17.12.2012 Views

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>KILIMO</strong> <strong>CHA</strong> <strong>VITUNGUU</strong> <strong>MAJI</strong><br />

Kipato kikubwa na hivyo huinua uchumi<br />

Unaweza kuuza mara moja au kuhifadhi<br />

UTANGULIZI<br />

Vitunguu maji hulimwa kama zao la biashara katika sehemu nyingi<br />

duniani zenye hali ya hewa ya ubaridi wastani. Zao hili lina wapatia<br />

watu shughuli za kufanya na hivyo kuwapatia kipato kuanzia kwenye<br />

nyanja za uzalishaji hadi kwenye matumizi. Nchini Tanzania,<br />

vitunguu maji hulimwa kwenye mikoa ya Iringa wilaya ya Kilolo<br />

mpakani mwa mkoa wa Morogoro na kwenye maeneo ya mto Ruaha,<br />

mkoani Arusha sehemu za Mang’ora na Babati, Kilimanjaro, na<br />

Morogoro wilayani Kilosa sehemu za Lumuma na Malolo na baadhi<br />

ya sehemu za Mkoa wa Singida.<br />

Hali ya Udongo<br />

Vitunguu maji huhitaji udongo wenye rutuba, usiopasuka,<br />

usiotuamisha maji na wenye mboji ya kutosha. Hali ya udongo katika<br />

kipimo cha pH iwe kati ya 6.0 na 7.0.


Hali ya hewa<br />

Hali ya hewa ifaayo ni ile ya ubaridi wastani. Joto linalohitajika ni<br />

kati ya nyuzi joto 13 hadi 24°C ingawa kwa miche iliyoko kwenye<br />

kitalu joto zuri ni la nyuzi 20 hadi 25°C. Joto la juu hufanikisha<br />

utengenezaji wa kitunguu na ukaukaji.<br />

Aina ya Vitunguu maji<br />

Kuna aina nyingi ya vitunguu maji. Aina hizi zinaweza<br />

kutofautishwa kulingana na:<br />

(i) rangi ya ganda la nje la kitunguu kilichoishavunwa;<br />

(ii) radha (utamu au ukali) wa kitunguu chenyewe;<br />

(iii) mahitaji ya mwanga katika uzaaji: kuna aina yenye kuhitaji<br />

siku fupi (mwanga wa saa 10 hadi 12 kwa siku) na aina<br />

ihitajio siku ndefu (saa 13 hadi 14 za mwanga kwa siku) ili<br />

kuweza kuweka kitunguu. Aina ya kwanza ndiyo ilimwayo<br />

katika nchi za tropic.<br />

Aina<br />

Red<br />

Creole<br />

Red<br />

Bombay<br />

Texas<br />

Grano<br />

Siku za<br />

kukomaa<br />

150<br />

Umbile<br />

la<br />

kitunguu<br />

Nusu<br />

bapa<br />

160 Duara<br />

165 Duara<br />

Rangi ya<br />

ganda<br />

Nyekundu<br />

Nyekundu<br />

angavu<br />

Njano<br />

(Kaki)<br />

Rangi ya<br />

ndani<br />

Nyekundu -<br />

kahawia<br />

Nyeupe -<br />

kahawia<br />

Nyeupe<br />

Uoteshaji miche na Upandaji<br />

Vitunguu maji huoteshwa zaidi kwa kutumia mbegu kwenye kitalu<br />

na kisha kupandikizwa shambani. Kiasi cha kilo 3.5 cha mbegu hutoa<br />

miche ya kutosha kupandikiza eneo la hekta moja ya shamba.<br />

Kusiha mbegu kwenye kitalu<br />

Mbegu zinasiwa kwenye kitalu kilichoandaliwa vizuri. Mbegu<br />

hupandwa kwenye kina cha sentimita moja kwa kumiminwa polepole<br />

kwenye mistari/mifereji iliyoandaliwa vizuri. Kisha mbegu hufukiwa<br />

kwa kunyunyizia udongo juu ya mbegu zilizoko kwenye mifereji.<br />

Mbegu huota baada ya siku 7 hadi 10. Lakini hii hutegemeana na hali<br />

ya hewa. Kwani mbegu huweza kuechelewa kuota hadi mpaka siku<br />

21 udongo unapokuwa wa baridi. Hali ya hewa ikiwa nzuri, mbegu<br />

uota mapema zaidi, hata ndani ya siku 4.


