24.04.2017 Views

Issue 1

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

!


7


11


Hakukata tamaa akaingia tena<br />

studio nakutoka na kitu ambacho<br />

kilikuwa kinajulikana kwa jina la<br />

‘Kibarua’ ambao alirekodia katika<br />

studio za master j wimbo huo<br />

uliweza kumtambulisha katika<br />

anga za muziki wa kizazi kipya.<br />

Baada ya kuona mafanikio yana -<br />

karibia akaingia tena studio na<br />

kutoka na wimbo ambao uliju -<br />

likana kwa jina la ‘mapepe’<br />

ambao aliufanyia katika studio za<br />

Mambo Jambo.<br />

Hapo ndipo ndoto zake zikaanza<br />

kukamilika akawa anafanya<br />

nyimbo katika studio mbalimbali<br />

akazidi kusimama bila kusita<br />

akaamua kutoa wimbo mwingine<br />

uliojulikana kama ‘Hoi’.<br />

Hoi ndio hasa ulioanza kum -<br />

nyanyua kwani ulipata muda<br />

mkubwa katika vituo vya redio<br />

jambo lililomfanya arejee studio<br />

na kuachia Zaidi Yako.<br />

“Niliamua kuachia nyimbo mfu -<br />

lulizo kwa sababu nina mashairi<br />

ya kutosha kwa hiyo sioni kama<br />

nikiachia hivyo nitaishiwa misitari<br />

na ndio maana nikawa ninaachia<br />

bila hesabu,” anajigamba.<br />

Na huo ndio ukawa mwanzo wa<br />

kujulikana kwa jina la Chidi Ben -<br />

zino kabla kubalidilisha.<br />

“Kipindi cha nyuma nilikuwa<br />

shabiki na mwanachama wa The<br />

Source Magazine ambalo linami -<br />

likiwa na rapa Benzino wa<br />

Marekani ilikuwa kila mwezi<br />

lazima nitumiwe magazine kuto -<br />

kana na kupenda kusoma hilo<br />

jarida.<br />

“Mshikaji wangu wa karibu na<br />

ambaye tulikuwa tunaishi naye<br />

Ilala, Dully Sykes akawa ananiita<br />

Benzino baadhi ya washikaji nao<br />

wakaanza kuniita hivyo jina<br />

likakua baada ya kuona<br />

limezoeleka sana na isitoshe jina<br />

lenyewe siyo langu nikaamua<br />

kulitohoa jina langu la Rashid<br />

nalifupisha likawa Chidi, sikue -<br />

nda mbali sana kwa kuhofia<br />

kupoteza maana ya Benzino na<br />

kutohoa na kuform Benz ukijum -<br />

lisha unapata jina kamili ambalo<br />

lina leta maana Chidi Benz hiyo<br />

ndio historia ya jina langu la kisa -<br />

nii,” anasema.<br />

Mkali huyu wa hip hop ame -<br />

onekana aking’ara sana katika<br />

vituo vya redio mbalimbali hapa<br />

nchini kiasi kwamba unaweza<br />

kusikia sauti yake kila baada ya<br />

dakika mbili katika kituo kimoja<br />

kwa siku moja.<br />

Katika chati ambazo zina<br />

endeshwa katika vituo mbalim -<br />

bali vya redio hapa nchini zaidi ya<br />

nyimbo saba ambazo ziko katika<br />

chati ya juu utakuta zina sauti ya<br />

mwana hip hop huyu kitu amba -<br />

cho hakijawahi kutokea katika<br />

muziki wetu wa kizazi kipya<br />

Ngoma zinazotamba ambazo<br />

ameshilikishwa chidi benz ni<br />

kama ‘Ombi langu’wa msanii<br />

chipukizi anayetoka katika kundi<br />

la Tip Top Conection anayeju -<br />

likana kwa jina la Spark, ‘NEILA<br />

wa msanii Tunda man ‘Bado<br />

umenuna’ wa Marlaw, ‘Hao’ wa<br />

mwanamuziki kutoka katika<br />

nyumba ya vipaji Tanzania House<br />

of Talent (THT) anayejulikana<br />

kama Mwasiti ‘Mchizi wangu<br />

remix ‘ wa kundi la Nako2Nako<br />

na ‘Hapo vipi remix ‘ wa Profesa<br />

Jay, Vidole vitatu wa Taarsis<br />

Masela wa Akudo Impact.<br />

“Ukaribu na utundu pamoja na<br />

