15.07.2013 Views

C:\Users\GITOGO\Documents\8 AI6 - Excel Exams

C:\Users\GITOGO\Documents\8 AI6 - Excel Exams

C:\Users\GITOGO\Documents\8 AI6 - Excel Exams

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

EXCEL EXAM<br />

A6<br />

KENYA EXAMS ONLINE<br />

DARASA LA NANE 2011<br />

KISWAHILI<br />

MUDA: SAA 1 DAKIKA<br />

40<br />

Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne. Chagua jibu lifaalo<br />

zaidi kati ya yale uliyopewa.<br />

Katika karia __1__, paliishi Mzee Kazi. Kondeni __2__ alikuwa amebuni wazo __3__ kuanzisha bustani iliyotoa<br />

mazao na matunda mengi. Kati ya matunda hayo yalikuwa machungwa aliyoyatumia kutengeneza __4__.<br />

Madhumuni ya sharubati yalikuwa ni matumizi yake binafsi na wanawe. Fauka ya hayo, alijitengea __5__ kwenye<br />

bonde __6__ sana. Aliyapa maudhi __7__ kwa adinasi yeyote. Pasina shaka __8__ uadilifu.<br />

1.A. chetu B. wetu C. yetu D. letu<br />

2.A. lake B. chake C. mwake D. vyake<br />

3.A. nzuri B. zuri C. mzuri D. wazuri<br />

4.A. mkandaa B. pure C. mashendea D. sharubati<br />

5.A. baiti B. kidurusi C. chumbani D. masika<br />

6.A. refu B. ndefu C. mrefu D. kurefu<br />

7.A. kipaumbele B. mawaidha C. kisogo D. jeki<br />

8.A. alitamani B. alithamiria C. alidhamania D. alithamani<br />

Serikali yetu __9__ kwa kutozingatia mchezo uitwao pool ambao unazidi kuwa __10__ katika sehemu mbalimbali<br />

nchini. Ni muhimu kuzingatia umuhimu wa __11__ kwani wachezaji wanaweza __12__ katika __13__ ya kimataifa.<br />

Mchezo huu ukichukuliwa kuwa kamari, juhudi za kuendeleza zitaambulia __14__ na mchezo __15__.<br />

9. A. imesifiwa B. imekashifiwa C. imeimarishwa D. imetukizwa<br />

10.A. maarufu B. marufuku C. changamoto D. duni<br />

11.A. kuudunisha B. kuuzorotesha C. kuupuuza D. kuuimarisha<br />

12.A. kushindwa B. kudhoofika C. kushindikana D. kutamba<br />

13.A. sifa B. safu C. siafu D. faifu<br />

14.A. pono B. ukingo C. nunge D. ushindi<br />

15.A. utaimarika B. utakufa C. utapendwa D. utafaulu<br />

Kutoka swali la 16 mpaka 30, chagua jibu lililo<br />

sahihi<br />

16. Safari iling’oa nanga wakati jua lilikuwa<br />

likivaa joho lake.<br />

A. Safari ilianza wakati wa machweo.<br />

B. Safari ilikamilika wakati wa adhuhuri.<br />

C. Safari ilianza wakati wa macheo.<br />

D. Safari ilikamilika wakati wa magharibi.<br />

17. Chagua orodha iliyo na vivumishi pekee.<br />

A. Kitisti, asteaste, uadilifu, ihsani<br />

B. Cheka, bingiri bingiri, imani, kashifu<br />

C. Kwa ajili, madhumuni, kichinichini,<br />

adhuhuri<br />

D. Sugu, kokote, mahiri, yapi<br />

18. Bainisha kundi ambalo lina visawe<br />

A. Fulusi, darhimu, ghawazi, njenje<br />

B. Amali, amani, amana, dhamana<br />

1<br />

Available at www.kenyaexams.com<br />

C. Gange, uganga, uchaga, changa<br />

D. Bashasha, bahasha, mabasha, mipasho<br />

19. Chagua sentensi iliyo katika mahali maalumu<br />

na ni dhahiri.<br />

A. Joka limejitoma humu shimoni<br />

B. Huko ndiko walikonaswa.<br />

C. Wachezaji wote wamefika hapa ugani.<br />

D. Aliingia humo.<br />

20. Umoja wa sentensi “Weledi wowote hawawezi<br />

kuiudhimisha mimea hiyo.”<br />

A. Mweledi yoyote hawezi kuidhinisha<br />

mmea huu.<br />

B. Mweledi yeyote hawezi kuidhinisha mmea<br />

huo.<br />

C. Mweledi yeyote hawezi kuidhinishwa na<br />

mmea huo.<br />

D. Mweledi yeyote hawezi kuidhinika na mmea<br />

huo.


