نﯾﺟوزﻟا نﯾﺑ قوﻘﺣﻟا Haki Za Mume Na Mke - Alhidaaya.com
نﯾﺟوزﻟا نﯾﺑ قوﻘﺣﻟا Haki Za Mume Na Mke - Alhidaaya.com
نﯾﺟوزﻟا نﯾﺑ قوﻘﺣﻟا Haki Za Mume Na Mke - Alhidaaya.com
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
نيجوزلا نيب قوقحلا<br />
<strong>Haki</strong> <strong>Za</strong> <strong>Mume</strong> <strong>Na</strong><br />
<strong>Mke</strong><br />
(<strong>Na</strong>saha <strong>Za</strong> Shaykh Kwa Wanandoa)<br />
ـھ 1432-11-02<br />
Muftiy al-´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah<br />
Aal ash-Shaykh<br />
Mfasiri:<br />
Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush<br />
©
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
يحرلا نمحرلا ﷲ مسب<br />
Himidi zote zi <strong>Za</strong>ke Allaah. Tunamhimidi na kumtaka msaada na<br />
tunamuomba msamaha na tunatubia Kwake. <strong>Na</strong> tunajikinga Kwake na shari<br />
za nafsi zetu na matendo yetu maovu.<br />
<strong>Haki</strong>ka yule Aliyemuongoza Allaah hakuna wa kumpoteza. <strong>Na</strong> Aliyempoteza<br />
hakuna wa kumuongoza.<br />
<strong>Na</strong>shuhudia ya kwamba hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah<br />
wa pekee Asiyekuwa na mshirika. <strong>Na</strong> ninashuhudia ya kwamba Muhammad<br />
ni mja Wake na Mtume Wake swalah za salaam zimuendee na ahli zake na<br />
Maswahaba wake mpaka siku ya mwisho. Amma ba´ad:<br />
Enyi watu! Mcheni Allaah ukweli wa kumcha. Enyi waja wa Allaah! <strong>Haki</strong>ka<br />
familia ndio msingi wa jamii; makazi ambayo Allaah Ameyafanya kwa mume<br />
kuwa ndio makazi yake na kukaa humo. Katika ndoa kuna utulivu wa nafsi,<br />
na kupumua, na mafanikio ya kutokufanya mapenzi na kuwa na usafi wa<br />
moyo. <strong>Na</strong> ndoa ni uhusiano uliyo imara, na mkataba madhubuti, [kama<br />
Asemavyo Allaah]:<br />
اظيلغ ً ِ َ اقاثيم ً َ ِّ مكنم ُ ِ نذخأو َ ْ َ َ َ<br />
“<strong>Na</strong> wao wanawake wamechukua kwenu ahadi iliyo madhubuti.” (04:21)<br />
<strong>Na</strong> ni ahadi ya wanandoa, kutendeana mema, na ni kuyawekea nguvu maisha<br />
ya kindoa. <strong>Na</strong> Katubainishia Allaah katika Kitabu Chake na Mtume Wake (<br />
ملسو هيلع ﷲ ىلص ) ahkaam za ndoa wazi kabisa. Zipi haki za mwanaume na yapi<br />
ya wajibu juu yake; na ni zipi haki za mwanamke na ni yapi ya wajibu juu<br />
yake.
