Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
www.<strong>annuur</strong>papers.co.tz<br />
Sauti ya Waislamu<br />
ISSN 0856 - 3861 Na. <strong>1052</strong> SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=<br />
Ujasiria mali<br />
washika kasi<br />
Baraza Kuu<br />
Uk. 12<br />
Kesi ya Sheikh Ponda mashahidi waingia ‘mitini’<br />
Hakimu aamuru mmoja akamatwe<br />
Wengine watoa visingizio, majina yao yafichwa<br />
Wakili wa utetezi amlima barua DPP<br />
SHEIKH Ponda Issa Ponda akiwa katika Mahakama ya Kisutu Jumatau wiki hii. (Picha na Bakari Mwakangwale<br />
Nyerere alikuwa kiongozi wa dini au siasa?<br />
Ndiye muasisi wa Mfumokristo nchini<br />
Na Bakari Mwakangwale kile kinachoelezwa na<br />
MAASKOFU wametakiwa<br />
k u t a m b u a k w a m b a<br />
W a i s l a m u k u h u s u<br />
hayati Mwalimu Julius<br />
Kambarage Nyerere,<br />
si upotoshaji bali ni<br />
uhalisia na kwamba,<br />
yale wanayodai kuwa ni<br />
upotoshaji yamo katika<br />
vitabu mbalimbali na<br />
mwenyewe (Nyerere)<br />
hakuwahi kukanusha<br />
Inaendelea Uk. 4<br />
Wajumbe ZEC<br />
acheni kufuata<br />
matakwa ya<br />
wanasiasa<br />
Wanaomaliza muda wao<br />
wamuaga Maalim Seif<br />
Akerwa kutohakikiwa daftari<br />
la wapiga kura<br />
Na Mwandishi Wetu,<br />
Zanzibar<br />
MAKAMU wa Kwanza wa<br />
Rais wa Zanzibar, Maalim<br />
Seif Sharif Hamad, amesema<br />
iwapo Tume ya Uchaguzi<br />
itafanya kazi kwa kujiamini<br />
na kuacha kufuata matakwa ya<br />
wanasiasa, itajenga imani kwa<br />
wananchi juu ya uwezekano<br />
wa kuwepo kwa chaguzi huru<br />
na za haki na kukidhi matakwa<br />
ya wananchi.<br />
Maalim Seif ametoa kauli hiyo<br />
mwishoni mwa wiki iliyopita<br />
nyumbani kwake Mbweni<br />
Zanzibar, wakati akizungumza na<br />
wajumbe wa Tume ya Uchaguzi<br />
Zanzibar-ZEC, waliofika kwa<br />
ajili ya kumkabidhi ripoti ya<br />
utendaji wa Tume hiyo kwa<br />
kipindi cha miaka mitano, pamoja<br />
na kumuaga baada ya kumaliza<br />
muda wao wa utumishi ndani ya<br />
Inaendelea Uk. 2<br />
HAYATI Mwalimu Julius<br />
Kambarage Nyerere.
2<br />
AN-NUUR<br />
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786<br />
Cel: 0784 370 208, 0755 260 087 , DSM.<br />
www.<strong>annuur</strong>papers.co.tz E-mail: <strong>annuur</strong>papers@yahoo.co.uk<br />
Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top<br />
Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam<br />
MAONI YETU<br />
Tatizo letu si wingi<br />
bali viongozi waadilifu<br />
SIKU ya Jumatatu Desemba<br />
31, Rais wa Jamhuri ya<br />
Muungano wa Tanzania,<br />
Jakaya Mrisho Kikwete,<br />
alitangaza matokeo ya awali<br />
ya Sensa ya Watu na Makazi<br />
iliyofanyika Agosti 26 hadi<br />
Septemba 4 mwaka jana.<br />
Rais Kikwete alituambia<br />
kuwa sasa Tanzania ina watu<br />
milioni 44,929,002 ambapo<br />
Tanzania Bara kuna watu<br />
43,625,434 na Zanzibar kuna<br />
watu 1,303,568.<br />
Alisema kuwa katika Sensa<br />
ya tatu ya mwaka 2002, Tanzania<br />
ilikuwa na watu milioni 34.4,<br />
hivyo kwa matokeo ya sensa<br />
hii watanzania wameongezeka<br />
watu milioni 10.5 ambao ni<br />
sawa na ongezeko la asilimia<br />
2.6 kwa mwaka.<br />
Rais Kikwete alisema hii ni<br />
sensa ya nne kufanyika nchini<br />
tangu kuasisiwa kwa Jamhuri<br />
ya Muungano wa Tanzania<br />
mwaka 1964. Sensa ya kwanza<br />
ilifanyika mwaka 1967 ambapo<br />
nchi yetu ilikuwa na watu<br />
12,313,054. Tanzania Bara<br />
ilikuwa na watu 11,958,654<br />
na Zanzibar watu 354,400.<br />
Kwa maana hiyo, katika miaka<br />
45 tangu Sensa ya kwanza<br />
na hii ya sasa, Watanzania<br />
wameongezeka watu milioni<br />
33. Tunaambiwa kuwa taarifa<br />
za takwimu hizi ni kwa ajili<br />
ya matumizi ya kuboresha<br />
maisha ya kila Mtanzania.<br />
Kwa kutumia sense ya watu<br />
na makazi, hupatikana taarifa<br />
muhimu kwa ajili ya kutumiwa<br />
na Serikali kupanga mipango<br />
ya maendeleo ya nchi na jinsi<br />
ya kuhudumia wananchi.<br />
Rais alisema kama kasi ya<br />
ongezeko la watu la asilimia<br />
2.6 halitapungua ifikapo<br />
mwaka 2016, nchi yetu itakuwa<br />
na watu milioni 51.6. kiasi<br />
kilichomtia hofu kuwa ni mzigo<br />
mkubwa kwa taifa kwa uchumi<br />
kuwahudumia.<br />
Hofu hii ndiyo iliyomlazimu<br />
Rais Kikwete kusisitiza kuwepo<br />
mikakati madhubuti katika<br />
mipango ya maendeleo kuanzia<br />
sasa juu ya jinsi ya kuhudumia<br />
watu hao milioni 51.6 na zaidi<br />
ya hao miaka inayofuata.<br />
Hili ndilo lililomfanya Rais<br />
Kikwete, asisitize suala la<br />
kupanga uzazi. Akiwa na maana<br />
kwamba kinyume na hatua<br />
hiyo, hali ya maisha itashuka<br />
sana kutokana na kupanda<br />
idadi ya watu. Anaona kuwa<br />
kuna uwezekano wa serikali<br />
kushindwa kutoa huduma<br />
muafaka kwa watu wake.<br />
Hoja yetu kwa leo imesimamia<br />
katika nukta hiyo ya Rais juu ya<br />
hofu yake ya kuongezeka watu,<br />
akilinganisha na uwezo wa<br />
serikali kuwahudumia.<br />
K w a m t a z a m o w e t u ,<br />
tunamuona Rais Kikwete kama<br />
anaamini kuwa watu wengi ni<br />
mzigo kwa serikali.<br />
Hata hivyo, katika mataifa<br />
yaliyoendelea na yanayokua kwa<br />
kasi kiuchumi, watu wamekuwa<br />
mtaji mkubwa wa kiuchumi kwa<br />
mataifa hayo. Watu ni soko, watu<br />
ni nguvu kazi.<br />
China, Malaysia, India, na<br />
mataifa mengi ya Bara Asia,<br />
yamekuwa yakipiga hatua kwa<br />
kasi kiuchumi, nyenzo kubwa<br />
ikiwa ni idadi kubwa ya watu.<br />
Watu wengi ni kigezo muhimu<br />
cha kukua uchumi wa soko na<br />
nguvu kazi kwa Taifa lolote<br />
lile. Hata wanaofanya biashara,<br />
hukimbilia sehemu zenye idadi<br />
kubwa ya watu ili kupata soko.<br />
Idadi ya sasa ya Watanzania,<br />
j a p o t u n a a m i n i w e n g i<br />
hawakuhesabiwa, lakini haiwezi<br />
kuzua hofu kwa serikali yeyote<br />
yenye mipango mizuri ya<br />
kiutawala kwa watu wake.<br />
Tuonavyo sisi, hofu ya Rais<br />
Kikwete isingekuwepo kama<br />
angekuwa na watu waadilifu wa<br />
kumsaidia kusimamia mapato<br />
namatumizi na rasilmali za Taifa,<br />
ili kuijenga nchi kiuchumi na<br />
kuiongezea serikali nguvu ya<br />
kuwahudumia watu wake.<br />
U k w e l i n i k w a m b a ,<br />
kukosekana kwa viongozi na<br />
watendaji waadilifu, ambao<br />
wangeweza kusimamia rasilmali<br />
za nchi kwa faida, ndio sababu<br />
kubwa ya kutiliwa shaka<br />
uwezo wa serikali kuhudumia<br />
watanzania, sio idadi yao<br />
inayokuwa.<br />
Hata kukiwa na idadi ndogo<br />
ya watu isiyokuwa kwa kasi,<br />
lakini waliopewa dhakama na<br />
kuongoza na kusimamia mali za<br />
watanzania wakikosa uadilifu na<br />
kutokuwa watu wa kutosheka,<br />
uwezo wa kuhudumia watu hao<br />
wacheche hautakuwepo pia.<br />
Kukosekana maadili kwa<br />
viongozi kumekua chachu ya<br />
matumizi mabaya ya rasilmali<br />
za nchi, kiasi cha kushindwa<br />
kutoa huduma nzuri na bora kwa<br />
watu wake.<br />
Hulka za wizi, dhuluma,<br />
ufisadi, ubinafsi, kukosa<br />
uzalendo, ni matokeo ya<br />
kukithiri utamadumi mbovu kwa<br />
viongozi na watendaji, ambao<br />
wameweka uadilifu pembeni na<br />
kuvaa ubinafsi na kulitia taifa<br />
katika hasara.<br />
Ukweli ni kwamba, Tanzania<br />
imekuwa ikipata taabu kufikia<br />
malengo yake ya kuwahudhumia<br />
watu wake, kutokana na watu<br />
waliopewa dhamana kuliingiza<br />
Taifa katika mikataba mibovu<br />
na ya kihasara kwa maslahi yao<br />
na familia zao, huku watanzania<br />
walio wengi wakiachwa kuishi<br />
katika maisha ya kilofa.<br />
Tunaona kwamba Tanzania<br />
ambayo ina eneo la nchi kavu<br />
la kilomita za mraba 945,000,<br />
ambazo kati ya hizo, Kilomita<br />
za mraba 881,000 ni eneo la<br />
Tanzania Bara pekee yake na<br />
kilomita za mraba 2,000 ni eneo<br />
la visiwa vya Zanzibar na Pemba,<br />
Tahariri/Habari/Tangazo<br />
kwa ukubwa huu wa nchini, ni<br />
dhahiri kwamba kuna uhaba<br />
makubwa ya watu kulingana na<br />
ukubwa wa ardhi yetu.<br />
China ina watu milioni 1,300,<br />
ikiwa na ukubwa wa eneo la km²<br />
9,596,960. Malaysia ina ukubwa<br />
wa eneo la km² 329,847 tu, lakini<br />
watu wake ni 26,888,000 kwa<br />
kadirio la mwaka 2006. Sensa ya<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Wajumbe ZEC acheni kufuata matakwa ya wanasiasa<br />
Inatoka Uk. 1<br />
Tume hiyo.<br />
Hata hivyo, Maalim Seif,<br />
amesema Tume hiyo inayomaliza<br />
muda wake mwishoni mwa<br />
mwezi huu, inaondoka huku<br />
ikiacha viporo ambavyo Tume<br />
inayokuja inapaswa kuvipa<br />
umuhimu wa kipekee.<br />
Miongoni mwa mambo<br />
ambayo hayakuweza kutekelezwa<br />
na Tume hiyo ni pamoja na<br />
kushindwa kulifanyia uhakiki<br />
daftari la kudumu la wapiga kura<br />
kwa vipindi viwili tofauti, jambo<br />
ambalo liliahidiwa na Tume hiyo<br />
kufanyika kila ifikapo mwezi wa<br />
Oktoba.<br />
Kamishna wa Tume hiyo Bw.<br />
Ayoub Bakar Hamad, amesema<br />
tatizo hilo lilitokana na ukosefu<br />
wa fedha za kuendeshea kazi<br />
hiyo na kwamba, kwa sasa<br />
Shirika la Umoja wa Mataifa la<br />
mwaka 2000 iliyofanyika nchini<br />
humo ilionyesha kuwa kulikuwa<br />
na idadi ya watu 23,953,136.<br />
India yenyewe ina idadi ya watu<br />
bilioni 1.2<br />
Utaona kuwa pamoja na kuwa<br />
na idadi kubwa ya watu, na nchi<br />
nyingine kuwa na ardhi ndogo,<br />
bado mataifa hayo yamekuwa<br />
ndio tishio kwa sasa katika<br />
UNDP tayari limekubali kutoa<br />
fedha kwa ajili ya kuendeleza<br />
kazi hiyo.<br />
Amesema iwapo fedha hizo<br />
zitapatikana kwa wakati mapema<br />
mwezi ujao, Tume ijayo itakuwa<br />
na uwezo wa kufanya uhakiki<br />
mara mbili kwa mwaka, ili<br />
kufidia muda uliopita.<br />
K w a u p a n d e w a k e ,<br />
Mwenyekiti wa Tume hiyo Bw.<br />
Khatib Mwinyichande, amesema<br />
jitihada za makusudi zinapaswa<br />
kuchukuliwa katika kuimarisha<br />
d e m o k r a s i a y a u c h a g u z i<br />
Zanzibar.<br />
Amesema Tume inayokuja<br />
inaweza kufanya kazi zake vizuri<br />
zaidi, iwapo wanasiasa watatoa<br />
ushirikiano wa kutosha kwa Tume<br />
hiyo sambamba na kukubali<br />
kufuata sheria zilizowekwa.<br />
“ N a o m b a w a n a s i a s a<br />
musioneane haya, shaurianeni<br />
na kubalini kukosoana, na kubwa<br />
Bismillahir Rahmaanir Rahiim<br />
uchumi wa dunia.<br />
Wingi wetu si hoja ya kuwa<br />
na hofu juu ya huduma ya<br />
serikali kwa watu wake. Tatizo<br />
ni kukosekana watu waadilifu<br />
wa kusimamia rasilmali za<br />
watanzania, ambazo ndio msingi<br />
wa mapato yanayowezesha<br />
huduma kukidhi.<br />
zaidi ni kukubali kufuata sharia.<br />
alishauri Mwinyichande na<br />
kuongeza.<br />
“Wanasiasa pia mnayo nafasi<br />
kubwa ya kuisaidia Tume kwa<br />
kuipa maelekezo yanayostahiki,<br />
na kufanya hivyo kunaweza<br />
kuipa nyenzo bora za kufanyika<br />
kazi”.<br />
Naye Mkurugenzi wa Tume<br />
hiyo Bw. Salum Kassim Ali,<br />
ameahidi kuzifanyia kazi<br />
changamoto zilizojitokeza katika<br />
chaguzi zilizopita, ili kuweka<br />
mazingira bora zaidi katika<br />
chaguzi zijazo.<br />
Pamoja na hayo, Maalim<br />
seif, alieleza haja ya Tume hiyo<br />
kuanzisha mfuko wake, ili<br />
mapato ya Tume yaingie moja<br />
kwa moja katika mfuko huo na<br />
kupunguza usumbufu wakati<br />
Tume inapohitaji fedha kwa ajili<br />
ya matumizi yake ya kawaida.<br />
ALJEBRA ISLAMIC SEMINARY<br />
KIKAO CHA WAZAZI, WALEZI<br />
NA WADAU WENGINE WA ELIMU<br />
SHULE YA ALJEBRA ISLAMIC SEMINARY ILIYOPO KIBADA<br />
KIGAMBONI DAR ES SALAAM INAPENDA KUKUTAARIFU<br />
KUWA IMEANZISHA SHULE YA MSINGI ENGLISH MEDIUM.<br />
UKIWA KAMA MZAZI, MLEZI AU MDAU WA ELIMU<br />
UNAKARIBISHWA KWENYE KIKAO CHA KUTAMBULISHA<br />
SHULE RASMI, KIKAO KITAFANYIKA SHULENI SIKU YA<br />
JUMAPILI TAREHE 6/1/2013 KUANZIA SAA 3 ASUBUHI HADI<br />
SAA 6 MCHANA.<br />
KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIMU NAMBA:<br />
0715/0752/0688 260241 AU 0655/0768 176700<br />
TAFADHALI ATAKAYESOMA TANGAZI HILI<br />
AMTAARIFU NA MWENZAKE<br />
WOTE MNAKARIBISHWA<br />
WABILLAH TAWFIIQ<br />
MKUU WA SHULE
3<br />
Habari<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Kesi ya Sheikh Ponda mashahidi waingia ‘mitini’<br />
Na Bakari Mwakangwale kesi hatufahamu ni kwanini<br />
hajafika.<br />
MASHAHIDI wa upande<br />
wa mlalamikaji katika<br />
kesi inayomkabili Sheikh<br />
Ponda Issa Ponda na<br />
wenzake, wameshindwa<br />
k u f i k a M a h a k a m a n i<br />
Desemba 31, 2012, kutoa<br />
u s h a h i d i w a o k a t i k a<br />
mashtaka yanayowakabili<br />
watuhumiwa hao.<br />
K u f u a t i a k u s h i n d w a<br />
kufika mahakamani hapo<br />
kutoa ushahidi wao kama<br />
walivyotakiwa, Hakimu Mkazi<br />
wa Mahakama ya Kisutu,<br />
Victoria Nongwa, alitoa hati<br />
ya kukamatwa mashahidi<br />
ambao awali walisaini hati<br />
ya kuitwa mahakamani kutoa<br />
ushahidi wao, lakini siku ya<br />
kusikilizwa kesi hawakutokea<br />
m a h a k a m a n i h a p o n a<br />
hawakutoa taarifa yoyote.<br />
Kesi hiyo, ambayo ilipangwa<br />
kusikilizwa Jumatatu ya<br />
wiki iliyopita mahakamani<br />
hapo, iliahirishwa na Hakimu<br />
Victoria Nongwa, hadi tarehe<br />
14, 2013, kwa ajili ya kutajwa,<br />
ambapo itasikilizwa Januari<br />
17, 2013 kwa kuendelea<br />
kusikiliza mashahidi wa<br />
upande wa mashtaka.<br />
Kwa mara ya mwisho, kesi<br />
hiyo ilisikilizwa Desemba<br />
13, 2012, ambapo Sheikh<br />
wa Bakwata, Mkoa wa<br />
Shinyanga, Ismail Habibu<br />
Makusanya, alitoa ushahidi<br />
kwa upande wa mlalamikaji<br />
na iliahirishwa hadi Desemba<br />
31, 2012, ambapo ilikuwa<br />
ni kwa ajili ya kuendelea<br />
kusikiliza mashahidi zaidi wa<br />
upande wa mlalamikaji.<br />
Awali Mwanasheria wa<br />
Serikali, Tumaini Kweka,<br />
aliieleza Mahakama kwamba,<br />
aliita mashahidi watatu<br />
kwa ajili ya kufika kutoa<br />
ushahidi wao, lakini wote<br />
wameshindwa kufika licha ya<br />
kwamba mmoja alisaini hati<br />
ya kuitwa mahakamani kutoa<br />
ushahidi.<br />
“Leo kesi imeitwa kuja<br />
kusikilizwa, upande wa<br />
Jamhuri unaendelea kuleta<br />
mashahidi, lakini kutokana<br />
na sababu ambazo hata<br />
sisi Jamhuri tunashangaa,<br />
hawajatokea. Niliita mashahidi<br />
watatu kati ya hao mmoja<br />
alisaini samansi.” Alisema<br />
Wakili wa Serikali, ikiieleza<br />
Mahakama.<br />
Akitoa sababu za kutokufika<br />
kwa mashahidi hao, Wakili<br />
Kweka, alisema shahidi<br />
mmoja alimpa taarifa kuwa<br />
amesafiri, mwingine alidai<br />
ni mgonjwa hivyo hakusaini<br />
kabisa samansi na shahidi<br />
mwingine alisaini samansi<br />
na kuahidi kufika, lakini<br />
mpaka muda huu wa kuanza<br />
Hata hivyo wakili Kweka<br />
hakuwa tayari kutaja majina<br />
ya mashahidi hao.<br />
B a a d a e a l i i o m b a<br />
Mahakama itaje tarehe<br />
nyingine ya kusikilizwa kesi<br />
