18.02.2015 Views

Kilimo bora cha zao - Ministry Of Agriculture, Food and Cooperatives

Kilimo bora cha zao - Ministry Of Agriculture, Food and Cooperatives

Kilimo bora cha zao - Ministry Of Agriculture, Food and Cooperatives

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA<br />

WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA<br />

<strong>Kilimo</strong> BORA <strong>cha</strong><br />

<strong>zao</strong> la Soya<br />

IDARA YA MAENDELEO YA MAZAO<br />

Sehemu ya Uendelezaji wa Ma<strong>zao</strong><br />

kijitabu hitimisho.indd 1<br />

5/17/06 11:36:00 PM


kijitabu hitimisho.indd 2<br />

5/17/06 11:36:01 PM


KILIMO BORA CHA<br />

ZAO LA SOYA<br />

Kime<strong>and</strong>ikwa na :-<br />

Bw. Beatus A. Malema<br />

Bibi Judith M. Kitivo<br />

Wizara ya <strong>Kilimo</strong>, Chakula na<br />

Ushirika,<br />

Sehemu ya Uendelezaji Ma<strong>zao</strong> (CPS)<br />

Dar es Salaam<br />

Wizara ya <strong>Kilimo</strong>, Chakula na<br />

Ushirika,<br />

Sehemu ya Uendelezaji Ma<strong>zao</strong> (CPS)<br />

Dar es Salaam<br />

Dkt. Catherine S. Madata Wizara ya <strong>Kilimo</strong>, Chakula na<br />

Ushirika,<br />

Kituo <strong>cha</strong> Utafiti K<strong>and</strong>a ya<br />

Ny<strong>and</strong>a za Juu Kusini,<br />

Uyole- Mbeya<br />

Dkt. Fidelis A. Myaka<br />

Wizara ya <strong>Kilimo</strong>, Chakula na<br />

Ushirika,<br />

Kituo <strong>cha</strong> Utafiti K<strong>and</strong>a ya<br />

Mashariki,<br />

Ilonga- Kilosa<br />

i<br />

kijitabu hitimisho.indd 3<br />

5/17/06 11:36:02 PM


<strong>Kilimo</strong> Bora <strong>cha</strong> Zao la Soya,<br />

Kimetayarishwa na kutolewa na:<br />

Wizara ya <strong>Kilimo</strong>, Chakula na Ushirika.<br />

S.L.P. 9192, Dar - es- salaam, Tanzania.<br />

Toleo ya Kwanza 2006<br />

Kwa ushauri zaidi wasiliana na:<br />

Idara ya Maendeleo ya Ma<strong>zao</strong>,<br />

Sehemu ya Uendelezaji Ma<strong>zao</strong>,<br />

S. L. P. 9192, Dar es Salaam, Tanzania<br />

Simu: 022 2864899<br />

Fax: 022 2864899<br />

Barua pepe: cps@kilimo.go.tz<br />

Tovuti: www.agriculture.go.tz<br />

Mkurugenzi wa Utafiti wa <strong>Kilimo</strong>,<br />

K<strong>and</strong>a ya Ny<strong>and</strong>a za Juu Kusini,<br />

S.L.P. 400, Mbeya, Tanzania.<br />

Simu: 025 2510062/2510363<br />

Fax: 025 2510065<br />

Barua pepe: uyole@ud.co.tz<br />

Mkurugenzi wa Utafiti,<br />

K<strong>and</strong>a ya Mashariki,<br />

S<strong>and</strong>uku la Pekee, Kilosa, Tanzania.<br />

Simu: 023 2623201<br />

Fax: 023 2623284<br />

Barua pepe: ilonga@africaonline.co.tz<br />

Michoro na Usanifu<br />

Comic Media Group, S. L. P. 3204 Morogoro, Tanzania<br />

ii<br />

kijitabu hitimisho.indd 4<br />

5/17/06 11:36:02 PM


YALIYOMO<br />

<strong>Kilimo</strong> Bora <strong>cha</strong> Soya<br />

UTANGULIZI<br />

i<br />

iv<br />

SURA YA KWANZA: HISTORIA, UMUHIMU NA AINA ZA SOYA<br />

Historia ya <strong>zao</strong> la Soya nchini Tanzania 1<br />

Umuhimu wa <strong>zao</strong> la Soya 2<br />

Aina za Soya 3<br />

SURA YA PILI: MAZINGIRA, MVUA NA RUTUBA YA UDONGO<br />

Mazingira na mikoa inayofaa kilimo <strong>cha</strong> soya 5<br />

Mahitaji ya Mvua 7<br />

Rutuba ya Udongo na Mahitaji ya Mbolea 7<br />

SURA YA TATU: UTAYARISHAJI NA UTUNZAJI WA SHAMBA LA SOYA<br />

Kutayarisha shamba 9<br />

Mbegu 9<br />

Wakati wa kup<strong>and</strong>a 11<br />

Nafasi ya kup<strong>and</strong>a 12<br />

Palizi 14<br />

SURA YA TANO: WADUDU, MAGONJWA NA WANYAMA<br />

WAHARIBIFU<br />

Wadudu 17<br />

Magonjwa 17<br />

Wanyama waharibifu 18<br />

SURA YA SITA: KUVUNA, KUPURA NA KUHIFADHI SOYA<br />

Kuvuna 19<br />

Kupura 19<br />

Kuhifadhi 22<br />

SURA YA SABA: MAVUNO NA MAPATO YATOKANAYO NA SOYA<br />

Mavuno 22<br />

Mapato 23<br />

KIAMBATANISHO : Wastani wa gharama na faida za<br />

uzalishaji wa soya ukilinganisha na ma<strong>zao</strong> mengine 24<br />

MAREJEO 26<br />

iii<br />

kijitabu hitimisho.indd 5<br />

5/17/06 11:36:03 PM


UTANGULIZI<br />

Zao la soya lina protini nyingi yenye u<strong>bora</strong> wa hali ya juu kuliko<br />

