26.09.2013 Views

نﯾﺟوزﻟا نﯾﺑ قوﻘﺣﻟا Haki Za Mume Na Mke - Alhidaaya.com

نﯾﺟوزﻟا نﯾﺑ قوﻘﺣﻟا Haki Za Mume Na Mke - Alhidaaya.com

نﯾﺟوزﻟا نﯾﺑ قوﻘﺣﻟا Haki Za Mume Na Mke - Alhidaaya.com

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

نيجوزلا نيب قوقحلا<br />

<strong>Haki</strong> <strong>Za</strong> <strong>Mume</strong> <strong>Na</strong><br />

<strong>Mke</strong><br />

(<strong>Na</strong>saha <strong>Za</strong> Shaykh Kwa Wanandoa)<br />

ـھ 1432-11-02<br />

Muftiy al-´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah<br />

Aal ash-Shaykh<br />

Mfasiri:<br />

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush<br />

©


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

يحرلا نمحرلا ﷲ مسب<br />

Himidi zote zi <strong>Za</strong>ke Allaah. Tunamhimidi na kumtaka msaada na<br />

tunamuomba msamaha na tunatubia Kwake. <strong>Na</strong> tunajikinga Kwake na shari<br />

za nafsi zetu na matendo yetu maovu.<br />

<strong>Haki</strong>ka yule Aliyemuongoza Allaah hakuna wa kumpoteza. <strong>Na</strong> Aliyempoteza<br />

hakuna wa kumuongoza.<br />

<strong>Na</strong>shuhudia ya kwamba hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah<br />

wa pekee Asiyekuwa na mshirika. <strong>Na</strong> ninashuhudia ya kwamba Muhammad<br />

ni mja Wake na Mtume Wake swalah za salaam zimuendee na ahli zake na<br />

Maswahaba wake mpaka siku ya mwisho. Amma ba´ad:<br />

Enyi watu! Mcheni Allaah ukweli wa kumcha. Enyi waja wa Allaah! <strong>Haki</strong>ka<br />

familia ndio msingi wa jamii; makazi ambayo Allaah Ameyafanya kwa mume<br />

kuwa ndio makazi yake na kukaa humo. Katika ndoa kuna utulivu wa nafsi,<br />

na kupumua, na mafanikio ya kutokufanya mapenzi na kuwa na usafi wa<br />

moyo. <strong>Na</strong> ndoa ni uhusiano uliyo imara, na mkataba madhubuti, [kama<br />

Asemavyo Allaah]:<br />

اظيلغ ً ِ َ اقاثيم ً َ ِّ مكنم ُ ِ نذخأو َ ْ َ َ َ<br />

“<strong>Na</strong> wao wanawake wamechukua kwenu ahadi iliyo madhubuti.” (04:21)<br />

<strong>Na</strong> ni ahadi ya wanandoa, kutendeana mema, na ni kuyawekea nguvu maisha<br />

ya kindoa. <strong>Na</strong> Katubainishia Allaah katika Kitabu Chake na Mtume Wake (<br />

ملسو هيلع ﷲ ىلص ) ahkaam za ndoa wazi kabisa. Zipi haki za mwanaume na yapi<br />

ya wajibu juu yake; na ni zipi haki za mwanamke na ni yapi ya wajibu juu<br />

yake.


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

Wakati wanandoa [mume na mke]watachunga haki hizi na yaliyo yawajibu<br />

kwa kila mmoja, yanakuwa maisha yao - maisha mazuri.<br />

Enyi wanandoa! Ikiwa kweli mnataka maisha mazuri yaliyo thabiti,<br />

yaliyojengeka katika misingi ya mahaba na mapenzi; mwatakiwa nyote<br />

wawili kumchungia [kumtekelezea] kila mmoja haki ya mwenzake kwa<br />

usawa katika maisha haya.<br />

Ewe dada mwenye thamani! <strong>Haki</strong>ka mume wako ana haki juu yako na ya<br />

wajibu; ni lazima kumtekelezea [kwa kufanya hivyo] ni utiifu kwa Allaah, na<br />

ni ukurubisho unajikurubisha kwao kwa Allaah. Katika haki kubwa za mume<br />

wako juu yako, ni kumtii katika mema. <strong>Haki</strong>ka kumtii katika mema ni jambo<br />

la wajibu kwako. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):<br />

“Wakikutiini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure.” (04:34)<br />

