02.06.2013 Views

ANNUUR 1006.indd

ANNUUR 1006.indd

ANNUUR 1006.indd

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

www.annuurpapers.co.tz<br />

Sauti ya Waislamu<br />

ISSN 0856 - 3861 Na. 1049 MUHARRAM 1434, IJUMAA DES. 14 - 20, 2012 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=<br />

Ubaguzi katika elimu<br />

wazidi kubainishwa<br />

’Zubeda’ wa Divisheni 1 alinyimwa nafasi F5<br />

Ustadh Monsignor Pengo anapotosha ukweli<br />

SHEIKH Ponda Issa Ponda (kushoto) akiwa na Ustadh Shaaban Mapeyo (kulia).<br />

Sheikh Ponda Issa bado<br />

yupo rumande Segerea<br />

Sheikh wa Bakwata atoa ushahidi<br />

Aliyeuziwa kiwanja naye ajieleza Uk. 12<br />

TATU alikosa nafasi shule<br />

kwa sababu jina lake<br />

lingine Zubeda ambalo<br />

kabisa ni la Kiislamu.<br />

Kwa kuwa Bint Shaaban,<br />

Binti wa Kitanzania<br />

inayodaiwa kutokuwa na<br />

udini, alinyimwa nafasi ya<br />

KOMANDO! Komando!<br />

Komando! Kibwagizo hiki<br />

ni cha kuwahadaa watu<br />

na kuihadaa hadhira,<br />

ili iweze kuamini kuwa<br />

watu hao ni waumini wa<br />

dhati wa Raisi Mstaafu<br />

wa Zanzibar wa CCM<br />

mwaka 1990- 2000,<br />

Salmin Amour.<br />

Huyu Salmin alipendelea<br />

mwenyewe jina la Komando,<br />

kutokana na hulka yake ya<br />

kukosa uvumilivu dhidi ya<br />

wapinzani hasa, CUF.<br />

Kuthibitisha imani hiyo<br />

ni pale alipowapeleka jela<br />

bila ya hatia, Viongozi 20<br />

wa Chama cha Wananchi,<br />

CUF.<br />

Vibaraka wahafidhina<br />

wanachohitaji ni CCM<br />

Zanzibar kutawaliwa na<br />

“Komando”.<br />

Ili hatimaye asisalimike<br />

yeyote kutokana na makucha<br />

Anachotaka<br />

Borafya katu<br />

hakiwezekani<br />

Uk. 3<br />

kusoma kidato cha 5 pamoja<br />

na kuwa na DIVISHENI<br />

ONE!!!<br />

N a h u o n i w a k a t i<br />

wa Mwalimu Nyerere<br />

anayetukuzwa leo kwamba<br />

eti aliondoa udini!<br />

(Soma Uk. 8)<br />

CCM wasaliti wa Zanzibar<br />

wajificha kwa Komandoo<br />

Sikiliza anachosema Bi Fatma Karume<br />

Wahafidhina wasirejeshe chuki, mikwaju<br />

RAIS mstaafu wa SMZ<br />

Amani Abeid Karume<br />

ya chuma wanayostahiki.<br />

H a o n d i o w a l e<br />

waliokasirishwa mno na<br />

hotuba ya Amani Abeid<br />

Karume na waliamua<br />

kuirarua na kuichanachana<br />

Picha kubwa ya Karume<br />

iliyokuwapo Michenzani,<br />

Zanzibar.<br />

(Soma Uk. 7)


2<br />

AN-NUUR<br />

S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786<br />

Cel: 0784 370 208, 0755 260 087 0713 110148, DSM.<br />

www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk<br />

Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top<br />

Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam<br />

MAONI YETU<br />

Miaka 51 ya kutumia uhuru vibaya<br />

JUMAPILI ya wiki<br />

iliyopita, Tanzania bara<br />

walisherehekea miaka 51<br />

tangu upatikane uhuru<br />

kutoka kwa mkoloni<br />

Muingereza.<br />

Sherehe zilifanyika pale<br />

Uwanja wa Uhuru, na<br />

kuhudhuriwa na Rais wa<br />

Jamhuri ya Muungano wa<br />

Tanzania na Amir Jeshi<br />

Mkuu Jakaya Mrisho<br />

Kikwete.<br />

Aidha alikuwepo Rais<br />

wa Zanzibar, Dk. Ali<br />

Mohammed Shein na<br />

viongozi wengine wa ngazi<br />

mbalimbali za kiserikali,<br />

vyama vya kisiasa na<br />

taasisi za kijamii.<br />

Sherehe kwa kiasi<br />

kikubwa zilichagizwa na<br />

burudani za ukakamavu,<br />

hususan magwaride ya<br />

vikosi vya Majeshi ya<br />

Ulinzi na Usalama.<br />

Hata hivyo tunadhani<br />

k w a m b a w a k a t i<br />

tunasherehekea hiyo miaka<br />

51 ya uhuru, kwa kiasi<br />

kikubwa uhuru wenyewe<br />

umetumika vibaya kwa<br />

walio wengi.<br />

T u n a s e m a h i v y o<br />

kutokana na kuwepo<br />

k w a o m b w e k u b w a<br />

kati ya viongozi na<br />

wanaoongozwa, matajiri<br />

n a m a s k i n i , w e n y e<br />

elimu na wasio bahatika<br />

kuipata, wanaodhulumu<br />

na wanaodhulumiwa.<br />

Miaka 51 baada ya<br />

uhuru tunashuhudia<br />

Watanzania ambao wengi<br />

ni maskini, makabwela,<br />

wavuja jasho na walala<br />

hoi, wakitakiwa kutoa kitu<br />

chochote wanapohitaji<br />

kupata huduma za msingi<br />

katika taasisi nyingi za<br />

huduma za kiserikali.<br />

Wa k a t i h u o h u o ,<br />

tunashuhudia wanaofuja<br />

kikweli kweli matunda ya<br />

uhuru, wakipewa huduma<br />

hizo kwa haraka na kwa<br />

wakati, tena kwa adabu<br />

na kwa unyenyekevu<br />

mkubwa, na wakati huo<br />

huo hakuna anayethubutu<br />

kudai chochote kwa watu<br />

wa kaliba hii japo wao ndio<br />

wenye ukwasi.<br />

Wakati mtoto wa mlala<br />

hoi akihaha kusaka ajira<br />

baada ya kumaliza elimu<br />

zao kwa taabu kutokana na<br />

umasikini wa wazazi wao,<br />

watoto wa wafuja uhuru<br />

hupeana vyeo na nafasi<br />

katika asasi za kiserikali<br />

na kwenye mashirika<br />

makubwa, bila shaka si<br />

kwa sababu ya ujuzi au<br />

elimu zaidi, bali ni kwa<br />

sababu tu ya kutumia nafasi<br />

za wazee wao, ambao ndio<br />

vinara wa kufuja uhuru<br />

wenyewe.<br />

Watoto wa makabwela<br />

wanaambiwa, mtaji wa<br />

masikini ni nguvu zake.<br />

Wanahamasishwa kujiunga<br />

vicoba, saccos, vibindo<br />

nk. kwa kuwa nafasi<br />

wanazotaka zina wenye<br />

uhuru wao.<br />

Tunaona hata katika<br />

huduma za afya, kwenye<br />

v y o m b o v y a s h e r i a<br />

mahakamani, vyombo vya<br />

dola kama polisi, huko<br />

wananchi wanalia kuwa<br />

hakuna haki. Umekuwa ni<br />

mtindo wa mwenye nguvu<br />

mpishe. Mwenye cheo<br />

na mwenye pesa ndiye<br />

mwenye ‘haki’ na mwenye<br />

‘sheria’.<br />

Kwa utaratibu huu,<br />

imekuwa miaka 51 ya<br />

uchungu na makali ya<br />

maisha ndani ya uhuru.<br />

Kuna haja ya suala hili<br />

kutizamwa kwa uzito wake.<br />

Ifikie mahali, Watanzania<br />

waishi maishi ya heshma<br />

kuanzia uwezo wa kupata<br />

mahitaji muhimu ya<br />

kimaisha na pia kupata<br />

haki zao za kibinadamu na<br />

za kiuwananchi.<br />

Vi o n g o z i w a a c h e<br />

kujitizama tu, watizame<br />

nchi na wananchi. Ifikie<br />

mahali kila anayemaliza<br />

muda wake wa uongozi,<br />

a j i v u n i e m a z u r i<br />

aliyowafanyia wananchi,<br />

na wananchi watamani<br />

lau angeendelea afanye<br />

mengi.<br />

Tahariri/Matangazo<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

KAMATI YA KUENDELEZA UISLAMU TANZANIA<br />

TAMASHA LA KANDA YA KASKAZINI,<br />

MASHARIKI NA VISIWANI KIRINJIKO - SAME<br />

21 – 26 DESEMBA, 2012<br />

Waislamu wote wa Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga,<br />

Morogoro, Dar – es – Salaam, Pwani na Visiwa vya Unguja na<br />

Pemba wanaalikwa kuhudhuria Tamasha la Ujenzi wa Chuo<br />

cha Ualimu na Ufundi Kirinjiko litakalofanyika 21 – 26 Desemba,<br />

2012.<br />

Shime Waislamu tujitahidi kuhudhuria kwa wingi. Wasio na<br />

wasaa wa kuhudhuria wachangie fedha na vifaa vya ujenzi.<br />

Tukumbuke, tukifanya hivyo tutakuwa tumefanya biashara na<br />

Allah (s.w) kwa mafanikio ya hapa duniani na malipo ya Pepo<br />

– Qur’an (61:10-13)<br />

Wabillah Tawfiiq<br />

AMIR<br />

MKUZO ISLAMIC HIGH SCHOOL<br />

P.O. Box 346, Songea Tel: +255 - 716791113, +255683155902 Email:<br />

mkuzoipc@rocketmail.com<br />

NAFASI ZA KIDATO CHA I - 2013<br />

Waislamu wote mnatangaziwa nafasi za kidato cha<br />

kwanza katika shule ya sekondari ya Kiislamu Mkuzo<br />

iliyopo Songea mkoani Ruvuma.<br />

Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 28/12/2012 na<br />

usaili utafanyika tarehe 29/12/2012 katika vituo vya<br />

mtihani vilivyoorodheshwa kwenye fomu ya maombi.<br />

Wahi kuchukua fomu mapema, nafasi zimebakia<br />

chache.<br />

NB: KWA WALE WALIOCHAGULIWA WAFUATE<br />

MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE (JOINING<br />

INSTRUCTION) KATIKA VITUO WALIVYOFANYIA<br />

USAILI.<br />

Kwa maelezo zaidi piga simu: 0716 791113,<br />

0683155902.<br />

MKUU WA SHULE


3<br />

Habari<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

Anachotaka Borafya katu hakiwezekani<br />

Na Mwandishi Wetu<br />

A N A C H O T A K A<br />

Mwenyekiti wa CCM wa<br />

Mkoa wa Mjini, Borafya<br />

Silima, katu hakiwezekani,<br />

wamesema wachambuzi<br />

wa siasa za Zanzibar.<br />

Wa c h a m b u z i h a o<br />

w a m e s e m a k u w a ,<br />

unaposema kuwa unataka<br />

muungano wa serikali mbili,<br />

huwezi tena kuja na hoja ya<br />

kutaka Rais wa Zanzibar<br />

kuwa na mamlaka sawa na<br />

yule wa muungano.<br />

Maoni na uchambuzi huo<br />

umekuja kufuatia maoni<br />

aliyotoa Mwenyekiti huyo<br />

wa CCM, Mjini Unguja<br />

akisema kuwa anataka<br />

Serikali Mbili, ya Muungano<br />

na ya Zanzibar, lakini kila<br />

Serikali iwe na mamlaka<br />

yake kamili.<br />

Mheshimiwa Borafya<br />

alitoa maoni hayo katika<br />

Uwanja wa Alabama,<br />

Shehia ya Miembeni katika<br />

mfululizo wa zoezi la<br />

kupokea maoni ya wananchi<br />

juu ya katiba mpya.<br />

Kwa mujibu wa taarifa<br />

zilizonukuliwa na baadhi ya<br />

vyombo vya habari, katika<br />

maoni yake mheshimiwa<br />

Borafya amesema pia<br />

a n a t a k a w a e n d e l e e<br />

kuwepo Marais wawili,<br />

wa Muungano na wa<br />

Zanzibar.<br />

Hata hivyo akasisitiza<br />

kuwa, Marais wote wawili<br />

wawe na hadhi sawa na<br />

wawe na mamlaka kamili.<br />

Huku akimalizia kwa<br />

kusema kuwa anahimiza<br />

umoja na mshikamano.<br />

Ni kwa maoni yake<br />

hayo wachambuzi wa<br />

mambo wanasema kuwa<br />

unaposema uwe na serikali<br />

mbili, ya muungano na ya<br />

Zanzibar, ni wazi kuwa<br />

Rais wa Zanzibar atakuwa<br />

chini ya Rais wa Muungano<br />

na serikali ya Zanzibar<br />

lazima iwe chini ya ile ya<br />

muungano.<br />

“Ile serikali, ile nchi,<br />

iliyoungana na Zanzibar,<br />

ndiyo inayoweza kuwa na<br />

hadhi sawa na Zanzibar,<br />

kisha juu yake iwepo hiyo<br />

ya muungano, lakini kwa<br />

maoni haya ya serikali mbili,<br />

inakuwa ni kiini macho au<br />

kujidanganya kutaka Rais<br />

wa Zanzibar awe sawa na<br />

wa muungano.”<br />

Amesema mchambuzi<br />

mmoja ambaye amehoji,<br />

“ipo wapi hiyo nchi<br />

inayoungana na Zanzibar na<br />

hiyo serikali inayoungana<br />

na ya Zanzibar ili izaliwe<br />

ya muungano?”<br />

K a t i k a k u f a f a n u a<br />

a k a s e m a k u w a<br />

kinachoonekana hapa ni<br />

kuwa wale walioungana<br />

na Zanzibar wamekuwa<br />

wajanja zaidi ambapo<br />

wamejivisha joho la<br />

muungano na hivyo Rais<br />

wao kuwa ndiye wa<br />

muungano na kuwa juu ya<br />

Zanzibar.<br />

Mchambuzi huyo ambaye<br />

hata hivyo hakutaka kutaja<br />

jina lake akasema kuwa<br />

ili Zanzibar iweze kuwa<br />

na mamlaka na kuwa Rais<br />

mwenye hadhi, hoja ya<br />

kuwa na ama serikali tatu<br />

au muungano wa mkataba<br />

haiwezi kuepukika.<br />

“Ni lazima itambulike<br />

kwanza nchi inayoungana<br />

na Zanzibar ikiwa na serikali<br />

yake kama inavyotambulika<br />

ya Zanzibar, ndio uweze<br />

kuzungumzia kuwa na<br />

serikali mbili na marais<br />

wawili wenye hadhi,<br />

mamlaka na haki sawa ndani<br />

ya muungano, kinyume cha<br />

hivyo ni kiini macho na<br />

kujidanganya.” Alisisitiza<br />

akimalizia maoni yake.<br />

N i k u t o k a n a n a<br />

uchambuzi huo baadhi ya<br />

wananchi waliomsikiliza<br />

kada huyo wa CCM akitoa<br />

maoni yake wanasema<br />

kuwa alichofanya mwana<br />

CCM huyo ni kuunga<br />

mkono msimamo wa wale<br />

wasiotaka muungano wa<br />

serikali mbili, lakini bila ya<br />

kutamka.<br />

“La kufurahisha ni kuwa<br />

pamoja na kukwepa neno<br />

Muungano wa Mkataba,<br />

lakini sasa viongozi<br />

wahafidhina wa CCM nao<br />

wanaungana na Wazanzibari<br />

kutaka mamlaka kamili.<br />

Sisi tunawaambia wasiwe<br />

na wasiwasi, tuko pamoja<br />

katika kutetea haki za nchi<br />

yetu tukufu ya Zanzibar.<br />

Pamoja Daima.” Amesema<br />

m t o a m a o n i m m o j a<br />

akichambua kile alichosema<br />

Borafya.<br />

MWENYEKITI wa CCM wa Mkoa wa Mjini, Borafya Silima.<br />

Mkutano Baraza Kuu kufanyika Kisarawe<br />

Kuzindua Chuo cha Maimam nchini<br />

Na Bakari Mwakangwale<br />

BARAZA Kuu la Jumuiya<br />

na Taasisi za Kiislamu (T),<br />

lipo mbioni kujenga Chuo<br />

Cha Maimam kitakacho<br />

kuwa kikitoa mafunzo<br />

ya uongozi kwa Maimam<br />

nchini.<br />

C h u o h i c h o<br />

kitakachojulikana kwa jina<br />

la Muhaga Imams Collage,<br />

k i t a j e n g w a W i l a y a n i<br />

Kisarawe, katika Mkoa wa<br />

Pwani, kikilenga kuwaandaa<br />

viongozi wa Waislamu<br />

kuanzia ngazi ya mtaa.<br />

U s t a d h i A b u b a k a r i<br />

Abdulswamadu, amebainisha<br />

hayo akiongea na gazeti<br />

hili, katikati ya wiki hii,<br />

akizungumzia mkutano<br />

Mkuu wa Baraza Kuu la<br />

Jumiya na Taasisi za Kiislamu<br />

(T) utakaofanyika Muhaga,<br />

Kisarawe, kuanzia Desemba<br />

14-21, mwaka huu.<br />

Abdulswamad, aliye<br />

Mkurugenzi wa Uchumi<br />

Mipango na Fedha wa<br />

Baraza Kuu, alisema lengo<br />

la kuanzisha Chuo hicho<br />

ni kuandaa viongozi wa<br />

Waislamu wakianzia kwa<br />

Maimam, kwa kuwa wao ndio<br />

viongozi wa daraja la chini na<br />

muhimu kwani ndio viungo<br />

kati ya waumini na viongozi<br />

wa ngazi za juuu.<br />

Alisema, mikakati hiyo ni<br />

kutokana na kile alichodai,<br />

kama kufeli kwa mipango<br />

na mikakati ya Waislamu<br />

kwa muda mrefu hivyo na<br />

kubaini kwamba huenda ni<br />

kwa kukosa viongozi wenye<br />

kujua malengo kuanzia ngazi<br />

ya chini.<br />

Alisema, Maimamu ni<br />

viongozi muhimu kwa jamii<br />

ya Kiislamu kwani wao ndio<br />

muda mwingi wanakuwa na<br />

Waislamu kwa kukutana nao<br />

mara tano kwa kutwa nzima,<br />

katika Misikiti.<br />

Alisema, Baraza Kuu<br />

limeona endapo Maimam<br />

watakuwa na taaluma ya<br />

uongozi na uratibu wa<br />

mipango na namna gani ya<br />

kuwatumia Waislamu kwa<br />

kuwapa mipango maaluma<br />

ya kimaendeleo bila shaka<br />

jamii ya Waislamu itapiga<br />

hatua kwa haraka.<br />

“Lengo la kuanzisha Chuo<br />

Cha Maimam, ni kuwaanda<br />

kuwa viongozi bora wajue<br />

n a m n a y a k u o n g o z a ,<br />

(utawala) wasiishie kuwa tu<br />

na uhodari wa kusoma Qur<br />

an vizuri wanaposwalisha.”<br />

Alisema Abdulswamadu.<br />

Akizungumzia mkutano<br />

huo, alisema mkutano<br />

utafanyika Desemba 21,<br />

mwaka huu, katika kijiji cha<br />

Muhaga, Kisarawe, ambao<br />

utatanguliwa na Mkutano<br />

Mkuu wa Kutayba Saccos,<br />

Desemba 20.<br />

Alisema, kufuatia mipango<br />

na utaratibu huo, Waislamu<br />

kutoka Jijini na Mikoani<br />

wataanza kuelekea huko<br />

(Kisarawe) kuanzia Desemba<br />

14, Ijumaa ya wiki hii (leo),<br />

kwa ajili ya kupiga kambi na<br />

kujiandaa na mikutano hiyo.<br />

Wakiwa huko sambamba<br />

na kufanyia usafi viwanja<br />

hivyo lakini kwa kipindi<br />

chote hicho cha wiki moja<br />

k a b l a y a k u a n z a k w a<br />

mikutano hiyo, Waislamu<br />

kwa ujumla watapata semina<br />

elekezi kutoka kwa viongozi<br />

(Masheikh) wao kutoka<br />

katika Jumuiya na Taasisi<br />

mbalimbali za Kiislamu<br />

nchini.<br />

Alisema, lengo la kuupeleka<br />

Kisarawe, Mkutano Mkuu wa<br />

Baraza Kuu, ni kuwaonyesha<br />

Waislamu ardhi zao zilizo<br />

chini ya Baraza hilo, na<br />

kuweka mipaka baada ya<br />

kufanyika kwa usafi, ili<br />

wawe tayari kuilinda na<br />

kuisimamia.


