Read - Polis
Read - Polis
Read - Polis
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
mabwawa ya Maratani, Namasogo, Mpwahia na Mpombe. Ni vizuri miradi hiyo<br />
ikakamilishwa ili wananchi waondokane na adha ya kukosa maji katika maeneo yao.<br />
Mheshimiwa Spika, naomba Serikali kuhakikisha huduma ya maji inaboreka<br />
katika jimbo la Nanyumbu kwa kupeleka miradi mingi zaidi ya maji.<br />
Mheshimiwa Spika, ni imani yangu kuwa Serikali itayafanyia kazi haya yote.<br />
Mwisho naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.<br />
MHE. FETEH SAAD MGENI: Mheshimiwa Spika, kwanza nakupongeza<br />
wewe binafsi kwa moyo na uwezo wako mkubwa kuliongoza Bunge lako hili Tukufu<br />
kwa vipindi vyote ulivyojaliwa kuongoza, Mungu akupe umri mrefu wenye kheri na<br />
baraka.<br />
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa mkono wa pole kwa wananchi wa Majimbo<br />
yale yaliopoteza Wabunge wao yaani Marehemu Balozi Ahmed Hassan Diria na<br />
Marehemu Abu Kiwanga. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema<br />
peponi. Amin.<br />
Aidha, nina heshima kubwa kukipongeza Chama cha Mapinduzi kwa kuwateua<br />
Mheshimiwa Jakaya Kikwete kuwa mgombea wa Urais wa Tanzania na Mheshimiwa Dr.<br />
Ali Mohamed Shein kuwa mgombea mwenza. Vile vile ninampongeza Mheshimiwa<br />
Amani Abeid Karume kuwa mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama chetu cha<br />
CCM. Mwenyezi Mungu Inshallah atajaalia kupatikana ushindi mkubwa kabisa.<br />
Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Mawaziri<br />
wake na Watendaji wake wote kwa hotuba nzuri iliyogusa maeneo yote ya Jamhuri yetu<br />
ya Tanzania kimaendeleo, naamini hotuba yake ni dira kuu kwa maendeleo ya Taifa hili.<br />
Naomba sana tuithamini na tuitekeleze kama dira ya maendeleo ya nchi yetu. Aidha,<br />
Mheshimiwa Waziri Mkuu nakupongeza sana kwa nia yako kwa kutaka kupumzika,<br />
nakutakia kila la kheri na mafanikio mema.<br />
Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia kwenye suala la kupanda kwa uchumi<br />
wetu Tanzania. Mimi nakubali kupanda kwa uchumi wetu, lakini naomba sana tuiangalie<br />
Hali ya Uchumi katika sehemu yetu ya pili ya Muungano wetu ya Zanzibar. Zanzibar<br />
bado iko chini kidogo kiuchumi. Biashara imeshuka sana kiuchumi, Uwanja wa Ndege<br />
umepungua mapato yake. Katika hali hiyo naomba sana tusaidiane kuhusu Zanzibar.<br />
Mheshimiwa Spika, hali ya Zanzibar juu ya mawasiliano bado yanahitaji msaada,<br />
barabara zake nyingi hali yake mbaya, hali ya usafiri wa bahari na anga unahitaji<br />
kuangaliwa zaidi.<br />
Mheshimiwa Spika, narejea kusema tena naipongeza hotuba ya Mheshimiwa<br />
Waziri Mkuu na ninaiunga mkono hotuba hiyo kwa asilimia kwa mia. Ahsante.<br />
63