ًلايبس<br />

ِ َ نھيلع َّ ِ ْ َ َ اوغبت ْ ُ ْ َ َلاف َ مكنعطأ ْ ُ َ ْ َ َ نإف ْ ِ َ<br />

Utiifu huwa katika mema tu. Hakuna utiifu kwa yeyote katika kumuasi<br />

Allaah. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):<br />

“<strong>Na</strong> kaeni nao kwa wema.” (04:19)<br />

فورعملاب ِ ُ ْ َ ْ<br />

ِ نھورشاعو َّ ُ ُ ِ َ َ<br />

Ewe mwanamke wa Kiislamu! <strong>Haki</strong>ka mume wako ana haki juu yako ya<br />

kumtii katika mema. <strong>Na</strong> Mtume ( ملسو هيلع ﷲ يلص ) anasema:


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

"Akimwita mume mke wake kitandani, [asije] na mume wake akamkasirikia,<br />

Malaika wanamlaani mpaka asubuhi."<br />

Katika kumtii mume wako kuna thawabu kubwa mbele ya Allaah. Anasema<br />

Mtume ( ملسو هيلع ﷲ يلص ):<br />

"Akiswali mwanamke [swalah zake] tano, na akafunga mwezi wake,<br />

akahifadhi tupu yake na akamtii mume wake ataingia Peponi katika mlango<br />

wowote aupendao [katika milango minane ya Peponi]."<br />

Hii ni fadhila kubwa na neema kubwa kwa Allaah kwako, ewe dada wa<br />

Kiislamu kwa kumtii mume wako katika mema.<br />

<strong>Na</strong> katika haki zake za wajibu juu yako, ni kumtekelezea haja zake atapotaka<br />

hilo. <strong>Haki</strong>ka katika ndoa kuna kuzihifadhi tupu kwa halali, kuilinda na<br />

aliyomuharamishia Allaah kwake.Anasema Mtume ( ملسو هيلع ﷲ يلص ):<br />

"Atapomwita mume mke wake juu ya kitanda na akakataa, akamghadhibikia,<br />

hivyo Malaika humlaani mpaka asubuhi."<br />

<strong>Na</strong> kwa hili kaelekezwa mume kwa mkewe, na wakajaaliwa hilo kuwa ni<br />

swadaqah kwa wote wawili - mume na mke. Anasema Mtume ( ملسو هيلع ﷲ يلص<br />

):<br />

"<strong>Na</strong> kumuingilia mkeo ni swadaqah.” Wakasema (Maswahabah) na je, katika<br />

kupata raha binafsi mmoja wetu analipwa??! Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص )<br />

akasema: “Je, mnaonaje lau mtu huyo angeingiza [tupu yake] katika haramu,<br />

je, ingelikuwa ni shari juu yake [ya madhambi, maradhi, adhabu]?, wakasema:<br />

ndio. Akasema Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ): “Hivyo ndivyo atakapoweka [tupu<br />

yake] katika halali atalipwa.” [Muslim]<br />

<strong>Na</strong> katika haki za mume wako juu yako, ni kuwa na adabu na kumheshimu,<br />

hii ni amaanah umeaminiwa kwayo.


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

Mwanamke mwema, mwenye mtazamo mzuri kumuangalia mume wake;<br />

mwenye kujihifadhi ili kudumisha sifa ya kitanda chake, hivyo ni bora.<br />

ُﷲ ّ ظفح َ ِ َ امب َ ِ بيغلل ِ ْ َ ْ ِّ تاظفاح ٌ َ ِ َ تاتناق ٌ َ ِ َ تاحلاصلاف ُ َ ِ َّ َ<br />

“Basi wanawake wema ni wale wenye kutii na wanaojilinda hata katika siri<br />

kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajilinde.” (04:34)<br />

<strong>Na</strong> katika Hadiyth, anasema ( ملسو هيلع ﷲ يلص ):<br />

"Bora ya raha kwa mwanaume ni kupata mke mwema, [ambaye] akimtazama<br />

anafurahi, na akimuamrisha [kitu] anamtii, na [mume] akiwa mbali naye<br />

hujihifadhi mwenyewe [mwanamke] na mali [ya mumewe]."<br />

Ewe dada ´Aziyzah! <strong>Haki</strong>ka kumridhisha kwako mume wako na<br />

kumheshimu, ni jambo jema, na ni kitu kizuri, na ni jambo la wajibu juu yako<br />

