08.06.2013 Views

sheria au roho.vp (Read Only) - Martin Bucer Seminar

sheria au roho.vp (Read Only) - Martin Bucer Seminar

sheria au roho.vp (Read Only) - Martin Bucer Seminar

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

WAGALATIA 3:8-14 : JE, SHERIA INAJIPINGA<br />

YENYEWE?<br />

Wagalatia 3:8-14: “Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani<br />

kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri<br />

Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote<br />

watabarikiwa. Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu<br />

aliyekuwa mwenye imani. Kwa maana wale wote walio wa matendo ya<br />

<strong>sheria</strong>, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu<br />

asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.<br />

Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu<br />

katika <strong>sheria</strong>; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani. Na torati<br />

haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo. Kristo<br />

alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili<br />

yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;<br />

ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Kristo Yesu,<br />

tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.”<br />

Kwa mujibu wa Ragnar Bring 53 , sura ya tatu ya Wagalatia, hususani<br />

mstari wa 12, unadhihirisha uwiano mkubwa na Warumi 10:4-5. Kwa<br />

sababu hii, basi tuchunguze Warumi 10:4-5.<br />

Katika Warumi 10:4-8, P<strong>au</strong>lo anasema, “Kwa maana Kristo ni mwisho<br />

wa <strong>sheria</strong>, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. Kwa maana Musa aliandika<br />

juu ya haki itokayo kwa <strong>sheria</strong>, ya kuwa, Mtu afanyaye hiyo ataishi kwa<br />

hiyo. Bali ile haki ipatikanayo kwa imani yanena hivi, Usiseme moyoni<br />

mwako, Ni nani atakayepanda kwenda mbinguni? (Yaani, ni kumletea<br />

Kristo chini), <strong>au</strong>, ni nani atakayeshuka kwenda kuzimuni? (Yaani ni<br />

kumleta Kristo juu, kutoka kwa wafu.) Lakini yanenaje? Lile neno li<br />

karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile<br />

neno tulihubirilo.”<br />

Kwa nini Waisraeli katika kumkataa Kristo, hawakujali haki na Sheria<br />

(Rum.10:2-3)? Walimkataa Kristo, aliye mwisho wa <strong>sheria</strong>. Neno la<br />

Kigriki ‘telos’ lina maana nyingi, na linapaswa kutafsiriwa kama ‘mwisho’<br />

<strong>au</strong> ‘kusudi’. Tafsiri hutegemea imani ya mtafsiri juu ya Sheria ya Musa.<br />

Kwa maoni yangu, tafsiri, “Kristo ni utimilifu (<strong>au</strong> lengo) la <strong>sheria</strong>” inaakisi<br />

vema maelezo ya P<strong>au</strong>lo juu ya Sheria katika Warumi (kwa mfano, 3:20,<br />

31; <strong>au</strong> 7:7, 12-16, 22-24; 8:3-4, 13:8-10). 54 Sheria yote inatafuta lengo<br />

lake, maana yake, ukamilifu wake na utimilifu wake katika Kristo.<br />

32

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!