iliyoko katika aina nyingine ya ma<strong>zao</strong> ya mimea. Kiasi <strong>cha</strong> protini<br />

katika soya inazidi hata kiasi <strong>cha</strong> protini katika nyama, mayai<br />

na maziwa. Sifa nyingine za <strong>zao</strong> la soya ni pamoja na kuwa na<br />

mafuta yasiyo kuwa na lehemu (cholesterol), uwezo wa mmea wa<br />

soya kuongeza mbolea aina ya nitrojeni kwenye udongo, gharama<br />

ndogo za uzalishaji ukilinganisha na ma<strong>zao</strong> mengine, uwingi wa<br />

protini unaoweza kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto na<br />

kinga kwa magonjwa ya kansa, shinikizo la damu na kuwaongezea<br />

nguvu wagonjwa wa UKIMWI na magonjwa mengine. Aidha,<br />

uwezo wa soya kustawi katika maeneo yanayostawisha mahindi<br />

na maharage unamaanisha kwamba <strong>zao</strong> hilo linaweza kulimwa<br />

sehemu nyingi nchini Tanzania. Sifa hizo zimefanya <strong>zao</strong> la soya<br />

kuwa muhimu katika <strong>cha</strong>kula <strong>cha</strong> binadamu na mifugo na katika<br />

kutengeneza bidhaa mbalimbali za vyakula na madawa.<br />

Pamoja na manufaa hayo ya <strong>zao</strong> la soya, <strong>zao</strong> hilo halifahamiki<br />

kama ilivyo ma<strong>zao</strong> mengine mfano maharage na mahindi. Wakulima<br />

wengi hawazijui kanuni za kilimo <strong>bora</strong> <strong>cha</strong> soya. Hii inatokana<br />

na kutojua umuhimu wa <strong>zao</strong> hilo na hivyo kutotilia maanani<br />

katika kulilima na kulitumia kuboresha afya na kipato hasa katika<br />

ngazi ya kaya.<br />

Lengo kuu la kijitabu hiki ni kuwafahamisha wakulima, maafisa<br />

ugani na wadau wengine faida zinazotokana na uzalishaji na<br />

matumizi ya soya. Pia kijitabu hiki kina lengo la kuhamasisha<br />

wakulima na kuendeleza uzalishaji na matumizi ya <strong>zao</strong> hilo<br />

lililoingizwa nchini kwa mara ya kwanza mwaka wa 1907. Ni<br />

matarajio ya Wizara ya kuwa wakulima na wadau wengine<br />

watafaidika kwa kutumia kijitabu hiki kwa ajili ya kuendeleza na<br />

kuongeza uzalishaji, tija na matumizi ya soya hapa nchini.<br />

iv<br />

kijitabu hitimisho.indd 6<br />

5/17/06 11:36:04 PM


SURA YA KWANZA<br />

HISTORIA, UMUHIMU NA AINA ZA SOYA<br />

Historia ya <strong>zao</strong> la Soya nchini Tanzania<br />

Soya (Glycine max) ni <strong>zao</strong> la jamii ya mikunde. Zao hilo asili yake<br />

ni nchi ya China ambako lilianza kulimwa takribani miaka 4800<br />

iliyopita. Zao la soya liliingizwa nchini Tanzania mwaka wa 1907<br />

katika maeneo ya Amani mkoani Tanga. Kati ya miaka ya 1930<br />

na 1960, kilimo <strong>cha</strong> soya kilipanuka na kuenea hadi maeneo ya<br />

Nachingwea mkoa wa Mtwara, Kilosa mkoa wa Morogoro na<br />

Peramiho mkoa wa Ruvuma. Kuenea kwa <strong>zao</strong> hilo katika maeneo<br />

hayo kulitokana na msukumo wa mashirika ya Overseas <strong>Food</strong><br />

Co-operation – (OFC), State Trading Cooperation (STC), General<br />

Agricultural Production for Export – (GAPEX) na<br />

National Milling<br />

Corporation – (NMC). Mashirika hayo yalisafirisha soya kwenda<br />

katika nchi za Japan na Singapore.<br />

Kwa kuwa uzalishaji wa <strong>zao</strong> hilo katika mikoa hiyo ulilenga soko<br />

la nje, wananchi hawakufundishwa matumizi yake na kwa sababu<br />

hiyo baada ya mashirika hayo kua<strong>cha</strong> biashara ya <strong>zao</strong> hilo kilimo<br />

