Al Rahman hua ni yenye kujumuisha jumla ya Rehma za
Allah Subhanah wa Ta’ala kwa kila kitu katika Ulimwengu huu, kwa Waumini na
wasiokua Waumini, kuhusiana na hali ya Maisha, Riziki, Afya, Akili, Ufahamu, n.k.
na Al Rahim hua inajumuisha Sifa za Allah Subhnah wa Ta’ala anaetoa fadhila zake
kwa Waumini, kwa kuwaongoza katika Uongofu, Imani, Kufanya Mema na
kuachana na Maovu katika uhai wa Ulimwenguni, na hapo hapo kuwalipa furaha
ya Milele na mafanikio ya kweli kesho Akhera.’
Ama kwa upande wa Amir ul Muuminin Fi Al Hadith Imam Abdullah Ibn Mubarak basi
yeye anasema kua: ‘Al Rahman maana yake ni yule Mwenye Kujibu kama ikiwa
utamuuomba, na Al Rahim maana yake hua ni yule mwenye Hasira kali usipo
muomba’
Na pia kuna wasemao kua Al Rahman maana yake hua ni kutoa riski kwa Viumbe wake
na Al Rahim ni mwenye Kusamehe Dhambi za Walimuamini. Hivyo basi mtegemee
Allah Subhanah wa Ta’ala katika kutafuta riski yako, na mtegemee yeye katika
kusamehe kasoro zako. Kwani kimaumbile Ibn Adam hua ni mwenye hali tatu zifuatazo:
‘Kwanza ni hali ya kutokuwepo kwa kiumbe kinachohitaji kuwepo. Pili ni hali ya
kuishi kwa kiumbe anaetaka kuwepo Milele na Tatu ni hali ya mtu anaehitaji
Usamehevu katika uhai wa Akhera, hivyo mja hua ni mwenye kumhitaji Mola wake
na Sifa zake katika kutafakkari majina haya ambayo ni: Allah ambae ndie Mwenye
kumjaalia Mja huyo kuwepo kwake, Al Rahman ambae ndie anaetoa Riski kwa ajili
ya Mja wake kuendelea na Uhai wake na Al Rahim ambae ndie mwenye Kusamehe
Kasoro na makosa ya Mja katika siku ya Malipo’
411
Anasema Baddiuzzamman Said Nursi katika Risale Nuri kua: ‘Kauli ya Biismi Allahi
imejaa Baraka ya hazina kiasi ya kua kutokana na kukuunganisha na Allah
Subhanah wa Taa’ala basi hukubadilishia udhaifu wako na umasikini na
kukuingiza katika ukumbi wa Allah Subhanah wa Ta’ala. Hivyo mtu anaeanza
jambo lake na Biismi Allahi basi hua ni mwenye kufanya jambo lake kwa jina la
Mola wake na hivyo hua ni sawa na anaejiunga na Jeshi na kisha akawa ni mwenye
kufanya mambo hayo chini ya ngao ya jina la Taifa husika. Hua si mwenye kua na
khofu na yeyote, kwani hufanya kila jambo lake kwa jina la Shariah husika na hivyo
kua na ngao imara dhidi ya yeyote atakaepingana nae’
Hivyo Jafar Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu alianza kuisoma Surat Maryam kwa
kuanza na Biismi Allahi Al Rahmani Al Rahim akatiririka na aya ya kwanza ya Sura hio
yasemayo Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad.
KAF – HA – YA – A’AYN – SAD
﴿ كهيعص﴾
Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad (Surat Maryam 19:1)
Tafsir: Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad
Kama tunavyoona kua hizi ni Harfu MuqattaaAt, ambapo Kaf ni harufi inayojitegemea,
Ha ni herufi inayojitegemea, Ya ni Herufi inayojitegemea, Aaayn ni herufi
inayojitegemea na Sad ni herufi inayojitegemea.
Ambapo kuna miongoni mwa Wanazuoni wasemao kua herufi hizi tano za Surat Maryam
zinajumuisha miongoni mwa Majina Matukufu ya Allah Subhanah wa Ta’ala (Min Al
Asmaaihi Al Husna). Na ndio maana Nabii Zakarriyah alikua akianza Kuomba dua zake
kwa kutumia herufi hizi tano, na hii ni kwa sababu kila Dua hua ina Siri yake peke yake
ambayo katika kuomba kwake hua ni yeye kumkaribisha Muombaji mbele ya Allah
Subhanah wa Ta’ala na kumfanya kua ni mwenye kukubaliwa maombi yake.
Ambapo Nabii Zakarriyah alikua akianza na Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad kwa sababu Harfu
Kaf inawakilisha Jina tukufu la Allah Subhanah wa Ta’ala ambalo ni Al Kafi yaani
Mwenye Kutosheleza na hii ni kutokana na namna Nabii Zakarriyah alivyokua akijihisi
udhaifu wake mbele ya Mola wake na hivyo kuonesha Unyenyekevu na kudhihirisha kua
412
huna atakaeweza kumtoshelezea mahitaji yake hapa Duniani isipokua Allah Subhanah
wa Ta’ala. Kwani Kaf pia ha inamanisha Hal Idhafa yaani Hali ya kuonesha Udhaifu.
Ambapo kuhusiana na Ha basi yeye ni Al Hadi yaani Muongozaji, ama kuhusiana na Ya
basi ni Yu/wiyi yaani Mwenye Kukaribisha Kimakazi, ama kuhusiana na Al Aaayn basi
ni Al Aalam yaani Ndie Chanzo cha Kila Kitu, ama kuhusiana na Sad basi ni Al Sadiq
yaani Mkweli mwenye kuaminika.
Na hivyo basi unaweza kuanza kusoma Dua yako kwa kusema kwa mfano unapokua na
uzito katika kipato ukaanza Dua yako kwa kusema: ‘Bismi Allahi ‘ar-Rahmani ‘ar-
Raheem, Kaf Ha Ya `Ayn Sad, Ha Mim `Ayn Sin Qaf, Iyyaka na`bud wa iyyaka
nasta`een. Allahu Lateefun bi `ibaadihi yarzuqu man yashaa..’ au unapokua unahitaji
usalama basi unaweza kuanza Dua yako kwa kusema Bismi Allahi ‘ar-Rahmani ‘ar-
Raheem, Bi Haqi Kaf Ha Ya `Ayn Sad, Kifayatuna Ha Mim `Ayn Sin Qaf, Himayatuna
Fasayakfikahumu Allahu wa Huwa Al SamiaAu Aaliimun.
بحق كهيعص كفايتنا ،حم عسق حمايتنا فسيكفيكهم الله وهو السمع العليم
Na pia maneno haya peke yake hua ni ulinzi wa Dua inayojitegemea ambapo unakua
unayasoma mara 313 au mara 11 kwani ‘Bismi Allahi ‘ar-Rahmani ‘ar-Raheem, Bi
Haqi Kaf Ha Ya `Ayn Sad, Kifayatuna Ha Mim `Ayn Sin Qaf, Himayatuna
Fasayakfikahumu Allahu wa Huwa Al SamiaAu Aaliimun.’ Maana yake hua ni ‘Kwa
jina la Allah Mwingi wa Rehma Mwingi wa Huruma kwa haki ya Kaf Ha Ya `Ayn
Sad, Inatutosheleza Ha Mim `Ayn Sin Qaf, Ni Himaya yetu inayotulinda
(Fasayakfikahumu Allahu wa Huwa Al SamiaAu Aaliimun) Allah anakutoshelezeni
nyinyi Dhidi yao kwani kwa hakika yeye ni mwenye kusikia kila kitu na mwenye kujua
kila kitu.
Ambapo maneno yasemayo Fasayakfikahumu Allahu wa Huwa Al SamiaAu Aaliimun
ndio yale yaliyomo kwenye aya ambayo imesema kua:
﴿فَإِنْ آمَنُواْ بمِِثْلِ مَآ آمَنْتُمْ بِهِ فَقَدِ ٱهْتَدَواْ و َّإِن تَوَل َّوْاْ فَإِنم ََّا هُ مْ فىِ شِ قَاقٍ
فَسَيَكْفِيكَهُمُ ٱهلل َُّ وَهُوَ ٱلس َّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ ﴾
413
Fa-in amanoo bimithli ma amantum bihi faqadi ihtadaw wa-in tawallaw fa-innama
hum fee shiqaqin fasayakfeekahumu Allahu wahuwa alssameeAAu alAAaleemu
(Surat Al Baqara 2:137)
Tafsir:Kisha kama wataamini mithili yake kile unachokiamini wewe basi watakua
wamongoka, lakini kama ikiwa watageuka basi watakua ni wanaopinga. Hivyo Allah
atakutosheleza wewe dhidi yao, na kwa hakika yeye ni mwenye kusikia kila kitu na ni
mwenye kujua kila kitu.
Ama kwa upande Amir Ul Muumin Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu basi alikua
akisikika akiwa anaomba Dua kwa kusema: ‘Kaf Ha Ya `Ayn Sad, Ighfirlii’ na kwa
Upande wa Imam Abd Rahman Al-Kalbi, Imam Mujahid Ibn Sulayman na Imam Al
Dahhak Ibn Muzahim basi wanasema kua: ‘Kaf ni yenye kumaanisha Karim, Ha ni Al
Hadi, Ya ni Mwingi wa Rehma Aayn ni Mwenye Kujua na Kuona na Sad ni Mkweli
Muaminifu’.
Na kwa upande mwengine anasema Imam Malik Ibn Dinar kua: ‘Katika Safari Moja
Mimi nilikua nikienda kwenye Ibada ya Hija, ambapo njiani nikakutana na mtu
ambae alikua hana Kipando wala Mzigo wowote. Nami nikamsalimia, kwa
kumwambia ‘Asalaam Alaykum wa Rahmat Allahi wa Barakatuh!’ nae akanijibu wa
kusema ‘Wa Alaykum Salam wa Rahmat Allahi wa Barakatuh!’’
Nami nikamuuliza: ‘Unatokea Wapi?’ nae akanijibu: ‘Kwa kinakotoka kila kitu’
nami nikamwambia: ‘Na Unaelekea Wapi?’ akanijibu kwa kusema: ‘Kwenye
Nyumba yake.’ Nikamuuliza: ‘Na jee iko wapi mzigo yako?’ nae akasema: ‘Kiko
Kwake kila kitu Changu’ hivyo nikamwambia kua: ‘Safari ni ndefu kama huna
chakula wala maji, jee unakitu chochote kile’ nae akasema: ‘Naam, nilipoanza
safari yangu nilichukuwa herufi tano’. Nami nikamuuliza: ‘Herufi gani hizo?’
Nae akasema: ‘Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad’ nami nikamuuliza : ‘Jee ni nini maana ya
Kaf?’ nae akajibu: ‘Kaf ni kua Yeye ni Al Kafi, yaani ni Mwenye Kutosheleza, ama
kuhusiana na Ha basi yeye ni Al Hadi yaani Muongozaji, ama kuhusiana na Ya basi
yeye ni Yu/wiyi yaani Mwenye Kukaribisha Kimakazi, ama kuhusiana na Aaayn
basi ni Al Aalam yaani Ndie Chanzo cha Kila Kitu, ama kuhusiana na Sad basi ni
Al Sadiq yaani yeye ni Mkweli.
Na hivyo yeyote yule ambae kufuatana na Mwenye Kutosheleza, Mwenye
Kuongoza, Mwenye Kukaribisha Kimakazi ambae ndie Chanzo cha Kila kitu na
ndie Mkweli basi hua si mwenye Kutokinai, hua si mwenye Kupotea njia, hua si
mwenye woga, na hua si mwenye kuhitaji chochote kua kama akiba katika Safari
yake’
414
Kisha Mtu huyo ulipoingia Usiku Akavua kanzu yake kwa ajili ya kujifunikia mwili
wake kabla ya kulala kwake, kisha akasema: ‘Dunia Uhalali wake ni katika
kuhesabiwa kwake yaliyofanyika ndani yake na Uharamu wake ni Katika Kulipwa
Malipo yake Kesho Akhera.’(Yaani ili kuishi Duniani basi inabidi uhesabiwe
uliyoyafanya ndani yake, na huwezi kulipwa uliyoyafanya ndani yake mpaka kwanza
uharamishiwe kuishi ndani yake kwa kufikwa na Mauti ili utoke Ulimwenguni uingie
Akhera.)
Na kisha mtu huyo akanyanyua Kichwa na Mikono juu na kusema: ‘Ewe
Usienufaika na Utiifu wa Waja juu yako, na wala usiedhurika na Uasi wa Waja juu
yako, Nijaalie mimi kua na kile ambacho Hakikunufaishi Na niepushe na Kile
Usichodhurika Nacho.’
Na tulipoingia kwenye Ihram na watu kuanza kuitikia: ‘Labbaika Allahuma
Labbaik, Labbaika La Sharka Laka Labbaik, Inna Alhamd Wa Niaamata Laka Wa
Mulk, Lasharika Laka Labbaik’ sikumuona kua yeye ni miongoni mwa Wenye
kuitikia. Hivyo nikamauuliza, vipi Mbona umekaa Kimya?
Nae akasema: Ewe Shaykh Hakika mimi nna khofu kua Huenda mimi nikaitikia
halafu yeye akaniambia: ‘La, Hakika mimi sitokuridhia, sitokusikia na wala
sitokuangalia’ kisha Mtu huyo akaondoka na sikumuona tena, katika macho yangu
hadi pale tulipofika katika maeneo ya Minna ambapo nilimuona akiwa analia sana
na kusema:
‘Ewe Kipenzi ulieridhika na Damu yangu, hakika Damu yangu ni halali juu yako.
Wa Allahi kama Roho yangu ingemjua yule nnaempenda zaidi yake, basi ingekaa
juu ya kichwa chake badala ya kwenye miguu yake.
Ewe Mama Yangu usinilaumu kwa mapenzi yangu juu yake, kwani usingelaumu
kama ungeujua uzuri wake.
Hakika watu wanaizunguka Al Kaabah bila ya ufahamu, lakini ya laiti kama
wangekua wanaizunguka kwa ufaham juu ya Mola wao basi wangehalalishiwa
Utukufu wao.
Ya Allah hakika watu wanafanya Hija, lakini mimi nna Hija ndani ya Makazi yangu
na hivyo naitolea Kafara Nafsi yangu na Damu yangu kwa ajili yako.
Ya Allah hakika watu wamechinja na kutafuta ukaribu nawe kwa kutoa Sadaka
kwa ajili ya kua ni zawadi kwako, lakini mimi sina chochote cha kutoa kwa
415
kunikaribisha karibu yako, isipokua hii Roho yangu ambayo ipo kwa ajili yako,
hivyo nakuomba nipokelee mimi kwa ajili yangu kwani tayari nimeiwaklisha mbele
yako.
Kisha akanyanyua juu Macho yake huku akiwa analia na kububujikwa na machozi
mengi sana, kisha ghafla akaanguka chini na kutulia tulii kwani alikua amekutana
na Malakat al Mauti.
Ambapo katika usiku wa siku hio, wakati nikiwa namfikiria yeye basi nilipolala
nikamuona usingizini, na nikamuuliza: ‘Vipi imekuaje?’ nae akasema: ‘Allah
amenijaaalia mimi kua ni sawa na Mashahidi wa Vita vya Badr na pia akaniongezea
Daraja’ nami nikamuuliza: ‘Kwanini akakuongezea Darja?’ nae akasema: ‘Kwa
sababu Mashahidi wa Badr wao waliuliwa kwa Mapanga ya Maadui zao, wakati
mimi nimeuawa kutokana na Mapenzi ya Mola wangu juu yake’
Na pia kuna mtizamo mwengine ambao ni ule unayoifafanua aya hii:
﴿ كهیعص﴾
Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad (Surat Maryam 19:1)
Tafsir: Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad
Kua Harfu Kaf hua inamanisha kua Allah Subhanah wa Ta’ala ni Al Kafi yaani ni
mwenye Kutosheleza kwa Mja wake ambapo hapa katika Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad basi
Mja aliejumuishwa ndani ya siri yake kimaaana maneno haya hua ni Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kama vile alivyosema katika Qur’an pale alipohoji kwa
kutumia neno Bikafin katika aya ifuatayo:
﴿أَلَيْسَ ٱهلل َُّ بِكَ افٍ عَبْدَ هُ وَيخَُوِّفُونَكَ بِٱل َّذِينَ مِن دُونِهِ وَمَن يُضْلِ لِ ٱهلل َُّ فَمَا لَهُ
مِنْ هَادٍ ﴾
Alaysa Allahu bikafin AAabdahu wayukhawwifoonaka bialladheena min doonihi
waman yudhlili Allahu fama lahu min hadin (Surat Az Zumar 39:36)
416
Tafsir: Hivi Jee Allah si mwenye Kutosheleza kwa Mja wake (Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam)? Lakini wao hua wanajaribu kuwatisha wale ambao
wanamshirikisha! Na anaepotoshwa na Allah basi hakuna wa kumuongoza.
Ambapo harfu Ha hua inamaanisha Hidaya yaani Muongozo kama vile alivyosema
katika aya ifuatayo:
﴿لِّيَغْفِرَ لَكَ ٱهلل َُّ مَا تَقَد َّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا أتََخ َّرَ وَيُتِم َّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَيَهْدِيَ كَ
صِرَاطاً م ُّسْتَقِيماً ﴾
Liyaghfira laka Allahu ma taqaddama min dhanbika wama taakhkhara
wayutimma niAAmatahu AAalayka wayahdiyaka siratan mustaqeeman (Surat Fath
48:2)
Tafsir: Amekusamehe (Wewe Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam)Allah katika
yaliyopita Katika Dhambi zako na yatakayokuja, na amekamiisha Neema yake juu
yako na amekuongoza katika njia iliyonyooka.
Ambapo neno Ya hua linaamanisha Yada yaani Mkono, Kuunga Mkono au Kutoa Mkono
katika kusaidi kitu au Jambo kama ilivyosema aya ifuatayo;
﴿وَٱذْكُرُو ۤ اْ إِذْ أَنتُمْ قَلِيلٌ م ُّسْتَضْعَفُونَ فىِ ٱلأَرْضِ تخََافُونَ أَني َ تَخَ ط َّفَ كُ مُ ٱلن َّاسُ
فَآوَاكُمْ وَأَي َّدَكُم بِنَصْرِهِ وَرَزَقَكُمْ مِّنَ ٱلط َّيِّبَاتِ لَعَل َّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴾
Waodhkuroo idh antum qaleelun mustadhAAafoona fee al-ardhi takhafoona an
yatakhattafakumu alnnasu faawakum waayyadakum binasrihi warazaqakum mina
alttayyibati laAAallakum tashkuroona (Surat Al Anfal 8:26)
Tafsir: Na kumbuka wakati mlipokua kidogo na mkichukuliwa kua ni dhaifu katika
Ardhi, na ulikua ukiogopa kua labda kuna watu watakuteka Nyara. Lakini yeye
akakupa (Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam) Makazi (Kwa kukuhamishia katika
Mji wa Madinah kutoka Makkah) na kukusaidia kwa nusura yake na akakuruzukuni
vizuri na vya halali ili mpate kushukuru.
417
Ambapo neno Harfu Ayn inamaanisha Aadha yaani Kukinga au Kuhifadhi kama
ilivyosema katika aya ifuatayo:
﴿يَۤ أَي ُّهَا ٱلر َّسُولُ بَلِّغْ مَآ أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن ر َّبِّكَ وَإِن لم َّْ تَفْعَلْ فَمَا بَل َّغْتَ رِسَالَ تَهُ وَٱهلل َُّ
يَعْصِمُكَ مِنَ ٱلن َّاسِ إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يَهْدِى ٱلْقَوْمَ ٱلْ ا َك فِرِي نَ ﴾
Ya ayyuha alrrasoolu balligh ma onzila ilayka min rabbika wa-in lam tafAAal fama
ballaghta risalatahu waAllahu yaAAsimuka mina alnnasi inna Allaha la yahdee
alqawma alkafireena (Surat Al Maidah 5:67)
Tafsir: Ewe Mtume (Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) Tangazia (Ujumbe)
ulioshushiwa kutoka kwa Mola wako, Na kwani kama hukufikisha basi utakua
hukufikisha Ujumbe wake. Na Allah atakuhifadhi wewe kutokana na Watu. Kwani
Allah hawaongozi watu wenye kumkufuru.
Na Harfu Sad hua ni yenye kumanisha Salat Ala Nabii kama vile ilivyosema Aya
ifuatayo:
﴿إِن َّ ٱهلل ََّ وَمَلاَئِكَتَهُ يُصَل ُّونَ عَلَى ٱلن َّبىِِّ َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ صَل ُّواْ عَلَيْهِ وَ سَلُِّمو اْ
تَسْلِيماً ﴾
Inna Allaha wamala-ikatahu yusalloona AAala alnnabiyyi ya ayyuha alladheena
amanoo salloo AAalayhi wasallimoo tasleeman(Surat Al Ahzab 33:56)
Tafsir: Hakika Allah (Subhanah wa Ta’ala amemsamehe) na Malaika wake
wanamsalia (Wanamuombea asamehewe) Nabii (Muhammad Salallahu Alayhi wa
Salam) hivyo enyi Mlioamini nanyi msalieni kwa kikamilifu kama inavyotakiwa.
Na hii ni kwa kwa sababu iliyowekwa wazi na aya isemayo:
418
﴿وَإِن تَظَاهَرَا عَلَيْهِ فَإِن َّ اهلل ََّ هُوَ مَوْلاَهُ وَجِ برِْيلُ وَصَالِحُ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمَلاَئِكَةُ بَعْدَ
ذٰلِ كَ ظَهِيرٌ ﴾
Wa-in tadhahara AAalayhi fa-inna Allaha huwa mawlahu wajibreelu wasalihu
almu/mineena waalmala-ikatu baAAda dhalika dhaheerun (Surat At Tahrim 66:4)
Tafsir: Na hata kama mkidhihirisha (katika kushirikiana) pamoja Dhidi yake
(Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) basi kwa hakika Allah ndie Mlinzi wake na
Jibril, na wema Miongoni mwa Waumini na Malaika baada yake wamedhahirisha.
Ambapo neno Mawla lililotumika hapa ni lenye kutokana na neno Waliya ambalo hua
linamaanisha Kua Karibu, Kua na Ukaribu, Fuata au Karibia. Lakini hua linabadilika
maana kulingana na namna lilivyotumika, ambapo kwa namna lilivyotumika hapa katika
hali ya kwanza ambayo ni yenye kuzungumzia Uhusiano baina ya Allah Subhanah wa
Ta’ala na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi hua linamaanisha maana kamilifu
ya kua Allah Subhanah wa Ta’ala ni Msimamizi wa kila kitu juu ya Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam.
Ambapo lilipotumika kwa upande wa uhusiano wa Malaika Jibril na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam basi hua linamanisha Mfikishaji wa Jumbe wa Allah
Subhanah wa Ta’ala, na lilipotumika kwa upande wa uhusiano wa baina ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na Waumini basi hua linamaanisha Wafuasi,
Wanaoshikamana nae kutokana na kile alichoshushiwa na Allah Subhanah wa Ta’ala
kupitia kwa Malaika Jibril, na lilipotumika kuhusiana na uhusiano baina baina ya Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Malaika wengine wa kawaida basi hua linamaanisha
Wanamuombea apate utulivu.
Hivyo Jafar akaendelea kutiririka na Surat Maryam mbele ya An Najash, kuanza kwenye
aya ya kwanza tuliyoifafanua ya Kaf-Ha-Ya-AAayn-Sad hadi kwenye aya 15, ambazo
zinazozungumia kuhusiana na Nabii Zakariyah na Nabii Yayha na Maryam Bint Imran
kama tulivyoona hapo kabla, kisha baada ya hapo akaendelea kusoma aya ambazo na
zenye kuelezea kisa cha kuzaliwa kwa Nabii Isa Ibn Maryam ambazo ndani yake ndio
Allah Subhanah wa Ta’ala anaelezea kuhusiana na kuumbwa na kuzaliwa kwake Nabii
Isa Ibn Maryam.
419
UJUMBE WA NAJRAN, THUMAMAH IBN UTHAL – UTHIBITSHO
WA WASIOKUA WAISLAM KURUHUSIKA KUINGIA MSIKITINI
Mnamo mwezi wa Dhul Hijja wa mwaka wa 10 Al Hijra wa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam, basi alipokea ujumbe wa watu 60 kutoka katika Mji wa Najran ambao walikua
ni Wafuasi wa Dini ya Kikristo. Mji wa Najran ni mji ambao upo kusini ya mji wa
Madinah kwa umbali wa kilomita 730, yaani hapa tunazungumzia maeneo ya karibu na
ardhi ya Yemen.
Ujumbe huu ulipokelewa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kukaribishwa
ndani ya Msikiti wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na wakaruhusiwa kusali
ndani yake ambapo walisali kwa kuelekea Kibla chao katika upande wa Mashariki kama
anavyosema Imam Muhammad Ibn Is-haq kua:
‘Amesema Muhammad Ibn Jafar Ibn Zubayr kua: ‘Ujumbe kutoka Najran ulikuja
kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na akaingia Msikitini baada ya kusali
sala ya Al Asr. Walikua wamefuatana na Msafara wa Ngamia ambao ulikua
unaongozwa na Ukoo wa Bani Al Harith Ibn Kab.
Ambapo Masahaba wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam walipowaona
wakasema kua hawakuwahi kukutana na Msafara kama huo baada yake. Na
ulipofika wakati wa kufanya Ibada yao, basi walisimama ndani ya Masjid Nabawi
na wakapiga kengele yao na kisha kufanya Ibada yao huku Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akiwaambia Masahaba zake kua: ‘Waacheni wafanye Ibada yao.’
Na wakasali huku wakielekea Mashariki’
Na kutokana na Uthibitisho huu basi tunaona kua Wanazuoni wametofautiana kuhusiana
na kuruhusika kwa wasiokua Waislamu kuingia Msikitini na hivyo pia kutokana na
kuruhusika huko basi kunamaanisha kua hata Wanawake wanapokua katika hali ya
kutokua Tohara hua wanaruhusika kuingia Msikitini iwe kwa ajili ya kutekeleza haja
fulani, kuenda kusoma Darsa n.k.
Ambapo pia wenye mtizamo huo hua wanatumia pia uthibitisho wa ile hadith ya Imam
Ibn Hazim ambayo inasema: ‘Amesema Umm Ul Muuminin Aisha Radhi Allahu Anha
kua: ‘Kulikua kuna Mtumwa Mweusi wa Kike wa ambae alikua anamilikwa na
Kabila Moja la Waarabu ambao walimuacha huru, hivyo Mwanamke huyo akaja
hadi kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na akasilimu, na akawa na hema
dogo ndani ya Msikiti’’(Al Muhalla Bi Al Athar)
420
Ambapo kwa upande mwengine basi anasema Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu kua:
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikutana nae katika njiani katika Mji wa
Madinah , wakati akiwa katika hali ya kua na Janaba. Hivyo Abu Hurayrah Radhi
Allahu Anhu akakimbilia kuenda kukoga Janaba. Hivyo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akaona kua Abu Hurayrah hayuko mbele yake kwenye Darsa lake,
na Abu Hurayrah Radhi Allahu Anhu aliporudi basi Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam akamuuliza Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu: ‘Ulikuwepo wapi ewe Abu
Hurayrah?’
Abu Hurayrah Radhi Allahu Anhu akajibu: ‘Ya Rasul Allah! Nilikua niko katika
hali ya kua na Janaba Hivyo sikutaka kukaa pamoja nawe hadi pale nitakapo kua
nimekoga na kujitoharisha.’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema:
‘Subhanah Allah! Muumini hua kamwe hawi Mchafu’’(Sahih Muslim)
Ambapo kuhusiana na ile hadithi isemayo kua: ‘Amesema Aisha Radhi Allahu Anha
kua amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Msikitini hua
hairuhusiki kuingia Mwanamke Mwenye Hedhi au yeyote yule ambae hayuko
tohara’(Sunnan Imam Abu Daud, Sunnan Imam Ibn Majah na Sunnan Imam Abu
Huzaymah)’
Basi kulingana na mtizamo wa baadhi ya Wanazuoni kuhusiana na hadithi hii wanasema
kua ni Hadith dhaif na huo ni mtizamo wa Imam Abu Sulayman Hamd Ibn
Muhammad Al Khattabi katika Maalim Sunnan Sharh Imam Abu Daud, Imam Abu
Zakarriyah Sharaf An Nawawi katika Al Majmua na Imam Ibn Hazim Al Andalus katika
Al Muhalla.
Ambapo kwa upande mwengine basi anasema Shaykh ul Islami Imam Abu Zakkariyah
Sharaf An Nawawi kua: ‘Kwa mtizamo wa Umar Abdul Aziz, Qatadah na Imam
Malik, basi ni kua hairuhusiki kwa Wasiokua Waislam, kuingia Msikitini’ (Sharh
Sahih Muslim)
Na huo pia ndio mtizamo wa Imam Abu Hasan Ali Ibn Muhammad Ibn Habib Al
Mawardi Al Shafii ambae yeye anasema kua kulingana na Mtizamo wa Imam Al Muzani
ambae ni mWanafunzi wa Imam Muhammad Idris Al Shafi basi ni kua: ‘Haikubaliki
kwa Wasiokua Waislam kuingia Msikitini na hii ni kwa sababu watu hawa hua kila
siku wamo katika hali ya kutokua tohara’ (Al-Hawi Al-Kabir)
Na kwa upande wa Imam Mansur Ibn Yunus Al Buhuti Al Hanbali basi yeye anasema
pia kua : ‘Haruhusiki kwa wasiokua Waislam kuingia Miskitini hata kama
wakipewa ruhusa na Waislam na hii ni kwa sababu amesema Allah Subhanah wa
Ta’ala kua:
421
﴿إِنم ََّا يَعْمُرُ مَسَاجِ دَ ٱهلل َِّ مَنْ آمَنَ بِٱهلل َِّ وَٱلْيَوْمِ ٱلآخِ رِ وَأَقَامَ ٱلص َّلاَةَ وَآتَى ٰ ٱلز َّكَواةَ
وَلمَْ يخَْشَ إِلا َّ ٱهلل ََّ فَعَسَ ى ٰ أُوْ لَٰئِكَ أَن يَكُ ونُواْ مِ نَ ٱلْمُ هْ تَدِينَ ﴾
Innama yaAAmuru masajida Allahi man amana biAllahi waalyawmi al-akhiri
waaqama alssalata waata alzzakata walam yakhsha illa Allaha faAAasa ola-ika an
yakoonoo mina almuhtadeena (Surah At Taubah 9:18)
Tafsir: Kwa hakika wenye kuisimamia Misikiti ni wale ambao ni wenye Kumuamini
Allah na siku ya Malipo, Wanaosali na kutoa Zakkah, na wasiomuogopa yeyote
isipokua Allah, kwani hawa hukaribia kua ni miongoni mwa Walioongoka.
Kwa upande mmoja basi tunaona kua ayah hii inazianisha sifa za wale watu ambao
wanatakiwa kusimamia Miskiti na kua ni wenye amri Miskitini, kua wenye kutakiwa kua
ni wenye Kumuamini Allah Subhanah wa Ta’ala na Siku ya Malipo yaani wasiwe
Wanafiq, na kisha ikaendelea kuwataja wale ambao Wanaosali na Kuota Zakkah na
Wasiomuogopa yeyote ispokua Allah Subhanah wa Ta’ala. Kwani hao ndio wenye
kuukaribia Uongofu.
Ambapo tunapojiangalia sisi leo basi tunaona kua tuko katika Mtihani mkubwa sana
kuhusiana na kua na sifa stahiki za usimamizi wa Misikiti, kwani wengi sana
wanaosimamia Miskiti katika jamii zetu wanojita Wenyeviti, Makatibu na Maimamu pia
hawana Sifa hizi stahiki, na hivyo hua ni wenye kuifanya Miskiti kama ya Baba zao, ni
wenye kufanyana uchawi, kuoneana vijicho na kuhasidiana, kutambiana na kuoneshana
kwa ajili ya kupigania Maslahi yao ya Kidunia wanayojitafutia wanapokua viongozi wa
Miskitini.
Tunaporudi katika mada yetu basi hua unaona kua hii ni aya ambayo imetumia neno A’sa
ambalo humaanisha Kukaribia Kitu, Kua na Uwezekano wa kukifikia kitu, Labda,
Inawezekana, Inategemewa na pia humaanisha kuelezea hali ya Mtu ambae ni mwenye
Ari, Juhudi, Mategemeo, Khofu au Matamanio juu ya kitu fulani. Ambapo Imam
Muhammad Ibn Is-haq anasema kua; ‘A’sa inapotoka kwa Allah Subhanah wa T a’ala
basi hua ni Ahadi iliyothibitishwa.’
Na hivyo mtizamo wa kua hairuhusiki kwa Wasiokua Waislam pia ndio Mtizamo
unaokubalika zaid wa Madhhab ya Imam Ahmad Ibn Hanbal kama anavyosema Imam
Muhammad Ibn Abd Al Qawi Al Mardawi Al Hanbali katika kitabu cha Al Kashaf al-
Qina’a.
422
Ambapo kuhusiana na kutoruhusika kwao katika Masjid Al Haram basi Wanazuoni
wanasimamia katika ile aya isemayo:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُو ۤ اْ إِنم ََّا ٱلْمُشْرِكُونَ نجََسٌ فَلاَ يَقْرَبُواْ ٱلْمَسْجِ دَ ٱلحَْرَامَ بَعْدَ عَ امِهِمْ
هَٰذَا وَإِنْ خِ فْتُمْ عَيْلَةً فَسَوْفَ يُغْنِيكُمُ ٱهلل َُّ مِن فَضْلِهِ إِن شَآءَ إِن َّ ٱهلل ََّ عَلِيمٌ حَ كِيمٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo innama almushrikoona najasun fala yaqraboo
almasjida alharama baAAda AAamihim hadha wa-in khiftum AAaylatan fasawfa
yughneekumu Allahu min fadhlihi in shaa inna Allaha AAaleemun hakeemun
(Surah al-Taubah 9:28)
Tafsir: Enyi Mlioamini kwa hakika Washirikina ni wenye Najis hivyo msiwakaribishe
kwenye Masjid Al Haram baada ya mwaka huu. Na kama mnakhofu juu ya Umasikini
basi Allah atakutajirisheni kutokana na fadhila zake akitaka. Kwa hakika Allah ni
mwenye kujua juu ya kla kitu na ni mwingi wa Hikma.
Ambapo aya imetumia neno Najasa ambalo hua linamaanisha Uchafu, Kutokua na usafi,
Kutokua Tohara, Kitu kinachohitajika kusafishwa.
Na anasema Imam Raghib Al Isfahani kua: ‘Ndani yake hua mnajumuishika Uchafu
unaohisika kwa viungo vya hisia kama Macho, Mdomo, Pua Masikio au Mikono.
Na pia ndani yake hua mnajumuishika Uchafu ambao hua unfahamika kwa njia ya
Akili na Ufaham. Hivyo uchafu hua huo wa aina 3 ambazo ni:
Kwanza kuna Najis ya Kweli ambayo kila mtu anaihesabu kua hio kweli ni Najis.
Halafu kuna aina ya pili ya Najis ambayo ni ya Kisharia ambayo inasababisha
ulazima wa kutia Udhu au Kukoga baada ya kuingia kweye hali ya mazingira yake,
kwa mfano: kua na Janaba, Hedhi, Nifasi, Kutokwa na kitu katika tupu mbili n.k.
Na kisha kuna aina tatu ya Najis ambayo ni ya Uchafu wa Kimoyo ambao ndani
yake hua kuna Imani ya Kishirikina au Tabia mbaya. Hivyo hizi zote hua ni Najis’
Na kutokana na maana hii basi tunaona kua pale Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
aliposema kumwambia Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu kua Muumini hkamwe hawezi
kua Mchafu basi alikua akimaanisha kuhusiana na Uchafu wa Kiimani ndani ya Moyo
na Ufahamu. Kwani huo ndio Najis Kubwa zaidi. Ambapo kwa upande wa wasioamini
basi wao hua ni wenye Aina zote tatu za Najis
423
Hivyo kwa mtizamo wa Imam Qatadah Al Sadusi na Amir ul Muuminin Umar Ibn Abd
Al Aziz basi amesema kuhusiana na aya hii kua: ‘Ingawa ya hii imezungumzia
kuhusiana na Masjid Al Haram lakini aya inajumuisha eneo zima la ardhi takatifu
ya Mji wa Makkah.’
Ambapo kwa upande wa Imam Abu Hanifa Nuuman Ibn Thabit basi yeye anasema kua:
‘Makafiri wanaruhusika kuingia katika Miskiti wanayoitaka na si lazima wawe na
sababu Maalum. Na wanaweza kuingia hata katika Masjid Al Haram kama
wakiruhusiwa na Waislam, yaani hii ya inawapa Waislam haki ya kuwazuia na
hapo hapo inawakatalia Makafiri kuingia.’
Ambapo hii hua ni sawa na Mtu kumwambia Mtu mwengine kua: ‘Sitaki kukuona
hapa mbele ya macho yangu’ na hivyo kua ni mwenye kuelezea kutopendezwa
kwake kuwepo kwa mtu huyo mbele yake katika sehemu aliyokuwepo lakini bila ya
kumharamishia mwenzake huyo kuingia katika sehemu hio.
Na kwa upande wa Mujaddid Ad Din Imam Muhammad Idrsis Al Shafii basi yeye
amesema kuhusiana na aya hii kua: ‘Aya hii imekataza Makafiri kutoingia kwenye
Masjid Al Haram, lakini haikuzungumzia juu ya Miskiti myengine yeyote. Na hivyo
hii inamaanisha kua inaruhusika kwa Wakristo na Mayahudi kuingia kwenye
Miskiti myengine lakini kwa sababu maalum’ ambao huu pia ndio Mtizamo wa
wafuasi wa Madhhab ya Imam Malik.
Na Hukmu hii hua ni kutokana na Uthibitisho wa Hadith ya kisa cha Thumamah Ibn
Uthal ambae alikua ni Chifu wa Banu Hanifa ambae alikua ni mmoja kati ya Machifu wa
Ardhi ya Yamamah. Na mnamo mwaka wa 9 Al Hijra Rasul Allah Sallahu Alayhi wa
Salam alituma Barua 8 kwa Viongozi tofauti wa eneo la Uarabuni na mipakani mwake,
ili kuwaelezea kuhusiana na Utume wake na pia kuhusiana na kuukubali Ujumbe huo wa
Allah Subhnah wa Ta’ala ambapo miongoni mwa waliopelekewa Barua hizo alikuwemo
pia Thumamah Ibn Uthal wa Yemen, nae akapingana na ujumbe wa Barua hio, na kisha
akasema kua atamuangamiza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Dini yake hio
mpya ya Uislam anayoitangazia.
Ambapo tunapozungumzia Mji wa Yamamah basi tunaona kua ni Mji ambao watu wake
walikua wakijisifa kutokana na mambo neema walizojaaliwa na Mola wao juu yao wani
walikua wakisema: Hakika sisi tumewapita Watu wa Duniani Mashariki na
Magharibi kwa Mambo Matano:
‘Tumewapita Kwanza kwa kua na Wanawake wazuri kuliko wote Ulimwenguni.
Tumewapita Pili kwa kua na Ngano Bora Zaidi Ulimwenguni.
Tumewapita Tatu kwa kua na Tende Tamu Sana.
424
Tumewapita Nne kwa kua na Wanyama wenye Nyama Tamu sana, na
Tumewapita Tano kwa kua na Maji Matamu na Mazuri sana yanayosafisha Koo
na Kifua.’
Hivyo kutokana na kua na hali ya mtizamo huo juu ya jamii yao basi Thumama Ibn Uthal
akaamua kupinga na kukataa matakwa ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
hivyo ingawa hakuwaua Wajumbe hao ambao ni Masahaba wa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam waliompelekea ujumbe huo hapo hapo lakini alitafuta nafasi nyengine
ya kuwaua Waislam atakapokutana nao na alipopata nafasi mara ya pili ya kukutana na
Msafara wa Masahaba wa Rasul Allah Salallahu Alayhiwa Salam wakati alipokua
anaelekea katika maeneo ya Yamamah basi aliuvamia na kuwaua Masahaba wote. Hivyo
Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam alipopata habari hio basi akatangaza kulipiza
kisasi dhidi yake kua kokote atakapoonekana basi hukumu yake pia kua ni kifo.
Baada ya tukio hilo basi haukupita mda mrefu isipokua Thumamah akaamua kufanya
Umra ya kikafiri katika mji wa Makkah, akafunga safari kutoka Yamamah kwa bahati
mbaya au nzuri katika safari yake akapitia katika maeneo ya Mipaka ya Mji wa Madinah
na akakutana na Jeshi la Waislam lililokua likifanya doria kuilinda mipaka ya Madinah
bila ya kumjua na walipomhoji anafanya nini katika maeneo hayo basi akawa ana kibri
na hataki kujieleza, hivyo nao wakamkamata na kumpeleka katika Mji wa Madinah kwa
Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam.
Na walipofika basi wakamfunga kamba kwenye moja kati ya nguzo za ndani ya Msikiti
wa Nabii Salallahu Alayhi wa Salam huku wakimsubiri Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa
Salam aje kumhoji kisha atoe hukmu yake juu ya mtu huyo wasiemjua na asietaka
kujieleza. Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam alipoaingia Msikitini na kumuona
mtu huyo aliefungwa kwenye Nguzo ya Msikitini basi akawauliza Masahaba zake: ‘Hivi
jee mnamjua ni nani huyu mliemkamata na kumfunga hapa?’ Masahaba wakajibu:
‘La Ya Rasul Allah sisi hatumjui ni nani.’
Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akawaambia Masahaba zake kua: ‘Huyu si
mwengine bali ni Thumamah Ibn Uthal Al-Hanafi, na bila ya shaka mmefanya
jambo zuri sana kumkamata.’ Kisha Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akatoka
Msikitini humo na kuelekea Nyumbani kwake ambayo ni yenye kupakana na Msikiti
wake kiasi ya kua akikaa Chumbani kwake hua ni mwenye kuona Msikitini kwa kupitia
Dirishani mwa chumba chake.
Alipofika nyumbai kwake basi Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akawaambia
watu wake: ‘Tayarisheni chakula chochote mlichokua nacho, kisha mpelekeeni
Thumamah Ibn Uthal’ na kisha akaamrisha Ngamia wake akamuliwe Maziwa, na kisha
akaelekea kwa Thumama kwa ajili ya kuzungumza nae kwa kumtaka asilimu, lakini
425
Thumamah akakataa katu katu. Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akamwambia: ‘Unaiteteaje Nafsi yako?’
Thumamah Ibn Uthal akasema: ‘Kama unataka kuniua basi bila ya shaka utakua
umepata damu yenye thamani kubwa sana ya kuua, kutokana na ulichokamata.
Kama unataka kusamehe basi hakika mimi nitakua na shukrani kutokana na
usamehevu wako. Na kama unataka pesa nikulipe kua ni kama fidya kwako basi
taja kiasi ukitakacho nitakulipa kama utakavyo.’
Baada ya kupata majibu hayo basi Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akaondoka
na kumuacha Thumamah Ibn Uthal akiwa amefungwa hapo hapo kwenye nguzo ya
Msikitini kwa siku 2 mfululizo huku akiwa ni mwenye kupelekewa chakula na Maziwa
kama kawaida. Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuuliza tena kwa
kumwambia: ‘Unaiteteaje Nafsi yako?’
Thumamah Ibn Uthal akasema tena: ‘Kama unataka kuniua basi bila ya shaka utakua
umepata damu yenye thamani kubwa sana ya kuua, kutokana na ulichokamata.
Kama unataka kusamehe basi hakika mimi nitakua na shukrani kutokana na
usamehevu wako. Na kama unataka pesa nikulipe kua ni kama fidya kwako basi
taja kiasi ukitakacho nitakulipa kama utakavyo.’
Baada ya kutoa majibu hayo basi Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akawaambia
Masahaba zake: ‘Mfungueni na kisha muachieni aende zake.’ Hivyo Masahaba
wakamfungua na kumuachia huru Thumamah Ibn Uthal ambae nae akatoka nje ya
Msikiti kisha akapanda Ngamia wake na kuelekea nje ya maeneo ya ardhi ya Madinah .
Lakini alipofika katika maeneo yenye Mitende na Maji ya Baqii, ambayo baadae
ilibadilishwa kua ni sehemu ya kuzikia Masahaba wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, basi Thumamah akashuka kwenye Ngamia wake na kumnywesha maji na kisha
akajisafisha mwili wake kwa kukoga.
Kisha akampandia tena Ngamia wake na kurudi katika Mji wa Madinah mpaka ndani ya
Msikiti wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Masahaba wakashangaa kumuona
kua amerudi na kuulizana imekuaje. Lakini Thumamah Ibn Uthal akasimama mbele yao
na kusema: ‘Ashhadu An La Ilaha Illa Allah, wa ashhadu Ana Muhammad Rasul
Allah’
Na kisha Thumamah Ibn Uthal akatoka hadi kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na kusema: ‘Ewe Muhammad! Wa Allahi, ilikua hakuna Uso unaochukiza mbele ya
macho yangu kama uso wako. Lakini sasa hivi hakuna Uso wa mtu unaonivutia na
nnaoupenda kama uso wako. Hakika mimi nimewaua baadhi ya watu wako, hivyo
niko chini ya Rehma zako. Hivyo jee utanifanya nini?’
426
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Sasa hivi hakuna hatia dhidi yako,
kwani kuingia kwako katika Uislam kumefuta makosa yako yote uliyoyafanya hapo
kabla na hivyo kukupa nafasi ya kuanza upya maisha yako.’
Hivyo Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu akafurahi sana na kusema: ‘Wa Allahi!
Nitajiweka mimi mwenyewe Nafsi yangu, na Upanga wangu na yeyote yule
atakaekua chini yako na chini ya ufuasi wa Dini yako. Hivyo Ya Rasul Allah!
Hakika Wapanda Farasi wako waliponikamata basi nilikua nikielekea kufanya
Umra. Kwa hivyo unanishauri nifanye nini?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hamna tatizo nenda kafanye Umra
yako, lakini fanya kwa njia iliyoamrishwa na Allah Subhanah wa Ta’ala’ na kisha
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamfahamisha Thumamah Radhi Allahu Anhu
namna ya kufanya Umra hio. Kisha baada ya hapo basi Thumamah Radhi Allahu Anhu
akatia nia yake na akafunga safari yake kuelekea katika kufanya Ibada ya Umra katika
njia ya Kiislam kama aliavyoamrishwa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Hivyo alipofika katika Bando la Mji wa Makkah akaanza kusoma Talbiyyah kwa sauti
kubwa sana hukua akisema: ‘Labbayk Allahumma labbayk. Labbayka la shareeka laka
labbayk. Innal hamda wa-n ni'mata laka wa-l mulk La shareeka lak.”
yaani ‘Naitikia, Allah wito wako, Naitikia kua hakuna mshirika dhidi yako. Naitikia
hakika wewe ni mwenye kustahiki shukrani zote na ni mmiliki wa Neema zote na
mmiliki wa Mamlaka juu ya kila kitu hakuna mshirika dhidi yako’
Kutokana na tukio hili basi Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu akawa ndie
Muislam wa Kwanza juu ya uso wa Ardhi kua ni mwenye kufanya Talbiyah huku
akiingia ndani ya mji wa Makkah. Ambapo ukubwa wa sauti ya Thumamah Ibn Uthal
Radhi Allahu Anhu uliwashtua Maquraysh wa Mji wa Makkah, na hivyo kujiuliza
kumetokea nini? Na walipomsikiliza maneno yake basi wakapandwa na hasira kubwa
sana na hivyo kujipanga na kutaka kumpiga anaesoma Talbiyah hio kabla ya kumjua
kutokana na chuki waliyokua nayo watu hao dhidi ya Uislam.
Hivyo ingawa watu wa Makkah walitoka na silaha zao kwa ajili ya kumshambulia mtu
huyo, lakini kutoka kwao huko hakukumshtua wala kumtia khofu Thumamah Ibn Uthal
Radhi Allahu Anhu kwani hali ilikua tofauti badala yake kwa sababu yeye alizidi kungiwa
na ari ufakhari na kuzidi kupaza sauti huku akiwa amejawa na hisia kubwa za mapenzi
juu ya Allah Subhanah wa Ta’ala, Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na dini yake
mpya aliyoiamini na kuingia siku kadha hapo kabla.
Hivyo miongoni mwa vijana wa Quraysh akanyayua Upinde wake akauweka baina ya
mikono yake na kuanza kutunga shabaha kwenye mwili wa Thumamah Ibn Uthal Radhi
Allahu Anhu, lakini hata hivyo miongoni mwa Wakubwa wanaomjua Thumamah Ibn
427
Uthal Radhi Allahu Anhu wakamzuia kijana huyo na kumwambia: ‘Laana iwe juu yako!
Ole wako uuwachie huo upinde wako kisha umpige kwenye mwili wake, hivi jee
unamjua ni nani huyo? Huyo ni Thumamah Ibn Uthal ambae ni Chifu wa
Yamammah, hivyo ukimdhuru tu basi watu wake watazuia misafara yetu yote ya
Kibiashara inayopita kwenye ardhi yao na matokeo yae tutapatwa na madhara
makubwa sana’
Ambapo Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu alipokaribia karibu basi Viongozi wa
Quraysh wakamfuta na kumuuliza: ‘Thumamah imekuaje, una wazimu au? Imekuaje
ukaachana na Dini ya Mababu zako ambayo ndio iliyokua Dini yako?’
Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Sikuachana na Dini ya Mababu
zangu, bali nimeamua kufuata Dini iliyokua bora zaidi ambayo ni Dini ya
Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam. Na Wallahi nnaapa kwa jina la Mungu wa
Jengo hili la Al Kaabah kua baada ya kurudi kwangu katika Ardhi yangu, basi
hakuna Ngano wala zao lolote litokanalo na ngano kua litakufikieni hadi pale
mtakapokua ni wenye kuifuata Dini ya Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam’
Na kisha baada ya hapo Thamamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu akafanya Umra ya
kwanza kufanywa kama ilivyoamrishwa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
kisha baada ya kumaliza akachinja kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala.
Kisha akarudi katika mji wake na kuwausia watu wake juu ya Allah Subhanah wa Ta’ala
na kuwaamrisha kua wazuie mazao yanayotokana na ngano zao wasiwapelekee watu wa
Mji wa Makkah wa Quraysh. Tukio ambalo lilipelekea kupanda kwa hali ya maisha
katika Mji wa Makkah, na baadhi ya watu wakafariki kwa sababu ya njaa.
Hivyo watu wa Makkah wakamwandikia barua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam,
kumlalamikia kwa kumwambia kua: ‘Ewe Muhammad Tunasikitika kua umevunja
makubaliano yetu, kwani Makubaliano yaliyokuwepo baina yetu katika Mkataba
wa Hudaybiyah ni kua hatutakiwi kuvunjiana udugu baina yetu, lakini wewe
Muhammad umeenda kinyume na makubaliano hayo kwani umevunja Udugu
baina ya watu. Na pia umeua na kusababisha vifo kwa kutumia njia ya njaa. Kwani
Mtu wako Thumamah Ibn Uthal ametukatia njia ya usambazaji wa mahitaji ya
Ngano tunayoitegemea kwa ajili ya chakula chetu. Hivyo sisi tuna matumaini
kutoka kwako utamwambia Thumamah asitukatie njia za usambazaji wa Chakula
chetu.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliposomewa Ujumbe huo basi akamtuma mtu
aende Yamamah kwa Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu kumjuulisha kua inabidi
awaondolee vikwazo watu wa Mji wa Makkah, ambapo Thumamah Ibn Uthal Radhi
428
Allahu Anhu baada ya kupokea ujumbe huo basi akawaondoelea Watu wa Makkah
vikwazo hivyo.
Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu aliendelea kuishi pamoja na watu wake huku
wakiendelea kufuata Dini ya Kiislam na kumtumikia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam hadi kufariki kwake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambapo katika ardhi
ya Yamamah kukazuka Upinzani dhidi yake kutoka kwa Musallima ambae alitangazia
kua yeye ndie Mtume mpya baada ya kufariki Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
hivyo baadhi ya watu wakaanza kumfuata na kumuamini Musallima Al Kadhdhab.
Kwani Musallima alikua akiwaambia Watu wake kua: ‘Hivi Nyinyi Mnajifikiriaje?
Yaani kitu kilichowafanya Watu wa Quraysh kua ni Bora zaidi yenu? Wakati wao
wako kidogo kuliko sisi, na Ardhi yetu ni Nzuri na Kubwa sana kuliko Ardhi yao.
Hivyo bila ya shaka Jibril ananishukia mie pia kama vile ambavyo alivyokua
akimshukia Muhammad’
Na kutokana na Kauli hio basi Musallima alikua hapingi kua Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam hakua Mtume La! Alikua anakubalia kua Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kua alikua ni Mtume, ila sasa na yeye pia anashirikiana nae katika Utume huo.
Hivyo Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu akawaambia watu wake wa Banu Hanifa
kwa kusema kua: ‘Enyi watu wa Banu Hanifa jihadharini na kosa hili la kufuata
upotovu mkubwa sana. Kwani hakuna Muongozo kama Muongozo wa Allah
Subhanah wa Ta’ala. Hivyo wa Allahi hakuna kitakachomnufaisha yeyote yule
atakaefuata Upotovu huo (wa Musallimah) isipokua maangamizo. Kwani enyi watu
wa Banu Hanifah fahamuni kua hakuna Mtume atakaefuatia baada ya Muhammad
Salallahu A’alayi wa Salam na hakuna Mtu yeyote anaeshirikiana nae katika Utume
wake huo, na hivi jee mnafaham kua amesema Allah Subhanah wa Ta’ala katika
Qur’an kua:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞حم ۤ ۞تَنزِيلُ ٱلْكِتَابِ مِنَ ٱهلل َِّ ٱلْعَزِيزِ ٱلْ عَلِيمِ۞غَافِرِ
ٱلذ َّنبِ وَقَابِلِ ٱلت َّوْبِ شَدِيدِ ٱلْعِقَابِ ذِى ٱلط َّوْلِ لاَ إِلَٰهَ إِلا َّ هُوَ إِلَيْهِ ٱلْمَصِيرُ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Ha-meem; Tanzeelu alkitabi mina Allahi
alAAazeezi alAAaleemi; Ghafiri aldhdhanbi waqabili alttawbi shadeedi
alAAiqabi dhee alttawli la ilaha illa huwa ilayhi almaseeru (Surat Ghafir 40:1-3)
Tafsir: Kwa Jina La Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma. Ha Mim. Teremsho
la Kitabu (Qur’an) ni Kutoka kwa Allah Mwenye Utukufu wa juu ya kila kitu na ni
429
mwingi wa Kujua juu ya Kila kitu. Mwenye Kusamehe Dhambi na ni mwenye Kukubali
Toba na ni Mkali wa Adhabu, na Mwingi wa Fadhila Hakuna Mungu isipokua yeye
na kwake yeye ndio marejeo yetu.
Hivyo rudini kwa Mola wenu, kwani jee mnawezaje nyinyi kufananisha maneno
haya matukufu ya Allah Subhanah wa Ta’ala na maneno ya Musayllima?’
Na kisha baada ya maneno hayo basi Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu
akawakusanya wote wale wanaokubaliana na msimamo wake wa kubakia kwenye
Uislam miongoni mwa watu wa Banu Hanifa na kuanza kujipanga kwa ajli ya kupigana
vita vya Jihadi dhidi ya Wanaopingana na Uislam wanaoongozwa na Musallimah Al
Kadhdhab aliejitangazia kua ni Mtume mpya ambae ndie mrithi wa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam.
Kwani hivyo ndivyo alivyojaribu Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu kuwatoa
kwenye Upotovu lakini wengi wao hawakumsikiliza. Hivyo akabakia nao kidogo wale
waliokua wakimsikiza kisha akamchagua Mmjoa na kumtuma kwa Amir Ul Muuminina
Abu Bakr Radhi Allahu Anhu kwa ajili ya Kuomba Msaada dhidi ya Wafuasi wa
Musallima.
Ambapo hiki kilikua ni kipindi cha Mwaka wa 11 Al Hijra. Hivyo baada ya Amir
Muuminin Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu kupata ujumbe huo basi nae
akaandika Barua 4.
Ambapo Moja ilirudi Yamamah kwa Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu ya
kumwambia kua astahamili kwanzi asifanye kitu hadi utakapomfikia msaada ambao uko
njiani unakuja.
Kisha ya pili akaituma kwa Shurahbil Ibn Hasan Radhi Allahu Anhu na kumwambia kua
anatakiwa apeleke Jeshi katika Ardhi ya Yamamah na akifika akutane Thumamah Radhi
Allahu Anhu na wasifanye chochote hadi afike Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu na
Jeshi lake.
Barua ya Pili ikatumwa kwa Ikrimah Ibn Abu Jahl Radhi Allahu Anhu ambae nae
akaambiwa apeleke Jeshi Yamamah na akifika akutane na Thumamah Radhi Allahu Anhu
na kisha asifanye Lolote Mpaka afike Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu.
Na Kisha barua ya nne ikatumwa kwa Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu na
Kuambiwa kua akishamalizana na Mitume wengine walioibuka maeneo ya Uarabuni basi
Aharakishe haraka sana kuelekea kwenye Mji wa Yamamah kwani Kuna Mtume
anaeitwa Musallimah kaibuka anatakiwa ashughulikiwe.
430
Na Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu akifika huko badi atakutana na Thumamah,
Shurahbil na Ikrima Radhi Allahu Anhum ambao wote wanamsubiri yeye tu na watakua
chini ya Uongozi wake
Kwani Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu aliwasili katika Mji wa Yamamah mnamo
mwezi 10 Shawwal Na mnamo Mwezi 11 Shawwal akawaongoza Waislam katika Vita
dhidi ya Musalima Al Kadhdhab.
Haya yalikua ni Mapigano Makali sana katika Historia ya Uislam. Na hapa ndio tunaona
Hikma na Busara na Imani za Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu kwani kama
angepigana peke yake basi asingechukua Mda isipokua angekua ni mwenye Kuangamia
yeye na Jeshi lake.
Lakini badala yake akaomba Msaada kwa Amir ul Muuminin Abu Baqr Radhi Allahu
Anhu ambae nae alitumia Busara, Hikma na Silaha Bora na Nzito kuliko zote alizokua
nazo ambayo ni Upanga wa Allah Subhanah wa Ta'ala yaani Khalid Ibn Walid Radhi
Allahu Anhu.
Kwani Amir Ul Muuminina Abu Baqr Radhi Allahu Anhu alimuuliza Amr Ibn Al Aas
Radhi Allahu Anhu kwa kusema: ‘Ewe Amr Ibn Al Aas hakika wewe Una Busara zaid
na kutoa Hukmu miongoni mwa Waarabu, hivi Jee Unasemaje kuhusiana na
Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu?’
Amr Ibn Al Aas Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Khalid Ibn Walid ni Mfalme wa Vita,
Rafiki wa Kifo, Mwenye Mvamio wa Simba na Subra ya Paka.’
Na Bila ya Shaka Amr Ibn Al Aas Radhi Allahu Anhu hakukosea!
Kwani kwa upande mwengine basi Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu alipofika katika
Mji wa Yamamah basi akakumbuka maneno ya Kiongozi wake Amir Ul Muuminina Abu
Baqr Radhi Allahu Anhu kua: ‘Ewe Khalid, kumbuka kua Hutokutana na Watu
Matata kama watu wa Al Yamamah, kwani watapigana na wewe Kwa kila hali
Hivyo basi Usisahau kua katika kushambulia kwao wakikushambulieni kwa Mkuki
basi nanyi Jibuni kwa Mikuki
Wakikushambulieni kwa Upinde basi Nanyi Jibuni kwa Mipinde
Wakianza kutumia Mapanga! Basi fahamu kua Mmeingia katika hali ambayo ni ya
Mapigano yanayompelekea Mama kukimbia na Kumsahau Mtoto wake.’
431
Kwani hapa jambo ambalo inabidi tuliweke wazi, kwani wengi wanafaham sivyo
kuhusiana na Vita vya Jihadi, kua inaruhusika kuua waliokuwemo na wasiokuwemo
kama wanavyofanya wale wanaojiripua kwa kujitolea Muhanga. Ukweli ni kua kufanya
hivyo hua si sehemu ya Jihad fi Sabili Allah na ni kinyume cha Mamrisho ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na pia makubaliano ya Wanazuoni, kwani Jihdi hua na
masharti yake ikiwemo kutoruhusiki kupiganwa pae inapokua hakuna kiongozi
Muadilifu katika Ardhi ya Waislam husika.
Na ndio maana Amir Ul Muuminina Abu Bakr Radhi Allahu Anhu akamwambia Khalid
Ibn Walid Radhi Allahu Anhu ambae ni Mpiganaji Mahiri kwa Silaha za aina zote, juu
ya vipando vyote, na pia hajawahi kushindwa, Hata kwa kutumia Silaha za Kimaumbile
ya Mwili wake.
Hivyo Amir Ul Muuminina Abu Bakr Radhi Allahu Anhu alimwambia Khalid Ibn Walid
Radhi Allahu Anhu kua: Mkuki kwa mkuki, upinde kwa upinde, upanga kwa upanga na
hivyo hii inamaanisha kua Kiislam hairuhusiki kumpiga mtu ambae hajashika Silaha.
Hio ni kwa Upande Mmoja, lakini kwa upande wa pili pia tunaona katika Wasia wa Amir
Ul Muuminina Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu kwa Khalid Ibn Walid Radhi
Allahu Anhu kwa kumwambia kua:
‘Ewe Khalid, Kama Mkiwakamata Askari wa Maaduie zenu basi kuweni na Rehma
na Huruma Juu yao.
Waoneeni Huruma Majeruhi wao.
Msiwaue Mateka wao.
Msiwatushie Kuwachoma Moto.
Na kuweni Makini katika kutekeleza Maamrisho yangu haya.
Salaam Alaykum wa Rahmat Allahi wa Barakatuh’
Naam...hayo ndio yaliyokua Maamrisho na ndio Sharia na Hukmu za Kiislam kuhusiana
na Vita Vya Jihadi na pia kuhusiana na Mateka wa Vita.
MAUMBILE YA ISA IBN MARYAM NI MITHLI YA NABII ADAM.
Tunaporudi katika ujumbe wa Najran uliomtembelea Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam baada ya kua ni Mmoja kati ya Jamii za watu ambao nao walitumiwa moja kati ya
miongoni mwa Barua 8 kama aliyopelekewa Thumamah Ibn Uthal Radhi Allahu Anhu
basi tunaona kua ujumbe huo ulikua ni wa watu 60 ambao ni wenye kuheshimika sana
katika Mji wa Najran ambao walichaguliwa maalum kwa ajili ya kujadiliana na Rasul
432
Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo walikua wakiongozwa na Viongozi watatu wa
Dini ya Kikristo ambao ni:
1. Abu Harith Ibin 'Alqamah ambae ni Padri Mkuu wa Najran na Muwakilishi
Mkuu wa Kanisa Katoliki wa Urabuni ambae ndie aliepokea Ujumbe wa Mualiko
wa kuingia katika Uislam miongoni mwa mialiko minane aliyotuma Rasul llah
Salallahu Alayhi wa Salam kwa viongozi wa Uarabuni na maeneo mengine ya
Mipakani mwake.
2. Abdul Masih, Muwakilishi Mkuu wa Watu wa Najran ambae alikua akisifika
kwa kua na Hikma na Busara na uzoefu wa Kidiplomasia.
3. Ayham, ambae ni Chifu wa Mji wa Najran.
Hivyo ujumbe huo wa watu 60 ulipowasili Mjini Madinah ulikua umevalia Majoho ya
Hariri, Pete na Mikufu ya Misalaba ya Dhahabu shingoni mwao, wakaingia Msikitini na
kumsalimia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambapo ingawa Rasul Allah
Salallahu layhi wa Salam alipowaona hakuvutiwa na mavazi yao, jambo ambalo Watu
hao wa Najran walilihisi na wakajiuliza imekuaje ikawa hivyo.
Hivyo Ujumbe huo wawatu hao ukaamua kutafuta utatuzi wa hali hio na wakaulizia na
kushauriwa kua wazungumze na Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu ambae
nae aliwashauri kua hawatakiwi Kuingia Msikitini umo kukutakana na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam wakati wakiwa katika hali hio ya mavazi waliyokua nayo
kwani Uislam haupendekezi na umeharamisha kuvaliwa kwa Mavazi hayo, hivyo
wakibadilisha mavazi hayo na kuvaa mavazi ya kawaida basi Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam atawapa heshima yao.
Baada ya ushauri huo basi Ujumbe wa watu hao ukabadilisha Mavazi yao na mapambo
yao, na kuvaa mavazi ya kawaida, kisha wakaingia katika Masjid An Nabawi na
kumsalimia tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Ambapo nae akasalimiana nao
kisha wakampa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam zawadi walizokuja nazo kwa ajili
yake akazipokea. Ambapo anasema Imam Bayhaqi kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alisema kua: ‘Wa Allahi mwanzoni hapo kabla walipokuja walikua
wamefuatana na Shaytan.’’
Hivyo baada ya kusalimiana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi kabla ya
kuanza majadiliano yao basi Wajumbe ho wakasema kua umewadia Mda wa kusali,
hivyo wakaomba wasali na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaruhusu wasali
ndani ya Msikiti wake huo. Nao wakasali huku wakielekea katika upande wa Mashariki
linakochomozea Jua.
Kisha baada ya kumaliza Ibada yao basi wakasogea karibu ya Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam na wakakaa nae na kuanza kujadiliana kuhusiana na alilowausia kwenye
433
Ujumbe wa barua yake kwa kuwaambia : ‘Nakukaribisheni katika Imani ya Dini ya
Kumpwekesha Mungu Mmoja bila ya kumshirikisha Mungu huyo wa Ulimwengu
na kila kilichomo ndani yake ambae ni Allah Subhanah wa Ta’ala ’ na waliposikia
ujumbe huo basi watu hao wa Najran wakataka kujua kuhusiana nae huyo Mungu aitwae
Allah Subhanah wa Ta’ala na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawasomea
Surat Al Ihlas kwa kusema:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞قُلْ هُوَ ٱهلل َُّ أَحَ دٌ ۞ٱهلل َُّ ٱلص َّمَدُ۞لمَْ يَلِدْ وَلمَْ يُولَدْ۞وَلمَْ
يَكُ نْ ل َّهُ كُ فُواً أَحَ دٌ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Qul huwa Allahu ahadun; Allahu alssamadu;
Lam yalid walam yooladu; Walam yakun lahu kufuwan ahadun (Surat Al Ikhlas
112:1-5)
Tafsir: Kwa Jina la Allah mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma; Sema (Ewe
Muhammad Salallahu Allahu Alayhi wa Salam) kua: ‘Yeye ni Allah ni Mmoja tu,
Allah ni Mwenye Kujitosheleza, Hakuzaa wala hakuzaliwa, na Hakuna hata mmoja
anaefanana nae.’
Ujumbe wa Watu hao ukasema: ‘Kama Uislam unamanisha Imani juu ya Mungu
mmoja tu wa Ulimwengu basi sisi tayari tushamuamini zamani na tunatii
maamrisho yake’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaambia: ‘Uislam unabeba baadhi ya
matendo mema yenu ndani yake lakini baadhi ya matendo yenu yanaonesha kua
nyinyi hamuuamini Uislam. Kwani inakuaje mnasema kua mnamuamini Allah
Subhanah wa Ta’ala na kumuabudu wakati mnaiabudu Misalaba na hamjizuii
kutokana na kula Nguruwe? Na mnaamini kua Allah Subhanah wa Ta’ala ana
Mtoto?’
Ujumbe wa Watu hao ukasema: ‘Sisi tunaamini yeye (Isa Ibn Maryam) kua ni Mungu
kwa sababu alikua akifufua waliokufa, aliponesha wanaoumwa, aliwafanya Ndege
aliowatengeneza kwa udongo kua ni walio hai na kuruka na hivyo haya yote
yanaonesha kua yeye ni Mungu.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaambia: ‘La yeye Mja wa Allah Subhanah
wa Ta’ala na hivyi yeye ni kiumbe. Allah Subhanah wa Ta’ala alimuweka yeye ndani
434
ya Tumbo la Maryam Bint Imran, na hivyo Nguvu zake zote na uwezo amepewa na
Mola wake’
Ujumbe wa Watu hao ukasema: ‘Ndio! Yeye ni Mtoto wa Mungu kwa sababu
Maryam Bint Imran alimzaa bila ya kuolewa wala kuingiliwa na mtu yeyote. Na
kwa Mtoto hua ni lazima awe na Baba, kwa hivyo huyu lazima Baba yake atakua
ni Mungu. Hivyo kubaliana nasi na kisha sisi tutakufuata katika Dini yako, Au
wewe unafikiria kua ni nani atakua Baba yake Isa ewe Muhammad?’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akashusha aya zifuatazo:
﴿إِن َّ مَثَلَ عِيسَى ٰ عِندَ ٱهلل َِّ كَمَثَلِ آدَمَ خَلَقَهُ مِنْ تُرَابٍ ثمِ َّ قَالَ لَهُ كُن فَيَ كُونُ
۞ٱلحَْق ُّ مِنْ ر َّبِّكَ فَلاَ تَكُنْ مِّنَ ٱلْمُمْترَِينَ ﴾
Inna mathala AAeesa AAinda Allahi kamathali adama khalaqahu min turabin
thumma qala lahu kun fayakoonu; Alhaqqu min rabbika fala takun mina
almumtareena; (Surat Al Imran 3:59-60)
Tafsir: Hakika Mithili ya Isa mbele ya Allah ni kama mithili ya Adam, ameumbwa
kutokana na Udongo kisha akaambiwa kua na akawa. Ni Ukweli kutoka kwa Mola
wako, hivyo usiwe miongoni mwa wenye kua na shaka.
Ambapo aya ni zenye kubainishia uhalisia wa Maumbile ya Nabii Isa, kua kutokana na
Miujiza ya maumbile yake basi pia hastahiki kuitwa Mungu wala Mtoto wa Mungu, na
hii ni kwa sababu maumbile ya Nabii Isa ni kama ya Nabii Adam, tena bado Maumbile
ya Nabii Adam yana Miujiza zaidi kwani yeye hana Baba wala Mama ambapo kwa
upande wa Nabii Isa basi angalau yeye anae Mama, kwa hivyo kama Nabii Isa atakua ni
Mungu hivyo jee Nabii Adam atakua ni nani? Na vile vile wakijiuliza suali hilo basi
itabidi pia wajiulize kuhusiana na Hawa ambae nae ametokana na Adam. Jee Mama yake
nae yuko wapi?
Hivyo hapa tunapoyaangalia Maumbile ya Viumbe watatu hawa basi hua tunaona kua
Allah Subhanah wa Ta’ala anaweka wazi kuhusiana na uwezo wake wa kua pale
anapokitaka kitu kua basi hua kwa kukiambia Kun fayakunu – Kua na Kitu kinakua. Na
hivyo ndivyo ilivyokua kwa Maumbile ya Nabii Adam kua bila ya kuwepo kabla yake
Mwanamme wala Mwanammke au Mama wala Baba, kwa Maumbile ya Hawa kutokana
na Nabii Adam ambalo na tukio la Mwanamke kutokana na Mwanamme lakini hapo hapo
435
kua bila ya kuwepo kwa Baba wala Mama na kisha kua kwa Maumbile ya Nabi Isa kua
kutokana na Mwanamke peke yake bila ya kushirikishwa Mwanamamme.
Ambapo anasema Hujjt u Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali kua; ‘Kuzaliwa kwa Mtoto yeyote yule hua kunaokana na
sababu mbili, ambapo sababu ya kwanza hua ni iliyowazi ambayo ni kutokana na
Manii ya Baba na Yai la Mama na Mfuko wa Uzazi wa Mama, ambapo sababu ya
pili hua ni ya Ghayb isiyoonekana na hivyo kua ni iliyofichika, na hii hua ni Kauli
ya Allah Subhanah wa Ta’ala ya kukiambia kitu Kun-Fayakunu kua na hivyo hua
kinakua. Hivyo basi kwa kua hapa kwa Nabii Musa hakukuwepo kwa asili ya
sababu ya kwanza ya Manii ya Baba basi bila ya shaka kuzaliwa kwake Nabii Isa
Ibn Maryam kunatokana na sababu ya pili ambayo ni Kun fayakunu.’
Kisha zinawabainishia wazi Watu hao wa Najran kwa kuwaambia kua Wasitilie shaka
kuhusiana na ukweli wa Maneno waambiwayo juu yake Nabii Isa na pia juu ya ukweli
wa kuhusiana na Maumbile yake Nabii Isa, ambapo hata hivyo Watu hao wa Najran
hawakukubaliana na ukweli huo, hata baada ya kubainishiwa ukweli huo na Rasul Allah
Salallahu A’layhi wa Salam baada ya kuupokea.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akashusha aya hii ya 61 ambayo inajulikana kama aya
ya Mubahala au aya ya Al Mula’anah. Neno Mubahila linatokana na neno Bahala ambalo
kwa lugha ya Kiarabu hua linamanisha Kulaani, Kuapiza, na pia hua linamaanisha
Kuomba Dua kwa Allah Subhanah wa Ta’ala kwa hali ya Unyenyekevu. Ambapo neno
Mubahala hua linamaanisha Mashindano ya Kuapizana, au Kulaanina au Kuombeana
Dua Mbaya, hivyo aya hio ni yenye kusema:
﴿فَمَنْ حَآج َّكَ فِيهِ مِنْ بَعْدِ مَا جَآءَكَ مِنَ ٱلْعِلْمِ فَقُلْ تَعَالَوْاْ نَدْعُ أَبْنَاءََ
وَأَبْنَآءَكُمْ وَنِسَآءََ وَنِسَآءَكُمْ وَأَنْفُسَنَا وأَنْفُسَكُمْ ثمُ َّ نَبْتَهِلْ فَنَجْعَلْ ل َّعْنَةَ ٱهلل َِّ عَلَى
ٱلْكَاذِبِينَ ﴾
Faman hajjaka feehi min baAAdi ma jaaka mina alAAilmi faqul taAAalaw nadAAu
abnaana waabnaakum wanisaana wanisaakum waanfusana waanfusakum thumma
nabtahil fanajAAal laAAnata Allahi AAala alkadhibeena (Surat Al Imran 3:61)
Tafsir: Hivyo yeyote yule atakaekua na hoja kwako juu ya Isa baada ya kukufikia Ilm
hii, basi waambie: ‘Wacha tuwaite Watoto wetu na Watoto wenu, Wanawake wetu na
436
Wanawake wenu, Sisi wenyewe na Nyinyi wenyewe kisha tusali na tuombe laana ya
Allah juu ya wale wanaokadhibisha’
Ambapo ndani yake aya hii basi tunaona Allah Subhanah wa Ta’ala kutokana na kujua
Maumbile ya viumbe wake Ibn Adam kua ni wenye kupenda Watoto wao, Wake zao na
familia zao kwa ujumla na hivyo hua yuko tayari kujihatarisha maisha yake kwa ajili ya
kuwaokoa watu wa familia yake kutokana na kuwapenda kwake, na hivyo kimaumbile
hua haiwezekani na ni vigumu kwa mtu kua ni mwenye kutaka kuhatarisha Maisha yake
na maisha ya familia yake kwa ujumla.
Na katika ya hii basi Allah Subhnah wa Ta’ala ametaja kwa mpangilio wa darja za watu
katika familia kwa namna wanavyopendwa kimaumbile, ambapo kama tulivyoona kua
kwanza Mtu hua ni mwenye kuwapenda Watoto wake, kisha Wake zake kisha ndio yeye
Mwenyewe na ndio utaona Mtu akiwa hana kitu kisha akajaaliwa kupata chakula basi
kwanza humpa Mtoto wake, kisha Mkewe kisha ndio atakula yeye kama kikibakia au
baada ya watoto basi atagawana na Mkewe, kwani asiefanya hivyo hua na kasoro ya
Kimaumbile ya kua na Ubinafsi ya kujijali na kujipendelea yeye kwanza katika kila kitu.
Hivyo ingawa waliokua wakihojiana hapa walikua ni Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam na Watu hawa wa Najran tu lakini Allah Subhanah wa Ta’ala anamwambia
Mtume wake kua yeyote yule ataekabisha juu ya maumbile ya Nabii Isa baada ya
kuwekewa wazi kila kitu kama zilivyosema aya, basi na wawajumuishe Watoto wa pande
zote zinazobishana, Wanawake wa pande zote zinazobishana, pamoja na wote
wanaobishana juu ya jambo hili kwa ni moja kisha wasali na kuomba laana ya Allah
Subhanah wa Ta’ala iwashukie wale wote wanaosema uongo pamoja na familia zao, na
hivyo kile kitakachotokea baada ya maombi hayo ya kulaaniana baina yao basi kiwe ni
Fundisho na Uthibitisho juu ya ni nani ambae yuko sahih katika madai yake juu ya Nabii
Isa Ibn Maryam.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akafikisha ujumbe wa Aya hii na
kukubaliana na watu hao wa Najran kua kesho yake In-sha Allah waje kwenye Mubahala
katika hali hio waliyokubaliana kama ilivyoelekeza Aya hii ya Mubahala. Na ilipofika
siku ya pili yake asubuhi basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akatoka huku akiwa
amefuatana na Hasan na Husayn ambao amewakamata mikono huku Fatma Bint Rasul
Salallahu Alayh wa Salam akiwa pamoja Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu wakiwa
wanafuata nyuma yake huku akielekea kwenye makabiliano ya Mubahala.
Na Abu Harth Ibn Alqamah alipoona hali hio basi akawaambia watu wake hao wa Najran
kua: ‘Wallahi hakika mimi nnaona kwenye Nyuso kama wangekua ni wenye
kumuomba Allah auondoe Mlima kutoka katika sehemu moja kuupeleka sehemu
nyengine basi Allah angewaondolea Mlima huo na kuupeleka katika sehemu hio
waitakayo. Hivyo msitoke kwenda kukabiliana nae katika Mubahala. ’ na hivyo watu
437
hao wa Najran wakakubaliana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua bora
watalipa Jizya yaani kodi kwa Waislam badala yake.
Ambapo anasema Imam Muhammad Ibn Jarir At Tabari kua: ‘Amesema Amr Ash
Shaabi kua: ‘Baada ya Wakristo hao kukubaliana makabiliano ya Mubahala basi
basi baadae waliomba Ushauri kutoa kwa miongoni mwa mmoja kati ya watu
wenye hikma miongoni mwao ambae aliwaambia kua kamwe wasikubali kuenda
kwenye Makabaliano hayo ya Mubahala.’’
Na kwa upande wa Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Sad Ibn Mani Al Basr basi
yeye anasema kua: ‘Wakristo hao walisema kumwambia Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam katika siku hio ya Mubahala kua: ‘Hakika sisi tunaona kua haina
haja na si sahih kukabiliana nawe kwenye Mubahala, hivyo unaweza kutuamrisha
unalotaka nasi tutakubaliana nawe ili kupatikane Usalama na Amani baina yetu’’
Ambapo amesema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Kama Abu Jahl
angemrushia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam Utumbo ya Ngamia basi
angezuliwa na Malaika mbele ya macho ya watu wote, na kama Mayahudi
wangetaka wafe baada ya kusema kua:
﴿وَقَالُواْ لَن تمََس َّنَا ٱلن َّارُ إِلا َّ أَ َّماً م َّعْدُودَةً ﴾
Lan tamassana alnnaru illa ayyaman maAAdoodatan (Surat Al Baqara 2:80)
Tafsir: Sisi hatutoguswa na Moto isipokua kwa siku kidogo tu’
Basi nao wangekufa na wangeiona sehemu yao kwenye Moto. Na kama Wakristo
wa Najran wangekabiliana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwenye
Mubahala huo, basi wangerudi Majumbani kwao na kisha wangekuta familia zao
na Mali zao zote kua zimeangamia badala yake.’
Hivyo baada ya watu hao wa Najran kukubali juu ya kulipa Jizya basi wakamuomba
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam kua awape mtu mmoja anaeaminika miongoni
mwa Masahaba zake aende pamoja nao ili akawasaidie kupatanisha ugomvi uliopo baina
yao katika Mji wa Najran. Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akakubaliana
na maombi hayo. Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaandikiana nao
Mkataba wa makubaliano baina yao ambao uliandikwa na Abd Allah Ibn Abu Bakr Radhi
Allahu Anhu na kushuhudiwa na Abu Sufyan Ibn Harb Radhi Allahu Anhu, Ghilan Ibn
Amr Radhi Allahu Anhu, Malik Ibn Awf Radhi Allahu Anhu, Aqra Ibn Habis Radhi
Allahu Anhu na Mughira Ibn Shuba Radhi Allahu Anhu ambapo maelezo yaliyomo ndani
yake makubaliano hayo ilikua ni kama ifuatavyo:
438
Biismi Allahi Al Rahmani Al Rahim.
Haya ndio makubaliano ambayo Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam
amekubaliana na Watu wa Najran, kua ana Mamlaka juu ya Matunda yao, Mazao
yao, Dhahabu zao, Fedha na Watumwa wao. Na hivyo amewachia wao vyote hivyo
kwa malipo ya Hulla 2000 kwa mwaka, ambapo Hulla 1000 watalipa katika mwezi wa
Rajab na Hulla 1000 watalipa katika mwezi wa Safar ambapo kila Hulla 1 ni sawa na
Waqia moja yaani Dirham 4.
Mbali ya hivyo, lakini watu wa Najran watatakiwa kulipa gharama za Makazi na
Matamizi ya Wajumbe wangu kwa si zaidi ya siku 20 na Wajumbe wangu hao
hawatowekwa katika Mji wa Najran kwa zaidi ya Mwezi mmoja. Na pia watu wa
Najran watatakiwa kutoa Mkopo wa Ngao 30, Farasi 30 na Ngamia 30, kama
itahitajika pale utakapotokea Uasi nchini Yeman. Na hivyo kama ikitokea kupotea kwa
kitu chochote katika hivyo vitakavyo kopeshwa kwa watu wangu, basi watu wangu
watakua wanadaiwa vitu hadi pale watakapovirudisha.
Watu wa Najran watastahiki Ulinzi kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala na
Makubaliano ya Muhammad Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuwahifadhia
Maisha yao, Imani yao, Mali zao kwa wale waliokua hawapo na waliokuwepo na
Famlia zao na Mrafiki zao. Na hawatotakiwa kubadilisha Utamaduni wao, Dini yao,
wala Makasisi wao, wala Watawa wao wala walinzi wa Makanisa yao hawato
badilishwa kutoka kwenye sehemu za kazi zao.
Kwani kila walichokua nacho ni chao, bila ya kujali kama kikubwa au kidogo,
hawatoshukiwa na wala hawatofanyiwa mauaji ya kisasi, hawatotakiwa kukusanya
jeshi na wala hakuna Jeshi litakaloingia kwenye ardhi yao. Na yeyote yule miongoni
mwa atakaeomba haki yake hasi itabidi apewe kwani haki itasimamiwa miongoni
mwao, na yeyote yule atakae chukua riba kutokana na kile alichopewa hapo kabla basi
hatokua chini ya Usimamizi wangu. Na hakuna Mtu yeyote katka Mji wa Najran
ambae atahukumiwa kutkana na kosa la mwengine.(Yahya Ibn Adam Ibn Sulayman,
Kitab al Kharaj)
Ama kuhusiana na Mubahala ambalo ndio neno lililotoa Nabtahil lililotumika kwenye
ya Mubahala na pia likatoa neno Ibtihal basi alisema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu
Anhu kua: ‘‘Hii ni Ikhlas’ (shahada) huku akinyoosha kidole cha Shahada, na kisha
akanyanyua Mikono yake kukaribia usawa wa Mabega huku Viganja vikitizama
juu na akasema: ‘Hii ni Dua’ na kisha akanyoosha Mikono yake mbele na kusema:
‘Hii ni Ibtahil’’(Sunnan Al Kubra Imam Al Bayhaqi)
Ambapo:
439
Kunyoosha kidole cha Shahada hua kunamaanisha Tawhid yaani kumpwekesha
Allah Subhanah wa Ta’ala.
Hua inapendekezwa sana kua Kidole cha Shahada lazima kinyanyuliwe pale Mtu
anapotamka Shahada iwe kwenye Sala au nje ya Sala.
Kauli ya ‘La Ilaha’ yaani ‘Hakuna Mungu’, hua inakanusha Kumshirikisha Allah
Subhanah wa Ta’ala na kauli ya ‘Illa Allah’ yaani ‘Isipokua Allah’ hua inaashiria
Tawhid.
Ambapo anasema pia Imam Al Bayhaqi kua: ‘Kuna mtu miongoni mwa watu wa
Madinah alisema kua: ‘Kuna siku mimi nilisali pembeni ya Khifafa Ibn Imaa Ibn
Rukhsa Radhi Allahu Anhu, na aliponiona nikiwa nimenyoosha kidole changu cha
Shahada basi akasema: ‘Ewe Ndugu yangu kwanini wewe ukafanya hivyo?’ nami
nikasema kua: ‘Hakika mimi nimewaona Watu walio bora na Wanazuoni wakiwa
ni wenye kufanya hivi’ hivyo Khifafa Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Uko sahih,
kwani mimi nilimuona Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akiwa ni mwenye
kunyanyua kidole chake cha Shahada katika wakati wa kukaa At Tahiyyat. Ambapo
Makafiri wakamshutumu kua alikua anawafanyia Uchawi, lakini waongo, kwani
Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam alifanya hivyo kwa sababu kufanya hivyo
hua inamaanisha kushuhudisha Umoja wa Allah Subhanah wa Ta’ala.’’
Ambapo amesema Imam Ibrahim An Nakhai kua: ‘Inapendekezwa kunyoosha Kidole
cha Shahada katika wakati unaposema Shahada, na inakirihisha kunyoosha vidole
viwili’
Na Imam Abū Muḥammad Al Ḥusayn Ibn Masʻud Ibn Muḥammad Al Farra Al Baghawi
amesema pa kua: ‘Wengi miongoni mwa Watu wenye Ilm wakiwemo Masahaba wa
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam, Tabiina na Tabii Tabiina walikua ni wenye
kunyoosha kidole cha shahada pale wanaposema Illa Allah katika Tashahud.’(Sharh
Al Sunnah)
Baada ya tukio hilo la Mubahala basi mnamo mwezi wa Rabiul Awwal 10 Al Hijra Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamtuma Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu na
jeshi la watu 400 katika Mji wa Najran kwa Banu Harith Ibn Kab na kumwambia kua:
‘Nenda katika Mji wa Najran na kisha wausie kuhusiana na Uislam, kama
wakikubaliana nao basi fanya kila linalostahiki, na kama wakipingana nawe basi
pigana nao.’
Hivyo Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu akatoka na jeshi lake hadi nje ya Mji wa
Najran. Kisha akapiga kambi katika maeneo hayo na kuwatuma Wajumbe wake
440
wakawausie watu wa Najran kuhusiana na Uislam kwa mda wa siku tatu. Na baada ya
siku tatu watu wote wa Najran wakaingia katika Uislam.
Baada ya watu hao kuingia kwenye Uislam basi Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu
akawafundisha watu hao kuhusiana na Dini ya Kislam, kisha akamuandikia barua Rasul
Allah Salallau Alayhi wa Salam kutaka kujua afanye nini baada yake.
Hivyo Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam akajibu barua hio kwa kusema:
Biismi Allahi Al Rahmani Al Rahim.
Kutoka kwa Muhammad Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kufikia kwa Khalid
Ibn Walid.
Al Salaam Alaykum!
Alhamd Lillah Ladhi La Ilaha illa Allah kwa lile ulilolifanya.
Nimepokea barua yako iliyoletwa na Mjumbe kutoka kwako, ambayo umesema ndani
yake kua watu wa Banu Harith Ibn Kab wamaeingia katika Uislamu bila ya upinzani,
wamemuamini Allah Subhanah wa Ta’ala ambae hana mshirika na wameshuhudia
kua Muhammad ni Mja na ni Rasul Allah na kua Allah Subhnah wa Ta’ala
amewaongoza kwenye njia iliyonyooka.
Wape habari ya kua watapata Malipo ya neema za Akhera kama ikiwa watafanya
kama alivyoamrisha Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume wake. Na watishe
kuhusiana na Adahabu za Akhera kama watafanya kinyume cha maamrisho ya Allah
na Mtume wake. Kisha unaweza kurudi huku ukwa na Mjumbe wao pamoja nao.
As Salaam Alaykum wa Rahmat Allahi wa Barakatuh.
Hivyo baada ya mda Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu akarudi na jeshi lake na
Ujumbe wa Najran katika Mji wa Madinah na moja kwa moja wakaenda kwa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na kumfahamisha kua kweli wote wamekua Waislam na
hivyo Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam akamteua Qays Ibn Husayn ambae alikua
ni miongoni mwao ujumbe huo wa Najran kua ndio awe Gavana wao, na kisha baada ya
mda Ujumbe huo ukarudi katika Mji wa Najran huku ukiwa umesheheni zawadi kutoka
kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
441
UTUKUFU WA KUTUNUKIWA UJA UZITO MARYAM BINT IMRAN
Tunapomuangalia Maryam Bint Imran basi tunaona kua ni Mwanamke ambae ni mwenye
sifa ya kumtii Allah Subhanah wa Ta’ala, mwenye kuachana na mambo ya kidunia na
kuyakmia mapambo ya Dunia, hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala amemchagua Maryam
Bint Imran kua ni mfano bora kwa Wanawake na pia kwa Wanaume kutokana na
Uchamungu wake, na hvo ndani yake kutuonesha mfano wa yale yanayoweza kutokea
pale Mtu unapokua Mcha na mitihani mbali mbali unayoweza kukumbana nayo kutoka
katika jamii unayoishi na hivyo kutakiwa kutorudi nyuma wala kutetereka katka
msimamo wako mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala na kukubaliana na Majaaliwa yake
juu yako.
Anasema Imam Abu Is-haq Ahmad Ibn Muhammad Ibn Ibrahim Al Thalabi Al Shafii
kua: ‘Wakati Maryam Bint Imran alipotimia umri wa miaka 15 basi alikua na
ujauzito wa Isa Ibn Maryam kwa mda wa siku 3. Ambapo pamoja nae katika
nyumba ya kufanyia ibada alikuwepo Yusuf ambae alikua ni Mtoto wa kaka yake
baba yake, ambae nae alikua pia ni mwenye kujitolea kwa ajili ya Mola wake. Yusuf
alikua ni mtu mstahmilivu na ni fundi Seremala ambae ni mwenye kuwasadia watu
katika kutengeneza fanicha zao. Yusuf na Maryam walikua na Jukumu la kuchota
Maji kutoka kwenye Pango lenye chemchem ya Mji na kisha huyapeleka katika
Jengo wanalofanyia Ibada Mayahudi.’
Ambapo mtu huyu anaetwa Yusuf basi hakua mtu mwengine yeyote isipokua ni yule
tuliemzungumzia hapo kabla ambae alikua pia ni Mlezi wake Maryam Bint Imran ambae
alikua anaitwa Yusuf Ibn Yaqub Ibn Mathan Ibn Amur Ibn Mishan Ibn Hizqil Ibn Ahraf
Ibn Buam Ibn Azaziyah Ibn Amasiyah Ibn Nawus Ibn Nutha Ibn Barid Ibn Yahushafat
Ibn Radim Ibn Ababa Ibn RajiAm Ibn Sulayman Ibn Daud.
Siku moja katika kipindi cha Kiangazi, Maryam Bint Imran kwani Allah Subhanahu wa
Ta’ala alimuamrisha Malaika Jibril Alayhi Salaam kujua na kuenda kwa Maryam bint
Imran kwa ajili ya kumshushia Wahyi na kumbashiria habari njema kama ilivyoelezewa
katika Surat Al Imran pale iliposema:
﴿وَإِذْ قَالَتِ ٱلْمَلاَئِكَةُ
يمَٰرْيمَُ إِن َّ ٱهلل ََّ ٱصْطَفَاكِ وَطَه َّرَكِ وَٱصْطَفَاكِ عَلَى ٰ نِسَآِء
ٱلْعَالَمِينَ ﴾
442
Wa-idh qalati almala-ikatu ya Maryamu inna Allaha istafaki watahharaki
waistafaki AAala nisa-i alAAalameena (Surat Al Imran 3:42)
Tafsir: Na (kumbuka) wakati Malaika aliposema: ‘Ewe Maryam! Kwa Hakika Allah
amekuchagua wewe na kukutakasa, na kukuchagua kua juu zaid ya Wanawake wote
wa Ulimwenguni’.
Hivyo alipofika kwenye Pango hilo basi akakutana na Mtu ambae alikua ni Malaika Jibril
ambae alimbashiria kuchaguliwa kwake na kupandishwa Darja ya Utakaso kutoka kwa
Mola wake na kuamriwa kua awe ni mwenye kudumu katika Ibada.
﴿ يمَٰرْيمَُ ٱقْنُتىِ لِرَبِّكِ وَٱسْجُدِى وَٱرْكَعِى مَعَ ٱلر َّاكِعِينَ ﴾
Ya maryamu oqnutee lirabbiki waosjudee wairkaAAee maAAa alrrakiAAeena
(Surat Al Imran 3:42)
Tafsir: Ewe Maryam Muabudu Mola wako, na Umsujudie na Urukuu pamoja na
wenye kurukuu.
Ambapo aya imetumia neno Uqnut ambalo hua lintokana na neno Qanata ambalo hua
linamaanisha Kujitolea. Kua Mtiifu, Kufanya Ibada kwa Ikhlasi na Unyenyekevu. Na
hivyo basi kwa uande wa Imam Mujahid Ibn Sulayman basi yeye anasema kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala anamwambia Maryam Bint Imran kua anatakiwa awe ni
Mwenye kudumu katika Ibada za Mda mrefu’ na kua anatakiwa ashikamane na wale
Wacha Mungu waliojitolea katika kufanya Ibada kwa Ikhlasi na Unyenyekevu kwani
Ikhlasi na Unyenyekevu hua ni vyenye kumuondolea Ibn Adam hisia za Kujiona, Kibri
na kua na Chuki.
Ambapo wanasema Wanazuoni kua baada ya Maryam Bint Imran kuambiwa hivyo bsi
akawa anasimama usiua na uali hadi miguu yake ikawa ni yenye kuimba
Mbali ya hivyo basi amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua:
‘Wanatosheleza kwenu, Wanawake wa Ulimwengu ni Maryam Bint Imran, Khadja
Bint Khuwylid na Fatma bint Muhammad Salallahu layhi wa Salam.’ (Tirmidhi)
Na akasema tena Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Miongoni mwa
Wanaume wamekuwepo wengi waliokua ni wenye kuufikia ukamilifu. Lakini kwa
upande wa Wanawake basi hakuna alieufikia ukamilifu wa Maryam Bint Imran,
443
Asiyah Bint Muzahim mke wa Fir’awn na Aisha ambapo utukufu wao dhidi ya
Wanawake wengine basi hua ni sawa na Tharid na vyakula Vyengine.’
Ambapo Tharid hua ni Chakula ambacho ni kitamu sana na tunu cha kipindi cha Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kilichokua ni chenye mchanganyiko wa Mkate, Nyama
na Mchuzi wa Nyama kama wa Biriani.
Utukufu wake Maryam Bint Imran tunauona wazi pale tunapoangalia Qur’an na kuona
kua ingawa Qur’an imezungumzia habari za Wanawake kadhaa ndani yake kama Mke
wa Nabii Adam, Mke wa Nabii Nuh, Mke wa Nabii Ibrahim, Mke wa Nabii Lut, Mke wa
Waziri aliempa Mtihani Nabi Yusuf, Mke wa Fir’awn, Wanawake wawili wa Shuayb
ambao mmoja wao alimuoa Nabi Musa, Dada yake Nabii Musa, Malkia wa Sheba lakini
hakuna hata mara moja ambapo kuna sehemu iliyotaja majina ya Wanawake hao,
isipokua katika Kisa cha Maaryam Bint Imran tu, ambae ndie Mwanamke pekee alietajwa
kwa jina, na si hivyo tu bali pia Maryam Bint Imran ndie Mwanamke pekee ambae Jina
lake limetumika kua ni jina la moja kati ya Majina ya Sura za Kitabu kikufu cha Qur’an.
Na hii ni kwa makusudio ya kumsafisha Maryam Bint Imran kutokana na Utukufu wake
na kutokana upatikanaji wa Uja uzito wake na pia wa mtoto wake, na hivyo kuondoa na
kufuta kila chembe ya shaka au wasiwasi kuhusiana na Utukufu wake na Miujiza yake
juu ya Upatikanaji wa Mtoto wake, hivyo katajwa moja kwa moja ili watu wasijiulize
yeye au si yeye au ni mwengine, na hii inathibitishwa mara kadhaa kuhusiana nae
Maryam Bint Imran kama zinavyosema aya:
﴿وَٱذْكُرْ فىِ ٱلْكِتَابِ مَرْيمََ إِذِ ٱنتَبَذَتْ مِ نْ أَهْ لِهَ ا مَكَ اً شَ رْقِياً ۞ فَٱتخ ََّذَ ْت
دُوِِم حِ جَاابً فَأَرْسَلْنَآ إِلَيْهَآ رُوحَنَا فَتَمَث َّلَ لهََا بَشَراً سَوًِّ﴾
مِن
Waodhkur fee alkitabi maryama idhi intabadhat min ahliha makanan sharqiyyan;
Faittakhadhat min doonihim hijaban faarsalna ilayha roohana fatamaththala laha
basharan sawiyyan; (Surat Maryam 19:16-17)
Tafsir: Na ametajwa katika kitabu, Maryam, wakati alipojitenga kutokana na familia
yake katika sehemu inayoelekea upande wa Mashariki; Akaweka pazia kabla yao,
kisha tukamtumia juu yake Ruhi (Malaika) wetu aliejimithilisha katika umbo la mtu
aliekamilia na kujaa heshima.
Aya inasema kua ametajwa, amekubukwa, amekumbushiwa tena na kuendelea
kukumbushiwa ili msije mkamsahau Maryam Bint Imran, na kuendelea kuelezea hususn
juu ya yaliyotokea kwa kutumia neno Intabadhat ambalo linatokana na neno Nabadha.
444
Neno Nabadha hua linaamanisha Kurusha, Kurembea, Kufukuza, Kutenga kitu au
Kuweka Kitu pembeni kutokana na kutokua na thamani kwake au kutokana na kutotaka
kukihesabu. Hivyo neno Intabadhat hua linamaanisha Mwanamke aliejitenga. Na hivyo
kumaanisha Kua Maryam Bint Imran aliamua kujitenga kwa sababu ya kua alikua ni
mwenye kuingia kwenye siku zake na hivyo haruhusiki kuingia kwenye Mihrab.
Na ndio maana Imam Al Abd Al Rahman Al Suddi, Imam Muqatil Ibn Sulayman Al
Balkhi na Imam Al Hassan basi wao wanasema kua: ‘Maryam Bint Imran alikua
akikaa katika Mihrab pale anapokua Tohara, na anapokua katika siku zake basi
hua ni mwenye kuenda kwa Isha Bint Faqudh ambae ni Dada wa Mama yake, na
hukaa huko hadi anapokua tohara tena na kurudi kwenye Mihrab.
Hivyo siku moja wakati alipokua anataka kujitoharisha kutokana na hedhi basi
alichagua sehemu ya upande wa Mashariki yenye kupigwa na jua kwa sababu hiki
kilikua ni kipindi cha Kipupwe. Na kisha akaiziba sehemu hio kwa pazia baina yake
na baina ya watu wake na alipokua katika mazingira hayo akatokea Malaika Jibril,
na kumpa habari ya Ujumbe kutoka kwa Mola wake kuhusiana na Ujauzito wake,
na kisha Malaika Jibril akaipulizia Kanzu ya Maryam Bint Imran.’
Na kwa upande mwengine basi kuna wasemao kua Maryam Bint Imran alijitenga katika
upande huo wa Mashariki si kwa sababu ya kua alikua ni mwenye kuingia kwenye siku
zake, bali ni kwa sababu alikua ni mwenye kutaka kuupata Ukaribu zaidi kwa Allah
Subhanah wa Ta’ala katika Ibada zake. Kwani kufanya kwake hivyo hua ni kweye
kumuongezea Imani kwa kumkumbuka Allah Subhanah wa Ta’ala na kumpa nguvu zaid
katika kukabiliana na mitihani atakayokumbana nayo hapo baadae katika maisha yake
kwani hukuonesha Uwezo na Ukubwa wa Allah Subhanah wa Ta’ala.
Na hii ni kwa sababu Ibn Adam unakua hujichanganyi na mambo ya Kidunia na
kujulikana na watu wengi basi hali hii hua inakusaidia kutoathirika na athari mbaya na
zenye kuenda kinyume na maadili ya Kiislam katika jamii zinazowaathiri wengi
kutokana na kua ni wenye kuiga na kufuata mambo yasiyotokana na Imani ya Dini ya
Kiislam kutokana na kutokuwepo kwa vizuizi vya athari hizo katika jamii.
Ambapo kwa upande wa Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas na pia Abd Allah Ibn Masud
Radhi Allahu Anhum basi wao wanasema kua Maryam Bint Imran aliingia katika siku
zake za kupata hedhi mara moja tu na hakuwahi kuingia tena ndani yake, hivyo alipopata
hedhi katika mara hio na kisha ikasita basi basi akaelekea katika upande wa Mashariki
kwa ajili ya kujitoharisha, na kisbha akaweka baina yake na sehemu aliyokuweo ili watu
wasimuone ambapo hapo ndio Allah Subhanah wa Ta’ala akamtuma Malaika Jibril kwa
ajili ya kumbashiria juu ya Kupata uja uzito kwake ambao kutokana nao basi atakua ni
mwenye kupata mtoto mtakatifu yaani Isa Ibn Maryam.
445
Ambapo hapa katika aya hii basi Allah Subhanah wa Ta’ala ametumia jina la Ruhi
ambalo hua ni lenye kutokana na neno Raha ambalo hua ni lenye kumaanisha Upepo,
Mamlaka, Roho. Pumzi au Hewa ya Uhai, Wahyi, Furaha na pia hua linamaanisha Qur’an
kwa sababu Qur’an hua ina sifa ya Kuhuisha Nyoyo. Hivyo neno Ruhina hua
linamaanisha Ruhi Wetu yaani Kiumbe mwenye Uhai anaemilikiwa na Ufalme wa Allah
Subhanah wa Ta’ala ambae ni Malaika Jibril.
Ambpapo unapomzungumzia Malaika Jibril basi tunaona kua ingawa ni mongoni mwa
Malaika wenye maumbo madogo miongoni mwa Malaika lakini hata hivyo Jibril ni
Malaika mwenye Darja kubwa sana mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala na hivyo kua
ndio Mkuu wa Malaika na ndio maana akakabidhiwa madaraka ya kua ni Mwenye
kuwashushiwa Wahyi na Vitabu vyote Mitume wake Allah Subhanah wa Ta’ala.
Na hivyo Malaika Jibril amekua na sifa ya Jina la Ruhi Al Qudus yaani Roho Mtakatifu
yaani ni Kiumbe asiekua na Kasoro na asiefanya Makosa, Ruhi Al Amin yaani Roho
Inayoaminiwa na hivyo kua ni mwenye kuaminiwa na Allah Subhanah wa Ta’ala katika
kutuma ujumbe wake kwa Mitume na Manabii wake na kama tunavyoona kwa Maryam
Bint Imran, ambae ni mwenye kua na sifa ya Unabii pia, kama tulivyoelezea hapo kabla
tulipozungumzia maana na tofauti baina ya Mtume na Manabii.
Hivyo anasema Ikrimah Mawla Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kuhusiana na
tuko hilo kua: ‘Maryam Bint Imran alitokezewa na Malaika Jibril ambae alikua
katika umbo la kijana Mwanamme mweupe asiekua na ndevu mzuri mwenye
kuvutia na nywele za singa na mwenye heshima kubwa sana’ hivyo Allah Subhana
wa Ta’ala alimtuma kwake Malaika Jibril katika Maumbile hayo ili Maryam Bint Imran
asiingiwe na Khofu baada ya kumuona kijana huyo, na hivyo aweze kumsikiliza atakapo
mfikishia ujumbe wake huo kutoka kwa Mola wake.
Ambapo tukio lililotokea baada ya hapo basi linaelezewa na Allah Subhanah wa Ta’ala
katika Qur’an pale aliposema:
﴿قَالَتْ
إِنيّ ِۤ أَعُوذُ بِٱلر َّحمَْٰنِ مِ نكَ إِن كُ نتَ تَقِيّاً ۞
لاًّهَبَ لَكِ غُلَماً زَكِيّاً﴾
قَالَ إِنم ََّآ أََْ رَ ُسولُ رَبِّ ِك
Qalat innee aAAoodhu bialrrahmani minka in kunta taqiyyan; Qala innama ana
rasoolu rabbiki li-ahaba laki ghulaman zakiyyan (Surat Maryam 19:18-19)
446
Tafsir: Nae (Maryam Bint Imran) akasema: ‘Hakika mimi ninajilinda kwako na kwa
Mwingi wa Rehma, ikiwa unamuogopa Allah’; Nae (Malaika Jibril) akasema: ‘Mimi
ni mjumbe kutoka kwa Mola wako, kukuzawadia mtoto wa kiume alie mwema’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamjaalia Maryam Bint Imran kua na utulivu
alipotokewa na Malaika Jibril katika Maumbile ya Kijana Mwanamme Mzuri, Mwenye
Heshima, Utulivu na Kuvutia kiasi ya kua haikua rahisi kwa Maryam Bint Imran
kushtuka kutokana na muonekano huo wa Kijana huyo. Kwani kama angemtokea kwa
ghafla au kwa muonekano unaoshtua basi huenda Maryam Bint Imran angekua ni
mwenye kupiga kelele na kukimbia na kutotaka hata kuzungumza na kijana huyo.
Na hivyo Malaika Jibril kutokua na uwezo wa kumpa Ujumbe huo kwa namna
ilivyokusudiwa Umfikie ujumbe huo Maryam Bint Imran, na pia Malaika Jibril alikua na
hali ya Utulivu na heshima kubwa kimuonekano kwa sababu tukio hili la kwanza
linalotokea hapa la kuonekana kwa Malaika Jibril mbele ya Maryam Bint Imran si kubwa
na halina uzito zaidi ya lile litakalofuatia, ambalo ni la kufikisha Ujumbe wa kutokea
tukio la Tukufu la Miujiza ya kipekee ambalo halijawahi kutokea Ulimwenguni tangu
kuumbwa kwa Ulimwengu wala halitotokea tena baada ya kutokea kwake tukio hilo
katika mazingira haya aliyokua nayo Maryam Bint Imran.
Hivyo kutokana na muonekano huo wa Malaika Jibril basi ulimfanya Maryam Bint Imran
kua Mnyenyekevu zaid na kumjali na mwenye kumuonea huruma kijana huyo asiemjua
kutokana na kuwepo katika sehemu asiyostahiki kuwepo kijana huyo basi akamuusia kwa
moja kwa moja kurudi kwa Mola wake ambae yeye Maryam Bint Imran ndie aliekua
akimjali na kumtumikia maisha yake yote tangu kuzaliwa kwake, hivyo akakimbilia
kujihifadhi vizuri mavazi yake na kwa kutumia Qawlan Sadida yaani kauli ya moja kwa
moja iliyojaa utulivu bila ya kutaka kujuana nae Kijana huyo ni nani na amekuja kufanya
nini katika sehemu hio na akasema: ‘Hakika mimi ninajilinda kwako na kwa Mwingi
wa Rehma, ikiwa unamuogopa Allah’’.
Ambapo nae (Malaika Jibril) akatumia Qawlan Sadidan kwa moja kwa moja
kujitambulisha na kudhirisha Dhumuni la kuwepo kwake mbele ya Maryam Bint Imran
katika mazingira kama hayo, ambayo kweli hastahiki kuwepo Mtu mwengine zaidi yake
kutokana na Maryam Bint Imran kua ni mwenye kuichagua sehemu hio maalum kwa ajili
ya kua peke yake na ndio maana akaweka pazia kwa ajili ya kujistiri, hivyo akamtuliza
zaidi Maryam Bint Imran ili amfikishie ujumbe aliopewa na Mola wake kumfikishia kwa
kusema: ‘Mimi ni mjumbe kutoka kwa Mola wako, kukubashiria kua Allah Subhanah
wa Ta’ala ametangazia kukutunukia Mtoto alie mwema’.
Ambapo hapa aya imetuma neno Ahaba ambalo ni lenye kutokana na neno Wahaba
ambalo hua linamaanisha Kuzawadia, Kutunuku au Kutoa Kitu kwa ajili ya kumpa mtu
kama zawadi. Hivyo Malaika Jibril ametumia kauli hii ya Ahaba kumaanisha kua Allah
447
Subhanah wa Ta’ala amesema kua anataka kumtunukia Maryam Bint Imran zawadi
Tukufu ya Mtoto kwani hivyo ndivyo alivyoamrishwa na Mola wake
Allah Subhanah wa Ta’ala anaendelea kuelezea kwa upande mwengine kwa kusema kua:
﴿إِذْ قَالَتِ ٱلْمَلا ۤ ئِكَةُ يمَٰرْيمَُ إِن َّ ٱهلل ََّ يُبَشِّ رُكِ بِكَلِمَةٍ مِّنْهُ ٱسمُْهُ ٱلْمَسِ يحُ عِيسَى ٱبْنُ
مَرْيمََ وَجِ يهاً فىِ ٱلد ُّنْيَا وَٱلآخِ رَةِ وَمِنَ ٱلْمُقَر َّبِينَ ﴾
Idh qalati almala-ikatu ya maryamu inna Allaha yubashshiruki bikalimatin minhu
ismuhu almaseehu AAeesa ibnu maryama wajeehan fee alddunya waal-akhirati
wamina almuqarrabeena; (Surat Al Imran 3:45)
Tafsir: Na (kumbuka) wakati aliposema Malaika: ‘Ewe Maryam, Allah
anakubashiria wewe habari njema za Kalimati (Maneno yake ya Kua na Akawa)
kutoka kwake, anaeitwa Al Massih Isa Ibn Maryam atakaeheshimiwa hapa Duniani
na Akhera na atakua ni miongoni mwa waliokaribu na Allah Subhanah wa Ta’ala.
Aya inatubainishia kua Malaika Jibril anamwambia Maryam Bint Imran kua Allah
Subhanah wa Ta’ala anambashiria yeye kuhusiana na Kalimati. Ambapo neno Kalimati
hua linatokana na neno Kalama ambalo hua linamaanisha Kusema, Kuzungumza,
Maneno, Sentensi, Lugha, Msemo, Amrisho, Hoja, Dalili, Bashirio, Utume, Ahadi au
Mawasiliano.
Na anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Ujio wa Nabii Isa
ulizungumziwa kwenye vitabu vyengine vilivyotangulia vya Mitume waliokuja
kabla yake, hivyo ulipowadia wakati wa kuja kwake basi ikasemwa kua hii ni
Kalimati iliyobashiriwa. Na hivyo kawa anaitwa Kalimati Allah.’
Ambapo kwa upande wa Imam Murtada Al Zabidi basi yeye anasema kua: ‘Nabii Ia
aliitwa Kalimati Allah kwa sababu Maneno yake yalikua ni yenye kuwasadia watu
katka kuwaongoza katika njia ya Allah Subhanah wa Ta’ala kutokana na thamani
yake kama vile ilivyokua kwa Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu ku ni mwenye
kuitwa Saifu Allah kutokana na Kuusaidia Uislam dhidi ya Makafiri kutokana na
Upanga wake’
Ambapo kwa Upande wa Shayh Al Akbar Imam Abu Bakr Ibn Arabi basi yeye anasema
kua: ‘Allah Subhanan wa Ta’ala aliposema kua: ‘Idha qadha amran fa-innama
yaqoolu lahu kun fayakoonu - Anapotaka kitu kiwe hua ni wenye kukiambia tu Kua
na Kikawa’ ambapo neno Kun hua si neno lenye Herufi mbili bali ni tatu, ambapo
448
harufi mbili ni za nje ambazo ni Kaf na Nun na herfu moja ni ya Ndani ambayo ni
Waw ambayo ipo baina ya Kaf na Nun. Kufichwa kwa herufi Waw kunatokana na
kutotamkika kwake kutokana na Nun, ambapo kufichikana huku kwa herufi Waw
baina ya herufi mbili hizi hua kunamaanisha kuwepo kwa Ulimwengu wa Ibn Adam
ambako ndiko kunakounganisha na kutofautisha baina ya herufi Kaf na Nun.’
‘Hivyo kuhusishwa kwa Isa na Maryam hua ni kuthibitisha kua Viumbe wote hua
ni wenye kutokana na Kauli ya Allah Subhanah wa Ta’ala ya KuN. Na hivyo Nabii
Isa hua ni muwakilishi wa uhalisia wa Kun na Maryam Bint Imran ambae ndie
alieamini katika Kalimati Allahi na Vitabu vyake na matokeo ya yote haya ni
kutokana na Neno hili Kun na maneno mengine ya Allah Subhanah wa Ta’ala.’
‘Hivyo neno KuN hua ni amrisho la Kuumba (Kalimat al Amr Al Taqwin), kwani
Allah Subhnah wa Ta’ala amesema kua Nabii Isa Ibn Maryam ni Kalimati Allah, na
kila kilichoumbwa hua ni kutokana na Kalimati Allah, na hivyo basi Allah Subhanah
wa Ta’ala hatumii neno zaid ya KuN katika Kuumba kwake, hili ni neno ambalo
linalobainisha kuwepo kwake na kuwepo kila kitu chake’
Katika aya hii pia Allah Subhanah wa Ta’ala anamwambia Maryam Bint Imran kua
Kalimati Allahi huyo atakua ni Masih atakaeitwa kwa jina la Isa Ibn Maryam. Ambapo
neno Masih hua ni lenye kutokana na neno Masaha ambalo hua linamaaisha Kupangusa,
Kufuta, Kupapasa kwa Utaratibu, Kupakaza Kitu, Kupaka kitu kwenye Mwili, Kupitisha
Mkono juu ya Kitu, Kupendeza, kua Nzuri na yenye Baraka na pia humaanisha Kufunga
safari ya Kutembea ardhini.
Hivyo Nabii Isa Bint Maryam ameitwa Masih kwa sababu alikua ameshaandikiwa kua
atakua ni mwenye Kutembea kwa unyenyekevu katika sehemu mbali mbali Ardhini kwa
ajili ya kufikisha Ujumbe wake kwa Makabila tofauti ya watu wa Bani Israil yaliyokua
yametawanyika katika sehemu mbalimbali ardhini ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala
amezizungumzia kua amewajaalia Isa Ibn Maryam na Maryam Bint Imran kua ni Makazi
kwa ajili yao pale aliposema katika aya ifuatayo:
﴿وَجَعَلْنَا ٱبْنَ مَرْيمََ وَأُم َّهُ آيَةً وَآوَيْنَاهمَُآ إِلىَٰ رَبْوَةٍ ذَاتِ قَرَارٍ وَمَعِينٍ ﴾
WajaAAalna ibna maryama waommahu ayatan waawaynahuma ila rabwatin dhati
qararin wamaAAeenin(Surat Al Muuminuun 23:50)
Tafsir: Na tumemjalia Ibn Maryam na Mama yake kua ni Dalili. Na tukawapa makazi
katika Ardhi iliyojuu sehemu ya usalama na amani na chemchem.
449
Na kwa upande mwengine basi tunaona kua Neno Masih kwa Lugha ya Kiyahudi hua
linamanisha kua ni Mfalme au Muokozi anaetegemewa.
Kisha aya inatuonesha kua Allah Subhanah wa Ta’ala anambainishia Maryam Bint Imran
kuhusiana na Utukufu wa Tunukio la Mtoto atakaempata kua atakua ni miongoni mwa
Minna Al Mukarrabin yaani watakokua karibu nae Allah Subhanah wa Ta’ala na
kumalizia kwa kusema kua:
﴿وَيُكَلِّمُ ٱلن َّاسَ فىِ ٱلْمَهْدِ وَكَهْلاً وَمِنَ ٱلص َّالحِِينَ ﴾
Wayukallimu alnnasa fee almahdi wakahlan wamina alssaliheena; (Surat Al Imran
3:46)
Tafsir: Na atazungumza na watu kutoka kwenye Kitenga cha Watoto wadogo na
Ukubwani na atakua ni miongoni mwa waja wema.
Ingawa kuna hadith ya Abu Hurayrah kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kua watoto watatu walizungumza kwenye Mikoba ya kubebea watoto ambao
ni Isa, Mtoto alieishi kwenye wakati wa Jurayj na Mtoto wa Mwanamke alietupwa
kwenye shimo la As-hab al Uhdud’
Ambapo tunapozungumzia Mtoto wa Kisa cha Jurayj basi amesema Abu Hurayrah Radhi
Allahi Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua hakuna
mtoto aliezungumza kwenye Mikoba ya kubebea watoto isipokua ni Isa Ibn
Maryam na sahaba yake Jurayj.’ Hivyo Abu Hurayrah Radhi Allahu Anhu akasema:
‘Ya Rasul Allah, Hivi jee huyu Sahaba wa Jurayj ndio nani?’
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Jurayj alikua ni Mtawa ambae
alikua akiishi katika eneo la nyumba ya kitawa peke yake. Ambapo katika eneo
alilokua akiishi kulikua kuna Mfugaji ambae alikua akitembelea katika eneo hilo
na mmoja kati ya Wanawake wa Kijijini hapo alikua pia akitembelea eneo hilo kwa
ajili ya kumtembelea Mfugaji huyo.’
Hivyo siku moja akaja mama yake Jurayj wakati Jurayj akiwa ndani ya Sala na
kumwita: ‘Ewe Jurayj!’
Hivyo Juray akajiuliza: ‘Mama yangu au Sala yangu?’hivyo akona bora amaliza
Sala yake, kisha mama yake akaita tena: ‘Jurayj!’ Jurayj akajiuliza tena: ‘Mama
yangu au Sala yangu?’ na akaona kua bora amalize Sala yake. Mama yake akaita
450
tena mara ya tatu: ‘Jurayj!’ Jurayj akajiuliza tena: ‘Mama yangu au Sala yangu?’
na akaona kua bora amalize Sala yake.’
Hivyo baada ya kua Jurayj hakumjibu mama yake basi mama yake akasema: ‘Ewe
Jurayj, Namuomba Allah asikujaalie Ufe hadi pale utakapotizama nyuso za
Wanawake waovu’ na kisha mama yake Jurayj akaondoka.’
Na baada mda yule Mwanamke wa Mji huo, akaletwa mbele ya Mfalme wa mji huo
baada ya kujifungua Mtoto, ambapo akaulizwa Mwanamke huyo, ‘Huyu Mtoto
Baba yake ni Nani?’ ambapo yule Mwanamke akasema: ‘Baba yake ni Jurayj’
Mfalme akauliza: ‘Jurayj yule Mtawa?’ Mwanamke akasema: ‘Naam.’
Mfalme akaamrisha kwa kusema: ‘Nendeni mkaivunje Nyumba yake na kisha
mlete mbele yangu’
Hiyvo watu wakaenda kwenye Nyumba ya Jurayj na kuivunja vunja yote, na kisha
wakamkamata Jurayj na kufunga kamba mikono yake shingoni mwake na
kumpeleka mbele ya Mfalme, hivyo wakati anapelekwa mbele ya Mfalme basi
akawa ni mwenye kuwaona Wanawake waovu na kutabasam.
Alipofika mbele ya Mfalme basi Mfalme akamuuliza Jurayj: ‘Hivi Jee Unayajua
madai ya Mwanamke huyu?’ Jurayj akauliza: ‘Ana madai gani?’
Mfalme akasema: ‘Anadai kua wewe ndie Baba wa Mtoto wake.’ Jurayk
akamuuliza Mwanamke huyo: ‘Yuko wapi huyo Mtoto wako?’ Watu wakasema:
‘Yuko chubani mwake’ Hivyo Jurayj akapelekwa kwenye chumba cha Mtoto huyo
na alipomuona mtoto huyo basi akamuuliza: ‘Jee ni Nani Baba yako?’ Mtoto
akajibu: ‘Baba yangu ni Mfugaji’
Kutokana na Majibu hayo basi Mfalme akasema: ‘Jee tukujengee Nyumba tupya kwa
Dhahabu?’ Jurayj akasema: ‘La’ Mfalme akauliza: ‘Kwa Fedha?’ Jurayj akasema:
‘La’ Mfalme akauliza: ‘Jee tuijenge kwa kitu gani?’ Jurayj akasema: ‘Ijengeni
kama ilivyokua hapo mwanzo’ Hivyo Mfalme akaamrisha kua nyumba ya Jurayj
ijengwe upya kama ilivyokua hapo awali.
Kisha Jurayj akatabasamu, na alipotabasam basi Mfalme akamuuliza Jurayj: ‘Kitu
gani kilichokufanya uwe ni mwenye Kutabsam?’
Jurayj akajibu: ‘Kuna kitu ambacho nimekitambua, Laana ya Mama yangu
imenipitia’ na kisha akamuelezea Mfalme juu ya ya yaliyotokea(Imam Bukhari)
451
Ambapo katika Hadithi hii basi tunaona kua Ingawa Rasul Allah Salallahu A’layhi wa
Salam alisema kua: ‘Mtoto inabidi anatakiwa anasibishwe na Kitanda na hivyo
mzinifu hua hana Mtoto.’(Bukhari na Muslim)
Na hivyo hadithi hii ya kua Kitanda cha wana Ndoa hakizai Haramu kua ni yenye
kutumika katika kutoa Fatwa isemayo kua: ‘Mtoto wa nje ya Ndoa hua hawezi
kunasibishwa na nasaba ya Mwanamme aliezini na Mwanamke, hata kama Mzinifu
huyo Mwanamme akikubali kua Mtoto huyo ni wake’ ambao huu ndio mtizamo
Unaokubalika zaidi miongoni mwa Wanazuoni kwani una makubalino juu yake.
Lakini kwa upande mwengine basi tunaona kua kuna mitizamo miwili tofauti, kwani
mbali ya mtizamo huo wa kwanza kua haikubaliki kumnasibisha Mzinifu wa kiume na
Mtoto wa Zinaa hata kama Mzinifu akikubalikua ni wake lakini kwa upande mwengine
kuna Wanazuoni ambao wana mtizamo tofauti kuhusiana na jambo hili na hii ni kutokana
na uthibitisho wa Hadith hii ya kisa cha Jurayj.
Kwani anasema Imam Ibn Qudamah Al Maqdisi kua: ‘Kwa upande wa Wanazuoni
wakubwa wa Fiqh wa kizazi cha mwanzoni mwa Uislam katika kipindi cha Tabiina
kama Urwa Ibn Az Zubayr, Sulayman Ibn Yasir, Hasan Al Basr, Muhammad Ibn
Sirin, Ibrahim An Nakhai na Is-haq Ibn Rahawayh basi wao wanasema kua: ‘Kama
Mzinifu Mwanamme akikubali kua Mtoto ni wake basi inakubalika kunasibishwa
nae.’
Na huu pia ndio mtizamo wa Shaykh Ibn Taymiyyah na Imam Ibn Al Qayyim, Shaykh
Muhammad Rashid Rida na pia Shaykh Muhammad Ibn Uthaymin, na hii ni kwa sababu
ya uthibitisho wa Mtoto wa Hadithi ya Jurayj ambae amejinasibisha na Mfugaji Kondoo
kupitia katika njia ya Miujiza ya usemaji wa Mtoto huyo kwa idhini ya Allah Subhanah
wa Ta’ala japo kua Mtoto huyo alitokana na kitendo cha Zina,
Na hivyo hii inaonesha kua inakubalika kumnasibisha Mtoto na Baba yake huyo kama
Baba atamkubali hata kama ni wa Zina, na hii ni kwa sababu Malengo ya Shariyah za
Allah Subhnah wa Ta’ala ni kuhifadhi Kizazi na kusimamia haki za watoto na kuwalea
katika hali nzuri na ya uongofu.
Hivyo basi kama itakua mtoto husika atakua ni mwenye kukosa malezi ya Kiislam na
huduma za kijamii pale itakapokua anahesabiwa kua ni Mtoto wa nje, basi hua kulingana
na mtizamo wa Wanazuoni hawa basi tunaona kua inakubalika kumnasibisha na Baba
yake hata kama ni wa nje ya Ndoa kama Baba atakubali kua ni Mtoto wake kwa ajili ya
kusimamia Msalahi yake mtoto husika ya kidunia na Kiakhera.
Ambapo kwa upande wa Encyclopedia Ya Fiqh ya Kiislam inayochapishwa nchini
Kuwait basi inasema kua: ‘Imam Is-haq Ibn Rahawayh, ibn Taymiyyah na wengineo
452
ni wenye kua na mtizamo usemao kua: ‘Uhusiano wa kinasaba baina ya Mtoto wa
Zina na Mwanamme aliezini na Mwanamke ambae hajamuoa hua unathibitishwa
kwa sababu kuzini kwake nae kumethibitishwa tayari. Hivyo kama ilivyo katika
kunasibishwa kwa uhusiano wa Mama, basi na uhusuiano wa Mzinifu pia
unathibitishwa, na hivyo nasaba yake mtoto huyo kutopotea na kutodhurika
kutokana na kosa la aibu la dhambi ambayo halimhusu mtoto huyo, kama
anavyosema Allah Subhanah wa Ta’ala’’
﴿وَلاَ تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْ رَىٰ ﴾
Wala taziru waziratun wizra okhra (Surat Al Isra 17:15 )
Tafsir: Na hakuna mbebaji atakaebeba mzigo wa mwenzake.
Ambapo mtizamo huu hua unalazimisha pia mirathi baina ya Mtoto na Mzinifu
huyo kuwepo kutokana na uthibitisho wa Nasaba, kwa sababu mirathi hua ni yenye
kusimamia misingi ya unasaba, na Wanazuoni hawa wamethibitisha hili katika hali
iliyotajwa.
Na mbali ya Hadith hio ya Jurayj lakini hata hivyo pia kuna hadithi isemayo kua
‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: Watoto wanne
Wamezungumza ndani ya mkoba wa kubebea Watoto wachanga ambao ni : Mtoto
wa Msusi wa Fir’awn, Shahidi wa Nabii Yusuf, Mtoto wa kisa cha Jurayj na Isa Ibn
Maryam.’
Ambapo mbali ya hivyo lakini pia Allah Subhanah wa Ta’ala amemsifu Nabii Isa kabla
ya kuzaliwa kwake kua atakua ni mwenye kuzungumza hadi ukubwani mwake, katika
kipindi cha Kahlan ambacho ni kipindi baina ya Ujana na Utu Uzima. Kwani neno
Kahlan linatokana na neno Kahala ambalo hua linamanisha Kufukia Umri wa Kupea na
Kukomaa Kiakili yaani kuanzia baina ya miaka 30 hadi 60.
Na hii haimaanishi kua Nabii Isa atazungumza Ukubwani kama ilivyo kawaida ya
kuzungumza mimi na wewe kama tulivyo Ibn Adam wengine na hivyo kua hakuna mana
yeyote ndani yake maneno haya. La! Kwani aya haikumaanisha hivyo bali imeamaanisha
kua Nabii Isa atakua ni mwenye kuzungumzia kuhusiana na Kalimat Allah yaani maneno
ya Allah Subhanah wa Ta’ala tangu mara tu baada ya kuzaliwa kwake wakati yupo
kwenye Kitenga cha Mtoto Mchanga hadi atakapofikia ukubwani mwake.
453
Na hivyo hapa Allah Subhanah wa Ta’ala anabainisha kua Nabii Isa Ibn Maryam ataishi
na kupita umri wa miaka 40, na katka kipindi chote hicho basi atakua ni miongoni mwa
Minna al Salihiin yaani Waja wema wenye kufanya Mema.
Ambapo baada ya Malaika Jibril kumbainishia Maryam Bint Imran ujumbe wake huo
kuhusiana na Utukufu wa Tunukio hilo ambalo ni lenye Uzito mkubwa sana na hikma
kubwa sana ndani yake basi Maryam Bint Imran akatulia huku akitafakkari kuhusiana na
utukufu wa Tunukio hilo atakalojaaliwa kutokana na Utukufu wake mbele ya Allah
Subhanah wa Ta’ala na hivyo akawa ni mwenye kujawa na mshangao mkubwa zaidi
kutokana na Tunukio hilo kutoka kwa Mola wake.
Kwani ingawa tukio la mwanzo la kutokewa na Malaika Jibril mbele yake halikumshtua
wala kumshangaza sana Maryam Bint Imran lakini hata hivyo bashirio la ujumbe wake
zikamshtua na kumshangaza sana Maryam Bint Imran, kwa sababu ingawa yeye anamjua
Mola wake, na hivyo kujua kua ndie pekee mwenye uwezo wa kumjaalia kiumbe kua na
uwezo wa kupata Mtoto, lakini hua ni baada ya Mja huyo kua ni mwenye kuingiliana na
Mwanamme kama ni Mwanamke au kua ni Mwenye kuingiliana na Mwanamke kama
mja huyo ni Mwanamme, hata hivyo hajawahi yeye kusikia kua kuna Mwanamke ambae
amepata ujauzito bila ya kuingiliana na Mwanamme, sasa itakuaje kwa kwake yeye
ambae hana Mume, wala hajawa na hamu ya kua na Mume na wala hajawahi kua na
ukaribu wala kuingiliwa na Mwanamme yeyote kua ni mwenye kuja kupata Mtoto, bila
ya shaka haya ni masuali ambayo ni ya kimaumbile kwa kiumbe Ibn Adam hivyo
haishangazi kuona kua Maryam Bint Imran anauliza masuali haya kutokana na maumbile
yake.
Hivyo Maryam Bint Imran akadhidhirsha Mshangao wake huo wa kimaumbile baada ya
kutafakkar kwake na hivyo akauliza kama zinavyosema aya:
﴿قَالَتْ أَنى َّٰ يَكُونُ لىِ غُلاَمٌ وَلمَْ يمَْسَسْنىِ بَشَرٌ وَلمَْ أَكُ بَغِيّاً ﴾
Qalat anna yakoonu lee ghulamun walam yamsasnee basharun walam aku
baghiyyan; (Surat Maryam 19:20)
Tafsir: Akasema (Maryam Bint Imran) kua: ‘Nitakua na Mtoto wa kiume mimi
wakati sijawahi kuguswa na mtu yeyote (Mwanamme) na wala mimi si Mwanamke
mwenye kutembea na Wanaume?’
Hapa tunaona kua Maryam Bint Imran anajitambulisha na kujitetea Mbele ya Malaika
Jibril kwa kusema kua yeye si Baghiya hivyo itakuaje apate Mtoto? ambapo neno
Baghiya hua ni lenye utokna na neno Bagha ambalo hua linamaanisha Kuvuka Mipaka,
454
Kufanya Uovu, Kuendekeza Matamanio, Kua Mwenye Kufanya Dhulma, Kutokua na
Haya, Kufanya mambo ya Aibu na pia hua inamanisha Kila Kitu ambacho si kitu Kiovu
tu kinachoonekana na kuhisikana na kuchukiwa na watu wengine lakini pia hua
kinamaanisha Kitu kiovu Kinachosababisha Madhara.
Neno Bagha ndio lililotoa neno Baghia ambalo hua linamaanisha pia linamaanisha kua
Uzinifu, Umalaya, Uasharati, Kuendekeza Matamanio.
Sultan Al Mutakkalimin Mujaddid Ad Din Imam Al Ghazali Al Thani Imam Fakhr Ad
Din Al Razi anasema kuhusiana na maneno haya ya Maryam Bint Imran kua: ‘Kwanini
hapa Maryam Bint Imran anasema kua yeye si Malaya? Jibu la suali hili ni kua
pale Maryam Bint Imran aliposema: ‘Sijawahi Kuguswa na Mwanamme’ alikua
akimaanisha kua: ‘Hajaolewa’ na hivyo ikabidi pia aongezee kwa kusema kua na
wala yeye si Mwanamke Malaya’
Hivyo baada ya kutoa hoja hio basi Malaika Jibril akasema kumwambia Maryam Bint
Imran kua:
﴿قَالَ كَذٰ لِكَ قَالَ رَب ُّكَ هُوَ عَلَى َّ هَينٌِّ وَلِنَجْعَلَهُ آيَةً لِّلْن َّاسِ وَرَحمَْةً مِّن َّا وَكَانَ أَمْ راً
م َّقْضِيّاً ﴾
Qala kadhaliki qala rabbuki huwa AAalayya hayyinun walinajAAalahu ayatan
lilnnasi warahmatan minna wakana amran maqdhiyyan; (Surat Maryam 19:21)
Tafsir: ‘Akasema (Malaika Jibril): ‘Kadhalika hivyo ndivyo alivyosema Mola wako:
‘Hivyo ni rahisi sana juu yangu mie’’Na tutamjaalia kua dalili kwa Watu na Rehma
kutoka kwetu, na ni Jambo ambalo tayari limeshatakiwa liwe’
Ambapo neno Hayyinun hua linatokana na neno Hana lenye kumaanisha Kua Rahisi,
Kua Jepesi, Kua na Udhaifu, Kufanyika kwa urahisi, Kua Kimya. Neno Hana pia ndio
lililotoa neno Ahana ambalo hua linamaanisha Kuchukiza, Kochokoza au Kuadhirisha.
Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anabainisha kua kwake yeye kufanya hivyo
kumjaalia Maryam Bint Imran kupata Mtoto bila ya kukutana na Mwanamme hua ni
Jambo dogo na ni rahisi sana.
Kama vile alivyoweza kumjalia kupata Ujauzito Sarah Mke wa Nabii Ibrahim, Nabii
Zakarriya na Isha Bint Faqudh na pia Mzee Imran na Hannah Bint Faqudh pale
455
Wanawake wote hao walipokua tasa na waume zao wakiwa wazee sana. Allah Subhanah
wa Ta’ala anaendelea kumuelezea Nabii Isa Ibn Maryam katika aya hizi kwa kusema kua
Na atamjaalia kua ni dalili ya uthibitisho kwa Watu na Rehma kutoka kweke, kwani hilo
ni Jambo ambalo tayari limeshatakiwa liwe.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anaendelea kumbainishia Nabii Muhammad Salallahu
Alayhi wa Salam juu ya habari za Ghayb kwa kina juu ya Maryam Bint Imran na
kubashiriwa kwake kushika Mimba ya Nabii Isa kua kunatokana na kutaka kwake yeye
iwe hivyo kwani yeye ndie Muumba wa kila kitu kama zinavyoendelea kufafanua aya za
Surat Al Imran kwa kusema:
﴿قَالَتْ رَبِّ أَنى َّٰ يَكُونُ لىِ وَلَدٌ وَلمَْ يمَْسَسْنىِ بَشَرٌ قَالَ كَذٰ لِكِ ٱهلل َُّ يخَْلُقُ مَا يَشَ آءُ
إِذَا قَضَى ٰ أَمْراً فَإِنم ََّا يَقُولُ لَهُ كُنْ فَيَكُونُ ﴾
Qalat rabbi anna yakoonu lee waladun walam yamsasnee basharun qala kadhaliki
Allahu yakhluqu ma yashao idha qadha amran fa-innama yaqoolu lahu kun
fayakoonu; (Surat Al Imran 3:47)
Tafsir: Akasema (Maryam Bint Imran): ‘Ewe Mola wangu itakuaje mimi niwe na
Mtoto, wakati sijawahi kuguswa na Mtu yeyote?’ Akasema (Allh Subhanah wa
Ta’ala): ‘Kadhalika hivyo ndivyo Allah anavyoumba atakacho, kwani anapotaka
jambo liwe basi hua ni mwenye kukiambia kitu hicho Kua na hivyo Kinakua’
Hapa tunaona kua kuna hali ya mtizamo tofauti ya mazingira ya mazungumzo
yaliyoelezewa na yale ya kwenye aya ya Surat Maryam 19:20 kwani wakati kule kulikua
kuna mazungumzo baina ya Maryam Bint Imran na Malaika Jibril katika aya hizi tunaona
kua moja kwa moja Maryam Bint Imran akiwa anazungumza na Mola wake yaani Allah
Subhanah wa Ta’ala kwa kurudisha hoja yake kwa Mola wake kutokana na maumbile
yake na hali ya mazingira yake anayoishi.
Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anambainishia Maryam bint Imran kua katika tukio
hili, kutokana na Utukufu wake Maryam Bint Imran na utukufu wa Mtoto wake yaani Isa
Ibn Maryam basi kutakua na upekee wa Miujiza ya Kimaumbile juu ya kile
kilichokadiriwa kiwe kua kitakua, kama inavyotakiwa kiwe na hii ni kwa sababu ya
Malengo na makusudio ya hicho kinachotakiwa kiwe, yaani Tunukio la kile kilicho bora
asichokitarajia na bila ya shaka Allah Subhanah wa Ta’ala hakutuwacha tukawa ni wenye
kujiuliza bila ya kujua ilitumika njia gani kufanikisha hilo kwani Qur’an inatubainishia
njia iliyotumia katika kumtunukia kwake huko kutokana na maumbile yake katika aya
isemayo:
456
﴿وَمَرْيمََ ٱبْنَةَ عِمْرَانَ ٱل َّتيِ ۤ أَحْصَنَتْ فَرْجَهَا فَنَفَخْنَا فِيهِ مِن ر ُّوحِ نَا وَصَد َّقَتْ
بِكَلِمَاتِ رَب َّهَا وَكُتُبِهِ وَكَانَتْ مِنَ ٱلْقَانِتِينَ ﴾
Wamaryama ibnata AAimrana allatee ahsanat farjaha fanafakhna feehi min
roohina wasaddaqat bikalimati rabbiha wakutubihi wakanat mina alqaniteena
(Surat At Tahrim 66:12)
Tafsir: Na Maryam Bint Imran ambae alijihifadhi sehemu zake za Siri, kisha
tukampulizia ndani yake Roho kutoka kwetu, na akathibitisha Kauli ya Mola wake na
Vitabu vyake, na alikua ni miongoni mwa wenye Kumcha Mungu.
Tunapoiangalia Ayah hii basi tunaona kua imetumia neno Ahssanat ambalo hua
linamaanisha Kukilinda Kitu, Kukihifadhi kisipatikane, au Kisiharibiwe, Kukiwekea
Ngao au Ngome Imara.
Na pia ikatumia neno Farjaha ambalo hua linatokana na neno Faraja linalomaanisha
Kufungua, Uwazi, Ufa, Kutanua, Kuachia wazi sehemu iliyo baina ya Vitu viwili na pa
humaanisha Sehemu ya Siri ya Mwanamke baina ya miguu miwili.
Na hivyo Aya kua ni zenye kuweka wazi kua Maryam Bint Imran alikua ni mwenye
kujihifadhi na kujilinda kikweli hasa sehemu zake za Siri kwa sababu Allah Subhanah
wa Ta’ala sehemu hizo ni Amanah ambayo amekabidhiwa na kuamriwa kua kama
ataitumia basi na aitumie kulingana na masharti yake aliyoyashurutisha Allah Subhanah
wa Ta’ala juu ya Amanah hio.
Na kisha aya ikaendelea kubainisha namna alivyotunukiwa Maryam Bint Imran
kuhusiana na Tunu hio kwa kusema baada ya Ahsanat Farjaha kua Fanafakhna Feehi
Min Roohina yaani Kisha Tukampulizia Ndani yake Roho kutoka kwetu, ambapo hapa
hua kunamaanisha kua aidha Maryam Bint Imran alipuliziwa Roho hio kutoka kwa Allah
Subhanah wa Ta’ala ndani ya Mwili wake kwa Ujumla au kwa kupitia katika sehemu
zake za Siri ambazo zimehifidhiwa kama zilivyozungumziwa hapa au kama
walizozisema Wanazuoni yaani kwa juu baina ya Mabega na Shingo yake, wa Allahu
Aaalam.
Na ingawa hivyo ndivyo hali ilivyokua na haikuwahi kutokea kabla yake wala baada
yake kwa Ibn Adam wengine lakini hata hivyo tunapoangalia kwa upande mwengine basi
tunaona kua katika wakati wa kipindi chetu Wanasayansi wamegundua kua hali hii ya
457
uzazi hua inatokea pia kwa aina fulani ya Nyoka, Samaki na baadhi ya Wadudu ambao
wanao uwezo wa kushika Mimba na kupata watoto bila ya kuingiliana.
Baada ya Maryam Bint Imran kupiliziwa Roho hio ndani yake basi Allah Subhanah wa
Ta’ala anaendelea kumbainishia Maryam Bint Imran kuhusiana na Darja na majukumu
atakayokua nayo Nabii Isa baada ya kuzaliwa kwake kwa kuelezea kama ilivyosema
Surat Al Imran katika aya zifuatazo:
﴿وَيُعَلِّمُهُ ٱلْكِتَابَ وَٱلحِْكْمَةَ وَٱلت َّوْرَاةَ وَٱلإِنجِْيلَ ﴾
WayuAAallimuhu alkitaba waalhikmata waalttawrata waal-injeela; (Surat Al Imran
3:48-51)
Tafsir: Na (Allah Subhanah wa Ta’ala) atamfundisha Kitabu na Hikma na Taurat na
Injil.
Ambapo katika aya hii tunaona kua Allah Subhanah wa Ta’ala anaahidi kua
atamfundisha Nabii Isa Ilm ya Kitabu, ambapo ndani yake ndio mna Ilm za vitabu
walivyoletewa Mitume wengine waliotangulia kabla yake, na hapa ndio tunaona kua kwa
upande mwengine basi tunapozungumzia somo la I’lm Ul Huruf ambalo linatokana na
Vitabu vya Nabii Idrisa Alayhi Salam basi Shaykh Al Akbar Imam Abu Bakr Ibn Arabi
ana mtizamo wa kua ni somo linalojulikana pia kwa jina la I’lm Issawi.
Na pia akaahidi kua atamfundisha na Hikma, ambapo kulingana na Bahr Ul Ilm Abd
Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi anasema kua: ‘Hikma iliyokusudiwa hapa
hua inamaaanisha Hukmu na Sharia za yaliyohalalishwa na yaliyoharamishwa.’
Na kuna wasemao kua Hikma iliyozungumziwa hapa hua inamaanisha Mitizamo tofauti
kuhusiana na Ilm ya Dini ya Kiislam kupitia katika Sunna za Mitume wengine wote
waliotangulia kabla yake.
Kisha aya ikamalizia kuhusiana na ahadi ya kupewa kwa Nabii Isa Ilm ya Taurat na Injil
ambapo ingawa Taurat alishushiwa Nabii Musa kwa ajili ya kuwaongoza Watu wa Bani
Israil lakini Allah Subhanah wa Ta’ala aliahidi kua atamfundisha Nabii Nabii Isa Taurat
pia na Hukmu zake, Hivyo Nabii Isa alikua na Ilm ya Taurat na Injil pia zote mbili
sambamba, ambapo tofauti yake ni kua Maamrisho na Makatazo yaliyokuwemo kwenye
Injil yalikua ni mepesi kuliko yale yaliyokuwemo kwenye Taurat.
458
Kisha aya zinaendelea kutuelezea namna Allah Subhnah wa Ta’ala alivyokua
akimwambia Maryam Bint Imran kuhusiana na Miujiza ya Allah Subhanah wa Ta’ala
kwa Ruhi wake Isa Ibn Maryam kua:
﴿وَرَسُولاً إِلىَٰ بَنىِ ۤ إِسْرَائِيلَ ِ أَنىّ قَدْ جِ ئْتُكُمْ آبِيَةٍ مِّ ن ر َّبِّكُمْ أَنىّ ِۤ أَخْ لُقُ لَكُ مْ مِّ نَ
ٱلطِّينِ كَهَيْئَةِ ٱلط َّيرِْ فَأَنفُخُ فِيهِ فَيَكُونُ طَيرْ اً إبِِذْنِ ٱهلل َِّ وَأُبْرِئُ ٱلأَكْمَهَ وٱلأَ بْرَ َص
وَأُحْيِى ٰ ٱلْمَوْتَى إبِِذْنِ ٱهلل َِّ وَأُنَبِّئُكُمْ بمَِا أتَْكُلُونَ وَمَا تَد َّخِ رُونَ فىِ بُيُوتِكُمْ إِن َّ ِفى
ذٰلِكَ لآيَةً ل َّكُمْ إِن كُنتُم م ُّؤْمِنِينَ ﴾
Warasoolan ila banee isra-eela annee qad ji/tukum bi-ayatin min rabbikum annee
akhluqu lakum mina altteeni kahay-ati alttayri faanfukhu feehi fayakoonu tayran
bi-idhni Allahi waobri-o al-akmaha waal-abrasa waohyee almawta bi-idhni Allahi
waonabbi-okum bima ta/kuloona wama taddakhiroona fee buyootikum inna
fee dhalika laayatan lakum in kuntum mu/mineena (Surat Al Imran 3:49)
Tafsir: Na tutamfanya Isa kua Mtume wa watu wa Bani Israil (Mwenye Kusema)
‘Nimekuja kwenu nikiwa na Vithibitisho kutoka kwa Mola wenu. Hivyo
nitakutengenezeeni kutokana na udongo kua kama Ndege na kisha nitampulizia, na
atakua Ndege aliekua hai kwa idhini ya Allah (Subhanah wa Ta’ala). Na
nitamponesha aliezaliwa Kipofu na mwenye Ukoma na nitawakhuisha waliokufa kwa
Idhini ya Allah, na nitakuambieni mtakachokula na mlichohifadhi Majumbani
mwenu. Kwa hakika katika haya kuna Vithibitisho kama kweli nyinyi ni wenye
Kuamini’
Naam, hii ni miongoni mwa aya ambazo zinatuonesha na kuthibitisha kua Nabii Isa
alikua ni Nabii na Mtume wa watu wa Bani Israil kwa ajili ya kuja kuendeleza na
kusimamia maamrisho yaliyomo ndani ya Taurat na Injil, na hivyo Allah Subhanah wa
Ta’ala anawataka watu wa Bani Israil kutokana na vithibitisho vyake atakavyokuja
navyo basi wawe ni wenye kufuata maamrisho yake kama kweli wao ni wenye
kumuamini Allah Subhanah wa Ta’ala.
Ambapo ndani yake vithibitisho hivyo pia ni Miujiza ya kua na uwezo wa kutengenezea
Ndege wa Udongo na kisha atakapompulizia basi Ndege huyo atakua hai kwa Idhini ya
Allah Subhanah wa Ta’ala na kuruka hewani.
459
Ambapo hii ni kwa sabau Nguvu za Kiroho za Nabii Isa ni zenye uwezo mkubwa sana
kwa sababu maumbile ya Roho yake yanatokana na kupuliziwa tumboni Mama yake
moja kwa moja, hivyo ni mwenye kua na uwezo mkubwa wa kiathari katika uwezekano
wa kuwasiliana moja kwa moja na Roho za viumbe wengine tofauti na walivyo viumbe
wengine wa kawaida.
Kiasi ya kua kwake yeye Nabii Isa ilikua rahisi kuufinyanga Udongo na kisha
Kumuomba tu, idhini ya Allah Subhanah wa Ta’ala ya kua baada ya kuupulizia Udongo
bsi uingizwe ndani yake Roho ya ndege ambayo iliyokua tayari imeshaumbwa na
inasubiri kuingizwa kwenye mwili wake ndege huyo alioufinyanga Nabii Isa. Na hii pa
hua kwa waliokufa pia pale alipopewa uwezo wa Kuwafufua kutokan na Idhini ya Allah
Subhanah wa Ta’ala
Na pia atakua na uwezo wa Kumponesha Kipofu kwa njia ya kumuwekea mkono na
kumpangusa usoni mwake, na pia kuwaponesha wanaoumwa na Ukoma kwa
kuwapangusa sehemu za mwili zilizoathirika na Maradhi hayo ambapo nao watakua ni
wenye kupona kutokana na mpanguso huo wa mikono yake, na hili pia hua ni miongoni
mwa maana ya jina lake la Al Masih.
Hii ni Miujiza maalum kwa ajili ya Nabii Isa Ibn Maryam ambayo Allah
Subhanah wa Ta’ala alimjaalia kua na uwezo nayo, kulingana na mazingira yake
atakayokua akiishi katika jamii za watu wao waliokuwepo katika wakati huo,
kwani huu ulikua ni wakati wa umahiri mkubwa sana wa fani ya Utabibu,
ambapo hata hivyo mbali ya kua na Wataalamu wa fani ya tiba lakini hakukua
na watu wanaoweza kutibu maradhi kama hayo, ambapo hii inakua kama vile
ilivyokua katika wakati wa kipindi cha Nabii Musa wakati watu wa Misri na
Bani Israil walipokua wamebobea katika fani ya Uchawi, hivyo Allah Subhanah
wa Ta’ala akampa Nabii Musa Miujiza ya Fimbo na myengineo, ili kukabiliana
nao na kuwathibitishia watu wake ukweli wa Ujumbe wake.
Kisha Allah Subhnah wa Ta’ala anasema kuhusiana na Muujiza mwengine mkubwa
atakaouonesha Nabii Isa ni kua atakua ni mwenye Kufufua watu waliokufa,
kuwahalalishia baadhi ya mambo ambayo waliharamishwa watu wa Bani Israil ndani ya
Taurat, na hivyo kua ni mwenye kuthibitisha juu ya kile alichokuja nacho kwenye Injil
na hivyo kutilia mkazo kua watu hao wa Bani Israil kua wanatakiwa warudi kwa Mola
wao, kama zinavyosema aya:
460
﴿وَمُصَدِّقاً لِّمَا بَينَْ يَدَى َّ مِنَ ٱلت َّوْرَاةِ وَلِأُحِ ل َّ لَكُمْ بَعْضَ ٱل َّذِى حُرِّمَ عَلَيْكُمْ
وَجِ ئْتُكُمْ آبِيَةٍ مِّن ر َّبِّ كُ مْ فَ ٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَأَطِيعُ ونِ ۞إِن َّ ٱهلل ََّ رَبىِّ وَرَب ُّكُمْ فَٱعْبُدُوهُ هَٰذَ ا
صِرَاطٌ م ُّسْتَقِيمٌ ﴾
Wamusaddiqan lima bayna yadayya mina alttawrati wali-ohilla lakum baAAdha
alladhee hurrima AAalaykum waji/tukum bi-ayatin min rabbikum faittaqoo Allaha
waateeAAooni; Inna Allaha rabbee warabbukum faoAAbudoohu hadha siratun
mustaqeemun (Surat Al Imran 3:50-51)
Tafsir: (Na atasema Nabii Isa): ‘Nimekuja kuthibitisha kile ambacho kimekuja kabla
yangu kilchomo ndani ya Taurat na kukuhalalishieni sehemu ambayo imeharamishwa
kwa ajili yenu. Na nimekuja kwenu na Uthibitisho kutoka kwa Mola wenu. Hivyo
Muogopeni Allah na Nifuteni. Kwa hakika Allah ni Mola wangu na Mola wenu hivyo
Muabuduni (yeye peke yake msimshirikishe). Hii ndio njia iliyo sahih’
Ambapo hapa tunaona kua Nabii Isa atakua ni mwenye kuwahalalishia watu wa Bani
Israil baadhi ya vile vilivyoharamishwa kwenye Taurat na hivyo basi hii haimaanishi kua
Vitabu viwili hivi Taurat na Injil kua vinapingana la, bali kuna baadhi ya Maamrisho ya
Taurat yamekuja kubatilishwa na baadhi ya maamrisho yaliyomo ndani ya Injil. Na hivyo
kumaanisha kua Watu wa Bani Israil walikua wanatakiwa wawe ni wenye kufuata
mitizamo mipya iliyomo kwenye Injil.
Hivyo baada ya Maryam Bint Imran kubainishwa yote hayo, juu ya Utukufu na umuhimu
wa Majukumu ya Mtoto wake huyo na namna atakavyopatikana ndani ya mwili wake
basi Malaika Jibril akaipulizia Nguo yake Maryam Bint Imran na kuna Mtizamo usemao
kua Malaika Jibril alimpulizia Maryam Bint Imran kwenye Shingo yake na hivyo
Mpulizio huo ukaingia Mwilini mwake, na katika hali ya kimiujiza basi Mwili wake
ukabeba ujauzito wa Isa Ibn Maryam kama anavyosema Allah Subhana wa Ta’ala katika
Qur’an:
﴿فَحَمَلَتْهُ فَٱنْتَبَذَتْ بِهِ مَكَاً قَصِيّاً ﴾
Fahamalat-hu faintabadhat bihi makanan qasiyyan (Surat Maryam 19: 22)
461
Tafsir: Na kisha ikatunga na kuibeba (Mimba hio ya Isa Ibn Maryam) na akajitenga
pamoja nae (Isa Ibn Maryam ndani ya Mwili wake) katika makazi ya kipekee.
Ambapo anasema Imam Wahb Ibn Munabih kua: ‘Wakati Mayram Bint Imran
alipobeba Ujauzito wa Isa Ibn Maryam basi dalili za ujauzito zikaanza kujionesha
na hivyo Maryam Bint Imran akahama kutoka Nasira na kuhamia katika maeneo
ya Bayt Al Lahm (Nyumba ya Nyama au Bethlehem) ili kua mbali na watu wake
wengine’
‘Na mara ya kwanza Maryam Bint Imran alipomhisi Isa Ibn Maryam ndani ya
mwili wake, ilikua yuko pamoja na Yusuf wakati walipokua wakielekea kwenye
Nyumba ya Ibada iliopo kwenye Mlima wa Zayuni, kwani wao ndio waliokua
wasimamizi wa Nyumba hio, na ilikua hakuna watu wacha Mungu zaidi yao. Hivyo
Yusuf alipojua kuhusiana na Ujauzito huo basi alishtuka sana, kwani hili lilikua ni
jambo la aibu sana kwake na kwa Maryam Bint Imran, na hakujua achukue hatua
gani.’
‘Kwani alipokua akitaka kumtuhumu, basi alishindwa kutokana na Ucha Mungu
wake, na kutokua na hali ya kutofanya makosa kwake, na kutokana na kua kila
wakati alikua pamoja nae, na hakuwahi hata mara moja kumuona akifanya
dhambi, hivyo alipoona kua ujauzito unaonesha basi akaamua kumwambia: ‘Kuna
jambo ambalo limo akilini mwangu kuhusiana nawe, na nimejitahid kulificha na
kujizuia lakini nimeshindwa, hivyo nimeona kua bora nilidhihirishe ili nipunguze
uzito kifuani mwangu. Hivyo niambe ewe Maryam, hivi Jee Mti huweza kuota bila
ya kupandikizwa kwa mbegu?’
Maryam akajibu: ‘Naam’
Yusuf akauliza: ‘Hivi Jee Mmea unaweza kuota bila Mvua?’
Maryam akajibu: ‘Naam!’
Yusuf akauliza: ‘Hivi jee inawezekana kuwepo kupatikana kwa Mtoto bila ya
kuwepo kwa Baba?’
Maryam akajibu: ‘Hivi Yusuf Jee wewe hujajifunza kua Allah Subhnah wa Ta’ala
aliisababisha Miti kukua bila ya kuwepo Mbegu zake katika siku aliyoiumba Miti
hio na hivyo Miti yote iliyofuatia ilitokana na mbegu zilizozalishwa na Miti hio?
Na Jee hukujifunza kua Allah Subhanah wa Ta’ala aliifanya Miti ikue bila ya
kuwepo Maji? Na kisha ndio makadirio ya Allah Subhanah wa Ta’ala yakafanya
Mvua kua ndo Uhai wa Miti baada ya kuiumba katika hali tofauti? Au wewe
462
unasema kua Allah Subhana wa Ta’ala hawezi kuiotesha Mimea hadi apate msaada
wa Maji?’
Hivyo Yusuf akasema: ‘La kwa hakika mimi sisemi hivyo bali nnasema kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala anaumba akitakacho na anapotaka kitu kiwe basi husema kwa
kukiambia tu Kua na Kinakua’’
Hivyo Maryam Bint Imran akasema: ‘Sawa ila Jee hukujifunza wewe kua, Allah
Subhanah wa Ta’ala alimuumba Adam na Hawa bila ya kuwepo kwa Mke na
Mume?’ Yusuf akasema: ‘Naam bila ya Shaka!’ kisha baada ya kujibu suali hilo
basi Yusuf ikamjia akilini kua kwa vyovyote vile itakavyokua basi hali aliyokua
nayo Maryam Bint Imran itakua ni moja kwa moja kutokana na Miujiza ya Allah
Subhanah wa Ta’ala juu yake Maryam Bint Imran, na hivyo haikubaliki kwake
yeye Yusuf kua ni mwenye kumuuliza Maryam Bint Imran kuhusiana na hali
aliyokua nayo.’
Hivyo habari hii ya Ujauzito wa Maryam Bint Imran kawa ni siri ndani ya familia yake
yaani baina yake yeye Yusuf na Nabii Zakarriyah mkewe ambae ni Isha Bint Faqudh
kwani watu wa Bani Israil wakijua basi watasema kua Yusuf amezini nae Maryam Bint
Imran kwa sababu mda wote wako pamoja na Maryam hakutani na Mwanamme yeyote
isipokua na Yusuf ambae ndie Mlezi wake.
Siku moja Maryam Bint Imran alienda kumtembelea Isha Bint Faqudh ambapo katika
kipindi hiki Isha bint Faqudh alikua na Ujauzito wa Nabii Yahya. Hivyo Maryam Bint
Imran aliposalimiana na Isha Bint Faqudh basi Isha Bint Faqudh akasema: ‘Hakika mimi
nnahisi kua hiki kilichomo ndani ya tumbo langu kinakiinamia kilichomo ndani ya
Tumbo lako.’
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala alielezea habari hii ya Nabii Yahya kua ni mwenye
kumsadikisha Nabii Isa Ibn Maryam pale aliposema kumwambia Nabi Zakarriyah:
﴿أَن َّ اهلل ََّ يُبَشِّ رُكَ بِيَحْيَى ٰ مُصَدِّقاً بِكَلِمَةٍ مِّنَ ٱهلل َِّ وَسَيِّداً وَحَصُوراً وَنَبِيّاً مِّ نَ
ٱلص َّالحِِينَ ﴾
Anna Allaha yubashshiruka bi Yahya musaddiqan bikalimatin mina Allahi
wasayyidan wahasooran wanabiyyan mina alssaliheena; (Surat Al Imran 3:39-41)
463
Tafsir: ‘Hakika Allah anakubashiria (Mtoto) Yahya kuthibitisha Kauli kutoka kwa
Allah (Nabii Isa), na mja mwema mwenye cheo, na msafi asiekua na dhambi na Nabii
na Miongoni mwa Waja wema’
Kisha baada ya hapo Allah Subhanah wa Ta’ala akamwambia Maryam Bint Imran kua:
‘Ukijifungua miongoni mwa Watu wako basi watakusimbulia na kukufukuza na
kukupiga mawe na kutaka kukuua wewe na Mtoto wako, na hivyo bora hama
kutoka katika Mji huo.’
Ambapo kwa upande wa Imam Abd Rahman Al-Kalbi, basi yeye anasema kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala alimwambia Yusuf kua kama Maryam akijifungua basi watu
watamuua kwa sababu watasema kua amezini hivyo hameni’
Hivyo Maryam Bint Imran akamwambia Yusuf kuhusiana na mtizamo huo, na hivyo
Yusuf akamwambia Maryam bora wahame kwenye Mji huo wa Nasira (Nazareti) ulioko
Kaskazini mwa ardhi ya Falestina, waelekee katika Mji mwengine kusini mwa Ardhi ya
Falestina, na hivyo siku ya pili alfajir mapema kabla ya watu hawajaamka wakatoka
katika Mji huo na kuelekea katika ardhi ya Bethlehem.
KUZALIWA KWA NABII ISA IBN MARYAM
Tunapoangalia kitabu cha Biblia basi tunaona vinasema kua wakati Malaika Jibril
alipomshukia Maryam Bint Imran kumbashiria kuhusiana na kutunukiwa kwake Ujauzito
wa Isa Ibn Maryam na Allah Subhanah wa Ta’ala basi tunaona kua ilikua ni katika
kipindi cha mwishoni kabisa cha Kipupwe cha Mwezi wa Adar ambao ni mwezi wa 6
katika kalenda ya Kiyahudi ambao nao hua ni wenye kufuatiwa na Mwezi wa Nisan
ambao ni mwezi wa 7 wa Kiyahudi ambapo ingawa Mayahudi hua wanatumia Nambari
za miezi badala ya Majina kwani mfumo wa Majina ya Miezi iliyokua ikitumika katika
kipindi hicho ilikua ni yenye kua na asili ya watu wa Iraq katika Ardhi ya Babylon ambao
ndio waliouhamishia Jerusalem baada ya wao kua ni watawala wa ardhi ya Mayahudi, na
hivyo wakawa wanatumia Kalenda inayotokana na asili yao.
Hivyo ili tufaham zaidi basi na tuangalie inavyoonesha kwenye mpangilio wa Kalenda
ya Miezi ya Kislam, Kiyahud na Kikristo hapo chini:
KALENDA ZA MIAKA ZA DINI KUU DUNIANI
KIISLAM KIYAHUDI KIKRISTO
Muharram Tishri January
Safar Heshvan February
464
Rabi Al Awwal Kislev March
Rabi Al Thani Tebet April
Jummada Al Awwal Shebat May
Jummada Al Thani Adar June
Rajab Aviv/Nisan July
Shaban Iyar August
Ramadhan Sivan September
Shawwal Tamuz October
Dhul Qaadah Ab November
Dhul Hijjah Elul December
Kwa maana hio basi tunapoiangalia Kalenda hii basi tunaona kua kama Malaika Jibril
alimbashiria Maryam Bint Imran kutunukiwa mtoto katika mwezi wa Adar basi kama
ikiwa ujauzito huo ulichukua miezi 9, basi Nabii Isa alizaliwa mnamo mwezi wa Heshvan
au Kislev yaani mwezi wa February au March na ndio maana kuna baadhi ya watafiti
wanasema kua Nabii Isa alizaliwa tarehe 28 March.
Na pia kuna wasemao kua alizaliwa tarehe 6 April, na hii pia ni kutokana na Imani ya
watu waliotangulia hapo kabla ya Kua Mitume hua ni wenye kufariki katika siku ambayo
walizaliwa. Ambapo kwa upande wa Waislam tunaamini kua Nabii Isa hakufariki
kulingana na vithibitisho tutakavyoviangalia hapo baadae lakini alisulubiwa tarehe 6
April.
Na hapa ndio tunaona tofauti ya kwanini Wakristo wakawa ni wenye kusheherekea
sikukuu ya Kuzaliwa kwa Nabii Isa tarehe 25 December ambayo kwa mara ya kwanza
ilianza kusheherekewa mnamo mwaka 725 C.E baada ya Kusulubiwa Nabii Isa, na hii ni
kwa sababu ya kua ni tarehe 25 December hua ni siku yenye kujulikana kama siku ya
Jua.
Kwani hii hua ndio siku ambayo masaa ya siku yanaaza kuongezeka ukubwa, kwa sababu
katika nchi za Baridi basi kinapoingia Kipindi cha Baridi Mchana hua mfupi na Usiku
hua mkubwa, hivyo kuanzia tarehe 25 December ndio Jua hua linaanza kuongezeka
kutokana na mabadiliko ya Nyakati za Muangaza wa Jua, hivyo Mapagani waikua
wakisema kua hii ni siku ya kuzaliwa kwa Jua na kwa kua siku hii ilikua inasheherekewa
na Mapagani wengi wa Scandinavia, Rome, Mashariki ya Kati, India, China n.k
Hivyo Wakuu wa Kanisa wakaamua kua bora siku hii ya tarehe 25 December ambayo ni
siku ya Sikukuu ya Jua kua inasibishwe na kuzaliwa kwa Nabii Isa kutokana na kua wengi
miongoni mwao walikua wakiadhimisha siku hio na pia wao ni wenye Imani ya kua Nabii
Isa ni mwenye nguvu kama ya Jua kwa Ulimwengu na ndio maana hua wanamwita pia
kwa jina la Jua la Uongofu.
465
Hivyo katika Alfajiri moja ya mwaka wa 65 baada ya Mfalme Aleksandriyah kuiteka
Ardhi ya Babylon katika wakati wa baina ya Mwezi wa Heshvan na Kislev yaani baina
ya mwezi wa February na March basi Yusuf na Maryam Bint Imran wakatoka katika
ardhi ya Nasira (Nazaret) ambayo iko katika maeneo ya Kaskazini na kuelekea kusini
mwa ardhi ya Falestina, ambapo katika siku ya 5 ya safari walipochoka siku hio wakaona
kua bora Maryam Bint Imran apumzike kutokana na hali yake aliyokua nayo. Kutokana
na Maumivu ya uchungu aliyokua akiyahisi, hivyo wakapiga kambi katika sehemu
ambayo kulikua na Mtende uliokauka ambao haukua na Tende kwani hata majani yake
yalikua ni makavu, sehemu hii ilikua ikijulikana kama Bayt Al Lahm (Bethlehem).
Allah Subhanah wa Ta’ala anaielezea hali ilivyokua mara baada ya Yusuf na Maryam
Bint Imran walipofika katika eneo hili kwa kusema:
﴿فَأَجَآءَهَا ٱلْمَخَاضُ إِلىَٰ جِ ذْعِ ٱلن َّخْلَةِ قَالَتْ يٰلَيْتَنىِ مِت ُّ قَبْلَ هَٰذَا وَكُنتُ نَسْياً
م َّنسِ يّاً ﴾
Faajaaha almakhadhu ila jidhAAi alnnakhlati qalat ya laytanee mittu qabla hadha
wakuntu nasyan mansiyyan; (Surat Maryam 19:23)
Tafsir: Yakamjia Machungu ya Uzazi yakampelekea kwenye shina la Mtende, na
akasema: ‘Ya Laiti! Bora ningekufa mimi kabla ya haya na nikawa sahauliko
lililosahauliwa zamani sana’
Ambapo tunaona kua Allah Subhanah wa Ta’ala anaielezea hali aliyokua akiihisi
Maryam bint Imran ndani ya Mwili wake Mtukufu kua ni Almakhadhu, ambalo ni neno
linalotokana na neno Makhadha ambalo hua linamaanisha Kuchanganya kitu kwa nguvu,
Kutikisa au Maumivu ya mwili yanayotokana na Uchungu wa Mja mzito.
Hii hua ni hali ambayo anaipata Mwanamke aliekua na ujauzito kutokana na Mwili wa
Mwanamke huyo kua tayari unataka kukitoa nje kiumbe kilichokuwemo ndani ya mwili
wake kutokana na kua Mda wa kutoka nje ya mwili wake na kuingia Duniani kwa kiumbe
huyo na kuishi maisha yake ya kujitegemea umewadia. Ambapo kwa kimaumbile basi
Mfupa wa kiuno wa Mwanamke hua ni mpana kuliko wa Mwanamme, na hii ni kwa
sababu ya kumuwezesha kubeba Mtoto ndani ya mwili wake na kukaa kwa urahisi.
Na kwa upande mwengine basi mifupa ya Mapaja ya Mwanamke pia kwa juu hua
imetanuka zaidi tofauti na ya Mwanamme, kutokana na upana wa Mfupa wa Kiuno chake
Mwanamke na mfumo wa mpangilio wa viungo vya mifupa yake katika maeneno hayo,
na hii pia humuwezesha Mwanamke kua na uwezo wa kubana zaidi miguu yake katika
466
wakati wa kukaa na pia pale inapohitajika kujilinda na madhara ya wanaotaka
kumuingilia kimwili bila ya ridhaa yake kwani kutanuka kwa viunganisho vya mifupa ya
mapaja yake kwa juu kuanzia kiunoni mwake kunapelekea kuingia ndani kwa viungo vya
mifupa ya magoti yake na hivyo kumuwezesha kirahisi kukutanisha magoti yake na
kubana mapaja yake, katika kukaa kwake na hapo hapo upana huo hua ni pambo la
kumfanya awe ni mwenye kuvutia maumbile yake mbele ya kiumbe mwenza wake yaani
Mwanamme.
Hivyo kutokana na sifa ya Ukamilifu wa Maumbile Ibn Adam, basi Allah Subhanah wa
Ta’ala ameujaala mwili wa Mwanamke kua ni wenye uwezo wa kujitayarisha kwa kila
hatua kwa ajli ya kubeba mtoto ndani yake na kisha kumtoa kwa kujifungua pale mda wa
kufanya hivyo unapowadia, kwa kumtayarishia njia Mtoto huyo ili atoke nje yake kwa
salama na amani, na hivyo mwili huo hua ni wenye kutanua mifupa ya nyonga na kiuno
huku fuko la uzazi likiwa na kazi ya kujibinya kwa kukaza na kuachia kwa ajili ya
kumsukuma mtoto aelekee kwenye njia yake ya kimaumbile kutoka nje ya Mwili, hii hua
ni hali ya maumivu inayofanana na kama maumivu ya kufungwa mpira na kukazwa sana
ndani ya fuko la uzazi, ambapo kwa baadhi hua wanainasibisha hali hii ya kujibinya kwa
fuko la uzazi la kumsukuma mtoto kuelekea chini katika njia yake kua kama vile mtu
unaekandamiziwa ndani kwa ndani ya tumbo lako na kitu chenye ncha kali sana.
Maumivu haya hua ni yenye kuchukua mda wa sekunde 45 hadi 60 ndani ya kipindi cha
kila dakika 10 kwa masaa kadhaa hadi pale njia ya kutokea mtoto yaani sehemu za Sri za
Mwanamke ziakapotanuka na kufikia kua na upana wa sentimita 10 ambapo utanukaji
wa kila sentimita moja huchukua saa moja mpaka mawili, inategemea na maumbile ya
Mwanamke na pia inategemea ni mtoto wa ngapi, kwani baada ya mtoto wa kwanza basi
mwili wa Mwanamke hua umeshazoea na hivyo hua haichukui mda mrefu kama masaa
matano ambapo hua na tofauti kubwa na pale inapokua ndio kwanza mara ya kwanza na
kwa mtoto wa kwanza kama hali ilivyokua katika wakati huu kwa Maryam Bint Imran.
Ambae kutokana na kuhisi maumivu hayo, kwa mara ya kwanza basi ndio maana akawa
ni mwenye kusema kutokana na machungu hayo kua: ‘Ya laytanee mittu qabla hadha
wakuntu nasyan mansiyyan yaani ‘Ya Laiti! Bora ningekufa mimi kabla ya haya na
nikawa sahauliko lililosahauliwa zamani sana’ (Surat Maryam 19:23) yaani alikua
anaona bora angekua ni mwenye kufariki kabla ya hata ya kufikiwa na jambo hilo
lililomtokea katika wakati huu, kwani bora angekua ameshakufa na ameshasahauliwa
zamani sana, kuliko kuhisi maumivu hayo anayoyahisi katika wakati huo.
Hali hii ya Maumivu ya kimaumble hua ni yenye kusababishwa na ufanyaji kazi kamilifu
wa Mifumo mbali mbali ya ndani ya Mwili wa Mwanamke katika utekelezaji wake wa
kimaumbile ikiwemo uzalishwaji wa kemikali muhimu zifuatazo:
467
Prostoglandin ambayo huzalishwa kabla ya kuzaliwa kwa mtoto kwa ajili ya kutayarisha
urahisi wa uzalishwaji wa kemikali nyeingine iitwayo Oxytocin. Katika mazingira haya
ya mwili basi kemikali za Oxytocin hua na kazi ya kuubinya mfuko wa uzazi na kumtoa
nje mtoto anapokua tayari kutoka na pia hua na kazi ya kuurudisha Mfuko wa uzazi katika
hali yake ya kawaida kwa ajili ya matayarisho ya kubeba mtoto mwengine, na hapo hapo
husaidia katika kuzalisha chakula cha Mtoto baada ya kuzaliwa kwake yaani Maziwa ya
Mama yake, na kusababisha hisia za mvuto wa mapenzi na kutotaka kuachana baina ya
Mama na Mtoto wake.
Katika kipindi hiki pia mwili wa mwanamke hua ni wenye kuzalisha kemikali ziitwazo
Relaxin ambazo huutanua mfuko wa Uzazi kwa ajili ya kujifungua na pia kulivunja chupa
la mtoto ndani ya fuko la Uzazi na kutanua mifupa ya kiuno cha Mama na hivyo
kusababisha Mtoto huyo kutoka kwa urahisi kutokana na Maji yaliyomo ndani ya chupa
la lililombebeba mtoto ndani ya fuko la Uzazi.
Na kuna pia kemikali ziitwazo Beta Endorphins ambazo hua ni zenye kuupoza mwili
kutokana na maumivu yote ya mwili aliyokua akiyahisi katika wakati wa kujifungua na
kuzima maumivu hayo mara tu bada ya mtoto kutoka nje ya Mwili wa Mama na
kumfanya Mama kua na hali ya hisia ya furaha baada ya kupata Mtoto huyo.
Kimaumbile mara baada ya Mama kujifungua basi mwili wa Mwanamke hua ni wenye
kulitoa nje chupa la Mtoto kutokana na sehemu liliyojiachia kwenye fuko la uzazi ili fuko
lake la uzazi lipate kupona haraka na pia kuzuia kutoka damu nyingi zaidi, na hivyo
katika kipindi hiki pia fuko la uzazi hua ni lenye kubana na kujikamua kidogo kidogo.
Na hivyo kumsababishia Mama aliejifungua kua ni mwenye kuhisi homa ya baridi baridi
kwa mda mfupi baada ya kujifungua kutokana na pia kua ni mwenye kupoteza maji
mengi na joto mwilini mwake. Na ili mtoto aweze kupata chakula chake basi mara baada
ya tukio hilo la kujifungua mwili wa Mama hua ni wenye kuendelea kuzalisha Kemikali
za Oxytocin na Prolactin kwa ajili ya kukijaza kifua cha Mama mtoto maziwa na hivyo
ndani ya siku tatu maziwa hua ni tayari yaliyojaa kwa ajili ya kumnyonyesha Mtoto wake
huyo ambayo nayo pia hua ni yaliyojaa Madini tofauti muhimu kwa ajili ya ulinzi wa
afya na ukuaji wa Mtoto huyo, kama vile Vitamin, Protein na Mafuta ambayo
yanahitajka ndani ya miezi 6 ya mwanzoni mwa maisha ya mtoto.
Hivyo kwa upande wa Maryam Bint Imran alipotokewa na hali hii ya uchungu, bila ya
kujua ni kitu gani kinachotaka kumtokea na kuanza kujuta kutokana na ukali wa
maumivu hayo ya kimaumbile na kisha kajifungua basi hakua ni mwenye kujua nini
afanye kwani alikua peke yake, hukua akiwa na wasi wasi zaidi juu ya kile kitakachofuta
baada ya kujifungua kwake Mtoto huyo, yaani watu wake watamchukuliaje? kwani Allah
Subhanah wa Ta’ala alimjaalia Maryam Bint Imran ujfungua wakati Yusuf akiwa
468
hayupo, ameenda katafuta mahitajio yanayohitajika kwa ajili ya kuandaa kambi ya
mapumziko ya mda mfupi katika maeneo hayo.
Ambapo anasema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Hali ya tukio hili
kutokana na mpangilio wa Aya na maneno yake kua haikumchukua mda mrefu
kwa Maryam Bint Imran kuondoka Nyumba kabla ya kujifungua’.
Baada ya kujifungua basi Maryam Bint Imran akajikuta nguvu zimemuishia lakini hapo
hapo akasikia sauti kutoka chini yake ikisema kama zinavyosema aya:
﴿فَنَادَاهَا مِن تحَْتِهَآ أَلا َّ تحَْزَنىِ قَدْ جَعَلَ رَب ُّكِ تحَْتَكِ سَرًِّ۞وَ هُزِّى ۤ إِلَيْكِ بجِِذْعِ
ٱلن َّخْلَةِ تُسَاقِطْ عَلَيْكِ رُطَباً جَنِيّاً ﴾
Fanadaha min tahtiha alla tahzanee qad jaAAala rabbuki tahtaki sariyyan;
Wahuzzee ilayki bijidhAAi alnnakhlati tusaqit AAalayki rutaban janiyyan (Surat
Maryam 19:24-25)
Tafsir: Kisha akanadiwa kutoka chini yake (na kuambiwa): ‘Usiwe na Huzuni, kwani
amejaalia Mola wako chini yako kua na chemchem ya maji. Na litikise shina la Mtende
nalo litaangusha kwa ajili yako Tende zilizopea.’’
Ambapo maneno yasemayo Min Tahtiha kama yakisomwa kwa kuwekewa alama ya
kisra chini ya harfu Mim na kua Min Tahtiha basi anaesema maneno haya hua ni Allah
Subhanah wa Ta’ala kupitia kwa Malaika Jibril ambae kwa wakati huo alikua chini
karibu yake na kama yakisomwa kama Man Tahtaha kwa kuwekewa Fat-ha, basi itakua
yanamaanisha kua anaesema maneno haya atakua ni Isa Ibn Maryam kutokana na Idhini
ya Allah Subhanah wa Ta’ala baada ya kuzaliwa kwake ambae kwa wakati huo alikua
chini yake Maryam Bint Imran.
Ambapo aya zinatuonesha kuhusiana na tukio hili kua mbali ya kua ni wenye kutakiwa
kua wenye kumtegemea Allah Subhanah wa Ta’ala katika kila kitu lakini pia tunatakiwa
kufanya jithada tusibweteke kua kila kitu kitakuja wenyewe kutokana na Majaaliwa ya
Allah Subhanah wa Ta’ala. Kwani hapa tunaona hali aliyokua nayo Maryam Bint Imran
kutokana na maumivu aliyokua akiyahisi kiasi ya kua alikua akiomba kua bora angekua
ni miongoni wa waliosahauliwa kabisa, yuko taabani na hivyo kwake yeye basi hakuna
kitu anachokihitaji zaidi katika wakati huo isipokua kupumzika, lakini anapokea amri ya
kua hatakiwi kupumzika bali anatakiwa ajitafutie riski yake kwa kusukuma kisiki cha mti
mkavu wa Mtende, ambao nao utamuangushia Tende mbivu zilizopea.
469
Hapa inabid tujue kua Mtende si Mpapai na hivo labda utautikisa na Mapapai yataanguka,
Kwa Mtende ni Mti Mgumu kama Mnazi hivyo si rahisi kuweza kuusukuma na
kuangusha tende zake hata kwa Mwanamme alietimia kimaumbile, lakini hii pia ni
sehemu ya ya Miujiza yake Allah Subhanah wa Ta’ala kwa Maryam Bint Imran kua
aliweza kuutikisa nao ukamuangushia Tende hizo.
Ambapo kwa upande wa Bahr ul ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi
anasema kua: ‘Chem chem hio ilitokea baada ya Malaika Jibril au Isa Ibn Maryam
kupiga chini mguu wake na hivyo ikatokea chemchem hio, na Mtende huo ambao
ulikua mkavu ukawa ni wenye kua mbichi na wenye Tende zilizopea na kuanguka
baada ya kutikiswa kwake na Maryam Bint Imran.’
Ambapo anasema Imam Al Rabi Ibn Al Khaytham kua: ‘Hakuna kitu bora kwa
Mwanamke aliejufungua Mtoto baada ya kujifunga kama Tende zilizopea, na kwa
mgonjwa hakuna kitu bora kama Asali.’
Na Imam Amr Ibn Maymun amesema kua: ‘Hakuna kitu bora zaidi kwa Mwanamke
aliejifungua kuliko Tende zilizopea’ na kisha akasoma aya hizi za Surat Maryam
19:24-25
Kisha baada ya tukio hilo basi Yusuf akamuwashia Moto Maryam Bint Imran na
kumzungushia kwa ajili ya kumuongezea joto la mwili ambalo lilikua limeshuka baada
ya kujifungua kwake. Kwani alikua anatetemeka mbali ya kua alikua ni mwenye kufanya
mazoezi ya kuupasha Moto mwili kutokana na amrisho la kutikisa Mtende. Kisha baada
ya hapo akamvunjia Lozi 7 ambazo alikua nazo ndani ya Mkoba wake na kumpa.
Ambapo anasema Imam Wahb Ibn Munabih kua: ‘Katika siku ambayo alizaliwa Nabii
Isa basi Masanam yote yalianguka chini, na Mashetani wote walianguka chini na
kushtuka, bila ya kujua ni kwa sababu gani. Hivyo moja kwa moja wakakimbilia
kwa Ibilis laanat Allah. Ambae alikua amekaa kwenye Kiti chake cha Ufalme, ndani
ya kina cha bahari, na walikutana nae katika wakati wa saa sita mchana. Na
alipowaona wasaidizi wake hao wote kwa pamoja basi akashtuka na kuwauliza
kimetokea nini?’
Wasaidizi hao wakamwambia mkuu wao Ibilisi Laanat Allahi kuhusiama na yaliyotokea,
na kisha wakasema kua: ‘Kwa kipindi hiki hakuna jambo zuri zaidi kwetu la
kuwaangamizia Ibn Adam zaidi ya Masanam na kutokana na tukio hili basi tuna
khofu kua hii huenda ikawa inamaanisha hawatokua na ushawishi wa kuendelea
kuyaabudu Masanam tena, na tumefukua kila sehemu ya Bahari na Ardhi kwa ajili
ya kutaka kujua nini kimetokea lakini hatukuweza kugundua.’
470
Hivyo Ibilisi akasema: ‘Bila ya shaka hili litakua jambo kubwa sana, hivyo subrini
wacha nikafuatilie’ kisha Ibilisi akatoka na kukaa kwa muda wa takriban masaa matatu
akiwa anaelea juu angani, na kisha ghafla akaona kila ambacho hawakukiona wasaidizi
wake, kwani aliona sehemu katika Ardhi ambayo ilikua ina utofauti na sehemu nyengine
na akahisi kua imezungukwa na Malaika. Lakini hata hivyo akajaribu kuisogelea sehemu
hio ili aone kuna nini kilichotokea lakini jithada zake zikagonga ukuta kwa sababu
alishindwa kuisogelea kwani kila upande anaojaribu kusogelea basi anakutana na ukuta
usioonekana.
Na ndio maana akasemaa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Shaytan
amemgusa kila mtoto wa Ibn Adam aliezaliwa katikati ya kifua chake kwa kidole
chake, isipokua Isa Ibn Maryam kwani ambae alikua na ngao ya Allah Subhanah
wa Ta’ala kwani ilikua kila akimgusa basi alikua akigusa ngao’
Hivyo Ibilisi Laanat Allahi akarudi kwa wafuasi wake na kuwaambia kua: ‘Hakika mimi
nimezunguka Duniani, Mbinguni na Ardhini na Baharini ndani ya masaa matatu
na nikagundua kuzaliwa kwa Isa Ibn Maryam. Ambae ni mtoto hajawahi kubebwa
na Fuko lolote la uzazi, bila ya kujulikana kwake nami. Au kwa Mwanamke
kujifungua bila ya mimi kuwepo. Na nnatarajia kua watu wengi zaidi
watapotoshwa kutokana nae huyu aliezaliwa kuliko watakaoonglewa. Lakini hata
hivyo basi hakuna Mtume ambae atatupa ushindani zaidi kuliko huyu aliezaliwa
leo.’
Ambapo Imam Mujahid Ibn Sulaiman basi yeye anasema kua : ‘Wakati nilipokua peke
yangu na Isa ndani ya Tumbo langu basi alikua akinizungumzisha, na ilipokua kuna
mtu anaenizungumzisha mimi basi yeye alikua akimtukuza Allah Subhanah wa
Ta’ala ndani ya Tumbo langu, nami nilikua nikisikia. ’
KUZUNGUMZA KWA HOJA KWA ISA IBN MARYAM UTOTONI.
Amesema Imam Mujahid Ibn Sulayman kua: ‘Baada ya Allah Subhanah wa Ta’ala
kumtayarishia mazingira yake Maryam bint Imran na kumrahisishia kujifungua
kwake basi akamwambia kua
﴿فَكُلِى وَٱشْرَبىِ وَقَرِّى عَيْناً فَإِم َّا تَرَيِن َّ مِنَ ٱلبَشَرِ أَحَداً فَقُوليِ ۤ إِ نىّ ِ نَذَرْتُ لِلر َّحمَْٰنِ
صَوْماً فَلَنْ أُكَلِّمَ ٱلْيَوْمَ إِنسِ يّاً ﴾
471
Fakulee waishrabee waqarree AAaynan fa-imma tarayinna mina albashari ahadan
faqoolee innee nadhartu lilrrahmani sawman falan okallima alyawma insiyyan
(Surat Maryam 19:26)
Tafsir: Hivyo kula na kunywa na kua na utulivu wa Jicho lako, na kama ukimuona
Mtu yeyote yule basi sema: ‘Kwa Hakika Mimi nimefunga kwa ajili ya Mwingi wa
Rehma na sitozungumza leo na mtu yeyote’
Ingawa aya imetumia neno Sawman ambalo ingawa hua linaamisha Kujizuia Kutokana
na kitu kilichokatazwa au Kufunga lakini Wanazuoni wametofautiana kuhusiana na
maana yake kwani kuna baadhi ya Wanazuoni ambao wamelitafsiri kama Samt yaani
Kukaa Kimya, yaani Kula kiapo cha Kutosema Kitu ambao pia ni Mtizamo wa Abd Allah
Ibn Masud Radhi Allahu Anhu na kuna wanaosema kua hii ni kwa sababu kuna baadhi
ya Funga za Kiyahudi hua ndani yake mnajumuishwa kujizuia Kusema kitu chochote kile
isipokua Dhikr Allah.
Ambapo kwa upande wa Imam Muhammad Ibn Jariri At Tabari basi yeye amesema kua
aya inamaanisha kua: ‘Maryam Bint Imran alikua anaamrishwa awataarifu watu
kuhusiana na kufunga kwake kwa kutumia alama za mikono’ ambapo
tunapozungumzia kuhusiana na kufunga kwa upande wa Kiislam basi tunaona kua
Hakukukatazwa kuzungumza ndani yake bali kumekatazwa kuzungumza maneno ya
Kipuuzi na yasiyokua na maana.
Na ndio maana siku moja Amir Ul Muuminin Au Bakr As Siddiq Radhi Allah Anhu
alipishana na Mwanamke ambae watu walikua wanasema kua ameapa kua hatozungumza
na Mtu yeyote ambapo nae akasema: ‘Hakika Uislam umebatilisha hilo.’
Amesema Imam Abd Rahman Al-Kalbi kua: ‘Yusuf alimbeba na kumpeleka Maryam
Bint Imran na Isa Ibn Maryam kwenye Pango, na akawawacha huko wa mda wa
siku 40 na kisha akatoka nao, wakati wanarudi katika Mji wa Nasira na Maryam
Bint Imran akiwa amembeba Isa Ibn Maryam mikononi mwake basi Isa Ibn
Maryam alisema kumwambia mama yake kua: ‘Ewe Mama furahia kwani mimi ni
Masih Mja wa Allah’’
Hivyo baada ya kupita siku 40 basi Maryam Bint Imran na Mtoto wake Mchanga ambae
ni Isa Ibn Maryam pamoja na Yusuf wakaanza safari ya kurudi katika Mji wa Nasira
ambako ndiko walikua wakiishi hapo kabla.
﴿فَأَتَتْ بِهِ قَوْمَهَا تحَْمِلُهُ قَالُواْ يمَٰرْيمَُ لَقَدْ جِ ئْتِ شَيْئاً فَرًِّ ﴾
472
Faatat bihi qawmaha tahmiluhu qaloo ya maryamu laqad ji/ti shay-an fariyyan
(Surat Maryam 19:27)
Tafsir: Kisha akamchukua Mtoto kwa Watu wake huku akiwa amembeba. Nao
wakasema: ‘Ewe Maryam kwa hakika umetuletea jambo ambalo halijawahi
kufanywa’
Hapa tunaona kua watu hawa wa Bani Israil wa Mji wa Nasira wanalielezea tukio hili
kutumia neno Fariyya ambalo ni lenye kumaanisha Kukata, Kugawa, Kusingizia Ubaya,
Kuzusha, La Kushangaza na Kustaajabisha ambalo halijawahi kusikika hapo kabla kwa
Ubaya au Uovu wake.
Na hii ni kwa sababu haijawahi kutokea kua Mtawa na Mtu Mcha Mungu awe ni mwenye
kua na sifa ya kutokewa au kufanya kama alivyofanya Maryam Bint Imran yaani kupata
Mtoto bila ya Kuolewa, na ndio maana hata Maryam Bint Imran mwenyewe
alipobashiriwa tunukio hili kutoka kwa Mola wake basi alisema kama vile ambavyo
walivyosema watu hawa kua:
﴿أَنى َّٰ يَكُونُ لىِ غُلاَمٌ وَلمَْ يمَْسَسْنىِ بَشَرٌ وَلمَْ أَكُ بَغِيّاً ﴾
Anna yakoonu lee ghulamun walam yamsasnee basharun walam aku baghiyyan;
(Surat Maryam 19:20)
Tafsir: ‘Nitakua na Mtoto wa kiume mimi wakati sijawahi kuguswa na mtu yeyote
(Mwanamme) na wala mimi si Mwanamke mwenye kutembea na Wanaume?’
Na hivyo kimaumbile pia hua ni jambo la kawaida kwa watu kutofahamu na hivyo kutaka
kujua ukweli juu tukio hilo, ambalo kwa mtizamo wa juu juu tu basi haiwezekani kupata
jawabu bila ya kufikiria vyenginevyo yaani itakuaje Mwanamke awe ni mwenye kupata
Mtoto bila ya Kuingiliwa na Mwanamme? Na kutokana na hali kua ni hivyo kimanitiki
hua kama Mwanamke amepata Ujauzito na Kujifungua basi hua inamaanisha kua hakuna
njia nyengine yeyote isipokua ameingiliwa na Mwanamme.
Na hivyo basi Watu hao wakasisitiza zaidi kua jambo hilo ni la kustaajabisha sana kwa
sababu kimaumbile baadhi ya mambo hua yanatokana kulingana na asili au urithi, lakini
kwa upande wake Maryam Bint Imran hakua na asili ya kua ni mwenye kuweza kupata
Mtoto bila ya kuolewa, kutokana na utukufu wake na pia Utukufu wa asili yake kifamilia
hivyo haiwezekani kua jambo hilo limetokea kutokana na kurithiwa kwa tabia mbaya
labda kutoka katika familia, au asili yake, kwani hakuna katika urithi wala asili na ndio
473
maana watu hao wakamwambia Maryam Bint Imran kwa kusema kama zinavyosema
Aya:
﴿ُٰخْتَ هَارُونَ مَا كَانَ أَبُوكِ ٱمْرَأَ سَوْءٍ وَمَا كَانَتْ أُم ُّكِ بَغِيّاً ﴾
Ya okhta haroona ma kana abooki imraa saw-in wama kanat ommuki baghiyyan
(Surat Maryam 19:28)
Tafsir: Wakasema Watu hao: ‘Ewe Dada yake Harun, hakuwahi kua Baba yako ni
Mzinifufu, na wala Mama yako kua ni Malaya’
Ambapo anasema Al Mughira Ibn Shubah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alinituma mimi kwa watu wa Najran. Na wakasema:
‘Hivi umefikiria kuhusiana na hii aya uliyotusomea kwenye Qur’an isemayo: Ewe
Dada yake Harun wakati Musa alikua ni mwenye kuja kabla ya Musa? Hivyo
niliporudi nikamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam ambae nae alisema
kua: ‘Jee hukuwaambia wewe kua walikua wamezoea kuitana kwa majina ya
Mitume na watu wacha Mungu kabla yao?’
Ambapo anasema Imam Qatadah Al Sadusi kua: ‘Kabla ya kipindi hiki watu wa Bani
Israil walikua na mtu mwema ambae alikua akiitwa Harun ambae ni tofauti na
Harun kaka yake Nabii Musa, ambapo katika siku aliyofariki basi Jeneza lake
lilishindikizwa na watu 40000 ambao wote walikua wakiitwa Harun.’
Anasema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al
Qurtubi kua: ‘Kuna mitizamo tofauti kuhusiana na mda ambao uliopita baina ya
Nabii Musa Ibn Imran na Nabii Isa Ibn Maryam. Kwani Imam Muhammad Ibn
Saad amesema katika Tabaqat Al Saadi kua: ‘Abd Alla Ibn Abbas Radhi Allahu
Anhu amesema kua: ‘Baina ya Nabii Musa Ibn Imran na Isa Ibn Maryam kulikua
na miaka 1,700 na kamwe hakukua na fatra (kipindi ambacho hakukua na Mitume
kwa watu wa Bani Israil) baina yao, kwani katika kipindi hiki watu wa Bani Israil
walitumiwa Mitume 1000. Ambayo ni mbali ya idadi ya Mitume myengine
iliyotumwa kwa Ummah wa watu wengine. Na baina ya Nabii Isa Ibn Maryam na
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi kuna miaka 599’ ’(Tafsir Jamii Al Ahkami
Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi )
Ama kwa upande wa Mujaddid Ad Din Al Hafidh Imam Shihab ad Din Imam Ibn Hajar
Al Asqalani basi yeye anasema kua: ‘Wanazuoni wanakubaliana kua kipindi cha
Mayahudi na hadi kipindi cha kuwasili Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ni
474
zaidi ya miaka 2000. Na Kipindi cha Wakristo na Rasul Allah Salallahu Alayhi w
Salam ni miaka 600’ (Fa-th Al Baari, 4/449 Mujaddid ad Din Al Hafidh Imam Ibn Hajar
Al Asqalani)
Naam anasema Imam Al Sabuni Al Hanbali kua: ‘Harun huyu anaezungumziwa hapa
si Nabii Harun ambae alikua pamoja na Nabii Musa kwani bila ya shaka utofauti
wa kipindi walichoishi wao na Maryam bint Imran ni zaid ya miaka 1000.’ (Safwat
Al Tafaasir)
Ama kwa upande wa Sultan Al Mutakallimin Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al
Razi basi yeye ameifafanua ayah hii katika sehemu nne ambazo tunaweza tukazifupisha
kama ifuatavyo:
1. Harun huyu alietajwa katika aya hii alikua ni mtu ambae ni Mcha Mungu
miongoni mwa Bani Israil, hivyo wale watu ambao walikua ni wacha Mungu
walikua wakinasibishwa nae Harun huyu.
2. Harun huyu alietajwa katika aya hii, ndio yule yule Nabii Harun ambae ni kaka
yake Nabii Musa. Hivyo Marymam bint Imran alikua ni mwenye kutoka katika
kizazi cha Nabii Harun, kama vile abavyo mtu alietoka katika ukoo wa Hamdan
kwa mfano kua ni mwenye kuitwa: ‘Ewe ndugu yake Hamdan’ yaani yule
anaetoka katika kizazi cha Hamdan.
3. Harun huyu alikua ni mtu mwenye umaarufu katika mambo ya kufanya maasi.
Hivyo Maryam alizungumziwa hapa katika hali ya ‘Tashbiih’ yaani
kumshabihisha. Kwani Bani Israil wao walimuona Maryam Bint Imrankua
alikua amefanya maasi.
4. Harun huyu alikua ni kaka yake Maryam Bint Imran ambae alikua ni mtu
mwema na mwenye ucha Mungu, ambapo maana hii hua ni yenye kuendana
sana kimaana kwa sababu kuu mbili zifuatazo:
i. Hii ndio maana ya juu ya Aya, hivyo hakutokua na uhitaji wowote ule wa kuingia
ndani kutafuta maana inayoainishwa au iliyofichwa na ayah hii.
ii. Hii ilitumika kuonesha ‘Tawbikh’ yaani Karipio. Kwani hali hii ya karipio hua
ni kubwa zaidi pale linaponasibishwa na Ndugu kwani hili pia hua
linamkumbushia Wazee wake yule anaekaripiwa na adabu alizofundishwa na
Wazee wake hao. Kwani Ayah hii pia imewaainisha wazee wake waliomzaa
475
Maryam Bint Amran. (Mafatih Al Ghayb /Al Tafsir Al Kabir, Imam Fakhrudin Al
Razi)
Na akasema Imam Wahb Ibn Munabih kua: ‘Jina Harun lilikua ni la Mtu mmoja
miongoni mwa watu waovu sana katika jamii ya Watu wa Bani Israil na alikua
anachukiza sana kwa maovu yake ikiwemo Uzinifu, hivyo watu hawa wa Bani Israil
moja kwa moja wakamfananisha Maryam Bint Imran na Harun huyo kutoka na
tukio hili.’
Ambapo kutokana na maana ya kauli hii kulingana na Mtizamowa Imam Wahb Ibn
Munabih basi tunaona kua Watu hawa walimlaani Maryam Bint Imran kwa
kumfananisha na Harun huyo Muovu na kisha hapo hapo wakamkasirikia na kumkosoa
kua itakuaje afanye hivyo wakati wazee wake hawakua ni wenye sifa hizo, na hivyo hii
ni kauli yenye kuonesha namna Watu hawa walivyokua wakimjali na kumthamni
Maryam Bint Imran na kua wamechukizwa sana na kuvunjwa Nyoyo zao kutokana na
Aibu aliyowatia ambayo imevunja Imani yao juu yake, kwani thamani yake juu yao baada
ya tukio hili imeanguka chini yote.
Hivyo Maryam Bint Imran akafanya kama alivyoamrishwa na Mola wake ambae ndie
aliembebesha jukumu hilo zito juu yake lenye kumletea Mitiani hii anayokabiliana nayo
mbele ya watu wake, kwa kutoa ishara kama inavyobainishwa na Aya:
﴿فَأَشَارَتْ إِلَيْهِ قَالُواْ كَيْفَ نُكَلِّمُ مَن كَانَ فىِ ٱلْمَهْدِ صَبِيّاً ﴾
Faasharat ilayhi qaloo kayfa nukallimu man kana fee almahdi sabiyyan (Surat
Maryam 19:29)
Tafsir: ‘Akaashiria juu yake (Mtoto wake wazungumze nae) Nao wakasema:
‘Tutazugumzaje sisi na Mtoto aliemo kwenye Mkoba wa kubebea Mtoto mchanga?’’
Lakini hata hivyo Maryam Bint Imran akaendelea kwa kufanya kama alivyoamrishwa na
Allah Subhanah wa Ta’ala kwa kumuashiria Isa Ibn Maryam kua umefika wakati wa
Kujitetea na kudhihirisha Miujiza yake itakayodhibitisha kua yeye hakupatikana
kutokana na kama wanavyofikiria na kudhania watu hao wa Najran kwa kujitetea kwa
hoja zinazoshiria Miujiza ya Kuzaliwa kwake siku 40 tu zilizopita kama zinavyosema
aya:
476
﴿ قَالَ ِ إِنىّ عَبْدُ ٱهلل َِّ آاتَنىِ َ ٱلْكِتَابَ وَجَعَلَنىِ نَبِيّاً ۞ وَجَعَلَنىِ مُبَارَكاً أَيْنَ مَا كُ نتُ
وَأَوْصَانىِ بِٱلص َّلاَةِ وَٱلز َّكَ ا وٰةَِم دُمْ تُحَيّاً ۞ وَبَرّاً بِوَالِدَتِى وَلمَْ يجَْعَ لْنىِ جَب َّاراً شَقِيّاً
۞ وَٱلس َّلاَمُ عَلَى َّ يَوْمَ وُلِدْت ُّ وَيَوْمَ أَمُوتُ وَيَوْمَ أُبْعَثُ حَيّاً ۞ ذٰ لِكَ عِيسَى ٱبْنُ
مَرْيمََ قَوْلَ ٱلحَْقِّ ٱل َّذِى فِيهِ يمَْتَ رُونَ ﴾
Qala innee AAabdu Allahi ataniya alkitaba wajaAAalanee Nabiyyan;
WajaAAalanee mubarakan aynama kuntu waawsanee bialssalati waalzzakati ma
dumtu hayyan; Wabarran biwalidatee walam yajAAalnee jabbaran shaqiyyan ;
Waalssalamu AAalayya yawma wulidtu wayawma amootu wayawma obAAathu
hayyan Dhalika AAeesa ibnu maryama qawla alhaqqi alladhee feehi yamtaroona
(Surat Maryam 19:30-34)
Tafsir: Akasema (Isa Ibn Maryam): ‘Hakika mimi ni Mja wa Allah ambae amenipa
Kitabu na kunijaalia kua ni Nabii. Na amenijaalia kua ni Barka popote pale
nitakapokuwepo na Kua ni mwenye kuusiwa juu ya Sala na Zakkah kudumu nazo
wakati niko hai. Na kumfanyia wema Mzazi wangu (Maryam Bint Imran) na wala
hakunijaalia kua ni mwenye Ujabari wa kutumia nguvu. Na Salama iko juu yangu
katika siku niliyozaliwa na siku nitakayokufa na katika siku nitakayofufuliwa. Huyo
ndio Isa Ibn Maryam Kauli ya haki ambae wao ni wenye shaka nae’
Aya inatuonesha kua ingawa Isa Ibn Maryam alikua na umri wa siku 40 lakini alikua na
uwezo wa kubainisha Hoja zake kutokana na kujaaliwa kwake na Allah Subhanah wa
Ta’ala kwa ajili ya kumtetea Mama yake na kujitetea kwa kujielezea yeye mwenyewe
kua yeye ni Mja wa Allah Subhanah wa Ta’ala sambamba kimaana maneno haya akiwa
anakanusha kua yeye pia si Mungu na wala si Mtoto wa Mungu kama wanavyodai au
watakavyodai watakaokuja baada yake.
Na kisha anabainisha kusudio la kutumwa kwake na Mola wake kwa watu wake hao kua
ni Ni mwenye Darja ya Unabii wa kuwaelekeza watu katika njia sahihi ya kumuelekea
Mola wao na kuwakataza Maovu na kuwaamrisha Mema na amekuja na Kitabu chake na
hivyo kua ni mwenye Barka popote pale atakapokuwepo Ulimwenguni. Na kamwe hakua
ni mwenye kujaaliwa kua na Kibri dhidi ya Maamrisho ya Mola wake na mbele ya Mama
yake.
477
Ambapo amesema Imam Abu Muhammad Abd Allah Sahl Al Tustari kua amesema Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kibriyah ni Vazi la Allah Subhanah wa Ta’ala
hivyo yeyote yule atakaeshindana na Allah Subhanah wa Ta’ala juu yake vazi hilo
na kulivaa, basi atatumbukizwa Motoni uso uso.’
Hivyo baada ya kujitetea kwake huko Nabii Isa Ibn Maryam basi habari zikafika kwa
Watawala ambao walikua ni wenye Mamlaka ya Ufalme ulio chini ya mwamvuli wa
utawala wa Roma Empire uliokua unaongozwa na Qaysar, ambae alikua akitawala
maeneo yote ya Mwambao wa Bahari ya Mediterenean, ambapo kwa wakati huu Mfalme
wa ardhi ya Israil alikua ni Mfalme Herod ambae alipanga kumuua Isa Ibn Maryam
kutokana na kubashiriwa na watu wake kuhusiana na kuzaliwa kwa Mtoto ambae ataleta
matatizo ya upinzani kwa Utawala wake na Utawala wa Roman Empire. Hivyo basi Allah
Subhanah wa Ta’ala akamwamrisha Maryam bint Imran na Yusuf kua umefika wakati
wa kuhama kutoka katika Ardhi ya Falestina kuelekea katika ardhi ya Misri.
HIJRA YA MARYAM BINT IMRAN NA NABII ISA BAINA YA MISRI
NA NASIRA
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamwambia Maryam Bint Imran na Yusuf kua
wahame na Isa Ibn Maryam kutoka katika Ardhi ya Falestina kuelekea katika Ardhi ya
Misri na hawatakiwa kurudi hadi pae atakapofariki Mfalme Herod, kwani Mfalme huyo
anapanga mipango ya kutaka kumuua Isa Ibn Maryam, hivyo alfajir ya siku ya pili basi
Yusuf akampakia Maryam Bint Imran na Isa Ibn Maryam kwenye Punda wake na kuanza
safari yao ya kuelekea katika ardhi ya Misri, hadi walipovuka katika maeneo yenye
Miinuko iliyokaribu na ardhi ya Misri ambayo Allah Subhanah wa Ta’ala anaielezea kwa
kusema kua:
﴿وَجَ عَلْنَا ٱبْنَ مَرْيمََ وَأُم َّهُ آيَةً وَآوَيْنَاهمَُآ إِلىَٰ رَبْوَةٍ ذَاتِ قَرَارٍ وَمَعِينٍ ﴾
WajaAAalna ibna maryama waommahu ayatan waawaynahuma ila rabwatin dhati
qararin wamaAAeenin (Surat Al Muuminun 23:50)
Tafsir: Na tukamjaalia Ibn Maryam na Mama yake Dalili tukawapa makazi katika
sehemu iliyojuu iliyobakia na chemchem ya maji.
Ambapo neno Rabwatin hua linamaanisha Kuongezeka, Kukuza, Kutuna, Kujaa,
Kupanda Juu, Kuelea juu juu, Kukuza kitu, Kukuza Ufahamu kwa kusomesha. Ambapo
neno hili limetokana na neno Rabwa ambalo ndio lililotoa neno Riba na hivyo pia
478
kumaanisha Riba au Kitu chochote kinachoongezeka na kua ni cha ziada kutokana na
Mkopo au Kiasi kilichozidi zaidi ya vile kilichokua kabla ya kuwekezwa kwake.
Ambapo kwa upande wa Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu na Imam Ad Dahhaq basi wao
wanasema kua: ‘Rabwah hii inamaanisha eneo zima la Ramallah, Misri na Syria’
lakini kwa upande wa Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi yeye amesema kua
:‘Hii inamaanisha ni Ardhi iliyonyanyua na kuwepo juu ya sehemu nyengine
zilizoizunguka’
Na kwa upande wa Imam Al Qazzaz basi amesema kua ni: ‘Sehemu ya Ardhi ambayo
inamwagiliwa Maji safi’ na Imam Abu Zayd basi yeye anasema kua hii ni Ardhi ya
Misri.
Na wengine wengi miongoni mwa Wanazuoni basi ni wenye kusema kua Maryam Bint
Imran alihamia katika Ardhi ya Misri na hii ni kwa sababu Ardhi ya Misri kwa wakati
huu ilikua iko mbali na mamlaka ya Mfalme Herod, na hivyo Maryam Bint Imran na Isa
Ibn Maryam alikaa katika ardhi hio ya Misri kwa Muda wa miaka 12 huku akiwa ni
mwenye kufanya kazi kuchuma Pamba mashambani.
Ambapo anasema Imam Muhammad Ali Al Baqr kua: ‘Wakati Nabii Isa alipozaliwa
basi alipokua na umri wa siku moja basi alikua akionekana kama ana umri wa
mwezi mmoja, hivyo baada ya miezi 9 alipelekewa Madrasa, na alipokaa darasani
basi Mwalimu wake akamwambia sema: ‘Biismi Allahi AlRahmani Al Rahim’ hivyo
nae akasema, kisha akaambiwa asome Abjad, hivyo Isa Ibn Maryam akamuuliza
Mwalimu wake kama anajua maana ya herufi za Abjad.’
‘Hivyo mwalimu akamsogelea Isa Ibn Maryam kwa ajili ya kutaka kumpiga bakora
Isa Ibn Maryam, lakini Isa Ibn Maryam akasema: ‘Tafadhal usinipige, kwani kama
unajua basi niambie na kama hujui basi niambie nikutafsirie.’ Hivyo Mwalimu
huyo akamwambia Isa Ibn Maryam kua: ‘Haya tuambie maana yake.’’ Isa Ibn
Maryam akasema:
‘ABJaD – Alif inamaanisha (La) Ilaha Illa Allah, Ba inamanisha Bazagha yaani
Mtandazo wa Nuru ya Allah, Jim inamanisha Jalalah yaani Ufalme wa Allah na Dal
inamanisha Dini.’
‘HaWaZ – Ha inamaanisha Hawwiyah yaani sehemu ya chini kabia ya Moto, Waw
inamanisha Waylun yaani Ole wao watakaouingia Moto huo, na Za inamaanisha
Zafir yaani Harufu mbaya ya watu wa Motoni.’
‘HaTaYa – Inamaanisha Hattat yaani wenye Dhambi watakua chini zaid kuliko wale
wenye Kutubu.’
479
‘KaLaMaN – Ka Inamanisha Kalam - Maneno ya Allah Subhanah wa Ta’ala Lam n
yenye kukataa kua si yenye kuumbwa na hayana Mubadala yaani Mim ambayo ndio
Mubadala ya hayana Mbadala wake.’
‘SaFaS – ni Saun Bi Sain ambayo inamanisha Kipimo kwa kipimo Adhabu kwa
Adhabu.’
‘QaRaShaT – Ni Taqrishuhum yaani Allah Subhanah wa Ta’ala atachukua kutoka
hapa na pale katika siku ya Malipo’
Hivyo ilipofika wakati wa kuena kuchukuliwa katika siku hio kutoka Madrasa basi
Mwalimu akamwambia Maryam Bint Imran kua: ‘Mchukue Mtoto wako kwani ni
mwenye kujua kila kitu hivyo hahitaji kusoma kama watoto wengine.’
Ambapo anasema Imam Kaab Al Akhbar kua: ‘Isa Ibn Maryam alikua ni mwenye
muonekano wa Mtu ambae ni mwenye rangi ya kiza kuelekea kwenye Weupe,
Nywele zake zilikua hazina Mafuta kabisa na alikua ni mwenye kutembea miguu
chini bila ya viatu, alikua hana nyumba wala mapambo wala matumizi isipokua juu
ya kile anachohitajia katika siku husika tu. Usiku unapoingia alikua ni mwenye
kusimama na Kusali Usiku kucha na alikua ni mwenye kuwaponya Vipofu wenye
na Ukoma kwa idhini ya Allah na alikua akifufua waliokufa pia kwa idhini ya
Allah.’
Hivyo miaka 12 baada ya kuhamia katika ardhi ya Misri basi Allah Subhnaah wa Ta’ala
akaichukua Roho ya Mfalme Herod na kisha akamtaarifu Maryam Bint Imran n Yusuf
na Isa Ibn Marym kua Mfalme Herod ameshafarki na hivyo wanaweza kurudi katika Mji
wa Nasira, hivyo na wakarudi na wakawa ni wenye kuishi kwenye Mji huo kwa miaka
kadhaa hadi pale Isa Ibn Maryam alipotimiza umri wa miaka 30, yaani miaka 18 baadae.
Ambapo katika kipindi hiki basi Allah Subhanah wa Ta’ala akamshushia Wahyi Isa Ibn
Maryam na kumwambia kua umefika wakati wa kujidhihirisha kwa ajili ya kufikisha
ujumbe wake aliotumiwa na Mola wake kwa ajili ya watu wa Bani Israil.
Nabii Isa Ibn Maryam akaanza kutangazia ujumbe wa Allah Subhanah wa Taa’la kwa
kutumia silaha ya Miujiza yake akiwa ni mwenye kuponya waliokua wamepooza,
waliokua na Ukoma, waliokua na Majini na Mashetani na hata waliokua vipofu
aliwapanguza nyuso zao na wakawa ni wenye kuona, bila ya kuchukua malipo yeyote
kutoka kwao, kwani yeye alikua ni mwenye kutaka watu hao wawe ni wenye kuamini
Imani yake anayowausia tu juu yao basi, hivyo watu wakaanza kumpenda na kumfuata
katika Imani yake nae akazidi kua maarufu na kila mtu alikua ni mwenye kutaka kujuana
nae Al Masih Isa Ibn Maryam Ruhi Allah ambapo miongoni mwa waliokua wakimkubali
kuhusiana na ujumbe wake wakawa wanajulikana kama Ansaru Allah
480
ANSARU ALLAH – AL HAWARIYINA
Neno Ansar hua linamaanisha Nusura, Usaidizi, Uhifadhi, Ulinzi, Msaada au kitu
kinachosababisha Utulivu au Mliwazo pale kinapopatikana.
Ambapo kama tulivyoona kua Nabii Isa alikubalika na kupata wafuasi ambao walikua
tayari wako pamoja nae na hivyo wako tayari kwa ajili yake na kwa ajili ya Allah
Subhanah wa Ta’ala na hivyo watu hawa kua na sifa ya kua ni Ansaru Allah katika kisa
cha Nabii Isa pale aliposema katika kuwathibitishia watu wake kwa kuwaonesha njia
sahih kua:
﴿وَمُصَدِّقاً لِّمَا بَينَْ يَدَى َّ مِنَ ٱلت َّوْرَاةِ وَلِ أُحِ ل َّ لَكُمْ بَعْضَ ٱل َّذِى حُ رِّمَ عَلَيْكُمْ
وَجِ ئْتُكُمْ آبِيَةٍ مِّن ر َّبِّكُمْ فَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَأَطِيعُونِ۞إِن َّ ٱهلل ََّ رَبىِّ وَرَب ُّكُمْ فَٱعْبُدُوهُ هَٰذَ ا
صِرَاطٌ م ُّسْتَقِيمٌ ﴾
Wamusaddiqan lima bayna yadayya mina alttawrati wali-ohilla lakum baAAda
alladhee hurrima AAalaykum waji/tukum bi-ayatin min rabbikum faittaqoo Allaha
waateeAAooni; Inna Allaha rabbee warabbukum faoAAbudoohu hadha siratun
mustaqeemun; (Surat Al Imran 3:50-51)
Tafsir: Na nimekuja kuthibitisha kile ambacho kimekuja kabla yangu, kutoka katika
Tawrat na kukuhalalishieni sehemu ya kile ambacho mliharamishiwa na nimekuja
kwenu nikiwa na uthibitisho kutoka kwa Mola wenu hivyo Mtiini Allah na Nifuateni
mie. Kwani kwa Hakika Allah Ni Mola wangu na ni Mola wenu hivyo Muabuduni, hii
ndio njia iliyonyooka.
Hivyo baaada ya kutoa uthibitisho huo basi Allah Subhanah wa Ta’ala akamjaalia Nabii
Isa kua na Wasaidizi ambao ni wenye kumkubali yeye Allah Subhanah wa Ta’ala na
kumkubali Nabii Isa Ibn Maryam kama zinavyosema aya pale Allah Subhanah wa Ta’ala
alipothibitisha kwa kusema:
481
﴿وَإِذْ أَوْحَيْتُ إِلىَ ٱلحَْوَارِيِّينَ أَنْ آمِنُواْ بىِ وَبِرَ سُ ولىِ ۤ قَالُو اْ آمَن َّا وَٱشْ هَ دْ أبَِ ن َّنَا
مُسْلِمُونَ ﴾
Wa-idh awhaytu ila alhawariyyeena an aminoo bee wabirasoolee qaloo amanna
waishhad bi-annana muslimoona (Surat Al Maidah 5:111)
Tafsir: Na wakati mimi (Allah) nilipowatilia ndani ya nyoyo zao Hawariyyina kua
waniamini mimi na kwa Mtume wangu basi wakasema: ‘Tumeamini na kushuhudia
kua sisi ni Waislam.’
Hapa tunaona kua aya yetu hii imetumia neno Awhaytu ambalo pia ni lenye kutokana na
neno Waha ambalo hua linamaanisha kua ni Wahyi, Maelekezo, Alama, Dalili, Uamsho
au Msukumo unaowekwa kwenye Moyo, Akili au Ufahamu na pia humaanisha
Mnong’onezo wa Siri.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anatueleze kua ni yeye ndie aliewatia Msukumo watu
hao nao wakawa ni wenye kumkubali na kumfuata Nabii Isa Ibn Maryam, na hivyo kua
n wenye kutaka kumsaidia Nabii Isa Ibn Maryam kwa kumunga mkono katika majukumu
yake aliyopewa na Mola wake ili ayafikishe kwa watu wake na hivyo watu hao ndio pia
wakawa wanaitwa Hawarriyin.
Na neno Hawariyiin ni neno lenye kutokana na neno Hara ambalo hua linamaanisha
Kurudi, Kurudia, Kuchanganyikiwa, Kugeuza Macho kutokana na kuchanganyikiwa na
kitu na hivyo kutokiona vizuri kitu hicho. Kua na Macho Makubwa mazuri na ya kuvutia.
Neno Hara ndio lililotoa neno Hur ambalo hua linamaanisha Kitu Kizuri Kisafi
kisichokua na Doa wala Uchafu, na hivyo kumaanisha Vumbe wa Wazuri na Wasafi wa
Peponi ambao ni wenye Jinsia ya Kike na ya Kiume, ambapo Hur wa kike hua ni kwa
ajili ya zawadi ya Waumini wa Kiume kutoka kwa Mola wao kutokana na yale Mema na
Mazuri waliyokua wakiyafanya kwa ajili ya Mola wao hapa Duniani.
Na Hur wa kiume hua ni kwa ajili ya zawadi ya Waumini wa Kike kutoka kwa Mola wao
kutokana na yale Mema na Mazuri waliyokua wakiyafanya kwa ajili ya Mola wao hapa
Duniani.
Hivyo neno Hawari hua linamaanisha Yule Mtu ambe alipewa Mitihani na Mola wake
na kisha akafuzu Mithani hio na kuonekana kua ni Muadilifu na ni Mtiifu wa Mola wake,
na hivyo basi katika aya yetu hua linamaanisha kutubainishia ukubwa wa Darja yao watu
hawa ambao walikua ni wasaidizi maalumu waliochaguliwa na Allah Subhanah wa
482
Ta’ala kwa ajili ya Nabii Isa Ibn Maryam na hivyo kua ni wenye kujisalimisha kwa
Allah Subhanah wa Ta’ala kama zinavyobainisha aya pale ziliposema:
﴿فَلَم َّآ أَحَس َّ عِيسَى ٰ مِنْهُمُ ٱلْكُفْرَ قَالَ مَنْ أَنصَارِ ى ۤ إِلىَ ٱهلل َِّ قَالَ ٱلحَْ وَارِي ُّونَ نحَْنُ
أَنْصَارُ ٱهلل َِّ آمَن َّا بِٱهلل َِّ وَٱشْهَدْ أبَِ َّ مُسْلِمُونَ ﴾
Falamma ahassa AAeesa minhumu alkufra qala man ansaree ila Allahi qala
alhawariyyoona nahnu ansaru Allahi amanna biAllahi waishhad bi-anna
muslimoona (Surat Al Imran 3:52)
Tafsir: Na kisha alivyohisi Isa kutokana na Kutoamini kwao basi akasema: ‘Jee ni
nani Ansaru Allah’ wakasema Hawwariyyun kua: ‘Sisi ndio Ansari Allah,
tuliemuamini Allah na tunashuhudia kua sisi tumejisalimisha (kwa Allah Subhanah
wa Ta’ala)’
Na tunapoangalia watu hawa wenye sifa ya Hawariyun basi tunaona kua Wanazuoni
wanma kua walikua ni watu 12 Ambao ni: ‘Simioni. Pita, Andrew, James Ibn Zebede,
John Ibn Zebede, Philip, Bartholomew, Thomas, Matthew, James Ibn Alphaeus,
Labaeus Ibn Thaddaeus, Simioni Ibn Kanan na Judas Iscarioti’
Ambapo anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Hawa
walikua ni Wavuvi ambapo Isa Ibn Maryam alikutana nao na kuwauliza: ‘Hivi jee
mnafanya nini?’ nao wakajibu: ‘Tunavua Samaki’ nae Isa Ibn Maryam akasema:
‘Hivi Jee hamtaki nyinyi kutembea pamoja na mimi ili tupate kuwavua Watu?’
Watu hao wakauliza: ‘Ndio vipi hivyo?’
Isa Ibn Maryam akasema: ‘Kwa Kuwaita kwa Ajili ya kumuelekea Allah Subhanah
wa Ta’ala’ nao watu hao wakauliza kwa kusema: ‘Kwani wewe ni Nani?’ Nabii Isa
akasema: ‘Mimi ni Isa Ibn Maryam ambae ni Mtume na Nabii wa Allah Subhanah
wa Ta’ala.’ Hivyo watu hao wakamuuliza : ‘Jee kuna Mtume baada yako?’ nae
akasema: ‘Naam Mtume kutoka Urabuni’’
Ambapo kwa upande wa Imam Ibn Arta basi yeye amesema kua: ‘Hawa walikua ni
Wafuaji Nguo na Wapakaji Rangi Vitambaa (Yuhawwirun)’ ambapo kwa upande wa
Imam Abd Allah Ibn Mubarak basi yeye anasema kua: ‘Hawa waliitwa Hawwariyun
kwa sababu walikua waking’ara kutokana na Nuru ya kufanya sana Ibada kwa ajili
ya Allah Subhanah wa Ta’ala’ na kwa upande wa Imam Ad Dahhaq Ibn Muzahim basi
yeye alisema kua: ‘Watu hawa walikua wanaitwa Hawwariyyun kwa sababu ya usafi
wa Ndani ya Nafsi na Nyoyo zao. Na walikua pia ni warithi wa Isa Ibn Maryam’
483
Ambapo amesema Imam Nasr Ibn Shaml kua: ‘Hawwariyyun ni miongoni mwa Watu
wema ambao watu hua wanawatumia kwa ajili ya kuomba Msaada wanapofikwa
na Mithani kama vile alivyosema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua : ‘Kila
Mtume hua na Hawwari wake, na Hawwari wangu mimi ni Al Zubayr’’
Na kwa upande wa Imam Qatadah Al Sadusi basi yeye anasema kua: ‘Hawwaryyun wa
Rasul Allah Salallahu Alyhi wa Salam walikua ni kutoka katika Ukoo wa Quraysh
ambao ni Abu Baqr As Siddiq, Umar Ibn Al Khattab, Uthman Ibn Affan, Ali Ibn
Abu Talib, Hamza Ibn Abd al Muttalib, Jafar Ibn Abu Talib, Abu Ubaydah Ibn
Jarrah, Uthman Ibn Mazun, Abd Rahman Ibn Awf, Saad Ibn Abi Waqqas. Talha
Ibn Abd Allah na Al Zubayr Ibn Awam Radhi Allahu Anhum’
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anaelezea kuhusiana na Umuhimu wa watu wenye
darja ya Hawwariyyun pamoja na wafuasi wa Mitume katika Ummah zao, kua katika
siku ya Malipo wataulizwa Mitume kuhusiana nao wafuasi wao kua jee waliupokeaje
Ujumbe wa Mola wao juu yao kwa kusema:
﴿يَوْمَ يجَْمَعُ ٱهلل َُّ ٱلر ُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَآ أُجْبْتُمْ قَالُواْ لاَ عِلْمَ لَنَآ إِن َّكَ أَنتَ عَلا َّمُ
ٱلْغُيُوبِ ﴾
Yawma yajmaAAu Allahu alrrusula fayaqoolu madha ojibtum qaloo la AAilma
lana innaka anta AAallamu alghuyoobi (Surat Al Maidah 5:109)
Tafsir: Katika siku ya Malipo wakati Allah Subhanah wa Ta’ala atakapowakusanya
Mitume na kuwaambia: ‘Hivi jee mlijibiwa nini (kutokana na watu wenu
mliowafikishia Ujumbe wenu)’ na wao watasema: ‘Hatuna sisi Ilm juu ya hilo, kwani
kwa hakika wewe ndie Mjuzi juu ya Kila kitu kilichofichakana’
Ambapo anasema Iman Abd Rahman Al Sudi kua: ‘Katika siku ya Malipo Mitume
watajibu kutokana na khofu baada ya kuulizwa suali hilo kua hakika sisi hatujui
walijibu vipi’ lakini baada ya hali ya khofu kutulia basi watatoa ushahidi dhidi ya
watu waliowafikishia Ujumbe wao’
Na akasema Sultan Al Balagha Imam Abu Al Qasim Al Zamakhshari kua: ‘Kutokana
na kua ni wenye kujua kuhusiana na kuulizwa basi Mtume hao, na hivyo
kutokuwepo wazi kwa uwezekano wa kuadhbiwa ama la basi Mitume hao watajibu
kua wao hawajui kuhusiana na Ilm ya Ghayb, na hivyo kua ni wenye kumuwachia
Allah Subhanah wa Ta’ala atoe hukmu kulingana na Hikma zake, ambapo kwa
484
upande mwengine hii inamaanisha kua watadhihirisha kua Ilm yao mbele ya Mola
wao si chochote si lolote’
Yaani hii inakua kama walivyojibu Malaika pale alipoumbwa Nabii Adam kama
zinavyosema aya:
﴿وَعَل َّمَ ءَادَمَ الأَسمَْآءَ كُل َّهَا ثمُ َّ عَرَضَهُمْ عَلَى الْمَلَئِكَةِ فَقَاَل أَ نْبِئُ وِنى
إِن كُ نتُمْ صَدِقِينَ ۞
قَالُواْ سُبْحَنَكَ لاَ عِلْمَ لَنَآ إِلا َّ مَا عَل َّمْتَنَآ إِن َّ َك أَن َت
أبَِسمَْآءِ هَؤُلاَِء
ٱلْعَلِيُم
ٱلحَْكِيمُ قَالَ يَاءَادَمُ أَنبِئْهُم أبَِسمَْآئِهِمْ فَلَم َّآ أَنْبَأَهُ ْم أبَِسمَْآئِهِم قَاَل أَقُلْ ل َّكُمْ إِنيّ ِ
ِض وَأَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا كُنتُمْ تَكْتُمُونَ﴾
أَعْلَمُ غَيْبَ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْ
WaAAallama adama al-asmaa kullaha thumma AAaradahum AAala almala-ikati
faqala anbi-oonee bi-asma-i haola-i in kuntum sadiqeena; Qaloo subhanaka la
AAilma lana illa ma AAallamtana innaka anta alAAaleemu alhakeemu; Qala ya
adamu anbi/hum bi-asma-ihim falamma anbaahum bi-asma-ihim qala alam aqul
lakum innee aAAlamu ghayba alssamawati waal-ardhi waaAAlamu ma tubdoona
wama kuntum taktumoona; (Surat Al Baqara 2:31-33)
Tafsir: Wao (Malaika) wakasema: ‘Utukufu ni wako, Sisi hatuna I’lm isipokua ya kile
ulichotufundisha, hakika wewe ni mjuzi wa kila kitu na mwingi wa busara’. (Allah)
Akasema: ‘Ewe Adam watajie majina yake’, na alipowatajia majina ya vitu hivyo
(Allah akasema): ‘Jee sikukwambieni kua mimi najua mambo ya Ghayb
(yaliyofichika) Mbinguni na Ardhini, na nnajua kile mnachokiweka wazi na kile
mnachokificha’.
