12.12.2012 Views

13. NABII YONA

13. NABII YONA

13. NABII YONA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>13.</strong> <strong>NABII</strong> <strong>YONA</strong><br />

''Ndipo watu wa Ninawi wakamwamini Mungu''<br />

Shabaha<br />

Kuonyesha jinsi rehema ya Mungu ambavyo hata watu wa mataifa walipewa. Nabii Yona<br />

alitabiri katika Israeli baada ya kufa kwa Elisha.Katika siku zake Mungu aliwatia Israeli katika<br />

mikono ya maadui zao wa kaskazini, lakini Yona alifahamu kuwa mpaka watu watubu na<br />

waache njia zao za uovu na wamgeukie Mungu, maana Mungu asinge wavumilia<br />

milele.Angewaadhibu kwa kuyaleta mataifa makubwa na yenye nguvu kuwaipiga na<br />

kuwateka na kuwafukuza katika nchi yao(Soma Kumbu kumbu la Torati 28:15,25). Na Yona<br />

mwenyewe pia alipata somo la kujifunza kuhusu rehema ya Mungu.<br />

Yona 1-3<br />

<strong>YONA</strong> ANAMWASI MUNGU: Yona1:1-3<br />

Neno la Mungu lilimjia Yona likiwa na agizo la ajabu: “Ondoka, uende Ninawi, mji ule<br />

mkubwa, ukapige kelele juu yake, kwa maana uovu wao umepnda juu mbele zangu”<br />

(mstari 2).<br />

Mungu angewapatia watu wa Ninawi siku 40 za kutubu la wasipotubu angewaangamiza<br />

(mstari 3-4). Ninawi ulikuwa ni mji mkuu wa Ashuru, lilikuwa ni taifa ambalo lilikuwa hodari<br />

kwa vita na wakatili sana na Israeli waliwaogopa sana kuliko mataifa mengine.<br />

Yona aliwapenda sana watu wa taifa lake na aliutumia muda wake kuwafundisha jinsi ya<br />

kumwabudu Mungu wao, ili Mungu aweze kuwabaliki. Hakuweza kuelewa nini Mungu alipatie<br />

taifa ambalo ni adui mkubwa na katili kwa Israeli nafasi ya kuokoka kutoka katika adhabu<br />

ambayo kwa hakika walistahili.<br />

Alihofia kuwa watatubu na Mungu angewatumia kuiadhibu Israeli.<br />

Kwa hiyo Yona aliamua kujichukulia maumuzi mikononi mwake.Akaona njia ya peke ili<br />

wasipone, ni yeye kwenda mbali kabisa na Ninawi, wasingeweza kusikia ujumbe wa Mungu<br />

unaowaita ili watubu na kwa hiyo wangeangamizwa. Alijua vizuri sana ubaya wa kutokumtii<br />

Mungu, lakini alikuwa tayari amekubali afe yeye ili aokoe maisha ya watu wake.<br />

Alikwenda moja kwa moja mpaka bandari Yopa na huko alipata pumziko la maumivu ya<br />

moyoni mwake, meli iliyokuwa ikienda Tarshishi, nchi kavu ambayo ilikuwa mbali sana kwa<br />

upande wa magharibi. Alilipa nauli yake na akapanda meli.<br />

MUNGU ANATUMA WIMBI KUBWA: Yona 1:4-7<br />

Ndipo meli ikawekwa tayari uelekeo wake na safari ikaanza.Kwa muda mfupi ilionekana<br />

kana kwamba Yona ameepuka jukumu la kuwahubiri watu wa Ninawi. Hata hivyo, Mungu, ni<br />

mkweli katika neno lake na anayaona yote yanayotendeka. Hapana hata moja ambalo<br />

limefichika machoni pake asilione. Neno analolisema Mungu ni lazima lifanyike hakuna mtu<br />

awezaye kubadilisha mpango wake (Isaya 55:10-11).<br />

Haukupita muda mrefu Mungu alituma wimbi kubwa baharini.Wimbi la tufani kubwa<br />

lililotishia kuivunja meli. Mabaharia wakajawa na hofu wakaanza kuililia miugu yao ili iwaokoe.<br />