4<br />

(i) WANAUME<br />

Na JINA MKOA<br />

1 IDDI R. NANA SINGIDA<br />

2 HAMIS J. CHURY SINGIDA<br />

3 OMARY MUSA KANIKI TANGA<br />

4 OMAR S. WAWA SINGIDA<br />

5 YASIN J. RAMADHAN SINGIDA<br />

6 ISMAIL S. MALUNGA SINGIDA<br />

7 YUNUS A. HASSAN SINGIDA<br />

8 RAMADHAN I. MWIRU SINGIDA<br />

9 WAZIRI SEKA TANGA<br />

10 AHMAD K. MENGI KIGOMA<br />

11 ISMAIL H. KULANDEA SINGIDA<br />

12 ABDILLAH SULEIMAN SINGIDA<br />

13 ISHAKA A. NYAMGUNDA DAR ES<br />

14 ALI MOHAMED AMEIR UNGUJA<br />

15 KHALFANI U. YUSUFU KIGOMA<br />

16 JUMA K. SALAZA KIGOMA<br />

17 JUMA JUMANNE SINGIDA<br />

18 MOHAME A. HASSAN PWANI<br />

19 MAHMOUD A. CHANDE RUVUMA<br />

20 HAMZA MAJIDI SHABANI DODOMA<br />

21 MWAZINI BAKARI MAHAMUDA UNGUJA<br />

22 MAHAMUD J. MOHAMADI SINGIDA<br />

23 ABDULLAH SALEH HASSAN UNGUJA<br />

24 MUSTAFA J. ALI MTWARA<br />

25 ABDALLAH HAMIDU MATA DAR ES<br />

26 ABDUMAJID S. MOHAMED KAGERA<br />

27 BASHIRI M. ATHUMAN SINGIDA<br />

28 ALLY H. KIDUMWU SINGIDA<br />

29 ABAS-ABDULRAHMAN SWALEHE ARUSHA<br />

30 ABDILLAH M. LALI SINGIDA<br />

31 KHALID KASSIMU DULLE MANYARA<br />

32 HAMIS HALIFA PIRI DODOMA<br />

33 MAKAME M. AHMAD PWANI<br />

34 HAJI S. ALLY SINGIDA<br />

35 ABDILLAHI HAMIS ARUSHA<br />

36 SHABANI ALLY ISSANI MANYARA<br />

37 BASHIRU OMARI HAMIS DODOMA<br />

38 MOHAMED M. YASIN KIGOMA<br />

39 ALLY M. SAID SINGIDA<br />

40 AL-JABIR H. MSUKUYA SINGIDA<br />

41 KUMSONI J. KUMMALA MTWARA<br />

41 RAMADHANI TENA OMARI<br />

43 SHABAN JUMA FAKI UNGUJA<br />

44 KASSIMU RAJABU<br />

45 MOHAMED R. MWIRU SINGIDA<br />

(ii) WANAWAKE<br />

Na JINA MKOA<br />

1 KURUTHUM OMARY SINGIDA<br />

2 KANJELU MUHAMMED RAJABU SINGIDA<br />

3 AMINA HUSSEIN SINGIDA<br />

4 MAIMUNA R. OMARY TABORA<br />

5 CHIKU S. KANGARA SINGIDA<br />

6 LINDA HUSSEIN MUSSA<br />

7 JAMILA SUDI SINGIDA<br />

8 HUSNA O. MUKHANDY SINGIDA<br />

9 AMINA RAJABU SINGIDA<br />

10 FADHILA M. MAJENGO SINGIDA<br />

11 HIDAYA OMARY SINGIDA<br />

12 ZAMDA I. MTUHI MTWARA<br />

13 REHEMA J. JUMA MANYARA<br />

14 NASRA MUNDA SINGIDA<br />

15 ZENA M. RUGAYA KIGOMA<br />

16 MARIAM H. SWALEHE SINGIDA<br />

17 SHEJUNA MBWANA HUSSEIN<br />

18 MARIAM FADHILI MNDEME ARUSHA<br />

19 AISHA MUSSA MAULID ARUSHA<br />

20 MWANAIMA H. CHAYOA ARUSHA<br />

21 ZAITUNI JUMA RAJABU SINGIDA<br />

22 TATU K. NYONI RUVUMA<br />

23 NICE J. LUTWE KIGOMA<br />

24 KHADIJA I. SENGE SINGIDA<br />

25 PILI A. JUMANNE SINGIDA<br />

26 KHADIJA VUAI HASSAN UNGUJA<br />

27 DIA HASSAN LINDI<br />

28 ASIA OMARY JUMA ARUSHA<br />

29 FAUDHIA J. ALI DAR ES<br />

30 ASHURA M. HAMIS KIGOMA<br />

31 PILI H. LISU SINGIDA<br />

32 ZUHURA ABDULRAHMANI KANGILE<br />

33 TIMA OMARY HAMIS TANGA<br />

34 ASHURA A. ANTHONY MOROGORO<br />

35 TWAINA HAMIS SINGIDA<br />

36 AISHA O. BENDERA TANGA<br />

37 MWANAIDI S. MBIAJI SINGIDA<br />

38 SHEILA MMARI<br />

39 MWANAIDDY IDDY RAMADHANI ARUSHA<br />

40 NZAINABU MWASHONGO<br />

41 NASRA J. SALUM SINGIDA<br />

42 ZAINABU ABUBAKAR SINGIDA<br />

43 RUSMA A. AMASI SINGIDA<br />

44 FARIDA JUMA SINGIDA<br />

45 HABIBA H. IGAE SINGIDA<br />

46 ZAKIA H. ATHUMAN SINGIDA<br />

Tangazo<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

Bismillaahir Rahmaanir Rahiim<br />

ISLAMIC PROPAGATION CENTRE<br />

MATOKEO YA USAILI WA WAOMBAJI WA MAFUNZO YA UALIMU KATIKA VYUO VYA UALIMU VYA IPC<br />

Wafuatao wamafaulu usaili na wamechaguliwa kujiunga na Mafunzo ya muda mfupi ya Ualimu yatakayoanza mwishoni mwa Januari ,2013<br />

katika vyuo vya Ualimu vya Kiislamu Kirinjiko na Ubungo.<br />

Barua za maelekezo ya kujiunga na chuo (joining instructions) yanapatikana vyuoni na katika vituo walikofanyia usaili mikoani.<br />

A: CHUO CHA UALIMU CHA KIISLAMU KIRINJIKO<br />

47 AMINA M. MASUDI SINGIDA<br />

48 AMINA S. KWIMBA SINGIDA<br />

49 KHADIJA UBWA ALI UNGUJA<br />

50 AMINA JUMA MGALA<br />

51 MARYAM ABDALLAH MUHAMMAD DAR ES<br />

52 ZAINAB JAMAL<br />

53 SAIDA A. NDUI SINGIDA<br />

54 AISHA S. HUSSEIN SINGIDA<br />

55 SUKAINA ALLY KHALIFA DAR ES<br />

56 RAHMA HAJI MOHAMED UNGUJA<br />

57 SALMA YAHYA MKILINDI<br />

58 MARIAM KADHI TANGA<br />

59 SUMMAYA M. SULEIMAN DAR ES<br />

60 AZIZA M. MTONDOHIMA DAR ES<br />

61 BIMKUBWA K. AMOUL DAR ES<br />

62 MWANTUMU BAKARY TANGA<br />

63 KHADIJA HUSSEIN MAURIDI<br />

64 RAMLA HASSAN AYUBU ARUSHA<br />

65 MWAJUMA A. IBRAHIM TANGA<br />

66 LULU JUMANNE SINGIDA<br />

67 HADIJA MBARUKU TANGA<br />

68 SICHANA SIMAI MOHAMED UNGUJA<br />

69 ASHA SALEHE MKILINDI<br />

70 ZAMZAM RAMADHANI GOMBO<br />

71 AMINA M. MANGU SINGIDA<br />

72 AISHA K. MITAGO MOROGORO<br />

73 MWAJUMA HAMISI ABEID DODOMA<br />

74 PATIMA ALI MRIDU<br />

75 TAUSI O. RASHID MWANZA<br />

76 JOHARIA HAMIS SINGIDA<br />

77 ZULPHA SHABANI RAMADHANI SINGIDA<br />

78 HAWA K. MOHAMED KIGOMA<br />

79 SWIVAMU R. DUDE SINGIDA<br />

80 ZANURA S. HAMIS SINGIDA<br />

81 AMINAH. O. SALUM KUWAKA DAR ES<br />

82 MWAJUMA A. MKWAHA MTWARA<br />

83 ASIA SAIDI LUBUVA DODOMA<br />

84 FATUMA BARAZA MANYARA<br />

85 SUMAIYA MSANGI<br />

86 SWALHA N. KASAGOLA SHINYANGA<br />

87 TATU R. LUAMBANO RUVUMA<br />

88 NURIAT H. ABRAHAMAN SINGIDA<br />

89 ASHA RAMADHANI DUMA DODOMA<br />

90 MAIMUNA SALIMU RAJABU<br />

91 SOFIA IDDI KIMUNGU RUKWA<br />

92 SOFIA A. NYONYI SINGIDA<br />

93 ASHURA J. ALLY SINGIDA<br />

94 FATMA MUSSA KIMARO<br />

95 ZAINAB MUSTAFA HASSAN DODOMA<br />

96 MAIMUNA A. ATHUMANI ARUSHA<br />

97 HIDAYA HAMISI SALIMU<br />

98 ZAINABU JUMANNE OMAR SINGIDA<br />

99 ASIA JUMA JULA MANYARA<br />

100 MARIAM B. HAMIS ARUSHA<br />

101 FATUMA YAHAYA RUKWA<br />

102 TABU Y. BAKARI SINGIDA<br />

103 SHANIFA R. SAID SINGIDA<br />

104 REHEMA ABBAS MOROGORO<br />

105 NAHIDA HUSSEIN HAMZA<br />

106 FARIDA J. KISUDA SINGIDA<br />

107 WIDADU MOHAMED RAMADHANI ARUSHA<br />

108 SHUFAA MUSSA IDDY ARUSHA<br />

109 HAWA MUSSA MOHAMMED ARUSHA<br />

110 RAMLA ISMAILI<br />

111 ASHA BAGHAMOYO MANYARA<br />

112 MARYAM L. JUMA<br />

113 MWAJUMA BAKARI MANYARA<br />

114 HAFSWA SULAYMAN PWANI<br />

115 HALMA K. RASHID DAR ES<br />

116 ZIADA S. RUSAMBO RUKWA<br />

117 FATUMA S. RUVAKO TABORA<br />

118 BINZUA HAJI MUSSA<br />

119 KHAIRATH A. SULEIMAN ARUSHA<br />

120 SAUDA YUSUFU JUMA DODOMA<br />

121 RAHMA JUMANNE MANGI MANYARA<br />

122 MWAJUMA SALIMU MADEGHE<br />

123 SALAMA S. KAMBI TANGA<br />

124 HAWA ABDALLAH SINGIDA<br />

125 ZUBEDA R. HEMED TANGA<br />

126 MWANAKHAMIS H. MOHAMED PWANI<br />

127 MWANAHARUSI SWALEHE TANGA<br />

128 RUKIA MOHAMEDI SINGIDA<br />

129 PILI H. BUHULU SINGIDA<br />

130 AMINA RAMADHANI MATEMANGA MOROGORO<br />

131 HADIJA S. KEJO<br />

132 FAUZIA ISSA MANYARA<br />

133 ZEINABU KARIMU JUMA ARUSHA<br />

134 AISHA ABDUL MSANGI<br />

135 MARIAMU M. MTANDU MOROGORO<br />

136 RUKIA B. KAYINGA MBEYA<br />

137 ZAINABU ABDUL HAMIS ARUSHA<br />

138 FATMA MUSSA<br />

139 SAADA A. ZAHOR DAR ES<br />

140 FATUMA HASSAN PWANI<br />

141 ZUHURA HAJI OTHMANI SINGIDA<br />

142 HAWA H. MTEPA DAR ES<br />

143 MARYAM A. MUSSA DAR ES<br />

144 HAWA J. HASSAN DAR ES<br />

145 ASIA H. PANGANI MBEYA<br />

146 SHADIA T. TWAIBU KAGERA<br />

147 AMINANI SUEDI DAUDI<br />

148 MWANAHAMIS K. MOHAMED TANGA<br />

149 SAUMU M. KIVURANDE TANGA<br />

150 MWAJUMA SEBA KIGOMA<br />

151 FADHILA ATHUMANI SINGIDA<br />

B: CHUO CHA UALIMU CHA<br />

KIISLAMU UBUNGO<br />

M A J I N A YA WA L I O C H A G U L I WA<br />

KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU YA<br />

MUDA MFUPI -2013<br />

(i) WANAUME<br />

Na JINA<br />

1 ISSA RASHID MASANJA<br />

2 MWINDADI BAUSI MZEE<br />

3 ILYASA JUMA SAIDI<br />

4 HAJI SAID MWINSHEHE<br />

5 HUSENI ALLY<br />

6 SAID MOHAMMED MIKONGO<br />

7 IDD ATHUMANI KAMBI<br />

8 ALLIY ABDALLAH ALIY KHAMIS<br />

9 MOHAMMED HUSSEIN JUMA<br />

10 JAMAL SHEIKH YAHYA<br />

11 ISSA YUSUPH KITENGE<br />

12 SALUM MOHAMED KINJULI<br />

13 ABUBAKARI ALLY NGINDIKA<br />

14 KISMA ABDILLAH ZABURA<br />

15 KIPUKA HASSANI ISMAIL<br />

(ii) WANAWAKE<br />

Na JINA<br />

1 HIDAYA ALLY KIBAVU<br />

2 HUSNA MUHAMMAD MBELA<br />

3 AISHA MUSSA SAIDI<br />

4 SALMA ABDALLAH KAISI<br />

5 HAWA HAMIDU MSANGI<br />

6 ARAFA ALLY<br />

7 FATMA ABDALLAH MASOUD<br />

8 NURU HAMISI NYUMBA<br />

9 SHARIFA JUMA IBRAHIM<br />

10 HAMIDA ABUBAKAR<br />

11 SOFIA YUSUF KIHAMBWE<br />

12 ZAINAB SULEIMAN MAGWATI<br />

13 TATU HAMZA MAALIM<br />

14 STARA MIGILA<br />

15 FATIMA SALUM KIMATILO<br />

16 HAWA MZEE MANGAMBA<br />

17 AISHA KIBWANA KASUKA<br />

18 REHEMA HASSANI HEMEDI<br />

19 SALMA MOHAMED ALLY<br />

20 TIMA KHAMIS MURI<br />

MUHIMU<br />

Nafasi kwa chuo cha Ubungo bado<br />

zipo<br />

Usaili wa mara ya pili kwa chuo cha<br />

Ubungo tu utafanyika chuoni siku ya<br />

Jumamosi ya tarehe 05/01/2013 saa<br />

2:00 asubuhi. Fomu za kujiunga na<br />

kozi zinaendelea kutolewa Chuoni kwa<br />

gharama ya Tsh 5,000/=<br />

Tafadhali wahi nafasi hii adhimu.<br />

Kwa maelezo zaidi fika chuoni au<br />

wasiliana na Mkuu wa Chuo kwa namba<br />

ya simu 0712557099 au 0688131397.<br />

Wabillaah Tawfiiq<br />

MKURUGENZI


5<br />

LUSAKA<br />

RAIS wa Zambia, Michael<br />

Satta, ametahadharisha<br />

juu ya harakati mpya za<br />

kundi linalotaka kujitenga<br />

la Barotseland Magharibi<br />

mwa nchi hiyo.<br />

Barotseland, ni jina la<br />

eneo lililoko nchini Zambia,<br />

ambalo hivi sasa linaitwa<br />

mkoa wa Magharibi.<br />

Wakati wa uhuru wa<br />

Zambia kwa mujibu wa<br />

makubaliano yaliyofikiwa<br />

kati ya mkoloni Muingereza<br />

na Keneth Kaunda, kiongozi<br />

wa mapambano ya uhuru wa<br />

nchi hiyo yaliyotiwa saini<br />

Oktoba 24 1964, eneo hilo<br />

lilitambuliwa kuwa ardhi ya<br />

Zambia.<br />

Hata hivyo kwa mtazamo<br />

wa watu wa kabila la Lozi,<br />

ambao ndio wakazi wengi<br />

wa eneo hilo la Barotseland,<br />

serikali ya Lusaka kamwe<br />

haikuyaheshimu makubaliano<br />

hayo.<br />

K w a m u j i b u w a<br />

makubaliano hayo, wakazi<br />

wa eneo hilo walipewa hiyari<br />

ya kuwa mamlaka ya ndani na<br />

kujitegemea katika masuala<br />

ya kiuchumi na kisiasa.<br />

Baada ya kupita karibu<br />

nusu karne tangu kutiwa<br />

saini makubaliano hayo,<br />

wananchi wa kabila la Lozi<br />

walikandamizwa na polisi<br />

katika vurugu kwenye<br />

maandamano yaliyoitishwa<br />

na harakati ya kukomboa<br />

eneo hilo kwenye mji wa<br />

Mongu, makao makuu ya<br />

mkoa wa Magharibi.<br />

Tukio hilo kwa mara<br />

nyingine liliamsha azma ya<br />

kutaka kujitenga Barotseland,<br />

ambayo ilijitokeza mwaka<br />

1999 nchini humo. Mwaka<br />

mmoja baadaye. pia maelfu<br />

ya wakazi wa mji wa Mongu<br />

walifanya uasi ambapo baadhi<br />

yao waliuawa.<br />

Licha ya hayo, viongozi<br />

wa harakati ya ukombozi wa<br />

Barotseland, wamesisitiza<br />

kwamba wataendeleza<br />

harakati zao za kudai uhuru<br />

wa eneo hilo kutoka kwa<br />

serikali kuu kwa njia za<br />

amani.<br />

Wachambuzi wa mambo<br />

wanaamini kuwa, makundi<br />

m a t a t u m a k u m b w a<br />

yanayopigania ukombozi<br />

wa eneo la Barotseland,<br />

yanapaswa kuunda chama na<br />

kuanza harakati za kisiasa.<br />

Mwaka 2011 wakati<br />

wa kampeni za uchaguzi,<br />

Rais Michael Satta aliahidi<br />

kuwa iwapo angeshinda<br />

angetekeleza matakwa ya<br />

kabila la Lozi.<br />

Lakini kiongozi huyo<br />

hakutekeleza ahadi hiyo na<br />

maandamano ya wakazi wa<br />

Habari za Kimataifa/Tangazo<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

