programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative
programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative
programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Historia na Mandhari<br />
Ukiwa unapatikana upande wa kusini mwa ziwa Victoria, mkoa wa<br />
Shin<strong>ya</strong>nga upo kaskazini magharibi mwa Tanzania na eneo lake<br />
kubwa ni la mazingira <strong>ya</strong> ukame ukiwa na wakazi karibu milioni<br />
tatu, kwa wastani wa watu 42 kwa kila kilometa <strong>ya</strong> mraba. Shin<strong>ya</strong>nga<br />
ni moja <strong>ya</strong> mikoa <strong>ya</strong> Tanzania maskini zaidi, wenye vilima v<strong>ya</strong> kimo<br />
cha chini na tambarare zenye kipindi kirefu cha kiangazi ukiwa<br />
na wastani wa milimeta 700 za mvua kwa mwaka. Kabila kubwa<br />
la mkoa huu ni Wasukuma ambao hujishughulisha na ufugaji na<br />
kilimo; mazao makubwa wanayozalisha ni mahindi, mtama, uwele,<br />
mihogo, pamba, na mchele. Zaidi <strong>ya</strong> asilimia 80 <strong>ya</strong> wakazi wa mkoa<br />
huu wanamiliki na kuendeleza mifugo kwenye malisho <strong>ya</strong> jamii zao.<br />
Kati <strong>ya</strong> mwaka 1986 na 2004, mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulianzisha Mpango<br />
wa Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga uliofahamika kwa kifupi kama HASHI<br />
(Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga). HASHI ilianzishwa na Rais Julius Nyerere<br />
baada <strong>ya</strong> kutembelea mkoa huo mwaka 1984 na akashtushwa na<br />
kiwango kikubwa cha ukataji miti. Kwa miaka <strong>ya</strong> 1980, Shin<strong>ya</strong>nga<br />
ilikuwa inajulikana kama ‘Jangwa la Tanzania ‘. Miongo kadhaa <strong>ya</strong><br />
usimamizi mbovu wa <strong>ardhi</strong> ilichangia kuendelea kuharibika kwa<br />
mazingira katika mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga, lakini mwanzo mkuu wa<br />
uharibifu huu ni mpango wa kukata misitu kipindi cha kabla <strong>ya</strong> vita v<strong>ya</strong><br />
pili v<strong>ya</strong> dunia. Hapo awali, mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulikuwa umefunikwa<br />
na uoto wa miombo na mshita, ambayo ilitoa lishe kwa mifugo na<br />
mafuta kwaajili <strong>ya</strong> kilimo na ufugaji kwa wasukuma. Hata hivyo<br />
misitu hii ilikuwa pia <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong> mbun’go, na magonjwa <strong>ya</strong> vimelea,<br />
na malale ambayo <strong>ya</strong>liwashambulia binadamu na wan<strong>ya</strong>ma. Katika<br />
miaka <strong>ya</strong> 1920, mamlaka <strong>ya</strong> kikoloni ilibuni mpango wa kuwalipa<br />
wenyeji kwa kukata miti kwenye maeneo makubwa <strong>ya</strong> miombo. Hii<br />
kwa kiasi kikubwa ilisaidia mafanikio katika kutokomeza Mbun’go,<br />
na pia kuanzisha maeneo map<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> malisho kwa ajili <strong>ya</strong> wasukuma,<br />
lakini kwa upande mwingine ikaathiri uzuri wa mazingira <strong>ya</strong> mkoa.<br />
Kadiri idadi <strong>ya</strong> mifugo na binadamu ilivyoongezeka katika nusu <strong>ya</strong><br />
mwisho <strong>ya</strong> karne <strong>ya</strong> ishirini, mahitaji kwa ajili <strong>ya</strong> kuni na kilimo pia<br />
<strong>ya</strong>liongezeka. Hii ilisababisha ufugaji uliokithiri kwenye malisho na<br />
mapori, wakati maeneo makubwa <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong>likuwa kwa ajili kilimo<br />
cha mazao <strong>ya</strong> biashara kama vile pamba na tumbaku, na kuacha<br />
<strong>ardhi</strong> kidogo kwa ajili <strong>ya</strong> kupanda mazao <strong>ya</strong> chakula. Zaidi <strong>ya</strong> hayo,<br />
mpango wa uanzishwaji wa vijiji wa Rais Nyerere wa miaka 1970<br />
ulilazimisha familia nyingi ku<strong>ya</strong>acha makazi <strong>ya</strong>o kuhamia maeneo<br />
map<strong>ya</strong>.<br />
Kupotea kwa mfumo wa kijadi wa usimamizi wa rasilimali<br />
Hali hizi zilisababisha mmomonyoko wa mfumo wa kijadi wa<br />
usimamizi wa <strong>ardhi</strong> ambao wasukuma walitumia ku<strong>hifadhi</strong><br />
chakula cha mifugokwaajili <strong>ya</strong> msimu wa kiangazi. Mfumo huu<br />
unaofahamika kama ngitili ulijumuisha utengaji wa maeneo<br />
maalumu <strong>ya</strong> ku<strong>hifadhi</strong> n<strong>ya</strong>si za mifugo kwa ajili <strong>ya</strong> matumizi <strong>ya</strong><br />
kifamilia au <strong>ya</strong> jamii kwa ku<strong>ya</strong>acha maeneo <strong>ya</strong>kiwa na n<strong>ya</strong>si mpaka<br />
msimu wa mvua unapoanza. Ngitili hugawanywa katika sehemu<br />
kadhaa: kila sehemu <strong>ya</strong> ngitili lazima itumike yote kwa malisho kabla<br />
<strong>ya</strong> kuhamia sehemu nyingine. Hifadhi za kifamilia au za mtu mmoja<br />
4