Ambapo tukio la kuulizwa kwa Malaika la Surat Al Baqara 2:31-33 limeshatokea kwani
lililotokea Mbinguni kabla ya Ibn Adam kushushwa Ulimwenguni na tukio la kuulizwa
Mitume la Surat Al Maidah 5:109 halijatokea na hivyo litatokea katika siku ya Malipo,
na kisha baada ya hapo Allah Subhanah wa Ta’ala atamkumbusha Nabii Isa Ibn Maryam
kuhusiana na neema alizomjaalia kwa idhini yake kama zinavyosema aya:
۞
485
﴿إِذْ قَالَ ٱهلل َُّ يٰعِيسَى ٱبْنَ مَرْيمََ ٱذْكُرْ نِعْمَتىِ عَلَيْكَ وَعَلَى ٰ وَالِدَتِكَ إِذْ أَي َّدت ُّ كَ
بِرُوحِ ٱلْقُدُسِ تُكَلِّمُ ٱلن َّاسَ فىِ ٱلْمَهْدِ وَكَهْلاً وَإِذْ عَل َّمْتُكَ ٱلْكِتَابَ وَٱلحِْكْمَةَ
وَٱلت َّوْرَاةَ وَٱلإِنجِْيلَ وَإِذْ تخَْلُقُ مِنَ ٱلطِّينِ كَهَيْئَةِ ٱلط َّيرِْ إبِِذْنىِ فَتَنفُخُ فِيهَا فَتَكُو ُن
طَيرْ اً إبِِذْنىِ وَتُبرِْىءُ ٱلأَكْمَهَ وَٱلأَبْرَصَ إبِِذْنىِ وَإِذْ تخُْرِجُ ٰ ٱلْمَوتَى إبِِذِْنى وَ إِذْ كَ فَفْ ُت
بَنيِ ۤ إِسْرَائِيلَ عَنكَ إِذْ جِ ئْتَهُمْ بِٱلْبَيِّنَاتِ فَقَالَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ مِنْهُمْ إِنْ هَٰذَا إِلا َّ
سِحْرٌ م ُّبِينٌ ﴾
Idh qala Allahu ya AAeesa ibna maryama odhkur niAAmatee AAalayka waAAala
walidatika idh ayyadtuka biroohi alqudusi tukallimu alnnasa fee almahdi wakahlan
wa-dth AAallamtuka alkitaba waalhikmata waalttawrata waal-injeela wa-idh
takhluqu mina altteeni kahay-ati alttayri bi-idhnee fatanfukhu feeha fatakoonu
tayran bi-idhnee watubri-o al-akmaha waal-abrasa bi-idhnee wa-idh tukhriju
almawta bi-idhnee wa-idh kafaftu banee isra-eela AAanka idh ji/tahum
bialbayyinati faqala alladheena kafaroo minhum in hadha illa sihrun mubeenun
(Surat Al Maidah 5:110)
Tafsir: (Kumbuka) Atakaposema Allah (katika siku ya Malipo): ‘Ewe Isa Ibn Maryam,
Unakumbuka Fadhila zangu juu yako na juu ya Mama yako pale nilipokuunga mkono
kwa Ruhul Qudus (Malaika Jibril) ili uwe ni mwenye kuzungumza na watu kutoka
kwenye Mkoba wa Mtoto Mchanga na Utakapokua Mkubwa, na nilipokufundisha
kuandika, na kukupa Hikma, na Tawrat na Injil. Na pale kile ulichokifanya kwa
udongo kwa umbile la Ndege, kwa idhini yangu nawe ukakipulizia na kikawa ndege
kwa Idhini yangu, na ukawaponyesha wale waliozaliwa vipofu kwa Idhini yangu, na
wenye maradhi ya Ukoma kwa Idhini yangu, na Kuwafufua waliofariki kwa Idhini
yangu, na nilipowazuia Bani Israil dhidi yako kutokna na kua umewajia na vithibitiso
vilivyo wazi kwao, na wasioamini miongoni mwao kua ni wenye kusema: ‘Hik si
chochote isipokua ni Uchawi uliowazi’’
Ambapo kuhusiana na maneno yasemayo kua Idh qala Allahu ya AAeesa ibna maryama
odhkur niAAmatee AAalayka waAAala walidatika idh ayyadtuka biroohi alqudusi -
(Kumbuka) Atakaposema Allah (katika siku ya Malipo): ‘Ewe Isa Ibn Maryam,
Unakumbuka Fadhila zangu juu yako na juu ya Mama yako pale nilipokuunga mkono
kwa Ruhul Qudus’ basi wanasema Wanazuoni kua hii ni Kuhusiana na Roho
486
aliyopuliziwa Isa Ibn Maryam ambayo Allah Subhanah wa Ta’ala amempulizia ili iwe
na upekee wa kiheshima na huu ni mtizamo wa Imam Al Rab Ibn Anas.
Ambapo kwa upande mwengine basi kuna wanaosema kua maneno Ruhi Al Qudus yaani
Roho Mtakatifu yanamaanisha kua Utakatifu wa Roho ya Nabii Isa unatokana na kua
Maumble yake hayakutokana na Matamanio ya Kibinadamu kwa upande wa Mwanamme
na wala hayakutokana na hakukumbatiwa na Fuko la Uzazi linaloingia kwenye siku zake.
Ambapo kwa upande wa Imam Abd Rahman Al Suddi basi yeye anasema kua: ‘Ruh Al
Qudus hapa ni Malaika Jibril ambapo Isa Ibn Maryam amepewa Nguvu kutokana
nae Malaika Jibril, kwa sababu alikua ni rafiki wa karibu wa Malaika Jibril, alikua
akiimsadia, akitembea pamoja nae ardhini, na pia ndie aliepaa nae Mbinguni’
Kwani miongoni mwa sifa za Mailaka Jibril ni zile zilitajwa kwenye na maneno ya aya
isemayo:
﴿ذُو مِر َّةٍ فَٱسْتَوَىٰ ﴾
Dhoo mirratin faistawa (Surat An Najm 53:6)
Tafsir: Mwenye uwezo Mkubwa akasimama.
Anasema Bahr Ul Ilm Abdallah Ibn Abbar Radhi Allahu Anhu kua: ‘Neno Dhumirratin
hua linamaanishsa Muonekano Mzuri sana na wenye ukubwa wa kupendeza’ na pia
hua linamaanisha Kiumbe ambae asiekua na Kasoro Mwenye Nguvu Kubwa sana,
Ufahamu Mzuri sana na Afya na hivyo kumaanisha sifa ya Malaika Jibril. Na pia
humaanisha Ufaham Mzuri sana wa Mas’ala ya Fiqh na Sharia.
Ambapo anasema Imam Abd Rahman Al-Kalbi kua: ‘Siku Moja Malaika Jibiril
alimuona Ibili akitaka kumgusa na Kumdhuru Nabii Isa, hivyo Malaika Jibril
akampiga Ibisi kwa Ncha ya Ubawa wake ambao ulimpeperusha Iblisi hadi katika
Mlima uliopo India. Ni kutokana na Nguvu na Uwezo wake Malaika Jibril basi
amekua ni mwenye Kuwaadhiabu watu wa Thamud bila kuwacheleweshea Adhabu
yao mbali ya wingi wa idadi yao na Ukubwa wa Miili yao, na kutokana na uwezo
wake huo basi hu ni mwenye kusafiri kwa kasi kubwa sana kuenda na kurudi
Mbinguni na Ardhini.’
Ambapo kwa upande wa Imam Said Ibn Jubayr basi yeye anasema kua: ‘Ruhi Al Qudus
ni moja kati ya Majina Matukufu ya Allah Subhanah wa Ta’ala ambalo Isa Ibn
Maryam alikua kilitumia katika kuwahuisha watu waliokufa na kuwaonesha watu
Miujiza hio.’
487
Ama kuhusiana na Kitabu basi Wanazuoni wanasema kua ilikua ni Kitabu ambacho
chenye Juzuu 10 ambapo 9 kati yao pamoja na Hikma na Tawrat ilikua ni kwa ajili ya
Nabii Isa Ibn Maryam, ambapo Nabii Isa alikua amezihifadhi ndani ya Moyo wake.
Na anasema Imam Wahb Ibn Munabh kuhusiana Ndege kua : ‘Nabii Isa alikua
akifinyanga Ndege wa Udongo na kisha kumpulizia na akawa Ndege alie hai
kutokana na Idhini ya Allah Subhanah waa Ta’ala na alikua akifinyanga Ndege aina
ya Popo kwa sababu Ndege wa aina hio ni Ndege ambao waliokamilia kwani wana
Meno, Maziwa na pia hua wanaingia kwenye siku zao na hua hawatagi bali hua ni
wenye kuzaa. Na kisha baada ya kuruka kwao ndege hao basi huruka hadi katika
upeo wa Macho na kutoweka’
Ambapo kuhusiana na kuponyesha kwake Maradhi basi Nabii Isa alikua ni mwenye
kuponyesha wale ambao wasiowezekana kutibika kwani maradhi hayo yalikua ni wenye
kuwachanganya Matabibu kutokana na kutokuwepo uwezekano wa kutibika kwake kwa
kuwapangusa watu hao katika kiungo chenye Ugonjwa na kisha hua ni mwenye kusema
Biismi Allahi Rahmani Rahim na kiungo husika hua ni chenye kupona.
Imam Abd Rahman Al-Kalbi anasema kua Nabii Isa aliua na uwezo wa Kufufua kwa
kutumia majina Matukufu ya Allah Subanah wa Ta’ala ambayo ni : ‘Ya Hayyu Ya
Qayyum’
Ama kuhusiana na miongoni mwa waliofufuliwa na Nabii Isa baada ya kufariki kwao bas
yumo pia Al Adhar (Lazarus) ambae alikua ni rafiki yake Nabii Isa, ambapo Nabii Isa
alifunga safari kwa ajili ya kumtembelea rafiki yake huyo, lakn alipofika nyumbani
kwake akaambiwa kua Al Adhar ameshafariki mda mrefu uliopita, hivyo Nabii Isa
akaomba apelekewe kwenye Kaburi la Al Adhar na alipofika mbele yake basi akasema:
‘Ewe Allah, Mola wa Mbingu Saba na Ardhi saba, Hakka wewe ndie ulienituma
mimi kwa watu wa Bani Israil kuwaita kwa ajili ya kuifuata Dini yako, na
umewaambia Kua mimi nnaweza kuwahuisha Waliokufa kwa Idhini yako, hvo
nakuomba Ewe Mola wangu kua Mfufue Al Adhar’ Na hivyo Al Adhar akafufuka, na
kisha akawa ni mwenye kuishi na kisa akaoa na akajaaliwa kupata Watoto.
Miongoni mwa Sifa za Nabii Isa ni pamoja na kua nauwezo wa kutembea Juu ya Maji
Baharni bila ya kuzama ambapo amesema Imam Abu Mansur Al Khamshawi kua
amesema Muadh Ibn Jabal Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayh Wa Salam kua: ‘Kama mngekua mnamjua Allah Subhanah wa Ta’ala kwa
Ilm ya Yaqini basi mngefikia Darja ya Ilm ambayo hamna tena Ujinga baada yake
na ambayo hakuna alieifika.’ Hivyo Masahaba wakasema: ‘Hata wewe Ya Rasul
Allah?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Naam..Hata mimi’
488
Hivyo Masahaba wakasema: ‘Ya Rasul Allah! Hakika sisi tumesika kua Isa Ibn
Maryam alikua akitembea Juu ya Bahari’’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasema: ‘Naam kama ikiwa Mtamcha Allah Subhanah wa Ta’ala na mkawa na
Imani zaidi basi pia angekua ni mwenye kutembea juu ya hewa’
Masahaba wakasema : ‘Ya Rasul Allah hakika sisi hatukufikria kua Mitume hua na
Kasoro pia’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hakika Allah
Subhanah wa Ta’ala ana darja zilizo juu zaidi kwa Mtu yeyote kuzifikia. ’.
Naam hio ni baadhi ya Miujiza ya Nabii Isa Ibn Maryam, ambapo hata hvyo ndan yake
mna Muujiza ambao hatujauzunguzma, kwani huu ni Muujiza ambao kutokana nna
upekee wake basi umepewa jina la Sura yake maalum ambayo ni Surat Al Maidah
inayoelezea ndani yake Muujiza wa Al Maidah kuanzia katika aya ya 112 ya Sura hio ya
5 ya Qur’an.
AL MAIDAH
Neno Maidah kwa Lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kukunuta. Kuondoa,
Kukereketwa, Kujaza au Kufunika Meza Funiko, Kitambaa au kwa Chakula, Kugawa
Chakula, Kutoa Riziki.
Neno Maidah ndio lililotoa neno Maidatun ambalo hua linamaanisha Kutandaza Meza
na Kuijaza Chakula juu yake, na pia humaanisha Kuujaza Ufahamu kwa Ilmu, kwani Ilm
hua ni chakula cha Ufaham.
Tunapokiangalia Kisa cha Nabii Isa Alayhi Salam basi Allah Subhana wa Ta’ala basi
tunaona kua amezungumzia kuhusiana na Neema na Muujiza wa Maidatun
aliyowatunukia watu wa Bani Israil pale aliposema katika Qur’an.
﴿إِذْ قَالَ ٱلحَْوَارِي ُّونَ يٰعِيسَى ٱبْنَ مَرْيمََ هَلْ يَسْتَطِيعُ رَب ُّكَ أَن يُنَزِّلَ عَلَيْنَا مَآئِ دَةً
مِّنَ ٱلس َّمَآءِ قَالَ ٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ إِن كُنْتُم م ُّؤْمِنِينَ۞ قَالُواْ نُرِيدُ أَن َّْكُل مِنْهَا وَتَطْمَئِ َّن
َ
قُلُوبُنَا وَنَعْلَمَ أَن قَدْ صَدَقْتَنَا وَنَكُونَ عَلَيْهَا مِنَ ٱلش َّاهِدِينَ ﴾
Idh qala alhawariyyoona ya AAeesa ibna maryama hal yastateeAAu rabbuka an
yunazzila AAalayna ma-idatan mina alssama-i qala ittaqoo Allaha in kuntum
mu/mineena; Qaloo nureedu an na/kula minha watatma-inna quloobuna
489
wanaAAlama an qad sadaqtana wanakoona AAalayha mina alshshahideena; (Surat
Al Maidah 5:112-13)
Tafsir: Na pale waliposema Al Hawariyyuuna: ‘Ewe Isa Ibn Maryam Jee anaweza
Mola wako kututeremshia sisi juu yetu Maidah Kutoka Mbinguni?’ akasema (Nabii
Isa): ‘Kuweni Wacha Mungu kama kweli nyinyi ni wenye kuamini.’ Nao wakasema:
‘Tunataka kula kutokana nayo kwa ajili ya kuzituliza Nyoyo zetu na kujua kua ni
ukweli unaotuambia na hivyo tutakua ni wenye kushuhudia.’
Aya zinatubanishia kua ndani yake watu hawa wa Hawariyyun kulikua kuna watu ambao
walikua wana hali ya kutaka kupima uwezo na nia ya Nabii Isa katika kua tayari
kufanikisha matakwa yao juu yake ili wapate kuzithibitishia Nyoyo zao zaidi, mbali ya
kua tayari wameshapandikiziwa dalili ya Imani kwenye nyoyo zao kutoka kwa Allah
Subhanah wa Ta’ala kuhusiana nae Nabii Isa, na ndio maana Nabii Isa akawaambia kua
wawe ni wenye kumcha Allah Subhanah wa Ta’ala kama kweli wameamini.
Ambapo kwa upande wa Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari basi yeye
anasema kua: ‘Ndani yake watu hawa kulikua kuna baadhi ya wachache ambao si
wenye Imani ya kweli nae, na walikua wakitafuta sababu ya kumtoa kasoro Nabii
Isa.’
Na kwa upande mwengine basi tunaona kua mbali ya kua neno Maidah hua inamaanisha
Meza iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwekewa Chakula cha Karamu juu yake lakini
kulingana na Mtizamo wa Wanazuoni basi wanasema kua neno hili Maidah katika aya
hii linamaanisha Aina ya Chombo kama Sufuria ambacho hua kinawekwa chini na
kuzungukwa na watu kwa ajili ya kula chakula kilichomo ndani yake. Na hivyo basi hua
linamaanisha Chakula.
Ama kwa upande wa Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi yeye
anaelezea tukio hili la Hawariyyun kuomba washushiwe Maidah kwa kusema kua: ‘Isa
Ibn Maryam aliwaomba Wanafunzi wake wafunge kwa siku 30 na kisha waombe
Dua ambayo itajibiwa. Kwani kila afanyae kazi basi hulipwa ujira wake mwishoni
baada ya kumaliza kazi yake. Hivyo watu hao wakafunga na mwishoni mwa
Mfungo wao basi wakaomba kua washushiwe Maidah kutoka Mbinguni.’
Na amesema Amar Ibn Yasi Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Maidah hii ilikua ikishuka ikiwa na Mkate na Nyama, na hii
ni kwa sababu walimuomba Nabii Isa chakula ambacho watakua wanakula bila ya
kukikinai’(Imam At Tirmidhi)
Na hivyo Nabii Isa akaahidi kua atawaombea chakula ambacho hawatakiwi kua na hiana
nacho, kwani wakati pale watakapokua hawakifichi au hawasalitiani miongoni mwao,
490
basi chakula hicho kitashuka kwa ajili yao, lakini wakiwa na hiana nacho basi
wataadhibiwa baada yake kutokana na hiana yao.
Hivyo baada ya watu hao kumaliza mda wa Ibada ya Kufunga kwao basi Nabii Isa Ibn
Maryam akanyanyua juu mikono na kumuomba Mola wake kwa kusema kama
zinavyosema aya:
﴿قَالَ عِيسَى ٱبْنُ مَرْيمََ ٱلل َّهُم َّ رَب َّنَآ أَنزِلْ عَلَيْنَا مَآئِدَةً مِّنَ ٱلس َّ مَآءِ تَكُونُ لَنَا عِيداً
ِ إِنىّ مُنَزِّلهَُا عَلَيْكُ ْم
لِّأَو َّلِنَا وَآخِ رَِ وَآيَةً مِّنْكَ وَٱرْزُقْنَا وَأَنتَ خَيْرُ ٱلر َّازِقِينَ۞قَالَ ٱهلل َُّ
فَمَن يَكْفُرْ بَعْدُ مِنكُمْ ِ فَإِنيّ ۤ أُعَذِّبُهُ عَذَاابً لا َّ أُعَذِّبُهُ أَحَداً مِّنَ ٱلْ عَ الَمِينَ ﴾
Qala AAeesa ibnu maryama allahumma rabbana anzil AAalayna ma-idatan mina
alssama-i takoonu lana AAeedan li-awwalina waakhirina waayatan minka
waorzuqna waanta khayru alrraziqeena; Qala Allahu innee munazziluha
AAalaykum faman yakfur baAAdu minkum fa-innee oAAadhdhibuhu AAadhaban
la oAAadhdhibuhu ahadan mina alAAalameena; (Surat Al Maidah 5:114-115)
Tafsir: Akasema Isa Ibn Maryam: ‘Ewe Allah, Ewe Mola wetu tushushie sisi Maidah
kutoka Mbinguni ili katika siku hii iwe ni Sikukuu kwa ajili ya wa Mwanzoni na wa
Mwishoni miongoni mwetu na iwe ni Dalili kutoka kwako, Turuzuku kwani wewe ni
m-bora wa kuruzuku. Akasema Allah (Subhanah wa Ta’ala): ‘Hakika mimi
nitakuteremshieni juu yenu(Maidah), lakini kama atakufuru baada yake mmoja wenu,
basi bila ya shaka nitamuadhibu yeye kama vile nitakavyomuadhibu kiumbe
mwengine yeyote’’
Hivyo baada ya Maombi hayo ya Nabii Isa Ibn Maryam kutoka kwa Watu wa Baani Israil
basi Allah Subhanah wa Ta’ala akajibu kwa kudhihirishwa kwa masharti ya kujibiwa
maombi hayo kua wanatakiwa waoneshe shukrani kutokana na kukubaliwa maombi yao
na kujaaliwa neema wanayoitaka, kwani kutoonesha shukrani hua kuna madhara
makubwa sana yanayotokana na adhabu ya alietoa Neema ambae ni Allah Subhanah wa
Ta’ala.
Ambapo tunapozungumzia kuhusiana na kuonesha Shukrani basi hua tunazungumzia
kuonesha Utiifu katika utumiaji wa neema hizo tulizokabidhiwa ambapo kutokana na
kuonesha kwetu huko utiifu basi hua pia ni wenye kudhihirisha shukrani zetu na
kuongezewa rehma za Allah Subhanah wa Ta’ala na ulinzi wake juu yetu kama
zinavyosema Aya:
491
﴿وَإِذْ أتََذ َّنَ رَب ُّكُمْ لَئِن شَكَرْتمُْ لأََزِيدَن َّكُمْ وَلَئِن كَفَرْتمُْ إِن َّ عَذَابىِ لَشَدِيدٌ ﴾
Wa-idh taadhdhana rabbukum la-in shakartum laazeedannakum wala-in kafartum
inna AAadhabee lashadeedun (Surat Ibrahim 14:7)
Tafsir: Na kumbuka wakati alipotangazia Mola wako kwa kusema: ‘Kama
Mtanishuruku basi nitakuzidshieni, lakini kama mkinikufuru basi kwa hakika adhabu
yangu ni kubwa sana.’
Kwani Nabii Daud alimwambia Allah Subhanah wa Ta’ala: ‘Ya Allah hivi nitawezaje
mimi kukushukuru wewe ipasavyo wakati katika kila nikikuonesha shukrani zangu
juu yako basi nawe hua unaniongezea Neema zaidi kutoka kwako?’ Allah Subhanah
wa Ta’ala akasema: ‘Hakika hivi sasa umenishukuru ipasavyo’
Ambapo anasema Imam Muqatil Ibn Sulayman kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala
akajibu maombi ya Nabii Isa na kumwambia nnakutumieni kile mlichokiomba. Na
yeyote yule atakaekula na kisha akawa si mwenye kuniamini basi nitamfanya kua
ni miongoni mwa Mifano na ni miongoni mwa laana kutoka kwangu na Onyo kwa
watu watakaokuja baadae’
Na baada ya watu wa Bani Israil kubainishiwa masharti hayo na Nabii Isa na kukubaliana
nayo basi mara wakashuka Malaika ambao walikua wamechukua Maidah ambayo ndani
yake mlikua mna Mikate 7 na Samaki 7 na kuwawekea mbele yao. Nao wakaanza kula
mmoja mmoja miongoni mwao tangu wa mwanzo wao hadi wa mwisho wao na kushiba
bila ya kupungua chakula hicho.
Ambapo anasema Imam Ata Ibn Saib kua: ‘Wakati Maidah hio iliposhushwa na
kuwekwa mbele yao watu wa Bani Israil, basi walikuja watu wengi sana na
wakaanza kutia mikono yao na kuchukua sehemu ya Maidah hio kwa ajili ya kula
na ilikua na kila aina za vyakula isipokua Nyama.’
Imam Qatadah Al Sadusi basi yeye anasema kua: ‘Wakati Maidah ilipokua ikishuka
basi ilikua na Matunda ya Peponi na ilikua inakuja Asubuhi na Jioni kwani ilikua
ni sawa na Manna na Salwa waliyopewa watu wa Bani Israil wa Nabii Musa.’
Amesema Salman Al Farisi Radhi Allahu Anhu kua: ‘Nabii Isa hakuwahi kua na
mpizani wala mtu aliekua na darja yake kwani hakua ni mwenye kuwafukuza
Mayatima, wala hakua ni mwenye kucheka, wala hakua ni mwenye kuwafukuza nzi
492
wanapotua mwilini mwake, hakua ni mwenye kukichukulia chochote kwa kujisifia,
hivyo Hawwariyyin walipomwabia kua wanataka Maidah washushiwe basi nae
akamuomba Mola wake ishuke Maidah hio.’
Baada ya Maidah hio kushushwa basi Nabii Isa akawa ni mwenye kulia huku akisema:
‘Ya Allah! Ewe Mola wangu, nijaalie mimi kua ni mwenye shukrani na ijaalie hii
Maidah iwe ni yenye kutufanya wenye kuonesha Shukrani, na wala usiijalie ikawa
ni mfano wa miongoni mwa Adhabu.’
Katika wakati huu watu wake hao wa Bani Israil walikua wamevutiwa na harufu nzuri
sana ya Maidah hio kiasi ya kua kila mmoja anataka kuionja kwa hamu kubwa kutokana
na harufu hio, hivyo Nabii Isa Ibn Maryam akawaambia watu wate wake kua: ‘Wacha
wabora Miongoni mwenu wawe ni wenye kuanza kuifunua Maidah hii, na waanze
kwa Biismi Allahi kabla ya kuanza kuila.’
Lakini Hawarriyyin wakasema: ‘La! Hakika wewe ndie mwenye kustahiki zaid
kuanza kuifungua Maidah hii na kwa kuanza kuila.’ Hivyo Nabii Isa Ibn Maryam
akanyanyuka akasali rakaa mbili ndefu na kisha akamuomba Mola wake tena kua asiijalie
kua ni Mtihani dhidi yao kisha akasema: ‘Bismi Allahi, Innaka Anta Khayrun Raziqiin’
Na hapo hapo akaifungua na Maidah ikawa aimejaa Vyakula na harufu yake nzuri ya
upekee na ya kuvutia ikahanikiza katika eneo lote hilo, ikawa kuna kila aina ya vitoweo
na kila aina ya mikate yenye Maziwa, yenye Siagi, yenye Asali, yenye Samli, yenye
mafuta ya Zaitun n.k
Watu wa Bani Israil wakawa ni wenye kula kutoka katika Maidah hio kwa mda wa siku
40. Ambapo kila siku asubuhi wanapokua na njaa na kutaka basi Maidah hua inatokea
na kila siku jioni baada ya kula na kushiba basi Maidah hio hua inatoweka, katika kipindi
hiki hakuna hata mtu mmoja aliekua akishinda na njaa wala alielala na njaa miongoni
mwao.
Ilipofika siku ya 40 miongoni mwa watu wa Bani Israil wenye uwezo wakapata habari
juu ya ya Maidah hio, hivyo nao wakawa wanakuja kula, lakini Allah Subhanah wa
Ta’ala akamwambia Nabii Isa kua: ‘Ifanye Maidah hii kua ni kwa ajili ya Masikini
na wala si kwa Matajiri’ hivyo Nabii Isa akafanya hivyo na akawazuia Matajiri
kutokana na kula vilivyomo ndani ya Miadah hio, na tukio hili liliwapelekea Matajiri
kuanzisha Fitna kuhusiana na ushukaji wa Maidah hio na kuanza kusambaza uvumi kua
wanashaka na Maidah hio, na hivyo kua ni wenye kuulizana na kuwauliza watu wa Bani
Israil kuhusiana na uhakika wa kushuka kwa Maidah hio kwa kusema: ‘Hivi Jee Maidah
hio mnaiona kua inateremka Kutoka Mbinguni au inatokea mbele yenu tu?’
493
Hivyo Nabii Isa akawaambia watu wake hao kua: ‘Jitayarisheni na Adhabu ya Mola
wenu kwani tayari mmeshavuka mipaka baada ya kutilia shaka Maamrisho yake’
Allah Subhanah wa Ta’ala akamwambia Nabii Isa kua: ‘Bila ya shaka nilisema kua
yeyote yule asieamini juu ya kushuka kwake basi kwa hakika nitamshushia Adhabu
kubwa juu yake’
Hivyo Nabii Isa akasema:
﴿إِن تُعَذِّبْهُمْ فَإِن َّهُمْ عِبَادُكَ وَإِن تَغْفِرْ لهَُمْ فَإِن َّكَ أَنتَ ٱلْعَزِيزُ ٱلحَْكِيمُ ﴾
In tuAAadhdhibhum fa-innahum AAibaduka wa-in taghfir lahum fa-innaka anta
alAAazeezu alhakeemu; (Surat Al Maidah 5:116-119)
Tafsir: Hakika kama utawaadhibu basi wao ni waja wako na kama utawasamehe basi
kwa hakika wewe ni Mwingi wa Uwezo na Mwingi wa Hikma’
Wanazuoni wanasema kua kua miongoni mwa watu waliokua na shaka baada ya kuona
Maidah hio walikua ni watu 330000 ambao siku ya pili asubuhi yake wote waligeuka kua
ni Nguruwe, ambao walitapakaa mitaani, na hivyo watu waliokua walioamini juu ya
kushuka kwa Maidah hio na kua wako salama basi wakawa na khofu kubwa sana,
wakamfuataNabii Isa kwani miongoni mwao walikau ni watu wa familia zao na walikua
wakiwaita kwa majina basi walikua wakiwafuata, lakini hawawezi kuzungumza baina
yao, na Nguruwe hao waliishi kwa mda wa siku 3 na kisha wakafariki wote.
Miongoni mwa Miujiza Nabii Isa Ibn Maryam ilikua pia ni kufufua kwake watu
waliokufa na kuwafanya wawe hai, ambapo mja kati ya matukio hayo ni kua siku kadhaa
alipokua akipita makaburini aliwahi kukutana na Mtu ambae alikua amekaa kwenye
Kaburi moja huku akiwa na huzuni kubwa sana, na hivyo kumuuliza imekuaje mpaka
ikawa kila siku anakaa hapo Kaburini? Ambapo mtu huyo akajibu kua aliezikwa hapo
alikua ni Mke wake ambae uzuri wake na maumbile yake yalikua mazuri sana, na yeye
alikua akimpenda sana.
Hivyo Nabii Isa Ibn Maryam akamwambia Mtu huyo kua: ‘Hivi Jee unataka nimuombe
Allah Subahanah wa Ta’ala amfufue?’ Yule Mtu akasema : ‘Naam’ hivyo Nabii Isa
Ibn Maryam akasali rakaa 2 na kisha akamuomba Allah Subhanah wa Ta’ala amfufue
Mtu huyo, na mara hapo hapo kaburi hilo likafunguka na akatoka Mtu ambae alikua
Mweusi na hivyo Nabii Isa Ibn Maryam akamuuliza Mtu huyo: ‘Wewe ni Nani?’
Ambapo Mtu huyo akasema: ‘Ya Rasul Allah hakika mimi ni Mtu ambae nipo kwenye
Adhabu kwa mda wa miaka 40, na katika wakati huu nimeambiwa Nijibu kwa
kufufuka nami nikajibu kwa kufufuka. Ya Rasul Allah hakika mimi nishaadhibiwa
494
kwa adhabu kali sana, hivyo kama Allah Subhanah wa Ta’ala atanirudsha Duniani
basi sitomuas tena, Hivyo nakuomba niombee.’
Hivyo Nabii Musa akamuonea huruma Mtu huyo na akamuombea, na kisha
akamwambia: ‘Haya Nenda zako.’ Mtu huyo akaondoka, ambapo yule mtu aliekua
amekaa kaburini analia akamwambia Nabii Isa Ibn Maryam kua: ‘Ya Rasul Allah hakika
mimi nilikosea kuhusiana na Kaburi la Mke wangu, sio hili alilotoka huyu bwana
bali ni hili hapa’
Hivyo Nabii Isa Ibn Maryam akamuomba tena Allah Subhanah wa Ta’ala na hapo hapo
Kaburi hilo jengine likafunguka na ndani yake akatoka Mwanamke Mzuri sana. Hivyo
Nabii Isa Ibn Maryam akamwambia Nabii Isa: ‘Jee unamjua huyu Mwanamke?’ yule
Mtu akasema: ‘Naam, huyu ndie Mke wangu’ hivyo Isa Ibn Maryam akamuomba Allah
Subhanah wa Ta’ala kua Mwanamke huyo aendelee kuishi, hivyo Mtu huyo na Mke
wake wakamshukuru Nabii Isa kisha wakaondoka.
Katika safari yao Mtu na mke wake huyo, basi wakapumzika chini ya Mti, na Mume
akalala, mara akapita Mtoto wa Mfalme na baada ya kumuona Mke huyo akampenda na
kuvutiwa nae, na akamuashiria Mke huyo amfuate, na Mke huyo akavutiwa na Mtoto wa
Mfalme na kuamua kumfuata.
Mwenye mke alipoamka bila ya kumuona Mke wake basi akaamua kumtafuta Mke wake,
na kwa bahati akamuona pamoja na Mtoto wa Mfalme na alipomkimbilia na kusema kua
ni Mke wake, basi Mtoto wa Mfalme akasema kua ni Mtumwa wake yeye, hivyo wakati
mvutano huo unaendelea mara akatokea Nabii Isa ambapo Mume wa Mke huyo
akamlalamikia kuhusiana na yaliyotokea, na Mke huyo alipotakiwa kurudi kwa Mume
wake basi akasema kua yeye ni Mtumwa wa Mtoto wa Mfalme na hamjui Mwanamme
huyo.
Hivyo Nabii Isa akamwambia Mke huyo: ‘Turudishe Amanah tuliyokupa.’ Na Mke
huyo akasema: ‘Bila ya shaka nitakurudishia’ na kisha hapo hapo Mke huyo akaanguka
chini na kufariki na hapo Nabii Isa akasema kumwambia yule Mume: ‘Hivi Jee umewahi
kuona Jambo la kustaajabisha zaidi ya yule Mwanamme? Allah Subhanah wa
Ta’ala alimpa Mtihani wa Kifo wakati akiwa ni Kafiri na kisha akamfufua na
akawa ni mwenye Kuamini’
‘Na jee umewahi kuona Mwanamke ambae Allah Subhanah wa Ta’ala alimuingiza
kwenye Mtihani wa Kifo huku akiwa Mwenye Kuamini lakini akawa Kafiri baada
ya kufufuliwa kwake?’
Nabii Isa aliwafufua watu wanane ambapo Watu wa Bani Israil wakamwambia Nabii Isa
kua: ‘Hakika wewe Isa ni mwenye kuwafufua watu ambao wamefariki Karibuni, na
495
hivyo hua hawajaondokewa na roho zao bado, kama kweli wewe na uwezo huo basi
tufufulie wale watu waliofariki zamani sana.’
Hivyo Nabii Isa akawaambia watu hao kua: ‘Sawa hivyo Jee mnataka nimfufue Nani?’
Watu hao wakasema: ‘Mfufue Sham Ibn Nuh’
Nabii Isa akasema: ‘Nionesheni Kaburi lake’ hivyo watu hao wakamuonesha Nabii Isa
Kaburi la Sham ambae ni Mtoto wa Nabii Nuh.
Nabii Isa Ibn Maryam alpofika kwenye Kaburi hilo basia akaomba Dua kisha akasema;
‘Ewe Sham, Fufuka kwa Idhini Ya Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Hivyo Sham akafufuka kutoka kwenye Kaburi hilo huku akiwa ni mwenye kusema: ‘Ya
Rasul Allah Hakika Mimi nipo chini ya Amri yako.’ Na watu wa Bani Israil
wakamuona kua ni mwenye Ndevu na Nywele Nyeupe, hivyo wakamuuliza: ‘Imekuaje
Na Mvi wakati ulipofariki ulikua Kijana’ na Sham akasema: ‘Hakika mimi nilisikia
Sauti ikiniamrisha Ninyanyuke, na hivyo kutokana na kua na khofu juu ya Siku ya
Malipo, na nikadhani kua ni sauti ya Israfil na hivyo Nywele zangu zikawa na rangi
nyeupe kwa khofu’
Nabii Isa akasema: ‘Vipi unasemaje? Unatakaa kuendelea kuishi au unataka kurudi
kaburini?’ Sham Ibn Nuh akauliza: ‘Ya Rasul Allah, jee kama nikiendelea Kuishi
halafu itakuaje nitakufa tena ama vipi?’ Nabii Isa akajibu: ‘Naam Mwisho wake
Utakufa’ Sham akasema: ‘Kwa maana hio basi hakika mimi sitoepukana na
Machungu ya Kifo’ Hivyo Sham akarudi tena Kaburini, ambapo wanasema wenye kujua
kua Sham alifariki miaka 4000 kabla ya kuja Nabii Isa Ibn Maryam.
Hivyo kutokana na Miujiza yake hii ya kufufua Watu na myengineo basi imewapelekea
Wakristo kusema kua Nabii Isa ni Mungu na pia ni Mtoto wa Mungu kama vile
wanavyoema Mayahudi kuhusiana na Uzayr kama inavyosema Qur’an;
﴿وَقَالَتِ ٱلْيَهُودُ عُزَيْرٌ ٱبْنُ ٱهلل َِّ وَقَالَتِ ٱلن َّصَارَى ٱلْمَسِ يحُ ٱبْنُ ٱهلل َِّ ذٰلِكَ قَوْلهُُ م
أبَِفْوَاهِهِمْ يُضَاهِئُونَ قَوْلَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ مِن قَبْلُ قَاتَلَهُمُ ٱهلل َُّ أَنى َّٰ يُؤْفَكُونَ ﴾
Waqalati alyahoodu AAuzayrun ibnu Allahi waqalati alnnasara almaseehu ibnu
Allahi dhalika qawluhum bi-afwahihim yudhahi-oona qawla alladheena kafaroo
min qablu qatalahumu Allahu anna yu/fakoona (Surat At Tawba 9:30)
496
Tafsir: Na wanasema Mayahud kua Uzayr ni Mtoto wa Allah na wanasema Manasara
kua Al Masih ni mtoto wa Allah, hii ni kauli kutoka kwenye Midomo yao, wanaiga
kauli za wale waliokufuru kabla yao. Laana ya Allah iwe juu yao kwani wako mbali
na Ukweli.
Na hivyo Allah Subhanah wa’a Ta’ala anatubainisha kwa vithibitisho kua wasemavyo
hiyo wako mbali na ukweli na hii ni kwa sababu Nabii Isa Ibn Maryam ni Nabii wake na
ni Mtume wake, na wala sio Mungu, hivyo kua na Mtizamo mwengine zaidi ya huo basi
hua ni kukufuru kama inavyosema Surat Al Maidah kua:
﴿ل َّ قَدْ كَفَرَ ٱل َّذِينَ قَآلُو ۤ اْ إِن َّ ٱهلل ََّ هُوَ ٱلْمَسِ يحُ ٱبْنُ مَرْيمََ قُلْ فَمَن يمَْلِكُ مِنَ ٱهلل َِّ
شَيْئاً إِنْ أَرَادَ أَن يُهْلِكَ ٱلْمَسِ يحَ ٱبْنَ مَرْيمََ وَأُم َّهُ وَمَن فىِ ٱلأَرْضِ جمَِيعاً وَهللِ َِّ مُلْ ُك
ّ كُل شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴾
ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا يخَْلُقُ مَا يَشَآءُ وَٱهلل َُّ ٰ عَلَى ِ
Laqad kafara alladheena qaloo inna Allaha huwa almaseehu ibnu maryama qul
faman yamliku mina Allahi shay-an in arada an yuhlika almaseeha ibna maryama
waommahu waman fee al-ardhi jameeAAan walillahi mulku alssamawati waalardhi
wama baynahuma yakhluqu ma yashao waAllahu AAala kulli shay-in
qadeerun (Surat Al Maidah 5:17)
Tafsir: Kwa hakika wamekufuru wale ambao wasemao kua Allah ni Masih Ibn
Maryam, waambie (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam): ‘Jee ni nani
atakaeweza kua na umiliki wa pamoja na Allah juu ya kitu chochote kile kama (Allah
Subhanah wa Ta’ala) akitaka kumuangamiza Masih Ibn Maryam na Mama na kila
kitu hapa ardhini kwa pamoja? Kwani kwa Allah ndiko kwenye Umiliki wa Mbingu
na Ardhi na kla klichomo baina yake Mwenye uwezo wa Kuumba akitakacho, Allah
ana uwezo juu ya kila kitu.’
Ambao hii ni aya inayokataa na kukanusha kuwepo kwa ushirika baina ya Allah
Subhanah wa Ta’ala katika Mamlaka yake ya Umungu si kwa Nabii Isa tu bali pia na
kwa Maryam Bint Imran, na hivyo kubainisha kua hakuna tofauti baina ya Isa bn Maryam
na Maryam Bint Imran kwani wote ni viumbe wa Allah Subhanah wa Ta’ala.
Ambapo katiika aya hii basi tunaona kua Allah Subhanah wa Ta’ala hakutumia jina la
Nabii Isa kama Isa Ibn Maryam, bali ametmia Jina la Sifa yake kuu ambayo inawapelekea
watu kua ni wenye kumdhania kua ni Mungu, yaani aya imetumia jina la Masih Ibn
Maryam ambalo tumesema kua linamaanisha Kupangusa, Kufuta, Kupapasa kwa
497
Utaratibu, Kupakaza Kitu, Kupaka kitu kwenye Mwili, Kupitisha Mkono juu ya Kitu,
Kupendeza, kua Nzuri na yenye Baraka, Kufunga safari ya Kutembea ardhini na pia
humaanisha Mfalme au Muokozi.
Na hivo kuanisha kua sifa yake hio ya kua na Uwezo wa kugusa Mgonjwa akapona na
ya Uokozi pia haimfanyi kua ni mwenye sifa za Kimungu, na kisha aya zinaweka wazi
kwa kuhoji kwa kusema kua: ‘Jee ni nani atakaeweza Kumzuia Allah Subhanah wa
Ta’ala kama akitaka kumuangamiza huyo Masih Ibn Maryam na Maryam Bint
Imran kama akiamua kuwaangamiza wao na kila kitu klichomo Ardhini?’
UTHIBITISHO WA ISA IBN MARYAM KUA SI MUNGU.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anawabainishia Wakristo na Mayahudi kua
wasishangazwe na Maumbile ya Isa Ibn Maryam kwani yeye ni Kiumbe kama viumbe
wengine, kwani nae Isa Ibn Maryam alibainisha juu ya hayo na hivyo wanaosema
kinyume na maneno yake mwenyewe Isa Ibn Maryam basi ni wenye kukufuru, kama
zinavyoendelea kubainisha tena Aya za Surat Al Maidah kua:
﴿لَقَدْ كَ فَ رَ ٱل َّذِينَ ۤ قَالُواْ إِن َّ ٱهلل ََّ هُوَ ٱلْمَسِ يحُ ٱبْنُ مَرْيمََ وَقَالَ ٱلْمَسِ يحُ َبَنيِ ۤ إِسْرَائِيل
ٱعْبُدُواْ ٱهلل ََّ رَبىِّ وَرَب َّكُمْ إِن َّهُ مَن يُشْرِكْ بِٱهلل َِّ فَقَدْ حَر َّمَ ٱهلل َُّ عَلَيهِ ٱلجَْن َّةَ وَ مَ أْوَاهُ ٱلن َّا ُر
وَمَا لِلظ َّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ۞ل َّقَدْ كَفَرَ ٱل َّذِينَ ۤ قَالُواْ إِن َّ ٱهلل ََّ اثَلِثُ ثَلاَثَةٍ َومَا مِنْ إِلَ ٍٰه
إِلا َّ إِلَٰهٌ وَاحِ دٌ وَإِن لم َّْ يَنتَهُواْ عَم َّا يَقُولُونَ لَيَمَس َّن َّ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ مِنْهُمْ عَذَابٌ أَلِ يمٌ ﴾
َ
Laqad kafara alladheena qaloo inna Allaha huwa almaseehu ibnu maryama waqala
almaseehu ya banee isra-eela oAAbudoo Allaha rabbee warabbakum innahu man
yushrik biAllahi faqad harrama Allahu AAalayhi aljannata wama/wahu alnnaru
wama lildhdhalimeena min ansarin; Laqad kafara alladheena qaloo inna Allaha
thalithu thalathatin wama min ilahin illa ilahun wahidun wa-in lam yantahoo
AAamma yaqooloona layamassanna alladheena kafaroo minhum AAadhabun
aleemun; (Surat Al Maidah 5:72-73)
Tafsir: Kwa hakika wamekufuru wale ambao ni wenye kusema kua Allah Masihu Ibn
Maryam’ wakati Masih Ibn Maryam mwenyewe amesema: ‘Enyi watu wa Bani Israil
Muabuduni Allah ambae ni Mola wangu na ni Mola wenu, kwani kwa hakika
498
anaemshirikisha Allah, basi Allah amemharamishia Pepo na makazi yake yatakua ni
Motoni na kwa wenye kufanya Dhulma basi hakuna wa kuwanusuru.’ Kwa hakika
Wamekufuru wale ambao ni wenye kusema kua kwa hakika Allah ni wa tatu katika
Watatu. Na hakuna aliekua Mungu isipokua Mungu ambae ni Mmoja, na kama
hawakusita kutokana na wayasemayo, basi kwa hakika watakumbana wale wenye
kukufuru na adhabu kali sana.
Naam baada ya Allah Subhanah wa T a’ala kudhihirisha maneno ya Al Masih Isa Ibn
Maryam kwa watu wake wa Bani Israil na Manasara, na kukanusha Utatu wa Kimungu
na kuthibisha Umoja wake basi Allah Subhanah wa Ta’ala anawaonya na kuwausia kwa
kuwaambia kua anawataka wale wenye kuamini kinyume chake kama alivyosema yeye
kua yeye yuko tayari kuwasamehe kama watamuomba Msamaha kwani yeye ni mwenye
Sifa ya kua ni Mwingi wa Usamehevu na Mwingi wa Huruma, kama zinavyosema aya:
﴿أَفَلاَ يَتُوبُونَ إِلىَٰ ٱهلل َِّ وَيَسْتَغْفِرُونَهُ وَٱهلل َُّ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ۞م َّا ٱلْمَسِ يحُ ٱبْنُ مَرْيمََ إِلا َّ
رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِ ٱلر ُّسُلُ وَأُم ُّهُ صِدِّيقَةٌ كَاَ َْكُلاَنِ ٱلط َّعَامَ ٱنْظُرْ كَيْفَ
نُبَينِّ ُ لهَُمُ ٱلآَتِ ثمُ َّ ٱنْظُرْ أَنى َّٰ يُؤْفَكُونَ ﴾
Afala yatooboona ila Allahi wayastaghfiroonahu waAllahu ghafoorun
raheemun; Ma almaseehu ibnu maryama illa rasoolun qad khalat min qablihi
alrrusulu waommuhu siddeeqatun kana ya/kulani alttaAAama ondhur kayfa
nubayyinu lahumu al-ayati thumma ondhur anna yu/fakoona (Surat Al Maidah 5:74-
75)
Tafsir: Hivyo jee hawatotubu kwa Allah na kuomba msamaha kwani kwa hakika Allah
ni mwingi wa Usamehevu na na mwingi wa Huruma. Hakua Masih Ibn Maryam
isipokua ni Mtume, kwa hakika wamekuja kabla yake Mitume. Na Mama yake alikua
ni aliesadiki wote walikua ni wenye kula Vyakula, angalia namna tunavyowabainisha
wazi Aya zetu lakini hata hivyo angalia wanavyopotoka.
Anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Aya hii
inatubainishia kua Mitume wote walikua ni Ibn Adam na hivyo hawakua na
Maumbile mengine yeyote ya Kimalaika wala ya Kijini’
Ambapo Sultan Mutakallimin Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye
anasema kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala anawaelezea Isa Ibn Maryam na Maryam
Bnt Imran kua walikua n wenye Kula vyakula na hivyo basi kuthibitisha kua ni
499
wenye kujisaida pia’ hivyo jee inakuaje wenye sifa ya kua ni Watu kua ni wenye
kuhesabiwa kua ni Miungu?
Kwani Allah Subhanah wa Ta’ala hakuwahi kuwaletea watu hapo kabla Mitume ambao
ni wenye maumbile ya Majini au Malaika, bali hua daima ni mwenye kuwatumia Ibn
Adam wenzao na ndio maana akasema:
﴿وَمَآ أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ إِلا َّ رِجَالاً ن ُّوحِ ي ۤ إِلَيْهِمْ مِّنْ أَهْلِ ٱلْقُرَىٰ أَفَلَمْ يَسِ يرُواْ فىِ
ٱلأَرْضِ فَيَنظُرُواْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ ٱل َّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ وَلَدَارُ ٱلآخِ رَةِ خَ يْرٌ لِّل َّذِينَ
ٱت َّقَواْ أَفَلاَ تَعْقِلُونَ ﴾
Wama arsalna min qablika illa rijalan noohee ilayhim min ahli alqura afalam
yaseeroo fee al-ardhi fayandhuroo kayfa kana AAaqibatu alladheena min qablihim
waladaru al-akhirati khayrun lilladheena ittaqaw afala taAAqiloona (Surat Yusuf
12:109)
Tafsir: Na Hatujawahi kutuma (Mtume) kabla yako isipokua ni watu miongoni mwao
kuwashushia wao. Hivi jee hawajatembea kwenye ardhi wakaona mwisho wa wale
waliokua kabla yao? Na kwa hakika makazi ya Akhera ni bora kwa wenye kua na
Taqwa. Jee hamna akili?
Aya imetumia neno Rijalan ambalo hua ni lenye kutokana na neno Rajila au Rajala
ambalo hua ni lenye kumaanisha Kutembea kwa miguu miwili, Kuhimiza kwa kutumia
miguu, Kuruhusu Mama kumnyonyesha Mtoto wake, Kuachia huru na Mama yake,
hivyo neno Rijalan humaanisha Mtu, ambapo Rijal hua ni Mwanamme.
Na Imani ya Dini ya Kislam ni yenye kusimamia kwenye msingi wa Imani ya
kumpwekesha Allah Subhnah wa Ta’ala pekee na hivyo haikubaliki kuwepo kwa Mungu
mwengine zaidi yake Allah Subhanah wa Ta’ala, kwani kufanya hivyo hua ni kwenye
Kumtoa Muislam katika Imani ya Dini yake, na kutokana na kua watu wa Ahl Al Kitab
yaani Wakristo hua ni wenye kuamini kua Nabii Isa ni mwenye Sifa ya Kiumbe
sambamba na ya Kimungu basi Allah Subhanah wa Ta’ala anawabanishia ukweli watu
hao kwa kuwaonya kwa kusema kua:
500
﴿َٰهْ لَ ٱلْكِتَابِ لاَ تَغْلُواْ فىِ دِينِكُمْ وَلاَ تَقُولُواْ عَلَى ٱهلل َِّ إِلا َّ ٱلحَْق َّ إِ نم ََّا ٱلْمَسِ يحُ
عِيسَى ٱبْنُ مَرْيمََ رَسُولُ ٱهلل َِّ وَكَلِمَتُهُ أَلْقَاهَا إِلىَٰ مَرْيمََ وَرُوحٌ مِّنْهُ فَآمِنُواْ بِٱهلل َِّ وَرُسُلِِه
وَلاَ تَقُولُواْ ثَلاَثَةٌ ٱنتَهُواْ خَيرْ اً ل َّكُمْ إِنم ََّا ٱهلل َُّ إِلَٰهٌ وَاحِ دٌ سُبْحَانَهُ أَن يَكُونَ لَهُ وَلَدٌ ل َّهُ
مَا فىِ ٱلس َّمَاوَا ِت وَمَا فىِ ٱلأَرْضِ ٰ وَكَفَى بِٱهلل َِّ وَكِيلاً۞ ل َّن يَسْتَنكِفَ ٱلْمَ سِ يحُ أَن
ْف عِبَادَتِهِ وَيَسْتَكْبرِْ
عَنْ ۤ ئِكَةُ ٱلْمُقَر َّبُونَ وَمَن يَسْتَنْكِ
يَكُونَ عَبْداً هللِ َِّ وَلاَ ٱلْمَلا
فَسَيَحْشُرُهُمْ إِلَيهِ جمَِيعاً ﴾
Ya ahla alkitabi la taghloo fee deenikum wala taqooloo AAala Allahi illa alhaqqa
innama almaseehu AAeesa ibnu maryama rasoolu Allahi wakalimatuhu alqaha ila
maryama waroohun minhu faaminoo biAllahi warusulihi wala taqooloo
thalathatun intahoo khayran lakum innama Allahu ilahun wahidun subhanahu an
yakoona lahu waladun lahu ma fee alssamawati wama fee al-ardhi wakafa biAllahi
wakeelan Lan yastankifa almaseehu an yakoona AAabdan lillahi wala almala-ikatu
almuqarraboona waman yastankif AAan AAibadatihi wayastakbir
fasayahshuruhum ilayhi jameeAAan (Surat AnNisaa 4:171-172)
Tafsir: Enyi watu wa Ahl Al Kitab msivuke mipaka katika Dini yenu na wala msiseme
kuhusiana na Allah ispokua Ukweli, kwa hakika Masih Isa Ibn Maryam ni Mtume wa
Allah na ni Kauli yake ambayo alibeba Maryam, na Ruh kutoka kwake, hivyo
Muaminini Allah na Mitume wake na wala msiseme : ‘Utatu, Kusitisha kwenu ni bora,
kwani Allah ni Mmoja tu, Utukufu ni wake peke yake na yuko mbali yeye kutokana na
kua na Mtoto’ Kwake yeye ndio kwenye umiliki wa kila kilichomo Mbinguni na
Ardhini, Hakika llah ni mwenye kutosheleza juu ya usimamizi wa kila kitu. Kwani
kamwe Masih hatokua na fakhari ya kukataa kua yeye ni Mja wa Allah, na Wala
Malaika waliokaribu nae Allah Subhanah wa Ta’ala, na yeyote yule atakaekosa fahari
ya Uja wake (mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala) na akawa na Kibri basi (Allah
Subhanah wa Ta’ala) atawakusanya wote kwa pamoja mbele yake (katika siku ya
malipo).
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anaendelea kutuambia kua atawauliza Mitume
kuhusiana na namna walivyopokewa na watu wao baada ya kuwafikishia Ujumbe wao,
kutoka kwake, ambapo mongoni mwao watakaoulizwa basi yumo pia Isa Ibn Maryam
ambapo hali itakua kama zisemavyo aya:
501
﴿وَإِذْ قَالَ ٱهلل َُّ يٰعِيسَى ٱبْنَ مَرْيمََ أَأَنتَ قُلتَ لِلن َّاسِ ٱتخ َِّذُونىِ وَأُمِّىَ إِلَٰهَينِْ مِن
دُونِ ٱهلل َِّ قَالَ سُبْحَانَكَ مَا يَكُونُ ليِ ۤ أَنْ أَقُولَ مَا لَيْسَ لىِ بحَِقٍّ إِن كُنتُ قُلْتُهُ
فَقَدْ عَلِمْتَهُ تَعْلَمُ مَا فىِ
نَفْسِ ى وَلاَ أَعْلَمُ مَا فىِ نَفْسِ كَ إِن َّكَ أَنتَ عَلا َّمُ
ٱلْغُيُوبِ ۞مَا قُلْتُ لهَُمْ إِلا َّ مَآ أَمَرْتَنىِ بِهِ أَنِ ٱعْبُدُواْ ٱهلل ََّ رَبىِّ وَرَب َّكُمْ وَكُن ُت عَلَيْهِ ْم
ل
ّ
شَهِيداً م َّا دُمْتُ فِيهِمْ فَلَم َّا تَوَف َّيْتَنىِ كُنتَ أَنتَ الر َّقِيبَ عَ لَيْهِ مْ وَأَنتَ ٰ عَلَى كُ ِ
شَيْءٍ شَهِيدٌ ﴾
Wa-idh qala Allahu ya AAeesa ibna maryama aanta qulta lilnnasi ittakhidhoonee
waommiya ilahayni min dooni Allahi qala subhanaka ma yakoonu lee an aqoola ma
laysa lee bihaqqin in kuntu qultuhu faqad AAalimtahu taAAlamu ma fee nafsee
wala aAAlamu ma fee nafsika innaka anta AAallamu alghuyoobi; Ma qultu lahum
illa ma amartanee bihi ani oAAbudoo Allaha rabbee warabbakum wakuntu
AAalayhim shaheedan ma dumtu feehim falamma tawaffaytanee kunta anta
alrraqeeba AAalayhim waanta AAala kulli shay-in shaheedun(Surat Al Maidah
5:116-117)
Tafsir: Na kumbuka wakati Allah Subhanah wa Ta’ala atakaposema (katika siku ya
Malipo); ‘Ewe Isa Ibn Maryam! Hivi jee uliwaambia wewe watu kua: ‘Nichukulieni
Mimi na Mama yangu kama Miungu wawili baada ya Allah?’ Atasema (Nabii Isa):
‘Utukufu ni wako Allah! Siwezi mimi kusema kile ambacho sina haki ya kusema juu
yake. Hivyo kama ningesema kitu kama hicho, basi kwa hakika wewe ni mwenye kujua
juu yake, kwani wewe ni mwenye kujua kile kilichomo ndani ya Nafsi yangu wakati
mimi si mwenye kujua kilichomo ndani ya Nafsi yako. Bila ya shaka ni wewe pekee
ndie mwenye kujua vilivyofichikana na visivyoonekana’’Hakika mimi sikuwaambia
isipokua kile ambacho uliniamrisha (niwaambie) kua: ‘Muabuduni Allah Mola wangu
na Mola wenu na mimi nilikua ni shahidi juu yao wakati nilipokua naishi pamoja nao.
Lakini uliponichukua Juu, basi wewe ndie uliekua Muangalizi juu yao na wewe ni
mwenye kushuhudia juu ya kila kitu’
Ambapo Aya zinatuwekea wazi kua wale wote wanaodai kua ni wafuasi wa Nabii Isa Ibn
Maryam, basi ni wafuasi ambao hawafanani na mafundisho yake, kwani wenye kuenda
kinyume na Maamrisho yake na hivyo hua ni wenye kufuata matamanio ya Nafsi zao na
matokeo yao wataingia Motoni badala yake, kwani Nabii Isa atatoa Ushahihi wake dhidi
502
yao na kuwakana kua wao sio wafuasi wake, kwa sababu hawakua ni wenye kushikamana
na usahih na ukweli wa Ujumbe wake juu yao.
Kwani Allah Subhanah wa Ta’ala anatubainishia kua Waumini wa kweli ni wale
waliokua na Msimamo katika Kuamini kwao kama zinazosema aya:
﴿مِّنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُواْ مَا عَاهَدُواْ ٱهلل ََّ عَلَيْهِ فَمِنْهُمْ م َّن قَضَى ٰ نحَْبَهُ
وَمِنْهُمْ م َّن يَنتَظِرُ وَمَا بَد َّلُواْ تَبْدِيلاً ﴾
Mina almu/mineena rijalun sadaqoo ma AAahadoo Allaha AAalayhi faminhum
man qada nahbahu waminhum man yantadhiru wama baddaloo tabdeelan (Surat
Al Ahzab 33:23)
Tafsir: Miongoni mwa Waumini Mna watu walioamini kile walichokiahidi kwa Allah
juu yao, na kuna baadhi yao wanasubiri na hawajabadilika hata kidogo (Imani yao)
Ambapo katika kuhojiwa kwake Isa Ibn Maryam katika siku hio ya Malipo na Allah
Subhanah wa Ta’ala basi ataanza kujibu kwa Kumtukuza Allah Subhnah wa Ta’ala kwa
kusema kua Utukufu ni wake yeye peke yake, na hivyo kudhihirisha kua yeye Isa Ibn
Maryam kamwe hastahiki kupewa Utukufu wa kufanyiwa hivyo walivyofanya wanaojiita
kua ni wafuasi wake.
Na kuthibitisha kua kutokana na Maumbile yake basi yeye si mwenye uwezo wa kuona
na kujua kila kitu, bali ni Allah Subhanah wa Ta’ala pekee ndie mwenye uwezo huo na
ameona wazi juu ya kila alichokisema kuwaambia watu wake na kila alichokifanya kwa
ajili yao watu hao, na kisha anamalizia kwa kusema kua:
﴿إِن تُعَذِّبْهُمْ فَإِن َّهُمْ عِبَادُكَ وَإِن تَغْفِرْ لهَُمْ فَإِن َّكَ أَنتَ ٱلْعَزِيزُ ٱلحَْكِيمُ ﴾
In tuAAadhdhibhum fa-innahum AAibaduka wa-in taghfir lahum fa-innaka anta
alAAazeezu alhakeemu; (Surat Al Maidah 5:118)
Tafsir: Hivyo kama utawaadhibu basi wao ni waja wako na kama utawasamehe basi
kwa hakika wewe ni Mwingi wa Uwezo na Mwingi wa Hikma’
Na hivyo Nabii Isa kua ni mwenye kuwarudisha watu wake hao alioambiwa awaongoze
na madai yao hayo kama yalivyokua Mbele ya Mola wake na kumuachia Maamuzi yake
503
juu yao watu hao, kua kama atataka kuwaadhibu basi ni haki yake kuwaadhibu watu hao,
na kama atataka kuwasamehe basi ni kutokana na Huruma, Rehma, Hikma na
Usamehevu wake Allah Subhanah wa Ta’ala.
Tunapoangalia Kwa upande mwengine basi amesema Abu Dhar Al Ghifari Radhi Allahu
Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisali na kuirudia aya hii ya Surat
Al Maidah 5:119 katika Qiyam Al Layl mpaka ikakaribia kuingia Alfajir, nami
nikamuuliza ni kwa sababu gani ambapo nae kaniambia kua: ‘Hakika mimi
nimeuombea Ummah Wangu na Wamepewa Uombezi wangu isipokua kwa wale
watakaomshirikisha Allah Subhanah wa Ta’ala’’
Na hi ni kwa sababu amesema Allah Subhanah wa Ta’ala katika Surat An Nisaa kua:
﴿إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذٰلِكَ لِمَن يَشَآءُ وَمَن يُشْرِكْ بِٱهلل َِّ
فَقَدْ ضَل َّ ضَلاَلاً بَعِيداً ﴾
Inna Allaha la yaghfiru an yushraka bihi wayaghfiru ma doona dhalika liman
yashao waman yushrik biAllahi faqad dhalla dhalalan baAAeedan (Surah An Nisaa
4:116)
Tafsir: Kwa Hakika Allah hasamehe wenye kumshirikisha, lakini husamehe dhambi
nyenginezo kwa amtakae. Na anaemshirikisha Allah basi kwa hakika hua ni mwenye
kupotoka katika upotovu wa mbali sana.
KUPANDISHWA MBINGUNI KWA ISA IBN MARYAM NA KIFO CHA
MARYAM BINT IMRAN.
Anasema Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Isa Ibn Maryam
alikutana na Mayahudi ambao walipomuona basi nao wakamnadia wa kusema:
‘Anakuja mbele yetu Mchawi na Mtoto wa Mchawi, Msaliti na Mtoto wa
Msaliti’’na kisha baada ya hapo wakaanza kumtukana Isa Ibn Maryam. Hivyo Isa
Ibn Maryam akamuomba Allah Subhanah wa Ta’ala kwa kusema: ‘Ya Allah! Wewe
ni Mola wangu, na Mimi natokana na Ruhi wako, Nimeumbwa kwa Kauli yako, na
sikuja kwao kwa Hiari yangu, Ya Allah mlaani yule ambae ni mwenye kunitukana
mimi na Mama yangu’
Hivyo hapo hapo watu hao waliokua wakimtukana Nabii Isa wakageuka na kua Kima
wote. Hivyo Chifu wa Mayahudi alipoona tukio hili basi basi akaingiwa na khofu kubwa
504
sana kutokana na Maombi yake hayo. Hivyo wakajikusanya na kuanza kuhoji kuhusiana
na hali ya hatari ya uwezo wake huo wa kuwageuza Watu Kima, ghafla moja na kuona
kua bora wamalizane nae Isa Ibn Maryam kwa kumkamata na kumuua.
Lakini walipoamua kufanya hivyo basi Allah Subhanah wa Ta’ala akamtuma Malaika
Jibril na kumwambia kua amlinde kwa yake ya Ukuta utakaomzunguka Nabii Isa ili
asidhuriwe na Mayahudi hao. Hivyo Mayahudi hao wakamteua mmoja miongoni mwao
aingie ndani ya ukuta huo kupitia kwenye Upenyo mdogo wa Ukuta huo ili akamuue
Nabii Isa, ambapo Mtu huyu aliechaguliwa alikua akiitwa Filitianus au Pilato.
Hivyo Filitianus alipoingia ndani kwenye upenyo wa Ukuta huo, akawa hakumkuta Isa
Ibn Maryam ndani yake, na akakaa kwa mda akimtafuta, huku Mayahudi wenzake
walioko nje wakidhani kua labda alikua akipigana nae Nabii Isa Ibn Maryam ndani yake,
lakini kumbe katika tukio la kuingia ndani kwake basi Allah Subhanah wa Ta’ala
akamjalia Filitianus kua na muonekano wa Mithili ya Nabii Isa Ibn Maryam badala yake,
na hivyo alipotoka nje basi Mayahudi wakadhani kua Filitianus ameuliwa na Isa Ibn
Maryam na hivyo Isa Ibn Maryam ndio ametoka nje baada ya kumuua Filitianus, hivyo
wakamkamata na kisha wakamuua na kumsulubu Filitianus huku wakidhani kua yeye
ndie Isa Ibn Maryam.
Ambapo kwa upande wa Imam Wahb Ibn Munabih basi yeye anasema kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala alimjaalia Isa Ibn Maryam kua ni mwenye kujua kua karibuni
ataondoka Ulimwenguni, hivyo nae akawa na khofu juu ya kuondoka kwake, na
akawaalika Wanafunzi wake na kuwatarishia Chakula cha Usiku na kuwaambia:
‘Kusanyikeni pamoja nami leo Usiku kwani ninakuhitajini.’
Ulipowadia Usiku wa siku hio, basi Isa Ibn Maryam akawatayarishia Wanafunzi
wake hao Chakula alichopika kwa ajili yao, wakala hadi wakamaliza na kisha
akawa ni mwenye kuwakosha mikono yao huku akiwausia juu ya Allah Subhanah
wa Ta’ala, huku akiwapangusa mikono yao kwa nguo yake. Ambapo hili lilikua ni
jambo ambalo halikuwavutia Wanafunzi wake. Na hivyo Nabii Isa akawaambia
Wanafunzi wake hao kua: ‘Hatokua miongoni mwangu yule ambae hakunifanyia
kile ambacho mimi nimemfanyia yeye’
Ambapo mimi nimekualikeni hapa leo hii, nimekulisheni na kukukosheni mikono
yenu kwa mikono yangu ili nanyi mpate kuona kutoka kwangu. Na kwa hakika
mnaona na kujua kua mimi ni mbora mongoni mwenu, hivyo haitakiwi kwa hata
mmoja miongoni mwenu kua ni mwenye kujiona kua yuko juu zaidi ya mwenzake,
hivyo ni wajibu wenu kwa kila mmoja miongoni mwenu kujitolea kwa ajili ya
mwenzake kama mimi nilivyojitolea kwa ajili yenu. Na baada ya haya nilikua
nataka kukuombeni kua mniombee kwa Allah Subhanah wa Ta’ala, huku mkiwa
na Ikhlasi kua Kifo kisinikaribe’
505
Hivyo baada ya hapo Wanafunzi wake hao wakaanza kumuombea Dua Nabii Isa
Ibn Maryam, lakini Allah Subhanah wa Ta’ala akawajaalia kua na usingizi mzito
sana, hivyo wakashindwa kuendelea na Dua hio na kuanza kusinzia na kulala
badala yake, hivyo Nabii Isa kawambia Wanafunzi wake hao: ‘Subhanah Allah
hamuwezi kunitekelezea maombi yangu hata kwa usiku mmoja?’
Ambapo Wanafunzi hao wakajibu: ‘Wa Allah hatujuia nini kimetukuta kwani
tmezoea kukesha katika Ibada pamoja nawe lakini leo hii inaonekana kua Usingizi
umekua mwingi kupita mipaka.’ Hivyo Nabii Isa akasema: ‘Basi Mchungaji
atandoka na Kondoo watabakia, na mmoja kati yenu miongoni mwenu atanisaliti
na kunuza kwa malipo ya fedha kidogo na kisha atakula fedha hizo bila kujali,
jambo ambalo litatokea kabla ya hata kuwika Jogoo wa kwanza wa Alfajiri.’ Kisha
Nabii Isa na Wanafunzi wake wakatawanyika kila mmoja akielekea katika sehemu
yake kuendelea na Usingizi wake.
Katika kipindi hiki Mayahudi walikua wakimtafuta Nabii Isa Ibn Maryam, na
njiani wakafanikiwa kumkamata Mwanafunzi wake Nabii Isa aitwae Simion,
ambae nae akamkana Nabii Isa kua si Mwalimu wake, na kisha alipoachiwa
akaanza kusikitika na kujilaumu kwanini akamkana Mwalimu wake, na kisha
akasikia Sauti ya Jogoo wa kwanza wa Alfajir na hivyo sauti hio ilimhuzunisha sana
kwani alikua akikumbuka maneno ya Isa Ibn Maryam kuhusiana na kusalitiwa
kwake.
Ilipoingia asubuhi basi Juda ambe ni mmoja kati ya Wanafunzi wa Isa Ibn Maryam
akaelekea kwa Mayahudi na kuwaambia kua wampe pesa za fedha 30 na kisha
atawapeleka katika sehemu aliyojificha Isa Ibn Maryam, na alipowapeleka na
kuingia ndani basi Mwanafunzi huyo akawa na muonekano wa Isa Ibn Maryam,
hivyo hao wakamkamata na kumfunga kamba na kisha wakamwambia kua: ‘Kama
kweli wewe unatibu wenye Ukoma na kufufua waliokufa, basi itakuaje uwe
simwenye kuweza kujifungua kutokana na kamba hizi tulizokufunga’ kisha
wakamtemea mate, wakamchoma na Miba na kisha wakamsulubu huku wakidhani
kua wanamsulubu Isa Ibn Maryam.
Ama kwa Upande wa Imam Qatadah Al Sadusi basi yeye anasema kua: ‘Mayahudi
walimuwekea Mlinzi Nabii Isa ili amfuate kila anapoenda ili iwe rahisi kwao
kumkamata pale itakapohitajika. Hivyo siku moja Isa Ibn Maryam akaelekea
Milimani na Mlinzi huyo akamfuata, na walipofika huko basi Allah Subhanah wa
Ta’ala akamchukua na kumpandisha Mbinguni Isa Ibn Maryam na kisha
akamvisha Myahudi huyo muonekano wa Nabii Isa, hivyo Mayahudi wenzake
walipotaka kumuua Nabii Isa basi wakamkamata yeye na Kumsulubu huku akiwa
ni mwenye kulalalamika kua yeye sie Isa Ibn Marayam.’
506
Allah Subhanah wa Ta’ala analielezea tukio hili katika Aya iliyotuma neno Makara
ambalo hua linamanisha Kupanga Njama, Kumuadhibi Mtu Muongo, Kupanga Njama
au Mbinu kwa kutumia Ustadi Mkubwa sana. Ambapo neno Makara ndio lililotoa neno
Makirin ambalo hua linamaanisha Mwenye Kuadhibu Mwishoni wenye kupanga Njama
baada ya kuwazidi kwa ubora wa mipango ya Kufanya Njama na hivyo kuwadhihirisha
ubya wa Njama zao waliopanga Njama, ambapo maneno haya yote yametumika kwenye
aya hio isemayo kua:
﴿وَمَكَرُواْ وَمَكَرَ ٱهلل َُّ وَٱهلل َُّ خَيْرُ ٱلْمَاكِرِينَ ﴾
Wamakaroo wamakara Allahu waAllahu khayru almakireena(Surat Al Imran 3:54)
Tafsir: Na wakapanga Njama, na Akapanga Allah, na Allah ni M-bora wa
Kuwaadhibu wenye Kupanga.
Kwani wakati Mayahudi wanapaga Njama zao za Kumuua Nabii Isa basi nae Allah
Subhanah wa Ta’ala ambae ni Mbora wa kupanga na kuadhibu kwa kila mwenye
kupanga njama zenye maovu ndani yake akapanga yake na kumbainishia Nabii Isa kwa
kusema:
﴿إِذْ قَالَ ٱهلل َُّ ٰ يٰعِيسَى ِ إِنىّ مُتَوَفِّيكَ وَرَافِعُكَ إِلىَ َّوَمُطَهِّرُكَمِنَ ٱل َّذِينَ كَ فَرُواْ
وَجَاعِلُ ٱل َّذِينَ ٱت َّبَعُوكَ فَوْقَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ إِلىَٰ يَوْمِ ٱلْقِيَامَةِ ثمُ َّ إِلىَ َّ َمرْجِعُكُْم
فَأَحْكُمُ بَيْنَكُمْ فِيمَا كُنتُمْ فِيهِ تخَْتَلِفُونَ ﴾
Idh qala Allahu ya AAeesa innee mutawaffeeka warafiAAuka ilayya
wamutahhiruka mina alladheena kafaroo wajaAAilu alladheena ittabaAAooka
fawqa alladheena kafaroo ila yawmi alqiyamati thumma ilayya marjiAAukum
faahkumu baynakum feema kuntum feehi takhtalifoona (Surat Al Imran 3:55)
Tafsir: Na akasema Allah (Subhanah wa Ta’ala): ‘Ewe Isa! Hakika mimi
nitakutimizia Ahadi niliyokuwekea, nitakunyanyua kwangu na kukusafisha kutokana
na wale ambao waliokufuru na nitawajaalia wle wanaokufuata kua juu ya
waliokufuru hadi katika siku ya Kiama. Na kisha mtarudi kwangu nami nitahukumu
baina yenu juu ya yale mliyokua mkikhitilafiana’
507
Ambapo aya imetuma neno Mutawaffika ambalo linatokana na neno Wafa ambalo hua
linamaanisha Kufikia Mwisho, Kutimiza Ahadi, Kurudisha Amanah, Kutekeleza Wajibu,
Kulipa Deni. Neno Wafa ndio lililotoa neno Wafat ambalo hua linamaanisha Kifo.
Ambapo kwa upande wa Raghib Al Isfahani basi yeye anasema kua: ‘Neno Rafa’a hua
linatumika kumaanisha Kunyanyua vitu Vilivyo hai na Kuvipandisha kutoka
katika sehemu moja na kuviweka kwenye sehemu nyengine’
Ambapo kwa Upande wa Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allah Anhu kua: ‘Neno
Mutawaffika linamanisha Mumituka (yaani Nitakusababishia Kifo)’ na kwa upande
wa Al Hasan Al Basri amesema kua; ‘Allah Subhanah wa Taála alimpaisha Mbinguni
Isa Ibn Maryam katika hali ya kimwili na kiroho.’
Hasan Radhi Allahu aAnhu anasema kua: ‘Rasul Allah Salallahu Aálayhi wa Salam
Aliwaambia Mayahudi kua: ‘Isa Ibn Maryam hajafariki, na atarudi Duniani kabla
ya Siku ya Kiama’’ (Imam Ibn Jarir Al Tabari)
Na kwa upande wa Imam Ibn Abi Hatim Abd Rahman Ibn Muhammad Ibn Idris Al Razi
basi yeye anasema kua: ‘Amesema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua:
Kabla ya Allah Subhanah wa Ta’ala kumnyanyua Isa Ibn Maryam Mbinguni, basi
Nabii Isa alienda kwa Wanafunzi wake’ ambao walikua ni 12 na alipofika alikua
kama ni mwenye nywele zinazotiririka Maji na akasema kuwaambia Wanafunzi
hao: ‘Kuna mmoja miongoni mwenu hatoniamini mimi kwa mara 12 baada ya
kuniamini kwake’ Kisha akawauliza Wanafunzi wake hao: ‘Jee ni nani miongoni
mwenu atajitolea kua muonekano wangu uonekane juu yake? Na kisha awe ni
mwenye kuuliwa baada yangu, na hivyo atakua ni mwenye kuingia Peponi pamoja
nami?’
Ambapo mmoja kati ya Wanafunzi wake ambae alikua ni kijana kuliko wote
akasimama na kusema kua yeye yuko tayari, lakini Nabii Isa Ibn Maryam
akamwambia akae chini, Nabii Isa akauliza tena atakakaejitolea lakini hakuna
aliesimama isipokua yule kijana alisimama tena. Nabii Isa akamwambia akae chini
tena, na kisha akauliza kwa mara ya tatu nani atajitolea kuchukua nafasi hio lakni
hakuna aliesimama, na yule kijana akasimama tena. Hivyo Nabii Isa akasema:
‘Wewe utakua ndie mwenye kuchukua Muonekano wangu.
Hivyo kijana huyo akawa na muonekano wa Nabii Isa na Nabii Isa akapaa angani,
hivyo Mayahudi walipoanza kumtafuta Nabii Isa wakamuona Kijana huyo na
Kumsulubu badala yake huku wakimdhani kua ni Nabii Isa. Ambapo wafuasi wa
Nabii Isa wakawa ni wasiomuamini Nabii Isa kwa mara 12 na wakagawika katika
makundi Matatu ambayo ni:
508
Yaqubiyah ambao wao wanasema kua: ‘Mungu alibakia pamoja nasi kwa mda
alioutaka na kisha akapanda Mbinguni’
An Nasturiya ambao wanasema kua: ‘Mtoto wa Mungu alikua pamoja nasi kwa
mda alioutaka na kisha Baba yake akamchukua juu Mbinguni. ’
Waislam ambao wanasema: ‘Mja na Mtume wa Allah alibakia pamoja nasi kwa
aliotaka Allah Subhanah wa Ta’ala na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akampaisha
Mbinguni’
Ambapo makundi mawili ya Yaqubiyah na Nasturyia yameshikamana na
kupingana na Waislam na kuwaua, na hivyo tangu baada ya tukio hilo basi Uislam
ulifichikana hadi pale Allah Subhanah wa Ta’ala alipomleta Nabii Muhammad
Salallahu Alayhi wa Salam’
Ambapo amesema Imam Qasim Muhammad Hasham katika Tafsir Al Azizi kua: ‘Ummu
ul Muuminin Safiya Radhi Allah Anha alipotembelea Bayt ul Maqdis na baada ya
kusali aktika Masjid Al Aqsa basi alipanda katika Mlima Tur akasali pia na
akasema: ‘Huu ndio Mlima ambao Isa Ibn Maryam alinyanyuliwa kupandishwa
Mbinguni’’
Na kwa upande wa Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi anasema kua;
‘Neno Tawaffa hua linamaanisha Kukichukua kitu katika hali ya Ukamilifu, hivyo
hii inamaanisha kua Allah Subhanah wa Ta’ala alimyanyua Juu Nabii Isa katika
hali ya kiroho na kimwili ili Mayahudi wasifanikiwe kumdhuru, na ndio maana
Allah Subhanah wa Ta’ala akawambia Nabii Isa Ibn Maryam kama alivyosema
katika Surat Al Imran 3:55’
Ambapo kiunganishi wa harfu Waw baina ya Mutawaffeeka wa rafiAAuka ilayya
hayamaanishi kua hapa kuna mfuatano wa jambo moja baada ya jengine. Hivyo
aya inamaanisha kua Allah Subhanah wa Ta’ala anafanya mambo yote haya lakini
kuhusiana na wakati gani, wapi na sehemu gani basi hua inategemea na vithibitisho,
na hivyo hii kua ni ushahidi kua Isa Ibn Maryam yuko hai.
Na kwa upande wa Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al
Ansari Al Qurtubi basi yeye anasema kua: ‘Mfumo wa mpangilio na maana ya Harfu
Waw hivyo maana ya maneno ya aya hii Mutawaffeeka wa rafiAAuka ilayya itakua
Nitakunyanyua kwangu mie na nitakusafisha kutokana na wale wanaoikataa Imani
ya Dini na nitakuchukua wewe kwangu mimi baada ya kupaa kwako Mbinguni.
509
Ambapo maana ya kwanza ya neno Mutawaffeeka hua inamaanisha kua
Nitakunyanyua wewe kutoka kwa watu hao na kukupandisha juu kwangu mie, na
maana ya pili ya Mutawaffeeka hua inamaanisha Nitakufanya Ulale Usingizi
ambapo Usingizi hua ni pacha wa Kifo na ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala
akatumia neno hilo kumaanisha Usingizi katika aya ifuatayo:
﴿وَهُوَ ٱل َّذِى يَتَوَف َّاكُم بِٱلل َّيْلِ وَيَعْلَمُ مَا جَرَحْتُم بِٱلن َّهَارِ ثمُ َّ يَبْعَثُكُمْ فِيهِ لِيُقْضَىٰ
’أَجَ لٌ م ُّ سَمًّى ثمُ َّ إِلَيْهِ مَرْجِ عُكُمْ ثمُ َّ يُنَبِّئُكُم بمَِا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴾
Wahuwa alladhee yatawaffakum biallayli wayaAAlamu ma jarahtum bialnnahari
thumma yabAAathukum feehi liyuqda ajalun musamman thumma ilayhi
marjiAAukum thumma yunabbi-okum bima kuntum taAAmaloona (Surat Al
Anaam 6:60)
Tafsir: Na ni yeye ndie ambae yatawaffakum anaechukua Roho zenu katika wakati wa
Usiku(wakati mmelala) na ni mwenye kujua juu ya mliyoyafanya wakati wa Mchana
na kisha hukuamsheni ili mpate kutimiza wakati wenu mlioandikiwa, na kisha kwake
yeye ndio marudio yenu na kisha mtabainishiwa mliyokua mkiyafanya.
Ambapo kwa upande wa Imam Al Sabuni basi yeye anasema kua: ‘Hikma ya Allah
Subhanah wa Ta’ala kutoa tangazo hilo ni kumbashiria Nabii Isa kua atamuokoa
kutokana na Mayahudi na atamnyanyua Juu Mbinguni huku akiwa Mzima mzima
bila ya kufikwa na Matatizo yeyote’(Safwat al-Tafasir)
Na kwa upande wa Imam Zahid Al Kawthar basi yeye anasema kua: ‘Maana halisi ya
neno Raf’a hua ni kusafirisha Kitu kutoka chini kuelekea Juu, hivyo haina haja ya
kutafuta maana nyengine yeyote kuhusiana na maneno haya katika aya hii’
Ambapo kwa upande wa Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari basi yeye
anasema kua: ‘Neno Mutawaffika hua linamaanisha kua Nitakulinda kutokana na
Kuuliwa na Watu na hivyo nitakupa haki kamilifu ya Kufariki kifo cha
Kimaumbile, na wala si cha Kuuliwa.’
Na hii ni kwa sababu anasema Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari kua
maana ya ile aya isemayo
510
﴿وَإِن َّهُ لَعِلْمٌ لِّلس َّاعَةِ فَلاَ تمَْتَرُن َّ هبَِا وَٱت َّبِعُونِ هَٰذَا صِرَاطٌ م ُّسْتَقِيمٌ ﴾
Wa-innahu laAAilmun lilssaAAati fala tamtarunna biha waittabiAAooni hadha
siratun mustaqeemun (Surat Az Zukhruf 43:61)
Tafsir: Na kwa Hakika Yeye atakua ni Alama ya kujulikana kwa Saa (Ya Kiama) hivyo
msiwe na shaka nayo na nifuateni Mimi katika njia hi iliyonyooka.
Ambapo aya inatuwekea wazi kua Kiama hakitofika (kwani neno Ilm hapa
limetumika kubainisha Shuruti la kua kitendo hakitotokea hadi kitokee kitnedo
chengine kwanza) Kabla ya Isa Ibn Maryam kurudi Duniani ambapo Aatamuua
Dajjal na Atafuata Qur’an na Atafanya Ibada ya Hija pia na kisha ndio kitakuja
Kiama
Ambapo kwa upande wa Imam Muqatil Ibn Sulayman basi nae amesema kua ‘Maneno
laAAilmun lilssaAAati linamaanisha Ukaribu wa wazi wa Saa ya Kiama utaonekana
mwishoni mwa Dunia baada ya Kushuka Nabii Isa’
Na kwa upande mwengine basi neno Wafa halikutumika tu kumaanisha Kifo ndani ya
Qur’an bali pia limetumika kumaanisha Kuitoa Roho moja kwa moja bila ya kuirudisha
Ndani ya Mwili, na pia limetumika kumaanisha Kuichukua Roho kutoka ndani ya Miwili
na kisha baadae kuirudisha tena Roho hio ndani ya Mwili kama ilivyobainisha aya
ifuatayo:
﴿ٱهلل َُّ يَتَوَفى َّ ٱلأَنفُسَ حِ ينَ مَ وْتِهَا وَٱل َّتىِ لمَْ تمَُتْ فىِ مَنَامِهَا فَيُمْ سِ كُ ٱل َّتىِ قَضَىٰ
عَلَيْهَا ٱلْمَوْتَ وَيُرْسِ لُ ٱلأُخْرَىٰ إِلىَٰ أَجَلٍ م ُّسَمًّى إِن َّ فىِ ذٰلِ كََ لآَ تٍ لِّقَوْمٍ
يَتَفَك َّرُونَ ﴾
Allahu yatawaffa al-anfusa heena mawtiha waallatee lam tamut fee manamiha
fayumsiku allatee qadha AAalayha almawta wayursilu al-okhra ila ajalin
musamman inna fee dhalika laayatin liqawmin yatafakkaroona(Surat Zumar 39:42)
Tafsir: Allah ni (Yatawaffa) mwenye Kuchukua Roho katika wakati wa (Mawtiha) kifo
chao na wale (Lam Tamut) ambao hawakufa katika usingizi wao, kisha huzizuia za
511
wale awatakiao Kifo na nyengine huzirudisha tena kwa ajili ya Mda waliowekewa,
hakika katika haya una dalili kwa watu wenye kutafakari.
Ambapo amesema Abu Hurayra kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kua: ‘Mitume ni ndugu wenye kutokana na Mama tofauti, lakini ni wenye
kutokana na Baba mmoja, hua ni wenye kushushiwa Dini moja, hivyo mimi ni
karibu sana kwa Isa Ibn Maryam na yeye atashuka tena, na mtakapomuona basi
mtamjua kwani ni Mtu wa urefu wa kati na kati na mwenye rangi ya mwangaza
wenye wekundu, na nywele zake atakua amezipasua kati kama zenye kuyaangusha
matone ya Maji ingawa hazijaroa. Ataivunja Misalaba, atawaua Nguruwe, atagawa
Mali na kupigana na Watu kwa ajili ya Uislam hadi pale itakapokua hakuna Dini
nyengine ardhini’
Ni katika kipindi cha wakati wake ambapo ndipo atakapotokea Massih Dajjal Al
Kadhaab ambae atauliwa na kutakua na Usalama Ardhini kiasi ya kua Simba
watakua wanatembea pamoja na Ngamia, Chui na Ng’ombe, Mbwa Mwitu na
Kondoo na Wototo watacheza na Nyoka, na hawatodhuriana na ataishi ardhini kwa
miaka 40 na kisha atakufa na Waislam watamsalia na Kumzika’(Sunan Abu Daud)
Tukio la kupandishwa Mbinguni kwa Nabii Isa lilitokea katika Mwezi wa Ramadhani
katika usiku wa Laylat Ul Qadir wa mwaka wa 33 baada ya kuzaliwa Nabii Isa.
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anabainisha kuhusiana na kitakachofuata baada ya
tukio hilo la Kuahidiwa Nabii Isa kua atapaishwa Mbinguni na kuepushwa na Kuuliwa
na Maadaui zake, na kisha waliokua hawakumuamini basi watalipwa hapa hapa Duniani
na watakaomini basi watalipwa kikamilifu kama ilivyolezewa katika aya nyengine tena
ambayo nayo pia imetumia neno lenye asili ya neno Wafa lakini likiwa katika hali ya
Fayuwafiihim Ujurahum lenye kumaanisha Kikamilishiwa Kikamilifu Malipo yao pale
ziliposema aya kua:
﴿فَأَم َّا ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ فَأُعَذِّبُهُمْ عَذَاابً شَدِيداً فىِ ٱلد ُّنْيَا وَٱلآخِ رَةِ وَمَا لهَُمْ مِّنْ
ُّب
َّصِرِينَ۞وَأَم َّا ٱل َّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُواْ ٱلص َّ الحَِاتِ فَيُوَفِّيهِمْ أُجُورَهُمْ وَٱهلل َُّ لاَ يحُِ
ٱلظ َّالِمِينَ۞ذٰلِكَ نَتْلُوهُ عَلَيْكَ مِنَ الآَتِ وَٱلذِّكْرِ ٱلحَْكِيمِ ﴾
Faamma alladheena kafaroo faoAAadhdhibuhum AAadhaban shadeedan fee
alddunya waal-akhirati wama lahum min nasireena; Waamma alladheena amanoo
waAAamiloo alssalihati fayuwaffeehim ojoorahum waAllahu la yuhibbu
512
aldhdhalimeena; Dhalika natloohu AAalayka mina al-ayati waaldhdhikri
alhakeemi (Surat Al Imran 3:56-58)
Tafsir: Ama kuhusiana na wale waliokufuru basi Wataadhibwa Adhabu kali sana
Duniani na Akhera na hawatokua na wa Kuwanusuru. Na ama kuhusiana na wale
walioamini na wakafanya Mema basi fayuwaffeehim ojoorahum (watakamlishiwa
Kikamilifu Ujira wao), na Allah hawapendi wenye kufanya Dhulma. Haya
tunakusomea juu yako (Ewe Muhammad) kutoka katika Aya zetu na ukumbusho
wenye Hikma.
Na anasema Imam Wahb Ibn Munabih kua: ‘Wakati Allah Subhanah wa Ta’ala
alipomtaarifu Isa Ibn Maryam kuhusiana na kupaishwa Mbinguni basi, Isa Ibn
Maryam akawachagua Wanafunzi wake wawili ambao ni Simiun na Yahya na
kuwataka wakae karibu na Mama yake yaani Maryam Bint Imran kwa ajili ya
kumuangalia na kuwataka wasiachane nae.
Hivyo wakaamua pamoja na Andrew na Maryam Bint Imran kua waelekee kwa
Mfalme Marut ambae ni wa Ardhi ya Bizantiyum na kumtaka awe ni mwenye
Kumuabudu Allah Subahanh wa Ta’ala, ambapo kabla ya hapo basi Allah
Subhanah wa Ta’ala alimtuma Nabii Yunus kwenye Ardhi hio, na walipofika huko
basi Mfalme Marut akaamrisha kua Andrew na Simiun wasulubiwe.
Ambapo Yahya na Maryam Bint Imran wakakimbia, lakini hata hivyo walipofika
njiani wakazingirwa, na hapo hapo Ardhi ikapasuka na hivyo Maryam Bint Imran
na Yahya wakatumbukia ndani yake, na watu wa Mfalme Marut walipokaribia
eneo hilo wakajaribu kufukua katika sehemu hio walilozama Maryam Bint Imran
na Yahya lakini hawakukuta kitu. Hivyo Mfalme Marut alipohadithiwa hali
ilivyokua basi akaamini kua hio ni Miujiza ya Allah Subhanah wa Ta’ala na hivyo
akasilimu…lakini mwenye kujua zaid ni Allah Subhanah wa Ta’ala.
ISA IBN MARYAM NA MARYAM MAJDALANIYAH
Mongoni mwa watu wa Bani Israil katika kipindi cha Nabii Isa aliekua ni Mcha Mungu
na mwenye kumuamini sana Nabii Isa alikuwepo Mwanamke ambae alikua akijulikana
kwa jina la Maryam Majdalaniyah, ambae alikua akiishi katika kijiji cha Majladan.
Maryam Majdalaniyah, alikua ni Mwanamke Mzuri sana lakini alikua na tatizo la
ugonjwa wa kutokukoma kwa Hedhi yake na hivyo alikua ni mwenye kukataa kuolewa
kutokana na tatizo lake hilo ingawa wengi miongoni mwa watu wa Ban Israil walipeleka
posa zao kwa ajili ya kutaka kumuoa.
513
Hivyo Maryam Majdalaniyah, alipopata habari kua Nabii Isa anatibu Maradhi
yasiyotibka basi akatafuta nafasi ya kuonana nae Nabi Isa lakini Allah Subhanah wa
Ta’ala alipomjaaalia Maryam Majdalaniyah, kuipata Nafasi hio ya kukutana nae Nabii
Isa basi akashindwa kumuelezea Nabii Isa kuhusiana na tatizo lake hilo, lakini
akafanikiwa kumgusa mgongo wake Nabii Isa, na kutokana na tukio hilo basi Allah
Subhanah wa Ta’ala akamjaalia Maryam Majdalaniyah kua ni mwenye kupona maradhi
yake, na hivyo akawa anampenda na kumuamini zaidi Nabii Isa.
Ambapo kuna wasemao kua Maryam Majdalaniyah aliombwa na Nabii Isa kua
awakusanye Wanafunzi wake Nabii Isa Ibn Maryam kwa ajili ya Chakula chake cha
Mwisho kabla ya kuwatawanya Wanafunzi wake katika maeneo mbali mbali ya ardhi
kama alivyoamrishwa na Allah Subhnah wa Ta’ala ambapo miongoni mwao ni wale
waliotajwa kwa kupigiwa mfano kwenye Surat Yasin.
WANAFUNZI WA NABII ISA IBN MARYAM KATIKA SURAT YASIN
Amesema Allah Subhanah wa Ta’ala katika Surat Yasin kua:
﴿وَٱضْرِبْ لهَُمْ م َّثَلاً أَصْحَابَ ٱلقَرْيَةِ إِذْ جَآءَهَا ٱلْمُرْسَلُونَ۞إِذْ أَرْسَ لْنَآ إِلَيْهِمُ
ٱثْنَينِْ فَكَذ َّبُوهمَُا فَعَز َّزَْ بِثَالِثٍ فَقَالُو ۤ اْ إِ َّ إِلَيْكُمْ م ُّرْسَلُونَ ﴾
Waidhrib lahum mathalan as-haba alqaryati idh jaaha almursaloona; Ith arsalna
ilayhimu ithnayni fakadhdhaboohuma faAAazzazna bithalithin faqaloo inna
ilaykum mursaloona; (Surat Yasin 36:13-14)
Tafsir: Na wapigie Mfano wa Watu wa Mji wakati walipokuja kwao Mitume. Wakati
tulowatumia Mitume wwili wakawakadhibisha wotehvyo tukawaongez na wa Tatu nao
kisha wakasema: ‘Kwa hakika sisi tumetumwa kwenu kama Mitume’
Nabii Isa aliwaambia Wanafunzi wake kua: ‘Enyi Hawarriyun umefika mda wa
kuondoka kwangu hivyo huu ni wasia wa mwisho juu yenu kutoka kwangu, ambao
ni kua Allah Subhanah wa Ta’ala atakutumeni nyie kwa jamii za watu, hvyo isihini
kwa heshima, kuweni wapole, wenye huruma na ukarimu. Mtakapokutana na
mithani basi kuweni na Subira. Ishini miongoni mwa watu kama wanavyoishi
Kondoo miongoni mwa Mbwa Mwitu na wala msishindane kwa ajili ya mambo ya
514
kidunia, katika kila jambo lenu msimsahau Mola wenu na daima kuweni ni wenye
kumtegemea yeye.
Nae atakusimamieni na kukupeni msaada atakupeni hoja na vithibitisho ambavyo
vitakavyokua vya nguvu. Katika maisha yenu mtakua na wapinzazni wa aina mbili
ambao ni Wafalme na Wanawake, hivyo iwachieni Dunia hii kwa wenye Mamlaka
nanyi mtakua Salama kutokana na Upinzani wao. Ama kuhusiana na Wanawake
basi fungeni na ishini katika njia ya Usafi, mtu akikupigeni kwenye shavu moja basi
mpeni na shavu la pili amalizie. Amkeni asubuhi mapema na sehemu yeyote ile ya
ardhi mtakayoelekea basi waiteni watu kwa Mungu wao kulingana na Lugha yao,
na Simiyun ndio kiongozi wenu.’
Simiyun akamuuliza Isa Ibn Maryam kwa kukema: ‘Hivi Jee mimi utanipeleka wapi,
Ya Rasul Allah?’ Nabii Isa akasema: ‘Nenda katika Ardhi ya Antakiya’ ambapo
Simiyun akasema: ‘Hakika mimi ni Mtu mzima sina nguvu, jee nitafanikisha vipi
jambo hilo?’ Hivyo Nabii Isa Ibn Maryam akasema: ‘Allah atakupa Nguvu’ Simiyun
akasema: ‘Ya Rasul Allah! Basi bora nipe wa kufuatana nao miongoni mwetu’. Nabii
Isa Ibn Maryam akasema: ‘Chagua uwatakao miongoni mwenu’ hivyo Simiyun
akamchagua Yahya.
Ambapo kwa upande wa Imam Muhammad Ibn Is-haq basi yeye anasema kua walioenda
katika mji wa Antakiya ambao ni watu waliotajwa kwenye Surat Yasin walikua ni Farud
na Marud, na kwa upande wa Imam Muqatil Ibn Sulayman basi yeye anasema kua
walikua ni Yuman na Malus, na kwa upande wa Imam Kaab Al Ahbari basi anasema kua
walikua ni Sadiq na Suduq na kwa upande wa Imam Wahb Ibn Munabih basi yeye
anasema kua hawa walikua ni Yahya na Yunus. Lakini kwa upande wa Imam Al Qarafi
Al Shashi basi yeye anasema kua hawa walikua ni Manabii wawili wa Allah Subhanah
wa Ta’ala.
Hivyo Simiyun na Yahya walipolala katika usiku wa siku hio, basi baada ya mda
wakaamka na kujikuta wapo nje kwenye sehemu iliyowazi tofauti na walivyolala hapo
awali, kwani walikua katika ardhi ya kigeni wasiyoifaham huku wakiwa ni kwenye eneo
ambalo ni lenye mandhari ya shamba wakafaham kua wamewasili kwenye ardhi
nyengine tofauti.
Hivyo asubuhi ya siku hio wakaona Lango la kuingilia kwenye mji ambao pia hawauijui,
hivyo wakaelekea kwenye Mlango wa Mji huo, na walipoulizia wakaambiwa kua huo ni
Mji wa Antakiya, na kabla hawajaingia ndani yake kwa ajili ya kuwausia watu wa Ardhi
hio kuhusiana na Allah Subhanah wa Ta’ala basi wakakamatwa na kutokana na
kushukiwa kua ni wapelelezi wa Maadui wa watu wa Mji huo.
515
lakini walipojitetea kua wao ni wafuasi wa Isa Ibn Maryam na kazi yao ni kutangazia
Dini ya Allah Subhanah wa Ta’ala Mwingi wa Rehma na mwingi wa Huruma basi
ingawa kuna baadhi waliowasikiliza na kuvutiwa na ujumbe wao lakini wengi zaidi
waliukataa na hivyo wakakumbana na upinzani mkubwa sana kama zinavyoelezea Aya
pale ziliposema:
﴿قَالُواْ مَآ أَنتُمْ إِلا َّ بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَمَآ أَنَزلَ ٱلر َّحمَْٰنُ مِن شَيْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلا َّ
تَكْذِبُونَ۞قَالُواْ رَب ُّنَا يَعْلَمُ إِ َّ إِلَيْكُمْ لَمُرْسَلُونَ۞وَمَا عَلَيْنَآ إِلا َّ ٱلْبَلاَغُ ٱلْمُبِينُ ﴾
Qaloo ma antum illa basharun mithluna wama anzala alrrahmanu min shay-in in
antum illa takdhiboona; Qaloo rabbuna yaAAlamu inna ilaykum lamursaloona;
Wama AAalayna illa albalaghu almubeenu; (Surat Yasin 36:15-17)
Tafsir: Wakasema (Watu hao kua): ‘Nyinyi ni Watu tu kama sisi, na hakushusha
Mwingi wa Rehma kitu chochote isipokua nyinyi ni wenye kusema Uongo’;
Wakasema: ‘Mola wetu ni mwenye kujua kua sisi ni Wajumbe tuliotumwa kwenu, Na
wajibu wetu ni kufikisha Ujumbe muhimu ulio wazi’
Hivyo ikawabidi watu hao wawadhihirishie watu wa Antakiya kua wayasemayo ni ya
kweli, kwani Mola wao ndie mwenye kujua zaidi ukweli huo juu yao, lakini tatizo sasa
wengi sana kati ya watu hao wakawa si wenye kutaka kufaham juu ya ujumbe huo
muhimu ulio wazi, na hivyo wakaona kua Wajumbe hao wanataka kuwagawanya watu
wao na kutengeneza ufa ndani ya jamii yao baina ya wanaowasikiliza na wasiowasikiliza,
hivyo wakasema wengi wao:
﴿قَالُو ۤ اْ إِ َّ تَطَي َّرَْ بِكُمْ لَئِن لم َّْ تَنتَهُواْ لَنَرْجمَُن َّكُمْ وَ لَيَمَس َّ ن َّكُ مْ مِّ ن َّا عَذَابٌ أَلِيمٌ ۞قَالُواْ
طَائِرُكُم م َّعَكُمْ أَإِن ذُكِّرْتمُ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ م ُّسْرِفُونَ ﴾
Qaloo inna tatayyarna bikum la-in lam tantahoo lanarjumannakum
walayamassannakum minna AAadhabun aleemun; Qaloo ta-irukum maAAakum
a-in dhukkirtum bal antum qawmun musrifoona; (Surat Yasin 36:18-19)
Tafsir: Wakasema (Watu wa Antakiya): ‘Hakika sisi tunaona Tatayyarna (bashirio la
Uovu) kutoka kwenu, na hivyo kama hamjakoma basi tutakupigeni Mawe na mtafikwa
na Adhabu Kali sana kutoka kwetu.’Wakasema (Wajumbe hao): ‘Bashirio lenu Uovu
516
lkopamoja navyi! Kwani (mnasema hivyo) kwa sababu ya kukumbushwa Tu? Hakika
nyinyi ni watu waliovuka Mipaka.’
Ambapo aya metumia neno Tatayyarna ambalo ni lenye kutokana na neno Tara ambalo
hua linamaanisha Kuruka Angani, Kuelea juu ya hewa, Kukimbilia kufanya jambo kwa
papara, Nuksi, Mikosi au Jambo baya au Ovu, Ndege warukao Angani, Mdudu, Mtu
anaepaa kiakili na kiroho na hivyo hua si mwenye kujishusha chini kutokana na mambo
ya kidunia.
Neno Tara pia hua linamaanisha Mtu mwenye kufanya kwa haraka Kitendo
kitakachosababisha Madhara au Faida. Ambapo ilikua ni kawaida ya Watu wa zamani
kua wenye kua na Imani ya kuangalia namna Ndege wanavyokua wanaruka na kutua na
kisha hua ni wenye kubashiri wema au uovu wa jambo fulani kutokana kitendo cha Kutua
na Kuruka kwa ndege husika na kutokana na kitendo hicho basi ndio likapatikana neno
Tatayyar.
Na hivyo aya kutubainishia kua watu hawa wa Antakiya walikua wanawaona wajumbe
wao hao kua kama ni Nuksi na kua wanataka kuwasababishia Mikosi kwani haiwezekani
kua Allah Subhanah wa Ta’ala awatumie wao Watu kama Mitume, kwani ilikua ni
kawaida ya watu wasioamini kuamini kua kama kweli Allah Subhanah wa Ta’ala anataka
kuwaongoza watu basi atawatume watu wawaongoze wao, kwani wao ni wenye kujua
zaidi, hivyo wakawaonya Watu hao na kusema kua kama hawakukoma kuwaambia
maneno yanayotaka kuwasababishia mikosi basi watawapiga mawe Wajumbe hao.
Hakuchukua mda isipokua tukio la habari za mabishano haya baina ya Wajumbe hawa
na watu wa Antakiya, likamfikia Mfalme wa Antakiya ambae nae alikua pia si mwenye
kumuamini Allah Subhanah wa Ta’ala bali alikua ni mwenye kumuabudu Mungu wao
aitwe Artems, hivyo alipopata habari hio basi akaamrisha kua wajumbe hao waadhibiwe
kwa kusababisha vurugu kwenye Ardhi ya Antakiya na kisha wafungwe Jela.
Wakati wakiwa Jela basi Allah Subhanah wa Ta’ala akamteua Mjumbe mwengine ili
aende akawongezee nguvu ili kuwathibitishia watu hao wa Antakiya kua Ujumbe wake
na Wajumbe wake ni wa Kweli, ambapo huyu alikua ni Mwanafunzi mwengine aitwae
Paul, ambae nae alipofika katika Mji huo basi akajaribu kutafuta njia ya kua na ukaribu
na Mfalme na bila ya saka Allah Subhanah wa Ta’ala akamrahisishia njia hio kwani ndani
ya Mda mfupi basi akafanikiwa kua ni mwenye ukaribu na Mfalme.
Baada ya Paul kuupata ukaribu huo basi siku moja wakati akiwa anazungumza na
Mfalme bas akamwambia Mfalme huyo kwa kusema: ‘Ewe Mfalme, nimesikia
kuhusiana na watu wawili ambao wako Jela na wanateswa kwa sababu ya kua ni
wenye kufuata Imani ya Dini tofauti na ya watu wako. Hivi jee umewasikiliza hoja
zao?’ Mfalme akajibu: ‘La Hasira zangu ziliingilia kati maamuzi yangu hayo’ Hivyo
517
Paul akasema: ‘Hivyo unaonaje kama tukitumia busara na kuwafanyia uadilifu wa
kuwaita na kuwasikiliza hoja zao?’
Hivyo Mfalme akatafakari kisha akakubaliana na mtizamo wa Paul, na kisha akaamrisha
watu wawili hao waitwe mbele yao, na walipofikishwa mbele yao basi Mfalme akasema
kumwambia Paul: ‘Haya wahoji tusikie hoja zao’ hivyo Paul akawauliza: ‘Jee ni nani
aliekutumeni kuja katika Ardhi ya nchi hii?’ ambapo nao wakajibu: ‘Sisi tumetumwa
na Mungu alieumba Ulimwengu na kila kitu kilichomo ndani yake.’
Paul akawauliza: ‘Jee Mna vithibitisho gani?’ nao wakajibu: ‘Tunavyo vithibitisho
vingi, ikiwemo kuponya wanaoumwa maradhi sugu na yasiyopoa na kuwaponesha
vipofu wasioona na kua ni wenye kuona kwa idhini ya Allah.’
Mfalme akaamrisha waletwe Vipofu, na kila mwenye maradhi Sugu ndani ya Ardhi yake
ili wawaponeshe, na walipoletwa wagonjwa hao basi wakaombewa na kupona. Mfalme
akashangaa kutokana na Miujiza hio, kisha Paul akamwambia Mfalme huyo: ‘Labda
tumuulize na Mungu wako kama anaweza kufanya Miujiza kama yaliyofanywa na
Mungu wa watu hawa.’ Mfalme huyo akamuangalia Paul kisha akasema: ‘Hakika
mimi siwezi kukuficha kutokana na kujua kua hakuna anaeweza kuyafanya haya,
isipokua hawa watu ni wachawi, hivyo wanataka kututoa kwenye Imani ya Mababu
zetu ambayo tumedumu nayo miaka na miaka.’
Na hivyo Paul alipojaribu kumfafanulia Mfalme kuhusiana na vithibitisho vya hoja za
Watu hao juu ya wa uwezo wa Mola wao watu hao walioponesha wagonjwa mbele yao
basi nae akaonekana kua kumbe yuko pamoja nao, hivyo akajumuishwa pamoja nao na
ikatoka amri kua kila anaewakubali na kuwafuata basi auawe pamoja nao.
Ambapo anasema Imam Wahb Ibn Munabih kua: ‘Mfalme huyo hakuwaamini
Wajumbe hao, na hivyo yeye na watu wake wakajipanga kwa ajili ya kuwaua
Wajumbe hao.’ Ambapo wakati anajiandaa kwa tukio hilo la kuwaua wajumbe wakiwa
kati kati ya Mji huo, katika sehemu ya uwanja wa kupitishia hukumu ya adhabu ya kifo
basi kwa mbali akatokea Mtu ambae alikua akiwakimbilia kwa ajili ya kuwakataza watu
hao wasifanye uovu wa dhulma hio ya kuwaua Wajumbe hao wa Allah Subhnah wa
Ta’ala kama zinavyosema aya:
﴿وَجَآءَ مِنْ أَقْصَى ٱلْمَدِينَةِ رَجُلٌ يَسْعَى ٰ قَالَ يٰقَوْمِ ٱت َّبِعُواْ ٱلْمُرْسَلِينَ۞ٱت َّبِعُواْ مَن
لا َّ يَسْ أَلُكُمْ أَجْ راً وَهُمْ م ُّهْ تَدُ ونَ ﴾
518
Wajaa min aqsa almadeenati rajulun yasAAa qala ya qawmi ittabiAAoo
almursaleena; IttabiAAoo man la yas-alukum ajran wahum muhtadoona(Surat
Yasin 36:20-21)
Tafsir: Na mara akaja Mtu kutoka mbali ya Mji akikimbilia akasema: ‘Eni watu
wangu Wafuateni Wajumbe hawa, wafuateni wale ambao hawakudaini Malipo kwani
wao wameongozwa’
Ambapo anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Jina lake
Mtu huyu lilikua ni Habib Al Najjar ambae alikua ni fundi Seremala.’ Ambapo
Imam Wahb Ibn Munabih anasema kua: ‘Habib likua ni mgonjwa mwenye maradhi
ya ukoma, na nyumba yake ilikua iko mwanzoni kabisa mwa Lango la kuingilia
kwenye mji wa Antakiya, na alikua ni Muumini mwenye ukarimu sana, alikua
akipata malipo ya kazi zake alikua akiyagawa sehemu mbili, sehemu ya kwanza ni
kwa ajili ya familia yake na sehemu ya pili ni kwa ajili ya kutoa Sadaqa.
Aliposikia kuhusiana na kua watu wake wanataka kuwaua Wajumbe hao basi
aliwakimbilia kuwaonya kwani kabla yake alikua akimuamini Allah Subhana wa
Ta’ala laakini aikua akifanya Ibada zake kwa siri, na aliposikia kuhusiana na
ujumbe wa watu hao basi alidhihirisha Iman yake na kuwausia watu wake.’
Hivyo watu wa Antakiya walipomuona Habib anawatetea watu hao basi nao
wakamjumuisha pamoja nao na kumwambia: ‘Ala kumbe na wewe ni miongoni mwao
watu hawa wanaopingana na Imani ya Dini yetu na ni mwenye kuamini mitizamo
ya Imani ya Dini yao?’
Hivyo Habib akasema kama zinavyobainisha aya:
﴿وَمَا لىَِ لاَ أَعْبُدُ ٱل َّذِى فَطَرَنىِ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ۞أَأَتخ َِّذُ مِ ن دُونِهِ آلهَِةً إِن يُرِدْنِ
ٱلر َّحمَْٰنُ بِضُرٍّ لا َّ تُغْنِ عَنىِّ شَفَاعَتُهُمْ شَيْئاً وَلاَ يُنقِذُونَ۞إِِ نيّ ۤ إِذاً ل َّفِى ضَلاٍَل
م ُّبِينٍ۞ ِ إِنيّ ۤ آمَنتُ بِرَبِّكُمْ فَٱسمَْعُونِ ﴾
Wama liya la aAAbudu alladhee fataranee wa-ilayhi turjaAAoona; Aattakhidhu
min doonihi alihatan in yuridni alrrahmanu bidhurrin la tughni AAannee
shafaAAatuhum shay-an wala yunqidhooni; Innee idhan lafee dalalin mubeenin;
Innee amantu birabbikum faismaAAooni; (Surat Yasin 36:22-25)
519
Tafsir: Jee kwanini nisimuabudu yule ambae alieanianzisha na ambae kwake yeye
ndio kwenye marudio yenu? Hivi nitachukuaje Miungu wengine ambao
hawatonisaidia kitu pale mwingi wa Rehma atakapoamua kunidhuru hawatonisaidia
kitu dhidi yake? Kwa hivyo basi nitakua kwenye upotovu. Hakika mimi nimemuamini
Mola wenu: ‘Hivyo nisikilizeni’
Lakini baada ya kusema maneno hayo basi watu wa Antakiya wakamvamia Habib na
wakamuua kama walivyowaua wale wengine ambao ni Wajumbe wa Allah Subhanah wa
Ta’ala ambapo anasema Imam Abd Rahman Al Suddi kua: ‘Watu hawa walimpiga
mawe Habib mpaka akafariki Dunia huku akiwa ni mwenye kusema: ‘Ya Allah
Waongoze watu wangu.’’
Ambapo amesema Imam Hasan Al Basr kua: ‘Walimtoboa Koo yake na kisha
wakamtundika kwenye mlango ya Mji huo na kisha wakamzika, hivyo Allah
Subhanah wa Ta’ala akamfaridhshia Pepo moja kwa moja na akaambiwa:
﴿قِيلَ ٱدْخُلِ ٱلجَْن َّةَ قَالَ يٰلَيْتَ قَوْمِى ا يَعْلَمُونَ۞بمَِ غَفَرَ لىِ رَ بىِّ وَ جَعَلَنىِ مِنَ
ٱلْمُكْرَمِينَ ﴾
Qeela odkhuli aljannata qala ya layta qawmee yaAAlamoona; Bima ghafara lee
rabbee wajaAAalanee mina almukrameena; (Surat Yasin 36:26-27)
Tafsir: ‘Akaambiwa: ‘Ingia Peponi’ nae akasema: ‘Ya Laiti kama watu wangu
wangejua’ Alivyonisamehe Mola wangu na kunifanya kua ni miongoni mwa
Waliokirimiwa.’
Hivyo baada ya watu wa Antakiya kuwaua Mtume hao na kisha wakamuua Habib basi
Allah Subhanah wa Ta’ala akawaghadhibikia na kuwaadhibu kama zinayosema aya:
﴿وَمَآ أَنزَلْنَا عَلَى ٰ قَوْمِهِ مِن بَعْدِهِ مِن جُندٍ مِّنَ ٱلس َّمَآءِ وَمَا كُن َّ ا مُنزِلِينَ۞نِإ
كَانَتْ إِلا َّ صَيْحَةً وَاحِ دَةً فَإِذَا هُمْ خَامِدُونَ ﴾
Wama anzalna AAala qawmihi min baAAdihi min jundin mina alssama-i wama
kunna munzileena; In kanat illa sayhatan wahidatan fa-idha hum khamidoona
(Surat Yasin 36:27-29)
520
Tafsir: Na hatukuwashushia Watu wa Kaumu yake baada yake Jeshi kutoka Mbinguni
na wala hatukuhitaji kua ni wenye kutuma. Kwani haikua ila Ukelele Mmoja tu nao
wakawa wameteketea.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anatuambia kua watu hawa wa Mji wa Antakiya
hawakuhitaji kushushiwa Jeshi kutoka Mbinguni kwani haikuhitajika kufanywa hivyo,
na hii ni kutokana na Muumbaji kua ni mwenye kujua udhaifu wa Viumbe wake na kila
kitu juu yao, kua pale anapotaka kuwaadhibu basi si lazima awatumie Adhabu
inayotokana na wingi wa kitu kinachoadhibu, kwani kwake yeye hakuna
kinachoshindikana, hivyo anaweza kutumia kitu kimoja tu kidogo ambacho ni chenye
kudharaulika sana lakini madhara yake yakawa ni ya mangamizo makubwa na ya hatari
sana.
Kwa mfano kama tulivyoona kwenye adhabu iliyowakuta watu wa Nabii Hud, ambao
tulisema kua walipigwa na Upepo wa hali ya Umoja wa Rihan wa Adhabu, hivyo basi na
watu hawa wa Antakiya aliamua pia kuwaadhibu kwa adhabu Moja ambayo ni yenye
kutokan na Sauti inayojulikana kama Sayhatun ambayo ni adhabu inayotokana na
Ukelele Mmoja mkubwa sana ambao matokeo yake hua ni kuwapelekea waliopigiwa
Ukelele huo kua hapo hapo ni wenye Kupoteza faham na kutoka Roho moja kwa moja
kutokn ana kuzimika kwa uhai wao, kwani Kuzimika ndio maana ya neno Khamidun
lililotumika kwenye aya yetu inayoelezea tukio hili lililowakuta watu wa Antakiya.
Ambapo wanasema Wanazuoni kua Allah Subhanah wa Ta’ala alimtuma Malaika Jibril
kua aende kwenye Lango kuu la kungilia kwenye Mji huo na kisha Anadie ndani ya Mji
huo kwa Ukele Mmoja tu, kua ndio iwe dhabu yao. Kwani kimaumbile Sauti hua
inasikika kutokana na kua ni yenye kua na Mtetemeko wa Mawimbi ya hewa ambao
hukusanywa katika sehemu ya nje ya sikio na kisha kusafirishwa hadi ndani kwa njia ya
Mawimbi ambayo huingia ndani sikioni na kugonga kwenye ngoma ya sikio, na kisha
kusukumwa ndani zaidi kwenye sehemu ya kati ya sikio kupitia kwenye mifupa laini ya
hisia ambayo huyapeleka mawimbi hayo kwenye mzunguko wa Tarumbeta au Koa ya
sikio ambayo ndani yake hua mna Majimaji ambayo yanapopokea mtetemeko huo wa
Hewa unaosababisha mawimbi kama ya bahari juu ya Maji hayo.
Mawimbi ya maji ya Sikio husababisha seli za Nywele ndogo ndogo sana za hisia za
Sikio zilizomo kwenye sehemu ya ndani yake kuichukua Sauti hio baada ya kuipima
udogo na ukubwa wa sauti kulingana na ukubwa wa Mawimbi ya Maji ya Sikio na kisha
kuisafirisha sauti hio hadi kwenye mapokezi ya sauti na kupelekwa kwenye mfumo wa
sauti wa Ubongo ambapo hutafsiriwa na Ufaham kua hii ni sauti ya aina fulani na
inamaanisha kitu fulani.
Hivyo kila sauti inavyokua kubwa basi na mawimbi yake hua ni makubwa pia na hua
inasafiri pamoja na Upepo ambao hua unaingia kwa kasi kubwa kwenye masikio na
521
kusababisha tabaka la hewa hio kuingia ndani ya Ngoma ya Sikio na Kuipasua kisha
hewa hio hukimbilia kwenye Mapafu kupitia kwenye Koo na hivyo kuyafanya Mapafu
kupasuka kutokana na ukubwa wa Nguvu ya Sauti ambapo nako hupelekea Mripuko wa
Moyo na kusababisha Kifo cha Ghafla.
Kwani tukio hili la kusikia hadi kutafsiriwa kwa sauti husika na ufaham hua ni lenye
kutokea ndani ya wakati ambao ukubwa wake ni sehemu moja kati ya sehemu kumi ya
sekunde moja, hivyo bila ya shaka Allah Subhanah wa Ta’ala ametuma neno
Khamiduuna kumaanisha kua kutokana na tukio la adhabu hii yenye maumivu makubwa
sana yasiyostahamilika ya miripuko na mipasuko ya viungo mbalimbali muhimu vya
ndani ya mwili lilielekea Watu hawa wote kua ni wenye Kuzimika kwa Ghafla moja Uhai
wao na hili ndilo lililowakuta watu wa Antakiya.
VITHIBITISHO VYA WANAZUONI JUU YA KUPANDISHWA JUU
MBINGUNI RUHI ALLAHI ISA IBN MARYAM WAKATI AKIWA HAI.
Amesema Rasul Allahi Salallahu Ala’ayhi wa Salam kua: ‘Katika kila baada ya miaka
100 basi wale wenye I’lm watakuja kuihifadhi hii Ilm ya Dini, na hivyo watakua ni
wenye kukanusha tafsiri za wajinga na uongo wa wenye kulaghai na wenye kuvuka
mipaka’ (Sunan Al Kubra , Mishkat Al Masabih, Bughya al Multamis)
Amesema tena Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam: ‘Ama kwa Hakika Allah
Subhanah wa Ta’ala atatuma kwa ajili ya Ummah huu kila baada ya miaka 100 mtu
ambae atakua ni mwenye kufanya Tajdid kwa ajili ya Dini yake’ (Sunan Abu Daud).
Na kulingana na mtizamo wa Imam Jalaluddin Al Suyuti katika kitabu chake Mirqat al
Saud ni kua: ‘Kuna makubaliano ya Wanazuoni wa Hadith kua Hadith hii ni Sahih’
Neno Tajdid kwa Kiarabu hua ni lenye kumaanisha Kurudisha upya, kurudisha kitu
katika hali yake ya awali au ya asili baada ya kitu hicho kua ni chenye kufanyiwa
marekebisho, au kusahaulika. Mtu ambae anaefanya kazi hii ya Tajdid hua anajulikana
kama Mujaddid.
Mujaddid maana yake hua mtu mwenye kufanya Tajdid. Hivyo kulingana na hadith
yetu hio ambayo ni hadith sahih basi Allah Subhanah wa Taála ameahidi kua katika kila
baada ya miaka 100 atajaalia kua na mtu ambae ni mwenye kufanya Tajdid na hivyo
kuirudisha Imani ya Dini ya Kiislam katika njia iliyosahih.
522
Anasema Shaykh Al Islam Imam Badr Al Din Abdal anasema: ‘Mujaddid hujulikana
kutokana na kuwepo kwa makubaliano yenye nguvu juu ya Mwanazuoni husika
kulingana na mtizamo wa Wanazuoni wenzake ambao wamenufaika sana na uwezo
wake mkubwa wa I’lm. Hudhihirika kutokana na sifa za ndani na za nje za I’lm ya
Dini ya Kiislamu zinazompelekea kuunga mkono na kulinda Sunnah za Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na pia kukabiliana na kuzishinda Bida’a.
(Risalah Mardhiyyah fi al-Nusrat Madhhab al-Asha'riyyah)
Imam As Suyuti ameorodhesha majina ya Wanazuoni wafuatao kua ni Mujaddid wa
karne zifuatazo katika kitabu chake kinachoitwa Tuhfat Al-Mujtahidin bi Asma' Al-
Mujaddidin.
Mujaddid wa karne ya kwanza ya ya Uislam: Amir al-Mu'minin Umar Ibn Abd al-
Aziz (682 - 720).
Mujaddid wa karne ya pili ya Uislam: Mujaddid Imam Muhammad Ibn Idris Al Shafi`i
(767 - 820).
Mujaddid wa karne ya tatu ya Uislam: Mujaddid Imam Abu Al Hasan Ali ibn Isma'il
Al-Ash'ari (874 –936). Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam Al Shafi’i.
Mujaddid wa karne ya nne ya Uislam: Mujaddid Imam Abu Bakr Muḥammad Ibn Al
Ṭayyib Al Baqillāni (930-1013), Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam Maliki.
Mujaddid wa karne ya tano ya Uislam: Mujaddid Imam Abu Hamid Ibn Muhammad
ibn Muhammad Al-Ghazali (445-505 A.H/1058–1111). Ambae ni mfuasi wa Madhhab
ya Imam Al Shafi’i kutoka Tus, Iran.
Mujaddid wa karne ya sita ya Uislam: Mujaddid Imam, Imām al-Mushakkikīn Abu
Abdullah Muhammad Ibn Umar Ibn al-Husayn at-Taymi al-Bakri at-Tabaristani Fakhr
ad-Din ar-Razi (544-606 A.H/1149-1209). Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam Al
Shafi’i kutoka Ray, Iran. na
Mujaddid Imam ad-Din Abu Al Qasim Abdul Karim Ibn Muhammad Ibn Abdul Karim
Ibn Al-Fadhl Ibn Hasan Ar Rafi'i Al Qazwini (557-623 A.H/1162-1226). Ambae ni
mfuasi wa Madhhab ya Imam Al Shafi’i kutoka Qazwini, Iran.
Mujaddid wa karne ya saba ya Uislam: Mujaddid Imam Muhammad Ibn Ali Ibn Wahb
Al Misri Al Maliki As Shafi’i maarufu kama Imam Ibn Daqeeq Al Eid (625-702 A.H).
Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam Al Shafi’i kutoka Misri.
Mujaddid wa karne ya nane ya Uislam: Mujaddid Imam, Al-Haafidh Shihabuddin Abu
ul Fadhl Ahmad Ibn Ali Ibn Muhammad maarufu kama Imam Ibn Hajar Al Asqalani.
Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam Al Shafi’i kutoka Asqalani, Palestina. na
Mujaddid Imam Sirajuddin `Umar Ibn Rastan Ibn Nasir Ibn Salih Ibn Ahmad Ibn
Muhammad Ibn Shihab Al Asqalani maarufu kama Imam Al Bulqini (724-810
A.H/1324-1403). Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam Al Shafi’i kutoka Bulqina,
Misri.
523
Mujaddid wa karne ya tisa ya Uislam: Mujaddid Imam, Hafidh Jallal Ad Din Abu
Bakr Abd Rahman Al Suyuti (849-911 A.H/1445-1505) Ambae ni mfuasi wa Madhab ya
Imam Al Shafi’i kutoka Al Qakhira (Cairo), Misri.
Wanazuoni waliofuatia baada ya Imam Al Suyuti wakaendeleza orodha hiyo kama
ifuatavyo:-
Mujaddid wa karne ya kumi ya Uislam: Mujaddid Imam Shams Ud Dîn Muhammad
Ibn Ahmad Al Ramli (919-1004 A.H). Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam Al Shafi’i
kutoka Al Ramlah, Misri.
Mujaddid wa karne ya kumi na moja ya Uislam: Mujaddid Imam Rabbani Al Alf Al
Thani Shaykh Ahmad Al Faruqi Al Sirhindi (1564-1624). Ambae ni mfuasi wa Madhhab
ya Hanafi kutoka Sirhind (Punjab) India.
Mujaddid wa karne ya kumi na mbili: Mujaddid Imam, Al-Qutb Abd Allah Ibn Alawi
Al Haddad (1634-1720). Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam Al Shafi’i kutoka
Hadhramawt, Yemen. na
Mujaddid Imam Shah Waliyu Allah Ad Dahlawi ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Imam
Abu Hanifa
Mujaddid wa karne ya kumi na tatu ya Uislam: Mujaddid Imam Muhammad Amin
Ibn Abidin ash Shami (1198–1252 AH/1783-1836). Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya
Hanafi kutoka Syria.
Mujaddid wa karne ya kumi na nne ya Uislam: Mujaddid Imam, Muhaddith al Akbar
Muḥammad Badr Al Dīn Ibn Yūsuf Al Marākishī Al Sibtī al Baybānī Al Dimashqī Al
Ḥasanī (1850-1935). Ambae ni mfuasi wa Madhhab ya Maliki kutoka Morocco. na
Mujaddid Imam Muhammad Zahid Ibn Hasan Al Kawthari (1879-1951). Ambae ni
mfuasi wa Madhhab ya Hanafi kutoka Uturuki.
Na zifuatazo ni kauli za Wanazuoni hao wenye Ilm ya juu na kufikia darja ya Mujaddid
Ad Din juu ya kurudi tena kwa Nabii Isa baada ya kupandishwa kwake mbiguni.
Mujaddid Imam wa Karne ya kwanza: Abdullah Ibn Abbas (618 – 687 AH) alisema
kua “Allah Subhanah wa Taála alimnyanyua Isa Ibn Maryam kumpelekea
Mbinguni.” (Imam Abu Bakr Ahmad Ibn Husayn Ibn Ali Ibn Musa Al Khosraji Al
Bayhaqi)
Mujaddid Imam wa Karne ya pili: Imam Abu ʿAbdullah Muhammad Ibn Idris al
Shafi‘i (767/150 – 820/204 CE/AH) Alisema kua: ‘Kama ilivyokua kwa Isa Ibn
Maryam alivyopandishwa juu Mbinguni, basi ndio hivyo hivyo atakavyoshushwa
Ulimwenguni kwa amri ya amri ya Allah Subhanah wa Taála ili kuja kueneza Dini
ya Allah Subhanah wa Taála, watu wenye Imani dhaifu wanaweza wakaona kua hii
524
haiwezekani. Lakini hili ni jambo rahisi pale tunapozungumzia Uwezo wa Allah
Subhanah wa Taála’
Mujaddid Imam wa Karne ya tatu: Abū Al-Hasan Alī Ibn Ismā’īl Al-Ash’arī
(874/260 – 936/324 CE/AH) anasema kua: ‘Kuna Makubaliano ya Ijmaa Ummat kua
Isa Ibn Maryam alinyanyuliwa juu mbinguni.’ (Al-Ash’ari’s al-Ibana ‘an Usul al-
Dina,)
Mujaddid Imam wa Karne ya nne: Abu Abd-Allah Muhammad ibn Abd-Allah al-
Hakim al-Nishaburi (933/321 – 1012/403 CE/AH) anasema katika kitabu chake cha
Mustadrak Al Hakim kua: Amesema Abd Allah Ibn Abbas kua kuhusiana na aya
isemayo:
﴿وَإِن مِّنْ أَهْلِ ٱلْكِتَابِ إِلا َّ لَيُؤْمِنَن َّ بِهِ قَبْلَ مَوْتِهِ وَيَوْمَ ٱلْقِيَامَةِ يَكُونُ عَلَيْهِ مْ
شَهِيداً ﴾
Wa-in min ahli alkitabi illa layu/minanna bihi qabla mawtihi wayawma alqiyamati
yakoonu AAalayhim shaheedan (Surat An Nisaa 4:159)
Tafsir: Na hakuna miongoni mwa watu wa Ahl ul kitabi isipokua watamuamini kabla
ya mauti yake na katika siku ya Kiama atakua ni shahidi dhidi yao.
Ayah hii ni uthibitisho kua Isa ibn Maryam atakuja tena na watu wa Ahl al Kitabi
wote watamuamini kabla ya kufariki kwake. (Imam Al-Hakim, Al-Mustadrak)
Mujaddid Imam wa Karne ya Tano: Hujjat ul Islami Imam Abū Hāmid Muhammad
Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali ‘Qurán itafutika kutoka katika Nyoyo
za watu na hakuna mtu ambae ataikumbuka, hivyo watu watarudi tena katika enzi
za kuimba nyimbo na kuimba mashairi na hikaya. Kisha Masih Dajal atatokea na
Isa Ibn Maryam Alayhi Salatu wa Salam atashuka na kumuua. Wakati
yatakapotokea yote haya itakua kama vile hali ya mwanamke mjamzito
anakapokua katika hali ya uchungu, akisubiri kujifungua ’(Ihya Ulum Ad Din)
Akasema tena Hujjat Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazal kua: ‘Mitume wote wameoa, isipokua Isa Ibn Maryam yeye
hakua ni miongoni mwa Waliooa lakini ataoa katika wakati wa kipindi chake cha
pili atakapokuja Duniani’ (Ihya Ulum Ad Din Siri ya Ndoa)
525
Imam Abu Bakar Ibn Al Arabi yeye anasema kua: ‘Ingawa miaka zaidi ya 1000 imepita
tangu kuzaliwa kwa Isa Ibn Maryam, lakini ukweli ni kua yeye bado yuko hai
kiroho na kimwili mbele ya Allah Subhanah wa Taála’ (Sharh Jamii Al Tirmidhii)
Mujaddid Imam wa Karne ya Sita: Al Ghawth Shaykh Abd al-Qadir al-Jilani (1077
– 1166 CE) yeye anasema kua: ‘Isa Ibn Maryam, hakuoa, lakini mwisho wa Dunia
utakapofika basi Allah Subhanah wa Taála atamrudisha tena Duniani, na ataoa
binti wa Quraysh ambae atazaa nae mtoto wa kiume’(Al Malfuzat.)
Mujaddid ud Din Imam Fakhr Al Din Al Razi anasema kua:
﴿بَل ر َّفَعَهُ ٱهلل َُّ إِلَيْهِ وَكَانَ ٱهلل َُّ عَزِيزاً حَكِيماً ﴾
Bal rafaAAahu Allahu ilayhi wakana Allahu AAazeezan hakeeman (Surat An Nisaa
4:158).
Tafsir: Bali alimnyanyua Allah kwake yeye, na kwa hakika Allah ni mwenye Uwezo
na ni mwingi wa Hikma.
Aya hii inatuwekea wazi kua Isa Ibn Maryam alinyanyuliwa mbinguni wakati
akiwa hai (Mafatih Al Ghayb/Tafsir al Kabir)
Ambapo neno Bal yaani Bali kimaana hua ni ni lenye kuonesha kukataa na kubatilisha
kitendo kilichofuatia kabla yake na hivyo kua ni lenye kuthibitisha kitendo kinachofuata
baada yake.
Mujaddid Imam wa Karne ya Nane: Imam Ibn Hajar Al-Asqalani (1372/773 – 1448/852
CE/AH) “Mahdi atatokana na Ummah huu, na Isa Ibn Maryam atashuka na kusali
nyuma yake’ na akasema tena pia kua; ‘Hakuna Mtume baina ya Isa Ibn Maryam na
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na yeye Isa Ibn Maryam hana kaburi’.
(Fath al-Baari)
Mujaddid Imam wa Karne ya Tisa: Jalaluddin Al-Suyuti (1445/849 – 1505/911
CE/AH) amesema kua “Mji Wa Jerusalem una utukufu wake kwa Waislam kwa
sababu, ni katika mji wa Jerusalem ndipo ambapo Isa Ibn Maryam alizaliwa, ni
katika mji wa Jerusalem ndipo Mitime wengi waliuliwa, ni katika Mji wa Jerusalem
ndio sehemu ambayo Isa Ibn Maryam alizungumza wakati akiwa ndani ya mkoba
wa kubebea mtoto mchanga, na ni katika mji wa Jerusalem ndio sehemu ambayo
526
alipandishwa juu mbinguni na ndipo atakaposhukia kutoka Mbinguni (Durr al-
Manthur)
Imam Al Suyuti amesema tena katika kuifafanua aya ifuatayo:
﴿إِذْ قَالَ ٱهلل َُّ يٰعِيسَى ٱبْنَ مَرْيمََ ٱذْكُرْ نِعْمَتىِ عَلَيْكَ وَعَلَى ٰ وَالِدَتِكَ إِذْ أَي َّدت ُّكَ
بِرُوحِ ٱلْقُدُسِ تُكَلِّمُ ٱلن َّاسَ فىِ ٱلْمَ هْ دِ وَكَ هْ لاً ﴾
Idh qala Allahu ya AAeesa ibna maryama udhkur niAAmatee AAalayka waAAala
walidatika idh ayyadtuka biroohi alqudusi tukallimu alnnasa fee almahdi wakahlan
(Surat Al Maidah 5:110)
Tafsir: Alisema Allah Subhanah wa Taála kua: ‘Ewe Isa Ibn Maryam kumbuka neema
zangu juu yako na juu ya mzazi wako (Mama yako Maryam Bint Imran) nilipokusaidia
mimi na Ruh ul Qudus (Malaika Jibril) hivyo ukazungumza na watu wakati upo katika
mkoba wa mtoto mchanga na utakapokua’
Neno Kahlan lililotumika hapa linamaanisha kua Isa Ibn Maryam atashuka chini
kutoka Mbinguni kabla ya siku ya Kiama, kwa sababu alipandishwa juu Mbinguni
kabla ya kuufikia uzee (Tafsir al-Jalalayn, Surah al-Ma’ida)
Imam Suyuti ameandika katika Durr Manthur kua: Imam Ahmad, Imam Bukhari, Imam
Muslim na Imam Baihaqi wamesema kua amesema Rasul Allah Salallahu A’lahi wa
Salam kua: ‘Jee Itakuaje hali yenu, katika wakati ambao Isa Ibn Maryam atashuka
na kua miongoni mwenu na Imam wenu atakua ni kutoka miongoni mwenu?’
Mujaddid Imam wa Karne ya Kumi na Moja: Rabbānī Shaykh Ahmad Al-Farūqī Al-
Sirhindī Mujaddid Alf Thānī (1564 – 1624 CE) ambae amesema: “Isa Ibn Maryam
atashuka kutoka mbinguni na atakua ni mfuasi wa Nabii Muhammad Salallahu
Alayhi wa Salam, kwa kauli nyengine basi, atakua ni mwenye kufuata shariah za
Allah Subhanah wa Taála alizokuja nazo Rasul Allah Salallahu aAlayhi wa Salam.’
(Rasail Imam Rabbani)
Mujaddid Imam wa Karne ya Kumi na Mbili: Shah Waliullah Dehlwi (1703 – 1762
CE) ambae amesema ‘Hakuna mtu hata mmoja miongoni mwa Ahl Ul Kitab
atakaekua hai isipokua ataka ni mwenye kumuamini Isa Ibn Maryam pale
atakaposhuka tena kabla ya kuufariki kwake, hata na Mayahudi watakaokuwepo
katika wakati huo watamuamini’ (Fath ur Rahmaan Fii Tarjumatul Qura’an, 4:159)
527
Mujaddid Imam wa Karne ya Kumi na mbili; Muhammad ash-Shawkani (1759–1834
CE) amesema kua: ‘Isa ibn Maryam alinyanyuliwa juu Mbinguni na atashuka
mwishoni mwa Ulimwengu’ (Fath al-Qadir)
Mujaddid Imam wa Karne ya kumi na nne; Bediüzzaman Said Nursî (1878 - 1960) :
‘Nabii Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam aliainisha miongoni mwa Miujiza
mikubwa Ulimwenguni ni kushuka kwa Isa Ibn Maryam pale aliposema: ‘Isa ibn
Maryam atashuka kutoka mbiguni, na ataishi kulingana na Sharia yangu’’ (Rasail
Bediuzzaman)
Mujaddid Imam Muhammad Ash-Shanqeeti (1907 – 1973 C.E) amesema kua:
‘Qur’an na Sunna zinathibitishha kua Isa Ibn Maryam yuko hai na anaishi mbiguni
na atashuka kabla ya siku ya Mwisho’(Adwaa Ul Bayaan fii Tafsir Il Qurán bil Qurán)
Na bila ya shaka amesema Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Isa Ibn
Maryam atarudi katika Ulimwengu huu na kujumuika na Ummah wangu na hivyo
kua ni mwenye kufuata sharia yangu.’ (Sahih Bukhari na Muslim na Sunan Imam Ibn
Majah)
TAQDIM WA TAAKHIR KATIKA QUR’AN
Tunapozunguzumzia llm Al Maani na Ilm al Balagha katika Uumu ul Qur’an basi
tunaona kua katika baadhi ya aya ndani ya Qur’an zimetumia mfumo wa maneno
unaojulikana kama Taqdim na Ta’akhir yaani Kuzungumziwa kwa vitu viwili katika hali
ambayo kimoja hua kinawahi kukitangulia chengine katika kutajwa kwake, ijapokua
kimaumbile basi kile kilichotangulizwa hua ni cha Mwisho na kile kilichotajwa Mwisho
hua ni cha Mwanzo.
Hivyo pale inapokua Kitu husika kimetangulizwa kwa kutajwa mwanzo basi hua
kinajulikana kama Taqdim na kile kilichotajwa Mwisho hua kinajulikana kama Taakhir
yaani Kilichowekwa Mwisho katika mpangilio wa kutajwa kwake.
Ambapo hata hivyo mfumo huo wa mpangilio wa maneno hayo ya Taqdim na Taakhir
katika aya husika hua hayabadilishi maana na badaa yake hua ni wenye kuthibitisha
maana halisi iliyokusudiwa kubainishwa na Aya na hivyo kuifanya Qur’an kua na sifa za
upekee katika mpangilio wa maneno yake.
Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi anatuambia kua: ‘Ndani katika Qur’an
kuna hali ya matukio ambayo hua inajulikana kama Taqdim wa Taakhir
528
(Kubainisha hali ya Utangulizi wa Kitu na hali ya Mwisho wa Kitu) ambayo ni
mengi sana, kwa mfano pale aliposema Allah Subhanah wa Ta’ala:
﴿وَٱهلل َُّ أَخْرَجَكُم مِّن بُطُونِ أُم َّهَاتِكُمْ لاَ تَعْلَمُونَ شَيْئاً وَجَعَلَ لَكُمُ ٱلْس َّمْعَ
وَٱلأَبْصَارَ وَٱلأَفْئِدَةَ لَعَل َّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴾
WaAllahu akhrajakum min butooni ommahatikum la taAAlamoona shay-an
wajaAAala lakumu alssamAAa waal-absara waal-af-idata laAAallakum
tashkuroona (Surat An Nahl 16:78)
Tafsir: Allah amekutoeni nyie kutoka kwenye matumbo ya Mama zenu huku mkiwa
hamjui kitu na amekujaalieni Masikio, Macho na Nyoyo ili mpate kua ni wenye
kuonesha Shukurani
Ambapo hali ya Taqdim na Taakhir hapa katika aya ni pale tunapoona kua ingawa
Allah Subhanah wa Ta’ala anawaumba Ibn Adam wakiwa na Masikio, Macho na
Nyoyo wakati wakiwa Matumboni mwa Mama zao kabla ya kuzaliwa kwao, lakini
hapa ametaja kuzaliwa kwao kabla ya kutaja viungo hivyo walivyoumbwa navyo.
Ambapo mifano myengine ya hali hii ya Taqdim wa Taakhir tunaziona katika Qu’ran
pale Allah Subhanah wa Ta’ala aliposema kua:
﴿وَلاَ تُعْجِ بْكَ أَمْوَالهُُمْ وَأَوْلاَدُهُمْ إِنم ََّا يُرِيدُ ٱهلل َُّ أَن يُعَذِّبَهُمْ هبَِا فىِ ٱلد ُّنْيَا وَ تَزْهَقَ
أَنفُسُهُمْ وَهُمْ كَ افِرُونَ ﴾
Wala tuAAjibka amwaluhum waawladuhum innama yureedu Allahu an
yuAAadhdhibahum biha fee alddunya watazhaqa anfusuhum wahum kafiroona
(Surat At Tawbah 9:85)
Tafsir: Na wala Msione Ajabu juu ya Mali zao na Watoto wao kwani Allah anataka
kuwaadhibu kutokana nao hapa Duniani na hivyo Roho zao zitoke huku wakiwa ni
Makafiri.
529
Na hivyo aya hii intakwa ifahamike kama : ‘Fa la tu`jibuka amwaluhum wa la
auladuhum fi al-hayat al-duniya;innama yuridu Allahu li yu`adhdhibahum biha fi al-
`akhira’ yaani ‘Na Kisha Msistajabishwe na Mali na Watoto wanaowamiliki katika
maisha ya Duniani. Kwani Allah anataka kuwaadhibu kutokana nao Kesho
Akhera’
Ambapo huu ni mfano wa hali ya Taqdim Kutangulizwa kwa Kitu katika kubainishwa
kwake kwani Makafiri hua ni wenye Kuadhibiwa Akhera ambapo kwa upande wa aya
ifuatayo basi hua ni yenye mfano wa hali ya Taakhir yaani ya Kucheleweshwa Mwisho
kwani inasema:
﴿وَ لَوْلاَ كَلِمَةٌ سَبَقَتْ مِن ر َّبِّكَ لَكَانَ لِزَاماً وَأَجَ لٌ م ُّسَمًّ ى﴾
Walawla kalimatun sabaqat min rabbika lakana lizaman waajalun musamman
(Surat Ta-Ha 20:129)
Tafsir: Na kama si Kauli iliyotangulia kutoka kwa Mola wako na jambo lisiloepukika
basi ni jambo ambalo limeshaamuliwa litokee (Adhabu yao ingewafika hapa Duniani)
Ambapo inatakiwa ifahamike kama ‘Wa laula kalimatun sabaqat min rabbika wa
ajalun musamma lakana lizama’ yaani ‘Na Kama si Kauli iliyotangulia kutoka kwa
Mola wako kua litokee basi lisingeepukika (Adhabu ingetokea hapo hapo)’
Ambapo mfano mwengine ni ule wa aya ya Mirathi ambayo inasema:
﴿يُوصِيكُمُ ٱهلل َُّ فيِ ۤ أَوْلاَدِكُمْ لِلذ َّكَرِ مِثْلُ حَظِّ ٱلأُنْثَيَينِْ فَإِن كُن َّ نِسَآءً فَوْقَ ٱثْنَتَينِْ
فَلَهُن َّ ثُلُثَا مَا تَرَكَ وَإِن كَانَتْ وَاحِ دَةً فَلَهَا ٱلنِّصْفُ وَلأَبَوَيْهِ ِ لِكُل وَاحِ دٍ مِّنْهُمَا
ٱلس ُّدُسُ ممِ َّا تَرَكَ إِن كَانَ لَهُ وَلَدٌ فَإِن لم َّْ يَكُنْ ل َّهُ وَلَدٌ وَوَرِثَهُ أَبَوَاهُ فَلِأُمِّهِ ٱلث ُّلُثُ فَإِن
ّ
كَانَ لَهُ إِخْوَةٌ فَلِأُمِّهِ ٱلس ُّدُسُ مِن بَعْدِ وَصِي َّةٍ يُوصِى هبَِآ أَوْ دَيْنٍ آآبَؤُكُمْ وَأَبناؤُكُ ْم
لاَ تَدْرُونَ أَي ُّهُمْ أَقْرَبُ لَكُمْ نَفْعاً فَرِيضَةً مِّنَ ٱهلل َِّ إِن َّ ٱهلل ََّ كَانَ عَلِيماً حَكِ يماً ﴾
530
Yooseekumu Allahu fee awladikum lildhdhakari mithlu hadhdhi alonthayayni fa-in
kunna nisaan fawqa ithnatayni falahunna thulutha ma taraka wa-in kanat
wahidatan falaha alnnisfu wali-abawayhi likulli wahidin minhuma alssudusu
mimma taraka in kana lahu waladun fa-in lam yakun lahu waladun wawarithahu
abawahu fali-ommihi alththuluthu fa-in kana lahu ikhwatun fali-ommihi alssudusu
min baAAdi wasiyyatin yoosee biha aw daynin abaokum waabnaokum la tadroona
ayyuhum aqrabu lakum nafAAan fareedatan mina Allahi inna Allaha kana
AAaleeman hakeeman(Surat An Nisaa 4:11)
Tafsir: Allah anakuamrisheni kuhusiana na Watoto wenu: Juu ya Mwanamme ni
sawa na sehemu ya Wanawake wawili. Lakini kama ikiwa kuna Watoto wa Kike peke
yao wawili au zaidi basi juu ya ni sehemu mbili kati ya tatu ya Mali ya Mtu, na kama
kuna mmoja tu basi juu yake yeye ni Nusu, na kwa Mzazi wa Mtu basi kila mmoja juu
yake ni Sehemu moja kati ya Sita ya Mali kama ikiwa amewacha Mtoto, lakini kama
ikiwa hakuacha Mtoto na Mzazi pekee anaerithi kutoka kwake basi juu ya Mama yake
ni sehemu moja kati ya tatu na kama ana Ndugu basi juu ya Mama ni moja kati ya
Sita, baada ya Wasia aliouacha (Kutekelezwa) au Deni (Kulipwa)
Ambapo ingawa Aya imetaja Kutekelezwa kwa Wasia kwanza lakini kwa upande wa
Hukumu za Fiqh basi kwanza hua ni Deni ndio linaloshughulikiwa mwanzo kabla ya
Wasia.
Mfano mwengine ni ule wa Aya inayosema:
﴿فَفَه َّمْنَاهَا سُلَيْمَانَ وَكُلاًّ آتَيْنَا حُكْماً وَعِلْماً وَسَخ َّرَْ مَعَ دَاوُودَ ٱلجِْبَالَ يُسَبِّحْ نَ
وَٱلط َّيْرَ وَكُن َّا فَ اعِلِينَ ﴾
Fafahhamnaha sulaymana wakullan atayna hukman waAAilman wasakhkharna
maAAa dawooda aljibala yusabbihna waalttayra wakunna faAAileena (Surat Al
Anbiyaa 21:79)
Tafsir: Na Tukamfahamisha juu yake Sulayman na kila mmoja wao tumempa Hikma
na Ilmu. Na tumeviweka chini yake Daudi, Majabali yanamsalimia na Ndege na ni
sisi wafanyaji wa hayo.
Ambapo kwa kikawaida basi Ilm huitangulia Hikma lakini katika ayah hii Hikma
imetajwa katika hali ya kuitangulia Ilm. Na mfano mwengine ni wa ile aya ya Surat Al
Mulk ambayo inasema:
531
﴿ٱل َّذِى خَلَقَ ٱلْمَوْتَ وَٱلحَْيَاةَ لِيَبْلُوَكُمْ أَي ُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلاً وَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلْغَفُورُ ﴾
Alladhee khalaqa almawta waalhayata liyabluwakum ayyukum ahsanu AAamalan
wahuwa alAAazeezu alghafooru(Surat Al Mulk 67:2)
Tafsir: Ni yeye ndie alieumba Mauti na Uhai ili akupimeni ni yupi miongoni mwenu
kua ni m-bora katika kufanya Mema, na yeye Ndie Mwenye Utukufu na ni Mwingi wa
Usamehevu.
Ambapo aya imetanguliza Maumbile ya Kifo kabla ya Maumbile ya Uhai wakati
kimaumbile kwanza hua kuna Uhai na kisha ndio hufuata Kifo.
Na mfano mwengine ni katika ile aya semayo:
﴿ٱلحَْمْدُ هللِ َِّ ٱل َّذِى أَنْزَلَ عَلَى ٰ عَبْدِهِ ٱلْكِتَابَ وَلمَْ يجَْعَل ل َّهُ عِوَجَا﴾
Alhamdu lillahi alladhee anzala AAala AAabdihi alkitaba walam yajAAal lahu
AAiwajan(Surat Al Kahf 18:1)
Tafsir: Shukran zote anastahiki Allah yule ambae amemshushia Mja wake Kitabu na
hakuweka ubaya ndani yake
Inatakiwa ifahamike kua ‘Alhamd lillahi Aladhii anzala `al `abdihi al-kitab qayyiman
wa lam yaj`al lahu iwaja’ yaani ‘Shukran zote anastahiki Allah yule ambae
amemshushia Mja wake Kitabu kilichokamilia bila ya kukijaalia kua na kasoro.
Kutokana na kuwepo kwa hali hii ya Taqdim na Taakhir ndani ya Qur’an basi Imam
Qatada Al Sadusi basi yeye amesema kua: ‘Aya hii ya Surat Al Imran 3:55:
﴿إِذْ قَالَ ٱهلل َُّ ٰ يٰعِيسَى ِ إِنىّ مُتَوَفِّيكَ وَرَافِعُكَ إِلىَ َّوَمُطَهِّرُكَمِنَ ٱل َّذِينَ كَ فَرُواْ
وَجَاعِلُ ٱل َّذِينَ ٱت َّبَعُوكَ فَوْقَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ إِلىَٰ يَوْمِ ٱلْقِيَامَةِ ثمُ َّ إِلىَ َّ َمرْجِعُكُْم
فَأَحْكُمُ بَيْنَكُمْ فِيمَا كُنتُمْ فِيهِ تخَْتَلِفُونَ ﴾
532
Idh qala Allahu ya AAeesa innee mutawaffeeka warafiAAuka ilayya
wamutahhiruka mina alladheena kafaroo wajaAAilu alladheena ittabaAAooka
fawqa alladheena kafaroo ila yawmi alqiyamati thumma ilayya marjiAAukum
faahkumu baynakum feema kuntum feehi takhtalifoona (Surat Al Imran 3:55)
Tafsir: Na akasema Allah (Subhanah wa Ta’ala): ‘Ewe Isa! Hakika mimi
nitakutimizia Ahadi niliyokuwekea, nitakunyanyua kwangu na kukusafisha kutokana
na wale ambao waliokufuru na nitawajaalia wale wanaokufuata kua juu ya
waliokufuru hadi katika siku ya Kiama. Na kisha mtarudi kwangu nami nitahukumu
baina yenu juu ya yale mliyokua mkikhitilafiana’
Kua inatakiwa ifahamike kama ‘Rafiyuka ilayya wa Mutawafeeka’ yaani Allah
Subhanah wa Ta’ala anamwambia Nabii Isa kua ‘Nitakunyanyua kwangu na
kukutimizia Ahadi niliyokuwekea’
ISA IBN MARYAM NA MAHDI, DAJJAL, JUJ WA MAJUUJ NA DHUL
QARNAYN.
Neno Mahdi ni neno linalotokana na neno Hada au Huda ambalo kwa Kiarabu hua ni
lenye kumaanisha Kuongoza njia, Kuonesha njia kwa Ukarimu au Kuongoza njia
iliyokua Sahih. Hivyo tunapozungumzia neno Mahdi basi hua tunazungumzia mtu
mwenye sifa ya kua ni mwenye kuongoka na kua ni mwenye kuelekea katika njia sahih.
Mara nyingi unapozungumzia juu ya Mahdi basi watu hua ni wenye kujiuiza kwa
kutoweza kujua juu ya uhalisia wa huyu Mahdi ndio nani yaani ni Nabii Isa, au ni mtu
mwengine zaidi?
Jibu la suali hili linapatikana pale tunapoangalia na kuona kua: Kuna Hadith ambazo
zinathibitisha kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliwaombea Dua baadhi ya
Masahaba zake wawe ni miongoni mwa Mahdi, Kuna hadith zinazothibitisha kua familia
ya watu wa Ahl Al Bayt watatoa mtu kabla ya kipindi cha mwisho wa Dunia ambae nae
atakua na darja ya Imam Mahdi ambae yeye alipotajwa katika hadith basi ametajwa kwa
jina la Al Mahdi jina ambao linaweka wazi kua yeye ndie atakaekua na Darja ya upekee
na sifa inayostahiki ya kua ni Al Mahdi.
Yaani kama vile ambavyo tunavyosema kua Imam wa Hadith kua ni Hafidh wa Hadith
kwa mfano Al Hafidh Imam Al Baghawi, Al Hafidh Imam Al Sakhawi, Al Hafidh Imam
Al Qastallani, Al Hafidh Imam Ibn Al Mundhri, n.k. lakini hapo hapo watu wanaposema
533
Al Hafidh pekee bila ya kutaja jina la Imam husika basi moja kwa moja wenye kujua hua
wanajua kua aliekususdiwa hapo si Al Hafidh yeyote mwengine isipokua Mujaddid ad
Din, Shaykh ul Islami Al Hafidh Imam Shihab Ad Din Ibn Hajjar Al Asqalani.
Hivyo basi tunapozungumzia Mahdi basi na Nabii Isa Ibn Maryam ambae ni Nabii na
Mtume wa Allah Subhanah wa Ta’ala nae pia anajulikana kwa cheo cha Mahdi lakini si
Al Mahdi.
Miongoni mwa hadith ambazo zinathibitisha kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alitumia jina hilo katika dua zake kuwaombea Masahaba zake wawe na daraja hio ni ile
ambayo alimuombea dua Jarir Ibn Abdullah Radhi Allah Anhu, kwa kusema:
الل َّهُم َّ ثَبِّتْهُ وَاجْعَلْهُ هَادًِ مَهْدًِّ
Ya Allah! Mjaalie msimamo thabit na umjaalie uongofu wenye darja ya Mahdi (Sahih
Bukhari)
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimuombea dua Muawwiyah Ibn Abu Sufyan
Radhi Allahu Anhu, kwa kusema:
Ya Allah! Mjaalie uongofu wa Mahdi (Jami’ Tirmidhi)
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimsifia Sayyidna Ali Ibn Abi Talib Karama
Allahu Wajh kwa kusema:
Mtamuona kua ni Muongofu na mwenye sifa ya Mahdi ambae atakuongozeni
katika njia iliyonyoooka (Al-Isaba fi Ma’rifatil Sahaba)
Ama kuhusiana na jina lake huyu mtu mwenye darja ya Al Mahdi, basi amesema Rasul
Allah Salallahu A’layhi wa Salam kua: ‘Kuna mtu atakaetoka katika familia yangu
ambae atakua jina lake kama jina langu, na jina la baba yake kama jina la baba
yangu.’(Sunan Abu Dawud)
Vile vile alisema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hata kama itabakia siku
moja tu kabla ya kufika Kiyama, basi Allah Subhanah wa Ta’ala atamtuma mtu
kutoka katika familia yangu ambae ataijaza hii Dunia haki na uadilifu kama vile
mwanzo ilivyokua imejaa dhulma.’(Sunan Abu Daud)
534
Ambapo amesema Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayh wa Salam kua: ‘Ukifika wakati, basi Isa Ibn Maryam ghafla
atashuka miongoni mwa Waislam. Na utakusanyika mkusanyiko kwa ajili ya Sala
nae ataambiwa: ‘Ewe Ruhi Allah njoo mbele utusalishe’ lakini nae atasema: ‘La,
Imamu wenu atakuja mbele na atakusalisheni’ hivyo baada ya Sala ya Alfajr
Waislamu waatoka kwa ajli ya kupigana na Masih Dajjal, ambapo Dajjal
atakapomuona Isa Ibn Maryam basi atayeyuka kama inavyoyeyuka Chumvi
kwenye Maji, hivyo Isa Ibn Maryam atamsogelea na Kumuua, na hali itafikia kua
hadi kila Jiwe litakua linasema: ‘Ewe Ruhi Allah, kuna Yahudi amejificha nyuma
yangu’ hivyo hakuna Mfuasi wake hata mmoja ambae ataepuka kuuliwa’’(Musnad
Imam Ahmad)
Na amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Wakati Mahdi
atakaposalisha Sala ya Al Fajr pamoja na Waumini katika Bayt ul Maqdis, basi
atamtambulisha Isa Ibn Maryam ambae atakuwepo, nae Isa Ibn Maryam
atamshika bega Mahdi na kumwambia: ‘Adhana imeadhiniwa kwa ajili yako, hivyo
ni wajibu wako kusalisha’’(Al-Qawl Al-Mukhtasar Fi alamat Al-Mahdi Al-Muntazar)
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam amesema kua: ‘Naapa kwa jina la Allah
Subhanah wa Taála, ambae ndie alienituma mimi kua ni Mtume wa kweli, kua bila
ya shaka Isa Ibn Maryam atakuta katika Umma wangu watu ambao watachukua
nafasi ya Wanafunzi wake hapo atakaporudi katika kipindi cha mwisho wa Dunia’
(Al-Tirmidhi, Nawadir al-Usul fi Ma'rifat Ahadith al-Rasul)
Ambapo anasema Imam Sa’id Nursi Bediuzzaman kua: ‘Kushuka kwa Isa Ibn Maryam
na kujulikana kua yeye ndie Masih Isa Ibn Maryam kutajulikana kwa kupitia njia
ya kua na Nuru ya Imani, kwani si kila mtu atakua ni mwenye kujua kuhusiana
nae’
‘Na atakapokuja atakua ni mwenye kusali nyuma ya Imam Mahdi na kumfuata
kwake kunadhihirisha Umoja wa Mamlaka ya Qur’an na kua ni yenye kufuatwa.’
Kama inavyothibitishwa na aya ifuatayo:
﴿وَعَدَ ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ مِنْكُمْ وَعَمِلُواْ ٱلص َّ الحَِاتِ لَيَسْتَخْلِفَن َّهُمْ فىِ ٱلأَرْضِ كَمَ ا
ٱسْتَخْلَفَ ٱل َّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ وَلَيُمَكِّنَن َّ لهَُمْ دِينَهُمُ ٱل َّذِى ٰ ٱرْتَضَى لهَُمْ ن وَلَيُبَدِّ لَ َّ هُْم
535
مِّن بَعْدِ خَوْفِهِمْ أَمْناً يَعْبُدُونَنىِ لاَ يُشْرِكُونَ بىِ شَيْئاً وَمَن كَفَرَ بَعْدَ ذٰلِ كَ فَأُوْلَٰئِكَ
هُمُ ٱلْفَاسِ قُون﴾
WaAAada Allahu alladheena amanoo minkum waAAamiloo alssalihati
layastakhlifannahum fee al-ardhi kama istakhlafa alladheena min qablihim
walayumakkinanna lahum deenahumu alladhee irtada lahum
walayubaddilannahum min baAAdi khawfihim amnan yaAAbudoonanee la
yushrikoona bee shay-an waman kafara baAAda dhalika faola-ika humu
alfasiqoona (Surat Nur 24:55)
Tafsir: Na anawaahidi Allah wale ambao Walioamini miongoni mwenu na wakafanya
Mema kua watakua ni Makhalifa wa Ardhini kama vile ambavyo alivyowafanya
waliotangulia kua ni Makhalifa na atawathibitishia kwa ajili yao Dini yao ambayo
ameiridhia na kuwapa wao baada ya khofu na Usalama wao: (kwa kuwaambia)
‘Niabuduni mimi msinishirikishe na yeyote’ Hivyo Mtu yeyote atakae kufuru baada ya
hapo basi atakua ni miongoni mwa Wapotovu.
Hivyo kuja kwa Mahdi na kurudi kwa Isa Ibn Maryam hua ni Rehma ya Allah Subhanah
wa Ta’ala kwa Waja wake wanaomtii na pia utimizwaji wa Ahadi yake kama
zinavyosema aya:
﴿وَمَن يَتَوَل َّ ٱهلل ََّ وَرَسُولَهُ وَٱل َّذِينَ آمَنُواْ فَإِن َّ حِ زْبَ ٱهلل َِّ هُمُ ٱلْغَالِبُونَ ﴾
Waman yatawalla Allaha warasoolahu waalladheena amanoo fa-inna hizba Allahi
humu alghaliboona(Surat Al Maidah 5:56)
Tafsir: Ama wale wanaotaka urafiki kwa Allah na Mtume wake na Walioamini, basi
kwa hakika ni Kikundi cha Allah ndio chenye kua na ushindi.
Ambapo pia tukio hili la kurudi kwa Nabii Isa Ibn Maryam na kushirikiana na Mahdi
kupigana na Dajjal litakua ni lenye kuenda sambamba na tukio la kufurika kwa Yajuj wa
Majuj ambao nao wataangamizwa kutokana na Dua ya Nabii Isa Alayhi Salam na hivyo
kuthibitisha ubainisho wa miongoni mwa dalili kubwa za mwisho za mwisho za Dunia,
kama anavyosema Allah Subhanah wa Ta’ala katika Qur’an:
536
﴿حَتى َّ ٰ إِذَا فُتِحَتْ َْجُوجُ وَمَأْجُوجُ وَهُمْ مِّن ِ كُل حَدَبٍ يَنسِ لُونَ۞وَ ٱقْتَرَبَ
ٱلْوَعْدُ ٱلحَْق ُّ فَإِذَا هِىَ شَاخِ صَةٌ أَبْصَارُ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ يٰوَيْلَنَا قَدْ كُ ن َّا فىِ غَفْ لَةٍ مِّ ْن
ّ
هَٰذَا بَلْ كُن َّا ظَالِمِينَ ﴾
Hatta idha futihat ya/jooju wama/jooju wahum min kulli hadabin yansiloona;
Waiqtaraba alwaAAdu alhaqqu fa-idha hiya shakhisatun absaru alladheena
kafaroo ya waylana qad kunna fee ghaflatin min hadha bal kunna dhalimeena(Surat
Al Anbiyah 21:96-97)
Tafsir: Hadi watakapofunguliwa Yajuj na Majuj, na kisha watatoka katika kila
sehemu kwa kasi. Na itakaribia Ahadi ya kweli na kisha utayaona Mtizamo wa Macko
ya wasioamini yakiwatoka na kusea: ‘Ole wetu hakika sisi tulikua tumeghafilika juu
ya hili na tumekua miongoni mwa Waliojidhulumu’
Katika kuelezea kwake tukio hilo basi aya zinasema kua hadi watakapofunguliwa Yajuj
na Majuj ‘min kulli hadabin yansiloona’ na neno Hadabin limetokana na neno Hadiba
ambalo hua linamanisha Mtuno, Mvimbo, Muinuko au Kilima.
Na hivyo maneno Min Kulli Hadabin hua yanamaanisha Kutoka katika kila Jamii, na
Sehemu na kutoka katika kila upande wa Dunia, na neno Yansiloona linatokana na neno
Nasala ambalo hua linamaanisha Kizazi, Kuzaliwa, Kutoka kwa wingi na kwa haraka
sana, na hivyo basi aya kua ni zenye kutubainishia kua tukio hili litakua ni la kutisha sana
kwa namna watakavyopotokea viumbe hawa ambao ni Yajuj wa Majuj, kiasi ya kua
itakua hakuna kwa kukimbilia kwa namna watakavyotoka kwa kasi kubwa sana na kwa
wingi sana.
Kwani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliwaambia Masahab zake kwa kusema:
‘Allah Subhanah wa Ta’ala atasema katika siku ya Malipo: ‘Adam’ na Nabii Adam
ataitikia: ‘Naam Ewe Mola wangu, hakika mimi niko chini ya Amri yako’ Hivyo
aitasema: ‘Waleteni watu wa Motoni.’ Nabii Adam atauliza: ‘Ndio wapi hao?’ Allah
Subhanah wa Ta’ala atasema: ‘Katika kila watu 1000 basi wao ni watu 999’ na
baada ya maneno hayo basi utawaona vijana wanakua wazee, waja wazito
wanajifungua, na utawaona watu kua kama wameleewa lakini hawakulewa bali
Adhabu ya Allah ni kali sana.’
Masahaba wakamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kusema: ‘Hivi jee
ni nani miongoni mwetu atakua ni mmoja kati yao kama ikiwa kila katika 1000 basi
999 watachukuliwa?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema:
537
‘Nakubashirieni kua kwa kila mmoja miongoni mwenu basi Yajuj wa Majuj ni
1000’(Sahih Bukhari)
Hivyo hii ni hadith ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam inayotuonesha namna
wingi wake Yajuj wa Majuj kulingana na wingi wake watakavyokua, hivyo bila ya shaka
itakua hamkani kubwa sana, ambapo kwa upande mwengine basi kuna hadithi ya An
Nawwas Ibn Sa’am Radhi Allahu Anhu ambae yeye anatuelezea hali itakavyokua katika
wakati huo kwa kusema kwa kutumia manano yafuatayo:
‘Asubuhi moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimzungumzia Dajjal, na
wakati tulipokua tukizungumzia kuhusiana na uovu na ubaya wake, basi Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kuhusiana na baadhi ya mambo ambayo
yanaonesha kua Kuja kwake itakua ni Mtihani mkubwa sana, Kisa chake kilitujaza
khofu kama kwamba Dajjal alikua amejificha Nyuma ya mashina ya Mitende na
wakati wowote atachomoza. ’
‘Tulipowasili mbele yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika wakati wa
Jioni basi akaona hali yetutuliyokua nayo na akatuuliza: ‘Vipi mbona mko hivyo?’
nasi tukasema: ‘Hakika wewe ulimzungumzia asubuhi, ambapo kuna baadhi ya
mambo uliyasema yalikua hayana athari kubwa katika uhatari wake, na kuna
mambo ambayo uliyasema ambayo yametuonesha sisi kua ni yenye kua katika hali
ya kua ni mtihani mkubwa sana kiasi ya kua tumekua na khofu sana na kufikiria
kua huenda ikawa Dajjal yuko karibu sana yetu yaani kama kwenye mashina ya
Mitende’’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Mtihani sio wa Dajjal tu, bali kuna
na mtihani myengine ambayo mimi nnaikhofia kua itakudhuruni zaidi kama
(Dajjal) akikutokeeni miongoni mwenu basi mimi nitakabaliana nae, na kama
akitokea na wakati mimi nikiwa siko miongoni mwenu basi kila mmoja wenu
atapingana nae kwa kadiri ya Ushujaa wake, na Allah Subhanah wa Ta’ala ni mlinzi
na Muongozaji wa Kila Muislam pale mimi nitakapokua sipo’
‘Nyinyi mtamjua (Dajjal) kutokana na kua ni mwenye kua ni kijana mwenye nywele
ngumu zenye kujipinda na mwenye Jicho moja lililoelekea Juu. Na kama ikibidi
nimfananishe na mtu basi namfananisha na Ab Al Uzza Ibn Qatan (Mmoja kati ya
watu wenye sura mbaya wa Kabila la Banu Khuza katika wakati wa Ujahiliya)’
‘Hivyo kama Muislam miongoni mwenu atakumbana nae basi anatakiwa asome aya
za mwanzoni za Surat Al Kahf dhidi yake. Dajjal atatokea katika maeneo yaliyokua
wazi ya Syria na Iraq na kusababisha tafrani kulia na kushoto: ‘Hivyo enyi waja
wa Allah kueni na msimamo dhidi yake.’
538
An Nawwas Ibn Sa’am Radhi Allahu Anhu anasema : ‘Nasi tukasema: ‘Ya Rasul Allah
hivi jee atatembea na kuyafanya hayo atakayoyafanya kwa siku ngapi Ardhini’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Kwa siku 40, lakini siku moja
itakua ni sawa na Mwaka mmoja na siku ya pili sawa na mwezi mmoja, na siku
zitakazobakia itakua ni sawa na kama siku za kawaida’
An Nawwas Ibn Sa’am Radhi Allahu Anhu anasema : ‘Nasi tukasema: ‘Ya Rasul Allah,
hivyo hii siku moja ambayo itakua ni sawa na mwaka mmoja sisi tutasali sala 5 kwa
ajili ya siku moja tu?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘La bali
mtakua ni wenye kusali kwa kukadiria wakati wa sala tano kwa mwaka huo mmoja’
An Nawwas Ibn Sa’am Radhi Allahu Anhu anasema : ‘Nasi tukasema: ‘Ya Rasul Allah
Jee atakua ni mwenye kutembea Ardhini kwa kasi gani?’ Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akasema: ‘Kwa kasi ya kama Kiwingu kinavyosukumwa na Upepo
na atakutana na watu atakaowaambia wamfuate katika Imani yake potofu, nao
watamuamini na kuitikia wito wake, na kisha atayakusanya Mawingu na itanyesha
Mvua, ataiamrisha Ardhi na itaota majani na watalishia Wanyama juu yake, na
watakaporudi malishoni basi Nundu zao zitakua kubwa zaidi ya hapo kabla na
Maziwa yao yatajaaa na Mapaja yatanona’
‘Na kisha Dajjal atapita kwa watu wengine na kuwaita katika Kufuru yake, lakini
watu hao wataukataa wito wake, na hivyo atavunjika moyo na kuondoka, ambapo
baada ya kuondoka kwake basi Watu hao walioamini watapatwa na Mtihani wa
njaa na hawatokua na kitu. Halafu Dajjal atapita katika sehemu hio iliyo kame na
ataiambia Ardhi hio: ‘Toa nje Hazina zako’ na Ardhi hio itatoa Hazina zake kama
Nyuki wanavyomfuata Malikia wao, na kisha Dajjal atamwita mmoja kati wa watu
ambae ni kijana na kisha atamkata kwa upanga wake katika sehemu mbili na
sehemu mbili hizo zitatengenganishwa na kuwekwa katika masafa ya kama Mtunga
shabaha na Upinde wake na sehemu ya kutungia shabaha, na kisha Dajjal atamwita
Mtu huyo na vipande vyake vitaungana na Mtu huyo atakuja mbele yake huku
akiwa na tabasam na furaha’
Katika kipindi hiki Allah Subhanah wa Ta’ala atamtuma Isa Ibn Maryam, ambae
atang’arisha Mnara mweupe wa Mashariki ya Damascus akiwa amevaa maguo
mawili ya Rangi na mikono yake yote miwili kua ni yenye kukaa juu ya Mbawa za
Malaika wawili, na atakapoinama itakua kama anatiririka maji (kwenye nywele
zake) na atakaponyanyuka itakua matone yake yanang’ara kama Lulu halisi.
Mtu yeyote asieamini Allah akivuta pumzi atakayoitoa basi atakufa katika wakati
huo huo na pumzi zake akitoa zitafikia umbali wa upeo wa macho yake. Na kisha
atamtafuta (Dajjal) hadi atamtokezea kwa mbele yake katika Mlango wa Ludd (Wa
Bayt ul Maqdis) na kumua. Baada ya hapo Isa Ibn Maryam atakuja kwa watu
539
ambao Allah Subhanah wa Ta’ala amewalinda dhidi ya Dajjal. Atawagusa nyuso
zao na kuwabashiria bashirio jema la kua na darja za juu Peponi.
Wakati Isa Ibn Maryam atakapokua katika hali hio Allah Subhanah wa Ta’ala
atamshushia Wahyi na kumwambia: ‘Hakika mimi natuma watu ambao ni
miongoni mwa waja wangu ambao hakuna mikono miwili itakayoweza kupigana
nao, hivyo wakusanye waja wangu katika Mlima Tur’ hivyo Isa Ibn Maryam atatii
amri hio. ‘Na kisha nitawaachia Yajuj wa Majuj na wataporomoka kutoka katika
kila pande, ambapo wimbi lao la kwanza litapita Buhairah Tabariyyah (Bahari ya
Galileo au Tiberias yenye upana wa kilomita 53 na urefu wa kilomita 21 na kina
cha maji wa mita 42), ambapo litakunywa kila kitu ndani yake. Na kundi la pili
litakapopita hapo na kuona kua hakuna kitu litasema: ‘Hakika hapa kulikua kuna
Maji’
Watakapofika kwenye Mlima Khamar katika maeneo ya Bayt ul Maqdis basi Yajuj
wa Majuj watasema: ‘Tumeshaua kila mtu kwenye ardhi hivyo sasa hivi tuwaue
wale waliopo Mbinguni’ na kisha watarusha Mishale yao Mbinguni na Allah
Subhanah wa Ta’ala atairudisha mipinde hio ikiwa na Damu.
Rasul Allah Isa Ibn Maryam na watu wake watajihifadhi kwenye Mlima Tur, na
Waumini wengine watapata hifadhi katika maeneo yao yaliyohifadhika, watakua
na vyakula lakini haitochukua mda vitamalizika na kufikia hali kua kichwa cha
ng’ombe kitakua ni bora kuliko Dinari 100 za Dhahabu. Kisha Rasul Allah Isa Ibn
Maryam na Masahaba zake watamgeukia Allah (Na kumuomba Dua awasitiri
kutokana na Yajuj wa Majuj) na atatuma maradhi ya kuwaambukiza Yajuj wa
Majuj (na hivyo kua ni wenye Kuliwa na funza kwenye Shingo zao) na
wataangamizwa hadi mtu wa mwisho Miongoni mwao.
Rasul Allah Isa Ibn Maryam na Masahaba zake watatoka kwenye Mlia wa Tur na
kushuka chini na kukuta hakuna sehemu ya ardhi isipokua ina Maiti ya Yajuj wa
Majuj na kutakua kuna harufu mbaya sana. Rasul Allah Isa Ibn Maryam na
Masahaba zake watamgeukia Allah Subhanah wa Ta’ala (Kumuomba dua
awaondolee Mtihani wa maiti hizo nae atawajibu) na atawajibu kwa kuwatuma
ndege ambao shingo zao ukubwa wake kama shingo za Ngamia na kuchukua Maiti
hizo na kuzirembea anakotaka Allah Subhanah wa Ta’ala.
Baada ya hapo Allah Subhanah wa Ta’ala atashusha Mvua ambayo hakuna hata
Nyumba ya Udongo wala hema la Bedui, itakayakosa kunyesewa na mvua hio. Na
aradhi itakoshwa na kua Nyeupe kama kioo na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala
ataiambia Ardhi: ‘Otesha Mimea yako na Matunda yako toa wingi wa vilivyomo
katika rehma yako’
540
Na kutakua na baraka sana kiasi ya kua Komamanga moja litatosheleza kua ni
chakula cha watu kadhaa, na gamba lake litatosheleza kua ni paa la kujilinda dhidi
ya Jua na Maziwa yatatosheleza kwa kila mtu kwani Maziwa kutoka kwa Ngombe
mmoja yatatosheleza Kabila zima na maziwa ya Mbuzi mmoja yatatosheleza kwa
Ukoo mzima (Miaka 40 baada ya kipindi cha neema hizi na usalama na Amani basi
ndio wakati wa Kiama utakaribia).
Allah Subhanah wa Ta’ala atatuma Upepo mzuri sana ambao utasababisha
kuifanya miili ya Waumini kua yenye kufa ganzi na kisha kila Roho ya Muumini
itatolewa. Na watabakia wabaya watupu miongoni mwa Ibn Adam, waovu na
wasioamini ambao watafanya mambo ya aibu na yasiyofaa ardhini kama Punda, na
ni dhidi yao ndio Saa ya Kiama itawafikia.(Imam Muslim)
Ama kuhusiana na Yajuj ya Majuj basi Allah Subhanah wa Ta’ala amewaelezea katika
kisa cha Dhul Qarnayn pale aliposema katika Qur’an:
﴿وَيَسْأَلُونَكَ عَن ذِى ٱلْقَرْنَينْ ِ قُلْ سَأَتْلُواْ عَلَيْكُم مِّ نْهُ ذِكْ راً۞إِ َّ مَ ك َّن َّا لَهُ فىِ ٱلأَرْ ضِ
وَآتَيْنَاهُ مِن ِ كُل فَأَتْبَعَ سَبَباً۞حَتى َّ ٰ شَيْءٍ سَبَباً۞ إِذَا بَلَغَ مَغْ ِربَ ٱلش َّمْسِ وَجَدَهَا
تَغْرُبُ فىِ عَينٍْ حمَِئَةٍ وَوَجَدَ عِندَهَا قَوْماً قُلْنَا يٰذَا ٱلْقَرْنَينِْ إِم َّآ أَن تُعَذِّبَ وَإِم َّآ أَن
ت َت َّ خِ ذَفِي هِمْحُْسن اً ۞قَالَ أَم َّا مَن ظَلَمَ فَسَوْفَ نُعَذِّبُهُ ثمُ َّ يُرَد ُّ إِلىَٰ رَبِّهِ فَيُعَذِّبُهُ عَذَاابً
ن ُّكْ راً۞وَأَم َّا مَنْ آمَنَ وَعَمِلَ صَالحِ اً فَلَهُ جَزَآءً ٱلحُْسْنىَٰ وَسَنَقُوُل
لَهُ مِ نْ أَمْ رَِ يُسْ راً۞ثمُ َّ
أَتْبَعَ سَبَباً۞حَتى َّ ٰ إِذَا بَلَغَ مَطْلِعَ ٱلش َّمْسِ وَجَدَهَا تَطْلُعُ عَلَى ٰ قَوْمٍ لم َّْ نجَْعَل له َُّمْ مِّن
دُوَِا سِ ترْ اً۞كَذٰ لِكَ وَقَدْ أَحَطْنَا بمَِا لَدَيْهِ خُبرْ اً ﴾
ّ
Wayas-aloonaka AAan dhee alqarnayni qul saatloo AAalaykum minhu dhikran ;
Inna makkanna lahu fee al-ardhi waataynahu min kulli shay-in sababan;
FaatbaAAa sababan; Hatta idha balagha maghriba alshshamsi wajadaha taghrubu
fee AAaynin hami-atin wawajada AAindaha qawman qulna ya dha alqarnayni
imma an tuAAadhdhiba wa-imma an tattakhidha feehim husnan; Qala amma man
dhalama fasawfa nuAAadhdhibuhu thumma yuraddu ila rabbihi
fayuAAadhdhibuhu AAadhaban nukran; Waamma man amana waAAamila
salihan falahu jazaan alhusna wasanaqoolu lahu min amrina yusran; Thumma
541
atbaAAa sababan; Hatta idha balagha matliAAa alshshamsi wajadaha tatluAAu
AAala qawmin lam najAAal lahum min dooniha sitran; Kadhalika waqad ahatna
bima ladayhi khubran (Surat al-Kahf 18:83-91)
Tafsir: Na wanakuuliza kuhusiana na Dhul Qarnayn waambie: ‘Nitakuambieni kitu
kutokana na ukumbusho juu yake’ Kwa hakika tumemueweka kwenye Ardhi na
tukampa njia (sababu) juu ya kila kitu; Hivyo akafuata Njia; hadi akafikia
(Magharibi) linakotua Jua akalikuta linatua kwenye chemchem ya maji ya tope
nyeusi, na akakutana karibu nayo watu Nasi tukasema: ‘Ewe Dhul Qarnayn Aidha
waadhibu au wafanyie wema’. Hae akasema: ‘Ama yule atakaefanya Dhulma basi
tutamuadhibu yake kisha atarudishwa kwa Mola wake ambae atamuadhibu kwa
adhabu kali zaidi; Na ama yule atakaeamini na Akafanya Amali njema basi atapata
malipo mema, na sisi tutazaungumza nae juua ya jambo letu (la Uongofu) kwa urahisi’
Na kisha akafuata Njia nyengine. Hadi akafikia katika sehemu inayochomoza Jua,
akalikuta linachomoza kwa watu ambao hatukuwajaalia chochote cha kujistiri
kutokana nalo; na kadhalika kwa hakika sisi ni wenye kujua kila kitu kuhusiana nae
(Dhul Qarnayn).
Ambapo amesema Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Dhul
Qarnayn alikua ni Nabii ambae Mshauri wake alikua ni Al Khidr ambae nae alikua
pia ni miongoni mwa Wanajeshi wa Dhul Qarnayn’
Na Imam Al Azraq basi yeye anasema kua: ‘Dhul Qarnayn aliingia katika Uislam
katika kipindi cha Nabii Ibrahim na aliwahi kufanya Tawwaf na Nabii Ibrahim na
Nabii Ismail na Nabii Ibrahim alimuombea Dua na Allah Subhanah wa Ta’ala
aliyasababisha Mawingu kua chini ya amri yake na hivyo alikua akienda nayo
atakako’
Na aliitwa Dhu Qarnayn kwa sababu alikua ni mwenye kutawala Ardhini kwa Karne
Mbili, na kuna wanaosema kua ni kwa sababu alitembelea na kutawala Pande zote mbili
za Dunia kuanzia Mashariki hadi Magharibi.
Ambapo Mujaddid ad Din, Shaykh ul Islami Al Hafidh Imam Shihab Ad Din Ibn Hajjar
Al Asqalani anasema kua Dhul Qarnayn alikua akiitwa Abdulla Ibn Dahhaq Ibn Mad, na
kuna wanaosema kua ni Mussab Ibn Abdulla Ibn Qattan, na kuna wasema kua ni
Mazuban Bin Marzaba na kuna wasemao kua ni Saib Ibn Maraid na pia kuna wasemao
kua ni Harmasa na Hardia.
Allah Subhanah wa Ta’ala anaendelea kutuelezea kuhusiana na Dhul Qarnayn na ukuta
alioujenga kwa ajili ya kuwazuia na kuwadhibiti Yajuj wa Majuj kwa kusema:
542
﴿ثمُ َّ أَتْبَعَ سَ بَباً۞حَتى َّ ٰ إِذَا بَلَغَ بَينَْ الس َّد َّيْنِ وَجَدَ مِن دُوِِمَا قَ وْماً لا َّ يَكَادُونَ
يَفْقَهُونَ قَوْلاً۞قَالُواْ يٰذَا ٱلْقَرْنَينِْ إِن َّ َْجُوجَ وَمَأْجُوجَ مُفْسِ دُونَ فىِ ٱلأَرْضِ فَهَ ْل
نجَْعَلُ لَكَ خَرْجاً عَلَى ٰ أَن تجَْعَلَ بَيْنَنَا وَبَيْنَهُمْ سَدّاً۞قَالَ مَا مَ َّكنىِّ
فِيهِ رَبىِّ خَيٌْر
فَأَعِينُونىِ بِقُو َّةٍ أَجْعَلْ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُمْ رَدْماً۞آتُونىِ زُبَرَ ٱلحَْ ِديدِ حَتى َّ ٰ إِذَا سَاوَىٰ بَينَْ
ٱلص َّدَفَينِْ قَالَ ٱنفُخُواْ حَتى َّ ٰ إِذَا جَعَلَهُ َراً قَالَ آتُونيِ ۤ أُفْرِغْ عَلَيْهِ قِطْراً۞فَمَا ٱسْطَاعُو ۤ اْ
أَن يَظْهَرُوهُ وَمَا ٱسْتَطَاعُواْ لَهُ نَقْباً۞قَالَ هَٰذَا رَحمَْةٌ مِّن ر َّبىِّ فَإِذَا جَآءَ َوعْدُ رَبىِّ
جَعَلَهُ دَك َّآءَ وَكَانَ وَعْدُ رَبىِّ حَقّاً۞وَتَرَكْنَا بَعْضَهُمْ يَوْمَئِذٍ يمَُوجُ ِفى
بَعْضٍ وَنُفِخَ ِفى
ٱلص ُّورِ فَجَمَعْنَاهُ مْ جمَْعاً ﴾
Thumma atbaAAa sababan; Hatta idha balagha bayna alssaddayni wajada min
doonihima qawman la yakadoona yafqahoona qawlan; Qaloo ya dha alqarnayni
inna ya/jooja wama/jooja mufsidoona fee al-ardhi fahal najAAalu laka kharjan
AAala an tajAAala baynana wabaynahum saddan; Qala ma makkannee feehi
rabbee khayrun faaAAeenoonee biquwwatin ajAAal baynakum wabaynahum
radman; Atoonee zubara alhadeedi hatta idha sawa bayna alsadafayni qala
onfukhoo hatta idha jaAAalahu naran qala atoonee ofrigh AAalayhi qitran; Fama
istaAAoo an yadhharoohu wama istataAAoo lahu naqban; Qala hadha rahmatun
min rabbee fa-idha jaa waAAdu rabbee jaAAalahu dakkaa wakana waAAdu
rabbee haqqan; Watarakna baAAdahum yawma-idhin yamooju fee baAAdin
wanufikha fee alssoori fajamaAAnahum jamAAan (Surah al-Kahf 18:92-99)
Tafsir: Na kisha akafuata njia hadi akafika baina ya Milima miwili na akakuta kabla
yao(Milima hio)Kaumu ya watu ambao hawafaham Kauli, na wakasema: ‘Ewe Dhul
Qarnayn! Hakika Yajun na Majuj wanafanya ufisadi kwenye Ardhi, hivyo jee tukupe
ujira ili utujengee Ukuta baina yetu na baina yao?’; Akasema (Dhul Qarnayn):
‘Alichoniwekea (katika kunipa Mali, Mamlaka na Uwezo wa kinguvu) Mola wangu ni
bora; Hivyo nisaidieni uwezo wa wasaidizi, nami nijataalia baina yenu na baina yao
Kizuizi; Nipeni Vipande vya Vyuma’ na kisha alipoujaza Uwazi baina ya Kingo za
Milima miwili akasema: ‘Pulizeni’ hadi akaifanya ikawa (nyekundu) kama Moto kisha
akasema: ‘Nileteeni Shaba iliyoyeyuka kuimiminia juu yake’ hivyo Yajuj na Majuj
wakawa hawana uwezo wa kuivunja au kuitoboa; Duhl Qarnayn akasema: ‘Hii ni
543
Rehma kutoka kwa Mola wangu, Lakini itakapowadi Ahadi ya Mola wangu, basi
atauangusha chini, na ahadi ya Mola wangu ni ya kweli’ katika siku hio
(watakapotoka nje Yajuj wa Majuj), basi tutawaachia kuvamia kama mawimbi moja
baada ya jengine, na kisha Baragumu litapulizwa na tutawakusanya wote kwa pamoja.
Ambapo amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kwa hakika Yajuj wa
Majuj wanachimba kwenye Ukuta kila siku, hadi plae wanapoona kua Mwangaza
wa Jua unapita baina yake, na kisha Kiongozi wao hua ni mwenye kusema:
‘Twendeni zetuni, mtakuja kesho kumalizia’ na wakifika katika siku ya pili yake
basi huukuta Ukuta huo kua uko imara kuliko jana yake, hadi pale itakapofikia
ahadi ya Allah atakapotaka kuwaachia wawavamie Ibn Adam, basi kiongozi wao
atasema: ‘Twendeni zetuni, In-Shaa Allah mtakuja kesho kumalizia’ na hivyo
wakifika kesho yake wataukuta ukuta uko katika hali kama walivyouacha hapo
jana yake, na watachimba na kutoka ndani yake na kuwavamia Ibn Adam.
Watakunywa Maji yote watakayokutana nayo, na Ibn Adam watakimbilia kwenye
ngome zao, na Yajuj wa Majuj watarusha Mipinde yao Juu angani na itakaporudi
itarudi huku ikiwa ina wekundu kama wa Damu nao watasema: ‘Tumewashinda
watu wa Ardhini na wa Mbinguni pia’ kisha hapo Allah atatuma Mafunza kwenye
shingo zao ambao wataua wote.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Wallahi naapa kwa yule ambae
Roho ya Muhammad iko mikononi mwake, kua Viumbe hai wa Ardhini (wadudu
na wanyama wa ardhini) watanenepa kutokana na kula nyama na kunywa damu
zao’(Musnad Imam Ahmad)
Ambapo anasema Shaykh ul Akbar Imam Ibn Arabi kuhusiana na maneno ya Hadith hii
kua: ‘Hadithi hii ina Miujiza mitatu kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala ambayo
ni:
1-Allah Subhanah wa Ta’ala hakuwajaalia Yajuj wa Majuj uwezo wa kujua katika
ufahamu wao kua ni wenye kua na uwezo wa kuchimba kwenye ukuta huo kwa
masaa 24 bila ya kusita usiku na mchana, kwani kama wangejaaliwa hivyo basi basi
isingewachukua mda mrefu kutokana na nguvu na wingi wao kuumaliza Ukuta
huo.
2-Akili zao na Ufahamu wao umeghafilishwa na kutokua na haja ya kuuparamia
juu Ukuta huo, kwa kutumia vifaa na zana mbali mbali. Ingawa kulingana na
mtizamo wa Wahb Ibn Munabih ni kua watu hawa wanalima kwenye ardhi yao na
hivyo kumaanisha kua wanazo zana tofauti. Hivyo pia kama hawakughafilishwa
basi ingekua ni rahisi sana kwao wao kukusanya zana zao na kutafuta njia ya
namna ya kuuparamia ukuta huo na kutoka ndani yake.
544
3-Allah Subhanah wa Ta’ala hakuwajaaliwa kua ni wenye kujua kua wenye
kutakiwa kusema In-shaa Allah, kwani kauli hii itawajia katika ufahamu wao pale
utakapofika wakati walioandikiwa kua waseme hivyo kwa ajili ya kutimiza jambo
linalotakiwa kutokea.
Kwani amesema Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
﴿ وَعْدَ ٱهلل َِّ لاَ يخُْلِفُ ٱهلل َُّ وَعْدَهُ وَلَٰكِن َّ أَكْثَرَ ٱلن َّاسِ لاَ يَعْلَمُونَ ﴾
WaAAda Allahi la yukhlifu Allahu waAAdahu walakinna akthara alnnasi la
yaAAlamoona (Surat Rum 30:6)
Tafsir: Hio ni Ahadi ya Allah, na havunji Allah Ahadi yake lakini wengi Miongoni
mwa watu si wenye Kujua.
KAULI ZA ISA IBN MARYAM A’LAYHI SALATU WA WASALAM KATIKA AL
RISALAT AL QUDSIYYAH.
Mujaddid ud Din Hujjat ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii alipokua akiishi katika msikiti wa Bayt ul
Maqdis katika Bab al Dhahab katika kipindi ambacho kilikua ni cha kutafuta ukaribu
zaid na Mola wake Allah Subhanah wa Taála basi alifanikiwa kuzipata na kuziandika
hadith za Nabii Isa Ibn Maryam A’layhi Salaam, katika kitabu chake kiitwacho Al Risalat
Al Qudsiyyah, miongoni mwa Hadith hizo ni pamoja na:
Allah Subhanah wa Taála alimwambia Isa Ibn Maryam: ‘Ya Isa Ibn Maryam baada
yako mimi nitatuma Ummah ambao hautokua na Huruma wala I’lm. Hivyo kuna
mambo watakayoyapenda na yatakapowafika basi watanitukuza na kunishukuru,
na kuna mambo watakayoyachukia na yatakapowafika, basi watakua na subra na
watanitegemea zaid mimi.’
Nabii Isa Ibn Maryam akauliza: ‘Itakuaje hali yao kua hivyo wakati watakua hawana
huruma wala I’lm?’
Allah Subhanah wa Taála akasema: ‘Hakika mimi nitawapa sehemu ya Huruma
zangu na Sehemu ya I’lm yangu.’
545
Allah Subhanah wa Taála akamwambia Nabii Isa Ibn Maryam: ‘Ya Isa Ibn Maryam!
Jiusie juu ya Hikma zangu, na ukinufaika nazo basi, basi wausie watu juu yangu na
vyenginevyo, basi jihadhari nami.
Allah Subhanah wa Taála alimshusia Nabii Isa Ibn Maryam katika maandiko asilia ya
Biblia kwa kumwambia kua: ‘Waambie Bani Israil kua, Mja yeyote yule atakaefunga
kwa ajili yangu basi nitamlipa mja huyo kwa kuufanya mwili wake uwe imara na
Akhera kumpa malipo bora zaidi’
Allah Subhanah wa Taála alimwambia Isa Ibn Maryam katika Biblia asilia kua: ‘Ya Bani
Adam nimekuumbeni na kukuleeni kimaisha nyinyi, lakini bado hua mnamuabudu
mwengine zaidi yangu, Enyi Waja wangu mimi nnakukaribisheni karibu lakini
nyinyi mnanikimbia. Mimi nna kukumbukeni lakini nyinyi mnanisahau, Hivi jee
Ya Ibn Adam mnarudi na kulala popote mnapotaka nyinyi?’
Allah Subhanah wa Taála alimwambia Isa Ibn Maryam katika Bibilia asilia kua: ‘Kila
mnavyokua na kupungua ufahamu wenu, basi mtalipwa na kuhesabiwa kila kitu
chenu.’
Imeandikwa katika Biblia asilia kua: ‘Usitafute I’lm ya kile usichokijua hadi pale
utakapokua ni mwenye kutekeleza kile unachokijua’
“Isa Ibn Maryam A’layhi Salaam aliwafufua kutokana na uwezo wa Allah Subhanah
wa Taála watu wanne ambao ni Al Adhir (Lazarus) ambae alikua ni Rafiki yake,
Mtoto wa kiume wa Mtu Mzima sana fulani, mtoto wa kike wa Mzee aitwae Al Ashir
na Sham ambae ni mtoto wa Nabii Nuh Alayhi Salaam.
Ama kuhusiana na Al Adhir basi alikua ni mwenye kufariki kwa muda mfupi kabla
ya Nabii Isa kumuomba Allah Subhanah wa Taála amfufue, na alipofufuliwa aliishi
akaoa na kupata watoto.
Ama kuhusiana na mtoto wa Mtu Mzima Mzee, basi Nabii Isa alikua akipita na
akamuona mtoto huyo akiwa ametiwa ndani ya Jeneza, Hivyo Isa Ibn Mayam
akamuomba Allah Subhanah wa Taála, amfufue na mtoto huyo wa kiume
alipofufuliwa basi akavaa nguo zake na kulibeba Jeneza lake na kurudi kwa watu
wake.
Ama kuhusiana na Bint wa Al Ashir, basi ulipita usiku mmoja tu tangu kufariki
kwake, hivyo Isa Ibn Maryam akamuomba Allah Subhanah wa Taála amfufue
ambapo alimfufua na akaolewa na kupata watoto.
546
Watu wa Bani Israil walioshuhudia Miujiza hii basi walimhoji Isa Ibn Maryam kwa
kumuambia kua : ‘Unawafufua waliokufa karibuni, hivyo inawezekana ikawa hawa
uliowafufua walikua hawajafa bali walikua ni wenye kuzimia tu, subiri tukuoneshe
kaburi la Sam mtoto wa Nuh utufufuie’
Isa Ibn Maryam akawaambia Bani Israil: ‘Nionesheni Kaburi lake’
Hapo watu wa Bani Israil wakamchukua hadi katika Kaburi la Sam Ibn Nuh. Isa Ibn
Maryam akaomba Dua na Allah Subhanah wa Taála akamfufua Sam Ibn Nuh huku
nywele zake zikiwa zimejaa mvi, hivyo Isa Ibn Maryam akamuuliza: ‘Imekuaje hadi
nywele zako zikawa ni zenye kujaa mvi, kwani katika kipindi chako ulichoishi
nywele za watu zilikua hazioti mvi?’
Sam Ibn Nuh akasema: ‘Ýa Ruhi Allah! Wakati uliponiita, nilisikisa sauti iliyokua
ikiniamrisha mimi kujibu ninayoulizwa na Ruh Allah na hivyo nikadhani kua Siku
ya Kiama imewasili, hivyo nikafufuka na nywele zenye mvi kutokana na khofu
niliyokua nayo’
Isa Ibn Maryam akamuuliza tena Sam Ibn Nuh: ‘Hebu niambie kuhusiana na maumivu
ya kutoka kwa Roho!’
Sam Ibn Nuh akajibu kwa kusema: ‘Ya Ruhi Allah! Kwa hakika uchungu wake bado
haujaondoka katika Roho yangu.’
Tafakkar! Kwani katika kipindi hicho alikua tayari ameshakaa kaburini kwa muda wa
miaka 4000. Kisha Sam Ibn Nuh akawageukia Bani Israil na kuwaambia: ‘Muaminini
kwani huyu ni kweli Mtume wa Allah’ lakini hata hivyo, baadhi wakamkubali Isa Ibn
Maryam na baadhi wakamkanusha na kusema kua huo ni uchawi.
Maryam bint Imran, alimchukua Isa Ibn Maryam akiwa mtoto na kumpelekea kwa wenye
ujuzi wa kazi za kutia na kutoa rangi nguo ili ajifunze kutoka kwao kazi hio. Baada ya
muda mwalimu wa Nabii Isa alifikwa na dharura na hivyo ikambidi asafiri lakini kabla
ya kusafiri, akamwambia Isa Ibn Maryam: ‘Mimi inanibidi nisafiri, na nina nguo
nyingi ambazo inabidi zitiwe rangi, hivyo itabidi unsaidie kuzutia rangi’.
Hivyo Nabii Isa Ibn Maryam akachemsha maji na kuzichanganya rangi zote pamoja na
kuzimimina ndani ya tangi na kuzichanganya nguo zote zilizokusudiwa kutiwa rangi
katika tangi moja na kusema: ‘Bismi Allahi Rahmani Rahim pakika Rangi’. Mara
mwalimu wake akaingia na kumkuta tayari ameshazichanganya nguo zote katika tangi
moja, wakati nguo inayotakiwa kua na rangi tofauti huingizwa katika tangi tofauti.
547
Hivyo baada ya kuona hali hio basi mwalimu huyo akasema: ‘Umeshaniharibia’. Lakini
hapo hapo Isa ibn Maryam akazitoa nguo hizo kutoka katika tangi hilo na kutoa kila nguo
ikiwa na rangi yake, kulingana na namna ilivyokususidwa, iliokusudiwa iwe kijani ikawa
kijani, nyekundu ikawa nyekundu na kadhalika. Hivyo Mwalimu wake huyo akashangaa
sana na akajua kua jambo hilo kamwe haliwezekani isipokua kutokana na uwezo wa
Allah Subhanah wa Ta’ala hivyo nae akawa ni miongoni mwa wenye kumuamini Isa Ibn
Maryam.
Siku moja Iblis alimfuata Nabii Isa kisirisiri kisha akasema: ‘La ilaha illa Allah’, ambapo
Nabii Isa Ibn Maryam akasema: ‘Ama kwa hakika hii ni kauli sahih lakini mimi
sitoitamka kwa ajili ya kukufuata wewe’
Alisema Isa Ibn Maryam: ‘Tuba (Bonde la Peponi) ni kwa ajili ya kila yule ambae
anajidhibiti kutokana na matamanio ya kidunia juu ya ahadi ambayo bado
haijatimia’ na akasema tena kua; ‘Tuba ni wa ajili wale wenye macho ambayo
hayalali na hayana nia ya kufanya dhambi na pale yanapoamka hua hayakusudii
kufanya dhambi’
Alisema Isa Ibn Maryam: ‘Enyi Wanafunzi wangu, yawekeni na njaa matumbo yenu
ili mmpate kumuona Mola wenu’
Alisema Isa Ibn Maryam: ‘Enyi Wanafunzi wangu, yawekeni matupu matumbo yenu
na miili yenu isipokua sehemu za siri zenu ili nyoyo zenu zimuone Mola wenu’
Maana ya kauli hii ni kua Ibn Adam tunatakiwa tufunge na kutosheka na mavazi
tuliyokua nayo bila ya kupenda fakhari ya kubadilisha kila mitindo ya mavazi inayoingia.
Isa Ibn Maryam alikaa kwa siku 40 huku akiwa anazungumza na Mola wake tu bila ya
kula kitu chochote, kisha likamjia wazo la mkate hapo akasita kuzungumza na Mola wake
na mkate ukatokea mbele yake. Isa Ibn Maryam akaanza kulia kutokana na kupoteza
utamu wa mazungumzo yake na Mola wake. Mara akaona kivuli cha mtu mzee kutoka
juu yake.
Isa Ibn Maryam akasema: ‘Allah akubariki ewe Walii wa Allah, Niombee kwa Allah
kwa ajili yangu kwani nilikua katika hali ya hiyo lakini mkate ukanijia katika
mawazo yangu na hali hio ikatoweka’. Yule Mzee akaomba dua kwa Allah Subhanah
wa Ta’ala akasema: ‘Ya Allah! Kama unajua kua mkate uliwahi kuingia katika
mawazo yangu tangu mimi kukujua wewe, basi usinisamehe. Kwa hakika mimi
nilikua nikila kile ambacho hukipata bila ya kukifikiria wala kukiwazia’
548
Isa Ibn Maryam alionya kwa kusema: ‘Tahadhari na kuangalia watu wa jinsia
nyengine kwani ni mbegu inayotosha kupandikiza matamanio ndani ya moyo, na
hutosheleza kua ni mtihani juu yako’
Isa Ibn Maryam aliulizwa: ‘Tuusie kuhusiana na jambo ambalo litatuingiza Peponi
kutokana na kulitekeleza kwake.’ Isa Ibn Maryam akajibu: ‘Kukaa kimya’, yule
alieuliza akasema: ‘Ama hio itakua haiwezekani’ Isa Ibn Maryam akajibu: ‘Basi
msizungumze chochote isipokua lililo Jema’
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Mambo manne hayawezi kufikiwa bila ya uchovu, ambayo
ni mwanzo wa Ibada, Unyenyekevu, Kunyamaza kimya, Dhikr Allah kwa wingi
zaidi na kwa uchache’.
Isa Ibn Maryam hakua na mnyama wa kupanda wala nyumba ya kujihifadhia. Hakua ni
mwenye kuhifadhi kwa ajili ya kesho na popote pale unapomfikia usiku basi hulala hapo
hapo.
Isa Ibn Maryam alikaa na kujipumzisha chini ya kivuli cha ukuta fulani. Mwenye ukuta
akamwambia aondoke chini ya ukuta wake huo. Isa Ibn Maryam akanyanyuka na kisha
akamgeukia yule mwenye ukuta na kusema: ‘Sio wewe unaeniondoa, kwenye kivuli
hiki bali ni yule asiependa mimi nifurahie kivuli hiki ndio anaeniachia niondoke’
Alisema Isa Ibn Maryam: ‘Enyi Bani Israil, kunyweni maji safi, kuleni Mbaazi, na
Mkate wa Shayiri, lakini jihadharini juu ya Mikate ya Ngano kwa sababu kamwe
hamtoweza kurudisha shukrani zake kwa aliekupeni’
Akasema tena Isa Ibn Maryam: ‘Waangalie ndege, hawapandi Miti wala hawavuni
lakini wanahifadhi kwa sababu Allah Subhanah wa Taála anampatia riziki yake
kila siku, na ukisema kua sisi Ibn Adam tuna matumbo makubwa ukilinganisha na
Ndege, basi waangalie Ngómbe na utaona namna Allah Subhanah wa Taála
anavyomjaalia rizki yake.’
Katika safari zake Isa Ibn Maryam alipishana na watu watatu, ambao walikua
wamekonda hadi rangi yao imebadilika, hivyo akawasimamisha na kuwauliza: ‘Jee ni
kitu gani kilichokufanyeni muwe hivi.’
Wale watu wakajibu: ‘Khofu ya Jahannam’, hivyo Isa Ibn Maryam akasema: ‘Allah
Subhanah wa Taála amejithibtishia kuziondoa khofu zenu’. Kisha akaendelea na
safari yake, na njiani akakutana na watu watatu wengine ambao wamekonda zaidi ya
wale wa kwanza, akasimamisha na kuwauliza pia: ‘Jee ni kitu gani kilichokufanyeni
muwe hivi?’.
549
Ambapo wale watu wakajibu: ‘Matamanio ya kupata Pepo’. Hapo Isa Ibn Maryam
akasema: ‘Allah Subhanah wa Taála amejithibitishia kuwa atakupeni kile
mnachokitamani’. kisha akaendelea na safari yake na kukutana na watu watatu wengine
ambao wamekonda zaidi ya wale aliowapita, lakini nyuso zao zilikua ni zenye kungára
sana, hivyo akawasimamisha na kuwauliza pia: ‘Jee ni kitu gani kilichokufanyeni
muwe hivi?’. Wale watu wakasema: ‘Sisi tunampenda Allah Subhanah wa Taála’.
Hapo Isa Ibn Maryam akasema: ‘Nyinyi ni miongoni mwa waliokaribu nae.’
Isa Ibn Maryam aliamuona mtu ambae ni kipofu, bubu na amepooza nusu mwili katika
pande zote, na mwili wake umeshaanza kuoza kwa ukoma, lakini hata hivyo huyo mtu
anasema: ‘Alhamd lillah! Namshukuru Allah kwa kile ambacho ameniepusha mimi
na mitihani aliyowapa viumbe wake wengine’, Isa Ibn Maryam akamuuliza yule
mgonjwa: ‘Jee ni mitihani gani uliyoepushwa.’ Yule mzee akajibu: ‘Ya Ruhi Allah!
Allah amenijaalia mimi I’lm ya kumjua yeye ndani ya moyo wangu, hivyo niko
katika hali nzuri kuliko waliyokua nayo wengine’, hapo Isa Ibn Maryam akasema:
‘Uko Sahih, nipe mkono wako’, yule mtu akampa mkono wake Isa Ibn Maryam na pale
pale yakaonekana mabadiliko katika mwili wa yule mtu kwani alipona na kua na sura
nzuri kabisa na akawa ni Mwanafunzi wake.
Isa Ibn Maryam aliwauliza Wanafunzi wake: ‘Jee miti hua inaota wapi?’ Wanafunzi
wakajibu: ‘Ardhini’ hivyo Isa Ibn Maryam akasema: ‘Naam, hivyo kwa hakika Hikma
haiwezi kukua isipokua kwenye Moyo kama ilivyo Ardhi na miti’
Bani Israil walimuuliza Isa Ibn Maryam: ‘Ya Ruhi Allah, jee yupo mtu kama wewe leo
hii Duniani?’ Isa Ibn Maryam akajibu: ‘Naam, kwani yeyote yule anaefanya dhikr
Allah huku akiwa n mwenye kukaa kimya, na mtizamo wake ukawa ni wenye
Tafakkur, basi hua ni sawa nami’
Wakati kifo kilipokua kinatajwa mbele ya Isa Ibn Maryam, basi muonekano wake
hubadilika, hivyo aliwaambia Wanafunzi wake: ‘Enyi Wanafunzi wangu! Ombeni dua
kwa Allah ili airahisishe adhabu ya kifo juu yangu, kwa sababu mimi naogopa kifo
kiasi ya kua khofu yangu inataka kuniingiza kwenye kifo chenyewe’
Katika kutembea kwake Isa Ibn Maryam alilikuta fuvu la kichwa na taratibu akalisogeza
pembeni kwa mguu wake na kisha akasema: ‘Sema kutokana idhini ya Allah’, ambapo
fuvu hilo likasema: ‘Ya Ruhi Allah, ama mimi nilikua ni Mfalme wa jamii ya watu
fulani na katika wakati fulani, na wakati nikiwa katika Mamlaka ya Ufalme wangu
huku nikiwa na kofia ya Ufalme wangu na kuzungukwa na walinzi, askari na
wafanyakazi wangu, Ghafla Malaika wa Mauti akatokea juu ya kiti cha ufalme
wangu, na hapo kila kitu katika viungo vyangu vikaanza kupoteza uezo wake, na
550
Roho yangu ikanitoka na kufuatana na Malaika wa Mauti, kiasi ya kua nilitamani
kua watu wote hao walionizunguka wakati wote huo wangeondoka na kuniacha
mimi peke yangu.’
Alihoji Isa Ibn Maryam: ‘Jee ni Miili mingapi mizima, yenye nyuso za kupendeza na
ndimi zenye ufasaha wa lugha ya kuvutia zitakua ni zenye kupiga makelele baina
ya matabaka tofauti ya Moto?’
Aliulizwa Isa Ibn Maryam: ‘Ya Isa Ibn Maryam! Hebu tuelezee juu ya kile ambacho
sisi tukikifanya kitatupelekea kuingia Peponi’. Hivyo Isa Ibn Maryam akajibu: ‘Uzuie
Ulimi wako kwa kutozungumza kabisa’ watu wakasema: ‘Jambo hilo
halitowezekana’ Isa Ibn Maryam akasema: ‘Basi msizungumze isipokua juu ya lile
liliokua jema’
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Kufanya Ibada kumegawika sehemu kumi, ambapo
sehemu tisa hua ni kukaa kimya na sehemu moja iliyobakia hua ni kukaa mbali na
watu.’
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Yeyote yule asemae uongo kila wakati, basi utatoweka
uzuri wa haiba yake. Na Yeyote yule anaemwambia mtu kile anachopenda kusikia
yule anaezungumza nae, basi itavunjika heshima yake. Yeyote yule anaefikiria sana
basi basi mwili wake utadhoofika. Na Yeyote yule asiekua na tabia njema basi hua
ni mwenye kujiadhibu Nafsi yake mwenyewe.’
Siku moja Isa Ibn Maryam alipishana na Nguruwe njiani na kumwambia Nguruwe huyo:
‘Pita kwa Amani’. Watu wakamuuliza Isa Ibn Maryam: ‘Ya Ruhi Allah! Unasema nae
hivyo Nguruwe?’. Isa Ibn Maryam akasema: ‘Nnachukia kuuzoesha Ulimi wangu
kusema maneno yasiyofaa’
Isa Ibn Maryam alikua akitembea na Wanafunzi wake, njiani wakakutana na mzoga wa
mbwa. Wanafunzi wake wakasema: ‘Hakuna harufu mbaya kama ya Mbwa’. Isa Ibn
Maryam akasema: ‘Hakuna Weupe mzuri kama wa Meno yake’.
Isa Ibn Maryam pamoja na Wanafunzi wake walikutana na Wayahudi na kuanza
kuwausia lakini Wayahudi hao wakamtukana Isa Ibn Maryam, lakini hata hivyo Isa Ibn
Maryam akawajibu Wayahudi hao kwa kauli nzuri. Wanafunzi wake wakamuuliza:
‘Inakuwaje watu hawa wamekutukana na kisha wewe unawajibu kwa kauli nzuri
nzuri?’ Isa Ibn Maryam akasema ‘Kila mtu hutumia kile alichokua nacho’
Akasema Isa Ibn Maryam: ‘Enyi Ibn Adam msiyachukulie Maisha kua ni Mola wenu,
kisha nayo yakakuchukulieni kua ni Waja wake. Hifadhini mali zenu na yule ambae
551
hatozipoteza, kwa sababu yule anaeandamana na mali katika maisha haya hua ni
mwenye kuogopa kutoweka kwa mali hio, wakati yule ambae mwenye
kuiandamanisha na Allah mali yake hua ni si mwenye kuogopa kitu chochote juu
ya mali hio’
Isa Ibn Maryam alisema kuwaambia Wanafunzi wake: ‘Enye Wanafunzi wangu,
hakika mimi nimeigeuza Dunia hii juu chini, hivyo msiipambe juu yangu, kwa
sababu uovu wa Dunia hii ni kua Allah anadhulumiwa ndani yake kwa kutotiiwa
amri zake, na uovu huo ni mkubwa kiasi ya kua Akhera haitoweza kupatikana
isipokua kwa kuachana na Dunia, hivyo ivukeni tu Dunia na msiishi juu yake.
Fahamuni kua mzizi wa kila Dhambi hutokana na kuipenda Dunia. Matamanio ya
saa moja tu humrithisha mtu urefu uliojaa huzuni’
Isa Ibn Maryam akasema kuwausia Wanafunzi wake: ‘Hakika mimi nimeuangusha
ulimwengu huu na kuukalia juu ya mgongo wake, hivyo nanyi msiwaruhusu
Wafalme na Wanawake kukushindanisheni juu yake, ama kuhusiana na Wafalme
basi msishindane nao katika Dunia hii kwa sababu hawatokukaribieni pale
mtakapowaacha wao na Dunia yao, ama kuhusiana na Wanawake, *Jizuieni nao
kwa kufunga na kusali.’
*Kujizuia na Wanawake kuliko kusudiwa hapa, hakumaanishi kua Watu wasioe bali
kunamaanisha kua Watu wasipende Wanawake wasiokua halali yao kwa kuzini.
Miongoni mwa wasia wa Isa Ibn Maryam ni pale aliposema: ‘Maisha yanadai na
yanadaiwa. Hivyo yeyote yule atakaeyadai maisha ya Akhera basi Akhera humdai
hadi imalizike riski yake, na yeyote yule anaeyadai maisha ya Dunia basi Akhera
humdai hadi mwisho wake kitakapomjia kifo na kumkamata shingo yake.’
‘Kamwe haiwezekani katika moyo wa Muumin kua na mapenzi ya Maisha ya Dunia
pamoja na Maisha ya Akhera, kama vile ambavyo isivyowezekana kwa Maji na
Moto kuchanganywa katika Jagi moja’
Isa Ibn Maryam Aliulizwa ‘Kwa nini hutaki kua na nyumba itakayokutosheleza?’,
ambapo nae akajibu ‘Kutoweka kwa waliotangulia kabla yetu kunatosheleza’’
Katika safari za Isa ibn Maryam basi siku moja ilitokea na mvua kubwa sana, radi na
upepo mkali, hivyo akaamua kujificha mvua hiyo katika moja kati ya bustani ya karibu,
lakini akaona kua kuna mwanamke nae amejificha katika bustani hivyo akaamua
kutojificha, akatoka na kukimbilia mbele zaidi ambapo aliona kuna pango kubwa sana
akaingia ndani ya pango hilo, na ghafla akakutana na Simba, hivyo taratibu akamkaribia
na kuanza kumpapasa ili kumtuliza Simba huyo huku akisema: ‘Ya Allah! Kwa hakika
552
wewe umekijaalia kila kitu kua na sehemu yake ya utulivu lakini hukuniwekea
mimi sehemu hio.’
Allah Subhanah wa Taála akasema kumwambia Isa Ibn Maryam: ‘Sehemu yako ya
Utulivu ni kati kati ya rehma zangu. Nnaapa kua Katika Sku ya Malipo nitakujaalia
kuoa Hawra (Wake wa Peponi) 100 ambao nimewaumba kwa mikono yangu, na
utashehereka katika harusi hio kwa miaka 4000 ambapo siku moja katika miaka
hio hua ni sawa na uhai mzima wa mtu, na nitaamrisha kutolewe wito
utakaotangazia kua: Jee Wako wapi wale ambao walikua hawana kitu katika
maisha yao? Njooni katika sherehe ya Harusi ya Isa Ibn Maryam ambae nae aliishi
bila ya kua na kitu katika uhai wake’
Amesema Isa Ibn Maryam kua: ‘Waylun! (Ole wao) wale wanaoendekeza Dunia! Jee
hawaoni kua mtu anakufa kisha anawacha kila kitu kilichomo ndani yake? Jee
hawaoni kua Duania inawakimbia lakini nao wanaiamini? Wanaiamini Dunia huku
nayo inawavunja Moyo?.
Na Waylun! kwa wale wenye kujidanganya Nafsi zao, Inakuaje kua wanakifuata
kile wanachokichukia na kukikimbia kile wanachokipenda? Na kinawakimbilia kile
walichokwisha ahidiwa?
Waylun! Kwa wale ambao mawazo yao ni juu ya Dunia hii tu! Na amali zao ni za
Dhambi tu! Kwani Kesho watakua maarufu kutokana na Dhambi zao!’
Siku moja Isa Ibn Maryam na Wanafunzi wake walipita katika kijiji kimoja na kukuta
watu wakiwa wamekufa katika hali na sehemu mbai mbali za kijiji hicho, hivyo Isa Ibn
Maryam akawaambia Wanafunzi wake: ‘Ama kwa hakika watu hawa wamefariki
kutokana na Adhabu ya Allah Subhanah wa Ta’ala juu yao, kwa sababu kama
wangekua wamekufa kwa sababu nyengine yeyote ile basi wangekua wamezikwa!’.
Wanafunzi wa Isa Ibn Maryam wakamwambia Isa Ibn Maryam: ‘Ya Ruhi Allah! Kama
ni hivyo basi sisi tungependa kusikia habari zao.’ Hapo Isa Ibn Maryam akamuuomba
Allah Subhanah wa Taála awajaalie waujue ukweli juu ya habari ya watu hao, ambapo
akashushiwa Wahyi na kuambiwa kua inabidi arudi katika sehemu hiyo katika wakati wa
usiku ambapo ataweza kuwauliza juu ya habari yao na watu hao watamjibu masuali yake
juu yao, wakati wa Usiku ulipowadia Isa Ibn Maryam akapanda katika sehemu ambayo
iliyo juu kidogo na kuanza kunadia katika maeneo hayo wa kusema:
‘Enyi Wakazi wa Kijiji hiki.’ Mmoja kati ya Watu walifariki katika kijiji hicho akajibu:
‘Naam Ya Ruhi Allah! Tuko chini yako kusikiliza amri yako!’
553
Isa Ibn Maryam akamwambia mtu huyo: ‘Hebu tuambieni yaliyo kusibuni hadi
mkawa katika hali hii’
Yule Mtu akasema: ‘Hakika sisi hua tuko kwenye mapumziko katika wakati wa
usiku na hua tuko katika adhabu katika wakati wa mchana’.
Isa Ibn Mayam akauliza: ‘Jee ilikuaje hadi ikawa mko hivyo?’
Yule mtu akajibu: ‘Kwa sababu sisi tulikua tuiipenda sana Dunia na hivyo kua ni
wenye kumuasi Mola wetu kwa kuwatii wasiokua waadilifu miongoni mwetu.’
Isa Ibn Maryam akauliza: ‘Jee ni kwa kiasi gani mlikua mkiipenda Dunia?’
Yule mtu akajibu: ‘Kama vile ambavyo Mama ampendavyo mtoto wake, kwani hua
pale mama anapomkaribia mtoto wake basi mtoto humfurahia mama yake, na
mama anapokaa mbali na mtoto wake basi mtoto humlilia mama yake na huingiwa
na huzuni kwa kua mbali na mama yake’.
Hapo Isa Ibn Maryam akauliza tena: ‘Mbona ni wewe peke yako tu ndie unaejibu
masuali yangu? Jee ni kwa nini wenzako hawajibu masuali yangu?’
Yule mtu akajibu: ‘Kwa sababu wanavijinga vya mtoto ndani ya midomo yao
ambavyo vimezuiwa na mikono imara ya Malaika wa Motoni!’
Isa In Maryam akauliza: ‘Sasa imekuaje kua wewe ukawa ni mwenye kuweza
kunijibu?’
Yule mtu akajibu : ‘Ama mimi nilikua ni miongoni mwa watu hawa lakini kamwe
sikuwa ni mmoja kati ya watu hawa, na hivyo adhabu ilipokuja ilinikumba na mimi
pia, hivyo mimi nnaning’inizwa kwenye ukingo wa Jahannam, na sijui kama
nitatumbukizwa ndani yake ama nitaokolewa dhidi yake’
Hapo Isa Ibn Maryam akawaambia Wanafunzi wake: ‘Kula mkate uliotokana na
shayiri iliyosagwa na chumvi na kuvaa ngozi na kulala kwenye uchafu ni bora na
salama zaidi kwa Ulimwengu huu na Ulimwengu wa Akhera’
Isa Ibn Maryam aliambiwa: ‘Tufundishe Ilm ambayo itatupelekea sisi kupendwa na
Allah Subhanah wa Taála’ ambapo nae akajibu: ‘Uchukieni Ulimwengu huu na hapo
ndipo Allah Subahanh wa Taála akatapokupendeni’ Isa in Maryam akaendelea kwa
kusema: ‘Enyi mnaoupenda Ulimwengu huu kwa ajili ya kufanya mema, basi
554
fahamuni kua kuachana nao na kuondoka ndani yake hua ni bora zaidi na ndio kua
na Taqwa zaidi’
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Enyi Wanafunzi wangu! Kuweni ni wenye kuridhika
kidogo Duniani, kwa kupata usalama wa Dini, kama vile ambavyo Wanaoipenda
Dunia wanavyokua wametosheka na udogo wa Dini na Usalam wao Duniani’
Isa Ibn Maryam Alisema : ‘Mimi Mkate wangu ni Njaa, Kauli yangu ni Khofu, Nguo
zangu ni Sufi, Sala zangu katika kipindi cha Baridi ni Alfajiri, Taa yangu ni Mwezi,
Chakula changu na Matunda yangu ni kila kitu kinachozalishwa na Ardhi,
Nnautumia Usiku wangu nikiwa sina kitu na Nnauamkia Usiku huo katika asubUhi
yake nikiwa Sina Kitu. Na Hakuna mtu alie Tajiri juu ya Ardhi kama mie ’
Nabii Isa Ibn Maryam alikua ni mwenye kuuona Ulimwengu katika hali ya uhalisia wake
ambao ni wa hali ya mwanamke Ajuza asiekua na meno lakini aliejaa mapambo ya
Wanja, Podari na Rangi za Mdomo tele. Hivyo aliuuliza Ulimwengu huo kwa kusema:
‘Jee tayari Umesholewa Mara ngapi?’ Ulimwengu ukamjibu: ‘Ama Siwezi
kuzihesabu mara nilizoolewa’. Isa Ibn Maryam akauliza: ‘Jee waliooana nawe wote
wamefariki au Wamekutaliki’. Ulimwengu ukajibu: ‘La Ni mimi ndie ambae
nimewateketeza kwa kuwaua wote’ Hapo Isa Ibn Maryam Akasema: ‘Adhabu ipo
kwa wale utakao oana nao, inakuaje kua wao hawajifunzi kutokana na yaliyowafika
waliotangulia? Inakuaje unawaangzamia mmoja baada ya mwengine lakini nao
hawana habari hio na kamwe hawakuchoki?’