Kupandikiza vitunguu shambani<br />

Miche hupandikizwa inapokuwa na urefu wa sentimita 15 na unene<br />

1 /2 au 3 /4 ya penseli kwenye shina. Miche hii huwa imetimiza umri<br />

kati ya wiki 7 hadi 9 kulingana na matunzo. Miche inapandikizwa<br />

kwenye nafasi ya upana wa sentimita 20 hadi 30 na nafasi ndani ya<br />

mstari ni sentimita 10 hadi 15.<br />

Kuandaa shamba<br />

Kabla ya kupandikiza udongo utifuliwe vizuri na majani yaondolewe<br />

kabisa. Kisha matuta au majaruba hutengenezwa ili kurahisisha<br />

umwagiliaji.<br />

Mbolea<br />

Vitunguu maji vinamahitaji makubwa ya rutuba ya udongo. Hukua<br />

vizuri vinapopata samadi ya kutosha kiasi cha tani 25 hadi 40. Kwa<br />

hekta. Mbolea isambazwe shambani baada ya kupandikiza, lakini ni<br />

vizuri zaidi kama ikichanganywa kwenye udongo kabla ya<br />

kupandikiza. Kwa kuzingatia mazao ya tani 18 kwa hekta, vitunguu<br />

huchukua kutoka katika udongo, kiasi cha wastani wa kilo 66, 11 na<br />

70 za virutubisho aina ya Nitrojeni, Fosiforasi na Potasiam.<br />

Hivyo kiasi cha mbolea kinachopendekezwa ni kilo 450 hadi 565 za<br />

mbolea ya NPK (10-10-20) kwa hekta. Mbolea huwekwa siku 7 hadi<br />

10 kabla ya kupandikiza. Kisha, inapendekezwa kuweka kiasi cha<br />

kilo 13 hadi 18 za Nitrojeni baada ya wiki tatu hadi nne, ili kuongeza<br />

ukuaji wa mimea. Upungufu wa kirutubisho cha Nitrojeni<br />

unaharakisha ukomaaji na unapunguza ukubwa wa kitunguu.<br />

Kirutubisho hiki kikizidi kupita kiasi huongeza ukubwa wa kitunguu<br />

na unene wa shingo ya kitunguu, tabia ambayo upunguza ubora.<br />

Umwagiliaji:<br />

Umwagiliaji mzuri unahitajika ili kupata vitunguu bora. Umwagiliaji<br />

wa maji yanayokwenda chini kiasi cha sentimeta moja au zaidi kwa<br />

wiki ni mzuri kwa kupata vitunguu vikubwa. Epuka umwagiliaji<br />

kupita kiasi au pungufu kwani hali hii huweza kusababisha<br />

mipasuko.<br />

Udhibiti wa magugu<br />

Ukuaji na mavuno yanaathirika sana endapo magugu hayatadhibitiwa<br />

mapema. Magugu yanadhibitiwa kwa kutumia madawa ama jembe<br />

dogo la mkono. Wakati mwingine ni mchanganyiko wa madawa,<br />

jembe la mkono na kungolea kwa mkono.<br />

Udhibiti wa magonjwa<br />

1. Ugonjwa wa doa la pinki (Purple blotch)<br />

Uanza kama doa dogo linalozama ndani ya jani na kisha<br />

linaongezeka ukubwa na kufanya rangi ya pinki. Kiini cha ugonjwa<br />

huu huanzia kwenye mbegu na pia hubaki kwenye maozo ya majani<br />

ya vitunguu. Aina ya Red Creole inaonyesha kutoshambuliwa sana<br />

na ugonjwa huu.<br />

Ugonjwa wa doa la pinki<br />

Kuoza kwa kitunguu


Mbinu za kudhibiti ugonjwa huu ni kuendesha mzunguko (crop<br />

rotation) wa muda mrefu wa mazao pamoja na kuzuia kutuama kwa<br />

maji shambani. Kupunguza msongamano wa mazao shambani na<br />

matumizi ya mbolea zenye calcium, phosphate and potassium<br />

hupunguza kuenea kwa ugonjwa huu. Kwa upande mwingine,<br />

matumizi ya mbolea ya nitrojeni kwa wingi au kwa kiasi pungufu<br />

uongeza mlipuko wa magonjwa. Viatilifu kama vile Mancozeb<br />

hutumika kuzuia mashmbulizi ya ugonjwa huu.<br />

2. Ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (Downy<br />

mildew)<br />

Magonjwa haya hushambulia majani ya mimea shamabani na hata<br />

miche michanga. Kwenye majani kunaonekana vidoa vyeupe hasa<br />

kwenye majani makuu ya mimea michanga. Ukungu mweupe<br />

unatokea na kuongezeka kwa haraka kwenye sehemu au nyakati za<br />

baridi. Viini huishi kwenye mabaki ya mimea ya vitunguu na huweza<br />

kupeperushwa mbali na upepo. Kwenye mimea michanga ugonjwa<br />

unaweza kudhibitiwa na madawa kama mancozeb.<br />

3. Kuoza kwa vitunguu (bulb rots)<br />

Hali hii inaweza kutokea shambani au wakati wa hifadhi ghalani.<br />

Ugonjwa huu ni hatari zaidi kwenye sehemu za joto na zenye<br />

kutuamisha maji. Ni vyema kuhakikisha kwamba shambani hakuna<br />

