12.12.2012 Views

46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI

46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI

46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>46</strong>:1-<strong>51</strong>:<strong>64</strong> <strong>UJUMBE</strong> <strong>KWA</strong> <strong>MATAIFA</strong> <strong>YA</strong> <strong>KIGENI</strong><br />

Ingawa huduma kubwa ya Yeremia ilihusu Yuda, pia aliitwa ili atangaze ujumbe wa Mungu kwa mataifa ya jirani<br />

(taz.l:5,10). Sehemu hii ya kitabu chake ina mkusanyo wa ujumbe ambao nabii aliutangaza kwa mataifa ya jirani katika<br />

muda wa miaka mingi ya huduma yake, (taz.25:13). Katika matangazo hayo nabii anaonyesha kwamba, kama vile<br />

Mungu alivyoshughulika na Yuda katika haki yake, ndivyo anavyoshughulika na mataifa ya jirani ya Yuda katika haki<br />

yake.<br />

Utaratibu wa matangazo hayo haufuati mfululizo wa matukio yaliyosababisha ujumbe wake. Utaratibu wake zaidi<br />

unafuata jiografia ya nchi zilizohusika, ukianza Misri kusini na kuendelea kaskazini na mashariki kuelekea<br />

Mesopotamia. Kilele cha mfululizo wa matangazo kinahusu taifa lililotawala mambo ya nchi nyingi zaidi ya maeneo<br />

yale, yaani Babeli. (Kuhusu mataifa yanayotajwa hapa, taz. ramani iliyopangwa katika Isaya 13-23, ambapo matangazo<br />

mengine kwa mataifa mbalimbali yameandikwa.)<br />

Ujumbe kuhusu Misri (<strong>46</strong>:1-12)<br />

Wamisri walishindwa na Wababeli mara ya kwanza katika mwaka wa 605 k.K. huko Karkemishi. Vita vile<br />

vilikuwa chanzo cha kumalizika kwa utawala mkuu wa Wamisri katika maeneo yale, navyo viliwaweka Wayuda chini<br />

ya mamlaka ya Wababeli mara ya kwanza (<strong>46</strong>:1-2). Yeremia anatoa mfano wa askari wa Misri wakijiandaa kwa vita (3-<br />

4). Wanaondoka kwa matumaini makubwa ya ushindi, lakini wanashtushwa na ukali wa mashambulio ya Wababeli.<br />

Wamisri wanageuka na kukimbia, lakini wanakatishwa njia katika Mto Frati (5-6).<br />

Katika mfano mwingine wa vita vile, nabii anaona majeshi ya Misri, yakiongezewa nguvu na askari hodari wa nchi<br />

nyingine, wakisonga mbele kama maji ya Mto Nile wakati wa kujaa na kufurika. Hivyo askari hao wanajiona kuwa na<br />

nguvu kiasi kwamba wangeweza kushinda dunia yote (7-9). Lakini siku hiyo siyo siku ya ushindi wa Wamisri. Ni siku<br />

ya hukumu ya Mungu, na Wamisri wanapata machinjo makali sana (10). Utaalamu wote wa Wamisri wa kutumia dawa<br />

hautaweza kuponya majeraha yao. Habari za kushindwa kwa Wamisri zitavuma mbali kabisa (11-12).<br />

Ujumbe wa pili kuhusu Misri (<strong>46</strong>:13-28)<br />

Wakati huo Yeremia anatabiri ushindi mwingine wa Wababeli juu ya Wamisri, lakini ushindi huo hautokei katika<br />

nchi ya kigeni, bali katika nchi ya Misri yenyewe (13). Kadiri majeshi ya Babeli yanavyozidi kusonga mbele ndivyo<br />

miji ya Misri inavyoanguka. Miungu ya Misri haiwezi kuwazuia maadui. Askari waliokodiwa wanatoroka kutoka<br />

uwanja wa vita, wakitafuta usalama katika nchi zao wenyewe (14-16). Farao anashtakiwa kuwa mtu wa kujisifu kwa<br />

maneno mengi ya bure, lakini hawezi kufanya lo lote wakati matendo yanapotakiwa (17).<br />