21. Chagua kinyume cha sentensi.<br />

Mimi ndimi niliyeibandika.<br />

A. Wewe ndiwe uliyeibandika.<br />

B. Mimi ndiye niliyeibandua.<br />

C. Yeye ndiye aliyeibandua.<br />

D. Sisi ndisi tuliyeibandua.<br />

22. Chagua usemi wa taarifa ulio sawa wa<br />

“Nitakusubiri hapa kesho.” Maksuudi<br />

akasema.<br />

A. Maksuudi akasema kwamba atamsubiri<br />

hapa siku ya kesho.<br />

B. Maksuudi alisema kwamba angemsubiri<br />

hapa siku ya kesho.<br />

C. Maksuudi alisema kana kwamba<br />

atamsubiri hapo siku iliyofuatia.<br />

D. Maksuudi alisema kwamba angemsubiri<br />

hapo siku iliyofuata.<br />

23. Jaribosi ni kwa sikio, kigwe ni kwa<br />

A. shingo B. mkono<br />

C. mguu D. kiuno<br />

24. Chagua kivumishi na kielezi mtawalia kutoka<br />

sentensi.<br />

Mdarisi huyo aliwasili shuleni mafungulia<br />

nyama.<br />

A. aliwasili, shuleni<br />

B. huyo, mafungulianyama<br />

C. shuleni, mafungulianyama<br />

D. huyo, aliwasili<br />

25. Bainisha sentensi iliyo sahihi kisarufi.<br />

A. Angekuwako shuleni angaliwaalika wageni.<br />

B. Asingekuwa shuleni angewaalika wageni.<br />

C. Angalikuwako shuleni angaliwaalika<br />

wageni.<br />

D. Asingalikuwako shuleni asingewaalika<br />

wageni.<br />

26. Chagua sentensi ambayo ni muungano sahihi<br />

wa hizi.<br />

Mwehu alijitoma darasani.<br />

Mwehu aliwaogofya wanagenzi.<br />

A. Mwehu alijitoma darasani kwa mintaarafu<br />

ya kuwaogofya wanagenzi.<br />

B. Mwehu alijitoma darasani lau aliwaogofya<br />

wanagenzi<br />

C. Mwehu alijitoma darasani na kuwaogofya<br />

wanagenzi.<br />

D. Mwehu alijitoma darasani na kuwaogofya<br />

wanagenzi.<br />

27. Methali, “Kozi halei kuku wa wana” ina<br />

maadili gani?<br />

A. Hutuonya dhidi ya kuwa na marafiki.<br />

B. Hutuonya kuwa waangalifu na vitu vyetu.<br />

C. Hutuonya kuwa tusitumie uwezo wetu<br />

ovyovyo<br />

D. Hutuonya tusiwadharau wale wanaokula<br />

chakula duni.<br />

28. ‘Kupata pashua la moyo’ ni<br />

A. Kutokuwa na hamu ya kutenda jambo.<br />

B. Kuwa na wasiwasi kabla ya kuamua kutenda<br />

jambo.<br />

C. Msukumo wa kufanya jambo<br />

D. Kutokuwa na hamu ya kuendelea kufanya<br />

jambo.<br />

29. Barua inayopokewa kupitia tarakilishi ni<br />

A. wavuti B. pataninga<br />

C. mdahalisi D. mtandao<br />

30. Kitendawili “Kabla sijala nyama, mwanangu<br />

huila kwanza.” Jibu lake ni<br />

A. Kuku B. Kisu<br />

C. Kinu D. Jua<br />

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 31- 40<br />

Mambo yalipochupa mipaka na kukithiri, Adili hakuweza kustahimili tena ila alimwasa na kumwambia<br />