hiyo ili aweze kuwapata na<br />
kuwapeleka mashahidi hao<br />
mahakamani kwa ajili ya<br />
kutoa ushahidi wao dhidi ya<br />
mashtaka yanayowakabili<br />
Sheikh Ponda na wenzake.<br />
Kwa upande wake, wakili<br />
wa Sheikh Ponda na wenzake,<br />
Bw. Juma Nassoro, alihoji<br />
kuwa katika kesi iliyopita,<br />
(yaani Desemba 13, 2012)<br />
wakili wa Jamhuri Bw.<br />
Kweka, aliieleza mahakama<br />
kuwa kesi hiyo itakuwa na<br />
mashahidi wasiopungua<br />
arobaini kwa upande wa<br />
mlalamikaji, hivyo inakuwa je<br />
wameitwa mashahidi watatu<br />
tu na wameshindwa kutokea<br />
mahakamani na hawajulikani<br />
walipo?<br />
Baada ya kuulizwa na<br />
Hakimu, kauli ya Wakili<br />
Kweka, ilibadilika na kutoa<br />
sababu kuwa mmoja kasafiri<br />
na mwingine anaumwa, jambo<br />
ambalo Bw. Nassoro alidai si<br />
sahihi.<br />
“Hii si sahihi Mheshimiwa<br />
Hakimu, kutoa maelezo hayo<br />
hata huyo aliyesaini samansi<br />
pia hajatokea, inaonyesha<br />
udhaifu kwani hata mwenye<br />
kesi Hafidhi (Mlalamikaji)<br />
hajafika.” Alisema Nassoro.<br />
Hakimu Victoria Nongwa,<br />
alitoa amri ya kukamatwa<br />
shahidi aliyesaini samansi na<br />
kushindwa kufika mahakamani<br />
bila taarifa, ili ajieleze kwa<br />
nini alishindwa kutokea.<br />
Mpaka sasa Mashahidi<br />
watatu tu wa upande wa<br />
mashataka ndio walioweza<br />
k u t o a u s h a h i d i w a o<br />
mahakamni hapo.<br />
Nao ni Sheikh Suleiman<br />
Lolila, Katibu wa Bakwata<br />
Makao Makuu, Sheikh<br />
Ismail Habib Makusanya,<br />
Sheikh wa Bakwata mkoa wa<br />
Shinyanga na Bw. Suleiman<br />
Nassor Mohammed, mmoja<br />
wa wamiliki wa kampuni ya<br />
Agritanza, ambayo ndiyo<br />
iliyopewa ekari nne za kiwanja<br />
cha Markaz Chang’ombe.<br />
H a k i m u N o n g w a ,<br />
alipendekeza kesi hiyo iendelee<br />
kusikilizwa Januari 17, 2013.<br />
Januari 14, mwaka huu, kesi<br />
hiyo itarejea Mahakani hapo<br />
kwa ajili ya kutajwa kwa<br />
mujibu wa sheria.<br />
H a k i m u N o n g w a ,<br />
a l i b a i n i s h a k w a m b a<br />
watakaokwenda Mahakamani<br />
hapo Januari 14, 2013, ni<br />
Sheikh Ponda na Mukadam<br />
Swaleh ambao wapo mahabusa<br />
mpaka sasa.<br />
WAKILI wa Sheikh Ponda Issa Ponda, Juma Nassoro akiongea na Waislamu nje ya<br />
Mahakama ya Kisutu Jumatatu wiki hii. (Picha na Bakari Mwakangwale)<br />
Washtakiwa wengine<br />
waliopo nje kwa dhamana,<br />
w a m e t a k i w a k u f i k a<br />
Mahakamani hapo Januari<br />
17, 2013, siku ambayo kesi<br />
hiyo itaendelea kwa kusikiliza<br />
mashahidi wa upande wa<br />
mashtaka.<br />
Akiongea na waandishi<br />
wa habari mara baada ya<br />
kuahirishwa kwa kesi hiyo,<br />
Wakili wa Sheikh Ponda,<br />
Juma Nassoro, alionyesha<br />
kushangazwa na mwenendo<br />
wa kesi hiyo kwa upande wa<br />
walalamikaji.<br />
Alisema, mbali ya mashahidi<br />
wanaoanza kukwepa kufika<br />
na kutoa ushahidi wao, lakini<br />
hata Hafidhi, ambaye ndiye<br />
mlalamikaji amekuwa hafiki<br />
Mahakamani bila sababu za<br />
msingi.<br />
Aidha alisikitishwa na<br />
kitendo cha upande wa<br />
mashtaka kushindwa hata<br />
kutaja majina na idadi halisi<br />
ya mashahidi, jambo alilodai<br />
kuwa si la kawaida kwani<br />
hata katika kesi za mauaji,<br />
mashahidi huwa wanatajwa<br />
tofauti na wale wa kesi ya<br />
mteja wake.<br />
Alipoulizwa na An-nuur juu<br />
ya mustakali wa dhamana kwa<br />
wateja wake (Sheikh Ponda<br />
na Mukadam), alisema bado<br />
Jamhuri inadai kuwa inaona<br />
watahatarisha amani endapo<br />
watakuwa nje. Hata hivyo<br />
alisema, wameandika barua<br />
kulalamikia suala hilo kwa<br />
DPP lakini bado hawajapata<br />
majibu yoyote.<br />
Alisema katika barua<br />
h i y o , w a m e m w e l e z a<br />
DPP kwamba kuendelea<br />
kumshikilia Sheikh Ponda na<br />
Mukadam, ni kinyume cha<br />
haki za binadam kwa sababu<br />
haiwezekani katika kesi moja<br />
washtakiwa wengine wote<br />
wapate dhamana na wengine<br />
wanyimwe haki hiyo.<br />
Alisema kitendo hicho ni cha<br />
kukandamiza haki za msingi<br />
za binadamu kwa sababu<br />
katika mtiririko wa maelezo<br />
ya kesi, hakuna hata mmoja<br />
anayezungumzia kuvurugwa<br />
amani ya nchi, zaidi mashahidi<br />
wanazungumzia uhalali<br />
au kutokuwapo uhalali wa<br />
kuuzwa kiwanja cha Markazi<br />
Chang’ombe.<br />
Kwamba hakuna sehemu<br />
yeyote ambayo inaonyesha<br />
kiwanja hicho kinagusa<br />
maslahi ya Taifa.<br />
“Tumeandika barua kwa<br />
DPP, Desemba 24, 2012,<br />
yenye kumbukumbu namba<br />
LJ/CC/245/2012, tumeomba<br />
k w a m b a D P P a o n d o e<br />
pingamizi lake la dhamana<br />
kwa sababu kesi na mtiririko<br />
wake unavyokwenda, hakuna<br />
1.2259 sqm - 8 Milion<br />
2.1470 sqm - 4.5Milion<br />
3.1341 sqm - 4 Milion<br />
4.1566 sqm - 5Milion<br />
5. 1115 sqm - 3.5Milion<br />
6. 1136 sqm - 3.6Milion<br />
lolote linaloonyesha maslahi<br />
ya Taifa au usalama wa nchi<br />
unaweza kuhatarika kwa<br />
Sheikh Ponda na Sheikh<br />
Mukadam kuwa nje kwa<br />
dhamana. Nao wapewe haki<br />
hiyo kama ambavyo wenzao<br />
waliopatiwa dhamana katika<br />
shauri hilo hilo.” Alisema<br />
Wakili Nassoro.<br />
Wakili Nasoro alisema,<br />
u s h a h i d i u n a o t o l e w a<br />
unaonyesha kabisa kuwa ni<br />
mashtaka ya kawaida kwani<br />
alidai kwamba, hata maelezo<br />
ya Bw. Hafidhi, (aliyenunua<br />
k i w a n j a ) a l i y o y a t a o a<br />
Polisi Chang’ombe akiwa<br />
mlalamikaji, hakuna mahala<br />
panapoeleza kuna kuhatarisha<br />
maslahi ya Taifa au Usalama<br />
wa Taifa.<br />
Alisema ndio maana<br />
amemuomba DPP, atoe<br />
pingamizi lake ili Mahakama<br />
iweze kuweka wazi dhamana<br />
kwa washtakiwa ili wapate<br />
haki yao ya dhamana.<br />
Viwanja vilivyopimwa vinauzwa<br />
Kongowe Kibaha<br />
Vipo Barabara ya Kongowe-Soga<br />
Kilomita moja toka barabara ya Morogoro.<br />
Simu No.0755 090 754/0715 090 754.
4<br />
Habari<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Nyerere alikuwa kiongozi wa dini au siasa?<br />
Inatoka Uk. 1<br />
alipokuwa hai.<br />
Aidha wamefahamishwa<br />
k w a m b a , i n a p o s e m w a<br />
kuwa hayati Mwalimu<br />
Nyerere alikuwa muasisi wa<br />
Mfumokristo, umekuwepo<br />
ushahidi kamili hivyo<br />
haisemwi kwa kuzusha tu<br />
au kumpakazia na kwamba,<br />
ndiyo sababu Kanisa Katoliki<br />
nchini linataka kumpa<br />
utakatifu kutokana na kazi<br />
nzuri alilolifanyia Kanisa hilo<br />
alipokuwa madarakani.<br />
Akihutubia ndani ya Masjid<br />
Idrisa, uliopo Kariakoo jijini<br />
Dar mara baada ya swala<br />
ya Ijumaa wiki iliyopita,<br />
Maalim Bassaleh, aliwataka<br />
Maaskofu nchini, kueleza<br />
kwa uwazi sababu za kubariki<br />
utakatifu wa hayati Julius<br />
Kambarage Nyerere, wakati<br />
hakuwa kiongozi wa dini.<br />
Alisema kabla ya kutaka<br />
kumkingia kifua Mwalimu<br />
Nyerere ambaye aliyekuwa<br />
kiongozi wa siasa, ni vyema<br />
kwanza wakaeleza misingi<br />
ya kumsimika utakatifu<br />
mkatoliki ambaye hakuwa<br />
kiongozi wa Kanisa.<br />
“Lakini tuliulize hilo<br />
Kanisa Katoliki, kwamba je,<br />
Mwalimu Nyerere, alikuwa<br />
kiongozi wa dini au kiongozi<br />
wa Siasa? Kama wa siasa, vipi<br />
Kanisa hilo linataka kumpa<br />
cheo cha utakatifu, cheo<br />
ambacho kinalihusu Kanisa<br />
hilo tu, wakati alikuwa ni<br />
kiongozi wa umma na si<br />
wa dini.” Alisema na kuhoji<br />
Maalim Bassaleh.<br />
Alisema kwa kawaida,<br />
Wakatoliki huwapa utakatifu<br />
watu ambao walikuwa nguzo<br />
(mihimili) ya Kanisa Katoliki<br />
na ambao wamefanya kazi<br />
zilizotukuka wakiwa ni<br />
Wachungaji au Watawa<br />
au watumishi wa kanisa<br />
waliowahi kujitolea kwa<br />
muda mrefu katika Kanisa.<br />
Akinukuu kitabu cha<br />
Rais mstaafu wa Zanzibar,<br />
Mzee Aboud Jumbe, ambaye<br />
alifanya kazi ya kwa karibu na<br />
mwalimu, Maalim Bassaleh<br />
alisema katika kitabu chake<br />
hicho cha ‘The Partnership’,<br />
ameeleza kwamba mwalimu<br />
Nyerere, alikuja kuimarisha<br />
Mfumokristo katika utawala<br />
wake kutokana na nafasi<br />
aliyokuwa nayo na zaidi<br />
alilipendelea Kanisa lake<br />
Katoliki.<br />
Alisema Alhaji Jumbe,<br />
aliyaeleza hayo kwa kutumia<br />
MAALIM Ally Bassaleh akiongea na Waislamu katika viwanja vya Biafra, jijini Dar es<br />
Salaam.<br />
ushahidi wa Padri Mkristo<br />
wa Kikatoliki, Dk. Sivalon,<br />
aliyefanya utafiti kuhusu<br />
Kanisa Katoliki na siasa za<br />
Tanganyika, ambapo kwa<br />
uwazi na mapana Padri<br />
huyo ameonyesha ni vipi<br />
mwalimu Nyerere, wakati<br />
wa utawala wake alivyokuwa<br />
akilipendelea Kanisa Katoliki<br />
nchini.<br />
Ufafanuzi wa Maalim<br />
Bassaleh umekuja kufuatia<br />
yaliyoelezwa katika tamko<br />
la Jumuia ya Maaskofu<br />
lililotolewa Kurasini Jijini<br />
Dar es Salaam siku za hivi<br />
karibuni.<br />
Katika tamko hilo, pia<br />
walijadili hali ya kuzorota kwa<br />
mahusiano baina ya dini mbili<br />
kubwa hapa nchini, Uislamu<br />
na Ukristo, kisha walieleza<br />
juu ya hatari inayolinyemelea<br />
Taifa kutokana na hali hiyo.<br />
M a a l i m B a s s a l e h ,<br />
alisema katika kipengele<br />
hicho, amewataka Waislamu<br />
kuwapongeze Maaskofu<br />
hao kwa kuiona hali hiyo<br />
na kisha kutoa wito wa<br />
kuyashughulikia haraka<br />
yale yanayoashiria hatari<br />
sambamba na kuboresha<br />
mahusiano mema baina ya<br />
Waislamu na Wakristo.<br />
“ K a m a n d u g u z e t u<br />
Maaskofu watakuwa wakweli,<br />
basi huo ni mwanzo mzuri wa<br />
kujenga msingi mwema wa<br />
amani ya kweli katika nchi<br />
yetu na wala isiwe amani<br />
ya kifaurongo (aina ya mti<br />
ukiguswa husinyaa baada ya<br />
muda huchanua)”. Alisema<br />
Maalim Bassaleh.<br />
Pamoja na kuwapongeza<br />
Maaskofu kwa kuiona hatari<br />
iliyo mbele, lakini alidai<br />
makundi hayo yanatofautiana<br />
kwa kiasi kikubwa katika<br />
kiini cha matatizo hayo na<br />
suluhisho lake.<br />
Akichambua tamko hilo,<br />
Maalim Bassaleh, alisema<br />
makundi hayo yanaanza<br />
kuachana pale ambapo<br />
Maaskofu hao wanapokataa<br />
kuwepo kwa Mfumo Kristo<br />
ulioota mizizi katika dola,<br />
wakidai kwamba ni dhana<br />
potevu.<br />
“Jukwaa la Wakristo nchini<br />
tunakanusha wazi wazi na<br />
kuelezea bayana kuwa nchi<br />
hii haiongozi kwa Mfumo<br />
Kristo, kwa watu walio<br />
makini hakuna kificho kuwa<br />
viongozi wote waandamizi<br />
wa ngazi ya juu serikalini<br />
awamu ya sasa asilimia tisini<br />
ni Waislamu.<br />
“Dhana ya kuwepo Mfumo<br />
Kristo ni uongo na ni dhana<br />
potevu, maneno hayo ni<br />
agenda za waamini wenye<br />
imani kali na waliojiandaa<br />
kwa mapambano maovu.”<br />
Alinukuu sehemu ya tamko<br />
hilo.<br />
A k i f a f a n u a n e n o<br />
‘Mfumokristo’ Maalim<br />
Bassaleh, alisema ni mfumo<br />
kandamizi dhidi ya Uislamu<br />
na Waislamu, japo kuwa<br />
kwa misingi ya kiserikali<br />
mfumo huo haupo rasmi,<br />
lakini kiutendaji mfumo<br />
huo umefanywa kuwa ni<br />
mila, desturi na utamaduni<br />
wa watendaji walio wengi<br />
serikalini na katika taasisi<br />
zake, ambazo mara nyingi<br />
zinatumika kuwakandamiza<br />
na kudhulumu haki za<br />
Waislamu.<br />
Alisema mfumo huo<br />
umekuwa kama utamaduni<br />
na umeenezwa hadi katika<br />
mashirika ya umma na katika<br />
Taasisi za kijamii.<br />
Mara kadhaa watekelezaji<br />
wa Mfumokristo wamekuwa<br />
wakikiuka hata Katiba na<br />
sheria za nchi, hususani<br />
masuala hayo yanapogusa<br />
Waislamu na Uislamu.<br />
Maalim Bassaleh alisema<br />
kwa utaratibu huo, hata kama<br />
Maaskofu wamenisha kuwa<br />
Rais na watendaji wa ngazi za<br />
juu wote ni Waislamu, lakini<br />
kutokana na Mfumokristo,<br />
wote waliotajwa wanatatizika<br />
katika kutekeleza majukumu<br />
yao ipasavyo.<br />
Wakijisafisha kuhusu<br />
suala la MoU, Maaskofu hao<br />
wanadai katika tamko lao<br />
kwamba mkataba huo ni baina<br />
ya Makanisa ya Tanzania na<br />
Makanisa ya Ujerumani na<br />
kwamba, serikali ilihusishwa<br />
tu.<br />
Katika maelezo yao kuhusu<br />
MoU, wao wamedai kuwa<br />
MoU ya mwaka 1992, ni kwa<br />
ajili ya huduma ya kijamii<br />
zinazotolewa na Makanisa<br />
kwa Watanzania wote, ikiwa<br />
ni pamoja na huduma za<br />
hospitali, vituo vya afya,<br />
zahanati na shule mbalimbali<br />
zinazoendeshwa na Makanisa<br />
nchini.<br />
Maalim Bassaleh alihoji,<br />
ikiwa mkataba huo ni wa<br />
Makanisa na kwamba serikali<br />
ilihusishwa tu, itahusishwa<br />
vipi katika masuala ya dini<br />
wakati Serikali yenyewe<br />
haina dini?<br />
Inafahamika kwamba<br />
kwamba hao Maaskofu,<br />
wamekuwa wakiigomea<br />
Serikali kujihusisha na<br />
Mahakama ya Kadhi na<br />
suala la OIC kwa Waislamu,<br />
wakidai serikali haina dini.<br />
“Mbona Serikali hiyo<br />
inahusishwa katika mikataba<br />
ya Makanisa ya Ulaya<br />
na yale ya humu nchini,<br />
lakini hawataki ihusihwe<br />
na OIC, ambayo nayo ikija<br />
itatengeneza barabara,<br />
madaraja, na watakaopita<br />
ni watu wote bila kuangalia<br />
waliovaa kofia, kanzu au<br />
kilemba, kusaidia taasisi<br />
za huduma za kijamii ya<br />
watanzania wote bila kujali<br />
dini zao kama inavyodaiwa<br />
kufanywa na taasisi za<br />
makanisa?.” Alihoji Maalim<br />
Bassaleh.<br />
H a t a h i v y o M a a l i m<br />
Bassaleh alisema maaskofu<br />
hawataki kusema kweli juu<br />
ya mkataba wao wa MoU kati<br />
yao na serikali.<br />
A l i s e m a , m a e l e z o<br />
wanayoyatoa Maaskofu ni<br />
tofauti na mkataba wenyewe<br />
ambao unasema, “Sisi<br />
tuliotia saini zetu ambao ndio<br />
wahusika katika maridhiano<br />
hayo, kwa kutaja Makanisa<br />
yaliyoungana chini ya Baraza<br />
la Makanisa Tanzania na<br />
B a r a z a l a M a a s k o f u<br />
Tanzania.<br />
“Ambayo katika mkataba<br />
huu yatakuwa yanajulikana<br />
kama ni Makanisa kwa<br />
upande mmoja na Serikali<br />
ya Muungano wa Jamhuri<br />
wa Tanzania, itatambulika<br />
kama ni Serikali kwa upande<br />
wa pili”. Alinukuu sehemu ya<br />
mkataba huo kati ya serikali<br />
na makanisa.<br />
Alisema, kutokana na<br />
kipengele hicho, inaonyesha<br />
makubaliano hayo ni ya<br />
pande mbili ambapo upande<br />
wa kwanza ni wa Makanisa,<br />
ambayo yameungana pamoja<br />
na upande wa pili ni wa<br />
Serikali. Katika Makanisa<br />
yaliyotajwa hapo, hakuna<br />
Kanisa la Kijerumani.<br />
Alisema kwa kupitia<br />
mkataba huo, Makanisa<br />
yanatumia pesa za Serikali<br />
ambazo ni za walipa kodi<br />
wote. Mwaka wa fedha wa<br />
2008-2009, Serikali ilitumia<br />
mamilioni ya fedha kwa ajili<br />
ya kufadhili Mahospitali na<br />
taasisi nyingine za huduma<br />
za afya zinazomilikiwa na<br />
Makanisa kwa ajili ya kulipa<br />
mishahara wafanya kazi.