Wababeli hukaa juu ya Misri kwa mfano wa mnara, sawa sawa na Mlima Tabori unavyokaa juu ya nchi ya jirani<br />

yake, na kama Mlima Karmeli unavyokaa juu ya bahari iliyo karibu nao. Wamizri hawawezi kuwapindua Wababeli,<br />

kwa hiyo wajiandae kwa kifungo (18-19). Kama vile wanyama wa kufuga wanavyokimbia baada ya kuumwa na ndege<br />

mkali aumaye (kipanga), ndivyo Wamisri wanavyowakimbia Wababeli wanaowashambulia (20-21). Kwa kutumia<br />

mfano mwingine, Wamisri huwa kama nyoka anayekimbia na kujificha katika pango lake, akitafuta usalama wake. Na<br />

kwa mfano mwingine tena, Wababeli katika mashambulio yao dhidi ya Wamisri huwa kama wakataji wa kuni<br />

wanaokata msitu mzima (22-24).<br />

Ingawa Wamisri pamoja na miungu yao wanaadhibiwa, hawataangamizwa kabisa. Siku moja watainuka tena (25-<br />

26). Kuhusu watu wa Yuda na Israeli, ingawa wamepelekwa kifungoni katika nchi za kigeni, siku moja watarudi tena<br />

katika nchi yao ambapo watafurahia amani na usalama (27-28).<br />

Ujumbe kuhusu Wafilisti (47:1-7) Nabii anaona kwamba Wababeli watateka nchi ya Wafilisti pia, wakipita juu ya<br />

nchi kama mto unaofurika na maji yake yanaenea katika mashamba yote (47:1-2). Farasi wa Wababeli pamoja na<br />

magari yao ya vita yatakaposhuka kutoka kaskazini, Wafilisti watakimbia kwa hofu kuu, kila mtu akiangalia usalama<br />

wake mwenyewe. Hakuna atakayejali shida ya mwenziwe. Msaada wo wote ambao labda ungeweza kutoka Tiro au<br />

Sidoni utakatishwa, na miji ya Ufilisti itaomboleza juu ya kuangamizwa kwake (3-5).<br />

Yeremia anawaona Wafilisti wakimlilia Mungu na kumsihi akomeshe mauaji ya Wababeli. Kisha nabii anajibu kwa<br />

niaba ya Mungu, akisisitiza kwamba hukumu ya Mungu lazima iendelee mpaka imalizike kabisa (6-7).<br />

Ujumbe kuhusu Moabu (48:1-47)<br />

Moabu lilikuwa taifa mojawapo lililojaribu kufanya mwungano wa kijeshi na Yuda dhidi ya Wababeli (taz.27:l-3).<br />

Wakati huo taifa hilo litateswa kwa hasira ya Wababeli. Yeremia anaonyesha mfano wa matukio yake: nchi<br />

imechafuliwa, ngome zimebomolewa, miji imeharibiwa, na wakimbizi kwa shida kubwa wanakimbia mbele ya majeshi<br />

yanayoingia (48:1-6).<br />

Kemoshi, mungu wa kitaifa wa Wamoabi hataweza kuokoa taifa lake. Kwa kweli, atachukuliwa kifungoni pamoja<br />

na viongozi wa dini na wa kiraia wa Moabu. Miji ya Wamoabi itaachwa mahame na ukiwa (7-9). Kwa kuangamiza<br />

Moabu, Wababeli wanatimiza kazi ya hukumu ya Mungu, kwa hiyo hawana budi kutimiza kazi hiyo sawa sawa (10).


Kwa kuwa hapo awali Wamoabi hawakuchukuliwa kifungoni, wanafananishwa na divai iliyoweza kukaa katika<br />

chombo chake tangu mwanzo bila kukorogwa. Lakini wakati huo, kwa kuwa watachukuliwa kifungoni Babeli,<br />

wanafananishwa na divai inayomiminwa kutoka chombo chake (11-12). Watu watapotewa na matumaini yao katika<br />

mungu wao wa kitaifa aliyeonekana kuwa hana uwezo wa kuwaokoa (13). Askari mashujaa wa Moabu watauawa<br />

katika mauaji ya kutisha sana, na maombolezo makubwa yatakuwepo juu ya taifa lililopondwa na kuangamia (14-17).<br />