Jeta ya kuwa vitendo vyake alivyovitenda vilikuwa alijojo na vinamchukiza: itakuwa bora akiviacha na akawaepuka<br />

nemsi zake Jeta alikuja juujuu na kupandwa na ghaidhi si haba, ati kwa kuwa Adili anamtuhumu anafanya<br />

vitendo vibaya. Chambilecho wahenga, moyo wa kupenda hauna kinyongo. Adili alisunyaa na kunyerereka.<br />

Mambo yaliendelea na kutia maji maziwani. Sasa Adili hakuweza kustahimili tena ila alimweleza mkewe vizuri.<br />

Jeta aliangua kilio cha kutaka kureja mastakimuni kwa wavyele wake. Adili alisema ya kuwa hapana haja ya<br />

hayo, lakini ingekuwa bora pindi wangekaa baiti mbalimbali mpaka hasira zao ziishe. Adili alihamia kiambo<br />

kingine akamwachia nyo Jeta.<br />

Baada ya kupita haya, manzili yao na mahaba yao yakawa segemnege. Zilipita siku ayami pasina ya<br />

kuonana ana kwa ana’ ingawa Jeta akipeleka waraka kwao na yeye huletewa kuelezewa kila kitu, lakini hajawaarifu<br />

yakuwa ana ugomvi na mumewe. Baada ya mwia ayami wa kupatikana ugomvi na sintofahamu, Jeta hakujali ila aliletewa<br />

barua za simanzi na misaada iliyohitajika.<br />

Makazi ya upweke na kuwa mbali na adinasi aliyemuenzi yalimchosha adili, na aliondoka pasina kusema<br />

wapi anakwenda na lini atarudi. Kabla ya kuondoka alikuja kumwaga Jeta na kumsabihia chochote atakacho na<br />

kumpa ruhusa ya kwenda atakapo. Adili aling’oa habta na kwenda zake. Jeta alisalia akicheza kidege jinsi<br />

2


alivyotaka; mambo yalifurutu alipokuwa mumewe hayupo. Nyumba yake ilikuwa mithani ya mkahawa kila atakaye alikuwa<br />

na fursa ya mja na kufanya atakavyo. Hazikupita siku nyingi Jeta alichoka na maisha ya namna hiyo, na akataka kwenda<br />

