C:\Users\GITOGO\Documents\8 AI6 - Excel Exams
C:\Users\GITOGO\Documents\8 AI6 - Excel Exams
C:\Users\GITOGO\Documents\8 AI6 - Excel Exams
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
EXCEL EXAM<br />
A6<br />
KENYA EXAMS ONLINE<br />
DARASA LA NANE 2011<br />
KISWAHILI<br />
MUDA: SAA 1 DAKIKA<br />
40<br />
Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne. Chagua jibu lifaalo<br />
zaidi kati ya yale uliyopewa.<br />
Katika karia __1__, paliishi Mzee Kazi. Kondeni __2__ alikuwa amebuni wazo __3__ kuanzisha bustani iliyotoa<br />
mazao na matunda mengi. Kati ya matunda hayo yalikuwa machungwa aliyoyatumia kutengeneza __4__.<br />
Madhumuni ya sharubati yalikuwa ni matumizi yake binafsi na wanawe. Fauka ya hayo, alijitengea __5__ kwenye<br />
bonde __6__ sana. Aliyapa maudhi __7__ kwa adinasi yeyote. Pasina shaka __8__ uadilifu.<br />
1.A. chetu B. wetu C. yetu D. letu<br />
2.A. lake B. chake C. mwake D. vyake<br />
3.A. nzuri B. zuri C. mzuri D. wazuri<br />
4.A. mkandaa B. pure C. mashendea D. sharubati<br />
5.A. baiti B. kidurusi C. chumbani D. masika<br />
6.A. refu B. ndefu C. mrefu D. kurefu<br />
7.A. kipaumbele B. mawaidha C. kisogo D. jeki<br />
8.A. alitamani B. alithamiria C. alidhamania D. alithamani<br />
Serikali yetu __9__ kwa kutozingatia mchezo uitwao pool ambao unazidi kuwa __10__ katika sehemu mbalimbali<br />
nchini. Ni muhimu kuzingatia umuhimu wa __11__ kwani wachezaji wanaweza __12__ katika __13__ ya kimataifa.<br />
Mchezo huu ukichukuliwa kuwa kamari, juhudi za kuendeleza zitaambulia __14__ na mchezo __15__.<br />
9. A. imesifiwa B. imekashifiwa C. imeimarishwa D. imetukizwa<br />
10.A. maarufu B. marufuku C. changamoto D. duni<br />
11.A. kuudunisha B. kuuzorotesha C. kuupuuza D. kuuimarisha<br />
12.A. kushindwa B. kudhoofika C. kushindikana D. kutamba<br />
13.A. sifa B. safu C. siafu D. faifu<br />
14.A. pono B. ukingo C. nunge D. ushindi<br />
15.A. utaimarika B. utakufa C. utapendwa D. utafaulu<br />
Kutoka swali la 16 mpaka 30, chagua jibu lililo<br />
sahihi<br />
16. Safari iling’oa nanga wakati jua lilikuwa<br />
likivaa joho lake.<br />
A. Safari ilianza wakati wa machweo.<br />
B. Safari ilikamilika wakati wa adhuhuri.<br />
C. Safari ilianza wakati wa macheo.<br />
D. Safari ilikamilika wakati wa magharibi.<br />
17. Chagua orodha iliyo na vivumishi pekee.<br />
A. Kitisti, asteaste, uadilifu, ihsani<br />
B. Cheka, bingiri bingiri, imani, kashifu<br />
C. Kwa ajili, madhumuni, kichinichini,<br />
adhuhuri<br />
D. Sugu, kokote, mahiri, yapi<br />
18. Bainisha kundi ambalo lina visawe<br />
A. Fulusi, darhimu, ghawazi, njenje<br />
B. Amali, amani, amana, dhamana<br />
1<br />
Available at www.kenyaexams.com<br />
C. Gange, uganga, uchaga, changa<br />
D. Bashasha, bahasha, mabasha, mipasho<br />
19. Chagua sentensi iliyo katika mahali maalumu<br />
na ni dhahiri.<br />
A. Joka limejitoma humu shimoni<br />
B. Huko ndiko walikonaswa.<br />
C. Wachezaji wote wamefika hapa ugani.<br />
D. Aliingia humo.<br />
20. Umoja wa sentensi “Weledi wowote hawawezi<br />
kuiudhimisha mimea hiyo.”<br />
A. Mweledi yoyote hawezi kuidhinisha<br />
mmea huu.<br />
B. Mweledi yeyote hawezi kuidhinisha mmea<br />
huo.<br />
C. Mweledi yeyote hawezi kuidhinishwa na<br />
mmea huo.<br />
D. Mweledi yeyote hawezi kuidhinika na mmea<br />
huo.