Watu wa sehemu zote za Moabu watashtuka wakisikia habari za kuangamia kwa majeshi yao. Taifa lililojivuna<br />

kwa kiburi chake litaaibishwa (18-20), na taifa lenye nguvu sana litapondwa, hukumu ya Mungu inapoenea kutoka mji<br />

mmoja wa Moabu hadi mwingine (21-25).<br />

Watu wale wa Moabu ambao awali waliwadharau na kuwadhihaki Waisraeli na Wayuda, wakati huo wenyewe<br />

wataaibishwa na kudhihakiwa. Watakunywa ghadhabu ya Mungu mpaka watakapolewa na kutapika (26-27). Wamoabi<br />

waliokuwa na kiburi na kuwadharau watu wengine, wakati huo watalazimishwa kukimbia katika aibu na kutafuta<br />

maficho katika mapango na mashimo milimani (28-30). Lakini sasa Yeremia anawaonea huruma anapoona mamlaka<br />

yao yaliyoenea sana yamevunjwa, mavuno yao mashambani na mizabibu vimeharibiwa, na nchi yao yote imechafuliwa<br />

(31-36). Watu hujinyoa nywele na ndevu zao wakijikata kata na kuvaa nguo za magunia kama alama ya maombolezo,<br />

lakini wamechelewa. Taifa la Moabu limekwisha. Limefanana na chombo kilichovunjika na kutupwa jalalani (37-39).<br />

Katika maelezo ya mwisho ya maangamizi, nabii anatoa mfano wa Wababeli wanaoshuka juu ya Moabu kama vile<br />

tai anavyoshuka juu ya mateka yake. Hakuna atakayeweza kutoroka (40-43). Mahali po pote wanapojaribu kukimbilia<br />

hakuna usalama kwa watu wanaoadhibiwa na Mungu (44). Miji ya maana katika Moabu itateketezwa kwa moto na<br />

wenyeji wake watachukuliwa kifungoni (45-<strong>46</strong>; taz.Hes 21:28-29). Lakini Mungu kwa neema yake, hata katika Moabu<br />

atawahifadhi watu wachache watakaosalia (47).<br />

Ujumbe kuhusu Amoni (49:1-6)<br />

Kama vile taifa la udugu wake Moabu, Amoni lilikuwa jamaa wa mbali wa taifa la Yuda. (Moabu na Amoni<br />

walikuwa wana wa Lutu, na Wayuda walitokana na baba mkubwa wa Lutu, Ibrahimu; taz.Mwa 12:5; 19:36-38.)<br />

Waamoni na Wamoabi waliishi katika sehemu za nyanda za nchi ya mashariki ya Yordani. Maana yake ni kwamba,<br />

walikuwa majirani kabisa wa Yuda na Israeli upande wa mashariki.<br />

Karne moja hivi kabla ya wakati wa Yeremia, Waashuri walikuwa wameteka ufalme wa kaskazini wa Israeli na<br />

kuwapeleka watu wake kifungoni (2Fal 15:29; 17:6). Inavyoonekana, Waamoni, wakati ule walichukua nafasi ya<br />

kujitwalia eneo la kabila la Gadi, yaani kabila la Israeli lililoishi mpakani. Lakini Waamoni walisahau kwamba<br />

Waisraeli bado waliendelea kuwa watu wa Mungu. Yeremia anawaambia Waamoni kwamba nchi yao itatekwa na mji<br />

wake mkuu, Raba, utabomolewa. Wakati huo Waisraeli watatwaa upya nchi yao wenyewe (49:1-2. Malkamu (au<br />

Moleki) alikuwa mungu wa kitaifa wa Amoni).<br />

Waamoni walijivunia utajiri waliojipatia, na hivyo walifikiri wako salama wala hawawezi kushambuliwa. Yeremia<br />

anawaambia kwamba utajiri wa mali hauwezi kuwaokoa maadui wanaposhambulia. Watapelekwa kifungoni (3-5),<br />

ingawa baada ya muda watu wachache watakaosalia watarudi tena (6).<br />

Ujumbe kuhusu Edomu (49:7-22)<br />

Waedomu, ambao ni wazao wa Esau, walijivuna kwamba wao walikuwa werevu kuliko mataifa ya jirani zao.<br />

