Notes to the Financial Statements (cont'd) - Kenya Airways
Notes to the Financial Statements (cont'd) - Kenya Airways
Notes to the Financial Statements (cont'd) - Kenya Airways
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
KENYA AIRWAYS LIMITED | ANNUAL REPORT & FINANCIAL STATEMENTS 2011 KENYA AIRWAYS LIMITED | ANNUAL REPORT & FINANCIAL STATEMENTS 2011<br />
Taarifa ya Mwenyekiti (unaendelea)<br />
Taarifa ya Mwenyekiti (unaendelea)<br />
cha asilimia 1.6. Ukuaji huo hasa uli<strong>to</strong>kana na kuimarika<br />
kwa hali ya kiuchumi na kuzinduliwa kwa maeneo mapya<br />
ya usafiri.<br />
Maeneo yaliyorekodi upungufu wa kiwango cha mizigo ni<br />
pamoja na Mashariki ya Kati (-11.2%), Mashariki ya Mbali<br />
(-12.9%) na Afrika Kaskazini (-3.5%). Upungufu katika<br />
maeneo hayo hasa ulikuwa mkubwa katika miezi mitatu<br />
ya mwisho wa mwaka ku<strong>to</strong>kana na misukosuko ya kisiasa<br />
katika Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini. Kudidimia<br />
huko pia kuli<strong>to</strong>kana na ukosefu wa nafasi ku<strong>to</strong>kana na<br />
mizigo mingi kupitia kiasi.<br />
Kiwango cha ubadilishanaji wa fedha<br />
Dola ya Amerika iliimarika dhidi ya Shilingi ya <strong>Kenya</strong><br />
huku kiwango cha wastani cha ubadilishanaji kikiwa Dola1<br />
kwa kila Ksh79.69 ikilinganishwa na kiwango cha mwaka<br />
uliotangulia cha Dola1 kwa Sh76.67. Kuimarika kwa Dola<br />
na kupungua kwa thamani ya Shilingi kulikuwa na ma<strong>to</strong>keo<br />
bora kwenye mapa<strong>to</strong> yanayo<strong>to</strong>kana na fedha za kigeni<br />
yanapogeuzwa kwa Shilingi za <strong>Kenya</strong>. Ma<strong>to</strong>keo hayo bora<br />
hata hivyo yaliathiriwa kwa kiasi fulani na gharama ambazo<br />
zililipiwa kwa kiwango kikubwa kwa fedha za kigeni.<br />
Gharama<br />
Gharama za mafuta<br />
Gharama za mafuta, bila kujumuisha gharama za mkakati<br />
wa kukabiliana na mabadiliko ya bei ya mafuta, ziliongezeka<br />
kwa Ksh5.96bilioni au asilimia 31.7, ikilinganishwa na<br />
mwaka uliotangulia. Nyongeza hii kubwa ili<strong>to</strong>kana hasa<br />
na bei ya juu ya gharama ya mafuta ya ndege ku<strong>to</strong>ka 216/<br />
cag mnamo 2010 hadi 258/cag mnamo 2011, nyongeza<br />
ya asilimia 19.4%. Shilingi ya <strong>Kenya</strong> iliyopungua thamani<br />
hivyo basi, iliathiri gharama ya mafuta kwa asilimia 3.9.<br />
Nyongeza iliyosalia ya asilimia 8.4 ili<strong>to</strong>kana na matumizi<br />
zaidi ku<strong>to</strong>kana na kuongezeka kwa shughuli zetu.<br />
Gharama za uendeshaji<br />
Gharama za uendeshaji zilipanda kwa Ksh 1.55billion au<br />
asilimia 10.1. Ma<strong>to</strong>keo yaliathiriwa vibaya na gharama za<br />
wafanyikazi za Ksh1.022bilioni na Ksh532milioni katika<br />
masuala ya jumla ya usimamizi na uzinduzi wa maeneo<br />
mapya ya usafiri.<br />
Matarajio ya baadaye<br />