<strong>cha</strong> soya kilififia hadi mwishoni mwa miaka ya 1980 na mwanzoni<br />

mwa miaka ya 1990 ambapo uzalishaji ulianza tena baada ya jamii<br />

kuhamasika katika matumizi ya soya hasa katika kutengeneza<br />

vyakula vya watoto.<br />

1<br />

kijitabu hitimisho.indd 7<br />

5/17/06 11:36:04 PM


Umuhimu wa <strong>zao</strong> la Soya<br />

Soya ni <strong>zao</strong> lenye virutubisho vingi vya aina ya protini ikilinganishwa<br />

na virutubisho vya aina hiyo katika ma<strong>zao</strong> mengine ya mimea na<br />

hata katika baadhi ya vyakula vinavyotokana na wanyama kama<br />

nyama na mayai na maziwa. Sifa hizo za soya zinafanya <strong>zao</strong> hilo,<br />

kuwa na umuhimu wa kipekee katika kutengeneza vyakula vya<br />

binadamu na mifugo na matumizi katika viw<strong>and</strong>a vya madawa<br />

na matumizi mengineyo.<br />

Mafuta yatokanayo na soya hayana<br />

lehemu (cholesterol) na hivyo kuwa na sifa ya kuboresha afya ya<br />

walaji. Zifuatazo ni faida za kutumia soya:-<br />

i. Soya ina virutubisho vingi na vilivyokamilika vya aina ya<br />

protini ambayo ni muhimu katika kuboresha lishe na afya kwa<br />

binadamu na mifugo;<br />

ii. Soya ni <strong>cha</strong>nzo rahisi na chenye gharama nafuu <strong>cha</strong> protini<br />

ambacho hata mtu wa kipato <strong>cha</strong> chini anaweza kumudu kwa<br />

kuwa <strong>zao</strong> hilo linaweza kulimwa maeneo mengi hapa nchini;<br />

iii. Kwa kuwa soya ina kiasi kikubwa <strong>cha</strong> protini ikilinganishwa<br />

na nyama na mayai na maziwa, inasaidia kupunguza kasi ya<br />

mashambulizi ya vijidudu vya maradhi mbalimbali ikiwa ni<br />

pamoja na magonjwa ya kansa, moyo, na kuwaongezea nguvu<br />

wagonjwa hasa wa UKIMWI;<br />

iv. Soya ni <strong>zao</strong> muhimu kwa watu wa kipato <strong>cha</strong> chini katika<br />

kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto kwa kuwa hawawezi<br />

kumudu gharama za vyanzo vingine vya protini kama nyama<br />

na mayai;<br />

v. Kutokana na uwingi wa protini, matumizi ya soya kwa watoto<br />

yanasaidia viungo kukua kwa haraka;<br />

vi. Soya hurutubisha udongo kwa kutumia njia ya nitrogen<br />

fixation. Kwa hiyo ni <strong>zao</strong> linalofaa kutumika katika kilimo <strong>cha</strong><br />

mzunguko (crop rotation) na katika kurutubisha ardhi ;<br />

2<br />

kijitabu hitimisho.indd 8<br />

5/17/06 11:36:05 PM


vii. Soya huongeza kipato na ni <strong>zao</strong> linaloweza ku<strong>cha</strong>ngia katika<br />

kuondoa umaskini kwa mkulima kutokana na gharama ndogo<br />

za uzalishaji. Aidha, ni <strong>zao</strong> linaloweza kuondoa umaskini<br />

kwa watengenezaji wa vyakula vya binadamu na mifugo,<br />

wafanyabiashara na wafugaji na kutoa ajira kwa rika zote<br />

yaani vijana na wazee, vijijini na mijini; na<br />

viii. Utafiti wa hivi karibuni unaonyesha kuwa mafuta ya soya<br />

yanaweza kutumika kwa kuendeshea mitambo yaani bio-fuel<br />

na bio-diesel.<br />

Aina za Soya<br />

Kuna aina mbalimbali za soya; aina zilizozoeleka Tanzania ni<br />

pamoja na Bossier, Uyole soya 1, Ezumu Tumu, Delma Hermon,<br />

Duiker na Kaleya. Kila aina inahitaji mazingira na hali ya hewa inakoweza<br />

kustawi, kukomaa kwa muda maalum na kutoa mavuno<br />

mazuri. Hata hivyo Bossier ni aina ambayo hustawi katika maeneo<br />

mengi nchini. Kwa wastani, aina mbalimbali za soya huchukua<br />

wastani wa miezi mitatu hadi saba kukomaa kutegemea na<br />

aina, mahali ilikop<strong>and</strong>wa na utunzaji katika shamba.<br />

3<br />

kijitabu hitimisho.indd 9<br />

5/17/06 11:36:06 PM


4<br />

kijitabu hitimisho.indd 10<br />

5/17/06 11:36:06 PM


SURA YA PILI<br />

MAZINGIRA, MVUA NA RUTUBA YA UDONGO<br />

Mazingira na mikoa inayofaa kilimo <strong>cha</strong> soya<br />

Soya inaweza kulimwa katika sehemu zote zenye sifa na zinazofaa<br />

kwa kilimo <strong>cha</strong> maharage na mahindi. Sifa hizo ni pamoja na<br />

mvua ya kutosha, udongo usiotuamisha maji na udongo tifutifu<br />

usio na m<strong>cha</strong>nga mwingi. Kutokana na kuwepo kwa maeneo<br />

mengi nchini yenye sifa hizo, ni dalili kuwa <strong>zao</strong> la soya linaweza<br />

kustawi katika maeneo hayo ambayo yapo karibu nchi nzima.<br />

Jambo muhimu linalotakiwa ni kufahamu na kup<strong>and</strong>a aina za<br />

soya zinazofaa katika eneo husika kulingana na maelekezo ya<br />

wataalamu. Kwa sasa mikoa inayoongoza kwa kilimo <strong>cha</strong> soya<br />

ni Ruvuma, Mbeya, Rukwa, Iringa na Morogoro. Mikoa mingine<br />

yenye uwezo na sifa za kuzalisha soya ni Tanga, Mtwara, Lindi,<br />

Kagera, Mara, Kigoma, Kilimanjaro, Arusha na Manyara (Mchoro<br />

Na. 1).<br />

Kwa mujibu wa tathmini iliyofanywa na Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na<br />