5<br />
Marekani<br />
yaonyesha<br />
kujizatiti<br />
kijeshi Afrika<br />
MAREKANI imetuma vikosi<br />
vyake nchini Chad, katika<br />
hatua ambayo inaonekana<br />
wazi kuwa ni kuzidi kujizatiti<br />
kijeshi barani Afrika.<br />
S a b a b u i l i y o t a j w a n a<br />
Marekani ya kutuma vikosi<br />
vyake nchini Chad, ni wasiwasi<br />
wa Washington kuhusu usalama<br />
wa raia wake kutokana na kuzidi<br />
kusonga mbele waasi katika<br />
nchi Jamhuri ya Afrika ya Kati,<br />
ambayo ni jirani na Chad.<br />
Katika barua yake kwa<br />
maspika wa mabunge mawili<br />
ya Marekani, Rais Barack<br />
Obama wa nchi hiyo amesema<br />
kuwa, raia kadhaa wa Marekani<br />
wameondolewa katika mji mkuu<br />
wa Jamhuri ya Afrika ya Kati,<br />
Bangui, tangu Desemba 27 na<br />
hivi sasa kikosi cha wanajeshi<br />
50 wa Marekani kimetumwa<br />
nchini Chad.<br />
Watu wanaokosoa hatua hiyo<br />
ya Marekani wanasema kuwa,<br />
hawaoni sababu ya Washington<br />
kutuma kikosi cha jeshi, tena<br />
katika nchi ambayo haina<br />
machafuko kwa madai kuwa<br />
nchi jirani ina machafuko.<br />
Itakumbukwa kuwa Marekani<br />
na Ufaransa zilikataa mwito<br />
wa Rais Francois Bozize, wa<br />
Jamhuri ya Afrika ya Kati wa<br />
kutaka kusaidiwa kukabiliana na<br />
waasi wa kundi la SELEKA.<br />
LONDON<br />
LICHA ya kutangazwa<br />
kwa propaganda mbaya<br />
kama dini ya magaidi,<br />
U i s l a m u u n a k u w a<br />
kwa kasi katika nchi<br />
za Magharibi ambazo<br />
kwa kawaida wanaishi<br />
wakristo wengi.<br />
Uingereza imekuwa<br />
mfano mzuri wa hali hii<br />
ambapo Wakristo wengi<br />
wanabadili dini na kuwa<br />
Waislamu na kuufanya<br />
U i s l a m u k u w a d i n i<br />
inayokuwa kwa kasi zaidi<br />
katika majimbo ya nchi<br />
hiyo.<br />
Kushamiri kwa Uislamu<br />
kumebainika hivi karibuni<br />
kufuatia sensa iliyofanyika<br />
hivi karibuni Uingereza,<br />
a m b a y o s i k w a m b a<br />
imebainisha ukuaji wa<br />
haraka wa Uislamu, lakini<br />
pia kumeifanya Uislamu<br />
kuwa dini ya pili nchini<br />
humo.<br />
Mmoja wa watathmini<br />
TEHRAN<br />
Jeshi la Wanamaji la<br />
Jamhuri ya Kiislamu ya<br />
Iran limefanyia majaribio<br />
makombora mawili ya<br />
Qader (Uwezo) na Nour<br />
(Nuru) katika mazoezi ya<br />
kijeshi yaliyofahamika<br />
kama ‘Velayat 91’.<br />
Kamanda wa Kitengo cha<br />
Makombora cha Jeshi la<br />
Wanamaji la Jamhuri ya<br />
Kiislamu ya Iran Admeli<br />
Habari za Kimataifa<br />
Iran yafanyia majaribio makombora mapya<br />
Ali Vafadar, amesema aina<br />
hizo mbili za makombora<br />
hayo yametengenezwa nchini<br />
humo na wataalamu Wairan<br />
wenyewe.<br />
A m e o n g e z a k u w a<br />
m a k o m b o r a h a y o<br />
yameimarisha kiwango cha<br />
uwezo wa Jeshi la Wanamaji<br />
la Iran baharini.<br />
Mazoezi hayo hayo ya siku<br />
sita yalianza Ijumaa, Desemba<br />
28, na yamefanyika katika<br />
eneo la fukweni, baharini<br />
na angani, kwenye lango la<br />
Hormuz, Bahari ya Oman,<br />
Kaskazini mwa Bahari ya<br />
Hindi, Ghuba ya Aden na<br />
lango la Babul Mandab.<br />
Kamanda wa Jeshi la<br />
Wanamaji la Jamhuri ya<br />
Kiislamu ya Iran Admeli<br />
Habibullah Sayyari, amesema<br />
mazoezi hayo ya kijeshi<br />
yamebeba ujumbe wa urafiki<br />
na udugu kwa mataifa rafiki<br />
na onyo kali kwa maadui.<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
WASHINGTON<br />
HABARI kutoka Marekani<br />
zinabainisha kuwa, viongozi<br />
wa kisiasa wa vyama vya<br />
Republican na Democrats,<br />
wameendelea kulumbana<br />
kutokana na hali mbaya ya<br />
uchumi wa nchi hiyo.<br />
Mvutano huo umetokea<br />
kuhusu juu ya namna gani ya<br />
kutatua matatizo ya kiuchumi<br />
ili kuweza kuwapunguzia<br />
wananchi mzigo wa mgogoro<br />
wa kiuchumi.<br />
Mkuu wa taasisi ya Centre for<br />
Corporate Policy, ya Washington<br />
Bw. Charlie Cray, amesema<br />
kuwa jamii ya watu wa tabaka<br />
la kati nchini Marekani, ndio<br />
waathirika wa malumbano ya<br />
kisiasa nchini humo.<br />
Ameongeza kuwa, hali<br />
hiyo imezidisha ongezeko la<br />
ukosefu wa ajira na mgogoro<br />
wa kiuchumi nchini humo.<br />
Mtaalamu huyo wa masuala ya<br />
kiuchumi pia amesisitiza kuwa,<br />
hali mbaya zaidi inawakabili<br />
Wamarekani wenye asili ya<br />
Kiafrika na kwamba, kiwango<br />
cha ukosefu wa ajira katika<br />
tabaka hilo kimefikia asilimia<br />
12.4, ambapo wengi wao ni<br />
vijana walio na umri wa kati ya<br />
miaka 18 hadi 29.<br />
Rais Barack Obama amekuwa<br />
akishinikiza mpango wake wa<br />
kuiongeza kodi kwa matajiri<br />
nchini humo, ikiwa nikatika<br />
harakati zake za kujaribu<br />
kupunguza nakisi ya bajeti ya<br />
nchi hiyo na kuongeza pato la<br />
serikali.<br />
Wakristo Uingereza wasilimu kwa kasi<br />
Waufanya Uislamu kukua kwa kasi zaidi<br />
amesema, “dalili zote<br />
ni kwamba idadi kubwa<br />
ya Waingereza ambao<br />
wamekulia katika Ukristo<br />
w a n a k u w a Wa i s l a m .<br />
Hii inaonyesha ni jinsi<br />
gani idadi ya Waislamu<br />
inaongezeka huku ile ya<br />
Wakristo ikipungua…<br />
kiwango hiki kinatarajiwa<br />
kuendelea.”<br />
K w a m u j i b u w a<br />
matokeo ya sensa hiyo,<br />
Waislamu sasa wanakuwa<br />
asilimia tano ya idadi ya<br />
watu wote wa Uingereza.<br />
Viwango vya ukuaji vya<br />
hivi karibuni vimeonyesha<br />
kuwa idadi ya Waislamu<br />
inaweza kuwa maradufu<br />
hadi kufikia sensa ijayo<br />
ambayo itafanyika mwaka<br />
2021, na hapo wanatarajiwa<br />
kuwa asilimia kumi ya<br />
idadi ya watu wote.<br />
Katika kipindi hicho,<br />
idadi ya Waislamu England<br />
na Wales inakadiriwa<br />
kuongezeka kwa asilimia<br />
80 (sawa na milioni 1.2),<br />
kutoka milioni 1.5 mwaka<br />
2001 hadi milioni 2.7<br />
mwaka 2011, na kuufanya<br />
Uislamu dini ya pili kwa<br />
ukubwa Uingereza.<br />
W a t a f i t i w e n g i<br />
wanaamini kuwa idadi<br />
k a m i l i y a Wa i s l a m<br />
Uingereza inaweza kuwa<br />
kubwa kuliko iliyojitokeza<br />
katika data za sensa hiyo.<br />
Hii ni kwasababu swali<br />
la dini lilikuwa swali la<br />
hiari katika sensa hiyo ya<br />
mwaka 2011 na asilimia<br />
7.2 ya watu hawakujibu<br />
swali hilo.<br />
D i n i y a t a t u k w a<br />
ukubwa England na Wales<br />
ni Hinduism (817,000),<br />
wakifuatiwa na Sikhism<br />
(423,000), Buddhism<br />
(248,000) na Judaism<br />
(263,000), ilieleza ripoti<br />
ya sensa hiyo.<br />
Katika sensa hiyo, idadi<br />
ya watu milioni 56.07<br />
walihesabiwa, idadi ya<br />
waliojieleza wenyewe<br />
kuwa ni Wakristo ilishuka<br />
kutoka asilimia 72 mwaka<br />
2001 hadi kufikia asilimia<br />
59 mwaka 2011. Idadi<br />
ya Waislamu iliongezeka<br />
kutoka asilimia 3 hadi<br />
kufikia asilimia 5 katika<br />
muongo mmoja.<br />
Takwimu za sensa hiyo<br />
zimeonyesha kuwa idadi ya<br />
Wakristo England na Wales<br />
imeshuka kwa silimia 11<br />
(milioni 4.1) katika karne<br />
iliyopita, aidha inaonyesha<br />
kupungua kutoka milioni<br />
37.3 mwaka 2001 hadi<br />
milioni 33.2 mwaka 2011.<br />
T a k w i m u h i z o<br />
zilionyesha dhahiri kuwa<br />
Uchumi waibua<br />
malumbano ya<br />
kisiasa Marekani<br />
WAZIRI Mkuu wa<br />
Uingereza, David Cameroon<br />
Uislamu unakuwa kwa<br />
kasi na idadi kubwa ya<br />
wasiokuwa Waislamu<br />
wameamua kuufuata,<br />
ingawa watu wa Magharibi<br />
wanauona kama ni dini<br />
ya magaidi na kusambaza<br />
propaganda potofu dhidi ya<br />
Waislamu.
