13.05.2014 Views

PANGANI BASIN WATER BOARD - IUCN

PANGANI BASIN WATER BOARD - IUCN

PANGANI BASIN WATER BOARD - IUCN

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>IUCN</strong> <strong>WATER</strong> AND NATURE INITIATIVE<br />

<strong>IUCN</strong> <strong>WATER</strong> AND NATURE INITIATIVE<br />

<strong>IUCN</strong> <strong>IUCN</strong> <strong>WATER</strong> <strong>WATER</strong> AND AND NATURE NATURE INITIATIVE<br />

INITIATIVE<br />

<strong>PANGANI</strong> <strong>BASIN</strong> <strong>WATER</strong> <strong>BOARD</strong> 1<br />

<strong>PANGANI</strong> <strong>PANGANI</strong> <strong>BASIN</strong> <strong>BASIN</strong> <strong>WATER</strong> <strong>WATER</strong> <strong>BOARD</strong> <strong>BOARD</strong> 1 1<br />

<strong>PANGANI</strong> <strong>BASIN</strong> <strong>WATER</strong> <strong>BOARD</strong> 1<br />

Basin Delineation Report<br />

Basin Delineation Report<br />

<strong>PANGANI</strong> RIVER <strong>BASIN</strong> FLOW ASSESSMENT<br />

Basin Delineation Report<br />

Final Report<br />

Bonde La Pangani: Uchambuzi wa Hali Halisi (Toleo la pili)<br />

Bonde J. King, C. Brown, La Pangani: J. Turpie, B. Clark, Uchambuzi A. Duffel-Graham, wa G. Lugomela, Hali Halisi H. Sadiki, (Toleo B. L. Benno, la A.<br />

pili)<br />

<strong>PANGANI</strong> RIVER <strong>BASIN</strong> FLOW ASSESSMENT<br />

Hepelwa, L. T Kaaya, D Salum, L. Lukambuzi, E. Materu, Felix Peter, S. Kamugisha, F. Mahay and H.<br />

Beuster<br />

Basin Delineation 2010 Report<br />

2010<br />

January 2008<br />

Final Report<br />

J. King, C. Brown, J. Turpie, B. Clark, A. Duffel-Graham, G. Lugomela, H. Sadiki, B. L. Benno, A.<br />

Hepelwa, L. T Kaaya, D Salum, L. Lukambuzi, E. Materu, Felix Peter, S. Kamugisha, F. Mahay and H.<br />

Beuster<br />

1 As of 2010, 1 As of Pangani 2010, Pangani Basin Basin Water Water Office Office is known is known as as Pangani Pangani Basin Water Board<br />

1 As of 2010, Pangani Basin Water Office is known as Pangani Basin Water Board<br />

January 2008


Coast Development Authority<br />

Bonde la Pangani:<br />

Uchambuzi wa Hali Halisi (Toleo la pili)


Bonde la Pangani:<br />

Uchambuzi wa Hali Halisi (Toleo la pili)<br />

Programu ya <strong>IUCN</strong> Afrika Mashariki na Kusini<br />

2009<br />

i


Mchapishaji:<br />

Hatimiliki:<br />

© 2009 Shirika la Kimataifa la Uhifadhi ya Uasili na Maliasili.<br />

Kitabu hiki kinaweza kutolewa chote au sehemu yake kwa njia yoyote kwa<br />

matumizi ya maendeleo ya elimu au matumizi mengine yasiyo ya biashara<br />

bila ya kuomba kibali kutoka kwa mmiliki, ilimradi rejeo litajwe. <strong>IUCN</strong><br />

ingependelea kupata nakala ya makala yoyote ambayo itatumia kitabu hiki<br />

kama rejea.<br />

Hairuhusiwi kuuza kitabu hiki, au kukitumia kwa madhumuni mengine ya<br />

kibiashara bila ya idhini ya maandishi ya <strong>IUCN</strong>.<br />

Jina kamili:<br />

Programu ya <strong>IUCN</strong> Afrika ya Mashariki, 2009. Uchambuzi wa Hali Halisi<br />

Bonde la Mto Pangani. Toleo la pili, xii + uk.83.<br />

ISBN: 978-2-8317-1191-1<br />

Usanifu na Mpangilio:<br />

Mpiga chapa:<br />

Gordon O. Arara<br />

Kulgraphics Ltd.<br />

1<br />

2 3 4<br />

5<br />

Picha ya 1: Kilele cha Mlima Kilimanjaro; Picha ya 2: Sehemu ya msitu wa<br />

Shiri Njoro; Picha ya 3: Banio la kudhibiti maji yanayoingia katika mfereji wa<br />

umwagiliaji; Picha ya 4: Watoto wakiogelea kwenye hodhi ya maji ya umwagiliaji;<br />

Picha ya 5: Shamba la mkonge; Picha ya 6: Mradi wa umwagiliaji wa mpunga<br />

; Picha ya 7: Kituo cha kupimia usawa wa maji- Chemchemi ya Chemka; Picha<br />

ya 8: Banio la mfereji wa umwagiliaji lililoharibiwa; Picha ya 9: Ukuta wa Bwawa<br />

la Nyumba ya Mungu (mabadiliko ya rangi yanaonesha upunguaji wa kina cha<br />

maji); Picha ya 10: Mchuuzi akiuza maji kutoka kwenye kisima.<br />

6<br />

7 8<br />

9 10<br />

Picha namba 1, 3, 5, 6, 8, 9 hatimiliki ya 2003 ya Kelly West; Picha namba<br />

2 na 7 hatimiliki ya 2002 ya Kim Geheb; Picha namba 4 na 10 hatimiliki ya<br />

2003 ya Ger Bergkamp.<br />

Kitabu hiki kinapatikana: Kitengo cha Huduma za Uchapishaji cha <strong>IUCN</strong>-ESARO, S.L.P. 68200–00200,<br />

Nairobi, Kenya; Simu ++254 20 890605-12 Faksi ++254 20 890615; Barua<br />

pepe; earo@iucn.org<br />

Uteuzi wa Maumbo ya kijiografia na nyenzo zilizotumika kuwasilisha ujumbe katika kitabu hiki,<br />

hayawakilishi kwa namna yoyote ile maoni ya asasi zinazoshiriki kuhusiana na sheria ya nchi yoyote, au<br />

eneo lake, au mamlaka zake, au kuhusu makazi na uwekaji wa mipaka yake.<br />

Maoni yaliyotolewa na waandishi katika kitabu hiki sio lazima kwamba yanawakilisha maoni ya PBWO,<br />

CDA, WANI au <strong>IUCN</strong>.<br />

ii


Yaliyomo<br />

Tafsiri ya vifupisho............................................................................................................................v<br />

Dibaji.................................................................................................................................................vii<br />

Muhtasari ........................................................................................................................................viii<br />

A<br />

B<br />

C<br />

Utangulizi wa Uchambuzi wa Hali Halisi wa Bonde la Mto Pangani....................................1<br />

A.1 Maelezo ya jumla ya Bonde la Mto Pangani....................................................................1<br />

A.2 Usimamizi wa Pamoja wa Mabonde ya Mito (wa)............................................................5<br />

A.3 Programu ya Hifadhi ya Maji na Uasili (WANI).................................................................6<br />

A.4 Uchambuzi wa Hali Halisi: madhumuni na matokeo.........................................................7<br />

A.5 Vyanzo vya data ..............................................................................................................7<br />

A.6 Muundo wa Uchambuzi wa Hali Halisi..............................................................................8<br />

Rasilimali za asili zilizopo katika Bonde la Mto Pangani.....................................................9<br />

B.1 Utangulizi.............................................................................................................................9<br />

B.2 Misitu iliyopo katika Bonde...................................................................................................9<br />

B.3 Maji na ardhioevu...............................................................................................................15<br />

B.4 Maeneo yaliyohifadhiwa.....................................................................................................19<br />

B.5 Bayoanuwai na Hifadhi......................................................................................................20<br />

B.6 Uvuvi .................................................................................................................................22<br />

B.7 Udongo..............................................................................................................................23<br />

B.8 Majumuisho ya hoja...........................................................................................................23<br />

Uchumi wa kijamii katika Bonde la Mto Pangani................................................................25<br />

C.1 Maelezo ya jumla...............................................................................................................25<br />

C.2 Shughuli za Viwanda.........................................................................................................27<br />

C.3 Shughuli za Kilimo.............................................................................................................27<br />

C.4 Shughuli za Wafugaji.........................................................................................................31<br />

C.5 Shughuli za Mijini...............................................................................................................32<br />

C.6 Shughuli za Asasi Zisizo za Kiserikali na Mashirika ya Kimataifa .....................................32<br />

C.7 Migogoro............................................................................................................................40<br />

C.8 Majumuisho ya hoja ..........................................................................................................46<br />

D Usimamizi wa Maliasili katika Bonde la Mto Pangani ........................................................47<br />

D.1 Utangulizi.........................................................................................................................47<br />

D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera............................................................................ 47<br />

D.3 Usimamizi katika ngazi ya jamii........................................................................................52<br />

D.4 Usimamizi wa bonde kimataifa.........................................................................................55<br />

D.5 Ukusanyaji na ufuatiliaji wa data.......................................................................................55<br />

D.6 Majumuisho ya hoja..........................................................................................................57<br />

E<br />

Matatizo na masuala mbalimbali katika Bonde la Mto Pangani......................................58<br />

E.1 Utangulizi...........................................................................................................................58<br />

E.2 Masuala na matatizo ya Bonde la Mto Pangani................................................................58<br />

E.3 Maeneo ya kipaumbele kwa Utendaji................................................................................62<br />

F Hitimisho................................................................................................................................64<br />

F.1 Majumuisho ya Matokeo....................................................................................................64<br />

G Rejea .....................................................................................................................................68<br />

H Kiambatanisho cha 1: Mabonde madogo yaliyojumuishwa kiutawala<br />

katika Bonde la Pangani...................................................................................................... 75<br />

H.1 Utangulizi..........................................................................................................................75<br />

iii


H.2 Bonde la Mto Umba..........................................................................................................75<br />

H.3 Bonde la Mto Msangazi....................................................................................................77<br />

H.4 Bonde la Mto Zigi..............................................................................................................78<br />

H.5 Bonde la Mto Mkulumuzi..................................................................................................82<br />

Orodha ya Majedwali<br />

Jedwali la 1: Aina, matumizi na hadhi ya kisheria ya misitu ya Tanzania...........................................9<br />

Jedwali la 2: Upotevu wa utando wa msitu wa Milima ya Tao la Mashariki katika<br />

Bonde la Mto Pangani..................................................................................................13<br />

Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya<br />

mahitaji ya maji mwaka 2015.......................................................................................18<br />

Jedwali la 4: Misingi ya Uchumi wa kijamii wa Tanzania na Kenya mwaka 2001.............................26<br />

Jedwali la 5 Idadi ya Mifugo katika baadhi ya maeneo ya Bonde la Mto Pangani (2002) ............. 31<br />

Jedwali la 6: Hati za kutumia maji katika Bonde la Mto Pangani (Tanzania), Mei, 2003..................50<br />

Jedwali la 7: Eneo la misitu chini ya Usimamizi wa Misitu wa Pamoja kwa mikoa...........................54<br />

Orodha ya Michoro<br />

Mchoro Na.1: Bonde la mto Pangani lilivyoenea Tanzania na Kenya..................................................2<br />

Mchoro Na 2: Bonde la Mto Pangani ..................................................................................................3<br />

Mchoro Na 3: Utawala wa Misitu Tanzania .......................................................................................51<br />

Mchoro Na 4: Ramani ya Bonde la Pangani- Utawala ......................................................................83<br />

Orodha ya Picha<br />

Picha ya 1: Ramani ya Bonde la Mto Pangani ..................................................................................33<br />

Picha ya 2: Ramani ya Bonde la Pangani kiutawala ........................................................................34<br />

Picha ya 3: Kilele maarufu chenye barafu cha Mlima Kilimanjaro mwaka<br />

1993 na 2000 .................................................................................................................35<br />

Picha ya 4: Mto Karanga - Moshi......................................................................................................36<br />

Picha ya 5: Mlima Kilimanjaro ...........................................................................................................36<br />

Picha ya 6: Mfereji wa umwagiliaji Wilayani Moshi............................................................................37<br />

Picha ya 7: Chemchemi iliyofunikwa ya Shiri-Njoro..........................................................................38<br />

Picha ya 8: Miteremko kwenye misitu ya Mlima Meru.......................................................................38<br />

Orodha ya Visanduku<br />

Kisanduku cha 1: Usimamizi wa Mahitaji ya maji................................................................................6<br />

Kisanduku cha 2: Taarifa za msingi za misitu ya Bonde la Mto Pangani...........................................10<br />

Kisanduku cha 3: Milima ya Taita.......................................................................................................11<br />

Kisanduku cha 4: Tishio kwa misitu ya Bonde la Mto Pangani..........................................................14<br />

Kisanduku cha 5: Taarifa za msingi za maji na ardhioevu katika Bonde la Mto Pangani ..............15<br />

Kisanduku cha 6: Tishio kwa rasilimali za maji na ardhioevu ya Bonde la Mto Pangani ..................16<br />

Kisanduku cha 7: Tishio kwa maeneo yaliyohifadhiwa ya Bonde la Mto Pangani.............................20<br />

Kisanduku cha 8: Maeneo muhimu sana kwa bayoanuwai ..............................................................21<br />

Kisanduku cha 9: Kundi la kwanza la spishi ya ndege wa Milima ya Usambara<br />

walio hatarini.........................................................................................................22<br />

Kisanduku cha 10: Kasoro za usanifu wa miundombinu ya mifereji ya asili .....................................28<br />

Kisanduku cha 11: Magadi na chumvichumvi....................................................................................30<br />

Kisanduku cha 12: Utawala wa Maji nchini Kenya.............................................................................51<br />

Kisanduku cha 13: Uanzishwaji wa usimamizi wa kijamii katika msitu wa Duru-Haitemba,<br />

Mkoani Manyara ............................................................................................53<br />

Kisanduku cha 14: Mfano wa Chama Cha Watumia Maji..................................................................56<br />

iv


Tafsiri ya Vifupisho<br />

ANR....................... Hifadhi ya Asili ya Amani<br />

ASL....................... Juu ya Usawa wa Bahari<br />

AUWSA................. Mamlaka ya Maji safi na na Maji taka Arusha<br />

BWB...................... Bodi ya Maji ya Bonde<br />

BWO..................... Afisa wa Maji wa Bonde<br />

CBNRM................. Usimamizi wa Maliasili Kijamii<br />

CCM...................... Chama Cha Mapinduzi<br />

CDA....................... Mamlaka ya Maendeleo Pwani (Kenya)<br />

CFR....................... Hifadhi ya Misitu ya Jamii<br />

CFP....................... Mradi wa Misitu Eneo la Chanzo cha Mto<br />

CPRs..................... Rasilimali za Jamii<br />

DFO....................... Afisa Misitu wa Wilaya<br />

DGIS..................... Wizara ya Mambo ya Nje ya Uholanzi<br />

EACBP.................. Mradi wa Bayoanuwai za kimataifa za Afrika Mashariki<br />

EU......................... Umoja wa Nchi za Ulaya<br />

EU-ACP................. Umoja wa Ulaya – Afrika, Caribbean na Pasifiki<br />

FAO....................... Shirika la Kilimo na Chakula la Umoja wa Mataifa<br />

FBD....................... Idara ya Misitu na Nyuki<br />

GEF....................... Mfuko wa huduma ya Mazingira Duniani<br />

GIS........................ Mifumo ya Habari wa Kijiografia<br />

GOK...................... Serikali ya Kenya<br />

Ha......................... Hekta<br />

IRBM..................... Usimamizi wa Pamoja wa Mabonde ya Mito<br />

IDA........................ Chama cha Maendeleo cha Kimataifa<br />

<strong>IUCN</strong>..................... Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Uasili<br />

JFM....................... Usimamizi wa Pamoja wa Misitu<br />

KWH...................... Kilowati kwa saa<br />

LGA....................... Serikali za Mitaa<br />

LMIS...................... Skimu ya Umwagiliaji ya “Lower Moshi”<br />

MAFS.................... Wizara ya Kilimo na Chakula<br />

MCM...................... Mita za ujazo Milioni<br />

MGR...................... Hifadhi ya Wanyamapori ya Mkomazi<br />

MMP...................... Mradi wa Usimamizi wa Mikoko<br />

MoU....................... Mkataba wa Makubaliano<br />

MoWLD................. Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo<br />

MTESM................. Mkakati wa Taifa Kuendeleza Sekta ya Maji<br />

MW........................ Megawati<br />

NAWAPO.............. Sera ya maji ya Taifa<br />

n.d......................... Hakuna Tarehe<br />

NEMC.................... Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira<br />

v


NGO...................... Shirika Lisilo la Kiserikali<br />

NPF....................... Mradi Mpya wa Maporomoko ya Mto Pangani<br />

NORAD................. Shirika la Kimataifa la Misaada la Norway<br />

NRM...................... Usimamizi wa Maliasili<br />

NWP...................... Sera ya Maji<br />

NyM....................... Bwawa la Nyumba ya Mungu<br />

PA.......................... Maeneo Yaliyohifadhiwa<br />

PBWB................... Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani<br />

PBWO................... Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani<br />

PRB....................... Bonde la Mto Pangani<br />

PRBMP................. Mradi wa Usimamizi wa Bonde la Mto Pangani<br />

RBM...................... Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Maji<br />

RBMSIIP............... Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Maji na Uboreshaji wa Kilimo cha<br />

Umwagiliaji cha Wakulima Wadogo wadogo<br />

RCE....................... Kituo cha Kanda cha viumbe vipatikanavyo kipekee<br />

RHO...................... Afisa Haidrolojia wa Mkoa<br />

RNRO.................... Afisa Maliasili wa Mkoa<br />

SA......................... Uchambuzi wa Hali Halisi<br />

SNV....................... Shirika la Maendeleo la Uholanzi<br />

TANAPA................ Mamlaka ya Hifadhi za Taifa<br />

TANESCO............. Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania<br />

TCMP.................... Ubia wa Usimamizi wa Pwani Tanzania<br />

ICZCDP................. Programu ya Hifadhi na Maendeleo ya Ukanda wa Pwani Tanga<br />

TFAP..................... Mpango wa Utekelezaji wa Misitu Tanzania<br />

TFCG.................... Kikundi cha Hifadhi ya Misitu Tanzania<br />

TIP......................... Shirika la Umwagiliaji Kiasili na Maendeleo ya Mazingira<br />

TPC....................... Kampuni ya Kiwanda cha Sukari Moshi (Tanzania)<br />

UNICEF................. Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Dharura kwa Watoto<br />

UNDP.................... Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa<br />

USAID................... Wakala wa Marekani kwa Maendeleo ya Kimataifa<br />

VNRC.................... Kamati ya Maliasili za Kijiji<br />

VWN...................... Dira ya Maji na Uasili<br />

WANI..................... Programu ya Hifadhi ya Maji na Uasili ya <strong>IUCN</strong><br />

WDM..................... Usimamizi wa Mahitaji ya Maji<br />

WHO..................... Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa<br />

WRMA................... Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji (Kenya)<br />

WRM Act............... Sheria ya Usimamizi wa Rasilimalui za Maji ya mwaka 2009<br />

WUA...................... Chama Cha Watumiaji Maji<br />

vi


Dibaji<br />

Madhumuni ya toleo la kwanza la Uchambuzi ya Hali ya Bonde la Mto Pangani yalikuwa kuainisha<br />

rasilimali za asili zilizomo katika Bonde hilo, matukio yanayoziathiri na kutambua maeneo ya kufanyia<br />

kazi. Madhumuni mengine yalikuwa kutambua mashirika, asasi na wadau wengine ambao <strong>IUCN</strong> ingeweza<br />

kushirikiana nao.<br />

Lengo la WANI ni kuhakikisha kwamba suala zima la ikolojia linazingatiwa katika sera, mipango, na<br />

usimamizi wa mabonde ya mito. Katika maeneo ya mabonde ya kufanyia maonyesho yaliyoteuliwa duniani,<br />

WANI imepania: kuonyesha namna ya kusimamia mfumo ikolojia, kuwawezesha wananchi kushiriki katika<br />

usimamizi endelevu wa rasilimali za maji, kuendeleza usimamizi bora wa vyanzo vya maji na ardhioevu,<br />

kuanzisha na kutumia nyenzo za kiuchumi na vivutio, kuongeza maarifa ya kusaidia kufikia maamuzi na<br />

kutoa mafunzo yatakayoleta mwamko wa matumizi bora ya maji.<br />

Kufuatia mashauriano na wadau katika Bonde na kwa kuzingatia maazimio ya warsha iliyoendeshwa na<br />

Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWO) kwa ushirikiano na <strong>IUCN</strong> - Shirika la Kimataifa la Kuhifadhi<br />

Uasili iliyofanyika Moshi, Tanzania, kuanzia tarehe 8 hadi 10 Mei, 2002, Bonde la Mto Pangani nchini<br />

Tanzania na Kenya lilichaguliwa kuwa eneo la maonyesho la WANI.<br />

Ikiwa ni sehemu ya shughuli zake za mradi wa maendeleo katika Bonde la Mto Pangani, <strong>IUCN</strong> ilimwajiri Mshauri<br />

Mtaalamu Dk. Kim Geheb, kufanya Uchambuzi wa Hali halisi ya bonde hili. Kazi za ugani kwa ajili ya uchambuzi<br />

wa hali halisi zilifanyika mwezi Novemba, mwaka 2002, na ilihusisha mahojiano na wadau mbalimbali katika<br />

bonde. Vyanzo vya ziada vya taarifa vilikuwa ni marejeo ya machapisho pamoja na mjadala wa warsha iliyotajwa<br />

hapo juu, iliyojulikana kwa jina la “Bonde la Mto Pangani: Usimamizi Shirikishi”<br />

Madhumuni ya Uchambuzi wa Hali halisi ni kama yafuatayo:-<br />

• Kuainisha rasilimali mbalimbali zilizomo katika Bonde la Mto Pangani , na kufahamu michakato na<br />

matukio yanayoziathiri.<br />

• Kutambua kwa mapana maeneo ya kiutendaji ambayo yanaweza kushughulikiwa kwa manufaa ya<br />

kimaendeleo.<br />

• Kutambua taasisi na asasi mbalimbali zilizopo, na zenye nia ya kujishughulisha na rasilimali za<br />

maji, ambazo <strong>IUCN</strong> inaweza kuingia nazo ubia kwa lengo la kuendeleza juhudi za WANI katika<br />

Bonde la Mto Pangani.<br />

Kitabu hiki “Uchambuzi wa Hali Halisi ya Bonde la Mto Pangani“ awali kilitafsiriwa na Ofisi ya Maji Bonde la<br />

Pangani. Bw. Ipyana E. Mwakalinga alikamilisha kwa kuboresha baadhi ya sehemu na kuhariri toleo hili la pili kwa<br />

lugha ya Kiswahili.<br />

Rasimu ya kwanza ya Uchambuzi wa Hali Halisi katika Bonde la Mto Pangani ilikamilika mwishoni mwa mwaka 2002<br />

na kusambazwa kwa wadau kwa ajili ya mapitio na maoni. Katika warsha iliyoandaliwa na PBWO na <strong>IUCN</strong> mjini<br />

Moshi mwezi Machi 2003, wadau walitoa maoni na kupendekeza marekebisho kadhaa. Maoni na mapendekezo<br />

ya ziada yalipokelewa kutoka PBWO na Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani (CDA - Kenya) kwenye mkutano wa<br />

<strong>IUCN</strong>, PBWO na CDA uliofanyika Nairobi mwezi Mei, mwaka 2003. Mwaka 2009 uchapishaji upya wa Uchambuzi<br />

ya Hali ya Bonde ulihitajika na ikaamuliwa kutumia nafasi hii kufanyia mapitio ya taarifa chache ikizingatiwa kuwa<br />

sheria mpya ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji iliyopitishwa July 2009 na inafanya kazi. Ieleweke kuwa taaarifa<br />

zilizofanyiwa mapitio ni zile tu zinazohusu miuondo ya utawala, mifumo ya kitaasisi, sheria na sera za maji, vilevile<br />

taarifa mpya kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa Mradi wa Usimamizi wa Bonde la Pangani zimeongezewa, lakini<br />

maeneo mengine yote ya uchambuzi yameachwa kama yalivyo. Kazi hii yakufanyia mapitio Uchambuzi ya Hali ya<br />

Bonde la Pangani imegharamiwa na Global Water initiative (mpango wa maji wa dunia) unaofadhiliwa na mfuko<br />

wa Howard G. Buffett (Howard G. Buffett Foundation).<br />

Felix Peter, Helen Lema, Fatuma Omar na Renalda Mukaja kutoka Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya<br />

Rasilimali za Maji uliopo chini ya Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo ya Tanzania walijitolea kutayarisha na<br />

kufanya makadirio ya maeneo katika ramani zilizopo katika kitabu hiki.<br />

vii


Muhtasari<br />

Bonde la Mto Pangani lina eneo la takriban kilomita za mraba 43,650, sehemu kubwa ikiwa nchini<br />

Tanzania na karibu asilimia 5 iko katika Jamhuri ya Kenya. Nchini Tanzania, bonde hili limeenea katika<br />

mikoa minne: Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Tanga. Katika Jamhuri ya Kenya eneo la bonde liko<br />

katika Wilaya ya Taita-Taveta. Mto Pangani unaundwa na matawi makubwa mawili , Mto Kikuletwa na<br />

Ruvu ambayo huunganika katika bwawa la Nyumba ya Mungu lenye eneo la kilomita za mraba 140.<br />

Mto unapotoka katika bwawa hili unajulikana kwa jina la Mto Pangani, ambao hutiririka kwa umbali wa<br />

kilomita 432 kabla ya kuingia Bahari ya Hindi.<br />

Bonde hili lina rasilimali nyingi. Bila shaka maji na ardhi inayofaa kwa kilimo ndizo rasilimali muhimu zaidi<br />

kwa wakazi wapatao milioni 3.7 wa bonde hili waishio upande wa Tanzania. Nyanda za juu za bonde<br />

hupata mvua nyingi zaidi ukilinganisha na uwanda wa chini. Hata hivyo kutokana na msongamano na<br />

ushindani wa kupata ardhi ulioko katika nyanda za juu, wakulima wamelazimika kuanza kumwagilia maji<br />

mashamba yao ili kuinua uzalishaji. Wale walioshindwa kupata ardhi katika nyanda za juu wamelazimika<br />

kutafuta maeneo katika uwanda wa chini wenye mvua haba, ambako kilimo cha umwagiliaji ni wa muhimu<br />

sana. Ugumu wa hali unazidishwa zaidi na mwenendo wa upungufu wa mvua katika bonde.<br />

Ushindani wa kupata ardhi umesababisha rasilimali nyingine katika bonde kama vile misitu, kuingia<br />

katika ushindani wa moja kwa moja na kilimo. Sehemu ya misitu inalindwa kutokana na hadhi yake<br />

ya hifadhi, kama vile Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) ambayo ipo chini ya Mamlaka ya<br />

Hifadhi za Taifa (TANAPA). Misitu mingine inalindwa na idara za misitu za Kenya na Tanzania. Kutokana<br />

na sababu mbalimbali, zikiwemo uhaba wa wafanyakazi na ukosefu wa fedha, misitu hii haifaidi viwango<br />

sawa vya hifadhi ikilinganishwa na ile iliyopo chini ya TANAPA. Kuwepo shinikizo kwenye misitu ya<br />

pwani na Milima ya Tao la Mashariki katika bonde la mto Pangani kunatia wasiwasi mkubwa sana, hasa<br />

ikizingatiwa kuwa maeneo hayo yana kiwango cha juu cha mimea na viumbe adimu ndani yake.<br />

Rasilimali nyingine katika bonde ni madini, ambayo ni pamoja na tanzanite, bati na vito. Nyingine ni<br />

uvuvi, maeneo ardhioevu na vivutio vingi vya utalii.<br />

Rasilimali hizi hutumika kwa namna mbali mbali. Uchambuzi huu wa hali halisi unaweka matumizi hayo<br />

katika makundi yafuatayo:<br />

• Shughuli za viwanda, ambazo ni pamoja na mchango mkubwa wa nishati ya umeme wa<br />

nguvu ya maji katika gridi ya taifa, uchimbaji wa madini na viwanda vya kilimo kama vile<br />

kiwanda cha sukari na vya usindikaji wa katani.<br />

• Shughuli za kilimo: Kwa sehemu kubwa kilimo katika bonde hili ni cha asili na hutegemea<br />

umwagiliaji. Mifereji ya umwagiliaji ina ufanisi mdogo sana, inaweza kupoteza kiasi cha<br />

asilimia 85 ya maji kati ya mahali yanapochukuliwa hadi yanapopelekwa. Kadhalika kuna<br />

kilimo cha umwagiliaji cha viwango vikubwa katika bonde, yakiwemo mashamba ya miwa,<br />

mkonge na maua. Kadiri ya hekta kati ya 29,000 na 40,000 humwagiliwa katika bonde la<br />

Pangani upande wa Tanzania. Kiasi cha maji kinachotumiwa kinakadiriwa kuwa kati ya mita<br />

za ujazo milioni 400 na 480 kwa mwaka.<br />

• Shughuli za ufugaji: Idadi kamili ya mifugo iliyopo katika bonde kwa sasa haifahamiki. Inadhaniwa<br />

kuwa, ifikapo mwaka 2015, ufugaji utatumia mita za ujazo 36,400 za maji kwa siku.<br />

• Shughuli za mijini: Bonde lina miji miwili mikubwa, yaani Arusha na Moshi. Kadri miji hii<br />

inavyokua, mahitaji ya maji yameongezeka katika nyanja mbili: kwa matumizi ya viwandani<br />

na nyumbani, na kama njia ya kuondolea maji taka. Inatarajiwa kuwa, ifikapo mwaka 2015,<br />

mahitaji ya maji mijini katika bonde yatafikia mita za ujazo 163,600 kwa siku.<br />

viii


Kutokana na hali hiyo kuna asasi na mashirika mbalimbali katika bonde, ambayo yanaweza kutumia<br />

madaraka ya viwango tofauti katika kumiliki rasilimali zilizoko katika bonde. Tofauti hii ya viwango vya<br />

madaraka ni msingi wa migogoro mingi ya matumizi ya rasilimali hizo. Uchambuzi huu wa hali halisi<br />

unainisha migogoro hiyo kama ifuatavyo:<br />

• Migogoro itokanayo na viwango: Uhusiano kati ya watumiaji wa maji wa ukubwa na uwezo<br />

tofauti katika bonde la Mto Pangani mara nyingi huelezewa katika hali mbili kinzani. Hivyo<br />

mashamba makubwa yatumiayo mamia ya lita za maji kwa sekunde na kutumia mifumo ya<br />

umwagiliaji maji yenye ufanisi wa hali ya juu, hutofautiana sana na watumiaji wadogo ambao<br />

hutumia maji kidogo na mifumo duni ya umwagiliaji yenye ufanisi mdogo. Tofauti hizi kubwa<br />

za matumizi ndiyo vyanzo halisi vya migogoro. Uchambuzi huu wa hali halisi unatoa mifano<br />

ya migogoro ya aina hii kuwa ni maslahi kati ya watumiaji wa mijini na vijijini; na kati ya<br />

wachimbaji madini wa viwango vikubwa na vidogo.<br />

• Migogoro itokanayo na umiliki: Kitabu hiki kinafafanua umiliki kama haki ya kusimamia<br />

rasilimali. Nchini Tanzania, Usimamizi wa Maliasili Kijamii (CBNRM) umeonekana kama njia<br />

ya kuvutia ya kuongeza ufanisi wa Usimamizi wa Maliasili za Taifa (NRM). Mwenendo huu<br />

haufuatwi sana nchini Kenya. Ukinzani katika mifumo hii unahusiana na matumizi na usanifu<br />

wake. Hapa, jamii zinaweza zisishirikishwe katika kubuni mkakati wa usimamizi, utekelezaji<br />

wake au hata mifumo yake ya kisheria. Hali hii inaweza kudhihirisha kuwa taasisi hizi<br />

hazitimizi wajibu wa usimamizi ulioundwa ili ziufanyie kazi. Mifano ni migogoro ya usimamizi<br />

wa misitu kati ya ngazi ya jamii na serikali; baina ya watumiaji rasilimali wa aina mbalimbali;<br />

na migogoro kuhusu nyanja mbali mbali za usimamizi.<br />

• Migogoro itokanayo na mahali: Watumiaji walioko maeneo ya juu ya mito wana nafasi nzuri ya<br />

kutumia maji kuliko walioko sehemu za chini. Kwa kiwango kikubwa matatizo haya yanaweza<br />

kuonekana kwenye mifereji ya umwagiliaji ambako watumiaji walio karibu na chanzo cha<br />

maji wanaweza kuotesha mazao yanayohitaji kiasi kikubwa cha maji (kama vile mpunga) na<br />

wale walioko mwishoni mwa mifereji wakilazimika kupanda mazao yanayohitaji maji kidogo.<br />

Matatizo makubwa yanayoikabili mitambo ya umeme wa maji iliyoko upande wa chini wa mito<br />

ni mfano mwingine. Mifano ya migogoro ya aina hii ni ile iliyopo kati ya watumiaji wa maji wa<br />

maeneo ya juu ya mto na wa maeneo ya chini ya mto, na migogoro kati ya wazalishaji wa<br />

umeme wa maji na wamwagiliaji wadogo wadogo.<br />

Migogoro juu ya rasilimali ni moja ya ushahidi wa ushindani mkubwa uliopo baina ya watumiaji wa<br />

rasilimali zilizoko katika bonde. Athari ya ongezeko la watu, tofauti ya mgawanyo wa rasilimali na hali ya<br />

kuwa na ukomo husababisha mbinu za matumizi yake mara nyingi kuwa mbaya. Mifano ya uharibifu wa<br />

rasilimali ni kama ifuatayo:<br />

• Misitu iliyopo katika bonde inakabiliwa na hatari ya ukataji hovyo wa miti, kuingiliwa ndani<br />

ya mipaka yake kwa mahitaji ya matumizi ya ardhi, uchomaji wa mkaa na ukusanyaji kuni.<br />

Inakisiwa kuwa karibu asilimia 77 ya misitu ya Milima ya Tao la Mashariki imepotea katika<br />

kipindi cha miaka 2,000 iliyopita kutokana na shughuli za binadamu, wakati kilomita za mraba<br />

41 za misitu asilia ya Kilimanjaro zimetoweka kati ya mwaka 1952 na 1982.<br />

• Ugawaji wa maji katika bonde unakabiliwa na tatizo la mahitaji makubwaambapo imedhihirika<br />

kuwa mahitaji ya rasilimali hiyo yanazidi upatikanaji wake. Sababu kuu ya ongezeko la mahitaji<br />

ni mifumo duni ya umwagiliaji kwa njia ya mifereji yenye ufanisi mdogo. Maeneo ya ardhioevu<br />

katika bonde yapo hatarini kutoweka kutokana na ujenzi wa mabwawa.<br />

• Maeneo yaliyohifadhiwa ya bonde yanakabiliwa na ujangili, na matatizo mengine kama yale<br />

yanayoikabili rasilimali ya misitu.<br />

• Sehemu kubwa ya viumbehai katika bonde inatokana na mazingira ya kipekee ya misitu iliyopo.<br />

Tishio la maisha ya viumbehai hutokea kutokana na hatari inayokabili mazingira.<br />

ix


• Uvuvi katika bonde la Mto Pangani unakabiliwa na shinikizo la uvuvi uliokithiri, na ukuaji wa<br />

magugumaji unaosababishwa na shehena kubwa ya virutubisho. Takriban tani 24 za udongo<br />

kwa hekta kutoka eneo la vyanzo vya mito huingia katika bwawa la Nyumba ya Mungu kila<br />

mwaka. Mwaka 1970, tani 28,509 za samaki zilivuliwa kutoka bwawa la Nyumba ya Mungu.<br />

Upatikanaji wa samaki umekuwa ukipungua kwa kiasi kikubwa tokea hapo, na katika mwaka<br />

1983, tani 2,430 za samaki zilipatikana.<br />

Kuna idadi kubwa ya mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali katika bonde hili yanayotaka<br />

kudhibiti uharibifu uliotajwa na kujaribu kuboresha maisha ya watumiaji wa rasilimali. Katika miaka ya<br />

karibuni, shughuli muhimu za kiwango kikubwa ni zile zilizogharamiwa na Benki ya Dunia kupitia Mradi<br />

wa Usimamizi wa Matumizi ya Rasilimali za Maji na Uboreshaji wa Kilimo cha Wamwagiliaji Wadogo<br />

Wadogo (RBMSIIP), na Mradi wa UNDP-GEF wa Viumbe anuwai wa Afrika Mashariki. Mradi wa kwanza<br />

ulikuwa maalum katika kuimarisha Ofisi ya Maji ya bBonde la Pangani (PBWO) na vilevile kuimarisha<br />

uwezo wa usimamizi wa matumizi ya maji katika bonde.<br />

Juhudi za mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) katika bonde hili ni pamoja na kujihusisha na Usimamizi<br />

Shirikishi wa ukanda wa pwani ya Tanzania na misitu yake ya mikoko, na Kaskazini mwa bonde ni<br />

uboreshaji wa umwagiliaji wa kiasili, na uwezeshaji wa njia za mawasiliano baina ya watumiaji wa ngazi<br />

ya chini wa rasilimali na uongozi wa bonde. Juhudi za ziada zinatilia mkazo hifadhi ya rasilimali za misitu<br />

na wanyamapori katika bonde.<br />

Mfumo wa Utawala wa bonde ni changamano. Nchini Tanzania, ni kawaida kutokea vyombo viwili kutawala<br />

rasilimali moja: Utawala unaotokana na serikali kuu na ule wa serikali za mitaa. Wakati huo huo, Bodi ya<br />

Maji ya Bonde la Pangani (BMBP) imeanzishwa katika bonde kwa lengo la kusimamia rasilimali ya maji<br />

katika bonde zima. Hii maana yake ni kuwa, mara nyingi, mipaka ya mamlaka baina ya watawala wa<br />

rasilimali na wasimamizi inaweza kuwa haieleweki na/ au yenye utata. Aina hii ya utata inajirudia katika<br />

ngazi za chini. Kama ilivyoelezwa awali, Tanzania imegeukia kwa kiasi kikubwa kwenye Usimamizi wa<br />

Maliasili Kijamii (CBNRM) kama njia ya kuboresha usimamizi wa rasilimali zake za asili. Hata hivyo,<br />

hali hii inamanisha kuwa kamati au mashirika mengine ya ngazi ya jamiii yameundwa kushughulikia<br />

rasilimali maalum, na sio maliasili kwa ujumla. Hivyo, kuna Kamati za Maliasili za Vijiji (VNRCs), Vyama<br />

vya Watumiaji Maji (WUAs), Serikali za Vijiji n.k, hali inayozidisha utata katika usimamizi na kuongeza<br />

gharama za uendeshaji kwa kiasi kikubwa.<br />

Nchini Kenya, hivi karibuni rasilimali za maji zimewekwa chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali<br />

za Maji (WRMA) inayotumia mabonde ya mito kama maeneo ya msingi ya usimamizi, na ambayo<br />

imekabidhiwa jukumu la kuratibu usimamizi shirikishi wa mabonde hayo na kuhusisha vikundi vya wadau<br />

katika muundo wa usimamizi. Huu ni utaratibu mpya kiasi, unaoweza kukabiliana na vikwazo kuhusiana<br />

na uhusishaji wa wadau katika muundo wa usimamizi, na ugumu wa kushirikisha sekta mbali mbali za<br />

utawala wa mabonde.<br />

Njia hii ya usimamizi kisekta ipo pande zote za mpaka na inajionesha katika hali ambapo idara zinahusika<br />

na usimamizi wa misitu, maji, umwagiliaji, wanyamapori na rasilimali nyingine. Hali hii inaweza<br />

kusababisha malengo ya usimamizi na njia za kuyafikia kwenda sambamba, na hivyo kuleta utata katika<br />

uwezekano wa kuweka usimamizi shirikishi wa bonde. Hata hivyo PBWO imeamua kuhakikisha angalau<br />

idara mbalimbali zinakuwa na mawasiliano baina yao kwa kutuma wawakilishi katika Bodi ya Maji ya<br />

Bonde la Pangani (PBWB). Hata hivyo Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani ina wawakilishi kutoka idara<br />

mbalimbali za serikali ili kuhakikisha kuwa angalau idara hizi zinawasiliana. Kwa mujibu wa sheria mpya<br />

ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji, bodi ina mamlaka ya kuandaa mipango ya usimamizi wa rasilimali<br />

za maji katika bonde, kwa kuwahamasisha na kuwahusisha wahusika wote, wakiwemo wasimamizi na<br />

watumia rasilimali za bonde.<br />

Uchambuzi huu wa Hali Halisi unaeleza kwa ufupi ugumu wa hali na matatizo yaliyotajwa juu kwa kuainisha<br />

masuala mbalimbali ambayo yanahitaji umakini mkubwa katika usimamizi wake. Kimsingi, matatizo ya<br />

mazingira ni matatizo ya kijamii. Kwa urahisi na kwa ajili ya kuonesha hali ya mazingira ya bonde la Mto<br />

Pangani, matatizo haya yanagawanywa kati ya masuala ya mazingira na ya kijamii kama ifuatavyo:<br />

x


Masuala ya mazingira:<br />

• Ukataji miti - husababisha matatizo katika uviaji wa maji ardhini, ongezeko la kasi ya mitiririko<br />

ya maji na hivyo kusababisha mmomonyoko wa udongo, mafuriko na ongezeko la usafirishaji<br />

wa mchangatope.<br />

• Mahitaji ya Ardhi – misitu mingi iko kwenye maeneo muhimu ya kilimo ambayo hupata kiasi<br />

kikubwa cha mvua. Jambo hili ni tishio kubwa kwa hifadhi ya misitu ya bonde hili.<br />

• Shughuli za kilimo: mbinu mbalimbali za kilimo katika bonde hili zilianzishwa wakati idadi<br />

ya watu ilikuwa ndogo sana, na upatikanaji wa rasilimali ulikuwa ni wa kutosha. Kwa kuwa<br />

idadi ya watu imeongezeka mbinu hizo sasa zinaweza kutishia uhai wa mazingira ya bonde<br />

hili. Mifumo iliyopo haina ufanisi wa matumizi ya maji na umwagiliaji wa mfululizo unaweza<br />

kusababisha hali ya chumvi chumvi na/au magadi ardhini.<br />

• Ongezeko la mifugo: suala hili halijulikani sana lakini linadhaniwa kuwa ni tatizo kubwa.<br />

Kutokana na kuongezeka kwa kilimo katika maeneo tambarare ya bonde, ardhi kwa ajili ya<br />

ufugaji imechukuliwa na wakulima, na hivyo kukuza zaidi ukubwa wa tatizo la wingi wa mifugo.<br />

• Maendeleo: maendeleo yasiyosimamiwa katika bonde hili ni chanzo cha uchafuzi wa mazingira<br />

kutokana na njia zisizotosheleza za uondoaji taka.<br />

• Ubora wa maji: ubora wa maji unaathiriwa na uchafuzi, lakini pia maji yanachafuliwa kutokana<br />

na hali ya kijiolojia inayosababisha ongezeko la madini ya floraidi majini.<br />

• Uvuvi unaokithiri: shughuli za uvuvi katika bwawa la Nyumba ya Mungu zinaonekana kukithiri.<br />

Uvuvi pia unatishiwa na ukuaji wa magugumaji kwenye mito na maziwa unaosababishwa na<br />

ongezeko la virutubisho katika bonde.<br />

• Uchimbaji madini: shughuli za uchimbaji madini zisizodhibitiwa katika bonde ni tishio kwa<br />

mandhari yake na manufaa ya ardhi katika siku zijazo. Aidha, hali hiyo ni tishio la uchafuzi wa<br />

mazingira. Uchimbaji wa mchanga mitoni hudhoofisha kingo za mito hiyo.<br />

• Ukosefu wa mwamko wa mazingira baina ya wakazi wa bonde.<br />

.<br />

Masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa<br />

• Umasikini: Kutokuwepo kwa shughuli za ngazi ya pili na ya tatu katika bonde ambazo ni ajira<br />

katika sekta za biashara na viwanda, wakazi wake wengi hujitafutia maisha katika shughuli za<br />

msingi kama vile kilimo, uvunaji wa mazao ya misitu, uvuvi n.k.<br />

• Migogoro: kwa vile watu wengi hujihusisha na shughuli za msingi, hali ya migogoro huibuka<br />

baina ya watumiaji wadogo, na kati ya watumiaji wadogo na wakubwa.<br />

• Manufaa ya kisiasa: wanasiasa wenye shauku ya kupata kura kutoka kwenye majimbo yao ya<br />

uchaguzi, wakati mwingine huchochea matumizi yasiyo endelevu ya rasilimali.<br />

Masuala ya usimamizi na utawala<br />

• Sera zisizotosheleza: sera zinazoonekana kuwa sahihi na zilizotungwa vizuri zinaweza zisifae<br />

kwa sababu utekelezaji wake hauwezi kufuatiliwa, na wahalifu hawaadhibiwi.<br />

• Matatizo ya kifedha: Haya hujitokeza karibu katika kila sehemu ya utawala wa bonde, kuanzia<br />

kwenye ugumu wa kutoa malipo ya kutosha hadi kwenye ununuzi wa teknolojia itakayosaidia<br />

ufuatiliaji katika bonde.<br />

xi


• Ukosefu wa Usimamizi Shirikishi: mgawanyo wa kiutawala kati ya ngazi ya mkoa na ya<br />

taifa ukiunganishwa na njia za usimamizi za kisekta unadhihirisha kuwa sehemu kubwa ya<br />

usimamizi wa rasilimali za asili (NRM) katika bonde siyo shirikishi, kwa kuwa sekta au ngazi<br />

moja ya utawala hutumia mbinu ya usimamizi iliyo tofauti na ngazi au sekta nyingine katika<br />

bonde. Tatizo hili vile vile linajitokeza katika ngazi ya kimataifa: hakuna utaratibu uliowekwa<br />

kati ya Kenya na Tanzania wa kuratibu usimamizi wao katika Bonde la Mto Pangani.<br />

• Matatizo na utawala wa jamii: hii huhusiana, kwanza na mchango hafifu unaotolewa na jamii<br />

katika ubunifu, utekelezaji na utiliaji mkazo wa mfumo wa usimamizi wa rasilimali za asili<br />

(NRM) ambao unawaelemea. Pili, nyingi ya njia hizi zinazoshinikizwa kutoka nje ya jamii,<br />

zinataka kuanzishwa kwa kamati za NRM za aina mbali mbali, hali ambayo matokeo yake<br />

ni mkanganyiko mwingi kupita kiasi katika ngazi ya jamii na hivyo kuchochea matatizo ya<br />

kisekta yaliyoelezwa hapo juu, migogoro ya mamlaka na mafanikio duni ya usimamizi.<br />

Kwa kuzingatia masuala yaliyoelezwa hapo juu, Uchambuzi wa Hali Halisi unabainisha maeneo<br />

mbalimbali ya kipaumbele katika utekelezaji kama ifuatavyo:<br />

Kuwepo kwa mikakati ya usimamizi inayounganisha sekta husika kwa ajili ya bonde la Mto Pangani<br />

ikishirikisha majukwaa mbalimbali. Hapana shaka hata kidogo kuwa bonde la Mto Pangani linahitaji haraka<br />

mikakati hiyo ambayo inaweza kukidhi upana na ugumu wa maswaala hayo. Mapendekezo yanayoweza<br />

kufikiriwa ni pamoja na kutengeneza mikakati ya kutambua mahitaji ya maji, kutathmini mahitaji ya maji<br />

ukanda wa chini wa mto kwa ajili ya watu na mazingira, kupanua wigo wa usimamizi wa maji na kuiongezea<br />

jamii wajibu wa kubuni na kutekeleza masuala ya usimamizi shirikishi wa rasilimali za asili (NRM).<br />

Kuwepo kwa mikakati madhubuti ya kuwezesha mazungumzo miongoni na kati ya watumiaji rasilimali na<br />

wasimamizi wa aina mbalimbali na waliohusishwa katika sekta mbalimbali kwa lengo la kuongeza uelewa<br />

katika ngazi zote za usimamizi. Taratibu zinahitajika ili kuhakikisha kuwa fursa za maongezi kati na miongoni<br />

mwa wadau na wasimamizi zinaongezeka kwa kiasi kikubwa, ili kuhakikisha kuwa ubadilishanaji wa habari<br />

kwa pande zote unakuwepo, usambazaji unaboreshwa na elimu ya jinsi wadau wote watakavyoshiriki<br />

katika ustawi wa bonde inatolewa. Ni muhimu uhamasishaji ufanyike kuhusu vipengele vyote na hali ya<br />

usimamizi wa bonde na wadau wake katika ngazi zote za usimamizi na uratibu wake. Sehemu ya ziada<br />

ya eneo hili la kipaumbele ni uanzishaji wa mabaraza yenye uwezo wa kuifanya kazi hii, na kutumika kama<br />

vyombo vya kutatua migogoro, na viungo kati ya ngazi mbalimbali za utawala.<br />

Kuainisha na kuanzisha mfumo sahihi wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data. Eneo hili la utendaji haliishii<br />

katika mifumo ya uendelezaji na ukusanyaji wa data za kihaidrolojia. Tathmini ya Setilaiti na GIS ya<br />

matumizi ya ardhi, viwango vya matumizi na mabadiliko ya kijiografia ni mahitaji ya msingi katika<br />

kupanga mipango na ufuatiliaji wa matumizi ya ardhi. Uundaji wa mbinu za kutathmini na kupima sababu<br />

za msingi za kijamii na za kiuchumi zinazosababisha uharibifu wa mazingira na utumiaji wa rasilimali<br />

uliokithiri pia zinahitaji kutambuliwa. Mifumo kama hii inabidi pia iwe na uwezo wa kutambua mahitaji ya<br />

maji katika Bonde. Mifumo ya data na ufuatiliaji iliyopendekezwa lazima iendane na uwezo wa ndani wa<br />

kifedha na matengenezo.<br />

xii


A<br />

Utangulizi wa Uchambuzi wa Hali<br />

Halisi Bonde la Mto Pangani<br />

A.1 Maelezo ya jumla ya Bonde la Mto Pangani<br />

Bonde la Pangani ni moja kati ya mabonde 9 yaliyoanzishwa na kuchapishwa katika gazeti la serikali kwa<br />

mujibu wa Sheria ya Maji ya 1074 (Usimamizi na Udhibiti) Na. 42 na marekebisho yake Na. 10 ya 1981<br />

(sheria hii ilifutwa na sheria mpya ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya mwaka 2009) kwa madhumuni ya<br />

kuhamisha madaraka ya usimamizi wa maji kutoka ngazi ya Taifa na kupeleka ngazi ya mabonde. Bonde<br />

la Pangani lina eneo kadiri ya kilomita za mraba 58,800 1 kiutawala na linajumuisha Bonde la Mto Pangani<br />

na mabonde ya mito midogo ya Umba, Msangazi, Zigi 2 na mito midogo ya pwani, ukiwemo Mkulumuzi.<br />

Uchambuzi huu wa hali halisi unahusu zaidi Bonde la Mto Pangani. Maelezo ya mabonde ya mito midogo<br />

yanayosimamiwa kiutawala na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani yanatolewa katika Kiambatanisho Na.1.<br />

Bonde la Mto Pangani lina eneo la kilomita za mraba 43,650 1 , kati ya hizo, kilomita za mraba 3,914 1 ziko<br />

Kenya (Mchoro wa 1). Nchini Tanzania, bonde hili lipo katika mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, Arusha na<br />

Tanga. Sehemu ya bonde iliyopo Kenya karibu yote ipo katika wilaya ya Taita- Taveta.<br />

Mto Pangani unaundwa na matawi makubwa mawili, ambayo yanatokea katika sehemu ya Kaskazini ya<br />

bonde. Tawi la kwanza ni Mto Kikuletwa unaonzia katika miteremko ya Mlima Meru na miteremko ya Kusini<br />

ya Mlima Kilimanjaro, na la pili ni Mto Ruvu, unaoanzia katika miteremko ya Mashariki ya Mlima Kilimanjaro<br />

na Ziwa Jipe. Mito hii inaungana katika bwawa la Nyumba ya Mungu, lenye eneo la kilomita za mraba 140<br />

(Rohr na Killingtveit, 2002). Mto Pangani 3 hutoka katika bwawa hili, ukitiririka kwa umbali wa kilomita 432<br />

kabla ya kuingia katika Bahari ya Hindi..<br />

Kwa ujumla, bonde hili lina mwinuko mdogo unaoteremka kuelekea upande wa Kusini na Kusini Mashariki hadi<br />

Bahari ya Hindi. Kwa wastani, sura hii ya nchi ijulikanayo kama Nyika za Masai ziko kwenye usawa wa mwinuko<br />

wa mita 800, na sehemu yake kubwa hupata mvua inayozidi kidogo milimita 500 kwa mwaka. Mkabala nayo ni<br />

safu ya milima inayoinuka kutoka uwanda huu ambayo mwinuko wake unafidia kwa kiwango kikubwa matatizo<br />

ya hali ngumu ya uwanda wa nyika. Katika sehemu hii ya juu, kiasi cha mvua kwa mwaka kinafikia milimita 2,000.<br />

Jinsi ilivyo, milima hii ni kama visiwa, wakati ambapo nyanda zinazoizunguka zinaonesha bayoanuwai duni, na<br />

hali ngumu ya kujitafutia riziki, milima hii ni visiwa vya bayoanuwai ya kuvutia na viumbe hai wengi. Binadamu<br />

hawakushindwa kuona ubora wa milima hii, na hata kabla ya ujio wa utawala wa kikoloni nchini Tanzania, milima<br />

iliyopo katika Bonde la Mto Pangani ilikuwa eneo linalokaliwa na idadi kubwa zaidi ya watu katika bonde hili.<br />

1<br />

Tafiti nyingi za awali zinalielezea eneo la chanzo cha mto lililoko kwenye utawala wa Bonde la Pangani nchini<br />

Tanzania kuwa ni kilomita za mraba 56,300, na eneo la Bonde la Mto Pangani katika Tanzania na Kenya kuwa ni<br />

kilomita za mraba 42,000 kulingana na makisio ya planimita yaliyofanywa na S. Kamugisha (1992). Hatimaye taasisi<br />

mbili tofauti (TANRIC ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Rasilimali ya<br />