Chakula mwaka wa 2005, zaidi ya tani milioni mbili za soya<br />

zinaweza kuzalishwa kwa mwaka endapo maeneo yote ya nchi<br />

yanayofaa kwa kilimo <strong>cha</strong> soya yakitumika ipasavyo. Uzalishaji wa<br />

sasa unakadiriwa kuwa tani elfu tano (5,000). Kiwango hiki <strong>cha</strong><br />

uzalishaji ni <strong>cha</strong> chini sana ukilinganisha na kiwango kinachoweza<br />

kufikiwa. Aidha, kiasi hiki kidogo na uwezo unaoweza kufikiwa ni<br />

<strong>cha</strong>ngamoto katika kuongeza uzalishaji na matumizi ya <strong>zao</strong> hilo.<br />

5<br />

kijitabu hitimisho.indd 11<br />

5/17/06 11:36:06 PM


Mchoro 1: Ramani ya Tanzania inayoonyesha Mikoa<br />

inayozalisha na yenye uwezo na sifa za<br />

kuzalisha soya<br />

Kagera<br />

Mara<br />

Kigoma<br />

Mwanza<br />

Shinyanga<br />

Ta<strong>bora</strong><br />

Singida<br />

Arusha<br />

Kilimanjaro<br />

Tanga<br />

Rukwa<br />

Mbeya<br />

Dodoma<br />

Iringa<br />

Pwani<br />

Dar es<br />

salaam<br />

Morogoro<br />

Lindi<br />

Ruvuma<br />

Mtwara<br />

Mikoa inayozalisha soya kwa wingi<br />

Mikoa yenye uwezo na sifa za kuzalisha soya<br />

Mikoa yenye uwezo wa kuzalisha soya katika<br />

maeneo maalum<br />

Maziwa na bahari ya Hindi<br />

6<br />

kijitabu hitimisho.indd 12<br />

5/17/06 11:36:12 PM


Mahitaji ya Mvua<br />

Soya huhitaji wastani wa mililita 350 hadi 1,500 za mvua kwa<br />

mwaka na inayonyesha kwa mtawanyiko mzuri hususan katika<br />

kipindi chote <strong>cha</strong> ukuaji wa <strong>zao</strong> hilo. Soya pia inafaa katika kilimo<br />

<strong>cha</strong> umwagiliaji kwani katika maeneo hayo kunakuwa na uhakika<br />

wa unyevu muda wote. Jambo la kuzingatia ni kutowepo kwa<br />

mvua wakati soya inapokauka.<br />

Rutuba ya Udongo na Mahitaji ya Mbolea<br />

Kama ilivyo kwa ma<strong>zao</strong> mengi, soya pia huhitaji udongo wenye<br />

rutuba na usiotuamisha maji. Hivyo endapo soya italimwa katika<br />

sehemu yenye rutuba hafifu, itahitaji mbolea kama ma<strong>zao</strong><br />

mengine ijapokuwa huvumilia udongo wenye rutuba hafifu. Kwa<br />

hiyo uamuzi wa kutumia au kutotumia mbolea na kiwango <strong>cha</strong><br />

kutumia utategemea rutuba iliyopo kwenye udongo katika eneo<br />

husika. Hata hivyo, soya huhitaji wastani wa kilo 80 hadi 100 za<br />

mbolea aina ya DAP na TSP kwa hekta moja na kilo 60 hadi 80 kwa<br />

mbolea aina ya CAN kwa hekta moja. Mtaalamu aliyepo karibu na<br />

mkulima anaweza kushauri hali ya rutuba ya udongo katika eneo<br />

husika. Jambo la kuzingatia wakati wa kup<strong>and</strong>a ni kuhakikisha<br />

kuwa mbolea haigusani na mbegu kwa sababu mbolea itaunguza<br />

mbegu na hazitaota. Samadi iliyoiva pamoja na mbolea nyingine<br />

za asili pia zinafaa kutumika katika kilimo <strong>cha</strong> soya.<br />

7<br />

kijitabu hitimisho.indd 13<br />

5/17/06 11:36:14 PM


8<br />

kijitabu hitimisho.indd 14<br />

5/17/06 11:36:14 PM


SURA YA TATU<br />

UTAYARISHAJI NA UTUNZAJI WA<br />

SHAMBA LA SOYA<br />

Kutayarisha shamba<br />

Shamba la soya linahitaji ma<strong>and</strong>alizi mazuri kama ilivyo kwa<br />

ma<strong>zao</strong> mengine. Utayarishaji huo wa shamba ni pamoja na<br />

kuondoa magugu yote kwa kuwa soya haivumilii magugu<br />

hasa ikiwa katika hatua za mwanzo za ukuaji (seedling stage).<br />

Shamba la soya linaweza kulimwa kwa sesa au matuta.<br />

<strong>Kilimo</strong> <strong>cha</strong> sesa (Mchoro Na. 2a) <strong>cha</strong>weza kulimwa kwa<br />

kutumia jembe la mkono au la kukokotwa na wanyama kazi<br />

kama maksai na punda au kwa kutumia trekta. <strong>Kilimo</strong> <strong>cha</strong><br />

matuta kukinga mteremko kinafaa na kinapendekezwa kwa<br />

maeneo yenye mwinuko (Mchoro Na. 2b). Vilevile kilimo<br />

<strong>cha</strong> matuta kinafaa sehemu tambarale lakini zenye mvua<br />

nyingi ili kupunguza madhara ya maji yanayotuama baada<br />

ya mvua kubwa kunyesha.<br />

Mbegu<br />

Ni muhimu ku<strong>and</strong>aa mbegu <strong>bora</strong> na safi mapema kabla ya msimu<br />