Kishari´ah; Usidanganyike na hayo mafilamu machafu, ambayo yanakuweka<br />

mbali na heshima yako na fadhila zako na yaliyojaa maovu. Allaah<br />

Atusamehe sote kwa hayo.<br />

<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako, usimruhusu yeyote kuingia nyumbani bila<br />

idhini [ruhusa] yake. Utaejua kuwa hatomridhia kuingia usimruhusu. Kwa<br />

kuwa Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) anasema:<br />

"Si halali kwa mwanamke kumruhusu yeyote kuingia nyumbani kwa mume<br />

wake ila kwa idhini [ruhusa] yake."<br />

<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako, kuchunga nyumba yake na mali yake.<br />

Katika Hadiyth [anasema Mtume]:


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

"Mwanamke ni mchungaji katika nyumba ya mume wake na ataulizwa [na<br />

Allaah] kwa alichokichunga."<br />

<strong>Na</strong> kakataza Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) kutoa katika mali ya mume wako ila<br />

kwa idhini yake [mume].<br />

<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako, usimkalifishe kukuhudumia [kukupatia<br />

matumizi] kile asichokiweza na ni kizito kwake na hakiwezi. <strong>Haki</strong>ka Allaah<br />

Anasema:<br />

ُﷲ َّ ُهاتآ َ امم َّ ِ قفنيلف ْ ِ ُ ْ َ هقزر ُ ُ ْ<br />

ِ هيلع ِ ْ َ َ ردق َ ِ ُ نمو َ َ هتعس ِ ِ َ َ نم ِّ ةعس ٍ َ َ وذ ُ قفنيل ْ ِ ُ ِ<br />

“Mwenye wasaa atoe kadiri ya wasaa wake, na mwenye dhiki atoe katika<br />

alichompa Allaah. Allaah Hamkalifishi mtu ila kwa kadiri ya alicho mpa.”<br />

(65:07)<br />

<strong>Na</strong> katika haki za mume juu mke, ni kuwapa malezi watoto na kuwaongoza;<br />

nyote wawili mume na mke ni wenye kushiriki katika jambo hili muhimu<br />

sana. Kuwapa malezi vijana na kuwaandaa wawe vizuri, na kuwaamrisha<br />

mema na kuwatahadharisha na shari. <strong>Na</strong> kule baba kuwa kwake kiigizo bora<br />

kwa watoto wakiume, katika kheri na wema. <strong>Na</strong> mama ana jukumu lakuwa<br />

kiigizo bora kwa mabanati wake, kwa kujisitiri vizuri na usafi wa moyo, na<br />

dhamira ya maadili ya thamani.<br />

<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako, ni wewe kubaki nyumbani na kutotoka ila<br />

tu kwa dharurah. Ama kutoka kwako nyumbani bila ya dharurah kunaifanya<br />

nyumba kuzorota na kukosekana mwenye kuilinda na kuihifadhi.<br />

<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako ni wewe kutomuudhi kwa maneno mabaya.<br />

Mwambie [muongeleshe] maneno mazuri yenye baraka. Kuuachia ulimi<br />

hovyo, haimpasi mwanaume wala mwanamke. <strong>Na</strong> imepokelewa kutoka kwa<br />

Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) kuwa amesema:<br />

"Akimuudhi mwanamke mume wake duniani, anasema mke wake katika<br />

Huur al-'Iyin "Allaah Akuangamize usimuudhi, kwani huyo ni mtu wetu -<br />

imekaribia kuachana nawe na kuja kwetu."


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

<strong>Na</strong> katika haki za mume wajibu juu yako, usijikurubishe kwa Allaah<br />

kwaswalah za naafilah [sunnah] na swawm [za sunnah] ila kwa idhini<br />

[ruhusa] ya mume wako.<br />

<strong>Haki</strong>ka haki yake [mume] ni yenye kutangulia. <strong>Na</strong> kwa hili anasema Mtume (<br />

ملسو هيلع ﷲ ىلص ):<br />

"Si halali kwa mwanamke kufunga, na mume wake yuko ila kwa idhini yake."<br />

Katika haki za mume juu yako, aliyobainisha Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص )<br />

kuwatahadharisha wanandoa [mume na mke] kutoa siri ya uhusiano wa<br />

kindoa [yafanyikayo ndani], akasema kuwa mwenye kufanya hivyo ni katika<br />

watu waovu sana. Kwa kuwa hii ni dalili ya ukosevu wa haya na adabu.<br />

(<strong>Haki</strong> <strong>Za</strong> <strong>Mke</strong> Juu Ya <strong>Mume</strong>)<br />