Zambia yakumbwa na harakati za kundi linalotaka kujitenga<br />

eneo hilo linalotaka kujitenga<br />

yakaendelea.<br />

Wakati huo huo, makabila<br />

ya Nkoya na Mbunda, ambayo<br />

yanaishi na kabila la Lozi<br />

kwenye eneo la Barotseland,<br />

yanapinga fikra ya kutaka<br />

kujitenga eneo hilo.<br />

Viongozi wa makabila<br />

hayo mwezi Juni mwaka<br />

2012 walisisitiza kwamba,<br />

makabila hayo kamwe<br />

h a y a t o h e s a b i w a k u w a<br />

sehemu ya sehemu ya eneo<br />

na yanapinga kugawanywa<br />

ardhi ya Zambia.<br />

Hata hivyo, Baraza la Taifa<br />

la Barotseland katika kikao<br />

cha dharura cha Julai mwaka<br />

huu, lilijitangazia uhuru<br />

wa upande mmoja. Taarifa<br />

ya kikao hicho ilitumwa<br />

kwa taasisi za kieneo za<br />

SADC, Umoja wa Afrika,<br />

Commonwealth na Umoja wa<br />

Mataifa ili jamii ya kimataifa<br />

iunge mkono na kutambua<br />

kujitenga eneo hilo.<br />

Hivi sasa harakati mpya<br />

za kundi hilo zimemtia<br />

wasiwasi Rais Michael Satta,<br />

hasa baada ya wanaharakati<br />

wapya 630 kujiunga na kundi<br />

hilo. Licha ya hayo, Satta<br />

amewataka maafisa wa jeshi<br />

wakabiliane kwa amani na<br />

wafuasi wa kundi hilo.<br />

Nchi nyingi za kusini mwa<br />

Jangwa la Sahara kama vile<br />

Zambia, Angola na Nigeria<br />

zinakabiliwa na makundi<br />

yanayotaka kujitenga na<br />

zinafanya jitihada za kutatua<br />

migogoro hiyo kwa amani na<br />

kuzuia kugawanyika ardhi za<br />

nchi hizo.<br />

The Hague kusikiliza mashtaka ya Wapalestina dhidi ya Israel<br />

BAADA ya Baraza Kuu<br />

la Umoja wa Mataifa<br />

kupandisha hadhi ya<br />

Palestina katika Umoja<br />

wa Mataifa, na kuwa nchi<br />

mtazamaji asiyekuwa<br />

mwanachama rasmi, sasa<br />

mahakama ya The Hague<br />

huko Uholanzi imetangaza<br />

kuwa itaanza kushughulikia<br />

mashtaka yaliyowasilishwa<br />

na Wapalestina dhidi ya<br />

utawala wa Israel.<br />

Ofisi ya Mwendesha<br />

M a s h t a k a M k u u w a<br />

mahakama ya The Hague<br />

imetangaza kuwa, hivi<br />

karibuni itachunguza suala<br />

la kupandishwa hadhi ya<br />

Palestina katika Umoja wa<br />

Mataifa na kushughulikia<br />

mashtaka ya Wapalestina<br />

kuhusu jinai zilizofanywa na<br />

askari wa Israel katika vita<br />

vya siku 22 dhidi ya watu<br />

wa Gaza.<br />

Mwaka 2009 Wapalestina<br />

waliwasilisha mashtaka<br />

rasmi katika Mahakama ya<br />

Jinai ya Kimataifa ya The<br />

Hague, wakiitaka ichunguze<br />

jinai zilizofanywa na jeshi la<br />

Israel katika vita vya siku 22<br />

huko Gaza.<br />

Hata hivyo mashtaka hayo<br />

yalikataliwa na mahakama ya<br />

The Hague kwa kuwa wakati<br />

huo, Palestina ilikuwa bado<br />

haijatambuliwa rasmi kuwa<br />

nchi mtazamaji katika Umoja<br />

wa Mataifa.<br />

K w a m s i n g i h u o ,<br />

kuanzia sasa Mahakama<br />

hiyo itakuwa na uwezo wa<br />

kisheria wa kuchunguza na<br />

kushughulikia mashtaka<br />

yote yanayowasilishwa na<br />

Wapalestina.<br />

Kwa mujibu wa sheria<br />

za kimataifa, nchi ndizo<br />

zinazoweza kuwasilisha<br />

mashtaka katika Mahakaya<br />

ya Kimataifa ya The Hague.<br />

Kabla ya uamuzi wa tarehe<br />

29 Novemba wa Baraza Kuu<br />

la Umoja wa Mataifa ambao<br />

uliitambua Palestina kuwa ni<br />

nchi mtazamaji, hapakuwepo<br />

uwezekano wa kusikilizwa<br />

mashtaka ya Wapalestina<br />

dhidi ya Israel.<br />

Hata hivyo utawala<br />

wa Israel na washirika<br />

wake wakubwa hususan<br />

Marekani, walifanya jitihada<br />

kubwa kukwamisha suala<br />

la kutambuliwa Palestina<br />

kuwa ni nchi, japo isiyo<br />

mwanachama katika Umoja<br />

wa Mataifa.<br />

Kufuatia utambuzi huo,<br />

Rais wa Mamlaka ya Ndani ya<br />

Palestina, Mahmoud Abbas,<br />

alitangaza mara tu baada ya<br />

kurejea Ramallah akitokea<br />

New York, kwamba Quds<br />

Tukufu ndio mji mkuu wa<br />

milele wa nchi ya Palestina.<br />

Alisema sasa Wapalestina<br />

wamepata nchi na wanaweza<br />

kuwasilisha matakwa yao<br />

halali katika jamii ya<br />

kimataifa. Karibu asilimia<br />

75 ya jamii ya kimataifa<br />

imewapigia kura ya ndio<br />

watu wa Palestina.<br />

Rais Abass amesema kuwa<br />

mafanikio hayo, yatabadilisha<br />

mlingano wa nguvu za kisiasa<br />

katika Mashariki ya Kati<br />

Ustadh Abdul Basit akumbukwa<br />

CAIRO<br />

Shughuli ya kumkumbuka<br />

hafidh na msomaji mashuhuri<br />

wa Qur’ani, Ustadh Abdul<br />

Basit Abdul Samad, imefanyika<br />

Ijumaa iliyopita nchini Misri<br />

na kuhudhuriwa na wasomi na<br />

wapenzi wa Qur’ani Tukufu.<br />

Wanafunzi na wapenzi wa<br />

Hafidh huyo mashuhuri wa<br />

Qur’ani, wanachama wa Jumuiya<br />

ya Masomaji Qur’ani ya Misri na<br />

Masheikh wakubwa kama Sheikh<br />

Mahmoud Tablawi, Mahmoud<br />

Siddiq Minshawi, Muhammad al<br />

Halbawi, wawakilishi wa Kituo<br />

cha Kiislamu cha al Azhar na<br />

Wizara ya Wakfu ya Misri na<br />

Mabalozi wa nchi za Kiarabu<br />

na Kiislamu nchini humo, pia<br />

walishiriki katika shughuli hiyo<br />

ya kumbumbuka msomaji huyo<br />

mashuhuri katika ulimwengu wa<br />

Kiislamu.<br />

U s t a d h A b d u l B a s i t<br />

Muhammad Abdul Samad aliaga<br />

dunia Desemba 30 mwaka 1988<br />

huko Cairo Misri.<br />

Alianza kujifunza Qur’ani<br />

Tukufu akiwa bado mtoto mdogo<br />

na alipewa tuzo ya kuhifadhi na<br />

kusoma Qur’ani akiwa na umri<br />

wa miaka 12. Kipindi fulani<br />

Ustadh Abdul Basit alitumia<br />

muda wake mwingi kusafiri<br />

katika nchi za Kiislamu na<br />

kuwahamasisha watu kusoma<br />

kitabu cha Mwenyezi Mungu.<br />

Ustadh Abdul Basit ameacha<br />

kanda nyingi za Sauti zake<br />

akisoma Qur ’ani Tukufu,<br />

ambazo bado zinawavutia<br />

wasomaji wengi wa Qur’ani.<br />

Alianza kujifunza Qur’ani<br />

Tukufu akiwa bado mtoto mdogo<br />

na alipewa tuzo ya kuhifadhi na<br />

kusoma Qur’ani akiwa na umri<br />

wa miaka 12.<br />

Ustadh Abdul Basit wakati wa<br />

uhai wake, alitumia muda wake<br />

mwingi kusafiri katika nchi za<br />

Kiislamu na kuwahamasisha<br />

watu kusoma kitabu cha<br />

Mwenyezi Mungu.<br />

Abdul Basit alizaliwa<br />

mwaka 1927 na kufariki mwaka<br />

1988. Ni msomaji Qur’an pekee<br />

aliyewahi kushinda mara tatu<br />

katika mashindano ya kusoma<br />

Qur’an duniani katika miaka<br />

ya 1970s.<br />

Aidha ni miongoni mwa<br />

wasomaji walioweza kuuza kazi<br />

nyingi zilizorekodiwa akisoma<br />

Qur’ani na alikuwa Rais wa<br />

chama cha wasomaji wa Qur’an<br />

Misri.<br />

DAEE YOUTH ART GROUP<br />

Inakutangazia Semina ya Ndoa na<br />

Talaka kwa mujibu wa Qur-aan na Sunnah<br />

itakayofanyika.<br />

Siku: Jumamosi na Jumapili, kwa wiki<br />

12.<br />

Kozi itaanza Tarehe 15-12-2012 Saa 2<br />

Asubuhi- 8 Mchana.<br />

Mahali: Answar Islamic Model School-<br />

Kinondoni Studio<br />

Vyeti vitatolewa kwa watakao maliza<br />

m a f u n z o m p a k a m w i s h o , M a d a<br />

zitakazofundishwa ni pamoja na, Taratibu<br />

ya kutafuta mchumba, sifa zake, Ndoa na<br />

Nguzo Zake, haki za Mke kwa Mume na<br />

Mume kwa Mke, Eda Talaka na athari zake,<br />

Mirathi kwa mjane, Ndoa ya Mke Zaidi ya<br />

Moja na taratibu zake, Malezi ya Watoto,<br />

Jimai na Migogoro ndani ya Ndoa N.k.<br />

Kwa mawasiliano zaidi piga simu 0715-24<br />

7262/ 0715- 114373.<br />

Nyote mnakaribishwa Wake kwa Waume


6<br />

MWEZI wa Oktoba, 2012<br />

yalitokea matukio makubwa<br />

mawili ya kusikitisha jijini Dar<br />

es Salaam eneo la Mbagala.<br />

Tukio la kwanza ni la kijana<br />

wa Kikristu kokojolea Quran<br />

tukufu lilofuatiwa na tukio<br />

la pili la uchomaji wa kanisa<br />

katika eneo hilo. Tukio la<br />

ukojoleaji Quran liliwaumiza<br />

sana Waislam na tukio la<br />

uchomaji kanisa liliwaumiza<br />

sana Wakristu pia liliwaudhi<br />

sana Waislamu. Liliwaudhi<br />

sana Waislamu kwa maana si<br />

katika mafundisho ya Uislamu<br />

kufanya vitendo kama hivyo.<br />

Wakristu wa KKKT kupitia<br />

kwa viongozi wao walitoa<br />

tamko kudhihirisha hisia zao.<br />

Katika tamko lao walielezea<br />

madhumuni yao makuu matatu<br />

ya kutembelea eneo la Mbagala.<br />

Madhumuni haya kwa ufupi<br />

ni haya yafuatayo: Kuwapa<br />

pole na kusimama pamoja na<br />

waumini wenzao wa Mbagla<br />

walioathirika na uchomaji<br />

kanisa. Kuonesha majonzi kwa<br />

vitendo vya uvunifu wa amani na<br />

kuporomoka kwa mshikamano<br />

wa Watanzania. Kushiriki pamoja<br />

kupokea matumaini ya Tanzania<br />

mpya itakayozaliwa, itakayojali<br />

upendo, uvumilivu, ustahmilivu,<br />

umoja, mshikamano, uhuru wa<br />

kuabudu na dola isiyo na dini.<br />

Dhumuni la tatu waliliandika<br />

kwa wino uliokolezwa kuonesha<br />

kuwa ndilo muhimu sana<br />

kulinganisha na madhumuni<br />

mengine mawili. Wanaeleza<br />

kuwa kilichotokea Mbagala ni<br />

matokeo ya mbegu iliyopandwa<br />

katika bustani njema na sasa<br />

inaanza kuzaa matunda, na<br />

kwamba hizi ni dalili zilizoanza<br />

kitambo na hazikushughulikiwa<br />

na waliomrithi baba wa taifa.<br />

Wanasema kuwa dalili hizo ni:<br />

Uchochezi wa wazi kuwa taifa<br />

hili linaendeshwa na unaoitwa<br />

mfumokristu. Ubishi juu ya idadi<br />

ya waumini wa dini mbalimbali.<br />

Matumizi mabaya ya baadhi ya<br />

vyombo vya habari. Ukimya wa<br />

vyombo vya dola juu ya vitendo<br />

vya uvunjifu wa sharia. Na<br />

Madai yasiyo ya kawaida kwa<br />

serikali inayodaiwa kutokuwa<br />

na dini.<br />

Wanayataja madai hayo<br />

kuwa ni: Kulazimisha uvaaji wa<br />

alama za dini katika taasisi za<br />

umma. Madai ya kutaka balozi<br />

za nchi fulani kufungwa hapa<br />

nchini. Madai na mashinikizo<br />

ya uanzishwaji wa mahakama<br />

za kidini. Mashinikizo ya<br />

kidini yanayoingilia mifumo ya<br />

kitaalam na kisheria. Mashinikizo<br />

ya kidini juu ya mfumo wa uteuzi<br />

wa watendaji wa serikali na<br />

katika ofisi za umma. Kuhoji<br />

juu ya ushirikiano wa serikali na<br />

mashirika ya dini katika utoaji<br />

wa huduma za afya na elimu.<br />

Nianze na nukta ya kwanza<br />

ya kuwa taifa linaendeshwa<br />

na mfumokristu. Nini maana<br />

ya mfumo? Sambamba na<br />

mfumokristu tumekuwa pia<br />

tukisikia MfumoDume. Hebu<br />

tuangalie mfumodume nini?<br />

Makala/Tangazo<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

Maaskofu wanapiga porojo kupotosha ukweli<br />

Na Ibni Mustafa<br />

Lengo kuendeleza dhulma ya mfumokristo<br />

Maana yake ni kwamba<br />

mfumo wa utawala wa nchi<br />

unawapendelea zaidi wanaume<br />

kuliko wanawake. Sasa chukua<br />

maana hii itumbukize katika<br />

neno mfumokristu, maana yake<br />

