KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center
KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center
KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>KILIMO</strong> <strong>CHA</strong> <strong>VITUNGUU</strong> <strong>MAJI</strong><br />
Kipato kikubwa na hivyo huinua uchumi<br />
Unaweza kuuza mara moja au kuhifadhi<br />
UTANGULIZI<br />
Vitunguu maji hulimwa kama zao la biashara katika sehemu nyingi<br />
duniani zenye hali ya hewa ya ubaridi wastani. Zao hili lina wapatia<br />
watu shughuli za kufanya na hivyo kuwapatia kipato kuanzia kwenye<br />
nyanja za uzalishaji hadi kwenye matumizi. Nchini Tanzania,<br />
vitunguu maji hulimwa kwenye mikoa ya Iringa wilaya ya Kilolo<br />
mpakani mwa mkoa wa Morogoro na kwenye maeneo ya mto Ruaha,<br />
mkoani Arusha sehemu za Mang’ora na Babati, Kilimanjaro, na<br />
Morogoro wilayani Kilosa sehemu za Lumuma na Malolo na baadhi<br />
ya sehemu za Mkoa wa Singida.<br />
Hali ya Udongo<br />
Vitunguu maji huhitaji udongo wenye rutuba, usiopasuka,<br />
usiotuamisha maji na wenye mboji ya kutosha. Hali ya udongo katika<br />
kipimo cha pH iwe kati ya 6.0 na 7.0.
Hali ya hewa<br />
Hali ya hewa ifaayo ni ile ya ubaridi wastani. Joto linalohitajika ni<br />
kati ya nyuzi joto 13 hadi 24°C ingawa kwa miche iliyoko kwenye<br />
kitalu joto zuri ni la nyuzi 20 hadi 25°C. Joto la juu hufanikisha<br />
utengenezaji wa kitunguu na ukaukaji.<br />
Aina ya Vitunguu maji<br />
Kuna aina nyingi ya vitunguu maji. Aina hizi zinaweza<br />
kutofautishwa kulingana na:<br />
(i) rangi ya ganda la nje la kitunguu kilichoishavunwa;<br />
(ii) radha (utamu au ukali) wa kitunguu chenyewe;<br />
(iii) mahitaji ya mwanga katika uzaaji: kuna aina yenye kuhitaji<br />
siku fupi (mwanga wa saa 10 hadi 12 kwa siku) na aina<br />
ihitajio siku ndefu (saa 13 hadi 14 za mwanga kwa siku) ili<br />
kuweza kuweka kitunguu. Aina ya kwanza ndiyo ilimwayo<br />
katika nchi za tropic.<br />
Aina<br />
Red<br />
Creole<br />
Red<br />
Bombay<br />
Texas<br />
Grano<br />
Siku za<br />
kukomaa<br />
150<br />
Umbile<br />
la<br />
kitunguu<br />
Nusu<br />
bapa<br />
160 Duara<br />
165 Duara<br />
Rangi ya<br />
ganda<br />
Nyekundu<br />
Nyekundu<br />
angavu<br />
Njano<br />
(Kaki)<br />
Rangi ya<br />
ndani<br />
Nyekundu -<br />
kahawia<br />
Nyeupe -<br />
kahawia<br />
Nyeupe<br />
Uoteshaji miche na Upandaji<br />
Vitunguu maji huoteshwa zaidi kwa kutumia mbegu kwenye kitalu<br />
na kisha kupandikizwa shambani. Kiasi cha kilo 3.5 cha mbegu hutoa<br />
miche ya kutosha kupandikiza eneo la hekta moja ya shamba.<br />
Kusiha mbegu kwenye kitalu<br />
Mbegu zinasiwa kwenye kitalu kilichoandaliwa vizuri. Mbegu<br />
hupandwa kwenye kina cha sentimita moja kwa kumiminwa polepole<br />
kwenye mistari/mifereji iliyoandaliwa vizuri. Kisha mbegu hufukiwa<br />
kwa kunyunyizia udongo juu ya mbegu zilizoko kwenye mifereji.<br />
Mbegu huota baada ya siku 7 hadi 10. Lakini hii hutegemeana na hali<br />
ya hewa. Kwani mbegu huweza kuechelewa kuota hadi mpaka siku<br />
21 udongo unapokuwa wa baridi. Hali ya hewa ikiwa nzuri, mbegu<br />
uota mapema zaidi, hata ndani ya siku 4.