6<br />
WAZUNGU wana msemo wao<br />
usemao, “Ukitaka kumuua<br />
mbwa mpe jina baya”.<br />
Jambo la kushangaza basi,<br />
katika uzoefu wa maisha ya<br />
mwanadamu si mara nyingi<br />
falsafa na ukweli uliomo katika<br />
methali kutumika kama falsafa<br />
ya nchi au taifa fulani.<br />
Lakini kwa sababu moja au<br />
nyengine, kuna misemo miwili<br />
mitatu hivi inaonekana kubakia<br />
kuwa misemo tu, bali imekuwa<br />
kama falsafa inayoongoza<br />
maisha na malengo ya watu<br />
hapa duniani.<br />
Kwa mfano, msemo mkongwe<br />
wa Wazungu utafsirikao<br />
kama ‘wagawe, uwatawale’<br />
umetumika ipasavyo katika<br />
kuzitawala nchi na Jumuiya<br />
mbalimbali duniani. Waingereza<br />
waliweza kuitawala dunia kwa<br />
msemo huu. Na Wamarekani<br />
wameweza kufanya watakalo<br />
duniani kwa kutumia falsafa hii.<br />
Pia Watanganyika wameweza<br />
kuitawala Zanzibar kimabavu<br />
kwa kutumia fasalafa hii pia.<br />
Wametugawa na kututawala.<br />
Wakati hubadilisha mambo.<br />
Kwa muda wa miongo ipatayo<br />
sita (six decades) tangu uhuru,<br />
falsafa hii imekuwa ikifichwa<br />
kutumiwa kwake. Inafichwa sio<br />
Makala<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Hujuma dhidi ya Waislamu wa Zanzibar<br />
SHEIKH Farid Had na viongozi wenzake wa UAMSHO wakiwa katika karandinga la Polisi.<br />
Na Mwandishi Wetu<br />
kama haipo, ipo lakini dunia ya<br />
sasa ya utandawazi na haki za<br />
binadamu, falsafa hii haipati<br />
nguvu ya kutembea utupu<br />
hadharani tena kama ilivyokuwa<br />
mwanzo.<br />
Na kwa vile silaha hii<br />
imekwisha nguvu, tumeletewa<br />
silaha nyengine isemayo,<br />
‘Ukitaka kumuuwa mbwa, mpe<br />
jina baya!’<br />
Zanzibar, katika ramani<br />
ya siasa za dunia imekuwa<br />
ikifanyiwa kila bidii na njama<br />
ili iwe sawa na Palestina, au<br />
mataifa mengine ya Kiislamu<br />
yaliyoharibiwa na Mayahudi<br />
na Manasara kupitia mataifa<br />
yao makubwa. Yaani Zanzibar<br />
inatakiwa isiwe na utaifa wala<br />
utambulisho wowote. Na hilo<br />
lilikuwa karibu mno kufanikiwa.<br />
Lakini kabla ya kufikia hatua<br />
hiyo, wazanzibari wameamka.<br />
Wakaanza kudai haki zao.<br />
Na kwa vile wanzanzibari<br />
hawalengwi wala kuthibitikiwa<br />
na kuwa na haki ya kudai chao,<br />
pao, lao, wala ya kwao, hili<br />
limekuwa kosa. Sasa tunabatizwa<br />
kwa kila jina baya ili kuhalalisha<br />
kuangamizwa kwetu.<br />
Tu n a i t w a m a g a i d i n a<br />
Waislamu wenye msimamo<br />
mkali. Tunaitwa hivi katika<br />
k i p i n d i a m b a c h o d u n i a<br />
imejengwa iamini kila Muislamu<br />
ni adui asiye na haki ya kuishi<br />
katika mgongo wa dunia hii.<br />
Kwa kusherehesha mjadala<br />
huu, katika siku za hivi karibuni,<br />
Zanzibar imekuwa ikiharibiwa<br />
sifa na jina lake kwa maksudi na<br />
vyombo vitatu. Kwanza, Kanisa<br />
ambalo limekuja Zanzibar<br />
sio kwa kufanya ibada, bali<br />
kuifitinisha Zanzibar mbele<br />
ya jamii za Kimataifa. Kanisa<br />
lilikuwapo Zanzibar tangu na<br />
kabla ya kuja kwa Edward<br />
Steere hapa Zanzibar.<br />
Kulikuwa kimya ilhali<br />
Waislamu walikuwepo, tena<br />
na wasomi wakubwa wa<br />
enzi hizo wakiwa hai hapa<br />
Zanzibar. Ilikuwa kimya na<br />
wala hakukuwa na Mzanzibari<br />
aliyewahi kuingilia uhuru wa<br />
kuabudu kwa wana Kanisa. Na<br />
hivi ndivyo ilivyo mpaka leo.<br />
Zanzibar ni nchi pekee duniani<br />
iliyo na ustahamilivu mkubwa<br />
wa kidini (Religious tolerance)<br />
kuliko nchi yoyote.<br />
Kwa vile wanaonekana<br />
Wazanzibari hawapendi ugomvi<br />
na wenzao wa Kikristo, la kufanya<br />
ni kuwapachika kila aina ya sifa<br />
mbovu ili kuwachafua, hata kama<br />
hawamchokozi mtu. Kanisa,<br />
Zanzibar hufanya kila liwezalo,<br />
kuhakisha wanawakorofisha<br />
Waislamu ili wajibu mapigo,<br />
wawaharabie sifa na malengo<br />
yao yatimie.<br />
Hili lilishindikana na sasa kuna<br />
njama za maksudi za kufanya<br />
matukio yao wenyewe kama<br />
vile kutia moto baa, makanisa<br />
yao, na hata kujeruhiana na<br />
kisha wakasingizia Waislamu<br />
wa Zanzibar, ambao wengi<br />
wao hawana habari na Wakristo<br />
waliopo. Wazanzibari wa sasa<br />
wametiwa dhiki za maisha kiasi<br />
kwamba hata hizo sala tano ni<br />
shida kuzisimamisha, seuze<br />
kugombana na kanisa.<br />
Chombo cha pili ni Serikali,<br />
ambayo ili kulinda maslahi ya<br />
Muungano, imeifanya Zanzibar<br />
kuwa ni eneo la hatari kidini<br />
na kisiasa. Na bila kujua athari<br />
ya maneno wanayosema mbele<br />
ya jamii za kimataifa, serikali<br />
imethubutu kuitangazia dunia<br />
kuwa Zanzibar kuna magaidi<br />
na wanaharakati wa Kiislamu<br />
wenye msimamo mkali.<br />
Huu ni ubaya ulio dhahiri wa<br />
Serikali dhidi ya wananchi wake<br />
wenyewe. Serikali haitambui<br />
kuwa kufanya hivi sio kuharibu<br />
taswira ya Zanzibar na Waislamu<br />
tu, bali hata nchi nzima, na<br />
kuathiri shughuli nyingi za<br />
kiuchumi, lakini nani anafikiri<br />
hayo. Tupo kisiasa zaidi.<br />
Taasisi ya tatu, Mayahudi na<br />
Manasara ambao kazi yao ni<br />
kuleta fitina katika ardhi, hasa<br />
hasa ardhi za Kiislamu. Watu<br />
hawa ambao wengi ni wazungu,<br />
huja hapa kama watalii na baadae<br />
kuanza kupanga hujuma na<br />
mitandao ya fitina zisizomithilika<br />
dhidi ya Waislamu. Baada ya<br />
hujuma zao hizo kutimia, ndio<br />
utaona wanatumia vyombo vya<br />
habari kuitangazia dunia kuwa<br />
Zanzibar kuna ‘ugaidi’ Waislamu<br />
wanawaonea wakristo. Hii ni<br />
fitna tupu.<br />
Zanzibar hakuna lolote kati ya<br />
hayo wanayoyataja. Na jambo la<br />
kushangaza, hakuna kiongozi<br />
wetu hata mmoja anayekanusha<br />
upuuzi na kasumba hizi. Leo hii<br />
Wazungu ndio wanaoongoza kwa<br />
kutembea uchi hapa Zanzibar.<br />
Waislamu wako kimya. Wao<br />
wapo hapa pia kuishawishi nchi<br />
hii ikubali ndoa za mashoga.<br />
Mambo ambayo huko kwao<br />
yameshawashinda, wanatuletea<br />
sisi huku.<br />
Wazungu ndio walioleta<br />
nakama ya mahoteli, kuigiza<br />
na kuingiza mikanda ya ngono,<br />
na ndio wanaojazana hapa<br />
mwezi wa Ramadhani kuja<br />
kula mchana barabarani ili<br />
kuwaudhi Waislamu. Hakuna<br />
anayesema. Tunafanyiwa<br />
maudhi na karaha ndani ya nchi<br />
yetu, bila kuheshimu mila na<br />
desturi za nchi yetu. Ukisema<br />
Serikalini unajibiwa, ‘Serikali<br />
haina dini’.<br />
Wanzanzibari tumekuwa<br />
watumwa, watwana katika nchi<br />
yetu kwa wageni wajao kwetu.<br />
Na bahati mbaya Waislamu<br />
wakisimama kudai haya, Serikali<br />
husimama kidedea kuwalaani<br />
Waislamu na kuwahujumu<br />
kupita kiasi. Serikali haijali<br />
wala kutambua kuwa katika<br />
nchi kama Zanzibar ambapo<br />
Waislamu ni wengi, mila na<br />
desturi za Waislamu hao hazina<br />
budi kulindwa na kuheshimiwa<br />
na kila mtu, licha ya kuwa<br />
serikali haina dini, lakini<br />
viongozi wanayo dini.<br />
Nionavyo, ni wajibu wa kila<br />
Muislamu, awe kiongozi wa<br />
siasa, wa nchi au raia wa kawaida,<br />
ni wajibu kwake kuilinda<br />
dini hii. Tuelewe kwamba<br />
wenzetu wasiokuwa Waislamu,<br />
wameandaliwa kuvuruga<br />
juhudi zote za kuimarisha na<br />
kuisimamisha dini ya Kiislamu.<br />
Na mbinu wanayoitumia ni hii<br />
ya kutuita majina mabaya ili<br />
kuhalalisha maovu yao.<br />
Wazanzibari na Waislamu<br />
wote, tuwe macho na tusimame<br />
na kamba ya mwenyezi Mungu<br />
bila kufarikiana. Kwani<br />
tutakaposimama kumnusuru<br />
M o l a w e t u , a t a t u n u s u r u<br />
na kuzithibisha nyoyo zetu.<br />
Tukumbuke kwamba, wenzetu<br />
w a s i o k u w a Wa i s l a m u<br />
hawapendezewi na ustaarabu na<br />
utamaduni sahihi wa dini hii, na<br />
ndio Mola mtukufu anaposema<br />
‘Hawataridhika hao Mayahudi<br />
na Manasara, mpaka muwafuate<br />
mila na nyendo zao’.<br />
Wallwahu a-alam!
7<br />
Na Mama mwanaharakati<br />
D e s e m b a 2 7 , 2 0 1 2 -<br />
‘Mtandao wa kupashana<br />
habari’<br />
Siku tatu kabla ya kijana<br />
wa miaka 20 Adam Lanza<br />
kumwua mama yake, na<br />
halafu akafyatua risasi<br />
katika darasa lililojaa<br />
watoto wa chekechea<br />
h u k o C o n n e c t i c u t<br />
n c h i n i M a r e k a n i ,<br />
mwanangu Michael (jina<br />
limebadilishwa) mwenye<br />
umri wa miaka 13 alikosa<br />
basi la kumpeleka shule kwa<br />
sababu alikuwa amevaa<br />
k a p t u r a y e n y e r a n g i<br />
zisizostahili.<br />
“Naweza kuvaa kaptura<br />
hii,” alisema, sauti yake<br />
ikiongeza ukali, chembe<br />
nyeusi ya katikati ya jicho<br />
ikimeza ukanda wa bluu<br />
unaozunguka.<br />
“Kaptura hii ni buluu ya<br />
bahari,” nilimwambia. “Sare<br />
za shule yako ni kaptura<br />
nyeusi au za khaki, basi.”<br />
“Waliniambia naweza<br />
kuvaa hizi,” aling’ang’ania.<br />
“Wewe ni dogi mpumbavu,<br />
Naweza kuvaa kaptura yoyote<br />
ninayotaka. Hii ni Amerika.<br />
Nina haki zangu.”<br />
“Huwezi kuvaa chochote<br />
unachotaka,” nilisema, kwa<br />
sauti ya upole, kumwelewesha.<br />
“Na kwa vyovyote huwezi<br />
kuniita dogi mpumbavu.<br />
Hutatumia chochote cha kielektroniki<br />
siku nzima, Sasa<br />
ingia kwenye gari nikupeleke<br />
shuleni.”<br />
Naishi na mtoto ambaye<br />
n i m g o n j w a w a a k i l i .<br />
Nampenda mwanangu. Lakini<br />
ananitisha.<br />
Wiki kadhaa zilizopita,<br />
Michael alinishikia kisu na<br />
kutishia kuniua na halafu<br />
ajiue baada ya kumwambia<br />
arudishe vitabu vya maktaba<br />
alivyochelewesha. Wadogo<br />
zake wa miaka 7 na 9<br />
wanafahamu mipango ya<br />
usalama - walikimbilia<br />
gari na kufunga milango<br />
kabla sijawaambia wafanye<br />
hivyo. Nilifaulu kukitoa<br />
kisu mikononi mwa Michael,<br />
na kwa uangalifu nikaokota<br />
chochote chenye ncha kali<br />
ndani ya nyumba na kuweka<br />
katika kasha ambalo kila<br />
nikisafiri naondoka nalo.<br />
Na muda wote huo alikuwa<br />
akiendelea kunitukana kwa<br />
sauti kubwa na kutishia<br />
kuniua au kunidhuru.<br />
Ugomvi huo uliisha wakati<br />
maofisa watatu wa polisi<br />
wenye vifua vipana na mganga<br />
msaidizi walipombana<br />
mwanangu aingie kwenye<br />
kiti cha gari la wagonjwa la<br />
gharama kubwa kupelekwa<br />
katika chumba cha dharura<br />
cha karibu. Hospitali ya<br />
magonjwa ya akili haikuwa na<br />
vitanda vyovyote siku hiyo, na<br />
Michael akatulia vyema katika<br />
Makala<br />
Watoto wauaji, na familia zenye hofu Marekani<br />
Baada ya mauaji mengine ya kutisha na<br />
janga la kitaifa, ni rahisi kuzungumzia<br />
bunduki. Lakini ni wakati pia wa kujadili<br />
magonjwa ya akili<br />
chumba cha dharura. Hivyo<br />
wakaturudisha nyumbani<br />
na maelekezo ya kutumia<br />
Zyprexa na kufika tena<br />
hospitalini hapo kumwona<br />
daktari wa magonjwa ya<br />
watoto wa kituo hicho.<br />
Bado hatufahamu tatizo<br />
na Michael ni nini. Kila<br />
aina ya ugonjwa wa watoto<br />
na mvurugiko wa akili na<br />
tiba yake vimejaribiwa, bila<br />
mabadiliko, katika mikutano<br />
na maofisa walezi wa watoto<br />
watukutu, wasimamizi jamii<br />
na washauri, na waalimu na<br />
watawala wa shule.<br />
A m e k u w a a k i t u m i a<br />
mchanganyiko wa dawa za<br />
kuzuia kuchanganyikiwa<br />
na za kupooza mawazo,<br />
mpangilio wa dawa unaotoka<br />
Russia kutibu magonjwa ya<br />
hulka. Hakuna mabadiliko.<br />
‘Alipokuwa anaingia darasa<br />
la saba (ni mwanzo wa elimu<br />
ya kati, sekondari) Michael<br />
alikubaliwa katika mchepuo<br />
wa masomo yaliyoharakishwa<br />
kwa watoto wenye vipaji<br />
katika hisabati na sayansi.<br />
Uwezo wake wa kuelewa<br />
ni nje ya kawaida. Akiwa<br />
anajisikia vizuri, atakufanya<br />
usikilize akiongea chochote,<br />
iwe ni habari za Uyunani ya<br />
kale au tofauti kati ya fizikia<br />
ya Einstein na Newton, au<br />
riwaya mashuhuri. Muda<br />
mwingi zaidi hali yake ni<br />
nzuri. Lakini anapobadilika,<br />
chunga sana. Na huwezi kujua<br />
ni kitu gani kitamtibua.<br />
Wiki kadhaa baada ya<br />
kuingia shule hiyo mpya,<br />
Michael alianza kuonyesha<br />
hulka ya kushangaza na<br />
kutishia watoto shuleni.<br />
Tuliamua kumhamisha<br />
kuingia mafunzo yenye<br />
vizuizi vikali katika wilaya,<br />
mazingira ya shule ambako<br />
watoto wasioweza kufuata<br />
m a d a r a s a y a k a w a i d a<br />
wanawekwa katika uangalizi<br />
bila malipo kuanzia saa moja<br />
na nusu asubuhi hadi saa nane<br />
kasoro kumi alasiri Jumatatu<br />
hadi Ijumaa hadi wafikie<br />
umri wa miaka 18.<br />
Asubuhi hiyo ya ugomvi wa<br />
kaptura, Michael aliendelea<br />
kubishana na mimi katika<br />
gari. Mara anaomba radhi<br />
na kuonekana kusikitishwa<br />
na alichofanya. Kabla<br />
hatujaingia katika eneo la<br />
kuegesha magari la shuleni<br />
kwake, akasema, “Mama<br />
samahani, nasikitika sana,<br />
Naweza kutumia michezo ya<br />
video baadaye leo?”<br />
“ H a t a k i d o g o , ”<br />
nilimwambia. “Huwezi<br />
kufanya ulichofanya asubuhi<br />
hii na udhani unaweza kupata<br />
zawadi zako za elektroniki<br />
mapema kiasi hicho.”<br />
Uso wake ukigeuka baridi,<br />
na macho yake yakiwa na<br />
hasira iliyopimwa. “Basi<br />
nitajiua,” alisema. “Nitaruka<br />
nje kutoka katika gari na<br />
kujiua.”<br />
Ilitosha. Baada ya kutoa<br />
kisu, nilimwambia kuwa<br />
kama akisema tena maneno<br />
hayo nitampeleka moja kwa<br />
moja hospitali ya magonjwa<br />
ya akili, bila lakini au labda.<br />
Sikumjibu, ila kuingiza gari<br />
katika njia mkabala, kugeukia<br />
kushoto badala ya kulia.<br />
“Unanipeleka wapi?”<br />
aliuliza, akianza kuwa na<br />
wasiwasi. “Unakwenda<br />
wapi?”<br />