ni kwamba utawala wa nchi<br />

unawapendelea zaidi wakristu<br />

na ukristu kuliko Waislamu na<br />

Uislamu. Kitendo cha wanaume<br />

kuwa ndio wengi katika nafasi<br />

za maamuzi na ajira kuliko<br />

wanawake ndio mfumodume<br />

wenyewe. Vilevile wanaodai<br />

kuwa kuna mfumokristu<br />

w a n a m a a n i s h a k w a m b a<br />

mfumo wa utawala wa nchi<br />

unawapendelea zaidi Wakristu<br />

na Ukristu kuliko Waislamu.<br />

Upendeleo kwa ukristu ni kama<br />

vile: Nchi kutambua kuwa<br />

siku za ibada za Wakristu za<br />

Jumamosi na Jumapili ndizo<br />

siku za mapumziko kwa wote<br />

wakati Ijumaa ambayo ndio<br />

siku ya ibada kwa Waislamu<br />

haitambuliwi. Kutambulika<br />

kwa tarehe ya kuanza kwa<br />

mwaka wa Kikristu kuwa ni<br />

siku kuu kitaifa, wakati siku ya<br />

kuanza kwa mwaka wa Kiislamu<br />

haitambuliwi, kwa taasisi za<br />

umma kama mashule kupumzika<br />

katika mwezi wa 12 katika<br />

mwaka ambao ni mwezi mtukufu<br />

kwa Wakristu wakati mwezi<br />

mtukufu wa Waislamu ambao ni<br />

Ramadhani hautambuliki. Haya<br />

ni machache yanayoonesha nchi<br />

kuongozwa na mfumokristu.<br />

Mfumokristu pia unaonekana<br />

katika idadi ya Wakristu katika<br />

nafasi za maamuzi, taasisi za<br />

umma zikiwemo elimu ya juu<br />

ambayo haizidi asilimia 25. Huu<br />

ndio mfumokristu.<br />

Wanaopinga kuwa hakuna<br />

mfumokristu watakwambia<br />

mbona Rais na makamo wake<br />

ni Waislamu. Hawa ama<br />

wanapotosha makusudi ama<br />

hawaelewi. Hawaangalii ni<br />

asilimia ngapi ya Waislamu ni<br />

Mawaziri, Wabunge, Wakuu<br />

wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya,<br />

Wakurugenzi wa mashirika<br />

ya umma na wafanyakazi wa<br />

umma kwa ujumla. Wanao<br />

dai mfumodume kwa mfano<br />

hawamaanishi kuwa hakuna<br />

wananwke kabisa katika nafasi<br />

za umma la hasha, wanajua<br />

kuwa wapo lakini idadi yao ni<br />

ndogo kulinganisha na idadi yao<br />

katika taifa. Wale wanaokana<br />

kuwepo mfumokristu kwa<br />

kumuangalia Rais na mkamu<br />

wake wanashindwa kuelewa<br />

kuwa hata Rais anamezwa na<br />

mfumo wa utawala ambao<br />

unaegemea ukristu, Rais kama<br />

yeye hana uwezo wa kubadilisha<br />

mfumo kwa mfano aseme<br />

kuanzia leo siku ya Ijumaa ni<br />

siku ya mapumziko kitaifa ili<br />

kwa vile yeye ni Muislamu apate<br />

nafasi ya kwenda kwenye ibada,<br />

hana uwezo wa kubadilisha<br />

wimbo wa Taifa ambao umo<br />

ndani ya Biblia ya Wakristu nk.<br />

Wanaodai mfumodume hawana<br />

nia ya kuwafarakanisha au kuleta<br />

uadui baina ya wanaume na<br />

ASKOFU Mkuu wa KKKT, Dkt. Alex Malasusa.<br />

wanawake bali wanchodai ni haki<br />

itendeke kwa wote bila ubaguzi<br />

wa kijinsia, vilevile wanaodai<br />

mfumokristu hawana nia wala<br />

lengo la kuwagombanisha<br />

Waislamu na Wakristu bali<br />

wanachotaka ni haki itendeke<br />

bila ubaguzi wa kidini, na hii ni<br />

kwa ajili ya mustaqabali mwema<br />

na ustawi wa nchi. Inaeleweka<br />

bayana kuwa mfumokristu<br />

kama ulivyo mfumodume ni<br />

mambo yaliyosababishwa na<br />

historia. Tanzania ilitawaliwa<br />

na wakoloni Wakristu kuanzia<br />

kwa Wareno, Wajerumani<br />

na Waingereza, mfumo wao<br />

wa utawala uliongozwa na<br />

Ukristu na asili ya sheria zao<br />

ni Ukristu. Tulipodai uhuru<br />

na hatimae kujitawala tulitaka<br />

mambo ya upendeleo wa kidini<br />

usiwepo, lakini bahati mbaya<br />

tuliishia kwenye maneno wakati<br />

matendo ni muendelzo uleule wa<br />

ukoloni.<br />

Kwa maoni yangu, yale<br />

mambo yanayoupendelea<br />

Ukristu kama vile siku za ibada<br />

za Jumamosi na Jumapili,<br />

sikukuu ya mwaka mpya wa<br />

Kikristu sina matatizo navyo,<br />

hapa ningedai kuwa siku ya<br />

Ijumaa kuanzia saa 6 mpaka<br />

8 mchana ambayo ni masaa<br />

matatu yatambuliwe kuwa ni<br />

muda wa ibada kwa Waislamu<br />

na hivyo kipindi hicho shughuli<br />

rasmi za serikali zisimamshwe<br />

ili Waislamu wafanye ibada<br />

halafu waendelee na kazi baada<br />

ya ibada. Pia tarehe 1 ya mwaka<br />

mpya wa Kiislamu itambuliwe<br />

kuwa ni siku ya mapumziko.<br />

Kwa mfumo unaowapendelea<br />

Wakristu uwekwe utaratibu<br />

wa kuhakikisha upendeleo<br />

h a u e n d e l e i k a m a v i l e<br />

ambavyo ubaguzi wa kijinsia<br />

unavyoshughulikiwa vilevile<br />

ubaguzi wa kidini katika<br />

ajira na utumishi wa umma<br />

ushughulikiwe. Ubaguzi ni<br />

ubaguzi tu uwe wa kijinsia au<br />

kidini. Tena wa kidini ni mbaya<br />

sana kwa sababu matokeo yake<br />

ni kuliparaganyisha taifa. Suala<br />

la dini limefanywa nyeti kiasi<br />

anayelizungumzia kwa ajili ya<br />

kurekebeshwa anaitwa kuwa<br />

ndie mdini.<br />

Nukta ya pili ya viongozi wa<br />

KKKT inahusu ubishi wa idadi<br />

ya waumini wa dini mbalimbali.<br />

Ni kwa vipi hili linaweza<br />

kuwa chanzo cha kuhatarisha<br />

amani? Hawakutufafanulia.<br />

Viongozi hawa wanaelewa wazi<br />

kuwa kujua idadi ya waumini<br />

halijawahi kuwa tatizo popote<br />

kama kila raia anapata haki yake<br />

stahiki, hili liliongelewa sana<br />

wakati wa sensa, kwa kuvuta tu<br />

kumbukumbu, nilifuatilia sensa<br />

mbalimbali duniani nchi nyingi<br />

kama sio zote zinafanya sensa<br />

kwa idadi ya kila kundi liwe la<br />

kidini au kabila, mfano majirani<br />

zetu wa Kenya na Uganda katika<br />

sensa zao wanafanya sio tu<br />

kujua idadi ya waumini wa dini<br />

mbalimbali bali hata madhehebu.<br />

Mtu yeyote akitaka kujua KKKT<br />

ni wangapi Kenya na Uganda<br />

anapata taarifa hizi kwenye ofisi<br />

za takwimu. Hatujasikia vita vya<br />

kidini katika nchi hizo eti kwa<br />

vile watu wa dini fulani ni wengi<br />

kuliko wengine.<br />

KKKT wanataja kuwa kuna<br />

madai yasiyo kawaida ambayo<br />

eti ni pamoja na kulazimisha<br />

uvaaji wa alama za dini katika<br />

taasisi za umma. Hawakufafanua<br />

ni kina nani wanalazimisha na<br />

ni alama zipi zinalazimishwa.<br />

Sijawahi kusikia mtu yeyote<br />

amelazimishwa kuvaa alama<br />

yoyote ya kidini uwe msalaba<br />

au labda hijabu. Jaalia kuwa<br />

labda hapa walimaanisha hijabu<br />

kwa akina mama na akina dada<br />

Waislamu. Kwa Waislamu hijabu<br />

ni suala la ibada.<br />

Katika kipindi cha Baba<br />

wa Taifa kwa kiwango fulani<br />

kilikuwa ni kipindi cha utata kwa<br />

Waislamu. Ilikuwa ni vigumu<br />

kwa Muislamu kutekeleza vema<br />

Uislamu wake bila kupoteza<br />

haki zake za kiraia. Kwa mfano<br />

ilikuwa haiwezekani mtoto wa<br />

kike wa Kiislamu kupata haki<br />

yake ya elimu bila kwenda<br />

kinyume na maamrisho na<br />

maadili ya dini yake ya kuvaa<br />

hijabu. Kwa Muislamu ilikuwa<br />

ni ama kunyoa au kusuka, yaani<br />

avunje amri ya hijabu apate haki<br />

ya elimu au akose haki yake ya<br />

ibada ya hijabu apate kusoma.<br />

Binafsi ninawafahamu akina<br />

dada walioikosa elimu kwa<br />

sababu wazazi wao hawakuwa<br />

tayari kuona mabinti zao<br />

wakitembea nusu uchi kwa<br />

vimini ambavyo ndio ilikuwa<br />

sare ya shule.<br />

Kitendo cha serikali ya<br />

awamu ya pili chini ya Mzee Ali<br />

Hassan Mwinyi kuruhusu hijabu<br />

mashuleni, ilikuwa kitendh cha<br />

kishujaa kwake na cha kihistoria<br />

na ukombozi kwa wanawake wa<br />

Tanzania. Hata hivyo pamoja<br />

na umuhimu wa hijabu kwa<br />

Waislamu bado kwa Watanzania<br />

ni suala la khiyari hakuna<br />

anayelazimishwa kuivaa. Ni<br />

wale tu ambao wanajua umuhimu<br />

wake na wenye mapenzi na dini<br />

yao wanaotekeleza ibada hii<br />

adhimu. Pamoja na kuchukizwa<br />

na uvaaji wa hijabu kwa akina<br />

mama na akina dada Waislamu<br />

bado tunawasihi wenzetu<br />

hawa wa KKKT na wenzao<br />

watuvumilie, watustahamilie<br />

kama walivyoeleza katika<br />

dhumuni lao la 3. Sitarajii kwa<br />

serikali yoyote kuturudisha tena<br />

gizani baada ya kupambazukiwa<br />

wala Waislamu wa nchi hii<br />

hawako tayari kurudishwa huko.<br />

Hata katika katiba mpya nina<br />

hakika kipengele cha uhuru wa<br />

kuabudu kitaendelea kuwepo.<br />

Kipengele hiki kinatoa hakikisho<br />

la uhuru wa ibada ikiwemo<br />

uvaaji wa hijabu bila kuwekewa<br />

vikwazo.<br />

Nimalizie kwa kutoa wito<br />

kwa Watanzania kujifunza<br />

k u v u m i l i a n a k w a y a l e<br />

tunayotafutiana na kushirikiana<br />

kwa yale yanayotushirikisha.<br />

Waislamu hata tungetamani vipi<br />

dunia yote wawe ni Waislamu<br />

haiwezekani labda atake<br />

Mwenyezi Mungu. Vilivile hata<br />

Wakristu wangetamani vipi hata<br />

kama kila mmoja wao angeacha<br />

shughuli zote ili afanye shughuli<br />

moja tu ya kuwabatiza watu<br />

haiwezekani kuifanya dunia<br />

kuwa ni Wakristu.<br />

Tukifuata mafundisho na<br />

maadili ya dini zetu yanayotutaka<br />

kutendeana haki, ninaamini<br />

tutaishi vizuri.<br />

(Kamaludin@yahoo.com)


7<br />

T U K I WA t u m e f u a t a n a<br />

tukifuatilia umbea (maongezi<br />

ya kawaida) kwenye simu,<br />

njia pekee ya mawasiliano<br />

iliyokuwapo, sambamba na<br />

hofu ya msongamano wa<br />

magari katika Jiji la Dar<br />

es Salaam, rafiki yangu<br />

mwanamke, aliniarifu juu ya<br />

msiba wa kifo cha rafiki wa<br />

baba yake.<br />

Kwa kuzivuta hisia, nilitamka,<br />

“sikudhania kwamba ulikuwa wa<br />

karibu na marehemu”. Ukimya<br />

na majibu yake yasiyoridhisha<br />

“siyo uhakika lakini unajua mara<br />

ya mwisho nilipokutana naye<br />

alisema hayo hayo ya kushangaza<br />

kuhusiana na baba yangu”,<br />

huenda bila hata ya kusema,<br />

rafiki yangu anamuhusudu sana<br />

baba yake; naweza kuamini<br />

sasa kwamba mawazo ni ya<br />

pande mbili, yenye kujigawa<br />

na hufanana. Yeye si tafauti na<br />

wanawake wengine wote ambao<br />

wamekuwa wakiwapenda na<br />

kuwahusudu au hata kuwabusu<br />

baba zao. Tungependa kusikia<br />

mazuri kuhusu baba zetu.<br />

Hadi anastaafu, baba<br />

wa rafiki yangu, alikuwa ni<br />

mfanyabiashara, sina shaka<br />

kwamba alikuwa na mazowea<br />

ya kuchukua gazeti na kupitia<br />

makala iliyoandikwa na mtu wa<br />

aina yangu, mwenye mtizamo<br />

tafauti kuhusu baba yake na<br />

akautangaza hadharani; au<br />

kusikiliza hotuba ya mjumbe<br />

wa upinzani mwenye azma ya<br />

kudhoofisha heshima yeyote ile ya<br />

kisiasa, hata ile ambayo alikuwa<br />

nayo baba yake; au mbaya zaidi<br />

akamsikiliza mjumbe wa chama<br />

chake anayerusha makombora ili<br />

Makala<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

Ni wakati wa CCM wahafidhina kupevuka<br />

Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhabib Amani Abeid Karume<br />

