26.05.2014 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA UCHUKUZI MHE.OMARI NUNDU (MB ...

HOTUBA YA WAZIRI WA UCHUKUZI MHE.OMARI NUNDU (MB ...

HOTUBA YA WAZIRI WA UCHUKUZI MHE.OMARI NUNDU (MB ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>HOTUBA</strong> <strong>YA</strong> <strong><strong>WA</strong>ZIRI</strong> <strong>WA</strong> <strong>UCHUKUZI</strong> <strong>MHE</strong>.<strong>OMARI</strong> <strong>NUNDU</strong> (<strong>MB</strong>.)<br />

<strong>WA</strong>KATI <strong>WA</strong> UFUNGUZI <strong>WA</strong> MKUTANO <strong>WA</strong> FUNGAMANO LA<br />

BANDARI ZA AFRIKA NA ULA<strong>YA</strong>, UTAKAOFANYIKA ARUSHA<br />

TANZANIA DESE<strong>MB</strong>A 6, 2010<br />

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPA<br />

Bwana Raphael Mollel<br />

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari,<br />

Katibu Mkuu wa IAPH Bw. Susumu Naruse,<br />

Wadau wa Sekta ya Usafiri Majini,<br />

Wageni waalikwa,<br />

Mabibi na Mabwana.<br />

Awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisha wadau wa Bandari<br />

kutoka hapa nchini na sehemu mbalimbali duniani kushiriki katika Kongamano<br />

kuhusu Kuboresha Huduma za Bandari kwa Lengo la Kuchochea Ukuaji wa<br />

Uchumi wa Bara la Afrika. Nimetaarifiwa kuwa kongamano hili muhimu<br />

linawakutanisha pamoja wahusika wakuu wa sekta ya usafirishaji, hususan ule<br />

wa majini kwa lengo la kubadilishana mawazo na uzoefu wa shughuli za bandari<br />

kwa lengo la kuziboresha na hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi Afrika. Mada<br />

kuu mliyochagua ni nzuri na imekuja wakati muafaka. Yaani kutafuta kwa njia<br />

ya mjadala mikakati ya kuziwezesha na kuzifanya bandari za Tanzania, Afrika<br />

na ulimwenguni kwa ujumla kufanya kazi zake ipasavyo kwa kasi, tija na<br />

ufanisi mkubwa.<br />

Kongamano hili ni muhimu kwa kuwa linatoa fursa kwa wadau wa Bandari<br />

kujadiliana kwa pamoja namna ya kuboresha huduma za Bandari na usimamizi<br />

wa Bandari katika eneo la Mashariki na Kusini mwa Afrika ili kuongeza ufanisi<br />

wao.<br />

Aidha, Kongamano hili ni fursa ya kuanzisha na kuendeleza mahusiano kati ya<br />

Mamlaka za Bandari au vyama, mashirika ya kikanda na kimataifa, Serikali au<br />

Taasisi nyingine, kwa ajili ya ushirikiano na utafiti wa masuala ya shughuli za<br />

bahari .<br />

Umuhimu wa Bandari:<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

1


Umuhimu wa Bandari duniani, hususani katika bara la Afrika, hauhitaji<br />

ufafanuzi wala msisitizo. Bandari ni chachu ya maendeleo na ukuaji wa uchumi<br />

wa taifa lolote lile, hata lisilo na bandari. Kwa sababu hiyo kila nchi yenye<br />

bandari na hasa nchi za Kiafrika kwa sasa inajitahidi kuwekeza katika kuboresha<br />

miundombinu ya bandari na mfumo mzima wa usafirishaji vifikie viwango vya<br />

kimataifa.<br />

Changamoto za Sekta ya Bandari<br />

Kwanini ninatilia msisitizo kwa Afrika, kwasababu kwa muda mrefu Bara la<br />

Afrika limekuwa likikabiliwa na changamoto nyingi hususani ukuaji wa<br />

shughuli za kiuchumi ambazo zimeongeza mahitaji ya huduma za bandari.<br />

Lakini kwa Afrika bandari hazijaweza kumudu au kukidhi mahitaji haya. Hali<br />

hiyo ipo pia katika usafirishaji wa nchi kavu kama barabara na reli ambayo<br />

vinapaswa viwe na uwezo unaowiana na ule wa bandari, na pia usafiri wa anga.<br />

Kwa ufupi ni tatizo la usafiri wa aina yeyote. Kwa Tanzania tatizo hili<br />

limepatiwa ufumbuzi kwa kuwa sasa nchi inayo Sera ya Taifa ya Usafirishaji<br />

ambayo inatoa muongozo wa namna ya kujenga miundombinu na utoaji huduma<br />

za uchukuzi zilizo salama, za uhakika na endelevu kwa sekta zote za usafishaji.<br />

