You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
www.annuurpapers.co.tz<br />
Sauti ya Waislamu<br />
ISSN 0856 - 3861 Na. 1049 MUHARRAM 1434, IJUMAA DES. 14 - 20, 2012 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=<br />
Ubaguzi katika elimu<br />
wazidi kubainishwa<br />
’Zubeda’ wa Divisheni 1 alinyimwa nafasi F5<br />
Ustadh Monsignor Pengo anapotosha ukweli<br />
SHEIKH Ponda Issa Ponda (kushoto) akiwa na Ustadh Shaaban Mapeyo (kulia).<br />
Sheikh Ponda Issa bado<br />
yupo rumande Segerea<br />
Sheikh wa Bakwata atoa ushahidi<br />
Aliyeuziwa kiwanja naye ajieleza Uk. 12<br />
TATU alikosa nafasi shule<br />
kwa sababu jina lake<br />
lingine Zubeda ambalo<br />
kabisa ni la Kiislamu.<br />
Kwa kuwa Bint Shaaban,<br />
Binti wa Kitanzania<br />
inayodaiwa kutokuwa na<br />
udini, alinyimwa nafasi ya<br />
KOMANDO! Komando!<br />
Komando! Kibwagizo hiki<br />
ni cha kuwahadaa watu<br />
na kuihadaa hadhira,<br />
ili iweze kuamini kuwa<br />
watu hao ni waumini wa<br />
dhati wa Raisi Mstaafu<br />
wa Zanzibar wa CCM<br />
mwaka 1990- 2000,<br />
Salmin Amour.<br />
Huyu Salmin alipendelea<br />
mwenyewe jina la Komando,<br />
kutokana na hulka yake ya<br />
kukosa uvumilivu dhidi ya<br />
wapinzani hasa, CUF.<br />
Kuthibitisha imani hiyo<br />
ni pale alipowapeleka jela<br />
bila ya hatia, Viongozi 20<br />
wa Chama cha Wananchi,<br />
CUF.<br />
Vibaraka wahafidhina<br />
wanachohitaji ni CCM<br />
Zanzibar kutawaliwa na<br />
“Komando”.<br />
Ili hatimaye asisalimike<br />
yeyote kutokana na makucha<br />
Anachotaka<br />
Borafya katu<br />
hakiwezekani<br />
Uk. 3<br />
kusoma kidato cha 5 pamoja<br />
na kuwa na DIVISHENI<br />
ONE!!!<br />
N a h u o n i w a k a t i<br />
wa Mwalimu Nyerere<br />
anayetukuzwa leo kwamba<br />
eti aliondoa udini!<br />
(Soma Uk. 8)<br />
CCM wasaliti wa Zanzibar<br />
wajificha kwa Komandoo<br />
Sikiliza anachosema Bi Fatma Karume<br />
Wahafidhina wasirejeshe chuki, mikwaju<br />
RAIS mstaafu wa SMZ<br />
Amani Abeid Karume<br />
ya chuma wanayostahiki.<br />
H a o n d i o w a l e<br />
waliokasirishwa mno na<br />
hotuba ya Amani Abeid<br />
Karume na waliamua<br />
kuirarua na kuichanachana<br />
Picha kubwa ya Karume<br />
iliyokuwapo Michenzani,<br />
Zanzibar.<br />
(Soma Uk. 7)
2<br />
AN-NUUR<br />
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786<br />
Cel: 0784 370 208, 0755 260 087 0713 110148, DSM.<br />
www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk<br />
Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top<br />
Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam<br />
MAONI YETU<br />
Miaka 51 ya kutumia uhuru vibaya<br />
JUMAPILI ya wiki<br />
iliyopita, Tanzania bara<br />
walisherehekea miaka 51<br />
tangu upatikane uhuru<br />
kutoka kwa mkoloni<br />
Muingereza.<br />
Sherehe zilifanyika pale<br />
Uwanja wa Uhuru, na<br />
kuhudhuriwa na Rais wa<br />
Jamhuri ya Muungano wa<br />
Tanzania na Amir Jeshi<br />
Mkuu Jakaya Mrisho<br />
Kikwete.<br />
Aidha alikuwepo Rais<br />
wa Zanzibar, Dk. Ali<br />
Mohammed Shein na<br />
viongozi wengine wa ngazi<br />
mbalimbali za kiserikali,<br />
vyama vya kisiasa na<br />
taasisi za kijamii.<br />
Sherehe kwa kiasi<br />
kikubwa zilichagizwa na<br />
burudani za ukakamavu,<br />
hususan magwaride ya<br />
vikosi vya Majeshi ya<br />
Ulinzi na Usalama.<br />
Hata hivyo tunadhani<br />
k w a m b a w a k a t i<br />
tunasherehekea hiyo miaka<br />
51 ya uhuru, kwa kiasi<br />
kikubwa uhuru wenyewe<br />
umetumika vibaya kwa<br />
walio wengi.<br />
T u n a s e m a h i v y o<br />
kutokana na kuwepo<br />
k w a o m b w e k u b w a<br />
kati ya viongozi na<br />
wanaoongozwa, matajiri<br />
n a m a s k i n i , w e n y e<br />
elimu na wasio bahatika<br />
kuipata, wanaodhulumu<br />
na wanaodhulumiwa.<br />
Miaka 51 baada ya<br />
uhuru tunashuhudia<br />
Watanzania ambao wengi<br />
ni maskini, makabwela,<br />
wavuja jasho na walala<br />
hoi, wakitakiwa kutoa kitu<br />
chochote wanapohitaji<br />
kupata huduma za msingi<br />
katika taasisi nyingi za<br />
huduma za kiserikali.<br />
Wa k a t i h u o h u o ,<br />
tunashuhudia wanaofuja<br />
kikweli kweli matunda ya<br />
uhuru, wakipewa huduma<br />
hizo kwa haraka na kwa<br />
wakati, tena kwa adabu<br />
na kwa unyenyekevu<br />
mkubwa, na wakati huo<br />
huo hakuna anayethubutu<br />
kudai chochote kwa watu<br />
wa kaliba hii japo wao ndio<br />
wenye ukwasi.<br />
Wakati mtoto wa mlala<br />
hoi akihaha kusaka ajira<br />
baada ya kumaliza elimu<br />
zao kwa taabu kutokana na<br />
umasikini wa wazazi wao,<br />
watoto wa wafuja uhuru<br />
hupeana vyeo na nafasi<br />
katika asasi za kiserikali<br />
na kwenye mashirika<br />
makubwa, bila shaka si<br />
kwa sababu ya ujuzi au<br />
elimu zaidi, bali ni kwa<br />
sababu tu ya kutumia nafasi<br />
za wazee wao, ambao ndio<br />
vinara wa kufuja uhuru<br />
wenyewe.<br />
Watoto wa makabwela<br />
wanaambiwa, mtaji wa<br />
masikini ni nguvu zake.<br />
Wanahamasishwa kujiunga<br />
vicoba, saccos, vibindo<br />
nk. kwa kuwa nafasi<br />
wanazotaka zina wenye<br />
uhuru wao.<br />
Tunaona hata katika<br />
huduma za afya, kwenye<br />
v y o m b o v y a s h e r i a<br />
mahakamani, vyombo vya<br />
dola kama polisi, huko<br />
wananchi wanalia kuwa<br />
hakuna haki. Umekuwa ni<br />
mtindo wa mwenye nguvu<br />
mpishe. Mwenye cheo<br />
na mwenye pesa ndiye<br />
mwenye ‘haki’ na mwenye<br />
‘sheria’.<br />
Kwa utaratibu huu,<br />
imekuwa miaka 51 ya<br />
uchungu na makali ya<br />
maisha ndani ya uhuru.<br />
Kuna haja ya suala hili<br />
kutizamwa kwa uzito wake.<br />
Ifikie mahali, Watanzania<br />
waishi maishi ya heshma<br />
kuanzia uwezo wa kupata<br />
mahitaji muhimu ya<br />
kimaisha na pia kupata<br />
haki zao za kibinadamu na<br />
za kiuwananchi.<br />
Vi o n g o z i w a a c h e<br />
kujitizama tu, watizame<br />
nchi na wananchi. Ifikie<br />
mahali kila anayemaliza<br />
muda wake wa uongozi,<br />
a j i v u n i e m a z u r i<br />
aliyowafanyia wananchi,<br />
na wananchi watamani<br />
lau angeendelea afanye<br />
mengi.<br />
Tahariri/Matangazo<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
KAMATI YA KUENDELEZA UISLAMU TANZANIA<br />
TAMASHA LA KANDA YA KASKAZINI,<br />
MASHARIKI NA VISIWANI KIRINJIKO - SAME<br />
21 – 26 DESEMBA, 2012<br />
Waislamu wote wa Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga,<br />
Morogoro, Dar – es – Salaam, Pwani na Visiwa vya Unguja na<br />
Pemba wanaalikwa kuhudhuria Tamasha la Ujenzi wa Chuo<br />
cha Ualimu na Ufundi Kirinjiko litakalofanyika 21 – 26 Desemba,<br />
2012.<br />
Shime Waislamu tujitahidi kuhudhuria kwa wingi. Wasio na<br />
wasaa wa kuhudhuria wachangie fedha na vifaa vya ujenzi.<br />
Tukumbuke, tukifanya hivyo tutakuwa tumefanya biashara na<br />
Allah (s.w) kwa mafanikio ya hapa duniani na malipo ya Pepo<br />
– Qur’an (61:10-13)<br />
Wabillah Tawfiiq<br />
AMIR<br />
MKUZO ISLAMIC HIGH SCHOOL<br />
P.O. Box 346, Songea Tel: +255 - 716791113, +255683155902 Email:<br />
mkuzoipc@rocketmail.com<br />
NAFASI ZA KIDATO CHA I - 2013<br />
Waislamu wote mnatangaziwa nafasi za kidato cha<br />
kwanza katika shule ya sekondari ya Kiislamu Mkuzo<br />
iliyopo Songea mkoani Ruvuma.<br />
Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 28/12/2012 na<br />
usaili utafanyika tarehe 29/12/2012 katika vituo vya<br />
mtihani vilivyoorodheshwa kwenye fomu ya maombi.<br />
Wahi kuchukua fomu mapema, nafasi zimebakia<br />
chache.<br />
NB: KWA WALE WALIOCHAGULIWA WAFUATE<br />
MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE (JOINING<br />
INSTRUCTION) KATIKA VITUO WALIVYOFANYIA<br />
USAILI.<br />
Kwa maelezo zaidi piga simu: 0716 791113,<br />
0683155902.<br />
MKUU WA SHULE
3<br />
Habari<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
Anachotaka Borafya katu hakiwezekani<br />
Na Mwandishi Wetu<br />
A N A C H O T A K A<br />
Mwenyekiti wa CCM wa<br />
Mkoa wa Mjini, Borafya<br />
Silima, katu hakiwezekani,<br />
wamesema wachambuzi<br />
wa siasa za Zanzibar.<br />
Wa c h a m b u z i h a o<br />
w a m e s e m a k u w a ,<br />
unaposema kuwa unataka<br />
muungano wa serikali mbili,<br />
huwezi tena kuja na hoja ya<br />
kutaka Rais wa Zanzibar<br />
kuwa na mamlaka sawa na<br />
yule wa muungano.<br />
Maoni na uchambuzi huo<br />
umekuja kufuatia maoni<br />
aliyotoa Mwenyekiti huyo<br />
wa CCM, Mjini Unguja<br />
akisema kuwa anataka<br />
Serikali Mbili, ya Muungano<br />
na ya Zanzibar, lakini kila<br />
Serikali iwe na mamlaka<br />
yake kamili.<br />
Mheshimiwa Borafya<br />
alitoa maoni hayo katika<br />
Uwanja wa Alabama,<br />
Shehia ya Miembeni katika<br />
mfululizo wa zoezi la<br />
kupokea maoni ya wananchi<br />
juu ya katiba mpya.<br />
Kwa mujibu wa taarifa<br />
zilizonukuliwa na baadhi ya<br />
vyombo vya habari, katika<br />
maoni yake mheshimiwa<br />
Borafya amesema pia<br />
a n a t a k a w a e n d e l e e<br />
kuwepo Marais wawili,<br />
wa Muungano na wa<br />
Zanzibar.<br />
Hata hivyo akasisitiza<br />
kuwa, Marais wote wawili<br />
wawe na hadhi sawa na<br />
wawe na mamlaka kamili.<br />
Huku akimalizia kwa<br />
kusema kuwa anahimiza<br />
umoja na mshikamano.<br />
Ni kwa maoni yake<br />
hayo wachambuzi wa<br />
mambo wanasema kuwa<br />
unaposema uwe na serikali<br />
mbili, ya muungano na ya<br />
Zanzibar, ni wazi kuwa<br />
Rais wa Zanzibar atakuwa<br />
chini ya Rais wa Muungano<br />
na serikali ya Zanzibar<br />
lazima iwe chini ya ile ya<br />
muungano.<br />
“Ile serikali, ile nchi,<br />
iliyoungana na Zanzibar,<br />
ndiyo inayoweza kuwa na<br />
hadhi sawa na Zanzibar,<br />
kisha juu yake iwepo hiyo<br />
ya muungano, lakini kwa<br />
maoni haya ya serikali mbili,<br />
inakuwa ni kiini macho au<br />
kujidanganya kutaka Rais<br />
wa Zanzibar awe sawa na<br />
wa muungano.”<br />
Amesema mchambuzi<br />
mmoja ambaye amehoji,<br />
“ipo wapi hiyo nchi<br />
inayoungana na Zanzibar na<br />
hiyo serikali inayoungana<br />
na ya Zanzibar ili izaliwe<br />
ya muungano?”<br />
K a t i k a k u f a f a n u a<br />
a k a s e m a k u w a<br />
kinachoonekana hapa ni<br />
kuwa wale walioungana<br />
na Zanzibar wamekuwa<br />
wajanja zaidi ambapo<br />
wamejivisha joho la<br />
muungano na hivyo Rais<br />
wao kuwa ndiye wa<br />
muungano na kuwa juu ya<br />
Zanzibar.<br />
Mchambuzi huyo ambaye<br />
hata hivyo hakutaka kutaja<br />
jina lake akasema kuwa<br />
ili Zanzibar iweze kuwa<br />
na mamlaka na kuwa Rais<br />
mwenye hadhi, hoja ya<br />
kuwa na ama serikali tatu<br />
au muungano wa mkataba<br />
haiwezi kuepukika.<br />
“Ni lazima itambulike<br />
kwanza nchi inayoungana<br />
na Zanzibar ikiwa na serikali<br />
yake kama inavyotambulika<br />
ya Zanzibar, ndio uweze<br />
kuzungumzia kuwa na<br />
serikali mbili na marais<br />
wawili wenye hadhi,<br />
mamlaka na haki sawa ndani<br />
ya muungano, kinyume cha<br />
hivyo ni kiini macho na<br />
kujidanganya.” Alisisitiza<br />
akimalizia maoni yake.<br />
N i k u t o k a n a n a<br />
uchambuzi huo baadhi ya<br />
wananchi waliomsikiliza<br />
kada huyo wa CCM akitoa<br />
maoni yake wanasema<br />
kuwa alichofanya mwana<br />
CCM huyo ni kuunga<br />
mkono msimamo wa wale<br />
wasiotaka muungano wa<br />
serikali mbili, lakini bila ya<br />
kutamka.<br />
“La kufurahisha ni kuwa<br />
pamoja na kukwepa neno<br />
Muungano wa Mkataba,<br />
lakini sasa viongozi<br />
wahafidhina wa CCM nao<br />
wanaungana na Wazanzibari<br />
kutaka mamlaka kamili.<br />
Sisi tunawaambia wasiwe<br />
na wasiwasi, tuko pamoja<br />
katika kutetea haki za nchi<br />
yetu tukufu ya Zanzibar.<br />
Pamoja Daima.” Amesema<br />
m t o a m a o n i m m o j a<br />
akichambua kile alichosema<br />
Borafya.<br />
MWENYEKITI wa CCM wa Mkoa wa Mjini, Borafya Silima.<br />
Mkutano Baraza Kuu kufanyika Kisarawe<br />
Kuzindua Chuo cha Maimam nchini<br />
Na Bakari Mwakangwale<br />
BARAZA Kuu la Jumuiya<br />
na Taasisi za Kiislamu (T),<br />
lipo mbioni kujenga Chuo<br />
Cha Maimam kitakacho<br />
kuwa kikitoa mafunzo<br />
ya uongozi kwa Maimam<br />
nchini.<br />
C h u o h i c h o<br />
kitakachojulikana kwa jina<br />
la Muhaga Imams Collage,<br />
k i t a j e n g w a W i l a y a n i<br />
Kisarawe, katika Mkoa wa<br />
Pwani, kikilenga kuwaandaa<br />
viongozi wa Waislamu<br />
kuanzia ngazi ya mtaa.<br />
U s t a d h i A b u b a k a r i<br />
Abdulswamadu, amebainisha<br />
hayo akiongea na gazeti<br />
hili, katikati ya wiki hii,<br />
akizungumzia mkutano<br />
Mkuu wa Baraza Kuu la<br />
Jumiya na Taasisi za Kiislamu<br />
(T) utakaofanyika Muhaga,<br />
Kisarawe, kuanzia Desemba<br />
14-21, mwaka huu.<br />
Abdulswamad, aliye<br />
Mkurugenzi wa Uchumi<br />
Mipango na Fedha wa<br />
Baraza Kuu, alisema lengo<br />
la kuanzisha Chuo hicho<br />
ni kuandaa viongozi wa<br />
Waislamu wakianzia kwa<br />
Maimam, kwa kuwa wao ndio<br />
viongozi wa daraja la chini na<br />
muhimu kwani ndio viungo<br />
kati ya waumini na viongozi<br />
wa ngazi za juuu.<br />
Alisema, mikakati hiyo ni<br />
kutokana na kile alichodai,<br />
kama kufeli kwa mipango<br />
na mikakati ya Waislamu<br />
kwa muda mrefu hivyo na<br />
kubaini kwamba huenda ni<br />
kwa kukosa viongozi wenye<br />
kujua malengo kuanzia ngazi<br />
ya chini.<br />
Alisema, Maimamu ni<br />
viongozi muhimu kwa jamii<br />
ya Kiislamu kwani wao ndio<br />
muda mwingi wanakuwa na<br />
Waislamu kwa kukutana nao<br />
mara tano kwa kutwa nzima,<br />
katika Misikiti.<br />
Alisema, Baraza Kuu<br />
limeona endapo Maimam<br />
watakuwa na taaluma ya<br />
uongozi na uratibu wa<br />
mipango na namna gani ya<br />
kuwatumia Waislamu kwa<br />
kuwapa mipango maaluma<br />
ya kimaendeleo bila shaka<br />
jamii ya Waislamu itapiga<br />
hatua kwa haraka.<br />
“Lengo la kuanzisha Chuo<br />
Cha Maimam, ni kuwaanda<br />
kuwa viongozi bora wajue<br />
n a m n a y a k u o n g o z a ,<br />
(utawala) wasiishie kuwa tu<br />
na uhodari wa kusoma Qur<br />
an vizuri wanaposwalisha.”<br />
Alisema Abdulswamadu.<br />
Akizungumzia mkutano<br />
huo, alisema mkutano<br />
utafanyika Desemba 21,<br />
mwaka huu, katika kijiji cha<br />
Muhaga, Kisarawe, ambao<br />
utatanguliwa na Mkutano<br />
Mkuu wa Kutayba Saccos,<br />
Desemba 20.<br />
Alisema, kufuatia mipango<br />
na utaratibu huo, Waislamu<br />
kutoka Jijini na Mikoani<br />
wataanza kuelekea huko<br />
(Kisarawe) kuanzia Desemba<br />
14, Ijumaa ya wiki hii (leo),<br />
kwa ajili ya kupiga kambi na<br />
kujiandaa na mikutano hiyo.<br />
Wakiwa huko sambamba<br />
na kufanyia usafi viwanja<br />
hivyo lakini kwa kipindi<br />
chote hicho cha wiki moja<br />
k a b l a y a k u a n z a k w a<br />
mikutano hiyo, Waislamu<br />
kwa ujumla watapata semina<br />
elekezi kutoka kwa viongozi<br />
(Masheikh) wao kutoka<br />
katika Jumuiya na Taasisi<br />
mbalimbali za Kiislamu<br />
nchini.<br />
Alisema, lengo la kuupeleka<br />
Kisarawe, Mkutano Mkuu wa<br />
Baraza Kuu, ni kuwaonyesha<br />
Waislamu ardhi zao zilizo<br />
chini ya Baraza hilo, na<br />
kuweka mipaka baada ya<br />
kufanyika kwa usafi, ili<br />
wawe tayari kuilinda na<br />
kuisimamia.