wa mvua kuanza. Kwa wastani kilo 20 hadi 30 za mbegu za soya<br />

zinatosha kwa hekta moja kutegemeana na aina ya mbegu. Kwa<br />

kuwa aina nyingi za soya hazistawi kila mahali, ni muhimu kwa<br />

mkulima kuhakikisha kuwa anatumia mbegu inayofaa katika<br />

9<br />

kijitabu hitimisho.indd 15<br />

5/17/06 11:36:14 PM


Mchoro Na. 2a: Shamba la soya - Sesa.<br />

Mchoro Na. 2b: Shamba la soya - Matuta ya kukinga mteremko.<br />

10<br />

kijitabu hitimisho.indd 16<br />

5/17/06 11:36:23 PM


eneo analotaka kulima soya hususani mahitaji ya mvua. Kwa<br />

sababu hiyo ni muhimu kwa mkulima kupata ushauri toka kwa<br />

mtaalam aliyekaribu naye kabla ya kuamua kulima soya. Aidha,<br />

mkulima anashauriwa kununua na kutumia mbegu kutoka katika<br />

sehemu ambazo <strong>cha</strong>nzo <strong>cha</strong> mbegu hizo kinaeleweka. Mfano<br />

wa sehemu hizo ni pamoja na maduka ya pembejeo, wakala<br />

wa mbegu, mashamba ya mbegu na vituo vya utafiti. Hii ni kwa<br />

sababu mbegu ya soya hupoteza nguvu ya uotaji katika msimu<br />

mmoja hasa katika sehemu za joto. Kwa hiyo mkulima anatakiwa<br />

kuhakikisha kuwa anap<strong>and</strong>a mbegu itakayoota. Kama mkulima<br />

hana uhakika na <strong>cha</strong>nzo <strong>cha</strong> mbegu au ana wasiwasi wa kuota<br />

kwa mbegu alizonazo anaweza kufanya majaribo ya uotaji<br />

(germination test) kabla ya kup<strong>and</strong>a. Njia rahisi ni kuzilowesha<br />

mbegu kwa maji na kisha kuziweka kwenye kitambaa mahali<br />

penye joto la kutosha. Mbegu ziloweshwe na maji kila siku mpaka<br />

zitakapoota. Hesabu mbegu zilizoota na iwapo mbegu zilizoota<br />

ni chini ya 75 kati ya mbegu 100 yaani asilimia 75, mkulima<br />

anashauriwa kutop<strong>and</strong>a mbegu hizo.<br />

Wakati wa kup<strong>and</strong>a<br />

Up<strong>and</strong>aji wa soya unategemea na aina na mahali husika. Kwa<br />

aina za soya zinazokomaa mapema, soya ikip<strong>and</strong>wa mwanzoni<br />

mwa msimu wa mvua katika maeneo yanayopata mvua kwa<br />

kipindi kirefu itakomaa wakati mvua bado zinaendelea kunyesha<br />

na hivyo kufanya uvunaji na ukaushaji kuwa mgumu na kuhitaji<br />

nguvu kazi na muda wa ziada la sivyo mbegu zitaoza au kuanza<br />

kuota na kupoteza u<strong>bora</strong> wake. Kwa hiyo ni budi kujua mwenendo<br />

wa mvua mahali husika ili kup<strong>and</strong>a kwa wakati na aina ya soya<br />

kulingana na mahali hapo. Jambo la muhimu ni kuhakikisha<br />

kuwa soya inakomaa wakati hakuna mvua ili kurahisisha uvunaji<br />

11<br />

kijitabu hitimisho.indd 17<br />

5/17/06 11:36:23 PM


na soya kutooza. Jedwali Namba 1 linaonyesha mahali, aina na<br />

muda wa kup<strong>and</strong>a soya.<br />

Jedwali Namba 1: Muda unaoshauriwa kup<strong>and</strong>a soya<br />

Na. Mahali Mbegu Muda<br />

1<br />

Sumbawanga, Nkasi, Songea,<br />

Mbeya, Njombe, Dabaga na sehemu<br />

zenye mvua nyingi/ndefu<br />

Uyole soya<br />

1<br />

Novemba/<br />

Desemba<br />

2<br />

Sumbawanga, Songea, Mbeya,<br />

Njombe na sehemu zenye mvua<br />

nyingi/ndefu<br />

Bossier<br />

Januari<br />

3<br />

Ileje, Mbarali, Chunya, Mtwara na<br />

sehemu zenye mvua kidogo na<br />

fupi<br />

Bossier<br />

Novemba/<br />

Desemba<br />

4<br />

Morogoro na Tanga Bossier Februari na<br />

Machi<br />

Nafasi ya kup<strong>and</strong>a<br />

Mkulima anashuriwa kup<strong>and</strong>a soya kwa nafasi zinazo pendekezwa<br />

na wataalamu. Nafasi hizo ni sentimeta 10 kwa sentimita 45<br />

(Mchoro Na. 3) kwa soya fupi kama bossier na kwenye sehemu<br />

zenye rutuba hafifu. Aidha, tumia sentimeta 10 kwa sentimita 60<br />

kwa soya ndefu kama Uyole Soya 1 na kwenye sehemu zenye<br />

rutuba nyingi. P<strong>and</strong>a mbegu moja kila shimo na zifukiwe kwa<br />

kina <strong>cha</strong> sentimeta mbili hadi sentimita tano ili zisiharibiwe au<br />

kuliwa na wanyama kama panya. Mkulima ahakikishe kuwa soya<br />

inap<strong>and</strong>wa kwenye udongo wenye unyevu wa kutosha; haitakiwi<br />