Ndugu mume karimu, hakika mke wako ana ya wajibu pia juu yako na haki<br />

zake. Lazima umtimizie - kama jinsi yeye kwako ana haki zake na ya wajibu,<br />

na wewe hali kadhalika una haki na ya wajibu juu yake. Lazima umtimizie.<br />

<strong>Haki</strong> yake kubwa juu yako, ni wewe kumpa mahari kwa ukamilifu; sawa<br />

akiwa ni mwenye uwezo au si mwenye uwezo. Kwa kuwa Allaah Anasema:<br />

ائيرم ً<br />

ِ َّ ائينھ ً ِ َ هولكف ُ ُ ُ َ اسفن ً ْ َ هنم ُ ْ ِّ ءيش ٍ ْ َ نع َ مكل ْ ُ َ نبط َ ْ ِ نإف ِ َ ةلحن ً َ ْ ِ نھتاقدص َّ ِ ِ َ ُ َ ءاسنلا َ َّ اوتآو ْ ُ َ<br />

“<strong>Na</strong> wapeni wanawake mahari yao hali ya kuwa nikipawa. Lakini<br />

wakikutunukieni kitu katika mahari - kwa radhi yao, basi kileni kiwashuke<br />

kwa raha.” (04:04)<br />

Ni wajibu kumpa haki yake kamili. Katika haki zake juu yako, ni kumpa<br />

matumizi [kumuhudumia] chakula, mavazi na makazi. Anasema Allaah<br />

(Ta´ala):


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

فورعملاب ِ ُ ْ َ ْ<br />

ِ نھتوسكو َّ ُ ُ َ ْ ِ َ نھقزر َّ ُ ُ ْ<br />

ِ هل ُ َ دولوملا ِ ُ ْ َ ْ ىلعو َ َ َ<br />

“<strong>Na</strong> ni juu ya mzazi wa kiume kuwapatia chakula chao na nguo kwa<br />

ma’aruwf (mujibu wa ada).” (02:233)<br />

Akasema tena:<br />

نھيلع َّ ِ ْ َ َ اوقيضتل ُ ِّ َ ُ ِ نھوراضت َّ ُ ُّ َ ُ لاو َ َ مكدجو ْ ُ ِ ْ ُ نم ِّ متنكس ُ َ َ ثيح ُ ْ َ نم ْ ِ نھونكسأ َّ ُ ُ ِ ْ َ<br />

“Wawekeni humo humo mnamokaa nyinyi kwa kadiri yapato lenu, wala<br />

msiwaletee madhara kwa kuwadhiki.”(65:06)<br />

Matumizi ni wajibu kwa mume kumpa mke wake, kwa mujibu wa mkataba<br />

wa ndoa baina yao. <strong>Na</strong> Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص )anasema kumwambia Saad<br />

bin Abi Waqqas kuhusiana na hili:<br />

"<strong>Haki</strong>ka hutotoa matumizi kwa kutaka Uso wa Allaah isipokuwa utapewa<br />

ujira kwalo, hata ikiwa ni kitu kidogo utachokiweka kwenye kinywa cha<br />

mkeo."<br />

<strong>Na</strong> katika haki zake juu yako, ni kukaa nae kwa wema kwa adabu za<br />

Kishari´ah. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):<br />

“<strong>Na</strong> kaeni nao kwa wema.” (04:19)<br />

Anasema tena:<br />

فورعملاب ِ ُ ْ َ ْ<br />

ِ نھورشاعو َّ ُ ُ ِ َ َ<br />

فورعملاب ِ ُ ْ َ ْ<br />

ِ نھيلع َّ ِ ْ َ َ يذلا ِ َّ لثم ُ ْ<br />

ِ نھلو َّ ُ َ َ


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

“<strong>Na</strong> hao wanawake wana kama ile (haki) iliyo juu yao kwa ma’aruwf (mujibu<br />

wa shari’ah).” (02:228)<br />

<strong>Na</strong> anasema Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ):<br />