Nabii Isa Ibn Maryam alisema: ‘Wa Allahi ukweli nakuambieni kua: Mgonjwa hua
ni mwenye kukiangalia chakula na hua hahisi ladha yake kulingana na maumivu
aliyokua nayo, na hali hii pia ndio waliyokuaa nayo wanaoiendekeza Dunia, kwani
hua hawaihisi ladha ya kufanya Ibada na hawauoni utamu wake kutokana na kile
anachokitafuta Duniani. Wallahi ukweli nakuambieni mnyama wa kipando
anapokua hajapandiwa na wala hajafundishwa kupandiwa basi hubadilika na kua
mgumu kudhibitika pale anapotaka kupandiwa, na hivyo hivyo ndivyo ulivyo Moyo
unapokua haujazoeshwa kukumbuka juu ya kifo na kufanya Ibada basi nao pia
hugeuka na kua mgumu kupita kiasi. Wallahi ukweli nakuambieni kua kama ikiwa
mtungi wa maji haujatoboka basi hua tayari kua ni sehemu ya kuhifadhia asali,
Nyoyo pia ziko hivyo hivyo, kama ikiwa hazijatobolewa na matamanio na ubahili
haujauchafua Moyo na anasa haijautia ugumu moyo huo, basi bila ya shaka Moyo
huo utakua ni Mtungi uliojaa Hikma na Busara ’,
Isa Ibn Maryam Alisema: ‘Mfano wa yeyote yule anaeiendekeza Dunia hua ni sawa
na mtu mwenye kunywa maji ya bahari. Kwani kila anavyozidi kula basi ndivyo
anavojzididhishia kiua yake hadi kufikia kifo chake’
555
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Katika Mali kuna maradhi matatu: Mtu kuipata kutoka
katika vyanzo visivyo halali. Na ikiwa kaipata kutoka katika vyanzo vya halali basi
ataitumia katika njia zisizo za halali.’ Wanafunzi wake wakamuuliza, ‘Vipi kama
akiwa atazitumia katika njia za halali?’ Isa Ibn Maryam akasema: ‘Basi
zitamshughulisha kiasi ya kua atamsahahu Mola wake.’
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Wanazuoni waovu hua ni sawa na Jabali ambalo
limeanguka kutoka juu hadi kwenye mlango wa pango lenye kutoa maji, na hivyo
kuyaziba maji hayo huku likiwa haliyatumii maji hayo wala haliyaachii maji hayo
kutiririka kwa ajili ya manufaa ya vitu vyengine’
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Mfano wa mtu anaetafuta Ilm kisha akawa si mwenye
kuifanyia kazi kwa vitendo hua ni sawa na mwanamke anaefanya zinaa kisiri siri
na kisha akawa na uja uzito. Na tumbo lake linapojitokeza na kua kubwa huanza
kuadhirika na kuona haya kutokana na ujauzito huo, hali hii ndio watakayokua
nayo watu wasioifanyia kazi Ilm yao, kwani Allah Subhanah wa Taalah
atawaadhirisha katika siku ya Malipo mbele ya watu wote.’
Isa Ibn Maryam alikutana na mtu mmoja aliejitambulisha kwake na Isa Ibn Maryam
akamuuliza: ‘Jee wewe unajishughulisha na nini?’ Yule mtu akajibu: ‘Mimi hua
nnajishughulisha na kufanya Ibada tu!’ Isa Ibn Maryam akamuuliza tena mtu huyo:
‘Jee ni nani anaekuhudumia katika kukutafutia mahitaji yako?’ yule mtu akajbu:
‘Nnahudumiwa na ndugu yangu’ Isa Ibn Maryam akamwambia mtu huyo: ‘Ama kwa
Hakika ndugu yako ni mwenye kufanya Ibada bora zaidi kuliko wewe.’
Allah Subhanah wa Ta’ala alimwambia Isa Ibn Maryam: ‘Kama ukiniabudu mimi kwa
Ibada zote za viumbe wa Ardhini na Mbinguni na ikawa hakuna mapenzi kwa ajili
ya jina la Allah na chuki kwa ajili ya jina la Allah basi Ibada yako hio
haitokunufaisha na kitu chochote.'
Isa Ibn Maryam aliwaambia Wanafunzi wake: ‘Tafuteni mapenzi ya Allah Subhanah
wa Taála kwa kuwachukia wafanyao maovu, ukaribu na Allah kwa kukaa mbali
nao, na tafuteni ridhaa ya Allah katika yale wayachukiayo wao.’ Wanafunzi
wakauliza: ‘Ya Ruhi Allah! Jee tukae na nani?’ Isa Ibn Maryam akajibu: ‘Kaeni na
wale ambao mtakapokaa nao watakukumbusheni juu ya Allah, na kukuzidishieni
mema yenu kutokana na kauli zao. Na wale ambao mambo yao yatakufanyeni
muipendelee Akhera yenu.’
Alisema Nabii Isa kuwaambia Wanafunzi wake kua: ‘Kaeni na njaa, na Kiu na Msivae
Nguo nzuri na Jichosheni ili Nyoyo zenu zipate kumjua Allah.’
556
KAULI ZA NABII MUHAMMAD SALALLAHU ALYHI WA SALAM
KUHUSIANA NA NABII ISA ALAYHI SALAM.
Amesema Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kua: ‘Mtume wa kwanza ni
Adam na wa mwisho ni Muhammad. Mtume wa mwanzo wa Bani Israil ni Musa na
wa mwisho ni Isa Ibn Maryam. Na Mtume wa mwanzo kuandika kwa kutumia
Kalamu ni Idrisa’
‘Yahya Ibn Zakariyyah alimwambia Isa Ibn Maryam: ‘Wewe ni Ruhi Allah na
kauli yake (Kun) na wewe ni bora kuliko mimi’ Isa Ibn Maryam akasema: ‘Wewe ni
bora kuliko mie kwani Allah Subhanah wa Taála amekujaalia wewe Usalama lakini
mimi amenisalimia kwa usalama.’
‘Ndugu zangu, Mitume waliotangulia, idadi yao ni 8000. Kisha akafuatia Isa Ibn
Maryam na kisha nikafuatia miebaada yake.’
‘M-bora miongoni mwa Ibn Adam ni Nuh, Ibrahim, Musa, Isa na Muhammad. Na
Muhammad ni m-bora wao zaidi.’
‘Iblis humgusa kila Ibn Adam anaezaliwa na mama yake isipokua Maryam bint
Imran na mtoto wake ambae ni Isa Ibn Maryam.’
Isa Ibn Maryam alimuona mtu anaiba kitu, hivyo akamuuliza mtu huyo: ‘Umeiba nini?’
Yule mtu akajibu ‘La! Wa Allahi la ilaha illa huwa!’ yaani La Sijaiba! Naapa kwa
yule ambae hakuna Mungu isipokua yeye’. Hivyo Isa Ibn Maryam akasema: ‘Naam,
namuamini Allah na siamini macho yangu.’
Kauli hii inaashiria namna Isa Ibn Maryam alivyokua akithamini kiapo kupitia kwa yule
ambae hakuna anaestahiki kuabudiwa kwa haki isipokua yeye, kiasi ya kua alikua yuko
tayari kutoyaamini macho yake, kuliko kutoamini kiapo cha mtu alieapa kwa ajili ya
Allah Subhanah wa Ta’ala.
‘Adam yuko katika Mbingu ya Kwanza, na vitendo vya kizazi chake vinawekwa
wazi mbele yake, na Yusuf yuko katika Mbingu ya Pili, na watoto wawili wa dada
wawili, Yahya na Isa wapo katika Mbingu ya Tatu, Idris yupo katika Mbingu ya
Nne. Harun yupo katika Mbingu ya Tano, Musa yupo katika Mbingu ya Sita na
Ibrahim yupo katika Mbingu ya Saba.’
557
KAULI ZA ALLAH SUBHANAH WA TAALA JUU YA NABII ISA IBN
MARYAM.
Amesema Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kua: ‘Allah Subahanah wa
Taála amesema: Ya Isa Ibn Maryam! Mimi ndie Mola wako na ndie Mola wa
Mababu zako waliotangulia, Jina Langu ni Ahad na ndie Ahad wa Pekee. Mimi ndie
pekee ninaeumba kila kitu na kila kitu kinatokana nami na hivyo kila kitu kitarejea
kwangu.
Ya Isa Ibn Maryam! Wewe ndie uliechaguliwa nami kutokana na amri yangu, na
umeumba kutokana na udongo umbo la ndege kutokana na idhini yangu, na
umekhuisha waliokufa kutokana na kauli yangu, hivyo kua ni mwenye kunihitaji
mimi na mwenye kua na khofu nami, kwani hakuna atakae kuokoa dhidi yangu
isipokua mimi.
Ya Isa Ibn Maryam! Nimekuchagua wewe kutokana na yule ambae ni Mwingi wa
Ukarimu na mwingi wa Rehma, nimeamua kukupa urafiki wangu kwa kukutumia
wewe furaha hivyo umebarikiwa wakati ulipokua mdogo na hadi utakapokua
mkubwa na popote pale utakapokuwepo. Mimi nnashuhudia kua wewe ni Mja
wangu na ni mtoto wa Mja wangu wa Kike. Hivyo niingize katika hali ya kua na
khofu nami katika nafsi yako, na uniweke katika ufahamu wako kwa kunikumbuka
mimi kwa ajili ya siku ya Malipo na nikaribie kwa kufanya Amali za ziada, na
nitegemee mimi kwani nitakutosheleza, na usimtegemee yeyote mwengine kwani
kufanya hivyo kutanifanya mimi nisikusaidie.
Ya Isa Ibn Maryam! Dumisha Dhikr kwa ulimi wako na uruhusu ukarimu wangu
uutawale Moyo wako.
Ya Isa Ibn Maryam amka kutoka katika nyakati za usahaulivu na kusanya kwa ajili
yangu mie ambae ndie pekee mwenye Hikma.
Ya Isa Ibn Maryam! Kua mwenye kuabudu kwa kunihitaji mimi na uue moyo wako
kutokana na khofu yake juu yangu.
Ya Isa Ibn Maryam! Ukhuishe Usiku kwa ajili ya kutafuta ridhaa yangu na kua na
kiu katika wakati wa mchana kwa ajili ya siku ya mahitaji yako mbele yangu.
558
MAELEZO YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA
SALAM KUTOKA KATIKA YALE WALIORITHI MAYAHUDI NA
WAKRISTO.
‘Muhammad Rasul Allah, Ni Mja wangu niliemchagua, hatokua tu si mpole wala
mpigaji kelele Masokoni. Hatoondoa Ovu kwa kutumia njia ya Uovu, bali atakua
ni mwenye kusamehe na kutotilia maanani maovu aliyofanyiwa. Atazaliwa katika
mji wa Makkah na atahamia katika mji wa Taba, na Utawala wake utakua katika
Ardhi ya Syria, yeye na kila atakaekua pamoja nae atakua ni mwenye kuvaa
mkanda kiunoni mwake, atahubiri Quran na Hadith na atatia udhu mikononi
mwake na miguuni mwake. ’
Amesema Isa Ibn Maryam: ‘Mliambiwa hapo kabla kua miaka kwa miaka, pua kwa
pua, nami nakuambieni msipingane na uovu kwa uovu. Lakini yeyote yule atakae
kupiga kibao shavu la kulia basi mpe na shavu la kushoto, na atakae kuchukulia
shati lako basi mpe na suruali yako, na yule atakae kutumia wewe kwa ajili ya
kutembea nae kwa maili moja basi tembea nae kwa maili mbili’
Kulikua na mtu ambae alikua ni mporaji aliekua akiwapora watu njiani kwa miaka 40,
hivyo wakati Isa Ibbn Maryam alipopishana na mtu huyu basi huyu mtu akasema
kuiambia nafsi yake: ‘Huyu ni Nabii wa Allah Subhanah wa Taála akiwa ni mwenye
kupita na MWanafunzi wake hivyo nami nitajiunga nao ili niwe mtu wa tatu
miongoni mwao’ Hivyo akajiunga nao kwa unyenyekevu huku akijaribu kua karibu na
yule mWanafunzi huku akiiambia nafsi yake: ‘Mtu kama mie sistahiki kutembea
pamoja na Mcha Mungu huyu’.
Yule MWanafunzi wa Nabii Isa Ibn Maryam nae akajiuliza katika Nafsi yake: ‘Ah kwa
nini mtu huyu anatembea karibu yangu kiasi hiki’ hivyo akaongeza mwendo kihatua
hadi akamfikia Nabii Isa na akawa ni mwenye kutembea pamoja nae ubavuni mguu kwa
mguu huku yule mwizi akiwa yuko nyuma yao. Hivyo Allah Subhanah wa Taála
akayaonesha haya yanayotokea kwa Nabii Isa Ibn Maryam kwa kumwambia kua tangu
walipoanza kutembea na yule mporaji basi Allah Subhanah wa Taála amemfutia dhambi
zake yule mporaji na pia amemfutia thawabu zake yule mWanafunzi wa Nabii Isa Ibn
Maryam. Hivyo Nabii Isa Ibn Maryam akawataarifu kilichotokea na hapo yule mporaji
akawa ni mWanafunzi wa Nabii isa Ibn Maryam.
559
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Enyi Wanafunzi! Wakati nyinyi hua ni wenye kukhofia
Dhambi basi sisi Mitume hua ni wenye kuikhofia Kufr’
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Enyi Wanafunzi wangu! Muogopeni Mola wenu, na
ipendeni Pepo na kuweni warithi wa ustahmilivu wakati wa Mitihani. Kila mtu
anatakiwa ajitenge na Dunia hii. Wa Allahi! Kula Majani na kulala kwenye uchafu
pamoja na mbwa hua si chochote katika kuitafuta Pepo’
Isa ibn Maryam alipokua akitembea njiani alimkuta mtu ambae alikua amelala huku
akiwa amejifunika guo lake na hivyo akaamua kumuamsha na kumwambia: ‘Ewe
ulielala! Amka na umkumbuke Mola wako Allah Subhanah wa Taála’, Ambapo yule
mtu alielala akasema: ‘Unataka nini kutoka kwangu wakati mimi nimeachana na
Ulimwengu na wamiliki wake?’ Hapo Isa Ibn Maryam akasema: ‘’Kama ni hivyo basi
endelea kulala ewe kipenzi changu’
Isa Ibn Maryam alisema: ‘Kwa Hakika mimi naupenda Umasikni na nnachukia
anasa’. Na ukweli ni kua Isa Ibn Maryam alikua akipenda kuitwa kwa jina la: ‘Ewe
Mtiifu na Mnyenyekevu’
Isa ibn Maryam alisema: ‘Kamwe msiangalie utajiri wa watu wa Duniani kwani
mng’aro wa utajiri wao utachukua mwangaza wa Imani yenu’
Aliambiwa Nabii Isa Ibn Maryam na Wanafunzi wake: ‘Ya Rasul Allah, ingekua vizuri
kama ungetuamrisha sisi kujenga Nyumba ya Kumuabudia Allah’, Isa Ibn Maryam
akajibu: ‘Nendeni kajengeni Nyumba hio kwenye maji Baharini’. Wanafunzi
wakauliza: ‘Jee Tutajengaje Nyumba katika sehemu iliyojaa maji?’ Isa Ibn Maryam
akajibu: ‘Na Jee itasimamishwa vipi Ibada katika sehemu iliyojaa mapenzi ya
Dunia?’
Katika kutekeleza moja kati ya maamrisho ya Allah Subhanah wa Taála kama
ilivyoelezewa katika Qurán pale iliposema:
﴿قَدْ خَلَتْ مِنْ قَبْلِكُمْ سُنَنٌ فَسِ يرُواْ فىِ ٱلأَرْضِ فَٱنْظُرُواْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ
ٱلْمُكَذِّبِينَ ﴾
Qad khalat min qablikum sunanun faseeroo fee al-Ardhi faondhuroo kayfa kana
AAaqibatu almukadhdhibeena (Al Imran 3:137)
560
Tafsir: Kwa hakika yamewafika mengi waliokuja kabla yenu (Walioamini na
Wasioamini), hivyo tembeeni katika Ardhi ili mpate kuona ni upi ulikua mwisho wa
wale waliokadhibisha.
Basi njiani Isa Ibn Maryam akakutana fuvu la kichwa la mtu aliekufa kwa mda mrefu,
hivyo akaingiwa na hamu ya kujua kilichomfika mwenye fuvu hilo, na kumuomba Allah
Subhanah wa Taála amfufue mwenye fuvu hilo ili azungumze nalo, ambapo Allah
Subhanah wa Taála akaliruhusu fuvu hilo na kuanza kusema:
"Ana Balwan Bin Hafs, Malikul Yaman. 'Ishtu alfa sanatin, waruziqtu alfa waladin,
waftadodtu alfa bikrin, wa fatahtu alfa madeenah. Famakaana kullu dhaalika illa
kanaaim. Faman sami'a qissotiy, fayaghtarra biddunya".
"Mimi ni Balwan Ibn Hafs aliekua Mfalme wa Yemen, Nimeishi miaka 1000,
niliruzukiwa watoto 1000 na niliwatoa bikra bikira 1000 na niliifungua Miji 1000,
na kisha hayakua haya yaliyonitokea ila ni kama ndoto. Hivyo yeyote yule
atakaekisikia kisa changu basi kamwe asihadaike na mapambo ya Dunia ".
Amesema Allah Subhanah wa Ta’ala katika Qur’an kua:
﴿وَإِذْ قَالَ عِيسَى ٱبْنُ مَرْيمََ يٰبَنىِ إِسْرَائِيلَ إِنىّ ِ رَسُولُ ٱهلل َِّ إِلَيْكُم م ُّصَدِّقاً لِّ مَا بَينَْ
يَدَى َّ مِنَ ٱلت َّوْرَاةِ وَمُبَشِّ راً بِرَسُولٍ َْتِى مِن بَعْدِى ٱسمُْهُ أَحمَْدُ فَلَم َّا جَاءَهُم
بِٱلْبَيِّنَاتِ قَالُواْ هَٰذَا سِ حْرٌ م ُّبِينٌ ﴾
Wa-idh qala AAeesa ibnu maryama ya banee isra-eela innee rasoolu Allahi ilaykum
musaddiqan lima bayna yadayya mina alttawrati wamubashshiran birasoolin
ya/tee min baAAdee ismuhu ahmadu falamma jaahum bialbayyinati qaloo hadha
sihrun mubeenun(Surat As Saffat 61:6)
Tafsir: Na alisema Isa Ibn Maryam: ‘Enyi watu wa Bani Israil, hakika mimi ni Rasul
Allah niliyeshushiwa juu yenu kuthibitisha kabla yangu Tawrat na kukubashirieni juu
ya Mtume ambae atakuja baada yangu jina lake Ahmad ambae atapokuja na
Ubainisho basi watasema: ‘Huu ni Uchawi uliowazi’’
Ambapo bashirio hili la Isa Ibn Maryam kua atakuja Mtume baada yake aitwae Ahmad
lilikuja kudhihirika miaka 1400 baada ya kufariki kwake Isa Ibn Maryam katika ardhi ya
Bara Arabu iliyokua ikijulikana kama Bakka au Makkah.
561
SURA YA TATU
الإمام الأنبياء والمرسلين
محمد صلى االله عليه وسلم
562
IMAM AL ANBIYAI WAL ALMURSALINA MUHAMMAD SALALLAHU
A’LAYHI WA SALAM
Miaka 2000 Kabla ya kuzaliwa Nabii Isa Ibn Maryam basi Nabii Ibrahim Alayhi Salam
aliuombea Mji wa Makkah ambao ndio uliokua ni Mji anaoishi Mke wake Hajar na Mtoto
wao ambae ni Nabii Ismail Alayhi Salam basi Nabii Ibrahim A’layhi Salaam aliomba
kuwaombea watu wa familia yake hio kwa kusema:
﴿رَب َّنَا وَٱبْعَثْ فِيهِمْ رَسُولاً مِّنْهُمْ يَتْلُواْ عَلَيْهِمْ آَتِكَ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلْكِتَابَ وَٱلحِْكْمَةَ
وَيُزَكِّيهِمْ إِن َّكَ أَنتَ ٱلعَزِيزُ ٱلحَكِيمُ ﴾
Rabbana waibAAath feehim rasoolan minhum yatloo AAalayhim ayatika
wayuAAallimuhumu alkitaba waalhikmata wayuzakkeehim innaka anta
alAAazeezu alhakeemu. (Surat Al Baqara 2:129)
Tafsir: Ya Rabb! Watumie miongoni mwao Mtume, Mtume ambae atakaewasomea aya
zako na kuwaamrishia yaliyomo ndani ya kitabu (Qur’an) na Al-Hikmah (Kilichojaa
Hikma na I’lm ya Sharia’h za kiislam n.k), na uwatukuze. Kwa hakika wewe ni
muweza kila kitu na ni mwingi wa Busara.
Ambapo kwa hakika Allah Subhanahu wa Ta’ala alimkubalia dua hizo na kizazi chake
kikawa kinaongezeka na kukua kidogo kidogo, hatua kwa hatua, watu kutoka miji mbali
mbali wakaanza kusikia kuhusiana na mji huo na nyumba hiyo na wakawa wanakuja
kuutembelea na kufanya Ibada katika mji huo na kizazi cha Nabii Ibrahim A’layhi Salaam
na Nabii Ismai’l A’layhi Salaam, kikaendelea kua ndicho kinachoshika funguo za
nyumba ya Al Ka’abah na wasimamizi wa nyumba hiyo, na kuendeleza usimamizi huo
kizazi baada ya kizazi hadi kufikia kwa muanzilishi wa kabila la Quraysh, na ndani ya
kabila hilo pia, na baada ya mda mrefu kupita Allah Subhanahu wa Ta’ala akaijibu dua
ya Nabii Ibrahim A’layhi Salaam, iliyotajwa katika aya 129 ya Surat Al Baqara kwa
kumtoa katika miongoni mwa kizazi hicho mbora wa viumbe vyote, ambae si mwengine
bali ni Nabii na ni Mtume wa Mwisho ulimwenguni, Habib Allah Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam.
563
ASILI YA UARABU NA YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU
A’LAYHI WA SALAM.
Vitabu vya historia vinasema kua asili ya Waarabu imetokana na miongoni mwa makundi
aina tatu ya watu:-
1. Al Arab ul Baidah ( البائد (العرب Waarabu waliopotea: Hawa ni wale watu waliokua
miongoni mwa kizazi kilichotoweka cha watu wa ‘Ad, Thamûd, Tasam, Jadis na
Imlaq ambao walikua wakiishi katika maeneo ya Al Ahqaf yaliyopo baina ya
Hadramawt na Oman ambao Mtume wao alikua ni Nabii Hud A’layhi Salaam.
2. Al Arab ul Ariba العاربة) (العرب Waarabu wenye Uarabu asilia: Hawa ni wale watu
waliokua ni miongoni mwa kizazi kilichotokana na Nabii Hud A’layhi Salaam
kupitia kwa Ya‘rub Ibn Yashjub Ibn Qahtan Ibn Hud ambao walikua wakijulikana
pia kama Waarabu wa Yarub wa Qahtan ambapo pia walikua wakitawala katika
maeneo ya Yemen.
3. Al Arab al Mustariba المستعربة) (العرب Waarabu waliopewa Uarabu kwa
kuchanganya vizazi: Hawa ni wale watu waliotokana na kizazi cha Nabii Ibrahim
A’layhi Salaam kupitia kwa Nabii Ismai’l A’layhi Salaam ambae alimuoa Sayyida
Bint Mudad ambae ni mtoto wa Mudad Ibn Amr aliekua kiongozi wa ukoo wa Banu
Jurhum wenye asili ya Al Arab ul Ariba na hivyo kizazi cha mchanganyiko baina ya
Nabii Ismai’l Ibn Ibrahim A’layhi Salaam na Sayyida Bint Mudad ndio ukawa ni
kizazi kinachojulikana kama Al Arab al Mustariba ambao pia hujulikana kama
Waarabu wa Adnan. Waarabu hawa wa Adnan ndio chanzo cha asili ya Ukoo wa
Quraysh.
ة
Kizazi hiki cha watoto wa Nabii Ismai’l A’layhi Salaam ambacho ndio asili halisi ya Al
Arab al Mustariba kilikua na watoto kumi na mbili ambao ni Qidar, Fidmah, Bana,
Buth, ‘Awil, Taqis, Masma’, Taima, Jasham, Haidir, Duma, Yatur, na Massa. Ambapo
kizazi cha Taima baadae kilihamia katika maeneo ya Madinah al Munawwara na kizazi
cha Massa kilihamia katika maeneo ya Yemen.
Watu wa kizazi cha Qidar ambacho kilitokana na mtoto wa kwanza wa Nabii Ismai’l
A’layhi Salaam kilikua ni chenye nguvu na uwezo na umuhimu mkubwa sana, kiasi ya
kua wametajwa pia katika vitabu vya Taurat, maandiko ya watu wa Ashur (Assyrian)
ambao ni wenye asili ya Babylon (Iraq kuelekea juu Uturuki), kimetajwa pia katika
historia za Wagiriki, Warumi na Wamisri kua ni watu wenye kukaa katika maeneo ya
Hijaz (Maeneo ya Uarabuni hususan maeneo ya nchi ya Saudi Arabia).
564
Kizazi hiki cha Qidar ndicho kilichotoa ukoo wa Quraysh ambao uliokua ni ukoo
mkubwa katika Mji Mtakatifu wa Makkah, na pia ulikua ni ukoo ambao ulikua ukitawala
mji huo kwani ndio uliokua ukisimamia na kushika ufunguo wa Al Kaabah, ingawa asili
ya ukoo huo ilikua inatokana na kizazi cha Nabii Ibrahim A’layhi Salaam kupitia kwa
Nabii Ismai’l A’layhi Salaam kupitia kwa Haidir na kupita vizazi na vizazi, lakini asili
ya kuanza kutumika kwa jina la jina la Quraysh ilianzia kwa Fihr Ibn Malik ambae pia
alikua akijulikana kwa jina la Quraysh ambalo ni neno la kiarabu lenye maana nyingi, na
miongoni mwao ikiwemo ‘Mwenye kutafuta na kukusanya’ na pia ‘Samaki mkubwa
wa baharini aina ya Papa’.
Fihr Ibn Malik aliitwa Quraysh kwa sababu yeye alikua ni mtu tajiri ambae aliekusanya
mali nyingi sana, ambazo hata hivyo alikua akizitumia kwa ajili ya kuwatafuta masikini
wa karibu wa eneo lake na kisha kuwasaidia katika kutimiza mahitaji ya maisha yao.
Ukoo wa Quraysh ulikua unafuata dini ya Uislam iliyoachwa na Nabii Ibrahim A’layhi
Salaam na Nabii Ismai’l A’layhi Salam, kizazi hadi pale Iblis laA’anatu Allahi Alayhi
alipofanikiwa kumpotosha Amr Ibn Luay ambae alikua ndie kiongozi wa mji huo katika
wakati huo, Amr Ibn Luay akateleza na kutoka katika njia ya maisha iliyoanzishwa na
Nabii Ibrahim A’layhi Salam.
Kwani kwa mara ya kwanza alifunga safari na kuelekea Sham kibiashara na alipofika
huko akawakuta watu wanaabudu masanamu, alivutiwa sana na jambo hilo kiasi ya kua
aliamua kununua masanamu na kurudi nayo katika mji wa Makkah na kuyaweka ndani
ya Al Kaabah na kisha kuwaamrisha watu wayatukuze na kuyaheshimu masanam hayo.
Miongoni mwa masanamu hayo lilikuwemo kubwa lao lilokuwa likiitwa Hubal, na
wengine wakiwa na majina ya Lata, Uzza, Manah, Wadd, Sawa, Yaghut, Nasr, Isaf, Naila
n.k.
Katika kipindi hiki mji wa Makkah ulikua hauna mfumo maalum wa uongozi uliokua
ukisimamia umoja na maslahi ya jamii ya watu wanaoishi maeneo hayo na vile vile
maslahi ya wageni wanaotembelea maeneo hayo kwa ajili ya biashara na pia kwa ajili ya
hija, ambayo ilikua si ya asili kama ilivyokua katika nyakati za mwanzoni, kwani hija hii
ilikua ni hija ambayo kila mtu alikua akienda kuhiji aidha na sanamu lake ama kwa ajili
ya sanamu lake maalum analoliamini kua linaweza kumtekelezea shida zake. Katika
kipindi hiki kila kitu kilikua kinaendeshwa kiukoo, kwa kila ukoo kujitegemea katika kila
kitu kwa ajili ya maslahi ya ukoo huo.
Hata hivyo baada kufikia wakati wa uongozi wa Qusay mambo yalianza kubadilika,
kwani yeye alijaaliwa akili na mbinu nzuri za uongozi. Hivyo alitumia akili yake na
kuanzisha mfumo wa uongozi ambao ulijenga umoja wa watu wa mji huo na hivyo
kuanza kuwanufaisha watu hao wa Makkah na vile vile kuwanufaisha wageni wanaoingia
na kutoka katika mji huo. Miongoni mwa yale aliyofanya ambayo bado yanaendelea
kufanyika hadi hii leo ni pamoja na:-
565
Kuunda baraza ambalo lilikua na kamati ya viongozi waliokua wakisimamia
makubaliano ya pamoja kiujumla. Aliunda Sharia’h ambayo ilikua ikitumiwa na kamati
hiyo katika mambo yao ya kiutawala, na akajenga nyumba pembeni ya Al Kaabah,
iliyokuaa ikitwa Daar un Nadwa ambayo ilikua ni nyumba ya baraza hilo kwa ajili ya
kukutana na kuzungumzia matatizo na kutatua mambo mbali mbali yanayowahusu watu
wa mji huo.
Aliunda mfumo wa kuwalipisha kodi wageni wanaoenda kwa ajili ya biashara na kwa
ajili ya kuhiji katika mji huo ili kuwanufaisha watu wa Makkah, na vile vile kuwanufaisha
watu wanaoenda kuhiji kwa kuwapatia huduma za chakula, maji na makazi.
Baada ya hapo Qusay akachukua na kuyasimamia majukumu yote yanayohusiana na:
1. Hijaba – Kuhifadhi funguo za Al Kaabah.
2. Nadwa – Kiongozi wa Daar un Nadwa (Baraza la mji Makkah).
3. Rifada – Kushughulikia chakula cha watu wanaohiji.
4. Saqaya – Kusimamia maji kwa ajili ya watu wanaohiji.
5. Liwa – Kuchagua kiongozi wa kuongoza vita.
6. Qiyada – Kiongozi wa Jeshi la Makkah.
Qusay alipofariki aliwacha watoto wawili ambao walikua ni Abd Darr na Abd Manaaf,
hivyo uongozi wa mji huo ulirithiwa na mtoto wake mkubwa aliekua akiitwa Abd Darr,
lakini kutokana na kua hakua na uwezo wala sifa nzuri zinazohitajika katika kutekeleza
majukumu hayo ya uongozi, akaamua kumuachia majukumu yake hayo ndugu yake
aliekua maarufu kama Abd Manaf lakini jina lake halisi lilikua ni Mughira, ambae alikua
ni mwenye sifa na uwezo wa majukumu hayo na hivyo aliendelea kuongoza hadi pale
alipofariki Abd Darr.
Baada ya Abd Darr kufariki, viongozi wa mji wa Makkah wakakutana na kukukubaliana
kua majukumu ya uongozi ya Abd Manaf, yagaiwe nusu ayabebe mtoto mkubwa wa Abd
Darr aliekua akiitwa Abd Shams na nusu yaliyobakia aendelee kuyatekeleza Abd Manaf.
Hivyo Abd Manaf akawa na majukumu ya kuwashughulikia watu wanaokuja kuhiji na
vile vile abakie kua kiongozi wa Jeshi la watu wa mji wa Makkah. Abd Shams yeye
(ambae alikua ni mtoto wa Abd Darr) akapewa jukumu la kusimamia Al Kaabah na
kiongozi wa wakati wa vita, na vile vile wote wawili kwa pamoja wakawa ni viongozi
wa baraza na kamati ya mji wa Makkah.
Baada ya Abd Manaf kufariki, majukumu yake yote yakahamia kwa mtoto wake wa
mwisho aliekua akiitwa Amr au maarufu alijulikana kama ‘Hashim’ yaani ‘Mkataji wa
Mikate’. Amr alikua na sifa za uwezo wa kuongoza tofauti na watoto wake wengine
kwani Hashim alikua ni kopi asilia ya Qusay (aliekua babu yake). Hili linaonekana wazi
pale ilipotokea katika wakati wa uongozi wake mji wa Makkah ulikumbwa na ukame
mkubwa sana, na hivyo Amr alitumia mali yake ili kununua chakula kutoka katika
sehemu zilizo nje ya mji wa Makkah kwa ajili ya watu wake wa mji wa Makkah.
566
Jambo hili la kununua mikate nje ya mji wa Makkah na kuwaletea watu wa mji wa
Makkah lilimpatia Amr jina la ‘Mkataji wa Mikate’. Hivyo Amr au Hashim alianzisha
misafara yake ya biashara iliyokua ikiwahudimia watu wa Makkah kwa kufanya biashara
kuanzia Yemen, Sham hadi Jerusalem, alisimamia mwenyewe mambo yote
yanayohusiana na usalama wa misafara yake hiyo inapokua njiani katika kila sehemu
kwa kujadiliana na kufunga mikataba na watu wa sehemu mbali mbali zinazopita
misafara yake.
Kutokana na cheo na ukarimu aliokua nao Hashim, watu wa Makkah wakaamua
kumuweka Hashim katika ngazi ya juu ya uongozi kuliko Abd Shams. Katika kuongoza
kwake mji wa Makkah, Hashim aliwahakikishia usalama wao na kuwahudumia watu
wote waliokua wakija Makkah kuhiji, hususan wale waliokua hawana uwezo na ambao
waliokua ni masikini na vile vile alishusha bei za vitu vyote katika msimu wa kuhiji.
Jambo ambalo lilimpelekea kupendwa sana na watu wa mji huo na pia wageni
wanaotembelea mji huo.
Baada ya kufariki Abd Shams, ikabidi uongozi kwa upande wake urithiwe na mtoto wake
mkubwa wa kiume aliekua akiitwa Umayyah. Lakini kutokana na kua Ummayah alikua
ni mtu mwenye kumuonea choyo na wivu Hashim kutokana na sifa alizokua nazo na
namna anavyoongoza, akaamua kumpiga vita Hashim na kutaka uongozi aliokua nao
Hashim avuliwe ili apewe yeye ambae ndie anaestahiki kwa sababu uongozi huo ulikua
ni wa baba yake ambae alikua ndie mtoto mkubwa katika familia.
Kutokana na hali hii kila mtu akawa anajua kua Ummayah alikua anataka utawala kwa
sababu ya Nafsi yake kupenda madaraka na hivyo alikua hafai, lakini Hashim alikua
akifaa kwa sababu alikua akiyatumia madaraka kwa ajili ya manufaa ya jamii ya watu
wa Makkah. Hivyo ili kutatua tatizo hili watu wa Makkah wakakutana na kuamua kupiga
kura, kwa masharti kua yeoyote yule atakeshindwa basi itambidi ahame katika mji huo
kwa miaka kumi. Matokeo ya kura hiyo yakaonesha kua Ummayah ameshindwa na hivyo
ikambidi ahame akahamie kaskazini ya Sham kwa miaka kumi halafu ndio arudi, na huu
ndio ukawa mwanzo wa kuwepo kwa upinzani baina ya ukoo wa Banu Hashim na ukoo
wa Banu Umayyah.
Hashim akaendelea kua kiongozi wa mji wa Makkah hadi pale alipofariki ambapo
uongozi wake ukarithiwa na mtoto wake wa kiume aliekua akiitwa Abd ul Muttalib
ambae jina lake halisi ni Shaibatul Al Hamd Ibn Hashim ambae nae alikua ni mtu
aliekulia na kufuata njia za kuongoza kwa uongozi bora ambao uliokuwepo kwa ajili ya
manufaa ya watu wa mji huo. Abd ul Muttalib alikua ni mtu mwenye kukubalika na
kuheshimika katika mji wa Makkah.
Ukoo wa Quraysh ulikua umegawika katika makabila makuu yafuatayo:-
Banu Abd Al Darr - kabila kutoka ukoo wa Quraysh.
Banu Abd Manaf - kabila kutoka ukoo wa Quraysh, ambao lilikua limegawika katika
makabila:-
567
• Banu Nawfal - kabila kutoka ukoo wa Banu Abd Manaf.
• Banu Muttalib - kabila kutoka ukoo wa Banu Abd Manaf.
• Banu Hashim - kabila kutoka ukoo wa Banu Abd Manaf, aliotoka Hashim, babu
yake mkubwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam.
• Banu Abd Shams - kabila kutoka ukoo wa Banu Abd Manaf, wazee wa Banu
Umayyah aliotoka Muawwiyah, Abu Sufyan na Uthman Ibn Affan.
Banu Makhzum - kabila kutoka ukoo wa Quraysh, aliotoka Khalid Ibn Al Walid (Saifu
Allah) na Ikrimah Ibn Abi Hisham.
Banu Zuhrah - kabila kutoka ukoo wa Quraysh, aliotoka Aminah Bint Wahb Ibn Abd
Manaf ambae ni mama yake Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na
Sahaba Sa'ad Ibn Abi Waqqas.
Banu Taym - kabila kutoka ukoo wa Quraysh, aliotoka Abu Bakr.
Banu Adi - kabila kutoka ukoo wa Quraysh, aliotoka Umar Ibn Al Khattab.
Banu Asad - kabila kutoka ukoo wa Quraysh, aliotoka Abd Allah Ibn Al Zubayr na mke
wa kwanza wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, Sayyida Khadijah Bint
Khuwaylid maarufu kama Khadija Al Kubra na pia Khadijah Amiral Qurayshi.
Banu Sahm - kabila kutoka ukoo wa Quraysh, aliotoka Amr Ibn Al Aas.
Banu Jumah - kabila kutoka ukoo wa Quraysh.
Katika kipindi hiki cha utawala wa Abd ul Muttalib, kulikua na baraza la kamati ya
uongozi wa mji wa Makkah uliokua na viongozi wa Quraysh (Sadat Quraysh) ambalo
lilikua ni lenye kuwajumuisha watu wafuatao:-
• Aaes Ibn Waeel (Banu Saham).
• Amr Ibn Hisham au Abu Jahl (Banu Makhzum).
• Abd Al Uzza au Abu Lahab (Banu Hashim).
• Abu Sufyan ibn Harb (Banu Umayyah).
• Akhnas Ibn Shariq (Haleef Banu Aadi).
• Aswad Ibn Mutlib (Banu Asad).
• Hakeem Ibn Huzaam (Banu Asad).
• Matum Ibn Aadi (Banu Nawfal).
• Mughirah Ibn Abd Allah (Banu Makhzum).
• Nabeeha Ibn Hujaj (Banu Jumah).
• Nazar Ibn Harris (Banu Abd Darr).
• Suhayl Ibn Amr (Banu Aamir).
• Umayyah Ibn Khalaf (Banu Jumah).
• Uqba Ibn Mui’t (Banu Abd Darr).
• Utba Ibn Rabi'ah (Banu Abdu Shams).
568
569
NDOTO YA ABD UL MUTTALIB NA KISIMA CHA ZAMZAM
Katika Mchana mmoja wa kipindi cha Kiangazi Siku moja wakati Abd Ul Muttalib akiwa
na umri wa maka 40 kamili basi alilala pembeni ya Al Kaabah kwenye kivuli cha Al
Kaabah basi akajiona kua amesimama kwenye Hajar na mara akasikia sauti ya mtu
asiemjua akiwa karibu yake akimuamrisha ndani ya usingizi wake kwa kusema: ‘Amka
ili upate kuchimba Tayyibah.’ Ambapo Neno Tayyiba maana yake hua ni Kitu Kizuri
chenye Manufaa kutokana na Usafi wake na Uhalali wake. Hivyo Abd ul Muttalib
akauliza: ‘Tayyibah ndio nini?’ lakini hata hivyo Mtu huyo hakumjibu suali hilo na
badala yake akatoweka Abd ul Muttalib akaamka huku akiwa amejawa na masuali
yasiyokua na jawabu akilini mwake, lakini hata hivyo akadharau na kuona kua labda
ilikua ni Adghathi Ahlami yaani ndoto isiyokua na mbele wala nyuma wala maana yeyote.
Lakini hata hivyo siku ya pili alipolala tena katika sehemu hio basi akasikia tena sauti ya
mtu asiemjua akiwa karibu yake akimuamrisha ndani ya usingizi wake kwa kusema:
‘Amka ili upate kuchimba Barra.’ Ambapo Neno Barra hua linamaanisha Kitu Kisafi
na Chenye Baraka. Hivyo Abd ul Muttalib akauliza: ‘Barra ndio nini?’ lakini hata hivyo
Mtu huyo hakumjibu suali hilo na badala yake akatoweka.
Ingwa hakua ni mwenye kujua kwanini anamuota mtu huyo anaemuamrisha kufanya
jambo asilolijua ndani ya Ndoto hizi ya mara ya pili na kisha mtu huyo kutoweka, lakini
amrisho hili la safari hii ya pili lilimfanya Abd Ul Muttalib kua ni mwenye kuamini kua
hizi ndoto zitakua zinamaanisha kua kuna jambo anatakiwa awe analifanya. Lakini hata
hivyo hakuweza kujua ni jambo gani, na kutojua kwake huko kulimpelekea kua ni
mwenye kujiuliza masuali mengi zaidi.
Na hivyo siku ya tatu alipolala tena katika sehemu hio basi akasikia tena sauti ya mtu
asiemjua akiwa karibu yake akimuamrisha ndani ya usingizi wake kwa kusema: ‘Amka
ili upate kuchimba Madnuna.’ Ambapo neno Madnuna maana yake hua ni kitu Kisafi
na chenye Thamani kubwa.
Hivyo Abd ul Muttalib akauliza: ‘Madnuna ndio nini?’ lakini hata hivyo Mtu huyo
hakumjibu suali hilo na badala yake akatoweka. Na tukio hili likamchnganya zaidi kwa
sababu mtu anaemuota hua hamtajii jina moja hilo hilo kila siku bali anamtajia majina
tofauti, na kwanini akilala nyumbani kwake usiku hua haoti ndoto hio, bali hua anaota
akiwa amelala kwenye Al Kaabah? N.k
Na ilipofika siku ya nne basi alipolala tena katika sehemu hio hio basi akasikia tena sauti
ya mtu asiemjua akiwa karibu yake akimuamrisha ndani ya usingizi wake kwa kusema:
‘Amka ili upate kuchimba Zamzam.’ Hivyo Abd ul Muttalib akauliza: ‘Zamzam ndio
nini?’ ambapo safari hii Mtu huyo hakuondoka bali alimjibu kwa kusema: ‘Zamzam ni
570
kisima cha Maji ambayo hayakauki wala hayasiti katika kutiririka kwake.
Kutokana na Maji Haya basi utakua ni mwenye kuweza kuwasaidia Mahujaji kwa
mahitajio yao ya Maji. Kisima kipo baina ya sehemu inayotiririka na kugawanyika
Damu ya Wanyama wa Kafara na baina ya sehemu inayozikwa mabaki ya vichinjo
hivyo. Hii ni sehemu ambayo hua wanakuja Kunguru na kupekua, na katika
sehemu hio kuna jumba la sisimizi pia. ’
Naam majibu haya yalimfurahisha sana Abd ul Muttalib hivyo mara tu baada ya kuamka
alikua ni mwenye kujawa na furaha, kwani kwa mara ya kwanza amepata ufumbuzi wa
tatizo lililokua likimtatiza ndani ya wiki hio nzima, ambao ni nini maana ya amrisho
alilokua akiamrishwa, na bila ya shaka mara kadhaa amewahi kusikia kuhusiana na
Kisima cha Maji ya Zamzam, lakini hakuna hata mtu mmoja ambae alikua ni mwenye
kujua kiko wapi kisima hicho.
Na hii ni kwa sababu katika kipindi cha kutoweka kwake kulitokea mapigano na hivyo
watu wa Banu Jurhum wakawa ni wenye kuukimbia Mji huo na hivyo wakatumbukiza
kila kitu chao ndani ya Kisima cha Zamzam, na kisha wakakifukia Kisima hicho. Hivyo
ilikua inajulikana kua kuna kisma cha Zamzam lakini hakuna anaejua kiko wapi, na hivyo
hii ndoto ilikua ikimbashiria yeye Abd Ul Mutallib kua ndie Mvumbuzi wa Kisima cha
Zamzam na anatakiwa akichimbe tena upya.
Hivyo Abd Ul Mutallib akanyanyuka kutoka katika sehemu aliyokua amelala huku
akitabasam na kuelekaa katika sehemu aliyoelekezwa ndani ya ndoto. Katika kuangalia
kwake sehemu hio basi akamuona Kunguru kwenye sehemu aliyoelekezwa ndani ya
ndoto yake na hivyo akatabasamu zaidi ndani ya Moyo wake, tabasam ambalo
lilionekana wazi juu ya Uso wake na kwenye mng’aro wa Macho yake, alipoisogelea
sehemu hio Kunguru huyo akaruka kuelekea angani na kumuacha Abd Ul Mutallib akiwa
ni mwenye kuizingatia na kuiwekea alama ndani ya ufahamu wake sehemu hio.
Kisha Abd Ul Mutallib akaondoka sehemu hio na akarudi tena siku ya pili yake huku
akiwa na Mtoto wake pekee kwa wakati huo aliekua akiitwa Harith ambae walipofika
katika sehemu hio basi wakaaza kuchimba kimya kimya, huku wakiwawacha watu wa
kabila la Quraysh wakiwa wamejawa na mshangao kutokana na tukio hilo bila ya kujua
nini kinachoendelea. Kwani Abd Ul Mutallib aliamua kulifanya tukio hilo la uchunguzi
kua ni siri kubwa sana, kwa sababu hakutaka wenzake wa kabila la Quraysh wajue juu
ya jambo hilo.
Kwani hii ilikua ni heshima kubwa kwake kama vile ambavyo ilivyokua heshima kubwa
kwa Babu wa Mababu zake alieuvumbe Mji wa Makkah ambae ni Nabii Ibrahim alipokua
pamoja na Mtoto wake Ismail walipokua wakiufukua Msingi wa Jengo la Al Kaabah kwa
ajili kulijenga upya jengo hilo. Hivyo na kwa upande wa Abd Ul Mutallib na Mtoto wake
Harith walifanya jambo lao hilo wakiwa wawili tu la kuchimbua Kisima cha Zamzam
571
Na baada ya kupita mda katika kuchimba kwao eneo hilo la ardhi hio, basi wakaanza
kuona dalili ya Ukuta wa Kisima hicho na hivyo wakazidi kujawa na furaha kua kile
wakitafutacho bila ya kukijua kiko wapi kwa miaka na miaka basi leo hii kimetokea na
kinaonekana dalili zake wazi chini ya macho yao, na hivyo Abd Ul Mutallib akajisikia
akisema: ‘Allahu Akbar… Allahu Akbar’
Ambapo tukio hili la kauli hii lilipelekea watu kusogea karibu zaidi kuona kuna maajabu
gani yaliyotokea, na haukuchukua mda mrefu isipokua Viongozi wengine wa Kabila la
Quraysh wakapata habari hio, hivyo nao haraka wakakimbilia kwenye eneo la tukio hilo,
na walipofika wakamwambia Abd Ul Mutallib: ‘Ewe Abd Ul Mutallib. Hiki kisima ni
cha Babu wa Mababu zetu sote ambae ni Ibrahim, hivyo bila ya shaka sisi pia tuna
haki ya juu ya Kisima hiki cha Zamzam, kwa hivyo nasi tunastahiki kushiriki katika
kukifukua Kisima hiki pamoja nawe.’
Abd Ul Mutallib akajibu: ‘La! Siwezi kukuachieni Mnisaidie kwani hili ni jukumu
langu mimi peke yangu kwani mimi ndie nilieamrishwa na kuoneshwa la kufanya
kwenye eneo hili.’
Ambapo hata hivyo watu hao wa Kabila la Quraysh hawakufurahishwa na Jibu hilo hivyo
nao wakasema: ‘Abd Ul Mutallib hakika wewe ni Mtu ambae hana mtu wa
kumtegemea isipokua huyu Mtoto wako mmoja, hivyo inakuaje unakua na hali
kama hii ya ukaidi wa kubishana na kupingana nasi?’
Bila ya shaka kauli hii ilimhuzunisha sana Abd Ul Mutallib kwani aliona kua tayari
anadharauliwa kutokana na kua na Mtoto mmoja tu hivyo akasema: ‘Kwa hivyo
mnanihukumu sio, kwa sababu niko peke yangu na sina Mtoto zaidi ya huyu
mmoja? Basi hakika mimi nnaapa kua kama Allah Atanijaalia kupata watoto 10
basi nitamtoa mmoja Kafara kwa ajili ya Al Kaabah.’
Ambapo maneno haya yalipotoka kwenye Moyo wake kupitia kwenye ulimi wake
yalikua ni Dua, Kiapo, Dhamira na pia Nadhiri mbele ya watu wake na Mungu wa jengo
la Al Kaabah. Na hivyo tukio hili halikuweza kuishia hapa, kwani hapo hapo akawacha
uchimbaji wake huo na kuwaambia watu hao kua: ‘Kama hamkubaliani nami basi
Mimi nataka tukamtafute mtu ambae atatatua kwa haki juu ya nani mwenye haki
zaidi ya kukifukua Kisima hiki na nataka mzozo huu utatuliwe na mtaalamu wa
Ilm ya kubashiri wa Banu Saad Ibn Huzaym wa Dimashq.’
Hivyo wakuu hao wa kabila la Quraysh wakakubaliana na rai hio na wakaamua kufunga
safari ya kuelekea katika Mji wa Syria katika siku ya pili yake, lakini Allah Subhanah wa
Ta’ala na makadirio yake basi akajalia kua walipofika njiani wakajishtukia kua maji yao
ya akiba waliyochukua yameisha yote, bila ya kujua yameisha ishaje isipokua kwa
wachache tu miongoni mwao ndio ambao waliobakiwa na maji ambayo ni kidogo sana.
572
Hali hii iliwapelekea kukaa na kujadiliana nini cha kufanya kwani hata hivyo hao
wachache waliokua na maji hayo basi walikua na ubinafsi wa kugawana Maji hayo na
wenzao miongoni mwao.
Na hakuna kitu kibaya na hatari zaidi kwa Msafara wa wasafiri wa Jangwani kuliko
kuishiwa na maji kwa msafara huo, hivyo baada ya kujadiliana basi Abd Ul Muttalib
akashauri kua bora kila mmoja achimbe Kaburi lake taratibu kisha aingie ndani yake kwa
ajili ya kusubri kifo chake, kuliko kuendelea na Safari kisha wakafa wote kwa pamoja.
Hivyo watu hao wakakubaliana na rai hio, na kisha wakaanza kujichimbia Makaburi yao.
Lakini ghafla Abd Ul Mutallib akapata wazo bora zaid akilini mwake, na hivyo
akawashauri wenzake kwa kuwaambia: ‘Mimi sasa hivi nadhani kua jambo bora zaidi
ni kutafuta Maji, kuliko kuchimba Makaburi, kwani huenda Allah akatuonesha
Maji.’ Hivyo watu hao wakakubaliana na wazo hilo, na kila mmoja akapanda kipando
chake kwa ajili ya kutafuta Maji, wakatoka Jangwani na kuelekea kwenye eneo la
tambarare, ambapo ghafla Ngamia wa Abd Ul Muttalib akajikwaa na jiwe ambalo nalo
lilipoondoka kwenye sehemu yake ya asili, basi ukatokea mbubujiko wa chemchem ya
Maji chini yake.
Abd Ul Mutallib alipoona mbubujiko huo wa Maji basi hakuamini macho yake, na hapo
hapo akashuka chini kutoka wenye Ngamia wake kwa ajili ya kuhakikisha juu ya kile
kinachoonekana na Macho yake, kama kua ni kweli anayoyaona ni Maji kweli ama la.
Na aliposegelea karibu eneo hilo akaona kua kweli hakua ni mwenye kudanganywa na
kile kilichoonekana na macho yake. Hivyo Abd Ul Muttalib akawaita wenzake kwa
kuwaambia: ‘Njooni Kwenye Maji, kwani Allah ametupatia Maji, kwa ajili yetu na
kwa ajili ya Wanyama wetu.’
Tukio hili la kupatikana kwa maji na Abd Ul Muttalib lilibadilisha mtizamo wa watu wa
Kabila la Quraysh juu ya Abd Ul Muttalib kwani tukio hili limedhihirisha ukubwa wa
Darja yake juu ya yao, na thamani ya ukubwa wa cheo chake juu yao na kukubalika zaidi
mbele yao hivyo wakasema:
‘Ewe Abd Ul Muttalib haka sisi hatuna haja ya kupingana na wewe sasa hivi kwani
umetudhihirishia kua unastahiki kua ndie mchimbaji pekee wa Kisima cha
Zamzam, hivyo tunaahidi kua hatutokusitisha wewe kuchimba Kisima hicho, na
hivyo haina haja ya kuelekea katika mji wa Dimashq kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi
wa lililokua tatizo letu, kwani limeshatatulika hivyo wacha turudi Nyumbani ili
ukaendelee na Uchimbaji wa Kisima cha Zamzam.’
Hivyo msafara huo ukageuza muelekeo wa Safari yao na kurudi nyumbani katika Mji wa
Makkah. Ambapo Imam Al Bayhaqi anasema kua: ‘Waliporudi katika Mji wa Makkah
basi Abd Ul Muttalib akaendelea kujenga Ukuta pembeni ya Kisima cha Zamzam,
573
lakini kuna watu miongoni mwa Wapinzani wake wakauvunja ukuta huo. Hivyo
akaujenga tena upya ukuta huo na kisha akaomba Dua kama alivyoamrishwa
kwenye ndoto kwa kusema: ‘Ya Allah, Hakika Mimi siyahalalishi maji haya kwa
ajili ya Mtu anaetaka kukoga, bali kwa ajili ya wale wanaotaka kunywa tu.’
Kisha akawaita watu wake na kuwataarifu kuhusiana na Ndoto yake, na Dua yake,
na kisha baada ya hapo, ikawa kila mtu anaetaka kufanya Israfu kwenye Kisima
hicho basi hua ni mwenye kuumwa sana badala yake.’
Wakati uchimbwaji au usafishwaji au Ufuwaji wa kisima cha Zamzam ukiwa unaendelea
basi ndani yake mlitolewa vitu vingi sana vya thamani vilivyotumbukizwa hapo kabla
ikiwemo sanamu la Mnyama aina Ghazali (Paa), Mapanga ya Kivita na Ngao za Dhahabu
vyote vikiwa katika hali nzuri kabisa, hivyo Watu wa kabila la Quraysh walipoona vitu
hivyo vya thamani basi wakaona choyo na kuhisi kua Abu Talib atafaidika zaidi. Hivyo
nao wakasema: ‘Ya Abd Ul Muttalib hakika na sisi pia tuna haki juu ya vitu hivi.’
Hivo Abd Ul Muttalib akasema: ‘Kwa hakika nyinyi hamna haki juu ya vitu hivi
lakini hata hivyo hamna tatizo kwani nitakua na huruma juu yenu, kwa kutoa
maamuzi baada ya kucheza bahati nasibu nanyi.’ Watu hao wakauliza: ‘Tutacheza
bahati nasibu gani?’
Abd Ul Mutallib akasema: ‘Tutabahatisha kwa kuangalia matokeo ya kuweka
majina ya kitakachotolewa kwa Hubal, ambapo ndani yake kitakachotolewa
mtakua na Alama mbili kwa ajili ya Al Kaabah. Alama mbili kwa Ajili yangu,
Alama mbili kwa ajili yenu, na Alama mbili kwa ajili ya kukosa sote.’ Na watu hao
wa Quraysh wakakubaliana na Mtizamo wa Bahati Nasibu hio.
Hivyo wakaenda kwa Hubal na kucheza bahati nasibu hio, wakaweka ndani yake alama
zao na matokeo yake Abd Ul Muttalib akashinda, hivyo Ghazali wa Dhahabu akaachwa
ndani ya Al Kaabah, na kisha Abd Ul Muttalib akayayeyusha Mapanga na Ngao za
Dhahabu na kisha akatengeneza pande kama bati la dhahabu kutokana nayo ambalo
akalitumia kwa ajili ya Mlango wa kuingilia ndani ya Jengo la Al Kaabah, na hivyo
akawa ni Mtu wa Mwanzo kulipamba Jengo la Al Kaabah kwa Dhahabu.
Baada ya tukio hilo basi alipita miaka 30 ambayo ndani yake miaka hio basi Allah
Subhanah wa Ta’ala alimjaalia Abd Ul Muttalib kuwa na watoto wengi wa kike na wa
kiume, ambao ni Harith, Hamza, Az Zubayr, Hajl, Al Muqqawwim, Dirar, Abu Lahab
Abd Ul Uzzah, Abu Talib, Abdullah, Al Abbas, Saffiyah, Ummu Al Hakkam Al Baydha,
Umaymah, Arwa na Barah.
Na mmoja miongoni mwao watoto wake hawa basi Abd ul Muttalib alikua akimpenda
sana kwa sababu alikua kua ni mtoto wake ambae ni mtoto wake bora na alie mzuri wa
574
sura na kitabia, mkweli na mwenye busara pia, mtoto huyu alizaliwa mwaka 545 C.E
miaka 25 kabla ya vita vya Tembo na alikua akiitwa Abdullah Ibn Abd ul Muttalib.
ABDULLAH IBN ABD UL MUTTALIB BABA YAKE RASUL ALLAH
SALALLAHU AAYHI WA SALAM
Abd Allah Ibn Abd ul Muttalib alikua ni mmoja kati ya Watoto 10 wa Mzee Abd Ul
Muttalib, ambapo mara tu baada ya kuzaliwa basi alikua na muonekano wenye upekee
unaovutia kwa kila mtu anaemuangalia. Hivyo watu wote wa Mji wa Makkah walikua ni
wenye kumpenda sana Abdullah kutokana na uzuri wa Maumbile na Nuru ya muonekano
wake.
Baada ya Abdullah kua mkubwa kidogo basi Abd Ul Muttalib akakumbuka kuhusiana na
Kiapo na Nadhiri aliyoiweka miaka 30 iliyopita wakati alipokua na Umri wa miaka 40
baada ya kuchekwa kua ana mtoto mmoja tu wakati akiwa anchimba Kisima cha
Zamzam, na kuapa kua kama akijaaliwa kua na watoto 10 basi mmoja atamtoa Kafara
kwa ajili ya Allah.
Hivyo Abd Ul Muttalib akawataarifu watoto wake na kuwaambia kua Mtoto mmoja
miongoni mwao itabidi awe ni mwenye kutolewa kafara kutokana na nadhiri hio
aliyoiweka miaka 30 iliyopita ambayo inabidi kutekelezwa, na bila ya shaka watoto wake
wote hao hawakua ni wenye kupinga juu ya hilo, bali waliuliza: ‘Hivyo Jee itaamuliwaje
kua ni yupi wa kutolewa kafara miongoni mwetu?’
Abd Ul Muttalib akasema: ‘Kila mmoja wenu itabidi achukue Upinde wa Mshale na
kisha auandike jina lake kisha anipe mie’ Hivyo watoto hao wote wakachukua upinde
kila mmoja na wake kisha wakaandika Majina yao na kumkabidhi Abd ul Muttalib, na
kisha wao wakabakia Nyumbani kwa ajili ya kusubiri matokeo ya Bahati nasibu hio,
huku watu wa kabila la Quraysh wakikusanyika mbele ya Hubal na kisha mishale hio ya
Upinde ikawekwa kwa Hubal, na kisha akaamrishwa mtu mmoja miongoni mwa watu
waliouwepo mbele hapo aende akatoe Upinde mmoja kwa Hubbal, mtu huyo alipoutoa
upinde huo na kusoma jina lililoandikwa kwenye upinde huo basi akasema: ‘Abdullah!’
Baada ya kusomwa upinde huo basi Abd ul Muttalib hakuamini masikio yake na hivyo
akamwita msomaji huyo na kumwambia ampe upinde huo ili ausome yeye mwenyewe,
na alipopewa na kuusoma akaona kua umeandikwa Abdullah, na kisha hapo hapo
akajisikia uchungu mkubwa sana kwani alikua akimpenda sana Abdullah kuliko Mtoto
wake yeyote, na si yeye tu peke yake ndie aliekua akimpenda kijana huyo bali Mji Mzima
wa Makkah Ulikua ukimpenda sana kijana huyo. kiasi ya kua bado kidogo Abd ul
575
Muttalib akatae kutekeleza Nadhiri hio, lakini akakumbuka ahadi aliyoiweka mbele ya
Allah na watu wake.
Hivyo Abd Ul Muttalib akageuka na kutoka kwenye Jengo la Al Kaabah kisha akaelekea
Nyumbani huku akiwa ni mnyonge na mwenye huzuni kubwa sana kutokana na
kuvunjika Moyo sana na matokeo ya bahati nasibu hio ya mshale huo, lakini hana budi
kwani lazima atimize nadhiri yake aliyoweka na hivyo alipoingia Nyumbani kwake
akawakuta Watu wa Nyumbani kwake wakiwa ni wenye kumsubiri ili wapate kujua juu
ya matokeo ya Bahati nasibu hio, hivyo nae akasema bila ya kuwatazama Watoto wake
hao kua: ‘Abdullah, Allah amekuchagua wewe kua ni mwenye kutakiwa kutolewa
kafara kwa ajili yake’
Habari hii iliwahuzunisha watu wote wa familia ya Abd Ul Muttalib lakini hata hivyo
haikua ni yenye kumuathiri Abd Allah mwenyewe kwani hata baada ya kusikia Jina lake
basi hakua ni mwenye kua na khofu wala huzuni, hivyo Abd Ul Muttalib akaukamata
mkono wa Abdullah na kisha akatoka nae nje kuelekea nae kwenye Al Kaabah.
Ambapo ingawa Abdullah alikua na maridhio kama ya Nabii Ismail alipoambiwa kua
anatakiwa kutolewa kafara kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala lakini kwa upande wa
watu wa Mji wa Makkah basi walikua ni wenye kujawa na simanzi na hivyo wakamuuliza
Abd Ul Muttalib: ‘Ewe Abd Ul Mutallib, unataka kumfanya nini Abd Allah?’
ambapo nae Abd Ul Muttalib akajibu: ‘Naenda kumtoa kafara kutimiza dhamira
yangu niliyoiweka hapo kabla’
Hivyo wakuu wa Quraysh wakasema: ‘Ewe Abd Ul Muttalib, inakuaje unataka
kufanya jambo hili? Wakati wewe ni mmoja kati ya watu wanaoheshimika katika
Mji huu? Hivi huoni wewe kua ukifanya hivyo basi watu wengine nao watafuata
mfano wako? Na hivyo watu wakiwatoa kafara watoto wao wa kiume basi
hakutokua na Wanaume katika Kabila letu?’
Kutokana na maneno hayo basi watu wote wa Mji wa Makkah wakawa ni wenye
kupingana na mtizamo huo wa Abd ul Muttalib, hivyo Al Mughira Ibn Abd Allah Ibn
Ibn Umar Ibn Makhzum ambae ni Mjomba wake Abdulla akasema: ‘Ewe Abd ul
Muttalib Wallahi, haiwezekani kwako wewe kumtoa kafara Mtoto wako ispokua
kama kutakuwepo na kisingizio kinachokubalika, hivyo hata kama itakubidi wewe
uwe ni mwenye kupoteza mali yetu yote kwa Ajili ya kuokoa Maisha yake basi kwa
hakika kwetu sisi ni bora kupoteza mali yote kuliko kumtoa kafara Abd Allah na
tuko tayari kujitolea kwa ajili yake.’
Kisha wakuu wa Quraysh wakasema: ‘Ewe Abd Ul Muttalib, mchukue Abd Allah na
kisha uende nae katika Mji wa Dimashq, ambapo kuna Mwanamke ambae anaitwa
Arrafa, Mwanamke huyu ni mwenye Hikma na Busara na Mtizamo wa kuona
576
Mbali sana kutokana na Muono wake, na kila Mtu kutoka Mashariki na Magharibi
ya Ardhi hua ni mwenye kuelekea kwake anapokua na Matatizo na ni mwenye
uwezo wa kutibu na kutatua matatizo mbali mbali. Hivyo kama akisema kua mtoe
Kafara Abdullah basi itabidi umtoe lakini akisema kua kuna njia nyengine
itakayotuepusha sisi kutokana na huzuni basi itabidi uitekeleze’
Shauri hili lilimpendezesha sana Abd Ul Muttalib na akaona kua ni bora kufanya kama
alivyoshauriwa na wenzake, hivyo akamchukua Abdullah na kisha wakafunga safari ya
kuelekea Syria kumtafuta Mwanamke huyo atakaewasaidia kutatua mtihani wao huo.
Lakini walipofika katika Mji wa Madinah basi wakapata habari kua Mwanamke huyo
hayuko katika Mji wa Dimashq bali ameelekea kwenye Mji wa Khaybar, hivyo nao
wakafunga safari hadi katika Mji wa Khaybar na kwa bahati nzuri wakakutana na
Mwanamke huyo aitwae Arrafa.
Na walipofika tu basi Abd Ul Muttalib akamuelezea hali ya mkasa wao ilivyokua tangu
mwanzo hadi mwisho na kisha baada ya kumaliza kuelezewa basi Arrafa akamuuliza
Abd Ul Muttalib: ‘Hivi Jee katika ardhi ya Mji wenu hua mnatoa fidya ya Ngamia
wangapi kwa ajili ya Mtu mmoja?’ Abd Ul Muttalib akajibu: ‘Hua tunatoa Ngamia
10’
Hivyo Arrafa akamwambia Abd Ul Muttaliab: ‘Vizuri sana, sasa rudini katika Mji
wenu na kisha katayarishe Ngamia 10, kisha wachukue Ngamia hao na Mtoto wako
kisha nendeni katika sehemu ambayo Mipinde ya Mishare hio hua inatolewa, halafu
muweke Mtoto wako katika upande mmoja na Ngamia 10 Upande mwengine. Kisha
andaa mipinde ya mishare miwili, mmoja kwa ajili ya Mtoto wako, na mwengine
kwa ajili ya Ngamia 10.
Kisha toeni Mshale wa Upinde kama kawaida na kama upinde utakaotolewa
utaonesha kua ni Ngamia basi utawachinja Ngamia na kumnusuru Mtoto, na kama
Upinde ukitoka utakua ni wa Mtoto basi itakubidi uongeze idadi ya Ngamia wa
Kafara hadi pale Mola wako atakaporidhika nawe, na hivyo kila ukitoka Upinde
wa Ngamia basi utawachinja Ngamia, na hivyo kwa njia hii utakua ni mwenye
kumnusuru Mtoto wako na hapo hapo utakua ni mwenye kumridhisha Mola wako’
Na bila ya shaka shauri hili lilimfurahisha sana Abd Ul Mutallib na kumridhisha, na hivyo
haraka sana yeye na Abdullah wakafunga safari kwa ajili ya kurudi katika Mji wa
Makkah. Na alipofika katika mji wa Makkah na kuelezea namna alivyofahamishwa basi
watu wa mji wa Makkah nao wakafurahia na kuunga mkono mtizamo huo.
Hivyo Abd Ul Mutallib akaamua kutafuta Ngamia wekundu wenye bei ghali kuliko wote,
kisha akawachukua Ngamia 10 miongoni mwao, na kisha akamchukua Abdullah na
kumuweka upande wa Hubal, na kisha ikachukuliwa mishale ya mipinde miwili na
577
mmoja ukaandikwa Abdullah na mwengine ukaandikwa Ngamia. Kisha mipinde hio
ikawekwa ndani ya sehemu yake ya kuchaguliwa na kisha akatumwa Mtu akachomoe
Mshale mmoja, na alipochomoa basi ukatoka Mshale ulioandikwa Abdullah.
Hivyo Abd Ul Mutallib akaongeza idadi ya Ngamia hao na kua Ngamia 20, ukawekwa
tena Mshale na kutolea na ulipotolea ukatolewa wa Abdullah tena, hivyo wakaongezwa
Ngamia 10 na wakawa Ngamia 30, ambapo mshale uliendelea kuwekwa na kutolewa
ukiwa na jina la Abd Allah kwa mara 10 hadi ikafikia Idadi ya Ngamia hao kua ni 100.
Ambapo watu wa Mji wa Makkah walikua ni wenye kupigwa na Mshangao sana
kutokana na tukio hili la upekee ambalo halijawahi kutokea kabla yake kwa kutakiwa
kuchinjwa Ngamia wengi zaidi, na pia halijawahi kutokea kwa kutokea Jina hilo hilo kwa
mara 10 mfululizo.
Na jambo la kushangaza basi ni kua baada ya idadi ya Ngamia kutimia 100, basi Mshale
huo ulipotolewa ukawa unaonesha kua na jina la Ngamia na hivyo kumaanisha kua
wanatakiwa wachinjwe Ngamia. Ambapo tukio hili liliwafurahisha sana watu wa Mij wa
Makkah kwani walikua wamepata afueni kubwa sana. Lakini Abd Al Muttalib akasema:
‘La itabidi turudie mara 3 kuhakikisha kua kweli hivyo ndivyo anavyotaka iwe
Allah’, na bila ya shaka ikafanywa kama alivyoamrishwa na mara zote 3 mishare
ikaashiria kua wanatakiwa wachinjwe Ngamia. Hivyo Abd Ul Muttalib akaridhia na
kuamrisha kuchinjwa kwa Ngamia hao 100, na hivyo Abdullah akawa amenusurika na
kutolewa Kafara. Ngamia hao wakachukuliwa hadi katika sehemu ya baina ya Safwa na
Marwa na kisha wakachinjwa na kutolewa sadaka.
Miongoni mwa waliokua wakiangalia tukio hili basi alikuwemo Mwanamke mmoja tajiri
na mwenye Ilm ya Kitabu ambae alikua akijulikana kama Ruqqiya, huyu alikua ni dada
yake Waraqah Ibn Nawfal. Ruqqiya aliwahi kusoma kwenye vitabu kuhusiana na kuja
kwa Mtume atakaetokea mwishoni mwa Dunia, hivyo alipomuangalia Abdullah na Nuru
aliyokua nayo Usoni basi akagundua kua Kijana huyo ana mbegu za Uzazi wa Mtume
huyo aliebashiriwa Vitabuni.
Jambo hili na alama aliyoiona Ruqqiya ilimvutia sana na akaona kua aitumie nafasi
aliyokua nayo kwa ajili ya kubeba mbegu hizo za Mtume huyo kutoka kwa Abdullah
kuingizwa kwenye fuko lake la uzazi kwa kuingiliana kimwili na Abdullah ili yeye awe
ndie mwenye utukufu wa kua ni Mama wa Mtume huyo, lakini hata hivyo
alimpomsogelea Abdullah na kumwambia kua anamtaka na atamlipa Ngamia 100 kama
waliochinjwa kwa ajili yake, basi Abdullah akakataa katakata na kumwambia Ruqqiya
kua:
‘Haram hua ina maumivu makubwa sana, kiasi ya kua hata maumivu ya kifo hua
hayaufikii ukubwa wake, lakini Halali haina maumivu na wala si chungu, hivyo
bora tafuta kile kilicho halali yako, kwani wenye kuamini hua ni wenye kuilinda
578
Imani yao ipasavyo, na haiwezekani kwao kufanya jambo ambalo hua linahesabika
kua ni kujivunjia heshima.’ Na kisha Abdullah akaondoka kurudi nyumbani huku
akimfuata baba yake.
Ambapo kwa upande mwengine basi Hisham Al Kalbi anasema kua: ‘Huyu alikua ni
mwanamke aitwae Fatmah Ibn Murrah na alikua ni mwanamke Mzuri sana na
Msafi miongoni mwa wasafi na mwenye Ilm ya Ahl al Kitab na baada ya kuona
dalili ya Nuru hio kwenye Paji la Uso la Abdullah basi akamtaka kimapenzi lakini
Abdullah akakataa.’
Ambapo Mwanamke huyu alimwambia hivyo Abdullah Ibn Abdul Muttalib kwa sababu
jambo hili lilikua linakubalika katika wakati huo wa enzi za Ujahiliya, kwani
tunapoiangalia mahusiano ya kimapenzi na Ndoa katika wakati wa Ujahiliya basi
tunaona kua kulikua na aina nne za mahusiano ya Ndoa ambazo ni:
1- Mahusiano ya Ndoa ambayo ndio yanayokubalika kwa Kisharia za Kiislam
ambapo Mwanamme anaenda Kumposa Mwanamke kupitia kwa Walii wake
Mwanamke huyo na wanapokubaliana basi yanatolewa Mahari na kufanyika
kwa Ndoa hio.
2- Mahusiano ambayo ilikua Mwanamme asiekua na utukufu kijamii
anamwambia Mke wake, kua nenda kalale na fulani Ibn fulani na kisha Mume
huyo hua si mwenye kumgusa Mke wake huyo hadi atakapohakikisha kua Mke
wake ni Mja mzito kutoka kwa Mwanamme aliemuamrisha aende akalale nae
Mke wake. Na walikua wanafanya hivi kwa sababu ya kuingiza utukufu wa
kizazi ndani ya familia ambayo haina utukufu katika jamii na hivyo kuupata
utukufu huo kutoka kwenye kizazi cha Mwanamme huyo mwenye utukufu
katika jamii.
3- Mahusiano ambayo Mwanamke yeyote anaetaka Mtoto basi anakua na
uhusiano na Wanaume wengi, ambao anaingiliana nao hadi anapata uja uzito
na akishajifungua basi huwaita Wanaume hao na kumchagua anaemtaka
mmoja miongoni mwao kua ndio Baba wa Mtoto wake na hivyo Mwanamme
aliechaguliwa hua hana hiari ya kukataa na wala waliobakia hua hawana uwezo
wa kupinga.
4- Mahusiano ambayo ni ya Mwanamke Malaya ambae hua anaweka bendera
kwenye nyumba yake kuashiria kua anafanya kazi hio, ambapo Wanaume nao
hua ni wenye kuenda kwa Wanawake hao, na kisha Mwanamke huyo
anapopata uja uzito kujifungua basi huitwa wale wote ambao aliigiliana nao, na
kisha anachaguliwa mtu na kuambiwa kua aague kuhusiana na huyo mtoto ni
579
wa nani kati ya watu hao, na anapoaguliwa Mwanamme huyo basi hapo hapo
Mwanamme huyo hua ndio Baba wa Mtoto huyo.
BARAKAH BINT THALABAH UMM AYMAN MAMA MLEZI WA
RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM
Mchana wa siku moja ya mwaka 569 C.E katika Ardhi hio Takatifu ya Mji wa Makka
katika Soko la Mji huo waliwasili Watumwa kutoka Ethiopia na hivyo kua ni wenye
Kuuzwa kwenye soko la Mji huo. Ambapo Miongoni mwa Watumwa hao alikuwepo
Binti mmoja Mwenye asili ya Kiafrika yaani alikua ni Mtu mweusi ambae alikua
akijulikana kwa jina la Barakah Bint Thalabah.
Haijulikani ilikua kuaje mpaka Binti huyu akajikuta yuko Sokoni akiuzwa kama
Mtumwa, ila kinachojulikana ni kua ingawa hii ilikua ni Bahati Mbaya sana kwake Binti
huyu kwa wakati huo, Lakini kutokana na Mipango ya Mbora wa Upangaji na Kukadiria
yaani Allah Subhanah wa Ta'ala basi alikua amelijaalia tukio hili kua ndio sababu ya
Kupanda Darja ya juu ya Binti huyu, kwani alimjaalia kua ni mwenye kutolewa
alikotolewa katika Bara la Afrika na kusafirishwa hadi katika Ardhi Takatifu ya Mji wa
Makkah.
Kwa ajili tu ya kuja kuuzwa na kununuliwa na kutolewa katika Madhila ya Utumwa na
si mtu mwengine yeyote isipokua Kijana Mtanashati, Mzuri wa Kitabia na Kimaumbile
mwenye umri wa miaka 24 aliekua akijulikana kama Abdulla Ibn Abd Al Muttalib ambae
ndie atakaekua Baba yake Nabii Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam.
Ambapo katika kipindi hiki ambacho Abdullah Ibn Abd al Muttalib anamnunua Baraka
basi Abdulla alikua bado hajamuoa Mke wake anaeendana nae kwa Utanashati wa
Kimaumbile na Kitabia aitwae Amina Bint Wahb ambae ndie Mama yake Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam.
Na haukuchukua Mda Mrefu tangu Barakah kuingia kwenye Nyumba hio isipokua
Abdullah Ibn Abd Al Mutallib alifikia umri wa kuoa, baba yake Abd ul Muttalib aliamua
kumtafutia Mwanamke bora kisura, msafi kitabia na kikabila alieweza kupatikana katika
mji wa Makkah kwa wakati huo, na Mwanamke huyo alipatikana kutoka katika kabila la
Banu Zuhra ambapo kulikua na Mwanamke aitwae Aminah Bint Wahb Ibn Abd Manaf.
Hivyo hii inamaanisha kua Barakah aliingia katika Nyumba ya Abdullah Ibn Abd
Muttalib kabla ya Kuingia kwa Amina Bint Wahb katika Nyumba hio. Ila sasa Barakah
alikua ni Mfanyakazi pekee wa Nyumba hio.
580
Hivyo Barakah akawa ni Mfanyakazi pekee na Rafiki wa Karibu wa Amina Bint Wahb
yaani mama yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na pia akawa ni Mtu ambae ni
rafiki yake wa karibu sana Amina Bint Wahb.
AMINAH BINT WAHB MAMA MZAZI WA RASUL ALLAH
SALALLAHU ALAYHI WA SALAM
Abd Ul Muttalib alipompata Bint huyo aitwae Amina Bint Wahb na kuridhika nae basi
akamwambia Wahb Ibn Abd Manaf ambae alikua ni Chifu wa kabila la Banu Zuhra kua
anataka kumpa posa ya Aminah kwa ajili ya Mtoto wa wake Abdullah, ambapo Wahb
Ibn Abd Manaf akasema:
‘Ewe Ibn Ami wangu, hakika sisi tumeshapokea Posa yako kabla yako, kwani
Mama yake Amina alipolala juzi usiku aliota kua kuna Nuru imeingia ndani ya
Nyumba yetu na kisha ikamurika Ardhini na Mbinguni kote, na mimi jana Usiku
nimemuota babu yetu Ibrahim ambae alikua akiniambia kua: ‘Hakika mimi
Nimemuozesha Abdullah Ibn Abd Ul Muttalib kwa Binti yako Amina, hivyo
atakapokuja basi ipokee Posa hio, na kutokana na ndoto hio basi nimekua najiuliza
tangu asubuhi leo nilipoamka Jee utakuja wakati gani? Na ndio umekuja’’ ambapo
baada ya kusikia habari hio basi Abd Ul Mutallib akasema: ‘Allahu Akbar! Allahu
Akbar!’
Hivyo Harusi hio tukufu ya watoto wa Machifu wawili wa Makkah Abd ul Muttalb na
Wahb Ibn Abd Manaf, ambao ni Abd Allah ambae alikua na umri wa miaka 24 na
Aminah ambae alikua na umri wa miaka 20 ikafanyika na watu wa Mji wa Makkah
wakafurahika sana. Hii ilikua ni harusi ambayo ilibadilisha Muelekeo wa Dunia kama
ilivyobashiriwa na ndoto ya Mama yake Amina Bint Wahb, kwani ndio ndoa ambayo
ndani yake alizaliwa Kiumbe bora kuliko viumbe wote, kiumbe ambae ni mwenye
jukumu la kuitoa Dunia kutoka kwenye kiza cha ujinga wa kutomjua Mola wao na
kuiingiza kwenye Nuru ya Dini ya Kiislam.
Siku kadhaa baada ya kufungwa Ndoa hii, basi Abdullah akakutana tena njiani na yule
mwanamke aiwate Ruqqiyah ambae alimtaka Abdullah, lakini cha kushangaza ni kua
safari hii Ruqqiyah hakua ni mwenye kumjali wala kumpapatikia Abdullah, hali hii
ilimshanganza sana Abdulla na hvyo akamuuliza Ruqqiya: ‘Imekuaje? Umepona ile
hali yako uliyokua nayo hapo kabla baada ya kuniona au?’
Ruqqiyah akajibu: ‘Naam katika siku zile uliua na Nuru kubwa sana Ambayo ilikua
imetapakaa kwenye paji lako la uso, na hivyo ilinichanganya sana kwa uzuri wake,
na uzuri wa muonekano wako, lakini sasa hivi ile Nuru siioni tena, imetoweka sijui
imeenda wapi’.
581
Kwani ni kweli Ruqqiya alikua haioni tena ile Nuru iliyokua kwenye paji la uso la
Abdullah kwa sababu Nuru ili ilikua tayari imeshahama kutoka kwa Abdullah na
kuhamia kwa Amin Bint Wahb ambae ndie aliembeba Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam ndani ya Tumbo lake la Uzazi.
Ambapo anasema Baraka kua: ‘Wiki mbili baada ya Abdullah Ibn Abd Al Muttalib
na Amina Bint Wahb kuoana basi jioni Moja alikuja Abd Al Muttalib na
kumtaarifu Abdullah kua ajitayarishe na Msafara wa Kibiashara unaoelekea
katika Ardhi ya Sham’
Taarifa hii ilimhuzunisha sana Amina kiasi ya kua alikua akilia huku akisema: ‘Itakuaje,
Itakuaje Mume wangu ndio kwanza tumeoana halafua anafunga safari kuelekea
Sham wakati mimi hata hina yangu ya harusi haijafutika kwenye Mikono yangu?’
Hivyo wakati ulipowadia wa Masafara wa Sham kuondoka basi Amina Bint Wahb
alianguka chini na kuzimia, kutokana na kua hali ya mapenzi ya kweli yaliyokuwepo
baina ya Abdullah Ibn Abd Mutallib na Amin Bint Wahb ambao ndio Baba na Mama wa
Nabii Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam.
Ambapo kwa upande mwengine basi Baraka anaendelea kusema kua: ‘Hakika mimi
nilipomuona Amina ameanguka chini na Kuzimia basi nililia kwa uchungu na
kusema: Masikini Sayyidati wangu’
Naam.. Baraka anaendelea kutuambia kua: ‘Niliposema Masikini Sayyidati wangu,
basi Amina akaufungua macho yake, akaniangalia huku machozi yakiwa
yanamtiririka na huku akijizuia kwa maumivi ya huzuni akasema: ‘Nipeleke
Kitandani Ewe Barakah’
Hivyo Amina akakaa Kitandani kwa mda Mrefu na kutokana na huzuni yake basi alikua
hazungumzi na mtu yeyote na wala hamuangalii mtu yeyote ambae anaekuja
kumtembelea na kumtizama hali yake isipokua Mzee Abd Ul Muttalib.
Kwani Barakah anaendelea kutuambia kua: ‘Miezi miwili baada ya Kuondoka
Abdullah, basi siku moja asubuhi Amina aliniita mimi na nilipomkaribia nikaona
kua uso wake Unang'ara kwa Nuru ya furaha kisha akaniambia:‘Ewe Barakah!
Hakika mimi usiku wa kuamkia Leo hii nimeona ndoto inayostaajabisha Sana’’
Baraka anasema: ‘Nami nikasema Itakua Ndoto inayobashiria wema Ewe Sayyidati
wangu.’
582
Baraka anaendelea kusema kua: ‘Amina akasema kua, Hakika mimi nimeona kwenye
Ndoto kua Kuna Nuru imetoka Tumboni mwangu na kisha Ikamurika na kutia
Nuru Milima yote na Mabonde yanayozunguka Mji wa Makka na nje yake’
Baraka anaendelea kusema kua: ‘Mimi nikamuuliza Amina: Jee hii inamaanisha kua
Unahisi kua una Uja uzito ewe Sayiddati Wangu?’
Hivyo Amina akajibu: ‘Naam, nna ujauzito ila sasa sihisi kama wanavyohisi
Wanawake wengine, kwani mimi nahisi kawaida tu’
Baraka akasema: ‘Ewe Sayyidati Wangu, Ama kwa Hakika Utapata Mtoto mwenye
Baraka kubwa sana na mwenye kuja na kila Jema na kheri ndani yake’
Kwani hii Ndoto ndio iliyokua ikibashiria kuzaliwa kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam, ambapo katika wakati huu wa kipindi chote hiki ambacho Abdullah Ibn Abd
ul Muttalib akiwa hayupo basi Amina Bint Wahb aliendelea kua na Huzuni kutokana na
kua mbali na Mumewe kipenzi.
KIFO CHA ABDULLAH NA KUZALIWA KWA RASUL ALLAH
SALALLAHU ALAYHI WA SALAM.
Hata hivyo ujauzito huo haukumtia wasiwasi wala kumletea matatizo yoyote, kwani mara
kwa mara ilikua usiku akilala usingizini humuona mtu anakuja na kumpa habari njema
za kile kilichokuwemo ndani ya tumbo lake la uzazi. Mara moja alipokua amelala
usingizini mtu huyo alimwambia ‘Una ujauzito wa kiongozi na Nabii wa Ummah
huu’, na karibu ya kujifungua akamwambia tena ‘Sema baada ya kujifungua sema ‘Ya
Allah, mlinde mtoto huyu kutokana na ubaya wa kila chenye ubaya’, halafu mpe
jina la Muhammad’.
Hivyo jukumu la kumliwaza na kumuondolea Mawazo hayo ya Kumfikiria na
Kumkumbuka Mumewe halikua chini ya usimamizi wa mtu yeyote yule lilikua chini ya
Baraka kwani Barakah ndie aliekua mtu wa karibu nae sana na hivyo alikua akijaribu
kumzungumzisha na kumchangamsha Aminah bint Wahb.
Jambo lilimsaidia Aminah katika wakati wa Mchana lakini kila inapoingia wakati wa
Usiku na kulala basi Aminah alikua akiweweseka Usingizini huku akitaja jina na
Mumewe kama anavyosema Barakah: ‘Katika kipindi hiki mimi nilikua nalala chini
ya Miguu yake Sayyidat wangu, na nilikua nikimsikia Usiku akinung’unika na
kuweweseka huku akilitaja jina la Mumewe ambae alikua hayupo, Kilio chake na
Kuweweseka kwake kulikua kunaniamsha Usiku na hivyo kunifanya niwe ni
583
mwenye kujaribu kumliwaza na kumtuliza na kumpa nguvu kutokana na hali
aliyokua nayo.’
Kwani katika kipindi hiki ndio Jeshi la Tembo la Abraham ambae aliekua Mfalme wa
Yemen alipoamua kuenda katika Mji wa Makkah kwa ajili ya Kulivunja Al Kaabah. Hii
ilikua mnamo mwaka huo huo wa 570, katika ardhi ya nchi ya Yemen iliyokua iko chini
ya utawala wa Mfalme wa Kikristo wa Abisinia (Ethiopia), mfalme huyu alikua na
Gavana wake anaesimamia eneo la Yemen ambae alikua anajulikana kwa jina la Abraha
Al Ashrah.
Abraha aliamua kuenda katika mji wa Makkah na jeshi la watu 60,000 pamoja na Tembo
13 ili kuivunja Nyumba tukufu ya Al Kaa’bah baada ya kujenga katika mji wake kanisa
refu na zuri kwa ajili ya kuwavuta zaid watu waliopo karibu na eneo analolitawala ili
waache kuenda Makkah katika Nyumba tukufu ya Al Ka’abah na badala yake waende
kuabudu katika Kanisa hilo, lakini hata hivyo watu wa Yemen walikataa kufanya hivyo
kwani woao taari wameshazoea kufanya Ibada ya Hija katika Mji wa Makkah, na badala
yake wakasubiri usiku kisha wakalitia Moto Kanisa hilo, hivyo akaona hakuna njia
nyengie isipokua kulibomoa Al Ka’abah.
Abrahah alipofika katika viunga vya mji wa Makkah, akapiga kambi na kisha akatuma
jeshi lake liende kuteka mali zote zilizokuwemo katika mji huo, na miongoni mwa mali
zilizotekwa walikuwemo Ngamia 200 wa Abd Ul Muttalib ambae ndie aliekua kiongozi
wa mji wa Makkah. Halafu akatuma wajumbe wenye ujumbe usemao kua hawakuja
kupigana vita bali wamekuja kwa nia ya kuibomoa nyumba ya Al Ka’abah, hivyo ikiwa
watu wa Makkah watamuachia aibomoe nyumba hiyo basi, itakua hakuna matatizo
ataibomoa halafu ataenda zake na jeshi lake, lakini ikiwa hawatomuachia kutimza nia
yake hio basi wajitayarishe na vita, na majibu ya ujumbe huo inabidi yatolewe na
kiongozi wa mji huo mbele ya Abraha tena kwa mdomo wake, hivyo ikabidi Abd ul
Muttalib aongozane na mjumbe huyo hadi kwa Abraha, kutoa jibu.
Na mara Mjumbe alipofika basi Abd ul Muttalib akamwambia mjumbe wa Abraha: ‘Sisi
hatuna nguvu wala uwezo wa kupigana na Abraha, na hii ni nyumba ya Allah, hivyo
kama Allah akitaka basi ataiepusha na msiba nyumba yake’ yule mjumbe
akamwambia Abd ul Muttalib kua itabidi amchukue ampeleke kwa Abraha ili ampe
mwenyewe ujumbe huo, hivyo wakaongozana hadi kwa Abraha, walipofika Abraha
akamuuliza Abd ul Muttalib ‘Unasemaje?’, Abd ul Muttalib akajibu ‘Nilikua nataka
unirudishie Ngamia wangu’
Abraha akacheka na kumwambia Abd ul Muttalib ‘Nilipokuona nilivutiwa nawe na
kukuheshimu, na nnajua namna watu mbali mbali wanavyokuheshimu lakini jibu
lako limekushusha hadhi mbele ya macho yangu: Yaani wewe unajali Ngamia wako
584
tu? Lakini husemi chochote kuhusiana na nyumba yenu tukufu ambayo
mnayoitukuza tangu enzi za mababu zenu?’.
Abd ul Muttalib akajibu ‘Mimi ni mmiliki wa hao Ngamia tu, hivyo nakuomba
unirudishie Ngamia wangu, ama kuhusiana na nyumba takatifu, basi nayo pia ina
mmiliki wake: Hivyo mmiliki wake atailinda yeye mwenyewe nyumba yake’.
Abd ul Muttalib akapewa Ngamia wake, na alipofika kwa watu wake akawaambia watu
wake waondoke wakakae mbali ili wasije wakaangamizwa au kudhuriwa na watu wa
Abraha mara tu baada ya Abraha kuivamia Al Ka’abah, na kisha akaenda katika Al
Ka’abah, na kusema ‘Ya Allah, mtu huilinda nyumba yake, hivyo nawe ilinde
nyumba yako, usiiwachie misalaba yao na ujuzi wao kuuzidi ujuzi wako, na ikiwa
unataka kuwaachia kufanya wanavyotaka basi ni hiari yako kuwaachia wafanye
watakavyo’, na kisha baada ya hapo akawachukua watu wake na kutoka nje ya mji wa
Makkah.
Tukio hilo liliwashtua wengi sana akiwemo Amina Bint Wahb ambae alikua na uja Uzito
wa Miezi kadhaa lakini Amina Bint Wahb akamwambia Abd Al Muttalib kua kwa hali
aliyokua nayo basi haina haja kwake yeye kutoka kwenye Mji huo kwani ana uhakika
kua Abrahah hatoweza kulivunja Al Kaabah kutokana na kua ni lenye kulindwa na Allah.
Ambapo kama alivyokua akihisi Aminah Bint Wahb ambae ndani ya tumbo lake alikua
amembeba Kiumbe Mtukufu ambae ni Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam kua
Abraha hatofanikiwa kuingia katika Mji wa Makkah kutokana na Uangalizi wa Allah juu
ya Ardhi hio kutokana na utukufu wake, basi Jeshi la Abraha halikufanikiwa kuingia
kwenye ardhi hio.
Kwani Siku ya pili asubuhi Abraha na jeshi lake, wakajitayarisha kuelekea katika Al
Ka’abah lakini Tembo wao mkubwa ambae alikua akifuatwa na tembo wengine kila
akielekezwa kuelekea upande wa Al Ka’abah basi hugoma kuelekea huko, lakini
wakimgeuzia upande mwengine basi huelekea upande huo na kutaka kuondoka, hivyo
watu wa Abraha nao wakawa kila akianza kuondoka basi haraka humgeuzia upande wa
Al Ka’abah na hapo Tembo huyo kukaa chini na hugoma kabisa kunyanyuka badala yake.
Tembo huyo alipigwa na kufanywa kila kitu ili anyanyuke aelekee upande wa Al Ka’abah
lakini wapi.
Na mara ghafla likatokea kundi kubwa la ndege weusi ambao midomoni mwao na
kwenye kucha zao walikua wamechukua kokoto, na hapo ikaanza kunyesha mvua ya
kokoto, kokoto hizo hazikua kokoto za kawaida bali zilikua ni kokoto za mawe ya motoni
(Sijjil), na kila ndege alikua amekuja maalum kwa ajili ya mtu wake, ikawa hakuna kwa
kukimbilia wala kwa kujificha na kila mtu anaeguswa na kokoto hiyo, basi huanza
585
kumomonyoka sehemu mbali mbali za mwili wake, kwa kuanza kuachia kwa ngozi yake
na nyama huanguka na damu kuanza kumwagika kama vile inavyomwagika chem chem
ya maji, hii ni hali ambayo liendelaea hadi jeshi la Abraha likaangamia lote na kua kama
‘a`Asf, Ma'aakul’ yaani chakula kilichotafunwa tafunwa na kisha kikatemwa. Allah
Subhanahu wa Ta’ala anatuhadithia kisa hiki katika Qur’an kwa kusema:
﴿أَلمَْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَب ُّكَ أبَِصْحَبِ
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ
﴾
ٱلْفِيلِ ۞أَلمَْ يجَْعَلْ َكيْدَهُمْ فىِ تَضْلِيلٍ ۞ وَأَرْسَل
َ
عَلَيْهِ مْ طَيرْ اً أَابَ بِيلَ۞تَرْمِيهِم بحِِجَارَةٍ مِّن سِ جِّ يلٍ ۞فَ َجعَلَهُمْ كَ عَصْ فٍ م َّأْكُولِ ﴾
Bismillahi Rahmani Rahim.
Alam tara kayfa faAAala rabbuka bi-as-habi alfeeli; Alam yajAAal kaydahum fee
tadhleelin; Waarsala AAalayhim tayran ababeela; Tarmeehim bihijaratin min
sijjeelin; FajaAAalahum kaAAasfin ma/koolin (Surat Al Fil 105:1-5)
Tafsir: Jee umeona namna gani Mola wako alivyowafanyia watu wa Tembo, Jee
hakuwafanyia mipango yao kua ni yenye kudhalilika, Na akawashushia dhidi yao
ndege kwa makundi (Ababil). Kuwapiga kwa mawe ya Sijjil, na akawafanya kua kama
(`Asf, Ma'kul).
Kutokana na kisa hiki, Waarabu wakawa wanauita mwaka huu wa 570 kua ni A’m al Fil
yaani Mwaka wa Tembo. Mwaka ambao Allah Subhanahu wa Ta’ala aliiokoa Al
Ka’abah kutokana na madhara ya watu wenye jeshi la Tembo na pia akawaokoa watu wa
ukoo wa Quraysh kutokana na madhara ya Watu wa Tembo ambao walikua na nia ya
kuliangamiza Al Ka’abah.
Hivyo baada ya tukio hilo la kuangamizwa kwa Jeshi la Abraha na Tembo wake, basi
haukuchukua mda mrefu isipokua Msafara wa kwanza kutoka Sham uliwasili katika Mji
wa Makkah. Na Barakah alipopata habari tu ya kuwasili kwa Msafara huo basi haraka
sana akakimbilia katika Nyumba ya Mzee Abd Al Muttalib ili kupata habari za Bwana
wake yaani Abdullah kwa ajili ya kumpelekea Sayyidati wake yaani Aminah.
Lakini kwa siku hio hakupata habari yeyote hivyo akarudi kimya kimya kwa Amina Bint
Wahb bila ya kumwambia chochote kutokana na kuogopa kumzidishia Machungu
Sayyidati wake.
586
Lakini baadae Barakah akaenda tena kwa Abd Al Muttalib na hapa sasa ndio akapata
habari kua Abdullah amefariki njiani. Ambapo anasema Barakah kua: ‘Nilipopata
habari hio, Nilipiga Ukelele na kisha sijui kilitokea nini kwani Nilikimbia kwa kasi
sana hadi kwa Aminah huku nikilia, na Kupiga Makelele kua alieenda Safarini,
anaesubiriwa kwa Hamu hatorudi tena’
‘Amina aliposikia habari hizo nzito basi alizimia tena nami nikawa ni mwenye
kukaa nae ubavuni mwa kitanda chake huku akiwa katika hali ya Nusu hai nusu
mfu hakukua na Mtu yeyote ndani ya Nyumba ya Amina isipokua mimi.’
‘Hivyo nilikaa nae Usiku na mchana na Kumuuguza mpaka alipojifungua Mtoto
wake ambae ni Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam katika Usiku ambao Mbingu
zilikua zinameremeta kwa Nuru ya Allah na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alipozaliwa basi mtu wa mwanzo kumbeba Mikononi mwake alikua ni Mimi’
(Barakah).
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala analitaja tukio hili la kuja kwa Rasul Alah Salallahu
Alayi wa Salam kwenye Qur’an pale aliposema:
﴿َ أَهْلَ ٱلْكِتَابِ قَدْ جَآءَكُمْ رَسُولُنَا يُبَينِّ ُ لَكُمْ كَثِيراً ممِّ َّا كُنْتُمْ تخُْفُونَ مِنَ ٱلْ كِتَابِ
وَيَعْفُواْ عَن كَثِيرٍ قَدْ جَآءَكُمْ مِّنَ ٱهلل َِّ نُورٌ وَكِتَابٌ م ُّبِينٌ۞يَْهدِى بِهِ ٱهلل َُّ مَنِ ٱت َّبَ َع
رِضْوَانَهُ سُبُلَ ٱلس َّلاَمِ وَيخُْرِجُهُمْ مِّنَ ٱلظ ُّلُمَاتِ إِلىَ ٱلن ُّورِ إبِِذْنِهِ وَيَهْدِيهِمْ إِلىَٰ صِرَاطٍ
م ُّسْتَقِيمٍ ﴾
Ya ahla alkitabi qad jaakum rasooluna yubayyinu lakum katheeran mimma
kuntum tukhfoona mina alkitabi wayaAAfoo AAan katheerin qad jaakum mina
Allahi noorun wakitabun mubeenun; Yahdee bihi Allahu mani ittabaAAa
ridwanahu subula alssalami wayukhrijuhum mina aldhdhulumati ila alnnoori biidhnihi
wayahdeehim ila siratin mustaqeemin (Surat Al Maidah 5:15-16)
Tafsir: Enyi watu wa Ahl Al Kitab amekujieni Mtume mwenye kubainisha juu yenu
mengi mliyokua mkiyaficha katika Kitabu ijapokua hayatilii maanani mengi sana
(mliyoyaficha) kwa hakika Imekujieni kwenu Nuru na kitabu chenye Mabainisho.
Ambavyo anawaongozea Allah wale wakataofuata njia yake ya usalama, na kuwatoa
kutoka kwenye kiza kuwaingiza kwenye Nuru kwa idhini yake na kuwaongoza katika
njia iliyonyooka.
587
Ambapo aya hizi zinawazungumzia Mayahudi waliokua ni wenye kujaribu kuuficha
ukweli kuhusiana na yaliyoandikwa kwenye vitabu vyao juu ya ukweli wa vithibitisho
vya kuja kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambapo ndani yake aya hizi pia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amewakilishwa na kunasibishwa na Nuru ya
Uongofu wa kuwatoa watu kwenye kiza cha kutofuata njia sahih ya kimaumbile
tuliyumbiwa Ibn Adam na kuwarudisha kwenye njia sahih iliyonyooka.
Hivyo baada ya tukio hili la kuzaliwa kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
lilitokea kwenye Nyumba ya Abu Talib katika mwezi 12 Rabi Al Awwal ya mwaka wa
Tembo, ambapo ni sawa na tarehe 8-6-570, na mkunga wake aliemzalisha alikua ni
Ashifa Bint Awf ambae ni mama yake Abd Rahman Ibn Awf, baada ya kuzaliwa kwake
akaitwa Babu yake yaani Abd ul Muttalib akamchukua na kumpa jina alilobashiriwa
Aminah Bint Whab yaani Muhammad.
Baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuzaliwa basi alinyonyeshwa kidogo
na Mama yake halafu akachukuliwa na kupelekwa kwa Bi Thuwayba ambae ndie aliekua
Mnyonyeshaji wake na mlezi wake wa pili baada ya Baraka ambae yeye kwa wakati huu
alikua ni mwenye kubakia na mzazi yaani Amina Bint Wahb.
THUWAYBAH AL ASLAMIYAH MAMA MNYONYESHAJI WA PILI
WA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM
Ni kawaida kwa desturi za Waarabu kua inapopatikana habari njema au nzuri basi watu
hua ni wenye kuonesha Ukarimu na Shukuran, hivyo katika siku aliyozaliwa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam basi Thuwaybah ambae alikua ni Mtumwa wa Ami yake
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae aliekua akiitwa Abd Al Uzza Ibn Abd Ul
Muttalib maarufu kama Abu Lahab ambae alikua pia na mtoto wake aitwae Masruh
ambae ndie aliekua akimnyonyesha, hivyo Thuwaybah alipopata habari ya kuzaliwa kwa
Rasul Allah Salal Alayhi wa Salam basi alikimbilia kwa Bwana wake na kumpa habari
hio kwa kusema: ‘Hivi Jee umesika kua, Aminah amejifungua Mtoto wa kiume?
Kwa Ajili ya ndugu yako Abdullah?’
Hivyo baada ya kupokea habari hio basi Abu Lahab kutokana na furaha yake basi
akasema kumwambia Thuwaybah kua: ‘Nenda kwani kwa hakika nimekuachia Huru’
na hivyo baada ya hapo Thuwaybah akamnyonyesha kwa muda Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam.
Ambapo Thuwaybah alikua pia ni mwenye kumnyonyesha Abu Salamah Ibn Abd Al
Asad Radhi Allahu Anhu na pia alimnyonyesha Hamza Ibn Abd Ul Muttalib Radhi Allahu
588
Anhu ambae ni Ami yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo pia nae akawa
ni Ndugu yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa upande wa Unyonyweshaji.
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Imam Abu Fadhl Ibn Hajjar Al Asqalani kua:
‘Thuwaybah ambae ni Mtumwa alieachiwa huru na Abu Lahab na ametajwa na
Ibn Mandah kua ni miongoni mwa Masahaba, lakini kuna tofauti baina ya
mitizamo, kuhusiana na kama alikua Ni Muislam ama la. Kwani Abu Nuaym
Amesema kua: ‘Hatujui sisi kua kama alisilimu na kua ni Muislam ama la, bali kile
kinachosemwa kwenye Vitabu vya Historia ya Kiislam ni kua Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alikua akimheshimu na akimtembelea baada ya kumuoa Bi
Khadija, na alikua akimtumia zawadi kutoka katika Mji wa Madinah na baada ya
kutekwa kwa Mji wa Khaybar basi alifariki Dunia na kama alivyofariki mtoto wake
Masruh.’’
Ambapo maana ya maneno yasemayo kua Abu Lahab alimuacha huru na
akamnyonyesha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam yanamaanisha kua
alimuachia huru kabla ya kumnyonyesha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam,
lakini kile kilichoandikwa kwenye Vitabu vya historia vinaonesha kua hali ni
kinyume chake, ambacho ni kua Abu Lahab alimuachia huru kabla ya Hijra
ambalo hili ni tukio lililotokea mda mrefu baada ya kumnyonyesha Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam, na As Suhayl amesema kua Kuachiwa huru kwake
kulitokea kabla ya kumnyonyeha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambapo
maneno ya As Suhayl yanasema kua:
‘Al Abbas amesema kua, Wakati Abu Lahab alipofariki, basi mimi nilimuona
kwenye ndoto mwaka mmoja baadae hukua kaiwa na hali mbaya kabisa, nae
akasema: ‘Hakika mimi sijapata utulivu kutokana na Adhabu ambayo hua haisiti
isipokua katika siku ya Jumatatu.’ Na hii ni kwa sababu Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alizaliwa siku ya Jumatatu na Thuwaybah alimpelekea habari hizo
Abu Lahab ambae nao akamuachia huru Thuwaybah’’
Hata hivyo hapa inabidi tujue kua kwa Upande wa Shaykh Ul Islami Al Hafidh Imam
Ahmad Ibn Muhammad Al Qastallani, yeye anasema kuhusiana na riwaya hii kua:
‘Kuhusiana na Kauli hii kua kama inaweza kutumika kama uthibitisho wa kua Mtu
asiekua Muislam anaweza akawa ni mwenye kulipwa wema wake baada ya kufariki
kwake, basi kama ingekua hakuna muunganishi anaejulikana katika hadithi hii,
basi hii ingekua haina nguvu kuhusiana na hukumu iliyopo kuhusiana na kulipwa
kwa wasiokua Waislam baada ya kufariki kwao, ila hadith hii, ina muunganiko
mzuri na inakubalika.
589
Lakini hata hivyo, Ndoto hua haiwezi kutumika kua kama uthibitisho wa
kubadilisha maana au kuathiri hukumu ya kisharia hususan pale inapokua
inapingana na Qur’an kama inavyoonesha katika hadithi hii, na hivyo inawezekana
ikawa adhabu iliondolewa kwa Abu Lahab peke yake kutokana na tukio la
kumuchia huru Thuwaybah katika siku aliyozaliwa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam’(Imam Al-Zurqani, Sharh Mawahib Laduniya)
Mujaddid Ad Din Imam Abu Fadhl Ibn Hajjar Al Asqalani basi yeye anasema kua:
‘Hakika haya yaliyotokea yametokea kutokana na Rehma za Allah kutoka na
Ukubwa wake na Uwezo wake juu ya wale wasiomuamini kutokana na Ukarimu
wao kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, w Aallahu Aalam.’(Fat-h Al Barr)
Hivyo basi Thuwayba alimnyonyesha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kua
mlezi wake kwa mda wa wiki moja, hadi pale katika Mji wa Makkah alipowasili
Mwanamke wa Banu Bakr aitwae Halimah Bint Abi Dhuab Abdullah Ibn Al-Harith Ibn
Shaghna Ibn Jabir Ibn Razam Ibn Nasera Ibn Fasiya Ibn Nasr Ibn Sa’ad Ibn Bakr Ibn
Hawazin Ibn Mansour Ibn Ikramah Ibn Khasfah Ibn Qays Ibn ‘Ilan marufu kama
Halimah Al Saadiah.
HALIMA BINT ABU DHUAYB AL SADIYA MAMA
ALIEMNYONYESHA WA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA
SALAM
Hali ya hewa ya Mji wa Makkah ilikua ni ya Joto sana na yenye nyevu nyevu, hivyo
ilikua si hali ya hewa yenye mandhari mazuri kwa afya ya ukuaji wa Watoto. Ambapo
hali ilikua tofauti katika maeneo ya Jangwani kwani kulikua na mazingira ya Utulivu,
urahisi wa Maisha na pia usafi wa kimazingira, na watu waishio Majangwani nje ya Miji
hua na Utamaduni mzuri Lugha asilia na tabia njema zaidi kuliko watu wa Mjini.
Hivyo hali hii ya utofauti wa kimazingira uliwapelekea watu wa Mji wa Makkah wenye
uwezo wa kimaisha na Darja kua ni wenye kuwatafutia watoto wao wanyonyeshaji wa
maalum wan je ya Mji ambako hua ni wenye kukaa na watoto wao hao hadi kipindi cha
kumaliza kunyonya cha miaka miwili au zaid na hivyo watoto hao hua na afya njema
zaidi na miili imara zaidi kutokana na maziwa yenye afya zaidi ya wanyonyeshaji hao.
Miongoni mwa wanawake wa Makabila ya watu wa Jangwani wanaosifika kwa umaarufu
wa kazi kama hizo za kunyonyesha Watoto walikua ni Wanawake wa Kabila la Said Ibn
Bakr ambao walikua wanaishi upande wa kaskazini nje ya Mji wa Makkah, kwani hawa
walikua ni watu ambao ni wenye kuheshimika sana kutokana na Utamaduni wao, Tabia
590
zao, Lugha yao, Unyenyekevu wao na Ukarimu wao, na hivyo wengi miongoni mwa
Watu wenye Darja wa Mji wa Makkah walikua wakipenda kuwakabidhi watoto wao kwa
Wanawake wa Bani Bakr.
Ambapo katika mwaka aliozaliwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi kulikua
na ukame mkubwa sana katika maeneo ya ardhi waliyokua wakiishi wa wa Kabila la
Banu Bakr nje ya Mji wa Makkah. Hivyo wanawake wa Kabila hilo wakaamua kua
hakuna njia ya kujirahisishia kupata kipato cha kuongeza riziki zao isipokua kuelekea
katika Mji wa Makkah kwa ajili ya kutafuta Watoto wa Kunyonyesha na hivyo kua ni
wenye kujipatia kipato kwa ajili ya riziki yao.
Miongoni mwa wanawake hao alikuwemo pia Mwanamke mmoja ambae alikua akiitwa
Halima Bint Abu Dhuayb na alikua ameenda katika Mji wa Makkah akiwa amefuatana
na Mumewe ambae alikua akijulikana kwa jina la Harith, na walikua na Mtoto mchanga
wa kiume aitwae Abdullah na walipowasili katika Mji wa Makkah basi walikua
wamechelewa kwa sababu usafiri wa Halima aliopanda ulikua ni wa Punda ambae nae
alikua ni dhaifu na mwenye kutembea taratibu.
Na kutokana na utaratibu huo wa Punda wake Halima basi wlpofika katika Mji wa
Makkah basi wakakuta kua Watoto wote wenye wazee wameshachukuliwa na
wanyonyeshaj na hivyo wakashindwa kupata Mtoto wa kunyonyesha, lakini kwa bahati
nzuri wakaambiwa kua kwa Mzee Abd Ul Muttalib kuna Mtoto mmoja ambae alikua ni
Yatima ambae Wanawake wengine wa Banu Bakr walikataa kumchukua kwa sababu ya
Uyatima wake.
Hivyo Halima alipofika kwa Abd Ul Muttalib basi akajitambulisha kwa kusema kua yeye
ni mwanamke wa Banu Bakr anaeitwa Halimah. Na hapo Abdu Ul Muttalib akamwambia
Halima kua: ‘Ewe Halima hakika mimi nina Mtoto ambae ni Yatima,
nilimpendekeza kwa Wanawake wengine wa Banu Bakr lakini wamemkataa, hivyo
nakuomba kua Mnyonyoshaji wake Mtoto huyu na hivyo huenda akakuongezea
mali na bahati katika Maisha yako kutokana na kumlea kwako.’
Hivyo kwa kua Halima hakutaka kurudi Nyumbani mikono mitupu basi akakubaliana na
rai hio ya Abd Ul Muttalib, lakini kwanza ikambidi akubaliane na mumewe juu ya
maamuzi hayo, ambapo nae akakubaliana na mtizamo huo wa Mkewe, na kisha Halima
akarudi kwa Abd Ul Muttalib kumwambia kua amekubaliana na makubaliano ya kumlea
mtoto huyo na kisha wakaelekea nyumbani kwa Abd Ul Muttalib kwa ajili ya kumchukua
Mtoto huyo.
Hivyo Abd Ul Muttalib akamchukua Halima na kuenda nae hadi kwenye Nyumba ya
Aminah Bint Wahb na alipoingia ndani akapelekwa Moja kwa Moja hadi kwenye
Kitanda cha Mtoto huyo anaetegemewa kua ni mwenye kumlea yaani Rasul Allah
591
Salallahu Alayhi wa Salam, ambapo macho ya Halima yalipomuona Mtoto huyo na uzuri
wake na nuru inayoakisi kwenye paji lake la uso, akiwa amekumbatiwa na kitambaa cha
sufi cha rangi nyeupe na blanketi la kijani huku akitoa harufu nzuri iliyohanikiza chumba
kizima, basi hapo hapo Halima alijawa na tabasamu kubwa sana lililokua likidhihirisha
mapenzi makubwa ya ghafla yaliyotokea na kuzizamisha hisia za mapenzi yake yote ya
mwili wake kwenye kina cha Moyo wake kwa ajili ya mtoto huyo alielala usingizi mbele
yake.
Halima Bint Abu Dhuayb akashindwa kujizuia na kujidhibiti mwili na ufaham wake na
hivyo taratibu akajikuta akiwa anainama na kumchukua Mtoto huyo kutoa ndani ya
Kitanda chake na kumuingiza ndani ya mikono yake huku akiwa amejawa na mapenzi
na huruma kubwa sana, akamsogeza Mtoto huyo kifuani mwake na kisha akainamisha
uso wake na kumbusu kwenye paji la uso wake huku ukiwa umejaa furaha Moyo wake,
na hapo hapo Mtoto huyo akaamka na kuonesha uzuri wa macho yake kwa yule anaebusu
paji la uso wake.
Hivyo macho mazuri na matukufu ya M-bora wa viumbe Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam yakakutana na macho ya mlezi wake mpya ambae ni Halima Bint Abu Dhuayb
na hapo hapo yakafungamana pamoja maisha yao yenye kua na ahadi ya Miujiza, Rehma,
Neema na Baraka zisizotarajiwa ndani ya kipindi cha miaka 5 ijayo watakapokua pamoja.
MIUJIZA YA UTOTONI MWA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI
WA SALAM WAKATI AKIWA KWA HALIMA BINT ABU DHUAYB
Halima Bint Abu Dhuayb akajaribu kumnyonyesha Mtoto huyo mtukufu kwenye ziwa
lake la kulia ambalo hapo kabla ilikua halina maziwa mengi na ya kutosha, lakini mara
tu baada ya kulipachika ziwa hilo ndani ya Mdomo wa Rasul Aallah Salallahu Alayhi wa
Salam basi hapo hapo Halima akahisi hali ya mabadiliko katika Maziwa yake kwani
aliyahisi maziwa yake hayo yakiwa ni yenye kujaa Maziwa ambapo hii ilikua ni hali
ambayo hakuitegemea.
Halima akamnyonesha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hadi akashiba na kisha
akarudi kwa Mumewe na kumuelezea maajabu yaliyotokea, ambapo Harith mwenyewe
hakua ni mwenye kutegemea hali hio ya mabadiliko ya ghafla, hivyo akashangaa na
kujawa na furaha kwani inaonekana wamejaaliwa kupata Baraka kwa sababu hata mtoto
wao pia aliezaliwa karibuni aitwae Abdulla atapata Maziwa ya kutosha kutokana na tukio
hili, hivyo kuanzia siku hio Rasul Aallah Salallahu Alayhi wa Salam akawa
ananyonyeshwa Ziwa la kulia huku Abdulla akiwa ananyonyeshwa Ziwa la Kushoto la
Halima Bint Abu Dhuayb na hivyo tangu siku hio basi Abdullah Ibn Harith akawa ni
Ndugu yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam wa kunyonya.
592
Baada ya makubaliano hayo baina ya Abd Ul Muttalib na familia ya Halima Bint Abu
Dhuayb kuhusiana na ulezi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi Halimah na
mtoto mpya mwenye baraka alieingia kwenye familia yao aitwae Muhammad Ibn
Abdullah yaani Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam wakamuaga Abd Ul Muttalib na
Aminah Bint Wahb na kisha wakaanza safari yao ya kutoka nje ya Mji wa Makkah.
Safari ilikua ndefu lakini hikua ni ya uchovu, na hivyo ulipofika wakati wa Magharibi
basi wakapiga kambi katika sehemu tulivu na yenye usalama na kumpumzika kwenye
hali ya utulivu mkubwa usiokua wa kawaida katika usiku huo, kiasi ya kua walipomka
Asubuhi yake basi Harith alipoenda kuwakama Maziwa Ngamia wake akaona
mabadiliko yasiyokua ya kawaida katika chuchu zao, kwani chuchu zilikua zimejaa
Maziwa mengi sana, hivyo akamwita Halima na kumwambia: ‘Ewe Halima hivi jee
unajua kua umechukua Ulezi wa Mtoto Mtukufu na baraka kubwa sana?’
Hivyo Halima akajibu kwa kusema: ‘Naam..Wa Allahi hata na mie naona ni hivyo
hivyo.’ Na hii ni kwa sababu Halima aliona mabadliko ya Punda wake pia ambae hapo
awali alikua ni dhaifu, lakini katika safari hii ya kurudi kwao basi Punda huyo alikua ni
mwenye nguvu na mwenye kutembea kwa mwendo wa haraka zaidi, kiasi ya kua
walipoanza safari baada ya asubuhi hio basi Punda huyo wa Halima aliwapita Wanyama
wengine wote na hivyo kua ni muongozaji wa Msafara na walipokua wanatembea basi
Watu waliulizana hivi huyu Punda alikua ndio yule yule au ni mwengine?
Na waliposhindwa kujizua basi wakamuuliza Halima: ‘Ewe Bint Abu Dhuayb, hivi kwa
nini umekua na haraka hivyo? Au umebadilisha Punda mwengine hivyo huyu ni
tofauti na yule uliepanda mwanzo?’
Halima Bint Dhuayb akajibu: ‘La Wallahi huyu ni Punda yule yule, tofauti ni kua
amekua na maajabu kwani sio mimi ninae muongoza, yaani hata sifaham ni kitu
gani kinachoendelea kwenye ufahamu wa Punda huyu.’
Kwani hakuna aliekua akijua kua mabadiliko ya ajabu ya Punda huyo yanatokana na kua
Punda huyo ni mwenye kujua kiumbe mchanga aliembeba kua ni M-bora wa Viumbe
ambae ni kipenzi cha Allah Subhanah wa Ta’ala yaani Nabii Muhammad Salallahu
Alayhi wa Salam.
Na walipofika Safari yao katika ardhi yao basi ingawa walipoondoka hapo awali ilikua
kuna Ukame na visima vya maji vimekauka na hali ya mazingira ya Ardhi yao
haikubadilika haraka sana, kwani maji yalikua bado yamekauka visimani, majani ya miti
yamepungua lakini Wanyama wa Halima walikua wanashiba na kutoa maziwa kwa wingi
zaidi mbali ya kua walikua wanalishiwa sehemu moja ya malisho na wanyama wa watu
wengine.
593
Watu wakaanza kuulizana kwa nini katika Wanyama wa Halima Bint Dhuayb wakawa
ni walionenepa na kutoa mziwa mengi zaidi wakati wanyama wake na wanyama wengine
wote wanalishwa kwenye eneo moja ambayo hata hivyo bado hali ya ukame iko vile vile?
Hivyo wakaanza kulaumiana kua huenda ikawa ni kwa sababu kukataa kwao kumlea
Yatima anaelelewa na Halimah.
Walipomfuata Halima na mumewe kumuuliza imekuaje mpaka Wanyam wao wakawa
na hali tofauti na ya wa kwake wakati wote wanalishwa kwenye eneo moja basi Halima
akasema: ‘Wa Allahi jambo hii halihusiani na Wanyam wala sehemu wanayolishiwa,
bali hii inahusiana na siri kubwa ya Allah mwenyewe, kwani ila kitu kilianza
kubadilika baada ya sisi kuanza safari ya kurudi kutoka katika Mji wa Makkah’ na
bila ya shaka Halima na Harith walikua ni wenye kujua kua Miujiza hii yote inatokana
na huyu mtoto Yatima wanaemlea yaani Muhammad Ibn Abdullah Salallahu Alayhi wa
Salam, hivyo nao wakwa ni wenye kumpenda zaid ya wanavyompenda na kumhifadhi
Mtoto wao waliomzaa.
Baada ya hali kuzidi kua ngumu katika maeneo hayo kutokana na ukame basi watu wa
maeneo hayo wakaamua bora wakusanyike kwa ajili ya kufanya maombi ya mvua kwa
Mungu wao. Hivyo wakakusanyika katika siku maalum katika eneo maalum kwa ajili ya
kufanya maombi hayo, na ingawa walikusanyika watu wote lakini kwa upande wa
Halima yeye hakutaka kuenda kwa sababu ya kua ni mwenye kutotaka kumuingiza juani
mtoto wake huyo anaemlea, kwani kwake yeye mtoto huyo ni Lulu ya jicho lake, hataki
hata kumtoa ndani mwake kutokana na baraka iliyojaa ndani yake wacha mbali
kumhangaisha kwa kumpeleka Milimani kupigwa na jua.
Hivyo baad ya majaribo kadhaa ya kuomba dua ya mvua bila ya mafanikio basi watu hao
wakakumbuka kua Halima ana Mtoto mwenye kua na baraka na Miujiza, hivyo
wakajadiliana kua wamuombe Halima aende nae Mtoto huyo kwenye Maombi yao hayo,
ambapo ingawa mwanzo Halima alikataa lakini mwisho ikambidi akubali kwa ajili ya
kuwasaida majirani zake, hivyo siku hio akamfunga funga vizuri Mtoto huyo kabla ya
kutoka nae kwa ajili ya kuelekea kwenye sehemu ya Maombi hayo ili asidhurike na Jua
kali linapiga ardhini.
Lakini cha kushangaza ni kuwa mara tu alipotoka nae kuelekea kwenye sehemu ya
maombi basi akajikuta kua kama mtu anaetembea chini ya mti mkubwa, na alipoangalia
juu basi akaona kua kuna Mawingu ambayo yalikua yakimfuata kwa juu yake na hivyo
kua ni yenye kumfayia kivuli yeye na Mtoto wake huyo. Halima akajawa na furaha ndani
ya Moyo wake kwani alikua akijua kua jambo alilolifanya la kutoka nae Mtoto huyo
kuenda nae kwenye maombi hayo na Miujiza yake basi bila ya shaka watu wake
watajibiwa maombi yao.
594
Na bila ya shaka baada ya kufika nae Mtoto huyo kwenye eneo husika basi na kuanza
kufanya maombi yao basi haikuchukua hata dakika isipokua walianza kuona kiwingu
kikubwa cha Mvua huku rasha rasha za mvua hio ikianza kuanguka anguka katika eneo
la ardhi yao, tukio ambalo liliwafanya watu hao kua ni wenye kuanza kushangiria na
kufurahia matokeo ya kukubaliwa kwa Maombi yao kutokana na utukufu wa Mtoto alie
Yatima anaelelewa na Halima ndani ya jamii yao miongoni mwao, na wakathibtisha kua
Mtoto huyo ni mwenye Barka na Miujiza, na wakaanza kumpenda sana na kufurahia kua
ni Mtoto Mtukufu kwenye Jamii yao.
Kutokana na Mvua hio basi hali ya mazingira ikaanza kubadilika katika maeneo ya Ardhi
yao, kwani ardhi iliyokua imekufa basi ikaanza kua ni yenye kuota majani na mimea
ikachipua na Wanyama wakawa ni wenye kushiba na kunawiri na kutoa maziwa yenye
kutosha na haop hapo kuanza kua ni wenye kuongezeka.
Ambapo kwa upande wa Mtoto huyo yaani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi
hali yake nae ikaanza kubadilika kila mda unavyoenda kutokana na kua ni mwenye kukua
tofauti kimaumbile na watoto wengine, kwani alianza kuzungumza akiwa na umri wa
miezi minane na kua ni mwenye kujiweza na kua na ukakamavu wa mwili wake
alipotimia umri wa miezi 10, huku kiwa ni mwenye uzuri wa kipekee unaovutia kwa kila
anaemuangalia na mwenye adabu na heshima kwa kila mtu katika jamii yake.
Baada ya kutimia miaka miwili basi ukawadia mda wa watoto waliokua wakilelewa na
kunyonyeshwa na watu wa Banu Sad kua ni wenye kurudishwa kwao wazee wao katika
Mji wa Makkah, hiki kilikua ni kipindi cha huzuni kubwa kwa Halima na familia yake
pamoja na jamii nzima y watu wake, kwani kwa hakika yeye hakua tayari kumrudisha
mtoto huyo kwa Mama yake, na wala watu wa mji huo hawakua tayari kumrudisha mtoto
huyo kutokana na Utukufu wake na manufaa na baraka yake juu yao watu hao.
Lakini ikawa hakuna nia nyengine ya kufanya kwani ahadi ni kua baadaa ya kumaliza
kipindi cha kunyonya mtoto basi inabidi arudishwe kwa wazee wake. Hivyo Halima na
mume wake wakafunga safari pamoja na Mtoto wao Muhammad Salallahu Alayhi wa
Salam kwa ajili yakurudi katika Mji wa Makkah kumkabidhi mtoto huyo kwa Aminah
Bint Wahb ambae alikua akimsubiri kwa hamu kubwa sana Mtoto wake pekee ndani ya
Maisha yake aliempata kutoka kwa Mume wake aliempenda kwa dhati, lakini hata hivyo
Allah kwa Hikma zake hakuwajaalia kua ni wenye kuishi pamoja kwa mda mrefu kwa
kumchukua Abdullah Ibn Abd Ul Muttalib na kumtanguliza katika Ulimwengu wa
Barzah hata kabla ya kuzaliwa Mtoto wake.
Aminah Bint Wahb alifurahia sana kuonana tena na Mtoto wake huyo ambae kipindi hiki
alikua amekua mkubwa lakini sasa, tatizo ni kua ingawa Amina Bint Wahb alikua na
hamu sana ya kua na Mtoto kutokana na kua mbali nae kwa mda mrefu na pia kutokana
na kumpenda kwake, lakini hata hivyo kipindi hiki Mji wa Makkah ulikua umekumbwa
595
na Mtihani wa maradhi ya Maambukizo, hivyo Aminah Bint Wahb akawa anakhofia juu
ya Afya ya Mtoto wake atakaporudishwa katika kipindi hiki katika Mji wa Makkah na
hivyo hali hii ikawa ni kheri kwa upande wa Halima nae akamwambia Aminah Bint
Wahb: ‘Hivi jee utaniruhusu mimi kuendelea kubakia na Mtoto wangu huyu
Muhammad kwa mda mrefu zaid? Kwani hata mimi nnakhofia kuhusiana na
Mripuko wa Maradhi haya usije ukamuathiri.’
Wazo hili kutoka kwa Halima Bint Dhuayb lilikua ni kama alikua ni mwenye kuona
anayoyawaza na kuyafikiria Aminah Bint Wahb hivyo bila ya kusita akaona kua kwa kua
mitizamo yao inaendana sambamba katika kusimamia Maslahi ya usalam wa Afya ya
Mtoto Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam kutokana na mapenzi yao juu ya mtoto
huyo basi nae akaona kua bora kwa Muhammad kuendelea kubakia na Halima Bint Wahb
katika ardhi ya nje ya Mji wa Makkah kwa mda zaidi na Muhammad Salallahu Alayhi
wa Salam akawa ni mwenye kubakia na Halima Bint Dhuayb.
Baada ya kurudi katika ardhi ya Watu wa Banu Sad basi Mtoto Muhammad Salallahu
Alayhi wa Salam akaendelea kuishi na watu huku akiwa ni mwenye kua ni mwenye
maumbile ya Muono wa mbali, mwenye kutafakkari, mwenye kupenda kuangalia
Mbinguni kwani mwenye kujiuliza kuhusiana na Maumbile ya Mbingu yalivyo au
kujiuliza kuhusiana na kivuli kinachomfuata katika kutembea kwake katika wakati wa
jua kali na alipokua akichunga kondoo na wenzake basi alikua ni kama mwenye
kuzungumza na kufahamiana vizuri na Mifugo yake kutokana na Majaaliwa ya Allah
Subhanah wa Ta’ala juu yake ambapo yeye hana habari yeyote kuhusiana nayo juu yake,
ambayo ni kutayarishwa kwa ajili ya Neema ya Sharh Sadr.
INSHIRAH SADR YA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM.
Neno Sharaha hua linamaanisha Kufungua, Kukata, Kutanua, Kuweka wazi, Kufunua,
Kutandaza, Kufafanua, Kuelezea, Kurahisisha Kiuzito na Kiufaham.
Ambapo amesema Allah Subhanah wa Ta’ala katika aya zilizotumia neno hili kua:
﴿فَمَن يُرِدِ ٱهلل َُّ أَن يَهْدِيَهُ يَشْرَحْ صَدْرَهُ لِلإِسْلاَمِ وَمَن يُرِدْ أَن يُضِل َّهُ يجَْعَلْ صَ دْرَهُ
ضَيِّقاً حَرَجاً كَأَنم ََّا يَص َّع َّدُ فىِ ٱلس َّمَآءِ كَذٰ لِكَ يجَْعَلُ ٱهلل َُّ ٱلرِّجْسَ عَلَى ٱل َّذِينَ لاَ
يُؤْمِنُونَ ﴾
596
Faman yuridi Allahu an yahdiyahu yashrah sadrahu lil-islami waman yurid an
yudhillahu yajAAal sadrahu dhayyiqan harajan kaannama yassaAAAAadu fee
alssama-i kadhalika yajAAalu Allahu alrrijsa AAala alladheena la yu/minoona
(Surat Al AnAam 6:125)
Tafsir: Ama kwa yule ambae Allah hutaka kumuogoza basi humfungulia kifua chake
kwa ajili ya Uislam, na kwa yule ambae hutaka kumdhalilisha basi humfungia kifua
chake na kua ni chenye kubana kama kwamba ni mwenye kupanda juu kuelekea
Angani. Hivyo ndivyo Allah anavyotoa adhabu kwa wale ambao hawakuamini.
Anasema Imam Muhammad Ibn Jarir Al Tabari Al Shafii kuhusiana na aya hii kua Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliulizwa: ‘Jee Moyo hufunguka vipi kwa ajili ya
Uislam?’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu: ‘Ni Nuru ya Allah
Subhanah wa Ta’ala ndio inayoingizwa ndani ya Nyoyo za Ibn Adam, hivyo Moyo
hua ni wenye kutulia na kufunguka.’
Na ingawa aya imetumia neno Harajan ambalo hua ni lenye kumanisha: Kubana kwa
matawi ya mti kiasi ya kua sehemu ya matawi hayo yaliyobanana haiwezi kufikika
na mtu wala na mnyama, lakini kwa upande wa Sayyidna Umar Ibn Al Khattab Radhi
Allahu Anhu alipoambiwa juu ya maana hiyo na Mabedui ambao wao ni wataalamu
wakubwa wa lugha ya Kiarabu, basi Sayyidna Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu
akasema: ‘Huo hua ni Mfano wa Nyoyo za Wanafiq, kwani kamwe hakuna jema
linaloweza kuingia ndani ya Nyoyo zao.’
Na anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala ametofautisha baina ya Murid (Mja anaemtafuta Mola wake)
na Murad (Mja anaetafutwa na Mola wake) ijapokua Waja wawili hawa wote ni
kutoka kwake yeye mwenyewe Allah Subhanah wa Ta’ala. Lakini yeye Allah
Subhaah wa Ta’ala ni mwenye kutofautisha baina ya Khusus (Wenye sifa hususan
maalum) na Umum (Wenye sifa ya Ujumla) na hivyo kawatofautisha wale Murad
(wanaotafutwa na Allah Subhanah wa Ta’ala) katika ayah hii na nyenginezo’
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari anaendelea kutufafanulia kwa
kusema kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala hua ni mwenye kuziangalia Nyoyo, zote
kwani nyoyo hua ziko mbele yake, hivyo anapoona Moyo fulani una unyenyekevu
juu yake basi huujalia jema atakalo juu yake Moyo huo, Kisha baada ya hapo
hufuata Nyoyo zenye kubadilika haraka na kurudi kwake yeye Allah Subhanah wa
Ta’ala. Hizo ni aina mbili za Nyoyo anazozijaalia mema.’
Na kisha Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abd Allah Al Tustari akasema: ‘Kila wakati
Allah anapouangalia Moyo na akauona kua ni wenye kua na hamu ya Ulimwengu
huu, basi huuchukia Moyo huo na kuchukia kwake huko, hua kunajionesha kupitia
597
katika kuuwachia Moyo huo pamoja na Nafsi ya Mtu huyo. Kwani Moyo
haumilikiwi na yeyote isipokua Allah Subhanah wa Ta’ala, na hivyo hautakiwi
kumtii yeyote isipokua Allah Subhanah wa Ta’ala. Hivyo kama ukiwa unaujali
Moyo wako basi Mfanye Mola wako awe ndie msiri wako.’
Ambapo pia tunaona kua aya imetuma neno Yas’adu ambalo hua linamaanisha
Kuhangaika Kupanda Juu na hii ni kwa sababu Mtu unapopanda juu kuelekea Angani
basi hua unaukandamiza Moyo wako kutokana na kua ni wenye Kudidimizwa chini
kunakotokana na Nguvu ya Mvutano ya Gravity kunakotokana na Mwili wako kua ni
wenye kupingana na nguvu huo katika wakati wa kuenda Juu, na hivyo aya hii hua pia ni
uthibitisho wa Miujiza ya Qur’an kua ni kitabu cha mwenyewe Muumba alieumba kila
kitu.
Ambapo hisia za kubanwa kwa Moyo na Kifua kwa upande wa Kiimani basi hua ni zenye
kuachia pale Ibn Adam anaposikia na kumjua Mola wake na hii ni kutokana na kua Moyo
huo hua ni wenye kuingia ndani yake Nuru ya Allah Subhanah wa Ta’ala, na hivyo kifua
na Moyo huo hua ni wenye kutanuliwa na Mwenyewe Muumba kutokana na Nuru yake
hio na kumrahisishia Mja wake katika kukimbilia na kupata ukaribu na Mola wake.
Mfano mwengine wa matumizi ya neno hili ni pale lilipotumika katika kuelezea Uhiari
wa Mtu katika Kutaka kuutanua na Kuufungua Moyo wake kwa ajili ya kuingiza kiza
cha Kufru ndani yake, kutokana na matamanio yake kama pale ziliposema aya:
﴿مَن كَفَرَ بِٱهلل َِّ مِن بَعْدِ إيمَانِهِ إِلا َّ مَنْ أُكْرِهَ وَقَلْبُهُ مُطْمَئِن ٌّ بِ ٱلإِيمَانِ وَلَٰكِن م َّن
شَرَحَ ابِلْكُفْرِ صَدْراً فَعَلَيْهِمْ غَضَبٌ مِّنَ ٱهلل َِّ وَلهَُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴾
Man kafara biAllahi min baAAdi eemanihi illa man okriha waqalbuhu mutmainnun
bial-eemani walakin man sharaha bialkufri sadran faAAalayhim ghadhabun
mina Allahi walahum AAadhabun AAadheemun (Surat An Nahl 16:106)
Tafsir: Yeyote yule atakaemkufuru Allah baada ya kua ni mwenye Imani, isipokua yule
ambae amelazimishwa juu yake (kukufuru), huku Moyo wake ukiwa umetulia kwenye
Imani (ya kumuamini Allah Subhanah wa Ta’ala), lakini atakae ufungua Moyo wake
kwa Kufru basi ni juu yao Adhabu ya Allah na watapata Adhabu kubwa sana.
Ambapo katika aya hii tunaona kua Allah Subhanah wa Ta’ala anatuthibitishia kua Imani
ya Mtu hua ni yenye kuthibitishwa Ndani ya Moyo wake Mtu huyo na wala si kutokana
na maneno yake, kwani Mdomo hua ni wenye kubainisha tu yale yaliyomo ndani ya
Moyo wa Mtu husika na kuyathibitisha kwa maneno.
598
Na hivyo kutuwekea wazi kua kama itatokea Mtu atalazimishwa kufanya Ovu baada ya
kutishwa Uhai wake, basi hua hawezi kulaumiwa kutokana na ovu hilo, na hii pia ni kwa
sababu amesema pia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hesabu
husimamishwa kwa Ummah wangu juu ya jambo alilofanya Mtu kwa bahati
mbaya, kwa kusahau au kwa kile alicholazimishwa kukifanya.’
Ambapo anasema Imam Abu Hanifa kuhusiana na Hadithi hii kua: ‘Kusamehewa huko
kwa Ummah hua kunakubalika kua kama ni kisingizio katika siku ya Malipo na
katika baadhi ya mambo ya kidunia, ambapo hapa kwanza itabidi Qadhi
achunguze na kuangalia kwanza, kisha ndio anaweza kutomhukumu kama kweli
ama la, na pia kwa baadhi ya mambo ya kidunia hua haikubaliki kwa mfano mtu
anapomuua mtu mwengine kwa bahati mbaya basi kisharia hua hasamehewi bali
hua anatakiwa kulipa Fidiya’
Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi
anatufafanulia kuhusiana na maana ya aya kwa mifano pale aliposema: ‘Pale inapokua
Muislam anajua kua maneno yake yanaweza yakasababisha madhara kwa Waislam
wasiokua na hatia, basi hua inakubalika kutoa ushahidi wa Uongo, na hivyo katika
tukio kama hili basi hua haina haja ya kulipa fidia kutokana na kula kiapo cha
Uongo’
Na kwa upande wa Imam Ibrahim An Nakhai basi yeye ansaema ni bora kusema kua:
‘Wa Allahi, kama mimi ningesema Jambo hilo, basi Allah Subhanah wa Ta’ala
angekua na habari nalo’ na hivyo Msikilizaji hua ni mwenye kuichukulia kauli hio kua
inamaanisha kua Mtu huyo hakusema kuhusiana na jambo hilo, na hapo hapo hakusema
uongo katika kuapa kwake, kutokana na kua na nia ya kutosema Uongo. Na ndio maana
Imam Ibrahim An Nakhai alikua kama hataki kuonana na mtu ambae amemfuata
Nyumbani kwake basi huingia kwenye chumba chake cha kusalia na kisha humwambia
Mtumwa wake kua amwambie Mtu huyo kua: ‘Wallahi yuko Msikitini.’
Hivyo ingawa Allah Subhanah wa Ta’ala ametumia neno Sharaha Sadran kumaanisha
Kukifungua Kifua kwa ajili ya kuingiza Kufru ndani ya Moyo wa Mtu kutokana na hiari
yake Mtu huyo, lakini mara nyingi zaidi Allah Subhanah wa Ta’ala ametumia neno hilo
Sharaha Sadran kumaanisha Kuingiza Imani na Ilm ndani yake kunakotokana na Hiari
na Jitihada za Mja katika kumkimbilia Mola wake na kutokana na Makadirio na matakwa
ya Allah Subhanah wa Ta’ala juu ya Mja wake, kama tunavyoona vile alivyoomba Nabii
Musa kwa Mola wake pale aliposema:
﴿قَالَ رَبِّ ٱشْرَحْ لىِ صَدْرِي﴾
599
Qala rabbi ishrah lee sadree (Surat Ta-Ha 20:25)
Tafsir: Akasema (Nabii Musa) Ewe Mola wangu nitanulie Kifua changu.
Ambapo katika aya hii tunaona kua Nabii Musa alikua ni mwenye kumuomba Allah
Subhanah wa Ta’ala juu ya Jambo hilo, lakini hali ilikua ni tofauti kwa upande wa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kama alivyobainisha Allah Subhanah wa Ta’ala pale
aliposema katika Surat Al Inshirah.
TAFSIR YA SURAT AL INSHIRAH.
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞أَلمَْ نَشْ رَحْ لَكَ صَدْ رَكَ ۞وَوَضَعْنَا عَنكَ وِزْرَكَ ۞ٱل َّذِيۤ
أَنقَضَ ظَهْ رَكَ ۞وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ ۞فَإِن َّ مَعَ ٱلْعُسْ رِ يُسْ راً۞إِن َّ مَ َع
يُسْ راً۞فَإِذَا فَرَغْتَ فَٱنصَبْ ۞وَإِلىَٰ رَبِّكَ فَٱرْغَبْ ﴾
ٱلْعُسْ ِر
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Alam nashrah laka sadraka; WawadhaAAna
AAanka wizraka; Alladhee anqadha dhahraka; Fa-inna maAAa alAAusri yusran;
Inna maAAa alAAusri yusran; Fa-idha faraghta fainsab; Wa-ila rabbika fairghab
(Surat Al Inshirah 94:1-8)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma Mwingi wa Huruma; Hivi jee
hatukukifungua kifua chako kwa ajili yako? (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa
Salam) Na kukuondolea wewe Uzito wa Mzigo wako?; Ambao ulikua
unakukandamiza; Na kukupadishia Darja kutajwa kwako? Hivyo katika Ugumu
mmoja hua kuna Urahisi mara mbili, Bila ya shaka kwenye Ugumu mara moja kuna
Urahisi mara mbili, Hivyo unapomaliza mambo yako basi simama kwa ajili ya Mola
wako, Na umgeukie Mola wako kwa Maombi yako.
Na akasema Imam Malik Ibn Dinar kua: ‘Hakuna Mtihani Mkubwa ambao anaweza
kuupata Mtu kuliko kua na Ugumu wa Moyo, na pia kwa Ummah kama
kuondolewa Huruma ndani ya Nyoyo zao’
Kwani amesema Allah Subhanah wa Ta’ala katika Qur’an kua:
600
﴿أَفَمَ ن شَ رَحَ ٱهلل َُّ صَدْرَهُ لِلإِسْلاَمِ فَهُوَ عَلَى ٰ نُورٍ مِّن ر َّبِّهِ فَوَيْلٌ لِّلْقَاسِ يَةِ قُلُوبُهُمْ
مِّ ن ذِكْ رِ ٱهلل َِّ أُوْ لَٰئِكَ فىِ ضَلاَلٍ م ُّبِينٍ ﴾
Afaman sharaha Allahu sadrahu lil-islami fahuwa AAala noorin min rabbihi
fawaylun lilqasiyati quloobuhum min dhikri Allahi ola-ika fee dhalalin
mubeenin(Surat Az Zumar 39: 22):
Tafsir: Hivi Jee aliefunguliwa Na Allah Kifua chake kwa Uislam na akawa kwenye
Nuru kutoka kwa Mola wake (ni sawa na asiekua katika Uislam?): Hivyo Ole wao
wale ambao Nyoyo zao zimekubuhu dhidi ya Kumkumbuka Allah, kwani kwa hakika
hao wako katika upotovu Mkubwa sana.
Hivyo ingawa Nabii Musa alimuomba Allah Subhanah wa Ta’ala kua amtanulie kifua
chake, lakini kwa upande wa Surat Al Inshirah basi aya zinatubainishia kua Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alijaaliwa kua ni mwenye kutanuliwa Moyo na kifua chake
na Allah Subhanah wa Ta’ala kwa ajili ya kumjaza Ilm na Imani juu yake Allah Subhanah
wa Ta’ala na hivyo kumtayarisha kwa ajili ya kua na maarifah na kujisalimsha kwa ajili
ya kumtii kikamilifu Mola wake.
Ambapo tunapozungumzia kuhusiana na tukio hili la Sharaha Sadr ya Rasul Allah
Salallah Alayhi wa Salam basi Wanazuoni wametofautiana juu ya kua ni wakati gani
lilitokea tukio hili kwani kuna wasemao kua inawezekana tukio hili lilitokea baadae
katika wakati wa Safari ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ya Isra na Miraj, na
pia kuna wanaosema kua tukio hili ni lile lilitokea wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam akiwa mdogo.
Ambalo linaelezewa na baadhi wanaosema kua lilitokea wakati Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alipokua kwa Halima Bint Dhuayb pamoja na Abd ullah wakati
walipokua wakichunga Kondoo karibu na Nyumba yao na kisha wakakaa kitako chini ya
kivuli cha Mti, ambapo hapo hapo usingizi ukampitia Abd Allah huku Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akiwa ni mwenye kufikiria kuhusiana na Muumbaji wa
Ulimwengu.
Mara Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaona kua Kondoo wao wameenda mbali
nao hivyo akaamua kuwafuata ilikuwarudisha karibu tena na Nyumbani, wakati
anawakimbilia Kondoo hao mara wakatokea Watu wawili ambao walikua wamevaa nguo
nyeupee ambao walikua wanamuangalia huku wakiwa ni wenye kutabasam tabasam
601
lenye kuvutia, huku mmoja wao akiwa amebeba Bakuli la dhahabu lililokua limejaa
Theluji mkononi mwake.
Watu hao wakamkaribia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kisha taratibu
wakamkamata na kumlaza juu ya Majani ambayo yalikua kama zulia huku wakiwa na
tabasamu, jambo ambalo halikumshtua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwani
aliadhani kua ni sawa ni wenye kutaka kucheza nae na hivyo hawatomdhuru kama ilivyo
kawaida ya Watu wenye kupenda watoto namna wanavyocheza na watoto.
Ingawa hali ilikua ni hivyo kulingana na mtizamo wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam lakini kwa upande wa Abdullah, ambae wakati tukio hili linatokea alikua
amezindukana, basi yeye alishtuka na hivyo haraka sana akakimbilia nyumbani kwa
Halima na kumwambia kuhusiana na aliyoyaona yanatokea huko nje, na hivyo habari
hizo ziliwafanya Halima na Harith waliokuwemo ndani ya Nyumba kuacha kila kitu
walichokua wanafanya na kukimbilia nje katika upande aliokua amelazwa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na watu wawili hao kama alivyoelezea Abdullah.
Lakini walipofika katika eneo hilo hawakuwaona watu wawili hao, bali walimuona Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwa ni mwenye kunyanyuka huku akiwa na uso
uliosawijika kutokana na tukio lililomtokea ambalo hata hivyo yeye hakua ni mwenye
kujua ni kwanini likatokea, na hivyo wakaamua kumuuliza ni kitu gani kilichotokea
ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema:
‘Walikuja watu wawili waliokua wamevaa nguo nyeupee, ambao mmoja wao alikua
ameshika Bakuli la Dhahabu likiwa limejaa Theluji ndani yake, waliponikaribia
wakanilaza chini kwenye majani na kisha wakanizuia na wakanipasua Kifua
changu, wakautoa Moyo wangu na kuupasua pia na kisha wakatoa ndani ya moyo
wangu kitu cheusi kama damu iliyoganda na kisha wakakirembea na kisha
wakanisafisha Moyo wangu na Kifua changu kwa theluji na kisha wakaniacha na
wakaondoka’
Ambapo kuhusiana na tukio hili basi kuna wanaosema watu hawa pia walimtahiri Rasul
Allah Sallahu Aalyhi wa Salam, na pia kwa upande mwengine basi wapo wasemao kua
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alitahiriwa hapo kabla na Babu yake ambae ni
mzee Abd Ul Muttalib kwani ilikua ni kawaida ya Waarabu kutahiriana, kutokana na kua
jambo hilo ni lenye asili ya kutoka kwa Nabii Ibrahim kupitia kwa Nabii Imail.
Na kwa upande mwengine tunapoliangalia tukio hili basi kua na Hadithi pia ambayo
ndani yake anasema Ubay Ibn Kaab Radhi Allahu Anhu kua: ‘Hakika Abu Hurayrah
alikua ni mwenye kupenda kumuuliza masuali Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kwani siku moja alimuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa
602
kusema: ‘Ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hivi jee ni alama gani ya
mwanzo iliyokuonesha wewe kuhusiana na Utume wako’’
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akakaa kitako kisha na kisha akasema:
‘Ama Masuali yako Abu Hurayrah! Naam ilikua nilipokua nna umri wa miaka 10
wakati nilipokua Jangwani, na mara nikasikia kuna mtu anazungumza na mie
kutoka juu hivyo nilipoangalia Juu nikaona watu wawili ambapo mmoja wao alikua
akisema kumwambia mwenzake: ‘Ndie huyu?’’
‘Na kisha wakatua mbele yangu, na hakika mimi sijawahi kuona watu kama hao
mfano wake, hata nguo walizokua wamevaa zilikua tofauti kwangu mie,
wakanikaribi na kisha kila mmoja wao akanizuia kwenye bega langu, na mpaka
sasa hivi nahisi ubaridi wa mguso wao, ambapo mmoja akamwambia mwenzake:
‘Mlaze chini’ hivyo wakanilaza chini bla ya kutumia nguvu yeyote kisha mmoja
wapo akamwambia mwenzake: ‘Mfungue kifua chake’ nami nikafukunguliwa
Kifua bila ya kutoka Damu wala kuhisi Maumivu.’
‘Kisha mmoja akamwambia mwenzake: ‘Toa Udanganyifu na Wivu’ mwenzake
akatoa kitu kama kama damu nyeusi na akaikirembea. Kisha mwengine akasema:
‘Mpandikize ndani yae Rehema na Huruma’ na kisha mwenzake huyo akatoa kitu
kama alichokitoa hapo mwanzo lakini hiki kilikua na rangi ya Fedha. Na kisha
akanikamata kidole changu cha gumba cha Mguu na kusema: ‘Rudi kua kama
ulivyokua’ nami baada ya hapo nikawa kama nilivyokua mzima nakimbia huku na
kule nikiwa na Rehema kwa wadogo na kua na Huruma kwa wazee ’
Hivyo kuhusiana na maneno haya ya aya hizi yenye kuhoji kwa njia ya kuthibitisha
kuhusina na Sharh Sadr ya Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam kama zilizivyosema
aya:
﴿أَلمَْ نَشْ رَحْ لَكَ صَدْ رَكَ ﴾
Alam nashrah laka sadraka; (Surat Al Inshirah 94:1)
Tafsir: Hivi jee hatukukifungua kifua chako kwa ajili yako? (Ewe Muhammad
Salallahu Alayhi wa Salam).
Basi tunaona kwa upande wa Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi
yeye anasema kua: Allah Subhanah wa Ta’ala alimtanulia kifua Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kwa kumjaza Nuru ya Ujumbe wa Dini ya Kiislam
603
Na Imam Hasan Al Basr basi yeye anasema kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala
alimtanulia kifua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kumjaza Ilm ya Dini
ya Kiislam na Hikma’ na pia kuna wanaosema kua maana ya maneno haya
yanamaanisha kua: ‘Hivi Jee sisi hatukukusafisha Moyo wako na hivyo ukawa
hauruhusu vishawishi vya Shaytan ndani yake?’
Na kisha aya za Surat Al Inshrah zinaendelea kusema:
﴿ وَوَضَعْنَا عَنكَ وِزْرَكَ ۞ٱل َّذِي ۤ أَنقَضَ ظَهْ رَكَ ﴾
WawadhaAAna AAanka wizraka; Alladhee anqadha dhahraka; (Surat Al Inshirah
94:2-4)
Tafsir: Na kukuondolea wewe Uzito wa Mzigo wako?; Ambao ulikua
unakukandamiza.
Na kwa upande mwengine basi Abu Ubaydah Ibn Jarrah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala amemrahisishia Uzito katika kazi ya Mtume wake Salallahu
Alayhi wa Salam, ili asihisi uzito mkubwa, kutokana na Neema na Rehma zake juu
yake. Kwani jukumu lake la kuitangaza Dini ya Allah Subhanah wa Ta’ala kwa
Makafiri lilileta upinzani mkubwa na madhara makubwa sana, ambayo hata hivyo
yalivumiliwa na Waislam bila ya kutaka kulipiza Kisasi hapo baadae, na hii pia
ndivyo hali ilivyokua kwa upande wa Masahaba.’
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abdallah Al Tustari Al Shafii anasema kua: ‘Maneno
haya yanamaanisha kua Tumekuondolea wewe kutokukubali Utulivu kutoka kwa
yeyote isipokua kutoka kwetu na kukupa wewe kua na utulivu na usalama kutokana
na kututetegemea kwa kila kitu’
Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi
anasema kuhusiana na aya hizi kua ni yenye maana na zile aya isemayo:
﴿لِّيَغْفِرَ لَكَ ٱهلل َُّ مَا تَقَد َّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا أتََخ َّرَ وَيُتِم َّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَيَ هْدِيَكَ
صِرَاطاً م ُّسْتَقِيماً ﴾
Liyaghfira laka Allahu ma taqaddama min dhanbika wama taakhkhara
wayutimma niAAmatahu AAalayka wayahdiyaka siratan mustaqeeman (Surat Al
Fat-h 48:2)
604
Tafsir: Amekusamehe juu yako Allah zilizotangulia miongoni mwa dhambi zako na
zitakazokuja na ametimiza neema yake juu yako na amekuongoza kwenye njia
iliyonyooka.
Anasema Imam Ashanqinti kua: ‘Hakuna kutofautiana juu ya Mitizamo ya
Wanazuoni kua Mitume wana ulinzi wa kutofanya dhambi.’
Ambapo alisema Abu Talib kumwambia ndugu yake Al Abbas kua: ‘Hakika mimi
nilimchukua (Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) chini ya uangalizi wangu na
sikuachana nae hata mara moja si usiku wala si mchana, na nilikua nikimlaza baina
ya watoto wangu katika sehemu ya kwanza ya usiku halafu katika sehemu ya pili
ya usiku nimekua nikimhamisha kwa tahadhari, na wala sijawahi kumsikia
akisema uongo, wala akicheka kwa sauti kubwa na wala sijawahi kumuona
akisimama kucheza na watoto wengine.’
Ambapo kwa upande wa Mujjadid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye
anasema kua: ‘Maneno WawadhaAAna AAanka wizraka; Alladhee
anqadha dhahraka yanamaanisha kuweka wazi hali aliyokua nayo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kuhusiana na Jamii ya watu wake walivyokua kabla yeye
kupata Utume wake kama alivyosema Allah Subhanah wa Ta’ala katika aya
ifuatayo:
﴿فَلَعَل َّكَ ابَخِ عٌ ن َّفْسَكَ عَلَى ٰ آاثَرِهِمْ إِن لم َّْ يُؤْمِنُواْ هبَِٰذَا ٱلحَْدِيثِ أَسَفاً ﴾
FalaAAallaka bakhiAAun nafsaka AAala atharihim in lam yu/minoo bihadha
alhadeethi asafan (Surat Al Kahf 18:6)
Tafsir: Na kisha labda utajimaliza Nafsi yako kwa huzuni zitokanazo na athar zao kwa
sababu ya kutoamini hizi hadithi.
Ambao hali hii hua pia ni sawa na ile hadithi ambayo ndani yake amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Mfano wangu mimi na watu wa Ummah wangu ni
sawa na Mtu aliewasha Moto unaomurika katika sehemu aliyokuwepo, lakini
jambo hilo linawasababishia wadudu wawe ni wenye kuangukia ndani ya moto huo.
Na hivyo Mtu huyo kua ni mwenye kujaribu kuwavuta wadudu hao wasiangukie
ndani ya moto huo, lakini wadudu hao hua wenye kumzidi mtu huyo na kujiingiza
ndani ya Moto huo. Hivyo hali yangu mimi ni ya kua ni mwenye kutafuta Njia ya
kukuepusheni nyinyi msiingie ndani ya Moto’
Ama kuhusiana na aya isemayo:
605
﴿وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ ﴾
WarafaAAna laka dhikraka (Surat Al Inshirah 94:4)
Tafsir: Na kukupadishia Darja kutajwa kwako?
Ambapo neno Dhikr hua linamaanisha Kukumbuka, Kusheherekea, Kutaja, Kuweka
Akilini, Kuonya, Kusifiia, Kupandisha Darja, Kufanya kua maarufu.
Na hivyo aya hii inamaanisha kua Allah Subhanah wa Ta’ala amempandisha Darja Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika Kutajwa na kukumbukwa kwake katika mambo
muhimu na ya msingi kiasi ya kua anapotajwa Allah Subhanah wa Ta’ala basi hua kuna
na ulazima wa kumtaja na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa mfano kama vile
katika mjumuisho wa maneno ya Shahada ‘La Ilaha Illa Allah, Muhammad Rasulu
Allah’ ambayo hutamkwa katika sehemu mbali mbali ikiwemo pale Mtu anapothibitisha
kuingia katika Iman ya Dini ya Uislam, katika Adhana, Katika Iqama, Katika Sala n.k
Na pia katika safari yake ya Miraj basi Jina la Rasul Salallahu Alayhi wa Salam lilikua
likitajwa katika kila Mbingu pale Malaika Jibril alipokua akiomba ruhusa kuingia kupitia
kwenye Milango ya Mbingu hizo, na bila ya shaka ndani yake kukumbukwa huko kwa
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ni pale atakapopata darja ya kupanda kwenye
darja ya Maqaman Mahmuda, Kukabidhiwa Chemchem ya Al Kawthar n.k
Na kwa upande mwengine bsi tunaona kua katika kupandishwa kwake huko darja Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi hata maadui zake imekua vigumu kwao wao kua
ni wenye Kumdharau na kushindwa kujizuia kwa kutomsifu kwa sifa bora Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kutokana na Utukufu wake mbele ya Viumbe wote.
Kisha Allah Subhanah wa Ta’ala anaendelea kutuambia kua:
﴿فَإِن َّ مَعَ ٱلْعُسْ رِ يُسْ راً۞إِن َّ مَعَ ٱلْعُسْ رِ يُسْ راً ﴾
Fa-inna maAAa alAAusri yusran; Inna maAAa alAAusri yusran (Surat Al Inshirah
94:5-6)
Tafsir: Hivyo katika Ugumu mmoja hua kuna Urahisi mara mbili, bila ya shaka
kwenye Ugumu mara moja kuna Urahisi mara mbili.
606
Kulingana na mfumo wa Lugha ya Kiarabu basi Nomino inaporudiwa katika kauli na
kisha ikawa imetanguliziwa na harfu Alif Lam kabla yake basi kila moja kati ya nomino
hizo hua zinahesabika kua ni Moja. Lakini pale inapokua Nomino hio inapokua
imerudiwa bila ya kutanguliziwa na Alif Lam, basi kila nomino moja hua inakua
inahesabika kua ni Moja na inayojitegemea.
Na katika aya zetu hizi mbili tunaona kua Nomino ‘Usr’ ambayo ni neno linalotafsirikia
kua ni Ugumu imerudiwa huku ikiwa imetanguliziwa na Alif Lam kabla yake yaani liko
katika hali ya Al Usr na hivyo hua linamaanisha kua ni hali ya Umoja ya Ugumu. Ambapo
neno Yusr ambalo linatafsirika kama Wepesi na hapa limetumiwa bila ya kutanguliziwa
Alif Lam kabla yake na hivyo kua ni lenye kumaanisha Wepesi mara mbili zaidi na hivyo
kumaanisha kua Katika kila Ugumu mmoja basi kuna Urahisi mara mbili yake.
Ambapo anasema Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua: ‘Kulikua kuna jiwe mbele
ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo akasema: ‘Kama ikiwa Ugumu
wowote utaingia kwenye jiwe hili basi utafuatia wepesi wake kwenye jiwe hili na
kuutoa Uzito huo’ na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akashusha aya isemayo: ‘Fainna
maAAa alAAusri yusran; Inna maAAa alAAusri yusran’’
Na akasema Hasan Radhi Allahu Anhu kua: ‘Siku moja Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alitoka nyumbani kwake huku akiwa na na hali ya furaha na kusema:
‘Fa-inna maAAa alAAusri yusran; Inna maAAa alAAusri yusran yaani Hivyo
katika Ugumu mmoja hua kuna Urahisi mara mbili, bila ya shaka kwenye Ugumu
mara moja kuna Urahisi mara mbili.’ (Dur Al Mandhur)
Kwani haiwezekani kua Mtu atafikwa na Ugumu tu katika kila kitu bila ya kupatikana
wepesi. Hivyo Allah Subhnaha wa Ta’ala amerudia Kauli hii ili Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam apate farijiko pale anapopata ugumu, na pia kwa kila Muislam anaepata
ugumu katka mambo yake basi anatakiwa ajue kua kuna Ahadi ya Allah Subhana wa
Ta’ala kua ‘Fa-inna maAAa alAAusri yusran; Inna maAAa alAAusri yusran yaani
Hivyo katika Ugumu mmoja hua kuna Urahisi mara mbili, bila ya shaka kwenye
Ugumu mara moja kuna Urahisi mara mbili.’
Ambapo kwa upande wa Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abdallah Al Tustari basi yeye
anasema kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala ameikuzisha hali ya Matarajio katika aya
hii kutokana na Ukarimu wake na ufichikano wa Rehma zake, na ndio maana
akautaja wepesi mara mbili’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisema: ‘Fa-inna maAAa alAAusri
yusran; Inna maAAa alAAusri yusran yaani Hivyo katika Ugumu mmoja hua kuna
Urahisi mara mbili, bila ya shaka kwenye Ugumu mara moja kuna Urahisi mara
607
mbili.’ Na hivyo kumaanisha Ufahamu wa Moyo na Akili kua ni Mambo mawili
mepesi ambayo ni yenye kuweza kuudhibiti ugumu mmoja ambao ni Nafsi na hivyo
kuirudisha katika hali ya Ikhlas’
Ama kuhusiana na
﴿فَإِذَا فَرَغْتَ فَٱنصَبْ ۞وَإِلىَٰ رَبِّكَ فَٱرْغَبْ ﴾
Fa-idha faraghta fainsab; Wa-ila rabbika fairghab (Surat Al Inshirah 94:8-9)
Tafsir: Hivyo unapomaliza mambo yako basi simama kwa ajili ya Mola wako, Na
umgeukie Mola wako kwa Maombi yako.
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abdallah Al Tustari anasema kua: ‘Aya inamanisha
kua Unapomaliza Sala zako na kisha ukakaa kitako basi jitahidi kwa ajili ya Mola
wako na rudi katika hali ya awali ya kimaumbile kabla ya viumbe wengine ukiwa
na Mola wako peke yako na hivyo kuingia katika hali kua ni siri ndani ya siri’ kama
alivyosema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kwa hakika mimi hua nna
wakati ambao nnakua na Mola wangu. Hii hua ni katika wakati ambao hua
simshughulikii yeyote isipokua Mola wangu.’
Ambapo kwa Upande wa Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu basi yeye
ni mwenye kusema kuhusiana na maneno ya Aya hizi kua: ‘Yanamaanisha kua
Unapomaliza Kusali basi jishughulishe na Kuomba Dua’ ambapo kwa Upande wa
Imam Jabir Ibn Zayd basi yeye amesema kua: ‘Unapomaliza mapigano yako kwa ajili
ya Allah basi rudi kwenye Sala na maombi’.
Imam Mujahid Ibn Sulayman amesema kua hua yanamanisha kua: ‘Unapomalizia
mambo yako ya kidunia basi geukia katika upande wa pili wa kiakhera’, na akasema
Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakkalimin Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Maneno
haya yanamaanisha kua fuatisha kwa kufanya mema zaidi baada ya kufanya
Mema’
Hivyo kulingana na Mtizamo wa baadhi ya Wanazuoni ni kua ilikua ni katika kipindi hiki
cha kukaa kwa Halima Bint Dhuyab ndio lilitokea tukio la kwanza la kutanuliwa kifua
kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae alikaa kwa Bi Halima Bint Dhuayb
kwa miaka mitano na kisha akarudishwa katika mji wa Makkah kwa Mama yake Mzazi
ambae ni Aminah Bint Wahb na kuendelea kuishi pia pamoja na Mama yake mlezi ambae
ni Ummu Ayman.
608
KIFO CHA AMINAH BINT WAHB MAMA YAKE RASUL ALLAH
SALALLAHU ALAYHI WA SALAM.
Baada ya Miaka mitano ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi alirudishwa katika Mji wa
Makkah basi akapokelewa kwa furaha mapenzi na Amina Bint Wahb pamoja na Barakah.
Na baada ya Mwaka Mmoja basi Bi Amina Bint Wahb akaamua kua anataka kutembelea
Kaburi la Mume wake Abdullah Ibn Abd Al Muttalib aliefariki miaka 6 iliyopita.
Ambapo kipindi hiki Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam alikua na umri wa miaka 6,
na Bi Aminah Bint Wahb aliamua kumchukua pia Mwanawe na Barakah katika safari
hio ndefu, na ingawa Abd Al Muttalib alijaribu kumnasihi Amina Bint Wahb kua
asifunge safari hio ndefu lakini Bi Amina bint Wahb alikua ni mtu wa misimamo na hivyo
akaamua kua hakuna atakemzuia kufanya ziara hio ya kutembelea Kaburi la Mume wake
Kipenzi ambae ndie pia baba wa Mtoto wake kipenzi.
Hivyo siku ya Safari ilipowadia Amina Bint Wahb, Baraka na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam wakapanda juu ya Ngamia mmoja kwenye Kibanda kilichojengwa juu
ya Mgongo wa Ngamia wao huku wakiwa ni wenye kufuatana na Msafara uliokua
ukielekea Katika Ardhi ya Sham.
Safari iliendelea huku Rasul Allah Alayhi wa Salam akiwa kwenye mikono ya Baraka.
Allah Subhanah wa Ta'ala akawajaalia Safari ya Utulivu na Salama mpaka walipofika
Katika Mji wa Madinah baada ya siku 10.
Walipofika katika Mji wa Madinah Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam na Barakah
wakaachwa kwenye Nyumba ya Mjomba wake Bi Amina Bint Wahb ya Banu Najjar na
kisha Bi Amina bint Wahb akawa anaenda Kaburini kwa Mumewe kila siku huku akiwa
ni mwenye kuhuzunika na kua na Majonzi makubwa sana.
Siku moja wakati Aminah Bint Wahb akiwa ameenda Makaburini huku Ummu Ayman
akiwa amebakia na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam huku wakiwa wamekaa mbele
ya nyumba waliyofikia, mara wakapita Rabi wawili wa Kiyahudi ambao walipomuona
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, basi wakasimama na kumwangalia kwa umakini
na mshangao. Jambo hili lilimsababishia Rasul Allah Salallahui Alayhi wa kunyanyuka
kutoka katika sehemu aliyokaa na kukimbilia ndani kutokana na kua na woga wa
Mtizamo wa watu hao.
Hivyo Mayahudi hao wakamkaribia Ummu Ayman na kumuuliza: ‘Huyu Mtoto uliekua
nae anaitwa nani?’
609
Ummu Ayman akashatuka, kwanini watu hawa walisimama na kumuangalia sana Rasul
Salallahu Alayhi wa Salam na kisha wakawa wanataka kujua jina lake.
Hivyo nae akawauliza: ‘Kwanini nyinyi mnataka kujua juu ya jina lake?’
Mayahudi hao wakasema: ‘Hakika sisi hatuna nia mbaya nae Mtoto huyo isipokua
huyu mtoto anaonekana kama ni Mtu ambae sisi tunamjua, hivyo jee jina lake ni
nani?’
Hivyo Ummu Ayman akasema: ‘Jina Lake ni Ahmad.’
Mayahudi hao wawili wakangaliana tena kwa mara ya pili huku wakiwa na mshangao
zaidi lakini wenye kuzijaza nyuso zao na tabasamu, kisha wakasema: ‘Jee unaweza
kumuita, tukamuangalia tukahakikisha zaidi?’
Hivyo Ummu Ayman akabakia anajiuliza imekuaje watu hawa wanataka kuhakikisha
zaidi juu yake, kwani kuna nini? Lakini kabla hajauliza suali hilo basi Mayahudi hao
wakaona muonekano wa Uso wake kua umekua ni wenye kujawa na wasi wasi, hivyo
nao wakamwambia Ummu Ayman: ‘Usiwe na khofu kwani sisi hatufikirii wala
hatutaki kitu chochote isipokua wema, na hivyo hatuna nia ya kumdhuru yeye au
mtu mwengine yeyote yule, hakika sisi tunampenda huyu Mtoto kwa ajili ya Allah.
Hivyo tafadhali muite aje japo kwa mda mdogo tu.’
Maneno haya kidogo yalimtuliza Ummu Ayman hivyo baada ya kutafakari basi akaingia
ndani na kutoka na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Ambapo alipotoka nae basi
Mayahudi hao wakainama na kumsujudia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
kisha wakanyanyuka huku wakiwa na nyuso zilizojaa tabasamu na kuanza kumuangalia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam tangu juu mpaka chini na kisha wakamgeuza na
kumuangalia mgongoni na kuambiana kwa kusema: ‘Huyu Mtoto ndio yule Mtume wa
Ummah Huu, atakuja kuhamia katika Mji huu. Kisha vitafuatilia Vita na Uhamiaji
na matukio mengi makubwa sana yatatokea katika Mji huu’ na kisha Mayahudi hao
wakamuaga Ummu Ayman na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kuondoka.
Na kisha baada ya Wiki Moja Bi Amina Bint Wahb na Barakah na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam wakafunga Safari kurudi katika Mji wa Makkah.
Ukweli ni kua hii ilikua ni safari yenye kuchosha Sana kuenda na Kurudi kwa Njia ya
Jangwani Hususan kwa Mwanamke. Na Msafara ulipofika katikati baina ya Madinah Na
Makkah basi Bi Amina Bint Wahb akapatwa na Homa Kali sana.
Msafara ukasimamishwa na hapo Bi Amina bint Wahb akazidi kuzidiwa hivyo
akamwamita Barakah na kumwambia: ‘Ewe Barakah hakika mimi sitoweza kuendelea
610
kuishi kwani mda wangu wa kuondoka Duniani umewadia, hivyo nakuachia Mtoto
wangu Muhammad chini ya Uangalizi wako, umlee kama mtoto wako kwani
alimpoteza Baba yake wakati akiwa tumboni mwangu na sasa hivi atampoteza
Mama yake mbele ya macho yake. Barakah kua nae Muhamamd na wala usiachane
nae.’
Barakah anasema: ‘Mimi nikaanza kulia kwa huzuni kwani nilihisi kua Moyo wangu
ulikua umevunjika vipande vipande Muhammad alipoona hali hio basi nae akaanza
kulia na kisha akamkumbatia Mama yake shingoni huku Amina akiwa ni mwenye
kutoka Roho yake’
Kwani tukio hili la Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuondokewa na Mama yake
mzazi ambae ni Aminah Bint Wahb lilitokea katika maeneo ya Al Abwa. Ambapo kipindi
hiki Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua na umri wa Miaka 6 tu akiwa hana
Baba wala Mama na Amina Bint Wahb akazikwa katika eneo hilo, na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akabakia na Baraka ambae ni Mama yake Mlezi
aliekabidhiwa na Mama yake Mzazi.
Subhana Allah!
Tunapokitafakkari kisa hiki mpaka hapa tulipofikia basi tunaona Hikma zake Allah
Subhanah wa Ta'ala katika Kila hatua ya Maisha ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kua lilikua linamtayarisha katika kukulia katika mazingira ya kubeba Majukumu
yake Matukufu aliyotayarishiwa na Fatiri Al Samawati wa Al Ardhi yaani Muumba wa
Mbingu na Ardhi.
Kwani kutokana Hikma zake basi Allah Subhanah wa Ta'ala alikua akimtayarisha Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kumuonesha Utukufu wake mbele ya Mola wake,
kua hakuna yeyote yule anaetakiwa amtegemee isipokua Allah Subhanah wa Ta'ala.
Yaani hapa inakua zaidi ya ile ya Nabii Musa ambae nae alifanyiwa kama hivi lakini
baadae akawekwa kwenye Jumba la Kifalme la Firawn, na Kulelewa na Wamisri wakati
yeye ni Muisrail na Nabii Musa alikua na Kaka na Dada na Mama mpaka Ukubwani.
Lakini kwa upande wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakua na Kaka wala Dada,
hakua na Mama wala Baba, bali alikua na Baraka ambae ni Mama Mlezi tu ambae nae
hakua Muarabu kama alivyokua yeye Mwenyewe.
Kwani kama tunakumbuka mwanzoni mwa Kisa basi tulisema kua ingawa Baraka
alijikuta anauzwa Kama Mtumwa na kujihisi kua ana Bahati mbaya sana, lakini kwa
upande wa Muumba yaani Allah Subhanah wa Ta'ala m-bora wa Kukadiria basi alikua
tayari amesha mkadiria Baraka Darja ya Juu kabisa miongoni mwa Waja wake.
611
Hivyo Bahati mbaya yake aliyoiona hapo mwanzo kumbe ilikua ndio Bahati ya Dhahabu
kwake kwa Sababu kutokana Baraka alitoka katika Darja ya Chini ya Kua Mtumwa na
Moja kwa Moja kupanda hadi kua Mama Mlezi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam.
Na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam mpaka alipokua Mtu mzima basi alikua
akijivunia Mama yake huyo aitwae Baraka kwa kumwita Ummmi yaani Mama.
Ambapo Ndani ya Hili pia kuna Hikma ya Allah Subhanah wa Ta'ala kutufunza sisi kua
Ibn Adam wote ni wamoja, iwe Mswahili, Muarabu, Mhindi, Mzungu, n.k
Tusidharauliane na Hivyo Usiwe na Kibri na kumwambia Mwenzio; Unajua mimi Nani?
Kwani unaweza kumdharau na kumfanyia Kibr Mtu ambae mbele ya Muumba na Mtume
wake akawa na Darja kubwa Sana kutokana na Nuru ya Imani Moyoni mwake.
Na tusiichukulie mitihani tunayokumbana nayo Duniani kua ni kwa ajili ya Kutudidimiza
kwani hua ni kwa ajili ya kutusafisha na Kutupandisha Darja zaid kama tutakua na Subra.
USAFI WA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA
USAFI WA WAZEE WAKE.
Aliulizwa Imam Muhammad Abdur Rauf Bin Taj Al Arifin Ibn Ali Bin Zainal Abidin
Ibn Yahya Ibn Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Ibn Ahmad Ibn Makhluf Ibn
Abd Salam Al Hadadiy Al Munawiy Al Qahiriy Al Mishriy Al Shafii: ‘Hivi Jee Wazee
wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam wako Motoni ama la?’ ambapo Imam Al
Munawi akasema kua: ‘Wazee wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam walifariki
katika kipindi ambacho hukukua na Mtume na bila ya shaka hua hakuna Adhabu
pale inapokua hakushushwa Mtume’ kwani amesema Allah Subhanah wa Ta’ala
katika Kitabu chake Kitukufu kua:
﴿م َّنِ ٱهْتَدَىٰ فَإِنم ََّا يَهْتَدِى لِنَفْسِ هِ وَمَن ضَل َّ فَإِنم ََّا يَضِل ُّ عَلَيْهَا وَلاَ تَزِرُ وَازِ رَةٌ وِزْرَ
أُخْرَىٰ وَمَا كُن َّا مُعَذِّبِينَ حَتى َّ ٰ نَبْعَثَ رَسُولاً ﴾
Mani ihtada fa-innama yahtadee linafsihi waman dhalla fa-innama yadhillu
AAalayha wala taziru waziratun wizra okhra wama kunna muAAadhdhibeena
hatta nabAAatha rasoolan (Surat Al Isra 17:15 )
612
Tafsir: Yeyote yule Atakaejiongoa basi atakua amejiongoa kwa ajili ya Nafsi yake na
atakaepotoka basi atakua amejipotosha kwa ajili ya Nafsi yake, na hakuna mbebaji
atakaebeba mzigo wa mwenzake, na hatukua sisi wenye kuadhibu hadi kwanza pale
tutakapotuma Mjumbe.
Hii ni aya ambayo inatubainishia kua Allah Subhanah wa Ta’ala hatowaadhibu wale
watu ambao hawakufikiwa na Ujumbe wa Dini ya Kiislam, ambapo kwa upande wa Abu
Hurayrah Radhi Allahu Anhu basi yeye amesema kuhusiana na ayah hii kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala atawakusanya watu wote ambao waliishi baina ya Mitume
Miwili yaani baada ya kufariki kwa Mtume wa kwanza na wa kabla ya kuwasili
Mtume wa pili, ambapo ndani yake kundi hili watakuwemo pia watu walioishi huku
wakiwa hawana akili, Viziwi na Mabubu na kisha atawajaalia Mtume miongoni
mwao. Na kuwaamrisha kua waingie Motoni na hivyo wao watakua ni wenye
kusema: ‘Tutaingiaje Motoni wakati sisi hatukutumiwa Mtume?’’
Abu Hurayrah Radhi Allahu Anhu anaendelea kusema kua: ‘Wa Allahi kama
wangekubali kuingia basi Moto huo wangeuona kua baridi na salama juu yao, hivyo
wale ambao wangekua ni wenye kumtii Allah Subhanah wa Ta’ala Duniani basi na
hapa wangetii amri hio’
Ambapo tunapoangalia hali hii kwa upande wa Wazee wake Rasul Salallahu Allahyi wa
Salam basi tunaona kua Wanazuoni wanasema kua: ‘Hakukua na Mtu katika
mnyororo wa wazee wake Rasul Salallahu Allahyi wa Salam ambae alikua ni
mwenye kumshirikisha Allah Subhanah wa Ta’ala tangu kutokea kwa Nabii
Ibrahim, na hakuna alieuchafua Moyo wake kwa kumshirikisha Allah Subhanah
wa Ta’ala’
Kwani amesema Al Imam, Al 'Allamah, Al Hafidh Al Awhad Sheikh Al Islam Qadhi
'Iyad Ibn Musa Al Yahsubi kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kua: ‘Mimi nimetokana na mpangilio wa kizazi cha Waliosafi daima katika Mababa
na Mamama’’
Na Qur’an inawazungumzia watu wasioamini Allah Subhanah wa Ta’ala kua ni Wachafu
kama zinavyosema aya:
613
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُو ۤ اْ إِنم ََّا ٱلْمُشْرِكُونَ نجََسٌ فَلاَ يَقْرَبُواْ ٱلْمَسْجِ دَ ٱلحَْرَامَ بَعْدَ عَامِهِمْ
هَٰذَا وَإِنْ خِ فْتُمْ عَيْلَةً فَسَوْفَ يُغْنِيكُمُ ٱهلل َُّ مِن فَضْلِهِ إِن شَآءَ إِن َّ ٱهلل ََّ عَلِيمٌ
حَكِيمٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo innama almushrikoona najasun fala yaqraboo
almasjida alharama baAAda AAamihim hadha wa-in khiftum AAaylatan fasawfa
yughneekumu Allahu min fadhlihi in shaa inna Allaha AAaleemun hakeemun(Surat
At Tawba 9:28)
Tafsir: Enyi Mlioamini, hakika ya Washirikina ni Najisi hivyo msiwaruhusu
kuukaribia Masjid Al Haram baada ya mwaka huu na kama mtakua mnaukhofia
Umasikini, basi Allah atakutajirisheni kutokana na fadhila zake akitaka, Hakika Allah
ni mwenye kujua kila kitu na ni mwenye Hikma nyingi sana.
Hivyo kutokana na kua Usafi ni tofauti na Uchafu na kua na Imani hua ni Usafi na
kutokua na Imani hua ni Uchafu basi inabidi kukubaliana kua hakukua na aliekua mchafu
miongoni mwa Wazazi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na ndio maana Allah
Subhanah wa Ta’ala akampandisha Darja Mtume wake huyo Salallahu Alayhi wa Salam
kama alivyosema katika Qur’an:
﴿لَقَدْ جَآءَكُمْ رَسُولٌ مِّنْ أَنفُسِ كُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِت ُّمْ حَرِيصٌ عَلَيْكُمْ بِٱلْمُؤْمِنِ ينَ
رَءُوفٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Laqad jaakum rasoolun min anfusikum AAazeezun AAalayhi ma AAanittum
hareesun AAalaykum bialmu/mineena raoofun raheemun (Surat At Tawbah 9:128)
Tafsir: Kwa hakika, amekujieni Mtume (Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam)
kutoka miongoni mwenu, Inamuuma sana kua nyinyi mdhurike au mpate matatizo,
ana wasiwasi juu yenu (ili mpate kuongoka, na mtubu kwa Mola wenu, ili mpate
kuingia Peponi na muokoke na moto) kwa Waumini Yeye (Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam) Ni mwingi wa Huruma na mwingi wa Rehma.
614
Ambapo amesema Imam Al Husayn Ibn Al Fadhl kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala
amempa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam Sifa mbili tukufu za majina yake
yeye Allah Subhanah wa Ta’ala ambazo ni Mwingi wa Huruma na ni mwingi wa
Rehma’,
Ambapo juu ya usafi wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi pia limeelezewa
na ile aya isemayo:
﴿لَقَدْ مَن َّ ٱهلل َُّ عَلَى ٱلْمُؤمِنِينَ إِذْ بَعَثَ فِيهِمْ رَسُولاً مِّنْ أَنْفُسِ هِمْ يَتْلُواْ عَلَيْهِ مْ آَتِهِ
وَيُزَكِّيهِمْ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلْكِتَابَ وَٱلحِْكْمَةَ وَإِن كَانُواْ مِنْ قَبْلُ لَفِى ضَلالٍ م ُّبِينٍ ﴾
Laqad manna Allahu AAala almu/mineena idh baAAatha feehim rasoolan min
anfusihim yatloo AAalayhim ayatihi wayuzakkeehim wayuAAallimuhumu alkitaba
waalhikmata wa-in kanoo min qablu lafee dhalalin mubeenin(Surat Al Imram 3:164)
Tafsir: Kwa hakika ametunuku Allah kwa Waumini pale alipotuma miongoni mwao
Mtume (Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) kutokana nao, akiwasomea aya zake
na kuwasafisha (Kutokana na dhambi zao) na kuwatukuza na kuwafahamisha Kitabu
chake na Hikma (Sunnah za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam), wakati hapo
kabla walikua kwenye upotovu mkubwa.
Ambapo kama tunavyojua kua haiwezekani kua kitu kinachosafisha kitu chengine kua ni
kichafu kwani badala ya kusafisha basi kitachafua zaidi, hivyo bila ya shaka kitu kisafi
ndio hua kina sifa ya kusafisha kile kilicho kichafu na hivyo usafi unaozungumziwa hapa
na ayah hii ni Usafi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutokana na asili yake na
yale aliyokuja nayo kutoka kwa Mola wake kwa ajili ya Waumini wa Dini yake, kama
alivyoomba Nabii Ibrahim Alayhi Salam pale aliposema.
﴿رَب َّنَا وَٱبْعَثْ فِيهِمْ رَسُولاً مِّنْهُمْ يَتْلُواْ عَلَيْهِمْ آَتِكَ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلْكِتَابَ وَٱلحِْكْمَةَ
وَيُزَكِّيهِمْ إِن َّكَ أَنتَ ٱلعَزِيزُ ٱلحَكِيمُ ﴾
Rabbana waibAAath feehim rasoolan minhum yatloo AAalayhim ayatika
wayuAAallimuhumu alkitaba waalhikmata wayuzakkeehim innaka anta
alAAazeezu alhakeemu (Surat Al Baqara 2:129)
615
Tafsir: Ewe Mola wetu! Watumie (Vizazi vyetu hivyo) kutoka miongoni mwao Mtume.
Ambae atawasomea aya zako na kuwaelimisha juu ya Kitabu chako na Hikma na wape
Utukufu. Kwani kwa hakika wewe ni mwenye uwezo juu ya kila kitu na ni mwingi wa
Hikma’
Ambapo amesema Imam Abu Muhammad Al Husayn Ibn Mas'ud Ibn Muhammad Al
Farra Al Baghawi kua: ‘Amesema Mujahid kua Maana ya neno Kitabu na neno
Hikma yaliyotajwa kwenye aya hii yanamaanisha kua: ‘Kitabu ni Qur’an na Hikma
hua inamaanisha Kuifaham Qur’an ambapo wengine wamesema kua neno Hikma
lililotumika hapa linamaanisha Hukmu. Na wengine wamesema kua ni Ilm
inayojumuishwa na kuifanyia kazi Ilm hio.’
Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akasema katika njia ya kuonesha kua ni mwenye
kujibu Dua ya Nabii Ibrahim ya kuletewa kwa Watu wa Mji wa Makkah Mtu
akataewasafisha na kuwafundisha Hikma na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala kua ni
mwenye kudhihirisha majibu ya Dua yake hio katika aya zifuatazo:
﴿هُوَ ٱل َّذِى بَعَثَ فىِ ٱلأُمِّيِّينَ رَسُولاً مِّنْهُمْ يَتْلُو عَلَيْهِمْ آَتِهِ وَ يُزَكِّيهِمْ وَيُعَلِّمُهُمُ
ٱلْكِتَابَ وَٱلحِْكْمَةَ وَإِن كَانُواْ مِن قَبْلُ لَفِى ضَلاَلٍ م ُّبِينٍ ﴾
Huwa alladhee baAAatha fee al-ommiyyeena rasoolan minhum yatloo AAalayhim
ayatihi wayuzakkeehim wayuAAallimuhumu alkitaba waalhikmata wa-in kanoo
min qablu lafee dalalin mubeenin(Surat Al Jumuah 62:2)
Tafsir: Yeye (Allah Subhanah wa Ta’ala) ndie ambae aliemleta kutokana na watu
wasiojua Mtume kuwaletea juu yao Aya zake na kuwasafisha na kuwasomesha kitabu
chake na hikma ijapokua hapo kabla walikua wapo katika upotovu mkubwa
Na pia kama alivyosema tena Allah Subhanah wa Ta’ala kua
﴿ كَمَآ أَرْسَلْنَا فِيكُمْ رَسُولاً مِّنْكُمْ يَتْلُواْ عَلَيْكُمْ آَتِنَا وَيُزَكِّيكُمْ وَيُعَلِّمُكُمُ
ٱلْكِتَابَ وَٱلحِْكْمَةَ وَيُعَلِّمُكُم م َّا لمَْ تَكُونُواْ تَعْلَمُونَ ﴾
616
Kama arsalna feekum rasoolan minkum yatloo AAalaykum ayatina
wayuzakkeekum wayuAAallimukumu alkitaba waalhikmata wayuAAallimukum
ma lam takoonoo taAAlamoona (Surat Al Baqara 2:151)
Tafsir: Kama tulivyokushushieni juu yenu Mtume kutoka miongoni mwenu
kukuleteeni Aya zetu na kukusafisheni na kukufundisheni Kitabu na Hikma nan a
kukufundisheni juu ya yale mliyokua hamyajui.
Ambapo amesema Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kuhusiana na maneno yasemayo
Rasoolan minhum na Rasulan Minkum kua yanamaanisha: ‘Kutokana na Wazee,
kutokana na Uhusiano wa Kindoa na Kizazi, kua hakuna Mchafu (wa Dhambi)
kutoka miongoni mwa Mababu zake tangu kuanzia kwa Nabii Adam, kwani Wazee
wake wote walikua ni waliooana Kisharia’
Ambapo Imam Ibn Qalbi basi alisema kua: ‘Hakika mimi nimeandika Kitabu chenye
Wazee 500 wa Kike wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na sikuwahi kukuta
yeyote miongoni mwao mwenye sifa mbaya ikiwemo uzinifu ambao ulikua
umetapakaa katika nyakati za Kijahiliyah’
Na akasema Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Maneno ya
Allah Subhanah wa Ta’ala yasemayo
﴿وَتَقَل ُّبَكَ فىِ ٱلس َّاجِ دِينَ ﴾
Wataqallubaka fee alssajideena (Surat Ash Shuara 26:219)
Tafsir: Na Unapogeuka (Ewe Muhammad) miongoni mwa Wanaosujudu.
Yanamaanisha kua Kutoka kwa Mitume na Mitume hadi nikakutoa kua kama
Mtume.
Hivyo ingawa Wazazi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam waliishi katika kipindi
cha Ujahiliyah na hawakuishi katika kipindi cha uhai wa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam lakini hii haimaanishi kua Wazee wake hao hawatopata Uokovu katika siku ya
Malipo kwa sababu wao ndio waliobeba na kutoa Nuru ya Utume na walikua katika hali
ya usafi ambayo kupitia katika hali yao hio ndio kulikomtoa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kwa hekima za Allah Subhanah wa Ta’ala.
Hivyo baada ya kuzikwa kwa Amina Bint Wahb basi Barakah akarudi katika Mji wa
Makkah Huku akiwa na Mtoto wake wa kulea ambae ni Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, ambapo wakaenda moja kwa moja hadi kwa Babu yake Rasul Allah Salallahu
617
Alayhi wa Salam ambae ni Abd Al Mutallib na hivyo wote wawili wakahamia na kua ni
wenye kuishi ndani ya Nyumba hio kwa mda wa Miaka miwili huku Abd Ul Muttalib
akiwa ni mwenye kumpendekeza Abu Talib kua ni msimamizi wa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kama yeye atakua hayupo.
Wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipokua na umri wa miaka 7, basi
Mfalme wa Yemen aitwae Seif Ibn Dhi Yazin Al Himyari aliiteka sehemu ya Ardhi ya
Abisyniya, hivyo wakuu mbali mbali wa ardhi za Kiarabu wakaelekea katika ardhi ya
Yemen kwa ajili ya kumpongeza, ambapo miongoni mwao alikuwemo pia Abd Ul
Muttalib ambae nae alikua ameongozana pia na Mjukuu wake yaani Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam.
Na walipofika basi Mfalme Dhi Yazin akamuita kwa faragha Mzee Abd Ul Muttalib kwa
umuhimu wa kua ndie Kiongozi wa Mji wa Makkah na kumwambia: ‘Ewe Abd Ul
Muttalib, hakika mim nna maelezo ya siri ambayo inabidi nikueleze na hatakiwi
ajue mtu mwengine, na mimi sijawahi kumwambia mtu mwengine isipokua wewe
na hi ni kutokana na maubile ya Sifa na Tabia zako’
‘Hivyo jambo nitakalokuambia litabakia kua ni siri yako hadi pale Allah
atakapoamua kulidhihirisha, kwani imedhihirika kwangu mie kua kuna Mtoto
atazaliwa ambae atakua na alama mgongoni baina ya mabega yake mawili, ambae
atakua ni kiongozi atakua anafuatwa na Watu hadi siku ya Kiama. Na Mtoto huyo
sijajua kama ameshazaliwa ama bado, ila akizaliwa basi atakua ni Yatima, atafiliwa
na Baba yake na Mama yake, na kisha atalelewa na Babu yake na kisha Babu yake
huyo atafariki, na kisha Mtoto huyo atalelelewa na Ami yake.’
‘Na ingawa wako wengi watakaofanana nae lakini huyu atakua ni alietumwa na
Allah na hivyo atapata wafuasi ambao watampenda na kumuunga mkono sana kwa
kila kitu, nae atapingana na watu wengi, na wafduasi wa Dini mbali mbali na
kuwaadhirisha maadui zake na kuziteka sehemu bora za Ardhi Ulimwenguni, na
kuwafanya watu wawe ni wenye kumuabudu Allah tu mwingi wa Rehma. Ambapo
maneno yake yatakua ni ya Hekima, Busara na Uadilifu, atawaamrisha watu
kuachana na maovu nae hatofanya maovu na atawaamrisha kufanya mema na yeye
atakua ni mwenye kufanya mema. Nami nnaapa juu ya haya nnayoyasema kwa
Mugu wa Al Kaabah.’
Abd Ul Muttalib akasema: ‘Ewe Mfalme Dhi Yazin, hakika mimi nilikua nnae mtoto
wa kiume ambae alikua anaitwa Abdullah nilikua nampenda sana, hivyo
nikamuozesha kwa mwanamke bora katika jamii yangu, mke wake alikua anaitwa
Amina, na ndoa yao imetoa mtoto wa kiume ambae ana alama mgongoni mwake na
ana kila dalili ulizoziainisha, kwani Baba yake na Mama yake wameshafariki na
618
sasa hivi niko nae mimi na nimempendekeza alelewe na Ami yake nitakapofariki
mimi’
Mfalme Dhi Yazin akasema: ‘Basi hilo ndio nililokua nataka kukuambia, kwa hivyo
mtunze mjukuu wako kutokana na madhara ya Mayahudi na Manasara kwani ndio
watakaokua maadui zake wakubwa. Lakini Allah atamlinda dhidi yao, hivyo fanya
hii iwe siri yako bila ya kuwataarifu watu kwani tamaa yao ya uongozi itawapelekea
kupingana nae pia. Mimi nimeona haya kwenye vitabu ambamo ndani yake
mmesemwa pia kua Mji wa Madinah utakua ndio utakaompa usalama ambao
kutokana nao atapata ushindi mkubwa sana.’
‘Ila nnamkhofia kua atapatwa na matatizo makubwa, hakika mimi nnao uwezo wa
kuwaambia Waarabu wote wamfuate, ila mimi nnakukabidhi wewe jukumu hilo
kwani sina uhakika kama watu wako watakubaliana nalo jukumu hilo. Hivyo mimi
na wewe tutawasiliana tena juu ya jambo hili baada ya mwaka’
Kisha Mfalme Dhi Yazin akawazawadia Wajumbe aliokuja nao Abd Ul Muttalib zawadi
ya Watumwa 10 kila Mjumbe, Fedha, Vitambaa na Mafuta Mazuri.
Na ingawa Abd Ul Mutalib alikua ni mtu wa kawaida kwa muonekano wake likini alikua
si Mtu wa Kawaida mbele ya watu wake, kwani alikua ni kiongozi wa Kabila la Quraysh,
na ilikua ni kawaida ya Viongozi wa Kabila la Quraysh kila siku asubuhi kukutana
kwenye Al Kaabah kwa ajili ya kuzungumzia kuhusiana na Jamii yao, hivyo alikua
akifika basi hutandika chini nguo yake kisha huikalia, na alikua hamruhusu mtu yeyote
yule kuikalia nguo yake hio anayoitandikia chini isipokua Mjukuu wake yaani Rasul
Allah Sallah Alayhi wa Salam ambae alikua akienda nae kila siku kwenye Mkutano huo.
Kwani Abd Ul Muttalib alikua hataki Mjukuu wake huo kutokana na Dalili zake na
mabashirio mema juu yake awe ni mwenye kucheza na Watoto wengine, na alikua akikaa
nae pembeni yake kwenye mikutano hio ya baraza basi hua ni mwenye kusema kuhusiana
na Rasul Allah Sallah Alayhi wa Salam kua: ‘Huyu Mtoto wangu atakuja kua Mtu
Mkubwa sana.’
Lakini hata hivyo Abd Ul Muttalib hakujaaliwa kua ni mwenye kuishi na kuithibitisha
kauli yake hio kwani mbali ya kua baada ya Abd Ul Muttalib mbali kuagana na Mfalme
Dhi Yazin basi Mfalme Dhi Yazin hakuishi kwa mda mrefu akafariki Dunia. lakini pia
baada ya kumalizika miaka miwili basi Mzee Abd Al Mutallib nae akafariki Dunia.
Hivyo Barakah na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam wakahamia kwa Ami yake
Abu Talib ambae ni Ami yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na pia Baba yake
Sayyidna Jaffar Ibn Abu Talib Radhi Allahi Anhu na Sayyidna Ali Ibn Abu Talib Radhi
Allahu Anhu, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikaa kwa Abu Talib kwa
takriban miaka 17 huku akiwa chini ya Uangalizi wa Baraka yaani Mama yake Mlezi.
619
RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA UMMU
AYMAN KATIKA NYUMBA YA ABU TALIB NA FATMA BINT ASAD
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipotimia umri wa miaka minane akawa
ni mwenye kuishi kwa Ami yake huyo Abu Talib aliependekezwa na Abd Ul Muttalib
kutokana na kua Abu Talib alikua ni mtu ambae mwenye huruma sana ingawa alikua ni
mtu masikini lakini ni mwenye uaminifu na mwenye kupendwa na watu wote wa kabila
la Quraysh na kamwe hakua ni mwenye kuishi maisha yake katika hali ya Kijahilia kama
walivyokua wakiishi watu wengine wa Mji wa Makkah.
Abu Talib alikua ni mtu mwenye kumiliki Ngamia wachache na alikua na ni mwenye
famila kubwa sana, kama vile ambavyo Ali Ibn Abu Talib alivyokua akimzungumzia
baba yake huyo kwa kusema: ‘Baba yangu alikua ni Kiongozi wa watu wa kabila la
Quraysh na ingawa alikua ni Masikini lakini hakuna mtu miongoni mwa watu wa
Quraysh aliekua anajiona ana darja ya juu zaidi yake’
Hivyo bila ya shaka Abu Talib alikua ni Mtu pekee ambae anatashiki kua ni msimamizi
wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Abu Talib alikua pia ndie Msimamizi wa Al
Kaabah na kuwagawia Maji Mahujaji wanaotembelea Mji wa Makkah lakini kutokana
na ugumu wa maisha yake basi akaamua kulihamishia Jukumu hili kwa ndugu yake
ambae ni Al Abbas. Abu Talib alikua ni mtu ambae anaempenda sana Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kuliko hata anavyowapenda watoto wake kiasi ya kua alikua
kila sehemu anayoenda au kukaa basi na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hua
yuko pembeni yake, hata wakati wa kula pia likua haiwezaki kwake kula bila ya kuwepo
Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam pembeni yake.
Na ingawa alikua ni mtoto mdogo lakini Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam alikua ni
mtoto ambae anapokaa na watu kula basi chakula hicho hua ni chenye barka kubwa sana
na ingawa hakua ni mtoto mwenye kupenda kula sana lakin pia hakua ni mtoto mwenye
kulalamika juu ya kua na njaa au kiu, kwani anasema Ummu Ayman kua: ‘Hakika mimi
sijawahi kumuona Mtume Muhammad Salallah Alayhi wa Salam akilalamika juu
ya Njaa au kiu katika wakati wa utoto wake. Kwani alikua akinywa funda moja la
maji ya Zamzam asubuhi na kisha kila tukitaka kumpa chakula alikua akisema kua
hakika yeye hana njaa kwani ameshiba’
Katika kipindi hiki cha Utotoni wakati akiwa anaishi kwa Abu Talib basi hali ya
mazingira ya Mji wa Makka ilibadilika tena na ikawa kuna ukame, baada ya kua mvua
haikunyesha kwa mda mrefu, hivyo watu wa kabila la Quraysh wakamwambia Abu
Talib: ‘Ewe Abu Talib, Watu wetu na wanyama wetu wanakufa kutokana na
Ukame, hivyo tuombee ili tuweze kupata Mvua kutoka kwa Allah.’
620
Hivyo Abu Talib akakubaliana na ushauri huo na akamchukua Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam na wakaenda hadi kwenye Al Kaabah, kisha Abu Talib akanyanyua
mikono juu na kuanza kuomba huku Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam akiwa
amesimama pembeni yake mkono wake wa kushoto ukiwa umekamata Kitambaa cha Al
Kaabah na mkono wake wa kulia ukiwa umenyoosha kidole cha shahada kuelekea
Mbinguni. Na haukuchukua mda isipokua Maombi hayo ya Abu Talib na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam yalijibiwa kwa kumwagika mvua kubwa sana na yenye
manufaa kwa watu wote wa Mji wa Makkah na maeneo ya Karibu yaliyokumbwa na
ukame huo.
Katika wakati huu ambao Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipokua akiishi kwa
Abu Talib basi ndani ya nyumba hio hakua ni mwenye kupendwa na Abu Talib tu bali
pia alikua akipendwa sana na Mke wake Abu Talib ambae alikua anaitwa Fatma Bint
Asad ambae nae pia aikua akmpenda zadi ya anavyowapenda watoto wake na hvyo alikua
akimuonesha kua yeye ni kama mama yake mzazi na hivyo kumfanya Rasul Allah
Salaahu Alayh wa Salam asijihisi kua ni Yatima.
Na hivyo mapenzi haya ya Fatma Bint Asad kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
yalimuathiri pia na yeye mwenye Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam kiasi ya kua
baadae alipokuja kuoa basi alimwita Mtoto wake wa kike kwa jina la Fatma kutokana na
mapenzi yake kwa mama yake huyu kipenzi, na mapenzi haya yalidhihirishwa wazi pale
baadae katika maziko ya Fatma Bint Asad ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam alivua Kanzu yake na kumzungushia nayo Fatma Bint Asad wakati alipokua
akimuweka kaburini huku akisema: ‘Leo Mama yangu amefariki, na baada ya Abu
Talib basi hakukua na mwanamke ambae alionesha mimi ukarimu na huruma
kama Mwanamke huyu, hivyo nimeifanya kanzu yangu hii kua ndio sanda yake
ambayo ndio itakayokua kanzu yake Peponi na nimemuwekea nayo ili ayapende na
kuyazowea maisha ya hapa kaburini.’
Wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipotimia umri wa maka 10 basi Abu
Talib alifunga safari nae kuelekea katika ardhi ya Sham, ambapo njiani walipofika
kwenye maeneo ya Ardhi ambayo linajulikana kama Busra, msafara wao ukasimama
kwenye eneo ambalo lilikua lina jengo la Makaazi ya Makasisi wa Kikristo ambao lilikua
linasimamiwa Mtawa aitwae Bahira.
Na Msafara huo uliposimama kwenye eneo lake basi Bahira akahisi kua kuna utofauti wa
hali ya muonekano wa kimazingira ya msafara huo na misafara myengine ilipokua
inakuja, hivyo akaamua kuwaalika watu wote waliomo kwenye msafara huo kwa ajili ya
chakula chake, ambapo watu wa msafara huo wakaingia na kujitayarisha kwa ajili ya
mualiko huo wa chakula lakini kwa kua Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam alikua
hana njaa sana kama kawaida ya maumbile yake, basi yeye akamuomba Abu Talib kua
621
bora abakie chini ya mmoja kati ya miti iliyopo nje ya Jengo hilo kwa ajili ya kusimamia
Ngamia wa Msafara huo.
Baaa ya watu wa Msafara huo kungia ndani basi Bahira akapita na kuwaangalia watu
wote waliomo kwenye Msafara huo kwenye nyuso zao, laini hata hivyo ikawa kama
hakuridhika na kile alichokiona kwenye nyuso hizo za watu wa Msafara huo, kwani
alikua anategemea kuona kile kilichomuonesha utofauti wa Msafara huo kabla ya
kuwasili kwake, hivyo akawauliza watu waliopo mbele yake kwa kusema: ‘Hakika mimi
nimemkaribisha kila mtu aliekuwepo pamoja nanyi kwenye Msafara wenu, hivyo
jee mna uhakika kua hamjamuacha mtu yeyote nje ya Msafara huu?’
Abu Talib akasema kua: ‘Kuna Mtoto mmoja aitwae Muhammad ambae yeye yuko
nje anasimamia Ngamia wa msafara wetu’
Bahira akasema: ‘Inabidi awepo kwani nae ni miongoni mwa walioalikwa kwenye
mualiko huu.’ Hivyo Bahira akatoka nje na kumuangalia Mtoto huyo, na alipofika nje
na kumuangalia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi akaona mti huo kua uko
katika hali ya kua kama ni wenye kuinama na ni wenye kumkumbatia Mtoto huyo. Na
hapo hapo akakiona kile ambacho alikua anakitegemea kukiona kwenye uso wa Mtoto
huyo ambayo ni Alama ya Nuru ya uso wa Mtoto huyo, na hivyo Bahira akafurahia sana
kuona alama ya Nuru hio.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akala pamoja na watu wake kwenye msafara huo,
na kisha baada ya kula chakula hicho basi Bahira akamwambia Abu Talib kua:
‘Mlipokua mnakuja kwenye msafara wenu, mimi niliona kiwingu ambacho kilikua
kinafuatana nanyi kwa ajili ya kukufanyieni kivuli msafara wenu, na pia kiwingu
hicho kilikuwepo juu ya Mti uliposimama msafara wenu ambao ndio alipokua
amekaa mtoto huyu.’
Kisha Bahira akamuangalia Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam Mgongoni na
akaona Alama ya Utume wa Mwisho ambayo ni alama ya mtokezo wa umbo la nusu
duara chini ya mfupa wa mabega ya Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam na akasema:
‘Hii ndio Alama inayoonesha kua huyu ndie Mtume wa mwisho alietajwa kwenye
Vitabu vyetu ambae Allah atamtuma kua ni Rehma kwa Walimwengu. Hivyo na
kushauri Abu Talib kua rudi nae nyumbani mtoto huyu kwani Mayahudi
wakimuona basi watajaribu kumuua Mtoto huyu.’ Na hivyo Abu Talib akaufanyia
kazi ushauri huo kwa kukatisha safari yao hio na kurudi nae Rasul Allah Salallahu
A’layhi wa Salam katika Mji wa Makkah.
622
Baada ya kurudi safari yao hio basi Rasul Allah Salallah Alayh wa Salam akawa ni
mwenye kumsaidia Abu Talib kuchunga Kondoo wake ingawa Abu Talib mwenyewe na
Fatma Bint Asad hawakupendelea jambo hilo. Lakini kutokana na kua yeye mwenyewe
lilimvutia sana basi wakamwamchia awe ni mwenye kuchunga Kondoo hao katika
maeneo ya ardhi ya Jiyad katika Mji wa Makkah, na pia baadae akawa ni mwenye kazi
ya kuchuma Matunda ya Siwak katika maeneo ya Marr Zahran.
Ambapo alisema Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam kua: ‘Mara kadhaa mimi
nilikua nataka kufanya mambo ambayo wanafanya watu wa zama za Kijahiliya,
lakini Allah Subhanah wa Ta’ala alinizua mimi kufanya mambo hayo, hivyo kuanza
hapo sikutaka kufanya yale mambo ambayo Allah Subhanah wa Ta’ala alikua
hataki niyafanye hadi pale nilipopata Utume. Ama kuhusiana na mambo
niliyokusudia kuyafanya basi hali ilikua kama hivi:
Siku moja Usiku mimi pamoja na vijana wa Quraysh tulikua tunachunga Kondoo
wetu kwenye mmoja kati ya milima ya Makkah, hivyo nami nikapendekeza kwa
rafiki yangu kua kama atanisaidia kuangalia Kondoo wangu basi mimi nitaenda
pamoja na marafiki zangu wengine kwenye viburudisho vya usiku ambapo watu
hua wanakaa na kutoleana hadithi, hivyo rafiki yangu huyo akasema kua
ataniangalizia Kondoo wangu kwa ajili yangu, nami nikaelekea Mjini Makkah.’
Na nilipoziona tu Nyumba za Makkah na kusikia sauti za watu waliokua wakipiga
kelele kwa kuburudika, basi nikamuuliza mtu mmoja kuna nini? Nae akaniambia
kua kuna mtu anaoa na wanasheherekea harusi yao. Hivyo nami nikakaa karibu na
harusi hio na kuanza kuangalia kinachotokea. Na mara nikapitiwa na usingizi
sikuweza kuamka hadi lilipochomoza jua na niliporudi kwa rafiki yangu akaniuliza
ni nini nilichofanya nami nikamwambia sikufanya chochote na kumuelezea
kilichotokea katika usiku wa kabla yake.
Usiku wa siku nyengine tena, nikamuomba rafiki yangu ruhusa ya kuondoka, nae
akanikubalia, hivyo nikaondoka na kuelekea kwenye mji wa Makkah, nami
nikaona yale niliyoyaona hapo kabla, na nikakaa na kuangalia, na nikalala tena na
sikuweza kuamka hadi asubuhi yake, kisha nikarudi na kumuelezea rafiki yangu
kilichotokea, na tangu siku hio sikujaribu kufanya jambo hilo tena hadi nilipopata
Utume. (Imam Al Munawi)
Ilikua ni kawaida ya watu wa Quraysh kukutana kwa mwaka mara moja mbele ya
Sanamu la Buwana ambapo hua wanakaa na kuzungumza, Kunyoa nywele zao, Kuchinja
wanyama wao na kusheherekea sherehe kubwa kubwa, hivyo wakati mmoja ulipowadia
mda wa kufanya hivyo basi wakajitayarisha na kutaka kukusanyika pamoja na kutaka
kumchukua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam pamoja nao, lakini hata hivyo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akakataa.
623
Hivyo Abu Talib na familia yake yote kwa ujumla wakamchukua na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kuelekea kwenye sehemu hio, lakini walipofika wakagundua
kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hayuko pamoja nao, hivyo wakakasirika na
kuanza kumtafuta, na walipompata basi walimuona kua yuko katika hali mbaya sana ya
kua taaban, hivyo wakamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwanini akawa
yuko katika hali kama hio, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema:
‘Nna khofu kubwa sana nisije nikadhurika’ Abu Talib akamwambia: ‘Hakika wewe
una sifa nzuri sana na hivyo hivyo Allah hawezi kuruhusu kua uwe ni mwenye
kudhurika, Hivyo hebu tuambie imekuaje?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hakika mimi nilipolikaribia ile
sanamu basi kuna mtu aliekua amevaa nguo nyeupe alitokea mbele yangu na
kunambia kua: ‘Ewe Muhammad Rudi unakotoka na kamwe usiliguse
Sanamu’’Hivyo tangu siku hio basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakuwahi
kuyasogelea Masanamu hayo.(Imam Ali Burhan Din A Halabi)
Huku Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, alikua ni kijana mwenye uso na
umbo la kuvutia si mrefu sana wala si mfupi sana alikua na nywele nyeusi, nyusi na kope
zilizofunika macho makubwa ya kupendeza yaliyoficha ndani yake sifa ya mamlaka na
uongozi juu ya watu wengine, pua yake ilikua ya kawaida na mdomo wake ulikua na
meno meupe yaliyopangika vizuri, kidevuni alikua na ndevu zilizojaa, shingo ndefu
inayopendeza na kifua kilichobebwa na mabega mapana, alikua ni mwenye ngozi nyeupe
na akitembea hutembea kwa mwendo wa ukakamavu wa mtu aliekua kama mtu anae
teremka kilimani hata kama anapandisha kilima, muonekano wa sura yake ni wa mtu
mwenye upeo wa kuona mbali ki mawazo, ki hikma na mwenye kutafakkar.
Kutokana na kua ni mwenye matayarisho ya Kuteuliwa na Allah Subhanah wa Ta’ala
kua Nabii na pia ni Mtume wa mwisho alieletwa na Allah Subhanahu wa Ta’ala ili
kuuweka sawa Ulimwengu na kuuelekeza katika njia iliyo sahih, kuitoa Dunia katika njia
iliyojaa giza, ujinga na kila aina ya dhulma na kuuingiza katika njia yenye Nuru, I’lm na
Uadilifu. Kama alivyosema Allah Subhanahu wa Ta’ala katika Qur’an.
﴿هُوَ ٰ ۤ ٱل َّذِي أَرْسَلَ رَ سُولَهُ بِٱلهُْدَىٰ وَدِينِ ٱلحَْقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى ٱلدِّينِ كُلِّهِ و كَفَى بِٱهلل َِّ
َ
شَهِيداً ﴾
Huwa alladhi arsala rasoolahu bialhuda wadeeni alhaqqi liyudhhirahu AAala
alddeeni kullihi wakafa biAllahi shaheedan. (Surat Al Fat-h 48:28)
624
Tafsir: Ni yeye alietuma Mtume wake kwa ajili ya njia ya Uongofu na Dini ya haki, ili
kuzifunika dini zote, na Allah anatosha kua Shahidi.
Ambapo miongoni mwa sifa zake basi alikua ni Al Amin yaani Muaminifu kama
anavyosema mwenye Allah Subhanah wa Ta’ala katika aya ifuatayo:
﴿وَمِنْهُمُ ٱل َّذِينَ يُؤْذُونَ ٱلن َّبىِ َّ وَيَ قُولُونَ هُوَ أُذُنٌ قُلْ أُذُنُ خَ يرٍْ ل َّكُ مْ يُ ؤْمِنُ بِٱهلل َِّ
وَيُؤْمِنُ لِلْمُؤْمِنِينَ وَرَحمَْةٌ لِّل َّذِينَ آمَنُواْ مِنكُمْ وَٱل َّذِينَ يُؤْذُونَ رَسُولَ ٱهلل َِّ لهَُمْ عَذَ ابٌ
أَلِيمٌ ﴾
Waminhumu alladheena yu/dhoona alnnabiyya wayaqooloona huwa odhunun qul
othunu khayrin lakum yu/minu biAllahi wayu/minu lilmu/mineena warahmatun
lilladheena amanoo minkum waalladheena yu/dhoona rasoola Allahi lahum
AAadhabun aleemun(Surat At Tawba, 9:61)
Tafsir: Na miongoni mwao mna watu wanaomuudhi Nabii (Salallahu Alayhi wa
Salam) na wanasema kua yeye ni mwenye kulipa sikio lake kila jambo: ‘Waambie
Hakika yeye anasikiliza yale yaliyo bora kwenu, Anamuamini Allah na Anawaamini
Waumini na ni mwenye rehma kwa wale walioamini miongoni mwenu, na kwa wale
wenye kumuudhi Mtume wa Allah (Salallahu Alayhi wa Salam) basi ni juu yao adhabu
kali.’
Ambapo aya hii inazungumzia sifa ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ya kua ni
mwenye kumuamini Allah Subhanah wa Ta’ala na Waumini wake pia na ni mwenye
huruma juu yao, ambapo hii pia ni kutokana kwake kua na ubora wa Tabia kiasi ya kua
alikua akijulikana pia kwa jina la Muhammad Al Amin, kutokana na kua ni mwenye kua
na Uaminifu hata kabla ya kua na darja ya Utume katika maisha yake.
RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA HILF AL
FUDUL
Eneo la Ukaz ni eneo maarufu sana kutokana na kua ni eneo linalojumuisha moja kati ya
masoko matatu makubwa na maarufu katika maeneo ya ardhi ya Uarabuni ambayo ni
Ukaz, Majanna na Dhul Majaz ambayo yote yalikua yakifanya kazi katika kipindi cha
wiki mbili za mwezi wa Dhul Qaidah. Ingawa Soko la Ukaz ambalo lipo mashariki ya
625
nje ya Mji wa Makkah na lilikua lipo ndani ya ardhi iliyopo baina ya Mji wa Nakhla na
Mji wa Taif ambayo ingawa ilikua inamilikiwa na Kabila la Banu Hawazin lakini soko
hilo lilikua likidhibitiwa na watu wa kabila la Banu Tamim.
Ambapo kama tunavyojua kua mwezi huu wa Dhu Al Qaidah, Dhu Al Hijjah, Muharram
na Rajab kua ni miongoni mwa miezi Mitukufu ambayo ilikua inaheshimiwa tangu
wakati wa kipindi cha Ujahiliyah na hivyo hua hairuhusiki kupigana vita ndani yake.
Hivyo ndani ya kipindi hiki cha Dhul Qaidah basi watu wa Uarabuni walikua ni wenye
kupumzika na kustarehe, na hivyo katika kipindi hiki soko la Ukaz hua ni lililojaa shamra
shamra za maonesho na starehe kila aina, ikiwemo mashindano ya Mashairi, Hadithi na
Mikasa, Kamari, Ulevi, Nyimbo na Ngoma zinazochezwa na Wanawake wa aina mbali
mbali, n.k
Na mbali ya kua madhumuni ya maonesho hayo ya soko la Ukaz ilikua ni kustarehe na
kutumia pesa zilizopatikana baada ya mzunguko wa mwaka wa kufanya kazi lakini
kutokana na kua ndani yake mlikua mna starehe za anasa za Ulevi basi ilikua lazima
kunatokea mapigano ndani yake ambayo yalikua yakijulikana kama mapigano ya Fijar.
Ambapo neno Fijar hua linatokana na neno Fajara linalomaanisha Dhulma, Maasi, Fujo
za Uovu, Kutokua na Aibu wala Haya, Kuzini, Kufanya Uasharati.
Na hivyo mapigano haya yalikua yakianzishwa na mambo yasiyokua na maana kama
inavyomaanisha maana ya jina la Mapigano hayo ya Fijar. Ambapo ndani ya miaka 10
yalitokea mapigano mara nne ambapo mnamo mwaka wa 10 baada ya kuzaliwa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi yalitokea mapigano ya mwanzo ya Fijar ndani ya
soko la Ukaz baada ya Mtu mmoja kutoka katika Kabila la Banu Ghifar kusema kua:
‘Mimi ndie Mtu anaeheshimka sana kuliko wote miongoni mwa watu wa Uarabuni’
Hivyo kutokana na kusema maneno hayo basi mmoja kati ya watu wa Kabila la Hawazin
ambao ndio wamilikia wa eneo hilo la Soko la Ukaz basi akachukulia kauli hio kua
Unyanyaso juu yake, na hivyo akatoa Upanga wake na kumpiga nao mtu huyo wa Kabila
la Banu Ghifar mguuni mwake na kumjeruhi, na hivyo hii ikawa ndio sababu ya kutokea
mapigano makubwa baina ya Makabila mawili hayo, katika Soko la Ukaz katika mwezi
wa Dhul Qaidah.
Ambapo mapigano ya pili yalitokea baadae baada ya Kijana wa kiume wa Kabila la Banu
Hawazin kumvua Hijab mwanamke wa Kabila la Quraysh, na hivyo kua ni mwenye
kumvunjia heshima Mwanamke huyo, kwani hata katika kipindi hicho basi Wanawake
wenye kujiheshimu walikua ni wenye kujitanda, tofauti na wanavyofikiria watu wengi
miongoni mwetu leo hii kua kujitanda na kujihifadhi kwa Mwanamke anapokua
hadharani hua ni kujikosesha uhuru wake Mwanamke. Hivyo watu wa Kabila la Quraysh
walipigana vita na watu wa Kabila la Banu Hawazin baada ya Mwanamke wa Quraysh
kuvuliwa Hijabu yake hadharani kwenye soko la Ukaz.
626
Mapigano ya tatu ya vita vya Fijar yalitokea baina ya Ukoo wa Banu Kinana na Ukoo wa
Watu wa Banu Hawazin baada ya mmoja kati ya watu wa Banu Kinana kukataa kulipa
deni kwa wakati alilokua akidaiwa na Mtu huyo wa Banu Hawazin
Na mapigano ya nne ya Fijar yalitokea katika kipindi cha wakati ambao Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alipokua na umri wa miaka 20, ambayo yalipiganwa baina ya
Watu wa Banu Kinana na watu wa Banu Qays baada ya Baraz Ibn Qays wa Banu Kinana
kumuua Urwa ambae ni mwenye kutokana na ukoo wa Banu Qays.
Hivyo katika wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipokua kijana wa umri wa
miaka 20, kulitokea mapigano hayo ambapo Abu Talib alimchukua Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwa ajili ya kuwasaidia watu wa Banu Kinana ambapo hata hivyo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakua ni mwenye kupigana kwenye vita hivyo bali
alikua ni mwenye kusaidia katika kuokota Mishale ya Upinde wa Maadui kwa ajili ya
kumpa Ami yake yaani Abu Talib.
Ambapo katika kutafuta suluhu ya mapigano hayo basi pande hizo mbili zikakubaliana
kua inabidi wahesabiwe Maiti wa Pande zote kisha pande iliyoua watu wengi zaidi basi
itabidi ilipe fidya, na baada ya kuhesabiwa maiti hao basi ikagundulika kua kuna Maiti
20 zaidi za Banu Qays, hivyo watu wa kabila la Quraysh na Banu Kinana wakalipa fidya
kwa ajili ya watu hao 20 na kisha ndio ikapatikana suluhu.
Na kutokana na hali ya matukio hayo ya vita vya Fijar kua ni vyenye kuanzishwa na
mambo yasiyokua na maana na kupelekea kumwagika kwa damu nyingi sana, na kuvunja
umoja wa Makabila ya Waarabu na kusababisha uadui baina yao, na kukosekana kwa
usalama kwa Wageni wanaotembelea na kupita njia kwenye Mji huo, kiasi ya kua mara
moja Asl Ibn Wail ambae ni ni miongoni mwa watu wakubwa wa mji wa Makkah
alipotaifisha mali za mmoja kati ya Watu wa Kabila la Al Zabidi la Yemen.
Ambapo mtu huyo wa kabila la Al Zabidi alipojaribu kuomba msaada wa kwa watu wa
Makkah basi walimfungia Mlango yao, na hivyo nae akaamua kuelekea kwenye Mlima
wa Abu Qubays na kuanza kulalamika kwa kupaza Sauti kuhusiana na namna
alivyodhulumiwa na kunyanyaswa na Asl Ibn Wail na kukosa Msaada kutoka kwa watu
wa Makkah. Na hivyo baada ya tukio hili basi Viongozi wa Kabila la Quraysh wakaamua
kuunda Jumuiya ya Usuluhishi ambayo itakua ni yenye kusimamia haki za watu
waliodhulumiwa na hivyo kuepusha dhulma na umwagaji wa Damu katika maeneo ya
ardhi yao na jirani pia.
Muanzilishi wa Jumuiya hii alikua ni Zubayr, ambae alishirikiana na viongozi wa Banu
Hashim, Banu Muttalib, Banu Zuhra, Banu Asad, Banu Harith na Banu Taym ambapo
makao makuu ya Jumuiya hii yalikua ni kwenye Nyumba ya Abdullah Ibn Juda ambae
alikua ni Tajiri sana na ni mwenye kuheshimika na watu wote wa Mji wa Makkah na
627
maeneo ya Jirani. Na Jumuiya ilikua ikiitwa Hilf Al Fudul ambapo Hilf maana yake ni
Kiapo na Fudul maana yake ni Watu wenye Kuheshimika Kitabia.
Ambapo kwa upande mwengine basi kuna wanaosema kua Tukio hili la makubaliano
haya liliitwa Hilf Al Fudul kwa sababu, katika kipindi cha Uanzishwaji wa Mji wa
Makkah basi pia kulikua kuna makubaliano baina ya Fudayl wa Banu Jurhum na Fudayl
wa Banu Qatura ambayo yalikua ni ya kuhusiana na Kuzuia Uovu usifanyike ndani ya
Mji wa Makkah, hivyo kutokana na kua watu wa Quraysh walikubaliana pia kuhusiana
na tukio hilo basi Jumuiya hio ikawa inaitwa Hilf Al Fudul kumaanisha Kumbukumbu
ya makubaliano baina ya Fudayl wawili hao wa awali.
Malengo ya Jumuiya hio ya Quraysh yalikua ni kusimamia mambo yafuatayo:
1- Hakuna Mtu ambae atakaenyanyaswa na kuvunjiwa haki zake bila ya
kuangalia kama ni Mtu wa Mji wa Makkah ama la.
2- Hakutokua na Fursa ya kufanya dhulma wala kunyanyasa Mtu, na hivyo
kila atakaenyanyasa na kudhulumu basi atachukuliwa hatua za nidhamu
dhidi yake.
3- Kusimamia Haki za Waliodhulumiwa hadi wapate haki zao ili wasiokua na
uwezo wasdhulumiwe haki zao na wenye uwezo.
Ambapo wanachama wa Jumuiya hii walikubaliana kwa kulishana kiapo kwa kusema
kua: ‘Tutalinda Viapo vyetu hadi pale Bahari itakapokua haina maji ya kutosha ya
kurowanisha hata unywele, hadi Milima itakapobubujika na kupeperushwa, hadi
pale Istilam (Tukio la kupangusa au kilipungia mkono kwa mbali Hajar Al Aswad
wakati wa kuzunguka Al Kaabah) litakapofutwa’
Na jukumu la mwanzo kabisa la Jumuiya hii lilikua ni kuzirudisha kwa mwenyewe
mmiliki wa Mali za Myemen wa Al Zabidi aliepokonywa na Asl Ibn Wail.
Hivyo tukio hili lilitokea wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipokua na
Umri wa miaka 20 na hivyo ingawa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua ni
mdogo Kiumri ukilinganisha na Umri wa Viongozi hawa wakubwa wa Quraysh lakini
nae pia aliingizwa kwenye Jumuiya hii kutokana na Uaminifu wake na Uadilifu wake
katika kusimamia haki za Watu tofauti wa Mji wa Makkah na wa maeneo mengineyo
wanaojuana nae.
Ambapo anasema Abu Muhammad Abd Al Malik Ibn Hisham Ibn Ayyub Al Himyari Al
Mu'afiri Al Baṣri kua alisema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hakika mimi
nilikuwepo katika nyumba ya Abdullah Ibn Juda wakati kiapo kilipothibitishwa,
628
na kwa mtizamo wangu basi ni kua kiapo hicho kilikua ni cha kupendeza kwangu
kuliko kumiliki Ngamia Mwekundu, na hata kama nikiitwa kuhudhuria katika
wakati huu wa Uislam basi nitakubali kuhudhuria.’
Kwani alisema pia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Fanyeni Makubaliano
ambayo ni yenye kusimamia haki za watu, ili wenye nguvu wasiwe na uwezo dhidi
ya wasiokua na nguvu’(Sunan Al Kubra)
SAFARI YA KIBIASHARA YA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI
WA SALAM KATIKA ARDHI YA SHAM.
Wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipotimia Umri wa miaka 24 alikua
tayari ameshaenda na misafara ya Kibiashara na Ami yake yaani Abu Talib katika Ardhi
ya Syria, na lakini hata hivyo safari hizo zilisita kwa sababu ya hali mbaya ya uchumi wa
Abu Talib kutokana na kua na Familia kubwa, vita baina ya makabila na vile vile hali ya
Ukame.
Katika kipindi hiki kigumu basi walioweza kudumu na Biashara walikua ni wale wenye
mitaji mikubwa tu ya biashara, ambapo mmoja miongoni mwao alikuwepo Mwanamke
Mzuri, anaehishimika katika Mji wa Makkah, huyu alikua Mwanamke anaejulikana kwa
jina la Khadija Bint Khuwaylid Ibn Asad ambae alikua ni mwanamke mwenye umri wa
miaka 39 ambae alierithi Utajiri wake kutoka kwa Baba yake Khuwaylid Ibn Asad ambae
alikua ni tajiri mkubwa sana na alifariki katika Vita vya Fujjar.