Kilichobaki sasa ni Tanzania kuhakikisha kuwa na mikakati madhubuti ambayo<br />

inazingatia uwiano na muingiliano wa miundombinu, na pia miundombinu yote<br />

inategemeana na kusaidiana katika kujijengea uwezo wa ufanisi.<br />

Mapungufu mengi bado yapo, ambayo ni pamoja na bandari zetu kuwa na<br />

uwezo mdogo wa kuhudumia shehena za aina yote; miundombinu ya bandari<br />

ambayo imechakaa na imepitwa na wakati; mtandao mdogo wa reli ambao ni wa<br />

zamani na usiokidhi matakwa; mtando mdogo wa barabara na ambao sio imara;<br />

na vyombo vya uchukuzi ambavyo havikidhi matakwa ya usafirishaji salama na<br />

wa bei nafuu. Mapungufu haya na changamoto nyingine nyingi zinazoikabili<br />

sekta ya bandari, zinafanya bandari za hapa nchini na Afrika kwa ujumla<br />

zisitumike ipasavyo na hivyo kudumaza maendeleo ya uchumi. Kazi kubwa<br />

tuliyonayo sasa ni kuyafanyia kazi mapungufu hayo na kuyapunguza sana katika<br />

kipindi kifupi na hatimaye kuyatokomeza kabisa yale ambayo hayana sababu<br />

kuwepo.<br />

Mabadiliko ya Uendeshaji wa Bandari<br />

Ili kukabiliana na changamoto hizo, mifumo ya uendeshaji wa bandari<br />

ulimwenguni umefanyiwa mabadiliko makubwa ukiwemo mfumo wa kuiwachia<br />

sekta binafsi kutowa huduma katika bandari Mfumo huu wa kushirikisha sekta<br />

2


inafsi ndiyo jibu la matatizo yaliyokuwepo awali kwa nchi nyingi<br />

zinazoendelea. Ili kuweza kunufaika na mfumo huu, inahitajika yawepo<br />

mazingira ya kuvutia sekta binafsi.<br />

Mojawapo ya mikakati iliyotumika kukabili changamoto hizi ni Serikali<br />

kuondokana na kubadili mfumo wa uendeshaji wa mashirika ya kibiashara<br />

ikiwemo bandari. Tumetoka kwenye bandari zilizoendeshwa na Serikali (state<br />

owned and operated ports), kwenda kwenye mfumo wa uendeshaji kwa Taasisi<br />

za Serikali (state owned but operated by semi autonomous Government<br />

institutions), na sasa tuna bandari zinazoendeshwa na Sekta binafsi (private<br />

operated ports).<br />

Tanzania hatukuachwa nyuma katika mabadiliko haya. Mfumo wa uendeshaji<br />

wa Bandari nchini umebadilika kutoka ule wa Mamlaka ya Bandari nchini<br />

kuhodhi shughuli zote za umiliki wa Bandari na uendeshaji wa shughuli za<br />

kuwezesha shehena zinazopita bandarini na kwenda kwenye mfumo wa kumiliki<br />

bandari tu na kukaribisha Sekta binafsi katika uendeshaji wa shughuli za<br />

bandari.<br />

Bandari za Tanzania kwa sasa zinasimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa<br />

Bandari (Tanzania Ports Authority - TPA) ambayo ndiyo mmiliki wa bandari<br />

zote nchini, yaani zile za mwambao na zilizoko kwenye maziwa makuu.<br />

Changamoto kwa Serikali na TPA sasa hivi ni kujenga bandari mpya na<br />

kuboresha na kuendeleza miundombinu ya bandari zilizopo ikiwa ni pamoja na<br />

kusimamia waendeshaji wa shughuli za kupakua na kupakia shehena, shughuli<br />

ambazo zinatakiwa kufanywa kupitia mfumo wa ushirikishwaji wa sekta<br />

binafsi..<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

Ushirikishwaji wa mitaji toka sekta binafsi hapa nchini sasa umewekewa sheria<br />

kamili inayoweka bayana jinsi gani sekta ya umma itashirikiana na ile ya binafsi<br />

katika maendeleo na miradi ya kibiashara.<br />

Kinachofanyika hivi sasa katika bandari ni kuboresha miundombinu yake<br />

pamoja na kubuni mifumo mipya ya kushughulikia shehena; usalama na ulinzi<br />

ili kuweza kuvutia wawekezaji binafsi; kuwezesha shughuli za biashara kuwa<br />

zenye ufanisi na tija ya hali ya juu, na endelevu.<br />

Malengo yote ya maendeleo, na changamoto zinazotokana na mipango hii ni ya<br />

umuhimu kwa bandari za Tanzania kwa sababu nchi hii ina majirani wasio na<br />

3


andari. Nchi hizi zinatutegemea kwa usafiri wa kufikisha bidhaa zao katika<br />

masoko ya kimataifa au zile wanazoagiza. Mapungufu yoyote yale ya kiutendaji<br />

