46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI
46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI
46:1-51:64 UJUMBE KWA MATAIFA YA KIGENI
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>46</strong>:1-<strong>51</strong>:<strong>64</strong> <strong>UJUMBE</strong> <strong>KWA</strong> <strong>MATAIFA</strong> <strong>YA</strong> <strong>KIGENI</strong><br />
Ingawa huduma kubwa ya Yeremia ilihusu Yuda, pia aliitwa ili atangaze ujumbe wa Mungu kwa mataifa ya jirani<br />
(taz.l:5,10). Sehemu hii ya kitabu chake ina mkusanyo wa ujumbe ambao nabii aliutangaza kwa mataifa ya jirani katika<br />
muda wa miaka mingi ya huduma yake, (taz.25:13). Katika matangazo hayo nabii anaonyesha kwamba, kama vile<br />
Mungu alivyoshughulika na Yuda katika haki yake, ndivyo anavyoshughulika na mataifa ya jirani ya Yuda katika haki<br />
yake.<br />
Utaratibu wa matangazo hayo haufuati mfululizo wa matukio yaliyosababisha ujumbe wake. Utaratibu wake zaidi<br />
unafuata jiografia ya nchi zilizohusika, ukianza Misri kusini na kuendelea kaskazini na mashariki kuelekea<br />
Mesopotamia. Kilele cha mfululizo wa matangazo kinahusu taifa lililotawala mambo ya nchi nyingi zaidi ya maeneo<br />
yale, yaani Babeli. (Kuhusu mataifa yanayotajwa hapa, taz. ramani iliyopangwa katika Isaya 13-23, ambapo matangazo<br />
mengine kwa mataifa mbalimbali yameandikwa.)<br />
Ujumbe kuhusu Misri (<strong>46</strong>:1-12)<br />
Wamisri walishindwa na Wababeli mara ya kwanza katika mwaka wa 605 k.K. huko Karkemishi. Vita vile<br />
vilikuwa chanzo cha kumalizika kwa utawala mkuu wa Wamisri katika maeneo yale, navyo viliwaweka Wayuda chini<br />
ya mamlaka ya Wababeli mara ya kwanza (<strong>46</strong>:1-2). Yeremia anatoa mfano wa askari wa Misri wakijiandaa kwa vita (3-<br />
4). Wanaondoka kwa matumaini makubwa ya ushindi, lakini wanashtushwa na ukali wa mashambulio ya Wababeli.<br />
Wamisri wanageuka na kukimbia, lakini wanakatishwa njia katika Mto Frati (5-6).<br />
Katika mfano mwingine wa vita vile, nabii anaona majeshi ya Misri, yakiongezewa nguvu na askari hodari wa nchi<br />
nyingine, wakisonga mbele kama maji ya Mto Nile wakati wa kujaa na kufurika. Hivyo askari hao wanajiona kuwa na<br />
nguvu kiasi kwamba wangeweza kushinda dunia yote (7-9). Lakini siku hiyo siyo siku ya ushindi wa Wamisri. Ni siku<br />
ya hukumu ya Mungu, na Wamisri wanapata machinjo makali sana (10). Utaalamu wote wa Wamisri wa kutumia dawa<br />
hautaweza kuponya majeraha yao. Habari za kushindwa kwa Wamisri zitavuma mbali kabisa (11-12).<br />
Ujumbe wa pili kuhusu Misri (<strong>46</strong>:13-28)<br />
Wakati huo Yeremia anatabiri ushindi mwingine wa Wababeli juu ya Wamisri, lakini ushindi huo hautokei katika<br />
nchi ya kigeni, bali katika nchi ya Misri yenyewe (13). Kadiri majeshi ya Babeli yanavyozidi kusonga mbele ndivyo<br />