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
Wakati wanandoa [mume na mke]watachunga haki hizi na yaliyo yawajibu<br />
kwa kila mmoja, yanakuwa maisha yao - maisha mazuri.<br />
Enyi wanandoa! Ikiwa kweli mnataka maisha mazuri yaliyo thabiti,<br />
yaliyojengeka katika misingi ya mahaba na mapenzi; mwatakiwa nyote<br />
wawili kumchungia [kumtekelezea] kila mmoja haki ya mwenzake kwa<br />
usawa katika maisha haya.<br />
Ewe dada mwenye thamani! <strong>Haki</strong>ka mume wako ana haki juu yako na ya<br />
wajibu; ni lazima kumtekelezea [kwa kufanya hivyo] ni utiifu kwa Allaah, na<br />
ni ukurubisho unajikurubisha kwao kwa Allaah. Katika haki kubwa za mume<br />
wako juu yako, ni kumtii katika mema. <strong>Haki</strong>ka kumtii katika mema ni jambo<br />
la wajibu kwako. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):<br />
“Wakikutiini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure.” (04:34)<br />
ًلايبس<br />
ِ َ نھيلع َّ ِ ْ َ َ اوغبت ْ ُ ْ َ َلاف َ مكنعطأ ْ ُ َ ْ َ َ نإف ْ ِ َ<br />
Utiifu huwa katika mema tu. Hakuna utiifu kwa yeyote katika kumuasi<br />
Allaah. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):<br />
“<strong>Na</strong> kaeni nao kwa wema.” (04:19)<br />
فورعملاب ِ ُ ْ َ ْ<br />
ِ نھورشاعو َّ ُ ُ ِ َ َ<br />
Ewe mwanamke wa Kiislamu! <strong>Haki</strong>ka mume wako ana haki juu yako ya<br />
kumtii katika mema. <strong>Na</strong> Mtume ( ملسو هيلع ﷲ يلص ) anasema:
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
"Akimwita mume mke wake kitandani, [asije] na mume wake akamkasirikia,<br />
Malaika wanamlaani mpaka asubuhi."<br />
Katika kumtii mume wako kuna thawabu kubwa mbele ya Allaah. Anasema<br />
Mtume ( ملسو هيلع ﷲ يلص ):<br />
"Akiswali mwanamke [swalah zake] tano, na akafunga mwezi wake,<br />
akahifadhi tupu yake na akamtii mume wake ataingia Peponi katika mlango<br />
wowote aupendao [katika milango minane ya Peponi]."<br />
Hii ni fadhila kubwa na neema kubwa kwa Allaah kwako, ewe dada wa<br />
Kiislamu kwa kumtii mume wako katika mema.<br />
<strong>Na</strong> katika haki zake za wajibu juu yako, ni kumtekelezea haja zake atapotaka<br />
hilo. <strong>Haki</strong>ka katika ndoa kuna kuzihifadhi tupu kwa halali, kuilinda na<br />
aliyomuharamishia Allaah kwake.Anasema Mtume ( ملسو هيلع ﷲ يلص ):<br />
"Atapomwita mume mke wake juu ya kitanda na akakataa, akamghadhibikia,<br />
hivyo Malaika humlaani mpaka asubuhi."<br />
<strong>Na</strong> kwa hili kaelekezwa mume kwa mkewe, na wakajaaliwa hilo kuwa ni<br />
swadaqah kwa wote wawili - mume na mke. Anasema Mtume ( ملسو هيلع ﷲ يلص<br />
):<br />
"<strong>Na</strong> kumuingilia mkeo ni swadaqah.” Wakasema (Maswahabah) na je, katika<br />
kupata raha binafsi mmoja wetu analipwa??! Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص )<br />
akasema: “Je, mnaonaje lau mtu huyo angeingiza [tupu yake] katika haramu,<br />
je, ingelikuwa ni shari juu yake [ya madhambi, maradhi, adhabu]?, wakasema:<br />
ndio. Akasema Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ): “Hivyo ndivyo atakapoweka [tupu<br />
yake] katika halali atalipwa.” [Muslim]<br />
<strong>Na</strong> katika haki za mume wako juu yako, ni kuwa na adabu na kumheshimu,<br />
hii ni amaanah umeaminiwa kwayo.