21. Chagua kinyume cha sentensi.<br />
Mimi ndimi niliyeibandika.<br />
A. Wewe ndiwe uliyeibandika.<br />
B. Mimi ndiye niliyeibandua.<br />
C. Yeye ndiye aliyeibandua.<br />
D. Sisi ndisi tuliyeibandua.<br />
22. Chagua usemi wa taarifa ulio sawa wa<br />
“Nitakusubiri hapa kesho.” Maksuudi<br />
akasema.<br />
A. Maksuudi akasema kwamba atamsubiri<br />
hapa siku ya kesho.<br />
B. Maksuudi alisema kwamba angemsubiri<br />
hapa siku ya kesho.<br />
C. Maksuudi alisema kana kwamba<br />
atamsubiri hapo siku iliyofuatia.<br />
D. Maksuudi alisema kwamba angemsubiri<br />
hapo siku iliyofuata.<br />
23. Jaribosi ni kwa sikio, kigwe ni kwa<br />
A. shingo B. mkono<br />
C. mguu D. kiuno<br />
24. Chagua kivumishi na kielezi mtawalia kutoka<br />
sentensi.<br />
Mdarisi huyo aliwasili shuleni mafungulia<br />
nyama.<br />
A. aliwasili, shuleni<br />
B. huyo, mafungulianyama<br />
C. shuleni, mafungulianyama<br />
D. huyo, aliwasili<br />
25. Bainisha sentensi iliyo sahihi kisarufi.<br />
A. Angekuwako shuleni angaliwaalika wageni.<br />
B. Asingekuwa shuleni angewaalika wageni.<br />
C. Angalikuwako shuleni angaliwaalika<br />
wageni.<br />
D. Asingalikuwako shuleni asingewaalika<br />
wageni.<br />
26. Chagua sentensi ambayo ni muungano sahihi<br />
wa hizi.<br />
Mwehu alijitoma darasani.<br />
Mwehu aliwaogofya wanagenzi.<br />
A. Mwehu alijitoma darasani kwa mintaarafu<br />
ya kuwaogofya wanagenzi.<br />
B. Mwehu alijitoma darasani lau aliwaogofya<br />
wanagenzi<br />
C. Mwehu alijitoma darasani na kuwaogofya<br />
wanagenzi.<br />
D. Mwehu alijitoma darasani na kuwaogofya<br />
wanagenzi.<br />
27. Methali, “Kozi halei kuku wa wana” ina<br />
maadili gani?<br />
A. Hutuonya dhidi ya kuwa na marafiki.<br />
B. Hutuonya kuwa waangalifu na vitu vyetu.<br />
C. Hutuonya kuwa tusitumie uwezo wetu<br />
ovyovyo<br />
D. Hutuonya tusiwadharau wale wanaokula<br />
chakula duni.<br />
28. ‘Kupata pashua la moyo’ ni<br />
A. Kutokuwa na hamu ya kutenda jambo.<br />
B. Kuwa na wasiwasi kabla ya kuamua kutenda<br />
jambo.<br />
C. Msukumo wa kufanya jambo<br />
D. Kutokuwa na hamu ya kuendelea kufanya<br />
jambo.<br />
29. Barua inayopokewa kupitia tarakilishi ni<br />
A. wavuti B. pataninga<br />
C. mdahalisi D. mtandao<br />
30. Kitendawili “Kabla sijala nyama, mwanangu<br />
huila kwanza.” Jibu lake ni<br />
A. Kuku B. Kisu<br />
C. Kinu D. Jua<br />
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 31- 40<br />
Mambo yalipochupa mipaka na kukithiri, Adili hakuweza kustahimili tena ila alimwasa na kumwambia<br />
Jeta ya kuwa vitendo vyake alivyovitenda vilikuwa alijojo na vinamchukiza: itakuwa bora akiviacha na akawaepuka<br />
nemsi zake Jeta alikuja juujuu na kupandwa na ghaidhi si haba, ati kwa kuwa Adili anamtuhumu anafanya<br />
vitendo vibaya. Chambilecho wahenga, moyo wa kupenda hauna kinyongo. Adili alisunyaa na kunyerereka.<br />