miji ya Misri inavyoanguka. Miungu ya Misri haiwezi kuwazuia maadui. Askari waliokodiwa wanatoroka kutoka<br />
uwanja wa vita, wakitafuta usalama katika nchi zao wenyewe (14-16). Farao anashtakiwa kuwa mtu wa kujisifu kwa<br />
maneno mengi ya bure, lakini hawezi kufanya lo lote wakati matendo yanapotakiwa (17).<br />
Wababeli hukaa juu ya Misri kwa mfano wa mnara, sawa sawa na Mlima Tabori unavyokaa juu ya nchi ya jirani<br />
yake, na kama Mlima Karmeli unavyokaa juu ya bahari iliyo karibu nao. Wamizri hawawezi kuwapindua Wababeli,<br />
kwa hiyo wajiandae kwa kifungo (18-19). Kama vile wanyama wa kufuga wanavyokimbia baada ya kuumwa na ndege<br />
mkali aumaye (kipanga), ndivyo Wamisri wanavyowakimbia Wababeli wanaowashambulia (20-21). Kwa kutumia<br />
mfano mwingine, Wamisri huwa kama nyoka anayekimbia na kujificha katika pango lake, akitafuta usalama wake. Na<br />
kwa mfano mwingine tena, Wababeli katika mashambulio yao dhidi ya Wamisri huwa kama wakataji wa kuni<br />
wanaokata msitu mzima (22-24).<br />
Ingawa Wamisri pamoja na miungu yao wanaadhibiwa, hawataangamizwa kabisa. Siku moja watainuka tena (25-<br />
26). Kuhusu watu wa Yuda na Israeli, ingawa wamepelekwa kifungoni katika nchi za kigeni, siku moja watarudi tena<br />
katika nchi yao ambapo watafurahia amani na usalama (27-28).<br />
Ujumbe kuhusu Wafilisti (47:1-7) Nabii anaona kwamba Wababeli watateka nchi ya Wafilisti pia, wakipita juu ya<br />
nchi kama mto unaofurika na maji yake yanaenea katika mashamba yote (47:1-2). Farasi wa Wababeli pamoja na<br />
magari yao ya vita yatakaposhuka kutoka kaskazini, Wafilisti watakimbia kwa hofu kuu, kila mtu akiangalia usalama<br />
wake mwenyewe. Hakuna atakayejali shida ya mwenziwe. Msaada wo wote ambao labda ungeweza kutoka Tiro au<br />
Sidoni utakatishwa, na miji ya Ufilisti itaomboleza juu ya kuangamizwa kwake (3-5).<br />
Yeremia anawaona Wafilisti wakimlilia Mungu na kumsihi akomeshe mauaji ya Wababeli. Kisha nabii anajibu kwa<br />
niaba ya Mungu, akisisitiza kwamba hukumu ya Mungu lazima iendelee mpaka imalizike kabisa (6-7).<br />
Ujumbe kuhusu Moabu (48:1-47)<br />
Moabu lilikuwa taifa mojawapo lililojaribu kufanya mwungano wa kijeshi na Yuda dhidi ya Wababeli (taz.27:l-3).<br />
Wakati huo taifa hilo litateswa kwa hasira ya Wababeli. Yeremia anaonyesha mfano wa matukio yake: nchi<br />
imechafuliwa, ngome zimebomolewa, miji imeharibiwa, na wakimbizi kwa shida kubwa wanakimbia mbele ya majeshi<br />
yanayoingia (48:1-6).<br />
Kemoshi, mungu wa kitaifa wa Wamoabi hataweza kuokoa taifa lake. Kwa kweli, atachukuliwa kifungoni pamoja<br />
na viongozi wa dini na wa kiraia wa Moabu. Miji ya Wamoabi itaachwa mahame na ukiwa (7-9). Kwa kuangamiza<br />
Moabu, Wababeli wanatimiza kazi ya hukumu ya Mungu, kwa hiyo hawana budi kutimiza kazi hiyo sawa sawa (10).