kutafuta umaarufu wa kisiasa.<br />

Lakini, kama mtoto wa<br />

mwanasiasa mashuhuri hapa<br />

Tanzania , ninao uzoefu wa<br />

yote hayo, au zaidi ya haya,<br />

siandiki hivi kutafuta huruma<br />

ya yeyote, kwani ninafahamu<br />

tosha kwamba ukosowaji wa<br />

wazi ni sehemu ya maish ya<br />

mwanasiasa, na kwa kawaida<br />

nadhani, lazima uhamasishwe,<br />

ndiyo sababu nikaandika hisia<br />

zangu. Kwa udhati ninaowakosea<br />

na kuwakera, ipo na kuangukia,<br />

na hivyo ndivyo nilivyoishi.<br />

Ipo kanuni muhimu isemayo,<br />

kuwa mtoto, hasa wa kike wa<br />

mwanasiasa ni kuchagua kuwa<br />

na ngozi (gamba) gumu, yaani<br />

si rahisi kukasirika. Pasi na<br />

ngozi ngumu, nachelea kusema,<br />

watoto wa kike wa wanasiasa,<br />

wote wangeliathirika kutokana<br />

na mitetemeko ya kisaikolojia.<br />

Kwa miaka mingi mgodi<br />

umegeuka kuwa kichaka cha<br />

ndovu (tembo) kizee.<br />

Kiasi ya wiki moja hivi,<br />

CCM (Chama cha Mapinduzi)<br />

kilihitimisha Mkutano wake<br />

Mkuu wa 8, kwa shangwe<br />

kubwa. Khadija Kopa, gwiji<br />

wa taarab, akawaburudisha<br />

takriban wajumbe 2400,<br />

wake zao na wafuasi wao,<br />

wote wakiwa wamevaa sare<br />

za kijani na manjano, za<br />

CCM, ndani ya ukumbi, mjini<br />

Dodoma . Vibendera tele vya<br />

CCM vikipepea, wakicheza<br />

kwa furaha iliyopelekea<br />

kuchagua viongozi wao wapya<br />

kwa umakini. Viongozi hao<br />

ni pamoja na Mwenyekiti wa<br />

CCM Taifa na wajumbe 20 wa<br />

NEC. Mkutano Mkuu wa 8 wa<br />

CCM pia ulihitimisha Miaka 10<br />

ya Uongozi wa Amani Abeid<br />

Karume aliyoitumikia kama<br />

Makamu Mwenyekiti wa CCM,<br />

upande wa Zanzibar .<br />

Kwa wale wasiomjua, mbali<br />

ya kuwa ni Raisi Mstaafu wa<br />

Zanzibar , pia ningelipenda<br />

kuwajulisha kwamba Amani<br />

Abeid Karume, ni mashuhuri<br />

sana kwangu kwa kuwa yeye ni<br />

baba yangu mzazi.<br />

Jioni ya Novemba 14, 2012,<br />

niliwasha TV kwa azma mahsusi<br />

ya kumuangalia Amani Abeid<br />

Karume akiagana na CCM,<br />

kama Makamo Mwenyekiti<br />

wa Zanzibar . Kusema ukweli,<br />

nilitamani kumsikia yeye<br />

akimshukuru mama yangu<br />

mzazi aliyekuwa naye imara<br />

kwa miaka 44. Nilimsikiliza<br />

Abdulrahman Kinana akitoa<br />

maazimio ya CCM; nikamuona<br />

Khadija Kopa pamoja na mama<br />

yangu wakicheza; nikamsikia<br />

Pius Msekwa akitoa hotuba yake<br />

ya kuaga, na hatimaye Amani<br />

Karume akipanda jukwaani ili<br />

naye atoe hotuba yake.<br />

Hotuba ya Karume ya Kuaga<br />

imekuwa gumzo na yenye<br />

kujadiliwa sana kati ya zote<br />

kutokea Mkutano Mkuu wa 8 wa<br />

CCM; siyo azma yangu kuijadili<br />

na kuifafanua hotuba hiyo, kwani<br />

ninayo fursa ya dhati kabisa ya<br />

kuelewa alichokusudia, wala<br />

haikuwa dhamira yangu kuitetea<br />

hotuba yake hiyo, kwamba<br />

kulikuwapo mamia ya mistari<br />

iliyoandikwa na kisha maelfu<br />

ya maneno yaliyosemwa kuunga<br />

mkono hotuba yake. Niko hapa<br />

kujadili, kile ninachoamini kuwa<br />

chanzo na mzizi wa fitna za<br />

kuirudi na kuipinga hotuba<br />

hiyo kwa baadhi ya Wana-CCM<br />

Zanzibar.<br />

Nilivyomsikiliza yeye<br />

nikamuelewa, kama ilivyo<br />

kawaida, hakuweza kuficha<br />

furaha yake anayochukulia kuwa<br />

ni mwisho mwema wa mafanikio<br />

makubwa ya tangu alipoitumikia<br />

CCM, zaidi ya miaka 10, huku<br />

pia ukiwa muda wake muafaka<br />

wa kuwasilisha mawazo ya<br />

umma na pia kwa kuzingatia<br />

mtazamo wa chama chake.<br />

Hapakuwa na hitilafu yoyote<br />

kutokana na kile alichokielezea,<br />

alijadili Historia ya CCM,<br />

Serikali ya Umoja wa Kitaifa<br />

ya Zanzibar, na Mchakato wa<br />

Marekebisho ya Katiba; Jukumu<br />

la Uongozi na Uongozi Bora;<br />

na pia furaha yake kuona damu<br />

changa au sura mpya zikiibuka<br />

ndani ya Uongozi wa CCM.<br />

Kwa ufupi, juu ya Historia ya<br />

CCM, Karume alilikumbusha<br />

Taifa kwamba CCM ni Muungano<br />

wa Vyama Viwili- Afro Shirazi<br />

Party kutoka Zanzibar, na TANU<br />

kwa upande wa Tanganyika-<br />

ambavyo viliamua kuungana<br />

na kwa azma ya kuufikia<br />

ufanisi, akatanabahisha warithi<br />

wasije kusahau azma ya<br />

Waasisi, hususan Waasisi wa<br />

ASP walioweka misingi imara,<br />

inayokwenda sambamba na<br />

utekelezaji wa dhati wa Azimio<br />

la Umoja wa Mataifa la Haki za<br />

Binaadamu; ili kuondosha hali<br />

zote za ubaguzi, ukandamizaji,<br />

na kadhalika.<br />

Kuhusiana na Serikali ya<br />

Umoja wa Kitaifa, Karume<br />

alionelea kwamba hili lilikuwa<br />

ni chaguo la Wazanzibari<br />

wenyewe kwa asilimia 64,<br />

ya wingi wa Kura ya Maoni,<br />

lililopelekea Mabadiliko ya<br />

Katiba ya Zanzibar , na hivyo<br />

CCM lazima waheshimu chaguo<br />

hilo .<br />

Kwa upande wa Mchakato<br />

wa Marekebisho ya Katiba<br />

unaoendelea sasa, Karume<br />

aliwataka wahusika wa Chama<br />

chake, pamoja na Viongozi,<br />

kuwacha watu watoe mawazo<br />

yao kwa uhuru, na hasa juu ya<br />

namna ya Muungano kati ya<br />

Tanganyika na Zanzibar ; uhuru<br />

huo unaweza kutekelezeka pale<br />

ambapo mamlaka hazitowateza<br />

nguvu.<br />

Hatimaye, Karume aliinasihi<br />

C C M k w a m b a i n a h i t a j i<br />

kushinda nyoyo na akili za<br />

watu, iwapo inataka kubakia<br />

yenye kukubalika, na hiyo<br />

inategemea utawala wa sheria<br />

na kwa heshima ya kujali, wala<br />

siyo kwa mabavu na vitisho.<br />

Kwa ukweli na kwa mkato<br />

kabisa, sitaomba radhi kwa<br />

kutamka hadharani kwamba<br />

Amani Karume ni mtu aliyeko<br />

moyoni kwangu, hasa ya<br />

kwamba pamoja na yote, aliweza<br />

k u k u m b u k a k u m s h u k u r u<br />

mama yangu. Baada ya kwisha<br />

kukubainishia uhusiano wangu<br />

na Amani Karume, na kwa<br />

nafasi yake maalumu ndani ya<br />

moyo wangu, nimeshaondosha<br />

dhima, lililobaki nasema “kuwa<br />

mwangalifu na utahadhari”.<br />

Hata hivyo, nilishitushwa<br />

kupita kiasi, kutokana na ile fitna<br />

ya sumu mbaya, pale baadhi<br />

ya wafuasi wa Chama chake<br />

walivyoichukulia hotuba yake.<br />

Kwa wafuatiliaji wa habari<br />

wanajua kwamba baadhi ya<br />

Wana-CCM walikasirishwa mno<br />

na hotuba hiyo na waliamua<br />

kuirarua (kuichanachana) Picha<br />

kubwa ya Karume iliyokuwapo<br />

Michenzani, Zanzibar .<br />

Kwanini makundi ndani ya<br />

CCM Zanzibar yakaguswa mno<br />

na maneno ambayo hayakuwa na<br />

lolote zaidi ya kueleza kwamba<br />

mamlaka ya Chama kuongoza<br />

inatokana na ridhaa ya watu,<br />

na ni watu hao ambao hapana<br />

budi kuwaheshimu, na kuachiwa<br />

wawasilishe mawazo yao kwa<br />

uwazi? Nahofia kwamba hii ni<br />

athari mbaya ya kutofahamu<br />

historia ya CCM na ya Nchi<br />

yetu.<br />

Kwa upande wa Zanzibar,<br />

Mzazi au Mtangulizi wa CCM,<br />

yaani Afro Shirazi Party, kilikuja<br />

madarakani baada ya Mapinduzi,<br />

na hadi Marekebisho ya Katiba<br />

ya mwaka 1992, haki ya CCM<br />

kuiongoza Tanzania , ikilindwa<br />

na Katiba. CCM haikuwa na hati<br />

ya kuongoza kutoka kwa Mungu,<br />

lakini kwa Taifa lisiloendeshwa<br />

kidini, kama ilivyo Jamhuri ya<br />

Muungano wa Tanzania, haki<br />

ya Katiba ilikaribia kwamba<br />

ni hati kutoka kwa Mungu,<br />

ambayo CCM ilipata. Kabla ya<br />

Marekebisho hayo ya Katiba,<br />

Sheria No 3 (1) ya Katiba ya<br />

Jamhuri ya Muungano wa<br />

Tanzania , ikisomeka kama<br />

ifuatavyo:<br />

“Jamhuri ya Muungano ni<br />

Taifa la Kidemokrasia na la<br />

Kijamaa la Chama kimoja”.<br />

Hakuna bahati nasibu hapa,<br />

ni “Chama Kimoja cha Siasa”<br />

kilichokusudiwa na Katiba.<br />

Uoni wangu ni kwamba,<br />

baadhi ya Wana-CCM Zanzibar,<br />

kwa bahati mbaya wanashindwa<br />

kupambanua baina ya ukweli<br />

halisi na mitizamo yao.<br />

Utengamano huo unahamasishwa<br />

zaidi na harakati ya hivi karibuni<br />

ya kikundi cha takriban watu 50<br />

hivi, akinamama na wasichana,<br />

wakiwa wamevalia sare za<br />

CCM, ambao kawaida hujiweka<br />

safu za usoni za mikutano; hawa<br />

ni kama kwamba huchochewa<br />

ghafla na mtu, nao wakaibuka<br />

kwa kuimba kwa kibwagizo<br />

cha Komando! Komando!<br />

Komando! Kibwagizo hiki ni<br />

cha kuwahadaa watu na kuihadaa<br />

hadhira, ili iweze kuamini kuwa<br />

watu hao ni waumini wa dhati<br />

wa Raisi Mstaafu wa Zanzibar<br />

wa CCM mwaka 1990- 2000,<br />

Salmin Amour, aliyependelea<br />

mwenyewe jina la Komando,<br />

kutokana na hulka yake ya kukosa<br />

uvumilivu dhidi ya wapinzani<br />

hasa, CUF, na kuthibitisha imani<br />

hiyo pale alipowapeleka jela bila<br />

ya hatia, Viongozi 20 wa Chama<br />

cha Wananchi, CUF.<br />

Bila shaka, watambuzi<br />

tambueni ujumbe ni huo,<br />

vibaraka wanausambaza wazi<br />

wazi pasi na kificho. Vibaraka<br />

wahafidhina wanachohitaji ni<br />

CCM Zanzibar kutawaliwa na<br />

“Komando” katika himaya zake,<br />

hatimaye asisalimike “adui”<br />

yeyote kutokana na makucha<br />

ya chuma wanayostahiki. Wapo<br />

wanaojidanganya vipembeni,<br />

chini ya vivuli vya Wahafidhina<br />

wa Chama, bado wakiamini<br />

kuwa na haki pekee ya kuendelea<br />

kutawala, ati waliikomboa<br />

Zanzibar kutokana na Usultani,<br />

na ati mabadiliko ya katiba<br />

yamewawacha solemba kama<br />

siyo kupotea kabisa, tena<br />

katika ulimwengu huu wa siasa<br />

makini za ushindani ambapo<br />

hata Watanzania wanahitaji<br />

kuchagua chama kipi kitawale<br />

na kinachowafaa kuwaongoza,<br />

wala si vinginevyo.<br />

Vyema sawa! wote ambao<br />

wamediriki kutoa hisia zao na<br />

ambao waliitumikia Zanzibar<br />

kutoka katika makucha ya<br />

Usultani, sasa wameshafariki au<br />

vinginevyo ni watu wazima sana<br />

; hao hawakuongoza Mapinduzi<br />

ili hatimaye waanze ulimbukeni<br />

waje kufia ndani ya Boma la<br />

Sultani lisilokuwa na kitu!<br />

La kuzingatia ni kwamba,<br />

kila baada ya miaka mitano<br />

tunahitaji vyama vyote vya siasa<br />

kuwatoa wagombea wao bora<br />

na kuwapanga mstari mbele<br />

yetu kama kwamba ni shindano<br />

Inaendelea Uk. 11


8<br />

Na Khalid S Mtwangi<br />

SALALAH! Hiyo ilikuwa<br />

dharuba kali!! Namshukuru<br />

sana Mhariri wa gazeti la<br />

Raia Mwema kunijulisha<br />

kuwa kimetokea kimbunga<br />

hicho kabla hakikupata<br />

nafasi ya kunisomba mpaka<br />

labda baharini!<br />

Wa s o m a j i w e n z a g u<br />

w a t a i k u m b u k a m a k a l a<br />

niliyoandika na kuchapishwa<br />

na AN NUUR toleo lake la<br />

tarehe 23 November, 2012.<br />

Hoja zangu zilikuwa zimelenga<br />

k u m u u n g a m k o n o B w<br />

Evarist Chahali kwa maoni na<br />

mawazo yake ya kimapinduzi<br />

yaliyochapishwa mara tatu kwa<br />

mfululizo. Namshukuru sana<br />

Mhariri wa RaiaMwema kwa<br />

hatua ya kijasiri aliyochukua<br />

kunitumia baadhi ya maoni ya<br />

wasomaji wenzangu ambayo<br />

yalitumwa kwake kupitia email.<br />

Amenifurahisha sana kwa<br />

kitendo hicho pia nawapongeza<br />

wale waliotoa maoni yao,<br />

naamini kwa moyo mkunjufu<br />

k a b i s a . N a m i n a j a r i b u<br />

kuyajibu hayo waliyouliza ama<br />

kunikosoa na ninafanya hivyo<br />

kwa moyo mkunjufu kabisa<br />

hasa kwa vile baadhi yao bila<br />

shaka, kama walivyoeleza<br />

wenyewe kwa majina ya<br />

bandia, wananifahamu sana<br />

na bila shaka tumekuwa na<br />

uhusianao mzuri kwa muda<br />

wote tuliofahamiana. Bahati<br />

mbaya wameficha majina yao.<br />

Mimi nipo wazi kabisa kwa<br />

majadiliano, waelewe hivyo.<br />

Hebu nianze na yale makali<br />

sana kutoka kwa anayejiita<br />

USTADH PENGO; namuomba<br />

aniruhusu nami nimwite<br />

U S TA D H M U K O M B E<br />

MONSIGNOR PENGO. Huyu<br />

Mukombe kweli ananifahamu<br />

vizuri pamoja na familia yangu,<br />

ila tu kamsahau mwanangu wa<br />

kiume aitwaye SHABANI<br />

MTOKA MTWANGI. Huyu<br />

ni Telecom Engineer akiwa<br />

na Masters. Sasa ningependa<br />

kumjibu kuhusu ama kuandika<br />

au kutokuandika nambari<br />

kwenye kartasi za mitihani.<br />

Ningemuomba afanye<br />

utafiti wa ndani kuhusu hili.<br />

Hata hivyo wacha nimueleze<br />

yaliyompata huyu Tatu sasa<br />

mwenye Ph D. (Shahada ya<br />

Uzamivu). Kama atakumbuka<br />

vizuri, kwanza hawa vijana<br />

wote walisota nyumbani<br />

kwa takriban mwaka mzima<br />

Makala<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

Mbagala Tena: Bado ni Uislam na Ukristo<br />

ikiwa wamekosa shule ya<br />

kuwapokea. Dhamira ilikuwa<br />

wapate nafasi katika shule za<br />

serekali. Hilo likawa gumu<br />

sana kwa sababu ambazo<br />

wakati ule sikuzielewa, baadae<br />

nilielewa kuwa ni majina yao<br />

ama langu ndiyo yalisababisha<br />

vikwazo.<br />

Tatu alikuwa kafaulu<br />

mtihani wa kidato cha nne<br />

(form IV) akiwa na Division<br />

One nzuri kabisa akiwa na<br />

dhamira ya kuendelea Form V<br />

mchepuo wa sayansi. Hakika<br />

alikuwa keshapata shule ya<br />

kumwezesha hayo kule Kenya.<br />

Waliofuata, yaani Mtoka na<br />

Asha walikuwa wakitafuta<br />

nafasi katika form III na II.<br />

Nilipata msaada wa kigogo<br />

(hakika huyu hakuwa kigogo<br />

bali, kutokana na nafasi<br />

yake serekalini, alikuwa ni<br />

GOGO na ndivyo iliwezekana<br />

kumpatia Tatu nafasi ya Form<br />

V katika shule moja hapa<br />

Dar es Salaam. Niliambiwa<br />

a s i n g e w e z a k u f u a t i l i a<br />

mchepuo wa sayansi kwa<br />

sababu katika mtihani wake<br />

wa Form IV ulichanganya<br />

“Physics with Chemistry”<br />

ilihali kwa kawaida masomo<br />

haya mawili hutahiniwa mbali<br />

mbali. Niliuliza inakuwaje<br />

wanafunzi kutoka Kenya<br />

wanapokewa katika vitivyo<br />

vya uhandisi na udaktari Chuo<br />

Kikuu cha Dar es Salaam?<br />

Niliambiwa kwa kifupi tu<br />

na kwa ukali kuwa nikubali<br />

alichopata huyu binti au iwe<br />

basi akae nyumbani. Kama<br />

wanavyosema Waswahili,<br />

Ustadh Monsignor Mukombe<br />

Pengo wewe hukuwepo lakini<br />

malaika wako alikuwepo.<br />

Ningependa kumshukiuru<br />

sana hili GOGO serekali kwa<br />

msaada alioutoa kwa sababu<br />

moja kubwa kwamba kumbe<br />

kukosa shule kwa binti huyu<br />

ilikuwa ni njama ambayo<br />

alijitoa wakati mmoja wa hawa<br />

wakubwa Wizara ya Elimu<br />

aliropoka baada ya kupata<br />

maagizo kutoka juu. Kumbe<br />

jambo hilo lilimuudhi sana na<br />

katika kuropoka ilijidhihirisha<br />

kuwa Tatu alikosa nafasi shule<br />

kwa sababu jina lake lingine<br />

Zubeda ambalo kabisa ni la<br />

Kiislamu. Kwa kuwa Bint<br />

Shaaban, Binti wa Kitanzinia<br />

inayodaiwa kutokuwa na udini,<br />

alinyimwa nafasi ya kusoma<br />

kidato cha 5 pamoja na kuwa<br />

na DIVISHENI ONE!!!<br />

Ningependa pia kuwajulisha<br />

wasomaji wenzangu kuwa hilo<br />

GOGO lililonisaidia kwanza<br />

nilikutana naye shule katika<br />

miaka ya hamsini ingawa<br />

yeye akiwa mkubwa kwa umri<br />

alikuwa madarasa ya mbele; pia<br />

nilipomuomba msaada tulikuwa<br />

tukikutana katika pilika pilika<br />

za kujenga nchi. Naongeza<br />

kuwajulisha wasomaji na hasa<br />

huyu Mokombe Monsignor<br />

Utadh Pengo kuwa hili Gogo<br />

ni Mkatoliki muumini wa<br />

dhati kabisa. Alinisaidia kwa<br />

kuangalia urafiki wetu na<br />

wenzake wakamshushukiwa<br />

kwa hasira! Na huo ni<br />

wakati wa Mwalimu Nyerere<br />

anayetukuzwa leo kwamba eti<br />

aliondoa udini!<br />

Bila kuwachosha wasomaji,<br />

itatosha kueleza kuwa hao<br />

watoto wangu wengine nao<br />

ilikuwa mbinde kupata nafasi<br />

shule ya Forodhani ambayo<br />

wakati ule ilikuwa imetaifishwa<br />

na imekuwa mali ya umma.<br />

Namshukuru sana rafiki yangu<br />

mmoja aliyenisaidia sana<br />

kufanikisha Hassan akaweza<br />

kuendelea na shule nzuri hapa<br />

Dar es Salaam mjini mpaka<br />

akafanikiwa kufuzu D DS<br />

(sio MD) kama alivyoandika<br />

Ustadh Mukombe Monsignor<br />

Pengo. Napenda kuwajulisha<br />

wasomaji wenzangu kuwa<br />

rafiki yangu huyu ni muumini<br />

thabit wa Kanisa Katoliki<br />

na mpaka kesho tutakuwa<br />

tunamshukuru rafiki yetu<br />

mpendwa.<br />

Sijasahau historia ya<br />

Tanganyika kuhusu elimu<br />

hata kidogo. Nakumbuka<br />

kweli kuwa palitungwa sera<br />

ya upendeleo kuwasaidia<br />

Wananchi waliokuwa nyuma<br />

kielimu na ambayo ilijumuisha<br />

Waislamu pia. Nadhani ni<br />

yeye huyu Ustadh Monsignor<br />

Pengo ambaye ama kasahau<br />

yaliyotokea au kapuuza tu<br />

ukweli. Kwanza nakumbuka<br />

s e r a h i y o h a i k u f u a t w a<br />

k w a v i t e n d o n a h i l i<br />

nilihakikishiwa na mwalimu<br />

mmoja ambaye alikuwa ni<br />

Mkaguzi Mwandamizi wa<br />

Shule na ambaye nilisoma<br />

naye sekondari. Huyu sasa<br />

ni marehemu. Halafu ni<br />

mkumbushe kuhusu mitihani<br />

ya darasa la saba katika miaka<br />

ya sabini. Kwa mbinu za ujanja<br />

sana haikuwa inajulikana kama<br />

wale walioendelea Kidatu cha<br />

Kwanza walikuwa wamepasi<br />

(kufaulu) mitihani yao ama<br />

hapana kwa vile kilikuja<br />

Kiswahili cha ama kachaguliwa<br />

au hakuchaguliwa basi. Hapa<br />

niruhusu ni mnukuu Professor<br />

William Ochieng’ wa Chuo<br />

Kikuu cha Maseno, Kenya.<br />

Aliandika hivi :-<br />

“The Muslims in our<br />

midst have a point when they<br />

complain that the Western<br />

Colonial powers in East Africa<br />

(mainly British) did very little<br />

to promote the welfare of the<br />

Islamic communities in our<br />

region……. While most Kenyan<br />

Christian communities and<br />

societies are today led by very<br />

highly educated leaders Islam<br />

and Islamic societies lack such<br />

leaders. AND IF THE MAIN<br />

RESPONSIBILITY OF THE<br />

NATIONAL LEADERSHIP IS<br />

THE DISTRIBUTION OF THE<br />

NATIONAL CAKE, THEN<br />

IT FOLLOWS THAT THOSE<br />

LIKE MUSLIMS WITHOUT<br />

STRONG REPRESENTATION<br />

AT THE TOP CANNOT HOPE<br />

TO GET A FAIR SHARE OF<br />

THE CAKE. (msisitizo ni<br />

mwandishi huyu)<br />

(The SUNDAY NATION,<br />

May 30, 1993)<br />

Nadhani hakuna haja<br />

