19.06.2013 Views

C:\Users\Home\Documents\My Webs - Excel Exams

C:\Users\Home\Documents\My Webs - Excel Exams

C:\Users\Home\Documents\My Webs - Excel Exams

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

KATA YA MANISPAA YA NAKURU MASHARIKI<br />

MTIHANI WA MAJARIBIO<br />

DARASA LA SABA MUHULA WA KWANZA 2009<br />

KISWAHILI<br />

MUDA: SAA MOJA DAKIKA 40<br />

Jaza nafasi kwa jibu lifaalo<br />

Milka alivikunjua tena vile __1__ vya majibu na __2__ kuvisoma __3__ mara __4__. Alikuwa haamini<br />

kabisa __5__ majibu __6__ yalikuwa kweli! Cheti __7__ kilionyesha __8__ ya uchunguzi __9__, yaani alikuwa<br />

na virusi __10__ ukimwi na majibu __11__ matokeo ya uchunguzi __12__ Bitrisa yalionyesha __13__ yakiwa<br />

maana __14__ na virusi __15__ ukimwi.<br />

1. A. waraka B. cheti C. vyeti D. vitu<br />

2. A. kwanza B. kuanza C. kuanzi D. kuwaza<br />

3. A. na B. wa C. kwa D. vya<br />

4. A. ingine B. mengine C. mingine D. nyingine<br />

5. A. kule B. kweli C. kama D. vile<br />

6. A. ile B. yale C. zile D. ule<br />

7. A. yake B. wake C. chake D. kwake<br />

8. A. jibu B. mfano C. tukio D. majibu<br />

9. A. chanya B. hasi C. jumlisha D. kutoa<br />

10. A. za B. wa C. na D. vya<br />

11. A. kwa B. ya C. za D. vya<br />

12. A. ya B. za C. na D. wa<br />

13. A. kuzindisha B. hasi C. chanya D. kutoa<br />

14. A. hakua B. hakukua C. hakuwa D. hakui<br />

15. A. wa B. za C. via D. vya<br />

Katika swali la 16-30, jibu kila swali kulingana na<br />

maagizo<br />

16. Kiyoyo ni kwa bata kama vile________ni kwa<br />

nguruwe.<br />

A. kichengo B. kivinimbi<br />

C. kiwengwe D. kiluwiluwi<br />

17. 5/<br />

7 inaitwa____________.<br />

A. tusui tano B. subui tano<br />

C. tano kwa saba D. saba kwa hamsa<br />

18. Adhuhuri ni wakati ambapo___________.<br />

A. watu hula chajio B. watu hula staftahi<br />

C. watu huamka D. watu hula kishuka<br />

19. Neno ndimi liko katika ngeli ya________.<br />

A. A-WA B. I-ZI C. U-ZI D. U-I<br />

20. Kuna misitu mingi katika________yetu.<br />

A. inchini B. nchi<br />

C. ncha D. inchi<br />

21. Tunasema thurea ya nyota na_____la nyuki.<br />

A. kipeto B. jozi<br />

C. safu D. bumba<br />

22. Kila mwanafunzi______anunue______la<br />

rangi ya manjano.<br />

A. sharti, shati B. zana, sana<br />

C. washa, warsha D. sabuni, zabuni<br />

23. Unipe, usinipe kwangu ni________. Yaani<br />

ni sawa tu.<br />

A. moja B. wamoja<br />

C. mamoja D. pamoja<br />

24. Siku za_____nyasi na majani huwa kijani<br />

kibichi.<br />

A. kiangazi B. masika<br />

C. kipupwe D. vuli<br />

25. Seremala alikereza mbao kwa________.<br />

A. msumeno B. patasi<br />

