programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative
programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative
programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Empowered lives.<br />
Resilient nations.<br />
PROGRAMU YA<br />
HIFADHI ARDHI<br />
SHINYANGA (HASHI)<br />
Tanzania<br />
Miradi <strong>ya</strong> <strong>Equator</strong><br />
Wanafijiji na Maendeleo Himili <strong>ya</strong> Jamii
MIRADI YA UNDP EQUATOR<br />
Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni mbinu zinazonuiwa ku<strong>ya</strong>kidhi mahitaji <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong> kila siku na <strong>ya</strong> kimazingira. Kuna kazi<br />
chache ambazo zimechapishwa za kuelezea kinagaubaga hizo mbinu bunifu na vile zilianzishwa,vile ziliathiri wakaaji wa<br />
sehemu mbali mbali na vile zimekuwa zikibadilika pindi wakati unapotita. Wachache wamejitokeza kuelezea wazi wazi juu<br />
<strong>ya</strong> miradi <strong>ya</strong>o, na hata wale ambao wamefan<strong>ya</strong> hivyo ni wakuu wa vijiji ambao wamefan<strong>ya</strong> kuelezea kufaulu kwao.<br />
Mradi huu wa <strong>Equator</strong> Katika unadhamiria kujaza hili pengo kama njia moja <strong>ya</strong> kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa<br />
kwake. Masimulizi juu <strong>ya</strong> huu mradi ni baadhi tu <strong>ya</strong> mingi ambayo imefaulu na kushinda tuzo za <strong>Equator</strong> baada <strong>ya</strong> kukaguliwa<br />
na kutathiminiwa katika kitengo cha makundi <strong>ya</strong> kijamii <strong>ya</strong>nayo <strong>hifadhi</strong> mazingira na kuinua maisha <strong>ya</strong> wanafijiji. Miradi hii<br />
inakusudiwa kuwa mifano <strong>ya</strong> kuiwa na kuwatia shime kuzungumzia ilivyofaulu ili kuhamasisha ulimwengu juu <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong><br />
wa mazingira.<br />
Bonyeza katika ramani <strong>ya</strong> miradi <strong>ya</strong> <strong>Equator</strong> ili upate kupata habari zaidi<br />
Wahariri<br />
Mhariri Mkuu :<br />
Muhariri Meneja :<br />
Wahariri Waliochangia :<br />
Joseph Corcoran<br />
Oliver Hughes<br />
Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Erin Lewis, Whitney Wilding<br />
Wahandishi Waliochangia<br />
Eda<strong>ya</strong>tu Abieodun Lamptey, Erin Atwell, Toni Blackman, Jonathan Clay, Joseph Corcoran, Larissa Currado, Sarah Gordon, Oliver Hughes,<br />
Wen-Juan Jiang, Sonal Kanabar, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Rachael Lader, Patrick Lee, Erin Lewis, Jona Liebl, Mengning Ma,<br />
Mary McGraw, Gabriele Orlandi, Juliana Quaresma, Peter Schecter, Martin Sommerschuh, Whitney Wilding, Luna Wu<br />
Uchoraji<br />
Oliver Hughes, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Amy Korngiebel, Kimberly Koserowski, Erin Lewis, John Mulqueen, Lorena de la Parra,<br />
Brandon Payne, Mariajosé Satizábal G.<br />
Shukrani<br />
<strong>Equator</strong> ingependa kuwashukuru wanachama wa Programu <strong>ya</strong> Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga (HASHI). Picha zote ni za HASHI na Charlie Pye-<br />
Smith, World Agroforestry Centre. Ramani ni za CIA World Factbook na Wikipedia. Masimulizi juu <strong>ya</strong> mradi huu <strong>ya</strong>litafsiriwa kwa Kiswahili<br />
na Dr. Ken Ramani.<br />
Nukuu ziada<br />
United Nations Development Programme. 2012. Shin<strong>ya</strong>nga Soil Conservation Programme (HASHI), Tanzania. <strong>Equator</strong> <strong>Initiative</strong> Case Study<br />
Series. New York, NY.