kwao. Safari ilitengenezwa na Jeta akaondoka na kwenda kiamboni kwao.<br />

31. Kwa mujibu wa aya ya kwanza, Adili<br />

hakuweza kustahimili tena mambo ya Jeta<br />

kwa sababu<br />

A. yalikiuka miigo<br />

B. yalipindukia hasara<br />

C. yalipita maelezo<br />

D. yalikiuka mipaka<br />

32. Jeta alipandwa na ghaidhi si haba. Hivi ni<br />

kusema alikuwa na<br />

A. hamaki na hasira kwa sababu ya kubezwa<br />

na mumewe<br />

B. hasira kwa sababu ya kupuuzwa kwa ajili ya<br />

vitendo vyake<br />

C. hamaki kwa sababu vitendo vyake viliigwa<br />

na mumewe<br />

D. hasira kwa sababu ya kukanywa dhidi ya<br />

vitendo vyake<br />

33. Jeta alikasirika kwa sababu<br />

A. alidai mumewe alikuwa akimsingizia uovu<br />

B. ni kweli kuwa yeye alikuwa mwadilifu<br />

lakini mumewe akamsingizia uovu<br />

C. Adili aliwataka nemsi zake kuja nyumbani<br />

kwao<br />

D. Yeye alikuwa mama aliyekasirika mara<br />

kwa mara<br />

34. “Mambo yaliendelea na kutia maji maziwani”<br />

hii ina maana kuwa<br />

A. Adili aliendelea kumkashifu akimsingizia<br />

uovu<br />

B. Jeta aliendelea kukataa kuchota maji<br />

ziwani<br />

C. Jeta aliendelea na tabia yake mbaya bila<br />

kujali maonyo<br />

D. Adili na mkewe Jeta waliendelea kupigana<br />

nyumbani<br />

35. Kulingana na kifungu hiki, Adili alihamaki<br />

akamwachia nyumba Jeta kwa mintaarafu ya<br />

nini?<br />

A. Adili aliona ilikuwa heri kuondoka mpaka<br />

hasira zake zipungue kabisa<br />

B. Adili alikuwa amemchukia sana Jeta kwa<br />

sababu ya tabia yake<br />

C. Adili alikuwa amechokeshwa sana na<br />

maisha ya Jeta<br />

D. Adili alikuwa akitaka Jeta awe na upuuzi<br />

3<br />

36. Kwa mujibu wa kifungu hiki, neno ‘kukithiri’<br />

lina maana gani?<br />

A. kudhihirisha<br />

B. kuzidi<br />

C. kupungua<br />

D. kuonekana waziwazi<br />

37. Kulingana na kifungu hiki ulichosoma, neno<br />

linalotumiwa badala ya kuudhi ni gani?<br />

A. kukereketa<br />

B. kutuhumu<br />

C. kuchupa mipika<br />

D. kuchukiza<br />

38. Jeta alituhumiwa na mumewe Adili kwa<br />

sababu ya tabia yake. Hivi ni kusema Jeta<br />

A. aliadhibiwa na mumewe<br />

B. alinasihiwa na mumewe<br />

C. alishukiwa na mumewe<br />

D. alishutumiwa na mumewe<br />

39. Baada ya kupita haya, manzili yao na mahaba<br />

yao yakawa segemnege. Hivi ni kusema<br />

baadaye<br />

A. mambo yao na mapenzi yao yalikuwa<br />

ndivyo sivyo<br />

B. mambo yao na mapenzi yao yalikuwa<br />

shwari<br />

C. mambo yao na mapenzi yao yalirudia hali<br />

ya kawaida<br />

D. mambo yao na mapenzi yao yalitengenea<br />

40. Kwa mujibu wa kifungu hiki, baada ya mume<br />

kuondoka nyumbani mwake kwa muda mrefu,<br />

A. hatimaye tabia ya mkewe Adili ilibadilika<br />

na mumewe akarejea kiamboni kwao<br />

B. hatimaye tabia ya mkewe ilimfanya ajute<br />

mpaka akahiari kuondoka na kwenda kwa<br />

wavyele wake.<br />

C. hatimaye marafiki zake Jeta walimsaidia<br />

mpaka nyumba ikawa kama mkahawa<br />

D. hatimaye wazazi wa Jeta walikuja<br />

kumchukuwa wakamrejesha kwao


Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali 41 mpaka 50<br />

Mwaka uliopita shule yetu ilichaguliwa kuwa kituo cha kukutania kimichezo. Tulikuwa na michezo aina<br />

ainati shuleni kwetu. Maandalizi yalikuwa kabambe bin kabambe. Mdarisi wa michezo ya riadha alikuwa na gange ya tija<br />

na tijaranya kusimamia maandalizi hayo. Sisi wanagenzi tulikuwa katika mstari wa mbele kabisa kuhakikisha kila kitu<br />

kiliendelea sawa kwa ajili ya kuwa nilikuwa kiranja mkuu.<br />

Siku moja ya Jumatatu wakati wa macheo, mdarisi Bw. Jagina aligonga kengele akatuita twende uwanjani.<br />

Alituambia tutengeneze uwanja wa kufanyia michezo ya riadha. Tulichora mistari yenye safu sita kuzunguka uwanja. Alituambia<br />

hiyo ni sehemu ya wakimbiaji wa masafa au vitalifa mbalimbali. Tulijua kwamba wakimbiaji<br />

wa masafa mafupi, kiasi cha mita mia moja, wangetimuka usawa wa goli moja hadi jingine. Wakimbiaji wa mita<br />

mia mbili wangezunguka nusu ya mzunguko wa uwanja mzima.<br />

Walikuwapo wakimbiaji ambao wangezunguka uwanja mzima mara moja, mara mbili na mara kadhaa<br />

kulingana na masafa ya mbio zao. Mbio nyingine zilikuwa ni za kupokezana vijiti. Mbio hizo husisimua sana.<br />