“Unajua tunapokwenda,”<br />
nilijibu.<br />
“ H a k u n a ! H u w e z i<br />
kunifanya hivyo! Unanipeleka<br />
motoni! Unanipeleka motoni<br />
moja kwa moja!”<br />
Nilisimamisha gari mbele<br />
ya hospitali, nikimpungia kwa<br />
nguvu mhudumu mmoja wa<br />
kliniki aliyekuwa amesimama<br />
nje. “Ita polisi,” nilisema,<br />
“Fanya haraka.”<br />
Michael alikuwa sasa<br />
chakaramu kabisa, akipiga<br />
kelele na kupiga huku na<br />
kule. Nilimbana kwa karibu<br />
ili asiweze kutoroka kutoka<br />
kwenye gari, Alinipiga mara<br />
kadhaa na kupiga kiwiko<br />
chake katika kufua changu<br />
kwa chini. Bado nina nguvu<br />
kuliko yeye lakini haitachukua<br />
muda.<br />
Polisi walifika haraka na<br />
kumbeba mwanangu akipiga<br />
kelele na mateke hadi ndani<br />
kabisa ya hospitali. Nilianza<br />
kutetemeka, na machozi<br />
yakaanza kurengarenga<br />
machoni wakati najaza fomu<br />
- “Kulikuwa na matatizo<br />
yoyote kati yako na ...<br />
mwanao ana umri gani ......<br />
kulikuwa na matatizo na....<br />
hivi mwanao ameshawahi<br />
ku.... mwanao ana....”<br />
Angalau sasa tuna bima ya<br />
afya. Hivi karibuni nilikubali<br />
kuanza kazi katika chuo<br />
kimoja cha karibu, nikaacha<br />
kufanya kazi za kujitegemea<br />
kwani unapokuwa na mtoto<br />
kama huyu, unahitaji mafao.<br />
Utafanya lolote kupata<br />
mafao, Hakuna mpango<br />
wa bima ambao utakubali<br />
kuweka bima ya maisha kwa<br />
mazingira hama haya.<br />
K w a s i k u k a d h a a ,<br />
mwanangu aling’ang’ania<br />
kuwa nilikuwa nadanganya -<br />
kuwa nilitunga tukio hilo lote<br />
ili niweze kumwondoa. Siku<br />
ya kwanza, nilipokwenda<br />
k u m w o n a , a l i s e m a<br />
“Nakuchukia, Na nitajilipiza<br />
mara nitakapotoka humu.”<br />
Kufikia siku ya tatu,<br />
alikuwa tena mwanangu<br />
mtulivu, anayefurahisha,<br />
akiomba msamaha na kuahidi<br />
kubadilika, Nimesikia ahadi<br />
hizo miaka mingi. Siziamini<br />
tena hata kidogo.<br />
Katika fomu za kumwingiza<br />
m g o n j w a , a n a p o u l i z a ,<br />
‘Nini matazamio yako ya<br />
tiba?” niliandika “Nahitaji<br />
msaada.”<br />
Na ninauhitaji. Tatizo<br />
hili ni kubwa mno kulibeba<br />
mwenyewe. Mara nyingine<br />
hakuna la kufanya dhahiri,<br />
Hivyo unatumainia tu hali iwe<br />
nzuri na kutazamia kuwa kwa<br />
kuangalia ulikotoka, labda<br />
maana yake itaeleweka.<br />
Naelezea jambo hili kwa<br />
sababu mimi ni mama wa<br />
Adam Lanza. Ni mama wa<br />
Dylan Klebold na mama wa<br />
Eric Harris. Ni mama wa<br />
Jason Holmes, Ni mama wa<br />
Jared Loughner. Ni mama<br />
wa Seung Hui Cho. Na<br />
wavulana hawa - na mama<br />
zao - wanahitaji msaada.<br />
Kufuatia msiba mwingine wa<br />
kutisha wa kitaifa, ni rahisi<br />
kuzungumzia bunduki. Lakini<br />
ni wakati wa kuzungumza<br />
kuhusu magonjwa ya akili.<br />
Mother Jones anasema<br />
kuwa tangu mwaka 1982,<br />
mauaji ya watu wengi kwa<br />
kutumia silaha yametokea<br />
m a r a 6 1 k o t e n c h i n i .<br />
(http://www.motherjones.<br />
com/politics/2012/07/massshootings-map)<br />
Kati ya hayo, wauaji<br />
43 walikuwa wanaume<br />
Wazungu, na mmoja tu<br />
alikuwa mwanamke. Mama<br />
Jones aliangalia kama wauaji<br />
walipata bunduki zao kihalali<br />
(wengi zaidi walizipata<br />
kihalali). Lakini dalili hizi<br />
za wazi za ugonjwa wa akili<br />
zituwezeshe tuangalie ni watu<br />
wangapi nchini Marekani<br />
wanaishi kwa woga, kama<br />
mimi.<br />
Nilipomuuliza msaidizi<br />
wa kijamii wa mwanangu<br />
nini naweza kufanya, alisema<br />
ambacho tu naweza kufanya<br />
ni kupeleka mashitaka<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
mahakamani. “Akirudishwa<br />
k a t i k a m z u n g u k o w a<br />
kufungwa, watafuatilia<br />
nakala za alikopitia,” alisema.<br />
“Ndiyo njia pekee ambako<br />
u n a w e z a k u h a k i k i s h a<br />
kunafanyika lolote. Hakuna<br />
atakayekusikiliza labda uwe<br />
na mashtaka.”<br />
Siamini kuwa mwanangu<br />
a n a f a a k u k a a j e l a .<br />
Mkanganyiko wa mazingira<br />
unamfanya aharibikiwe<br />
z a i d i a k i i n g i l i a n a n a<br />
vinavyomsumbua na haugusi<br />
chochote katika tatizo la<br />
awali. Lakini inaelekea<br />
kuwa Marekani inatumia<br />
jela kama jawabu la watu<br />
wote wenye magonjwa<br />
ya akili. Kwa mujibu wa<br />
shirika la Human Rights<br />
Watch, idadi ya wagonjwa<br />
wa akili wanatumikia vifungo<br />
iliongezeka mara nne kuanzia<br />
2000 hadi 2006 na inaendelea<br />
kuongezeka. Cha ziada,<br />
kiwango cha ugonjwa wa<br />
akili kwa waliofungwa ni<br />
mara tano zaidi (asilimia 56)<br />
ukilinganisha na watu walio<br />
huru.<br />
(http://www.hrw.org/<br />
n e w s / 2 0 0 6 / 0 9 / 0 5 / u s -<br />
number-mentally-ill-prisonsquadrupled)<br />
Baada ya vituo cha misaada<br />
na tiba vya serikali kufungwa,<br />
jela ndiyo njia pekee iliyobaki<br />
kwa wenye magonjwa ya<br />
akili - kisiwa cha Rikers,<br />
jela ya Los Angeles County<br />
(wilaya), na ile ya Cook<br />
jimboni Illinois vilikuwa<br />
na vituo vikubwa zaidi vya<br />
kutibu wenye magonjwa ya<br />
akili mwaka 2011.<br />
( h t t p : / / w w w . n p r .<br />
org/2011/09/04/140167676/<br />
nations-jails-struggle-withmentally-ill-prisoners)<br />
H a k u n a a n a y e t a k a<br />
kumpeleka mtoto wa miaka 13<br />
mwenye kipaji anayempenda<br />
Harry Potter na mkusanyiko<br />
wa midoli ya wanyama ya<br />
kulalia, jela. Lakini katika<br />
jamii yetu, ambayo haitaki<br />
kusikia habari za magonjwa<br />
ya akili na mparaganyiko<br />
katika mfumo wake wa<br />
tiba, haitupatii njia nyingine<br />
yoyote. Hivyo mgonjwa<br />
mwingine anayeteseka<br />
moyoni anavamia mgahawa<br />
wa ‘\chips-kuku’ anafyatua<br />
risasi, au ‘supermarket.’ darasa<br />
la chekechea, Na tunakamua<br />
mikono yetu tunasema ‘Hii<br />
lazima ikomeshwe.’<br />
Nakubaliana kuwa lazima<br />
hali hii ikome. Ni mwanzo<br />
wa kuanza mazungumzo ya<br />
kina, yenye maana, kuhusu<br />
magonjwa ya akili. Ndiyo<br />
njia pekee ambayo taifa letu<br />
linaweza kupona kikamilifu.<br />
Mungu nisaidie. Mungu<br />
msaidie Michael. Mungu<br />
tusaidie sote.<br />
Mama mwanaharakati<br />
Mimi napenda sana<br />
kinanda, wanangu wanne,<br />
na michezo ya kubuni ya<br />
elekroniki, ingawa siyo kwa<br />
mpangilio huo.
8<br />
Na Ibrahim Mohammed<br />
Hussein<br />
HABARI za Musa si ngeni<br />
kwa wanaosoma vitabu vya<br />
historia na vya dini. Musa<br />
alikuwa muongozi wa wana wa<br />
Israil. Mheshimiwa Firauni,<br />
aliwakilisha tawala za kidikteta.<br />
Namwita mheshimiwa kwa<br />
makusudi kwa sababu ndiyo<br />
wanavyopenda kujiita watu<br />
hawa (watawala).<br />
Hawajuwi kwamba mtu huwa<br />
mheshimiwa kwa kujiheshimu.<br />
F i r a u n i a n a w a k i l i s h a<br />
tawala mbalimbali za kidikteta<br />
zinazoendesha serikali kwa<br />
mabavu na ukandamizaji,<br />
kama vile kuwaonea wananchi,<br />
kuwabana na kuwadhulumu<br />
wananchi kwa maslahi binafsi<br />
ya mtawala na kikundi kidogo<br />
kinacho muunga mkono.<br />
K i b a y a z a i d i , t a w a l a<br />
zinazoongozwa Kifirauni huwa<br />
hazijali raia na mara nyingi<br />
hutatua matatizo kwa kutumia<br />
rungu la dola ambalo huchukua<br />
nafasi ya majadiliano.<br />
Wingi wa matukio katika kisa<br />
cha Musa, unatufanya tuweze<br />
kutafakari masuala ya msingi,<br />
ambayo Wazanzibari tunaweza<br />
kujifunza na kuyaangalia kama<br />
kioo cha kujitazamia, ili penye<br />
kuharibika tujue na kutafuta<br />
namna ya kurekebisha.<br />
Matukio ya kisa hicho yatufae<br />
kwa lengo la kuendeleza umoja<br />
na ustawi wa jamii yetu. Kuja<br />
kwa Musa kulisaidia kuchochea<br />
na kuamsha ari ya mapambano<br />
dhidi ya maovu. Mifumo ya<br />
kidikteta bado ingalipo na<br />
watawala kama Firauni bado<br />
wapo, wakila kuku chini ya<br />
ulinzi mkali unaogharimiwa na<br />
walipa kodi.<br />
Na wananchi walala hoi bado<br />
wapo kwa wingi katika maeneo<br />
mbalimbali ya nchi, wakiendelea<br />
kutaabika na kusulubika katika<br />
hali ya uonevu, dhiki na kukata<br />
tamaa. Maskini hawa, hakuna wa<br />
kuwahurumia.<br />
Tujiulize, Musa aliwezaje<br />
kuwa hodari mpaka kushinda vita<br />
dhidi ya unyanyasaji, dhulma,<br />
ufisadi na maonevu?<br />
Huku tukio kubwa kabisa<br />
likiwa ni kumshinda mungu<br />
– mtu Firauni, mtawala aliyejaa<br />
kiburi, aliyetisha na kuogopwa<br />
na kujizolea umaarufu kwa watu<br />
wake kama jemedari wa vita<br />
asiye shindwa.<br />
Bila shaka siri ya Mussa<br />
kushinda dhulima, unyanyasaji<br />
na utesaji wa Firauni ilikua ni<br />
kumuogopa Mola wake peke<br />
yake. Mola wake naye akavifanya<br />
vitu vyote vilivyokuwa juu ya<br />
uso wa ardhi vimuogope Musa<br />
na wale wote wasio muogopa<br />
Mola. Walifanywa waviogope<br />
Makala/Tangazo<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Zanzibar bado inamuhitaji Musa atayetuonesha mchawi<br />
vitu vyote juu ya ardhi.<br />
Mussa mwana demokrasia,<br />
anaufundisha ulimwengu<br />
uelewe kwamba, utawala ni<br />
dhamana inayohitaji uadilifu,<br />
na sehemu kubwa katika uadilifu<br />
ni ushirikishwaji wa kila mmoja<br />
kwa nafasi ya ufahamu, utaalamu<br />
alionao.<br />
Ili kuyafikia malengo<br />
yake kwa ufanisi anaamua<br />
kupendekeza ndugu yake Haruni,<br />
amsaidie katika ukalimani na<br />
kazi nyingine za ushauri.<br />
Kisa cha Musa kinafundisha<br />
kwamba, kupitia utaratibu wa<br />
sheria pekee ndio unaweza<br />
kuwasimamisha watu katika<br />
uadilifu, hisia za kupendana na<br />
kusaidiana, kutumainiana na<br />
kushikamana. Aliwafundisha<br />
wana wa Israil kufanya kazi<br />
kwa bidii kama njia moja wapo<br />
ya kujenga taifa imara.<br />
Funzo jengine tunalolipata<br />
katika kisa cha Musa ni kwamba<br />
katika mapambano dhidi ya<br />
udikteta, silaha kubwa ni<br />
ujasiri, mbinu, ukakamavu na<br />
uwerevu. Hekima aliyopewa<br />
Musa na Mola wake, ilishinda<br />
vita vya nyoka wa Firauni<br />
walioongozwa na baraza la<br />
wachawi, akaipiga Bahari ya<br />
Sham kwenda ng’ambo ya pili.<br />
Mussa aliongoza mapambano<br />
katika haki na kuyazamisha<br />
maovu na waovu baharini.<br />
Jambo hili tumelikosa hapa<br />
kwetu licha kuwepo mamia, kama<br />
sio maelfu ya wasomi tulionao.<br />
Wasomi wetu wamefanya nini<br />
kuonesha kwamba wapo na<br />
wanajali masilahi ya watu wa<br />
nchi hii?<br />
V i o n g o z i w e n g i<br />
wameshindwa kuifaa jamii,<br />
wamebaki silolote wala chochote<br />
zaidi ya kufurahikia maslahi<br />
baada ya kuwakamua wanyonge<br />
na kuhodhi rasilmali za nchi.<br />
Wamebaki kimya bila ya<br />
kukemea ubeberu unaendeshwa<br />
na baadhi ya viongozi wasio<br />
pendelea umoja na utulivu wa<br />
nchi hii. Viongozi wameweka<br />
pamba maskioni, hawataki<br />
kusikia kilio na matakwa yenye<br />
nguvu za hoja kutoka kwa wenye<br />
nchi.<br />
W a n a n c h i w a n a d a i<br />
kuonyeshwa mkataba wa<br />
Muungano ili wapate kuandika<br />
katiba mpya. Serikali haikuona<br />
umuhimu wowote juu ya mkataba<br />
huo. Wao wamesimamia Sera<br />
ya CCM Serikali mbili. Kwa<br />
mkataba gani huo?<br />
Vipi utaiandika katiba wakati<br />
hujawahi kuona mkataba<br />
wenyewe? Kipi kilichokupa<br />
imani kwamba mkataba umeeleza<br />
nini na kwa makubaliano gani au<br />
kwa muda gani?<br />
Ni sahihi kabisa kukataa<br />
Muungano wa katiba wakati<br />
m k a t a b a w a m u u n g a n o<br />
hapana aliyeuona. Hapa ndipo<br />
niliposema Zanzibar inahitaji<br />
Musa atakayetuonyesha mchawi,<br />
akiitoa nchi bila ya mkataba, na<br />
kama ilitolewa kwa mkataba,<br />
uko wapo?<br />
Kwa nini walazimishwe<br />
wananchi waandike katiba<br />
huku wakikataliwa madai yao<br />
ya kutaka kuonyeshwa mkataba?<br />
Bila ya kuoneshwa mkataba ni<br />
vigumu kuota tunakoelekea.<br />
Nchi inaendeshwa kwa matakwa<br />
ya watawala tulio nao.<br />
Viongozi wanaongozwa na<br />
utashi wa matamanio ya nafsi<br />
au ubinafsi katika kutumikia<br />
umma. Wanaosinzia Bungeni<br />
na kwenye vikao muhimu vya<br />
maamuzi katu hawatoweza<br />
kuikomboa Zanzibar kiuchumi.<br />
Zanzibar inamuhitaji Musa<br />
atakayeonyesha wachawi na<br />
kuwashinda, Musa atakayekuwa<br />
tayari kusikiliza na kupokea<br />
maoni na ushauri, atakayesikia<br />
na kufanyia kazi malalamiko ya<br />
wananchi wake.<br />
Mheshimiwa Jaji Joseph<br />
Warioba, aliwahi kukizindua<br />
kitabu cha ‘TUTAFIKA’ Mei<br />
2003. Kitabu hicho kilitoa<br />
nadharia ya kumezwa kwa<br />
Zanzibar na kuwa jimbo la<br />
Mashariki (Eastern Province),<br />
k a t i k a m f u m o m p y a w a<br />
Kiserikali wa Tanzania .<br />
Hayo ni mawazo na mtizamo<br />
wa yaliyomo katika kitabu hicho,<br />
ambacho ndio kimetoa nadharia<br />
hiyo katika kile kinachoelezwa<br />
kama, kuitazama Tanzania katika<br />
kipindi cha miaka 20 ijayo<br />
. Kitabu hichi kilichapishwa<br />
na Tanzania Printers Limited<br />
(2003).<br />
Kitabu hicho kina azma ya<br />
kuitayarisha Tanzania juu ya<br />
matokeo ya baadae, ili iweze<br />
kuwa ni kinga ya matukio<br />
ya ghafla katika maeneo ya<br />
kiuchumi, kijamii na kisiasa.<br />
Kitabu hicho kimegawanywa<br />
katika maeneo makuu matatu,<br />
nayo ni ya ‘Yale Yale’ ‘Mibaka<br />
Uchumi’ na ‘Amka Kumekucha’<br />
.<br />
Katika twasira ndogo ya<br />
‘Yale Yale’ inaelezewa<br />
namna ambavyo Watanzania<br />
walivyokata tamaa na kutoamini<br />
kuwa, nchi inaweza kubadilika<br />
na kushindwa kuwashirikisha<br />
vijana juu ya kuchukua nafasi<br />
yao kujitengenezea khatima yao<br />
na ya nchi.<br />