4<br />
(i) WANAUME<br />
Na JINA MKOA<br />
1 IDDI R. NANA SINGIDA<br />
2 HAMIS J. CHURY SINGIDA<br />
3 OMARY MUSA KANIKI TANGA<br />
4 OMAR S. WAWA SINGIDA<br />
5 YASIN J. RAMADHAN SINGIDA<br />
6 ISMAIL S. MALUNGA SINGIDA<br />
7 YUNUS A. HASSAN SINGIDA<br />
8 RAMADHAN I. MWIRU SINGIDA<br />
9 WAZIRI SEKA TANGA<br />
10 AHMAD K. MENGI KIGOMA<br />
11 ISMAIL H. KULANDEA SINGIDA<br />
12 ABDILLAH SULEIMAN SINGIDA<br />
13 ISHAKA A. NYAMGUNDA DAR ES<br />
14 ALI MOHAMED AMEIR UNGUJA<br />
15 KHALFANI U. YUSUFU KIGOMA<br />
16 JUMA K. SALAZA KIGOMA<br />
17 JUMA JUMANNE SINGIDA<br />
18 MOHAME A. HASSAN PWANI<br />
19 MAHMOUD A. CHANDE RUVUMA<br />
20 HAMZA MAJIDI SHABANI DODOMA<br />
21 MWAZINI BAKARI MAHAMUDA UNGUJA<br />
22 MAHAMUD J. MOHAMADI SINGIDA<br />
23 ABDULLAH SALEH HASSAN UNGUJA<br />
24 MUSTAFA J. ALI MTWARA<br />
25 ABDALLAH HAMIDU MATA DAR ES<br />
26 ABDUMAJID S. MOHAMED KAGERA<br />
27 BASHIRI M. ATHUMAN SINGIDA<br />
28 ALLY H. KIDUMWU SINGIDA<br />
29 ABAS-ABDULRAHMAN SWALEHE ARUSHA<br />
30 ABDILLAH M. LALI SINGIDA<br />
31 KHALID KASSIMU DULLE MANYARA<br />
32 HAMIS HALIFA PIRI DODOMA<br />
33 MAKAME M. AHMAD PWANI<br />
34 HAJI S. ALLY SINGIDA<br />
35 ABDILLAHI HAMIS ARUSHA<br />
36 SHABANI ALLY ISSANI MANYARA<br />
37 BASHIRU OMARI HAMIS DODOMA<br />
38 MOHAMED M. YASIN KIGOMA<br />
39 ALLY M. SAID SINGIDA<br />
40 AL-JABIR H. MSUKUYA SINGIDA<br />
41 KUMSONI J. KUMMALA MTWARA<br />
41 RAMADHANI TENA OMARI<br />
43 SHABAN JUMA FAKI UNGUJA<br />
44 KASSIMU RAJABU<br />
45 MOHAMED R. MWIRU SINGIDA<br />
(ii) WANAWAKE<br />
Na JINA MKOA<br />
1 KURUTHUM OMARY SINGIDA<br />
2 KANJELU MUHAMMED RAJABU SINGIDA<br />
3 AMINA HUSSEIN SINGIDA<br />
4 MAIMUNA R. OMARY TABORA<br />
5 CHIKU S. KANGARA SINGIDA<br />
6 LINDA HUSSEIN MUSSA<br />
7 JAMILA SUDI SINGIDA<br />
8 HUSNA O. MUKHANDY SINGIDA<br />
9 AMINA RAJABU SINGIDA<br />
10 FADHILA M. MAJENGO SINGIDA<br />
11 HIDAYA OMARY SINGIDA<br />
12 ZAMDA I. MTUHI MTWARA<br />
13 REHEMA J. JUMA MANYARA<br />
14 NASRA MUNDA SINGIDA<br />
15 ZENA M. RUGAYA KIGOMA<br />
16 MARIAM H. SWALEHE SINGIDA<br />
17 SHEJUNA MBWANA HUSSEIN<br />
18 MARIAM FADHILI MNDEME ARUSHA<br />
19 AISHA MUSSA MAULID ARUSHA<br />
20 MWANAIMA H. CHAYOA ARUSHA<br />
21 ZAITUNI JUMA RAJABU SINGIDA<br />
22 TATU K. NYONI RUVUMA<br />
23 NICE J. LUTWE KIGOMA<br />
24 KHADIJA I. SENGE SINGIDA<br />
25 PILI A. JUMANNE SINGIDA<br />
26 KHADIJA VUAI HASSAN UNGUJA<br />
27 DIA HASSAN LINDI<br />
28 ASIA OMARY JUMA ARUSHA<br />
29 FAUDHIA J. ALI DAR ES<br />
30 ASHURA M. HAMIS KIGOMA<br />
31 PILI H. LISU SINGIDA<br />
32 ZUHURA ABDULRAHMANI KANGILE<br />
33 TIMA OMARY HAMIS TANGA<br />
34 ASHURA A. ANTHONY MOROGORO<br />
35 TWAINA HAMIS SINGIDA<br />
36 AISHA O. BENDERA TANGA<br />
37 MWANAIDI S. MBIAJI SINGIDA<br />
38 SHEILA MMARI<br />
39 MWANAIDDY IDDY RAMADHANI ARUSHA<br />
40 NZAINABU MWASHONGO<br />
41 NASRA J. SALUM SINGIDA<br />
42 ZAINABU ABUBAKAR SINGIDA<br />
43 RUSMA A. AMASI SINGIDA<br />
44 FARIDA JUMA SINGIDA<br />
45 HABIBA H. IGAE SINGIDA<br />
46 ZAKIA H. ATHUMAN SINGIDA<br />
Tangazo<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
Bismillaahir Rahmaanir Rahiim<br />
ISLAMIC PROPAGATION CENTRE<br />
MATOKEO YA USAILI WA WAOMBAJI WA MAFUNZO YA UALIMU KATIKA VYUO VYA UALIMU VYA IPC<br />
Wafuatao wamafaulu usaili na wamechaguliwa kujiunga na Mafunzo ya muda mfupi ya Ualimu yatakayoanza mwishoni mwa Januari ,2013<br />
katika vyuo vya Ualimu vya Kiislamu Kirinjiko na Ubungo.<br />
Barua za maelekezo ya kujiunga na chuo (joining instructions) yanapatikana vyuoni na katika vituo walikofanyia usaili mikoani.<br />
A: CHUO CHA UALIMU CHA KIISLAMU KIRINJIKO<br />
47 AMINA M. MASUDI SINGIDA<br />
48 AMINA S. KWIMBA SINGIDA<br />
49 KHADIJA UBWA ALI UNGUJA<br />
50 AMINA JUMA MGALA<br />
51 MARYAM ABDALLAH MUHAMMAD DAR ES<br />
52 ZAINAB JAMAL<br />
53 SAIDA A. NDUI SINGIDA<br />
54 AISHA S. HUSSEIN SINGIDA<br />
55 SUKAINA ALLY KHALIFA DAR ES<br />
56 RAHMA HAJI MOHAMED UNGUJA<br />
57 SALMA YAHYA MKILINDI<br />
58 MARIAM KADHI TANGA<br />
59 SUMMAYA M. SULEIMAN DAR ES<br />
60 AZIZA M. MTONDOHIMA DAR ES<br />
61 BIMKUBWA K. AMOUL DAR ES<br />
62 MWANTUMU BAKARY TANGA<br />
63 KHADIJA HUSSEIN MAURIDI<br />
64 RAMLA HASSAN AYUBU ARUSHA<br />
65 MWAJUMA A. IBRAHIM TANGA<br />
66 LULU JUMANNE SINGIDA<br />
67 HADIJA MBARUKU TANGA<br />
68 SICHANA SIMAI MOHAMED UNGUJA<br />
69 ASHA SALEHE MKILINDI<br />
70 ZAMZAM RAMADHANI GOMBO<br />
71 AMINA M. MANGU SINGIDA<br />
72 AISHA K. MITAGO MOROGORO<br />
73 MWAJUMA HAMISI ABEID DODOMA<br />
74 PATIMA ALI MRIDU<br />
75 TAUSI O. RASHID MWANZA<br />
76 JOHARIA HAMIS SINGIDA<br />
77 ZULPHA SHABANI RAMADHANI SINGIDA<br />
78 HAWA K. MOHAMED KIGOMA<br />
79 SWIVAMU R. DUDE SINGIDA<br />
80 ZANURA S. HAMIS SINGIDA<br />
81 AMINAH. O. SALUM KUWAKA DAR ES<br />
82 MWAJUMA A. MKWAHA MTWARA<br />
83 ASIA SAIDI LUBUVA DODOMA<br />
84 FATUMA BARAZA MANYARA<br />
85 SUMAIYA MSANGI<br />
86 SWALHA N. KASAGOLA SHINYANGA<br />
87 TATU R. LUAMBANO RUVUMA<br />
88 NURIAT H. ABRAHAMAN SINGIDA<br />
89 ASHA RAMADHANI DUMA DODOMA<br />
90 MAIMUNA SALIMU RAJABU<br />
91 SOFIA IDDI KIMUNGU RUKWA<br />
92 SOFIA A. NYONYI SINGIDA<br />
93 ASHURA J. ALLY SINGIDA<br />
94 FATMA MUSSA KIMARO<br />
95 ZAINAB MUSTAFA HASSAN DODOMA<br />
96 MAIMUNA A. ATHUMANI ARUSHA<br />
97 HIDAYA HAMISI SALIMU<br />
98 ZAINABU JUMANNE OMAR SINGIDA<br />
99 ASIA JUMA JULA MANYARA<br />
100 MARIAM B. HAMIS ARUSHA<br />
101 FATUMA YAHAYA RUKWA<br />
102 TABU Y. BAKARI SINGIDA<br />
103 SHANIFA R. SAID SINGIDA<br />
104 REHEMA ABBAS MOROGORO<br />
105 NAHIDA HUSSEIN HAMZA<br />
106 FARIDA J. KISUDA SINGIDA<br />
107 WIDADU MOHAMED RAMADHANI ARUSHA<br />
108 SHUFAA MUSSA IDDY ARUSHA<br />
109 HAWA MUSSA MOHAMMED ARUSHA<br />
110 RAMLA ISMAILI<br />
111 ASHA BAGHAMOYO MANYARA<br />
112 MARYAM L. JUMA<br />
113 MWAJUMA BAKARI MANYARA<br />
114 HAFSWA SULAYMAN PWANI<br />
115 HALMA K. RASHID DAR ES<br />
116 ZIADA S. RUSAMBO RUKWA<br />
117 FATUMA S. RUVAKO TABORA<br />
118 BINZUA HAJI MUSSA<br />
119 KHAIRATH A. SULEIMAN ARUSHA<br />
120 SAUDA YUSUFU JUMA DODOMA<br />
121 RAHMA JUMANNE MANGI MANYARA<br />
122 MWAJUMA SALIMU MADEGHE<br />
123 SALAMA S. KAMBI TANGA<br />
124 HAWA ABDALLAH SINGIDA<br />
125 ZUBEDA R. HEMED TANGA<br />
126 MWANAKHAMIS H. MOHAMED PWANI<br />
127 MWANAHARUSI SWALEHE TANGA<br />
128 RUKIA MOHAMEDI SINGIDA<br />
129 PILI H. BUHULU SINGIDA<br />
130 AMINA RAMADHANI MATEMANGA MOROGORO<br />
131 HADIJA S. KEJO<br />
132 FAUZIA ISSA MANYARA<br />
133 ZEINABU KARIMU JUMA ARUSHA<br />
134 AISHA ABDUL MSANGI<br />
135 MARIAMU M. MTANDU MOROGORO<br />
136 RUKIA B. KAYINGA MBEYA<br />
137 ZAINABU ABDUL HAMIS ARUSHA<br />
138 FATMA MUSSA<br />
139 SAADA A. ZAHOR DAR ES<br />
140 FATUMA HASSAN PWANI<br />
141 ZUHURA HAJI OTHMANI SINGIDA<br />
142 HAWA H. MTEPA DAR ES<br />
143 MARYAM A. MUSSA DAR ES<br />
144 HAWA J. HASSAN DAR ES<br />
145 ASIA H. PANGANI MBEYA<br />
146 SHADIA T. TWAIBU KAGERA<br />
147 AMINANI SUEDI DAUDI<br />
148 MWANAHAMIS K. MOHAMED TANGA<br />
149 SAUMU M. KIVURANDE TANGA<br />
150 MWAJUMA SEBA KIGOMA<br />
151 FADHILA ATHUMANI SINGIDA<br />
B: CHUO CHA UALIMU CHA<br />
KIISLAMU UBUNGO<br />
M A J I N A YA WA L I O C H A G U L I WA<br />
KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU YA<br />
MUDA MFUPI -2013<br />
(i) WANAUME<br />
Na JINA<br />
1 ISSA RASHID MASANJA<br />
2 MWINDADI BAUSI MZEE<br />
3 ILYASA JUMA SAIDI<br />
4 HAJI SAID MWINSHEHE<br />
5 HUSENI ALLY<br />
6 SAID MOHAMMED MIKONGO<br />
7 IDD ATHUMANI KAMBI<br />
8 ALLIY ABDALLAH ALIY KHAMIS<br />
9 MOHAMMED HUSSEIN JUMA<br />
10 JAMAL SHEIKH YAHYA<br />
11 ISSA YUSUPH KITENGE<br />
12 SALUM MOHAMED KINJULI<br />
13 ABUBAKARI ALLY NGINDIKA<br />
14 KISMA ABDILLAH ZABURA<br />
15 KIPUKA HASSANI ISMAIL<br />
(ii) WANAWAKE<br />
Na JINA<br />
1 HIDAYA ALLY KIBAVU<br />
2 HUSNA MUHAMMAD MBELA<br />
3 AISHA MUSSA SAIDI<br />
4 SALMA ABDALLAH KAISI<br />
5 HAWA HAMIDU MSANGI<br />
6 ARAFA ALLY<br />
7 FATMA ABDALLAH MASOUD<br />
8 NURU HAMISI NYUMBA<br />
9 SHARIFA JUMA IBRAHIM<br />
10 HAMIDA ABUBAKAR<br />
11 SOFIA YUSUF KIHAMBWE<br />
12 ZAINAB SULEIMAN MAGWATI<br />
13 TATU HAMZA MAALIM<br />
14 STARA MIGILA<br />
15 FATIMA SALUM KIMATILO<br />
16 HAWA MZEE MANGAMBA<br />
17 AISHA KIBWANA KASUKA<br />
18 REHEMA HASSANI HEMEDI<br />
19 SALMA MOHAMED ALLY<br />
20 TIMA KHAMIS MURI<br />
MUHIMU<br />
Nafasi kwa chuo cha Ubungo bado<br />
zipo<br />
Usaili wa mara ya pili kwa chuo cha<br />
Ubungo tu utafanyika chuoni siku ya<br />
Jumamosi ya tarehe 05/01/2013 saa<br />
2:00 asubuhi. Fomu za kujiunga na<br />
kozi zinaendelea kutolewa Chuoni kwa<br />
gharama ya Tsh 5,000/=<br />
Tafadhali wahi nafasi hii adhimu.<br />
Kwa maelezo zaidi fika chuoni au<br />
wasiliana na Mkuu wa Chuo kwa namba<br />
ya simu 0712557099 au 0688131397.<br />
Wabillaah Tawfiiq<br />
MKURUGENZI
5<br />
LUSAKA<br />
RAIS wa Zambia, Michael<br />
Satta, ametahadharisha<br />
juu ya harakati mpya za<br />
kundi linalotaka kujitenga<br />
la Barotseland Magharibi<br />
mwa nchi hiyo.<br />
Barotseland, ni jina la<br />
eneo lililoko nchini Zambia,<br />
ambalo hivi sasa linaitwa<br />
mkoa wa Magharibi.<br />
Wakati wa uhuru wa<br />
Zambia kwa mujibu wa<br />
makubaliano yaliyofikiwa<br />
kati ya mkoloni Muingereza<br />
na Keneth Kaunda, kiongozi<br />
wa mapambano ya uhuru wa<br />
nchi hiyo yaliyotiwa saini<br />
Oktoba 24 1964, eneo hilo<br />
lilitambuliwa kuwa ardhi ya<br />
Zambia.<br />
Hata hivyo kwa mtazamo<br />
wa watu wa kabila la Lozi,<br />
ambao ndio wakazi wengi<br />
wa eneo hilo la Barotseland,<br />
serikali ya Lusaka kamwe<br />
haikuyaheshimu makubaliano<br />
hayo.<br />
K w a m u j i b u w a<br />
makubaliano hayo, wakazi<br />
wa eneo hilo walipewa hiyari<br />
ya kuwa mamlaka ya ndani na<br />
kujitegemea katika masuala<br />
ya kiuchumi na kisiasa.<br />
Baada ya kupita karibu<br />
nusu karne tangu kutiwa<br />
saini makubaliano hayo,<br />
wananchi wa kabila la Lozi<br />
walikandamizwa na polisi<br />
katika vurugu kwenye<br />
maandamano yaliyoitishwa<br />
na harakati ya kukomboa<br />
eneo hilo kwenye mji wa<br />
Mongu, makao makuu ya<br />
mkoa wa Magharibi.<br />
Tukio hilo kwa mara<br />
nyingine liliamsha azma ya<br />
kutaka kujitenga Barotseland,<br />
ambayo ilijitokeza mwaka<br />
1999 nchini humo. Mwaka<br />
mmoja baadaye. pia maelfu<br />
ya wakazi wa mji wa Mongu<br />
walifanya uasi ambapo baadhi<br />
yao waliuawa.<br />
Licha ya hayo, viongozi<br />
wa harakati ya ukombozi wa<br />
Barotseland, wamesisitiza<br />
kwamba wataendeleza<br />
harakati zao za kudai uhuru<br />
wa eneo hilo kutoka kwa<br />
serikali kuu kwa njia za<br />
amani.<br />
Wachambuzi wa mambo<br />
wanaamini kuwa, makundi<br />
m a t a t u m a k u m b w a<br />
yanayopigania ukombozi<br />
wa eneo la Barotseland,<br />
yanapaswa kuunda chama na<br />
kuanza harakati za kisiasa.<br />
Mwaka 2011 wakati<br />
wa kampeni za uchaguzi,<br />
Rais Michael Satta aliahidi<br />
kuwa iwapo angeshinda<br />
angetekeleza matakwa ya<br />
kabila la Lozi.<br />
Lakini kiongozi huyo<br />
hakutekeleza ahadi hiyo na<br />
maandamano ya wakazi wa<br />
Habari za Kimataifa/Tangazo<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
Zambia yakumbwa na harakati za kundi linalotaka kujitenga<br />
eneo hilo linalotaka kujitenga<br />
yakaendelea.<br />
Wakati huo huo, makabila<br />
ya Nkoya na Mbunda, ambayo<br />
yanaishi na kabila la Lozi<br />
kwenye eneo la Barotseland,<br />
yanapinga fikra ya kutaka<br />
kujitenga eneo hilo.<br />
Viongozi wa makabila<br />
hayo mwezi Juni mwaka<br />
2012 walisisitiza kwamba,<br />
makabila hayo kamwe<br />
h a y a t o h e s a b i w a k u w a<br />
sehemu ya sehemu ya eneo<br />
na yanapinga kugawanywa<br />
ardhi ya Zambia.<br />
Hata hivyo, Baraza la Taifa<br />
la Barotseland katika kikao<br />
cha dharura cha Julai mwaka<br />
huu, lilijitangazia uhuru<br />
wa upande mmoja. Taarifa<br />
ya kikao hicho ilitumwa<br />
kwa taasisi za kieneo za<br />
SADC, Umoja wa Afrika,<br />
Commonwealth na Umoja wa<br />
Mataifa ili jamii ya kimataifa<br />
iunge mkono na kutambua<br />
kujitenga eneo hilo.<br />
Hivi sasa harakati mpya<br />
za kundi hilo zimemtia<br />
wasiwasi Rais Michael Satta,<br />
hasa baada ya wanaharakati<br />
wapya 630 kujiunga na kundi<br />
hilo. Licha ya hayo, Satta<br />
amewataka maafisa wa jeshi<br />
wakabiliane kwa amani na<br />
wafuasi wa kundi hilo.<br />
Nchi nyingi za kusini mwa<br />
Jangwa la Sahara kama vile<br />
Zambia, Angola na Nigeria<br />
zinakabiliwa na makundi<br />
yanayotaka kujitenga na<br />
zinafanya jitihada za kutatua<br />
migogoro hiyo kwa amani na<br />
kuzuia kugawanyika ardhi za<br />
nchi hizo.<br />
The Hague kusikiliza mashtaka ya Wapalestina dhidi ya Israel<br />
BAADA ya Baraza Kuu<br />
la Umoja wa Mataifa<br />
kupandisha hadhi ya<br />
Palestina katika Umoja<br />
wa Mataifa, na kuwa nchi<br />
mtazamaji asiyekuwa<br />
mwanachama rasmi, sasa<br />
mahakama ya The Hague<br />
huko Uholanzi imetangaza<br />
kuwa itaanza kushughulikia<br />
mashtaka yaliyowasilishwa<br />
na Wapalestina dhidi ya<br />
utawala wa Israel.<br />
Ofisi ya Mwendesha<br />
M a s h t a k a M k u u w a<br />
mahakama ya The Hague<br />
imetangaza kuwa, hivi<br />
karibuni itachunguza suala<br />
la kupandishwa hadhi ya<br />
Palestina katika Umoja wa<br />
Mataifa na kushughulikia<br />
mashtaka ya Wapalestina<br />
kuhusu jinai zilizofanywa na<br />
askari wa Israel katika vita<br />
vya siku 22 dhidi ya watu<br />
wa Gaza.<br />
Mwaka 2009 Wapalestina<br />