kabisa kup<strong>and</strong>a soya kwenye udongo mkavu au kuloweka soya<br />

kabla ya kup<strong>and</strong>a.<br />

12<br />

kijitabu hitimisho.indd 18<br />

5/17/06 11:36:25 PM


Sm 45<br />

Sm 10<br />

Mchoro Na. 3: Nafasi za kup<strong>and</strong>a soya katika sesa<br />

Sm 45<br />

Sm 10<br />

Mchoro Na. 4: Nafasi za kup<strong>and</strong>a soya katika matuta<br />

13<br />

kijitabu hitimisho.indd 19<br />

5/17/06 11:36:29 PM


Palizi<br />

Soya ni <strong>zao</strong> ambalo huzongwa na magugu hususani ikiwa<br />

katika hatua za mwanzo za ukuaji. Kwa hiyo mkulima<br />

anashauriwa kuwahi palizi katika kipindi <strong>cha</strong> wiki mbili<br />

baada ya soya kuota. Palizi ya mara ya pili inategemeana na<br />

kiwango <strong>cha</strong> magugu shambani. Endapo magugu yatakuwa<br />

yamefunikwa na majani ya soya palizi ya pili inaweza<br />

isihitajike kama inavyoonekana kwenye Pi<strong>cha</strong> Namba 1<br />

ambapo soya iliyop<strong>and</strong>wa kwa nafasi zinazotakiwa imekua<br />

na kufunika magugu yote na hivyo palizi ya pili kutohitajika.<br />

Pi<strong>cha</strong> Namba 2 inaonyesha soya iliyop<strong>and</strong>wa kwa nafasi<br />

pana na isiyotakiwa ambayo haijakua kufikia kiwango <strong>cha</strong><br />

kufunika magugu na hivyo kulazimisha palizi ya pili kufanyika.<br />

Magugu katika shamba la soya yanaweza kudhibitiwa pia<br />

kwa katumia dawa ya kuzuia magugu kama GALEX; hata<br />

hivyo inafaa kufuata maelekezo ya kutumia ya dawa husika.<br />

14<br />

kijitabu hitimisho.indd 20<br />

5/17/06 11:36:30 PM


Pi<strong>cha</strong> Namba 1: Soya iliyop<strong>and</strong>wa kwa nafasi zinazotakiwa imefunika<br />

magugu.<br />

Pi<strong>cha</strong> Namba 2: Soya iliyop<strong>and</strong>wa kwa nafasi pana zisizotakiwa haijafunika<br />

magugu.<br />

15<br />

kijitabu hitimisho.indd 21<br />

5/17/06 11:36:54 PM


16<br />

kijitabu hitimisho.indd 22<br />

5/17/06 11:36:54 PM


SURA YA TANO<br />

WADUDU, MAGONJWA NA WANYAMA WAHARIBIFU<br />

Wadudu<br />

Kwa sasa, nchini Tanzania soya haishambuliwi sana na wadudu<br />

kama ilivyo sehemu nyingine ambako <strong>zao</strong> hilo hulimwa kwa wingi.<br />

Hata hivyo endapo wadudu watatokea mkulima anashauriwa<br />

kutumia dawa za wadudu kama Thiodan 35% EC na Sumithion<br />

50% EC kwenye kipimo <strong>cha</strong> mililita 40 za dawa na lita 20 za maji<br />

au kipimo kinacho pendekezwa katika dawa husika. Upuliziaji wa<br />

dawa ufanywe kulingana na kiasi <strong>cha</strong> mashambulizi ya wadudu<br />

kwenye ma<strong>zao</strong>.<br />

Tofauti na ma<strong>zao</strong> kama mahindi na maharage, hakuna wadudu<br />

waharibifu wa soya ghalani. Hivyo <strong>zao</strong> hilo linaweza kutunzwa<br />

kwa muda mrefu ghalani bila kuwa na athari za wadudu. Kwa<br />

mkulima na wafanyabiashara, kutokuwepo wadudu waharibifu<br />

ghalani kunapunguza gharama za utunzaji hadi bei nzuri<br />

itakapofikiwa.<br />

Magonjwa<br />

Kama ilivyo kwa wadudu, magonjwa ya soya ni ma<strong>cha</strong>che. Hata<br />

hivyo magonjwa ambayo hutokea kwa nadra ni yale yanayotokana<br />

na vimelea vya ukungu na bakteria. Magonjwa hayo huenezwa<br />

kwa mbegu, masalia ya mimea shambani na wadudu mafuta.<br />

17<br />

kijitabu hitimisho.indd 23<br />

5/17/06 11:36:54 PM


Hivyo ni <strong>bora</strong> kwa mkulima kuzingatia kanuni za kilimo <strong>bora</strong><br />

au kupata ushauri wa kitaalamu ili kuepukana na magonjwa<br />

hayo. Njia mojawapo ya kuzuia kuenea kwa magonjwa katika<br />

<strong>zao</strong> la soya ni kup<strong>and</strong>a mbegu safi na zilizopendekezwa mahali<br />

husika. Aidha, p<strong>and</strong>a kwa mzunguko (crop rotation) kwa kutumia<br />

ma<strong>zao</strong> yasiyoshambuliwa na magonjwa ya soya kama alizeti na<br />

mahindi.<br />

Wanyama waharibifu<br />

Kwa kawaida soya hupendwa sana na panya wa shambani na<br />

ghalani. Wanyama wengine ni pamoja na sungura, paa, swala,<br />

n.k. Mkulima anashauriwa kutumia mbinu na njia mbalimbali<br />

zikiwemo za asili, kukabiliana na wanyama hao bila kuharibu<br />

mazingira.<br />

18<br />

kijitabu hitimisho.indd 24<br />

5/17/06 11:36:55 PM


Kuvuna<br />

SURA YA SITA<br />

KUVUNA, KUPURA NA KUHIFADHI SOYA<br />

Soya huchukua wastani wa miezi mitatu hadi saba kukomaa<br />

kutegemea na aina, mahali ilikop<strong>and</strong>wa na utunzaji wa shamba.<br />