PROGRAMU YA HIFADHI ARDHI<br />
SHINYANGA (HASHI)<br />
Tanzania<br />
MAELEZO KUHUSU MRADI HUU<br />
Programu <strong>ya</strong> Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga inafahamika<br />
zaidi kwa Kiswahili kwa kifupi cha HASHI (Hifadhi Ardhi<br />
Shin<strong>ya</strong>nga) iliyodumu kutoka mwaka 1986 hadi 2004 ikiwa<br />
na lengo la kurejesha rutuba <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> iliyoharibika <strong>ya</strong> mkoa<br />
wa Shin<strong>ya</strong>nga ulioko kaskazini magharibi mwa Tanzania;<br />
mkoa ambao ulipewa jina la “Jangwa la Tanzania” na Rais<br />
wa wakati huo Julius Nyerere katikati <strong>ya</strong> miaka <strong>ya</strong> 1980.<br />
Mkoa huu ambao ni ukanda wa miombo umeharibiwa kwa<br />
miongo kadhaa kwa kukata na kuchoma misitu (kwa ajili<br />
<strong>ya</strong> kutokomeza mbung’o) na kulazimishwa makazi map<strong>ya</strong><br />
chini <strong>ya</strong> mpango wa taifa wa kuanzisha vijiji Tanzania.<br />
Jitihada hizi zilifanywa kwa ushirikiano wa pamoja kati<br />
<strong>ya</strong> serikali na washirika wa kimataifa, lakini hata hivyo ni<br />
muhimu kutambua kuwa upandaji miti katika eneo hilo<br />
lazima ushirikishe wanajamii ili wawe mstari wa mbele<br />
katika juhudi hizi. Mfumo wa jadi wa kuishi pamoja kwenye<br />
eneo moja, au ngitili ulianzishwa, na wasukuma ambao<br />
ni wakulima na wafugaji walipewa jukumu la ku<strong>hifadhi</strong><br />
maeneo <strong>ya</strong> misitu. Matokeo ni kwamba hadi mwaka 2004,<br />
angalau hekta 350,000 za ngitili zilikuwa zimerejeshwa au<br />
kuanzishwa katika vijiji 833 kwa mkoa mzima.<br />
MUHTASARI<br />
ULISHINDA TUZO YA EQUATOR: Mwaka 2002<br />
ULIANZISHWA: Mwaka 1986<br />
ENEO: Shin<strong>ya</strong>nga kaskazini magharibi mwa Tanzania<br />
WANAOFAIDIKA: 833 villages<br />
MAZINGIRA: 145 bird species, 152 tree and shrub species<br />
YALIYOMO<br />
Historia na Mandhari 4<br />
Majukumu Makuu na Ubunifu 6<br />
Matokeo <strong>ya</strong> Kimazingira 8<br />
Matokeo <strong>ya</strong> Kijamii 8<br />
Matokeo <strong>ya</strong> Kisera 10<br />
Jinsi <strong>ya</strong> Kudumisha Mradi Huu 12<br />
Wahisani 13<br />
3
Historia na Mandhari<br />
Ukiwa unapatikana upande wa kusini mwa ziwa Victoria, mkoa wa<br />
Shin<strong>ya</strong>nga upo kaskazini magharibi mwa Tanzania na eneo lake<br />
kubwa ni la mazingira <strong>ya</strong> ukame ukiwa na wakazi karibu milioni<br />
tatu, kwa wastani wa watu 42 kwa kila kilometa <strong>ya</strong> mraba. Shin<strong>ya</strong>nga<br />
ni moja <strong>ya</strong> mikoa <strong>ya</strong> Tanzania maskini zaidi, wenye vilima v<strong>ya</strong> kimo<br />
cha chini na tambarare zenye kipindi kirefu cha kiangazi ukiwa<br />
na wastani wa milimeta 700 za mvua kwa mwaka. Kabila kubwa<br />
la mkoa huu ni Wasukuma ambao hujishughulisha na ufugaji na<br />
kilimo; mazao makubwa wanayozalisha ni mahindi, mtama, uwele,<br />
mihogo, pamba, na mchele. Zaidi <strong>ya</strong> asilimia 80 <strong>ya</strong> wakazi wa mkoa<br />
huu wanamiliki na kuendeleza mifugo kwenye malisho <strong>ya</strong> jamii zao.<br />