waliwasilisha mashtaka<br />
rasmi katika Mahakama ya<br />
Jinai ya Kimataifa ya The<br />
Hague, wakiitaka ichunguze<br />
jinai zilizofanywa na jeshi la<br />
Israel katika vita vya siku 22<br />
huko Gaza.<br />
Hata hivyo mashtaka hayo<br />
yalikataliwa na mahakama ya<br />
The Hague kwa kuwa wakati<br />
huo, Palestina ilikuwa bado<br />
haijatambuliwa rasmi kuwa<br />
nchi mtazamaji katika Umoja<br />
wa Mataifa.<br />
K w a m s i n g i h u o ,<br />
kuanzia sasa Mahakama<br />
hiyo itakuwa na uwezo wa<br />
kisheria wa kuchunguza na<br />
kushughulikia mashtaka<br />
yote yanayowasilishwa na<br />
Wapalestina.<br />
Kwa mujibu wa sheria<br />
za kimataifa, nchi ndizo<br />
zinazoweza kuwasilisha<br />
mashtaka katika Mahakaya<br />
ya Kimataifa ya The Hague.<br />
Kabla ya uamuzi wa tarehe<br />
29 Novemba wa Baraza Kuu<br />
la Umoja wa Mataifa ambao<br />
uliitambua Palestina kuwa ni<br />
nchi mtazamaji, hapakuwepo<br />
uwezekano wa kusikilizwa<br />
mashtaka ya Wapalestina<br />
dhidi ya Israel.<br />
Hata hivyo utawala<br />
wa Israel na washirika<br />
wake wakubwa hususan<br />
Marekani, walifanya jitihada<br />
kubwa kukwamisha suala<br />
la kutambuliwa Palestina<br />
kuwa ni nchi, japo isiyo<br />
mwanachama katika Umoja<br />
wa Mataifa.<br />
Kufuatia utambuzi huo,<br />
Rais wa Mamlaka ya Ndani ya<br />
Palestina, Mahmoud Abbas,<br />
alitangaza mara tu baada ya<br />
kurejea Ramallah akitokea<br />
New York, kwamba Quds<br />
Tukufu ndio mji mkuu wa<br />
milele wa nchi ya Palestina.<br />
Alisema sasa Wapalestina<br />
wamepata nchi na wanaweza<br />
kuwasilisha matakwa yao<br />
halali katika jamii ya<br />
kimataifa. Karibu asilimia<br />
75 ya jamii ya kimataifa<br />
imewapigia kura ya ndio<br />
watu wa Palestina.<br />
Rais Abass amesema kuwa<br />
mafanikio hayo, yatabadilisha<br />
mlingano wa nguvu za kisiasa<br />
katika Mashariki ya Kati<br />
Ustadh Abdul Basit akumbukwa<br />
CAIRO<br />
Shughuli ya kumkumbuka<br />
hafidh na msomaji mashuhuri<br />
wa Qur’ani, Ustadh Abdul<br />
Basit Abdul Samad, imefanyika<br />
Ijumaa iliyopita nchini Misri<br />
na kuhudhuriwa na wasomi na<br />
wapenzi wa Qur’ani Tukufu.<br />
Wanafunzi na wapenzi wa<br />
Hafidh huyo mashuhuri wa<br />
Qur’ani, wanachama wa Jumuiya<br />
ya Masomaji Qur’ani ya Misri na<br />
Masheikh wakubwa kama Sheikh<br />
Mahmoud Tablawi, Mahmoud<br />
Siddiq Minshawi, Muhammad al<br />
Halbawi, wawakilishi wa Kituo<br />
cha Kiislamu cha al Azhar na<br />
Wizara ya Wakfu ya Misri na<br />
Mabalozi wa nchi za Kiarabu<br />
na Kiislamu nchini humo, pia<br />
walishiriki katika shughuli hiyo<br />
ya kumbumbuka msomaji huyo<br />
mashuhuri katika ulimwengu wa<br />
Kiislamu.<br />
U s t a d h A b d u l B a s i t<br />
Muhammad Abdul Samad aliaga<br />
dunia Desemba 30 mwaka 1988<br />
huko Cairo Misri.<br />
Alianza kujifunza Qur’ani<br />
Tukufu akiwa bado mtoto mdogo<br />
na alipewa tuzo ya kuhifadhi na<br />
kusoma Qur’ani akiwa na umri<br />
wa miaka 12. Kipindi fulani<br />
Ustadh Abdul Basit alitumia<br />
muda wake mwingi kusafiri<br />
katika nchi za Kiislamu na<br />
kuwahamasisha watu kusoma<br />
kitabu cha Mwenyezi Mungu.<br />
Ustadh Abdul Basit ameacha<br />
kanda nyingi za Sauti zake<br />
akisoma Qur ’ani Tukufu,<br />
ambazo bado zinawavutia<br />
wasomaji wengi wa Qur’ani.<br />
Alianza kujifunza Qur’ani<br />
Tukufu akiwa bado mtoto mdogo<br />
na alipewa tuzo ya kuhifadhi na<br />
kusoma Qur’ani akiwa na umri<br />
wa miaka 12.<br />
Ustadh Abdul Basit wakati wa<br />
uhai wake, alitumia muda wake<br />
mwingi kusafiri katika nchi za<br />
Kiislamu na kuwahamasisha<br />
watu kusoma kitabu cha<br />
Mwenyezi Mungu.<br />
Abdul Basit alizaliwa<br />
mwaka 1927 na kufariki mwaka<br />
1988. Ni msomaji Qur’an pekee<br />
aliyewahi kushinda mara tatu<br />
katika mashindano ya kusoma<br />
Qur’an duniani katika miaka<br />
ya 1970s.<br />
Aidha ni miongoni mwa<br />
wasomaji walioweza kuuza kazi<br />
nyingi zilizorekodiwa akisoma<br />
Qur’ani na alikuwa Rais wa<br />
chama cha wasomaji wa Qur’an<br />
Misri.<br />
DAEE YOUTH ART GROUP<br />
Inakutangazia Semina ya Ndoa na<br />
Talaka kwa mujibu wa Qur-aan na Sunnah<br />
itakayofanyika.<br />
Siku: Jumamosi na Jumapili, kwa wiki<br />
12.<br />
Kozi itaanza Tarehe 15-12-2012 Saa 2<br />
Asubuhi- 8 Mchana.<br />
Mahali: Answar Islamic Model School-<br />
Kinondoni Studio<br />
Vyeti vitatolewa kwa watakao maliza<br />
m a f u n z o m p a k a m w i s h o , M a d a<br />
zitakazofundishwa ni pamoja na, Taratibu<br />
ya kutafuta mchumba, sifa zake, Ndoa na<br />
Nguzo Zake, haki za Mke kwa Mume na<br />
Mume kwa Mke, Eda Talaka na athari zake,<br />
Mirathi kwa mjane, Ndoa ya Mke Zaidi ya<br />
Moja na taratibu zake, Malezi ya Watoto,<br />
Jimai na Migogoro ndani ya Ndoa N.k.<br />
Kwa mawasiliano zaidi piga simu 0715-24<br />
7262/ 0715- 114373.<br />
Nyote mnakaribishwa Wake kwa Waume
6<br />
MWEZI wa Oktoba, 2012<br />
yalitokea matukio makubwa<br />
mawili ya kusikitisha jijini Dar<br />
es Salaam eneo la Mbagala.<br />
Tukio la kwanza ni la kijana<br />
wa Kikristu kokojolea Quran<br />
tukufu lilofuatiwa na tukio<br />
la pili la uchomaji wa kanisa<br />
katika eneo hilo. Tukio la<br />
ukojoleaji Quran liliwaumiza<br />
sana Waislam na tukio la<br />
uchomaji kanisa liliwaumiza<br />
sana Wakristu pia liliwaudhi<br />
sana Waislamu. Liliwaudhi<br />
sana Waislamu kwa maana si<br />
katika mafundisho ya Uislamu<br />
kufanya vitendo kama hivyo.<br />
Wakristu wa KKKT kupitia<br />
kwa viongozi wao walitoa<br />
tamko kudhihirisha hisia zao.<br />
Katika tamko lao walielezea<br />
madhumuni yao makuu matatu<br />
ya kutembelea eneo la Mbagala.<br />
Madhumuni haya kwa ufupi<br />
ni haya yafuatayo: Kuwapa<br />
pole na kusimama pamoja na<br />
waumini wenzao wa Mbagla<br />
walioathirika na uchomaji<br />
kanisa. Kuonesha majonzi kwa<br />
vitendo vya uvunifu wa amani na<br />
kuporomoka kwa mshikamano<br />
wa Watanzania. Kushiriki pamoja<br />
kupokea matumaini ya Tanzania<br />
mpya itakayozaliwa, itakayojali<br />
upendo, uvumilivu, ustahmilivu,<br />
umoja, mshikamano, uhuru wa<br />
kuabudu na dola isiyo na dini.<br />
Dhumuni la tatu waliliandika<br />
kwa wino uliokolezwa kuonesha<br />
kuwa ndilo muhimu sana<br />
kulinganisha na madhumuni<br />
mengine mawili. Wanaeleza<br />
kuwa kilichotokea Mbagala ni<br />
matokeo ya mbegu iliyopandwa<br />
katika bustani njema na sasa<br />
inaanza kuzaa matunda, na<br />
kwamba hizi ni dalili zilizoanza<br />
kitambo na hazikushughulikiwa<br />
na waliomrithi baba wa taifa.<br />
Wanasema kuwa dalili hizo ni:<br />
Uchochezi wa wazi kuwa taifa<br />
hili linaendeshwa na unaoitwa<br />
mfumokristu. Ubishi juu ya idadi<br />
ya waumini wa dini mbalimbali.<br />
Matumizi mabaya ya baadhi ya<br />
vyombo vya habari. Ukimya wa<br />
vyombo vya dola juu ya vitendo<br />
vya uvunjifu wa sharia. Na<br />
Madai yasiyo ya kawaida kwa<br />
serikali inayodaiwa kutokuwa<br />
na dini.<br />
Wanayataja madai hayo<br />
kuwa ni: Kulazimisha uvaaji wa<br />
alama za dini katika taasisi za<br />
umma. Madai ya kutaka balozi<br />
za nchi fulani kufungwa hapa<br />
nchini. Madai na mashinikizo<br />
ya uanzishwaji wa mahakama<br />
za kidini. Mashinikizo ya<br />
kidini yanayoingilia mifumo ya<br />
kitaalam na kisheria. Mashinikizo<br />
ya kidini juu ya mfumo wa uteuzi<br />
wa watendaji wa serikali na<br />
katika ofisi za umma. Kuhoji<br />
juu ya ushirikiano wa serikali na<br />
mashirika ya dini katika utoaji<br />
wa huduma za afya na elimu.<br />
Nianze na nukta ya kwanza<br />
ya kuwa taifa linaendeshwa<br />
na mfumokristu. Nini maana<br />
ya mfumo? Sambamba na<br />
mfumokristu tumekuwa pia<br />
tukisikia MfumoDume. Hebu<br />
tuangalie mfumodume nini?<br />
Makala/Tangazo<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
Maaskofu wanapiga porojo kupotosha ukweli<br />
Na Ibni Mustafa<br />
Lengo kuendeleza dhulma ya mfumokristo<br />
Maana yake ni kwamba<br />
mfumo wa utawala wa nchi<br />
unawapendelea zaidi wanaume<br />
kuliko wanawake. Sasa chukua<br />
maana hii itumbukize katika<br />
neno mfumokristu, maana yake<br />
ni kwamba utawala wa nchi<br />
unawapendelea zaidi wakristu<br />
na ukristu kuliko Waislamu na<br />
Uislamu. Kitendo cha wanaume<br />
kuwa ndio wengi katika nafasi<br />
za maamuzi na ajira kuliko<br />
wanawake ndio mfumodume<br />
wenyewe. Vilevile wanaodai<br />
kuwa kuna mfumokristu<br />
w a n a m a a n i s h a k w a m b a<br />
mfumo wa utawala wa nchi<br />
unawapendelea zaidi Wakristu<br />
na Ukristu kuliko Waislamu.<br />
Upendeleo kwa ukristu ni kama<br />
vile: Nchi kutambua kuwa<br />
siku za ibada za Wakristu za<br />
Jumamosi na Jumapili ndizo<br />
siku za mapumziko kwa wote<br />
wakati Ijumaa ambayo ndio<br />
siku ya ibada kwa Waislamu<br />
haitambuliwi. Kutambulika<br />
kwa tarehe ya kuanza kwa<br />
mwaka wa Kikristu kuwa ni<br />
siku kuu kitaifa, wakati siku ya<br />
kuanza kwa mwaka wa Kiislamu<br />
haitambuliwi, kwa taasisi za<br />
umma kama mashule kupumzika<br />
katika mwezi wa 12 katika<br />
mwaka ambao ni mwezi mtukufu<br />
kwa Wakristu wakati mwezi<br />
mtukufu wa Waislamu ambao ni<br />
Ramadhani hautambuliki. Haya<br />
ni machache yanayoonesha nchi<br />
kuongozwa na mfumokristu.<br />
Mfumokristu pia unaonekana<br />
katika idadi ya Wakristu katika<br />
nafasi za maamuzi, taasisi za<br />
umma zikiwemo elimu ya juu<br />
ambayo haizidi asilimia 25. Huu<br />
ndio mfumokristu.<br />
Wanaopinga kuwa hakuna<br />
mfumokristu watakwambia<br />
mbona Rais na makamo wake<br />
ni Waislamu. Hawa ama<br />
wanapotosha makusudi ama<br />
hawaelewi. Hawaangalii ni<br />
asilimia ngapi ya Waislamu ni<br />
Mawaziri, Wabunge, Wakuu<br />
wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya,<br />
Wakurugenzi wa mashirika<br />
ya umma na wafanyakazi wa<br />
umma kwa ujumla. Wanao<br />
dai mfumodume kwa mfano<br />
hawamaanishi kuwa hakuna<br />
wananwke kabisa katika nafasi<br />
za umma la hasha, wanajua<br />
kuwa wapo lakini idadi yao ni<br />
ndogo kulinganisha na idadi yao<br />
katika taifa. Wale wanaokana<br />
kuwepo mfumokristu kwa<br />
kumuangalia Rais na mkamu<br />
wake wanashindwa kuelewa<br />
kuwa hata Rais anamezwa na<br />
mfumo wa utawala ambao<br />
unaegemea ukristu, Rais kama<br />
yeye hana uwezo wa kubadilisha<br />
mfumo kwa mfano aseme<br />
kuanzia leo siku ya Ijumaa ni<br />
siku ya mapumziko kitaifa ili<br />
kwa vile yeye ni Muislamu apate<br />
nafasi ya kwenda kwenye ibada,<br />
hana uwezo wa kubadilisha<br />
wimbo wa Taifa ambao umo<br />
ndani ya Biblia ya Wakristu nk.<br />
Wanaodai mfumodume hawana<br />
nia ya kuwafarakanisha au kuleta<br />
uadui baina ya wanaume na<br />
ASKOFU Mkuu wa KKKT, Dkt. Alex Malasusa.<br />
wanawake bali wanchodai ni haki<br />
itendeke kwa wote bila ubaguzi<br />
wa kijinsia, vilevile wanaodai<br />
mfumokristu hawana nia wala<br />
lengo la kuwagombanisha<br />
Waislamu na Wakristu bali<br />
wanachotaka ni haki itendeke<br />
bila ubaguzi wa kidini, na hii ni<br />
kwa ajili ya mustaqabali mwema<br />
na ustawi wa nchi. Inaeleweka<br />
bayana kuwa mfumokristu<br />
kama ulivyo mfumodume ni<br />
mambo yaliyosababishwa na<br />
historia. Tanzania ilitawaliwa<br />
na wakoloni Wakristu kuanzia<br />
kwa Wareno, Wajerumani<br />
na Waingereza, mfumo wao<br />
wa utawala uliongozwa na<br />
Ukristu na asili ya sheria zao<br />
ni Ukristu. Tulipodai uhuru<br />
na hatimae kujitawala tulitaka<br />
mambo ya upendeleo wa kidini<br />
usiwepo, lakini bahati mbaya<br />
tuliishia kwenye maneno wakati<br />
matendo ni muendelzo uleule wa<br />
ukoloni.<br />
Kwa maoni yangu, yale<br />
mambo yanayoupendelea<br />
Ukristu kama vile siku za ibada<br />
za Jumamosi na Jumapili,<br />
sikukuu ya mwaka mpya wa<br />
Kikristu sina matatizo navyo,<br />
hapa ningedai kuwa siku ya<br />
Ijumaa kuanzia saa 6 mpaka<br />
8 mchana ambayo ni masaa<br />
matatu yatambuliwe kuwa ni<br />
muda wa ibada kwa Waislamu<br />
na hivyo kipindi hicho shughuli<br />
rasmi za serikali zisimamshwe<br />
ili Waislamu wafanye ibada<br />
halafu waendelee na kazi baada<br />
ya ibada. Pia tarehe 1 ya mwaka<br />
mpya wa Kiislamu itambuliwe<br />
kuwa ni siku ya mapumziko.<br />
Kwa mfumo unaowapendelea<br />
Wakristu uwekwe utaratibu<br />
wa kuhakikisha upendeleo<br />
h a u e n d e l e i k a m a v i l e<br />
ambavyo ubaguzi wa kijinsia<br />
unavyoshughulikiwa vilevile<br />
ubaguzi wa kidini katika<br />
ajira na utumishi wa umma<br />
ushughulikiwe. Ubaguzi ni<br />
ubaguzi tu uwe wa kijinsia au<br />
kidini. Tena wa kidini ni mbaya<br />
sana kwa sababu matokeo yake<br />
ni kuliparaganyisha taifa. Suala<br />
la dini limefanywa nyeti kiasi<br />
anayelizungumzia kwa ajili ya<br />
kurekebeshwa anaitwa kuwa<br />
ndie mdini.<br />
Nukta ya pili ya viongozi wa<br />
KKKT inahusu ubishi wa idadi<br />
ya waumini wa dini mbalimbali.<br />
Ni kwa vipi hili linaweza<br />
kuwa chanzo cha kuhatarisha<br />
amani? Hawakutufafanulia.<br />
Viongozi hawa wanaelewa wazi<br />
kuwa kujua idadi ya waumini<br />
halijawahi kuwa tatizo popote<br />
kama kila raia anapata haki yake<br />
stahiki, hili liliongelewa sana<br />
wakati wa sensa, kwa kuvuta tu<br />
kumbukumbu, nilifuatilia sensa<br />
mbalimbali duniani nchi nyingi<br />
kama sio zote zinafanya sensa<br />
kwa idadi ya kila kundi liwe la<br />
kidini au kabila, mfano majirani<br />
zetu wa Kenya na Uganda katika<br />
sensa zao wanafanya sio tu<br />
kujua idadi ya waumini wa dini<br />
mbalimbali bali hata madhehebu.<br />