umahiri wa kuchezea sauti<br />

yangu ndio vinavyo nipa nafasi<br />

ya kushirikishwa kwenye nyimbo<br />

nyingi. Vile vile mi ni mkali,”<br />

anasema.<br />

Mbali na kutamba na nyimbo<br />

alizoshirikishwa vilevile nyimbo<br />

za Chid ambazo zinafanya vizuri<br />

ni pamoja na ‘Hasira za nini’,<br />

‘Mmenisoma’ pamoja na ‘Naitwa<br />

nani’ aliomshirikisha mwana<br />

dada K-Lynn.<br />

Tofauti na wasanii wengi ambao<br />

kwa sasa wamekuwa<br />

wakilalamika kuwa wanalazimika<br />

kuhonga katika vituo vya redio<br />

Chid anasema kwake hapana.<br />

“Tangu naanza muziki sijawahi<br />

kulipa katika studio wala<br />

sijawahi kuhonga katika redio<br />

yoyote hapa nchini ilinipigiwe<br />

nyimbo zangu nasintakuja<br />

kuhonga kamwe,” anasema.<br />

Anasema anaamini msanii wa<br />

kweli hawezi kuhonga ili kazi<br />

zake ziweze kupigwa kwenye<br />

redio.<br />

Rapa huyo alifanikiwa kutwaa<br />

tuzo za Killimanjaro Music Award<br />

kwa nafasi ya Msanii bora wa Hip<br />

Hop mwaka 2007.<br />

Kwake anaeleza kuwa tuzo hiyo<br />

imempa moyo wa kusonga<br />

mbele zaidi<br />

“Katika gemu hawawezi wakaku -<br />

penda wote lazima wengine<br />

watakuchukia tu,wengi walifurahi<br />

mimi kupata tuzo, kwa vile<br />

nilikuwa na kiwango cha kupewa<br />

tuzo katika kipindi hicho,” anas -<br />

ema.<br />

Miezi kadhaa iliyopita Chidi<br />

alipeleka Albam yake sokoni<br />

ikiwa na nyimbo 17<br />

“Kama nilionyesha mfano wa<br />

albam yangu kukaa namba ONE<br />

katika chati sokoni kwa majuma<br />

kadhaa lakini bado ninaungana<br />

na mwana hiphop kutoka katika<br />

kundi la Tip Top Conection<br />

aitwaye Madee kwa kusema hip<br />

hop haiuzi Lakini mimi chidi benz<br />

nauza.”<br />

Albamu amefanyia katika studio<br />

mbalimbali za hapa nchini, akiwa<br />

amewashirikisha wasanii K-Lyyn,<br />

Wa2pori, AY, Matonya, Mr Ebo,<br />

Dogo Hamidu, Makamua, Ali<br />

Kiba, Maunda Zorro, Gaza<br />

pamoja na K-Voo kutoka Kenya.<br />

”Nimeamua kufanya hivi iliniweze<br />

kuwateka washabiki wao mfano<br />

mtu akiona nimefanya collabo na<br />

Ali kiba na yeye anampenda so<br />

nilazima anunue albam, kingine<br />

ni kwamba nilikuwa najua<br />

kwamba bongo flava inauza<br />

nikaona nikiwaweka hawa na<br />

mimi nitauza, na kweli nikafan -<br />

ikwa kubamba soko.”<br />

Chidi anasema hiphop haiuzi<br />

kutokana na kutokuwepo na<br />

ushirikiano kati ya wasanii<br />

wenyewe, tamaa ya kutaka<br />

kulipwa fedha nyingi tofauti lakini<br />

kubwa zaidi anasema nyimbo<br />

nyingi hazina ujumbe ambao<br />

mashabiki wanataka kuusikia.<br />

Msanii huyu ambaye alitumbuiza<br />

awali wakati wa onyesho la<br />

msanii 50 Cent anasema hiyo<br />

imesaidia pia kupiga hatua.<br />

“Ni bonge la hatua kwangu kwa<br />

sababu mchizi nilikuwa namuona<br />

tu kwenye luninga, magazetini<br />

pamoja na internet, kikubwa zaidi<br />

ni kuona ujanja anaotumia wakati<br />

anapokuwa stejini pamoja na<br />

kumsikia angesema nini juu ya<br />

muziki wetu.”<br />

15


16


19


20


Event<br />

Marlaw<br />

Jirambe Jirambe<br />

Q-jay<br />

Mwasiti


DJ Fetty<br />

A Mchomvu<br />

2008<br />

Prof Jay Dark Master Ngwasuma


48 Hotspot September Edition 2008

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!