Maji katika Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo) zimekadiria maeneo haya kwa kutumia GIS. Makadirio haya<br />

ya hivi karibuni ni makubwa zaidi kuliko yale ya awali ya makisio ya planimita. Tofauti hizi huenda ni matokeo ya<br />

tafsiri mbalimbali za mipaka ya bonde, hasa upande wa magharibi na tofauti kati ya njia za planimeta na zile za GIS<br />

(Kamugisha na Mwakalinga pers. Wahojiwa, 2003).<br />

2<br />

Baadhi ya Waandishi hutumia tahajia za “Sigi”, “Zigi” ndiyo tahajia inayopendelewa na wakazi wa eneo la chanzo<br />

cha mto huu (Wahojiwa, 2003).<br />

3<br />

Baadhi ya tafiti na ramani zinataja Mto utokao katika Bwawa la Nyumba ya Mungu kuwa ni Ruvu mpaka unapoungana<br />

na Mto Mkomazi, mahali ambapo unakuwa Mto Pangani. Utafiti huu unataja Mto huu kutoka unapotoka Nyumba ya<br />

Mungu hadi unapoingia baharini kuwa ni Mto Pangani.<br />

1


Jinsi Mto Pangani unavyoambaa kuelekea Mashariki, na kushukia uwanda wa pwani ya Tanzania,<br />

ndivyo unavyozidi kukabiliana na hali ya hewa na mazingira ya kutatanisha. Kinyume na hali ya hewa<br />

ya Kaskazini, ambayo imebadilika kwa kiasi kikubwa katika kipindi cha miaka elfu moja kutoka kipindi<br />

kimoja cha barafu hadi kingine, hali ya hewa inayotokana na Bahari ya Hindi imebakia bila mabadiliko<br />

makubwa. Mwambao wote wa pwani ya Afrika Mashariki unaonesha viunga vya misitu ya kale, na hali<br />

yake ya hewa imewezesha misitu hii kuhifadhiwa kutokana na uthabiti wake.<br />

Mabadiliko ya tabianchi katika maeneo mengine barani<br />

Afrika yamebadili kabisa hali ya mazingira, na kusababisha<br />

kwa kiwango kikubwa kutoweka kwa viumbe hai na kuanza<br />

upya mchakato wa hatua za mabadiliko, kiasi cha kufanya<br />

misitu ya mwambao mwa Tanzania ifanane kidogo na<br />

misitu ya sehemu nyingine barani. Katika milima iliyopo<br />

bonde la Mto Pangani, mistiu hii inaonesha kutetereka kwa<br />

bayoanuwai na upatikanaji wake katika maeneo haya.<br />

Leo hii idadi ya watu wanaokadiriwa kufikia milioni 3.7<br />

huishi katika sehemu ya bonde iliyoko Tanzania, wakati<br />

ambapo nchini Kenya idadi ya watu wa Taita -Taveta<br />

inakaribia 40,900. Mtindo wa makazi katika bonde ni<br />

taswira ya kutowiana kwa hali ya mazingira ya bonde<br />

hili. Nchini Tanzania asilimia 90 ya watu wanaoishi katika<br />

bonde hili huishi katika nyanda za juu, asilimia 80 ya hao<br />

kwa njia moja au nyingine hutegemea kilimo kwa ajili ya<br />

mahitaji yao (Mwamfupe, 2002). Mkusanyiko huu wa<br />

makazi huleta msongamano wa watu unaofikia hadi watu<br />

300 kwa kilometa ya mraba. Mwaka 1988, mikoa ya pwani<br />

ya Tanzania ilikuwa na idadi ya watu 28.4 kwa kilometa ya<br />

mraba (ukiacha Dar es Salaam), ongezeko la kutoka watu<br />

18 tu kwa kilometa ya mraba mwaka 1967. Katika Milima<br />

ya Usambara Magharibi, idadi ya watu imekua kwa mara<br />

Mchoro wa 1: Bonde la Mto Pangani<br />

lilivyoenea Tanzania na Kenya (Rejea:Mradi wa<br />

Usimamizi wa Matumizi Bora ya Rasilimali za Maji)<br />

23 tangu mwaka 1900, wakati katika maeneo ya nyanda za juu za Mlima Kilimanjaro, msongamano wa watu<br />

ni mkubwa kiasi cha watu 900 kwa kilomita ya mraba (Gillingham, 1999). Kinyume chake, maeneo ya nyanda<br />

za chini yameonesha kuwa na msongamano mdogo wa kiasi cha watu 65 kwa kilomita ya mraba.<br />

Kihistoria, wakazi wa bonde hili wamekuwa na shughuli za kiuchumi ambazo ni kielelezo cha hali<br />

zilizotofauti za mazingira katika bonde. Nyanda za chini zilikimu wafugaji, wakati nyanda za juu zilikimu<br />

wakulima. Kutokana na ujio wa wakoloni kutoka Ulaya, maeneo makubwa ya ardhi ya kilimo yalitengwa<br />

kwa kilimo cha mashamba makubwa. Katika wilaya ya Taita – Taveta ya Kenya, karibu ardhi yote<br />

ilitengwa kwa ajili ya kilimo cha mkonge. Hali hii ilisababisha kukua kwa kiwango cha kilimo. Johnston<br />

(1946) anasema kuwa, mwaka 1943, umilikaji ardhi katika nyanda za juu za Kilimanjaro kwa wastani<br />

ulikuwa hekta 1.2 kwa mtu mmoja. Katika mwaka 1946, ulikuwa mita za mraba 2.5 tu.<br />

Wastani wa kiwango cha umilikaji wa ardhi katika nyanda za juu za Kilimanjaro umeongezeka tokea<br />

hapo, na Lein (2002) anasema kiwango cha umilikaji ardhi kuwa ni wastani wa hekta 0.6 kwa kaya. Kaya<br />

za nyanda za chini hulima mashamba ya wastani wa eneo la hekta 10.4.<br />

Wastani huo unaelekea kupungua. Kadiri ukubwa wa mashamba katika nyanda za juu unavyokuwa mdogo<br />

zaidi na zaidi, uwezo wake wa kukidhi mahitaji ya maisha ya watu unapungua, na udongo umechoshwa<br />

kutokana na kupanda mazao mfululizo pamoja na umwagiliaji uliokithiri, watu wamelazimika kutafuta<br />

ardhi katika maeneo ya nyanda za chini. Kwa sababu hiyo, idadi ya watu imekuwa kubwa kando ya mito<br />

ya bonde la mto Pangani na umwagiliaji umeenea kwa kiasi kikubwa sana. Matokeo yake, maeneo ya<br />

bayoanuwai yaliyopo hapa na pale katika uwanda wa bonde yako katika shinikizo la kutoweka.<br />

2


Mchoro wa 2: Bonde la Mto Pangani<br />

Angalia pia Picha ya 1, ukurasa wa 33<br />

(Rejea: Mradi wa Usimamizi wa Matumizi<br />

Bora ya Rasilimali za Maji)<br />

3


Kwa hiyo, kiini cha matatizo ya Bonde la Mto Pangani kinahusiana na msogamano wa watu na mahitaji<br />

yao mawili makuu na muhimu kwa kilimo na ufugaji: ardhi na maji. Mwingiliano wa mambo haya, na<br />

mahitaji waliyo nayo watu katika rasilimali za bonde, yamesababisha migogoro ya aina mbalimbali:<br />

Migogoro itokanayo na viwango<br />

Uhusiano baina ya watumiaji maji wa ukubwa tofauti katika Bonde la Mto Pangani mara nyingi unajieleza<br />

katika namma mbili, yaani mashamba makubwa yanayotumia mamia ya lita za maji kwa sekunde na kutumia<br />

mifumo ya umwagiliaji yenye ufanisi mkubwa, tofauti kabisa na watumiaji wadogo wanaotumia maji kidogo na<br />

mifumo duni ya umwagiliaji. Tofauti hizi za viwango vya matumizi haziishii kwenye teknolojia pekee, bali hata<br />

ardhi. Watumiaji wakubwa karibu wakati wote hutumia ardhi kubwa zaidi kuliko watumiaji wadogo. Jambo<br />

jingine tofauti na la pekee ni kuwepo kwa mitambo ya uzalishaji umeme katika bonde. Ardhi inayokaliwa na<br />

mitambo hii siyo kubwa sana, lakini mahitaji yake ya maji ni makubwa sana. Ni dhahiri maji haya hurudishwa<br />

mtoni, hii ikiwa na maana uzalishaji umeme huyaacha maji katika hali na kiasi kile kile kilichochukuliwa. Pamoja<br />

na hayo matumizi hayo ni kwa maslahi ya taifa. Bonde la Mto Pangani huzalisha kiasi kinachofikia asilimia<br />

17 ya umeme wa Tanzania, na vinu vyake vingi vimesanifiwa maalum kwa kutilia maanani mtiririko wa maji.<br />

Iwapo matumizi ya maji kati ya vyanzo vya maji na mitambo ya umeme yatazidi, inabidi mitambo izalishe kwa<br />

kiwango chini ya uwezo wake. Mgogoro uliopo hapa ni kulinda maslahi ya kitaifa dhidi ya watumiaji wadogo.<br />

Migogoro itokanayo na umiliki<br />

Kitabu hiki kinatumia neno umiliki kama haki ya kusimamia rasilimali. Kama ilivyo kwenye sehemu nyingi<br />

ulimwenguni, dhana ya usimamizi kwa misingi ya kijamii katika Tanzania na Kenya ni mpya. Katika nchi<br />

ambazo mifumo ya usimamizi inayotegemea serikali, imedumu kwa zaidi ya nusu karne, bila mafanikio<br />

mazuri na kusababisha ongezeko la matatizo ya mazingira, usimamizi wa maliasili kwa misingi ya kijamii<br />

(CBNRM) unaonekana kuwa chaguo la kuvutia. Kwa hali hiyo nchini Tanzania kuna asasi nyingi mno za<br />

usimamizi wa kijamii. Dhana ya usimamizi wa maliasili kijamii inabakia kuwa mpya sana nchini Kenya.<br />

Ukinzani wa mifumo hii unahusiana na mwenendo wa matumizi na miundo yao. Hapa, jamii zinaweza<br />

zisihusishwe katika uundaji wa mfumo wa usimamizi, utekelezaji wake au hata mifumo yake ya kisheria.<br />

Migogoro itokanayo na mahali<br />

Maeneo ya watumiaji maji yaliyoko juu hutoa nafasi nzuri zaidi ya matumizi ya rasilimali kuliko ilivyo kwa watumiaji<br />

wa maeneo ya chini. Kimsingi, matatizo haya yanaweza kuonekana katika mifereji ya umwagiliaji ambapo<br />

watumiaji walio karibu na chanzo cha maji wanaweza kuotesha mazao yanayohitaji maji mengi sana (kama vile<br />

mpunga) na wale wanaoishi mwishoni mwa mfereji hulazimika kupanda mazao yenye mahitaji madogo ya maji.<br />

Matatizo makubwa yanayoikabili mitambo ya umeme wa maji iliyopo upande wa chini ni mfano mwingine.<br />

Taasisi kuu mbili zinatawala rasilimali ya maji ya Bonde la Mto Pangani. Nchini Tanzania ni Ofisi ya<br />

Maji ya Bonde la Pangani (PBWO), wakati katika Kenya ni Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali za<br />

Maji (WRMA). Chini ya sheria ya hivi karibuni ya Tanzania, mabonde yote yamewekwa (au yatawekwa)<br />

chini ya ofisi kama hizo. Hata hivyo, mabonde mengine ni madogo mno kustahili kuanzishiwa ofisi<br />

zitakazojitegemea kiusimamizi. Bonde la Pangani limezungukwa na mabonde manne ya aina hiyo (mito<br />

ya Umba, Zigi, Msangazi, na mabonde madogo ya mito ya pwani). Haya kiutawala yanawekwa chini ya<br />

PBWO, na hayakujumuishwa katika uchambuzi wa hali halisi katika kitabu hiki. Hata hivyo, muhtasari wa<br />

taarifa kuhusu mabonde hayo unaambatanishwa(Kiambatanisho Na 1).<br />

Bonde la Mto Pangani linakabiliana na matatizo kadhaa makubwa ya kiusimamizi. Kwa kuzingatia tofauti<br />

kubwa za aina za maliasili za bonde, pamoja na mahitaji na matarajio mbalimbali ya matumizi, haja ya kuwa<br />

na usimamizi shirikishi haiwezi kupuuzwa. Hapo nyuma, njia ile ile ya usimamizi wa ‘kisekta’ kwa bonde hili<br />

ilimaanisha kuwa rasilimali ya wanyamapori ilisimamiwa kipekee tofauti na shughuli za misitu, bila kujua, kwa<br />

upande mwingine kipaumbele cha usimamizi wa maji. Tatizo pia linajitokeza katika utoaji kipaumbele, sekta ya<br />

maji ikidai kuwa maji ni kiungo kinachounganisha rasilimali zote za bonde, lakini watu wa misitu wakilalamika<br />

kuwa sehemu kubwa ya maji ya bonde yanatoka katika misitu iliyo kwenye mamlaka yao kisheria.<br />

4


A.2 Usimamizi wa Pamoja wa Mabonde ya Mito (IRBM)<br />

Kwa vyovyote vile, mfumo wa usimamizi wa maliasili kimabonde ndio unaofaa. Mabonde ya mito<br />

yanahusisha vyanzo na michakato yote ambayo hatimaye itahakikisha kuwa maji yanafika hadi mwisho<br />

wa mto. Hivyo, bonde la mto linahusisha vijito vya awali vya mto, mito midogo na mabonde yake. Pia ni<br />

pamoja na delta iliyohusiana na mto, na maji ya ardhini, ardhioevu na mabwawa yoyote yaliyomo.<br />

Mchanganyiko wa michakato inayohakikisha kuwa maji yanasafiri kutoka kwenye chanzo cha mto hadi<br />

mwisho wake ni mgumu na una mambo mengi. Rasilimali za ziada, kama vile misitu na ardhioevu,<br />

zinachangia mchakato huu. Kiasi cha maji ambacho hatimaye hufika mwishoni mwa mto pia kitategemea<br />

kiasi cha maji yanayochukuliwa kwa matumizi yanapopita katika mkondo wake pamoja na kiwango cha<br />

uvukizaji katika maeneo ardhioevu na mimea ya majini na ya kandokando ya mto. Mwisho, ubora wa<br />

maji yatakayofika mwishoni mwa mto pia utaonesha michakato iliyopo katika bonde kama vile mbinu za<br />

kilimo ambazo huongeza au kupunguza mmomonyoko, maendeleo ya miji au viwanda n.k.<br />

Usimamizi wa Mabonde ya Mito (RBM) unatambua kuwa usimamiaji wa mto hauwezi kutekelezwa kwa<br />

kutenganisha michakato na hali nyingi mbalimbali zinazoathiri mtiririko wa mto na ubora wa maji yake.<br />

RBM hulichukulia bonde la mto kama kitengo cha usimamizi kinachohusisha matumizi na uhifadhi wa<br />

(a) mifumo midogo ya ikolojia (mabonde madogo ya mito, misitu, ardhioevu, maeneo ya milima, ardhi<br />

kame, n.k); na (b) mifumo ya matumizi ya binadamu iliyomo ndani ya eneo la maji (kilimo, umwagiliaji,<br />

uvuvi, usafirishaji, uchimbaji madini, viwanda, n.k). RBM kwa kawaida hufuata kanuni ya kuwa maji<br />

huunganisha mifumo ikolojia iliyomo ndani ya bonde la mto (Howard, 2002).<br />

Usimamizi wa Pamoja wa Bonde wa Mto hujaribu kuleta uwiano wa masilahi ya watumiaji wote waliopo katika<br />

bonde, na wakati huo huo kukuza ufanisi wa matumizi ya rasilimali na kuhakikisha kunaendelea kuwepo maji<br />

ambayo kwayo mifumo hii inategemea (Howard, 2002). IRBM inaweza kufafanuliwa kama ifuatavyo:<br />

”… ni mchakato unaokuza uratibu wa maendeleo na usimamizi wa maji, ardhi na rasilimali<br />

zinazohusiana nazo ili kuzidisha ustawi wa kiuchumi na kijamii kwa njia ya usawa bila ya<br />

kuathiri uendelevu wa mifumo muhimu ya ikolojia (GWP, 2002:1).<br />

IRBM hushughulika na rasilimali kwa mapana zaidi iwezekanavyo. Inabidi kuziangalia rasilimali za maji<br />

kwa mtazamo mzima wa mifumo ya kijamii, kiuchumi na kiikolojia ya mkoa au nchi. Kiutendaji, hii ina<br />

maana ya kuwa sera na programu katika maeneo mengine ya rasilimali hazina budi kuchambuliwa kwa<br />

makini ili kuona jinsi zinavyoathiri mahitaji yanayoshughulikiwa na sekta ya maji (GWP, 2002) IRBM<br />

inayapa mazingira umuhimu sawa na watu katika mahitaji ya rasilimali za maji. IRBM lazima ifanye kazi<br />

kulingana na malengo yaliyokubaliwa na wadau wa bonde walio wengi na kufuata kanuni za usimamizi<br />

wa rasilimali za maji, usimamizi wa mfumo ikolojia, uhifadhi wa bayoanuwai, usimamizi endelevu wa<br />

maliasili na ufufuaji wa mfumo ikolojia. (Howard, 2002).<br />

Sehemu muhimu ya Usimamizi wa Pamoja wa Bonde wa Mto ni mpango wa matumizi ya ardhi. Kwa<br />

kuwa mambo mengi sana yanayotokea kuhusu maji yanahusu maendeleo ya ardhi, ni muhimu matumizi<br />

ya ardhi yasimamiwe kwa njia ambayo itahakikisha upatikanaji wa maji na kwamba michakato ya<br />

kihaidrolojia haiingiliwi. Kwa mfano, ukuaji wa miji mara nyingi umekuwa na athari kubwa kwa rasilimali<br />

ya maji kutokana na ongezeko kubwa la majitaka. Kwa njia hiyo hiyo, misitu na kilimo vinaweza kuwa na<br />

athari kwa wingi na ubora wa maji.<br />

Mifano ya mapendekezo ya usimamizi wa matumizi ya ardhi ni pamoja na (a) kugawa kanda-hapa<br />

maeneo maalum hubainishwa ambamo aina fulani za matumizi ya ardhi hukatazwa. Kwa mfano kanda<br />

za maji ya kunywa, au maeneo ambayo ujenzi hupigwa marufuku kutokana na hofu ya mafuriko. (b)<br />

hatua za kulinda udongo na kudhibiti mmomonyoko, kama vile kilimo cha kontua, au ushauri wa upandaji<br />

wa miti (c) kanuni za uondoaji taka, kama vile kuweka maeneo ya kutupa taka (GWP,2002).<br />

5


Kisanduku cha 1: Usimamizi wa Mahitaji ya Maji<br />

Usimamizi wa Mahitaji ya Maji (WDM) umetokana na kutambua kuwa (a) mahitaji ya maji yanaongezeka<br />

bila ya kuambatana na ongezeko la upatikanaji wa maji; (b) matokeo yake, gharama ya<br />

kuongeza usambazaji wa maji hupanda kwa sababu uchukuaji maji kutoka katika vyanzo vipya<br />

unakuwa mgumu zaidi. Gharama zinazoambatana na uanzishaji wa teknolojia au mbinu mpya ya<br />

uchukuaji maji inawezekana zisikubalike. WDM, basi, inajaribu kuokoa maji yachukuliwayo kutoka<br />

vyanzo vilivyopo vya maji, yalete manufaa kwa vyote viwili, uchumi na mazingira. WDM inaweza<br />

kufafanuliwa kama mkakati wa kuboresha matumizi fanisi na endelevu ya rasilimali za maji kwa<br />

kuzingatia masuala ya kiuchumi, kijamii na kimazingira (Wegelin-Schuringa, 1998). Lengo kuu la<br />

WDM ni kuchangia katika utoaji huduma za maji na uondoaji majitaka kwa ufanisi na usawa. <strong>IUCN</strong><br />

inaamini kuwa hili linaweza kufikiwa kupitia utumiaji wa vivutio mbalimbali vya kiuchumi, kukuza<br />

ufanisi na usawa wa matumizi ya maji na vile vile hatua kadhaa za kuhifadhi maji zitakazolenga<br />

katika kukuza uelewa juu ya uhaba na tabia ya asili ya kumalizika kwa rasilimali hii. WDM huchukua<br />

hatua mbalimbali zinazolenga kuleta usimamizi endelevu. Nazo ni pamoja na:<br />

• kulinda ubora wa maji<br />

• kupunguza upotevu wa maji<br />

• kuboresha ugawaji wa maji baina ya watumiaji<br />

• kuweka mfumo sahihi wa upangaji bei<br />

• hatua za kuhifadhi maji<br />

A.3 Programu ya Maji na Uasili (WANI)<br />

<strong>IUCN</strong> (shirika la kimataifa la kuhifadhi uasili) inasaidia kupata utatuzi wa busara wa changamoto<br />

zinazotukabili duniani katika maendeleo ya jamii na utunzaji wa mazingia. <strong>IUCN</strong> inafadhili tafiti za<br />

kisayansi, na inasimamia miradi na huunganisha serikali za kimataifa, asasi zisizo za kiserikali, mashirika<br />

ya Umoja wa Mataifa, makampuni na jamii katika kutunga na kutekeleza sera, sheria na utendaji bora.<br />

<strong>IUCN</strong> ni mtandao wa masuala ya mazingira ulio mkubwa kuliko yote duniani. Ni umoja wa kidemokrasia<br />

wenye wanachama 1,000 kutoka serikali na asasi zisizo za kiserikali, mashirika na wanasayansi 10,000<br />

wa kujitolea katika nchi zaidi ya 160. Ina waajiriwa wataalamu 1,100 katika ofisi zake 62 na mamia ya<br />

washiriki kutoka jamii, asasi na sekta isiyo rasmi ulimwenguni kote. Makao makuu yake yapo Gland,<br />

karibu na Geneva, Uswisi.<br />

<strong>IUCN</strong> ilizindua mpango wa maji na uasili (Water and Nature Initiative (WANI)) mwaka wa 2001. WANI ni<br />

mpango wa utendaji unaofanya kazi na washiriki 80 katika nchi 30 katika kuhusisha kwa kiasi kikubwa<br />

mambo ya mazingira na jamii wakati wa utayarishaji wa mipangao ya usimamizi wa rasilimali za maji.<br />

Mpango wa WANI hutumia menejimenti ya mfumo wa ikologia kama mkakati wa usimamizi uwiano na<br />

wa pamoja wa ardhi maji, bayoanuai na jamii. WANI husaidia katika utatuzi wa kuchagua katika mtanziko<br />

wa maendeleo ya jamii na hifadhi ya rasilimali zilizo majini kwa kutanzua migogoro ya matumizi ya maji,<br />

na kufufua mito na kuchochea maendeleo ya jamii.<br />

WANI huandaa na kuonyesha njia sahihi ya utendaji katika kutekeleza usimamizi wa rasilimali za maji<br />

wa uwiano. Husaidia katika kufanyia mageuzo ya kudumu na kujenga uwezo wa jamii unaohitajika<br />

katika kutekeleza mageuzi hayo. Katika awamu ya kwanza, kuanzia mwaka wa 2001 hadi mwaka wa<br />

2008 WANI ilifanya kazi katika mabonde ya maji 12 katika nchi zaidi ya 30 ulimwenguni kote, kazi<br />

iliyogharimu dola za Marekani 40m. Sehemu kubwa ya fedha hizi zilitolewa na Wizara ya Mambo ya Nje<br />

ya Uholanzi. Miradi ya majaribio ya WANI ilionyesha nama hali ya watu na mifumo ya ikolojia inavyoweza<br />

kunufaika kwa kutumia usimamizi endelevu wa mabonde ya maji. Miradi ya WANI ni washiriki wa jumuia,<br />

wanachama wa <strong>IUCN</strong>, jamii za kiraia na serikali.<br />

6


WANI inasaidia kufanya mabadiliko kwa kuunganisha vipaumbele vya maendeleo, huduma zitolewazo<br />

na mifumo ya ikolojia, utawala bora wa rasilimali za maji, ushiriki wa wadau, mapato endelevu ya fedha,<br />

kujifunza na uongozi.katika utendaji.<br />

Toleo la kwanza la Uchambuzi ya Hali ya Bonde llikuwa tokeo la kazi ya awali katika bonde la Pangani<br />

na liliweka msingi wa miradi iliyofuata awamu ya kwanza ya WANI ilianza kufanya kazi katika bonde lote<br />

la Pangani na kufuatana na matokeo ya kazi hii Ofisi ya Maji Bonde la Pangani iliweza kupata ufadhili<br />

wa nyongeza kutoka Kamisheni ya Ulaya kupia msaada wa mfuko wa maji wa Umoja wa Ulaya, Mfuko<br />

wa Mazingira wa Ulimwengu (Global Environment Facility) kupitia Shirika la Maendeleo la Umoja wa<br />

Mataifa (UNDP).<br />

A.4 Uchambuzi wa Hali halisi: madhumuni na matokeo<br />

Uchambuzi wa Hali halisi ni hatua muhimu ya mradi wa <strong>IUCN</strong>. Ni uchambuzi wa hadhi, hali, mienendo na<br />

masuala muhimu yanayoathiri mifumo ikolojia, watu na taasisi katika hali ya kijiografia ya ngazi yoyote<br />

(jamii, taifa, kanda, kimataifa)’ (<strong>IUCN</strong>, 1999:1). Madhumuni ya Uchambuzi wa Hali halisi ni kutoa tathmini<br />

inayotosheleza dhamira ya kipaumbele au maeneo ya utendaji yatakayoendelezwa.<br />

Kwa mantiki hii madhumuni ya Uchambuzi huu ni kama yafuatayo:<br />

• Kutambua rasilimali zilizomo katika Bonde la Mto Pangani na michakato na matukio yanayoziathiri.<br />

Uchambuzi utayaonesha maeneo hayo maalum ambayo yanahitaji kushughulikiwa ili kuyanusuru,<br />

kwa kuzingatia ushahidi unaoonesha kuwa uwiano kati ya upatikanaji wa riziki ya kutosha kwa<br />

wakazi wa Bonde hili na uendelevu wa rasilimali za Bonde umeharibiwa.<br />

• Kutambua maeneo ya utendaji kwa mapana ambamo hatua zinaweza kuchukuliwa kwa manufaa.<br />

Uchambuzi unatambua kuwa nyingi ya hatua hizo zinaweza zisiwe ndani ya utaalam wa <strong>IUCN</strong>.<br />

Hivyo utataka kuainisha mashirika, vikundi au taasisi nyingine ambazo <strong>IUCN</strong> inaweza kuingia<br />

nazo ubia kadri inavyotaka kuendeleza juhudi za WANI katika Bonde la Mto Pangani.<br />

A.5. Vyanzo vya data<br />

Uchambuzi huu wa Hali halisi umefanyika kwa kutumia data zilizopatikana kutokana na vyanzo vikuu viwili:<br />

• Taarifa iliyochapishwa. Umuhimu wa kipekee upo katika matokeo ya tafiti juu ya Usimamizi<br />

wa Rasilimali za Maji zilizofanyika katika Bonde la Mto Pangani, ambazo ni juhudi za pamoja<br />

kati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Teknolojia na Sayansi cha Norway.<br />

Kwa nyongeza, Uchambuzi wa Hali halisi pia umetumia taarifa ya warsha iliyoitwa “Bonde la<br />

Mto Pangani: Mapendekezo ya Usimamizi Shirikishi”, iliyofanyika hoteli ya “Kilimanjaro Crane”<br />

, Moshi, Tanzania, tarehe 8 –10 Mei, 2002.<br />

• Mahojiano yasiyoandaliwa kikamilifu baina ya mwandishi na wadau wa Bonde la Mto<br />

Pangani. Waliohusika ni pamoja na watawala wa maji, watu wa misitu, jamii za wakulima,<br />

wahifadhi wa wanyamapori na watumiaji binafsi wa maji. Mahojiano yalifanyika Arusha, Moshi,<br />

Hale, Tanga na Dar es Salaam kati ya Novemba 12 na 22, 2002. Mahojiano, wahojiwa na<br />

ushirikishwaji wa taasisi zao vimetolewa kama sehemu ya rejea za waraka huu.<br />

Uchambuzi huu wa hali halisi umefanyiwa mapitio na idadi kubwa ya wadau wa Bonde la Mto Pangani.<br />

Wakati wa warsha iliyofanyika Moshi-Tanzania, kati ya tarehe 10 na 12 Machi, 2003, Uchambuzi wa<br />

Hali halisi uliwasilishwa kwa wadau kwa ajili ya mapitio na maoni. Mwezi Mei, 2003, maoni ya nyongeza<br />

yalipokelewa kutoka Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani na Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani (CDA<br />

Kenya). Marekebisho yaliyopendekezwa hatimaye yalizingatiwa na yamejumuishwa.<br />

7


A.6 Muundo wa Uchambuzi wa Hali halisi<br />

Uchambuzi huu wa hali halisi unaanza kwa maoni ya jumla ya rasilimali za bonde hili na matatizo<br />

yanayozikabili. Kisha unaangalia shughuli za rasilimali watu katika bonde, uchumi wao, matatizo na<br />

vikwazo vya upatikanaji wa rasilimali. Kisha uchambuzi unaendelea kuangalia matatizo na masuala<br />

ambayo wadau mbalimbali wanaona kuwa yapo katika bonde kama msingi wa kujadili muundo wa<br />

Usimamizi wa Maliasili za bonde. Katika sura nyingi, uchambuzi umefupisha dondoo muhimu ambazo<br />

msomaji anatakiwa kuzifahamu na kuzizingatia kadiri anavyoendelea na sehemu za uchambuzi<br />

zinazofuata. Mihutasari hii imewekwa pamoja katika hitimisho la kitabu hiki, ambapo majadiliano yatarudi<br />

kwenye madhumuni yake, na kuangalia jinsi matatizo yaliyotambuliwa, juhudi za usimamizi ambazo<br />

zimechukuliwa na mapendekezo ambayo yamefikiriwa kwenye kitabu hiki kwa pamoja yanaweza kuwa<br />

kichocheo na msingi wa uchukuaji wa hatua muafaka na ushirikiano wa WANI.<br />

8


B Maliasili za Bonde la Mto Pangani<br />

B.1 Utangulizi<br />

Utangulizi wa Uchambuzi huu wa Hali halisi umetoa mwanga kuhusu rasilimali anuwai zilizomo katika Bonde<br />

la Mto Pangani. Katika sura hii, tunaanza kwa kuangalia misitu iliyopo katika bonde, mchango wake na tishio<br />

la hifadhi ambalo linatoa changamoto kwa misitu hiyo. Mfumo kama huo huo utatumika kuangalia rasilimali za<br />

ziada katika bonde, zikiwemo maji na maeneo ardhioevu, maeneo yaliyohifadhiwa na bayoanuwai. Sura hii<br />

itahitimishwa kwa muhtasari wa dondoo muhimu. Sura hii kimsingi inahusika na rasilimali za maji na viumbe<br />

hai. Mashapo ya madini yaliyopo katika bonde hayakuzingatiwa sana kutokana na ukosefu wa data.<br />

B.2 Misitu ya Bonde<br />

Mgawanyo wa misitu, aina na hadhi yake kisheria nchini Tanzania iko kama ifuatavyo:<br />

Jedwali la 1: Aina, matumizi na hadhi ya kisheria ya misitu nchini Tanzania.<br />

Hekta 1,000 %<br />

Aina ya Msitu<br />

Misitu (mingine mbali ya misitu ya mikoko) 1,141 3.4<br />

Misitu ya Mikoko 115 0.3<br />

Misitu ya Mbao 32,299 96.3<br />

Jumla 33,555 100.0<br />

Matumizi ya Ardhi ya Misitu<br />

Eneo la misitu ya uzalishaji 23,810 71.0<br />

Eneo la misitu inayohifadhiwa (hasa maeneo ya vyanzo vya mito) 9,745 29.0<br />

Jumla 33,555 100.0<br />

Hadhi ya Kisheria<br />

Hifadhi ya Misitu 12,517 37.3<br />

Misitu/misitu ya mbao katika mbuga za taifa, n.k. 2,000 6.0<br />

Ardhi ya misitu isiyohifadhiwa 19,038 56.7<br />

Jumla 33,555 100.0<br />

(Rejea: Lambrechts et al., 2002).<br />

Misitu ya Bonde la Mto Pangani huwakilishwa na aina kuu tano: (a) Misitu ya milima ya Afrika (b) Misitu ya Mikoko<br />

(c) Misitu ya Mwambao (d) Misitu ya Miombo (e) Misitu ya kandokando ya mito. Misitu hii inaweza kuwa ya hifadhi,<br />

uzalishaji au misitu isiyokuwa na hadhi maalum. Misitu ya Pwani na ya milima ya Afrika, kutokana na upekee<br />

wake wa bayoanuwai, hupata nafasi ya kufikiriwa zaidi. Shughuli za kimataifa za bayoanuwai katika misitu hii pia<br />

zinasaidia upatikanaji zaidi wa data kuliko ilivyo kwenye aina nyingine za misitu. Hili linajionesha katika kitabu hiki.<br />

Sehemu kubwa ya uwezo wa Bonde la Mto Pangani katika upatikanaji wa maji inachangiwa na<br />

misitu yake. Kwa mfano kwenye Mlima Kilimanjaro, kiasi cha asilimia 96 ya maji yanayotiririka<br />

kutoka mlimani chanzo chake ni kwenye ukanda wa msitu pekee (Lambrechts et al., 1992), na<br />

Mlima Kilimanjaro unakadiriwa kutoa asilimia 60 ya maji yanayoingia Bwawa la Nyumba ya Mungu,<br />

na asilimia 55 ya maji yatiririkayo juu ya ardhi katika bonde (Rohr na Killingtveit, 2002).<br />

9


Kisanduku cha 2: Taarifa za Msingi za Misitu iliyomo katika Bonde la Mto Pangani<br />

Misitu ya Bonde la Mto Pangani ni muhimu kwa haidrolojia yake kwa sababu:<br />

• hurekebisha kasi ya maji, huzuia mmomonyoko wa udongo, huhifadhi maji na kuboresha<br />

ubora wa maji;<br />

• huchangia katika matengenezo na hifadhi ya mkusanyiko wa jeni;<br />

• hutoa mbao na madawa kwa matumizi ya jamii .<br />

Kuna aina kuu tano za misitu katika Bonde:<br />

• Misitu ya mikoko: Hutoa mchango mkubwa katika kuhifadhi ukanda wa pwani. Huhifadhi<br />

mashapo laini yaliyoko kando ya bahari kutokana na mmomonyoko, huzuia masimbi na<br />

hutumika kama virutubisho. Miti yenyewe na matope kuzunguka mizizi yake ni makazi<br />

muhimu kwa viumbe mbalimbali vya majini na maficho yao.<br />

• Misitu ya pwani ya Afrika Mashariki: Hii ni misitu ya kipekee iliyoko Afrika Mashariki na<br />

ina bayoanuwai na viumbe wengi. Iko katika uwanda wa pwani kati ya misitu ya mikoko na<br />

Milima ya Tao la Mashariki.<br />

• Misitu ya milima ya Afrika (Afromontane): Misitu ya Milima ya Tao la Mashariki ina kiwango<br />

cha juu cha bayoanuwai na viumbe wengi kama ilivyo katika misitu ya pwani. Katika Milima<br />

ya Kilimanjaro na Meru, misitu hii haionyeshi anuwai inayofanana, lakini inatoa mchango<br />

muhimu kihaidrolojia.<br />

• Misitu ya kandokando ya mito: hii huimarisha kingo za mito, na mto Pangani unapotiririka<br />

kupitia nyanda za chini zilizo kavu na kame, huwa maeneo ya kipekee ya miti na vichemchemi<br />

kwa matumizi ya binadamu na wanyama pori.<br />

• Msitu wa miombo: hii inajumuisha kundi kubwa la miti ya jamii ya mnondondo (Brachystegia,<br />

Isoberlinia na Julbernadia). Tofauti na misitu ya mvua, misitu ya miombo haisongamani sana kiasi<br />

cha kuzuia mwanga usifike ardhini. Matokeo yake ni kuwa, nyasi hufunika eneo kubwa la ardhi<br />

chini ya msitu, na wakati wa msimu wa mvua, nyasi hukua hadi kufikia kimo cha mita moja.<br />

Misitu ya vyanzo vya maji inafanya kazi tatu muhimu (Akitanda, 2002):<br />

• Misitu huchangia kwenye hifadhi ya maji kwa kurekebisha kasi ya maji, kuzuia mmomonyoko wa<br />

udongo, kuweka akiba ya maji na kuboresha ubora wa maji.<br />

• Huhifadhi mkusanyiko wa jeni: Misitu kama ile ya unyevunyevu ya kitropiki huonesha viwango<br />

vya juu sana vya bayoanuwai, na huchangia udumishaji wa mkusanyiko wa jeni wa dunia.<br />

• Misitu hutoa mazao kwa ajili ya matumizi ya jamii, kama vile mbao na mimea ya madawa.<br />

Misitu ya Mikoko<br />

Misitu ya mikoko hutoa mchango mkubwa katika kuhifadhi ukanda wa pwani. Huhifadhi mashapo laini<br />

yaliyoko kando ya bahari kutokana na mmomonyoko, huzuia masimbi na kutumika kama virutubisho.<br />

Miti yenyewe na matope kuzunguka mizizi yake ni makazi muhimu kwa viumbe mbalimbali wa majini<br />

na wale wajifichao. Wakati wa mawimbi makubwa, mamia ya aina za samaki huhamia katika misitu ya<br />

mikoko ili kujipatia chakula au mazalio. Samaki wengi na kamba hutegemea mikoko kama sehemu za<br />

kulelea vifaranga vyao. Miti ya mikoko ni migumu sana na hivyo inastahimili mchwa na kuvu. Inatumika<br />

kwa shughuli mbalimbali. Matawi ya Rhizophora, Ceriops na Bruguiera ni marefu na yamenyooka, kwa<br />

hiyo hutumika maalum kama miti ya kujengea ingawa hutumika pia kama nguzo, na katika utengenezaji<br />

wa mitego ya samaki na samani. Katika miaka ya karibuni, mikoko pia imetumika kutengeneza mkaa na pia<br />

10


hukusanywa kama kuni. Misitu ya mikoko iliyoko karibu na miji hutumika kwa wingi kwa madhumuni haya.<br />

Mikoko inaweza kupunguzwa matawi ili kuongeza ukuaji wake na upandikizaji upya pia ni rahisi. Hata hivyo<br />

hakuna shughuli yoyote kati ya hizi inayofanyika katika mwambao wa Tanzania (Richmond, 1997).<br />

Karibu mwambao wote wa pwani ya Tanzania umepambwa na misitu ya mikoko. Katika eneo la Bonde<br />

la Mto Pangani, inapatikana katika mkoa wa Tanga pekee, ambako karibu asilimia 11 ya mikoko ya<br />

Tanzania hupatikana. (Bwathondi na Mwamsojo, 1993) Hii ni pamoja na hekta 753 za misitu ya mikoko<br />

iliyosongamana kuzunguka mdomo wa mto Pangani (Kijazi, 2002).<br />

Misitu ya Pwani ya Afrika Mashariki<br />

Misitu ya pwani ya Afrika Mashariki iko katika uwanda wa pwani, kati ya Milima ya Tao la Mashariki na mikoko<br />

ya pwani. Misitu hii imetawanyika sana, na viunga vya misitu vimetenganishwa na maeneo ya mifumo ikolojia<br />

nusu kame. Imeenea kati ya mwinuko wa mita 500 na 1,000 juu ya usawa wa bahari. Tabia muhimu ya misitu<br />

ya pwani (ambayo ipo pia katika misitu ya Milima ya Tao la Mashariki) ni ile ya kuitegemea hali ya hewa<br />

ya Bahari ya Hindi na uthabiti wa kihistoria iliyoipatia. Kwa kuwa pekee katika uwanda wa pwani ya Afrika<br />

Mashariki, kujitenga kwa misitu hii kutoka mifumo mingine ya misitu ya Afrika kumesababisha viwango vya<br />

juu vya upatikanaji wa spishi (tazama hapa chini) (Burgess et al.,1996). Inasadikiwa kuwa kuna misitu 76 ya<br />

pwani nchini Tanzania (Burgess et al.,1996). Mingi ipo katika uwanda wa nyasi wa pwani kati ya mdomo wa<br />

mto Pangani hadi chini ya milima ya Usambara (tazama Baker na Baker, 2001).<br />

Misitu ya milima ya Afrika (Afromontane)<br />

Milima ya Tao la Mashariki inaambaa kutoka<br />

mpaka wa Tanzania na Zambia hadi milima<br />

ya Taita nchini Kenya. Inahusisha milima ya<br />

kale ya fuwele iliyopo Mashariki ya Tanzania<br />

na Kusini Mashariki ya Kenya ambako<br />

inakabiliana moja kwa moja ya hali ya<br />

hewa ya Bahari ya Hindi. Katika Bonde la<br />

Mto Pangani inahusisha milima ya Pare ya<br />

Kaskazini na Kusini, milima ya Usambara<br />

ya Mashariki na Magharibi na Milima ya<br />

Taita. Milima hii ni ya zamani sana, na<br />

kipindi cha karibuni zaidi cha uharibifu wa<br />

miamba iliyoiathiri kilitokea miaka milioni 7<br />

iliyopita. Kwa kulinganisha, lava ya zamani<br />

zaidi katika Mlima Kilimanjaro ina umri wa<br />

miaka milioni 1 tu. (Burgess et al., 1996).<br />

Ukaribu wa milima hii na bahari pia<br />

umefanya hali yake ya hewa kubaki kuwa<br />

thabiti kabisa. Wakati wa zama za mwisho<br />

za barafu, hali ya joto la uso wa bahari ya<br />

Hindi haikubadilika. Hivyo, ingawa zama<br />

Kisanduku cha 3: Milima ya Taita<br />

Milima ya Taita ni Milima pekee ya Tao la Mashariki katika<br />

Kenya. Milima hii na misitu yake inachukua spishi zaidi<br />

ya 2,000 za mimea yote (flora) na wanyama wote (fauna),<br />

ambapo aina 13 kati ya hizo zinapatikana kwa wingi.<br />

Mimea 67 ya asili inayojulikana, ikiwemo kahawa mwitu<br />

(Coffee fademi), husitawi milimani. Milima ya Taita ni Eneo<br />

Muhimu la Ndege (IBA), na ina spishi tatu zinazopatikana<br />

kwa wingi: Taita Apalis, Taita Thrush na Taita White – eye.<br />

Misitu ya milima hii pia ina utajiri wa amfibia (wanyama<br />

waishio majini na nchi kavu), wadudu na viumbe vingine.<br />

Ni kilomita za mraba 6 tu ndizo zinazobaki katika Milima<br />

ya Taita, zikiwa zimegawanyika katika viunga 13 vya<br />

misitu. Newmark (1998) anakadiria kuwa mabaki haya<br />

ya milima huwakilisha asilimia 2 tu ya mtandao wa misitu<br />

hii miaka 2,000 iliyopita. Milima ya Taita imepoteza misitu<br />

zaidi kuliko mlima wowote wa Tao la Mashariki.<br />

za barafu zinaweza kuwa zimebadili hali ya hewa katika sehemu nyingine za Afrika, haikufanya hivyo kwa<br />

milima ya Tao la Mashariki. Kwa hiyo milima hii imefaidi kipindi kirefu sana cha uthabiti wa mazingira, na pia<br />

imetengwa na misitu mingine na kwa hakika, kati ya msitu mmoja na mwingine (Burgess et al.,1996).<br />

Matokeo ya mabadiliko haya ni kuwa tabia za viumbe hai vya milima hii ni za namna mbalimbali na<br />

zinaainishwa na viwango vya juu vya upatikanaji kwa wingi au unaokaribia kuwa kwa wingi (tazama<br />

chini). Inawezekana kuwa kwa kiasi fulani kiwango cha chini cha spishi anuwai na upatikanaji wake<br />

katika Mlima Kilimanjaro ni matokeo ya uchanga wake.<br />

11


Msitu wa Mlima Kilimanjaro umegawanyika katika aina mbalimbali za uoto: kanda ya savana, eneo la kilimo<br />

na misitu lililo na watu wengi, ukanda wa misitu, ukanda wa mimea (alpine) mirefu kiasi na mirefu. Kwa<br />

mifumo ikolojia na bayoanuwai, ukanda wa misitu ni muhimu zaidi katika mlima huu, na una karibu nusu ya<br />

spishi zote za mimea ya milima huu (Lambrechts et al., 2002).<br />

Misitu ya kandokando ya mito (Riverine)<br />

Misitu ya kandokando ya mto kuzunguka sehemu ya Kinamasi ya Kirua inaweza kugawanywa katika<br />

makundi saba kama ifuatavyo (IVO-NORPLAN, 1997):<br />

• Uoto wa kando ya mto: huu ni pamoja na uoto unaokwenda hadi mita 50 kila upande wa kingo za mto.<br />

Kwa upande wa mashariki, spishi kuu ni Cyperaceae (mf. Cyperus alticulatus C. laevigatus) Gramineae<br />

(mf. Phragmites mauritianus, Echnochloa Colonum) na Typhaceae (eg. Typha domingensis). Pale<br />

ambapo kina cha ukingo wa mto ni kirefu Ficus Sur na Acacia Zanzibarica ndizo maarufu. Ukingo wa<br />

magharibi umetawaliwa na Ficus sur, Trichilia emetica, Elaeis guineense, jamii ya Mchenje/Msesewe<br />

(Albizia graberrima, Antidesma Venosum na A. Zanzibarica). Tabaka la vichaka vya kando ya mto<br />

linatawaliwa na spishi kama vile Sesbania Sesbans na Phyllanthus muellerianus.<br />

• Ardhi ya kinamasi cha Cyperus na Sesbania: katika maeneo ambayo maji hutuwama wakati wote, spishi<br />

kama Cyperus axaltatus na Typha domingensis ndizo zinazotawala. Katika maeneo yale ambayo hupata<br />

mafuriko kwa vipindi, Sesbania sesbands, Cyperus Laevigatus na Mkongoe (Acacia Xanthophloea) ndio<br />

aina za pekee za miti zinazohusishwa na aina hii ya uoto. Hii ni aina ya uoto iliyo maarufu sana kwenye<br />

eneo la kinamasi la Kirua, ingawa ni maarufu zaidi katika ukingo wa mashariki wa mto kuliko ukingo wa<br />

magharibi. Kwa upande wa mashariki, inaweza kutanda hadi kilomita 3 kutoka mtoni, wakati ambapo<br />

umbali mrefu zaidi ni kiasi cha mita 700 tu kutoka mtoni kwa upande wa magharibi wa mto.<br />

• Nyanda za nyasi za Sporobolus pyramidalis na Cynodon dactylon: Jamii ya Poaceae ndio<br />

inayotawala hapa, ikiambatana na miti michache iliyotawanyika na vichaka. Katika eneo la<br />

Kinamasi la Kirua, aina hii ya uoto inaenea katika eneo kubwa zaidi. Inaweza kutokea kama<br />

viunga au maeneo makubwa ya nyasi.<br />

• Misitu ya mbao ya Mkongoe (Acacia Xanthophloea): Aina hii ya uoto hutawaliwa na spishi ya<br />

Acacia, ambayo hufikia urefu wa hadi mita 18, na ikiwa na utando ulioziba eneo la kiasi cha<br />

asilimia 20 ya eneo la ardhi. Aina hii ya uoto ina thamani kubwa kijamii na kiuchumi kwa wakazi<br />

wa eneo hili oevu.<br />

• Jangwa lenye vifungu vya Suaeda monoica: Aina ya uoto inayojieleza, ambayo kwa kawaida<br />

hupatikana mbali kidogo na mto baada ya sehemu za uoto wa nyasi.<br />

• Eneo la vichaka vya mpoma wa Afrika (Commiphora africana): Mwendelezo wa ukanda wa<br />

eneo la vichaka linalotawaliwa na C. Africana ambao hupatikana chini ya Mwinuko wa Martin.<br />

Kwa kawaida, kila kichaka kina urefu pungufu ya mita 6, na utando wake unaziba zaidi ya<br />

asilimia 20 ya eneo la ardhi.<br />

• Ardhi ya kilimo: Mnamo mwaka 1997, kilimo katika eneo la Kinamasi cha Kirua kilikomea kuwa<br />

cha maeneo madogo, na kutawaliwa na mazao yanayohitaji maji mengi kama migomba na<br />

miwa, pamoja na mahindi.<br />

Misitu ya miombo<br />

Misitu ya Miombo imeenea katika eneo la asilimia 50 ya Tanzania na ni uoto wa aina moja ulio mkubwa<br />

zaidi katika Afrika ya Mashariki. Misitu ya miombo ya Afrika Mashariki ni mfumo uliodhoofishwa wa spishi<br />

ya miombo iliyoenea sana katika Afrika ya Kati (Rogers, 1997).Inaweza kuelezewa kama ifuatavyo; ‘miti<br />

inayopukutisha majani isiyokuwa na miiba (yenye spishi chache zenye miiba) inayojitokeza katika maeneo<br />

ya mvua za msimu mmoja katika ardhi chakavu kijiolojia, yenye asidi, na ya mchanga. Inajulikana kwa miti<br />

ya jamii ndogo ya Caesalpinoideae, hususan spishi za jamii ya myombo (Brachystegia na Julbernadia).<br />

12


Tabaka la vichaka linatofautiana kwa unene, asilimia ya ueneaji na spishi zilizomo. Mara nyingi hutawaliwa<br />

na Mgoto/Mtobwe (Diplorhynchus na Combretum spp). Utando wa ardhi hutofautiana kutoka kwenye nyasi<br />

nyingi hadi kwenye vichaka haba na nyasi ndogo ndogo. Muundo na spishi zilizomo kwa kiwango kikubwa<br />

unadumishwa na mioto ya vipindi vya msimu (Rogers, 1996:301). Kiasi cha kilomita za mraba millioni 3 za<br />

Afrika zimefunikwa na misitu ya miombo. Katika Bonde la Mto Pangani imeenea zaidi katika maeneo ya<br />

mwambao, pande zote mbili za Kaskazini na Kusini mwa mdomo wa Mto Pangani.<br />

Tishio na Hadhi ya Hifadhi<br />

Kwenye Mlima Kilimanjaro, misitu inaendelea kutishiwa kuingiliwa zaidi na zaidi kutokana na uvamizi wa kilimo,<br />

ambacho kinatokana na ongezeko la idadi ya watu. Vitisho vingine vya ziada ni ukataji wa miti kwa ajili ya mbao,<br />

uanzishwaji wa mashamba ya miti ya mbao laini, moto, uvunaji haramu uliokithiri wa miti ya mbao, ujangili<br />

na urinaji haramu wa asali (Yanda na Shishira, 2001). Katika sehemu zote isipokuwa katika mitelemko ya<br />

Kaskazini, ukataji haramu wa magogo hufanyika kwa wingi katika maeneo ya msitu yaliyo chini ya mita 2,500,<br />

ilikoenea zaidi miti ya kafuri, seda na miti mingine ya asili (Lambrechts et al., 2002). Tishio la ziada ni pamoja<br />

na uanzishaji wa ‘vijiji vya misituni’ (ambako viko 18 kwenye eneo la hekta 215) ndani ya hifadhi ya msitu.<br />

Mashamba pia yanazidi kuwa ya kawaida katika hifadhi. Mwezi Agosti, mwaka 2001, kulikuwa na matanuru 125<br />

ya mkaa yaliyoonekana katika mitelemko ya Kusini Mashariki ya mlima (Lambrechts et al., 2002). Uchungaji wa<br />

mifugo hufanyika kufikia kilomita 8 ndani ya msitu, na katika mwezi Agosti, mwaka 2001 wanyama wafugwao<br />

814 walihesabiwa, wengi wao wakiwa kwenye mitelemko ya Kaskazini ya mlima (Lambrechts et al., 2002).<br />

Kati ya mwaka 1952 na 1982, eneo la misitu ya asili ya Kilimanjaro ilipungua kwa kilomita za mraba 41. Maeneo<br />

ambapo awali misitu ya asili ilikuwepo sasa nafasi yake imechukuliwa na kilimo au uoto ulioharibiwa. Kingo za misitu<br />

ya hifadhi ndizo zilizoharibiwa vibaya zaidi, (Yanda na Shishira, 2001) hususan kwenye sehemu zijulikanazo kama<br />

‘ukanda wa nusu maili’. Mnamo mwaka 1941, serikali ya kikoloni ilitenga eneo la hifadhi ya msitu wa Kilimanjaro<br />

kama eneo la msitu wa kilimo. Ukanda huu umeenea kati ya Mito Kikuletwa na Sanya, na mwendo wa nusu maili<br />

kwenda juu ya mlima kutoka kwenye ukingo wa hifadhi. Huu ‘ukanda wa nusu maili’ ulikusudiwa kupandwa miti<br />

ikuayo haraka kwa ajili ya matumizi ya jamii za Wachaga waishio chini ya hifadhi, ambako uhaba wa ardhi ulizuia<br />

upandaji wa miti (Baldwin, 1946). Leo, kadiri ya asilimia 66 ya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mashamba ya<br />

misitu yamekuwa ya kilimo au yamesafishwa, (Lambrechts et al., 2002).<br />

Jedwali la 2: Upotevu wa utando wa msitu wa Milima ya Tao la<br />

Mashariki katika Bonde la Mto Pangani<br />

Msitu Msitu wa asili Idadi ya Viunga Msitu Upotevu wa tando<br />

(km 2 ) vya misitu uliofungwa wa asili wa<br />

(km 2 ) msitu (%)<br />

Pare ya Kaskasini 151 2 28 50<br />

Pare ya Kusini 333 5 120 73<br />

Usambara Magharibi 328 17 245 84<br />

Usambara Mashariki 413 8 221 57<br />

Taita 6 13 4 98<br />

Rejea: Newmark, 1998:4)<br />

Katika Bonde la Mto Pangani, Milima ya Tao la Mashariki ipo kwenye maeneo yenye msongamano mkubwa wa<br />

watu. Katika Milima ya Usambara Magharibi kwa mfano, idadi ya watu imeongezeka kwa mara 23 tangu 1900<br />