Kwa kuwa hapo awali Wamoabi hawakuchukuliwa kifungoni, wanafananishwa na divai iliyoweza kukaa katika<br />
chombo chake tangu mwanzo bila kukorogwa. Lakini wakati huo, kwa kuwa watachukuliwa kifungoni Babeli,<br />
wanafananishwa na divai inayomiminwa kutoka chombo chake (11-12). Watu watapotewa na matumaini yao katika<br />
mungu wao wa kitaifa aliyeonekana kuwa hana uwezo wa kuwaokoa (13). Askari mashujaa wa Moabu watauawa<br />
katika mauaji ya kutisha sana, na maombolezo makubwa yatakuwepo juu ya taifa lililopondwa na kuangamia (14-17).<br />
Watu wa sehemu zote za Moabu watashtuka wakisikia habari za kuangamia kwa majeshi yao. Taifa lililojivuna<br />
kwa kiburi chake litaaibishwa (18-20), na taifa lenye nguvu sana litapondwa, hukumu ya Mungu inapoenea kutoka mji<br />
mmoja wa Moabu hadi mwingine (21-25).<br />
Watu wale wa Moabu ambao awali waliwadharau na kuwadhihaki Waisraeli na Wayuda, wakati huo wenyewe<br />
wataaibishwa na kudhihakiwa. Watakunywa ghadhabu ya Mungu mpaka watakapolewa na kutapika (26-27). Wamoabi<br />
waliokuwa na kiburi na kuwadharau watu wengine, wakati huo watalazimishwa kukimbia katika aibu na kutafuta<br />
maficho katika mapango na mashimo milimani (28-30). Lakini sasa Yeremia anawaonea huruma anapoona mamlaka<br />
yao yaliyoenea sana yamevunjwa, mavuno yao mashambani na mizabibu vimeharibiwa, na nchi yao yote imechafuliwa<br />
(31-36). Watu hujinyoa nywele na ndevu zao wakijikata kata na kuvaa nguo za magunia kama alama ya maombolezo,<br />
lakini wamechelewa. Taifa la Moabu limekwisha. Limefanana na chombo kilichovunjika na kutupwa jalalani (37-39).<br />
Katika maelezo ya mwisho ya maangamizi, nabii anatoa mfano wa Wababeli wanaoshuka juu ya Moabu kama vile<br />
tai anavyoshuka juu ya mateka yake. Hakuna atakayeweza kutoroka (40-43). Mahali po pote wanapojaribu kukimbilia<br />
hakuna usalama kwa watu wanaoadhibiwa na Mungu (44). Miji ya maana katika Moabu itateketezwa kwa moto na<br />
wenyeji wake watachukuliwa kifungoni (45-<strong>46</strong>; taz.Hes 21:28-29). Lakini Mungu kwa neema yake, hata katika Moabu<br />
atawahifadhi watu wachache watakaosalia (47).<br />
Ujumbe kuhusu Amoni (49:1-6)<br />
Kama vile taifa la udugu wake Moabu, Amoni lilikuwa jamaa wa mbali wa taifa la Yuda. (Moabu na Amoni<br />
walikuwa wana wa Lutu, na Wayuda walitokana na baba mkubwa wa Lutu, Ibrahimu; taz.Mwa 12:5; 19:36-38.)<br />
Waamoni na Wamoabi waliishi katika sehemu za nyanda za nchi ya mashariki ya Yordani. Maana yake ni kwamba,<br />
walikuwa majirani kabisa wa Yuda na Israeli upande wa mashariki.<br />
Karne moja hivi kabla ya wakati wa Yeremia, Waashuri walikuwa wameteka ufalme wa kaskazini wa Israeli na<br />
kuwapeleka watu wake kifungoni (2Fal 15:29; 17:6). Inavyoonekana, Waamoni, wakati ule walichukua nafasi ya<br />
kujitwalia eneo la kabila la Gadi, yaani kabila la Israeli lililoishi mpakani. Lakini Waamoni walisahau kwamba<br />
Waisraeli bado waliendelea kuwa watu wa Mungu. Yeremia anawaambia Waamoni kwamba nchi yao itatekwa na mji<br />
wake mkuu, Raba, utabomolewa. Wakati huo Waisraeli watatwaa upya nchi yao wenyewe (49:1-2. Malkamu (au<br />
Moleki) alikuwa mungu wa kitaifa wa Amoni).<br />
Waamoni walijivunia utajiri waliojipatia, na hivyo walifikiri wako salama wala hawawezi kushambuliwa. Yeremia<br />
anawaambia kwamba utajiri wa mali hauwezi kuwaokoa maadui wanaposhambulia. Watapelekwa kifungoni (3-5),<br />
ingawa baada ya muda watu wachache watakaosalia watarudi tena (6).<br />