C. randa D. bisibisi<br />

26. Andika idadi ya tarakimu ifuatayo<br />

Millioni mbili, mia mbili tisini na sita elfu,<br />

mia tisa na sita.<br />

A. 2029,966 B. 2,269,609<br />

C. 2,296,966 D. 2,296,906<br />

27. Tegua kitendawili kifuatacho: “Kafa huku<br />

ananing’inia,”<br />

A. uyoga<br />

B. nyanya<br />

C. biringanya<br />

D. mwiko<br />

1 Typeset and Printed by: <strong>Excel</strong> Printers Nakuru


28. Kanusha sentensi ifuatayo - “Mngepanda miti<br />

mngepata mvua,”<br />

A. hamngepanda miti mngepata mvua<br />

B. msingepanda miti msingepata mvua<br />

C. mngepanda miti msingepata mvua<br />

D. hamngepanda miti msipata mvua<br />

29. Mwana kandanda alirukaruka kama______.<br />

A. chura B. mtumwa<br />

C. komba D. samaki<br />

30. Neno jingine sawa na ugonjwa ni______.<br />

A. chelea B. udhi<br />

C. uwele D. mkwasi<br />

Soma taarifa kisha ujibu maswali 31-40<br />

Mahafali ni mkusanyiko mkubwa wa watu kwa ajili ya sherehe ya kuhitimu katika masomo yoyote.<br />

Wakati huo, waliomaliza masomo hupewa vyeti vya aina mbalimbali katika masomo yao. Ni juzi tu tarehe<br />

ishirini na nane mwezi wa kumi na moja ambapo mimi na jamaa yangu tulihudhuria mahafali ya mwana wetu<br />

Jittu Kamaliza. Bwana mdogo huyu alikuwa akisomea katika chuo cha Amani ndogo au kwa kimombo, Peace<br />

Junior. Chuo hiki hupatikana katika mtaa wa Magiwa jijini Nairobi.<br />

Vijana waliohitimu walitunukiwa vyeti mbalimbali vya kuhitimu kwa pamoja na vyeti hivyo walipewa<br />

zawadi za aina nyingi kutokan na sifa au mafanikio yao ya hapa na pale chuoni.<br />

Jittu Kamaliza alipokea zawadi za aina nyingi mno. Kwa mfano alikuwa kati ya wasomi bora wa mwaka.<br />

Kisha alipokea zawadi kwa kuwa mwanafunzi mwenye nidhamu ya hali ya juu.<br />

Baada ya mahafali ya Jittu Kamaliza, tulishuhudia mafahali ya Lilian Binti Wagallah. Huyo alikuwa<br />

mwanafunzi katika chuo kikuu cha Nairobi. Alihitimu katika taaluma ya iktisadi. Iktisadi ni elimu inayohusika na<br />

uchumi na biashara.<br />

Mwalimu Wagallah William ambaye amekuwa mfunzi zaidi ya miaka thelathini alifika jijini Nairobi akiwa<br />

na mkewe Mama Poya, kushuhudia mafahali ya mwana wao Lillian. Baada ya mafahali hayo ya Lillian, tulipata<br />

nafasi ya kuzuru viunga vya Nairobi hadi Kangundo, ardhi ya wakamba penye mvua kwa wingi sana. Pamoja na<br />

Wagallah na wengine katika ziara hiyo walikuwa ni Sammy Ndiwa na Mama Bobi. Sote tulikuwa katika gari<br />

langu tukiwatembeza watoto wetu waliohitimu elimu katika vyuo vyao kwenye mahafali yaliyofana jinsi hiyo. Je<br />

wewe umeshajua ni lini utakapokuwa na mahafali yako? Je, utatualika tuihudhurie?<br />