(Newmark, 1998). Katika mazingira ya kijamii yenye sifa ya umaskini, umuhimu wa ardhi ya kilimo hauwiani kwa<br />

kiasi kikubwa. Shinikizo linalowakilishwa na tatizo hili kwenye hifadhi zilizobaki za misitu katika bonde linatisha.<br />

Ikidhaniwa kuwa Milima ya Tao la Mashariki, kihistoria ilikuwa karibu muda wote imejaa misitu, asilimia yake 77<br />

itakuwa imepotea kutokana na shughuli za binadamu na/au moto katika miaka 2,000 iliyopita (Newmark, 1998).<br />

Tatizo la ziada ni kuwa mingi ya michakato hii imesababisha kutokea kwa viunga vya misitu, na spishi za wanyama<br />

13


mara nyingi haziko tayari kuvuka nafasi wazi kati ya viunga vya misitu. Hii ina maana kuwa katika viunga kimoja<br />

kimoja, mkusanyiko wa jeni hupungua na uhai wa spishi huhatarishwa kutokana na kuzaliana wenyewe kwa<br />

wenyewe. Katika Bonde la Mto Pangani upotevu huu ni kama inavyoonyeshwa katika jedwali la 2.<br />

Hadhi ya msitu kuwa “msitu wa hifadhi” inaonekana kushindwa kupunguza viwango vya ukataji miti. Katika Hifadhi<br />

ya Msitu ya Nilo (hekta 5872.1), katika Milima ya Usambara, kuna hekta 33.8 za ‘kilimo chini ya msitu’, hekta 372.3<br />

za kilimo cha ‘wakulima wadogo wadogo’, hekta 37.2 za ardhi tupu na hekta 1.9 za makazi ya binadamu (Cordeiro,<br />

1998). Misitu ya Pwani ya Tongwe-Muheza ilikuwa na eneo la hekta 1,202, lakini ni hekta 300 tu za msitu zilizobaki,<br />

wakati ambapo Hifadhi ya Msitu wa Gombero imefyekwa kabisa kwa ajili ya kilimo (Baker na Baker, 2002).<br />

Kwenye Mlima Meru, matatizo yanayoikabili misitu yanafanana na yale yanayoutishia Mlima Kilimanjaro,<br />

nayo ni kama yafuatavyo (Bwoyo, mhojiwa):<br />

• Ukataji haramu wa miti – Misitu ya milimani huvunwa miti inayovutia kibiashara ya mireteni<br />

(Juniper) na Mshio (Olea Capensis).<br />

• Malisho – Wakati wa msimu wa kiangazi, jamii za jirani hulisha mifugo yao ndani ya msitu.<br />

• Uhaba wa ardhi – upande wa Mashariki wa mlima, uvamizi wa ardhi ni tatizo kubwa<br />

linaloongezeka.<br />

• Kutokuungwa mkono - katika baadhi ya vijiji, mradi wa msitu wa maeneo ya vyanzo vya maji<br />

(CFP – utakaoelezwa chini) huungwa mkono kwa kiwango kidogo na viongozi wa vijiji, ambao<br />

baadhi yao wanahusika binafsi na uvunaji wa msitu.<br />

• Moto – hili lilikuwa tatizo kubwa kati ya miaka ya 1998 na 1999.<br />

Kisanduku cha 4: Tishio kwa Misitu ya Bonde la Mto Pangani<br />

• Mahitaji ya ardhi: kadri msongamano wa watu unavyoongezeka na uchumi unavyobaki kuwa duni,<br />

mahitaji ya ardhi ya kilimo huongezeka, na hivyo, misitu hukatwa kutoa nafasi ya kilimo.<br />

• Mahitaji ya mbao: misitu mingi iliyobaki katika PRB ina spishi za mbao zenye thamani ya kiuchumi,<br />

ambayo, jinsi inavyoadimika, ndivyo inavyopata bei kubwa. Miti pia hukatwa kwa ajili ya kuni na<br />

utengenezaji wa mkaa.<br />

• Mahitaji ya malisho: idadi ya mifugo katika bonde inaonekana kuongezeka. Jinsi ardhi ya kilimo<br />

inavyoongezeka, ardhi ya malisho hupungua, na wafugaji hupanda milima kutafuta malisho.<br />

• Makazi ya msituni: kadri watu wanavyojitahidi kutafuta kuongeza ardhi ya kilimo na malisho, hivyo<br />

pia hufanya makazi ndani ya mipaka ya misitu.<br />

• Udhaifu wa Sheria: licha ya hadhi ya uhifadhi wa misitu mingi ya bonde, mamlaka haziwezi kutekeleza<br />

sheria zinazotakikana kwa sababu ya uchache wa wafanyakazi, mishahara duni na rushwa. Kwa<br />

nyongeza, Idara ya Misitu na Nyuki na Mradi wa Misitu ya vyanzo vya maji inapatiwa fedha karibu<br />

zote na wahisani pekee, hali inayoibua maswali kuhusu uendelevu wake. Mwisho, ushirikishwaji wa<br />

jamii katika usimamizi wa misitu ya bonde ni dhana ngeni na kwa sasa haijawa na ufanisi mkubwa.<br />

• Uendelezaji wa misitu: uendelezaji wa misitu ya mashamba badala ya misitu ya asili huongeza<br />

matatizo ya uhifadhi.<br />

• Kugawanyika kwa misitu: Jinsi shinikizo linavyozidi kwenye misitu ya bonde mara nyingi hugawanyika<br />

vipande vipande. Spishi nyingi za msituni haziwezi kuvuka nafasi wazi kati ya msitu, na hivyo<br />

kusababisha matatizo ya uhifadhi wa bayoanuwai.<br />

• Moto: Kwa kawaida huanzishwa na binadamu ama makusudi (ili kuharibu misitu inayodhaniwa<br />

kuhifadhiwa isivyostahili na iliyozuiliwa) au kwa kawaida zaidi, ajali (kwa mfano, kutokana na ajali<br />

wakati wa kuchoma mkaa au kurina asali kutoka kwenye mizinga).<br />

14


• Fedha – CFP haipati fedha zozote kwa ajili ya kuendeshea shughuli zake kutoka serikalini.<br />

Bwoyo (mhojiwa) anadai kuwa kwa sababu ya mchango muhimu wa misitu katika Bonde la Mto<br />

Pangani, kiasi cha fedha lazima kitengwe kwa ajili ya CFP kutoka kwa makampuni yazalishayo<br />

umeme wa maji au Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (angalia pia Evans, 1997).<br />

B.3 Maji na ardhioevu<br />

Mto Pangani unaundwa na matawi ya mito mikubwa miwili: Mto Ruvu, ambao hutokea kwenye miteremko<br />

ya Mashariki ya Mlima Kilimanjaro; na Kikuletwa, ambao hutokea kwenye Mlima Meru na mitelemko ya<br />

Kusini ya Mlima Kilimanjaro. Mito ya Ruvu na Kikuletwa huungana katika Bwawa la Nyumba ya Mungu,<br />

lenye eneo la kadiri ya kilomita za mraba 140 (Rohr na Killingtveit, 2002). Maji yanayoingia katika bwawa<br />

yanakaribia kuwa mita za ujazo 43.37 kwa sekunde (TANESCO, 1994). Mto unapotoka kwenye bwawa,<br />

huitwa Mto Pangani, na hutiririka kwa kilomita 432 kabla ya kuingia katika Bahari ya Hindi, ambako<br />

humwaga maji ya kiasi cha kilomita za ujazo 0.85 kwa mwaka (Vanden Bossche na Beracsek, 1990).<br />

Ndani ya Bonde la Mto Pangani, Mlima Kilimanjaro ndio sehemu yenye umuhimu wa pekee<br />

kihaidrolojia(Lambrechts et al., 2002). Kama ilivyoelezwa awali, mvua kwenye mlima huu zinakadiriwa<br />

kutoa asilimia 60 ya maji yanayoingia katika Bwawa la Nyumba ya Mungu, na asilimia 55 ya maji ya juu<br />

ya ardhi katika Bonde (Rohr na Killingtveit, 2002). Pia, cha muhimu – ingawa kiasi hakijulikani, ni maji<br />

yatokanayo na kuyeyuka kwa barafu kutoka milimani. Barafu inayoyeyuka kutoka mlimani huipa nguvu<br />

chemchemi kuu katika hifadhi maarufu ya Taifa ya Amboseli nchini Kenya. Myeyuko pia huzipa nguvu<br />

chemchemi ambazo mradi wa Ugavi wa Maji wa Nol Turesh ya Kenya hutegemea, unasambaza maji<br />

kwenye miji kadhaa mashuhuri ya Kenya, ikiwa ni pamoja na Machakos na Kajiado.<br />

Maji katika Bonde la Mto Pangani kwa kiasi kikubwa hutokana na mvua, ambayo mgawanyo wake hauko<br />

sawa ndani ya bonde. Kwa wastani, bonde hili hupata mita za ujazo 34, 773.4 kwa mwaka na kiasi cha<br />

wastani cha upoteaji maji kwa uchavushaji ni milimita 1,410 kwa mwaka. Kwa kuzingatia tofauti za mvua,<br />

bonde hili, linaweza kugawanywa katika mifumo miwili ya kihaidrolojia.<br />

Maeneo ya nyanda za juu yanachukuliwa kuwa ni yale yaliyoko mita 900 juu ya usawa wa bahari, kama vile<br />

mitelemko ya Milima Meru na Kilimanjaro, pamoja na maeneo ya Milima ya Usambara na Pare, ambayo<br />

hupata mvua kati ya milimita 1,200 na 2,000 kwa mwaka. Misimu ya mvua huwa miwili katika maeneo haya,<br />

nyingi ikiwa kati ya miezi ya Machi na Mei na kidogo kati ya miezi ya Oktoba na Novemba. Mvua katika<br />

kipindi cha kwanza inaweza kuzidi milimita 600 kwa mwezi, na milimita 300 katika kipindi kinachofuata.<br />

Kisanduku 5: Taarifa za Msingi za Maji na Ardhioevu<br />

katika Bonde la Mto Pangani<br />

• Maeneo ya nyanda za juu ya Bonde la Mto Pangani hupata mvua nyingi kuliko nyanda za chini.<br />

Hivyo kilimo kinafanyika zaidi kwenye nyanda za juu wakati nyanda za chini zinafaa kwa ufugaji.<br />

• Sehemu kubwa ya maji ya Mto Pangani hutokana na mvua na myeyuko wa barafu.<br />

• Kiasi kikubwa cha maji yanayoingia kwenye Bwawa la Nyumba ya Mungu yanatoka Mlima<br />

Kilimanjaro. Yaliyobaki yote yanatoka Mlima Meru na Milima ya Pare Kaskazini.<br />

• Matumizi makuu ya maji katika Bonde hili ni umwagiliaji mashamba. Uzalishaji umeme na uvuvi<br />

ni matumizi ya muhimu ya ziada, kama yalivyo mahitaji ya mijini na viwandani.<br />

• Bonde la mto Pangani lina rasilimali kubwa ya maeneo ardhioevu, ikiwa ni pamoja na ziwa Jipe<br />

na Chala, na Bwawa la Nyumba ya Mungu. Yote haya husaidia uvuvi. Bonde hili lina rasilimali<br />

nyingi za kinamasi, ingawa mchango wake kihaidrolojia na bayoanuwai haujulikani sana.<br />

15


Juu ya bwawa la Nyumba ya Mungu, kwa<br />

ujumla mvua imepungua tangu uwekaji<br />

wa kumbukumbu ulipoanza mwanzoni<br />

mwa miaka ya 1930. Mfumo wa sasa<br />

wa mvua kwa kawaida hutofautiana kwa<br />

asilimia 10 kutoka wastani. (Mkhandi na<br />

Ngana, 2001).<br />

Maeneo yaliyo chini ya mita 900 hupata<br />

mvua kidogo zaidi katika Bonde hili,<br />

ikipungua kufikia milimita 500 kwa mwaka<br />

(Mkhandi na Ngana, 2001). Kwa hakika<br />

asilimia 50 ya Bonde la Mto Pangani<br />

inachukuliwa kuwa kame au nusu kame<br />

(Rohr na Killingtveit, 2002).<br />

Vyanzo vya ziada vya maji katika<br />

bonde hili ni chemchemi. Baadhi ya<br />

chemchemi zilizo kubwa katika bonde<br />

hili huchangia kadri ya mita za ujazo 20<br />

kwa sekunde za maji yaingiayo bwawa<br />

la Nyumba ya Mungu, kiasi ambacho<br />

kinakuwa muhimu sana wakati wa<br />

kiangazi ambapo mchango wa mvua<br />

hupungua (Rohr et al., 2002). Sehemu<br />

kubwa ya chemchemi zinazozalisha maji<br />

katika Bonde imejikusanya zaidi katika<br />

maeneo matatu ya mkoa wa Kilimanjaro:<br />

Kambi ya Choka, Rundugai na Chemka<br />

Kisanduku 6: Tishio kwa rasilimali za maji na<br />

ardhioevu ya Bonde la Mto Pangani<br />

• Ifikapo mwaka 2015, mahitaji ya maji katika Bonde<br />

hili yanatarajiwa kuwa mara mbili, wakati huo huo<br />

kuna ushahidi uhaba wa maji umekuwepo tangu<br />

miaka ya 1940.<br />

• Maeneo muhimu ya matatizo ni ongezeko la mahitaji<br />

ya umwagiliaji na mijini. Katika umwagiliaji, upotevu<br />

wa maji unaweza kufikia kiasi cha asilimia 85.<br />

• Kadri idadi ya watumiaji maji inavyoongezeka,<br />

pamoja na ushindani baina yao, kuna uwezekano<br />

wa migogoro baina ya watumiaji maji kuongezeka.<br />

• Uvuvi katika Bwawa la Nyumba ya Mungu<br />

unasemekana kuwa katika matatizo makubwa<br />

kutokana na uvuvi uliokithiri.<br />

• Sehemu kubwa ya eneo ardhioevu kubwa zaidi katika<br />

Bonde hili - Kinamasi cha Kirua – imekauka kutokana<br />

na utaratibu wa mtiririko wa maji yanayotoka kwenye<br />

Bwawa la Nyumba ya Mungu kudhibitiwa.<br />

• Kiasi kikubwa cha virutubisho vinavyoingia kwenye<br />

Ziwa Jipe vimestawisha kwa wingi mafunjo na Typha<br />

ambazo zinatishia kulifunika ziwa.<br />

(Rohr et al., 2002). Chanzo cha maji ya chemchemi iliyotajwa mwisho haijulikani na kiwango cha maji<br />

kitokacho hubaki kuwa sawa kwa mwaka mzima. Mfumo wa mvua kwenye Mlima Kilimanjaro, ambao<br />

uko upande wa Kaskazini wa chemchemi, unaonekana kutokuwa na athari yoyote kwenye utoaji wa<br />

maji wa chemchemi hiyo (Rohr et al. 2002). Nchini Kenya, Mto Lumi hukusanya maji kutoka mitelemko<br />

ya Kusini ya Mlima Kilimanjaro na ndio chanzo kikuu cha maji ya Ziwa Jipe. Karibu maji yote ya mto<br />

yanayoingia kwenye ziwa hili yanatoka kwenye chemchemi (Musyoki, 2003).<br />

Kiasi cha asilimia 5 ya maji yote yanayotumika katika Bonde la Mto Pangani yanatoka katika vyanzo vya<br />

chini ya ardhi. Visima virefu vitoavyo zaidi ya mita za ujazo 100 kwa saa vimechimbwa kwenye ukanda<br />

wa Kahe wakati visima vinavyotoa kati ya mita za ujazo10–50 kwa saa vimechimbwa katika ukanda<br />

wa Sanya na Miamba ya Karoo ya Tanga. Uongezekaji wa maji ya chini ya ardhi kwa kiasi kikubwa<br />

unatokana na mvua na mito (Makule n.d.).<br />

Mto Pangani unapotoka kwenye Bwawa la Nyumba ya Mungu, hukabiliwa na mahitaji yafuatayo<br />

(Mujwahuzi 2001):<br />

Kiasi cha chini kwa kuzalisha umeme.................................mita za ujazo 24 kwa sekunde<br />

(Firm Power Production)<br />

Umwagiliaji..........................................................................mita za ujazo 7 kwa sekunde<br />

Matumizi ya nyumbani .......................................................mita za ujazo 1-2 kwa sekunde<br />

Jumla..................................................................................mita za ujazo 32-33 kwa sekunde<br />

16


Hata hivyo, Sarmett (Mhojiwa) anaeleza kuwa, ni mara chache sana Nyumba ya Mungu huwa na uwezo<br />

wa kutoa mita za ujazo 22 kwa sekunde.<br />

Bwawa la Nyumba ya Mungu ndiyo hifadhi kubwa zaidi ya maji katika bonde hili. Nyingine tatu zilizopo<br />

ni: ziwa Ambusseli, na maziwa Chala na Jipe yaliyoko mpakani mwa Tanzania na Kenya. Maziwa haya<br />

huonekana mara nyingi kwenye mipango ya umwagiliaji na ya kihaidrolojia ya wilaya ya Taita -Taveta ya<br />

Kenya. Usawa wa maji ya Ziwa Jipe na eneo lake hubadilika kwa kiwango kikubwa kutokana na kiasi<br />

cha mvua. Hivyo, eneo lake hutofautiana kutoka kilomita za mraba 28 (1947) hadi kilomita za mraba 18<br />

(1954), wakati kiasi cha maji yaliyomo hutofautiana kutoka mita za ujazo milioni 20 hadi 60, (Musyoki<br />

na Mwandotto, 1999). Ndani ya Kenya sehemu ambayo ni chanzo cha maji ya Ziwa Jipe kuna sehemu<br />

ya Mbuga ya Taifa ya Tsavo Magharibi, kilomita za mraba 48.5 za kinamasi, kilomita za mraba 435<br />

za mashamba ya mkonge na kilomita za mraba 196.5 za kile kinachoelezwa kuwa ni ‘ardhi ya umma’<br />

iliyotengwa kwa ajili ya Mpango wa Makazi wa Ziwa Jipe (Musyoki na Mwandotto 1999). Kiasi cha<br />

mchangatope unaokadiriwa kufikia tani 300,000 huingia kwenye ziwa kwa mwaka (Musyoki, 2003).<br />

Ziwa Chala liko kwenye kreta ndogo ya volkano ya miteremko ya kusini ya Mlima Kilimanjaro. Lina<br />

kina cha kati ya mita 85 na 90 na lina eneo la kiasi cha kilomita za mraba 3.15. Lina kiasi cha maji ya<br />

kati ya mita za ujazo milioni 300-350 (Musyoki na Mwandotto 1999). Kwa ubora, maji yake ni mzuri<br />

sana, na kwa sababu hii yanaonekana kuwa ndiyo chanzo cha ukuaji wa maeneo ya miji ya pwani ya<br />

Kenya. Viwango vya matumizi ya maji kwa siku zijazo vinatazamiwa kufikia mita za ujazo 7 kwa mwaka<br />

(Musyoki, 2003). Hali yake ya mwinuko inamaanisha kuwa maji yanaweza kusafirishwa kwa nguvu ya<br />

mteremko hadi yanakotakiwa.<br />

Bonde la Mto Pangani linadhaniwa kuwa na hekta 90,000 za kinamasi, sehemu yake kubwa ikiwa ni<br />

Kinamasi ya Kirua iliyopo Kusini mwa Bwawa la Nyumba ya Mungu. Vinamasi hivi tayari vimekwisha<br />

athirika kwa kiasi kikubwa kutokana na udhibiti wa mtiririko wa maji ya mto kutoka bwawani, na maeneo<br />

makubwa ya kinamasi yamekauka. Hata hivyo, bado yanadhaniwa kuhifadhi kiasi kikubwa cha maji<br />

ya Mto Pangani. Laiti kama Mto ungeelekezwa njia na mfereji kuchimbwa kupitia kwenye kinamasi,<br />

ongezeko la mita za ujazo milioni 42.4 zingeyafikia mabwawa yaliyoko upande wa chini ya mto kwa<br />

mwaka (IVO - NORPLAN,1997). Uoto wa ardhi hizi za kinamasi umeelezewa juu kuwa ni mifano ya<br />

misitu ya kandokando ya mito.<br />

Ardhi nyingine ya Kinamasi ni Ruvu (karibu kilomita za mraba 35) ambayo iko mahali Mto Ruvu<br />

unapotoka kwenye Ziwa Jipe, na kinamasi iliyopo mahali mito ya Ruvu na Kikuletwa inapokutana na<br />

kuingia Nyumba ya Mungu. Eneo la kinamasi lililotajwa mwisho linasemekana kuwa na kilomita za<br />

mraba 40 (Baker na Baker 2001).<br />

Tishio na hadhi ya Hifadhi<br />

Katika sehemu ya Bonde iliyoko Tanzania, makisio na matarajio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na<br />

2015 yanaonyeshwa kwenye Jedwali la 3.<br />

Katika Wilaya ya Taita – Taveta iliyoko katika sehemu ya bonde upande wa Kenya, mahitaji ya maji<br />

yanakadiriwa kufikia mita za ujazo 5,625 kwa siku. Hadi kufikia mwaka 2005 mahitaji yanatazamiwa<br />

kuongezeka kufikia mita za ujazo 8,844 kwa siku, na kufikia mita za ujazo 12,521 kwa siku ifikapo<br />

mwaka 2015 (Mpango wa Maji wa Wilaya ya Taita – Taveta wa mwaka 1995, kama inavyonekana katika<br />

Musyoki, 2003). Kutokana na mahitaji ya maji kukadiriwa kuwa mara mbili itakapofika mwaka 2015,<br />

shinikizo kwa rasilimali za maji katika bonde linafikiriwa kuwa kubwa mno. Tayari bonde linachukuliwa<br />

kuwa lina matumizi makubwa ya maji, na kwa kukosekana msisitizo wowote mkubwa wa udhibiti hadi<br />

sasa, inaonekana hakuna uwezekano wa tishio hili kupungua.<br />

17


Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji mwaka 1995 na<br />

matarajio ya mahitaji ya maji mwaka 2015<br />

Mahitaji ya maji m 3 /siku<br />

Matumizi 1995 2015<br />

Mijini 71,200 163,600<br />

Vijijini 52,000 83,500<br />

Mifugo 30,500 36,400<br />

Mkonge 1,300 1,300<br />

Jumla 155,000 284700<br />

(Rejea: IVO- NORPLAN, 1997)<br />

Upo ushahidi wa kutosha wa matatizo ya maji. Mujwahuzi (2001) anabainisha kuwa katika kituo 1DC1<br />

cha Mto Ruvu, wastani wa mtiririko wa maji kwa mwezi umepungua kutoka mita za ujazo 14.2 kwa<br />

sekunde kati ya mwaka 1958 – 65 hadi mita za ujazo 11.45 kwa sekunde kati ya mwaka 1987-97. Vijito<br />

vingi katika nyanda za juu za bonde havitiririshi maji wakati wa msimu wa kiangazi (mwezi Septemba<br />

hadi Februari) kwa sababu ya wingi wa shughuli za umwagiliaji. Baada ya maji kuchukuliwa kwa ajili<br />

ya umwagiliaji, Mto Rau hukauka kabisa (Mujwahuzi 2001). Mahitaji ya maji kutoka kwenye mito ya<br />

Kikafu na Weruweru huwa ni kati ya asilimia 90 –125, ambayo ni makubwa zaidi ya kiasi cha maji<br />

kinachopatikana kwa uhakika mtoni cha asilimia 80. (Mwamfupe, 2002). Maji yanayotoka katika Bwawa<br />

la Nyumba ya Mungu, huchepushwa kwa matumizi mbalimbali kabla ya kufika kwenye maporomoko<br />

ya Pangani. Mara nyingi na hususan wakati wa kiangazi, maji yanayofika hayatoshelezi kuendesha<br />

mitambo ya kituo cha umeme wa maji iliyopo hapo (Lugeiyamu, Mhojiwa). Ushahidi wenye nguvu sana<br />

wa tatizo la maji unaweza kuwa ni ongezeko la idadi ya migogoro inayohusiana na maji katika bonde hili.<br />

Migogoro hii inaangaliwa kikamilifu hapa chini.<br />

Kati ya mwaka 1992 na 1989, eneo la kilele cha barafu cha Mlima Kilimanjaro lilipungua kwa asilimia 75<br />

kutoka kilomita za mraba 12.5 hadi kilomita za mraba 2.6. Kati ya mwaka 1989 hadi 2000 karibu robo<br />

ya barafu iliyosalia ilitoweka. Kuhusu sababu ya badiliko hili la ghafla na haraka, lawama zinaelekezwa<br />

katika shughuli za binadamu, ingawa hili kwa vyovyote haliko dhahiri (Hastenrath na Greischar, 1997).<br />

Kama upunguaji huu utaendelea Bonde la Mto Pangani hivi karibuni litakoma kupata maji yatokanayo<br />

na kuyeyuka kwa barafu.<br />

Ukuaji wa magugu aina ya Typha kwenye Ziwa Jipe unasemekana kutodhibitiwa vya kutosha kiasi<br />

kwamba magugu haya yamekaribia kufunika ziwa. Mwelekeo huu ni dhahiri umetokana na virutubisho<br />

na mchangatope unaochukuliwa na maji kutoka kwenye Mlima Kilimanjaro na Milima ya Pare Kaskazini.<br />

Mchangatope umepunguza kina cha Ziwa na kusababisha kupanda kidogo kwa usawa wa maji. Uingiaji<br />

wa virutubisho kwenye ziwa unadhaniwa kusababisha ongezeko la alikali na/au magadi na kusababisha<br />

mayungiyungi kutoweka. Uingiaji wa mchangatope pia huathiri bwawa la Nyumba ya Mungu, lakini hili si<br />

tatizo kwa sasa kutokana na bwawa kuwa na eneo kubwa la kuhifadhi maji.<br />

Kama ilivyojadiliwa awali, udhibiti wa Mto Pangani umepunguza mafuriko katika kinamasi ya Kirua, na hivyo<br />

maeneo makubwa ya kinamasi kukauka. Kwa kiasi cha utoaji wa maji cha mita za ujazo 25 kwa sekunde kutoka<br />

NYM, kinamasi kinafurika, lakini wakulima waliovamia ardhi hii hulalamika vikali (Ngula, Mhojiwa). Bwawa la<br />

Nyumba ya Mungu husaidia uvuvi ambao hufanyika kwa kiwango kikubwa, kama itakavyojadiliwa zaidi chini.<br />

18


B.4 Maeneo Yaliyohifadhiwa<br />

Katika Tanzania, Bonde la Mto Pangani lina hifadhi moja ya akiba ya wanyamapori (Mkomazi – kilomita<br />

za mraba 3,276), wakati sehemu za Hifadhi za Taifa za Kilimanjaro (kilomita za mraba 756) na Arusha<br />

(kilomita za mraba 137) pia zipo katika bonde hili. Sehemu ya Mbuga ya Hifadhi ya Taifa ya Tsavo<br />

Magharibi nchini Kenya (kilomita za mraba 9,065) pia inaangukia katika bonde hili, na inapakana na<br />

hifadhi ya akiba ya Wanyamapori ya Mkomazi. Sehemu ya Hifadhi ya Taifa ya Sadani iko katika bonde hili,<br />

lakini haitajadiliwa hapa. Kihoja, hifadhi za misitu pia ni maeneo yaliyohifadhiwa, lakini haya hayajadiliwi<br />

hapa (angalia juu). Zote hizi zina mchango wenye thamani kwa uchumi wa Tanzania kwa kuvutia watalii.<br />

Kilimanjaro pekee hupokea wageni wapatao 67,000 kwa mwaka (WCMC, 1987).<br />

Mlima Kilimanjaro ni mlima mrefu zaidi uliosimama wenyewe duniani na mrefu zaidi kuliko yote katika<br />

Afrika. Una mwinuko wa mita 5,000 juu ya uwanda wazi wenye milima na mabonde wa wastani wa<br />

mita 800 juu ya usawa wa bahari (Lambrechts et al., 2002). Mbuga hii ni eneo lililohifadhiwa zamani<br />

zaidi katika Afrika, likiwa limepata hadhi hii mwanzoni mwa karne ya 20. Mnamo mwaka 1921 mbuga hii<br />

ilitangazwa kuwa hifadhi ya msitu, na kisha, katika mwaka 1973, eneo lililo juu ya mita 2,700 za kontua,<br />

lilipewa hadhi ya Hifadhi ya Taifa. Kwa sasa, mbuga hii ina eneo la hekta 75,353 na imezungukwa na<br />

hekta 107,828 za hifadhi ya misitu (Lambrechts et al,2002). Mnamo mwaka 1987 Mbuga ya Hifadhi<br />

ya Taifa ya Kilimanjaro iliwekwa katika orodha ya maeneo ya Urithi wa Dunia, ikiwa eneo la saba la<br />

Tanzania la Urithi wa Dunia (Lambrechts et al.,2002).<br />

Hifadhi ya akiba ya Wanyamapori ya Mkomazi ni mwendelezo wa Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi<br />

ya Kenya. Kama zilivyo Hifadhi za Taifa za Tsavo na Arusha, Mkomazi ipo katika mpango wa kituo cha<br />

uendelezaji wa wanyama cha ukanda wa Somali – Masai (Somali – Maasai Regional Centre of Endemism,<br />

RCE). Inatanda toka mpakani mwa Tanzania na Kenya hadi chini ya milima ya Pare na Usambara Magharibi.<br />

Hifadhi hii ina tabia ya misitu ya savana, na mpaka mwaka 1988, wafugaji kutoka makabila mbalimbali<br />

waliruhusiwa kunufaika na malisho yake. Homewood na Brockington (1999) wanaeleza kuwa ingawa<br />

hifadhi hii ina manufaa makubwa kwa Tanzania kwa kuwa na hazina kubwa ya bayoanuwai umuhimu wake<br />

umefunikwa kwa kiasi kikubwa na kanda nyingine zenye hazina kubwa zaidi za bayoanuwai, bila kusahau<br />

Milima ya Pare na Usambara. Keith Eltringham et al., (1999) alibainisha kuwepo kwa spishi 102 za wanyama<br />

wanaonyonyesha (mamalia) ndani ya Mkomazi, wakiwemo Faru weusi walioletwa tena hivi karibuni.<br />

Mbuga ya Taifa ya Arusha iko kwenye kingo za Mlima Meru (mita 4,565) na ilianzishwa mwaka 1967.<br />

Mbuga ina mazingira ya aina nyingi mbalimbali, mifano mizuri ni pamoja na misitu ya milimani kwenye<br />

Mlima Meru, Maziwa ya Kreta ya Momela na nyanda za chini za nyika za savana na misitu ya miombo.<br />

Orodha ya ndege waliopo katika mbuga hii ina spishi 400, na ni moja ya mbuga chache za Tanzania<br />

ambazo mbega weusi na weupe huonekana kwa kawaida. Mbuga hii inapakana na Hifadhi ya akiba ya<br />

Wanyama ya Mlima Meru yenye eneo la kilometa za mraba 300. Mbuga ya Hifadhi ya Taifa ya Arusha<br />

inaaminika kuwa na msongamano mkubwa zaidi wa twiga duniani.<br />

Barabara kuu ya Nairobi-Mombasa hutenganisha Mbuga za Hifadhi za Tsavo Magharibi na Tsavo Mashariki.<br />

Hifadhi hizi zilizoanzishwa mwaka 1948, kwa pamoja zinaunda mbuga ya hifadhi ya Taifa kubwa kuliko<br />

zote nchini Kenya, na moja ya maeneo makubwa zaidi yaliyohifadhiwa duniani. Mnamo mwaka 1983,<br />

mipaka ya Kaskazini Magharibi ya hifadhi ya Tsavo Magharibi ilipanuliwa na kuchukua vilima vya Chyulu<br />

ambavyo ndivyo chanzo kikuu cha chemchemi za Mzima ambazo ni maarufu katika mbuga hii. Lita milioni<br />

225 za maji hububujika kutoka kwenye chemchemi hizi kila siku, ambayo huipatia maji Mombasa, jiji la<br />

pili kwa ukubwa nchini Kenya. Zaidi ya watu 150,000 hutembelea Tsavo Magharibi kila mwaka. Sura ya<br />

makunyanzi ya hifadhi hii ilisababishwa na milipuko ya zamani ya volkano, iliyoacha mikondo ya mtiririko<br />

wa lava yake, maeneo ya vipande vya lava na pia koni ndogo ndogo za volkano. Mbuga hii ina idadi kubwa<br />

zaidi ya tembo walioko Kenya. Eneo la mbuga la Ngulia limekuwa moja ya maeneo muhimu sana nchini<br />

Kenya ya hifadhi ya faru. Milima ya miamba iliyoko Ngulia ndiyo kituo muhimu cha mapumziko kwa ndege<br />

wahamaji wanaotoka katika Kizio cha Kaskazini, ambao wengi wao ni adimu sana.<br />

19


Tishio na hadhi ya Hifadhi<br />

Mwishoni mwa miaka ya 1980, Idara ya<br />

Wanyamapori nchini Tanzania iliona Mkomazi<br />

kuwa ni eneo lililoishiwa na mimea na<br />

wanyama. Miongoni mwa matatizo yaliyoikabili<br />

mbuga ilikuwa kutoweka kwa faru. Katikati ya<br />

miaka ya 1960 kulikuwa na takriban faru 150<br />

katika hifadhi hii, lakini spishi hii ilimalizwa,<br />

hasa kutokana ujangili. Mnamo mwaka 1997<br />

faru waliletwa tena kwenye hifadhi hii (Keith<br />

Eltringham et al., 1999) pamoja na mbwa<br />

mwitu. Hali ya mbuga hii kuwepo jirani na<br />

mpaka wa Kenya inaleta tishio la ujangili.<br />

Kisanduku cha 7: Tishio kwa Maeneo<br />

yaliyohifadhiwa ya Bonde la Mto Pangani<br />

• Sehemu kubwa ya mbuga katika Bonde la Mto<br />

Pangani ziko katika tishio la ujangili.<br />

• Hatari zinazoikabili Mbuga ya Taifa ya Kilimanjaro<br />

zinahusiana zaidi na kuingiliwa katika hifadhi yake<br />

ya misitu na uvuniaji wa mbao.<br />

• Idadi kubwa ya watalii katika Mlima Kilimanjaro<br />

husababisha matatizo makubwa ya utupaji<br />

hovyo na kiasi kikubwa cha taka, kwani takataka<br />

huganda na haziozi<br />

Kilimanjaro haionekani kukabiliwa na tishio la aina hii la ujangili. Hapa, tishio lipo hasa kwenye mipaka ya<br />

hifadhi ya misitu, ambako ukataji miti, kilimo, ukusanyaji wa kuni na uchomaji wa mkaa umeshamiri. Tatizo<br />

la ziada kwenye mbuga hii ya hifadhi ya taifa ni idadi kubwa ya wageni wanaoitembelea, ambao huacha<br />

takataka nyingi , ambazo haziwezi kuoza katika hewa nyepesi na baridi sana ya mlimani.<br />

Maeneo yanayozunguka Mbuga ya Taifa ya Arusha yana idadi kubwa ya watu na inasemekana mbuga<br />

inakabiliwa na tishio la kuingiliwa na shughuli za binadamu na kiwango kikubwa cha ujangili (WCMC, 1985).<br />

Mbuga ya Taifa ya Tsavo Magharibi inakabiliwa na matatizo makubwa ya ujangili. Uuaji wa tembo katika<br />

mbuga siku zilizopita mara nyingi ulikuwa ukielezewa mfululizo katika vyombo vya habari. Zaidi ya hayo,<br />

mbuga hii iko katika ukanda wa ukame na hali ya hewa inayobadilika badilika, hali inayoifanya mbuga hii<br />

kuwa katika hatari ya moto. Mioto pia ni tatizo katika Mlima Kilimanjaro, kama ilivyojadiliwa hapo juu.<br />

Rasilimali nyingine za wanyamapori pia hupatikana katika bonde zima, wakiwemo wengi wa wanyamapori<br />

wanaopatikana katika misitu ya milima ya Tao la Mashariki na ile ya Pwani. Tishio kwa msitu huu uliotajwa<br />

mwisho ni kubwa sana (angalia chini). Katika nyika za Masai za uwanda wa chini wa bonde, wanyama<br />

wenye kwato hupatikana, wakati mto na maeneo ardhioevu mengine yana hazina ya wanyama pori pia.<br />

B.5 Bayoanuwai na hifadhi<br />

Kenya na Tanzania zina utajiri mkubwa wa rasilimali za bayoanuwai. Kulingana na idadi ya spishi kwa<br />

eneo, Kenya ina kiwango cha juu cha tatu kwa mamalia anuwai katika Afrika, cha pili kwa ndege anuwai<br />

na cha tatu kwa reptilia anuwai.<br />

Tanzania ina kiwango cha juu cha pili kwa reptilia, amfibia na mimea anuwai katika bara la Afrika (Rodgers<br />

et al., 2001). Misitu ya Tao la Mashariki na ile ya Pwani ni moja kati ya ‘sehemu 25 zenye umuhimu mkubwa<br />

kwa bayoanuwai’ duniani. Bayoanuwai na upatikanaji wa spishi adimu zinazohusiana nazo katika milima<br />

hii hazina mfano wake duniani. Kadri ya asilimia 30 ya spishi za mimea kama 2000 hivi na zaidi ya asilimia<br />

80 ya makundi ya buibui na majongoo hupatikana katika milima hii pekee. Mimea maarufu ya urujuani<br />

(Saintpaulia) inatipakana kiasili katika misitu ya Milima ya Tao la Mashariki na Pwani pekee.<br />

Walau spishi nne za mamalia, tano za ndege, nne za amfibia, ishirini na saba za watambazi (reptilia), arobaini<br />

za vipepeo, ishirini za majongoo, mia nne za mimea na idadi isiyojulikana ya nzi, aina za mende na wanyama<br />

wengine wasio na uti wa mgongo hupatikana katika misitu ya pwani ya Afrika Mashariki pekee (Burgess et<br />

al., 1996). Kiwango hiki cha uadimu kimetokea kwa sababu ya kujitenga kwa misitu hii na misitu mingine ya<br />

Afrika, kuwepo kwake kwa miaka mingi na ukweli kwamba hali ya hewa ya Bahari ya Hindi imebaki thabiti<br />

bila mabadiliko kwa muda mrefu sana.<br />

20


Matokeo yake, vitishio ambavyo vinakabili<br />

nyingi ya spishi hizi vinahusiana na<br />

uhifadhi wa mazingira yao. Kwa kuwa<br />

sehemu kubwa ya misitu ya Tao la<br />

Mashariki na ile ya Pwani iko hatarini,<br />

spishi zake nyingi za wanyama ziko<br />

hatarini (angalia kisanduku hapo chini).<br />

Katika Mlima Kilimanjaro spishi za mimea<br />

2,500 zimetambuliwa, zikiwemo spishi<br />

130 za miti kutoka jenasi (spishi zenye sifa<br />

zinazofanana) 100 na jamii 50. Spishi 170<br />

za vichaka zimetambuliwa kutoka misitu ya<br />

milima huu, na hii iko kwenye zaidi ya jenasi<br />

100 na jamii 40 (Lambrechts, et al., 2002).<br />

Spishi 140 za mamalia zimetambuliwa<br />

kuwepo mlimani, ikiwemo kundi kubwa<br />

zaidi linalojulikana duniani la mindi<br />

(Abbot’s duiker), spishi iliyo hatarini sana<br />

ulimwenguni (Lambrechts et al., 2002).<br />

Mbuga hii ina panya wadogo wapatikanao<br />

katika eneo hili pekee, spishi nne na spishi<br />

ndogo za vipepeo zipatikanazo kipekee,<br />

mimea ya aina 6 ya kipekee, kuvumwani<br />

kumi na mbili wanaopatikana eneo hili<br />

pekee na mmea aina ya liverworts (Baker<br />

na Baker, 2001).<br />

Papa dume (Carcharrhinus leucas) walio<br />

adimu na hatarini mara chache huogelea<br />

kuelekea juu katika Mto Pangani kutoka<br />

kwenye delta zake, na wameonekena<br />

katika mkondo wake kuelekea juu hadi Jambe (TANESCO, 1994). Hata hivyo, mbali na papa, hakuna<br />

spishi zozote kati ya 41 za samaki wa mto huu, zinazofikiriwa kuwa hatarini. Kuna spishi kadhaa zilizoko<br />

kwa wingi kukiwa na samaki wa aina mbili za “cyprinids” (Barbus paegnstecheri na Labeo coubie), aina<br />

moja ya “characin” (Rhabdalestes leleupi) na aina tatu za “cichlids” (Ctenochromis pectoralis, Oreochromis<br />

korogwe na O. pangani) (TANESCO, 1994).<br />

Jenasi ya perege, Oreochromis, imepata jina lake kutoka lugha ya kilatini la Mlima ‘Chromis’ ambalo Gunther<br />

aliipa mwaka 1889 baada ya kugundua Orechromis hunterti katika Ziwa Chala, lililopo kwenye miteremko<br />

ya Mlima Kilimanjaro (Dadzie et al, 1988). Kwenye Ziwa Jipe aina mbili za ziada za perege walio adimu<br />

zinapatikana: Perege jipe na perege girigan. Orechromis esculentus wanaopatikana katika Ziwa Victoria<br />

pekee 4 , wamepandikizwa katika Bonde, na wamekuwa ni sehemu kubwa ya samaki wanaovuliwa kutoka<br />

Bwawa la Nyumba ya Mungu. Perege wa ziada wa kigeni, T. rendalii, wamevuliwa kutoka Ziwa Chala.<br />

Tishio na hadhi ya Hifadhi<br />

Kisanduku cha 8: Sehemu zenye umuhimu<br />

mkubwa wa bayoanuwai<br />

Sehemu zenye umuhimu mkubwa wa bayoanuwai huteuliwa na<br />

Shirika la Hifadhi la Amerika, Conservation International. Ni maeneo<br />

ambayo yana aina mbali mbali za spishi duniani, lakini ambayo<br />

wakati huo huo, yameathiriwa na kubadilishwa sana na shughuli za<br />

binadamu. Mimea anuwai ndiyo kigezo cha uteuzi wa maeneo hayo,<br />

kwa kuwa mimea ni msingi wa anuwai katika kuainisha kisayansi<br />

makundi mengine. Ili kustahili hadhi hii, lazima eneo liwe na walau<br />

spishi 1,500 za mimea inayopatikana katika eneo hilo pekee, kwa<br />

ukamilifu asilimia 0.5 ya jumla ya mimea inayojulikana ulimwenguni.<br />

Kwa nyongeza, asilimia 70 au zaidi ya makazi ya asili ya eneo hilo<br />

lazima yawe yameharibiwa au kubadilishwa.<br />

Kati ya hizo, sehemu 25 zenye umuhimu mkubwa zaidi wa<br />

bayoanuwai duniani zinachukua asilimia 1.4 tu ya eneo la dunia,<br />

lakini zina asilimia 44 ya mimea inayojulikana duniani, na asilimia 35<br />

ya wanyama wote wenye uti wa mgongo wanaojulikana duniani.<br />

Sehemu hizo muhimu mara nyingi ni ‘visiwa’ vya bayoanuwai<br />

vilivyozungukwa na maeneo ya bayoanuwai duni kiasi.<br />

Kama ilivyo kwa Milima ya Tao la Mashariki, maeneo haya<br />

kiasili yamepata bayoanuwai yake kama matokeo ya hali za<br />

mazingira ambazo hazikubadilika kwa kipindi kirefu.<br />

Mbali na sehemu za umuhimu mkubwa wa bayoanuwai za<br />

Misitu ya Tao la Mashariki na ile ya Pwani, kuna sehemu<br />

nyingine nne za namna hiyo katika Afrika. Madagascar na<br />

visiwa vya Bahari ya Hindi, Misitu ya Guinea ya Afrika ya<br />

Magharibi, Jimbo la Cape maarufu kwa maua na Karoo zenye<br />

utomvu katika pwani ya kusini magharibi ya Afrika.<br />

Tishio kuu linalokabili bayoanuwai ya Bonde la Mto Pangani linahusiana na uharibifu wa makazi. Kiwango<br />

cha juu sana cha wingi wa bayoanuwai huendana na viwango vya juu vya upekee na anuwai za makazi<br />

katika bonde, hususan misitu yake ya milima ya Afrika na ya pwani. Kwa mfano, karibu spishi zote za<br />

ndege zinazopatikana katika bonde hili pekee, pia huchukuliwa kuwa spishi za eneo hili tu, na hivyo<br />

kuwa hatarini zaidi kudhuriwa kutokana na uharibifu na kugawanyika kwa makazi.<br />

4<br />

Katika hali ya mabadiliko ya kushangaza, spishi hii sasa imetoweka kabisa katika Ziwa Viktoria<br />

21


Kisanduku cha 9: Kundi la 1 la spishi za ndege wa Milima ya Usambara lililo hatarini<br />

Walio hatarini sana<br />

• Mbayuwayu mwenye mdomo mrefu (Orthotomus moreaui): hawakujulikana mpaka mwaka 1931<br />

na bado ni spishi inayojulikana kidogo<br />

Wasio salama (wenye kuweza kudhuriwa)<br />

• Bundi wa Sokoke (Octus ireneae): waligunduliwa mnamo mwaka 1965 katika msitu wa Arabuko-<br />

Sokoke ya pwani ya Kenya, ambapo ilichukuliwa kama spishi inayopatikana hapo pekee mpaka<br />

kundi lingine lilipogunduliwa katika milima ya Usambara mnamo mwaka 1995.<br />

• Bundi Tai wa Usambara (Bubo vosseleri): Waligunduliwa kati ya misitu ya uwanda wa chini wa<br />

Usambara katika mwaka 1992, baada ya kufikiriwa kama ndege wa msongamano mdogo wa<br />

mwinuko wa juu hapo awali.<br />

• Zuwanende bakajeupe/kirumbizi (Swynnertonia Swynnertoni): aligunduliwa katika Usambara<br />

pekee mnamo mwaka 1990.<br />

• Zuwanende wa pwani ya Mashariki (Shepperdia gunningi): aligunduliwa katika milima ya Usambara<br />

mnamo mwaka 1992.<br />

• Zuwanende mabaka meusi wa milimani (Modulatrix orostruthus): uadimu wake katika milima ya<br />

Usambara ya Mashariki huenda ni matokeo ya kugawanyika vipande vipande kwa mistiu.<br />

• Chozi wa Amani (Hedydipna pallidigaster): alielezwa kwanza na Sclater na mtaalamu maarufu wa<br />

elimu ndege, Moreau, katika mwaka 1935, ndege huyu mdogo sana anafahamika kutoka sehemu<br />

tatu tu za Afrika Mashariki. Katika milima ya Usambara, ni eneo la kilomita za mraba 320 tu la<br />

makazi yanayofaa ndiyo limebaki (Cheke et al., 2001).<br />

• Chozi mwenye mistari (Anthreptes rubritorgues): anajulikana kutoka sehemu nne tu katika Tanzania.<br />

Makazi yake makubwa zaidi ni milima ya Udzungwa.<br />

• Kwera wa Usambara (Ploceus nicolli): kwera hupatikana katika milima ya Usambara pekee ambako,<br />

Zimmerman et al., (1996) anakadiria wamebaki chini ya 100.<br />

Walio hatarini kidogo:<br />

• Tai-miraba kusi (Circaetus fasciolatus): Awali alidhaniwa kuwa mkazi wa kawaida katika misitu<br />

ya pwani inayotanda kutoka Kaskazini Mashariki ya Kenya hadi Kaskazini Mashariki ya Afrika ya<br />

Kusini. Sasa anafikiriwa kutishiwa na msongamano wa binadamu na matumizi yaliyokithiri ya misitu<br />

ambayo ni makazi yake makuu. Makadirio ya jozi moja kwa kilomita za mraba 100 yanabaki katika<br />

kiwango hicho (Ferguson-Lees na Christie, 2001).<br />

• Kulukulu (Tauraco fischeri); kwa kawaida hupatikana msituni pote. Anatishiwa na biashara ya<br />

Kimataifa ya ndege mwitu.<br />

Hofu ya uharibifu wa makazi haya ya msitu yenye thamani imefanya misitu ya pwani ya Tanzania na<br />

Milima ya Tao la Mashariki ipate uangalizi wa Kimataifa. Hakika yote ina hadhi ya Eneo Muhimu la<br />

Ndege (IBA) (Baker na Baker, 2001), inayowezesha kulenga uangalizi wa Hifadhi ya Kimataifa kwenye<br />

hii mifumo ikolojia ya kupendeza na nyepesi kudhuriwa. Hata hivyo, ni misitu michache sana ya Tao la<br />

Mashariki au ya Pwani katika bonde ambayo siyo hifadhi ya misitu.<br />

B. 6 Uvuvi<br />

Samaki mara nyingi ni chanzo muhimu cha protini ya wanyama kwa jamii za vijijini za Afrika. Mwaka<br />

1970, uvuvi katika bwawa la Nyumba ya Mungu ulikimu wavuvi 3,161, ambao walivua tani 28,509 za<br />

samaki kwa ujumla wao. Kufikia mwaka 1983, kulikuwa na wavuvi 1,342, ambao waliweza kupata tani<br />

2,430 za samaki (Vanden Bossche na Bernacsek, 1999).<br />

22


Typha na mafunjo hutanda karibu katika nusu ya uso wa Ziwa Jipe, na karibu yakwamishe shughuli za<br />

uvuvi upande wa Tanzania wa ziwa (Sarmett na Kamugisha, 2002). Kwa upande wa Kenya wa Ziwa<br />

Jipe, wanavijiji 200 katika vijiji vitatu wanasemekana kutegemea uvuvi wa ziwani. Mbali na matatizo<br />

yanayohusiana na magugu maji, ziwa kujaa mchangatope pia ni tishio kwa uvuvi (Musyoki, 2003).<br />

Wanavijiji wanaoishi kuzunguka Kinamasi ya Kirua chini ya bwawa la Nyumba ya Mungu wanalalamikia<br />

upungufu wa samaki kutokana na taratibu za kudhibitiwa mtiririko wa maji kutoka bwawani (Sarmett na<br />

Kamugisha, 2002).<br />

B.7 Udongo<br />

Sehemu kubwa ya Bonde la Mto Pangani ina safu ya jiolojia ya fuwele na mawe ya chokaa, pamoja na<br />

viunga vya mashapo kutoka ziwani. Karibu zaidi na pwani, jiolojia ni ya mashapo ya katika mlango wa<br />

mto. Maeneo karibu na Mlima Meru na Mlima Kilimanjaro kwa asili ni Volkano za alikali zenye rutuba<br />

nyingi (Geological Survey, 1960). Mchanganyiko huu wa udongo wenye asili ya ziwa na ile ya volkano,<br />

na vilevile maeneo yenye wastani wa juu wa mvua kwa mwaka umezifanya sehemu za Bonde la Mto<br />

Pangani kuonekana kama eneo zuri la uzalishaji chakula nchini Tanzania.<br />

Matatizo makuu kuhusiana na udongo wa Bonde la Mto Pangani ni kupungua kwa rutuba ya ardhi,<br />

na upotevu wa udongo kutokana na mmomonyoko. Stoorvogel na Smaling (1990) walikadiria kuwa<br />

ardhi inayofaa kwa kilimo katika Tanzania hupoteza kilogramu 27 za Naitrojeni, kilogramu 9 za Fosfeti<br />

na kilogramu 21 za Potasiamu kwa hekta kwa mwaka kwa mwaka 1983. Walikadiria kwamba ikifikia<br />

mwaka 2000, viwango hivi vya upotevu vitaongezeka na kufikia kilogramu 32 za Nitrogen, kilogramu<br />

12 za Fosfeti na kilogramu 25 za Potasiam ikiwa upotevu wa virutubisho ulioonekana mwaka 1983<br />

haukubadilika. Kwa naitrojeni na fosforasi, viwango hivi vya upotevu ni sawa na tani 251,448 na tani<br />

115,1122 kwa mwaka. Stoorvogel na Smaling walieleza kuwa upotevu huu ulitokana na mambo matatu:<br />

kwanza uvunaji wa kawaida wa mazao ambapo virutubisho vingi hupotea. Pili, uondoaji wa mabaki<br />

ya mazao. Kwa mfano, maharage yanapovunwa katika wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, mmea<br />

mzima unang’olewa toka ardhini. Tatu, kutokana na mmomonyoko, hususan kutokana na kilimo katika<br />

mitelemko mikali (Kaihura et al. 2001). Ifahamike kwamba si kilimo chote katika Bonde la Mto Pangani<br />

ni cha kiharibifu (Kaihura et al. 2001).<br />

B.8 Majumuisho ya hoja<br />

Rasilimali za Bonde la Mto Pangani zinatumika kwa kiwango kikubwa sana. Katika sehemu hii, kwanza<br />

tunatoa muhtasari wa mchango muhimu unaotolewa na rasilimali hizi katika bonde na katika sehemu ya<br />

pili, tunatoa muhtasari wa hatari zinazozikabili.<br />

Rasilimali za Bonde la Mto Pangani<br />

• Misitu ina mchango muhimu sana katika haidrojia ya bonde, inarekebisha kasi ya maji, kupunguza<br />

mmomonyoko, kuhifadhi na kusafisha maji. Misitu iliyopo Bonde la Mto Pangani inatoa mchango<br />

muhimu kwa bayoanuwai ya ulimwengu. Katika misitu ya bonde hili baadhi ya spishi za kiwango<br />

cha juu cha upatikanaji kwa wingi ulimwenguni na bayoanuwai hupatikana.<br />

• Maji katika Bonde la Pangani ni ya muhimu kwa uchumi wa kilimo wa bonde, uzalishaji wa umeme,<br />

maendeleo ya miji, mahitaji ya viwandani na majumbani, na kwa ajili ya mifugo. Vinamasi pia<br />

katika bonde huchangia sana katika hifadhi na urekebishaji mwenendo wa maji.<br />

• Bonde hili lina maeneo manne yaliyohifadhiwa. Kilimanjaro, kipekee ina mchango muhimu katika<br />

uchumi wa taifa kutokana na utalii, na pia huhifadhi spishi nyingi ya mimea na wanyama.<br />