Mtu yeyote akitaka kujua KKKT<br />
ni wangapi Kenya na Uganda<br />
anapata taarifa hizi kwenye ofisi<br />
za takwimu. Hatujasikia vita vya<br />
kidini katika nchi hizo eti kwa<br />
vile watu wa dini fulani ni wengi<br />
kuliko wengine.<br />
KKKT wanataja kuwa kuna<br />
madai yasiyo kawaida ambayo<br />
eti ni pamoja na kulazimisha<br />
uvaaji wa alama za dini katika<br />
taasisi za umma. Hawakufafanua<br />
ni kina nani wanalazimisha na<br />
ni alama zipi zinalazimishwa.<br />
Sijawahi kusikia mtu yeyote<br />
amelazimishwa kuvaa alama<br />
yoyote ya kidini uwe msalaba<br />
au labda hijabu. Jaalia kuwa<br />
labda hapa walimaanisha hijabu<br />
kwa akina mama na akina dada<br />
Waislamu. Kwa Waislamu hijabu<br />
ni suala la ibada.<br />
Katika kipindi cha Baba<br />
wa Taifa kwa kiwango fulani<br />
kilikuwa ni kipindi cha utata kwa<br />
Waislamu. Ilikuwa ni vigumu<br />
kwa Muislamu kutekeleza vema<br />
Uislamu wake bila kupoteza<br />
haki zake za kiraia. Kwa mfano<br />
ilikuwa haiwezekani mtoto wa<br />
kike wa Kiislamu kupata haki<br />
yake ya elimu bila kwenda<br />
kinyume na maamrisho na<br />
maadili ya dini yake ya kuvaa<br />
hijabu. Kwa Muislamu ilikuwa<br />
ni ama kunyoa au kusuka, yaani<br />
avunje amri ya hijabu apate haki<br />
ya elimu au akose haki yake ya<br />
ibada ya hijabu apate kusoma.<br />
Binafsi ninawafahamu akina<br />
dada walioikosa elimu kwa<br />
sababu wazazi wao hawakuwa<br />
tayari kuona mabinti zao<br />
wakitembea nusu uchi kwa<br />
vimini ambavyo ndio ilikuwa<br />
sare ya shule.<br />
Kitendo cha serikali ya<br />
awamu ya pili chini ya Mzee Ali<br />
Hassan Mwinyi kuruhusu hijabu<br />
mashuleni, ilikuwa kitendh cha<br />
kishujaa kwake na cha kihistoria<br />
na ukombozi kwa wanawake wa<br />
Tanzania. Hata hivyo pamoja<br />
na umuhimu wa hijabu kwa<br />
Waislamu bado kwa Watanzania<br />
ni suala la khiyari hakuna<br />
anayelazimishwa kuivaa. Ni<br />
wale tu ambao wanajua umuhimu<br />
wake na wenye mapenzi na dini<br />
yao wanaotekeleza ibada hii<br />
adhimu. Pamoja na kuchukizwa<br />
na uvaaji wa hijabu kwa akina<br />
mama na akina dada Waislamu<br />
bado tunawasihi wenzetu<br />
hawa wa KKKT na wenzao<br />
watuvumilie, watustahamilie<br />
kama walivyoeleza katika<br />
dhumuni lao la 3. Sitarajii kwa<br />
serikali yoyote kuturudisha tena<br />
gizani baada ya kupambazukiwa<br />
wala Waislamu wa nchi hii<br />
hawako tayari kurudishwa huko.<br />
Hata katika katiba mpya nina<br />
hakika kipengele cha uhuru wa<br />
kuabudu kitaendelea kuwepo.<br />
Kipengele hiki kinatoa hakikisho<br />
la uhuru wa ibada ikiwemo<br />
uvaaji wa hijabu bila kuwekewa<br />
vikwazo.<br />
Nimalizie kwa kutoa wito<br />
kwa Watanzania kujifunza<br />
k u v u m i l i a n a k w a y a l e<br />
tunayotafutiana na kushirikiana<br />
kwa yale yanayotushirikisha.<br />
Waislamu hata tungetamani vipi<br />
dunia yote wawe ni Waislamu<br />
haiwezekani labda atake<br />
Mwenyezi Mungu. Vilivile hata<br />
Wakristu wangetamani vipi hata<br />
kama kila mmoja wao angeacha<br />
shughuli zote ili afanye shughuli<br />
moja tu ya kuwabatiza watu<br />
haiwezekani kuifanya dunia<br />
kuwa ni Wakristu.<br />
Tukifuata mafundisho na<br />
maadili ya dini zetu yanayotutaka<br />
kutendeana haki, ninaamini<br />
tutaishi vizuri.<br />
(Kamaludin@yahoo.com)
7<br />
T U K I WA t u m e f u a t a n a<br />
tukifuatilia umbea (maongezi<br />
ya kawaida) kwenye simu,<br />
njia pekee ya mawasiliano<br />
iliyokuwapo, sambamba na<br />
hofu ya msongamano wa<br />
magari katika Jiji la Dar<br />
es Salaam, rafiki yangu<br />
mwanamke, aliniarifu juu ya<br />
msiba wa kifo cha rafiki wa<br />
baba yake.<br />
Kwa kuzivuta hisia, nilitamka,<br />
“sikudhania kwamba ulikuwa wa<br />
karibu na marehemu”. Ukimya<br />
na majibu yake yasiyoridhisha<br />
“siyo uhakika lakini unajua mara<br />
ya mwisho nilipokutana naye<br />
alisema hayo hayo ya kushangaza<br />
kuhusiana na baba yangu”,<br />
huenda bila hata ya kusema,<br />
rafiki yangu anamuhusudu sana<br />
baba yake; naweza kuamini<br />
sasa kwamba mawazo ni ya<br />
pande mbili, yenye kujigawa<br />
na hufanana. Yeye si tafauti na<br />
wanawake wengine wote ambao<br />
wamekuwa wakiwapenda na<br />
kuwahusudu au hata kuwabusu<br />
baba zao. Tungependa kusikia<br />
mazuri kuhusu baba zetu.<br />
Hadi anastaafu, baba<br />
wa rafiki yangu, alikuwa ni<br />
mfanyabiashara, sina shaka<br />
kwamba alikuwa na mazowea<br />
ya kuchukua gazeti na kupitia<br />
makala iliyoandikwa na mtu wa<br />
aina yangu, mwenye mtizamo<br />
tafauti kuhusu baba yake na<br />
akautangaza hadharani; au<br />
kusikiliza hotuba ya mjumbe<br />
wa upinzani mwenye azma ya<br />
kudhoofisha heshima yeyote ile ya<br />
kisiasa, hata ile ambayo alikuwa<br />
nayo baba yake; au mbaya zaidi<br />
akamsikiliza mjumbe wa chama<br />
chake anayerusha makombora ili<br />
Makala<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
Ni wakati wa CCM wahafidhina kupevuka<br />
Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhabib Amani Abeid Karume<br />
kutafuta umaarufu wa kisiasa.<br />
Lakini, kama mtoto wa<br />
mwanasiasa mashuhuri hapa<br />
Tanzania , ninao uzoefu wa<br />
yote hayo, au zaidi ya haya,<br />
siandiki hivi kutafuta huruma<br />
ya yeyote, kwani ninafahamu<br />
tosha kwamba ukosowaji wa<br />
wazi ni sehemu ya maish ya<br />
mwanasiasa, na kwa kawaida<br />
nadhani, lazima uhamasishwe,<br />
ndiyo sababu nikaandika hisia<br />
zangu. Kwa udhati ninaowakosea<br />
na kuwakera, ipo na kuangukia,<br />
na hivyo ndivyo nilivyoishi.<br />
Ipo kanuni muhimu isemayo,<br />
kuwa mtoto, hasa wa kike wa<br />
mwanasiasa ni kuchagua kuwa<br />
na ngozi (gamba) gumu, yaani<br />
si rahisi kukasirika. Pasi na<br />
ngozi ngumu, nachelea kusema,<br />
watoto wa kike wa wanasiasa,<br />
wote wangeliathirika kutokana<br />
na mitetemeko ya kisaikolojia.<br />
Kwa miaka mingi mgodi<br />
umegeuka kuwa kichaka cha<br />
ndovu (tembo) kizee.<br />
Kiasi ya wiki moja hivi,<br />
CCM (Chama cha Mapinduzi)<br />
kilihitimisha Mkutano wake<br />
Mkuu wa 8, kwa shangwe<br />
kubwa. Khadija Kopa, gwiji<br />
wa taarab, akawaburudisha<br />
takriban wajumbe 2400,<br />
wake zao na wafuasi wao,<br />
wote wakiwa wamevaa sare<br />
za kijani na manjano, za<br />
CCM, ndani ya ukumbi, mjini<br />
Dodoma . Vibendera tele vya<br />
CCM vikipepea, wakicheza<br />
kwa furaha iliyopelekea<br />
kuchagua viongozi wao wapya<br />
kwa umakini. Viongozi hao<br />
ni pamoja na Mwenyekiti wa<br />
CCM Taifa na wajumbe 20 wa<br />
NEC. Mkutano Mkuu wa 8 wa<br />
CCM pia ulihitimisha Miaka 10<br />
ya Uongozi wa Amani Abeid<br />
Karume aliyoitumikia kama<br />
Makamu Mwenyekiti wa CCM,<br />
upande wa Zanzibar .<br />
Kwa wale wasiomjua, mbali<br />
ya kuwa ni Raisi Mstaafu wa<br />
Zanzibar , pia ningelipenda<br />
kuwajulisha kwamba Amani<br />
Abeid Karume, ni mashuhuri<br />
sana kwangu kwa kuwa yeye ni<br />
baba yangu mzazi.<br />
Jioni ya Novemba 14, 2012,<br />
niliwasha TV kwa azma mahsusi<br />
ya kumuangalia Amani Abeid<br />
Karume akiagana na CCM,<br />
kama Makamo Mwenyekiti<br />
wa Zanzibar . Kusema ukweli,<br />
nilitamani kumsikia yeye<br />
akimshukuru mama yangu<br />
mzazi aliyekuwa naye imara<br />
kwa miaka 44. Nilimsikiliza<br />
Abdulrahman Kinana akitoa<br />
maazimio ya CCM; nikamuona<br />
Khadija Kopa pamoja na mama<br />
yangu wakicheza; nikamsikia<br />
Pius Msekwa akitoa hotuba yake<br />
ya kuaga, na hatimaye Amani<br />
Karume akipanda jukwaani ili<br />
naye atoe hotuba yake.<br />
Hotuba ya Karume ya Kuaga<br />
imekuwa gumzo na yenye<br />
kujadiliwa sana kati ya zote<br />
kutokea Mkutano Mkuu wa 8 wa<br />
CCM; siyo azma yangu kuijadili<br />
na kuifafanua hotuba hiyo, kwani<br />
ninayo fursa ya dhati kabisa ya<br />
kuelewa alichokusudia, wala<br />
haikuwa dhamira yangu kuitetea<br />
hotuba yake hiyo, kwamba<br />
kulikuwapo mamia ya mistari<br />
iliyoandikwa na kisha maelfu<br />
ya maneno yaliyosemwa kuunga<br />
mkono hotuba yake. Niko hapa<br />
kujadili, kile ninachoamini kuwa<br />
chanzo na mzizi wa fitna za<br />
kuirudi na kuipinga hotuba<br />
hiyo kwa baadhi ya Wana-CCM<br />
Zanzibar.<br />
Nilivyomsikiliza yeye<br />
nikamuelewa, kama ilivyo<br />
kawaida, hakuweza kuficha<br />
furaha yake anayochukulia kuwa<br />
ni mwisho mwema wa mafanikio<br />
makubwa ya tangu alipoitumikia<br />
CCM, zaidi ya miaka 10, huku<br />
pia ukiwa muda wake muafaka<br />
wa kuwasilisha mawazo ya<br />
umma na pia kwa kuzingatia<br />
mtazamo wa chama chake.<br />
Hapakuwa na hitilafu yoyote<br />
kutokana na kile alichokielezea,<br />
alijadili Historia ya CCM,<br />
Serikali ya Umoja wa Kitaifa<br />
ya Zanzibar, na Mchakato wa<br />
Marekebisho ya Katiba; Jukumu<br />
la Uongozi na Uongozi Bora;<br />
na pia furaha yake kuona damu<br />
changa au sura mpya zikiibuka<br />
ndani ya Uongozi wa CCM.<br />
Kwa ufupi, juu ya Historia ya<br />
CCM, Karume alilikumbusha<br />
Taifa kwamba CCM ni Muungano<br />
wa Vyama Viwili- Afro Shirazi<br />
Party kutoka Zanzibar, na TANU<br />
kwa upande wa Tanganyika-<br />
ambavyo viliamua kuungana<br />
na kwa azma ya kuufikia<br />
ufanisi, akatanabahisha warithi<br />
wasije kusahau azma ya<br />
Waasisi, hususan Waasisi wa<br />
ASP walioweka misingi imara,<br />
inayokwenda sambamba na<br />
utekelezaji wa dhati wa Azimio<br />
la Umoja wa Mataifa la Haki za<br />
Binaadamu; ili kuondosha hali<br />
zote za ubaguzi, ukandamizaji,<br />
na kadhalika.<br />
Kuhusiana na Serikali ya<br />
Umoja wa Kitaifa, Karume<br />
alionelea kwamba hili lilikuwa<br />
ni chaguo la Wazanzibari<br />
wenyewe kwa asilimia 64,<br />
ya wingi wa Kura ya Maoni,<br />
lililopelekea Mabadiliko ya<br />
Katiba ya Zanzibar , na hivyo<br />
CCM lazima waheshimu chaguo<br />
hilo .<br />
Kwa upande wa Mchakato<br />
wa Marekebisho ya Katiba<br />
unaoendelea sasa, Karume<br />
aliwataka wahusika wa Chama<br />
chake, pamoja na Viongozi,<br />
kuwacha watu watoe mawazo<br />
yao kwa uhuru, na hasa juu ya<br />
namna ya Muungano kati ya<br />
Tanganyika na Zanzibar ; uhuru<br />
huo unaweza kutekelezeka pale<br />
ambapo mamlaka hazitowateza<br />
nguvu.<br />
Hatimaye, Karume aliinasihi<br />
C C M k w a m b a i n a h i t a j i<br />
kushinda nyoyo na akili za<br />
watu, iwapo inataka kubakia<br />
yenye kukubalika, na hiyo<br />
inategemea utawala wa sheria<br />
na kwa heshima ya kujali, wala<br />
siyo kwa mabavu na vitisho.<br />
Kwa ukweli na kwa mkato<br />
kabisa, sitaomba radhi kwa<br />
kutamka hadharani kwamba<br />
Amani Karume ni mtu aliyeko<br />
moyoni kwangu, hasa ya<br />
kwamba pamoja na yote, aliweza<br />
k u k u m b u k a k u m s h u k u r u<br />
mama yangu. Baada ya kwisha<br />
kukubainishia uhusiano wangu<br />
na Amani Karume, na kwa<br />
nafasi yake maalumu ndani ya<br />
moyo wangu, nimeshaondosha<br />
dhima, lililobaki nasema “kuwa<br />
mwangalifu na utahadhari”.<br />
Hata hivyo, nilishitushwa<br />
kupita kiasi, kutokana na ile fitna<br />
ya sumu mbaya, pale baadhi<br />
ya wafuasi wa Chama chake<br />
walivyoichukulia hotuba yake.<br />
Kwa wafuatiliaji wa habari<br />
wanajua kwamba baadhi ya<br />
Wana-CCM walikasirishwa mno<br />
na hotuba hiyo na waliamua<br />
kuirarua (kuichanachana) Picha<br />
kubwa ya Karume iliyokuwapo<br />
Michenzani, Zanzibar .<br />
Kwanini makundi ndani ya<br />
CCM Zanzibar yakaguswa mno<br />
na maneno ambayo hayakuwa na<br />
lolote zaidi ya kueleza kwamba<br />
mamlaka ya Chama kuongoza<br />
inatokana na ridhaa ya watu,<br />
na ni watu hao ambao hapana<br />
budi kuwaheshimu, na kuachiwa<br />
wawasilishe mawazo yao kwa<br />
uwazi? Nahofia kwamba hii ni<br />
athari mbaya ya kutofahamu<br />
historia ya CCM na ya Nchi<br />
yetu.<br />
Kwa upande wa Zanzibar,<br />
Mzazi au Mtangulizi wa CCM,<br />
yaani Afro Shirazi Party, kilikuja<br />
madarakani baada ya Mapinduzi,<br />
na hadi Marekebisho ya Katiba<br />
ya mwaka 1992, haki ya CCM<br />
kuiongoza Tanzania , ikilindwa<br />
na Katiba. CCM haikuwa na hati<br />
ya kuongoza kutoka kwa Mungu,<br />
lakini kwa Taifa lisiloendeshwa<br />
kidini, kama ilivyo Jamhuri ya<br />
Muungano wa Tanzania, haki<br />
ya Katiba ilikaribia kwamba<br />
ni hati kutoka kwa Mungu,<br />
ambayo CCM ilipata. Kabla ya<br />
Marekebisho hayo ya Katiba,<br />
Sheria No 3 (1) ya Katiba ya<br />
Jamhuri ya Muungano wa<br />
Tanzania , ikisomeka kama<br />
ifuatavyo:<br />
“Jamhuri ya Muungano ni<br />
Taifa la Kidemokrasia na la<br />
Kijamaa la Chama kimoja”.<br />
Hakuna bahati nasibu hapa,<br />
ni “Chama Kimoja cha Siasa”<br />
kilichokusudiwa na Katiba.<br />
Uoni wangu ni kwamba,<br />
baadhi ya Wana-CCM Zanzibar,<br />
kwa bahati mbaya wanashindwa<br />
kupambanua baina ya ukweli<br />
halisi na mitizamo yao.<br />
Utengamano huo unahamasishwa<br />
zaidi na harakati ya hivi karibuni<br />
ya kikundi cha takriban watu 50<br />
hivi, akinamama na wasichana,<br />
wakiwa wamevalia sare za<br />
CCM, ambao kawaida hujiweka<br />
safu za usoni za mikutano; hawa<br />
ni kama kwamba huchochewa<br />
ghafla na mtu, nao wakaibuka<br />
kwa kuimba kwa kibwagizo<br />
cha Komando! Komando!<br />
Komando! Kibwagizo hiki ni<br />
cha kuwahadaa watu na kuihadaa<br />
hadhira, ili iweze kuamini kuwa<br />
watu hao ni waumini wa dhati<br />
wa Raisi Mstaafu wa Zanzibar<br />
wa CCM mwaka 1990- 2000,<br />
Salmin Amour, aliyependelea<br />
mwenyewe jina la Komando,<br />
kutokana na hulka yake ya kukosa<br />
uvumilivu dhidi ya wapinzani<br />
hasa, CUF, na kuthibitisha imani<br />
