sheria au roho.vp (Read Only) - Martin Bucer Seminar
sheria au roho.vp (Read Only) - Martin Bucer Seminar
sheria au roho.vp (Read Only) - Martin Bucer Seminar
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
WAGALATIA 3:8-14 : JE, SHERIA INAJIPINGA<br />
YENYEWE?<br />
Wagalatia 3:8-14: “Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani<br />
kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri<br />
Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote<br />
watabarikiwa. Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu<br />
aliyekuwa mwenye imani. Kwa maana wale wote walio wa matendo ya<br />
<strong>sheria</strong>, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu<br />
asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.<br />
Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu<br />
katika <strong>sheria</strong>; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani. Na torati<br />
haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo. Kristo<br />
alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili<br />
yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;<br />
ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Kristo Yesu,<br />
tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.”<br />
Kwa mujibu wa Ragnar Bring 53 , sura ya tatu ya Wagalatia, hususani<br />
mstari wa 12, unadhihirisha uwiano mkubwa na Warumi 10:4-5. Kwa<br />
sababu hii, basi tuchunguze Warumi 10:4-5.<br />
Katika Warumi 10:4-8, P<strong>au</strong>lo anasema, “Kwa maana Kristo ni mwisho<br />
wa <strong>sheria</strong>, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. Kwa maana Musa aliandika<br />
juu ya haki itokayo kwa <strong>sheria</strong>, ya kuwa, Mtu afanyaye hiyo ataishi kwa<br />
hiyo. Bali ile haki ipatikanayo kwa imani yanena hivi, Usiseme moyoni<br />
mwako, Ni nani atakayepanda kwenda mbinguni? (Yaani, ni kumletea<br />
Kristo chini), <strong>au</strong>, ni nani atakayeshuka kwenda kuzimuni? (Yaani ni<br />
kumleta Kristo juu, kutoka kwa wafu.) Lakini yanenaje? Lile neno li<br />
karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile<br />
neno tulihubirilo.”<br />
Kwa nini Waisraeli katika kumkataa Kristo, hawakujali haki na Sheria<br />
(Rum.10:2-3)? Walimkataa Kristo, aliye mwisho wa <strong>sheria</strong>. Neno la<br />
Kigriki ‘telos’ lina maana nyingi, na linapaswa kutafsiriwa kama ‘mwisho’<br />
<strong>au</strong> ‘kusudi’. Tafsiri hutegemea imani ya mtafsiri juu ya Sheria ya Musa.<br />
Kwa maoni yangu, tafsiri, “Kristo ni utimilifu (<strong>au</strong> lengo) la <strong>sheria</strong>” inaakisi<br />
vema maelezo ya P<strong>au</strong>lo juu ya Sheria katika Warumi (kwa mfano, 3:20,<br />
31; <strong>au</strong> 7:7, 12-16, 22-24; 8:3-4, 13:8-10). 54 Sheria yote inatafuta lengo<br />
lake, maana yake, ukamilifu wake na utimilifu wake katika Kristo.<br />
32