(Hii miungu ilikuwa ni sanamu tu na kamwe isingeweza kuwasaidia). Waipunguza shehena<br />

kwa kuitupa mizigo yao baharini ili kupunguza uzito wake.<br />

Yona alikuwa upande chini wa meli, alikuwa amelala. Nahodha wa meli alimkuta huko<br />

akamwamsha. Akamwambia, “Una nini ewe ulalaye usingiziamka; ukamwombe Mungu<br />

wako, labda Mungu huyo atatukumbuka tusipotee” (mstari 6).<br />

Na kila mmoja ndani ya ile meli aliamini kuwa wimbi lile la tufani ya kutisha ni adhabu<br />

ambayo imetoka kwa Mungu. Kwa walipiga kura wajue ni nani aliyesababisha hilo ili<br />

alaumiwe yeye, “nayo kura ikamwangukia Yona” (mstari 7).


Wote wakaanza kumwuliza: “Kazi yako ni kazi gani? nawe umetoka wapi? nchi yako<br />

ni nchi ipi? nawe u mtu wa kabila gani?” (mstari 8).<br />

Ni hapo sasa Yona alipoamka kabisa. Mawimbi hayakumhofisha Yona, maana<br />

aliwaambia, “Nami namcha BWANA, Mungu wa mbingu, aliyeziumba bahari na nchi<br />

kavu” ( mstari 9). Alikiri kuwa alikuwa amejaribu kuutoroka uso wa BWANA na watu wale<br />

wakaogopa mno walipotambua nguvu za Mungu ambaye Yona alimwabudu. Ni lazima jambo<br />

fulani litendeke, maana bahari ilikuwa inazidi kuchafuka na tufani ikiongezeka zaidi.Basi<br />

wakamwuliza, “Basi tukutende nini, ili bahari itutulilie?” ( mstari 11). Naye akawajibu,<br />

“Nikamateni, mnitupe baharini; basi bahari itawatulilia; kwa maana ninajua ya kuwa ni<br />

kwa ajili yangu tufani hii imewapata” (mstari 12).<br />

Na ingawa watu walikuwa na nia na hofu ya kutaka kuokoa maisha yao, wazo hili la<br />

kumtupa kwa makusudi Yona baharini liliwaogopesha sana. Walijaribu kuipeleka meli<br />

kuelekea nchi kavu, lakini walishindwa. Watu wakamlilia BWANA. Ikaonekana kuwa ni lazima<br />

wafanye kama Yona alivyokuwa amewaambia, uku wakimwomba ili Mungu asiwahsabie<br />

dhambi hiyo, maana walimwamini Yona, kuwa ni Mungu aliyeleta mawimbi hayo kw sbabu<br />

yake.<br />

Basi wakamkata Yona, wakamtupa baharini nayo bahari ikatulia. Yoha alikuwa ameongea<br />

kweli-Mungu wake ni kwelindiye aliyeumba bahari na nchi kavu. Wakamtolea dhmbihu ili<br />

kuonyesha shukrani na wakeweka nadhiri ya kumtumikia BWANA. Kwa hiyo wale watu<br />

wakapona kwa kuwa walimpeleka katika mauti.<br />

Hata hivyo, Yona hakufa, Kwa upendo na rehema za ajabu, alikuwa ameshamwadaa<br />

samaki mkubwa kummeza .Yona akawa katika tumbo la la samaki yule mkubwa muda siku<br />

tatu mchanana usiku.<br />

<strong>YONA</strong> ANALITII NENO LA MUNGU: Yona 2 na 3<br />

Wakati Yona kw mwujiza alikuwa ndani tumbo la samaki mkubwa,alimkumbuka<br />

Mungu,na akakumbu upumbavu wake wa kujaribu kukimbia ili asifanye kazi ya<br />

Mungu.Aliomba na Mungu akamsamehe, akaahidi kuwa atafanya kama Mungu<br />

alivyomwagiza.Kwa hiyo Yoona akajinyenyekeza na akatumbu kwa kutokutii agizo la Mungu.<br />