hiyo pale alipowapeleka jela bila<br />
ya hatia, Viongozi 20 wa Chama<br />
cha Wananchi, CUF.<br />
Bila shaka, watambuzi<br />
tambueni ujumbe ni huo,<br />
vibaraka wanausambaza wazi<br />
wazi pasi na kificho. Vibaraka<br />
wahafidhina wanachohitaji ni<br />
CCM Zanzibar kutawaliwa na<br />
“Komando” katika himaya zake,<br />
hatimaye asisalimike “adui”<br />
yeyote kutokana na makucha<br />
ya chuma wanayostahiki. Wapo<br />
wanaojidanganya vipembeni,<br />
chini ya vivuli vya Wahafidhina<br />
wa Chama, bado wakiamini<br />
kuwa na haki pekee ya kuendelea<br />
kutawala, ati waliikomboa<br />
Zanzibar kutokana na Usultani,<br />
na ati mabadiliko ya katiba<br />
yamewawacha solemba kama<br />
siyo kupotea kabisa, tena<br />
katika ulimwengu huu wa siasa<br />
makini za ushindani ambapo<br />
hata Watanzania wanahitaji<br />
kuchagua chama kipi kitawale<br />
na kinachowafaa kuwaongoza,<br />
wala si vinginevyo.<br />
Vyema sawa! wote ambao<br />
wamediriki kutoa hisia zao na<br />
ambao waliitumikia Zanzibar<br />
kutoka katika makucha ya<br />
Usultani, sasa wameshafariki au<br />
vinginevyo ni watu wazima sana<br />
; hao hawakuongoza Mapinduzi<br />
ili hatimaye waanze ulimbukeni<br />
waje kufia ndani ya Boma la<br />
Sultani lisilokuwa na kitu!<br />
La kuzingatia ni kwamba,<br />
kila baada ya miaka mitano<br />
tunahitaji vyama vyote vya siasa<br />
kuwatoa wagombea wao bora<br />
na kuwapanga mstari mbele<br />
yetu kama kwamba ni shindano<br />
Inaendelea Uk. 11
8<br />
Na Khalid S Mtwangi<br />
SALALAH! Hiyo ilikuwa<br />
dharuba kali!! Namshukuru<br />
sana Mhariri wa gazeti la<br />
Raia Mwema kunijulisha<br />
kuwa kimetokea kimbunga<br />
hicho kabla hakikupata<br />
nafasi ya kunisomba mpaka<br />
labda baharini!<br />
Wa s o m a j i w e n z a g u<br />
w a t a i k u m b u k a m a k a l a<br />
niliyoandika na kuchapishwa<br />
na AN NUUR toleo lake la<br />
tarehe 23 November, 2012.<br />
Hoja zangu zilikuwa zimelenga<br />
k u m u u n g a m k o n o B w<br />
Evarist Chahali kwa maoni na<br />
mawazo yake ya kimapinduzi<br />
yaliyochapishwa mara tatu kwa<br />
mfululizo. Namshukuru sana<br />
Mhariri wa RaiaMwema kwa<br />
hatua ya kijasiri aliyochukua<br />
kunitumia baadhi ya maoni ya<br />
wasomaji wenzangu ambayo<br />
yalitumwa kwake kupitia email.<br />
Amenifurahisha sana kwa<br />
kitendo hicho pia nawapongeza<br />
wale waliotoa maoni yao,<br />
naamini kwa moyo mkunjufu<br />
k a b i s a . N a m i n a j a r i b u<br />
kuyajibu hayo waliyouliza ama<br />
kunikosoa na ninafanya hivyo<br />
kwa moyo mkunjufu kabisa<br />
hasa kwa vile baadhi yao bila<br />
shaka, kama walivyoeleza<br />
wenyewe kwa majina ya<br />
bandia, wananifahamu sana<br />
na bila shaka tumekuwa na<br />
uhusianao mzuri kwa muda<br />
wote tuliofahamiana. Bahati<br />
mbaya wameficha majina yao.<br />
Mimi nipo wazi kabisa kwa<br />
majadiliano, waelewe hivyo.<br />
Hebu nianze na yale makali<br />
sana kutoka kwa anayejiita<br />
USTADH PENGO; namuomba<br />
aniruhusu nami nimwite<br />
U S TA D H M U K O M B E<br />
MONSIGNOR PENGO. Huyu<br />
Mukombe kweli ananifahamu<br />
vizuri pamoja na familia yangu,<br />
ila tu kamsahau mwanangu wa<br />
kiume aitwaye SHABANI<br />
MTOKA MTWANGI. Huyu<br />
ni Telecom Engineer akiwa<br />
na Masters. Sasa ningependa<br />
kumjibu kuhusu ama kuandika<br />
au kutokuandika nambari<br />
kwenye kartasi za mitihani.<br />
Ningemuomba afanye<br />
utafiti wa ndani kuhusu hili.<br />
Hata hivyo wacha nimueleze<br />
yaliyompata huyu Tatu sasa<br />
mwenye Ph D. (Shahada ya<br />
Uzamivu). Kama atakumbuka<br />
vizuri, kwanza hawa vijana<br />
wote walisota nyumbani<br />
kwa takriban mwaka mzima<br />
Makala<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
Mbagala Tena: Bado ni Uislam na Ukristo<br />
ikiwa wamekosa shule ya<br />
kuwapokea. Dhamira ilikuwa<br />
wapate nafasi katika shule za<br />
serekali. Hilo likawa gumu<br />
sana kwa sababu ambazo<br />
wakati ule sikuzielewa, baadae<br />
nilielewa kuwa ni majina yao<br />
ama langu ndiyo yalisababisha<br />
vikwazo.<br />
Tatu alikuwa kafaulu<br />
mtihani wa kidato cha nne<br />
(form IV) akiwa na Division<br />
One nzuri kabisa akiwa na<br />
dhamira ya kuendelea Form V<br />
mchepuo wa sayansi. Hakika<br />
alikuwa keshapata shule ya<br />
kumwezesha hayo kule Kenya.<br />
Waliofuata, yaani Mtoka na<br />
Asha walikuwa wakitafuta<br />
nafasi katika form III na II.<br />
Nilipata msaada wa kigogo<br />
(hakika huyu hakuwa kigogo<br />
bali, kutokana na nafasi<br />
yake serekalini, alikuwa ni<br />
GOGO na ndivyo iliwezekana<br />
kumpatia Tatu nafasi ya Form<br />
V katika shule moja hapa<br />
Dar es Salaam. Niliambiwa<br />
a s i n g e w e z a k u f u a t i l i a<br />
mchepuo wa sayansi kwa<br />
sababu katika mtihani wake<br />
wa Form IV ulichanganya<br />
“Physics with Chemistry”<br />
ilihali kwa kawaida masomo<br />
haya mawili hutahiniwa mbali<br />
mbali. Niliuliza inakuwaje<br />
wanafunzi kutoka Kenya<br />
wanapokewa katika vitivyo<br />
vya uhandisi na udaktari Chuo<br />
Kikuu cha Dar es Salaam?<br />
Niliambiwa kwa kifupi tu<br />
na kwa ukali kuwa nikubali<br />
alichopata huyu binti au iwe<br />
basi akae nyumbani. Kama<br />
wanavyosema Waswahili,<br />
Ustadh Monsignor Mukombe<br />
Pengo wewe hukuwepo lakini<br />
malaika wako alikuwepo.<br />
Ningependa kumshukiuru<br />
sana hili GOGO serekali kwa<br />
msaada alioutoa kwa sababu<br />
moja kubwa kwamba kumbe<br />
kukosa shule kwa binti huyu<br />
ilikuwa ni njama ambayo<br />
alijitoa wakati mmoja wa hawa<br />
wakubwa Wizara ya Elimu<br />
aliropoka baada ya kupata<br />
maagizo kutoka juu. Kumbe<br />
jambo hilo lilimuudhi sana na<br />
katika kuropoka ilijidhihirisha<br />
kuwa Tatu alikosa nafasi shule<br />
kwa sababu jina lake lingine<br />
Zubeda ambalo kabisa ni la<br />
Kiislamu. Kwa kuwa Bint<br />
Shaaban, Binti wa Kitanzinia<br />
inayodaiwa kutokuwa na udini,<br />
alinyimwa nafasi ya kusoma<br />
kidato cha 5 pamoja na kuwa<br />
na DIVISHENI ONE!!!<br />
Ningependa pia kuwajulisha<br />
wasomaji wenzangu kuwa hilo<br />
GOGO lililonisaidia kwanza<br />
nilikutana naye shule katika<br />
miaka ya hamsini ingawa<br />
yeye akiwa mkubwa kwa umri<br />
alikuwa madarasa ya mbele; pia<br />
nilipomuomba msaada tulikuwa<br />
tukikutana katika pilika pilika<br />
za kujenga nchi. Naongeza<br />
kuwajulisha wasomaji na hasa<br />
huyu Mokombe Monsignor<br />
Utadh Pengo kuwa hili Gogo<br />
ni Mkatoliki muumini wa<br />
dhati kabisa. Alinisaidia kwa<br />
kuangalia urafiki wetu na<br />
wenzake wakamshushukiwa<br />
kwa hasira! Na huo ni<br />
wakati wa Mwalimu Nyerere<br />
anayetukuzwa leo kwamba eti<br />
aliondoa udini!<br />
Bila kuwachosha wasomaji,<br />
itatosha kueleza kuwa hao<br />
watoto wangu wengine nao<br />
ilikuwa mbinde kupata nafasi<br />
shule ya Forodhani ambayo<br />
wakati ule ilikuwa imetaifishwa<br />
na imekuwa mali ya umma.<br />
Namshukuru sana rafiki yangu<br />
mmoja aliyenisaidia sana<br />
kufanikisha Hassan akaweza<br />
kuendelea na shule nzuri hapa<br />
Dar es Salaam mjini mpaka<br />
akafanikiwa kufuzu D DS<br />
(sio MD) kama alivyoandika<br />
Ustadh Mukombe Monsignor<br />
Pengo. Napenda kuwajulisha<br />
wasomaji wenzangu kuwa<br />
rafiki yangu huyu ni muumini<br />
thabit wa Kanisa Katoliki<br />
na mpaka kesho tutakuwa<br />
tunamshukuru rafiki yetu<br />
mpendwa.<br />
Sijasahau historia ya<br />
Tanganyika kuhusu elimu<br />
hata kidogo. Nakumbuka<br />
kweli kuwa palitungwa sera<br />
ya upendeleo kuwasaidia<br />
Wananchi waliokuwa nyuma<br />
kielimu na ambayo ilijumuisha<br />
Waislamu pia. Nadhani ni<br />
yeye huyu Ustadh Monsignor<br />
Pengo ambaye ama kasahau<br />
yaliyotokea au kapuuza tu<br />
ukweli. Kwanza nakumbuka<br />
s e r a h i y o h a i k u f u a t w a<br />
k w a v i t e n d o n a h i l i<br />
nilihakikishiwa na mwalimu<br />
mmoja ambaye alikuwa ni<br />
Mkaguzi Mwandamizi wa<br />
Shule na ambaye nilisoma<br />
naye sekondari. Huyu sasa<br />
ni marehemu. Halafu ni<br />
mkumbushe kuhusu mitihani<br />
ya darasa la saba katika miaka<br />
ya sabini. Kwa mbinu za ujanja<br />
sana haikuwa inajulikana kama<br />
wale walioendelea Kidatu cha<br />
Kwanza walikuwa wamepasi<br />
(kufaulu) mitihani yao ama<br />
hapana kwa vile kilikuja<br />
Kiswahili cha ama kachaguliwa<br />
au hakuchaguliwa basi. Hapa<br />
niruhusu ni mnukuu Professor<br />
William Ochieng’ wa Chuo<br />
Kikuu cha Maseno, Kenya.<br />
Aliandika hivi :-<br />
“The Muslims in our<br />
midst have a point when they<br />
complain that the Western<br />
Colonial powers in East Africa<br />
(mainly British) did very little<br />
to promote the welfare of the<br />
Islamic communities in our<br />
region……. While most Kenyan<br />
Christian communities and<br />
societies are today led by very<br />
highly educated leaders Islam<br />
and Islamic societies lack such<br />
leaders. AND IF THE MAIN<br />
RESPONSIBILITY OF THE<br />
NATIONAL LEADERSHIP IS<br />
THE DISTRIBUTION OF THE<br />
NATIONAL CAKE, THEN<br />
IT FOLLOWS THAT THOSE<br />
LIKE MUSLIMS WITHOUT<br />
STRONG REPRESENTATION<br />
AT THE TOP CANNOT HOPE<br />
TO GET A FAIR SHARE OF<br />
THE CAKE. (msisitizo ni<br />
mwandishi huyu)<br />
(The SUNDAY NATION,<br />
May 30, 1993)<br />
Nadhani hakuna haja<br />
ya kutafsiri kipande hiki<br />
wasomaji wenzangu wengi<br />
watakielewa.<br />
Baada ya hayo nchi nzima<br />
ilizuka na shangwe pale shule<br />
binafsi zikiwemo za makanisa<br />
zilipotaifishwa. Lakini yale<br />
yaliyofuata baadae kwa ujanja<br />
mkubwa yalifuta kabisa sifa<br />
ile iliyotolewa mwanzoni.<br />
Lililotokea ni kwamba shule<br />
nyingi sana za makanisa (za<br />
misheni) ziligeuzwa kuwa<br />
seminari; hivyo zilipokea<br />
waumini wa makanisa hayo<br />
tu. Baada ya kubaini ujanja<br />
huo Waislamu nao walitaka<br />
kuigeuza shule yao moja ya<br />
Kinondoni kuwa seminari.<br />
Ni jambo la kusikitisha sana<br />
kwamba hakuwa mwingine<br />
bali Malimu Julius Nyerere<br />
ambaye alitia guu na kukataza<br />
jambo hilo kutokea. Wakati huo<br />
tayari kulikuwa na seminari za<br />
misheni zaidi ya kumi na tatu<br />
mbazo zilikuwa zikipokea<br />
wanafunzi wa masomo ya<br />
kawaida na wala siyo ya upadri<br />
au uchungaji.<br />
Lakini hata ukija katika<br />
hizo za serikali, waliopewa<br />
nafasi za uongozi walikuwa<br />
‘mapadiri’ na wafuasi wao na<br />
ndio hao waliokuwa wanaamua<br />
nani kachaguliwa. Watoto<br />
wa Kikristo waliochaguliwa<br />
wakawa asilimia 90 wakati<br />
wale wa Kiislamu, haikuwahi<br />
idadi yao kuzidi aslimia 15<br />
japo walikuwa ndio wengi<br />
kwa zaidi ya asilimia 70 katika<br />
shule za msingi.<br />
Hebu nimnukuu Waziri<br />
Mkuu mstaafu Muheshimiwa<br />
Frederick Sumaye:-<br />
“The Prime Minister,<br />
Frederick Sumaye, has<br />
cautioned Tanzanians not to<br />
harp on their religious beliefs<br />
when undertaking development<br />
a c t i v i t i e s , p a r t i c u l a r l y<br />
education. Speaking at the<br />
event (sic)at fund raising event<br />
at the Karimjee Hall in Dar<br />
es Salaam over the weekend,<br />
Premier Sumaye said whereas<br />
seminaries are thought to<br />
be preparing students for<br />
priesthood, in actual fact few<br />
of them became (sic) priests<br />
and the rest took up (sic)<br />
responsible positions in the<br />
society.<br />
“Evidence has shown that<br />
most of the students from<br />
seminary schools are the ones<br />
who held (sic) some similar<br />
government positions, whereas<br />
few of them have become priests<br />
and bishops in Tanzania.” Said<br />
Sumaye, adding that there is<br />
need to support such schools.<br />
H e t h e re f o re u rg e d<br />
Tanzanians to avoid religious<br />
ideologies because at the end<br />
of the day, those in responsible<br />
positions render services to<br />
all people regardless of their<br />
religious leanings.”…………..<br />
(The African 19/07/2004)<br />
Alisema hayo katika<br />
harambee ya kukusanya pesa<br />
iliyoandaliwa na Kanisa<br />
Katoliki naye akiwa mgeni<br />
rasmi.<br />
Naye Kipepeo anapaa<br />
kwa kujiamini kabisa kuwa<br />
n i m a k o s a k u w a l a u m u<br />
wamishionari kwa ukosefu<br />
wa elimu miongoni mwa<br />
Waislamu. Nakubaliana naye.<br />
Wanachosema Waislamu ni<br />
kupinga ile dhana potofu<br />
kuwa Waislamu hawatafuti<br />
ile elimu ya mzingira, ati<br />
wao wanashughulika kufika<br />
Madrasa tu. Ukweli ni kwamba<br />
katika kutafuta elimu vijana<br />
wengi wa Kiislamu walidiriki<br />
kuingia zile shule za White<br />
Fathers, Benedictine Fathers<br />
na kadhalika. Badala ya<br />
kuwapa elimu vijana hawa,<br />
wale maFather walichukua<br />
muda wao mwingi kuwapoteza<br />
vijana wale na kuwabatiza.<br />
Ni ajabu kuwa hasa Kanisa<br />
Katoliki kamwe hawastahimili<br />
kuwaona watu wengine<br />
wanafuata dini zao, hasa ikiwa<br />
dini hiyo ni Uislamu. Jambo<br />
hilo linawakera sana. Bwana<br />
Kipepeo atakumbuka kuwa<br />
nilitoa mfano wa Mzazi wangu<br />
mikasa kama hiyo ilimpata<br />
pale Central School, Ujiji<br />
katika miaka ya ishirini. Mpaka<br />
leo hii vijana wa Kiislam<br />
wanaosoma shule za Kikristo<br />
wanalazimishwa kuhudhuria<br />
misa kanisani.<br />
Waislamu wanafundishwa<br />
na dini yao kuwa ni kosa<br />
kumlazimisha mtu kufuata<br />
dini yeyote ile. Uhispania<br />
ilitawaliwa na Waislamu<br />
takriban karne saba na<br />
wakati wote huo Wakristo<br />
waliruhusiwa kufuata dini yao<br />