Kwa mfano soya aina ya Bossier huchukua miezi mitatu hadi<br />

minne kukomaa na aina ya Uyole Soya 1 miezi minne hadi mitano.<br />

Dalili za soya kukomaa ni wakati majani yanapokuwa na rangi ya<br />

njano. Anza kuvuna baada ya majani kuanza kupukutika.<br />

Soya ikikauka, mag<strong>and</strong>a yake hupasuka na mbegu hupukutikia<br />

chini. Kwa hiyo mkulima anashauriwa kuwahi kuvuna soya<br />

mara inapokomaa na kuanza kukauka. Ili kuzuia upotevu wa<br />

<strong>zao</strong> shambani, inashauriwa kuvuna majira ya asubuhi au majira<br />

ambayo sio ya jua kali endapo soya imekauka na kuanza kupasuka<br />

wakati wa kuvuna.<br />

Kupura<br />

Soya haitakiwi kupigwa kwa nguvu kwa sababu mbegu zake<br />

hupasuka kirahisi (Mchoro Na 5). . Mara baada ya kupura, ondoa<br />

takataka na u<strong>cha</strong>fu mwingine kwenye soya kwa kupepeta<br />

(Mchoro Na. 6) na kupembua. Kausha soya kufikia wastani wa<br />

asilimia 10 ya kiasi <strong>cha</strong> maji (moisture content) kisha ihifadhi<br />

ghalani kwa matumizi au kusubiri soko.<br />

19<br />

kijitabu hitimisho.indd 25<br />

5/17/06 11:36:55 PM


Mchoro Na. 5: Kupura soya<br />

18<br />

kijitabu hitimisho.indd 26<br />

5/17/06 11:37:10 PM


Mchoro Na. 6: Mama anapepeta soya kabla ya kuhifadhi<br />

19<br />

kijitabu hitimisho.indd 27<br />

5/17/06 11:37:31 PM


Kuhifadhi<br />

Hifadhi soya baada ya kuhakikisha kuwa imekauka vizuri. Ni<br />

muhimu kuhifadhi soya mahali pakavu ili soya isipate uvundo na<br />

kuharibu soya ya mbegu na ya <strong>cha</strong>kula. Soya inaweza kuhifadhiwa<br />

kwenye vihenge au kwenye magunia kama ma<strong>zao</strong> mengine,<br />

tofauti ni kutohitajika dawa ya kuhifadhia.<br />

20<br />

kijitabu hitimisho.indd 28<br />

5/17/06 11:37:31 PM


SURA YA SABA<br />

MAVUNO NA MAPATO YATOKANAYO NA ZAO LA SOYA<br />

Mavuno<br />

Soya ina uwezo wa kutoa kilo 1,500 hadi 2,500 kwa hekta kutegemea<br />

na aina,<br />

hali ya hewa, rutuba ya udongo, matumizi ya mbolea na<br />

utunzaji kuanzia wakati wa ku<strong>cha</strong>gua mbegu, kulima, kup<strong>and</strong>a<br />

na kuvuna. Kiasi hicho <strong>cha</strong> mavuno ni sawa na kilo 600 hadi 1,000<br />

kwa ekari moja.<br />

Mapato<br />

Kutokana na mavuno ya soya, mkulima anaweza kupata mapato<br />

mengi ukilinganisha na ma<strong>zao</strong> kama mahindi na maharage<br />

kwa eneo lililosawa na eneo la soya. Ukweli huu unabainishwa<br />

na tathmini iliyofanyika mwaka wa 2005 na Wizara ya <strong>Kilimo</strong><br />

na Chakula, juu ya hali kilimo <strong>cha</strong> soya nchini. Tathmini hiyo<br />

ilionyesha kuwa wastani wa gharama za kuzalisha kilo moja ya<br />

soya kwa mikoa ya Ny<strong>and</strong>a za Juu za Kusini hususan Songea Vijijini<br />