“BWANA akasema na yule samaki, naye kmtapika Yona pwani” (Yona 2:10).<br />

Ndipo neno la BWANA likamjia Yona mara ya pili, akiagizwa aondoke akarihubiri neno la<br />

Mungu kule Ninawi. Ulikuwa ni mji mkubwa sana, yapata kama km 80 mzunguko wake. Ikawa<br />

Yona alipoingia katika mji alianza kupaza sauti yake ili kila mmoja asikie, “Baada ya siku<br />

arobaini Ninawi utaangamizwa” (mstari 3:4)<br />

Watu wa Ninawi wakaogopa sana hiyo hukumu ambayo Yona alikuwa anaitangaza nao<br />

“wakamwamini Mungu”<br />

Na ikawa Mfalme aliposikia habari hii akaondoka katika kiti cha enzi akavua mavazi yake<br />

ya kifalme akavaa magunia na akakaa katika majivu, hii ikiwa ni ishara ya huzuni na<br />

kutubu.Na watu wote kuanzia aliyekuwa mdogo mpaka aliyekuwa mkuu, wakafanya hivyo<br />

hivyo.Mfalme akatangaza kuwa kila mtu asile chakula na “wakamlilie Mungu kwa nguvu”<br />

na wageuke, wakaache njia zao mbaya.Mfalme wa Ninawi akasema, “Ni nani ajuaye<br />

kwamba Mungu hatageuka na kughairi, a kuiacha hasira yake kali, ili tusiangamizwe?”<br />

(mstari 9)<br />

Mungu alipoona jinsi walivyotubu na kugeuka kuziacha njia zao mbaya, kwa kweli Mungu<br />

aliwaonyesha rehema na hakuwaangamiza.<br />

FUNDISHO KWETU<br />

Habari hiiinazungumzia sana kuhusu kutubu.Mungu aliwataka watu wa Ninawi watubu<br />

kwa ajili ya njia zao mbaya au Mungu awaangamize.


'Kutubu' ni kuomba msamaha kwa ajili ya dhambi zetu tulizozifanya wakati uliopita na<br />

kubadilisha njia zetu na tabia zetu pia.Yona alimwasi Mungu lakini alitubu akanyeyekea na<br />

akaokolewa badala ya kufa akiwa katika maji. Wakati watu wa Ninawi walipomsikia Yona<br />

akihubiri walitubu-mawazo ya mioyo yao ilibadilika na wakawomba Mungu awasamehe.Kila<br />

mmoja wetu ni lazima atafakari njia yake kila siku.Kama wazazi wetu au walimu wetu<br />

atatuambia mahali ambapo hatukuwafurahisha ni lazima tunyenyekee na kubadili njia<br />

zetu.Maneno ya mtume Petro aliyoyatamka siku ile ya pentekoste ni ya mhimu kwetu na kwa<br />

kila mmoja wetu.Petro alisema, “Tubuni, na kila mmpja abatizwe kwa jina lake Kristo,<br />

mpate ondoleo la dhambi zenu” (Matendo ya Mitume 2:38)<br />

MAELEZO YA NYONGEZA<br />

<strong>YONA</strong> ANAJIFUNZA REHEMA YA MUNGU: Yona 4<br />

Yona hakupenda kabisa.Basi jambo lile lile alilokuwa akilifikiria ndilo lililotokea.Alikasirika<br />

sana.Akamwomba Mungu akasema “Kwa maana nalijua ya kuwa wewe u Mungu mwenye<br />

neema, umejaa huruma”. Yona alifikiria kuwa Mungu angeonyesha huruma hiyo kwa Israeli<br />

tu, lakini huruma hiyo wasipewe maadui wao.Akamwomba Mungu auchukue uhai wake ili<br />

yeye afe.Mungu, hata hivyo alimhifadhi Yona ili apate kujifunza kwamba Mungu, “hapendi<br />

mtu yeyote apotee, bali wote wafikirie toba” (2 Petro 3:9).<br />

Mungu atawaangamiza watu wale wanaokataa kulisikia neno lake tu -kwamba ni<br />

Wayahudi au Watu wa mataifa.<br />

Mtume Petro naye aliweza kujifunza somo hili miaka mingi baadaye. Alijifunza kwamba<br />