Ujumbe kuhusu Edomu (49:7-22)<br />
Waedomu, ambao ni wazao wa Esau, walijivuna kwamba wao walikuwa werevu kuliko mataifa ya jirani zao.<br />
Walitumaini kwamba nchi yao ilikuwa salama wala haikuweza kutekwa, kwa sababu milima mirefu ya mipakani<br />
mwake ilitoa nafasi nzuri sanaya kujitetea. Nabii anawaambia kwamba, si hekima wala silaha na nguvu ya kujitetea<br />
vitaweza kuwaokoa na maafa na maangamizi ambayo Mungu aliwapangia (7-8).<br />
Mkulima wa mizabibu huchuma zabibu zilizoiva na kuziacha zisizoiva bado; mwizi avunjaye nyumba huiba vitu<br />
vile tu anavyovitaka na kuviacha vingine katika nyumba, lakini uharibifu wa maadui juu ya Edomu utakuwa kamili.<br />
Hata watu wale watakaojificha katika mapango ya milimani hawataepukana na maafa hayo (9-10). Lakini Mungu<br />
atawaangalia wale watakaokuwa yatima au wajane kutokana na vita vile (11).<br />
Iwapo watu wasiostahili sana ghadhabu ya Mungu wanapaswa kuvumilia adhabu yake, sembuse watu waovu kama<br />
Waedomu. Wataadhibiwa vikali zaidi. Mungu anawahakikishia kwamba miji yao iliyoendelea na kujivuna juu yake,<br />
itaachwa magofu na kuwa mahali pa kutisha (12-13).<br />
Waedomu walijidanganya walipofikiri kwamba, kwa sababu ya ngome zao za kujitetea walizoziweka sehemu<br />
nyingi milimani hawakuweza kushindwa na maadui. Yeremia anawaonya kwamba, haidhum wamekwea milima mirefu<br />
mpaka juu au walijenga ngome imara sana, hakuna kitu kitakachowaokoa na hukumu ijayo (14-16).<br />
Kuangamizwa kwao kutakuwa moja kwa moja. Kama vile Sodoma na Gomora, Edomu itaachwa ukiwa (17-18).<br />
Kama vile simba atokavyo msituni na kushambulia kundi la kondoo, ndivyo maadui watakavyokuja na kuangamiza<br />
Edomu. Hakuna atakayeweza kujitetea dhidi ya jeshi ambalo Mungu atalichagua ili litekeleze hukumu yake (19-20).<br />
Askari wa Edomu hawatakuwa na nguvu dhidi ya washambulizi. Kilio cha Waedomu kitasikika mbali sana kupita
mipaka yao (21-22).<br />
Ujumbe kuhusu Dameski (49:23-27)<br />
Dameski ilikuwa jiji kuu la nchi ambayo hapo kale ilijulikana kuwa Aramu, na baadaye ilijulikana kuwa Shamu au<br />
Siria. Jiji hilo lilitekwa na Waashuri mwaka wa 612 k.K. (2Fal 16:9), lakini Yeremia alipoanza huduma yake, Dameski<br />
bado ilikaliwa na Waashuri hao, ikiwa makao makuu ya mkoa katika ufalme wao. Wakati huo Yeremia anatabiri<br />
kutekwa kwa nchi ya Shamu (Siria) tena, kwa sababu Wababeli walikuwa tayari kuwashinda Waashuri.<br />
Bila shaka unabii huo ulitolewa wakati wa mwanzo wa huduma ya Yeremia, kwa sababu huduma yake ilianza<br />
mwaka wa 627 k.K., na Wababeli waliwashinda Waashuri baada ya miaka 15 tu, yaani mwaka wa 612 k.K. Yeremia<br />
anawaona Washami wakijaa hofu katika hali yao ya kutoweza kujitetea, wakisikia majeshi ya Wababeli yanakaribia<br />
(23-24). Dameski itakuwa uwanja wa majinjio na uharibifu tena, majeshi ya Wababeli yatakapotekajiji hilo (25-27).<br />
Ujumbe kuhusu Kedari (49:28-33)<br />
Hata makabila ya jangwani yanayohama hama kila wakati yatapata taabu kutokana na mashambulio ya Wababeli.<br />
Kabila linalotajwa na Yeremia ni Wakedari walioishi katika eneo liitwalo Hazori. Wakedari waliishi katika mahema,<br />
walifuga kondoo nao walikuwa wafanya biashara hodari (Zab 120:5; Isa 60:7; Eze 27:21). Yeremia anatabiri kwamba<br />
makao yao yatachafuliwa, wanyama wao watachukuliwa, na wao wenyewe watakimbia kwa hofu (28-30).<br />
Lakini maafa hayo pia ni hukumu ya Mungu juu ya makabila hayo ya jangwani. Desturi yao ilikuwa kuiba katika<br />