Kwa mujibu wa IATA, bei ya juu ya mafuta, iliyo<strong>to</strong>kana<br />
na misukosuko ya kisiasa Mashariki ya Kati na Afrika<br />
Kaskazini zitapunguza faida za shirka hili 2011. Ku<strong>to</strong>kana<br />
na hali hiyo, makadirio ya faida katika mashirika ya ndege<br />
kote duniani ambayo yalitarajiwa kuwa Dola 9.1bilioni<br />
mnamo 2011 yatapungua hadi Dola8.6bilioni. Bodi imetilia<br />
maanani nyongeza ya mahitaji ya usafiri yanayotarajiwa<br />
kuongezeka na shinikizo kwa mapa<strong>to</strong> ku<strong>to</strong>kana na kupanda<br />
kwa bei ya mafuta. Hii inamaanisha kuwa, <strong>Kenya</strong> <strong>Airways</strong> ni<br />
lazima itekeleze mikakati ifaayo kuimarisha ukuaji na faida<br />
yake. Vichocheo vikuu vya ukuaji ni idadi kubwa ya wasafiri,<br />
mapa<strong>to</strong> mazuri na mpango mahususi wa kupunguza<br />
gharama. Hivyo basi, shirika hili litaendelea kufungua njia<br />
mpya za kuhudumu kwa mpango, kununua ndege mpya,<br />
ku<strong>to</strong>a mafunzo kwa wafanyikazi na kuimarisha mitambo<br />
yake. Wasimamizi wanaji<strong>to</strong>lea ku<strong>to</strong>a huduma zifaazo<br />
kupitia, miongoni mwa mengine, utenda kazi kwa wakati ili<br />
ku<strong>to</strong>sheleza na kuzidisha matarajio ya wateja.<br />
Faida ya <strong>Kenya</strong> <strong>Airways</strong> baada ya ushuru kwa 2010/11 ni<br />
bora ikilinganishwa na faida ya mwaka uliotangulia. Bodi<br />
ina matumaini kuwa ma<strong>to</strong>keo ya kampuni yataendelea<br />
kuimarika katika miaka ijayo.<br />
Mikataba ya angani na kufikia masoko<br />
<strong>Kenya</strong> <strong>Airways</strong> iliendeela kufungua Afrika kwa mataifa<br />
mengine ya ulimwengu katika kipindi kinachotathminiwa.<br />
Njia 6 mpya zilizinduliwa mwaka huo nazo ni: Muscat-<br />
Oman, Juba – Kusini mwa Sudan, Luanda-Angola, Nampula<br />
- Mozambique, Rome-Italia na Malindi. Safari hizo mpya<br />
zimeongeza idadi ya maeneo tunakohudumu hadi 53<br />
ku<strong>to</strong>ka 47 mwaka uliotangulia.<br />
Kwa kufungua maeneo mpya, <strong>Kenya</strong> <strong>Airways</strong> imeendelea<br />
kuchangia katika ustawi wa Afrika wa kutegemewa<br />
kwa kufanikisha utalii na biashara; kuchangia ukuaji<br />
wa uchumi, ku<strong>to</strong>a nafasi za kazi na kuongeza mapa<strong>to</strong><br />
ku<strong>to</strong>kana na ushuru. Kundi la Pande mbili la Huduma za<br />
Angani linaloongozwa na Wizara ya Uchukuzi lilijadiliana,<br />
kutathmini na kupitisha mapatano kadha ya pande<br />
mbili kuhusu huduma za angani (BASA) katika kipindi<br />
kinachochunguzwa.<br />
Serikali ya Nigeria ilichunguza mkataba wa sasa wa BASA<br />
na kukubali kuanzishwa kwa safari za moja kwa moja<br />
ku<strong>to</strong>ka Nairobi hadi Abuja mara nne kwa wiki na <strong>Kenya</strong><br />
<strong>Airways</strong>, na nyongeza ya safari za kila wiki hadi Lagos<br />