“katika kila taifa mtu amchaye Mungu, na kutenda haki hukubaliwa na yeye” (Matendo<br />

ya Mitume 10:35). Ni furaha kubwa iliyoje tuliyonayo kuwa na Mungu aliye na tabia hii, kwa<br />

maana sisi ni watu wa mataifa ambao Mungu ametuonyesha kweli yake na ametupatia<br />

tumaini la wokovu<br />

ISHARA YA <strong>NABII</strong> <strong>YONA</strong>: Mathayo12:38-41<br />

Bwana Yesu Kristo alitumia habari hii inayomhusu Yona kama ishara kwa Wayahudi wale<br />

waliokuwapo siku za Yesu. Waandishi na Mafarisayo walikuwa na mashaka ya yeye kuwa<br />

masiya, “mpakwa mafuta” wa Mungu.Kwa hiyo alitumia ishara hii kutaja yatakayompata<br />

baadaye kuhusu kifo chake na kufufuka kwake.<br />

Ni kwa ajili ya kufufuka kwake katika wafu kulikosababisha atu wengi waamwamini Yesu.<br />

“Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la<br />

nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku<br />

katika moyo wa nchi” (mstari 40)<br />

Mungu akamtoa Yona katika tumbo la samaki baada ya siku tatu, ambapo alipokuwa<br />

tumboni yeye alikuwa ni sawa kabisa na aliyekufa. Kisha akaenda Ninawi moja kwa moja,<br />

ambapo aliwahubiri watu ujumbe wa Mungu, uliowataka watu watubu.<br />

Yesu alikuwa kaburini siku tatu mchana na usiku na baadaye alifufuka kutoka katika wafu<br />

(Luka 24:5-7 Matendo ya Mitume 2:31)<br />

Na baada yapo, aliwafundisha wanafunzi wake kwa muda siku arobaini, kabla hajapaa<br />

kwenda mbinguni (Matendo ya Mitume 1:3, 9)<br />

Bwana Yesu Kristo ni wa kwanza kufufuka katika wafu na kupewa uzima wa milele, lakini<br />

Mungu ameweka neema hii ya tumaini moja la uzima wa milele kwa watu wote watakao<br />

mwamini Mungu na kumtii (1Wakorintho 15:20-23)<br />

MASWALI<br />

Majibu Mafupi<br />

1. Ninawi ilikuwa wapi?<br />

2. Ni ujumbe gani ambao Mungu alimpatia Yona awambie watu wa Ninawi?<br />

3. Yona aliamua kufanya nini?<br />

4. Yona alikuwa akifanya nini wakati wimbi lilipozidi?


5. Ni jinsi gani mabaharia walivyojua kuwa Yona ndiye wakulaumiwa kwa ajili ya mawimbi<br />

yale?<br />

6. Je! Yona alimwabudu nani?<br />

7. Yona aliwaambia mabaharia wamfanyaje?<br />

8. Mabaharia walifanya nini kabla ya kumtupa Yona baharini?<br />

9. Palitokea nini baada ya mabaharia kumtupa Yona baharini?<br />

10. Yona hakufa katika maji Ilitokea nini kwake?<br />

11. Yona alikwenda wapi baada ya kufika nchi kavu?<br />

12. Watu wa Ninawi walifanya nini baada ya kusikia ujumbe wa Yona?<br />

Majibu ya Kina<br />

<strong>13.</strong> Yona alijaribu kutoroka asifanye kazi aliyoagizwa na Mungu?<br />

(a) Ni kwa nini alijaribu kutoroka uso wa Mungu?<br />

(b) Yona alifanya nini?<br />

14. Eleza palitokea nini wakati Mungu alipotuma mawimbi ya tufani kubwa na jinsi Yona<br />

alivyofika nchi kavu salama?<br />

15. Eleza kilichotokea wakati Yona alipofika Ninawi?<br />

Majibu ya Nyongeza<br />

16. (a) Nini maana ya kutubu?<br />

(b) Ni kwa watu gani ambao Mungu anawaonyesha rehema?<br />

(c) Je! hili linatusaidiaje sisi?

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!