Walitumaini kwamba nchi yao ilikuwa salama wala haikuweza kutekwa, kwa sababu milima mirefu ya mipakani<br />

mwake ilitoa nafasi nzuri sanaya kujitetea. Nabii anawaambia kwamba, si hekima wala silaha na nguvu ya kujitetea<br />

vitaweza kuwaokoa na maafa na maangamizi ambayo Mungu aliwapangia (7-8).<br />

Mkulima wa mizabibu huchuma zabibu zilizoiva na kuziacha zisizoiva bado; mwizi avunjaye nyumba huiba vitu<br />

vile tu anavyovitaka na kuviacha vingine katika nyumba, lakini uharibifu wa maadui juu ya Edomu utakuwa kamili.<br />

Hata watu wale watakaojificha katika mapango ya milimani hawataepukana na maafa hayo (9-10). Lakini Mungu<br />

atawaangalia wale watakaokuwa yatima au wajane kutokana na vita vile (11).<br />

Iwapo watu wasiostahili sana ghadhabu ya Mungu wanapaswa kuvumilia adhabu yake, sembuse watu waovu kama<br />

Waedomu. Wataadhibiwa vikali zaidi. Mungu anawahakikishia kwamba miji yao iliyoendelea na kujivuna juu yake,<br />

itaachwa magofu na kuwa mahali pa kutisha (12-13).<br />

Waedomu walijidanganya walipofikiri kwamba, kwa sababu ya ngome zao za kujitetea walizoziweka sehemu<br />

nyingi milimani hawakuweza kushindwa na maadui. Yeremia anawaonya kwamba, haidhum wamekwea milima mirefu<br />

mpaka juu au walijenga ngome imara sana, hakuna kitu kitakachowaokoa na hukumu ijayo (14-16).<br />

Kuangamizwa kwao kutakuwa moja kwa moja. Kama vile Sodoma na Gomora, Edomu itaachwa ukiwa (17-18).<br />

Kama vile simba atokavyo msituni na kushambulia kundi la kondoo, ndivyo maadui watakavyokuja na kuangamiza<br />

Edomu. Hakuna atakayeweza kujitetea dhidi ya jeshi ambalo Mungu atalichagua ili litekeleze hukumu yake (19-20).<br />

Askari wa Edomu hawatakuwa na nguvu dhidi ya washambulizi. Kilio cha Waedomu kitasikika mbali sana kupita


mipaka yao (21-22).<br />

Ujumbe kuhusu Dameski (49:23-27)<br />

Dameski ilikuwa jiji kuu la nchi ambayo hapo kale ilijulikana kuwa Aramu, na baadaye ilijulikana kuwa Shamu au<br />

Siria. Jiji hilo lilitekwa na Waashuri mwaka wa 612 k.K. (2Fal 16:9), lakini Yeremia alipoanza huduma yake, Dameski<br />

bado ilikaliwa na Waashuri hao, ikiwa makao makuu ya mkoa katika ufalme wao. Wakati huo Yeremia anatabiri<br />

kutekwa kwa nchi ya Shamu (Siria) tena, kwa sababu Wababeli walikuwa tayari kuwashinda Waashuri.<br />

Bila shaka unabii huo ulitolewa wakati wa mwanzo wa huduma ya Yeremia, kwa sababu huduma yake ilianza<br />

mwaka wa 627 k.K., na Wababeli waliwashinda Waashuri baada ya miaka 15 tu, yaani mwaka wa 612 k.K. Yeremia<br />

anawaona Washami wakijaa hofu katika hali yao ya kutoweza kujitetea, wakisikia majeshi ya Wababeli yanakaribia<br />

(23-24). Dameski itakuwa uwanja wa majinjio na uharibifu tena, majeshi ya Wababeli yatakapotekajiji hilo (25-27).<br />

Ujumbe kuhusu Kedari (49:28-33)<br />

Hata makabila ya jangwani yanayohama hama kila wakati yatapata taabu kutokana na mashambulio ya Wababeli.<br />

Kabila linalotajwa na Yeremia ni Wakedari walioishi katika eneo liitwalo Hazori. Wakedari waliishi katika mahema,<br />

walifuga kondoo nao walikuwa wafanya biashara hodari (Zab 120:5; Isa 60:7; Eze 27:21). Yeremia anatabiri kwamba<br />

makao yao yatachafuliwa, wanyama wao watachukuliwa, na wao wenyewe watakimbia kwa hofu (28-30).<br />