Mambo yaliendelea na kutia maji maziwani. Sasa Adili hakuweza kustahimili tena ila alimweleza mkewe vizuri.<br />
Jeta aliangua kilio cha kutaka kureja mastakimuni kwa wavyele wake. Adili alisema ya kuwa hapana haja ya<br />
hayo, lakini ingekuwa bora pindi wangekaa baiti mbalimbali mpaka hasira zao ziishe. Adili alihamia kiambo<br />
kingine akamwachia nyo Jeta.<br />
Baada ya kupita haya, manzili yao na mahaba yao yakawa segemnege. Zilipita siku ayami pasina ya<br />
kuonana ana kwa ana’ ingawa Jeta akipeleka waraka kwao na yeye huletewa kuelezewa kila kitu, lakini hajawaarifu<br />
yakuwa ana ugomvi na mumewe. Baada ya mwia ayami wa kupatikana ugomvi na sintofahamu, Jeta hakujali ila aliletewa<br />
barua za simanzi na misaada iliyohitajika.<br />
Makazi ya upweke na kuwa mbali na adinasi aliyemuenzi yalimchosha adili, na aliondoka pasina kusema<br />
wapi anakwenda na lini atarudi. Kabla ya kuondoka alikuja kumwaga Jeta na kumsabihia chochote atakacho na<br />
kumpa ruhusa ya kwenda atakapo. Adili aling’oa habta na kwenda zake. Jeta alisalia akicheza kidege jinsi<br />
2
alivyotaka; mambo yalifurutu alipokuwa mumewe hayupo. Nyumba yake ilikuwa mithani ya mkahawa kila atakaye alikuwa<br />
na fursa ya mja na kufanya atakavyo. Hazikupita siku nyingi Jeta alichoka na maisha ya namna hiyo, na akataka kwenda<br />
kwao. Safari ilitengenezwa na Jeta akaondoka na kwenda kiamboni kwao.<br />
31. Kwa mujibu wa aya ya kwanza, Adili<br />
hakuweza kustahimili tena mambo ya Jeta<br />
kwa sababu<br />
A. yalikiuka miigo<br />
B. yalipindukia hasara<br />
C. yalipita maelezo<br />
D. yalikiuka mipaka<br />
32. Jeta alipandwa na ghaidhi si haba. Hivi ni<br />
kusema alikuwa na<br />
A. hamaki na hasira kwa sababu ya kubezwa<br />
na mumewe<br />
B. hasira kwa sababu ya kupuuzwa kwa ajili ya<br />
vitendo vyake<br />
C. hamaki kwa sababu vitendo vyake viliigwa<br />
na mumewe<br />
D. hasira kwa sababu ya kukanywa dhidi ya<br />
vitendo vyake<br />
33. Jeta alikasirika kwa sababu<br />
A. alidai mumewe alikuwa akimsingizia uovu<br />
B. ni kweli kuwa yeye alikuwa mwadilifu<br />
lakini mumewe akamsingizia uovu<br />
C. Adili aliwataka nemsi zake kuja nyumbani<br />
kwao<br />
D. Yeye alikuwa mama aliyekasirika mara<br />
kwa mara<br />
34. “Mambo yaliendelea na kutia maji maziwani”<br />
hii ina maana kuwa<br />
A. Adili aliendelea kumkashifu akimsingizia<br />
uovu<br />
B. Jeta aliendelea kukataa kuchota maji<br />
ziwani<br />
C. Jeta aliendelea na tabia yake mbaya bila<br />
kujali maonyo<br />
D. Adili na mkewe Jeta waliendelea kupigana<br />
nyumbani<br />
35. Kulingana na kifungu hiki, Adili alihamaki<br />
akamwachia nyumba Jeta kwa mintaarafu ya<br />
nini?<br />
A. Adili aliona ilikuwa heri kuondoka mpaka<br />
hasira zake zipungue kabisa<br />
B. Adili alikuwa amemchukia sana Jeta kwa<br />
sababu ya tabia yake<br />