ya Katoliki. Lakini mara nchi<br />
hiyo ilipotekwa na Wakristo<br />
kukatokea “INQUISITION”,<br />
jambo ambalo mpaka leo hata<br />
Wakristo wanaona lilikuwa<br />
ni jambo la aibu. Nako India,<br />
takriban nchi nzima ilikuwa<br />
chini ya wafalme Waislamu<br />
mpaka Waingereza walipoingia<br />
kuitawala nchi hiyo. Mpaka leo<br />
Wahindi wengi wamebakia<br />
na dini zao za KIHINDU<br />
a m a B U D D H A . H a p a<br />
nyumbani Sultani wa Zanzibar<br />
aliwakaribisha mishionari kwa<br />
moyo safi kabisa; lakini leo<br />
hii makanisa wanaupiga vita<br />
sana Uislamu. Inanikumbusha<br />
yule mwandishi mmoja wa<br />
magazeti aliyeapa kuwa kamwe<br />
hataruhusu Tanzania kujiunga<br />
na OIC; yaani atatumia kalamu<br />
yake kupiga vita jambo hilo.<br />
Hana sababu ya msingi zaidi<br />
ya chuki.<br />
M w i s h o n i n g e p e n d a<br />
kutoa sikitiko langu. Katika<br />
makala zake Bwana Evarist<br />
Chahali alionyesha kuelewa<br />
na kutetea kidogo ile hali duni<br />
Inaendelea Uk. 9
9<br />
KATIKA toleo la gazeti moja<br />
litokalo hapa nchini kwetu<br />
kila siku ya Alhamisi, wiki<br />
iliyopita 22/ 11/2012, ukurasa<br />
wa 18 kulikuwa na makala<br />
iliyoandikwa na kaka yangu<br />
mpenzi isemayo Si lazima<br />
Seif kuwa Makamo wa Rais.<br />
Katika makala hiyo mwandishi<br />
a l i a n d i k a m e n g i l a k i n i<br />
alionekana wazi kutamani<br />
na kuegemea zaidi katika<br />
‘episode’ ya siasa za chuki,<br />
ubaguzi na uhasama.<br />
Mwandishi ameonekana<br />
kutamani yale yaliyopita enzi<br />
zile za utawala wa siasa za chuki<br />
na ubaguzi zirejee visiwani bila<br />
ya kueleza hassa faida na mazuri<br />
yaliyopatikana enzi za siasa hizo<br />
chafu za kupigana bila sababu na<br />
kufikia hadi kuamuriwa kulala<br />
saa moja jioni kwa kisingizio<br />
cha uvunjifu wa amani enzi zile<br />
za utawala wa Komandoo. Kwa<br />
hapa tulipofika sasa, sidhani<br />
kwamba kuna Mzanzibari<br />
(halisi) mwenye akili timamu<br />
anaependa turudi kule tulikotoka<br />
ambapo mwana CUF hakwenda<br />
harusini wala kumzika mwana<br />
CCM na mwana CCM hakwenda<br />
kununua bidhaa dukani kwa<br />
mwana CUF. Kipindi ambacho<br />
hata wanafamilia walifikia<br />
kutengana eti kwa kisingizio<br />
cha utofauti wa kisiasa bila ya<br />
kujali mustakbali na khatma ya<br />
Zanzibar na watu wake.<br />
Mwandishi huyo alimtaja<br />
Maalim Seif kuwa ni mtu<br />
ambae anataka kuona Zanzibar<br />
haitawaliki. Naona tumeanza<br />
kusahau historia. Hivi kama<br />
Maalim Seif anataka kuona<br />
Zanzibar haitawaliki angesimama<br />
na kuwa mstari wa mbele yeye na<br />
chama chake cha CUF kutafuta<br />
maridhiano (muafaka) kila<br />
pale palipotokea sintofahamu<br />
Zanzibar hasa kila baada ya<br />
matokeo ya chaguzi mbali mbali<br />
ambazo wananchi na wapiga<br />
kura hawakuwa na imani nazo<br />
kutokana na kugubikwa na kila<br />
aina ya uchakachuaji..!!?<br />
Hivi tumesahau kwamba<br />
amani na utulivu uliopo Zanzibar<br />
sasa ni zao la hali ya maridhiano<br />
na mshikamano wa Wazanzibari<br />
ambao uliasisiwa na Katibu<br />
Mkuu wa CUF na Makamo wa<br />
Kwanza wa Rais Maalim Seif<br />
Sharif Hamad pamoja nae Rais<br />
Mstaafu wa Zanzibar Alhabib<br />
Amani Abeid Karume chini ya<br />
kamati ya maridhiano..!!? Si<br />
Maalim Seif huyu aliyekuwa<br />
wa kwanza kuyakubali na<br />
kuyapokea kwa moyo mkunjufu<br />
matokeo ya uchaguzi mkuu wa<br />
mwaka 2010 pale Bwawani na<br />
kumuweka Ikulu Rais Dkt Shein<br />
huku wafuasi na wanachama wa<br />
CUF kuonekana kutoridhishwa<br />
na matokeo hayo kwa kipindi<br />
kile..?<br />
Unajuwa nini kiliwafanya<br />
wafuasi wa CUF kukusanyika<br />
karibu na sehemu ilopangwa<br />
kutangaza matokea ya uchaguzi<br />
kusindikiza tume ya uchaguzi<br />
kutangaza matokeo ya uchaguzi<br />
Makala<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
Kwa haya ya Ummar Mukhtar…Zenji hayana nafasi tena..!<br />
Na Soud Marhoun Al-<br />
Slemy, Zanzibar<br />
Rais Mstaafu wa Zanzibar<br />
Alhabib Amani Abeid<br />
Karume<br />
huo kwa kuhofia “up side<br />
down” ya matokeo hayo ya<br />
uchaguzi..!!?<br />
Tukumbuke ya kwamba<br />
mkusanyiko kama ule uliotokea<br />
pale Bwawani, watu wenye kudai<br />
haki kwa kuhisi kudhulumiwa<br />
inapelekea madhara makubwa<br />
(negative effects) kwa serikali<br />
au mamlaka husika pale subra<br />
inapofikia kikomo kwa wale<br />
wanaochoshwa kuomba haki<br />
ambayo siyo ya kuombwa na<br />
kuamuwa kupambana ili kupata<br />
haki.<br />
Tukumbuke ya kwamba<br />
Rais wa Misri Hosni Mubarak<br />
aliondoka madarakani bila<br />
khiyari baada ya Wamisri<br />
kukusanyika pale Tahrir Square<br />
na maeneo mengine ya Cairo<br />
baada ya kuona “enough is<br />
enough” kwa yaliyowakuta.<br />
Maalim Seif aliliona hilo na<br />
akaamuwa kujitoa muhanga<br />
na kuwakabili wafuasi wake<br />
na kuwaomba wapowe moto,<br />
ingawa hawakumuelewa vyema<br />
kwa kipindi kile pale Bwawani.<br />
Je! si busara na hekima zake<br />
Maalim Seif zilizozima jazba<br />
za wafuasi wale wa CUF<br />
pale Bwawani siku ile..!!?<br />
Je! mkusanyiko ule kama<br />
haukuzimwa usingeliligharimu<br />
taifa na amani yake..!? Vipi leo<br />
useme Maalim Seif hataki kuona<br />
Zanzibar inatawalika..!!?<br />
Ni kweli kwamba Maalim<br />
Seif ameteuliwa (appointed) na<br />
Rais Dkt Shein kuwa makamo<br />
wa kwanza wa rais Zanzibar.<br />
Lakini uteuzi huo haukuja<br />
kwa bahati mbaya wala kwa<br />
matakwa na mapenzi binafsi ya<br />
mheshimiwa rais, bali uteuzi<br />
huo umekuja kutokana na katiba<br />
ya Zanzibar iliyotungwa na<br />
wawakilishi wa Wazanzibari<br />
wote baada ya kuitishwa kwa<br />
kura ya maoni iliyokusanya<br />
maoni ya Wazanzibari waliotaka<br />
muundo huo wa serikali baada<br />
ya kuchoshwa na siasa chafu<br />
za ubaguzi, kutoaminiana na<br />
kupigana ambazo hazikuzaa<br />
matunda yoyote kwao. Ingawa<br />
kuna baadhi yetu tunaona hayo<br />
ndio maisha. Hivyo Chama Cha<br />
Wananchi CUF kilipendekeza<br />
kwa rais Dkt Shein baada ya<br />
kuridhishwa na sifa zake jina<br />
la Maalim Seif Sharif kwenda<br />
kukiwakilisha chama katika<br />
Katibu Mkuu wa CUF na<br />
Makamo wa Kwanza wa Rais<br />
Maalim Seif Sharif Hamad<br />
serikali ya Umoja wa Kitaifa<br />
(GNU) kutokana na kupata<br />
nafasi ya pili katika uchaguzi<br />
mkuu wa 2010.<br />
I n g a w a M a a l i m S e i f<br />
ameteuliwa na rais Dkt Shein<br />
haimaanishi ya kwamba abaki<br />
kimya bila ya kusema au kufanya<br />
chochote hata kama kuna<br />
dhulma au ukiukwaji mkubwa<br />
wa haki za kiraia ilimradi tu eti<br />
yumo serikalini. Sasa huyo ni<br />
kiongozi au gogo la mkarafuu<br />
linalosubiri kupasuliwa kwa<br />
shoka liingizwe kwenye moto<br />
kupika chakula cha wengine bila<br />
ya yeye kuonja..!!?<br />
Maalim Seif ni kiongozi,<br />
msaidizi na mshauri wa karibu<br />
sana wa rais kwa mujibu wa<br />
katiba ya Zanzibar. Maalim Seif<br />
amekula kiapo kwa jina la Mungu<br />
wake kutetea Zanzibar na watu<br />
wake mbele ya rais. Iweje leo<br />
aone haki haitendeki aendelee<br />
kubaki kimya huku wananchi<br />
ambao anawajibu wa kuwatetea<br />
wakiwa wanalalamika..??<br />
Ukiona ubaya uondowe kwa<br />
mikono yako, huwezi kuondoa<br />
ukemee au kama huwezi pia<br />
basi uchukie. Maalim Seif<br />
hakuwa na uwezo wa moja kwa<br />
moja kutumia mikono yake<br />
kuondosha ubaya ulojitokeza,<br />
lakini alionekana kuuchukia<br />
kwa asilimia mia moja na ndio<br />
mana akakemea kwa sauti<br />
kubwa iliyosikika kila ncha ya<br />
ulimwengu huu ambapo miale<br />
ya jua inapiga.<br />
Kila mmoja ni mchunga na<br />
ataulizwa kwa alichokichunga.<br />
Kwa hili Maalim Seif Mungu<br />
amemungoa Hamdullah!! Lakini<br />
pia tusisahau ya kuwa uongozi<br />
ni dhamana na utaulizwa kwa<br />
dhamana hiyo.<br />
Maalim Seif na chama chake<br />
cha CUF ni chimbuko la GNU, na<br />
umoja wa kitaifa ni sera ya CUF<br />
tokea 1992, iweje leo unamtaka<br />
Maalim Seif akiondoshe<br />
chama chake katika GNU eti<br />
kwa sababu hakuridhishwa<br />
na yaliyofanyika Zanzibar na<br />
ameikosoa serikali..!!? Zile zama<br />
za divide and rule zimepitwa na<br />
wakati na wala sidhani kwamba<br />
zitarejea ndani ya Zanzibar<br />
kwa sasa ambapo agenda kuu<br />
ya Wazanzibari walio wengi<br />
ni kudai Zanzibar huru yenye<br />
mamlaka kamili na kutambulika<br />
kwa heshima zote kitaifa na<br />
kimataifa.<br />
Tuchunge sana na kalamu<br />
zetu, ukitumia vizuri kalamu<br />
yako utajenga na utanufaika kwa<br />
kalamu hiyo, kushindwa kufanya<br />
hivyo ni kubomoa na likitokea<br />
lolote baya na la kuchukiza na<br />
wewe pia utaingia katika matata<br />
kwa namna moja au nyengine,<br />
kwa njia ya moja kwa moja au<br />
isiwe moja kwa moja, akiumia<br />
jirani yako umeumia wewe.<br />
Elewa ya kwamba Zanzibar<br />
sio mali ya CCM, CUF, taasisi<br />
za kidini, sio ya kwangu<br />
binafsi wala ya kwako, bali<br />
ni mali ya Wazanzibari wote<br />
na kila anaependa amani na<br />
maendeleo ya Zanzibar bila ya<br />
kujali dini, kabila, rangi wala<br />
tofauti za kisiasa. Na katika<br />
ulimwengu wa leo wenye<br />
kuongozwa na kutawaliwa<br />
kwa misingi ya kidemokrasia,<br />
uwazi (transparency) umetawala<br />
zaidi na kila mtu anakuwa huru<br />
kusema alichonacho na kutoa<br />
mawazo kuhusu juu ya kile<br />
anachokiamini yeye akilini<br />
mwake, na kwa upande wa<br />
maamuzi, walio wengi (mass)<br />
ndio wanaofuatwa. Hivyo basi<br />
si vyema kuanza kufanya roho<br />
mbaya, kijicho na husda juu ya<br />
amani ya Zanzibar na mwelekeo<br />
wa Wazanzibari walioshikana<br />
pamoja juu ya utoaji maoni<br />
kuhusu katiba mpya ambao<br />
umeonekana dhahir shahir bila<br />
ya woga, bila ya kumun’gunya<br />
maneno wala kupepesa macho<br />
wanadai mamlaka kamili ya<br />
nchi yao na haki zao kiujumla<br />
ambazo wamezikosa kwa miaka<br />
mingi sasa. Hili limekuwa<br />
mwiba na linawanyima usingizi<br />
na kusosa hata hamu ya kula<br />
baadhi ya watu wasioitakia<br />
mema Zanzibar ambao lengo<br />
lao ni kuifuta Zanzibar katika<br />
uso wa dunia kwa kuizamisha<br />
kusikojulikana. Kwa nini iwe<br />
nongwa na kioja cha mwaka<br />
wakati kila Mtanzania ana uhuru<br />
wa kutoa maoni kwa mujibu wa<br />
katiba iliyopo..!!?<br />
Sikubaliani kabisa na<br />
mtazamo finyu wa kuwagawa<br />
Wazanzibari, kuibana Zanzibar<br />
kwa maslahi binafsi, tena ya<br />
watu wachache wasio hata<br />
uzalendo wa Zanzibar.<br />
Mungu ibariki Zanzibar na<br />
watu wake!!<br />
Mbagala tena: Bado ni Uislam na Ukristo<br />
Inatoka Uk. 8<br />
waliyonayo idadi kubwa ya<br />
Waislamu nchini humu. Naona<br />
kuwa hakueleweka kabisa<br />
kama haya wanayoyasema<br />
kina Ustadh Mosingnor<br />
Mukombe Pengo na wenzake.<br />
Nami niliandika makala ile<br />
kujaribu kuziba mapengo<br />
niliyoyaona katika makala za<br />
Bw Chahali. Nilipokuwa shule<br />
ya sekondari (takriban miaka<br />
sitini iliyopita) kulikuwa na<br />
somo la “comprehension”<br />
ambalo lilikuwepo kuwasaidia<br />
wanafunzi mbinu za kuweza<br />
kuelewa kwa urahisi yale<br />
wanayoyasoma. Sijui kama<br />
somo hili liliendelea kuwepo<br />
kwa muda gani. Sasa hivi kweli<br />
hawa kina Ustadh (Monsognor,<br />
Mukombe) Pengo, Bw Kali,<br />
Bw Kipepeo, Bw (Mtume)<br />
Moses na (Malaika) Gabriel<br />
walishindwa kumuelewa Bw<br />
Chahali. Tukiwa karibu zaidi<br />
tujiulize walishindwa kuelewa<br />
yale niliyoandika mimi?<br />
Sidhani ilikuwa hivyo.<br />
Nilibahatika kusoma nakala<br />
ya jarida NEWSWEEK la tarehe<br />
January 23, 2012. Ukurasa wa<br />
kumi na tatu kulikuwa na<br />
mchoro (cartoon) ulioonyesha<br />
moyo wa BinAdam na ubongo<br />
pia wa BinAdam wakipigana<br />
mieleka. Katika jitihada ya<br />
kufumbua fumbo hilo kulikuwa<br />
na maelezo yafuatayo:-<br />
“……..the brain operates<br />
fundamentally in two modes.<br />
O n e i s a u t o m a t i c a n d<br />
emotional – in essence – a gut<br />
reaction………….Green has<br />
found that most of the time<br />
when we are deciding what is<br />
the right thing to do, what is<br />
happening in the brain is the<br />
emotional response, not the<br />
reasoned one…….”<br />
Haya ni maandishi ya Joshua<br />
Green “a leading researcher<br />
on morality and the brain.<br />
Green, 37, is a professor at<br />
Havard and a leader in moral<br />
psychology”. Inawezekana<br />
haya ndiyo yaliyowasibu<br />
hawa ndugu zangu walioshika<br />
kalamu “kunishambulia” kiasi<br />
hicho.<br />
Kwa hali ilivyo humu<br />
Tanzania na nikikumbuka<br />
u t a b i r i w a n d u g u y e t u<br />
Omwami Salva Rweyemamu<br />
nigependekeza kwa nguvu zote,<br />
kwa unyenyekevu kabisa kuwa<br />
ndugu zetu waKristo wapige<br />
konde nyoyo zao. Katika<br />
nyanja nyingi muhimu sana za<br />
nchi hii wao ndio wameshika<br />
mpini na Waislamu wameshika<br />
kwenye makali. Ingawa kuna<br />
viongozi kama Askofu Mkuu<br />
Mokiwa wa Anglican Church<br />
hakubaliani na hilo ukweli<br />
ni kwamba mfumo mzima<br />
katika nyanja nyingi nchini<br />
n i “ M F U M O K R I S TO ” .<br />
Kanisa Katoliki wanakubali<br />
na kujigamba katika kuongoza<br />
nchi.<br />
H i v y o h a w a n d u g u<br />
waKristo wanaweza kuwa<br />
“ M A G N A N I M O U S ”<br />
(samahani nimeshindwa<br />
kupata neno kama hilo la<br />
Kiswahili) na wakalegeza<br />
kamba kidogo ili Waislam nao<br />
wakaweza kujitikisa kidogo?<br />
Hivi hakuna aipendaye<br />
Tanzania akatuepusha na janga<br />
alilotabiri ndugu yetu Salva<br />
Rweyemamu?