miji iliyoshambuliwa na Wababeli, kisha kukimbilia makao yao ambapo walikuwa mbali na njia za mashambulio ya<br />
Wababeli. Usalama wao waliodhania kuwa nao wakati huo unafikishwa mwisho wake, na mali yao ya wizi itapotea<br />
(31-33).<br />
Ujumbe kuhusu Elamu (49:34-39)<br />
Ujumbe kuhusu ufalme wa kale wa Elamu ulikuja katika mwanzo wa enzi ya Sedekia, yeye Sedekia alipojaribu<br />
kuunda mwungano wa kijeshi na mataifa mengine magharibi ya Babeli, kwa makusudi ya kuzuia kuenea kwa mamlaka<br />
ya Babeli (34; taz.27: 1-3,12).<br />
Ujumbe wa Yeremia hapa unaonyesha kwamba Sedekia alipoteza wakati wake bure. Mamlaka ya Wababeli<br />
yangeenea mbali sana, hata nchi zilizo upande wa mashariki ya Babeli, kama vile Elamu, zingepinduliwa (35-38).<br />
Lakini kupinduliwa kwa Elamu kusingekuwa kwa muda wote (39). Ripoti za historia zinatueleza kwamba baadaye nchi<br />
ya Elamu ilikuwa sehemu ya ufalme wa Uajemi ambao ulipindua Babeli (Ezra 1:2).<br />
Ujumbe kuhusu Babeli (50:1-<strong>46</strong>)<br />
Hatimaye Yeremia anaona kwamba taifa lile ambalo Mungu alilitumia kwa kuadhibu taifa la Yuda litaadhibiwa<br />
vile vile. Beli au Merodaki, mungu mkuu wa Wababeli, hataweza kuwaokoa watu wake na mashambulio yatakapokuja<br />
juu yao (50:1-3).<br />
Wayahudi ambao wakati huo watakuwa wamejinyenyekeza katika toba mbele ya Mungu, kwa sababu ya kuanguka<br />
kwa Babeli watapewa nafasi ya kurudi katika nchi yao (4-5).(Koreshi wa Uajemi aliposhinda na kupindua Babeli<br />
mwaka wa 539 k.K., mara moja aliwapa Wayuda ruhusa kurudi katika nchi yao; taz.2Nya 36:22-23.)<br />
Viongozi wa Yuda walikuwa na hatia, kwa sababu walipoteza taifa lao katika njia mbaya (6), lakini Wababeli pia<br />
walikuwa na hatia (ingawa walikanusha jambo hili), kwa sababu wao waliwatendea Wayuda kadiri ya mapenzi yao<br />
wenyewe (7). Kwa hiyo, wakati Wayahudi watakaporudi kutoka Babeli (kwa kweli, watakuwa taifa la kwanza kati ya<br />
yale yaliyopelekwa kifungoni litakalopata uhuru), Babeli yenyewe itaadhibiwa (8-10).<br />
Wababeli walijivuna katika kiburi chao kwamba walishinda na kuteka nyara taifa la <strong>YA</strong>HWEH, yaani Yuda (11).<br />
Wakati huo wataadhibiwa, ghadhabu ya Mungu itakapomiminwa juu yao (12-13). Washambulizi wake watakuwa<br />
wakali sana kwao, kama vile wao walivyokuwa kwa watu wengine. Baada ya kushindwa kwao, watu wote walio<br />
wafungwa wao, watatoroka kwenda katika nchi zao (14-16).<br />
Ufalme wa kaskazini, yaani Israeli, ulitekwa na Waashuri, halafu Uashuru ulitekwa na Wababeli, na hivyo watu wa<br />
Israeli sawa sawa na wale wa Yuda, hatimaye walikuwa chini ya mamlaka ya Babeli. Lakini wakati huo Babeli<br />
itaanguka, na Waisraeli sawa sawa na Wayuda watarudi katika nchi yao, wakiwa watu waliounganika tena na<br />
kusamehewa dhambi zao (17-20).<br />
Nabii akiendelea kuonyesha mfano wa kuanguka kwa Babeli, anawaona washambulizi wake wakihimizwa wasonge<br />
mbele na kushambulia miji mbalimbali ya Babeli (21-22). Taifa lile ambalo kama nyundo lilivunja mataifa mengine,<br />
wakati huo litavunjwa lenyewe. Ghala zake za chakula zitavunjwa, na askari wake watauawa (23-27). Wafungwa wa<br />
Yuda wakati huo watafunguliwa, nao watarudi nyumbani kwao wakimsifu Mungu kwa kuwakomboa watu wake na<br />
kuwaadhibu kwa haki wanyanyasaji wao (28), lakini Wababeli wenye kiburi wataachwa bila mtu wa kuwasaidia (29-<br />
32). Mungu anawaokoa wanaonyanyaswa, lakini anawaadhibu wale wanaowanyanyasa (33-34).