hali ya kutuamisha maji na pia kwenye ghala kunakuwa na hali nzuri<br />

ya mzuunguko wa hewa.<br />

Udhibiti wa wadudu<br />

Utitiri wa vitunguu (Onion thrips), Funza wa vitunguu (Onion<br />

maggots) na Minyoo wa vitunguu (Onion wireworms) ni miongoni<br />

mwa wadudu wasumbufu kwenye zao la kitunguu.<br />

1. Utitiri wa vitunguu (Onion thrips)<br />

Hawa ni wadudu wadogodogo sana ambao hula kwa kukwaruza juu<br />

ya jani na kunyonya majimaji ya kwenye mmea. Hali husababisha<br />

kutoka kwa mikwaruzo meupe kwenye majani ya vitunguu.<br />

Mashambulizi yakizidi majani huanguka na kunyauka. Ukubwa wa<br />

vitunguu hupungua. Hili ni tatizo kubwa zaidi hasa wakati wa ukame<br />

kuliko wakati wa unyevu.<br />

Utitiri wa vitunguu Madhara ya utitiri<br />

2. Bungua weupe (White grub)<br />

Huyu ni aina ya funza mkubwa. Hutaga mayai yake kwenye uozo wa<br />

majani na samadi na hivyo mashamba ya vitunguu yaliyoko karibu<br />

au kwenye maeneo ya jinsi hiyo huwa kwenye hatari zaidi.<br />

Hushambulia mizizi na kusababisha kukauka kwa mimea. Kutifulia<br />

shamba na kuwaweka wazi wadudu hawa kunapunguza idadi yao.


Bungua mweupe Funza wa Kitunguu<br />

3. Minyoo ya vitunguu (Onion wireworms)<br />

Hawa ni funza ambao mayai yao hutagwa kwenye maeneo yenye<br />

magugu. Wadudu hawa huwa ni tatizo kubwa kwenye sehemu zenye<br />

kutuamisha maji. Kutifulia udongo ili upitishe maji vizuri pamoja na<br />

udhibiti wa maguu ni njia nzuri ya kuwadhibiti wadudu hawa.<br />

Uvunaji<br />

Inapowezekana mwezi mmoja kabla ya kuvuna udongo uanze<br />

kuondolewa polepole ili kuviacha wazi vitunguu kwa ajili ya<br />

ukaukaji mzuri. Zoezi hili linalenga kufanya angalau theluthi moja ya<br />

sehemu ya kitunguu kiwe hakijafunikwa na udongo kwa siku kati ya<br />

7 hadi kumi kabla ya kuvuna ili kuharikisha ukaukaji. Vuna wakati<br />

asilimia 75 ya shingo za vitunguu zimelala. Mara nyingi vitunguu<br />

hung’olewa na kurundikwa kwenye matuta na baadaye kukusanywa<br />

na kuwekwa kwa ajili ya kukata shingo. Mizizi pia inapunguzwa na<br />

vitunguu vinajazwa kwenye magunia tayari kwa kusafirishwa<br />

nyumbani kwa ukaushaji zaidi na kisha kuwekwa galani au kuuzwa.<br />

Ukaushaji<br />

Madhumuni ya kukausha ni kuvifanya vitunguu visiweze kuota kwa<br />

muda na pia kuvifanya visiharibike. Vitunguu vilivyokauka vizuri<br />

huwa na shingo iliyonywea vizuri na ganda kavu. Kama shingo ya<br />

kitunguu haikukauka sawasawa kutatokea hali ya uozo.<br />

Soko la vitunguu<br />

Ukubwa wa vitunguu ni sifa ingaliwayo na wanunuzi. Vitunguu<br />

vidogodogo sana au vinene sana huwa havipendwi. Vitunguu<br />

vinavyopendwa ni vile vyenye wastani wa unene wa sentimita nne.<br />

Vitunguu vilivyochubuka, mapacha na vyenye shingo ya chupa huwa<br />

havipendwi. Vitunguu vilivyooza na vile vilivyobabuka na jua pia<br />

havifai. Kwa Tanzania wakulima wengi wanauza vitunguu kwa<br />

vipimo vya magunia na ama ndoo za plastiki. Kwa miaka kadhaa<br />

vitunguu vimekuwa vikiuzwa kati ya shilingi 20,000/= hadi 30,000/=<br />

kwa gunia.<br />

Hifadhi ya vitunguu<br />

Vitunguu vipya vilivyovunwa huwa havioti upesi. Hifadhi sahihi<br />

hurefusha muda wa kutoota. Kwenye hifadhi ni vizuri vitunguu<br />

vipate hewa yenye mzunguuko mzuri na ndiyo maana maghala ya<br />

kuhifadhia vitunguu yanajengwa kama vichanja ili kuruhusu hewa<br />

kuzunguuka hata kwa kupitia sehemu za chini. Ndani ya ghala<br />

vitunguu humwagwa na kusambazwa kama inavyonyesha kwenye<br />

picha namba.. Vitunguu vinaweza kuhifadhiwa kwa miezi sita au<br />

zaidi bila kuharibika.<br />

Mavuno<br />

Mavuno ya vitunguu yanategeme huduma za shamba pamoja na hali<br />

ya hewa. Vitunguu pia hutofautiana katika mavuno kulingana na aina<br />

ya kitunguu. Kwa wastani vitunguu vinaweza kutoa mavuno kati ya<br />

tani 10 hadi 18 kwa hekta moja.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!