Katika ‘Mibaka Uchumi’<br />
kinachoelezewa ni juu ya uchumi<br />
utayokuwa umeshikiliwa na<br />
mapapa makubwa ya ndani na<br />
nje huku rushwa ikiwa imetawala<br />
kabisa, wafadhili kuwa na sauti<br />
kupita kiasi hata kuamua kutoa<br />
maamuzi ya kila aina ndani ya<br />
nchi.<br />
Kwenye ‘Amka Kumekucha’<br />
ni taswira ambayo inaonyesha<br />
namna ambavyo Tanzania<br />
ya kesho itakavyokuwa, na<br />
hapo ndipo inapoonekana<br />
kuwa kutakuwa na matatizo<br />
ya kisiasa yatakayoanzia na<br />
suala la rushwa, mgawanyo<br />
wa madaraka na kuwepo tishio<br />
la kupasuka kwa Chama Cha<br />
Mapinduzi ( CCM) .<br />
Twasira hiyo inasema, hapo<br />
ndipo ambapo kutakuwa<br />
na shinikizo kubwa ambazo<br />
zitasababisha kwa mara ya<br />
kwanza, Tanzania kuitisha<br />
kura ya maoni (Referendum)<br />
na majadiliano makali ya<br />
kitaifa yatafwata. Kinaeleza<br />
kuwa kubwa litakalokua<br />
katika mada ni kuundwa<br />
kwa Serikali ya Shirikisho la<br />
Jamuhuri ya Tanzania.<br />
Waandaji wa twasira<br />
hiyo wanasema, hapo<br />
ndipo muundo wa shirikisho<br />
utakapokuwa tayari na<br />
Tanzania itakuwa na majimbo<br />
matano yakiwa ni Kusini,<br />
Kati, Kaskazini, Magharibi<br />
na jimbo la Mashariki, ambalo<br />
litakuwa na mikoa ya sasa ya<br />
Tanga Lindi, Dar es Salaam<br />
na Zanzibar yenyewe.<br />
Kitabu hicho cha ‘Tutafika’<br />
a m b a c h o k i l i t o l e w a<br />
bure, ni dhihirisho kuwa<br />
tayari mikakati imeanza<br />
kuandaliwa, ili kujenga njia<br />
ya makusudi kuelekea katika<br />
lengo la kuwa na mabadiliko<br />
makubwa. Mabadiliko<br />
yatakayojumuisha pamoja<br />
na mambo mengine, suala<br />
la Zanzibar inachukuliwa<br />
yote ndani ya Tanganyika<br />
ya sasa.<br />
Wenzetu wamo katika<br />
kulikamilisha lengo la<br />
kuichukua Zanzibar milele<br />
na milele.<br />
Zanzibar inahitaji Musa<br />
aliye Mzanzibar aliyerithi<br />
damu ya uzalendo toka<br />
tumboni kwa mama yake.<br />
Vyenginevyo, tusije kuusaidia<br />
mpango wao kupitia sera ya<br />
CCM mwishowe ikawa ni<br />
vilio.<br />
0715 - 498363<br />
ANSWAAR ISLAMIC MODEL SCHOOL<br />
Uongozi wa Shule ya Answaar Islamic Model School inawatangazia<br />
waislamu wote nafasi za masomo kwa mwaka 2013, kama<br />
ifuatavyo.<br />
1. Shule ya awali ( Nursery School)<br />
Kg - 1 and Kg 11 Umri kuanzia miaka mitatu na nusu<br />
na kuendelea.<br />
2. Shule ya msingi ( Primary School)<br />
Darasa la kwanza hadi la Sita, kwa wale wanaotaka<br />
kuhamia nafasi pia zipo.<br />
ADA:<br />
shule ya awali ( Nursery school) 550,000/= kwa mwaka.<br />
Shule ya msingi (Primary school).<br />
i) Darasa la kwanza hadi la tano ni Tsh. 650,000/=<br />
ii) Darasa la sita na la saba Tsh. 750,000/= ada inalipwa<br />
kwa awamu tatu.<br />
- Shule ipo kinondoni Studio/ karibu na vijana Social Hall<br />
au nyuma ya vijana.<br />
- fomu zinapatikana shuleni Kinondoni studio Masjid<br />
Answaar.<br />
- Tarehe ya USAILI ni Tarehe 6/01/2013, usaili utafanyika<br />
shuleni Answaar Islamic Model School, Siku ya Kufungua<br />
shule ni Tarehe 14/01/2013.<br />
Kwa mawasiliano zaidi piga simu. 0767- 121555,0777-790283, 0712<br />
790283. Au Email answaarislami@yahoo.com au tembelea Tovuti<br />
yetu: www.answaarislamic.co.tz<br />
Mlete mwanao apate elimu na malezi bora ya Kiislamu
9<br />
Na Said Rajab.<br />
DESEMBA 25 mwaka 2012,<br />
Maaskofu wa makanisa<br />
takriban yote hapa nchini,<br />
walitoa maneno mazito ya<br />
vitisho, kejeli na vijembe<br />
kupitia ibada zao za Krismasi<br />
dhidi ya Serikali ya Tanzania<br />
na Waislamu. Maneno hayo<br />
kimsingi yametokana na<br />
maazimio ya kikao cha nne cha<br />
Jukwaa la Wakristo Tanzania<br />
TCF, kilichoketi Desemba 6<br />
mwaka 2012, Kurasini jijini<br />
Dar es salaam.<br />
Ukisoma tamko la Maaskofu<br />
kwa makini, kimsingi hakuna<br />
hoja yoyote ya maana inayoweza<br />
kudumisha amani ya Watanzania.<br />
Kwa sababu amani haijengwi<br />
kwa kufumbia macho dhulma.<br />
Waislamu kwa muda mrefu<br />
wamekuwa wakilalamikia<br />
dhulma wanazofanyiwa na<br />
mfumo usio rasmi serikalini,<br />
ambao unawapendelea Wakristo.<br />
Waislamu wamekuwa wakitoa<br />
ushahidi wa kihistoria, kisayansi,<br />
kimazingira na hata kitakwimu<br />
kuhusu dhulma hizo.<br />
Lakini kichekesho cha<br />
mwaka, zaidi ya Maaskofu 35<br />
wanakutana jijini Dar es salaam,<br />
wanajadiliana kisha wanaona<br />
watoke na vitisho, kejeli na<br />
vijembe dhidi ya Waislamu na<br />
Serikali, badala ya kuleta hoja<br />
za msingi zitakazolinusuru taifa<br />
na hatari za upendeleo wa kidini,<br />
unaofanywa na mawakala wa<br />
kanisa serikalini!<br />
Ta m k o l a M a a s k o f u<br />
limeonyesha hofu kwamba<br />
Waislamu wameshagundua<br />
dhulma wanazofanyiwa. Na<br />
anayewadhulumu pia wanamjua.<br />
Sasa Maaskofu wanajaribu<br />
kuficha uhalifu wao kwa<br />
kutumia vitisho, propaganda,<br />
porojo na vijembe. Hiyo ni<br />
namna ya kujihamu tu (Defence<br />
Mechanism).<br />
Siyo lengo langu hasa kujibu<br />
tamko la Maaskofu kupitia<br />
makala hii. Kwa sababu<br />
tamko lenyewe, kwa kiasi<br />
kikubwa, halikuzingatia ukweli<br />
wala uhalisia wa mambo, na<br />
limesimamia zaidi kwenye<br />
propaganda na porojo. Ni sawa<br />
na maneno ya kwenye khanga!<br />
Wanataka kuchora picha<br />
potofu kwenye jamii kwamba<br />
Wakristo nchini Tanzania<br />
wanaonewa sana na Waislamu!<br />
Makanisa yao yanachomwa,<br />
wakati serikali ikiaangalia tu!<br />
Wanajaribu kupandikiza fikra<br />
potofu kwenye jamii kwamba<br />
Wakristo ndiyo watu wa amani<br />
na Waislamu ni watu wa vurugu!<br />
Wanadhani wanaweza kugeuza<br />
ukweli kuwa uongo na uongo<br />
kuwa ukweli!<br />
Ni ukweli usiopingika<br />
kwamba Waislamu wa Tanzania<br />
wamedhulumiwa na Mfumo<br />
Kristo ulioasisiwa na baba<br />
wa taifa. Ukweli huu kamwe<br />
hautakuwa uongo kwa sababu<br />
Makala<br />
Hongera Waislamu, Maaskofu wanagwaya!<br />
ya propaganda na porojo<br />
za Maaskofu. Na tatizo hili<br />
lisiposhughulikiwa kwa dhati,<br />
lazima litaleta maafa huko<br />
mbele. Waislamu wanapigania<br />
haki yao iliyodhulumiwa<br />
na katika hili, wanaonekana<br />
hawamuogopi yeyote. Hilo<br />
Maaskofu walifahamu vizuri<br />
sana.<br />
Nawapongeza sana Waislamu<br />
wa Tanzania kwa juhudi zao<br />
za muda mrefu za kubainisha<br />
d h u l m a w a n a z o f a n y i w a<br />
na Mfumo Kristo, ambazo<br />
pamoja na kupuuzwa, lakini<br />
sasa zimeanza kuzaa matunda.<br />
Harakati za Waislamu za miaka<br />
mingi za kupigania haki yao<br />
iliyoporwa na mawakala wa<br />
kanisa serikalini, haziwezi<br />
kuishia hewani. Maaskofu<br />
wameliona hilo na bila shaka<br />
hofu yao ni kwa sababu Waislamu<br />
wameshagundua ubaya wao.<br />
Kitendo cha Maaskofu<br />
kushindwa kujibu hoja za<br />
Waislamu kuhusu dhulma za<br />
Mfumo Kristo, na badala yake<br />
kuleta porojo za kuhamisha<br />
ajenda, ni ushindi mkubwa kwa<br />
hoja za Waislamu. Tafsiri yake<br />
ni kwamba Maaskofu hawana<br />
la kusema kuhusu ukweli wa<br />
madai ya Waislamu. Mwanzoni<br />
ASKOFU Laizer<br />
waliamua kuwapuuza Waislamu,<br />
wakidhani madai yao yangejifia<br />
yenyewe kifo cha kawaida.<br />
Lakini waliposhuhudia<br />
wanavyoendelea kusimama<br />
kidete kupaza sauti zao, sasa<br />
wameanza kutoa maazimio<br />
ya woga kuficha uhalifu<br />
uliofanyika. Wanataka kuzima<br />
sauti za wanaokandamizwa na<br />
hilo kamwe halitawezekana.<br />
Wanafanana na Maquraysh<br />
wa Makka, ambao walidhani<br />
wangeweza kuzuia ujumbe wa<br />
Qur’an kwa kuwakataza watu<br />
wasiisikilize:<br />
‘Na walisema waliokufuru:<br />
“ M s i s i k i l i z e Q u r ’ a n h i i<br />
inaposomwa na ipigieni makelele<br />
isomwapo, huenda mkashinda”<br />
Qur 41:26.<br />
Lakini jambo la kuzingatia,<br />
kama vile Maqurayshi wa<br />
Makkah, ambao hawakuwa na<br />
uwezo wa kupambana na Qur’an<br />
kwa hoja za kiakili, Maaskofu<br />
wa Tanzania nao hawana<br />
uwezo wa kupambanisha hoja<br />
na Waislamu. Vurugu zao zote<br />
dhidi ya Waislamu siyo za<br />
kifikra, zaidi ni propaganda na<br />
porojo za kuficha ukweli!<br />
Lugha zao zimejaa chuki<br />
na fitna dhidi ya Waislamu.<br />
Kila mnapotaka kujadiliana<br />
kwa haki, kitaalamu, kisomi<br />
na kiuadilifu, hawako tayari<br />
na zaidi wataendelea kutoa<br />
m a e l e k e z o n a m a s h t a k a<br />
serikalini. (Uchonganishi).<br />
M f a n o h a l i s i w a h i l o<br />
ulishawahi kutokea hapa nchini,<br />
wakati Rais Ali Hassan Mwinyi<br />
alipowakutanisha Masheikh na<br />
Maaskofu Ikulu jijini Dar es<br />
salaam, kuzungumzia tatizo la<br />
mihadhara ya kashfa. Maaskofu<br />
walikuwa wakilalamika,<br />
wakiibana Serikali ipige<br />
m a r u f u k u m i h a d h a r a y a<br />
Waislamu waliyodai kuwa<br />
inakashifu Ukristo. Waislamu<br />
kwa upande wao, walipinga<br />
dai la Maaskofu, wakileta hoja<br />
kwamba hawakashifu Ukristo,<br />
bali wanaelimisha watu kwa<br />
kutumia maandiko matakatifu.<br />
Busara za Mzee Mwinyi<br />
z i k a m u e l e k e z a k u w a i t a<br />
Wahadhiri wa Kiislamu,<br />
w a n a o d a i w a k u u k a s h i f u<br />
Ukristo upande mmoja, na<br />
Maaskofu wanaolalamika<br />
upande mwingine, ili kujadiliana<br />
kidugu, kiuadilifu na kitaalamu,<br />
lengo likiwa kubaini ukweli ili<br />
kuondoa mgogoro uliojitokeza.<br />
Maaskofu hawakuwa tayari<br />
kudhihirisha! Hawakuwa na<br />
hoja zinazothibiti na kwa bahati<br />
pale propaganda haikuwa na<br />
nafasi. Matokeo yake malengo<br />
ya mkutano ule hayakufikiwa.<br />
Hawakurudi tena Ikulu kusaka<br />
muafaka hadi Mzee Mwinyi<br />
alipostaafu!<br />
Tizama, lakini angalia,<br />
alipoingia Rais Mwingine Ikulu,<br />
waliendesha kampeni zile zile<br />
za propaganda ya ‘mihadhara<br />
ya kashfa’ kupitia vyombo<br />
vya habari, na matokeo yake<br />
Serikali ikaenda kuua Waislamu<br />
wasio na hatia pale Msikiti wa<br />
Mwembechai mwaka 1998.<br />
Wa i s l a m u w a l i u a w a<br />
Mwembechai kwa sababu tu ya<br />
chuki, fitina, propaganda, porojo<br />
na ulaghai wa Maaskofu.<br />
Waislamu walipoitaka<br />
Serikali kuunda Tume ya<br />
uchunguzi wa mauaji ya<br />
Mwembechai, ili kubaini ukweli<br />
wake, Rais Benjamin Mkapa<br />
alisema “hajaona haja na hoja”<br />
ya kuunda Tume hiyo. Hivyo<br />
ndivyo walivyo.<br />
Lakini Prof. Hamza Njozi,<br />
alipoandika kitabu kubainisha<br />
u k w e l i w a M a u a j i y a<br />
Mwembechai, ili Ulimwengu<br />
ufahamu kilichotokea, Serikali<br />
ya yule yule, ambaye “hakuona<br />
haja na hoja” ya kuunda Tume<br />
ya uchunguzi akapiga kukipiga<br />
marufuku kusambazwa kitabu<br />
hicho nchini! Hawasemi ukweli,<br />
lakini pia hawataki hata watu<br />
wengine waseme ukweli huo!<br />
Hivyo ndivyo walivyo!<br />
Siyo sifa ya Maaskofu<br />
kulinda na kudumisha amani.<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Sifa kubwa ya Maaskofu<br />
imekuwa ni kudumaza akili za<br />
watu ili waweze kutawaliwa au<br />
kudhulumiwa. Sote tunafahamu<br />
jinsi Kanisa lilivyotumika<br />
kuingiza ukoloni barani Afrika.<br />
Wamissionari wa Kikristo<br />
(Mapadri na Maaskofu) ndiyo<br />
waliopalilia Ukoloni Afrika.<br />
Alipata kusema Askofu<br />
Desmond Tutu wa Afrika Kusini,<br />
jinsi wakoloni walivyotumia<br />
kanisa kuingia nchini mwake:<br />
“Walipokuja sisi tulikuwa na<br />
ardhi na wao walikuwa na<br />
Biblia, tulipogutuka tukajikuta<br />
tumebaki na Biblia na wao<br />
wamebaki na ardhi”.<br />
Maaskofu hawatasema<br />
ukweli kwamba Makanisa<br />
nchini Tanganyika yaliikataa<br />
TANU; mara mbili mwaka<br />
1958 mjini Sumbawanga na<br />
mwaka 1965 mjini Mbulu.<br />
Makanisa yalikuwa yakifanya<br />
kazi kwa karibu sana na<br />
Serikali ya kikoloni, ambayo<br />
ndiyo iliyomlea Mwalimu<br />
Nyerere, ili aje kuwa Rais wa<br />
kwanza wa Tanganyika baada<br />
ya Waingereza kuondoka.<br />
Baada ya uhuru kupatikana,<br />
nchi ikiwa chini ya uongozi<br />
wa Mwalimu Nyerere,<br />
Wakristo wa Tanzania<br />
wanavuna kile ambacho<br />
hawakupanda. Wanafurahia<br />
matunda ya uhuru kila sekta<br />
kutokana na Mfumo Kristo<br />
ulioasisiwa na Mwalimu<br />
Nyerere, akiungwa mkono<br />
na mataifa ya Magharibi. Leo<br />
wanataka kuaminisha watu<br />
kuwa wao ndio wazalendo<br />
zaidi kuliko Waislamu!<br />
Maaskofu wanaeneza<br />
propaganda za sumu kwamba<br />
Waislamu wanahatarisha<br />
a m a n i n a u m o j a w a<br />
Watanzania, licha ya ukweli<br />
kwamba amani na umoja<br />
huo imekuwa ikitunzwa na<br />
Waislamu, tangu kipindi cha<br />
harakati za kupigania uhuru na<br />
baada ya uhuru kupatikana.<br />
Inajulikana vizuri kwamba,<br />
u k i w a o n d o a m a r e h e m u<br />
Hassan bin Amir na Sheikh<br />
Zubeir Mtemvu, Waislamu wa<br />
Tanganyika walikataa kukiunga<br />
mkono chama chao wenyewe cha<br />
‘All-Muslim National Union of<br />
Tanganyika’ (AMNUT), ili<br />
kulinda umoja wa kitaifa chini<br />
ya TANU, ambacho Rais wake<br />
alikuwa Nyerere, Mkatoliki.<br />
Lakini hali inavyoonekana,<br />
Maaskofu wamejiandaa kuleta<br />
machafuko makubwa ya<br />
kidini hapa nchini, ili wapate<br />
kizingizio cha kuwachinja<br />
Waislamu wanaopigania haki<br />
zao, kwa kutumia mawakala<br />
wao serikalini.<br />
Lakini Waislamu hawana<br />
sababu hata moja ya kupigana<br />
vita isiyo na macho, ambayo<br />
nadhani Maaskofu wanaitafuta<br />
kwa udi na uvumba hapa<br />
Tanzania.<br />
Ila katika mapambano ya<br />
kupigania haki, Waislamu<br />
hawarudi nyuma na wako<br />
tayari.