10<br />
SIKU moja aliyekuwa Rais<br />
wa Kwanza wa Jamhuri wa<br />
Muungano wa Tanzania,<br />
ambae pia huitwa baba<br />
wa Taifa, hayati Mwalimu<br />
Julius Nyerere, alikuwa<br />
akitembelea kisiwa cha<br />
Pemba, kikazi. Katika safari<br />
yake hiyo ya mzunguko<br />
wa kikazi ilisadifu kupitia<br />
b a r a b a r a y a m k o a n i<br />
kwendea Chake Chake.<br />
Karibu na kichunjuu, hivi<br />
kuna krosi moja kubwa<br />
sana iliyokuwa na muundo<br />
wa herufi ‘S’.<br />
Wakati wakipita pale na<br />
msafara wa magari na jinsi<br />
njia ilivyokuwa mbovu,<br />
na makarama ya krosi ile<br />
ilivyochongeka, Mwalimu<br />
hakuamini kama anapelekwa<br />
Chake chake. Akauliza;<br />
“Tunakwenda, tunarudi?”<br />
Akaambiwa tunakwenda,<br />
il’hali gari ikiwa limeelekeza<br />
uso kule linakotoka na<br />
likiendelea na mwendo ule<br />
ule katika msafara. Mwalimu<br />
akasubiri ajionee kioja,<br />
akatulia.<br />
Miaka zaidi ya 30 tangu<br />
Mwalimu aulize suali hili,<br />
na sasa ni karibu miaka 13<br />
tangu Mwalimu afariki,<br />
hakuna mmoja wetu aliepata<br />
kufikiria falsafa ya maneno<br />
haya, yaliyochukuliwa<br />
kama mzaha wa Mwalimu<br />
tu wakati ule na hadi sasa.<br />
Kusema ukweli maneno haya<br />
hayakustahili kutiwa kapuni<br />
na kama kuna aliyefanya<br />
hivyo amekosea. Ndio maana<br />
mimi nilie yaweka akiba<br />
leo nayavongonyowa na<br />
kuwatunukia. As’aa huenda<br />
mukazinduka.<br />
Zanzibar, nchi kinyonga,<br />
mara nchi, mara si nchi,<br />
vyovyote tukavyoiita, itaitika.<br />
Hadi sasa Visiwa hivi vinapata<br />
umri wa miaka isiyopungua<br />
48 tangu kuachwa na mkoloni<br />
mweupe na kujitawala.<br />
Miaka hii si kidogo hasa<br />
kwa kuyatathmini maendeleo<br />
yetu na ya nchi kwa ujumla.<br />
Naamini huu ni wakati<br />
muafaka wa kujiuliza, ikiwa<br />
SMZ ndie mtawala mkuu wa<br />
visiwa hivi tangu miaka hio,<br />
na anaehubiri maendeleo<br />
kila uchao, tuiulize Serikali<br />
yetu ya SMZ suali lile<br />
lile, ‘TUNAKWENDA,<br />
TUNARUDI?’<br />
Nchi hii ilikuwa ina<br />
maendeleo makubwa na<br />
ilikuwa na akiba isiyomithilika<br />
katika mahakibizo ya fedha<br />
duniani mpaka zama za miaka<br />
ya mwisho ya 1970. Serikali<br />
zetu za SMZ zilizopita<br />
zilikuwa zimetawaliwa<br />
kimabavu kweli kweli<br />
lakini mengi tuliyaona sasa<br />
hatuyaoni. Ndani ya miaka<br />
Makala<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
SMZ na kasumba za maendeleo - ‘tunakwenda, tunarudi?’<br />
nane ya Mzee Abeid Karume,<br />
tulipata majumba makubwa<br />
nchi nzima. Tukajengewa<br />
sipitali na vituo vya afya.<br />
N d a n i y a m i a k a y a<br />
Karume, Jumbe hadi karibu<br />
ya Ali Hassan Mwinyi, wazee<br />
wakipewa pesa za matumizi<br />
zikiitwa ‘ulufea’ (Welfare<br />
benefits) na zikiwasaidia<br />
sana. Wakati wa tawala za<br />
SMZ za siku hizo, sipitali<br />
zilikuwa zimejaa madawa,<br />
usafi na hudumua za kulla<br />
aina. Skuli zetu zilijengwa<br />
hatua kwa hatua, hakuna<br />
alielipia mchango wa skuli,<br />
hakuna alienunua daftari,<br />
kalamu wala penseli. Hakuna<br />
mwanafunzi aliekosa huduma<br />
za afya za kichocho, vipimo<br />
kila muda fulani.<br />
Ilifika wakati kwa jinsi<br />
Serikali ilivyoikiwajali<br />
wanafunzi, Waziri wetu<br />
wa Elimu wa mwanzo<br />
hapa Zanzibar, aliwahi<br />
kupendekeza kuwa vichwa<br />
v y a N g ’ o m b e v y o t e<br />
vinavyochinjwa nchi nzima<br />
v i p e l e k w e m a s h u l e n i<br />
wanafunzi wapikiwe supu,<br />
ili wapate wanywe wakati<br />
wa mapumziko (recess).<br />
Bahati mbaya mpango huu<br />
ulivunjwa na Sheikh Karume,<br />
pale alipomwambia Waziri<br />
wa Elimu kuwa asijefanya<br />
hivyo mpaka ahakikishe kila<br />
mwanafunzi ameshapata<br />
kijiko na kibakuli cha<br />
kunywea supu. Mapango huu<br />
ukafa hapo, lakini ulikuwa na<br />
nia njema.<br />
Enzi za SMZ ya wakati<br />
huo, kulikuwa na huduma za<br />
dakhalia (boarding). Ukipasi<br />
ukipelekwa huko kupatiwa<br />
mafunzo ya kuwa mtu<br />
utakaejitegemea. Tukipewa<br />
kula asubuhi mchana na jioni.<br />
Japo tukiita bondo, lakini<br />
tukipewa tena bure na kwa<br />
wakati bila kuchangishwa<br />
g h a r a m a . Wa n a f u n z i<br />
wakiletewa meli bure kupanda<br />
au wakifanyiwa tiketi kabisa<br />
wakifika huchukuwa na<br />
kusafiri tu kwenda Unguja<br />
na Pemba. Tuache huko.<br />
Hospitali, kula kunywa<br />
na huduma masaa ishirini na<br />
nne. Mgonjwa akipembejewa<br />
na madaktari wa kikwetu na<br />
wa kigeni. Serikali haikuwa<br />
na meli zilizoenda kwa kasi<br />
wala madege, lakini watu<br />
wakisafiria meli za Serikali<br />
za uhakika na unafuu wa<br />
bei. Huo ndio wakati ambao<br />
tunaweza kusema kuwa<br />
nchi yetu ilikuwa changa,<br />
na ilikuwa na matongo ya<br />
ukoloni, haikuwa na uoni<br />
wa mbali wala uwezo wa<br />
kutuletea maendeleo.<br />
Tupige dira ya SMZ leo.<br />
Serikali yahubiri na kutangaza<br />
kila siku kuwa nchi hii imepiga<br />
hatua kubwa kimaendeleo<br />
ukilinganisha na Zamani.<br />
Sikatai. Maendeleo wakati<br />
mwengine hupimwa kwa<br />
miwani ya macho, ambayo<br />
kigari kidogo huwa TATA,<br />
au FUSO. Maendeleo siku<br />
hizi hupimwa kwa kutazama<br />
ndege zipitazo juu ya anga<br />
letu, tivii pana majumbani, au<br />
kila mtu ana simu ya kiganjani.<br />
Maendeleo yetu hupimwa<br />
kwa viongozi kuwa katika<br />
magari makubwa ambayo<br />
wakiwa ndani ya magari<br />
hayo hawasikii ule uvundo<br />
unaonuka pale Darajani kituo<br />
cha dala dala.<br />
Maendeleo hupimwa<br />
wakiwa katika magari<br />
ambayo pia yakipita njia<br />
m b o v u h a w a h i s i w a l a<br />
hawapati vumbi mle ndani.<br />
Na pia licha ya kuwa nchi<br />
ina joto la tanuri ya mbata<br />
siku hizi kwa uchafuzi wa<br />
mazingira, viongozi wetu<br />
wa SMZ hawalihisi joto hili<br />
na vuke kali, katika magari<br />
na majumba yao yaliyo ‘full<br />
kipupwe, full kiyoyozi, full<br />
kujiachia’. Raha zote hizi<br />
zilizowazunguka viongozi<br />
wetu unawategemea kuwa<br />
siku moja watasema kuwa<br />
nchi hii inarudi nyuma badala<br />
ya kwenda mbele? Ungekuwa<br />
wewe ungetia ulimi wako<br />
puani ukasema ukweli huu<br />
wakati yote hayo huyaoni kwa<br />
maraha yaliyokuzunguka?<br />
Hebu linganisha hayo<br />
machache niliyoyasema<br />
yalifanywa, enzi za Karume,<br />
Jumbe na kidogo Mwinyi<br />
na uone. Sasa tudurusu kwa<br />
pamoja. Nitawauliza maswali<br />
munijibu mpaka nimalize,<br />
sawa? Bismillah! Ule ‘ulefea’<br />
ALHAJ Ali Hassan Mwinyi.<br />
bado upo? Skuli zetu zina<br />
vifaa, madafatri na kalamu<br />
bure? Dkahalia zipo? Elimu<br />
bado ni bure? Ndio ni bure<br />
maana haina maana yoyote,<br />
lakini inalipiwa. Samahani<br />
hili nimejijibu mwenyewe.<br />
Haya tuendelee.<br />
Kule spitali dawa ziko?<br />
Ndio lakini kwa pesa. Kile<br />
chakula vipi bado wanapatiwa<br />
wagonjwa? Ahh! Bajeti<br />
ya Wizara ya afya ndogo,<br />
kimefutwa Chakula. Lakini<br />
Waziri wa Afya ana prado la<br />
milioni 70, na mafuta yake ya<br />
laki moja kwa wiki pengine.<br />
Hawasemi kuwa mawaziri<br />
waendeshe gari ndogo kama<br />
Starlet, na Vizt kujenga taifa.<br />
Heri wafe wagonjwa wao<br />
waendeshe magari mazuri.<br />
Ndio sisi bwana, wakoloni<br />
weusi. Nani anajali kama<br />
wagonjwa wanakufa kwa<br />
kutukanwa tu kule Spitali,<br />
kwa kukosa dawa tu na<br />
hata kula sasa? Hawa ndio<br />
viongozi wetu bwana, ni zaidi<br />
ya majoka ya mdimu.<br />
M a d a k t a r i j e e<br />
wanashuhulikia wagonjwa?<br />
Hapana, wanawatukana wala<br />
hakuna anejali serikalini<br />
kwani wao hawatibiwi hapa<br />
hata wakiumwa na tambazi<br />
(uvimbe) huenda nje ya nchi.<br />
Kwa nini? Tumeendelea hivyo.<br />
Tuendelee, au mshachoka?<br />
Mmeona wapi Serikali<br />
kujenga tena majumba ya<br />
watu na makazi? Hapana.<br />
Ule usafiri wa meli dhamana<br />
za Serikali ungalipo? Hapana<br />
zilizopo ni za matajiri na<br />
hata tukizama SMZ husema,<br />
haina la kufanya. Tumezama,<br />
tunazama, na tutaendelea<br />
kuzama. Ndio maendeleo!<br />
Ya kale hayako tena, kweli.<br />
Lakini pia ya sasa hayapo na<br />
wala tusiyatarajie. Nchi hii<br />
kama ingekuwa gari, mmoja<br />
kati ya madereva hawa saba<br />
tuliojaaliwa na Chimwaga<br />
kutuongoza, lazima bila<br />
shaka alizitowa gia zote na<br />
kuibakishia gia ya kurudi<br />
nyuma tu (reverse gear). Na<br />
ndio hivi tunapelekwa msobe<br />
msobe. SMZ wakisimama<br />
majukwaani, huhubiri chuki,<br />
na uhasama na uongo mwingi<br />
kisha wakikutana katika<br />
vyombo vya habari husema<br />
wameleta maendeleo. Hivi ni<br />
kweli jamani. Sikupata nafasi<br />
ya kuchambuwa sana lakini<br />
mpaka hapa tu jiulize ndugu<br />
yangu, ‘TUNAKWENDA,<br />
TUNARUDI?’<br />
Tangazo<br />
Kwa niaba ya Masjid Qiblatain:-<br />
Sheikh Bawaziri na Sheikh Awadhi<br />
wanawaalika Waislamu kuhudhuria<br />
katika hafla ya kuhitimisha kitabu<br />
‘BULUGHUL MARAMI’.<br />
Mahali: Masjidi Qiblatain,<br />
Kariakoo.<br />
Siku: Ijumaa (Leo) Desemba,<br />
14/201.<br />
Muda: Baada ya Swala ya<br />
Magharib.<br />
Mgeni rasmi: Dkt. Babasila, Katibu<br />
Mkuu wa Umoja wa Wanazuoni wa<br />
Kiislamu wa Bara la Afrika.<br />
Wabillah Tawfiq
11<br />
WAKATI wa Ukhalifa wa<br />
Seyyidna Umar bin al-Khattab,<br />
Masahaba walikubaliana<br />
kuanza kalenda ya Kiislamu<br />
pale Mtume wa Mwenyezi<br />
Mungu alipofanya Hijra<br />
kutoka Makka kuelekea<br />
Madina, na kuasisi Dola ya<br />
kwanza ya Kiislamu. Sasa<br />
tunapouanza mwezi huu<br />
Mtukufu wa Muharram,<br />
mwaka mpya wa Kiislamu<br />
wa 1434, basi tujikumbushe<br />
kidogo kuhusu tukio hili la<br />
kihistoria la Hijra na tufute<br />
dhana potofu zinazoambatana<br />
nalo.<br />
M a r a n y i n g i H i j r a h<br />
inapojadiliwa, tumekuwa<br />
tukiishia zaidi kwenye maelezo<br />
yanayoonyesha jinsi Mtume wa<br />
Mwenyezi Mungu alivyojificha<br />
pangoni au nani alilala kwenye<br />
kitanda chake. Hali hii imekuwa<br />
ikituondoa kwenye mjadala<br />
wa maana, wenye kina kuhusu<br />
masuala ya Hijra. Sisi tunaishia<br />
kujadili matukio tu ya Hijra.<br />
Lakini hata hivyo, matukio<br />
ya Hijra tunayoyadili lazima<br />
yatukumbushe kwamba Mtume<br />
wa Mwenyezi Mungu, ingawa<br />
alikuwa akitegemea ‘Wahyi’<br />
kama chanzo cha ujumbe wa<br />
Kiislamu; alikuwa akifanya<br />
harakati za kusimamisha Uislamu<br />
AN-NUUR<br />
MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
Tukio la Hijra, mazingatio yaliyosahaulika!<br />
Said Rajab<br />
kama binadamu na kupitia mbinu<br />
na mikakati ya kibinadamu.<br />
Hijrah ya kuelekea Madina<br />
haikufanyika kwa sababu<br />
Waislamu kule Makka walitaka<br />
kuepuka manyanyaso, au kwa<br />
sababu walitaka kutafuta eneo<br />
salama zaidi la kujinusuru, au<br />
kukimbia mateso ya Maqurayshi.<br />
Isipokuwa, Hijrah lilikuwa ni<br />
tukio kubwa ambalo limebadili<br />
mkondo mzima wa historia<br />
kuelekea upande mwingine.<br />
Hii inaweza kuonekana iwapo<br />
tutaiangalia Sira katika mtazamo<br />
wake sahihi.<br />
Sira ya Mtume wa Mwenyezi<br />
Mungu ni sehemu muhimu<br />
sana ya Sunna, na ndiyo tafsiri<br />
ya vitendo ya Qur’an Tukufu,<br />
ambayo ni ufunuo wa Mwenyezi<br />
Mungu kwa wanadamu. Ukisoma<br />
Sira kwa umakini, utaona kuna<br />
mbinu maalumu ya kuendesha<br />
harakati, na kama lengo letu<br />
ni kutafuta radhi za Mwenyezi<br />
Mungu, basi ni jukumu letu<br />
kuzingatia mbinu hii, hatua kwa<br />
hatua katika kila awamu:<br />
S e m a : “ I k i w a n i n y i<br />
m n a m p e n d a M w e n y e z i<br />
Mungu, basi nifuateni, (hapo)<br />
Mwenyezi Mungu atakupendeni<br />
na atakughufirieni madhambi<br />
yenu. Na Mwenyezi Mungu ni<br />
mwenye maghufira na mwenye<br />
rehema” Qur (3:31).<br />
“Na anachokupeni Mtume basi<br />
pokeeni, na anachokukatazeni<br />
jiepusheni nacho” Qur (59:7)<br />
Kwa mujibu wa Sira, Hijrah<br />
inahitimisha kipindi cha mpito<br />
katika harakati kinachojulikana<br />
kama “Kutafuta Nusra”,<br />
kuelekea kwenye kipindi kingine<br />
ambacho Uislamu unatekelezwa<br />
kwa vitendo katika kiwango<br />
cha Dola. Nusra ni kuhamisha<br />
mamlaka kutoka kwa mtu<br />
mmoja, kupitia kuungwa mkono<br />
au kiapo cha utii, kutoka kwa<br />
watu wenye nguvu katika jamii.<br />
Kwa hiyo, Hijrah ni matokeo ya<br />
moja kwa moja ya kutafuta na<br />
hatimaye kupata Nusra.<br />
Wakati Mus’ab bin Umair<br />
(ra) alipotumwa Madina kueneza<br />
ujumbe wa Uislamu, ilimchukua<br />
mwaka mmoja wa kazi ngumu<br />
katika mji huo, kabla ya viongozi<br />
wake kusafiri mpaka Makka, na<br />
kusalimisha mamlaka zao kwa<br />
Mtume wa Mwenyezi Mungu<br />
kwa kumpa Ba’yah (kiapo cha<br />
utii). Ba’yah hii iliitwa Bayat-ul<br />
Harb (kiapo cha vita).<br />
Ingawa hakukuwa na vita<br />
kipindi kile, iliitwa ‘Bayat- ul<br />
Harb’ kwa sababu ilionyesha<br />
nia ya Waislamu kupigana,<br />
iwapo watalazimika, ili kulinda<br />
harakati na Dola changa ya<br />
Kiislamu wakati ule. Mtume<br />
wa Mwenyezi Mungu alitumia<br />
miaka minne ya Da’wah kwa<br />
makabila mengi ya Najd (eneo<br />
kubwa kati ya Makka na Madina)<br />
kabla ya kupata Nusra.<br />
Ni vizuri kutambua kwamba<br />
mpaka kipindi hiki katika<br />
Sira, licha ya shinikizo lote<br />
ambalo Mtume wa Mwenyezi<br />
Mungu aliliweka kwa jamii<br />
ya Kikafiri ya Makka, mateso<br />
ambayo Maquraysh walimpa<br />
Mtume wa Mwenyezi Mungu<br />
na Waislamu wa awali yalikuwa<br />
ni cha mtoto, ikilinganishwa na<br />
mateso ambayo yalikuja baada<br />
ya Mtume kupata Nusra kutoka<br />
kwa viongozi wa Madina.<br />
Kuanzia hapo na kuendelea,<br />
Makafiri walikuwa wakipanga<br />
kumuua Mtume wa Mwenyezi<br />
Mungu. Hakika ni ukweli<br />
kwamba Shetani na wafuasi wake<br />
wanaogopa sana utekelezaji wa<br />
Sheria za Mwenyezi Mungu<br />
katika ardhi.<br />
Kwa kuzingatia nukta hizi<br />
muhimu, kila tunapoijadili<br />
Hijrah, ambayo watu wengi<br />
wameishusha mpaka kufikia<br />
kuwa kama safari ya kiroho<br />
tu iliyofanywa na Mtume, pia<br />
tujadili umuhimu wa Kiitikadi<br />
wa tukio hili, kwa kuangalia<br />
Uislamu kwa ujumla wake na<br />
uendeshaji wa harakati.<br />
Ni muhimu sana kwa Waislamu<br />
kutambua kwamba tukio hili la<br />
Hijrah si tu linaadhimisha kuanza<br />
kwa kalenda yetu, lakini muhimu<br />
zaidi linakumbusha kuasisiwa<br />
kwa kiini (nucleus) cha dola<br />
ya kwanza kabisa ya Kiislamu.<br />
Mamia ya miaka iliyofuatia,<br />
Ni wakati wa CCM wahafidhina kupevuka<br />
Inatoka Uk. 7<br />
la urembo lililopambika ili<br />
kuwashindanisha, na hiyo ni<br />
sifa au alama ya demokrasia<br />
ulimwenguni kote, na kisha<br />
tuchague aliyependeza zaidi ili<br />
tumvishe taji.<br />
Wacha mshindi atambe katika<br />
Ikulu ya Zanzibar ama ya Dar es<br />
Salaam , tunachohitaji aje ajipange<br />
tena mbele yetu baada ya miaka<br />
mitano, tutakapomuepuka yeye<br />
na tukamvisha taji mwengine<br />
pamoja na zawadi yake ya<br />
fedha. Akibahatika kushinda na<br />
akalivaa taji kwa mara ya pili,<br />
kama ilivyo ada, tutamfikisha<br />
ukingoni mwa awamu yake ya<br />
pili ofisini pamoja na fungu lake<br />
nono la pensheni na tumkabidhi<br />
mkononi kisha tuendelee na<br />
shindano la kumpata mrembo<br />