ya kutafsiri kipande hiki<br />

wasomaji wenzangu wengi<br />

watakielewa.<br />

Baada ya hayo nchi nzima<br />

ilizuka na shangwe pale shule<br />

binafsi zikiwemo za makanisa<br />

zilipotaifishwa. Lakini yale<br />

yaliyofuata baadae kwa ujanja<br />

mkubwa yalifuta kabisa sifa<br />

ile iliyotolewa mwanzoni.<br />

Lililotokea ni kwamba shule<br />

nyingi sana za makanisa (za<br />

misheni) ziligeuzwa kuwa<br />

seminari; hivyo zilipokea<br />

waumini wa makanisa hayo<br />

tu. Baada ya kubaini ujanja<br />

huo Waislamu nao walitaka<br />

kuigeuza shule yao moja ya<br />

Kinondoni kuwa seminari.<br />

Ni jambo la kusikitisha sana<br />

kwamba hakuwa mwingine<br />

bali Malimu Julius Nyerere<br />

ambaye alitia guu na kukataza<br />

jambo hilo kutokea. Wakati huo<br />

tayari kulikuwa na seminari za<br />

misheni zaidi ya kumi na tatu<br />

mbazo zilikuwa zikipokea<br />

wanafunzi wa masomo ya<br />

kawaida na wala siyo ya upadri<br />

au uchungaji.<br />

Lakini hata ukija katika<br />

hizo za serikali, waliopewa<br />

nafasi za uongozi walikuwa<br />

‘mapadiri’ na wafuasi wao na<br />

ndio hao waliokuwa wanaamua<br />

nani kachaguliwa. Watoto<br />

wa Kikristo waliochaguliwa<br />

wakawa asilimia 90 wakati<br />

wale wa Kiislamu, haikuwahi<br />

idadi yao kuzidi aslimia 15<br />

japo walikuwa ndio wengi<br />

kwa zaidi ya asilimia 70 katika<br />

shule za msingi.<br />

Hebu nimnukuu Waziri<br />

Mkuu mstaafu Muheshimiwa<br />

Frederick Sumaye:-<br />

“The Prime Minister,<br />

Frederick Sumaye, has<br />

cautioned Tanzanians not to<br />

harp on their religious beliefs<br />

when undertaking development<br />

a c t i v i t i e s , p a r t i c u l a r l y<br />

education. Speaking at the<br />

event (sic)at fund raising event<br />

at the Karimjee Hall in Dar<br />

es Salaam over the weekend,<br />

Premier Sumaye said whereas<br />

seminaries are thought to<br />

be preparing students for<br />

priesthood, in actual fact few<br />

of them became (sic) priests<br />

and the rest took up (sic)<br />

responsible positions in the<br />

society.<br />

“Evidence has shown that<br />

most of the students from<br />

seminary schools are the ones<br />

who held (sic) some similar<br />

government positions, whereas<br />

few of them have become priests<br />

and bishops in Tanzania.” Said<br />

Sumaye, adding that there is<br />

need to support such schools.<br />

H e t h e re f o re u rg e d<br />

Tanzanians to avoid religious<br />

ideologies because at the end<br />

of the day, those in responsible<br />

positions render services to<br />

all people regardless of their<br />

religious leanings.”…………..<br />

(The African 19/07/2004)<br />

Alisema hayo katika<br />

harambee ya kukusanya pesa<br />

iliyoandaliwa na Kanisa<br />

Katoliki naye akiwa mgeni<br />

rasmi.<br />

Naye Kipepeo anapaa<br />

kwa kujiamini kabisa kuwa<br />

n i m a k o s a k u w a l a u m u<br />

wamishionari kwa ukosefu<br />

wa elimu miongoni mwa<br />

Waislamu. Nakubaliana naye.<br />

Wanachosema Waislamu ni<br />

kupinga ile dhana potofu<br />

kuwa Waislamu hawatafuti<br />

ile elimu ya mzingira, ati<br />

wao wanashughulika kufika<br />

Madrasa tu. Ukweli ni kwamba<br />

katika kutafuta elimu vijana<br />

wengi wa Kiislamu walidiriki<br />

kuingia zile shule za White<br />

Fathers, Benedictine Fathers<br />

na kadhalika. Badala ya<br />

kuwapa elimu vijana hawa,<br />

wale maFather walichukua<br />

muda wao mwingi kuwapoteza<br />

vijana wale na kuwabatiza.<br />

Ni ajabu kuwa hasa Kanisa<br />

Katoliki kamwe hawastahimili<br />

kuwaona watu wengine<br />

wanafuata dini zao, hasa ikiwa<br />

dini hiyo ni Uislamu. Jambo<br />

hilo linawakera sana. Bwana<br />

Kipepeo atakumbuka kuwa<br />

nilitoa mfano wa Mzazi wangu<br />

mikasa kama hiyo ilimpata<br />

pale Central School, Ujiji<br />

katika miaka ya ishirini. Mpaka<br />

leo hii vijana wa Kiislam<br />

wanaosoma shule za Kikristo<br />

wanalazimishwa kuhudhuria<br />

misa kanisani.<br />

Waislamu wanafundishwa<br />

na dini yao kuwa ni kosa<br />

kumlazimisha mtu kufuata<br />

dini yeyote ile. Uhispania<br />

ilitawaliwa na Waislamu<br />

takriban karne saba na<br />

wakati wote huo Wakristo<br />

waliruhusiwa kufuata dini yao<br />

ya Katoliki. Lakini mara nchi<br />

hiyo ilipotekwa na Wakristo<br />

kukatokea “INQUISITION”,<br />

jambo ambalo mpaka leo hata<br />

Wakristo wanaona lilikuwa<br />

ni jambo la aibu. Nako India,<br />

takriban nchi nzima ilikuwa<br />

chini ya wafalme Waislamu<br />

mpaka Waingereza walipoingia<br />

kuitawala nchi hiyo. Mpaka leo<br />

Wahindi wengi wamebakia<br />

na dini zao za KIHINDU<br />

a m a B U D D H A . H a p a<br />

nyumbani Sultani wa Zanzibar<br />

aliwakaribisha mishionari kwa<br />

moyo safi kabisa; lakini leo<br />

hii makanisa wanaupiga vita<br />

sana Uislamu. Inanikumbusha<br />

yule mwandishi mmoja wa<br />

magazeti aliyeapa kuwa kamwe<br />

hataruhusu Tanzania kujiunga<br />

na OIC; yaani atatumia kalamu<br />

yake kupiga vita jambo hilo.<br />

Hana sababu ya msingi zaidi<br />

ya chuki.<br />

M w i s h o n i n g e p e n d a<br />

kutoa sikitiko langu. Katika<br />

makala zake Bwana Evarist<br />

Chahali alionyesha kuelewa<br />

na kutetea kidogo ile hali duni<br />

Inaendelea Uk. 9


9<br />

KATIKA toleo la gazeti moja<br />

litokalo hapa nchini kwetu<br />

kila siku ya Alhamisi, wiki<br />

iliyopita 22/ 11/2012, ukurasa<br />

wa 18 kulikuwa na makala<br />

iliyoandikwa na kaka yangu<br />

mpenzi isemayo Si lazima<br />

Seif kuwa Makamo wa Rais.<br />

Katika makala hiyo mwandishi<br />

a l i a n d i k a m e n g i l a k i n i<br />

alionekana wazi kutamani<br />

na kuegemea zaidi katika<br />

‘episode’ ya siasa za chuki,<br />

ubaguzi na uhasama.<br />

Mwandishi ameonekana<br />

kutamani yale yaliyopita enzi<br />

zile za utawala wa siasa za chuki<br />

na ubaguzi zirejee visiwani bila<br />

ya kueleza hassa faida na mazuri<br />

yaliyopatikana enzi za siasa hizo<br />

chafu za kupigana bila sababu na<br />

kufikia hadi kuamuriwa kulala<br />

saa moja jioni kwa kisingizio<br />

cha uvunjifu wa amani enzi zile<br />

za utawala wa Komandoo. Kwa<br />

hapa tulipofika sasa, sidhani<br />

kwamba kuna Mzanzibari<br />

(halisi) mwenye akili timamu<br />

anaependa turudi kule tulikotoka<br />

ambapo mwana CUF hakwenda<br />

harusini wala kumzika mwana<br />

CCM na mwana CCM hakwenda<br />

kununua bidhaa dukani kwa<br />

mwana CUF. Kipindi ambacho<br />

hata wanafamilia walifikia<br />

kutengana eti kwa kisingizio<br />

cha utofauti wa kisiasa bila ya<br />

kujali mustakbali na khatma ya<br />

Zanzibar na watu wake.<br />

Mwandishi huyo alimtaja<br />

Maalim Seif kuwa ni mtu<br />

ambae anataka kuona Zanzibar<br />

haitawaliki. Naona tumeanza<br />

kusahau historia. Hivi kama<br />

Maalim Seif anataka kuona<br />

Zanzibar haitawaliki angesimama<br />

na kuwa mstari wa mbele yeye na<br />

chama chake cha CUF kutafuta<br />

maridhiano (muafaka) kila<br />

pale palipotokea sintofahamu<br />

Zanzibar hasa kila baada ya<br />

matokeo ya chaguzi mbali mbali<br />

ambazo wananchi na wapiga<br />

kura hawakuwa na imani nazo<br />

kutokana na kugubikwa na kila<br />

aina ya uchakachuaji..!!?<br />

Hivi tumesahau kwamba<br />

amani na utulivu uliopo Zanzibar<br />

sasa ni zao la hali ya maridhiano<br />

na mshikamano wa Wazanzibari<br />

ambao uliasisiwa na Katibu<br />

Mkuu wa CUF na Makamo wa<br />

Kwanza wa Rais Maalim Seif<br />

Sharif Hamad pamoja nae Rais<br />

Mstaafu wa Zanzibar Alhabib<br />

Amani Abeid Karume chini ya<br />

kamati ya maridhiano..!!? Si<br />

Maalim Seif huyu aliyekuwa<br />

wa kwanza kuyakubali na<br />

kuyapokea kwa moyo mkunjufu<br />

matokeo ya uchaguzi mkuu wa<br />

mwaka 2010 pale Bwawani na<br />

kumuweka Ikulu Rais Dkt Shein<br />

huku wafuasi na wanachama wa<br />

CUF kuonekana kutoridhishwa<br />

na matokeo hayo kwa kipindi<br />

kile..?<br />

Unajuwa nini kiliwafanya<br />

wafuasi wa CUF kukusanyika<br />

karibu na sehemu ilopangwa<br />

kutangaza matokea ya uchaguzi<br />

kusindikiza tume ya uchaguzi<br />

kutangaza matokeo ya uchaguzi<br />

Makala<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

Kwa haya ya Ummar Mukhtar…Zenji hayana nafasi tena..!<br />

Na Soud Marhoun Al-<br />

Slemy, Zanzibar<br />

Rais Mstaafu wa Zanzibar<br />

Alhabib Amani Abeid<br />

Karume<br />

huo kwa kuhofia “up side<br />

down” ya matokeo hayo ya<br />

uchaguzi..!!?<br />

Tukumbuke ya kwamba<br />

mkusanyiko kama ule uliotokea<br />

pale Bwawani, watu wenye kudai<br />

haki kwa kuhisi kudhulumiwa<br />

inapelekea madhara makubwa<br />

(negative effects) kwa serikali<br />

au mamlaka husika pale subra<br />

inapofikia kikomo kwa wale<br />

wanaochoshwa kuomba haki<br />

ambayo siyo ya kuombwa na<br />

kuamuwa kupambana ili kupata<br />

haki.<br />

Tukumbuke ya kwamba<br />

Rais wa Misri Hosni Mubarak<br />

aliondoka madarakani bila<br />

khiyari baada ya Wamisri<br />

kukusanyika pale Tahrir Square<br />

na maeneo mengine ya Cairo<br />

baada ya kuona “enough is<br />

enough” kwa yaliyowakuta.<br />

Maalim Seif aliliona hilo na<br />

akaamuwa kujitoa muhanga<br />

na kuwakabili wafuasi wake<br />

na kuwaomba wapowe moto,<br />

ingawa hawakumuelewa vyema<br />

kwa kipindi kile pale Bwawani.<br />

Je! si busara na hekima zake<br />

Maalim Seif zilizozima jazba<br />

za wafuasi wale wa CUF<br />

pale Bwawani siku ile..!!?<br />

Je! mkusanyiko ule kama<br />

haukuzimwa usingeliligharimu<br />

taifa na amani yake..!? Vipi leo<br />

useme Maalim Seif hataki kuona<br />

Zanzibar inatawalika..!!?<br />

Ni kweli kwamba Maalim<br />

Seif ameteuliwa (appointed) na<br />

Rais Dkt Shein kuwa makamo<br />

wa kwanza wa rais Zanzibar.<br />

Lakini uteuzi huo haukuja<br />

kwa bahati mbaya wala kwa<br />

matakwa na mapenzi binafsi ya<br />

mheshimiwa rais, bali uteuzi<br />

huo umekuja kutokana na katiba<br />

ya Zanzibar iliyotungwa na<br />

wawakilishi wa Wazanzibari<br />

wote baada ya kuitishwa kwa<br />

kura ya maoni iliyokusanya<br />

maoni ya Wazanzibari waliotaka<br />

muundo huo wa serikali baada<br />

ya kuchoshwa na siasa chafu<br />

za ubaguzi, kutoaminiana na<br />

kupigana ambazo hazikuzaa<br />

matunda yoyote kwao. Ingawa<br />

kuna baadhi yetu tunaona hayo<br />

ndio maisha. Hivyo Chama Cha<br />

Wananchi CUF kilipendekeza<br />

kwa rais Dkt Shein baada ya<br />

kuridhishwa na sifa zake jina<br />

la Maalim Seif Sharif kwenda<br />

kukiwakilisha chama katika<br />

Katibu Mkuu wa CUF na<br />

Makamo wa Kwanza wa Rais<br />

Maalim Seif Sharif Hamad<br />

serikali ya Umoja wa Kitaifa<br />

(GNU) kutokana na kupata<br />

nafasi ya pili katika uchaguzi<br />

mkuu wa 2010.<br />

I n g a w a M a a l i m S e i f<br />

ameteuliwa na rais Dkt Shein<br />

haimaanishi ya kwamba abaki<br />

kimya bila ya kusema au kufanya<br />

chochote hata kama kuna<br />

dhulma au ukiukwaji mkubwa<br />

wa haki za kiraia ilimradi tu eti<br />

yumo serikalini. Sasa huyo ni<br />

kiongozi au gogo la mkarafuu<br />

linalosubiri kupasuliwa kwa<br />

shoka liingizwe kwenye moto<br />

kupika chakula cha wengine bila<br />

ya yeye kuonja..!!?<br />

Maalim Seif ni kiongozi,<br />

msaidizi na mshauri wa karibu<br />

sana wa rais kwa mujibu wa<br />

katiba ya Zanzibar. Maalim Seif<br />

amekula kiapo kwa jina la Mungu<br />

wake kutetea Zanzibar na watu<br />

wake mbele ya rais. Iweje leo<br />

aone haki haitendeki aendelee<br />

kubaki kimya huku wananchi<br />

ambao anawajibu wa kuwatetea<br />

wakiwa wanalalamika..??<br />

Ukiona ubaya uondowe kwa<br />

mikono yako, huwezi kuondoa<br />

ukemee au kama huwezi pia<br />

basi uchukie. Maalim Seif<br />

hakuwa na uwezo wa moja kwa<br />

moja kutumia mikono yake<br />

kuondosha ubaya ulojitokeza,<br />

lakini alionekana kuuchukia<br />

kwa asilimia mia moja na ndio<br />

mana akakemea kwa sauti<br />

kubwa iliyosikika kila ncha ya<br />

ulimwengu huu ambapo miale<br />

ya jua inapiga.<br />

Kila mmoja ni mchunga na<br />

ataulizwa kwa alichokichunga.<br />

Kwa hili Maalim Seif Mungu<br />

amemungoa Hamdullah!! Lakini<br />

pia tusisahau ya kuwa uongozi<br />

ni dhamana na utaulizwa kwa<br />

dhamana hiyo.<br />

Maalim Seif na chama chake<br />

cha CUF ni chimbuko la GNU, na<br />

umoja wa kitaifa ni sera ya CUF<br />

tokea 1992, iweje leo unamtaka<br />

Maalim Seif akiondoshe<br />

chama chake katika GNU eti<br />

kwa sababu hakuridhishwa<br />

na yaliyofanyika Zanzibar na<br />

ameikosoa serikali..!!? Zile zama<br />

za divide and rule zimepitwa na<br />

wakati na wala sidhani kwamba<br />

zitarejea ndani ya Zanzibar<br />

kwa sasa ambapo agenda kuu<br />

ya Wazanzibari walio wengi<br />

ni kudai Zanzibar huru yenye<br />

mamlaka kamili na kutambulika<br />

kwa heshima zote kitaifa na<br />

kimataifa.<br />

Tuchunge sana na kalamu<br />

zetu, ukitumia vizuri kalamu<br />

yako utajenga na utanufaika kwa<br />

kalamu hiyo, kushindwa kufanya<br />

hivyo ni kubomoa na likitokea<br />

lolote baya na la kuchukiza na<br />

wewe pia utaingia katika matata<br />

kwa namna moja au nyengine,<br />

kwa njia ya moja kwa moja au<br />

isiwe moja kwa moja, akiumia<br />

jirani yako umeumia wewe.<br />

Elewa ya kwamba Zanzibar<br />

sio mali ya CCM, CUF, taasisi<br />

za kidini, sio ya kwangu<br />

binafsi wala ya kwako, bali<br />

ni mali ya Wazanzibari wote<br />

na kila anaependa amani na<br />

maendeleo ya Zanzibar bila ya<br />

kujali dini, kabila, rangi wala<br />

tofauti za kisiasa. Na katika<br />

ulimwengu wa leo wenye<br />

kuongozwa na kutawaliwa<br />

kwa misingi ya kidemokrasia,<br />

uwazi (transparency) umetawala<br />

zaidi na kila mtu anakuwa huru<br />

kusema alichonacho na kutoa<br />

mawazo kuhusu juu ya kile<br />

anachokiamini yeye akilini<br />

mwake, na kwa upande wa<br />

maamuzi, walio wengi (mass)<br />

ndio wanaofuatwa. Hivyo basi<br />

si vyema kuanza kufanya roho<br />

mbaya, kijicho na husda juu ya<br />

amani ya Zanzibar na mwelekeo<br />

wa Wazanzibari walioshikana<br />

pamoja juu ya utoaji maoni<br />

kuhusu katiba mpya ambao<br />

umeonekana dhahir shahir bila<br />

ya woga, bila ya kumun’gunya<br />

maneno wala kupepesa macho<br />

wanadai mamlaka kamili ya<br />

nchi yao na haki zao kiujumla<br />

ambazo wamezikosa kwa miaka<br />

mingi sasa. Hili limekuwa<br />

mwiba na linawanyima usingizi<br />

na kusosa hata hamu ya kula<br />

baadhi ya watu wasioitakia<br />

mema Zanzibar ambao lengo<br />

lao ni kuifuta Zanzibar katika<br />

uso wa dunia kwa kuizamisha<br />

kusikojulikana. Kwa nini iwe<br />

nongwa na kioja cha mwaka<br />

wakati kila Mtanzania ana uhuru<br />

wa kutoa maoni kwa mujibu wa<br />

katiba iliyopo..!!?<br />

Sikubaliani kabisa na<br />

mtazamo finyu wa kuwagawa<br />

Wazanzibari, kuibana Zanzibar<br />

kwa maslahi binafsi, tena ya<br />

watu wachache wasio hata<br />

uzalendo wa Zanzibar.<br />

Mungu ibariki Zanzibar na<br />

watu wake!!<br />

Mbagala tena: Bado ni Uislam na Ukristo<br />

Inatoka Uk. 8<br />

waliyonayo idadi kubwa ya<br />

Waislamu nchini humu. Naona<br />

kuwa hakueleweka kabisa<br />

kama haya wanayoyasema<br />

kina Ustadh Mosingnor<br />

Mukombe Pengo na wenzake.<br />

Nami niliandika makala ile<br />

kujaribu kuziba mapengo<br />

niliyoyaona katika makala za<br />

Bw Chahali. Nilipokuwa shule<br />

ya sekondari (takriban miaka<br />

sitini iliyopita) kulikuwa na<br />

somo la “comprehension”<br />

ambalo lilikuwepo kuwasaidia<br />

wanafunzi mbinu za kuweza<br />

kuelewa kwa urahisi yale<br />

wanayoyasoma. Sijui kama<br />

somo hili liliendelea kuwepo<br />

kwa muda gani. Sasa hivi kweli<br />

hawa kina Ustadh (Monsognor,<br />

Mukombe) Pengo, Bw Kali,<br />

Bw Kipepeo, Bw (Mtume)<br />

Moses na (Malaika) Gabriel<br />

walishindwa kumuelewa Bw<br />

Chahali. Tukiwa karibu zaidi<br />

tujiulize walishindwa kuelewa<br />

yale niliyoandika mimi?<br />

Sidhani ilikuwa hivyo.<br />

Nilibahatika kusoma nakala<br />

ya jarida NEWSWEEK la tarehe<br />

January 23, 2012. Ukurasa wa<br />

kumi na tatu kulikuwa na<br />

mchoro (cartoon) ulioonyesha<br />

moyo wa BinAdam na ubongo<br />

pia wa BinAdam wakipigana<br />

mieleka. Katika jitihada ya<br />

kufumbua fumbo hilo kulikuwa<br />

na maelezo yafuatayo:-<br />

“……..the brain operates<br />

fundamentally in two modes.<br />

O n e i s a u t o m a t i c a n d<br />

emotional – in essence – a gut<br />

reaction………….Green has<br />

found that most of the time<br />

when we are deciding what is<br />

the right thing to do, what is<br />

happening in the brain is the<br />

emotional response, not the<br />

reasoned one…….”<br />

Haya ni maandishi ya Joshua<br />

Green “a leading researcher<br />

on morality and the brain.<br />

Green, 37, is a professor at<br />

Havard and a leader in moral<br />

psychology”. Inawezekana<br />

haya ndiyo yaliyowasibu<br />

hawa ndugu zangu walioshika<br />

kalamu “kunishambulia” kiasi<br />

hicho.<br />

Kwa hali ilivyo humu<br />

Tanzania na nikikumbuka<br />

u t a b i r i w a n d u g u y e t u<br />

Omwami Salva Rweyemamu<br />

nigependekeza kwa nguvu zote,<br />

kwa unyenyekevu kabisa kuwa<br />

ndugu zetu waKristo wapige<br />

konde nyoyo zao. Katika<br />

nyanja nyingi muhimu sana za<br />

nchi hii wao ndio wameshika<br />

mpini na Waislamu wameshika<br />

kwenye makali. Ingawa kuna<br />

viongozi kama Askofu Mkuu<br />

Mokiwa wa Anglican Church<br />

hakubaliani na hilo ukweli<br />

ni kwamba mfumo mzima<br />

katika nyanja nyingi nchini<br />

n i “ M F U M O K R I S TO ” .<br />

Kanisa Katoliki wanakubali<br />

na kujigamba katika kuongoza<br />

nchi.<br />

H i v y o h a w a n d u g u<br />

waKristo wanaweza kuwa<br />

“ M A G N A N I M O U S ”<br />

(samahani nimeshindwa<br />

kupata neno kama hilo la<br />

Kiswahili) na wakalegeza<br />

kamba kidogo ili Waislam nao<br />

wakaweza kujitikisa kidogo?<br />

Hivi hakuna aipendaye<br />

Tanzania akatuepusha na janga<br />

alilotabiri ndugu yetu Salva<br />

Rweyemamu?


