Read - Polis
Read - Polis
Read - Polis
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.<br />
MHE. MARGARETH A. MKANGA: Mheshimiwa Spika, natoa pongezi kwa<br />
Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mawaziri Mheshimiwa William Lukuvi na Mheshimiwa<br />
Muhammed Seif Khatib, Katibu Mkuu mama Rose Lugembe na watendaji wote kwa<br />
kuandaa hotuba nzuri ya Bajeti inayoeleweka. Hotuba hiyo pia ni majumuisho ya yote<br />
yaliyotekelezwa na Serikali ya CCM ya Awamu ya Tatu na matarajio yote<br />
yatakayoendelea kutekelezwa na Serikali ya CCM Awamu ya Nne.<br />
Pamoja na kueleweka kwa hotuba hii naomba kuchangia mawazo katika maeneo<br />
kadhaa kama ifuatavyo:-<br />
Mheshimiwa Spika, umuhimu wa kudumisha amani na utulivu tulionao nchini.<br />
Suala hili limefafanuliwa vizuri kwenye hotuba, sasa ni wajibu wa viongozi wa vyama<br />
vyote vya siasa, mashabiki wa kisiasa na wananchi kwa ujumla kujihadhari na maneno na<br />
vitendo vitakavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani kwa vile ni rahisi kuvunja amani<br />
kuliko kuijenga amani na mifano ya nchi jirani tunayo na madhara yake ni mengi.<br />
Mheshimiwa Spika, huduma za jamii ni kweli kabisa Tanzania, tumepiga hatua<br />
kubwa katika uandikishaji wa wanafunzi kuanza darasa la kwanza toka 712,467 mwaka<br />
1998 mpaka wanafunzi 1,376,467 mwaka 2005 kadhalika idadi ya Walimu imeongezeka.<br />
Hata hivyo, ieleweke kwamba idadi kubwa ya wanafunzi wenye ulemavu wa aina aina<br />
hawaandikishwi shule kutokana na ama wazazi kuwaficha, Walimu kukataa<br />
kuwaandikisha kutokana na kutokuwa na Walimu wa kuwahudumia wanafunzi wenye<br />
ulemavu. Kwa msingi huo, nashauri suala hili litazamwe kwa makini zaidi ili jamii hii ya<br />
wanafunzi waweze kupata haki yao ya msingi ya Elimu.<br />
Mheshimiwa Spika, Sekta ya Afya, katika sekta hii pia kumekuwa na maendeleo<br />
ya utoaji na upanuzi wa huduma. Tatizo ni kwamba bado taratibu za kupata msamaha wa<br />
kupata huduma bure kwa wazee, walemavu, wagonjwa wasiojiweza, waathirika wa<br />
UKIMWI, wagonjwa wa kifua kikuu ni ndefu kiasi kwani zinazua kunyanyasika kwa<br />
wahusika badala ya kusaidiwa haraka. Hivyo, utaratibu wa utoaji misamaha uangaliwe<br />
upya kwani imekuwa ni usumbufu mkubwa kwa walengwa.<br />
Mheshimiwa Spika, uwezeshaji wananchi kiuchumi, ingawa sera iko tayari juu ya<br />
suala hili, mikopo ya Kiserikali ya wanawake na vijana hutolewa kwa utaratibu uliopo<br />
sasa, lakini jamii ya watu wenye ulemavu bado wengi hawafaidiki na fursa hizi, kwanza<br />
kwa mfano mikopo niliyoitaja wengi wanaopewa ni wale waishio Mijini tu, mikopo hii<br />
haijawafikia wanajamii waishio Vijijini walemavu wakiwemo kwa hali hiyo kujikwamua<br />
katika dimbwi la umaskini ambalo walemavu wengi ndimo walimo inakuwa ni kama<br />
ndoto za alinacha.<br />
Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali iangalie upya taratibu za njia mbalimbali za<br />
uwezeshaji wananchi ili fursa hizo ziwafaidie walengwa walio wengi nchini wakiwemo<br />
walemavu.<br />
81