Lakini maafa hayo pia ni hukumu ya Mungu juu ya makabila hayo ya jangwani. Desturi yao ilikuwa kuiba katika<br />

miji iliyoshambuliwa na Wababeli, kisha kukimbilia makao yao ambapo walikuwa mbali na njia za mashambulio ya<br />

Wababeli. Usalama wao waliodhania kuwa nao wakati huo unafikishwa mwisho wake, na mali yao ya wizi itapotea<br />

(31-33).<br />

Ujumbe kuhusu Elamu (49:34-39)<br />

Ujumbe kuhusu ufalme wa kale wa Elamu ulikuja katika mwanzo wa enzi ya Sedekia, yeye Sedekia alipojaribu<br />

kuunda mwungano wa kijeshi na mataifa mengine magharibi ya Babeli, kwa makusudi ya kuzuia kuenea kwa mamlaka<br />

ya Babeli (34; taz.27: 1-3,12).<br />

Ujumbe wa Yeremia hapa unaonyesha kwamba Sedekia alipoteza wakati wake bure. Mamlaka ya Wababeli<br />

yangeenea mbali sana, hata nchi zilizo upande wa mashariki ya Babeli, kama vile Elamu, zingepinduliwa (35-38).<br />

Lakini kupinduliwa kwa Elamu kusingekuwa kwa muda wote (39). Ripoti za historia zinatueleza kwamba baadaye nchi<br />

ya Elamu ilikuwa sehemu ya ufalme wa Uajemi ambao ulipindua Babeli (Ezra 1:2).<br />

Ujumbe kuhusu Babeli (50:1-<strong>46</strong>)<br />

Hatimaye Yeremia anaona kwamba taifa lile ambalo Mungu alilitumia kwa kuadhibu taifa la Yuda litaadhibiwa<br />

vile vile. Beli au Merodaki, mungu mkuu wa Wababeli, hataweza kuwaokoa watu wake na mashambulio yatakapokuja<br />

juu yao (50:1-3).<br />

Wayahudi ambao wakati huo watakuwa wamejinyenyekeza katika toba mbele ya Mungu, kwa sababu ya kuanguka<br />

kwa Babeli watapewa nafasi ya kurudi katika nchi yao (4-5).(Koreshi wa Uajemi aliposhinda na kupindua Babeli<br />

mwaka wa 539 k.K., mara moja aliwapa Wayuda ruhusa kurudi katika nchi yao; taz.2Nya 36:22-23.)<br />

Viongozi wa Yuda walikuwa na hatia, kwa sababu walipoteza taifa lao katika njia mbaya (6), lakini Wababeli pia<br />

walikuwa na hatia (ingawa walikanusha jambo hili), kwa sababu wao waliwatendea Wayuda kadiri ya mapenzi yao<br />

wenyewe (7). Kwa hiyo, wakati Wayahudi watakaporudi kutoka Babeli (kwa kweli, watakuwa taifa la kwanza kati ya<br />

yale yaliyopelekwa kifungoni litakalopata uhuru), Babeli yenyewe itaadhibiwa (8-10).<br />

Wababeli walijivuna katika kiburi chao kwamba walishinda na kuteka nyara taifa la <strong>YA</strong>HWEH, yaani Yuda (11).<br />

Wakati huo wataadhibiwa, ghadhabu ya Mungu itakapomiminwa juu yao (12-13). Washambulizi wake watakuwa<br />

wakali sana kwao, kama vile wao walivyokuwa kwa watu wengine. Baada ya kushindwa kwao, watu wote walio<br />

wafungwa wao, watatoroka kwenda katika nchi zao (14-16).<br />

Ufalme wa kaskazini, yaani Israeli, ulitekwa na Waashuri, halafu Uashuru ulitekwa na Wababeli, na hivyo watu wa<br />

Israeli sawa sawa na wale wa Yuda, hatimaye walikuwa chini ya mamlaka ya Babeli. Lakini wakati huo Babeli<br />

itaanguka, na Waisraeli sawa sawa na Wayuda watarudi katika nchi yao, wakiwa watu waliounganika tena na<br />

kusamehewa dhambi zao (17-20).<br />

Nabii akiendelea kuonyesha mfano wa kuanguka kwa Babeli, anawaona washambulizi wake wakihimizwa wasonge<br />

mbele na kushambulia miji mbalimbali ya Babeli (21-22). Taifa lile ambalo kama nyundo lilivunja mataifa mengine,<br />

wakati huo litavunjwa lenyewe. Ghala zake za chakula zitavunjwa, na askari wake watauawa (23-27). Wafungwa wa<br />