• Bayoanuwai ya bonde hili kwa kiasi fulani haina mfano ulimwenguni, na ni eneo la shughuli nyingi<br />

za Kimataifa za masuala ya hifadhi.<br />

23


• Uvuvi katika Bonde la Pangani unatoa mchango muhimu wa chakula na kiuchumi kwa jamii za<br />

vijijini katika bonde.<br />

• Ardhi ndiyo msingi mkuu wa uchumi wa kilimo wa bonde hili. Historia ya mlipuko wa volkano ya<br />

eneo hili na viunga vya mashapo ya mto yenye rutuba, huchangia katika umaarufu wa Bonde la<br />

Mto Pangani kuwa eneo la kutegemewa kwa uzalishaji chakula nchini Tanzania.<br />

Tishio kwa rasilimali za Bonde la Mto Pangani<br />

• Misitu iliyopo katika bonde inahatarishwa na ukataji miti, uingiliwaji eneo lake la pembezoni,<br />

mahitaji ya ardhi, utengenezaji wa mkaa na ukusanyaji wa kuni.<br />

• Upatikanaji wa maji katika Bonde unahatarishwa na mahitaji makubwa mno ambayo yamedhihirisha<br />

kuwa rasilimali za maji zinaonekana kuelemewa. Chanzo kikuu cha mahitaji hayo ni mifumo duni<br />

ya mifereji ya umwagiliaji. Vinamasi vya bonde hili vinahatarishwa na utaratibu wa udhibiti wa maji<br />

kwa kutumia mabwawa.<br />

• Maeneo yaliyohifadhiwa katika bonde yanahatarishwa, kwa upande mmoja na ujangili, na kwa<br />

upande mwingine, vitisho sawa na vile vinavyokabiliwa na rasilimali za misitu.<br />

• Sehemu kubwa ya bayoanuwai ya bonde imepatikana kutokana na safu za aina ya kipekee za<br />

makazi katika misitu yake. Matokeo yake, hatari ya kutoweka kwa bayoanuwai zinatokea kwa<br />

sababu ya tishio kwa makazi.<br />

• Uvuvi katika bonde unatishiwa na shinikizo la uvuvi lililokithiri, na ukuaji wa magugu unaosababishwa<br />

na kiasi kikubwa cha virutubisho.<br />

• Viwango vya chini vya kurudishia rutuba na matumizi ya pembejeo, na vile vile viwango vya juu<br />

vya mmomonyoko, vinahatarisha udongo katika bonde.<br />

24


C Uchumi wa Jamii katika<br />

Bonde la Mto Pangani<br />

C.1 Maelezo ya jumla<br />

Inakadiriwa kuwa kuna watu wapatao milioni 3.7 katika Bonde la Mto Pangani, asilimia 80 wakitegemea<br />

ama moja kwa moja au kwa njia moja au nyingine, kilimo kwa maisha yao. Asilimia 90 ya idadi ya wakazi<br />

wa bonde hili huishi katika sehemu za ukanda wa juu. Msongamano huo wa makazi hufikia watu 300<br />

kwa kilomita moja ya mraba. Katika maeneo ya nyanda za juu za Kilimanjaro kuna watu 900 kwa kilomita<br />

moja ya mraba yenye wastani wa vishamba vya hekta 0.2 tu kwa kaya. Wakati huo huo, katika maeneo<br />

ya nyanda za chini kulikuwa na watu 65 tu kwa kilometa ya mraba, na kila kaya ililima wastani wa eneo<br />

la hekta 10.4 (Lein, 2002).<br />

Shughuli za kiuchumi katika Miji na viwanda ndani ya bonde si kubwa kiasi cha kutosha kuchukua<br />

nguvu kazi hii. Matokeo yake, idadi ya watu ambayo inazidi kukua, hupata riziki yake kutokana na kilimo,<br />

ambacho kwa sehemu kubwa ni cha umwagiliaji. Kadiri matumizi ya maji yanavyoongezeka, ndivyo<br />

migogoro inavyoongezeka. Mahitaji ya maji ni ishara ya mahitaji makubwa zaidi ya kufikia aina zote za<br />

rasilimali, ikiwemo ardhi, mazao ya misitu, malisho, madini na hatimaye kujipatia riziki. Kujipatia riziki<br />

kunaweza kuelezwa kama ifuatavyo:<br />

“….. njia ya kujihakikishia maisha …Ndani yake kukiwa na rasilimali kwa ujumla wake, shughuli<br />

na mazao yanayowezesha kuishi. Inategemea umiliki wa, au upatikanaji wa mazao au shughuli<br />

za uzalishaji. Upatikanaji wa riziki hupimwa kwa kutumia vipimo vyote viwili vya mali -yaani<br />

hifadhi na vyombo- na upatikanaji wa chakula na fedha “(Conway na Barbier, 1990: 117).<br />

Dhana ya kufikia rasilimali ni kigezo cha muhimu sana katika kuamua kuwa utafutaji wa riziki ni wa<br />

mafanikio au la (cf. Ellis, 2000). Hivyo ina maana kuwa pale ambapo rasilimali inayotegemewa na jamii<br />

inakuwa haba, basi upatikanaji wake unapungua. Kadiri rasilimali zinavyokuwa haba zaidi, basi hatua<br />

watakazochukua watu ili kujaribu kujipatia rasilimali zinaweza kuwa mbaya zaidi, na kuwa vigumu zaidi<br />

kwa rasilimali husika kudumu. Mtindo huu hatimaye unaweza kufikia mahali ambapo utafutaji riziki<br />

ukapuuza uwezo wa rasilimali kujizalisha upya.<br />

Jambo linalokuza matatizo yanayohusiana na mahitaji ya riziki ni kama rasilimali zinazohusika ni<br />

Rasilimali za Pamoja za Jamii (CPRs). Hizi ni rasilimali ambazo zina tabia mbili za msingi zinazofanana;<br />

(a) ‘zinapunguzika’. Upunguzaji wa kiasi cha maji sehemu ya juu ya mto husababisha upungufu wa<br />

kiasi cha maji sehemu ya chini ya mto. Vivyo hivyo, mvuvi anayevua kilogramu 100 za samaki anafanya<br />

kuwe na kilogramu 100 pungufu za samaki kwa ajili ya wavuvi wengine. (b) Ni vigumu au haiwezekani<br />

‘kuzikinga’ rasilimali za pamoja za jamii. “Kulinda” kisitiari inamaanisha matatizo makubwa ya kuzisimamia.<br />

Kutokana na asili zao, rasilimali za pamoja za jamii (kama vile bahari, angahewa au mikondo ya mto)<br />

haziwezi kujengewa uzio, na pia ni vigumu sana kuzifuatilia na kuzisimamia. Rasilimali za pamoja za<br />

jamii kwa hiyo, husimamiwa vizuri zaidi kwa pamoja, kukiwa na mchango wa watumiaji wote. Ikiwa<br />

mtindo huo wa usimamizi wa pamoja haupo, zitakuwa hatarini sana kuwa wazi kuingiliwa’, ambapo<br />

muundo wa utumiaji ni wa ‘huru-kwa-wote’, watumiaji wa rasilimali wakichukua zaidi ya wanachohitaji<br />

leo kwa kuhofia kuwa wanaweza wasipate kitu kesho. Mitindo ya utumiaji kama hiyo ina viwango vya juu<br />

sana vya ushindani baina ya watumiaji, na thamani halisi zinazohusiana na hifadhi ya rasilimali hazijaliwi<br />

kabisa. Wakati rasilimali zinapotumika katika mtindo kama huu, ‘mwisho wa wanyonge’, unasemekana<br />

kuwa umewadia na kutoweka kwa rasilimali kunakuwa ni jambo la wazi.<br />

Kwa viwango mbalimbali, na kutegemeana na aina ya rasilimali, rasilimali nyingi za Bonde la Mto Pangani<br />

zina tabia ya kuwa wazi kuingiliwa na matatizo makubwa sana kutokana na utafutaji wa riziki. Mahusiano<br />

yanayoainisha utumiaji wa rasilimali za bonde mara nyingi yanaelezwa kama yenye kuhitilafiana. Ili<br />

25


kurahisisha na kufafanua matatizo haya, sura hii inazingatia matakwa ya shughuli mbali mbali za kiuchumi,<br />

ikianzia na shughuli za viwanda ambazo ni pamoja na uzalishaji wa umeme, na kisha kuendelea kuangalia<br />

sehemu kubwa ya uchumi wa bonde, ambayo ni kilimo. Shughuli nyingine pia zinazingatiwa, na sura hii<br />

inamalizia na tathmini ya migogoro ya kawaida katika uendelezaji wa bonde hili.<br />

Jedwali la 4:Taarifa ya msingi ya uchumi wa kijamii wa Tanzania na Kenya<br />

mwaka 2001 isipokuwa ikionyeshwa vinginevyo<br />

Kenya<br />

Tanzania<br />

Idadi ya watu Milioni 29 Milioni 32<br />

Kwango cha ongezeko la idadi ya watu kwa mwaka, mwaka 2000 2.6 2.8<br />

Kiwango cha vifo vya watoto wachanga kwa 1000 waliozaliwa hai 75.0 91.0<br />

Kiwango cha vifo vya watoto wenye umri chini ya miaka 5 kwa 117.0 142.0<br />

1000 waliozaliwa hai<br />

Uwezekano wa kufa, wanaume < miaka 5, (katika kila 1000) 100.0 157.0<br />

Uwezekano wa kufa, wanawake < miaka 5, (katika kila 1000) 99.0 148.0<br />

Matarajio ya umri wa kuishi wakati wa kuzaliwa (wanaume) 47.3 44.4<br />

Matarajio ya umri wa kuishi wakati wa kuzaliwa (wanawake) 48.1 45.6<br />

Asilimia ya upatikanaji wa maji salama ya kunywa 44.0 66.0<br />

Asilimia ya upatikanaji wa usafi wa kutosha 85.0 86.0<br />

Asilimia ya watoto waliozaliwa na uzito mdogo1 16.0 14.0<br />

Asilimia ya watoto waliodumaa (wastani na kiasi kikubwa)2 33.0 42.0<br />

Asilimia ya watoto waliodhoofika )3 6.0 6.0<br />

Wastani wa kula kalori kwa mtu kwa siku (1999)4 1,886.0 1,940.0<br />

GNP (Dola za Kimarekani) kwa mtu 340.0 210.0<br />

Dondoo<br />

1 kuzaliwa na uzito mdogo mara nyingi kunaashiria shinikizo la uzazi wakati kijusi kiko tumboni, kama<br />

vile kuugua (ikiwemo utapiamlo).<br />

2 Kudumaa ni aina ya kudumu ya utapiamlo unaotokana na kutopata lishe ya kutosha, iliyo bora, kwa<br />

kipindi kirefu<br />

3 Kudhoofika ni aina hatari na kali, ya utapiamlo iletwayo na kutopata lishe ya kutosha, iliyo bora, kwa<br />

kipindi kifupi.<br />

4 FAO imeweka mahitaji ya nguvu ya chini kabisa kwa binadamu kuwa kilo kalori (kcal) 2,600 kwa siku<br />

Rejea: UNICEF; 2001; FAO, 2001; WHO, 2001<br />

26


C.2 Shughuli za viwanda<br />

Kuna uwezekano kuwa shughuli iliyo kubwa zaidi ya viwanda katika Bonde la Mto Pangani ni uzalishaji wa<br />

umeme. Mzalishaji mkuu wa umeme ni Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO), linalomilikiwa<br />

na serikali, ambalo linamiliki mitambo minne ya uzalishaji umeme wa maji katika Mto Pangani. Nayo<br />

ni Nyumba ya Mungu (yenye uwezo wa MW 8), Hale (MW 21) na Mitambo mipya ya Maporomoko ya<br />

Mto Pangani (MW 68). Mitambo hii ya umeme imeunganishwa na gridi ya taifa na huchangia kadiri ya<br />

asilimia 17 ya jumla ya nishati ya umeme wa maji unaozalishwa nchini (Ngula, 2002). Mahitaji ya kiasi<br />

cha maji kwa uzalishaji wa uhakika (Firm power) kwa mitambo ya umeme ni kadiri ya mita za ujazo<br />

24 kwa sekunde, ambapo mahitaji ya juu kabisa ni mita za ujazo 45 kwa sekunde. Mitambo ya “Old<br />

Pangani” hufanya kazi mara chache kutokana na ukosefu wa maji ya kutosha (Lugeiyamu, Mhojiwa).<br />

Wakati wa msimu wa kiangazi, upungufu wa maji unaweza kusababisha uzalishaji wa umeme katika<br />

bonde kupungua hadi MW 32 (Sarmett na Kamugisha, 2002).<br />

Kuna shughuli nyingi za uchimbaji wa madini katika Bonde la Mto Pangani. Hizi ni pamoja na machimbo<br />

ya bati eneo la Korogwe, machimbo ya tanzanaiti na fosfati katika mkoa wa Arusha, na machimbo ya<br />

mawe ya chokaa katika mkoa wa Tanga (Mkuula, 1993). Vito johari pia vinapatikana kwa kiasi cha<br />

kutosha, na asilimia 80 ya hifadhi za tanzanaiti ijulikanayo duniani inapatikana Mererani, kilomita 50<br />

Kaskazini Mashariki ya Arusha. Uchimbaji wa mchanga kwa shughuli za ujenzi hufanyika zaidi katika<br />

kingo za mito, na katika sehemu za bonde kwa upande wa Kenya, uchimbaji wa rubi hufanyika.<br />

Viwanda vingine katika bonde ni vile vinavyohusiana na kilimo, kama vile vya uzalishaji wa sukari na vya<br />

mchakato wa usafishaji wa katani. Katika wilaya ya Taita-Taveta nchini Kenya, uzalishaji wa katani ndio<br />

shughuli kuu ya kilimo.<br />

C. 3 Shughuli za Kilimo<br />

Watu wa jamii ya Wachaga wameishi katika miteremko ya Mlima Kilimanjaro kwa miaka kati ya 300 hadi<br />

450. Umilikaji wao wa ardhi kwa ajili ya kilimo umegawanywa katika namna mbili. Kwanza ni “shamba”,<br />

ambapo yametengwa maeneo maalum katika ukanda wa chini ya mlima ambapo mvua si ya uhakika, na<br />

umwagiliaji wa kadiri unahitajika sana. Matumizi ya ardhi ya shamba yalikuwa yakisimamiwa na machifu wa<br />

Kichaga, ambao waliwapangia wakulima sehemu za ardhi kwa msimu. Ingawa mkulima aliweza kutumia<br />

ardhi kwa kipindi kirefu, haikuwa mali yake hata kidogo (Johnston, 1946). Aina ya pili ya umilikaji ardhi ya<br />

uchaga ni ‘kihamba’, ambacho kilitengwa kwa matumizi binafsi ya wakazi wa uchagani. Kihamba kilikuwa,<br />

na bado kinalimwa kwa kiwango kikubwa. Hata katika miaka ya 1940, wakati wa maandishi ya Johnston<br />

(1942), kulikuwa na ardhi ndogo sana ya kihamba iliyobaki ambayo ingeweza kutumika kama malisho,<br />

hivyo mifugo mingi ilifungiwa na kulishwa mazizini. Katika maeneo yale ambapo mkazo wa kilimo ulikuwa<br />

juu, na hakikupatikana kihamba kingine, machifu wa Kichaga walipaswa kubadilisha ardhi ya shamba kuwa<br />

kihamba, matokeo yake, kitendo hiki kilichangia kuhamisha kilimo kilichokuwa kimezidi katika miteremko<br />

ya juu, kwenda katika miteremko ya chini ya milima. Wachaga hawakuweza kujitanua mpaka mlimani<br />

kwa vile eneo hili lilikwishatengwa kama hifadhi ya msitu, na hawakuweza kujitanua kwenye maeneo ya<br />

mteremko wa kati kwa kuwa hii ilikuwa ardhi iliyotengwa kwa ajili ya walowezi wa kizungu (Lein, 2002).<br />

Kutokana na hali hii ya msongamano mkubwa wa kilimo, Wachaga walibuni mifumo ya mifereji ya maji<br />

kutoka kwenye vyanzo vya asili hadi kwenye mimea yao. Mfumo huu unasemekana kuwa mmojawapo wa<br />

mifumo ya zamani sana (inafikiriwa kuwa ulianza katika karne ya 18, Gillingham, 1999) na mifumo mikubwa<br />

zaidi ya mifereji ya umwagiliaji katika Afrika (Rohr et al., n.d.). Ili kupata maji hayo ya mfereji, ilibidi mtu awe<br />

mwanachama wa bodi ya mfereji, ambayo iliongozwa na wazee wa mifereji ambao maagizo yao yalibidi<br />

wakulima wayafuate kwa kuhofia adhabu ya faini au kuzuiliwa kutumia maji ya mfereji (Johnston, 1946).<br />

Wajumbe wa bodi ya mfereji pia walitegemewa kushughulikia utunzaji wa mifereji. Watumiaji wa maji ambao<br />

waliyachukua kutoka katika mifereji inayomilikiwa na watu binafsi ilibidi walipe ada ya kufanya hivyo.<br />

27


Licha ya ukubwa wa kilimo na shinikizo la idadi ya watu kwenye ardhi ya kihamba, taratibu za kijadi za<br />

utawala na uzuiaji migogoro zinaonekana kuwa na ufanisi. Johnston (1942) alisema “…….ni jambo la<br />

kuvutia kuwa, pamoja na kuwa na mfumo wa mifereji yenye utata , lakini mambo yanaendeshwa vizuri<br />

sana na wazee wa mifereji, kiasi kwamba idadi ya mashauri yatokanayo na migogoro ya haki ya kutumia<br />

maji imekuwa ndogo sana” (uk. 4).<br />

Kwa upande wa kusini, msongamano wa shughuli za kilimo katika milima ya Usambara, pia ulianza<br />

kuwa wa matatizo machoni mwa wakoloni. “Ulazima wa wenyeji kulima mfululizo kwenye kingo za mlima<br />

hufanya mmonyoko wa udongo kuwa tatizo kubwa sana, na maeneo makubwa ya ardhi ….huchukuliwa<br />

na maji (Dobson 1940:3). Wasambaa walikabiliwa na matatizo yaliyofanana na yale ya Wachaga. Maeneo<br />

ya miteremko ya kati ya milima yalikuwa na hali ya hewa iliyowapendeza wakulima wa Kijerumani,<br />

ambao walitenga maeneo makubwa ya ardhi kwa ajili ya kilimo cha mkonge.<br />

Maji katika jamii ya Wasambaa yalichukuliwa kuwa ni mali ya jamii, na mtu ambaye alikuwa na chanzo<br />

cha asili cha maji katika ardhi yake hakuweza kuzuia watu kutoka nje kuyatumia. Wamiliki wa ardhi<br />

waliweza kuwatoza faini wafugaji iwapo mifugo yao iliharibu mazao yao, au kama maji yalichafuliwa.<br />

Maji kutoka kwenye mfereji, ambayo yalitumiwa sana katika miaka ya awali ya 1940, yalikuwa ni mali<br />

ya wale waliochimba mfereji huo (Dobson 1940).“Mfereji ulipokuwa unachimbwa, wenye mashamba<br />

waliamua baina yao wenyewe kuhusu nani apate maji na kwa siku zipi”(uk. 22). Aidha, licha ya ukubwa<br />

wa kilimo na msongamano wa watu, migogoro ya haki ya kutumia maji ilikuwa michache. “Kulionekana<br />

kuwa na migogoro michache kiasi cha kushangaza” aliandika Dobson (1940) ….” lakini kwa suala la<br />

mifereji mirefu sana, wazee kwa ujumla walimweka mtu anayeaminika kusimamia na kuhakikisha kuwa<br />

kila mmoja anapata mgao wake wa maji kwa usawa na hakuna maji yanayopotea bure …” (uk. 22).<br />

Tofauti na Wachaga, Wasambaa hawakutaka<br />

kabisa kuteremka chini ya milima kutafuta vyanzo<br />

mbadala vya ardhi ya kilimo. Kutokuwepo kwa<br />

migogoro ya haki ya kutumia maji na ukweli<br />

kuwa kuhamia kwenye nyanda za chini lilikuwa ni<br />

jambo la hiari, inaonesha kuwa msongamano wa<br />

kilimo haukuwa mkubwa katika miaka ya 1940,<br />

kama ilivyo leo.<br />

Bonde la Mto Pangani wakati wa kipindi cha<br />

ukoloni, lilikuwa eneo muhimu la maendeleo,<br />

lililokuwa na mashamba makubwa ya kahawa,<br />

mkonge, ngano na shughuli za uzalishaji sukari<br />

zilizoanzishwa ndani ya bonde hili. Hivyo, mahitaji<br />

ya wafanyakazi yaliongezeka, na hivyo kuwavutia<br />

wahamiaji kutoka sehemu yote ya nchi na hata<br />

kutoka nje ya nchi kama vile Rwanda, Burundi na<br />

Msumbiji (Mbonile, 2002)<br />

Haijafahamika wazi ni eneo kiasi gani la Bonde<br />

la Mto Pangani linamwagiliwa kwa sasa. Kwa<br />

eneo la bonde ambalo liko upande wa Tanzania,<br />

Mujwahuzi (2001) anakadiria kuwa hekta 40,000<br />

zinamwagiliwa, Rohr et al. (n.d.) anasema<br />

kuwa hekta 29,000 zinamwagiliwa kwa ufanisi,<br />

wakati ambapo Ngula (2002) anakadiria kuwa<br />

hekta 31,075 katika Bonde la Mto Pangani<br />

zinamwagiliwa.<br />

Kisanduku cha 10: Kasoro za usanifu<br />

wa mifereji ya asili<br />

Kwa mujibu wa Mwamfupe (2001), matatizo ya<br />

usanifu wa mifereji ya asili katika Bonde la Mto<br />

Pangani ni kama yafuatayo:<br />

• Maji mengi hupotea pale yanapochukuliwa<br />

kwa sababu ya nyenzo duni (mashina ya<br />

migomba) zinazotumiwa kuchepusha maji<br />

yaingie katika mifereji ya kumwagilia;<br />

• Muundo wa vishamba ni duni<br />

–hayakusawazishwa, jambo linalosababisha<br />

maji kutuwama, yakisababisha chumvi chumvi<br />

na mazao haba.<br />

• Mifereji haikujengwa imara na ina kingo<br />

dhaifu, jambo linalosababisha maji kuzivunja.<br />

Matatizo mengine ni kuwa mara nyingi wakulima<br />

huhusisha kiasi cha maji cha kuchukua na ukubwa<br />

wa ardhi ambayo wanahitaji kuimwagilia, na si<br />

kwa maji yanayopatikana. Maji yanayochukuliwa<br />

hayarudishwi mtoni, na mara nyingi hutuama.<br />

Si kawaida kwa wakulima kujenga mitaro ya<br />

kurudisha maji kwenye vyanzo vya maji. “Mifumo<br />

ya ya umwagiliaji ya Tanzania ni upotezaji tu wa<br />

maji” ( Nasari, Mhojiwa)<br />

28


Katika sehemu ya bonde iliyoko Kenya, mahitaji pekee makubwa ya maji ya Ziwa Jipe ni umwagiliaji.<br />

Eneo linalotegemea Ziwa hili upande wa Kenya lina miradi 10 ya umwagiliaji yenye ujumla wa hekta<br />

1,717. Eneo hili linatarajiwa kuongezeka. Mpango wa Umwagiliaji maji wa Ziwa Jipe utakuwa kwenye<br />

mwambao wa Ziwa Jipe na utachukua eneo la hekta 77.2 na utahitaji mita za ujazo 308 za maji kwa<br />

saa (Musyoki na Mwandotto 1999). Kwa sasa, kiasi kikubwa cha maji kinachukuliwa kutoka sehemu<br />

ambayo mto Lumi unatiririka kupitia Kenya, ambamo ndani yake kuna miradi 21 ya maji. Jumla ya kiasi<br />

kinachochukuliwa katika eneo la Kenya la Bonde la ziwa hili ni mita za ujazo 77,274 kwa siku. Mita za<br />

ujazo 54,681 za ziada huchukuliwa wakati wa kipindi cha mafuriko (Musyoki na Mwandotto, 1999).<br />

Kwa mujibu wa Ngula (2002) mahitaji ya maji kwa sasa ndani ya sehemu ya bonde iliyoko Tanzania<br />

ni mita za ujazo milioni 807.99 kwa ufanisi wa umwagiliaji wa asilimia 20. Umwagiliaji katika bonde<br />

hili hutumia kati ya mita za ujazo milioni 400 na 480 za maji kwa mwaka (Mujwahuzi, 2001). Mgao wa<br />

matumizi haya unaonekana kutokuwa na usawa – nusu ya jumla ya matumizi yote ya maji katika bonde<br />

ikiwa imesongamana kuzunguka Mlima Kilimanjaro. Hapa, mifereji ya jadi 500 ya umwagiliaji yenye<br />

urefu wa jumla wa kilomita 1800, huchukua maji ya kadiri ya mita za ujazo milioni 200 kwa mwaka kutoka<br />

kwenye mito ya mlima huu (Gillingham, 1999). Rohr et al. (n.d.) anarejea kazi inayoonesha kuwa, kati<br />

ya mwaka 1997 na 2007, kwa kila ongezeko la asilimia 1.5 la idadi ya watu wa bonde hili, mtiririko<br />

wa mito katika msimu wa mvua haba hupungua kwa mita za ujazo 8 kwa sekunde. Katika mkoa wa<br />

Kilimanjaro asilimia 80 ya matumizi ya maji ni kwa umwagiliaji (Ngana 2001). Maeneo ya Wilaya za Hai<br />

na Moshi Vijijini (kuzunguka Mlima Kilimanjaro) yanaonesha msongamano mkubwa zaidi wa mifereji ya<br />

jadi barani Afrika (Tagseth, 2002). Matokeo yake, viwango vya mmomonyoko wa ardhi kutoka kwenye<br />

Mlima Kilimanjaro viko juu (Mtalo na Ndomba, 2002). Tani 24 za udongo kwa hekta kutoka eneo la<br />

vyanzo vya mito husafirishwa na kuingia katika bwawa la Nyumba ya Mungu kila mwaka (Mtalo na<br />

Ndomba, 2002).<br />

Umwagiliaji wote huu unatumia mifereji 2000 ya jadi ya Bonde la Mto Pangani (Mujwahuzi, 2001),<br />

ambayo inawiana na asilimia 80 ya eneo la bonde linalomwagiliwa (Mwamfupe 2001). Hata hivyo<br />

huenda hii si ishara ya ukubwa wa kilimo. Tagseth (2002), kutokana na data za eneo lake la utafiti lenye<br />

sehemu tatu kusini mwa Wilaya ya Moshi Vijijini, anasema kwamba kiasi cha maji yanayotumika kwa<br />

kweli kimepungua kati ya mwaka 1940 na 1993, kama ilivyopungua idadi ya mifereji.<br />

Sababu za umwagiliaji ziko za namna mbili. Katika maeneo ya uwanda wa juu, wastani wa ukubwa<br />

wa shamba ni kati ya hekta 0.1 na 0.2. Hapa msongamano wa watu uko kati ya watu 700 – 1000 kwa<br />

kilomita ya mraba (Mwamfupe, 2001). Ili kufidia udogo huo wa mashamba na kuhakikisha kuwa ardhi<br />

iliyopo inazalisha kadiri iwezekanavyo, umwagiliaji unafanyika. Eneo la chini la bonde, katika maeneo<br />

ya mashamba ya asili, mashamba ni makubwa zaidi (hekta 0.8 – 1.5) na msongamano wa kilimo ni<br />

mdogo (Mwamfupe, 2001). Hata hivyo, hapa mvua hazina kanuni maalum, na umwagiliaji unafanyika ili<br />

kupunguza athari mbaya za hali ya hewa.<br />

Ni wazi kuwa kwa viwango hivi vya umwagiliaji, watumiaji wa maji wa maeneo ya juu ya mto wako<br />

mahali pazuri zaidi kuliko watumiaji walioko upande wa chini. Upungufu wa maji katika bonde hili ni<br />

jambo la kawaida sana. Utafiti wa Mwamfupe (2001) umefanyika katika sehemu mbili: Makuyuni, katika<br />

miteremko ya Kilimanjaro, na Kahe, chini zaidi ya mlima. Wahojiwa wake walisema kuwa hawapati maji<br />

ya kutosha kwa umwagiliaji. Sehemu kubwa ya wahojiwa - ambao wengi wao walitoka Kahe - walitupia<br />

lawama za upungufu huu kwa ukame wa muda mrefu; wakifuatiwa na wale - hasa kutoka Makuyuni –<br />

ambao walilaumu ongezeko la matumizi na mahitaji ya maji. Ni asilimia 7.3 tu waliolaumu matatizo ya<br />

maji kuwa yametokana na usanifu usiofaa wa mifereji.<br />

Ni muhimu kutambua kuwa sehemu kubwa ya sababu za kutobadilika kwa mifumo hii ya umwagiliaji wa<br />

asili, licha ya ufanisi mdogo, ni kwa sababu ya gharama zinazohusika kuweza kupata mifumo mbadala<br />

ya umwagiliaji yenye ufanisi, inayohitaji matengenezo madogo na ya kudumu. Ni muhimu pia kutambua<br />

kuwa usanifu wa mfereji unaweza kuleta manufaa ya kijamii na kiuchumi ambayo ni makubwa kuliko<br />

hasara zinazotokana na usafirishaji maji wenye ufanisi mdogo.<br />

29


Kisanduku cha 11: Magadi na chumvichumvi<br />

Magadi ni kuwepo kwa ziada ya ‘sodiamu inayobadilishika’ (chumvi chumvi za sodiamu zenye uwezo<br />

wa alikali ya ‘haidrolisis’) na kusababisha mpenyo na ucheu duni wa udongo. Chumvi chumvi ipo<br />

sana katika maeneo kame na nusu kame kwa kuwa hakuna maji ya kutosha kuondoa chumvichumvi<br />

zilizojikusanya katika sehemu ya mizizi ya mimea. Hali ya chumvichumvi inaweza kutokea pale uingiaji<br />

chumvi unapozidi uondoaji wake kwa kufurika au kuchujwa. Kati ya matatizo mengi yanayohusiana<br />

na chumvichumvi ardhini ni athari yake katika ufyonzaji wa udongo na uwekaji unyevu. Uvunjaji wa<br />

vitu asili katika udongo husababisha tabaka lake la juu kujigandamiza, na kusababisha upenyezaji<br />

wa maji kutoka tabaka la juu kwenda eneo la mizizi uzuiliwe. Katika Bonde la Mto Pangani, tatizo la<br />

chumvi limetolewa taarifa katika miradi kadhaa ya umwagiliaji, ikiwemo Musa Mwijanga, Kikafu Chini<br />

(yote wawili katika Wilaya ya Hai) na Mawala (Wilaya ya Moshi Vijijini) (Misana na Makoi, 2001), na<br />

vile vile katika baadhi ya miradi mikubwa ya binafsi ya umwagiliaji katika bonde (Sahib, 2002).<br />

Kiasi cha uoto katika bonde kimepungua, kikichangia katika kupungua kwa mtiririko wa maji wakati<br />

wa kiangazi, na kutishia upatikanaji wa riziki. Wakulima wamekabiliana na upungufu wa maji kwa njia<br />

kadhaa. Wamepunguza kiasi cha kahawa wanayolima, na kupendelea kulima nyanya, ambazo zinahitaji<br />

muda mfupi kustawi na zina soko zuri 5 . Mwamfupe (2001) pia anaeleza kuwa kahawa inatelekezwa kwa<br />

sababu ya kupanda na kushuka kwa bei. Kaya za wakulima pia zimepanua wigo wa kujipatia maisha<br />

kwa kujitafutia mapato yasiyotokana na kilimo. Kinachoshangaza ni kuwa aina ya shughuli mbadala<br />

zinatofautiana kulingana na eneo analotoka mkulima. Shughuli mbadala walizozipata kaya za nyanda za<br />

juu ilikuwa pamoja na ushonaji, utengenezaji wa redio na televisheni, utengenezaji wa saa na ushonaji<br />

wa viatu. Katika nyanda za chini, shughuli mbadala ilikuwa pamoja na uuzaji wa majani ya kulishia<br />

ngo’mbe, uvunjaji mawe, utengenezaji mkaa na kazi za vibarua. Mwamfupe (2002) anadokeza kuwa hii<br />

ni kwa sababu eneo la nyanda za juu limeendelea zaidi na lina maeneo ya miji zaidi kuliko maeneo ya<br />

nyanda za chini, hivyo fursa za kuingia katika sekta ya huduma ni kubwa zaidi.<br />

Miongoni mwa matatizo yanayotokana na wingi wa shughuli za umwagiliaji ni magadi na chumvichumvi.<br />

Katika maeneo matatu ya utafiti (yote katika Wilaya ya Moshi Vijijini) wa Misana na Makoi (2001), maji<br />

ya umwagiliaji, hayakuwa sababu ya chumvichumvi, ingawa kumekuwa na kukwama kwa kiwango<br />

kidogo hadi kikubwa cha upenyaji wa maji katika tabaka la juu la udongo kwa maeneo yote ya utafiti.<br />

Katika maeneo mawili umwagiliaji ulichangia katika kusababisha magadi. Wanasema, maji yenye ‘ubora<br />

mzuri’ yanahitajika ili kushughulikia tatizo hili. Umwagiliaji haukuonekana kuathiri rutuba ya udongo<br />

isipokuwa katika eneo moja. Misana na Makoi (2001) walipendekeza matumizi ya viwango vya chini vya<br />

mbolea za aina mbalimbali kutatua tatizo hili la kutotosheleza kwa rutuba ya udongo. Wanatoa rai kuwa<br />

chumvichumvi zinaweza kuchujwa vizuri kwa umwagiliaji, lakini pale maji yanaposimama basi tatizo hili<br />

halitatuliki kwa vile inasababisha mabadiliko ya kimuundo kwa tabaka la udongo wa juu, ikiathiri upenyaji<br />

wa maji kutoka udongo wa juu kwenda kwenye sehemu ya mizizi ya mmea.<br />

Mashamba makubwa zaidi katika Bonde ni shamba la miwa la Kampuni ya Sukari (TPC) (hekta 17,000),<br />

Skimu ya Umwagiliaji ya Moshi (Lower Moshi Irrigation Scheme) chini ya Programu ya Maendeleo ya<br />

Kilimo Kilimanjaro (KADP - hekta 6,320), na Shamba la Kahawa la Burka, Arusha.<br />

TPC ipo kusini ya mji wa Moshi, na ilianzishwa kwa mara ya kwanza na wawekezaji wa Kiholanzi katika<br />

miaka ya mwanzo ya 1930. Ilitaifishwa mwaka 1980, na kubinafsishwa tena mwaka 2000 kwa wawekezaji<br />

5<br />

Ni lazima itambulike kuwa kupanda na kushuka kwa bei katika soko la dunia la kahawa, na vile vile kwa bidhaa<br />

nyingine za kilimo na ubadilikaji wa mitindo ya uchumi wa kitalii, vyote huchangia katika kubadilisha uthabiti wa<br />

uchumi wa Bonde lenyewe na kuathiri uwezo wa wakazi wake kupata riziki ya kutosha.<br />

30


wa Mauritius (Deep River Bean Champ Sugar Estate, Mauritius) na wa Kifaransa (Group Quartier Francais<br />

Reunion Island). Shamba hili lina ukubwa wa hekta 17,000 ambapo hekta 5,750 kati ya hizo kwa sasa zina<br />

miwa. Inafikiriwa kuongeza eneo hili kufikia hekta 7,500 katika siku za karibuni (Sahib, 2002).<br />

Eneo hili linapata milimita 450 tu za mvua, hivyo umwagiliaji ni lazima kwa kilimo cha miwa. Kiasi cha<br />

upungufu wa maji kwa mimea umekadiriwa kwa kiwango cha chini zaidi cha milimita 1,200 kwa mwaka<br />

hivyo kuhitaji matumizi ya umwagiliaji yanayotofautiana kati ya milimita 1,500 – 1,900 kwa mwaka<br />

kutegemeana na mfumo na mbinu za umwagiliaji. Takriban nusu ya shamba humwagiliwa kwa kutumia<br />

mabomba ya juu, wakati sehemu iliyobaki inamwagiliwa kwa mifereji ya juu ya ardhi. Mito iliyopo katika<br />

mpaka wa upande wa Magharibi wa shamba hutoa sehemu ya maji ya umwagiliaji, na yaliyobaki<br />

huchukuliwa kutoka hazina ya maji ya chini ardhi kupitia visima virefu vinavyotoa maji mengi (meta za<br />

ujazo 500 kwa saa) (Sahib, 2002).<br />

Nchini Tanzania, maji yanaweza kuchukuliwa kisheria iwapo tu watumiaji wana hati ya haki ya kutumia<br />

maji, ambayo, kwa Bonde la Pangani, hutolewa na Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWB), na<br />

kupangiwa ada kutegemeana na aina ya matumizi ya maji. Bodi hii inakabiliana na matatizo makubwa<br />

katika kutekeleza mfumo wa vibali vya maji kwani watumiaji wengi wa viwango vidogo wanaamini kuwa<br />

maji ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’. Ingawa wanataka kutumia maji kisheria, kiasili hawaamini kuwa<br />

wanapaswa kulipa kwa kufanya hivyo. Hata hivyo watumiaji wengi wa viwango vikubwa hulipa ada ya<br />

matumizi ya maji (Sarmett, Mhojiwa).<br />

C. 4 Shughuli za Wafugaji<br />

Kati ya mwaka 1994 na 1995, mifugo ilichangia asilimia 30 ya pato la taifa (GDP) la Tanzania. Nchi<br />

inakadiriwa kuwa na hekta milioni 60 za ardhi nzuri kwa ufugaji, na inaaminika kuwa inaweza kuhifadhi<br />

mifugo milioni 20. Nchi inakadiriwa kuwa na mifugo milioni 16 kwa sasa.<br />

Kuna data chache kuhusu wafugaji katika Bonde la Mto Pangani. Mnamo mwaka 1995, mifugo katika<br />

Bonde ilikadiriwa kuhitaji mita za ujazo 30,500 za maji kwa siku, wakati inategemewa kuhitaji mita za<br />

ujazo 36,400 kwa siku ifikapo mwaka 2015 (IVO-NORPLAN, 1997). Idadi kamili ya mifugo katika Bonde<br />

kwa sasa haijulikani. Tarakimu za karibuni zaidi zilizopatikana kwa utafiti huu ni za mwaka 2002, na<br />

zimechukuliwa kutoka wilaya na manispaa mbalimbali katika Bonde zima (Jedwali la 4).<br />

Jedwali la 5: Idadi ya mifugo katika baadhi ya maeneo ya Bonde la Mto Pangani (2002)<br />

Mkoa Ng’ombe *Mbuko Punda<br />

Wilaya ya Simanjiro, Mkoa wa Manyara 305,075 133,000 11,000<br />

Manispaa ya Arusha na Wilaya ya Arumeru, 470,000 461,450 21,991<br />

Mkoa wa Arusha<br />

Mkoa wa Kilimanjaro 568,689 534,420 12,380<br />

Mkoa wa Tanga 421,261 378,442 Hawakuhesabiwa<br />

Wilaya ya Taita – Taveta (Kenya) 37,800 40,277 Hawakuhesabiwa<br />

Jumla 1,765,025 902,972<br />

Rejea: Marejeo mbalimbali. *‘mbuko’ ni mchanganyiko wa mbuzi na kondoo.<br />

31


C. 5 Shughuli za Mijini<br />

Bonde la Mto Pangani lina maeneo makuu mawili ya miji. Upande wa Kaskazini, iko miji ya Moshi na<br />

Arusha ambayo iko karibu karibu sana. Mwaka 1995, matumizi ya maji mijini katika bonde yalikadiriwa<br />

kuwa mita za ujazo 71,200 kwa siku, na yanakadiriwa kufikia mita za ujazo 163,600 kwa siku ifikapo<br />

mwaka 2015 (IVO-NORPLAN, 1997). Ujazo wa maji yanayotumika kwa sasa, Sarmett na Kamugisha<br />

(2002) wanakadiria kuwa wa chini, na si zaidi ya mita za ujazo 1.1 kwa sekunde.<br />

Manispaa ya Arusha ina idadi ya watu kati ya 250,000 na 350,000 (wanaoitegemea mamlaka). Ingawa<br />

maji mengi zaidi yanayotoka Mlima Meru yanatumika kwa umwagiliaji na matumizi ya nyumbani, mtumiaji<br />

mkubwa kuliko wote wa maji kibiashara ni Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Mjini Arusha (AUWSA). Ina<br />

visima 15 na wastani wa uwezo wa mita za ujazo milioni 7.4 kwa mwaka (Sechambo, 2002). Mamlaka<br />

pia inapata maji kutoka chemchemi mbili zenye wastani wa jumla wa karibu mita za ujazo milioni 6.4 kwa<br />

mwaka (Sechambo, 2002).<br />

Mito pia hutumika kutupia takataka za mji. Manispaa ya Moshi, Ngana (2001) anasema inatupa majitaka<br />

moja kwa moja katika mito, wakati Mkuula (1993) anadai kuwa mito ya Themi (karibu na Arusha),<br />

Karanga, Njoro na Rau (karibu na Moshi) yote inachafuliwa na takataka za viwanda vya mijini.<br />

C.6 Shughuli za NGO na mashirika ya kimataifa katika Bonde la<br />

Mto Pangani<br />

Kuna mashirika mengi yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi katika Bonde la Mto Pangani, na mashirika<br />

machache ya kimataifa. Katika sehemu hii, inaeleweka kuwa mashirika haya kimsingi hayana mahitaji<br />

katika maliasili za bonde, bali shughuli zao mara nyingi zinalenga katika Usimamizi wa Maliasili (NRM),<br />

kuhifadhi, kuendeleza na kudumisha kazi za kujitafutia riziki. Kuna shughuli nyingi za mashirika yasiyo ya<br />

kiserikali na wahisani wa kimataifa kuliko vile inavyofikiriwa. Haya yatakayojadiliwa hapa chini yanaweza<br />

kuweka msingi kwa shughuli za usimamizi shirikishi katika bonde, kama itakavyoelezwa katika hitimisho.<br />

Asasi Zisizo za Kiserikali (NGO’s)<br />

PAMOJA ni NGO ya Kitanzania inayoamini kuwa majadiliano ni muhimu katika hali ya migogoro. Inatoa<br />

hoja kuwa kama sauti za vikundi vya jamii visivyo rasmi na vya pembezoni zinasikiwa na kusikilizwa<br />

na watunga sera na watoaji wa maamuzi, watendaji wenyeji wanaweza kuchangia kwa ufanisi ulinzi<br />

na ukarabati wa vyanzo vya maji, na wakati huo huo wakiongeza ufanisi wa uzalishaji wa kiuchumi na<br />

matumizi ya maji (PAMOJA, 2002:3). Wanasema, makubaliano ya pande mbili, yanafanya kazi nzuri<br />

zaidi kuliko sheria. Hivi sasa, PAMOJA imeonekana kutambulika na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani,<br />

kuwa ni njia itakayowezesha majadiliano na maelewano ya pande mbili baina yake na watumiaji maji wa<br />

bonde kuendelezwa.<br />

Ukiwa umezinduliwa mwaka 1992, Mradi wa Mpango wa Kazi ya Misitu Tanzania (TFAP) katika Milima<br />

ya Pare ya Kaskazini ulijihusisha na matatizo kadhaa makubwa, yakiwemo msongamano mkubwa wa<br />

watu, mashamba madogo, uchakavu wa udongo na viwango vya kutisha vya kuvamiwa kwa misitu.<br />

Kwa kutumia njia ya kuandaa mipango ya usimamizi wa maeneo maalum, na kwa ushirikiano na jamii<br />

za eneo la mradi, mradi uliweza kuboresha rutuba ya udongo, kupunguza kasi ya mtiririko wa maji na<br />

kuimarisha kingo za mito. TFAP pia ilijaribu kutumia mifumo ya umwagiliaji iliyoanzishwa na kutumiwa na<br />

Wapare kwa karne nyingi. Hata hivyo, ukubwa wa mashamba, umebaki kuwa mdogo, na zao pekee la<br />

biashara lililolimwa katika eneo hili lilikuwa kahawa, linalofanya Mndeme (n.d.) atoe hoja kuwa uanzishaji<br />

wa fursa za kutafuta kipato kwa njia isiyo ya kilimo na ubadilishaji wa msingi wa zao la biashara itakuwa<br />

muhimu kwa mafanikio ya baadaye ya mradi huu (rejea: Mndeme, n.d.).<br />

Shirika la Umwagiliaji wa Kiasili na Maendeleo ya Mazingira (TIP) lilisajiliwa Tanzania tangu mwaka 1999.<br />

Shirika hili lilirithi mali na shughuli za mradi wa awali wa miaka 13 uliokuwa ukifadhiliwa na wahisani ulioitwa<br />

32


Picha ya 1: Bonde la Mto Pangani<br />

(Rejea: Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Maji)<br />

33


34<br />

Picha ya 2: Bonde la Pangani - Utawala<br />

(Rejea: Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Maji)


Picha ya 3: Kilele maarufu cha theluji cha Mlima Kilimanjaro<br />

katika mwaka 1993 (juu) na mwaka 2000<br />

(Rejea: Bergkamp et al. 2003)<br />

35


Picha ya 4: Mto Karanga - Moshi (Kim<br />

Geheb 2002)<br />

Picha ya 5: Mlima Kilimanjaro<br />

(Kim Geheb, 2002)<br />

36


Picha ya 6: Mfereji wa umwagiliaji katika<br />

Wilaya ya Moshi Vijijini. Picha ya juu<br />

inauonesha karibu na chanzo chake,<br />

wakati ya chini inauonesha karibu na<br />

mwisho wake. (Kim Geheb, 2002)<br />

37


Picha ya 7: Chemchemi iliyojengewa Shiri-Njoro. Ukuta unaogawanya maji katika sehemu ya mbele<br />

inaelekeza maji kuingia katika mifereji ya kijiji, wakati lango la udhibiti lililojengewa katika jengo imara<br />

la zege kwa nyuma linayaelekeza maji kwenda Moshi.<br />

(Kim Geheb, 2002)<br />

Picha ya 8: Miteremko yenye msitu katika Mlima Meru (Kim Geheb, 2002)<br />

38


Programu ya Umwagiliaji wa Kiasili. Kama ilivyokuwa kwa Programu ya awali, lengo kubwa la TIP ni kusaidia<br />

kwenye uondoaji umaskini na kuendeleza upatikanaji wa chakula kwa jamii ya wakulima wadogo wadogo<br />

wa umwagiliaji wa kiasili kwenye maeneo teule ya Tanzania kwa kuboresha njia za kijadi za umwagiliaji. TIP<br />

inasisitiza mpango wa matumizi ya ardhi kuwa ni msingi wa usimamizi wa bonde, na inatoa hoja kuwa, kama<br />

hatua ya kuanzia, bonde hili lazima ligawanywe katika maeneo madogo madogo. Katika kila moja, lazima<br />

kuwe na bodi ya eneo dogo yenye wawakilishi kutoka katika kila kijiji kilichomo kwenye eneo hilo. Kila bodi<br />

ya eneo dogo itakuwa na wawakilishi kwenye Bodi ya Maji ya Bonde (Mjata, Mhojiwa).<br />

TIP inafanya kazi kupitia Hati ya Muafaka (MOUs) baina yake na wilaya nne za Tanzania: Same na Mwanga<br />

katika mkoa wa Kilimanjaro, Lushoto mkoani Tanga na Arumeru katika mkoa wa Arusha. Huwafikia wateja<br />

na wahitaji wengine kwa njia ya mikataba na shughuli mbalimbali pale wanapohitajiwa (Mjata, 2002).<br />

Programu ya Hifadhi na Maendeleo ya Kanda ya Mwambao wa Tanga (TCZCDP) ina ubia na Halmashauri ya<br />

Wilaya za Pangani na Muheza, Halmashauri ya Manispaa ya Tanga, Mamlaka ya Mkoa wa Tanga, Wahisani<br />

wa Irish Aid, na <strong>IUCN</strong> kwa ajili ya ushauri wa kiufundi na kiusimamizi. Madhumuni ya jumla ya TCZCDP ni<br />

matumizi endelevu ya rasilimali za pwani. Programu hii ina lengo la kuinua hali ya jamii za pwani mkoani kwa<br />

kuboresha afya ya mazingira ambayo wanayategemea na kuzipanua njia za matumizi ya mazingira ya pwani.<br />

TCZCDP ilianza kazi zake mwaka 1987 na shughuli zake zinaendelea (Mgongo 2002).<br />

Ubia wa Usimamizi wa Mwambao wa Tanzania (TCMP) ni juhudi za pamoja kati ya Baraza la Taifa la<br />

Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Kituo cha Rasilimali za Pwani/Chuo Kikuu cha Kisiwa<br />

cha Rhode na USAID. Ubia huu ulianzishwa mwaka 1997 ili kuendeleza na kutumia mfumo wa kitaifa<br />

wa usimamizi wa mwambao. Mfumo huu uko kwenye msingi wa mikakati yenye lengo la kuendeleza<br />

mpango wa usimamizi shirikishi wa ukanda wa pwani wa Tanzania na kuanzisha shughuli endelevu za<br />

uchumi zenye kutunza mazingira katika eneo hili (Luhikula 2002).<br />

Kikundi cha Hifadhi ya Misitu Tanzania (TFCG) kilianzishwa mwaka 1985, na kinakuza uhifadhi wa misitu<br />

yenye bayoanuwai nyingi katika Tanzania. Kati ya mafanikio ya kikundi hiki, ni ushawishi wa uundaji wa<br />

Mbuga ya Taifa ya Udzungwa, mbuga ya kwanza nchini Tanzania ya msitu wa mvua; ununuzi wa Msitu<br />

wa Mazumbai katika Milima ya Usambara Magharibi kwa madhumuni ya utafiti wa Chuo Kikuu cha Dar es<br />

Salaam; na kushawishi EU-<strong>IUCN</strong>/Wizara ya Mifugo na Kilimo kufadhili Mradi wa Hifadhi na Maendeleo ya<br />

Usambara Mashariki. Kati ya shughuli zake za sasa katika Bonde la Mto Pangani ni kuendeleza mfumo<br />

wa Usimamizi Shirikishi wa Misitu (JFM) kwa msitu wa Ambangulu (Milima ya Usambara Magharibi)<br />

kati ya jamii za wenyeji, serikali za mitaa na shamba la chai lililopo karibu. Kutokana na kufanya kazi<br />

kwa pamoja na jamii zilizo jirani na Msitu wa Kambai (Milima ya Usambara Magharibi), TFCG imeweza<br />

kupanda miti 600,000. Huko Ngulwi (Milima ya Usambara Magharibi), TFGG inajaribu kupanda miti<br />

katika miteremko iliyoachwa wazi bila miti na kuanzisha programu ya utalii wa ikolojia.<br />

Shughuli za Kimataifa Katika Bonde<br />

Inasadikiwa kuwa programu ya usimamizi bora ya maji na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji cha<br />

wakulima wadogo wadogo (RBMSIIP) ndiyo mradi mkubwa zaidi ya yote uliotekelezwa katka Bonde la<br />

Mto Pangani. Huu ni mradi wenye sehemu kubwa mbili ulitekelezwa na Wizara ya Maji na Maendeleo<br />

ya Mifugo kupitia Idara yake ya Rasilimali za Maji, na Wizara ya Kilimo na Chakula kupitia Idara ya<br />

Umwagiliaji. RBMSIIP awali ilibuniwa kama mpango wa miaka sita (1996/97 – 2001/02) ukifadhiliwa<br />

na mfuko wa mkopo wa IDA pamoja na serikali. Kufuatia mapitio ya nusu kipindi katika mwaka 2001,<br />

tarehe mpya ya mradi kukamilika ilipelekwa mbele kwa mwaka mmoja kufikia mwezi Juni mwaka 2003<br />

kukamilisha shughuli zilizopangwa.<br />

Madhumuni makuu ya mradi huu ni kuimarisha uwezo wa serikali kusimamia rasilimali zake za maji<br />

kwa njia shirikishi na pana ambayo italeta usawa, ufanisi na maendeleo endelevu ya rasilimali na<br />

kushughulikia masuala ya mazingira yahusianayo na maji katika ngazi ya taifa na katika mabonde ya<br />

mito Rufiji na Pangani; na kuboresha ufanisi wa umwagiliaji wa miradi iliyoteuliwa ya umwagiliaji wa kiasili<br />

39


wa mashamba ya wakulima wadogo katika mabonde haya mawili yaliyokusudiwa. Mafanikio makuu ya<br />

mradi mpaka sasa ni mapitio ya sera ya maji ya taifa na kuandikwa rasimu ya sera mpya ya maji. Rasimu<br />

hii iliidhinishwa na Serikali ya Tanzania mnamo mwezi Julai 2002.<br />

Mradi wa UNDP GEF wa Bayoanuwai ya kimataifa ya Afrika ya Mashariki (EACBP) ni mradi wa kikanda<br />

unaofadhiliwa na Huduma ya Mazingira Duniani (GEF) kupitia UNDP, na katika Tanzania, unatekelezwa<br />

na Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). Mradi huu unafanya kazi kwa kutumia<br />

miundo ya utawala iliyopo katika kanda hii, na ushirikishaji mkubwa wa jamii kama nguzo yake. Lengo kuu<br />

la mradi ni kupunguza kiwango cha upotevu wa bayoanuwai katika maeneo ya mipakani yaliyochaguliwa<br />

katika Afrika ya Mashariki. Mradi una malengo mawili yanayohitaji utekelezaji wa haraka. La kwanza<br />

ni kuunda mazingira yanayowezesha ambayo mawakala wa serikali na jamii kwa pamoja wanaweza<br />

kurekebisha matumizi ya rasilimali; la pili ni kuweka uwiano wa upatikanaji na mahitaji, mambo ambayo<br />

huathiri hifadhi na matumizi bora ya bayoanuwai. Katika eneo la bonde, EACBP imekuwa ikifanya kazi<br />

katika Hifadhi ya Msitu ya Shegena, ambao ni msitu mkubwa zaidi katika Milima ya Pare ya Kaskazini,<br />

ambapo ilifanyika jitihada ya kuanzisha mfumo wa JFM na jamii za wenyeji.<br />

PRBMP hutoa taarifa nyingi za kisayansi na huanzisha mabaraza ya ushirikishwaji kwa madhumuni ya<br />

kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji wa pamoja unaojumuisha mabadiliko ya hali ya hewa duniani,<br />

matumizi ya maji kwa usawa na utawala bora wa maji kwa ajili ya kujipatia riziki na kutunza mazingira kwa<br />

ajili ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo. Ofisi ya Maji Bonde la Pangani inatekeleza mradi huu kwa msaada<br />

wa kitaaluma kutoka <strong>IUCN</strong> (shirika la kimataifa la kuhifadhi uasili) Shirika la Maendeleo la Uholanzi (SNV)<br />

na asasi isiyo ya serikali inayoitwa PAMOJA. Mradi unafadhiliwa na mpango wa <strong>IUCN</strong> wa hifadhi ya maji na<br />

uasili, serikali ya Tanzania, Mfuko wa Maji wa Umoja wa Ulaya, Mfuko wa Mazingira wa Ulimwengu (Global<br />

