01.11.2014 Views

Read - Polis

Read - Polis

Read - Polis

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

nilitoa malalamiko kwa kijiji kimoja cha Nata ambao umeme ulikuwa unapita juu,<br />

wanapitwa tu umeme unatoka Shinyanga unakimbia kwenda Nzega.<br />

Mheshimiwa Soika, nikalalamika kwenye Bunge na watu wa Nzega wakanisaidia<br />

kwa sababu watu waliokuwa wanajenga nguzo za umeme wa gridi kutoka Shinyanga<br />

kuupeleka Tabora, wananchi wakawa wanafungua zile bolt na nut wanatumia<br />

kutengenezea mikokoteni. Nikamkuta OCD kakamata mikokoteni yao mingi ameirundika<br />

pale, nikamwambia huna haki hawa wamechukua hizo nuts wakazitumie, kwa sababu<br />

hizi nguzo zinajengwa hazitawafaa, basi waachie.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa bahati wakawaachia na wakateremsha umeme, lakini<br />

bado kitu cha kusikitisha sisi tunaonekana Wabunge wa Nzega hatufanyi kazi. Umeme<br />

waliu-step down katika kijiji cha Nzega Ndogo ili waupeleke Chomachankola kwenye<br />

kiwanda, kwenye ginnery na kutoka kule uende Igunga. Pale walipouteremsha<br />

hawakuuweka umeme kwenye kijiji kile na pale pana Kituo cha Afya, kuna shule, kuna<br />

mgodi mdogo wa Isungangwanda. Lakini waliteremsha wakauchukua kupeleka<br />

Chomachankola, nimelalamika nashukuru Mheshimiwa Omar Kwaang’, alikuja<br />

kutembea kuona miradi ya umwagiliaji, nikampeleka kwenye kijiji hicho. Tukaja<br />

tukalalamika hapa na Mheshimiwa Omar Kwaang’, akatoa ushuhuda kwamba ni kweli na<br />

ameona naye kwa macho watu hawa wakaona haya wakateremsha pale. (Makofi)<br />

Sasa Nzega pamoja na kuachwa na wakoloni kama Wilaya ina vijiji viwili tu<br />

vyenye umeme na Nzega yenyewe. Sasa unabaki unajiuliza hivi vijiji vya kando ya njia<br />

ya umeme ni kilometa ngapi? Maana tunashangaa wameutoa Chomachankola<br />

wamepeleka kijiji kimoja kule Igunga cha Ziba. Wakatoka Ziba wakapeleka Nkinga<br />

kama maili nane, tukajiuliza swali sisi pale Nkinga ni hospitali kubwa tunakwenda hata<br />

sisi, lakini wameutoa pale wanapeleka Simbo kilometa 42.<br />

Sasa na sisi tunajiuliza kutoka Nzega kwenda Bukeni ni kilometa 42, kutoka Ziba<br />

kwenda Simbo ni kilometa 42. Hivi kilometa 42 zinazoonekana ziko kando ya njia ya<br />

umeme ni zipi? Sisi tuna kilometa za majini hawa wana kilometa za nchi kavu, unabaki<br />

unashangaa. Basi ndio maana mimi nasema wameshindwa kushirikiana nasi, nawaomba<br />

basi sina kinyongo nao, nawaomba Mbunge atakayekuja kushika Jimbo la Bukene<br />

wamsaidie, washirikiane naye. Kama walishindwa kushirikiana na mimi labda kwa<br />

sababu ni mzee huyo atakuja kijana, washirikiane naye. Pamoja na hayo nawaomba sana<br />

watu wa Jimbo la Bukene wanisamehe kwamba hilo sikuweza.<br />

Mheshimiwa Spika, nilijaribu kubadili mbinu nikasema labda niombe Bukene iwe<br />

Wilaya kusudi niweze kuuwa ndege wawili kwa jiwe moja, na yenyewe hakuna.<br />

Nikiuliza maswali naambiwa sifa zote za Bukene kuwa Wilaya zipo, lakini kuwa Wilaya<br />

fedha hazipo sasa hizi fedha huwa zinakosa kwetu tu kwingine mnapeleka.<br />

Mheshimiwa Spika, kitu cha muhimu ambacho nataka kusema hapa cha mwisho<br />

kabisa sitaki kukupotezea muda, ni kwamba mimi nimekwishaonja yote.<br />

Nimekwishaonja kuanguka Ubunge nikakaa mstari wa nyuma huko na nimekwishaonja<br />

kuushinda Ubunge. Mimi kitu ambacho kilikuwa kinanikera ambacho nasema na<br />

38

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!