01.11.2014 Views

Read - Polis

Read - Polis

Read - Polis

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

kupitika kwa kipindi kirefu cha mwaka. Juhudi ambazo zimekuwa zikifanywa hadi sasa<br />

ni pamoja na hizi zifuatazo:-<br />

Moja, Kufanya matengenezo ya mara kwa mara kulingana na upatikanaji wa<br />

fedha. Katika mwaka wa fedha 2003/2004 jumla ya kilomita 35 za barabara ya Kapalala<br />

– Gua zimechongwa kwa Greda na mifereji ya maji ya mvua imetengenezwa . Kiasi cha<br />

shilingi 34,500,000/= zilitumika kukamilisha kazi hiyo.<br />

Pili, Katika mwaka 2004/2005 madaraja mawili ya Kikamba na Lukwati katika<br />

barabara ya Kapalala - Gua yamekarabatiwa kwa kuondoa mbao na kuwekewa deki ya<br />

zege na iligharimu shilingi milioni 28.<br />

Vile vile katika kipindi hicho daraja la Manda Juu kwenye barabara ya Kapalala –<br />

Udinde limefanyiwa matengenezo kwa gharama ya shilingi milioni 3.<br />

Mheshimiwa Spika, ili barabara ya Kapalala – Gua iweze kupitika kwa mwaka<br />

mzima, Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa mwaka wa fedha 2005/2006 itaifanyia<br />

matengenezo ya sehemu korofi kilomita 35 kwa gharama ya shilingi milioni 5.5 kutoka<br />

katika mfuko wa barabara.<br />

Mheshimiwa Spika, juhudi hizo zote nilizo zieleza hapa zinatokana na fedha za<br />

Serikali na wala siyo Halmashauri kwa maana ya mapato yake yenyewe. Serikali<br />

itaendelea kuzifanyia matengenezo barabara hizo hadi ziweze kufikia kiwango ambacho<br />

kinaridhisha.<br />

MHE. PAUL E. NTWINA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi<br />

niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.<br />

Kwa kuwa Vijiji vya Gua, Ngwala, Udinde, Some Kapalala na Kininga vinapakana<br />

na Mbuga za wanyama za Lukwati, eneo zuri kwa Utalli na eneo ambalo pia linalimwa<br />

Tumbaku; na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amesema kuwa barabara hizi<br />

zitatengenezwa.<br />

Je, anaweza kunihakikishia kuwa kwa baadaye hizi ni vyema kutengeneza kwa<br />

kima cha changarawe hizi barabara kwa sababu mara kwa mara zimekuwa<br />

zikitengenezwa na mvua inayonyesha maeneo yale imekuwa ikiziharibu?<br />

Swali la pili, kwa kuwa hizi barabara zimeunganishwa na barabara ya Mkoa, Saza –<br />

Kapalala kwa maana ya Mbalizi–Saza; na kwa kuwa yapo maeneo ambayo nimeyasema<br />

sana huko nyuma ambayo yako na udongo mwekundu na udongo mweusi.<br />

Je, yale maeneo nayo Waziri anaweza kutusaidia kuyaimarisha ili barabara yote<br />

sasa mpaka kule Gua na Udinde ipitike?<br />

4

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!