C. Adili alikuwa amechokeshwa sana na<br />
maisha ya Jeta<br />
D. Adili alikuwa akitaka Jeta awe na upuuzi<br />
3<br />
36. Kwa mujibu wa kifungu hiki, neno ‘kukithiri’<br />
lina maana gani?<br />
A. kudhihirisha<br />
B. kuzidi<br />
C. kupungua<br />
D. kuonekana waziwazi<br />
37. Kulingana na kifungu hiki ulichosoma, neno<br />
linalotumiwa badala ya kuudhi ni gani?<br />
A. kukereketa<br />
B. kutuhumu<br />
C. kuchupa mipika<br />
D. kuchukiza<br />
38. Jeta alituhumiwa na mumewe Adili kwa<br />
sababu ya tabia yake. Hivi ni kusema Jeta<br />
A. aliadhibiwa na mumewe<br />
B. alinasihiwa na mumewe<br />
C. alishukiwa na mumewe<br />
D. alishutumiwa na mumewe<br />
39. Baada ya kupita haya, manzili yao na mahaba<br />
yao yakawa segemnege. Hivi ni kusema<br />
baadaye<br />
A. mambo yao na mapenzi yao yalikuwa<br />
ndivyo sivyo<br />
B. mambo yao na mapenzi yao yalikuwa<br />
shwari<br />
C. mambo yao na mapenzi yao yalirudia hali<br />
ya kawaida<br />
D. mambo yao na mapenzi yao yalitengenea<br />
40. Kwa mujibu wa kifungu hiki, baada ya mume<br />
kuondoka nyumbani mwake kwa muda mrefu,<br />
A. hatimaye tabia ya mkewe Adili ilibadilika<br />
na mumewe akarejea kiamboni kwao<br />
B. hatimaye tabia ya mkewe ilimfanya ajute<br />
mpaka akahiari kuondoka na kwenda kwa<br />
wavyele wake.<br />
C. hatimaye marafiki zake Jeta walimsaidia<br />
mpaka nyumba ikawa kama mkahawa<br />
D. hatimaye wazazi wa Jeta walikuja<br />
kumchukuwa wakamrejesha kwao
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali 41 mpaka 50<br />
Mwaka uliopita shule yetu ilichaguliwa kuwa kituo cha kukutania kimichezo. Tulikuwa na michezo aina<br />
ainati shuleni kwetu. Maandalizi yalikuwa kabambe bin kabambe. Mdarisi wa michezo ya riadha alikuwa na gange ya tija<br />
na tijaranya kusimamia maandalizi hayo. Sisi wanagenzi tulikuwa katika mstari wa mbele kabisa kuhakikisha kila kitu<br />
kiliendelea sawa kwa ajili ya kuwa nilikuwa kiranja mkuu.<br />
Siku moja ya Jumatatu wakati wa macheo, mdarisi Bw. Jagina aligonga kengele akatuita twende uwanjani.<br />
Alituambia tutengeneze uwanja wa kufanyia michezo ya riadha. Tulichora mistari yenye safu sita kuzunguka uwanja. Alituambia<br />
hiyo ni sehemu ya wakimbiaji wa masafa au vitalifa mbalimbali. Tulijua kwamba wakimbiaji<br />
wa masafa mafupi, kiasi cha mita mia moja, wangetimuka usawa wa goli moja hadi jingine. Wakimbiaji wa mita<br />
mia mbili wangezunguka nusu ya mzunguko wa uwanja mzima.<br />
Walikuwapo wakimbiaji ambao wangezunguka uwanja mzima mara moja, mara mbili na mara kadhaa<br />
kulingana na masafa ya mbio zao. Mbio nyingine zilikuwa ni za kupokezana vijiti. Mbio hizo husisimua sana.<br />
Wapo wanariadha waliokimbia kwa kuchupachupa mithili ya kangaruu au Abunuwasi. Watoto wadogo walipaswa<br />
kukimbia kwa kusukuma magurudumu huku wengine wakiwa na mayai kwenye vijiko. Wengine walicheza mchezo<br />
