46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI
46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI
46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kwa kuwa hapo awali Wamoabi hawakuchukuliwa kifungoni, wanafananishwa na divai iliyoweza kukaa katika<br />
chombo chake tangu mwanzo bila kukorogwa. Lakini wakati huo, kwa kuwa watachukuliwa kifungoni Babeli,<br />
wanafananishwa na divai inayomiminwa kutoka chombo chake (11-12). Watu watapotewa na matumaini yao katika<br />
mungu wao wa kitaifa aliyeonekana kuwa hana uwezo wa kuwaokoa (13). Askari mashujaa wa Moabu watauawa<br />
katika mauaji ya kutisha sana, na maombolezo makubwa yatakuwepo juu ya taifa lililopondwa na kuangamia (14-17).<br />
Watu wa sehemu zote za Moabu watashtuka wakisikia habari za kuangamia kwa majeshi yao. Taifa lililojivuna<br />
kwa kiburi chake litaaibishwa (18-20), na taifa lenye nguvu sana litapondwa, hukumu ya Mungu inapoenea kutoka mji<br />
mmoja wa Moabu hadi mwingine (21-25).<br />
Watu wale wa Moabu ambao awali waliwadharau na kuwadhihaki Waisraeli na Wayuda, wakati huo wenyewe<br />
wataaibishwa na kudhihakiwa. Watakunywa ghadhabu ya Mungu mpaka watakapolewa na kutapika (26-27). Wamoabi<br />
waliokuwa na kiburi na kuwadharau watu wengine, wakati huo watalazimishwa kukimbia katika aibu na kutafuta<br />
maficho katika mapango na mashimo milimani (28-30). Lakini sasa Yeremia anawaonea huruma anapoona mamlaka<br />
yao yaliyoenea sana yamevunjwa, mavuno yao mashambani na mizabibu vimeharibiwa, na nchi yao yote imechafuliwa<br />
(31-36). Watu hujinyoa nywele na ndevu zao wakijikata kata na kuvaa nguo za magunia kama alama ya maombolezo,<br />
lakini wamechelewa. Taifa la Moabu limekwisha. Limefanana na chombo kilichovunjika na kutupwa jalalani (37-39).<br />
Katika maelezo ya mwisho ya maangamizi, nabii anatoa mfano wa Wababeli wanaoshuka juu ya Moabu kama vile<br />
tai anavyoshuka juu ya mateka yake. Hakuna atakayeweza kutoroka (40-43). Mahali po pote wanapojaribu kukimbilia<br />
hakuna usalama kwa watu wanaoadhibiwa na Mungu (44). Miji ya maana katika Moabu itateketezwa kwa moto na<br />
wenyeji wake watachukuliwa kifungoni (45-<strong>46</strong>; taz.Hes 21:28-29). Lakini Mungu kwa neema yake, hata katika Moabu<br />
atawahifadhi watu wachache watakaosalia (47).<br />
Ujumbe kuhusu Amoni (49:1-6)<br />
Kama vile taifa la udugu wake Moabu, Amoni lilikuwa jamaa wa mbali wa taifa la Yuda. (Moabu na Amoni<br />
walikuwa wana wa Lutu, na Wayuda walitokana na baba mkubwa wa Lutu, Ibrahimu; taz.Mwa 12:5; 19:36-38.)<br />
Waamoni na Wamoabi waliishi katika sehemu za nyanda za nchi ya mashariki ya Yordani. Maana yake ni kwamba,<br />
walikuwa majirani kabisa wa Yuda na Israeli upande wa mashariki.<br />
Karne moja hivi kabla ya wakati wa Yeremia, Waashuri walikuwa wameteka ufalme wa kaskazini wa Israeli na<br />
kuwapeleka watu wake kifungoni (2Fal 15:29; 17:6). Inavyoonekana, Waamoni, wakati ule walichukua nafasi ya<br />
kujitwalia eneo la kabila la Gadi, yaani kabila la Israeli lililoishi mpakani. Lakini Waamoni walisahau kwamba<br />
Waisraeli bado waliendelea kuwa watu wa Mungu. Yeremia anawaambia Waamoni kwamba nchi yao itatekwa na mji<br />
wake mkuu, Raba, utabomolewa. Wakati huo Waisraeli watatwaa upya nchi yao wenyewe (49:1-2. Malkamu (au<br />
Moleki) alikuwa mungu wa kitaifa wa Amoni).<br />
Waamoni walijivunia utajiri waliojipatia, na hivyo walifikiri wako salama wala hawawezi kushambuliwa. Yeremia<br />
anawaambia kwamba utajiri wa mali hauwezi kuwaokoa maadui wanaposhambulia. Watapelekwa kifungoni (3-5),<br />
ingawa baada ya muda watu wachache watakaosalia watarudi tena (6).<br />
Ujumbe kuhusu Edomu (49:7-22)<br />
Waedomu, ambao ni wazao wa Esau, walijivuna kwamba wao walikuwa werevu kuliko mataifa ya jirani zao.<br />
Walitumaini kwamba nchi yao ilikuwa salama wala haikuweza kutekwa, kwa sababu milima mirefu ya mipakani<br />
mwake ilitoa nafasi nzuri sanaya kujitetea. Nabii anawaambia kwamba, si hekima wala silaha na nguvu ya kujitetea<br />
vitaweza kuwaokoa na maafa na maangamizi ambayo Mungu aliwapangia (7-8).<br />
Mkulima wa mizabibu huchuma zabibu zilizoiva na kuziacha zisizoiva bado; mwizi avunjaye nyumba huiba vitu<br />
vile tu anavyovitaka na kuviacha vingine katika nyumba, lakini uharibifu wa maadui juu ya Edomu utakuwa kamili.<br />
Hata watu wale watakaojificha katika mapango ya milimani hawataepukana na maafa hayo (9-10). Lakini Mungu<br />
atawaangalia wale watakaokuwa yatima au wajane kutokana na vita vile (11).<br />
Iwapo watu wasiostahili sana ghadhabu ya Mungu wanapaswa kuvumilia adhabu yake, sembuse watu waovu kama<br />
Waedomu. Wataadhibiwa vikali zaidi. Mungu anawahakikishia kwamba miji yao iliyoendelea na kujivuna juu yake,<br />
itaachwa magofu na kuwa mahali pa kutisha (12-13).<br />
Waedomu walijidanganya walipofikiri kwamba, kwa sababu ya ngome zao za kujitetea walizoziweka sehemu<br />
nyingi milimani hawakuweza kushindwa na maadui. Yeremia anawaonya kwamba, haidhum wamekwea milima mirefu<br />
mpaka juu au walijenga ngome imara sana, hakuna kitu kitakachowaokoa na hukumu ijayo (14-16).<br />
Kuangamizwa kwao kutakuwa moja kwa moja. Kama vile Sodoma na Gomora, Edomu itaachwa ukiwa (17-18).<br />
Kama vile simba atokavyo msituni na kushambulia kundi la kondoo, ndivyo maadui watakavyokuja na kuangamiza<br />
Edomu. Hakuna atakayeweza kujitetea dhidi ya jeshi ambalo Mungu atalichagua ili litekeleze hukumu yake (19-20).<br />
Askari wa Edomu hawatakuwa na nguvu dhidi ya washambulizi. Kilio cha Waedomu kitasikika mbali sana kupita