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
Mwanamke mwema, mwenye mtazamo mzuri kumuangalia mume wake;<br />
mwenye kujihifadhi ili kudumisha sifa ya kitanda chake, hivyo ni bora.<br />
ُﷲ ّ ظفح َ ِ َ امب َ ِ بيغلل ِ ْ َ ْ ِّ تاظفاح ٌ َ ِ َ تاتناق ٌ َ ِ َ تاحلاصلاف ُ َ ِ َّ َ<br />
“Basi wanawake wema ni wale wenye kutii na wanaojilinda hata katika siri<br />
kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajilinde.” (04:34)<br />
<strong>Na</strong> katika Hadiyth, anasema ( ملسو هيلع ﷲ يلص ):<br />
"Bora ya raha kwa mwanaume ni kupata mke mwema, [ambaye] akimtazama<br />
anafurahi, na akimuamrisha [kitu] anamtii, na [mume] akiwa mbali naye<br />
hujihifadhi mwenyewe [mwanamke] na mali [ya mumewe]."<br />
Ewe dada ´Aziyzah! <strong>Haki</strong>ka kumridhisha kwako mume wako na<br />
kumheshimu, ni jambo jema, na ni kitu kizuri, na ni jambo la wajibu juu yako<br />
Kishari´ah; Usidanganyike na hayo mafilamu machafu, ambayo yanakuweka<br />
mbali na heshima yako na fadhila zako na yaliyojaa maovu. Allaah<br />
Atusamehe sote kwa hayo.<br />
<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako, usimruhusu yeyote kuingia nyumbani bila<br />
idhini [ruhusa] yake. Utaejua kuwa hatomridhia kuingia usimruhusu. Kwa<br />
kuwa Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) anasema:<br />
"Si halali kwa mwanamke kumruhusu yeyote kuingia nyumbani kwa mume<br />
wake ila kwa idhini [ruhusa] yake."<br />
<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako, kuchunga nyumba yake na mali yake.<br />
Katika Hadiyth [anasema Mtume]:
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
"Mwanamke ni mchungaji katika nyumba ya mume wake na ataulizwa [na<br />
Allaah] kwa alichokichunga."<br />
<strong>Na</strong> kakataza Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) kutoa katika mali ya mume wako ila<br />
kwa idhini yake [mume].<br />
<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako, usimkalifishe kukuhudumia [kukupatia<br />
matumizi] kile asichokiweza na ni kizito kwake na hakiwezi. <strong>Haki</strong>ka Allaah<br />
Anasema:<br />
ُﷲ َّ ُهاتآ َ امم َّ ِ قفنيلف ْ ِ ُ ْ َ هقزر ُ ُ ْ<br />
ِ هيلع ِ ْ َ َ ردق َ ِ ُ نمو َ َ هتعس ِ ِ َ َ نم ِّ ةعس ٍ َ َ وذ ُ قفنيل ْ ِ ُ ِ<br />
“Mwenye wasaa atoe kadiri ya wasaa wake, na mwenye dhiki atoe katika<br />
alichompa Allaah. Allaah Hamkalifishi mtu ila kwa kadiri ya alicho mpa.”<br />
(65:07)<br />
<strong>Na</strong> katika haki za mume juu mke, ni kuwapa malezi watoto na kuwaongoza;<br />
nyote wawili mume na mke ni wenye kushiriki katika jambo hili muhimu<br />
sana. Kuwapa malezi vijana na kuwaandaa wawe vizuri, na kuwaamrisha<br />
mema na kuwatahadharisha na shari. <strong>Na</strong> kule baba kuwa kwake kiigizo bora<br />
kwa watoto wakiume, katika kheri na wema. <strong>Na</strong> mama ana jukumu lakuwa<br />
kiigizo bora kwa mabanati wake, kwa kujisitiri vizuri na usafi wa moyo, na<br />
dhamira ya maadili ya thamani.<br />
<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako, ni wewe kubaki nyumbani na kutotoka ila<br />
tu kwa dharurah. Ama kutoka kwako nyumbani bila ya dharurah kunaifanya<br />
nyumba kuzorota na kukosekana mwenye kuilinda na kuihifadhi.<br />
<strong>Na</strong> katika haki za mume juu yako ni wewe kutomuudhi kwa maneno mabaya.<br />
Mwambie [muongeleshe] maneno mazuri yenye baraka. Kuuachia ulimi<br />
hovyo, haimpasi mwanaume wala mwanamke. <strong>Na</strong> imepokelewa kutoka kwa<br />
Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) kuwa amesema:<br />
"Akimuudhi mwanamke mume wake duniani, anasema mke wake katika<br />
Huur al-'Iyin "Allaah Akuangamize usimuudhi, kwani huyo ni mtu wetu -<br />
imekaribia kuachana nawe na kuja kwetu."