Environment Facility) kupitia Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).<br />

C.7 Migogoro<br />

Kama ilivyoelezwa hapo juu, watumiaji wa maji wanapaswa kisheria kupata kibali cha kutumia maji<br />

kitolewacho na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani. Gharama vibali vya kutumia maji zinategemea aina<br />

ya matumizi ya maji. Watumiaji wadogo mara nyingi hawapendi kuomba hati na kulipa ada ya maji,<br />

wakitoa hoja kuwa maji ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’. Kwa mujibu wa Mujwahuzi (2001) kuna hati za<br />

maji 1,028 katika bonde zenye uwezo wa kuchukua mita za ujazo 30.7 kwa sekunde. Hata hivyo, kuna<br />

matoleo ya ziada ya maji 2,094 yenye uwezo wa kuchukua mita za ujazo 40 kwa sekunde. “Migogoro<br />

iliyopo sasa na inayotazamiwa kuwepo hapo baadaye ya matumizi ya maji katika bonde, ni matokeo<br />

ya maendeleo ambayo hayakuratibiwa tangu zamani na yanayoongezeka sasa ya rasilimali za maji za<br />

bonde hususan juu ya Bwawa la Nyumba ya Mungu” (Mujwahuzi, 2001:131).<br />

Migogoro katika Bonde la Mto Pangani, hata hivyo, haiishii kwa watumiaji maji peke yao. Katika mifano<br />

inayotolewa hapo chini, itaonekana wazi kuwa migogoro mingi inayoikabili sekta ya maji ipo pia kwa<br />

sekta nyingine zinazotumia rasilimali, na kati ya matumizi na mahitaji mbalimbali juu ya rasilimali. Aina<br />

za migogoro iliyobainishwa hapa inarahisisha kueleza utatanishi wa hali ya juu na asili ya ushindani<br />

unaoanzisha migogoro. Uchambuzi huu wa Hali halisi unaiweka migogoro hii katika makundi matatu<br />

makuu, yaliyobuniwa ili kutoa maoni ya jumla ya aina mbalimbali na viwango vya migogoro iliyopo katika<br />

bonde. Makundi haya hayatengani, ikichukuliwa kuwa ni kawaida kwa migogoro ya maliasili na mahitaji<br />

ya riziki kuwa matatizo yanayoathiri upatikanaji wa rasilimali yanaingiliana, na mara nyingi yanazidishana.<br />

Hivyo, migogoro ya viwango inaweza kuzidisha migogoro ya umiliki na kinyume chake. Makundi haya ni:<br />

migogoro ya viwango, migogoro ya umiliki na migogoro ya mahali.<br />

Migogoro inayotokana na viwango<br />

Uhusiano kati ya watumiaji wa maji wa ukubwa na uwezo tofauti katika Bonde la Mto Pangani mara<br />

nyingi huelezwa katika namna mbili zinazokinzana. Hivyo, mashamba makubwa yanayotumia mamia ya<br />

lita za maji kwa sekunde na kutumia mifumo ya umwagiliaji yenye ufanisi mkubwa, yanatofautiana kabisa<br />

40


na watumiaji wadogo wanaotumia maji kidogo na mifumo ya umwagiliaji iliyo duni sana. Itambulike kuwa<br />

migogoro kama hiyo hiyo inaweza kutokea pia ndani ya jamii, kati ya taasisi zilizokabidhiwa madaraka<br />

(kama vile serikali za vijiji) na wanajamii wengine. Tofauti kubwa hizi ni sababu ya kutosha kwa migogoro<br />

kuzuka. Mifano ya aina hizi za migogoro ni kama ifuatayo:<br />

Mamlaka ya Maji safi na Majitaka Moshi dhidi ya Kijiji cha Shiri-Njoro<br />

Shiri – Njoro ni kijiji kilichopo kando ya barabara ya Moshi – Arusha, karibu na mji wa Moshi. Moshi ni eneo la mji<br />

linalokua kwa haraka sana likisaidiwa kwa kiwango kikubwa na kilimo. Kadiri mji huu unavyokua, ndivyo mahitaji<br />

ya maji yanavyoongezeka pia. Mnamo mwaka 2000, wahandisi kutoka Mamlaka ya Maji safi na Maji taka ya<br />

Manispaa ya Moshi (MUWSA) walifika Shiri-Njoro na kujengea mfuniko chemchemi kuu ya jamii. Chemchemi<br />

hiyo hutoa lita 218 kwa sekunde, na MUWSA ilipata kibali cha kutumia maji ya lita 116 kwa sekunde. Kijiji<br />

kilikuwa na mifereji mitatu inayotoka katika chemchemi hiyo, kila mmoja ukiwa na kibali cha kuchukua lita 30<br />

kwa sekunde. MUWSA , kwa hiyo, ilitakiwa kuacha kiasi cha maji cha kutosha mahitaji ya mifereji ya jamii.<br />

Hata hivyo, MUWSA, huchukua maji kadiri ya lita 24 kwa sekunde zaidi ya ilivyoruhusiwa. Serikali ya<br />

Kijiji cha Shiri – Njoro inadai kuwa haiwezi kuendelea kutumia kikamilifu mifereji yake mitatu kutoka<br />

kwenye chemchemi, na kwamba jamii pamoja na uchumi wake wa kilimo vimeathirika vibaya. Ni nia<br />

yao kuipeleka MUWSA mahakamani na wanasema “tutauza mbuzi na mbwa wetu ili tupate fedha” za<br />

kufanya hivyo (Wahojiwa: Serikali ya Kijiji cha Shiri – Njoro).<br />

Afgem na wachimbaji wadogo wa Mererani<br />

Tanzanaiti ni madini ya mawe ya thamani yenye rangi ya zambarau ya kibuluu, yanayopatikana Tanzania pekee.<br />

Eneo la ardhi yenye tanzanaiti inasemekana lipo katika eneo la kilometa za mraba 20 tu huko Mererani. Eneo hili<br />

limegawanywa katika safu ya vitalu, A, B, C na D. Kitalu C chenye kilomita za mraba 8 kinasemekana kuwa na<br />

mashapo ya madini mengi zaidi, tani milioni 2.2 za tanzanaiti kwa makisio. Tanzanaiti iligunduliwa katika eneo hili<br />

mwaka 1967, na mji wa Mererani sasa una wakazi 75,000 (Majtenyi na Muindi, 2001). Ni makazi yenye ‘vurugu na<br />

uhalifu yanayoweza kufananishwa na mji wa machimbo ya dhahabu wa California (Lovgren, 2001:1).<br />

Mnamo mwaka 1999, Kampuni ya Kimataifa ya Afrika ya Kusini, (Afgem Ltd.), ilitafuta na kupata miliki ya<br />

miaka 13 ya uchimbaji madini katika Kitalu C.Ilipofika mwaka 2001, Afgem ilishawekeza dola za kimarekani<br />

milioni 8 katika miliki hiyo, na dola nyingine milioni 12 zingefuata mara Kampuni itakapoanza uzalishaji<br />

kamili (Majtenyi na Muindi, 2001).<br />

Hata hivyo, Afgem si wachimbaji madini pekee waliopo Mererani. Kwa kweli shughuli hii inatawaliwa na wachimbaji<br />

wadogo 10,000, ambao wanapinga shughuli za Afgem kwa sababu zifuatazo (Majtenyi na Muindi, 2001):<br />

• Wanaishutumu Afgem kwa kujaribu kuhodhi uchimbaji wa tanzanaiti katika eneo hili, na kwa kujaribu<br />

kuwaondoa wachimbaji wadogo kutoka eneo hili. Afgem inajibu vikali hoja hiyo kuwa: asilimia 70<br />

ya miliki yake inachimbwa kinyume cha sheria. Katika shimo la pili kati ya mawili ya mgodi wake,<br />

wafanyakazi waligundua njia ya chini kwa chini inayokwenda mpaka kwenye eneo la machimbo ya<br />

wachimbaji wadogo katika Kitalu B (Lovgren, 2001).<br />

• Mara baada ya kupata miliki, Afgem ilianza kuzungushia uzio Kitalu C. Hata hivyo wachimbaji<br />

wenyeji wanadai kuwa, mipaka kati ya sehemu hizi nne haiko wazi na kwamba Afgem haina haki ya<br />

kulitenga eneo hilo.<br />

• Inadaiwa kuwa Afgem ilijaribu hata kupiga chapa vito vyake kama alama ya ubora na uhalali.<br />

Wachimbaji wenyeji wanatoa rai kuwa hii kwa kweli, ni hila ya kuhakikisha kuwa vito vyao<br />

vinaonekana kuwa vya bandia, hali inayowalazimisha kuuza vito vyao kwa wakala wa Afgem tu.<br />

Mwaka 2000, mara Afgem ilipotaka kuzungushia uzio eneo la miliki yake, wachimbaji wadogo waliwavamia.<br />

Askari wa ulinzi wa Afgem walifyatua risasi, wakawaua wachimbaji wadogo saba na kujeruhi wengine<br />

wengi. Mwezi Aprili, 2001, lilifanyika shambulio jingine na kijana mmoja aliuawa. Mwezi Mei uliofuata,<br />

wachimbaji wadogo makumi kadhaa walijeruhiwa wakati wachimbaji 400 walipovamia Kitalu C, wakitaka<br />

Afgem iondolewe kwenye eneo hilo (Majtenyi na Muindi, 2001).<br />

41


Kutoka hapo wachimbaji wadogo wakaifungulia mashitaka Kampuni ya Afgem, wakidai kuwa askari wake<br />

wa usalama waliwatesa wachimbaji wadogo sita. Katika hati ya mashitaka mahakamani, walidai pia kuwa<br />

leseni ya uchimbaji ya Afgem ni batili, kwamba viongozi wa Kampuni huwapekua isivyo halali watembea<br />

kwa miguu na wamewazika wachimbaji wadogo 30 katika mgodi uliotelekezwa. Kutokana na kugubikwa<br />

na hali hii ya vurugu, Waziri wa Nishati na Madini akatangaza Mererani kuwa eneo lililodhibitiwa, na<br />

askari polisi hufanya doria katika kipande cha barabara kinachounganisha mji na barabara kuu eneo la<br />

uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro, umbali wa km. 14. Vilevile serikali imeunda kamati mbili<br />

kuchunguza mapigano hayo (Majtenyi na Muindi, 2001).<br />

Afgem inaungwa mkono na Serikali ya Tanzania, ambayo inatoa rai kuwa kuifukuza kampuni hiyo itakuwa<br />

kinyume na sera inayotetea Sheria ya Madini ya Mwaka 1998. Zaidi ya hayo, Mkuu wa Mkoa, anatoa hoja<br />

kuwa kuifukuza Afgem itakuwa sawa na kukubali kushindwa na uhalifu (Majtenyi na Muindi, 2001).<br />

Migogoro inayotokana na umilki<br />

Kitabu hiki kinafafanua umiliki kama haki ya kusimamia rasilimali. Nchini kote Tanzania (na kiasi fulani cha<br />

Kenya), Usimamizi wa Maliasili Kijamii, umeonekana kuwa ni njia bora ya kuongeza ufanisi wa Usimamizi wa<br />

Maliasili za Taifa. Hivyo Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe katika uvuvi, Kamati za Maliasili za Vijiji katika misitu<br />

na Vyama vya Watumiaji Maji kwenye mikondo ya mito, vyote vimeundwa. Ukinzani katika mifumo hii unatokana<br />

na jinsi vinavyotumiwa na kuundwa. Hapa, jamii zinaweza zisihusishwe katika uundaji wa mifumo ya usimamizi,<br />

utekelezaji wake au hata mifumo yake ya sheria. Hali hii inaweza kufanya taasisi hizi zishindwe kutimiza<br />

kazi za usimamizi zilizokusudiwa kutekelezwa. Kwa kuongezea, mitindo ya aina hii ya utekelezaji inaweza<br />

kusababisha taasisi mpya za wenyeji zilizoundwa za usimamizi wa rasilimali kuingia kwenye mgogoro na taasisi<br />

za kijamii zilizokuwepo awali. Litakalokuwa dhahiri kutokana na mifano itakayotolewa hapa chini ni kuwa umiliki<br />

unahusiana na haki ya kuchagua matumizi ya rasilimali, na uwezo wa kuwazuia wengine wasiitumie kwa kazi<br />

tofauti. Hivyo, migogoro ya umiliki pia itahusisha migogoro baina ya aina tofauti za watumiaji wa rasilimali.<br />

Mgogoro wa usimamizi wa Msitu wa Duru – Haitemba<br />

Msitu wa Duru – Haitemba ni msitu wa miombo wenye eneo la hekta 40,000. Katika kingo za msitu<br />

huu kuna vijiji vinane vilivyoanzishwa zamani, ambavyo wakazi wake walikuwa na udhibiti wa msitu –<br />

ingawaje haukuwa imara sana. Utengenezaji mkaa, ulimaji ndani ya msitu na makazi, na uchomaji moto<br />

wa misitu, vyote vilipigwa marufuku. Kutokana na mwongozo wa sera ya serikali, mnamo mwaka 1983 vijiji<br />

hivi vilianza hatua ya kuomba umiliki wa ardhi ya vijiji, ikiwa ni pamoja na miinuko ya misitu inayopakana<br />

navyo. Mnamo mwaka 1985 hata hivyo, Msitu wa Duru – Haitemba uliteuliwa kuwa hifadhi ili kuhakikisha<br />

kuendeleza uzalishaji wake wa siku zijazo, kuhakikisha uhifadhi wake, na likiwa ni jambo geni (wakati ule),<br />

kuufanya msitu ujigharamie wenyewe kwa usimamizi wake kwa kupitia kwa mfano, uwekaji wa vibali vya<br />

kuutumia, au faini. Udumishaji wa uhifadhi wa msitu ulikuwa ufanywe kupitia idadi kubwa ya walinzi wa<br />

msitu. Wawakilishi wa vijiji waliwaonesha waziwazi maofisa msitu wa serikali kuwa ingawaje wanaunga<br />

mkono uhifadhi wa msitu, hawakupenda kuukosa msitu wao kwa ajili ya kufanikisha jambo hili. Mara<br />

tu walinzi wa Msitu walipoanza kazi, shughuli zote za jumuia zilizofanana na hizi ziliachwa. Mashamba<br />

yalilimwa ndani ya msitu, uchomaji mkaa ulianza, ukataji miti ulianza na watu wa nje ya vijiji walipoona<br />

kuwa udhibiti wa serikali ulikuwa ni sawa na kuwa ‘huru-kwa-wote’, walianza kuleta ng’ombe wao msituni<br />

kuwalisha. “Kwa kuondoa hali ya umiliki kwa wenyeji, hata kama ni kwa udhaifu kiasi gani haki za wenyeji<br />

ziliungwa mkono na sheria au zilitekelezwa kwa vitendo, serikali pia iliondoa ulinzi wa kijadi, au utambuzi<br />

katika jamii kwa ujumla kuwa misitu haikuwa mali ya umma…” (Wiley, 1999:53-54). (Rejea: Wiley,1999).<br />

Migogoro baina ya watumiaji rasilimali wa aina tofauti<br />

Jinsi ardhi inavyozidi kuwa adimu katika maeneo ya juu ya Bonde la Mto Pangani, wakulima wanatafuta<br />

ardhi ya ziada na nafasi za umwagiliaji maji kwenye maeneo ya chini. Mapema mwaka 1946, Johnston<br />

alisema kuwa “…kadiri Wachaga wanavyopanua makazi (vihamba) yao kuelekea upande wa chini ya<br />

mitelemko ya Mlima Kilimanjaro, ndivyo watakavyoanza kuwachukia wageni ambao machifu hapo awali<br />

42


waliwaruhusu kufanya makazi” (uk.4). Mgogoro huu baina ya watu wa makabila mbalimbali huzidi pale<br />

ambapo mahitaji ya pande zote ni ardhi na maji. Mahitaji tofauti ya rasilimali hata hivyo, siyo lazima<br />

yaondoe msingi wa mgogoro. Sehemu kubwa ya ardhi katika maeneo ya nyanda za chini za bonde kiasili<br />

zilitumiwa na wafugaji wa Kimasai. Wamasai wanachukulia uhamiaji kuingia kwenye ardhi yao ya jadi<br />

kama uvamizi kwenye eneo lao, na ubadilishaji wa eneo zuri kwa malisho kwa matumizi mengine.<br />

Wilaya ya Simanjiro iko upande wa Kusini wa mji wa Arusha na ndani yake kuna mji wa Machimbo wa<br />

Mererani. Mwaka 1995, asilimia 85 ya wakazi wake 65,000 walikuwa ni wafugaji wa Kimasai. Ufugaji mara<br />

nyingi huchukuliwa kuwa ni njia muafaka zaidi ya matumizi ya ardhi katika ardhi kame na nusu kame za Afrika.<br />

(cf Warren,1995). Mifumo hii, hata hivyo, huchukulia kiwango fulani cha rasilimali kuwa cha kudumu. Taasisi<br />

za usimamizi wa rasilimali za mifugo, mitindo ya maisha inayohusiana na miundo ya kijamii mara nyingi<br />

hujengwa katika msingi wa kuwa eneo lao halitabadilishwa matumizi yake. Hali haikuwa hivyo Simanjiro.<br />

Ardhi ya jadi ya malisho ya Wamasai wa Simanjiro imekuwa katika tishio kutoka pande tatu:<br />

• Kilimo cha Biashara: hadi kufika mwaka 1994, hekta 50,000 za ardhi ya Simanjiro zilikuwa zimetengwa<br />

kwa matumizi ya kilimo cha mashamba makubwa ya kati ya hekta 90 na 13,000. Mashamba haya<br />

yalizalisha zaidi maharage kwa ajili ya kusafirishwa kwenda Uholanzi. Ili kuwakatisha tamaa na kuwazuia<br />

wafugaji kuchungia ng’ombe wao katika mashamba haya, mabaki yote ya mimea huchomwa mara tu<br />

baada ya mavuno (Ole Sikar, 1996:1)). Wenye ardhi pia waliwakamata ng’ombe, waliwatoza faini watu<br />

walioingia bila ruhusa, na ole Sikar anadai kuwa, waliwapiga risasi mifugo na wachungaji wao.<br />

• Uchimbaji madini – wa viwango vidogo na vikubwa, umezuia maeneo makubwa ya ardhi ya<br />

Simanjiro ambayo ama yameharibiwa vibaya kiasi kwamba hayatoi malisho mazuri, au<br />

yamefungwa kabisa kwa kuchungia wanyama.<br />

• Utalii: Kama ilivyokuwa kwa wafugaji ndani na kuzunguka Hifadhi ya Wanyamapori ya Mkomazi,<br />

ardhi ya Simanjiro imetengwa kwa madhumuni ya kuwalinda wanyamapori. Wamasai wa wilaya hii<br />

wanatoa hoja kuwa hii haina umuhimu, ikichukuliwa kwamba wameishi pamoja na wanyamapori kwa<br />

karne nyingi. ‘Kaya zimelazimishwa kuacha kuchunga wanyama wao katika maeneo haya. Wakati<br />

huo huo wanyamapori wameruhusiwa kula majani pamoja na wanyama wafugwao katika maeneo<br />

ya asili ya kuchungia kama vile nyanda tambarare za Simanjiro’ (ole Sikar, 1996:2). Kwa nyongeza,<br />

Wamasai wanalalamika, wanyamapori huambukiza mifugo yao maradhi. Wamasai wa Simanjiro<br />

hawakufidiwa kwa malisho yaliyopotea wala mifugo iliyokufa kwa magonjwa ya wanyamapori.<br />

Mielekeo hii imetokea kinyume na misingi ya sera rasmi ya serikali inayotaka kuwepo,hususan, uwekezaji<br />

wa viwango vikubwa katika kilimo na viwanda unaokusudia kukidhi mahitaji ya nchi zaidi ya maslahi ya<br />

wafugaji wenyeji. Hivyo mikakati inayokusudiwa kufikia malengo ya taifa inaweza kusababisha ugumu<br />

wa kutatua matatizo ya usimamizi wa ndani, na matatizo ya kutumia rasilimali zenye ugumu kuzisimamia<br />

hivyo kusababisha matumizi yaliyokithiri na migogoro mahali hapo. Kwa maana hii, migogoro ya Simanjiro<br />

na maeneo mengine ya Wamasai pia ni migogoro ya viwango, na hutoa kielelezo cha mfano wa jinsi<br />

migogoro ya viwango inavyoweza pia kuwa migogoro ya umiliki wakati huo huo.<br />

Wilaya ya Taita–Taveta nchini Kenya haina kinga ya migogoro hii.Theluthi mbili ya ardhi ya wilaya iko chini<br />

ya wamiliki wawili tu wa ardhi na halmashauri ya jimbo. Matokeo yake, idadi kubwa ya wenyeji wa Taita–<br />

Taveta wanakaa katika maeneo kinyume cha sheria. Vilevile kuna mgogoro mkubwa kati ya watu wasio<br />

na ardhi na wale wanaomiliki ardhi. Migogoro kama hii inaleta utata sana katika usimamizi wa maliasili za<br />

wilaya, tatizo ambalo linakwenda hadi kwenye sekta ya maji.Wakazi wasio rasmi wanaolima katika eneo<br />

hili nusu kame wanategemea zaidi umwagiliaji (Musyoki, pers.comm.). Hata hivyo, hawana vibali vya maji<br />

kama inavyotakiwa wawe, na maji mengi zaidi hata hivyo, yanatumiwa katika maeneo ya juu ya mto na<br />

makampuni makubwa ya katani wilayani. Kwa kiasi fulani katika juhudi za kushughulikia mgogoro wa eneo<br />

hili, serikali imenunua hekta 9,700 katika jitihada za kutafuta ardhi kwa ajili ya wakulima wadogo wadogo.<br />

43


Migogoro kati ya mitazamo inayotofautiana ya usimamizi wa maji: mfano<br />

kutoka Mlima Kilimanjaro<br />

Tagseth (2002) anaonelea kuwa kushindwa kwa mifumo ya utawala rasmi katika bonde kutambua haki za kimila<br />

za maji na utawala wake umekuwa chanzo cha mgogoro kati ya maslahi ya kimila na utawala rasmi wa Bonde la<br />

Mto Pangani. Moja ya njia iliyotumiwa na utawala rasmi katika bonde ni utumiaji wa milango (banio) ya kudhibiti<br />

maji. Inasemekana kuwa, kwa kuwa jamii za wamwagiliaji wa viwango vidogo hawakushirikishwa kwanza,<br />

walichukulia udhibiti huo kama ukiukaji mkubwa wa haki zao za kupata maji. Kwa sehemu kubwa, milango hiyo<br />

imehujumiwa au imeharibiwa kabisa (Mchoro wa 4).Katika maeneo mengine, wanavijiji wamechimba sehemu<br />

mpya za kuchukulia maji katika kingo za mto kuzunguka milango ya kudhibiti maji (Shishira, 2002).<br />

PAMOJA (2002) inaeleza kuwa jamii zilizoko katika bonde zinachukulia kupata maji kama moja ya haki zao za<br />

msingi, na hawaridhiki na jitihada za serikali za kuweka ada na sheria kwa matumizi yake. Sehemu kubwa ya<br />

ukinzani wa jamii kwa utawala wa Bonde la Mto Pangani unatokana na mtazamo wao kuwa watumiaji wakubwa<br />

wa kibiashara wanapendelewa kuliko wao wenye matumizi madogo zaidi ya maji. PAMOJA inadai kuwa utaratibu<br />

wa Serikali wa amri kutoka juu kwenda chini, ambao hauna majadiliano ya pande mbili, huleta ugumu wa<br />

kutatua migogoro. Wanafikiri kuwa njia za majadiliano, zina uwezo wa “kutoa mwelekeo kwenda mbele na<br />

kuyafikia mahitaji na dhamira za watunga sera, watunga sheria na jamii kadhalika” (PAMOJA 2002:2).<br />

Katika Mlima Kilimanjaro, Mwenyekiti wa kamati ya mfereji alikuwa akisimamia kijadi mfereji wa umwagiliaji.<br />

Daima wenyeviti huwa wanaume, na wanapatikana kutokana na ukoo wa mtu ambaye ndiye aliyechimba<br />

mfereji huo. Mfereji hupitia kwenye ardhi ya watumiaji mbalimbali maarufu wa maji, wengi wao wakiwa wanahitaji<br />

kuyatumia kwa madhumuni ya umwagiliaji. Ili kuweza kupatiwa maji, watumiaji lazima wawachangie<br />

wafanyakazi wa ukarabati ambao mara kwa mara hufanya doria kwenye mfereji kukagua uharibifu. Sheria<br />

mbalimbali za ziada zinasimamia matumizi ya maji, kama vile nyakati ambazo maji yanaweza kuchukuliwa,<br />

zamu za matumizi ya maji baina ya watumiaji na kadhalika. Sheria hizi sio kuwa hazibadiliki. Hii ni muhimu<br />

kwa sababu baadhi ya watu walio kando kando ya mifereji wanaweza kuhitaji maji kidogo kuliko wengine,<br />

wakati wengine wanahitaji maji mengi zaidi. Gillingham (1999) anaelezea njia tano ambazo watu wanaohitaji<br />

maji zaidi kuliko vibali vyao vinavyoruhusu wanaweza kupata maji ya ziada: ya kwanza ni ‘kuazima’<br />

maji - mtu anayehitaji maji zaidi anaweza kuazima maji kutoka kwa mtu anayemfahamu kuwa anahitaji maji<br />

kidogo. Hii ndiyo njia inayotumika zaidi ya kupata maji ya ziada kwa mtu anayehitaji. Njia ya pili ni ya kupata<br />

maji ya ziada kutoka kwenye mfereji wa jirani. Njia ya tatu ni kununua maji – hapa, mtu aliyetumia maji<br />

kidogo kuliko anayohitaji anaamua kuuza yaliyobaki kwa mtu anayemjua kuwa anahitaji maji mengi kuliko<br />

mgao wake. Kwa vile maji yanachukuliwa kuwa ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’, hivyo si halali kuyanunua<br />

wazi wazi. Wauzaji hukwepa ukweli huu kwa kutoa kazi kwa mnunuzi, na hivyo wakiulizwa husema kuwa<br />

mnunuzi anaazima mabaki ya mgao wao wa maji. Njia ya nne ni kumwagilia usiku wakati ambapo hakuna<br />

mgao wa maji. Mwisho, njia ya tano ya kupata maji ya ziada ni kwa kuiba, kwa mfano kumwagilia wakati ni<br />

siku ya zamu ya mtu mwingine, ingawaje hii haitokei mara kwa mara (Gillingham, 1999).<br />

Sheria kuweza kubadilika badilika, Gillingham (1999) anaeleza, ‘….ni muhimu kwa ufanisi wa mgao<br />

na uendelevu wa mfumo wa umwagiliaji …… kama watumiaji wote wa mifereji wangelazimika kutumia<br />

mgao wao rasmi tu, mfumo wa umwagiliaji wa kutumia mifereji ungetosheleza mahitaji ya umwagiliaji<br />

ya watumiaji mifereji wachache sana’. Gillingham anasema mfumo huu ni wa kutegemewa, kwa sababu<br />

wizi hauruhusiwi chini ya mfumo rasmi wa ugawaji wala chini ya kanuni za kazi – laiti kama mfumo huu<br />

ungekuwa si wa kutegemewa, watu wasingechangia ukarabati wa mifereji. Uhusiano mkamilifu baina ya<br />

sheria rasmi na za kazi unachukua muda mrefu kukua – mifereji ya kwanza kwenye Mlima Kilimanjaro<br />

ilichimbwa katika karne ya 18. Katika maeneo ya nyanda za chini, ambako makazi yameanza hivi<br />

karibuni, hali ya hewa imekuwa kavu zaidi, watu wametawanyika zaidi na tofauti za kijamii zimekuwa<br />

kubwa zaidi, hivyo uhusiano kati ya sheria rasmi na za kazi sio mkubwa sana.<br />

Sheria hizi zinasisitiza usawa wa jamii na kupunguza migogoro. Hazikai vizuri na sheria mpya, zinazoshinikizwa<br />

kutoka nje ambazo zinataka matumizi bora ya maji. Kwa nyongeza, sheria hizi mpya zinataka kuanzisha<br />

Vyama vya Watumiaji Maji (WUAs), ambavyo si sawa na Kamati za Mifereji. Vyama vya watumiaji maji<br />

44


vinategemewa kukusanya ada kutoka kwa watumiaji maji ambazo zitachangia kulipia kibali cha kutumia maji,<br />

inayopatikana kutoka Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani. Katika utamaduni ambapo maji yanaonekana kuwa<br />

ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’, wazo kuwa ni lazima maji yalipiwe halina mantiki. Kwa nyongeza, Gillingham<br />

anahofia kuwa sheria zilizoamriwa kutoka nje hazielekei kufanikiwa kuliko zile zilizotokea ndani ya jamii,<br />

ambazo zimebadilishwa kulingana na sifa za utamaduni na mazingira ya jamii kwa muda wa kipindi kirefu.<br />

Gillingham anaamini kuwa kutooana kati ya mchakato wa usimamizi katika ngazi ya wenyeji na ile ya ngazi<br />

ya nje kunaweza kuhatarisha mafanikio ya juhudi za usimamizi zilizoanzia nje.<br />

Migogoro inayotokana na mahali<br />

Watumiaji maji waliopo katika maeneo ya juu ya mto wapo mahali pazuri zaidi pa kupatia maji kuliko watumiaji<br />

wa eneo la chini. Kama msingi wake mkubwa, matatizo haya yanaonekana katika mifereji ya umwagiliaji<br />

ambapo watumiaji walio karibu na chanzo cha maji wanaweza kulima mazao yanayohitaji maji mengi sana.<br />

Kwa mfano, mpunga wa kumwagiliwa unahitaji lita 3,000 za maji kutoa mavuno ya kilogramu moja. Watumiaji<br />

waliopo mwishoni mwa mfereji, wanalazimika kulima mazao yanayohitaji maji kidogo. Matatizo makubwa<br />

yanayoikabili mitambo ya umeme wa maji iliyoko katika maeneo ya chini ya mto ni mfano mwingine.<br />

Skimu ya Umwagiliaji ya “Lower Moshi”<br />

Kabla ya kuanzishwa kwa Skimu ya Umwagiliaji ya “Lower Moshi” mnamo mwaka 1987, kulikuwa na kiwango<br />

kidogo sana cha kilimo cha mpunga wa umwagiliaji katika eneo hili, na wakulima walitegemea kuvuna kadiri ya<br />

tani 2 za mpunga kwa hekta. Kufuatia kukamilika kwa skimu hiyo, mavuno yaliongezeka kufikia tani 8 kwa hekta,<br />

hali iliyoshawishi wakulima wa nje ya mradi kujaribu kuiga mbinu za kilimo za skimu hiyo. Matokeo yake, mahitaji<br />

ya maji yaliongezeka sana, kiasi cha kusababisha tatizo la kudumu la upungufu wa maji katika maeneo ya upande<br />

wa chini ya skimu. Skimu yenyewe imekabiliwa na upungufu wa maji kwa sababu ya matumizi makubwa ya maji<br />

katika maeneo ya juu, na imelazimika kupunguza eneo la umwagiliaji kutoka hekta 2,300 hadi 647 mnamo mwaka<br />

1994. Wakulima waliohusishwa katika Skimu hawakufurahia kabisa hali hiyo, walieleza kuwa mgao wao wa maji<br />

ulifuata programu iliyopangwa vizuri. Watumiaji wa maeneo ya upande wa juu hawakuwa na programu kama hii,<br />

hivyo walisababisha upungufu wa maji katika eneo la Skimu. Zaidi ya hayo, wakulima walidai kuwa watumiaji maji<br />

wa maeneo ya upande wa juu walikuwa na ushawishi katika serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM), (chama<br />

tawala cha Tanzania), hivyo wasingeweza kubughudhiwa (Mujwahuzi, 2001; 134 na 136).<br />

Mgogoro baina ya wamwagiliaji wadogo na Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania<br />

TANESCO inadai kuwa inahitaji angalau mita za ujazo 40 kwa sekunde kuendesha mitambo ya umeme<br />

wa maji ya Maporomoko ya Pangani . Baada ya maji kufunguliwa kutoka katika Bwawa la Nyumba ya<br />

Mungu na kuingia mto Pangani, maji ya nyongeza yanaungana na mto huo kupitia vijito vyake vichache.<br />

Hata hivyo hadi maji yafikapo kituo hicho, mara nyingi huwa hayatoshelezi kuendesha mitambo. “Wakati<br />

mwingine tunakuwa na maji kidogo mno kiasi kwamba inabidi tufunge kituo na kuacha maji kujikusanya<br />

kwa usiku mzima, ili tuweze kufungua tena asubuhi” (Lugeiyamu, Mhojiwa).<br />

Kadiri ardhi inavyokuwa adimu zaidi na zaidi katika sehemu za juu za bwawa la Nyumba ya Mungu,<br />

kilimo katika eneo la upande wa chini wa bwawa pia kimeongezeka. Kwa kuwa hali hapa ni ya joto zaidi<br />

na mvua ni haba, haja ya kumwagilia ni kubwa zaidi. Kwa hiyo, Meneja wa kituo cha uzalishaji umeme<br />

cha maporomoko ya Pangani analalamikia uchukuaji wa maji usiodhibitiwa ambao unasababisha wao<br />

kupata kiasi cha maji kisichotosheleza mahitaji. Anafafanua kuwa wakati ambapo maji kwa ajili ya<br />

mitambo yake yamepungua, maeneo ya umwagiliaji hayapungukiwi. “Wamwagiliaji wadogo hawatumii<br />

umeme, hivyo hawayaelewi matatizo haya” (Lugeiyamu, Mhojiwa).<br />

Wakati huo huo, udhibiti wa uchukuaji wa maji umepungua. Wakati mradi mpya wa Maporomoko ya<br />

Pangani ulipojengwa, kulikuwa na fedha za kujengea milango (banio) ya kudhibiti maji kwenye sehemu<br />

muhimu za kuchukulia maji kutoka mitoni na ufuatiliaji wake. Kwa vile utoaji wa fedha umepungua,<br />

ufuatiliaji umekuwa siyo wa mara kwa mara, milango ya kudhibiti uchukuaji maji imeharibiwa na /au vituo<br />

vipya vya kutolea maji vimeanzishwa kwenye kingo za mito.<br />

45


Matokeo ya hali hii ni kupungua kwa uzalishaji wa umeme. Katika mwezi Aprili mwaka 1999, kituo cha uzalishaji<br />

umeme cha maporomoko ya Pangani kilizalisha kWh milioni 45. Mwezi Aprili mwaka 2002 zilizalishwa kWh<br />

milioni 25. Ni dhahiri kuwa hili lina athari ya wazi kwenye uvutiaji wa uwekezaji kwenye mtambo. TANESCO,<br />

kwa sasa, inataka kubinafsishwa. “Kama mtambo wa kuzalisha umeme wa Nyumba ya Mungu una uwezo<br />

wa kuzalisha MW 8 na tunaweza kutoa 3 tu, ni nani atakayewekeza kwetu?” (Lugeiyamu, Mhojiwa).<br />

C.8 Majumuisho ya hoja<br />

Kwa undani wake, matatizo yanayokabili matumizi ya rasilimali katika Bonde la Mto Pangani yanahusiana<br />

na ongezeko la watu katika mazingira ya viwango vikubwa vya umasikini. Umasikini na uharibifu wa<br />

mazingira mara nyingi huonekana vinahusiana (cf. WCED, 1987). Matatizo ya kusimamia Rasilimali za<br />

Jamii (CPRs) mara nyingi yanafikiriwa kuongezeka kunapokuwa na idadi kubwa ya watu wanaohusika,<br />

hususan pale umoja wao wa kijadi unapokuwa dhaifu (cf. Ostrom, 1990). Muundo na kazi za utafutaji<br />

maisha vijijini unaweza kuhatarishwa endapo uwezo wa watu wa vijijini wa kutawala na kujihakikishia<br />

njia za kutosha za kujipatia riziki zitakuwa hatarini.<br />

Sura hii imepitia matatizo haya kwanza kwa kuainisha ‘vivutio’ vikuu ndani ya bonde. Baada ya hapo<br />

ikaendelea kuangalia migogoro mbalimbali iliyomo baina yao. Dondoo muhimu zinazoweza kupatikana<br />

kutokana na majadiliano haya ni kama ifuatayo:<br />

• Shughuli muhimu katika bonde ni pamoja na shughuli za viwanda (umeme, madini na kilimo),<br />

kilimo (mashamba makubwa na madogo, yote kwa kiasi kikubwa yanategemea umwagiliaji),<br />

shughuli za ufugaji (hususan katika nyanda za chini), na shughuli za mijini ambazo zinakua.<br />

Sura hii ililenga kimsingi kwenye matumizi ya maji ya shughuli hizi. Waliofanya kazi kati ya<br />

shughuli hizi mbalimbali na wingi wa maliasili ndani ya bonde hili ni pamoja na mashirika yasiyo<br />

ya kiserikali na wakala wa wahisani wa kimataifa. Mamlaka yao kimsingi ni kuhifadhi na/ au<br />

kuendeleza na kuwezesha upatikanaji wa riziki vijijini.<br />

• Ni muhimu kutambua kuwa idadi ya watu katika bonde hili ni kubwa, na kwamba kwa wengi wao, riziki<br />

hupatikana kutokana na kilimo, na kwamba kuna mengi yanayoashiria kwamba wako hatarini kiuchumi.<br />

Kwa kuongezea, utofauti na utajiri wa rasilimali za bonde hili una maana kuwa wenye shughuli kubwa<br />

kubwa wanavutiwa na bonde hili, na uwekezaji wa kutosha umefanyika. Kati ya shughuli hizi za viwango<br />

vikubwa na shughuli za viwango vidogo vya kujipatia riziki, kuna mwanya mkubwa wa migogoro.<br />

• Sura hii inaigawa migogoro katika makundi makuu matatu yanayohusiana. Kundi la kwanza<br />

linahusiana na migogoro ya viwango, ambapo imeelezwa kuwa watumiaji wadogo wadogo<br />

mara nyingi inabidi washindane dhidi ya watumiaji wakubwa kwa rasilimali hizo hizo. Kundi<br />

la pili linahusiana na migogoro ya umiliki. ‘Umiliki’ hapa una maana ya haki ya mtu kusimamia<br />

rasilimali zake, na mgogoro hutokea baina ya vyanzo tofauti vya usimamizi na kipaumbele.<br />

Daraja la tatu la mgogoro linahusiana na mahali. Hapa, jinsi mahali pa kundi la watumiaji wa<br />

rasilimali panavyoweza kuwaingiza kwenye mgogoro na watumiaji wa mahali pengine, ni jambo<br />

lililoangaliwa. Mfano mzuri wa mgogoro kama huo ni ule baina ya watumiaji wa maeneo ya juu<br />

na wale wa maeneo ya chini ya mto.<br />

• Kwa hiyo, ni wazi kuwa tofauti ya rasilimali katika Bonde la Mto Pangani husababisha pia aina<br />

tofauti za migogoro. Changamoto ya Bonde la Mto Pangani ni kwa kiasi gani menejimenti<br />

inaweza kushughulikia migogoro ya viwango vyote na matatizo ya ugawaji wa maliasili<br />

yanayoambatana.<br />

46


D<br />

Usimamizi wa Maliasili katika<br />

Bonde la Mto Pangani<br />

D.1 Utangulizi<br />

Sura hii inaangalia Usimamizi wa Maliasili za Bonde la Mto Pangani. Katika sehemu ya kwanza, utawala<br />

‘rasmi’ wa bonde unaangaliwa. Mikono mingi ya serikali inalitawala bonde hili. Hili pekee ni tatizo kwa<br />

sababu inaweza kumaanisha kuwa juhudi za tawi lolote zinaweza kudhoofisha shughuli za matawi mengine.<br />

Kwa mfano, juhudi za hifadhi ya maji zinaweza kudhoofishwa na shughuli za maendeleo ya umwagiliaji.<br />

Zaidi ya hayo, serikali kuu inaweza kutaka kutekeleza sera za taifa katika bonde bila kuzingatia hali ya<br />

mahali, mahitaji na matatizo ya rasilimali. Mwishowe, humaanisha pia kupatikana usimamizi ambao kwa<br />

kiwango kikubwa ni mwelekeo wa kisekta unaosababisha,idara za misitu kutokuwa na habari, kwa mfano,<br />

kuhusu juhudi za uendelezaji wa wanyamapori. Wakati juhudi za uendelezaji wa wanyamapori zinaweza<br />

zisihusike na misitu moja kwa moja, huwa zinahusika na usimamizi wa jumla wa bonde, ambao sekta hizi<br />

zote ni sehemu yake muhimu. Sehemu ya kwanza ya Sura hii inazingatia shughuli za sekta kuu mbili katika<br />

Bonde: maji na misitu, na kuzitathmini katika mtazamo wa utoaji huduma ya usimamizi.<br />

Sehemu ya pili inazitathmini shughuli za usimamizi katika ngazi ya jamii, wakati ya tatu inazingatia<br />

usimamizi wa bonde kuvuka mipaka ya nchi. Sehemu ya nne inashughulikia matatizo ya ufuatiliaji na<br />

ukusanyaji data katika bonde. Sehemu ya mwisho itatoa muhtasari wa matokeo ya Sura hii.<br />

D. 2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na sera<br />

Utawala wa maji: sheria na sera<br />

Sheria mama ya kusimamia rasilimali za maji Tanzania ni Sheria ya Usimamizi wa Rasilimalui za Maji ya<br />

mwaka 2009 inayoweka misingi ya kutekeleza Sera ya Maji 2002. Sheria hii inafuta sheria ya zamani ya<br />

Udhibiti wa Matumizi ya Maji ya mwaka 1974. Sheria ya Udhibiti wa maji ilianzisha mfumo wa kusimamia<br />

rasilimali za maji kwa kufuata mipaka ya mabonde. Kwa mujibu wa sheria hiyo na marekebisho yake<br />

ya 1981 mabonde 9 yalianzishwa na kuchapishwa katika gazeti la serikali lakini ilichukua miaka 10 kwa<br />

mamlaka (ofisi za maji) za kudhiti matumizi ya maji kuanzishwa Ofisi ya Maji Bonde la Pangani ilikuwa<br />

ya kwanza kuanzishwa mwaka 1991 ikifuatiwa na Ofisi ya Maji Bonde la Rufiji mwaka 1993, kufikia 2004<br />

ofisi za mabonde yote 9 zilikuwa zimeanzishwa. Kuanzishwa kwa ofisi ya Pangani ilitokana na shauku ya<br />

wafadhili wa mradi wa umeme kwenye maanguko ya Pangani kuwa maji yasingetosha kwa mradi huo<br />

kama kusingekuwa na udhibiti wa matumizi ya maji ya mto Pangani na wakati huohuo migogoro mingi ya<br />

matumizi ya maji inajitokeza na kuongezeka katika mabonde ya Pangani na Rufiji.<br />

Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji inaweka mfumo wa kisheria na kitaasisi kwa usimamizi<br />

wa mabonde ya mito kama sera inavyoelekeza na imeweka ngazi tatu za usimamizi: Taifa, Bonde na<br />

Mabonde madogo. Serikali za mitaa na vyombo vya kijamii au jumuiya za watumia maji ni washirika<br />

wakuu katika baadhi ya taasisi hizi na Waziri anaweza kukasimu baadhi ya majukumu kwa vyombo hivi.<br />

Maji ni rasilimali ya umma na yamekasimiwa kwa Rais kwa faida ya raia; hivyo kitaifa Waziri mwenye<br />

dhamana ya maji ni msimamizi mkuu wa shughuli zote za rasilimali za maji na mwenye mamlaka ya<br />

rufaa. Waziri anao wajibu wa kutayarisha wa Sera ya Taifa na mkakati, kuteua Wajumbe wa Bodi ya Maji<br />

ya Taifa, Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji na Maafisa wa Maji wa Bodi za Madonde. Waziri anaunda<br />

Bodi za Maji za Mabonde na kamati za mabonde madogo na kuwezesha uratibu na upangaji mipango<br />

wa kisekta. Waziri anasaidiwa na Mkurugezi wa Rasilimali za Maji, kushauriwa na Bodi ya Maji ya Taifa<br />

katika masuala ya uratibu wa sekta mbalimbali kuhusu mipango na usimamizi shirikishi wa rasilimali za<br />

47


maji. Mkurugenzi ni mshauri mkuu wa Serikali juu ya masuala yote ya rasilimali za maji, anasimamia na<br />

kuratibu shughuli za Bodi za Mabonde, kuandaa Mpango wa Kitaifa wa Rasilimali za Maji na kutayarisha<br />

mkakati wa utekelezaji wake, kuratibu utayarishaji wa mipango ya mabonde na kwa ujumla kuhakikisha<br />

uratibu wa maendeleo ya rasilimali za maji, usimamizi na udhibiti wake.<br />

Bodi mpya za maji zina mamlaka katika mambo yote yanayohusu ugawaji usimamizi na kulinda rasilimali<br />

za maji katika bonde husika na uandaaji wa sera na mipango inayolenga katika usimamizi na uendelezaji<br />

wa rasilimali za maji na kuzuia uchafuzi wa maji. Bodi za maji zina uwezo wa kisheria na kiutendaji katika<br />

kuandaa mipango ya maji inayojumuisha mipango ya sekta zingine na mipango ya wilaya. Bodi huratibu<br />

shughuli za sekta mbalimbali katika mambo yanayohusu maji, zinaidhinisha utoaji wa vibali vya kutumia<br />

maji, hufuatilia, hutathmini na kuidhinisha ujenzi wa miundo mbinu ya maji na kwa ujumla hufuatilia hali ya<br />

mito, maji chini ya ardhi, mabwawa na maziwa, ardhioevu na hutekeleza sheria. Bodi za maji humshauri<br />

mkurugenzi wa maji na huratibu shughuli za kamati za mabonde madogo. Afisa wa Maji wa Bonde ni<br />

mtendaji mkuu wa bodi mwenye majukumu ya kusimamia shughuli zote za bodi na ni katibu wa bodi. Bodi<br />

ya maji ya Pangani inategemewa kufanya kazi kwa kufuata mfumo wa kitaasisi kama unavyoelekezwa na<br />

Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya mwaka 2009.<br />

Ofisi ya Maji Bonde la Pangani hushawishi uundaji wa vyombo vya watumiaji maji na kwa kawaida wakulima<br />

wadogo wadogo wanaotumia chanzo kimoja cha maji na miundombinu moja ya kuchukua maji wanajiunga<br />

katika umoja wa watumiaji maji ambao huomba kibali cha kutumia maji kwa niaba ya wanaumoja wake.<br />

Ingawa vyombo vya watumiaji wa maji ni vya manufaa kwa washiriki mitazamo ya watu wengine ni kuwa<br />

vyombo vya watumiaji wa maji ni vya manufaa kwa ofisi ya bonde kwani hukusanya ada ya maji kutoka<br />

kwa mtumiaji maji mmoja mmoja. Umoja wa watumiaji wa maji hukusanya maduhuli kutoka kwa washiriki<br />

wake kwa ajili ya uendeshaji wa mradi na kiasi kidogo hutumika katika kulipia ada ya hutumia maji.<br />

Ofisi ya Maji ya Bonde inahimiza uundaji wa Vyama vya Watumiaji Maji (WUAs), na kwa hakika, maji kwa<br />

ajili ya umwagiliaji yanaweza kuombwa na vyama hivyo pekee. Hili linasemekana kuwa linarahisisha<br />

shughuli za utawala, kwa sababu Ofisi ya Bonde itakuwa inashughulika na Vyama badala ya watu<br />

wengi binafsi. Vyama vya watumiaji maji vinatarajiwa kukusanya ada kutoka kwa watumiaji maji ambayo<br />

hatimaye itatumika kulipia hati zao za maji.<br />

Mwanzoni mwa miaka ya 1990, wenye hati za maji katika Bonde la Mto Pangani walitumia jumla ya mita<br />

za ujazo 33.4 kwa sekunde, lakini ukaguzi uliofanywa na Ofisi ya Bonde mwaka 1992/93 ulionesha kuwa<br />

matumizi halisi yalifikia mita za ujazo 48 kwa sekunde (Mujwahuzi, 2002). Kuna hati za maji 567 za kudumu<br />

katika mikoa minne ya Tanzania ambayo imo katika Bonde la Mto Pangani, wakati ambapo hati za muda<br />

zilizotolewa ni 300. Hata hivyo, kuna karibu matumizi mara mbili zaidi yanayofanyika bila ya hati za maji<br />

(Jedwali la 6). Karibu asilimia 46 ya hati za kudumu na za muda zilizotolewa zinatoka mkoa wa Kilimanjaro.<br />

Karibu asilimia 66 ya matumizi ya maji yasiyo rasmi kisheria katika bonde hutokea katika mkoa huu.<br />

Kwa hiyo ni wazi kuwa kuna matatizo makubwa katika kufuatilia matumizi ya maji na katika kutekeleza vifungu<br />

vya sheria ya maji ya Tanzania. Baadhi ya matatizo yanayoikabili Ofisi ya Maji ya Bonde ni haya yafuatayo:<br />

• Ingawa kuna vituo vingi vya upimaji/ufuatiliaji katika eneo lote la bonde, uendeshaji wake siyo<br />

sahihi, na mara nyingi data zinapingana kwa sababu vituo vinakwama kufanya kazi. Ufuatiliaji<br />

kwa kutumia watu pia unafanyika lakini wakusanyaji data mara nyingi hawalipwi vizuri na hukosa<br />

motisha ya kukusanya data hizi. Matokeo yake, hati za maji hutolewa bila kujua kwa hakika kiasi<br />

cha maji kinachopaswa kugawanywa. Data muhimu za ziada, kama vile data za mtiririko wa maji<br />

kwa ajili ya mahitaji ya mazingira, hazipatikani, na Ofisi ya Bonde haifahamu ni kiasi gani cha maji<br />

ni lazima kibakizwe katika bonde kwa matumizi ya mifumo ikolojia (Sarmmet, Mhojiwa)<br />

• Kwa vile matumizi mengi ya maji hayana hati za kisheria, si rahisi kwa Ofisi ya Maji Bonde la<br />

Pangani kujua kiasi halisi cha maji kinachukuliwa.<br />

• Ofisi ya Maji ya Bonde la Mto Pangani na ofisi za mabonde mengine hazina uwezo wa kitaasisi<br />

na kifedha wa kusimamia kufuatilia na kudhibiti matumizi yote ya maji katika bonde. Ndiyo maana,<br />

milango mingi ya kudhiti maji iliyojengwa na ofisi ya bonde la Pangani katika makutano ya mifereji<br />

na mito mwaka wa 1994 ilibomolewa na wananchi ambao hawakutambua matumizi yake na<br />

48


ambao walikuwa hawataki kulipa ada za maji. Uharibufu huu ungeweza kuzuilika kama wahusika<br />

wangeelewa manufaa ya milango hiyo na kama serikali za mitaa zingehusishwa mapema katika<br />

kuandaa mpango wa ujenzi huo.<br />

• Ofisi ya Maji Bonde la Pangani inapaswa ijitegemee kiutawala na kifedha. Hata hivyo, watumiaji wengi<br />

wa maji wanaamini kuwa maji ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’, na hukataa kulipia hati zao za maji, pamoja<br />

na viwango kuwa vya chini sana. Hivyo Ofisi ya Bonde inakabiliana na matatizo makubwa ya uhaba wa<br />

fedha. Sheria iko kimya kuhusu jinsi ya kuwashughulikia wadaiwa. Matokeo yake, karibu asilimia 60 ya<br />

madai ya ada ya matumizi ya maji kwa mwaka hayalipwi (Sarmett na Kamugisha, 2002).<br />

• Sheria ya usimamizi wa rasilimali za maji hajaweka uhusiano wa moja kwa moja kati ya Bodi ya Maji<br />

Bonde la Pangani na Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs) au ngazi za chini za utawala kusaidia<br />

uwakilishi katika bodi ya bonde na kamati za mabonde madogo. Hata hivyo, Waziri anaweza<br />

kukasimu utekelezaji wa jukumu lolote kwa mamlaka ya serikali za mitaa kama ilivyoelekezwa<br />

katika sheria. Maafisa wa Maji si sehemu ya mamlaka za serikali za mitaa na hawana majukumu<br />

sawa katika bonde, lakini ni muhimu wakafanya kazi pamoja kwa misingi ya shabaha moja lakini<br />

yenye utekelezaji tofauti. Kufanya kazi na LGAs na mkusanyiko wa wadau wengine na mahitaji<br />

mbalimbali ya kisekta ni changamoto kwa Maafisa wa Maji ambao wanatakiwa kuwa weledi kwa<br />

mtazamo huu. Kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji, Bodi za Mabonde<br />

zinatakiwa kujumuisha mipango ya Wilaya ndani ya mipango ya usimamizi wa rasilimali za maji<br />

wa mabonde yao ambayo itakuwa na nguvu za kisheria kwa wahusika wote ndani ya bonde.<br />

• Mipaka ya kisheria ya utawala wa Ofisi ya Bonde ni Bonde la Mto Pangani, ambalo halifuati<br />

mipaka rasmi ya kiutawala. Katika bonde hili, Ofisi ya Maji Bonde Pangani inatakiwa kufanya kazi<br />

na serikali za mitaa nyingi sana.<br />

• Mabonde ya mito yana idadi kubwa ya rasilimali zinazohusiana na mabadiliko ya rasilimali moja<br />

yanaweza kuwa na athari kwa rasilimali nyingine. Katika Bonde la Mto Pangani, upangaji wa mipango ni<br />

wa mgawanyiko, kwa misingi ya kisekta, kimkoa au kiwilaya. Bodi za maji zina mamlaka na zinaagizwa<br />

na sheria ya maji kuandaa mipango jumuishi ya usimamizi wa rasilimali za maji katika mabonde yao<br />

ambayo itakuwa na nguvu za kisheria kwa uendelezaji, usimamizi na utunzaji wa maji wowote.<br />