Khadija Bint Khuwaylid alikua ni Mwanamke alieachwa baada ya kuolewa mara mbili
ambapo mara ya kwanza ilikua ni pale alipoolewa na Abu Halah Ibn Zurara Ibn Al
Nabbash Al Tamimi ambae kutokana nae alipata watoto wawili, mmoja alikua akiitwa
Hind na mwengine akiitwa Hala, na baada ya kuachika kwenye Ndoa hio basi akaolewa
na Atiq Ibn Idd Ibn Umar Ibn Makhzum ambapo alipata mtoto mmoja aitwae Hind bint
Atiq.
Ambapo Hind Bint Atiq baadae aliolewa na Saffiy Ibn Ummayah Ibn Aabid Ibn Abdullah
Ibn Mahkzum ambapo katika ndoa hio wakapata Mtoto wa kiume waliemwita
Muhammad ambae Ukoo wake ukawa unaitwa Banu Tahirah, yaani Ukoo wa
Mwanamke aliekua Masafi ambae ni Khadija Bint Khuwaylid na hii ni kutokana na usafi
wa Khadijah Bint Khuwaylid, na akawa anaitwa Bint Tahira na pia alikua akiitwa kwa
jina la Amirat Al Quraysh yaani Malkia au kiongozi wa Kike wa Quraysh, na pia alikua
akiitwa Khadija Al Kubra yaani Khadija Mkuu wa Kike wa Quraysh na hii ni kutokana
na Uadilifu wake na namna anavyosimamia na kuendeleza Biashara zake ambazo zilikua
hazina Mpinzani kwa Ukubwa na wingi wa Mali zake, kwani alikua na uwezo wa
kubadilisha Vumbi akilitia mkononi mwake na kulifanya likawa Dhahabu badala yake.
629
Misafara ya kibiashara ya Khadija Bint Khuwaylid ilikua ikizunguka sana na kupata
umaarufu baina ya Makkah na Yemena na pia baina ya Makkah na Sham, na kutokana
na Ukarimu, Uadilifu na mafanikio yake basi Khadija Bint Khuwalid alikua akipendwa
sana na watu wa Mji wa Makkah hususan Wanawake na alikua kila anapoenda basi
lazima hua na Msafara wake wa Wanawake wanaopenda kua karibu yake.
Safari moja wakati Khadija Al Kubra alipokua akizunguka Al Kaabah pamoja na
marafiki zake, basi akatokea Myahudi mmoja ambae alisema: ‘Ewe Amirat Al Quraysh,
Jee unajua kua atatokea Mtume katika zama hizi? Hivyo yeyote yule anaetaka
kuolewa nae basi na aolewe.’ Ambapo hata hivyo Wanawake waliokua wamemzunguka
Khadija Al Kubra wakakasirika kusikia maneno hayo kutokana na kua Khadija Bint
Khuwaylid alikua ni mwanamke anaejiheshimu na tayari ameshakataa posa za Wanaume
kadhaa ambao walikua hawana vigezo stahiki mbele yake. Hivyo marafiki zake hao
wakamrushia Mawe Myahudi huyo nae akaondoka.
Ndani ya mwaka huu Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam watu wa Quraysh
waliandaa Msafara wa Biashara mkubwa sana wa kuelekea Sham, ambapo ndani yake
Msafara huu pia zilikuwemo Mali za Khadijah Bint Khuwaylid lakini alikua hajapata mtu
wa kuusimamia biashara hizo kwani alikua hajapata mtu stahiki wa kusimamia mali zake
zake hizo, hivyo akawa ni mwenye kutafuta mtu wa kusimamia Biashara zake hizo.
Habari za utafutwaji wa Msimamizi wa Biashara za Khadija Bint Khuwaylid kwenye
Msafara huo zilimfikia Abu Talib basi akamtaarifu Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kwa kumwambia: ‘Ewe Mtoto wa Kaka yangu, hakika wewe unajua kua mimi
si mwenye umiliki wa kitu wala mali yeyote kwani hali hii ya njaa na ukame
imekausha kila kitu katika mali zangu, kiasi ya kua hakuna sehemu ya kutegemea
kwa upande wangu, lakini kuna msafara wa Biashara unaoelekea Sham ambao
ndani yake pia mna Mali za Khadija Bint Khuwaylid’
‘Na Khadija Bint Khuwaylid anatafuta Msimamizi wa Mali zake kutoka kwenye
Kabila letu,na kama unavyojua ni kua Khadija ni mwanamke Tajiri sana na watu
wengi sana ni wenye kunufaika na Biashara zake, hivyo anahitaji mtu kama wewe
kua ni msimamizi wake, mtu anaeaminika, mkweli na muadilifu, hivyo kama
ukienda kuzungumza nae kuhusiana na kusimamia Mali zake katika Msafara huu
basi bila ya shaka atakufaham na kukukubali kutokana na sifa zako na Uaminifu
wako. Ingawa mimi sifurahii kukupeleka Sham kwa sababu ya kuogopa kuja
kudhuriwa kwako na Mayahudi, lakini hakuna njia nyengine ya kufanya kwa
upande wangu katika hali kama hii tuliyokua nayo isipokua kukuruhusu kuenda
pamoja na Msafara huo.’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Ami yangu, hamna tatizo
mimi niko pamoja nawe hivyo fanya lile unaloliona kua ni sahih’
630
Bila ya shaka alitakalo Allah Subhanah wa Ta’ala kua basi hua ni lenye kutokea na kua
bila ya kua na kipingamzi chechote, kwani ingawa mazungumzo haya walikubaliana
baina ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Abu Talib lakini hali ilikua ni kama
vile Khadija Bint Khuwaylid alikua akiwasikiliza, kwani wakati mazungumzo ya Watu
waili hawa yanaendelea basi na kwa upande wa Khadija Bint Khuwaylid nae likamjia
wazo la kujaribu kumuomba Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam awe msimamizi wa
Mali yake katika Msafara huu kua ndio yeye peke yake mwenye sifa za kusimamia Mali
yake, hivyo akamtuma mtu aende kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ili
amuombe aje mbele yake kwani anataka kuzungumza nae.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipofika mbele ya Khadija Bint Khuwalid na
kusalimiana nae basi Khadija Bint Khuwaylid akasema: ‘Nimekuita kwa sababu
nilikua nataka kupendekeza kutuma Mali zangu katika Mji wa Dimashq pamoja
nawe ili uwe msimamizi wake, kwani najua kua kwa hakika wewe ni Mtu mwema,
Muaminifua sana na Muadilifu, hivyo niko tayari kukulipa wewe malipo ambayo
kamwe sikuwahi kumlipa mtu yeyote kabla yake, hivyo jee unaonaje?’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu: ‘Bila ya shaka hii ni Rehma
ambayo Allah amekujaalia kuipata’ na hivyo kumaanisha kua amekubaliana na
mapendekezo hayo ya Khadija Bint Khuwaylid.
Na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliporudi nyumbani na kumuelezea Abu
Talib kuhusiana na yaliyotokea basi Abu Talib akamwambia Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua bora akapatane nae Khadija Bint Khuwaylid ili apate kujua atalipwa
kiasi gani, lakini hata hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kua
ameridhika na makubaliano hayo, hivyo Abu Talib akaona bora aende yeye mwenyewe
kwa Khadija Bint Khuwaylid ili akapatane nae kuhusiana na malipo hayo, hivyo akatoka
na kuelekea kwa Khadijah Bint Khuwaylid na alipofika akamwambia:
‘Ewe Khadija hakika sisi tumesikia kua umelipa Ngamia wawili kwa wasimamizi
wa Msafara uliopita hivyo na sisi kwa upande wetu hatuwezi kubaliana na kua
Muhammad asimamie Msafara wako isipokua kama utampa Ngamia si chini ya
wanne.’
Ambapo Khadija Bint Khuwaylid akamwambia Abu Talib: ‘Ewe Abu Talib hakika
wewe umeamua kupendekeza bei ya chini zaidi ya nilivyofikiria, kwani mimi
nilikua tayari kutoa zaidi ya hio’ hivyo Abu Talib akafurahia makubaliano hayo.
Hivyo Msafara ulipokua tayari basi Khadija Bint Khuwaylid akamteua Mtumwa wake
aitwae Maysara ambae alimwambia kua awe Msaidizi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kwa kumwambia: ‘Fuatana nae Muhammad kwenye msafara huu na ni
jukumu lako kumtii katika kila atakalokuamrisha, na wala usiende kinyume na
631
maamrisho yake, jitahid uwe ni mwenye kuja kunielezea kila kitu kitakachotokezea
kwenye msafara huu.’
Baada ya siku kadhaa za maandalizi ya msafara huo kumalizika basi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akakabidhiwa Mali za Khadija Bint Khuwaylid hukua akiwa
na msaidizi wake ambae ni Maysara, ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akaagana na watu wa familia yake na Bi Khadija bint Khuwaylid na kisha Msafara huo
ukaanza safari yake.
Msafara huo ulikua ni msafara wa safari ndefu ambao hua ni yenye kuchukua mda wa
miezi mitatu hadi kuwasili katika Ardhi ya Sham, baada ya safari ya siku kadhaa kabla
ya kuwasili mwishoni mwa safari yake basi msafara huo ukawasili katika ardhi yenye
jengo la Makuhani wa Busra ambayo hapo awali Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alipokua mdogo alipofuatana na Babu yake ambae ni Abd Ul Muttalib basi alikutana na
Bahira, hivyo msafara huo ukasimama kwenye eneo hilo kwa mapumziko ya muda mfupi
ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasimama chini ya Mti ule ule
aliosimama katika wakati alipokua Mdogo na Babu yake.
Na katika kipindi hiki Bahira alikua ameshafariki na hivyo Msimamizi wa jengo lililopo
kwenye eneo hilo alikua ni Kuhani mwengine aitwae Nastura, ambae nae alishanganzwa
na tukio la kumuona Mtu asiemjua akiwa amekaa chini ya Mti huo mkubwa uliopo karibu
yake, hivyo akamuona Maysara ambae aliwahi kuonana nae hapo kabla katika misafara
kadhaa yenye mali za Khaidja Bint Khuwaylid na kumuliza: ‘Jee yule aliekaa chini ya
Mti wa Mzaituni ndie ni nani’
Maysara akasema: ‘Yule ni kijana anaeheshimaka sana katika Mji wa Makkah na
mwenye sifa za upekee miongoni mwa watu wa Kabila la Quraysh’
Nastura akakaa kimya na kutafakari kisha akasema: ‘Inashangaza sana kwani hakuna
mtu anaekaa chini ya Mti ule isipokua atakua ni Mtume’ hivyo akamuuliza Maysara:
‘Hivi jee macho yake yana wekundu ndani yake?’ ambapo Maysara akajibu: ‘Naam.’
Hivyo Nastura akasema: ‘Basi atakua ni Mtume, yaani ndie Mtume wa Mwisho’
Maneno haya yalimtia wazimu wa furaha Maysara kwani yalikua ni maneno
yasiyosahaulika, yalikua kama yaliyooteshwa kwenye ufahamu wake na hivyo kuganda
kwenye ufahamu wake. Kiasi ya kua hakujali hata baada ya msafara huo kuondoka na
kumalizia Safari yake katika Mji wa Dimashq na kufanya Biashara zake na kufunga safari
ya kurudi katika Mji wa Makkah kua mara hii mmiliki wake Bi Khadija Bint Khuwaylid
amepata faida kubwa sana baada ya kusimamiwa mali zake na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam katika Biashara yake aliyoifanya katika Mji wa Dimashq na pia katika
mzigo wanaorudi nao katika Mji wa Makkah, kwani kwake yeye habari ya faida haikua
632
na thamani wala maana yeyote kuliko yale maneno aliyoambiwa na Nastura kua
Muhammad ndie atakaekua Mtume wa Mwisho.
Kwani pia kuna jambo jengine ambalo lilimshangaza zaidi Maysara na kuthibitisha
maneno ya Nastura baada ya kuyatafakari na kuanza kumfuatilia Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam na kugundua kua pale wakati msafara huo unarudi katika Mji wa
Makkah basi mbali ya kua hali ya Jangwani ilikua ni ya Jua kali lakini kwa upande wao
ilikua kama kuna kivuli katika kila sehemu wanayopita na hivyo kutokua ni wenye
kuathiriwa na Ujoto wa Jua hilo, na hivyo Maysara akajaribu kujizuia kwa kutowaambia
wasafiri wenzake kutokana na ugunduzi wake huo, kwani alikua anasubiri kufikisha
habari hio njema kuliko zote kwa mtu mmoja tu pekee ambae ni mmiliki wake yaani ni
Khadija Bint Khuwaylid.
Msafara huo ulipokaribia katika Mji wa Makkah basi Khadija Bint Khuwaylid nae
akakugundua kua Msafara huo ulikua ukifuatwa na Kiwingu ambacho ni chenye kuupa
Kivuli Msafara huo, ambacho kilisimama pia karibu ya Nyumba yake pale Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alipokaribi na kukabidhi mzigo wa Mali alizonunua kutoka
katika Mji wa Dimashq kwa ajili ya kuja kuuzwa kwenye Mji wa Makkah.
Na bila ya shaka Maysara nae alipofika mbele ya Khadija Bint Khuawaylid na kumpa
habari juu ya kila kilichotokea na alichosikia kutoka kwa Nastura na kisha kuongezea
yale aliyoyaona kwa uchunguzi wake mwenyewe kua hakuna Mtu muaminifu, mkweli
na mwenye barka kwenye Biashara kama Muhammad Salallahu Aalyhi wa Salam na
uthibitisho unaonekana wazi juu ya mali alizokuja nazo ambazo wingi wake na fadiya
yake ni tofauti na hali ya biashara ya Bi Khadija Bint Khuwaylid ya hapo kabla ya
Misafara yake yote ya kibiashara.
Ambapo mara baada ya kuelezewa kila kilichotokea basi Bi Khadija Bint Khuwaylid nae
akakumbuka maneno ya yule Yahudi aliesema katika ile sikua liyokua akizunguka Al
Kaabah na marafiki zake, na hivyo hakuweza kufikiria tena kuhusiana na faida
iliyopatikaan kwenye Biashara yake, kwani kilichogangda akilini mwake ni Ukweli wa
maneno aliyoyasikia kabla yake ambayo ni kuhusiana na Mtume wa mwisho katika
wakati wa uhai wake, ambae tayari yuko chini yake katika usimamizi wa Biashara zake.
Hivyo bila ya kupoteza mda basi Khadija Bint Khuwaylid akatoka moja kwa moja hadi
kwa mtoto wa Mjomba wake aitwae Waraqah Ibn Nawfal ambae ni mwenye Ilm ya Ahl
al Kitab na kisha akamuelezea kuhusiana na yaliyotokea, ambapo baada ya kusikia habari
hio basi Waraqah akakaa kimya huku akitafakkar juu ya habari hizo na kisha akasema:
‘Kama unayoyasema ni kweli basi Muhammad atakua kweli ndie Mtume wa
mwisho atakaetumwa kwenye Ummah huu, ambae mimi pia nilikua nikijua
kuhusiana na kua atakuja na nilikua namsubiri ila sikuwa ni mwenye kujua kua
ndio ameshawasili.’
633
Ambapo kauli hii ilimfurahisha sana Khadija Bint Khuwaylid, kwani mbali ya kua alikua
ni mwenye kuvutiwa na uzuri wake, uaminifua na uadilifu wake, kiasi ya kua alikua
tayari kumlipa zaidi ya mara mbili yake katika kusimamia biashara zake lakini pia habari
hii ya kua yeye ndie Mtume wa mwisho ilimuathiri sana ndani ya Moyo wake hivyo
akatamani kua Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam awe ndie Mume wake kutokana
na upekee wa sifa zake, mbali ya kua kwa mda mrefu hakua ni mwenye kufikria
kuhusiana kua na haja kuolewa tena maishani mwake, lakini ghalfa moja mfumuko wa
matukio haya yaliyojitokeza mbele ya macho yake na ufaham wake yalimpeleka kua ni
mwenye kujikuta akiwa amezama kwenye bahari ya hisia nzito za kimaumbile za
mapenzi ndani ya Moyo wake.
Ambapo kimaumbile hizi hua ni hisia zisizokua na maana pale inapokua ni za upande
mmoja tu, kwani ili hisia hizi zikamilike basi inabidi kuwepo kwa hali ya uwiano wa
makubaliano wa ndani ya nyoyo baina ya pande mbili ya hisia za Mwanamke na
Mwanamme, kwani vyenginevyo basi anaependa bila ya kupendwa hua ni mwenye
kuumizwa na athari ya mapenzi yake kwa yule asiekua na hisia za kumpenda juu yake.
Kwani kwa lugha ya Kiarabu mapenzi hua yanafafanulika na kuelezewa kwa maneno
mengi, ikiwemo:
1. Hawa – hii ni hali ya mwanzo ambayo hua ni hali ambayo unauteka nyara Moyo na
hivyo hua ni wenye matamanio mengi sana na ya ghafla na ndio maana Waarabu wakawa
wananasibisha hali hii na Hawa al Najm yaani Mapenzi yanayofanana na Kuanguka kwa
Nyota.
2. Wadd – Baada ya Hawa basi hali inyofuatia hua ni ile inayoitwa Wadd ambayo hua ni
hali ya kupenda kwa kuendelea na kwa uaminifu.
3. Hubb – Baada ya Wadd ndio hua inafuatia hali ya Hubb ambayo hua ni hali ya Mapenzi
ya kimaumbile kunakotokana na kua na Mapenzi yaliyo safi ambayo ndani yake basi yule
anaependa hua hana khiari wala uthibitisho wa kuwepo kwa khiari ya anaependwa.
4. Ishq – ambayo hua ni hali ya kudhibitiwa na matamanio yanayotokana na mapenzi
yaliyouzunguka Moyo wa anaependa. Kwani neno Ishq hua ni lenye kutokana na neno
Ashaqa ambalo hua ni lenye kumaanisha Kupanda, Kuzunguka, Kuzonga katika Miti
tofauti, na hivyo Ishq hua ni hali ya kuzongwa wa Moyo wa anaependa kiasi ya kua hua
haoni mwengine zaidi ya yule anaempenda.
Ambapo mara nyingi hua linatumika neno Hubb, ambapo neno Hubb hua ni lenye
kutokana na harfu 2 za Kiarabu ambazo ni:
634
1- Hu Ambayo unapoitamka basi hua inasababisha mdomo kuachana na kutanuka,
na
2- Bb Ambayo unapoitamka basi hua inasababisha Midomo Kufunga na Kuungana.
Neno Hubb ambalo linamaanisha Hisia za Mapenzi au Kupenda hua linaweka wazi kua
‘Moyo wa Mtu unapopenda hua unatanuka na kisha unamuingiza mhusika
anaependwa na Moyo wa huyo unaopenda ndani yake katika kina chake, na
kumbakisha anaependwa ndani ya kina cha Moyo wa anaependa, kama vile kitu
kilichoingizwa Mdomoni kisha Mdomo Ukafumbwa na kilichoingizwa ndani yake
ikawa kimemezwa, bila ya kutakiwa kutoka ndani yake kama vile linavyoonesha
neno Hubb katika wakati wa kulitamka kwake.’
Na hivyo basi neno Hubb ambalo ndio lililotoa neno Mahabba hua linatumika kuelezea
Mapenzi ambayo ni yenye kudumu kiasi ya kua anaependwa hua hawezi kusahaulika
ndani ya Akili na Moyo wa anaependa, na hivyo hisia hizo hua ni zenye usafi usiokua
na shaka ndani yake wala kuchujwa na hisia nyengine zozote. Na ndio maana Allah
Subhanah wa Ta’ala akasema katika Qur’an kua:
﴿وَمِنَ ٱلن َّاسِ مَن يَت َّخِ ذُ مِن دُونِ ٱهلل َِّ أَندَاداً يحُِب ُّونَهُمْ كَحُبِّ ٱهلل َِّ وَٱل َّذِينَ آمَنُواْ
أَشَد ُّ حُبّاً﴾
Wamina alnnasi man yattakhidhu min dooni Allahi andadan yuhibboonahum
kahubbi Allahi waalladheena amanoo ashaddu hubban lillahi (Surat Al Baqar 2:165)
Tafsir: Na miongoni mwa watu wale wanaowachukua Miungu myengine zaidi ya Allah
kama wapinzani hua ni wenye kuwapenda kama wanavyompenda Allah, lakini wale
walioamini basi hua ni wenye kumpenda sana Allah (kuliko kitu chochote).
Ambapo tunapozungumzia Mahabat na Mawaddah yaani Mapenzi kwa Upande wa
Viumbe basi tunaona kua Allah Subhanah wa Ta’ala amesema katika Qur’an kua:
﴿وَمِنْ آَتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِ كُمْ أَزْوَاجاً لِّتَسْكُنُو ۤ اْ إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُم
م َّوَد َّةً وَرَحمَْةً إِن َّ فىِ ذٰلِكََ لآَتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَك َّرُونَ ﴾
635
Wamin ayatihi an khalaqa lakum min anfusikum azwajan litaskunoo ilayha
wajaAAala baynakum mawaddatan warahmatan inna fee dhalika laayatin
liqawmin yatafakkaroona (Surat Rum 30:21)
Tafsir: Na katika dalili zake ni kukumbieni nyinyi kutokana na Nafsi zenu miongoni
mwenu pea (Wake na Waume) ili mpate utulivu kutokana nao, na akajaalia baaina
yenu Mapenzi na Huruma, kwa hakika katika haya mna Vithitisho kwa watu wenye
kutafakkari.
Kwani hisia za hali hii ya Mahabat na Mawaddat baina ya Mwanamme na Mwanamke
hua ni yenye kutokana na Maumbile kamilifu ya Mwili wa Ibn Adam ambayo hua ni
yenye sifa ya kuzalisha kemikali nyingi miongoni mwao ikiwemo za Dopamine na
Oxytocin ambazo zinazosimamia hisia za Mapenzi, Matamanio, Mshikamano,
Kusaidiana, Kuhurumiana, n.k baina ya Mke na Mume, Baba na Mama, Kaka na Dada,
Ndugu na Familia, n.k kulingana na uhusiano wa hali ya hisia hizo zinazosababishwa
kuzalishwa kutokana na nguvu na uwezo wa Moyo na pia Ubongo wa Ibn Adam.
Kwani tunapozungumzia Oxytocin basi hua tunazungumzia kemikali ambazo kimaarufu
hua zinajulikana kama kemikali za ‘Mapenzi na Uaminifu’ na huzalishwa ndani ya miili
yetu baada ya kupatikana hisia zinazotokana na ufanyaji kazi wa viungo vya hisia za
Mwili za Kuona, Kusikia Sauti, Kuhisi Harufu au Kugusana na hivyo hutupelekea kua
na hali ya kujisikia kua na Raha, Upendo, Utulivu, Usalama, Amani pale tunapokua
karibu na wale tunaowapenda na hivyo kutuzidishia hisia za kutotaka kukosana au
kuachana na watu hao na kuwapenda, kuwajali, kuwafanyia ukarimu na kuwaonea
huruma.
Kemikali za Oxytocin pia hua ndizo zinazosimamia jukumu la kuvitayarisha viungo vya
mwili wa Mwanamme na Mwanamke kwa ajili ya kua tayari katika hali ya kuingiliana
kimwili, kwa ajili ya kuendeleza vizazi na pia kwa ajili ya kuupa utulivu na kuupumzisha
mwili kwa kuupa hisia za Raha inayotokana na kitendo cha kuingiliana kimwili, ambayo
hutegemeana na wingi wa uzalishwaji wa Oxytocin kwani kila zinavyozidi kuzalishwa
kwa wingi zaidi katika wakati wa tendo hilo basi ndio inavyozidi kupatikana hisia za
Raha ambayo haina mfano wake katika tendo hilo kama anavyoelezea Hujjat ul Islami
Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali pale aliposema kua: ‘Raha ya mda mfupi inayopatikana
katika kuingiliana kimwili basi hua ni Raha ambayo kamwe haiwezi kufananishwa
na Raha nyengine, na kama ingekua ni yenye kudumu basi ingekua ni moja kati ya
dalili ya moja kati ya Raha za Milele tulizoahidiwa Peponi’
Hujjat ul Islami Mujaddid Ad Din Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali anatufafanulia zaidi pale aliposema: ‘Hikma ya Allah Subhanah wa
Ta’ala na Rehma zake zinaonekana pale unapoangalia katika kuweka Matamanio ya aina
636
mbili katika Maisha yetu. Matamanio ya kwanza hua ni ya muonekano wa kimaisha wa nje
pale mtu anapokua anaendeleza kizazi chake kupitia kwa watoto wake. Na muonekano wa
pili ni wa muonekano wa kimaisha ya ndani unaohusiana na maisha ya baadae kesho
Akhera. Kwani raha ya kuingiliana kimwili hua si yenye kudumu katika ulimwengu huu na
ni lazima iwe ni ya mda mfupi, na yenye kikomo kwa kumalizika mara tu baada ya kuihisi
raha hio kiasi ya kua humpelekea Ibn Adam kua na hamu ya kutaka raha hio iwe ni yenye
kudumu, na hivyo hii humfanya Ibn Adam kua ni mwenye kudumu katika kufanya Mema
kiibada ambayo yatampelekea kupata Raha kama hizo milele.’
Na ukweli ni kua tunapozungumzia hisia za Mapenzi na kupenda, basi hua ni miongoni
mwa neema ya Hisia za Kimaumbile na ndio maana Allah Subhanah wa Ta'ala akasema
katika Surat Al Imran kua:
﴿زُيِّنَ لِلن َّاسِ حُب ُّ ٱلش َّهَوَاتِ مِنَ ٱلنِّسَاءِ وَٱلْبَنِينَ وَٱلْقَنَاطِيرِ ٱلْمُقَنْطَرَةِ مِنَ
ٱلذ َّهَبِ وَٱلْفِض َّةِ وَٱلخَْيْلِ ٱلْمُسَو َّمَةِ وَٱلأَنْعَامِ وَٱلحَْرْثِ ذٰلِكَ مَتَاعُ ٱلحَْيَاةِ ٱلد ُّنْيَا وَٱهلل َُّ
عِنْدَ هُ حُسْ نُ ٱلْمَآبِ ﴾
Zuyyina lilnnasi hubbu alshshahawati mina alnnisa-i waalbaneena waalqanateeri
almuqantarati mina aldhdhahabi waalfidhdhati waalkhayli almusawwamati waalanAAami
waalharthi dhalika mataAAu alhayati alddunya waAllahu AAindahu
husnu almaabi (Surat Al Imran 3:14)
Tafsir: Vimependezeshwa kwa ajili ya Watu kupenda vyenye kutamanisha
vinavyotokana na Wanawake na Watoto na Wingi wa Marundo ya Dhahabu na Fedha
na Farasi (Vipando) Wazuri na Ngombe na Ardhi yenye Rutba, Hakika Haya ni
Mapambo ya Maisha ya Dunia na Kwa Allah ndiko kwenye Marudio Bora.
Ambapo kutokana na kujua hali ya uhalisia wa hisia hizo basi Bi Khadija Bint
Khuwaylid, mbali ya kua amevutiwa na anapenda Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
awe ndie Mume wake, lakini akasita na kuanza kujiuliza kwanza, hivi jee Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam atakua na hisia kama zake juu yake? Hivi jee atakubaliana na
mapendekezo yangu ya kutaka kuolewa nae kutokana na tofauti ya umri baina yao, kwani
Khadija Bint Khuwaylid alikua na umri wa miaka 40, wakati Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alikua na umri wa miaka 25 katika kipindi hiki.
Yaani hiki hua ni kitendawili kisichoteguka, na ndio maana akasema Imam Abu Hasan
Al Shadhili katika kumuomba kwake Allah Subhanah wa Ta’ala kua: ‘Ya Allah!
637
Zifanye Amali zangu mbaya kua ni amali za watu uwapendao, na wala usizifanye
Amali zangu Njema kua ni za watu usiowapenda’ na hivyo kumaanisha kua: ‘Bora
niwe na Amali sizo huku nikiwa ni mtu nnaependwa nawe kuliko kua mtu mwenye
amali ndizo lakini hapo hapo nikawa ni mtu nisie pendwa nawe, ya Allah’
Hivyo Khadija bint Khuwaylid akarudi nyumbani kwake na kubakia akitafakari athari ya
hisia zake za kimaumbile kwa Kijana Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam, na
kujiuliza masuali yasiyokua na majibu kuhusiana na hisia zake, na mara akatembelewa
na rafiki yake aitwae Nufaysa Bint Munabih ambapo Khadija Bint Khuwaylid akaanza
kumuelezea kuhusiana na hisia zake juu ya Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam na
sifa zake.
Ambapo mara baada ya Khadija Bint Khuwaylid kubainisha hisia zake kwa Nufaysa basi
Nufaysa alipotoka akaelekea moja kwa moja kwa Abu Talib na kuanza kuzungumza na
Rasul Aallah Salallahu Alayhi wa Salam kuhusiana na habari za safari na kisha
akumuuliza kwa kusema: ‘Hivi kwanini mpaka leo hii hujaoa ewe Muhammad?’
ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Sijawa na uwezo wa Kuoa
bado.’
Nufaysa akapendekeza kwa kusema: ‘Hivi jee kama atatokea Mwanamke ambae anao
uwezo utakubali kuoana nae?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akauliza:
‘Kama nani kwa mfano? ’ Nuwayla akasema: ‘Kama Khadija Bint Khuwaylid’, hapo
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Bila ya shaka nitakubaliana nae
kama akikubali.’
NDOA YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’ALAYHI WA SALAM
NA KHADIJA BINT KHUWAYLID RADHI ALLAHU ANHA.
Baada ya Nufaysa kuzungumza na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kuthibitisha
kua upo uwezekano wa kua pamoja kwa kisharia katika ndoa baina ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na Khadijah Bint Khuwaylid basi Nufaysa akatoka na
kukimbilia kwa Khadija Bint Khuwaylid kwa ajili ya kumpa habari njema ambazo ni
zenye kumfurahisha zaidi Khadija Bint Khuwaylid kuliko hata zile za mwanzo alizokua
nazo za kupata faida kubwa kwenye biashara yake katika kipindi hicho, na kua
anaemsimamia Biashara zake atakua ni mwenye Darja ya Utume.
Ambapo kwa upande wa Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam baada ya kupata habari
ya kua Khadija yuko tayari kuolewa nae, basi nae akamfuata Abu Talib na Hamza na
kuwapa habari njema hizo, habari hizi zilikua ni nzuri sana pia kwa upande wa Abu Talib
638
na Hamza kwa sababu katika Mji wa Makkah hakukua na Mwanamke Mzuri, Mkarimu,
Mwenye tabia Nzuri, Tajiri na mwenye kujiheshimu na kuheshimika kama Kahdija Bint
Khuwaylid, kwani katika Mji wa Makkah na maeneo ya Jirani kila mtu alikua anataka
kumuoa yeye lakini Khadija Bint Khuwaylid mwenyewe alikua ni mwenye kuwakataa
wengi sana, kiasi ya kua kila mtu alikua anaogopa kwenda kuposa kutokana na kujua kua
atakataliwa, na bila ya shaka hakuna hata Mwanamme mmoja ambae angeikataa nafasi
kama hii aliyoipata Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutoka kwa Khadijah Bint
Khuwaylid.
Hivyo Abu Talib na Hamza wakatoka na kuenda moja kwa amoja kwa Amr Ibn Asad
ambae alikua ndie Ami yake Khadijah Bint Khuwaylid Ibn Asad, ambae nae
akawakilisha posa hio na kuithibitisha kwa mwenyewe mhusika mkuu ambae ni Khadija
Bint Khuwaylid, alieipokea na kuikubali kwa Mapenzi, furaha na ridhaa kubwa ndani ya
Moyo wake kwa kujaaliwa kile kilichobora kuliko vyote kutoka kwa Mola wake,
ambacho ni kupata majibu ya kukubalika kwa mapenzi yake ya dhati yasiyokua na mfano
wake kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Baada ya makubaliano hayo basi ikapangwa siku ya harusi na Khadija Bint Khuwaylid
mwenyewe na sehemu itakayofanyika akaichagua kua ni ndani ya Nyumba yake, kwani
hii ilikua ni harusi kubwa na ya kifahari baina ya mwanamke bora wa Quraysh mwenye
darja ya Amirat Al Quraysh na Mwanamme bora kuwahi kuumbwa ambae ni Muhammad
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae pia ni Mtoto wa ndugu yake Chifu Mkuu
wa Mji wa Makkah yaani Abu Talib, hivyo kila mtu ndani ya mji wa Makkah alikua
anategemewa kualikwa na kufurahika ndani yake.
Na bila ya shaka watu walifurahika na kuburudika kwa kila kitu kizuri na kisafi na kisha
baada ya sherehe basi Abu Talib ambae ndie Mkuu wa Mji wa Makkah akasimama na
kusema: ‘Alhamd lillah, shukurani zote anastahiki Allah kwani yeye ndie
alietuumba kutokana na kizazi cha Ibrahim, kupitia kwa Ismail, kutoka kwa vizazi
vya Maada na kwa Mudar.
Ambapo kama mnavyovyojua, mtoto wa ndugu yangu Muhammad Ibn Abdullah,
ni jamaa yenu, na hakuna Kijana kutoka katika Ukoo wa Quraysh ambae anaweza
kufanana nae kwa ubora wa sifa zake, kuanzia wa sifa za Kimaumbile, Kitabia,
Kiakili, Kiheshima na Kidarja, na bila ya shaka yeye ni mtu asiekua na Mali nyingi,
lakini Mali ni nini? Mali ni kitu kilichofichikana chenye hali ya mpito, kisichokua
ni cha kudumu na ni chenye hali ya kupewa na kupokonywa kwa kila mtu.’
Hakika mimi Abu Talib nnaapa kwa jina la Allah kua Darja ya Muhammad
inapanda na itazidi kukua hivyo sasa hivi anaomba mkono wa binti yenu Khadijah
kwa kuoana nae na atalipa Ngamia 20 wa kiume kua ni Mahari.’
639
Baada ya Abu Talib kumaliza kuzungumza basi Akanyanyuka Waraqah Ibn Nawfal na
kusema: ‘Alhamd lillah, kwani Allah ndie alietuumba kama ulivyoelezea Abu Talib,
na bila ya shaka ametupa heshima kubwa zaidi kuliko ya ulivyoelezea Abu Talib,
hivyo nasi tunapenda kuendeleza na kudumisha heshima hio kwa kuunganisha
familia yetu na yenu. Hivyo Enyi watu wa Quraysh! Nataka kua muwe mashahidi
kua mimi namuozesha Bint wa Khuwaylid kwa Muhamamd Ibn Abdalla kwa
Mahari yaliyotolewa.’
Na kisha baada ya Waraqah Ibn Nawfal kumaliza khutba hio basi akasimama Amr Ibn
Asad na kusema: ‘Enyi watu wa Quraysh, Hakika mimi Amr Ibn Asad
nimewaunganisha Muhammad Ibn Abd Abdullah na Bint Khuwaylid kwa
kuwaozesha.’
Kisha baada ya hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamchukua na kumpeleka
Khadija Bint Khuwaylid kwa Ami yake ambako nako kukachinjwa Ngamia wawili na
kisha ikafanywa karamu watu wakafurahika. Na baada ya hapo Rasul Allah Sallahu
Alayhi wa Salam akahamia kwa Khadijah Bint Khuwaylid pamoja na Ummu Ayman,
kwani Rasul Al Salallahu Aalayhi wa Salam kamwe hakumsahau Baraka - Mama yake
Mlezi.
Ambapo Baraka naelezea haya kwa kusema: ‘Kwa Hakika mimi tangu
nilipokabidhiwa na Amina Bint Wahb kua kama Mwanangu basi Mimi sikuachana
nae na wala yeye Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam hakuachana na mimi,’ Kwani
Barakah anaendelea kutuambia kua: ‘Siku Moja wakati tukiwa kwa Bi Khadija, basi
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliniita Ya Ummah! (Ewe Mama)’
Kisha nilipoenda aliponiita basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: Ewe
Mama! Hakika mimi nimeshaoa na wewe Hujaolewa Bado, Hivi jee unaonaje kama
akija Mtu na kutaka kukuoa?’
Baraka akamwangalia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa Mapenzi ya Mama
kwa Mtoto wake kisha akasema kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam:
‘Hakika mimi kamwe sitoachana na wewe, hivi jee umeshawahi kuona wapi kua
Mama akaachana na Mtoto wake?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akatabasam kisha akamsogelea Barakah
akamshika Uso wake na kisha akalibusu Paji la Uso la Barakah huku akiwa amejawa na
furaha na kisha akamgeukia Bi Khadijah na kumwambia: ‘Khadija Huyu ni Baraka,
Huyu ni Mama yangu Mlezi baada ya Mama yangu Mzazi, hivyo yeye pia ni mmoja
kati ya Watu wa Familia yangu.’
640
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaendelea kua msimamizi wa Biashara ya
Khadijah Bibt Khuwaylid na kuziendeleza bila ya kua ni mwenye kufanya israf wala
kujionesha kutokana na kua Mkewe ni Tajiri mkubwa sana, kwani Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam aliendelea kuishi maisha ya kawaida na ya unyenyekevu kama ilivyokua
hapo kabla, ambapo kabla ya wakati huu basi Khadija Bint Khuwaylid alizawadiwa
Mtumwa ambae ni mtoto wa kiume aitwae Zayd Ibn Harith ambae alikamatwa alipokua
safarini na mama yake, na kisha akauzwa sokoni na kununuliwa na Hakim Ibn Hizam
Ibn Khuwaylid kwa Dirham 400.
Hivyo baada ya harusi Khadija Bint Khuwaylid akamzawadia Rasul Allah Salallahu
Aalyhi wa Salam Zayd Ibn Harith ili awe mtumwa wake ambae kwa wakati huo alikua
na umri wa miaka 14 na hivyo Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam akamwachia huru
na kumfanya kua mtoto wake wa kulea na pia msaidizi wake katika shughuli zake mbali
mbali badala ya kua Mtumwa wake.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Khadija Bint Khuwaylid, Ummu
Ayman na Zayd Ibn Harith wakawa ni wenye kuishi pamoja ndani ya nyumba ya Bi
Khadija Bint Khuwaylid, nyumba ambayo ilikua imejaa furaha, mapenzi, huruma,
heshima, utulivu na ukarimu ndani yake.
Tunapoangalia kuhusiana na mapenzi ndani ya Nyumba ya Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam basi tunaona pale siku moja baada ya Rasul Allah Salallahbu Alayhi wa Salam
wakati akiwa ndani ya nyumba yake basi alisikia Mlango unagongwa huku yeye
mwenyewe akiwa amevaa Suruali tu, huku akiwa kifua wazi, na alipouliza ni nani
anaegona Mlango na kujibiwa kua ni Zayd Ibn Harith basi Rasul Allah Salallahu Aalyhi
wa Salam alinyanyuka kwa furaha na akenda kufungua Mlango huo na kisha
akamkumbatia Zayd Ibn Harith kwa nguvu na kumbusu Paji lake la uso na kumkumbatia
zaidi, yaani Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam alisahau hata kuvaa joho lake juu na
kufunika kifua chake kutokana na furaha na mapenzi yake kwa watu wake.
Ambapo tunapoangalia ukarimu wake Khadija Bint Khuwaylid basi ni pale siku moja
alipotembelewa na Halima Bint Dhuayb aliemnyonyesha Rasul Allah Salallahu Aalahyi
wa Salam alipokua mdogo, na Khadija Bint Khuwaylid akamzawadia Halima Kondoo
40 kutokana na kua ndie Mama aliemnyonyesha na kumlea vizuri Mume wake.
Kwani bila ya shaka Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam na Khadija Bint Khuwaylid
walikua ni watu ambao wenye kupendana sana kiasi ya kua mapenzi haya yalikua wazi
hata baada ya kufariki wa Khadija Bint Khuwaylid basi alisema Aisha Radhi Allahu Anha
kua: ‘Hakika mimi sikua ni mwenye kumuonea wivu mke yeyote wa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kama nilivyokua nikimuonea wivu Khadija bint
Khuwaylid.’
641
Ndoa hii ya Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam na Khadija Bint Khuwaylid ilitoa pia
matunda mema ya watoto 6 ambao ni Qasim, Zaynab, Ruqqayah, Umm Kulthum, Fatma
na Abd Allah, ambapo Qasim Ibn Muhammad ambae ndie mtoto wa mwanzo aliezaliwa
ndani ya miaka mitatu ya mwanzo ya ndoa hii yaani wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alipokua na umri wa miaka 28 na Bi Khadijah Bint Khuwaylid alikiwa na umri
wa miaka 43, ambapo Qasim aliishi kwa mda wa miaka mitatu tu na kisha akafariki.
MUHAMMAD AL AMIN SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA
UJENZI WA AL KAABAH.
Miaka 10 baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kumuoa Khadija Bint
Khuwaylid basi katika Mji wa Makkah ilitokea mvua kubwa sana ambayo ilisababisha
mafuriko ambayo yalisababisha mdhara makubwa sana ikiwemo Jengo la Al Kaabah,
kiasi ya kus jengo hilo likawa ni lazima lifanyiwe matengenezo, kwani vyenginevyo
litasababisha madhara makubwa zaidi kutokaa na kuwaangukia watu.
Na ili litengenezwe upya basi ilikua inabidi livunjwe lote kwanza kisha linyanyuliwe kwa
kujengwa upya, na ingawa hali ilikua kama hivyo lakini hata hivyo hakuna hata mtu
mmoja aliethubutu kulivunja jengo hilo, kutokana na khofu ya kua huenda mwenye Jengo
lake yaani Allah Subhanah wa Ta’ala atapitisha adhabu yake kwa yeyote yule
atakaelivunja jengo hilo na hivyo kwa kusababisha kutokea kama yaliyotokea miaka 35
hapo kabla katika mwaka wa Tembo dhidi ya Jeshi la watu wa Tembo.
Katika mwaka huo baada ya Mvua kumalizika basi kwa bahati mbaya kuna mwanamke
aliwasha Moto ambao cheche zake zilirukia kwenye Kitambaa cha Al Kaabah na Al
Kaabah ikawaka moto, na kama haitoshi basi baada ya tukio hilo usiku mmoja wakatokea
wezi na kuiba Dhahabu zote zilizokua ni mapambo ndani ya Jengo la Al Kaabah, hivyo
watu wa Kabila la Quraysh wakaamua kua umefika wakati wa kulivunja na kulijenga
Upya jengo hilo, lakini suali likabakia, ni kua: ‘Jee ni nani miongoni mwao atakaeweza
kuanzisha kuchukua hatua hio ya kulivunja Jengo hilo tukufu la miaka na miaka?’
Tunapozungumzia Watu wa Kabila la Quraysh basi tunaona kua ni watu ambao kwa
miaka na miaka, walikua na mfumo wa kupeana majukumu tofauti ya kuhudumia jamii
yao ya Mji wa Makkah, na kabila la Banu Makhzum lilikua lina jukumu la kusimamia na
kulinda usalama wa mji wa Makkah, kuandaa viongozi watakao ongoza mapambano
vinapotokea vita na pia kusimamia na kulinda misafara ya wafanya biashara wa Makkah
wanapoenda kufanya biashara katika maeneo mengine kama vile Sham, Yemen n.k. hili
ndio lililokua Kabila la Khalid Ibn Al Walid Al Mughirah Ibn Abdullah Ibn Umar Ibn
Makhzum Ibn Yaqza Ibn Murra Radhi Allahu Anhu.
642
Baba yake Khalid Ibn Walid ambae ni Al Walid Ibn Mughira alikua ni tajiri mkubwa
sana na pia ndie aliekua msimamizi mkuu wa kusimamia usalama wote wa watu wa mji
wa Makkah, ambapo hali hii ya kimazingira na kimajukumu katika jamii ya watu wa
Qurays ilimpelekea Khalid Ibn Walid kua hana haja ya kufanya kazi nyengine isipokua
kufanya mazoezi ya kupigana. Mazingira ya kimaisha ya kabila hili yalimfanya Khalid
kua kijana asiekua na mpinzani katika zama zake, kwani baba yake alimfundisha
kupigana kwa kutumia mwili wake na kwa kutumia silaha aina zote za kivita za wakati
huo, na pia kupigana katika mazingira yeyote yale iwe chini au juu na kwa kutumia
vipando vya wanyama wa aina zote.
Mama yake Khalid Ibn Walid alikua akiitwa Lubabah As Saghira Bint Harith Ibn Hazan
Al Hilalieh, ambae alikua ni dada yake Maymuna Bint Harith Ibn Hazan Al Hilalieh
ambae aliekua ni Mke wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na pia dada wa
Lubaba Al Ghubra Bint Harith Ibn Hazan Al Hilalieh aliekua mke wa Al Abbas Ibn Abd
Al Muttalib ambae ni Ami yake Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ambae
pia ndie aliekua baba yake Sahaba maarufu aitwae Abd Allah Ibn Abbas (Bahr ul I’lm).
Hivyo baada ya watu wa Quraysh kuamua kutaka kulivunja Jengeo la Al Kaabah basi
alikua ni kiongozi Mkuu wa Usalam wa Mji wa Makkah ambae ni Al Walid Ibn Mughira
ambae yeye ndie aliejitolea kua jukumu hilo atalianza kulibeba yeye kwa mikono yake,
huku watu wote wakiwa na khofu kubwa na kusema kua wanasubiri kitakachomtokea Al
Walid Ibn Mughira, kama akidhurika basi hakuna atakediriki kulivunja Jengo hilo, lakini
kama akiwa hajadhurika basi nao watasaidia katika kulivunja lote Jengo hilo na kulijenga
upya.
Hivyo Al Walid Ibn Mughira akachukua Nyundo yake kisha akaenda hadi kwenye Al
Kaabah na kusema: ‘Ya Allah hakika mimi sio kama siiamini Dini yako, isipokua
inabidi tufanye hivyi tunavyofanya ili kuliboresha hili jengo lako tukufu.’ Na baada
ya hapo akvunja upande mmoja wa Al Kaabah, na kisha akondoka, hukua akiwaacha
watu wakisubiri kitakachomtokea baada yake. Lakini baada ya tukio hilo hakuna
lililotokea hivyo sikua ya pili asubuhi basi Al Walid Ibn Mughira akaendelea na kazi ya
kulivunja jengo hilo, huku watu wengine nao wakaanza kumsaidia hadi likamalizika na
kuanguka lote na kukutana na msingi wa awali wa jengo hilo.
Na walipoendelea kuchimba zaidi, basi wakatutana na mawe ya rangi ya Kijani ambayo
yameshikamana pamoja, na walipoendelea kuchimba basi ghafla ukatokea Mtetemeko
wa Ardhi, hivyo watu hao wa Quraysh wakaingiwa na khofu kubwa sana, na kuanza
kutaka kuimbia, lakini walipoacvha kuchimba basi Ardhi ikatulia, hivyo wakajua kua hio
ni dalili kua hawatakiwi kuendelea kuchimba zaidi. Kwa hivyo wakawacha haliiwe kama
ilivyo.
643
Baada ya kulivunja jengo hilo basi wakuu wa kabila Quraysh wakakaa na kufikiria
watumie kitu gani kwa ajili ya kulijenga upya jengo hilo, na mara wakapata habari kua
kuna Jahazi inayotoka ambayo Misri imefunga gati katika bahari Nyekundu karibu na
Mji wa Makkah, hivyo wakatuma ujumbe ukaangalie shehena ya Jahazi hio kwani
huenda labda wakapata vifaa vitakavyowafaa kwa ujenzi wa Jengo lao hilo. Na hivyo
ujumbe huo ukarudisha Majibu yasemayo kua Jahazi hio imebeba vifaa vya ujenzi
ikiwemo Vigae, Vyuma, Mbao, n.k
Hivi ni vitu ambavyo walikua wakivihitaji sana katika ujenzi wao huo, hivyo wakaamua
kua bora wafanya mazungumzo na wafanya biashara wa bidhaa hizo kua hawatowatoza
ushuru watakapokuja kwenye Mji wao kama watakubali kuwauzia vifaa hivyo kwa
urahisi kwa ajili ya ujenzi wao huo, na hivyo watu hao wakakubaliana na wazo hilo, na
kwa kua ndani ya Jahazi hilo pia fundi Muwashi mzuri sana aitwae Bakum ambae alikua
ni Mturuki hivyo wakazungumza nae na akakubaliana nao kuwajengea Jengo hilo.
Hivyo jengo hilo likajengwa huku ikiwa kila Ukoo ukiwa unasimamia upande wake
kulingana na makubaliano waliyoafikiana hapo kabla, na lilipofikia kwenye usawa wa
sehemu ya kuliweka Jiwe Jeusi, basi katokea mvutano mkubwa sana, kwani kutokana na
utukufu wake basi hawakuweza kufikia makubaliano juu ya nani ndie anaestahiki
kuliweka jiwe hilo katika sehemu yake. Na tayari kila mmoja alikua yuko tayari kupigana
kama akipewa mwenzake jukumu hilo na kukoseshwa yeye kuliweka jiwe hilo.
Kiasi ya kua kazi ya kujenga Al Kaabah ikasita kwa siku 4 tangu kuanzia siku ya
Alkhamis hadi siku ya Jumatatu kwa ajili tu ya kutopatikana makubaliano juu ya nani
anaestahiki kuliweka Hajar Al Aswad katika sehemu yake. Hivyo viongozi wa Kabila la
Quraysh wakapanga kua wakutane katika eneo la Masjid Haram ili watafute utatuzi wa
tatizo hilo. Na baada ya kukutana kwao katika siku hio ya Jumatatu na kuvutana kwa
takriban saa moja basi mmoja wao miongoni mwao aliekua akiitwa Hudhayfah Ibn
Mughira akasema: ‘Enyi watu wa Quraysh, hakika mimi naona kua hakuna mwisho
wa kujadiliana juu ya jambo hili isipokua kumteua mtu wa mwanzo atakaeingia
kuja humu Ndani kwa kupitia mlango ule pale wa Bani Shayba basi awe ndie
mtatuzi wa Jambo hili.’
Hivyo Viongozi hao wa Kabila la Quraysh wakakubaliana na mtizamo huo wa
Hudhayfah na kusema kua huo ndio utatuzi pekee utakaotatua mzozo huo, hivyo wakakaa
kimya huku wakiwa ni wenye kuutolea macho Mlango wa Banu Shayba kwa umakini
mkubwa sana, na haukuchukua mda mrefu mara wakaona kua kuna mtu anaingia kupitia
kwenye Mlango huo wa Banu Shayba na anakuja katika sehemu waliyokaa, na watu hao
wakatizamana na kisha wakaendelea kumtizama Mtu huyo kama hawaamini macho yao
huku wakitaka wapate kumjua ni nani?
644
Na bila ya shaka Mtu huyo hakua mtu mwengine isipokua alikua ni Al Amin na hapo
hapo watu hao wakashangilia kwa sauti kubwa zilizojaa furaha na ridhaa huku wakisema:
‘Ni Muhammahd Al Amin, bila ya shaka tutakubaliana na kuridhia kutokana na
hukumu yake.’
Kiasi ya kua Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam alishangazwa na furaha hio
waliyokua nayo Viongozi hao baada ya kutaja jina lake na hakuweza kuJua juu ya
linaloendelea hadi pale alipofika mbele yao kisha nao wakamuelezea tatizo lao. Ambapo
Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akatafakari kisha akasema: ‘Nipeni Kitambaa’
ambapo Al Walid Ibn Mughira akatoa Kilemba chake na kumpa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam.
Na pia kuna wasemao kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alivua Kilemba chake
na kukitandaza ardhini na kisha akalichukua Hajar Al Aswad na kuliweka katikati ya
kilemba hicho huku akiwaacha watu wakiwa wamejawa na mshangao, kwa kujiuliza ni
kitu gani kinachotakiwa kufanywa na Al Amin na kisha Rasul Allah Salallahu Aalayhi
wa Salam akasema: ‘Nataka kila Mtu kutoka kwenye kila Ukoo awe ni mwenye
kushika ncha ya kilemba hiki’
Na baada ya watu hao kushika kitambaa hicho basi Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa
Salam akawaambia kua walisogeze Jiwe hilo karibu na sehemu yake, na liliposogezwa
basi Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akalichukua kutoka kwenye kitambaa hicho
na kulipachika kwenye sehemu yake, na baada ya hapo ujenzi wa Al Kaabah ukaendelea
na kumalizika kwa salama na amani kwani kila mmoja katia ya waliohudhuria katika
tukio hilo walikua wameridhia na maamuzi hayo ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam.
RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM NA ALI IBN ABI
TALIB
Wakati Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam alipotimia umri wa miaka 36, basi Mji
wa Makkah ukakumbwa tena na ukame mkubwa na hivyo watu wake wakawa wana njaa,
na kila mtu akawa anahitaji Msaada kutoka kwa Mwenzake, hivyo katika kipindi hiki
ingawa Abu Talib ambae ni Ami yake mkubwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alikua ni Chifu wa Mji wa Makkah, lakini kama tulivyosema hapo awali kua alikua ni
Masikini, kwani Uchifu wake haukua ni wenye Kutokana na Mali bali Ulikua ni wenye
Kutokana na Utukufu wa Kabila lake na Ukoo wake.
Ambapo Miongoni mwa Watu wa Karibu wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
katika Maami zake yaani Mababa zake wadogo na wakubwa basi alikua ni Al Abbas
645
Radhi Allahu Anhu ambae ni baba yake Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, na
huyu alikua ni rafiki yake wa karibu sana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa
sababu ingawa Al Abbas alikua ni Baba mdogo lakini alikua amepishana na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kwa miaka mitano tu.
Hivyo walikua Mtu na Baba yake mdogo na pia mtu na rafiki yake wa karibu sana kwa
sababu ya kua walicheza pamoja, hivyo katika mwaka huo wa Ukame na Njaa basi Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia Al Abbas Ibn Abd Al Mutallib kua: ‘Ya
Al Abbas, hivi Jee unajua kua Kaka yako, Abu Talib ana familia kubwa sana? Na
kama unavyoona kua hali imekua ngumu kwa Ukame, hivyo wacha mimi nawe
tuende kwa Abu Talib tukamsaidie Majukumu yake, wewe utamsaidia Kulea
Mtoto Mmoja na Mimi nitachukua Mtoto mmoja kulea.’
Hivyo hapa tunaona kua ingawa Abu Talib Ibn Abd Al Mutallib alikua na watoto 7 lakini
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakusema kua Mimi nitachukua watoto Watatu
nilee na wewe utachukua Watatu kisha tukishindwa tutaomba msaada, La!..bali alisema
kua Wewe utachukua Mtoto Mmoja na Mimi nitachukua Mtoto Mmoja, na hii ni
kutokana na kujua hali ya Uwezo wake yeye Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
uwezo wa Ami yake.
Na ndio maana Allah Subhanah wa Ta’ala akasema kuhusiana nae Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua:
﴿ل َّقَدْ كَانَ لَكُمْ فىِ رَسُولِ ٱهلل َِّ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو ٱهلل ََّ وَٱلْيَوْمَ ٱلآخِ رَ
وَذَكَرَٱ هلل ََّكَثِير اً﴾
Laqad kana lakum fee rasooli Allahi oswatun hasanatun liman kana yarjoo Allaha
waalyawma al-akhira wadhakara Allaha katheeran (Surat Al Ahzab 33:21)
Tafsir: Kwa hakika mmepata kutoka kwa Rasul Allah mfano bora sana, kwa yule
mwenye matumaini juu ya Allah na siku ya Akhera na akamkumbuka Allah kwa
wingi.
Hivyo baada ya Makubaliano hayo basi Rasul Allah Salalahu Alayhi wa Salam na Ami
yake yaani Abbas Ibn Abd Al Mutallib Radhi Allahu Anhu wakatoka hadi kwa Abu Talib
Ibn Abd Al Mutallib na wakampa ushauri wao huo wa kutaka kumsaidia Ulezi. Hivyo
Abu Talib akakubaliana na shauri hilo la kusaidiwa Ulezi na Rasul Allah Sallahu Alayhi
646
wa Salam akapewa mtoto mmoja wa Kiume ambae ndie Ali Ibn Abu Talib Radhi Allahu
Anhu na akawa analelewa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Hivyo Nyumba ya Bi Khadija Bint Khuwaylid ikawa ameongezeka mtu mmoja ambae
ni Ali Ibn Abu Talib ambae katika kipindi hiki alikua na umri wa miaka mitano. Na Al
Abbas Radhi Allahu Anhu akapewa mtoto mwengine wa kiume amlee ambae ni Jafar Ibn
Abu Talib Radhi Allahu Anhu.
Ambapo siku moja katika nyumba hio ya Bi Khadija Bint Khuwaylid alikuja Mgeni
kutoka katika Mji wa Madinah ambae alikua anaitwa Ubayd Ibn Zayd na akamuona
Barakah na akampenda, hivyo Ubayd akazungumza na Bi Khadija na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam ambapo Bi Khadija akamwambia Baraka: ‘Barakah, hakika
wewe tayari umeshatumia Ujana wako wote kwa Ajili ya Muhammad (Salallahu
Alayhi wa Salam), hivyo nae anataka akulipe baadhi ya Majukumu yako juu yake.
Hivyo tunakuomba mimi na Muhammad (Salallahu Alayhi wa Salam) kua bora
Uolewe, hivyo usitukatalie maombi yetu juu yako’
Baraka akashangaa huku akitafakkari, kisha akauliza: ‘Hivi ni Nani atakaenitaka mimi
kunioa?’
Bi Khadija akasema: ‘Kuna mtu amekuja anaitwa Ubayd Ibn Zayd kutoka katika
Kabila la Al Khazraj la Madinah amekuja kuomba kuunga Udugu nasi, anataka
mkono wako, hivyo kwa ajili yetu, usikatae tafadhali’
Hivyo bila ya shaka Barakah akakubaliana na kuridhia Jambo hilo kwa ajili ya
Kumfurahisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Bi Khadija Bint Khuwaylid.
Hivyo Baraka akaolewa na Ubayd Ibn Zayd na kisha akahama katika Mji wa Makkah
akahamia katika Mji wa Madinah lakini hata hivyo hakukaa kwa mda mrefu kwani nae
kwa upande wake hali ilikua kama ilivyokua ya aliekua Sayyida wake yaani Bi Amina
Bint Wahb mama yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae alifiliwa na
mumewe muda mfupi baada ya kuolewa.
Hivyo na Barakah nae alikua na majaaliwa hayo hayo, kwani Allah Subhanah wa Ta'ala
alimuandikia kua aondoke katika Mji wa Makkah kwa mfupi kisha arudi tena kwa Mtoto
wake kipenzi kwani alipofika katika Mji wa Madinah baada ya kuolewa hakukaa mda
mrefu kwani Mumewe akafariki huku akimwacha Barakah akiwa Mja Mzito ambapo
baadae alijifungua mtoto wa Kiume aitwae Ayman.
Na Wanazuoni wametofautiana kuhusiana na sehemu aliyozaliwa Ayman, kwani kuna
wasemao kua alizaliwa katika Mji wa Madinah na kuna wanaosema kua Barakah alirudi
katika Mji wa Makkah akiwa mja mzito na akamzaa Ayman katika Mji wa Makkah.
647
Ambapo baada ya kujifungua mtoto huyo basi Jina la Barakah likafutika kwani kila mtu
akawa anamwita kwa jina la Mtoto wake yaani Ummu Ayman yaani Mama Ayman,
isipokua kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, kwani kwake yeye Barakah hakua
Barakah wala hakua Ummu Ayman bali alikua ni Ummu - Mama!
Hivyo baada ya kufariki Mumewe katika Mji wa Madinah basi Ummu Ayman akarudi
katika Mji wa Makka na hakua na sehemu yeyote ya kufikia na kuishi isipokua kwenye
Nyumba ya Mtoto wake Kipenzi yaani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Ingawa katika kipindi hiki Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua hajapata
Utume bado, lakini alikua anajua kua watu wa Makkah walikua wanaishi katika hali ya
Kijahiliyah katika Imani zao, vitendo vyao na hata katika maneno yao, kwani ujinga
ilikua ndio maisha yao.
Hivyo akawa anajaribu kutafakkar hali hiyo imekua kuaje? Na itaendelea hadi lini? Na
katika kipindi hiki alikua usiku anapolala hua anaona ndoto za ukweli halisia, na
zinazotokea kweli, ndoto zenye kumuingiza kwenye nuru ya muangaza wenye kung’ara,
na mchana husikia sauti na kuona nuru fulani isiyojulikana asili yake, sauti zenye
kumuusia mema na kumuonesha kua maisha wanayoishi watu wake ni maisha ya
upotovu, hivyo akawa anahisi anahitaji mda wa kukaa peke yake na kutafakari.
Hivyo akaanza kujitenga nao watu wa Makkah kwa kutafuta mda wa kukaa mbali kidogo
na aina hiyo ya maisha, kwa muda wa mwezi mmoja kila mwaka, na katika kipindi hicho
ambacho hua ni mwezi mzima wa Ramadhan na katika baadhi ya siku za miezi myengine
ndani ya miaka mitatu basi alikua akitumia mda wake mwingi peke yake, kukaa kwenye
pango liliopo katika Jabal al Hirra ambalo liko katika umbali wa Kilomita 3 kutoka
kwenye Jengo la Al Kaabah kwa ajili ya kutafakari.
Na ndio maana akasema Imam Amir Abd Kays kua: ‘Hakika mimi nimewasikia
Masahaba 10 wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam wakisema kua: ‘Nuru ya
Uislam hupatikana katika Kutafakkar’’ Imam Hasan Al Basr kua: ‘Saa moja ya
Kutafakkar ni bora kuliko Mwaka mzima wa Qiyam Al Layl’
Na anasema Aisha Radhi Allahu Anha kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi alikua
akienda kwenye Jabal Al Hira kwa ajili ya Kumuabudu Allah Subhanah wa Ta’ala
peke yake’ (Sahih Bukhari) ambapo tunapoiangalia hadithi hii basi tunaona kua sio
kwamba Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam alikua akisali sala tano, la, kwa sababu
katika kipindi hiki bado hakua ni Mtume na wala Sala hazikuamrishwa bado, hivyo alikua
akikaa na kutafakkari kama vile ambavyo alivyokua akitafakari Nabii Ibrahim:
648
﴿وَكَذٰ لِكَ نُرِي ۤ إِبْرَاهِيمَ مَلَكُوتَ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَلِيَكُونَ مِنَ ٱلْمُوقِنِينَ ﴾
Wakadhalika nuree ibraheema malakoota alssamawati waal-Ardhi waliyakoona
mina almooqineena (Surat Al AnAam 6:75)
Tafsir: Na Kadhalika tukamuonesha Ibrahim Ufalme wa Mbingu na Ardhi ili awe
miongoni mwa wenye Imani na Yaqini.
Ama kuhusiana na maneno yasemayo ‘Wakadhalika nuree ibraheema malakoota
alssamawati waal-Ardhi waliyakoona mina almooqineena’ yaani ‘Na Kadhalika
tukamuonesha Ibrahim Ufalme wa Mbinguni na Ardhini ili awe miongoni mwa wenye
Imani na Yaqini.’
Basi anasema Mujaddid ad Din, Sultan al Mutakallimin Imam Fakhr ad Din al Razi kua:
‘Juu ya neno Nuriy basi amesema Imam Abu Al Ma’ali Al Juwayni Al Haramayn
kua: I’lm ya Allah Subhanah wa Taála ni kubwa isiyokua na mpaka. Na bila ya
shaka I’lm yake juu ya kila kitu haina mwisho. Kwani kila sehemu za viumbe wake
hua zinaweza kuchukua maumbo yasiyokua na mwisho.
Hivyo I’lm ya Ufalme wake haina mwisho, na bila ya shaka kuipata I’lm hio kwa
yeyote yule miongoni mwa Viumbe wake hua haiwezekani, hivyo hubidi kupatikana
kidogo kidogo hatua kwa hatua. Na Vile vile tunaona kua hapa Allah Subhana wa
Taála hakutumia neno ‘Araynahu’ ambalo hua linamaanisha ‘Tulimuonesha’ yaani
katika hali ya kitendo kilichopita lakini ni chenye kumaanisha kuoneshwa kitu
chote kwa ghafla moja hapo kwa hapo, bali ametumia neno ‘Nuriy’ ambalo
linajumuisha hali iliyopo na hali inayokuja ambako ni kwenye kumaanisha kuwepo
kwa kitendo ambacho kinachoendelea na hivyo chenye kuambatana na muendelezo
unaoongezeka kidogo kidogo hatua kwa hatua’
Mujaddid ad Din, Sultan al Mutakallimin Imam Fakhr ad Din al Razi anamalizia
kutuelezea kuhusiana na neno Malakut lililotumika hapa kwa kusema kua: ‘Roho za Ibn
Adam hua haiwezi kukosa kuiona Nuru ya Allah Subhanah wa Taála, isipokua kuwa
sababu ya kuwepo kwa vizuizi. Na Jee ni vizuizi gani hivyo? Hivi ni vizuizi vya yale
mambo ambayo mtu hujishughulisha nayo ambayo hua hayahusiani na Muumba
na kumpelekea mtu kua mbali na Allah Subhanah wa Taála. Na bila ya shaka vizuizi
vikubwa hua ni Masanamu.
Kwani wakati Ibrahim alipoondoa kizuizi chake kwa kujitolea kwa ajili ya Allah
Subhanah wa Taála na akakataa kuwepo kwa chengine chochote kile zaidi yake
Allah Subhanah wa Taála basi alifanikiwa kupata ubainisho wa kuwepo kwa
649
Muumba. Aina hii ya Ubainisho wa kuwepo kwa Muumba hua hauonekani kwa
mtizamo wa jicho la kawaida, bali hua ni wenye kuonekana kwa mtizamo wa jicho
la ndani ya Moyo, na hili ndio jambo lililomuwezesha Nabii Ibrahim kujenga hoja
zake ambazo aliziwakilisha kwa watu wake kama inayoelezewa na aya
tunazoziangalia.
Ama kuhusiana na neno Yaqin basi ni hali ya kujihakikishia kwa Moyo ambayo
hupatikana pale wakati inapokua hakuna shaka yeyote ndani ya Moyo kutokana na
vithibitisho vinavyoonekana na Moyo husika.
Ambapo katika kipindi hiki Khadija Bint Khuwaylid alikua nae anaenda kumtembelea
Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam kwani alikua ni mwenye kumuunga mkono
mume wake katika kila kitu kiasi ya kua kuna baadhi ya siku nae alikua anakesha nae
pamoja huko huko kwenye pango hilo kwa ajili ya kutafakkar pamoja nae Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam mbali ya kua alikua ni mwanamke mwenye umri mkubwa wa
miaka 55 lakini alikua akipanda Mlima huo wa Hira kwa ajili ya kua pamoja na mtu
ampendae na kumuamini kikamilifu na kumjali sana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam
Na hivyo haishangazi kuona kua akasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua:
‘Mwanamke bora wa Dunia katika wakati wake alikua ni Maryam Bint Imran, na
Mwanamke Bora wa Dunia ni Khadija katika wakati wake(Sahih Bukhari)
Na pia Allah Subhanah wa Ta’ala aliliona hili na kumpandisha Darja ya juu zaidi Khadija
Bint Khuwaylid pale alimwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua:
‘Mbashirie Khadija kua atakua na Kasri lililojengwa kutokana na Qasab (Lulu
kubwa na Nzuri sana za Peponi yenye Pango ndani yake) na hamtokua na sauti
wala zogo lolote ndani yake’’(Sahih Bukhari)
MAISHA YA UTUME WA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI
WA SALAM NA UPINZANI KUTOKA KWA WATU WAKE.
Jumatatu moja ya mwezi 27 wa Ramadhani, ambayo ni sawa na mwezi Julai wa mwaka
610, wakati Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akiwa na miaka 40, ilikua
kama ilivyo kawaida yake katika kutafakari kwake ndani ya pango hilo, lakini Jumatatu
hiyo ilikua tofauti na Jumatatu nyengine kwani alijihisi kua katika pango hilo hayuko
peke yake, lakini kila akitazama haoni mtu wala hasikii sauti yeyote kwani kulikua tulii
na kimya. Mara ghafla akasikia sauti inaamrisha:
650
‘Iqraa!’ (Soma!)
﴾ ﴿ٱقْرَأْ
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alishtuka akageuka kutafuta sauti imetoka
wapi na nani anaepewa amri hiyo. Lakini hakuona mtu wala kitu chochote kinachotoa
sauti hiyo wala yule anaepewa amri hiyo, hapo akajua kua yeyote yule anaetoa amri hiyo,
alikua anamuamrisha yeye amri hiyo, na kwa kua yeye alikua si miongoni mwa
waliosoma basi akajibu: ‘Ma ana bi Qari’i’ (Mimi si miongoni mwa wasomaji).
Sauti hiyo ikaamrisha tena kwa ukali: ‘Iqraa!’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu tena huku akiwa na khofu ‘Ma
ana bi Qari’i’.
Sauti hiyo ikaamrisha tena kwa ukali zaid: ‘Iqraa!’.
Kwa kua Nabii Muhammad Salallahu A’alayhi wa Salam, alikua hajui kusoma, na vile
vile alikua hakioni kitu anachoambiwa akisome, basi akajua kua kwa vyovyote vile
itakavyokua amri hiyo anayopewa yeye inamtaka asome kwa kurudia kile anachokisema
mwenye sauti hiyo. Hivyo sauti hiyo ilipoendelea kusema, ilisema kwa upole na huruma
zaid, hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam nae akafuatisha kama vile
namna inavyosema sauti hiyo kwa kusoma:
﴿ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱل َّذِى خَلَقَ ﴾
Iqraa bi-ismi rabbika alladhii khalaqa. (Soma kwa jina la Mola wako alieumba).
﴿خَلَقَ ٱلإِنسَانَ مِنْ عَلَقٍ ﴾
Khalaqa al insana min A’alaqin. (Aliemuumba mtu kutokana na pande la damu).
﴾
ٱ ق ْرَأْوَرَب ُّ كَ ٱ لأَكْرَمُ ﴿
Iqraa warabbuka al akramu. (Soma. Na Mola wako ni mwingi wa Ukarimu).
﴿ٱل َّذِى عَل َّمَ بِٱلْقَلَمِ ﴾
Alladhii A’allama bialqalami. (Aliesomesha kwa kutumia Kalamu).
﴿عَل َّمَ ٱلإِنسَانَ مَا لمَْ يَعْلَمْ ﴾
A’allama al-insana ma lam yaA’lam. (Aliemfundisha mtu kile asichokijua).(Surat Al
A’laq 96: 1-5).
651
Naam, huo ndio uliokua mwanzo wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam,
kupokea ujumbe (Wahy) wake wa mwanzo kutoka kwa Allah Subhanahu wa Ta’ala
kupitia kwa njia ya Malaika wake Jibril A’layhi Salatu wa Salam. Na ujumbe huo ulikua
ni aya tano za mwanzo za sura ya 96 iliyomo katika Qur’an, nayo ni Surat Al A’laq, na
neno la mwanzo la ujumbe huo ambao ni ujumbe uliomo ndani ya Qur’an, lilikua ni neno
lenye maana ya kutafuta I’lm, ‘Iqraa!’(Soma!).
Katika kuifafanua Surat Al A’laq 95: 4-5 basi Imam Abu Hamid Ibn Muhammad Al
Ghazal anasema kua hapa haizungumziwi peni au kalamu tunayoitumia leo mimi na
wewe, bali hapa panazungumziwa: ‘Kila kitu kilichoonekana kua kipo kutokana na
I’lm ya maumbile ambayo imepandikizwa au kupigiwa muhuri ndani ya Nafsi za
Ibn Adam…Kalamu hii hua ni ya hali ya kujulikana kwa Kiroho, kwani hali ya
kujulikana kuwepo kwake hua ni kwa kupitia njia ya kiroho ambayo ndio
hututhibitishia uhalisia wa undani wake…Kwani Kalamu ya kijiti au ya unyoya
unaotumiwa kuandikia hua si miongoni mwa vinavyohisabiwa kua na uhalisia wa
Kalamu hii.’
Labda baadhi wanaweza kujiuliza kwa nini ikawa ni Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam na kwanini hakupewa Utume hadi alipofikia umri wa miaka 40?
Jawabu la swali hili linapatikana katika aya zisemazo:
﴿وَإِذَا جَآءَتْهُمْ آيَةٌ قَالُواْ لَن ن ُّؤْمِنَ حَتى َّ ٰ ٰ نُؤْتَى مِثْلَ مَآ أُوتِىَ رُسُلُ ٱهلل َِّ ٱهلل َُّ أَعْلَمُ
حَيْثُ يجَْعَلُ رِسَالَتَهُ سَيُصِيبُ ٱل َّذِينَ أَجْرَمُواْ صَغَارٌ عِندَ ٱهلل َِّ وَعَذَابٌ شَدِيدٌ ا بمَِ
كَانُواْ يمَْكُرُونَ ﴾
Wa-idha jaat-hum ayatun qaloo lan nu/mina hatta nu/ta mithla ma ootiya rusulu
Allahi Allahu aAAlamu haythu yajAAalu risalatahu sayuseebu alladheena ajramoo
sagharun AAinda Allahi waAAadhabun shadeedun bima kanoo yamkuroona (Surat
Al An Aaam 6:124)
Tafsir: Na wakati zinapowajia Aya zetu hua ni wenye kusema: ‘Hatutoamini hadi
tutakapopewa mithili ya kile ambacho amepewa Mtume wa Allah, Allah ni mwenye
kujua wapi bora kujaalia Ujumbe wake. Yatawasibu wale ambao ni wenye kuasi,
maadhirisho kutoka kwa Allah na adhabu kali sana kutokana na yale waliyokua
wakiyapanga.’
652
Ambapo Aya inatuonesha kua Allah Subhanah wa Ta’ala ni mwenye kujua wapi aweke
ujumbe wake, na nani ampe kipi, vipi na katika wakati gani, hivyo hata mimi na wewe
tunafikwa na mitihani basi hatakiwi kuuliza kwanini mimi? Au kwanini fulani akawa
zaidi yangu, n.k
Na jibu la pili linapatikana katika aya 15 ya Surat Al Ahqaf ambayo inatufundisha hikma
na busara inayopatikana pale mtu kufikia umri wa miaka 40 kama inavyosema Qur’an:
﴿وَوَ ص َّيْ نَا ٱلإِ نسَ انَ بِوَالِدَ يْهِ إِحْ سَ اً حمََلَتْهُ أُم ُّهُ كُرْهاً وَوَضَعَتْهُ كُرْهاً وَحمَْلُهُ وَا فَِص لُهُ
ثَلاَثُونَ شَهْراً حَتى َّ ٰ إِذَا بَلَغَ أَشُد َّهُ وَبَلَغَ أَرْبَعِينَ سَنَةً قَالَ رَبِّ أَوْزِعْنيِ ۤ أَْن أَشكُ َر
نِعْمَ تَكَ ٱل َّتيِۤ أَنْعَمْ تَ َّ عَلَى ٰ وَعَلَى وَالِدَ ى َّ وَأَنْ أَعْمَ لَ صَالحِ اً تَرْضَاهُ وَأَصْ لِحْ لىِ فىِ
ذُرِّي َّتيِ ۤ إِنىّ ِ تُبْتُ إِلَيْكَ وَ ﴾
َين إِنىّ مِنَ ِ ٱلْمُسْلِمِ
Wawassayna al-insana biwalidayhi ihsanan hamalat-hu ommuhu kurhan
wawadaAAat-hu kurhan wahamluhu wafisaluhu thalathoona shahran hatta itha
balagha ashuddahu wabalagha arbaAAeena sanatan qala rabbi awziAAnee an
ashkura niAAmataka allatee anAAamta AAalayya waAAala walidayya waan
aAAmala salihan tardhahu waaslih lee fee dhurriyyatee innee tubtu ilayka wa-innee
mina almuslimeena (Surat Al Ahqaf 46:15)
Tafsir: Na tunamuusia Bani Adam kuwajibika na kua na huruma kwa wazazi wake.
Kwani Mama yake alimbeba kwa ugumu na akamzaa kwa ugumu, na akamlea na
kumyonyesha kwa miezi 30. hadi pale anapofikia kukua na kukamilia kinguvu na
anapokua ni mwenye kufikia miaka 40, husema: ‘Ya Rabb! Nijaalie nguvu na uwezo
ili niwe mwenye shukurani kwa Neema zako ulizonijaalia juu yangu na wazee wangu,
na ili niweze kufanya mambo mema, yatakayo kuridhisha, na kijaalie kizazi changu
kiwe chema, kwa Hakika nimekugeukia kutubia kwako na hakika mimi ni miongoni
mwa Muslimina (Waliojisalimisha kwako)’
Hivyo kipindi cha umri wa miaka 40 ni kipindi muhimu kwa kila mtu aliejaaliwa
kukifikia kimaisha, kwani katika kipindi hiki kila mtu hua tayari ameshatumia robo tatu
ya uhai wake, na hivyo hua ameshakamilika kinguvu na kukomaa kiakili na kiufahamu
na hivyo hua na busara na uwezo mzuri sana wa kutafakkar majukumu yake mbali mbali
katika maisha ya duniani na akhera, kwani vile vile kuna Manabii na Mitume wengi
ambao waliopewa Utume wakati walipoingia umri wa miaka 40 akiwemo Nabii Nuh
Alayhi Salaam, Nabii Musa A’layhi Salaam, Nabii Harun Alayhi Salaam n.k
653
Kwa upande wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, ingawa wakati huo
alikua ameshakamilia umri wa miaka 40, lakini tukio hili lilimtokezea katika pango la
Jabal al Hira lilimtia khofu kubwa sana Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam,
hivyo haraka sana akaamua kuondoka katika pango hilo la Jabal Al Hira lakini kabla ya
kufika popote alionana na umbo kubwa la Malaika Jibril A’layhi Salam, ambae
alimwambia: ‘Ewe Muhammad, wewe ni Rasul Allah na mimi ni Jibril’, kisha
Malaika Jibril akatoweka.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, akaona hii ishakua balaa kwani
haiwezekani kusikia aliyoyasikia pangoni na kuona aliyoyaona njiani wakati akikimbilia
nyumbani hivyo akaongeza kasi mwendo wake na alipofika nyumbani akaingia
chumbani na kukimbilia kitandani moja kwa moja, huku akiwa katika hali ya kutetemeka
akamwambia mfariji wake mkubwa Sayyida Khadija Al Kubra: ‘Zamiluni! Zamiluni!’
‘Nifunike! Nifunike!’ ‘Dathiruni! Dathiruni!’ ‘Nikumbatie kwa kunigubika!
Nikumbatie kwa kunigubika!’.
Khadijah Bint Khuwalid Al Kubra akamfunika, akamkumbatia na kumgubika, kisha
baada ya kurudi hali yake ya kawaida basi Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
akamhadithia yaliyomkuta na kumwambia kua ana khofu kua ufahamu wake unamsaliti,
lakini Khadijah Bint Khuwalid Al Kubra akamwambia: ‘La! Huu ni ubashirio mwema.
Wa Allahi! Allah hatokudhalilisha, kwani wewe ni mwenye kuwapatanisha ndugu
waliogombana, unawasaidia waliokua dhaifu, unawasaidia wasiokua na uwezo na
masikini, unawahudumia na kuwajali wageni wako na unastahmili mitihani
migumu katika kutafuta haki’, kisha akakaa nae na kumliwaza Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam hadi alipolala.
Baadae Khadijah Bint Khuwalid Al Kubra na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam wakaelekea kwa binamu yake Khadijah Bint Khuwalid Al Kubra aitwae Warraqah
Ibn Nawfal Ibn Asad Ibn Abd ul Uzza Ibn Qusay, ambae alikua ni mzee mwenye I’lm ya
vitabu vya Ahlu al Kitab, na kumhadithia yaliyotokea. Warraqah Ibn Nawfal
akaakasema: ‘Huyo ni Namus ambae Allah alimtuma kwa Musa. Nnatamani
ningelikua kijana hadi pale utakapofikia mda ambao watu watu wako
watakufukuza’, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akauliza:
’أَوَ مخُْرِجِ ي َّ هُمْ ؟‘
‘Watanifukuza?’.
Warraqah akajibu: ‘Hakuna mtu yeyote yule aliewahi kuja na ujumbe kama wako
kwa watu wake bila ya kufanyiwa yasiyokua siyo na kufanyiwa uadui mkubwa, Na
654
kama ikiwa nitaishi hadi kufikia wakati huo basi bila ya shaka nitakuunga mkono
kwa kila hali’. Lakini hata hivyo Warraqah hakuishi kwa muda mrefu kuyashuhudia
aliyoyabashiria kwani baada ya kupita muda mfupi akafariki.
Khadijah Bint Khuwalid Al Kubra alikua ni mtu wa mwanzo kabisa kua Muislam baada
ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na pia ndie mke pekee aliezaa nae
watoto wake sita, Khadijah Bint Khuwalid Al Kubra alifanya jitihada kubwa sana katika
kumuunga mkono na kumliwaza Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam katika
wakati wote wa mitihani alipokua pamoja nae wakati wa uhai wake, kama alivyosema
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kuhusiana nae katika Hadith yake:
‘Allah Subhanah wa Ta’ala, hakuwahi kunipa mimi mtu yeyote aliekua bora kama
yeye. Alikua pamoja nami pale watu walipokaa mbali nami, Aliniamini pale watu
walipokua na shaka nami, Alitumia utajiri wake pamoja nami pale watu
waliponitenga, na Allah amenipa watoto kupitia kwake yeye.’(Sahih Muslim)
Baada ya tukio la kushushwa kwa aya tano za mwanzo za Surat Al A’laq, kilipita kipindi
kirefu cha ukimya, kipindi hiki kilijulikana kama kipindi cha Falrat Al-Wahy (kukatika
kwa Wahy). Imam Az Zuhri anaielezea hali ya kipindi hiki kwa kusema: ‘Kushushiwa
Wahy Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kulisimama kwa muda, hiki
kilikua ni kipindi kirefu kilichojaa huzuni na kisichokua na utulivu akilini (mwa
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam) kiasi ya kua akaanza kuenda mara
kadhaa katika Jabal al Hira ili akajitupe. Lakini kila akifika juu pembezoni ya
Mlima huo, Malaika Jibril alimtokea na kumuambia kua yeye ni Rasul Allah.
Jambo hili liliimliwaza Rasul Allah na kumrudishia utulivu wa akili yake’.(Imam
Ibn Jarir)
Imam Az Zuhri anasema baada ya habari hiyo, kua kutoka kwa Jabir Ibn Abdullah kua:
‘Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua akikielezea kipindi cha falrat
al-wahy (kukatika kwa wahy) kwa kusema: ‘Siku moja nilikua nikipita njiani, mara
ghafla nikasikia sauti kutoka juu Mbinguni. Nikanyayua kichwa changu na
kuangalia juu nikamuona Malaika yule yule ambae alienitembelea katika pango la
Al Hira, akiwa amekaa kwenye kiti baina ya mbingu na ardhi. Jambo hili liliushtua
moyo wangu na nikakimbilia nyumbani nilipofika nyumba nikasema ‘Zamiluni!
Zamiluni!’ ‘Nifunike! Nifunike!’. Hivyo watu wa nyumbani kwangu wakanifunika
guo. Katika wakati huo Allah akanishushia: Ya Ayyuhal Muddaththiru (Ewe
uliejifunika gubi gubi)...Kuanzia hapo Wahy ukawa unateremka kwa nguvu na kwa
kuendelea.’’ (Bukhari, Muslim, Musnad Imam Ahmad, Imam Ibn Jarir)
Hiyo ilikua ni Surat Al Mudaththir isemayo:-
655
ٱ َٰي ُّهَا د َّ لُْم ثِّرُ ۞ قُمْ فَأَنذِرْ ۞وَرَب َّكَ فَكَبرِّْ۞وَثِيَابَكَ فَ طَهِّرْ ۞وَٱلر ُّجْزَ فَٱهْجُرْ ۞وَلاَ
تمَْنُن تَسْتَكْثِرُ۞وَلِرَبِّكَ فَٱصْبرِْ﴾
﴿
Ya ayyuha almuddaththiru; Qum faandhir; Warabbaka fakabbir; Wathiyabaka
fatahhir; Waalrrujza faohjur; Wala tamnun tastakthiru; Walirabbika faisbir
(Surat Al Mudaththir 74:1-7)
Tafsir: Ewe uliejizungushia (mashuka); Amka na utoe onyo, na umkuzishe Mola
wako, Na Usafishe kivazi chako, Na ukae mbali na Ar-Rujz! (Masanamu) Na usitoe
kitu kwa ajili ya kupata kingi zaidi (usifikirie kufanya wema kwa kumtii Allah kua
unamsaidia Allah), Na kua ni mwenye Subra kwa ajili ya Mola wako (kwa kutekeleza
yale atakayokuamrisha).
Baada ya kushuka aya hizo za mwanzo mwanzo za Surat Al Muddaththir, kila kitu
katika maisha ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kikabadilika kwani
maamrisho hayo hayakumfanya yeye kua ni Nabii Salallahu A’layhi wa Salam tu bali pia
yalimuwekea wazi kua yeye pia ni Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam.
Siku chache baadae zikafuatia aya za mwanzo mwanzo za Surat Al Muzammil ambayo
ilikua ikimtayarisha kwa kumtaarifu kua jukumu lake litakua ni zito na kubwa sana kama
anavyosema Allah Subhanahu wa Ta’ala katika Qur’an:
ا ي ٱ َُّه لْمُز َّمِّل قُمِ ٱلْل َّيْلَ إِلا َّ قَلِيلاً ۞ ن نِّ أ َ صْفَهُ ٱ وِ ن قُصْ مِنْهُ قَلِيلاً ۞ أَوْ زِدْ
۞ هِى
َ
عَلَيْهِ وَرَتِّلِ ٱلْقُرْآنَ تَرْتِيلاً إِ َّ سَنُلْقِى عَلَيْكَ قَوْلاً ثَقِيلاً ۞ إِن َّ َشِ ئَةَ ٱلل َّيْلِ
أَشَد ُّ وَطْأً وَأَقْوَمُ قِيلاً إِن َّ لَكَ فىِ ٱلن َّهَارِ سَبْحَاً طَوِيلاً وَٱذْكُرِ ٱسْمَ ۞ ۞ رَبِّكَ
وَتَبَت َّلْ إِلَيْهِ تَبْتِيلاً ر َّب ُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ لاَ إِلَٰهَ إِلا َّ هُوَ ۞ فَٱتخ َِّذْهُ وَكِيلاً﴾
۞
ُ
َٰ ﴿
Ya ayuha almuzzammilu; Qumi allayla illa qaleelan; Nisfahu awi onqus minhu
qaleelan; Aw zid AAalayhi warattili alqur-ana tarteelan; Inna sanulqee AAalayka
qawlan thaqeelan; Inna nashi-ata allayli hiya ashaddu wat-an waaqwamu qeelan;
Inna laka fee alnnahari sabhan taweelan; Waodhkuri isma rabbika watabattal
656
ilayhi tabteelan; Rabbu almashriqi waalmaghribi la ilaha illa huwa faittakhidhhu
wakeelan (Surat Al Muzamil 73:1-9)
Tafsir: Ewe uliejifunika; Simama (Usali) usiku wote isipokua kidogo tu; Nusu yake au
karibia nusu yake, kidogo; Au kidogo zaidi. Na Rattil (usome kwa sauti) Qur’an kwa
Tartil (kwa kutiririka nayo kunakopendeza); Kwani kwa hakika tutakushushia wewe
Kaulan Thaqilan (Kauli nzito, yenye kuzingatia shariah na Hukmu); Kwa hakika
Nashia’h (kuamka)usiku ni kugumu na bora (kwa kuidhibiti Nafsi), hufaa zaidi kwa
(kufahamu) maneno (ya Allah); Hakika kwako wewe, mchana ni mkubwa (kwa
kutekeleza mambo yako ya kawaida); Na likumbuke Jina la Mola wako na Tabattil
(jitolee) kwake yeye kwa Tabtiilan (kwa kujitolea kikamilifu); Mola wa Mashariki na
Magharibi La ilaha illa Huwa, (Hakuna Mungu mwengine isipokua yeye) hivyo
mfanye kua Wakilan (Wakili wako wa kumtegemea).
Kuanzia hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akawa tayari
ameshaondokwa na wasi wasi, khofu na woga na tayari ameshayajua majukumu yake
kutoka kwa Mola wake na kufahamu uzito wake, uzito ambao haupo katika utekelezaji
wa majukumu hayo tu, bali pia katika upokeaji wa ujumbe wa majukumu hayo, kwani
wakati wa kupokea ujumbe wa majukumu hayo alikua akitokwa na jasho katika paji lake
la uso hata kama hali ya hewa ilikua ni ya baridi kali, uso wake hua ni wenye Tarrabad
(kwanza hubadilika rangi na kua kama mtu asiekua na damu halafu unakua ni mwekundu
wenye kuvilia damu), na vile vile uzito wa mwili wake huongezeka zaidi ya mara mbili
yake kiasi ya kua anapokua juu ya Ngamia basi Ngamia wake hua ni mwenye
ku Fataḍhrib bi jirāniha (Kunyoosha shingo yake, kuonesha kua mzigo alioubeba ni
mzito sana na umeshamchosha hivyo anahitaji kupumzika kwa kulala ardhini).
Katika kuielezea hali hiyo, Zayd Ibn Thabit Radhi Allahu Anahu ambae alikua amekaa
kitako na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam katika moja kati ya nyakati
ambazo Wahy ulikua ukishuka, na katika kukaa huko paja lake likawa liko chini ya paja
la Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, anasema Zayd Ibn Thabit Radhi Allahu
Anahu kua: ‘Allah Subhanahu wa Ta’ala alimshushia Wahy Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam wakati paja lake lilikua juu ya paja langu hivyo likaanza
kunifanya niuhisi uzito wake mkubwa sana kiasi ya kua nilikhofia kua huenda paja
langu litavurugika.’
Huo ni mmoja kati ya uzito wa majukumu yaliyokua yakishushwa Malaika Jibril A’layhi
Salaam kwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, Qur’an kupitia kwa njia ya
katika umbo la mtu asieonekana na watu wengine isipokua yeye au kwa njia ya sauti
ambayo kwa wale waliokaribu yake husikia kama mlio wa nyuki asieonekana karibu na
uso wake, lakini katika hali aliyokua nayo yeye mwenyewe Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam basi hua anasikia kama mlio wa kengele, na hivyo hujaribu haraka
657
haraka kuyahifadhi maneno yanayosikika katika ujumbe huo ili yasije yakamponyoka na
akayasahau.
Hivyo Allah Subhanahu wa Ta’ala akamwambia:
﴿لاَ تحَُرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ ۞ إِن َّ عَلَيْنَا جمَْعَهُ وَقُرْءَانَهُ ۞ فَ إِ ذَ ا قَ رَأْنَ هُ فَٱت َّبِعْ
قُرْآنَهُ ۞ ثمُ َّ إِن َّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ﴾
La tuharrik bihi lisanaka litaAAjala bihi; Inna AAalayna jamAAahu waqur-anahu;
Fa-idha qara/nahu faittabiAA qur-anahu; Thumma inna AAalayna bayanahu
(Surat Al Qiyamah 75:16-19)
Tafsir: Usiuharakishe ulimi wako (kuhusiana na Qur’an) katika kuiharakisha kwake;
Kwani ni juu yetu kuikusanya na kukupa uwezo wa kuisoma; Na tunapokusomea
(kupitia kwa Jibril), wewe kifuatishie kisomo chake; Kisha ni juu yetu sisi kuibainisha
juu yako.
Anasema Abd Allah Ibn ʿAbbas Radhi Allahu Anhu, kuhusiana na aya hizo kua : ‘Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua akihisi uzito anaposhushiwa aya za
Qur’an na alikua akijaribu kuharakisha kufuatishia pamoja na maneno
anayoyasikia. Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala, akamwambia ‘Usiuharakishe ulimi
wako, kwa kuiharakisha, kwani ni juu yetu kuikusanya na kuifanya isomwe’, yaani
Allah Subhanahu wa Ta’ala ataihifadhi ndani ya kifua chake ili aweze kuisoma,
‘Hivyo tutakapokusomea, basi wewe fuatisha kisomo chake’, yaani kisikilize na
ufuatishe kwa makini. ‘Kisha ni juu yetu sisi kuibainisha’, yaani ni juu yetu sisi
kuhakikisha kua wewe unaisoma. Kuanzia hapo Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam, ikawa kila anapokuja Jibril hua anamsikiliza kwanza hadi
anapomaliza na kuondoka, na baada ya hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam huanza kusoma kama alivyosoma Jibril.’
Wakati Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu A’nhu alipokuwa anaishi ndani ya Nyumba ya
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi siku moja usiku aliwaona Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam na mkewe Khadija Ummul Mu’minina Radhi Allahu A’nhu
wakiwa wanarukuu na kusjudu, akashangaa na kuwauliza kufanya hivyo ndio maana
yake nini? Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamjibu kua kufanya hivyo
ni kumuabudu Allah Subhanah wa Taala, hivyo kama anataka anaweza kujiunga nao, Ali
akasema kesho atamuuliza baba yake kama ma yeye anaweza kufanya hivyo ama la.
658
Lakini usiku kucha akawa akifikiria jambo hilo, na asubuhi yake akamfuata Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na kumwambia ‘Wakati Allah aliponiumba
mimi hakumuuliza baba yangu, hivyo kwa nini nimuulize baba yangu katika
kumtumikia Allah?’. Hivyo akaingia katika Uislam na kuwa ni mtoto wa mwanzo na
pia mwanamme wa mwanzo kuingia katika Uislam.
Anasema Yahya Ibn Afiif Radhi Allahu Anhu kua: ‘Katika kipindi cha Ujahiliyyah
mimi nilimtembelea Abbas Ibn Abd Ul Muttalib, na lilipoanza kuchomoza Jua,
nikamuona Mtu ametoka kwenye Nyumba yake sio mbali kutoka tulipokuwepo
akalielekea Al Kaabah na akaanza kusali, na haikuchukua mda mrefu mara
akatokea Mtoto wa Kiume ambae alisimama Kulia kwake na kisha akatokea
Mwanamke nae akasimama Nyuma yake. Na alipokua akiinama basi na wao
wakawa wanainama, alipokua akisujudu basi nao walisujudu, alipokua
wakasimama nao wakasimama’
Hivyo mimi nikaona ajabu na kusema: ‘Hili ni jambo la Ewe Al Abbas’ Hivyo Al
Abbas akasema: ‘Hivi jee unamjua ni nani huyo?’ nami nikajibu: ‘La Simjui’ Al
Abbas akasema: ‘Huyo ni Muhammad Ibn Abdullah mtoto wa kaka yangu, na jee
unamjua huyo Mtoto ni nani?’ Nami nikasema : ‘La’ Al Abbas akasema: ‘Huyo ni
Ali Ibn Abi Talib, na Jee unamjua huyo mwanamke ni nani?’ nami nikasema :
‘La’Al Abbas akasema: ‘Huyo ni Khadija Bint Khuwaylid ambae ndie mke wa
Mtoto wa kaka yangu’ (Imam At Tirmidhii, Musnad Imam Ahmad)
Ambapo Al Abbas Ibn Abd Ul Muttalib alikua na mkewe aitwae Lubaba Al Kubra ambae
ndie Mama yake Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu na alikua
akijulikana pia kama Umm Fadhl ambae alikua ni rafiki yake Khadija Bint Khuwaylid
na hivyo akawa ni mwanamke wa pili kusilimu baada ya Khadijah Bint Khuwaylid kwani
nae alisilimu katika siku hio hio aliyosilimu Khadija Bint Khuwaylid na hii ni kutokana
na urafiki wa karibu sana baina ya Khadija Al Kubra na Lubaba Al Kubra..
Mama yake Lubaba Al Kubra alikua akiitwa Khawla na pia kama Hind Bint Awf Ibn
Zuyahr Ibn Harith na mama yake ni Aisha Bint Muhazzam. Ambapo tunapomzungumzia
Hind Bint Awf basi hua tunamzungumzia mwanamke ambae anaejulikana kama ‘Mama
Mkwe Bora kuliko wote Ardhini’ na hii ni kwa sababu watoto wake wawili waliolewa
na Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam ambao ni Maymuna Bint Harith na Zaynab
Bint Khuzaymah na watoto wake wengine waliolewa na Masahaba mbali mbali.
Kwani Hind Bint Awf aliolewa zaidi ya mara 4, ambapo ndoa yake ya kwanza ilikua ni
kwa Jazi Al Zubaydi ambae alikua ni miongoni mwa Waislam wa mwanzo na
akachaguliwa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua ni Muweka Mahesabu wa
Jamii ya Kiislam.
659
Halafu Hind Bint Awf akaachwa na akaolewa na Harith Ibn Hazan ambapo ndoa hii
ikatoka watoto wanne ambapo wa kwanza ni Lubaba Al Kubra ambae ndie mwanamke
wa pili kusilimu na ndie aliekua mke wa Al Abbas Ibn Abd Ul Muttalib ambae ndie Ami
yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na wa pili ni Maymuna Bint Harith ambae
aliolewa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, wa tatu ni Saayib Ibn Harith na wa
nne ni Qatn Ibn Harith.
Halafu Harith Ibn Hazan akafariki na Hind Bint Awf akaolewa na Khuzaymah Ibn Harith
Al Hilali ndo ambayo ilitoa mtoto wa kike mmoja tu aitwae Zaynab Bint Khuzaymah
ambae aliolewa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Halafu Hind Bint Awf akaachwa na akaolewa na Umays Ibn Maad Ibn Tamim ndoa
ambayo ilitoa watoto watatu ambao ni Asma Bint Uways ambae aliolewa na Rabia Ibn
Riyab, na kisha akaolewa na Jafar Ibn Abi Talib Ibn Abd ul Muttalib, na kisha akaolewa
na Abu Baqr As Siddiq na kisha akaolewa na Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhum.
Mtoto wake wa pili ni Salma Bint Uways ambae aliolewa na Hamza Ibn Abd Al Muttalib
aliekua Ami yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na kisha akaolewa na Shaddad
Ibn Usama.
Na mtoto wake wa tatu katika ndoa hii alikua ni Awn Ibn Umays.
Halafu Hind Bint Awf akaachwa na akaolewa na Al Harith Ibn Hazan ambae alikua na
mke mwengine aitwae Fakhta Bint Amr ambae mtoto wake wa kike ni Al Lubaba Al
Saghir ambae ndie Mama yake Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu.
Hivyo Lubaba Al Kubra Bint Harith Ibn Hazan Al Hilal alikua ni mtu mwenye asili ya
Yemen kama alivyokua mama yake ambae ni Hind Bint Awf kwani kabila lao halikua ni
la Quraysh bali lilikuani lenye asili ya Yemen, ila lilikua ni kabila linaloheshimika,
ambapo ndoa baina Lubaba Al Kubra na Abbas Ibn Abi Talib ilitoa watoto 7 ambao ni Al
Fadhl, Abdullah, Ubaydullah, Quthum, Mabad, Abdur-Rahman na Umm Habib.
Hivyo alisema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Madada Waumini ni Asma
na Salma na Watoto ni Lubaba na Maymuna mabinti wa Harith’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua na Rafiki yake wa karibu sana ambae
alikua akiitwa Abd Allah Ibn Abi Quhafa Ibn Uthman Ibn Amir Ibn Qaab Ibn Taymi Ibn
Murra ambapo anasema Al Hafidh Imam Ibn Asakir kua amesema Isa Ibn Yazi kua:
‘Amesema Abu Bakr As Siddiq kua: ‘Mimi nilikua nimekaa kwenye uwanja wa Al
Kaabah na pembeni yangu alikua amekaa Zayd Ibn Amr Ibn Nufayl, na mara
akapita Ummayah Ibn Abi Salt na akasema: ‘Hali zenu Enyi watafutaji Mema’
660
Nami nikasema: ‘Nzuri’ Ummayah akasema: ‘Jee mmekiona (mnachokitafuta?)’
Nami nikasema: ‘La’ nae akasema: ‘Kila Dini katika siku ya Malipo itaangamia
isipkua ile ambayo Allah ameshaikadiria, ama kuhusiana na Mtume huyo
anaesubiriwa basi jee atakua ni miongoni mwetu au ni miongoni mwenu?’
Abu Bakr anasema: ‘Mimi sikuwahi kusikia kuhusiana na Mtume anesubiriwa hapo
kabla hivyo nikatoka hadi kwa Waraqh Ibn Nawfa ambae alikua anapenda
kuangalia Mbinguni, na alikua ni mwenye kushangaza sana. Nikamuelezea
kuusiana na niliyoyasikia, nae akasema: ‘Naam ndie Ewe Mtoto wa Kaka yangu,
hakika sisi ni watu wa Ilm ya Kitabu, lakini Mtume anaesubiriwa atakua ni
miongoni mwa walio bora katika Waarabu kulingana na Kiukoo’
Nami nikasema : ‘Ami Jee Mtue huyo atakua nasema nini?’ nae akasema: ‘Atakua
naasema kile alichoambiwa seme, isipokua hatokua ni mwenye kuwadhulumu watu
na wala hatoduhlumiwa na wala hatowatafutia watu kudhulumuiwa’ Hivyo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipotumwa basi mimi nikamkubali na
kumthibitisha’’
Hivyo Abu Bakr As Siddiq akawa ni Muislam wa pili Mtu Mzima mwanamme baada ya
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, ambapo katika kipindi cha mwanzoni Waislam
walikua wanasilimu kisiri siri hadi pale Allah Subhanh wa Ta’ala aliposhusha aya
isemayo:
﴿وَأَنذِرْ عَشِ يرَتَكَ الأَْقْرَبِينَ﴾
Waandhir AAasheerataka al-aqrabeena (Surat Ash Shu’ara 26:214),
Tafsir: ‘Na wausie ndugu zako wa karibu’
Ambapo watu wa karibu wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika kipindi hiki
walikua ni wale ambao wako karibu nae kiukoo na kikabila yaani watu wa Al-Sha`b yaani
Banu `Adnan na Banu Qahtan, Al Qabeelah yaani Banu Rabi`ah na Banu Mudar, Al-
`Imarah yaani Banu Quraysh na Banu Kinanah, Al Batn yaani Banu `Abd Munaf, Banu
`Abd Makhzun, Al Fakhz yaani Banu Hashim, Banu Umayyah, na Al Faseelah Banu
`Abbas, Banu `Abd Al Muttalib, n,k.
Ambapo amesema Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wakati iliposhushwa
ayah hii (Surat Ash Shu’ara 26:214), basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akawakusanya Watu wake Nyumbani kwake kwa ajili ya chakula cha Jioni,
ambapo nao wakala na kunywa vizuri lakini hata hivyo chakula hicho na vinywaji
vilikua kama havijaguswa, na kasha akawaambia: ‘Enyi watu wa Abd Ul Muttalib
661
hakika mimi nimetumwa maalum kwa ajili yenu na kwa watu wengine, kama
mlivyosikia kwenye aya hii (Surat Ash Shu’ara 26:214), hivyo Jee mtakubaliana
nami ili muwe pamoja name Peponi?’
Na hakuna hata mtu mmoja aliesimama kwa ajili ya kukubaliana nae, hivyo mimi
nikasimama ingawa nilikua ndie mdogo kuliko wote, nae Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akawa ananiiambia: ‘Kaa chini’ hadi mara ya tatu akanishika
mkono’ (Musnad Imam Ahmad)
Ambapo anasema Abd Allah Ibn Ababs Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam aliwaita watu wa Quraysh na wakaja wenyewe na baadhi
waliwatuma watu kusikiliza kuna nini, na miongoni mwao aliekuja alikuwemo Abu
Lahab, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kwa kuwaambia:
‘Hivi jee mtasemaje kama nikikuambieni kua Nyuma ya Mlima kuna jeshi
linalokuja kukuvamieni? Mtaniamini ama la?’ Watu hao wakasema: ‘Naam
tutakuamini, kwa sababu sisi hatujawahi kusikia neno la uongo kutoka kwako’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Sasa wacheni nikuambieni kua
hakika Mimi ni Mtume wa Allah nilie mbele yenu nimetumwa kukuepusheni
kutokana Adhabu kali sana’ na hapo Abu Lahab akasema: ‘Uangamizo uwe juu
yako yaani umetuita sisi kwa ajili ya kutuambia Jambo hilo? ’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akashusha Surat Masad isemayo:
﴿بِ سْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞تَب َّتْ يَدَآ أَبىِ لهََبٍ وَتَب َّ آ ۞َم أَ غْ نىَٰ عَنْهَُما ا لُهُوََم
كَسَبَ ۞سَيَصْ ٰ لَى َ راً ذَاتَ لهََبٍ ۞وَٱمْ رَأَتُهُ حمَ َّالَةَ ٱلحَْطَبِ ۞ فىِ جِ يدِهَا حَبْلٌ مِّن
م َّسَدٍ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Tabbat yada abee lahabin watabba; Ma aghna
AAanhu maluhu wama kasaba; Sayasla naran thata lahabin; Waimraatuhu
hammalata alhatabi; Fee jeediha hablun min masadin (Surat Masad 111:1-6)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehema Mwingi wa Huruma; Imeangamia
Mikono miwili ya Abu Lahab, na yeye mwenyewe; hawatomfaa kitu Watoto wake wala
Mali yake, Ataungua katika Moto Mkali sana, na Mke wake anaebeba Kuni; Shingoni
mwake kuna Kamba ya Kitanzi ya Masad.
662
Neno Lahab linatokana na neno Lahiba ambalo hua ni lenye kumaanisha Kua na Rangi
ya Wekundu wa Moto, Kuunguza kwa Moto, Kua na Hasira hadi Uso ukawa mwekundu,
na pia humaanisha Harufu ya Moto.
Hivyo ingawa Abu Lahab mwanzoni aliitwa Abu Lahab kwa sababu ya maumbile ya
muonekano wa Rangi ya ngozi yake ambayo ilikua ni nyeupe yenye wekundu wa damu
unaomaanisha kua ni mtu mwenye mwili wenye Afya na hivyo kua ni mzuri na wa
kuvutia kimaumbile, kutokana na kuonekana kua na damu nyingi Mwilini.
Lakini baada ya kushuka Surat Masad basi sifa yake nzuri hio ya muonekano wa kuvutia
wa Lahiba uliompatia jina la Abu Lahabi ukabadilika na kua ni muonekano wa Laana
Juu yake na hivyo kua Abu Lahabi kumaanisha Mtu mwenye Hasira kubwa sana alieingia
Motoni kwa Ujinga wake, Kibri na Hasira zake na hivyo kua ni Baba wa Moto.
Kwani kutokana na kua Nyumba ya Khadijah Bint Khuwaylid ilikua ni nyumba ambayo
ipo jirani na Nyuma ya Abu Lahabi, Hakam Ibn Al As. Uqbah Ibn Muait na Adi Ibn
Hamra ambao walikua ni miongoni mwa maadui wakubwa wa Uislam na kwa kua
walikua wakiishi jirani na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, basi walikua
wakimfanyia inda na maudhi makubwa sana kiasi ya kua walikua baadhi ya wakati
wakiona chakula kinapikwa ndani ya Nyumba ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
basi hukirushia uchafu chakula hicho, na baadhi ya wakati wakimuona Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam anasali basi humrushia Matumbo ya Mbuzi.
Ambapo kwa upande wa Arwa Bint Harb maarufu kama Ummu Jamil ambae ndie mke
wake Abu Lahab na pia ndie dada yake Abu Sufyan basi nae alikua akiamka usiku na
kisha hukusanya kuni zenye miba na kuziweka chini ya mlango wa nyumba ya Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam ili watu watakaotoka ndani yake wakanyage kisha
wapate maumivu makali sana.
Hivyo siku moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua amekaa na Abu Bakr As
Siddiq, hivyo Abu Bakr As Siddiq akamuona Arwa anakuja katika upande wao, na hivyo
aaksema kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam: ‘Ya Rasul Allah Arwa
anakuja hakika mimi nnakhofu kua atakuona’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hakika Arwa hatoweza
kuniona mimi.’Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasoma aya isemayo:
﴿وَإِذَا قَرَأْتَ ٱلْقُرآنَ جَعَلْنَا بَيْنَكَ وَبَينَْ ٱل َّذِينَ لاَ يُؤْمِنُونَ بِٱلآخِ رَةِ حِ جَاابً م َّسْتُوراً ﴾
663
Wa-idha qara/ta alqur-ana jaAAalna baynaka wabayna alladheena la yu/minoona
bial-akhirati hijaban mastooran (Surat Al Israh 17:45)
Tafsir: Na unaposoma Qur’an (Ewe Muhammad) tunajaalia baina yako na baina ya
wale wasioamini juu ya Akhera pazia lisiloonekana lenye kustiri.
Hivyo Arwa Bint Harb akaja mpaka mbele ya Abu Bakr As Siddiq na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na kisha bila ya kua ni mwenye kumuona Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam basi akasema: ‘Ewe Abu Bakr! Hakika mimi
nimetaarifiwa kua Rafiki yako ametunga Mashairi ya kunilaani’ hivyo Abu Bakr
akasema: ‘La Naapa kwa Mungu wa Al Kaabah kua hajakulaani’ na hapo Arwa
akageuka na kusema: ‘Hakika Watu wa Quraysh wanajua kua mimi ni Binti wa
Kiongozi wao’
Hivyo baada ya tukio hili la kulaaniwa kwa Abu Lahabi na Ummu Jamil kutokana na
maneno na vitimbi vyao kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Allah Subhanah
wa Ta’ala kutokana na kua ni mwenye kujua kitakachofuatia baada yake kwa Waislam
basi akasema:
﴿وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱت َّبَعَكَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ۞فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنىّ ِ بَرِي ۤ ءٌ ممِّ َّا
تَعْمَلُونَ۞ وَتَوك َّلْ عَلَى ٱلْعَزِيزِ ٱلر َّحِ يمِ ﴾
Waikhfidh janahaka limani ittabaAAaka mina almu/mineena; Fa-in AAasawka
faqul innee baree-on mimma taAAmaloona; Watawakkal AAala alAAazeezi
alrraheemi (Surat Ash Shu’ara 26:215-217)
Tafsir: Na washushie Bawa lako wale watakaokufuata miongoni mwa Waumini, na
kama wakiuasi basei sema: ‘Mimi sina makosa juu ya mnayoyafanya’ na kua na
utegemezi juu ya Mwenye mwingi wa uwezo na mwingi wa Rehma.
Ambapo aya imetumia maneno Waikhfidh janahaka yaani Washushie Bawa Lako
ambapo neno Janaha hua linamaanisha Kuinamia, Kuelemea, Kua karibu katika wakati
wa Usiku. Kwani neno Janaha ndio lililotoa neno Ajnihatun ambalo hua linamaanisha
Mbawa za Ndege, Mikono, Kwapa, Pande mbili za Kulia na kushoto za washambuliaji
iwe katika vita au katika Mpira, Wasaidizi na pia humaanisha Walinzi.
Hivyo maneno Waikhfidh janahaka hua yanamaanisha Kua Mkarimu nao, Kua na
Huruma nao, Kua na Unyenyekevu nao, Kua ni mwenye Kujali juu yao na kua na Upole
juu yao.
664
Mfano hai kimaana wa Aya ni mmithilisho wa namna Ndege anavyokua anayashushia
na kuyahifadhi Makinda yake ndani ya Mbawa zake na kuwaonesha Mapenzi Rehma na
Huruma Makinda wake hao na kuwahifadhi dhidi ya maadui zao wanaoweza kuyadhuru
Makinda hayo, na pia kuwahifadhi na mazingira ya hali ya hewa, kwa kua hawana nguvu
wala uwezo wa kuruka kutokana na udogo wao na kua, hawana manyoya mengi,n,k Kiasi
ya kua Ndege huyo yeye hua tayari kujitolea Muhanga kwa kuathirika na athari za nje
za kimaumbile kwa kupigwa na Jua, kunyeshewa na Mvua, kuangukiwa na Theluji, n,k
lakini kamwe hawachi kuyafunika makinda yake hayo kwa Mbawa zake ili yasidhurike
na Madhara hayo.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anamwambia Rasul Allh Salallahu Alayhi wa Salam
kuwaonea huruma wale watakaomuamini kwani bila ya shaka watakutwa na mitihani
baada ya kuachana na Imani yao ya zamani, na kwa wale watakaompinga basi
asiwalazimishe kwani yeye atakua hana makosa juu ya yale watakayoyafanya baada ya
kuwabainishia ukweli ulivyo.
Ama kuhusiana na Tawwakul basi anasema Jarrah Allah Imam Al Zamakhshari kua:
‘Tawakkul hua ni pale Mtu anapokabidhi mambo yake yote kwa yule ambae ni
mwenye uwezo wa kuyasimamia mambo hayo, iwe kwa njia ya kudhuru au
kunufaisha.’
Na pia Tawwakul hua ni :‘Pale mtu anapokua hashangazwi na matokeo ya jambo
wala hajaribu kujitetea kutokana na matokeo hayo kwa njia ambayo imekatazwa
na Allah Subhanah wa Ta’ala’
Kwani amesema Abd Al Wahid Al Dimashq kua: ‘Safari Moja nilimuona Abu Dardaa
Radhi Allahu Aanhu akitoa Darsa kwa watu ambao nao wakawa wanamuulliza
masuali, wakati hali hio inaendelea basi miongoni mwa watu wa familia yake
walikua wanazungumza mazungumzo ya kawaida katika upande wa pili wa
Msikiti’ hivyo nami nikasema kumwambia Abu Dardaa Radhi Allahu Aanhu: ‘Inakuaje
hadi ikawa kuna watu ambao wana ya kupata elimu kutoka kwake lakini watu
wako wa karibu hawajali na wanajishughulisha na mapambo ya kidunia?’
Abu Dardaa Radhi Allahu Aanhu akasema: ‘Hii ni kwa sababu Wacha Mungu
wanaoachana na Dunia ni Mitume, na hakuna watu wagumu dhidi yao kuliko wale
walio karibu yao zaidi’
Siku moja Abu Lahab alikutana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hivyo
akamuuliza: ‘Ewe Muhamamd hivi kama mimi nikikubaliana na Dini yako
nitanufaika na nini?’Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Utanufaika na
kile ambacho watanufaika nacho Waumini wengine’
Abu Lahab akauliza: ‘Hivi Jee hakuna upendeleo na utofauti kwa ajili yangu?’ Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Kwani unataka nini zaidi?’Abu Lahab
665
akasema: ‘Natamani kua dini hii yako iangamie katika kile ambacho kitatupelekea
mimi na wengineo kua sawasawa katika kila kitu.’
Kabla ya Kupewa Utume, basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimuozesha
Mtoto wake wa kike aitwae Ruqqaya ambae alikua ni Mashaa Allah ni Mzuri sana,
Utbah Ibn Abu Lahab, na pia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimuozesha Mtoto
wake wa kike aitwae Umm Kulthoum kwa Utayibah Ibn Abu Lahab, hivyo baada ya
kushushwa Surat Masad basi Abu Lahab akawaambia watoto wake hao wa kiume kua:
‘Hakika mimi najizuia kuonana navyo hadi pale mtakapowaacha mabinti wa
Muhammad’
Na hivyo Utaibah alikua ni mwenye uadui mkubwa sana na Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam na Waislam kwa ujumla, kiasi ya kua siku moja Utaibah alikutana na Rasul
Allah Salallahu Aalayhi wa Salam: ‘Siwezi kukubaliana na An-najmi idha hawa na
Alladhi dana fatadalla’ na kisha akamtemea mate Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa
Salam.
Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akamwambia Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
‘Ya Allah, Mdhibitishe Utaibah kupitia kwa kwenye nguvu ya Mbwa miongoni
mwa Mbwa wako’
Ambapo Abu Labah aliposikia kuhusiana na apizo hilo basi akamwambia Utaibah:
‘Hakika mimi nna khofu juu ya Apizo hili La Muhammad Juu yako kua huenda
litakudhuru.’
Hivyo baada ya apizo hilo basi Utaibah Ibn Abu Lahab akafunga safari na Baba yake
kuelekea Syria, ambapo walipofika katika eneo la kupiga Kambi ambalo waliambiwa kua
hua kuna Simba wa Jangwani anaevamia wakati wa usiku, hivyo akapiga kambi na kisha
Abu Lahab akawaambia walinzi wa Msafara huo kua: ‘Hakikisheni kua Utaibah
anakua chini ya Ulinzi mkubwa sana kwani nnakhofia sana apizo la Muhammad
juu yake’
Hivyo siku hio Utaibah akawa chini ya ulinzi mkubwa sana wa kuzungukwa na watu na
Wanyama, lakini hata hivyo haukumsaidia kitu Ulinzi huo kwani Simba alipotokea Usiku
basi aliwaacha watu wote na Wanyama wote na kuenda moja kwa moja hadi kwa Utaibah
na kumrarua rarua hadi kumsababishia Kifo chake, ambapo kwa upande wa Utbah basi
yeye alisimu baada ya Kutekwa kwa Mji wa Makkah.
Ingawa kazi aliyopewa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ya kutangazia na
kuieneza Dini ya Kiislam ya Allah Subhanahu wa Ta’ala ilikua ni ngumu na nzito sana.
Kwani alipata matatizo, vikwazo na mitihani mingi sana hususan kutoka katika baadhi
ya viongozi wa kabila lake la Quraysh na baadae watu wa maeneo mengine pia, lakini
hakuvunjika moyo kutokana na iman aliyokua nayo, subra, ustahmilivu na ukarimu wake
aliendelea kuueneza ujumbe wa Uislam, na Allah Subhanahu wa Ta’ala alimsaidia na
666
kumuongoza, kama alivyobainishia Allah Subhanah wa Ta’ala kwenye Qur’an pale
alipomwambia Mtume wake Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam katika mwaka wa
nne wa Utume wake kua:
﴿فَٱصْ دَعْ بمَِا تُؤْ مَرُ وَأَعْرِضْ عَنِ ٱلْمُشْ رِكِينَ ۞إِ َّ كَفَيْنَاكَ ٱلْمُسْتَهْزِ ئِينَ۞ٱل َّذِينَ
يجَْعَلُونَ مَعَ ٱهلل َِّ إِلٰهاً آخَرَ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ۞وَلَقَدْ نَعْلَمُ أَن َّكَ يَضِ يقُ صَدْ رُكَ بمَِا
يَقُولُونَ۞فَسَبِّحْ بحَِمْدِ رَبِّكَ وَكُنْ مِّنَ ٱلس َّاجِ دِينَ۞وَٱعْبُدْ رَب َّكَ حَ تى َّ ٰ َْتِيَكَ
ٱلْيَقِينُ ﴾
FaisdaAA bima tu/maru waaAArid AAani almushrikeena; Inna kafaynaka
almustahzi-eena; Alladheena yajAAaloona maAAa Allahi ilahan akhara fasawfa
yaAAlamoona; Walaqad naAAlamu annaka yadeequ sadruka bima yaqooloona
Fasabbih bihamdi rabbika wakun mina alssajideena; WaoAAbud rabbaka hatta
ya/tiyaka alyaqeenu (Surat Al Hijr 15:94-99)
Tafsir: Hivyo Toa Dawa waziwazi Kama ulivyoamrishwa na wape mgongo
Washirikina; Kwani kwa Hakika tutakutosheleza sisi dhidi ya wanaokufanyia Vioja;
Wale ambao ni wenye kuwafanya pamoja na Allah Miungu myengine, watakuja kujua,
Kwani kwa hakika sisi tunajua kua Kifua chako kimekaza kutokana na
wanayoyasema; Hivyo Mtukuze Mola wako na kua miongoni mwa wanaosujudu; Na
muabudu Mola wako hadi utakapopata Yaqini.
Na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawausia watu hadharani kama anavyosema
Numan Ibn Bishr Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alipanda juu ya jukwaa na akaanza kutoa Khutba ambayo ilikua inasema:
‘Nakuonyeni Juu ya Moto! Nakuonyeni Juu ya Moto! Nakuonyeni Juu ya Moto!
Nakuonyeni Juu ya Moto!’ na aliendelea kuyasema maneno haya huku sauti yake
ikipanda juu na kupanda juu hadi kufikia hali ya kua watu waliokua Sokoni
walikua na uwezo wa kumsikia Muhamamd kutoka Msikitini’(Musnad Imam
Ahmad)
Anasema Imam Said Ibn Jubayr kua: ‘Miongoni mwa waliokua wakiongoza
kumfanyia Vioja Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam walikua ni Walid Ibn
Mughira, As Ibn Wail, Aswad Ibn Abd Yaghush, Aswad Ibn Abd Ul Muttalib na
Harith Ibn Qays ambao wote walifariki kabla ya vita vya Badr’
667
Ambapo anasema Imam Muhammad Ibn Ishaq kua: ‘Siku moja watu hawa walikua
wanatufu kwenye Al Kaabah, huku Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam akiwa
amesimama pembeni, na mara akashuka Malaika Jibril, na alipopita mbele yao
Aswad Ibn Abd Ul Muttalib basi Malaika Jibril akarembea Jani la kijani kwenye
Uso wake, na hapo hapo Macho ya Aswad yakapofuka, kisha akapita Aswad Ibn
Yaghush ambapo Malaika Jibril akamnyooshea Kidole na hapo hapo Tumbo lake
likaanza kuvimba na akafariki siku chache baadae kutokana na Kujaa kwa Tumbo
lake.’
‘Ambapo kwa upande wa Walid Ibn Mughira basi nae alipotokea Malaika Jibril
akamnyooshea kidole kwenye Jeraha lake ambalo alikua nalo hapo kabla kwenye
kisigino chake, na Jeraha hilo likatanuka nae akafariki kutokana nalo. Na
alipotokea As Ibn Wail basi Malaika Jibril akamuoneshea kwenye shimo la mgongo
wa Nyayo yake, nae akafariki kutokana na kuchomwa na mwiba kwenye mguu
wake huo wakati alipokua safarini kuelekea kwenye mji wa Tai’f, na Harith Ibn
Qays alipopita mbele yao basi Malaika Jibril akamuoneshea kwenye kichwa chake
nacho kikajaa Usaha ambao ndio uliomuua.’(Imam Muhammad Ibn Jarir At Tabari)
Ambapo anasema Rabia Ibn Abbad kua: ‘Hakika mimi nilipokua Mtoto mdogo
nilipokua nimefuatana na baba yangu katika Maonesho ya Dhul Majaz basi
nilimuona Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwaita watu kwa kusema: ‘Enyi
watu, Semeni Hakuna Mungu isipokua Allah na hivyo mtapata Uongovu’ huku
kukiwa na Mtu mmoja ambae alikua akimfuata nyuma yake na kuwaambia watu
kua: ‘Huyu Mtu ni Muongo, amepotoka yeye kutokana na kuachana na Imani ya
Mababu zake’ hivyo nami nikauliza: ‘Huyu wa nyuma ndio nani?’ na watu
wakasema: ‘Ni Ami yake aitwae Abu Lahab.’’(Musnad Imam Ahmad)
Anasema pia Tariq Ibn Abdullah Al Muharibi Kua : ‘Nilimuona kwenye Maonesho ya
Dhul Majaz kua Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam akiwa ni mwenye kusema:
‘Enyi watu semeni La Ilaha Illah, na mtakua ni wenye kufuzu.’ Na nyuma yake
kukiwa na mtu ambae alikua akimpopoa mawe hadi nyayo zake zinatoka damu, na
mtu huyo alikua akisema: ‘Msimsikilize, wani huyu ni Muongo’ nami nikawauliza
watu huyo ndie nani? Ambapo nao wakasema: ‘Ni Ami yake, Abu Lahab’(Imam
Tirmidhii)
Na katika mwaka huu wa 5 wa Utume wake Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam basi
alifikwa na msiba wa Mtoto wake wa kiume aliekua na umri wa miaka miwili ambae ni
Abdullah au maarufu pia kwa jina la Tahir Ibn Muhamamd na pia kama Tayyib Ibn
Muhammad, hivyo baada ya Abu Lahab kupata habari ya kifo hicho basi akakimbilia
kwa Viongozi wa Quraysh na kuwapa habari hio huku akiwa ni mwenye kufurahia na
kusema kua Muhammad hana tena kizazi.
668
Ambapo anasema Ikrimah kua: ‘Mara baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kuanza kuwaita watu katika Dini ya Uislam, basi watu wa Quraysh walikua
wakisema: ‘Muhammad amekatwa kutokana na watu wake kama vile Mti
ulivyokatwa kutokana na Mzizi wake, na hivyo kua ni wenye kuweza kuanguka
katika wakati wowote ule’: ’
Na Imam Muhammad Ibn Ishaq basi yeye anasema kua: ‘Kila wakati ilipokua Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipokua akitajwa mbele ya As Ibn Wail As Sehmi
ambae ni miongoni mwa Chifu wa Makkah basi alikua akisema: ‘Mwacheni, kwani
yeye hana Mtoto wa kiume wa kuendeleza kizazi, hivyo atakapofariki basi itakua
hakuna wa kumkumbuka’’
MAISHA YA DAR AL ARQAM NA HIJRA YA ABISINIYAH
Mnamo mwaka 615 yaani mwaka wa 5 wa Utume wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kutoka Makkah kuelekea katika Mji wa Madinah basi Waislam walikua
wakifanya Ibada zao katika Mji wa Makkah kwa Kisiri siri bila ya kujionesha na kutotaka
kuonekana. Kwa sababu ilikua ukionekana basi Makafiri huenda wakakuua. Hivyo katika
kipindi hicho basi Waislam walikua hawajioneshi.
Kama anavyosema Suhayb Ibn Sinan Ibn Malik Radhi Allahu Anhu ambae alikua ni
Sahaba mwenye kujulikana pia kama Suhayb Al Rumi kwa sababu alikua ni Sahaba
Mzungu mwenye nywele za Dhahabu, ambapo miaka 20 kabla ya Allah Subhanah wa
Ta'ala kumshuhia Utume Mtume wake Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam, basi mji
wa Basra ulikua na Gavana aitwae Sinan Ibn Malik ambae alikua na watoto kadhaa
ambapo mmoja miongoni mwao alikua ni wa Kiume aitwae Suhayb.
Mtoto Suhayb alikua na utofauti na Watoto wengine wote wa Gavana Sinan Ibn Malik
kwani ingawa Suhayb alikua na Umri wa miaka mitano lakini na baba yake ni mwenye
asili ya Kiarabu lakini yeye alikua ni mwenye weupe wa Kizungu na nywele zake pia
zilikua za rangi ya Dhahabu. Siku Moja familia ya Gavana Sinan Ibn Malik ilitoka nje ya
Mji wa Basra kwa ajili ya Mapumziko.
Ambapo kwa bahati mbaya au nzuri Mapumziko hayo yaligeuka na kua Jinamizi pale
kambi yao ilipovamiwa na kisha watu wote waliomo kwenye Kambi hio kukamatwa na
kupelekwa hadi Uturuki na kisha kuanza kuuzwa mmoja mmoja kama samaki. Ambapo
ndani yake alikuwemo pia Mtoto Suhayb, ambae nae hali yake ilibadilika ghafla baada
669
ya tukio hilo kujikuta akiwa ni Mtumwa wakati hapo kabla alikua ni Mtoto wa Gavana
anaeishi kama mtoto wa Mfalme.
Hivyo Suhayb Ibn Sinan alikua alitumia Utoto wake wote na ujana wake akiwa kama
Mtumwa kutoka Nyumba moja kuelekea Nyumba nyengine kutokana na Kuuzwa na
Kununuliwa mara kadha baina ya Nyumba za Matajiri wa Nchini Uturuki. Ambapo
katika kipindi hiki nchi ya Uturuki ilikua kikijulikana kama Konstantinopal na ilikua
ikitawaliwa na Utawala wa Roman Empire.
Ambapo kutokana na kua ni mwenye kuishi sana kama Mtumwa ndani ya Nyumba za
Wazungu, na kutokana na kuishi katika hali hio basi Suhayb Ibn Sinan akasahau hadi
Lugha yake ya Asili na hivyo akawa anazungumza Lugha ya Roman Empire na pia
kutokana na muonekano wake wa Kizungu basi Suhayb Ibn Sinan akawa moja kwa moja
ni Muzungu hivyo akawa anajulikana kama Suhayb Al Rumi.
Lakini hata hivyo Suhayb Ibn Sinan hakusasahau asili yake na yaliomtokea alipokua
mtoto mdogo hivyo siku moja aliamua kutafuta Njia ya Kutoroka kutoka kwa Wamiliki
wake na wakati alipokua na Msafara wa Watu wake katika ardhi ya Sham katika maeneo
ya Jerusalem na alipopata nafasi hio basi akatoroka na kufunga Safari ya Miezi miwili
kutoka katika Ardhi ya Sham na kukimbilia katika Ardhi ya Mji wa Makkah, kwani
alisikia kua ukifika katika Mji wa Makkah basi hata kama ukiwa Mtumwa ulietoroka basi
ndani yake ardhi hio unakua Mtu huria.
Hivyo Suhayb Ibn Sinan akakimbilia katika Mji wa Makkah kwa bahati nzuri Suhayb Al
Rumi alipofika katika Mji wa Makkah akakutana na Mfanyabiashara mmoja aitwae
Abdullah Ibn Juddan.
Na ingawa Suhayb Al Rumi alikua ni Mzungu mwenye Nywele Dhahabu na asiejua
Kiarabu vizuri kwani anazungumza Kirumi tu, lakini hapo hapo ni mwenye kujua mengi
sana kuhusiana na Biashara ya Warumi basi aliefahamiana vizuri sana na Abdullah Ibn
Juddan na hivyo wakashirikiana katika Biashara na haukuchukua mda mrefu katika
kuishi kwake Suhayb Al Rumi katika Mji wa Makkah isipokua Allah Subhanah wa
Ta'ala alimtilia Baraka katika Biashara zake hizo pamoja na Abdullah Ibn Judan na
hatimae. Suhayb Al Rumi akawa ni mwenye kujitegemea katika Biashara na akawa Tajiri
Mkubwa sana miongoni mwa Matajiri wa Mji wa Makkah.
Kwani Suhayb Al Rumi alikua na Misafara yake Mwenyewe ya Biashara kutoka Makkah
kuelekea Yemen na kutoka katika Mji wa Makkah kuelekea Syria. Ambapo safari moja
baada ya Msafara wake wa Biashara kurudi tu katika Mji wa Makka kutoka Sham basi
Suhayb Al Rumi akapata habari kua Muhammad Ibn Abdullah Salallahu Alayhi wa
670
Salam anatangazia watu kwa Siri kuhusiana na Dini mpya iitwayo Uislam, hivyo
akaulizia anapopatikana Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam na akaambiwa kua:
‘Anapatikana kwenye Nyumba ya Al Arqam Ibn Abi Al Arqam, lakini unatakiwa
uwe na tahadhari ili watu wa Quraysh wasikuone, kwani wakikuona na kujua kua
uko pamoja na Muhammad basi watakusababishia Madhara makubwa sana,
hususan kwa mtu kama wewe ambae ni mgeni aisekua na watu wa kumtetea na
kumlinda, kwani huna Ukoo wala Kabila katika Mji wa Makkah.’
Lakini hata hivyo onyo hili na tahadhari hio aliyopewa Suhayb Al Rumi halikumshtua
wala kumtia wasiwasi, bali aliondoka Moja kwa Moja hadi kwenye Nyumba ya Al
Arqam ambayo ilikua ikijulikana kama Dar Al Arqam.
Na anasema Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi nilikutana na Suhayb Ibn
Sinan katika mlango wa Al Arqam wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akiwa ndani yake, nami nikamuuliza: ‘Jee unataka nini?’ nae akaniuliza: ‘Na wewe
unataka nini?’ hivyo mimi nikajibu: ‘Nataka kuenda kwa Muhammad na
kumsikiliza anachokisema’ ambapo nae akasema: ‘Na mimi hivyo hivyo pia’ Hivyo
sote kwa pamoja tukaingia ndani ya Nyumba hio na Muhammad akatuelezea
kuhusiana na Uislam. Na tukakaa siku nzima hadi kilipoingia kiza ndio tukatoka
huku tukijficha.’
Hivyo ukweli ni kua hali ilifikia kiasi ya kua hadi Mtoto alikua akimficha Baba yake kua
yeye ni Muislam na Baba alikua akimficha Mtoto wake kua yeye ni Muislam. Mfano wa
hali hii tunaiona pale tunapoangalia katika mfano wa Nyumba ya mwanzo ambayo
Waislam walikua wakikutana kisiri na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa ajili
ya kufundishwa Dini ya Kiislam. Hii ilikua ni katika Nyumba ya Sahaba Mtoto aliekua
na Umri wa miaka 14 ambae alikua ni mwenye Nyumba alioirithi kwa Baba yake Abi
Arqam
Hivyo Mtoto huyu alikua akiitwa Arqam Ibn Abi Arqam Radhi Allahu Anhu, na Nyumba
yake ikawa inaitwa Dar Al Arqam. Hivyo katika Nyumba hii ya Arqam Radhi Allahu
Anhu Waislam walikua wakikutana kwa siri kila siku usiku. Ambapo Miongoni mwao
wanaokutana ndani ya Nyumba hio na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alikuwemo pia Sahaba Mtoto aitwae Imran Ibn Husein Radhi Allahu Anhu
Hivyo Usiku Mmoja wakati Masahaba wamo ndani ya Dar Al Arqam, mara mlango
ukagongwa Waislam wakatizamana na kuulizana ni nani agongae wakati wao
wameshatimia? Na hakuna anaejua siri ya Mkutano wao huo? Hivyo mmoja miongoni
mwa Masahaba akaenda Mlangoni na kuuliza kabla ya kufungua Mlango huo: ‘Jee ni
nani anaegonga Mlango?’
671
Sauti iliyojibu kutoka nje ikajibu: ‘Ni Mimi Husein Abu Imran’ Yaani alie Mlangoni
ni Mzee Husein ambae ni Baba yake Imran ambae yumo ndani ya Nyumba. Hivyo Sahaba
huyo akamuuliza Mzee Husein : ‘Una Shida gani?', na Mzee Husein akasema ‘Naomba
niruhusuni nataka kuingia Ndani’
Subhanah Allah! Hapo Hapo Masahaba kusikia Maombia hayo, basi Wakamficha kijana
Imran Chini ya Mapaja yao kwa kumkalia, kwani walikua wanajua kua Baba amekuja
Kumuua Mtoto wake. Kisha Baada ya kumkalia Imran Wakamfungulia Mlango Baba
Mtu yaani Mzee Husein. Na kisha akafunguliwa Mlango Mzee Husein ambae nae
alipoingia hakuuliza mtoto wake wala nini bali ailiuza : ‘Nilikua nnashida nae Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam, yuko wapi?’
Na alipoonyeshwa unajua alipofika mbele ya Rasul Allah Salallahu Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alifanyanya nini? Naam..Alimwambia Rasul Allah Salallahu Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua anataka kuingia katika Uislam, hivyo baada ya Imran
kusikia Sauti ya Baba yake ikitamka Shahada mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, basi Imran alitoka haraka chini miguu ya Masahaba na kumkimbilia Baba yake,
na kisha akamkumbatia kwa nguvu huku macho yake yakiwa yamejawa na Machozi ya
Mapenzi Imani ya Dini yake na Machozi ya mapenzi ya Baba yake yakimtiririka Kijana
Imran Ibn Husein Radhi Allahu Anhu
Kwani kijana Imran Radhi Allahu Anhu hakufikiria kua na Baba yake alikua na Imani
kama yake, na kuingia katika Uislam kama alivyoingia yeye hapo Kabla, ambapo tukio
hili la Imran Kulia kwa Mapenzi na Imani lilisababisha kila Muislam aliekuwemo ndani
Dar Al Arqam kua ni mwenye kulia na kutokwa na Machozi kwa Iman,Mapenzi,Furaha
na Umoja wa Waliokuwemo Ndani yake. Huo ni Mmoja kati ya Mifano ya hali ilivyokua
kabla ya Al Hijra.
Waislam walikua wanapendana kihisia kwa upande wa Kiimani na upande wa Kimapenzi
na kua na Umoja ndani ya Nyumba moja waliyokutana Ndani yake Majirani wenye Imani
ya Dini Moja ya Kiislam Kutoka ndani ya Mji mmoja. Hivi Jee hivi ndivyo tulivyo sisi
leo hii? Kua Waislam wa Nyumba Moja, wa Mji mmoja wa Nchi Moja tunapendana kwa
Umoja wa Kiimani na kihisia?
Hivyo hapa kila mmoja wetu anatakiwa ajue kua kama tutakua hatupendani na hatuna
Umoja na kila mmoja anafanya Ibada yake kivyake, na anaona fakhari na kujionesha
kwa kawatangulia wenzake, Wazee wake majirani zake tofauti na walivyokua Masahaba,
kwa kuchukulia mfano mmoja tu ambao ni wa Muandamo wa Mwezi basi hii
inamaanisha kua Ndani yetu Miongoni mwetu kuna Wanafiq ambao wana pia Unafiq wa
ndani ya Nafsi. Ambapo hata Wanafiq walioanzia Madinah baada ya kupatikana Uhuru
wa kuabudu basi walijifakharisha Kiibada.
672
Nyumba hii ya Dar Al Arqam ilikua ni nyumba yenye historia ya upekee katika Uislam
kwani ndani yake walisilimu Waislam wengi sana, ambapo Arqam mwenyewe aliusia
kizazi chake kua Nyumba hio isiuzwe, na ipo hadi hii leo na inajulikana kama Dar
Khayzuran na bado ina madrasa ndani yake.
Miongoni mwa Waislam waliopata mitihani ya Quraysh alikuwemo pia Ummu Ayman
na Zayd Ibn Harith walikua pia ni watu wa Mwanzo kupata mitihani ya Makuraysh dhidi
ya Uislam kutokana na kuamini Dini ya Kiislam na pia kutokana na kua ni wenye asili
ya Utumwa.
Safari Moja wakati Waislam walipokua wakikutana Usiku katika Nyumba ya Al Arqam
kufundishana Dini ya Kiislam, basi Makafiri walipogundua hilo wakaamua kuifunga njia
inayoelekea kwenye Nyumba hio na kuweka ulinzi ili Waislam wasikutane kwenye
Nyumba hio.
Lakini Hata hivyo kutokana na Bidii na ari na Imani waliyokua nayo basi Waislam
walitafuta kila njia mpaka wakawa wanaweza kukutana bila kujulikana. Hivyo siku hio
wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwa yupo kwenye Nyumba ya Al
Arqam basi Bi Khadijah akawa anataka kumpa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
Ujumbe muhimu sana ambae ulikua unatakiwa umfikie wakati huo huo na kipindi hicho
Simu ilikua hakuna.
Hivyo wakati Bi Khadija anatafakkari afanye nini basi Ummu Ayman akamwambia Bi
Khadija kua yeye yuko tayari kuhatarisha maisha yake hata akamatwe lakini ujumbe huo
ataufikisha kwa Mtoto wake yaani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Bi Khadija
akajaribu kumnasihi lakini Ummu Ayman akasema hamna tatizo atafikisha Ujumbe,
hivyo akapewa ujumbe huo na kutoka nao usiku akajificha jificha mpaka akafika kwenye
Nyumba ya Al Arqam
Na alipofika akagonga Mlango na kufunguliwa basi akampa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam ujumbe wake kutoka kwa Bi Khadija ambapo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akatabasam kutokana na Ujasiri wa Umm Ayman na kusema:
‘Hakika Umebarikiwa Ya Ummi, kwani wewe ni Miongoni mwa watu ambao
wameshapata Nafasi zao katika Pepo ya Allah Subhana wa Ta'ala.’
Kisha baada ya Umm Ayman kuondoka basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akamalizia kwa kuwaambia Masahaba zake kua:: ‘Kama ikiwa kuna mtu miongoni
mwenu anataka kumuoa mwanamke wa Peponi basi na amuoe Ummu Ayman’
Kwani Ingawa Pepo ndio Pepo na ni kitu chenye Raha za Upekee za Milele zisizo na
Kifani chake, Ambapo Hujjat ul Islami Imam Abu Hamid Muhamamd Ibn Muhammad
673
Al Ghazali anasema kua Allah Subhanah wa Ta'ala ametujaalia Ibn Adam kutuonjesha
Mfano wa Ladha ya Raha ya Peponi ambayo kwa sekunde Kadhaa hapa Duniani.
Ambayo ni ile Ladha ya Raha inayopatikana katika Tendo la Kuingiliana Kimwili kwa
Mume na Mke na Utulivu wa Akili na Mwili unaopatikana baada yake Tendo hilo. Hivyo
Mfano huo wa Raha hio ya sekunde chache ya hapa Duniani ndio Unakaribiana na Raha
ya Milele inayopatikana Peponi.
Lakini hata hivyo hakuna hata Sahaba mmoja aliefumbua Mdomo wake na kumwambia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua anataka kumuoa Umm Ayman. Na bila ya
shaka, hii inatokana na Maumbile na Maazingira ya asili ya Umm Ayman.
Kwani Kwanza Ummu Ayaman alikua tayari Mtu Mzima, fikiria kua Alikuja katika Mji
wa Makkah Kabla ya hata kufungwa ndoa ya Baba na Mama wa Rasul Allah Sallahu
Alayhi wa Salam na alipokuja alikua Mwari, akanunuliwa na Abdulla Ibn Abd Muttalib,
Abd Mutallib Akamuoa Mama yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, akazaliwa
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kisha akakaa nae Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam mpaka Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipotimia umri wa miaka 25
alipomuoa Bi Khadija Radhi Allahu Anha. Na akawa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam mpaka alipopata Utume yaani katika Mwaka 610 wakati Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akiwa na miaka 40.
Hivyo basi katika wakati huu ambao Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anawaambia
Masahaba zake wamuoe Ummy Ayman basi Ummu Ayman alikua tayari ana Umri wa
Miaka 50 na kitu. Sababu ya pili ni kua Asili ya Kua Ummu Ayman alikua Mwafrika
Mweusi, na Sababu ya tatu ni kua Ummu Ayman alikua ni mwenye asili ya kua ni
Mtumwa.
Kwani hayo yote tunapoyaangalia kwa wakati wa kipindi hicho ambacho ilikua kuna
Ubaguzi mkubwa wa Kikabila baina ya Kabila la Quraysh na Makabila mengine katika
Mji wa Makka kwa Kabila la Quraysh lilikua liko Juu kidarja. Na Ndio Maana Allah
Subhanah wa Ta'ala kwa Hikma zake akamjaalia Umm Ayman kua ingawa alikua si wa
Kabila la Quraysh na alikua Mtumwa alimjaalia kua na Darja kubwa ya kua Mama Mlezi
wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kua ni mwenye kumuita Umm Ayman Kwa jina la Ummi - Mama.
Kwa sababu tu ya kua ni Mfano bora wa kuvunja Mila na Desturi na Tabia za Watu hao
kuwadharau Wasiokua wa Kabila la Quraysh na kutowadharau Watumwa. Yaani Mfano
hai hapa wa kuwarekebisha watu basi unaanza moja kwa moja kwa Mtume wake.
674
Hivyo sifa hii ya kua ni Mama Mlezi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
inatakiwa iwe inampasisha moja kwa moja Umm Ayman kua mwanamke Bora na
anaestahiki kuolewa na Masahaba bila kuangalia rangi yake au asili.
Vile vile kuna sifa ya pili bora aliyokua nayo Umm Ayman ambayo tayari Masahaba
wameshaekewa wazi na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam juu yake mbele yao kua
ni Mwanamke atakaeingia Peponi. Hii pia ni sababu ambayo inafuta kasoro zote za Awali
yaani Umri Mkubwa, Rangi na asili ya Utumwa.
Lakini hata hivyo kama tunavyoona kua Masahaba walikaa kimyaa na kisha baada ya
dakika kadhaa za Ukimya unaoweka wazi kua hakuna hata mmoja kati ya Masahaba
anaetaka kumuoa Umm Ayman Mwanamke alieingia Peponi hapa hapa Duniani basi
Zayd Ibn Harith akanyanyuka na kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kua:
‘Ya Rasul Allah! Hakika mimi nitamuoa Umm Ayman kwani kutokana na sifa zake
basi amewashinda hata Wanawake Vijana na wenye uzuri wa kuvutia’
Hivyo Zayd Ibn Harith Radhi Allahu Anhu akamuoa Ummu Ayamn, ambapo ndoa yao
hio ilibarikiwa na Allah Subhanah wa Ta'ala ambae aliwajaalia Zayd Ibn Harith na Umm
Ayman kupata mtoto wa kume aliepewa jina la Usamah.
Ambapo mtoto huyu alikua akipendwa Sana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na alikua akicheza nae na kumfanyia kila kitu kama vile anavuowafanyia Watoto wake.
Kwani mtoto huyo aliekulia katika mazingira bora chini ya Uangalizi wa M-bora wa
Viumbe, na hivyo alikua na sifa ya kua na ubora wa takriban kila kitu, mpaka katika
mbinu za Mapigano ya Vita pia.
Na ingawa hakumfikia Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu ambae mpaka leo hii rekodi
yake haijavunjwa katika fani hio ya Mapigano lakini, Hata hivyo Usamah Ibn Zayd Ibn
Harith Radhi Allahu Anhu alikua mpiganaji Mahiri kiasi ya kua aliongoza Jeshi la
Mapigano yake ya mwanzo dhidi ya Makafiri wakati akiwa na umri wa miaka 17 tu.
Usamah Ibn Harith alikua akijulikana kua kama Jenerali Kijana ambae ni Mtoto wa watu
wanaopendwa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam yaani Zayd Ibn Harith Radhi
Allahu Anhu na Umm Ayman Radhi Allahu Anha.
Na mambo yalipozidi kua magumu katika mwaka huu wa 5 wa Uislam basi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akawaambia Masahaba zake kua wahamie Uhabeshi, kwani
ndani ya Ardhi hio kuna ‘An Najash’ yaani ‘Mfalme’ ambae anajulikana kwa jina la An
Najash Ashama Ibn Abjar ambae ni Muadilifu na hakuna anaepata madhara kutokana nae
675
kama wanavyoelezewa miongnoni mwa Ahl Al Kitab wenye sifa ya Uadilifu kama
tulivyoona hapo awali tulipozungumzia kisa cha Nabii Isa.
Kama tulivyosema kua Masahaba 10 Wanaume na Masahaba wa 4 Wanawake
wakahamia kisiri siri, ambao ni Sad Ibn Abi Waqqas, Jahsh Ibn Riyab, Abd Allah Ibn
Jahsh, Jafar Ibn Ab Talib, Uthman Ibin Affan na mkewe Ruqayyah Bint Rasul llah
Salallahu Alayhi wa Salam, Abu Hudhayfah Ibn Utbah na Mkewe Sahla Bint Suhayl
Zubayr Ibn Awwam, Musab Ibn Umair, Abd Rahman Ibn Awf, Abu Salama Abd Allah
Ibn Al Asad na mkewe Ummu Salamah Hind Bint Abi Umayyah, Uthman Ibn Mazun,
Amr Ibn Rabiah na Laylat Bint Asmah Radhi Allahu Anhum.
Masahaba hawa walisafiri kwa kutumia Jahazi kutoka katika mji wa Shuaiba na kufikia
katika mji wa Adulis, na ingawa leo hii hua liko katika ardhi ya maeneo ya Eritrea lakini
katika wakati huo eneo hilo lote lilikua linajulikana kama Abissiniyah yaani Ethiopia. Na
kisha baada ya hapo ukafuatia msafara wa Masahaba 83 ambao ni Wanaume na
Masahaba 18 ambao ni Wanawake wakahamia pia.
DAMU YA KWANZA YA MASHAHIDI WA KIISLAM.
Miongoni mwa watu walioathirika vibaya sana kutokana na adhabu na madhila ya
Makafiri ndani ya kipindi cha miaka mitano ya mwanzo ya Uislam basi ilikuwemo
familia ya Yasir Ibn Amar Ibn Malik Ibn Ansi ambae alikua ni mtu mwenye asili ya
Yemen aliehamia katika Mji wa Makkah baada ya kua ni mwenye kumtafuta Kaka yake
aliepotea na hivyo kufikia kwa Abu Hudhayfah Ibn Al Mughira Banu Makhzum, ambapo
baada ya mda Abu Hudhayfa akamuozesha Yasir Ibn Amar kwa Mtumwa wake aitwae
Summayah Bint Khabbat, ambae alikua ni Mwanamke mwenye asili ya Kiafrika hii ni
ndoa iliyotoa watoto watatu ambao ni Abd Allah Ibn Yasir, Harith Ibn Yasir na Ammar
Ibn Yasir ambae ni maarufu kama Abu Yaqzan aliezaliwa katika mwaka wa Tembo
ambao ni sawa na mwaka aliozaliwa Rasul Allah Salallahu alayhi wa Salam.
Na Abu Hudhayfah Ibn Al Mughira Banu Makhzum alipofariki basi watu wa Banu
Makhzum wakawa wanaoongoza katika kuwanyanyasa Waislam na kuwasababishia
Madhara, makubwa sana na walianza na familia ya mzee Yasir Ibn Amar kwa
kuwachukua na kuwapelekea katika sehemu ambayo ilikua na Majabali katika kipindi
cha mchana wa Jua kali sana, na kisha kuwabakisha na nguo nyepesi na kuwalaza juu ya
mawe hayo ya moto, huku wakiwaadhibu na kuwataka waikane Dini yao mpya.
Siku moja wakati Makafiri walipokua wanawatesa wanafamilia wa Yasir Ibn Amar basi
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akapita na akawaona namna wanavyoteswa huku
wakiwa wanalia hivyo akawaonea huruma sana, na kuwaambia: ‘Kuweni na Subra Enyi
676
familia ya Yasir, kuweni na Subra kwani Allah atakulipeni Pepo, hivyo kuweni na
Subra’
Hivyo Yasir Ibn Amar akamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam: ‘Ya Rasul
Allah! Hivi jee yataisha lini madhila haya?’ hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala
akawaombe Dua kwa kusema: ‘Ewe Mola wangu, Usizuie Rehma na huruma juu ya
familia ya Yasir.’
Ambapo baada ya Dua hio basi Summayah Bint Khabbat Radhi Allahu Anha akapanda
Darja ya kua ni shahidi wa kwanza na kua Mwanamke ambae ni mwafrika na kua ni mtu
wa kwanza kufa shahidi kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala baada ya kuchomwa
Mkuki wa Tumbo na kupasuliwa pasuliwa tumbo lake kwa mkuki huo na Abu Jahal
ambae nie aliekua Chifu wa Banu Makhzum ambae alikua akisema kua: ‘Hakika
Umeingia kwenye hii Dini ya Muhammad kwa sababu ya uzuri wake wa
kimaumbile ewe Summayah eh?’
Lakini hata hivyo masuali hayo ya dhihaka na kuteswa kwake hayakumvunja Mopyo
Sumayyah Bint Khabbat Radhi Allahu Anha bali yalimzidishia Imani yake, na hivyo kua
ni miongoni mwa waliothibitisha kua wako tayari kujitolea muhanga kwa ajili ya Allah
Subhanah wa Ta’ala ambae ametuambia katika Qur’an kua:
﴿أَمْ حَسِ بْتُمْ أَن تَدْخُلُواْ ٱلجَْن َّةَ وَلَم َّا َْتِكُم م َّثَلُ ٱل َّذِينَ خَلَوْاْ مِن قَبْلِكُم م َّس َّتْ هُمُ
ٱلْبَأْسَآءُ وَٱلض َّر َّآءُ وَزُلْزِلُواْ حَتى َّٰ يَقُولَ ٱلر َّسُولُ وَٱل َّذِينَ آمَنُواْ مَعَهُ مَتىَٰ نَصْ رُ ٱهلل َِّ أَلا
إِن َّ نَصْرَ ٱهلل َِّ قَرِيبٌ ﴾
ۤ
Am hasibtum an tadkhuloo aljannata walamma ya/tikum mathalu allatheena
khalaw min qablikum massat-humu alba/sao waaldhdharrao wazulziloo hatta
yaqoola alrrasoolu waalladheena amanoo maAAahu mata nasru Allahi ala inna
nasra Allahi qareebun (Surah Al-Baqarah 2:214)
Tafsir: Ama mnajihesabu kua mmtaingia Peponi na wala hamtopewa mithili ya
(Mitihani) wale ambao waliotangulia kabla yenu? Kwani wao walifikwa na Umasikini
na Madhara na mitikisiko hadi akasema Mtume na pamoja Waliomaini pamoja nae
kua: ‘Hivi Jee ikowapi Nusra yaAllah?’ Bila ya Shaka Nusra ya Allah iko Karibu.
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amesema kua: ‘Na kisha atakuja Mtu
miongoni mwa watu wa Duniani ambae alikua anaisha maisha ya Tabu sana
677
Duniani lakini ni miongoni mwa Watu wa Peponi, na ataingizwa mara moja Peponi
na ataambiwa Ewe Ibn Adam Hivi Jee uliwahi kua na Matatizo yeyote? Au
Mashaka uliwahi kua nayo?’ nae atasema: ‘Wallahi La! Ewe Mola wanguhakika
mimi sikuwahi kua na matatizo wala mashaka yeyote’(Sahih Muslim)
Hivyo hio ndio hali watakayokua nayo watu wa Peponi akiwemo Summaya Bint Khabbat
Radhi Allahu Anha ambae ni shahidi wa kwanza na pia atakayokua nayo mumewe
aliefuatia baada ya kufariki kwake na hivyo kua ni shahidi wa Pili katika Uislam ambae
ni Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu akafarikia Dunia na kupanda darja kwa kuupata
Ushahidi mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala kutokana na mateso hayo na hivyo Yasir
Ibn Amar Radhi Allahu Anhu kua ndio Mtu wa pili na ndie Mwanamme wa mwanzo
kuupata ushahid katika Uislam ambapo malipo yao ni kama zinavyosema aya:
﴿إِن َّ ٱهلل ََّ ٱشْتَرَىٰ مِ نَ ٱلْمُ ؤْ مِ نِينَ أَنفُسَ هُ مْ وَأَمْ وَالهَُمْ أبَِن َّ لهَُمُ ٱلجَّ ن َّةَ يُقَاتِلُونَ فىِ سَبِيلِ
ٱهلل َِّ فَيَقْتُلُونَ وَيُقْتَلُونَ وَعْداً عَلَيْهِ حَقّاً فىِ ٱلت َّوْرَاةِ وَٱلإِنجِْيلِ وَٱلْقُرْآنِ وَمَنْ أَوْ فىَٰ
بِعَهْدِهِ مِنَ ٱهلل َِّ فَٱسْتَبْشِ رُواْ بِبَيْعِكُمُ ٱل َّذِى ابَيَعْتُمْ بِهِ وَذٰ لِ كَ هُ وَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ ﴾
Inna Allaha ishtara mina almu/mineena anfusahum waamwalahum bi-anna
lahumu aljannata yuqatiloona fee sabeeli Allahi fayaqtuloona wayuqtaloona
waAAdan AAalayhi haqqan fee alttawrati waal-injeeli waalqur-ani waman awfa
biAAahdihi mina Allahi faistabshiroo bibayAAikumu allathee bayaAAtum bihi
wadhalika huwa alfawzu alAAadheemu(Surat At Tawba 9:111)
Tafsir: Na kwa hakika Allah amenunua kutoka kwa Waumini Maisha yao na Mali zao,
kwa Bei ambayo kwao wao itakua ni Pepo. Kwani wanaigana kwa ajili ya Allah,
Wanaua na Kuuliwa. Na ahadi ya Allah ni ya Kweli katika Tawrat, katika Injil na
katika Qur’an, na jee ni yupi yule ambae ni mkweli kwa ahadi zake zaidi ya Allah?
Hivyo furahieni bei ambayo mmeshapatana nae, kwani huko ndiko Kufuzu kukubwa
zaidi.
Ambapo kwa upande wa Yasir Ibn Amar basi yeye alikua akilazimishwa kuvaa bangili
kubwa la chuma lenye kufuli mguuni mwake na kusimamishwa Juani hadi bangili hio
ikapata moto na kuanza kumuunguza mguu wake huo. Ambapo siku moja Amar Ibn
Yasir Radhi Allahu Anhu alipomuona Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam basi
akasema: ‘Ya Rasul Allah hakika sisi tayari tumeshateswa na kila aina ya mateso’
678
Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Mola wangu Usimjaalie mtu
yeyote kutoka kwenye Familia ya Yasir kua ni mwenye kuingia Motoni.’
Na siku nyengine pia Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Moto Kua
baridi na Salama kwa Ibrahim na pia kua hivyo kwa Amar’ na kisha akamwambia
Amar Ibn Yasi Radhi Allahu Anhu kwa kusema: ‘Ewe Amar! Hakika wewe hutokufa
kutokana na mateso haya bali utaishi kwa mda mrefu, na kifo chako kitatokana na
mikono ya watu wengi’
Hivyo mateso haya juu ya Amar Radhi Allahu Anhu yaliendelea hadi siku moja wakati
Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam alipomuona Amar Radhi Allahu Anhu akiwa
analia hivyo nae akatokwa na machozi na kisha akamwambia kwa kumuuliza: ‘Hivi jee
Makafiri wamekukamata na kukutumbukiza kwenye Maji tena? Hivyo mara
nyangine wakikukamanta na kusema kua useme wanayotaka useme na
wakaendelea kukutesa basi sema watakayokuambia ili wakuachie huru.’
Baada ya siku moja basi Amar Radhi Allahu Anhu akakamatwa tena na kuteswa sana na
akaambiwa kua: ‘Hakika sisi hatutokoma kukutesa hadi utakapomlaani Muhammad
na kusema kua unamuabudu Lata na Uzza na unawapenda zaidi kuliko Dini yake
Muhammad’ Hivyo ingawa Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu aligoma kwanza
kutamka maneno hayo lakini alipoendela kuteswa basi nae akayatamka maneno hayo, na
hivyo akaachiwa huru.
Baada ya kuachiwa huru basi Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu akaenda moja kwa
moja hadi kwa Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam na alipofika mbele yake, Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuuliza: ‘Naona kutokana na muonekano wa uso
wako kua umeachiwa huru’ Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Wa Allahi,
sijaachiwa huru.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akauliza: ‘Kwanini?’ Amar Ibn Yasir Radhi
Allahu Anhu akasema: ‘Kwa sababu nimelazimishwa kua nikane, wamenilazimisha
niseme kua Dini ya Lata na Uza ni bora zaidi ya Dini yako.’ Huku Amar Ibn Yasir
Radhi Allahu Anhu akiwa ni mwenye kujawa na huzuni kubwa sana na kuchanganyikiwa
kwani mbali ya kua ameokoka kutokana na Adhabu na mateso ya Makafiri lakini alikua
akijihisi kua kama kwamba ameangikiwa na Mlima mzima wa Uhud kwa sababu ya
kufikiria uzito wa Adhabu ya Mola wake na hali yake.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuuliza Amar Ibn Yasir Radhi Allahu
Anhu kwa kusema: ‘Hivi jee ulikuaje Moyo wako wakati uliposema maneno hayo’
Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Najiona kua Moyo wangu umetulia na
wenye uimara zaidi juu ya Imani yangu’
679
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia Amar Ibn Yasir Radhi Allahu Anhu
kua: ‘Huna makosa juu yako ewe Amar, kwani hata kama wakikukamata tena na
kukutesa tena na wakataka urudie maneno hayo basi, rudia maneno hayo ili
wakuachie huru.’
Na hivyo baada ya maneno hayo ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi Allah
Subhanah wa Ta’ala akashusha Aya ifuatayo:
﴿مَن كَ فَرَ بِٱهلل َِّ مِن بَعْدِ إيمَانِهِ إِلا َّ مَنْ أُكْرِهَ وَقَلْبُهُ مُطْمَئِن ٌّ بِٱلإِيمَانِ وَلَٰكِن م َّن
شَرَحَ ابِلْكُفْرِ صَدْراً فَعَلَيْهِمْ غَضَبٌ مِّنَ ٱهلل َِّ وَلهَُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴾
Man kafara biAllahi min baAAdi eemanihi illa man okriha waqalbuhu mutmainnun
bial-eemani walakin man sharaha bialkufri sadran faAAalayhim ghadhabun
mina Allahi walahum AAadhabun AAadheemun (Surat An Nahl 16:106)
Tafsir: Yeyote yule atakaekufuru baada ya kuikubali Imani yake Allah Subhanah wa
Ta’ala, isipokua yule ambae alielazimishwa huku Moyo wake ukiwa una utulivu wa
Kiimani, lakini kwa yule alieufungulia Moyo wake kwa Kufuru basi juu yao ni Adhabu
kutoka kwa Allah na watapata adhabu kali sana.
Na hivyo ikawa imeruhusika kwa Waumini ambao wameikubali Imani ya Dini ya
Kiislam ndani ya Moyo wao, kua watakapofikwa na mitihani ya kulazimishwa kuiasi
Imani yao hio la sivyo watadhuriwa au kuuliwa basi na waseme wanayotakiwa kukubali
kwa ndimi zao ilia wasidhuriwe.
Na kisha baada ya hapo basi Allah Subhanah wa Ta’ala akawashushia Waislam Surat Al
Buruj kwa ajili ya kuwatia Moyo zaidi kiimani ambayo inasema baada ya:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞وَٱلس َّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ ۞وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُ ودِ۞وَشَاهِدٍ
وَمَشْهُودٍ۞قُتِلَ أَصْ حَ ابُ ٱلأُخْ دُ ودِ۞ٱلن َّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ۞إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ۞وَهُ ْم
ٰ عَلَى مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ۞وَمَا نَقَمُواْ مِنْهُمْ إِلا َّ أَن يُؤْمِنُواْ بِٱهلل َِّ ٱلْعَزِيِز
ٱلحَْمِيدِ۞ ٱل َّذِى لَهُ مُلْكُ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَٱهلل َُّ عَلَى ِ كُل شَيْءٍ شَهِيدٌ۞ إِ َّن
ّ
680
ٱل َّذِينَ فَتَنُواْ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَاتِ ثمُ َّ لمَْ يَتُوبُواْ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَن َّمَ وَلهَُمْ عَذَا ُب
ٱلحَْرِيقِ ۞إِن َّ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلص َّ الحَِاتِ لهَُمْ جَن َّاتٌ تجَْرِى مِن تحَْتِهَا ٱلأَنْهَاُر
ذٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِ يرُ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Waalssama-i dhati alburooji; Waalyawmi
almawAAoodi; Washahidin wamashhoodin; Qutila as-habu alukhdoodi;
Alnnari thati alwaqoodi; Idh hum AAalayha quAAoodun; Wahum AAala ma
yafAAaloona bialmu/mineena shuhoodun; Wama naqamoo minhum illa an
yu/minoo biAllahi alAAazeezi alhameedi; Alladhee lahu mulku alssamawati waalardhi
waAllahu AAala kulli shay-in shaheedun; Inna alladheena fatanoo
almu/mineena waalmu/minati thumma lam yatooboo falahum AAadhabu
jahannama walahum AAadhabu alhareeqi; Inna alladheena amanoo waAAamiloo
alssalihati lahum jannatun tajree min tahtiha al-anharu dhalika alfawzu alkabeeru
(Surat Al Buruj 85:1-11)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma; Naapa kwa Mbingu
na Mapambo ya mkusanyiko wa Nyota zilizomo kwenye mwendo, Na siku
iliyoahidiwa; Na Mashahidi na Walioshudiwa; Walikatiliwa watu wa Shimoni;Na
Moto uliojazwa Kuni. Huku wao (Mashahidi) wakiwa wamekaa pembeni yake. Na
huku wakishuhudia wanayoyafanya dhidi ya Waumini. Hawakua na chochote dhidi
yao isipokua ni kua wenye kuamini Allah mwenye Utukufu na mwenye kustahiki sifa
zote; Ambae kwake kuna umiliki wa Mamlaka ya Mbinguni na Ardhini, na Allah ni
mwenye kuhudia kila kitu. Kwa hakika wale waliowafitinisha (kwa kuwapa Mtihani)
Waumini wa Kiume na Waumini wa Kike (kwa kuwachoma moto kwenye shimo hilo),
Kisha wakawa hawakutubu, basi ni juu yao Adhabu ya Jahannama, na ni adhabu ya
moto mkali sana. Hakika kwa wale walioamini na wakafanya Mema basi juu yao wao
ni Malipo ya Pepo yenye mabustani yenye ipitayo ndani yake. Na huko ni Kufuzu
kukubwa sana.
Na ingawa Imam Abu Muḥammad Al Ḥusayn Ibn Masʻud Ibn Muḥammad Al Farra Al
Baghawi anasema kua ‘Tukio la Watu wa As-hab ul Ukhdud lilitokea katika kipindi
cha Mfalme Nebuchardnezzer alipowatia kwenye shimo la Moto Mayahudi’
Na Imam Muḥammad Ibn Is-haq basi yeye anasema kua ‘Tukio la Watu wa As-hab ul
Ukhdud lilitokea katikaArdhi ya Yemen’
Lakini kwa upande wa Suhayb Ibn Sinan Radhi Allahu Anhu basi yeye anasema kua: ‘
Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: Hapo zamani kulikua na na
681
Mfalme ambae alikua na Mchawi wake, hivyo Mchawi huyo alipofikia umri wa
uzeeni basi, basi akamwambia Mfalme kua: ‘Hakika mimi nimeshakua Mzee, na
uhai wangu unakaribia mwisho wake, hivyo nitumie Mtoto mwenye kipaji ili
nimfundishe fani yangu’
Hivyo Mfalme huyo akamtafuta Mtoto husika mwenye Kipaji na akampeleka kwa
Mchawi wake ili apate kufundishwa fani hio, ambapo katikati ya masafa baina ya
njia kutoka kwa Mfalme kuelekea kwa Mchawi wake kulikua kuna Mcha Mungu
ambae alikua akiishi, na huyu Mtoto katika kuenda na kurudi kwake alikua akipita
kwa huyu Mcha Mungu, kwa sababu alikua akivutiwa sana na Maneno ya Mcha
Mungu huyo, na hivyo ilikua kila siku alikua akiadhibiwa na Mchawi wakati
anapofika kwake kwa sababu ya kuchelewa kwake baada ya kupitia kwa Mcha
Mungu huyo na pia hupigwa anaporudi nyumbani wakati anapochelewa kurudi.
Hivyo Mtoto huyo akamlalamikia Mcha Mungu huyo na kumwambia ambae nae
akamwambia kua akifika kwa Mchawi basi amwambie amechelewa kwa sababu
alizuiliwa na watu wake, na akichelewa Nyumbani basi awaambie kua amechelewa
kwa sababu ya Mchawi, ambapo hali hii iliendelea hadi pale siku moja wakati Mtoto
huyo alipokutana na mnyama mkubwa njiani, na hivyo akasema: ‘Hakika leo
nitajua ni njia ipi ndio njia ambayo ni sahih zaidi kuelekea kwa Allah baina ya Njia
ya Mchawi na Mcha Mungu.’
Akaokota jiwe na kisha akasema: ‘Ya Allah kama njia ya Mcha Mungu ndio Sahih
kwako wewe kuliko ya Mchawi basi Muue mnyama huyu kutokana na jiwe hili ili
watu waweze kupita katika njia hii’ Na kisha akalirusha Jiwe hilo kwa Mnyama
huyo na likamuua Mnyama huyo. Baadae akamwambia Mcha Mungu kuhusiana
na tukio hilo, ambae nae akamwambia: ‘Ewe Mtoto wangu hakika wewe umenizidi
mimi sasa hivi na hiyvo utaanza kupatwa na mitihani, lakini utakapopatwa na
Mitiani hiyo basi mimi usinitaje.’
Hivyo Mtoto huyo akwa anawatibu Vipofu, wenye ukoma na wenye Maradhi
tofauti, ambapo miongoni mwa alikuwepo Mtumishi wa Mfalme ambae alikua ni
Kipofu na alikuja na zawadi nyingi ili atibiwe huku akisema: ‘Nitibu na hizi zawadi
zote zitakua zako’ Hivyo Mtoto akasema: ‘Sio mie nnaetibu bali ni Allah Mtukufu
hivyo kama ukimuamini basi nitakuombea kwake na atakuponesha.’
Hivyo Mtu huyo akamuamini Allah na Mtoto akamuombea Dua na akapona. Kisha
Mtumishi huyo akaenda kwa Mfalme na kumuuliza ni nani aliemponyesha.
Mtumishi huyo akasema: ‘Ni Mungu wangu’ hivyo Mfalme akauliza:
‘Unamaanisha kua ni Mimi?’ Mtumishi huyo akasema: ‘La sio wewe’ Mfalme
akauliza: ‘Jee una Mungu zaidi yangu?’ Mtumishi akajibu: ‘Naam ni Mungu
682
wangu na Mungu wako.’ Hivyo Mfalme huyo akamuadhibu Mtumishi huyo hadi
akalitaja jina la Mtoto aliemponesha.
Na hivyo Mtoto huyo akafikishwa mbele ya Mfalme na akamuuliza: ‘Ewe Mtoto
inaonekana umeendela sana katika fani ya Uchawi, kiasi ya kua sasa hivi unaweza
kutibu Vipofu, wenye Ukoma na maradhi mengineyo.’
Mtoto akajibu: ‘Sio mie nnaetibu, bali nia Allah Subhanah wa Ta’ala ndie anaetibu.’
Mfalme akauliza: ‘Umanaanisha mimi?’ Mtoto akasema: ‘La’ Mfalme akasema:
‘Jee una Mungu mwengine zaidi yangu?’ Mtoto akasema: ‘Mungu wangu na wako
wewe ni Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Hivyo Mfalme akamuadhibu Mtoto huyu hadi akamtaja Mcha Mungu na
kuwapeleka anapoishi, na alipoletwa mbele ya Mfalme basi Mfalme akasema:
‘Kubali kua mimi ndie Mungu wako.’ Lakini Mcha Mungu akakataa.
Hivyo akachukuliwa Mcha Mungu huyo na kaunzwa kukawa na Msumeno katika
pande mbili tofauti, na kisha Mtumishi alietibiwa Upofu akaambiwa amkubali
Mfalme kua ndie Mungu wake lakini nae akakataa, nae akakatwa kwa Msumeno
katika pande mbili pia.
Na kisha Mtoto akatakiwa kumkana Allah Subhanah wa Ta’ala lakini nae akakataa,
hivyo Mfalme akaamua kumpa nafasi ya mwisho, akawakabidhi Askari wake
Mtoto huyo na kuwaambia kua wakamtupe kwenye Pembe ya Jabali kubwa la
Ardhi hio kama ataendela kukataa kukubali mfalme kua ndie Mungu wake. Hivyo
walipopanda Kwenye Jabali hilo basi Mtoto akaomba Dua kwa kusema: ‘Ya Allah
hakika wewe ni mwenye kunitosheleza mimi Juu ya hali yangu dhidi yao vyovyote
vile itakavyokua’
Hivyo Jabali likatetemeka na kuwangusha Askari hao nao wakafariki wote, hivyo
Mtoto huy akashua chini na kurudi kwa Mfalme, na Mfalme alipouliza imekuaje
wako wapi Askari wake basi Mtoto akasema kua: ‘Hakika Allah amenitosheleza
Dhidi yao.’. Mfalme akaamrisha kua Mtoto huyo akamatwe halafu apelekwe
Baharini na kama atamkataa Mfalme kua ni Mungu basi, atoswe Baharini. Na
walipofikia kwenye Maji mengi ya Bahari basi Mtoto huyo akasema: ‘Ya Allah
hakika wewe ni mwenye kunitosheleza mimi Juu ya hali yangu dhidi yao
itakavyokua’ na hapo hapo Jahazi ikazama na watu wote isipokua Mtoto huyo.
Ambae nae akarudi kwa Mfalme.
Mfalme akamuuliza kuhusiana na Askari wake, Mtoto huyo nae akasema: ‘Hakika
Allah amenitosheleza mimi Dhidi yao, na hutoweza kuniua mimi hadi pale
683
utakapofanya kama nitakavyosema’ Mfalme akauliza: ‘Nifanye Kitu gani?’ Mtoto
akasema: ‘Wakusanye watu wote kwenye eneo la Uwazi, na kisha utanifunga
kwenye Msalaba, na kuchukua Mshale kutoka kwenye upinde wangu. Na kisha
utanitunga shabaha huku ukisema: ‘Kwa Jina Allah ambae ndie Mungu wa Mtoto
huyo’ hivyo ukisema hivyo kisha uanipiga Upinde huo basi utafanikiwa kua ni
mwenye kuniua’
Hivyo Mfalme akafanya kama alivyoelekezwa na Mtoto huyo na kisha akachukua
Upinde, huo na kusema: ‘Kwa Jina la Allah ambae ndie Mungu wa Mtoto huyu.’
Na kisha akauachia Mshale huo ambao ulipiga Mtoto huyo kwenye Ndewe ya Sikio.
Mtoto huyo akauchuua mkono wake na kuigusa ndewe ya Siko lake na hapo hapo
akafariki Dunia.’
Na hapo hapo watu wakasema kwa sauti kubwa: ‘Hakika sisi tunamkubali Mungu
wa Mtoto huyu.’ Hivyo Mfalme akaambiwa: ‘Hivyi jee hivi sio yale ambayo wewe
ulikua ukiogopa kua yasitokee? Hivyo bila ya shaka umetumbukia kwenye Mtego
na watu wako wameingia kwenye Imani ya Allah.’
Hivyo Mfalme huyo akaamrisha kua lichimbwe Shimo katika kila Mtaa wa Mji huo
na kisha Uwashwe Moto ndani yake, na kisha akasema: ‘Waamrisheni watu
wachague, yeyote yule atakaeikana Dini Mpya basi atakua ameokoka na
watakaobakia basi wataingia kwenye mashimo ya Moto.’ Hivyo Waumini
wakajisalimisha bila ya kusita na kutumbukizwa ndani ya mashimo ya Moto, hadi
akabakia Mama na Mtoto wake mchanga aliekua akimnyonyesha ambae alisita
lakini Mtoto huyo akamwambia Mama yake: ‘Ewe Mama yangu kua na msimamo
thabiti kwani uko kwenye njia ya Haki.’’ Hivyo Mama na mtoto wake wakaingia ndani
yake Moto huo.
Amaa baada ya kuzungumzia hali hio kwa njia ya kuwakumbushia Waislam kuhusiana
na fitna iliyowakuta Waumini wa As-hab ul Ukhdud na kuwaonesha Waislam kua
wanatakiwa wawe na subra na ustahmilivu mkubwa kwani wenzao yaliwakuta machungu
zaidi ya wanayowakuta wao Waislam wa Makkah basi tunaona kua Allah Subhanah wa
Ta’ala anawaambia Waumini hao wapya kua, mbali ya kua watu hao waliwapa Mtihani
Waumini wa kuwachoma moto lakini hata hivyo basi kama wangetubu, baada ya tukio
hilo basi yeye alikua tayari kuwasamehe.
Ambapo anasema Hasan Al Basr kua: ‘Angalia Ukarimu wa Allah Subhanah wa
Ta’ala. Yaani watu hawa wamewachoma Moto watu wake, lakini yeye yuko tayari
kuwasamehe.’
Ambapo kwa upande wa Mujaddid Ad Din Imam Fakhr AD Din Al Razi basi yeye
amesema kua: ‘Kisa hiki cha Waumini hawa waliowachomwa moto hadi wakafariki
684
kinaonesha kua Waumini wanapofikwa na Mitihani basi wanatakiwa wawe na
misimamo mikali kua bora wake kuliko kuishi na kua Makafiri, lakini hata hivyo
maamuzi yako wazi, kwani inaruhusika pia kukubalia kukufuru kwa maneno kama
walivyokua alifanya Sahaba, pale alipoulizwa na Mussalima Al Kadhab kama
anamuamini yeye, ambapo nae akasema naam. Na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam alipojua kuhusiana na jambo hilo basi akasema: ‘Ama kwa yule alieachiwa
kutokana na kuchukua msimamo mwepesi basi hamna dhambi juu yake.’’
Ambapo kwa upande mwengine basi ni kama tulivyoona kwenye kisa cha Amar Ibn
Yasir na sababu ya kushuswa kwa aya tuliyoiangalia ya Surat An Nahl 16:106.
Hivyo watu waliowachoma As-hab Al Ukhdud kosa lao kubwa pia ni kua hawakua ni
wenye kutubu baada ya kufanya madhambi yao hayo ya kuwachoma Waumini, na bila
ya shaka adhabu yake na mkamato wake Allah Subhana hwa Ta’ala ni mkali sana lakini
hapo hapo pia yeye ni mwingi wa Huruma na Usamehevu wake ni Mkubwa sana kama
zinavyoendela kutuambia aya za Surat ul Buruj:
﴿إِن َّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ۞إِن َّهُ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ۞وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ۞ذُو ٱلْعَرْشِ
ٱلْمَجِ يدُ ﴾
Inna batsha rabbika lashadeedun; Innahu huwa yubdi-o wayuAAeedu; Wahuwa
alghafooru alwadoodu; Thoo alAAarshi almajeedi(Surat Al Buruj 85:12-15)
Tafsir: Hakika Mkamato wa Mola wako ni wenye nguvu na mkubwa sana; na kwa
hakika yeye ndie Muanzishaji na ndie Muendelezeshaji. Na ni yeye Mwenye Kusamehe
na mwenye kua na Mapenzi Makubwa sana yenye kudumu kwa Milele; Mmiliki wa
Arshi Tukufu.
Hivyo Surat Al Buruj ni Sura ambayo ni yenye kuwatia ari na Imani Waumini kwa ujumla
kuhusiana na umuhimu wa kua na ithibati katika Imani ndani ya Nyoyo zao, ambapo kwa
wakati huo iliposhuka basi iliwatia hamasa kubwa sana Waislam wa Dar Al Arqam, kiasi
ya kua siku moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua amekaa na Waislam
huku Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akiwa mbele yake, huku wakiwa wamejawa
na hamu kubwa sana ya Kutangazia kuhusiana na Imani yao hiyo hadharani, hivyo
wakamuomba ruhusa Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam kufanya hivyo.
Miongoni mwa Walioteswa pia alikuwemo mwanamke aitwae Al Nahdiya Radhi Allahu
Anha ambae alidhibiw ana Mkafiri hadi akapoteza macho yake kutokana na Imani yake,
na pia kuna mwanamke mwengine aitwae Zimmira Radhi Allahu Anha amabae yeye
685
alikau ni Mtumwa pia. Kwa upande wa Wanaume kuna kina Bilal, Musab Ibn Umayr,
Talha Ibn Ubayd Allah Radhi Allah Anhum,n.k
Lakini hata hivyo Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam akawa na tahadhari bado na
hivyo akawaambia Masahaba zake kua: ‘Hakika sisi bado tuko kidogo, hatujafikia
wingi wa kubeba jukumu hili bado’ lakini hata hivyo Waislam wakatilia mkazo kua
wako tayari vyovyote itakavyokua, hivyo Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam
akatoka nao na wakaelekea kwenye Al Kaabah na walipofika wakakutana na Makafiri.
Na walipofika mbele yao basi Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akanadia Allahu
Akbar! Na kuanza kuwalaani Lata na Uza, ambapo tukio hili likaanzisha matatizo
makubwa sana kwai zilitokea fujo na watu wakavamiana baina ya Waislamu na Makafiri
ambapo Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu alipigwa na hakuweza kuachiwa hadi
pale watu wa Kabila lake walipoamua kuingilia kati na baada ya kumalzika mashambulzi
hya basi Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu alikua ameanguka chini na kuzimia
akabebwa na kukepelekwa nyumbani kwake huku akiwa katika hali hio ya kuzimia
hakuzindukana hadi jioni yake siku hio.
Ambapo baada ya kuzindukana tu basi akauliza: ‘Vipi kuhusiana na Rasul Allah
Salallahu A’alayhi wa Salam? Mzima hawakumdhuru?’ Abu Bakr As Siddiq Radhi
Allahu Anhu akaletewa chakula na kuambiwa kua hajala siku nzima hivyo bora ale
kwanza, lakini hata hivyo akili yake ilikua si katika hali ya nafsi yake bali katika hali ya
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kuuliza tena: ‘Vipi kuhusiana na Rasul
Allah Salallahu A’alayhi wa Salam? Yuko wapi?’
Kisha Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akamwambia Mama yake ambae alikua
hajasilimu bado na alikau akiitwa Salma Ummu al Khayr kwa kusema: ‘Nakuomba ewe
mama yangu nenda kamuulize Umm Jamil Bint Hattab na kisha nilete habari za
Muhammad kwangu mie’ Ummu Jamil Bint Hattab alikua ni miongni mwa
Waislam waliosilimu mwanzoni kisiri siri.
Hivyo Umm Khayr akatoka hadi kwa Umm Jamil Bint Hattab na kumwambia: ‘Abu
Bakr anakuulizia kuhusiana na hali ya Muhamamd Ibn Abdulla’ hivyo Umm Jamil
Bint Hattab kwa kua laikua anaogopa kua isije kua huo ni mtego basi akasema: ‘Sijui
kitu kuhusiana ane ila, wacha twende kwa Mtoto wako nikamuone anataka nini’
Kwa Umm Khayr na Umm Jamil wakatoka hadi Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu
na hapo hapo Umm Jamil Bint Hattab alipomuona Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu
Anhu na hali ya uso wake ulivyokua umechubuka sana basi akashindwa kujizuia na
akasema: ‘Namuomba Allah akulipize kisasi dhidi ya watu waliokufanyia hivi’ na
kisha akamwambia Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu kua Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam yuko salama.
686
Lakini hata hivyo maneno haya hayakumridhisha Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu
hivyo akamuomba Umm Jamil Bint Hattab na Mama yake wamcsaidie kumpeleka katika
Dar Al Arqam ili akaonane na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam uso kwa uso ili
ahakikishe kwa macho yake, hivyo Umm Khayr na Umm Jamil wakatoka huku wakiwa
wamegemewa nae na walipofika mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi
maerafiki hawa wawili wakakumbatiana kama vile watu waliokua wamepoteana kwa
mda mrefu na kisha Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu ndio akaridhika na kusema:
‘Mama yangu na Baba yangu watolewe Kafara kwa ajili yako Ya Rasul Allah, kwani
mimi nilihuzunika sana pale Utba Ibn Rabia aliponiburura na kuusugua uso wangu
kwenye ardhi na kuufanya kua usijulikane kua ni wangu, lakini vyenginevo mimi
niko mzima’ na kisha Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akamtambulisha Mama
yake kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kusema: ‘Ya Rasul Allah huyu ni
Salma ni mama yangu, na nakuomba umuombee kwa ajili yake ili Allah Amuokoe
na Adhabu ya Moto.’ Na hivyo Salma Umm Khayr akaingia katika Dini ya Kiislam.
Ama kwa upande mwengine basi baada ya kuonesha Uadui wao dhidi ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam basi viongozi wa Quraysh wakiwemo Abu Sufyan, Abu Jahl
na Al Akhnas Ibn-Shurayq, walikua kila siku kinapoingia usiku wa kiza basi mmoja
mmoja wakienda kwa Nyumbani kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
kumsikiliza alivyokua akisoma Qur’an, hicyo Allah Subhanah wa Ta’ala akawajaalia kua
ni wenye kukutana walipokua wakitoka kusikiliza Qur’an, na kisha kukubaliana na
hawatoenda tena kusikiliza Qur’an lakini badala yake wakawa ni wenye kukutana tena
katika eneo hilo ilo kila siku katika usiku wake, hadi ilipotokea tukio hilo mara tatu
mfululizo basi wakakubaliana kua hawatoenda kumsikiliza Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam wakati akisoma Qur’an.
Na hii ni kwa sababu ya mpangilio wake Qur’an kwani ingawa ilishushwa aya moja moja
baada ya nyengine kwa kipindi cha miaka 23, lakini aya hizi zilizokua katika mpangilio
wa Tawqifi (Mpangilio alioupanga Allah Subhanah wa Ta’ala), hivyo Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam alikua akiambiwa aya fulani inakaa katika sehemu fulani
baina ya aya fulani na aya fulani hadi kukamilika kwa Sura 114, ambapo kati yake Sura
86 zimeshuka Makkah na zinajulikana kama Makki Surat na 28 zimeshuka Madinah
ambazo zinajulikana kama Madani Surat.
Na baada ya miaka 23, katika jioni ya siku ya Arafah mwezi 9 Dhul Hija ya mwaka wa
9 Al Hijr, siku ya Ijumaa ilishuka aya ya mwisho ya Qur’an isemayo:
687
﴿وَٱخْشَوْنِ ٱلْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتمَْمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتىِ وَرَضِيتُ لَكُمُ
﴾ ٱلأِسْلاَمَ دِيناً
Alyawma akmaltu lakum deenakum waatmamtu AAalaykum niAAmatee
waradeetu lakumu al-islama deenan (Surat Al Imran 3:5)
Tafsir: Leo hii nimeikamilisha kwa ajili yenu Dini yenu, Nimekamilisha Neema yangu
juu yenu, na nimekuchagulieni Uislam kua ndio Dini yenu.
Katika kuweka wazi umuhimu wa ujumbe aliokua akipewa Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam, ambao aliamrishwa kuwatangazia watu wengine ujumbe huo, basi
tunaona kua Allah Subhanahu wa Ta’ala anamsifu Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam kwa kumfananisha na Nuru na Muangaza pale alipowaambia Ahlu al Kitab
kwa kusema katika Qur’an:
﴿َ أَهْلَ ٱلْكِتَابِ قَدْ جَآءَكُمْ رَسُولُنَا يُبَينِّ ُ لَكُمْ كَثِيراً ممِّ َّا كُنْتُمْ تخُْفُونَ مِنَ
ٱلْكِتَابِ وَيَعْفُواْ عَن كَثِيرٍ قَ دْ جَآءَكُمْ مِّنَ ٱهلل َِّ نُورٌ وَكِتَابٌ م ُّبِينٌ ۞ يَهْدِى بِهِ ٱهلل َُّ
مَنِ ٱت َّبَعَ رِضْوَانَهُ سُبُلَ ٱلس َّلاَمِ وَيخُْرِجُهُمْ مِّنَ ٱلظ ُّلُمَاتِ إِلىَ ٱلن ُّورِ إبِِذْنِهِ وَيَهْدِيهِ ْم
إِلىَٰ صِرَاطٍ م ُّسْتَقِيمٍ ﴾
Ya ahla alkitabi qad jaakum rasooluna yubayyinu lakum katheeran mimma
kuntum tukhfoona mina alkitabi wayaAAfoo AAan katheerin qad jaakum mina
Allahi noorun wakitabun mubeenun; Yahdee bihi Allahu mani ittabaAAa
ridhwanahu subula alssalami wayukhrijuhum mina aldhdhulumati ila alnnoori biidhnihi
wayahdeehim ila siratin mustaqeemin (Surat Al Maidah 5:15-16)
Tafsir: Enyi Ahl Al Kitab! Sasa hivi amekujieni Mtume wetu kukuwekeeni wazi yale
mengi ambayo mlikua mkiyaficha katika vitabu na mengi yaliyopita. Hakika
imekujieni kutoka kwa Allah Nuru na Kitabu kilichowazi. Ambacho ndani yake Allah
anawaongoza wote wale wanaotafuta ridhaa yake kuelekea katika njia ya salama, na
akawatoa kutoka katika kiza cha Dhulma kwa ruhusa yake na kuwaingiza katika
Muangaza na kuwaongoza katika njia iliyonyoooka.
688
Na vile vile Allah Subhanahu wa Ta’ala anamwambia na kumsifu Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam kwa kumfananisha na Taa na Muangaza pale alipomwambia
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na pia wale Walioamini kwa kusema
katika Qur’an:
﴿َٰي ُّهَا ٱلن َّبىِ ُّ إِ َّ أَرْسَلْنَاكَ شَاهِداً وَمُبَشِّ راً وَنَذِيراً ۞ وَدَاعِياً إِ لىَ ٱهلل َِّ إبِِذْنِهِ وَسِ رَاجاً
﴾ م ُّنِيراً
Ya ayyuha alnnabiyyu inna arsalnaka shahidan wamubashshiran wanadheeran;
WadaAAiyan ila Allahi bi-idhnihi wasirajan muneeran. (Surat Al Ahzab :33:45-46)
Tafsir: Ewe Nabii (Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam)! Hakika sisi
tumekutuma wewe kama shahidi, na vile vile mbebaji wa habari njema, na mwenye
kuonya. Na kua ni yule anaewaita watu kumuelekea Allah kwa idhini yake, na Taa
inayoeneza Nuru.
Ingawa Allah Subhanahu wa Ta’ala amempa sifa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam kua ni Nuru, Taa na Muangaza kwa Ummah kutoka kwake lakini pia ameweka
wazi kua Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ni mtu vile vile kama walivyo
watu wengine pale aliposema katika Qur’an.
﴿قُلْ إِنم ََّآ أََْ بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ ٰ يُوحَى إِلىَ َّ أَنم ََّآ إِلَٰهُكُمْ إِلَٰهٌ وَاحِ دٌ ۤ فَٱسْتَقِيمُواْ إِلَيِْه
وَٱسْتَغْفِرُوهُ وَوَيْلٌ لِّلْمُشْ رِكِينَ ﴾
Qul innama ana basharun mithlukum yooha ilayya annama ilahukum ilahun
wahidun faistaqeemoo ilayhi waistaghfiroohu wawaylun lilmushrikeena (Surat
Fusilat 41:6)
Tafsir: Sema (Ewe Muhammad): ‘Mimi ni Mtu kama nyinyi, Nimeteremshiwa Wahy
kua Mungu wenu ni Mungu mmoja, hivyo fuateni njia iliyonyooka kuelekea kwake na
mumtii na kumuomba masamaha. Na Ole wao kwa wale wenye kumshirikisha’ .
Ama kuhusiana na na muonekano wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam basi
anasema Rabi'ah Ibn Abi 'Abd al-Rahmaan: ‘Nimemsikia Anas Ibn Malik akimuelezea
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kwa kusema: ‘Alikua si mrefu wala
689
si mfupi, ngozi yake ilikua nyeupe inayokaribiana na wekundu kwa mbali, kwani
ilikua si nyeupe sana wala si ya kiza, na nywele zake hazikukunjana sana wala
hazikunyooka sana, aliposhushiwa Wahy alikua na umri wa miaka 40, alikaa
Makkah kwa miaka 10 baada ya kuanza kushushwa Wahy, na kisha akakaa
Madinah kwa miaka 10. Alipofariki ilikua hamna zaidi ya mvi 20 kwenye nywele
zake na ndevu zake.’ (Bukhari).
Imam Ahmad Ibn Hanbal anasema kua amesema `Ata' Ibn Yasar kua alikutana na `Abd
Allah Ibn`Amr Ibn Al`As, ambae alimwambia: ‘Hebu nielezee kuhusiana na Rasul
Allah katika Taurat’, nae akasema: ‘Naam, Wa Allahi, ameelezewa katika Taurat
akiwa na sifa ambazo alizoelezewa katika Qur’an, yaani : ‘Ewe Mtume, Hakika
sisi tumekutuma wewe kama shahidi, na mwenye habari njema, na muokozi wa
wasiokua na I’lm. Wewe ni Mjumbe wangu na Mtume wangu na nimekuita Al
Mutawakkil (mwenye kutegemewa). Wewe si mkali sana wala si mwenye kupiga
kelele masokoni. Huwalipi wabaya kwa wakufanyiao ubaya, na badala yake ni
msamehevu. Allah hatoichukua roho yako hadi utakapo warekebisha wale
waliopotea waweze kusema La ilaha illa Allah, maneno ambayo hufunua macho ya
vipofu, masikio ya viziwi na nyoyo zilizozibwa’’
KUSILIMU KWA UMAR IBN AL KHATTAB RADHI ALLAHU ANHU
Mnamo Mwaka wa 5 wa Uislam ndani ya Mwezi wa Ramadhani Allah Subhanah wa
Ta’ala alimshushia Mtume wake Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam Surat An Najm
ambayo ni Sura ya mwanzo ya Quran kushushwa ndani yake katika aya ya Mwisho kuna
Sijda.
Ambapo anasema Imam Ahmad Ibn Hanbal kua: ‘Amesema Muttalib Ibn Abi Wadaa
kua Wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipoisoma Surat An Najm mbele
ya Hadhara basi alipofika mwisho wake Akasjudu na mhadhara wote ukasjudu.
Lakini mimi sikusjudu, hivyo sasa kila nikiisoma Sura hii hua nahakikisha kua
siwachi kitendo hicho cha Kusjudu.’
Kwani anasema Imam Muhammad Ibn Saad kua: ‘Kabla ya Kushuka Sura hii basi
kuna Kikundi cha Waislam kilihamia Uhabeshi. Hivyo Ramadhani ya Mwaka wa 5
ilipowadia na kutokea tukio hili la Kusjudu hadhara nzima ya watu wa Quraysh
pamoja na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Basi Waislam wa Uhabeshi
wakasikia juu tukio hili, na hivyo wakaona kua Mji mzima wa Makkah
Umeshasilimu, kutokana na kusjudu kwao huko, na hivyo baadhi ya Waislam
wakaamua kurudi katika Mji wa Makkah, lakini walipofika walikuta kua hali ya
Kunyanyaswa Waislam bado iko pale pale. Hivyo baada ya kurudi kwao na kukuta
690
kua Mji wa Makkah haukaliki basi wakarudi tena Uhabeshi na safari hii
wakuondoka kuelekea Uhabeshi na watu wengi zaid’
Ambapo Neno Najm hua linatokana na neno Najama ambalo hua linamaanisha
Kuchomoza, Kutokea, Kuanza, Muendeleo wa kuendela kwa Kitu. Ambapo neno Najm
hua linamaanisha Majani yanayotambaa na pia humaanisha Nyota. Hivyo anasema Allah
Subhanah wa Ta'ala katika Surat An Najm:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞وَٱلن َّجْ مِ إِذَا هَ وَىٰ ۞مَا ضَل َّ صَاحِ بُكُمْ وَمَ ا غَوَىٰ ۞وَمَا
يَنطِقُ عَنِ ٱلهَْوَىٰ ۞إِنْ هُوَ إِلا َّ وَحْ يٌ يُوحَ ى ٰ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Waalnnajmi idha hawa;
Ma dhalla sahibukum wama ghawa; Wama yantiqu AAani alhawa; In huwa illa
wahyun yooha(Surat An Najm 53:1-4)
Tafsir: Kwa Jina La Allah Mwingi wa Rehma na Mwingi wa Huruma; Naapa Kwa
Najm pale inapozama; Hajapotoka Rafiki yenu (Muhammad Salallahu Alayhi wa
Salam) Wala Hajakosea; Na Wala Hasemi Kutokana na Matamanio (Ya Nafsi) yake;
Hakika hayo (maneno ayasemayo) si chochote Isipokua ni Wahyi anaoshushiwa.
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakkalimin Imam Al Mushaqqiqin
Imam Al Ghazali Al Thani Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Umar Ibn Husayn Al
Razi Al Shafii kuhusiana na Kiapo hiki cha Aya hii kua: ‘Allah Suhana wa Ta’ala
anaapa kwa Nyota kwa sababu baadhi ya Mapagani walikua wanaabudu Nyota
zenye Kung’ara sana Angani. Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala anabainisha Kasoro
ya Nyota hizo kua ni zenye kutoweka baada mda, na hivyo haziwezi kua ni Miungu,
bali ni kitu kilichoumbwa.’
Ambapo Wanazuoni wametofautiana kuhusiana na Nyota hii iliyoapiwa hapa, kwani
kuna wasemao kua ni Surrayah (Sirius) ambayo ni Nyota inayoonekana Alfajiri na kisha
huzama kabla ya Kuchomoza Jua. Ambapo huu ni mtizamo wa Bahr Ul Ilm Abd Allah
Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu na pia Imam Sufyan Ath Thawry. Na pia kuna waosema
kua Ni Nyota ya Zuhra (Venus) ambao ni Mtizamo wa Imam Abd Rahman Al Suddi.
Kwani kwa upande mwengine basi unapotafakkar maana ya Aya hii kwa juu bila kuingia
ndani basi tunaona pia inatuonesha Umuhimu wa Kutafakkar pale unapoangalia Miujiza
ya Allah Subhanah wa T'aala katika kuumba kwake.
691
Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala anawaambia Watu wa Makkah kwa Huyu Mtu
anaezungumziwa Ndani ya Aya hii yaani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, ni mtu
ambae ni Sahibu yao, yaani Rafiki yao anaeishi nao pamoja katika Mji na Mtaa Mmoja,
hivyo anajulikama ndani nje kua si Mtu wa kubabaisha, bali ni Mtu anaeaminika, na
hivyo hayuko Dhala wala Ghawa.
Ambapo neno Dhala hua Linamaanisha Mtu aliepotoka kutokana na kutoona Njia Sahihi,
na neno Ghawa hua linamaanisha Mtu aliepotoka Mbali ya kua ameiona Njia Sahih yaani
Aliifuata kisha akaachana nayo.
Hivyo hapa Allah Subhanah wa Ta'ala anabainisha kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam yuko katika Nji Iliyonyooka Sawia ya Kumuelekea Mola wake ambayo inastahiki
kufuatwa na kila Mmoja wetu.
Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala anawabainishia wazi Makafiri wa Makkah kua Rafiki
yao huyo yaani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hazungumzi yale anayoyasema
kutokana na Matamanio yake Labda kwa kua anataka Madaraka, au Mali au Cheo n.k.
Na kwa kua ni Alieshusha Qur'an ni Allah Subhanah wa Ta'ala na ni mwenye kujua juu
ya kila kitu basi Allah Subhanah wa Ta'ala anajua kua kama hajafafanua baada ya aya
hio basi watu watakua na masuali mengi, yaani kama Rasul Allah Salalahu Alayhi wa
Salam hazungumzi kwa Matamanio yake, basi maneno yake ayasemayo yanatokana na
nini?
Naam yaani Mbali ya Aya za Qur'an lakini kila kitu akisemacho Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam hua si kitu chochote kile isipokua ni Wahyi alioshushiwa na Allah
Subhanah wa Ta'ala kupitia kwa Malaika Jibril na kupitia kwa njia ya kushushiwa Moja
kwa moja kwenye Ufaham wake.
Ambapo kutokana na uthibitisho wa maneno hayo basi tunaona kua hata anayoyaomba
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa Mola wake hua yanakua ambapo amesema
Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu alayhi wa Salam
alisema kua: ‘Ya Allah Uongeze Nguvu Uislam kwa kupitia mmoja kati ya watu
wawili unaowapenda zaidi, Abu Jahl au Umar Ibn Al Khattab’ Abd Allah Ibn Umar
Radhi Allahu Anhu anaendelea kusema kua: ‘Aliekua akipendwa zaidi ni Umar’(Imam
At Tirmidhii)’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliomba dua hii kwa sababu watu wawili hawa
walikua ndio wanaadhibu sana Waislamna wenye chuki kubwa sana dhidi ya Uislam,
kiasi ya kua Umar Ibn Al Khattab siku moja ya mwaka mmoja baada ya kushushwa Surat
An Najm basi Umar Ibn Al Khattab alikua tayari ameshachoka na namna Uislam
unavyovunja umoja wa watu wa Makkah na kusababisha uasi kwa Viungozi wa Mji wa
692
Makkah, hivyo akaamua kua amalize tatizo hili, kwa kuukata mzizi wa fitina yote hii
inayoendelea, ambao ni Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam.
Umar Ibn Al Khattab alikua ni kijana mwenye misimamo na wenye kujiamini kwa kila
kitu miongoni mwa Vijana wa Quraysh kama vila alivyokua kijana mwenzake alifanana
nae kwa kila kitu kuanzia sura hadi maumbile ya miili yao ambae ni Khalid Ibn Walid
lakini Umar Ibn Al Khattab alikua ni mwenye kumzidi Khalid Ibn Walid kwa urefu wa
Inchi moja. Ambapo vijana hawa mbali ya kua ni waliofanana sura lakini pia ni ndugu
na wenye kufanana kwa nguvu na Ubabe wao ambao unaonekana wazi pale mwaka
mmoja walipokutana katika fainali ya kumtafuta Bingwa wa kupigana katika Mji wa
Makkah.
Ambapo katika fainali ya mwaka mmoja ya vijana wasiozidi umri wa miaka 20 waliingia
na kukutana vijana wawili ambao mmoja kati yao alikua ni Khalid Ibn Walid na
mwengine alikua ni Umar Ibn Al Khattab, ambapo Umar Ibn Al Khattab alikua na uwezo
wa kutumia mikono yote miwili wa kulia na kushoto kwa nguvu zilizo sawa, tofauti na
Khalid Ibn Walid ambae alikua hana sifa hiyo
Kutokana na kufahamu uwezo zaid aliokua nao Umar Ibn Al Khattab, basi Khalid Ibn
Walid ilimbidi atumie mbinu na ujuzi wa kiakili zaid ili kumshinda mpinzani wake huyo.
Na hapo haikuchukua muda kwani Khalid Ibn Walid alimkamata mpinzani wake na kisha
ghafla akamuangusha chini. Kwa mbali ikasikika sauti ya kuvunjika kwa mfupa. Khalid
Ibn Walid alimuangalia kwa huruma Umar Ibn Al Khattab ambae alikua amelala chini
huku akilia kwa maumivu. Matokeo ya mapigano haya yalibadilisha mtizamo mzima wa
historia ya maisha ya Masahaba wawili hawa wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam na hivyo kuzidisha upinzani baina yao, Masahaba hawa walikua na udugu wa
karibu sana. Kwani mama yake Sayyidna Umar Ibn Al Khattab ambae alikua anaitwa
Hantam Bint Hisham Al Mughira alikua ni binamu yake mkubwa Khalid Ibn Walid Al
Mughira.
Ambapo Khalid Ibn Walid alikua na marafiki wengi wa karibu na ambao majina yao
ukiyaangalia katika historia ya Kiislam utaona kua yote yalikua yanatajika kwa sifa za
kua na uwezo wa kuongoza katika mapigano ya aina zote, miongoni mwao alikuwemo
Umar Ibn Al Khattab, Ikrimah Ibn Abi Hisham na Amr Ibn Al Aas. Kati ya marafiki
hawa wanne, basi hakuna yule ambae ilikua inamuuma sana kuhusiana na matukio
yanayotokea katika Mji wa Makkah tangu kushuka kwa Uislam kama Umar Ibn Al
Khattab.
Hivyo siku moja Umar Ibn Al Khattab akachukua Upanga wake na kutoka nyumbani
kwake huku akiwa ni mwenye kuamua kumtafuta Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
popote pale alipo ili amuue na hakua ni mwenye kuelekea katika maeneo ya Dar Ul
693
Arqam kwa sababu alikua hajui kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam yuko sehemu
gani, na maana baada ya kusilimu kwake aliuliza Waislam: ‘Jee Muhamamd
anapatikana wapi?’
Hivyo katika kumtafuta kwake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam njiani akakutana
na Nuaym Ibn Abd Allah Radhi Allah Anhu ambae nae alikua ni miongoni mwa Waislam
waliosilimu kisiri siri na alipomuona Umar Ibn Al Khattab yuko katika hali aliyokua nayo
basi akamuuliza: ‘Ya Umar unaenda wapi ukiwa katika kama hio?’ ambapo Umar
Ibn Al Khattab akasema: ‘Naenda kumtafuta Muhammad, ili nimuue kwani
amewachana na Dini yetu, amevunja umoja wa watu wetu na kuidhalilisha Miungu
yetu, hivyo nataka nimalizane nae ili hili tatizo liishe’
Nuaym Ibn Abd Allah Radhi Allah Anhu akasema: ‘Ama kweli Hasira zako
zimekupofua Macho kwani umekua huoni. Hivyo kwanini usiishughulikie familia
yako kwanza kabla ya kutaka kumalizana na Muhammad?’
Suali hili lilimshtua Umar Ibn Al Khattab, na kujiuliza kwani kuna nini kwenye familia
yangu? Hivyo hapo ahpo akamuuliza Nuaym Ibn Abd Allah Radhi Allah Anhu: ‘Kwani
kuna nini kwenye familia yangu?’ ambapo Nuaym Ibn Abd Allah Radhi Allah Anhu
akasema: ‘Mume wa Dada yako na Ibn Ami yako Said Ibn Zayd na Dada yako
Fatma, kwani wameingia kwenye Dini ya Muhammad na wamekubaliana nayo
hivyo kawashughulikie wao kwanza.’
Ambapo baada ya kupata habari hio basi safari ya kumtafuta Rasul Allah
Salallahu Aalyhi wa Salam ilikufa hapo hapo, na badala yae umar Ibn Al Khattab
akageuza muelekeo na kuelekea katika nyumba ya dada yake huku akiwa amejawa
na hasira zaidi, na haukuchukua mda Umar Ibn Al Khattab akawasili kwa dada
yake na kusikia katika wakati huo sauti ya Khabbab Radhi Allah Anhu
akiwasomea Said Ibn Zayd na Fatma Bint Al Khattab Radhi Allahu Anhum aya za
mwanzoni za Surat Ta-Ha.
Hivyo Umar akanyatia na kusikiliza lakini hasikii vizuri, hivyo akaharikisha
kutaka kuingia ndani ya Nyumba hio kugonga mlango hukua akitaka afunguliwa
na waliokuwemo ndani ya Nyumba ya Fatma Binti Al Khattab Radhi Allahu Anhu
waliposikia sauti ya Umar Ibn Al Kahattab basi wakataharuki na Khabbab Radhi
Allahu Anhu akakimbilia haraka sana kujificha kwenye chumba cha pembeni,
huku akimuwacha Fatma akiwa ameshikilia maandiko ya Surat Ta-Ha na
kuyaficha chini ya Mapaja yake.
Hivyo Said Ibn Zayd Radhi Allahu Anhu akaenda Mlangoni, na alipoufungua
Umar Ibn Al Khattab akauingia moja kwa moja hadi ndani na kuanza kuuliza kwa
694
ukali na hasira: ‘Kuna ujinga gani ambao nimekua nikiusikia humu ndani
mkinong’onezana?’
Ambapo Fatma na Said Ibn Zayd Radhi Allahu Anhum wakasema: ‘Hatuja
nong’onezana kitu, kwani wewe umesikia nini?’
Umar Ibn Al Khattab akasema: ‘Naam, nimegundua kua nyinyi nyote mmeingia
kwenye Kundi la Muhamamd.’ Na kisha baada ya Maneno hayo akamvamia Said
Ibn Zady Radhi Allahu Anhu na kuanza kupgana nae, katika purukushani hizo
Fatma Bint Al Khattab Radhi Allahu Anha ambae mwanzo alikua amekaa kitako
akanyanyuka na kukimbilia kuingilia kati kwa ajili ya kumtetea na kumuokoa
Mumewe, lakini alipokaribia purukushani hizo basi Umar Ibn Al Khattab
akampiga kibao kimoja na hapo hapo Fatma Bint Al Khattab Radhi Allahu Anha
akaanguka chini huku akitokwa na damu baada ya kujeruhiwa na kibao hicho.
Hapo hapo Said Ibn Zaid Radhi Allahu Anhu akamuangalia Fatma Bint Al Khattab
Radhi Allahu Anha aliyekuwepo chini akitokwa na Damu kisha wote wawili kwa
pamoja wakasema: ‘Naam tumejiunga na Dini ya Muhammad, na
tunamuamini Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume wake, hivyo wewe fanya
utakalofanya’
Umar Ibn Al Khattab hakuamini masikio yake kutokana na kusikia umoja wa kauli
hio, na kushangazwa na ujasiri wa Dada yake, hivyo akajiuliza kwani huu ujumbe
wa Muhamamd una maajabu gani hasa mpaka Fatma Bint Al Khattab Radhi
Allahu Anha anakua na msimamo kiasi hicho kutokana nao, hivyo akamuacha
Said Ibn Zayd Radhi Allahu Anhu na kumuangalia Dada yake ambae aliekua
anasimama huku akiwa anajipangusa Damu ambayo kuonekana kwake na macho
ya Umar Ibn Al Khattab kulimfanya Umar aingiwe na huruma na kujisikia aibu
kutokana na kumjeruhi Dada yake ambae nae alikua ni mwenye kua na ari na
msimamo juu ya Imani yake hio mpya, hivyo Umar Ibn Al Khattab akasema kwa
sauti tofauti na aliyoingia nayo hapo mwanzo, kwani hii ilikua ni sauti ya huruma
na upole: ‘Tafadhalini nionesheni nami njiue huu ujumbe wa Muhammad
unasemaje’
Fatma Bint Al Khattab Radhi Allahu Anha akasema : ‘La, kwani mimi nna khofu
juu ya kile utakachokifanya ukiuona’ Umar Ibn Al Khattab akasema: ‘Usiwe
na Khofu kwani sitouchana’hivyo Fatma Bint Al Khattab Radhi Allahu Anha
akasema: ‘Ewe Kaka yangu hakika wewe huko tohara kutoka na ushirikina
wako, kwani ni wale walio tohara tu ndio wanaoruhusika kugusa maandiko
ya ujumbe huu’
695
Hivyo Umar Ibn Al Khattab akatoka na akaenda kukoga na kisha alipokua msafi
akarudi kisha Fatma Bint Al Khattab Radhi Allahu Anha akampa maandiko hayo,
na mara baada ya kupewa basi akasoma maneno hayo ambayo yanasema:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞طه۞مَآ أَنَزَلْنَا عَلَيْكَ ٱلْقُرْآنَ لِتَشْقَى ٰ ۞ إِ لا َّ تَذْكِرَةً لِّمَن
يخَْشَى ٰ ۞ تَنزِيلاً ممِّ َّنْ خَلَق ٱلأَرْضَ وَٱلس َّمَاوَاتِ ٱلْعُلَى۞ ٱلر َّحمَْٰنُ عَ لَى ٱلْعَرْشِ
ٱسْتَوَى ٰ ۞ لَهُ مَا فىِ ٱلس َّمَاوَاتِ وَمَا فىِ ٱلأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَمَا تحَْتَ ٱلث َّرَىٰ ۞
وَإِن تجَْهَرْ بِٱلْقَوْلِ فَإِن َّهُ يَعْلَمُ ٱلسِّ ر َّ وَأَخْفَى۞ ٱهلل َُّ لا ۤ إِلَٰهَ إِلا َّ هُوَ لَهُ ٱلأَسمَْآءُ
ٱلحُْسْنىَٰ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Ta-Ha; Ma anzalna AAalayka alqur-ana
litashqa; Illa tadhkiratan liman yakhsha; Tanzeelan mimman khalaqa al-ardha
waalssamawati alAAula; Alrrahmanu AAala alAAarshi istawa; Lahu ma fee
alssamawati wama fee al-Ardhi wama baynahuma wama tahta alththara; Wa-in
tajhar bialqawli fa-innahu yaAAlamu alssirra waakhfa; Allahu la ilaha illa huwa
lahu al-asmao alhusna.(Surat Ta-Ha 20:1-8)
Tafsir: Kwa Jina La Allah Mwingi wa Rehma na Mwingi wa Huruma; Ta-Ha, Kwa
Hakika hatukuiteremsha hii Qur’an kwa ajili ya kukuingiza katika Khofu, Ila huu ni
ukumbusho kwa wenye kua na khofu. Imeteremshwa kutoka kwa Muumba wa Ardhi
na Mbingu alietukuka. Mwingi wa Rehma kwenye ya Arshi amesimama. Ni vyake
vilivyomo Mbinguni na Ardhini na baina yake na vilivyomo chini ya udongo wake. Na
hata kama wewe (Muhammad) utanyanyua sauti yako basi kwa hakika yeye, anajua
yaliyo ya siri na yale ambayo yamefichikana zaid. Hakuna Mungu isipokua yeye. Na
kwake yeye ndio kwenye umiliki wa Majina Bora.
Na baada ya kusoma aya hizi basi Umar Ibn Al Khattab akasema: ‘Sijawahi
kuona maneno ya heshima na Utukufu kama haya.’ Ambapo baada ya kusikia
maneno hayo ya Umar basi Khabbab akatoka kutoka kwenye sehemu aliyojifichia
na kusema: ‘Ya Umar! Nna matumaini kua Allah atakuneemesha wewe
kutokana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa sababu mimi
nilimsikia jana usiku Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akisema kua:
‘Ya Allah uimarishe Uislamkwa Abu Al Hakam au kwa Umar Ibn Al Khattab,
hivyo Umar Muogope Mola wako’’
696
Umar Ibn Al Khattab akamuomba Khabbab amuelekeze katika sehemu ambayo
anapatikana Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam ambapo nae akamfahamisha
ilipo Dar Al Arqam, hivyo Umar Ibn A Khattab akatoka na upanga wake kwenye
Nyumba ya Fatma bint Al Khattab Radhi Allahu Anha na moja kwa moja kuelekea
kwenye Dar Al Arqam na kugonga mlango wa Nyumba hio.
Ambapo mmoja kati ya Waislam alipoenda kutaka kufungua Mlango basi
alichungulia kwenye ufa wa Mlango huo na akamuona Umar Ibn Al Khattab akiwa
amesimama nje na upanga wake, hivyo akarudi haraka sana hadi kwa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na kumwambia kua anaegonga Mlango ni Umar Ibn
Al Khattab huku akiwa na Upanga wake.
Ambapo Hamza Ibn Abu Talib Radhi Allahu Anhu akaingilia kati na kusema:
‘Mwache aingie ndani, kwani kama amekuja kwa nia safi basi hamna tatizo
lakini kama ikiwa amekuja kwa mbaya basi tutamuua kwa kutumia huo huo
upanga wake Mwenyewe’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akawaambia Masahaba zake kwa kusema kua: ‘Mfungulieni Mlango aingie’
hivyo Mlango ukafunguliwa na Umar Ibn Al Khattab akaingia ndani ya Nyumba
hio.
Wakati Umar Ibn Al Khattab anaingia ndani basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akanyanyuka na kumfuata huku akilifunga joho lake vizuri na kisha
akampokea Umar Ibn Al Khattab kwa kusema: ‘Umekuja kufanya nini ewe Ibn
Al Khattab? Wallahi mimi nnaona kua kama kuna mkosi unataka kukufika
kabla ya kumaliza uliyoyafuata’
Ambapo Umar Ibn Al Khattab nae akasema kwa unyenyekevu: ‘Wa Allahi, Ya
Rasul Allah hakika mimi nimekuja kwa ajili ya Kuthibitisha Imani yangu
kwa Allah na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kile kilichoteremshwa
kutoka kwa Allah.’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akatamka ‘Takbir!!’ hivyo
Waislam wote waliomo ndani ya Dar Al Arqam wakajawa na furaha kwani Uislam
ulikua umepata Nguvu zaidi kutokana na kusilimu kwa Umar Ibn Al Khattab
Radhi Allahu Anhu ambae baadae alitangazia imani yake hio hadharani, na
kusema kua anaetaka kupigana nae kwa sababu ya Imani yake mpya basi na
amfuate.
KIFO CHA ABU TALIB NA KHADIJA BINT KHUWAYLID RADHI
ALLAHU ANHA
697
Amesema Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mara moja Ka’ab
Ibn Ashraf ambae ni Chifu wa Mayahudi wa Mji wa Madinah alikuja katika Mji
wa Makkah na Machifu wa Quraysh wakamwambia: ‘Muangalie Kijana huyu,
ambae ni Abtar (amekatwa kutokana na kendelea kizazi chake), anajifikiria kua
yuko juu zaidi yetu wakati sisi ni wasimamizi wa Ibada ya Hija tunasimamia Al
Kaabah na Kuwapa maji ya kunywa Mahujaji’’(Imam Al Bazaar)
Na akasema tena Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mtoto
Mkubwa wa Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam ni Qasim, kisha anafuatia
Zaynab, kisha Abd Allah, kisha wanafuatia mabinti watatu ambao ni Umm
Kulthoum, Fatma na Ruqqaya, wa mwanzo wao ambae ni Qasim alifariki na kisha
akafariki Abd Allah. Ambapo baada ya tukio hilo basi As Wail akasema: ‘Kizazi
chake kimekatika sasa hivi yuko Abtar’’
Hivyo tangu mwanzoni mwa kipindi cha kuanza kutangazia kuhusiana na Utume wake
na kueneza Ujumbe wa Allah Subhanah wa Ta’ala hadharani kwa watu wake basi Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akikabiliana na upinzani mkubwa sana wa
vitendo na maneno huku wafuasi wake wakiwa ni wenye kunyanyaswa na kudhulumiwa
hadharani, hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamshushia Mtume wake Surat Al Kawthar
ambayo inasema:
ّ ٱلْكَوْثَرَ۞فَصَل لِرَبِّ كََوٱ نحَْرْ ۞إِن َّ شَانِئَكَ
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞إِ َّ أَعْطَيْنَاكَ ِ
هُوَ ٱلأَبْتَرُ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Inna aAAtaynaka alkawthara; Fasalli
lirabbika wainhar; Inna shani-aka huwa al-abtaru (Surat Al Kawthar 108:1-4)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma; Hakika sisi
tumekupa wewe (Muhammad Sallahu Alayhi wa Salam)Al Kawthar; Hivyo mgeukie
Mola wako kwa Kusali na Uchinje (kwa ajili yake pekee); Kwani kwa Hakika
anaekuchukia (Wewe Muhammad Sallahu Alayhi wa Salam) basi yeye atakatiwa
(kutokana na kila kitu cha Kheri cha Duniani na Akhera).
Hii Sura inatiwa Surat Al Kawthar, ambalo ni neno Kathara ambalo hua linamaanisha
Kuzidi idadi ya wingi wa kitu, Kuongezeka, Kua na wingi wa Mali au wa vitu
anavyovitaka na kuvitamani Mtu.
698
Hivyo kwa upande mmoja Allah Subhanah wa Ta’ala anamwambia Mtume wake Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Ingawa watu wako wanasema kua wewe
umekatiwa muendelezo wako na hivyo wanakuona kua huna kitu, lakini Mimi
nnakupa wewe Kila Kitu ambacho unachokitaka na kukitamani wewe hapa
Duniani na Akhera. Unachotakiwa kufanya wewe ni kuniabudu mimi na kufanya
kila kitu kwa ajili yangu, na kisha hao wanaokuchukia basi bila ya shaka ndio
nitakaowakatia kutokana na kupata kila kitu chema hapa Duniani na Akhera.’
Ambapo kwa upande mwengine basi wanasema Abd Allah Ibn Abbas, Abd Allah Ibn
Umar na Aisha Radhi Allahu Anhum kua: ‘Al Kawthar ni Mto wa Peponi ambao katika
mwambao wake umepambwa kwa Madini ya thamani na Maji yake ni Meupe
kuliko Maziwa, Utamu wake ni zaid ya Asali na Harufu yake ni zaid ya harufu ya
Miski’(Imam Tirmidhi)
Ambapo anasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Niliingia Peponi na
nikakutana na Mto ambao Mwambao wake una Mahema ambayo yametengenezwa
kwa Mapambo ya Lulu, nami nikaingiza Mkono wangu ndani ya Maji yake
yanayotiririka na kuona kua yananukia zaidi ya harufu ya Miski nami nikamuuliza
Jibril.: ‘Jibril, Ndio nini huu?’ ambapo nae akasema: ‘Huo ndio Kawthar ambao
Allah Subhanah wa Ta’ala amejaalia kukupa wewe.’’
Na kwa upande mwengine basi kuna wasemao kua : ‘Kawthar hua inamaanisha Mto
ambao Ummah wa Kiislam utaenda Kunywa Maji yake Peponi’ na kuna wasemao
kua: ‘Kawthar humaanisha Mambo mengi mazuri ikiwemo Utume, Shaira, Qur’an,
Ilm, Wanazuoni wa Kiislam na pia Wafuasi wa Dini ya Kiislam na Amali njema
zao’
Mnamo mwaka wa 9 wa Uislam basi Ami yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
yaani Mzee Abu Talib ambae alikua na takriban Umri wa miaka 86 akaanza kuumwa na
hivyo Makafiri walipoiona hali hii basi wakaamua kumkabili Abu Talib ili amsalimishe
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ndani ya Mikono yao, na kumwambia : ‘Ewe
Abu Talib, hakika wewe ni kiongozi wetu, na sisi sasa hivi tumekua na wasiwasi juu
ya kile kinachondelea baina yetu na Mtoto wa Abdullah. Hivyo bora mwite kisha
nawe uwe hakimu baina yetu kwa aidha atengane nasi au sisi tutengane nae bila ya
kutumia nguvu, na bila ya kutuingilia katika Imani yetu’
Hivyo Abu Talib akaagizia kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aitwe mbele yake
na alipofika basi akasema: ‘Ewe Mtoto wa Kaka yangu, hawa ni viongozi wa Quraysh
wamekuja hapa wa ajili ya majadiliano kuhusiana nawe, hivyo watakuambia kile
wanachokitaka na watapokea kile unachokitaka.’
699
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Ami yangu, hakika mimi
nnataka neno moja tu ambalo walipokee na kulikubali, kwa kutokana na neno hilo
moja basi watakua na mamlaka ya Ardhi za Waarabu na za wasiokua Waarabu.’
Abu Talib akashangaa na kusema: ‘Neno Moja tu?’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Naam Neno Moja Tu.’
Ambapo jibu hili lilimuacha kila mtu akiwa ni mwenye kushangaa pia na kujiuliza ni
neno gani hilo lenye uwezo wa kuwapa Viongozi hawa wa Quraysh mamlaka juu ya kila
sehemu ya ardhi, hivyo Abu Jahal akasogea karibu ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam na kusema: ‘Sawa, tuambie ewe Muhammad hilo neno Moja, kisha nasi
tutaongezea maneno 100 zaid yake’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Semeni La Ilaha Illa Allah, na kisha
rembeeni Msanamu yenu yote mnayo yaabudu’
Viongozi hao wa Quraysh wakasema: ‘Muhammad, unatushangaza, hivi wewe
unataka tuwarembee miungu yetu yote kwa ajili ya Mungu wako Mmoja tu?’ kisha
wakakaa na kunong’onezana na kusema: ‘Wa Allahi Huyu Mtu hatotupa kile
tukitakacho, hivyo twendeni zetuni tukafuate Imani ya Dini yetu hadi pale Mungu
atakapoamua baina yetu.’ Allah Subhanah wa Ta’ala analizungumzia tukio hili pale
aliposema:
كَذ َّابٌ۞أَجَعَل
ۤ ﴿وَعَجِبُواْ أَن جَآءَهُم م ٌّنذِرٌ مِّنْهُمْ وَقَالَ ٱلْكَافِرُونَ هَٰذَا سَاحِرٌ َ
ٱلآلهَِةَ إِلَٰهاً وَاحِ داً إِن َّ هَٰذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌ ۞وَٱنطَلَقَ ٱلْمَلَأُ مِنْهُمْ أَنِ ٱمْشُواْ وَاْ ْصبرُِواْ
ٰ عَلَى آلهَِتِكُمْ إِن َّ هَٰذَا لَشَيْءٌ يُرَادُ۞مَا سمَِعْنَا هبَِٰذَا فىِ ٱلْمِل َّةِ ٱلآخِ رَةِ إِ ْن هَٰذَا إِلا َّ
ٱخْتِلاَقٌ۞أَأُنزِلَ عَلَيْهِ ٱلذِّكْرُ مِن بَيْنِنَا بْل هُمْ فىِ شَكٍّ مِّن ذِكْرِى بَل ل َّم َّا يَذُوقُ واْ
عَذَابِ ﴾
WaAAajiboo an jaahum mundhirun minhum waqala alkafiroona hadha sahirun
kadhdhabun; AjaAAala al-alihata ilahan wahidan inna hadha lashay-on AAujabun
; Waintalaqa almalao minhum ani imshoo waisbiroo AAala alihatikum inna hadha
lashay-on yuradu; Ma samiAAna bihadha fee almillati al-akhirati in hadha illa
ikhtilaqun; Aonzila AAalayhi aldhdhikru min baynina bal hum fee shakkin
min dhikree bal lamma yadhooqoo AAadhabi (Surat Sad 38:4-8)
700
Tafsir: Na wao wanaona Ajabu kua amekuja kwao Muonyaji kutoka miongoni mwao
na wakasema Makafiri: ‘Huyu ni Mchawi na ni Muongo’ Amejaalia Miungu yetu yote
kua Mungu Moja hakika hili ni jambo la ajabu sana. Na viongozi miongoni mwao
wakasema: ‘Nendeni Mkabakie na Miungu yenu, kwani kwa hiki hili ni jambo
lililoandaliwa dhidi yenu; Hatujawahi kusikia sisi kuhusiana na jambo hili kutoka kwa
watu wetu wa mwishoni. Hauwi huu ila ni Uzushi. Hivi Jee (inawezekana kua)Uonyaji
ashushiwe yeye peke yake miongoni mwetu?’(Allah Subhanah wa Ta’ala anasema)La,
bali wao (Makafiri) ni wenye kua na shaka na Uonyaji wangu (Qur’an) na bado
hawajaonja Adhabu yangu.