Yuda wakati huo watafunguliwa, nao watarudi nyumbani kwao wakimsifu Mungu kwa kuwakomboa watu wake na<br />

kuwaadhibu kwa haki wanyanyasaji wao (28), lakini Wababeli wenye kiburi wataachwa bila mtu wa kuwasaidia (29-<br />

32). Mungu anawaokoa wanaonyanyaswa, lakini anawaadhibu wale wanaowanyanyasa (33-34).


Haidhuru watawala wa Babeli walikuwa na hekima gani, wachawi wao walikuwa wajanja kiasi gani au askari wao<br />

walikuwa hodari na wenye nguvu gani, wote pamoja watauawa. Majeshi yao ya magari yataangamizwa, na hazina zao<br />

zitatekwa nyara (35-37). Kwa njia ya ukame na vita, nchi yote itaharibika na kuachwa katika hali mbaya, hata watu<br />

wasiweze kuishi huko tena (38-40).<br />

Nabii anaonyesha mfano wa hofu ya mfalme wa Babeli anaposikia habari za ushindi wa haraka wa Waajemi na<br />

majeshi ya mwungano wake yakikaribia kwa kasi (41-43). Mungu akichukua hatua dhidi ya Wababeli, hayatakuwepo<br />

matumaini ya kukimbia. Wababeli wanafananishwa na kundi la kondoo linaloshambuliwa na simba. Kwa hofu kubwa<br />

watapiga yowe wanapofikia mwisho wao wa uchungu na ukatili (44-<strong>46</strong>).<br />

Kupinduliwa kwa Babeli (<strong>51</strong>:1-58)<br />

Baada ya kuvuna ngano yake, mkulima anapepeta nafaka zake kwa njia ya kuitupa juu, ili upepo upeperushe<br />

makapi yake, na hivyo anaweza kupata ngano safi. Hali kadhalika Mungu atakapopepeta Babeli, yaani atabagua kati ya<br />

watu wake na watu wa Babeli. Atapeperusha Wababeli katika hukumu yake, lakini atawahifadhi watu wake kwa ajili<br />

yake mwenyewe (<strong>51</strong>:1-5).<br />

Mungu aliwatumia Wababeli ili kuadhibu mataifa mengine, lakini wakati huo wao wenyewe watakunywa<br />

ghadhabu ya Mungu. Watafanana na mlevi aangukaye asiweze kuinuka tena, na mtu aliyejeruhiwa asiweze kupona.<br />

Wakati huo mataifa yaliyoteswa na kupelekwa kifungoni na Wababeli yatapewa uhuru wao, yaani wafungwa wote<br />

wataweza kurudi nyumbani kwao (6-9). Mungu atahakikisha kwamba hukumu ya mwisho itatekelezwa (10).<br />

Kisha nabii anatoa mfano wa jeshi la Wamedi na Waajemi yakijiandaa kwa mashambulio ya mwisho dhidi ya<br />

Babeli. Anawaonya Wababeli kwamba mwisho wao unakaribia, na baada ya muda mfupi jiji lao litajaa askari wa<br />

maadui (11-14). Miungu yote ya Babeli haitakuwa na uwezo wa kuokoa. Miungu hiyo haina uhai, haina maana wala<br />

haifai. Kuna Mungu mmoja tu wa kweli, naye ndiye aliyeumba na kutawala ulimwengu (15-18). Mungu huyo alichagua<br />

taifa la Israeli, yaani wazao wa Yakobo kuwa watu wake (19). Yeye anatawala historia ya mataifa, akitumia taifa moja<br />

kwa kuadhibu lingine kwa kadiri ya makusudi yake (20-23).<br />

Babeli itaadhibiwa kwa sababu ya jinsi ilivyofanya ukatili kwa Wayuda (24). Inaonekana kuwa imara na isiyoweza<br />

kushindwa kama mlima mkubwa, lakini Mungu ataiponda kuwa vipande vipande, itakuwa mahali pa ukiwa wala<br />