Kati <strong>ya</strong> mwaka 1986 na 2004, mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulianzisha Mpango<br />
wa Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga uliofahamika kwa kifupi kama HASHI<br />
(Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga). HASHI ilianzishwa na Rais Julius Nyerere<br />
baada <strong>ya</strong> kutembelea mkoa huo mwaka 1984 na akashtushwa na<br />
kiwango kikubwa cha ukataji miti. Kwa miaka <strong>ya</strong> 1980, Shin<strong>ya</strong>nga<br />
ilikuwa inajulikana kama ‘Jangwa la Tanzania ‘. Miongo kadhaa <strong>ya</strong><br />
usimamizi mbovu wa <strong>ardhi</strong> ilichangia kuendelea kuharibika kwa<br />
mazingira katika mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga, lakini mwanzo mkuu wa<br />
uharibifu huu ni mpango wa kukata misitu kipindi cha kabla <strong>ya</strong> vita v<strong>ya</strong><br />
pili v<strong>ya</strong> dunia. Hapo awali, mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulikuwa umefunikwa<br />
na uoto wa miombo na mshita, ambayo ilitoa lishe kwa mifugo na<br />
mafuta kwaajili <strong>ya</strong> kilimo na ufugaji kwa wasukuma. Hata hivyo<br />
misitu hii ilikuwa pia <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong> mbun’go, na magonjwa <strong>ya</strong> vimelea,<br />
na malale ambayo <strong>ya</strong>liwashambulia binadamu na wan<strong>ya</strong>ma. Katika<br />
miaka <strong>ya</strong> 1920, mamlaka <strong>ya</strong> kikoloni ilibuni mpango wa kuwalipa<br />
wenyeji kwa kukata miti kwenye maeneo makubwa <strong>ya</strong> miombo. Hii<br />
kwa kiasi kikubwa ilisaidia mafanikio katika kutokomeza Mbun’go,<br />
na pia kuanzisha maeneo map<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> malisho kwa ajili <strong>ya</strong> wasukuma,<br />
lakini kwa upande mwingine ikaathiri uzuri wa mazingira <strong>ya</strong> mkoa.<br />
Kadiri idadi <strong>ya</strong> mifugo na binadamu ilivyoongezeka katika nusu <strong>ya</strong><br />
mwisho <strong>ya</strong> karne <strong>ya</strong> ishirini, mahitaji kwa ajili <strong>ya</strong> kuni na kilimo pia<br />
<strong>ya</strong>liongezeka. Hii ilisababisha ufugaji uliokithiri kwenye malisho na<br />
mapori, wakati maeneo makubwa <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong>likuwa kwa ajili kilimo<br />
cha mazao <strong>ya</strong> biashara kama vile pamba na tumbaku, na kuacha<br />
<strong>ardhi</strong> kidogo kwa ajili <strong>ya</strong> kupanda mazao <strong>ya</strong> chakula. Zaidi <strong>ya</strong> hayo,<br />
mpango wa uanzishwaji wa vijiji wa Rais Nyerere wa miaka 1970<br />
ulilazimisha familia nyingi ku<strong>ya</strong>acha makazi <strong>ya</strong>o kuhamia maeneo<br />
map<strong>ya</strong>.<br />
Kupotea kwa mfumo wa kijadi wa usimamizi wa rasilimali<br />
Hali hizi zilisababisha mmomonyoko wa mfumo wa kijadi wa<br />
usimamizi wa <strong>ardhi</strong> ambao wasukuma walitumia ku<strong>hifadhi</strong><br />
chakula cha mifugokwaajili <strong>ya</strong> msimu wa kiangazi. Mfumo huu<br />
unaofahamika kama ngitili ulijumuisha utengaji wa maeneo<br />
maalumu <strong>ya</strong> ku<strong>hifadhi</strong> n<strong>ya</strong>si za mifugo kwa ajili <strong>ya</strong> matumizi <strong>ya</strong><br />