Hivyo kwa mtizamo wao basi Viongozi wa Qurayshi walikua wakimuita Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua ni Mchawi na Muongo, kwa sababu mbali ya kusema
anayoyasema ambayo kwao wao hayaingii akilini lakini watu walikua wakimsikiliza na
kumfuata, hivyo kwao wao ilikua hakuna njia nyengine anayoitumia Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam katika kuwapata watu wengi zaidi isipokua ni kwa kutumia
Uchawi.
Ambapo kwa upande mwengine basi Allah Subhanah wa Ta’ala analizungumzia tukio
hili kwa kusema:
﴿بَلْ مَت َّعْتُ هَٰؤُلاَءِ وَآآبَءَهُمْ حَتى َّ ٰ جَآءَهُمُ ٱلحَْق ُّ وَرَسُولٌ م ُّبِينٌ۞وَ لَم َّا جَآءَهُمُ
ٱلْقُرْآنُ ٰ سِ حْرٌ وَإِ َّ بِهِ كَافِرُونَ۞وَقَالُواْ لَوْلاَ نُزِّلَ هَٰذَا عَلَى رَجُ ٍل
ٱلحَْق ُّ قَالُواْ هَٰذَا
مِّنَ ٱلْقَرْيَتَينِْ عَظِيمٍ۞أَهُمْ يَقْسِ مُونَ رَحمَْةَ رَبِّكَ نحَْنُ قَسَمْنَا بَيْنَهُمْ م َّعِيشَتَهُمْ ِفى
ٱلحَْيَاةِ ٱلد ُّنْيَا وَرَفَعْنَا بَعْضَهُمْ فَوْقَ بَعْضٍ دَرَجَاتٍ لِّيَت َّخِ ذَ بَعْضُهُم بَعْضاً سُخْرًِّ
وَرَحمَْ ةُ رَبِّكَ خَيْرٌ ممِّ َّا يجَْمَعُونَ ﴾
Bal mattaAAtu haola-i waabaahum hatta jaahumu alhaqqu warasoolun mubeenun;
Walamma jaahumu alhaqqu qaloo hadha sihrun wa-inna bihi kafiroona; Waqaloo
lawla nuzzila hadha alqur-anu AAala rajulin mina alqaryatayni AAadheemun;
Ahum yaqsimoona rahmata rabbika nahnu qasamna baynahum maAAeeshatahum
fee alhayati alddunya warafaAAna baAAdhahum fawqa baAAdinn darajatin
liyattakhidha baAAdhuhum baAAdhan sukhriyyan warahmatu rabbika khayrun
mimma yajmaAAoona (Surat Az Zukhruf 43:29-32)
701
Tafsir: Bali nimewapa (Makafiri) wao na Mababa zao mapambo ya kufurahia
(Uongozi na usimamizi wa Mji Mtukufu wa Makkah na jengo Tukufu la Al Kaabah)
hadi pale ulipowajia wao Ukweli (Ujumbe wa Qur’an) na Mtume (Muhammad
Salallahu Alayhi wa Salam), Na Ukweli (Ujumbe wa Qur’an) ulipowafikia basi
wakasema: ‘Huu ni Uchawi na Tunaukufuru’ Wakawa wanasema: ‘Kwanini (Kama
ni kweli basi Hii Qur’an); Na wakasema: ‘Kwanini hakushushwa hii Qur’an kwa
Watu watukufu wa Miji yetu hii mimi (Makkah na Taif)’ Hivi Jee ni wao ndio wenye
kugawa Rehma za Mola wako? Bali ni sisi ndio tunaogawa baina yao katika riziki ya
maisha yao ya Dunia na tunawapandisha juu baadhi yao miongoni mwao darja, ili
wawaajiri baadhi yao katika kazi zao, na Rehma za Mola wako ni bora zaidi ya (Mali)
wanayojikusanyia.’
Ambapo baada tu ya Viongozi hao wa Quraysh kuanza kujadiliana kwa kunong’onezana
basi Abu Talib akasema: ‘Ewe Mtoto wa Ngugu yangu, hakika mimi sioni kua wewe
umekosea kutokana na matakwa yako.’ Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alipoyasikia haya basi akafurahia sana na kumwambia Abu Talib: ‘Ewe Ami Ynagu
sema La Ilaha Illa Allah’
Lakini Abu Talib akasema: ‘Ewe Mtoto wa Ndugu yangu, hakika mimi nnapa kwa
Allah kua kama siogopi mimi kua kubadilika kwangu kutawapelekea kua watu
hawa ni wenye kusema kua kumetokana na Uzee na kupungukiwa na kumbukumbu
na wao kua ni wenye kudumu katika kukukumbusha wewe na watoto wa mababu
zako baada ya kuodoka kwangu hapa Duniani, basi mimi ningesema maneno
unayotaka niyaseme na kukufuata, lakini watu wa Quraysh watadhani kua mimi
nimeyasema kutokana na kuogopa kifo, hivyo siwezi kuyasema maneno hayo.’
Ambapo hata hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliendelea kumuuisia Ami
yake huyo kua ashuhudie mara kadhaa lakini Abu Talib alisema kua: ‘Mimi ni Mfuasi
wa Imani ya Abd Ul Muttalib’na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala:
﴿إِن َّكَ لاَ تَهْ دِى مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَٰكِن َّ ٱهلل ََّ يَهْدِى مَن يَشَآءُ وَهُوَ أَعْلَمُ بِ ٱلْمُهْتَدِينَ ﴾
Innaka la tahdee man ahbabta walakinna Allaha yahdee man yashao wahuwa
aAAlamu bialmuhtadeena (Surat Al Qasas 28:56)
Tafsir: Ni kwa hakika wewe hutoweza kumuongoza kila mtu unaempenda zaidi, lakini
Allah humuongoza amtakae na ni mwenye kuwajuwa wale walioongoka.
Hatimae Abu Talib akafariki Dunia huku akiwa na umri wa miaka 87, ambapo wakati
Abu Alib alipokua anafariki basi Al Abbas alikua amekaa pembeni yake na hivyo
702
akamuona Abu Talib wakati anakata roho kua midomo yake kama inasema kitu na hivyo
akamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam huku akitabasama kua: ‘Ewe Ibn
Ami nimemsikia Abu Talib akitamka kile ambacho ulichomtaka aseme.’ Kwani
katika ipindi hiki pia hata Al Abbas alikua hajasilimu bado.
Hivyo Rasul Allah Saallahu Alayhi wa Salam akasema kumuombea Ami yake huyo kua:
‘Allah, akuingize kwenye Rehma zake na akulipe kila la kheri’ na hivyo Allah
Subhanah wa Ta’ala akashusha aya isemayo:
﴿مَا كَانَ لِلن َّبىِِّ وَٱل َّذِينَ آمَنُو ۤ اْ أَن يَسْتَغْفِرُواْ لِلْمُشْرِكِينَ وَلَوْ كَانُو ۤ اْ أُوْلىِ قُ رْبىَٰ مِن
بَعْدِ مَا تَبَين ََّ لهَُمْ أَن َّهُمْ أَصْحَابُ ٱلجَْحِ يمِ ﴾
Ma kana lilnnabiyyi waalladheena amanoo an yastaghfiroo lilmushrikeena walaw
kanoo olee qurba min baAAdi ma tabayyana lahum annahum as-habu aljaheemi
(Surat At Tawbah 9:113)
Tafsir: Na si juu ya Nabii na wale Walioamini kua ni wawaombee Dua za kusamehewa
Washirikina, hata kama wakiwa ni watu wa karibu yao baada ya kubainishiwa kua
wao ni wtau wa Motoni.
Kifo hiki cha Abu Talib kilimhuzinisha sana Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam
kwani Abu Talib alikua ni Ngao yake dhidi ya Makafiri wa Makkah ambayo sasa hivi
ilikua imeanguka na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawa peke yake.
Na baada ya kufariki Abu Talib basi haikuchukua mda mrefu ulipoingia mwezi wa
Ramadhan basi Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam akafikwa na msiba mwengine
kwani akafariki na Khadija Ibn Khuwaylid Radhi Allah Anha akiwa na umri wa miaka
65.
Ambapo ingawa Khadija Bint Khuwaylid Radhi Allahu Anha alikua ni Tajiri katika
wakati wa Uhai wake lakini alipofariki alikua hana hata dinari moja, na hii ni kwa sababu
Mali yake yote alikua ni mwenye kuitumia kwa ajili ya kuusaidia Uislam na kuwasaidia
Waislam waliokua na hali mbaya ya kiuchumi na mateso yaliyotokana na vikwazo vya
Makafiri dhidi ya Waislam.
Msiba huu nao pia ulikua mzito sana kwake Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam na
hii kwa sababu ama tunavyojua kua Bi Khadijah Bint Khuwaylid Radhi Allahu Anha
alikua ni nguzo muhimu katika maisha yake na ndie mtu aliekua akimpa utulivu
anaporudi nyumbani kwake kwani ndie Mama watoto wake na ndie furaha ya Moyo
703
wake, kwani Bi Khadija Bint Khuwaylid Radhi Allah Anha alikua ni mwanamke ambae
ni mwenye sifa ya kumpenda, kumjali, kuhurumia na kumliwaza Mume wake katika kila
hali kutokana na mapenzi yake juu yake.
Bi Khadija Bint Khuwaylid Radhi Allahu Anha alikua ndie mwanamke mwenye Darja
ya Amirat Ul Quraysh kwani hata Malaika Jibril alithibitisha haya pale siku moja
alipokua pamoja na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kisha akawa anakuja
Amirat Al Quraysh akiwa na sahani ya chakula kwa ajili ya Mume wake yaani Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Ya Rasul Allah, huyo anaekuja kutoka mbali
ni Khadija, akiwa amechukua chombo cha kubebea chakula, atakapofika mbele
yako basi mpe salam zake kutoka kwa Mola wake na kwangu mie mwambie kua
Amejengewa Kasri Peponi litokanalo na Lulu kwa ajili yake ambalo ndani yake
hyamtokua na kasi wala matatizo.’
Hivyo mwaka huu kutokana na misiba hii iliyotoeka ndani yake basi ulikua unajulikana
kama Mwaka wa Huzuni. Na huzuni ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ilizidi
zaidi pale Makafiri walipozidisha Adha na kero zao juu ya Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam, kwani walikua wanajua kua hakuna wa kumlinda na kumtetea hivyo umefika
wakati wao wa kufanya wayatakayo, kiasi ya kua siku moja wakati Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alipokua akirudi Nyumbani kwake basi mmoja katika ya Majirani zake
alichukua Taka zake na kumwagia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuanzia
kichwani mwake.
Lakini hata hivyo kutokana na subra zake basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
hakumfanya kitu chochote mwanamke huyo bali alijipangusa takataka hizo kutoka
mwilini mwake na kurudi Nyumbani kwake, na alipofika Nyumbani kwake alisababisha
kilio kutoka kwa bint yake Fatma ambae alishindwa kujizuia kutokana na uchungu wa
maovu anayofanyiwa baba yake, na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akamnyamazisha Fatma na kisha akamwambia: ‘Ewe Binti yangu usilie kwani kwa
Hakika Allah atamhifadhi Baba yako’
Hali ilipozidi kua mbaya ya Manyanyaso basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akaamua kua bora atoke akatafute Wafuasi zaid katika maeneo ya Nje ya Mji wa Makkah
yaani Taif ambao uko umbali wa kilomita 75 kutoka katika Mji wa Makkah, kwani
kwenye kabila la watu wa Bani Thaqif ambao ni tofauti na watru wa Quraysh, na kama
wakimkubali basi itakua vizuri kwani atahama yeye na Wafuasi wake kuelekea kwenye
Mji wa Taif.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akafunga safari kuelekea katika Mji wa
Taif hukua akiwa amefuatana na msaidizi wake ambae ni Zaid Ibn Harith Radhi Allahu
Anhu, na alipofika katika Mji wa Taif basi hali iikua tofauti na namna alivyotegemea,
kwani watu wa Mji huo waliukataa Ujumbe wa Allah Subhanah wa Ta’ala alioshushiwa
704
kwa ajili ya kuwausia watu wake na Ibn Adam wote kwa ujumla, na kisha wakaanza
kumtukana na kuwaamrisha Watoto wao wawafukuze kwa kuwapiga mawe Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam pamoja na Zaid Ibn Harith Radhi Allahu Anhu.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Zaid Ibn Harith Radhi Allahu Anhu
wakakimbia kutoka katika Mji wa Taif huku wakiwa wamejeruhiwa na kuchuruzikwa na
Damu na kutafuta hifadhi katika moja kati ya Mashamba ya mpakani mwa Mji huo, kisha
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaomba Dua kwa kusema:
اللهم إليك أشكو ضعف قوتي ، وقلة حيلتي ، وهواني على الناس ، أرحم
الراحمين ، أنت أرحم الراحمين ، إلى من تكلني ، إلى عدو يتجهمني ، أو إلى
قريب ملكته أمري ، إن لم تكن غضبان علي فلا أابلي ، غير أن عافيتك
أوسع لي ، أعوذ بنور وجهك الذي أشرقت له الظلمات ، وصلح عليه أمر
الدنيا والآخرة ، أن تنز ل بي غضبك ، أو تحل علي سخطك ، لك العتبى حتى
ترضى ، ولا حول ولا قوة إلا بك
‘Kwako wewe Ya Allah, Nakusikitikia juu ya Udhaifu wangu, kukosa msaada
kuungwa mkono kwangu na manyanyaso ninayoyapata, Ewe Mwingi wa Rehma
ewe Mwingi wa Huurma Wewe ndie Mola wa Wanyonge, wewe ndie Mola wangu,
Jee unaniacha kwa nani? Kwa watu wa Mbali wanaonifanyia Uadui? Au kwa
Maadui uliowapa Uwezo zaidi yangu? Hivyo kama kuhuridhika nami, basi mimi
sijali nitakabaliana na nini lakini nitakua ni mwenye kufarahia zaid Rehma zako,
Hakika mimi natafuta hifadhi kutokana na Nuru ya Muonekano wako, ambay ni
yenye kuondosha kila sehemu yenye kiza katika Maisha haya na ya baadae baada
ya kuyarekebisha dhidi ya kupatwa na adhabu zake au kua chini ya ghadhabu zako.
Hakika mimi najisalimisha kwako kikamilifu hadi nitakapopata ridhaa yako,
kwani hakuna chenye kuwezekana bila ya uwezo wako.’
Ambapo mara baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuomba Dua hii basi
akashuka Malaika Jibril na kumuambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua
kama anataka basi basi Allah Subhnaha wa Ta’ala anaweza Kumtuma Malaika kisha
akaiangushia Milima Miwili iliyozunguka Mji wa Ta’if na kuwaangamiza watu hao
ndani yake, lakini hata hivyo kutokana na Ubora wa Maumbile na Tabia zake na wingi
705
wa Rehma zake na Upole wake basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema:
‘La, haina haja kwani mimi nnategemea kua ndani yao watu hawa watatoka watu
ambao watakua ni wenye Kumuabudu Allah Subhanah wa Ta’ala na
kutomshirikisha na chochote.’
Hivyo wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwa amekaa na kupumzika
kwenye jiwe moja la shamba hilo, basi mara akatokea Kijana ambae alikua na shada la
Zabibu na kumpa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Zaid Ibn Harith Radhi
Allahu Anhu. Kijana huyo alipofika mbele yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
basi akajitambulisha kua anaitwa Addas na kua ametumwa amletee Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam Zabibu hizo kutoka kwa wamiliki wawili wa Shamba hilo ambao
waliowaona namna Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Zaid Ibn Harith Radhi
Allahu Anhu walivyokua wamekaa huua wakiwa taabani na kuamua kuwakirimu Zabibu
hizo.
Baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Zaid Ibn Harith Radhi Allahu Anhu
kupewa Zabibu hizo na kushukuru basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaanza
kula kwa kusema: ‘Biismi Allah’. Ambapo tukio hili lilimshangaza sana Addas kwani
hakuwahi kusikia mtu yeyote akisema maneno hayo hapo kabla. Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akaona mshangao wake huo na akamuuliza Addas: ‘Wewe ni Mtu wa
wapi?’ ambapo Addas akasema: ‘Ni Mtu wa Nineveh’.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akatabasam kisha akasema: ‘Mji wa Yunus
Muadilifu Ibn Mata.’ Ambapo jibu hili lilimshangaza zaidi Addas, kua inakuaje mtu
huyu alie mbele yake anajua kuhusiana na Mji wake ambao ni Mji wa Nabii Yunus, na
hivyo akamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam: ‘Hivi Jee umejuaje
kuhusiana na habari hio?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Yunus ni Kaka yangu. Kwani yeye
alikua ni Mtume na Mimi pia ni Mtume.’ Hivyo hapo hapo Addas akamshika kichwa
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kisha akambusu kwenye paji lake la Uso, na
kisha akaingia katika Dini ya Uislam.
SHAQQ AL QAMAR - MUUJIZA WA KUPASUKA KWA MWEZI
Mnamo mwaka wa 7 wa Utume miongoni mwa Viongozi wa watu wa kabila la Quraysh
akiwemo Walid Ibn Al Mughira, Abu Jahl, Aas Ibn Hisham. Aswad Ibn Abd Yaghush,
Aas Ibn Wail, Aswad Ibn Mutallib na wengineo walimfuata Rasul Allah Salallahu
A’alyhi wa Salam na kumwambia: ‘Kama wewe Muhammad ni Mtume kweli wa
Allah basi tuoneshe Muujiza wa Kuupasua Mwezi, kiasi ya kua sehemu yake moja
706
itatokea kwenye upande wa Mlima wa Abu Qubais na nyengine itatokea kwenye
upande wa Abu QuayQan’
Na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawauliza Makafiri hao kua: ‘Jee kama
nikifanya hivyo, Mtaingia katika Uislamu?’ ambapo nao wakasema: ‘Naam’. Hivyo
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuomba Allah Subhanah wa Ta’ala amjaalie
uwezo wa kufanya Miujiza hio kama wanavyotaka Makafiri hao katika usiku wa mwezi
mpevu yaani tarehe 14 ya Muandamo wa Mwezi ambao hua ndio mwezi mkamilifu na I
wenye kuonekana wote. Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamuamrisha Malaika
Jibril kua ashuke kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua amekubaliwa
Dua yake hio, na itatekelezwa kama alivyotaka iwe.
Hivyo ilipowadia siku hio basi baada ya Salat al Isha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akatoka na Waislam pamoja na Maquraysh hao na kuenda katika maeneo ya
Minna huku kukiwa na mwezi Kamilifu na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akaupasua
Mwezi huo na akaupeleka upande mmoja wa mwezi huo kwenye upande wa Mlima wa
Abu Qubais sambamba na upande mwengine wa mwezi huo kwenye mlima Quayqan, na
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawanadia Waislam kwa kuwaambia:
‘Ewe Abu Salama Ibn Abd Salam, Ewe Arqam Ibn Abi Al Arqam! Shuhudieni’ na
kisha akawa geukia Makafiri hao na kuwanadia: ‘Enyi Watu wa Quraysh Shuhudieni!’
lakini hata hivyo Maquraysh hao wakasema: ‘Hakika huu ni Uchawi wa Mtoto wa Abu
Kabsha’ na kusema: ‘Hakika Muhamamd leo hii ameturoga, lakini hawezi kumroga
kila mtu hivyo wacha tuwaulize Wafasiri watakaokuja kama nao waliona ama la.’
Na siku ya pili yake watu wa Quraysh walipowauliza watu wengine waliokua ni wasafiri
waliotoka nje ya mji wa Makkah basi nao wakasema: ‘Hakika sisi tumeuona Mwezi
ulipopasuka, tumeuona mwezi ukiwa umepasuka.’ Lakini hata hivyo Makafiri hao
hawakukubaliana na Miujiza hio hivyo wakawa ni wenye kuendelea kusema kua :
‘Mjukuu wa Abd ul Muttalib ameziroga mpaka Mbingu kwa uchawi wake.’
Ambapo anasema Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wakati tukiwa
tumekaa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika maeneo ya Minna basi
Mwezi ukapasuka na upande mmoja ukaenda nyuma ya Mlima mmoja na upande
mwengine ukaenda upande mwengine na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasema: ‘Shuhudieni.’’(Imam Bukhari)
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akayakanusha maneno hayo ya Makafiri na
kuyathibitisha ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam pale aliposema katika Surat Al
Qamar kua:
707
﴿بِ سْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞ٱقْتَرَبَتِ ٱلس َّاعَةُ وَٱنشَق َّ ٱلْقَمَرُ۞وَ إِن يَرَوْاْ آيَةً يُعْرِضُواْ
وَيَقُولُواْ سِ حْرٌ م ُّسْتَمِر ٌّ۞وَكَ ذ َّ بُواْ وَٱت َّبَعُو ۤ اْ أَهْ وَآءَهُ مْ وَكُ ل ُّ أَمْ رٍ م ُّسْ تَقِر ٌّ ۞َولَقَدْ جَآءَهُم
مِّنَ ٱلأَنبَآءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ۞حِ كْمَةٌ ابَلِغَةٌ فَمَا تُغْنِى ٱلن ُّذُرُ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Iqtarabati alssaAAatu wainshaqqa alqamaru;
Wa-in yaraw ayatan yuAAridhoo wayaqooloo sihrun mustamirrun;
Wakadhdhaboo waittabaAAoo ahwaahum wakullu amrin mustaqirrun; Walaqad
jaahum mina al-anba-i ma feehi muzdajarun; Hikmatun balighatun fama tughnee
alnnudhuru (Surat Al Qamar 54:1-5)
Tafsir: Kwa Jina la Allah mwingi wa Rehma na mwingi wa huruma; Imekaribia Saa
na Mwezi umepasuka; Lakini wanapoiona Dalili basi hua ni wenye kugeuka na
kusema: ‘Ni tukio lisilodumu la Uchawi wenye Kupita’; Wamekadhibisha na kufuata
Matamanio yao; Na kila jambo hua lina mwisho wake; Kwani kwa hakika imewajia
Habari, ambayo ndani yake mna Uonyo; Na Hikma kubwa sana, lakini hata hivyo
hauwafai uonyo huo.
Na kwa upande mwengine basi tunaona kua tukio hili limehadithiwa pia na Masahaba
kadhaa waliolishuhudia kiasi ya kua Hadith zake ni Mutawattir yaani wingi wake
mkubwa sana kiasi haiwezekani kwa Masahaba hao kua ni wenye kukubaliana kusema
uwongo juu ya jambo hilo, na bila ya shaka tukio hili ni lenye kuwezekana kutokana na
Maumbile ya mwezi kua ni yenye kutokana na Mawe kama ya Volcano na hivyo
kuwezekana kutokea Mripuko na Mwezi ukagawika na kwa makadirio yake Allah
Subhanah wa Ta’ala basi mwezi huo ukaungana tena upya.
Lakini kwa wasioamini hii hua haiwezi kuwasaidia kitu kwani amesema Allah Subhanah
wa Ta’ala kua:
﴿قُلِ ٱنظُرُواْ مَاذَا فىِ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَمَا تُغْنىِ ٱلآَتُ وَٱلن ُّذُرُ عَن قَوْمٍ لا َّ
يُؤْمِنُونَ ﴾
Quli ondhuroo madha fee alssamawati waal-ardhi wama tughnee al-ayatu
waalnnudhuru AAan qawmin la yu/minoona (Surat Yunus 10:101)
708
Tafsir: Waambie (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam): ‘Angalieni yote
yaliyomo Mbinguni na Ardhini’ Lakini si dalili hizo wala si Waonyaji wanaowafaa
wale Wasioamini.
SIFA ZA UPEKEE WA KIMAUMBILE WA NABII MUHAMMAD
SALALLAHU ALAYHI WA SALAM:
﴿م َّا كَانَ محَُم َّدٌ أَآبَ أَحَدٍ مِّن رِّجَالِكُمْ وَلَٰكِن ر َّسُولَ ٱهلل َِّ وَخَاتمََ ٱلن َّبِيِّينَ وَكَانَ ٱهلل َُّ
ّ شَيْءٍ عَلِيماً ﴾
بِكُل ِ
Ma kana muhammadun aba ahadin min rijalikum walakin rasoola Allahi
wakhatama alnnabiyyeena wakana Allahu bikulli shay-in AAaleeman(Surat Al
Ahzab 33:40)
Tafsir: Na hakua Muhammad ni Baba wa Mtu yeyote Miongoni mwenu, lakini ni
Mtume wa Allah, na Nabii wa Mwisho na Allah ni mwenye kujua juu ya kila kitu.
Anasema Umar Ibn Al Khattab kua: ‘Katika kipindi cha Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kulikua na Mtu ambae alikua akiitwa Abd Allah ambae jina lake la Utani
lilikua ni Khimar (Punda), na alikua anapenda kumchekesha Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwa mambo yake. Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akampa
adhabu ya kupigwa bakora kwa sababu alikua amelewa. Siku moja akaletwa tena
mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo akapewa tena adhabu ya
bakora, mara mmoja miongoni mwa watu akasema: ‘Ya Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam mlaani! Kwani ni mara ngapi tayari analetwa kwa kosa hilo hilo.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema ‘La Msimlaani kwani Wallahi mimi
najua kua huyu ni mwenye kumpenda Allah na Mtume wake’’ (Sahih Bukhari)
Imam Bukhari anasema kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakutoka nje
kwa siku tatu, na hivyo Abu Bakr akawa ni mwenye kuongoza Sala. Wakati
Waislam wanasali basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akafunua pazia lake.
Hivyo wakati pazia liliponyanyuka basi Uso wake Mzuri wenye kung’ara
ukaonekana, basi haijawahi kuonekana muonekano unaovutia kwa uzuri kabla
yake’ (Sahih Bukhari)
709
Hadith hii pia ipo katika kitabu cha Imam Muslim ambae yeye anasema kua Masahaba
walisema: ‘Kutokana na kuzidiwa kwa Furaha ya kuuona uzuri wake, basi tukawa
ni wenye kuchanganyikiwa ndani ya Sala zetu ’(Sahih Muslim)
Mtume Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam alisema kua : ‘Mlima wa Uhud ni
Mlima katika Milima ya Peponi Unatupenda nasi Tunaupenda’(Sahih Bukhari).
Na akasema tena Nabii Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Mlima wa Uhud
Unatupenda nasi tunaupenda, Ya Allah Hakika Ibrahim ameufanya Mji wa Makkah
kua ni Mtukufu, hivyo nami nakifanya Kitukufu kila kilicho baina ya Mlima wa Uhud
(Yaani Mji wa Madinah )’(Imam At Tirmidhii)
Na baada ya vita vya Uhud Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Sayyidna
Abubakar, Sayyidna Umar na Sayyidna Uthman w Radhi Allahu Anhum alikua
wamepanda juu ya Mlima wa Uhud, ambapo nao Ukatikisika. Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akatabasam kisha akaupiga mguu wake chini huku akisema: ‘Tulia
Ewe Uhud kwani juu yako hakuna yeyote yule isipokua Rasul Allah, na Mashahidi
wawili’ hapo Mlima wa Uhud ukatulia.(Sahih Bukhari, Imam Tirmidhi)
Tunapoziangalia hadith hizi mbili basi tunaona kua Mlima wa Uhud ni Mlima wa
Volcano ambao haujawahi kuripoka tangu uliporipuka. Hivyo Mlima huu ulitikisika si
kwa ripuka la, bali ni kwa sababu ulikua umefurahia kua juu yake amepanda Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam, na hivyo ulikua unataka kuonesha kua unajua darja ya yule
aliepanda juu yake ambae ni Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Kwa upande mwengine basi tunaona kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisema
kua Mlima wa Uhud unawapenda kwa sababu Mlima huo ndio Uliomhifadhi yeye pale
walipovamiwa na Jeshi la makafiri lililokua likiongozwa na Khalid Ibn Walid kabla ya
Kusilimu katika vita vya Uhud, na vile vile mazingira ya Mlima wa Uhud ambao ni
wenye urefu wa kilomita moja kwenda juu, na ni wenye rangi Nyekundu kutokana na
udongo wake kua ni wenye asili ya Volkano wenye mchanganyiko wa madini ya quartz,
sanidine na plagioclase. Mlima wa Uhud upo kaskazini ya Mji wa Madinah kilomita 5
kutoka katika Masjid An Nabawi yanaufanya mlima huu kua ni ngao na hivyo kuua kama
vile unaukumbatia Mji wa Madinah na hivyo kua kama ngao kwa Watu wake kutokana
na Mashambulizi ya maadui zao.
Na hii pia ni kulingana na uthibitisho wa ile hadith ya Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu
Anhu ambae alisema: ‘Hakika mimi nilimuona Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam katika Usiku wa mwezi Mpevu akiwa amevaa Joho Jekundu, Kisha
nikaangalia juu na nikaona mwezi Mpevu, na nikaona kua Rasul Allah Salallahu
710
Alayhi wa Salam alikua ni mzuri zaidi mbele ya macho yangu kuliko hata Uzuri wa
Mwezi mpevu’ (Shamail Tirmidhii)
Na pia Anas bin Malik Radhi Allahu Anhu amesema kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alikua si mrefu wala si mfupi, na muonekano wake haukua mweupe sana
kama wa alietiwa limau na wala hakua mwenye rangi ya kiza, wala rangi ya
kahawia ya kiza (alikua anang’ara)’(Shamail Tirmidhii)
Kwani tunapozungumzia Uzuri wa Mwezi Mpevu au Mwezi Mweupe Unaong'ara basi
hua tunazungumzia hali wanayoiona Ibn Adam wenye kujua Uzuri wa Maumbile ya Kitu
kutokana na uwezo wa Muumba usiokua na Kifani juu ya hicho alichokiumba.
Kiasi ya Kua mwenye kujua huyo hua ni mwenye kupigwa na bumbuwazi na uzuri huo
anapouona Uzuri wa kitu husika. Wengi hatuna kawaida ya kuuona na kuangalia Mwezi
kwa utulivu na hivyo hua hatuoni uzuri wake, kwani uzuri wa mwezi tena katika kiza cha
usiku basi hua ni Uzuri wa kustaajabisha, kuvutia, kutuliza Moyo wa mwenye kuuangalia
na kuutizama, lakini sisi hatuoni uzuri huo kwa sababu hatuangalii na pia kwa sababu
tumeathirika na mazingira ya taa za umeme kila sehemu.
Ndio maana wenye lugha yao hua wanasifia uzuri kwa kumithilisha kwa kusema: ‘Zayy
Al Qamar’ yaani: ‘Uzuri wa Mwezi’ Waarabu hua pia ni wenye kutumia sifa ya Uzuri
wa mwezi kiasi ya kua mtu anafikia kumsifu Mwanamke mzuri anaempenda kwa
kumwita Ya Amar! yaani Ya Qamar!
Na bila ya shaka Mwanamke wa Kiarabu ukimsifia kwa kua na sifa ya uzuri wa Mwezi
basi hua anajiona kua yuko kama Hur Al Ayn hivyo Uzuri wa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam hua ni wenye kupita Uzuri wa mwezi.
Imam Ibn Kathir anasema kua : 'Hasan bin Thabit Radhi Allahu Anhu amesema kua:
‘Rasul Allah Salallahu Alyhi wa Salam ni Sayari ambayo hata mwezi wa mwezi 14
hua ni wenye kuchukua Nuru yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam’ (Tarikh
Ibn Kathir)
Tunapomuangalia Imam At Tirmidhii basi tunaona kua kuna Hadith ya Qaylah Bint
Mabramah Radhi Allahu Anha ambae anasema kua: ‘Nilimuona Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akiwa amekaa Msikitini katika mkao wa Qarfasa (Kukaa kitako
huku akiwa amekumbatia miguu yake) na kutokana na Utukufu wa Muonekano
wake basi nikaanza kuetetemeka. Na hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alisema bila ya kuniangalia ‘Masikini, Ewe Mwanamke Kua na Utulivu. Na mara
tu baada ya kusikia maneno hayo ya Rasul Allahu Alayhi wa Salam, basi Khofu hio
ikaniondoka’.(Sharmail At Tirmidhi)
711
Ama tunapozungumzia kuhusiana na Sifa ya Kutisha, kwake Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam basi hua kuna aina mbili, kwanza kuna uzuri wa Kutisha kulingana na
mtizamo wa wale wanaompenda na pia hua ni kulingana na mtizamo wa maadui zake,
kwani kuna kutisha kwa uzuri wa kupita kiasi unaoenda sambamba na kutisha kwa kua
na Darja ya juu kupita kiasi miongoni mwa Viumbe wa Allah Subhanah wa Ta’ala, na
hii hua ni kwa wale wenye kumpenda.
Ama kwa wale waliokua maadui zake basi ilikua pia kuna hali ya kutisha ya mtu
kuingiwa na khofu baada ya kumuangalia kwake ambayo huambatana na khofu ya
kutoweza kufanya chochote hata uwe na uwezo gani mbele yake.
Hivyo kwanza na tuangalie kutisha kunakotokana na Uzuri na pia Utukufu wa Darja yake
Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam. Ambapo tunaona kua anasema Sahaba Abd Allah
Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu alipokua mdogo siku moja usiku aliamka akamuona Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kaamka anataka kusali, hivyo haraka sana akakurupuka
na akaenda kumchukulia Maji ili atie Udhu. Na kisha nae akaambiwa na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam atie udhu.
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasimama kwa ajili ya kusali. Lakini
kabla ya kusali basi akamwambia Abd Allah Ibn Abbas, njoo hapa,kaa pembeni yangu
Usali. Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Saalam akasali hadi akamaliza. Na
alipomaliza basi alimuona Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu akiwa hajasali
pembeni yake. Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuuliza: Ya Abda Allah,
kwani mimi nilipokuambia usali pamoja nami hukusali?
Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu alijibu: ‘Ya Rasul Allah! Hakika wewe Ni
Mwenye Darja Kubwa sana kwangu kiasi ya kua haiwezekani mimi na wewe kua
ni wenye kusali pamoja mbele ya Allah Subhanah wa Ta'ala’.
Hapa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akanyanyua mikono juu na kumuomba
Allah Subhanah wa Ta'ala kwa kusema: Ya Allah Mjaalie kua ni Mwenye Hikma.
Kutisha kwa aina nyengine ni kule kunakoelezewa na Asbab Nuzul ya aya inayofuatia
ambako hua ni kutisha kwa Utukufu wa heshima.
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ لاَ تَرْفَعُو ۤ اْ أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ ٱلن َّبىِ ِّ وَلاَ تجَْهَرُواْ لَهُ بِٱلْقَوْلِ
كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن تحَْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لاَ تَشْعُرُونَ ﴾
712
Ya ayyuha alladheena amanoo la tarfaAAoo aswatakum fawqa sawti
alnnabiyyi wala tajharoo lahu bialqawli kajahri baAAdhikum libaAAdhin an tahbata
aAAmalukum waantum la tashAAuroona (Surat Al Hujurat 49:2)
Tafsir: Enyi Mlioamini Msinyanyue Sauti zenu juu ya sauti ya Nabii (Muhammad
Sallahu Alayhi wa Salam) na wala msizungumze nae kama mnavyozungumza
miongoni mwenu, ili amali zenu zisije zikawa ni za bure wakati nyinyi mkiwa hamjui.
Anasema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari
Al Qurtubi kuhusiana na ayah hii kua : ‘Amesema Imam Ibn Abi Mulaykah kua kuna
watu wawili wema ambao ni Abu Bakr na`Umar ilikua bado kidogo tu waangamie,
kutokana na kupaza kwao sauti mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam,
baada ya kuwasili kwa ujumbe wa Banu Tamim, ambapo mmoja kati yao alitaka
kua Aqra Ibn Rabia awe kiongozi wao, wakati mwengine alipendekeza kua kiongozi
awe mtu mwengine.’
Hivyo Abu Bakr akamwambia Umar: ‘Inaonekana kua wewe hutaki lolote isipokua
kupingana nami’ na Umar akamwambia Abu Bakr : ‘La sikua na haja hio mie!’
Hivyo wakapandishiana sauti, hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akaishusha aya hii
ya Surat Al Hujurat 49:2,’
Na kwa Abd Allah Ibn Zubayr Radhi Allahu Anhu basi yeye anasema kua: ‘Mara tu
baada ya kushushwa ayah hii basi ilikua kila mara wakati Umar alipokua
akizungumza na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akizunguumza kwa
sauti ya chini sana kiasi ya kua ilimbidi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akimuomba Umar kurudia rudia maneno aliyokua akiyasema’ (Imam Ibn Jarir).
Na kuhusiana na ayah hii basi tunaona kua Wanazuoni wanasema kua: ‘Hairuhusiki
kupaza Sauti hata ukiwa pembeni ya Kaburi la Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, kwa sababu kupaza sauti kwa mtu karibu na kaburi lake basi hua ni sawa
na kupaza sauti wakati alipokua hai,’ na hii ni kulingana na mtizamo wa Imam Abu
Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi, Imam Ibn
Kathir n.k
Kwa upande mwengine basi anasema Imam Bukhari kua: ‘Siku Moja Umar Ibn Al
Khattab aliwasikia watu wawili wakipaza sauti zao, hivyo akawafuata na
kuwauliza: ‘Jee nyinyi mnajua mko katika sehemu gani? Na jee mnatoka katika
Mji gani?’. Wale watu wakasema kua wanatoka katika Mji wa Taif, ambapo Umar
Ibn Al Khattab akawaambia: ‘Kama nyinyi mngekua ni watu wa Madinah basi
nigekupeni adhabu ya kupigwa bakora.’’
713
Miongoni mwa Khofu ambazo walizopata maadui zake waliokua wanataka kumuua basi
pia ilikua ile Khofu ya kufa ganzi ya Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu ambae
anasema kua kabla ya kusilimu kwake basi katika Vita vya Khandaq, alimuona Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwa anawasalisha Waislam Sala ya Al Asr, kama
inavyoelezewa na aya:
﴿وَإِذَا كُنتَ فِيهِمْ فَأَقَمْتَ لهَُمُ ٱلص َّلاَةَ فَلْتَقُمْ طَآئِفَةٌ مِّنْهُمْ م َّ عَكَ وَلْيَأْخُذُو ۤ اْ
أَسْلِحَتَهُمْ فَإِذَا سَجَدُواْ فَلْيَكُونُواْ مِن وَرَآئِكُمْ وَلْتَأْتِ طَآئِفَةٌ أُخْرَىٰ لمَْ يُصَل ُّواْ
فَلْيُصَل ُّواْ مَعَكَ وَلْيَأْخُذُواْ حِ ذْرَهُمْ وَأَسْلِحَتَهُمْ وَد َّ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ لَوْ تَغْفُلُونَ عَ ْن
أَسْلِحَتِكُمْ وَأَمْتِعَتِكُمْ فَيَمِيلُونَ عَلَيْكُمْ م َّيْلَةً وَاحِ دَةً وَلاَ جُنَاحَ عَلَيْكُمْ إِن كَانَ
بِكُمْ أَذًى مِّ ن م َّطَرٍ أَوْ كُ نتُمْ م َّرْضَى ۤ أَن تَضَعُو ۤ اْ أَسْ لِحَ تَكُ مْ وَخُ ذُ واْ حِ ذْ رَكُمْ إِن َّ ٱهلل ََّ
أََعد َّ لِلْ كَا فِ رِي نَ عَذَاابً م ُّهِيناً ﴾
Wa-idha kunta feehim faaqamta lahumu alssalata faltaqum ta-ifatun minhum
maAAaka walya/khudhoo aslihatahum fa-idha sajadoo falyakoonoo min waraikum
walta/ti ta-ifatun okhra lam yusalloo falyusalloo maAAaka walya/khudhoo
hidhrahum waaslihatahum wadda alladheena kafaroo law taghfuloona AAan
aslihatikum waamtiAAatikum fayameeloona AAalaykum maylatan wahidatan
wala junaha AAalaykum in kana bikum adhan min matarin aw kuntum mardha an
tadaAAoo aslihatakum wakhudhoo hidhrakum inna Allaha aAAadda lilkafireena
AAadhaban muheenan (Surat An Nisa’ 4:102)
Tafsir: Wakati wewe (Muhamamd Salallahu Alayhi wa Salam) unapokua pamoja nao
na kuwaongoza katika Sala, wacha kundi moja miongoni mwao lisimame pamoja
nawe wakiwa na silaha zao, na wanapomaliza Sijda zao basi na wachuue nafasi ya
Nyuma na kisha wale waliokua hawakusali wacha wasali huku nyie mkiwa na jukumu
la silaha zenu, nkwani wanatamani waliokufuru kua laiiti mghafilike na silaha zenu
na mizigo yenu kukushambulieni kwa pigo moja, lakini hakuna dhambi juu yenu
kama mkiweka pembeni silaha zenu kutokana na usumbufu wa Mvua au wa sababu
ya maradhi lakini chukueni tahadhari juu yenu, kwani kwa hakika Allah
ametayarisha Adhabu kali kwa ajili ya Makafiri.
714
Ambapo kama zinavyosema aya basi Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu alikua ana
uhakika kua anaweza akaingia katika Upande huo aliokuwepo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam na akafanya mashambulizi ya Kumuua, na kisha akatoka katika kambi
hio ya Waislam bila ya madhara yeyote, Lakini hata hivyo anasema Khalid Ibn Walid
Radhi Allahu Anhu kua: ‘Kila nikijaribu kutaka kuelekea katika eneo hilo
alilokuwepo Muhammad Salallah Alayhi wa Salam, basi kulikua kuna nguvu fulani
nzito isiyoonekana ambayo ilikua inanizuia mimi kutekeleza azma yangu hio.’
Tukio hili ndilo lilimpelekea Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu kuuona Ukweli kua
haiwezekani kua na uadui na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, kwani atakushinda
tu kutokana na anavyotisha kwani kuna nguvu za kimaumbile zisizonekana ambazo si za
kawaida ambazo hua zinamsaidia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Hapa kwanza Inabidi tujue Uwezo wa Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu ambae kama
tunavyojua kua ndie Mtu pekee katika historia ya Uislam alieuhatarisha Uislam wakati
alipokua kafiri na hii ni katika vita vya Uhud, na hii ni kutokana na Mbinu zake katika
mapigano, Nguvu zake, Ujasiri wake wa kutoogopa kitu chochote na pia ukubwa wa
Subra zake, na pia ndie mtu pekee alieuongoza Uislam na Kuueneza katika Ardhi ya
Uarabuni baada ya Kusilimu kwake.
Tunapoangalia kwa upande wa waliofuatia baada ya Masahaba ambao ni Tabiina basi
tunakutana na Imam Malik ambae tunaona kuhusiana nae kua amesema Musab Ibn
Abdullah kua: ‘Kila wakati ambapo ilikua Nabii Muhammad Sallahu Salayhi wa
Salam, akitajwa mbele ya Imam Malik Radhi Allahu Anhu basi Imam Malik
muonekano wa uso wake hua ni wenye kubadilika na hata mkao wake hua ni wenye
kuwatia khofu wale aliokaa nao karibu yake. Siku Moja akaulizwa kwa nini anakua
katika hali hiyo? Nae akajibu: ‘Kama mngekua mnaona yale nnayoyaona mimi
kwenye Ufaham wangu basi nanyi mngekua na hali kama yangu.’’ (Ash Shifa)
Vile vile Allah Subhanah wa Ta’ala amempa Rasul Allah Sallahu Salayhi wa Salam Sifa
za upekee ambazo ni:
Kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam Ndio Mfano Bora Ulimwenguni kama
zinavyosema aya:
﴿ل َّقَدْ كَانَ لَكُمْ فىِ رَسُولِ ٱهلل َِّ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو ٱهلل ََّ وَٱلْيَوْمَ ٱلآخِ رَ
وَذَكَرَٱ هلل ََّكَثِير اً﴾
715
Laqad kana lakum fee rasooli Allahi oswatun hasanatun liman kana yarjoo Allaha
waalyawma al-akhira wadhakara Allaha katheeran (Surat Al Ahzab 33:21)
Tafsir: Kwa Hakika mnao kwa Rasul Allah mfano Bora kabisa kwa yule mwenye
kutarajia kurudia kwa Allah na Siku ya Mwisho na mkumbukeni Allah kwa Wingi
sana.
Kua yeye Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam ni Mtume wa watu wote kama
zinavyoonesha aya:
﴿قُلْ َٰي ُّهَا ٱلن َّاسُ ِ إِنىّ رَسُولُ ٱهلل َِّ إِلَيْكُمْ جمَِيعاً ٱل َّذِى لَهُ مُلْكُ ٱلس َّمَاوَاتِ
وَٱلأَرْضِ لا إِلَٰهَ ۤ إِلا َّ هُوَ يحُْيِى وَيمُِيتُ فَآمِنُواْ بِٱهلل َِّ وَرَسُولِهِ ٱلن َّبىِِّ ٱلأُمِّىِّ ٱل َّذِى يُؤْمِ ُن
بِٱهلل َِّ وَكَلِمَاتِهِ وَٱت َّبِعُوهُ لَعَل َّكُمْ تَهْتَدُونَ ﴾
Qul ya ayyuha alnnasu innee rasoolu Allahi ilaykum jameeAAan alladhee lahu
mulku alssamawati waal-ardhi la ilaha illa huwa yuhyee wayumeetu faaminoo
biAllahi warasoolihi alnnabiyyi al-ommiyyi alladhee yu/minu biAllahi wakalimatihi
waittabiAAoohu laAAallakum tahtadoona(Surat Al Araf 7:158)
Tafsir: Sema (Ewe Muhamamd): ‘Enyi watu hakika mimi ni Mtume wa Allah juu yenu
nyote, (Allah) ambae ndie mmiliki wa kila kilichomo Mbinguni na Ardhini, na hakuna
Mola isipokua yeye ambae ni mwenye kusababisha uhai na ni mwenye kusababisha
kifo, hivyo Muaminini Allah na Mtume wake (Muhammad Salallahu Alayhi wa
Salam) na Nabii wake asiejua kuandika wala kusoma ambae ni mwenye kumuamini
Allah na Kauli yake, hivyo nifuateni mpate kuongoka.’
Ambapo amesema Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hakika mimi nimepewa mambo matano ambayo
hakuna Mtume aliepewa hapo kabla. Kwanza: Nimesaidiwa kua na hali ya
kuogopewa kwa masafa ya umbali wa safari ya Mwezi mmoja. Pili: Ardhi yote
imetangaziwa kua ni Tohara kwa jili yangu, hivyo popote pale mtu atakapokuwepo
anaweza Kusali wakati mda unapomfikia; Tatu: Ngawira ya Vita imehalalishwa
juu yangu, kwani ilikua ni haramu kwa mtu yeyote yule kabla yangu; Nne:
Nimejaaliwa kua na Uombezi Katika Siku ya Malipo na Tano: Kabla yangu Mitume
walitumwa kwa watu wao tu lakini mimi nimetumwa kwa Watu wote’’."(Sahih
Muslim)
716
Ambapo miongoni mwa mambo haya aliyoyaainisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kwenye Hadith hii basi pia yameainishwa kwenye Aya zifuatazo:
Kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amepewa Haki ya kua Shahidi na Kua
Mombezi katika Siku ya Malipo:
﴿وَكَذٰ لِكَ جَعَلْنَاكُمْ أُم َّةً وَسَطاً لِّتَكُونُواْ شُهَدَآءَ عَلَى ٱلن َّاسِ وَيَكُونَ ٱلر َّسُولُ عَلَيْكُ مْ
شَهِيداً وَمَا جَعَلْنَا ٱلْقِبْلَةَ ٱل َّتىِ كُنتَ عَلَيْهَآ إِلا َّ
لِنَعْلَمَ مَن يَت َّبِعُ ٱلر َّسُولَ ممِ َّن يَنقَلِ ُب
ٰ عَلَى عَقِبَيْهِ وَإِن كَانَتْ لَكَبِيرَةً إِلا َّ عَلَى ٱل َّذِينَ هَدَى ٱهلل َُّ وَمَا كَانَ ٱهلل َُّ لِيُضِي َع
إِيمَانَكُمْ إِن َّ ٱهلل ََّ بِٱلن َّاسِ لَرَءُوفٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Wakadhalika jaAAalnakum ommatan wasatan litakoonoo shuhadaa AAala alnnasi
wayakoona alrrasoolu AAalaykum shaheedan wama jaAAalna alqiblata allatee
kunta AAalayha illa linaAAlama man yattabiAAu alrrasoola mimman yanqalibu
AAala AAaqibayhi wa-in kanat lakabeeratan illa AAala alladheena hada Allahu
wama kana Allahu liyudheeAAa eemanakum inna Allaha bialnnasi laraoofun
raheemun (Surat Al Baqarah, 2:143).
Tafsir: Na Kadhalika tumekujaalieni kua ni umma wa Kati na Kati ili mpate kua
Mashahidi Juu ya Watu na ili awe Shahidi Mtume juu yenu, na tumekijaalia Kibla
ambacho Mlikua Mkikieleka, kwa ajili ya kuwajaribu wale watakaomfuata Mtume
kutokana na watakaomgeuka, kwa hakika hili lilikua ni jambo kubwa isipokua kwa
wale ambao walioongozwa na Allah. Na Allah kamwe hawezi kuifanya ipotee Imani
yenu (Katika Ibada mlizofanya hapo kabla), kwa hakika Allah juu ya Watu ni
Mkarimu na ni mwingi wa Rehma.
Kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amepandishwa Darja ya kuifikia Maqam
Al Mahmudan ambayo ni sehemu ya Darja isiyowezekana kufikiwa na kiumbe yeyote
isipokua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam:
﴿وَمِنَ ٱلْل َّيْلِ فَتَهَج َّدْ بِهِ َفِلَةً ل َّكَ عَسَى ٰ أَن يَبْعَثَكَ رَب ُّكَ مَقَ اماً مح َّْمُوداً ﴾
717
Wamina allayli fatahajjad bihi nafilatan laka AAasa an yabAAathaka rabbuka
maqaman mahmoodan(Surat al-Isra, 17:79).
Tafsir: Na katika sehemu ya Usiku Sali Tahajjud ndani yake kama Sunna kwa ajili
yako huenda akakupandisha Mol wako katika Maqaman Mahmudan.
Kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amepewa Darja na Kuahidiwa
kuaminiwa na Mitume wengine Wote:
﴿وَإِذْ أَخَذَ ٱهلل َُّ مِيثَاقَ ٱلن َّبِيِّينَْ لَمَآ آتَيْتُكُمْ مِّنْ كِتَابٍ وَحِ كْمَةٍ ثمُ َّ جَ آءَكُمْ رَسُولٌ
م ُّصَدِّقٌ لِّمَ ا مَعَكُمْ لَتُؤْ مِ نُن َّ بِهِ وَلَتَ نْصُرُن َّهُ قَالَ أَأَقْرَرْتمُْ وَأَخَ ذْ تمُْ عَلَى ٰ ذٰ لِكُ مْ إِصْرِى
قَالُو ۤ اْ أَقْرَرَْ قَالَ فَٱشْهَدُواْ وَأََْ مَعَكُمْ مِّنَ ٱلش َّاهِدِينَ ﴾
Wa-idh akhadha Allahu meethaqa alnnabiyyeena lama ataytukum min kitabin
wahikmatin thumma jaakum rasoolun musaddiqun lima maAAakum latu/minunna
bihi walatansurunnahu qala aaqrartum waakhadhtum AAala dhalikum isree qaloo
aqrarna qala faishhadoo waana maAAakum mina alshshahideena(Surat Al Imran
3:81).
Tafsir: Na kumbuka tulipochukua Ahadi kutoka kwa Manabii tukiwaambia:
‘Chukueni kile tunachokupeni kutoka katika Kitabu na Hikma, na kisha atakuja
baada yenu Mtume atakaesadikisha mlichokuja nacho. Hivyo ni lazima juu yenu
Kumuamini na Kumsaidia; Allah akasema: Hivi Jee mnakubali na Makubaliano
yangu? Nao (Mitume) wakasema: ‘Tumekubali’ nae (Allah Subhanah wa Ta’ala)
Akasema: ‘Basi Shuhudieni, na Mimi nipo pamoja nanyi kua ni miongoni mwa mwa
Wanaoshuhudia’’
Kua Sifa zake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam zinajulikana na Watu wa Ahl
ul Kitab kama zinavyosema aya:
718
ُ
﴿وَلَم َّا جَآءَهُمْ كِتَابٌ مِّنْ عِندِ ٱهلل َِّ مُصَدِّقٌ لِّمَا مَعَهُمْ وَكَانُواْ مِن قَبْل
يَسْتَفْتِحُونَ عَلَى ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ فَلَم َّا جَآءَهُمْ م َّا عَرَفُواْ كَفَرُواْ بِهِ فَلَعْنَةُ ٱهلل َِّ عَلَى
ٱلْكَافِرِينَ ﴾
Walamma jaahum kitabun min AAindi Allahi musaddiqun lima maAAahum
wakanoo min qablu yastaftihoona AAala alladheena kafaroo falamma jaahum ma
AAarafoo kafaroo bihi falaAAnatu Allahi AAala alkafireena (Surat Al Baqarah,
2:89).
Tafsir: Na (Mayahudi na Wakristo) kilipowajia Kitabu kutoka kwa Allah chenye
kuthibitisha juu ya vile walivyokua navyo wao, ingawa hapo kabla walikua wakiomba
ushindi juu ya wale waliokua wakikufuru, na kisha kilipowajia kile wanachokijua
wakakufuru juu yake hivyo laana ya Allah iwe juu ya Makafiri.
Na pale ziliposema aya kuhusiana na kujulikana kwake Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam na watu wa Ahl ul kitab kua:
﴿ٱل َّذِينَ آتَيْنَاهُمُ ٱلْكِتَابَ يَعْرِفُونَهُ كَمَا يَعْرِفُونَ أَبْنَاءَهُمْ وَإِن َّ فَ رِيقاً مِّنْهُمْ
لَيَكْتُمُونَ ٱلحَْق َّ وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴾
Alladheena ataynahumu alkitaba yaAArifoonahu kama yaAArifoona abnaahum
wa-inna fareeqan minhum layaktumoona alhaqqa wahum yaAAlamoona (Surat al-
Baqarah, 2:146).
Tafsir: Wale ambao tumewapa Kitabu wanamjua (Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam) kama wanavyowajua Watoto wao na kwa hakika baadhi miongoni mwao
wanauficha ukweli wakati wanaujua ukweli.
Kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Naapa kwa yule ambae
mkono wake uko kwenye Roho yangu, hakuna Mkristo wala Yahudi wa Ummah
huu atakaesikia kuhusiana nami na kisha akafa bila ya kuamini juu ya ujumbe
wangu, isipokua atakua ni Mtu wa Motoni’(Sahih Muslim)
Kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakutumwa kwa Ibn Adam tu bali pia
hata kwa Majini kama zinavyosema Aya:
719
﴿وَإِذْ صَرَفْنَآ إِلَيْكَ نَفَراً مِّنَ ٱلجِْنِّ يَسْتَمِعُونَ ٱلْقُرْآنَ فَلَم َّا حَضَرُوهُ قَالُو ۤ اْ أَنصِتُ واْ
فَلَم َّا قُضِىَ وَل َّوْاْ إِلىَٰ قَوْمِهِم م ُّنذِرِينَ ﴾
Wa-idh sarafna ilayka nafaran mina aljinni yastamiAAoona alqur-ana falamma
hadharoohu qaloo ansitoo falamma qudiya wallaw ila qawmihim mundhireena
(Surat al-Akhaf 46:29)
Tafsir: Na kumbuka (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) tulipokutumia
wewe kwa Kikundi cha Majini kusikiliza Qur’an, na kisha walipohudhuria wakasema:
‘Kaeni Kimya’ na ilipomalizika wakarudi kwa Jamii yao huku wakiwa Wausiaji.
Kua wake zake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ni Mama wa Waumini kama
zinavyosema Aya:
﴿ ٱلن َّبىِ ُّ
أَوْ لىَٰ بِٱلْمُ ؤْ مِ نِينَ مِ نْ أَنْفُسِ هِ ْم
وَأَزْوَاجُهُ أُم َّهَاتُهُ ْم﴾
Alnnabiyyu awla bialmu/mineena min anfusihim waazwajuhu ommahatuhum
(Surat Al Ahzab 33:6).
Tafsir: ‘Nabii yuko karibu na Waumini kuliko wao na Nafsi zao, na wake zake ni
mama zao (kwa waumini, kuwaheshimu na kutowaoa)’
Kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amesamehewa Dhambi zake zote
zilizotangulia hapo kabla yake na zilizofuatia baada yake:
﴿لِّيَغْفِرَ لَكَ ٱهلل َُّ مَا تَقَد َّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا أتََخ َّرَ وَيُتِم َّ نِعْمَتَ هُ عَلَيْكَ وَيَهْدِيَكَ
صِرَاطاً م ُّسْتَقِيماً ﴾
Liyaghfira laka Allahu ma taqaddama min dhanbika wama taakhkhara
wayutimma niAAmatahu AAalayka wayahdiyaka siratan mustaqeeman (Surat Fath
48:2)
720
Tafsir: Amekusamehe (Wewe Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam) Allah katika
yaliyopita Katika Dhambi zako na yatakayokuja, na amekamilisha Neema yake juu
yako na amekuongoza katika njia iliyonyooka.
Kua ameahidiwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua Dini yake aliyokuja
nayo itakua juu na kuhifadhiwa:
﴿هُوَ ٱل َّذِي ۤ أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِٱلهُْدَىٰ وَدِينِ ٱلحَْقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى ٱلدِّينِ كُلِّهِ وَلَوْ كَرِهَ
ٱلْمُشْرِكُونَ ﴾
Huwa alladhee arsala rasoolahu bialhuda wadeeni alhaqqi liyudhhirahu AAala
alddeeni kullihi walaw kariha almushrikoona (Surat al-Tawbah, 9:33)
Tafsir: Ni yeye ndie ambae aliemtuma Mtume wake na Uongofu na Dini ya Haki
ambayo inajidhidhirisha juu ya Dini zote, japo kua inawakirihisha Makafiri.
Kua Malaika walikua ni wenye kumsaidia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kila mara inapohitajika:
﴿قَدْ كَانَ لَكُمْ آيَةٌ فىِ فِئَتَينِْ ٱلْتَقَتَا فِئَةٌ تُقَاتِلُ فىِ سَبِيلِ ٱهلل َِّ وَأُخْرَىٰ كَ افِرَةٌ
يَرَوْنَهُمْ مِّثْلَيْهِمْ رَأْىَ ٱلْعَينِْ وَٱهلل َُّ يُؤَيِّدُ بِنَصْرِهِ مَن يَشَآءُ إِ ن َّ فىِ ذٰلِكَ لَعِبْرَةً لِأُوْلىِ
ٱلأَبْصَارِ ﴾
Qad kana lakum ayatun fee fi-atayni iltaqata fi-atun tuqatilu fee sabeeli Allahi
waokhra kafiratun yarawnahum mithlayhim ra/ya alAAayni waAllahu yu-ayyidu
binasrihi man yashao inna fee dhalika laAAibratan li-olee al-absari(Surat Al Imran,
3:13).
Tafsir: Kwa hakika tayari (Katika vita vya Badr) imeshakujieni Dalili katika pande
mbili za Majeshi zilizokutana , ambapo Moja walikua wanapigana kwa ajili ya Allah
na pande nyegine kwa Ukafiri Wao (Waumini) Wameona Makafiri kwa macho yao
mara mbili zaid yao (Wingi wao) na Allah huwasaidia kwa ushindi wake yule amtakae.
Hakika katika haya kuna dalili kuna Somo kwa wale wenye kuona.
721
Kua Kumtii Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hua ni Kumtii Allah Subhanah
wa Ta’ala kama zinavyosema Aya:
﴿م َّنْ يُطِعِ ٱلر َّسُولَ فَقَدْ أَطَاعَ ٱهلل ََّ وَمَن تَوَلى َّ ٰ فَمَآ أَرْسَلْنَاكَ عَلَيْهِمْ حَفِيظاً ﴾
Man yutiAAi alrrasoola faqad ataAAa Allaha waman tawalla fama
arsalnaka AAalayhim hafeedhan (Surat al-Nisa, 4:80).
Tafsir: Yule atakaemtii Rasul (Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi hua ni sawa na
mwenye)Kumtii Allah Subhanah wa Ta’ala na Mwenye kumpa mgongo basi
hatukukutuma wewe (Muhamamd Salallahu Alayhi wa Salam) kua ni Msimamizi wao.
Kua Ummah wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ndio Ummah bora Kuliko
Ummah zote kama zinavyosema Aya:
﴿كُنْتُمْ خَيْرَ أُم َّةٍ أُخْرِجَتْ لِلن َّاسِ أتَْمُرُونَ بِٱلْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ ٱلْمُنْكَرِ
ت َو ُؤْمِنُو نَ بِٱ آ هلل َِّوَلَوْ أ َ مَنَ هْلُ ٱلْكِتَابِ لَكَانَ خَيرْ اً له َُّمْ مِّنْهُمُ ٱلْمُؤْمِنُونَ وَأَكْثَرُهُ مُ
ٱلْفَاسِ قُونَ ﴾
Kuntum khayra ommatin okhrijat lilnnasi ta/muroona bialmaAAroofi
watanhawna AAani almunkari watu/minoona biAllahi walaw amana ahlu alkitabi
lakana khayran lahum minhumu almu/minoona waaktharuhumu alfasiqoona
(Surat Al Imran 3:110).
Tafsir: Hakika Nyinyi ndio Umma Bora uliotokana na Watu, kwani mnaamrishana
Mema na kukatazana Mabaya na Mnamuamini Allah na lau kama wangeamini watu
wa Ahli Kitabu ingekua bora kwao, kwani miongoni mwao kuna baadhi wenye Imani.
Kua Uhai wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam umeapiwa Ndani ya Qur’an
kama zinavyoonesha Aya:
﴿لَعَمْرُكَ إِن َّهُمْ لَفِى سَكْرَهتِِمْ يَعْمَهُونَ ﴾
722
LaAAamruka innahum lafee sakratihim yaAAmahoona (Surat Al-Hijr, 15:72)
Tafsir: Kwa Hakika Naapa kwa Uhai wako, kua Katika kuchanganyikiwa kwao
wamekua ni wenye kutojua wanaeleeka wapi.
Kua Mji wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam umeapiwa Ndani ya Qur’an
kama zinavyoonesha Aya:
﴿ بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰ نِ ٱلر َّحِ يمِ۞لاَ أُقْسِ مُ هبَِٰذَا ٱلْبَلَدِ۞وَأَنتَ حِ ل ٌّ هبَِ ٰذَا ٱلْبَلَدِ ﴾
Biismi Allahi AlrRahmani AlrRahim; La oqsimu bihadha albaladi; Waanta hillun
bihadha albaladi (Surat al-Balad, 90:1-3)
Tafsir: Kwa Jina La Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma, Hakika mimi
Nnaapa kwa Mji huu; Nawe uko huru katika Mji huu.
Kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Ummah wake umejaaliwa Usiku wa
Laylat ul Qadr kama zinavyoonesha Aya:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞إِ َّ أَنزَلْنَاهُ فىِ لَيْلَةِ ٱلْقَدْرِ۞وَمَ آ أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ
ٱلْقَدْرِ۞لَيْلَةُ ٱلْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ۞تَنَز َّلُ ٱلْمَلاَئِكَةُ وَٱلر ُّوحُ فِيهَا إبِِذْنِ رَهبِِّم
ّ ل أَمْ رٍ۞سَلاَمٌ هِىَ حَتى َّ ٰ مَطْلَعِ ٱلْفَجْرِ ﴾
مِّ ن كُ ِ
Biismi Allahi AlrRahmani AlrRahim Inna anzalnahu fee laylati alqadri; Wama
adraka ma laylatu alqadri; Laylatu alqadri khayrun min alfi shahrin; Tanazzalu
almala-ikatu waalrroohu feeha bi-idhni rabbihim min kulli amrin; Salamun hiya
hatta matlaAAi alfajri (Surat Al Qadr 97:1-6)
Tafsir: Kwa Jina La Allah Mwingi wa Rehema mwingi wa Huruma, Hakika
tumeishusha (Qur’an) ndani ya usiku wa Al Qadr; Na jee ni nini kitakachokujuulisha
ni nini huo Usikua wa Al Qadr?; Usiku wa Al Qadr ni bora kuliko Miezi Alfu Moja;
Ndani yake anashuka Malaika na Ruhi kwa Idhini ya Mola wake juu ya kila kitu;
Usalama hutawala ndani yake hadi inapoingia Alfajir.
723
Ambapo mbali ya kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam amejaaliwa Miujiza ya
Usiku wa Laylat ul Qadr unaowakilisha kushushiwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kitabu kitukufu cha Qur’an lakini pia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alijaaliwa Laylat ul Miraj ambao ni Usiku unaowakilisha kupandishwa kwake Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutoka ardhini kuelekea Mbinguni kwa Allah Subhanah
wa Ta’ala.
SAFARI YA ISRA NA MIRAJ.
Mnamo Mwaka wa 9 wa Uislam Allah Subhanah wa Ta’ala alimpandisha Mtume wake
Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam Mbinguni katika Usiku unaojulikana kua kama
Usiku wa Miraj ambamo ndani yake mlitokea tukio ambalo Allah Subhanah wa Ta’ala
analithibitisha na kulielezea katika Sura mbili tofauti ambapo moja wapo ni ile
inayojulikana kama Surat Al Isra au pia kama Surat Bani Israil ambamo ndani yake
limeelezewa tukio la safari ya Isra ambayo ilifanyika katika Mazingira ya Ulimwengu
Unaoonekana na Ibn Adam yaani Alam Al Mulk wa Al Shahadah kwa kusema:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰ نِ ٱلر َّحِ يمِ۞ سُبْحَانَ ٱل َّذِى أَسْرَىٰ بِعَبْدِهِ لَيْلاً مِّنَ ٱلْمَ سْجِ دِ
ٱلحَْرَامِ إِلىَٰ ٱلْمَسْجِ دِ ٱلأَقْصَى ٱل َّذِى ابَرَكْنَا حَوْلَهُ لِنُرِيَهُ مِنْ آَتِنَآ إِن َّهُ هُوَ ٱلس َّمِ يعُ
ٱلبَصِيرُ ﴾
Bismi Allahi Alrrahmani Alrrahim; Subhana alladhee asra biAAabdihi laylan mina
almasjidi alharami ila almasjidi al-aqsa alladhee barakna hawlahu linuriyahu min
ayatina innahu huwa alssameeAAu albaseeru (Surat Al Isra 17:1)
Tafsir: Utukufu ni wake yule ambae amemsafirisha Usiku Mja wake katika Usiku
kutoka katika Masjid Al Haram kueleka katika Masjid Al Aqsa ambao ameyabariki
maeneo yake kwa ajili ya kumuonesha Dalili zetu, kwani kwa hakika yeye ni mwingi
wa kusikia na ni mwenye kuona juu ya kila kitu.
Neno Asra linatokana na neno Sara ambalo hua linamaanisha Kusafiri katika wakati wa
Usiku, hivyo neno Asra hua linamaanisha Yule ambae aliemfanya Mtu asafiri Usiku.
Ambapo kwa upande wa Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari basi yeye
anahoji kwa kusema : ‘Hivi kwa nini Allah Subhanah wa Taa’ala akatumia neno
Laylan ambalo ni lenye kumaanisha Usiku wakati tayari aya imetumia neno Asra
ambalo linamaanisha kutembea Usiku? Hivyo jibu la suali hili ni kua kusisitiza
724
kuhusiana na hii Safari ambayo kawaida hua ni ya Miezi kadhaa lakini hii ilitokea
ndani ya sehemu ya Usiku mmoja tu’
Ambapo kuhusiana na Masjid Al Haram umeitwa hivyo kwa sababu ndani ya eneo lake
mna mambo ambayo yameharamishwa lakini nje yake na sehemu nyengine basi
yamehalalishwa kufanyika kwa mfano, Hairuhusiki ndani yake Kuingia asiekua
Muislam, Kung’olewa majani, Kukata miti, na Kuwinda Wanyama ndani ya eneo la
Masjid Haram hua hakuruhusiki.
Ama kwa upande wa Masjid Al Aqsa basi umeitwa hivyo kwa sababu upo katika ardhi
ya Jersualem ambayo ni Ardhi Takatifu ambayo ipo mbali kimasafa kutoka katika Masjid
Al Haram.
Ambapo aya imetumia pia neno Abd ambalo hua linamaanisha Mja na hivyo kumaanisha
kua Safari hio ilifanyika kwa Kimwili na Kiroho ambapo ndio pia neno lililotumika
kwenye tukio la pili ndani ya Usiku huu ni lile la safari ya kuanzia kwenye Masjid Al
Aqsa kuelekea Mbinguni ambalo linajulikana kama tukio la safari ya Miraj.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipowasili katika Ardhi ya Bayt Al
Maqdis ambapo alikutana na Mitume wote waliotangulia hapo kabla na kisha
akawasalisha ndani ya Msikiti huo wa Al Aqsa na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kua ni mwenye kudhihirisha kua Dini ya Kiislam ndio Dini ya asili, ya
Mwanzo na ya Mwisho na ya Ulimwengu mzima, tangu mwanzo wa kuumbwa
kwake hadi mwisho wake Ulimwengu huu.
Ambapo anasema Allamah Badr Ad Din Al Ayni Al Hanafi kua: ‘Tunapoangalia suali
la kwanini Nabii Ibrahim akawa ni Nabii Pekee alietajwa kwenye Sala (katika
Attahiyat) basi jibu lake ni kua: ‘Katika Usiku wa Miraj, Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alikutana na Mitume wote, na akawasalimia, lakini hakuna Mtume
ambae alirudisha Salam kwa Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam huku
akimjumuishia Umma wake wote isipokua Nabii Ibrahim, na hivyo basi ndio maana
Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam akauamrisha Ummah wake Kumsalia Nabii
Ibrahim kutokana na ukarimu wake huo kwa Ummah wake. ’’
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akapelekwa katika Hatim Sharif
akapokewa na Hur Layn ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliwasalimia
na kisha nao wakamrudishia Salam hio, kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akashushiwa Ngazi ambayo ni hakuna kiumbe aliewahi kuona kitu kizuri kama hicho,
ambacho kina vidaraja vilivyopishana vya Dhahabu na Fedha, na kua ni yenye kushuka
moja kwa moja kutoka Peponi huku ikiwa imezungushiwa mapambo ya Lulu na Malaika
kushoto na kulia.
725
Ambapo anasema Imam Muhammad Ibn Is-haq kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam amesema kua: ‘Ngazi iliyoshushwa kwangu mie ilikua ni nyororo kuliko kitu
chochote kile nilichowahi kukiona, kwani ndio kitu anachokiangalia Mtu pale
anapotolewa roho.’’
Ambapo tunapoangalia mapambo haya ya Dhahabu na Fedha basi tunaona kua haya ni
Madini ambayo yana sifa za upekee katika usafirishaji wa nguvu za Umeme, ambapo
Fedha ndio Madini yenye kutegemewa kwa kua na asilimia 105% ya kasi ya usafirishaji
wa nguvu ya Umeme, na upekee wa urudishaji wa Nuru wa hali ya juu kabisa, na hii hua
ni kutokana na kutoshikamana kwa elektroni zake ambao unazifanya ziwe huru na
kurahisisha zaidi usafirishaji wa Nguvu za Umeme.
Ambapo kwa upande wa Dhahabu basi ni Madini yanayoongoza kwa Umakini wa
Kutopoteza nguvu za Umeme, na ndio maana hua inatumika katika viunganisho vya
mifumo ya vifaa mbali mbali vya Umeme na chenye kuchukua sehemu ya tatu katika
usafirishaji wa umeme baada ya Shaba kwa kua na uwezo wa kusafirisha kwa kasi ya
asilimia 70%.
Hivyo mchanganyiko huu wa Madini haya katika kupitisha na kusafirisha kwake nguvu
ya Umeme au pia nguvu ya Nuru yameufanya mfumo wa Ngazi hio ya Miraj kua na
upekee wa kasi ya Usafirishaji wake, yaani hali yake inakua kama vile ukiigusa tu basi
Umefika.
Ambapo neno Miraj hua linamaanisha Ngazi au Kipandio cha Kuelekea Juu ambapo
tukio la safari hii nalo limeelezewa kwenye aya za Surat An Najm ambazo zinasema kua:
ٰ ﴿فَأَوْحَى إِلىَٰ عَبْدِهِ مَآ ٰ أَوْحَى۞ مَا كَذَبَ ٱلْفُؤَادُ مَا رَأَىٰ ۞ أَفَتُمَ ارُونَ هُ ٰ عَلَى مَا
وَلَقَدْ رَآهُ نَزْلَةً أُخْرَىٰ ۞ عِن دَ سِ دْ رَةِ ٱ ن ت لُْم َ هَ ٰ ى ۞ عِندَهَا جَن َّةُ ٱلْمَأْوَىٰ ۞ إِْذ
يَغْشَىٰ ٱلسِّ دْرَةَ مَا ٰ يَغْشَى۞ مَا زَاغَ ٱلْبَصَرُ وَمَا ٰ طَغَى۞ لَقَدْ رَأَىٰ مِنْ آَ تِ رَبِّهِ
ٱلْكُبْرَىٰ ﴾
يَرَىٰ ۞
Faawha ila AAabdihi ma awha; Ma kadhaba alfu-adu ma raa; Afatumaroonahu
AAala ma yara; Walaqad raahu nazlatan okhra; AAinda sidrati
almuntaha; AAindaha jannatu alma/wa; Idh yaghsha alssidrata ma yaghsha; Ma
zagha albasaru wama tagha; Laqad raa min ayati rabbihi alkubra (Surat An Najm
53:10-18)
726
Tafsir: Hivyo akamshushia Mja wake kile alichomshushia, Hakikadhibishi Kifua
chake kutokana na aliyoyaona. Hivi Jee mtabishana nae (Muhammad Salallahu
Alayhi wa Salam) Juu ya kile alichokiona? (Katika Safari ya Miraj); Na bila ya shaka
alimuona tena katika mteremko wa Pili; Karibu na Sidrat Ul Muntaha (Mti ambao
ndio Mpaka wa eneo ambalo haiwezekani kwa kiumbe yeyote kusogea Mbele yake);
Karibu yake ambapo kuna Makaazi ya Pepo (Katika Upande wa Kulia wa Arshi
Tukufu); Wakati pale kilichoufunika Mti wa Sidrat Al Muntaha kilipoufunika;
Haukugeuka Mtizamo (wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam) wala haukuvuka
mpaka; Kwani kwa Hakika ameona (Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam) Katika
Dalili zetu Kubwa sana.
Ambapo tunapoziangalia aya hizi basi tunaona kua zinazungumzia namna ya hali
ilivyokua wakati Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam alipokua katika kumuona
kwake Malaika Jibril na katika Safari ya Miraj ambayo ilifanyika katika Mazingira ya
kuingia ndani ya Ulimwengu Usiionekana na Viumbe Ibn Adam bali Unaonekana na
Viumbe Malaika yaani Al Alam Ghayb wa Al Malakut ambapo anasema Masruq Abu
Aisha kua: ‘Hakika mimi nilikua nimekaa na Aisha ambae alikua ameegemea na
akasema: ‘Ewe Abu Aisha, kuna mambo matatu ambayo kama mtu
atayazungumzia basi atakua ni mwenye kumzulia Allah Subhanah wa Ta’ala’ hivyo
nami nikauliza : ‘Ni Yepi Hayo?’’
Nae akasema: ‘Yeyote yule atakaesema kua Muhammad (Salallahu Alayhi wa
Salam) amemuona Allah Subhanah wa Ta’ala basi amesema uongo kuhusiana na
Allah Subhanah wa Ta’ala’ hivyo nami nikakakaa vizuri kisha nikauliza: ‘Ewe Ummu
Ul Muuminin, niruhusu niseme, usiwe na haraka, hivi Jee Allah Subhanah wa Ta’ala
hakusema kua:
﴿وَلَقَدْ رَآهُ بِٱلأُفُقِ ٱلْمُبِينِ ﴾
Walaqad raahu bialofuqi almubeeni (Surat At Takwir 81:23)
Tafsir: Kwa Hakika alimuona katika Upeo wa Macho ulio wazi
Na pia hakusema kua:
﴿وَلَقَدْ رَآهُ نَزْلَةً أُخْ رَىٰ ﴾
Walaqad raahu nazlatan okhra; (Surat An Najm 53:13)
Tafsir: Na bila ya shaka alimuona tena katika mshuko wa Pili;?
727
Hivyo Aisha Radhi Allahu Anha akasema: ‘Hakika mimi ndie mtu wa mwanzo katika
Ummah huu kumuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, kuhusiana na hayo
ambapo nae akasema: ‘Huyo alikua ni Jibril, nami sikumuona katika maumbile
yake aliyoumbiwa isipokua mara mbili, na nilimuona akishuka kutoka Mbiguni,
huku akiwa amefunika Upepo wote wa Macho baina ya Mbingu na Ardhi.’’
Na kisha Aisha Radhi Allahu Anha akasema: ‘Hivi jee wewe hujawahi kusikia maneno
ya Allah yasemayo?’
﴿لا َّ تُدْرِكُهُ ٱلأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ ٱلأَبْصَارَ وَهُوَ ٱلل َّطِيفُ ٱلخَْبِيرُ ﴾
La tudrikuhu al-absaru wahuwa yudriku al-absara wahuwa allateefu alkhabeeru
(Surat Al Anaam 6:103)
Tafsir: Haiwezekani kumfikia Mtizamo wa Macho, lakini yeye ni mwenye kuona kila
kitu, kwani yeye ni Mpole na mwenye habari juu ya kila kitu.
Na pale aliposema:
﴿وَمَا كَانَ لِبَشَرٍ أَن يُكَلِّمَهُ ٱهلل َُّ إِلا َّ وَحْياً أَوْ مِن وَرَآءِ حِ جَابٍ أَوْ يُرْسِ لَ رَسُولاً
فَيُوحِ ىَ إبِِذْنِهِ مَا يَشَآءُ إِن َّهُ عَلِي ٌّ حَكِيمٌ ﴾
Wama kana libasharin an yukallimahu Allahu illa wahyan aw min wara-i hijabin
aw yursila rasoolan fayoohiya bi-idhnihi ma yashao innahu AAaliyyun hakeemun
(Surat Shura 42:51)
Tafsir: Na kamwe haiwezekani kwa Allah kuzungumza na Mtu yeyote isipokua kwa
njia ya Wahyi, au kwa Pazia, au kwa Kumtumia Mjumbe kufikisha Ujumbe kwa Idhini
yake juu ya kile akitakacho, kwani kwa hakika yeye ni mwenye Utukufu na ni mwingi
wa Hikma.
Na pia kua:
﴿يَۤ أَي ُّهَا ٱلر َّسُولُ بَلِّغْ مَآ أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن ر َّبِّكَ وَإِن لم َّْ تَفْعَلْ فَمَا بَل َّغْتَ رِسَالَ تَهُ
وَٱهلل َُّ يَعْصِمُكَ مِنَ ٱلن َّاسِ إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يَهْدِى ٱلْقَوْمَ ٱلْكَافِرِينَ ﴾
728
Ya ayyuha alrrasoolu balligh ma onzila ilayka min rabbika wa-in lam tafAAal fama
ballaghta risalatahu waAllahu yaAAsimuka mina alnnasi inna Allaha la yahdee
alqawma alkafireena (Surat Al Maidah 5:67)
Tafsir: Ewe Mtume fikisha kama ulivyoshushiwa kutoka kwa Mola wako, kwani kama
hukufanya hivyo basi utakua hukufikisha Ujumbe wake, na Allah atakulinda
kutokana na Watu, Kwa hakika Allah hawaongoi watu wenye kukufuru.
Na kisha Aisha Radhi Allahu Anha akasema: ‘Hivyo yeyote yule atakaemsingizia
Mtume Salallahu Alayhi wa Salam alikua anajua kitakachotokea kesho, basi
amesema uongo kuhusiana na Allah Subhanah wa Ta’ala, kwani Allah Subhanah
wa Ta’ala amesema kua:
﴿قُل لا َّ يَعْلَمُ مَن فىِ ٱلس َّمَاواتِ وٱلأَرْضِ ٱلْغَيْبَ إِلا َّ ٱهلل َُّ وَمَا يَشْعُرُونَ أَ َّنَ
يُبْعَثُونَ ﴾
Qul la yaAAlamu man fee alssamawati waal-ardhi alghayba illa Allahu wama
yashAAuroona ayyana yubAAathoona (Surat An Naml 27:65)
Tafsir: ‘Sema, Hakuna anaejua yaliyomo Mbinguni na Ardhini yaliyofichikana
ispokua Allah na hakuna anaeona na kujua lini watafufuliwa.
Ambapo amesema Abu Dhar Al Ghifari Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi nilimuuliza
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hivi Jee Ulimuona Mola wako?’ nae
akajibu: ‘Yeye ni Nuru, Hivyo Jee nitamuonaje?’’(Sahih Muslim)
Na kwa upande wa Al Hafidh Imam Abu Hatim Abd Rahman Muhammad Ibn Idris Al
Razi Ibn Hibban Al Basti basi yeye anasema kua: ‘Muhammad Ibn Kaab Radhi Allahu
Anhu amesema kua, wao walimuuliza Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam:
‘Hivi Jee ulimuona Mola wako?’ ambapo nae akasema: ‘Naam nilimuona mara
mbili kwa Mtizamo wa Moyo wangu.’ Na kisha akasoma aya isemayo:
﴿مَا كَذَبَ ٱلْفُؤَادُ مَا رَأَىٰ ﴾
Ma kadhaba alfu-adu ma raa; (Surat An Najm 53:11)
Tafsir:Hakikadhibishi Kifua chake kutokana na aliyoyaona.
729
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala alimchukua Mtume wake Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam katika safari ya Isra na Miraj na kumsafirisha ndani ya sehemu ya
Usiku mmoja kutoka katika Masjid Al Haram kuelekea Masjid Al Aqsa na kisha
kumpandisha Juu Mbinguni kwa ajili ya kumuonesha Miujiza Mikubwa sana yaani
Ayati Al Kubra.
Ambapo anasema Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abdallah Al Tustari Al Shafii
kuhusiana na Ayati Al Kubra kua: ‘Hizi ni miongoni mwa Dalili zake zinazodhihirika
kutokana na Dalili zake, na ingawa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliziona,
lakini hakuteteresha mtizamo wake kutokana na anachokishuhudia, na hakutoka
katika eneo la mwenye kuabudiwa, bali kile alichokiona kilikua ni chenye
kumzidishia Mapenzi (Mahabba) yake, Kutamani (Shawq) kwake na Uwezo
(Quwwa) wake.
Kwani Allah Subhanah wa Ta’ala alimpa Uwezo ambao ulimuwezesha kustahmili
muonekano wa Nuru yake, na hivyo hii kua ni sehemu ya Kumpandisha Darja na
kumpendelea Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam zaidi ya Mitume wengine, hivi
Jee hukuona wewe namna Nabii Musa alipozimia kutokana na Muonekano wa
Allah, lakini kwa Muhamamd Salallahu Alayhi wa Salam alistahmili wakati Nuru
hio ilipopita ndani ya Ufaham wake katika kuonana na Mola wake kupitia katika
Mtizamo wa Moyo wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hapo hapo
kutokana na hali ya Uwezo wake na hivyo akapandishiwa hali ya Darja yake.’
Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abdallah Al Tustari Al Shafii anaendelea kusema kua:
‘Imenifikia mimi kua Allah Subhanah wa Ta’ala alimwambia Nabii Daud kua:
‘Hakikisha kua hughafiliki na mie kwani ikitokea hivyo basi utakosa kila kitu.
Kwani kwa hakika mimi nimemuumba Muhammad kwa ajili yangu, na
nimemuumba Adam kwa Ajili yake, na nimewaumba Viumbe wangu wanaoniamini
kwa ajili ya kuniabudu, na nimeumba kila kitu chengine kwa ajili ya manufaa ya
Ibn Adam, hivyo kama Ibn Adam akitumia mda wake kutokana na kile
nilichomuumbia kwa ajili ya Manufaa yake, basi nitamfunikia pazia juu ya kila kitu
ambacho nimekiumba kwa ajili yangu.’’
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Sultan Mutakalimin Imam Al Mushakikkin
Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisafiri
katika safari mbili, ambapo ya kwanza ni kutoka katika Masjid Al Haram
kuelekea katika Masjid Al Aqsa, na ya pili ni ya kipindi cha Safari ya kuelekea
Juu Mbinguni kwenye Ufalme wa Allah. Ambao huu ni mtizamo ambao
unabainisha yale yaliyotokea dhahiri’
Na tunapozungumzia kuhusiana na yale yaliyotokea kwa upande wa Kiroho
basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisafiri pia katika safari mbili
ambapo kwanza ni hali ya kusafiri kutoa kwenye Ulimwengu Unaoonekana (Al
Alam Al Shahadah) na kuingia kwenye Ulimwengu Usioonekana (Al Alam Al
730
Ghayb) ambapo Ulimwengu miwili hii imepakana ndani ya Masafa ya Baina ya
Mipinde Miwili, kama zilivyosema Aya.
﴿فَكَ انَ قَابَ قَوْسَ ينْ ِ أَوْ أَدْ نىَٰ ﴾
Fakana qaba qawsayni aw adna (Surat An Najm 53:9)
Tafsir: Na ilikua ni masafa ya Mipinde Miwili au karibu zaidi.
Hivyo Maneno Fakana qaba qawsayni aw adna hua ni yenye kumaanisha hali ya
Uteketezo wa Nafsi yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo Nafsi
hio kuingia katika hali ya kua na ukaribu sana kwa Mola wake.
Kwani darja ya chini kabisa ya Ulimwengu usioonekana hua ni ile ya Roho ya Ibn
Adam, na Roho ya Ibn Adam hua ni yenye kupanda juu kuanzia kwenye Mbingu
ya chini, na kisha kupanda zaidi kuelekea kwenye darja ukamilifu na furaha na
kisha huingia kwenye hali ya kiroho ya Mbingu ya pili, na kisha hufikia darja ya
wakaazi wa ngazi ya chini ya Arshi, na kisha hufikia Darja ya Malaika ambayo
ndio iliyozungumziwa kwenye aya isemayo:
﴿وَتَرَى ٱلْمَلاَئِكَةَ حَآفِّينَ مِنْ حَوْلِ ٱلْعَرْشِ يُسَبِّحُونَ بحَِمْدِ رَهبِِّمْ وَقُضِىَ بَيْنَ هُمْ
بِٱلحَْقِّ وَقِيلَ ٱلحَْمْدُ هللِ َِّ رَبِّ ٱلْعَالَمِينَ ﴾
Watara almala-ikata haffeena min hawli alAAarshi yusabbihoona bihamdi
rabbihim waqudhiya baynahum bialhaqqi waqeela alhamdu lillahi rabbi
alAAalameena (Surat Az Zumar 39:75)
Tafsir: Na Utawaona Malaika wakiwa wanazunguka Arshi katika pande zote,
wakimtukuza na kusifu sifa za Mola wao, na (Viumbe wote) watahukumiwa kwa haki
na kisha itasemwa: ‘Sifa zote na Shukrani zote anastahiki Mola wa Ulimwengu’
Na kisha Roho ya Ibn Adam inafika inapanda juu na kufikia darja ya Malaika
waliozungumziwa kwenye aya ifuatayo:
﴿وَٱلْمَلَكُ عَلَى ٰ أَرْجَآئِهَآ وَيحَْمِلُ عَرْشَ رَبِّكَ فَوْقَهُمْ يَوْمَئِذٍ ثمََانِيَةٌ ﴾
Waalmalaku AAala arja-iha wayahmilu AAarsha rabbika fawqahum yawma-idhin
thamaniyatun. (Surat Al Haqqah 69: 17).
Tafsir: Na Malaika watakua pembeni mwake na wataibeba Arshi juu yao watakua
Wanane.
731
Ambapo idadi ya nambari nane ina Siri yake ambayo haiwezi kufunguliwa hapa,
Na Roho ya Ibn Adam kisha inafika inapanda juu na kufikia darja ya Roho Tukufu
ambazo hazimo ndani ya Miili, ambazo vyakula vyao Roho hizo hua ni Dhikr Allah,
Vinywaji vyao hu ni Kumpenda Allah Subhanah wa Ta’ala, Starehe yao ni
Kumtumikia Allah Subhanah wa Ta’ala, na ukaribu wao ni Kumsifu Allah
Subhanah wa Ta’ala, hawa ndio wale Malaika waliotajwa kwenye aya zifuatazo:
﴿وَلَهُ مَن فىِ ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَمَنْ عِنْدَهُ لاَ يَسْتَكْ برُِونَ عَنْ عِبَادَ تِهِ وَلاَ
يَسْتَحْ سِ رُونَ۞ يُسَبِّحُونَ ٱلْل َّيْلَ وَٱلن َّهَارَ لاَ يَفْتُرُونَ ﴾
Walahu man fee alssamawati waal-ardhi waman AAindahu la yastakbiroona AAan
AAibadatihi wala yastahsiroona; Yusabbihoona allayla waalnnahara la
yafturoona(Surat Al Anbiyah 21:19-20)
Tafsir: Kwake yeye ndiko kwenye umiliki wa kila kilichoo Mbinguni na Ardhini. Na
wale waliokaribu nae hawana Kiburi cha kutomuabudia yeye si wenye kuchoka katika
Ibada zao; Wanamtukuza Usiku na Mchana bila ya kupumzika.
Ambapo hii hua ni darja ambayo Ufahamu wa Ibn Adam kamwe hauwezi kufahamu hali
yake, na kupanda kwake Roho inapofika katika Darja hii hua ni kwenye kuendelea hadi
pale inapomfikia Muumba, ambae ni Nuru juu ya Nuru, Sababu ya kila Sababu, Mwanzo
wa kila kitu, Chanzo cha Rehma, Asili ya kila Jema kama inavyobainishwa na Aya
isemayo:
ّ كُل ذِى عِلْمٍ عَلِيمٌ ﴾
﴿وَفَوْقَ ِ
Wafawqa kulli dhiAAilmin AAaleemun(Surat Yusuf 12:76)
Tafsir: Na Kwa kila alie juu kwa Ilm, basi kuna ajuae zaid.
Wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipopandishwa Juu Mbinguni basi
alisoma aya ya mwisho ya Surat Al Baqara isemayo:
﴿لاَ يُكَلِّفُ ٱهلل َُّ نَفْساً إِلا َّ وُسْعَهَا لهََا مَا كَسَبَتْ وَعَلَيْهَا مَا ٱكْتَسَبَتْ رَب َّنَا لاَ
تُؤَاخِ ذَْ إِن ن َّسِ ينَآ أَوْ أَخْطَأَْ رَب َّنَا وَلاَ تحَْمِلْ عَلَيْنَآ إِصْراً كَمَا حمََلْتَهُ عَلَى ٱل َّذِي َن
732
مِن قَبْلِنَا رَب َّنَا وَلاَ تحَُمِّلْنَا مَا لاَ طَاقَةَ لَنَا بِهِ وَٱعْفُ عَن َّا وَٱغْفِرْ لَنَا وَٱرْحمَْنَآ أَن َت
مَوْلاََ فَٱنْصُرَْ عَلَى ٱلْقَوْمِ ٱلْكَافِرِينَ ﴾
La yukallifu Allahu nafsan illa wusAAaha laha ma kasabat waAAalayha ma
iktasabat rabbana la tu-akhidhna in naseena aw akhta/na rabbana wala tahmil
AAalayna isran kama hamaltahu AAala alladheena min qablina rabbana wala
tuhammilna ma la taqata lana bihi waoAAfu AAanna waighfir lana wairhamna
anta mawlana faonsurna AAala alqawmi alkafireena.(Surat Al Baqara 2:286)
Tafsir: Haikalifishi Allah Nafsi (ya mtu yeyote)isipokua juu ya kile inachokiweza,
inalipwa (Nafsi ya Mtu) kutokana na (mema) iliyoyachuma na itaadhibiwa kutokana
na (dhambi) ilizozichuma. ‘Ewe Mola wetu Usituadhibu kutokana na tulichokisahau
au tulichokikosea. Ewe Mola wetu usitubebeshe mizigo kama ulivyowabebesha
waliotangulia kabla yetu. Ewe Mola wetu Usitubebeshe mizigo zaidi ya uwezo wetu,
Tusamehe na utuingize kweye Msamaha wako na utuingize kwenye Rehma zako kwani
wewe ndie Msimamizi wetu na tunusuru dhidi ya watu wenye kukufuru’
Na katika kutilia mkazo umuhimu wa Dua iliyomo ndani ya aya hii basi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam amesema kuhusiana na aya hii pamoja na ile kabla ya aya hii
yaani aya ya 285 ya Surat Al Baqara kua: ‘Hakika mimi nimepewa aya mbili ambazo
zilikuwemo kwenye hazina iliyomo chini ya Arshi, ambazo hakuwahi kupewa
Mtume yeyote yule hapo kabla.’
Na wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipokua akishuka kutoka Mbinguni
basi alisoma Surat al Fatiha ambayo nayo ni yenye aya 7:-
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞ٱلحَْمْدُ هللِ َِّ رَبِّ ٱلْعَالَمِينَ۞ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞مَٰلِكِ يَوْمِ
ٱلدِّينِ۞إِ َّ كَ نَعْبُدُ وإِ َّ كَ نَسْتَعِينُ۞ٱهْدَِ ٱلصِّرَاطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ۞
أَنْعَمْ تَ عَلَيْ هِمْ غَيرِْ ٱلْمَغْضُوبِ عَلَيْهِم وَلاَ ٱلض َّآلِّينَ ﴾
ِصرَاطَ ٱل َّذِينَ
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Alhamdu lillahi rabbi alAAalameena;
Alrrahmani alrraheemi; Maliki yawmi alddeeni; Iyyaka naAAbudu wa-iyyaka
nastaAAeenu; Ihdina alssirata almustaqeema; Sirata alladheena anAAamta
AAalayhim ghayri almaghdoobi AAalayhim wala aldhdhalleena (Surat Al Fatiha
1:1-7)
733
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma Mwingi wa Huruma; Shukrani zote
anastahiki Mola wa Ulimwengu wote na kila kilichomo ndani ndani yake; Mfalme wa
Siku ya Malipo, Ni wewe tu ndie tunaekuabudu na ni wewe tu tunaekuomba msaada;
Tuongoze kwenye njia iliyonyoooka; Njia ya wale ambao umewaneemesha, na wala
sio njia ya wale uliowaghadhibikia na wala sio ya wale waliopotea.
Hivyo katika tukio hili la Miraj katika kushuka kwake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam basi athari ya Nuru ya Rehma yake aya hizi za Surat Al Fatiha zilikua
zikimmiminikia na kumdhihirikia kutoka kwenye Ulimwengu wa Ghayb wa kiroho na
kuingia kwenye Ulimwengu wa Dhahir wa kimwili, hivyo kila mtu anaesoma Surat Al
Fatiha katika Sala basi hua ni mwenye kumiminikiwa na athari ya Nuru ya Rehma yake
kutoka kwenye Ulimwengu wa Ghayb kuingia kwenye Ulimwengu wa Dhahir kama
alivyomiminikiwa na kudhihirikiwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipokua
akirudi katika safari ya Miraj, na hivyo kua ni kiunganisho baina ya aina mbili hizo za
Ulimwengu na ndio maana akasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Sala
ndio Miraj ya Waumini.’
Ambapo kwa upande wa Imam Abu Bakr Ibn Abd Allah Ibn Muhammad Najm Al
Din Raz anasema kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua ni mwenye
Miujiza ya kusafiri kwa njia ya haraka na kuvuka mipaka ya kimaumbile na
kuingia kwenye hali ya mazingira ambayo waliishi Mitume waliotangulia hapo
kabla yake, huku kila mmoja wao Mitume hao akiwa ni mwenye kubakia
kwenye hali ya darja yake husika.
Kwa mfano: Nabii Adam ambae alikua kwenye darja yake ya hali ya kua
Aliechaguliwa, Nabii Nuh ambae alikua kwenye Darja yake ya Ukaribisho,
Nabii Ibrahim ambae alikua katika Darja yake ya Urafiki wa Karibu, Nabii
Musa ambae alikua kwenye Darja yake ya kua ni Mwenye Kuzungumza na
Allah, Nabii Isa Ibn Maryam ambae alikua kwenye Darja yake ya Kauli ya
Allah na Utambulisho, Nabii Daud akiwa kwenye Darja ya Ukhalifa na Nabii
Sulaiman akiwa kwenye Darja ya Ufalme.
Lakini kwa upande Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutokana na Rehma
za Mola wake na Msaada wake basi yeye alifanikiwa kuzipita Darja zote hote
hizo za Kiroho na kuingia kwenye hali ambayo hakuna Kiumbe aliewahi
kuruhusiwa kuifikia na hivyo kua ni mwenye kupewa heshima kubwa sana
ambayo hajawahi kupewa kiumbe yeyote yule hapo kabla.’ (Mirsad Al 'Ibad)
Hivyo kuhusiana na safari ya Isra na Miraj basi anasema Fakhta Ummu Hani Bint Abu
Talib kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alichukuliwa katika safari yake
ya Usiku akitokea kwangu mie ambapo alisali Sala zake za Usiku na kila Mtu
akaelekea Kitandani kulala, na katika siku ya pili yake, tukasali Nyuma yake,
na kisha baada ya Kusali akasema: ‘Ummu Hani, nimesali pamoja nanyi Sala
734
ya Isha kama mlivyoniona, na kisha nikaelekea Bayt Ul Maqdis nikasali ndani
yake na sasa hivi nimesali nanyi Alfajir kama mnavyoniona’(Imam Muhammad Ibn
Jarir At Tabari)
Katika kuelezea tukio lililotokea kabla ya Safari ya Miraj basi wanasema Masahaba
akiwemo Anas Ibn Malik Umar Ibn al-Khattab, Ali ibn Abi Talib, Abdallah Ibn Mas`ud,
Abd Allah Ibn `Abbas, Malik Ibn Sa`sa`, Abu Dharr Al Ghifari, Abu Hurayrah, Abu
Sa`id, Shaddad Ibn Aws, Ubay Ibn. Ka`b, Jabir, Hudhayfah Ibn Al Yaman, Buraydah,
Abu Ayyub Al Ansari, Samurah Ibn Jundab, Umm Hani’, `A’isha, Asma Radhi Allahu
Anhum katika Hadith zenye Maneno tofauti kua:
‘Usiku mmoja Malaika watatu walikuja kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam wakati akiwa amelala Msikitini, ambapo mmoja miongoni mwa Malaika
hao watatu akamuuliza Malaika mwengine kwa kusema: ‘Ndie yupi kati ya
hawa?’ na Malaika wa katikati miongoni mwao akasema: ‘Mchukueni aliebora
kuliko wote’ Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaona Malaika
hao tena katika Usiku wa Miraj huku akiwa katika hali Kulala lakini Moyo
wake ukiwa Macho, na hawakuzungumza nae, lakini walimchukua hadi kwenye
kisima cha Zamzam’
Alipofikishwa kwenye Kisima cha Zamzam basi akalazwa chini na kisha akashuka
Malaika Jibril ambae alimpasua Kifua chake ambapo : ‘Alisema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua : ‘Wakati niko kwenye Hatim nikiwa nimelala, akatokea
Mtu akanipasua kuanzia kwenye mfupa wa kifua hadi kitovuni akautoa Moyo
wangu na kisha ikatolewa sahani iliyojaa Imani na Moyo wangu ukakoshwa
kutokana nayo na kujazwa na kujazwa Hikma, kisha akaletwa Mnyama ambae
alikua ni mweupe na Mkubwa kuliko Punda na ni Mdogo kuliko Farasi’’
Ambapo huyu Mnyama alikua ni Buraq ambae alikua tayari ameshatayarishwa kwa
safari yake ya kumbeba Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa ajili ya Safari hio
ya Isra na Miraj.
MAUMBILE YA BURAQ NA MIUJIZA YA SAFARI YA ISRA NA
MIRAJ.
Neno Buraq linatokana na neno Barq ambalo ni lenye kutokana na neno Baraqa ambalo
hua linamaanisha Kushangaza, Kuchanganya, Kupigwa na Mshangao Mkubwa sana,
hivyo neno Barq hua linamaanisha Nuru au Mwangaza wa Radi pale inapopiga.
Ambapo amesema Imam Uthman Ibn Hasan Al Juwayri kua: ‘Safari ya Miraj
imesababishwa na Ardhi kua ni yenye kujiona dhidi ya Mbingu pale iliposema
735
kuziambia Mbingu kua: ‘Hakika Mimi ni mbora zaidi yako kwa sababu Allah
Subhanah wa Ta’ala, amenipamba mimi kwa Milima, Mimea, Bahari Mito na
Maziwa’’Ambapo Mbingu zikasema kua: ‘La Mimi ni bora kwa sababu Allah
Subhanah wa Ta’ala amenipamba kwa Jua, Mwezi, Sayari na Nyota’
Ardhi ikasema: ‘La, kwani mimi nna Baytu Allahi Al Haram Nyumba ambayo
Mitume na Manabii na Mawalii na Waumini hua wanafanya Tawwaf.’ Ambapo
Mbingu zikasema: ‘La Mimi nna Bayt Al Maamur Nyumba ambayo Malaika
wanafanya Tawwaf, nna na Pepo ambazo ndani yake Wanaishi Mitume, Manabii,
Mawalii na Waumini.’
Ardhi ikasema: ‘Kwa hakika Bwana wa Mitume, Alama ya Mitume, Kiumbe
anaependwa zaidi na Allah Subhanah wa Ta’ala, na Mbora wa Viumbe, Mkamilifu
wa Viumbe yuko Juu yangu na Mafunzo yake yanasomeshwa juu yangu.’ Kutokana
na hoja hii basi Mbingu zikaona kua zimeshindwa kihoja, hivyo nazo zikamuomba Allah
Subhanah wa Ta’ala kwa kusema: ‘Ya Allah, hakika wewe ni mwenye Kujibu
unaopoombwa, nami nimeshindwa dhidi ya hoja za Ardhi juu yangu hivyo
nakuomba kua Mpandishe juu kwangu Muhammad ili nami nipate heshima na
utukufu kama uliopata Ardhi kutokana nae.’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akayakubali maombi ya Mbingu na kisha akamwambia
Malaika Jibril: ‘Nenda Peponi kisha kamchukue Buraq, kisha kamchukue
Muhammad’ hivyo Malaika Jibril akaenda Peponi na akakuta kuna Buraq 40,000 ambao
wote wakiwa na Jina la Muhammad kwenye Paji la Uso wao, na miongoni mwao
akamuona Buraq mmoja akiwa anang’ara kichwani mwake lakini akiwa na hali ya
kutokwa na Machozi.
Hivyo Malaika Jibril akamsogelea Buraq Huyo na kumuuliza: ‘Ewe Buraq, Kwanini
umekua mnyonge na mwenye kulia?’
Buraq huyo akasema: ‘Ewe Jibril, hakika mimi nimeanza kulisikia Jina la
Muhammad kwa mda wa miaka 40,000 iliyopia, nami nimempenda mwenye Jina
hili na namtamani kumuona kwa mda mrefu sana’ hivyo Malaika Jibril akasema:
‘Hakika mimi nitakupelekea kwa yule umpendae.’ Hivyo Malaika Jibril akamchukua
Buraq huyo na kushuka nae Ardhini kwa Nabii Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam.
(Nuur Dhalam)
Buraq ni Mnyama wa Peponi mwenye miguu minne, si Mnyama Jike wala si Mnyama
Dume, Si Punda wala si Farasi na anapokimbia hua ni mwenye kutua hatua zake za miguu
yake ya mbele kwenye masafa ya upeo wa Jicho huku miguu yake ya nyuma ikiwa juu
ardhini, na ameitwa Buraq kwa sababu ya nguvu, uwezo na kasi yake ni zaidi ya kasi ya
736
Nuru ya Mwangaza wa Radi pale inapopiga na rangi yake ni Nyeupe ya Nuru ya
Muangaza.
Hivyo tunapomuangalia Buraq na sifa zake basi tunaona kua kama lilivyo jina lake na
kasi yake kua ni isiyoweza kufikirika kwani safari ya kutoka katika Mji wa Makkah hadi
Jerusalem ni yenye masafa ya kilomita 1500 ambayo kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam akiwa juu ya Buraq ilikua ni kufumba na kufumbua kama inavyopiga radi
kwani unaona kwanza na kisha ndio unasikia, na ukisikia basi ndio imeshafika.
Yaani hapa tunazungumzia kasi ya mahesabu ya ndani ya sehemu ya sekunde kwa masafa
hayo kwani hii hua ni Kasi ya Muangaza wa Jua ambayo hua ni Kilomita 300,000 kwa
sekunde, yaani kufumba na kufumbua, kama kilivyoletwa na Asif Ibn Barkhiya kiti cha
Malkia Bilqis mbele ya Nabii Sulayman.
Ambapo kwa upande wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi anatuambia
kua:‘Nikaambiwa nipande Buraq, na kisha Jibril akaanza safari na mie hadi
tukafika Bayt Ul Maqdis’ huku Malaika Jibril akiwa ni mwenye kukamata sehemu za
kuwekea Miguu na Malaika Mikail akiwa ni mwenye kukamata hatamu ya Buraq huyo.
Hivyo ili kufahamu hili tunalozungumzia la kuhusiana na Buraq na juu yake Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam, basi inabidi tuingie kwenye somo la Fizikia ambapo ndani
yake mna Kanuni ya mfumo wa Uteketezaji ambao hua unaelezea kile kinachotokea pale
baada ya kupatikana mkusanyiko wa Nguvu kubwa sana inayotokana na mgongano baina
ya kitu chenye kuchukua nafasi na kitu kisichochukua nafasi katika sehemu husika na
hivyo matokeo yake kusababisha kutoweka kwa umbo la kitu hicho chenye kuchukua
nafasi na kisha baada yake hutokea Nguvu kubwa sana ya Mionzi ya Nuru ambayo nguvu
yake hua ni zaidi ya nguvu ya Mionzi ya X-ray.
Ambapo hapa tunarudi tena kwa Mujaddid Ad Din Sultan Mutakalimin Imam Al
Mushakikkin Imam Fakhr Ad Din Al Razi pale aliposema kua: ‘Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alisafiri pia katika safari mbili ambapo kwanza ni
hali ya kusafiri kutoa kwenye Ulimwengu Unaoonekana (Al Alam Al Shahadah)
na kuingia kwenye Ulimwengu Usioonekana (Al Alam Al Ghayb) ambapo
Ulimwengu miwili hii imepakana ndani ya Masafa ya Baina ya Mipinde Miwili,
kama zilivyosema Aya.
﴿فَكَ انَ قَابَ قَوْسَ ينْ ِ أَوْ أَدْ نىَٰ ﴾
Fakana qaba qawsayni aw adna(Surat An Najm 53:9)
Tafsir: Na ilikua ni masafa ya Mipinde Miwili au karibu zaidi.
737
Hivyo Maneno Fakana qaba qawsayni aw adna hua ni yenye kumaanisha
Uteketezo wa Nafsi yake na hivyo Nafsi hio kuingia katika hali ya kua na
ukaribu sana kwa Mola wake.
Hivyo tunapozungumzia Uteketezo aliouzugumzia Mujaddid Ad Din Sultan
Mutakalimin Imam Al Mushakikkin Imam Fakhr Ad Din Al Razi wa Nafsi ya Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi tunaona kua kulingana na Kanuni ya Mfumo wa
mahusiano ya Uteketezo wa kitu basi hupelekea kutoweka kwa kitu husika baada ya
kutokea mgongano mkubwa baina ya kituhusika chenye kuchukua Nafasi na kitu
kisichochukua Nafasi, kwa maana hio basi kulitokea mtoweko wa Maumbile ya
muonekano wa mwili wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam wenye kuchukua Nafasi
ya sehemu kutokana na Uteketezo huo, kutoka katika sehemu aliyokuwepo na kuibuka
katika sehemu nyengine kuliosababishwa na mgongano wa Maumbile yake Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na Maumbile ya Malaika Jibril ambayo ni ya kutokuchukua
nafasi katika sehemu kutokana na Makadirio ya Allah Subhanah wa Ta’ala na hapo hapo
pia ikatokea Nguvu kubwa zaidi ya Nuru ambayo ilifungamana na Nuru iliyowakilishwa
na Mnyama Buraq na kutokea yaliyotokea katika kukamilisha safari hio.
Ambapo tunapoangalia kwa upande mwengine wa utaratibu wa Elimu ya Fizikia basi hua
tunaona kua Kitu chochote kile chenye kuchukua nafasi kinapoingizwa katika hali fulani
basi kitu hicho chenyewe hua kinageuka na kua ni aina ya Nguvu ambayo inaweza
kutumika kutoa kitu chengine chenye nguvu kubwa zaidi ambacho hakikuwepo kabla
yake.
Yaani hii hua ni kulingana na ile kanuni isemayo E=mc2, ambapo E hua ni Nguvu ya
Mvutano ya ndani ya Kitu husika ambayo hua ni sawa na M ambayo hua ni Uzito wa
Kitu husika na C2 ambayo hua ni Kasi ya Muangaza wa Jua ambayo hua ni Kilomita
300,000 kwa sekunde moja mara mbili yake. Ambapo hii ndio kanuni ya Nguvu
inayotumika katika kuendeshea mashine mbali mbali kuanzia kwenye Vyombo vya
usafiri kama Gari, Ndege, Meli, Pikipiki n.k
Kwani kwenye mashine za vyombo hivi zinazotumia Mafuta iwe Petroli au Diesel basi
matone ya mafuta hayo hua yanamwagwa kwenye chumba maalum ndani ya mashine
husika na kisha kukandamizwa pamoja na hewa ndani ya sehemu hio ya mashine na hapo
hapo Mafuta hayo hutoweka na badala yake ndani sehemu hio huzalishwa Nguvu kubwa
sana ambayo huifanya Mashine kua ni yenye kuzunguka na kufanya kazi, n.k ambapo
kanuni ya mfumo huu pia hutumika kwenye Taa za Umeme, Vinu vya kusagia Nafaka.n.k
Hivyo kitu chochote kile chenye kuchukua nafasi kitakachosafiri kwa kasi ya Mwangaza
basi Maumbile ya Umbo lake hugeuka na kua ni Nguvu inayotokana ndani yake, ambapo
hapo hapo Nguvu hio inapohitajika kurudishwa katika hali ya awali ya kitu hicho basi
738
hua pia kuna uwezekano wa kurudishwa kwake katika hali yake ya asili, ingawa hata
hivyo kutakua na upungufu wa baadhi ya sehemu za Umbo lake la maumbile kitu hicho.
Ambapo ingawa kwa hali ya maumbile ya Mtu wa kawaida hua haiwezekani kusafiri kwa
kasi hio ya Mwangaza wa Jua na hii ni kwa sababu kila Kitu kinavyoongeza kasi yake
basi hua pia ni chenye kuongezeka Uzito wake kutokana na nguvu iliyomo ndani yake,
na kutokana na hali hio basi kwa upande wa maumbile ya Ibn Adam, basi yeye hua ni
mwenye hali kupoteza uwezo wa kujidhibiti yeye mwenyewe na kila kitu kilichomo
ndani ya mwili wake kutokana na nguvu inayozalishwa ndani ya mwili wake kutokana
na kasi ya mwendo huo.
Na kisha baada ya hapo Ibn Adam husika hatokua na uwezo wa kuona sawasawa kwani
ataanza kujiona kua kama mtu mwenye kusafiri kwa kasi kubwa kwa kupitia kwenye
bomba jembamba lisilokua na mwisho kwao na kila kitu atakiona kua kimejikusanya
katika sehemu ndogo iliyopo mbele yake na kisha macho yake yataanza kutofahamu nini
yanaona na taratibu huanza kuona kiza kitupu, na ufahamu wake utapoteza muelekeo na
huenda kitakachofuatia hapo ikawa ni kifo chake.
Lakini bila ya shaka tunapozungumzia Maumbile ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam basi tunaona alikua katika hali ya Maumbile ya Nuru ya Mitume kabla ya
Kuumbwa kwake, na baada ya Kuumbwa kwake, na baada ya kuzaliwa kwake na kua
hata kabla ya safari yake hio basi alikua ni mwenye kupasuliwa na kujazwa Nuru ya Iman
na Hikma ndani ya kifua chake, na bila ya shaka maumbile ya Nuru yalivyo hua ni yenye
kusambaa kwa kasi kubwa sana na kuwepo katika kila sehemu pale inapoachiwa
muangaza wake Nuru hio, kama ilivyo Nuru ya muangaza wa Jua linapoangaza Duniani,
hua ni yenye kutoka Juu Mbinguni kwa masafa ya kilomita Milioni 150 na moja kwa
moja kufika Ardhini katika wakati huo huo.
Kwani amesema Jabir Ibn Abdallah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi nilisema
kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam : ‘Ya Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam Baba yangu na Mama yangu watolewe Kafara kwa ajili yako, hebu
niambie ni kitu gani kilichoumbwa kabla ya Allah Kuumba kila kila kitu?’’ ‘Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Jabir, kitu cha Mwanzo
alichokiumba Allah ilikua ni Nuru ya Mtume wako, kutokana na Nuru yake, na
kisha Nuru hio ikabakia ikiangaza baina ya Uwezo wake kwa namna alivyotaka
Mwenyewe, na katika wakati huo ilikua hakuna Kitabu wala Kalamu wala Pepo
wala Moto wala Malaika wala Mbingu wala Ardhi.
Na hivyo Allah alipotaka kuumba Viumbe wake basi akaigawa Nuru hio katika
sehemu nne na kutokana na sehemu ya kwanza akatoa Kalamu, katika sehemu ya
pili akatoa Kitabu, katika sehemu ya tatu akatoa Arshi na katika sehemu ya nne
akatoa Kila kitu’’(Mawahib al Laduniyya Imam Al Qastallani)
739
Na pia yeye mwenyewe Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akiomba dua kua
aendelee kua Nuru katika kila sehemu ya Kiungo chake kwa kusema:
اللّهُم َّ اجْعَلْ فيِ قَلْبي نُوراً ، وَفي لِسَانيِ نُوراً، وَفيِ سمَْعِي نُوراً, وَفيِ بَصَرِيِ نُوراً,
وَمِ نْ فَوْقِي نُوراً , وَ مِنْ تحَْتيِ نُوراً, وَ عَنْ يمَِينيِ نُوراَ, وعَنْ شمِ َاليِ نُوراً,
وَمْن
أَماَمِي نُوراً, وَمِنْ خَلْفيِ نُوراَ, واجْعَلْ فيِ نَفْسِ ي نُوراً, وأَعْظِمْ ليِ نُوراً, وَعظِّمْ ِلي
نُوراً, وَاجْ عَلْ ليِ نُوراً, واجْ عَلنيِ نُوراً, ألل َّهُم َّ أَعْطِنيِ نُوراً, واجْ عَلْ فيِ َعصَبيِ نُوراً,
وَفيِ لحَْمِي نُوراً, وَفيِ دَمِي نُوراً وَفيِ شَعْرِي نُوراً, وفيِ بَشَرِي نُوراً (أَلل َّهُم َّ اجِ عَلْ ِلي
نُوراً فيِ قّبرِْي وَ نُوراَ فيِ عِظاَمِي) (وَزِدْنيِ نُوراً , وَ زِدْ نيِ نُو راَ , وَزِدْنيِ نُوراً) (وَهَ ْب
ليِ نُوراً عَلَى نُوراً (
Allāhummaj'al fī qalbī nūran, wa fī lisānī nūran, wa fī sam`ī nūran, wa fī baṣarī
nūran, wa min fawqī nūran, wa min taḥtī nūran, wa `an yamīnī nūran, wa `an
shimālī nūran, wa min 'amāmī nūran, wa min khalfī nūran, waj`al fī nafsī nūran,
wa 'a`dhim lī nūran, wa `dhim lī nūran, waj`allī nūran, waj`alnī nūran, Allāhumma
'a`tinī nūran, waj'al fī `aṣabī nūran, wa fī laḥmī nūran, wa fī damī nūran, wa fī
sha`rī nūran, wa fī basharī nūran. [Allāhummaj`allī nūran fī qabrī wa nūran fī
`idhāmī.] [Wa zidnī nūran, wa zidnī nūran, wa zidnī nūran.] [Wa hab lī nūran `alā
nūr.]
Tafsir: Ya Allah, Nijaalie Nuru kwenye Moyo wangu, Na kwenye Ulimi wangu Nuru;
Na kwenye Masikio yangu Nuru; Na kwenye Macho yangu Nuru; Na juu yangu Nuru;
Na chini Yangu Nuru; Na kulia kwangu Nuru; Na Kushoto kwangu Nuru; Na mbele
yangu Nuru; Na Nyuma yangu Nuru; Na ndani ya Nafsi yangu Nuru; Itukuze Nuru
yangu; Na Ikuzishe Nuru yangu; Nijaalie niwe Nuru; Na Nijaalie niwe Nuru; Ya
Allah Nipe Nuru; Nijaalie Nuru ndani ya Hisia zangu; Ndani ya Mwili wangu Nuru;
Ndani ya Damu yangu Nuru; Kwenye Nywele zangu Nuru; Kwenye Umbo langu
Nuru; Ya Allah Nijaalie Nuru Kaburini mwangu; na Nijaalie mimi Nuru kwenye
Mifupa yangu; Na Niongezee Nuru; Na Niongezee Nuru, Na Niongezee Nuru;Na
unipe Nuru Juu ya Nuru (Imam Bukhari, Fath-Al Bari)
Kwa hivyo Maumbile yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam sio maumbile kama
ya kawaida ya viumbe wengine, kwani ndani kila kiungo cha mwili wake mna Nuru na
740
hivyo katika safari yake ya kuenda na kurudi kwa mwendo wa zaidi ya kasi ya Nuru ya
Muangaza wa Jua, basi hakukutokea mabadiliko yeyote kwenye Mwili wake Mtukufu
kutokana na Matakwa yake mwenyewe Muumba Allah Subhanah wa Ta’ala kutokana
na Utukufu wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam wa Kimaumbile mbali ya kua
alikua ni mwenye kusafiri kwa kasi ya zaidi ya Mwangaza katika Safari yake kwa
Kimwili, Kiroho na Kinafsi.
Hivyo anasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam : ‘Wakati nikiwa safarini
alitokea Mtu katika upande wangu wa kulia na kuniita kwa kusema: ‘Muhamamd
mimi nataka kuzungumza nawe’ lakini nami sikumjibu, kisha kwa mbele zaidi mtu
mwengine akaniita kwa upande wa kushoto na kusema: ‘Muhamamd mimi nataka
kuzungumza nawe’ nami sikumjibu na ilipofikia mbele zaidi nikamuona
Mwanamke alievaa vizuri na kujipamba na kila aina ya mapambo ambae alisema:
‘Muhamamd, nataka kuzungumza nawe.’’
Ambapo ni baadae Malaika Jibril akasema kua: ‘Mtu wa kwanza alikua ni Myahudi
na wa pili alikua ni Mkristo ambao wote walikua wanataka kumuondolea umakini
kwenye safari yake ama kuhusiana na Mwanamke basi alikua ni Dunia. Hivyo
kama Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam angemsikiliza basi Ummah wake
ungeipendelea zaidi Dunia kuliko Akhera.’
Katika safari yake hio ya Isra Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisimama katika
sehemu kadhaa ambapo kwanza ilikua ni katika Mji wa Madina na kisha akasimama
kwenye Mlima Sinai katika sehemu ambayo Allah Subhanah wa Ta’ala alimkabidhi
Nabii Musa Tawrat, na kisha akasimama kwenye eneo la Bethlehem katika sehemu
aliyozaliwa Nabii Isa.
Na kisha pia wakasimama kwenye Kaburi la Nabii Musa ambapo alimuona Nabii Musa
akiwa ndani kabuirni mwake amesimama akiwa anasali kama alivyosema katika hadith
kua: ‘Nilipita kwa Musa katika safari ya Isra pembeni ya kilima chekundu alipokua
amesimama akisali ndani ya Kaburi lake’(Sahih Muslim)
Walipofika Bayt Al Maqdis basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anasema kua:
‘Nami nikamfunga Buraq kwenye sehemu ambayo alikua akifungwa na Mitume
wengine, na kisha nikaingia ndani ya Msikiti huo na nikasalisha Mitume wengine
wote waliotangulia kabla yangu akiwemo Adam na waliokuja baada yake.
Ambao walikua ni Mitume 124000 waliokua wakimsubiri ndani yake, hivyo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam anasema kua: ‘Mitume wakatambulishwa kwangu mie na
Musa alikua ni mwembamba mwenye kufanana na watu wa kabila la Shanuah, na
nikamuona Isa Ibn Maryam alikua akifanana sana na miongoni mwa niliowaona
kua ni na Urwah Ibn Masud, na nikamuona Ibrahim na mtu wa karibu aliefanana
741
nae miongoni mwa niliowaona ni Sahaba yenu (yaani yeye mwenyewe Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam), na nikamuona Jibril na wa karibu aliefanana nae
miongoni mwa niliowaonani Dihya’(Imam At Tirmidhi)
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anaendelea kusema kua: Wakati nikitoka basi
Jibril aliniletea Mabakuli mawili ambapo moja limetiwa Kilevi na jengine limetiwa
Maziwa, nami nikachukua lenye kutiwa Maziwa, hivyo Jibril akasema: ‘Maamuzi
yako yanaendana na Maumbile ya Fitra.’’
‘Na kisha tukapanda juu na Jibril hadi tulipofika katika Mbingu ya kwanza ya
karibu na Dunia’, hivyo Jibril akaomba kuruhusiwa kuingia ndani yake nae
akaulizwa: ‘Ni nani?’ nae akajibu: ‘Jibril’ akaulizwa tena: ‘Umefuatana na nani?’
nae akajibu: ‘Muhammad’ nae akaulizwa: ‘Hivi Jee amealikwa?’ Nae akajibu:
‘Naam’ hivyo akaambiwa: ‘Mkabiribishe, kwani mbora zaidi aliealikwa amewasili’
Hivyo Mbingu hio ikafunguliwa, na wakati nilipokua naingia nikakutana na Adam,
na Jibril akaniambia: ‘Huyu ndio Baba yako, hivyo Msalimie’ Nami Nikamsalimia
nae akanirudishia salamu hio na kusema: ‘Karibu Ewe Mtoto Mcha Mungu na
Mtume Mcha Mungu’
Na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuona akiwa na watu wengi sana
katika upande wake wa kulia na pia watu wengi sana katika upande wake wa kushoto,
akiangalia katika upande wake wa Kulia hua ni mwenye kutabasamu, na akiangalia
katika upande wake wa kushoto hua ni mwenye kulia. Hivyo Malaika Jibril akaelezea
kua: ‘Walio upande wake wa Kulia ni Kushoto ni Roho za kizazi chake na waliokua
katika upande wa Kulia ni watu wa Peponi na waliokua upande wa kushoto ni wa
Motoni’
‘Na kisha tukapanda juu na Jibril hadi tulipofika katika Mbingu ya pili’ hivyo Jibril
akaomba kuruhusiwa kuingia ndani yake nae akaulizwa: ‘Ni nani?’ nae akajibu:
‘Jibril’ akaulizwa tena: ‘Umefuatana na nani?’ nae akajibu: ‘Muhammad’ nae
akaulizwa: ‘Hivi Jee amealikwa?’ Nae akajibu: ‘Naam’ hivyo akaambiwa:
‘Mkabiribishe, kwani mbora zaidi aliealikwa amewasili’
Hivyo Mbingu hio ikafunguliwa, na wakati nilipokua naingia nikakutana na Isa na
Yahya, na Jibril akaniambia: ‘Hawa ndio Isa na Yahya, hivyo wasalimie’ Nami
Nikawasalimia nao wakanirudishia salamu hio na kusema: ‘Karibu Ewe Ndugu
Mcha Mungu na Mtume Mcha Mungu’
‘Na kisha tukapanda juu na Jibril hadi tulipofika katika Mbingu ya tatu’ hivyo
Jibril akaomba kuruhusiwa kuingia ndani yake nae akaulizwa: ‘Ni nani?’ nae
akajibu: ‘Jibril’ akaulizwa tena: ‘Umefuatana na nani?’ nae akajibu: ‘Muhammad’
742
nae akaulizwa: ‘Hivi Jee amealikwa?’ Nae akajibu: ‘Naam’ hivyo akaambiwa:
‘Mkabiribishe, kwani mbora zaidi aliealikwa amewasili’
Hivyo Mbingu hio ikafunguliwa, na wakati nilipokua naingia nikakutana na Yusuf,
na Jibril akaniambia: ‘Huyu ndio Yusuf, hivyo Msalimie’ Nami Nikamsalimia nae
akanirudishia salamu hio na kusema: ‘Karibu Ewe Ndugu Mcha Mungu na Mtume
Mcha Mungu’
‘Na kisha tukapanda juu na Jibril hadi tulipofika katika Mbingu ya nne’ hivyo
Jibril akaomba kuruhusiwa kuingia ndani yake nae akaulizwa: ‘Ni nani?’ nae
akajibu: ‘Jibril’ akaulizwa tena: ‘Umefuatana na nani?’ nae akajibu: ‘Muhammad’
nae akaulizwa: ‘Hivi Jee amealikwa?’ Nae akajibu: ‘Naam’ hivyo akaambiwa:
‘Mkaribishe, kwani mbora zaidi aliealikwa amewasili’
Hivyo Mbingu hio ikafunguliwa, na wakati nilipokua naingia nikakutana na Idris,
na Jibril akaniambia: ‘Huyu ndio Idris, hivyo Msalimie’ Nami Nikamsalimia nae
akanirudishia salamu hio na kusema: ‘Karibu Ewe Ndugu Mcha Mungu na Mtume
Mcha Mungu’
‘Na kisha tukapanda juu na Jibril hadi tulipofika katika Mbingu ya tano’ hivyo
Jibril akaomba kuruhusiwa kuingia ndani yake nae akaulizwa: ‘Ni nani?’ nae
akajibu: ‘Jibril’ akaulizwa tena: ‘Umefuatana na nani?’ nae akajibu: ‘Muhammad’
nae akaulizwa: ‘Hivi Jee amealikwa?’ Nae akajibu: ‘Naam’ hivyo akaambiwa:
‘Mkabiribishe, kwani mbora zaidi aliealikwa amewasili’
Hivyo Mbingu hio ikafunguliwa, na wakati nilipokua naingia nikakutana Harun,
na Jibril akaniambia: ‘Huyu ndio Harun, hivyo Msalimie’ Nami Nikamsalimia nae
akanirudishia salamu hio na kusema: ‘Karibu Ndugu Mcha Mungu na Mtume
Mcha Mungu’
‘Na kisha tukapanda juu na Jibril hadi tulipofika katika Mbingu ya sita hivyo Jibril
akaomba kuruhusiwa kuingia ndani yake nae akaulizwa: ‘Ni nani?’ nae akajibu:
‘Jibril’ akaulizwa tena: ‘Umefuatana na nani?’ nae akajibu: ‘Muhammad’ nae
akaulizwa: ‘Hivi Jee amealikwa?’ Nae akajibu: ‘Naam’ hivyo akaambiwa:
‘Mkabiribishe, kwani mbora zaidi aliealikwa amewasili’
Hivyo Mbingu hio ikafunguliwa, na wakati nilipokua naingia nikakutana na Musa
ambae alikua ni mwenye rangi ya kiza na mwili mkubwa na mwenye nyingi nyingi,
na Jibril akaniambia: ‘Huyu ndio Musa, hivyo Msalimie’ Nami Nikamsalimia nae
akanirudishia salamu hio na kusema: ‘Karibu Ewe Ndugu Mcha Mungu na Mtume
Mcha Mungu’
743
Wakati nilipokua natoka mara akaanza kulia: ‘Nami nikauliza Jee ni nini
kinachokufanya Ulie?’ nae akasema: ‘Mimi nalia kwa sababu Kijana Mdogo
alietumwa baada yangu atakua na wafuasi wengie zaidi yangu ambao wataingia
Peponi kwa wingi zaidi ya wafuasi wangu’
‘Na kisha tukapanda juu na Jibril hadi tulipofika katika Mbingu ya saba hivyo
Jibril akaomba kuruhusiwa kuingia ndani yake nae akaulizwa: ‘Ni nani?’ nae
akajibu: ‘Jibril’ akaulizwa tena: ‘Umefuatana na nani?’ nae akajibu: ‘Muhammad’
nae akaulizwa: ‘Hivi Jee amealikwa?’ Nae akajibu: ‘Naam’ hivyo akaambiwa:
‘Mkabiribishe, kwani mbora zaidi aliealikwa amewasili’
Hivyo Mbingu hio ikafunguliwa, na wakati nilipokua naingia nikakutana na
Ibrahim, na Jibril akaniambia: ‘Huyu ndio Baba yako Ibrahim, hivyo Msalimie’
Nami Nikamsalimia nae akanirudishia salamu hio na kusema: ‘Karibu Ewe Mtoto
Mcha Mungu na Mtume Mcha Mungu’
Na kisha nikachukuliwa hadi katika Bayt Al Maamur na kupewa Kikombe cha
Ulevi, Kikombe cha Maziwa, na Kikombe cha Asali nami nikachukua Maziwa na
Malaika Jibril akasema: ‘Umechagua Jambo la kimaumbile hivyo wewe na Ummah
wako watalifuata’
Katika safari yake hii Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alioneshwa Miujiza mingi
sana ambapo kwenye Bayt Maamur ambacho ndio Kibla cha Malaika kilichopo juu ya
eneo la Al Kaabah Mbinguni, na baadae akaoneshwa Pepo na Moto na yanayotokea ndani
yake sehemu hizo kwa wanaoadhiabiwa kwa makosa ya dhambi zao na kwa wanaolipwa
kutokana na amali njema zao na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua ni
mwenye kuona yale ambayo hakuna jicho lililowahi kuona wala hakuna ufahamu
uliowahi kufikiria.
Na kisha akapandishwa Juu zaidi hadi akafika katika Sidrat al Muntaha, na akaona kua
Matunda yake ni makubwa kama ya Hijr na Majani yake makubwa kama masikio ya
Tembo nae Jibril akamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Huu ndio
Sidrat Al Muntaha’ nami nikaona Mito minne inatokana nao, na hivyo nikauliza: ‘Hii
ndio nini ewe Jibril?’
Jibril akasema: ‘Mito itokanayo ndani yake ni ni Mito ya Peponi na itokayo nje yake
ni Mto Nile na Mto Furat (Euphrate)’
Na kisha baada ya hapo Malaika Jibril akamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kua amalizie safari yake peke yake kwani hakuna kiumbe mwengine ambae
aliewahi kuvuka katika eneo la Sidrat Al Muntaha, ambapo mbele yake kuna Arshi
Tukufu ya Allah Subhanah wa Ta’ala. Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
744
akaendelea mbele zaidi peke yake kumalizia safari yake hio hadi kufikia katika masafa
ya Qaba Qawsayni aw Adna mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala.
Ambapo kilichotokea hapa hakijulikana kwani hakijaelezewa wala kuhadithiwa isipokua
kuhusiana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua ni mwenye kuambiwa kua:
‘Nimekabidhi jukumu la kusali sala 50 kwa Ummah wako katika kila sikua na
katika kila mchana.’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anaelezea kwa kusema: Kisha
nikafardhishiwa Sala 50 nami nikarudi na kukutana na Musa ambae aliuliza: ‘Jee
umeamrishwa nini?’ nami nikajibu: ‘Nimekabidhiwa Sala 50’ nae akasema: ‘Watu
wako hawatoweza kusali Sala 50 ndani ya siku moja. Wa Allahi mimi niliwajaribu
watu kabla yako na niliadhibika sana na watu wa Bani Israil, hivyo rudi kwa Mola
wako, kawaombee watu wako’
Nami nikarudi na Allah akanipunguzia Sala 10, na nikarudi kwa Musa nae
akasema tena aliyoyasema hapo kabla, hivyo nikarudi kwa Allah na nikapunguziwa
10 tena, na nikarudi kwa Musa nae akasema tena aliyoyasema hapo kabla, hivyo
nikarudi kwa Allah na nikapunguziwa 10 tena, na nikarudi kwa Musa nae akasema
tena aliyoyasema hapo kabla, hivyo nikarudi kwa Allah na nikapunguziwa 10 tena,
na nikarudi kwa Musa nae akasema tena aliyoyasema hapo kabla, hivyo nikarudi
kwa Allah na nikapunguziwa 5.
Na nikarudi kwa Musa nae akasema Watu wako hawatoweza kusali Sala 5 ndani
ya siku moja. Wa Allahi mimi niliewajaribu watu kabla yako na niliadhibika sana
na watu wa Bani Israil, hivyo rudi kwa Mola wako, kawaombee watu wako. Nami
nikasema: ‘Hakika mimi nimeshamuomba Mola wangu mpaka naona aibu, hivyo
bora niridhike na kujisalimisha’
Ambapo kwa upande mwengine basi anasema Imam Bukhari kua: ‘Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam aliambiwa na Allah Subhanah wa Ta’ala kua: ‘Ewe
Muhamamd. Maneno yangu hayabadiliki kwani hivyo ndivyo nilivyoandika
kwenye Umm Ul Kitab, kila jema litalipwa mara 10 zaidi yake, hivyo haya ni mema
50 katika Umm Ul Kitab na ni matano kwa ajili yako’’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaendelea kusema kua: ‘Nilipovuka Mbinguni
nikasikia sauti ikinadia: ‘Nimetimza Ahadi yangu na nimewapunguzia Waja
wangu’’
Na kisha baada ya hapo kuna matukio mbali mbali aliyoyaona Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam katika safari yake hio kabla ya kurudi kwake kutoka Mbinguni kwa
kushukia tena katika sehemu aliyopandia yaani Bayt Ul Maqdis, kisha akapanda tena
745
Buraq na akaanza Safari ya kurudi katika Mji wa Makkah, ambapo njiani akakutana na
msafara wa Quraysh ambao ulikua umepotelewa na Ngamia wao, nae alikua akiwajua
viongozi wa Msafara huo na akawasalimia nao wakasema: ‘Hii ni sauti ya Muhammad’
Ambapo asubuhi yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipotoka nje akakutana
na Abu jahl ambaea lipomsalimia basi akamuuliza: ‘Kuna mpya Gani leo?’ Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam aaelezea yaliyomtokea ndani ya usiku huo, ambapo Abu
Jahal akasema: ‘Hivi Jee kama nitawakusanya watu utarudia kusema mbele yao
kama uliyoniambia mimi?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Naam’
Hivyo Abu Jahl akawakusanya watu na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akawaelezea yaliyotokea lakini watu wa Mji wa Makkah hawakukubaliania nae, hivyo
mmoja kati ya watuwaliowahi kuenda Bayt Al Maqdis akamwambia Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam aelezee namna Ulivyo Msikiti wa Bayt Ul Maqdis, hivyo
Allah Subhanh wa Ta’ala akauleta Msikiti wa Bayt Ul Maqdis mbele ya macho ya Mtume
wake Salallahu Alayhi wa Salam na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akauelezea
kama ulivyo, na hivyo Mtu huyo akathibitisha kua kweli ni sahih hivyo ndivyo ulivyo
lakini hata hivyo watu hao hawakwueza kukubali ukweli wa kua alienda sehemu hio na
kupanda Mbinguni pia, na hii ni kwa sababu ya Umbali wa kimasafa wa Safari hio,
haiwezekani kufanyika hata kwa mwezi moja wacha mbali ndani ya masaa machache ya
usiku mmoja.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaambia watu hao kua, wakati aliokua
anarudi alikutana na Ngamia aina fulani aliekua amepotea kutoka kwenye Msafara wake,
akawaonesha watu wenye msafara huo alipokimbilia Ngamia huyo, na ulipowasili
Msafara huo basi wenye Msafara huo walikubalia kua Ngamia wao huyo alipotea Usiku
mmoja na wakasikia sauti ya Mtu ikiwelekeza alipo Ngamia huyo.
Lakini kwa upande wa Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu alipopewa habari hio basi
akasema: ‘Wa Allahi kama hivyo ndivyo anavyosema basi ni kweli, kwa nini kuwe
na shaka juu yake? Hivi jee hasemi yeye kua amepata habari kutoka Juu Mbinguni
katika wakati wowote iwe Usiku au Mchana, hivyi jee ni lipi jambo la Miujiza zaidi
kati ya haya?’
Na kisha Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akaenda kwa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam na akamwambia amuelezee maeneo aliyoyaona na alipoyaelezea basi
Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Nashuhudia kua wewe ni Rasul
Allah’
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anathibitisha ayasemayo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kuhusiana nayo kua:
746
﴿فَلاَ أُقْسِ مُ بمَِا تُبْصِ رُونَ ۞ وَمَا لاَ تُبْصِرُونَ ۞ إِن َّهُ لَقَوْ لُ رَسُولٍ كَ رِيمٍ ۞ وَمَا هُوَ
بِقَوْ لِشَا ا عِرٍقَلِي ت لاً َّم ُؤْمِنُو نَ ۞ وَلاَ بِقَوْلِ كَاهِنٍ قَلِيلاً م َّا تَذَك َّرُونَ ۞تَن ِزي لٌ مِّن
ر َّبِّ ٱلْعَالَمِينَ۞وَلَوْ تَقَو َّلَ عَلَيْنَا بَعْضَ ٱلأَقَاوِيلِ ۞لأَخَذَْ مِنْهُ بِٱلْيَمِينِ۞ثمُ َّ لَقَطَعْنَا
مِنْهُ ٱلْوَتِينَ۞فَمَا مِنكُمْ مِّنْ أَحَدٍ عَنْهُ حَاجِ زِينَ ﴾
Fala oqsimu bima tubsiroona; Wama la tubsiroona; Innahu laqawlu rasoolin
kareemin ; Wama huwa biqawli shaAAirin qaleelan ma tu/minoona ; Wala biqawli
kahinin qaleelan ma tadhakkaroona ; Tanzeelun min rabbi alAAalameena; Walaw
taqawwala AAalayna baAAda al-aqaweeli; Laakhadhna minhu bialyameeni;
Thumma laqataAAna minhu alwateena; Fama minkum min ahadin
AAanhu hajizeena (Surat Al Haaqah 69:38-47)
Tafsir: Hivyo Naapa kwa kila mnachokiona; Na kwa kila msichokiona; Hakika haya
ni maeno ya Mtume mwenye kuheshimika; Na wala si maneno ya Mshairi lakini
mnayaamini kidogo tu; Wala si kauli ya Mtabiri, ambapo mnakumbuka kidogo yake
tu; Haya ni yaliyoteremka kutoka kwa Mola wa Ulimwengu; Na kama angekua
amezua kuhusiana nasi; Basi tungemkamata kwa mkono wa kulia (kwa nguvu na
uwezo mkubwa); Na kisha tungemkata mshipa wake wa uhai; Na hakuna hata mmoja
miongoni mwenu ambae angeweza kutuzuia.
Tunaona katika aya hizi kua Allah Subhanh wa Ta’ala anatuambia kua: ‘Hakika katika
kila alilosema Muhammad Salallah Alayhi wa Salam halikua ni lenye kutokana na
Uzushi au matamanio ya nafsi yake au labda kwa Ilm ya utabiri, bali ni yenye
kutoka kwa Mola wake kwani kwa kua yeye ni Mtume ambae ni mwenye jukumu
la kufikisha Ujumbe anaopewa na Mola wake, basi haruhusikia kuzua au kusema
Uongo kuhusiana na na kitu chochote, kwani akifanya hivyo basi bila ya shaka
angeadhibiwa hapahapa Ulimwenguni, kwa adhabu kali sana, na hakuna hata
kiumbe mmoja ambae angekua ni mwenye uwezo wa kumuepusha na adhabu hio
au kumuombea kua asifikwe na adhabu hio.’
Safari ya Isra na Miraj ina umuhimu mkubwa sana na hikma kubwa sana ndani yake, si
kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Ta’ala peke yake bali kwa Waislam wote kwa
ujumla, kwani tukio hili la Isra na Miraji hua linawakilisha safari ya Kiroho ndani ya
Nafsi zetu katika kuutafuta Ukaribu wa Allah Subhanah wa Ta’ala na kuingia katika hali
747
ya Qaba Qawsayni aw Adna na Mola wetu, kama vile walivyofanya Masahaba wengi
akiwemo Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu.
MUSAB IBN UMARY BALOZI WA KWANZA WA UISLAM NA
MAKUBALIANO YA AQABAH.
Miongoni mwa Vijana waliokua wakipendeza na kuvutia kwa uzuri wa kimaumbile na
kimavazi katika Mji wa Makkah alikuwa ni kijana Musab Ibn Umayr, ambae alizaliwa
miaka 24 baada ya kuzaliwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, tunapomzungumzia
Musab Ibn Umayr basi tunamzingumzia kijana ambae alikua ni mwenye kupendwa sana
na wazee wake ambao nao ni Umayr Ibn Hashim na Khunaas Bint Malik waliokua ni
matajiri sana, kiasi walikua wakimnunulia Mtoto wao huyo wampendae aitwae Musab
Ibn Umayr kila kitu akitakacho kwa ajili yake.
Hivyo Musab Ibn Umayr alikua ni kijana mtanashati ambae alikua akivaa nguo na viatu
vya kipekeee katika mji wa Makkah, yaani ilikua kila dizain mpya ya viatu au nguo kabla
ya kuingia katika Mji wa Makkah basi kwanza alikua anaonekana nayo Musab Ibn
Umayr, na hivyo basi kila mwanamke kijana wa Mji wa Makkah alikua akivutiwa sana
na kijana Musab Ibn Umayr na kutaka kuolewa nae.
Mbali ya Uzuri wake na kupendeza kwake lakini pia kijana Musab Ibn Umayr alikua ni
kijana mwenye ufaham mzuri sana kuwapita wengi miongoni mwa vijana wenzake na
pia baadhi ya watu wazima katika jamii yake kiasi ya kua alikua ni mwenye kujumuishwa
kwenye Mikutano ya Viongozi wa Mji wa Makkah.
Wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anapokea Utume wake basi kijana Musab
Ibn Umayr alikua na umri wa miaka 15, na hivyo alipotimia umri wa miaka 19 katika
mwaka wa 4 wa Uislam, basi Musab Ibn Umayr akasikia kuhusiana na kile
kinachoendelea katika Nyumba ya Dar Al Arqam, na hivyo bila ya kupoteza mda basi
akakimbilia kisirisiri katika nyumba hio na akasilimu kisirisiri, ambapo hata hivyo siri
hio haikudumu kwa mda mrefu kwani siku moja Uthman Ibn Talha alimuona Musab Ibn
Umayr wakati akiingia ndani ya nyumba ya Dar Al Arqam, habasi zikatapakaa kwenye
Mji wa Makkah na Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu akafungiwa kifungo cha Ndani
na Mama yake na kupokonyonywa kila kitu kilichokua kinampendezesha alichonunuliwa
na wazee wake.
Lakini hata hivyo kifungo hiki hakikumvunja Moyo kijana Musab Ibn Umayr, kwani
alibakia kuendelea kudumu katika imani mpya ya Dini yake, na ilipotokea nafasi ya
Msafara wa kwanza wa Hijra ulioelekea Abyssinia basi Musab Ibn Umayr Radhi Allahu
Anhu akatoroka na kuukimbia mji wa Makkah pamoja na Msafar huo kwa ajili ya
748
kuendelea kuimarisha Imani yake ya Dini ya Kiislam kwa uhuru na Usalama, ambako
alikaa huko hadi mambo yalipopungua uzito wake katika Mji Wa Makkah na kisha
akarudi tena katika Ardhi ya Makkah huku akiwa ni mwenye Imani kubwa zaidi kuliko
hata hapo kabla yake.
Lakini akiwa katika hali inayosikitisha katika maisha yake, kwani alikua ni mtu mwenye
kukosa raha zote na mapambo yote aliyokua akiyapata hapo kabla yake kutoka kwa
wazee wake. Ambapo hata hivyo Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu alikua ni mwenye
kuvitolea kafara vitu vyote hivyo kwa ajili ya Akhera yake na akaamua kumkaribisha
mama yake kwenye Imani ya dini yake, lakini hata hivyo mama yake huyo akasema
kumwambia Musab Ibn Umayr kua:
‘Nenda zako, hakika mimi sina hamu tena ya mimi kua ni Mama yako’ Musab Ibn
Umayr Radhi Allahu Anhu akamkaribia Mama yake na kumwambia: ‘Ewe Mama yangu
nakuusia kwa Moyo wangu wote na kutokana na kua ni mwenye kukujali, hivyo
jisalimishe kwa Mola wako, kwa kusema kua Hakuna Mola anaestahiki kuabudiwa
kwa haki isipokua Allah na Muhammad ni Mja na Mtume wake.’ Lakini hata hivyo
Mama yake huyo akasema: ‘Naapa kwa Nyota zenye kutembea kwa kasi Usiku kua
sitoingia kwenye Dini yako hata kama nikionekana kua mimi sina akili.’
Hivyo Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu akaachana na Mama yake kipenzi na
kuendelea kujitolea kwa ajili ya Mola wake. Ambapo jitihada zake hizo na ufahamu wake
ulimpeleka Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kumchagua kua Balozi wake wa
kwanza kwa ajili ya kumuwakilisha yeye Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Dini
ya Allah Subhanah wa Ta’ala katika ardhi iliyo nje ya Mji wa Makkah, pale ulipowadia
mda wa kuchukua hatua hio kwa kuutambulisha Uislam katika Ardhi ya Mji wa Madinah
.
Baada ya makubaliano ya Al Aqaba yaliyofanyika katika eneo Al Aqaba ambalo ni la
kimlima kidogo kiliopo pembezoni ya mji wa Makkah, katika sherehe hizi walikuja watu
12 kutoka Madinah ambao walikua ni Abu Umamah S’ad Ibn Zurarah, Awf Ibn Al Harith
na kaka yake Mu’adh Ibn Harith, Rafi’ Ibn Malik, Thakwan Ibn Abdil Qays, Ubaadah
Ibn As Samit, Yazid Ibn Tha’labah, Al Abbas Ibn Ubadah, Uqbah Ibn Aamir, Qutbah
Ibn Aamir Radhi Allahu Anhum, waliotoka katika ukoo wa Al Khazraj, Uwaym Ibn
Sa’idah, na Abu ul Haytham Malik Ibn At Tayyihan Radhi Allahu Anhum waliotoka
katika ukoo wa Al Aws na kukutana na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
na wakakukubaliana makubaliano ya ushirikiano baina yao na Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam, na katika kiapo hicho walikubaliana kua: Watampwekesha
na kumtii Allah Subhanahu wa Ta’ala na amri zake zote, hawatoiba, hawatozini,
hawatofanya maovu, n.k
749
Watu hao waliridhika kua kama watafanikiwa katika kuishi maisha ya utiifu kwa Allah
Subhanahu wa Ta’ala basi malipo yao yatakua ni Pepo, vyenginevyo malipo yao yatakua
kwa Allah Subhanah wa Ta’ala, ikiwemo kuwaadhibu na pia akitaka kuwasamahe
atawasamehe. Baada ya makubaliano hayo Nabii Salallahu A’layhi wa Salam akawapa
Sahaba Musab Ibn Umayr aende nao Madinah ili akawasomeshe Qur’an na mambo
mengine yahusuyo dini ya Kiislam.
Bila ya shaka Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakukosea pale alipomchagua
Kijan Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu kwa ajili ya Kubeba bendera ya Uislam na
kuuwakilisha katika ardhi ya Mji wa Madinah kwani Musab Ibn Umayr Radhi Allahu
Anhu alikua ni Kijana ambae mwenye sifa stahiki na zinazotosheleza kubeba uzito wa
Jukumu hilo la kipekee.
Hivyo Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu akafunga safari na kuelekea katika Mji wa
Madinah mnamo mwaka 621 huku akiwa ni Mgeni wa Saad Ibn Zurarah Radhi Allahu
Anhu, ambapo kwa pamoja walikua ni wenye kupita nyumba hadi nyumba kuwaelezea
watu kuhusiana na dini ya Uislam na Alhamd Lillah wengi miongoni mwa watu wa
Madinah wakaukubali ujumbe wa Dini ya Kiislam.
Katika harakati zao Musab Ibn Umayr na Saad Ibn Zurarah Radhi Allahu Anhum
wakafanikia kuwakusnaya Waislam wapya kadhaa na kuaza kuwapa Mafunzo ya Imni
yao mpya, ambpo mara akatokea Usayd Ibn Khuday ambae alikua ni miongoni mwa
Machifu wa Mji wa Madinah na alipofika mbele yao huku akiwa na mkuki wake basi
alikua ni mwenye kujawa na hasira kutokana na kusikia kuhusiana na jitihada za Musab
Ibn Umayr na Saad Ibn Zurarah Radhi Allahu Anhum na hivyo akasema: ‘Hivi kwanini
nyinyi mmekuja kwenye Mji wetu na kuanzisha uchochezi kwa waliokua dhaifu
miongoni mwetu? Kwanini hamuachani nasi kama mnataka kuendelea kuishi?’
Ambapo Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu akatabasam na kisha akasema: ‘Jee
unaweza kukaa kitako wanza na kisha ukanisikiliza? Na hivyo kama utakua ni
mwenye kuridhika na ujumbe wetu basi utakubaliana nao na kama ukiwa
hukuridhika basi sisi hatutoendelea kusema tunayoyasema ambayo
hayakuridhishini na tutaondoka.’ Hivyo Usayd Ibn Khuday akachomeka Mkuki wake
ardhini na kisha akasema: ‘Naam, bila ya shaka hio itakua ni sahih kabisa’ na kisha
akakaa kitako chini.
Kisha Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu akaanza kusoma Qur’an na kufafanua aya
na Hadith za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo haukuchukua mda isipokua
Usayd Ibn Khuday akasema: ‘Kwa hakika ujumbe wa maneno yake ni mzuri sana,
hivi jee ili mtu kuingia kwenye Dini hii anatakiwa afanye nini?’ Musab Ibn Umayr
Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Jitoharishe kwa kukoga na kua na nguo safi kisha
750
shuhudia kua hauna Mola anaestahiki kuabudiwa kwa Haki isipokua Allah na
Muhamamd ni Mtume wake na uwe ni mwenye kusali’
Kisha baada ya hapo Usayd Ibn Khudayr akaondoka na baada ya mda akarudi akiwa
amebadilika na akatoa shahada kisha akasali Rakaa mbili na akasema: ‘Baada yangu
basi kuna mtu ambae akikubalia kukufuateni basi kila mtu kwenye Kabila lake
atakua ni mwenye kumfuata yeye na hivyo wacha nikupelekeni katika mahali alipo
kwani yeye ni Sad Ibn Muadh.’ Na bila ya shaka baada ya Musab Ibn Umayr Radhi
Allahu Anhu kuzungumza na Sad Ibn Muadh basi moja kwa moja nae akaingia kwenye
Uislam na kisha baada ya hapo makundi kwa makundi ya watu wa Madinah wakaingia
katika Dini ya Uislam.
Hivyo Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu alikua ni mwenye kuiwakilisha Dini ya
Kiislam ipasavyo na ni mwenye kuyajua majukumu yake ambayo ndio yaliyopelekea
kuzaliwa kwa Taifa Jipya la Kiislam katika Ardhi ya Mji wa Madinah . Na kuandaa
matayarisho ya Maisha mapya ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na miezi
baadae basi Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu akarudi katika Mji wa Makkah huku
akiwa na Waislam 70 na kukutana kwa mara ya pili na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam katika maeneo ya Aqabah.
Ambapo anasema Jabir Ibn Abdallah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Watu 70 miongoni
mwetu tulisafiri kukutana nae katika mwezi wa Dhl Hijjah, tuliahidiana kua
tukutane nae Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika maeneo ya Al Aqabah,
hivyo tukawasili mmoja mmoja, wawili wawili hadi tukatimia, kisha tukasema: ‘Ya
Rasul Allah unataka tukubaliane juu ya nini?’’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Mnatakiwa Mkubali kua mtakua ni
wenye kunitii katika kila jambo, kutumia Mali zenu katika wakati wa raha na shida,
kuamrishana mema na kukatazana Mabaya kusimama kwa ajili ya Allah
Subhbanah wa Ta’ala bila ya kujali kulalamikiwa na kunilinda mimi na kunisaidia
nitakapokuja kwenu kutokana na kila kitu ambacho mnawalinda watu wenu, wake
zenu na watoto wenu na badala yake malipo yenu yatakua ni Pepo’
Jabir Ibn Abdallah Radhi Allahu Anhu anaendelea kusema kua: ‘Wakati sisi tukiwa
tumesimama tunamsikiliza na Asaad Ibn Zurarah ambae alikua ni kijana moja
miongoni mwetu akanyanyua mkono kisha akasema: ‘Taratibu Enyi watu wa
Yathrib! Sisi hatukutoka na kusafiri kuja hapa kwake bila ya kujua kua yeye ni
Rasul Allah, na kukubaliana nae kwa sasa hivi ni mvutano kwa wengi miongoni
mwa Waarabu, yaani hapa tunazungumzia Kupigana na mtu wa Karibu yako, kwa
kutumia upanga wako hivyo inabidi mfahama hivyo na Malipo yako yatakua Allah
Subhanah wa Ta’ala. Au mnakhofia Maisha yenu, hivyo bora kubalini wazi wazi na
kitakua ni kisingizo chenu mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala’
751
Hivyo watu wakasema: ‘Ewe Asaad shusha chini mkono wako, kwani kwa hakika
sisi hatutoachana na Makubalino haya na wala hatutoondoka’ kisha mmoja baada
ya mmoja tukakubaliana na makubaliano hayo’
Ambapo kwa upande wa Kaab Ibn Malik Radhi Allahu Anhu basi yeye anasema kua:
‘Katika usiku huo tulilala kwenye kambi yetu, na ilipoingia robo tatu ya Usiku basi
tukaondoka mmoja kwa ajili y amakutano yetu na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam katika maeneo ya Aqabah, tulikua Wanaume 73 na Wanawake wawili ambao
ni Nasiba Bint Kaab na Asma Bint Am Ibn Adi’
‘Tukamsubiri Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na mara akatokea huku akiwa
amefuatana na Abbas Ibn Abd Ul Muttalib ambae alikua bado kwa wakati huo
akiwa na dini ya Quraysh, lakini mbali ya hivyo basi alikuja kumuwakilisha Mtoto
wa kaka yake na kuthibitisha Ukweli wake na uaminifu wake, na alipokaa chini
Rasal Allah Salallahu Alayhi wa Salam (baada ya kusema) basi yeye alikua ndio mtu
wa mwanzo kusema’
Abbas Ibn Abd Ul Muttalib akasema: ‘Enyi watu wa Yayhrib, fahamuni kua Darja
ya Muhammad miongoni mwetu ni kama mnavyoijua. Na hakika sisi tumemlinda
kutokana na madhara ya Watu wetu, ambao ni wenye mtizamo kama tuliokua nao,
na anaheshimika kwa watu wake na katika ardhi yake na sasa hivi anasisitiza
kuungana nanyi na kuhamia kwenu nyie, hivyo kama mnadhani kua mtaweza
kutimiza ahadi yenu ya kumlinda na kumhifadhi kutokana na watakaotaka
kumpinga na kumdhuru, basi hilo litakua ni jukumu lenu, lakini kama mnafikiria
kua hamtoweza kufanya hivyo na hivyo mtakua ni wenye kumsaliti basi bora
achaneni nae, kwani hapa ni kwake na yuko salama’
Kaab Ibn Malik Radhi Allahu Anhu anasema kua: ‘Sisi tukasema: ‘Tumekusikia
uliyoyasema Ya Rasul Allah, na hivyo amua mwenyewe kwa ajili yako na kwa ajili
ya Mola wako’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasoma baadhi ya aya za Qur’an, aktuusia
kuhusiana na Allah Subhanah wa Ta’ala na kisha akatualika katika Uislam na kisha
akasema: ‘Mimi nimekubaliana na makubaliano ya kua Nyinyi mtanihifadhi mimi
kutokana na kile mnachowahifadhi dhidi yao watu wenu, wake zenu na watoto
wenu.’’
Kisha Al Barra Ibn Marir Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Naam Tunaapa kwa yule
ambae aliekutuma wewe kwa haki, kua tutakulinda na kukuhifadhi kutoka na kile
ambacho tunawalinda na kuwahifadhi dhidi yake watu wetu, tumekubaliana nawe
752
Ya Rasul Allah, Wallahi sisi ni watoto wa Vita kwani tumerithi hayo kutokana na
Mababa zetu na Mababu zetu.’
Ambapo Abu Haytham Ibn Al Tahin Radhi Allahu Anhu akasema : ‘Ya Rasul Allah
hakika sisi tuna mikataba na Mayahudi, na hivyo tutaibatilisha Mikataba hio, Jee
inawezekana kua kama tukifanya hivyo basi Allah Subhanah wa Ta’ala atakupa
Ushindi na kisha utarudi wewe kwa watu na utauacha sisi?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam atabasamu na kisha akasema ‘La Damu ni Damu
na Maangamizo ni Maangamizo, Mimi ni mmoja miongoni mwenu na Nyinyi ni
Miongoni mwangu, nitapigana na yule mtakaepigana nae na nitatafuta usuluhishi
na yule mtakaesuluhishana nae’
Kisha baada ya hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawachagua Viongozi 12
ambao 9 walikua ni wenye kutoka katika Kabila la Khazraj na 3 kutoka katika Kabila la
Aws. Na kisha akawaambia kwa kusema: ‘Nyinyi ndio wasimamizi wa watu wenu
kama vile ilivyokua wale wasimizi wa Ibn Maryam na mimi ni Msimamizi wa watu
wangu.’
DARJA ZA MASAHABA WA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI
WA SALAM.
Anasema Imam Ibn Hajar Al Asqalani, kua Wanazuoni wanasema kua Sahaba ni: Mtu
alieamini na akamuona Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam japo kwa
mara moja, na mtu huyo akafa wakati akiwa ni Muislam. (Ibn Hajar, Al Isaba)
Masahaba wamegawika katika darja tofauti kutokana na nyakati za kusilimu kwao, hivyo
wale waliosilimu mwanzo hua na darja ya juu kuliko wale waliosilimu baadae. Darja hizi
zilionekana wazi katika maisha ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kwa
namna ya vile alivyokua akiishi na Masahaba zake, kwani siku moja Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam, alimkataza Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu pale
alipokua akigombana na Abd Rahman Ibn Awf Radhi Allahu A’nhu na Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam akamwambia Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu:
‘Msiwakere Masahaba zangu, kwani nnaapa kwa yule ambae Nafsi yangu imo
mikononi mwake! Hata kama mkitumia thamani ya Dhahabu yenye ukubwa wa
Mlima wa Uhud, basi hamtoweka kufikisha thamani ya vitendo vyao’.
753
Hii inatokana na ukweli kua Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu alikua ni miongoni
mwa Masahaba waliochelewa kusilimu kwani yeye aliingia katika Uislam katika kipindi
cha baina ya Mkataba wa Hudaibiyyah na kutekwa kwa mji wa Makkah lakini Abd
Rahman Ibn Awf Radhi Allahu A’nhu alikua ni miongoni mwa watu wa mwanzo kuingia
katika Uislam na pia ni miongoni mwa watu kumi waliobashiriwa Pepo.
Vile vile tunaona mfano mwengine juu ya hili pale ilipotokea siku walipogombana Umar
Ibn Al Khattab na Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu A’nhu, Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam akaingilia kati na kumwambia Umar Ibn Al Khattab: ‘Kwa nini
humuachi Sahaba yangu, kwa ajli yangu? Abu Bakr aliniamini katika wakati
ambao nyinyi nyote mlinikataa’, hapo Abu Bakr akainama na kusema: ‘Ya Rasul Allah
lilikua ni kosa langu’.
Hivyo tunapozungumzia Masahaba, tunatakiwa tujue kua kutokana na mitizamo ya
Wanazuoni basi Masahaba hua wamegawika katika makundi kumi na mbili yafuatayo:-
1. Makhalifah wanne ambao ni Abu Bakr As Siddiq, Umar ibn Al Khattab, Uthman Ibn
Affan na Ali Ibn Abi Talib, na wale waliobashiriwa Pepo wakati wakiwa bado hai, ambao
ni Zubair Ibn Al-Awwam, Abu Ubaidah Ibn Al-Jarrah, Abdur-Rahman Ibn Awf, Talha
Ibn Ubaidullah, Sa‘d Ibn Abi Waqqas na Said Ibn Zad, Radhi za Allah ziwafikie.
2. Wale waliowahi kuamini kabla ya kuamini Umar Ibn Al Khattab, ambao walikua
wakienda katika nyumba ya Arqam kisiri siri kusikiliza ujumbe wa Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam.
3. Muhajjirina waliohamia Uhabeshi (Ethiopia) kwa ajili ya Allah: katika Hijra ya
mwanzo.
4. Ansar au wale walionusuru na kuwepo wakati wa sherehe za kwanza za kula
kiapo cha kumuamini na kuwa pamoja na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam katika Al-Aqaba: Sherehe za Al Aqaba ni sherehe zilizofayika katika eneo Al
Aqaba ambalo ni la kimlima kidogo kiliopo pembezoni ya mji wa Makkah, katika sherehe
hizi walikuja watu 12 kutoka Yathrib (Madina) ambao walikua ni Abu Umamah As’ad
Ibn Zurarah, Awf Ibn Al Harith na kaka yake Mu’adh Ibn Harith, Rafi’ Ibn Malik,
Thakwan Ibn Abdil Qays, Ubaadah Ibn As Samit, Yazid Ibn Tha’labah, Al Abbas Ibn
Ubadah, Uqbah Ibn Aamir, Qutbah Ibn Aamir, waliotoka katika ukoo wa Al Khazraj,
Uwaym Ibn Sa’idah, na Abul Haytham Malik Ibn At Tayyihan waliotoka katika ukoo wa
Al Aws na kukutana na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na
wakakukubaliana makubaliano ya ushirikiano baina yao na Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam, na katika kiapo hicho walikubaliana kua: Watampwekesha na kumtii
Allah Subhanahu wa Ta’ala na amri zake zote, hawatoiba, hawatozini, hawatofanya
754
maovu, n.k na waliridhika kua kama watafanikiwa katika kuishi maisha ya utiifu kwa
Allah Subhanahu wa Ta’ala basi malipo yao yatakua ni Pepo, vyenginevyo malipo yao
yatakua kwa Allah Subhanah wa Ta’ala, ikiwemo kuwaadhibu na pia akitaka
kuwasamahe atawasamehe. Baada ya makubaliano hayo Nabii Salallahu A’layhi wa
Salam akawapa Sahaba Musab Ibn Umayr aende nao Madina ili akawasomeshe Qur’an
na mambo mengine yahusuyo dini ya Kiislam.
5. Ansar au wale walionusuru na kula kiapo cha kuwa pamoja na Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam baada ya Al-Aqaba: Hii ilikua ni katika mwaka uliofuatia
baada ya kiapo cha kwanza cha Al Aqaba, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
alikubaliana kukutana nao tena sehemu ile ile lakini safari hii watu walikua wengi zaid
kwani wanaume walikua wako 73 na wanawake wawili ambao walikua ni Umm Ammara
Nusaibat bint Ka'ab, na Umm Manee’ Asma’ bint Amr. Na hivyo wakakaubaliana
kukutana katika siku za Tashrik (Yaum Tashrik – siku za kuanzia mwezi 11, 12 hadi 13
za mwezi wa Dhul Hija), na katika kiapo hiki wakakubaliana pia kumsikiliza na kumtii
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam katika kila kitu, kujitolea kutumia kila
alichokua nacho mtu kwa ajili ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam iwe
katika wakati wa raha ama katika wakati wa shida, kumlinda Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam kutokana na kila kile anachojilinda mtu na Nafsi yake, na mke wake,
na watoto wake na familia yake, na kukatazana mabaya na kuamrishana mema kwa ajili
ya Allah, na wakifanikiwa kuyatekeleza hayo basi Pepo iko mikononi mwao.
6. Muhajjirina (Waliohama Makkah kuelekea Madinah ) wa mwanzo kuungana
na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kabla ya kuwasili katika mji wa
Madinah , alipokua Qubah ambapo alikua amepumzika kidogo akitokea Makkah katika
wakati wa Hijrah ya kwanza (Kuhama kutoka katika mji wa Makkah kwenda katika mji
wa Madinah ).
7. Ahl ul Badr : Masahaba waliopigana vita vya Badr.
8. Wale waliohamia Madinah baina ya kipindi cha vita vya Badr na mkataba wa
Hudaybiyah.
9. Masahaba waliokula kiapo kushirikiana na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam chini ya mti wakati wa mkataba wa Hudaybiyah.
10. Masahaba waliosilimu na kuhamia Madinah baada ya mkataba wa Hudaybiyah.
11. Masahaba waliosilimu baada ya kutekwa kwa mji wa Makkah.
755
12. Watoto waliomuona Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam wakati wa
uhai wake, aidha wakati wa kutekwa Makkah au katika wakati wa Hija ya mwisho ya
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, au waliomuona katika sehemu tofauti na
nyakati tofauti.
KUZALIWA KWA BAHR UL ILM ABDA ALLAH IBN ABBAS RADHI
ALLAHU ANHU.
A’bd Allah ni mtoto alietokana na baba aitwae Al ‘Abbas Ibn Al Muttalib Radhi Allahu
A’nhu, ambae ni Ami ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, na Mama aitwae
Al Lubaba Al Ghubra Bint Harith Ibn Hazan Al Hilalieh ambae alikua ni dada wa Al
Lubabab As Saghira Bint Harith Ibn Hazan Al Hilalieh ambae alikua ni mama yake
Khalid Ibn Walid na alikua ni dada yake Maymunah Bint Harith Ibn Hazan Al Hilalieh
ambae aliekua ni Mke wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam.
Abd Allah Ibn ‘Abbas Radhi Allahu A’nhu alizaliwa miaka mitatu kabla ya Hijra, wakati
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam anafariki Abd Allah Ibn ‘Abbas Radhi
Allahu A’nhu alikua na umri wa miaka kumi na tatu. Ingawa alikua ni kijana mdogo
lakini alikua na I’lm kubwa sana na hii inatokana na kua, baada ya kuzaliwa tu, mama
yake alimchukua Abd Allah Ibn ‘Abbas Radhi Allahu A’nhu na kumpeleka moja kwa
moja kwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ambae alimuwekea sehemu ya
mate yake yenye baraka kabla hata ya kuanza kunyonya.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua na ukaribu sana na binamu yake
huyu ambae alikua akiishi nyumbani kwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam,
na mara kwa mara alikua akikaa nae humuombea dua ‘Ya Rabb, mfanye awe na
ufahamu mkubwa wa I’lm ya Dini na umpe uwezo wa Tafsir’.
Anasema Abd Allah Ibn ‘Abbas Radhi Allahu A’nhu ‘Mara moja Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam alikua anataka kutia udhu, nikakimbilia kumpelekea
maji ya kutia udhu, alifurahia jambo hilo, na alipokua anataka kusali, akaniambia
nisimame pembeni yake, hata hivyo nilisimama nyuma yake, na baada ya kumaliza
kusali akaniuliza kitu gani kilichokufanya usisimame pembeni yangu, Ya Abd
Allah?’ nami nikajibu ‘Una cheo kikubwa sana katika macho yangu, kiasi ya
kwamba mimi siwezi kusimama pembeni na wewe’, hapo Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam akatabasamu na kunyanyua mikono juu na kusema ‘Ya Allah!
Mzidishie hikma’.
Bila ya shaka dua ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam hukubaliwa, Abd
Allah Ibn ‘Abbas Radhi Allahu A’nhu alipata I’lm wakati wa uhai wa Nabii Muhammad
756
Salallahu A’layhi wa Salam na baada ya kufariki kwake alikua Bahr ul I’lm (Bahari ya
I’lm ya Ummah wa Kiislamu) na alikua ni mwenye busara sana. Kila Abd Allah Ibn
‘Abbas Radhi Allahu A’nhu alipokua akikua kiumri na kiumbo alikua akikua kia I’lm,
kiufaham na kibusara pia, anasema Masruq Ibn al Ajda: ‘Kila nimuonapo Abd Allah
Ibn ‘Abbas Radhi Allahu A’nhu, hua nnasema: ni kijana anaependeza sana, na
anapozungumza hua nnasema: Ni kijana mwenye I’lm kubwa kupita watu wote’
Abd Allah Ibn ‘Abbas Radhi Allahu A’nhu alikua na kumbukumbu nzuri sana,
anapoelezea kitu huelezea kwa uwazi na kwa hoja zinazofahamika mara moja.
Sad Ibn Abi Waqqas Radhi Allahu A’nhu anamuelezea Abd Allah Ibn ‘Abbas Radhi
Allahu A’nhu kwa kusema ‘Sijawahi kuona mtu mwenye kufahamu haraka, na
mwenye I’lm kubwa na busara kuliko Abd Allah Ibn ‘Abbas, nimemuona Umar
akimwita katika kujadili matatizo magumu mbele ya Masahaba wakongwe
waliopigana vita vya Badr. Miongoni mwa Ansar na Muhajirin, Ibn ‘Abbas
anaweza akatoa hoja na Umar hatoweza kuipinga hoja yake.’ Abd Allah Ibn ‘Abbas
Radhi Allahu A’nhu alikua mrefu, mweupe mwenye sura ya kupendeza na uso
unaong’ara na alikua akipaka hina nywele zake na ndevu zake.
Na kisha baada ya hapo Waislam mmoja baada ya mmoja wakawa kidogo kidogo
wanafanya Hijra na kuhamia katika Mji wa Madinah kabla ya Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kuamrishwa na Allah Subhanah wa Ta’ala kuhamia katika mji wa
Madinah baada ya Makafiri kuamua kupanga Njama za kutaka kumuua Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam.
HIJRA YA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM
Katika kulala kwake Usiku, siku mmoja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alilala
na kuota kua ameamrishwa na Allah Subhanah wa Ta’ala ahame kutoka katika Mji wa
Makkah kisha ahamie katika mji wenye Mitende mingi sana, na alipouona Mji huo basi
kwanza akadhania kua ni Mji wa Al Yamamah kutokana na mazingira yake lakini Allah
Subhanah wa Ta’ala akamwambia kua Mji huo ni Madina, lakini mda wa kuhama ulikua
haujawasili bado kwani ndoto hio ilikua kabla ya Safari ya Isra na Miraj.
Hivyo mda huo ulipowadia basi akataarifiwa na hivyo katika mchana wa siku moja ya
Jumatano ya mwezi Rabbi al Awwal ambao ni sawa na September ya mwaka 622 basi
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akatoka na kuelekea katika nyumba ya Abu Bakr
Saddiq Radhi Allahu Anhu ambapo Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu aliposikia
kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliposikia ugeni huo basi alishangaa sana
kwani ilikua ni mchana wa siku ya joto kali sana hivyo akasema: ‘Wallahi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam hakuwahi kuja Nyumbani wangu katika wakati kama
757
huu, hivyo itakua lazima kuna jambo muhimu sana.’ Na kisha akamkaribisha ndani
na kusema: ‘Ya Rasul Allah! Kuna jambo gani?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala
ameniruhusu nihame katika Mji Wa Makkah nielekee katia Mji wa Madinah ’
Abu Bakr Saddiq Radhi Allahu Anhu akauliza: ‘Jee na mimi nimepata heshima hio ya
kuenda pamoja nawe?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Naam’
ambapo Abu Bakr Saddiq Radhi Allahu Anhu akafurahia sana kupata fursa hio kiasi ya
kua furaha yae ilimpekea kulia kwa hisia, za mapenzi yake kwa rafiki yake kipenzi ambae
ni Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Kisha baada ya hapo, Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akakubaliana na Abu Baqr
As Siddiq Radhi Allahu Anhu kua wazungumze na Abdullah Ibn Urayqit ambae ni Kafiri
anaeaminika katika utimizaji wa ahadi kua awasaidie kuwaongoza njia kuelekea katika
mji wa Madinah kwa malipo ya Ngamia wawili, na wakakubaliana kua wakutane kwenye
Mlima wa Thawr.
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akarudi Nyumbani kwake na alipofika
mara akatokea Malaika Jibril na kumwambia kua: ‘Leo Usiku usilale katika Kitanda
chako ambacho umezoea kila siku kulala’ na kisha akamfahamisha nini cha kufanya,
hivyo ulipoingia wakati wa kulala usiku basi Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam
akamwambia Ali ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kua: ‘Leo lala kitandani kwangu,
chukua hili guo langu la kijani ujifunike na wala usiwe na khofu kwani hakuna
madhara yatakayokufika.’
Na kisha akamkabidhi Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu na Ummu Ayman Radhi
Allahu Anha amana zote alizokabidhiwa na watu wa Makkah kwa ajili ya kuwakabidhi
wenye katika siku zitakazofuata wakati yeye akiwa hayupo. Na ulipoingia wakati wa
Usiku wa Manane wa siku hio ya kuamkia Alkhamis basi Makafiri wakajiandaa kwa ajili
ya kumsubiri Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam atakapotoka alfajir wamuue, kwani
kwa mila za Kiarabu hua haikubaliki kumuua Mtu wakati akiwa ndani ya nyumba yake.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipoamua kutoka basi akatoka na
kuwakuta Makafiri hao wakiwa wamelala nje ya nyumba yake wakiwa na Silaha zao,
hivyo akachukua Mchanga na kisha akausomea aya za Surat Yasin zisemazo:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞يس ۤ ۞وَٱلْقُرْآنِ ٱلحَْكِيمِ۞إِن َّ كَ لَمِنَ ٱلْمُ رْسَلِينَ۞عَلَىٰ
صِرَاطٍ م ُّسْتَقِيمٍ۞تَنزِيلَ ٱلْعَزِيزِ ٱلر َّحِ يمِ۞لِتُنذِرَ قَوْماً م َّآ أُنذِرَ آآبَ ُؤهُمْ فَهُ ْم
758
غَافِلُونَ۞لَقَدْ حَق َّ ٱلْقَوْلُ ٰ عَلَى أَكْثَرِهِمْ فَهُمْ لاَ يُؤْمِنُونَ۞إِ َّ َج عَلْنَا فيِۤ ن ا أَْع قِهِْم
أَغْلاَلاً فَهِىَ إِلىَ ٱلأَذْقَانِ فَهُم م ُّقْمَحُونَ۞وَجَعَلْنَا مِن بَينِْ أَيْدِيهِمْ سَ ّداً ومِ ْن
خَلْفِهِمْ سَدّاً فَأغْشَيْنَاهُمْ فَهُمْ لاَ يُبْصِرُونَ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Ya-seen; Waalqur-ani alhakeemi; Innaka
lamina almursaleena; AAala siratin mustaqeemin; Tanzeela alAAazeezi
alrraheemi; Litundhira qawman ma ondhira abaohum fahum ghafiloona; Laqad
haqqa alqawlu AAala aktharihim fahum la yu/minoona; Inna jaAAalna fee
aAAnaqihim aghlalan fahiya ila al-athqani fahum muqmahoona; WajaAAalna min
bayni aydeehim saddan wamin khalfihim saddan faaghshaynahum fahum la
yubsiroona (Surat Yasin 36:1-9)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma, Yasiin, Naapa kwa
Qur’an iliyojaa hikma; Hakika wewe (Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) ni
Miongoni mwa Mitume; Ulie katika njia iliyonyooka; Hii (Qur’an) ni uteremsho
kutoka kwa Mtukufu mwenye Rehma; Ili upate kuwaonya Watu, ambao wazee wao
hawakuonywa hivyo wakawa ni wenye kughafilika; Kwa hakika kauli ya haki
imedhibitika juu yao lakini wengi wao si wenye kuamini; Kwa hakika tumeweka
Shingoni mwao vifungio vya vyuma hadi Videvuni mwao, hivyo Vichwa vyao
vimeelekea Juu; Na tumeweka pazia baina yao mbele yao, na baina yao nyuma yao na
tumewafunika hivyo hawawezi kuona kitu.
Na kisha akawarushia rushia mchanga huo kichwani na vifuani mwao, na kuwaacha
wakiwa wanaendelea kulala. Baada ya mda Makafiri hao wakaamshwa na wenzao na
wakaulizwa: ‘Mbona mmelala hapa mkiwa katika hali kama hii imekuaje?’ nao
wakajibu: ‘Tunamsubiri Muhammad’ hivyo wakaambiwa: ‘Mnaemsubiri hayupo
kwani amekumwagieni mchanga mwilini mwenu na kukuacheni kama mlivyo na
kisha akaenda zake, jiangalie namna mlivyo’
Makafiri hao wakajiangalia na kujikuta wamejaa michanga, na hapo hapo kwa haraka
sana wakanyanyuka na kukimbilia ndani ya Nyumba ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, na moja kwa moja hadi chumbani kwake, na walipofika Kitandani mwake
wakamkuta mtu ambae alikua amelala na kujifunika, wakakimbilia kumfunua guo hilo
mtu aliejifunika, na kwa mshangao wao badala ya kumuona Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam basi wakamuona Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu akiwa amelala kitandani
hapo badala yake.
759
Hivyo kwa hasira wakamkamata Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu na kumuuliza,:
‘Yuko wapi Muhammad?’ nae akajibu: ‘Hakika mimi si mwenye kujua kua
ameenda wapi.’
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala analielezea hili katika Qur’an pale aliposema:
﴿وَإِذْ يمَْكُرُ بِكَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ لِيُثْبِتُوكَ أَوْ يَقْتُلُوكَ أَوْ يخُْرِجُوكَ وَيمَْكُرُونَ وَيمَْ كُرُ ٱهلل َُّ
وَٱهلل َُّ خَيْرُ ٱلْمَاكِرِينَ ﴾
Wa-idh yamkuru bika alladheena kafaroo liyuthbitooka aw yaqtulooka aw
yukhrijooka wayamkuroona wayamkuru Allahu waAllahu khayru almakireena
(Surat Al Anfal 8:30)
Tafsir: Na kumbuka pale walipokupangia njama wale waliokufuru wakufunge ili
wakuue au wakufukuze (Kutoka kwako), na wakapanga njama na akapanga Allah
lakini Allah ni mbora wa kupanga.
Baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuwamwagia mchanga Watu hao na
kuondoka basi alielekea moja kwa moja hadi kwa Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu
Anhu na kisha wakachukua mahitajio yao, na wakaondoka huku Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akitumia mlango wa Nyuma na kisha wakaelekea kwenye Mlima wa
Thawr ambao upo katika umbali wa masafa ya kilomita 3 kutoka katika mji wa Makkah.
Ambapo safari yao hio ilimalizika ndani ya saa moja, na walipofika Mlimani hapo
wakakuta Pango ambalo lilikua tupu, huku ikiwa bado kiza kiza basi Abu Bakr Radhi
Allahu Anhu akaingia ndani ya Pango hilo na kisha akaanza kusafisha safisha ndani yake
ili angalau wapate kujihifadhi na kujificha ndani yake. Baada ya sehemu hio kua tayari
basi akamwita Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae nae akaingia ndani yake
na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akaziba uwazi wa pango hilo kwa kutumia
nguo yake na sehemu iliyobakia basi akaziba kwa kutumia unyayo wake.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuegemea rafiki yake kutokana na
uchovu wake na hapo hapo Allah Subhanah wa Ta’ala akamletea usngizi mzito sana kwa
ajili ya mapumziko yake. Ambapo ghafla Abu Baqr Radhi Allahu Anhu akahisi maumivu
makali sana katika Mguu wake ambao ndio uliokua umeegemewa na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo akashindwa kuuangalia mguu wake kutokana na kua
na khofu kua kufanya kwake hivyo kutamwamsha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam na kumkatisha usingizi wake mbali ya kua aligundua kua maumivu hayo
yametokana na sumu ya nyoka aliekua akiondoka baada ya kumtafuta mguu wake.
760
Abu Baqr Radhi Allahu Anhu aliendelea kustahmili maumivu hayo hadi taratibu machozi
yakaanza kumtoka na kumdondokea Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam usoni
mwake, jambo ambalo lilipelekea kumwamsha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na kumuuliza: ‘Vipi mbona unalia kuna kuna nini?’ ambapo Abu Baqr Radhi Allahu
Anhu akasema: ‘Ya Rasul Allah kuna Mdudu kanitafuna mguu wangu, lakini hamna
tatizo kwani bora Baba yangu na Mama yangu watolewe kafara kwa ajili yako.’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akalipaka Mate jeraha hilo na hapo hapo
maumivu aliyokua akiyahisi Abu Baqr Radhi Allahu Anhu yakatoweka na ukapona mguu
wake.
Wakati yote haya yanaendelea ya kuamka kwake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na kisha kua ni mwenye kutibu Jeraha la Abu Bakr Radhi Allahu Anhu basi Allah
Subhanah wa Ta’ala kwa makadirio yake akatokea Mdudu Buibui na kuanza kutandaza
uzi wake kwenye Mlango wa pango hilo, na kisha kwa juu yake akatokea Njiwa akataga
na hapo hapo akawa ni mwenye kulalia Mayai yake.
Na kwa upande mwengine basi watu wa Makkah wakawa wamehamanika kwani
waliekua wakimtaka amewaponyoka, hivyo wakakimbilia kwenye Nyumba ya Abu Baqr
Radhi Allahu Anhu, kwani labda huenda wamtafutae ikawa amejificha kwake, lakini
walipofika nyumbani kwake basi wakakuta pia kua hata Abu Baqr Radhi Allahu Anhu
mwenyewe hayuko kwenye nyumba yake, hivyo wakajawa na hasira zaid kwani hata
Abu Baqr Radhi Allahu Anhu nae haionekani hata dalili yake.
Makafiri hao wakatangazia zawadi ya Ngamia 100, kwa yeyote yuleatakaemkamata au
kumuua Muhamamd Salallahu Alayhi wa Salam na kuuleta mbele yao Mwili wake, hili
lilikua ni dau kubwa sana kwa kila mtu wa Mji wa Makkah kwani hata kama ukiwa
masikini basi hua ni mwenye kuagana nao umasikini kama ukipata Ngamia hao, hivyo
kila mtu akafanya jitihada kwa ajili ya kumtafuta Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam,
na kuna baadhi wakakodi watu wenye uwezo wa kusoma nyao ardhini ili kujua muelekeo
na mda wa safari ya mwenye alama ya nyayo hizo.
Na hivyo Wataalamu hao wakafuatilia Nyao za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na Abu Bakr Radhi Allahu Anhu hadi kwenye Pango liliopo kwenye Mlima Thawr,
ambapo ndipo zilipomalizikia lakini sasa kila wakiangalia ndani ya pango hio basi
walikua wakiona yale wasiyoyategemea, kwani mtandao wa uzi wa Buibui ulikua
umetanda kwenye mlango mzima wa Pango hilo, na hakuna hata dalili ya kua labda
ulipanguswa na kutengenezwa tea, kwani uzi huo ulikua mkamilifu na buibui mwenyewe
yuko juu yake, kisha na pembeni yake kwa juu zaidi kuna Njiwa ambae alikua amelalia
Mayai yake.
Mazingira ya muonekano huu yaliwafanya watu hao kutoamini kua kile wanachokitafuta
kua kinawezekana kikawa kimo ndani yake, lakini sasa haiwezekani kwa kitu chochote
761
kuingia ndani yake pango hilo bila ya kuharibu mazingira wanayoaona mbele ya macho
yao ambapo wakati Makafiri hao wanashangaa kuona kua nyao hizo zimeishia hapo
halafu zikayayuka bila kuacha athari yeyote na kushangazwa na mazingira ya mlango wa
pango hilo basi kwa upande wa Abu Baqr Radhi Allahu Anhu alikua amejawa na khofu
kwani alikua ni mwenye kumuona kila mtu anaechungulia ndani ya pango hilo, na kuhisi
kua mda wa uhai wake umeifikia ukingoni kwani mda wowote wanaweza wakaangukia
ndani ya mikono ya maadui zao.
Lakini cha kushangaza ni kua hakuna hata mtu mmoja alieonesha kua amemuona Abu
Baqr Radhi Allahu Anhu, hivyo kwa tahadhari basi Abu Baqr Radhi Allahu Anhu
akasema kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Ya Rasul Allah
hakika mimi sitohisi vibaya wala sitojisikia huzuni kama watu hawa wataniona na
kuniua mimi, kwa sababu mimi ni mtu mmoja peke yake, lakini kwako wewe
wakikuua basi itakua wamesababisha maangamizi kwa Ummah wako.’.
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia Abu Baqr Radhi Allahu
Anhu kua: ‘Usiwe na khofu wa huzuni ewe Abu Baqr kwani kwa hakika Allah
Subhanah wa Ta’ala yuko pamoja nasi.’ Abu Baqr Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Ya
Rasul Allah hakika watu hawa kama mmoja wao atainama na kuchungulia kidogo
tu basi atatuona’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia Abu Baqr Radhi
Allahu Anhu kua: ‘Ewe Abu Baqr hivi unafikiria ni nini kitakachotokea kwetu
wakati sisi ni wawili na watu aliepo pamoja nasi ni Allah Subhanah wa Ta’ala? Hivi
unadhani kua itawezekana kukamatwa kwetu?’
Wakati wanajadiliana haya basi wakasikia sauti ya Ummayah Ibn Khalaf akiwaambia
Makafiri waliokua wakishangaa juu ya pango hilo kwa kusema: ‘Hivi jee mnafikiria
kua hawa watakua wameingia ndani ya Pango hili, hivi jee nyinyi hamuoni mtandao
wa Buibui huo? Wa Allahi mimi nnaona kua huyu Buibui amejenga hapa hata
kabla ya Muhammad mwenyewe hajazaliwa’
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuombea dua Abu Baqr Radhi Allahu
Anhu ili apate utulivu ndani ya nafsi yake aondokewe na khofu na wasiwasi wake,
ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala analielezea hili kwa kusema:
﴿إِلا َّ تَنصُرُوهُ فَقَدْ نَصَرَهُ ٱهلل َُّ إِذْ أَخْرَجَهُ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ اثَنىِ َ ٱثْنَينِْ إِذْ همَُا فىِ ٱلْغَارِ
إِذْ يَقُولُ لِصَاحِ بِهِ لاَ تحَْزَنْ إِن َّ ٱهلل ََّ مَعَنَا فَأَنزَلَ ٱهلل َُّ سَكِينَتَهُ عَلَيْهِ وَأَي َّدَهُ بجُِنُودٍ لم َّْ
762
وَجَعَلَ كَلِمَةَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ ٱلس ُّفْلَى ٰ وَكَلِمَةُ ٱهلل َِّ هِىَ ٱلْعُلْيَا وَٱهلل َُّ عَزِيزٌ تَرَوْهَا
حَكِيمٌ ﴾
Illa tansuroohu faqad nasarahu Allahu idh akhrajahu alladheena kafaroo thaniya
ithnayni idh huma fee alghari idh yaqoolu lisahibihi la tahzan inna Allaha
maAAana faanzala Allahu sakeenatahu AAalayhi waayyadahu bijunoodin lam
tarawha wajaAAala kalimata alladheena kafaroo alssufla wakalimatu Allahi hiya
alAAulya waAllahu AAazeezun hakeemun (Surat At Tawba 9:40)
Tafsir: Kama hamtomnusuru (Mtume wenu Salallahu Aalyhi wa Salam basi sio
tatizo)kwani Allah atamnusuru, (kama alivyomnusuru) wakati Makafiri
walipomfukuza na wa pili kati ya wawili baina yao walipokua kwenye pango alisema
kumwambia rafiki yake: ‘Usiwe na Khofu kwani Allah yuko pamoja nasi’ kisha Allah
akatuma utulivu juu yake na kumzidishia nguvu jambo ambalo hamkuliona, na
tukajaalia kauli za wale ambao waliokufuru kua zimedhalilika, na maneno ya Allah
kua yako juu na yametukuka, kwani kwa hakika Allah ni mwenye utukufu na ni
mwenye hikma.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu
Anhu walikaa na kupata utulivu ndani ya Pango hilo na kupumzika vya kutosha, kwani
walikaa kwa siku tatu kuanzia alfajir ya Alkhamis hadi Jumapili, kwa sababu walikua
wanajua kua Makafiri wataendelea kuwatafuta kwa siku mbili tatu kabla ya kukata tamaa
kwao.
Ambapo katika kipindi hiki basi Abdullah Ibn Abu Bakr Radhi Allahu Anhu alikua akikaa
katika mji wa Makkah na kusikiliza kinachoendelea katika jamii yake kasha usiku huenda
kwenye Pango la Mlima Thawr na kuwaelezea Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu kinachoendelea katika akili na ufahamu wa
watu wa Makkah kuhusiana nao, na kisha Alfajir hurudi katika Mji wa Makkah.
Na kwa upande mwengine basi Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu alikua na
Mtumwa wake aitwae Amir Ibn Fuhayra Radhi Allahu Anhu ambae yeye alikua akifuga
Mbuzi na kazi yake ilikua ni asubuhi kuwapelekea Maziwa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu na pia kufuta alama za nyayo za
Abdallah Ibn Abu Baqr Radhi Allahu Anhu.
Hivyo baada ya siku tatu basi Makafiri wa Makkah wakakata tamaa ya kuwapata Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu na hivyo
Abdullah Ibn Abu Bakr Radhi Allahu Anhu akawasilisha habari hio, ili Abdullah Ibn Abu
Bakr Radhi Allahu Anhu ili wajitayarishe kwa ajili ya kuchukua hatua ya pili ya mipango
763
yao ya safari ambayo ni kutoka kwenye Pango hilo na kuendelea na safari yao kueleka
katika Mji wa Madinah .
Na ulipoingia Alfajiri ya kuamkia siku ya Jumatatu basi wakatoka nje ya Pango hilo na
wakakutana na Abdullah Ibn Urayqit huku akiwa na Ngamia wake wawili ambao ndio
Malipoa yake waliyokubaliana nae Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Abu Baqr
As Siddiq Radhi Allahu Anhu hapo awali, huku pembeni yake akiwepo Asma Bint Abu
Baqr Radhi Allahu Anha ambae alikua amewatayarishia chakula cha safari yao hio.
Asma Bint Abu Baqr Radhi Allahu Anha alikua ametayarsisha Nyama ya Mbuzi na Maji
kwa ajili ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu
Anhu ambapo kutokana na haraka basi akasahau kuifunga mikoba hio ya ngozi yenye
Maji na Nyama, na hivyo ikambidi achane mkanda wa kanzu yake kwa ajili hio ili maji
hayo na Nyama zisimwagike na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipojua
kuhusiana na tukio hilo basi akampa Asma Bint Abu Baqr Radhi Allahu Anha jina la
Dhat an-Nitaqayn yaani mwenye Mikanda Miwili kwa ajili yake kesho Peponi.
Kisha baada ya hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Abu Baqr As Siddiq
Radhi Allahu Anhu wakapanda Ngamia wao hao wawili, huku Amir Ibn Furayha Radhi
Allahu Anhu kwa amepanda pia nyuma ya Ngamia wa na Abu Baqr As Siddiq Radhi
Allahu Anhu na safari yao ikaanza, lakini kabla ya kufika mbali basi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akageuka nyuma na kuuangalia Mji wake anaoupenda, Mji
aliokaa Miaka yote, Mji ulioanzishwa na Nabii Ibrahim na Nabii Ismail, hivyo kua ni Mji
ambao hataki kuachana nao, kutokana na utukufu wake, lakini alikua hana budi kwani
kama akibakia basi Maisha yake yatakua hatarini.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Wa Allahi Hakika wewe ni
Mji bora kuwahi kuumbwa na Allah Subhanah wa Taala, wewe ndie Mji
unaependwa zaidi na Allah Subhanah wa Ta’ala, na pia hakuna Mji nnaoupenda na
unaonivutia mie kama Mji wewe, hivyo wa hakika kama si kufukuzwa kwangu basi
mimi nisingekuhama na nisigetaka kuhamia katika Mji mwengine wowote zaidi
yako.’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
huyo kua:
﴿إِن َّ ٱل َّذِى فَرَضَ عَلَيْكَ ٱلْقُرْآنَ لَرَآد ُّكَ إِلىَٰ مَعَادٍ قُل ر َّبيّ ِ ۤ أَعْلَمُ مَن جَآءَ بِ ٱلهُْدَىٰ
وَمَنْ هُوَ فىِ ضَلاَلٍ م ُّبِينٍ ﴾
764
Inna alladhee faradha AAalayka alqur-ana laradduka ila maAAadin qul rabbee
aAAlamu man jaa bialhuda waman huwa fee dhalalin mubeenin (Surat Al Qasas
28:85)
Tafsir: Hakika ya yule ambae amekufaridhishia juu yako Qur’an, atakurudisha katika
sehemu ya kurudia (katika Mji wa Makkah), sema: ‘Mola Wangu ni mwenye Kujua ni
nani aliekuja na uongofu nani alie katika upotofu mkubwa sana’
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu
Anhu, Amir Ibn Furayha Radhi Allahu Anhu na Abdullah Ibn Urayqit wakaendelea na
safari yao ya kueleka Madinah lakini iliwabidi kubadilisha njia na kutumia njia ya
mzunguko ili wasije wakafuatwa na Makafiri, hivyo kwanza walielekea upande wa
Kusini Magharibi katika maeneo ya ardhi ya Mji wa Tihama na kisha wakageuza na
kuelekea juu katika upande wa Kaskazini wakikaribia kuambaa ambaa na mwambao wa
Bahari Nyekundu.
Ambapo katika kipindi hiki cha safari yao basi mara Ngamia wa Abu Baqr As Siddiq
Radhi Allahu Anhu anamkazanisha akae mbele ya Ngamia wa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam na mara anamrudi Nyuma ya Ngamia wa Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuuliza Abu Baqr As Siddiq
Radhi Allahu Anhu : ‘Ya Abu Baqr mbona hivyo mara unaenda mbele mara unarudi
nyuma yangu kuna nini?’
Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Ya Rasul Allah, hakika mimi
nikikaa nyuma yako basi siridhiki hua nahisi bora niwe mbele yako ili nipate
kukulinda kwa ajili ya usalama wako, na nikakaa nyuma yako basi hua siridhiki na
hua nahisi bora nikae mbele yako kwa ajili ya kukulinda usalama wako kwa upande
wa mbele yako.’
Safari ilikua ndefu a ya uchovu kwani siku hio walisafiri siku nzima wakiwa juu ya
Ngamia hadi siku ya pili yake asubuhi wakaamua kupumzika kwenye mmoja katika mti
iliyokua na kivuli, Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akashuka na kulala, huku Abu
Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akiwa ni mwenye kusimamia usalama, katika
kuangalia kwake basi kwa mbali akaona kuna mfugaji wa Kondoo, hivyo akamfuata na
kisha akarudi huku akiwa na maziwa na kumpa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
ambae alikua ameshaamka, na alipopewa akanywa.
Na kisha baada ya hapo wakaondoka na kuelekea tena kwa Mfugaji huyo ili wapate
maziwa mengine zaid lakini, mfugaji akasema: ‘Sina maziwa zaidi ya yale niliyokupeni
kwani maziwa ya Mbuzi wangu yamekauka’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akaomba kumuangalia Mbuzi huyo na kisha akazishika chuchu za Mbuzi huyo na
hapo hapo chuchu hizo zikawa ni zenye kujaa Maziwa. Tukio hili lilimstaajabisha sana
765
Mfugaji huyo a akauliza: ‘Hebu niambie wewe nani mbona mimi sijawahi kukutana
na mtu mwenye maajabu kama wewe.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia Mchungaji huyo kua:
‘Nitakuambia kama utakubalia kua hili nitakalokuambia litabakia kua ni siri yako’
Mfugaji huyo akasema: ‘Naam..sitomwambia Mtu yeyote’ Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akasema: ‘Mimi ni Muhammad Rasul Allah’
Mfugaji huyo akasema: ‘Hivyo wewe ndio yule mtu ambae watu wa Quraysh
wanasema kua umepotoka?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Naam
hivyo ndivyo wasemavyo’ Mfugaji huyo akasema: ‘Hakika mimi nnashuhudia kua
wewe ni Rasul Allah na kile ulichokuja nacho ni cha haki, kwani ni Mtume tu ndio
mwenye uwezo wa kufanya unayoyafanya wewe, hivyo nami nitakufuata na kukutii,
hivyo jee nami nnaweza kujumuika nanyi?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasema: ‘La bado kwanza, hivyo subiri kwanza hadi pale utakaposikia kua
nimefanikiwa ndio unaweza kujumuika nasi.’
Msafara huo wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ukaendelea na safari yake hadi
pale ulipofika katika maeneo ya Qudayd ambapo waliichagua sehemu hii pia kua ni ya
kumpumzikia kutokana na umbali wa masafa waliyotembea kutoka katika kituo cha
kwanza cha mapumziko, na walipofika katika maeneo hayo walikuta kuna hema la bwana
mmoja aliekua akijulikana kama Abu Mabad, ambae hata hivyo mwenye alikua hayupo
na badala yake alikuwepo Mke wake aliekua akiitwa Umm Mabad na hivyo wakamuuliza
baada ya kusalimiana nae kua: ‘Jee unaweza kutusaidia aina yeyote ya chakula
ulichonacho?’ ambapo nae akajibu kua hana chakula chochote cha ziada.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipoangalia pembeni akaona kuna Mbuzi
ambae alikua amekonda na kudhoofika, hivyo akasema: ‘Jee Mbuzi huyu hana Maziwa
yeyote?’ Hivyo Umm Mabad akasema: ‘Huyu mbuzi hana hata damu jee atakua na
maziwa kweli?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Kama utaniruhusu
nimkame basi nitamkama.’
Hivyo Umm Mabad akaona huyu hawa wageni wanataka kuleta ubishi, hivyo
kuwakomesha ubishi wao basi bora awaruhusu wamkame Mbuzi huyo ili wajiridhishe
kua kweli hana Maziwa, hivyo akasema: ‘Sawa Nakuruhusu Mkame’ ambapo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamsogelea Mbuzi huyo na kisha akamshika chuchu
zake na kusema: ‘Biismi Allahi Al Rahmani Al Rahim’ na kisha akaomba dua na
kuomba aletewe chombo cha kuhifadhia maziwa.
Na alipoletewa akaanza kumkama Mbuzi huyo, na taratibu Mbuzi huyo akaanza kutoa
Maziwa ambayo kadri anavyokamwa basi ndivyo yalivyokua yakiongezeka wingi wake
maziwa hayo, chombo kilicholetwa kikajaa, Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
766
akanywa maziwa yeye na watu wake, na mengine yakabakia na Mbuzi akawa anaendelea
kutoa Maziwa, na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaomba kua Mbuzi
huyo asichinjwe.
Na kisha msafara wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ukaendelea na safari yake,
na huku nyuma Abu Mabad aliporudi kwake akashangaa alipokuta Maziwa mengi
Nyumbani kwake, hivyo akauliza yametokea wapi maziwa hayo, basi Umm Mabad
akajibu: ‘Kuna Mtu wa Maajabu yenye Baraka alipita leo hapa kwetu, akaomba
chakula nilipomwambia hakuna basi akaomba kumkama Mbuzi wetu aliedhoofu,
mwanzo nilisita kumruhusu lakini baadae nikamruhusu, na alipomkama basi alitoa
maziwa mengi sana yaliyotosheleza watu wake na mengine yaliyobakia ndio haya
kwa ajili yetu. Na amesema kua Mbuzi huyu asichinjwe.’
Hivyo Abu Mabad akaomba aelezewe muonekano wa Mtu huyo, ambapo baada ya
Umma Mabad kumuelezea basi Abu Mabad akasema kua: ‘Wa Allahi huyu Mtu
unaemuelezea ndie mtu ambae ni Rasul Allah alieibuka katika Mji wa Makkah
miongoni mwa watu wa Quraysh, na kwa hakika kama mimi ningekuwepo hapa
wakati alipokuja basi mimi ningemkubali na kumtii na kisha ningefuatana nae.’
Ambapo anasema Umm Mabad Radhi Allahu Anha kua: ‘Mbuzi alieamrisha Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua asichinjwe aliishi hadi mnamo mwama 18 wa
Al Hijra katika wakati wa Utawala wa Amir ul Muumini Umar Ibn Al Khattab
ambapo hata pale ilipokua kuna ukame na Wanyama hawatoi Maziwa kutokana na
kukosa chakula basi Mbuzi huyo alikua akitoa maziwa asubuhi na jioni.’
Ingawa Makafiri wa Makkah walikua wamekata tamaa kuhusiana na kumkamata Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam lakini hata hivyo tamaa hio ilirudi tena upya baada ya
kupata habari kua na msafara wa Watu wanne umeonekana katika maeneo ya karibu na
Mwambao wa Bahari Nyekundu, hivyo mmoja kati ya watu wenye umahiri wa kufuata
nyayo za Watu aliekua akiitwa Suraka Ibn Malik basi akaamua kuufuatilia msafara huo
wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, kwa kutumia Farasi wake kwani Msafara wa
Ngamia hua hauna mwendo tofauti na safari ya Mpanda Farasi.
Na hivyo katika jitihada zake basi haukuchukua mda isipokua aligundua alama za nyayo
hizo na akaanza kuzifuata, na baada ya siku kadhaa akanza kuuona kwa macho yake
msafara huo na kufurahia kwa kuukimbilia, ambapo watu wote waliokuwemo kwenye
msafara huo basi waliingiwa na khofu isipokua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
ambae yeye aliwatuliza watu wake hao kwa kuwaambia kua wasiwe na khofu ya aina
yeyote.
Hivyo baada ya kuhakikishiwa usalama wao basi wakamuangalia Suraka ambae alikua
anawakaribia, lakini ghafla wakamuona kua ingawa alikua anapita mle mle walikopita
767
wao kwenye Nyayo za Ngamia wao lakini miguu ya Farasi wake Suraka ikazama hadi
magotini, na hivyo akashindwa kuwasogelea karibu, baada ya mda Farasi huyo
akakwamuka na kupiga hatu ambili tatu lakini hata hivyo farasi huyo akazama tena
kwenye mchanga na kisha mbele yake ardhini ukatoka kama Moshi Mubwa sana,
ambapo tukio hili lilimshtua sana Suraka na hivyo akanadia wa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwa kusema: ‘Ewe Muhammad niombee ili nipate kuokoka na kisha
sitokufuata tena na wala sitowaambia watu wanaokutrafuta kuhusiana nawe’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuombea dua Suraka na akajihisi kua
yuko salama kwani Farasi wake akakwamuka na kisha yeye akamkaribia Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na kumwambia kua anataka kutoka kwake Barua ya
uthibitisho wa usalama wake, kwani anajua kua Dini ya Kiislam itaibuka na kua juu
kiutawala, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuamrisha Abu Baqr Radhi
Allahu Anhu amuandikie Barua hio, ambapo baada ya kukabidhiwa basi Suraka akasema:
‘Ya Rasul Allah niamrishe mimi kitu chochote kile unachotaka nikitekeleze nami
nitatekeleza’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaamwambia: ‘Hakika mimi
nataka uwazuie watu wengine kutokana na kunifuata nyayo zangu katika safari
yangu hii ya kuelekea Madinah ’
Hivyo Suraka akarudi katika Mji wa Makkah na kuwaambia watu wa Quraysh kua kwa
hakika baari walizsipata kuhusiana na msafara wa watu wanne ulioonekana katika
maeneo ya mwambao wa Bahari Nyekundu hazikua ni habari za kweli, kwani walikua ni
watu wengine na hakua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na msafara wake. Na
kisha mnamo mwaka wa 8 Al Hijra Suraka akahamia katika Mji wa Madinah na kuingia
katika Dini ya Uislam.
Ambapo baada ya tukio hili basi mmoja kati ya Wafugaji aliuona Msafara huo na
akaamua kua aende akapeleke habari katika Mji wa Makkah, na alipofika basi ilikua kila
akitaka kuenda kuwaambia watu wa Kabila la Qurash kuhusiana na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam ilikua mara tu anapofika mbele yao alikua ni mwenye kusahau
kuhusiana na dhumuni la safari yake hio.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na msafara wake wakaendelea na safari yao na
njiani wakakutana na Zubayr Ibn Awaam Radhi Allahu Anhu ambae alikua akitokea
Madinah kuelekea Makkah na Biashara zake na alipowaona akasalimaiana nao na kasha
akawapa zawadi ya nguo za kutoka Syria zinazoitwa Mashlah na kasha akawaambia kua
Waislam wa Madinah wanasema kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
anachelewa kufika, wakati wao wana hamu nae sana kumpokea. Hivyo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akaongeza kasi katika Msafara wake huo ili wasipate
kuwachosha watu wa Madinah wanaowasubiri kwa hamu.
768
Lakini hata hivyo kabla hawajafika katika Mji wa Madinah basi njiani wakakutana na
kundi la watu wapatao 80 ambao walikua wako kwenye maeneo ya Amim. Watu hawa
walikua ni watu ambao walipata habari kua watu wa Makkah wametayarisha zawadi ya
Ngamia 100 kwa atakampeleka Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika Mji wa
Makkah aidha akiwa hai au amekufa, hivyo msafara wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam ulipofika mbele yao na kuwasimamisha basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akamuuliza kiongozi wa watu hao ni nani?
Akatoka mbele na kusema kua yeye anaitwa Burayda Ibn Husayb ambapo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Abu Baqr hakika hali yetu imekua Baridi
na ya kupendeza’ (Kwani neno Burayda kwa kiarabu ni lenye kutoikana na neno Baridi)
kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuuliza Burayda: ‘Na Ukoo wenu
unaitwaje?’ Burayda akajibu: ‘Aslam’ ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasema: ‘Ewe Abu Baqr hakika sisi tayari tumeshaupata Usalama’(Kwani neno
Aslam linatokana na neno Salam)
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akauliza: ‘Jee ukoo wa Aslam unatokana
na kabila gani?’ Burayda akasema: ‘Kutokana na Banu Sahm’ hivyo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Abu Baqr, hakika Upinde wako
Umechomoza’ (kwani kwa Lugha ya Kiarabu neno Sahm hua linamanisha Upinde)
ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alifanya hivi kwa sababu alikua ni mtu
ambae hapendi kunasibisha Majina na au vitu na mambo mabaya mabaya bali alikua ni
mtu mwenye kupenda kila kitu na kila jambo kunasibisha na Vitu vizuri.
Hivyo kutokana na uzuri wake huo wa kunasibisha kila kitu na kitu kizuri basi Burayda
akavutiwa na maumbile hayo ya kitabia na akamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kwa kusema: ‘Jee na wewe ni nani?’ ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akajibu kwa kusema: ‘Mimi ni Muhammad Ibn Abdullah Ibn Abdul Mutallib
na pia ni Rasul Allah, hivyo nakukaribisha katika dini ya Kiislam’
Maumbile, Tabia na kauli za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam zilimvutia sana
Burayda kiasi ya kua hapo hapo bila ya kusita akakubalia kuingia kwenye Dini ya
Kiislam yeye pamoja na watu wake wote aliokua nao, na kisha wakamkaribisha Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam na msafara wake kwa ajili ya kupumzika katika eneo
lao kabla ya kumalizia safari yake kuelekea Madinah .
Na ilipowadia asubuhi yake basi Buraydah akamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam : ‘Ya Rasul Allah Sio Vizuri kuingia kwenye Mji wa Madinah bila ya kua
na Bendera’
Na kisha Buraydah akavua kilemba chake na akatengeneza Bendera kwa ajili ya Msafara
wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambapo kutokana na tukio hili Rasul Allah
769
Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Miongoni mwa Masahaba zangu basi mmoja
wao atakufa katika Nchi, ambapo atafufuliwa katika siku ya Malipo huku akiwa ni
Nuru ya Nchi hio na kiongozi wa Nchi hio’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaendelea na safari yake kuelekea katika
mji wa Madinah . Ambapo nao Watu wa Madinah walikua wametoka nje ya Mji wa
Madinah kwa hamu yao kubwa sana kiasi ya kua wameshindwa kujizuia kukaa ndani ya
Mji wao na kuamua kumsubiri Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika maeneo ya
Harra mara tu baada ya kumaliza kusali sala ya Alfajiri.
Na ilipoingia wakati wa mchana huku jua likiwa kali basi mara Myahudi mmoja aliekua
juu ya nyumba yake akanadia baada ya kuona kutoka katika maeneo ya Amim basi
akanadia: ‘Enyi Waarabu, Mtu wenu mliekua mkimsubiri yule kule anakuja!’
ambapo habari ya sauti hii ilivyosambaa kwa kasi basi ilikua kama vile hali ya moto
ulioingia wenye shamba lenye nyasi kavu, kwani Mji mzima wa Madinah ulikua kama
uliokua umelala halafu ghafla ukaamka kwa zogo linalotokana na shangwe na vigelegele
na nuru ya furaha, na hivyo kila sehemu ya Mji huo ikawa ni yenye kusheherekea juu ya
tangazo hilo, na kukimbilia kutoka nje ya Mji wa Madinah na kuelekea kwenye upande
wa maeneo ya Amim.
Ambapo walimuona Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na msafara wake akiwa
amesimama chini ya kivuli cha Mtende kutokana na Jua kali la siku hio, hivyo
wakamkaribia na kumkaribisha kwa furaha, ambapo miongoni mwao pia kulikua na watu
wa Mji wa Quba ambao walimuomba Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua
kwanza aende katika kijiji chao kabla ya kuingia na kuhamia rasmin katika mji wa
Madinah na hivyo baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuzungumza na watu
wa Madinah na watu hao wa Quba basi akaamua kuelekea katika maeneo ya upande wa
kulia wa Mji wa Madinah katika maeneo ya kijiji cha Quba ambacho kilikua kiko katika
umbali wa masafa ya kilomita 3 ambayo ni sawa na safari kama ya saa moja kutoka
Madinah .
MUHAMMAD SALALLAHU ALAYHI WA SALAM, ALI IBN ABI TALIB NA
SUHAYB AL AL RUMI RADHI ALLAHU ANHUM NDANI YA ARDHI YA
QUBA
Msafara ulipofika katika Mji wa Quba basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akafikia kwenye Nyumba ya Kulthum Ibn Hidam ambae ndie aliekua Mkuu wa kabila la
Banu Amr Ibn Awf na alikua ni mtu mzima sana, na kisha akaelekea kwenye Nyumba
ya Sad Ibn Haytham katika Nyumba iliyokua ikijulikana kama Dar ul Uzab, kwani hii
ilikua ni nyumba inayokaa Masahaba wajane watupu. Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
770
Salam alikaa katika Kijiji cha Quba kwa kama wa wiki mbili kwa ajili ya matayarisho
kadhaa.
Ikiwemo kumsubiri Ali Ibn Talib Radhi Allahu anhu ambae yeye aliondoka katika Mji
wa Makkah siku tatu baada ya kuondoka Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na hi
hivyo alipofika katika mji wa Quba basi alikua taabani, kwani alitembea kwa masafa yote
na hivyo Miguu yake ilikua imevimba na kufanya malengelenge, aambapo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alipomuona basi alimkubatia na kumonea huruma sana huku
akitokwa na machozi kutokana na hali yake na kisha akamuombea Dua na kumgusa
kwenye miguu yake hio na hapo hapo miguu yake ikapona.
Na pia katika wakati huo huo wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwa bado
yupo katika Mji wa Qubah akawasili pia Suhayb Ibn Sinan Al Rumi Radhi Allahu Anhu
ambae alikua ni miongoni mwa Masahaba waliokua hawajahama kutokana na kumuunga
Mkono Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae nae alikua awemo ndani ya
Msafara wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu
Anhu, lakini Allah Subhanah wa Ta'ala akaamua kumjaribu zaidi Suhayb Al Rumi, kwani
katika siku hio alipotaka kuondoka nao basi yeye akakamatwa na kuwekwa chini ya
Ulinzi kwa masaa 24 kwa siku kadhaa.
Lakini mtihani huu haukua mkubwa sana kwa Suhayb Al Rumi kwani kutokana na
Ufaham wake, basi siku moja wakati akiwa chini ya ulinzi akaanza maradhi ya kuharisha,
ikawa kila wakati anaenda chooni, tumbo limembana na akienda anaharisha.
Katika siku hio walinzi hao wake walimfuata Chooni zaidi ya mara 10 mpaka wakachoka,
ikafika hali wakasema: ‘Mwache akaharishe kwani hio ni Adhabu yake kutoka kwa
Al Lata na Al Uzza kajitafutia mwenyewe’
Hali hii ya kuharisha iliendelea mpaka usiku, na hivyo usiku huo Walinzi hao wakawa
hawana khofu ya kua huenda Suhayb Al Rumi Radhi Allahu Anhu atakimbia, kwani hata
Kukimbia hawezi kwa kuharisha, hivyo wakasinzia na kulala, na hii ndio fursa dhahabiya
yaani fursa ya Dhahabu aliyokua akiisubiri Suhayb Al Rumi Radhi Allahu Anhu, na hivyo
waliposinzia walinzi wake basi alipotoka kuenda Chooni hakurudi tena ndani, bali
alitokomea moja kwa moja na Farasi wake kuelekea katika Mji wa Madinah .
Lakini hata hivyo walinzi wake wakawahi kuamka na kugundua kua amekimbia na Farasi
wake hayupo, hivyo nao wakapanda Farasi wao na kukimbilia Upande wa Madinah . Na
hakuchukua Mda isipokua Walinzi hao wakamuona na kumkaribia Suhayb Al Rumi
Radhi Allahu Anhu, ambae nao akaongeza kasi lakini hata hivyo, akaona bora asimame
ilia akabialiane nao walinzi hao kwa silaha.
771
Hivyo Suhayb Al Rumi Radhi Allahu Anhu akasimama kisha akatoa Upinde na kuanza
kuwatunga Shabaha watu wao wanaomkimbilia, na walipomkaribia basi akasema: ‘Enyi
watu wa Quraysh hakika nyinyi mnanijua mimi kwa Umahiri wangu wa Kutunga
Shabaha kwa kutumia Upinde! Mnajua kua hakuna mbora zaid yangu, na
nikiachia basi sikosei, hivyo naapa mimi kua atakaenikaribia, basi naanza ane kwa
upinde na kisha namalizana na mwengine kwa upinde mwengine na kwa upanga
pia.’
Ambapo Makuraysh hao nao wakasema: ‘Wallahi na sisi pia hatuwezi kukuachia
wewe ukiwa hai na pia ukiwa na baadhi ya mali zako zilizobakia Makkah, kwani
ulikuja katika Mji wa Makkah ukiwa masikini dhaifu na huna kitu lakini sasa hivi
umeshachuma ulichokichuma, haiwezekani tukuachie...hivyo leo ama ni siku yako
ama ni siku yetu’
Hivyo Suhayb Ibn Sinan Al Rumi Radhi Allahu Anhu akawaambia watu hao: ‘Sawa,
hivyo jee kama nikiamua kukuwachieni mali zangu zote zilizobakia katika Mji wa
Makkah, mtaachaana na Mimi?’ hivyo Makafiri hao wakakubaliana na makubaliao
hayo na kusema: ‘Naam.’
Hivyo Suhayb Al Rumi Radhi Allahu Anhu akawaelekeza alipozificha Mali zake kwenye
nyumba yake katika Mji wa Makkah, na hivyo Makafiri hao wakamwachia hivyo Suhayb
Al Rumi Radhi Allahu Anhu akaendelea na safari yake huku akiwa na hamu na ari kubwa
zaidi ya kukutana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika Mji wa Quba ambapo
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipomuona Suhayb Al Rumi Radhi Allahu Anhu
basi alifurahia sana kuwasili kwake na kisha akaMwambia Suhayb Al Rumi Radhi Allahu
Anhu kua: ‘Hakika mabadilishano ya Biashara yako yamekua na faida kubwa sana
ya Abu Yahya, biashara yako imekua na faida kubwa sana, Hakika Biashara yako
imekua na faida kubwa sana ya Abu Yahya.’
Ambapo maneno haya yalimshangaza na kumfurahisha sana Suhayb Al Rumi Radhi
Allahu Anhu na hivyo akasema: ‘Ya Rasul Allah! Wallahi, hakika mimi sijamuambia
Mtu yeyote, na hakuna mtu yeyote aliekuja kabla yangu mbele yako na kukutaarifu
juu ya hili labda kutokana na kuona yaliyotokea, hivyo inaonekana ni Jibril tu
pekee ndie atakaekua aliekuletea habari hizi’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Naam, kwani Allah
Subhanah wa Ta’ala amenishushia kupitia kwake aya isemayo:
﴿وَمِنَ ٱلن َّاسِ مَن يَشْرِى نَفْسَهُ ٱبْتِغَآءَ مَرْضَاتِ ٱهلل َِّ وَٱهلل َُّ رَؤُوفٌ بِ ٱلْعِبَادِ ﴾
772
Wamina alnnasi man yashree nafsahu ibtighaa mardhati Allahi waAllahu raoofun
bialAAibadi (Surah al-Baqarah, 2:207)
Tafsir: Na miongoni mwa Watu kuna yule ambae amejitolea kuiuza Nafsi yake kwa
ajili ya kufanya vitendo vitakavyomridhisha Allah, na Allah ni Mwingi wa Upole kwa
Waja wake.
Aya zinatuonesha tunaona namna walivyokua Masahaba mbele ya Mola wao na mbele
ya Mtume wao Salallahu Alayhi wa Salam. Kiasi ya kua kutoka na Imani yao na kujitolea
kwao basi Allah Subhanah wa Ta'ala anawataja waziwazi katika Kitabu chake kitukufu
cha Qur'an kua kama Mfano kwetu mimi na wewe.
Ambapo Allah Subhanah wa Ta'ala katika aya hii anamsifia Sahaba huyu aliekua
Mzungu mwenye Nywele za Dhahabu Suhayb Al Rumi. Kutokana na namna
alivyojitolea kwa Ajili ya Mola wake, na hivyo Allah Subhanah wa Ta'ala kututhibitishia
wazi kua:
Yeye Allah Subhanah wa Ta'ala haangalii kama wewe ni Muarabu, Mzungu, Mswahili,
Mchina au Mhindi, bali anachokiangalia na Kukithamini ni Imani yako Juu yake Ndani
ya Moyo wako.
Kwani Ngozi ya Rangi yako ni Tofauti ya kukutambulisha tu asili yako ni Mtu wa wapi,
ambayo haina maana kwani chenye maana ni Kua Unaelekea Wapi Maishani Mwako!
Ambapo kama kwamba aya hio haitoshelezi, yaani labda kuna watu hawajafahamu bado,
basi Allah Subhanah wa Ta'ala akaendelea Kupigilia Msumari kuhusiana na Ubora wa
Imani ya Suhayb Al Rumi kwa Kila alieamini kua awe ni mwenye kufuata Mfano wake
pale aliposema katika Aya unayofuatia baada ya hio kua:
﴿َٰي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ ٱدْخُلُواْ فىِ ٱلسِّ لْمِ كَآف َّةً وَلاَ تَت َّبِعُواْ خُطُوَاتِ ٱلش َّ يْطَانِ إِن َّهُ لَكُمْ
عَدُو ٌّ م ُّبِينٌ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo odkhuloo fee alssilmi kaffatan wala tattabiAAoo
khutuwati alshshaytani innahu lakum AAaduwwun mubeenun (Surat Al Baqara
2:208)
Tafsir: Enyi wale ambao ni Mlioamini, ingieni katika Uislam kikamilifu kwa Moyo
wote na wala msifuate hatua za Shaytan kwani kwa hakika yeye kwenu nyie ni adui
Mkubwa sana wa asili na wa mda mrefu.
773
Ambapo katika wakati huu pia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alibakia katika
kijiji cha Quba kwa ajili ya kujenga Msikiti wa Mwanzo katika historia ya Kiislam ambao
ulikua unajulikana kama Masjid Quba.
MASJID TAQWA - MSIKITI WA MWANZO KUJENGWA NA RASUL ALLAH
SALALLAHU ALAYHI WA SALAM.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliofika katika Mji wa Quba basi alisimamia
kujenga Msikiti wa mwanzo mara baada ya kupewa Utume wake, Ambapo ujenzi wa
Msikiti huu ulikua ukihudumiwa maji yake kutokana na kisima cha Abu Al Ansari Radhi
Allahu Anhu, ambacho ndicho kilichopata heshima ya kua ndio kima ambacho Ngamia
wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisimama na kunyweshwa maji yake baada
ya mda mrefu wa safari ya Jangwani.
Msikiti huu wa Quba ulijengwa katika Ardhi ya Kulthum Ibn Hidam Radhi Allahu Anhu
ambayo alikua akiitumia kwa ajili ya kuanika na kukaushia Tende zake, baada ya yeye
mwenyewe Kulthum Ibn Hidam Radhi Allahu Anhu kuitoa ardhi hio kwa ajili ya kutafuta
ridhaa za Allah Subhanah wa Ta’ala juu yake. Na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam hakusimamia tu ujenzi huo bali pia alishiriki kikamilifu katika kuujenga kwake,
kiasi ya kua hata Masahaba walikua wakimuonea huruma kwa namna alivyokua akibeba
Mawe makubwa makubwa kwa ajili ya kusimamisha ukuta wa Msikiti huo.
Kutokana na jitihada zake hizo basi mmoja kati ya Masahaba alimwambia Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Ya Rasul Allah Baba yangu na Mama yangu atolewe
kafara kwa ajili yako, nipe mie hilo jiwe wewe pumzika’ Rasul Allah Salallah Alayhi
wa Salam akasema: ‘La. Haiwezekani hivyo wewe nenda chukua jiwe jengine.’ Na
hivyo baada ya Msikiti huo kumalizika ukawa unaitwa Masjid Taqwa kutokana na
maneno ya zile aya zisemayo juu yake kua:
﴿وَٱل َّذِينَ ٱتخ ََّذُواْ مَسْجِ داً ضِرَاراً وَكُفْراً وَتَفْرِيقاً بَينَْ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَإِرْصَاداً لِّمَنْ
حَارَبَ ٱهلل ََّ وَرَسُولَهُ مِن قَبْلُ وَلَيَحْلِفُن َّ إِنْ أَرَدَْ إِلا َّ ٱلحُْسْنىَٰ وَٱهلل َُّ يَشْهَدُ إِن َّهُ ْم
لَكَاذِبُونَ۞لاَ تَقُمْ فِيهِ أَبَداً ل َّمَسْجِ دٌ أُسِّ سَ عَلَى ٱلت َّقْوَىٰ مِنْ أَو َّلِ يَوْمٍ أَحَ ُّق أَن
تَقُومَ فِيهِ فِيهِ رِجَالٌ يحُِب ُّونَ أَن يَتَطَه َّرُواْ وَٱهلل َُّ يحُِب ُّ ٱلْمُط َّهِّرِينَ۞
أَفَمَنْ أَس َّسَ بُنْيَانَهُ
عَلَى ٰ تَقْوَىٰ مِنَ اهلل َِّ وَرِضْوَانٍ خَيْرٌ أَم م َّنْ أَس َّسَ بُنْيَانَهُ عَلَى ٰ شَفَا جُرُفٍ هَارٍ
774
فَٱنْهَارَ بِهِ فىِ َرِ جَهَن َّمَ وَٱهلل َُّ لاَ يَهْدِى ٱلْقَوْمَ ٱلظ َّالِمِينَ۞ لاَ يَزَالُ بُنْيَانُهُمُ ٱل َّذِى
بَنَوْاْ رِيبَةً فىِ قُلُوهبِِمْ إِلا َّ أَن تَقَط َّعَ قُلُوبُهُمْ وَٱهلل َُّ عَلِيمٌ حَكِيمٌ ﴾
Waalladheena ittakhadhoo masjidan diraran wakufran watafreeqan bayna
almu/mineena wa-irsadan liman haraba Allaha warasoolahu min qablu
walayahlifunna in aradna illa alhusna waAllahu yashhadu innahum lakadhiboona;
La taqum feehi abadan lamasjidun ossisa AAala alttaqwa min awwali yawmin
ahaqqu an taqooma feehi feehi rijalun yuhibboona an yatatahharoo waAllahu
yuhibbu almuttahhireena; Afaman assasa bunyanahu AAala taqwa mina Allahi
waridhwanin khayrun am man assasa bunyanahu AAala shafa jurufin harin
fainhara bihi fee nari jahannama waAllahu la yahdee alqawma aldhdhalimeena; La
yazalu bunyanuhumu alladhee banaw reebatan fee quloobihim illa an taqattaAAa
quloobuhum waAllahu AAaleemun hakeemun (Surat At Twaba 9:107-110)
Tafsir: Ama kwa wale ambao ni wenye kuweka Msikiti kwa ajili ya kusababisha
Madhara na kukufuru, na kuvunja umoja baina ya Waumini na kua kama kituo cha
wale wenye kupigana dhidi ya Allah na Mtume wake kabla yake basi wataapa kua nia
yao si chochote isipokua wema, lakini Allah Ni mwenye kushuhudia kua wao ni
waongo; Hivyo usiingie ndani yake (Msikiti huo) Ama kwa hakika Msikiti ulioasisiwa
kutokana na Taqwa, basi ni bora kwako kusimama ndani yake, kwani ndani yake mna
watu wanaopenda kujitoharisha. Na Aallah ni mwenye kupenda wanaojitoharisha.