"Mbora [wa wanaume ni] aliye mbora kwa familia yake, na mimi ni mbora<br />

kwa familia yangu."<br />

<strong>Na</strong> katika haki zake juu yako, ni kumlinda [asipatwe na] adhabu ya Allaah<br />

kwa kumuamrisha mema na kumtahadharisha na shari [maovu].<br />

ةراجحلاوسانلا ُ َ َ ِ ْ َ ُ َّ اھدوقو َ ُ ُ َ اران ً َ مكي ْ ُ ِلھأو ْ َ َ مكسفنأ ْ ُ َ ُ َ اوق ُ اونمآ ُ َ نيذلا َ ِ َّ اھيأ َ ُّ َ ايَ<br />

“Enyi mlioamini! Jilindeni nafsi zenu na ahli zenu na Moto ambao kuni zake<br />

ni watu na mawe.” (66:06)<br />

Anasema tena:<br />

ىوقتلل َ ْ َّ ِ ةبقاعلاو ُ َ ِ َ ْ َ كقزرن َ ُ ُ ْ َ نحن ُ ْ َّ اقزر ً ْ<br />

ِ كلأسن َ ُ َ ْ َ لا َ اھيلع َ ْ َ َ ربطصاو ْ ِ<br />

َ ْ َ ةلاصلاب ِ َ َّ ِ كلھأ َ َ ْ َ رمأو ْ ُ ْ َ<br />

“<strong>Na</strong> waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo. Sisi<br />

hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. <strong>Na</strong> mwisho mwema ni<br />

kwa mcha Mungu.” (20:132)<br />

Katika haki zake juu yako, ni wewe kuwa na wivu kwake, wivu ambao ni<br />

wakweli [mzuri] - kwa kumtakia kheri, na kumuonya na kila shari uijuayo;<br />

bila ya kuwa na wasiwasi [katika wivu wako] na mashaka, na matarajio ya<br />

makosa; bali iwe ni wivu ulioubeba kwa ajili ya kumtakia kheri na kumlinda<br />

asipatwe na shari. Usiwe ni wivu wa wasiwasi na mashaka na kuangalia tu<br />

udhaifu [wake]. Ni watu wangapi wamekuwa na aina ya maradhi kama haya,<br />

na kuona wengine si kama yeye. Ni wajibu kumcha Allaah.


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

Kama inavyotakikana kwa mwanamke pia kuwa na wivu kwa mume wake.<br />

Lakini anapaswa kuwa na wivu uliojengeka katika mambo ya wazi; si kwa<br />

uchunguzi wa fujo na vurugu na kuchunguza namba za simu - ukaguzi<br />

nakadhalika, jambo ambalo linaweza kusababisha shari na balaa baina yao.<br />

<strong>Na</strong> katika haki za mwanamke juu ya mume wake, ni kumfunza mambo ya<br />

dini yake asiyoyajua na yatamsaidia kufanya mema.<br />

<strong>Na</strong> katika haki zake juu yako, ni [wewe] mwanaume kuwa mwadilifu baina<br />

ya wake [zako] ukioa wake wengi [ukewenza]. Anasema Mtume ( هيلع ﷲ ىلص<br />

ملسو ):<br />

"Yule mwenye wake wawili, akamkandamiza mmoja zaidi kuliko mwengine,<br />

atakuja siku ya Qiyaamah na bega lake likiwa limepinda."<br />

<strong>Na</strong> katika haki zake juu yako, usimkandamize na kumnyima haki zake kwa<br />

kumdhulumu na kumfanyia uadui, kwani hakika dhuluma ni gizo siku ya<br />

Qiyaamah. Usitumii udhaifu wake na ukosevu wake wa mabavu, ukamuonea<br />

[mkandamiza] bila ya hatia yoyote, ukamtusi na kumtuhumu kwa mambo<br />

ambayo kajitenga nayo mbali.<br />

Katika haki zake juu yako, ni kumhifadhia mali yake na usimtumie na<br />

ukaitumia mali yake; ukawa unamtisha kwa talaka akiomba haki yake na<br />

ukawa unaitumia. Yote haya ni katika uonevu. <strong>Haki</strong>ka wajibu wako ni wewe<br />

kumhudumia sawa na uwezo wako, umejiingiza katika [maisha ya] ndoa<br />

pambana na ndoa hii.<br />

Wakati mke atapotekeleza [timiza] wajibu alionao juu ya mume wake, na<br />

wakati mume atapotekeleza [timiza] wajibu alionao juu ya mke wake; hivyo<br />

maisha na hali huwa nzuri. <strong>Na</strong> wakati nyumba itaachwa, wakati kila mmoja<br />

atapoacha kutekeleza haki ya mwenzake; wakati mke atapoacha kumtimizia<br />

mume haki zake, au mume akaacha kumtimizia mwanamke haki zake; hivyo<br />

hutokea shari na uharibifu.


