Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Wote wakaanza kumwuliza: “Kazi yako ni kazi gani? nawe umetoka wapi? nchi yako<br />
ni nchi ipi? nawe u mtu wa kabila gani?” (mstari 8).<br />
Ni hapo sasa Yona alipoamka kabisa. Mawimbi hayakumhofisha Yona, maana<br />
aliwaambia, “Nami namcha BWANA, Mungu wa mbingu, aliyeziumba bahari na nchi<br />
kavu” ( mstari 9). Alikiri kuwa alikuwa amejaribu kuutoroka uso wa BWANA na watu wale<br />
wakaogopa mno walipotambua nguvu za Mungu ambaye Yona alimwabudu. Ni lazima jambo<br />
fulani litendeke, maana bahari ilikuwa inazidi kuchafuka na tufani ikiongezeka zaidi.Basi<br />
wakamwuliza, “Basi tukutende nini, ili bahari itutulilie?” ( mstari 11). Naye akawajibu,<br />
“Nikamateni, mnitupe baharini; basi bahari itawatulilia; kwa maana ninajua ya kuwa ni<br />
kwa ajili yangu tufani hii imewapata” (mstari 12).<br />
Na ingawa watu walikuwa na nia na hofu ya kutaka kuokoa maisha yao, wazo hili la<br />
kumtupa kwa makusudi Yona baharini liliwaogopesha sana. Walijaribu kuipeleka meli<br />
kuelekea nchi kavu, lakini walishindwa. Watu wakamlilia BWANA. Ikaonekana kuwa ni lazima<br />
wafanye kama Yona alivyokuwa amewaambia, uku wakimwomba ili Mungu asiwahsabie<br />
dhambi hiyo, maana walimwamini Yona, kuwa ni Mungu aliyeleta mawimbi hayo kw sbabu<br />
yake.<br />
Basi wakamkata Yona, wakamtupa baharini nayo bahari ikatulia. Yoha alikuwa ameongea<br />
kweli-Mungu wake ni kwelindiye aliyeumba bahari na nchi kavu. Wakamtolea dhmbihu ili<br />
kuonyesha shukrani na wakeweka nadhiri ya kumtumikia BWANA. Kwa hiyo wale watu<br />
wakapona kwa kuwa walimpeleka katika mauti.<br />
Hata hivyo, Yona hakufa, Kwa upendo na rehema za ajabu, alikuwa ameshamwadaa<br />
samaki mkubwa kummeza .Yona akawa katika tumbo la la samaki yule mkubwa muda siku<br />
tatu mchanana usiku.<br />
<strong>YONA</strong> ANALITII NENO LA MUNGU: Yona 2 na 3<br />
Wakati Yona kw mwujiza alikuwa ndani tumbo la samaki mkubwa,alimkumbuka<br />
Mungu,na akakumbu upumbavu wake wa kujaribu kukimbia ili asifanye kazi ya<br />
Mungu.Aliomba na Mungu akamsamehe, akaahidi kuwa atafanya kama Mungu<br />
alivyomwagiza.Kwa hiyo Yoona akajinyenyekeza na akatumbu kwa kutokutii agizo la Mungu.<br />
“BWANA akasema na yule samaki, naye kmtapika Yona pwani” (Yona 2:10).<br />
Ndipo neno la BWANA likamjia Yona mara ya pili, akiagizwa aondoke akarihubiri neno la<br />
Mungu kule Ninawi. Ulikuwa ni mji mkubwa sana, yapata kama km 80 mzunguko wake. Ikawa<br />
Yona alipoingia katika mji alianza kupaza sauti yake ili kila mmoja asikie, “Baada ya siku<br />
arobaini Ninawi utaangamizwa” (mstari 3:4)<br />
Watu wa Ninawi wakaogopa sana hiyo hukumu ambayo Yona alikuwa anaitangaza nao<br />
“wakamwamini Mungu”<br />
Na ikawa Mfalme aliposikia habari hii akaondoka katika kiti cha enzi akavua mavazi yake<br />
ya kifalme akavaa magunia na akakaa katika majivu, hii ikiwa ni ishara ya huzuni na<br />
kutubu.Na watu wote kuanzia aliyekuwa mdogo mpaka aliyekuwa mkuu, wakafanya hivyo<br />
hivyo.Mfalme akatangaza kuwa kila mtu asile chakula na “wakamlilie Mungu kwa nguvu”<br />
na wageuke, wakaache njia zao mbaya.Mfalme wa Ninawi akasema, “Ni nani ajuaye<br />
kwamba Mungu hatageuka na kughairi, a kuiacha hasira yake kali, ili tusiangamizwe?”<br />
(mstari 9)<br />
Mungu alipoona jinsi walivyotubu na kugeuka kuziacha njia zao mbaya, kwa kweli Mungu<br />
aliwaonyesha rehema na hakuwaangamiza.<br />
FUNDISHO KWETU<br />
Habari hiiinazungumzia sana kuhusu kutubu.Mungu aliwataka watu wa Ninawi watubu<br />
kwa ajili ya njia zao mbaya au Mungu awaangamize.