Haidhuru watawala wa Babeli walikuwa na hekima gani, wachawi wao walikuwa wajanja kiasi gani au askari wao<br />
walikuwa hodari na wenye nguvu gani, wote pamoja watauawa. Majeshi yao ya magari yataangamizwa, na hazina zao<br />
zitatekwa nyara (35-37). Kwa njia ya ukame na vita, nchi yote itaharibika na kuachwa katika hali mbaya, hata watu<br />
wasiweze kuishi huko tena (38-40).<br />
Nabii anaonyesha mfano wa hofu ya mfalme wa Babeli anaposikia habari za ushindi wa haraka wa Waajemi na<br />
majeshi ya mwungano wake yakikaribia kwa kasi (41-43). Mungu akichukua hatua dhidi ya Wababeli, hayatakuwepo<br />
matumaini ya kukimbia. Wababeli wanafananishwa na kundi la kondoo linaloshambuliwa na simba. Kwa hofu kubwa<br />
watapiga yowe wanapofikia mwisho wao wa uchungu na ukatili (44-<strong>46</strong>).<br />
Kupinduliwa kwa Babeli (<strong>51</strong>:1-58)<br />
Baada ya kuvuna ngano yake, mkulima anapepeta nafaka zake kwa njia ya kuitupa juu, ili upepo upeperushe<br />
makapi yake, na hivyo anaweza kupata ngano safi. Hali kadhalika Mungu atakapopepeta Babeli, yaani atabagua kati ya<br />
watu wake na watu wa Babeli. Atapeperusha Wababeli katika hukumu yake, lakini atawahifadhi watu wake kwa ajili<br />
yake mwenyewe (<strong>51</strong>:1-5).<br />
Mungu aliwatumia Wababeli ili kuadhibu mataifa mengine, lakini wakati huo wao wenyewe watakunywa<br />
ghadhabu ya Mungu. Watafanana na mlevi aangukaye asiweze kuinuka tena, na mtu aliyejeruhiwa asiweze kupona.<br />
Wakati huo mataifa yaliyoteswa na kupelekwa kifungoni na Wababeli yatapewa uhuru wao, yaani wafungwa wote<br />
wataweza kurudi nyumbani kwao (6-9). Mungu atahakikisha kwamba hukumu ya mwisho itatekelezwa (10).<br />
Kisha nabii anatoa mfano wa jeshi la Wamedi na Waajemi yakijiandaa kwa mashambulio ya mwisho dhidi ya<br />
Babeli. Anawaonya Wababeli kwamba mwisho wao unakaribia, na baada ya muda mfupi jiji lao litajaa askari wa<br />
maadui (11-14). Miungu yote ya Babeli haitakuwa na uwezo wa kuokoa. Miungu hiyo haina uhai, haina maana wala<br />
haifai. Kuna Mungu mmoja tu wa kweli, naye ndiye aliyeumba na kutawala ulimwengu (15-18). Mungu huyo alichagua<br />
taifa la Israeli, yaani wazao wa Yakobo kuwa watu wake (19). Yeye anatawala historia ya mataifa, akitumia taifa moja<br />
kwa kuadhibu lingine kwa kadiri ya makusudi yake (20-23).<br />
Babeli itaadhibiwa kwa sababu ya jinsi ilivyofanya ukatili kwa Wayuda (24). Inaonekana kuwa imara na isiyoweza<br />
kushindwa kama mlima mkubwa, lakini Mungu ataiponda kuwa vipande vipande, itakuwa mahali pa ukiwa wala<br />
haitajengwa tena (25-26). Nabii anatoa mfano mwingine jinsi majeshi ya mataifa mbalimbali yanavyounganika ili<br />
yapigane vita na Babeli (27-29). Huko Babeli watu wanahangaika wakati ngome zao zinapotekwa, na habari za<br />
kushindwa kwa majeshi yao zinapopelekwa kwa mfalme kwamba majeshi yake yamepata hasara kubwa. Yanapondwa<br />