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

Ama kila mmoja akichunga haki alionayo juu ya mwenzake, hakika hii ndio<br />

sababu ya furaha na kuwa na maisha mazuri na familia huishi katika<br />

muelekeo na usalama.<br />

Enyi watu! Mcheni Allaah (Ta´ala) ukweli wa kumcha. Shari´ah ya Uislamu<br />

imekuja kutekeleza uadilifu kwa njia zote. <strong>Na</strong> katika hayo ni uadilifu baina ya<br />

wanandoa, kwa kila mwanandoa mmoja kumtimizia mwengine. Mwanamke<br />

atimize yaliyo ya wajibu juu yake kwa mume wake; na mume atimizeyaliyo<br />

ya wajibu juu yake kwa mke wake.<br />

Hivyo ndivyo yalivyo maisha ya ndoa yaliyofanywa na Uislamu kwa<br />

wanandoa ili waishi maisha ya furaha; maisha ya furaha na ridhaa.<br />

Tumcheni Allaah katika nafsi zetu [kwa kila mmoja kumtimizia mwenzake<br />

haki yake].<br />

Ewe mume ´Aziyz! <strong>Haki</strong>ka kutania [kucheza] na mke [wako], wacheza naye<br />

na huku wamuelekeza katika mema ni katika sababu zinazoimarisha misingi<br />

ya maisha ya ndoa. <strong>Na</strong> hakika utoaji onyo mara kwa mara pasina sababu za<br />

kueleweka, ni katika sababu ya kufarakana.<br />

Tahadhari muwe na kukithirisha maonyo ya mara kwa mara bila sababu.<br />

Tahadhari na kufuatilia vijikosa vidogo vidogo ambavyo havina uziro<br />

wowote. Kuwa mwenye kupuuza vijikosa ilimraditu havina kasoro katika<br />

heshima na cheochako, ni juu yako kuwa na subira kwa baadhi ya makosa;<br />

hakuna yeyote aliyesalimika kutokana na makosa. Anasema Mtume ( ﷲ ىلص<br />

ملسو هيلع ):<br />

"Mwanaume asimchukie muumini mwanamke [mkewe], akichukizwa na<br />

moja ya tabia yake atapendezwa na nyingine."<br />

Anasema tena [Mtume]:<br />

"Ninawahusieni kuwatendea wanawake wema."<br />

Subira kwa kila mmoja kumvumilia mwenzake ni jambo linalotakikana.<br />

Mwanamke awe na subira kwa mume wake, na kwa baadhi ya makosa<br />

kunako tabia yake na mwenendo wake ilimradi haijafikia katika kumvulia<br />

cheo na heshima. <strong>Na</strong> mume awe na subira juu ya baadhi ya makosa ya mke


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

wake, ilimradi haijafika kumvulia cheo na heshima. Iwe wote wanasaidizana<br />

kutengeneza na kumezea [kasoro] za kila mmoja kwa mwenzake.<br />

<strong>Na</strong> Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) kamtahadharisha mwanamke wa Kiislamu kwa<br />

kukufuru kwake wema na kumlalamikia sana mume. Akasema kuwa ameona<br />

moto na wakazi wake wengi ni wanawake; kwa tuoacha kwao kulalama na<br />

kukufuru kwao wema.<br />

Lau utamtendea mmoja wao wema maisha yote, akaona kutoka kwako kitu<br />

[kasoro], atasema "Sijawahi kuona kheri [wema] wowote kutoka kwako katu."<br />

Ndugu wapenzi! Matatizo ya kindoa yanakuwa wakati mwingine kwa sababu<br />

zisizokuwa na maana. Wakati wakutafakari na kuzingatia vizuri mtu anakuja<br />

kuona kuwa sababu [zilizoleta matatizo] ni za kijinga zisizo na maana yoyote.<br />