Utawala wa maji nchini Kenya unaongozwa na Sheria ya Maji ya Mwaka 2002 (RoK, 2002). Mpaka sasa,<br />

kadiri usimamizi wa mabonde kwa mapana unavyohusika (kipengele ambacho kimo katika Sheria ya Maji),<br />

Mkakati wa Usimamizi wa Rasilimali za Maji wa Taifa (RoK, 2003) unakuwa na umuhimu mkubwa.<br />

Sheria ya Maji ilianzisha Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji (WRMA) yenye jukumu la<br />

usimamizi na utawala wa sehemu kubwa ya rasilimali za maji za Kenya. Kuna asasi kadhaa zilizopangwa<br />

chini ya WRMA, ambazo zinaelezwa katika Kisanduku kifuatacho. Hapa, ushirikishwaji wa wadau katika<br />

usimamizi na utawala wa Sheria unazingatiwa.<br />

Kitengo cha usimamizi ambacho WRMA inategemewa kulenga ni eneo la chanzo cha mto, ambalo linatakiwa<br />

kuliaainisha. Kila eneo la chanzo cha mto linapaswa kuwa na Kamati ya Ushauri (CAAC) ya watu 15, walioteuliwa<br />

na WRMA, na kuwa na wawakilishi kutoka sekta mbalimbali za wadau binafsi na za umma. Chini ya Sheria ya<br />

Maji, CAAC ina wajibu wa ‘kuwashauri maafisa wa mamlaka hii (WRMA) katika ofisi stahiki ya mkoa kuhusu:<br />

a) hifadhi, matumizi na mgao wa rasilimali ya maji;<br />

b) utoaji, urekebishaji, ufutaji au ubadilishaji wa kibali chochote [cha maji]; na<br />

c) masuala mengine yoyote yanayoambatana na usimamizi mzuri wa rasilimali ya maji (RoK, 2000: 953).<br />

Mamlaka halisi ya usimamizi wa Sheria ya Maji (ikiwa ni pamoja na uwezo wa kumtia mtu nguvuni, kushtaki<br />

na kutoa vibali vya maji) yako mikononi mwa WRMA. Aidha imepewa wajibu wa kuendeleza mkakati wa<br />

maji wa taifa ambao ulichapishwa mwaka 2003 (Rok, 2003). Mkakati huo unaelezea uhusishwaji wa<br />

wadau katika usimamizi na utawala wa maji ya Kenya kama ifuatavyo: Sera ya Maji ya Taifa (NWP)<br />

inatambua hali ambapo mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) na jamii zitakuwa na majukumu makubwa<br />

katika sekta ya maji ikiwa ni pamoja na usimamizi wa rasilimali za maji. Kwa hali hii itahitajika watendaji<br />

wapya kupatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo …. (RoK 203:73).<br />

49


Jedwali la 6: Hati za kutumia maji katika Bonde la Mto Pangani (Tanzania), Mei 2003<br />

Mkoa Hati za Hati za Maombi Bila Hati Jumla<br />

kudumu muda ya hati ya hati zisizotumika<br />

kwa muda<br />

Arusha 184 135 57 141 144 661<br />

Manyara 3 3 2 10 0 18<br />

Kilimanjaro 264 138 118 1224 203 1947<br />

Tanga 116 24 25 488 118 771<br />

Jumla 567 300 202 1863 465 3397<br />

Dondoo<br />

Hati ya kudumu: Hati ya iliyotolewa kuwa ya kudumu na inayotumika.<br />

Hati ya muda: Hati iliyotolewa kwa muda, ili mwombaji amalizie ujenzi wa mifumo ya kupitisha maji kama<br />

inavyotakiwa na PBWO. Kwa kawaida mtumiaji hupewa mwaka mmoja wa kufanya hivyo, baada ya muda<br />

huo lazima aombe kuongeza muda kama hajamaliza.<br />

Maombi ya hati: Ombi linalotolewa kwa PBWO, ambayo inashughulikia maombi hayo kwa kufuata taratibu<br />

zilizopo kabla ya kufikisha katika kikao cha PBWB kwa ajili ya idhini na utoaji wa kibali.<br />

Bila ya hati: hawa ni watumiaji wasio na hati ya kisheria (wanatumia bila hati). Nusu ya hawa wanakisiwa kila<br />

mmoja anachukua lita 10 kwa sekunde; makadirio haya yanahitaji kuthibitishwa.<br />

Hati zisizotumika kwa muda: Hizi ni hati zilizotolewa, lakini wamiliki wake kwa sasa hawatumii maji. Kama<br />

hati haitumiki kwa miaka mitatu, hufutwa. Tathmini ya hati na matumizi ya maji inahitajika ili kubainisha idadi<br />

ya hati zilizolala katika bonde hili, na kupitisha uamuzi kama zifutwe au la.<br />

Rejea: Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani.<br />

Mkakati unasisitiza uhifadhi wa mazingira katika maeneo yote ya vyanzo vya mito, na unatoa mwongozo<br />

wa sera ufuatao:<br />

‘Kuhakikisha maendeleo endelevu ya kimazingira, yanayolenga katika ushirikishaji na uimarishaji<br />

wa thamani ya mazingira na utiliaji maanani upangaji wa mipango ya rasilimali za maji, usimamizi<br />

na maendeleo na kuongeza ufahamu wa [sic] athari zake kwa afya ya binadamu, maendeleo na<br />

maliasili nyingine. Mkazo kimsingi utazidishwa kwenye kufafanua, kuboresha na kuweka wazi<br />

taasisi na michakato itakayohusika katika ushirikishwaji wa masuala ya mazingira katika usimamizi<br />

wa rasilimali za maji kwa ujumla (RoK, 2003:23).<br />

Kwa nyongeza, Mkakati huu unasisitiza kuhifadhi vyanzo vya mito, hususan katika kuhifadhi misitu ya<br />

Kenya ambayo inapungua kwa kasi kubwa:<br />

‘Maeneo ya vyanzo vya maji yanahitaji … kuainishwa na kuonyeshwa katika mchoro na programu<br />

za uhifadhi na ulinzi zianzishwe na wizara zinazohusika na misitu. Kwa nyongeza, kanda za hifadhi<br />

ya maji ya chini ya ardhi zitahitajika kuainishwa kuepuka umalizikaji wa rasilimali hii ili kukuza<br />

usimamizi shirikishi wa vyanzo vya mito. Wadau wote watahimizwa kutumia rasilimali zao katika<br />

kulinda vyanzo vya maji vya nchi yao (RoK, 2003:33).<br />

Katika hali hii, Sera ya Maji ya Kenya inaeleza misingi ambayo usimamizi wa rasilimali za Bonde la Mto<br />

Pangani zinazovuka mipaka ya nchi unaweza kufanyika, ikitiliwa maanani kuwa ukataji miti kwenye<br />

mitelemko ya Mlima Kilimanjaro (nchini Tanzania) huathiri moja kwa moja kina na ubora wa maji ya Ziwa<br />

Jipe (nchini Kenya).<br />

50


Kisanduku 12: Utawala wa Maji Kenya<br />

• Waziri wa Maji: Hudhibiti rasilimali zote za maji kulingana na Sheria ya Maji ya Mwaka 2002.<br />

• Mkurugenzi wa Maji: humsaidia Waziri kutekeleza kazi zake.<br />

• Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali ya Maji (WRMA): inafanya kazi ya usimamizi wa rasilimali ya maji.<br />

• Kamati ya Ushauri ya Eneo la chanzo cha mto (CAAC): huwashauri maafisa wa WRMA kwa masuala<br />

ya usimamizi wa maji yanayohusiana na eneo la chanzo cha mto lililoko chini ya mamlaka yake.<br />

• Hifadhi ya Maji ya Taifa na Shirika la Mabomba (NWC & PC): kwa niaba ya Waziri, hushughulika na<br />

uendelezaji wa miradi ya taifa inayotoa huduma ya maji mengi ya matumizi kwa wenye leseni na<br />

watoaji wengine wa huduma za maji<br />

• Bodi ya Rufaa ya Maji (WAB): husikiliza na kuamua kesi yoyote ya mtu mwenye kibali au mali ambayo<br />

inaathirika moja kwa moja na uamuzi wa kisheria wa Mamlaka.<br />

• Vyama vya Watumiaji wa Rasilimali ya Maji: husaidia mamlaka katika ulinzi wa rasilimali za maji<br />

katika ngazi ya chini kabisa.<br />

Utawala wa misitu, sheria na sera<br />

Usimamizi wa misitu ya Tanzania<br />

umegawanywa kati ya mamlaka kuu mbili.<br />

Mlinzi mkuu wa misitu ya taifa ni Idara ya Misitu<br />

na Nyuki (FBD), ambayo iko chini ya Wizara ya<br />

Maliasili na Utalii. Ofisi ya Rais pia ni mhusika<br />

katika usimamizi wa misitu ya Tanzania kwa<br />

kupitia kazi zinazofanywa na tawala za mikoa<br />

na serikali za mitaa. Chombo cha tatu cha<br />

usimamizi ni Mamlaka ya Hifadhi za Taifa<br />

(TANAPA) ambazo husimamia misitu iliyopo<br />

katika mipaka ya mbuga za hifadhi za Taifa<br />

(Lambrechts et al., 2002).<br />

Kama ulivyo utawala wa maji wa sasa, utawala<br />

wa misitu pia una pande mbili. Katika ngazi ya<br />

mkoa, Afisa Maliasili wa Mkoa (RNRO) hukaa<br />

kwenye Sekretarieti ya Mkoa akiwakilisha<br />

misitu. Wanaowajibika kwa RNRO ni Maafisa<br />

Watendaji wa Wilaya, ambao chini yao kuna<br />

Maafisa Maliasili wa Wilaya.<br />

Serikali kuu<br />

FBD<br />

RNRO<br />

FCFO<br />

Serikali za Mitaa<br />

Mkurugenzi<br />

Mtendaji (Wilaya)<br />

DNRO<br />

DFO<br />

Utawala wa mkoa hauna mamlaka ya kisheria<br />

kwenye Misitu ya Eneo la Chanzo cha Mto. Mradi<br />

wa Misitu ya maeneo ya vyanzo vya mito (CFP)<br />

ulizinduliwa mwaka 1976 na Idara ya Misitu na<br />

Nyuki. Katika mkoa wa Arusha, hekta 118,921<br />

za misitu zimo kwenye mradi. Katika mkoa wa<br />

Kilimanjaro ni hekta 138,785 wakati ambapo<br />

Tanga ni hekta 107,499 (Kijazi 2002). Misitu<br />

ya maeneo la vyanzo vya mito huchukuliwa<br />

kuwa ‘maeneo muhimu yaliyohifadhiwa’ na<br />

yanatawaliwa kutoka kwenye ofisi ya CFP katika<br />

Misitu ya vyanzo<br />

vya maji wilayani<br />

Misitu ya<br />

uzalishaji<br />

Misitu<br />

Misitu ya Hifadhi<br />

ya asili<br />

Mchoro wa 3: Utawala wa misitu nchini<br />

Tanzania<br />

51


makao makuu ya Idara ya Misitu na Nyuki, ambayo huwajibika kwa serikali kuu. Wanaowajibika kwenye ofisi<br />

ya CFP ni Mameneja wa Misitu ya maeneo ya vyanzo vya mito wa mikoa- mmoja kwa kila mkoa. Mameneja<br />

wa wilaya wa misitu ya maeneo ya vyanzo vya mito huwajibika kwa Meneja wa Mkoa. Mameneja hawa<br />

hupata fedha moja kwa moja kutoka kwenye ofisi ya CFP, na lazima wawe na mpango wa usimamizi kwa<br />

kila msitu ulio chini ya mamlaka yao. Ngazi hizi mbili tofauti za utawala zinaonyeshwa kwenye Mchoro wa 2.<br />

Katika ngazi ya wilaya, Maafisa wa Misitu wa Wilaya (DFOs) hutekeleza shughuli za Idara ya Misitu na Nyuki,<br />

ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa mapato. Mara nyingi, misitu ya asili na ya uzalishaji huwa chini ya utawala<br />

wa wilaya, lakini misitu ya eneo la chanzo cha mto inaweza pia kuwa chini yao. Kwa vile Maafisa Misitu wa<br />

Wilaya hukusanya mapato kwa niaba ya Idara ya Misitu na Nyuki, hivyo wale wote wenye elimu ya diploma<br />

au zaidi hulipwa na Idara ya Misitu na Nyuki (Kijazi na Nashanda, Wahojiwa).<br />

Sera ya Misitu ya mwaka 1998 inahimiza ushirikishwaji wa jamii katika usimamizi wa maliasili na hii ni<br />

pamoja na zile jamii zinazopakana na hifadhi ya misitu ya mikoko. Mkakati wa Usimamizi unataka juhudi<br />

zifanyike ili kujumuisha jamii za wenyeji katika shughuli mbalimbali kutoka kwenye upangaji hadi kwenye<br />

utekelezaji. Shughuli hizo ni pamoja na udhibiti wa uvunaji, upandaji mikoko katika maeneo yaliyo wazi,<br />

shughuli za ulinzi kama vile doria, na uhamasishaji (Kijazi, 2002).<br />

Nchini Kenya, misitu kwa kiasi kikubwa haijasimamiwa kikamilifu, ukweli unaoonyeshwa na kiwango cha<br />

ukataji miti cha kutisha kiasi cha kusababisha asilimia 2 hadi 3 tu ya nchi kubaki na misitu. Hatua za<br />

haraka za urekebishaji zinazofanywa na serikali, ikiwa ni pamoja na marekebisho muhimu katika Idara<br />

ya Misitu na uanzishaji wa sheria mpya ya Misitu, hazijazaa matunda. Katika sehemu ya Bonde la Mto<br />

Pangani iliyoko Kenya kuna hifadhi za misitu chache zilizosalia, isipokuwa viunga vidogo vidogo vya<br />

misitu katika Milima ya Taita, kiwakilishi pekee cha Milima ya Tao la Mashariki nchini Kenya. Matatizo<br />

mengi yahusianayo na uharibifu wa misitu yanayotokea Kenya yanahusiana na ukataji miti kuvuka<br />

mpaka wa Tanzania, hali inayotoa mfano mzuri wa haja ya kuwa na mkakati wa kutosha katika usimamizi<br />

wa kimataifa wa bonde.<br />

D.3 Utawala wa ngazi ya jamii<br />

Mawazo kuhusu usimamizi wa pamoja wa rasilimali, hivi karibuni, yamekuwa ndio chaguo linalopendelewa<br />

katika usimamizi wa maliasili. Mara nyingi (lakini sio mara zote) wadau wanaohusika katika mpango<br />

wa usimamizi ni serikali na jamii zinazotumia rasilimali. Katika hatua hii ya majadiliano ya kina, dhana<br />

ya usimamizi wa pamoja haieleweki vizuri, kwa upande mmoja, kwa sababu ya kuwepo kwa haja ya<br />

kuendeleza mifumo ya Usimamizi wa Maliasili ambayo inalenga moja kwa moja mahali na jamii.<br />

Mara nyingi, katika hatua hizi za mwingiliano katika usimamizi, menejimenti hutumia taasisi kama sehemu<br />

ya utawala wake. Taasisi ni “…sheria za kuendesha mambo katika jamii au, kuwa rasmi zaidi … vikwazo<br />

vilivyobuniwa na binadamu ili kutengeneza mifumo ya maingiliano ya binadamu“ (North, 1993:3). Kwa hali<br />

hii, taasisi huweka vikomo ambavyo ndani yake maisha ya watu huendeshwa. Lazima tahadhari ichukuliwe<br />

ili kuelewa kuwa taasisi sio matokeo tuli, bali ni hatua pana ambazo hubadilika ili kukabiliana na misukumo<br />

kutoka nje, mabadiliko ya ndani, migogoro na shinikizo nyingine. Taasisi za jamii zinaweza kufanya kazi<br />

muhimu katika kujitafutia njia ya kuendeleza uchumi wake na hasa, jinsi inavyopokea uchumi kutoka nje.<br />

Taasisi sio mashirika, ambayo mafanikio na utendaji wake daima unategemea taasisi.<br />

Katika maandishi mengi kuhusu usimamizi wa rasilimali za pamoja, ni taasisi za kijadi ndizo zinazopendekezwa<br />

kuwa msingi wa maendeleo ya usimamizi wa pamoja (angalia mifano katika Berkes, 1989 na Mackay na<br />

Acheson, 1983). Kila mara hawa wanachukuliwa kuwa ushahidi kwamba jamii zina uwezo wa kusimamia<br />

rasilimali zao. Hata hivyo taasisi zina kazi maalum na ni za muda, na zinaendelezwa kutegemeana na<br />

mahitaji maalum ya kijamii na kiuchumi katika wakati na mahali maalum (North, 1993; Ostrom, 1990 Crean<br />

na Gehib 2001). Hivyo taasisi za kijadi zilizoundwa kusimamia misitu huenda zilifanya kazi katika mazingira<br />

ambayo vibali vya utumiaji vilikuwepo, masoko yalikuwa haba, na watu walikuwa wachache. Kinyume cha<br />

hali hiyo, taasisi hizi inawezekana hazikuwa na thamani kubwa kiusimamizi. Hata hivyo zinabaki na mvuto<br />

kwani huenda zinaweza kuwa na mvuto kijamii na kiutamaduni, kuliko zilivyo taasisi ngeni, zilizotoka nje.<br />

52


Kundi la pili la taasisi za muhimu za usimamizi ni miundo na mashirika ya serikali ambayo yamekuwepo<br />

kwa muda mrefu wa kutosha kiasi kwamba jamii inayaona kuwa ya ‘kawaida’ katika mazingira ya maisha<br />

yao ya kila siku. Kwa maana hii, miundo kama hii imefanywa kuwa rasmi kwa jamii ya wenyeji.<br />

Kama ilivyojadiliwa kabla, Tanzania imekuwa na bidii ya kuanzisha taasisi za Usimamizi wa Maliasili za<br />

Jamii (CBNRM) katika maeneo yake yote ya rasilimali. Katika Bonde la Mto Pangani, miongoni mwa<br />

taasisi muhimu zaidi ni Vyama vya Watumiaji Maji na Kamati za Maliasili za Vijiji (VNRCs). Zote hizi mbili<br />

zinazingatiwa katika sehemu hii.<br />

Tagseth (2002) aliainisha aina mbili za uongozi wa mifereji katika ngazi ya kijiji. Wa kwanza kati ya<br />

hizi umelenga katika vikundi vya watumiaji visivyo na majina na visivyo rasmi vilivyoelezwa hapo juu,<br />

vikiongozwa na mwenyekiti ambaye hupanga watumiaji katika vikundi kazi ili kukarabati mifereji kwa malipo<br />

ya kugawiwa maji. Wenyeviti wamekuwa wakimiliki mifereji yao kwa vizazi vingi. Mfumo huu wa kihistroria<br />

wa uongozi wa mifereji na maji yake humaanisha kuwa uongozi unaona kuwa kutafuta kibali cha kutumia<br />

maji ya mfereji, kwa mfano kutoka Ofisi ya Maji Bonde la Pangani, kuwa jambo geni kabisa.<br />

Aina ya pili ya uongozi wa mifereji ulioainishwa na Tagseth (2002) ni utaratibu rasmi zaidi. Kiongozi wake<br />

anachaguliwa au kuteuliwa. Kuna sheria nyingi zaidi zinazotawala, kwa mfano, michango kwa skimu<br />

hiyo na ugawaji wa maji. Ugawaji wa maji unapangwa kwa kutumia ada ya uanachama, faini zitokanazo<br />

na uvunjaji wa sheria na pengine rushwa.<br />

Ni wazi kuwa aina ya kwanza kati ya taasisi hizi mbili si rasmi, ambayo inaweza isivutie mifumo ya<br />

utawala wa serikali yenye bidii ya kuunda miundo ya kirasimu na ya kueleweka. Hata hivyo, pia ina<br />

misingi ya itikadi za asili za jamii ambayo huenda inamaanisha kuwa (a) inaweza kuwa bora zaidi katika<br />

kushughulikia matatizo na migogoro ya wenyeji; na (b) inalingana zaidi na mitazamo na mawazo ya<br />

wenyeji. Kwa maana hii, taasisi ya kwanza, isiyo rasmi, inaweza zaidi kushughulikia viwango vya juu<br />

vya tofauti za kijamii, rasilimali na kiutamaduni zilizopo katika Bonde la Mto Pangani, wakati ile ya pili<br />

isingeweza kushughulikia mawazo kama haya, yasiyo na sababu.<br />

Awali, mawazo yanayoshutumu uanzishaji na utekelezaji wa Vyama vya Watumiaji Maji yalijadiliwa.<br />

Ilidaiwa kuwa licha ya msisitizo wa jamii uliomo katika dhana hii, Vyama vya Watumiaji Maji bado viliweka<br />

vikwazo kwa jamii ambazo hazikuviheshimu sana (PAMOJA, 2002). Hata hivyo ni lazima isisitizwe kuwa<br />

taasisi kama hizi, mbali na kuingizwa kwa nguvu katika jamii, bado ‘zinaweza kufanywa kuwa za jamii’;<br />

kwa maana kwamba zinaweza kupindishwa kukidhi mahitaji ya jamii na ili zisihatarishe matakwa ya<br />

Kisanduku cha 13: Uanzishwaji wa usimamizi wa kijamii katika<br />

msitu wa Duru-Haitemba, Mkoani Manyara<br />

Hapo juu, mgogoro ulioibuka kati ya wanajamii wanaoishi kandokando ya msitu wa Duru-Haitemba na serikali<br />

ya Tanzania wakati msitu ulipogeuzwa kuwa hifadhi umeelezewa. Mara ilipodhihirika kuwa msitu huu haufaidiki<br />

na usimamizi wa serikali, na kwa vile serikali za mitaa zilibakiwa na rasilimali chache za kuweza kuwahudumia<br />

wafanyakazi wa msitu, iliamuliwa kuzipa jamii nafasi ya kuuendesha msitu wao wenyewe. Sharti pekee<br />

lililowekwa ni ufanisi: kwamba Duru-Haitemba inabaki bila kukaliwa na watu, kwamba hali yake iliyoharibiwa<br />

inarejeshwa ilivyokuwa na kwamba mazao yake yavunwe kwa uendelevu.<br />

Hatua za awali zilizochukuliwa na jamii zilianza kwa kuugawa msitu katika kanda ambazo kila jamii inazozizunguka<br />

zingewajibika nazo. Kisha mpango rahisi sana wa usimamizi ulitolewa kwa kila kanda. Mipango hii ilieleza (a) ni<br />

nani alipaswa na hakupaswa kuutumia msitu, (b) matumizi ya msitu ambayo jamii zilijiruhusu kuyatumia, (c) ni<br />

matumizi gani yangeweza kufanyika kwa mgao unaosimamiwa na kijiji na mfumo wa vibali tu; na (d) ni matumizi<br />

gani ya msitu ambayo yalizuiwa kabisa. Wavamizi walifukuzwa mara moja, uchomaji mkaa, uwindaji na ukataji<br />

miti vilipigwa marufuku, na wakataji magogo wasiokuwa wenyeji ‘walihimizwa’ kuondoka. Maeneo yaliyoharibiwa<br />

yalifungwa yasitumiwe na jamii, wakati ambapo sheria nyingi mbalimbali zilisaidia kuhakikisha kuwa matumizi<br />

yoyote yaliyofanyika yalikuwa endelevu. Misimu mipya ya “kufungwa” na “kufunguliwa” ilianzishwa ikiruhusu<br />

aina fulani za matumizi zifanyike katika maeneo fulani na nyakati fulani za mwaka (kama vile ulishaji mifugo).<br />

Mwisho vijana wa kiume kutoka katika jamii walipelekwa kufanyia doria msitu, na kuzawadiwa sehemu ya faini<br />

walizofanikiwa kukusanya (Rejea: Willy, 1999)<br />

53


jamii ya kujitafutia riziki. Hata hivyo hii haina maana kuwa taasisi ndiyo itakuwa inafanya usimamizi<br />

uliotarajiwa. Ili hili litokee, malengo ya usimamizi kwa namna fulani pia lazima yazuie hofu za jamii, na<br />

kwa kiasi fulani kuhakikisha kuwa inachangia katika kukidhi matarajio yao. Ili hili litokee, jamii lazima<br />

ishiriki katika majukumu muhimu ya kupanga na kutekeleza mifumo ya usimamizi, hususan mifumo<br />

inayohusiana na utoaji wa adhabu.<br />

Mradi wa misitu ya maeneo ya vyanzo vya mito (CFP) katika Tanzania unasimamia misitu kwa pamoja<br />

na jamii za wenyeji zinazopakana na misitu 23 ya aina hiyo kwa majaribio. Asilimia 36.5 ya misitu katika<br />

mikoa mitatu ya Tanzania inayochangia Bonde la Mto Pangani iko chini ya Usimamizi wa Misitu wa<br />

Pamoja (JFM: Jedwali la 6). Sehemu kuu ya jamii katika juhudi hizi ni Kamati za Maliasili za Vijiji (VNRC).<br />

Kila kamati ina wajumbe kati ya 8 na 15 ambao wamechaguliwa kidemokrasia. Angalau wajumbe wawili<br />

lazima wawe wanawake. Kadiri ya kamati 129 (asilimia 70) za Maliasili za Vijiji zinashiriki katika kupanga<br />

na kufanya maamuzi, vile vile kuhamasisha wanavijiji katika Usimamizi wa Misitu wa Pamoja. Rasimu<br />

ya mipango ya usimamizi kwa ajili ya Hifadhi ya Misitu ya Jamii (CFRs) tisa zilizopewa kipaumbele<br />

imetolewa, ikiwemo Mlima Kilimanjaro, Chome na Kindoroko katika mkoa wa Kilimanjaro na hifadhi ya<br />

Kwani/Tongwe na msitu wa kilima cha Mafi katika mkoa wa Tanga.<br />

Idara ya Misitu na Nyuki pia imetekeleza Mradi wa Usimamizi wa Mikoko (MMP), ambao ulizinduliwa<br />

mnamo mwaka 1988. Hii ilianza na utayarishaji wa mpango wa usimamizi kwa mifumo ikolojia ya mikoko<br />

ya Tanzania bara. Mkakati wa usimamizi uliobuniwa ulihitaji juhudi zifanywe kuhusisha jamii za wenyeji<br />

katika shughuli mbalimbali, kuanzia upangaji hadi utekelezaji. Shughuli hizo ni pamoja na kudhibiti uvunaji,<br />

upandaji wa mikoko katika maeneo ilikopungua, shughuli za ulinzi kama vile doria, na uhamasishaji.<br />

Mradi wa Usimamizi wa Mikoko umehusisha vijiji 100 kati ya 130 vilivyo karibu na misitu ya mikoko katika<br />

usimamizi wake. Zaidi ya hayo, mradi umekuwa ukiboresha msitu wa mikoko kwa kukata mitambaazi<br />

katika hekta 430, na kukuza shughuli mbadala za uzalishaji kwa jamii za wenyeji, kama vile shughuli za<br />

kilimo cha mimea ya baharini na ufugaji nyuki (Kijazi, 2002).<br />

Mradi wa Usimamizi wa Mikoko umerudisha upya uhai wa misitu ya mikoko katika hekta 1,300 kati ya hekta<br />

2,000 zilizokusudiwa, ambapo hekta 100 zilifanyiwa kazi kwa njia ya kujitolea na wanavijiji na mashirika<br />

yasiyo ya kiserikali yanayojishughulisha na mazingira. Ufanisi wa misitu iliyopandwa upya unatofautiana<br />

kwa asilimia kutoka 80 hadi 40. Hali ni duni zaidi katika maeneo ambayo kilimo cha mpunga kinafanyika,<br />

kama vile Delta ya Mto Rufiji, kutokana na baadhi ya wamiliki wa mashamba kutokubali kuruhusu mikoko<br />

kukua upya.<br />

Kamati za Maliasili za Vijiji zinashirikiana na menejimenti ya mradi kwa kuangalia taratibu za uvunaji.<br />

Chini ya usimamizi huu, mapato ya Serikali Kuu yameongezeka kutoka TSh. milioni 12 mwaka 1999/2000<br />

hadi milioni 17 mwaka 2001 kutokana na uuzaji wa miti ya ujenzi na ada za usimamizi kutoka kwenye<br />

visima vya chumvi (Kijazi, 2002).<br />

Mpaka sasa katika kubuni shughuli mbadala za uzalishaji, mradi wa usimamizi wa mikoko ulipeleka<br />

mizinga 830 ya asili na 28 ya kisasa ya nyuki katika misitu ya mikoko mnamo mwaka 2001. Zaidi ya<br />

hayo, kilimo cha mimea ya baharini kinafanyika katika mwambao wa pwani.<br />

54<br />

Jedwali la 7: Eneo la misitu chini ya Usimamizi wa Misitu wa Pamoja kwa mikoa<br />

Mkoa Eneo (Hekta) Idadi ya vijiji vilivyohusishwa<br />

Arusha* 7,0248 70<br />

Kilimanjaro 122,996 63<br />

Morogoro 58,579 33<br />

Tanga 15,233 19<br />

Jumla 267,056 185<br />

(Rejea: Kijazi, 2002). * inajumuisha na Mkoa wa Manyara


Katika mchakato wa uhamasishaji, programu ya kutoa elimu ya ikolojia ya mikoko ilifanyika katika shule<br />

za msingi 47 katika Kanda za Kaskazini na Kusini. Mikutano ya vijiji, programu za redio, na maonesho<br />

ya majadiliano ya video yalitumika pia.<br />

D.4 Usimamizi wa Bonde kimataifa<br />

Nyenzo za kusimamia rasilimali za Bonde la Mto Pangani, kati ya mataifa wafadhili ya Kenya na Tanzania<br />

hazitoshelezi. Jitihada za kurekebisha tatizo hili kwa kiasi kikubwa zinategemea juhudi za <strong>IUCN</strong>-EARO za<br />

kuhifadhi Ziwa Jipe. Nchini Kenya Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani (CDA) ina madaraka ya kuratibu na kupanga<br />

maendeleo ya sehemu ya bonde iliyoko Kenya. Mnamo mwaka 1993, iliamuliwa kuwa CDA ijitahidi kuandaa<br />

mpango kabambe wa usimamizi na maendeleo kwa ajili ya sehemu ya bonde iliyoko Kenya, pamoja na kutafuta<br />

njia za kushughulikia matatizo mahsusi ya Ziwa Jipe. CDA iliona kuwa ni lazima ishirikiane na mamlaka za aina<br />

yake za upande wa Tanzania (Howard, 1999).<br />

Mnamo mwaka 1994, CDA na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWO) walikutana Mombasa, Kenya ili<br />

kujadili masuala ya pamoja na njia zitakazowawezesha kufanya kazi pamoja ili kuendeleza mfumo wa usimamizi<br />

ulioratibiwa kwa ajili ya bonde, ardhioevu na maji ya Ziwa Jipe. Mwaka 1996, PBWO na CDA zilikamilisha tathmini<br />

ya mahitaji ya eneo la chanzo cha maji na ardhioevu ya Ziwa Jipe. Katika mwaka 1999, CDA, PBWB na wadau<br />

wengine walishiriki katika warsha ya kuanzisha mfumo wa kusimamia Ziwa Jipe (Howard, 1999).<br />

PBWO hivi sasa imelifikisha shauri la magugu maji yaliyoko Ziwa Jipe katika Bunge la Jumuia ya Afrika<br />

Mashariki kwa kufanyiwa kazi. Kutoka hapo, kasi imepungua, na haja ya kuendeleza mfumo wa kuweza<br />

kuratibu usimamizi kati ya nchi mbili hizi unabaki kuwa muhimu kuliko wakati mwingine wowote. Hili ni<br />

dhahiri zaidi ikitiliwa maanani maendeleo ya hivi karibuni ya Kenya ambayo yameshuhudia uanzishwaji<br />

wa mamlaka za Usimamizi wa Rasilimali za Maji. Umuhimu wa uundwaji wake kwa Bonde la Mto Pangani<br />

na jinsi watakavyoshirikiana na wenzao wa Tanzania bado haifahamiki.<br />

D.5 Ukusanyaji wa data na ufuatiliaji<br />

Wasiwasi unaoibuka mara kwa mara baina ya wataalam waliohojiwa kwa ajili ya Uchambuzi huu wa hali<br />

halisi na katika maandishi kuhusu Bonde la Mto Pangani unahusiana na ukosefu wa data za kutosha<br />

katika Bonde hili. Mara kwa mara, wasiwasi huo unalenga kwenye ukosefu wa data za kihaidrolojia,<br />

na wasiwasi ni kwamba mfumo wa sheria inayohusu utoaji wa hati za maji lazima uweze kujua wingi<br />

wa maji yaliyopo. Katika mito iliyopo Bonde la Mto Pangani, kuna vituo vingi vya kihaidrolojia. Kwa<br />

sababu mbalimbali – kama vile udhaifu wa utunzaji na kumalizika kwa betri – vituo vingi kati ya hivi<br />

havikuendeshwa kwa muda wa kutosha kitakwimu. Wakati mwingine, vituo hivi vimeacha kufanya kazi<br />

baada ya miaka miwili tu, na hakuna kilichofanyika kuvirejesha katika hali ya utoaji huduma.<br />

Inawezekana kuchukua vipimo kwa kutumia watu, lakini motisha za kufanyia hivyo kwa fundi, kama wanavyodai<br />

watoa habari, lazima ziwianishwe na mafao yake ambayo hayatoshelezi. Mara nyingi wahojiwa wameonekana<br />

kupendelea uendelezaji wa mfumo wa haidrolojia unaojiendesha wenyewe ambao vipimo vinavyofanywa na watu<br />

vinaweza kulinganishwa navyo, na ambavyo vinaweza kuwa uti wa mgongo wa mfumo wa ufuatiliaji wa kutosha.<br />

Kwa hakika, ufuatiliaji, sio ukusanyaji wa data pekee. Kuzitafsiri data hizo katika mfumo wa taratibu za<br />

matumizi kutakuwa na manufaa endapo kutakuwa na kanuni fulani inayounga mkono ili kuhakikisha<br />

kuwa data hizi zinatoa mchango muhimu katika kazi za usimamizi. Hivyo, kujua ni samaki kiasi gani<br />

wapo katika Bwawa la Nyumba ya Mungu haina maana kama taarifa hiyo haiwezi kutafsiriwa katika<br />

utendaji wa usimamizi. Katika hali inayofanana na hiyo, uendelezaji wa mfumo wa ukusanyaji data za<br />

haidrolojia wa kujiendesha wenyewe hauna maana kama utumiaji haramu wa maji hauwezi kuzuiliwa.<br />

55


Kisanduku cha 14: Mfano wa Chama cha Watumiaji Maji<br />

Chama cha Watumiaji Maji cha Tegemeo, Kijiji cha Kawaya, Wilaya ya Hai<br />

Chama cha Watumiaji Maji cha Tegemeo kilianzishwa mwaka 1999 na PBWO ili kutatua tatizo la<br />

ugawaji wa maji katika vijiji vitano wilayani Hai. Watu 5,000 hutumia maji ambayo Tegemeo huchukua,<br />

lakini ni watu 300 tu ambao wamesajiliwa nacho. WUA inasema watu wanahitaji kuelimishwa kuhusu<br />

manufaa ya uanachama. Manufaa hayo ni (a) kwamba watajifunza kuhusu sera na sheria za maji,<br />

(b) wanaweza kupata kibali cha kutumia maji kwa urahisi zaidi, (c) kwamba wanaweza kuvutia<br />

wahisani na shughuli za NGO (d) wanaweza kurekebisha miundombinu yao ya maji kwa urahisi<br />

zaidi wakiwa kama kikundi; na (e) wanaweza kutatua matatizo yao kama kikundi. Vyanzo vyao vikuu<br />

vya maji ni chemchemi kadhaa. Maji huingizwa kwenye mifereji ya kijadi, ambayo mara nyingi huwa<br />

imepewa majina ya watu ambao waliichimba hapo zamani. Baadhi huwa mirefu sana-ulio mrefu<br />

zaidi una kilomita 14. Tegemeo kwa sasa ina hati tatu za maji zenye jumla ya lita 720 kwa sekunde,<br />

na imeomba kuongezewa. Chama hukusanya ada kutoka kwa watumiaji wenye mashamba, na kila<br />

mtumiaji analazimika kulipa bila kujali kama ni mwanachama au la.<br />

Watumiaji walioko mwanzoni mwa mfereji hufaidika zaidi ya wale walioko mwishoni. Chama kina sheria<br />

ndogondogo zinazowapangia kiasi cha maji ambacho watumiaji walioko kwenye chanzo cha mfereji<br />

wanaruhusiwa kutumia, lakini watu hudanganya. Tatizo lingine wanalokabiliana nalo ni kuwa eneo hilo<br />

ni tambarare sana. Kwa kutokuwepo na mteremko, maji daima hutuwama na hayatiririki. Matatizo ya<br />

ziada yanayowakabili ni pamoja na:<br />

• Migogoro kati ya watumiaji wa maji wa sehemu ya juu na ya chini.<br />

• Ulimaji katika maeneo ya chanzo cha maji na ukataji miti.<br />

• Wakulima wa mpunga mara nyingi hawarudishi maji yasiyotumika kwenye mfereji.<br />

• Chumvichumvi.<br />

• Wafugaji huleta mifugo yao kunywa maji miferejini na kuharibu kingo zake.<br />

• Eneo la huduma la WUA ni kubwa mno na mara nyingi huwa vigumu kwa wanachama kufika<br />

kwenye eneo la tatizo.<br />

• Maji siyo safi. Wakati wa mvua kina cha maji ardhini hupanda na kufanya vyoo vifurike. Baadhi<br />

ya watu hawayachemshi maji wanayochota na hupata maradhi<br />

• Umwagiliaji kwa vipindi virefu hupunguza rutuba ya ardhi.<br />

Chanzo: Jumuiya ya Watumiaji Maji Tegemeo na Serikali ya Kjiji cha Kawaya<br />

Pia ni muhimu kusisitiza kuwa data za vipimo vya kiufundi vya mabadiliko ya rasilimali (kama vile<br />

upunguaji wa mtiririko wa maji, au mabadiliko ya eneo la msitu) hutoa tu taarifa kuhusu matokeo ya<br />

mienendo na michakato itokeayo kwingineko, mara nyingi katika uga wa kijamii na kiuchumi (ingawaje<br />

siyo mara zote k.m. mabadiliko ya hali ya hewa). Kama sababu za mabadiliko ya kimazingira na maliasili<br />

zina asili ya kijamii na kiuchumi, ni muhimu kuendeleza mifumo yenye nguvu ya ufuatiliaji wa tofauti za<br />

uchumi wa jamii, kinachosababisha hali hiyo na kuendeleza migogoro. Mifumo hii lazima pia iwe na<br />

uwezo wa kutambua mahitaji ya maji katika bonde.<br />

56


D.6 Majumuisho ya hoja<br />

Utawala wa maliasili za Bonde la Mto Pangani ni wa kisekta. Shughuli za idara za misitu sio lazima ziwe<br />

zimeoanishwa kwa kiasi kikubwa na kukiuka mpango wa usimamizi wa Bonde la Mto Pangani, bali matokeo<br />

ya sera za misitu, kama ilivyo kwa shughuli za taasisi zinazohusika na usimamizi wa maji zinavyoshughulikia<br />

Sera ya Maji ya Taifa. Hali hii ya kisekta huenda chini hadi kwenye mikakati ya utawala ya ngazi za jamii.<br />

Hivyo Kamati za Maliasili za Vijiji zinazotumika katika Usimamizi wa Pamoja wa Misitu sio sawa na Vyama<br />

vya Watumiaji Maji. Jamii zilizo jirani na maeneo ya uvuvi na yaliyohifadhiwa, zinaweza pia zikalazimika<br />

kuunda Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe na kamati za hifadhi ya wanyamapori kama ilivyo kwenye sera<br />

za Idara ya Wanyamapori na Idara ya Uvuvi. Wingi wa kupita kiasi wa taasisi za vijijini nchini Tanzania<br />

unazifunika zile zilizoundwa hapo awali kama vile Serikali za Vijiji. Mara nyingi, kazi ambazo kila kikundi<br />

kinafanya hazitofautiani na kazi zinazofanywa na vikundi vingine. Hatimaye, taasisi hizi zote hazina budi<br />

kushughulika mgao wa haki wa rasilimali katika jamii, matumizi endelevu na uhifadhi wake.<br />

Kutokana na majadiliano ya hapo juu, dondoo zifuatazo zinatiliwa mkazo:<br />

• Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya mwaka 2009 inaipa mamlaka ya kiutetendaji Bodi ya Maji<br />

ya Bonde la Pangani kuandaa mipango ya usimamizi wa bonde na ambayo itakuwa msingi wa ugawaji<br />

wa maji. Sheria hii mpya imeweka mfumo wa ngazi za utawala zenye ufanisi na mfumo wa kitaasisi<br />

ulio wazi ambao unaonyesha majukumu ya kila mmoja katika kutekeleza sera na sheria. Usimamizi<br />

wa maji Kenya umegawa katika mabonde 6 (kuna mabonde 5 lakini bonde la Ziwa Victoria limegawa<br />

katika maeneo mawiili, Kasikazini na Kusini) kama ifuatavyo: Ziwa Victoria kasikazini, Ziwa Victoria<br />

Kusini. Bonde la Ufa, Athi, Tana, na Iwaso Ng’iro. Sehemu ya bonde la Pangani upande wa Kenya<br />

huangukia katika bonde la Athi. Sheria ya maji 2002 ya Kenya imeweka mfumo mpya wa kitaasisi wa<br />

kusimamia na kutunza rasilimali za maji katika ngazi ya taifa, mabonde na mabonde madogo.<br />

• Idara ya Misitu na Nyuki inaonekana kutokuwa na mipango yoyote ya aina hii ya kuundwa upya,<br />

na utawala wa misitu katika bonde unabaki kuwa wa pande mbili kati ya watawala wa ngazi ya<br />

taifa na ile ya mkoa, na kati ya nchi mbili ambamo Bonde la Mto Pangani limo.<br />

• Sera zote, ya maji na ya misitu katika bonde hili zinazidi kutilia mkazo matumizi ya taasisi za kijamii<br />

katika utekelezaji wake. Wasiwasi umejitokeza kuhusu ni kiasi gani taasisi hizi zimeshinikizwa<br />

kuingia katika jamii. Kama jamii hazikushirikishwa katika uundaji na utekelezaji wa taasisi hizi,<br />

kunaweza kuwa na matokeo yasiyofaa katika usimamizi wake. Kulielewa tatizo hili kunaweza kutoa<br />

mafunzo kwa Kenya ambayo inataka kujumuisha watumiaji katika usimamizi wa rasilimali za taifa.<br />

• Usimamizi wa kimataifa wa bonde ni muhimu. Zipo mamlaka, hata hivyo, zenye madaraka<br />

ya kulisimamia na kuliendeleza Bonde hili katika pande zote mbili za mpaka wa Tanzania na<br />

Kenya, na majadiliano yanayolenga katika kutambua ufumbuzi wa matatizo ya usimamizi wa<br />

bonde hili yameanza.<br />

• Mfumo wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data katika bonde unaonekana kuwa dhaifu, bila ya kujali<br />

sekta ya rasilimali. Sura hii imetahadharisha kuwa kutilia mkazo ukusanyaji wa data kama<br />

jambo muhimu kwenye mfumo wa usimamizi hakutakuwa na maana iwapo data hizo haziwezi<br />

kusaidia ufuatiliaji kamili wa usimamizi. Pia inasisitiza haja ya kuanzisha njia za ufuatiliaji wa<br />

mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, na kubainisha mahitaji ya maji katika bonde, kama nyongeza<br />

kwenye vipimo vya kiufundi vya mabadiliko ya rasilimali.<br />

Sura inayofuata inatoa muhtasari wa ‘masuala’ yanayolikabili Bonde la Mto Pangani. Inaanzia<br />

na muhtasari wa masula yaliyopatikana kutoka katika kumbukumbu za warsha ya hivi karibuni<br />

ya Bonde la Mto Pangani, pamoja na yale yaliyojitokeza wakati wa mahojiano yaliyofanyika<br />

kwa ajili ya Uchambuzi huu wa Hali halisi. Sura hii inayatathmini masuala haya kama msingi<br />

wa uwekaji wa maeneo ya kipaumbele kwa ajili ya kuyafanyia kazi, na mapendekezo kuhusiana<br />

na hali hii yanatolewa katika sehemu yake ya mwisho.<br />

57


E<br />

Matatizo na masuala ya Bonde la Mto Pangani<br />

E.1 Utangulizi<br />

Sura hii msingi wake ni vyanzo viwili vya taarifa. Cha kwanza ni kumbukumbu za warsha kuhusu Bonde<br />

la Mto Pangani, iliyofanyika Mei, 2002 mjini Moshi. Cha pili ni mahojiano yaliyofanyika kwa ajili ya<br />

Uchambuzi huu wa hali halisi. Sura hii inajaribu kuunganisha maoni ya wadau mbalimbali katika Bonde<br />

la Mto Pangani kama msingi mkuu wa kuweza kutambua maeneo ya kipaumbele kwa ajili ya utendaji wa<br />

siku zijazo. Masuala ya Bonde la Mto Pangani yamegawanywa kati ya masuala ya mazingira, masuala<br />

ya uchumi wa jamii na siasa, masuala ya usimamizi na utawala, maeneo ya utafiti, na mwisho, mawazo<br />

ya wahojiwa kuhusu nini kipewe kipaumbele katika usimamizi wa bonde. Kwa misngi ya masuala haya,<br />

sehemu ya hitimisho inorodhesha maeneo kadhaa ya kipaumbele kwa ajili ya kuyafanyia kazi.<br />

Takriban katika kila jambo, masuala yaliyoangaliwa hapa chini yanajitokeza katika mazingira ya ukuaji wa<br />

haraka na wa kiwango kikubwa cha idadi ya watu na ongezeko la msongamano wa watu. Hali ya rasilimali<br />

za bonde kuwa na kikomo inafanya ongezeko la watu na ukuaji wa polepole wa maendeleo katika bonde<br />

kusababisha uwezekano wa kuleta matatizo na masuala yaliyoangaliwa hapa, au pengine kuyazidisha.<br />

E.2 Matatizo na masuala ya Bonde la Mto Pangani<br />

Masuala ya mazingira<br />

Kati ya matatizo ya bonde hili, kubwa zaidi ni ukataji miti, tatizo ambalo huathiri moja kwa moja uwezo<br />

wa kuhifadhi maji, huongeza kasi ya mtiririko wa maji na hivyo kusababisha mmomonyoko wa udongo<br />

katika bonde. Upande wa chini wa mto, mchakato huo huweza kusababisha mafuriko kutokea na hivyo<br />

wingi wa mchangatope kwenye mikondo ya maji katika bonde kuwa mkubwa.<br />

Katika hatua nyingne, ukataji miti umesababishwa na mahitaji makubwa ya mazao ya misitu. Mingi ya misitu<br />

iliyobaki katika bonde ina mbao zenye thamani kubwa, ambazo kunapokosekana mfumo imara wa ufuatiliaji<br />

na utoaji adhabu, hukatwa kwa urahisi. Misitu pia hukatwa kwa ajili ya utengenezaji wa mkaa, pamoja na<br />

kuni kukidhi mahitaji ya nyumbani. Zaidi ya hayo, misitu ya bonde mara nyingi imo kwenye maeneo muhimu<br />

ya kilimo. Misitu ya Tao la Mashariki, kwa mfano, iko katika maeneo ya mwinuko ambayo mvua ni nzuri.<br />

Kadiri idadi ya watu kwenye bonde inavyoongezeka na idadi ya wakazi katika kingo za misitu huongezeka na<br />

kuzidisha hatari ya moto katika misitu. Moto pia hutumika kwa kusafisha ardhi kwa ajili ya kilimo.<br />

Katika sehemu nyingi, kilimo kinachotumika kilianzishwa wakati ambapo rasilimali zilikuwa nyingi zaidi<br />

kuliko zilivyo hivi sasa, na huenda kisiweze kuendana na hali ya uhaba wa rasilimali uliopo. Hivyo,<br />

sehemu kubwa ya kilimo cha umwagiliaji wa kijadi kilichopo katika bonde hili hakina ufanisi kabisa na<br />

kilianzishwa katika mazingira ambapo kulikuwepo na maji ya kutosha kwa kila mtu. Kwa vile uchukuaji wa<br />

maji umeongezeka kutegemeana na msongamano wa watu, mifumo hii ya kilimo inaweza kuwa na athari<br />

kubwa kwa mazingira ya bonde. Mashinikizo haya yamesababisha kujitokeza kwa kilimo kwenye kingo<br />

za mto, ndani ya mabonde ya vijito na kwenye vyanzo vya chemchemi. Ongezeko la mchangatope lina<br />

madhara kwenye mkondo wa mto (inaweza kusababisha kubadili mkondo) pamoja na viwanda vilivyoko<br />

eneo la chini la mto, hususan mabwawa yatumikayo kuhifadhi maji kwa ajili ya nishati ya umeme.<br />

Wingi wa shughuli za kilimo katika bonde hili umesababisha udongo kuendelea kuchoka kwa vile nafasi<br />

ya mfumo wa mzunguko wa mazao imechukuliwa na kilimo cha mwaka mzima. Kwa vile ardhi sasa<br />

ni nadra kuachwa bila mazao, inabidi imwagiliwe maji ili kuendelea kutoa mazao. Mifumo ya kijadi ya<br />

uchukuaji maji ina ufanisi mdogo sana na kiasi cha maji kinachoifikia mimea kinaweza kufikia asilimia<br />

85 pungufu ya kiasi kilichochukuliwa kutoka kwenye chanzo. Umwagiliaji wa kurudiarudia huongeza<br />

uwezekano wa kuongeza chumvichumvi na/au magadi kwenye udongo. Zaidi ya hivyo, kiasi kikubwa<br />

sana cha maji yanayochukuliwa kutoka kwenye vyanzo katika bonde hili, kimepunguza mtiririko wa maji,<br />

inadhaniwa kuwa ni pamoja na kiasi cha maji yanayohitajika kwa ajili ya mazingira.<br />

58


Katika maeneo ya nyanda za chini ya bonde hili inaonekana kuwa idadi ya mifugo imeongezeka kwa kiasi<br />

kikubwa, wakati ambapo kiasi cha malisho kimepungua kutokana na maendeleo ya kilimo. Hii imesababisha<br />

kujitokeza kwa tatizo la ufugaji wa kupita kiasi na matokeo yake ni uharibifu wa ardhi ya wafugaji.<br />

Kadiri maendeleo yanavyoongezeka ndani ya bonde bila ya mifumo ya uondoaji taka inayoambatana<br />

nayo, pia ndivyo uwezekano wa uchafuzi katika ngazi ya jamii na ya bonde kwa ujumla unavyoongezeka.<br />

Matatizo ya ubora wa maji pia yanajitokeza kwa sura tofauti – hali ya viwango vya floraidi kuwa juu<br />

inaweza kuwa na matokeo mabaya kwa watu waishio kando kando ya mito.<br />

Kama ilivyo katika sehemu nyingine za Tanzania, uvuvi uliokithiri katika bonde ni tatizo, uvuvi wa pwani<br />

na katika bwawa la Nyumba ya Mungu ukiwa ndiyo suala lenye uzito mkubwa. Katika Ziwa Jipe ukuaji wa<br />

magugumaji umekuwa mkubwa kiasi cha kukwamisha uvuvi. Magugu hayo yametokana na ongezeko<br />

la virutubisho vinavyoingia na maji yatokayo kwenye maeneo ya kilimo kwenye Mlima Kilimanjaro na<br />

Milima ya Pare Kaskazini. Kwingineko katika bonde, magugumaji aina ya “water hyacinth” ni tatizo.<br />

Matatizo yanayokabili ardhi ya kinamasi ya bonde hili yanatofautiana. Kwa upande mmoja, ukaushaji<br />

wa maji kwenye vinamasi una matokeo mabaya kwa urekebishaji wa mtiririko wa mto, pamoja na<br />

bayoanuwai zinazotegemea ardhioevu. Kwa upande mwingine, uelekezaji wa mikondo ya maji (pamoja<br />

na ile inayopita kwenye ardhi ya kinamasi) unaweza kuongeza kiasi cha maji kitakachopatikana sehemu<br />

za chini za mto, hususan kwa ajili ya uzalishaji wa umeme. Siyo tu maji yanayobaki katika vinamasi<br />

hivyo hupunguza mtiririko wa mto, bali pia ongezeko la viwango vya mchavusho vinavyosababisha.<br />

Uchimbaji madini usiodhibitiwa unaweza kuathiri sura ya nchi, na unaweza hata kusababisha uchafuzi<br />

kama uchimbaji huo unahitaji mchakato unaotumia kemikali. Uchimbaji wa mchanga kwenye mikondo<br />

ya mito unaweza kuharibu uimara wa kingo za mito.<br />

Nyingi za tabia zilizotajwa hapo juu hutokana na uelewa mdogo kuhusu mazingira. Kwa upande<br />

mmoja, haya yanahusiana na ukosefu wa data kuhusu mtiririko wa maji kwenye bonde na kiasi cha maji<br />

yanayohitajika kutosheleza mahitaji ya mazingira. Kwa upande mwingine, wengi wa watu walioko katika<br />

bonde hili hawana uelewa wa athari za mazingira yatakayotokana na shughuli zao za kiuchumi.<br />

Ukubwa wa matumizi ya rasilimali, maendeleo, uendeshaji na mabadiliko ndani ya bonde vina matokeo<br />

mabaya kwa bayoanuwai za bonde hili. Bonde lina baadhi ya rasilimali za bayoanuwai za pekee duniani<br />

zenye viwango vya juu vya spishi zinazopatikana katika sehemu hiyo na spishi nyingi zinazozuiliwa.<br />