31. Watu hasa wanafunzi, hufanyiwa mahafali hivi<br />

A. baada ya kuhitimu masomo<br />

B. wanaposoma<br />

C. wakianza masomo<br />

D. kabla ya kuhitimu masomo<br />

32. Katika mahafali waliohitimu hupewa_____.<br />

A. shada<br />

B. shadaa<br />

C. shahada<br />

D. shadidi<br />

33. Hivi karibuni mwandishi alihudhuria mahafali<br />

ya nani aliye aila yake?<br />

A. Amani ndogo<br />

B. Bwana mdogo<br />

C. Lillian Wagallah<br />

D. Jittu Kamaliza<br />

34. Pamoja na vyeti vya kuhitimu, vijana hupewa<br />

A. sifa<br />

B. zawadi<br />

C. nidhamu<br />

D. mafanikio<br />

35. Zawadi ya nidhamu bora hupewa mtu mwenye<br />

A. adhabu njema<br />

B. dhahabu njema<br />

C. elimu njema<br />

D. adabu njema<br />

36. Aliyehitimu katika elimu ya iktisadi ni____.<br />

A. Wagallah<br />

B. Magiwa<br />

C. Lillian<br />

D. Jittu<br />

37. Baada ya mahafali, jamaa walizuru______.<br />

A. Nairobi B. Magiwa<br />

C. Kangundo D. Gari<br />

38. Kuzuru ni sawa na_________.<br />

A. kuona B. kufika<br />

C. kutazama D. kutembelea<br />

39. Mtoto huhitimu___________.<br />

A. anapofuzu B. anapozuru<br />

C. anapofeli D. anapozulu<br />

40. Taarifa hii ni juu ya_________.<br />

A. Hasara za kusoma<br />

B. Elimu ni mali<br />

C. Mvua ya Kangundo<br />

D. Mahafali<br />

2


Soma habari ifuatayo, kisha uchague majibu sahihi zaidi ya maswali 41-50<br />

Mavazi aidha humpamba mwanadamu au humuaibisha. Mavazi humpamba anapotaka kupambika na<br />

humuaibisha anapotaka kujiaibisha.<br />

Sababu kuu ya watu kuvaa mavazi ni kujisitiri ingawa zipo sababu mbalimbali kama vile kujikinga na<br />

baridi, kuhifadhi utamaduni wake, kutambuliwa kwa cheo chake mbali na kule kutaka kuvutia watu.<br />

Jambo la kustaajabisha ni kuona kwamba ile sababu kuu ya kujisitiri, siku hizi huwa haina uzito wowote<br />

kwa mwanadamu hasa vijana. Nguo fupi na za kukaba mwili zimekuwa ni mtindo wala si aibu kwa wengi. Nguo<br />

nyembamba zenye kuonyesha yasiyofaa kuonekana ndizo zinazotia fora. Ulimwengu umebadilika haraka kiasi<br />

kwamba watoto hawa hutoka mbele ya wazazi wao bila ya kukatazwa na wazazi wao wala kaka au dada zao.<br />

Wahenga hawakukosea waliposema yale waliyoyasema juu ya kukatazama makosa.<br />

Wamasai ni kabila linalosifika ulimwenguni kote kwa kuweza mpaka leo kuhifadhi na kudumisha utamaduni<br />

wao hasa katika mavazi. Ni kabila liloamini kwa dhati kwamba mwacha asili....................<br />

41. Sababu alizozitaja mwandishi zinazomfanya<br />

mwanadamu kuvaa mavazi ni_______.<br />

A. mbili<br />

B. tatu<br />

C. nne<br />

D. tano<br />

42. Neno gani halina maana sawa na neno vijana?<br />

A. Adinasi<br />

B. Barobaro<br />

C. Uledi<br />

D. Shababi<br />

43. Mwandishi awalaumu vijana kwa______.<br />

A. kupenda kuhifadhi utamaduni<br />

B. kuvuja pesa nyingi juu ya vazi<br />

C. kutotilia maanani umuhimu wa kujisitiri<br />

D. kusahau utamaduni wao<br />

44. Nguo aina ngapi zilimuudhi mwandishi?<br />

A. Mbili<br />

B. Kabuti<br />

C. Nne<br />

D. Tano<br />

45. Wamaasai pia wangeweza kutumia methali<br />

“usiache mbachao..........”<br />

A. kumpatia nduguyo<br />

B. utajuta mwishowe<br />

C. kufuata kila lijalo<br />

D. kwa msala upitao<br />

3<br />

46. Kutia fora inamaanisha<br />

A. kutia adabu<br />

B. kutia wasiwasi<br />

C. kutakiwa zaidi<br />

D. kuhofiwa<br />

47. Methali gani haingeweza kutumiwa juu ya<br />

kukataza makosa?<br />

A. Usipoziba ufa utajenga ukuta<br />

B. Mtaka cha mvunguni sharti ainame<br />

C. Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na<br />

ulimwengu<br />

D. Ukicha mwana kulia mwisho utalia wewe<br />

48. Ni nani kati ya hawa huvaa nguo ili ajitambulishe<br />

cheo chake?<br />

A. Mwalimu<br />

B. Daktari<br />

C. Hakimu<br />

D. mkulima<br />

49. Wamaasai____________.<br />

A. wamelaumiwa kwa kusahau utamaduni wao<br />

B. wamesifiwa kwa kujinaki na utamaduni wao<br />

C. hawapendelei kuonekana na nguo zao<br />

D. wamleta mabadiliko katika utamaduni wao<br />

50. Maliza methali: Mwacha asili_______.<br />

A. na asili humwacha<br />

B. atadharauliwa<br />

C. hana mwisho mwema<br />

D. ni mtumwa

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!