kama vile nafaka zinavyokanyagwa katika uwanja wa kuzipiga piga (30-33).<br />
Itikio la kupinduliwa kwa Babeli (<strong>51</strong>:34-58)<br />
Nabii anakumbuka maombi mengi ya watu wa Yuda ambao mara nyingi walilalamikia juu ya tamaa na ukatili wa<br />
Wababeli usiokuwa na mwisho. Walimsihi Mungu ashughulike na taifa hilo kwa sababu ya ukatili waliotendewa, na<br />
wakati huo Mungu yuko tayari kujibu maombi yao (34-35).<br />
Mungu atatekeleza mambo mazuri kwa watu wake naye ataadhibu Babeli kwa njia ya kuiangamiza. Taifa litatekwa<br />
nyara na jiji lao litaachwa kuwa fungu la kifusi (36-37). Wababeli walioua kondoo kama simba, wakati huo<br />
watachinjwa wenyewe kama kondoo (36-40). Jiji lao lililokuwa na mamlaka na kiburi (ambalo pia liliitwa Sheshaki),<br />
pamoja na mungu wake, Beli, litashindwa na kuaibishwa. Askari wa maadui wataingia jijini kama maji ya bahari<br />
yanapofurika, na hivyo mamlaka yake juu ya mataifa yaliyofungwa yanavunjwa (41-44).<br />
Yeremia anawaonya watu wa Mungu wasisitesite wala wasitie mashaka kwa sababu ya mivumo ya matatizo<br />
mbalimbali huko Babeli. Wawe tayari kukimbia nafasi inapopatikana (45-<strong>46</strong>). Babeli lazima iangamizwe kwa sababu<br />
ya dhambi zake nyingi, na hasa dhambi yake dhidi ya watu wa Mungu. Mtawala mwenye kiburi ataaibishwa, na mataifa<br />
ya kila mahali yatafurahi (47-49).<br />
Wakitazamia mambo hayo yatakayotokea, wafungwa kutoka Yuda wanapaswa kuacha ulalamishi wao wa siku zote<br />
kwamba wameaibishwa, na hekalu la Mungu limetukanwa na kudharauliwa na majeshi ya Babeli. Wakati umewadia<br />
ambapo watu waanze kufikiri sana kuhusu kurudi Yerusalemu, kwa sababu mwisho wa Babeli unakaribia (50-53).<br />
Mungu wa Israeli (<strong>YA</strong>HWEH) ndiye aliyeamua uharibifu wa Babeli. Yeye ndiye Mungu mwenye mamlaka yote na<br />
mfalme wa pekee. Kazi yake ya hukumu italeta uharibifu juu ya jiji na mauti juu ya wenye mamlaka wote wa taifa (54-<br />
57). Hata kuta imara sana za jiji hazitaweza kuwazuia maadui ambao Yeye atawatuma ili washambulie jiji hilo (58).<br />
Yeremia atuma ujumbe wake Babeli (<strong>51</strong>:59-<strong>64</strong>)<br />
Baada ya kuandika maelezo hayo ya kuanguka kwa Babeli, Yeremia alituma ujumbe wake Babeli kwa mkono wa<br />
Seraya, ili ausome kwa wafungwa walioishi huko. (Seraya alikuwa ndugu yake Baruku, na inavyoonekana alikuwa<br />
afisa wa mahakama; ling.mst.59 na 32:12). Wakati huo Seraya alifuatana na mfalme Sedekia aliyetembelea Babeli<br />
katika mwaka wa nne wa utawala wake (59-62).
Baada ya kuwasomea wafungwa mane no ya Yeremia, Seraya afungie jiwe katika gombo lake na kulitupa katika<br />
Mto Frati, ambao kando yake jiji la Babeli lilijengwa. Jambo hilo lilikuwa mfano kwamba jiji hilo lingezama wala<br />
lisingeinuka tena kamwe (63-<strong>64</strong>).