10<br />
RAIS Mstaafu wa awamu<br />
ya pili, Alh-haji Ali Hassan<br />
M w i n y i , a m e w a t a k a<br />
Waislamu kushughulika<br />
zaidi na utafutaji wa elimu<br />
kwani kufanya hivyo ndio<br />
siri kubwa ya kupata<br />
maendeleo ya jamii nzima<br />
na taifa kwa ujumla.<br />
Alhaji Mwinyi, ambaye<br />
alikuwa mgeni rasmi katika<br />
kongamano hilo, aliyasema<br />
hayo alipokuwa akitoa<br />
nasaha zake kwa Waislamu<br />
waliohudhuria kongamano la<br />
Kuzaliwa Mtume Muhammad<br />
(S.a.w) lililofanyika Lushoto<br />
Jijini Tanga.<br />
Amesema kuwa, jambo<br />
lolote haliwezi kufanikiwa<br />
bila kuwa na elimu nalo,<br />
hivyo aliwataka Waislamu<br />
kujikita katika kutafuta elimu<br />
na kutoa elimu ili kuweza<br />
kuleta maendeleo ya Taifa<br />
kwa ujumla.<br />
Aliongeza kuwa Uislamu<br />
haukutenganisha elimu,<br />
hivyo ni vyema Waislamu<br />
wakatoa kipaumbele kwa<br />
masomo yote, ili kuweza<br />
kuandaa Waislamu walio<br />
na maadili mema na wenye<br />
uelewa wa dini yao.<br />
A i d h a a m e w a t a k a<br />
Waislamu kutambua kua<br />
elimu ndio siri ya maendeleo<br />
kwa taifa na dunia nzima,<br />
na ndio maana elimu katika<br />
Uislamu imefanywa kuwa<br />
jambo la lazima, kama<br />
ambavyo Mtume Muhammad<br />
Habari/Tamgazp<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Lushoto wafanya kongamano kubwa la Waislamu<br />
Na Mwandishi Wetu<br />
MAKAMU wa Kwanza wa<br />
Rais wa Zanzibar Maalim<br />
Seif Sharif Hamad, amesema<br />
wananchi wanahitaji<br />
kuelimishwa zaidi juu ya<br />
uhifadhi wa mazingira<br />
ili kuweza kuyalinda na<br />
kuepuka kuyachafua.<br />
Amesema uchafuzi wa<br />
mazingira mara nyingi<br />
umekuwa ukisababishwa na<br />
wananchi wenyewe, jambo<br />
ambalo linapaswa kupigwa<br />
vita kwa wananchi hao<br />
kupatiwa elimu ya sahihi<br />
mazingira ili kuepusha<br />
uharibifu huo.<br />
Maalim Seif alisema hayo<br />
wakati akizungumza na<br />
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,<br />
Bi. Chiku Galawa, mara<br />
baada ya kuwasili katika<br />
uwanja wa ndege wa Tanga<br />
(s.a.w) aliposhushiwa aya<br />
ya kwanza ya kusoma na<br />
wala hakuainishiwa kitu gani<br />
asome.<br />
Naye mwanachuoni<br />
mkubwa kutoka nchini<br />
Kenya, Sheikh Sharifu<br />
Ahmad Al- Badawi, ambaye<br />
alikuwa miongoni mwa<br />
w a n a c h u o n i w a k u b w a<br />
waliohudhuria kongamano<br />
hilo, alipokuwa akiwasilisha<br />
mada yake aliwataka Waislam<br />
kuwafundisha watoto kuijua<br />
vema Qur’an na kuihifadhi<br />
kwa ufasaha, ili kuwa na<br />
kizazi bora chenye kumhofu<br />
Mola pamoja na kumjua<br />
m w e n y e z i M u n g u n a<br />
kuitumikia dunia yao kwa<br />
kufuata sheria, kanuni na<br />
taratibu.<br />
Amewataka wazazi na<br />
walezi kuhakikisha kuwa<br />
watoto wao wanasoma<br />
sawasawa na walimu wao<br />
nao wana utaalamu na<br />
uelewa mkubwa wa masomo<br />
wanayofundisha ili watoto<br />
wapate elimu sahihi.<br />
K w a u p a n d e w a k e ,<br />
Mkurugenzi wa Kituo<br />
cha Kiislamu cha Markaz<br />
Chang’ombe, Jijini Dar<br />
es Salaam Dk. Ossama<br />
M a h a m o u d I s m a i l i ,<br />
amewakumbusha Waislam<br />
kufuata yale yote aliyoyafanya<br />
Mtume (s.a.w).<br />
Aidha wanapoazimisha<br />
mazazi ya Mtume (S.A.W)<br />
iwe ni moja ya njia za<br />
kuhuisha upendo uadilifu<br />
na msamaha wa Kiislam, na<br />
RAIS Mstaafu wa awamu ya pili, Alh-haji Ali Hassan Mwinyi (wanne kutoka kulia) akiwa<br />
katika kongamano la Waislamu Lushoto, mkoani Tanga. Watatu kulia ni Spika wa Baraza<br />
la Wawakilishi Zanzibar, Pandu Amir Kificho, kushoto kwake ni Sheikh Alhad Musa.Wa<br />
kwanza kulia ni Sheikh Ismail Osama, Mkurugenzi wa chuo cha Markaz Chang'ombe<br />
kwa kufanya hivyo itakuwa ni<br />
sawa na kuiga tabia za Mtume<br />
(S.A.W) juu ya uadilifu<br />
wake, upole na msamaha<br />
aliokuwa akiwasamehe wale<br />
waliokuwa wakimkosea.<br />
Sheikh Osama, alisema<br />
kuwa kumbukumbu ya Mazazi<br />
ya Mtume yanayofanyika kila<br />
mwaka, yawe na athari kwa<br />
Waislamu ili kuthibitisha<br />
matunda ya kujifunza na<br />
k u m f u a t a M t u m e k w a<br />
vitendo.<br />
Alisema mafundisho<br />
yanayopatikana katika<br />
historia ya Mtume, hayawezi<br />
k u p a t i k a n a k a m a m t u<br />
atakuwa hajausoma Uislamu<br />
na Qur an, historia ( Sira ya<br />
Mtume) na hadithi za Mtume<br />
Muhammad (s.a.w).<br />
Naye Spika wa Baraza<br />
la Wawakilishi Zanzibar,<br />
a m e k u m b u s h a j u u y a<br />
Waislamu kuyafanyia kazi<br />
yote yaliyoongelewa katika<br />
Kongamano hilo. Aidha alitoa<br />
pongezi zake za dhati kwa<br />
Sharifu Hussein Al-Badawi,<br />
kwa juhudi zake kubwa za<br />
kuendeleza dini ya Mwenyezi<br />
Mungu na kuitetea.<br />
K o n g a m a n o h i l o<br />
lilifanyika Desemba 2<br />
mwaka huu Wilayani Lushoto<br />
Tanga na kuhudhuriwa na<br />
viongozi mbalimbali wa dini<br />
na kisiasa, pamoja na mamia<br />
ya Waislamu kutoka Lushoto<br />
na vijiji vya jirani.<br />
Maalim Seif asisitiza elimu ya kuhifadhi mazingira<br />
Na Mwandishi Wetu,<br />
Tanga<br />
kwa ziara ya siku mbili.<br />
Amesema iwapo wananchi<br />
wataelimishwa ipasavyo<br />
kuhusu umuhimu na faida<br />
za kuhifadhi mazingira,<br />
wataweza kujiepusha na<br />
uharibifu, hasa ukataji wa miti<br />
kiholela bila ya kuzingatia<br />
athari za kimazingira.<br />
Naye Mkuu wa Mkoa<br />
w a Ta n g a , B i . C h i k u<br />
Galawa, alisema uharibifu<br />
wa mazingira ni moja kati<br />
ya changamoto kubwa<br />
zinazoukabili mkoa huo,<br />
jambo ambalo linarejesha<br />
n y u m a m a e n d e l e o y a<br />
kiuchumi katika mkoa.<br />
Alisema serikali ya mkoa<br />
inatafuta njia mbadala ya<br />
kutumia nishati nyingine<br />
ili kupunguza matumizi<br />
ya kuni na mkaa, ambayo<br />
yanachangia zaidi ukataji wa<br />
miti kiholela.<br />
“Iwapo serikali itazuia<br />
matumizi ya mkaa na kuni,<br />
serikali na wananchi watapata<br />
nafasi ya kufikiria nishati<br />
mbadala ya kutumia kwa ajili<br />
ya kupikia. Lakini tukiendelea<br />
kutumia kuni, mawazo yetu<br />
yatabakia hapo hapo tu na<br />
tutaendelea kutumia kuni kila<br />
siku”, alisema Bi. Galawa.<br />
Mkuu huyo wa mkoa<br />
abainisha kuwa, ukataji<br />
miti kiholela mkoani humo,<br />
umekuwa ukichangia kuwepo<br />
kwa athari za mabadiliko ya<br />
tabianchi, yanayosababisha<br />
upungufu wa mvua pamoja<br />
na kuongezeka kwa hali ya<br />
joto.<br />
Hata hivyo Bi. Galawa<br />
alisema mkoa huo umepiga<br />
hatua kimaendeleo, ikiwa ni<br />
pamoja na kuimarika kwa<br />
miundombinu ya barabara.<br />
Akiwa Mkoani Tanga,<br />
Maalim Seif ambaye pia ni<br />
Katibu Mkuu wa Chama Cha<br />
Wananchi CUF anatarajiwa<br />
kuhutubia mikutano mitatu<br />
ya hadhara katika viwanja<br />
vya Tangamano, Kwadiboma<br />
Sokoni na Handeni.<br />
Masjid Muzdalifa Mbezi kwa Yusufu inawashukuru waislamu<br />
wote waliofanikisha ujenzi wa msikiti kufikia mahala hapa<br />
ulipofikia. Lakini pamoja na shukrani hizo bado tunaomba msada<br />
kwa waislamu wenye moyo wa kujitolea waendelee kutusaidia ili<br />
tukamilishe ulipobakia kwa uwezo wa Allah Inshaalah.<br />
Kwa yeyote mwenye kutaka kuchangia chochote ulicho nacho<br />
wasiliana nasi kwa namba hizi 0717 649313/ 0713 673216/ 0715<br />
874127 au 0657 531367 au unaweza kufika katika msikitini.
11<br />
Na Sheikh Abubakar<br />
Selemani<br />
S H U K U R A N I z o t e<br />
anastahiki Mwenyezi<br />
Mungu, na inatosha na<br />
rehema na amani ziwafikie<br />
waja wa Mwenyezi Mungu<br />
ambao amewachagua.<br />
Baada ya utangulizi huo,<br />
miongoni mwa vyanzo<br />
ambavyo vimechungwa sana<br />
na Uislamu ni upande wa<br />
hukumu za kisheria, Juu ya<br />
wepesi na kuondoa ugumu<br />
na kutatua mambo katika<br />
dini, na miongoni mwa<br />
mambo magumu ambayo<br />
yamefahamika katika baadhi<br />
ya dini zilizopita.<br />
M w e n y e z i M u n g u<br />
amewafundisha waumini<br />
kumuomba yeye. “Ewe<br />
Mola wetu, usitubebeshe<br />
t u s i y o y a w e z a k a m a<br />
ZAIDI ya vijana 2000<br />
walioathirika na matumizi<br />
ya dawa za kulevya Zanzibar<br />
wamepatiwa huduma ya<br />
kuwawezesha kuacha<br />
matumizi ya dawa hizo,<br />
ambapo zaidi ya vijana 400<br />
wameweza kuacha kabisa<br />
matumizi ya dawa hizo na<br />
wanaendelea na harakati<br />
zao za kimaendeleo.<br />
Hayo yameelezwa na<br />
Makamu wa Kwanza wa<br />
Rais Zanzibar, Maalim<br />
S e i f u S h a r i f H a m a d ,<br />
Jumapili iliyopita wakati<br />
akizindua Tume ya Kitaifa<br />
ya Kuratibu na Kudhibiti<br />
wa Dawa za Kulevya, katika<br />
hafla iliyofanyika Jumba la<br />
Wananchi Forodhani.<br />
Tume hiyo imeanzishwa<br />
kufuatia mabadiliko ya sheria<br />
namba 12 ya mwaka 2011,<br />
juu ya udhibiti wa dawa za<br />
kulevya, ambayo kwa sasa<br />
inatoa mamlaka kamili ya<br />
kisheria katika mambano<br />
dhidi ya dawa za kulevya<br />
Makala/Habari<br />
AN-NUUR<br />
SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Wepesi wa hukumu za kisheria<br />
ulivyowabebesha wale<br />
waliokuwa kabla yetu”.<br />
Surat Bakara, aya ya 286.<br />
Na Magumu ni yale yaliyo<br />
mazito.<br />
Kuyafikiria yaliyokuwa<br />
kabla yetu miongoni mwa<br />
sheria zilizopita katika<br />
hukumu ngumu. Umma<br />
huu umepunguziwa kwa<br />
kuondolewa magumu mengi<br />
yaliyokuwepo, nayo ni bahati<br />
kubwa.<br />
Kwani hakuna dini yoyote<br />
ikiwa hakuna kumuabudu<br />
Mungu. Lakini dini zilizopita<br />
kwa upande wa wafuasi<br />
wake, ilikuwa inawaamrisha<br />
kuukera mwili na kuuadhibu.<br />
Na malengo yaliyokuwa kwa<br />
waumini wake ni kujiumiza<br />
katika mwili. Na mwili<br />
unapozidi maumivu yake<br />
inakuwa ndio kujisafisha roho<br />
yake na kuosha nafsi.<br />
Imekuja sheria ya Kiislam<br />
ili kuondoa mambo hayo<br />
magumu, na amejulishwa<br />
Mtume (saw) juu ya mambo<br />
hayo katika vitabu vya watu<br />
wa mwanzo, ambayo ni<br />
tofauti (Anawaamrisha mema<br />
na kuwakataza maovu, na<br />
kuwahalalishia yalio mazuri<br />
na kuwakataza wao mabaya<br />
na kuwaondolea magumu).<br />
Surat Aaraf, aya ya 157.<br />
Amejisifu Mwenyezi<br />
Mungu juu ya Mtume wake<br />
kwa watu akasema, “Kwa<br />
hakika amekuja kwenu<br />
Mtume kutokana na nyinyi,<br />
anaathirika na yale mlionayo,<br />
mwenye pupa na mambo yenu<br />
waumini, ni mpole mwenye<br />
huruma). Surat Tauba, aya<br />
ya 128.<br />
Amesema Mtume (S.A.W)<br />
“nimeletwa kwa dini nyepesi<br />
yenye msamaha”. Dini hii<br />
ni nyepesi katika imani, ni<br />
nyepesi katika maamrisho<br />
yake na hukumu. Na Mwenyezi<br />
Mungu ameuhusisha umma<br />
huu na msamaha na uwepesi<br />
kwa sababu ni hukumu na<br />
ujumbe wa watu wote. Na<br />
kwa dunia nzima na kwa<br />
nyakati zote.<br />
Na ujumbe huu kwa kuwa<br />
ni kwa ajili ya watu wote<br />
na ni wa kudumu, hapana<br />
budi aufanye Mwenyezi<br />
Mungu mwenye hekima<br />
k a t i k a h u k u m u z a k e ,<br />
uwepesi na urahisi na upole<br />
unaokubaliana na watu na<br />
zama hizi na mahitaji yake.<br />
Na haya yapo wazi katika<br />
hukumu za kisheria peke<br />
yake. Amesema Mwenyezi<br />
Mungu mtukufu, “Enyi<br />
ambao mlioamini, rukuuni na<br />
sujuduni na muabuduni Mola<br />
wenu na fanyeni kheri kwa<br />
hakika mtafaulu, na piganeni<br />
jihadi kwa ajili ya Mwenyezi<br />
Mungu, ubora wa jihadi yeye<br />
amewateuweni nyinyi. Na<br />
hakufanya Mwenyezi Mungu<br />
kwenu katika dini ugumu)<br />
Surat al-Haji, aya ya 77 hadi<br />
78. Na anasema mwishoni<br />
mwa aya ya Udhu, “Hataki<br />
Mwenyezi kuweka uzito<br />
na ugumu kwenu. Lakini<br />
anataka mjisafishe na atimize<br />
neema zake kwenu, ili mpate<br />
kushukuru” Surat Maida, aya<br />
ya 6.<br />
Na anasema mwisho wa<br />
aya ya Funga, “Anataka<br />
Mwenyezi Mungu kwenu<br />
uwepesi na wala hataki kwenu<br />
uzito”. Surat Al-Bakarat, aya<br />
ya 185.<br />
“Anataka Mwenyezi<br />
Mungu kuwafanyia wepesi<br />
na ameumbwa binadamu ni<br />
dhaifu” Surat Nnisai, aya<br />
28. Na amewatuma Mtume<br />
(S.A.W) Muadhina Aba<br />
Mussa Al-Ashariyi, wakawe<br />
viongozi nchini Yemen ikiwa<br />
ni miongoni mwa usia wake<br />
Mtume kwao. (Wafanyieni<br />
wepesi na wala msitie uzito,<br />
na wabashirieni na wala<br />
msiwagawe, na mkubaliane<br />
na wala msitofautiane).<br />
Na miongoni mwa sifa zake<br />
Mtume (S.A.W), alikuwa<br />
Vijana 2000 wapatiwa matibabu dawa za kulevya Z’bar<br />
Na Mwandishi Wetu,<br />
Zanzibar<br />
Zaidi ya 400 waacha kabisa<br />
nchini.<br />
Serikali ya Zanzibar<br />
imeamua kuandaa programu<br />
mbalimbali kwa ajili ya<br />
kudhibiti matumizi ya dawa<br />
za kulevya, chini ya ofisi ya<br />
Makamu wa Kwanza wa Rais<br />
ikiwa ni pamoja na kuwepo<br />
kwa huduma za nyumba za<br />
kurekebisha tabia “sober<br />
houses” kwa ajili ya vijana<br />
walioamua kuachana na<br />
matumizi ya dawa hizo.<br />