Wapo wanariadha waliokimbia kwa kuchupachupa mithili ya kangaruu au Abunuwasi. Watoto wadogo walipaswa<br />

kukimbia kwa kusukuma magurudumu huku wengine wakiwa na mayai kwenye vijiko. Wengine walicheza mchezo<br />

wa kubururana kwa kamba. Hayo yote tulielezwa na mdarisi Bw. Jagina. Katikati ya uwanja paliandaliwa michezo anuwai<br />

kama vile; kutupa tufe, kurusha mkuki, kutupa kitumbua na ulengaji shebaha. Papo hapo palikuwa na sehemu iliyotengwa<br />

kwa michezo ya kuruka chini na kuruka juu. Fauka ya hayo, kulikuwa na kuruka kwa upondo.<br />

Tuliandaa mzunguko wa uwanja, mahali pa kukimbia kwa kuruka viunzi. mchezo huu ni wa ajabu zaidi.<br />

Ilipofika siku ya Jumamosi, shule yetu ilijaa na kufurika furifuri umati wa mahuluki kiasi cha kwamba mwenzako akikupotea,<br />

usingeweza kukutana naye tena, labda kwa bahati nasibu tu. Mimi nilikuwa mkimbiaji mahiri kiasi cha kusimama na<br />

kushindana na swara. Basi, kabla ya kwenda kwenye mbio zangu, nilipata nafasi ya kuangalia na kutazamatazama michezo<br />

ya kandanda, raga, mpira wa pete, magongo, jugwe, voliboli na netiboli. Hatimaye, nilijiunga na wapasua hewa wenzi<br />

wangu kama kina Maksudi, Hekima na wengineo.<br />

41. Shuleni kulikuwa na michezo aina ainati. Hivi<br />

ni kusema michezo ilikuwa<br />

A. haba<br />

B. anuwai<br />

C. aina ya kuchokesha<br />

D. migumu mno<br />

42. Shule yetu ilichaguliwa kuwa kituo chao<br />

kukutania kimichezo. Hivi ni kusema shule<br />

yetu<br />

A. ndiyo iliyokuwa kituo cha maandalizi<br />

B. ndiyo iliyowaalika wenyeji wa michezo<br />

hiyo<br />

C. ndiyo iliyokuwa mwenyeji<br />

D. ndiyo ingekutana na wachezaji wote wa<br />

michezo<br />

43. Wanagenzi walishirikiana na mdarisi wa<br />

michezo<br />

A. kuandaa timu yetu ya michezo<br />

B. kuwapokea wachezaji mbalimbali<br />

C. kuwa katika msitari wa mbele<br />

D. kuandaa yaliyohitajika kukimarisha<br />

michezo<br />

44. Kwa mujibu wa taarifa hii, mchezo wa<br />

kubururana kwa kamba ni<br />

A. jugwe B. magongo<br />

C. raga D. tufe<br />

45. Mbio za masafa marefu ni kama vile<br />

A. kuruka viunzi<br />

Available at www.kenyaexams.com<br />

4<br />

B. mbio za kupokezana vijiti<br />

C. mbio za mita mia moja<br />

D. mbio za nyikani<br />

46. Mchezo mwingine wa watoto wadogo ni<br />

A. kurusha mkuki<br />

B. kuruka kwa upande<br />

C. kukimbia mbio za kuchupachupa<br />

D. kucheza raga<br />

47. Kutupa vitumbua ni mchezo unaoshirikisha<br />

A. wazee pekee yake<br />

B. wazee na vijana<br />

C. wavulana na wazee<br />

D. wasichana na wazee<br />

48. Mwalimu wa michezo katika shule yetu<br />

alikuwa<br />

A. Hekima B. Maksuudi<br />

C. Hakutajwa jina D. Jagina<br />

49. Msimulizi wa taarifa hii alikuwa ni<br />

A. mwanariadha wa masafa marefu<br />

B. mwanariadha wa mbio za kuruka viunzi<br />

C. mwanariadha wa masafa mafupi<br />

D. kiranja mkuu lakini sio mwanariadha<br />

50. Kwa mujibu wa taarifa hii, ni mchezo upi<br />

mmoja ambao hauwezi kuchezwa na<br />

wasichana<br />

A. mwereka B. hakuna<br />

C. ndondi D. kuruka viunzi

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!