wa kubururana kwa kamba. Hayo yote tulielezwa na mdarisi Bw. Jagina. Katikati ya uwanja paliandaliwa michezo anuwai<br />
kama vile; kutupa tufe, kurusha mkuki, kutupa kitumbua na ulengaji shebaha. Papo hapo palikuwa na sehemu iliyotengwa<br />
kwa michezo ya kuruka chini na kuruka juu. Fauka ya hayo, kulikuwa na kuruka kwa upondo.<br />
Tuliandaa mzunguko wa uwanja, mahali pa kukimbia kwa kuruka viunzi. mchezo huu ni wa ajabu zaidi.<br />
Ilipofika siku ya Jumamosi, shule yetu ilijaa na kufurika furifuri umati wa mahuluki kiasi cha kwamba mwenzako akikupotea,<br />
usingeweza kukutana naye tena, labda kwa bahati nasibu tu. Mimi nilikuwa mkimbiaji mahiri kiasi cha kusimama na<br />
kushindana na swara. Basi, kabla ya kwenda kwenye mbio zangu, nilipata nafasi ya kuangalia na kutazamatazama michezo<br />
ya kandanda, raga, mpira wa pete, magongo, jugwe, voliboli na netiboli. Hatimaye, nilijiunga na wapasua hewa wenzi<br />
wangu kama kina Maksudi, Hekima na wengineo.<br />
41. Shuleni kulikuwa na michezo aina ainati. Hivi<br />
ni kusema michezo ilikuwa<br />
A. haba<br />
B. anuwai<br />
C. aina ya kuchokesha<br />
D. migumu mno<br />
42. Shule yetu ilichaguliwa kuwa kituo chao<br />
kukutania kimichezo. Hivi ni kusema shule<br />
yetu<br />
A. ndiyo iliyokuwa kituo cha maandalizi<br />
B. ndiyo iliyowaalika wenyeji wa michezo<br />
hiyo<br />
C. ndiyo iliyokuwa mwenyeji<br />
D. ndiyo ingekutana na wachezaji wote wa<br />
michezo<br />
43. Wanagenzi walishirikiana na mdarisi wa<br />
michezo<br />
A. kuandaa timu yetu ya michezo<br />
B. kuwapokea wachezaji mbalimbali<br />
C. kuwa katika msitari wa mbele<br />
D. kuandaa yaliyohitajika kukimarisha<br />
michezo<br />
44. Kwa mujibu wa taarifa hii, mchezo wa<br />
kubururana kwa kamba ni<br />
A. jugwe B. magongo<br />
C. raga D. tufe<br />
45. Mbio za masafa marefu ni kama vile<br />
A. kuruka viunzi<br />
Available at www.kenyaexams.com<br />
4<br />
B. mbio za kupokezana vijiti<br />
C. mbio za mita mia moja<br />
D. mbio za nyikani<br />
46. Mchezo mwingine wa watoto wadogo ni<br />
A. kurusha mkuki<br />
B. kuruka kwa upande<br />
C. kukimbia mbio za kuchupachupa<br />
D. kucheza raga<br />
47. Kutupa vitumbua ni mchezo unaoshirikisha<br />
A. wazee pekee yake<br />
B. wazee na vijana<br />
C. wavulana na wazee<br />
D. wasichana na wazee<br />
48. Mwalimu wa michezo katika shule yetu<br />
alikuwa<br />
A. Hekima B. Maksuudi<br />
C. Hakutajwa jina D. Jagina<br />
49. Msimulizi wa taarifa hii alikuwa ni<br />
A. mwanariadha wa masafa marefu<br />
B. mwanariadha wa mbio za kuruka viunzi<br />
C. mwanariadha wa masafa mafupi<br />
D. kiranja mkuu lakini sio mwanariadha<br />
50. Kwa mujibu wa taarifa hii, ni mchezo upi<br />
mmoja ambao hauwezi kuchezwa na<br />
wasichana<br />
A. mwereka B. hakuna<br />
C. ndondi D. kuruka viunzi