Alisema hayo ni mafanikio<br />
y a l i y o p a t i k a n a t a n g u<br />
kuanzishwa kwa mpango huo<br />
kwa miaka mitatu iliyopita.<br />
Hata hivyo Maalim Seif<br />
amesema mafanikio hayo<br />
hayatokuwa endelevu iwapo<br />
harakati za usafirishaji,<br />
uingizaji na matumizi ya dawa<br />
za kulevya hazitoendelea<br />
kupigwa vita.<br />
Alisema kuna hatari ya<br />
vijana kuendelea kuwa<br />
wahanga wa matumizi ya<br />
dawa za kulevya iwapo<br />
juhudi za serikali za kuleta<br />
maendeleo hazitakuwa na<br />
tija.<br />
Aliongeza kuwa hatma ya<br />
Taifa inategemea zaidi vijana<br />
wenye mwelekeo makini na<br />
waliojiepusha na matumizi<br />
ya mihadharati kwa vile wao<br />
ndio nguvu kazi kubwa ya<br />
taifa.<br />
Amewata wajumbe wa<br />
Tume hiyo kufanya kazi<br />
kwa bidii ili kufikia malengo<br />
yaliyomo kwenye kauli mbiu<br />
ya “Zanzibar bila ya dawa za<br />
kulevya inawezekana”.<br />
Februari mwisho wa kuhamia digitali Zanzibar<br />
Inatoka Uk. 1<br />
Channel zipatazo 36 zitapatikana<br />
kwa uhakika ambapo kutakuwa<br />
Channel za hapa nchini,<br />
michezo, burudani ya tamthilia<br />
na sinema za Kiswahili, Kiarabu<br />
Kihindi na Kizungu. Alisema pia<br />
kutakuwa na Channel nyingi za<br />
habari kama vile BBC, CNN,<br />
Al-jazira, Deutschewelle, CCTV<br />
na nyenginezo.<br />
Waziri huyo alisema<br />
serikali ya Mapinduzi Zanzibar<br />
inafanya kila jitihada, kuona<br />
kwamba wananchi hawana<br />
sababu ya kuhamanika na<br />
kununua ving’amuzi ghali na<br />
dhaifu hivyo aliwahakikishia<br />
kwamba, wataalamu wa serikali<br />
wanahangaika ili kuona kituo<br />
cha televisheni cha ZBC TV<br />
wanaendelea kukiona bila<br />
ya usumbufu hadi Februari<br />
28,2013.<br />
Waziri Mbarouk, alisema<br />
mabadiliko ya mfumo wa<br />
matangazo ya analogue<br />
kwenda digital, yamekuja<br />
kufuatia agizo lililotolewa<br />
na Shirikisho la Mawasiliano la<br />
Afrika Mashariki (EACO) kuwa,<br />
nchi wanachama wa Shirikisho<br />
hilo zinatakiwa ziwe zimehamia<br />
katika mfumo wa digital ifikapo<br />
mwaka huu.<br />
hapewi mambo ya kuchagua<br />
isipokuwa huchagua lililo<br />
jepesi zaidi likiwa halina<br />
makosa (madhambi). Na<br />
miongoni mwa maneno yake<br />
Mtume (S.A.W) ni kuwa,<br />
“Dini hii ni nyepesi na<br />
wala hatoitia ugumu yeyote<br />
isipokuwa itamshinda. Basi<br />
jisogezeni katika mema. Na<br />
ikiwa muongozo wa Uislam<br />
ni uwepesi katika hukumu za<br />
kisheria na Muislamu yeyote<br />
atakayeweka uzito na ugumu<br />
atakuwa ametoka nje ya dini<br />
ya Kiislam”.<br />
Na kwa hivyo ndipo<br />
aliposimama Mtume Mtukufu<br />
m b e l e y a w a n a o w e k a<br />
ugumu katika Uislamu na<br />
akawaambia juu ya kuangamia<br />
kwao na ubaya wa mambo<br />
yao akasema, “Zindukeni na<br />
jueni kuwa wameangamia<br />
wenye kuitia uzito dini”.<br />
Amesema hivi mara tatu.<br />
Na hakuwa mwenye kurudia<br />
maneno isipokuwa kwa ubora<br />
wa maneno hayo na hatari ya<br />
madhumuni yake.<br />
Amepokea Bin Abbas<br />
(R.A) kutoka kwa Mtume,<br />
“Jiepusheni na kuongeza<br />
mambo katika dini kwani<br />
wameangamia waliopita<br />
kabla yenu kwa kuongeza<br />
vitu katika dini”.<br />
Dini ambayo imejazwa<br />
Qur-ani kwa waliopewa<br />
na amesema Mwenyezi<br />
Mungu mtukufu, “Sema enyi<br />
mliopewa kitabu msiongeze<br />
katika dini yenu ya haki, na<br />
wala msifuate matamanio<br />
ya watu waliopotea kabla<br />
na wakawapoteza wengi<br />
na wakapotea katika njia<br />
iliyonyooka”. Surat Mainda,<br />
aya ya 77.<br />
Amepokea Abu Daudi toka<br />
kwa Sahali Bin Abii Umma<br />
kwamba, ameingia yeye na<br />
baba yake kwa Anasi, wakati<br />
wa uongozi wa Omari Bin<br />
Abul-Azizi, naye akiwa Amiri<br />
wao, naye alikuwa akiswali<br />
swala nyepesi kwa muda wa<br />
dakika moja, ni kama swala<br />
ya msafiri au inakaribiana<br />
na hiyo na alipotoa salamu<br />
akaniambia, hakika Mtume<br />
(S.A.W) alikuwa anasema<br />
“Msitie ugumu wenyewe ili<br />
asije kuweka ugumu kwenu<br />
Mwenyezi Mungu, kwani<br />
wapo watu walitia ugumu<br />
wenyewe Mwenyezi Mungu<br />
akawawekea ugumu kwao”.<br />
Hilo ndilo lililobakia katika<br />
nyumba zao za ibada na<br />
viongozi wao wakajizushia<br />
na wala hatukuwalazimisha<br />
sisi wao.<br />
Tunamuomba Mwenyezi<br />
Mungu ajaalie tuwe wenye<br />
kuyajua mambo na kuyafanyia<br />
kazi na kuyafundisha wengine<br />
na wayafuate kwa ubora zaidi<br />
na wayakubali.
AN-NUUR<br />
12 SAFAR 1434, IJUMAA JANUARI 4 - 10, 2013<br />
Usikose nakala yako ya<br />
AN-NUUR kila<br />
Ijumaa<br />
Ujasiria mali washika kasi Baraza Kuu<br />
Zaidi ya milioni 400 zatolewa mikopo<br />
KATIBU Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T) Sheikh<br />
Ramadhan Sanze.<br />
Februari mwisho wa kuhamia digitali Zanzibar<br />
Na Nassor Khamis,<br />
Zanzibar<br />
WA Z I R I w a H a b a r i ,<br />
Utamaduni, Utalii na Michezo<br />
Bw. Said Ally Mbarouk,<br />
amesema kuwa uhamaji<br />
kutoka katika mfumo wa<br />
matangazo wa analogue<br />
kwenda digital utakamilika<br />
rasmi ifikapo Februari 28<br />
mwaka huu, ambapo mitambo<br />
ya analogue katika kanda ya<br />
mikoa mitano ya Zanzibar<br />
itazimwa.<br />
Bw. Mbarouk, aliyaeleza<br />
hayo wakati akizungumza na<br />
waandishi wa Habari katika<br />
ukumbi wa Idara ya Habari<br />
Maelezo Kikwajuni, mjini<br />
Zanzibar.<br />
Alisema kuwa Mamlaka ya<br />
Mawasiliano Tanzania (TCRA)<br />
na Kamisheni ya Utangazaji<br />
Zanzibar (ZBC), pamoja na<br />
taasisi zinazohusika na shughuli<br />
za utangazaji katika Jamhuri<br />
ya Muungano wa Tanzania,<br />
zimeshauriana juu ya namna<br />
Taifa la Tanzania litakavyoingia<br />
katika mfumo wa digital kwa<br />
awamu, ambapo kwa Zanzibar<br />
utakamilika Februari mwakani<br />
badala ya mwishoni mwa<br />
mwaka huu.<br />
Katika kukamilisha kuingia<br />
katika mfumo wa utangazaji<br />
wa digital, Waziri Mbarouk<br />
alisema kuwa Wizara ya Habari<br />
imefanya kazi kwa mafanikio<br />
makubwa ikiwemo kujenga<br />
kituo cha usambazaji mawimbi<br />
(signal) katika eneo la Rahaleo<br />
pamoja kutayarisha maeneo ya<br />
kurushia matangazo ya digital<br />
katika visiwa vya Unguja na<br />
Pemba.<br />
Aidha alisema kuwa Wizara<br />
imeandaa utaratibu wa kuwepo<br />
msambazaji mawimbi (signal)<br />
wa serikali ambao utafanya kazi<br />
kwa ubia na Wizara ya Habari,<br />
Utamaduni, Utalii na Michezo,<br />
Shirika la Utangazaji Zanzibar<br />
na Wizara ya Fedha Uchumi<br />
na Mipango ya Maendeleo,<br />
pamoja na kuandaa utaratibu<br />
wa upatikanaji wa ving’amuzi<br />
na maudhui kwa bei nafuu.<br />
Aidha alisema kuwa uzinduzi<br />
wa mitambo na matangazo<br />
ya digital utafanyika wakati<br />
wa sherehe za Mapinduzi,<br />
ambapo tukio hilo limepangwa<br />
kufanyika Machi 08, 2013<br />
Rahaleo, mjini Zanzibar pamoja<br />
na kusambazwa kwa ving’amuzi<br />
katika wilaya zote za Zanzibar<br />
kwa ajili ya majabio.<br />
“Tutasambaza ving’amuzi<br />
vichache katika Wilaya zote za<br />
Unguja na Pemba, ili mafundi<br />
wetu waweze kuangalia kama<br />
matangazo hayo yanaweza<br />
kupokewa katika pembe zote<br />
za Zanzibar.”alisema Waziri<br />
Mbarouk.<br />
Alisema kuwa ving’muzi kwa<br />
ajili ya matumizi ya wananchi<br />
vitaanza kuuzwa mwishoni<br />
mwa mwezi wa Januari kwa<br />
bei ya shilingi 50,000, vikiwa<br />
na punguzo la shilingi 22,000<br />
kutoka bei halisi ya ving’amizi<br />
hivyo na kutakuwa na kulipia<br />
ada ya shilingi 8,000 kwa mwezi<br />
mmoja.<br />
Vi n g ’ a m u z i 3 0 0 , 0 0 0<br />
vinatarajiwa kuuzwa katika<br />
kipindi cha miaka miwili.<br />
Alisema kuwa ving’amuzi<br />
hivyo vitakavyosambazwa,<br />
Inaendelea Uk. 11<br />
Na Bakari Mwakangwale imewezekana kuwakopesha<br />
Waislamu kupitia vikundi zaidi<br />
KATIBU Mkuu wa Baraza<br />
Kuu la Jumuiya na Taasisi<br />
za Kiislamu (T) Sheikh<br />
Ramadhan Sanze, amewaasa<br />
Waislamu kwamba huu<br />
si wakati wa kulalamika<br />
kupitia historia na mwenendo<br />
wao nchini, bali ni wakati<br />
wa kupanga mikakati ya<br />
kutenda.<br />
Sheikh Sanze, ametoa<br />
ushauri huo mwishoni mwa<br />
wiki iliyopita katika kituo cha<br />
Kiislamu, Mwenge Jijini Dar<br />
es salama, wakati alipokuwa<br />
akizungumza katika mahafali<br />
ya nne ya kuhitimu wakufunzi<br />
wa Kutayba, yanayoendeshwa<br />
na kusimamiwa na Baraza hilo<br />
kwa lengo kuendesha vikundi<br />
vya fedha vya Kutayba Saccos<br />
na Kutayba Vikundi.<br />
Sheikh Sanze, alisema<br />
k w a m u d a m r e f u s a s a<br />
Waislamu wamekuwa katika<br />
hali ya kulalamika kuwa<br />
wamedhulumiwa baada ya<br />
kupigania uhuru, jambo ambalo<br />
linawapotezea muda wa kufikiri<br />
juu ya hatua za kuchukua baada<br />
ya kubaini dhulma hizo.<br />
Alisema historia hiyo ipo<br />
sahihi na itabakia hivyo tu,<br />
lakini haitusaidia isipokuwa<br />
ni kuitumia kwa kupata ari ya<br />
kufanya vizuri zaidi.” Alisema<br />
Sheikh Sanze.<br />
Alibainisha kwamba kwa<br />
sasa hakuna haja ya kulalamika<br />
wala kunung’unika baada ya<br />
kubaini kuwa kuna tatizo, zaidi<br />
Waislamu wajipange upya ili<br />
mambo yao yaende.<br />
“Mwenyezi Mungu katika<br />
Qur an, amewataka Waislamu<br />
wasihuzunike, wasilalamike<br />
wala wasiogope kwa kuwa wao<br />
wapo juu, lakini ikiwa tu ni<br />
waumini”. Alitoa somo Sheikh<br />
Sanze.<br />
Kupitia Kutayba Vikundi na<br />
Kutayba Saccos, sasa Waislamu<br />
wameanza kuonyesha njia ya<br />
kutambulika kwenye vyombo<br />
vya fedha, kwani tayari<br />
wameanza kuwakimbilia<br />
baada ya kuona kuna watu<br />
wameanza kuonyesha juhyudi<br />
zao wenyewe, hivyo wanaona<br />
wakisaidiwa watafanya vizuri<br />
zaidi.<br />
Alisema awali mpango huo<br />
ulikuwa katika vichwa, kisha<br />
kuhamishiwa katika makaratasi<br />
na baadae uliingizwa katika<br />
utendaji na matokeo yake<br />
yameonekana kwani hapakuwa<br />
na utaratibu kama huo kwa<br />
Waislamu nchini.<br />
Sheikh Sanze alifafanua<br />
zaidi kwamba unapouwezesha<br />
umma wa Kiislamu, unakuwa<br />
umewezesha zaidi ya asilimia<br />
50 ya Watanzania, na zaidi<br />
utakuwa umeisaidia Serikali<br />
tawala kuinua hali za kiuchumi<br />
wa raia wake.<br />
Mpaka sasa Baraza Kuu<br />
la Jumuiya na Taasisi za<br />
Kiislamu (T), chini ya Kutayba<br />
ya shilingi milioni mia tano.<br />
Akitoa nasaha zake kwa<br />
wakufunzi wa mafunzo ya<br />
wanakutayba, Sheikh Sanze,<br />
aliwaeleza wahitimu hao kuwa,<br />
kuhitimu kwao ni mwanzo wa<br />
mafanikio makubwa iwapo<br />
wanataka.<br />
Kwa upande wake Sheikh<br />
Mtoe, alitanabaisha kwamba<br />
pamoja na mafanikio yenye tija<br />
ambayo yanaanza kuonekana<br />
k w a Wa i s l a m u k a t i k a<br />
kujiletea maendeleo, lakini<br />
wasijisahau kwani kuna wenzao<br />
wameshapiga hatua kubwa<br />
kuliko hiyo waliyofikia.<br />
Aliwataka wakufunzi hao<br />
kuhakikisha kila mmoja,<br />
ahakikishe kwamba mipango<br />
na mikakati hiyo ya Kutayba<br />
Vikundi na Kutayba Saccos,<br />
anaifikisha katika Msikiti wake<br />
na kuizalisha kwa wengine<br />
ambao hawajabahatika kuipata<br />
taaluma hiyo.<br />
Naye Ustadhi Iddi Uvuruge,<br />
ambaye ni Meneja mikopo wa<br />
Kutayba Saccos, alisema mpaka<br />
sasa wana matawi takriban 23<br />
katika mikoa yote nchini na<br />
baadhi ya Wilaya.<br />
Alisema kupitia Kutayba,<br />
zaidi ya shilingi Milioni mia<br />
nne, zimetolewa kama mikopo<br />
kwa wanachama mbalimbali wa<br />
Kutayba Saccos nchini.<br />
Ustadhi Uvuruge, aliitaja<br />
mikopo hiyo kuwa ni pesa<br />
tasilimu, vifaa vya ujenzi,<br />
pikipiki zaidi ya mia moja,<br />
magari, bajaji pamoja na<br />
nyumba.<br />
Akianisha aina ya mikopo<br />
wanayoitoa, aliitaja kuwa ni<br />
Karbanhasana (mikopo mema),<br />
inayohusiana na pesa tasilimu<br />
kuanzia elfu ishirini hadi<br />
milioni moja. Katika mkopo<br />
huu, mwanachama akikopa<br />
kiasi hicho anatakiwa kurejesha<br />
kiasi hicho hicho bila kuongeza<br />
kiasi chochote.<br />
Aina ya pili ya mikopo<br />
ni Mudhwaraba (Mikopo ya<br />
kibiashara). Hii ni mikopo<br />
inayozidi kiasi cha shilingi<br />
milioni moja. Mkopo huu<br />
haitolewi pesa tasilimu, bali<br />
mwanachama hukopeshwa<br />
bidhaa, vifaa, magari au hata<br />
nyumba kulingana na mahitaji<br />
ya mwanachama.<br />
Akizungumzia changamoto<br />
wanazokumbana nazo, meneja<br />
huyo alisema baada ya huduma<br />
hiyo kuwafikia Waislamu wengi<br />
nchini, kumekuwa na ongezeko<br />
kubwa la Waislamu kutoka<br />
sehemu mbalimbali wanaohitaji<br />
kufikiwa au kufungua Kutayba<br />
zao. Changamoto nyingine<br />
ni uelewa mdogo wa jamii<br />
hususani katika mikopo hii<br />
ya Mudhwaraba, ambapo ule<br />
utaratibu wa kununua kitu kisha<br />
ukamkopesha mwanachama<br />
kwa bei ya juu anadhani kuwa<br />
bado hiyo ni riba.<br />
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.