ku<strong>to</strong>ka 10 hadi 14. Mapatano na Tanzania na Sudan pia<br />
yalichunguzwa upya, na kuhusiana na Tanzania, idadi<br />
ya safari ku<strong>to</strong>ka Nairobi hadi Dar es Salaam ziliongezwa<br />
ku<strong>to</strong>ka safari 21 kwa wiki hadi 42 na za zile saba za kila wiki<br />
kuelekea Sudan pia ziliongezwa bila kipimo na uwezo.<br />
Ufanisi wa kihis<strong>to</strong>ria ulipatikana kupitia kuanzishwa<br />
kwa operesheni za <strong>Kenya</strong> <strong>Airways</strong> hadi Luanda, Angola.<br />
<strong>Kenya</strong> <strong>Airways</strong> inaendelea kuchunguza makubaliano<br />
yaliyopo na kutia sahihi ushirikiano wa kibiashara na<br />
mashirika mengine, kwa lengo la kupanua mtandao wake<br />
Afrika na kwingineko duniani.<br />
Serikali na Shirika la Kusimamia Viwanja vya Ndege (KAA)<br />
zinaendelea kuunga mkono mashirika ya ndege ya humu<br />
nchini. Hasa katika kipindi kinachoangaziwa, shughuli za<br />
upanuzi wa uwanja wa JKIA zilianza. Imebainika kuwa JKIA<br />
inaendelea kuzidiwa, na miundomsingi inapasa kuimarishwa.<br />
Mabadiliko hayo yatahakikisha JKIA inaimarisha hadhi yake<br />
kama ki<strong>to</strong>vu cha kibiashara katika eneo hili, pamoja na<br />
kuwa na uwezo wa kuhudumia wasafiri zaidi.<br />
Ku<strong>to</strong>kana na utandawazi wa huduma za usafiri wa angani<br />
katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, <strong>Kenya</strong> <strong>Airways</strong><br />
inajiandaa kupanua mtandao wa maeneo inakohudumu<br />
kwa ushirikiano na Precision Air na washirika wengine<br />
katika sekta hiyo. Na katika sehemu zingine za Afrika,<br />
licha ya Uamuzi wa Yamoussoukro, masoko mengi bado<br />
yanadhibitiwa kupita kiasi na <strong>Kenya</strong> <strong>Airways</strong> kwa usaidizi<br />
wa Serikali, inaendelea kufuatilia masoko hayo.<br />
Wenyehisa<br />
Idadi ya wenyehisa kwenye Sajili ya Wanachama kufikia<br />
Machi 31, 2011 ni 73,249. Kati ya hizi, wenyehisa 32,923<br />
wamekinda hisa zao dhidi ya hasara na kuchagua CDSC<br />
Nominees Limited na kufungua akaunti kwenye Central<br />
Depositary System. Maelezo kuhusu wenyehisa kufikia<br />
Machi 31, 2011 yamo kwenye ukurasa 103.<br />
Mgao wa faida wa mwisho<br />
Bodi inapendekeza kuidhinishwa na wenyehisa mgao wa<br />
mwisho wa Ksh1.50 kwa hisa, kulipwa kwa wenyehisa wa<br />
kampuni walio kwenye Sajili ya Wanachama kufikia mwisho<br />
wa shughuli za siku mnamo Ok<strong>to</strong>ba 14, 2011 ambazo<br />
zitalipwa mnamo au kufikia Novemba 16, 2011.<br />
Shukrani<br />
Ninachukua fursa hii ku<strong>to</strong>a shukrani zangu kwa wateja<br />
wetu, wenyehisa, serikali, wasimamizi na wafanyikazi na<br />
wakurugenzi wenzangu kwa ushirikiano wao wa kila mara.<br />
Wakurugenzi<br />
Wanachama wa Bodi waliohudumu mwaka uliomalizika<br />
wamo kwenye ripoti kuhusu Wakurugenzi katika<br />
ukurasa 56.<br />
EVANSON MWANIKI<br />
MWENYEKITI<br />
20 21