Sehemu kubwa ya spishi hizi (lakini kwa vyovyote si zote) ziko kwenye misitu. Wakati rasilimali nyingi za<br />

kimsingi za bonde zikiwa kwenye tishio kutokana na njia zilizoelezwa juu, rasilimali hizi za bayoanuwai<br />

zinakabiliwa na hatari zilizo dhahiri na mbaya kabisa.<br />

Masuala ya kiuchumi wa jamii na kisiasa<br />

Kama ilivyo kwa watu wengine wa Tanzania, wakazi wengi wa Bonde la Mto Pangani sio matajiri. Ingawa<br />

bonde hili lina miji mingi, lakini siyo mikubwa kiasi cha kuweza kupokea ziada ya nguvukazi iliyoko<br />

vijijini. Wengi (kama si karibu wote) wa wakazi wa bonde hili hawana elimu ya kutosha na/au hawana<br />

stadi za kutosha. Kwa hali yoyote ile, hata kama stadi zingekuwepo, kuna shaka kama soko la ajira<br />

limeendelezwa vya kutosha kuweza kuwaajiri wote. Maendeleo katika bonde - kama ilivyo kwingineko<br />

nchini Tanzania - yameshindwa kuzalisha nafasi mbadala za kuingiza mapato zinazooana na viwango<br />

vya ufundi na stadi vya wakazi wa bonde.<br />

Matokeo yake, njia pekee iliyopo ya kujipatia riziki kwa wengi walioko katika bonde ni ile ya msingi , yaani riziki<br />

kutokana na utumiaji wa moja kwa moja wa rasilimali za bonde iwe ni misitu, uvuvi, rasilimali za wanyamapori<br />

au, la muhimu zaidi, kilimo. Kwa walio wengi, mafanikio ya shughuli hizi ndogo ndogo, yanahusiana<br />

moja kwa moja na upatikanaji wa ardhi na maji. Kadiri idadi ya watu inavyoongezeka, ndivyo pia migogoro<br />

inavyoongezeka baina ya watumiaji wa aina na viwango mbalimbali. Kwa matokeo hayo, Uchambuzi huu wa<br />

Hali halisi umewasilisha mifano ya migogoro ambayo hutokea kati ya watumiaji maji wa upande wa juu na wa<br />

chini wa mto, pamoja na ule wa kati ya watumiaji wa viwango vikubwa na wa viwango vidogo.<br />

59


Ni dhahiri kuwa migogoro ni ishara moja ya ushindani kwa ajili ya rasilimali. Kadiri hali hii inavyozidi<br />

kuenea katika maeneo ya juu ya mto katika bonde, wakulima wanalazimika kuelekea upande wa chini<br />

wa mto ili kujaribu kilimo katika hali isiyotosheleza ya kilimo. Kama ilivyojadiliwa mapema, jambo hili<br />

huwanyang’anya ardhi wafugaji na hivyo kuwaingiza wakulima kwenye mgogoro na wafugaji.<br />

Kama ilivyoelezwa hapo juu, matumizi makubwa ya ardhi katika bonde hili yanaweza kuwa na matokeo<br />

mabaya kwa mazingira. Kwa kweli, matokeo haya yanaweza moja kwa moja kuathiri uwezo wa ardhi<br />

kusaidia kwenye matumizi ya kiuchumi yatakayofanyika kwayo. Katika hali nyingine, msaada wa kisiasa<br />

wa kubadili au kuzuia mienendo hii haupo, au huwa ni kinyume, kwa wanasiasa kuwahimiza watu<br />

kutumia rasilimali kwa wingi ili wao waweze kujipatia kura.<br />

Tatizo la mwisho la kisiasa lililotolewa na wahojiwa lilikuwa lile la Serikali Kuu ya Tanzania, katika juhudi<br />

zake za kutekeleza sera, inaweza kufanya maamuzi ya usimamizi yahusianayo na rasilimali bila ya<br />

kuwashirikisha watawala na wasimamizi wa rasilimali katika bonde. Kilichotia wasiwasi hasa ni miradi<br />

mikubwa ya maendeleo (kama vile miradi ya umwagiliaji na vibali vya uchimbaji madini) vilivyoonekana<br />

kusababisha migogoro ya ziada ya ndani au kuathiri vibaya hali ya rasilimali.<br />

Masuala ya usimamizi na utawala<br />

Sheria na sera za usimamizi wa maliasili za bonde hili, mara nyingi zinajitosheleza, lakini zinafanya<br />

kazi pale tu zinapopata msaada wa usimamizi na ufuatiliaji wa kutosha wa utekelezaji wa kisheria.<br />

Ufuatiliaji sio tu uwezo wa kuangalia matumizi haramu ya rasilimali, bali pia uwezo wa kupima uzalishaji<br />

na mabadiliko ya rasilimali. Kwa mfano, kukosekana kwa mtandao wa kutosha wa ufuatiliaji wa mtiririko<br />

wa maji maana yake ni kuwa mamlaka zinazohusika na maji hazijui kiasi cha maji kinachopita katika<br />

bonde, kwa hiyo haziwezi kutoa vibali vya matumizi ya maji kwa msingi huo. Vivyo hivyo, hakuna njia<br />

yoyote ya kufuatilia na kupima sababu za kijamii na kiuchumi ambazo zinasababisha sehemu kubwa ya<br />

uharibifu wa mazingira na utumiaji wa kupita kiasi wa rasilimali.<br />

Wafuatiliaji waliowekwa na taifa kuangalia mienendo ya matumizi ya rasilimali wanaweza wakashindwa<br />

kufuatilia rasilimali hizo kama hawalipwi vizuri. Ujira duni unaweza pia kuwa sababu ya kuwafanya maafisa<br />

wapokee rushwa hivyo kutoangalia matumizi haramu ya rasilimali. Viwango vya chini vya utaalamu, au<br />

kukosekana kwa teknolojia ya kutosha kunaweza pia kuzidisha matatizo ya ufuatiliaji.<br />

Matatizo ya fedha yanaweza kuathiri sehemu nyingine za mfumo wa usimamizi. Kwa kukosekana kwa fedha<br />

za kutosha kwa mfano, inakuwa vigumu kuona jinsi mfumo wa kufaa wa ufuatiliaji unavyoweza kutekelezwa<br />

ndani ya bonde bila ya kujali rasilimali zinazohusika. Ukosefu wa fedha unaweza pia kusababisha hata data<br />

zinazoweza kukusanywa zisiweze kuchambuliwa au matokeo yasiweze kutafsiriwa kwa usahihi. Mwisho,<br />

matatizo ya fedha yanaweza pia kukwamisha maendeleo ya uwezo na ufanisi wa usimamizi.<br />

Zaidi ya hayo, usimamizi unaweza kudhoofishwa kutokana na namna unavyopangwa. Katika Bonde la Mto<br />

Pangani, tatizo hili linaonekana kutokea katika ngazi mbili. Kwa upande mmoja, menejimenti siyo shirikishi,<br />

kiasi kwamba shughuli za usimamizi katika sekta moja, kama vile maendeleo ya umwagiliaji- zinaweza kuwa<br />

na athari kubwa katika sekta nyingine kama vile hifadhi ya maji. Kwa upande mwingine, mipaka ya mamlaka<br />

mara nyingi hutokea kuwa na utata, kwa kuingiliana kwa mamlaka za kiutawala au kwa hakika mamlaka<br />

za kisheria zisizotosheleza. Hivyo, mfumo wa Tanzania wa serikali kuu na serikali za mitaa husababisha<br />

kuwapo kwa watendaji wakuu wa kiutawala wawili wanaohusika katika usimamizi wa kila rasilimali moja.<br />

Nchini Kenya, madaraka ya kimaendeleo ya Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani yanaonekana kuingiliana na<br />

yale ya Mamlaka iliyoundwa hivi karibuni ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji.<br />

Jamii za watumiaji rasilimali zinaweza kutatua mengi ya matatizo ya utata wa kiutawala na ufuatiliaji<br />

usiotosheleza kwa kupitia viwango mbalimbali vya ushirikishwaji. Katika Bonde la Mto Pangani,<br />

utekelezaji wa mchakato huu umekabiliwa na matatizo kadhaa. Kwanza, mifumo mingi ambayo<br />

imekusudiwa jamii zihusishwe katika usimamizi imefikishwa kwao, bila kuishirikisha jamii katika<br />

kubuni muundo wa utawala, katika utekelezaji wa mikakati ya usimamizi au kuadhibu wahalifu. Pili,<br />

kwa kuwa jamii inaweza isiwe na mchango mkubwa katika muundo na utekelezaji wa usimamizi,<br />

aina hizi za mifumo kwa kweli zinaweza kudhoofisha uwezo wa jamii kukidhi mahitaji ya maisha au<br />

60


uwezo wao wa kushindana vizuri na watumiaji wengine wa rasilimali. Tatu, aina nyingi za ‘kamati’ za<br />

rasilimali mbalimbali zimeundwa kote katika bonde, badala ya kuziongezea mamlaka serikali za vijiji<br />

zilizokuwepo kabla. Hivyo, utawala wa ngazi ya vijiji umefanywa kuwa mgumu na kamati nyingi za<br />

Usimamizi wa Maliasili zina majukumu yanayoingiliana au kukinzana. Mwisho, njia za mawasiliano kati<br />

ya mamlaka kuu za usimamizi wa maliasili na jamii zinaweza kuwa hazijaendelezwa kiasi cha kutosha.<br />

Matokeo yake, mahitaji na maoni ya jamii yanaweza yasizingatiwe au yasitambuliwe. Kwa namna hiyo<br />

hiyo, malengo ya usimamizi wa rasilimali au hifadhi ya mamlaka za usimamizi wa maliasili zilizowekwa<br />

chini ya makao makuu hazitaeleweka au hata kueleweka vibaya kwa ujumla na jamii.<br />

Mchakato wa kiutawala na wenye urasimu unaweza kukwamisha au kudhoofisha shughuli za usimamizi<br />

zilizokusudiwa kwa nia njema. Kwa mfano, jamii za watumiaji wa rasilimali zimepewa madaraka ya<br />

kutunga sheria ndogo ndogo ambazo zinatambuliwa na serikali kuu, mamlaka za mkoa na wilaya. Hata<br />

hivyo, hatua ya kuziidhinisha itachukua muda mrefu kiasi kwamba juhudi za jamii na msukumo wa<br />

uongozi unadhoofishwa na mamlaka kuonekana kutoziunga mkono.<br />

Bonde la Mto Pangani ni rasilimali inayovuka mipaka ya nchi. Utaratibu unaohitajika ili kuhakikisha kuwa<br />

usimamizi unalingana kwa pande zote Kenya na Tanzania haupo.<br />

Maeneo ya Utafiti<br />

Matatizo yaliyotajwa hapo juu, mara nyingi yanazidishwa na ukosefu wa data sahihi na za kutosha juu<br />

ya mienendo na michakato inayoipa Bonde la Mto Pangani sura yake, na kuathiri usimamizi wake.<br />

Haieleweki wazi jinsi ongezeko la idadi ya watu katika bonde litakavyoathiri rasilimali zake hapo baadaye.<br />

Wala haieleweki vizuri ni aina gani za mbinu za usimamizi wa maliasili zitakazotumiwa, zinazoweza<br />

kufanya kazi katika misongamano kama hii ya watu.<br />

Mengi ya mahitaji ya utafiti katika bonde hili yanahusu maji na haidrolojia. Hivyo, wakati idadi ya matoleo<br />

ya maji yenye hati yanajulikana, uchukuaji usio halali uliojilimbikiza haujulikani. Kwa nyongeza kiasi cha<br />

maji yanayohitajika ili kudumisha mifumo ya mazingira ya bonde pia hakijulikani. Athari za kuelekeza maji<br />

ya Mto Pangani katika eneo la Vinamasi vya Kirua zinahitaji utafiti wa ziada (angalia IVO-NORPLAN,<br />

1997). Mchango wa theluji ya kilele cha Mlima Kilimanjaro kwenye mtiririko wa maji ya Bonde hili<br />

haujulikani, kama ilivyo kwa matokeo ya upunguaji wa theluji hiyo.<br />

Mwisho, utafiti mdogo umefanywa ili kubainisha shughuli za usimamizi zinazofaa ambazo zitaweza<br />

kuendana na tabia na matatizo mahsusi ya bonde hili. Haieleweki jinsi maji yanavyoweza kusambazwa<br />

kwa kiasi cha kutosha na kwa usawa kati ya watumiaji wa maeneo ya juu ya mto na wale wa chini.<br />

Hakuna ufahamu wa jinsi mfumo wa usimamizi unavyoweza kufuatiliwa na kutekelezwa kwa ufanisi<br />

katika mazingira ya utoaji fedha usiotosheleza na usio wa kudumu, mchango mdogo wa kiufundi, viwango<br />

vya chini vya stadi na ushirikishwaji duni wa jamii. Muhimu zaidi, uendelezwaji wa mifumo ya usimamizi<br />

inayoweza kuendelea kuwepo chini ya vikwazo kama hivi hapo baadaye haujatokea. Mwisho, misingi ya<br />

kitaasisi yenye ufanisi ya usimamizi shirikishi wa rasilimali za Bonde bado haijaanzishwa.<br />

Usimamizi wa Bonde la Mto Pangani<br />

Majadiliano yaliyofanyika wakati wa warsha ya mwezi Mei 2002 kuhusu Bonde la Mto Pangani, pamoja na<br />

mahojiano yaliyofanyika ili kusaidia Uchambuzi huu wa Hali halisi, yalipendekeza mambo kadhaa ambayo<br />

menejimenti ya bonde inaweza kuyafikiria. Kati ya hayo ilikuwa hoja kuwa wakazi wa bonde wanahitaji<br />

kufahamu kuhusu Bonde la Mto Pangani na majukumu yake. Kumeibuka malalamiko kwamba bonde hili la<br />

mto halitambuliwi vya kutosha kama kitengo cha utawala, na kuwa watawala na wenye urasimu waliokabidhiwa<br />

madaraka wanashindania kudumisha msisitizo wa utawala wa nchi kimkoa na kitaifa. Wahojiwa walisema fedha<br />

zinazotolewa zinatakiwa ziwe za kutosha na taratibu zinazohusika za utoaji wa fedha ziwe zenye ufanisi.<br />

Menejimenti ya bonde itahitaji kuhakikisha kuwa idara za serikali zinashirikiana na taasisi nyingine za<br />

usimamizi. Data zenye ubora wa hali ya juu zinahitajika kukusanywa ili kuipa taarifa menejimenti, na<br />

menejimenti lazima iwe shirikishi. Mwisho, kati ya mapendekezo kadhaa ya mipango ya kitaifa iliyotolewa<br />

ni kuwa usimamizi wa Bonde la Mto Pangani uunganishwe na mikakati ya kudhibiti ongezeko la watu.<br />

61


Kwa kuwa wengi wa washiriki wa Warsha na watu waliohojiwa kwa ajili ya Uchambuzi huu wa Hali<br />

halisi wametoka kwenye sekta ya maji, mapendekezo mengi ya usimamizi yaliyokusanywa yalihusiana<br />

moja kwa moja na matumizi ya maji na sheria zake. Hivyo, ilipendekezwa kuwa menejimenti itakuwa<br />

na haja ya kufuata mipango ya kazi iliyo wazi ambayo lazima iwe na hatua za kuchukuliwa kutokana na<br />

upotevu wa maji na matumizi ya maji yasiyo ya ufanisi. Menejimenti itatakiwa kuwa na uwezo wa kutoa<br />

mgao wa maji ya kutosha na kwa usawa, na matumizi haramu au yasiyofaa ya maji lazima yafuatiliwe<br />

na kuchukuliwa hatua za kisheria. Matoleo ya maji lazima yawe na hati ili uchukuaji uweze kufuatiliwa.<br />

Wahojiwa walidai kuwa, menejimenti ya bonde pia lazima iwe na uwezo wa kurekebisha uharibifu wa<br />

vyanzo vya maji, na Ofisi ya Bonde lazima iwe na muundo ulioboreshwa wa ukusanyaji ada.<br />

Baadhi ya washiriki wa warsha walikuwa na maoni kuwa upungufu wa maji haukutambuliwa vya kutosha<br />

katika sera za Tanzania na kwamba hili lilihitaji kurekebishwa. Ili kuhakikisha kuwa maoni ya wadau<br />

yanawakilishwa inavyofaa kwenye menejimenti ya maji ya bonde, wito ulitolewa kuwe na uwakilishi mzuri<br />

zaidi wa wadau katika Bodi ya Maji ya Bonde. Mwisho, mkakati wa kutosha unahitajika ili kusimamia<br />

utekelezaji wa Sera mpya ya Maji ya Tanzania.<br />

Baada ya Baraza la Mawaziri kuidhinisha sera mpya ya maji Julai 21, 2002 Mkakati wa Taifa Kuendeleza<br />

Sekta ya Maji (MTESM), uliandaliwa. Mkakati unaainisha namna sera ya maji itakavyotekelezwa na<br />

unaeleza mabadiliko ya ki-sheria na kitaasisi yanayohitajika ili kufikia malengo yaliyoainishwa katika<br />

mkakati huo. Kuhusu mifumo ya kitaasisi mkakati unasema: Maji ni rasilimali ya taifa na kimataifa ambayo<br />

upatikanaji wake haufuati mipaka ya vijiji, wilaya, mikoa, au nchi na zinaweza kusimamiwa vizuri katika<br />

mabonde na bodi za mabonde na kamati za mabonde madogo. Uwakilishi wa halmashauri za wilaya na<br />

serikali za mitaa katika bodi na kamati hizo unahakikisha kuwa kuna sauti ya waliochaguliwa kidemokrasia<br />

katika maamuzi yanayohusu uhifadhi, usimamizi, ugawaji, uendelezaji na utumiaji wa rasilimali za maji.<br />

Pia mkakati unahimiza uainishaji wa maeneo ya sera za sekta muhimu yanayohusu rasilimali za maji<br />

ili yawiane na Sera ya Maji na kuweka wazi wajibu wa kila mhusika katika mfumo unaoweka bayana<br />

majukumu na wajibu na kuepuka kufanya shughuli kwa kurudia au nyingine kusahaulika. Sheria ya maji<br />

ya 2009 ilitungwa ili kuweka mfumo wa kisheria wa usimamizi wa rasilimali za maji.<br />

E. 3 Maeneo ya Kipaumbele ya Kufanyiwa kazi<br />

Kwa msingi wa majadiliano hapo juu, maeneo matatu ya kipaumbele yameainishwa:<br />

1. Uendelezaji wa mikakati ya usimamizi shirikishi ya Bonde la Mto Pangani pamoja na mabaraza<br />

yanayoambatana nayo. Bila shaka Bonde la Mto Pangani linahitaji kwa haraka mikakati ya usimamizi<br />

shirikishi ambayo inaweza kuendana na masuala mbalimbali na yenye utata ambayo yameelezwa katika<br />

Uchambuzi huu wa Hali halisi. Kwa hivyo, inapendekezwa kuwa eneo la kwanza la kipaumbele ambalo<br />

linahitaji kufikiriwa ni uendelezaji wa mikakati hiyo. Katika hatua hii, mkazo unaelekezwa kwenye sehemu<br />

zifuatazo za mkakati huo:<br />

• Ushirikishaji ni muhimu katika mtazamo wa mazingira wa wapangaji mipango na watawala ili<br />

kuhakikisha kuwa menejimenti inafuata mikakati ya mipango ya jumla, na ya bonde lote yenye<br />

uwezo wa kushughulikia rasilimali mbalimbali na matatizo yanayolikabili bonde.<br />

• Ni muhimu Bonde la mto lionekane kama kitengo cha utawala ambamo ndani yake ushirikishwaji<br />

wa usimamizi utatokea na migogoro ya rasilimali itatatuliwa. Pia ni muhimu kuwa matumizi ya<br />

bonde la mto kama kitengo cha utawala yasiwe kinyume cha ukamilifu wa utawala wa kitaifa<br />

na kimkoa na malengo ya sera.<br />

• Chombo cha ziada cha utawala ambacho kinaweza kufikiriwa ni kufuata mfumo wa Usimamizi<br />

wa Mahitaji ya Maji (WDM) (angalia A.2 hapo juu). Kwa kuzingatia ushahidi uliopo, kuwa<br />

upatikanaji wa maji katika bonde umeelemewa, na kwamba mahitaji ya sasa yanazidi<br />

upatikanaji, utekelezaji wa mifumo ambayo itasaidia kuhifadhi maji na kuhimiza matumizi bora<br />

ingekuwa wa muhimu katika mazingira ya usimamizi shirikishi wa bonde.<br />

62


• Upo umuhimu wa kubuni mikakati ambayo katika hatua zake za awali, inaweza kutekelezwa<br />

kwa kuongezwa kadiri mipango na upatikanaji wa fedha unavyoruhusu. Kwa kukosekana<br />

msaada wa kutosha wa mipango na kifedha, mikakati pekee ambayo inaweza kufanya kazi<br />

kupitia matumizi ya haraka na yasiyo na uhakika inaweza kushindikana. Uwezekano mmoja<br />

ni kulenga mipango kwenye mabonde madogo (sub-basin).<br />

• Wingi wa taasisi za kijamii zinazoshughulika na sekta zote zitumiazo maliasili unatatanisha na<br />

hauna ufanisi kiutawala. Hivyo, inafaa kutafuta njia ambazo taasisi za mahali husika zenye<br />

mwelekeo mpana zinaweza kuendelezwa kuwa na uwezo na madaraka ya kutatua matatizo<br />

yote ya usimamiazi wa maliasili katika eneo lake. Kila taasisi itahitaji msaada wa taifa, hususan<br />

katika kuweka sheria ndogondogo za jamii, na kusaidia juhudi za usimamizi za jamii.<br />

• Mipango ya matumizi ya ardhi lazima ifikiriwe kuwa ni sehemu muhimu ya mkakati wa mpango<br />

shirikishi toka mwanzoni.<br />

• Mikakati ya mipango ioane na uelewa wa uwezo na hali ya kifedha kwa baadaye. Haina maana<br />

sana kuanzisha mikakati ya mipango inayotegemea msaada wa fedha, data na mipango<br />

ambavyo ama vitatoweka mara fedha za wahisani zitakapokosekana, au ambayo haioani na<br />

msingi wa muundo wa kitaasisi wa bonde.<br />

2. Uanzishaji wa mikakati inayofaa kuwezesha mazungumzo miongoni na kati ya watumiaji rasilimali<br />

na wasimamizi wa aina mbalimbali na kushirikishwa katika sekta mbalimbali kwa lengo la<br />

kuboresha uelewa katika ngazi zote za usimamizi. Zinahitajika taratibu za kuhakikisha kuwa fursa<br />

za mazungumzo kati na miongoni mwa wadau na wasimamizi zinakuzwa, ili kuhakikisha kuwa<br />

upashanaji habari wa pande mbili unakuwepo, usambazaji habari unaboreshwa na kujua jinsi<br />

wadau wote wanavyofanya kazi katika ustawi wa bonde zima. Ni muhimu uhamasishaji ufanyike<br />

kuhusu nyanja zote za hali na usimamizi wa bonde na wadau wake katika ngazi zote za usimamizi<br />

na uratibu wake. Inapendekezwa kuwa yaanzishwe mabaraza kwa madhumuni haya, ambayo<br />

yatakuwa na mamlaka hadi kwenye usuluhishi wa migogoro.<br />

Kwa nyongeza, mabaraza hayo yangeweza kuwa na uwezo wa kiutawala na utendaji, ambao<br />

sekta zote za utawala katika bonde zinawakilishwa. Kipengele muhimu cha mchakato huu ni<br />

kuhakikisha kuwa njia za kutosha za mawasiliano na mazungumzo zinaanzishwa kati ya ngazi za<br />

juu za utawala na zile za chini kabisa, ngazi ya jamii.<br />

Uwezekano wa kutumia redio na njia nyigine za habari lazima zifikiriwe kama njia zinazoweza<br />

kutumiwa katika uanzishaji wa mazungumzo na zinazofaa kwa usambazaji na ubadilishanaji wa<br />

taarifa. Tahadhari lazima ichukuliwe kuhakikisha kuwa wadau wote na wasimamizi wanafahamu<br />

maendeleo ya sera mpya na mabadiliko katika utawala na kanuni za rasilimali. Majukumu ya<br />

mabaraza yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya ushirikishi lazima yapanuliwe ili kuhusisha wajibu<br />

wa majadiliano na kupashana habari. Juhudi hizi zingeweza kusaidiwa na juhudi za ughani<br />

ambazo pia zingeweza kutumika kupata maoni na kero za jamii husika.<br />

3. Kubainisha na kuendeleza mfumo wa kutosha wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data. Eneo hili la<br />

utendaji halikomei katika uendelezaji wa mifumo ya ukusanyaji data kwa ajili ya data za kihaidrolojia.<br />

Tathmini ya matumizi ya ardhi kwa kutumia Setilaiti na Mfumo wa Habari wa Kijiografia (GIS),<br />

viwango vya matumizi ya ardhi na mabadiliko ya kijiografia ni mahitaji ya msingi katika kuendeleza<br />

upangaji na ufuatiliaji wa matumizi ya ardhi. Kwa nyongeza, njia zitakazofaa kufuatilia na kupima<br />

mabadiliko ya kijamii na kiuchumi na kuongezeka kwa migogoro zinahitajika kuainishwa na<br />

kutekelezwa. Mifumo ya data na ufuatiliaji iliyopendekezwa lazima iendane na uwezo wa ndani<br />

wa kifedha na uendeshaji. Mwisho, matumizi ya mashirika ya kijamii ya usimamizi wa maliasili,<br />

kama njia ya ufuatiliaji wa matumizi ya rasilimali pia lazima yazingatiwe.<br />

63


F Hitimisho<br />

F. 1 Majumuisho ya Matokeo<br />

Itakumbukwa kuwa lengo la awali la Uchambuzi wa Hali halisi lilikuwa kubainisha rasilimali zilizopo<br />

katika Bonde la Mto Pangani na michakato na matukio yanayoziathiri.<br />

Bonde la Mto Pangani lina aina nyingi sana za rasilimali. Baadhi ya rasilimali hizi, na kazi muhimu<br />

zinazofanya katika bonde ni kama zifuatazo:<br />

• Misitu, inafanya kazi muhimu katika haidrolojia ya Bonde, ya kurekebisha kasi ya maji, kupunguza<br />

mmomonyoko, kuhifadhi na kutakasa maji. Aidha, inatoa mchango muhimu wa Bonde la Mto<br />

Pangani kwa bayoanuwai ya dunia.<br />

• Maji katika bonde la mto Pangani ni muhimu kwa uchumi wa kilimo, uzalishaji wa umeme, mahitaji ya<br />

mijini, majumbani, viwandani na mifugo. Maji yanaendeleza maisha ya viumbe vyote katika bonde.<br />

• Bonde hili lina maeneo manne yaliyohifadhiwa. Mlima Kilimanjaro, kipekee una mchango muhimu<br />

sana katika uchumi wa utalii wa taifa, na pia unahifadhi spishi nyingi za mimea na wanyama.<br />

Hifadhi ya wanyamapori ya Mkomazi na Mbuga ya Taifa ya Tsavo Magharibi ni mifano ya Kituo<br />

cha kanda ya Masai-Somali cha Spishi zipatikanazo eneo hilo pekee (Regional Centre of<br />

Endemism).<br />

• Bayoanuwai ya bonde hili haina mfano wake ulimwenguni, na ni eneo lenye umuhimu mkubwa<br />

kimataifa katika masuala ya hifadhi.<br />

• Uvuvi katika bonde la mto Pangani unatoa mchango muhimu wa lishe na uchumi kwa jamii za<br />

vijijini katika bonde.<br />

• Udongo wenye rutuba wa volkano katika bonde la mto Pangani ndio msingi wa uchumi wake wa<br />

kilimo, na kulifanya kuwa ‘eneo muhimu la uzalishaji mazao nchini Tanzania’.<br />

• Uchimbaji madini unatoa mchango muhimu katika uchumi wa taifa na katika kutoa ajira. Manufaa<br />

yake ni lazima yafikiriwe dhidi ya athari zake mbaya, ikiwa ni pamoja na uchafuzi wa mazingira<br />

na udhoofishaji wa kingo za mito.<br />

Hatari zinazokabiliwa na rasilimali za bonde karibu zote zinahusiana na utumiaji uliokithiri. Kiini cha<br />

hatari hizi kinahusiana na ongezeko la idadi ya watu katika mazingira ya umaskini uliokithiri. Umaskini na<br />

uharibifu wa mazingira mara nyingi vinaonekana kwenda pamoja (cf. WCED, 1987). Matatizo ya Usimamizi<br />

wa Rasilimali za Jamii (CPRs) mara nyingi yanafikiriwa kuongezeka kunapokuwa na idadi kubwa ya<br />

watu waliohusishwa, hususan pale mshikamano wa tamaduni zao unapokuwa dhaifu (cf. Ostrom, 1990).<br />

Muundo na uwezo wa kufanya kazi za kujipatia riziki vijijini unanaweza kuhatarishwa wakati uwezo wa<br />

watu wa vijijini kumiliki na kutunza vyanzo vya kutosha vya kujipatia riziki unapotishiwa.<br />

Hapo juu, wadau wa bonde na shughuli zao zilielezwa kama ifuatavyo:<br />

• Shughuli kuu katika bonde ni za viwanda (umeme, uchimbaji madini na kilimo), kilimo (kilimo<br />

cha viwango vikubwa na viwango vidogo, vyote vikitegemea kwa sehemu kubwa umwagiliaji),<br />

shughuli za wafugaji (hususan katika maeneo ya nyanda za chini), na shughuli zinazokua za<br />

mijini. Mashirika yasiyo ya kiserikali na mawakala wa wahisani wa kimataifa wanafanya kazi kati<br />

ya shughuli hizi mbalimbali na maliasili nyingi zilizopo katika bonde hili. Wajibu wa mashirika<br />

haya kimsingi ni kuhifadhi na/au kuendeleza na kuongeza uwezo wa utafutaji riziki vijijini.<br />

64


• Ni muhimu kutambua kuwa, idadi ya watu katika bonde hili ni kubwa. Sehemu kubwa ya idadi hii ya<br />

watu riziki yao inatokana na kilimo, na kuna mengi yanayoonesha kuwa wako hatarini kiuchumi. Kwa<br />

nyongeza, aina mbalimbali na utajiri wa rasilimali uliopo katika bonde hili huwa kivutio cha shughuli za<br />

viwango vikubwa, na hivyo uwekezaji mkubwa umefanyika. Baina ya shughuli hizi kubwa za uwekezaji<br />

na zile zilizo ndogo ndogo za kujitafutia riziki, uwezekano wa kuwepo migogoro ni dhahiri.<br />

• Uchambuzi huu wa Hali halisi umeigawa migogoro ya Bonde la Mto Pangani katika makundi<br />

makuu matatu. Kundi la kwanza linahusiana na migogoro ya viwango, ambayo ilitolewa hoja<br />

kuwa watumiaji wa viwango vidogo mara nyingi inabidi washindane dhidi ya mahitaji makubwa<br />

zaidi ya wenye nguvu katika kuwania rasilimali moja. Eneo la pili la migogoro lililobainishwa<br />

lilihusiana na migogoro ya umiliki. ‘Umiliki’ hapa unahusiana na haki ya mtu ya kusimamia<br />

rasilimali. Ilielezwa kuwa utaratibu wa kuzipangia jamii za watumiaji rasilimali aina tofauti za<br />

vyama na/ au kamati zitakazosimamia rasilimali hizo unazidi kupata umarufu nchini Tanzania.<br />

Matumaini ni kuwa uundaji wa taasisi kama hizi utatoa matokeo bora ya usimamizi. Hata hivyo,<br />

kulikuwa na hoja kuwa namna taasisi hizi mara nyingi zilivyolazimishwa kuiingizwa katika jamii,<br />

ambazo awali hazikuwa na mchango katika ubunifu, malengo au kanuni zake, zingeweza<br />

kudhoofisha ubora wa matokeo ya kazi zao. Kundi la tatu la migogoro linahusiana na mahali.<br />

Hapa, jinsi eneo la kikundi cha watumiaji rasilimali linavyoweza kuwaingiza katika mgogoro na<br />

watumiaji wa mahali pengine, ilizingatiwa. Mfano mzuri wa mgogoro wa aina hii wa ‘mahali’<br />

unaotokea kati ya watumiaji wa sehemu ya juu ya mto na wale wa chini ya mto ulitolewa.<br />

Hapa, watumiaji wa upande wa chini ya mto huathiriwa na matumizi yaliyokithiri ya watumiaji<br />

wa upande wa juu.<br />

Sura D ilieleza kuwa utawala wa maliasili za Bonde la Mto Pangani ni wa kisekta. Shughuli za Idara ya<br />

Misitu na Nyuki hazikulazimika kuoanishwa na baadhi ya seti ya mikakati mipana na mikuu ya usimamzi<br />

wa Bonde la Mto Pangani, bali inafuata sera ya misitu na nyuki kama shughuli za Ofisi ya Maji Bonde la<br />

Pangani zinavyofuata Sera ya Maji ya Taifa.<br />

Utawala huu wa kisekta unapenya hadi kwenye mikakati ya utawala katika ngazi ya jamii. Hivyo, Kamati za<br />

Maliasili za Vijiji vya Tanzania zilizotumika katika Usimamizi wa Pamoja wa Misitu si sawa na Vyama vya<br />

Watumiaji Maji. Jamii zilizo karibu na maeneo ya uvuvi na yaliyohifadhiwa, pia zinaweza kulazimika kuunda<br />

Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe na kamati za ulinzi wa wanyamapori kwa mujibu wa sera za Idara ya<br />

Wanyamapori na Idara ya Uvuvi. Wingi wa asasi za vijijini nchini Tanzania umezifunika zile zilizoundwa<br />

hapo awali kama Serikali za Vijiji. Mara nyingi, kazi ambazo kikundi kimoja kinatakiwa kifanye hazitofautiani<br />

na kazi ambazo vikundi vingine vinafanya. Hatimaye inabidi asasi zote hizi zijishughulishe na ugawaji wa<br />

haki wa rasilimali katika jamii, matumizi yake endelevu na kuzilinda kutokana uvamizi wa watu kutoka nje.<br />

Nchini Kenya, kinyume chake, kuna vikundi vichache sana vya namna hiyo, ingawa sera mpya za<br />

maliasili zinazidi kutaka kuwashirikisha watumiaji katika miundo yake ya usimamizi.<br />

Sura D ilitilia mkazo vipengele vifuatavyo:<br />

• Sheria ya maji inaipa madaraka bodi ya maji kuandaa mipango ya usimamizi wa wa rasilimali za<br />

maji ambayo itakuwa msingi wa kugawa maji Sheria mpya imeweka mfumo wa ngazi za utawala<br />

zenye ufanisi na mfumo wa kitaasisi ulio wazi ambao unaonyesha majukumu ya kila mmoja katika<br />

kutekeleza sera na sheria. Sera mpya ya maji ya Kenya inaelekeza uundwaji wa mamlaka ya<br />

usimamizi wa rasilimali za maji unaohusisha wadau wote katika kusimamia rasilimali za mabonde.<br />

• Idara ya Misitu na Nyuki inaonekana kutokuwa na mipango yoyote inayofanana na hii ya<br />

kujipanga upya, na utawala wa misitu katika bonde unabaki kati ya tawala mbili za ngazi ya<br />

taifa na mkoa. Nchini Kenya, uundaji upya wa Idara ya misitu bado haujatoa matunda. Hii<br />

inaweza kuwa na matokeo ya ustawi mdogo kwa sehemu ya Bonde iliyoko Kenya, ambayo<br />

inapata matatizo hasa yatokanayo na ukataji miti nchini Tanzania.<br />

• Sera zote, ya maji na ya misitu katika bonde zinazidi kutilia mkazo matumizi ya mashirika<br />

ya kijamii katika utekelezaji wao. Kwa upande wa Tanzania, kuna hofu juu ya kiasi ambacho<br />

mashirika haya yamepandikizwa katika jamii. Ikiwa jamii hazikushirikishwa katika ubunifu na<br />

65


utekelezaji wake, matokeo ya usimamizi yanaweza yasiwe ya kuridhisha. Mafunzo wanayoyapata<br />

Watanzania kutokana na uzoefu huu yanaweza kuwa na manufaa katika ubunifu na utekelezaji<br />

wa mifumo ya namna hii huko Kenya.<br />

• Mtandao wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data katika bonde unaonekana kuwa duni, bila kujali<br />

sekta ya rasilimali. Sura hii imetahadharisha kuwa kusisitiza ukusanyaji data kama jambo muhimu<br />

kwa mfumo wa usimamizi hakuna maana ikiwa data hazitawezesha ufuatiliaji wa kiusimamizi.<br />

Dhumuni la pili la Uchambuzi wa Hali halisi lilikuwa kubainisha kwa mapana maeneo ya utendaji ambamo<br />

hatua zinaweza kuchukuliwa kwa manufaa.<br />

Sura E ilitumia kumbukumbu za warsha kuhusu Bonde la Mto Pangani na mfululizo wa mahojiano na<br />

wadau wa bonde kuorodhesha matatizo na masuala ya bonde. Kwa msingi huo maeneo matatu ya<br />

kipaumbele cha utendaji yalibainishwa. Maeneo haya yalikuwa:<br />

• Kuendeleza mikakati ya usimamizi shirikishi kwa ajili ya Bonde la Mto Pangani pamoja na<br />

mabaraza yanayoambatana nayo. Bila shaka Bonde la Mto Pangani linahitaji mikakati ya<br />

usimamizi shirikishi inayoweza kuendana na masuala mbalimbali na yenye utata yaliyoelezwa<br />

katika uchambuzi huu wa hali halisi.<br />

• Uanzishaji wa mikakati inayofaa kuwezesha mazungumzo miongoni na kati ya watumiaji<br />

rasilimali na wasimamizi wa aina mbalimbali na kushirikishwa katika sekta mbalimbali kwa<br />

lengo la kuboresha uelewa katika ngazi zote za usimamizi. Inahitajika mifumo ya kuhakikisha<br />

kuwa nafasi za mazungumzo baina na kati ya wadau na wasimamizi zinaongezwa, ili<br />

kuhakikisha kuwa kunakuwepo na upashanaji taarifa wa pande mbili, usambazaji wa taarifa<br />

unaboreshwa na maarifa ya jinsi wadau wote wanavyotimiza wajibu wao katika ustawi wa<br />

bonde hili unafikiwa. Ni muhimu uelewa ujengwe kwenye vipengele vyote vya hali na usimamizi<br />

wa Bonde na wadau wake kwenye ngazi zote za usimamizi na uratibu wake. Vipengele vingine<br />

vya ziada katika eneo hili la kipaumbele ni uanzishaji wa mabaraza yenye uwezo wa kufanya<br />

kazi hii, pamoja na kufanya kazi kama nyenzo ya kuondoa migogoro, na kupunguza tofauti kati<br />

ya ngazi mbalimbali za utawala.<br />

• Kuainisha na kuendeleza mfumo wa kutosha wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data. Eneo hili<br />

la utendaji halikomei katika uendelezaji wa mifumo ya ukusanyaji data kwa ajili ya data za<br />

kihaidrolojia. Tathmini za Setilaiti na GIS za matumizi ya ardhi, viwango vya matumizi na<br />

mabadiliko ya kijiografia ni mahitaji ya awali katika kupanga na ufuatiliaji wa matumizi ya ardhi.<br />

Kuendeleza mbinu za kutathmini na kupima sababu za kijamii na za kiuchumi za uharibifu<br />

wa mazingira na matumizi yaliyokithiri ya rasilimali pia zinahitajika kutambuliwa. Mifumo hiyo<br />

lazima pia iwe na uwezo wa kutambua mahitaji ya maji katika bonde. Mifumo ya data na<br />

ufuatiliaji inayopendekezwa lazima ioane na uwezo wa ndani kifedha na uendeshaji.<br />

Lengo la tatu ya Uchambuzi wa Hali Halisi ilikuwa ni kutambua mashirika mengine, shughuli au asasi<br />

ambazo <strong>IUCN</strong> inaweza kuingia nazo ubia wakati inapojaribu kuanzisha juhudi za WANI katika Bonde<br />

la Mto Pangani.<br />

Katika kifungu cha C6, ushiriki wa mashirika yasiyo ya kiserikali na mashirika ya kimataifa ulizingatiwa<br />

na kufanyiwa tathmini kufuatana na mchango wao muhimu katika kuendeleza na kutekeleza mikakati<br />

ya usimamizi shirikishi kwa ajili ya bonde hili. Hapa tunauendeleza zaidi ule uchambuzi na kupendekeza<br />

njia ambazo asasi hizi zinaweza kuchangia katika usimamizi shirikishi wa Bonde la Mto Pangani.<br />

• Utaalamu wa PAMOJA uko kwenye eneo la kukuza majadiliano, hususan kati ya Serikali<br />

na shughuli za kijamii. Utaalamu huu unaweza kutoa mchango wa muhimu sana katika<br />

kuunganisha mipango na utawala wa serikali na ngazi ya chini ya jamii katika usimamizi wa<br />

rasilimali. Wakati huo huo, ni muhimu kuwa matatizo na mawazo ya jamii yazingatiwe vya<br />

kutosha katika utoaji maamuzi na utendaji wa serikali. PAMOJA ina uwezo wa kuhakikisha<br />

kuwa hili linafanyika.<br />

66


• Shirika la Umwagiliaji maji Kiasili na Uendelezaji wa Mazingira (TIP) lina uzoefu sawa na<br />

PAMOJA, na linaweza kuboresha matumizi yake. Hata hivyo, la kuvutia zaidi ni michango ya<br />

kiufundi ambayo TIP inaweza kutoa katika kusanifu na kuendeleza miundombinu itakayoboresha<br />

usafirishaji maji (mifereji ya umwagiliaji ) na utawala wake.<br />

• Uzoefu wa Mpango wa Utendaji wa Misitu Tanzania (TFAP) wa kuendeleza ngazi ya jamii na<br />

kuishirikisha katika ufumbuzi wa matatizo ya rasilimali , unaonekana kuwa wa manufaa katika<br />

Bonde la Mto Pangani. Uendelezaji wa mifumo hii kwa jamii zinazoishi kando ya misitu ya bonde<br />

hili ungekuwa ni jambo la kufurahiwa kwa mpango wowote wa usimamizi katika bonde. Kama<br />

ingeunganishwa na shughuli za Kikundi cha Hifadhi ya Misitu Tanzania (TFCG), ueneaji wa<br />

juhudi hizi ungeongezeka zaidi, mashirika yote haya mawili yangefaidika kwa pamoja kutokana<br />

na kubadilishana uzoefu na maarifa na mkakati wenye ufanisi wa kushughulikia upotevu na<br />

uharibifu wa misitu ungeanzishwa.<br />

• Programu ya Hifadhi na Maendeleo ya Kanda ya Pwani ya Tanga (TCZCDP) ina uzoefu muhimu<br />

kivitendo katika uundaji wa mkakati wa usimamizi shirikishi wa maliasili, ambao Bonde la Mto<br />

Pangani ungeweza kujifunza kutoka kwake na kuweza kujijenga kiuwezo, ikieneza mafunzo<br />

haya kuelekea juu na mbali zaidi kutoka eneo la mamlaka ya kisheria la TCZCDP. Eneo la<br />

mamlaka ya kisheria la Ubia wa Usimamizi wa Pwani ya Tanzania (TCMP) ni kubwa zaidi, na<br />

kwa sababu hiyo, shirika hili lingeweza kuwa na uzoefu wa hali ya juu wa usimamizi shirikishi<br />

wa maeneo makubwa yenye aina nyingi sana za maliasili.<br />

• Mradi wa Usimamizi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Maji na Uboreshaji wa Kilimo cha<br />

Umwagiliaji cha Wakulima Wadogo wadogo (RBMSIIP) ni mradi pekee uliojaribu kutumia mwelekeo<br />

wa kimabonde katika kutatua matatizo ya Bonde la Mto Pangani. Kwa nyongeza, pia umejaribu<br />

kushirikisha masuala ya hifadhi ya maji na juhudi za maendeleo ya maji. Maarifa yaliyomo kwenye<br />

Mradi huu katika maeneo haya ni muhimu sana katika kuendeleza mikakati ya usimamizi kwa ajili<br />

ya bonde. Zaidi ya hayo, uzoefu wa Mradi huu katika kuendeleza mtandao wa ukusanyaji data za<br />

kihaidrolojia kwa ajili ya bonde pia ni wa manufaa makubwa kwa Bonde la Mto Pangani.<br />

• Uzoefu wa Mradi wa Bayoanuwai za kimataifa za Afrika Mashariki (EACBP) wa UNDP-GEF<br />

katika usimamizi wa rasilimali za kimataifa ni muhimu kwa Bonde la Mto Pangani. Kwa<br />

nyongeza, uzoefu wa EACBP wa uundaji na utekelezaji wa usimamizi wa pamoja wa misitu<br />

kijamii ungeweza kuwa wenye manufaa kwa usimamizi shirikishi wa bonde.<br />

Ofisi ya Maji Bonde la Pangani inashirikiana na baadhi ya mashirika haya na kwa hiyo hii inaweza kuwa<br />

orodha ya manufaa kwa kumbukumbu ya baadaye.<br />

67


G<br />

Rejea<br />

Published sources:<br />

Akitanda, P. 2002. South Kilimanjaro catchment forestry management strategies: perspectives and<br />

constraints for integrated water resources management in Pangani Basin. In Ngana, J. O.<br />

(ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches.<br />

Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 152 – 160.<br />

Baker, N. E. and Baker, L. M. 2001. Tanzania. In Fishpool, L. D. C. and Evans, M. I. (eds.) Important<br />

bird areas of Africa and its associated islands: priority areas for conservation. Newbury and<br />

Cambridge, UK, Pisces Publications and BirdLife International (BirdLife Conservation Series<br />

No. 11).<br />

Baldwin, R. R. 1946. Native Authority afforestation on Mt. Kilimanjaro. Tanzania Notes and Records 21<br />

(1946): 81 – 84.<br />

Bergkamp, G., Orlando, B. and Burton, I. 2003. Change: Adaptation of water resources to climate change.<br />

<strong>IUCN</strong>/WANI. Gland, Switzerland and Cambridge, UK, World Conservation Union.<br />

Berkes, F. (ed.) 1989. Common property resources: ecology and community based sustainable<br />

development. London, Belhaven Press.<br />

Burgess, N., FitzGibbon, C. and Clarke, P. 1996. Coastal Forests. In: McClanahan, T. R. and Young, T.<br />

P. (eds.) East African ecosystems and their conservation. New York, Oxford University Press:<br />

329 – 359.<br />

Bwathondi, P. O. J. and Mwamsojo, G. U. J. 1993. The status of the fishery resource in the wetlands of<br />

Tanzania. G. L. and Crafter, S. A. (eds.) Wetlands of Tanzania: proceedings of a seminar on<br />

the wetlands of Tanzania, Morogoro, 27 – 29 November, 1991. <strong>IUCN</strong>, Gland, Switzerland:<br />

49 – 60.<br />

Cheke, R. A., Mann, C. F. and Allen, R. 2001. Sunbirds: A guide to the sunbirds, flowerpeckers,<br />

spiderhunters and sugarbirds of the world. Helm Identification Guides. London, Christopher<br />

Helm.<br />

Conway, G. R. and Barbier, E. B. 1990. After the green revolution: sustainable agriculture for development.<br />

London, Earthscan Publications Ltd.<br />

Cordeiro, N. J. 1998. A preliminary survey of the montane avifauna of Mt Nilo, East Usambaras, Tanzania.<br />

Scopus 20 (May 1998): 1 – 18.<br />

Crean, K. and Geheb, K. 2001. Sustaining appearances: sustainable development and the fisheries of<br />

Lake Victoria. Natural Resources Forum 25 (2001): 215 – 224.<br />

Dadzie, S., Haller, R. D. and Trewavas, E. 1988. A note on the fishes of Lake Jipe and Chale [sic.] on the<br />

Kenya – Tanzania Border. Journal of the East African Natural History Society and National<br />

Museum 78 (192): 46 –51.<br />

Dobson, E. B. 1940. Land tenure of the Wasambaa. Tanzania Notes and Records 10 (1940): 1 – 27.<br />

Ellis, F. 2000. Rural livelihoods and diversity in developing countries. Oxford, Oxford University Press.<br />

Evans, T. D. 1997. Records of birds from the forests of the East Usambara lowlands, Tanzania, August<br />

1994 – February 1995. Scopus 19 (1997): 92 – 108.<br />

FAO (Food and Agricultural Organization), 2001. Food Balance Sheets. www.fao.org. Rome, Food and<br />

Agricultural Organization.<br />

68


Ferguson-Lees, J. and Christie, D. A. 2001. Raptors of the world. Boston, Houghton Mifflin Company.<br />

Geological Survey, 1960. Summary of the geology of Tanganyika. Part II: Geological map. Dar es<br />

Salaam, Geological Survey, Ministry of Mines and Commerce.<br />

Gillingham, M. E. 1999. Gaining access to water: formal and working rules of indigenous irrigation<br />

management on Mount Kilimanjaro, Tanzania. Natural Resources Journal 39 (3): 419 – 441.<br />

GWP, 2002. Policy guidance and operational tools. ToolBox: Integrated Water Resources Management,<br />

Version 1. Global Water Partnership.<br />

Hastenrath, S. and Greischar, L. 1997. Glacier recession on Kilimanjaro, East Africa. Journal of Glaciology<br />

43 (145): 455 – 459.<br />

Homewood, K. and Brockington, D. 1999. Biodiversity, conservation and development in Mkomazi Game<br />

Reserve, Tanzania. Global Ecology and Biodiversity 1999 (8): 301 – 313.<br />

Howard, G. (ed.). 1999. Lake Jipe Cross-border Planning Workshop on a Proposal for the Development of<br />

Mechanisms for Trans-boundary Management of a Shared Ecosystem. 13th - 15th October,<br />

1999, Moshi (Tanzania and Taveta (Kenya). <strong>IUCN</strong> - The World Conservation Union, Eastern<br />

Africa Regional Programme. Nairobi, December, 1999.<br />

Howard, G. 2002. Integrated River Basin Management (IRBM). In: The Pangani River Basin: Options for<br />

Integrated Management. Report on a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi,<br />

Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 92 - 95.<br />

<strong>IUCN</strong>, 1999. Situation Analysis: an <strong>IUCN</strong> approach and method for strategic analysis and planning based<br />

on the experience of <strong>IUCN</strong> Regional and HQ programmes. Prepared by the M&E Initiative.<br />

Revised July 1999. Gland, The World Conservation Union (<strong>IUCN</strong>).<br />

IVO – NORPLAN 1997. Pangani River Training Project Feasibility Study. PBWO – TANESCO, Pangani<br />

Falls Redevelopment. IVO International and NORPLAN A/S.<br />

Johnston, P. H. 1946. Some notes on land tenure on Kilimanjaro and the kihamba of the Wachagga.<br />

Tanzania Notes and Records 21 (1946): 1 – 20.<br />

Kaihura, F. B. S., Stocking, M. and Kahembe, E. 2001. Soil management and agrodiversity: a case<br />

study from Arumeru, Arusha, Tanzania. Paper presented to the symposium on Managing<br />

Biodiversity in Agricultural Systems, Montreal, Canada, November 8 - 12, 2001.<br />

Keith Eltringham, S., Morley, R. J., Kingdon, J., Coe, M. J. and McWilliam, N. C. 1999. Checklist:<br />

Mammals of Mkomazi. In Coe, M. J., McWilliam, N. C., Stone, G. N. and Packer, M. J. (eds.).<br />

Mkomazi: the ecology, biodiversity and conservation of a Tanzanian Savanna. London, Royal<br />

Geographical Society (with the Institute of British Geographers): 505 – 510.<br />

Keith Eltringham, S., Cooksey, I. A., Dixon, W. J. B., Raine, N. E., Sheldrick, C. J., McWilliam, N. C. and<br />

Packer, M. J. 1999. Large mammals of Mkomazi. In Coe, M. J., McWilliam, N. C., Stone, G. N.<br />

and Packer, M. J. (eds.). Mkomazi: the ecology, biodiversity and conservation of a Tanzanian<br />

Savanna. London, Royal Geographical Society (with the Institute of British Geographers):<br />

485 – 504.<br />

Kijazi, A. S. 2002. Catchment and mangrove management programmes: activities and environmental<br />

concerns in the Pangani Basin. In: The Pangani River Basin: options for management.<br />

Report of a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002.<br />

December 2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 36 - 40.<br />

Lambrechts, C., Woodley, B., Hemp, A., Hemp, C. and Nnyiti, P. 2002. Aerial survey of the threats to Mt.<br />

Kilimanjaro forests. Dar es Salaam, GEF Small Grants Programme, UNDP.<br />

69


Lein, H. 2002. Migration, irrigation and land-use changes in the lowlands of Kilimanjaro, Tanzania. In<br />

Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues<br />

and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 28 – 38.<br />

Lovgren, S. 2001. All That Glitters. With Rena Singer and David Enrich. U.S. News & World Report, 131<br />

(6), 13/8/2001.<br />

Luhikula, G. 2002. The Tanzania Coastal Management Partnership (TCMP): a partner in conservation. In:<br />

The Pangani River Basin: Options for Integrated Management. Report on a Workshop held at the<br />

Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 86 – 90.<br />

Majtenyi, C. and Muindi, M. 2001. Tanzania: big is beautiful at Merelani. New African, Oct. 2001, Issue 400.<br />

Makule, D. E. n.d. The Pangani Basin Water Resources Management. http://srdis.ciesin.columbia. edu/<br />

cases/tanzania-019.html<br />

Mbonile, M. J. 2002. Rural population mobility in the Pangani Basin, Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.)<br />

Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches.<br />

Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 14 – 27.<br />

McCay, B. J. and Acheson, J. M. (eds.) 1987. The question of the commons: the culture and ecology of<br />

communal resources. Tucson, University of Arizona Press.<br />

McClanahan, T. R. and Young, T. P. (eds.) 1996. East African ecosystems and their conservation. New<br />

York, Oxford University Press.<br />

Mgongo, E. N. E. 2002. Tanga Coastal Zone Conservation and Development Programme: activities<br />

and concerns in the Lower Pangani River Basin. In: The Pangani River Basin: Options for<br />

Integrated Management. Report on a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi,<br />

Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 81 – 85.<br />

Misana, S. and Makoi, J. 2001. The impact of irrigation on soil fertility and salinity/sodicity in the Pangani<br />

River Basin. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin:<br />

challenges and opportunities. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 83 – 103.<br />

Mjata, P. J. 2002. The Traditional Irrigation and Environmental Development Organisation (TIP). In: The<br />

Pangani River Basin: Options for Integrated Management. Report on a Workshop held at the<br />

Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 78 – 80.<br />

Mkhandi, S. and J. O. Ngana 2001. Trend analysis and spatial variability of annual rainfall. In Ngana,<br />