Hivi jee yule alieasisi Jengo (La Msikiti) kutokana na Taqwa kwa Allah na kutaka
fadhila zake, ni bora zaidi au yule ambae alieasisi Jengo kwenye Mmchongoko wa
mmomonyoko wa ardhi wa ukingoni mwa Mto unaosubiri kuanguka? Ili liangamie
pamoja nae kwenye Moto wa Jahannam? Na Allah hawaongozi watu waovu.
Halitobakia Jengo lao walilolijenga isipokua ni chanzo cha shaka na unafiq ndani ya
Nyoyo zao, hadi pale zitakapokatwa katwa Nyoyo zao na Allah ni mwenye kujua juu
ya kila kitu na ni mwingi wa Hikma.
Ambapo hizi ni aya zinazozungumzia Miskiti miwili tofauti kutokana na utofauti wa
kuasisiwa kwake ambayo ni Masjid Dhirar na Masjid Taqwa yaani Masjid Quba.
Ambapo Masjid Dhirar jina lake limetokana na nene Dhara ambalo hua linamaanisha
Dhara au Dhuru, ulijengwa miaka minane baada ya kujengwa Masjid Quba na hii ilikua
ni kabla ya Vita vya Tabuq mnamo mwaka wa 8 Al Hijra, wakati Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alipokua akijitayarisha kwa ajili ya Vita hivyo, na kisha akatoka na jeshi
lake kuelekea Tabuk.
Lakini alipofika katika eneo la Dhu Awan alipokea ujumbe kutoka kwa baadhi ya watu
waliomwambia kua: ‘Ya Rasul Allah Hakika sisi tumejenga Msikiti katika eneo letu
775
kwa ajili ya Wazee, wagonjwa na inapokua kuna hali mbaya ya hewa hivyo tulikua
tunakuomba uje kuufungua kwa kusali ndani yake.’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hakika sasa hivi
nnashughulikia kuhusina na vita vya Tabuk lakini In-shaa Allah nitakuja kusali
pamoja nanyi nikirudi’
Ambapo Allah Subhana wa Ta’ala akamshushia aya hizi Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam zenye kumaanisha kua Masjid Dhirar alioalikwa akaufungue kua ni Miskiti
ambao umejengewa na Wanafiq wenye nia ya kuugawanya Uislam na kusababisha
madhara yatakayopelekea kuvunjika kwa umoja wa Kiislam, hivyo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam hatakiwi kuingia ndani yake, na kwa maana hio basi Msikiti huo
hautakiwi kuwepo, na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwita Malik Ibn
Dukhshum wa Banu Salim na Asim Ibn Adi wa Banu Ajlan akawaambia wakusanye watu
kisha: ‘Kisha nendeni kwenye huu Msikiti ambao watu wake si waadilifu na kisha
utieni Moto’
Ambapo anasema Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari kua: ‘Msikiti wowote
ule ambao utakua umejengwa kwa ajili ya watu kujionesha na kushindana na
Msikiti mwengine au kwa sababu nyengine yeyote ile isiyokua ya kumridhisha Allah
Subhanah wa Ta’ala, au kwa pesa za Haramu basi hua ni wenye na sifa kama
Msikiti huu wa Dhirar’ ambapo Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi basi yeye anasema kua: ‘Ni kutokana na sababu hio
basi ndio maana Wanazuoni wakakataza Kusaliwa kwa Jamaa mbili kwenye
Msikiti mmoja, kwani hii hua inavunja Umoja wa Kiislam’
Ambapo wanazuoni wanasema kua asili ya Msikiti huu wa Dhirar ilikua ni kutokana na
Mkristo mmoja wa Madinah aliekua akiitwa kwa jina la Abu Amir Rahib ambae alisimu
kinafiki kwa ajili ya kuuteketeza Uislam ndani kwa ndani, na katika vita vya Badr baada
ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kushinda Vita basi alihama kutoka katika Mji
wa Madinah na kuhamia katika mji wa Makkah na alisema: ‘Wakati mimi nitakua nao
watu wa kupingana nawe Muhamamd basi mimi nitapingana na wewe tu’
Amir Al Rahib alipanga njama nyingi sana dhidi ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam na pia dhidi ya Waislam, kwani alishirikiana na Makafiri na kuwaambia kua bora
waungane pamoja katika kupigana na Waislam katika vita vya Khandaq, kuliko kupigana
kivikundi vikundi dhidi ya Waislam, na waliposhindwa Makafiri kwenye vita vya
Khandaq basi Amir Al Rahib akakimbilia katika Ardhi ya Syria na kushirikiana na
Warumi katika mipango ya vita dhidi ya Waislam vitakavyotokea katika ardhi ya Tabuk.
Na hivyo akawaamrisha watu wake wa Banu Ghanam katika Mji wa Madinah kua
wakajenge Msitiki ambao utakua ni sehemu ya kukutana kwao yeye baada ya kurudi tena
776
katika Mji wa Madinah katika jitihada zake za kuupiga vita Uislam, huku wakiandaa
jeshi katika Mji wa Tabuk kwa ajili ya kuuvamia Mji wa Madinah na hivyo Rasul Allah
Salallahu Alahyhi wa Salam akapata habari hio ya maandalizi hayo akaamua bora
akavamie kabla hajavamiwa, na huku Wanafiq wakataka kumchelewesha kwa kuufungua
Msikiti huo, na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akamtaarifu kua huo ni Msikiti
ulioasisiwa kwa ajili ya kuanzisha Madhara ndani ya Uislam kama zinavyosema aya.
Na bila ya shaka kutokana na kua Msikiti huo uliasisiwa kwa ajili ya Madhara, ambayo
hayakufikiwa malengo yake kama walivotaka wanafiq basi Allah Subhanah wa Ta’ala
anamtahadharisha Mtume wake Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Jengo walilolijenga
litakua ni lenye kubakia kua chanzo cha Athari ya Unafiq na shaka ndani ya Nyoyo
zao hadi pale Nyoyo hizo zitakapokatwa vipande vipande’
Na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akausifu Miskiti wa Quba ambao ni Msikiti
ulioasisiwa kutokana na Taqwa kwani watu wake waliouasisi walikua ni wenye kupenda
Usafi wa Nyoyo zao na Miili yao, na hivyo akamuamrisha Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kua anatakiwa awe ni mwenye kuenda na kusali ndani yake, na hivyo kutokana
na amrisho hilo basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawauliza watu wa Qubah:
‘Hivi nyinyi hua mnafanya nini, hadi Allah Subhanah wa Ta’ala akasema kuhusiana
nanyi kua ndani yake Msikitini wenu kuna watu wanaopenda Kujitoharisha?’
ambapo nao wakajibu kua: ‘Sisi daima tumekua ni watu ambao tunaopenda
kujitoharisha kwa kutumia mji pale tunapoenda Chooni’
Na kutokana na kuambiwa kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anatakiwa kua ni
mwenye kuenda kusali ndani ya Msikiti wa Qubah hivyo hata baada ya kuhamia katika
mji wa Madinah basi ingawa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akiishi katika
Mji wa Madinah katika eneo ambalo nyumba ya jirani yake ni Msikiti wake, na mbali ya
kua Mji wa Madinah uko mbali kwa kilomita 3 kutoka katika eneo la Qubah lakini haikua
vigumu kwake yeye Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutekeleza amrisho hilo la
Mola wake kwani alikua katika kila siku ya Jumamosi akifunga safari kwa miguu au kwa
Ngamia na kuelekea katika Mji wa Quba kwajili ya kusali ndani yake kwenye Msikiti
huu wa Taqwa au Masjid Qubah.
Kama anavyoseama Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alikua kila siku ya Jumamosi anaenda kwenye Msikiti
wa Qubah iwe kwa miguu au kwa kipando’
Kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Yeyote yule
atakaejitoharisha nyumbani kwake na kisha akaja katika Masjid Qubah na akasali
Rakaa 2 ndani yake basi atakua ni mwenye kuzawadiwa malipo yako kua ni sawa
na mtualiefanya Umra.’(Imam Ibn Majah)
777
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayi wa Salam alikaa kwa mda wa wiki mbili katika Mji
wa Quba na mara baada ya kumalizika kujenga Msikiti wa Quba basi akapumzika na
kisha, baada ya hapo akaamua kaelekea katika kituo cha mwisho cha safari yake ambacho
ni katika Mji wa Madinah katika siku ya Ijumaa, ambapo kabla ya tukio hili basi
aliwaalika watu wa Banu Najjar ambao ni wa bibi yake wa upande wa Mama yake
waliokua wakiishi katika Mji wa Madinah kua waje kwenye Mji wa Quba ili akiondoka
katika siku ya Ijumaa basi aondoke nao pamoja kurudi katika Mji wa Madinah na hivyo
Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam aliwasili katika Mji wa Madinah akiwa na Mamia
ya wafuasi waliokua nyuma yake huku pia akiwa na mamia ya wafuasi waliokua
wakimsubiri kwa hamu katika Mji wa Madinah.
KUWASILI KWA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA SALAM
KATIKA MJI WA MADINAH AN NABI.
Neno Yathrib linatokana na neno Tharaba ambalo hua linamanisha Kulaumu, Kukosoa,
Kutoa kasoro juu ya Kitu.
Na kuna wanaosema kua Mji huu uliasisiwa na watu waliotokana na kizazi cha Nabii
Nuh ambao kiongozi wao alikua anaitwa Yathrib, hivyo watu hao walihama kutoka
katika makazi yao katika Mji wa Babylon baada ya kukumbwa na mafuriko na hivyo
katika kutafuta kwao eneo salama basi wakafika katika ardhi hio ambayo ilikua ni nzuri
kimazingira kwani ina Mitende na Maji ya kutosha.
Ambapo asili ya watu wa Mji wa Yathrib ni mchanganyiko na hii ni kwa sababu ya hali
ya mazingira yake, kwani kuna watu wenye asili ya Iraq, ambao ndio waliotokana na
Yathrib mwenyewe, kuna Mayahudi ambao nao pia walitoka katika ardhi ya Iraq na
Jerusalem kutokana na kukimbia Madhila waliyokua nayo katika jamii zao na pia kuna
Wakristo waliokua ni wenye asili ya Yemen ambao nao walikimbilia katika Mji wa
Yathrib kwa ajili ya kutafuta usalama wao.
Hivyo Jina la Yathrib lilibadilishwa na Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam pale baadae
alipohamia katika Mji huo na hivyo akauita Taibah yaani Mji Uliomsafi au Taba yaani
Mji Mzuri, na baadae ukaitwa Madinat An Nabi yaani Mji wa Nabii Sallahu Alayhi wa
Salam ambapo uzuri wa Mji huu basi ulionekana wazi kutokana na ari na furaha ya watu
wake wakati walipokua wakimshindikiza Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam kutoka
katika maeneo ya Quba kuelekea katika Mji huo wa Yathrib walikua ni wenye kujawa na
Imani juu ya Dini yao Mpya na kumuamini Allah Subhanah wa Ta’ala na kumpenda
Mtume wake Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam ana hivyo kua ni wenye kua na darja
ya Ansaru Al Muslimin.
778
Katika safari yao ya kutoka Qubah kuelekea Yathrib katika siku hio ya Ijumaa, basi
ulipingia wakati wa Sala ya Ijumaa wakafika katika maeneo ya Ranuna, hivyo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akashuka kutoka kwenye Ngamia wake na
akajitayarisha kwa ajili ya Sala ya Ijumaa katika eneo hilo la ardhi ambalo lilikua
linamilikiwa na watu wa Banu Salim Ibn Awf, na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasalisha sala ya kwanza katika ardhi ya eneo hilo ambayo ilikua ni sala ya Ijumaa
ambayo ndani yake baada ya kumshukuru na kumtukuza Allah Subhanah wa Ta’ala basi
akasoma Khutba Ifuatayo:
‘Enyi watu! Jitayarisheni kwa ajili ya Akhera yenu, wakati bado mkiwa na Afya
zenu, kwani mnajua kua kila mmoja wenu ataulizwa katika siku ya Malipo hata juu
ya Kondoo aliowaacha bila ya kuwasimamia wakati alipokua akiwachunga, kwani
Allah Subhaah wa Ta’ala atakuambieni moja kwa moja kwa kusema:
Hivi Jee hakuja Mtume Wangu na kukujuulisheni juu ya hili? Na jee sikukupeni
nyinyi neema nyingi sana kutoka kwangu? Jee mmejitayarishia nini kwa ajili yenu
kutokana nazo?’ hivyo mtu ataangalia upande wa kulia na kushoto na wala asione
kitu, na atakapoangalia mbele yake hatoona kitu isipokua Moto wa Jahannam.
Hivyo mtu yeyote yule atakaeweza kujiokoa nao Moto huo hata kwa nusu ya Kokwa
ya Tende, basi na aitoe, na kama hakupata Kokwa ya Tende basi na ajiokoe kwa
Kutumia Kalima Tayyiba (Kauli Njema). Kwani kutokana nayo basi Jambo jema
moja hua linamalipo ya mara 700, Nakutakieni Rehma, Salama na Amani iwe Juu
yenu.
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akakaa kitako kidogo kisha akasimama na
kuendelea na sehmu ya pili ya Khutba yake kwa kusema: ‘Namtukuza Allah,
Namtukuza Allah na namuomba msaada wake, Tunamuomba Allah atuhifadhi
kutokana na matamanio ya Nafsi zetu na makosa yetu, kwani amuongozae Allah
basi hua ni mwenye kuongoka lakini aliepotoshwa nae basi kamwe hatopata
muongozaji wa kumrudisha kwenye njia iliyonyooka’
Nnashuhudia kua hakuna Mola anaestahiki kuabudiwa kwa Haki isipokua Allah,
ambae yuko peke yake na asiekua na Mshirika. Hakika ya Kauli bora ni maneno
ya Allah Subhanah wa Ta’ala. Kwani mtu ambae amepambwa ndani ya Moyo wake
kwa Qur’an na Allah Subhanah wa Ta’ala, Mtu ambae Allah Subhanah wa Ta’ala
amemuingiza kwenye Uislam ingawa hapo kabla alikua ni mtu asieamini, Mtu
ambae ni mwenye kuipendelea zaidi Qur’an kuliko maneno mengine basi Mtu huyu
hua ni mwenye Kuokoka.
Bila ya Shaka, Kitabu cha Allah Subhanah wa Ta’ala ni kitabu bora na chenye
maneno yaliyo fasaha, hivyo Pendeni kile anachokipenda Allah Subhanah wa
779
Taa’ala, msiyachoke maneno ya Allah Subhanah wa Ta’ala na msichoke kumtukuza
na kumkumbuka kwa sifa zake, na wala msiyafanye maneno ya Allah kua ni yenye
kuhuzunisheni nyoyoni mwenu, kwani Maneno yake yanawatofautisha waliobora
miongoni mwenu katika kila kitu.
Maneno ya Allah Subhanah wa Ta’ala yanabainisha kuhusiana na Amali njema, na
Mitume ambao ni watu bora, na hadithi bora, Maneno ya Allah Subhanah wa Ta’ala
yanabainisha kile kilicho halali na kilicho haramu. Hivyo Muabuduni Allah na wala
msimshirikishe na kitu chochote, na muogopeni ipasavyo.
Fanyeni Mema na yathibitisheni kwa Ndimi zenu. Pendaneni kutokana na Maneno
ya Allah Subhanah wa Ta’ala. Jueni kua Allah Subhanah wa Ta’ala anawaadhibu
vibaya sana wale ambao wanaovunja Ahadi zao. As Salaam Alaykum.
Na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasalisha Sala ya Ijumaa na kisha
akeingia katika Mji wa Madina, ambapo katika Khutba yake hii basi tunaona kua alikua
anawakumbusha watu wa Madina kua wameahidi kua watamlinda na kumhifadhi, hivyo
anawataka watimize ahadi yao, na wasije wakavunja ahadi yao na kuwawekea wazi kua
Allah Subhanah wa Ta’ala anawachukia wenye kuvunja Ahadi, na atawaadhibu kwa
adhabu kali sana wavunjao Ahadi.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipowasili katika mji wa Madina, basi akakuta
kua Mji huo hauna sehemu ya kukusanyikia na kusali pamoja kama vile ilivyokua katika
Mji wa Quba, na Ngamia wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipopiga Magoti
kwenye kiwanja cha Mayatima wawili wa Banu Najjar waitwao Sahl na Suhayl ambao
walikua chini ya uangalizi wa Muadh Ibn Afra Radhi Allahu Anhu, basi Rasul Allah
Salallahu A’layhi wa Salam akasema kua anataka kuinunua Ardhi hio kama watamuuzia.
Lakini Muadh Ibn Afra Radhi Allahu Anhu akasema kua atatoa sadaka malipo ya kiwanja
hicho kwa ajili ya Uislam, na Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akakataa juu ya
shauri hilo hivyo wakaitwa wahusika wenyewe na walipofika Mayatima hao wawili Sahl
na Suhayl basi wakasema kua: ‘Ya Rasul Allah, hakika sisi tunataka malipo yake
yalipwe na Allah Subhanah wa Ta’ala, hivyo tutakupa bure Ardhi yetu hii kwa ajili
ya Allah Subhanah wa Ta’ala’ lakini hata hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
hakukubaliana na shauri hilo kwa sababu wao ni Mayatima, na hivyo akainunua ardhi
hio kwa pesa 10 za dhahabu ambazo zililipwa na Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu
hapo hapo baada ya makubaliano hayo.
Na kisha haukuchukua muda isipokua ukajengwa Msikiti wa Madina ambao unajulikana
kama Masjid An Nabawi kwa kasi ya haraka sana. Masjid huu ulikua ni wa pembe 4 na
Kibla chake kimeelekea upande wa Jerusalem, na ulikua una milango mitatu na Mihrab
ambayo ilikua ni ya Vigogo vya Mitende, na pia kulikua na Kigogo cha Mtende ambacho
780
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akikiegemea katika wakati wa kutoa
Khutba.
Pembeni yake Msikiti huo kulikua na Vyumba viwili ambavyo ni vya Umm Ul Muuminin
Sawdah Radhi Allahu Anha na chengine cha Umm ul Muuminin Aisha Radhi Allahu Anha
na hii ni kwa sababu katika wakati huu Rasul Allah Sallahu Alayhi wa Salam alikua na
wake wawili hao tu, ambapo baadae Nyumba yake iliongezwa vyumba vengine.
Ambapo baadae Masahaba wakaamua kujenga Mimbar yenye vigazi vitatu ndani ya
Msikiti huo ambayo ilikua ni ya vigogo vya Mtende, hivyo mara ya kwanza Rasul Allah
Sallahu Alayhi wa Salam alipopanda kwenye Mimbar hio, basi Masahab walisikia sauti
kama Ngamia anaetaka kuzaa, na hivyo Masahaba wakaangalia huku na kule na kisha
wakaangaliana, kwa sababu hakukua na Ngamia karibu yao, lakini sauti hio iliendelea
kusikika kutoka mbele yao pembeni ya Mimbar mpya ya Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam ambayo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua amepanda juu yake.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akashuka kutoka kwenye Mimbar hio na
kuelekea kwenye kigogo cha Mtende ambacho alikua akikiegemea kabla ya kujengwa
Mimbar hio mpya, na kisha akakikaribia akakikumbatia na kukipapasa Kigogo hicho, na
mara sauti iliyokua ikisikika ikasita kusikika. Masahaba wakaanza kutokwa na machozi
kutokana na kufahamu kua Kigogo hicho ndio kilichokua kikilia kwa ajili ya kukosa
mguso wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kuwaambia Masahaba zake kua:
‘Hakika kama mimi sikukikumbatia na kukiliwaza Kigogo hiki basi kingeendelea
kulia hadi siku ya Kiama kutokana na kutengenishwa kwake na Rasul Allah.’
Ambapo baadae Kigogo hicho kikachimbiwa shimo na kuzikwa chini ya Mimbar hio
kutokana na amrisho lake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Ambapo alisema Imam Hasan Al Basr kuwaambia Wanafunzi wake kutokana na tukio
hili la kulia kwa kigogo hicho cha Mtende kutokana na kutenganishwa na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kama ikiwa Hata Kigogo kinaonesha hisia za
Mapenzi na Mwamko kwa ajili ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, basi
nyinyi mnastahiki kuonesha Mapenzi na Mwamko wa kihisia zaidi juu yake Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam’
Ambapo kuna kauli nyengine isemayo kua: ‘Wakati Kigogo hicho kilipokua kinalia
basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akakipapasa na kusema: ‘Nitakupeleka
Peponi ambapo ulipokua hapo kabla kama unataka, ambako nako utaota tena
mizizi na kunawiri na kuzaa, na kama utataka basi nitakupanda Peponi ili
waliokaribu miongoni mwa waja wa Allah wale Matunda yako.’’
781
Kigogo hiki kikasema: ‘Bora nipande Peponi ili waliokaribu miongoni mwa waja wa
Allah wale matunda yangu, na Peponi ni sehemu ambayo hakuna hali ya kuoza,
wacha nipate kuishi milele ndani yake.’ Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasema kuwaambia Masahaba zake: ‘Kimependelea Maisha ya Akhera zaidi ya
Duniani’
Ambapo anasema Imam Muhamamd Ibn Is-haq kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam aliunganisha Udugu wa Kiislam baina ya marafiki zake wa Muhajjirin na
Ansari, na hivyo wakawa ni Ndugu wawili wawili, na kisha akachukua mkono wa
Ali Ibn Abi Talib na kusema: ‘Huyu ni Ndugu yangu’ hivi ndivyo alivyokua Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam, Bwana wa Mitume wote, Kiongozi wa wenye
Kumuogopa Allah Subhanah wa Ta’ala, Mtume wa Mola wa Viumbe wote asiekua
na mfano wake. Ambapo Hamza Ibn Abd Ul Muttalib na Zayd Ibn Harith nao
wakawa Ndugu pia. ’
Miongoni mwa Sifa za Maansari ni kama vile alivyosema Allah Subhanah wa Ta’ala
katika Qur’an kuhusiana nao kua:
﴿وَٱل َّذِينَ تَبَو َّءُوا ٱلد َّارَ وَٱلإِيمَانَ مِن قَبْلِهِمْ يحُِب ُّونَ مَنْ هَاجَرَ إِلَيْهِمْ وَلاَ يجَِدُونَ فىِ
صُدُورِهِمْ حَاجَةً ممِّ َّآ أُوتُواْ وَيُؤْثِرُونَ عَلَى ٰ أَنفُسِ هِمْ وَلَوْ كَانَ هبِِْم خَصَاصَةٌ وَمَن
يُوقَ شُح َّ نَفْسِ هِ فَأُوْلَٰئِكَ هُمُ ٱلْمُفْلِحُونَ ﴾
Waalladheena tabawwaoo alddara waal-eemana min qablihim yuhibboona man
hajara ilayhim wala yajidoona fee sudoorihim hajatan mimma ootoo wayu/thiroona
AAala anfusihim walaw kana bihim khasasatun waman yooqa shuhha nafsihi faolaika
humu almuflihoona(Surat Al Hashar 59:9)
Tafsir:Na wale ambao kabla yao walikua na makazi(katika Mji wa Madina) na
wakawa na Imani waliwapenda wale waliohamia kwao na hawakua na wivu juu yao
kwenye vifua vyao kutokana na vile walivyopewa (Muhajjirina) na wakawapendelea
wao zaidi ya Nafsi zao, japo ingawa walikua wanahitajia pia, na yeyote yule
atakaeokolewa kutokana na kua ni mwenye kuidhibiti ya nafsi yake, basi hao ndio
watakaofuzu.
Ambapo anasema Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi nilitoka na Walid Ibn
Walid na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawauliza Maansari : ‘Jee hali
yao itakuaje kama wakipewa Bahrayn?’ ambapo Maansari wakasema:
‘Hatutoridhika hadi ndugu zetu wa Muhajjirina watakapopewa kitu kama hicho
pia.’ Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Kama ni La basi kueni
782
na Subra hadi pale mtakaponiona akhera kwani baada yangu mtakabiliana na
upendeleo juu yenu’’
Miongoni mwa mifano ya Udugu huo baina ya Muhajirina na Ansari alianzisha Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi pia ni baina ya Abd Rahman Ibn Awf Radhi Allahu
Anhu na Sad Ibn Rabia Radhi Allahu Anhu. Ambapo mara baada ya kuunganishwa udugu
wao huo, basi Saad Ibn Rabiah Radhi Allahu Anhu akasema kumwambia Abd Rahman
Ibn Awf kua: ‘Ewe Ndugu yangu hakika mimi ni tajiri sana katika Mji wa Madina,
nna mashamba mawili na nnao wake wawili, hivyo angalia Mashamba yangu kisha
uchague unalotaka, na pia waangalie wake zangu basi atakaekuvutia miongoni
mwao mimi nitamuacha ili umuoe awe wako wewe’ ambapo hata hivyo Abd
Rahman Ibn Awf akajibu: ‘Allah akungezee barka katika Mali yako na familia
yako, ila mimi nilikua nataka unioneshe wapi lilipo soko la Madina.’
Hivyo haishangazi kuona namna walivyokua Maansari kwa ukarimu wao kwa
Muhajjirina kiasi ya kua Allah Subhanah wa Ta’ala anawaelezea zaidi kwa kusema:
﴿وَأَل َّفَ بَينَْ قُلُوهبِِمْ لَوْ أَنفَقْتَ مَا فىِ ٱلأَرْضِ جمَِيعاً م َّآ أَل َّفْ تَ بَينَْ قُلُوهبِِمْ وَلَٰكِ َّن
ٱهلل ََّ أَل َّفَ بَيْنَهُمْ إِن َّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾
Waallafa bayna quloobihim law anfaqta ma fee al-ardhi jameeAAan ma allafta
bayna quloobihim walakinna Allaha allafa baynahum innahu AAazeezun
hakeemun(Surat Al Anfal 8:63)
Tafsir: Na yeye (Allah Subhanah wa Ta’ala) ameunganisha baina Nyoyo zao hivyo
Hata kama mtatumia kila kilichomo ardhini basi msingeweza kuziunganisha Nyoyo
zao, lakini Allah amezinganisha baina yao. Kwani kwa hakika yeye ni mwenye uwezo
juu ya kila kitu na ni mwingi wa Hikma.
Kwani kutokana na Hikma za Allah Subhanah wa Ta’ala basi aliziunganisha Nyoyo za
Waumini na hivyo kuwajaalia kua ni wenye kua na umoja na kupata ushindi baada ya
ushindi dhidi ya maadui zao, kwa kuanzia kuwaunganisha watu wa Mji wa Madina baina
ya Makabila ya Banu Aws na Al Khazraj ambao kabla ya Uislam walikua ni maadui
wakubwa sana, na kisha kuwauganisha Ansari na Muhajjirina kwa Ansari kujitolea na
kuwasaidia kila Muhajirrin.
Ambapo amesema Ansa Ibn Malik Radhi Allahu Anhu Kua: ‘Muhajirrina walisema:
‘Ya Rasul Allah hakika sisi hatujawahi kuona watu ambao wamepata malipo
makubwa kutokana na mengi tuliyoyapoteza, na hatukuwahi kuona maliwazo
makubwa kutokana na kile kidogo walichokua nacho. Kwani wametuokoa sisi
783
kutokana na kuomba, wamegawana nasi na kila neema waliyojaaliwa hadi imefikia
wakati wa kua sisi kua na khofu kua watavuna malipo yetu yote.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘La hilo halitotokea wakati pale
mtakapokua mnawashukuru na pia kuwaombea Dua kwa Allah kwa ajili yao.’
Anasema Abd Rahman Ibn Zayd Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam aliwaambia Maansari kua: ‘Ndugu zenu wamewacha Mali na Watoto wao
na kuja kwenu’ hivyo Maansari wakasema: ‘Hakika sisi tutagawana nao Mali zetu
nusu kwa nusu’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Jee tufanye lipi
zaidi?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Watu hawa (Muhajjirina)
hawakua wakifanya kazi, hivi jee mtagawana nao mazao yenu’ Maansari
wakasema: ‘Naam’’
Hii ndio hali wanayotakiwa wawe nao Waislam katika udugu wao ili kudumisha umoja
wao. hivyo tunatakiwa tujifunze kwa Waliotangulia kabla yetu, ambapo anasema Imam
Abu Yazid Al Bustami kua: ‘Hakika mimi sikuwahi kuzidiwa na yeyote kama vile
nilivyozidiwa na Kijana mmoja kutoka katika Mji wa Balk, ambae nilikutana na
alipokua akielekea katika Ibada ya Hija, na aliponiona basi alinifuata na kusema:
‘Ya Abu Yazid, hivi jee ni kipimo gani cha Kuidhibiti Nafsi na Kuachana na
Matamanio ya Dunia kwa upande wako?’
Nami nikajibu: ‘Hakika sisi kama tukipata riziki yetu basi tunakula na kama
tukikosa basi hua tunakua na Subra.’ Ambapo nae akasema: ‘Hiyo hua ni
kuidhibiti Nafsi na kuachana na Matamanio ya Mbwa wa Balkh’ hivyo mimi
nikamuuliza: ‘Sasa jee ni kipimo gani cha Kuidhibiti Nafsi na Kuachana na
Matamanio ya Dunia kwa upande wako?’
Ambapo nae akasema: ‘Tunapokua hatuna hua tunashukuru, na tunapopata hua
tunawapa wenye shida zaidi yetu’’
Ambapo Dhunun al Misri aliulizwa: ‘Jee ni nini hali ya Mwenye kuachana na Dunia
kwa Moyo mkunjufu’ ambapo ane akajibu: ‘Huonekana katika hali tatu, anapokua
anacho hua ni mwenye kutoa, anapokua hana hua si mwenye kuomba na
kuwapendelea wengine pale anapopewa yeye.’
Na ansema Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Muhamamd Ibn Muhammad Al Ghazali
kua: ‘Amesema Abu Hasan Al Antaki kua: ‘Kulikua kuna watu 20 katika mji wa
Ray ambao walikua wana njaa na wana vipande vya mkate ambavyo vilikua
haviwatoshelezi wao wote hata wakila. Hivyo wakachukua Mikate hio na kisha
wakaikatakata katika vipande vipande, wakaviweka juu ya meza na kisha wakakaa
784
na kuzima taa huku vipande hivyo vya mikate vikiwa mbele ya Mezani. Kisha baada
ya mda wakawasha taa na kuona kua vipande vya mikate vike vile vile, kwa sababu
kila mmoja miongoni mwao hakula kipande hata kimoja kutokana na kuona bora
ale kipande hicho ale mwenzake.’’
MAKUBALIANO BAINA RASUL ALLAH SALALLAHU ALAYHI WA
SALAM NA WATU WA MADINAH
1. Haya ni Makubaliano kutoka kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kuhusiana na Uhusiano baina ya Waumini wa Quraysh na wa Madina na wale
wanaowafuata na kujumuika nao katika Ummah wa Kiislam.
2. Muhajirrin wa Quraysh wataendelea Kulipia fidya Malipo ya Umwagaji Damu
kulingana na Mila zao.
3. Inapotokea vita basi kila pande itasimamia Mateka wake kwa Ukarimu na
kusimamia haki za Ibn Adam kama ilivyo miongoni mwa Waumini.
4. Watu wa Bani Awf wataendelea na Malipo ya kulipia fidya ya Umwagaji Damu
kuligana na Mila zao.
5. Kama ikitokea Vita dhidi ya Mtu yeyote basi pande zote zizisokua Waislam
wataendelea kuwasimamia Mateka wao kwa huruma na haki kama
inavyosimamiwa na Waislam na wala si kulingana na zama za Kijahiliyah.
6. Watu wa Banu Sidah, Banu Harith, Banu Jusham na Banu Najjar wataongozwa
kulingana na kanuni zilizotajwa hapo juu.
7. Watu wa Banu Amr, Banu Awf, Banu Nabit na Banu Aws watasimamiwa
kulingana na kanuni hizo pia.
8. Waislam hawatosita kuendelea kuwasimamia Mateka wao na watawalipia fidya
kwa ajili yao, ambalo litakua ni jukumu la Umma wa Kiislam na wala halitokua
jukumu la familia ya Waislam hao.
9. Muumini kamwe hatomfanya Mtu alieachiwa huru na Muumini mwengine kua
ni mtu wake bila ya kuwepo kwa ridhaa ya Muumini husika.
10. Waumini wanaomuogopa Allah daima watakua ni wenye kupingana na Uasi na
Dhulma na vitendo vinavyounga mkono Dhulma au Uadui au Upotovu
miongoni mwa Waumini.
11. Kama ikitokea kua kuna Mtu atafanya maovu basi Waumini wote watapingana
nae Mtu huyo hata kama mtu huyo akiwa ni Mtoto wa Mmoja kati ya Waumini
hao
12. Muumini hatomuua Muumini mwenzake kwa ajili ya Kafiri hata kama Kafiri
huyo ataka ni ndugu yake Muumini huyo.
785
13. Muumini kamwe hatomsaidia asiekua Muumini dhidi ya Muumini.
14. Hifadhi itakapotolewa kwa jina la Allah Subhnaha wa Ta’ala itakua ndio
inayotambulika, hivyo Wasiokua na Nguvu miongoni mwa Waumini
watahifadhiwa kwa jina la Allah Subhanah wa Ta’ala na juu ya hili
litasimamiwa kwa Waumini wote.
15. Waumini wote ni Marafiki miongoni mwao bila ya kujumuishwa wasiokua
Waumini.
16. Mayahudi wanaowafuatana na Waumini watasaidiwa na kusimamiwa haki zao.
17. Hakuna Yahudi atakaedhulumiwa kwa sababu ya Uyahudi wake.
18. Maadui wa Mayahudi watakaowafuata Waislam ili wasaidiwe dhidi ya
Mayahudi basi hawatosaidiwa.
19. Uslama baina ya Waumini hauwezi kuvunjwa, yaani Waumini wote wawe
kwenye Usalama au wote wawe kwenye vita, haiwezekani kua Nusu wawe
kwenye Vita na Nusu wawe kwenye Usalama.
20. Haiwezekani kutafutwe njia ya kupatikana kwa Usalama ndani ya Mji wa
Madina pale inapokua Waislam wanapigana kwa ajili ya Allah.
21. Wakati Waumini watakapoenda Vitani basi watakaopanda kipando itawabidi
kushirikiana katika kupanda kipando hicho kwa zamu.
22. Waumini lazima wawe ni wenye kulipiza Kisasi damu ya Waislam wenzao
wanapokua wanapigana kwa ajili ya Allah, yaani mapigano kwa ajili ya Allah
Subhanah wa Ta’ala hua yanawahusisha Waislam wote na kuwaathiri Waislam
wote.
23. Waumini ni wabora katika kuonesha misimamo yao kutokana na kumuogopa
Mola wao jambo ambalo hupelekea kupata uongofu kutoka kwa Allah
Subhanah wa Ta’ala na hivyo Kila Muislam anatakiwa awe na ari katika
kuonesha msimamo huo.
24. Hakuna Kafiri atakaeruhusiwa kuhodhi mali ya Quraysh aliechini ya
Usimamizi wake, kwani Mali zote za Maadui lazima zisalimishwe kwa Kiongozi
wa Kiislam.
25. Hakuna Kafiri atakaeruhsiwa kuingilia kati kwa kumpendelea Quraysh kwa
sababu watu wa Quraysh wa Makkah ni maadui.
26. Kama Kafiri akimuua Muumini bila ya sababu inayokubalika, basi Kafiri huyo
atauliwa badala yake, isipokua pale walioliwa Mtu wao watakaporidhika na
kusamehe. Na hivyo Waumini wote wanatakiwa kua ni wenye kupingana na
uovu huo, na hakuna Muumini anaeruhusiwa kumhifadhi aliefanya uovu huo.
786
27. Mtakapotofautiana juu ya Jambo lolote kuhusiana na Makubaliano haya basi
jambo hilo lilirudishwa kwa Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume wake
Salallahu Alayhi wa Salam.
28. Mayahudi watachangishwa mchango pale watakapokua wanapigana pamoja na
Waislam dhidi ya Maadui zao.
29. Mayahudi wa Bani Awf, Bani Al-Najjar, Bani Al Harith, Bani Saeeda, Bani
Jusham, Bani Al Aws, Thaalba, Jaffna, (ambao ni wa ukoo wa Bani Thaalba)
ana Bani Al Shutayba watahesabiwa kua ni Ummah mmoja na Wasialm,
ingawa Mayahudi wana Imani yao na Uhuru wao, lakini hawatotofautishwa
isipokua kwa wale watakaofanya dhulma na uovu kwani kutokana na kufanya
kwao hivyo hua ni wenye kujidhulumu nafsi zao na watu wa familia zao.
30. Ukweli hua ni wenye kutoa hifadhi dhidi ya Uongo, yaani Wakweli na
waaminifu watalindwa dhidi ya Uongo, na hivyo Mtu muaminifu na mkweli
kwa Ummah basi hua ni mwenye kujilinda kutokana na kua na usaliti.
31. Watu walio huru wa Thaalba watapewa Darja sawia kama watu wa Thaalba
wenyewe, hii ni kutokana na uadilifu wao katika mambo yao ya kimaisha na
watapewa haki yao kamilifu wanapokua katika mapigano.
32. Watakaoshirikiana na Mayahudi basi watafanyiwa kama wanavyofanyiwa
Mayahudi.
33. Hakuna hata mmoja alie katika makubalino haya atakeenda Vitani bila ya
Ruhusa ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na hivyo yeyote
atakaedhulumiwa basi atasimamiwa haki yake.
34. Mayauhudi watasimamia matumizi ya Majeshi yao katika vita na Waislam pia
watasimamia matumizi ya Majeshi yao.
35. Yeyote yule atakaemshambulia yule aliekuwemo kwenye Makubaliano haya
basi waliokuwemo kwenye Makubaliano haya watamsaidia alieshambuliwa.
36. Wote waliokuwemo kwenye Makubaliano haya lazima wawe ni wenye
kushauriana na kutaarifiana juu ya mambo muhimu.
37. Hakuna mtu atakaehukumiwa kutokana na makosa ya mwenzake.
38. Mtu yeyote yule atakaedhulumiwa basi anastahiki kusaidiwa.
39. Mayahudi wanatakiwa walipie matumizi ya vita wa ajili ya Waislam pale
itakapokua wao hawatopigana Vita hivyo.
40. Mji wa Madina utakua ni Mji wa Usalama kwa kila aliekubaliana na
makubaliano haya.
41. Mgeni yeyote atakaehifadhiwa na aliekubaliana na makubaliano haya
atahesabika kua kama mgeni wa mtu huyo pale itakapokua hakufanya makosa
787
wala hakudhulumu, kwani kila atakaedhulumu au kufanya kosa basi
atahukumiwa.
42. Mwanamke atahifadhiwa kutokana na ridhaa ya walii au familia yake.
43. Kama ikitokea kua kutakua na ugomvi au matatizo basi moja kwa moja
yatatauliwe kupitia kwa Allah Subhanah wa Ta’ala na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam, na kwamba Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
atakubaliana na kila kilichomondani ya makubaliano haya kwa ajili ya
manufaa yaliyomo ndani yake.
44. Watu wa Quraysh hawatopewa hifadhi yeyote katika mji wa Madina.
45. Waliokubaliana na makubaliano haya wanakubaliana wataungana pamoja
katika kushirikiana kusaidia pale inapotokea kuvamiwa kwa mjiwa Madina.
46. Waliokubaliana na makubaliano haya wanatakiwa wasiamamie usalama ndani
ya mji wa Madina, na ikitakiwa iwe hivyo kwa Waislam basi ni wajibu wao
kutekeleza jukumu hilo isipokua pale itakapokua Waislam wanapigania kwa
ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala.
47. Kila mmoja kati ya waliokubaliana na makubaliano haya atakua na haki stahiki
kulingana upande aliokuwepo wa makubaliano, hivyo kila mtu ataathirika au
atanufaika kutokana na upande aliokuwepo.
48. Mayahudi wa Banu Aws na watu wao watakua na haki sawa kama ilivyokua
kwa watu wengine waliokubaliana na makubaliano haya. Ukweli na uaminifu
ni hifadhi dhidi ya Udanganyifu.
49. Kila afanyae jema au kinyume chake basi atakua ni mwenye kufanya hivyo kwa
ajili ya Nafsi yake.
50. Allah Subhnaha wa Ta’ala amekubaliana na makubaliano haya.
51. Makubaliano haya hayatomhusu atakaefanya dhulma.
52. Pale inapotokea mmoja kati ya waliokubaliana na makubaliano haya kua
ataenda vitani au atabakia nyumbani basi atakua salama isipokua kama
atafanya dhulma.
53. Allah ni mwenye kuwahifadhi wenye kufanya mema na wenye kumtii na
kumuogopa yeye na Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam ni Mtume wake na
ni mwenye kuhakikisha juu ya hilo.
KUWASILI KWA UMMU AYMAN KATIKA MJI WA MADINAH AN NABI.
788
Tunaporudi kwa upande wa Umm Ayman pia nae aliachiwa Majukumu ya kuyatekeleza
kwa ajili ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, hivyo baada ya kuyatekeleza
Majukumu hayo basi Ummu Ayman nae akafunga Safari na kufanya Hijra kutoka katika
Mji wa Makkah kuelekea Madinah kwa miguu ikiwa ni safari yake ya pili baada ya ile
aliyoifanya wakati akiwa Na Mama yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam yaani
Amina Bint Wahb pamoja na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam wakati akiwa
mdogo sana.
Ambapo mara hio ya kwanza alikua kijana na pia Walikua ni wenye kupanda Ngamia
na hivyo kua ndani ya Kibanda kinachowekwa juu ya Mgongo wa Ngamia na safari hio
ilichukua Siku 10.
Kwani Safari hii ya pili ya Barakah au Ummu Ayman kutoka Makka kuenda Madinah
ilikua ngumu zaid, kwani alikua peke yake, halafu alikua akitembea kwa miguu kwa
wasiojua basi tunazungumzka safari kama ya kutoka Dar kuelekea Tanga kwa miguu
tena kwa Mwanamke Mtu Mzima anaekaribia miaka umri wa miaka 60 tena Jangwani
hakuna miti wala Majumba bali kuna marundo na Marundo ya Mchanga, anauzamisha
mguu mchangani kisha anautoa ili kupiga hatua nyengine usiku na mchana.
Na ingawa ilikua safari ndefu na nzito lakini kwake yeye iliku rahisi kwani Umm Ayman
alikua katika hali ya Mama anaesafiri kumkimbilia Mtoto wake kipenzi ambae
hajamuona kwa siku nyingi sana yaani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Hivyo Ummu Ayman alikua ni Mwenye kufanya Hijra ya kusafiri Jangwani kwa miguu
katika umbali wa kilomita 450 kwa Ajili ya Allah Subhanah wa Ta'ala, na pia kwa ajili
ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Ambapo ndani ya tukio hili basi mna mafuzo pia ya Umuhimu wa Nia katika kila Jambo
analolifanya Ibn Adam, kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua:
‘Ama hakika ya Amali hua inategemeana na Nia, na Kwa Hakika Kila mtu atalipwa
Kulingana na Nia yake, Hivyo yeyote Yule aliefanya Hijra kwa Ajili ya Kidunia au
kwa ajili ya Mwanamke Basi Hijra yake hua ni kwa Ajili ya alichokifanyia
Hijra’(Sahih Bukhari)
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliisema maneno ya Hadith hii kutokana
na kuainisha Umuhimu wa Nia katika Kila Jambo.
Na tunapoangalia hadith basi tunaona kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
anazungumzia Hijra kisha ndani yake akainisha aina za Nia na Madhumuni ya Hijra.
Kwani katika Wakati huo, na hadi katika wakati wa leo pia Kuna watu hua ni wenye
Kufanya Hijra kwa ajili ya Dini yao, na kuna wanaofanya Hijra kwa ajili ya Dunia yao.
789
Na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kuhusiana na Wanawake kwa sababu
kuna Watu walifanya Hijra ya kutoka Makkah kuelekea katika Mji wa Madinah si kwa
sababu ya Dini yao wala si kwa sababu ya Mola wao na Mtume wake basi kwa sababu
tu ya Kusikia kua katika Mji wa Madinah kuna Wanawake wazuri zaid kuliko Wanawake
wa Makkah.
Kwani anasema Imam Maaruf Al Kharki kua: ‘Kila kinapotokea Kitendo
kinachofanywa na Ibn Adam basi hua ni chenye kutokana na Nia Ndani yake, Hivyo
Kama Nia ni Sahih basi na Kitendo hua Sahih. Na kama Nia si Sahih basi na
Kitendo hua pia si Sahih’
Ambapo Nia Sahih juu ya Kitendo Sahih hua katika hali 3 zifuatazo;
1-Kama ikiwa Nia juu ya Kitendo Husika hua ni yenye kutokana na Kumuogopa
Allah Subhanah wa Ta'ala - Basi kitendo hicho hua ni sawa na kufanya biashara
kwa Mja huyo mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala.
2-Kama ikiwa Nia Juu ya Kitendo Hua ni yenye kutokana na Kuikimbilia Pepo ya
Allah Subhanah wa Ta'ala – Basi kitendo hicho hua ni sawa na kufanya Biashara
kwa mja huyo mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala.
3-Kama ikiwa Nia juu ya Kitendo hicho hua ni yenye kutokana na Kuona aibu kwa
Mja Mbele ya Mola wake, na hivyo hua ni kutekeleza Wajibu wake na kuonesha
Shukrani kwa Mja huyo mbele ya Mola wake – Basi kitendo hicho hua ni sawa na
Ibada ya Mtu mwenye kujikomboa na kutaka kujitafutia uhuru uliotokana na uzito
wa Majukumu yake mbele ya Mola wake.
Naam, Inasikitisha kuona kua wengi wetu pia leo hii hua tunafanya Ibada zetu nyingi
huku tukiwa na nia ya hali ya 3 yaani kwa sababu tu ya kujipunguzia Uzito wa
Majukumu.
Yaani kwa Mfano: Watu Wanafanya Ibada fulani kwa Sababu tu ya Kumrishwa Na
Muumba kufanya Ibada hio, bila kutilia maanani kua kufanya kwao Ibada husika mbali
ya kua ni Jukumu lao lakini hua ni kwa ajili ya Manufaa yao wao wenyewe.
Na hivyo hatufanyi Vitendo kwa ajili ya Nia ya Aina ya kwanza yaani kwa Ikhlasi au
kwa ajili ya Nia ya Aina ya pili yaani kujitolea kufanya Biashara na Allah Subhanah wa
Ta’ala kwa ajili ya kuwekeza katika Akhera yetu.
Kwani mbaya zaid ni kua kutokana na kuwepo kwa Mitandao ya Kijamii, na kuendekeza
Matamanio ya Kidunia basi wengi wetu pia hukosa Nia Sahih na hivyo Waislam hufikia
790
hatua ya, Kutumia Dini yao kwa ajili ya kujitafutia maisha, Kudhalilishana, Kuanikiana
Aibu wazi wazi n.k
Kwa ajili tu ya kutafuta Wafuatiliaji wengi na watizamaji wengi kwenye Video za
Youtube zao na Instagram zao, kwani watu wanajua kua kila wakipata wafuasi wengi
zaid basi hua wanalipwa zaidi na Mitandao ya Jamii kutokana na kua Kila Ukiangaliwa
zaid na Kufuatiliwa basi unapata nafasi zaid ya kua unapata kuingiza pesa za Malipo ya
kutangazia Matangazo ya biashara mbali mbali Mtandaoni kulingana na idadi ya
Waangalizi wanakufuatilia au kukuangalia, hivyo hio hua sio Nia Sahih ya Kufanya
Mambo yako Mbele ya Mola wako
Hivyo ingawa Safari ya Ummu Ayman ilikua Ngumu na ya Taabu sana kutokana na Jua
kali na Upepo mkali unaopeperusha Mchanga wa Jangwani Usoni mwake, lakini hata
hivyo hakuvunjika Moyo kwani alikua ni Mwenye Nia Sahih na hivyo Allah Subhanah
wa Ta'ala alikua pamoja nae.
Na baada ya masiku kadhaa basi Ummu Ayman akawasili katika wa Madinah huku
akiwa taabani, kwani Miguu yake imemvimba na uso wake ulikua utadhani alievaa Mask,
ila si Mask ya Barakoa kama msimavyo Waswahili. Kwani Muonekano wa uso wake
yeye Ummu Ayman ulikua wote Umejaa Vumbi Jembamba na michanga kutokana na
Upepo mkali wa Jangwani.
Kwani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipomuona Ummu Ayman basi Machozi
yalimlenga lenga na akawa ni mwenye kusema: ‘Ya Umm Ayman! Ya Ummi! Kwa
Hakika Allah Subhanah wa Ta'ala ameweka Nafasi kwa ajili yako Peponi’
Kisha baada ya hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaupangusa Uso wa Ummu
Ayman na kisha akamnawisha Uso wake kwa mikono yake Mitukufu na si hivyo tu.
Lakini pia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaikanda kanda Miguu na Mabega
ya Mama yake huyo Mlezi kwa Mikono yake mwenyewe Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam. Naam hivyo ndivyo alivyokua Mbora wa Viumbe kwa Mama yake Mlezi, na
kama huyu alikua ni Mama yake mlezi tu, Alimfanyia hivyo Jee hali ingekuaje kama
angekua ni Mama yake Mzazi?
Kwani Baada ya hapo basi Ummu Ayman akawa ni mwenye kuishi maisha yake kama
kawaida katika kumsaidia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kila awezalo na
hukua ni mtu wa kukaa kaa tu kwani alikua akisikia Jeshi la Waislam linatoka na kuenda
Vitani basi Ummu Ayman mbali ya kua ni mwenye Umri Mkubwa, na mbali ya kua
ameshatabiriwa Pepo mara mbili lakini hata hivyo alikua akifuatana na Jeshi la Kiislam
chini ya Uongozi wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo kua ni mwenye
791
kuhudumia Wanajeshi kwa kuwapa Maji na pia kuwahudumia Wapiganaji wa Kiiislam
waliojeruhiwa vitani.
Ambapo tunapozungumzia Vita kwa ajili ya Allah Subhnah wa Ta’ala basi hua
tunazungumzia Mapigano yaliyoamrishwa na Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume
wake Salallahu Alayhi wa Salam au na viongozi wa Kiislam kwa ajili ya kugombania
haki za Waislam na kuwatoa Waislam katika Dhulma kwa kutumia njia zinazokubalika
kisharia bila ya kufanya Israfu, kama hali ilivyokua katika maamrisho ya Vita mbali
mbali alivyosimamia kupigana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika wakati wa
uhai wake ambapo vita vya kwanza vilikua ni vita vya Badr.
RASUL ALLAH SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM NA MSAFARA WA
BIASHARA WA ABU SUFYAN
Ambapo tunapoangalia historia ya maisha ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi
tunaona kua alikua ni mtu mwenye Subra na Ustahamilivu kama ilivyo Dini ya Kiislam
yenyewe ambayo ni yenye kutokana na Ujumbe wa Allah Subhanah wa Ta’ala kupitia
kwa Mtume wake Salallahu Alayhi wa Salam, ambapo Allah Subhnah wa Ta’ala
anasema katika Qur’an kuhusiana na Ustahamilivu na Subra ya Mtume wake kua:
﴿وَٱصْبرِْ وَمَا صَبْرُكَ إِلا َّ بِٱهلل َِّ وَلاَ تحَْزَنْ عَلَيْهِمْ وَلاَ تَكُ فىِ ضَيْقٍ ممِّ َّا يمَْكُرُو نَ ﴾
Waisbir wama sabruka illa biAllahi wala tahzan AAalayhim wala taku fee dhayqin
mimma yamkuroona (Surat An Nahl 16:127)
Tafsir: Na kua na Subra kwani Subra yako ni kutokana msaada wa Allah na wala
usiwe na Huzuni juu yao na wala usitaabike na mbinu zao za uovu.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakua ni mtu mwenye kupenda vita na
mapigano kama wanavyodhania wengi wasiojua kutokana na kuamini kua Dini ya
Kiislam ilienezwa kwa Upanga. Kwani Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua ni
mtu mwenye huruma, upole, mwenye kupenda salama na amani si katika maisha yake tu
bali kwa kila kiumbe Ulimwenguni kwa ujumla hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam hakuwahi kushika Upanga dhidi ya Maadui zake hadi pale ilipombidi, yaani
alipoamrishwa na Allah Subhanah wa Ta’ala kua afanye hivyo kwa ajili ya kugombania
haki zake na haki za Waislam kwa ujumla.
Na hivyo Amrisho hilo la kupigana kwa ajili ya kusimamia haki za Waumini kua pia ni
mtihani wa Majaribio ya Kiimani juu ya Waumini wa Dini ya Kiislam kua jee kweli
792
wameamini, wanaweza kutii amri kikamilifu? na wanaweza kusimamia na kupigania
haki zao ipasavyo? Kama zinavyosema aya:
﴿وَلَنَبْلُوَن َّكُمْ حَتى َّ ٰ نَعْلَمَ ٱلْمُجَاهِدِينَ مِنكُمْ وَٱلص َّابِرِينَ وَنَبْلُوَ أَخْبَارَكُمْ ﴾
Walanabluwannakum hatta naAAlama almujahideena minkum waalssabireena
wanabluwa akhbarakum (Surat Muhammad 47:31)
Tafsir: Na kwa hakika tutakujaribuni hata tutakapojua Wanaojitolea miongoni
mwenu na wenye Subra, na tutaujaribu ukweli wa habari zenu.
Aya inatuonesha kua Allah Subhanah wa Ta’ala anathibitisha kua atawajaribu Waislam
hadi Waumini watakapowajua ni nani miongoni mwetu Wanaojitolea kwa ajili yake na
wanaokua na subra kwa ajili yake, na hii haimaanishi kua yeye hajui juu ya hayo la, bali
amesema hapa maneno haya kuweka wazi kua atawadhihirisha wazi Waislam wenye
imani dhaifu hivyo wasiokua na sifa stahiki kuhusiana na imani zao, ndani ya nyoyo zao
na pia mbele ya Waislam wengine.
Na kuhusiana na aya hii basi Imam Fudayl Ibn Iyad alikua akilia pale anapoisoma aya hii
huku akisema: ‘Ya Allah Usitujaribu kwani ukitujaribu basi Utatudhihirisha wazi
na kutuadhirisha.’
Hivyo baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuhamia katika Mji wa Madina,
na Waislam kupata nusura na hifadhi basi miaka miwili baadae Allah Subhanah wa
Ta’ala akashusha aya ya kwanza yeye amrisho la kupigana vita vya Jihad kama
alivyosema Imam Qatadah Al Sadusi ambayo hii ni ile aya inasema:
﴿أُذِنَ لِل َّذِينَ يُقَاتَلُونَ أبَِن َّهُمْ ظُلِمُواْ وَإِن َّ ٱهلل ََّ ٰ عَلَى نَصْرِهِمْ لَقَدِيرٌ۞ٱل َّذِينَ أُخْ رِجُواْ
مِن دَِرِهِم بِغَيرِْ حَقٍّ إِلا َّ أَن يَقُولُواْ رَب ُّنَا ٱهلل َُّ وَلَوْلاَ دَفْعُ ٱهلل َِّ ٱلن َّاسَ بَعْضَ ُهمْ بِبَعْ ٍض
له َُّدِّمَتْ صَوَامِعُ وَبِيَعٌ وَصَلَوَاتٌ وَمَسَاجِ دُ يُذْكَرُ فِيهَا ٱسمُ ٱهلل َِّ كَثِيراً وَلَيَنصُرَن َّ ٱهلل َُّ
مَن يَنصُرُهُ إِن َّ ٱهلل ََّ لَقَوِي ٌّ عَزِيزٌ ﴾
793
Odhina lilladheena yuqataloona bi-annahum dhulimoo wa-inna Allaha AAala
nasrihim laqadeerun; Alladheena okhrijoo min diyarihim bighayri haqqin illa an
yaqooloo rabbuna Allahu walawla dafAAu Allahi alnnasa baAAdhahum
bibaAAdhin lahuddimat sawamiAAu wabiyaAAun wasalawatun wamasajidu
yudhkaru feeha ismu Allahi katheeran walayansuranna Allahu man yansuruhu
inna Allaha laqawiyyun AAazeezun (Surat Al Hajj 22:39-40)
Tafsir: Wametangaziwa (Waislam kupigana dhidi ya Makafiri) wale ambao
wanapigana nao kwa sababu ya kudhulumiwa na kwa hakika Allah ni mwenye uwezo
wa kuwanusuru (kwa kuwapa uwezo). Wale (Waumini) ambao wamefukuzwa kutoka
katika Majumba yao bila ya haki kwa sababu tu ya kua wamesema: ‘Mola wetu ni
Allah’ Na kama ingekua Allah hawajaribu watu baadhi yao miongoni mwa baadhi yao
basi bila ya shaka Nyumba za Makasisi, Makanisa, Masinagogi na Miskiti inayotajwa
jina la Allah kwa wingi ndani yake basi ingevunjwa. Kwa hakika Allah atawanusuru
wale watakaomnusuru kwa hakika Allah ni mwenye uwezo juu ya kila kitu na mwenye
utukufu.
Hivyo hizi ni miongoni mwa aya za mwanzo kabisa kushushwa kuzungumzia kuhusiana
na kutangaziwa kwa mapigano ya vita vya Jihadi na kama tunavyoona kua ndani yake
hayakutajwa mapigano ya kushambulia bali yametajwa mapigano ya Kujihami kwa ajili
ya wale waliodhulumiwa, na hivyo hivyo Waislam wanaamrishwa kulipiza kisasi juu ya
yale waliyofanyiwa na kudhulumiwa katika kipindi cha miaka 10 ya Uislam ndani ya Mji
wa Makkah, hivyo walikua wanaambiwa kua umewadia wakati wa kuchukua haki zenu.
Anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Ib Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wakati Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alipohama kutoka katika Mji wa Makka, basi Abu Bakr
Radhi Allahu Anhu alisema kua: ‘Wamemfukuza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, Inna lillahi wa ina Ilayhi RajiA’un - Hakika sisi ni wa Allah na hakika kwake
yeye ndio marejeo yetu, basi msiba mkubwa kwani wataangamia’’ na hivyo Allah
Subhnaha wa Ta’ala aliposhusha aya hii ya Kuwatangazia wale wanaopigana nao
kwa sababu ya kudhulumiwa basi Abu Bakr Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Nilijua
kua itatokea hali ya kuja kua na Vita’
Hivyo katika tangazo hilo basi tunaona kua Allah Subhnaha wa Ta’ala alikua akiwajaribu
Waislam kuangalia Imani zao juu yake na Mtume wake na Waumini wengine kama
zinavyosema aya:
794
﴿أَمْ حَسِ بْتُمْ أَن تُتْرَكُواْ وَلَم َّا يَعْلَمِ ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ جَاهَدُواْ مِنكُمْ وَلمَْ يَت َّخِ ذُواْ مِن دُ ونِ
ٱهلل َِّ وَلاَ رَسُولِهِ وَلاَ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَلِيجَةً وَٱهلل َُّ خَبِيرٌ بمَِا تَعْمَلُونَ ﴾
Am hasibtum an tutrakoo walamma yaAAlami Allahu alladheena jahadoo minkum
walam yattakhithoo min dooni Allahi wala rasoolihi wala almu/mineena waleejatan
waAllahu khabeerun bima taAAmaloona(Surat At Tawbah 9:16)
Tafsir: Hivi Jee Mnafikiria kua Mtaachiwa tu wakati Allah hajakujaribuni
miongoni mwenu kati ya wale watakaojitahidi kupigana miongoni mwenu bila ya
kua na mnaowategemea wengine isipokua Allah na Mtume wake na Waumini na
Allah ni mwenye Habari juu ya kila mnachokifanya.
Kama pia pale aliposema tena kua:
﴿أَمْ حَسِ بْتُمْ أَنْ تَدْخُلُواْ ٱلجَْن َّةَ وَلَم َّا يَعْلَمِ ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ جَاهَدُواْ مِنْكُمْ وَيَعْلَمَ
ٱلص َّابِرِينَ ﴾
Am hasibtum an tadkhuloo aljannata walamma yaAAlami Allahu alladheena
jahadoo minkum wayaAAlama alssabireena (Surat Al Imran 3:142)
Tafsir: Hivi mnajihesabu kua Mtaingia Peponi wakati Allah hajajua bado ni wepi
watakaojitahidi kupigana miongoni mwenu na wale wenye kua na Subra?
Hivyo anasema Bahr Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Allah
Subhanah wa Ta’ala ametangazia Jihadi katika wakati muwafaka, kwani hiki
kilikua ni kipindi ambacho Makafiri wa Makka walikua wako wengi kiidadi, hivyo
kama Allah Subhanah wa Ta’ala angewataka wapigane nao wakati wakiwa na wingi
si wa asilimia 10 tu ya watu wao, basi ingekua vigumu kwao wao.
Kwani ingawa walikua ni 80 tu lakini Ansari walikubaliana na makubaliano ya
Aqabah ya kumuunga mkono Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam pale
walipomuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam : ‘Hivi Jee hatutakiwi
kuwavamia Makafiri hapa katika maeneo ya Minna?’’ ambapo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘La Hakika mimi sikuamrishwa hivyo’
Lakini Waislam walipofukuzwa kwenye Mji wa Makkah, wengine wakaenda
Abyssina na wengine Madina na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akawapa makazi
795
katika Mji wa Madina na hivyo kua tayari ni wenye kuanzisha Mamlaka yao
kwenye ardhi yao, basi ndio Allah Subhanah wa Ta’ala akatangazia Jihadi kwa
kushusha aya yenye tangazo hili la Odhina lilladheena yuqataloona biannahum
dhulimoo wa-inna Allaha AAala nasrihim laqadeerun - Wametangaziwa
(Waislam kupigana dhidi ya Makafiri) wale ambao wanapigana nao kwa sababu ya
kudhulumiwa na kwa hakika Allah ni mwenye uwezo wa kuwanusuru’(Surat Al Hajj
22:39)’
Ama kuhusiana na maneno ya aya inayofuatia baada ya hio ya Surat Al Hajj 22:39 yaani
aya ya 40 yasemayo:
﴿وَلَوْلاَ دَفْعُ ٱهلل َِّ ٱلن َّاسَ بَعْضَهُمْ بِبَعْضٍ له َُّدِّمَتْ صَوَامِعُ وَبِيَعٌ وَصَلَوَاتٌ وَمَ سَاجِ دُ
يُذْكَرُ فِيهَا ٱسمُ ٱهلل َِّ كَثِيراً وَلَيَنصُرَن َّ ٱهلل َُّ مَن يَنصُرُهُ إِن َّ ٱهلل ََّ لَقَوِي ٌّ عَزِيزٌ ﴾
Walawla dafAAu Allahi alnnasa baAAdhahum bibaAAdhin lahuddimat
sawamiAAu wabiyaAAun wasalawatun wamasajidu yudhkaru feeha ismu Allahi
katheeran walayansuranna Allahu man yansuruhu inna Allaha laqawiyyun
AAazeezun (Surat Al Hajj 22:40)
Tafsir: Na kama ingekua Allah hawajaribu watu baadhi yao miongoni mwa baadhi
yao basi bila ya shaka Nyumba za Makasisi, Makanisa, Masinagogi na Miskiti
inayotajwa jina la Allah kwa wingi ndani yake basi ingevunjwa. Kwa hakika Allah
atawanusuru wale watakaomnusuru kwa hakika Allah ni mwenye uwezo juu ya kila
kitu na mwenye utukufu.
Basi yanamaanisha kua: ‘Lau Kama Allah Subhanah wa Ta’ala hakuhalalisha
Mapigano juu ya Mitume na Waumini, basi Makafiri wangewakandamiza
Waumini na kusababisha kutelekezwa kwa Majumba ya Ibada yanayompwekesha
Allah Subhanah wa Ta’ala, lakini Allah Subhnaha wa Ta’ala ameyanusuru kwa
kuhalalisha mapigano ili mwishowe watu wawe huyu kumuabudia ndani yake Mola
wao’
Ambapo kwa upande wa Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye
anasema kuhusiana na kutajwa kwa Majumba haya ya watu wa Ahl al Kitab ya Nyumba
za Makasisi, Makanisa na Masinagogi ndani ya aya hii ni kua: ‘Kwa sababu Allah
Subhnaha wa Ta’ala aliyakubali Majumba hayo katika Nyakati za Mitume wao,
lakini si katika Nyakati za alipowaleta Mitume wengine baada yake na watu hao
wakawakufuru Mitume hao waliofuata. Yaani Aya hii inasema kua Kama Allah
796
Subhaah wa Ta’ala hakua ni mwenye kuyalinda Majengo hayo katika Nyakati zake
basi yangekua tayari yameshavunjwa’
Hivyo baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuambiwa na Allah Subhanah
wa Ta’ala kua Waislam wametangaziwa kupigania haki zao walizodhulumiwa, basi
kwanza akaamua kuzidhibiti njia kuu za misafara ya kibiashara ya Mji wa Makkah
zinazopitia katika Mji wa Madina, na hivyo akatia saini mikataba ya kukubaliana amani
na usalama baina ya watu wa Waislam na Mayahudi na watu wa maeneo mengine ya
jirani ya Madina.
Na kisha akaanza kuwatuma Masahaba zake kuivamia misafara ya Makafiri wa Makkah
na kuiteka nyara Mali zao kwa ajili ya kulipiza kisasi walivyofanyiwa Waislam na
Makafiri wa Makkah kwa kuwataifishia mali zao, hivyo walifanya matukio ya uvamizi
ambayo yalitokea mara kadhaa lakini hayakua na athari kubwa hadi pale mnamo mwezi
wa Ramadhani wa mwaka wa 2 Al Hijra wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alipopata habari kua kuna Msafara wa Abu Sufyan utokao katika ardhi ya Sham kuelekea
katika Mji wa Makkah thamani ya Dinari za Dhahabu 50,000 ambao uko chini ya walinzi
40.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaona kua huu ndio Msafara unaotakiwa
zaidi kutaifishwa kwa sababu Abu Sufyan alikua ni miongoni mwa viongozi wa
wataifishaji wa Mali za Waislam katika mji wa Makkah, hivyo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akawakusanya Masahaba zake kwa ajili ya kukutana na Msafara huo
katika maeneo ya Badr akiwa na nia ya Kuuteka na kutaifisha kila kitu kwenye Msafara
huo, lakini Allah Subhanah wa Ta’ala alikua amepanga mipango myengine ambayo
ambayo ni ya kuwapima Imani Waumini wake kama zinavyosema aya:
﴿وَإِذْ يَ عِدُكُمُ ٱهلل َُّ إِحْدَى ٱلط َّائِفَتِينِْ أَن َّهَا لَكُمْ وَتَوَد ُّونَ أَن َّ غَيْرَ ذَاتِ ٱلش َّوْكَةِ
تَكُونُ لَكُمْ وَيُرِيدُ ٱهلل َُّ أَن يحُِق َّ الحَق َّ بِكَلِمَاتِهِ وَيَقْطَعَ دَابِرَ ٱلْكَافِرِينَ ﴾
Wa-idh yaAAidukumu Allahu ihda altta-ifatayni annaha lakum watawaddoona
anna ghayra dhati alshshawkati takoonu lakum wayureedu Allahu an yuhiqqa
alhaqqa bikalimatihi wayaqtaAAa dabira alkafireena (Surat Al Anfal 8:7)
Tafsir: Na kumbuka wakati Allah alipokuahidini nyie moja kati ya makundi mawili
(ya maadui zako aidha Msafara wao au Jeshi lao) ambapo nyinyi mlikua mnatamani
kua lisiokua na Jeshi ndio iwe lenu, Lakini Allah alikua anataka kuisimamisha haki
kwa maneno yake na kukata mizizi ya Ukafiri.
797
Ambapo anasema Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari kua: ‘Yaani hapa
Allah Subhanah wa Ta’ala anawaambia Waislam kua: ‘Mnatafuta mafanikio ya
haraka na ya juu juu, na mnataka kujiepusha na kile kitakacho kusababishieni
madhara kwa miili yenu au Afya zenu, lakini Allah alilenga malengo bora zaidi
ambayo ni yenye kupelekea kuisimamisha hii Dini, Ushindi juu ya ukweli, Kupanda
darja juu zaidi na kupata mafanikio ya Kidunia na Kiakhera, Ingawa Malengo
mawili hayo (Yenu na yake) yana tofauti kubwa sana baina yao, lakini hata hivyo
yeye Allah Subhanah wa Ta’ala anakuchagulieni kukabiliana na Jehi lao kubwa na
kuwaangamizia Nguvu zao kutokana na udhaifu wenu na kukujaalieni kuwazidi
wingi wa idadi yao kutokana na udogo wa idadi yeu, kuwaadhirisha wao na
kukupandisheni darja nyie na anakupeni kile ambacho hakiwezi kulinganishwa na
kile kilichobebwa na Msafara wao.’’
Tunapoiangalia aya hii tunaona kua Allah Subahan wa Ta’ala anazungumzia tukio bora
alilowachagulia Waislam kua liwatokee kua kama kipimo cha Imani yao katika siku ya
Yawm Al Furqan.
YAWM AL FURQAN – SIKU YA VITA VYA BADR.
Neno Faraqa kwa lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kubagua, Kutenganisha,
Kutofautisha, Kugawanya, Kukata katikati. Neno Faraqa ndio lililotoa neno Furqan
ambalo hua linamaanisha Uthibitisho wa tofauti baina ya mambo au vitu tofauti,
Tofautisho la Jema na Ovu.
Neno Furqan ndio lililotoa Jina la Qur’an Al Furqan yaani Kitabu kinachotofautisha
baina ya Jema na Ovu, na pia ndio lilotoa jina la siku inayojulikana kama Yawm Al
Furqan yaani Siku ya Uthibitisho wa tofauti baina ya Jema na Ovu, Nuru na Kiza, Haki
na Batil.
Ambapo tunapozungumzia Yawm Al Furqan basi hua hatuzunguzmii siku yeyote ile
isipokua ni ile siku iliyotokea tukio ambalo lilibadilisha muelekeo na mtizamo mzima wa
Historia ya Ulimwenguni, ambayo ni hii inayojulikana kua kama Siku ya Badr kama
ilivyoelezewa na Allah Subhanah wa Ta’ala katika aya ifuatayo:
798
﴿وَٱعْلَمُو ۤ ا أَنم ََّا غَنِمْتُمْ مِّن شَيْءٍ فَأَن َّ هللِ َِّ خمُُسَهُ وَلِلر َّسُولِ وَلِذِى ٱلْ قُرْبىَٰ وَٱلْيَتَامَىٰ
وَٱلْمَسَاكِينِ وَٱبْنِ ٱلس َّبِيلِ إِن كُنتُمْ آمَنْتُمْ بِٱهلل َِّ وَمَآ أَنزَلْنَا عَلَى ٰ عَبْدَِ يَوْمَ ٱلْفُرْقَا ِن
ّ كُل شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴾
يَوْمَ ٱلْتَقَى ٱلجَْمْعَانِ وَٱهلل َُّ ٰ عَلَى ِ
WaiAAlamoo annama ghanimtum min shay-in faanna lillahi khumusahu
walilrrasooli walidhee alqurba waalyatama waalmasakeeni waibni alssabeeli in
kuntum amantum biAllahi wama anzalna AAala AAabdina yawma alfurqani
yawma iltaqa aljamAAani waAllahu AAala kulli shay-in qadeerun (Surat Al Anfal
8:41)
Tafsir: Na fahamuni kua katika Ngawira chochote kile mtakachokipata, basi sehemu
moja kati ya tano ni kwa ajili ya Allah na Mtume wake na Waliokaribu nae na
Mayatima na Masikini, na Wasafiri, kama kweli nyinyi mnamuamini Allah na kile
tulichomshushia Mja wetu. Katika Yawm Al Furqan – Siku ya Uthibitisho wa tofauti
baina ya Jema na Ovu, Nuru na Kiza, Haki na Batil – Siku ambayo zilikutana nguvu
mbili na Allah ni mwenye Makadirio juu ya kila kitu.
Hivyo kwa upande mwengine basi Abu Sufyan alikua ni mwenye kujua kua njia ya
kawaida anayotaka kupitia kua haina usalama baada ya mashambulizi madogo madogo
yaliyokua yakitokea hapo kabla dhidi ya misafara ya watu wa Makkah, na hivyo akawa
na wasi wasi, na alipofuatilia zaidi akagundua kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam na jeshi lake ameandaa mashambulizi kwenye maeneo ya Badr, hivyo kwanza
akatuma Mjumbe apeleke habari hizo za matayarisho ya uvamizi wa Msafara wake katika
Mji wa Makkah na kisha akaamua kubadilisha njia kwa ajili ya kuunusuru Msafara wake
huo.
Mjumbe huyo wa Abu Sufyan aitwae Damdam Ibn Amr alipofika katika Mji wa Makkah,
akamkata pua na masikio Ngamia wake kisha akachana nguo zake mgongoni na kifuani
kuashiria kua kuna vita kisha akatangazia kwa kusema: ‘Enyi Watu wa Kabila la
Quraysh, hakika mali zenu ziko pamoja na Abu Sufyan, na msafara wake unataka
kuvamiwa na Muhammad na Masahaba zake, siwezi kusema nini kitatokea
isipokua ni kuomba msaada wenu.’
Makafiri wa Makkah baada ya kupata ujumbe huo basi haraka sana wakakusanya jeshi
la watu 1300 lenye wapanda Farasi 100 na wapanda ngamia zaidi ya 100 na kisha
likaondoka na kuelekea katika Maeneo ya Badr. Ambapo kwa upande wake Abu Sufyan
akaelekea upande wa Mwambao wa Bahari Nyekundu kwa ajili ya kuliepuka eneo la
799
Badr na alipohakikisha kua yuko salama basi akatua ujumbe tena kwa watu Makkah
kuwaambia kua basi haina haja ya kupigana na Muhammad kwani Msafara na Mali zake
ziko salama, na ingawa miongoi mwa wanajeshi wa watu wa Makkah waliamua kurudi
katika Mji wa Makkah
Lakini kwa Upande wa Abu Jahal basi akatilia mkazo kua lazima wakakutane na
Waislam katika maeneo ya Badr kwa kusema: ‘Wallahi, haiwezekani kurudi hadi
tutakapofika kwenye visima vya Badr, tukachinje Ngamia, kisha Wanamuziki wa
kike wacheze kwa ajili yetu, na kutokana na tukio hili basi Waarabu watasema
kwenye historia namna tulivyosheherekea tukio hili.’ Hivyo Jeshi hilo likaendelea na
Msafara wao kuelekea kwenye maeneo ya Badr.
Baada ya mda Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akapata habari ya kubadilisha kwa
njia ya Msafara wa Abu Sufyan, na hapo hapo akapata habari ya kukaribia karibu yao
kwa jeshi kubwa la Makafiri wa Makka, hivyo akashauriana na Masahaba zake kuhusiana
na kinachotaka kutokea ambapo wao Waislam walikua hawajajitayarisha kwa ajili ya
Vita lakini kwa hali inavyokwenda basi itabidi wapigane Vita dhidi ya maaduai zao hao
ambao wingi wao ni zaidi ya 1000 huku wao wakiwa ni watu 313 tu. Hivyo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akaomba Ushauri kwa kuwauliza Waislam; ‘Jee tufanye
nini?’
Hivyo wakati Waislam wamekaa kimya na kufikiria cha kufanya, basi akasimama
Miqdad Ibn Aswad Al Kindi Radhi Allahu Anhu kisha akasema: ‘Ya Rasul Allah
(Salallahu Alayhi wa Salam) Tekeleza mipango ambayo Allah Subhanah wa Ta’ala
ameiweka, kwani kwa hakika sisi hatutosema kama walivyosema Mayahudi
kumwambia Nabii wao Musa kua:
﴿فَٱذْهَبْ أَنتَ وَرَب ُّكَ فَقَاتِلا ۤ إِ َّ هَاهُنَا قَاعِدُونَ ﴾
Fa-idhhab anta warabbuka faqatila inna hahuna qaAAidoona; (Surat Al Maidah
5:24)
Tafsir: Hivyo nenda wewe na Mola wako mkapigane nao, sisi tunakaa hapa
(kukusubirini)’
Badala yake sisi tunasema: ‘Nenda wewe na Mola wako mkapigane na sisi tuko
pamoja nanyi na tutapigana. Wa Allahi! Nnaapa kwa yule ambae amekutuma wewe
kwa Haki, kua hata kama ukituongoza kwenye Birkul Ghimad (Maeneo ya
Ethiopia) basi sisi tutapigana pamoja nawe dhidi ya wale watakaopingana na haki
na hata kama ikiwa kuna makundi na makundi ya Makabila baina ya Madina na
Birkul Ghimad basi tutapigana mpaka tufike huko, na bila ya shaka tutapigana kwa
800
upande wa Kulia kwako, Kushoto kwako, Mbele yako na Nyuma yako mpaka Allah
Subhanah wa Ta’ala atupe Ushindi.’
Hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akafurahi na kutabasam kisha akawageukia
watu wa Madina na kuwauliza: ‘Jee mnasemaje? Tufanye nini?’
Ambapo kwa upande wa watu wa Madina akasimama Saad Ibn Muadh Radhi Allahu
Anhu na kasema: ‘Ya Rasul Allah (Salallahu Alayhi wa Salam) Hakika sisi
tumekuamini wewe, Tumekuamini wewe, na tumekubali kua ukisemacho ni cha
kweli. Hivyo tumeahidi kua ni wenye kukusikiliza na kukutii. Hivyo Ya Rasul Allah
(Salallahu Alayhi wa Salam) fanya unavyotaka kufanya kwani hata ukituambia
tuvuke Bahari Nyekudu basi Tutavuka.’’
Hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam pamoja na Masahaba zake
wakaamua kupiga kambi na kujitayarisha kwa ajili ya vita katika maeneo hayo ya Badr,
na hapo Hubab Ibn Al Mundhir ambae alikua anasifika kwa uzoefu wa mbinu za vita
wakati huo, akamuuliza Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, ‘Ya Rasul
Allah, jee sehemu hii tuliokuwepo sasa hivi, Allah amekushushia aya kua tukae
hapa, ili tusikimbie vitani na kuikimbia sehemu hii, au ni kwa sababu ya mtazamo
wa mbinu za kivita?’
Hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu kua ni kwa sababu ya
mtazamo wake wa mbinu za kivita, hapo Hubab akasema, ‘Ya Rasul Allah, hii si
sehemu nzuri ya kukaa, bali chukua watu wako hadi karibu na visima vya maji
vilivyo karibu na Maadui. Twende tukapige kambi hapo, na kuvizuia visima viwe
nyuma yetu, tujaze maji vyombo vyetu, na kisha tupigane na maadui zetu, sisi
tutakunywa maji lakini wao watakua hawana maji ya kunywa’, hapo Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akafikiria na kuona kua hii ni mbinu bora hivyo
akaamua kufanya kama alivyosema Hubab.
Walipokaribia na bonde la Badr, Sa’d Ibn Mu’adh ambae aliekuwa Chifu wa kabila la
Banu Aws akamfuata Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na kumwambia,
‘Ya Rasul Allah, turuhusu tukujengee sehemu nyuma yetu, ambapo wewe utakaa,
na kumuweka Ngamia wako pia. Nasi tutavaana na maadui zetu. Ikiwa Allah
atatupa nguvu na kushinda basi hilo ndio tunalolitaka, lakini ikiwa litatokea jengine
zaidi ya hilo, basi wewe itakubidi upande Ngamia wako na urudi kuungana na wale
waliobakia. Kwani, Ya Rasul Allah, mapenzi yetu juu yako si makubwa kama ya
wale waliobakia juu yako, kwani kama wangelijua kua utakutana na vita basi
wasingekubali kubakia. Allah akulinde wewe kupita kwao, watakupa ushauri mzuri
na watapigana pamoja nawe’.
801
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akakubaliana na ushauri huo na
kumuombea dua Sa’d Ibn Muadh. Hivyo Waislam wakapiga kambi katika eneo hilo la
mbele ya visima vya Badr, katika siku ya Ijumaa ya mwezi 17 wa Ramadhan na hali
ilikua kama zinavyosema aya:
﴿إِذْ يُغَشِّ يكُمُ ٱلن ُّعَاسَ أَمَنَةً مِّنْهُ وَيُنَزِّلُ عَلَيْكُم مِّنَ ٱلس َّمَآءِ مَآءً لِّيُطَهِّرَكُمْ بِهِ وَيُذْهِبَ
عَنكُمْ رِجْزَ ٱلش َّيْطَانِ وَلِيَرْبِطَ عَلَى ٰ قُلُوبِكُمْ وَيُثَبِّتَ بِهِ ٱلأَقْدَامَ ﴾
Idh yughashsheekumu alnnuAAasa amanatan minhu wayunazzilu AAalaykum
mina alssama-i maan liyutahhirakum bihi wayuthhiba AAankum rijza alshshaytani
waliyarbita AAala quloobikum wayuthabbita bihi al-aqdama (Surat Al Anfal 8: 11)
Tafsir: Kumbuka wakati alipokufunikeni kwa usingizi kua kama ulinzi kutoka kwake,
na akajaalia Maji kumwagika kutoka Mbinguni kwa ajili ya kukusafisheni na
kukuondeleeni athari za uchafu wa Shaytan na kukutieni nguvu nyoyo zenu na
kuithibitishia uimara miguu yenu.
Anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Kutokana na kua Ibn
Adam hua hawezi kulala anapokua katika hali ya Khofu basi ndio maana hapa
Allah Subhanah wa Ta’ala akasema: ‘Wakati alipokusababishieni kuweza kusinzia,
kwani kama wangelala moja kwa moja basi Maadui wangewavamia’’
Ambapo anasema Imam Muhamammad Ibn Is-haq amesema Ali Ibn Abu Talib Radhi
Allahu Anhu kua: ‘Hakika sisi hatukua na Mpanda Farasi isipokua Miqdad Al
Aswad nami sikuona yeyote miongoni mwetu aliekua macho isipokua Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam ambae alikua amekaa chini ya Mti huku akiomba Dua
na kulia hadi Alfajiri’
Ambapo Asubuhi yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akitabasamu na
kumwambia Abu Bakr Radhi Allahu Anhu kua: ‘Kua na hali nzuri ewe Abu Bakr.
Kwani amewasili Jibril kwenye Vilele vya milima’ na kisha akasoma aya isemayo:
﴿سَيُهْزَمُ ٱلجَْمْعُ وَيُوَل ُّونَ ٱلد ُّبُرَ ﴾
Sayuhzamu aljamAAu wayuwalloona alddubura (Surat Al Qamar 54:45)
Tafsir: Watashindwa na kuimbizwa kwa wingi wao na watageukia Nyuma yao.
802
Ambapo kwa upande mwengine basi anasema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu
kua: ‘Wakati Waislam walipowasili kwenye Badr basi walikuta Makafiri wa
Makkah wakiwa wameshafika katika eneo hilo na kuhodhi visima vya Maji. Hili
liliwavunja nguvu Waislam kwani Makafiri walikua wametulia na kufurahia hali
ya mazingira mazuri ya kimbinu za Vita, kwa sababu wao walikua wako kwenye
eneo la juu na Waislam walikua wako bondeni, huku wakiwa ni wenye kuteleza
miguu yao kutokana na ardhi yenye mchanga iliyopo chini ya miguu yao. Vile vile
wakati wa usiku kulikua kuna wenye Janaba, na hivyo ikawabidi wasali kwa
kutayammam bila ya kutumia maji’
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akajaalia kunyesha kwa mvua, na Waislam
wakajitoharisha, wakalishia Wanyama wao na kujaza maji kwenye vyombo vyao vya
maji, na pia wakachimba mashimo kwa ajili ya kuhifadhia Maji, na Mvua hio pia
ikasababisha Mchanga uliokua laini kwenye miguu yao kua ni wenye kushikamana na
kua mgumu na hivyo kua ni wenye kuirahisishia uwezo wa uthibiti wa Miguu yao katika
harakati zao.
Ambapo Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu anasema kua: ‘Wakati Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alipowaangalia watu wa Quraysh na wingi wao na
kuwalinganisha na wingi wa Wafuasi wake waliozidiwa basi akageukia Kibla na
akaanza kuomba dua kwa kusema: ‘Ya Allah! Hakika wewe umeniahidi, hivyo
nitimizie ahadi yangu, kwani watu wangu hawa wakiamgamia basi hakutokua na
wenye kukubadu badala yake.’ Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam aliendelea
kuomba hivyo hadi pale lilipomuanguka Joho lake kutoka begani mwake, na Abu
Bakr akalirudisha Joho hilo begani mwake. Na kisha Abu Bakr akaondoka kutoka
nyuma mgongoni mwa Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam na kusema: ‘Basi
Inatosha ya Rasul Allah, hakika wazazi wangu watolewe kafara kwa ajili yako,
Hakika Allah atatimiza ahadi yake juu yako’’
Na hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akaishusha aya hii isemayo:
﴿إِذْ تَسْتَغِيثُونَ رَب َّكُمْ فَٱسْتَجَابَ لَكُمْ أَنىّ ِ ممُِد ُّكُمْ أبَِلْفٍ مِّنَ ٱلْمَلا ۤ ئِ كَ ةِ مُرْدِفِينَ۞وَمَا
جَعَلَهُ ٱهلل َُّ إِلا َّ بُشْرَىٰ وَلِتَطْمَئِن َّ بِهِ قُلُوبُكُمْ وَمَا ٱلن َّصْرُ إِلا َّ مِنْ عِندِ ٱهلل َِّ إِن َّ ٱهلل ََّ عَزِ يزٌ
حَكِيمٌ ﴾
803
Idh tastagheedhoona rabbakum faistajaba lakum annee mumiddukum bi-alfin
mina almala-ikati murdifeena; Wama jaAAalahu Allahu illa bushra walitatmainna
bihi quloobukum wama alnnasru illa min AAindi Allahi inna Allaha
AAazeezun hakeemun; (Surat Al Anfal 8:9-10)
Tafsir: Na Kumbuka wakati mlipoomba msaada kwa Mola wenu nae akajibu kwa
kusema: ‘Nitakusaidia mimi kwa Maelfu kutoka katika Malaika wangu wenye
kufuatana mmoja nyuma ya mwengine’ Allah amelijaalia hili kua kama bashirio jema
ili Nyoyo zenu zipate utulivu kutokana nalo, kwani hakuna ushindi isipokua kutoka
kwa Allah.
Anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Aya imetumia hali ya
Uombaji wa Dua wa wingi kuonesha kua pale wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alipokua anamuomba Allah Subhanah wa Ta’ala basi Waislam wengine
pia walikua wakiomba hivyo.’
Ambapo anasema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Malaika Jibril na
Mikail wote wawili walishuka wakiongoza Malaika 500 wakiwa mbele ya Jeshi la
Waislam’
Hivyo ingawa Waislam walikua ni robo tatu ya Makafiri lakini Majeshi yote mawili haya
ya Waislam na Makafiri yalipokutana, basi vita vilianza kama ilivyo kawaida ya Vita vya
asili vya Kiarabu ambapo hua ni kwenye kuwepo kwa ufunguzi mapigano ya wapiganaji
mahiri kutoka pande zote mbili kwa ajili ya kupigana wao kwanza mbele ya Majeshi
mawili hayo.
Ambapo kwa upande wa Makafiri uliwakilishwa na Utbah Ibn Rabia, na Walid Ibn Utbah
Ibn Rabia na Shaybah, wakati Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipotaka kuteua
Wapiganaji wake basi kila mmoja miongoni mwa Waislam alijitolea kwa ajili ya kua ni
muanzilishi wa Mapigano hayo kutokana na ari waliyokua nayo Waislam, lakini hata
hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akateuwa wapiganaji kutoka kwenye
familia yake kwa kumteua Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu, Hamza Ibn Abu Talib
Radhi Allahu Anhu na Ubaydah Radhi Allahu Anhu.
Ambapo mapigano hayo ya ufunguzi yalipoanza basi Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu
Anhu akashinda, Hamza Ibn Abu Talim Radhi Allahu Anhu nae pia akashinda na
Ubaydah Radhi Allahu Anhu nae akashinda lakini alijeruhiwa vibaya sana, na baadae
akafariki kutokana na majeraha hayo.
Baada ya mapigano hayo basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akachota mchanga
wa sehemu aliyokuwepo kwenye ardhi ya Badr na kisha akaurembea katika upande wa
Makafiri huku akisema: ‘Uchanganyikiwe muonekano wa Nyuso zao’ na hapo hapo
kikatokea kimbuga chenye upepo mkubwa na Mavumbi yaliyokua yakipeperukia katika
804
upande wa Makafiri na mapigano yakaanza huku yakitokea maajabu makubwa sana
kwani Waislam walikua wapo katika upande wa Kusini Magharibi wa bonde la Badr
ambapo Makafiri walikua wap katika upande wa Kaskazini Mashariki wa Bonde hilo,
huku Waislam wakiwa wako nyuma ya Mlima Asfal kwenye seheu inayojulikana kama
Jabal Malaikah.
Na hii ni kwa sababu kimbunga hicho kilianzia kutoka kwenye Mlima huo na kuelekea
katika Upnde wa Makafiri, na ingawa ilikua ni siku iliyonyehsa mvua kabla yake na
hivyo kutowekezakana kuwepo kwa vumbi lakni hali ilikua tofauti katika siku hio, kwani
Makafiri walichanganyikiwa baada ya kuona mchanga kutoka kusiko julikana unaingia
kwenye macho yao na hapo hapo kupata mashambulizi kutoka kwa viumbe wasiowaona
wala kuwajua.
Hivyo Makafiri wakageuka na kukimbia baada ya hali kubadilika hivyo ingawa Waislam
walikua kidogo lakini wakawa ni wenye kushinda na Makafiri waliokua wengi wakawa
ni wenye kushindwa na kutokana na kuzidiwana kukimbia. Ambapo Allah Subhanah wa
Ta’ala analielezea tukio hili kwa kusema kua:
يُبْلِى
﴿فَلَمْ تَقْتُلُوهُمْ وَلَٰكِن َّ ٱهلل ََّ قَتَلَهُمْ وَمَا رَمَيْتَ إِذْ رَمَيْتَ وَلَٰكِن َّ ٱهلل ََّ ٰ رَمَى وَلِ َ
ٱلْمُؤْمِنِينَ مِنْهُ بَلا ءً ۤ حَسَناً إِن َّ ٱهلل ََّ سمَِيعٌ عَلِيمٌ ﴾
Falam taqtuloohum walakinna Allaha qatalahum wama ramayta idh ramayta
walakinna Allaha rama waliyubliya almu/mineena minhu balaan hasanan inna
Allaha sameeAAun AAaleemun (Quran, 8: 17)
Tafsir: Na hamkuwaua wao lakini Allah ndie aliewaua, nawe (Muhammad Salallahu
Alayhi wa Salam) hukurembea pale uliporemembea bali ni Allah ndie alierembea kwa
ajili kuwajaribu Waumini kwa majaribio Mema, na kwa hakika Allah ni Mwingi wa
Kusikia na ni mwenye kujua.
Hivyo katika vita hivi vya Badr, Waislamu waliwaua Makafir wa Makkah 70 na
kuwateka mateka wengine 70, ambapo Waislamu waliokufa Mashahidi walikua ni 14 tu
Na hivyo Malaika Jibril akamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa kusema:
‘Ya Rasul Allah hivi wewe unawachukulia vipi wale ambao waliopigana kwenye
vita vya Badr?’ ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Hakika sisi
tunawahesabu kua ni wabora miongoni mwa Waislam’ na hivyo Malaika Jibril
akajibu : ‘Na Sisi pia tunawahesabu Malaiak waliopigana kwenye Vita vya Badr’
805
Naam na hii ni kwa sababu Waislam waliopigana Vita Vya Badr walipigana vita Vya
Furqan ambavyo ndivyo vilivyosimamisha Msingi Imara wa Dini ya Kiislam. Kama
alivyosema Allah Subhanah wa Ta’ala pale aliposema katika Qur’an kua:
﴿وَيُسَبِّحُ ٱلر َّعْدُ بحَِمْدِهِ وَٱلْمَلاَئِكَةُ مِنْ خِ يفَتِهِ وَيُرْسِ لُ ٱلص َّ وَاعِقَ فَيُصِيبُ هبَِا مَن
يَشَآءُ وَهُمْ يجَُادِلُونَ فىِ ٱهلل َِّ وَهُوَ شَدِيدُ ٱلْمِحَالِ ﴾
Qad kana lakum ayatun fee fi-atayni iltaqata fi-atun tuqatilu fee sabeeli Allahi
waokhra kafiratun yarawnahum mithlayhim ra/ya alAAayni waAllahu yu-ayyidu
binasrihi man yashao inna fee dhalika laAAibratan li-olee al-absari (Surat Al Imran
3:13)
Tafsir: Kwa hakika tayari (Katika vita vya Badr) imeshakujieni Dalili katika pande
mbili za Majeshi zilizokutana, ambapo upande mmoja walikua wanapigana kwa ajili
ya Allah na upande mwengine kwa ajili ya Ukafiri Wao (Waumini) Wameona
Makafiri kwa macho yao mara mbili zaid yao (Wingi wao) na Allah humsaidia kwa
ushindi wake yule amtakae. Hakika katika haya kuna dalili kuna Somo kwa wale
wenye kuona.
Kisha Allah Subhanah Subhanah wa Ta’ala anawaambia Waislam kua:
﴿وَلَقَدْ نَصَرَكُ مُ ٱهلل َُّ بِبَدْ رٍ وَأَنْتُمْ أَذِل َّةٌ فَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ لَعَل َّكُمْ تَشْ كُ رُونَ ۞إِ ذْ تَقُولُ لِلْمُؤْمِنِينَ
أَلَنْ يَكْ فِيَكُمْ أَنْ يمُِد َّكُ مْ رَب ُّكُمْ بِثَلاَثَةِ آلاَفٍ مِّنَ ۤ ٱلْمَلا ئِكَةِ ۤ مُنزَلِينَ۞بَلَى إِن تَصْبرُِواْ
وَتَت َّقُواْ وََْتُوكُمْ مِّنْ فَوْرِهِمْ هَٰذَا يمُْدِدْكُمْ رَب ُّكُمْ بخَِمْسَةِ ۤ آلا فٍ مِّنَ ۤ ٱلْمَلا ئِكَةِ
مُسَوِّمِينَ۞وَمَا جَعَلَهُ ٱهلل َُّ إِلا َّ بُشْرَىٰ لَكُ ْم
وَلِتَطْمَئِن َّ قُلُوبُكُمْ بِِه وَ مَا ٱلن َّصْ رُ إِلا َّ مِ ْن
عِندِ ٱهلل َِّ ٱلْعَزِيزِ ٱلحَْكِيمِ ﴾
Walaqad nasarakumu Allahu bibadrin waantum adhillatun faittaqoo Allaha
laAAallakum tashkuroona; Idh taqoolu lilmu/mineena alan yakfiyakum an
yumiddakum rabbukum bithalathati alafin mina almala-ikati munzaleena; Bala in
tasbiroo watattaqoo waya/tookum min fawrihim hadha yumdidkum rabbukum
bikhamsati alafin mina almala-ikati musawwimeena; Wama jaAAalahu Allahu illa
806
bushra lakum walitatma-inna quloobukum bihi wama alnnasru illa min AAindi
Allahi alAAazeezi alhakeemi (Surat Al Imran 3:123-126)
Tafsir: Na Allah amekunusuruni nyinyi na kukupeni Ushindi kwenye Badr wakati
mlipokua hamna nguvu, hivyo Mcheni Allah ili mpate kua ni wenye shukrani.
Kumbuka (Ewe Muhammad) wakati ulipowaambia Waumini: ‘Hivi jee haitoshelezi
kwenu nyinyi kua Mola wenu atakusaidieni kwa Malaika 3000 atakaokushushieni?
Naam, kama Mkiwa na Subra na Ucha Mungu na maadui wakija kukuvamieni basi
Mola wenu atakusaidieni nyie kwa Malaika 5000 wenye Alama za kuwatofautisha. Na
hakujaalia Allah isipokua ni ujumbe wenye habari nzuri kwa ajili yenu na
kukuhakikishieni utulivu ndani ya Nyoyo zenu. Na hakuna Ushindi isipokua kutoka
kwa Allah Mwenye wingi wa uwezo na mwenye wingi wa Hikma’
Ambapo amesema Mujaddid Ad Din Imam Ibn Hajar Al Asqalani kua: ‘Rabii Ibn Anas
amesema kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala aliwasaidia Waislam katika Vita vya Badr
kwa Malaiak 1000, na kisha akawaongezea Msaadwa Malaika 3000 na kisha
akawaongezea Msaada wa Malaika 5000’
Baada ya kumalizika Vita na kukusanywa mateka waliotekwa na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kuwaona mateka hao, basi akawa hajui awafanye nini, hivyo ikabidi
akae na Masahaba zake ili washauriane na kuamua wawafanye nini, hapo Abu Bakr as
Siddiq Radhi Allahu Anhu akashauri mateka walipishwe fidya halafu waachiwe, na Umar
Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akashauri wauliwe, hapo Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam akaona bora kufanya kama alivyosema Abu Bakr Radhi Allahu Anhu
na kwa baadhi ya wanaojua kusoma miongoni mwao mateka hao basi wakapewa
Waislam wasiokua kusoma wawasomeshe, wapate kujua kusoma na kuandika.
Ambapo miongoni mwa waliokamatwa pia alikuwemo Al Abbas Ibn Abd Ul Muttalib
Radhi Allahu Anhu ambae anaelezewa na Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua:
‘Baada ya vita vya Badr basi miongoni mwa Mateka wa Vita waliletwa, na miongoni
mwao alikuwemo Al Abbas, ambae alikua hana shati hivyo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akamtafutia Shati kwa ajili yake, na likapatikana shati la Abdullah
Ibn Ubbay lililokua ni saizi yake, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akampa Al Abbas avae na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamfidia
Abdulla kwa kumpa Shati lake yeye.’
Ambapo baadae Al Abbas akajilipia fidya kwa ajili ya kujikomboa na kuachiwa baada
yake na akasilimu baada ya mkataba wa Huddaybiyah ambapo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akampa jina la Muhajirun wa Mwisho, na hivyo kua ni mwenye
kuingizwa kua miongoni mwa wenye kurithi Ngawira ya Vita na kurudishiwa kazi yake
ya Usimamiaji wa Kisima cha Maji ya Zamzam.
807
Miongoni mwa waliokamatwa pia alikuwemo Abu Aziz Ibn Umayr ambae ni kaka
yake Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu, ambapo anasema Abu Azizi Ibn Umayr
kua: ‘Hakika mimi nilikua pamoja na kikundi cha Ansar, ambao ilikua kila
wakila chakula walikua wakinigaia Tende na Mkate ili nile kutokana na
maamrisho ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua wasituvunjie haki
zetu’
‘Mara kaka yangu Musab Ibn Umayr akapita karibu yangu na akaniona na hivyo
akamwambia mmoja kati ya Maansari hao wanaonisimamia kama mateka kua
‘Huyu mfunge kamba yake madhubuti sana, kwani Mama yake ni Mtu tajiri sana
na huenda akalipa pesa nzuri sana kwa ajili ya kumkomboa’’
Abu Aziz Ibn Umayr hauamini masikio yake pale aliposikia maneno hayo kutoka kwa
ndugu yake baba mmoja mama mmoja ambae ni Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu
na hivyo Abu Aziz Ibn Umayr akamuuliza Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu kwa
kusema: ‘Ewe Kaka yangu maelezo hayo unayoyatoa yaninihusu mimi?’ ambapo
Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu akamjibu kaka yake huyo kwa kumkana huku
akimnyooshea kidole yule Ansari aliempa maelekezo hayo kua: ‘Huyu Ndio Ndugu
yangu, sio wewe’’ na hivyo kuthibitisha kua Katika mapigano baina ya Imani na Kufr
basi Udugu wa Iman ni mkubwa zaidi kuliko udugu wa Kidamu
Ambapo tunapoangalia kuhuiana na watu wa Ahl Al Kitab basi tunaona kua wao walikua
hawaruhusiwi kuchukua Ngawira baada ya Vita, na kwa watu wengine basi hali ilikua
kila mpiganaji anachukua kile anachokipata katika mapigano husika, au ngawira hizo hua
zinachukuliwa na kiongozi wa Jeshi lililoshinda, na hii hupelekea kwa abadhi ya
wapiganaji kuia ngawira hizo au kuzificha kwa ajili ya manufaa yao wenyewe, lakini
kwa upande wa Waislam baada ya tukio hili la vita vya mwanzo ambavyo ni vya Badr
basi wakawa hawajuia pia wafanye nini kuhusiana na ngawira hizo, hivyo wakamuuliza
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam juu yake, ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala
akashusha aya isemayo:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞يَسْأَلُونَكَ عَنِ ٱلأَنْفَالِ قُلِ ٱلأَنفَالُ هللِ َِّ وَ ٱلر َّسُولِ
فَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَأَصْلِحُواْ ذَاتَ بَيْنِكُمْ وَأَطِيعُواْ ٱهلل ََّ وَرَسُولَ هُ إِ ن كُنتُم م ُّؤْمِنِينَ ﴾
Biismi Allahi Alrrahmani Alrrahim; Yas-aloonaka AAani al-anfali quli al-anfalu
lillahi waalrrasooli faittaqoo Allaha waaslihoo dhata baynikum waateeAAoo Allaha
warasoolahu in kuntum mu/mineena (Surat Al Anfal 8:1)
808
Tafsir: Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma; Na wanakuuliza
kuhusiana na Ngawira hivyo waambie kua (Maamuzi yake) Ngawira ni kwa ajili ya
Allah na Mtume wake, hivyo Mcheni Allah na suluhisheni yaliyopo baina yenu na
Mtiini Allah na Mtume wake kama nyinyi ni Waumini.
Hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala alipotangazia katika ayah hii ya Surat Al Anfal kua
Ngawira itasimamiwa na Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume wake Salallahu Alayhi
wa Salam basi ilikua inamaanisha kila kinachopatikana kinatakiwa kifikishwe mbele ya
Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam na kisha yeye ndie atakaeamua nini cha kufanya
kutokana nacho kwa kugawa kwa namna inavyostahiki.
Ambapo neno Anfal hua linatokana na neno Nafala ambalo hua linaaminisha Kumpa
Mtu zawadi, Kutoa au kufanya jambo zuri zaidi ya ilivyoamrishwa, Kutoa zawadi bila
ya kuamrishwa yaani kwa hiari, Kutunuku au Kuzawadia, Kutoa au kumpa Mtu au Watu
Ngawira au iliyopatikana vitani
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Kulikua kuna
watu watatu kutoka miongoni mwa Muhajjiruna na watu watano miongoni mwa
Maansari ambao ingawa hawakua ni wenye kupigana kwenye vita vya Badr lakini
walipewa Ngawira, ambao ni:
Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu, kwa saabu ya kua alikua akimsimamia Mke
wake aliekua akiumwa ambae ni Ruqqayah Bint Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam.’
Talha na Sad Ibn Zayd Radhi Allahu Anhum ambaowao walitumwa na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam katika ardhi ya Sham kwa ajili ya kufanya Upelelezi.
Abu Lubabah Ibn Marwan Radhi Allahu Anhu ambae aliachwa katika Mji wa
Madina Na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua ndie Msimamizi Mkuu wa
Mji.
Asim Radhi Allahu Anhu ambae yeye aliachwa asimamie Ulinzi wa maeneo ya Nje
ya mipaka ya Madina.
Harth Ib Hatib Radhi Allahu Anhu ambae yeye alitoka na jeshi la Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam lakini njiani kaambiwa arudi aende akasimamie kitu
Fulani katika mji wa Madina.
809
Harth Ibn Sumh Radhi Allahu Anhu ambae yeye alikua akiumwa njian
alipofikakatika maeneno ya Rawha hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akamwambia bora arudi Madina akapumzike.
Khuwat Ibn Jubayra Radhi Allahu Ahu.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipowapa Masahaba hawa wanane
sehemu ya Ngawira basi kuna baadhi ya Masahaba wakalalamika, na hivyo Allah
Subhanah wa Ta’ala akaishusha ayah hii ya kwanza ya Al Anfal.
Ambapo anasema Imam Abu Yalah kua: ‘Amesema Ans Ibn Malik Radhi Allahu Anhu
kua: ‘Siku moja tulikua tumekaa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na mara
akaw ani mwenye kutabasam sana, hivyo Umar akamuuliza : ‘Hakika Wazazi
wangu watolewe Kafara kwa ajili yako ya Rasul Allah, hivi jee ni kitu gani
kilichokufurahisha?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Kuna waja
wangu wawili walifikishwa mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala ambapo mmoja kati
yao alisema: ‘Ewe Mola wangu mfanye kua awe ni mwenye kunilipa Fidiya mimi
kutokana na makosa aliyonifanyia’
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala akasema kumwambia yule anaeshtakiwa kua:
‘Mlipe Fidya yake kutokana na yale maovu uliyokuya ukimfanyia’ Hivyo yule
anaeshitakiwa akasema: ‘Ya Allah hakika mimi sina hata Jema moja langu
lililobakia’
Hivyo yule anaeshtaki akasema: ‘Ewe Mola wangu basi mpe sehemu ya Madhambi
yangu’
Hapa macho ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam yakajawa na Machozi kisha
akasema: ‘Hio itakua ni siku mbaya kabisa, siku ambayo watu watakua wanatafuta
watu wa kuwamwagia Mzigo wao wa Madhambi.’
Na kisha baada ya hapo basi Allah Subhanah wa Ta’ala akasema kumwambia yule
mtu anaeshtaki kua: ‘Angalia Juu kwenye Bustani za Peponi’ na Mtu huyo
akaangalia juu kisha akasema: ‘Ewe Mola wangu hakika mimi mashamba ambayo
yamejaa fedha, na Makasri yaliyopambwa Dhahabu na Lulu, hivi jee yamewekwa
kwa ajili ya Mtume gani? Kwa Siddiqina Gani? Kwa Shuhadaa gani?’
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala atasema: ‘Hayo yamewekwa kwa ajili ya yeyote
yule atakaelipia kwa Malipo yake,’ ambapo Mtu huyo atasema: ‘Hivi Jee Malipo
yake ni kiasi gani na nani mwenye uwezo nayo?’ Allah Subhanah wa Ta’ala
810
atamwambia Mtu huyo kua: ‘Hata wewe unao uwezo nayo’ hivyo mtu huyo
atauliza: ‘Malipo gani?’
Allah Subhanah wa Ta’ala akasema: ‘Msamehe Ndugu yako huyu’ na hapo Mtu
huyo akasema: ‘Ya Allah hakika mimi nimeshamsamehe Ndugu yangu huyu’. Hapo
Allah Subhanah wa Ta’ala akasema: ‘Mshike mkono wake Ndugu yako Uingie nae
Peponi’ kisha Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam akasoma aya ifuatayo:
﴿فَٱت َّقُواْ ٱهلل ََّ وَأَصْلِحُواْ ذَاتَ بَيْنِكُمْ وَأَطِيعُواْ ٱهلل ََّ وَرَسُولَهُ إِن كُنتُم م ُّؤْ مِ نِينَ ﴾
Faittaqoo Allaha waaslihoo dhata baynikum waateeAAoo Allaha warasoolahu in
kuntum mu/mineena (Surat Al Anfal 8:1)
Tafsir: Hivyo Mcheni Allah na suluhisheni yaliyopo baina yenu na Mtiini Allah na
Mtume wake kama nyinyi ni Waumini.’’’
Ambapo kwa upande mwengine basi anasema Sad Ibn Abi Waqqas Radhi Allahu Anhu
kua: ‘Ndugu yangu Umayr alikua ni miongoni mwa waliouliwa katika vita vya Badr,
kisha nami nikamuua Said Ibn Al Aas aliemuua Ndugu yangu huyo na kisha
nikachukua Upanga wake, na kisha nikaenda kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam ambae akaniambia kua niuweke Upanga huo pamoja na vitu vyengine
vilivyopatikana kama ngawira, nami nikafanya hivyo lakini sasa Allah Subhanah
wa Ta’ala ni mwenye kujua kuhusiana na yaliyokua yakiendelea akilini mwangu,
hivyo nilipokua nikirudi kuuweka Upanga huo basi Allah Subhanah wa Ta’ala
akaishusha aya hii, na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaniambia kua:
‘Unaweza kua nao Ule Upanga’’ (Imam At Tirmidhi)
Na kwa upande mwengine basi kuhusiana na Ngawira basi Allah Subhanah wa Ta’Ala
alifafanua tena baadae katika Sura hii pale aliposema:
﴿وَٱعْلَمُو ۤ ا أَنم ََّا غَنِمْتُمْ مِّن شَيْءٍ فَأَن َّ هللِ َِّ خمُُسَهُ وَلِلر َّسُولِ وَلِذِى ٱلْ قُرْبىَٰ وَٱلْيَتَامَىٰ
وَٱلْمَسَاكِينِ وَٱبْنِ ٱلس َّبِيلِ إِن كُنتُمْ آمَنْتُمْ بِٱهلل َِّ وَمَآ أَنزَلْنَا عَلَى ٰ عَبْدَِ يَوْمَ ٱلْفُرْقَا ِن
ّ كُل شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴾
يَوْمَ ٱلْتَقَى ٱلجَْمْعَانِ وَٱهلل َُّ ٰ عَلَى ِ
811
WaiAAlamoo annama ghanimtum min shay-in faanna lillahi khumusahu
walilrrasooli walithee alqurba waalyatama waalmasakeeni waibni alssabeeli in
kuntum amantum biAllahi wama anzalna AAala AAabdina yawma alfurqani
yawma iltaqa aljamAAani waAllahu AAala kulli shay-in qadeerun(Surat Al Anfal
8:41)
Tafsir: Na Jueni kua chechote kile kutokana na Ngawira mtakachopata basi sehemu
moja kati ya 5 hua ni kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala na Mtume wake Salallahu
Alayhi wa Salam na kwa Watu wa Karibu yake Rasul Allah Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, na kwa Mayatima, na kwa Masikini, na Wasafiri, na kama ni wenye
kumuamini Allah Subhanah wa Ta’ala na kile tulichokiteremsha kwenye Qur’an kwa
Mja wetu(Muhamamd Salallahu Alayhi wa Salam) na Siku ya Malipo na siku
yaliyokutana Majeshi ya pande mbili (Badr)Na Allah ni mwenye uwezo juu ya kila
kitu.
Tunaporudi kwenye matukio ya baada ya vita vya Badr basi tunaona kua miogoni mwa
Makafiri waliouliwa katika vita hivi basi watu 17 walikua wanatokea katika ukoo wa
Khalid Ibn Walid wa Banu Makhzum, na katika waliotekwa pia alikuwemo Al Walid Ibn
Walid ambae ni alikua mdogo wake Khalid Ibn Walid.
Baada ya Khalid Ibn Walid kurudi safarini na kusikia yaliyotokea aliamua kushirikiana
na ndugu yake Hisham Ibn Al Walid na Ikrimah katika kupanga majadiliano na Waislam
ya kuwalipia fidya mateka waliokamatwa katika vita hivyo ili waachiwe huru baada ya
kulipwa fidiya hiyo. Waislam walitaka walipwe dirham 4000 ili waweze kumuachia huru
Walid Ibn Al Walid, lakini Hisham alikataa na kuanza kupatana ili ashushiwe kidogo,
hata hivyo Khalid Ibn Walid alimgombeza ndugu yake huyo kwa kuona kua anataka
kuitia aibu familia yao, hivyo wakakubaliana kulipa fidia hiyo hiyo bila ya mapatano.
Baada ya kumlipia Walid Ibn Al Walid fidya, ndugu hao wote watatu waliondoka
Madinah kwa pamoja na kuanza safari ya kurudi Makkah, ulipoingia usiku, wakaamua
kupiga kambi katika eneo linaloitwa Zul Halifa, na ilipofika usiku wa manane Walid Ibn
Al Walid akatoroka na kurudi tena Madinah ambapo alipofika huko alikwenda moja kwa
moja kwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na kusilimu, na huko
akathibitisha Uislamu wake kwa kua karibu sana na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam.
KHALID IBN WALID NA VITA VYA UHUD, KHANDAK NA MUTAA.
812
Mnamo mwaka 625, miaka mitatu baada ya Hijra Waislamu walipigana vita vya pili na
Makafiri, vita ambavyo vilijulikana kama vita vya Uhud. Viliitwa vita vya Uhud kwa
sababu vilipiganwa chini ya mlima wa Uhud uliopo katika umbali wa kilomita tatu
kaskazini mwa mji wa Madinah .
Vita vya Uhud viliandaliwa mashambulizi yake na watu wa Makakh wakiongozwa na
Abu Sufyan kwa ajili ya Kulipiza kisasi juu ya yale yaliyotokea katika Vita Vya Badr na
hivyo Makafiri hao kua na malengo ya Kuumua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na Kuuangamiza Uislam, hususan kutona na kua Waislam walikua bado ni kidogo kiidadi
kwani Waislam walikua na jeshi la watu 700 ukilinganisha na Makafiri ambao walikua
na jeshi la watu 3000.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam aliwapanga baadhi ya wanajeshi wake
chini ya mlima wa Uhud, na kuwaambia vyovyote itakavyokua wasiondoke chini ya
mlima huo, ili kuwalinda Waislam wasije wakapata mashambulizi ya kushtukiza kutoka
nyuma ya mlima huo. Katika vita hivi Khalid Ibn Walid alikuwa akiongoza kikundi cha
wapiganaji wa farasi waliokua katika upande wa Makafiri.
Mapigano yalipoanza na kuendelea ikawa kuna muonekano wa Waislam kushinda, na
Makafiri kushindwa, hata hivyo Khalid Ibn Walid ambae alikua amejitenga na kuangalia
mapigano alijaribu kuwavuta Waislam waliokuwepo chini ya mlima waondoke ili
akiongoze kikundi chake kuwavamia kwa nyuma Waislam lakini ikawa kazi bure, kwani
nao walijibu mapigo kwa kuwarushia mishare ya upinde.
Katikati ya mapigano Makafiri hao walizidiwa nguvu na kuanza kukimbia ovyo, hivyo
Waislam walioambiwa wasiondoke katika sehemu zao, ikabidi waingie tamaa na kuanza
kuwafuata na kufukuzia ngawira za wale Makafiri waliokua wakikimbia. Jambo ambalo
lilisababisha madhara makubwa sana baadae, kwani Khalid Ibn Walid aliekua amekaa na
subra kubwa, aliipata nafasi aliyokuwa akiisubiri kwa muda mrefu na hivyo akaitumia
kwa kukiongoza kikundi chake na kuwapa Waislamu shambulizi la kushtukiza, kwa
kuwatokezea kwa nyuma yao, kuona hivyo wale Makafiri waliokua wakikimbia
wakaamua kugeuka na kuwavamia Waislam, hivyo ikawa Waislamu wamewekwa kati
kati baina ya Makafiri na kuchanganyikiwa kutokana na kuzidiwa nguvu na Makafiri hao
baada ya Hamza Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kupigwa Mkuki na Wahshi na kufariki
Dunia.
Katika Vita hivi Rasul Allah Salallau Alyhi wa Salam alimchagua Musab Ib Umayr Radhi
Allahu Anhu kua ndie Mshika bendera ya Waislam na hivyo kua ni mwenye kuchukua
jukumu la kuwatia ari waislam katika kuongoza mapigano hayo, na hali ilipobadilika ya
mapigano basi Makafiri ikawa wanakimbilia katika sehemu aliyokuwepo Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam ili wamuue, ambapo Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu
813
akagundua juu ya jambo hili na hivyo akazidisha kuinyanyua juu bendera ya Uislam kwa
mkono mmoja huku akitamka ‘Takbir’ na kushambulia maadui zake kwa mkono wake
wa kulia, ambapo mara ghafla mpanda Farasi wa makafiri akamkaribia Muadh Ibn
Umayr Radhi Allahu Anhu na kumpiga upanga na kumkata mkono wake wa kulia,
ambapo kilichofuatia baada ya hapo ilikua ni kusikika sauti ya Musab Ibn Umayr Radhi
Allahu Anhu ikisema:
﴿وَمَا محَُم َّدٌ إِلا َّ رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِنْ قَبْلِهِ ٱلر ُّسُلُ أَفإِنْ م َّاتَ أَوْ قُتِلَ ٱنْقَلَبْتُمْ
عَلَى ٰ أَعْقَابِكُمْ ﴾
Wama Muhammadun illa rasoolun qad khalat min qablihi alrrusulu afa-in mata
aw qutila inqalabtum AAala aAAqabikum (Surat Al Imran 3:144)
Tafsir: Na hakua Muhamamd isipokua ni Rasul, na wamekuja kabla yake Mitume
hivyo jee hata kama ikiwa atakufa au atauliwa, mtageuka kutokana na muelekeo wa
visigino vyenu?
Baada ya kusema maneno hayo basi Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu akapigwa tena
upanga kwenye mkono wake wa kushoto hukua akiendelea kutamka maneno haya
ayatamkayo, kisha akapigwa na Mkuki ambao ulimpeleka moja kwa moja kuanguka
chini na hvivyo Bendera ya Uislam kua ni yenye kuanguka chini pamoja nae, na
haukuchukua mda akafariki Dunia.
Ambapo maneno yake hayo aliyokua akiyasema Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu
baada ya kushambuliwa kwake katika vita hivi, basi Allah Subhanah wa Ta’ala
akayashusha kua in sehemu ya aya ya Qur’an ambayo inasema:
﴿وَمَا محَُم َّدٌ إِلا َّ رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِنْ قَبْلِهِ ٱلر ُّسُلُ أَفإِنْ م َّاتَ أَوْ قُ تِلَ ٱنْقَلَبْتُمْ
عَلَى ٰ أَعْقَابِكُمْ وَمَن يَنْقَلِبْ عَلَى ٰ عَقِبَيْهِ فَلَنْ يَضُر َّ ٱهلل ََّ شَيْئاً وَسَيَجْزِى ٱهلل َُّ
ٱلش َّاكِرِينَ ﴾
814
Wama muhammadun illa rasoolun qad khalat min qablihi alrrusulu afa-in mata aw
qutila inqalabtum AAala aAAqabikum waman yanqalib AAala AAaqibayhi falan
yadurra Allaha shay-an wasayajzee Allahu alshshakireena (Surat Al Imran 3:144)
Tafsir: Na hakua Muhamamd isipokua ni Rasul, na wamekuja kabla yake Mitume
hivyo jee hata kama ikiwa atakufa au atauliwa, mtageuka kutokana na muelekeo wa
visigino vyenu? Na atakaegeuka kutokana na muelekeo wa visigino vyake basi
hatomdhuru Allah Subhanah wa Ta’ala hata kidogo na Allah Subhanah wa Ta’ala
atawalipa wale wenye kuonesha shukurani.
Mapigano yakaendelea na hali ilipokua ngumu zaidi kwa upande wa Waislamu basi
baadhi walikimbilia juu ya mlima wa Uhud, wengine walikimbilia kujificha ili kuokoa
maisha yao na wengine walikimbilia kusiko julikana na kurudi siku mbili baada yake.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alijeruhiwa na kutoka na nyingi kichwani
na kung’oka meno mawili, hivyo mtoto wake, Fatma na Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu
Anhum wakamshughulikia kumpa huduma ya kwanza kwa kumfunga kitambaa kuzuia
damu na mara baadae Abu Bakr As Siddiq na Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhum
wakaungana nao.
Baada ya mapigano hayo Waislam wakakusanyika kwa ajili ya kuokota Maiti wao
waliopata Ushahidi ambao walikua ni watu 70 kwa ajili ya kuzikwa na ingawa miongoni
mwao alikuwemo pia Hamza Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu ambae ni Ami yake Rasul
Allah Salallahu Aalyhi wa Salam lakini hata hivyo, Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam hakusikitikia sana kwani ilikua ni pale alipoiona maiti ya Musab Ibn Umayr Raddi
Allahu Anhu basi ndio machozi yakamtiririka.
Ambapo kila walipokua wakijaribu kumfunika Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu
kwa Sanda yake, basi haikuwezekana kumfunika mwili wake wote kwani wakimfunika
kichwani basi miguu inabakia wazi na kila wakimfunika kichwa basi miguu inabakia
wazi, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Mfunikeni kwa Sanda
kichwani mwake na miguu yake mfunikeni kwa majani ya idhkir’
Huku akimkumbuka Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu namna alivyokua ni kijana
mtanashaji, mwenye kupendeza kwa kila kitu na kwa kila hali na nama alivyojitolea na
kuachana na yote hayo kwa ajili ya Mola wake na kufikia mwisho wake huku akiwa hata
sanda yake haimtoshi kutokana na Malaika kugombaniana na Waislam namna ya
kumvisha Sanda yake, na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema:
815
﴿مِّنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُواْ مَا عَاهَدُواْ ٱهلل ََّ عَلَيْهِ فَمِنْهُمْ م َّن قَضَى ٰ نحَْبَهُ وَمِنْ هُمْ
م َّن يَنتَظِرُ وَمَا بَد َّلُواْ تَبْدِيلاً ﴾
Mina almu/mineena rijalun sadaqoo ma AAahadoo Allaha AAalayhi faminhum
man qada nahbahu waminhum man yantadhiru wama baddaloo tabdeelan (Surat
Al Ahzab 33:23)
Tafsir: Miongoni mwa Waumini kuna watu waliosadikisha juu ya kile walichomuahidi
Allah miongoni mwao wametekeleza majukumu yao na baadhi yao bado wanasubiri
lakini hawajabadilika hata kidogo.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Musab Ibn Umayr hakika
Rasul Allah anashuhudia kua wewe ni Shahidi mbele ya Allah Subhanah wa Ta’ala
na katika siku ya Malipo’ na kisha akawageukia Waislam na kuwaambia: ‘Enyi
Waislam watembeleeni Mashahidi, Wasalimieni kwani nnapa kwa yule ambae ni
mwenye kuimiliki Roho yangu ndai ya mikono yake kua Muislam yeyote
atakaewatumia salam mashahidi hadi katika siku ya Malipo basi nao
watamrudishia salama hio.’
As-salaamu alaykum, ma'shar ash-shudhadaa. As-salaamu alaykum wa rahmatullah wa
barakatuhu.
Ingawa hivi vilikua ni vita vya mwanzo vikubwa kwa Khalid Ibn Walid kupigana lakini
alifanikiwa kuwapa ushindi mkubwa Makafiri wa Makkah kutokana na uwezo wake wa
kua na subra, kutokukubali kushindwa, na vile vile kutokana na mbinu zake za hali ya
juu. Khalid Ibn Walid alikua ni mtu wa mwanzo katika historia ya Uislam kuuhatarisha
usalama wa Waislam a Uislam kutokana na vita hivi.
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anawadhihirishia Waislam kuhusiana na kile
kilichotokea katika vita hivi vya Uhud kwa kusema:
816
﴿وَلَقَدْ صَدَقَكُمُ ٱهلل َُّ وَعْدَهُ إِذْ تحَُس ُّونَهُمْ إبِِذْنِهِ حَتى َّ ٰ إِذَا فَشِ لْتُمْ وَتَنَازَعْتُمْ فىِ ٱلأَمْرِ
وَعَصَيْتُمْ مِّنْ بَعْدِ مَآ أَرَاكُمْ م َّا تحُِب ُّونَ مِنْكُمْ م َّنْ يُرِيدُ الد ُّنْيَا وَمِنْكُمْ َّمنْ يُرِيدُ ٱلآخِ رََة
ثمُ َّ صَرَفَكُمْ عَنْهُمْ لِيَبْتَلِيَكُمْ وَلَقَدْ عَفَا عَنْكُمْ وَٱهلل َُّ ذُو فَضْلٍ عَلَى ٱلْمُؤْمِنِينَ ﴾
Walaqad sadaqakumu Allahu waAAdahu idh tahussoonahum bi-ithnihi hatta itha
fashiltum watanazaAAtum fee al-amri waAAasaytum min baAAdi ma arakum ma
tuhibboona minkum man yureedu alddunya waminkum man yureedu al-akhirata
thumma sarafakum AAanhum liyabtaliyakum walaqad AAafa AAankum
waAllahu dhoo fadlin AAala almu/mineena.(Surat Al Imran 3:152)
Tafsir: Na kwa hakika ametimiza Allah ahadi yake pale mlipokuwa mkiwaua
(Maadui zenu) kwa idhini yake; hadi pale mlipopoteza matumaini na ushujaa wenu
baada ya kuvutana kuhusiana na mlioamrishwa na mkaasi baada ya yeye (Allah
Subhah wa Ta’ala) kukuonesheni Ngawira mnayoipenda. Ambapo miongoni mwenu
kuna wenye kutamani Dunia hii na kuna wanaoitamani Akhera, kisha akakufanyeni
nyinyi kua ni wenye kuwakimbia maadui zenu ili apate kukujaribuni, lakini kwa
hakika amekusameheni kwani Allah ni mwenye kupenda kulipa fadhila kwa Waumini.
Ambapo aya inatuwekea wazi kua yote yaliyotekea ni kutokana na Waislam kughafilika
na kutotii amri ya Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam kwa hivyo huo ulikua ni mtihani
mwengine dhidi yao, baada ya kushindwa kujidhibiti dhidi ya tamaa na kukosa
unyenyekevu mbele ya Mola wao na kua niwenye kushindwa katika mtihani wa
kujaribiwa kwao, na kisha Allah Subhnaha wa Ta’ala akaendelea kudhidhirisha kwa
kuwaambia Waislam kua wasifananishe haya yaliyotokea kwenye Vita vya vya Badr na
hivi vya Uhud na yasiwe ni yenye kuwapelekea Waislam kujiuliza imekuaje? Kama
zinavyosema Aya:
﴿أَوَ لَم َّا أَصَابَتْكُمْ م ُّصِيبَةٌ قَدْ أَصَبْتُمْ مِّثْلَيْهَا قُلْتُمْ أَنى َّٰ هَٰذَا قُلْ هُوَ مِ نْ عِنْدِ
أَنْفُسِ كُمْ إِن َّ ٱهلل ََّ ٰ عَلَى كُ ِل شَ يْ ءٍ قَدِيرٌ۞ وَمَآ أَصَابَكُمْ يَوْمَ ٱلْتَقَى ٱلجَْمْعَانِ فَبِإِذْ ِن
ٱهلل َِّ وَلِيَعْلَمَ ٱلْمُؤْمِنِينَ ﴾
ّ
817
Awa lamma asabatkum museebatun qad asabtum mithlayha qultum anna hadha
qul huwa min AAindi anfusikum inna Allaha AAala kulli shay-in qadeerun; Wama
asabakum yawma iltaqa aljamAAani fabi-idhni Allahi waliyaAAlama
almu/mineena (Surat Al- Imran 3:165-166)
Tafsir: (Inakuaje) Wakati mnapofikwa na Msiba mbali ya kua mmewashinda mithili
yenu mara mbili (maadui zenu) basi mnakua mnasema: ‘Imekuaje?’ Waambaie(Ewe
Muhammad): ‘Ni kutokana na Nafsi zenu kwani kwa hakika Allah ni mwenye uwezo
juu ya kila kitu.’ Ama kile kilichokufikieni katika siku yaliyokutana majeshi mawili
(katika Uhud) basi ni kutokana na matakwa ya Allah ili apate kuwajua Waumini.
Na kisha Allah Subhnaha wa Ta’ala akamalizia kwa kusema:
﴿إِنْ يمَْسَسْكُمْ قَرْحٌ فَقَدْ مَس َّ ٱلْقَوْمَ قَرْحٌ مِّثْلُهُ وَتِلْكَ ٱلأَ َّمُ نُدَاوِلهَُا بَ ينْ َ ٱلن َّاسِ
وَلِيَعْلَمَ ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ وَيَت َّخِ ذَ مِنْكُمْ شُهَدَآءَ وَٱهلل َُّ لاَ يحُِب ُّ ٱلظ َّالِمِينَ ﴾
In yamsaskum qarhun faqad massa alqawma qarhun mithluhu watilka al-ayyamu
nudawiluha bayna alnnasi waliyaAAlama Allahu alladheena amanoo
wayattakhidha minkum shuhadaa waAllahu la yuhibbu aldhdhalimeena (Surat Al
Imran 3:140)
Tafsir: kama ikiwa karaha imekuguseni (Kwa Majeruhi na Vifo) basi kueni na
uhakika kua karaha imewagusa na wengine pia. Kama inavyokua katika masiku
(mazuri na mabaya) hua tunawapa baina ya watu kwa zamu ili Allah apate kuwajaribu
wale walioamini na apate kuchukua Mashahidi miongoni mwenu na Allah si mwenye
kuwapenda Madhalimu.
Ambapo baada ya vita vya Uhud basi Khalid Ibn Walid na Abu Sufyan walikimbilia na
Farasi wao katika eneo alilokuwepo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kisha Abu
Sufyan akanadia kwa kusema: ‘Jee Yuko wapi Muhammad? Yuko wapi Abu Baqr?
Yuko wapi Umar?’
Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akajibu: ‘Sisi hapa!’ Abu Sufyan akasema:
‘Siku kwa Siku kwani Siku hua zinabadilika, na vita hua ni kama ndoo inayoingia
na kutoka kisimani.’ Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akajibu: ‘Hakika sisi
hatuko sawia kwnai Maiti wetu wako Peponi wakati wenu wako Jahannam’ Abu
Sufyan akasema: ‘Kama ni kweli hivyo msemavyo basi kwa hakika sisi ndio
tulioshindwa.’
818
Miaka miwili baadae vikatokea vita vya tatu baina ya Waislam na Makafir wa Makkah,
vita ambavyo vilijulikana kama vita vya Khandaq, baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kupewa Ushauri na Salman Al Farisi Radhi Allahu Anhu kua wachimbe
kuchimba handaki ili kuulinda wa mji wa Madinah usivamiwe na Makafiri ambao
walikau wamekuja na jeshi kubwa sana, Miongoni mwa Viongozi wa Jeshi la Makafiri
alikuwemo pia Khalid Ibn Walid alikuwemo katika jeshi la Makafiri na ingawa kulikua
na majaribio ya hapa na pale ya kuzidiana akili, lakini vita hivi havikupiganwa kwani
baada ya muda mrefu, Makafiri walishindwa kuliruka Khandaq lililochimbwa na
Waislam.
Ingawa Khalid Ibn Walid alijitahidi kwa mbinu zake zote kama kiongozi wa Jeshi la
Makafiri kutafuta sehemu ya kuanzisha Mashambulio hadi akaipata, kwani alikua ni
miongoni mwa waliomkamia sana Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam hivyo
akafanikiwa kulijua hema la Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na kisha
kuwapanga wapiganaji wake wa kurusha upinde lakini hata hivyo Waislam waliwahi
kuwaona na hivyo wakamtaarifu Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam nae
akawahi kuhama katika hema hilo kabla ya mashambulizi hayo.
Na hatimae mwishoni usiku mmoja kulitokea kimbunga cha jangwani ambacho
hakijawahi kutokea, na hivyo kambi ya Makafiri, ikavunjika baada ya mahema yao
kung’oka na kupeperuka, kamba za Ngamia na Farasi wao kukatika na baadhi ya
wanyama hao kukimbia, vyakula vyao pia viliharibika kwa kujaa mchanga wa jangwani
na hivyo bada ya muda kidogo wakaamua kurudi Makkah bila ya kupigana.
Harith Ibn Hisham, anasema katika Tabqat Ibn Sad kua: ‘Khalid Ibn Walid alisema
kua kabla ya kusilimu, ilikua kila akiingia vitani kupigana na Waislam alikua
anapata nafasi ya kumpiga upanga Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam,
lakini kila inavyotokea nafasi hiyo basi kutokana na ukubwa na utukufu wa Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, hutokea kama miale fulani ya mwangaza
inayong’ara na kuingia katika moyo wa Khalid Ibn Walid’, ambayo baadae iliotesha
mapenzi ya dini ya Uislam ndani ya moyo yake.
Kisa hiki kilitokea wakati Waislam walipokua wakitoka Madina kuelekea Makkah
kufanya Umra, walipofika katika maeneo ya Usfan ambapo ni karibu na mji wa Makkah,
walipiga kambi na hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akawa anasalisha
sala ya adh Dhuhr na wakati huo Khalid Ibn Walid akaona kua ameshapata nafasi
anayoihitaji kwa ajili ya kumuua Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam pamoja
na Waislam wengine, hivyo akakaa na majeshi yake mbele baina ya Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam na Kibla lakini hata hivyo kulikua kuna nguvu fulani ambayo
alikua akiihisi inamzuia bila ya kuiona nguvu hiyo inatokea wapi. Siku hiyo hiyo wakati
wa Sala ya Al Asr, Khalid Ibn Walid anasema akapata nafasi nyengine tena lakini
819
kilitokea kile kile kilichomzuia wakati wa Ad Dhuhr. Na hapo akajua hakuna kitu
kitakachoweza kumzuia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam katika kueneza
Dini ya Uislam.
Imam Ibn Kathir anazungumzia tukio hili pale alipozungumzia Sala ya khofu katika
Taafsir ya Surat An Nisaa kwa kusema kua:
Amesema Imam Ahmad kua amesema Abu `Ayyash Az-Zuraqi, ‘Tulikua pamoja na
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam katika maeneo ya U’sfan, na mara
wakatokea Makafir waliokua chini ya uongozi wa Khalid Ibn Walid, na
wakasimama baina yetu na Qibla, Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam
akatusalisha Salat Dhuhr na hapo Makafiri wakasema: ‘Walikua wameshughulika
na kitu fulani, tulikua na nafasi ya kuwavamia’ lakini baadae wakasema: ‘Itafuata
Sala baadae ambayo inathamani zaid kwao wao kuliko watoto wao na Nafsi zao’’.
Mara Jibril A’layhi Salaam akashuka baina ya Salat Dhuhr na Al Asr na aya isemayo:
﴿وَإِذَا كُنتَ فِيهِمْ فَأَقَمْتَ لهَُمُ ٱلص َّلاَةَ فَلْتَقُمْ طَآئِفَةٌ مِّنْهُمْ م َّعَكَ وَلْيَأْ ُخذُو ۤ اْ
أَسْلِحَتَهُمْ فَإِذَا سَجَدُواْ فَلْيَكُونُواْ مِن وَرَآئِكُمْ وَلْتَأْتِ طَآئِفَةٌ أُخْرَىٰ لمَْ يُصَل ُّواْ
فَلْيُصَل ُّواْ مَعَكَ وَلْيَأْخُذُواْ حِ ذْ رَهُمْ وَأَسْلِحَتَهُ مْ وَد َّ ٱل َّذِينَ كَ فَرُواْ لَْو تَغْفُلُونَ عَ ْن
أَسْلِحَتِكُمْ وَأَمْتِعَتِكُمْ فَيَمِيلُونَ عَلَيْكُمْ م َّيْلَةً وَاحِ دَةً وَلاَ جُنَاحَ عَلَيْكُمْ إِن كَانَ
بِكُمْ أَذًى مِّ ن م َّطَرٍ أَوْ كُ نتُمْ ۤ م َّرْضَى أَن ۤ تَضَعُو اْ أَسْ لِحَ تَكُ مْ وَخُ ذُ واْ ِحذْرَكُمْ إِن َّ ٱهلل ََّ
أَعَد َّ لِلْكَافِرِينَ عَذَاابً م ُّهِيناً
﴾
Wa-idha kunta feehim faaqamta lahumu alssalata faltaqum ta-ifatun minhum
maAAaka walya/khudhoo aslihatahum fa-idha sajadoo falyakoonoo min waraikum
walta/ti ta-ifatun okhra lam yusalloo falyusalloo maAAaka walya/khudhoo
hidhrahum waaslihatahum wadda alladhina kafaroo law taghfuloona AAan
aslihatikum waamtiAAatikum fayameeloona AAalaykum maylatan wahidatan
wala junaha AAalaykum in kana bikum adhan min matarin aw kuntum mardha an
tadaAAoo aslihatakum wakhudhoo hidhrakum inna Allaha aAAadda lilkafireena
AAadhaban muheenan. (Surat An Nisaa 4:102)
820
Tafsir: Na unapokua (Ewe Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam) pamoja nao na
ukawongoza katika Sala, basi liruhusu kundi moja lisali pamoja nawe huku wakiwa
na Silaha zao; na watakapomaliza sijda zao basi wacha wabadilishe nafasi zao na
kukaa nyuma ili kuruhusu wale waliokua hawajasali kuja mbele, na waruhusu wasali
pamoja nawe wakiwa na tahadhari huku wakibeba silaha zao. Kwani wale wasioamini
wanatamani kua nyinyi msahau silaha zenu na mizigo yenu ili wakuvamieni kwa mara
moja. Lakini hakuna dhambi juu yenu ikiwa mtaweka pembeni silaha zenu kutokana
na usumbufu wa mvua au kwa sababu ya maradhi, lakini chukueni tahadhari kwa
Nafsi zenu. Kwa hakika Allah ametayarisha adhabu ifedheheshayo sana kwa
Makafiri.
Hivyo katika pindi hiki ambacho Khalid Ibn Walid alikua akihisi hisia za nguvu za ajabu
ambazo alikua hazioni na wala hajui zilikua zikitokea wapi zilikua ni miongoni mwa
miujiza ya kushuka kwa Malaika Jibril A’layhi Salaam na aya hiyo.
Muda si mrefu kupita baada ya vita vya Khandaq, Khalid Ibn Walid alipokea barua
kutoka Madinah kwa ndugu yake ambae ni Al Walid Ibn Walid, Al Walid alikua
akimpenda sana kaka yake huyo mkubwa na alikua kila mara anamuandikia barua
kumjuulia hali na pia kujua maendeleo ya muelekeo wake katika maisha, lakini katika
barua ya safari hii, Al Walid alimuuliza kaka yake masuala tofauti kabisa. Kwani ndugu
yake alikua anataka kujua, kaka yake atakaa hadi lini katika hali aliyokua nayo ya
kuendelea kutokua Muislam kwa kusema katika barua hiyo:
‘Mara kwa mara Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam anakuulizia,
kutaka kujua uko wapi na unafanya nini? Nami humjibu Insha Allah, Allah
atakuleta kwetu karibuni, na hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
hua anasema ‘Mtu mwenye akili na ujuzi kama Khalid hawezi kukaa kwa mda
mrefu bila ya kujiunga nasi, ikiwa atatumia akili na ujuzi wake huo kwa ajili ya
Uislam, atanufaika zaid, hivyo ni lazima tumpe kipaumbele’
Usiku moja kabla ya kuamua kusilimu, Khalid Ibn Walid alilala na akaota yupo katika
sehemu ndogo iliyokiza na nyembamba inayombana na kumpa dhiki, na kwa mbali
akawa anaona mwangaza, hivyo akawa anajivuta kidogo kidogo kuelekea katika
mwangaza huo, na kila akisogea mbele zaid basi hua anapata unafuu na upana wa sehemu
hiyo huongezeka hadi alipofikia katika mwangaza huo na kujiona yuko katika sehemu
nzuri inayovutia na iliyonawiri na kujisikia raha na huru katika Nafsi yake kuliko pale
alipokua kua mwanzo.
Ingawa Khalid Ibn Walid alikua si mtu mwenye imani kubwa ya dini ya kuabudu
masanamu lakini Allah Subhanahu wa Ta’ala alimuonesha njia iliyonyooka na baada ya
821
mkataba wa Hudaybiyyah, Khalid Ibn Walid akaamua na kuona kua bora aifuate dini ya
Uislam ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam.
MAKUBALIANO YA SULHU AL HUDAYBIYYAH
Mnamo mwaka wa 6 Al Hijra ambao ni sawa na mwaka 628 C.E katika mwezi wa Dhul
Qaidah huu ni mwezi ambao n mmoja kati ya miezi mitukufu ambayo ndani yake
imekatazwa kupigana, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alilala na kisha
akaota ndoto ambayo ndani yake aliona yeye na wafuasi wake wakiwa wanaingia katika
Mji wa Makkah na kufanya Tawwaf. Hivyo akaona kua hii ni Dalili njema na hivyo bora
kwake yeye kutekeleza azimio hilo.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajaribu kuwaambia baadhi ya watu wa
Makablia ya Madina kua wasafiri nae katika msafara huo lakini hata hivyo wakakataa na
kutoa visingizio, hivyo nae akawakusanya watu wake miongoni mwa Muhajjirina na
Maansari na wengine aliowapata baada ya kukubaliana nae na kuanza safari yao hio bila
ya kuchukua silaha yeyote.
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anawazngumzia wale waliokataa kuungana nae
katika safari yake hio ambao ni watu wa Juhaynah, Banu Bakr, Muzaynah kwa kusema:
﴿سَيَقُولُ لَكَ ٱلْمُخَل َّفُونَ مِنَ ٱلأَعْرَابِ شَغَلَتْنَآ أَمْوَالُنَا وَأَهْلُوَ فَٱسْتَغْفِرْ لَنَا
يَقُولُونَ أبَِلْسِ نَتِهِمْ م َّا لَيْسَ فىِ قُلُوهبِِمْ قُلْ فَمَن يمَْلِكُ لَكُمْ مِّنَ ٱهلل َِّ َشيْئاً إِنْ أَرَا َد
بِكُمْ ضَرّاً أَوْ أَرَادَ بِكُمْ نَفْعاً بَلْ كَانَ ٱهلل َُّ بمَِا تَعْمَلُونَ خَبِيراً ﴾
Sayaqoolu laka almukhallafoona mina al-aAArabi shaghalatna amwaluna
waahloona faistaghfir lana yaqooloona bi-alsinatihim ma laysa fee quloobihim qul
faman yamliku lakum mina Allahi shay-an in arada bikum dharran aw arada
bikum nafAAan bal kana Allahu bima taAAmaloona khabeeran (Surat Al Fat-h
48:11)
Tafsir: Watasema kukuambia wale miongoni mwa Mabedui waliobakia kua: ‘Mali
zetu na familia zetu zimetuzuia, hivyo tuombee Msamaha juu yatu’ wanasema kwa
Ndimi zao kile ambacho hakimo ndani ya Nyoyo zao, hivyo waambie: ‘Hivi jee ni nani
atakaekua na uwezo wa kuingilia kati juu yenu dhidi ya Allah, kama akiamua
kukudhuruni na kukunufaisheni?’ La bali Allah ni mwenye kujua juu ya kila
mnachokifanya.
822
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam Waislam 1400 wakavaa Ihram katika Mji
wa Madina na kufuga safari kuelekea katika Mji wa Makkah huku wakiwa na Ngamia
70 na Kondoo kadhaa waliowatia alama inayoonesha kua ni kwa ajili ya kuchinja,
ambapo ilikua ni kawaida kwa watu wa Quraysh kua ni wenye kuruhusu Mahujaji
kuingia katika Mji wa Makkah kufanya Umra lakini bila ya kubeba Silaha.
Lakini kutokana na wingi wa Mahujaji hao wa Kiislam pamoja na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kutoka katika mji wa Madina basi watu wa Quraysh, wakaingiwa na
khofu na kuamua kutowaruhusu kuingia katika mji wa Makkah, baada ya kumtuma
Khalid Ibn Walid na jeshi la watu 200, kwa ajili ya kuwazuia Waislam hao wasiingie
katika Mji wa Makkah kwa kuwasubiri katika maeneo ya Kurah Al Ghamim.
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipopata habari hio ya kukutana na
makabaliano ya jeshi la Khalid Ibn Walid basi akaamua kushauriana na Masahaba zake
kua kama wapigane na Jeshi la Khalid Ibn Walid ama la? Lakini Abu Baqr Radhi Allah
Anhu akashauri kwa kusema kua: ‘Hakika sisi tulitia nia kufanya Ibada ya Umra na
hatukutia nia ya kupigana kwa hivyo, wacha tuenedelee na safari haina haja ya
kupigana hadi pale tutakapokatzwa kuinga ndani ya Mji wa Makkah.’
Na hivyo Waislam wakakubaliana kubadilisha njia ya msafara wao huo ili kuepuka
mapigano ya aina yeyote baina yao hivyo badala ya kutumia njia ya kawaida ya kupitia
katika maeneo ya Taniim basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaamua kukupitia
njia isiyotumika sana ambayo ni njia ya kupitia katika maeneno ya Hudaybiyyah na hivyo
kutaka kua ni mwenye kuingia katika Mji wa Makkah katika upande wa Magharibi wa
Mji huo.
Hivyo Khalid Ibn Walid alipopata habari hio basi akaamua kurudi katika mji wa Makkah
na Jeshi lake, huku Watu wa Quraysh wakaamua kutuma ujumbe wao kwa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kwa ajili ya kupanga majadiliano ya makubaliano baina yao,
kabla ya kuingia kwenye Mji wa Makkah, kwenye maeneo ya Hudaybiyyah kwa
kumtuma Urwa Ibn Masud ambae alikua ni mtaalamu mkubwa sana wa Majadiliano ya
kimataifa miongoni mwa Waarabu.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na watu wake walipofika kwenye maeneo hayo
ya Hudaybiyyah akakuta kua visima vya maji vya maeneo hayo vina maji kidogo sana
kiasi ya kua hayatoshelezi kuwanyweseha maji wao na Wanyama wao, hivyo akachukua
upinde wake na kisha akawaambia Masahaba zake wauchomeke kwenye moja kati ya
visima hivyo.
Hivyo Khirash Ibn Ummayah Radhi Allahu Anhu akauchukua Upande huo na kushuka
nao ndani ya moja kati ya Visima hivyo huku Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
823
akiwa ni mwenye kusoma dua na Khirash Ibn Ummayah Radhi Allahu Anhu akiwa ni
mwenye kuuchomeka Upinde huo kisimani humo na hapo hapo maji yakaanza
kumiminika kwa kufoka kutoka kwenye ukuta wa Kisima hicho ambayo yalijaza kila
kisima na hivyo Waislam wakawa na Maji ya kutosha kabisa kwa ajili yao na Wanyama
wao.
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Watu wa Quraysh wana
bahati mbaya sana, kwani Vita vimewaangamiza wakati kama wangeniachia mimi
bila ya kuniiingilia katika kuwausia watu na watu wakaingia kwenye Uislam basi
wangekua ni wenye kunufaika, kwani kama watu wangenipinga na kunikataa basi
nao wangeweza kupigana nami kutokana na hali yao kinguvu katika kila jambo,
wanafikiria nini hawa watu wa Quraysh? Wa Allahi mimi nitapingana nao kwa ajili
ya Allah hadi nitakapopata Ushindi au nitakapofariki kwa ajili yake’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaamua kumtuma Umar Ibn Al Khattab
Radhi Allahu Anhu kwa ajili ya kuzungumza na watu wa Quraysh, lakini hata hivyo
Umar Ibn Al Khattab akawa na khofu kwani alikua hana mtu wa kumlinda kutokana na
nasaba ya kiukoo, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamteua Uthman Ibn
Affan Radhi Allahu Anhu ambae alikua na nasaba yeye nguvu kikabila miongoni mwa
watu wa Makkah.
Hivyo Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu akaelekea katika mji wa Makkah na akawa
ni mwenye kufikisha ujumbe wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Waislam
kwa ujumla kua wamekuja kwa ajili ya kufanya Ibada ya Umra. Hivyo watu hao wa
Quraysh wakamruhusu Uthmna Ibn Affan Radhi Allahu Anhu kua yeye afanye ibada hio
kama anataka hata hivyo akakataa na kusema kua hawezi kufanya Ibada hio kabla ya
kufanya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Ambapo jibu hilo la Uthman Ibn Affan
Radhi Allahu Anhu liliwakasirisha sana watu wa Quraysh na wakaamua kumkamata
Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu na kumfunga na hivyo kutokua na njia ya
kurudisha majibu kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam juu ya kile kilichotokea
katika mji wa Makkah.
Tukio hili la kukamatwa na kuzuiwa kwa Uthman Ibn Affan liliwatia wasiwasi Waislam
na hasira kwani walikua hawajui kimemfika kitu gani Uthman Ibn Affan Radhi Allahu
Anhu na hivyo Waislam wakawa wako tayari kupigana kwa ajili kumuokoa Uthman Ibn
Affan Radhi Allahu Anhu kama yuko hai, au kulipiza kisasi kama itakua ameuliwa mbali
ya kua tukio hili lilitokea ndani ya mwezi Mtukufu wa Dhul Qaidah ulioharamishwa
kupigana ndani yake.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akanyoosha mkono wake wa kulia na
kuuweka juu ya mkono wake wa kushoto hukua akisema: ‘Haya ni makubaliano ya
824
Uthman’ na baada ya hapo Masahaba wakaweka mikono yao juu ya Mkono wa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kukubaliana juu ya makubaliano hayo ambayo
Masahaba wote walikubaliana nayo isipokua mmoja tu miongoni mwao ambae alikua ni
Jadd Ibn Qays aliekua ni Mnafiq aliejificha nyuma ya Ngamia katika wakati wa
makubaliano hayo.
Ambapo Allah Subhnah wa Ta’ala anayazungumzia Makubaliano haya ambayo yalikua
yanajulikana pia kua kama Makubaliano ya Walioridhwa na Allah Subhnah wa Ta’ala
Bay’iA Ridhwan kwa kusema:
﴿ل َّقَدْ رَضِىَ ٱهلل َُّ عَنِ ٱلْمُؤْمِنِينَ إِذْ يُبَايِعُونَكَ تحَْتَ ٱلش َّجَرَةِ فَعَلِمَ مَا فىِ قُلُو هبِِمْ
فَأنزَلَ ٱلس َّكِينَةَ عَلَيْهِمْ وَأَاثَبَهُمْ فَتْحاً قَرِيباً ﴾
Laqad radhiya Allahu AAani almu/mineena idh yubayiAAoonaka tahta
alshshajarati faAAalima ma fee quloobihim faanzala alsakeenata AAalayhim
waathabahum fat-han qareeban(Surat Al Fat-h 48:18)
Tafsir: Hakika ameridhia Allah juu ya Waumini walipokubaliana nawe (Muhammad
Salallahu Alayhi wa Salam) chini ya Mti, kwani yeye ni mwenye kujua kile kilichomo
ndani ya Nyoyo zao na amewashushia Utulivu juu yao na kuwazawadia wao kwa
ushindi unaokuja karibuni.
Ambapo alisema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Wale waliokubaliana
kwa kutoa Mikono yao katika siku ya Hudayybiyah basi hawatoingia Motoni hata
mmoja’(Imam At Tirmidhi)
Baada ya tukio hilo basi watu wa Quraysh wakatuma Mjumbe kwa Waislam kwa ajili ya
mazungumzo na wakamchagua Urwa Ibn Masud Al Thaqafi ambae alipofika mbele ya
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi akamlaumu kwanza Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwa kusababisha maangamizo kwa watu wake wa Quraysh, na kusema
kua hakuwa ni mwenye kuona watu anaowaamini miongoni mwa Masahaba, kwani
anaona kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kazungukwa na watu ambao ni woga
na watamkimbia katika wakati wowote watakapotishwa.
Masahaba waliposikia maneno haya basi walijawa na hasira lakini wakajizuia, hadi pale
Urwa aliponyoosha mkono wake na kutaka kuzigusa Ndevu za Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam, ambapo ghafla moja alishutukia mkono wake huko ukipigwa na mpini
wa upanga wa Mughiran Ibn Shubah Radhi Allahu Anhu ambae alikua akionya kwa sauti
yenye hasira isemayo: ‘Kaa mbali na Ndevu za Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam’
825
Hivyo Urwa Ibn Masud baada ya kuzungumza na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
ambae alisema kua wao hawataki chochote isipokua kufanya Ibada ya Umra na kuondoka
bila ya mapigano, lakini kama watu wa Quraysh wanataka kupigana na Waislam basi
yeye yuko yuko tayari pia kwa ajili ya mapigano hivyo Urwa Ibn Masud akaondoka huku
akiwa na hali ya kua ni mwenye kuvutiwa sana na heshima, mapenzi na utiifu wa
Waislam kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kuwaambia watu wa Quraysh
kua: ‘Hakika mimi nimetembelea Kumbi za Wafalme wa Uajemi, Warumi na
Wahabeshi lakini kamwe sikuwahi kuona mfano wa heshima na namna
anavyochukuliwa kiongozi na watu wake kama wafuasi wa Muhammad
wanavyomchukulia Muhammad, wamekuja kwa ajili ya kufanya Ibada hivyo
waacheni tu waingie’ lakini hata hivyo watu hao wa Quraysh waligoma katakata.
Baada ya Urwa Ibn Masud kufikisha ujumbe huo kwa watu wa Quraysh wakamchagua
Hulays ambae alikua ni kiongozi wa Kabila la watu waliokua nje ya Mji wa Makkah
lakini walikua wakishirikiana na watu wa Quraysh katika mambo mbali mbali na Hulays
alipokaribia katika eneo la Hudaybiyah na kuona Wanyama waliotiwa alama maalum
inayoonesha kua ni kwa ajili ya kuchinjwa, basi akarudi katika Mji wa Makkah basi
akawaambia Watu wa Quraysh kua: ‘Haina haja ya kujadiliana au kupigana na mtu
ambae amekuja kwa ajilia ya kufanya Ibada ya Umra’
Lakini hata hivyo watu wa Quraysha wakamwita Hulays kua ni mwoga, ambapo nae
akawaambia watu wa Quraysh kua: ‘Kama mkiamua kupigana nao basi mimi
sitoingiza Jeshi la watu wangu kwa ajili ya kupigana nao pamoja nanyi’ Hivyo watu
wa Kabila la Quraysh wakamuomba msamaha Hulays.
Kisha baadae watu wa Quraysh wakamwachia Uthman Ibn Affan Radi Allahu Anhu huku
wakiwa ni wenye kumtuma pamoja nae Suhayl Ibn Amr Al Thaqafi ambae alikua mahiri
zaid ya Amr Ibn Al Aas na Urwa Ibn Masud katika kujadiliana, hivyo walimchamgua
makusudi kwa ajili ya kujadiliana makubaliano hayo pamoja na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam ambapo baada ya mda wa majadaliano yake na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam basi wakaubaliana katika makubaliano yanayojulikana kama
makubaliano ya Sulh Al Hudaybiyah ambayo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
aliyasema huku akimuamrisha Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu aandike yale
ayasemayo ambayo ni:
‘Bismi Allahi AlrRahmani AlrRahim’
Ambapo Suhayl Ibn Amr Al Thaqafi akapingana na kauli hio kwa kusema: ‘Hakika
mimi simjui huyu Al Rahman ndio Nani, hivyo Bismi Allahi tu inatosha’
826
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaendelea kusema: ‘Kutoka kwa
Muhamamd Rasul Allah’ ambapo Suhayl nae akatabasam kisha akasema: ‘Kama wewe
ni Rasul Allah basi bila ya shaka itakua sisi tumekukosea wewe, hivyo andika jina
Muhammad peke yake.’ Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamwambia
Ali Ibn Ali Talib Radhi Allahu Anhu ayafute maneno yasemayo Rasul Allah, lakini hata
hivyo Ali Ibn Abi Talib akagoma, na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akafuta
maneno hayo yeye mwenyewe kisha akaendelea kusema:
Bismi Allahi’
‘Haya ni makubaliano ya Sulhu baina ya Muhammad Ibn Abdullah na Suhayl Ibn
Amr ambae ni Mjumbe kutoka katika Mji wa Makkah.
1-Kutakua na kuweka silaha chini na kutosababishiana madhara baina ya pande
mbili na hakutokua na vita kwa mda wa miaka 10 inayofuata’
2-Mtu yeyote yule au Kabila lolote lile litakalotaka kujiunga na Muhammad au
kuingia katika makubaliano nae basi atakua huru kufanya hivyo, na vile vile mtu
yeyote au kabila lolote litakalotaka kujiunga na watu wa Quraysh au kushirikiana
nao basi wako huru pia kufanya hivyo.
3-Kama ikitokea kua Mtu yeyote yule wa Makkah ataebda katika Mji wa Madina
basi Waislam watamrudisha mtu huyo katika Mji wa Makkah, lakini kama
Muislam kutoka katika Mji wa Madina ataenda katika Mji wa Makkah basi
hatorudishwa.
4-Kama kijana yeyote yule ambae Baba yake yuko hai, akatoka na kuenda kwa
Muhammad bila ya idhini ya Baba yake au Msimamizi wake, basi Kijana huyo
atarudishwa kwa Baba yake au Msimamizi wake, lakini kijana yeyote atakaenda
kwa watu wa Quraysh wa Makkah basi hatorudishwa.
5-Katika mwaka huu Waislam watarudi katika mji wa Madina bila y akuingia
kwenye mji wa Makkah, lakini katika mwaka utakofuatia basi Muhamamd na
wafuasi wake wataingia katika Mji wa Makkah na kutumia sikua 3 kwa ajili ya
kufanya Ibada ya Umra.
Naam hayo ndio makubaliano ya Sulhu Al Hudaybiyah ambayo ingawa kwa upande
mmoja yanaoneana kua kama ni yenye kupendelea kusimamia maslahi ya upande wa
watu wa Quraysh zaidi kuliko maslahi ya Waislam na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kua ni mwenye kuonesha Subra na Ustahmilivu katika kukubaliana na namna
ilivyotakiwa iwe na Suhayl Ibn Amr kiasi ya kua Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu
827
Anhu alikua ni miongoni mwa wasiovutiwa na kutoridhika na Makubaliano hayo hivyo
akamfuata Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kumwambia: ‘Ya Rasul Allah!
Hivi jee wewe si Rasul Allah wa Haki?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu : ‘Naam, bila ya shaka mimi ni Rasul
Allah wa Haki’ Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Hivi jee sisi hatuko
katika njia Sahih na Makafiri wako kwenye njia ya Batil?’ Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akajibu : ‘Naam.’
Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Sasa kama ni hivyo Jee ni kwanini
sisi inatubidi tukubaliane na makubaliano ambayo yanapingana na Imani yetu?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu : ‘Hakika mimi ni Rasul Allah, na
hivyo siwezi kuenda kinyume na maamrisho yake kwani yeye ndie nnaemtegemea
na ndie anaenisaidia’
Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Hivi jee hukuambia sisi kua tunakuja
kwa ajili ya kufanya Ibada ya Umra?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu :
‘Naam, ndio lakini hivi jee mimi nilisema kua tutaifanya Ibada hio ndani ya mwaka
huu?’
Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Bila ya shaka hukusema hivyo’ hivo
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu : ‘Basi bila ya shaka mtakuja tena na
kufanya Ibada ya Umra’ ambapo jibu hili pia halikumfurahisha Umar Ibn Al Khattab
Radhi Allahu Anhu na hivyo akaelekea kwa Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu na
kumwambia kuhusiana na mahojiano yake na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
ambapo Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu akajibu: ‘Hakika yeye ni Rasul Allah,
hivyo hawezi kumuasi Mola wake’ ambapo miaka baadae Umar Ibn Al Khattab Radhi
Allahu Anhu akaona manufaa yaliyomo ndani ya Makubaliano hayo kwa Waislam, na
hivyo akafunga, akatoa sadaka na kuachia Watumwa huru kwa ajili ya kujuta na kuomba
msahama kwa Allah Subhaah wa Ta’ala kutokana na mmajadiliano yake haya dhidi ya
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Lakini kwa upande mwengine makubaliano haya yalikua ni yenye manufaa makubwa
zaidi kwa Waislam kuliko vile walivyokua wakifikiria Waislam wenyewe.
Kwani kwanza Makubaliano haya yalikua yanabainisha wazi kukubalika kwa
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam kua ndio Kiongozi wa watu wa Madina na
Taifa jipya la Kiislam kwa Ujumla mbele ya watu wa Quraysh ambao walikua
hawataki kumkubali Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutokana na chuki zao
juu yake.
828
Pili Makubaliano haya pia yalikua ni yenye kuhakikisha na kusimamia usalama wa
Waislam kutokana na madhara ya watu wa Quraysh.
Tatu Makubaliano haya yalikua yanawapa fursa Waislam kuungana na Makabila
mengineyo bila ya kua na uadui baina yao na watu wa Quraysh.
Nne Makubaliano haya yalikua yanawaahidi Waislam miaka 10 ya usalama na
kutosababishiana madhara kutoka kwa maadui zao wakubwa yaani watu wa
Quraysh na hivyo kufungua njia mpya ya kueneza ujumbe wa Kiislam katika
maeneo mbali mbali ya Uarabuni bila ya kubughudhiwa na kupata upinzani kutoka
kwa watu wa Quraysh.
Ambapo baada ya Suhayl Ibn Amr Ath Thaqafi kupitia upya makubaliano hayo na kisha
kutia saini, basi na kwa upande wa Waislam nao wakatia saini kwa kuanza na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam, Abu Bakr Radhi Allahu Anhu, `Umar Radhi Allahu Anhu, `Abd
Al Rahman Ibn `Awf Radhi Allahu Anhu,`Abdullah Ibn Suhayl Radhi Allahu Anhu, Sa`d Ibn
Abi Waqqas Radhi Allahu Anhu na muandishi mwenyewe Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu
Anhu.
Na baada ya kuwekwa saini hizo basi hapo hapo akatokea kijana Muislam ambae alikua
amefungwa minyororo na kuonekana kua kama ametoroka hivyo alikua akiomba msaada
kwa Waislam afunguliwe, na Suhayl Ibn Amr alipomuangalia kijana huyo basi akamuona
kua ni mtoto wake mwenyewe aitwae Abu Jandal Radhi Allahu Anhu, ambae alikua
amemfungia nyumbani kwake hivyo hapo hapo Suhayl Ibn Amr akasema: ‘Katika huu
Mkataba kuna kipengele nambari 4, na kulingana nacho basi kinasema kua
mumrudishe huyu mtoto kwangu mie’
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kwa kumliwaza Abu Jandal
Radhi Allahu Anhu kua : ‘Nasikitika kua ndio kwanza tumemaliza kukubaliana
makubaliano baina yetu na watu wa Quraysh, na hivyo ni wajibu wetu
kuyaheshimu makubaliano haya, hivyo kua na Subra kwa kukubaliana na
Majaaliwa ya Allah Subhana wa Ta’ala, atakujaaalia njia ya kutokea kwa wepesi’
Hivyo Abu Jandal akakabidhiwa kwa Baba yake, na baadae akatoroka tena kutoka katika
Mji wa Makkah na kukimbilia mafichoni katika maeneo ya mwambao wa Bahari
Nyekundu, ambako walikimbilia wengi miongoni mwa Waislam, na wakawa
wanaivamia Misafara ya watu wa Quraysh ipitayo katika meneo hayo, hivyo baadae watu
wa Quraysh wakaomba kua kipengele hicho kifutwe ili Waislam hao wasiihatarishe
misafara ya Quraysh na hivyo bora wakaishi katika mji wa Madina. Na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akamuandikia barua kiongozi wa Waislam hao katika
maeneno hayo aitwae Abu Basir Radhi Allahu Anhu.
829
Ambae nae pia alikua ni miongoni mwa waliokimbilia katika Mji wa Madina baada ya
kutoroka katika Mji wa Makkah, na alipofika katika Mji wa Madina basi wakatokea
Makafiri wawili ambao wakaomba kua arudishwe kwao kama ilivyokua katika
makubaliano ya Mkataba wa Hudaybiyyah, hivyo Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa
Salam akamkabidhi Abu Basir Radhi Allahu Anhu kwa Makafiri hao, na walipoondoka
basi njiani Abu Basir Radhi Allahu Anhu akapigana nao Makafiri hao na akamuua mmoja
wao na mwengine akakimbia.
Hivyo Abu Basir Radhi Allahu Anhu akarudi tena katika Mji wa Madina kwa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na kumwambia: ‘Ya Rasul Allah bila ya shaka umetekeleza
kipengele cha Makubalaino ya mkataba wa Hudaybiyyah kwa upande wako na
kunirudisha mimi kwa watu wa Makkah, lakini kwa upande wangu mie basi Allah
Subhanah wa Ta’ala amenipatia uhuru wangu.’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ole wake mama yake Abu
Musar, hata kama angekua na mtu mwengine pamoja nae’, haya yalikua ni maneno
yanayomaanihsa kua hata kama Abu Basir Radhi Allahu Anhu angekua na mtu mwegine
wa pili alietoroka pamoja nae basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam asingevunja
makubaliano ya Mkataba huo, kwani angewarudisha tu kwa watu wa Makkah.
Hivyo Abu Basir Radhi Allahu Anhu akafaham maana ya maneno hayo na hapo hapo
akaona bora aondoke kutoka kwenye Mji wa Madina na kukimbilia kwenye mwambao
wa Bahari nyekundu ambako alikaa na kuwaongoza Waislam wengine vijana wenzake
hadi pale alipopata barua ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua wanaruhusika
kurudi katika Mji wa Madina ambayo aliifurahia mbali ya kua alikua taabani anaumwa
na kukaribia kifo chake, na akafariki Dunia, hivyo Abu Jandal Radhi Allahu Anhu na
Masahaba wengine 70 wakahama katika maeneo hayo na kuelekea katika Mji wa Madina
na kuungana na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae alipopata habari ya kifo
cha Abu Basir Radhi Allahu Anhu basi akamsalia na kumuombea dua.
Baada ya Makubaliano haya ya Hudaybiyyah basi Waislam walikua wamevunjika Moyo
kutokana na makubaliano hayo na yaliyotokea kwa Abu Jandal Radhi Allahu Anhu na
kutoruhusiwa kufanya Ibada ya Umrah kwa mwaka huo kiasi ya kua baada ya Rasul
Allah Salallahu A’layhi wa Salam kusaini Mkataba wa Hudaybiyyah, alisema kuwaambia
Masahaba zake ‘Nyanyukeni, mchinje wanyama wenu na kisha mnyoe nywele zenu’,
lakini hakuna hata Sahaba mmoja alienyanyua mguu wake kufanya vile alivyoamrisha
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam, kutokana na kuvunjika moyo kwa yale
yaliyotokea katika makubaliano ya mkataba huo.
Hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akanyanyuka na kuenda kwa
Ummu Salama Radhi Allahu Anha na kumwambia yaliyotokea na hapo Ummu
830
Salama Radhi Allahu Anha akamwambia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam ‘Ya Rasul Allah, unataka maneno yako yafanyiwe kazi? Basi nenda nje na
usizungumze na mtu yeyote hadi pale utakapomaliza kuchinja mnyama wako na
kunyoa nywele zako’, hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akatoka
nje akachinja mnyama wake na kuanza kunyoa nywele zake, na baada ya
Masahaba kumuona Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam anafanya hivyo
basi na wao wakanyanyuka na kufanya kama vile alivyokua akifanya. (Imam
Bukhari)
Hivyo baada ya makubaliano hayo ya Hudaybiyyah basi Waislam walikaa katika eneo
hilo la Hudaybiyyah kwa mda wa siku 10 na kisha wakaanza safari yao kurudi katika Mji
wa Madina na walipofika kwenye maeneo ya Usfan wakaishiwa na vyakula vyao, hivyo
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaamrisha kua Vyakula vyao Waislam vyote
vikusanywe pamoja na kisha vilipokusanywa basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akaviombea Dua vyakula hivyo kidogo vilivyobakia na kisha akaamrisha kua
Waislam wale vyakula hivyo na walipokua kila mtu akala hadi akashiba na chakula
chengine kikabakia na kutosheleza kwa ajili ya kumalizia safari yao.
Kisha wakalala katika eneo hilo na asubuhi yake msafara ukaendelea na safari yake, na
ni katika wakati huu ndio Allah Subhnah wa Ta’ala akashusha aya za Surat Al Fat-h
zisemazo:
﴿بِ سْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ ۞ إِ َّ فَتَحْنَا لَكَ فَتْحاً م ُّبِيناً۞ لِّ يَغْفِرَ لَكَ ٱهلل َُّ مَا
تَقَد َّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا أتََخ َّرَ وَيُتِم َّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَيَهْدِيَكَ صِرَاطاً م ُّ سْتَقِيماً ۞
وَيَنصُرَكَ ٱهلل َُّ نَصْراً عَزِيزاً ﴾
Bismi Allahi Alrrahmani Alrrahim; Inna fatahna laka fat-han mubeenan;
Liyaghfira laka Allahu ma taqaddama min dhanbika wama taakhkhara
wayutimma niAAmatahu AAalayka wayahdiyaka siratan mustaqeeman;
Wayansuraka Allahu nasran AAazeezan (Surat Al Fat-h 48:1-4)
Tafsir: Kwa Jina la Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma: Hakika tumekupa
wewe (Muhamamd Salallahu Alayhi wa Salam) Ushindi uliowazi. Atakusamehe juu
yako Allah yaliyotangulia katika Madhambi yako na Yatakayokuja Na
amemkukamilishia Neema zake juu yako na kukuongoza wewe kwenye njia
iliyonyooka; Na atakunusuru Allah kwa nusura iliyotukufu.
831
Ambapo baada ya kushushwa kwa aya hii basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasema: ‘Kuna aya nimeshushiwa ambayo ni yenye thamani kubwa kwangu kuliko
Dunia na kila kitu kilichomo ndani yake’ na kisha akaisoma aya hii ya kwanza ya
Surat Al Fat-h.
Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu akauliza: ‘Hivi jee ni ushindi gani?’ ambapo
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam: ‘Naam, Wa Allahi Ni ushindi mkubwa sana’
hivyo hapa ndio Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu ndio akaridhika Nafsi yake.
Na mmoja kati ya Masahaba akasema: ‘Nakuombea Ya Rasul Allah kuwe na manufaa
nawe, kwani Allah amezungumzia kuhusiana nawe, lakini jee amesemaje kuhusiana
nasi?’ hivyo Allah Subhanah wa Ta’ala akashusha aya zisemayo:
﴿هُوَ ٱل َّذِي ۤ أَنزَلَ ٱلس َّكِينَةَ فىِ قُلُوبِ ٱلْمُؤْمِنِينَ لِيَزْدَادُو ۤ اْ إِيمَ اً م َّعَ إِيمَاِِمْ وَ هللِ َِّ جُنُودُ
ٱلس َّمَاوَاتِ وَٱلأَرْضِ وَكَانَ ٱهلل َُّ عَلِيماً حَكِيماً ۞ لِّيُدْخِ لَ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُ ؤْمِنَاتِ
جَن َّاتٍ تجَْرِى مِن تحَْتِهَا ٱلأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاهتِِمْ وَكَانَ ذٰ لِكَ
عِندَ ٱهلل َِّ فَوْزاً عَظِيماً ﴾
Huwa alladhee anzala alssakeenata fee quloobi almu/mineena liyazdadoo eemanan
maAAa eemanihim walillahi junoodu alssamawati waal-ardhi wakana Allahu
AAaleeman hakeeman; Liyudkhila almu/mineena waalmu/minati jannatin tajree
min tahtiha al-anharu khalideena feeha wayukaffira AAanhum sayyi-atihim
wakana dhalika AAinda Allahi fawzan AAadheeman(Surat Al Fat-h 48:5-6)
Tafsir:Yeye (Allah Subhanah wa Ta’ala) ndie ambae ni mwenye kushusha utulivu
ndani ya Nyoyo za Waumini kuwazidishia Imani kutokana na Imani waliyokua nayo,
na kwake yeye Allah ndiko kwenye Majeshi ya Mbiguni na Ardhini na kwa hakika
Allah ni mwenye kujua juu ya kila kitu na ni mwingi wa Hikma. Atawaingiza Waumini
wa Kiume na Waumini wa Kike Peponi ambako chini yake kuna Mito watakamoishi
ndani yake milele na kuwasamehe juu yao Dhambi zao na kwa hilo mbele ya Allah
kuna malipo Makubwa.
Ambao Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu alikua akipenda kusema kuwaambia
Masahaba wenzake kua: ‘Nyinyi Mlikua mkifikiria kua Fat-han Mubina ni Ushindi
wa ufunguzi wa Mji wa Makkah, ambao ndio bila ya shaka ulikua ni ushindi lakini
sisi tulikua tukihesabu Sulhu Hudaybiyyah kua ndio Ushindi’
832
Tunapoangalia kwa upande mwengine basi tunaona kua Makubaliano ya Hudaybiyyah
basi tunaona kua ni Ushindi Mkubwa sana kwa sababu ilikua baada ya Makubalaino haya
ndio wakasilimua wengi miongoni mwa watu wakubwa wa Mji wa Makkah akiwemo Al
Abbas Ibn Abdul Muttalib Radhi Allahu Anhu, Abu Sufyan Radhi Allahu Anhu, Amr Ibn
Al Aas Radhi Allahu Anhu,Ikrimah Ibn Abi Jahal Radhi Allahu Anhu, Utba Ibn Abi
Lahab Radhi Allahu Anhu, Safwan Ibn Umayyah Radhi Allahu Anhu, Kaab Ibn Zuhayr
Radhi Allahu Anhu, Suhayl Ibn Amr Radhi Allahu Anhu, Hakim Ibn Hizam Radhi Allahu
Anhu, Wahshi Radhi Allahu Anhu, Uthman Ibn Talha Radhi Allahu Anhu. Hind Bint
Rabia Radhi Allahu Anha, Sayfu Allah Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu n.k
KUSILIMU KWA KHALID IBN WALID.
Anasema kabla ya kusilimu kwake kua: ‘Wakati Allah Subhanahu wa Ta’ala
aliponitakia mema kwangu mie, alinivisha mapenzi ya dini ya Kiislam ndani ya
moyo wangu. Akilini ikanijia nami nikasema: ‘Nimeshuhudia mapigano yote dhidi
ya Muhammad, na katika kila mapigano niliyoyashuhudia, nilijishuhudia
kuondoka kwenye mapigano hayo huku nikiamini kua nipo katika upande sio wa
mapigano na hakika Muhammad atakua ni miongoni mwa wenye ushindi’.
Hivyo akaamua kuwafuata marafiki zake ambao waliokua bado hawajasilimu akiwemo
Ikrimah Ibn Abi Hisham na kuwaambia: ‘Ni jambo lililo dhahir kua kutokana Bani
Adam mwenye ufahamu mzuri kujua kua Muhammad si mtunga mashairi wala si
mchawi, kama wanavyosema Maquraish, kweli ujumbe wake unatoka kwa Allah,
hivyo ni lazima kwa kila mtu mwenye akili timamu kumfuata’.
Ikrimah Ibn Abi Hisham alishangazwa na kauli hiyo na kumuuliza Khalid Ibn Walid ‘Ina
maana unaachana na imani yetu?’
Khalid Ibn Walid akajibu ‘Naam, nimeshaanza kumuamini Mungu wa kweli’
Ikrimah Ibn Abi Hisham akasema ‘Inashangaza kuona kua katika Maquraish wote
waliopo, kua wewe uwe ndie wa kusema hivyo’
Khalid Ibn Walid akauliza ‘Kwa nini?’
Ikrimah Ibn Abi Hisham akajibu: ‘Kwa sababu kuna jamaa zako wengi wapendwa
waliouliwa vitani na Waislam, kuliko jamaa wa Quraysh yeyote yule miongoni
mwetu, mimi kwa hakika sitozungumza nawe wala sitoikubali dini ya Muhammad
hadi pale utakapoyakana mawazo yako hayo, huoni kua Maquraysh wanaitaka
damu ya Muhammad?’
Khalid Ibn Walid akajibu, ‘Wanaitaka damu hiyo kwa sababu inayotokana na ujinga
wao wa kutofahamu’.
833
Abu Sufyan ambae alikua ndie kiongozi wa Quraysh wakati huo aliposikia kua Khalid
Ibn Walid anataka kusilimu, akawaita wote Ikrimah Ibn Abi Hisham na Khalid Ibn
Walid, kisha akamuuliza Khalid Ibn Walid, ‘Jee ni kweli yale ninayoyasikia?’
Khalid Ibn Walid akamuuliza ‘Na umesikia nini?’
Abu Sufyan akajibu ‘Nimesikia kua unataka kujiunga na Muhammad’
Khalid Ibn Walid akajibu ‘Na kwa nini nisijiunge nae wakati yeye Muhammad ni
ndugu yetu na ametoka katika ukoo wetu?’
Abu Sufyan akakasirika na kutaka kumtishia Khalid Ibn Walid, lakini Ikrimah Ibn Abi
Hisham akaingilia kati na kusema ‘Pole pole, Ya Abu Sufyan, kwani hasira zako
zitanifanya na mimi nimfuate Muhammad, Khalid yuko huru kufuata dini
anayoitaka.’
Ikrimah Ibn Abi Hisham ambae ni binamu wa Khalid Ibn Walid na pia rafiki yake kipenzi
alisimama na kumtetea ndugu yake, ingawa walikua wana utofauti wa iman, hivyo Khalid
Ibn Walid akaondoka na kumuacha rafiki yake huyo na kuanza safari ya Madinah ,
kuingia katika Uislam na pia kua pamoja na ndugu yake, Al Walid na vile vile kua pamoja
na binamu yake, rafiki na mpinzani wake pia ambae ni Umar Ibn Al Khattab Radhi
Allahu Anhu, lakini safari hii mpinzani wake huyo alikua yuko juu zaid na katika sehemu
bora zaid kwani Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu alikua ni Muislam wa arubaini
kusilimu, wakati Khalid Ibn Walid alisilimu baada ya mamia ya Makafir kusilimu.
Tarehe 31-5-629, Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu akiwa na umri wa miaka 43
aliwasili katika mji Madinah akiwa pamoja na Amr Ibn Al Aas Radhi Allahu Anhu na
Uthman Ibn Talha Radhi Allahu Anhu.ambao alikutana nao njiani wote wakielekea
Madinah wakiwa na nia ya kuingia katika Uislamu. Walipofika Madina kwa Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, Khalid Ibn Walid akawa wa kwanza kati yao
kuingia katika nyumba ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na kusilimu
akifuatiwa na Amr Ibn Al Aas Radhi Allahu A’nhu na Uthman Ibn Talha Radhi Allahu
A’nhu.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alipowaona tu na kusikia kua wamekuja
kusilimu akawaambia Masahaba zake ‘Makkah imekurushieni vipande vya Moyo
wake’, hii ni kuonesha thamani aliyokua nayo Khalid Ibn Walid pamoja na wenzake
wawili hao. Baada ya kuingia ndani Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
akamwambia Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu huku akitabasamu ‘Nilikua na
uhakika kua kutokana na ufahamu wako, ujuzi wako na uwezo wako wa kuona
mbali, kua iko siku utakuja kujiunga pamoja nami’. Baada ya kutoa shahada, Khalid
Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu alimwambia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam ‘Ya Rasul Allah, niombee msamaha kwa Allah kwani mimi nimewauwa
Waislamu wengi sana kabla ya kua Muislam’.
834
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamjibu kwa kumwambia ‘Unapoingia
katika Uislam basi dhambi zako zote ulizozifanya wakati wa Ujahiliyah hua
zimefutika’, ingawa kauli hiyo inatoka kwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam na hivyo usahihi wake huweza kumsadikisha mtu yeyote yule lakini hata hivyo
Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu hakuamini kua dhambi zake kubwa alizozifanya
zilikua zimefutika, hivyo akamshikilia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na
kumuomba mara tatu kua amuombee msamaha kwa Allah Subhanah wa Ta’ala,
mwishoni Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamuombea, na hapo ndipo
moyo wa Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu ukapata utulivu.
Anasema Amr Ibn Al Aas Radhi Allahu A’nhu : ‘Rasul Allah Salallahu A’layhi wa
Salam hakuwa akiwachukulia Masahaba zake kama vile alivyokua akituchukulia
mimi na Khalid Ibn Walid baada ya kusilim kwetu.’(Mustadrak al Hakim, Al-Musnad
ya Abu Ya’la na Majma’ al-Zawaa’id ya Imam Al-Haythami)
Baada ya Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu kusilim na kuhamia katika mji wa
Madinah , akawa ni mwenye kumtembelea Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam mara kwa mara jambo ambalo lilimuongezea sifa nyengine badala ya ile
anayosifika nayo kimaumbile kama tutakavyoona hapo baadae, sifa aliyojiongezea hapa
ni ile ya kupokea baadhi ya Hadith na hivyo kujiongezea I’lm ya dini, na miongoni mwa
Hadith zake zinazofundisha kuhusiana na dini ya Kiislam ni pamoja na ile isemayo:-
Anasema Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu kua, ‘Siku moja alikuja Bedui kwa
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na kumwambia:
‘Ya Rasul Allah! Nimekuja kukuuliza maswali kidogo kuhusiana na mambo ya
maisha ya kidunia na kiakhera’’,
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu kwa kumwambia Bedui huyo,
‘Uliza unachotaka’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niwe miongoni mwa wenye I’lm sana?’
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Muogope Allah Subhanahu
wa Ta’ala na utakua ni miongoni mwa wenye I’lm sana’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niwe miongoni mwa watu matajiri Duniani?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Kinai, na utakua ni miongoni
mwa watu matajiri sana Duniani’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niwe muadilifu?’
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Watakie wenzako kile
unachokitaka wewe, na utakua muadilifu kuliko wote’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili miongoni mwa walio bora?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Wafanyie wema wenzako na
utakua miongoni mwa walio bora’.
835
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili nipendelewe na Allah?’
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Mtukuze sana Allah na utakua
ni mwenye kupendelewa na Allah’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili nikamilishe Dini yangu?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukiwa na tabia nzuri utakua
umekamilisha dini yako’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niwe miongoni mwa wafanyo mema?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Mpende sana Allah kama vile
unaemuona, na kama humuoni basi yeye anakuona, kutokana na kufanya jambo
hilo basi utakua ni miongoni mwa wenye kufanya mema’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niwe mtiifu kwa Allah?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukitii amri za Allah utakua
Mtiifu’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niwe msafi asiekua na Dhambi?’ .
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Jikoshe na kila lililochafu na
utakua msafi usiekua na Dhambi’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili nifufuliwe na nuru katika siku ya Malipo?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Usiwadhulumu viumbe
wengine na wala usijidhulumu Nafsi yako, na utafufuliwa na nuru katika siku ya
Malipo’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili nipate Rehma za Allah siku ya Malipo?’ .
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukiwa na Rehma juu ya
viumbe wenzako, basi na Allah atakurehemu katika siku ya Malipo’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili dhambi zangu ziwe kidogo?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukifanya Istighfar kadri
uwezavyo basi Dhambi zako zitakua ni kidogo sana’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niwe miongoni mwa mwenye heshima sana?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukiwa hutomlalamikia
kiumbe yeyote yule basi utakua ni mwenye heshima sana’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niwe ni mwenye nguvu?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukimtegemea Allah utakua ni
miongoni mwa wenye nguvu kabisa’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niongeze rizki yangu?’
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukiwa na moyo msafi, basi
Allah atakuongezea rizki yako’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili nipendwe na Allah na Mtume wake?’ .
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukikipenda kile
anachokipenda Allah na Mtume wake, utakua ni miongoni mwa wanaopendwa
nao’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili niepuke adhabu za siku ya Malipo?’.
836
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukiwa si mwenye hasira dhidi
ya viumbe wenzako, utaokoka na adhabu za Allah iku ya Malipo’. Bedui akauliza:
‘Nifanye nini ili dua zangu zikubaliwe?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukiwacha mambo maovu, basi
dua zako zitakubaliwa’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili Allah asiniadhirishe siku ya Malipo?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukiulinda usafi na utukufu
wako, basi Allah hatokuadhirisha katika siku ya Malipo’.
Bedui akauliza: ‘Nifanye nini ili Allah anihifadhi siku ya Malipo?’
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukiyahifadhi makosa ya
viumbe wenzako, basi na Allah atakuhifadhi siku ya malipo’.
Bedui akauliza: ‘Ni nini kitakachoniokoa na madhambi?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Machozi, Unyenyekevu na
Maradhi’.
Bedui akauliza: ‘Ni jambo gani bora zaid mbele ya Allah?’
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Ukarimu, Haya na Subra’.
Bedui akauliza: ‘Ni jambo gani baya zaid mbele ya Allah?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Hasira na Ubakhili’.
Bedui akauliza: ‘Ni kitu gani kinachopunguza adhabu za Allah hapa Duniani na
kesho Akhera?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Sadaka iliyojificha na
ukarimu kwa jamaa zako’.
Bedui akauliza: ‘Ni kitu gani kitakachozima moto wa Jahannam siku ya Malipo?’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu: ‘Subra wakati wa Fitna na
Mitihani’.(Musnad Imam Ahmad Ibn Hanbal)
SAYFU ALLAH KHALID IBN WALID RADHI ALLAHU ANHU NA VITA
VYA MUTAH
Kwa muda wa miezi mitatu baada ya Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu kusilimu mji
wa Madinah ulikua uko shwari na hakuna matatizo ya vita, lakini mara Nabii Salallahu
A’layhi wa Salam akamtuma mjumbe wake na barua kwa Ghasan ambae alikua ni Chifu
wa Busra ili kumkaribisha kuingia katika uislam, lakini kabla hajafika huko alipofika
katika sehemu inayoitwa Mutah, mjumbe huyo alikamatwa na kuuliwa na chifu
mwengine wa Ghasan aliekua akiitwa Shurahbil Ibn Amr. Jambo hili la kumuua mjumbe
lilikua ni kosa kubwa sana kwani mjumbe siku zote hua hauawi, hivyo mji wa Madinah
ulipandwa na hasira kubwa sana.
837
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akaamua kuwaadhibu wauaji hao wa
Ghasan na hivyo kutayarisha jeshi lake ili liende likapigane na kabila la watu hao, na
akamchagua Zaid Ibn Harith Radhi Allahu A’nhu kua kiongozi wa jeshi hilo, kisha
akasema ikiwa Zaid Radhi Allahu A’nhu atauwa katika vita hivyo basi uongozi ashike
Jafar Ibn Abi Talib Radhi Allahu A’nhu, na akiuliwa pia basi aongoze Abd Allah Ibn
Rawah Radhi Allahu A’nhu na kumalizia kwa kusema ‘Ikiwa watauawa wote watatu
basi nyinyi wenyewe mtachagua kiongozi wa kukuongozeni’.
Vita vya Mutah vilikua ndio vita vya mwanzo kwa Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu
tangu aingie katika Uislam, na pia ilikua ndio vita vya mwanzo kuenda kupigana yeye
kama mpiganaji aliekua hana cheo chochote, askari wa chini kabisa, walipofika Mutah,
wakapigana vita hivyo na kwa bahati mbaya kati ya viongozi wote waliochaguliwa na
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam wakauawa, hivyo ikabidi Waislam
wajipange upya na kuchagua kiongozi mpya ili kuwaongoza katika vita hivyo.
Vita hivyo vilikua vikali sana kwani Waislamu walikua na jeshi la watu 3000 na Makafir
walikua na jeshi la watu 200000, vilevile Waislamu walikua wameshavunjika moyo
kutokana na kuuliwa kwa viongozi wao wakubwa wote watatu, na hapo Thabit Ibn
Akram akamwambia Khalid Ibn Walid ‘Tafadhali, kua kiongozi wetu utuongoze
kwani tuko katika hali mbaya na miongoni mwetu ni wewe peke yako mwenye
uwezo wa kutuongoza nasi tuko tayari kukufuata kama kiongozi wetu’, hata hivyo
Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu alikataa kwa sababu Thabit Ibn Akram Radhi
Allahu A’nhu alikua ni miongoni mwa waislam wa mwanzo na pia alikua ni miongoni
mwa Masahaba waliopigana katika vita vya Badr. Vile vile Khalid Ibn Walid alikua
akihisi kua Waislam watakua na Imani kubwa zaid na Thabit Ibn Akram Radhi Allahu
A’nhu kuliko watakavyokua na Iman juu yake kwa sababu yeye alikua ndio kwanza
amesilimu.
Hata vivyo kwa kulazimishwa sana ikambidi akubali wadhifa huo na kulipanga upya
jeshi la waislam, Ingawa waislamu walikua kidogo na waliokwisha vunjika moyo kama
tulivyoona lakini kutokana na utaalamu na ujuzi wa Khalid Ibn Walid Radhi Allahu
A’nhu, aliwaaacha nusu ya Waislam wajifiche nyuma yao halafu akawaambia wamfuate
baada ya kuwaonesha ishara, yeye akaelekea katika uwanja wa vita na nusu ya watu
wake, alipofika, vita vikaanza kupiganwa na haikuchukua muda Khalid Ibn Walid Radhi
Allahu A’nhu akawaashiria wale Waislamu waliojificha kuja kusaidia, na hapo likaoneka
vumbi kubwa linalosababishwa na askari wengi waliopanda farasi wakitokea nyuma ya
majeshi ya waislamu, kama kwamba kuna jeshi jengine kubwa la Waislamu ambalo
linakuja kuwaongezea nguvu.
Hapo wanajeshi wa Ghasan wakaanza kuingiwa na khofu na kuchanganyikiwa kwa
nguvu na ari za Waislamu na vile vile kuona kua ndio bado wanazidi kuongozeka zaid,
838
hivyo wakapungukiwa na ari na kuanza kujihami maisha yao, katika vita hivi Khalid Ibn
Walid Radhi Allahu A’nhu alipigana na panga tisa kuvunjikia katika mikono yake,
anasema Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu ‘Katika vita vya Mut’ah, mapanga tisa
yalivunjika, katika mkono wangu na hakuna lililobakia katika mkono wangu
isipokua hili panga langu la Yemen’.
Anasema Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua ‘Nabii Salallahu A’layhi wa Salam
aliwatangazia watu kuhusiana na vifo vya Mashahidi Zayd Ibn Harith, Jafar Ibn
Abi Talib na Abdullah Ibn Rawah kabla ya kuwafikia habari ya vifo vyao, alisema
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ‘Zaid alibeba bendera (aliongoza
jeshi) na akafa Shahidi, baadae akaibeba Jafar nae akafa Shahid, na kisha akaibeba
Ibn Rawah naye pia akafa Shahid’, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
akamalizia kwa kusema huku macho yake yakiwa yamejawa na machozi ‘Baada ya
hapo, bendera ikabebwa na Upanga (Khalid Ib Walid) miongoni mwa Mapanga ya
Allah na Allah akawafanya Waislam wawe ni wenye washindi’ (Imam Bukhari).
Waislamu waliporudi katika vita hivi, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
akasema ‘Khalid ni Saifu Allah (Upanga wa Allah)’ kauli ambayo ilikua ni dua ambayo
ilimpelekea Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu kujulikana kwa jina hilo la Saifu Allah,
na vile vile dua ambayo ilimpa ushindi zaid Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu dhidi
ya maadui zake katika kila mapigano atakayopigana hadi mwisho mwa maisha yake.
FAT-H MAKKIYAH - UFUNGUZI WA MJI WA MAKKAH.
Baada ya vita vya Mu’tah, basi hali ilikua shwari katika Mji wa Madina, lakini mara watu
wa Mj wa Makkah wakavunja makubalino ya Mkataba wa Hudaybiyah, kwani ndani
yake ilikua mna makubaliano ya kutoshambuliana baina ya watu wa Mji wa Madina na
watu wa Mji wa Makkah wala na washirika wao, ambapo katika wakati huu watu wa
Makkah walikua wakishirikiana na watu wa Banu Bakr, na watu wa Madina walikua
wakishirikiana a watu wa Banu Khuza.
Ila sasa tatizo ni kua watu Banu Bakr na watu wa Banu Khuza walikua ni maadui wa
mda mrefu, hivyo mara baada ya kumalizika Vita vya Mutah ukatokea ugomvi kwenye
Mji wa Makkah na watu wa Banu Bakr wakawavamia watu wa Banu Khuza walipokua
wanatufu na hata walipokimbilia kutafuta hifadhi kwenye Al Kaabah, hivyo kiongozi
wa Banu Khuza akiwa na watu wake 40 wakaenda Madina na kuomba msaada juu ya
yaliyotokea, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawataka Watu wa
Quraysh walipe fidia kwa watu wa Banu Khuza waliouliwa, au wavunje
makubaliano ya Ushirikiano na watu wa Banu Bakr au Uvunjwe Mkataba wa
Hudaybiyah.
839
Na kwa kua masharti mawili ya mwanzo ni magumu kwa upande wa watu wa
Quraysh kwa sababu ni yenye kuwavunjia heshima yao, basi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akapata habari kua watu wa Makkah wamechagua
sharti la tatu, na akona kua kutokana na mtizamo huo basi itakua umewadia mda
wa kuuteka Mji wa Makkah na kuuingiza kwenye Uislam.
Hili pia ni jambo ambalo watu wa Makkah walikua hawalitaki, kwani walikua
wanajua kua Idadi ya Waislam imekua kubwa sana na haiwezekani tena kupigana
nao bila ya kushindwa, hivyo watu wa Makkah wakaamua kua bora watume
mjumbe katika Mji wa Madina kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ili
wajadiliane zaidi kuhusiana na kusimamia kutovunjika kwa makubaliano ya
Hudaybiyah.
Hivyo watu wa Makkah wakaamua kumtuma Abu Sufyan akajadiliane na Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam ili kuuokoa mkataba wa Hudaybiyah, hivyo Abu
Sufyan akaelekea katika Mji wa Madina kwa ajili ya kujaribu kuzungumza na
mtoto wake Ramla Bint Abu Sufyan Radhi Allahu Anha ambae ni mke wa Rasul
Salallahu alayhi wa Salam, lakini hata hivyo hakufanikiwa kumshawishi kwani
Ralma Radhi Allahu Anha alikataa katakata hata kukaa kwenye kitanda chake
ambacho analala pia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakumruhusu ingawa
Abu Sufyan alikua ni baba yake.
Hivyo Abu Sufyan akamfuata, Abu Bakr Radhi Allahu Anhu na kumuomba
amsaidie kuzungumza na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, lakini Abu Bakr
Radhi Allahu Anhu akakataa, hivyo Abu Sufyan akamfuata Umar Ibn Al Khattab
Radhi Allahu Anhu, kisha akamfuata Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anha na pia
akamfuata Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu lakini wote walikataa kumsaidia
juu ya jambo hilo, hivyo Abu Sufyan akarudi katika Mji wa Makkah huku akiwa
ni mtu alievunjika moyo sana kutokana na kutofanikiwa kwa safari yake hio.
Ambapo kwa upande mwengine basi Allah Subhanah wa Ta’ala akamshushia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aya zifuatazo zenye kumfahamisha namna
ya anavyotakiwa kufanya katika Mji wa Makkah ambazo zinasema:
﴿وَقَاتِلُواْ فىِ سَبِيلِ ٱهلل َِّ ٱل َّذِينَ يُقَاتِلُونَكُمْ وَلاَ تَعْتَدُو ۤ اْ إِن َّ ٱهلل ََّ لاَ يحُِ ُّب
ٱلْمُعْتَدِينَ۞وَٱقْتُلُوهُمْ حَيْثُ ثَقِفْتُمُوهُم وَأَخْ رِجُوهُمْ مِّنْ حَيْثُ أَخْ رَجُوكُمْ وَٱلْفِتْنَةُ
840
أَشَد ُّ مِنَ ٱلْقَتْلِ وَلاَ تُقَاتِلُوهُمْ عِنْدَ ٱلْمَسْجِ دِ ٱلحَْرَامِ حَتى َّ ٰ يُقَاتِلُوكُمْ فِيهِ فَإِن ا ت قَ َلُوكُْم
فَٱقْتُلُوهُمْ كَذٰ لِكَ جَزَآءُ ٱلْكَافِرِينَ۞فَإِنِ ٱنتَهَوْاْ فَإِن َّ ٱهلل ََّ غَفُورٌ ر َِّحيمٌ۞وَقَاتِلُوهُمْ حَتى َّٰ
لاَ تَكُونَ فِتْنَةٌ وَيَكُونَ ٱلدِّينُ هلل َِّ فَإِنِ ٱنْتَهَواْ فَلاَ عُدْوَانَ إِلا َّ عَلَى ٱلظ َّالِمِينَ ﴾
Waqatiloo fee sabeeli Allahi alladheena yuqatiloonakum wala taAAtadoo inna
Allaha la yuhibbu almuAAtadeena; Waoqtuloohum haythu thaqiftumoohum
waakhrijoohum min haythu akhrajookum waalfitnatu ashaddu mina alqatli wala
tuqatiloohum AAinda almasjidi alharami hatta yuqatilookum feehi fa-in
qatalookum faoqtuloohum kadhalika jazao alkafireena; Fa-ini intahaw fa-inna
Allaha ghafoorun raheemun; Waqatiloohum hatta la takoona fitnatun wayakoona
alddeenu lillahi fa-ini intahaw fala AAudwana illa AAala aldhdhalimeena (Surat Al
Baqara 2:190-193)
Tafsir: Na piganeni kwa ajili ya Allah dhidi ya wale ambao wanaopigana nanyi na
wala msivuke mipaka, kwani kwa hakika Allah hawapendi wenye kuvuka mipaka. Na
waueni popote pale mtakapowakuta na wafukuzeni kutoka katika sehemu
waliyokufukuzeni na Fitna ni mbaya zaidi ya kuua. Na msipigane nao ndani ya Masjid
Al Haram isipokua pale watakapokupigeni nyinyi ndani yake, na kama
wakaikushambulieni basi waueni, kwani hayo ndio malipo ya Makafiri; Lakini kama
wakikoma basi Allah ni mwingi wa Usamehevu na ni mwingi wa Huruma. Na
piganeni nao mpaka iwe hakuna fitna tena, na dini ni ya Allah pekee lakini kama
wakisita basi msivuke mipaka isipokua dhidi ya watakaofanya dhulma.
Imam Taher Ibn 'Ashur anasema kua: ‘Amesema Abd Allah Ibn 'Abbas na 'Umar Ibn
'Abdul 'Aziz na Mujahid kua aya hii ya Surat Al Baqar 2:190 imejiweka wazi na
haihitaji ufafanuzi na haijabatilishwa’. Kisha akaendelea na kusema: ‘Ujumbe wake
halisi ni kupigana na wale watakaopigana nanyi, wale ambao wamejitayarisha
kupigana nanyi, yaani msiwavamie na kuwapiga Wazee, Wanawake na Watoto.’
Ambapo hapa inabidi tufafanue aya hizi kwani kuna watu ambao hua wamefaham sivyo
na hivyo hua ni wenye kutuma aya hizi kwa ajili ya kutangazia na kuhalalisha mapigano
ya Jihadi bila ya kuangalia kusudio na malengo ya Jihadi kisharia.
Wakati kusudio la uhalali wa kupigana Jihad au kupigana vita kwa ajili ya Allah
Subhanahu wa Ta’ala hujumisha mambo yafuatayo:
1- Kwa ajili ya kujilinda na kurudisha mashambulizi ya maadui.
841
2- Kuondoa dhulma ya kidini na kusimamisha uhuru wa kuabudu ili watu wapate uhuru
wa kuabudu na na nafasi ya kufanya Ibada zao kwa uhuru bila ya madhara.
Na masharti ya mapigano hayo huhusisha mambo yafuatayo:
1- Kusudio lake kuu lisiwe ni lenye kutokana na mapendekezo ya kibinafsi au kutafuta
faida kwa mtu fulani katika mapigano hayo.
2- Mapigano yawe ni lazima dhidi ya wale wapiganaji husika na wala sio wananchi
wasiokua na hatia ambao hawapo katika maeneo ya uwanja wa vita au wale ambao
hawahusiki kwa kutokua na silaha ama si miongoni mwa wapiganaji wa maadui.
3- Kuua wanawake na watoto hakuruhusiki kabisa. Katika Sahih Muslim kuna Hadith ya
Abd Allah Ibn Umar isemayo kua Nabii Muhammad Salallahu A’layi wa Salam aliwaona
watoto na wanawake wameuliwa katika vita na hapo akalaani kuwaua wanawake na
watoto na katika Hadith nyengine inasema kua ‘Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam ameharamisha kuua wanawake na watoto’. Anasema Imam An Nawawi
kuhusiana na Hadith hizi kua: ‘Kuna Ijma’a ya Wanazuoni kuhusiana na Hadith hizi
kua hukmu yake inatumika katika vita pale itakapokua wanawake na watoto
hawapigani na Waislam. Lakini ikiwa wanapigana basi Wanazuoni wengi
wanasema inaruhusika kuwaua’ (Sharh Sahih Muslim 12/48).
4- Kuyalinda maisha ya mateka wa vita kutovunjiwa haki zao za kibinaadamu.
5- Kuyalinda mazingira ambako kunajumuisha, makatazo ya kuua wanyama, kukata miti,
kuteketeza mazao mashambani, kuharibu mali, kuvunja majumba, kutia sumu na
kuchafua vyanzo vya maji iwe mto,visima, n.k
6- Kuulinda uhuru wa kuabudu kwa waumini wengine iwe majumbani mwao,
makanisani, mahekalu,n.k.
7- Kuvamia maadui kwa kuwashtukizia kumeharamishwa kabisa. Kwani amesema Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kua: ‘Mu’umini hawaui wenzake. Imani
huondoka kwa kuua’. Imam Ibn Athir anasema kuhusiana na Hadithi hii kua ‘Mauaji
yaliyokusudiwa hapa ni kwa kuwashtukizia wengine bila ya kuwapa onyo, wakati
wakiwa hawajajitayarisha’ (Al-Nihaya fi Gharib al-Hadith wa al-Athar 3/775)
8- Ruhusa ya kuingia katika nchi hua inahesabika kama makubaliano ya kiusalama ya
ukimya kua hairuhusiki kufanya ufisadi katika nchi ya maadui. Imam al-Khurqī anasema
katika Mukhtasr wake: ‘Yeyote yule anaeingia katika nchi ya maadui zake
haruhusiwi kuwalaghai mali zao’, katika kuielezea kauli hii Imam Ibn Qudama
anasema katika Al Mughni, ‘Hairuhusiki kuwasaliti wao [Wasiokua Waislamu katika
nchi isiyokua si ya Waislam], kwa sababu kuna makubaliano ya kimya ya mtu
842
kuingia katika mji kwa usalama kutokana na sharti la kua mtu huyo anaeomba
ruhusa ya kuingia katika mji wa kigeni hatowadhuru au hatowasaliti watu wa mji
huo. Hivyo mtu yeyote yule atakaeingia katika mji wetu kwa usalama na kisha
akatusaliti hua anavunja makubaliano hayo. Hivyo hili hua ni katazo kwa sababu
kufanya hivyo hua kunasababisha hadaa ambayo imaharamishwa katika dini yetu.’
(Al-Mughn̄ i 9/237).
9- Adui ni lazima awe ni miongoni mwa wale ambao Muislam ameruhusika kupigana
nao, kwani ikiwa adui ni yule ambae kuna makubalianao ya kusitisha makubaliano na
Waislam, basi hua hairuhusiki kumvamia adui wakati wa usiku kwa sababu kufanya
hivyo hua ni kuvunja makubaliano ya usalama baina yao katika mambo yanayohusu
uhai, mali na heshima.
10- Hairuhusiki kuwatumia watu kama ngao ili kujilinda isipokua katika wakati wa vita
na katika hali maalum, ambavyo ni kama ilivyoelezewa na Wanazuoni. (Bahr Ra`iq 80\5,
Hashiyat ibn 'Abn Abdin 223\3, Rawdat al Talibin 239\10, Mughni al Muhtaj223\4,
Mughn̄ i ibn Qudama 449\8, 386/10).
Hivyo mnamo tarehe 10 ya mwezi wa Ramadhan ya mwaka wa 8 Al Hijra ambayo
ni sawa na mwaka 630, basi Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam alikusanya
Jeshi la watu 10,000 la Waislam na kueleka katika Mji wa Makkah, ambapo
walipofika katika maeneo ya Marr Az Zahran basi jeshi hilo likapiga kambi katika
eneo hilo, ambapo katika usiku huo Waislam wakamkamata Abu Sufyan ambae
alikua akifanya Upelelezi kutaka kujua kinachoendelea katika kambi hio.
Abu Sufyan alipopelekwa mbele ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi
nae akasilimu. Na siku ya pili yake asubuhi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam akaligawa Jeshi lake katika sehemu 4 kwa ajili ya kuuvamia Mji wa
Makkah na akawachagua viongozi wanne wakuu wa jeshi hilo ambao ni yeye
mwenyewe Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kisha Khalid Ibn Walid Radhi
Allahu Anhu, kisha Abu Ubaydah Ibn Jarrah Radhi Allahu Anhu na kisha Saad Ibn
Ubaidah Radhi Allahu Anhu.
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaagiza Viongozi wake hao kwa
kusema: ‘Hairuhusiki kutumia silaha ya aina yeyote kumshambulia mtu
yeyote isipokua yule atakaeanzisha mashambulizi, Jaribuni kwa kila hali
kuepuka umwagaji damu, na jizuieni kuwadhuru Wazee, Wanawake na
Watoto’
Hili lilikua ni tukio la pili muhimu lililofuatia kutokea baada ya kusilimu Khalid Ibn
Walid Radhi Allahu A’nhu ambalo ni wakati wa kuuteka mji wa Makkah, kwani Nabii
843
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, alimkabidhi Khalid Ibn Walid kuongoza kundi
la wapiganaji wanaotoka katika makabila ya Banu Salim, Banu Khazima, Banu Ghaffar
na Jaheena, na kumwambia ikiwa watatokea watu ambao wataanzisha mapigano basi
anayo ruhusa ya kuutumia upanga wake na ikiwa hakuna upinzani basi haina haja ya
kuutumia upanga huo.
Walipoingia katika viunga vya Mji wa Makkah, vijana wapya waliokua wamechukua
nafasi ya Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu katika wapiganaji wa Makafiri wa
Makkah, baada ya yeye kusilimu na kuhama Makkah, waliokua wakiongozwa na Ikrimah
Ibn Abu Jahal, Safwan Ibn Ummayah na Sahal Ibn Amr, walijaribu kuwazuia Waislamu
kwa silaha zao wasiingie katika mji wa Makkah katika maeneno ya Khandamah na hapo
baada ya kuona silaha zimetolewa dhidi yao, Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu
akaamrisha vijana hao washughulikiwe na hivyo wakawaua baadhi miongoni mwao na
baadhi Ikrimah Ibn Abu Jahal wakakimbia.
Baadae Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam aliposikia Habari hii, alikasirika
kwanini Waislamu wakawapiga vijana hao, lakini hata hivyo baada ya kuambiwa kua
Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu alitoa amri hiyo, basi Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam akasema: ‘Allah hutekeleza yale yalio bora’, akimaanisha kua hayo
yalikua yameshaandikwa na Allah Subhanahu wa Ta’ala yatokee.
Baada ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kuingia katika mji wa Makkah
na kuingia ndani ya Al Kaabah kuyaangusha masaamu yaliyomo ndani yake, alikua ni
Khlaid Ibn Walid ambae ndie aliekaa nje ya mlango wa Al Kaabah kusimamia asiingie
mtu mwengine yeyote. Na baada ya kuuweka chini ya mamlaka yao, Mji wa Makkah.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akasema:
﴿ٰ َ ي ُّهَا ٱلن َّاسُ إِ َّ خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ ٰ وَأُنْثَى وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوابً وَقَبَآئِلَ لِتَ ۤ عَارَفُو اْ إِ َّن
أَكْ رَمَكُمْ عِ ندَ ٱهلل َِّ أَتْقَاكُمْ إِن َّ ٱهلل ََّ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴾
Ya ayyuha alnnasu inna khalaqnakum min thakarin waontha wajaAAalnakum
shuAAooban waqaba-ila litaAAarafoo inna akramakum AAinda Allahi atqakum
inna Allaha AAaleemun khabeerun (Surat Al Hujrat 49:13)
Tafsir: Enyi Watu hakika sisi tumekuumbeni nyinyi kutokana na Mume na Mke, na
tukakujaalieni nyinyi kua katika Mataifa na Koo ili pate kujuana, Hakika Mwenye
Utukufu zaid mbele ya Allah ni yule Mwenye Taqwa zaidi, kwa Hakika Allah ni
mwingi wa Kujua juu ya kila kitu na ni mwenye kua na habari juu ya kila kitu.
844
Baada ya hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamuamrisha Bilal Ibn Rabah
Radhi Allahu Anhu asome Adhana na kisha akauchukua Ufunguo wa Al Jengo la Al
Kaabah na kuukabidhi kwa Uthman Ibn Talha Radhi Allahu Anhu kua yeye na kizazi
chake kua ndio wasimamizi wa Al Kaabah.
Na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamtuma Khalid Ibn Walid Radhi
Allahu A’nhu kuenda kuteketeza makazi ya Al Uzza, lakini hata hivyo Khalid Ibn Walid
Radhi Allahu A’nhu aliporudi alisema kua hakukuta kitu chochote katika sehemu hiyo
aliyotumwa, na hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamwambia Khalid
Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu nenda tena kaangalie vizuri, hivyo alipokwenda tena mara
ya pili katika sehemu hiyo Khalid Ibn Walid Radhi Allahu A’nhu akayakuta makazi hayo
na pia akamkuta mwanamke mweusi aliekua hana nguo, hivyo akayateketeza makazi
hayo na pia akamteketeza kwa upanga wake mwanamke huyo. Aliporudi safari hii Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamwambia huyo ndie aliekua Al Uzza.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akatoa Khutba katika maeneo ya Safa na
kisha akawauliza watu wa Makkah: ‘Hivi Jee mnajua nnataka kukupeni Adhabu Gani?’
Watu hao wa Makkah wakasema: ‘Hakika wewe ni Ndugu mwenye Utukufu kwetu
na ni Mtoto wa Ndugu yetu Mtukufu’ hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam akasema: ‘Hamna kulaumiwa leo hii juu yenu hivyo nendeni kwani mko
huru.’
Ambapo kauli hii ya Huruma na Unyenyekevu iliwafurahisha sana watu wa Makkah na
hivyo wote wakaingia kwenye Uislam akiwemo Hind Bint Utbah, Ikrimah Ibn Abu Jahal
na Suhail Ibn Amr Radhi Allahu Anhum. Ambapo baada ya tukio hili basi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akakaa katika Mji wa Makkah kwa siku 20 kumalizia
mipangilio ya mipaka ya eneo Takatifu la Al Kaabah.
WAKE WA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM.
Mchoro unaofuatia unaonesha namna ilivyokua familia ya Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam kutoka kwa babu yake ambae ni Abd ul Mutalib, kwa baadhi ya Ami
zake, wake zake, watoto wake na wajukuu zake.
845
846
Kama tunavyoona katika mchoro huo wa familia ya Rasul Allahu salallahu A’layhi wa
Salam kua kuna idadi kubwa ya wake wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
idadi ambayo imepindukia idadi iliyoruhikaa kisharia, hivyo kwa wasiofahamu huenda
wakajiuliza ni kwa sababu gani yeye akawa na idadi kubwa ya wake wakati Uislam
unasema kua mwanamme anaruhusika kuoa mwisho wake wanne?
Jibu la swali hili linaelezeka katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ni kua hapo zamani
ilikua ni jambo la kawaida si kwa jamii ya Kiarabu tu kwa mwanamme kua na wake
wengi bali pia kwa jamii mbalimbali. Hivyo aya ya kushurutisha mwisho wake wanne
iliposhuka, ilikuja ili kurekebisha kwa kupunguza idadi ya wake anaotakiwa kua nao
mwanamme na vile vile kuwahifadhi Wajane na Mayatima tena kwa sharti la kuwafanyia
uadilifu wa kisharia wanawake.
Kwani aya hiyo ya Surat An Nisaa’ inasema:
﴿وَإِنْ خِ فْتُمْ أَلا َّ تُقْسِ طُواْ فىِ ٱلْيَتَامَى ٰ فَٱنكِحُواْ مَا طَابَ لَكُمْ مِّنَ ٱلنِّسَآءِ مَثْنىَٰ
وَثُلاَثَ وَرُابَعَ فَإِنْ خِ فْتُمْ أَلا َّ تَعْدِلُواْ فَوَاحِ دَةً أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيمَْانُكُ مْ ذٰ لِكَ أَدْ نىَٰ
أَلا َّ تَعُولُواْ ﴾
Wa-in khiftum alla tuqsituu fii alyatama fainkihuu ma taba lakum mina alnnisa-i
mathna wathulatha warubaAAa fa-in khiftum alla taAAdiloo fawahidatan aw ma
malakat aymanukum dhalika adna alla taAAooloo. (Surat An Nisaa’ 4:3).
Tafsir: Na ikiwa mnakhofu kua hamtoweza kuwafanyia haki mayatima wa kike, basi
Oeni wanawake wengine mnaowataka, wawili, au watatu, au wanne; lakini ikiwa
mnakhofu kua hamtoweza kuwafanyia uadilifu basi oeni mmoja tu, au wale
mnaowamiliki mikononi mwenu (Mliowateka vitani na Watumwa). Kufanya hivyo ni
kukaribia kujilinda na kutokua waadilifu.
Aya hii ilishuka siku ya mwezi tatu Shawwal, baada ya vita vya pili vilivyopiganwa baina
ya Waislam na Makafir wa Makkah, vita hivi vilikua ni vita vya Uhud ambapo Waislamu
walishindwa na miongoni mwao watu Masahaba 70 wakafa mashahidi, hivyo ghafla
ikawa takriban familia 70 katika mji wa Madinah hazina wa kuwasimamia, hili lilikua
ni tatizo kubwa sana kwa jamii ya Taifa changa la Kiislam, hivyo ufumbuzi wa tatizo hili
ukapatikana baada ya kushuka kwa aya hii, ilioruhusu kuwahudumia na kuwahifadhi
Wajane na Mayatima.
847
Anasema Imam Muhammad Tahir Ibn Ashur kuhusiana na aya hii kua “Aya hii ni yenye
kutoa onyo kwa Wanaume kua wasitumie uhusiano wao wa udugu wa Damu, kama
kisingizio cha kutowalipa mahari yao kamilifu Mayatima kama vile ambavyo
hawakuutumia uhusiano wao wa udugu huo wa damu kwa kutowaoa Mayatima
hao, na bali waliwaoa kwa sababu ya mali yao au kwa sababu ya kuvutiwa nao”
Imam Muhammad Tahir Ibn Ashur anaendelea kwa kusema kua : ‘Na neno Dhalika
liliomo katika aya hio (Dhalika Adna alla Taáuluu – Na kufanya hivyo ni kwa ajili
ya kukaribia kujilinda na kutokua waadilifu) ni Ismi al Ishara – Kiashirio
kinamaanisha aidha moja kati ya mambo mawili yafuatayo:
1- Sharti – Yaani na ikiwa mnakhofu kua hamtoweza kuwafanyia haki
mayatima wa kike
2- Hukmu – Yaani basi oeni mmoja tu, au wale mnaowamiliki mikononi
mwenu (Mliowateka vitani na Watumwa)
Hivyo kama ikiwa Dhalika - Ismi al Ishara hio ikiwa inamaanisha jambo la pili basi
hii inamaanisha kua Mwanamme anatakiwa apunguze idadi ya Wanawake
anaotaka kuwaoa hadi afikie katika hali ya kua hatokua na khofu ya kutokua
Muadilifu. Na hii ni kwa sababu kua na wake wengi humpelekea Mwanamme
kutofanya Uadilifu, hata kama akijitahid kwa uwezo wake wote kufanya Uadilifu
na hii ni kutokana na maumbile ya Nafsi ya Ibn Adam hua ni yenye matamanio na
kufanya makosa.’(Al Tahrir wa Al Tanwir)
Hivyo kuoa wake zaidi ya mmoja katika Uislam hakukupendekezwa, bali kumeruhusiwa,
chini ya muongozo maalum ambao ni kutooa kwa kuendekeza matamanio ya mwanamme
tu bali kwa kufanya uadilifu na kuwaonea huruma Wanawake, Wajane na Mayatima,
kama ilivyosema tena Qur’an:
وَلَن تَسْتَطِيعُو ۤ اْ أَن تَعْدِلُواْ بَينَْ ٱلنّسَآءِ وَلَوْ حَرَصْتُمْ فَلاَ تمَِيلُواْ كُ ل َّ ٱلْمَ يْ ِل
فَتَذَرُوهَا كَٱلْمُعَل َّقَةِ وَإِن تُصْلِحُواْ وَتَت َّقُواْ فَإِن َّ ٱهلل ََّ كَانَ غَفُوراً ر َّحِ يماً ﴾
Walan tastateeAAoo an taAAdiloo bayna alnnisa-i walaw harastum fala tameeloo
kulla almayli fatadharooha kaalmuAAallaqati wa-in tuslihoo watattaqoo fa-inna
Allaha kana ghafooran raheeman (Surat An-Nisaa’ 4:129)
Tafsir: Na hamtoweza kufanya uadilifu baina ya wanawake hata kama ikiwa hivyo
ndivyo mnavyotaka, hivyo msiegemee sana upande mmoja na hivyo kupelekea
ِ
﴿
848
mwengine kudharaulika. Mkifanya uadilifu na yote ya haki na mkamuogopa Allah
kwa kujitenga na kila ovu, basi Allah ni mwingi wa kusamehe na mwingi wa Rehma.
Anasema Imam Al-Fakhr Ad Din Al Razi kuhusiana na aya hii kua: ‘Aya hii inamaanisha
kua kamwe hamtoweza kuweka usawa, au kua na hisia sawa juu yao wote, kwani
jambo hili haliko chini ya uwezo wenu, na kwa sababu hiyo basi hamtakiwi
kulifanya’.(Mafatih Al-Ghayb)
Hii inamaanisha kua sio kama imeharamishiwa kuzidisha hisia upande mmoja, kwani
hilo ni jambo ambalo halidhibiti, lakini haikuruhusiwa kuonesha kua hisia hizo zimezidi
upande mmoja iwe aidha kwa vitendo au kwa maneno.
Anasema Imam Muhammad Idris Al Shafii kua Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam alikua akiwafanyia uadilifu sawia wake zake, na kisha husema: ‘Ya Allah hivi
ndivyo niwezavyo kujidhibiti na wewe ni mwenye kujua kuhusiana na yale
nisiyoweza kuyadhibiti’.
Amesema Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam katika hadith iliyopokelewa na
Abu Hurayra kua: ‘Atakaekua na wake wawili na kisha akampendelea mke mmoja
(kwa kutofanya uadilifu baina yao) basi atafufuliwa siku ya kiama akiwa amepooza
upande mmoja wa mwili wake’. (Imam Abu Daud)
Hivyo baada ya kushuka aya inayoshurutisha mwisho kua na wake wanne, baadhi ya
Masahaba waliokua na wake zaidi ya wanne iliwabidi kuwaacha wake zao na kubakisha
wanne tu, na hata wale ambao waliosilimu baadae pia iliwabidi kuwaacha wake wengine
na kubakia na wanne tu, idadi ambayo Uislamu umeruhusu.
Kwa mfano Al Harth Ibn Qays alisema kua kabla ya kusilimu alikua na wake wanane na
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamwambia kua katika wake zake hao
aliokua nao itambidi achague wanne tu na wanne waliobakia aachane nao. Imam Al
Tirmidhi anasema kua Ghaylan Ibn Salmah al Thaqafi Radhi Allahu Anhu alikua na
wake kumi katika siku za Ujahiliya lakini baada ya kusilimu ikambidi achague wake
wanne miongoni mwao na sita waliobakia aachane nao, Sahaba mwengine ni Nawfal Ibn
Mu’awiyah Radhi Allahu Anhu ambae alikua na wake watano na alipoamua kusilimu
ikambidi nae pia amuache mmoja kati yao ili abakie na wanne tu.
Sehemu ya pili ya jibu la swali hilo, hua inafafanulika vizuri zaidi pale tunapoiangalia
historia inayofuatia, ambayo ni ya maisha ya ndoa ya Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam.
Ingawa historia inasema kua Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alioa wake
13 lakini wakati aya Surat An Nisaa’ 4:3 inayoruhusu kuoa mwisho wake wanne
849
inashuka, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kwa wakati huo alikua na wake
tisa ambao walikua ni wafuatao:-
1. Umm al Mu’uminin Sawdah Bint Zumah.
2. Umm al Mu’uminin Aisha Bint Abu Bakr As Siddiq.
3. Umm al Mu’uminin Hafsah Bint Umar Ibn Al Khattab.
4. Umm al Mu’uminin Hind Bint Umayyah (Ummu Salamah).
5. Umm al Mu’uminin Zaynab Bint Jahsh.
6. Umm al Mu’uminin Juwayriyyah Bint Harith.
7. Umm al Mu’uminin Safiyyah Bint Huyay.
8. Umm al Mu’uminin Ramla Bint Abu Sufyan (Ummu Habiba).
9. Umm al Mu’uminin Maymunah Bint Harith Ibn Hazan Al Hilalieh.
Lakini hata hivyo aya hiyo haikumhusu kabisa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam kwani Allah Subhanahu wa Ta’ala alimshushia Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam, aya maalum kwa ajili yake inayomshurutisha kutowaacha wake
aliokua nao, wala kutoongeza mke mwengine zaid ya wale aliokua nao, kama
inavyosema Qur’an:
﴿لا َّ يحَِل ُّ لَكَ ٱلنِّسَآءُ مِن بَعْدُ وَلاَ أَن تَبَد َّلَ هبِِن َّ مِنْ أَزْوَاجٍ وَلَوْ أَعْجَبَكَ
حُسْنُهُن َّ إِلا َّ مَا مَلَكَتْ يمَِينُكَ وَكَانَ ٱهلل َُّ ٰ عَلَى ِ كُل شَيْءٍ ر َّقِيباً
﴾
ّ
La yahillu laka alnnisao min baAAdu wala an tabaddala bihinna min azwajin
walaw aAAjabaka husnuhunna illa ma malakat yameenuka wakana Allahu AAala
kulli shay-in raqeeban. (Surat Al Ahzab 33:52).
Tafsir: ‘Si halali kwako, [Muhammad], kuoa wake baada ya hao, wala kuwabadilisha
kwa ajili ya wake wengine hata kama ikiwa uzuri wao unakuvutia, isipokua wale
unawamiliki (Waliotekwa vitani ama watumwa) na Allah ni muangalizi wa Kila kitu.’
Imam Al Baidawi anasema katika Tafsir yake kua, ‘Aya hii ilikua inamuelezea Nabii
Muhammad Sallahu A’layhi wa Salam kua haruhusiwi kuoa wake wengine hata
kama ikiwa mmoja kati ya wake zake hao amefariki dunia wala haruhusiwi
kuwabadilisha kwa kumpa talaka mmoja na kuoa mwengine’.
Anasema Abd Allah Ibn Abbas kuhusiana na habari hiyo kua hata wakati Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alipoamua kuuwacha wazi mlango kwa
kuwaambia wake zake kua wanayohaki ya kuamua kama kubakia na yeye na na kupata
Radhi za Allah ama kuamua kuachwa na kuwa huru na kuanza maisha mapya na bora
850
kuliko aliyokua nayo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam wakati huo ambao
ulikua ni mgumu sana, lakini wake zake hao walikataa na kusema kua watastahamili
ugumu wa maisha waliyokua nayo na kubakia na kuishi na Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam.
Na baada ya hapo Allah Subhanahu wa Ta’ala aliwapa cheo wake wa Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam pale aliposema katika Qur’an kua:
﴿ٱلن َّبىِ ُّ أَوْ لىَٰ بِٱلْمُ ؤْ مِنِينَ مِ نْ أَنْفُ سِ هِ مْ
وَأَزْوَاجُهُ أُم َّهَاتُهُ ْم﴾
Alnnabiyyu awla bialmu/mineena min anfusihim waazwajuhu ommahatuhum ..
(Surat Al Ahzab 33:6).
Tafsir: ‘Nabii yuko karibu na waumini kuliko wao na Nafsi zao, na wake zake ni mama
zao (kwa waumini, kuwaheshimu na kutowaoa)’
Tunapoangalia historia kwa kina basi tunaona kua Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam, alipomuoa Sayyida Khadija Radhi Allahu Anha, alikaa nae takriban kwa
miaka 23 bila kuongeza mke mwengine hadi pale alipofariki Sayyida Khadija, ambapo
wakati huo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua na umri wa miaka 50,
Baada ya kufariki Sayyida Khadija Radhi Allahu Anha,, Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam alikaa miaka miwili bila ya kua na mke yeyote, na alikua akikaa peke
yake pamoja na watoto wake.
Hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, hakuwahi kuoa mke zaid ya
mmoja hadi pale alipohamia Madinah baada ya kuanzisha Taifa jipya la Kiislamu, kipindi
ambacho kilianza wakati akiwa na umri wa miaka 53 hadi 60, jambo hili linatuonesha
kua kuoa kwake huko wake wengi kunatokana na njia za kujenga na kuimarisha udugu
na ujamaa wa makabila tofauti katika Taifa lililokua changa la Kiislam na vile vile kwa
nia ya kuwalinda na kuwahurumia Wajane na Mayatima. Aya iliyomkataza Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kutoongeza au kutowawacha wake zake
alishushiwa wakati akiwa na umri wa miaka 60, na akiwa na wake zake hao 9, Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alitii amri hiyo hadi alipofariki akiwa na umri
wa miaka 63.
Wake zake wengine aliowahi kuwaoa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
kabla ya kushuka aya iliyomkataza kuoa au kuacha wake zake ni pamoja na Umm al
Mu’uminin Khadija Bint Khuwaylid Radhi Allahu Anha, ambae alifariki dunia miaka
mitatu kabla ya Hijra.
851
Tukiangalia kwa upande mwengine basi tunaona kua ilikua pia ni vigumu kwa Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kuwaacha wake zake hao kwa sababu ya
utukufu waliokua nao wake hao ambao mbali ya kua ni wake wa Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam lakini pia katika ukubwa na utukufu wa asili waliotoka wake
zake hao, kama inavyooneshwa hapa chini:
Umm Ul
Muuminin.
Khadija Bint
Khuwaylid.
Sawdah Bint
Zammah.
Aisha Bint
Abu Bakr
Hafsa Bin
Umar
Hind Umm
Salama
Zaynab Bint
Khuzaymah
Juwayriyah
Bint Harith
Zaynab Bint
Jahsh
Rayhana Bint
Zayd
Maria Bint
Sham
Ramla Umm
Habiba
Safiyah Bint
Huayih
Maymuna
Bint Harith
Ukoo
Wake.
Aliolewa
Akiwa.
Umri Wake
Alipoolewa.
Mwaka Alioolewa.
Banu Asad Mjane Wa Miaka 40 Miaka 25 Baada ya
Talaka
Mwaka wa Tembo
Banu Amir Mjane wa Miaka 50 Miaka 10 Baada ya
Kufiwa
Utume.
Banu Taymi Mwari Miaka 14 Mwaka wa 2 Al Hijra
Banu Adi Mjane wa Miaka 20 Mwaka wa 4 Al Hijra.
Kufiwa
Banu Amir Mjane wa Miaka 50 Mwaka wa 4 Al Hijra.
Kufiwa
Banu Amir Mjane wa Miaka 30 Mwaka wa 5 Al Hijra.
Kufiwa
Banu Mjane wa Miaka 20 Mwaka wa 5 Al Hijra.
Mustalaq Kutekwa
Banu Asad Mjane wa Miaka 38 Mwaka wa 5 Al Hijra.
Talaka
Banu Nadir Mjane wa Miaka 18 Mwaka wa 6 Al Hijra.
Kutekwa
Al Surriyah Miaka 18 Mwaka wa 7 Al Hijra
Qitbiyyah
Banu Shams Mjane wa Miaka 36 Mwaka wa 7 Al Hijra
Talaka
Banu Nazir Mjane wa Miaka 17 Mwaka wa 7 Al Hijra.
Kutekwa
Banu Amir Mjane wa Miaka 27 Mwaka wa 7 A Hijra.
Talaka
852
UMM AL MU’MININ SAWDAH BINT ZUMAH
Ingelikuaje kama Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam angempa talaka Umm
Al Mu’uminin Sawdah Bint Zumah Ibn Qays Ibn `Abdush-Shams Ibn `Abdi Widdi Ibn
Nasr Ibn Maalik Ibn Hasl Ibn `Amir Ibn Lu'ay, ambae alikua ni mke wake wa kwanza
kumuoa baada ya kufariki Sayyida Khadija Bint Khuwaylid Radhi Allahu Anha, kwani
Umm al Mu’uminin Sawdah Bint Zumah Radhi Allahu Anha alikua ni miongoni mwa
Waislam wa mwanzo kusilimu na pia miongoni mwa Waislamu wa mwazo kufanya Hijra
kwa kuhamia Uhabeshi (Ethiopia) pamoja na mumewe, aitwae Sakran Ibn Amar Radhi
Allahu Anhu ambae alisilimu kutokana na ushawishi wa Sawdah Radhi Allahu Anha
ambae alisilimu mwanzo kuliko Sakran Radhi Allahu Anhu.
Hivyo wakati walipokua wakirudi Makkah kutoka Uhabeshi ambapo Sawda Radhi
Allahu Anha alilala akaota kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akimkaribia na
kisha alipofika karibu yake basi akapiga goti pembeni yake, ambapo alipomwambia
Mume wake Ndoto hio, basi Sakran akasema kua: ‘Hii Ndoto inamaanisha kua mimi
nitafariki karibuni na kisha wewe utaolewa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam’ na haukuchukua mda isipokua akran Ibn Amar Radhi Allahu Anhu akafariki
Na baada ya kurudi katika Mji wa Makkah huku Sawdah Radhi Anha mwenye umri wa
wa miaka mitano zaidi ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na huku akiwa
Mjane mwenye watoto watano na baba yake akiwa ni kipofu, basi Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam aliamua kumuoa Sawdah Radhi Allahu Anha baada ya
kufiwa na mumewe kwa sababu kama asingemuoa basi ingembidi Sawdah Radhi Allahu
Anha abakie katika Mji wa Makkah kama mjane, jambo ambalo lingempelekea kua
katika mtihani mkubwa, kwani wakati huo mji wa Makkah ulikua bado ni wa Kikafir
hivyo familia yake ingemtenga na pia watu wa mji wa Makkah wangemlazimisha kurudi
katika ukafiri kwa kumuadhibu na pia kulikua na uwezekano wa kumuua kutokana na
kua Muislam.
Mbali ya hivyo lakini pia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alimuoa Sawdah
mnamo mwaka wa 10 wa Utume wake katika mwezi wa Ramadhan kwa ajili ya
kumsimamia na kuwahudumia watoto wake na bila ya shaka Sawdah Radhi Allahu Anha
alikua ni mwenye kutekeleza wajibu wake mbele ya Mume wake ipasavyo, kwani alikua
ni mwenye kumpenda na kumliwaza yeye na watoto wake na pia alikua ni mfano wa
kuigwa hata kwa Aisha Radhi Allahu Anha ambae anasema kuhusiana nae kua: ‘Sijawahi
kuona Mwanamke ambae ni mwenye kunitia ari zaidi kuliko Sawdah Radhi Allahu
Anha, kiasi ya kua hata mimi ningependa kua kama yeye.’
853
Sauda Bint Zummah Radhi Allahu Anha alikua ni mwanamke mwenye kufuata
kikamilifu maamrisho ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kwani katika
Hiija yake ya mwisho Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam basi aliwaambia
wake zake kua: ‘Twendeni Hija mara hii kisha mtabaki nyumbani’ ambapo Sawdah
Bint Zumah Radhi Allahu Anha akasema: ‘Hakika mimi sitoenda tena Hija baada ya
Hija hii.’
UMM AL MU’MININ AISHA BINT ABU BAKR AS SIDDIQ
Ingelikuaje kama Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam angempa talaka Umm
al Mu’uminin Aisha Bint Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu ambae alikua ni mtoto
wa Sahaba yake kipenzi cha moyo wake, Sahaba Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu
Anhu.ambae alijitolea kila kitu kwa hali na mali kwa ajili ya Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam na pia kwa ajili ya Waislamu na kueneza ujumbe wa dini ya Kiislam.
Ambapo aliulizwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na Amr Ibn Al Aas Radhi
Allahu Anhu pale aliposema: ‘Hivi Jee ni nani ambae unampenda zaidi kuliko wote?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu: ‘Aisha’ na kisha Amr Ibn Al Aas Radhi
Allahu Anhu akauliza tena: ‘Na Katika Wanaume?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam Akajibu: ‘Baba yake.’
Ambapo anasema Aisha Radhi Allahu Anha kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
aliniambia mie kua: ‘Nimekuona Aisha ndani ya Ndoto yangu, wakati Malaika Jibril
aliponiletea ukiwa kwenye Nguo ya Hariri ya rangi kijani na kuniambia: ‘Huyu
ndio Mke wako hapa Duniani na kesho Akhera’’’
Kwa kua alikua na umri mdogo basi Aisha Radhi Allahu Anha aliposwa kwanza na kisha
akaolewa miaka mitatu baada ya Vita vya Badr, ambapo anasema mwenye Aisha Radhi
Allahu Anha kutokana na Udogo wake kua: ‘Siku Moja Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alikuja Nyumbani wakati mimi nikiwa nachezea visanamu ambapo nae
aliponiona akasema: ‘Ya Aisha, Jee ndio Mchezo gani huo unaocheza?’ nami
nikasema: ‘Farasi wa Sulayman’ ambapo Rasul Allahu Salallahu Alayhi wa Salam
akacheka’
Anasema Aisha Radhi Allahu Anha kua : ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
aliniambia mimi kua: ‘Hakika wewe kwangu mie nakupenda zaidi ya Tende
inapochanganywa na Siagi’ ambapo nami nikamwambia: ‘Ya Rasul Allah hakika
wewe kwangu mimi nakupenda kuliko Asali inapochanganywa na Siagi’’
854
Ambapo ilikua ni kawaida ya Masahaba kumtumia zawadi Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam wakati inapokua ni zamu ya kulala kwa Aisha Radhi Allahu Anha kwani
walikua wanajua kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akimpenda sana
Aisha Radhi Allahu Anha, hivyo siku moja Wake zake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam walikusanyika kwenye nyumba ya Ummu Salama Radhi Allahu Anha, na
wakamwambia Ummu Salama Radhi Allahu Anha amwambie Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua awaambie Masahaba kua wanapotaka kumtumia zawadi basi sio
lazima wasubiri inapokua zamu ya Aisha Radhi Allahu Anha bali wamtumie na katika
siku nyengine za kawaida pia.
Hivyo Ummu Salamah Radhi Allahu Anha akamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam mara ya kwanza lakini Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakumjibu,
hivyo akamwambia tena mara ya pili na ikawa hakujibiwa, na hivyo akamwambia mara
ya tatu ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kumwambia Ummu
Salama Radhi Allahu Anha kua: ‘Usiniumize kuhusiana na Aisha, kwani haijawahi
kutokea kua Wahyi kushuka katika nyumba yeyote isipokua ya Aisha’ ambapo
Ummu Salama Radhi Allahu Anha akasema: ‘Naomba msamaha kwa Allah kutokana
na kukumiza hali yako’
Miongoni mwa sifa za upekee za mahusiano baina ya Aisha Radhi Allahu Anha, ni pale
Siku moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimwambia Aisha Radhi Allahu
Anha: ‘Ya Aisha hakika mimi hua nnajua pale unapokua umenikasirikia na pale
unapokua hukunikasirikia’ Aisha Radhi Allahu Anha akauliza: ‘Unajuaje ya Rasul
Allah?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajibu: ‘Unapokua unafuraha nami
basi hua unasema: ‘La, naapa kwa Mola wa Muhammad’ lakini unapokua una
hasira basi hua unasema: ‘La Naapa kwa Mola wa Ibrahim’’ hivyo Aisha Radhi
Allahu Anha akasema: ‘Naam. Ya Rasul Allah, Hua hua silitaji Jina lako.’
Ambapo anasema Imam An Nasafi kua: ‘Siku moja Aisha Radhi Allahu Anha alikua
na hasira kwa sababu hakukua na chakula ndani ya Nyumba yao, na hivyo Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakupenda namna Aisha Radhi Allahu Anha
alivyokua akizungumza nae, kwa hivyo akaingiwa na hasira na kutoka ndani ya
Nyumba yake na kuelekea Msikitini. Ambapo Aisha Radhi Allahu Anha alijaribu
kumkimbilia kumuomba msamaha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam lakini
hakuwahi kukutana ane na akaanguka chini na kuweka shavu lake ardhini na
kuanza kuomba Msamaha kwa Allah Subhanah wa Ta’ala.’
Ambapo hapo hapo akashuka Malaika Jibril na kumuwahi Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kabla hajaingiza mguu wake Msikitini na kumwambia Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala anataka urudi kwa
Aisha na kisha umsamehe’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akarudi
kwa Aisha Radhi Allahu Anha na kisha akamsamehe makosa yake, na kisha baada
855
ya hapo Malaika Jibril akashuka hukua kiwa na Kibakuli cha Vyakula vitamu na
kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua : ‘Allah Subhanah wa
Ta’ala anasema kua Upatanisho ulikua ni kutoka kwetu na chakula cha upatanisho
pia ni kutoka kwetu.’
Miongoni mwa sifa za kimaumbile za Aisha Radhi Allahu Anha basi ni kama
anavyomuelezea Hisham Ibn Urwa Radhi Allahu Anhu ambae amesema: ‘Hakika mimi
sijawahi kuona mtu yeyote yule ambae nimwenye Ilm kubwa ya Aaya za Qur’an,
Ibada za Wajib, Ibada za Sunnah, Ushairi, Ukoo na Makabila, Hikma na Utabibu
kama Aisha’
Naam bila ya shaka hili halishangazi kwani tunapomuangalia Aisha Radhi Allahu Anha
basi tunaona kua kutokana na ufahamu wake basi amekua ni miongoni mwa watu wanne
muhimu sana wanaotegemewa katika Ilm ya Fiqh na Hadith kwani Hadith zake ni Sahih
na ni zaidi ya 2000 ambapo anashindana na Abu Hurayrah, Abd Allah Ibn Umar na Anas
Ibn Malik Radhi Allahu Anhum kwa upokeaji wa wingi wa Hadithi na alikua si mwenye
kusita kuuliza jambo lolote kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam pale inapokua
hajafaham.
Aisha Radhi Allahu Anha alifariki katika siku ya Jumanne ya mwezi 17 Ramadhani ya
mwaka 57 Al Hijr huku akiwa na umri wa miaka 66.
UMM AL MU’MININ HAFSAH BINT UMAR IBN AL KHATTAB.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam asingeliweza kumpa talaka Umm al
Mu’uminin Hafsah Bint Umar Ibn Al Khattab ambae ni mtoto wa Sahaba Umar Ibn Al
Khattab, Imam Bukhari anasema kua siku moja Ansar mmoja aliingia katika nyumba ya
Umar Ibn Al Khattab na kusema ‘Ya Umar! kuna jambo baya sana limetokea’, Umar
akauliza ‘Jee kabila la Ghasan limetuvamia?’(Katika wakati huo kabila la Ghasan
lilikua linajitayarisha kuwavamia Waislam), Yule Ansari akajibu ‘La! Lakini limetokea
jambo baya zaidi ya hilo, kwani Rasul Allah amewataliki wake zake’, hapo Umar
akasema ‘Ama sasa hivi Hafsah ameangamia na kupotea’. Siku ya pili yake asubuhi
na mapema akaenda kwa bint yake Hafsa na akamkuta analia sana, na akamuuliza
‘Jee, Rasul Allah amekutaliki?’ nae akajibu ‘Sijui kwani, amejifungia chumbani
kwake’, hivyo Umar akaomba ruhusa ya kuingia chumbani kwa Rasul Allah, na
aliporuhusiwa, akamsalimia Rasul Allah na akamuuliza kuhusu undani wa
kuwataliki wake zake, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akajibu kua
hakuwataliki na hapo Umar akaridhika na jibu hilo’.
856
Hadithi hii inaonesha kua kwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kuwataliki
wake zake ni jambo kubwa sana kwa Waislamu kuliko hata kuvamiwa na Maadui zao.
Katika kipindi hicho Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alijitenga nao wake
zake hao kwa muda unaokaribia mwezi mmoja, kutokana na wake zake hao kutaka
kuongezewa kiwango katika matumizi yao ya maisha kwa sababu hali ya maisha yao
ilikua ni ngumu, hivyo Ummah wa Kiislamu ulifikiria kua Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam amewaacha wake zake, jambo ambalo lilileta tafrani miongoni mwao.
Kuna Hadith nyengine pia ambayo inasema kua kuliwahi kutokea mgogoro baina ya
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na Hafsa Bint Umar Ibn Al Khattab na
baada ya kufikiria kua wameachana, Umar Ibn Al Khattab akalalamika na kusema ‘Allah
hatomjali tena Umar na bint yake’, Hadith hizi na nyenginezo zinaoneyesha ukubwa
wa athari wa kutokea jambo kama hilo katika Ummah wa Kiislam.
Ambapo mwanzoni Hafsa Radhi Allahu Anha aliolewa na Khunis Ibn Hudhafa Ibn Qay
ambae alifanya Hijra mara mbili ambazo ni kelekea katika ardhi ya Uhabeshi na pia
Yathrib, na pia alipigana vita vya Badr na vita vya Uhud na akafariki kutokana na
majeraha aliyoyapata katika Vita vya Uhud, wakati Hafsa Radhi Allahu Anha akiwa na
umri wa miaka 18.
Hivyo Umar Ibn Al Khattab akawa na huzuni kubwa sana kutokana na tukio hili la binti
yake kua Mjane katika umri mdogo, basi akamfuata Abu Bakr Radhi Allahu Anhu na
kumtaka kua amuoe Hafsa lakini hata hivyo Abu Bakr Radhi Allahu Anhu akakataa kwa
sababu alimskikia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anataka kumuoa yeye Hafsa,
lakini hata hivyo Abu Bakr Radhi Allahu Anhu hakumwambia Umar Ibn Al Khattab
Radhi Allahu Anhu juu ya hilo, kwa sababu alikua anataka kua Umar Ibn Al Khattab
Radhi Allahu Anhu apate habari hio kutoka kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Na Umar Radhi Allahu Anhu alipoenda kwa Uthman Ibn Affan Radhi Allah Anhu
kumuomba amuoe bint yake basi na Uthman Radhi Allah Anhu nae akakataa kwani
alisema kua yeye ndio kwanza amefiwa na mke wake ampendae Ruqqayah Bint Rasul
Salallahu Alayhi wa Salam hivyo hawezi kuoa kwa wakati huo.
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipopata habari hio basi akatabasam na
kisha akasema: ‘Hafsa atapata Mume aliebora zaidi ya Uthman na Uthman ataoa
mwanamke bora kuliko Hafsa.’ Na Umar Radhi Allahu Anhu alifurahia sana habari hio
na hivyo akakubali kumuozesha Hafsa Bint Umar Radhi Allahu Anha kwa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na ndoa yao ikafungwa katika mwaka wa 3 Al Hijra.
Na kisha Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu nae akaozeshwa binti wa pili wa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam aitwae Ummu Kulthoum Bint Rasul Radhi Allahu
Anha.
857
Kwa upande wa Hafsa Bint Umar Radhi Allahu Anha basi alikua na ukaribu sana na
Aisha Radhi Allahu Anha ambapo Hafsa Bint Umar Radhi Allahu Anha nae pia alikua ni
mwenye Ilm kubwa sana kutokana na kuihifadhi Qur’an ndani ya Moyo wake, ambapo
anasema Aisha Radhi Allahu Anha kuhusiana nae kua: ‘Hafsa alikua ni mtu mwenye
Msimamo katika Vitendo vyake na Kauli zake kama alivyokua Baba yake, Hakika
Hafsa alikua ni Mtoto wa Umar Ibn Al Khattab’
Hafsa Bint Umar Radhi Allahu Anha alifariki mnamo mwaka 47 Al Hijra hukua akiwa
na umri wa miaka 63.
UMM AL MU’MININ ZAYNAB BINT KUZAYMAH.
Umm al Mu’uminin Zaynab bint Khuzaymah Radhi Allahu Anha ambae pia anajulikana
kwa jina la Ummu ul Masakin kutokana na alikaa na Nabii Muhammad Salallahu Alayhi
wa Salaam kwa miezi minane halafu akafariki dunia baada ya kuumwa kwa mda mfupi
na hivyo kua ni Mke wa pili wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kufariki kabla
ya kufariki Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na kua ni mke wa Kwanza Kusaliwa
Sala ya Jenenza na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Umm al Mu’uminin Zaynab bint Khuzaymah Radhi Allahu Anha alikua ni Mke wa Abd
Allah Ibn Jahsh Radhi Allahu Anhu ambae alikua ni Ibn Ami yake Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwani Mama yake Abd Allah Ibn Jahsh Radhi Allahu Anhu alikua ni
Umamah Bint Abd Ul Muttalib, ambapo Abd Allah Ibn Jahsh Radhi Allahu Anhu alifariki
pia katika vita vya Uhud na hivyo kumuacha Zaynab Bint Khuzaimah Radhi Allahu Anha
akiwa mjane katika wakati huo ambao akiwa na umri wa miaka 30.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaepeleka posa yake kwa wazee wake
Zaynab Bint Khuzaymah Radhi Allahu Anha kwa ajili ya Kumsitiri, kwani amesema
Safwan Ibn Sulaim Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu A’alayhi
wa Salam kua: ‘Yeyote yule anaewahudumia Wajane na Masikini basi hua ni sawa
na Mwenyekupigana Jihad kwa ajili ya Allah Subhanah wa Ta’ala, hua sawa na
aliesimama kusali kwa miaka yote na aliefunga kwa miaka yote’’(Imam Tirmdhii)
Mama yake Zaynab bint Khuzaymah Radhi Allahu Anha alikua akiitwa Khawla na pia
kama Hind Bint Awf Ibn Zuyahr Ibn Harith ambae ndie anaejulikana kama ‘Mama
Mkwe Bora kuliko wote Ardhini’ na hii ni kwa sababu watoto wake wawili waliolewa
na Rasul Allah Salallahu Aalayhi wa Salam ambao ni Maymuna Bint Harith na Zaynab
Bint Khuzaymah na watoto wake wengine waliolewa na Masahaba mbali mbali.
858
Kwani Hind Bint Awf aliolewa zaidi ya mara 4, ambapo ndoa yake ya kwanza ilikua ni
kwa Jazi Al Zubaydi ambae alikua ni miongoni mwa Waislam wa mwanzo na
akachaguliwa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua ni Muweka Mahesabu wa
Jamii ya Kiislam.
Halafu Hind Bint Awf akaachwa na akaolewa na Harith Ibn Hazan ambapo ndoa hii
ikatoka watoto wanne ambapo wa kwanza ni Lubaba Al Kubra ambae ndie mwanamke
wa pili kusilimu na ndie aliekua mke wa Al Abbas Ibn Abd Ul Muttalib ambae ndie Ami
yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na wa pili ni Maymuna Bint Harith ambae
aliolewa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, wa tatu ni Saayib Ibn Harith na wa
nne ni Qatn Ibn Harith.
Halafu Harith Ibn Hazan akafariki na Hind Bint Awf akaolewa na Khuzaymah Ibn Harith
Al Hilali ndo ambayo ilitoa mtoto wa kike mmoja tu aitwae Zaynab Bint Khuzaymah
ambae aliolewa na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Halafu Hind Bint Awf akaachwa na akaolewa na Umays Ibn Maad Ibn Tamim ndoa
ambayo ilitoa watoto watatu ambao ni Asma Bint Uways ambae aliolewa na Rabia Ibn
Riyab, na kisha akaolewa na Jafar Ibn Abi Talib Ibn Abd ul Muttalib, na kisha akaolewa
na Abu Baqr As Siddiq na kisha akaolewa na Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhum.
Mtoto wake wa pili ni Salma Bint Uways ambae aliolewa na Hamza Ibn Abd Al Muttalib
aliekua Ami yake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, na kisha akaolewa na Shaddad
Ibn Usama.
Na mtoto wake wa tatu katika ndoa hii alikua ni Awn Ibn Umays.
Halafu Hind Bint Awf akaachwa na akaolewa na Al Harith Ibn Hazan ambae alikua na
mke mwengine aitwae Fakhta Bint Amr ambae mtoto wake wa kike ni Al Lubaba Al
Saghir ambae ndie Mama yake Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu.
Hivyo Lubaba Al Kubra Bint Harith Ibn Hazan Al Hilal alikua ni mtu mwenye asili ya
Yemen kama alivyokua mama yake ambae ni Hind Bint Awf kwani kabila lao halikua ni
la Quraysh bali lilikuani lenye asili ya Yemen, ila lilikua ni kabila linaloheshimika,
ambapo ndoa baina Lubaba Al Kubra na Abbas Ibn Abi Talib iliyotoa watoto 7 ambao
ni Al Fadhl, Abdullah, Ubaydullah, Quthum, Mabad, Abdur-Rahman na Umm Habib.
Miongoni mwa sifa za Zaynab bint Khuzaymah Radhi Allahu Anha ni kama
zinavyoelezewa na Aisha Radhi Allahu Anhu pale aliposema: ‘Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alituambia sisi wake zake kua: ‘Miongoni mwenu atakakutana na
mie mwanzoni Akhera ni yule mwenye Mikono mirefu’’(Imam Bukhari) na bila ya
859
shaka miongoni mwa Wake zake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi aliekua na
mikono miruf kwa kutoa Sadaka ni Zaynab Bint Khuzayama Radhi Allahu Anha ambae
kutokana na kutoa kwake na kusaidia watu kwa ukarimu wake mkubwa basi alipewa jina
la Ummu al Masakin.
Ambapo safari moja kuna Masikini alipita kwenye nyumba yake Zaynab Bint Khuzayma
Radhi Allahu Anha akiwa hana chakula hivyo Zaynab Bint Khuzayma Radhi Allahu Anha
akampa chakula cake pekee kilichobakia nyumbani kwake yaani chakula cha usiku chote
na hivyo kwa usiku wa siku hio Zaynab Bint Khuzayma Radhi Allahu Anha akalala na
njaa, baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kujua juu ya tukio hilo basi ndio
akasema maneno ambayo ndio ya ile hadithi isemayo: ‘Kama ukiwa unamuamini Allah
Subhanah wa Ta’ala kama inavyostahiki basi atakuruzuku riziki yako, kama vile
ambavyo anavyowaruzuku Ndege ambapo asubuhi hua wanatoka kwenye vijumba
vyao wakiwa na njaa lakini hua ni wenye kurudi Usiku huku wakiwa wameshiba.’
UMM AL MU’MININ RAYHANA BINT ZAYD
Umm al Mu’uminin Rayhana bint Zaid ambae alikua ni mwenye asili ya Kiyahudi kutoka
katika kabila la Banu Nadir ambapo baaada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kulishinda Jeshi la Banu Qurayza katika Vita vya Khaybar kutokana na kuwazingira kwa
siku 25 na kutaka wajisalimishe, lakini wakatakataa na hivyo Wanaume wote wa Banu
Qurayza wakauliwa wakabakishwa Wanawake na Watoto ambao walifanywa kua
Watumwa wa Waislam.
Rayhan Bint Zayd alikua ni miongoni mwa Wanawake wazuri sana waliokua wajane
katika tukio hilo, na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akataka kumuoa lakini
Rayhana kwanza akakataa kutokana na kua na mapenzi makubwa sana kwa Mume wake
aliefariki, lakini baada ya mda akasilimu na kisha akolewa na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kama anavyosema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Sad Al Basr
Al Hashim kua:
‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimteka Rayhana Bint Zayd Ibn Amr Ibn
Khunafa, ambae alikua na Mumewe ambae alikua akimpenda sana, hivyo nae
akasema kua: ‘Sitompenda Yeyote baada yake (Mume wake)’ na alikua ni
Mwanamke Mzuri sana, Rayhana amesema kua: ‘Na wakati Watu wa kabila la
Qurayza walipotekwa, basi Wanawake waliletwa mbele ya Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam. Na mimi nilikua ni mmoja wao mingoni mwao, ambapo
niliamrishwa kuja mbele yake kisha nikategenashwa na wengine, na hivyo nikawa
ni sehemu ya Ngawira ambazo ni kwa ajili yake.
860
Nilipotengenishwa na wengine basi Allah alikua amenichagua na kisha wakanituma
kwenye Nyumba ya Umm al Mundhir Salma Bint Qays kwa ajili ya kukaa kwa siku
kadhaa, hadi pale Mateka walioasi walipoadhibiwa na Wanawake wakagawanywa.
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaja mbele yangu huku mimi nikiwa
nimejawa na aibu, na kisha akakaa mbele yangu na kusema: ‘Kama Ukimchagua
Allah na Rasul Allah, basi Rasul Allah nae atakuchagua wewe kwa ajili yake’ Hivyo
Nami nikajibu: ‘Kwa hakika mimi nimemchagua Allah na Rasul Allah.’
Nilisilimu basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaniwachia huru, na kisha
akanioa, na akanipa Waqqiya 12 na nahssha moja amabcho ni kiasi alichoawalipa
wake zake wengine kwa ajili ya Mahari yao. Akanichukua mimi kama mke wake
na kunipeleka kwa Ummu ul Mundhir na akanichukua na nikawa navaa Hijab.’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimpenda sana na kumfurahia na alimpa
kila alichokitaka. Na ndio maana akamwambia kua: ‘Kama ungemuomba Rasul
Allah kuhusiana na Banu Qurayza basi angewaachia huru’ na Rayhana alikua
akisema: ‘Kamwe hakua peke yake kabla ya kuwagawanya Mateka’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimuoa katika mwezi wa Muharram mwaka
wa 6 baada ya Hijra na alikaa nae hadi pale alipofariki baada ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kurudi Hija.’
UMM AL MU’MININ HIND UMMU SALAMAH.
Kuhusiana na Umm al Mu’uminin Hind (Ummu Salamah), alikua pia ni mjane wa Abd
Allah ibn ‘Abd al Asad, ambae alikua akijulikana kama Abu Salamah ambae alikua ni
mtoto wa shangazi yake Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, aliekua akiitwa
Barah bint Abd Al Muttalib na pia alikua ni kaka yake wa kulelewa. Nao pia walihamia
Uhabeshi, Abu Salama na baada ya kurudi Abu Salamah akawa ni miongoni mwa
waliofariki katika vita vya Uhud, na kuwacha mjane, Hind ambae pia alikua ni mtu
mzima na alikua na watoto mayatima wanne. Hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam akaamua kumuoa ili amhifadhi na kumsaidia ulezi wa mayatima hao.
Umm al Mu’uminin Hind au Umm ul Mu’uminin Ummu Salamah Radhi Allahu Anha
hakukubali moja kwa moja kuolewa na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
kwa kusema kua alikua ni mtu mzima sana, mwenye watoto na kimaumbile ni mtu
mwenye wivu sana, hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam hakujali sana
kuhusiana na umri wa Ummu Salamah kwani kwa sababu ya utu uzima wake alikua
akihitaji kuhifadhiwa na kuhudumiwa na hivyo akamwambia, ‘Ama kwa watoto wako
nitawashughulikia, na kuhusiana na wivu wako nitamuomba Allah auondoe’
861
Miongoni mwa sifa tukufu za Umm Salama Radhi Allahu Anha ni kua mbali ya kua
alikua ni mwanamke mzee miongoni mwa wake wa Rasul Allahu Alayhi wa Salam lakini
alikua ni mwanamke mwenye ari kubwa sana ya kutafuta Ilm na hivyo alikua ni makini
sana katika kufuatilia Hadithi za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na pia likua ni
Mwanamke ambae sauti nzuri sana na ya kuvutia katika usomaji wake wa Qur’an.
Siku moja Abu Hurayrah Radhi Allahu Anhu alisema: ‘Mtu yeyote yule ambae aliekua
na janaba katika usiku wa mwezi wa Ramadhani basi ni wajibu wake kujitoharisha
kabla ya Alfajir au funga yake itabatilika’ ambapo habari hii ilipomfika Umm
Salama Radhi Allahu Anha basi akasema: ‘La, hii sio sahih kwani Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alipokua katika hali kama hii basi alikua ni mwenye
kuendelea kufunga’
Hivyo Uthibitisho huu wa Umm Salama Radhi Allahu Anha umekua ndio hukmu juu ya
jambo hili kwa kila mwenye kuamka na Janaba katika mwezi wa Ramadhani basi Janaba
hua halibatilishia funga yake. Miongoni mwa Hadith alizonukuu Ummu Salama Radhi
Allahi Anha ni 378.
Na kutokana na Busara zake Ummu Salama Radhi Allahu Anha basi Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam alikua akisikiliza ushauri wake na moja kati ya mfano wa
hilo ni pale baada ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kusaini Mkataba wa
Hudaybiyyah, aliposema kuwaambia Masahaba zake ‘Nyanyukeni, mchinje wanyama
wenu na kisha mnyoe nywele zenu’, hata hivyo hakuna hata Sahaba mmoja alienyanyua
mguu wake kufanya vile alivyoamrisha Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam,
kutokana na kuvunjika moyo kwa yale yaliyotokea katika makubaliano ya mkataba huo.
Hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akanyanyuka na kuenda kwa Ummu
Salama Radhi Allahu Anha na kumwambia yaliyotokea na hapo Ummu Salama Radhi
Allahu Anha akamwambia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ‘Ya Rasul
Allah, unataka maneno yako yafanyiwe kazi? Basi nenda nje na usizungumze na
mtu yeyote hadi pale utakapomaliza kuchinja mnyama wako na kunyoa nywele
zako’, hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akatoka nje akachinja
mnyama wake na kuanza kunyoa nywele zake, na baada ya Masahaba kumuona Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam anafanya hivyo basi na wao wakanyanyuka na
kufanya kama vile alivyokua akifanya. (Imam Bukhari)
862
UMM AL MU’MININ MAYMUNA BINT HARITH IBN HAZAN AL
HILALIEH
Ama kuhusiana na Maymuna Bint Al Harith Ibn Hazan Ibn Bujair, Ibn Al Hazm Ibn
Rubwaiba Ibn Abdullah Ibn Hilal Ibn Amir Ibn Sa'sa'a Al-Hilaliyya ambae pia
anajulikana kwa jina Barra basi ni mtoto wa Hind Bint Awf ambae tayari
tumeshamzungumzia tulipomzungumzia mke wake Al Abbas Ibn Abd Ul Muttalib
Radhi Allahu Anhu ambae pia ndie Mama ya Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu.
Ambapo Maymuna alikua ni Mwanamke Mtukufu na ni mwenye hamu ya kuolewa na
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, kutokana na kumpenda kwake sana Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na kutokana na kushindwa kujizuia kwake basi akamfuata
dada yake ambae ni Umm Fadhl ambae ndie mama yake Abd Allah Ibn Abbas Radhi
Allahu Anhu, na alipomuelezea kuhusiana na mapenzi yake hayo na hamu yake ya
kuolewa kwake na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi Umm Fadhl
akazungumza na Mumewe ambae ni Al Abbas Radhi Allahu Anhu ambae ndie Ami yake
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Hivyo Al Abbas Radhi Allahu Anhu akafikisha ujumbe wake huo wa Maymuna Bint
Harith Radhi Allahu Anha kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae nae
akaupokea na kuyakubali maombi hayo ya kumuoa Maymuna Bint Harith. Habari za
kukubaliwa kwa maombi yake hayo zilipomfika mwenyewe Maymuna Bint Hartith basi
alikua amekaa Juu ya Ngamia wake, na hivyo hapo hapo akashuka na kusema kua:
‘Ngamia na kilichokuwepo juu ya Ngamia hapo awali vyote ni vya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam.’
Ndoa yao hii ilifungwa mnamo mwezi wa Shawwal wa mwaka wa 7 Al Hijra mara tu
baada ya Makubaliano ya Huddaybiyah, ambapo Waislam waliruhusiwa kuingia katika
Mji wa Makkah kwa ajili ya kufanya Umra, ambapo baada yake Allah Subhanah wa
Ta’ala akashusha aya ifuatayo:
﴿َٰٰي ُّهَا ٱلن َّبىِ ُّ إِ َّ أَحْلَلْنَا لَكَ أَزْوَاجَكَ ٱللا َّتيِ ۤ آتَيْتَ أُجُورَهُن َّ وََما مَلَكَتْ يمَِينُ َك
ممِ َّآ أَفَآءَ ٱهلل َُّ عَلَيْكَ وَبَنَاتِ عَمِّكَ وَبَنَاتِ عَم َّاتِكَ وَبَنَاتِ خَالِكَ وَبَنَاتِ
خَالاَتِكَ ٱللا َّتِى هَاجَرْنَ مَعَكَ وَٱمْرَأَةً م ُّؤْمِنَةً إِن وَهَبَتْ نَفْسَهَا لِلن َّبىِ ِّ إِنْ أَرَاَد
ٱلن َّبىِ ُّ أَن يَسْتَنكِحَهَا خَالِصَةً ل َّكَ مِن دُونِ ٱلْمُؤْمِنِينَ قَدْ عَلِمْنَا مَا فَرَضْنَا عَلَيْهِمْ
863
فيِ ۤ أَزْوَاجِ هِمْ وَمَا مَلَكَتْ أَيمَْانُهُمْ لِكَيْلاَ يَكُونَ عَلَيْكَ حَرَجٌ وَكَانَ ٱهلل َُّ غَفُوراً
ر َّحِ يماً ﴾
Ya ayyuha alnnabiyyu inna ahlalna laka azwajaka allatee atayta ojoorahunna
wama malakat yameenuka mimma afaa Allahu AAalayka wabanati AAammika
wabanati AAammatika wabanati khalika wabanati khalatika allatee hajarna
maAAaka waimraatan mu/minatan in wahabat nafsaha lilnnabiyyi in arada
alnnabiyyu an yastankihaha khalisatan laka min dooni almu/mineena qad
AAalimna ma faradhna AAalayhim fee azwajihim wama malakat aymanuhum
likayla yakoona AAalayka harajun wakana Allahu ghafooran raheeman(Surat Al
Ahzab 33:50)
Tafsir: Ewe Nabii (Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam)! Kwa Hakika
tumekuhalalishia wake zako, ambao umewalipia mahari yao, na ambao mkono wako
wa kulia unawamiliki (wanawake waliotekwa vitani na watumwa) ambao Allah
amekupa, na binti wa Ami zako, bint wa Ammah (shangazi) zako, binti wa Khal
(wajomba) zako, binti wa Khalah (mama wadogo) ambao walihama (kutoka Makkah)
pamoja nawe, na mwanawake alieamini ikiwa atajipeleka (kutaka kuolewa) kwa
Mtume, na Mtume akataka kumuoa; Haki ambayo ni yako tu (kwa Nabii Muhammad
peke yake), lakini si kwa waumini wengine. Hakika tunajua ni kipi tulichowaamrisha
kuhusiana na wake zao na wale wanaomilikiwa na mikono yao ya kulia - Ili kusiwe na
uzito kwako wewe. Na Allah ni mwingi wa Kusamehe na mwingi wa Rehma.
Ingawa alikua akiitwa Barra lakini Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimbadilisha
jina na kumuita Maymuna ambalo ni lenye kumaanisha Mtu alieneemeshwa, na hii ni
kwa sababu Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua anapenda majina Mazuri na
pia alimuoa katikamwaka wa 7 Al Hijra ambao ulikua ni mwaka wa Utulivu ndani yake.
Ambapo anasema Aisha Radhi Allahu Anha kua: ‘Miongoni mwetu basi alikua na
Taqwa zaidi alikua ni Maymuna Bint Harith, na alikua ni mweye kupenda
kuunganisha Udugu, na kutokana na sifa hii basi ndio maana Rasul Allah Salallhu
Alayhi wa Salam akasema: ‘Myamuna na Umm Fadhl na Salam na Asmaa ni
Madada waumini’’
Miongoni mwa Hadith zinazojumuisha watu wa watatu wa Familia ya Rasul Salallahu
Alayhi wa Salam na hapo hapo watu watatu wa Maymuna Bit Harith Radhi Allah Anha
ni ile inayoelezea kuhusiana na Bidaa Hasan yaani Bidaa nzuri ambayo ingawa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakuyafanya, lakini hata hivyo hakuwakataza watu
864
kutoyafanya, na watu waliojumuishwa kwenye hadithi hii ni Maymuna Bint Harith Radhi
Allahu Anha, Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu ambae mama yake ni Umm Fadhl
Radhi Allahu Anha na Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu ambae mama yake ni Lubaba
Al Saghira Radhi Allahu Anha ambapo wote Mama hao wawili ni madada zake Maimuna
Bint Harith Radhi Allahu Anha.
Imam Malik anasema kutoka kwa Ibn Shihab kutoka kwa Abu Umama Ibn Sahl Ibn
Hunayf kua ‘Amesema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu: ‘Amesema Khalid
Ibn Walid kua alimtembelea Maymunah pamoja na Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam, nae Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akapewa
nyama ya mjusi mkubwa wa jangwani wa kuchoma, Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam akanyoosha mkono wake kuchukua, ambapo baadhi ya
wanawake waliokuweo katika nyumba ya Maymunah wakamwambia Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam juu ya kile anachotaka kukila, na hapo
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akarejesha mkono wake. Khalid Ibn
Walid anasema: Mimi nikasema ‘Ya Rasul Allah, jee ni Haram?’ Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam akasema ‘La! Ila hakuna katika ardhi ya watu wangu
na sijisikii kuipenda nyama hiyo’ Khalid Ibn Walid anasema ‘Mimi nikaendelea
kuitafuna na kuila huku Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
akiniangalia’ ’.
Anasema Imam Muhamamd Ibn Saad kua: ‘Amesema Maymuna kua siku moja Rasul
Allah Sallahu Alyhi wa Salam alitoka chumbani mwangu nami nikamfungia mlango,
na baadae akarudi na kugonga mlango lakini mimi nikagoma kumfungulia mlango
na kumwambia kua : ‘Unaenda kwa wke zako wengine katika usiku wangu?’ nae
Rasul Allah Salallahu Alahyi wa Salam aakajibu kwa kusema: ‘La sikufanya hivyo
bali Mkojo ulikua hautaki kutoka’
Maymuna Bint Harith alikua pia ni mwalimu wa Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu
Anhu ambae alikua ni shangazi yake pia ambapo mamo mwaka 51 Al HIjra alipofariki
Maymuna basi Ibn Ataa kua: ‘Wakati Maymuna alipofariki, mimi nilienda Mazikoni
na Abd Allah Ibn Abbas ambae alikua akiwaambia watu: ‘Msimtikise, kuweni na
upole nae kwanini Mama yangu’’
Ambapo anasema Imam Abu Sulayman Hamd ibn Muhammad Al Khattabi Al Busti kua:
‘Maymuna Radhi Allahu Anha ana Hadith 7, ambapo mbili katika yake zimo katka
Sahih Muslim na Sahih Bukhari, moja imenukuliwa katika Bukhari peke yake na
5 zimenukuliwa kwenye Sahih Muslim hivyo hadith zake kwa ujumla ni 13’
865
UMM AL MU’MININ ZAYNAB BINT JAHSH.
Mke wake wa tano alikua ni Umm al Mu’uminin Zaynab Bint Jahsh. Ilikua ni dasturi ya
waarabu kuwachukulia watoto wa kulea kuwapa jina la baba mlezi na hivyo kua kama
watoto wao wa kuwazaa hususan katika mambo ya harusi na mirathi, hivyo mke
alieachika wa mtoto wa kulea hawezi kuolewa na baba yake mlezi. Baada ya kuingia
Uislam, Allah Subhanahu wa Ta’ala alitaka kuondoa desturi hii na kutaka kuwepo kwa
tofauti baina ya mtoto wa kulea na mtoto wa kuzaa, mtu anaweza kulea mtoto lakini
mtoto huyo haruhusiwi kuchukua asili ya baba yake mlezi, ni lazima achukue asili na jina
la baba yake mzazi.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua na mtoto wa kulea aliekua akiitwa
Zayd Ibn Harith, ambae kama tulivyoona hapo kabla kua alikua mtumwa, aliezawadiwa
Bi Khadija Bint Khuwaylid Radhi Allahu Anha, kisha nae akampa Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam kama msaidizi wake hivvyo Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salaam akawa anamlea na akawa anaitwa Zayd Ibn Muhammad, na baada ya
muda ukashuka wahy ambao ulikua unashurutisha watoto wa kulea kuchukua na kutumia
majina ya baba mzazi kwa ajili ya kusimamia haki na ili kulinda asili ya watoto hao,
hivyo Zayd Ibn Muhammad akabadilishwa jina na kurudishwa katika asili yake na akawa
anaitwa Zayd Ibn Harith.
Na akasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Yeyote yule ambae anadai
kua Fulani ni baba yake wakati akiwa ni mwenye kujua kua si Baba yake basi Mtu
huyo anaharamishiwa Pepo’ (Sahih Muslim)
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamuozesha mtoto wake huyo wa kulea
kwa binamu yake ambae ni Zaynab Bint Jahsh ambae alikua akitoka katika miongoni
mwa familia tukufu ya Quraysh, kutokana na utofauti wao wa kidarja na kimaisha, ndoa
hiyo baina ya Zayd Ibn Harith na Zaynab Bint Jahsh haikudumu mda mrefu na hivyo
wakaachana.
Allah Subhanahu wa Ta’ala akamjaalia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
kumuoa Zaynab Bint Jahsh na kushusha aya katika Qur’an kuhusiana na jambo hili pale
aliposema:
﴿وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلاَ مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى ٱهلل َُّ وَرَسُولُهُ أَمْراً أَن يَكُونَ لهَُمُ ٱلخِْيَرَةُ مِ ْن
أَمْرِهِمْ وَمَن يَعْصِ ٱهلل ََّ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَل َّ ضَلاَلاً م ُّبِيناً ﴾
866
Wama kana limu/minin wala mu/minatin idha qadha Allahu warasooluhu amran
an yakoona lahumu alkhiyaratu min amrihim waman yaAAsi Allaha warasoolahu
faqad dhalla dhalalan mubeenan (Surat Al Ahzab 33:36).
Tafsir: Si juu ya Waumini wa Kiume wala Waumini wa Kike pale Allah na Mtume
wake wanapoamrisha kitu, kwao wao kua na hiari yeyote juu ya maamuzi yao, na
anaemuasi Allah na Mtume wake, hua amepotea na kuingia katika dhulma kubwa.
Na kisha aya inayofuatia katika Sura hiyo inaendelea kwa kusema kua:
﴿وَإِذْ تَقُولُ ۤ لِل َّذِي أَنعَمَ ٱهلل َُّ عَلَيْهِ وَأَنْعَمْتَ عَلَيْهِ أَمْسِ كْ عَلَيْكَ زَوْجَكَ وَٱت َّقِ ٱهلل ََّ
وَتخُْفِى فىِ نِفْسِ كَ مَا ٱهلل َُّ مُبْدِيهِ وَتخَْشَى ٱلن َّاسَ وَٱهلل َُّ أَحَق ُّ أَن تخَْشَاهُ فَلَ َّما قَضَ ٰ ى
ْم
زَيْدٌ مِّنْهَا وَطَراً زَو َّجْنَاكَهَا لِكَىْ لاَ يَكُونَ عَلَى ٱلْمُؤْمِنِينَ حَرَجٌ فيِ ۤ أَزْوَاجِ أَدْعِيَآئِهِ
إِذَا قَضَوْاْ مِنْهُن َّ وَطَراً وَكَانَ أَمْرُ ٱهلل َِّ مَفْعُولاً ﴾
Wa-idh taqoolu lilladhi anAAama Allahu AAalayhi waanAAamta AAalayhi amsik
AAalayka zawjaka waittaqi Allaha watukhfee fee Nafsika ma Allahu mubdeehi
watakhsha alnnasa waAllahu ahaqqu an takhshahu falamma qadha zaydun minha
wataran zawwajnakaha likay la yakoona AAala almu/mineena harajun fee azwaji
adAAiya-ihim itha qadaw minhunna wataran wakana amru Allahi mafAAoolan
(Surat Al Ahzab 33:37)
Tafsir: Na kumbuka pale ulipomwambia yeye (Zayd Ibn Harith) ambae juu yake Allah
amemuongoa (kwa kumuingiza katika Uislam), nawe (Muhammad pia) umemsaidia
(kwa kumkomboa utumwani), ‘Kaa nae Mke wako na muogope Mola wako’, lakini
kama ungelificha ndani ya Nafsi yako (kile alichokuwekea wazi Allah kua atakupa
Zaynab umuoe) kile Allah alichoweka wazi, ungeliwaogopa watu ambapo Allah ana
haki zaid ya kuogopewa, hivyo baada ya Zayd kutimiza hamu yake (kwa kumuacha),
Sisi tumekupa wewe umuoe, ili (baadae) iwe kuwe hakuna ugumu kwa Waumini
kuhusiana na (kuwaoa) wake wa watoto wa kuwalea wakati watoto hao wakiwa
hawana haja nao tena (Wameaacha). Na amri ya Allah ni lazima itekelezwe.
Dhumuni na kusudio la ndoa hii lilikua ni kukata mzizi mkuu wa desturi ya Jamii za
Kiarabu za kutoruhusu kuwaoa wake waliotalikiwa na watoto wao wa kulea. Na hapo
hapo kudhihirisha uthibitisho wa kufungishwa kwa Ndoa hio baina ya Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na Zaynab Bint Harith Radhi Allah Anha kutoka Mbinguni,
867
na hivyo Zayna Bint Harith Radhi Allahu Anha akawa ni mwenye kujisifu mbele ya Wake
wenzake wa Rasul Allah Salallah Alayhi wa Salam kwa kusema: ‘Hakika ni familia
zenu ndio zilizowafungishieni ndoa zenu lakini Ndoa yangu mimi imefungishwa na
Allah Subhanah wa Ta’ala kutoka kwenye Arshi yake.’ Na pia alisema: ‘Hakika
mimi nimekua na Walii bora kwani nyinyi ni familia zenu ndio zilizowafungishieni
ndoa zenu lakini Ndoa yangu mimi imefungishwa na Allah Subhanah wa Ta’ala
kutoka juu kwenye Mbingu ya 7.’
Ambapo kutokana na kuhisi utukufu wake na utofauti wake kidarja na wake wengine wa
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam basi Zaynab Bint Harith Radhi Allahu Anha
alikua ni mwenye kupenda sana kusali kuliko kitu chochote kile, kiasi ya kua hali ilifikia
kama anavyosema Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua: ‘Siku moja Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam aliingia Msikitini akakuta kuna kamba inaning’inia
baina ya nguzo mbili, hivyo akauliza: ‘Hii kamba ya nini?’ nae akajibiwa kwa
kuambiwa kua: ‘Ni kwa ajili ya Zaynab Bint Harith ambayo hua anaitumia
kujishikizia wakati anapokua amechoka kutokana na kusali sana na kwa mda
mrefu’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ifungueni, kwani
Mtu anatakiwa asali wakati akiwa anajisikia yuko vizuri na mwenye umakini,
lakini anapokosa umakini au anapokua amechoka basi hua anatakiwa apumzike’’
Hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam hakuweza kumtaliki mke wake
huyu kwa sababu ndoa yake hii ilikua imeshaandikwa na kuozeshwa na Allah Subhanahu
wa Ta’ala na pia mke huyo alikua anatoka katika ukoo mtukufu.
UMM AL MU’MININ RAMLA BINT ABU SUFYAN – UMMU HABIBA.
Mke wa sita wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua ni Umm Al
Muuminun Ramlah Bint Abu Sufyan au Umm Al Muuminun Ummu Habibah, alikua ni
mtoto wa Abu Sufyan ambae alikua ni mmoja kati ya mtu mkubwa na mwenye cheo
kikubwa katika kabila la Quraysh, Ummu Habibah aliingia katika Uislam na kupingana
na wazee wake na pia akahamia Uhabeshi yeye pamoja na mumewe aliekua akiitwa
Ubaidullah Ibn Jahsh ambapo baada ya kufika Uhabeshi, Ubaidullah aliingia katika
Ukristo na kumshawishi sana Ummu Habiba kuingia katika dini hiyo, lakini hata hivyo
Ummu Habibah akakataa, ingawa alikua Ummu Habibah ameachana na mume wake
huyo huku akiwa na mtoto wake mchanga aitwae Habibah, lakini Ummu Habibah alikua
na msimamo madhubuti ‘Mashaallah’ hakutetereka wala kuwa na wasi wasi wowote
bali alibakia na Imani yake ya Uislam na kuzidi kuikumbatia.
868
Subhana Allah! Ummu al Muuminina Ramlah Bint Abu Sufyan, Umm Habiba alibakia
na ile Imaan iliyomtoa katika giza la Ujahiliyyah na kumuingiza katika mwangaza, Imani
ambayo ilimfanya kua miongoni mwa Muhajirina wa mwanzo waliohama kwa ajili ya
kuinusuru na kuendeleza dini yao ya Kiislam, Imaan ambayo ndio ilimtoa katika mji wa
Makkah na kumpeleka katika ardhi ngeni ya Uhabesh na huko akabakia peke yake na
kumpoteza mume wake. Iman ambayo ilimtenganisha na iliyomvua cheo, hadhi ya
ukubwa unaotokana na jina la familia yake, ilimnyima utajiri na mali iliokuwepo katika
familia yake, familia ya kiongozi mkuu wa mji wa Makkah ambae ni Abu Sufyan.
Siku moja Ummu Habiba alilala kisha akaota kua ndani ya ndoto yake kuna mtu
anamwita: ‘Ya Umm Ul Muuminin!’ ambapo akaitafsiri ndoto hii maana yake kua
atakua ni mke wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam. Hazikupita siku nyingi
mara siku moja wakati yuko nyumbani kwake katika ardhi ya Habeshi akasikia Mlango
wake ukiwa unagongwa na alipoufungua mlango huo akakutana na Mfanyakazi wa Kike
wa An Najash ambae alileta Ujumbe kwa ajili yake kutoka kwa Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam kupitia kwa An Najash usemao kua Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam anataka amuoe Umm Habiba ili awe mke wake.
Ummu Habiba hakuamini masikio yake hivyo akamumba Mfanyakazi huyo wa An
Najash aurudie ujumbe huo mara 3 na kisha akasema: ‘Alhamd Lillah, Hakika Allah
amekupa Habari njema sana ewe Ummu Habibah.’ Na hapo hapo akavua mapambo
yote aliyokua nayo kwa furaha zake na kumpa Mtumwa huyo wa Mfalme Najash. Na
baada ya hapo Waislam waliokua kwenye ardhi ya Habeshi wakakusanyika kwenye
Kasri la An Najash kushuhudia ndoa hio ambayo ilifungishwa na An Najash mwenyewe
na Walii wa Ummu Habiba Radhi Allahu Anha akawa ni Khalid Ibn Said Radhi Allahu
Anhu ambae nae alikua ni mwenye kutoka katika Ukoo wa Banu Ummayah anaotoka
Umm Habiba pia.
Kisha ikafanywa Karamu kubwa na hii ilikua ni siku ya furaha kubwa sana ambapo
Ummu Habiba Radhi Allahu Anha mwenyewe anaielezea kwa kusema: ‘Wakati
nilipopokea Mahari yangu, basi nikachukua Mithakal 50 za dhahabu na kumtumia
yule mfanyakazi ambae alieniletea habari njema hizo kwa mara ya kwanza na
kumwambia : ‘Nakupa tena kile nilichokupa kwa sababu kwa wakati ule nilikua
sina pesa’ ambapo baadae Mfanyakazi huyo akanirudishia zile dhahabu nilizompa
mwanzo na kisha akanipa kisanduku ambacho kilikua kina Kidani nilichompa
hapo kabla, huku akisema: ‘An Najash ameniambia kua nisichukue kitu chochote
kutoka kwako, na badala yake amewaamrisha Wanawake wa Nyumbani kwake
kukuzawadia wewe Mafuta mazuri ya manukato ’’
‘Katika siku iliyofuata basi Yule mfanyakazi akaniletea mafuta ya manukato ya
kila aina na kisha akasema: ‘Nakuomba unisaidie kitu kimoja, kwani mimi sasa hivi
nimeingia kwenye Dini ya Kiislam na namfuata Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
869
Salam, hivyo nifikishie Salam zangu kwake na mwambie kua Mimi namuamini
Allah na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, nakuomba usisahau tafadhali.’’
Mnamo mwaka wa 7 Al Hijra basi Waislam waliokua wakishi katika Ardhi ya Uhabeshi
wakarudi katika Mji wa Madina ambapo miongoni mwao alikuwemo pia Umm Habiba
ambae anaelezea hali ilivyokua kwa kusema: ‘Wakati Rasul Allah Salalalhu Alayhi wa
Salam nilipokutana nae, basi nikamwambia kuhusiana na mipango yote ya harusi
namna ilivyokua imetayarishwa, na kuhusiana na uhusiano wangu na yule
Mfanyakazi wa kike, na kumwambia kua amekua Muislam na anamtumia salam
zake kwake, ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawa amejawa na
furaha kutokana na habari hizo na akasema: ‘Wa Alayha as Salaam wa Rahmat
Allahi wa Barakatuh’’
Umm Habiba Radhi Allahu Anha alikua ni mwanamke aliejitolea kwa ajili ya kutii
maamrisho ya Allah Subhaanh wa Ta’ala na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kiasi ya kua mara tu baada ya Makafiri wa Makkah, walipovunja makubaliano ya
Hudaybiyah basi wakaamua kutafuta suluhisho jipya kuhusiana na makubaliano hayo.
Hivyo wakamtuma Abu Sufyan kwa ajili ya kuenda Madina kwa ajili ya Kuzungumza
na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Hivyo Abu Sufyan alipofika akaenda kwanza kwa Bint yake ambae ni Umm Habiba
Radhi Allahu Anha ambae alikua na hamu nae sana kwa sababu hajamuona kwa mda wa
takriban miaka 6 na alipofika Chumbani kwake na kusalimiana nae basi akataka kukaa
Kitako kwenye kitanda kilichomo ndani yake, lakini Umm Habiba akamkataza kua
hatakiwi hata kukaa kwenye kitanda hicho.
Hivyo Abu Sufyan akauliza: ‘Kwanini? Jee mimi ni mzuri zaidi kukaa kwenye
kitanda hicho au?’ ambapo Umm Habiba akasema kumwambia Baba yake: ‘Itakuaje
Adui Mkubwa wa Uislam awe ni mwenye kukaa kwenye Kitanda cha Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam?’
Ingawa hali ilikua ni hivyo lakini mwaka mmoja baadae Umm Habiba Radhi Allahu Anha
alifurahi sana pale aliposikia kua Baba yake huyo na kaka yake yaani Abu Sufyan na
Muawwiya wamesilimu na kua Waislam, na hivyo akasujudu kwa ajili ya Kumshukuru
Allah Subhanah wa Ta’ala. Ummu Habiba Radhi Allahu Anha aliofarikai mnamo mwaka
44 Al Hijra akiwa na umri wa miaka 70
Hivyo ndoa hii baina ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na Ramlah Radhi
Allahu Anha ikawa ndio sababu kubwa iliyomfanya Abu Sufyan aingie katika Uislam
mwaka mmoja tu baadae. Tafakar ingelikuaje kama Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam angelimuacha Ummu al Muuminun Ramlah Bint Abu Sufyan.
870
UMM AL MU’MININ JUWAYRIYAH BINT HARITH.
Mke wa saba wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua ni Ummu Al
Muuminun Juwayriyyah Bint Al Harith ambae alikua ni mtoto Chifu mkuu wa kabila la
Bani Mustalaq. Kabila la Bani Mustalaq lilikua likiishi vituo vitano (vituo vya
kupumzikia wasafiri wa jangwani) kutoka katika mji wa Al Madinah . Watu wa kabila
hili walishirikiana na waarabu wa makabila mengine na kupanga shambulizi la
kushtukiza la kushambulia mji wa Madinah .
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akapata habari yao na hivyo akamtuma
mpelelezi aliekua akijulikana kwa jina la Barid ili kuenda kupeleleza habari hizo, baada
ya Barid kurudi na kuthibitiisha habari hizo, alirudi pia na habari zenye manufaa kwa
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, kua watu wa Bani Mustalaq pia
wametuma mpelelezi kuja kuwapeleleza Waislamu, wakati huo huo mpelelezi wao
akakamatwa na kuwafanya watu wa Bani Mustalaq kua hawana habari nini kinaendelea.
Hivyo kutokana na mipango hayo Waislamu wakawapa watu wa Bani Mustalaq pamoja
na wale walioshirikiana nao shambulizi la kushtukia na kuwashinda watu hao, na
kuwateka watu wengi na mali zao pia. Miongoni mwa waliotekwa alikuwemo pia mtoto
mkubwa wa kike wa Chifu wa kabila la Bani Mustalaq aliekua akiitwa Juwayriyyah
ambae alikataa kua mateka na kusema kua atajilipia fidya ili aachiwe huru.
Baada ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kujua hadhi na ukubwa wa bint
huyo kwa watu wake, akamuambia kua itakua haina haja ya kulipa fidya kama ikiwa
atakubali kuunganisha ukoo wake na kua pamoja na Waislam kwa kuolewa na Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, na Juwayriyyah akakubaliana na wazo hilo.
Hivyo wale wote waliokamatwa mateka kutokana na vita hivyo wakaachiwa huru baada
ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kumuoa Juwayriyyah.
Sayyida Aisha aliwahi kusema kua ‘Simjui mwanamke yeyote aliekua na bahati kwa
ukoo wake kama Juwayriyyah’. Watu wote wa ukoo wa Bani Mustalaq walisilimu
kutokana na ndoa hiyo baina ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na
Juwayriyyah, hivyo ingelikua tafrani pia kama Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam angeliamua kumuacha Ummu Al Muuminun Juwayriyyah.
871
UMM AL MU’MININ SAFIYYHA BINT HUYAY IBN AKHTTAB.
Ummu al Muuminun Safiyyah Bint Huyay Ibn Akhtab, alikua ni mke wa nane wa Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, nae alikua ni bint wa kiongozi wa kabila la
Bunu Nadir ambe alikua pia ni kiongozi wa Kiyahudi lililokua likiishi katika mji wa
Yathrib. Watu wa kabila la Banu Nadir waliandikiana mkataba na Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam kutopigana na Waislam, lakini baba yake Safiyah ambae
alikua ni Kiongozi wa Banu Nadir akapanga njama ya Kumuua Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwa kutaka kumtupia Jiwe juu ya kichwa wakati akiwa amekaa
akizungumza pamoja na Viongozi wengine wa Kiyahudi.
Hivyo Huyay akakamatwa na kufukuzwa katika Mji wa Madina, ambapo tukio hili
lilitokea mwaka wa 4 Al Hijra. Na akakimbilia katika maeneo ya Khaybar pamoja na
familia yake, ambapo miaka mitatu baadae Mayahudi hao wakavunja tena mkataba huo,
hivyo Waislamu wakawavamia na kuiteka ngome yao ya Khaybar.
Kuna Sahaba aliposikia kua ndani ya ngome hiyo alikuwemo pia Saffiyah, na alikua pia
ametekwa, hivyo akamfuata Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na
kumwambia kutokana na hadhi yake kwa watu wake, basi itakua si vizuri nae kuendelea
kukamatwa na kuwekwa pamoja na mateka wenzake kutokana na cheo chake na darja
yake. Ambapo akatumwa Bilal Ibn Rabah Radhi Allahu Anhu akamtoe katika sehemu
aliyowekwa na hivyo Bilal Ibn Rabah Radhi Allahu Anhu akamchukua Saffiyah na
Binamu yake na kuwapitisha mbele ya maiti za Wanaume wa Kiyahudi wa Khaybar
waliouliwa ambapo miongoni mwao alikuwemo pia Mumewe Saffiyah.
Wakati anapita kwenye eneo hilo basi Saffiyah alikua ni Binti mwenye Subra na
Ustahailivu jambo ambalo lilikua tofauti kwa upande wa Binamu yake ambae alikua
akilia kwa machungu, hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipoona tukio hili
basi akamwambia Bilal Ibn Rabah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Ewe Bilal hivi Allah
ameichomoa huruma ndani ya Moyo wako, kiasi ya kua umewapitisha Wanawake
wawili hawa mbele ya Waume zao waliouliwa?’
Ambapo anasema Safiyyah Radhi Allahu Anha kua: ‘Hakika Mimi nilikua ni m-bora
na kipenzi cha Baba yangu na pia kipenzi cha Mjomba wangu Yasir, kwani ilikua
kamwe haitokezei kwao wao kuniona mimi nikiwa pamoja na mmoja kati ya watoto
wao bila ya kunibeba mimi kabla ya wengine. Wakati alipokuja Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam katika Mji wa Madina, basi Baba yangu na Mjomba
wangu walienda kumsalimia, walitoka asubuhi mapema sana na hawakurudi
Nyumbani hadi jioni, huku wakiwa taabani wamechoka na pia wamevunjika
Moyo.’
872
‘Nilipowaona wanakuja basi nikawatabasamlia kama ilivyo kawaida, lakini hakuna
hata mmoja wao alieliona tabasam langu kutokana na hali yao, mara nikamsikia
Yasir akimuuliza Baba yangu: ‘Jee una uhakika Ndio Yeye?’ Baba yangu akasema:
‘Naam ndie yeye’ Yasir akauliza: ‘Jee unaweza ukathibitisha kua ndie yeye?’ Baba
yangu akajibu : ‘Naam, ndie yeye kwani mimi namjua vizuri’, Yasir akauliza: ‘Jee
unahisi nini juu yake?’ Baba akasema: ‘Uadui mkubwa nae, Uadui hadi mwisho wa
maisha yangu.’
Hali hii ilimstaajabisha sana Safiyyah kuona kua Baba yake na Mjomba wake ambao ni
miongoni mwa Viongozi wa Mayahudi wa Madina wanataka kumpiga vita Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam, Mtume ambae amebashiriwa kutokea kwake kwenye vitabu
vyao, hivyo Saffiya akajua kua Baba yake na Mjomba wake wanataka kumpiga vita Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwa sababu si Myahudi, bali ni Muarabu, na wao
walikua wanataka Mtume huyo awe Myahudi, ambapo tukio hili lilimvutia sana kihisia
Safiyyah kwa kumpenda Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika kipindi akiwa
bado ni Myahudi.
Hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akaamua kumuachia huru, lakini
Safiyyah akasilimu na hapo akaambiwa anaweza kuchagua kuondoka na kurudi katika
mji wake ama aolewe na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na kisha abakie
katika mji wa Madinah . Hivyo Saffiyah akaona kua bora kuolewa na Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam na kisha abakie Madinah na kusema: ‘Ya Rasul Allah,
hakika mimi nilipokua Myahudi nilikua naomba kua niolewe nawe, hivyo jee hali
yangu itakuaje baada ya kusilimu kwangu?’
Anasema Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam alikaa kwa siku tatu katia sehemu ya baina ya Khaybar na Madina, na katika
sehemu hio ndio akamuoa Saffiyah Bint Huyay, nami nikawaalika Waislam katika
karamu ambayo hakikua na Nyama wala Mkate, kwani Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam aliamrisha kutandikwe ngozi za kukalia wakati wa kula ardhini
na kisha ikawekwa Tende na Jibini na Siagi juu yake, na hio ndio iliyokua Karamu
ya Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam katika siku hio’
‘Waislam wakaulizana kama Saffiyah Bint Huyay atakua ni Mke wake Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam au atakua ni Mtumwa, na kisha wakaambiana kua:
‘Kama Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam atapita nae huku akiwa amemfunika
ili asionekane na Watu basi atakua ni Mke wake na kama atakua amepita nae akiwa
hakumfunika basi atakua ni Mtumwa wake’ Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alipokua tayari kwa safari basi akatayarisha Ngamia wake na
kumpandisha Safiyyah Nyuma yake huku akiwa amemfunika asionekane na
watu.’(Imam Bukhari)
873
Jeshi na msafara wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ulipowasilia katika Mji wa
Madina basi watu walizingira nyuma ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutaka
kumuona Mke mpya wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambapo miongoni mwao
walikuwemo pia wake wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, akiwemo Aisha Radhi
Allahu Anha ambae alikua amejificha miongoni mwa Wanawake hao, na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alipomuona basi akamkamata kanzu yake na kisha
akamuuliza: ‘Jee umeona nini ewe Shuqaira?’ Shuqaira ni mwanamke mwenye nywele
za Dhahabu.
Aisha Radhi Allahu Anha akasema huku akiwa amejawa na Wivu kua: ‘Ni Mwanamke
tu wa Kiyahudi’ ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Usiseme
Hivyo, Kwani ameingia na kuikumbatia Dini ya Kiislam.’ Ndoa hii baina ya Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na Safiyyah ilisababisha usalama na kuvunja
uadui wa wakati huo baina ya Waislam na Mayahudi wa Madinah .
UMM AL MU’MININ MARIA BINT SHAM.
Kuhusiana na Umm ul Mu’uminin Maria Bint Sham alikua ni Mtumwa aliekua
akimilikiwa na Gavana wa Misri aliekua akiitwa Muqawqis ambae alikua ni Mkristo,
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alimpelekea mwaliko wa kuingia katika
Uislam Gavana huyo kupitia kwa Hatib Ibn Abi Baltaa Radhi Allahu Anhu, na baada ya
kupata mualiko huo Muqawqis alimchukua Maria na Dada yake aitwa Sherine na zawadi
nyengine ikiwemo mifuko 1000 ya Dhahabu na Kanzu 20 na kumpelekea Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kama zawadi ya kualikwa katika jambo jema.
Wakati Maria akiwa njiani kuelekea Madinah alijifunza mambo mengi kuhusiana na
mmiliki wake mpya ambae ni Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam pamoja na
dini yake mpya ya Kiislamu, hivyo akaamua kusilimu kabla ya kukutana na Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam.
Maria Bint Sham Radhi Allahu Anha alikua akitoka kusini mwa ardhi ya Misri katika
kijiji kinachoitwa Hifn Ahzaaka katika upande wa Mashariki ya Mto Nile, Baba yake
alikua ni Mtu wa Misri na Mama yake alikua ni mtu mwenye asili ya Rumi. Maria Bint
Sham na Sherine walipofika katika Mji wa Madina basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam alikua ndio kwanza amerudi kutoka kwenye kufunga mkataba wa Hudaybiyyah,
hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamchukua Maria na kisha Sherine
akamkabidhi kwa Hasan Ibn Thabit Radhi Allahu Anhu.
Ambapo anasema Aisha Radhi Allahu Anah kua: ‘Mimi sikua na wivu wa wake
wengine wa Rasul Allah miongoni mwetu kama nilivyokua na wivu kwa Maria kwa
sababu alikua Mzuri na ni mwenye Nywele nzuri zilizo jipinda’
874
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutokana na mapenzi yake kwa Maria Bint Sham
Radhi Allahu Anha basi alimtafutia sehemu ya kuishi ambayo ni yenye mazingira ya
Misri katika ardhi ya Madina na hivyo akamchagulia eneo linalojulikana kama Aliaa
ambalo lina Miti na majani mengi mazingira ambayo yalikua ni kama mazingira ya
pembeni ya Mto Nile.
Ambapo kimaumbile na kimazingira basi tunaona kua kuna mfanano baina ya Maria na
Hajr ambae aliekua ni Mke wa Nabii Ibrahim ambae ndie mama yake Nabi Ismil, ambapo
wote wanawake wawili hawa ni wenye asili ya Misri, na haishangazi kuona kua Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipopata motto wake wa kiume kupitia kwa Maria
mwaka mmoja baadae basi akaamua kumuita Ibrahim, na huyu alikua ni Mtoto ambae
Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam akimpenda sana, kwani alipozaliwa tu alimchukua
na kumuonesha kwa Masahaba zake wote.
Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam alikaa na kumlea Ibrahim huku akiwa anakua
katika maumbile ya kawaida na ni mwenye kumfurahisha Rasul Allah Salallau Alayhi
wa Salam kutokana na afya yake na uzuri wake. Lakini ghafla mnamo mwaka wa pili wa
uhai wake, Ibrahim akaanza kuumwa na kisha akafariki dunia katika siku ya mwezi 10
Rabbi Al Awwal mwaka 10 Al Hijra.
Tukio hili lilimhuzunisha sana Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam na kasema: ‘Macho
yamejawa na machozi, na Moyo umejawa na Huzuni huku mimi nikiwa sina la
kusema isipokua lile litakalo mfurahisha Allah Subhanah wa Ta’ala, kua Ewe
Ibrahm hakika sisi tuna huzuni juu yako lakini hatuwezi kupingana na matakwa
yake Allah Subhanah wa Ta’ala’ kisha Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam
akamgekia Maria na kumwambia: ‘Hakika anae mlezi wake Peponi, hivyo miaka
iliyobakia ya kulelewa kwake atelelewa Peponi’
Katika siku ya Maziko yake Ibrahim Ibn Muhammad Rasul Allah Salallau Alayhi wa
Salam basi Jua na Mwezi vikapatwa ikawa kiza, na watu wakadhani kua hii ni kutokana
na kifo cha Ibrahim, lakini Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam akasema: ‘Jua na
Mwezi ni Dalili mbili kutoka kwa Allah, na hazihusiana na kufariki kwa mtu hivyo
mtakapoona vimepatwa basi kimbilieni katika Kumkumbuka Mola wenu katika
Sala.’
Abu Dhar Radhi Allahu Anhu anasema kuhusiana na Rasul Allah Salallau Alayhi wa
Salam na Maria Bint Sham na Ibrahim na Ardhi ya Misri kua: ‘Amesema Rasul Allah
Salallau Alayhi wa Salam kua: ‘Karibuni mtaiteka ardhi ya Misri na inajulikana
kua kam Ardhi ya Qirat, hivyo mtakapoiteka basi kuweni na huruma na watu wake
kwani ndani yake kuna jukumu la udugu wa kuoana nao na mnapowaona watu
wawli wanagombana baina yao hata kwa eneo la tofali basi msiiingilie’’
875
Ambapo anasema Abu Dhar Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi niliwaona Abd Rahman
Ibn Shurahbil Ibn Hasan na ndugu yake Rabia wanagombana juu ya eneo la Tofali,
hivyo nikaondoka’(Sahih Muslim)
Wanazuoni wamekhitilafiana kuhusiana na Maria bint Sham wengine wanasema kua
alikua ni Suria wake na wengine wanasema kua, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam hakumfanya Maria bint Sham kua Suria wake na badala yake alimuoa kisharia na
hivyo kuinyanyua darja yake baada ya kumuoa. Hivyo kabla ya kuendelea mbele zaid
katika kusoma kitabu hiki basi itakua ni vizuri kuweka wazi kwa kufafanua zaid
kuhusiana na neno Suria.
SURIYYAH NA MILK AL YAMIN KATIKA UISLAM
Neno la kiarabu Sariyyah ambalo kwa kiswahili tunaliita Suria linatokana na mzizi wa
neno Sin-Ra-Ra, lenye maana ya Siri, Furahia, Moyo, Asili, Chaguo, Harusi na Faragha.
Hivyo kwa matumizi na maana iliyokusudiwa hapa hua linamaanisha kua ni mwanamke
mtumwa au mwanamke alietekwa katika vita na hivyo mtumwa au mateka huyo wa kike
humilikiwa na mwanamme pasipo kuolewa na ambapo ameruhusiwa mwanamme huyo
kuwa na uhusiano nae wa faragha, wa kimapenzi na kuingiliana nae bila ya mwanamke
huyo kua na haki ya kisharia kwa mwanamme huyo. Hali hii ya kua na Suria ilikua ni
mila na desturi ambazo zilikuwepo na zilikua zinatumika tangu enzi za zamani katika
jamii mbali mbali duniani kabla ya kuja Uislam. Suria walikua ni miongoni mwa
watumwa wanawake au miongoni mwa mateka wanawake waliokamatwa vitani.
Hivyo baada ya kuanza Uislam baadhi ya mila na desturi zilikua zinaendelea kua kama
zilivyokua hadi pale iliposhuka amri ya kukataza mila na desturi hizo, miongoni mwa
mila na desturi hizo kama tulivyoona hapo awali ni pamoja na kua na wake zaidi ya
wanne, kua na Suria, kua na watumwa n.k ambapo ruhusa ya mambo yanayotokana na
mila na desturi hizo iliondolewa kidogo kidogo hatua kwa hatua.
Moja katika sifa ya Dini ya Kislam ni kua na ustahmilivu, hivyo inapotokea kukataza
kitu fulani basi kitu hicho huanzwa kukatazwa hatua baada ya hatua au kwa masharti,
hadi kufikia katika hali ya kukataza kabisa, mfano mmoja wa makatazo yaliyokatazwa
kwa njia kama hizo ni kuharamishwa kwa ulevi na vile vile kua na Suria, ingawa kua na
Suria hakujatazwa moja kwa moja lakini Qur’an na Sunnah zilipunguza uungaji mkono
wa jambo hilo pale ziliposhuka aya zilizokua zikisisitizia kua kuwaachia huru hua ni bora
zaid.
876
Tukiangalia kwa mfano aya ya 3 ya Surat an Nisaa tuliyokwisha itizama ambayo ilikua
inakataza mwisho kua na wake wanne, tunaona kua iliposhuka kukataza Waislam kua na
zaidi ya wake wanne haikukataza kua na Suria bali ilikua ikikhiyarisha kwa wale
watakaokosa kua na uadilifu basi waoe mke mmoja au wabakie na ‘Milk al Yamin’
(Kilichomo ndani ya umiliki wa kisharia wa mkono wa kulia) yaani wale wanaomilikiwa
baada ya kutekwa vitani au baada ya kua ni miongoni mwa wanaomilikiwa katika hali ya
utumwa katika wakati huo, aya hiyo imetumia hali ya maneno ya Malakat Aymanukum
kwa kusema:
﴿وَإِنْ خِ فْتُمْ أَلا َّ تُقْسِ طُواْ فىِ
ٱلْيَتَامَى ٰ فَٱنكِحُواْ مَا طَابَ لَكُمْ مِّنَ ٱلنِّسَآءِ مَثْنىَٰ
وَثُلاَثَ وَرُابَعَ فَإِنْ خِ فْتُمْ أَلا َّ تَعْدِلُواْ فَوَاحِ دَةً أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيمَْانُكُمْ ذٰلِكَ أَدْنىَٰ
أَلا َّ تَعُولُواْ ﴾
Wa-in khiftum alla tuqsitoo fee alyatama fainkihoo ma taba lakum mina alnnisa-i
mathna wathulatha warubaAAa fa-in khiftum alla taAAdiloo fawahidatan aw ma
malakat aymanukum dhalika adna alla taAAooloo. (Surat An-Nisaa’ 4:3).
Tafsir: Na ikiwa mnakhofu kua hamtoweza kuwafanyia haki mayatima, basi Oeni
wanawake wengine mnaowataka, wawili, au watatu, au wanne; lakini ikiwa mnakhofu
kua hamtoweza kuwafanyia uadilifu basi oeni mmoja tu, au wale mnaowamiliki
mikononi mwenu (Mliowateka vitani na Watumwa). Kufanya hivyo ni kukaribia
kujilinda na kutokua waadilifu.
Neno hili ‘Malakat aymanukum’ lenye kumaanisha ‘Kilichokuwemo ndani ya umiliki
wa mikono ya kulia’, limetumika mara kadhaa katika Qur’an katika hali na sehemu
tofauti kama vile:-
﴿مَا مَلَكْتَ أَيمَْنُكُمْ﴾
Ma malakat aymanukum - Kile kinachomilikiwa na mikono yenu ya kulia. (Surat An
Nisaa 4:24-25; Surat An Nisaa 4:36; Surat An Noor 24:33)
﴿وَمَا مَلَكَتْ يمَِينُكَ ﴾
Wa Ma malakat yaminuka – Na kile kinachomilikiwa na mkono wenu wa kulia.(Surat
Al Ahzab 33:50; Surat Al Ahzab 33:52)
﴿ٱل َّذِينَ مَلَكَ تْ أَيمَْانُكُ ْم ﴾
877
Aladhina malakat aymanukum - Wale ambao wanamilikiwa na mikono yenu ya
kulia.(Surat An Noor 24:58)
﴿مَا مَلَكَتْ أَيمَْنُهُمْ﴾
Ma malakat aymanuhum – Kile kinachomilikiwa na mikono yao ya kulia. (Surat An
Nahl 16:71; Surat Al Mu’minun 23:6)
﴿مَا
مَلَكَ تْ أَيمَْ نُهُ ن َّ ﴾
Ma malakat aymanuhunna – Kile kinachomilikiwa na mikono yao ya kulia
(Wanawake). (Surat An Noor 24:31; Surat Al Ahzab 33:55)
Tunapoangalia mfano wa aya ya 50 ya Surat Al Ahzab, tunaona kua Allah Subhanahu wa
Ta’ala alimhalalishia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kuoa wake
awatakao, na pia kua na Suria, (Aya hii ilishuka kabla ya kushuka ile aya
iliyomshuruitisha Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kutoongeza mke wala
kuacha mke) pale aliposema katika Qur’an kua:
﴿َٰٰي ُّهَا ٱلن َّبىِ ُّ إِ َّ أَحْلَلْنَا لَكَ أَزْوَاجَكَ ٱللا َّتيِ ۤ آتَيْتَ أُجُورَهُن َّ وَمَا مَلَكَتْ يمَِينُكَ
ممِ َّآ أَفَآءَ ٱهلل َُّ عَلَيْكَ وَبَنَاتِ عَمِّكَ وَبَنَاتِ عَم َّاتِكَ وَبَنَاتِ خَالِكَ وَبَنَاتِ
خَالاَتِكَ ٱللا َّتِى هَاجَرْنَ مَعَكَ وَٱمْرَأَةً م ُّؤْمِنَةً إِن وَهَبَتْ نَفْسَهَا لِلن َّبىِِّ إِنْ أََر اَد
ٱلن َّبىِ ُّ أَن يَسْتَنكِحَهَا خَالِصَةً ل َّكَ مِن دُونِ ٱلْمُؤْمِنِينَ قَدْ عَلِمْنَا مَا فَرَضْنَا عَلَيْهِمْ
فيِ ۤ أَزْوَاجِ هِمْ وَمَا مَلَكَتْ أَيمَْانُهُمْ لِكَيْلاَ يَكُونَ عَلَيْكَ حَرَجٌ وَكَانَ ٱهلل َُّ غَفُوراً
ر َّحِ يماً ﴾
Ya ayyuha alnnabiyyu inna ahlalna laka azwajaka allatee atayta ojoorahunna
wama malakat yameenuka mimma afaa Allahu AAalayka wabanati AAammika
wabanati AAammatika wabanati khalika wabanati khalatika allatee hajarna
maAAaka waimraatan mu/minatan in wahabat nafsaha lilnnabiyyi in arada
alnnabiyyu an yastankihaha khalisatan laka min dooni almu/mineena qad
AAalimna ma faradhna AAalayhim fee azwajihim wama malakat aymanuhum
likayla yakoona AAalayka harajun wakana Allahu ghafooran raheeman(Surat Al
Ahzab 33:50)
878
Tafsir: Ewe Nabii (Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam)! Kwa Hakika
tumekuhalalishia wake zako, ambao umewalipia mahari yao, na ambao mkono wako
wa kulia unawamiliki (wanawake waliotekwa vitani na watumwa) ambao Allah
amekupa, na binti wa Ami zako, bint wa Ammah (shangazi) zako, binti wa Khal
(wajomba) zako, binti wa Khalah (mama wadogo) ambao walihama (kutoka Makkah)
pamoja nawe, na mwanawake alieamini ikiwa atajipeleka (kutaka kuolewa) kwa
Mtume, na Mtume akataka kumuoa; Haki ambayo ni yako tu (kwa Nabii Muhammad
peke yake), lakini si kwa waumini wengine. Hakika tunajua ni kipi tulichowaamrisha
kuhusiana na wake zao na wale wanaomilikiwa na mikono yao ya kulia - Ili kusiwe na
uzito kwako wewe. Na Allah ni mwingi wa Kusamehe na mwingi wa Rehma.
Sehemu ya kwanza aya hii imewekwa wazi kua inamhusu Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam peke yake kwa kumwambia kua amehalalishiwa kuwaoa wanawake
wengine walioainishwa katika aya hiyo na pia kua na Masuria. Sehemu ya pili ya aya hii
ni kwa ajili ya Waumini waliobakia, kwani wao hawakuruhusiwa kuoa wanawake kama
wale ambao alioruhusiwa kuwaoa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam,
ingawa na wao pia waliruhusiwa kua na Suria, aya inaendelea kwa kusema kua hakika
Allah anajua ni kipi amewaamrisha Waislamu waliobakia kuhusiana na wanawake
wanaotakiwa kuwaoa, kwani aya ya 23-24 ya Surat An Nisaa tayari zimeshaainisha
wanawake ambao wameharamishwa kwa Waumini kuwaowa na baada ya kuainishiwa
aina za wanawake hao, aya hizo zikawaruhusu pia Waislamu kua na Suria kwa kutumia
maneno ‘illa ma malakat aymanukum’ yaani ‘Isipokua wale ambao mkono wenu wa
kulia unawamiliki’, kwa ufafanuzi zaid tuangalie zinavyosema aya hizo za Surat An
Nisaa:
﴿حُرِّمَتْ عَلَيْكُمْ أُم َّهَاتُكُمْ وَبَنَاتُكُمْ وَأَخَوَاتُكُمْ وَعَم َّاتُكُمْ وَخَالاَتُكُمْ وَبَنَاتُ ٱلأَخِ
وَبَنَاتُ ٱلأُخْتِ وَأُم َّهَاتُكُمُ اللا َّتِى أَرْضَعْنَكُمْ وَأَخَوَاتُكُم مِّنَ ٱلر َّضَاعَةِ َوأُم َّهَ ا ُت
نِسَآئِكُمْ وَرَابَئِبُكُمُ ٱللا َّتِى فىِ حُجُورِكُمْ مِّن نِّسَآئِكُمُ ٱللا َّتِى دَخَلْتُمْ هبِِن َّ فَإِن لم َّْ
ِمنْ أَصْ لاَبِكُ مْ وَأَن
تَكُونُواْ دَخَلْتُمْ هبِِن َّ فَلاَ جُنَاحَ عَلَيْكُمْ وَحَلاَئِلُ أَبْنَائِكُمُ ٱل َّذِينَ
تجَْمَعُواْ بَينَْ ٱلاخْتَينِْ إَلا َّ مَا قَدْ سَلَفَ إِن َّ ٱهلل ََّ كَانَ غَفُوراً ر َّحِ يماً
﴾
Hurrimat AAalaykum ommahatukum wabanatukum waakhawatukum
waAAammatukum wakhalatukum wabanatu al-akhi wabanatu al-okhti
waommahatukumu allatee ardaAAnakum waakhawatukum mina alrradaAAati
879
waommahatu nisa-ikum waraba-ibukumu allatee fee hujoorikum min nisa-ikumu
allatee dakhaltum bihinna fa-in lam takoonoo dakhaltum bihinna fala junaha
AAalaykum wahala-ilu abna-ikumu alladhina min aslabikum waan tajmaAAoo
bayna al-okhtayni illa ma qad salafa inna Allaha kana ghafooran raheeman (Surat
An Nisaa 4:23)
Tafsir: Mmeharamishiwa (Kuwaoa) mama zenu, dada zenu, dada wa baba zenu, dada
wa mama zenu, watoto wa ndugu zenu wa kiume, watoto wa ndugu zenu wa kike,
mama zenu waliokunyonyesheni, dada zenu mlionyonya nao, mama wa wake zenu,
watoto zenu wa kike wa kambo walio chini ya usimamizi wenu, waliozaliwa na wake
ambao mmeshawaingilia, lakini hamna tatizo ikiwa hamjawaingilia wake hao
(kuwaoa mabint zao), wake wa watoto wenu wa kiume waliotoka katika tupu zenu na
ndugu wawili wa kike kwa wakati mmoja, isipokua kwa yale yaliyokwisha pita;
Hakina, Allah ni mwingi wa kusamehe na ni mwingi wa Rehma.
Aya ya 24 ya sura hiyo ikamalizia kwa kuweka wazi aina ya wanawake wasioruhusika
kuolewa na wanaoruhusika kuolewa kwa kusema:
﴿وَٱلْمُحْصَنَاتُ مِنَ ٱلنِّسَآءِ إِلا َّ مَا مَلَكْتَ أَيمَْانُكُمْ كِتَابَ ٱهلل َِّ عَلَيْكُمْ وَأُحِ ل َّ لَكُمْ
م َّا وَرَاءَ ذٰلِكُمْ أَن تَبْتَغُواْ أبَِمْوَالِكُمْ مح ُّْصِنِينَ غَيْرَ مُسافِحِ ينَ فَمَا ٱسْتَمْتَعْتُمْ بِِه
ِد
مِنْهُن َّ فَآتُوهُن َّ أُجُورَهُن َّ فَرِيضَةً وَلاَ جُنَاحَ عَلَيْكُمْ فِيمَا تَرَاضَيْتُمْ بِهِ مِن بَعْ
﴾
َ
ٱلْفَرِيضَةِ إِن َّ ٱهلل ََّ كَانَ عَلِيماً حَكِيماً
Waalmuhsanatu mina alnnisa-i illa ma malakat aymanukum kitaba Allahi
AAalaykum waohilla lakum ma waraa dhalikum an tabtaghoo bi-amwalikum
muhsineena ghayra musafiheena fama istamtaAAtum bihi minhunna faatoohunna
ojoorahunna fareedhatan wala junaha AAalaykum feema taradaytum bihi min
baAAdi alfareedhati inna Allaha kana AAaleeman hakeeman (Surat An Nisaa 4:24)
Tafsir: Na (mmeharamishiwa) wanawake waliokwishaolewa, isipokua wale (illa ma
malakat aymanukum) ambao mkono wenu wa kulia unawamiliki. Hivyo Allah
amekupambieni, wote waliobakia kua ni halali juu yenu, pale mnapowataka kwa kutoa
Mahari kutoka katika mali zenu mkitaka usafi, bila ya kuingiliana ambako si kwa
kisheria, hivyo kwa wale ambao mshawaingilia basi wapeni mahari yao kama
ilivyoamrishwa, lakini baada ya kuamrishwa mahari mkikubaliana kupeana (zaid),
basi hamna dhambi. Kwa Hakika Allah ni mwenye kujua na ni Mwingi wa Busara.
880
Aya imetumia Neno Musafihiina linalotokana na neno Safaha ambalo hua linamaanisha
Kumwaga, Kutiririka au Kumimina. Hivyo neno Musafihun ambalo hua linamaanisha
Mtu anaemmwagia mwenzake au anaemwagiwa yaani anaefanya Usharati au Uzinifu.
MFUMO WA UTUMWA NA MATEKA WA VITA KATIKA UISLAM.
Tunapozungumzia asili ya Utumwa katika Uislam, basi inabidi lazima kuwekeana wazi
kua mfumo wa Maisha ya Dini ya Kiislam si mfumo ambao ndio ulioanzisha mfumo wa
kua na Watumwa Duniani, na pia si mfumo unaounga mkono Utumwa Duniani. Kwani
asili ya mfumo wa Utumwa inatokana na asili ya kutokea mapigano au vita baina ya
vizazi vya Ibn Adam, hivyo basi tunaweza kusema kua asili ya Utumwa inaenda
sambamba na asili ya vita, na Utumwa hutokana na matokeo ya vita, kwani mara tu baada
ya takriban kila vita kumalizika basi hua hutokea miongoni mwa mambo mawili
yafuatayo:
1- Kuwepo kwa watu watakaofariki, aidha iwe kwa upande wa walioshindwa, au
upande ulioshindwa au kwa pande zote mbili zilizopigana.
2- Kuwepo kwa watu watakaotekwa iwe kwa upande ulioshinda, ulioshindwa au
pande zote mbili. Na hivyo hali ya watu hao hutegemea na uhasama baina ya
pande mbili husika, kwani aidha wanaweza wakabadilishana mateka hao,
wakawaachia huru Mateka hao au wakabaki nao kama maadui zao na hivyo
kuwafanyisha kazi za Kitumwa dhidi yao.
Kwa upande wa Dini ya Kiislamu basi tunaona Uislam unakubaliana na mfumo wa
kukamata mateka katika wakati wa vita, kwani hali hiyo hua haiepukiki, kwa sababu hata
kama ikiwa Waislamu hawakukamata mateka, au watakamana lakini hawakuruhusiika
kuwafanya Watumwa mateka hao, basi Waislamu huenda nao wakakamatwa mateka na
kufanywa kua Watumwa.
Ingawa mara tu baada ya Waislamu kuwakamata mateka maadui zao, basi huchukuliwa
na kupelekwa kwa Amir mkuu wa Waislam ambae ndie hua na jukumu la kuwagawa
Mateka hao ambapo kama ikionekana kua kuna Wanawake miongoni mwa mateka hao,
basi kwa kila mpiganaji alieshiriki mapigano hayo, humilikishwa Mateka wake ambae
kisharia hua tayari ni Milk Al Yamin wake kulingana na idadi ya mateka hao, na hivyo
kila mtu aliepewa Milk al Yamin wake basi kisharia hua na haki ya kumuingilia
mwanamke kama anavyoweza kumuingilia mke wake, lakini vile vile kabla ya
kuingiliana nae huko basi kwanza hua kuna masharti yake kama vile ilivyokua kuna
masharti ya ndoa. Miongoni mwa masharti hayo ni:-
881
Kama vile ilivyokua hairuhusiki kwa Mwanamke kuolewa na waume wawili basi
vile vile Hairuhusiki kwa mwanamke mmoja kua na wamiliki wawili.
Hairuhusiki kumuingilia mwanamke alietekwa hadi pale ijulikane kama
mwanamke huyo alikua na mumewe hapo kabla katika ardhi ya Makafiri ama la,
na kama alikua ni mwenye kuolewa na hivyo amekamatwa peke yake bila ya mume
wake, basi inabidi kwanza ndoa hiyo ibatilishwe, kwa kumhamishia mwanamke
huyo katika ardhi ya Kiislam kiasi ya kua hakutokua na uwezekano wa kukutana
tena baina ya mwanamke huyo na Mumewe aliemuoa hapo kabla. Kumhamishia
mwanamke huyo katika ardhi ya Kiislam na Mumewe kubakia katika ardhi
isiyokua ya Kiislam, basi hubatilisha moja kwa moja ndoa hiyo.
Hairuhusiki kumuingilia Mwanamke alietekwa wakati mume wake akiwa pia ni
miongoni mwa waliotekwa.
Kama ilivyokua mwanamke alieachwa humbidi kusubiri kumalizika kipindi cha
‘Iddah’ basi vile vile kwa mwanamke alietekwa hua ni lazima nae asubiriwe amalize
kipindi kama hicho ambacho hua kinaitwa ’Istibraa’. Hivyo hairuhusiki
kumuingilia Mwanamke alietekwa hadi pale atakapomaliza Istibraa.
Kama ilivyokua kwa Mwanamke alieoloewa hua ni mwenye kumtegemea mume
wake kiusimamizi katika majukumu, basi vile vile Hairuhusiki kwa Mateka
kutomshughulikia kimajukumu, kwani ni jukumu la mmiliki kumshughulikia
Mateka wake kama anavyo mshughulikia mke wake.
Kama ilivyokua ndoa inamharamishia Mume kuwaoa ndugu wa damu wa Mke basi
vile vile Hairuhusiki kwa mmiliki kumuingilia au kumuoa ndugu wa damu wa
Mateka wake. n.k.
Lakini pia kwa upande mwengine ili kuondoa udhalilishwaji na uvunjwaji haki za
wanaokamatwa mateka basi Uislam unapendekeza kwani umeweka wazi kua inabidi
mateka hao waachiwe huru kwa makubaliano maalum baina ya pande mbili zilizopigana
iwe kwa kulipa fidya au bila kulipa fidya.
Qur’an na Sunnah zimetilia mkazo kua ni jambo jema kuwafanyia wema na kuwaachia
mateka na watumwa kama alivyosema Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
kua: ‘Mtu atakaekua na mateka wa kike, akamsomesha, na kumlea na
kumshughulikia kwa heshima na kisha akamuachia huru na kumuoa basi mtu huyo
hua na malipo mara mbili’(Sahih Bukhari).
882
Na katika Hadith nyengine amesema Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kua
‘Yeyote yule atakaemuacha huru Mtumwa Muislam, basi Allah ataviachia huru
viungo vyote vya mwili wake visiguswe na moto wa Jahannam kama vile yeye
alivyomuachia mtumwa huru huyo’(Muslim)
Moja katika A’mal njema ni kuwaoa mateka waliosilimu au watumwa walioachiwa huru
kwa sababu ya kuilinda heshima yao, kwani hua vigumu kwa mateka au mtumwa
kuolewa baada ya kuachwa huru, na vile vile hua rahisi kwa Waislamu wasiokua na
uwezo, kuwaoa mateka au watumwa hao, kama inavyotueleza Qur’an:
﴿وَمَن لم َّْ يَسْتَطِعْ مِنكُمْ طَوْلاً أَن يَنكِحَ ٱلْمُحْصَنَاتِ ٱلْمُؤْمِنَاتِ فَمِنْ م َّا مَلَكَتْ
أَيمَْانُكُم مِّن فَتَيَاتِكُمُ ٱلْمُؤْمِنَاتِ وَٱهلل َُّ أَعْلَمُ إبِِيمَانِكُمْ بَعْضُكُمْ مِّن بَْع ٍض
فَٱنكِحُوهُن َّ إبِِذْنِ أَهْلِهِن َّ وَآتُوهُن َّ أُجُورَهُن َّ بِٱلْمَعْرُوفِ محُْصَنَاتٍ غَيْرَ مُسَافِحَاتٍ
وَلاَ مُت َّخِ ذَاتِ أَخْدَانٍ فَإِذَآ أُحْصِن َّ فَإِنْ أَتَينَْ بِفَاحِ شَةٍ فَعَلَيِْهن َّ نِصْفُ مَا عَلَى
ٱلْمُحْصَنَاتِ مِنَ ٱلْعَذَابِ ذٰلِكَ لِمَنْ خَشِ ىَ ٱلْعَنَتَ مِنْكُمْ وَأَن تَصْبرُِواْ خَيْرٌ ل َّكُمْ
وَٱهلل َُّ غَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Waman lam yastatiAA minkum tawlan an yankiha almuhsanati almu/minati famin
ma malakat aymanukum min fatayatikumu almu/minati waAllahu aAAlamu bieemanikum
baAAdhukum min baAAdhin fainkihoohunna bi-idhni ahlihinna
waatoohunna ojoorahunna bialmaAAroofi muhsanatin ghayra masafihatin wala
muttakhidhati akhdanin fa-idha ohsinna fa-in atayna bifahishatin faAAalayhinna
nisfu ma AAala almuhsanati mina alAAadhabi dhalika liman khashiya alAAanata
minkum waan tasbiroo khayrun lakum waAllahu ghafoorun raheemun (Surat An
Nisaa 4:25)
Tafsir: Na ikiwa hamna uwezo wa kuoa wanawake walioamini waliokua huru, basi
mnaweza kuwaoa wanawake walioamini miongoni mwa waliotekwa na watumwa, na
Allah anajua kila kitu kuhusiana na Imani zenu baina yenu. Waoeni kwa ruhusa za
watu wao (wanaowamiliki, au waangangalizi wao) na mmwape mahari yao kutokana
na kile kinachotosheleza, wao (watumwa na mateka) wawe wasafi, na wasiwe wenye
kufanya zina, wala wasichukue wanaume na baada ya kuolewa, ikiwa watafanya zinaa
basi adhabu yao ni nusu ya wale wanawake waliokua (hawajaolewa) huru, Hii ni kwa
883
yule anaeogopa kudhuriwa kwa dini yake au kwa mwili wake. Lakini bora kwenu nyie
ikiwa mtakua na subra, Allah ni mwingi wa Kusamehe na mwingi wa rehma.
Miongoni mwa aya zilizosisitizia kuwakomboa, kuwaoa watumwa wa kike au
kuwaozesha watumwa wa kike kwa watumwa wa kiume ni pamoja na aya za 32 na 33 za
Surat An Noor zisemazo:
﴿وَأَنْكِحُواْ ٰ ٱلأََمَى مِنْكُمْ وَٱلص َّالحِِينَ مِنْ عِبَادِكُمْ وَإِمائِكُمْ إِن يَكُونُواْ فُقَرَآءَ
يُغْنِهِمُ ٱهلل َُّ مِن فَضْلِهِ وَٱهلل َُّ وَاسِ عٌ عَلِيمٌ ﴾
Waankihoo al-ayama minkum waalssaliheena min AAibadikum wa-ima-ikum in
yakoonoo fuqaraa yughnihimu Allahu min fadhlihi waAllahu wasiAAun
AAaleemun. (Surat An Noor 24:32)
Tafsir: Na ozesheni miongoni mwa Al Ayyama, au wafanyao a’mali njema miongoni
mwa watumwa wenu wa kiume na wa kike: Ikiwa wako katika hali ya umasikini Allah
atawapa fadhila zake, kwani kwa hakika Allah ni mwingi wa kila kitu na ni mwenye
kujua kila kitu.
Neno ‘Al Ayyama’ ambalo ni wingi wa Ayyim linamaanisha mjane awe mwanamme au
mwanammke awe aliewahi kuoa au kuolewa kabla au hajawahi kuoa au kuolewa kabla.
Kisha ikafuatia aya isemayo:
﴿وَلْيَسْتَعْفِفِ ٱل َّذِينَ لاَ يجَِدُونَ نِكَاحاً حَتى َّ ٰ يُغْنِيَهُمُ ٱهلل َُّ مِن فَضْلِهِ وَٱل َّذِينَ
يَبْتَغُونَ الْكِتَابَ ممِ َّا مَلَكَتْ أَيمَْانُكُمْ فَكَاتِبُوهُمْ إِنْ عَلِمُتُمْ فِيهِمْ خَيرْ اً وَآتُوهُمْ مِّن
م َّالِ ٱهلل َِّ ۤ ٱل َّذِي آاتَكُمْ وَلاَ تُكْرِهُواْ فَتَيَاتِكُمْ عَلَى ٱلْبِغَآءِ إِنْ أَرَدْنَ تحََص ُّناً لِّتَبْتَغُواْ
عَرَضَ ٱلحَْيَاةِ ٱلد ُّنْيَا وَمَن يُكْرِههُن َّ فِإِن َّ ٱهلل ََّ مِن بَعْدِ إِكْرَاهِهِن َّ غَفُورٌ ر َّحِ يٌم ﴾
WalyastaAAfifi alladhina la yajidoona nikahan hatta yughniyahumu Allahu min
fadhlihi waalladhina yabtaghoona alkitaba mimma malakat aymanukum
fakatiboohum in AAalimtum feehim khayran waatoohum min mali Allahi alladhi
atakum wala tukrihoo fatayatikum AAala albigha-i in aradna tahassunan
884
litabtaghoo AAarada alhayati alddunya waman yukrihhunna fa-inna Allaha min
baAAdi ikrahihinna ghafoorun raheemun (Surat An Noor 24:33)
Tafsir: Na waachieni wale waliokua hawana uwezo wa kipesa wa kuoa wakae
wajihifadhi (wasifanye maasi), hadi pale Allah atakapowapa uwezo kwa fadhila zake.
Na miongoni mwa mnaowamiliki wakitaka kuandikiwa mkataba wa uhuru wao,
waandikieni hivyo, ikiwa mnawajua kua ni waaminifu. Na wapeni baadhi ya mali zenu
zinazotokana na utajiri wa Allah aliokupeni juu yenu. Na msiwalazimishe kufanya
ukahaba, ikiwa wanataka usafi, ili mpate kunufaika kidunia. Lakini ikiwa mmoja
wenu atawalizimisha (ukahaba), basi baada ya kulazimishwa huko, Allah ni mwenye
kusamehe na ni mwingi wa rehma (Atawasamehe wanawake hao kutokana na
kulazimishwa kwao kufanya dhambi hiyo).
Tukiangalia katika aya hizo tutaona kua Allah Subhanahu wa Ta’ala anatoa ruhsa ya
kuwaoa Milk al yamiin au waliokua wakimilikiwa kwa njia ya utumwa na mateka wa
vita, hii ni moja ya kati ya njia za kuwaachia huru, na njia nyengine ni kufungiana nao
mkataba usemao kua mtumwa au mateka anaweza kufanya kazi halafu akakatwa
mshahara wake hadi kumaliziana kiwango watakachokubaliana na mmiliki wake, na
baada ya kutimia kiwango hicho mtumwa huyo anaweza kua huru kutokana na
makubaliano ya mkataba huo, vile vile aya hizo zinakataza kuwavunjia haki watumwa
au mateka hao.
Miongoni mwa njia alizotumia Allah Subhanahu wa Ta’ala kuondoa utumwa kidogo
kidogo hatua kwa hatua ni pamoja na kafara za viapo, kama inavyoonesha Qur’an:
﴿لاَ يُؤَاخِ ذُكُمُ ٱهلل َُّ بِٱلل َّغْوِ فيِ ۤ أَيمَْانِكُمْ وَلَٰكِن يُؤَاخِ ذُكُم بمَِا عَق َّدتم ُُّ ٱلأَيمَْانَ فَكَف َّارَتُهُ
إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِ نْ أَوْ سَ طِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْ لِيكُمْ أَوْ كِسْ وَتُهُ مْ أَوْ تحَْرِيُر رَقَبٍَة
فَمَن لم َّْ يجَِدْ فَصِيَامُ ثَلاَثَةِ أَ َّمٍ ذٰلِكَ كَف َّارَةُ أَيمَْانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۤ وَٱحْفَظُواْ ا أَيمَْ نَ كُْم
كَذٰ لِكَ يُبَينِّ ُ ٱهلل َُّ لَكُمْ آَتِهِ لَعَل َّكُمْ تَشْ كُرُو َن
﴾
La yu-akhidhukumu Allahu biallaghwi fee aymanikum walakin yu-akhidhukum
bima AAaqqadtumu al-aymana fakaffaratuhu itAAamu AAasharati masakeena
min awsati ma tutAAimoona ahleekum aw kiswatuhum aw tahreeru raqabatin
faman lam yajid fasiyamu thalathati ayyamin dhalika kaffaratu aymanikum itha
halaftum waihfadhoo aymanakum kadhalika yubayyinu Allahu lakum ayatihi
laAAallakum tashkuroona (Surat Al Maidah 5:89)
Tafsir: Allah hatokuadhibuni kwa viapo vyenu msivyovikusudia, lakini atakuadhibuni
885
kwa yale mliyoyakusudia kuyaapia, na kafara yake ni kuwalisha maskini kumi,
kutokana na kipomo cha kile mnachoilisha familia zenu, au kuwavisha, au kuachia
huru watumwa, lakini asiekua na uwezo wa hayo basi na afunge kwa siku tatu; hii ni
kafara kwa viapo vyenu pale mnapo apa; hivyo lindeni viapo vyenu (msiape ovyo ovyo),
hivyo Allah anaweka wazi ili muwe na shukran.
Miongoni mwa mifano miengine ni katika aya inayozungumzia kafara ya Talaka ya
Zihar, n.k.
﴿وَٱل َّذِينَ يُظَاهِرُونَ مِن نِّسَآئِهِمْ ثمُ َّ يَعُودُونَ لِمَا قَالُواْ فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مِّن قَبْلِ أَن
يَتَمَآس َّا ذٰلِكُمْ تُوعَظُونَ بِهِ وَٱهلل َُّ بمَِا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴾
Waalladhina yudhahiroona min nisa-ihim thumma yaAAoodoona lima qaloo
fatahreeru raqabatin min qabli an yatamassa dhalikum tooAAadhoona bihi
waAllahu bima taAAmaloona khabeerun (Surat Al Mujadala 58:3)
Tafsir: Na kwa wale wanaojiharamishia wake zao kwa kuwafananisha migongo yao
na migongo ya mama zao, basi huweza kuyarudisha yale waliyoyasema, wamuachie
huru mtumwa kabla ya kugusana tena (kurudiana) juu ya hayo mnapewa onyo (ili
msirudie mambo hayo) na Allah anajua kila mnachokifanya.
Kwa upande wa Hadith ziko nyingi na moja miongoni mwao ni ile ya Abd Allah Ibn
Umar Radhi Allahu Anhu, ambae alimwita mtumwa wake na akamuona ana alama ya
kupigwa mgongoni mwake, Abd Allah Ibn Umar Radhi Allahu Anhu akamuuliza
‘Nimekusababishia maumivu?’ yule mtumwa akajibu ‘La’ hapo Abd Allah Ibn Umar
Radhi Allahu Anhu akasema ‘Hapana, kuanzia sasa hivi uko huru’. Halafu akaokota
kijiwe ardhini na kusema, ‘Sina nililolipata, hata kulingana na uzito wa hiki, kwani
nimemsikia Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akisema kua: Yeyote
yule anaempiga mtumwa wake bila ya kosa linalofahamika, au akampiga kibao tu
basi kafara yake ni kumuachia huru mtumwa huyo.’ (Sahih Muslim)
Kwa kutilia mkazo umuhimu wa kuwaachia huru na kuwalipia fidya zao watumwa na
mateka waliokua hawana uwezo wa kujilipia ili kua huru, basi Qur’an katika kuainisha
watu wanaohitaji kufaidika na pesa za Zakkah, imesema kua miongoni mwao ni
watumwa, iwe kwa kuwalipia kwa wamiliki wao wawe huru ama kuwapa wao wenyewe
wakajikomboa, kama inavyosema Surat At Tawba:
﴿إِنم ََّا ٱلص َّدَقَاتُ لِلْفُقَرَآءِ وَٱلْمَسَاكِينِ وَٱلْعَامِلِينَ عَلَيْهَا وَٱلْمُؤَل َّفَةِ قُلُوبُهُمْ وَِفى
ٱلرِّقَابِ وَٱلْغَارِمِينَ وَفىِ سَبِيلِ ٱهلل َِّ وَٱبْنِ ٱلس َّبِيلِ فَرِيضَةً مِّنَ ٱهلل َِّ وَٱهلل َُّ َعلِيٌم
886
حَكِيمٌ ﴾
Innama alssadaqatu lilfuqara-i waalmasakeeni waalAAamileena AAalayha
waalmu-allafati quloobuhum wafee alrriqabi waalgharimeena wafee sabeeli Allahi
waibni alssabeeli fareedatan mina Allahi waAllahu AAaleemun hakeemun (Surat At
Tawba 9:60)
Tafsir: Hakika ya Sadaka (Zakkah) ni kwa ajili aya Mafukara, Masikini, na
walioajiriwa kukusanya Zakkah; na kuzivutia nyoyo za wale waliokua wamevutiwa na
Uislam; na kuwaachia huru Watumwa; na wale wanye madeni; na kwa ajili ya njia ya
Allah, na kwa msafiri (aliefikwa na matatizo na kukwama na akawa hana pesa za
kuendelea na safari yake); huo ni wajibu uliowekwa na Allah. Kwa hakika Allah ni
mjuzi wa kila kitu na ni mwingi wa Busara.
Baada ya kuangalia maana ya Suria na Milk al Yamini basi tunatakiwa tufahamu kua hali
inayoruhusu watu kua na Suria na Milk al Yamini kwa kisharia haipo tena katika wakati
huu tuliokua nao, na hii ni kutokana na mambo mengi sana miongoni mwao ni pamoja
na uhimizwaji wa kuondolewa kwa utumwa, kutokuwepo kwa uadilifu miongoni mwa
Waislam na hivyo kutoweka kwa hali ya kuhalisha mapigano ya vita vya Jihad kwa ajili
ya Allah Subhanah wa Ta’ala, n.k
Kwani Sharia’h ya Kiislam inasema kua kukakamata mateka na kua na watumwa
hairuhusiwi pale inapokua hakuna kiongozi Muadilifu anaeongoza Ummah wa Kiislam
yaani Khalifah Muadilifu, na kunaruhusika pale inapotokea vita vya Jihad
vilivyoruhusika kisharia, hata hivyo bado kuna kipingamizi cha kuwaachia huru bila ya
kuwalipisha fidya wale waliotekwa ili kuonesha ukarimu.
Ingawa katika ulimwengu wa leo hakuna hali ya kuhalalisha utumwa kutokana na
mtizamo wa Sharia’h wa dini ya Kiislam na pia Sharia’h za kilimwengu, lakini hata
hivyo utumwa bado upo na miongoni mwa utumwa huo ni pamoja na watu kufungwa
jela bila ya kua na makosa, au kua na hatia, kwa mfano wakati Marekani na washirika
wake, walipoamua kueneza mamlaka yao ili kuweza kuchota mafuta na gesi kwa urahisi
katika maeneo ya Mashariki ya kati na hivyo kuvamia nchi kama Afghanistan, Iraq,
Yemen, Libya n.k walikamata watu mbali mbali waliokuwemo na wasiokuwemo kwa
kisingizio cha ugaidi na kuwaweka ndani jela za nchi mbali mbali, na si katika nchi hizo
tu bali watumwa au mateka wa aina hii wamo katika takriban magereza ya kila nchi
duniani.
Vile vile kuna utumwa mwengine ambao bado unaendelea katika baadhi ya sehemu
duniani kutokana na umasikini, ambapo watu masikini huhadaiwa kupatiwa kazi kutoka
887
katika nchi moja hadi nchi nyengine, lakini matokeo yake mambo hua si kama
walivyotegemea hivyo hufanyishwa kazi ambazo hazina tofauti na utumwa kutokana na
kunyanyaswa au pia kulipwa chini ya kiwango kinachoridhisha kisharia, hivyo watu hao
hubakia katika kazi hizo kwa sababu hawana tena uwezo wa kurudi walikotoka, na pia
hata wakirudi wengine walikopa pesa za matayarisho ya safari hizo wakiwa na malengo
ya kua watalipa baada ya kupata mshahara unaotokana na kazi hizo, hivyo inabidi
hawawezi kurudi bila ya kua na uwezo wa kurudisha walichokopa.
Huu pia hua ni utumwa, unaoendelea katika nchi mbali mbali duniani, hususan katika
nchi za Uarabuni, na ukweli ni kua Uislamu unapinga sana mambo kama haya, na ndio
maana ukawainisha watu kama hawa kua ni miongoni mwa wanaofaa kupewa pesa za
Zakkah ili waweze kujikomboa kutokana na matatizo yao, katika kusisitizia kuwaonea
huruma watu kama hawa na watu walio chini ya mamalaka yetu, anasema Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kua:
‘Wafanyakazi wenu ni ndugu zenu, Allah amewaweka chini ya usimamizi wenu.
Kama angelitaka basi angelikuwekeni nyinyi chini ya usimamizi wao, hivyo yeyote
yule ambae ana ndugu yake chini ya usimamizi wake, basi amlishe kile anachokula
yeye na amvishe kile anachovaa yeye, msiwape kazi zilizokuwepo nje ya uwezo wao,
ikiwa kazi ni ngumu kwao basi wasaidieni’.
Vile vile anasema Abu Mas'ud Al Ansari : ‘Nilikua nikimpiga mfanyakazi wangu,
mara nikasikia sauti ikisema kutoka nyuma kwangu: ‘Ya Abu Masoud, kumbuka
kua Allah ana mamlaka makubwa zaid ya hayo uliyokua nayo wewe kwake yeye
(huyo anaempiga)’, nilipogeuka nikamuona Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam.
Nikasema: ‘Nimemuachia huru kwa ajili ya Allah’. Na hapo Rasul Allah Salallahu
A’layhi wa Salam akasema: ‘Kama usingelifanya hivyo basi mlango wa Jahannam
ungelifunguka kwa ajili yako, au moto wa Jahannam ungelikuunguza.’’ (Sahih
Muslim, Kitab Al Iman)
Alisema Nabii Muhammad Sallahu A’layhi wa Salam alisema katika khutba yake ya
kuagia kua: ‘Na watumwa wenu hakikisheni kua mnawalisha kile ambacho mnakula
nyinyi na mnawavisha kile ambacho mnavaa nyinyi, na wanapofanya makosa
ambapo mtashindwa kuwasamehe basi wauzeni, kwani wao ni waja wa Allah na
hawastahiki kuadhibiwa’.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua akihimiza uadilifu baina ya watu
katika familia, katika jamii n.k, kwani Uislam haukutofautisha baina ya alie juu
kimamlaka na alie chini, mwenye nguvu na alie dhaifu, masikini na tajiri, mwanamme
na mwanamke n.k, na uadilifu huu ndio uliowavutia watu wengi miongoni mwa wasiokua
Waislamu kuingia katika mfumo wa maisha ya dini ya Kiislamu.
888
AAL, AHL, ZAWJ NA QAWWAM KATIKA UISLAM.
Maneno ya kiarabu A’hl na Al kwa kilugha yana maana moja ambayo hua ni kuoa,
kuzoea, kukaribisha, familia, jamii ya watu wenye kuishi ndani ya nyumba moja au
sehemu moja walio chini ya msimamizi mmoja ambae hua ni Mume au Baba, vile vile
maana ya neno hili pia hutumika kuelezea uhusiano wa kutegemeana baina ya mume na
mke ambapo ndani ya uhusiano huo huingia pia watoto, ndugu na jamaa wanaohudumiwa
na msimamizi wa familia husika.
Ambapo neno Zawj kwa kilugha humaanisha ‘Pea moja ya kitu’ na vie vile humaanisha
ndoa, na pia hua na maana ya Mume pale mzungumzaji anapokua ni Mke na humaanisha
Mke pale mzungumzaji anapokua ni Mume. Kiislam tunapozungumzia kuhusiana na
suala la Zawj yaani familia ya Mume na Mke, basi hua hamna suali la ni nani bora
miongoni mwao, kwa sababu Qur’an inawaona wote wawili kua ni “Zawj” (Wawili
wanaokamilishana bila ya mmoja kuonekana bora na kujaribu kua juu ya mwenzake),
anasema Ibn Manzur katika Lisan Al Arab kua : ‘Mfano mzuri wa maana ya neno
Zawaj hua ni ‘Zawja Na’il’ (Pea ya viatu), kwani mtu hua hajiulizi ni kipi kiatu bora,
cha kulia au cha kushoto?’
Tukiangalia jamii za watu wa zamani kabla ya kuja kwa Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam basi tuaona kua ilikua hakuna hali ya kuthaminiwa kwa A’hl, Aila wala
Zawj ambao hua wanajumuisha familia katika jamii, hususan pale inapokua wanafamilia
hao wanapokua ni wanawake. Kiasi ya kua hali ilifikia watu kuona aibu kubwa sana pale
wanapojaaliwa kupata mtoto wa kike na hivyo kua ni jambo la kawaida kwa mzee
kumzika mzima mzima mtoto wake wa kike asiekua na hatia yeyote. Allah Subhanahu
wa Ta’ala anatuthibitishia haya katika Qurán kwa kuhoji na kukataza pale aliposema:
﴿وَإِذَا ٱلْمَوْءُودَةُ سُئِلَتْ -
أبَِىِّ ذَنبٍ قُتِلَتْ ﴾
Waidha almawuudat suilat, Bi ayyi dhanbi Qutilat (Surat At Takwir 81:8-9)
Tafsir: Na Mtoto wa kike aliezikwa akiwa hai atakapoenda kuulizwa, Alifanya dhambi
gani iliyompelekea yeye kukatiliwa Nafsi yake.
Hivyo ndivyo hali ilivyokua katika zama Jahiliyah, lakini mitizamo hiyo katika jamii
ilianza kubadilika, baada ya kuja Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam baada
ya kushuka aya tuliyoiangalia na aya nyenginezo ambazo zinazosisitizia kua Wanaume
na Wanawake si mtu na mmiliki wake bali ni wenye kusaidiana kimajukumu baina yao,
kama tunavyoona vile isemavyo aya inayofuatia:
889
﴿وَٱلْمُؤْمِنُونَ وَٱلْمُؤْمِنَاتِ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَآءُ بَعْضٍ َْمُرُونَ بِٱلْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ
ٱلْمُنْكَرِ وَيُقِيمُونَ ٱلص َّلواَةَ وَيُؤْتُونَ ٱلز َّكَواةَ وَيُطِيعُونَ ٱهلل ََّ وَرَسُولَهُ أُوْلَٰئِكَ سَيَرْحمَُهُ ُم
ٱهلل َُّ إِن َّ ٱهلل ََّ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾
Waalmu/minoona waalmu/minatu baAAduhum awliyao baAAdin ya/muroona
bialmaAAroofi wayanhawna AAani almunkari wayuqeemoona alssalata
wayu/toona alzzakata wayuteeAAoona Allaha warasoolahu ola-ika
sayarhamuhumu Allahu inna Allaha AAazeezun hakeemun (Surat At Tawba 9:71)
Tafsir: Na Waumini, Wanaume na Wanawake wao kwa wao ni wasaidizi wenye
kusaidiana, huamrishana mema na kukatazana maovu, wanasali, na kutoa Zakkah na
kumtii Allah na Mtume wake (Sala Allahu A’layhi wa Salam). Allah atawaingiza
katika Rehma zake. Hakika Allah ni mwenye uwezo na mwenye Hikma.
Hii inaonesha kua Waumini wa kiume na wa kike wako sawa sawa kiutukufu lakini
wanatofautiana katika baadhi ya mambo ya kimajukumu kama inavyoweka wazi aya
inayofuatia kwa kusema:
﴿وَلهَُن َّ مِثْلُ ٱل َّذِى عَلَيْهِن َّ بِٱلْمَعْرُوفِ وَلِلرِّجَالِ عَلَيْهِن َّ دَرَجَةٌ وَٱهلل َُّ عَزِيزٌ حَكُيٌم ﴾
Walahunna mithlu alladhee AAalayhinna bialmaAAroofi walilrrijali AAalayhinna
darajatun waAllahu AAazeezun hakeemun (Surat Al Baqara 2:228)
Tafsir: Na wao (Wake) wana haki (juu ya Waume zao) kama vile (zilivyo haki za
Waume) juu yao kwa namna inavyofaa. Lakini Wanaume wana darja juu yao. Na
hakika Allah ni mwenye Uwezo na mwingi wa Hikma.
Darja hiyo ya Wanaume dhidi ya wanawake katika familia hua si ya kiutukufu bali hua
ni ya kimajukumu ya kuwashughulikia katika kuwahudumia wanawake na familia nzima
kwa ujumla, hali hii inafafanulika zaidi pale tunapoangalia katika aya inayofuatia ambayo
inasema kua:
890
﴿ٱلرِّجَالُ قَو َّامُونَ عَلَى ٱلنِّسَآءِ بمَِا فَ َّضلَ ٱهلل َُّ بَعْضَهُمْ عَلَى ٰ بَعْضٍ وَبمَِآ أَنْفَقُواْ مِ ْن
أَمْ وَالهِِمْ﴾
Alrrijalu qawwamoona AAala alnnisa-i bima fadhdhala Allahu baAAdhahum
AAala baAAdhin wabima anfaqoo min amwalihim (Surat An Nisaa 4:34)
Tafsir: Wanaume ni Qawwamoona (wasimamizi) juu ya Wanawake kwa sababu Allah
amewafadhili baadhi yao (Wanaume) juu ya baadhi yao (Wanawake) kutokana na kile
wanachokichuma na kukitumia juu yao.
Maana ya neno Qawwam kwa kilugha hua linamaanisha kusimamia au kuhudumia kitu
kwa muda mrefu, hivyo tunapozungumzia kifamilia basi neno hili hua linajumuisha
jukumu la kusimamia kimwili, kimahitaji, kiheshima na kimajukumu kwa upande wa
kidunia na kiakhera.
Hivyo maana ya neno Qawwam hua kamwe haimaanishi kama vile wanavyofikiria watu
wengi kua maana yake ni kudhibiti, kuweka chini yake au chini ya mamlaka yake, kwani
kufikiria hivyo basi hua ni kama walivyokua wakifanya jamii za watu wa Kijahiliyyah.
Katika kuieleze maana ya aya hii, basi anasema Imam Fakhr al Din Al Razi kuhusiana
na aya hii ya Surat An Nisaa 4:34 kua: ‘Alrrijalu qawwamoona AAala alnnisa-i
(Wanaume ni wasimamizi wa Wanawake) ina uhusiano na aya nyengine kabla yake
isemayo:
﴿وَلاَ تَتَمَن َّوْاْ مَا فَض َّلَ ٱهلل َُّ بِهِ بَعْضَكُمْ عَلَى ٰ بَعْضٍ ﴾
Wala tatamannaw ma fadhala Allahu bihi baAAdhakum AAala baAAdhin’(Surat
An Nisaa 4:32)
Tafsir: Na wala msitamani kile ambacho Allah amewafadhili baadhi yenu kuliko
wengine.
Imam Fakhr Ad Din Al Razi anaendelea kwa kusema: Aya ambayo tulisema kua
ilishushwa kwa sababu baadhi ya Wanawake walitoa kauli kuhusiana na Allah
kuwapendelea katika Urithi Wanaume. Hivyo Allah ameweka wazi katika ayah hii
kua amewafadhili tu Wanaume juu ya Wanwake kwa sababu Wanaume ni
Wasimamizi wa Wanawake. Kwani ingawa wote Mke na Mume wanafaidika na
matunda na haki zinazotokana na kua pamoja, basi Allah amemuamrisha
891
Mwanamme kumlipa Mwanamke sehemu ya ndoa yao, na kumhudumia katika
mahitaji ya kila siku, hivyo ongezeko la upande mmoja hukabiliana na ongezeko la
upande wa pili – na hivyo hua kama vile hamna pendeleo baina yao. Jambo hili
linaweka wazi mpangilio wa namna zilivyopangika aya.’
Hivyo darja ya Qawwam aliyokua nayo mwanamme kwa familia yake hua ni kuilinda,
kuisimania na kuwahudumia A’al, Ahl, Zawj au familia yake katika hali ya kiuadilifu, na
hapa msimamizi husika hua anatakiwa kuitumia fadhila hiyo aliyopewa na Allah
Subhanah wa Ta’ala, kwa kua na umakini, huruma, busara na subra katika kutekeleza
majukumu hayo, kwani vyenginevyo itakua ni kuenda kinyume na matakwa ya mfadhili
na mtoaji wa majukumu hayo na hivyo mwanamme husika hupoteza haki ya kua na Darja
hiyo ya Qawwam.
Ndio maana Allah Subhanahu wa Ta’ala akawaambia wale walioamini katika Qur’an
kwa kusema:
﴿أَي ُّهَا ٱل َّذِينَ آمَنُواْ ۤ قُواْ أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ َراً وَقُودُهَا ٱلن َّاسُ وَٱلحِْجَارَةُ عَلَْيهَا
مَلاَئِكَةٌ غِلاَظٌ شِ دَادٌ لا َّ يَعْصُونَ ٱهلل ََّ مَآ أَمَرَهُمْ وَيَفْعَلُونَ مَا يُؤْمَرُونَ ﴾
Ya ayyuha alladheena amanoo qoo anfusakum waahleekum naran waqooduha
alnnasu waalhijaratu AAalayha mala-ikatun ghiladhun shidadun la yaAAsoona
Allaha ma amarahum wayafAAaloona ma yu/maroona(Surat At Tahrim 66:6)
Tafsir: Enyi mlioamini, ziokoeni Nafsi zenu na Ahlikum (familia zenu) kutokana na
Moto ambao kuni zake ni watu na mawe, ambao unasimamiwa na Malaika wakali na
wenye nguvu, ambao kamwe hawaasi amri wanazozipokea kutoka kwa Allah, bali
hufanya kile wanachoamrishwa.
Hivyo basi hadhi ya Darja hiyo aliyopewa Msimamizi wa familia na ugumu wa jukumu
hilo unaoneka wazi pale tuunapoona una jukumu la Qawwam ni pamoja na kuwaokoa
ahli zake kutokana na moto kwani vyenginevyo atakuja kukimbizana nao katika siku ya
siku kama unavyoelezewa katika aya zinayofuatia:
﴿ يَوْ مَ يَفِر ُّ ٱلْمَ رْءُ مِ نْ أَخِ يهِ -
وَأَبِيهِ وَأُمِّ هِ
- وَ صَ حِبَتِهُوَبَنِي هِ ﴾
Yawma yafirru almaro min akheehi; Waommihi waabeehi; Wasahibatihi
wabaneehi (Surat Abasa 80:34-36)
892
Tafsir: Siku ambayo mtu atamkimbia ndugu yake; Na Mama yake na Baba yake; na
Mke wake na Watoto wake.
Aya hii inaweka wazi kua Mtu au Qawwam atakaikimbia familia yake, Mama yake, Baba
yake mke wake na Watoto wake yaani Ahl zake, Aila wake na Zawj wake ambao ni
jukumu lake, pale watakapomtaka awajibu ni kwa sababu gani hakuwa muadilifu juu yao
katika kuwatekelezea majukumu yao ipasavyo.
Amesema Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kua:
Khayrukum, khayrukum li ahlihi, wa ana khayrukum li ahlihi.
خَيْرُكُمْ خَيْرُكُمْ لأَِهْلِهِ، وَأََ خَيْرُكُمْ لأَِهْلِي
‘Mbora miongoni mwenu ni yule alie mbora kwa familia yake, na mimi ni mbora
miongoni mwenu kwa familia yangu’. (Imam Ibn Majah)
Hivyo Kiislam ni wajibu kwa Mwanamme ambae ni Baba, Kaka au Mume kua mbora
kwa kuwasimamia, kuwahudumia na kuwatekelezea majukumu yao yote wale walio
chini yake katika familia. Kwani wakati Mwanamme yupo katika kazi ya kuwatafutia
rizki na mahitaji yao mengine ya lazima, basi Mwanamke ambae hua ni Mama, Dada au
Mke yeye jukumu lake hua ni kuwasimamia, kuwatunza, kuwalea na kuwaanda watoto
na familia katika muelekeo wa maisha yao ya baadae. Kutokana na hali hii basi ndio
maana Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alipoulizwa baina ya wazee wawili
Baba na Mama ni yupi wa kumheshimu na kumpenda na kumshughulikia zaidi alijibu:
‘Mama, kisha Mama, kisha Mama kisha Baba’.
Uislam haukumpa hadhi Mama pekee, bali umeupa hadhi upande wote wa mzee wa Kike
ambao kwa Kiislam hujumuisha Mama, Shangazi wa Upande wa Mama, Shangazi wa
Upande wa Baba, Bibi, Mke wa Baba n.k, kama tunavyoona katika Hadith ya Abd Allah
Ibn ‘Umar isemayo: ‘Kuna mtu alikuja kwa Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam
na kusema: ‘Hakika mimi nimefanya dhambi kubwa, Jee kuna jambo ambalo
nnaweza kulifanya kufidia dhambi hiyo?’ Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam
akamuuliza: ‘Jee unae Mama?’ Yule mtu akajibu: ‘La!’, Rasul Allah Salallahu
A’layhi wa Salam akamuuliza tena : ‘Unae Shangazi wa Upande wa Mama?’ Yule
mtu akajibu: ‘Naam’ Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akamwambia yule
mtu: ‘Basi mfanyie wema na umhumdumie sana.’’
Hadhi hii haipo kwa wanawake watu wazima tu bali pia kwa watoto wa kike na ndugu
zetu wa kike kwani amesema Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam: ‘Hakuna yeyote
katika Ummah wangu ambae mwenye watoto watatu wa kike au ndugu watatu wa
893
kike, na kisha akawasimamia na kuwahudumia hadi wakawa wakubwa, isipokua
atakua pamoja nami Peponi kama hivi – Huku akionesha vidole vyake viwili cha
shahada na cha kati vikiwa pamoja’ (Al Awsat na Majmaá Al Zawaid)
Anasema pia Abu Hurayrah kua amesema Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam kua
: ‘Yeyote yule mwenye watoto watatu wa kike, akawahudumia, akawafurahisha
huku akiwa na subira, basi Allah Subhanahu wa Ta’ala atamuingiza Peponi mtu
huyo kutokana na kuwa na huruma juu yao’ mtu mmoja akauliza: ‘Vipi kama
ikiwa mtu huyo ana watoto wawili wa kike?’ Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam
akasema: ‘Hata kama akiwa na wawili’, mtu mwengine akauliza: ‘Ya Rasul Allah,
Vipi akiwa na mmoja tu?’, Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Hata
kama akiwa na mmoja tu.’’
Anasema Abd Allah Ibn `Abbas kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu A’layhi wa
Salam kua : ‘Yeyote yule mwenye kupata mtoto wa kike, na akawa hakumzika au
kumfedhehesha na akawa hakumpendelea mtoto wake wa kiume dhidi ya mtoto
wake wa kike, basi Allah Subhanahu wa Ta’ala atamuingiza Peponi kwa ajili yake.’’
Tukiangalia hali ilivyokua kabla ya kuja kwa Nabii Muhammad Sallahu A’layhi wa
Salam, kutokana na Hadith ya Jafar Ibn Abu Talib ambae ni Ibn Ami wa Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam katika kumuainishia Ashama Ibn Abjar ambae
ni maarufu kama Mfalme Najash baada ya kuwauliza Waislam mara tu walipowasili
nchini Uhabeshi au Ethiopia kwa kujibu swali lifuatalo alilowauliza, ‘Jee ni ipi iliyokua
dini yenu ya kwanza kabla ya dini yenu hii mpya? Jee ni hii dini yenu mpya ni dini
gani? Na kwanini mkahamia katika nchi yangu?’
Jafar Ibn Abu Talib aliuelzea Uislam kwa kusema: ‘Ewe Mfalme, sisi tulikua ni watu
wajinga, tuliokua tukiishi kama wanyama wa mwituni, mwenye nguvu miongoni
mwetu aliishi kwa kuwatumia wasiokua na nguvu. Tulikua hatuna sheria yeyote,
na tulikua hatuna mamlaka isipokua wenye nguvu dhidi ya wasiokua na nguvu.
Tulikua tukiabudu masanamu yaliyotengenezwa kutokana na udongo au miti, na
hatukujua heshima wala maana ya utu. Halafu Mungu akatushushia Rehma zake,
akatutumia Mtume kutoka miongoni mwetu, ambae anafahamika kutokana na
ukweli na uaminifu wake, tabia zake ni mfano wa kuingwa miongoni mwetu, na ni
mwenye kutoka katika ukoo bora miongoni mwa waarabu. Akatuita katika
kumuabudu Mungu mmoja, na akatukataza kuyaabudia masanamu, akatuamrisha
kusema ukweli, kuwalinda wasiokua na nguvu, masikini, wanyonge, wajane na
mayatima. Ametuamrisha kuwaheshimu wanawake na tusiwasingizie mambo ya
uongo. Wengi miongoni mwa watu wetu bado ni wenye kua na miungu mingi na
wanachukia maamuzi yetu ya kujiunga na Imani mpya ambayo inayoitwa Uislam.
894
Hivyo wameanza kututeketeza, na ni katika kukimbia mauaji yao ndio tukafuata
usalama katika Ufalme wako.’
Ingawa Jafar Ibn Abi Talib alikua ni Ibn Ami wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam lakini pia alikua ni miongoni mwa Masahaba watano waliotoka katika ukoo
wa Banu Hashim waliofanana sana kisura na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam wakiwemo pia Hasan Ibn Ali Ibn Abi Talib (mjukuu wa Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam), Abu Sufyan Ibn Al Harith, As Sayb Ibn Ubayd (Babu wa
babu yake Imam Al Shafi’i) na Qutham Ibn Al Abbas.
Bila ya kuyatumia maneno aliyoyasema Jabir Ibn Abi Talib kua kama ushahidi wa
ukombozi wa watu wa aina tofauti basi tunaona wazi kua Nabii Salallahu A’layhi wa
Salam alikua ni mfano wa kuigwa na ni Nuru iliyokuja kumurika mambo mengi
yaliyokua hayafai lakini yalikua yakifanywa katika jamii, na hivyo kumurika na
kuonesha heshima na haki za wanyonge, watumwa, masikini, wanawake, mayatima na
kadhalika katika jamii.
Anasema Abu Huraira, kua: ‘Alikuja mtu kwa Rasul Allah Salallahu A’layhi wa
Salam na kumlalamikia, kuhusiana na ugumu wa Moyo wake, ambapo Rasul Allah
Salallahu A’layhi wa Salam akamwambia: ‘Kama unataka kua na Moyo mlaini basi
walishe Masikini na wafariji Mayatima’
Vile vile akasema Sahl Ibn Sa’d kua, ‘Nabii Salallahu A’layhi wa Salam alisema ‘Mimi
na anaelea Mayatima tuko kama hivi Peponi’ na akagusanisha kidole chake cha
Shahada na kidole chake cha kati kwa pamoja.’
Tukiangalia katika Hadith nyengine basi tunaona jinsi Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam anavyotufundisha namna unavyotakiwa kua uhusiano katika familia
kama vile anavyosema, Sayyida Aisha kua: ‘Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam
amesema: ‘Kwa hakika miongoni mwa Waumini waliokua na Imani bora kabisa,
basi ni wale wenye tabia nzuri za kupendeza na wale wenye kuzifanyia wema zaidi
familia zao.’’ Vile vile tunayaona haya katika ile Hadith maarufu ya Jabir Ibn Abd Allah
ambae alikua ni miongoni mwa Masahaba vijana waliooa wakiwa na umri wa miaka 18
kua:
Safari moja alikua katika msafara pamoja na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi
wa Salam, na walipokaribia mji wa Madinah , yeye akaanza kuongeza mwendo juu
ya kipando chake. Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamuuliza
imekuaje mbona anaharakia kurudi nyumbani? Jabir akajibu: ‘Mimi nimeoa hivi
karibuni’, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamuuliza : ‘Umeoa
mjane au mwari?’ Jabir akajibu: ‘Mjane’.
895
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Ah sasa kwa nini hukuoa
mwanamke kijana, ambae ungeweza kucheza nae, na yeye akacheza pamoja nawe,
akakuchekesha na wewe ukamchekesha?’
Jabir akasema: ‘Ya Rasul Allah! Baba yangu alikufa Shahid katika vita vya Uhud,
hivyo akawacha nyuma yake watoto wadogo wa kike, hivyo sikuona haja ya kuoa
mwanamke mdogo kama wao, niliona bora nioe mwanamke mkubwa ambae
atakaeweza kuwasimamia wadogo zangu’, Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam akasema: ‘Naam, Umefanya uamuzi wa Busara kabisa’
Jabir anaendelea kusema: ‘Hivyo tulipo karibia kuingia mjini, Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam akaniambia, punguza mwendo, na usubiri usiku ndio
uingie, ili kwa yule ambae hajachana nywele zake azichane, na yule aliekua
hakunyoa sehemu zake za siri apate kunyoa’. Kisha akaniambia: ‘Utakapomuingilia
basi kua na busara na upole’. (Sahih Bukhari na Sahih Muslim)
Hadith hii inatuonesha ukweli na uwazi kua Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam katika familia kuhusiana na kuishi kwa kupendana, kuhurumiana, kuridhiana,
kufurahishana, kusaidiana n.k baina ya mwanamme na mwanamke, watu wazima na
watoto, familia na jamii nzima kwa ujumla.
Anasema Al-Aswad kua siku moja: ‘Nilimuuliza Aisha, `Jee Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam alikua akikaa nyumbani hufanya nini?’ Aisha akajibu,
‘Alikua akisaidia familia yake na akisikia Adhana basi hutoka nje kuenda kusali.’
(Imam Bukhari).
Hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, alikua akikaa na wake zake na pia
kuwasaidia kazi mbali mbali, ijapokua miongoni mwa wake zake wote aliowaoa, hakuna
aliekua mke aliekua mdogo kiumri, mwari na bikra isipokua Ummu ul Mu’minina A’isha
bint Abu Bakr pekee na wengine waliobakia walikua ni wajane, waliofiwa na waume zao
vitani na pia walikua ni watu wazima na wakubwa pia kiumri lakini alikua akikaa nao na
kuwasadia bila kupendelea.
Wanazuoni wa Hadith wanasema kua kuna Hadith zilizopokewa na wake wa Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ziko takriban 3000, kati ya hizo Hadith 2210
zinatoka kwa Aisha Umm ul Mu’minina, 378 zinatoka kwa Ummu Salama Umm ul
Mu’minin na wake wengine waliobakia wamepokea Hadith baina ya 11 hadi 65, na hii
inategemea na mda aliokaa mke huyo kwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
kabla ya kufariki kwake na vile vile inategemea na mda wa kuolewa kwa mke huyo na
kukaa na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kabla ya kufariki kwake.
896
Mbali ya kua na wake wengi katika maisha yake, lakini tukiyazingatia maisha ya Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kabla ya kuoa kwake, baada ya kuoa kwake na
namna alivyokua akiishi na wake zake tutaona kua ni ya mfano wa kuigwa katika kuishi
kwa uadilifu, heshima, upendo, ukarimu na huruma kwa wake zetu na familia zetu.
Anasema Sayyida Aisha kua: ‘Siku moja alikuja Bedui kwa Rasul Allah na akasema:
‘Unawabusu watoto wako, wakati sisi hatufanyi hivyo.’ Rasul Allahi Salallahu
A’layhi wa Salam akasema: ‘Sina la kukufanyieni pale itakapotokea kua Allah
Subhanahu wa Ta’ala atakapoziondoa Rehma katika nyoyo zenu’’(Imam Bukhari)
Maisha yake na wake zake yanatufundisha kua wanawake ni watu walio huru kisharia,
hawawezi kuolewa bila ya ridhaa yao, wanayo haki ya kukaa na majina yao baada ya
kuolewa, wanayo haki ya kudhibiti mali zao, wanayo haki ya kurithi mali, wanayo haki
ya kubatilisha ndoa zao pale inapotokea unyanyaswaji au kuvunjiwa haki zao, wanayo
haki ya kuishi katika jamii kama vile wanavyoishi watu wengine, wanayo haki ya
kufanya Ibada zote zinazofanywa na wanaume n.k.
Kama anavyosema Allah Subhanahu wa Ta’ala katika Qur’an:
﴿مَنْ عَمِلَ صَالحِ اً مِّن ذَكَرٍ أَوْ ٰ أُنْثَى وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَنُحْيِيَن َّهُ حَيَاةً طَيِّبَةً وَلَنَجْزِيَ ن َّ هُ ْم
أَجْرَهُم أبَِحْسَنِ مَا كَانُواْ يَعْمَلُونَ ﴾
Man AAamila salihan min dhakarin aw untha wahuwa mu/minun
falanuhyiyannahu hayatan tayyibatan walanajziyannahum ajrahum bi-ahsani ma
kanoo yaAAmaloona. (Surat An Nahl 16:97)
Tafsir: Yeyote yule atakaefanya jema awe mwanamme au mwanamke na akawa ni
Mu’umini wa kweli, basi kwa hakika tutampa maisha mapya yaliyo masafi na mazuri,
na tutamlipa kutokana na ubora wa vitendo vyake.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua pia akikaa na kushauriana nao
wake zake na kusikiliza ushauri wao na moja kati ya mfano wa hilo ni pale baada ya
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kusaini Mkataba wa Hudaybiyyah,
aliposema kuwaambia Masahaba zake ‘Nyanyukeni, mchinje wanyama wenu na kisha
mnyoe nywele zenu’, hata hivyo hakuna hata Sahaba mmoja alienyanyua mguu wake
kufanya vile alivyoamrisha Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, kutokana na
kuvunjika moyo kwa yale yaliyotokea katika makubaliano ya mkataba huo.
897
Hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akanyanyuka na kuenda kwa Ummu
Salama na kumwambia yaliyotokea na hapo Ummu Salama akamwambia Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ‘Ya Rasul Allah, unataka maneno yako
yafanyiwe kazi? Basi nenda nje na usizungumze na mtu yeyote hadi pale
utakapomaliza kuchinja mnyama wako na kunyoa nywele zako’, hapo Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akatoka nje akachinja mnyama wake na kuanza
kunyoa nywele zake, na baada ya Masahaba kumuona Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam anafanya hivyo basi na wao wakanyanyuka na kufanya kama vile
alivyofanya. (Imam Bukhari)
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua pia akikaa na kutaniana na wake
zake, kama inavyothibitisha Hadith ya Nu’man Ibn Bishr isemayo kua siku moja ‘Abu
Bakr alikuja na kugonga mlango na kuomba ruhusa kuingia ndani kwa Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, akamsikia A’isha akimpandishia sauti
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, hivyo baada ya kuruhusiwa kuingia
ndani, Abu Bakr akaingia ndani na kumkamata A’isha na kumwambia, ‘Ewe mtoto
wa Umm Ruman kwa nini unanyanyua sauti zaid ya Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam?’.
Hapo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akaingilia kati na kumzuia
Abu Bakr asimpige mtoto wake mbele yake, Abu Bakr alipoondoka Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akamliwaza A’isha na kumwambia
‘Unaona nilivyokuokoa kutoka kwake?’, baada ya muda Abu Bakr akarudi na
kupiga hodi, alipokaribishwa, akawaona Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam na A’isha wanacheka na kutaniana. ‘Abu Bakr akasema, niruhusuni niwe
sehemu ya amani yenu kama mlivyoniruhusu kua sehemu ya mgogoro
wenu.’’(Imam Ahmad)
Katika Hadith nyengine ya Imam Al Tirmidhi isemayo kua, ‘Siku moja kutokana na
wivu aliokua nao A’isha kwa Safiyyah, A’isha alimwambia Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam, jee umeona jinsi Saffiyah alivyokua mfupi?, hapo Nabii
Muhammad Salallahu Alayhi wa Salaam akajibu ‘Hakika umesema kitu ambacho,
kama kingelichanganywa na bahari basi bahari yote ingelichafuka’’, hapa tunaona
namna Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alivyokua akiishi na wake zake
wote kwa uadilifu.
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alisema: Muogopeni Allah kuhusiana
na Mwanamke, kwani kwa hakika mmewaoa kutokana na Amanah ya Allah na
kuihalalisha miili yao juu yenu kwa kutumia maneno ya Allah, Mna haki juu yao
na wao wana haki juu yenu, kuhusiana na mavazi na vyakula vyao.
898
Mwanazuoni wa Hadith na mtafiti wa mambo ya Kiislam katika karne yetu aitwae
Muhammad Akram Nadwi anasema katika kufanya uchunguzi wake juu ya hadhi na darja
wa Wanawake katika Uislamu katika Qur’an na vitabu mbali mbali vya Hadith kua:
‘Mwanammke anapokua Mtoto, basi humfungulia mlango wa Pepo baba yake,
anapokua Mke, hukamilisha nusu ya Dini ya Mume wake na anapokua Mama basi
Pepo hua chini ya Miguu yake.’, Muhammad Akram Nadwi anaendelea kwa kusema:
‘Kama kila mtu angelikua anaijua thamani hasa ya mwanamke katika dini ya
Kiislam, basi hata wanaume wangeliona kua bora wangelikua Wanawake’.
Vile vile Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, alikua ni mwenye
kuwashirikisha wanawake katika mambo mbali mbali wenye utaalamu nayo katika
kunyanyua mapato yao na kujenga uchumi wa jamii ya Kiislam, kwani vile vile
wanawake wanayo haki ya kuendelea kufanya kazi za kiuchumi kwa ajili ya maisha yao,
kwa mfano Umm ul Mu’minina Zaynab bint Jahsh al Asadiya alikua ni mtaalamu
mkubwa wa kazi za mikono ikiwemo, kufuma vitambaa na kushona nguo na mapambo
mbali mbali, na vile vile mke wa Abd Allah Ibn Masoud ambae aliekua mahiri katika
utengenezaji wa mafuta mazuri na walikua wakiendeleza fani zao na bila kuvunjiwa haki
zao katika uendelezaji wa shughuli zao mbali mbali ikiwemo pia kupigana katika vita
vya Jihad kwa waliokua na uwezo huo.
Miongoni mwa wanawake waliokua katika harakati za kupigana Jihad wakati wa Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ni pamoja na : Umm Salim Ibn Malhan, Umm
Haram bint Malhan, Umm Al-Harith Al-Ansariyah, Ar-Rubayy’ bint Mu‘widh, Umm
Sanan al-Aslamiyyah, Umm Salit, Layla Al-Ghiffariyah, Ku‘aybah Bint Sa‘id Al-
Aslamiyah, Himnah, Umm Ziyad Al-Ashja‘yah bint Jahsh, Rufaidat bint Ka’ab al
Aslamiyyat; Aminat Bint Qays al Ghifariyyat; Umm ‘Atiyyah al Anasariyyat; Nusaibat
Bint Ka’ab al Maziniyyat; Umm 'Atiyyah al Ansariyat al Khadfidhat, Zainab Al Awd
ambae alikua ni mtaalamu wa macho na Rufaydah Bint Saad Al-Ansariyah n.k
Ambapo Rufaydah Bint Saad Al Ansariyah alietoka katika ukooo wa Bani Aslam kabila
la Al Khazraj alikua ni Daktari mkuu wa Jeshi la Kiislam takriban katika kila vita
alivyopigana Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, kiasi ya kua ilikua ni jambo
la kawaida katika uwanja wa vita kusikia kauli zisemazo ‘Mpelekeni katika Hema la
Rufaydah’, pale Mujahidina wanapojeruhiwa katika vita, kwani Hema la Rufaydah
lilikua ndio hospitali ya kila majeruhi miongoni mwa majeshi ya Kiislam, hospitali
ambayo ilikua ikihama na kuhamia katika kila sehemu wanayopigana vita Waislam.
Miongoni mwa wasaidizi wa Rufayda Al Ansarriya ni pamoja na Aminah, Umm Ayman,
Safiyat, Umm Sulaim na Hind.
Vile vile kuna Umm Ammara ambae pia anajulikana kama Nusaibat bint Ka'ab bin Amru
bin 'Awf bin Mabdhool bin 'Amru bin Ghanam bin Mazin bin al Najjar al Ansariyat,
ambae aliolewa na Zayd Ibn Asim na hivyo kupata watoto wawili Abd Allah na Habiib.
899
Ummu Ammara alikua anaiongoza familia yake yote kwa pamoja katika kuwahudumia
Waislam vitani kwa matibabu na majumbani. Umm Ammara alikua na familia yake
alikua ni miongoni mwa waliopigana na kusaidia katika vita vya Uhud kiasi ya kua hali
ya vita ilipobadilika na kua mbaya kwa upande wa Waislam aliamua kukamata upanga
na kumhami Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam. Umm Ammara pia
alihudhuria katika vita vya Yamammah.
Vile vile kuna Layla bint Abdullah bin Abd Shams bin Khalaf bin Shadad al-Qurashiyah
al-Adawiyah, ambae maarufu kama Shifaa Al Adawiyah au Umm Sulaiman, aliitwa Ash
Shifaa kwa sababu ya kua ni mwenye I’lm kubwa ya mambo mbali mbali ikiwemo
kuandika, kusoma na vile vile uwezo mkubwa wa kutibu kwa kutumia Ruqya, alipewa
ruhusa na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kutibu kwa kutumia Ruqya na
pia akawa mwalimu wa wanawake wengine akiwemo pia Hafsah Umm ul Muuminina.
Hali hii ni tofauti na wanavyofikiria wengi wasiomjua Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam, wasioujua Uislam na kuupinga na vile vile wasioijua historia ya watu
wa Magharibi, kwani wao huona kua Uislam unawabana kiakili, kifikra na pia
kuwavunjia wanawake haki zao, wakati ukweli ni kua Uislamu umewakomboa
Wanawake na kuwapa haki zao kwa miaka 1000 kabla ya hata watu wa Magharibi
kuanza kufikiria kuhusu haki za Wanawake, na ndio maana Hairunisaa Gul ambae ni
mke wa aliekua Rais wa Uturuki kuhusiana na Hijab yake akasema kua: ‘Hijabu yangu
ni kwa ajili ya kufunika kichwa changu, si kwa ajili ya kufunika akili zangu.’
Kwani hadi kufikia katika karne ya 17 wanawake wa Magharibi walikua kama
anavyoelezea Muingereza aliekua mpiganiaji wa haki za wanawake wa nchi za
Magharibi, aitwae Mary Wollstonecraft (1759-1797) kua: ‘Wanawake wa wakati
wangu wanafungwa kama vile ndege kwenye vijumba vyao, hawana la kufanya ila
kujipamba kwa kutumia unyoya na kuruka ruka kutoka katika tawi moja kuelekea
jengine’(A Vindication of the Rights of Woman), na kisha Mary Wollstonecraft
akawalaumu wanaume wa nchi za Magharibi kwa kuwatumia wanawake nyumbani na
kuwadhoofisha miili yao na kuzifinya akili zao kwa kutowapa kipaumbele.
Anasema Edward Turner ‘Wanawake wa Magharbi walikua hawana haki yeyote
isipokua haki ya waume zao. Hadi mwanzoni mwa karne ya 19, hali ya mwanamke
alieolewa katika nchi za Magharibi ilikua haimruhusu kufanya kazi ofisini, kupiga
kura katika uchaguzi, kuwemo katika mambo ya Sharia’h, kumiliki mali na
mwanamke anapoolewa basi mali yake yote ilikua inakua chini ya usimamizi wa
mumewe na inapotokea mke na mume kuachana basi mwanamke hua hana haki ya
kukaa na watoto.’(Edward Raymond Turner, ‘The Women's Suffrage Movement in
England’)
900
Tukirudi kwa mambo yalivyokua katika upande wa watu wa Arabuni kabla ya kuja
Uislam na namna yalivyobadilika ghafla na wanawake kujisikia kua wako huru baada ya
kuja Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam mfano mzuri ni pale tunapoangalia
Hadith ya Ubayd Ibn Umayr isemayo kua: ‘Aisha alilalamika kua Rasul Allah alikua
akikaa sana katika nyumba ya Zaynab bint Jahsh na kunywa Asali katika nyumba
yake, hivyo akasema: ‘Mimi na Hafsah tukakubaliana kua kila mmoja wetu
amuulize Mbona ninasikia harufu ya Maghafir katika mwili wako? Umekula
Maghafir?’’
Maghafir ni aina ya tunda kama ndimu tamu ambalo hutoa utufyuri au mvuke wenye
harufu, hivyo Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam alipoulizwa akasema
«لاَ ، بَلْ شَرِبْتُ عَسَلاً عِنْدَ زَيْنَبَ بِنْتِ جَحْشٍ وَلَنْ أَعُودَ لَه»
La! Bal sharibtu aA’salan ainda Zaynab bint Jahshi walan aAuuda lahu
‘La, sikula bali nilikunywa Asali kwa Zaynab bint Jahsh, lakini sitokula tena. ’
Kisa hiki ndio ikawa sababu ya kushuka aya ifuatayo:
﴿ َٰ ي ُّهَا ٱلن َّبىِ ُّ لمَِ
تحَُرِّمُ مَآ أَحَل َّ ٱهلل َُّ لَكَ تَبْتَغِى مَرْضَاةَ أَزْوَاجِ كَ وَٱهلل َُّ غَفُوٌر
ر َّحِ يمٌ﴾
Ya ayyuha alnnabiyyu lima tuharrimu ma ahalla Allahu laka tabtaghee mardhata
azwajika waAllahu ghafoorun raheemun (Surat At Tahrim 66:1)
Tafsir: Ewe Nabii! Kwa nini unaharamisha kile ambacho Allah amekihalalisha juu
yako, Jee unatafuta kuwaridhisha wake zako? Hakika Allah ni mwingi wa Usamehevu
na ni mwingi wa Rehma.
Ingawa Hadith hii ya Ubayd In Umayr imemalizikia hapo lakini Allah Subhanahu wa
Ta’ala alimuwekea wazi Mtume wake Salallahu A’layhi wa Salam yale yaliyotokea na
hivyo Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam akawakasirikia wake zake, kama
anavyohadithia Abd Allah Ibn Abbas katika Hadith nyengine kwa kusema:
901
‘Nilikua na hamu kubwa ya kumuuliza Umar, kuhusiana na wake wawili ambao
walishirikiana dhidi ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam na hivyo
wakashushiwa aya aisemayo:
﴿إِن تَتُوآبَ إِلىَ ٱهلل َِّ فَقَدْ صَغَتْ قُلُوبُكُمَا وَإِن تَظَاهَرَا عَلَيْهِ فَإِن َّ اهلل ََّ هُوَ مَوْلاَهُ
وَجِ برِْيلُ وَصَالِحُ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمَلاَئِكَةُ بَعْدَ ذٰلِكَ ظَهِيرٌ ﴾
In tatooba ila Allahi faqad saghat quloobukuma wa-in tadhahara AAalayhi fa-inna
Allaha huwa mawlahu wajibreelu wasalihu almu/mineena waalmala-ikatu baAAda
dhalika dhaheerun (Surat At Tahrim 66:4)
Tafsir : Ikiwa nyie wawili (Wake wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
ambao ni Aisha na Hafsah) mtatubu kwa Allah. Kwani kwa hakika nyoyo zenu
zimeegemea sana (katika kumpinga Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam
katika kile anachokipenda), lakini kama mkisaidiana dhidi yake, basi kwa hakika
Allah ni Msaidizi wake, na Jibril, na wachamungu miongoni mwa walioamini, na pia
Malaika ni wasaidizi wake.
Hadi pale Umar alipoenda Hija nami nikaenda pamoja nae, tulipokua njiani
alishuka kutoka katika kipando chake na akaenda kujisaidia, aliporudi
nikammiminia maji akanawa mikono yake na kutia udhu nami nikamuuliza, nae
akasema ‘Unashangaza Ya Ibn Abbas!’. (Az Zuhri ambae alikuwepo pia wakati huo
anasema kua: Wa Allahi Umar hakulipenda suali hilo lakini hakuficha kitu). Umar
Akajibu: ‘Walikua ni A’isha na Hafsah’, kisha Umar akaendelea: ‘Sisi Maquraysh
tulikua tunawamiliki Wanawake, hivyo tulikua hatuwaruhusu kuingilia mambo
yetu. Lakini tulipokuja Madinah tukakuta watu wamedhibitiwa na wanawake
wao, na wanawake wetu wakaanza kujifunza kutoka kwa wanawake wao.
Nyumba yangu ilikua iko karibu na nyumba za Banu Umayyah ibn Zayd, katika
Al Awali. Siku moja nilimkaripia mke wangu, nae akanijibu. Nikamwambia,
‘Inashangaza umefikia kiasi hiki sasa?!’, ‘Nae akaniambia, unakasirika kujibiwa
wakati wake wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, wanafanya hivyo
hivyo? Na mmoja kati yao atajitenga nae leo kwa siku nzima hadi usiku.’
Hivyo nikatoka na kuenda hadi kwa Hafsa na kumwambia ‘Jee unajibishana na
Rasul Allahi Salallahu A’layhi wa Salam?’ akasema ‘Naam’, nikamuuliza jee kuna
mmoja wenu ambae leo hii atajitenga nae?, nae akajibu ‘Naam’. Nami nikasema :
‘Yeyote yule miongoni mwenu atakaefanya hivyo basi atakua ameangamia, na ni
mwenye kupotea, Jee yuko yeyote yule miongoni mwenu mwenye uhakika kua
902
Allah atakua radhi nae kutokana na kumkasirisha Mtume wake Salallahu A’layhi
wa Salam? Kwani kama ni vyenginevyo basi atakua ameangamia, Usijibishane na
Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam, usimshurutishe kitu chochote, bora
unaweza kunishurutishe mimi chochote kile unachokitaka, na usihadaike na
kumuiga jirani yako (yaani Aisha) kwani yeye ni mzuri zaidi kuliko wewe, na Rasul
Allah Salallahu A’layhi wa Salam anapenda zaidi kuliko wewe.’
Kisha Umar akaendelea kwa kusema ‘Kulikua na jirani yangu mmoja miongoni
mwa Ansari ambae nilikua nimepanga nae kua, ikiwa yeye atakua hayupo nami
nitakua na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, basi nitamwambia kile
alichokua hajakisikia, na mimi nikiwa sipo lakini yeye yupo basi ataniambia kile
nilichokua sijakisikia. Kwa wakati huo viongozi wa miji miengine walikua
washasalimu amri kwa Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam, isipokua mfalme
wa Ghasan, ambae tulikua na wasi wasi kua huenda ikawa anajitayarisha
kutuvamia, na mara ghafla usiku mmoja yule jirani yangu akaja kuniambia:
‘Msiba! kuna jambo baya limetokea!’ nami nikamuuliza: Nini kimetokea? Mfalme
wa Ghasan kavamia?’ naye akanijibu : ‘La! Msiba mkubwa zaid ya huo, kwani
Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kaachana na wake zake wote’.
Nami nikasema ‘Hafsa ameshaangamia na kupotea, yale niliyoyafikiria yatatokea
ndio yaliyotokea’. Baada ya kusali Alfajir nikaenda kwa Hafsa na kumkuta analia na
nikamuuliza ‘Jee Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam kakuacheni?’ nae akanijibu
‘Sijui ila amejitenga katika chumba cha juu’ nikaenda katika sehemu hiyo na kumkuta
mtumwa, nikamwambia nnataka kuonana na Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam,
akaingia ndani na kisha akarudi na kuniambia: ‘Nimemuambia kua unataka kuonana
nae lakini amenyamaza kimya’, nikaondoka na kuenda katika Minbar na kukuta watu
wakiwa wanalia, nikashindwa kustahmili nikarudi tena kwa yule mtumwa na
kumwambia aniombee ruhusa nionane nae Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam,
akaingia ndani na kurudi na kunijibu kama alivyonijibu mwanzo, nikaonodoka tena na
kurudi tena nikakataliwa na nilipokua nataka kuondoka nikaruhusiwa kuingia,
nilipoingia nikatoa salam na kumkuta Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam, kalala
juu ya mkeka, na mwili wake una alama ya mkeka.
Nikamuuliza ‘Ya Rasul Allah kweli umeachana na wake zako?’, akaniangalia na
kunijibu ‘La!’ Nami nikasema ‘Allahu Akbar! Ya Rasul Allah! Angalia sasa hivi
tulivyokua! Sisi Maquraysh tulikua ni wenye kuwatawala wanawake, lakini
tulipokuja Madinah tukakuta watu ambao wanatawaliwa na wanawake, na
wanawake wetu wakaanza kuwaiga wanawake hao, niligombana na mke wangu nae
akanijibu, hivyo nikakasirika na kumwambia umefikia kiasi hiki sasa hivi?’ Nae
akasema ‘Unanishangaa mie wakati wake wa Rasul Allah wanamfanyia hivyo
hivyo? Na mmoja miongoni mwao atatengana nae mchana na usiku wa leo!’ Nami
nikasema, ‘Yeyote atakaefanya hivyo basi atakua ni mwenye kuangamia, Jee yuko
903
miongoni mwao mwenye uhakika kua Allah ataridhika nae kutokana na
kumkasirisha Mtume wake?’ Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akatabasamu,
nami nikasema ‘Ya Rasul Allah nilienda kwa Hafsa na kumwambia Usihadaike na
kumuiga jirani yako (Aisha) kwani yeye ni mzuri zaid yako na anapendwa zaidi na
Rasu Allah kuliko wewe.’ Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akatabasamu tena.
Nikamwambia Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam: ‘Jee nijisikie huru kukuambia
jambo lolote?’ nae akasema ‘Naam’, hivyo nikakaa kitako chini na kuangaza chumbani
na kumwambia: ‘Uombee Ummah wako Ya Rasul Allah kwa Allah ili aujaalie uwe
Ummah ulionawiri, kwani amewajaalia Warumi na Waajemi kua ni watu
wanaoishi maisha mazuri, lakini hawamuamini Allah Subhanahu wa Ta’ala.’ Rasul
Allah Salallahu A’layhi wa Salam akakaa kitako na kusema: ‘Unatilia shaka Ya Ibn ul
Khattab! Hao ni watu ambao raha zao zimeharakishwa kwa ajili yao hapa Duniani.’
Hivyo nami nikasema : ‘Niombee maghfira kwa Allah, Ya Rasul Allah’. Rasul Allah
Salallahu A’layhi wa Salam aliapa kutowakaribia wake zake kwa mwezi mmoja kwani
alikua amewakasirikia sana, hadi pale Allah alipomkaripia. (Musnad Imam Ahmad, Imam
Bukhari na Imam Muslim)
Hivyo ingawa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam, alikua akiwakasirikia na
kuwakaripia lakini hakuwahi kuwapiga ahl zake, bali alikua ni mpole, mwenye huruma,
mstahmilivu na muadilifu kwao kwa kila mtu na kila kitu. Allah Subhanahu wa Ta’ala
anatuthibitisha haya katika Qur’an pale aliposema:
﴿لَقَدْ جَآءَكُمْ رَسُولٌ مِّنْ أَنفُسِ كُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِت ُّمْ حَرِيصٌ عَلَيْكُمْ بِٱلْمُؤْمِنِ
رَءُوفٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
َين
Laqad jaakum rasoolun min anfusikum AAazeezun AAalayhi ma AAanittum
hareesun AAalaykum bialmu/mineena raoofun raheemun. (Surat At Tawba 9:128)
Tafsir: Kwa hakika, amekujieni Mtume (Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam)
kutoka miongoni mwenu, Inamuuma sana kua nyinyi mdhurike au mpate matatizo,
ana wasiwasi juu yenu (ili mpate kuongoka, na mtubu kwa Mola wenu, ili mpate
kuingia Peponi na muokoke na moto) kwa waumini Yeye (Nabii Muhammad Salallahu
A’layhi wa Salam) Ni mwingi wa Huruma na mwingi wa Rehma.
Na huu ndio msingi wa Dini ya Kiislam kama inavyojionesha wazi, kwani katika kipindi
cha uhai wa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam mambo mbali mbali
yahusuyo jamii ya Kiislam, matatizo na utatuzi wake yaliainishwa na kuwekwa wazi
904
hatua kwa hatua kwa manufaa ya Ummah wa Kiislam kupitia katika njia ya hukmu na
Sharia’h za Kiislam zilizokua zinaendelea kutolewa na kuteremshwa kutokana na
mazingira na maisha ya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam.
Katika kipindi hiki ilikua kila Waislam wanapotokewa na tatizo basi humfuata Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam ili kuulizia utatuzi wa tatizo hilo na Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam alikua akitoa hukmu, na aidha hukmu hiyo
ilikua imepitia katika aya ya Qur’an aliyoteremshiwa, au kwa Hadith na baadhi ya wakati
hukmu zilikua zinapatikana kutokana na vitendo vyake mwenyewe Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam na pia kutokana na kukubali ama kukemea vitendo vya
Masahaba zake.
Vyovyote vile alivyoamua na kuhukumu Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam,
basi alikua hasemi tu kwa matamanio yake, bali hua ni Wahy kutoka kwa Mola wake,
iwe kwa njia ya Hadith ul Quds ama kwa njia ya Qur’an. Kwani Allah Subhanahu wa
Ta’ala amesema katika Qur’an:
﴿وَمَا يَنطِقُ عَنِ - يُوحَ ٰ ى ﴾
ٱلهَْوَىٰ
وَحْى
ٌ
إِنْ هُوَ إِلا َّ
Wama yantiqu A’ani alhawa; In huwa illa wahyun yooha (Surat An Najm 53: 3-4).
Tafsir: Na hazungumzi kutokana na matamanio yake, kwa hakika haikua ila ni Wahy
tuliomshushia.
Hukmu na Sharia’h zilizokua zinatoka kwa Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam, zilikua zinategemea njia mbili ambazo ni Qur’an na Sunnah. Na inapotokea kua
kumetolewa hukmu ambayo haikutokana na Qur’an na ikawa ina kasoro basi Malaika
Jibril A’layhi Salatu wa Salam ambae alikua kama mwalimu wa Nabii Muhammad
Salallahu A’layhi wa Salam hushuka na aya ya Qur’an na kurekebisha hukmu au jambo
hilo kama tulivyoona katika Hadith inayoelezea sababu ya kushuka aya ya Surat A
Tahrim 66:1.
﴿ َٰ ي ُّهَا ٱلن َّبىِ ُّ لمَِ تحَُرِّمُ
مَآ أَحَل َّ ٱهلل َُّ لَكَ تَبْتَغِى مَرْضَاةَ أَزْوَاجِ كَ وَٱهلل َُّ غَفُوٌر
ر َّحِ يمٌ﴾
Ya ayyuha alnnabiyyu lima tuharrimu ma ahalla Allahu laka tabtaghee mardata
azwajika waAllahu ghafoorun raheemun (Surat At Tahrim 66:1)
905
Tafsir: Ewe Nabii! Kwa nini unaharamisha kile ambacho Allah amekihalalisha juu
yako, Jee unatafuta kuwafurahisha wake zako? Hakika Allah ni mwingi wa
Usamehevu na ni mwingi wa Rehma.
Hivyo kuna baadhi ya aya za Qur’an zilizoteremshwa kutokana na matukio maalum, au
kwa ajili ya kujibu masuala maalum, na vile vile kuna baadhi ya aya zilizoteremshwa bila
ya kutokea matokeo au maswali maalum ambayo yaliyopelekea kushuka kwa aya hizo.
Tukiiangalia Qur’an kwa ujumla basi tunaona kua kuna aya ambazo zilishuka katika mji
wa Makkah, ambazo zinahusisha theluthi mbili ya aya zote za Qur’an ambazo hizi
hujulikana kama aya za Makkah (Makki). Kwa ujumla zinajumuisha asilimia ndogo ya
hukmu (Ahkami), kwani zinazungumzia zaid kuhusiana na kuelezea na kufundisha
misingi ya Kiislam na kuwaita watu katika dini ya Kiislam, kama vile kuhusiana na
Kumuamini Allah Subhanahu wa Ta’ala na Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa
Salam, kuamini siku ya Malipo, Kuamrisha kusimamisha Sala, kufahamisha Maadili na
Akhlaq za Kiislam kama kusema ukweli, kua na uaminifu, kukataza mambo maovu,
mauaji, kuzikwa watoto wa kike walio hai, kupunja katika mizani n.k
Na vile vile kuna aya ambazo zilishuka katika mji wa Madinah ambazo hizi
zinajumuisha robo tatu ya aya zote Qur’an na zinajulikana kama aya za Madinah
(Madani). Aya hizi zinazungumzia Mu’amalat (Mambo ya kubadilishana katika biashara
kuuza, kununua, kukodishana, riba n.k). Vile vile katika aya hizi pia ziko zile
zinazozungumzia kuhusiana na Hudud (zinazohusiana na Adhabu za makosa ya Zina,
Wizi, Riba n.k ), Jinayat (zinazohusiana na adhabu za makosa ya Jinai kuhusiana na
adhabu ya mauaji ya mtu alieua kwa kukusudia, adhabu za Majambazi, n.k), Bayyinat
(zinazohusiana na namna ya kupata ushahidi katika kesi mbali mbali). Hukmu zilizobakia
zinazozungumzia kuhusiana na Ibada za Sala, Zakkah, Hijjah na Jihadi pia
ziliteremshwa katika kipindi hiki cha Madinah .
Tofauti na namna vilivyoteremshwa vitabu vyengine vyote vilivyotajwa katika Qur’an,
yaani Taurat, Zabur na Injil, ambavyo viliteremshwa kila kimoja kwa wakati mmoja,
kwani kama tulivyoona kua Qur’an ilishushwa hatua kwa hatua, na sababu ya kushuka
kwake hivyo inawekwa wazi na Allah Subhanahu wa Ta’ala pale aliposema katika Surat
al Furqan kua:
﴿كَذٰ لِكَ لِنُثَبِّتَ بِهِ فُؤَادَكَ وَرَت َّلْنَاهُ تَرْتِيلاً ﴾
Kadhalika linuthabbita bihi fu-adaka warattalnahu tarteelan (Surat Al Furqan
25:32)
906
Tafsir: Kadhalika ili kukipa ithibati (kukipa nguvu) kifua chako juu yake (ya Qur’an),
na tukakushushia kwa mpangilio.
Na pia katika Surat al Israa iliposema:
﴿وَقُرْآً فَرَقْنَاهُ لِتَقْرَأَهُ عَلَى ٱلن َّاسِ ٰ عَلَى مُكْثٍ وَنَز َّلْنَاهُ تَنْزِيلاً ﴾
Waqur-anan faraqnahu litaqraahu AAala alnnasi AAala mukthin wanazzalnahu
tanzeelan (Surat Al Israa 17:106)
Tafsir: Na Qur’an tuliyoigawa (katika sehemu sehemu), ili upate kuwasomea watu
hatua kwa hatua, Na kwa uteremsho uliopangika kwa vituo.
Hikma kubwa iliyomo ndani ya kuteremshwa kwake Qur’an hatua kwa hatua ni
kumfunza mambo mapya Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam kila baada ya
mda, na kidogo kidogo kumuongoza katika njia sahih ili kumpa msimamo thabit, na hivyo
hua rahisi kwake yeye na kwa wafuasi wake kuweza kuihifadhi, huku wakiifanyia kazi
kwa vitendo, vile vile kwa kua Allah Subhanahu wa Ta’ala anawajua viumbe wake basi
alikua akijua kua itakua ni vigumu kwa ghafla moja kubadilisha kila njia na mifumo ya
maisha waliyokua wakiishi viumbe vyake, na hivyo katika mteremsho huo Qur’an ikawa
kidogo kidogo inafungamana na mfumo mpya wa maisha ya Kiislam unaongoza na
kubagua baya na zuri kwa manufaa yao.
Kulingana na mtizamo wa Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazal
basi tunaona kua kimpangilio Qurán ina aya ambazo zina Marijani na pia ina aya zenye
Lulu. Aya zenye Marijani ni zile aya ambazo maalum zinazungumzia kuhusiana na Allah
Subhanah wa Ta’ala, Majina yake, Sifa zake na Kazi zake. Hizi zinawakilisha
utambulisho wake Allah Subhanahu wa Ta’ala kwa ufahamu wa waja wake. Aya hizi
ziko 763 ambapo aya 7 miongoni mwao zinajumuisha aya zote za Surat al Fatiha.
Aya zenye Lulu ni zile aya ambazo zinazoielezea njia iliyonyooka na kuamrisha,
kuhamasisha na kumtia ari mtu kuifuata njia hiyo. Hizi zinawakilisha utambulisho wa
namna ya kuifanyia kazi kivitendo njia hiyo iliyonyooka. Aya hizi ziko 741, ambapo aya
46 miongoni mwao zinapatikana katika Surat Al Baqara zikiwemo aya 5 za mwanzo za
Sura hiyo.
Kutokana na mpangilio na utaratibu wa uteremsho huo basi tunaweza kuona kua
Maamrisho, Makatazo, Hukmu na Sharia’h za Kiislam hazikuteremshwa zote kwa
pamoja bali ziliteremshwa kidogo kidogo kupitia aya moja moja za Qur’an ambazo
907
baadhi yao zilikua zikijifafanua wenyewe na nyengine zilikua zikifafanulika kupitia kwa
aya nyengine na pia zikiungwa mkono na kufafanuliwa katika njia ya Hadith na Sunnah
za Nabii Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam.
Hivyo basi bila ya shaka ni jambo lililowazi kua ni vigumu kufafanua au kutoa Hukmu
na Sharia’h Sahih kutoka katika vyanzo hivyo vya Qur’an na Sunnah, kwa yule ambae
mtu hana utaalam unaotakiwa ambao utamfanya ajue ni Hukmu na Sharia’h zipi
zilizokuja kabla na ni zipi zilizokuja baadae, kutokana na kutojua aya ipi inaifafanua aya
ipi, Hadith ipi inaunga mkono aya ipi, Hadith ipi inafafanua aya ipi n.k.
WANAWAKE WALIO JIPENDEKEZESHA KINDOA NA
WALIOCHIKA WA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA
SALAM.
Naam kama tulivyoona kuhusiana na namna ilivyokua ndoa ya Maymuna Bint Harith
Radhi Allahu Anha basi tunaona pia kua kuna Wanawake wengi sana Wacha Mungu
ambao walijipendekeza pia kwa Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam ili wapate
kuolewa nae, kama inavyothibitisha hadithi isemayo : ‘Anasema Thabit Al Bunani
Radhi Allahu Anhu kua: ‘Hakika mimi nilikua niko pamoja na Anas, ambae alikua
na Bint yake. Hivyo Anas akasema: ‘Kuna Mwanamke alikuja kwa Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na akajipendekezesha kwake ili aolewe nae kwa kusema:
‘Ya Rasul Allah, Hivi Jee unaweza kunitaka mimi?’ ambapo Bint yake Anas
akasema: ‘Inakuaje mpaka inafikia hali hii kua watu hawana haya?’
Ambapo Anas akasema: ‘Hakika huyu Mwanamke ni bora zaidi kuliko wewe kwani
yeye alitaka kua aolewe na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
akajipendekezesha kwake kwa ajili ya Ndoa.’’’(Imam Bukhari)
Imam Al Bukhari ana hadith nyengine pia ambayo inayosema kuhusiana na jambo hili
kua: ‘Aisha Radhi Allahu Anha alisema kua: ‘Hakika mimi nilikua ni mwanamke
mwenye Wivu sana dhidi ya Wanawake wanaojipendekeza wenyewe kwa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam, hadi pale Allah Subhanah wa Ta’ala aliposhusha
aya ifuatayo’’
908
﴿تُرْجِ ى مَن تَشَآءُ مِنْهُن َّ وَتُؤْوِي ۤ إِلَيْكَ مَن تَشَآءُ وَمَنِ ٱبْتَغَيْتَ ممِ َّنْ عَزَ لْتَ فَلاَ
جُنَاحَ عَلَيْكَ ذٰلِكَ أَدْنىَٰ أَن تَقَر َّ أَعْيُنُهُن َّ وَلاَ يحَْزَن َّ وَيَرْضَينَْ بمَِآ آتَيْتَهُن َّ كُل ُّهُ َّن
وَٱهلل َُّ يَعْلَمُ مَا فىِ قلُوبِكُمْ وَكَانَ ٱهلل َُّ عَلِيماً حَلِيماً ﴾
Turjee man tashao minhunna watu/wee ilayka man tashao wamani ibtaghayta
mimman AAazalta fala junaha AAalayka dhalika adna an taqarra aAAyunuhunna
wala yahzanna wayardhayna bima ataytahunna kulluhunna waAllahu yaAAlamu
ma fee quloobikum wakana Allahu AAaleeman haleeman(Surat Al Ahzab 33:51)
Tafsir: Nawe (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) unaweza kumrudisha
umtakae miongoni mwao (wake zako) na unaweza kumpokea umtakae. Na yeyote yule
unaemtamani miongoni mwa wale uliowaweka kando (kwa kumuacha kwa muda),
basi hamna kosa kwako (Kumrudia) hivyo ni bora, ili wawe ni wenye kuliwazika na
wasiwe ni wenye kuhuzunika na hivyo wote kua ni wenye kuridhika kutokana na kile
utakachowapa. Allah anajua kile kilichomo ndani ya Nyoyo zenu na yeye ni mwenye
kujua juu ya kila kitu na ni mwenye ustahmilivu.
Aisha Radhi Allahu Anha anaendelea kusema kua: ‘Baada ya kushuka aya hii basi
nikamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Inaonekana kua Mola
wako anaharakisha kufuatilia matamanio yako’’
Hivyo Wanawake ambao waliojipendekeza kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
ili waolewe nae wako wengi kiidadi kama vile ilivyokua pia kua kuna Wanawake wengi
ambao aliwahi kuwaposa lakini hakuwahi kuwaoa na pia aliowaposa kuwaoa na kisha
akawaaacha bila ya kuwaoa kwa sababu mbali mbali zinazokubalika kisharia, ambapo
miongoni mwao Wanawake hao basi ni pamoja na:
Amra bint Yazid Al Ghifariyya ambae alipotakiwa kuolewa na Rasul Allah Salallahu
A’layhi wa Salam basi akasema: A`udhu billah mink, hakika mimi naomba ulinzi kutoka
kwa Allah dhidi yako, na hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakumuoa.
Asma’ bint Ka`b ambae alikua mzuri sana lakini alipoolewa alizidiwa akili na wivu wa
wake wengine wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo katika usiku wake
wa ndoa akamwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua A`udhu billah mink,
hakika mimi naomba ulinzi kutoka kwa Allah dhidi yako, na hivyo Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akaachana nae na hakuolewa tena Mwanamke huyu hadi kufariki
kwake.
909
Azza Bint Abi Sufyan Ibn Harb ambae ni Dada yake Ummu Habiba, ambapo Azza
mwenyewe na baba ambae ni Abu Sufyan Radhi Allahu Anhu walitaka kua Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam amuoe Azza lakini Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akasema kua hairuhusiki kwa Muislam kuwaoa Wanawake ndugu wawili kwa wakati
mmoja.
Duba`a Bint `Amir Ibn Qurt ambae aliposwa lakini hakuolewa na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam
Ummu Hani Fakhta Bint Abu Talib ambae alikua ni Bint Ami yake Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam ambae alichumbiwa na Hubayra Ibn Makhzum na Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam pia lakini Abu Talib akamuozesha kwa Hubayra na
alipoingia katika Uislam na kuachika basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akataka kumuoa lakini Umm Hani akasema: ‘Hakika mimi nilikupenda wewe tangu
wakati wa Ujahiliyah hivyo nitasema nini katika wakati wa Uislam, lakini sasa
mimi nina watoto wadogo na nnakhofu kua Watakua wanakukera wewe’ hivyo
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Wanawake bora ni wenye kupanda
Ngamia miongoni mwa Wanawake wa Quraysh, kwani wao ni wenye kuwapenda
sana watoto wao na ni wenye kujitolea kwa ajili yao na ni wenye uadilifu mkubwa
juu ya haki za Waume zao’(Imam Muslim)
Fatma Bint Al Dahhak Ibn Sufyan Al Kilabiyya ambae aliamua kuchagua Dunia yake
na akawa na hali ya Umasikini Mkubwa sana pale Allah Subhanah wa Ta’ala
alipomwamrisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuwapa hiari wake zake
wachague Dunia yao au Akhera yao ama ilivyosema aya:
﴿َٰي ُّهَا ٱلن َّبىِ ُّ قُلِ لأَزْوَاجِ كَ إِن كُنتنُ َّ تُرِدْنَ ٱلحَْيَاةَ ٱلد ُّنْيَا وَزِينَتَهَا فَتَعَالَينَْ أ ُ مَتِّعْكُ َّن
وَأُسَرِّحْكُن َّ سَرَاحاً جمَِيلاً ۞وَإِن كُنتنُ َّ تُرِدْنَ ٱهلل ََّ وَرَسُولَهُ وَٱلد َّارَ ٱلآخِ رَةَ فَإِن َّ ٱهلل ََّ
أََعد َّ لِلْ مُحْسِ نَاتِ مِنكُن َّ أَجْراً عَظِيماً ﴾
Ya ayyuha alnnabiyyu qul li-azwajika in kuntunna turidna alhayata alddunya
wazeenataha fataAAalayna omattiAAkunna waosarrihkunna sarahan jameelan;
Wa-in kuntunna turidna Allaha warasoolahu waalddara al-akhirata fa-inna Allaha
aAAadda lilmuhsinati minkunna ajran AAadheeman (Surat Al Ahzab 33:28-29)
Tafsir: Ewe Nabii waambie wake zako kua: ‘Kama mnataka Maisha ya Dunia na
mapambo yake basi njooni nitakupeni na nitaachana nanyi kwa njia nzuri’. Lakini
kama mnamtaka Allah na Mtume wake na maisha ya Akhera basi basi Allah
amewatayarishia wenye kufanya Mema miongoni mwenu Malipo bora sana.
910
Ambapo kuhusiana na sababu ya kushushwa aya hii pia basi anasema Jabir Ibn `Abdullah
kua: ‘Alikuja Abu Bakr kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kuomba
ruhusua kuinga ndani, lakini akakuta watu wamekaa kitako na hakuruhusiwa
kuingia Ndani, kisha akaja Umar na akaomba ruhusa kuingia Ndani lakini nae
hakuruhusiwa kuingia. Halafu wote Abu Bakr na Umar wakaruhusiwa kuingia
ndani na kumkuta Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwa amekaa kimyaa
akiwa na wake zake waliokua wamemzuguka.’
Hivyo Umar akasema ndani ya Nafsi yake kua: ‘Wacha mimi niseme kile ambacho
kitamfurahisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam’ hivyo akasema: ‘Ya Rasul
Allah natamani kama ungemuona Bint Zayd pale aliposema kuniambia kua
anataka nimuongezee pesa za Matumizi, kwani nilimpatia maumivu ya kwenye
shingo badala yake (yaani alimpiga kibao cha shingo)’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akacheka na kisha akasema: ‘Naam..kama
mnavyoona hata hawa walionizunguka mimi pia wanataka muongezo wa pesa za
Matumizi’. Ambapo baada ya kusikia maneno hayo basi Abu Bakr na Umar Radhi
Allahu Anhum kila mmoja akasimama na kumpiga Binti yake Kibao cha shingo yaani
Abu Bakr Radhi Allahu Anhu akampiga Aisha Radhi Allahu Anha na Umar Ibn Al
Khattab Radhi Allahu Anha akampiga Hafsa Radhi Allahu Anha.
Huku Abu Bakr na Umar Radhi Allahu Anhum wakisema: ‘Hivi Nyinyi mnamuomba
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kile ambacho asichokua na uwezo nacho?’
ambapo hapo hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaingilia kati kuwaombea
wake zake na wake zake hao Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam wakasema kua:
‘Wa Allahi kuanzia sasa hivi hatutomuomba tena kile kitu ambacho hana.’ Halafu
baaa ya hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akajitenga nao wake zake kwa
mwezi mzima na kisha Allah Subhanah wa Ta’ala akazishusha aya hizi Surat Al Ahzab
33:28-29
Hivyo baada ya hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaambia wake zake
kuhusiana na aya hizi kwa kuanza na Aisha Radhi Allahu Anha kwa kusema kua:
‘Nilikua nataka kupendekeza kitu kwako, lakini sitaki uwe ni mwenye kua na
papapara katika kunijibu na bora ushauriane na wazee wako kwanza.’ Ambapo
Aisha Radhi Allahu Anha akauliza: ‘Kuhusiana na nini?’ Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam akamsomea aya hizi:
﴿َٰي ُّهَا ٱلن َّبىِ ُّ قُلِ لأَزْوَاجِ كَ إِن كُنتنُ َّ تُرِدْنَ ٱلحَْيَاةَ ٱلد ُّنْيَا وَزِينَتَهَا فَتَعَالَينَْ أ ُ مَتِّعْكُ َّن
وَأُسَرِّحْ كُن َّ سَرَاحاً جمَِيلاً۞وَإِن كُنتنُ َّ تُرِدْنَ ٱهلل ََّ وَرَسُولَهُ وَٱلد َّارَ ٱلآخِ رَةَ فَإِن َّ ٱهلل ََّ
911
أَعَد َّ لِلْمُحْسِ نَاتِ مِنكُن َّ أَجْراً عَظِيماً ﴾
Ya ayyuha alnnabiyyu qul li-azwajika in kuntunna turidna alhayata alddunya
wazeenataha fataAAalayna omattiAAkunna waosarrihkunna sarahan jameelan;
Wa-in kuntunna turidna Allaha warasoolahu waalddara al-akhirata fa-inna Allaha
aAAadda lilmuhsinati minkunna ajran AAadheeman (Surat Al Ahzab 33:28-29)
Tafsir: Ewe Nabii waambie wake zako kua: ‘Kama mnataka Maisha ya Dunia na
mapambo yake basi njooni nitakupeni na nitaachana nanyi kwa njia nzuri’. Lakini
kama mnamtaka Allah na Mtume wake na maisha ya Akhera basi basi Allah
amewatayarishia wenye kufanya Mema miongoni mwenu Malipo bora sana.
Ambapo Aisha Radhi Allahu Anha akasema: ‘Ya Rasul Allah hivi jee mimi nahitajiwa
kushauriana na wazee wangu kuhusiana nawe? hakika mimi namchagua Allah na
Mtume wake, lakini usiwaambie wake zako wengine kuhusiana na Maamuzi yangu
haya.’ Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Allah hakunituma mimi kua
mtu mwenye kuzidisha ugumu, bali amenituma kwa ajili ya kufundisha na
kurahisisha mambo, hakuna atakaeniuliza kuhusiana na maamuzi yako lakini mimi
nitabainisha maamuzi yako.’
Ambapo kwa upande mwengine basi hii aya inajulikana kua kama ni Aya ya Takhyir
yaani aya ya Khiyari, ambapo Kifiqh basi hua ni yenye kutumika kubainisha Hukmu
inayohusiana na talaka.
Pale Mume anapomwambia Mkewe kua: ‘Una khiyari aidha ya kubaki nami ama
kuondoka’
Hivyo kama Mwanamke akiamua kuondoka basi hukmu yake inakua ni kaachika
kwa Talaka Moja kati ya Talaka tatu kwa mpigo yaani Talaqa Bayin na kama
akiamua Kubakia basi hua hajaachika. Na hivyo Mume hua hawezi kua nae Mke
huyo hadi atakapomrudia tena upya kwa mahari mapya na makubaliano mapya,
ambapo hii hua inamaanisha kua Mke anaweza kukataa kurudiwa jambo ambalo
hua ni la hali tofauti na Talaq al Rajii ambayo hua inamapa Mume haki ya
Kumrudia Mke bila ya makubaliano mapya.
Na pia pale Mwanamke anapopewa haki hii basi hua hakuna upande wowote
utakaoweza kubadilisha maamuzi pale inapokua Mwanamke ameamua Kuondoka,
lakini kama Mwanamke akikaa kimya basi hua inamaanisha kua kauli ya Mume
haina nguvu ya kisharia na hivyo masharti yake hua yanabatilika.
Habiba Bint Sahl Ibn Tha`laba Al Najjariyya: Ambae hakuoana nae.
912
Jumra Bint Al Harith Ibn `Awf Al Muzani: Ambapo kulikua na Posa lakini hakukua
na Ndoa baada ya Baba Jumra kusema uongo kua Binti yake anaumwa ambapo baada ya
kusema kwake huko basi Binti huyo akapata maradhi ya Ukoma.
Khawla Bint Al Hudhayl Ibn Hubayra Al Tha`labiyya: Ambae aliolewa baada ya
kujipendekezesha kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na kukubaliwa wakati
Mwanamke huyu alipokua katika Ardhi ya Sham kabla ya kuonana na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na hivyo baada ya Ndoa hio na alipofunga Safari kutoka
Sham kuelekea Madina basi akafariki njiani.
Safiyya Bint Bashama Ibn Nadla Al`Anbariyya. Ambae alikua ni mateka wa Vita na
alipewa hiari ya kuolewa na Rasul Allah Salallahu A’alayhi wa Salam au kuachiwa huru
na kurudishwa kwa Mumewe na akachaga kuridhishwa kwa Mumewe.
Shanba’ Bint `Amr Al Ghifariyya: Aliolewa akaachika baada ya kusema kua: ‘Kama
Ibrahim alikua ni Mtoto wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi
asingefariki’
Umamah Bint Hamza Ibn Abd Ul Muttalib: Ambae alijipendekezesha kwa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam, lakini Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akakataa
kwa sababu ya kua Hamza Ibn Abd ul Muttalib Radhi Allahu Anhu alikua pia ni kaka
yake walienyonya ziwa moja.
Khuwayla Bint Hakim Ibn Umayya Al Sulamiyya: Ambae alijipendekezesha kwa
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, lakini Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam,
akamkataa na hivyo badala yake akaolewa na Uthman Ibn Madhun Radhi Allahu Anhu.
MAVAZI YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM.
Tunapoangalia mavazi ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi kuna mavazi ya
aina tofauti ambazo aliyokua akipenda kuyavaa kama ilivyokuja kwenye vitabu Hadith
tofuati za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambapo miongoni mwao kuna
zisemazo kua alikua ni mwenye kuvaa mavazi yafuatayo:
Kwani amesema Amr Ibn Hurayth Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mimi nilimuona Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwa juu ya Minbar huku akiwa amevaa Kilemba
cheusi ambacho ncha zake mbili zilikua zinanig’inia mabegani mwake’
Na amesema Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam aliingia kwenye Mji wa Makkah huku akiwa amevaa Kilemba
Cheusi’(Sahih Muslim)
913
Hivyo basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akivaa Kilemba cha kawaida
kama vile wanavyovyaa watu wa Yemen au Sudan ambacho hua kinajulikana kama As
Sahaab ambacho baadhi ya wakati alikua akikiwachia pembe zake ziwe ni zenye
kuning’inia kwenye mabega yake na baadhi ya wakati alikua hakiwachii na baadhi ya
wakati alikua akiupitisha upande mmoja wa kilemba hicho chini ya kidevu chake na chini
yake kilemba hicho alikua akivaa Kofia laini za kawaida zinazojulikana kama
Qalansuwah na baadhi ya wakati alikua akivaa Kilemba bila ya kofia.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua akivaa pia Qamis yaani Kanzu za Msikitni
za Mikoni mirefu na hili lilikua ndio vazi analolipenda zaidi, na pia alikua akivaa kanzu
za mikono mifupi na alikua akivaa Jubba au Joho mfano wake ambayo kama wanavyovaa
Wanazuoni wa Al Azhar Misri.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua anapokua safarini basi hua ni mwenye
kuvaa Joho ambalo ni lenye Mikono iliyobana mwishoni, na pia alikua akivaa Izzar yaani
Seruni au Kikoi kutoka Oman na kisha juu yake alikua akijifunika Ridhaa yaani
Kitambaa kama kivaachwo wakati wa Ihram.
Na pia alikua akivaa Hulla yaani Nguo mbili za juu na chini zinazofanana rangi ambazo
mara nyingi ilikua ni kutokana na kitambaa cha Mavazi ya Yemen chenye rangi
Nyekundu na mistari myeusi.
Alikua akivaa Bantaloon yaani Suruali na Khuffaayn viatu vya ngozi laini na Taasumah
yaani kama kanda mbili za Ngozi.
Imam Ibn Sa’ad anasema kutoka kwa (Sahaba) Niyar al Aslami Radhi Allahu Anhu kua
wakati Umar alipotoka kuenda kusali Sala ya mvua, alitoka akiwa amevaa burd (joho) la
Nabii Salallahu A’layhi wa Salam.
Na Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu anasema pia kua: ‘Mimi nilimuona Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akitia udhu huku akiwa amevaa Kilemba cha Qitr’(Imam
Abu Daud) ambapo Qitr hua ni iana ya Kilemba chenye kitambaa kigumu chenye rangi
Nyekundu.
Na Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua: ‘Mfalme wa Rumi alimtumia Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam zawadi ya Koti la Manyoya lenye mikono mirefu ambalo
ambalo lilifumwa pembeni yake kwa upindo wa Hariri na akalivaa’(Imam Ahmad)
Ama kuhusiana na Taylasaan yaani Kilemba cha kuweka tu juu ya kichwa
kinachoangukia mabegani au kinachowekwa mabegani tu, basi amesema Anas Ibn Malik
Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam amesema kua Dajjal
914
ataibuka huku akiwa amefuatana na Mayahudi 70000 wa Asbahaan watakaokua
wamevaa Taylasaan’(Sahih Muslim) hivyo ni makruh kuvaa Taylasaan.
Na amesema Abu Rimthah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Nilimuona Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam akitoa Khutba huku akiwa amevaa Nguo mbili za rangi ya
Kijani.’(Sunan An Nasai) ambapo nguo hizi za rangi ya Kijani hua ni kama ilivyokua
nguo zake nyekundu yaani hua ni zenye mistari ya hapa na pale.
HIJA YA KUAGA YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA
SALAM.
Anasema Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alikua alifanya Hija mara mbili kabla ya Hijra.’
Na Sufyan Ath Thawry anasema kua: ‘Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
Alifanya Hija mara kadhaa kabla ya Hijra’
Ambapo mnamo mwaka wa 9 wa Utume wake basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam alishushiwa na Allah Subhanah wa Ta’ala aya inayoamrisha Ibada ya Hija kwa
Waumini wote ambayo ni yenye kusema:
﴿فِيهِ آَتٌ بَيِّ نَاتٌ مَقَامُ إِبْرَاهِيمَ وَمَنْ دَخَلَهُ كَانَ آمِنًا وَ هللِ َِّ عَلَى الن َّاسِ حِ ج ُّ الْبَيْتِ
مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلاً وَمَنْ كَفَرَ فَإِن َّ اهلل ََّ غَنيِ ٌّ عَنِ الْعَالَمِينَ ﴾
Feehi ayatun bayyinatun maqamu ibraheema waman dakhalahu kana aminan
walillahi AAala alnnasi hijju albayti mani istataAAa ilayhi sabeelan waman kafara
fa-inna Allaha ghaniyyun AAani alAAalameena (Surat Al Imran 3:97)
Tafsir: Ndani yake mna dalili ambazo zilizowazi katika Maqam Ibrahim, na yeyote
atakeingia ndani yake basi atakua Salama, na Allah anataka kutoka kwa watu kua
wahiji kwenye Nyumba yake kwa mwenye Uwezo, lakini kwa asieweza basi kwa hakika
Allah ni tajiri wa kuhitaji kutoka kwa Walimwengu.
Ambapo anasema Mujaddid Ad Din Imama Fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam amesema: ‘Allah ameiwajibisha Hija juu yenu hivyo ni
wajibu wenu kuenda katika Hija’ hapo kuna mtu akasimama na akauliza: ‘Ya
Rasul Allah, Jee ni wajibu wa kila mwaka?’ ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam akakaa kimya hadi pale mtu huyo alipouliza suali hilo mara 3 kisha
915
akasema: ‘Kama ningesema naam basi ingekua ni Wajib juu yenu na nyinyi
msingeweza kutekeleza hilo.’
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamalizia kwa kusema: ‘Niwacheni hadi
pale nitakapokuwacheni, kwani Umah wa watu waliotangulia uliagamizwa kwa
sababu ya kuzidi kuuliza masuali na kuhoji kwao Mitume wao. Hivyo
ninapoamrisha jambo basi lifanyeni kwa kadri mtakavyoweza kulingana na uwezo
wenu na ninapokataza jambo basi liepukeni’
Kwa maana hio basi kama Muislam anao uwezo na kisha akwa hajaenda Hija basi
ataulizwa juu yake, na jukumu lake hilo kamwe haiwezekanni kutekelezewa na mtu
mwengine badala yake. Ambapo ingawa kuna hadith isemayo kua: ‘Amesema Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Yeyote yule mwenye uwezo wa kutembelea
Nyumba ya Allah na kisha akawa hajaenda Hija basi akifariki hua ni mwenye
kufarikia katika hali ya Uyahudi au Ukristo’’ basi kulingana na Mtizamo wa
Wanazuoni miongoi mwao akiwemo Imam Ibn Kathir, Imam Ashanqiti n.k basi wao
wanasema kua hii ni Hadith Dhaif.
Na kulingana na hukmu ya kisharia kuhusiana na Hija basi kuna mitizamo ifuatayo:
1-Wengi mingoni mwa wanazuni wanasema kua Ibada ya Hija inaweza
ikacheleweshwa kutokana na hali ya Mazingira aliyokua nayo mtu isipokua
kufanywa kwa kutocheleweshwa ni bora zaidi.
2-Kama ikiwa Mtu alifanya Ibada ya Hija wakati akiwa Mtoto mdogo ambae
hajafikia Balegh basi akifikia umri wa Baleghe hua na Wajib wa kufanya Tena
Ibada hio.
3-Kama Ibada ya Hija ikimuwajibikia yule mtu ambae ana matatizo ya ulemavu au
ya kudumu basi inaruhusika kufanyiwa Ibada hio kwa ajili yake.
Hivyo kama tulivyoona kua katika mwaka huu wa 9 ilipoamrishiwa Ibada ya Hija basi
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua na ugeni wa Najran na hivyo hakuweza
kuhudhuria na kuongoza Ibada hio na badala yake Ibada hio ikaongozwa na Abu Baqr
Radhi Allahu Anhu na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akamteua Ali Ibn
Abi Talib Radhi Allahu Anhu kutangazia ujumbe wa maamrisho ya kukataza mambo
ambayo yalikua siyo, ambayo yalikua yakifanywa na Makafiri katika wakati wa Ibada
zao za Hija, ambapo kuna wengine walikua wakizuguka Al Kaabah huku wakiwa Uchi,
wengine walikua wakizunguka huku wakiwa wamebeba Wanyama wao n.k
916
Ambapo ndani yake tangazo hilo mlikua pia na amrisho la kuvunjwa kwa makubaliano
baina ya Waislam na Makafiri kua huo ndio mwaka wao wa mwisho kwa Makafiri
kufanya Ibada ya Hija na haitakiwi kwa Muislam anaetaka kuingia kufanya Ibada ya Hija
kua azuiliwe au atishiwe kwa adhabu au kwa uhai wake katika kipindi cha Hija na
makubaliano mengineyo waliyokubaliana kama zinavyosema aya:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞بَرَاءَةٌ مِّنَ اهلل َِّ وَرَسُولِهِ إِلىَ ال َّذِينَ عَاهَدتم ُّ مِّنَ
الْمُشْرِكِينَ۞فَسِ ي ُحوا فيِ الأَْرْضِ أَرْبَعَةَ أَشْ هُ رٍ وَاعْلَمُ وا أَن َّكُ مْ غَيْ رُ مُعْجِ زِي اهلل َِّ
ۙ وَأَ َّن
اهلل ََّ مخُْزِي الْكَافِرِينَ۞وَأَذَانٌ مِّنَ اهلل َِّ وَرَسُولِهِ إِلىَ الن َّاسِ يَوْمَ الحَْجِّ الأَْ ْكبرَِ أَن َّ اهلل ََّ
بَرِيءٌ مِّنَ الْمُشْرِكِينَ ۙ وَرَسُولُ هُ ﴾
Baraatun mina Allahi warasoolihi ila alladheena AAahadtum mina almushrikeena;
Faseehoo fee al-ardhi arbaAAata ashhurin waiAAlamoo annakum ghayru
muAAjizee Allahi waanna Allaha mukhzee alkafireena; Waadhanun mina Allahi
warasoolihi ila alnnasi yawma alhajji al-akbari anna Allaha baree-on mina
almushrikeena warasooluhu fa-in tubtum fahuwa khayrun lakum wa-in
tawallaytum faiAAlamoo annakum ghayru muAAjizee Allahi wabashshiri
alladheena kafaroo biAAadhabin aleemin (Surat At Tawba 9:1-3)
Tafsir: Uhuru dhidi ya Majukumu yote unatangaziwa na Allah na Mtume wake
kutokana na mliyokubaliana na Washirikina, Hivyo tembeeni huku mkiwa huria (enyi
Washrikina) kwa miezi minne ardhini lakini mnatakiwa mjue kua kamwe hamtoweza
kukimbia (Adhabu za Allah) na Allah atawaadhirisha Makafiri; Na tangazo kutoka
Allah na Mtume wake kwa Watu katia siku kubwa kua Allah yuko huru kutokana na
Washirikina na pia (Yuko huru) Mtume wake. Hivyo kama nyinyi Washirikina
mkitubu basi ni bora kwenu lakini kama mkigeuka basi jueni kua hamuwezi
kuikimbia Adhabu ya Allah na wabashirie (Ewe Muhammad) wale ambao
waliokufuru juu ya Adhabu kali sana.
Ambapo aya imetaja miezi minne kua ni kipindi maalum cha mda waliopewa Makafiri
wale ambao waliingia kwenye makubaliano na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na hapo hapo kuwapa mda wale ambao walikua hawajaingia kwenye makubaliano hayo.
Na anasema Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshshari kua: ‘Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam alimtuma Ali Ibn Abi Talib kuvunja makubaliano yake
hayo kwa sababu ni kawaida ya Waarabu wanapokubaliana juu ya jambo basi
917
litakapohitajika kuvunjwa basi atakaevunja hua ni yule mhusika mkuu au mtu wa
kutoka Ndani Nyumbani mwake’
Ambapo amesema Abu Huraira Radhi Allahu Anhu kua: ‘Katika Hija hio wakati Abu
Bakr alipokua akiongoza Hija, basi alinituma mimi kwenye siku ya Nahar ya mwezi
10 Dhulhija kua niende katika eneo la Mina kisha nitangazie kua: ‘Kuanzia mwaka
huu hakuna Kafiri atakaefanya Hija na hakuna atakaefanya Tawwaf akiwa uchi’’
Ambapo Humaid Ibn Abd Rahman Radhi Allahu Anhu anasema kua: ‘Kisha Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akamtuma Ali Ib Abi Talib Radhi Allahu Anhu baada ya
Abu Bakr kuondoka na kumuamrisha kua asome Surat At Tawbah kwa sauti
Kubwa hadharani.’ Na Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu anaendela kusema kua:
‘Hivyo Ali akasoma pamoja nasi Surath At Tawbah wa sauti mbele ya watu katika
eneo la Mina katika sikua ya Kuchinja na kisha akatangazia kwa kusema kua:
‘Hakuna Kafiri atakaeruhusiwa kufanya Ibada ya Hija baada ya mwaka huu, na
hakuna atakaefanya Tawwaf akiwa Uchi’’(Imam Bukhari)
Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam alikua alipotimia umri wa miaka 63 basi alishuka
Malaika Jibril na kumwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua katika mwaka
huo watasoma Qur’n mara mbili, kwani ilikua ni kawaida ya Malaika Jibril kushuka
katika kila mwezi wa Ramadhan na kumsomesha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
Qur’an yote hadi ilipofikia katika Ramdhani hio, ambapo mnamo mwaka wa 10 wa Al
Hijra, na Rasul Allah Salallau Alayhi wa Salam akafahamu kua mda wake wa kuishi
Ulimweguni umemalizika, na kisha Malaika Jibril alishuka na Surat Nasr ambayo
inasema:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞إِذَا جَآءَ نَصْرُ ٱهلل َِّ وَٱلْفَتْحُ۞وَرَأَيْ تَ ٱلن َّاسَ يَدْخُلُونَ
فىِ دِينِ ٱهلل َِّ أَفْ وَاجاً۞فَسَبِّحْ بحَِمْدِ رَبِّكَ وَٱسْتَغْفِرْهُ إِن َّهُ كَانَ تَو َّاابَ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Idha jaa nasru Allahi waalfat-hu; Waraayta
alnnasa yadkhuloona fee deeni Allahi afwajan; Fasabbih bihamdi rabbika
waistaghfirhu innahu kana tawwaban (Surat An Nasr 110:1-3)
Tafsir: Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehma na Mwingi wa Huruma; Itakapokuja
Nusra ya Allah na Ushindi; Na utawaona watu wanaingia kwenye Dini ya Allah
Makundi kwa makundi; Basi litukuze na ulisifu jina la Mola wako na umuombe
msamaha kwani kwa hakika yeye ni mwenye kupokea maombi ya Msamaha.
918
Khalifah Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu A’nhu alikua akimchukua Abd Allah Ibn
‘Abbas Radhi Allahu A’nhu wakati huo alikua mdogo kiumri katika Ijma’a, na alikua
akimwita ‘Kijana mdogo aliepevuka’, Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu A’nhu alikua
akipenda kutumia Ijma’a katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo mbali mbali, kwani
alikua akipenda kuwepo ufahamu zaid wa matatizo na hivyo kua na uwezo mkubwa na
unaofaa zaid katika kutatua matatizo mbali mbali.
Hivyo katika mara ya kwanza baadhi Masahaba wazee wakiwemo waliopigana vita vya
Badr walikasirika kwani walikua wakimuona mdogo na asiejua kitu na hivyo
kumlalamikia Umar Ibn Al Khattab kwa kumwambia, ‘Umar inakuaje unamchukua
mtoto mdogo aje kutoa Fatwa nasi?’ Umar akawaambia mbele ya Abd Allah Ibn
‘Abbas Radhi Allahu A’nhu ‘Hebu niambieni kama ikiwa kweli mnajua, Jee Surat
An Nasr iliposhuka ilibashiria kitu gani?’ Masahaba wakajibu, ilikua inaashiria
ushindi mkubwa kwa Uislam. Umar akamgeukia Abd Allah Ibn ‘Abbas Radhi Allahu
A’nhu na kumuuliza ‘Jee unasemaje kuhusiana na majibu hayo?’, Abd Allah Ibn
‘Abbas Radhi Allahu A’nhu akajibu ‘Surat An Nasr ilikua inatabari kifo cha Nabii
Muhammad Salallahu A’layhi wa Salam’. Hapo Masahaba wakashangaa na kukubali
uwezo wa I’lm aliokua nao Abd Allah Ibn ‘Abbas Radhi Allahu A’nhu pamoja na udogo
wa umri wake.
Ambapo anasema Mujjadid Ad Din Imam fakhr Ad Din Al Razi kua: ‘Kuna uhusiano
wa baina ya Sura 3 ambazo zimefuatana sambamba ambazo ni ni Surat Al Kafirun
(109) ambayo ni yenye kubainisha kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ni
mwenye Kumuamini na Kumuabudu Allah Subhanah wa Ta’ala pekee na
kuwakanusha Miungu wengine, ambapo kutokana nayo Sura hio basi hua kuna
suali ambalo linasema: Hivi jee kutakua na Malipo gani kutokana na Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua ni mwenye kumuamini Allah Subhanah wa Ta’ala?
Na Jibu lake linapatikana kwenye hii Surat Nasr (110) ambayo inajibu kua Malipo
yake ni Kupatikana kwa Nusura na Ushindi katika Ulimwengu huu wa Dunia na
wa Akhera, na kisha Sura inayofuatia baada ya hii yaani Surat Masad(111) ni yenye
kuthibitisha Malipo waliyotayarishiwa wale ambao ni wenye kupingana na Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam.’
Na kwa Upande mwengine basi tunaona kua Allah Subhanah wa Ta’ala anamwambia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam awe ni mwenye kufanya Istighfar, na hivyo kuna
baadhi wanaweza wakajuliza, hivi inakuaje Allah Subhanah wa Ta’ala anamwambia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam afanye Istighfar wakati tayari katika Surat Fat-h
ameshamwambia kua amemsamehe Madhambi yake yaliyotangulia na yajayo?
Ambapo Jibu la suali hili ni kua: ‘Istighfar za Mitume wote hua ni sehemu ya Ibada
kwao wao yaani ni sehemu ya kufanya mema ambayo hua hali tofauti na Istighfar
919
zetu sisi mimi na wewe ambazo hua ni zenye kumaanisha kuomba Msahama kwa
makosa yetu mbele ya Mola wetu, na vile vile Istighfar za Mitume hua pia ni kwa
ajili ya Watu waliomo katika Ummah wao yaani hua ni wenye kuwaombea watu
wawasamehe madhambi yao’
Mnamo mwaka wa 10 Al Hijra basi Rasul Allah Salallahu Alayh wa Salam akatangazia
rasmi nia yake ya kuenda katika Ibada ya Hija ya mwaka huo, tangazo ambalo lilisambaa
kwa kasi kubwa sana kuliko moto unavyosambaa kwenye msitu uliokauka kwa ukame,
na hivyo watu wengi sana nao wakajianda kwa ajili ya kuenda katika Ibada ya Hija ya
Mwaka huo kiasi ya kua idadi ya Mahujaji mwaka huo walikua ni zaidi ya watu 100,000
ambapo anasema Jabir Ib Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Watu walikua wengi kiasi
ya kua ilikua nnaona watu hadi kwenye upeo wa Macho yangu.’
Ambapo anasema Jabir Ibn Abd Allah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alikaa katika Mji wa Madina kwa mda wa miaka 9 ambayo ndani
yake hakua ni mwenye kuhudhuria kwenye Ibada ya Hija.
Hivyo ndani ya mwaka huu wa 10 watu wengi sana walikuja katika Mji Wa Madina
kwa ajili ya kua na matumaini ya kujifunza kufanya Ibada kama afanyavyo yeye.
Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alianza safari yake kuelekea Makkah
pale ilipokua zimebakia siku 5 kabla ya kumalizika Mwezi wa Dhul Qadah, nasi
tukafunga safari pamoja nae’(Imam Ahmad, Imam Muslim)
Na anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Watu wa
Ujahiliyah walikua wakifikiria kua kufanya Umra katika wakati wa mwezi wa Dhul
Hija ni moja katia ya Dhambi kubwa sana juu ya Ardhi, na pia walikua wakifikiria
kua Mwezi wa Safar ni mwezi Mtukufu na walikua wakisema kua: ‘Wakati Jeraha
la mgongoni mwa Ngamia linapopona (baada ya kurudi katika Ibada ya Hija) na
alama ya Jeraha hilo inapotoweka, na mwezi wa Safar unapopita basi Umra hua
inaruhusiwa kwa yule anaetaka’
Hivyo Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam na Masahaba zake aliwasili katika
Mji wa Makka katika siku ya mwezi 4 ya Dhul Hijjah, wakavaa Ihram kwa ajili ya
Hija, na kisha Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akawaamrisha Masahaba
zake watie nia zao kwa ajili ya Umra tu, na hivyo Masahaba wakashangaa na
wakamuuliza Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam kwa kusema: ‘Ya Rasul Allah!
Hivi jee ni aina gani ya Ihram ya kumalizia iliyoruhusiwa?’’ na Rasul Allah
Salallahu A’layhi wa Salam akasema: ‘Malizeni Ihram kikamilifu kwani
mmeruhusiwa kufanya kila kitu’(Imam Bukhari)
920
Baada ya kuondoka katika Mji wa Madina msafara wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam ukawasili kata meneo ya Dhul Hulayfah ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi Wa
Salam akawafundisha Waislam namna ya kufanya Ibada ya HIja, na kisha akavaa Ihram
na kuelekea katika Mji wa Makkah ambapo aliwasili nje ya mipaka yake katika maeneo
ya Dhi Tuwa baada ya wiki moja na wakapiga tena kambi katika meneo hayo hadi siku
ya pili yake ndio wakaingia katika Mji wa Makkah na kuelekea moja kwa moja kwenye
Masjid Al Haram kupita katika upande wa Mlango wa Bab Al Salam.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na msafara wake wa Mahujaj hao ukafanya
Tawwaf na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akalibusu Hajar Al Aswad na
kisha akasali na kuomba dua na kunywa Maji ya Zamzam. Na kisha akaelekea kwenye
milima ya Safa na Marwah akafanya Sa’i ba kisha akaelekea kwenye maeneo ya Al
Hujjun. Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawaamrisha Masahaba zake
ambao walikua wamewasili bila ya kua na wanyama wa kuchinja kua wavae Ihram kwa
ajili ya Umra kisha wafanya Tawwaf na Saai na hii ni kwa sababu Waislam walikua na
malengo ya kufanya Hijjat Qiran ambayo ni yenye kujumiisha Umra na Haji kwa pamoja.
Hivvyo mnamo mwezi 8 Dhulhijja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akawasili
kwenye maeneo ya Minna na kusali Sala ya Adhuhuri na kushinda na kulala katika eneo
hilo hadi katika siku ya pili yake baada ya Sala ya Alfajir ya mwezi 9 akaondoka na
kuelekea kwenye maeneo ya Arafah akapiga kambi kwenye eneo la Namirah lilopo
upande wa Mashariki wa Mlima wa Arafah ambapo alipumzika kidogo na kisha
akaeleekea katika maeneo ya Uranah na kutoa Khutba yake ya Mwisho.
Na kisha akaelekea katika maeneo ya Muzdalifah katika wakati wa Magharibi ambapo
alisali Sala ya Magharibi na Isha na kupumzika hadi Alfajiri ya siku ya pili yake akarudi
tea katika maeneo ya Minna na kuelekea kwenye maeneo ya Jammarah na kufanya Ibada
ya kurusha mawe na kisha akachinja na kisha akarudi katika Mji wa Makkah na kufanya
tena Ibada ya Tawwaf na kusali sala ya Adhuhuri ndani ya Masjid Al Haram, kisha
akanywa maji ya Zamzam na kurudi katika meneo ya Minna ambapo alikaa kwa siku 3
za Ayyami Tashriq kuanzia mwezi 10,12 na mwezi 13 Dhul Hijjah na kisha akaanza
safari ya kurudi katika Mji wa Madina.
KHUTBA YA KUAGA YA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI
WA SALAM.
Mnamo siku ya Ijumaa ya mwezi 9 Dhul Hijjah ya mwaka huo wa 10 Al Hijr alipokua
katika Ibada ya Hija katika maeneo ya Arafah basi Rasul Allah Salallahu A’layhi wa
921
Salam baada ya Kumshukuru Allah Subhanah wa Ta’ala na kumtukuza alitoa Khutba
ifuatayo:
‘Enyi watu, nakuombeni mnisikilize kwa umakini, kwani kwa hakika mimi ni
mwenye kujua kua baada ya mwaka huu basi sitoweza kua tena miongoni mwenu.
Hivyo nisikilizeni vizuri kuhusiana na kile nitakachokisema ili mpate kufikisha
haya nitakayoyasema kwa wale wasiokuwepo leo hii hapa tulipo.
Enyi watu ama kuhusiana na Mwezi huu, na siku hii na Mji huu na Utukufu wake,
na kuhusiana na Uhai na Mali za kila Muislam kua ni Amanah Tukufu. Hivyo
rudisheni Amanah za watu mlizopewa kwa waliokukabidhini Amana hizo. Ili
Msidhuru na wala Msipate kudhuriwa. Kumbukeni kua Mtakutana na Mola wenu
ambae nae atayahesabu Matendo yenu.
Allah Subhanah wa Ta’ala amekuharamishieni kula Riba, hivyo Kila chenye Riba
inabidi iondolewe Riba yake, Mitaji yenu ni mitaji yenu hivyo ihifadhini na
hamtodhurika wala hamtodhuru kutokana nayo Allah Subhanah wa Ta’ala ametoa
Hukmu kua: ‘Riba zate anazodaiwa Abbas Ibn Abd Al Mutallib zifutwe.’
Hivyo kila haki ambayo ilitokana na mauaji ya Ujahiliya basi imefutwa na haki ya
mwanzo ambayo nnaifuta ni ya mauaji ya Rabiah Ibn Al Harithah’
Enyi watu, hakika ya wale wasioamini hua ni wenye kuiingilia kuhusiana na
Kalenda ili kuhalalisha kile ambacho Allah Subhnaha wa Ta’ala amekiharamisha,
na kuharamisha kile ambacho amekihalalisha, ambapo Mbele ya Allah Subhanah
wa Ta’ala kuna miezi 12 na ndani yake mna miezi minne ambayo ni Mitukufu na
miongoni mwao ni yenye kuendana sambamba na mmoja kati yao ni wenye kuwepo
baina ya Jumada na Shaaban.
Hivyo kuweni na umakini dhidi ya Shaytan wa ajili ya usalama wa Dini yenu, kwani
amepoteza matumaini kutokana na kutoweza kukupotosheni katika mambo
makubwa hivyo kuweni na umakini nae katika mambo madogo madogo.
Enyi watu ni kweli kua mna haki juu ya Wanawake zenu, lakini na wao pia wana
haki juu yenu. Kumbukeni kua mmewachukua wao kua ni wake zenu kutokana na
Kuaminiwa na Allah Subhanah wa Ta’ala na kutokana na Ruhusa yake. Hivyo
kama wakikutiini basi juu yao watakua wanastahiki kulishwa na kuvishwa
kutokana nanyi kwa upole na ukarimu. Hivyo kaeni nao vizuri Wanawake wenu
kuweni na huruma nao kwani wao ni wenza wenu na ni wasaidizi wenu. Na ni haki
yenu kua wasiwe na urafiki na yeyote yule ambae hamkubaliani nae na pia wasiwe
ni wenye kufanya machafu.
922
Enyi Watu, nisikilizeni kwa umakini sana, muabudini Allah Subhanah wa Ta’ala,
salini Sala zenu 5, Fungeni Ramadhani, Toweni Zakkah na Fanyeni Ibada ya Hija
kama mtakua na uwezo.
Fahamuni kua Watu wote ni wenyekutokana na Adam na Hawa, hivyo Muarabu
hana utukufu mbele ya asiekua Muarabu na wala asiekua Muarabu hana utukufu
mbele ya Muarabu, pia Mweupe hana utukufu mbele ya Mweusi na wala Mweusi
hana utukufu mbele ya Mweupe isipokua kwa Ucha Mungu wake na wema wake.
Jifunzeni kuaKila Muislam ni ndugu wa Kila aliekua Muislam na Uislam ni Udugu,
hivyo hakitokua halalia kitu chochote cha Muislam kwa Muislam mwengine
isipokua pale kitu hicho kitakapotolewa na kugaiwa kwa uhuru na hiari.
Hivyo msifanye dhulma na wala msijidhulumu. Kumbukeni kua kuna siku ambayo
mtakutana na Mola wenu na mtaulizwa juu ya amali zenu. Hivyo tahadharini msije
mkapotoka kutoka katika njia iliyonyooka baada ya kuondoka kwangu.
Enyi watu hakika hakuna Nabii wala Mtume atakaekuja baada yangu, na hakuna
Imani mpya itakayotokea baada yangu, hivyo tafakarini ninachokuambieni Enyi
watu ili mpate kufaham ninayokuambieni, kwani nnawacha vitu viwili baada yangu
ambavyo ni Quran na Sunah hivyo mkivifuata hivi basi hamtopotoka. Na kila
aliesikia kutoka kwangu basi ni wajibu wake kufikisha maneno yangu kwa wengine
na wengine kwa wengine na naomba kua wa mwisho wawe ni wenye kunifaham
zaidi kuliko wanaonisikiliza leo hapa mbele yangu.
Hivyo Msije mkaasi baada yangu kama walivyofanya Makafiri, na mkaanza
kukatana vichwa wenyewe kwa wenyewe.
Ya Allah kua shahidi wangu kua nimefikisha ujumbe wako kwa waja wako.
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasoma aya aliyoshushiwa katika wakati
huo huo ambayo ni ile isemayo:
﴿ٱلْيَوْمَ يَئِسَ ٱل َّذِينَ كَفَرُواْ مِن دِينِكُمْ فَلاَ تخَْشَوْهُمْ وَٱخْشَوْنِ ٱلْيَوْ مَ أَكْ مَ لْتُ لَكُ مْ
دِينَكُمْ وَأَتمَْمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتىِ وَرَضِيتُ لَكُمُ ٱلأِسْلاَمَ دِيناً ﴾
923
Alyawma ya-isa alladheena kafaroo min deenikum fala takhshawhum waikhshawni
Alyawma akmaltu lakum deenakum waatmamtu AAalaykum niAAmatee
waradheetu lakumu al-islama deenan (Surat Al Maidah 5:3)
Tafsir: Leo hii Makafiri wamevunjika Moyo dhidi ya Dini yenu, hivyo msiwe na khofu
nao bali kuweni na khofu nami (Allah Subhanah wa Ta’ala). Siku hii nimeikamilisha
Dini kwa ajili yenu na nimekukamilishieni Neema yangu juu yenu na nimeridhia juu
yenu kua Uislam ni Dini yenu.
Ambapo khutba hii ilikua ikirudiwa na neno kwa neno na Rabiah Radhi Aallahu Anhu
ambae alikua ni mwenye sauti kali sana baada ya kuombwa na Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua afanye hivyo ili wasikie watu wengi zaidi, kisha Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akauliza: ‘Enyi watu, hivi jee nimefikisha Ujumbe kwenu
nyie ama la?’ na hapo watu wakaitikia kwa sauti kubwa sana kama radi isemayo:
‘Allahuma Naam’ hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akanyoosha juu kidole
chake cha shahada ma kusema: ‘Ya Allah, hakika wewe ni shahidi kua nimefikisha
ujumbe wako kwa waja wako.’
Miezi miwili baada ya kumalizika Ibada yake ya Hija basi Rasul Allah Salallahu A’layhi
wa Salam alifariki Dunia tukio ambalo liliwachaganya na kuwahuzunisha Viumbe wengi
sana Ulimwenguni.
KIFO CHA NABII MUHAMMAD SALALLAHU A’LAYHI WA SALAM.
Neno Baka kwa Kilugha hua linamaanisha Kulia Machozi, Kutokwa na Machozi,
Kulalamika huku Machozi yakiwa yanatoka.
Katika wakati tunaoishi leo hii basi tuko katika kipindi ambacho kimejaa matukio ya
Kusikitisha na hivyo kua ni yenye kupelekea kuwatoa watu Machozi kutokana na
Uchungu wa Ubaya wake kwa wanaofanyiwa Ubaya na pia kutokwa na machozi kwa
wale wanaoyaona Matukio hayo wakiwa mbali kwa Macho yao, na kuingiwa Uchungu
na huruma ndani ya Nyoyo zao kutokana na Madhara yanayowafika Waislam wengi sana
Ulimwenguni kutokana na kuachana na Wasia wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
katika khutba yake ya mwisho hususan tukiangalia maneno yasemayo: ‘Hivyo Msije
mkaasi baada yangu kama walivyofanya Makafiri, na mkaanza kukatana vichwa
wenyewe kwa wenyewe.’