mwengine. Jee Wahafidhina wa<br />
CCM wataelewa na kubaini hali<br />
ya kutofaa kwao na woga juu ya<br />
mazingira magumu ya urembo<br />
ama uzuri wa kisiasa, hasa<br />
usoni kwa wapigakura ambao<br />
hapana shaka wameshaona hawa<br />
hawapendezi?<br />
Mazito zaidi ya hayo, ni<br />
kwa upande wa Zanzibar ,<br />
mshindi wa taji na anayemfuatia,<br />
wanalazimika kugawana ile<br />
hawala ya fedha, zawadi yao.<br />
Wazanzibari wanachotarajia sasa<br />
ni kuona mshindi anashikamana<br />
na kufanyakazi bega kwa<br />
bega na mshindani wake wa<br />
karibu. Hili bila shaka linahitaji<br />
kuona mahasimu wawili<br />
wakiheshimiana wakati wa<br />
kampeni na baada ya chaguzi,<br />
na kisha kutanguliza maslahi ya<br />
Zanzibar . Hii ni adabu iliyofaa,<br />
naweza kusema, iliyothibitishwa<br />
na Kura ya Maoni ya Serikali<br />
ya Umoja wa Kitaifa kwa<br />
asilimia 64 ya Wapigakura,<br />
ambao walichoshwa na siasa za<br />
chuki, za kibaguzi zilizotumika,<br />
ikibidi kote kote CUF na CCM,<br />
kuidhoofisha Zanzibar , na<br />
pia kuchoshwa na vilio vya<br />
mchezo mchafu kila baada ya<br />
Uchaguzi.<br />
Kwa bahati mbaya, wapo<br />
baadhi ya Wana-CCM wa<br />
Zanzibar, wanaosumbuliwa na<br />
ugonjwa wa kusahau kabisa juu<br />
ya Maridhiano na Mabadiliko ya<br />
Katiba, yaliyopelekea kuundwa<br />
kwa Serikali ya Umoja wa<br />
K i t a i f a ; w a p o w e n g i n e<br />
wasioridhika na mfumo huu,<br />
wamekuwa wakiweka vizuizi<br />
na kunong’ona chini kwa chini,<br />
kutokana na kukosa ustahamilivu<br />
na pia ukosefu wa kubaini athari<br />
za mifarakano, ndiyo maana<br />
wanamvurumishia lawama<br />
Amani Abeid Karume, ati yeye<br />
ndiye aliyeasisi mizizi ya hili;<br />
wapo waliokubali na kuridhia<br />
matakwa ya Wazanzibari;<br />
ingawa kwa Wahafidhina, hao ni<br />
wasaliti, kwa chochote ambacho<br />
ni kinyume na matakwa yao wao<br />
(wahafidhina).<br />
Katika Mkutano wa hivi<br />
karibuni wa CCM uliofanyika<br />
Zanzibar, Wahafidhina wa CCM<br />
walitumia lugha chafu, matusi,<br />
uchochezi, na maneno yasiyofaa<br />
kuchochea na kukumbusha<br />
mambo yaliyopita ambayo<br />
yakitumiwa na Wanamapinduzi<br />
dhidi ya Wana-CCM waliodaiwa<br />
kuwa na msimamo wa wastani;<br />
kwa udhati kabisa Mapinduzi ni<br />
matokeo ya kuondosha ubaguzi,<br />
ingawa yanatumiwa sasa na<br />
baadhi ya Wahafidhina kufungua<br />
na kurejesha majeraha ya zamani<br />
yaliyokwishapoa, ili kujitafutia<br />
umaarufu wa kisiasa.<br />
Kama Mzanzibari mwenye<br />
asili ya pande mbili, Muarabu na<br />
Muafrika, ambapo Babu yangu<br />
Muarabu aliuwawa gerezani<br />
mara tu baada ya Mapinduzi,<br />
bila ya sababu, zaidi ya imani<br />
yake ya kisiasa, ambapo pia<br />
Babu yangu mwenye asili ya<br />
Afrika naye aliuliwa miaka 8<br />
baada ya Mapinduzi, si kwa<br />
lolote bali, kwa hali ile ile kama<br />
mtangulia wake, imani yake ya<br />
kisiasa, sijaridhika wala sifurahii<br />
hata kidogo.<br />
Huu ni mchezo wa biashara<br />
ya kujinufaisha, unaoweza<br />
kupelekea umwagaji damu. Sasa<br />
ni wakati wa Wahafidhina ndani<br />
ya CCM Zanzibar kupevuka,<br />
na wakabaini kwamba hiki siyo<br />
kiwanja cha watoto wa skuli,<br />
wababe kuwapora wenzao<br />
pesa yao ya chakula cha<br />
mchana.<br />
M i a k a 4 8 b a a d a y a<br />
M a p i n d u z i , Z a n z i b a r<br />
imebadilika sana. Wengi wa<br />
Wazanzibari ni wa umri wa<br />
chini ya miaka 40. Hawakuishi<br />
katika Mapinduzi wala<br />
ubaguzi wa rangi wa kisiasa,<br />
unaotajwa kusababisha<br />
Mapinduzi ndani ya Zanzibar<br />
. Siasa zetu haziwezi kubaki<br />
za kale, ingawa historia<br />
inaweza kutumika kutuarifu,<br />
wapi tulikuwa vile, na wapi<br />
tunahitaji kwenda, na hivyo<br />
kuepuka siasa chafu.<br />
Kama CCM Zanzibar,<br />
inaburuzwa na wahafidhina,<br />
hivyo basi CUF inateka<br />
ushindi wa kisiasa wa Zanzibar<br />
. Iwapo CCM inahitaji<br />
kutetea taji lake la urembo<br />
mwaka 2015, lazima ijijenge,<br />
ijirekebishe, yenyewe, na<br />
ijiunde upya, ipambane na<br />
iweze kuteka ushindi, kwa<br />
sababu ni kura za Wazanzibari<br />
wenye msimamo wa wastani,<br />
zitakazoamua Raisi wa<br />
baadaye wa Zanzibar .<br />
( M A K A L A H I I<br />
IMETAFSIRIWA KUTOKA<br />
GAZETI LA THE GUARDIAN<br />
LA JUMAPILI TAREHE 25<br />
NOVEMBA, 2012, AMBAYO<br />
ILIANDIKWA NA BI FATMA<br />
AMANI)<br />
kiini hiki kilisambaa katika<br />
nchi jirani, kikiwakomboa<br />
watu wanaokandamizwa<br />
kwa kuwaleletea neema ya<br />
Mwenyezi Mungu inayoitwa<br />
Uislamu.<br />
Kwa hiyo, tunapotaka<br />
kuzungumzia umuhimu wa<br />
Hijrah, basi tutambue kwamba<br />
tukio hili linaadhimisha pia<br />
kipindi ambacho Uislamu<br />
kama Itikadi, umebadilika<br />
kutoka kuwa wazo na kuwa<br />
vitendo.<br />
W a t u w a M a d i n a<br />
walimkubali Muhammad<br />
(saw) kama Mtume tu. Lakini,<br />
hata hivyo baada ya kuhamisha<br />
mamlaka yao (Nusra) kwa<br />
Mtume wa Mwenyezi Mungu<br />
wakati alipowasili Madina,<br />
walimpokea kama mtawala<br />
na Mtume.<br />
Kabla Muhammad (saw)<br />
hajafanya Hijrah, alikuwa<br />
Mtume aliyefunuliwa sheria<br />
mpya kutoka kwa Mwenyezi<br />
Mungu. Baada ya Hijrah,<br />
akawa ndiye mtekelezaji<br />
wa sheria hizo. Uislamu<br />
ukahama kutoka uanishaji<br />
na ufafanuzi wa matatizo na<br />
masuala, ukaelekea kwenye<br />
kupambana na matatizo na<br />
masuala hayo, ikiwa ni pamoja<br />
na kutoa ufumbuzi wake.<br />
Hiki ndiyo kipindi ambacho<br />
Mtume wa Mwenyezi Mungu<br />
aliweza kutekeleza kanuni na<br />
mifumo ya Kiislamu katika<br />
maisha halisi.<br />
Hijrah, kama sehemu ya<br />
Sira, ni tukio linalohitaji<br />
kusomwa kwa kina sana, ili<br />
kufahamu maana za ndani na<br />
hekima zake.<br />
Haina maana kwamba<br />
maelezo madogo madogo<br />
ya Hijrah, kama jinsi Mtume<br />
w a M w e n y e z i M u n g u<br />
alivyomfanya Seyyidna<br />
Ali bin Abu Talib(ra) alale<br />
kwenye kitanda chake, au jinsi<br />
yeye mwenyewe alivyojificha<br />
pangoni si muhimu. Hayo ni<br />
matukio muhimu pia kwa<br />
sababu yanatukumbusha<br />
kwamba mbinu na mikakati<br />
iliyotumiwa na Mtume<br />
w a M w e n y e z i M u n g u<br />
kufikia lengo, ilikuwa ni<br />
ya kibinadamu na siyo<br />
ya binadamu wa ajabu<br />
(superhuman). Hazikuwa<br />
mbinu zilizohitaji miujiza<br />
kuzitekeleza.<br />
Hatuwezi kudai kwamba,<br />
kwa kuwa Muhammad<br />
(saw) alikuwa Mtume,<br />
na sisi siyo Mitume, basi<br />
hatuwezi kufuata nyayo zake<br />
kikamilifu, hasa linapokuja<br />
s u a l a l a j i n s i M t u m e<br />
alivyoendesha harakati za<br />
kusimamisha Uislamu. Kama<br />
Waislamu, lazima tukumbuke<br />
kwamba mbinu na mikakati<br />
iliyotumiwa na Mtume katika<br />
harakati za kusimamisha<br />
dini ya Mwenyezi Mungu<br />
ipo kwa ajili yetu kufuata,<br />
na kutofuata ni kumuasi<br />
Mwenyezi Mungu.
AN-NUUR<br />
12 MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />
IMEELEZWA kuwa viongozi<br />
wa Jumuia ya UAMSHO<br />
visiwani Zanzibar, ambao<br />
bado wanashikiliwa rumande,<br />
sasa wameanza kupatiwa<br />
huduma muhimu kama<br />
mahabusu wengine gerezani<br />
Kiinua Mguu Juu Unguja.<br />
Kabla ya hapo, viongozi hao<br />
walidai kufanyiwa vitendo vya<br />
kidhalilishaji huko gerezani<br />
ikiwa ni pamoja na kukataliwa<br />
kupewa chakula cha ndugu zao,<br />
kusoma Qur’an, kubadili nguo<br />
wala kukutana na wahabusu<br />
wengine.<br />
Wa k i l i a n a y e w a t e t e a<br />
viongozi hao wa Kiislamu, Bw.<br />
Salum Taufiq, amenukuliwa<br />
akisema kuwa wateja wake<br />
tayari wameruhusiwa kula<br />
chakula kutoka nyumbani,<br />
kusoma Qur’ani, kubadilisha<br />
nguo na kutoka kwenye vyumba<br />
vyao na kuchanganyika na<br />
mahabusu wengine.<br />
Awali, baada ya kushikiliwa<br />
mahabusu bila dhamana,<br />
viongozi hao walifungua kesi<br />
ya kupinga kubaguliwa na<br />
kutopewa huduma bora tangu<br />
Usikose nakala yako ya<br />
AN-NUUR kila<br />
Ijumaa<br />
Uamsho Zanzibar waanza kupatiwa huduma muhim<br />
Na Mwandishi Wetu<br />
walipofunguliwa mashtaka<br />
Oktoba 21 mwaka huu.<br />
B a a d h i y a m a s h i t a k a<br />
yanayowakabili viongozi hao<br />
wa UAMSHO ni kuhatarisha<br />
usalama wa taifa na kusababisha<br />
uharibifu wa mali.<br />
Viongozi hao ni maarufu<br />
kwa kupigania mabadiliko<br />
katika muundo wa muungano<br />
wa Tanganyika na Zanzibar<br />
na walifanya mikutano mingi<br />
kuhamasisha wananchi kukataa<br />
mfumo wa hivi sasa wa<br />
muungano wa serikali mbili.<br />
Jumuia ya UAMSHO kabla<br />
ya kukamatwa viongozi wake,<br />
imekuwa mstari wa mbele<br />
kutetea maslahi ya Mamlaka<br />
ya Zanzibar, na kutaka uwepo<br />
utaratibu wa kupigwa kura<br />
ya maoni kabla ya kuendelea<br />
mchakato wa kukusanya maoni<br />
juu ya kuandikwa katiba mpya<br />
visiwani humo.<br />
Aidha Taasisi hiyo imekuwa<br />
na jitihada za kutaka kuwepo<br />
muungano wenye maslahi<br />
kwa pande zote za nchi, kwa<br />
maana ya Tanzania Bara na<br />
Zanzibar na pendekezo kubwa<br />
likiwa ni kuwepo muungano wa<br />
mkataba.<br />
SHEIKH Farid Hadd akiwa katika karandinga la Polisi Zanzibar.<br />
Sheikh Ponda Issa bado yupo rumande Segerea<br />
Na Shaban Rajab wakili wa washitakiwa Juma mambo ni ya kiutendaji zaidi. Aidha alisema walikaa kwamba, sahihi ya mlalamikaji<br />
Nassoro.<br />
Wakili Nassoro, aidha alihoji pamoja na Balozi wa Misri haikuwekwa siku ya mkataba.<br />
SHEIKH Ponda Issa jana Aliongeza kuwa hajui kwamba Bakwata inahusika na na kujadiliana, ambapo Balozi Hivyo walisema kuna hofu ya<br />
alirejeshwa tena rumande kiwanja hicho huko nyuma watu gani.<br />
huyo aliwataka kuwajengea kughushiwa mkataba huo.<br />
b a a d a y a k e s i y a k e madhumuni yake yalikuwa ni Sheikh Makusanya alijibu jengo la ghorofa chuoni Hata hivyo upande wa wa<br />
kusikilizwa.<br />
nini na namna kilivyopatikana kuwa Baraza hilo linawahusu Markazi kwa ajili ya mabweni Jamhuri ulisema kuwa kutizama<br />
Ponda anaendelea kukaa pia hajui.<br />
Waislamu wote wa Tanzania. na madarasa ya wanachuo<br />
rumande baada ya kukataliwa Hata hivyo Wakili Nassoro Jibu hilo lilitoa mwanya<br />
uhalali wa sahihi zilizomo<br />
na kuwafanyia ukarabati wa<br />
dhamana.<br />
alipomtaka kurejea kipengele wa kuhoji iwapo Waislamu Markaz Chang’ombe.<br />
katika mkataba huo sio kazi<br />
Jana kesi hiyo iliposikilizwa, cha muhtasari wa kikao cha walishirikishwa vipi katika Baadae ndipo Bakwata ya mlalamikaji na kwamba,<br />
s h a h i d i w a u p a n d e w a Baraza la Maulamaa kilichojadili mpango huo wa kubadilishana wakakabidhiwa kiwanja kwa mkataba uliowasilishwa ni<br />
mlalamikaji katika kesi suala la kubadilishana umiliki umiliki wa ardhi na Agritanza mkataba na Agritanza.<br />
halali kimatiki kwa kuwa<br />
inayomkabili Sheikh Ponda wa ardhi kati ya ekari nne za na kwamba sasa ujenzi wa N y a r a k a z a m k a t a b a unakidhi uwepo wa pande mbili<br />
Issa Ponda, ambaye ni Bakwata na ekari 40 za kampuni chuo kikuu utafanyika huko ziliwasilishwa mahakamani zilizokubaliana.<br />
Sheikh na Kadhi wa Bakwata ya Agritanza zilizopo Kisarawe Kisarawe? Sheikh Makusanya kama kielelezo cha ushahidi Kesi hiyo iliahirishwa hadi<br />
mkoa wa Shinyanga, Ismail Pwani, alikuta kipengele hicho alijibu kuwa hajui.<br />
na 3.<br />
hapo itakapotajwa ambapo<br />
Habib Makusanya, ameieleza kikieleza kuwa Bakwata ilikuwa Shahidi mwingine aliyetoa Bw. Mohammed alisema hata<br />
mahakama ya Hakimu Mkazi na mpango wa Kujenga Chuo utetezi wake mahakamani hapo<br />
Sheikh Ponda na wenzake<br />
hivyo baada ya makabidhiano na<br />
Kisutu, Jijini Dar es Salaam Kikuu cha Kiislamu hapo alikuwa ni mmoja wa wamiliki<br />
w a t a n o , w a l i r e j e s h w a<br />
kuanza kuandaa vifaa vya ujenzi<br />
kuwa, hajui ni namna gani Markazi Chang’ombe.<br />
wa kampuni ya Agritanza Bw.<br />
rumande.<br />
eneo hilo limemegwa kiasi cha Hata hivyo kabla ya kukubali Suleiman Nassoro Mohammed,<br />
wa ukuta kuzunguka kiwanja kesi hiyo imeahirishwa<br />
kubakia kiwanja cha ekari nne kipengele hicho, shahidi huyo ambaye ni mfanyabishara wa chao, ndipo alipokuja Sheikh hadi Desemba 18 itakapotajwa<br />
ambacho kimepewa kampuni ya alishikilia kuwa Bakwata mtaa wa India jijini Dar es Ponda na kumtaka kuacha kazi ambapo itasikilizwa tena<br />
Agritanza Ltd.<br />
ilikuwa na mpango huo katika Salaam.<br />
hiyo.<br />
Desemba 31 mwaka huu.<br />
Aidha Sheikh Makusanya eneo la chuo cha Kiislamu Yeye alisema mbele ya Alisema baadae wakaja watu Katika kesi nyingine,<br />
ameeleza mahakamani kuwa Al haramain cha jijini Dar es mahakama kuwa wanamiliki takriban ya 500 na kukaa eneo watuhumiwa saba waliokuwa<br />
pamoja na kwamba yeye ni Salaam.<br />
kiwanja cha ekari 40 huko hilo la kiwanja kwa takriban<br />
mjumbe wa Baraza la Ulamaa Hata hivyo alipoulizwa na Kisarawe Pwani.<br />
wakikabiliwa na kesi ya<br />
siku saba.<br />
la Bakwata, Sheikh Mkuu wakili huyo kuwa Aritanza K w a m b a w a l i p o s i k i a<br />
kuchomwa Kanisa la KKKT<br />
Hata hivyo Bw. Mohammed<br />
na Kadhi mkoa Mkoa wa ilipatikana vipi hadi kupewa Bwakata wanahitaji eneo la<br />
Mbagala Zakheem, wameachwa<br />
Shinyanga, hakufahamu kuwa eneo hilo la Chang’ombe, kujenga Chuo Kikuu, walionana<br />
alisema shitaka lao ni la huru baada ya upande wa<br />
eneo hilo na lile kilichopo alikataa kusema lolote. Sheikh na kuwaeleza kuwa wana eneo kuvamiwa kiwanja tu lakini upelelezi kukosa ushahidi wa<br />
Chuo cha Kiislamu Markaz M a k u s a n y a p i a h a k u w a la kutosha huko Kisarawe na hawana shitaka jingine. kuwatia hatiani.<br />
Chang’ombe, kinachoendeshwa tayari kujibu swali lililohoji kwamba iwapo watapatiwa Baadae mawakili wa upande H a t a h i v y o P o l i s i<br />
na Wamisri, lilipangwa na thamani ya mita mraba moja ekari nne chang’ombe, wao wa washitakiwa Bw. Juma wamewakamata watuhumiwa<br />
Bakwata kujengwa Chuo Kikuu ya ardhi ya kiwanja hicho cha watatoa eneo lao hilo.<br />
Nassoro na Bw. Yahya Njama, wengine watano, ambapo<br />
cha Kiislamu nchini.<br />
Chang’ombe.<br />
Alisema Bwakata walituma walipotizama mkataba huo,<br />
“Inasemekana eneo lilikuwa Alipoulizwa kwamba kwa wajumbe wao kuangalia<br />
wameunganishwa na makosa<br />
walieleza kuwa mkataba huo<br />
na ekari 27 hivi, lakini nani nini Bakwata walibadilisha eneo hilo huko Kisarawe na<br />
hayo hayo ya kupora mali za<br />
una kasoro katika uwekaji<br />
aliyefanya eneo hilo kuwa uamuzi wa kujenga Chuo wakaridhika nalo.<br />
Kanisa la KKKT Mbagala<br />
dogo hadi lisitoshe kujengwa Kikuu hapo Chang’ombe kama Kuafuatia kuridhika huko,<br />
wa sahihi, ambapo sahihi Zakheem kwa kutumia nguvu.<br />
chuo sijui, haya ni mambo ilivyokusudia, na kama Wamisri waliahidiwa kuwa Masheikh ya mawakili wa kampuni Kesi hiyo nayo iliahirishwa<br />
ya kiutendaji,” alijibu Sheikh wanaoendesha Chuo cha Markaz B a k w a t a w a t a j a d i l i a n a ya uwakili ya MJ Diamond, hadi Desemba 18, 2012<br />
Makusanya kufuatia maswali Chang’ombe nao walihusishwa na kitafuatia kikao cha ambao ndio waliotengeneza itakapokuja kwa ajili ya<br />
aliyokuwa akiulizwa na katika mabadiliko hayo, Sheikh Wadhamini kabla ya kufikia mkataba huo hazionekanai na usikilizwaji wa awali.<br />
Makusanya alisema hayo makabidhiano.<br />
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.