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
<strong>Na</strong> katika haki za mume wajibu juu yako, usijikurubishe kwa Allaah<br />
kwaswalah za naafilah [sunnah] na swawm [za sunnah] ila kwa idhini<br />
[ruhusa] ya mume wako.<br />
<strong>Haki</strong>ka haki yake [mume] ni yenye kutangulia. <strong>Na</strong> kwa hili anasema Mtume (<br />
ملسو هيلع ﷲ ىلص ):<br />
"Si halali kwa mwanamke kufunga, na mume wake yuko ila kwa idhini yake."<br />
Katika haki za mume juu yako, aliyobainisha Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص )<br />
kuwatahadharisha wanandoa [mume na mke] kutoa siri ya uhusiano wa<br />
kindoa [yafanyikayo ndani], akasema kuwa mwenye kufanya hivyo ni katika<br />
watu waovu sana. Kwa kuwa hii ni dalili ya ukosevu wa haya na adabu.<br />
(<strong>Haki</strong> <strong>Za</strong> <strong>Mke</strong> Juu Ya <strong>Mume</strong>)<br />
Ndugu mume karimu, hakika mke wako ana ya wajibu pia juu yako na haki<br />
zake. Lazima umtimizie - kama jinsi yeye kwako ana haki zake na ya wajibu,<br />
na wewe hali kadhalika una haki na ya wajibu juu yake. Lazima umtimizie.<br />
<strong>Haki</strong> yake kubwa juu yako, ni wewe kumpa mahari kwa ukamilifu; sawa<br />
akiwa ni mwenye uwezo au si mwenye uwezo. Kwa kuwa Allaah Anasema:<br />
ائيرم ً<br />
ِ َّ ائينھ ً ِ َ هولكف ُ ُ ُ َ اسفن ً ْ َ هنم ُ ْ ِّ ءيش ٍ ْ َ نع َ مكل ْ ُ َ نبط َ ْ ِ نإف ِ َ ةلحن ً َ ْ ِ نھتاقدص َّ ِ ِ َ ُ َ ءاسنلا َ َّ اوتآو ْ ُ َ<br />
“<strong>Na</strong> wapeni wanawake mahari yao hali ya kuwa nikipawa. Lakini<br />
wakikutunukieni kitu katika mahari - kwa radhi yao, basi kileni kiwashuke<br />
kwa raha.” (04:04)<br />
Ni wajibu kumpa haki yake kamili. Katika haki zake juu yako, ni kumpa<br />
matumizi [kumuhudumia] chakula, mavazi na makazi. Anasema Allaah<br />
(Ta´ala):
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
فورعملاب ِ ُ ْ َ ْ<br />
ِ نھتوسكو َّ ُ ُ َ ْ ِ َ نھقزر َّ ُ ُ ْ<br />
ِ هل ُ َ دولوملا ِ ُ ْ َ ْ ىلعو َ َ َ<br />
“<strong>Na</strong> ni juu ya mzazi wa kiume kuwapatia chakula chao na nguo kwa<br />
ma’aruwf (mujibu wa ada).” (02:233)<br />
Akasema tena:<br />
نھيلع َّ ِ ْ َ َ اوقيضتل ُ ِّ َ ُ ِ نھوراضت َّ ُ ُّ َ ُ لاو َ َ مكدجو ْ ُ ِ ْ ُ نم ِّ متنكس ُ َ َ ثيح ُ ْ َ نم ْ ِ نھونكسأ َّ ُ ُ ِ ْ َ<br />
“Wawekeni humo humo mnamokaa nyinyi kwa kadiri yapato lenu, wala<br />
msiwaletee madhara kwa kuwadhiki.”(65:06)<br />
Matumizi ni wajibu kwa mume kumpa mke wake, kwa mujibu wa mkataba<br />
wa ndoa baina yao. <strong>Na</strong> Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص )anasema kumwambia Saad<br />
bin Abi Waqqas kuhusiana na hili:<br />
"<strong>Haki</strong>ka hutotoa matumizi kwa kutaka Uso wa Allaah isipokuwa utapewa<br />
ujira kwalo, hata ikiwa ni kitu kidogo utachokiweka kwenye kinywa cha<br />
mkeo."<br />
<strong>Na</strong> katika haki zake juu yako, ni kukaa nae kwa wema kwa adabu za<br />
Kishari´ah. Anasema Allaah (Jalla wa ´Alaa):<br />
“<strong>Na</strong> kaeni nao kwa wema.” (04:19)<br />
Anasema tena:<br />
فورعملاب ِ ُ ْ َ ْ<br />
ِ نھورشاعو َّ ُ ُ ِ َ َ<br />
فورعملاب ِ ُ ْ َ ْ<br />
ِ نھيلع َّ ِ ْ َ َ يذلا ِ َّ لثم ُ ْ<br />
ِ نھلو َّ ُ َ َ
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
“<strong>Na</strong> hao wanawake wana kama ile (haki) iliyo juu yao kwa ma’aruwf (mujibu<br />
wa shari’ah).” (02:228)<br />
<strong>Na</strong> anasema Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ):<br />