kifamilia au <strong>ya</strong> jamii kwa ku<strong>ya</strong>acha maeneo <strong>ya</strong>kiwa na n<strong>ya</strong>si mpaka<br />
msimu wa mvua unapoanza. Ngitili hugawanywa katika sehemu<br />
kadhaa: kila sehemu <strong>ya</strong> ngitili lazima itumike yote kwa malisho kabla<br />
<strong>ya</strong> kuhamia sehemu nyingine. Hifadhi za kifamilia au za mtu mmoja<br />
4
mmoja huanzishwa kwenye <strong>ardhi</strong> binafsi; maeneo <strong>ya</strong> <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong> jamii<br />
nzima hutengwa kutoka kwenye maeneo <strong>ya</strong>nayofaa kwa malisho<br />
<strong>ya</strong> wakati wa kiangazi.Ngitili kwaajili <strong>ya</strong> jamii nzima mara nyingi<br />
hupatikana kandokando <strong>ya</strong> mito na kwenye vilima. Chini <strong>ya</strong> mfumo<br />
wa usimamizi wa kijadi wa umiliki <strong>ardhi</strong>, umiliki wa ngitili na <strong>ardhi</strong><br />
katika mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulisimamiwa na sheria ndogo za serikali<br />
za mitaa. Uanzishwaji wa vijiji na sheria <strong>ya</strong> vijiji v<strong>ya</strong> ujamaa <strong>ya</strong> mwaka<br />
1975 ilimaanisha kuwa mali zote za kifamilia kama vile nyumba,<br />
mashamba na ngitili viliachwa na wanaka<strong>ya</strong> kuhamia kwenye makazi<br />
<strong>ya</strong> pamoja. Mfumo mp<strong>ya</strong> wa vijiji, ingawa ulikuwa na manufaa<br />
kiutawala, ulisababisha ugumu wa kuendeleza utaratibu wa kijadi<br />
wa ku<strong>hifadhi</strong> mazingira.Hali hizi ziliendelea kuathirika kwa sababu<br />
<strong>ya</strong> kuongezeka kwa idadi <strong>ya</strong> watu na upanuzi wa maeneo <strong>ya</strong> kilimo.<br />
Matokeo <strong>ya</strong>ke ni kwamba mambo ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>lisababisha kujitokeza<br />
kwa changamoto mbili: uharibifu wa haraka wa <strong>ardhi</strong>, na ukosefu wa<br />
kuni kwaajili <strong>ya</strong> nishati. Ka<strong>ya</strong> nyingi zililazimika kusafiri umbali mrefu<br />
zaidi <strong>ya</strong> kilometa kumi kwaajili kukusan<strong>ya</strong> kuni, jukumu linalofanywa<br />
na wanawake.<br />
HASHI: urithi wa kudumu Shin<strong>ya</strong>nga<br />
Kwa miaka <strong>ya</strong> 1980 hekta 600 za ngitili zilikuwa zime<strong>hifadhi</strong>wa. Kuanzia<br />
1986, Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga ikahuisha mfumo huu kwa lengo<br />
la kuendeleza u<strong>hifadhi</strong> wa uoto wa maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa. Mpaka<br />
mwaka 2004, inakadiriwa kuwa hekta 350,000 za ngitili, zikiwemo<br />
<strong>hifadhi</strong> binafsi za miti, zilikuwa zime<strong>hifadhi</strong>wa au kuanzishwa katika<br />
vijiji 833 yenye idadi <strong>ya</strong> watu milioni 2.8.Programu iliendeshwa na<br />
kufadhiliwa na serikali <strong>ya</strong> Tanzania, na kwa muda mrefu ikisaidiwa<br />
na Mfuko wa Ushirikiano Maendeleo wa Norway (NORAD) na Kituo<br />
cha Kimataifa cha Kilimo cha Misitu (ICRAF). Mafanikio makubwa <strong>ya</strong><br />