J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin: challenges and<br />

opportunities. Dar es Salaam University Press, Dar es Salaam. 150pp.: 11 - 20<br />

Mkuula, S. 1993. Pollution of wetlands in Tanzania. In: Kamukala, G. L. and Crafter, S. A. (eds.) Wetlands<br />

of Tanzania: proceedings of a seminar on the wetlands of Tanzania, Morogoro, 27 – 29<br />

November, 1991. <strong>IUCN</strong>, Gland, Switzerland: 85 – 93.<br />

Mpemba, E. B. 1993. Wildlife resources and tourism in wetlands of Tanzania. In: Kamukala, G. L. and<br />

Crafter, S. A. (eds.) Wetlands of Tanzania: proceedings of a seminar on the wetlands of<br />

Tanzania, Morogoro, 27 – 29 November, 1991. <strong>IUCN</strong>, Gland, Switzerland: 61 – 66.<br />

Mtalo, F. W. and Ndomba, P. M. Estimation of soil erosion in the Pangani Basin upstream of Nyumba ya<br />

Mungu Reservoir. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani<br />

River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 196<br />

– 210.<br />

Mujwahuzi, M. R. 2001. Water use conflicts in the Pangani Basin. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources<br />

management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es Salaam, Dar<br />

es Salaam University Press: 128 – 137.<br />

70


Musyoki, M. M. 2003. The situation analysis of the Kenyan part of the Pangani River Basin Catchment: the Lake<br />

Jipe Watershed and system. Mombasa, Kenya: The Coast Development Authority, April 2003.<br />

Musyoki, M. M. and Mwandotto, B. A. J. 1999. Presentation of results/reports on the assessment of<br />

management needs for the watershed wetlands and waters of Lake Jipe. Paper presented at<br />

the Lake Jipe Cross-border Workshop, 13th - 15th October, 1999.<br />

Mwamfupe, D. 2001. Shortage of water for irrigation and farmers’ response: a case study of Makuyuni<br />

and Kahe wards of Kilimanjaro Region, Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources<br />

management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es Salaam, Dar<br />

es Salaam University Press: 73 - 82.<br />

Mwamfupe, D. G., 2002. The role of non-farm activities in household economies: a case study of Pangani<br />

Basin, Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River<br />

Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 39 – 47.<br />

Newmark, W. D. 1998. Forest area, fragmentation, and loss in the Eastern Arc Mountains: implications for the<br />

conservation of biological diversity. Journal of East African Natural History 87 (1998): 1 – 8.<br />

Ngana, J. O. 2001. Integrated water resources management: the case of the Pangani River Basin. In<br />

Ngana, J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin: challenges<br />

and opportunities. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 1 - 8.<br />

Ngula, D. E. P. 2002. Pangani River Basin: power generation and the environment. In: The Pangani<br />

River Basin: options for management. Report of a Workshop held at the Kilimanjaro Crane<br />

Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002. December 2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 67 – 71.<br />

North, D. 1990. Institutions, institutional change and economic performance. Cambridge, Cambridge<br />

University Press.<br />

Nshubemuki, L. 1993. Forestry resources in Tanzania’s wetlands: concepts and potentials. In: Kamukala,<br />

G. L. and Crafter, S. A. (eds.) Wetlands of Tanzania: proceedings of a seminar on the wetlands<br />

of Tanzania, Morogoro, 27 – 29 November, 1991. <strong>IUCN</strong>, Gland, Switzerland:<br />

Ole Sikar, T. Conflicts over natural resources in Maasai district of Simanjiro, Tanzania. Forests, trees and<br />

people - Newsletter No. 30, March 1996.<br />

Ostrom, E. 1990. Governing the commons: the evolution of institutions for collective action. Cambridge<br />

University Press, Cambridge.<br />

PAMOJA, 2002. Dialogue on Water: A concept paper on water resource use and management of conflicts<br />

in the Pangani River Basin: the possible role of PAMOJA. Moshi, PAMOJA.<br />

Richmond, M. D. (ed.) 1997. A guide to the seashores of Eastern Africa and the Western Indian Ocean<br />

Islands. SIDA/Department for Research Cooperation, SAREC.<br />

Rodgers, A. Mugabe, J. and Muthenge, C. 2001. Beyond Boundaries: Regional Overview of Transboundary<br />

Natural Resource Management in Eastern Africa. In Biodiversity Support Program, Beyond<br />

Boundaries: Transboundary Natural Resource Management in Eastern Africa. Washington,<br />

D.C., U.S.A.: Biodiversity Support Program.<br />

Rodgers, W. A. The Miombo Woodlands. In McClanahan, T. R. and Young, T. P. (eds.) East African<br />

ecosystems and their conservation. New York, Oxford University Press: 299 - 325.<br />

RoK (Republic of Kenya) 2002. Kenya Gazette Supplement. Acts, 2002 (no. 9); The Water Act, 2002.<br />

Nairobi, October 24th, 2002. Nairobi, The Government Printer.<br />

RoK (Republic of Kenya) 2003. The First National Water Resources Management Strategy. Nairobi,<br />

Ministry of Water Resources Management and Development, April 2003.<br />

71


Røhr, P. C. and Killingtveit, Å. 2002. Study of two catchments on the hillside of Mt. Kilimanjaro. In Ngana,<br />

J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and<br />

approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 211 – 231.<br />

Røhr, P. C. , Ngana, J. and Killingtveit, Å. 2002. Investigations of Chemka Spring, Kilimanjaro Region,<br />

Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River<br />

Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 265 - 272.<br />

Røhr, P. C., Killingtveit, Å., Nderingo, G. M. and Kigadye, P. E. n.d. Water and environmental conflicts in<br />

the Pangani River Basin – hydropower or irrigation? Undated manuscript.<br />

Røhr, P. C., Killingtveit, Å Rumambo, O. H. 2002. Brief report on the River Basin Management Project in<br />

Tanzania. In: The Pangani River Basin: options for management. Report of a Workshop held<br />

at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002. December 2002. Nairobi,<br />

<strong>IUCN</strong> – EARO: 44 – 48.<br />

Sahib, I. 2002. The Tanzania Planting Company. In: The Pangani River Basin: options for management.<br />

Report of a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002.<br />

December 2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 72 – 73.<br />

Sarmett, J. D. and Kamugisha, S. M. 2002 Control of water utilisation in the Pangani Basin: the role<br />

of PBWO and PBWB. In: The Pangani River Basin: options for management. Report of a<br />

Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002. December<br />

2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 19 – 24.<br />

Schechambo, F. 2002. Forest valuation and economic policies: learning from Mount Meru Forest Reserve.<br />

In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues<br />

and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 161 – 169.<br />

Sishira, E. K. 2002. Land use change and sustainability of water resource utilisation in The Pangani<br />

River Basin downstream of the Nyumba ya Mungu. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources<br />

management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam,<br />

Dar es Salaam University Press: 83 – 89.<br />

Sjöholm, H. and Luono, S. 2002. The green forest pastures of Suledo - Maasai communities organise<br />

to save their forests and secure their livelihoods. Forests, trees and people - Newsletter<br />

No. 46, September, 2002.<br />

Stoorvogel, J. J. and Smaling, E. M. A. 1990. Assessment of soil nutrient depletion in subsaharan Africa:<br />

1983 - 2000. Vol. 1, Main Report. Wageningen, The Netherlands, Winand Staring Centre for<br />

Integrated Land, Soil and Water Research.<br />

Tagseth, M. 2002. Local practises and changes in farmer-managed irrigation in the Himo Catchment,<br />

Kilimanjaro. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River<br />

Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 48 - 63.<br />

TANESCO, 1994. Environmental Impact Assessment of the redevelopment of the hydroelectric power<br />

station at Pangani Falls: Baseline studies: mitigation of adverse impacts and monitoring the<br />

attainment of intended mitigation. IVO – NORPLAN Joint Venture.<br />

URT (United Republic of Tanzania), 2002. National Water Policy. Dar es Salaam, Ministry of Water and<br />

Livestock Development.<br />

Vanden Bossche, J.-P. and Bernacsek, G. M. 1990. Sourcebook for the inland fishery resources of<br />

Africa. Vol. 1. Cifa Technical Paper 18/1. Rome, Food and Agricultural Organization.<br />

Warren, A. 1995. Changing understandings of the nature of environmental paradigms. Transactions of<br />

the Institute of British Geographers NS 20 (1995): 193 - 203.<br />

72


W.C.E.D. 1987. Our common future. Oxford, O.U.P for the World Commission on Environment and<br />

Development.<br />

W.C.M.C. (World Conservation Monitoring Centre). 1985. Arusha National Park Factsheet. www.unep.<br />

wcmc. org<br />

W.C.M.C. (World Conservation Monitoring Centre). 1987. Kilimanjaro National Park Factsheet. www.<br />

unep. wcmc.org<br />

Wegelin-Schuringa, M. 1998. Water Demand Management and the Urban Poor. The Netherlands, IRC<br />

International Water and Sanitation Centre.<br />

West, K. 2002. The Water and Nature Initiative Challenge. In: The Pangani River Basin: Options for<br />

Integrated Management. Report on a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi,<br />

Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, <strong>IUCN</strong> – EARO: 95 – 96.<br />

WHO (World Health Organization). 2001. National health statistics. www.who.org. Geneva, World Health<br />

Organization.<br />

Wily, L. 1999. Moving forward in African community forestry: trading power, not use rights. Society and<br />

Natural Resources 12 (1999): 49 – 61.<br />

Wilson, D. C., Medard, M. Harris, C. K. and Wiley, D. S. 1996. Potentials for comanagement of the Nile perch<br />

fishery – Lake Victoria, Tanzania. Paper presented at the ‘Voices from the Commons’ conference,<br />

International Association for the study of common property, Berkeley, CA, June 5-8, 1996.<br />

UNICEF (United Nations International Children’s Emergency Fund). 2001. The State of the World’s<br />

Children 2000. www.unicef.org. New York, UNICEF.<br />

Yanda, P. Z. and Shishira, E. K. 2001. Forestry conservation and resource utilisation on the southern<br />

slopes of Mount Kilimanjaro: trends, conflicts and resolutions. In Ngana, J. O. (ed.). Water<br />

resources management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es<br />

Salaam, Dar es Salaam University Press: 104 - 117.<br />

Zimmerman, D., Turner, D. Pratt, D Willis, I. 1996. Birds of Kenya and Northern Tanzania. London,<br />

Christopher Helm.<br />

.<br />

73


Wahojiwa<br />

Burra, R., Mshauri, PAMOJA, Arusha tarehe 13, Novemba, 2002<br />

Bwoyo, D., Meneja Misitu wa Eneo la Chanzo cha Mto, Arusha, tarehe 22, Novemba, 2002<br />

Fundi, H., Mtaalam wa Haidrolojia wa Mkoa, Mkoa wa Tanga, Tanga, tarehe 18, Novemba 2002.<br />

Kijazi, A., na Nashanda, E. Idara ya Misitu na Nyuki, Dar es Salaam, tarehe 15, Novemba, 2002<br />

Lugaiyamu, J., Meneja, Mfumo wa Mitambo ya Umeme wa maji Pangani TANESCO, Hale, tarehe 18, Novemba,<br />

2002<br />

Mihayo, J. M., Mkurugenzi, Rasilimali za Maji, Dar es Salaam, tarehe 15, Novemba, 2002<br />

Mjata, P.J., Afisa Mipango wa Matumizi ya Ardhi, TIP, Moshi, tarehe 21, Novemba, 2002<br />

Msuha, M. Afisa ndege, Chama cha Hifadhi ya Wanyama pori cha Tanzania, Dar es Salaam, tarehe 14,<br />

Novemba, 2002<br />

Nasari, J., Mhaidrolojia wa Mkoa, Mkoa wa Arusha, Arusha, tarehe 13, Novemba, 2002<br />

Ngana, J., Profesa Mwandamizi wa Utafiti, Taasisi ya Tathmini ya Rasilimali, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,<br />

tarehe 14, Novemba, 2002<br />

Ngula, D., Meneja- Utafiti na Maendeleo, TANESCO, tarehe 14 Novemba, 2002<br />

Rumambo, O., Mshauri wa Usimamizi wa Bonde, Mradi wa Usimamizi wa Mabonde ya Mito, Wizara ya Maji na<br />

Maendeleo ya Mifugo, Dar es Salaam, tarehe 15, Novemba, 2002<br />

Salehe, J., Meneja Mradi wa Taifa, UNDP/GEF- Mradi wa Bayoanuwai za kimataifa za Afrika ya Mashariki,<br />

Arusha, Novemba, tarehe 22, Novemba, 2002<br />

Sarmett, J., Afisa wa Maji, Ofisi ya Maji Bonde la Pangani, Dar es Salaam, tarehe 14, Novemba, 2002<br />

Serikali ya Kijiji cha Shiri – Njoro, Moshi, tarehe 22, Novemba, 2002;<br />

Tegemeo na Serikali ya kijiji cha Kawaya- Kawaya, tarehe 21, Novemba, 2002.<br />

Waliohojiwa kwa ajili ya kiambatanisho cha 1<br />

Aram, F. V. – Mamlaka ya Maji safi na Majitaka Mjini Tanga.<br />

Denis, E. M. –Ofisi ya Mhandisi wa Maji Wilaya ya Handeni.<br />

Fundi, H. – Afisa wa Haidrolojia wa Mkoa wa Tanga<br />

Hamisi, H. – Mratibu, Hellen Keller International (APOC)<br />

Kisheru, N. – Afisa Maliasili wa Mkoa, RAS Tanga<br />

Lyimo, Z.C.- Afisa Mifugo wa Mkoa, RAS Tanga<br />

Maggid, R.E. B. – Mratibu, Mradi wa CDTI Tanga.<br />

Malange, J. P. –Mhandisi wa maji Mkoa wa Tanga, RAS Tanga<br />

Materu, E.A. – Maabara ya Maji Tanga<br />

Matiku, W. – Misitu ya Eneo la Vyanzo vya Mito Usambara Mashariki<br />

Mwakibuzi, H. – Afisa Mipango wa Wilaya, Muheza<br />

Mzee, R. S. – Hifadhi ya Asili Amani<br />

Mtemi, A. - Hifadhi ya Asili Amani<br />

Sesame, M. – Ofisi ya Mhandisi wa Maji Wilaya ya Handeni<br />

Tungu, L.S. M. – Afisa Kilimo wa Mkoa, RAS Tanga<br />

74


H. Kiambatanisho cha 1: Mabonde madogo<br />

yaliyojumuishwa kiutawala katika<br />

Bonde la Pangani 6<br />

H.1 Utangulizi<br />

Bonde la Mto Pangani lina eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 43,650. Bonde hili limezungukwa na<br />

mabonde madogo yanayojitegemea, amabayo si sehemu hasa ya Bonde la Mto Pangani kihaidrolojia.<br />

Kiutawala yapo chini ya Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWO) kwa sababu ni madogo mno kustahili<br />

kuwa na ofisi za mabonde yao yenyewe. Eneo linalosimamiwa kiutawala na Ofisi ya Maji ya Bonde la<br />

Pangani ni pamoja na Bonde la Mto Pangani, mabonde madogo ya Umba, Zigi 7 , Msangazi, Mkulumuzi<br />

na mito midogo ya pwani, yote pamoja hufanya jumla ya kilomita za mraba 58,510. Katika kiambatanisho<br />

hiki, taarifa kuhusu mabonde haya ya nyongeza zimetolewa kwa muhtasari kama msingi ambapo<br />

shughuli za mradi katika Bonde la Mto Pangani zinaweza kupanuka baadaye ili kujumuisha mabonde<br />

haya ya ziada. Mabonde yanayohusika ni:<br />

• Bonde la Mto Umba (kilomita za mraba 8,070)<br />

• Bonde la Mto Msangazi (kilomita za mraba 5,030)<br />

• Bonde la Mto Zigi (angalia mito ya Pwani)<br />

• Bonde la Mito ya Pwani (kilomita za mraba 2,080 ikiwemo Zigi na Mkulumuzi): mbali na<br />

Mkulumuzi mito mingi ya Eneo la Chanzo cha Mito ya Pwani ni ya msimu.<br />

Kila moja ya maeneo haya ya vyanzo vya mito linajadiliwa kipekee.<br />

H.2 Bonde la Mto Umba<br />

Bonde la Mto Umba lina eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 8,070 (kilomita za mraba 2,560 kati ya<br />

hizo ziko nchini Kenya), ambapo mdomo wa Mto Umba uko eneo la Vanga katika pwani ya Kenya. Mto<br />

huu una mtandao mkubwa wa vijito vingi vikitokea katika miteremko ya Kaskazini Magharibi ya Milima<br />

ya Usambara. Vijito hivi huingia katika mto Umba kutokea Kusini. Mto huu unapata vijito vichache sana<br />

kutoka Kaskazini. Eneo hili hupata mvua ya wastani wa milimita 600 kwa mwaka.<br />

Hifadhi ya wanyamapori ya Umba, ambayo awali ilikuwa sehemu ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Mkomazi,<br />

ipo katika bonde hili. Uoto wa asili wa mbuga hii unachukua eneo kubwa la chanzo cha mto huu:<br />

vichaka vya aina ya Savana ya ukame iliyotawanyika na miti mifupi. Miteremko ya milima katika bonde<br />

inafunikwa na msitu wa milima ya Afrika. Bonde la Mto Umba lina watu wachache. Matumizi makubwa<br />

ya ardhi katika sehemu yake ya Kaskazini ni hifadhi ya wanyamapori, wakati ufugaji wa ngo’mbe ni<br />

matumizi makubwa ya ardhi upande wa Kusini.<br />

6<br />

Kiambatanisho hiki kimetayarishwa na Ofisi ya Maji Bonde la Pangani<br />

7<br />

Baadhi ya Waandishi hutumia tahajia ‘Sigi’, ‘Zigi’ ndio tahajia inayopendelewa na wakazi wa eneo la chanzo cha<br />

mto (pers. Comm., 2003).<br />

75


Kilimo na Umwagiliaji<br />

Kilimo kinachotegemea mvua kinafanyika zaidi kuliko kilimo cha umwagiliaji. Hata hivyo, mbali na<br />

mabonde ya Mkomazi na Luengera, ambayo yapo katika eneo la Bonde la Mto Pangani, miradi mingi<br />

midogo ya umwagiliaji iliyopo au iliyopendekezwa katika mkoa wa Tanga ipo katika bonde la mto Umba<br />

na vijito vyake. Miradi hii ni pamoja na Mnazi, Kitivo, kijiji cha Kivingo Mnazi na mradi wa umwagiliaji<br />

wa Mwakijembe. Zao linalomwagiliwa zaidi ni mpunga, likifuatiwa na mahindi. Katika sehemu za juu za<br />

bonde; mbogamboga na viazi mviringo pia vinalimwa kwa kumwagiliwa. Eneo lililo chini ya mpango wa<br />

umwagiliaji kwa ujumla linakadiriwa kuwa hekta 1475, likitumia kiasi cha maji kinachokadiriwa kuwa mita<br />

za ujazo 25.2 x 106 kwa mwaka.<br />

Maliasili<br />

Maeneo yaliyohifadhiwa<br />

Hifadhi ya wanyamapori ya Umba ina eneo la kilomita za mraba 450 likipakana na mbuga ya Taifa ya<br />

Tsavo ya Kenya. Wanyamapori wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na nyati, tembo, simba na<br />

aina nyingi za swala. Tishio kubwa linaloikabili hifadhi hii ni ujangili unaofanywa na wenyeji na watu<br />

wanaoingia katika eneo hili kutoka Kenya.<br />

Misitu<br />

Eneo la Chanzo cha Mto Umba hapo awali lilikuwa na utajiri wa misitu mingi ambamo zilikuwemo spishi<br />

za miti kama Mkarambati na Mkingu. Mkarambati unatumika zaidi kwa kutengeneza sanaa za uchongaji,<br />

miti ya kujengea na samani. Inavunwa kwa wingi na inadhaniwa kuwa spishi iliyo hatarini kutoweka.<br />

Uvunaji haramu wa misitu kwa ajili ya kutengeneza mkaa pia hufanyika.<br />

Ili kushughulikia tazizo la uvunaji haramu wa misitu, njia za usimamizi wa misitu kijamii zimeanzishwa na<br />

wanavijiji kama vile vijiji vya Mwakijembe, Mwanyumba, Mavovo na Daluni.<br />

Madini<br />

Bonde la Mto Umba lina utajiri wa mashapo ya madini, hususan kuzunguka maeneo ya Mghwashi na<br />

Kararani, johari ya bluu inapatikana, pamoja na ‘tomalini’ ya kijani na ganeti ya waridi. Uchimbaji madini<br />

kwa sasa unafanywa na wachimbaji wadogo ambao hawana masoko ya ndani, na hulazimika kuuza vito<br />

johari vyao kwa njia ya magendo nchini Kenya (Kisheru, Mhojiwa)<br />

Mgogoro wa matumizi ya maji<br />

Kuna migogoro kati ya watumiaji maji kutokana na ugavi usiotosheleza, hasa katika maeneo ambako<br />

kilimo cha umwagiliaji kinafanyika.<br />

Mtandao wa ukusanyaji data<br />

• Kituo cha Mto Umba kilichoko Mlalo (Namba IB 1): kituo kidogo, chenye safu ya geji 0-3 m: kituo<br />

hiki kinafanya kazi, “rating curve” inahitaji kuboreshwa.<br />

• Kituo cha Mto Umba kilichoko Mwakijembe (Namba IB 4A): kituo kikuu, chenye safu ya geji<br />

0-4m; Kituo kina kiingiza data aina ‘orpheus’, kinafanya kazi japo kinahitaji marekebisho.<br />

• Kituo cha Mto Mbalamo kilichoko Kivingo (Namba IB1A): kituo kidogo chenye safu ya geji 0-2m.<br />

Kinahitaji ukarabati.<br />

• Kituo cha Mto Bombo kilichoko Kwamkole (Namba IB 5): kituo kidogo, kinachofanya kazi, kina<br />

safu ya geji 0-3m.<br />

• Kituo cha mvua cha Mlalo (Namba 94.38068); kinafanya kazi na kiko katika hali nzuri.<br />

• Kituo cha hali ya hewa cha Mnazi (Namba 94.38075): kinafanya kazi vizuri, kina vifaa vya upimaji<br />

vya kawaida na kinachojiendesha chenyewe.<br />

76


H. 3 Bonde la Mto Msangazi<br />

Bonde la Mto Msangazi lina ukubwa wa kilomita za mraba 5,030 na linafikiriwa kujumuisha maeneo<br />

ya vyanzo vyembamba vya mito vilivyotanda kutoka Magharibi mpaka Mashariki, karibu upana mzima<br />

wa mkoa wa Tanga. Linapakana na Bonde la Mto Pangani kwa upande wa Kusini. Vijito vingi hutiririka<br />

wakati wa majira ya mvua nyingi kuliko kawaida katika maeneo yake ya juu. Hata hivyo katika sehemu<br />

za upande wa chini wa mji wa Handeni, mto Msangazi hutiririka kwa utaratibu wa kawaida wakati wa<br />

msimu wa masika.<br />

Bonde lina sura ya nchi inayofanana, na linaweza kuainishwa kama vilima, ingawa sehemu za chini<br />

ambako kuna mashamba ya mkonge na minazi ni tambarare. Uoto uliopo ni vichaka na miti michache<br />

ya savana. Mbali na kilimo cha mtawanyiko, sehemu kubwa ya ardhi haijatumika kiuchumi. Wastani wa<br />

mvua kwa mwaka ni kadiri ya milimita 900.<br />

Idadi ya watu<br />

Bonde la Mto Msangazi limeenea wilaya tatu za mkoa waTanga: Kilindi, Handeni na Pangani. Idadi<br />

ya watu katika eneo lilopo katika wilaya ya Kilindi ilikuwa 31,177 mwaka 2002, na Handeni walikuwa<br />

141,263. Idadi hii inawakilisha kadiri ya asilimia 44 ya idadi ya watu wa wilaya hizi mbili. Idadi ya watu<br />

katika bonde la mto Msangazi katika wilaya ya Pangani ni watu 10, 298.<br />

Matumizi ya ardhi<br />

• Kilimo: kilimo ni cha kujikimu. Mazao yanayolimwa ni pamoja na mahindi, mihogo, maharage,<br />

ndizi, miwa na aina mbalimbali za mboga. Zao jipya lililoanzishwa hivi karibuni, mirongeronge,<br />

inatumika kwa kutengeneza mafuta ya kupikia na usafishaji wa maji.<br />

• Mifugo: idadi ndogo ya ng’ombe, mbuzi na kondoo hufugwa katika bonde.<br />

Maliasili<br />

Maji<br />

Mji mkubwa katika bonde la mto Msangazi ni Handeni (watu 7,700). Kiasi kikubwa cha maji kwa<br />

matumizi ya mji huu huchukuliwa kutoka Mto Pangani. Kwa nyongeza, mji huu hupata maji kutoka<br />

kwenye visima virefu viwili: Nderema (mita za ujazo 9 kwa saa) na Mnazini (mita za ujazo 12<br />

kwa saa). Visima hivi huhudumia asilimia 35 ya wakazi wa mji huu. Chanzo cha mwisho cha<br />

maji cha mji huu kinatoka katika moja ya vijito vya mto Msangazi, ambacho kimejengewa bwawa<br />

dogo. Bwawa hili lina uwezo wa kuhifadhi mita za ujazo 22,500, na kadiri ya mita za ujazo 12<br />

huchukuliwa kwa saa.<br />

Misitu<br />

Misitu ya Bondo na Kwamsisi yote miwili ipo katika bonde hili. Spishi za miti zinazopatikana ni<br />

mtondoro, mpingu, mninga na mkomba.<br />

Wanyamapori<br />

Wanyamapori wavumilivu hupatikana sehemu za juu za maeneo ya chanzo cha mto, ikiwa ni pamoja<br />

na nguruwe mwitu, kima, nyani na palahala. Katika sehemu ya chini ya maeneo ya chanzo cha mto<br />

(katika Wilaya ya Pangani) kuna Mbuga ya Taifa ya Sadani, ambamo kuna tembo, twiga, na aina za<br />

paa/palahala<br />

Madini<br />

Bonde la mto Msangazi halina madini muhimu yanayojulikana.<br />

77


Matatizo na migogoro Inayoweza kutokea<br />

• Kuingiliwa na kilimo kuzunguka vyanzo vya maji, zikiwemo kingo za mto.<br />

• Mioto ya vichakani/misituni: Haya ni matatizo makubwa, moto huwashwa ili kusafisha vichaka<br />

kwa ajili ya kilimo.<br />

• Uvunaji haramu wa miti: kwa ajili ya mbao, miti ya kujengea na mkaa. Miti ya mbao inayotakiwa<br />

sana ni mninga, mpingu, mtondoro na mkomba.<br />

• Kuna mgogoro unaoibuka kati ya wafugaji na wakulima juu ya maeneo ya kunyweshea<br />

mifugo.<br />

Magonjwa<br />

Magonjwa yanayotokea kwa wingi katika bonde la mto Msangazi ni malaria na homa ya matumbo.<br />

Kipindupindu na magonjwa mengine yanayosababisha kuharisha hutokea mara chache.<br />

Mtandao wa ukusanyaji data<br />

• Kituo cha Mto Msangazi kilichoko Kideleko (Namba IE 3): kituo kidogo, kinafanya kazi, kina geji<br />

0-1m<br />

• Kituo cha Mto Msangazi kilichoko Kwedilomba (Namba IE 1): kituo kinafanya kazi, safu ya geji<br />

0-2m, kina kiingiza data aina ya ‘Thalamides’.<br />

• Kituo cha hali ya hewa cha Handeni (Namba 95.38079): kinafanya kazi pamoja na kituo<br />

kinachojiendesha chenyewe.<br />

• Kituo cha mvua kilichoko Kwedilomba: kinafanya kazi.<br />

Mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi katika Bonde<br />

la mto Msangazi<br />

• World Vission (shirika lisilo la kiserikali)<br />

• HADEA (Chama cha Maendeleo Handeni)<br />

• HIAP – Mradi Shirikishi wa Kilimo mseto Handeni (lilimaliza shughuli zake mwaka 2002)<br />

• Ded-GTZ-Msaada wa kiufundi na ushauri katika wilaya (maji)<br />

H.4 Bonde la Mto Zigi<br />

Mto wa kudumu wa Zigi huanzia katika miteremko ya mashariki ya Milima ya Usambara, na una vijito<br />

vikuu viwili vinavyotiririka kutoka Kaskazini na Kusini (Muzi na Kihuhwi). Baada ya kuungana, Mto Zigi<br />

hutiririka kuelekea Mashariki na kuingia katika Bahari ya Hindi kupitia Bwawa la Mabayani, chanzo kikuu<br />

cha maji kwa Jiji la Tanga.<br />

Maeneo ya juu ya chanzo cha mto Zigi ni ya milima, ambayo kwa sehemu kubwa ina misitu minene<br />

iliyopakana na mashamba ya chai. Sehemu zake za chini ni za vilima vyenye vichaka vya aina ya savana<br />

kame na miti mifupi, pia mashamba ya mkonge. Katika ukanda wa pwani, minazi na michikichi iko kwa<br />

wingi. Kwa ujumla eneo zima la bonde hili lina uoto wa kutosha na hatari ya mmomonyoko ni ndogo.<br />

Mvua katika Bonde la Mto Zigi ni za misimu miwili. Hata hivyo, mgawanyo wake hutofautiana kati<br />

milimita 1,000 mpaka 2,000. Wastani wa mvua kwa mwaka unakadiriwa kuwa milimita 1,200 hadi<br />

milimita 1,400.<br />

78


Maliasili<br />

Misitu<br />

Kuna hekta 30,000 za msitu katika eneo la Chanzo cha Mto Zigi, ambao unajumuisha msitu wa eneo<br />

la vyanzo cha mito wa Usambara Mashariki (EUCF), ambao ni sehemu ya misitu ya Milima ya Tao la<br />

Mashariki. Umuhimu wa misitu ya eneo la chanzo cha mto ni pamoja na:<br />

• Utoaji mbao na mimea ya dawa kwa jamii;<br />

• Misitu hii ni chanzo cha Mto Zigi, ambao hutoa maji ya matumizi ya nyumbani kwa Jiji la Tanga;<br />

• Kuhifadhi maji kwa kurekebisha kasi ya mtiririko wa maji, kuzuia mmomonyoko wa udongo,<br />

kuboresha upenyaji wa maji kwenye hazina ya maji ya ardhini na ubora wa maji;<br />

• Ni makazi ya viwango vya juu sana vya bayoanuwai, na huchangia kudumisha makundi ya jeni<br />

kidunia;<br />

• Misitu ya kwenye genge la Milima ya Usambara Mashariki huzuia mmomonyoko na mporomoko<br />

wa ardhi.<br />

Bayoanuwai na maeneo yaliyohifadhiwa<br />

Hifadhi ya Asili ya Amani (ANR) ilianzishwa mwaka 1997 na ina jumla ya eneo la hekta 8,380. Hifadhi hii<br />

iko kwenye misitu ya vyanzo vya mito ya Usambara Mashariki (EUCF). Milima ya Usambara Mashariki<br />

ni fungu la mlima lililo kubwa zaidi katika safu ya Milima ya Tao la Mashariki. Hifadhi ya Asili ya Amani ina<br />

misitu mirefu ya kuvutia ya milimani na misitu inayopukutisha majani ya nyanda za chini zenye wastani<br />

wa kikomo cha mwinuko cha mita 850.<br />

Kibayolojia, Hifadhi ya Asili ya Amani ina utajiri mkubwa wa mchanganyiko wa spishi. Milima ya Usambara<br />

Mashariki inachukuliwa kama kituo cha kidunia cha mimea anuwai. Miongoni mwa jenasi na spishi za mimea<br />

inayopatikana katika hifadhi hii ya msitu pekee ni ‘Saintapaulia’ (spishi 9), Cynometra (spishi 4), ‘Streptokapus’<br />

(spishi 2), Impatients katae, Vernonia amaniencis, Dolichometra leucantha na Cordia peter;<br />

Kwa kuongezea, Milima ya Usambara Mashariki inatambuliwa kuwa ni ya pili kwa kuwa na aina mbalimbali<br />

za wanyama barani Afrika. Baadhi ya mamalia wa Hifadhi ya Asili ya Amani wamewekwa kwenye kundi<br />

la walio hatarini kutoweka duniani, kama vile Popo Matunda wa Afrika Mashariki (Myonyctaris relicta),<br />

Panya wadogo (wanaofanana na tembo) wekundu na weusi (Rhyncoyon petersi), Nguchiro wenye mikia<br />

yenye manyoya (Bdeo-grade crassicaud omnivore) na Palahala wa Abbot (Cephalophus spadix).<br />

Halmashauri ya Kimataifa ya Kuhifadhi Ndege (ICBP) imeainisha misitu ya milimani na ya nyanda za<br />

chini ya Usambara ya Mashariki kama eneo maalum la ndege wanaopatikana kipekee (EBA). Spishi kumi<br />

na tatu za ndege walio hatarini kutoweka duniani, kama vile Bundi Tai wa Usambara (Bubo vosseleri)<br />

Kwera Usambara (Ploseus nicolli), Chozi Pwani (Anthreptes pallidigaster), na Kolokolo domorefu<br />

(Apalismoreaui moreaui), wanajulikana kuwa huishi katika Hifadhi ya Asili ya Amani.<br />

Miongoni mwa spishi za amfibia za Hifadhi na Misitu hii, spishi za watambaazi, wanyama wasio na uti<br />

wa mgongo na bayoanuwai pia hupatikana kwa wingi kipekee katika sehemu hii kwa kiwango cha juu<br />

sana. Amfibia wengi huzaliana na kujipatia makazi ndani na kandokando ya Mto Zigi, ambao pia hufanya<br />

makazi kwa spishi nyingi za watambaazi na wadudu.<br />

Maji na Udongo<br />

Hifadhi ya Asili ya Amani ni mojawapo ya maeneo ya chanzo cha maji iliyo muhimu sana katika Milima ya<br />

Usambara Mashariki. Misitu ya mvua ya milimani ambayo huenea sehemu kubwa zaidi ya Hifadhi hii hutoa<br />

mchango muhimu katika haidrolojia ya Mkoa wa Tanga. Mto Zigi hutoa maji kwa matumizi ya nyumbani<br />

kwa Jiji la Tanga (lenye watu 300,000), viwanda vilivyopo, mashamba na jamii zinazopakana nayo.<br />

Bwawa la Mabayani liko katika Mto Zigi, ambalo maji yake hukimu Jiji la Tanga. Hodhi yake ni takriban<br />

mita 3,500 kwa urefu na wastani wa upana wa mita 400. Hapo awali (mwaka 1978), hodhi hii ilikuwa na<br />

79


uwezo wa kuhifadhi mita za ujazo milioni 7.7, lakini kiasi hiki kimepungua polepole kutokana na kujaa<br />

kwa mchangatope kunakosababishwa na mmomonyoko na mporomoko wa ardhi. Mashapo ya ziada<br />

yanatokana na mimea iliyong’olewa na maji ya mafuriko, maji machafu yatokanayo na mchakato wa<br />

kuponoa katani na mata zizalishwazo katika bwawa lenyewe na jamii za mimea na wanyama wadogo<br />

wadogo wanaoishi katika maji, samaki na wanyama wengine wasio na uti wa mgongo.<br />

Uozaji wa mata za viumbe hai unahitaji hewa ya oksijeni, hali inayosababisha uondoaji oksijeni kwenye maji<br />

yanayozizunguka. Kuwepo kwa virutubisho hivyo pia kunachochea uzalishaji wa mimea zaidi, na kusababisha<br />

uzalishaji zaidi wa mata za viumbe hai na hatimaye upunguaji wa oksijeni chini ya bwawa. Mchanganyiko wa<br />

michakato hii ya uingiaji wa virutubisho na hatimaye uondoaji wa oksijeni vinaweza kusababisha ongezeko la<br />

viwango vya virutubisho, ingawa hakujapatikana ushahidi wa jambo hii kutoka kwenye bwawa hilo. Hata hivyo,<br />

shaka ya kuwa hii inaweza kutokea ipo, na yafuatayo ni mapendekezo ya hatua zinazoweza kupunguza:<br />

• Kufuatilia ulimbikizaji wa masimbi/mata za viumbe hai katika bwawa;<br />

• Kuondoa mara kwa mara magugu ya majini (mfano hyacinth na makabichi ya Mto Nile) kutoka<br />

bwawani kwa mikono, kibayolojia au kwa mashine.<br />

• Kudhibiti ubora na ujazo wa maji machafu kutoka viwanda vya katani vilivyopo eneo la juu la<br />

mto;<br />

• Kutambua uwiano wa kiasi cha mimea ya majini ambayo huzolewa kupitia njia ya kupunguzia<br />

maji ya bwawa hili. Ikiwa kiasi ni kidogo, mbinu za kuongeza lazima zitafutwe.<br />

Uvuvi<br />

Uvuvi unafanyika zaidi katika pwani ya Bahari ya Hindi, ambako mdomo wa Mto Zigi ndipo ulipo. Uvuvi<br />

mdogo mdogo upo katika mkondo wake, ukilenga samaki kama kambare, perege, ningu, ngogogo, kuyu<br />

na wengineo. Uvuvi katika bwawa la Mabayani umepigwa marufuku kwa sababu maji yake yamekusudiwa<br />

kama chanzo cha maji ya matumizi ya nyumbani kwa Manispaa ya Tanga.<br />

Ardhi<br />

Matumizi makuu ya ardhi katika bonde ni kilimo, kinachofanyika zaidi katika ngazi ya kiwango kidogo.<br />

Mazao kama mahindi, mihogo, ndizi na matunda yanalimwa, wakati mazao ya biashara ni mkonge, chai na<br />

misitu (kama mradi wa Shamba la Mitiki la Longuza).Kwa kiasi kidogo, ufugaji wa ng’ombe pia hufanyika.<br />

Matatizo<br />

• Uharibifu wa misitu: hii hutokea hasa kama matokeo ya uvunaji haramu wa miti kwa ajili ya mbao,<br />

kuni miti ya kujengea, usafishaji kwa ajili ya kilimo, nk., na husababisha kuongeza kasi ya mtiririko<br />

wa maji juu ya ardhi, wakati ikipunguza kiasi cha maji kinachopenya ardhini.<br />

• Uondoaji wa maji machafu: Maji machafu yanayoondolewa kutoka viwanda vya katani bila<br />

kusafishwa au yasiyosafishwa kikamilifu husababisha uondoaji oksijeni katika maji ambayo uchafu<br />

huu huingia, na hufanya kazi kama virutubisho, hivyo kusaidia kukuza ongezeko la virutubisho.<br />

• Matumizi ya kemikali za kilimo: ingawa hakujapatikana data juu ya athari ya kemikali za kilimo<br />

kwenye vyanzo vya maji katika bonde hili, upo uwezekano kuwa mabaki ya kemikali za kilimo hufikia<br />

vyanzo vya maji kupitia maji ya mvua. Kutegemeana na aina ya kemikali ya kilimo na kiwango cha<br />

kukolea, afya ya binadamu na viumbe vya majini inaweza kuathirika kwa mabaki hayo. Katika eneo<br />

la chanzo cha Mto Zigi, kemikali za kilimo, yakiwemo madawa ya kuulia wadudu, dawa za mimea<br />

na mbolea hutumika zaidi katika mashamba ya chai ya Amani na vitalu vya miti (Materu, Mhojiwa).<br />

• Makazi ya binadamu karibu na vyanzo vya maji: hii husababisha uharibifu wa ardhi na ukusanyikaji wa<br />

mabaki kuongezeka katika maji, uchafuzi wa maji kwa upenyaji wa kinyesi kutoka vyooni au utupaji wa<br />

kinyesi moja kwa moja, na pia kiasili na kikemikali kwa utupaji wa taka ngumu katika maji.<br />

80


• Magugu ya majini: spishi kadhaa za magugu ya majini hupatikana katika Mto Zigi na Bwawa<br />

la Mabayani, kwa mfano magugumaji “water hycinth” (Eichhornia crassipes), makabichi ya Nile<br />

(Pistia stratiotes) na water ivy, (Lpomoea aquatica). Magugumaji yana uwezo wa kufunika uso<br />

wa maji kiasi cha kuathiri ubora wa maji. Hali hii pia inaweza kuathiri afya za binadamu kwa<br />

kuboresha hali zinazohitajika kuwezesha vijidudu vya maradhi kuzaliana, ambavyo ni muhimu<br />

katika mzunguko wa maisha ya pathojeni mbalimbali za binadamu, kama vile mbu (malaria), na<br />

konokono (kichocho).<br />

• Mbinu duni za kilimo: matumizi ya moto kwa kusafisha mashamba, kilimo kwenye miteremko ya<br />

milima, ukataji miti na shughuli nyingine za binadamu katika maeneo ya vyanzo vya maji yanaweza<br />

kuchafua maji kwa kuongeza tope katika maji, rangi na shehena ya masimbi, hususan wakati wa<br />

msimu wa mvua. Sababu hizi zinafikiriwa kusababisha ongezeko la tope katika Bwawa la Mabayani<br />

mwezi Desemba, 1999 kutoka kipimo cha NTU 20-30 hadi NTU 1,400 (Materu, Mhojiwa).<br />

• Magonjwa: Ugonjwa wa Usubi hutokea katika Wilaya ya Muheza, Bonde la Mto Zigi. Husababishwa<br />

na mnyoo (filaria) anayeitwa Onchocerca volvulus. Kimelea hiki huambukizwa kwa binadamu<br />

kwa kuumwa na nzi wadogo weusi. Mbali na upofu, ugonjwa huu pia unasababisha matatizo<br />

makubwa ya ngozi. Nzi hawa huzaliana katika maji yanayotiririka kwa kasi yaliyo na oksijeni<br />

nyingi. Magonjwa mengine katika Bonde la Mto Zigi yanayohusiana na maji ni kipindupindu, homa<br />

ya matumbo na malaria (Maggid, Mhojiwa)<br />

Migogoro iliyopo na Inayoweza Kutokea<br />

• Mgogoro unatarajiwa kutokea kati ya watumiaji maji wa Manispaa ya Tanga na mji wa Muheza.<br />

Upatikanaji wa maji kwa mji wa Muheza kwa sasa hautoshelezi mahitaji, na kuna pendekezo la<br />

kuchukua maji kutoka mto Zigi ambao ni tegemeo pekee la watu wa Jiji la Tanga kwa sasa.<br />

• Mgogoro kati ya matumizi ya maji majumbani na mahitaji ya mazingira: kiasi cha chini kabisa cha<br />

mtiririko wa maji unaotakiwa kuhimili mfumo ikolojia chini ya bwawa la Mabayani hakijulikani.<br />

• Mgogoro kati ya wachafuzi na wasimamizi wa maji: kwa mfano, mgogoro kati ya wasimamizi wa maji<br />

na wenye shughuli za kilimo, pale wasimamizi wa maji wanapojaribu kudhibiti uchafuzi wa maji, kwa<br />

mfano, uchafuzi utokanao na mchakato wa viwanda vya mashamba ya mkonge (Mjesani, Kibaranga,<br />

Lanconi na Bamba), na uchafuzi kutokana na madawa ya kilimo kutoka mashamba ya chai.<br />

Mtandao wa ukusanyaji data<br />

• Kituo cha mto Zigi kilichopo Lancon (Namba IC 1): kituo kikuu, kinafanya kazi, kina safu ya geji<br />

0-10m; kituo kina kiingiza data cha aina ya ‘orpheus’.<br />

• Kituo cha mto Zigi kilichopo Miembeni (Namba IC 2); kituo kidogo, kinafanya kazi na kina safu<br />

ya geji 0-4m; “rating curve” inahitaji kuboreshwa.<br />

• Kituo cha mto Zigi kilichopo Kisiwani (IC 4); kituo kidogo chenye safu ya geji 0-3m. Kipo maalum<br />

kwa matumizi ya misitu ya Bonde la Mto Zigi. “rating curve” inahitaji kuboreshwa. Geji ya 0-1m<br />

imechukuliwa na mafuriko.<br />

• Kituo cha mto Muzi kilichopo Msakazi (ICA 1): kinafanya kazi, lakini “rating curve” inahitaji<br />

kuboreshwa<br />

.•<br />

Kutuo cha mvua cha Zigi-Lancon: kinafanya kazi.<br />

• Vituo vya usawa wa maji na mvua vya Bwawa la Mabayani: vinafanya kazi.<br />

• Vituo vya mvua vya ziada katika bonde vinavyoendeshwa na taasisi mbalimbali, kama vile Msitu<br />

wa Longuza, Msitu wa eneo la vyanzo vya mito, Usambara Mashariki (EUCF) n.k.<br />

81


H.5 Bonde la Mto Mkulumuzi (na mito ya Pwani )<br />

Mito ya pwani huanzia katika genge linaloenda sambamba na pwani kwa umbali wa kilomita 20-30.<br />

Wastani wa mvua katika eneo hili la chanzo cha mto ni milimita 1,100. Ikolojia inalingana kwa kiasi.<br />

Miteremko ya awali ni vilima kwa ujumla, na polepole inakuwa tambarare kadiri inavyoingia uwanda<br />

wa pwani. Minazi, michikichi na mikorosho inatawala uoto. Mkonge pia hustawishwa katika mashamba<br />

makubwa. Matatizo ya mmomonyoko wa udongo hayajaonekana katika maeneo haya..<br />

Mito mingi ya pwani hutiririka kwa vipindi vifupi tu katika msimu wa mvua na huwa mikavu kwa kipindi<br />

kinachobaki cha mwaka. Mto pekee wa kudumu ni Mkulumuzi. Eneo la chanzo cha mto huu ni kilomita<br />

za mraba 337, ambalo lipo upande wa Kusini la eneo la chanzo cha Mto Zigi. Chanzo chake kipo katika<br />

Msitu wa Magoroto.<br />

Maliasili<br />

Maji<br />

Mto Mkulumuzi ni chanzo cha maji cha mji wa Muheza, wenye idadi ya watu wapatao 25,700.<br />

Kilimo<br />

Kilimo katika eneo hili kwa kiwango kikubwa ni cha kujikimu, isipokuwa mkonge, ambao hulimwa katika<br />

viwango vya kibiashara. Mazao ya kujikimu yalimwayo ni pamoja na mahindi, ndizi, mihogo, mpunga, na viazi<br />

vitamu. Matunda (hususan machungwa), nazi, korosho na viungo hulimwa kama mazao ya biashara.<br />

Mifugo<br />

Ufugaji katika maeneo haya si mkubwa sana. Idadi ndogo ya ngo’mbe wa maziwa, mbuzi na nguruwe<br />

hufugwa.<br />

Uvuvi<br />

Ingawa uvuvi ni shughuli inayofanywa na watu wengi katika pwani, hakuna shughuli kubwa ya uvuvi<br />

inayofanyika katika maeneo ya vyanzo vya mito ya pwani.<br />

Migogoro muhimu iliyopo<br />

• Makazi: Mahitaji makubwa ya ardhi ya makazi yametokea baada ya mashamba ya Mkonge kufa,<br />

na wafanyakazi kufukuzwa.<br />

• Maji yasiyotosheleza kwa mji wa Muheza.<br />

Mtandao wa ukusanyaji data<br />

• Kituo cha mto Mkulumuzi kilichoko Upare (hakijasajiliwa): kituo kipya cha upimaji maji mtoni,<br />

kilicho na kiingiza data cha aina ya ‘Thalimedes’<br />

• Kituo cha mto Msimbazi kilichopo Lugongo: kituo kipya cha upimaji maji mtoni chenye safu<br />

ya geji 0-2m.<br />

• Kituo cha hali ya hewa cha Mlingano (chini ya wizara ya Kilimo na Chakula): kinafanya kazi.<br />

Mashirika yanayofadhili<br />

• Irish Aid: hufadhili programu shirikishi zilizopangwa katika eneo hili<br />

• TASAF-Mfuko wa hifadhi ya jamii<br />

• NORAD: hufadhili Programu ya Usafiri na Usafirishaji Vijijini (VTTP)<br />

• <strong>IUCN</strong>: inajishughulisha na Hifadhi ya Mazingira ya Pwani, kwa ushirikiano na Ireland Aid<br />

• AXIOS International: husaidia yatima na watoto walio katika mazingira magumu<br />

• GTZ: husaidia miundombinu ya afya, ufadhili wa ugawaji wa madawa ya msingi kwa vituo vya afya<br />

• APOC/CDTI: Udhibiti wa ugonjwa wa Usubi<br />

82


Mchoro Na 4: Utawala wa Bonde la Pangani<br />

Angalia pia picha ya 2, ukurasa wa 34<br />

(Rejea; Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Maji)<br />

83


Coast Development Authority<br />

<strong>IUCN</strong> – Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Uasili<br />

Likiwa limeanzishwa mwaka 1948, Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Uasili linakutanisha pamoja nchi, mawakala wa nchi<br />

na mashirika mbalimbali yasiyo ya serikali katika ubia wa pekee duniani: zaidi ya wanachama wake 1000, wameenea<br />

katika nchi zaidi ya 160.<br />

Kama shirika, <strong>IUCN</strong> inalenga kushawishi, kutia moyo na kusaidia jamii ulimwenguni kuhifadhi hadhi na anuwai ya uasili<br />

na kuhakikisha kwamba matumizi yoyote ya maliasili yanafanywa kwa stahili na yanakuwa endelevu kiikolojia.<br />

Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Uasili linategemea nguvu ya wanachama wake, mitandao na ubia katika kuendeleza<br />

uwezo wao na kusaidia muungano wa kilimwengu wa kulinda maliasili katika ngazi ya kitaifa, kikanda na kiulimwengu.<br />

Programu ya Maji na Uasili ya <strong>IUCN</strong> (WANI)<br />

Programu ya Maji na Uasili ya <strong>IUCN</strong> (WANI) ni mpango wa utekelezaji wa miaka 5 wa kuonesha kwamba usimamizi<br />

wenye misingi ya mifumo ya ikolojia na ushirikshwaji wa wadau utasaidia katika kukabiliana na changamoto zihusuzo maji<br />

kwa sasa – kuhuisha mito na kuidumisha rasilimali hii kwa manufaa ya wengi.<br />

Ofisi ya Bonde la Pangani (PBWO)<br />

Marekebisho ya sheria ya matumizi ya maji (Na. 10 ya 1981) ya Tanzania yalianzisha utaratibu wa Usimamizi na<br />

Ugawaji wa maji kufuata mipaka ya kihaidrolojia. Kutokana na hiyo Ofisi ya Maji Bonde la Pangani ilianzishwa mwaka<br />

1991. Majukumu yake makuu ni kudhibiti na kusimamia matumizi ya maji, kwa kuzingatia ubora na wingi wake katika<br />

Bonde la Pangani.<br />

Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani (CDA)<br />

Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani ni Mamlaka ya Maendeleo ya Kanda iliyoanzishwa kufanikisha mipango shirikishi ya<br />

maendeleo, uwezeshaji, uanzishwaji, uratibu na utekelezaji wa miradi na programu ndani ya eneo la mamlaka, ambalo ni<br />

Jimbo la Pwani lote na Wilaya ya Ijara na Ukanda Maalumu wa Uchumi wa Kenya (EEZ).<br />

Mpango wa Maji wa Dunia (Global Water Initiative)<br />

Mpango wa Maji wa Dunia unaofadhiliwa na mfuko wa Howard G. Buffet ulianzishwa Septemba 2006 kwa lengo la kuhakikisha jamii<br />

zilizopo katika mazingira hatarishi duniani zinapata huduma ya maji safi na salama bila kuathiri hadhi, haki, utamaduni na mazingira<br />

yao ya asili. Malengo mkakati ya mpango huu ni kusaidia usimamizi wa pamoja wa rasilimali maji katika nchi zilizoainishwa, kuanzisha<br />

na kuendeleza umoja wa watumia maji katika maeneo yao, na pia kueneza ushawishi hata nje ya mipaka ya eneo la mpango huu<br />

ili kufikia wigo mpana zaidi. Mpango unalenga katika kuanzisha ubia baina ya asasi mahsusi katika kanda tatu za kijiografia duniani<br />

kama ifuatavyo: Afrika Mashariki (Ethiopia, Kenya, Tanzania na Uganda), Afrika Magharibi (Burkina Faso, Ghana, Mali, Niger na<br />

Senegal) na Amerika ya Kati (El Salvador, Guatemala, Honduras na Nicaragua). Asasi zinazohusika katika mpango huu kwa sasa ni<br />

“Action against Hunger (AAH), CARE, Catholic Relief Services (CRS), International Institute of Environment and Development (IIED),<br />

International Union of Conservation of Nature (<strong>IUCN</strong>), Oxfam America na SOS Sahel”<br />

Katika kanda ya Afrika ya Mashariki, mpango huu unajulikana kama mkakati wa kukabiliana na ukame (GWI Running Dry) na<br />

unaratibiwa na ofisi ya kanda yenye makao yake Addis Ababa, Ethiopia (chini ya kivuli cha CARE International, Ethiopia).<br />

Pangani Basin Water Board<br />

P.O. Box 5978<br />

Hale Tanga Tanzania<br />

Tel ++ 255 27 2640836<br />

Fax ++ 255 27 2641031<br />

E-mail: pbwo@panganibasin.com<br />

<strong>IUCN</strong> Eastern and Southern Africa<br />

Regional Office<br />

P.O. Box 68200-00200<br />

Nairobi Kenya<br />

T: +254 20 890605-12;<br />

W:+254 20 249 3561/65/70<br />

M: +254 724 256 804 or + 254 734 768 770<br />

F:+254 20 890615<br />

E-mail: earo@iucn.org<br />

Coastal Development Authority (CDA)<br />

P.O. Box 1322<br />

Mombasa Kenya<br />

Tel + 254 41 22440<br />

E-mail: cda@africaonline.co.ke<br />

<strong>IUCN</strong> Water and Nature Initiative<br />

Rue Mauverney 28<br />

CH-1196 Gland<br />

Switzerland<br />

Tel + 41 22 999 0001<br />

Faxl + 41 22 999 0002<br />

E-mail: waterandnature@iucn.org<br />

GWI Running Dry Program<br />

CARE International in Ethiopia<br />

P.O.Box 4710; Addis Ababa, Ethiopia<br />

Phone: +251-11-618 3294 Ext 160<br />

Fax: +251-11-618 3295<br />

Web: http://www.care.org.et

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!