01.11.2014 Views

Read - Polis

Read - Polis

Read - Polis

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

mabwawa ya Maratani, Namasogo, Mpwahia na Mpombe. Ni vizuri miradi hiyo<br />

ikakamilishwa ili wananchi waondokane na adha ya kukosa maji katika maeneo yao.<br />

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali kuhakikisha huduma ya maji inaboreka<br />

katika jimbo la Nanyumbu kwa kupeleka miradi mingi zaidi ya maji.<br />

Mheshimiwa Spika, ni imani yangu kuwa Serikali itayafanyia kazi haya yote.<br />

Mwisho naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.<br />

MHE. FETEH SAAD MGENI: Mheshimiwa Spika, kwanza nakupongeza<br />

wewe binafsi kwa moyo na uwezo wako mkubwa kuliongoza Bunge lako hili Tukufu<br />

kwa vipindi vyote ulivyojaliwa kuongoza, Mungu akupe umri mrefu wenye kheri na<br />

baraka.<br />

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa mkono wa pole kwa wananchi wa Majimbo<br />

yale yaliopoteza Wabunge wao yaani Marehemu Balozi Ahmed Hassan Diria na<br />

Marehemu Abu Kiwanga. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema<br />

peponi. Amin.<br />

Aidha, nina heshima kubwa kukipongeza Chama cha Mapinduzi kwa kuwateua<br />

Mheshimiwa Jakaya Kikwete kuwa mgombea wa Urais wa Tanzania na Mheshimiwa Dr.<br />

Ali Mohamed Shein kuwa mgombea mwenza. Vile vile ninampongeza Mheshimiwa<br />

Amani Abeid Karume kuwa mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama chetu cha<br />

CCM. Mwenyezi Mungu Inshallah atajaalia kupatikana ushindi mkubwa kabisa.<br />

Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Mawaziri<br />

wake na Watendaji wake wote kwa hotuba nzuri iliyogusa maeneo yote ya Jamhuri yetu<br />

ya Tanzania kimaendeleo, naamini hotuba yake ni dira kuu kwa maendeleo ya Taifa hili.<br />

Naomba sana tuithamini na tuitekeleze kama dira ya maendeleo ya nchi yetu. Aidha,<br />

Mheshimiwa Waziri Mkuu nakupongeza sana kwa nia yako kwa kutaka kupumzika,<br />

nakutakia kila la kheri na mafanikio mema.<br />

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia kwenye suala la kupanda kwa uchumi<br />

wetu Tanzania. Mimi nakubali kupanda kwa uchumi wetu, lakini naomba sana tuiangalie<br />

Hali ya Uchumi katika sehemu yetu ya pili ya Muungano wetu ya Zanzibar. Zanzibar<br />

bado iko chini kidogo kiuchumi. Biashara imeshuka sana kiuchumi, Uwanja wa Ndege<br />

umepungua mapato yake. Katika hali hiyo naomba sana tusaidiane kuhusu Zanzibar.<br />

Mheshimiwa Spika, hali ya Zanzibar juu ya mawasiliano bado yanahitaji msaada,<br />

barabara zake nyingi hali yake mbaya, hali ya usafiri wa bahari na anga unahitaji<br />

kuangaliwa zaidi.<br />

Mheshimiwa Spika, narejea kusema tena naipongeza hotuba ya Mheshimiwa<br />

Waziri Mkuu na ninaiunga mkono hotuba hiyo kwa asilimia kwa mia. Ahsante.<br />

63

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!