yatagusa na pia kudumaza kasi ya uchumi wa Tanzania na pia ule wa majirani<br />

zake. Ni matarajio yangu kwamba Kongamano hili litatupa uzoefu wa<br />

ushirikishwaji wa sekta binafsi katika kutoa huduma bora zenye ufanisi na kwa<br />

gharama nafuu katika bandari zetu na hivyo kuchangia katika ukuaji wa uchumi<br />

wa Tanzania na Kanda hii ya Afrika. Ni kwa kuzingatia hili, Serikali ya Jamhuri<br />

ya Muungano ya Tanzania inaipa umuhimu mkubwa sekta ya bandari na<br />

imeifanya kuwa moja ya vipaumbele vyake.<br />

Mipango ya kuendeleza Bandari<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

Wakati tukiweka mipango mizuri ya kutatua tatizo la miundombinu ikumbukwe<br />

kuwa utekelezaji wa miradi hii unahitaji fedha kutoka kwa Washiriki wa<br />

Maendeleo na pia kutoka sekta binafsi wa ndani na nje ya nchi kwa ajili ya<br />

kuwekeza kwenye miundombinu ya uchukuzi. Napenda kuchukua fursa hii kwa<br />

niaba ya serikali kuwakaribisha Washiriki wa Maendeleo na wenzetu wa Sekta<br />

binafsi kushirikiana nasi kwa kuwekeza katika maeneo mbalimbali yanayohitaji<br />

kuendelezwa. Baadhi ya maeneo ni kupanua na kuboresha miundombinu ya<br />

bandari, reli na barabara. Fursa zipo, milango ipo wazi, miongozo ya kisera ipo<br />

na taratibu za kisheria nazo pia zipo. Karibuni sana.<br />

Umuhimu wa Teknohama<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

Teknolojia ya usafirishaji duniani inakua kwa kasi ya ajabu ambao unahitaji<br />

kwenda sambamba na huduma bora za mawasiliano. Ni dhahiri kuwa mageuzi<br />

makubwa yamefanywa kwenye eneo hili la teknohama kwenye bandari ambazo<br />

zina ufanisi mkubwa. Hali haipo hivyo katika bandari zilizopo kwenye nchi<br />

zinazoendelea hasa za Afrika. Kwa upande wa Tanzania, Mamlaka ya<br />

Usimamizi wa bandari imeonesha mwelekeo mzuri kwani imeanza na<br />

inakamilisha mradi mkubwa kwa kuboresha mawasiliano haya. Katika mkakati<br />

huu, TPA kwa udhamini wa Benki ya Dunia inaanda mfumo ambao<br />

utaunganisha na kutumika na wadau wake wote. Ushauri wangu kwa nchi<br />

zinazoendelea ni kwamba kama wenzetu wanatembea, basi sisi tukimbie<br />

kuelekea matumizi sahihi ya teknohama. Tuboreshe teknolojia hii kwenye<br />

bandari zetu ili zichangie katika ufanisi wa bandari zetu.<br />

4


Uharamia<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

Hivi sasa dunia inapambana na tatizo kubwa lililoikumba sekta ya usafiri majini<br />

na biashara ya kimataifa kwa ujumla ambalo ni janga la uharamia. Katika Bara<br />

la Afrika, janga hili limeenea kutoka Ghuba ya Aden hadi Afrika ya Mashariki.<br />

Hivi karibuni tumeshuhudia uharamia ukitokea kwenye Ziwa Tanganyika.<br />

Kutokana na ukubwa wa suala hili ambalo linatishia uchumi wa dunia na maisha<br />

ya watu na mali hatuna budi kulipa umuhimu wa pekee katika kongamano hili<br />

kwa kuwa kimsingi ni suala linalohitaji nguvu ya pamoja.<br />

Naomba kutumia fursa hii pekee, kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya<br />

Muungano wa Tanzania kuzishukuru nchi na Taasisi zote za Kimataifa ambazo<br />

zimejitolea kwa hali na mali kupambana na uharamia. Mapambano dhidi ya<br />

uharamia yanahitaji rasilimali kubwa, utaalamu na vifaa vyenye teknolojia ya<br />

hali ya juu kuweza kupambana nao, ambapo sisi peke yetu tusingeweza kumudu<br />

mapambano hayo. Taasisi hizi zimekuwa mstari wa mbele kuziwezesha nchi<br />

zetu za Afrika Mashariki kupambana na uharamia kwa kutuimarisha kupitia<br />

elimu, kutupa vifaa na teknolojia ya namna ya kupambana na uharamia huu.<br />

Nawashukuru sana na naomba waendelee kutusaidia.<br />

Maelekezo yangu kwa Kongamano<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