"Mbora [wa wanaume ni] aliye mbora kwa familia yake, na mimi ni mbora<br />
kwa familia yangu."<br />
<strong>Na</strong> katika haki zake juu yako, ni kumlinda [asipatwe na] adhabu ya Allaah<br />
kwa kumuamrisha mema na kumtahadharisha na shari [maovu].<br />
ةراجحلاوسانلا ُ َ َ ِ ْ َ ُ َّ اھدوقو َ ُ ُ َ اران ً َ مكي ْ ُ ِلھأو ْ َ َ مكسفنأ ْ ُ َ ُ َ اوق ُ اونمآ ُ َ نيذلا َ ِ َّ اھيأ َ ُّ َ ايَ<br />
“Enyi mlioamini! Jilindeni nafsi zenu na ahli zenu na Moto ambao kuni zake<br />
ni watu na mawe.” (66:06)<br />
Anasema tena:<br />
ىوقتلل َ ْ َّ ِ ةبقاعلاو ُ َ ِ َ ْ َ كقزرن َ ُ ُ ْ َ نحن ُ ْ َّ اقزر ً ْ<br />
ِ كلأسن َ ُ َ ْ َ لا َ اھيلع َ ْ َ َ ربطصاو ْ ِ<br />
َ ْ َ ةلاصلاب ِ َ َّ ِ كلھأ َ َ ْ َ رمأو ْ ُ ْ َ<br />
“<strong>Na</strong> waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo. Sisi<br />
hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. <strong>Na</strong> mwisho mwema ni<br />
kwa mcha Mungu.” (20:132)<br />
Katika haki zake juu yako, ni wewe kuwa na wivu kwake, wivu ambao ni<br />
wakweli [mzuri] - kwa kumtakia kheri, na kumuonya na kila shari uijuayo;<br />
bila ya kuwa na wasiwasi [katika wivu wako] na mashaka, na matarajio ya<br />
makosa; bali iwe ni wivu ulioubeba kwa ajili ya kumtakia kheri na kumlinda<br />
asipatwe na shari. Usiwe ni wivu wa wasiwasi na mashaka na kuangalia tu<br />
udhaifu [wake]. Ni watu wangapi wamekuwa na aina ya maradhi kama haya,<br />
na kuona wengine si kama yeye. Ni wajibu kumcha Allaah.
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
Kama inavyotakikana kwa mwanamke pia kuwa na wivu kwa mume wake.<br />
Lakini anapaswa kuwa na wivu uliojengeka katika mambo ya wazi; si kwa<br />
uchunguzi wa fujo na vurugu na kuchunguza namba za simu - ukaguzi<br />
nakadhalika, jambo ambalo linaweza kusababisha shari na balaa baina yao.<br />
<strong>Na</strong> katika haki za mwanamke juu ya mume wake, ni kumfunza mambo ya<br />
dini yake asiyoyajua na yatamsaidia kufanya mema.<br />
<strong>Na</strong> katika haki zake juu yako, ni [wewe] mwanaume kuwa mwadilifu baina<br />
ya wake [zako] ukioa wake wengi [ukewenza]. Anasema Mtume ( هيلع ﷲ ىلص<br />
ملسو ):<br />
"Yule mwenye wake wawili, akamkandamiza mmoja zaidi kuliko mwengine,<br />
atakuja siku ya Qiyaamah na bega lake likiwa limepinda."<br />
<strong>Na</strong> katika haki zake juu yako, usimkandamize na kumnyima haki zake kwa<br />
kumdhulumu na kumfanyia uadui, kwani hakika dhuluma ni gizo siku ya<br />
Qiyaamah. Usitumii udhaifu wake na ukosevu wake wa mabavu, ukamuonea<br />
[mkandamiza] bila ya hatia yoyote, ukamtusi na kumtuhumu kwa mambo<br />
ambayo kajitenga nayo mbali.<br />
Katika haki zake juu yako, ni kumhifadhia mali yake na usimtumie na<br />
ukaitumia mali yake; ukawa unamtisha kwa talaka akiomba haki yake na<br />
ukawa unaitumia. Yote haya ni katika uonevu. <strong>Haki</strong>ka wajibu wako ni wewe<br />
kumhudumia sawa na uwezo wako, umejiingiza katika [maisha ya] ndoa<br />
pambana na ndoa hii.<br />
Wakati mke atapotekeleza [timiza] wajibu alionao juu ya mume wake, na<br />
wakati mume atapotekeleza [timiza] wajibu alionao juu ya mke wake; hivyo<br />
maisha na hali huwa nzuri. <strong>Na</strong> wakati nyumba itaachwa, wakati kila mmoja<br />
atapoacha kutekeleza haki ya mwenzake; wakati mke atapoacha kumtimizia<br />
mume haki zake, au mume akaacha kumtimizia mwanamke haki zake; hivyo<br />
hutokea shari na uharibifu.