<strong>programu</strong> <strong>ya</strong>litokana na uelewa mzuri kuhusu maswala <strong>ya</strong> mazingira<br />
wa jamii <strong>ya</strong> watu wa mkoa huu, wasukuma, ambao ni wafugaji na<br />
wakulima.<br />
Kwa mwaka 2004, <strong>programu</strong> hii ilirithiwa na Kituo cha Usimamizi<br />
wa Rasilimali za Misitu <strong>ya</strong> Asili na Kilimo cha Misitu (NAFRAC), lakini<br />
mfumo wa ngitili bado unaendelea. Kwa sasa ngitili zinakadiriwa<br />
kuchukua eneo la ukubwa wa hekta 500,000<br />
Faida za u<strong>hifadhi</strong> wa mfumo wa ekolojia zilizotokana na mradi<br />
wa HASHI ni pamoja na ongezeko la kipato cha ka<strong>ya</strong> kitokanacho<br />
na kilimo na ufugaji, lishe bora, na uhakika wa maisha kwenye<br />
familia ndani <strong>ya</strong> mkoa. Pia bayoanuai imenufaika na mradi huu<br />
kwa kuongezeka idadi <strong>ya</strong> miti, vichaka, n<strong>ya</strong>si, na aina mbalimbali za<br />
mitishamba, pamoja na ndege na spishi kadhaa za wan<strong>ya</strong>ma. Aina<br />
mbalimbali za mitishamba zimevunwa na kuuzwa kwa wenyeji kwa<br />
ajili <strong>ya</strong> kutengeneza dawa. Wakulima wamenufaika pia na kilimo cha<br />
misitu kwa njia mbalimbali kama vile upandaji wa mimea <strong>ya</strong> mfumo<br />
wa kinaitrojeni iliyosaidia kuongezaa tija katika kilimo. Mradi wa<br />
HASHI na washirika wake wa kimataifa wameweza kutoa mafunzo<br />
kwa walimu zaidi <strong>ya</strong> 150 kwaajili <strong>ya</strong> kusambaza uelewa kuhusu<br />
maswala <strong>ya</strong> mazingira kwenye shule za ndani <strong>ya</strong> mkoa.<br />
5
Majukumu Makuu na Ubunifu<br />
Kabla <strong>ya</strong> kuanzishwa kwa HASHI, jitihada za kupanda miti<br />
zilizoanzishwa na serikali <strong>ya</strong> Tanzania na mashirika <strong>ya</strong> kimaendeleo<br />
kama vile Benki <strong>ya</strong> Dunia zilishindwa kwa kiasi kikubwa kuzuia<br />
upotevu wa uoto wa misitu katika mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga. Mkabala wa<br />
mradi wa HASHI ulitofautiana na jitihada zilizotangulia kwa kufan<strong>ya</strong><br />
kazi karibu zaidi na wenyeji, kwanza kwa kubainisha maeneo<br />
<strong>ya</strong>liyohitaji kupewa umuhimu zaidi wa u<strong>hifadhi</strong>, na ku<strong>ya</strong><strong>hifadhi</strong> kwa<br />
kutumia mbinu za kijadi. Maofisa misitu walioajiriwa na Idara <strong>ya</strong><br />
Misitu na Nyuki ndani <strong>ya</strong> Wizara <strong>ya</strong> Maliasili na Utalii walifan<strong>ya</strong> kazi<br />
kwa ukaribu sana na wafan<strong>ya</strong>kazi wa wila<strong>ya</strong> na wa serikali za vijiji<br />
Kuunganisha maarifa <strong>ya</strong> jadi na msaada wa kimataifa<br />
Mafanikio <strong>ya</strong> awali <strong>ya</strong> mradi <strong>ya</strong>lichangiwa sana na msaada wa kifedha<br />
na kiufundi kutoka nje. Hadi mwaka 1987 HASHI ilikuwa inafan<strong>ya</strong><br />
kazi kikamilifu, na mwaka 1989 iliweza kuvutia ufadhili wa Shirika la<br />
Ushirikiano wa Maendeleo la Norway (NORAD).<br />
Mwongozo wa kiufundi na mawasiliano ulitolewa Kituo cha Utafiti<br />
wa Kilimo cha Misitu (ICRAF) kilichopo Nairobi, ambacho tangu<br />
mwaka 2002 kinajulikana kama Kituo cha Kimataifa cha Kilimo cha<br />