Kongamano hili limejaa Wajumbe wenye utajiri na manguli wa Masuala ya<br />

Usafiri Majini, ni mategemeo yangu kuwa tutapata ushauri mwingi kutoka<br />

kwenu na mkutano huu utatowa suluhisho la matatizo mengi yanayotukabili.<br />

Ushauri wenu utatusaidia kuboresha sekta hii katika Tanzania na Bara zima la<br />

Afrika.<br />

Kazi iliyo mbele yenu katika siku tatu hizi ni kubwa hivyo nisingependa<br />

kuchukua muda wenu mwingi kwa hotuba ndefu badala ya kuwaachia mfanye<br />

kazi iliyowaleta. Napenda kuwashukuru TPA kwa niaba ya Serikali kwa<br />

kuandaa mkutano huu muhimu. Vilevile shukrani zangu nyingi ni kwenu ninyi<br />

washiriki pamoja na serikali zenu na mashirika yenu yaliyowawezesha<br />

kughudhuria kongamano hili.<br />

Nawasihi mwendeleze ushirikiano huu miongoni mwenu. Kwa upande wangu<br />

nina maelekezo yafuatayo kwa Kongamano hili:<br />

5


(i) Mjadili kwa kina changamoto za utandawazi kwenye sekta ya<br />

uchukuzi kwa njia ya maji na huduma za bandari.<br />

(ii) Mtupatie mikakati sahihi ya kuendeleza miundombinu ya bandari.<br />

Hapa mtaazimia namna bora ya kupanga, kusimamia na kupata<br />

fedha za kuendeleza miundombinu ya bandari.<br />

(iii) Mje na mkakati wa kuhakikisha kwamba sekta ya bandari<br />

inaendeshwa na watu waliobobea kielimu kwenye sekta.<br />

(iv) Mtupatie mkakati wa kumaliza tatizo la uharamia.<br />

(v) Mje na mkakati wa kuhakikisha kwamba bandari zetu ni salama na<br />

zina mazingira mazuri.<br />

Tuko tayari kuyapokea maazimio ya mkutano huu kama mtakavyoona inafaa<br />

kuzishirikisha Serikali mbalimbali, ikiwa ni pamoja na ya Tanzania, Jumuiya za<br />

kikanda za uchumi pamoja na Taasisi mbalimbali za kimataifa kwa lengo la<br />

kuboresha biashara na uchumi wa nchi zetu. Nawahakikishia kuwa Serikali ya<br />

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itapokea dawa mtakayotupa na kwa<br />

kuangalia namna bora ya kuitumia.<br />

Kutembelea Vivutio vya Utalii<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

Pamoja na kazi kubwa mliyonayo waswahili tunasema kazi na dawa. Nchi yetu<br />

imeberikiwa kuwa na maliasili nyingi za asili na kwamba mkoa huu wa Arusha<br />

ambapo Kongamano hili linafanyika ni eneo moja wapo linaloongoza kwa<br />

vivutio hivyo na kwa kweli Arusha ni kitovu cha utalii.Nawasisitizia kutumia<br />

fursa ya kuwepo kwenu hapa kwenda kufaidi mandhari nzuri ya nchi yetu na<br />

hazina yetu. Tembeleeni Ngorongoro Crater ambayo iko karibu na hapa kiasi<br />

cha wa mwendo wa saa mbili. Waliokwisha kutembelea Tanzania wanasema<br />

kama hujafika Ngorongoro, basi hujafika Tanzania. Karibuni sana.<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

Napenda pia kuwahakikishia washiriki wa mkutano huu kwamba Watanzania ni<br />

watu wenye upendo na wapenda amani, hivyo jisikieni mpo huru katika kipindi<br />

chote mtakapokuwa hapa nchini. Jisikieni mpo nyumbani mkiwa mbali na<br />

nyumbani.<br />

Ndugu Mwenyekiti,<br />

6


Kwa haya machache, naomba sasa kutangaza rasmi kuwa mkutano wa<br />

fungamano wa sekta ya bandari ulimwenguni kwa nchi za Afrika na Ulaya<br />

umefunguliwa. Nawatakieni mkutano wenye mafanikio,<br />

Asanteni kwa kunisikiliza.<br />

Mungu Ibariki Tanzania,<br />

Mungu Ibariki Afrika.<br />

7

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!