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
Ama kila mmoja akichunga haki alionayo juu ya mwenzake, hakika hii ndio<br />
sababu ya furaha na kuwa na maisha mazuri na familia huishi katika<br />
muelekeo na usalama.<br />
Enyi watu! Mcheni Allaah (Ta´ala) ukweli wa kumcha. Shari´ah ya Uislamu<br />
imekuja kutekeleza uadilifu kwa njia zote. <strong>Na</strong> katika hayo ni uadilifu baina ya<br />
wanandoa, kwa kila mwanandoa mmoja kumtimizia mwengine. Mwanamke<br />
atimize yaliyo ya wajibu juu yake kwa mume wake; na mume atimizeyaliyo<br />
ya wajibu juu yake kwa mke wake.<br />
Hivyo ndivyo yalivyo maisha ya ndoa yaliyofanywa na Uislamu kwa<br />
wanandoa ili waishi maisha ya furaha; maisha ya furaha na ridhaa.<br />
Tumcheni Allaah katika nafsi zetu [kwa kila mmoja kumtimizia mwenzake<br />
haki yake].<br />
Ewe mume ´Aziyz! <strong>Haki</strong>ka kutania [kucheza] na mke [wako], wacheza naye<br />
na huku wamuelekeza katika mema ni katika sababu zinazoimarisha misingi<br />
ya maisha ya ndoa. <strong>Na</strong> hakika utoaji onyo mara kwa mara pasina sababu za<br />
kueleweka, ni katika sababu ya kufarakana.<br />
Tahadhari muwe na kukithirisha maonyo ya mara kwa mara bila sababu.<br />
Tahadhari na kufuatilia vijikosa vidogo vidogo ambavyo havina uziro<br />
wowote. Kuwa mwenye kupuuza vijikosa ilimraditu havina kasoro katika<br />
heshima na cheochako, ni juu yako kuwa na subira kwa baadhi ya makosa;<br />
hakuna yeyote aliyesalimika kutokana na makosa. Anasema Mtume ( ﷲ ىلص<br />
ملسو هيلع ):<br />
"Mwanaume asimchukie muumini mwanamke [mkewe], akichukizwa na<br />
moja ya tabia yake atapendezwa na nyingine."<br />
Anasema tena [Mtume]:<br />
"Ninawahusieni kuwatendea wanawake wema."<br />
Subira kwa kila mmoja kumvumilia mwenzake ni jambo linalotakikana.<br />
Mwanamke awe na subira kwa mume wake, na kwa baadhi ya makosa<br />
kunako tabia yake na mwenendo wake ilimradi haijafikia katika kumvulia<br />
cheo na heshima. <strong>Na</strong> mume awe na subira juu ya baadhi ya makosa ya mke
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
wake, ilimradi haijafika kumvulia cheo na heshima. Iwe wote wanasaidizana<br />
kutengeneza na kumezea [kasoro] za kila mmoja kwa mwenzake.<br />
<strong>Na</strong> Mtume ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) kamtahadharisha mwanamke wa Kiislamu kwa<br />
kukufuru kwake wema na kumlalamikia sana mume. Akasema kuwa ameona<br />
moto na wakazi wake wengi ni wanawake; kwa tuoacha kwao kulalama na<br />
kukufuru kwao wema.<br />
Lau utamtendea mmoja wao wema maisha yote, akaona kutoka kwako kitu<br />
[kasoro], atasema "Sijawahi kuona kheri [wema] wowote kutoka kwako katu."<br />
Ndugu wapenzi! Matatizo ya kindoa yanakuwa wakati mwingine kwa sababu<br />
zisizokuwa na maana. Wakati wakutafakari na kuzingatia vizuri mtu anakuja<br />
kuona kuwa sababu [zilizoleta matatizo] ni za kijinga zisizo na maana yoyote.<br />
Ni juu ya wazazi wa ndugu wa mume au mke kutatua matatizo haya ndani ya<br />
nyumba, na yasiendelee mambo kama haya hadi yakatoka nje ya nyumba.<br />