Ni juu ya wazazi wa ndugu wa mume au mke kutatua matatizo haya ndani ya<br />

nyumba, na yasiendelee mambo kama haya hadi yakatoka nje ya nyumba.<br />

<strong>Mume</strong> amalize tatizo lake na mke wake au na famili yake. <strong>Na</strong> juu ya familia<br />

yake mwanamke kumkanya wakiona yeye ndo yuko makosani. <strong>Na</strong> familia ya<br />

mwanamume hali kadhalika wamkanye watapoona kuwa yeye [mume] ndo<br />

yuko makosani.<br />

Familia zote mbili zikisaidizana pamoja na mume na mke kutatua tatizo hili,<br />

hupatikana ufumbuzi mzuri. Ama ikiwa hawatokuwa makini na kujichunga,<br />

huwaka fitna. Mwanaume [baba mkwe] akawa na kasumba kwa binti yake<br />

bila kujali makosa yake; au mwanamume akawa na kasumba ya kushikilia rai<br />

yake bila kujali makosa yake. <strong>Haki</strong>ka huo ni msiba mkubwa.<br />

<strong>Na</strong> Mtume wetu ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) kamtahadharisha mwanamke wa Kiislamu<br />

kuomba talaka pasina sababu ya msingi. Akasema:<br />

"Mwanamke akimuomba mume wake talaka pasina sababu muhimu, ni<br />

haramu juu yake harufu ya Pepo."<br />

Hivyo ni wajibu kwao mauqif yao iwe ya heshima, mauqif ya kutatua tatizo,<br />

na kumaliza mgogoro huu, na kuzingatia tatizo hili - liangaliwe vizuri.<br />

Iangaliwe sababu na itatuliwe, na qadhiya hii ishughulikiwe ndani ya


www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />

nyumba. Isende ikatoka nje, khabari ikawafikia watu nje wasiyokuwa na<br />

thamani kwao, na wasiyowapendea kheri - wakaja kuiharibu nyumba na<br />

kuingamiza katika msingi wake. Hukumsikia Allaah Akisema:<br />

ريخ ٌ ْ َ حلصلاو ُ ْ ُّ َ احلص ً ْ ُ امھنيب َ ُ َ ْ َ احلصي َ ِ ْ ُ نأ َ امھيلع َ ِ ْ َ َ حانج َ ْ َ ُ َلاف َ اضارعإ ً َ ْ ِ وأ ْ َ ازوشن ً ُ ُ اھلعب َ ِ ْ َ نم ِ تفاخ ْ َ َ ةأرما ٌ َ َ ْ نإو ِ ِ َ<br />

“<strong>Na</strong> mwanamke akichelea kutupwa au kutojaliwa na mumewe, basi si vibaya<br />

kwao wakisikizana kwa suluhu.<strong>Na</strong> suluhu ni bora.” (04:128)<br />

Kutafuta suluhu baina ya wanandoa ni kheri, suluhu inayohitaji kuhifadhi<br />

haki ya kila mmoja, suluhu ya kutaka kutatua tatizo na kumaliza ugomvi,<br />

suluhu kurudi katika hali ya kawaida, na maisha ya ndoa kuendelea utulivu<br />

wake, suluhu inayolengo kupata Uso wa Allah na Nyumba ya Aakhirah.<br />

Tumche Allaah katika nafsi zetu.<br />

<strong>Na</strong> hakika wengi hawatafakari katika sababu ya talaka zilizoko kati ya<br />

wanandoa; unaweza kuona imejengeka katika misingi ya kukosekana kwa<br />

utulivu, na sababu ya talaka hii na mwenye kuiomba si kitu muhimu kwa<br />

kweli bali ni upumbavu wa baadhi ya wanaume au haraka za baadhi ya<br />

familia ya mwanamke; mambo ambayo badala yake yangeliweza kutatuliwa<br />

katika ngazi ya familia bila ya kutoka nje ya nyumba. <strong>Na</strong>muomba Allaah kwa<br />

sote Atupe Tawfiyq na Sadaad, na msaada wa mwongozo wa kila kheri.<br />

<strong>Haki</strong>ka Yeye ni Muweza wa kila kitu.<br />

Swalah za salaam zimuendee Mtume wetu Muhammad ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) na<br />

ahli zake na Maswahaba wake na watakaomfuata kwa wema mpaka siku ya<br />

Qiyaamah.<br />

Chanzo: http://www.mufti.af.org.sa/node/1757<br />

Chanzo: http://www.youtube.<strong>com</strong>/watch?v=KiMB0LP_OWE

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!