01.11.2014 Views

Read - Polis

Read - Polis

Read - Polis

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.<br />

MHE. MARGARETH A. MKANGA: Mheshimiwa Spika, natoa pongezi kwa<br />

Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mawaziri Mheshimiwa William Lukuvi na Mheshimiwa<br />

Muhammed Seif Khatib, Katibu Mkuu mama Rose Lugembe na watendaji wote kwa<br />

kuandaa hotuba nzuri ya Bajeti inayoeleweka. Hotuba hiyo pia ni majumuisho ya yote<br />

yaliyotekelezwa na Serikali ya CCM ya Awamu ya Tatu na matarajio yote<br />

yatakayoendelea kutekelezwa na Serikali ya CCM Awamu ya Nne.<br />

Pamoja na kueleweka kwa hotuba hii naomba kuchangia mawazo katika maeneo<br />

kadhaa kama ifuatavyo:-<br />

Mheshimiwa Spika, umuhimu wa kudumisha amani na utulivu tulionao nchini.<br />

Suala hili limefafanuliwa vizuri kwenye hotuba, sasa ni wajibu wa viongozi wa vyama<br />

vyote vya siasa, mashabiki wa kisiasa na wananchi kwa ujumla kujihadhari na maneno na<br />

vitendo vitakavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani kwa vile ni rahisi kuvunja amani<br />

kuliko kuijenga amani na mifano ya nchi jirani tunayo na madhara yake ni mengi.<br />

Mheshimiwa Spika, huduma za jamii ni kweli kabisa Tanzania, tumepiga hatua<br />

kubwa katika uandikishaji wa wanafunzi kuanza darasa la kwanza toka 712,467 mwaka<br />

1998 mpaka wanafunzi 1,376,467 mwaka 2005 kadhalika idadi ya Walimu imeongezeka.<br />

Hata hivyo, ieleweke kwamba idadi kubwa ya wanafunzi wenye ulemavu wa aina aina<br />

hawaandikishwi shule kutokana na ama wazazi kuwaficha, Walimu kukataa<br />

kuwaandikisha kutokana na kutokuwa na Walimu wa kuwahudumia wanafunzi wenye<br />

ulemavu. Kwa msingi huo, nashauri suala hili litazamwe kwa makini zaidi ili jamii hii ya<br />

wanafunzi waweze kupata haki yao ya msingi ya Elimu.<br />

Mheshimiwa Spika, Sekta ya Afya, katika sekta hii pia kumekuwa na maendeleo<br />

ya utoaji na upanuzi wa huduma. Tatizo ni kwamba bado taratibu za kupata msamaha wa<br />

kupata huduma bure kwa wazee, walemavu, wagonjwa wasiojiweza, waathirika wa<br />

UKIMWI, wagonjwa wa kifua kikuu ni ndefu kiasi kwani zinazua kunyanyasika kwa<br />

wahusika badala ya kusaidiwa haraka. Hivyo, utaratibu wa utoaji misamaha uangaliwe<br />

upya kwani imekuwa ni usumbufu mkubwa kwa walengwa.<br />

Mheshimiwa Spika, uwezeshaji wananchi kiuchumi, ingawa sera iko tayari juu ya<br />

suala hili, mikopo ya Kiserikali ya wanawake na vijana hutolewa kwa utaratibu uliopo<br />

sasa, lakini jamii ya watu wenye ulemavu bado wengi hawafaidiki na fursa hizi, kwanza<br />

kwa mfano mikopo niliyoitaja wengi wanaopewa ni wale waishio Mijini tu, mikopo hii<br />

haijawafikia wanajamii waishio Vijijini walemavu wakiwemo kwa hali hiyo kujikwamua<br />

katika dimbwi la umaskini ambalo walemavu wengi ndimo walimo inakuwa ni kama<br />

ndoto za alinacha.<br />

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali iangalie upya taratibu za njia mbalimbali za<br />

uwezeshaji wananchi ili fursa hizo ziwafaidie walengwa walio wengi nchini wakiwemo<br />

walemavu.<br />

81

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!