Read - Polis
Read - Polis
Read - Polis
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
kupitika kwa kipindi kirefu cha mwaka. Juhudi ambazo zimekuwa zikifanywa hadi sasa<br />
ni pamoja na hizi zifuatazo:-<br />
Moja, Kufanya matengenezo ya mara kwa mara kulingana na upatikanaji wa<br />
fedha. Katika mwaka wa fedha 2003/2004 jumla ya kilomita 35 za barabara ya Kapalala<br />
– Gua zimechongwa kwa Greda na mifereji ya maji ya mvua imetengenezwa . Kiasi cha<br />
shilingi 34,500,000/= zilitumika kukamilisha kazi hiyo.<br />
Pili, Katika mwaka 2004/2005 madaraja mawili ya Kikamba na Lukwati katika<br />
barabara ya Kapalala - Gua yamekarabatiwa kwa kuondoa mbao na kuwekewa deki ya<br />
zege na iligharimu shilingi milioni 28.<br />
Vile vile katika kipindi hicho daraja la Manda Juu kwenye barabara ya Kapalala –<br />
Udinde limefanyiwa matengenezo kwa gharama ya shilingi milioni 3.<br />
Mheshimiwa Spika, ili barabara ya Kapalala – Gua iweze kupitika kwa mwaka<br />
mzima, Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa mwaka wa fedha 2005/2006 itaifanyia<br />
matengenezo ya sehemu korofi kilomita 35 kwa gharama ya shilingi milioni 5.5 kutoka<br />
katika mfuko wa barabara.<br />
Mheshimiwa Spika, juhudi hizo zote nilizo zieleza hapa zinatokana na fedha za<br />
Serikali na wala siyo Halmashauri kwa maana ya mapato yake yenyewe. Serikali<br />
itaendelea kuzifanyia matengenezo barabara hizo hadi ziweze kufikia kiwango ambacho<br />
kinaridhisha.<br />
MHE. PAUL E. NTWINA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi<br />
niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.<br />
Kwa kuwa Vijiji vya Gua, Ngwala, Udinde, Some Kapalala na Kininga vinapakana<br />
na Mbuga za wanyama za Lukwati, eneo zuri kwa Utalli na eneo ambalo pia linalimwa<br />
Tumbaku; na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amesema kuwa barabara hizi<br />
zitatengenezwa.<br />
Je, anaweza kunihakikishia kuwa kwa baadaye hizi ni vyema kutengeneza kwa<br />
kima cha changarawe hizi barabara kwa sababu mara kwa mara zimekuwa<br />
zikitengenezwa na mvua inayonyesha maeneo yale imekuwa ikiziharibu?<br />
Swali la pili, kwa kuwa hizi barabara zimeunganishwa na barabara ya Mkoa, Saza –<br />
Kapalala kwa maana ya Mbalizi–Saza; na kwa kuwa yapo maeneo ambayo nimeyasema<br />
sana huko nyuma ambayo yako na udongo mwekundu na udongo mweusi.<br />
Je, yale maeneo nayo Waziri anaweza kutusaidia kuyaimarisha ili barabara yote<br />
sasa mpaka kule Gua na Udinde ipitike?<br />
4