Na tunapozungumzia kuhusiana na Baka yaani Kulia Machozi basi si mimi na wewe tu
tuliojaaliwa uwezo wa kulia bali hata Mbingu na Ardhi pia nazo katika wakati huu
924
zinalia, kama anavyosema Allah Subhanah wa Ta'ala Katika Qur'an alipowazungumzia
watu wa Fir'awn kua;
﴿فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ ٱلس َّمَآءُ وَٱلأَرْضُ وَمَا كَانُواْ مُنظَرِينَ ﴾
Fama Bakat aA’layhim Alssamau wa Al Ardhu wama kanuu mundhirina (Surat Ad
Dukhan 44:29)
Tafsir: Na Hawakuliliwa (Na) Mbingu na Ardhi na Wala hawakucheleweshewa Mda
Kwani amaesema Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wakati Muumini
anapofariki basi ile sehemu ambayo alikua akiisujudia katika wakati wa kusali
kwake hua inalia kwa ajili yake, na pia ile sehemu ya Mbingu ambayo Amali njema
zake hua zinapitia kwenda juu hua pia inalia kwa ajili yake. ’
Hivyo kwa Mtu yeyote yule asiemuamini Allah Subhanah wa Ta'ala na Asiesali basi
anapofariki hali yake hua kama ya Kina Fir'awn kwani hua Haliliwi na Mbingu wala na
Ardhi kwa ajili yake.
Kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Hakuna Muumini
isipokua hua kuna Milango Miwili Mbinguni kwa ajili yake kuna Mlango ambao
Riziki yake hua inashuka kupitia kwake na kuna Mlango Ambao Mema yake na
Maneno yake hua Yanapanda kupitia kwake Na anapokufa basi Humtamani na
hivyo Hulia kwa ajili yake ‘(Imam At Tirmidhii)
Na akasema Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Ardhi hua ni
yenye Kumlilia Muumini wa Allah Subhanah wa Ta'ala kwa siku 40 baada ya
kufariki kwake’(Mustadrak Al Hakim)
Na akasema tena Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Ukimona Muislam
anakaribia kufariki basi muelezee kuhusiana na Mambo Mema ili akutane na Mola
wake huku kiwa anamfikiria kwa Mema Juu yake, na ukimuona Mtu Mzima ana
Afya basi Mtie khofu juu ya Mola wake’
Naam..Waislam wa leo tuna Unafiq na Imani Dhaifu kwa sababu Hatuna Khofu juu ya
Mola wetu!
Kwani nasi pia Alhamd lillah inaonekana kua tuna Afya na wenye nguvu kimwili, na
hivyo kulingana na hadith basi sisi ni bora kuliko Waumini waliokua Dhaifu kiafya.
925
Na ingawa ni wenye Uimara wa Nguvu za Mwili na Afya lakini tuna Udhaifu wa Imani,
hivyo na tujinufaishe na wasia wa Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu
kuhusiana na Kumuogopa Allah Subhanah wa Ta'ala kwa kukumbushana kuhusiana na
Kifo Ambapo anasema Imam Abd Allah Ibn Muhammad Ibn Ad Duniyah kua:
Wakati Amir ul Muuminin Umar Ibn Abd Al Aziz anataka kukata roho, basi
aliwaambia wale waliokaribu yake wasogee Karibu
Kisha waliposogea basi akawa anasema; ‘Kwa hakika nyinyi mliniamrisha mimi
lakini nami sikutekeleza maamrisho yenu Mlinikataza nami nikawa Muasi’
akayasema kwa kuyarudia maneno hayo mara 3.
Kisha akasema: ‘Lakini La Ilaha illa Allah!’
Watu waliokuwepo hapo wakatizamana, kisha wakasema: ‘Ewe Amir ul Muuminin
Unaonekana kama Umezidiwa’
Amir ul Muuminin Umar Ibn Abd Al Azizi akasema: ‘Hakika Mimi nnaona hali ya
sehemu ambayo haina Ibn Adam wala Majini’ Na kisha akakata roho.’
Hivyo tunapozungumzia Mauti basi hua tunazungumzia kitu ambacho hakuna anaejua
siri yake isipokua Mwenyewe Rabbi Al Alamiin ambae ndie Muumba wa Kila kitu na
ambae ni Allah Subhanah wa Ta'ala.
Na ndio Maana Allah Subhanah wa Ta'ala akahoji kuhusiana na wale wasiomuamini kwa
kusema katika Qur'an:
﴿تَنزِيلٌ مِّن ر َّبِّ ٱلْعَالَمِينَ۞أَفَبِهَٰذَ ا ٱلحَْدِيثِ أَنتُمْ م ُّدْ هِ نُونَ ۞وَتجَْعَلُونَ رِزْقَكُ مْ أَن َّكُمْ
تُكَذِّبُونَ۞فَلَوْلاَ إِذَا بَلَغَتِ ٱلحُْلْقُومَ۞وَأَنتُمْ حِ ينَئِذٍ تَنظُرُونَ۞َونحَْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُ ْم
وَلَٰكِن لا َّ تُبْصِرُونَ ﴾
Tanzeelun min rabbi alAAalameena; Afabihadha alhadeethi antum mudhinoona;
WatajAAaloona rizqakum annakum tukadhdhiboona, Falawla idha balaghati
alhulqooma; Waantum heena-idhin tandhuroona; Wanahnu aqrabu ilayhi minkum
walakin la tubsiroona; (Surat Al Waqiah 56:80-85)
926
Tafsir: (Hii Qur'an) Ni Teremsho kutoka kwa Mola wa Ulimwengu wote na Kila
kilichomo ndani yake. Hivi Jee (Mnaiona Qur'an) kua hizi ni Hadith tu ambazo Nyinyi
Mnazikadhibisha? Na kwa Kukujaalieni Nyinyi Riziki zenu, Basi ndio
Mnamkadhibisha? Kwanini Basi Humiuingilii kati Wakati (Roho ya Mtu wenu
anapotaka kufa) Inapofika Kooni? Wakati Nyinyi Mkiwa hapo hapo huku
Mnangalia? Na Nasi tuko Karibu Nae kuliko Mlivyokua nae nyinyi, Lakini Nyinyi
Hamui wenye kuona.
Kwani aya inatuonesha kua kwa Muumini kukifikiria Kifo basi hua Kunamtosheleza kua
ni Sababu ya Kua na Taqwa. Kwani Haram Ibn Hayan alisema : ‘Inakuaje hali ya Mtu
anautumia Mda wake wa Mchana huku akiwa hana uhakika kama atafika Usiku
wake siku hio ama la, na kama ataenda Peponi au Motoni. Hivyo Unapoenda Kulala
Usiku basi Tegemea kukutana na Kifo, na Unapoamka Basi Sali na Umuombe Allah
akurekebishie na auweke sawa Moyo na Nia yako katika Amali zako.’
Neno Faniya kwa lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kuteketea, Kukoma kuwepo,
Kuharibika na hakifai tena, Kufariki, Kuaga Dunia, Kuyayuka, Kuoza. Na pia hua
linamanisha Kitu ambacho hua Hakiwezi kudumu Milele yaani Kitu ambacho hata kikae
vipi lakini mwisho wake kitaharibika na kutoweka.
Ambapo Neno Faniya ndio lililotoa Neno Fanin ambalo Humaanisha hali ya Umoja wa
Kitu ya Kutoweka kwake.
Kwani amesema Allah Subhanah wa Ta'ala kua:
﴿كُل ُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ۞وَيَبْقَى ٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو ٱلجَْلاَلِ وَٱلإِكْرَامِ ﴾
Kullu man AAalayha fanin; Wayabqa wajhu rabbika thoo aljalali waalikrami
(Surat Ar Rahman 55:26-27)
Tafsir: Kila Kitu Kilichopo Juu yake (Ulimwenguni) kitatoweka Na Utabakia Milele
Uso wa Mola wako Mkamilifu wa Ufalme na Utukufu.
Ambapo maana ya Neno Wajhu Ambalo nimelitafsiri kama Uso wake basi limetokana
na neno Wajaha ambalo hua linamaanisha Kueleka, Kupiga kibao cha uso, Kutunga,
Kuelekeza, Kutuma, Kuelekea.
Neno Wajaha ndio lililotoa neno Wajhun ambalo hua linamaanisha Uso, Muelekeo,
Qibla, Moyo, Nafsi, Roho, Muonekano, Mwili na pia humaanisha Lengo au Dhumuni
927
Hivyo Aya imesema kua: Kila kilichopo Juu yake Ulimwenguni hakitodumu
Kitatoweka au kitaangamia, au kitakufa na kitakachobakia Milele ni Wajhu
Rabbika yaani Uso au Muonekano wake Muumba.
Na hapa pamezungumziwa Muonekano kwa sababu ya kutubainishia sisi Ibn Adam ili
tufaham zaidi kwani hua tunajuana kutokana na Muonekano wetu, na hivyo basi Aya
unamaanisha kua ni Ufalme Kamilifu wa Allah Subhanah wa Ta'ala ndio utakaobakia
Milele
Kwani tunaona kua aya yetu zimemalizia na Neno Ikrami ambalo ni lenye kutokana na
neno Karama au Karuma ambalo hua linamaanisha Kua na Ukarimu, Kua Na Huruma
Katika kutoa, Kutokua na Ubakhili, Kua ni Mfano wa Kuigwa Katika Kutoa Msaada na
kusaidia kwa kutoa vitu vyenye Manufaa kwa wingi bila ya Kujali kupungukiwa katika
utoaji huo.
Ambapo bila ya shaka mara Nyingi hua Tunaambiana Ramadhani Karim au Ijumaa
Karim na kwa baadhi yetu bila ya Kujua maana yake. Hivyo Maana ya Ramadhani au
Ijumaa Karim hua inamaanisha Ramadhani au Ijumaa yenye Huruma na Ukarimu wa
Rehma za Allah kimanufaa.
Na pia kutokana na kua Al Karim ni Kati ya Majina Matukufu ya Allah Subhanah wa
Ta'ala basi hua pia unaposema Ramadhan Karim au Ijumaa Karim hua unamaanisha
Ramadhani au Ijumaa iliyotokana na Mwenye sifa ya Utukufu wa Mwing wa Ukarimu
yaani Allah Subhanah wa Ta'ala.
Na ndio Maana mtu unapoambiwa Ramadhan Karim au Ijumaa Karim basi unakua
unajibu Allahu Akram yaani unarhibitisha kua hii Ijumaa au hii Ramadhani imepatikana
kutokana na Allah Subhnaha wa Ta'ala ambae ni Mbora zaid wa Ukarimu kwa
kutuneemesha kila Neema tunayoihitaji katika Maisha yetu hpa Duniani kutokana na
Ukarimu wake.
Na hivyo Ukisema Ijumaa Karim basi tayari umeshainesha Shukran kwa Mola wako kwa
kukujaalia Ukarimu wa Siku ya Ijumaa au Ramadhani. Na ukijibu Allahu Akram basi
tayari hua ushafanya Dhikr Allah!
Subhanah Allah! Hio ndio sifa ya Ukarimu wa Dini ya Uislam ambayo ni Dini ya Mwingi
wa Ukarimu alietukirimu kila kitu kwa Ukarimu wake
Lakini sasa hayo mpaka uyajue, ambapo ukweli ni kua hali iko kama alivyosema Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua kila kitu chema hua ni Sadaqa
928
Na tunapoiangalia aya yetu basi tunaona kua imemalizia na neno Ikrami, Ambapo nalo
tumesema kua limetokana na neno Karama na hivyo basi hapa maneno Dhu Al Jalali wa
Al Ikrami hili hua yanamaanisha kua: Kutokana na Ukamilifu wake wa Ufalme Mtukufu
na Ukarimu wake basi Allah Subhanah wa Ta'ala hastahiki kushirikishwa na kitu
chochote kile kwani yeye ndie pekee mwenye Uwezo wa Kukirimu Viumbe wake wote
kwa Milele kwa Makadirio yake na kwa kadri atakavyo bila ya Kuathirika kwa
kupungukiwa na chochote katika Kukirimu kwake
Kwani Maneno haya yanatuwekea Wazi kua Kila Kitu na kila Kiumbe Ulimwenguni si
kua tu ni chenye kumilikiwa na Allah Subhanah wa Ta'ala, lakini pia yanaamaanisha kua
Kila kitu kilichopo Ulimwenguni Kinamhitaji yeye Allah Subhanah wa Ta'ala na pia kua
ni chenye kuhitaji Ukarimu wake, kwani vyengine basi hakuna kitakachoweza kuwepo.
Yaani kutokana na kua kila kitu kinamilikiwa na kinamhitaji yeye Mmiliki ambae ndie
Muumba wa Kila kitu yaani Allah Subhanah wa Ta'ala.
Basi Bila ya Shaka Kila kitu Alichokiumba na Kukitoa kikaja Ulimwenguni, basi
Kitarudi kwake yeye mwenyewe Muumba kulingana na Ukarimu wa Makadirio yake juu
ya kitu hicho kiishi kwa mda gani hapa Ulimwenguni.
Na bila ya Shaka kwa kua vitu hivyo kavikirimu na kuvionjesha Uhai hapa Ulimwenguni
basi pia atavikirimu kwa kuvirudisha kwake kwa kuvionjesha na Kifo. Kwani Allah
Subhanah wa Ta'ala anaelezea haya katika Qur'an pale aliposema:
﴿قُتِلَ ٱلإِنسَانُ مَآ أَكْفَرَهُ۞مِ نْ أَىِّ شَ يءٍ خَ لَقَهُ۞مِن ن ُّطْفَةٍ خَلَقَهُ فَقَ د َّ رَهُ ۞ثمُ َّ
ٱلس َّبِيلَ يَس َّرَهُ۞ثمُ َّ أَمَاتَهُ فَأَقْبَرَهُ۞ثمُ َّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُ۞كَلا َّ لَم َّا يَقْضِ مَآ أَمَرَهُ ﴾
Qutila al-insanu ma akfarahu; Min ayyi shay-in khalaqahu; Min nutfatin
khalaqahu faqaddarahu; Thumma alssabeela yassarahu; Thumma amatahu
faaqbarahu ; Thumma idha shaa ansharahu; Kalla lamma yaqdi ma amarahu
(Surat Abasa 80:17-23)
Tafsir: Ameangamia Mtu, (Jee ni)Nini Kilichomfanya Akufuru? Hiji Jee(Anajua)
Amemuumba Kutoka na Nini? Ni Kutokana na Tone Amemuumba na Akamkadiria
katika Umbo alilokua nalo, Na Kisha akamuonesha Njia (Sahih ya kumelekea Mola
wake) rahisu kwa ajili yake Na Kisha Akamsababishia Kifo na Kumtia ndani ya Kaburi
Na Kisha pale atakapotaka (Allah Subhanah wa Ta'ala) Atamfufua (Kiumbe wake)
929
Kwani Amir Ul Muuminin Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kumwambia Mtoto wake
Hasan Ibn Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhu kuhusiana na Uhai wake hapa Duniani
na kuhusiana na Kifo chake kua: ‘Ewe Hasan, Ewe Mtoto Wangu, Kifuatilie Kifo
Vizuri sana mpaka ukijue, ili uwe ni mwenye kukikumbuka bila ya kukisahau. Ili
kinapokujia basi kisikushangaze wala kisikughafilishe’
Kwani anasema Imam Wahb Ibn Munabih kua: ‘Kila siku asubuhi Malaika
wanatangazia kutoka Mbingu ya Nne kuwambia watu kwa kusema: Enyi Mlio
kwenye umri wa miaka 40, hakika mmepea na kuvunwa kwenu kunakaribia
Enyi Mlio kwenye Umri wa miaka 50, mmeshatangulia, Jee ni nini kilichokuzuieni
Enyi Mlio kwenye Umri wa miaka 60 Hamna kisingizio, kwani kila kiumbe
alieubwa anajua kwanini akaumbwa, hivyo mda wenu umeshawadia Jitayarisheni’
Kwani Allah Subhanah wa Ta'ala amesema katika Qur'an kua atawahoji watu kwa
kusema:
﴿وَهُ مْ يَصْطَرِخُونَ فِيهَا رَب َّنَآ أَخْرِجْنَا نَعْمَلْ صَالحِ اً غَيْرَ ٱل َّذِى كُن َّا نَعْمَلُ أَوَلمَْ
نُعَمِّرْكُمْ م َّا يَتَذَك َّرُ فِيهِ مَن تَذَك َّرَ وَجَآءَكُمُ ٱلن َّذِيرُ فَذُوقُواْ فَمَا لِلظ َّالِمِينَ مِن
ن َّصِيرٍ ﴾
Wahum yastarikhoona feeha rabbana akhrijna naAAmal salihan ghayra alladhee
kunna naAAmalu awa lam nuAAammirkum ma yatadhakkaru feehi man ta
dhakkara wajaakumu alnnadheeru fadhooqoo fama lildhdhalimeena min
naseerin(Surat Fatir 35:37)
Tafsir: Huku wakiwa ni wenye kulia ndani yake kwa kusema: ‘Ewe Mola wetu tutoe
ndani yake, tutfanya Mema na hatutofanya tuliyokua tukiyafanya ’(Allah Subhanah
wa Ta’ala atawajbu)kwa kuwaambia: ‘Hivi Jee Hatukukupeni Nyinyi Umri Mrefu
Ili atakaeweza Kukumbuka Ndani yake Aweze kukuumbuka anachotakiwa
kukumbuka Wakati alikujieni Muonyaji. Hivyo onjeni kwani kwa Madhaimu basi
hakuna wa kuwasaidia.
Kwani kuhusiana na Umri mrefu uliotajwa hapa kwenye aya basi Wanazuoni
wametofautiana juu yake kwani Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu na
Hasan Al Basr basi wao wanasema kua Umri unaozungumziwa hapa ni wa kuanzia miaka
930
40. Ambapo kwa wengine kama kina Imam Qatadah Al Sadusi basi yeye anasema kua ni
miaka 18 tu.
Na bila ya shaka Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi yeye amesema katika
Hadith kua: ‘Allah hataki kisingizio kwa mtu ambae amempa mda mpaka kufikia
umri wa miaka 60’
Hivyo Ibn Adam kupewa Umri mrefu na Mola wako bila ya kua ni mwenye kufanya
mema basi kutampelekea mru huyo kua ni mwenye Kujuta kesho Akhera. Kwani
asiejisalimisha hadi kufikia Umri huo basi bila ya shaka atakua hana kisingizio kwani
atakua ni Muasi wa kukusudia mbali ya kua alipata Ukumbusho.
Kwani amesema Mujtahid Imam Imam Malik Ibn Anas ambae ndie Muanzilishi wa
Madhhab ya Maliki kua: ‘Hakika mimi nimeona Watu katika Mji wangu ambao
walikua wakitafuta Mali na Ilm na kujichanganya na watu kabla ya kufikia Umri
wa miaka 40. Na walipofikia Umri wa miaka 40 basi waliachana na Dunia na
wakajiandaa kujitafutia yale yatakayo wanufaisha na Akhera yao hadi kufa kwao’
Ambapo kuhusiana na maneno Wajaakum Al Nadhiru - Na Wakati alikujieni Muonyaji
Basi kuna wasemao kua ni Mitume
Ambapo kwa upande wa Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, Imam
Sufyan Ath Thawri, Imam Husayn Ibn Al Fadhl nk basi wao wamesema kua: ‘Muonyaji
aliekusudiwa hapa hua ni Mvi unapokua Mtu mzima, na pia hua Ni Maradhi pale
baada ya kua na Afya na Kifo cha Mwenzio pale wewe unapokua wewe upo hai.’
Naam..hivyo kila mtu ahesabu umri wake na Muonyaji wake kisha ayaangalie Malengo
yake! Kwani anasema Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu kua: Siku moja nilikua
natembea na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam katika Mashamba ya Mitende
Kisha tukasimama na Kupumzika, ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alisimama karibu na Jani la Mtende.
Mara wakapita Mayahudi ambao wakaambiana wenyewe kwa wenyewe kwa kusema
kua: Muulize kuhusiana na Roho kisha mwenzake akasema: 'Una Shaka kuhusiana na
kumuuliza kuhusiana nayo?
Mwengine akasema: Usimpe Ruhusa kukujibu juu ya kile kitu ambacho
hutokipenda kupata Jawabu lake
931
Hivyo Mayahudi hao wakamuuliza Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuhusiana na
Roho, lakini nae akakaa kimya hakuwajibu, na hapo ikanijia wazi kuhisi kua Anataka
kushushiwa Wahy, hivyo nami nikasimama karibu yake wakati inashushwa aya isemayo
﴿وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ ٱلر ُّوحِ قُلِ ٱلر ُّوحُ مِنْ أَمْرِ رَبىِّ وَمَآ أُوتِيتُم مِّنَ ٱلْعِلْمِ إِلا َّ قَلِيلاً ﴾
Wayas-aloonaka AAani alrroohi quli alrroohu min amri rabbee wama ooteetum
mina alAAilmi illa qaleelan (Surat Al Isra 17:85)
Tafsir: Na Wanakuuliza (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) Kuhusiana
na Roho,Waambie Kua Roho Ni kitu ambacho Ilm Yake iko Chini ya Mola Wangu,
Na Mmepewa Ilm juu yake Ila Kidoogo tu.
Kwani anasema pia Bahr Ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kuhusiana na
aya hii kua: Aya hii ilishuka kwa sababu Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
aliulizwa na Mayahudi kuhusiana na Roho, Maumbile yake, Iko vipi na itakuaje
iadhibiwe wakati Inakaa Ndani ya Mwili wa Kiumbe
Ambapo tunapoifuatilia aya hii basi Kulingana na Hadith ya Kwanza ya Abd Allah Ibn
Masud Radhi Allahu Anhu basi tunaona kua Hii aya ilishushwa katika Mji wa Madinah
ambako ndio kwenye Mashamba Makubwa ya Mitende na pia ndio kwenye Makazi ya
Mayahudi kwa kipindi cha Wakati huo.
Lakini pia kwa Upande mwengine basi tunapoifutailia kwa kina basi tunaona pia kuna
Mtizamo usemao kua: ‘Aya hii Ilishuka pale Mayahudi walipowapa Mbinu
Maquraysh wa Makkah ili wamkwamishe Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kwa Hoja na Masuali, hivyo wakawaambia Maquraysh kua Wamuulize kuhusiana
na Roho na Wakamuuliza’
Na pia inawezekana kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aliulizwa Suali hili
alipokua katika Mji wa Makkah na pia akaulizwa tena alipokua katika Mji wa Madinah
.
Na hii pia ni kwa Sababu Miongoni mwa Masahaba na Wanazuoni hua Wanalitafsiri
Neno Ruhi liliomo kwenye Aya hii kua Linahusiana na Jina la Malaika Jibril, ambalo ni
Ruhi Al Qudus.
Kama tulivyoona pale tulipokizungumzia kisa cha Nabii Isa Ibn Maryam pale Maryam
bint Imran aliposhukiwa na Malaika Jibril kuambiwa kua atapata Mtoto, lakini
tunaporudi kwa Masahaba tulioanza nao kwenye hadithi yaani Masahaba Abd Allah
932
Wawili ambao ni Masahaba Wanazuoni Wawili yaani Abd Allah Ibn Masud Radhi
Allahu Anhu na Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu, ambapo ingawa Abd Allah Ibn
Masud Radhi Allahu Anhu alikua mkubwa kiumri kuliko Abd Allah Ibn Abbas Radhi
Allahu Anhu.
Lakini Mtizamo wao na Ilm yao basi zinatuwekea wazi kua Hili jibu la Suali hili halikua
likihusiana na Malaika Jibril bali lilikua kama walivyosema wao kua linahusiana na Roho
ya Viumbe wakiwemo Ibn Adam.
Ambapo Suali na Jawabu lake bado linabakia pale pale, kua iwe ni Malaika Jibril au iwe
ni kuhusiana na Roho zetu basi Bila ya shaka hakuna anaejua kuhusiana navyo vitu viwili
hivyo ila Qalilan.
Kwani alisema Hujjat Ul Islami Mujaddid Ad Din Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii
Al Thani Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhqmmad Al Ghazali kua: Hakika ya Mimi kila ninavyozidi Kusoma na Kuzidi
Kujua basi Ndivyo Ninavyozidi kujiona kua Kumbe Mimi ndio Sijui kitu Chochote.
Na ndio maana unapokutana na Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye
alisema kuhusiana na Imam Al Ghazali kua: ‘Hujjat Ul Islam alikua na Ilm kubwa
Sana kama vile ambavyo Allah Subhanah wa Ta'ala aliikusanya Ilm Tofauti katika
sehemu Moja na kisha akamuonesha Imam Al Ghazali sehemu alipoiweka Ilm hio’
Na bila ya shaka hii hua linaonekana wazi pale unajua kua Miongoni mwa Watu
wanaofanyiwa Uchunguzi sana Ulimwenguni kuhusiana na Ilm zao na maneno yao basi
baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi wa pili ni Hujjat ul Islami Imam
Al Ghazali. Na hata hivyo mbali ya kua ni mwenye Kufanyiwa Utafiti sana na kukubalika
sana kwa Upekee wa Ukubwa wa Ilm yake lakini yeye mwenyewe alikua anasema kua
hajui kitu na Kila akisoma basi anazidi kujiona kua Yeye Hajui Kitu.
Na hivyo kwangu mimi huu ni Mmoja kati ya Mifano ambayo inabainisha maana ya
maneno:
﴿وَمَآ أُوتِيتُم مِّنَ ٱلْعِلْمِ إِلا َّ قَلِيلاً ﴾
Wama Utitum mina al Aa’alman illa Qaliilan(Surat Al Isra 17:85)
Tafsir: Na Mmepewa Ilm juu yake Ila Kidoogo tu
933
Kwani tunapozungumzia Kuhusiana na Ilm ya Roho kama Roho, basi bila ya shaka, hiki
ni kitu ambacho kiko kama alivyosema Mwenyewe Allah Subhanah wa Ta'ala kua: Ibn
Adam Hatuwezi kujua juu yake isipokua kidoogo tu.
Hapa inabidi Mtu utafakari kuhusiana na hii idadi ya Maarifa juu ya kitu husika ambayo
mbali ya kua na ukubwa Mkubwa sana lakini sisi tumejaaliwa kua ni wenye kujua
Kidoogo tu. Kwa Sababu hakuna kitu Kikubwa na chenye Thamani cha Kiumbe mbele
ya Allah Subhanah wa Ta'ala kama Roho yake kiumbe Ibn Adam.
Na ndio maana Aya zikasema kua Ukiua Roho Moja ni kama Umeua Ulimwengu Mzima,
na Ukiokoa Roho Moja ni kama Umeokoa Ulimwengu Mzima. Hivyo hii inaonesha
Ukubwa na Uzito na Thamani wa hiki Kitu kinachojulikana kama Roho ambacho Mbali
ya Thamani yake na Ukubwa wake Basi hatujui chochote bali kidogo tu.
Kwani miaka na miaka Wanasayansi wamekua wakifanya Uchunguzi wa kila kitu
kuhusiana na Mwili wa Ibn Adam, na wamefanikiwa hadi kugundua DNA ambacho ni
Kitu kinachomnasibisha Ibn Adam na Asili yake kwa vizazi na vizazi, kisha Ndani yake
wakakutana na kitu Kidooogo zaid kinachoitwa Atom.
Ambapo tunapozungumzia na Atom basi tunazungumzia asili ya Mfumo wa kila kitu
Ulimwenguni, Hata Mfumo wa Jua, Nyota na Sayari zinazoelea Ulimwenguni na
kukukua na kutanuka kila miaka inavyoongezeka basi zimeanzia na kitu kinachoitwa
Atom.
Hivyo Wamegundua kuhusiana na Atom, lakini hawajagundua kuhusiana na Roho,
kwani tunapozungumzia Ilm ya Juu ya Roho basi Ilm ambayo ni imo ndani ya Mamlaka
ya Muumba yaani Allah Subhanah wa Ta'ala na hivyo tunazungumzia Kitu ambacho ni
Kizingiti cha Upeo wa Ilm ya Viumbe.
Hivyo kulingana na maneno haya ya Aya hii basi Ibn Adam wasome watakavyosoma,
wajue watakavyojua lakini hawatojua kuhusiana na Roho, isipokua Qaliilan.
Yaani hio Qaliilan ni Kua Roho ipo, na Kila Ibn Adam anayo yake, na Inakuwepo hata
Kabla ya Kuzaliwa kwake Ibn Adam husika, na anakua nayo anapokua ndani ya Mfuko
wa Uzazi wa Tumbo la Mama yake, baada ya Kuzaliwa kwake, katika kuishi kwake,
katika kufa kwake na pia baada ya Kufa kwake.n.k
Yaani hii Ibn Adam hua tunajua kutokana na kile Kidoogo tu tulichopewa na Allah
Subhanah wa Ta'ala juu yake kupitia katika Hadith na aya za Qur'an.
934
Ambapo Uthibitisho wa wazi juu ya hili ni katika kutojua ni nini Roho na hivyo
kutojulikana kutoka kwake ndani ya Mwili wa Ibn Adam yaani hakuna ajuae Vipi, Wapi
wala Saa ngapi, kwani majibu ya Masuali haya ndio Ilm Kubwa zaid.
Ingawa hivyo ndivyo ilivyo hali ya uhalisia kwetu sisi Ibn Adam lakini kwa upande
mwengine basi anasema Imam Ahmad Ibn Hanbal kua: ‘Amesema Muadh Ibn Jabal
Radhi Allahu Anhu kua: Siku Moja Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alitukawilisha Kusali mpaka ikawa tunakaribia kuliona Jua linataka kuchomoza.
Hapo akatokezea Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akiwa ni mwenye Haraka
sana na kisha Ikaakimiwa sala na kisha Akasalisha Sala ya Al Fajir kwa kuifupisha
Kisha baada ya Kusali akatuambia tubakie katika Safu zetu kama tulivyokua
tumekaa
Kisha akatugeukia na kutuambia: 'Wacheni nikuambieni kile ambacho kilinizuia
mimi leo hii Alfajir
Niliamka Usiku nikatia Udhu na kisha nikasali Qiyam Al Layl kwa kadri
nilivyojaaliwa
Na kisha nikalala, Usingizi Mzito sana, na ghafla nikajihisi nipo mbele ya Mola
wangu
Allah Subhanah wa Ta'ala, nikiwa katika hali bora kabisa
Allah Subhanah wa Ta'ala akaniambia: ‘Ewe Muhammad!’
Nami nikajibu: ‘Niko Mbele yako ya Rabb’
Allah Subhanah wa Ta'ala akasema: ‘Hivi Jee Malaika walioko kwenye Mbingu ya
Juu Wanabishaniana nini?’
Nami nikasema: ‘Sijui ya Rabb!’
Allah Subhanah wa Ta'ala akaniuliza mimi Suali hilo mara tatu nami nikamjibu
kua Sijui kisha Allah Subhanah wa Ta'ala akanigusa baina ya Kifua changu, hadi
nikahisi Ubaridi wa Mguso wake kwenye Kifua changu, na hapo kila kitu kikawa
kipo wazi kwangu mie.
Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala akaniuliza tena: ‘Ewe Muhammad Malaika walio
Kwenye Mbingu ya Juu wanabishaniania nini?’
Nami nikajibu: ‘Wanabishana kuhusiana na Kufutiwa Dhambi na Darja zake’
935
Allah Subhanah wa Ta'ala akaniuliza tena: ‘Jee ni Kipi kinachofuta Dhambi?’
Nami nikajibu: Ni kuiendesha miguu kuelekea Msikitini Kusali na kubakia ndani
yake baada ya Sala, na Kutia Udhu ipasavyo hata kama ikiwa kuna Uzito katika
Jambo hilo
Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala akaniuliza: Kisha na Jengine?(Yaani kuhusiana
na Darja)
Nami nikajibu: Kuwalisha Masikini, Kutumia Qawlan Layyina na Kusali wakati
watu wamelala
Allah Subhanah wa Ta'ala akaniambia: ‘Omba Ewe Muhammad’
Nami nikaomba: ‘Ya Allah nakuomba niwe ni mwenye kufanya mema, niachane na
mambo maovu, niwapende Masikini, nawe unisamehe na kuniiingiza kwenye rehma
zako na kama ukitaka kuwapa mtihani watu basi usinijaalie mimi kufa huku nikiwa
na mitihani, na nnaomba mapenzi yako na mapenzi ya wale unaowapenda na niwe
ni mwenye kupenda kufanya mema yanayokaribisha karibu nawe na karibu ya
mapenzi yako.’
Muadh Ibn Jabal Radhi Allahu Anhu anamalizia kwa kusema kua: Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akatuambia kua: Huu ni Ukweli hivyo jifunzeni
kutokana nao (Musnad Imam Ahmad)
Kwani hii ni Hadith ambayo inajulikana kua kama Hadith Al Manam, na pia inajulikana
kama Hadith Ikhtisam al Mala Al A'ala.
Na bila ya shaka hadith hii inataka ufafanuzi, na tutaifafanua ila sio leo, kwani leo
nimeitumia Hadith hii kwa lengo la kubainisha Mtizamo wa Wanazuoni ambao unasema
kua:
Ingawa aya yetu imesema kua kuhusiana na Roho basi Ibn Adam hawakupewa Ilm
juu yake isipokua Qaliilan, lakini hadith hii inarubainishia kua Hali ilikua ni tofauti
kwa upande wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, kwani yeye alibainishiwa
Kila kitu pale alipoguswa na kusema sema Ndani ya Hadhithi hii kua ‘Baada ya
hapo basi kila kitu kikawa kiko wazi kwangu mie’
Na hivyo baada ya tukio hilo basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, basi hata
kuhusiana na Roho na Kifo Alikua akijua pia, hivyo ili tufahamiane vizuri zaid
nnazungumzia kuhusiana na nini basi hapa sasa inabidi tuangalie hali ilivyokua katika
936
siku za mwishoni kabla ya kufariki Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambazo
zilikua ni siku zisizozidi wiki mbili.
Ambapo anasema Abu Said Al Khudhri Radhi Allahu Anhu kua: ‘Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam alisema kua: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala amemjaalia bahati Mja
wake ya kuchagua baina ya kile anachokipenda katika alivyomruzuku hapa Dunani
na kla anachoktaa katika Dunia hii, lakini Mja wake huyo ameamua kuichagua
Akhera yake’’
Abu Said Al Khudri Radhi Allahu Anhu anaendelea kusema kua: ‘Baada ya Abu Bakr
As Siddiq Radhi Allahu Anhu kusikia kuhusiana na maneno haya, basi akaanza
Kulia na kusema: Ya Rasul Allah Hakika Sisi tumewatoa Kafara Mama zetu na
Baba zetu’
Hivyo sisi tukajiuliza kwanini Abu Bakr akasema Maneno hayo? Kwani watu
walikua wakisema: ‘Mwangalie yule Mzee Abu Bakr! Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam’ Amezungumzia kuhusiana na Mja wa Allah amabae amejaaliwa
kuchagua baina ya Neema za Dunia na za Akhera na akachagua Neema za Akhera.
Halafu yeye anajibu kua Mama zetu na Baba zetu tumewatoa Kafara kwa Ajili yako
ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam!
Kwani Abu Said Al Khudri Radhi Allahu Anhu anaendelea kutuambia kua:
‘Baadae sisi ndio tukajua maana aliyoikusudia Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu
Anhu, kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ndie Mja ambae amejaaliwa
Bahati ya kuchagua (kuhusiana na Kubakia Duniani kuendelea na Neema za Allah
Subhanah wa Ta'ala na kila atakachokitaka au Arudi kwa Mola wake) Na baada ya
hapo ndio tukakubaliana kua Abu Bakr Radhi Allahu Anhu kua ndie mwenye Ilm
kubwa zaid kuliko sote miongoni mwetu.(Mishkat al Masabih)
Naam..siku 5 Kabla ya kufariki kwake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi
aliingia Msikitini na kusema: ‘Kama kuna yeyote yule ambae ni iwahi kumpiga
mjeledi kwenye mgongo wake, basi nami natoa Mgongo wangu aje kunipiga leo hii,
na kama kuna yeyote yule niliemvujia heshima basi nami leo nampa heshima yangu
aivunje’
Kisha baada ya hapo akawausia Waislam kufanya mema na kuachana na Mabaya na
kupendana na kutochukiana kisha baada ya kumaliza basi kuna Mtu Alisimama Msikitini
na kusema: ‘Ya Rasul Allah hakika mimi nnakudai Dirham 3’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Ewe Fadhl Mlipe pesa zake
anazonidai’
937
Kisha akasema: ‘Enyi Waislam hakika mimi nakuusieni, kua idadi ya Waumini
itaongezeka sana lakini idadi ya watakaoinusuru Dini itapungua kiasi ya kua wingi
wao itafikia kua kama vile wingi wa matumizi ya chumvi kwenye chakula. Hivyo
yeyote yule atakaekua na Madaraka, basi asiwaaadhuru na kuwadhulumu walio
chini yake. Bali anatakiwa awe ni miongoni mwa wenye kuonesha shukran na
kuthamini alivyotaminiwa na Mola wake kwa kutoziangalia na kuzisamehe kasoro
za wale walio chini yake.’
Katika siku ambayo kesho yake anafariki basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alitoa Sadaqa vitu vyake vyote, Pesa zake ambazo zilikua ni Dirham 7 tu, Upanga wake,
n.k, na katika siku ya mwisho ya Uhai wake Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam,
basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alimwita Binti yake Fatma Bint Rasul
Salallahu Alayhi wa Salam na kisha akamnong'oneza kitu, na hapo Fatma bint Rasul
Allahu Salallahu Alayhi wa Salam akaanza kulia.
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alipomuona kua analia basi akamvuta na
akamnong'oneza neno jengine na hapo Fatma bint Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa
Salam akaanza kucheka kwa Furaha Baada yake.
Ambapo alipoulizwa Fatma bint Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam kwanini akalia
na kisha akacheka basi alisema:
Mara ya Kwanza aliniambia kua hatopona na atakufa kutokana na Maradhi yake,
na kisha akaniambia kua Mimi nitakua ndie Mtu wa mwanzo kujumuika nae
Peponi (baada ya kufariki kwake)(Sahih Bukhari)
Naam..hivyo alipoulizwa Fatma bint Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam alipoulizwa
na Umm ul Muuminin Aisha Radhi Allahu Anha kwanini aliponong'onezwa na Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam kwanza akalia na kisha akacheka basi alisema: ‘Mara
ya Kwanza aliniambia kua hatopona na atakufa kutokana na Maradhi yake, na
kisha akaniambia kua Mimi nitakua ndie Mtu wa mwanzo kujumuika nae Peponi
(baada ya kufariki kwake) (Sahih Bukhari)
Kwani Kauli hio ya Ubashirio wa Kifo cha Fatma Bint Rasul kutoka kwa mwenyewe
Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam kua yeye atakua ni mtu wa Mwanzo kukutana
na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam miongoni mwa wengine wote waliokaribu nae
haikua ni Kauli ilianguka!
Na hii ni kwa Sababu Baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kufariki basi
ilipita miezi miwili tu na kisha na Fatma Bint Rasul Salallahu Alayhi wa Salam nae
akafariki, Hivyo hii pia ilikua inaonesha kua Rasul Allah Salalahu Alayhi wa Salam
alikua anajua kuhusiana na kifo cha Binti yake baada ya kufariki kwake.
938
Na Katika Siku ambayo anafariki basi Alimuona Fatma kua Yuko Mnyonge Sana juu
yake hivyo akamwambia: Ewe Binti Yangu, Usiwe Mnyonge Sana kwani kwa Hakika
Mimi Sitoumwa zaidi tena baada ya kumalizika Siku hii ya Leo!
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambapo moja kati ya siku hizo basi alisema:
‘Enyi Watu nimesikia kua Mnataka Kuchanganyikiwa kwa sababu tu ya kua Mimi
nnataka Kufariki, hivyo fahamuni kua Hakuna Mtume ambae aliishi Milele pamoja
na Watu wake, hivyo Itakuaje kwangu mimi kuwezekana hivyo? Fahamuni kua
Mimi karibuni nitakutana na Mola wangu, na bila ya shaka, Nyiny pia Mtakutana
nae.
Hivyo Enyi Maansari Wasaidieni Muhajjirina na Enyi Muhajirina Wasaidieni
Maansari, kwani nao wamekupokeeni, wakakupeni ardhi yao, wakakukaribisheni
majumbani mwao, Ingawa walikua katika Mda mgumu wa Kiuchumi hivyo
Wasaidieni na kama ikiwa mmoja wenu atawatawala basi na awaonee huruma’
Enyi Watu kila kitu hua ni chenye kutokea kulingana na Makadirio na Mipango ya
Allah Subhanah wa Ta'ala. Hivyo msijaribu kupingana na makadirio ya Allah
Subhanah wa Ta’ala, kwani ni nyinyi ndio mtakao kua walioshindwa dhidi yake.
Msijaribu kumhadaa Allah Subhanah wa Ta’ala kwani ni nnyinyi ndio mtakaokua
mkijihadaa Nafsi zenu. Hakika mimi ni mwingi wa Rehma na Huruma juu yenu,
na bila ya shaka tutakutana tena In-shaa Allah, na sehemu tutakayokutana ni
pembeni ya Chemchem ya Al Kawthar.
Hivyo kama mnataka kukutana na mimi basi kila mmoja wenu ahifadhi mikono
yake na ulimi wake kutokana na mambo yasiyomhusu. Enyi watu fahamuni kua,
kufanya dhambi hua ni sababu yakukubadilishieni Neema na Rehma zenu juu
yenu, hivyo kama ikiwa wengi katika jamii ya Watu wenu ni wenye kufanya Mema
basi hata Mamlaka yatakayokua juu yenu yatakua ni ya Kiuadilifu. Na kama wengi
katika jamii yenu watakua ni Waasi na wenye kufanya Dhambi katika jamii yenu
basi hata Mamlaka yatakayokua juu yenu yatakua ni ya Dhulma na ni yenye
kukukandamizeni (Musnad Imam Ahmad)
Kisha baada ya Maneno hayo basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akaingia ndani
katika Chumba cha Bi Aisha Radhi Allahu Anha na kuenda kulala
Naam, Man Jada Wajadda yaani Mwenye Kutafuta hupata, Hivyo nasi tufanye jitihada
katika kujistiri na Nafsi zetu na kisha na Allah Subhanah wa Ta'ala nae ndio atatustiri
kutokana na Nafsi zetu na atatusamehe kutokana na kasoro zilizosababishwa na Nafsi
zetu, lakini baada ya kujitahidi kwetu.
939
Kwani katika siku ya Mwisho wa Uhai wake basi Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alifanikiwa kusali Sala ya Alfajir ndani mwake kwani alishindwa kutoka na hivyo
hakufanikiwa kusali sala ya Adhuhuri akatangulia kwa Mola wake
Ambapo anasema Anas Ibn Malik Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wakati Waislam
wanajitayarisha Kusali Sala ya Alfajir ya Siku ya Jumatatu ambayo ilikua
inaongozwa na Abu Bakr, basi Waislam walishangaa walipomuona Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akinyanyua Pazia la Chumba cha Aisha, huku
akawatizama Waislam namna walivyojipanga Safu kwa ajili ya Sala na kisha
akatabasamu, Abu Bakr alipomuona Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, basi
akarudi Nyuma kutoka katika Sehemu ya Uimamu na Kujiunga na Safu ya
Maamuma, kwani alidhania kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anakuja
kusali pamoja nao
Hivyo Waislam walifurahi sana kua Watasalishwa Na Rasul Allah Salalahu Alayhi
wa Salam katika Sala yao Lakini Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam, Akaashiria
kwa mkono kua Abu Bakr aendelee kusalisha, na kisha yeye akarudi Ndani
Chumbani na Kufunga Pazia hilo’
Kisha Asubuhi yake akaomba waitwe wajukuu zake Hasan na Husein akawabusu na
Kuisia kua waangaliwe na kusimamiwa ipasavyo, kisha akawaita Wake zake wote na
Akawausia kua wawe ni wenye kumkumbuka Allah Subhanah wa Ta'ala na kisha
akasema: ‘Hakika bado nnahisi Maumivu kutokana na Chakula nilichokila katika
maeneo ya Khaybar, na nnahisi kua Kifo kimewadia’
Akawausia Watu wawe wanasali, na kisha akawamrisha wawaonee huruma Watumwa
wao, kwa kusisitizia juu ya jambo hilo mara kadhaa, kisha akasugua Meno yake na
akanawa Uso wake Mtukufu kisha akasema: ‘Hakuna Mola anaestahiki Kuabudiwa
kwa Haki isipokua Allah Subhanah wa Ta'ala..Ama kwa Hakika Kifo kina maumivu
makali sana’
Kisha akaangalia Juu na akasema: ‘Pamoja na wale ambao umewaingiza katika
Rehma zako, miongoni mwa Mitume na Waliosadiki, Mashahidi na wenye kufanya
Mema, Ya Allah Nakuomba Unisamehe na uniingize katika rehma zako na uniweke
pamoja na Waliokua na Darja ya Juu
Ya Allah Nijaalie niwe ni Miongoni mwa waliokua Karibu nawe Miongoni mwa
waliokua katika Darja ya juu. Hakika ya sisi Marejeo yetu ni kwa Allah Subhanah
wa Ta'ala na kwake yeye ndiko tunakokutegemea kwa ajilo ya msaada na Maisha
ya Milele’
940
Baada ya hapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akafariki huku akiwa
amemuegemea Umm ul Muuminina Aisha Radhi Allahu Anha, Dunia huku akiwa na
Umri wa miaka 63.
Ambapo habari ya kifo ikamfikia Abu Bakr Radhi Allahu Anhu aliondoka na kueleka
Msikitini alipofika akaingia ndnai bila ya kuzungumza na mtu yeyote hadi alipofika
kwenye chumba cha Aisha Radhi Allahu Anha na kumuangalia Rasul Allah Salallahu
Allahu Alayhi wa Salam ambae alikua amefunikwa shuka la Yemen, hivyo akamfunua
uso wake na kisha akamgusa na kumbusu na kisha akaanza kulia hukua akisema:
‘Hakika mimi nimemtoa Kafara Mama yangu na Baba yangu kwa ajili yako, hivyo
sitokusababishia kufariki mara mbili, kwani tayari umeshaonja mauti ambayo
Allah Subhanah wa Ta’ala ameiandikia kila Nafsi kua itayaonja.’
Na kisha Abu Bakr Radhi Allahu Anhu akatoka na kuelekea kwa Umar Radhi Allahu
Anhu ambae alimwambia: ‘Umar kaa kitako chini’ hivyo Umar Radhi Allahu Anhu
akagoma na watu wakaanza kuondoka, Umar Radhi Allahu Anhu akamsogelea Abu Bakr
Radhi Allahu Anhu ambae alisimama na kuanza kusema: ‘Ama kwa sasa hivi, kila
aliekua akimubudu Muhamamd Salallahu Aalyhi wa Salam, basi Muhammad
amefariki, lakini kwa yeyote yule aliekua akimuabudu Allah Subhanah wa Ta’ala
basi Allah Subhanah wa Ta’ala ni mwenye uhai wa Milele na kamwe hawezi kufa,
kwani Allah Subhanah wa Ta’ala amesema:
﴿وَمَا محَُم َّدٌ إِلا َّ رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِنْ قَبْلِهِ ٱل ُّر سُ لُ أَفإِنْ م َّاتَ أَوْ قُتِلَ ٱنْقَلَبْتُمْ عَلَىٰ
أَعْقَابِكُمْ وَمَن يَنْ قَلِبْ عَلَى ٰ عَقِبَيْهِ فَلَنْ يَضُر َّ ٱهلل ََّ شَيْئاً وَسَيَ جْزِى ٱهلل َُّ ٱلش َّاكِرِينَ ﴾
Wama muhammadun illa rasoolun qad khalat min qablihi alrrusulu afa-in mata aw
qutila inqalabtum AAala aAAqabikum waman yanqalib AAala AAaqibayhi falan
yadurra Allaha shay-an wasayajzee Allahu alshshakireena (Surat Al Imran 3:144)
Tafsir: Na hakua Muhammad isipokua ni Rasul, na wamekuja kabla yake Mitume
hivyo jee hata kama ikiwa atakufa au atauliwa, mtageuka kutokana na muelekeo wa
visigino vyenu? Na atakaegeuka kutokana na muelekeo wa visigino vyake basi
hatomdhuru Allah Subhanah wa Ta’ala hata kidogo na Allah Subhanah wa Ta’ala
atawalipa wale wenye kuonesha shukurani.
Ambapo anasema Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua: ‘Wa Allahi ilikua
kama vile watu hawakuwahi kusikia aya ya Qur’an kama hii hadi pale Abu Bakr
alipoisoma na kuifanya kua kama ni ukumbusho, na hivyo kila mtu akawa ni
mwenye kuisoma aya hii hadi ikawa hakuna hata mmoja ambae si mwenye
kuisoma’
941
Na anasema Said Ibn Al Musayyib kua : ‘Umar alisema, Wa Allahi mara tu
nilipomsikia Abu Bakr akiisoma aya hii basi nilianguka chini ardhini, kwani nilihisi
kua kama miguu yangu haiwezi tena kunibeba, ni pale tu nilipoisikia ndi nikajua
kua Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam amefariki kweli’(Sahih Bukhari)
Mbali ya kua hiki ni Kifo kilicho wasikitisha wengi lakini pia kilimsikitisha zaid
UmmuAyman kwani hali yake yeye ilikua ni Mama aliepoteza Mtoto wake Kipenzi na
pia kama mtu aliepoteza Dira ya Muelekeo wake ambao alikua ana matumaini kua
ataondoka yeye na kuiwacha hapa Duniani baada yake.
Ummu Ayman alipoulizwa mbona unalia sana kiasi hicho basi akajibu: ‘Hakika mimi
nilikua najua kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam iko siku atakufa, hivyo
sasa hivi nalia kwa sababu ndio nimegundua kua Hautoshuka tena Ujumbe wa
Allah Subhanah wa Ta'ala juu yetu.’
Baada ya kufariki kwa Rasul Allah Salallahu Aalyhi wa Salam kulitokea mgogoro
mkubwa sana na mvutano na mazungumzo makubwa hata kabla ya kuuzika mwili huo,
baina ya Ansari na Muhajjirun, na mwisho wakakubaliana kua Abu Bakr Radhi Allahu
Anhu awe ndie Khalifa.
Waislam walitumia siku nzima ya majadiliano na amakubaliano tangua siku hio ya
Jumatatu hadi ilipoingia Alfajir ya siku ya Jumanne ambapo mwili Mtukufu wa Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam ukakoshwa na Al Abbas Ibn Abd ul Mutalib na Al
Fadhl Ibn Abbas, Ali Ibn Abi Talib, Usama Ibn Zayd na Quthan Ibn Abbas Radhi Allahu
Anhum.
Na kisha wakamvisha Sanda na baada ya hapo Waislam wakabakia kuulizana anatakiwa
azikwe wapi? Ambapo Abu Bakr Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Mimi nimemsikia Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam akisema kua: ‘Mitume hua wanazikwa katika
sehemu waliyofia’’ hivyo Abu Talha Radhi Allahu Anhu akaondoa Kitanda kilichopo
chumbani humo na kisha chini yake likachimbwa kaburi lake Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam.
Kisha baada ya hapo watu wakaingia ndani mwake na kumsalia Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwa zamu, ambapo watu kwanza walikua ni watu wa Kabila lake, kisha
wakafuatia Muhajirina na kisha wakafuatia Maansari na kisha Wanawake wakamsalia na
kisha Watoto na kisha akazikwa, na hivyo ndivyo ambavyo Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam alivyolakiana na kifo chake.
942
MAUTI, BARZAKH NA KABURI KATIKA AYA NA HADITH
Neno Laqiyah kwa Lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kumlaki Mtu; Kupokea Mtu au
Kitu; Kumkaribisha Mtu; Kumuegemea Mtu; Kukutana uso kwa uso na Mtu au na Kitu;
Kukiona Kitu; Kukijua Kitu; Kuelekea kwenye Muelekeo Ambao Kuna Mtu au Kitu;
Kupitiwa na hali ya Kitu au Kuhisi Hali Ya Kitu.
Naam..amesema Allah Subhanah wa Ta'ala katika aya iliyotumia neno Laqiyah kua:
﴿قُلْ إِن َّ ٱلْمَوْتَ ٱل َّذِى تَفِر ُّونَ مِنْهُ فَإِن َّهُ مُلاَقِيكُمْ ثمُ َّ تُرَد ُّونَ إِلىَٰ عَ المِ ٱلْغَيْبِ
وَٱلش َّهَادَةِ فَيُنَبِّئُكُم بمَِا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴾
Qul inna almawta alladhee tafirroona minhu fa-innahu mulaqeekum thumma
turaddoona ila AAalimi alghaybi waalshshahadati fayunabbi-okum bima kuntum
taAAmaloona(Surat Al Jumuah 62:8)
Tafsir: Sema (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam kua) Hakika Ya Mauti,
Ambayo Mnayakimbia Kutokana Nayo basi Kwa Hakika Yatakulakini
(Yatakupokeeni) Kisha Mtarudishwa kwa yule Mwenye Kujua Juu ya
Yasiyojulikana na Kutoonekana na Yanayojulikana na Kuonekana kisha
Mtawekewa wazi Juu ya Yale Mliyokua Mkiyafanya.
Katika Aya hii tunaona kua Allah Subhanah wa Ta'ala anatuwekea Wazi kua Mauti ni
Kitu ambacho kila Mmoja wetu Atakumbana nacho. Hivyo hiki ni kitu ambacho
hakikimbiliki. Kwani hali yetu kuhusiana na Mauti hua inakua Kama hali ya Mtu ambae
alikua Ugenini na hivyo yuko Safarini Kurudi Nyumbani. Hivyo Bila ya Shaka Hukutana
na Wanaomsubiri kwa ajili ya Kumpokea pale atakaporudi Nyumbani baada ya kuondoka
kwa muda mrefu. Hivyo sisi Hua ni Wageni, Akhera hua Nyumbani na Mauti hua ni
yenye Kutupokea kutoka katika Safari yetu ya Ugenini na Kutukaribisha Nyumbani.
Kwa Upande Mwengine Mauti hua Kama Jini yule ambae akakushtua kutokana na
kuamua kukufanyishia, hivyo nawe ukaanza kumkimbia kwa Khofu na kuhisi kua yuko
Nyuma yako, lakini Ghafla Unashtukia Ametua Mbele yako na kwa kasi yako basi
huwezi kusimama ghafla na hivyo ukawa ni mwenye Kuvaana nae kutokana na
Kukumbana na wewe.
Naam..hio ndio maana ya Mulaqiikum hivyo aya inaendelea kutuambia kua: Thuma
Turadduuna Ila Aalimi - Kisha Mtarudishwa kwa yule mwenye Kujua
943
Na hivyo Kutuwekea wazi kua kutokana na kua Akhera ndio Nyumbani na Mauti ndio
yatakayotupokea kutukaribisha Nyumbani ambako ingawa tumeondoka kwa kitambo
lakini Mwenye Umiliki wa Makaazi yetu hayo ya Nyumbani huko tulikotoka, kua ni
Mwenye kujua juu ya kila kitu tulichokifanya katika wakati huo tulipokua Safarini.
Kwani yeye ni mwenye sifa ya kua ni AAalimi alghaybi waalshshahadati - Mwenye Ilm
ya yaliyofichikana na yaliyowazi, ya Ulimwengu unaoonekana wa hapa Safarini Duniani
Tulipo na Ulimwengu wa Nyumbani Kabla ya Kuondoka kwetu na kurudi kwetu na
kitakachofuata baada ya Kurudi kwetu Akhera
Na Kisha atabainishia Kila kitu chetu tulichokifanya hapa Ulimwenguni kimoja baada ya
kimoja. Na akasema Hasan Al Basr kwa kuusia kuhusiana na Kifo kua: ‘Ibn Adam
anapofariki Dunia basi Ibn Adam hua wanaulizana kwa kusema kua: Hivi huyu
Mtu aliefariki amewacha nini?
Lakini kwa Upande wa Malaika hua ni wenye Kuulizana kwa kusema: Hivi Huyu
Mtu aliefariki ametanguliza nini?
Na Luqman Al Hakim alimuusia Mtoto wake kuhusiana na Kifo kua: ‘Ewe Mtoto
Wangu Hakika Juu ya Kile Utakachokutana nacho bila ya Kukitarajia’ - Bora
Ujitayarishe Nacho kwani ili tufahamiane kwanini Wenye Kujua wakausia hivyo, basi
na Tuangalie maana ya Maneno ya Aya tunayoiangalia ambayo inasema kua: Hakika ya
Hayo Mauti tunayoyakimbia kutokana nayo basi tutakumbana nayo kwani yatatupokea
kwa kuwepo huko tunakokukimbilia kutokana na Ujinga wa kudhania kwetu kua
tunakoyakimbia kua ndio yalikokuwepo.
Basi tumwangalie Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Al Ghazali ambae
anatuelezea namna tutakavyokumbana nayo Mauti pale aliposema katika Ihya Ulim Ad
Din kuhusiana na Kifo na Maumivu yake kua:
Fahamuni kua Maumivu Makali ya Kifo Hua ni yenye Kujulikana na Kuhisikana
Kikamilifu na Yule tu aliekionja Kifo hicho: Hivyo Mtu yeyote yule ambae hajakionja
basi hua ni mwenye kukifikiria kutokana na hisia za Maumivu aliyowahi kuyapata,
na kukisia Ukali wake kulingana na Maumivu ya Hali ya Juu Kabisa.
Ambapo Mwili unapodhurika kwa Moto Au kwa Jeraha, basi Hisia hizo za
Maumivu husafiri kuelekea Kwenye Roho kulingana na kiwango cha Madhara
katika Kiungo husika, Na katika Kutembea kwake hisia hizo za Maumivu hua ni
Zenye kupingua kasi yake zinaposafirishwa ndani ya Mwili kupitia kwa njia ya
Ngozi, Damu n.k hadi kuifikia sehemu kuua ya Maumivu ambayo ni Roho.
Hivyo Fikiria wewe Kua Hisia hizi unazohisi hua ni zenye kuanzia kwenye Kiongo
chengine kuelekea kwenye kiungo kikuu yani Roho sasa tunapozungumzia
Maumivu ya Kutolewa Roho basi Hua tunazungumzia Maumivu yanayohisiwa
944
Moja kwa moja kutoka kwenye Kiungo kikuu cha Hisia za Maumivu ambacho ni
Roho ambacho ndio Hua chanzo cha Maumivu ya Kuvamiwa kwake Roho yako.
Kwani kwa Mtizamo mwengine basi Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad
Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali anatuambia kua: ‘Mtu anapochomwa na
Mwiba basi Maumivu yake hua ni yenye Kusambaa katika eneo lililodhurika, yaani
Kama ni Kidole basi ni sehemu ya Kidole iliyojichoma ndio Hupata maumivu zaid.
Na maumivu ya Moto hua makubwa kwa sababu ya namna unavyosambaa Moto
katika Kuunguza kwake ambapo Maumivu ya anaechomwa na Upanga hua ni
katika Sehemu ilichomwa na Upanga Husika na Kudhurika, na ndio maana
maumivu ya Upanga hua Madogo kuliko ya Moto, lakini tunapozungumzia
Maumivu ya Kutolewa Roho basi hua ni makali sana kwa sababu hua ni yenye
kuivamia Roho yenyewe ya Mtu Husika.
Na hivyo Mtu Husika anaekufa hua ni mwenye kuhisi kua anachomolewa kila kila
mshipa wa Damu wa kila sehemu ya Mwili wake, kila mshipa wa fahamu kila
mshipa wa hisia na kila sehemu ya Mwili wake. Kila mfupa wa Mwili wake na Kila
Msuli wa Mwili wake. Tangu kuanzia kwenye Mzizi wa Nywele zake hadi chini
kwenye Nyayo za Miguu yake.
Hivyo usiulize hisia za Maumivu anayohusu Mtu aliekuwepo kwenye Sakarat Al
Mawt, na ndio maana ukaambiwa kua Maumivu ya Kifo hua ni Makali sana Kuliko
Kukatwa kwa Mapanga, au kukatwa kwa Msumeno au Mkasi.
Hivyo Mtu aliekatwa na Upanga hua ni Mwenye kuweza kulia na kupiga kelele na
hivyo kupunguza Maumivu kwa kutumia Nguvu zake na Ulimi na Mdomo wake.
Lakini Mtu anaekufa hua na Maumivu katika Kila kiungo chake na hivyo hukosa
hata Nguvu na uwezo wa Kujipinguzia Maumivu yake Kwani Kifo huvamia Viungo
vyake vyote mpaka Akili na Ufaham wake.
Hua anataka kupiga Kelele kujipunguzia Maumivu ya Mwili wake au kuomba
Msaada kwa waliokaribu yake, lakini hawezi kwani hana nguvu hata kipande ndani
ya Misuli yake kutokana na Maumivu yake.
Hivyo ndivyo Roho Inavyovutwa na Kutolewa, na hivyo huanza kufa kiungo chako
kimoja baada ya kimoja na kukiwacha kikiwa Kibariidi huku Macho yako
yakiangalia unayoyaona kwa mtizamo wa Mwisho’
Hivyo amesema Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali kua: ‘Kifo huvamia Viungo vyote mpaka Akili na Ufaham
wote Mtu hutaka kupiga Kelele kujipunguzia Maumivu ya Mwili wake au kuomba
Msaada kwa waliokaribu yake, lakini hawezi kwani hana nguvu hata kipande ndani
945
ya Misuli yake kutokana na Maumivu yake hivyo ndivyo Roho Inavyovutwa na
Kutolewa, na hivyo huanza kufa kiungo chako kimoja baada ya kimoja na
kukiwacha kikiwa Kibariiidi Huku Macho yako yakiwa Yanaangalia yale
unayoyaona kwa mtizamo wa Mwisho’
Kwani amesema Umm Salamah Radhi Allahu Anha kua: Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: Wakati Roho Inapotolewa basi Macho hua ni yenye
Kuifuata
Na akasema Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu kua: Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: Hivi Jee hamuoni nyie kua Mtu anapokufa hua ni mwenye
kuutolea Macho Upeo wa Jicho? Hii hutokea kwa sababu Mtu hua ni mwenye
Kuifuata Roho yake wakati inapotolewa(Sahih Muslim)
Hivyo kutokana na Hadith hizi na pia na Mtizamo wa Hujjat Ul Islami Imam Al Ghazali
ambao unasema kua Macho hua ni yenye Kuangalia kwa mtizamo wa Mwisho yale
Yanayoyaona basi tunaona kua Kama ikiwa Mtizamo wa Macho unafuata Roho
inapotoka hii inamaanisha kua:
Mtu unapokua katika Sakarat Al Mawt basi mbali ya kuhisi Maumivi hayo Makali
Lakini pia Macho yako hua yanaona Roho yako inavyotoka Na Hivyo basi Hua si
Unaona Roho inavyoyolewa mpaka kutoka kwake na Unahisi Maumivu hayo
Makali sana, lakini pia hua unawaona pia Malaika Wanaokutoa Roho Hivyo kama
Ukiwa Mtu mwema basi Unawaona namna wanavyokupokea Malaika wema
waliokutayarishia Makazi yako Katika kurudi kwako Nyumbani baada ya kua
Safarini hapa Duniani.
Na kama Ukiwa Mtu Muovu basi Unawaona namna wanavyokupokea Malaika wa
Motoni waliokutayarishia Makazi yako Katika kurudi kwako Nyumbani baada ya
kua Safarini hapa Duniani,
Na pia amesema Imam Salamh Ibn Dinar kua: ‘Ka hakika Kila atakaekua Mtiifu kwa
Allah Subhanah wa Ta’ala basi atapokewa na Mola wake kama mtu aliekua Safarini
kisha akarudi Nyumbani kwake ana kupokewa na Familia yake.
Na kama Mtu Muasi kwa Mola wake basi tapokewa kwa Mola wake kama vile
Mtumwa aliekimbia kwa Bwana wake na kisha akakamatwa na kurudishwa kwa
Bwana wake’
Yaani hii hua kama zinavyosema aya:
946
﴿وَهُوَ ٱلْقَاهِرُ فَوْقَ عِبَادِهِ وَيُرْسِ لُ عَلَيْكُم حَفَظَةً حَتى َّ ٰ إِذَا جَآءَ أَحَدَكُمُ ٱلْمَوْتُ
تَوَف َّتْهُ رُسُلُنَا وَهُمْ لاَ يُفَرِّطُونَ ۞ ثمُ َّ رُد ُّو ۤ اْ إِلىَٰ ٱهلل َِّ مَوْلاَهُمُ ٱلحَْقِّ أَلاَ لَهُ ٱلحُْكْ مُ وَهُ وَ
أَسْ رَعُ ٱلحَْاسِ بِينَ ﴾
Wahuwa alqahiru fawqa AAibadihi wayursilu AAalaykum hafadhatan hatta idha
jaa ahadakumu almawtu tawaffat-hu rusuluna wahum la yufarritoona; Thumma
ruddoo ila Allahi mawlahumu alhaqqi ala lahu alhukmu wahuwa asraAAu
alhasibeena (Surat Al Anaam 6:61-62)
Tafsir: Na yeye ni Mwenye Uwezo wa Kinguvu juu ya waja wake, na anawatuma
Wasimamizi wake juu yenu, hadi pale kifo kinapomfikia mmoja wenu, Wajumbe wetu
huchukua Roho yake, na si wenye kudharau majukumu yao. Kisha wanarudi kwa
Allah Mola wao, Muadilifu, kwa hakika yeye ni mwenye kuhukumu na ni mwepesi
katika kuhesabu.
Kwani amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: Malaika hua wanakuja
kwa Mtu anaefariki, na kama Mtu huyo ni Mwema basi hua wanasema: ‘Toka Nje
Ewe Roho Nzuri uliekuwepo kwenye Mwili wa Ya Mja Mwema, Toka Nje Ewe
Mwenye Thamani Ili Upate Habari Njema na Rehma na Manukato kutoka kwa
Mola wako asiekua na Hasira nawe.’
Na kisha Roho hio hutolewa na kupelekwa Mbinguni, huku Maneno hayo hurudiwa
rudiwa hadi Mbinguni ya kwanza na kufunguliwa Mbingu na kuulizwa: ‘Huyu ndio
Nani?’
Ambapo Malaika hua ni wenye kujibu kwa kusema kua: ‘Huyu ni Fulani Ibn
Fulani’.
Ambapo hapo pia Malaika Huiambia Roho hio kwa kusema: Karibu Ewe Roho
Njema uliekua kwenye Mwili wa Mja mwema karibu ewe mwenye Thamani! Upate
Bashirio Jema la Rehma na Manukato kutoka kwa Mola wako asiekua na Hasira
nawe.
Kwani kama ikiwa Mtu huyo si Mwema basi Malaika hao hua ni wenye kusema:
‘Toka Nje Ewe Roho Ovu iliyokua ndani ya Mwili wa Mtu aliekua akimuasi Mola
wake toka huku ukiwa Umelaaniwa na hivyo Kubashiriwa Habari za Maji Yamoto
yachemkayo, na Usaha na kila lililobaya’
947
Hali hii huendelea hadi Roho hio kutewa kwake na kuchukuliwa na kupandishwa
juu Mbinguni lakini Malaika wakifika Mbinguni basi Milango ya Mbingu
haitofunguka kwani Wataambiwa: ‘Hakaribishwi ndani yake Roho Mbovu iliyokua
ndani ya Mwili wa Mtu Muovu, Rudi Ardhini Ulikotoka na Laana zako kwani
Milango ya Mbingu Haiwezi kufunga kwa ajili yako’ Hivyo Malaika hurudi na
Roho hio Ardhini hadi ndani ya Kaburi lake(Imam Ibn Majah)
Kwani hadithi inatuwekea wazi kua Kila mtu anapotolewa Roho hua hapo hapo anaona
kwa Macho yake kabla hayajakata Mawasiliano na Ufahamu wake kua yeye ni Mtu wa
wapi.
Hivyo kama ni ya Mja Mwema basi Roho hio ikipandishwa Mbinguni husofiwa na hua
ni iliyoridhiwa na Mola wake na Malaika wake na hivyo huwekwa Peponi. Na ndio
maana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kua: Kwa Mja mwema basi
Kaburi ni Bustani katika Mabustani Ya Peponi.
Na kama ni ya Mtu Muasi basi tangu inatolewa hadi Kupelekwa Mbinguni hua
inalaaniwa tu kutokana na kua Roho hio imekosa Ridhaa ya Mola wake kwa Uasi wake.
Na hivyo inapofika Mbinguni basi hukataliwa kuingia ndani yake na kuamriwa
kurudishwa Ardhini kaburini kwa ajili ya Adhabu ya Kaburi.
Na ndio maana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Akasema kua: Kwa Mja Muovu basi
Kaburi hua ni Shimo kati ya Mashimo ya Motoni.
Neno Rahuba kwa Kilugha hua linamaanisha Kukaribisha, Kua Kua Mkarimu,
Kutosheleza, Kua na Nafasi Kubwa, Kua na Upana wa Nafasi, Kua Mkubwa.
Kwani Allah Subhanah wa Ta'ala ametumia neno Rahuba pale aliposema katika Qur'an
kuelezea yaliyotokea kwenye Vita vya Hunain ambalo ni tukio liliozungumziwa katika
aya ya 25 ya Surat At Tawba na pia akalitumia tena katika Sura hio hio katika aya ya 118
pale alipozungumzia kuhusiana na Vita vya Tabuq, ambapo katika aya ya 25 basi
amesema:
﴿لَقَدْ نَصَرَكُمُ ٱهلل َُّ فىِ مَوَاطِنَ كَثِيرَةٍ وَيَوْمَ حُنَينٍْ إِذْ أَعْجَبَتْكُمْ كَثْرَتُكُمْ فَلَ مْ تُغْنِ
عَنكُمْ شَيْئاً وَضَاقَتْ عَلَيْكُمُ ٱلأَرْضُ بمَِا رَحُبَتْ ثمُ َّ وَل َّيْتُم م ُّدْبِرِينَ ﴾
Laqad nasarakumu Allahu fee mawatina katheeratin wayawma hunaynin idh
aAAjabatkum kathratukum falam tughni AAankum shay-an wadhaqat
AAalaykumu al-ardu bima rahubat thumma wallaytum mudbireena(Surat At
Tawba 9:25)
948
Tafsir: Kwa Hakika Allah amekunusuruni (Na kukupeni Ushindi) Katika Viwanja
Vingi vya Vita vya Katika Siku ya Vita vya Hunayn Wakati Mlipofurahia Wingi wenu
ambako Hakukusaidieni kitu chochote wakati Imetandazwa kwa ajili yenu Ardhi Kwa
Mapana halafu Mkageuka na Kukimbia
Kwani mara nyingi watu wakikaribishana kwa Kuambiana Ahlan wa Sahlan Wa
Marhaban yaani Jihisi Huru kama Uko Nyumbani kwenu, Karibu.
Naam..Neno Marhaba limetokana pia na neno Rahiba ambalo tumesema kua pia hua
linamaanisha Kukaribisha, hivyo basi neno Marhaban linamaanisha Karibu!
Ambapo tunapoiangalia Qur'an basi tunaona kua pia imetumia neno Marhaban pale
ilipowaelezea wale watu wetu tuliowazungumzia Jana. Yaani wale watu ambao ni
Waovu, na hivyo wanapotolewa Roho hua wanalaaniwa tangu mwanzo mpaka mwisho,
kuanzia Ardhini mpaka Mbinguni.
Ambapo Roho zao zikishafikishwa Mbinguni basi hawatokaribirshwa ndani yake na
badala yake watarudishwa Ardhini kwenye Makaburi yao ambayo hua ni Mashimo
miongoni mwa mashimo ya Motoni…Allah Atupe Mwisho mwema na pia atuepushe na
Adhabu ya moto.
Kwani Allah Subhanah wa Ta'ala anasema Katika Qur'an katika aya zilizotumia neno
Marhaban lakini Katika Hali ya Kukanusha Ukaribisho yaani La Marhaban pale
ziliposema:
﴿جَهَن َّمَ يَصْلَوْنَهَا فَبِئْسَ ٱلْمِهَادُ۞هَٰذَا فَلْيَذُوقُوهُ حمَِيمٌ وَغَس َّاقٌ۞وَ آخَرُ مِن شَكْلِهِ
أَزْوَاجٌ۞هَٰذَا فَوْجٌ م ُّقْتَحِ مٌ م َّعَكُمْ لاَ مَرْحَباً هبِِمْ إِن َّهُمْ صَالُو ٱلن َّارِ۞قَالُواْ بَلْ أَنتُمْ لاَ
مَرْحَباً بِكُمْ أَنتُمْ قَد َّمْتُمُوهُ لَنَا فَبِئْسَ ٱلْقَرَارُ ﴾
Jahannama yaslawnaha fabi/sa almihadu; Hadha falyadhooqoohu hameemun
waghassaqun; Waakharu min shaklihi azwajun; Hadha fawjun muqtahimun
maAAakum la marhaban bihim innahum saloo alnnari; Qaloo bal antum la
marhaban bikum antum qaddamtumoohu lana fabi/sa alqararu (Surat Sad 38:56-
60)
Tafsir: Jahanama Wataungua ndani yake, na ni Mafikio Mabaya sana Ndio Hii
Wache Waionje Maji Yanayochemka na Usaha Na Adhabu Nyengine kama hizo kwa
pamoja (Wataambiwa) Hiki ni Kikundi Kitakachoingia pamoja Nanyi (Motoni)
Hakuna Marhaba (Kukaribishwa Peponi,Mbinguni) Kwao wao Kwani kwa Hakika
949
Wataungua kwenye Moto Wataambiwa (Wanaofuata Upotovu) La Na Nyie pia hakuna
Marhaban (Kukaribishwa Peponi)Kwenu Nyie(Nao watasema kuwaambia
waliowapotosha kua) Ni Nyinyi ndio MliotupotoshaHii ni sehemu Mbaya sana kufikia.
Ya Allah! Hali inatisha tena Sana! Kwani aya zinawaelezea wale watu ambao watakaokua
ni wenye Kufuata Upande sio, yaani Upande wa Upotovu kutokana na Upande wa Njia
sahih ya Allah Subhanah wa Ta'ala na hivyo kua ni wenye kumuasi Mola wao, na
kutolewa Roho zao huku wakulaaniwa na hivyo kua ni miongoni mwa Watakaoambiwa
kua "La Marhaban - Hakuna Kukaribishwa"
Leo Mtaingia Motoni tu Pamoja na Kundi lenu na Viongozi wenu Mliokua
mkiwafuataAmbapo hapo hapo Mtu akifa hua anakufa bila ya kufuatana na wenzake
aliokua anawafuata au kufuatana nao, hivyo kila mmoja anaondoka Duniani na kurudi
kwa Mola wake kivyake, Lakini katika wakati wa kukutana akishakufa basi atakutana
nao wenzake hao wenye Lebo ya ‘La Marhaban’ na kisha wataanza kulaumiana wenye
kwa wenyewe. Allah atustiri..Aamin
Ambapo kwa upande Mwengine basi pia kuna Hadith ya Al Bara Radhi Allahu Anhu
ambae yeye anasema kua: ‘Hakika sisi tulitoka na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam kwa ajili ya Maziko ya Mmoja kati ya Maansari tulipofika Makaburini
Tukazika na kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akakaa kitako nasi
tukakaa kimyaa bila ya kumzunguka kama vile kuna Ndege ambao wanaruka juu
ya vichwa vyetu kwa ukimya wetu. Huku Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Akiwa na ujiti ambao alikua akichora chora ardhini, kisha akanyanyua kichwa na
kusema na kusema: 'Ombeni hifadhi kutoka kwa Allah Subhanah wa Ta’ala
kutokana na Adhabu ya Kaburi’
Na baada ya kusema hivyo mara 2-3 basi akasema: ‘Mja Mwema anapoondoka hapa
Duniani na Kuingia Akhera, basi hua ni mwenye kushukiwa na Malaika Kutoka
Mbinguni ambao hua ni wenye Nyuso Nyeupee kama Jua, na hukaa pamoja nae na
kujaa hadi kwenye upeo wa Macho.
Hua ni wenye kuja na Sanda kutoka Peponi ambayo inanukia Marashi ya Peponi,
kisha anashuka Malakat ul Mawt na kukaa pembeni ya Kichwa Chake na kusema:
'Ewe Roho Njema Njoo Katika Usamahevu wa Allah Subhanah wa Ta'ala na Radhi
zake.
Kisha Roho hio hutoka taratibu kama Tone la Maji kutoka kwenye Kibuyu cha
Ngozi cha Maji, Na Malakat ul Mawt akishaikamata Roho hio basi Malaika hao
walioshuka Kutoka Peponi hua hawamuachii Roho hio, humpokonya haraka, na
kuitia kwenye Sanda iliyojaa Marashi ya Peponi, na hapo huenea Harufu nzuri sana
ya Miski juu Ardhini. Na kisha Hupaa na hua hawapishani na Malaika yeyoye
isipokua hua ni wenye Kuulizwa: ‘Roho ya Nani Hii Nzuri?’.
950
Malaika hao hua ni wenye Kujibu: 'Ni ya Fulani Ibn Fulani'.
Huku wakitumia Majina Mazuri Mazuri ambayo alikua akijulikana hapa Ardhini.
Hali hii huendelea hadi katika Mbingu ya kwanza na kuomba wafunguliwe waingie,
na hapo Roho hio Hukaribishwa na kushindikizwa katika Mbingu ya juu zaid na
waliokua Karibu na Allah Subhanah wa Ta'ala hadi kufikia katika Mbingu ya 7
Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala husema: ‘Andikeni katika Kitabu cha Mja wangu
Illiyun katika Mbingu ya 7 Kisha Mrudisheni Ardhini.’
Ambapo Allah Subhanah wa Ta’ala anakielezea kitabu cha Illiyun pale aliposema katika
ya azifuatazo:
﴿ كَلا َّ إِن َّ كِتَابَ ٱلأَبْرَارِ لَفِى عِلِّيِّينَ ۞ وَمَآ أَدَْرا ا كََم عِلِّي ُّو نَ ۞ كِتَا بٌم َّرْقُو مٌ ۞
يَشْ هَدُ هُ ٱلْمُقَر َّبُونَ ﴾
Kalla inna kitaba al-abrari lafee AAilliyyeena; Wama adraka ma AAilliyyoona;
Kitabun marqoomun; Yashhaduhu almuqarraboona(Surat Al Mutaffifin 83:18-21)
Tafsir: Hakika ya Kitabu cha Hesabu za Waja wema zitawekwa kwenye Illiyinna. Jee
ni nini kitakachokujuulisha hio Illiyin? Ni Kitabu Kilichoandikwa, Ambacho
kinawashuhudia wale walio karibu na Allah Subhanah wa Ta’ala.
Kisha Allah Subhanah wa Tala anabainisha kwanini akataka Roho hizo zirudishwe
Ardhini kwa kusema : ‘Kwani kutokana nayo Ardhi ndio nimemuumba, hivyo ndani
yake Watarudia na kutokana nayo nitawafufua Upya.’ Kama alivyosema tena katika
aya kua:
﴿ٱل َّذِى جَعَلَ لَكُمُ ٱلأَرْضَ مَهْداً وَسَلَكَ لَكُمْ فِيهَا سُبُلاً وَأَنزَلَ مِنَ ٱلس َّمَآءِ َم آءً
فَأَخْرَجْنَا بِهِ أَزْوَاجاً مِّن ن َّبَاتٍ شَتى َّ ٰ ۞ كُلُواْ وَٱرْعَوْا أَنْعَامَكُمْ إِن َّ فىِ ذٰلِكَ َلآ ٍت
لأُِ وْ لىِ ٱ ل ن ُّ هَ ٰ ى ۞ مِنْهَا خَلَقْنَاكُمْ وَفِيهَا نُعِيدُكُمْ وَمِنْهَا نخُْرِجُ ُك ْم اتَ رَةً أُخْ رَ ٰى
َ
﴾
Alladhee jaAAala lakumu al-ardha mahdan wasalaka lakum feeha subulan
waanzala mina alssama-i maan faakhrajna bihi azwajan min nabatin shatta; Kuloo
wairAAaw anAAamakum inna fee dhalika laayatin li-olee alnnuha; Minha
khalaqnakum wa fiha nu`idukum wa minha nukhrijukum taratan ukhra (Surat Ta-
Ha 20:53-55).
951
Tafsir: Ni yeye ndie aliejaalia Ardhi kua ni Tandiko kwa ajili yenu, na akatoa kutokana
nayo njia tofauti (mpate kutembea juu yake), kwa ajili yenu, na akashusha Maji
kutoka Mbinguni. Na kutokana nayo tukatoa mimea ya aina tofauti; Kuleni na lisheni
wanyama wenu hakika katuika haya kuna dalili kwa wenye kufahamu; Kwani
kutokana nao (udongo) tumekuumbeni, na tutakurudisheni ndani yake, na kutokana
nao tutakutoeni upya.
Hivyo Roho hio hurududishwa ndani ya Mwili wa Mtu huyo aliekufa ndai ya udongo
baada ya kuzikwa kwake yaani kua ndani ya Kaburi na kisha hushuka Malaika Wawili
na kumkalisha na Kumuuliza Mtu huyo: 'Jee ni Nani Mola wako?' Nae atajibu : ‘Ni
Allah Subhanah wa Ta'ala’
Malaika watamuuliza Mtu huyo: ‘Jee Ni ipi Dini yako? Nae atajibu : Dini yangu ni
Uislam.’
Malaika watamuuliza Mtu huyo : ‘Jee ni Nani alietumwa Miongoni mwenu?’ Nae
atajibu: ‘Muhammad Rasul Allah Salallahu Alayhu wa Salam’’
Malaika watamuuliza Mtu huyo : ‘Jee wewe ulifanya nini?’ Nae atajibu: ‘Nilisoma
kitabu cha Allah Subhanah wa Ta'ala Na nilikuamini’
Kisha Sauti itasema Kutoka Mbinguni: ‘Hakika Mja wangu amesema Ukweli hivyo
Mtayarishieni Kitanda cha Peponi na Mvisheni Nguo za Peponi na Mfungulieni
Mlango wa Peponi’
Kisha baada ya hapo Kaburi lake huanza kunukia na kutanuka kwa ukubwa wa upeo wa
Macho, kisha anatokea Mtu aliependeza akiwa na Nguo na Manukato ya za Peponi na
kumwambia
Pokea habari njema za Peponi ambazo zitakufurahisha leo hii, nae atasema: ‘Wewe ni
Nani? Mbona uso wako ni Muonekano wenye kubashiria Habari Njema?’
Mtu huyo atasema: ‘Mimi ni Amali zako njema’, nae Mja huyo atasema: ‘Ya Allah
Harakisha Siku ya Malipo nipate kua na Jamaa zangu na Mali zangu’
Ambapo baada ya Kutolewa Roho basi Malaika watasifiana kuhusiana na Mtu huyo
kutokana na Majina Mazuri yake.
Kwa mfano, Mwenye Kusali, Mkarimu, mwenye Kutoa Sadaqah na Zakkah, Mwenye
Kufunga, Kusoma Qur'an, Kufanya Dhikr, Kupenda Kusaidia Watu, Mpole, Mcha
Mungu, Mwenye Kukataza Mabaya na Kuamrisha Mema,n.k
Na kisha Mtu huyo atapongezwa na Malaika na ataoneshwa Sehemu yake Peponi
akishaingizwa kaburini.
952
Kisha Al Baraa Radhi Allahu Anhu anaendelea kutuambia kua Rasul Allah Salallahu
aAlayhi wa Salam akasema:
‘Lakini Mtu Muovu anapofariki na kutaka kuondoka hapa Duniani basi na kuingia
Akhera basi hushukiwa na Malaika ambao Wamevaa Maguo Meusi, huku wakiwa
na Gunia Jeusi na kukaa kwa kumzunguka Mtu huyo.Wingi wake Malaika hao hua
ni wa kujaza Upeo wa Macho kwa kila upande’
Halafu anashuka Malakut Al Mawt na Kukaa pembeni ya Kichwa cha Mtu huyo,
na kusema: ‘Ewe Roho Ovu! Toka nje kwenye Laana na Adhabu ya Allah Subhanah
wa Ta'ala, Kisha Roho yake Mtu huyo hutoka nje nya Mwili wake Mtu Huyo na
kuchana chana Mishipa yake na Neva zake za Hisia kama vile Reki inavyopita
kwenye Sufi iliyoroa’
Hapa tunaoan kua namna Rasul Allah Salallahu Alayhi w Salam alivyofananua Tukio
hili, la mtu ambae kua ni Muovu basi ni hali mbaya sana Kwani kwanza anashukiwa na
Malaika waliovaa Nguo Nyeusi. Na hii inatuonesha Kwanini Majaji Mahkamani wakawa
hawavai Nguo Nyeupe, kwani Nguo Nyeusi hua zinatia Khofu zaid, tofauti na kama
Wangekua wanavaa nguo Nyeupe hua inatuliza.
Halafu Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anaelezea namna Roho inavyotoka kwa
kusema kama Reki linavyopita kwenuye Sufi iliyoroa maji.
Hapa inabidi tuchukulie Mfano wa Pamba ili tupate kufaham Zaidi Ambapo Pamba ikiwa
Kavu basi hua haishikamani hivyo hua rahisi na ina wepesi kuchambulika Lakini ikiroa
hua inashikamana na kua ngumu na hivyo hua ili kuichambua basi inabidi utumie Nguvu
nyingi zaid.
Na ndio maana Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kua: Inachana chana
mishipa yote na neva za hisia sasa fikira Maumivu yake, kwani tukio hililinaonesha kua
kama hujaandikiwa kufa tu basi lazima Uzimie na kupoteza Faham.
Lakini kwa kua hii ni adhabu ya Allah Subhanah wa Ta'ala, basi unahisi maumivu hayo
na unaona bora uzimie lakini huzimii na maumivu yanazidi.
Naam..Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anaendelea kutuambia kua: ‘Roho hio
ikitoka tu na Malakatul Mawt kuikamata basi Malaika waliovaa nguo nyeusi hawaiwachi
kwenye Mikono ya Malakat ul Mawt bali wanampokonya Hapo hapo na kuitia kwenye
Gunia Jeusi walilokuja nalo, Na hivyo Gunia hilo hutoa Harufu Mbaya sana
isiyostahmilika ya Mtu aliekufa juu ya Ardhi.
Na kisha wanapaa Nayo Mbinguni na katika kila hatua yao wanayopita hukutana na
Malaika ambao
953
Huwauliza: ‘Roho ya Nani hio yenye Uovu kama huo?'
Malaika hao nao husema: ‘Ni ya Fulani Ibn Fulani’, kwa kumuita kwa Majina Mabaya
kabisa aliyokua akiitwa Ulimwenguni, hadi watakapofika Mbinguni, Malaika hao
wataomba kua Milango ya Mbingu ifunguliwe lakini haifunguliwi.
Subhana Allah!
Naam...Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anasema kua Malaika watakapoulizwa,
Ni nani huyo mwenye Roho Ovu inayonuka kama hivyo na Malaika wenzao basi Malaika
hao watamtaja Mtu huyo kwa Majina mabaya aliyokua akiitwa kutokana na amali zake
alipokua hai hapa Ulimwenguni.
Yaani kama Mtu Huyo ni Dhalim, Basi watamwita Dhalim.
Kama ni Tapeli watamwita kua ni Tapeli.
Kama ni Mwizi basi watamwita kua ni Mwizi.
Kama ni Mzinifu basi Watamwita kua ni Mzinifu.
Kama ni Mnafiq basi watamwita kua ni Mnafiq.
Kama ni Mwenye kudharau Sala basi watamwita kua ni mwenye kudharau Sala.
Kama Mfitinishaji basi watamwita kua ni Mfitinishaji.
Kama Muongo watakuita Muongo n.k.
Kwani hayo Masafa ya kutoka Ardhini mpaka Mbinguni na Malaika hao Mpaka Upeo
wa Macho Wanailaani Roho hio Ovu. Na Wanapishana na Malaika wangapi hadi
Mbinguni? Yaani hizo Laana za Malaika hao tu basi zinatosha Kumuangamiza Mtu
Muovu. Hapo bado Roho hio haijahesabiwa Makosa ya Uovu wake. Hii hua ni
Maangamizo juu ya Maangamizo.
Ambapo sehemu hii tu basi inatuonesha Umuhimu wa Kujipamba kwa Sifa Nzuri, Kuishi
vizuri na Watu, kwa Kufanya Mema, Kua na Tabia Nzuri,na Kuitana kwa Majina Mazuri
kama ilivyoamrishwa na Allah na Mtume wake Salallahu Alayhi wa Salam
Na kuzikimbia Sifa Mbaya na Yaliyokatazwa na Allah na Mtume wake Salallahu Alayhi
wa Salam
Kisha anasema Al Baraa Radhi Allahu Anhu kua Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi
wa Salam kua: Malaika hao walioichukua Roho ya Mja huyo Muovu wanapofika
kwenye Milango ya Mbingu na Kugonga, basi Milango hio hua haifunguliwi
954
Kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasoma aya ifuatayo:
﴿إِن َّ ٱل َّذِينَ كَذ َّبُواْ آبَِتِنَا وَٱسْتَكْبَرُواْ عَنْهَا لاَ تُفَت َّحُ لهَُمْ أَبْوَابُ ٱلس َّمَآءِ وَلاَ
يَدْخُلُونَ ٱلجَْن َّةَ حَتى َّ ٰ يَلِجَ ٱلجَْمَلُ فىِ سَمِّ ٱلخِْيَاطِ وَكَذٰ لِكَ نجَْزِى ٱلْمُجْرِمِينَ ﴾
Inna allatheena kadhdhaboo bi-ayatina waistakbaroo AAanha la tufattahu lahum
abwabu alssama-i wala yadkhuloona aljannata hatta yalija aljamalu fee sammi
alkhiyati wakadhalika najzee almujrimeena(Surat Al Araf 7:40)
Tafsiri: Ama kwa Hakika wale ambao wamekadhibisha Aya zetu na Wakawa wana
Kibri juu yake Haitofunguliwa kwa ajili yao Milango Ya Mbingu Na Wala
Hawatoingia Peponi Hadi Pale Atakapoingia Ngamia na Kupenya kwenye tundu ya
Sindano Na Hivyo Ndivyo Titakavyowalipa Wahalifu walioasi.
Aya zinasema kua Watu waovu hawatofunguliwa Milango ya Mbingu na hivyo
hawatopata Rehma za Mola wao hadi pale Itakapowezeakana kwa Ngamia Kupenya
kwenye tundu ya Sindano. Jambo Ambalo Kamwe Haliwezekani...au linawezekana?
Ambapo kwa Upande mwengine Basi wale wanaosafiri Baharini hua ni wenye Kuzijua
zile Kamba nene ambazo hutumika kufungia Nanga ya Meli, au Kuizuia Meli isiondoke
Bandarini na kwa wasiojua basi yaani tunazungumzia Kamba ambayo unene wake hua
kama wa inchi mbili mpaka tatu.
Hivyo Wenye Lugha yao basi hua wanaziita Kamba zenye Unene huo kua ni Jumal yaani
Kamba Nene iliyopatikana kutokana na kuzongwa pamoja kwa Kujumuishwa kamba
mbili mpaka tatu.
Kwa hivyo kama tukichukulia mfano wa kua Ngamia hawezi Kupenya kwenye Tundu
ya Sindano kwa sababu hilo si Jambo la kawaida, basi Wanazuoni wamesema kua
unaweza ukatafsiri neno Jamal kua ni Jumal kutokana na kua Kamba au Uzi hua una
maumbile ya Kuingia Kwenye tundu ya Sindano au Shazia.
Lakini jee hata hii kamba ya kuzulia Meli Bandarini itaweza kupenya kwenye Tunu ya
Sindano? Kwani Jambo hilo ni Jambo lisilowezekana kamwe kutokea.
Kisha baada ya kusema Maneno ya aya hii ya Surat Al Aaraf 7:40 basi Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akaendelea kusema kua: Kisha Allah Subhanah wa Ta'ala
955
atasema : Muandikieni Mja wangu ndani ya Kitabu cha Sijjin chini Kabisa ya
Ardhi
Na kisha Mrudisheni Ardhini kwani kwa hakika Nimewaumba Kutokana nayo, na
Ndani yake nitawarudisha na Kutokana nayo nitawafufua tena Kisha Roho ya Mtu
huyo itavurumishwa Ardhini kisha Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasoma
aya ifuatayo:
﴿حُنَفَآءَ هلل َِّ غَيْرَ مُشْرِكِينَ بِهِ وَمَن يُشْرِكْ بِٱهلل َِّ فَكَأَنم ََّا خَر َّ مِنَ ٱلس َّمَآءِ فَتَ خْطَفُهُ
ٱلط َّيْرُ أَوْ تَهْوِى بِهِ ٱلرِّيحُ فىِ مَكَانٍ سَحِ يقٍ ﴾
Hunafaa lillahi ghayra mushrikeena bihi waman yushrik biAllahi fakaannama
kharra mina alssama-i fatakhtafuhu alttayru aw tahwee bihi alrreehu fee makanin
saheeqin(Surat Al Hajj 22:31)
Tafsir: Na Wenye Kumshirikisha Allah Basi hua Kama alieanguka Kutoka Mbinguni
Kisha Akanyakuliwa na Ndege (kama anavyonyakua Eagle) Au Akapeperushwa na
Upepo katika sehemu ya Mbali Kabisa (Na hivyo kutojulikana ameangukia wapi, na
ana hali gani kama mzima au amekufa)
Kwani aya hii tumeshaitafsiri tulipozungumzia aina za upepo ndani ya Qur'an katika
juzuu ya kwanza ya Kitabu hiki ambapo tulisema kua Qur'an inapozungumzia Upepo
Katika Hali ya Umoja yaani Rihan basi hua ni Upepo wa Adhabu.
Na inapozungumzia Upepo Katika Hali ya wingi yaani Riyah basi hua ni Upepo wa
Rehma, ambapo hapa tunaona kua Aya imezungumzia Hali ya Umoja ya Upepo...yaani
Upepo wa Rihu
Ambapo ili kuujua Upepo huu basi Tukumbuke yaliyowakuta watu wa Nabii Hud, ambao
tulisema kua Walipigwa na Upepo wa hali ya Umoja wa Rihan wa Adhabu ambao
Ukikupiga Tumboni basi unatokea Upande wa Piki na Kuunguza kila kitu ndani ya tumbo
lako na kuacha Mifupa mitupu Unakua Kama Bua
Hivyo hii ndio hali ambayo Roho ya Mtu Muasi kwa Mola wake Itakutana nayo katika
kushushwa kwake Ardhini, yaani itapata kama ya Adhabu ya Watu wa Nabii Hud au
itakutana na hali ya kua Kama Mtu anaeanguka Kutoka Juu Angani kisha akanyakuliwa
na Kucha za Eagle (Tai) na kisha kunyofolewa nyofolewa na Mdomo wa Tai
956
Naam..hivyo Al Baraa Radhi Allahu Anhu anaendelea kutuambia kua Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam aliendelea kusema baada ya Roho ya mtu Muovu kukataliwa
kufunguliwa Milango ya Pepo na Kuamrishwa kurudishwa Chini Ardhini kua:
Roho hio Inarudishwa ndani ya Mwili wake Mtu muovu huyo, na kisha anatokewa na
Malaika Wawili ambao wanamkalisha kitako kisha wanaanza kumhoji kwa kusema: ‘Jee
ni Nani wewe Mola wako? Na atasema Sijui Ataulizwa Jee ni Ipi Dini yako?’
Nae atasema: ‘Sijui’
Kisha Itasikika Sauti Kutoka Mbinguni ambayo itanadia kwa kusema: ‘Mtayarishieni
kwa ajili yake Kitanda cha Motoni, Na kisha Mvalisheni Mavazi ya Motoni, na
Mfungulieni Mlango wa Motoni’ Kisha baada ya hapo Unamjia Mvuke Wa Moto wa
Jahannam na Kaburi lake linaanza Kubana na kubana hadi Mifupa ya Mbavu zake
zinaanza Kuvaana.
Kisha anakuja mbele yake Mtu Mwenye Sura Mbaya Sana, na Nguo Mbovu Mbaya Sana
hukua akiwa amejawa na Harufu Mbaya isiokua na mfano wake, ambae atasema ‘Pokea
Bashirio la Habari Mbaya Kabisa, Kua hii ndio Siku Ambayo mliahidiwa kua
Itafika’
Hivyo Maiti huyo atauliza kwa kusema: ‘Wewe Ndio Ndani, Mbona Uso wako ni Uso
ambao Umebeba Mambo Mabaya Maovu sana?’
Mtu huyo Mwenye Sura Mbaya aliemtokea Maiti huyo Muovu anaeulizwa nae atajibu:
‘Mimi Ndio Uovu wa Amali zako!’
Maiti hio itasema: ‘Ya Rabb! Usiiharakishe Siku ya Malipo! Usiijalie Kuja Siku ya
Malipo’ (Musnad Imam Ahmad).
Ambapo Hadithi hii iliyopokewa na Al Baraa Radhi Allahu Anhu inatuonesha kua Wale
watu watakao kua ni wenye kutii Maamrisho ya Allah Subhanah wa Ta'ala na hivyo kua
ni Waja wema basi ingawa Watakua na hali ya Maumivu katika Wakati wa kutolewa
Roho, lakini hapo hapo Watakua wanatolewa kwa Huruma huku waliombewa dua na
Mamilioni ya Malaika.
Kiasi ya Kitakachofuatia baada ya Kutolewa Roho yake basi itakua ni hali ya kua katika
Mazingira ya Raha na Utulivu kwani itakua ni yenye kuingizwa kwenye Mazingira ya
Peponi, kiasi ya kua Roho ya Mtu huyo atajuta kwanini hakua ni mwenye kufanya Mema
zaid hapo kabla alipokua Duniani.
957
Na Akirudishwa Kaburini ambalo ingawa litatanuka na kua na Mapana ya Mbingu na
Ardhi, lakini hatotosheka na hivyo kuomba kwa Mola wake kua Siku ya Malipo
iharakishwe, kwani anahamu aone Malipo yake na Pepo yake.
Kwani kwa upande mwengine basi tunaona kua sehemu ya pili ya Hadithi hii
inawazungumzia wale Wenye Kukadhibisha Dini na Siku ya Malipo. Na matokeo yake
katika siku ya kitolewa Roho watu hao basi watakua ni wenye kuonja Uchungu wa
Kutolewa Roho mara 100 zaidi ya Watu Wema.
Kwani Watu waovu hawa Watatolewa Roho bila ya huruma, huku Wakilaaaniwa na
Mamilioni ya Malaika, na Huyo Mtoaji mwenye nae anatoa kwa Hasira. Hapa tuchukulie
Mfano Mdogo ambao si chochote si lolote.
Ambao ni Mfano wa Mtu anaeumwa na Jino kisha akaenda kung'olewa Jino kwa
Kupigwa Sindano ya Ganzi kwanza na Daktari Mzuri anaependeza na kisha Unapewa
Kilo ya Dhahabu kwa Jino hilo..na kisha anaambiwa kuna Mlima wa Dhahabu katika
siku ya Malipo kwa ajili yake
Naam huu ni Mfano wa kutolewa Roho na kuingizwa Kaburini kwa Mja mwema..Atakua
anaomba kua Siku ya Malipo Ifike haraka ili apate na Huo Mlima wa Dhahabu kutoka
kwa Mola wake
Halafu Mtu Mwengine kuenda kung'olewa na Mtu anaetisha sana tena hana sindano ya
Ganzi na anakung'oa kwa Nyundo na Patasi, na kisha baada ya hapo kuna Watakao
kushindikiza kwa Mijeledi hadi Rumande baada ya kutoa Jino
Huku akijua kua Adhabu zinazomsubiri Rumande basi si chochote si lolote ukilinganisha
na Adhabu ya Jela ya Kutumbukizwa kwenye Shimo la Moto wa Milele unaomsubiri
katika siku ya Malipo
Hivyo mtu huyo atakua anaomba kua Hio Siku ya Kuhukumiwa kwa ajili ya Kuenda Jela
ya Shimo La Moto kua isifike, kwani bora kupata hio Mijeledi na Mvuke wa Moto kuliko
Moto wenyewe
Naam.. Hio ndio hali ya Mtu Muovu anaemuasi Mola wake na kukadhibisha kuwepo kwa
siku ya Malipo ambapo amesema Umm Ul Muuminina Aisha Radhi Allahu Anha kua:
‘Alikuja Mwanamke Mmoja wa Kiyahudi Mlangoni kwangu akaniomba Chakula
huku akisema: ‘Nisaidie Chakula, Allah atakuhifadhi na Mtihani wa Dajjal na
Mtihani wa Adhabu ya Kaburi’
958
Aisha Radhi Allahu Anha anaendelea kusema kua: Hivyo Nami nikaendelea kumfanya
awe ni Mwenye kuzungumza hadi akatokea Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kisha
nikasema: ‘Ya Rasul Allah, Hivi Huyu Mwanamke anazungumzia kuhusiana na
nini? Hivi anavyosema kua Allah Akuhifadhi na Mtihani wa Dajjal na Mtihani wa
Adhabu ya Kaburi?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akanyanyua Mikono yake juu na kisha akaomba
Dua ya kupata Hifadhi ya Fitna ya Dajjal na Fitna ya Adhabu ya Kaburi, kisha akasema:
‘Ama kuhusiana na Fitna ya Dajjal basi hakuna Mtume isipokua alikua ni mwenye
kuwausia watu wake kutokana nae Lakini mimi nitakuambieni kitu ambacho
hakuna Mtume aliewaambia watu wake: Ambacho ni kua Dajjal ni mwenye Jicho
Moja, na Allah si mwenye Jicho Moja, Dajjal ana maandishi kwenye Paji lake la
Uso yasemayo Kaffir ambayo kila Muumini atayasoma’
Ama kuhusiana na Mtihani wa Adhabu…basi Maiti hio itaulizwa: ‘Jee ni kipi kile
ambacho ulikua ukisema kuhusiana na Uislam? Jee ni mtu gani alikua ni Miongoni
mwenu? Nae atasema Muhammad ni Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam ambae
ndie alieleta vithibitisho dhahir kuhusiana na Allah Subhanah wa Ta'ala na sisi
tukamuamini.’
Kisha baada ya hapo Litafunguliwa Shimo ambalo ndani yake ataona Moto ambao
sehemu yake moja inaiunguza sehemu nyengine na kisha ataambiwa: ‘Angalia kile
Ambacho Allah amekuepusha Nacho!’
Na kisha atafunguliwa Shimo Jengine ambapo ndani yake ataiona Pepo na Mapambo
yake yote na kisha ataambiwa, Haya ndio Makazo yake Ataambiwa tena: ‘Hakika wewe
ulikua na Imani Thabiti na utafufuliwa na Imani Thabiti Inshaa Allah,’
Na kama atakuwa ni Mja Muovu basi atakalishwa kitako kwenye Kaburi huku akiwa na
khofu na wasi wasi, na kisha ataulizwa. ‘Jee ulikua ukisema nini?’
Nae atasema: ‘Mimi nilikua nikisikia watu wakisema kadhaa w kadhaa hivyo na
mimi nikasema hivyo hivyo’
Hivyo shimo litafunguliwa ambalo ndani yake ataona Pepo na Mapambo take na kisha
ataambiwa: ‘Angalia kile ambacho Allah Subhanah wa Ta'ala amekukosesha!’
Kisha atafunguliwa Shimo Jengine na ataoneshwa Moto ambao sehemu yake moja
inaiunguza sehemu Nyengine na ataambiwa: ‘Haya ndio Makazi yako ambayo ulikua
ukiyatilia shaka na utaufuliwa, Huku ukiwa na shaka Juu yake na kisha
ataadhibiwa’
959
Naam, hivyo ndivyo hali inavyokua Ndani ya Qaburi na ndio maana Amr Ibn Al Aas
Radhi Allahu Anhu akasema kua: ‘Baada ya kunizika basi Msioondoke, tumieni mda
kiasi kama wa kuchinja Ngamia na Kumtawanya Nyama yake, ili niwe na utulivu
kutokana na kuwepo kwenu, hadi pale nitakapoona nitawajibu vipi Wajumbe wa
Mola wangu.’
Hivyo hii ni kuhusiana na hali Kaburi ambalo hua ni neno lenye kutokana na neno
Qabara ambalo kwa Kilugha bua linamaamisha Kuzika Maiti, Neno Qabara ndio
lililotoa neno Aqabara ambalo hua linamaanisha Kusababisha Mtu Kuzikwa, Kua na
Siku Mbaya iliyojaa Huzuni
Na pia neno Qabara ndio lililotoa neno Qabur ambalo hua linamaanisha Kaburi, au hali
ya Roho wakati inapotoka baada ya Kufariki mtu hadi katika siku ya Kufufuliwa.
Ambapo hali ya Qabur hua pia inajulikana kama Barzakh Kwani neno Qabur hua pia
linamaanisha neno Barzakh kwa sababu neno Barzakh hua linamaanisha Kizuizi, Kitu
kinachotengenisha baina ya vitu viwili.
Na hivyo Barzakh hua ni Hali Baina ya Kuishi kwa Roho baina ya hali za Maisha Mawili
tofauti. Ambapo hali ya kwanza hua ni ya Maisha ya Mpito ya Kidunia na hali ya pili ni
ya Maisha ya Milele ya Kiakhera.
Hivyo tunapozungumzia kuhusiana na Qabur au Barzakh basi hua tunazungumzia hali
ya 4 kati ya 5 za Maisha ya Viumbe Ibn Adam ambazo ni:
Ambapo hali ya kwanza hua ni ile ya kua Ndani ya Kiza cha Mapazia ya kuwemo
ndani ya Sehemu za Siri za Wazee wetu kwa miaka na miaka kutoka kizazi mpaka
kizazi.
Hali ya pili hua ni hali ya Kutoka kwenye Sehemu za Siri za Baba na Kuanza Kuishi
Ndani ya Kiza ndani ya Fuko la Uzazi la Mama, Fuko la Uzazi la Mama ambalo Ibn
Adam hua katika Hali ya Ndani ya Kiza cha Matabaka Matatu, Ambayo ni Ndani
ya Fuko la Uzazi, liliomo ndani ya Sehemu ya Kizazi kilichomo ndani ya Tumbo la
Mama.
Hali ya 3 hua ni Pale unapotoka katika katika Tumbo la Mama baada ya kuzaliwa
na kuanza Maisha ya Kuishi Duniani Mpaka Kufariki kwa Mtu Husika Na Hali ya
4 hua ni Maisha ya Barzakh au ya Qabur ambayo huanzia mara baada ya Kufariki
na kuendelea hado siku ya Kufufuliwa.
Na Hali ya 5 hua ndio hali inayoanza baada ya kufufliwa katika Siku ya Malipo
Kwani hali zote hizo hua ni za Mpito isipokua hali ya Mwisho ambayo ni hali ya
960
baada ya kufufuliwa kwa ajili ya kuhesabiwa Amali zetu Ambayo hii hua ni hali ya
Milele.
Ambapo katika hali zote hizi basi hali ya kwanza hua ni Hali ya Maumbile ya baada ya
Kiapo na Ahadi ya Kubeba Amanah mbele ya Muumba hadi ndani ya sehemu za Siri za
Baba. Hali ya pili ni hali ya Ndani ya Kizazi cha Mama kwa ajili ya Matayarisho ya
kutimiza Ahadi na Kiapo tulichokila kama tulivyoona hapo kabla. Hali ya tatu ni hali ya
Duniani ya Utekelezaji wa Amana na Utimizaji wa Ahadi na Mitihani ndani yake. Kwani
Hali hizi tatu za Mwanzo hua ni kama hali za Kua katika Ndoto.
Na ndio maana akasema Hujjati Ul Islam Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad
Al Ghazali kua: ‘Watu wote hua ni wenye kulala na kuota Hapa Ulimwenguni hadi
watakapoingia Makaburini ndio hua ni wenye kuamka na Kuuona Uhalisia
Isipokua wale wenye Taqwa ndio hua si wenye Kua Usingizini’
Ambapo hii inawekwa wazi na Surat At Takathur pale iliposema:
﴿بِسْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞أَلهَْاكُ مُ ٱلت َّك َّاثُرُ ۞حَتى َّ ٰ زُرْتمُُ ٱلْمَقَ ابِرَ۞كَلا َّ سَوْفَ
تَعْلَمُونَ۞ثمُ َّ كَ لا َّ سَ وْ فَ تَعْلَمُ ونَ ۞كَلا َّ لَوْ تَعْلَمُونَ عِلْمَ ٱلْيَقِينِ۞لَتَرَوُ َّن
ٱلجَْحِ يمَ۞ثمُ َّ لَتَرَوُن َّهَا عَينَْ ٱلْيَقِينِ۞ثمُ َّ لَتُسْأَلُن َّ يَوْمَئِذٍ عَنِ ٱلن َّ عِيمِ ﴾
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi; Alhakumu alttakathuru; Hatta zurtumu
almaqabira; Kalla sawfa taAAlamoona; Thumma kalla sawfa taAAlamoona; Kalla
law taAAlamoona AAilma alyaqeeni; Latarawunna aljaheema; Thumma
latarawunnaha AAayna alyaqeeni; Thumma latus-alunna yawma-dthin AAani
alnnaAAeemi(Surat At Takathur 102:1-8)
Tafsir: Kwa jina la Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma, Ushindani wa
kukusanya Mapambo ya Kidunia unakutoeni kwenye Malengo ya kiakhera, hadi pale
mtakapotembelea na kuingia Makaburini, Lakini baada yake Mtakuja kujua, Kisha
baada yake mtakuja kujua, Kama mngejua kwa Ilm ya Yaqini, basi wa hakika
Mngeuona Moto Mkali, Kisha Mtaona kwa Mtizamo wa Jicho la Yaqini, Kisha katika
siku hio mtaulizwa kuhusiana na Neema mlizopewa.
Ambapo tunaona kua Sura hii inatuwekea wazi kuhusiana madhara ya kukumbatia
mapambo ya kidunia na kukusanya Mali kunakowapelekea watu kuisahau Akhera na
961
kuhusiana na kuulizwa juu ya Mali tulizochuma, ambapo amesema: ‘Abd Allah Ibn
Habib kua kutoka kwa Baba yake, kuptia kwa Mjomba wake kua: ‘Siku moja Rasul
Allah Salallahu A’layh wa Salam alitoka nje huku akiwa ameroa maji kwenye
nywele zake huku kiwa na uchangamfu kwenye Uso wake, hivyo nasi tukasema kua:
‘Tunakuona kua una muonekano wa Furaha ya Rasul Allah!’.
Rasul Allah Salallahu A’layh wa Salam akasema: ‘Naam’ kisha akakaa pamoja nasi
na kutufahamisha kuhusiana na Neema za Allah Subhanah wa Ta’ala, kisha
akamalizia kwa kusema: ‘Mali hua haina madhara kwa yule ambae ni mwenye kua
na Taqwa, lakini Afya njema hua ni bora kuliko mali kwa yule mwenye kumuogopa
Allah Subhanah wa Ta’la. Na uchangamfu hua ni Neema’(Musnad Imam Ahmad Ibn
Hanbal)
Naam, hii ni kwa sababu mtu anapokua Mcha Mungu basi hua ni mweye kutafakkar sana
kuhusiana na hali hii ya nne ya Maisha ya kuingia Kaburini baada ya Kufa na ya tano
baada ya Kufufuliwa hua ni Hali ambazo ni za Uhalisia, ambazo hua zenye kuonekana
kwa mtizamo wa Yaqini kwani kila kitu kinakua wazi kutokana na kupata Ufunuo na
hivyo kua ni mwenye kuona bila ya kuwepo kwa Pazia la macho au mara baada ya
kuingia kwenye Barzakh hadi katika Siku ya Malipo kwa ajili ya kulipwa kutokana na
tuliyoyafanya.
Ambapo tunapoangalia kuhusiana na Ilm Al Yaqin na Ayn Al Yaqin basi anasema Shaykh
Muhammad Al Naquib Ibn Ali al Attas ambae ni Mwanzuoni wa Kiislam kutoka
Malaysia kua: ‘Hikma hua ni Ilm lakini si Kila I’lm hua ni Hikma’ yaani baadhi ya
wakati hua kile ambacho hua kinachukuliwa kua ni Ilm hua si chengine bali hua ni
Ufaham wa Mtu kutokana na Kutafakkari kwake, hivyo kila mtu anavyotafakkari
zaidi basi hua ni mwenye kupata vithibitisho zaidi na hivyo hua ni mwenye kua na
Hikma zaidi. Na hivyo basi Hikma hua ni hitimisho linalotokana na Tafakkur ya
Mtu. Na hii ndio hua ile ambayo Qur’an imeizungumzia kua ni Ilm Al Yaqin, Ayn
Al Yaqin na Haq al Yaqin.
Hivyo tofauti baina ya Hikma na Ilm hua ni katika Upana wa Ufaham wa Mtu husika.
Kwa maana hio basi bila ya shaka haitowezekana Kujua uhalisia wa Barzakh had pale
tutakapokaa na kua ni wenye Kutafakkari Uhalisia halisi wa Jambo hili, ambalo haliwezi
kufahamka kiufaham wakati ukiwa hai hapa Duniani hadi pale utakapokua na Ilm na
Hikma au baada ya kuondolewa pazia la macho baada ya kuinga Kaburini kwenye hatua
ya nne ya Maisha.
Hivyo tuamshane tusizinzie na Kulala ili tuamke kabla hatujaamshwa na Mauti kwa
kuangala maana ya neno Umm ambalo hua linamaanisha Mama, Chanzo, Kanuni, Asili,
Mwanzo, Mfano au Kigezo cha asili. Kwani nalo pia linahusika katika kuifafanua hali ya
962
kile kinachotokea baada ya Mtu Kutolewa Roho yake Ambapo anasema Allah Subhanah
wa Ta'ala katika Surat Al Qaria katika aya zilizotumia neno Umm kua:
﴿وَأَم َّا مَنْ خَ ف َّتْ مَوَازِينُهُ۞فَأُم ُّهُ هَاوِيَةٌ۞وَمَآ أَدْرَاكَ مَا هِيَهْ۞َرٌ حَ امِيَةٌ ﴾
Waamma man khaffat mawazeenuhu; Faommuhu hawiyatun; Wama adraka ma
hiyah; Narun hamiyatun (Surat Al Qaria 101:8-11)
Tafsir: Ama Kwa Yule Ambae itakua Hafifu Mezani yake (ya Amali Njema) Basi
Mama yake (atakua) ni Hawiyah. Na Nini Kitakacho kujuulisha ni nini hio (Hawiya)?
(Ni) Moto Mkali Sana
Naam...aya zinatuonesha kua: Yeyote yule atakaekua ni mwenye kufanya maovu mengi
zaid kuliko mema na hivyo mema yake kua ni kidogo basi atakapoingia Kaburini Mama
yake atakua ni Moto wa Hawiya
Na bila ya shaka sisi sote ni wenye kujua kua Kimaumbile Jukumu la Mama hua ni
Kumlea Mtoto wake tangu Mwanzoni anapobeba Ujauzito ndani ya Tumbo lake mpaka
kumtoa mtoto huyo nje ya Tumbo lake na kumlea hadi kua mkubwa na pia kamaa kuna
majaaliwa basi hadi kufa kwake. Yaani siku zote Mtu hata awe na miaka 100 basi kama
Mama yake yuko hai basi Mtu huyo hua ni Mtoto kwa Mama yake, na Mama hua ni
Mama kwa Mtoto wake hachoki kumjalia na kumsimamia.
Sasa Aya zinatuambia kua Kama Mizani ya Mema yako itakua Nyepesi zaidi ya Maovu
yako basi na wewe Mara tu utakapotolewa Roho Utakua ni Mwenye Kulelewa na Mama
yako, ambae ni Moto wa Jahannam yaani hutotoka ndani yake!
Ambapo anasema Imam Muhammad Ibn Jariri At Tabari kua: ‘Amesema Abu Hurayra
Radhi Allahu Anhu kua: Amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua:
Wakati Muumini anapofariki, basi Malaika wa Rehma humjia na Nguo za Hariri
na kumwambia: ‘Njoo ewe Roho kwa Allah Subhanah wa Ta'ala, na hivyo Roho hio
hutoka huku ikiwa inanukia kwa harufu ya Miski nzuri kabisa
Na kisha Malaika hupokezana Roho hio huku wakiinusa hadi katika Mbingu ya
kwanza, na kuambiana ‘Hakika inanukia harufu Nzuri Sana kutoka Duniani’ Roho
hio hupandishwa Juu Mbingu baada ya Mbingu na kujumuishwa na Roho za
Waumini wengine, Ambapo Roho za Waumini hao wengine hufurahia kukutakana
na Roho hio na Kuikaribisha kwa Furaha zaid ya anavyokaribishwa Mtu aliekua
hayupo kwa mda Mrefu pale anaporudi Nyumbani.
963
Kisha Roho hizo zilizoikaribisha Roho hio Huiuliza Roho hio iliyowasili kwa
kusema: ‘Ni nini Kimetokea Kwa Fulani Ibn Fulani?’
Hapo Malaika husema: ‘Iwacheni Ipimzike (Kwanza hii Roho) Kwani Imechoka
kutokana na ya Duniani’
Kisha Roho hio husema (Kujibu kuhusiana na hio Roho ya fulani alieuliziwa na
Roho hizo za Peponi) kua ‘(Fulani Ibn Fulani) Amekufa Hivi Hajaja Huku kwenu?’
Ambapo hapa Malaika hua ni wenye kujibu Suali hio kwa kusema kua:
‘Faommuhu hawiyatun’ yaani Huku Peponi hajaja kwa sababu ameenda kwa
Mama yake Mlezi atakaemlea ambae ni Shimo la Moto Mkali sana.
Ambapo Kwa Upande wa Imam Qatadah Al Sadusi basi yeye anasema kua: ‘Maneno
Faommuhu hawiyatun yanamaanisha kua Mtu huyo atatumbukia kwenye Shimo
hilo la Motoni Kichwa kichwa’ na hivyo aya kua ni zenye kutukumbusha Umuhimu
wa Kuzidisha kufanya Mema kabla hatujaingia Kaburini!’
Kwani alisema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kaburi hua linabana na
kama kuna Mtu ambae ataweza kuepukana na m-bano wa Kaburi basi ni Saad Ibn
Muadh.’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alisema hivyo kuhusiana na Saad Ibn
Muadh Radhi Allahu Anhu kwa sababu alikua ni Chifu wa Kabila la Banu Aws la Watu
wa Madinah .
Saad Ibn Muadh Radhi Allahu Anhu alisilimu wakati akiwa na Umri wa miaka 31 baada
ya kusikia Ujumbe wa Allah Subhanah wa Ta'ala kutoka kwa Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kupitia kwa Balozi wa kwanza kumuwakilisha Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam katika Mji wa Madinah ambae ni Musab Ibn Umayr Radhi Allahu Anhu
ambae alikua anakaa katika Nyumba ya Asad Ibn Dhurara Radhi Allahu Anhu ambae
alkua ni Mtoto wa Dada yake Saad Ibn Muadh Radhi Allahu Anhu.
Hivyo Waislam walipohamia Madinah basi Kabila la Saad Ibn Muadh Radhi Allahu
Anhu lilijitolea kwa kila kitu na kuwakaribisha Waislam hao katika Majumba yao ya
Banu Ashshal bila ya kujisifu wala kujiona wala kuweka mipaka kwa ajili ya Waislam
hao waliohama kutoka Makkah kuelekea Madinah .
Ambapo katika Vita vya Badr baada ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
kukusanya Jeshi lake la watu wa Makkah basi alipomuuliza Saad Ibn Muadh Radhi Allah
964
Anhu kama Watu wa Madinah wako tayari kupigana pamoja nao katika vita hivyo
ambapo Saad Ibn Muadh Radhi Allahu Anhu akasimama na kusema:
‘Ya Rasul Allah! Hakika sisi Tunakuamini wewe kikamilifu na tunashuhudia kua
Ujumbe wako ni wa Haki. Tunaapa na kuahidi kua sisi tuko Pamoja nawe kayika
kila kitu, hivyo qmua unaloamua na sisi tutafuata na kusimama ubavuni mwako.
Tunaapa kwa Jina la Allah Subhanah wa Ta'ala kua, ukienda Kwenye Bahari
pamoja nasi na kuvuka basi nasi tutavuka pamoja nawe, hakuna hata mmoja kati
ya Watu wangu atakaebakia bila kukufuata. Hivyo kwa hakika Sisi tuko Pamoja
nawe kupigana vita dhidi ya Maadui zetu Kesho kwani Tunahamu nao
Kupigana nao na tunahamu ya kukutana na Mola wetu, na tuna matumaini kua
Allah Subhanah wa Ta'ala atatuwezesha sisi kua ni wenye Kufanya kile ambacho
kitakufanya Ujivune kutokana nasi, Hivyo ya Rasul Allah! Panga unavyopanga
hakika sisi tuko pamoja nawe’
Kwani majibu haya ya Sad Ibn Muadh Radhi Allahu Anhu yaliusababishia Uso mtukufu
wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua ni Wenye Kung'ara kwa Furaha na hivyo
akasema: ‘Sherehekeni kwani Allah Subhanah wa Ta'ala ameniahidi mimi sehemu
moja kati ya sehemu mbili za Maaduni zetu.(Msafara wao au Jeshi lao) Wallahi
nnakaribia kuona mimi kwa macho katika kila sehemu ambayo utalala mwili wa
Maiti wa maadui zetu’
Saad Ibn Muadh Radhi Allahu Anhu alifariki miaka 7 baadae katika Vita vya Khandaq
kutokana na Majeraha baada ya kushabuliwa kwa upinde kadhaa kwenye mwili wake, na
hivyo alipokua kumwa basi akawa ni mwenye kusema kua: ‘Ya Allah! Kama mapigano
ya vita hivi dhidi ya Quraysh yataendelea zaid, basi usiniwache mimi nikabaki hivi
bila ya kuendelea kupigana nao. Kwani kwa hakika kwangu mimi hakuna kitu
nnachokipenda zaidi kuliko kuigana na Watu wanaotaka kumdhuru Mtume wako
Salallahu Alayhi wa Salam, kutokana na kutomuamini kwao hadi kufikia
kumfukuza katika ardhi ya kwao. Lakini kama mapigano yamemalizika basi
yasababishie majeraha yangu kusafisha njia ya kuupata Ushahidi. Ya Allah
nakuomba usinasababishie mimi kufariki kabla ya kulipiza dhidi ya Banu
Qurayza.’
Wakati akiwa bado yuko taabani kitandani akiendelea kuuguza majeraha basi
alitembelewa na Rasul Allah Salallahu Alayhi Wa Salam ambae alikichukua kichwa cha
Saad Ibn Muadh Radhi Allahu Anhu na kukiweka kwenye mapaja yake, kisha Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akaomba dua kwa kusema: ‘Ya Allah! Saad amejitahidi
965
kwa ajili yako, Saad amemuamini Mtume wako na amefanya jitihada zote kwa ajili
yake, hivyo tafadhali ipokee Roho yake kwa mapokeo yaliyo mema.’
Maneno haya ya Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam yalikua kama ni utulivu wa
Macho ya Roho ya Saad Ibn Muadh Radhi Allahu Anhu ambayo ilikua ni yenye kutoka
ndani ya Mwili wake, huku akijaribu kufumbua macho yake kumuangalia kwa mtizamo
wa Mwisho kipenzi chake kiliopo mbele yake ambae ni Rasul Allah Salallahu Alyhi wa
Salam na kisha Saad Ibn Muadh Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Ya Rasul Allah Hakika
mimi nnashuhudia kua wewe ni Rasul Allah.’
Ambapo alisema Abu Said Al Hudri Radhi Allahu Anhu kua: Hakika mimi nilikua ni
mmoja kato ya Waliochimba Kaburi la Saad Ibn Muadh ambapo kila tukichimba
basi Ardhini ilikua ikitoka Harufu nzuri ya Miski hadi kwenye Mwana wa Ndani.
Na akasema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Arshi ya Allah Subhanah wa
Ta'ala imetikisika kutokana na Kifo cha Saad Ibn Muadh.’
Turudi tena katika kisa cha Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu kupitia katika Hii ndoto
yake, aliyoiota kua yuko kwenye sehemu inayobana na yenye kiza kikubwa sana lakini
mbele yake kuna sehemu yenye Muangaza, akajihisia kua kuna ulazima wa kujitoa
kwenye kizo hicho na akafanya jitihada hadi akafanikiwa kutoka kwenye kiza hizo na
sehemu hio inayombana, na tunazungumzia kuhusiana na Ndoto kwa sababu kila mmoja
wetu ni Mwenye kujua kuhusiana na Ndoto, ambapo hua unaweza kua Umelala kwenye
Kitanda chako cha Kingsize 8x8 lakini Ukaota uko Mwituni unafukuzwa na Joka Au
Chui, Au Unazama Baharini au Uko Shimoni na kua na hali ambayo isiyoelezeka
kutokana na Khofu na Tafrani ziliomo ndani ya Ndoto hio ambayo unaota huku ukiwa
Chumbani Mwako na Kitandani Mwako Pembeni ya Mkeo au Mume wako na ukamshtua
kutokana na Kelele au Mateke yako ndani ya Ndoto zako. Ambapo Athari zake
zinavyoitokeza basi huenda ukapiga Kelele: Nisaidie Nakufa!
Hivyo Mwenza wako alie pembeni yako akakutuliza na Kusema: ‘Ya Albi! (Ewe Moyo
wangu) Usiwe na Khofu kwani uko kwenye Jinamizi Unaota Sauti hio na Utulizo
wake ndio hua Salama yako!’
Ambapo tumeona kua amesema Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kaburi
hua linabana na kama kuna Mtu ambae ataweza kuepukana na m-bano wa Kaburi
basi ni Saad Ibn Muadh.’
Hivyo kama hali inavyokua wakati unapoona Jinamizi kwenye Kitanda cha kingsize
chako basi ndio hivyo hivyo hali Inavyokua wakati unapokua Umefariki. Yaani Wakati
unapokua Maiti, basi Uwe Kaburini, Uwe kwenye Chumba kilichosakafiwa na kigae, iwe
966
kwenye Sanduku la Dhahabu, Uwe kwenye Tumbo la Nyangumi, Au Umeunguzwa na
kua Jivu, basi Ukishafariki na Kuingia kwenye Barzakh basi wewe mbele ya Mola wako
hua Unahesabiwa kua Uko Kaburini.
Na utajikuta Kaburini na kupatwa na Adhabu kama za walio kaburini, kama vile ambavyo
unapokua unaota uko Mwituni unakimbia, au umetumbukia Shimoni mna Nyoka, wakati
Uko Kitandani, tofauti ni kua badala ya kua Unaota, basi Kaburini hua Huoti bli uko
katika hali ya uhalisia wa mazingira ya Kiroho, kwani ndio hali mpya ya Maisha yako ya
Barzakh, na unapatwa na Maumivu na kila kiumbe hua anasikia Kelele na Vilio
vitokanavyo na Maumivu yako, isipokua Majini na Ibn Adam wenzako ambao wao
hawakusikii kwani Mola wako ameyawekea pazia Masikio yao, ili waendelee na Maisha
yao!
Allah atustiri hapa Juu ya Ardhi, Na Ndani ya Ardhi na Katika Siku ya Kutoka Ndani ya
Ardhi...Allahuma Amiin!
Kwani amesema Al Muhaqiq Al Imam Shihab Ad Din Abu Al Abbas Ahmad Ibn
Muhammad Ibn Ali Ibn Hajjar Al Haytami Al Maki Al Ansari Al Shafii kua: ‘Amesema
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kua: Wakati Maiti inaingizwa Kaburini basi
Kaburi hua ni Lenye Kumuuliza Maiti huyo kwa kusema: ‘Ole wako ewe Ibn
Adam! Hivi ni Kitu Gani kilichokufanya wewe Usitafakari kuhusiana nami?’
Hivi Jee Hukujua wewe Kua mimi ni Nyumba ya Mitihani? Kua mimi ni Nyumba
ya Kiza?
Nyumba ya Upweke na Mafunza? Ni Kitu gani kilichokughafilisha Nami?’ Ulikua
Ukinipita Juu yangu kwa Kudunda na Maringo.’
Hivyo kama Maiti ya Mtu huyo ni ya Mtu mwema basi Maiti itasikia Sauti nyengine
Ikisema Kuliambia Kaburi: ‘Hivi Hukuona wewe Kua huyu Mtu alikua ni Mwenye
Kuamrisha Mema na Kukataza Mabaya?’
Hivyo Kaburi hilo litajibu: ‘Kama ni hivyo basi kwa ajili yake Mtu huyu Mimi
nitabadilika na kua Ardhi Nzuri na ya Kupendeza kwa ajili yake ili Mwili wake
Ubakie katika hali nzuro ya Kunga'ara’
Na Roho yake Ipate Kupaa na Kuelea Juu kwa Allah Subhanah wa Ta'ala (Imam
Ibn Hajar Al Haytami, Imam At Tirmidhii na Imam Abu YaAla)
Hivyo ndivyo hali inavyokua..kwa kila Roho na Mwili wa Ibn Adam na Jini hivyo kama
ni Mtu mwemwa Basi Ardhi ya Kaburi itajibadilisha na Kua Pepo kwa ajili yake. Na
967
kama ni Mtu Muovu basi hali itakua kama Inavyotakiwa tutafakkari kuhusiana na Kaburi
kua ndani yake Mnabana, Mna Kiza, Mna Upweke na Mna Adhabu na Wadudu.
Na akasema Imam Said Ibn Ubaid Ibn Umar Al Layth kua: ‘Hakuna Mtu hata mmoja
atakaekufa Isipokua ataitwa na Kaburi lake ambalo litamnadia kwa kusema:
Hakika mimi Ndio Nyumba ya Huzuni, Ndio Nyumba ya Upweke. Hivyo kama
ulikua ni Mtiifu kwa Allah Subhanah wa Ta’ala katika Uhai wako Duniani basi
Mimi leo Nitakua na Rehma na Huruma kwako. Lakini Kama Ulikua Muasi kwa
Allah Subhanah wa Ta’ala katika Uhai waki Duniani, basi Mimi Ninalipiza Kisasi
Juu yako. Ambapo kwa kila aliekua Mtiifu basi atakua na Raha na Furaha ndani
yangu. Na kwa kile aliekua Muovu basi atakua katika hali ya Maangamizo ndani
yangu.’
Hivyo kila mmoja wetu anatakiwa kujaribu kua Mtiifu kwa Mola wake na pia kuwausia
wenzake na kuwakataza anapowaona wanafanya maovu wakati bado yuko Juu Ardhini
ya kabla hajaingia Ndani ya Ardhi Kaburini. Kwani amesema Imam Said Ibn Jubayr kua:
‘Kuna Ansari Mmoja alikuja kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam huku
akiwa na Uso wenye Huzuni sana. Hivyo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
akamuuliza Ansari huyo kwanini ana huzuni?
Ansari huyo akasema: ‘Ya Rasul Allah hakika mimi nilikua nafikiria Jambo fulani’
Na alipoulizwa ni Jambo Gani, basi nae akasema: ‘Ya Rasul Allah (Salallahu Alayhi
wa Salam) Hakika sisi tuko pamoja nawe Mchana na Jioni hua tunakaa pamoja
nawe. Lakini kesho Akhera wewe Utakua ni mwenye Kukaa pamoja na Mitume
Wenzako, hivyo Sisi hatutokua na uwezo wa Kukufikia wewe Katika sehemu
utakayokuwepo.’
Naam..hili lilikua ni Suali kwa Rasul Allah Salalalhu Alayhi wa Salam ambalo
aliloulizwa na Sahaba ambae ni mwenye hamu ya kutaka kujua Ya Kaburini na Akhera
yake.
Rasul Allah Salallahu Alayh Wa Salam, akawa hana la Kujibu akakaa kimya. Hivyo hapo
hapo Allah Subhanah wa Ta'ala akamtuma Malaika Jibri amshukie Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua anasema Allah Subhanah wa Ta'ala kua:
﴿وَمَن يُطِعِ ٱهلل ََّ وَٱلر َّسُولَ فَأُوْلَٰئِكَ مَعَ ٱل َّذِينَ أَنْعَمَ ٱهلل َُّ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلن َّبِيِّينَ
وَٱلصِّدِّيقِينَ وَٱلش ُّهَدَآءِ وَٱلص َّالحِِينَ وَحَ سُنَ أُولَٰئِكَ رَفِيقاً ﴾
968
Waman yutiAAi Allaha waalrrasoola faola-ika maAAa alladheena anAAama
Allahu AAalayhim mina alnnabiyyeena waalssiddeeqeena waalshshuhada-i
waalssaliheena wahasuna ola-ika rafeeqan(Surat An Nisaa 4:69)
Tafsir: Na Yeyote atakaemtii Allah (Subhanah wa Ta'ala) na Mtume (Salallahu Alayhi
wa Salam) basi Atakua Pamoja na wale Ambao Wameneemeshwa na Allah Juu yao
Miongoni mwa Manabii na Waliosadikisha (Kwa Kukubali kumfuata Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam) Na Mashahidi (Waliokufa Katika Vita vya Jihadi), Na
Waja Wafanyao Mema Na Hawa ni Wabora Miongoni mwa Marafiki.
Hii ni Aya inayobainisha wazi kua Roho za Viumbe Ibn Adam na Majini zitakutana
baada ya Kutoka Duniani na Kuingia Akhera baada ya Kufariki kwa Kiumbe husika
kama vile ambavyo zilivyokua zikikutana wakati watu hao walipokua hai. Yaani Roho
Hukutana na Kuwasiliana katika Mazingira Matatu ambayo ni ya:
Wakati tuko hai kama sasa hivi tunavyokaa na kuishi pamoja hapa Duniani.
Baada ya Kuingia katika Barzakh wakati zinapokua Makaburini.
Katika Siku ya Malipo na baada yake ambapo kila Mmoja atakua na yule
ampendae.
Kwani amesema Amir ul Muuminin Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhua kua: ‘Kulikua
na Waumini wawili ambao walikua ni Marafiki, hivyo mmoja kati yao akafariki,
na alipofika Kaburini na kubashiriwa Pepo basi akamkumbuka Rafiki yake na
kusema: Ya Allah Rafiki yangu Fulani alikua kila siku ananihimiza Kukutii wewe
na Mtume wako Salallahu Alayhi wa Salam. Na alikua akiniamrisha kufanya mema
na kuachana na mabaya.
Hivyo Maiti huyo atamuombea Rafiki yake huyo aliekua hai kua asipotoke na hivyo
akija kufariki basi Roho zao hukutana na kuambiana Mashaa Allah Hakika wewe
ni Rafiki Mzuri sana.
Kwani kwa upande Wasioamini basi anapokufa na kuingizwa Kaburini na kubashiriwa
kuhusiana na Moto, basi hua ni mwenye kumkumbuka Rafiki yake na kusema: ‘Ya Allah
Hakika mimi nna Rafiki yangu Fulani ambae alikua kila siku akinisihi kukuasi
wewe na Mtume wako Salallahu Alayhi wa Salam na kufanya Mambo maovu, na
hakunihimiza kuhusiana na mambo mema’
969
Hivyo Mpotoshe ili nae aadhibiwe kama nitakavyoadhibiwa mie, umkasirikie kama
unavyonikasirikia mie. Hivyo Rafiki huyo Fulani anapofariki basi hukutana na
Rafiki yake Muovu mwenzake na kusema Hakika wewe ni Rafiki Mbaya sana!.
Na ndio maana wakati Bilal Ibn Rabbah Radhi Allahu Anhu alipokua anataka kufariki
basi Mkewe alikua anataka kulia, hivyo Bilal Ibn Rabah Radhi Allahu Anhu akamwambia
Mke wake huyo kua: ‘Hakika mimi nna furaha hivyo Usilie bali furahia kuondoka
kwangu kwa sababu nitakua Pamoja na Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na
Masahaba zake waliotangulia Kabla yangu.’
Ambapo kwa upande wa Imam Said Ibn Al Musayyad basi yeye amesema kua: ‘Hakika
Mtu anapokufa basi hua ni mwenye kupokelewa na Mtoto wake aliefariki, kama
vile ambavyo anavyopokewa anapokua anarudi Nyumbani kutoka Vitani’
Na akasema Imam Abd Allah Ibn Mubarak kua: ‘Amesema Ayub Al Ansari Radhi
Allahu Anhu kua: Amali njema za watu walio hai Hua ni zenye kuwafikia habari
zake Maiti, na hivyo kama wakipata Habari nzuri basi nao hufurahika na wakipata
habari za Uasi basi huhuzunika na kuomba kua Allah amuongoze Mtu huyo.’
Kwani kasema Imam Said Ibn Jubayr kua: ‘Kwa hakika Watu waliofariki hua ni
wenye kupata habari za Watu waliokua hai. Kwani hakuna Mtu ambae Jamaa yake
amefariki na akawa hajapeleka Habari kuhusiana na Watu aliowaacha hai kwa
jamaa zake Waliofariki baada ya kukutana nao Kiroho Akhera’
Naam..na ndio Maana Abu Dardaa Radhi Allahu Anhu alikua akipenda sana kuomba Dua
isemayo: ‘Ya Allah hakika mimi naomba Ulinzi wako kutoka kwa maiti ambao
watawanyafanya Ndugu zangu waliotangulia Akhera kua ni wenye kuona aibu
kuhusiana na mimi.’
Subhana Allah! Sijui kama tunafahamiana ama la! Lakini kama hatujafahamiana basi
tuchukulie Mfano wa Mtu ambae anafiliwa na Ndugu yake wa Karibu, Kisha Mtu huyo
aliekua hai anapolala Usiku anamuota Ndugu yake huyo na kisha Kumpa maelezo kua
Nifanyie hivi na hivi na ukweli ni kua Tunapozungumzia kuhusiana na Ndoto basi
Ukimuota Maiti basi Ujue hua hasemi Uongo.
Hivyo kama kakuamrisha kitu kwenye Ndoto hio basi wajibu wako kukifanya kitu hicho
iwe kwa ajili yake au kwa ajili yako na kama amekukataza kitu basi inabidi uachane
nacho kitu hicho iwe kwa ajili yake au kwa ajili yako.
Na tuangalie mfano wa Imam Sufyan Ibn Uyaynah ambae ni mwalimu wa Mujaddid Ad
Din Imam Al Madhhab Al Shafii Imam Muhammad Idris Al Shafii siku moja alipolala
970
alimuona Mwalimu wake ambae ni Imam Sufyan Al Thawry ambae katika wakati huo
alikua ameshafariki na hivyo akamuuliza: ‘Ya Ath Thawry hivi jee ni Amali gani
ambayo imemfanya Allah Subhanah wa Ta’ala akupende?’
Imam Sufyan Ath Thawry akasema: ‘Kutokujua kitu juu ya Watu’ Imam Sufyan Ibn
Uyaynah akasema kumwambia Imam Sufyan Ath Thawry: ‘Naomba uniusie ewe Ath
Thawry!’ Imam Sufyan Ath Thawry akasema: ‘Kifanyie kazi hicho nilichokuambia’
Imam Sufyan Ibn Uyaynah akasema: ‘Allah Subhanah wa Ta’ala akuingize kwenye
Rehma zake ewe Ath Thawry, kwani huku kuna ndugu wengi wazuri na kila mmoja
mongoni mwao anaweza akamuombea mwenzake katika siku ya Malipo.’
Imam Sufyan Ath Thawry akasema: ‘Ya Ibn Uyaynah, hakika mimi sitaki kujuana
nawe tena kuanza leo. Hivi wewe umeshawahi kuona madhara yanayotokana na
mtu mwengine yeyote yule zaidi ya unaejuana nae? ’ Imam Sufyan Ibn Uyaynah
anaendelea kusema: ‘Hapo hapo mimi nikaamka kutoka usingizini huku nikiwa
nnalia kwa sauti.’
Kwani Miongoni mwa Masahaba basi walikuwepo Saab Ibn Jasama na Awf Ibn Malik
Radhi Allahu Anhum, hawa walikua ni Masahaba ambao walikua na Udugu wa Waislam
wa Madinah kuwapokea Waislam wa Makkah walipohamia Madinah na kugawana Mali
zao sawa kwa sawa.
Na hivyo wakaahidiana kua Udugu wao na Urafiki utaendelea hadi baada ya Kufariki
kwao. Ambapo Allah Subhanah wa Ta'ala akajaaliwa kua Saab Radhi Allahu Anhu kua
ni mwenye Kufariki mwanzo. Hivyo baada ya Saab Radhi Allahu Anhu kufariki basi Aws
Radhi Allahu Anhu alipolala akamuona Saab usingizini. Ambapo ndani ya Usingizi huo
ndotoni basi Saab Radhi Allahu Anhu alikua akimwambia Aws Radhi Allahu Anhu kua
Alhamd lillah Masuali aliyoulizwa Na Malaika ameyajibu kikamilifu
Awf Radhi Allahu Anhu akamuuliza Saab: ‘Mbona hapo kifuani una Doa Jeusi
ambalo ulikua huna ulipokua hai? imekuaje?’
Saab Radhi Allahu Anhu akasema: ‘Hakika mimi nilipofariki niliacha Deni, kwani
kuna Yahudi fulani ananidai Dirham 10, na Dirham zake sijawahi kumpa, zipo
sehemu fulani kampe’
Kisha Saab Radhi Allahu Anhu akaendelea kusema: ‘Halafu pia ya Aws fahamu kua
Binti yangu nae pia karibuni atanifuata huku Akhera, hivyo usihuzunike pale hili
pia litakapotokea’
971
Asubuhi ilipofika na Aws Radhi Allahu Anhu alipoamka basi akaenda Nyumbani kwa
Rafiki yake aliefariki yaani Saab Radhi Allahu Anhu, na akazikuta Dirham 10 katika
sehemu aliyofahamishwa kwenye Ndoto, hivyo akazichukua kisha akamfuata yule
Yahudi na kumuuloza kama anamjua Saab, na Yahudi akasema ndio kwani anamdai
Dirham 10. Hivyo Awf Radhi Allahu Anhu akamlipa Dirham hizo 10
Kwani amesema pia Imam Mujahid Ibn Sulayman kua: ‘Mtu aliefariki hua anapewa
Habari za Amali njema Amali njema anazofanya Mtoto wake baada ya Kufariki
kwake.’
Na kwa kua Maiti hua ni mwenye kupata habari Njema za Mema ya Mtoto wake aliehai
na pia Maovu ya Mtoto wake aliemuacha hai basi hii inatuonesha pia na inatufunza kua
haifai kabisa kua Muislam anapofariki basi Ndugu zake walio hai wakawa wanagombana
kwa sababu ya Mali alizowacha Marehemu, kwani Maiti wanapata Habari na Kuaibika
kutokana na Matendo hayo ya watu wao Walio hai.
Kwani Amir ul Muuminin Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu alikua kila akizungumzia
kuhusiana na Jahanama na akisimama pembeni ya Kaburi alikua akilia sana kiasi ya kua
hadi Ndevu zake hua ni zenye Kuroa kwa Machozi. Hivyo Masahaba wenzake
wakamuuliza: ‘Ya Amir ul Muuminin Mbona Ukizungumzia kuhusiana na Pepo hua
si Mwenye Kulia? Lakini Ukizungumzia kuhusiana na Moto na Kaburi hua ni
mwenye Kulia?’
Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu akajibu: ‘Kwa sababu amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Kaburi ndio hatua ya mwanzo ya kuingia Akhera,
hivyo yeyote yule atakaefuzu na kuokoka na Mitihani ya Kaburi, basi
kitakachofuatia baada yake huko Akhera kitakua ni chepesi sana kwake, na
asieokoka na Mitihani ya Kaburini basi bila ya shaka kitakachofuatia baaada yake
huko Akhera basi kitakua kibaya zaid na kwa Hakika mimi sijawahi kuona Kitu
chenye Matukio Mabaya kama Kaburi’’
Kwani Aya, Hadithi na Habari zinazothibitisha kuwepo kwa Uhai wa Kaburini baada ya
Mauti na Kaburi ziko nyingi sana ambazo ni zenye kutubainishia kua Jambo muhimu
zaidi kwetu sisi Waislam ni kujitayarisha na Kifo na Maisha yanayofuatia baada yake.
Kwani Kinachofariki na Kufufuliwa tena Upya hua ni Miili yenu na wala haiwi Roho
zetu.
Na hii ni kwa Sababu Roho hua zina Maumbile ya Kutokufa, bali hua na Maumbile ya
Kutolewa katika hali Moja ya Mazingira na Kuingizwa katika hali nyengine. Yaani kama
tulivyosema kua Roho zetu zilikubali kuchukua Amanah Kutoka kwa Mola wetu, na
zikala Kiapo na Kuthibitisha kua Allah Subhanah wa Ta'ala ndie Mola wetu.
972
Roho zetu ndio zilizokua hai Miaka yote hio huku zikisubiri wakati wake wa kuingia
kwenye hali ya Manii ya Mababa zetu na kisha kuingia kwenye Matumbo ya Mama zetu
kwa ajili ya Kuvaliwa na Miili yetu itakayotuwezesha kuja Kuishi katika mazingira yetu
Ulimwenguni. Hivyo Mda wa kuishi unapomalizika basi inabidi tuhame kwenye
Maumbile ya Mazingira ya Ulimwenguni na kurudi Akhera kurudisha Amanah kwa
Muumba wetu aliyotukabidhi baada ya kutuumba.
Hivyo tunapotoka Ulimwenguni basi inabidi tuyavue Mavazi ya Ulimwenguni ambayo
ni Miili yetu yenye kuonekana na yenye kua na uwezo wa Kuoza. Kwa ajili ya Kuingia
kwenye Maisha yanayofuata ambayo unapatiwa Maumbile ya Mwili Mpya ambao Ubora
wake hua unategemeana na namna Ulivyoishi hapa Ulimwenguni kabla ya Kuyavua
Mavazi ya Mwili uliokuwezesha kuishi Duniani.
Kama Uliishia kwa Kuisimamia Ipasavyo Amanah Uliyokabidhiwa na Mola wako, basi
Utaepukana na Mitihani ya Kaburini na Utafurahia Akhera yako. Na kama uliishi kwa
kutoijali na kutoisimamia Amanah yako Amanah yako uliyokabidhiwa na Mola wako
basi Utafeli Mitihani ya Kaburini na Utaijutia Akhera yako.
Kwani Roho na Mwili hua ni sawa na Balbu ya Umeme. Roho ni Umeme na Balbu ni
Mwili. Hivyo Inapoungua Balbu basi hua haimaanishi kua Umeme kwenye Waya
hakuna, kwa sababu Umeme ni Kama Roho haionekani. Hivyo Roho inakuwepo kwa
Allah Subhanah wa Ta’ala na inalipwa malipo ya amali ulizokua unazifanya kama mbaya
basi malipo mabaya na kama nzuri basi malipo mazuri, hivyo ijali Balbu yako kwa
kufanya amali njema kabla Haijaungua kwani Umeme wa Muumba Haukatiki na
unakuwepo katika mazingira stahiki na wakati stahiki.
Tunapoagalia Lugha ya Kiarabu basi tunaona kua Neno Sabaha ambalo hua ni Jina la
Mtu Mwanamke hua linamaanisha kipindi cha wakati Unaochomoza Jua yaani Asubuhi.
Ambapo kwa Upande Mwengine basi Wakati huu pia hua unajulikana kama Ghuduwan.
Neno Ghuduwan linatokana na neno Ghada ambalo kwa lugha ya Kiarabu hua
linamaanisha Kuenda, Kuendeleza, Kutoka, Kufanya Kitu katka wakati wa Asubuhi,
Wakati ulopo au wakati wowote. Neno Ghada pia limelotoa neno Ghadan ambalo hua
linamaanisha Kesho. Na pia Likatoa neno Ghadaun ambalo hua linamaanisha Chakula
cha Asubuhi.
Naam..hio ni kuhusiana na wakati wa Asubuhi yaani Sabaha au Ghuduwwan. Ambapo
kwa upande mwengine basi neno A'asha ambalo pia hua ni Jina la Mtu Mwanamke yaani
Asha, hua limetokana na neno A'asha ambalo hua linamaanisha Kipindi Cha wakati wa
Siku ambacho hua ni chenye Kuanza Mara baada ya Kuzama Jua na Kuingia Kiza
ambacho pia ndio wakati ulitoa jina la Sala ya Isha.
973
Na tunaangalia na kufahamishana kuhusiana na Nyakati hizi kwa sababu Tuko katika
kukumbushana kuhusiana na Mauti na Hali inavyokua Mara baada ya kuingia kwenye
Barzakh au Kaburini.
Ambapo anasema Allah Subhanah wa Ta'ala katika aya iliyotumia maneno tuliyaanza
nayo kuyaangalia maana zake ambayo ni Ghuduwwan yaani Asubuhi, Wakati wa
Mapambazuko ya Jua na A’ashiyyan yaani wakati wa Isha kinapoingia Kiza kuhusiana
na Watu waovu kua:
﴿ٱلن َّارُ يُعْرَضُونَ عَلَيْهَا غُدُوّاً وَعَشِ يّاً وَيَوْمَ تَقُومُ ٱلس َّاعَةُ أَدْخِ لُو ۤ اْ آلَ فِرْعَوْنَ أَشَ َّد
ٱلْعَذَابِ ﴾
Alnnaru yuAAradoona AAalayha ghuduwwan waAAashiyyan wayawma taqoomu
alssaAAatu adkhiloo ala firAAawna ashadda alAAadhabi (Surat Al Ghafir 40:46)
Tafsir: Moto ambao Wanapambanishwa Nao (Wakati wakiwa Makaburini) Asubuhi
Kunapopambazuka na Usiku Kinapoingia kiza, Na Itakapofika Saa ya Siku ya Malipo
(Wataambiwa Malaika) Waingizeni Kina Fir'awn katika Adhabu Kali
Ambapo ingawa baadhi wanaweza kusema kua hii aya ni yenye kuwazungumzia kina
Fir'awn na Watu wake na bila ya shaka hawajakosea, lakini kwa Upande mwengine basi
wanasema Mujaddid Ad Din Sultan Al Mutakallimin, Imam Al Mushakikin Imam Fakhr
Ad Din Al Razi, na pia Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari kua:
‘Aya hii ni Miongoni mwa aya zenye Kuthibitisha kuhusiana na Maisha ya Barzakh
yaani Ndani ya Kaburi hususan kuhusiana na maneno Ghuduwwan waA’ashiyan
Yaani Asubuhi na Usiku kua Katika Makaburi Hakutokua na Jahannama Bali
kutakua Na Adhabu ya Moto wa Jahannam Asubuhi na Jioni, Kwani Jahannam
yenyewe hua ni katika Siku ya Malipo ambapo itakua ni Adhabu ya Kudumu’
Hivyo Aya inatuwekea wazi kua kwa watu waovu basi baada ya kuingia Kaburini basi
hua Kuna Adhabu ya Moto ambayo hua inarudiwa Kila Masaa 12 yaani Asubuhi na Jioni.
Ambapo amesema Abd Allah Ibn Masud Radhi Allahu Anhu kua: Amesema Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam kua: ‘Waliokufa hua wanaadhibiwa Makaburini Mwao
na hata Wanyama hua wansikia sauti zao’ Na akasema tena Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Ummah huu utapata Mtihani wa Ndani ya Makaburi. Hivyo
kma mimi sikua ni mwenye kuogopa kua nyinyi mtaingiwa na Khofu ya Kuwazika
974
watu wenu. Bas nngekuombeeni kwa Allah Subhanah wa Ta’ala mkawa na uwezo
wa kusikia ninayoyasikia mimi.’(Musnad Imam Hanbal)
Kwani alisema Amr Ibn Dinar kua: ‘Kuna Dada wa Mmoja kati ya Watu wa Madinah
alifariki nasi tukamzika lakini ndugu yake aliporudi baada ya kuzika basi
akakumbuka kua amedondosha kitu chake Kaburini hivyo akaomba msaada kwa
mmoja kati ya Marafiki zake ili aende akamsaidie Kufukua Kaburi ili akitoe kitu
chake hicho kilichomdondoka. Hivyo wakaenda na Kufukua na mara akaiona kitu
chake hicho, akakichukua lakini akamwambia Rafiki yake huyo, kua Wacha
tuendelee Kufukua ili tupate kuona hali yake Dada yangu ikoje baada ya Kumzika.
Wakafukua hadi kwenye Mwana wa ndani na mara wakakutana na Moto, hivyo
wakafunika na kufukia kwa khofu, Kisha wakarudi Nyumbani walipofika
Nyumbani Kaka mtu akaulizwa kuhusiana na Dada yake.
Nae akajibu: ‘Kwanini Mnamuulizia wakati ni Mtu ambae ameshafariki?’
Akaambiwa ‘Sema kwani tumesikia kua ulienda kufukua’.
Akasema ‘Niambieni kwani alikua akifanya nini?
Hivyo akaambiwa: ‘Alikua akichelewasha Sala zake, na pia alikua anapenda
kusikiliza maneno ya watu na kuyasambaza.’
Na anasema Mujaddid Ad Din Shaykh Ul Islam Imam Abd Rahman Al Suyuti kua:
‘Hadith zinazozungumzia Adhabu ya Kaburi ziko Nyingi sana kiasi ya kua
zimefikia hali ya Kua zimefikia hali ya kua ni zenye kuthibitisha Uhakika wa
kuwepo kwake, kwani zimenukuliwa na Masahaba wengi sana’
Na akasema Imam Al Mufasir Abu Abd Allah Muhammad Al Qurtubi kua: ‘Kuamini
kuhusiana na Adhabu ya Kaburi na Mitihani yake Ni Wajib na Kudhibitisha ni
Wajibu’
Na ingawa tumeona katika aya na hadith kua kuna Watu wataadhibiwa kwa kupata
Adhabu za Milele hadi katika siku ya Kufufuliwa.
Lakini kwa upande mwengine basi tunapoiangalia Qur'an basi tunaona kua anasema
Allah Subhanah wa TaAla kua kuna watu watasema katika Siku ya Kufufuliwa kua:
﴿قَالُواْ يٰوَيْلَنَا مَن بَعَثَنَا مِن م َّرْقَدَِ هَذَا مَا وَعَدَ ٱلر َّحمْ ٰنُ وَصَدَقَ ٱلْمُرْسَلُونَ ﴾
975
Qaloo ya waylana man baAAathana min marqadina hadha ma waAAada
alrrahmanu wasadaqa almursaloona(Surat Yasin 36:52)
Tafsir: Watasema Ole Wetu ni Nani alietufufua kutoka katika Usingizi wetu
(Wataambiwa kua) Haya Ndio aliyoyaahidi Mwingi wa Rehma na Wakasadikisha
Mitume.
Ambapo Aya hii inatuonesha kua Hawa Watakaojuta watakua ni waliofanya Maovu, na
aya inaonesha kua Walikua Wamelela Hivi Jee walipumzishwa au?
Kwani Neno Ruqud kwa Lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kulala, Kusinzia, Kua
Mregevu, Kua na hali ya Uchovu, Kua na Muonekano wa Mtu ambae ndie kwanza
ameamka hata uso hajanawa.
Neno Ruqud limetumika pia kwenye kisa cha As-hab Al Kahf pale Allah Subhanah wa
Ta'ala alipomwambia Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kuhusiana na watu wa Ashab
Al Kahf walivyokua wamelala kwa kusema:
﴿وَتحَْسَبُهُمْ أَيْقَاظاً وَهُمْ رُقُودٌ وَنُقَلِّبُهُمْ ذَاتَ ٱليَمِينِ وَذَاتَ ٱلشِّ مَ الِ وَكَلْبُهُمْ ابَسِ طٌ
ذِرَاعَيْهِ بِٱلوَصِيدِ
لَوِ ٱط َّلَعْتَ عَلَيْهِمْ لَوَ ل َّيْتَ مِنْهُمْ فِرَاراً وَلَمُلِئْ تَ مِنْهُمْ رُعْباً ﴾
Watahsabuhum ayqadhan wahum ruqoodun wanuqallibuhum dhata alyameeni
wadhata alshshimali wakalbuhum basitun dhiraAAayhi bialwaseedi lawi
ittalaAAta AAalayhim lawallayta minhum firaran walamuli/ta minhum
ruAAban(Surat Al Kahf 18:18)
Tafsir: (Kama ungewaona) Ungewadhania kua Wako Macho, wakati wakiwa
Wamelela, nasi tulikua tukiwageuza katika upande wa kulia kwao na kushoto kwao,
huku Mbwa wao akiwa amenyoosha miguu yake kwenye mlango (wa kuingilia Pango
hilo) kama ungewaona basi bila ya shaka ungegeuka na kukimbia kutokana nao na
ungeshangazwa nao.
Yaani kama Rasul Salallahu Alayhi wa Salam, au pia kama mimi na wewe tunaosoma
Qur'an tungewaona Watu hao walivyokua Ruqudun (Wamelala Usingizi) basi
tungedhania kua Wako macho, huku Mbwa wao akiwa amelala kwenye mlango wa
Pango hilo, na bila ya shaka tungekimbia kutokana na muonekano wao unaoshangaza,
Hivyo hapa tunaoneshana wa neno Raqada kwa Sababu neno hili ndio lililotoa neno
976
Marqad, ambalo hua linamaanisha Kitanda au Sehemu ya Kulalia iwe kwa Mtu alie hai
au aliefariki.
Ambapo kuhusiana na Aya yetu hii ya Surat Yasin 36:52 basi nayo pia imetumia neno
Raqada katika hali ya Marqadina yaani Malazi au Vitanda vyetu vya kupumzikia basi
anasema Abu Hurayrah Radhi Allahu Anhu kua: ‘Amesema Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kua: ‘Baina ya Kupulizwa Baragumu kutakua na kipindi cha
Arubaini Abu Hurayra Radhi Allahu Anhu akamuuliza Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam kwa kusema kua: Ya Rasul Allah hivi Unamaanisha Arubaini
MaSiku au?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Siwezi kusema chochote zaid’
Masahaba Wakauliza: ‘Unamaanisha Arubaini miezi?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘La siwezi kusema’
Masahaba wakauliza: ‘Arubaini Miaka?’
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema: ‘Siwezi kusema chochote, lakini
baada ya hapo Allah atajaalia Maji kushuka kutoka Mbinguni na kisha Watu
watachipua kama inavyochipua Mimea, kwani ni kitu kimoja tu cha Ibn Adam
ambacho hakitooza ambacho ni kimfupa kidogo cha mwisho cha Uti wa mgongo,
ambacho ndicho kitakachochipua Ibn Adam kutokana nacho katika Siku ya
Malipo’ (Sahih Muslim)
Naam..hii ni hadith ambayo inatuelezea kuhusiana na tukio la Kupulizwa kwa Baragumu
mara 2 yaani katika siku ya Kiama. Ambapo anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas
Radhi Allahu Anhu, na Ubay Ibn Kaab Radhi Allahu Anhu kua: ‘Baragumu litapulizwa
mara mbili, ambapo litakapopulizwa mara ya kwanza basi adhabu za Kaburi
zitasitishwa na hivyo Watu watalala usingizi hadi litakapopigwa kwa mara ya pili
ndio watu wataamka na kutakua na kpindi cha miaka arubaini baina yake’
Kutokana na Hali hio basi wale waliolala watasema Ya Waylana Ma Baathana Min
Marqadina (Surat Yasin 36:52)
Ama kwa Upande wa Mujaddid Ad Din Imam Fakhr Ad Din Al Razi basi yeye anasema
kuhusiana na aya hii kua: Maneno haya yanamaanisha kua: ‘Watu hao watasema Jee
ni Nani alietuamsha kutoka katika Sehemu zetu za Kulalia na Mapumziko? Yaani
watakua ni wenye kujiuliza Jee ni Allah Subhanah wa Ta'ala ndio Ametufufua au
Tumeamshwa kutoka Usingizini? Na hivyo hii inamaanisha kua watu hawa
977
hawatokua na Uhakika kama walikua wamelala na kuamshwa au kua walikua
wamekufa kisha wakafufuliwa’
Na kuna hadith kadhaa za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salan zinazohimiza
kuwaombea Dua Maiti wetu, kuwatolea Sadaqat Al Jariah n.k. Na hii ni kwa sababu
unavyofanya hivyo basi hua inawasaidia kuwapunguzia Adhabu za Kaburi Maiti hao. Na
pia kufanya kwetu huko hua pia ni sehemu ya sisi pia kuja kufanyiwa hivyo na Vizazi
vyetu katika wakati ambao tutakua tunahihitaji msaada kutoka kwao wao ndugu zetu hao
waliohai.
Na kuhusiana na haya basi Imam Abd Allah Ibn Muhammad Ibn Abi Duniya ambae yeye
amesema Imam Ibn Abi Duniya kua: ‘Abu Ubayd Ibn Buhayr aliniambia mimi kua:
Rafiki yangu aliniambia kua: Hakika mimi nilimuona usingizi Ndugu yangu baada
ya kufariki kwake Hivyo nikamwambia, Nakuombea kua Dua zetu zikufikie, nae
akajibu Naam Allah Subhanah wa Ta'ala anatumurika na Nuru ya Dua hizo.’
Imam Abd Allah Ibn Muhammad Ibn Abi Duniya anaendelea kutuambia kua: ‘Amesema
Bashar Ibn Ghalib kua, hakika mimi nilimuona Ndugu yangu kwenye Ndoto ambae
nilikua nikimuombea Dua sana baada ya Kufariki kwake, Nilipomuona usingizini
akaniambia kua Ewe Bashir hakika ya zawadi zako hua zinatufikia zikiwa kwenye
Sahani iliyojaa Nuru yenye Vitambaa vya hariri’
Nami nikamuuliza: ‘Imekuaje?’
Nae akasema: ‘Hua tunapokea Dua kutoka kwa Waumini waliohai pale
wanapowaombea wale waliofariki, hivyo wakiwaombea basi hua zinajibiwa na
Allah Subhanah wa Ta'ala na kisha zinawekwa kwenye Sahani za Nuru na
kupelekewa yule alieombewa kwa jina lake na kuambiwa kua Maombezi yako haya
yametoka kwa fulani ibn Fulani’.
Kuna mtu alikua anampenda sana Rabia Al Adawiyyah na hivyo alkua anapenda
sana kumuombea Dua. Hivo siku moja alpoalala akamuona usingizini akiwa na
tabasam na kumwambia kua: ‘Zawadi zako hua tnaletewa zikiwa kwenye Sahani
iliyojaa Nuru na zenyewe zikiwa zimejaa Nuru.’’
Hivyo kutokana na vithibitisho hivyo basi tunaona kua Kuna baadhi ya Adhabu za
Kaburini hua zinasitishwa kutokana na Maombi ya Waumini juu ya Waumini. Na
tunapozungumzia Waumini basi hua tunamaanisha Kila Waislam wakisoma Dua au
wakisoma Quran ambayo ndani yake mna aya zenye Kuwaombea Waislam waliotangulia
basi Dua na aya hizo hua zinawanufaisha Maiti hao, kama alivyosema Allah Subhanah
wa Ta'ala kua:
978
﴿وَ ٱل َّذِينَ جَآءُوا مِن بَعْدِهِمْ يَقُولُونَ رَب َّنَا ٱغْفِرْ لَنَا وَلإِخْوَانِنَا ٱل َّذِينَ سَبَقُوَ بِ ٱلإِيمَانِ
وَلاَ تجَْعَلْ فىِ قُلُوبِنَا غِلاًّ لِّل َّذِينَ آمَنُواْ رَب َّنَآ إِن َّكَ رَءُوفٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
Waalladheena jaoo min baAAdihim yaqooloona rabbana ighfir lana waliikhwanina
alladheena sabaqoona bial-eemani wala tajAAal fee quloobina ghillan
lilladheena amanoo rabbana innaka raoofun raheemun(Surat Al Hashr 59:10)
Tafsir: Na Wale waliokuja baada yao Wakasema Ewe Mola wetu Tusamehe sisi Na
Ndugu zetu waliotutangulia kwenye Imani ya Dini ya Kiislam Na Wala Usijaalie
kwenye Nyoyo zetu kinyongo na Chuki dhidi ya Walioamini wenzetu, Kwani ewe Mola
wetu Hakika wewe ni Mwingi wa Ukarimu na Huruma
Ambapo kwa Upande mwengine basi anasema Mujaddid Ad Din Imam Shihab Ad Din
Abd Fadhl Ibn Hajar Al Asqallani kua: ‘Adhabu ya Kaburi hua ni ya Kudumu pale
mtu anapokua ni Kafiri au Mnafiq. Ama kuhusiana na Muislam mwenye
Madhambi basi hali yake hua inategemea na madhambi yake, kwani kuna makosa
yanayosamehewa, kuna makosa yasiyosamehewa, kuna makosa yanayoendelea
adhabu zake kwa mda mrefu na kuna makosa yatakayositishwa adhabu zake.’
Ambapo tumeona kuhusiana na vithibisho vya kuwepo kwa adhabu za Kaburini na pia
Kusimamishwa kwa Adhabu kutokana na msaada wa Waumini walio hai wanaoufanya
kwa ajili ya kuwasaidia waliotangulia mbele ya Mola wao ambao wao hua hawana uwezo
tena wa kuyafanya mambo mema hayo na hivyo kututia ari ya kua ni wenye kutakiwa
kukumbukana na kupendana si tu katika wakato wa uhai wetu bali pia katika wakati wa
baada ya Kufariki kwetu baina yetu.
Na tunapoangalia kwa upande wa mifano ya Hadith za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa
Salam, basi tunaona ile hadith ya Sahaba aitwae Sad Ibn Ubaidah Radhi Allahu Anhu
ambae yeye alifiliwa na Mama yake. Ambapo baada ya kumzika na mda kidogo kupita
basi siku moja Saad Radhi Allahu Anhu alimfuata Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
na kumwambia: ‘Ya Rasul Allah, hakika Ummu Saad ameshafariki, hivi jee nimtolee
Sadaqa gani?’
Ambapo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam akasema kumwambia Saad Radhi
Allahu Anhu kua: ‘Sadaqa bora ni Maji’
979
Hivyo Saad Radhi Allahu Anhu akachimba Kisima na kisha akatangazia kua: Hiki ni
kisima cha Maji cha Ummu Saad (Imam An Nasai, Imam Abu Daud, Imqm Ibn Majah
na Musnad Imam Ahmad)
Kwani Amesema Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu kua: ‘ Kila mara Rasul Allahi
Salallahu Alayhi wa Salam alipomaliza kumzika Mtu yeyote yule basi alikua
akisimama Pembeni ya Kaburi na kisha alikua akisema: Ninachokuombeni hivi
sasa Nyote kua ni wenye kumuomba Allah Subhanah wa Ta'ala kumpa Msimamo
Thabit, Maiti huyu kwani sasa hivi yuko Katika hali ya Kuhojiwa’
Ambapo haya yote yanatuonesha kua:
Maiti hua anasikia Manemo ya Mtu aliehai.
Maiti hua anaulizwa Kaburini.
Ni halali na hakuna Ubaya wowote Kumuomba Allah Subhanah wa Ta'ala
amsamehe Maiti mara tu baada ya kuzikwa na kumpa Msimamo Thabit Maiti huyo
katika wakati wa kuhojiwa na Malaika wawili Kaburini.
Inakukubalika Kufanya Jambo la Kheri kwa ajili ya Mtu alietangulia Akhera, iwe
Kumtolea Sadaqa, kwa kumchimbia Kisima, Kumjengea Msikiti, n.k Kumuombea
Dua, Kumuombea Msamaha, Kusoma Qur'an kwa nia ya kua Allah Subhanah wa
Ta'ala amfikishie malipo ya kisomo hicho yamfikie Maiti wako au Maiti wote wa
Kiislam.
Kwani kweli Amesema Allah Subhanah wa Ta'ala amesema kua:
﴿وَأَن ل َّيْسَ لِلإِنسَانِ إِلا َّ مَا سَعَى ٰ ﴾
Waan laysa lil-insani illa ma saAAa (Surat An Najm 53:39)
Tafsir: Na Hana Mtu (Malipo) isipokua juu ya kile alichokifanya.
Ambapo maana ya aya hii ni kua Hatopata Mtu malpo isipokua juu ya lile alilolifanya
Mtu huyo iwe zuri au ovu. Hivyo aya hii inamzungumzia Mtu kama Mtu na amali zake
kua hatodhulumiwa alichokifanya iwe chema au kiovu bali atalipwa ipasavyo.
980
Na maana ya Aya na Hadith za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam tulizoziangalia
basi ni kua: Muislam aliefariki anapofanyiwa mema na Mrithi wake au Muislam
mwenzake au na Waislam wenzake waliokua hai basi malipo hayo humfikia Maiti
huyo, kwani jema hilo hua hakufanya mwenyewe bali amefanyiwa kwa ajili yake.
Hii hua pia ni Sawa na Pale Maiti anapodaiwa kisha watu wakaulizwa wanaomdai
na wanaodaiwa nae ili Maiti ili walipe au walipwe.
Kwani amesema Imam Ahmad Ibn Hanbal kua: ‘Mnapoingia Makaburini someni Ayat
ul Qursy mara 3, Surat Ikhlas mara Moja halafu semeni: Ya Allah Ya Rahim hizi ni
kwa ajili ya Watu wa Makaburini’
Na akasema Hujjat Ul Islami Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn
Muhammad Al Ghazali kua: ‘Mnapoingia Makaburini Someni Surat Al Fatiha na
Surat Nas na Surat Al Falaq na Surat Al Ikhlas kisha semeni: Allahu La Ilaha Illa
Huwa, Ya Rahim hizi ni kwa ajili ya watu wa Makaburini’
Ambapo hapa inabidi tukumbuke kua hili ni jambo rahisi sana na la kujipatia Thawabu
za bure tena za kumwaga kwa sababu kwa kila harufi ya Qur'an utakayoisoma kisha
ukaitoa Sadaqa kwa Maiti waliozikwa Makaburi basi wewe unalipwa 10 bila ya
kuwapunguzia wao. Ambapo ayat Kursiy ina herufi 170 mara 10 hua ni 1700..sasa
Tafakkar makaburini hapo kuna maiti wangapi waliozikwa tangu miaka na miaka?
Naam..Hivyo, tusisahau Sadaqat Jarriyah, Kuwaombea Dua Maiti wetu, Kujidhibiti
Nafsi zetu ili tusiwe na Dhambi zenye kutudumisha kwenye Adhabu, bali tuwe ni wenye
kushikamana na Qur’an.
KUHIFADHIWA NA KURAHISISHWA KWA QUR’AN.
Mnamo Mwezi 11 Shawwal wa mwaka 11 Al Hijra Waislam wakiwa chini ya Uongozi
wa Amir ul Muumin Sayyidna Abu Bakr As Siddiq Radhi Allahu Anhu basi Jeshi la
Waislam lilikokuwa chini ya Uongozi wa Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu liliingia
vitani kupigana dhidi ya watu waliokua wakijiita kua Mitume walioibuka baada ya
kufariki Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam. Ambapo mmoja kati ya watu hawa
alikuwepo aliekua akiitwa Musalima Al Kadhaab ambae alikua na Jeshi kubwa sana.
Hivyo Khalid Ibn Walid Radhi Allahu Anhu akawaongoza Waislam walio chini yake na
kufanikiwa kuliteketeza jeshi la watu 21000 la Musalimah na pia kufanikiwa kumuua
Musalimah mwenyewe. Hivyo ingawa Waislam walishinda lakini na wao walipoteza
wanajeshi 1200 ambapo wengi ndani yao walikua 70 ambao ni wale waliohifadhi Qur'an.
981
Na ingawa Waislam walishinda lakini tukio hili la kufariki kwa wengi miongoni mwa
waliohifadhi Qur'an lilimshtua sana Umar Ibn Khattab Radhi Allahu Anhu, hivyo
akamwambia Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu kua, yeye anakhofu kua ikitokea
tena hali kama hio basi huenda Qur'an ikatoweka.
Hivyo bora Qur'an ikusanywe yote kwenye sehemu moja, yaani kwenye Mas-haf. Wazo
hili lilimshtua pia Abu Bakar Radhi Allahu Anhu kwani hakuwahi kumsikia Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akiwa na wazo hilo, hivyo nae akasita kufanya hivyo.
Kwani akifanya basi itakua tayari imeshakua ni Bidaa, kwa sababu Rasul Allah Salallahu
Alayhi wa Salam hakufanya hivyo. Lakini Allah Subhanah wa Ta'ala akamtulia wepesi
Moyo wa Abu Baqr As Siddiq Radhi Allahu Anhu nae akaona kua kuna kweli haja ya
kufanya hivyo.
Na ingawa kulikua na Khalifa ambae ni Abu Baqr Radhi Allahu Anhu na msaidizi wake
ambae ni Umar Ibn Al Khattan katika Mji wa Madinah Lakini Mji huo ulikua na Qadhi
Mkuu wa Mji wa Madinah ambae ni Sahaba mwanazuoni aitwae Zayd Ibn Thabit Radhi
Allahu Anhu.
Hivyo Abu Bakr Radhi Allahu Anhu na Umar Ibn Al Khattab Radhi Allahu Anhu
wakalifikisha shauri lao hilo kwa Qadhi Zayd Ibn Thabit Radhi Allahu Anhu ambae nae
akagoma.
Kwani nae aliona kua hawezi kufanya lile ambalo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
hakulifanya, kiasi ya kwamba alisema kua kwake yeye bora aambiwe auhamishe Mlima
wa Uhud kuliko kuambia aikusanye Qur'an katika sehemu moja.
Lakini hata hivyo Abu Baqr Radhi Allahu Anhu na Umar Ibn Al Khattab wakaweka wazi
sababu zao na kusema kua hilo ni jambo jema kufanywa kwani lina manufaa. Hivyo Zayd
Ibn Thabit Radhi Allahu Anhu akakubalina nalo jambo hilo Na hivyo Qur'an
ikakusanywa juzuu 30 katika kitabu kimoja kwa mara ya kwanza na ndio ambayo
tunayoisoma leo Waislam.
Na amesema Imam Abu Sulayman Al Khattabi kua: ‘Imam Abu Amr Ibn Al A’ala
amesema kua: ‘Lugha ya Qur’an iliyoshushiwa ilikua ni lugha ambayo Waarabu
walikua wakiizungumza katika wakati wa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam,
na hivyo h ni lugha tofauti na yetu sisi leo hii, na wale waliokua ni mabingwa wa
Lugha hio wametoweka kwa mda mrefu.’’
Kwani katika kipindi cha Khalifa Abu Bakr Radhi Allahu Anhu na kipindi cha Umar Ibn
Al Khattab Radhi Allahu Anhu basi Qur'an ilikua inasomwa katika Lafdhi 7 tofauti.
982
Hivyo siku moja katika kipindi cha Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu basi Sahaba
Hudhayfah Ibn Yaman Radhi Allahu Anhu baada ya kutoka katika Vita vya Jihad basi
alienda moja kwa moja mpaka kwa Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu na
kumwambia, kua ‘Inashangaza kua kila anakopita katika Miji aliyoenda basi
anakuta Waislam wanasoma Qur'an kwa Lafdhi zao, na hakuna hata mmoja
anaefaham lafdhi ya Mwenzake’
Kwani watu wa Basra wanasoma kivyao, Watu wa Syria wanasoma kivayo, Wayemen
kivyao.n.k Hivyo basi Hudhayfah aIbn Al Yaman Radhi Allahu Anhu kamwambia
Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu kua kutokana na hali hii basi bora Qur'an iwe
inasomwa katika Lafdhi moja tu ya Kiarabu cha Quraysh.
Hivyo Sayyidna Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu akaona kweli Hili ni Jambo Sahih,
hivyo hakuzibatilisha Lafdhi nyengine zote hizo bali alisema kua Qur'an isomwe kwa
lafdhi ya Kikureish yaani ndio iwe Lafdhi ya Umoja wa Kimataifa wa Qur'an.
Naam, hayo ni miongoni mwa matukio makubwa yaliyotokea kuhisiana na uhifadhiwaji
wa Qur'an baada ya kufariki Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam na ndio ambayo
yalifanyika ndani ya kipindi cha Makhalifa wanne wa Kiislam yaani Abu Bakar As
Siddiq, Umar Ibn Al Khattab, Uthman Ibn Affan na Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu
Anhum. Ambapo kwa kipindi chote hicho basi Qur'an ilikua inasomwa lakini haijatiwa
Harkah yaani Fat-ha, Kisra, Shadda, Dhuma na Sekn.
Na Alhamdlillah kua Masahaba waliyafanya yote haya kwa ajili yetu sisi mimi na wewe
ili Itufikie Qur'an pamoja na Vizazi vyetu na hivyo Masahaba hao kua ni wenye kufanya
yale ambayo Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam hakuwahi kuyafanya na kisharia
haya yote waliyoyafanya yalikua ni mambo ambayo waliyaanzisha wao wenyewe na
hivyo ingawa inakua ni Bidaa lakini hata hivyo ni kwa manufaa yetu sote, kwa hivyo hii
inakua ni Bidaa nzuri yenye manufaa.
Kwa sababu kama isingefanywa basi sijui mimi nawe Waislam wa leo tungekua na hali
gani na Qur'an yetu kwani imekusanywa pamoja tu na hatuiihifadhi Nyoyoni jee ingekua
ipo kama ilivyokua katika wakati wa Nabi Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam
ingekuaje? hivyo makusudi nimeanza kwa Masahaba kuhusiana na Qur'an kwa sababu
nataka tufahamiane kama inavyotakiwa tujue na pia inavyotakiwa tufaham.
Kwani anasema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al
Ansari Al Qurtubi kua: ‘Ama kuhusiana na Harkah (Hamza, Sukn, Shadda, Dhuma,
na Kisra) na Vidoto vyake Qur'an, Basi Wanasema Wanazuoni kua alikua ni
Khalifa Abdul Malik Ibn Marwan ambae ndie alieamrisha Viongezwe vitu hivyo.
983
Na Kazi hio ilifanywa na Hajjaj Ibn Yusuf alipokua katika Mji wa Al Wasit Nchini
Iraq, ambae ndie alieisimamia, na akamuamrisha Al Hasan na Yahya Ibn Ya'mur
kufanya Hivyo
Ambapo Muhammad Ibn Sirin alikua na Mas-haf ambayo iliongezewa hivyo na
Yahya Ibn Ya'mur.’
Ambapo tunapomzungumzia Hajjaj Ibn Yusuf ambaea alikau ni Kiongozi katili sana
katika kusimamia Maslahi ya Khalifa Abdul Malik Ibn Marwan ambao ni Utawala wa
Kiislam wa Banu Ummayah uliokua wenye Makao makuu yao Mjini Damascus nchini
Syria ambapo mnamo mwaka 86 Al Hijra Abdul Malik Ibn Marwan Alifariki Dunia na
pia ndio mwaka ambao Khaifa Umar Ibn Abdul Aziz Ibn Marwan alikua Gavana wa Mji
wa Madina na katika wakati wa mwaka huu basi Imam basi Imam Jabir Ibn Zayd wa
Ibadhi alikua na umri wa miaka 66, Imama Abu Hanifa alikua na miaka 6 na Imam Jafar
As Sadiq pia.
Wakati Imam Malik alizaliwa miaka 7 baadae, na kwa upande wa Imam Muhammad
Idris Al Shafii na Imam Ahmad Ibn Hanbal nao ndio hata mababa zao hawajazaliwa.
Hivyo Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al
Qurtubi anaendelea kutuambia kua: ‘Ama kuhusiana na idadi ya Herufi zake na
Juzuu basi amesema Salam Al Himani kua: Al Hajjaj Ibn Yusuf aliwakusanya
Wasomaji wa Qur'an, Waliohifadhi na Waandishi na Kuwahoji, kwa kusema jee
katika Qur'an mna Herufi ngapi?
Nami nilikuwemo kwenye wenye Kuulizwa hivyo tukazihesabu na kukubaliana kua
Qur'an ina herufi 340,740 Kisha Hajjaj Ibn Yusuf akaniuliza Jee ni Herufi Gani
inamalizia Sehemu ya Mwanzo ya Katikati ya Qur'an nami nikasema ni katika
Surat Al Kahf katika herufi Fe ya neno Walyatallataf :
Walyatallataf (Surat Al Kahf 18:19)
﴿وَلْيَتَلَط َّفْ ﴾
Tafsir: Na wacha awe Makini kwa ukarimu.
Ambapo neno hili lina herufi 7, na herufi Waw,Lam,Ya na Ta ziko katika nusu ya
kwanza ya Qur’an na herufi Lam,Tta na Fa ziko kwenye nusu ya pili ya Qur’an.
984
Akaniuliza Niambie kuhusiana na Sehemu zake 3 nasi tukamwambia inaanzia
mwanzoni mwa Surat Tawba 9:10, ya pili mwanzoni mwa Surat Ash Shuara 26:100
na ya tatu ni kuanzia hapo mpaka mwisho wa Qur'an.
Salam Al Himani anaendelea kusema kua: Hakika sisi tuliifanya kazi hii kwa mda
wa miezi minne na kila siku Usiku Al Hajjaj Ibn Yusuf alikua anakuja na tunasoma
Robo yake
Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi
anatuelezea pia mitizamo myengine ambayo ni kua: ‘Ama kuhusiana na Harkah
(Hamza, Sukn, Shadda, Dhuma, na Kisra) na Vidoto vyake Qur'an basi Wanasema
Wanazuoni kua alikua ni Abdul Malik Ibn Marwan ambae ndie alieamrisha
Viongezwe vitu hivyo, Na Kazi hio ilifanywa na Hajjaj Ibn Yusuf alipokua katika
Mji wa Al Wasit Nchini Iraq, ambae ndie aliemuamrisha Al Hasan na Yahya Ibn
Ya'mur kufanya Hivyo’
Na vile vile akasema Imam Abu Muhammad Abd Al Haqq Ibn Ghalib Ibn Attiyah kua:
‘Hakika mimi nimesoma katika moja kati ya Vitabu kua alikua ni Khalifa Al
Mamun wa Utawala Al Abbas ndie aliemarisha kufanywa hivyo’
Na pia kuna wanaosema kua alikua ni Hajjaj Ibn Yusuf ndie aliefanya hivyo, Na si hivyo
tu kwani Qur'an asili yake ilikua haina hata vidoto kwa mfano kimoja chini ya herufi Ba,
Kimoja juu ya Herufi Nun, Fe, Viwili juu ya herufi Ta, n.k.
Ambapo anasema Imam Yahya Ibn Abi Kathir kua: ‘Qur'an katika kopi zake za asilia
ilikua tupu haina hata vidoto, ambapo jambo la kwanza walilolifanya ilikua ni kutia
Vidoto, juu ya Ba, Ta, That, na kusema kua hakuna tatizo lolote, bali kufanya hivyo
kunaifanya Qur'an iwe inafahamika zaidi, na kisha wakatia alama mwishoni mwa
kila aya, na ikatiwa alama mwanzoni na mwishoni mwa kila Sura.’
Kwa upande wmengine basi anasema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad
Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi kua amesema Ad Dani kua: ‘Kauli zote hizo
zilizoruhusu kuanzishwa kutiwa alama kwa mwanzo mwa kila aya na mwishoni,
mwa kila sura, mwisho mwa kila sura, n.k zilifanywa na Masahaba ambao
walifanya hivyo kutokana na Jitihada zilizowapelekea kufanya hivyo, Na nnadhani
kua wale waliopinga kuhusiana na hayo basi walipinga pale ilipokua imetumika
Rangi katika kutiwa alama hizo kwa mfano rangi nyekundu, manjano n.k
Ingawa Waislam wa Maeneo mengine hawakupinga na walikubaliana na jambo
hilo baada ya kulinganisha na kopi za asilia na hivyo zilizokokosewa kuondolewa
kasoro zake katika waliyokubaliana, wa Allahu Aalam.’
985
Ambapo amesema Imam Muhammd Ibn Sirin kua: ‘Hakika mimi nnao Msahafu
ambao umetiwa vidoto na Yahya Ibn Ya’mur’ na kwa upande wa Akhbar Al Fuquha
Imam Muḥammad Ibn Al Ḥasan Ibn Abd Allah Ibn Madḥij Al Faqih Muḥammad Ibn Al
Ḥasan Al Zubaydi basi anasema kua: ‘Al Mubarrad amesema kua Mtu wa mwanzo
kutia vidoto kwenye Qur’an ni Abu Al Aswad.’
Kwani tunapoangalia juhusiana na idadi ya aya za Qur'an basi pia Wanazuoni
wametofautiana kwani anasema Imam Muhammad Ibn Isa kua: Jumla ya aya katika
Msahafu wa Madinah ni 6000.
Na akasema Imam Ismail Ibn Jafar kua: ‘Msahafu wa Madinah una aya 6214.’
Ambapo kwa upande wa Imama Al Fadhl basi yeye anasema kua:
‘Msahafu wa Makkah una aya 6219.’
Ambapo kwa upande wa Imam Muhammad Al Kisai basi anasema kua: ‘Idadi ya aya
za Qur'an kwa mtizamo wa watu wa Basra ni 6204.’
Na kwa upande wa Imama Yahya Ibn Harith basi anasema kua : ‘Msahafu wa Syria una
aya 6226.’
Naam..hapa kuhusiana na hili la habari ya Aya basi nadhani nifafanue kidogo Ili
tufahamiane, na hivyo watu wasije wakafaham sivyo.
Hivyo kwa wale wasiofaham ili wasichanganyikiwe ilikuaje ukawa Misahafu hii ina
idadi ya aya tofauti basi inabidi wajue kua haya tote yametokea kwa sababu baada ya
Kufariki Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam basi Uislam ulizidi kutanuka katika
maeneo tofauti. Hivyo na Masahaba nao pia walitawanyika katika maeneo tofauti. Na
kutokana na kutawanyika kwao basi watu wa Maeneo husika wakawa wanafuata
mitizamo ya Masahaba husika.
Kwa mfano Sahaba Abd Allah Ibn Masud ambae ni Sahaba mwanazuoni alihamia Iraq,
hivyo Watu wa Iraq wakawa anafuata Mtizamo wake, na ndio maana unakuta Fiqh ya
Madhhab ya Imama Abu Hanifa imejaa mitizamo ya Abdullah Ibn Masud Radhi Allahu
Anhu.
Ambapo Abd Allah Ibn Umar, Zayd Ibn Thabit, Ubbay Ibn Qaab Radhi Allahu Anhum
walibakia Madinah na ndio maana pia Fiqh ya Madhhab ya Imam Malik imejaa Mitizamo
yao.
Na Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu alikua Makkah na Hivyo bila ya Shaka
ingawa imechukua sehemu tofauti lakini Mitizamo ya Imam Al Shafii imeegemea kwa
986
Abd Allah Ibn Abbas kwa Sababu Msingi wa Ilm ya Imam Al Shafii ni kwa Imam Al
Zuhri na Imam Sufyan Ibn Uyayna ambao wametoa kwa Abd Allah Ibn Abbas Radhi
Allahu Anhu n.k.
Hivyo utawanyikaji huo wa Masahaba Wanazuoni ndio uliopelekea kutokea kwa sababu
ya pili ya kua na kila Sehemu na Idadi yake ya Aya. Na labda tuchukulie mfano hai ili
tufaham zaid.
Katika Upande wa Madhhab ya Imam Al Shafii unaposali kwa Sala ya kutoa Sauti basi
Bismi Allahi Rahmani Rahim lazima uitamke kwa sauti. Na kila unapoanza na Mwanzo
wa Sura basi lazima Utamke Bismi Allahi kwa Sauti, ila ukianza kati kati ya Sura basi
hua si lazima kusema Bismi Allahi kwa Sauti.
Jee unajua kwanini?
Naam hii ni kwa Sababu kwa upande wa Madhhab ya Imam Al Shafii basi Biismi Allahi
hua ni aya miongoni mwa aya za Qur'an na ni sehemu ya Sura hivyo lazima uisome kwa
sauti ukisali sala ya sauti. Isipokua kama utasoma Sura ya 9 ambayo ni. Surat At Tawba.
Na anasema Imam An Nawawi kua: ‘Mtu atakapoanza mwanzo wa Sura bila kuisoma
Biismi Allahi basi hua amewacha sehemu ya Qur'an.’
Ambapo kwa Upande mwengine kuna Wanaosali sala za Sauti lakini baada ya Surat Al
Fatiha kisha kwa mfano akasoma Surat An Nas basi moja kwa moja hua wanaanza na
Qul aAuudhu Birabbi AlNass, Maliki Nnnas...mpaka mwisho.
Na hii ni kwa sababu kwao wao Biismilahi hua ni sehemu ya Ufunguzi tu wa Sura, hivyo
hii nikutokana na utofauti wa Mitizamo kulingana na Vithibitisho vya Wanazuoni kupitia
kwenye Hadith za Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam.
Na ni kwa upande wa Madhhab ya Imam Al Shafii basi Biismi Allahi ni Aya na ni sehemu
ya Sura yeyote utakaoianza kuisoma mwanzo wake isipokua Surat At Tawba.
Ambapo awali watu wa kabila la Quraysh walikua na mazoea ya kuweka kichwa cha
habari katika barua zao ambacho kilikua kinasema Biismika Liihumma ambapo na Rasul
Allah Salallahu Alayh wa Salam alikua akifanya hivyo pia, hadi pale Allah Subhanah wa
Ta’ala aliposhusha aya ya Surat Hud ambayo inamzungumzia Nabii Nuh kwa kusema:
﴿وَقَالَ ٱرْكَبُواْ فِيهَا بِسْمِ ٱهلل َِّ مجَْرَاهَا وَمُرْسَاهَا إِن َّ رَبىِّ لَغَفُورٌ ر َّحِ يمٌ ﴾
987
Waqala irkaboo feeha bismi Allahi majraha wamursaha inna rabbee laghafoorun
raheemun (Surat Hud 11:40-41)
Tafsir: Na yeye (Nuh) akasema: Ingieni ndani yake, Kwa Jina la Allah katika Kuelea
kwake na katika Kutia Nanga kwake, kwani kwa hakika Mola wangu ni mwingi wa
Usamehevu na ni mwingi wa Rehma.
Hivyo baada ya kushushwa aya hii basi Rasul Allahi Salallahu Alayhi wa Salam
akamrisha kutumiwa kwa maneno Biismi Allahi Al Rahmani, na iliposhushwa aya ya
Surat An Naml isemayo:
﴿إِن َّهُ مِن سُلَيْمَانَ وَإِن َّهُ بِسْ مِ ٱهلل َِّ ٱلر َّحمَْٰنِ ٱلر َّحِ يمِ ﴾
Innahu min sulaymana wa-innahu bismi Allahi alrrahmani alrraheemi (Surat An
Naml 27:30)
Tafsir: Kwa hakika hii ni kutoka kwa Sulaymani na kwa hakika (Inasema) Kutoka
kwa Allah Mwingi wa Rehma mwingi wa Huruma.
Hivyo baada ya kushushwa aya hii basi Rasul Allah Salallahu A’layhi wa Salam akaamua
kutumia Biismi Allahi Al Rahmani Al Rahim baada ya kusema: ‘Ndugu yangu Sulayman
ameanza aya na jina lake hivyo mimi nitaanza na Jina la Allah’ hivyo akaanzisha
Biismi Allahi Al Rahmani Al Rahim kua ndio kichwa cha Barua zake na kianzio cha Kila
Sura isispokua Surat At Tawbah.
Na ndio maana ikawa kuna wengine mongoni mwa Wanazuoni wakawa wamesema kua
hua sio lazima kuitamka Biismi Allahi kwa Sauti kwa sababu kwao wao hua ni Ufunguo
tu wa Kila Sura lakini si sehemu ya Sura.
Kwani hio ni sababu ya kwaza na mfano hai, hivyo kabla ya kuendelea basi nataka
tufahamiane vizuri sana kua:
Ingawa Wanazuoni wametofautiana kuhusiana na Idadi ya Aya za Qur'an, lakini hii
haimaanishi Kua Qur'an imetiwa mikono, au imetofautiana baina ya Msahafu mmoja na
Mwengine la!
Sio Hivyo na wala hatutakiwi tufahamu kua ni hivyo, kwa sababu tukifahamu hivyo basi
tayari tunakua tushavunja Nguzo ya Imani. Hivyo basi ili tusiwe ni wenye kuvunja Nguzo
ya Imani na badala yake tuwe ni wenye kuipa nguvu Imani yetu kuhusiana na Qur'an basi
na tuangalie sababu ya pili ambayo ilipelekea kuparaganyika idadi ya Aya.
988
Kwani anasema Mujaddid Ad Din Shaykh Ul Islami Imam Abd Rahma Al Suyuti Al
Shafii katika kitabu cha Al Itiqan fi Ulum ul Qur'an kua: ‘Mtizamo Sahih wa Idadi za
Aya za Qur’an ni 6236, na sababu ya kuwepo kwa utofuti wa Idadi hio ni kua kuna
baadhi ya Watu walizifupisha Aya zilizokua Ndefu na kuzigawa aya hizo katika
sehemu mbili mpaka tatu’
Sijui hapa tumefahamiana ama la? Hivyo kama hatujafahamiana basi na tuangalie mfano
wa hio sababu aliyoitoa Imam Al Suyuti ambapo hapo mimi nimeelezea kwa kutumia
maneno 41, bila ya kuweka nukta isipokua nimeweka koma.
Sasa kwa kua maneno hayo ni mengi basi ili kurahisisha ufahamu wake zaid ilikua
niyagawe katika sehemu mbili...yaani maneno hayo hayo lakini badala ya kuyaandika
kama yalivyo basi ni vizuri kuyagawa mara 2 badala ya mara moja ili watu wafaham,
wahifadhi na wazingatie mara moja.
Sasa hivi ndivyo walivyofanya baadhi ya Masahaba kwani wao walizigawa aya kubwa
na ndefu katika mara mbili mpaka tatu kulingana na ukubwa wa aya bila ya kupunguza
maneno ya aya.
Kwani pia hata tukichukulia mfano wa hio idadi ya Wanayokubaliana Wanazuoni kua ni
6236, basi hii pia hua ni Idadi ya aya bila ya kuihesabu Biismi Allahi ya Kila Sura na
hivyo idadi hii hua ya wale wasioihesabu Biismi Allahi ya kila Sura kua ni sehemu ya
Sura. Na hivyo basi kama tukiihesabu pamoja na Biismi Allahi basi aya zinakua 6348.
Kwani pia kwa upande wa Imam Ibn Huzaymah basi yeye anasema kua Qur'an ina aina
ya aya zifuatazo:
Aya 1000 kuhusiana na Ahadi.
Aya 1000 kuhusiana na Mawaidha.
Aya 1000 kuhusiana na Maamrisho.
Aya 1000 kuhusiana na Makatazo
Aya 1000 kuhusiana na Visa
Aya 1000 maonyo
Aya 500 kuhusiana na Hukmu
Aya 100 kuhusiana na Dua
Aya 66 kuhusiana na Mabatilisho na Yaliyobatilishwa
Hivyo ukijumlisha idadi hio basi unapata aya 6666, ambapo idadi hii pia ndio Idadi sahih
kulingana na Mtizamo wa Jarrah Allah Imam Abu Qasim Al Zamakhshari.
989
Hivyo basi Ukweli ni kua Allah Subhanah wa Ta'ala na Mtume wake ndie mwenye kujua
zaid juu ya hili, kwani kwa Upande wa Masahaba na Wanazuoni ndio kama tulivyoona
kua kila mtu na Mtizamo wake kulingana na Usomaji wake wa Qur'an yenyewe na namna
alivyofahamu, na kutokana na Kufanya Jitihada kwake na namna alivyojaaliwa na Allah
Subhanah wa Ta'ala.
Qur'an ni ile ile haijazidi wala haijapungua ila Mitizamo ya Watu tu juu yake ndio
Inayotofautiana katika kuifaham kwake, Kuitafakkari na kuifafanua kwake
Hivyo Wanazuoni Wanakubaliana na kufungamana na Mtizamo wa Masahaba wa Mji
wa Kufa ulioko Iraq na hivyo basi hapa inamaana tunazungumzia Mtizamo wa Sahaba
Abd Allah Ibn Masud na pia Ali Ibn Abi Talib Radhi Allahu Anhum ambao ilm yao ndio
chanzo kikuu cha Fiqh ya watu wa Iraq hususan watu wa Madhhab ya Imam Abu Hanifa.
Ambapo kwa upande mwengine basi tunaona kua huo pia ndio mtizamo wa Ummu Ul
Muuminin Aisha Radhi Allahu Anha ambao unasema kua Qur'an ina aya 6236. Na hizo
ndio aya zilizomo ndani ya Qur'an leo hii.
Kwani kwa kua Mada hii ni pana na kubwa na hivyo inataka utulivu wa ufaham na
umakini wa kutafakkari basi wacha tuzame zaidi kidogo ili tupate kufaham vizuri zaid.
Ambapo anasema Bahr ul Ilm Abd Allah Ibn Abbas Radhi Allahu Anhu kua:
Mimi nilimwambia Uthman Ibn Affan, hivi kwa ufaham wako ilikuaje Surat Al
Anfal ambayo ni Muthani (Sura yenye aya zisizozidi 100) na Surat Baraa (Surat At
Tawba) ambayo ni Mii'in (Sura yenye aya zaid ya 100) ukaziweka pamoja bila ya
kuandika Biismi Allah Rahmani Rahiim baina yake? Na kisha ukaziweka pamoja
na Sura 7 ambazo ni ndefu zaidi yake?
Uthman Ibn Affan Radhi Allahu Anhu akajibu: Kwa sababu unapita mda mrefu bila ya
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kupokea aya yeyote na kisha baadhi ya Wakati
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam anashushiwa Sura yenye aya nyingi. Hivyo
anaposhushiwa aya basi Humwita mtu anaeweza kuandika na kumwambia: Iweke
Aya hii kwenye Sura inayozungumzia hili na hili ndani yake kisha atashushiwa aya
nyengine na kusema: Iweke aya hii kwenye Sura inayozungumzia hili na hili.
Sasa Surat Al Anfal ni miongoni mwa Sura za Mwanzo zilizoshushwa katika Mji wa
Madinah na Surat Baraa (At Tawba) ni miongoji mwa Sura za Mwisho kushushwa.
Na Maneno yake (Surat At Tawba) yanafanana na maneno ya Surat Al Anfal hivyo
sisi tukadhani kua ni sehemu ya Sura hio (ya Al Anfal) Na kisha Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam akafariki, na haikuwekwa wazi juu yetu kua kama ni
sehemu ya Sura hio ama la. Hivyo ni kutokana na sababu hii ndio tukaweka Biismi
990
Allahi Rahmani Rahim baina yake na tukaiweka pamoja na Sura 7 ndefu (Imam At
Tirmidhii)
Kwani tunapozungumzia Ushushwaji wa Qur'an basi hua tunazungumzia Ushushwaji wa
Aya za Qur'an kuanzia Moja na Kuendelea kwa wakati mmoja au nyakati tofauti.
Ambapo katika Nzima basi hakuna Sura iliyoshushwa nzima nzima isipokua sura 2 tu.
Ambazo ni Surat Al Fatiha na Surat Al Mulk. Na hapo hapo kuna Wanazuoni wasemao
ni Surat Al Fatiha tu peke yake.
Na bila ya shaka katika upangwaji wa aya zake basi ni kama tulivyowahi kusema mara
kadhaa yaani zaidi ya mara 4 nishasema juu ya hili kua Malaika Jibri alikua akimwambia
Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam aya hii iweke sehemu fulani kabla au baada ya
Aya fulani.
Sasa pia tunapozungumzia kuhusiana na hesabu ya idadi ya aya basi pia Masahaba
waliokua wakiandika kutoka kwa Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam kutoka kwa
Malaika Jibril walikua wakiandika na kuifunga aya kulingana na kisomo cha Rasul Allah
Salallahu Alayhi wa Salam na hii ni kulingana na hadith ya Ummu Salamah Radhi Allahu
Anha ambapo anasema Ummu Salamah kua: Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam
alikua akisoma: Bismi Allahi Al Rahmani Al Rahim Al Hamd lillahi Rabbi Al Alamiin
Al Rahmani Al Rahiim, Malik yawm Ad Din (Imam Ahmad)
Hivyo basi ukweli ni kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua hasemi kua Sura
fulani ina aya ngapi isipokua mara moja moja kama kwenye Surat Al Fatiha. Hivyo
Masahaba walikua wakijua kua hapa ndio mwisho wa aya kulingana na namna Rasul
Allah Salallahu Alayhi wa Salam alivyokua akisita anapofika kwenye kituo cha kusitia
kwenye aya na wao hujua kua hapa ndio mwisho wa aya katika kuandika kwao.
Kutokana na hali hio basi ndio maana pia Masahaba wakatofautiana kuhusiana na idadi
ya aya hapo kabla, kwani kama tulivyoona kwenye Mfano jana kua Walipoona aya ni
ndefu sana basi waliigawa mara 2 hadi 3 bila ya kupunguza maneno wala maana ya aya.
Na ndio maana pia kuna baadhi ya Masahaba wakaihesamu Bismi Allahi kua ni sehemu
ya Sura na kuna baadhi wakawa hawakuihesabu kua ni sehemu ya sura kama
tulivyofafanua jana.
Hivyo Qur'an ina aya 6236 lakini kwa wale wanaosema kua Bismi Allahi Al Rahmani Al
Rahim si sehemu ya Sura.
Ambapo kwa wale wanaosema kua ni sehemu ya Sura basi unaongeza Bismi Allahi Al
Rahmani Al Rahim 112 yaani baada ya kuitoa Bismi Allahi Al Rahmani Al Rahim ya Surat
991
Al Fatiha na Bismi Allahi Al Rahmani Al Rahim iliyomo ndani ya Surat At Tawba hivyo
inakua aya 6236+112 = 6348.
Kwani Neno Sara kwa Lugha ya Kiarabu hua linamaanisha Kupanda Mlima au Ukuta,
Kushambulia au Kukimbilia.
Neno Sara ndio lililotoa neno Suratun ambalo hua linamaanisha Heshima, Darja, Cheo,
Alama, Utukufu, Mpangilio wa Mawe au Matofali Katika Ukuta, Jengo zuri linalovutia,
Kitu kizuri kilichokamilika vizuri.
Na Neno Sara ndio lililotoa neno Suratun ambalo hua Jina la Sehemu moja kamilifu
miongoni mwa sehemu 114 kamilifu za Qur’an yaani Sura.
Hivyo Sura za Qur'an zimeitwa Sura kwa sababu:
1-Mtu anaposoma Sehemu hio ya Qur'an basi Hua ni Mwenye Kupanda Darja
kutokana na Malipo yaliyomo ndani yake kutokana na Kuisoma kwake.
2-Kila Sura Moja ya Qur'an ni kama Jengo au Umbo Kamilifu linalojitegemea na
Kupendeza na Kuvutia.
3-Kwa Sababu Hua ni alama inayowakilisha Sehemu ya Qur'an ambayo yenye
Mwanzo wake na Mwisho wake, kulingana na mada husika ndani yake.
Ambapo neno Sura limetajwa ndani ya Qur'an katika Surat Al Baqara pale iliposema:
﴿وَإِن كُنْتُمْ فىِ رَيْبٍ ممِّ َّا نَز َّلْنَا عَلَى ٰ عَبْدَِ فَأْتُواْ بِسُورَةٍ مِّن مِّ ثْلِهِ وَٱدْعُواْ شُهَدَ آءَكُم
مِّن دُونِ ٱهلل َِّ إِنْ كُنْتُمْ صَادِقِينَ ﴾
Wa-in kuntum fee raybin mimma nazzalna AAala AAabdina fa/too bisooratin min
mithlihi waodAAoo shuhadaakum min dooni Allahi in kuntum sadiqeena (Surat Al
Baqara 2:23)
Tafsir: Na Kama Nyinyi (Makafiri) mkiwa mnashaka kuhusiana na Tulichomshushia
Mja wetu (Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) Basi Toeni Sura Yenye Mfano
Kama Mithili yake na waiteni Mashahidi wenu (mnaowaabudu) zaidi ya Allah kama
nyinyi kweli ni wakweli.
992
Kwani neno Sura limetajwa tena pale aliposema Allah Subhanah wa Ta'ala:
﴿أَمْ يَقُولُونَ ٱفْتَرَاهُ قُلْ فَأْتُواْ بِسُورَةٍ مِّثْلِهِ وَٱدْعُواْ مَنِ ٱسْتَطَعْتُمْ مِّن دُونِ ٱهلل َِّ نِإ
كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴾
Am yaqooloona iftarahu qul fa/too bisooratin mithlihi waodAAoo mani
istataAAtum min dooni Allahi in kuntum sadiqeena (Surat Yunus 10:38)
Tafsiri: Wanasema kua ‘(Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) Kaighushi
(Qur’an)’ Waambie (Ewe Muhammad Salallahu Alayhi wa Salam) Basi Leteni Sura
Mithili yake Na Waiteni Muwatakao Zaidi ya Allah Kama nyinyi ni Wakweli.
Kwani Masahaba walikua wakijua kua Sura humaanisha sehemu kamilifu ya Qur'an
kutokana na kua Rasul Allah Salallahu Alayhi wa Salam alikua anaposhushiwa Sura ya
Qur'an basi husema Sasa hivi nimeshushiwa Sura ambayo inasema kadha w kadha w
kadha, na anaposhushiwa aya husema nimeshushiwa aya inasema kadha w kadha w
kadha.
Kwani anasema Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al
Ansari Al Qurtubi kua: ‘Aya Maana yake hua ni Alama, na hua ni Alama kwa sababu
hua ni tofauti kimaneno na maneno yaliyo kabla yake na maneno yaliyo baada yake
na hivyo hua inajitegemea peke yake, Aya vile vile hua inamaanisha kua ni
Uthibitisho au Dalili, na imeitwa Aya kwa sababu Aya hua ni mchanganyiko wa
herufi za Qur'an, na pia imeitwa Aya kwa sababu hua ni Dalili au Uthibitisho wa
kimaajabu ambao hakuna anaeweza kuuiga.’
Na Wanazuoni wa Lugha wametofautiana kuhusiana na asili ya Mzizi wa Neno Aya,
Kwani Imam As Sibawayh basi yeye anasema kua : 'Neno Aya limetokana na neno
Ayaya na kwa sababu Ye ni herufi ambayo ikiwa na Fat-ha kabla yake, basi hua
inageuka na kua Alif basi ndio baada ya Kuitwa Ayay ikawa ni Aya Ambapo kwa
upande wa Imam Muhammad Al Kisai basi yeye anasema kua: 'Mzizi wa neno Aya
ni Ayaya na Ye inapokua na Alif yenye Fat-ha kabla yake basi hua ni kitu kimoja na
zote hua moja na ndio maana ikawa Aya'
Na akasema Imam Al Farra kua: ‘Aya inatokana na Mzizi wa neno Ayaya ambalo hua
linajumuishwa na Alif kutokana kutopendeza kutamkwa Maradufu na hivyo
huitwa Aya’
993
Hapa nataka watu wawe makini tena kwa sababu ndani yake kuna uthibitisho pia wa lile
jambo nililolirudia juzi kulifafanua hapo kabla ambalo ni kuhusiana na idadi ya Aya za
Qur'an na kwanini Masahaba wakatofautiana juu yake.
Kwani ingawa mara nyingi Aya hua ni kikundi cha maneno lakini pia baadhi ya wakati
Aya hua pia ni neno Moja tu na ndio maana Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn
Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi akasema pia Aya hua pia ni
Mchanganyiko wa Herufi za Kiarabu za Qur'an.
Hivyo basi hata neno moja lenye Mchanganyiko wa Herufi za Kiarabu katika sehemu ya
Mwanzo wa Sura za Qur'an hua ni Aya kwa mfano:
Wa Al Fajr, Wa Al Asr, Alif-Lam-Mim Alif-Lam-Sad, Ha-Mim, Ta-Ha, Ya-Sin, Alif-Lam-
Mim-Sad n.k
Hivyo ingawa humu ndani yake mna Harfu Muqataat yaani Harufi zilizotengana kama
Alif-Lam n,k lakini nazo pia hua ni Aya pale inapokua ziko mwanzoni mwa Sura.
Ambapo kwa Upande wa Wanazuoni wa Kufah Iraq basi wao walikua wakisema kua:
Maneno Ha-Mim-Ayn-Sin-Qadf ni Aya Mbili badala ya Moja, yaani Ha-Mim ni Aya
moja na Ayn-Sin-Qaf hua ni aya ya Pili
Hivyo ingawa wengine walikua wanaona kua Ha-Mim-Ayn-Sin-Qaf (Surat Ashuara
42:1)
﴿بِ سْمِ اهلل َِّ ٱلر َّحمْ ٰنِ ٱلر َّحِ يمِ۞حم ۤ ۞ع ۤ س ۤ ق ۤ ﴾
Kua ni aya moja lakini wao walikua wanaona kua ni aya 2 tofauti na ndio tunavyofuata
sisi leo, kwani tulisema kua Wanazuoni wamekubaliana na Mfumo wa idadi ya Aya wa
Watu wa Kufah, Iraq.
Ambapo hali hii hua pale inapokua mwanzo mwa Sura lakini kama herufi hizi zikiwa
ndani ya Sura basi hua si Aya bali hua ni maneno ya aya, kwani hua zinajumuishwa na
herufi nyenzake ili kukamilisha aya.
Na anasema Imam Abu Amr Ad Dani : ‘Hakika mimi sijawahi kuona Neno Lolote lile
liliomo kwenye Quran ambalo hua linajitegemea peke yake kua ni Aya isipokua
neno: ‘Mud-hammatan’ liliomo katika Surat Al Rahman’
994
Pale iliposema aya ya 55:64 inayozungumzia Bustani za Peponi zenye majani
yaliyonawiri katika aya zifuatazo:
﴿فَبِأَىِّ آلا ۤ ءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّابَنِ۞مُدْهَآم َّتَانِ۞فَبِأَىِّ آلا ۤ ءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّ ابَنِ ﴾
Fabi-ayyi ala-i rabbikuma tukadhdhibani; Mud-hammatani; Fabi-ayyi ala-i
rabbikuma tukadhdhibani (Surat Rahman 55:63-65)
Tafsir :Jee Ni zipi kati ya Neema za Mola wenu nyinyi Mtazikadhibisha?(Majini na
Ibn Adam); Zenye Rangi Ya Kijani Iliyovia; Jee Ni zipi kati ya Neema za Mola wenu
nyinyi Mtazikadhibisha?(Majini na Ibn Adam)
Naam bila ya shaka hakuna neema hata moja kutoka kwa Mola wenu tutakayoweza
kuikadhibisha, isipokua wengi wetu wamo katika hali ambayo inaelezewa na Mujaddid
Ad Din Hujjat Ul Islami, Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani Imam Abu Hamid
Ibn Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al Shafii kua:
‘Kulikua Na Kijana ambae alikua anatembea Msituni, na mara Ghafla moja
akashtukia amekumbana na Simba uso kwa Uso.
Khofu ikamjaa Kijana na Hivyo akaona aokoe Maisha yake kwa Kukimbia, hivyo
kijana huyo akakimbia kwa kadiri ya uwezo wake wote, akatumia nguvu zake zote
kumkimbia Simba huyo.
Katika kukimbia kwake akaona kua kuna Kisima Mbele yake, hivyo akaamua Bora
Ajitupe ndani yake kuliko kuendelea Kukimbia kisha akaliwa na Simba badala
yake.
Kwani kisima hicho ndio Tegemeo lake peke yake la kuokoa Maisha yake, Hivyo
Kijana akajivuta kuelekea Kisimani na alipokukaribia akaruka na kabla ya kutua
akajikuta kua ni mwenye kuingia kwa kuangukia ndani yake.
Wakati anaanguka ndani yake, mikono yake ikawahi kukamata Kamba iliyokua
ikining'ingia ndani yake.
Alipoikamata kamba akapata afueni na utulivu wa Nafsi yake, kua Alhamd lillah
ameokoka kutpkana na kuliwa na Simba na hivyo boa ilivyokua ananing'inia
kisimani kutokana na kamba aliyoishikilia mkononi, Wakati kijana anamshukuru
Mola wake kutokana na hali ya kuokoka kwake, basi akasikia sauti kutoka ndani
chini kisimani.
995
Kijana akatupa Jicho chini, na Hamad! Akaona Kuna Joka Kubwa ndani chini
Kisimani, Kijana akachanganyikiwa akajiona kumbe hajaokoka, hivyo ili aokoke
basi bora kwake apande juu awe nje ya Kisima Kwani ameshayasahau ya Simba na
anayafikiria ya Joka lilimo Kisimani likimsubiri tu atue chini.
Hivyo Kijana akaangalia juu, ili ajivute kuelekea nje ya Kisima hicho, lakini mara
akaona Panya wawili mmoja mweusi na mwengine mweupe anaitafuna Kamba
yake aliyoikamata na kuitegemea kwa ajili ya kuokoa Maisha yake. Kisha
alipoangalia juu zaid akaona Simba amekaaa anamsubiri ili atoke kisimani awe ni
chakula kwa ajili ya njaa yake.
Hivyo Kijana akataharuki kutokana na kuzidiwa na vishindo vinavyo hisika ndani
ya mwili wake vinavyotokana na mapigo ya Moyo wake kwani utulivu
umemuondoka na amejawa na khofu kutokana na kua katika hali mbaya na ya
hatari ambao inayonekana kutokana na hali ya mazingira yake.
Wakati anafikiria nini afanye mara akili yake ikamwambia aangalie Upande wa
Ukutani, alipoangalia Ukutani akaona Sega lililojaa Asali ambayo inatiririka
taratibu kisimani, Kijana akapeleka Kidole kwenye sega la Asali akakutana na
alipokitoa kilikua kimejaa asali.
Moja kwa moja akakipeleka Kidole hicho Mdomoni kuonja Utamu wa Asali hio na
hapo hapo akasahau kuhusiana na sehemu aliyokuwepo kwenye kamba
anayoning'inia, akamsahau Simba aliejuu, akawasahau Panya wawili Mweupe na
Mweusi wanaoitafuna Kamba hio, na akalosahau hata Joka liliokua linamsubiri
ndani chini kisimani.
Kwani Hujjat Ul Islam Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad
Al Ghazali anaendelea kutuambia kua: ‘Hali aliyokua nayo Ibn Adam Duniani,
ambapo Simba aliekua akimfukuza basi ndio Malakat ul Mawt ambae kila siku yuko
nyuma ya kila mtu katika maisha yake. Joka aliloliona Kisimani ndio Adhabu ya
Kaburini inayomsubiri baada ya kufariki kwake kutokana na maasi yake, na Panya
Mweusi na Mweupe wanaashiria, nyakati za Usiku na Mchana na namna
zinavyokula Uzi wa Uhai wetu hapa Duniani. Na Asali ni mapambo ya Mpito ya
Kidunia yanayomhadaa kila Ibn Adam na kumfanya aisahau Akhera yake na
kuiendekeza Dunia yake’
Mujaddid Ad Din Hujjat Ul Islami, Az Zukhruf Ad Din Imam Al Shafii Al Thani Imam
Abu Hamid Ibn Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Tusi Al
Shafii anatuusia cha kufanya ili tusihadaike na Dunia kwa kutuambia kua: ‘Taqwa hua
hua inararua Matamanio na Kuyachafua Mapambo ya Dunia, kiasi ya kua dhambi
996
huonekana kua ni zenye kuchukiza, kama vile Mtu mwenye kupenda Asali
anapochukizwa nayo pale anapoona kua Asali hio imetiwa sumu ndani yake, hivyo
ndivyo Taqwa inavyoyaangamiza Matamanio.
Hivyo Taqwa huidibiti iungo vyako, na huutuliza Moyo wako na kuupa utulivu.
Taqwa huufanya Moyo utupilie mbali Kiburi, Kujiona, Kua na wivu na kuuwacha
ukiwa na khofu juu ya Mola wake. Na hivyo Moyo hua hua unajihesabia makosa
yake na kuanza kufuatilia kuhusiana na maslahi yake ya baadae kwa kutafakkari
ndani yake na kujiangalia na hivyo Moyo hua ni wenye kuthamini kila mda na
wakati uliopo mbele yake.’
Na amesema Allah Subhanah wa Ta’ala kua:
﴿مح َُّم َّدٌ ر َّسُولُ ٱهلل َِّ وَٱل َّذِينَ مَعَهُ أَشِ د َّآءُ عَلَى ٱلْكُف َّارِ رُحمََآءُ بَيْنَهُمْ تَرَاهُمْ رُك َّ عاً
سُج َّداً يَبْتَغُونَ فَضْلاً مِّنَ ٱهلل َِّ وَرِضْوَاً سِ يمَاهُمْ فىِ وُجُوهِهِمْ مِّنْ أَثَرِ ٱلس ُّجُودِ
ذٰلِكَ مَثَلُُهمْ فىِ ٱلت َّوْرَاةِ وَمَثَلُهُمْ فىِ ٱلإِنجِيلِ كَزَرْعٍ أَخْرَجَ شَطْأَهُ فَآزَرَهُ فَٱسْتَغْلَ َظ
فَٱسْتَوَىٰ عَلَى ٰ سُوقِهِ يُعْجِ بُ ٱلز ُّر َّاعَ لِيَغِيظَ هبِِمُ ٱلْكُف َّارَ وَعَدَ ٱهلل َُّ ٱل َّذِينَ آمَنُواْ
وَعَمِلُواْ ٱلص َّ الحَِاتِ مِنْهُم م َّغْفِرَةً وَأَجْ راً عَظِيماً ﴾
Muhammadun rasoolu Allahi waalladheena maAAahu ashiddao AAala alkuffari
ruhamao baynahum tarahum rukkaAAan sujjadan yabtaghoona fadhlan mina
Allahi waridhwanan seemahum fee wujoohihim min athari alssujoodi dhalika
mathaluhum fee alttawrati wamathaluhum fee al-injeeli kazarAAin akhraja shatahu
faazarahu faistaghladha faistawa AAala sooqihi yuAAjibu alzzurraAAa
liyagheedha bihimu alkuffara waAAada Allahu alladheena amanoo waAAamiloo
alssalihati minhum maghfiratan waajran AAadheeman(Surat Al Fat-h 48:29)
Tafsir: Muhammad ni Rasul Allah na wale waliokua pamoja nae ni wakali dhidi ya
Makafiri na ni wenye kuhurumiana miongoni mwao, hakika mnawaona wao
wakirukuu na kusjudu wakitafuta rehma za Allah na Fadhila zake. Alama walizokua
nayo kwenye mapaji ya Nyuso zao zinatokana na athari ya kusujudu kwao, huu ndio
utambulisho wao kwenye Tawrat lakini utambulisho wao kwenye Injil hua ni kama
mbegu inayochipua na kua imara na kua nene na kusimamia kwenye shina lake na
kumfurahisha mkulima na hivyo kua ni mwenye kwa kukasirisha Makafiri kutokana
997
nayo. Allah amewaahidi wale walioamini na kufanya mema na usamehevu na malipo
yaliyo bora zaidi.
Wa Billahi Tawfiq
998
MARUDIO YA VITABU VILIVYOTUMIKA KATIKA KITABU HIKI:
AL BURHANI FII ULUM UL QUR’AN – Shaykh Islami Imam Abu Abd Allah Badr
Ad Din Muhammad Ibn Abd Allah Ibn Bahadir Al Zarkashi Al Shafii.
AL DIWAN AL IMAM AL SHAFII – Mujaddid Ad Din Imam Abu Abd Allah
Muhammad Idris Al Shafii.
AL HAWI AL KABBIR FII FIQH MADHHAB AL IMAM AL SHAFII - Imam Abu
Hasan Ali Ibn Muhammad Ibn Habib Al Mawardi Al Shafii
AL ITQAN FII ULUM UL QUR’AN – Mujaddid ud Din ImamAbu Fadhl Abd Rahman
Ibn Kamal Al Din Abi Baqr Ibn Muhammad Ibn Sabiq Al Din Jalal Ad Din Al Misri Al
Suyuti Al Shafii.
AL MUTAMMAD FI FIQH UL SHAFII – Imam Muhammad Al Zuhayly Ad Dimashq
Al Shafii.
AL RISALAT AL QUDSIYYAH FII QAWAID AL AQAID – Hujjat ul Islami Mujaddid
Ad Din Imam Abu Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al
Shafii.
AR RUH AL MAÁNI FI TAFSIR AL QURAN AL ADHIM WA SABAA AL
MATHANI - Imam Abu Al Thana Shihab Din Sayyid Mahmud Ibn Abd Allah Al Husayn
Al Alusi Al Baghdadi Al Hanafi.
ARAIS FI MAJALIS FI QASAS AL ANBIYAH – Imam Abu Is-haq Ahmad Ibn
Muhammad Ibn Ibrahim Al Thalabi Al Shafii.
BAYAN AL FARQ BAYN AL SADR WA AL QALB WA AL FUAD WA AL LUBB -
Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Ali Ibn Hasan Ibn Bashir Al Hakim Al Tirmidhi
Al Shafii.
FAYDHUL AL QADIR – Imam Muhammad Abdur Rauf Bin Taj Al Arifin Ibn Ali Bin
Zainal Abidin Ibn Yahya Ibn Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Ibn Ahmad
Ibn Makhluf Ibn Abd Salam Al Hadadiy Al Munawiy Al Qahiriy Al Misriy Al Shafii
FUSUS AL HIKAM – Shaykh Al Akbar Muhyi ad Din Imam Abu Bakar Ibn Arabi Al
Andalus Al Maliki.
HUJJAT UL BALIGHA - Mujaddid ud Din Qutb Ad Din Imam Ahmad Shah Waliyyu
Allah Ibn Abd Rahman Ibn Umar Ad Dahlawi.
INSAN UL UYUNI – Al Imam Al Ulamaa Imam Al Burhan Din Al Halabi.
JAMI’I LI AHKAM AL QUR’AN - TAFSIR AL QURTUBI - Imam Abu Abd Allah
Muhammad Ibn Muhammad Ibn Abu Bakr Al Ansari Al Qurtubi.
KASHF AL ASRAR WA UDDAT AL ABRAR – Imam Rashid Al Din Al Maybudi.
KITAB AL ARBAIN FI USUL AD DIN - Hujjat ul Islami Mujaddid ad Din Imam Abu
Hamid Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Shafii.
KITAB JAWAHIR AL QUR’AN - Hujjat ul Islami Mujaddid ad Din Imam Abu Hamid
Muhammad Ibn Muhammad Ibn Muhammad Al Ghazali Al Shafii.
MASNAWI NURIYA - Baddiuzzamman Said Nursi Al Turkiy Al Hanafi.
999
MISHKAT UL MASABIH – Shaykh Waliuddin Abu Abdullah Al Khatib Al Tibrizi Al
Hanafi.
MUFRADAT FI GHARIB AL QURAN - Allamah Abu Qasim Ibn Husein Ibn Mufadal
Ibn Muhammad Raghib Al Isfahani.
QISAS AL ANBIYAAH- Allamah Nasiruddin Burhan Ad Din Al Rabghuzi.
RISALAT AL QUSHAYRIYAH - Imam Jamal Islam Abu Qasim Abd Al Karim Ibn
Hawazin Al Qushayri
RISALE NURI - Baddiuzzamman Said Nursi Al Turkiy Al Hanafi.
TAFHIM AL QURAN – Allamah Sayyid Abu Ala Mawdudi Al Hanafi.
TAFSIR AL KABIR – MAFATIH AL GHAYB – Sultan al Mutakallimin Mujaddid ud
Din Imam Abu Abd Allah Muhammad Ibn Umar Ibn Al Husayn Al Taymi Al Bakri Al
Tabaristan Fakhr Ad Din Al Razi Al Shafii.
TAFSIR AL KASHSHAF AN TAHQIQ AL TANZIL - Sultan Al Balagha Jarrah Allah
Imam Abu Al Qasim Mahmud Ibn Umar Ibn Ahmad Al Zamakhshari Al Hanafi Al
Mutazila.
TAFSIR AL MAWARDI AN NUQAT WA AL UYUN - Imam Abu Hasan Ali Ibn
Muhammad Ibn Habib Al Mawardi Al Shafii.
TAFSIR AL QURÁN AL ADHIM – Imam Abu Muhammad Sahl Ibn Abdallah Al
Tustari Al Shafii.
TARIKH AL RUSUL W AL MULUK– Imam Abu Jafar Muhammad Ibn Jarir at Tabari
Al Shafii.
TAFSIR AL QASIMI AL MUSSAMA MAHASIN AL TA’WIL- Imam Jamal Al Din
Muhammad Al Qasimi Al Dimashq.
TARIKH AL KHULAFA – Mujaddid ud Din Imam Abu Fadhl Abd Rahman Ibn Kamal
Al Din Abi Baqr Ibn Muhammad Ibn Sabiq Al Din Jalal Ad Din Al Misri Al Suyuti Al
Shafii.
MARUDIO YA MITANDAO ILIVYOTUMIKA KATIKA KITABU HIKI
www.aliftaa.jo
www.dar-alifta.org
www.eshaykh.com
www.islamqa.org
www.muftiwp.gov.my
www.seekersguidance.com
www.shafiifiqh.com
www.sunnahmuakada.wordpress.com
www.questionsonislam.com