Kupandikiza vitunguu shambani<br />
Miche hupandikizwa inapokuwa na urefu wa sentimita 15 na unene<br />
1 /2 au 3 /4 ya penseli kwenye shina. Miche hii huwa imetimiza umri<br />
kati ya wiki 7 hadi 9 kulingana na matunzo. Miche inapandikizwa<br />
kwenye nafasi ya upana wa sentimita 20 hadi 30 na nafasi ndani ya<br />
mstari ni sentimita 10 hadi 15.<br />
Kuandaa shamba<br />
Kabla ya kupandikiza udongo utifuliwe vizuri na majani yaondolewe<br />
kabisa. Kisha matuta au majaruba hutengenezwa ili kurahisisha<br />
umwagiliaji.<br />
Mbolea<br />
Vitunguu maji vinamahitaji makubwa ya rutuba ya udongo. Hukua<br />
vizuri vinapopata samadi ya kutosha kiasi cha tani 25 hadi 40. Kwa<br />
hekta. Mbolea isambazwe shambani baada ya kupandikiza, lakini ni<br />
vizuri zaidi kama ikichanganywa kwenye udongo kabla ya<br />
kupandikiza. Kwa kuzingatia mazao ya tani 18 kwa hekta, vitunguu<br />
huchukua kutoka katika udongo, kiasi cha wastani wa kilo 66, 11 na<br />
70 za virutubisho aina ya Nitrojeni, Fosiforasi na Potasiam.<br />
Hivyo kiasi cha mbolea kinachopendekezwa ni kilo 450 hadi 565 za<br />
mbolea ya NPK (10-10-20) kwa hekta. Mbolea huwekwa siku 7 hadi<br />
10 kabla ya kupandikiza. Kisha, inapendekezwa kuweka kiasi cha<br />
kilo 13 hadi 18 za Nitrojeni baada ya wiki tatu hadi nne, ili kuongeza<br />
ukuaji wa mimea. Upungufu wa kirutubisho cha Nitrojeni<br />
unaharakisha ukomaaji na unapunguza ukubwa wa kitunguu.<br />
Kirutubisho hiki kikizidi kupita kiasi huongeza ukubwa wa kitunguu<br />
na unene wa shingo ya kitunguu, tabia ambayo upunguza ubora.<br />
Umwagiliaji:<br />
Umwagiliaji mzuri unahitajika ili kupata vitunguu bora. Umwagiliaji<br />
wa maji yanayokwenda chini kiasi cha sentimeta moja au zaidi kwa<br />
wiki ni mzuri kwa kupata vitunguu vikubwa. Epuka umwagiliaji<br />
kupita kiasi au pungufu kwani hali hii huweza kusababisha<br />
mipasuko.<br />
Udhibiti wa magugu<br />
Ukuaji na mavuno yanaathirika sana endapo magugu hayatadhibitiwa<br />
mapema. Magugu yanadhibitiwa kwa kutumia madawa ama jembe<br />
dogo la mkono. Wakati mwingine ni mchanganyiko wa madawa,<br />
jembe la mkono na kungolea kwa mkono.<br />
Udhibiti wa magonjwa<br />
1. Ugonjwa wa doa la pinki (Purple blotch)<br />
Uanza kama doa dogo linalozama ndani ya jani na kisha<br />
linaongezeka ukubwa na kufanya rangi ya pinki. Kiini cha ugonjwa<br />
huu huanzia kwenye mbegu na pia hubaki kwenye maozo ya majani<br />
ya vitunguu. Aina ya Red Creole inaonyesha kutoshambuliwa sana<br />
na ugonjwa huu.<br />
Ugonjwa wa doa la pinki<br />
Kuoza kwa kitunguu
Mbinu za kudhibiti ugonjwa huu ni kuendesha mzunguko (crop<br />
rotation) wa muda mrefu wa mazao pamoja na kuzuia kutuama kwa<br />
maji shambani. Kupunguza msongamano wa mazao shambani na<br />
matumizi ya mbolea zenye calcium, phosphate and potassium<br />
hupunguza kuenea kwa ugonjwa huu. Kwa upande mwingine,<br />
matumizi ya mbolea ya nitrojeni kwa wingi au kwa kiasi pungufu<br />
uongeza mlipuko wa magonjwa. Viatilifu kama vile Mancozeb<br />
hutumika kuzuia mashmbulizi ya ugonjwa huu.<br />
2. Ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (Downy<br />
mildew)<br />
Magonjwa haya hushambulia majani ya mimea shamabani na hata<br />
miche michanga. Kwenye majani kunaonekana vidoa vyeupe hasa<br />
kwenye majani makuu ya mimea michanga. Ukungu mweupe<br />
unatokea na kuongezeka kwa haraka kwenye sehemu au nyakati za<br />
baridi. Viini huishi kwenye mabaki ya mimea ya vitunguu na huweza<br />
kupeperushwa mbali na upepo. Kwenye mimea michanga ugonjwa<br />
unaweza kudhibitiwa na madawa kama mancozeb.<br />
3. Kuoza kwa vitunguu (bulb rots)<br />
Hali hii inaweza kutokea shambani au wakati wa hifadhi ghalani.<br />
Ugonjwa huu ni hatari zaidi kwenye sehemu za joto na zenye<br />
kutuamisha maji. Ni vyema kuhakikisha kwamba shambani hakuna<br />
hali ya kutuamisha maji na pia kwenye ghala kunakuwa na hali nzuri<br />
ya mzuunguko wa hewa.<br />
Udhibiti wa wadudu<br />
Utitiri wa vitunguu (Onion thrips), Funza wa vitunguu (Onion<br />
maggots) na Minyoo wa vitunguu (Onion wireworms) ni miongoni<br />
mwa wadudu wasumbufu kwenye zao la kitunguu.<br />
1. Utitiri wa vitunguu (Onion thrips)<br />
Hawa ni wadudu wadogodogo sana ambao hula kwa kukwaruza juu<br />
ya jani na kunyonya majimaji ya kwenye mmea. Hali husababisha<br />
kutoka kwa mikwaruzo meupe kwenye majani ya vitunguu.<br />
Mashambulizi yakizidi majani huanguka na kunyauka. Ukubwa wa<br />
vitunguu hupungua. Hili ni tatizo kubwa zaidi hasa wakati wa ukame<br />
kuliko wakati wa unyevu.<br />
Utitiri wa vitunguu Madhara ya utitiri<br />
2. Bungua weupe (White grub)<br />
Huyu ni aina ya funza mkubwa. Hutaga mayai yake kwenye uozo wa<br />
majani na samadi na hivyo mashamba ya vitunguu yaliyoko karibu<br />
au kwenye maeneo ya jinsi hiyo huwa kwenye hatari zaidi.<br />
Hushambulia mizizi na kusababisha kukauka kwa mimea. Kutifulia<br />
shamba na kuwaweka wazi wadudu hawa kunapunguza idadi yao.