<strong>Mume</strong> amalize tatizo lake na mke wake au na famili yake. <strong>Na</strong> juu ya familia<br />
yake mwanamke kumkanya wakiona yeye ndo yuko makosani. <strong>Na</strong> familia ya<br />
mwanamume hali kadhalika wamkanye watapoona kuwa yeye [mume] ndo<br />
yuko makosani.<br />
Familia zote mbili zikisaidizana pamoja na mume na mke kutatua tatizo hili,<br />
hupatikana ufumbuzi mzuri. Ama ikiwa hawatokuwa makini na kujichunga,<br />
huwaka fitna. Mwanaume [baba mkwe] akawa na kasumba kwa binti yake<br />
bila kujali makosa yake; au mwanamume akawa na kasumba ya kushikilia rai<br />
yake bila kujali makosa yake. <strong>Haki</strong>ka huo ni msiba mkubwa.<br />
<strong>Na</strong> Mtume wetu ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) kamtahadharisha mwanamke wa Kiislamu<br />
kuomba talaka pasina sababu ya msingi. Akasema:<br />
"Mwanamke akimuomba mume wake talaka pasina sababu muhimu, ni<br />
haramu juu yake harufu ya Pepo."<br />
Hivyo ni wajibu kwao mauqif yao iwe ya heshima, mauqif ya kutatua tatizo,<br />
na kumaliza mgogoro huu, na kuzingatia tatizo hili - liangaliwe vizuri.<br />
Iangaliwe sababu na itatuliwe, na qadhiya hii ishughulikiwe ndani ya
www.alhidaaya.<strong>com</strong><br />
nyumba. Isende ikatoka nje, khabari ikawafikia watu nje wasiyokuwa na<br />
thamani kwao, na wasiyowapendea kheri - wakaja kuiharibu nyumba na<br />
kuingamiza katika msingi wake. Hukumsikia Allaah Akisema:<br />
ريخ ٌ ْ َ حلصلاو ُ ْ ُّ َ احلص ً ْ ُ امھنيب َ ُ َ ْ َ احلصي َ ِ ْ ُ نأ َ امھيلع َ ِ ْ َ َ حانج َ ْ َ ُ َلاف َ اضارعإ ً َ ْ ِ وأ ْ َ ازوشن ً ُ ُ اھلعب َ ِ ْ َ نم ِ تفاخ ْ َ َ ةأرما ٌ َ َ ْ نإو ِ ِ َ<br />
“<strong>Na</strong> mwanamke akichelea kutupwa au kutojaliwa na mumewe, basi si vibaya<br />
kwao wakisikizana kwa suluhu.<strong>Na</strong> suluhu ni bora.” (04:128)<br />
Kutafuta suluhu baina ya wanandoa ni kheri, suluhu inayohitaji kuhifadhi<br />
haki ya kila mmoja, suluhu ya kutaka kutatua tatizo na kumaliza ugomvi,<br />
suluhu kurudi katika hali ya kawaida, na maisha ya ndoa kuendelea utulivu<br />
wake, suluhu inayolengo kupata Uso wa Allah na Nyumba ya Aakhirah.<br />
Tumche Allaah katika nafsi zetu.<br />
<strong>Na</strong> hakika wengi hawatafakari katika sababu ya talaka zilizoko kati ya<br />
wanandoa; unaweza kuona imejengeka katika misingi ya kukosekana kwa<br />
utulivu, na sababu ya talaka hii na mwenye kuiomba si kitu muhimu kwa<br />
kweli bali ni upumbavu wa baadhi ya wanaume au haraka za baadhi ya<br />
familia ya mwanamke; mambo ambayo badala yake yangeliweza kutatuliwa<br />
katika ngazi ya familia bila ya kutoka nje ya nyumba. <strong>Na</strong>muomba Allaah kwa<br />
sote Atupe Tawfiyq na Sadaad, na msaada wa mwongozo wa kila kheri.<br />
<strong>Haki</strong>ka Yeye ni Muweza wa kila kitu.<br />
Swalah za salaam zimuendee Mtume wetu Muhammad ( ملسو هيلع ﷲ ىلص ) na<br />
ahli zake na Maswahaba wake na watakaomfuata kwa wema mpaka siku ya<br />
Qiyaamah.<br />
Chanzo: http://www.mufti.af.org.sa/node/1757<br />
Chanzo: http://www.youtube.<strong>com</strong>/watch?v=KiMB0LP_OWE