01.11.2014 Views

Read - Polis

Read - Polis

Read - Polis

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(b)Mheshimiwa Spika, Serikali kwa sasa haina mpango wa kuondoa karo katika<br />

shule za sekondari za Serikali kwa sababu inafaa wazazi walio na uwezo wachangie<br />

angalau kiasi kidogo katika kugharimia elimu ya watoto wao. Serikali imepunguza<br />

kiwango cha karo ya shule za kutwa kutoka shs. 40,000 hadi 20,000 lakini pia Serikali<br />

inatoa ruzuku ya uendeshaji wa shule ya shs. 40,000 kwa kila mwanafunzi kwa<br />

Sekondari za Serikali zikiwemo shs.20,000/= zinazofidia ada iliyopunguzwa. Aidha ada<br />

ya shs. 20,000 inayolipwa inabakia shuleni na kufanya jumla ya fedha za uendeshaji<br />

kuwa shs. 60,000 kwa mwanafunzi. Ada ya 20,000 inaweza kulipwa kwa awamu mbili za<br />

shs. 10,000/= kila muhula.<br />

MHE. JOEL N. BENDERA: Mheshimiwa Spika, katika Bajeti ya mwaka huu<br />

ambayo Mheshimiwa Waziri wa Fedha alishatoa na alitoa ahadi mwaka jana kwamba<br />

fedha hizi zitakuwa zinaongezwa kila mwaka ili kuongeza idadi ya wanafunzi ya kusaidia<br />

wanafunzi ambao wazazi hawajiwezi. Je, katika mwaka huu Bajeti hiyo ipo, maana safari<br />

sikumwona Mheshimiwa Mramba akijitanua kwa hilo? (Makofi)<br />

Katika wanafunzi hao 111 na wengine ambao wamesaidiwa Wilaya ya Serengeti<br />

na Wilaya zingine zote, yako matatizo ya wanafunzi hawa kurudishwa majumbani kwa<br />

ajili ya kukosa ada na kutoa usumbufu sana kwa wanafunzi hawa. Je, kwa nini hili<br />

linatokea na watoto hawa hawana uwezo, wazazi wao hawana uwezo kwa nini inatokea<br />

Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba fedha hizi zinafika kwenye shule<br />

husika? (Makofi)<br />

NAIBU WAZIRI WA KAZI, MAENDELEO YA VIJANA NA MICHEZO<br />

(K.n.y. WAZIRI WA ELIMU NA UTAMADUNI): Mheshimiwa Spika, napenda<br />

kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Joel Bendera, kama ifuatavyo:-<br />

Juu ya kama fedha hizi zitaendelea kuwepo katika mwaka huu wa fedha<br />

ningemwomba Mheshimiwa Mbunge avute subiri, asubiri siku ya Hotuba ya Bajeti ya<br />

Waziri wa Elimu na Utamaduni, aweze kuona mambo yakoje ambayo ni mazuri tu.<br />

(Makofi/Kicheko)<br />

Juu ya watoto kurejeshwa nyumbani kwa kweli ni tatizo la utendaji. Fedha<br />

zinatolewa na Wizara kupelekwa kwenye Halmashauri. Inawezekana zikachelewa hapa<br />

au pale, lakini ni suala tu la Halmashauri husika ambayo inasimamia mfuko huo<br />

kuwasiliana na shule inayohusika badala ya kuwanyanyasa hawa watoto kuwarejesha<br />

nyumbani wanajisikia wanyonge. Halmashauri iwasiliane na shule zinazohusika na<br />

mambo haya bila shaka hayana sababu ya kutokea tena. Naomba nitoe wito kupitia<br />

Bunge lako Tukufu, kwamba uongozi wa Halmashauri uwasiliane na shule hizi kwamba<br />

inapotokea fedha zimechelewa kufika watoto hawa wasibugudhiwe waendelee kusoma<br />

iwe ni suala la Halmashauri na uongozi wa shule za sekondari zenyewe. (Makofi)<br />

WAZIRI WA KAZI, MAENDELEO YA VIJANA MICHEZO (K.n.y.<br />

WAZIRI WA ELIMU): Mheshimiwa Spika, nyongeza kidogo ni kwamba Serikali<br />

imeshatambua udhaifu huo kwa hiyo, kwa maana hiyo, wameshafungua mawasiliano ya<br />

moja kwa moja kati ya Wizara ya Elimu na Utamaduni na shule husika. Kwa hiyo, kama<br />

16

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!