ni shilingi 130 (Kiambatanisho Na 1), kwa hiyo kama mkulima<br />

atauza soya kwa wastani wa shilingi mia mbili (200) kwa kilo<br />

moja bila gharama ya kusafirisha mbali na kijijini kwake anaweza<br />

kupata faida ya kati ya shilingi 105,000 hadi 175,000 kwa hekta<br />

moja au kati ya shilingi 42,000 na 70,000 kwa ekari moja. Hata<br />

hivyo mapato yanaweza kuongezeka endapo mkulima atatunza<br />

na kuuza soya wakati bei imep<strong>and</strong>a kwa kuwa soya inaweza<br />

kutunzwa muda mrefu bila kuharibiwa na wadudu. Nidhahiri<br />

kuwa <strong>zao</strong> la soya linaweza kumuongezea mkulima kipato na<br />

kumuondolea umaskini.<br />

21<br />

kijitabu hitimisho.indd 29<br />

5/17/06 11:37:32 PM


KIAMBATANISHO NA 1: Wastani wa gharama za uzalishaji wa soya,<br />

mahindi, maharage na alizeti kwa ekari moja<br />

Huduma Gharama kwa kila <strong>zao</strong><br />

Mahindi Maharage Alizeti Soya<br />

Kusafi sha shamba<br />

8,000 8,000 8,000 8,000<br />

Kulima 15,000 15,000 15,000 15,000<br />

Kup<strong>and</strong>a 5,000 10,000 5,000 10,000<br />

Palizi ya kwanza 10,000 10,000 8,000 8,000<br />

Kuweka mbolea 5,000 - - -<br />

Kuweka dawa ya wadudu shambani 3,000 3,000<br />

Palizi ya pili 5,000 5,000 - -<br />

Kuvuna 5,000 5,000 5,000 5,000<br />

Kusafi risha 25,000 5,000 10,000 5,000<br />

Kupiga 5,000 3,000 3,000 3,000<br />

Kupepeta 3,000 2,000 2,000 2,000<br />

Kuweka kwenye magunia 2,000 1,000 1,000 1,000<br />

21<br />

kijitabu hitimisho.indd 30<br />

5/17/06 11:37:33 PM


Huduma Gharama kwa kila <strong>zao</strong><br />

Mahindi Maharage Alizeti Soya<br />

Kiasi <strong>cha</strong> mbegu 15 40 18 30<br />

Gharama ya mbegu 1,500 10,000 3,000 12,000<br />

Kiasi <strong>cha</strong> dawa (Kg) 2 1 - -<br />

Gharama ya dawa (Tsh) 12,000 5,000 - -<br />

Magumia ya kamba 8,000 3,000 3,500 3,000<br />

Usafi rishaji kwenda DSM 6,000 6,000 6,000 6,000<br />

Jumla ya gharama 118,500 91,000 69,500 78,000<br />

Mavuna (Kg/Eka) 800 500 400 600<br />

Gharama kwa kilo (Tshs) (Break even price) 148 182 174 130<br />

Bei ya ma<strong>zao</strong> msimu wa mavuno (Tshs / Kg) 120 200 150 200<br />

Faida kwa kilo moja (28) 18 (24) 70<br />

Faida kwa ekari moja (22,500) 9,000 (9,500) 42,000<br />

22<br />

kijitabu hitimisho.indd 31<br />

5/17/06 11:37:34 PM


MAREJEO<br />

1. File NAL/S./17/124. (2005). Soybean in Southern regions<br />

of Tanzania. Dr. Mponda, O. K. K. ARI Naliendele. Personal<br />

communication<br />

2. Laswai, H. S., Kulwa, K. B. M., Ballegu, W. R. W., Silayo, V. C.<br />

K., Ishengoma, C. G.; Makindara, J. A.; Mpagalile, J. J. <strong>and</strong><br />

Rweyemamu, C. L. (2005).<br />

Soya kwa lishe <strong>bora</strong>. Virutubisho<br />

na matayarisho yake kwa mapishi mbalimbali. SUA NORAD<br />

Focal Programme.<br />

3. Mhagama, G. (2005). Soya: The golden seed in Tanzania.<br />

Sunnhemp seed bank. Mruma Centre, Peramiho Songea.<br />

Personal communication.<br />

4. Madata, C. (Januari, 2005). Jamhuri ya Muungano wa<br />

Tanzania. ilimo <strong>bora</strong> <strong>cha</strong> soya ny<strong>and</strong>a za juu kusini na Vyakula<br />

vya soya na mapishi yake: Soya kwa afya yako. Toleo la Tatu.<br />

5. Myaka, F. A. (1990). Soybean- “the golden bean”. Its past, present<br />

<strong>and</strong> future in Tanzania. In Research <strong>and</strong> Training Newsletter<br />

Vol. V, No. 1, March, 1990. <strong>Ministry</strong> of <strong>Agriculture</strong>, Livestock<br />

Development <strong>and</strong> Co-operatives<br />

6. Myaka, F. A. <strong>and</strong> Mwemezi E. T. (1990). Soyabean village<br />

production <strong>and</strong> utilization: first year of prospects. In Research<br />

<strong>and</strong> Training Newsletter Vol. V, No. 4, December, 1990. <strong>Ministry</strong> of<br />

<strong>Agriculture</strong>, Livestock Development <strong>and</strong> Co-operatives<br />

7. Ngeze, P. B. (1993). Jifunze kustawisha maharage ya soya.<br />

Kagera Writer <strong>and</strong> Publishers Co-operative Society Ltd. Bukoba<br />

Tanzania.<br />

23<br />

kijitabu hitimisho.indd 32<br />

5/17/06 11:37:35 PM


8. URT (November, 2005). Soybean Study in Tanzania. <strong>Ministry</strong> of<br />

<strong>Agriculture</strong> <strong>and</strong> <strong>Food</strong> Security.<br />

24<br />

kijitabu hitimisho.indd 33<br />

5/17/06 11:37:35 PM


kijitabu hitimisho.indd 34<br />

5/17/06 11:37:37 PM


kijitabu hitimisho.indd 35<br />

5/17/06 11:37:38 PM


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA<br />

WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA<br />

<strong>Kilimo</strong> BORA <strong>cha</strong><br />

<strong>zao</strong> la Soya<br />

IDARA YA MAENDELEO YA MAZAO<br />

Sehemu ya Uendelezaji wa Ma<strong>zao</strong><br />

kijitabu hitimisho.indd 36<br />

5/17/06 11:38:37 PM


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA<br />

WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA<br />

<strong>Kilimo</strong> BORA <strong>cha</strong><br />

<strong>zao</strong> la Soya<br />

IDARA YA MAENDELEO YA MAZAO<br />

Sehemu ya Uendelezaji wa Ma<strong>zao</strong><br />

kijitabu hitimisho.indd 37<br />

5/17/06 11:39:12 PM

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!