10<br />

SIKU moja aliyekuwa Rais<br />

wa Kwanza wa Jamhuri wa<br />

Muungano wa Tanzania,<br />

ambae pia huitwa baba<br />

wa Taifa, hayati Mwalimu<br />

Julius Nyerere, alikuwa<br />

akitembelea kisiwa cha<br />

Pemba, kikazi. Katika safari<br />

yake hiyo ya mzunguko<br />

wa kikazi ilisadifu kupitia<br />

b a r a b a r a y a m k o a n i<br />

kwendea Chake Chake.<br />

Karibu na kichunjuu, hivi<br />

kuna krosi moja kubwa<br />

sana iliyokuwa na muundo<br />

wa herufi ‘S’.<br />

Wakati wakipita pale na<br />

msafara wa magari na jinsi<br />

njia ilivyokuwa mbovu,<br />

na makarama ya krosi ile<br />

ilivyochongeka, Mwalimu<br />

hakuamini kama anapelekwa<br />

Chake chake. Akauliza;<br />

“Tunakwenda, tunarudi?”<br />

Akaambiwa tunakwenda,<br />

il’hali gari ikiwa limeelekeza<br />

uso kule linakotoka na<br />

likiendelea na mwendo ule<br />

ule katika msafara. Mwalimu<br />

akasubiri ajionee kioja,<br />

akatulia.<br />

Miaka zaidi ya 30 tangu<br />

Mwalimu aulize suali hili,<br />

na sasa ni karibu miaka 13<br />

tangu Mwalimu afariki,<br />

hakuna mmoja wetu aliepata<br />

kufikiria falsafa ya maneno<br />

haya, yaliyochukuliwa<br />

kama mzaha wa Mwalimu<br />

tu wakati ule na hadi sasa.<br />

Kusema ukweli maneno haya<br />

hayakustahili kutiwa kapuni<br />

na kama kuna aliyefanya<br />

hivyo amekosea. Ndio maana<br />

mimi nilie yaweka akiba<br />

leo nayavongonyowa na<br />

kuwatunukia. As’aa huenda<br />

mukazinduka.<br />

Zanzibar, nchi kinyonga,<br />

mara nchi, mara si nchi,<br />

vyovyote tukavyoiita, itaitika.<br />

Hadi sasa Visiwa hivi vinapata<br />

umri wa miaka isiyopungua<br />

48 tangu kuachwa na mkoloni<br />

mweupe na kujitawala.<br />

Miaka hii si kidogo hasa<br />

kwa kuyatathmini maendeleo<br />

yetu na ya nchi kwa ujumla.<br />

Naamini huu ni wakati<br />

muafaka wa kujiuliza, ikiwa<br />

SMZ ndie mtawala mkuu wa<br />

visiwa hivi tangu miaka hio,<br />

na anaehubiri maendeleo<br />

kila uchao, tuiulize Serikali<br />

yetu ya SMZ suali lile<br />

lile, ‘TUNAKWENDA,<br />

TUNARUDI?’<br />

Nchi hii ilikuwa ina<br />

maendeleo makubwa na<br />

ilikuwa na akiba isiyomithilika<br />

katika mahakibizo ya fedha<br />

duniani mpaka zama za miaka<br />

ya mwisho ya 1970. Serikali<br />

zetu za SMZ zilizopita<br />

zilikuwa zimetawaliwa<br />

kimabavu kweli kweli<br />

lakini mengi tuliyaona sasa<br />

hatuyaoni. Ndani ya miaka<br />

Makala<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

SMZ na kasumba za maendeleo - ‘tunakwenda, tunarudi?’<br />

nane ya Mzee Abeid Karume,<br />

tulipata majumba makubwa<br />

nchi nzima. Tukajengewa<br />

sipitali na vituo vya afya.<br />

N d a n i y a m i a k a y a<br />

Karume, Jumbe hadi karibu<br />

ya Ali Hassan Mwinyi, wazee<br />

wakipewa pesa za matumizi<br />

zikiitwa ‘ulufea’ (Welfare<br />

benefits) na zikiwasaidia<br />

sana. Wakati wa tawala za<br />

SMZ za siku hizo, sipitali<br />

zilikuwa zimejaa madawa,<br />

usafi na hudumua za kulla<br />

aina. Skuli zetu zilijengwa<br />

hatua kwa hatua, hakuna<br />

alielipia mchango wa skuli,<br />

hakuna alienunua daftari,<br />

kalamu wala penseli. Hakuna<br />

mwanafunzi aliekosa huduma<br />

za afya za kichocho, vipimo<br />

kila muda fulani.<br />

Ilifika wakati kwa jinsi<br />

Serikali ilivyoikiwajali<br />

wanafunzi, Waziri wetu<br />

wa Elimu wa mwanzo<br />

hapa Zanzibar, aliwahi<br />

kupendekeza kuwa vichwa<br />

v y a N g ’ o m b e v y o t e<br />

vinavyochinjwa nchi nzima<br />

v i p e l e k w e m a s h u l e n i<br />

wanafunzi wapikiwe supu,<br />

ili wapate wanywe wakati<br />

wa mapumziko (recess).<br />

Bahati mbaya mpango huu<br />

ulivunjwa na Sheikh Karume,<br />

pale alipomwambia Waziri<br />

wa Elimu kuwa asijefanya<br />

hivyo mpaka ahakikishe kila<br />

mwanafunzi ameshapata<br />

kijiko na kibakuli cha<br />

kunywea supu. Mapango huu<br />

ukafa hapo, lakini ulikuwa na<br />

nia njema.<br />

Enzi za SMZ ya wakati<br />

huo, kulikuwa na huduma za<br />

dakhalia (boarding). Ukipasi<br />

ukipelekwa huko kupatiwa<br />

mafunzo ya kuwa mtu<br />

utakaejitegemea. Tukipewa<br />

kula asubuhi mchana na jioni.<br />

Japo tukiita bondo, lakini<br />

tukipewa tena bure na kwa<br />

wakati bila kuchangishwa<br />

g h a r a m a . Wa n a f u n z i<br />

wakiletewa meli bure kupanda<br />

au wakifanyiwa tiketi kabisa<br />

wakifika huchukuwa na<br />

kusafiri tu kwenda Unguja<br />

na Pemba. Tuache huko.<br />

Hospitali, kula kunywa<br />

na huduma masaa ishirini na<br />

nne. Mgonjwa akipembejewa<br />

na madaktari wa kikwetu na<br />

wa kigeni. Serikali haikuwa<br />

na meli zilizoenda kwa kasi<br />

wala madege, lakini watu<br />

wakisafiria meli za Serikali<br />

za uhakika na unafuu wa<br />

bei. Huo ndio wakati ambao<br />

tunaweza kusema kuwa<br />

nchi yetu ilikuwa changa,<br />

na ilikuwa na matongo ya<br />

ukoloni, haikuwa na uoni<br />

wa mbali wala uwezo wa<br />

kutuletea maendeleo.<br />

Tupige dira ya SMZ leo.<br />

Serikali yahubiri na kutangaza<br />

kila siku kuwa nchi hii imepiga<br />

hatua kubwa kimaendeleo<br />

ukilinganisha na Zamani.<br />

Sikatai. Maendeleo wakati<br />

mwengine hupimwa kwa<br />

miwani ya macho, ambayo<br />

kigari kidogo huwa TATA,<br />

au FUSO. Maendeleo siku<br />

hizi hupimwa kwa kutazama<br />

ndege zipitazo juu ya anga<br />

letu, tivii pana majumbani, au<br />

kila mtu ana simu ya kiganjani.<br />

Maendeleo yetu hupimwa<br />

kwa viongozi kuwa katika<br />

magari makubwa ambayo<br />

wakiwa ndani ya magari<br />

hayo hawasikii ule uvundo<br />

unaonuka pale Darajani kituo<br />

cha dala dala.<br />

Maendeleo hupimwa<br />

wakiwa katika magari<br />

ambayo pia yakipita njia<br />

m b o v u h a w a h i s i w a l a<br />

hawapati vumbi mle ndani.<br />

Na pia licha ya kuwa nchi<br />

ina joto la tanuri ya mbata<br />

siku hizi kwa uchafuzi wa<br />

mazingira, viongozi wetu<br />

wa SMZ hawalihisi joto hili<br />

na vuke kali, katika magari<br />

na majumba yao yaliyo ‘full<br />

kipupwe, full kiyoyozi, full<br />

kujiachia’. Raha zote hizi<br />

zilizowazunguka viongozi<br />

wetu unawategemea kuwa<br />

siku moja watasema kuwa<br />

nchi hii inarudi nyuma badala<br />

ya kwenda mbele? Ungekuwa<br />

wewe ungetia ulimi wako<br />

puani ukasema ukweli huu<br />

wakati yote hayo huyaoni kwa<br />

maraha yaliyokuzunguka?<br />

Hebu linganisha hayo<br />

machache niliyoyasema<br />

yalifanywa, enzi za Karume,<br />

Jumbe na kidogo Mwinyi<br />

na uone. Sasa tudurusu kwa<br />

pamoja. Nitawauliza maswali<br />

munijibu mpaka nimalize,<br />

sawa? Bismillah! Ule ‘ulefea’<br />

ALHAJ Ali Hassan Mwinyi.<br />

bado upo? Skuli zetu zina<br />

vifaa, madafatri na kalamu<br />

bure? Dkahalia zipo? Elimu<br />

bado ni bure? Ndio ni bure<br />

maana haina maana yoyote,<br />

lakini inalipiwa. Samahani<br />

hili nimejijibu mwenyewe.<br />

Haya tuendelee.<br />

Kule spitali dawa ziko?<br />

Ndio lakini kwa pesa. Kile<br />

chakula vipi bado wanapatiwa<br />

wagonjwa? Ahh! Bajeti<br />

ya Wizara ya afya ndogo,<br />

kimefutwa Chakula. Lakini<br />

Waziri wa Afya ana prado la<br />

milioni 70, na mafuta yake ya<br />

laki moja kwa wiki pengine.<br />

Hawasemi kuwa mawaziri<br />

waendeshe gari ndogo kama<br />

Starlet, na Vizt kujenga taifa.<br />

Heri wafe wagonjwa wao<br />

waendeshe magari mazuri.<br />

Ndio sisi bwana, wakoloni<br />

weusi. Nani anajali kama<br />

wagonjwa wanakufa kwa<br />

kutukanwa tu kule Spitali,<br />

kwa kukosa dawa tu na<br />

hata kula sasa? Hawa ndio<br />

viongozi wetu bwana, ni zaidi<br />

ya majoka ya mdimu.<br />

M a d a k t a r i j e e<br />

wanashuhulikia wagonjwa?<br />

Hapana, wanawatukana wala<br />

hakuna anejali serikalini<br />

kwani wao hawatibiwi hapa<br />

hata wakiumwa na tambazi<br />

(uvimbe) huenda nje ya nchi.<br />

Kwa nini? Tumeendelea hivyo.<br />

Tuendelee, au mshachoka?<br />

Mmeona wapi Serikali<br />

kujenga tena majumba ya<br />

watu na makazi? Hapana.<br />

Ule usafiri wa meli dhamana<br />

za Serikali ungalipo? Hapana<br />

zilizopo ni za matajiri na<br />

hata tukizama SMZ husema,<br />

haina la kufanya. Tumezama,<br />

tunazama, na tutaendelea<br />

kuzama. Ndio maendeleo!<br />

Ya kale hayako tena, kweli.<br />

Lakini pia ya sasa hayapo na<br />

wala tusiyatarajie. Nchi hii<br />

kama ingekuwa gari, mmoja<br />

kati ya madereva hawa saba<br />

tuliojaaliwa na Chimwaga<br />

kutuongoza, lazima bila<br />

shaka alizitowa gia zote na<br />

kuibakishia gia ya kurudi<br />

nyuma tu (reverse gear). Na<br />

ndio hivi tunapelekwa msobe<br />

msobe. SMZ wakisimama<br />

majukwaani, huhubiri chuki,<br />

na uhasama na uongo mwingi<br />

kisha wakikutana katika<br />

vyombo vya habari husema<br />

wameleta maendeleo. Hivi ni<br />

kweli jamani. Sikupata nafasi<br />

ya kuchambuwa sana lakini<br />

mpaka hapa tu jiulize ndugu<br />

yangu, ‘TUNAKWENDA,<br />

TUNARUDI?’<br />

Tangazo<br />

Kwa niaba ya Masjid Qiblatain:-<br />

Sheikh Bawaziri na Sheikh Awadhi<br />

wanawaalika Waislamu kuhudhuria<br />

katika hafla ya kuhitimisha kitabu<br />

‘BULUGHUL MARAMI’.<br />

Mahali: Masjidi Qiblatain,<br />

Kariakoo.<br />

Siku: Ijumaa (Leo) Desemba,<br />

14/201.<br />

Muda: Baada ya Swala ya<br />

Magharib.<br />

Mgeni rasmi: Dkt. Babasila, Katibu<br />

Mkuu wa Umoja wa Wanazuoni wa<br />

Kiislamu wa Bara la Afrika.<br />

Wabillah Tawfiq


11<br />

WAKATI wa Ukhalifa wa<br />

Seyyidna Umar bin al-Khattab,<br />

Masahaba walikubaliana<br />

kuanza kalenda ya Kiislamu<br />

pale Mtume wa Mwenyezi<br />

Mungu alipofanya Hijra<br />

kutoka Makka kuelekea<br />

Madina, na kuasisi Dola ya<br />

kwanza ya Kiislamu. Sasa<br />

tunapouanza mwezi huu<br />

Mtukufu wa Muharram,<br />

mwaka mpya wa Kiislamu<br />

wa 1434, basi tujikumbushe<br />

kidogo kuhusu tukio hili la<br />

kihistoria la Hijra na tufute<br />

dhana potofu zinazoambatana<br />

nalo.<br />

M a r a n y i n g i H i j r a h<br />

inapojadiliwa, tumekuwa<br />

tukiishia zaidi kwenye maelezo<br />

yanayoonyesha jinsi Mtume wa<br />

Mwenyezi Mungu alivyojificha<br />

pangoni au nani alilala kwenye<br />

kitanda chake. Hali hii imekuwa<br />

ikituondoa kwenye mjadala<br />

wa maana, wenye kina kuhusu<br />

masuala ya Hijra. Sisi tunaishia<br />

kujadili matukio tu ya Hijra.<br />

Lakini hata hivyo, matukio<br />

ya Hijra tunayoyadili lazima<br />

yatukumbushe kwamba Mtume<br />

wa Mwenyezi Mungu, ingawa<br />

alikuwa akitegemea ‘Wahyi’<br />

kama chanzo cha ujumbe wa<br />

Kiislamu; alikuwa akifanya<br />

harakati za kusimamisha Uislamu<br />

AN-NUUR<br />

MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

Tukio la Hijra, mazingatio yaliyosahaulika!<br />

Said Rajab<br />

kama binadamu na kupitia mbinu<br />

na mikakati ya kibinadamu.<br />

Hijrah ya kuelekea Madina<br />

haikufanyika kwa sababu<br />

Waislamu kule Makka walitaka<br />

kuepuka manyanyaso, au kwa<br />

sababu walitaka kutafuta eneo<br />

salama zaidi la kujinusuru, au<br />

kukimbia mateso ya Maqurayshi.<br />

Isipokuwa, Hijrah lilikuwa ni<br />

tukio kubwa ambalo limebadili<br />

mkondo mzima wa historia<br />

kuelekea upande mwingine.<br />

Hii inaweza kuonekana iwapo<br />

tutaiangalia Sira katika mtazamo<br />

wake sahihi.<br />

Sira ya Mtume wa Mwenyezi<br />

Mungu ni sehemu muhimu<br />

sana ya Sunna, na ndiyo tafsiri<br />

ya vitendo ya Qur’an Tukufu,<br />

ambayo ni ufunuo wa Mwenyezi<br />

Mungu kwa wanadamu. Ukisoma<br />

Sira kwa umakini, utaona kuna<br />

mbinu maalumu ya kuendesha<br />

harakati, na kama lengo letu<br />

ni kutafuta radhi za Mwenyezi<br />

Mungu, basi ni jukumu letu<br />

kuzingatia mbinu hii, hatua kwa<br />

hatua katika kila awamu:<br />

S e m a : “ I k i w a n i n y i<br />

m n a m p e n d a M w e n y e z i<br />

Mungu, basi nifuateni, (hapo)<br />

Mwenyezi Mungu atakupendeni<br />

na atakughufirieni madhambi<br />

yenu. Na Mwenyezi Mungu ni<br />

mwenye maghufira na mwenye<br />

rehema” Qur (3:31).<br />

“Na anachokupeni Mtume basi<br />

pokeeni, na anachokukatazeni<br />

jiepusheni nacho” Qur (59:7)<br />

Kwa mujibu wa Sira, Hijrah<br />

inahitimisha kipindi cha mpito<br />

katika harakati kinachojulikana<br />

kama “Kutafuta Nusra”,<br />

kuelekea kwenye kipindi kingine<br />

ambacho Uislamu unatekelezwa<br />

kwa vitendo katika kiwango<br />

cha Dola. Nusra ni kuhamisha<br />

mamlaka kutoka kwa mtu<br />

mmoja, kupitia kuungwa mkono<br />

au kiapo cha utii, kutoka kwa<br />

watu wenye nguvu katika jamii.<br />

Kwa hiyo, Hijrah ni matokeo ya<br />

moja kwa moja ya kutafuta na<br />

hatimaye kupata Nusra.<br />

Wakati Mus’ab bin Umair<br />

(ra) alipotumwa Madina kueneza<br />

ujumbe wa Uislamu, ilimchukua<br />

mwaka mmoja wa kazi ngumu<br />

katika mji huo, kabla ya viongozi<br />

wake kusafiri mpaka Makka, na<br />

kusalimisha mamlaka zao kwa<br />

Mtume wa Mwenyezi Mungu<br />

kwa kumpa Ba’yah (kiapo cha<br />

utii). Ba’yah hii iliitwa Bayat-ul<br />

Harb (kiapo cha vita).<br />

Ingawa hakukuwa na vita<br />

kipindi kile, iliitwa ‘Bayat- ul<br />

Harb’ kwa sababu ilionyesha<br />

nia ya Waislamu kupigana,<br />

iwapo watalazimika, ili kulinda<br />

harakati na Dola changa ya<br />

Kiislamu wakati ule. Mtume<br />

wa Mwenyezi Mungu alitumia<br />

miaka minne ya Da’wah kwa<br />

makabila mengi ya Najd (eneo<br />

kubwa kati ya Makka na Madina)<br />

kabla ya kupata Nusra.<br />

Ni vizuri kutambua kwamba<br />

mpaka kipindi hiki katika<br />

Sira, licha ya shinikizo lote<br />

ambalo Mtume wa Mwenyezi<br />

Mungu aliliweka kwa jamii<br />

ya Kikafiri ya Makka, mateso<br />

ambayo Maquraysh walimpa<br />

Mtume wa Mwenyezi Mungu<br />

na Waislamu wa awali yalikuwa<br />

ni cha mtoto, ikilinganishwa na<br />

mateso ambayo yalikuja baada<br />

ya Mtume kupata Nusra kutoka<br />

kwa viongozi wa Madina.<br />

Kuanzia hapo na kuendelea,<br />

Makafiri walikuwa wakipanga<br />

kumuua Mtume wa Mwenyezi<br />

Mungu. Hakika ni ukweli<br />

kwamba Shetani na wafuasi wake<br />

wanaogopa sana utekelezaji wa<br />

Sheria za Mwenyezi Mungu<br />

katika ardhi.<br />

Kwa kuzingatia nukta hizi<br />

muhimu, kila tunapoijadili<br />

Hijrah, ambayo watu wengi<br />

wameishusha mpaka kufikia<br />

kuwa kama safari ya kiroho<br />

tu iliyofanywa na Mtume, pia<br />

tujadili umuhimu wa Kiitikadi<br />

wa tukio hili, kwa kuangalia<br />

Uislamu kwa ujumla wake na<br />

uendeshaji wa harakati.<br />

Ni muhimu sana kwa Waislamu<br />

kutambua kwamba tukio hili la<br />

Hijrah si tu linaadhimisha kuanza<br />

kwa kalenda yetu, lakini muhimu<br />

zaidi linakumbusha kuasisiwa<br />

kwa kiini (nucleus) cha dola<br />

ya kwanza kabisa ya Kiislamu.<br />

Mamia ya miaka iliyofuatia,<br />

Ni wakati wa CCM wahafidhina kupevuka<br />

Inatoka Uk. 7<br />

la urembo lililopambika ili<br />

kuwashindanisha, na hiyo ni<br />

sifa au alama ya demokrasia<br />

ulimwenguni kote, na kisha<br />

tuchague aliyependeza zaidi ili<br />

tumvishe taji.<br />

Wacha mshindi atambe katika<br />

Ikulu ya Zanzibar ama ya Dar es<br />

Salaam , tunachohitaji aje ajipange<br />

tena mbele yetu baada ya miaka<br />

mitano, tutakapomuepuka yeye<br />

na tukamvisha taji mwengine<br />

pamoja na zawadi yake ya<br />

fedha. Akibahatika kushinda na<br />

akalivaa taji kwa mara ya pili,<br />

kama ilivyo ada, tutamfikisha<br />

ukingoni mwa awamu yake ya<br />

pili ofisini pamoja na fungu lake<br />

nono la pensheni na tumkabidhi<br />

mkononi kisha tuendelee na<br />