Bungua mweupe Funza wa Kitunguu<br />
3. Minyoo ya vitunguu (Onion wireworms)<br />
Hawa ni funza ambao mayai yao hutagwa kwenye maeneo yenye<br />
magugu. Wadudu hawa huwa ni tatizo kubwa kwenye sehemu zenye<br />
kutuamisha maji. Kutifulia udongo ili upitishe maji vizuri pamoja na<br />
udhibiti wa maguu ni njia nzuri ya kuwadhibiti wadudu hawa.<br />
Uvunaji<br />
Inapowezekana mwezi mmoja kabla ya kuvuna udongo uanze<br />
kuondolewa polepole ili kuviacha wazi vitunguu kwa ajili ya<br />
ukaukaji mzuri. Zoezi hili linalenga kufanya angalau theluthi moja ya<br />
sehemu ya kitunguu kiwe hakijafunikwa na udongo kwa siku kati ya<br />
7 hadi kumi kabla ya kuvuna ili kuharikisha ukaukaji. Vuna wakati<br />
asilimia 75 ya shingo za vitunguu zimelala. Mara nyingi vitunguu<br />
hung’olewa na kurundikwa kwenye matuta na baadaye kukusanywa<br />
na kuwekwa kwa ajili ya kukata shingo. Mizizi pia inapunguzwa na<br />
vitunguu vinajazwa kwenye magunia tayari kwa kusafirishwa<br />
nyumbani kwa ukaushaji zaidi na kisha kuwekwa galani au kuuzwa.<br />
Ukaushaji<br />
Madhumuni ya kukausha ni kuvifanya vitunguu visiweze kuota kwa<br />
muda na pia kuvifanya visiharibike. Vitunguu vilivyokauka vizuri<br />
huwa na shingo iliyonywea vizuri na ganda kavu. Kama shingo ya<br />
kitunguu haikukauka sawasawa kutatokea hali ya uozo.<br />
Soko la vitunguu<br />
Ukubwa wa vitunguu ni sifa ingaliwayo na wanunuzi. Vitunguu<br />
vidogodogo sana au vinene sana huwa havipendwi. Vitunguu<br />
vinavyopendwa ni vile vyenye wastani wa unene wa sentimita nne.<br />
Vitunguu vilivyochubuka, mapacha na vyenye shingo ya chupa huwa<br />
havipendwi. Vitunguu vilivyooza na vile vilivyobabuka na jua pia<br />
havifai. Kwa Tanzania wakulima wengi wanauza vitunguu kwa<br />
vipimo vya magunia na ama ndoo za plastiki. Kwa miaka kadhaa<br />
vitunguu vimekuwa vikiuzwa kati ya shilingi 20,000/= hadi 30,000/=<br />
kwa gunia.<br />
Hifadhi ya vitunguu<br />
Vitunguu vipya vilivyovunwa huwa havioti upesi. Hifadhi sahihi<br />
hurefusha muda wa kutoota. Kwenye hifadhi ni vizuri vitunguu<br />
vipate hewa yenye mzunguuko mzuri na ndiyo maana maghala ya<br />
kuhifadhia vitunguu yanajengwa kama vichanja ili kuruhusu hewa<br />
kuzunguuka hata kwa kupitia sehemu za chini. Ndani ya ghala<br />
vitunguu humwagwa na kusambazwa kama inavyonyesha kwenye<br />
picha namba.. Vitunguu vinaweza kuhifadhiwa kwa miezi sita au<br />
zaidi bila kuharibika.<br />
Mavuno<br />
Mavuno ya vitunguu yanategeme huduma za shamba pamoja na hali<br />
ya hewa. Vitunguu pia hutofautiana katika mavuno kulingana na aina<br />
ya kitunguu. Kwa wastani vitunguu vinaweza kutoa mavuno kati ya<br />
tani 10 hadi 18 kwa hekta moja.