haitajengwa tena (25-26). Nabii anatoa mfano mwingine jinsi majeshi ya mataifa mbalimbali yanavyounganika ili<br />

yapigane vita na Babeli (27-29). Huko Babeli watu wanahangaika wakati ngome zao zinapotekwa, na habari za<br />

kushindwa kwa majeshi yao zinapopelekwa kwa mfalme kwamba majeshi yake yamepata hasara kubwa. Yanapondwa<br />

kama vile nafaka zinavyokanyagwa katika uwanja wa kuzipiga piga (30-33).<br />

Itikio la kupinduliwa kwa Babeli (<strong>51</strong>:34-58)<br />

Nabii anakumbuka maombi mengi ya watu wa Yuda ambao mara nyingi walilalamikia juu ya tamaa na ukatili wa<br />

Wababeli usiokuwa na mwisho. Walimsihi Mungu ashughulike na taifa hilo kwa sababu ya ukatili waliotendewa, na<br />

wakati huo Mungu yuko tayari kujibu maombi yao (34-35).<br />

Mungu atatekeleza mambo mazuri kwa watu wake naye ataadhibu Babeli kwa njia ya kuiangamiza. Taifa litatekwa<br />

nyara na jiji lao litaachwa kuwa fungu la kifusi (36-37). Wababeli walioua kondoo kama simba, wakati huo<br />

watachinjwa wenyewe kama kondoo (36-40). Jiji lao lililokuwa na mamlaka na kiburi (ambalo pia liliitwa Sheshaki),<br />

pamoja na mungu wake, Beli, litashindwa na kuaibishwa. Askari wa maadui wataingia jijini kama maji ya bahari<br />

yanapofurika, na hivyo mamlaka yake juu ya mataifa yaliyofungwa yanavunjwa (41-44).<br />

Yeremia anawaonya watu wa Mungu wasisitesite wala wasitie mashaka kwa sababu ya mivumo ya matatizo<br />

mbalimbali huko Babeli. Wawe tayari kukimbia nafasi inapopatikana (45-<strong>46</strong>). Babeli lazima iangamizwe kwa sababu<br />

ya dhambi zake nyingi, na hasa dhambi yake dhidi ya watu wa Mungu. Mtawala mwenye kiburi ataaibishwa, na mataifa<br />

ya kila mahali yatafurahi (47-49).<br />

Wakitazamia mambo hayo yatakayotokea, wafungwa kutoka Yuda wanapaswa kuacha ulalamishi wao wa siku zote<br />

kwamba wameaibishwa, na hekalu la Mungu limetukanwa na kudharauliwa na majeshi ya Babeli. Wakati umewadia<br />

ambapo watu waanze kufikiri sana kuhusu kurudi Yerusalemu, kwa sababu mwisho wa Babeli unakaribia (50-53).<br />

Mungu wa Israeli (<strong>YA</strong>HWEH) ndiye aliyeamua uharibifu wa Babeli. Yeye ndiye Mungu mwenye mamlaka yote na<br />

mfalme wa pekee. Kazi yake ya hukumu italeta uharibifu juu ya jiji na mauti juu ya wenye mamlaka wote wa taifa (54-<br />

57). Hata kuta imara sana za jiji hazitaweza kuwazuia maadui ambao Yeye atawatuma ili washambulie jiji hilo (58).<br />

Yeremia atuma ujumbe wake Babeli (<strong>51</strong>:59-<strong>64</strong>)<br />

Baada ya kuandika maelezo hayo ya kuanguka kwa Babeli, Yeremia alituma ujumbe wake Babeli kwa mkono wa<br />

Seraya, ili ausome kwa wafungwa walioishi huko. (Seraya alikuwa ndugu yake Baruku, na inavyoonekana alikuwa<br />

afisa wa mahakama; ling.mst.59 na 32:12). Wakati huo Seraya alifuatana na mfalme Sedekia aliyetembelea Babeli<br />

katika mwaka wa nne wa utawala wake (59-62).


Baada ya kuwasomea wafungwa mane no ya Yeremia, Seraya afungie jiwe katika gombo lake na kulitupa katika<br />

Mto Frati, ambao kando yake jiji la Babeli lilijengwa. Jambo hilo lilikuwa mfano kwamba jiji hilo lingezama wala<br />

lisingeinuka tena kamwe (63-<strong>64</strong>).

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!