shindano la kumpata mrembo<br />

mwengine. Jee Wahafidhina wa<br />

CCM wataelewa na kubaini hali<br />

ya kutofaa kwao na woga juu ya<br />

mazingira magumu ya urembo<br />

ama uzuri wa kisiasa, hasa<br />

usoni kwa wapigakura ambao<br />

hapana shaka wameshaona hawa<br />

hawapendezi?<br />

Mazito zaidi ya hayo, ni<br />

kwa upande wa Zanzibar ,<br />

mshindi wa taji na anayemfuatia,<br />

wanalazimika kugawana ile<br />

hawala ya fedha, zawadi yao.<br />

Wazanzibari wanachotarajia sasa<br />

ni kuona mshindi anashikamana<br />

na kufanyakazi bega kwa<br />

bega na mshindani wake wa<br />

karibu. Hili bila shaka linahitaji<br />

kuona mahasimu wawili<br />

wakiheshimiana wakati wa<br />

kampeni na baada ya chaguzi,<br />

na kisha kutanguliza maslahi ya<br />

Zanzibar . Hii ni adabu iliyofaa,<br />

naweza kusema, iliyothibitishwa<br />

na Kura ya Maoni ya Serikali<br />

ya Umoja wa Kitaifa kwa<br />

asilimia 64 ya Wapigakura,<br />

ambao walichoshwa na siasa za<br />

chuki, za kibaguzi zilizotumika,<br />

ikibidi kote kote CUF na CCM,<br />

kuidhoofisha Zanzibar , na<br />

pia kuchoshwa na vilio vya<br />

mchezo mchafu kila baada ya<br />

Uchaguzi.<br />

Kwa bahati mbaya, wapo<br />

baadhi ya Wana-CCM wa<br />

Zanzibar, wanaosumbuliwa na<br />

ugonjwa wa kusahau kabisa juu<br />

ya Maridhiano na Mabadiliko ya<br />

Katiba, yaliyopelekea kuundwa<br />

kwa Serikali ya Umoja wa<br />

K i t a i f a ; w a p o w e n g i n e<br />

wasioridhika na mfumo huu,<br />

wamekuwa wakiweka vizuizi<br />

na kunong’ona chini kwa chini,<br />

kutokana na kukosa ustahamilivu<br />

na pia ukosefu wa kubaini athari<br />

za mifarakano, ndiyo maana<br />

wanamvurumishia lawama<br />

Amani Abeid Karume, ati yeye<br />

ndiye aliyeasisi mizizi ya hili;<br />

wapo waliokubali na kuridhia<br />

matakwa ya Wazanzibari;<br />

ingawa kwa Wahafidhina, hao ni<br />

wasaliti, kwa chochote ambacho<br />

ni kinyume na matakwa yao wao<br />

(wahafidhina).<br />

Katika Mkutano wa hivi<br />

karibuni wa CCM uliofanyika<br />

Zanzibar, Wahafidhina wa CCM<br />

walitumia lugha chafu, matusi,<br />

uchochezi, na maneno yasiyofaa<br />

kuchochea na kukumbusha<br />

mambo yaliyopita ambayo<br />

yakitumiwa na Wanamapinduzi<br />

dhidi ya Wana-CCM waliodaiwa<br />

kuwa na msimamo wa wastani;<br />

kwa udhati kabisa Mapinduzi ni<br />

matokeo ya kuondosha ubaguzi,<br />

ingawa yanatumiwa sasa na<br />

baadhi ya Wahafidhina kufungua<br />

na kurejesha majeraha ya zamani<br />

yaliyokwishapoa, ili kujitafutia<br />

umaarufu wa kisiasa.<br />

Kama Mzanzibari mwenye<br />

asili ya pande mbili, Muarabu na<br />

Muafrika, ambapo Babu yangu<br />

Muarabu aliuwawa gerezani<br />

mara tu baada ya Mapinduzi,<br />

bila ya sababu, zaidi ya imani<br />

yake ya kisiasa, ambapo pia<br />

Babu yangu mwenye asili ya<br />

Afrika naye aliuliwa miaka 8<br />

baada ya Mapinduzi, si kwa<br />

lolote bali, kwa hali ile ile kama<br />

mtangulia wake, imani yake ya<br />

kisiasa, sijaridhika wala sifurahii<br />

hata kidogo.<br />

Huu ni mchezo wa biashara<br />

ya kujinufaisha, unaoweza<br />

kupelekea umwagaji damu. Sasa<br />

ni wakati wa Wahafidhina ndani<br />

ya CCM Zanzibar kupevuka,<br />

na wakabaini kwamba hiki siyo<br />

kiwanja cha watoto wa skuli,<br />

wababe kuwapora wenzao<br />

pesa yao ya chakula cha<br />

mchana.<br />

M i a k a 4 8 b a a d a y a<br />

M a p i n d u z i , Z a n z i b a r<br />

imebadilika sana. Wengi wa<br />

Wazanzibari ni wa umri wa<br />

chini ya miaka 40. Hawakuishi<br />

katika Mapinduzi wala<br />

ubaguzi wa rangi wa kisiasa,<br />

unaotajwa kusababisha<br />

Mapinduzi ndani ya Zanzibar<br />

. Siasa zetu haziwezi kubaki<br />

za kale, ingawa historia<br />

inaweza kutumika kutuarifu,<br />

wapi tulikuwa vile, na wapi<br />

tunahitaji kwenda, na hivyo<br />

kuepuka siasa chafu.<br />

Kama CCM Zanzibar,<br />

inaburuzwa na wahafidhina,<br />

hivyo basi CUF inateka<br />

ushindi wa kisiasa wa Zanzibar<br />

. Iwapo CCM inahitaji<br />

kutetea taji lake la urembo<br />

mwaka 2015, lazima ijijenge,<br />

ijirekebishe, yenyewe, na<br />

ijiunde upya, ipambane na<br />

iweze kuteka ushindi, kwa<br />

sababu ni kura za Wazanzibari<br />

wenye msimamo wa wastani,<br />

zitakazoamua Raisi wa<br />

baadaye wa Zanzibar .<br />

( M A K A L A H I I<br />

IMETAFSIRIWA KUTOKA<br />

GAZETI LA THE GUARDIAN<br />

LA JUMAPILI TAREHE 25<br />

NOVEMBA, 2012, AMBAYO<br />

ILIANDIKWA NA BI FATMA<br />

AMANI)<br />

kiini hiki kilisambaa katika<br />

nchi jirani, kikiwakomboa<br />

watu wanaokandamizwa<br />

kwa kuwaleletea neema ya<br />

Mwenyezi Mungu inayoitwa<br />

Uislamu.<br />

Kwa hiyo, tunapotaka<br />

kuzungumzia umuhimu wa<br />

Hijrah, basi tutambue kwamba<br />

tukio hili linaadhimisha pia<br />

kipindi ambacho Uislamu<br />

kama Itikadi, umebadilika<br />

kutoka kuwa wazo na kuwa<br />

vitendo.<br />

W a t u w a M a d i n a<br />

walimkubali Muhammad<br />

(saw) kama Mtume tu. Lakini,<br />

hata hivyo baada ya kuhamisha<br />

mamlaka yao (Nusra) kwa<br />

Mtume wa Mwenyezi Mungu<br />

wakati alipowasili Madina,<br />

walimpokea kama mtawala<br />

na Mtume.<br />

Kabla Muhammad (saw)<br />

hajafanya Hijrah, alikuwa<br />

Mtume aliyefunuliwa sheria<br />

mpya kutoka kwa Mwenyezi<br />

Mungu. Baada ya Hijrah,<br />

akawa ndiye mtekelezaji<br />

wa sheria hizo. Uislamu<br />

ukahama kutoka uanishaji<br />

na ufafanuzi wa matatizo na<br />

masuala, ukaelekea kwenye<br />

kupambana na matatizo na<br />

masuala hayo, ikiwa ni pamoja<br />

na kutoa ufumbuzi wake.<br />

Hiki ndiyo kipindi ambacho<br />

Mtume wa Mwenyezi Mungu<br />

aliweza kutekeleza kanuni na<br />

mifumo ya Kiislamu katika<br />

maisha halisi.<br />

Hijrah, kama sehemu ya<br />

Sira, ni tukio linalohitaji<br />

kusomwa kwa kina sana, ili<br />

kufahamu maana za ndani na<br />

hekima zake.<br />

Haina maana kwamba<br />

maelezo madogo madogo<br />

ya Hijrah, kama jinsi Mtume<br />

w a M w e n y e z i M u n g u<br />

alivyomfanya Seyyidna<br />

Ali bin Abu Talib(ra) alale<br />

kwenye kitanda chake, au jinsi<br />

yeye mwenyewe alivyojificha<br />

pangoni si muhimu. Hayo ni<br />

matukio muhimu pia kwa<br />

sababu yanatukumbusha<br />

kwamba mbinu na mikakati<br />

iliyotumiwa na Mtume<br />

w a M w e n y e z i M u n g u<br />

kufikia lengo, ilikuwa ni<br />

ya kibinadamu na siyo<br />

ya binadamu wa ajabu<br />

(superhuman). Hazikuwa<br />

mbinu zilizohitaji miujiza<br />

kuzitekeleza.<br />

Hatuwezi kudai kwamba,<br />

kwa kuwa Muhammad<br />

(saw) alikuwa Mtume,<br />

na sisi siyo Mitume, basi<br />

hatuwezi kufuata nyayo zake<br />

kikamilifu, hasa linapokuja<br />

s u a l a l a j i n s i M t u m e<br />

alivyoendesha harakati za<br />

kusimamisha Uislamu. Kama<br />

Waislamu, lazima tukumbuke<br />

kwamba mbinu na mikakati<br />

iliyotumiwa na Mtume katika<br />

harakati za kusimamisha<br />

dini ya Mwenyezi Mungu<br />

ipo kwa ajili yetu kufuata,<br />

na kutofuata ni kumuasi<br />

Mwenyezi Mungu.


AN-NUUR<br />

12 MUHARRAM 1434, IJUMAA DESEMBA 14 - 20, 2012<br />

IMEELEZWA kuwa viongozi<br />

wa Jumuia ya UAMSHO<br />

visiwani Zanzibar, ambao<br />

bado wanashikiliwa rumande,<br />

sasa wameanza kupatiwa<br />

huduma muhimu kama<br />

mahabusu wengine gerezani<br />

Kiinua Mguu Juu Unguja.<br />

Kabla ya hapo, viongozi hao<br />

walidai kufanyiwa vitendo vya<br />

kidhalilishaji huko gerezani<br />

ikiwa ni pamoja na kukataliwa<br />

kupewa chakula cha ndugu zao,<br />

kusoma Qur’an, kubadili nguo<br />

wala kukutana na wahabusu<br />

wengine.<br />

Wa k i l i a n a y e w a t e t e a<br />

viongozi hao wa Kiislamu, Bw.<br />

Salum Taufiq, amenukuliwa<br />

akisema kuwa wateja wake<br />

tayari wameruhusiwa kula<br />

chakula kutoka nyumbani,<br />

kusoma Qur’ani, kubadilisha<br />

nguo na kutoka kwenye vyumba<br />

vyao na kuchanganyika na<br />

mahabusu wengine.<br />

Awali, baada ya kushikiliwa<br />

mahabusu bila dhamana,<br />

viongozi hao walifungua kesi<br />

ya kupinga kubaguliwa na<br />

kutopewa huduma bora tangu<br />

Usikose nakala yako ya<br />

AN-NUUR kila<br />

Ijumaa<br />

Uamsho Zanzibar waanza kupatiwa huduma muhim<br />

Na Mwandishi Wetu<br />

walipofunguliwa mashtaka<br />

Oktoba 21 mwaka huu.<br />

B a a d h i y a m a s h i t a k a<br />

yanayowakabili viongozi hao<br />

wa UAMSHO ni kuhatarisha<br />

usalama wa taifa na kusababisha<br />

uharibifu wa mali.<br />

Viongozi hao ni maarufu<br />

kwa kupigania mabadiliko<br />

katika muundo wa muungano<br />

wa Tanganyika na Zanzibar<br />

na walifanya mikutano mingi<br />

kuhamasisha wananchi kukataa<br />

mfumo wa hivi sasa wa<br />

muungano wa serikali mbili.<br />

Jumuia ya UAMSHO kabla<br />

ya kukamatwa viongozi wake,<br />

imekuwa mstari wa mbele<br />

kutetea maslahi ya Mamlaka<br />

ya Zanzibar, na kutaka uwepo<br />

utaratibu wa kupigwa kura<br />

ya maoni kabla ya kuendelea<br />

mchakato wa kukusanya maoni<br />

juu ya kuandikwa katiba mpya<br />

visiwani humo.<br />

Aidha Taasisi hiyo imekuwa<br />

na jitihada za kutaka kuwepo<br />

muungano wenye maslahi<br />

kwa pande zote za nchi, kwa<br />

maana ya Tanzania Bara na<br />

Zanzibar na pendekezo kubwa<br />

likiwa ni kuwepo muungano wa<br />

mkataba.<br />

SHEIKH Farid Hadd akiwa katika karandinga la Polisi Zanzibar.<br />

Sheikh Ponda Issa bado yupo rumande Segerea<br />

Na Shaban Rajab wakili wa washitakiwa Juma mambo ni ya kiutendaji zaidi. Aidha alisema walikaa kwamba, sahihi ya mlalamikaji<br />

Nassoro.<br />

Wakili Nassoro, aidha alihoji pamoja na Balozi wa Misri haikuwekwa siku ya mkataba.<br />

SHEIKH Ponda Issa jana Aliongeza kuwa hajui kwamba Bakwata inahusika na na kujadiliana, ambapo Balozi Hivyo walisema kuna hofu ya<br />

alirejeshwa tena rumande kiwanja hicho huko nyuma watu gani.<br />

huyo aliwataka kuwajengea kughushiwa mkataba huo.<br />

b a a d a y a k e s i y a k e madhumuni yake yalikuwa ni Sheikh Makusanya alijibu jengo la ghorofa chuoni Hata hivyo upande wa wa<br />

kusikilizwa.<br />

nini na namna kilivyopatikana kuwa Baraza hilo linawahusu Markazi kwa ajili ya mabweni Jamhuri ulisema kuwa kutizama<br />

Ponda anaendelea kukaa pia hajui.<br />

Waislamu wote wa Tanzania. na madarasa ya wanachuo<br />

rumande baada ya kukataliwa Hata hivyo Wakili Nassoro Jibu hilo lilitoa mwanya<br />

uhalali wa sahihi zilizomo<br />

na kuwafanyia ukarabati wa<br />

dhamana.<br />

alipomtaka kurejea kipengele wa kuhoji iwapo Waislamu Markaz Chang’ombe.<br />

katika mkataba huo sio kazi<br />

Jana kesi hiyo iliposikilizwa, cha muhtasari wa kikao cha walishirikishwa vipi katika Baadae ndipo Bakwata ya mlalamikaji na kwamba,<br />

s h a h i d i w a u p a n d e w a Baraza la Maulamaa kilichojadili mpango huo wa kubadilishana wakakabidhiwa kiwanja kwa mkataba uliowasilishwa ni<br />

mlalamikaji katika kesi suala la kubadilishana umiliki umiliki wa ardhi na Agritanza mkataba na Agritanza.<br />

halali kimatiki kwa kuwa<br />

inayomkabili Sheikh Ponda wa ardhi kati ya ekari nne za na kwamba sasa ujenzi wa N y a r a k a z a m k a t a b a unakidhi uwepo wa pande mbili<br />

Issa Ponda, ambaye ni Bakwata na ekari 40 za kampuni chuo kikuu utafanyika huko ziliwasilishwa mahakamani zilizokubaliana.<br />

Sheikh na Kadhi wa Bakwata ya Agritanza zilizopo Kisarawe Kisarawe? Sheikh Makusanya kama kielelezo cha ushahidi Kesi hiyo iliahirishwa hadi<br />

mkoa wa Shinyanga, Ismail Pwani, alikuta kipengele hicho alijibu kuwa hajui.<br />

na 3.<br />

hapo itakapotajwa ambapo<br />

Habib Makusanya, ameieleza kikieleza kuwa Bakwata ilikuwa Shahidi mwingine aliyetoa Bw. Mohammed alisema hata<br />

mahakama ya Hakimu Mkazi na mpango wa Kujenga Chuo utetezi wake mahakamani hapo<br />

Sheikh Ponda na wenzake<br />

hivyo baada ya makabidhiano na<br />

Kisutu, Jijini Dar es Salaam Kikuu cha Kiislamu hapo alikuwa ni mmoja wa wamiliki<br />

w a t a n o , w a l i r e j e s h w a<br />

kuanza kuandaa vifaa vya ujenzi<br />

kuwa, hajui ni namna gani Markazi Chang’ombe.<br />

wa kampuni ya Agritanza Bw.<br />

rumande.<br />

eneo hilo limemegwa kiasi cha Hata hivyo kabla ya kukubali Suleiman Nassoro Mohammed,<br />

wa ukuta kuzunguka kiwanja kesi hiyo imeahirishwa<br />

kubakia kiwanja cha ekari nne kipengele hicho, shahidi huyo ambaye ni mfanyabishara wa chao, ndipo alipokuja Sheikh hadi Desemba 18 itakapotajwa<br />

ambacho kimepewa kampuni ya alishikilia kuwa Bakwata mtaa wa India jijini Dar es Ponda na kumtaka kuacha kazi ambapo itasikilizwa tena<br />

Agritanza Ltd.<br />

ilikuwa na mpango huo katika Salaam.<br />

hiyo.<br />

Desemba 31 mwaka huu.<br />

Aidha Sheikh Makusanya eneo la chuo cha Kiislamu Yeye alisema mbele ya Alisema baadae wakaja watu Katika kesi nyingine,<br />

ameeleza mahakamani kuwa Al haramain cha jijini Dar es mahakama kuwa wanamiliki takriban ya 500 na kukaa eneo watuhumiwa saba waliokuwa<br />

pamoja na kwamba yeye ni Salaam.<br />

kiwanja cha ekari 40 huko hilo la kiwanja kwa takriban<br />

mjumbe wa Baraza la Ulamaa Hata hivyo alipoulizwa na Kisarawe Pwani.<br />

wakikabiliwa na kesi ya<br />

siku saba.<br />

la Bakwata, Sheikh Mkuu wakili huyo kuwa Aritanza K w a m b a w a l i p o s i k i a<br />

kuchomwa Kanisa la KKKT<br />

Hata hivyo Bw. Mohammed<br />

na Kadhi mkoa Mkoa wa ilipatikana vipi hadi kupewa Bwakata wanahitaji eneo la<br />

Mbagala Zakheem, wameachwa<br />

Shinyanga, hakufahamu kuwa eneo hilo la Chang’ombe, kujenga Chuo Kikuu, walionana<br />

alisema shitaka lao ni la huru baada ya upande wa<br />

eneo hilo na lile kilichopo alikataa kusema lolote. Sheikh na kuwaeleza kuwa wana eneo kuvamiwa kiwanja tu lakini upelelezi kukosa ushahidi wa<br />

Chuo cha Kiislamu Markaz M a k u s a n y a p i a h a k u w a la kutosha huko Kisarawe na hawana shitaka jingine. kuwatia hatiani.<br />

Chang’ombe, kinachoendeshwa tayari kujibu swali lililohoji kwamba iwapo watapatiwa Baadae mawakili wa upande H a t a h i v y o P o l i s i<br />

na Wamisri, lilipangwa na thamani ya mita mraba moja ekari nne chang’ombe, wao wa washitakiwa Bw. Juma wamewakamata watuhumiwa<br />

Bakwata kujengwa Chuo Kikuu ya ardhi ya kiwanja hicho cha watatoa eneo lao hilo.<br />

Nassoro na Bw. Yahya Njama, wengine watano, ambapo<br />

cha Kiislamu nchini.<br />

Chang’ombe.<br />

Alisema Bwakata walituma walipotizama mkataba huo,<br />

“Inasemekana eneo lilikuwa Alipoulizwa kwamba kwa wajumbe wao kuangalia<br />

wameunganishwa na makosa<br />

walieleza kuwa mkataba huo<br />

na ekari 27 hivi, lakini nani nini Bakwata walibadilisha eneo hilo huko Kisarawe na<br />

hayo hayo ya kupora mali za<br />

una kasoro katika uwekaji<br />

aliyefanya eneo hilo kuwa uamuzi wa kujenga Chuo wakaridhika nalo.<br />

Kanisa la KKKT Mbagala<br />

dogo hadi lisitoshe kujengwa Kikuu hapo Chang’ombe kama Kuafuatia kuridhika huko,<br />

wa sahihi, ambapo sahihi Zakheem kwa kutumia nguvu.<br />

chuo sijui, haya ni mambo ilivyokusudia, na kama Wamisri waliahidiwa kuwa Masheikh ya mawakili wa kampuni Kesi hiyo nayo iliahirishwa<br />

ya kiutendaji,” alijibu Sheikh wanaoendesha Chuo cha Markaz B a k w a t a w a t a j a d i l i a n a ya uwakili ya MJ Diamond, hadi Desemba 18, 2012<br />

Makusanya kufuatia maswali Chang’ombe nao walihusishwa na kitafuatia kikao cha ambao ndio waliotengeneza itakapokuja kwa ajili ya<br />

aliyokuwa akiulizwa na katika mabadiliko hayo, Sheikh Wadhamini kabla ya kufikia mkataba huo hazionekanai na usikilizwaji wa awali.<br />

Makusanya alisema hayo makabidhiano.<br />

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!