Misitu. Tafiti za ICRAF zinaonyesha mbinu sahihi za usimamizi wa<br />
uoto na malisho, na kuonyesha mchango wa maarifa <strong>ya</strong> kijadi na<br />
njia za kienyeji kama vile ngitili katika usimamizi wa <strong>ardhi</strong> wenye<br />
mafanikio.<br />
Malengo <strong>ya</strong> awali <strong>ya</strong> mradi<br />
Katika hatua za awali, mradi ulihusisha shughuli za upandaji miti<br />
na uhamasishaji kuhusu uelewa wa maswala <strong>ya</strong> mazingira. Katika<br />
vijiji vingi, maofisa misitu wa HASHI walitumia mbegu za miti <strong>ya</strong><br />
asili na vipingili v<strong>ya</strong> mizizi kwa ku<strong>hifadhi</strong> maeneo kwa ajili <strong>ya</strong> ngitili.<br />
Mahali pengine, upandaji wa miti mip<strong>ya</strong> (miti <strong>ya</strong> kigeni, na aina za<br />
miti <strong>ya</strong> asili inayopendelewa na wenyeji) ulifanyika, hasa kuzunguka<br />
maeneo <strong>ya</strong> karibu na nyumba.<br />
Baadhi <strong>ya</strong> ngitili zilikuwepo hata kabla <strong>ya</strong> mpango wa uanzishwaji wa<br />
vijiji, wakati ngitili nyingine zilianzishwa na wakulima na wanakijiji.<br />
Mbali na ku<strong>hifadhi</strong> ngitili, wanakijiji walihamasishwa kupanda<br />
mti kuzunguka nyumba zao (hasa miti <strong>ya</strong> matunda na kivuli), miti<br />
kwaajili <strong>ya</strong> kuonyesha mipaka <strong>ya</strong> maeneo na mashamba. Hii ilisaidia<br />
kuongeza rutuba na kutoa kuni, na ilisaidia pia kuonyesha mipaka<br />
<strong>ya</strong> wakulima na kuhalalisha umiliki wa <strong>ardhi</strong> ndani <strong>ya</strong> kijiji.<br />
Uelewa kuhusu mazingira uliongezeka na wanakijiji waliwezeshwa<br />
kwa njia mbalimbali. Njia hizi ni pamoja na video, uigizaji, n<strong>ya</strong>raka,<br />
na makongamano kwa ajili <strong>ya</strong> kuonyesha uhusiano baina <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong><br />
wa <strong>ardhi</strong>, u<strong>hifadhi</strong> wa misitu, na uhakika wa maisha.<br />
Mbinu shirikishi <strong>ya</strong> tathmini vijijini ilisaidia wanavijiji kubainisha<br />
matatizo kuhusiana na maliasili zao na kukubaliana kuhusu mbinu za<br />
utatuzi. Wakulima na wanavijiji walipata mafunzo juu <strong>ya</strong> namna bora<br />
<strong>ya</strong> kusimamia ngitili zao. Mathalani, wataalamu wa HASHI na ICRAF<br />
walitoa ushauri kuhusu aina za miti <strong>ya</strong> kienyeji zilizofaa kuboresha<br />
<strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong> wakulima au mimea inayofaa kwa mipaka imara.<br />
Ukuaji wa Biashara na mipango<br />
Jamii za vijijini zikiwa zimejitosheleza kimaarifa na kushiriki v<strong>ya</strong><br />
kutosha katika kuhuisha maarifa <strong>ya</strong> jadi, wanavijiji katika mkoa<br />
mzima wa Shin<strong>ya</strong>nga walipanua uwigo wa matumizi <strong>ya</strong> ngitili kutoka<br />
kwenye u<strong>hifadhi</strong> wa <strong>ardhi</strong> na n<strong>ya</strong>si za mifugo hadi kuwa <strong>hifadhi</strong><br />
<strong>ya</strong> maeneo <strong>ya</strong> miti kwa ajili <strong>ya</strong> bidhaa mbalimbali za miti, n<strong>ya</strong>si za<br />
mifugo, kuni, mitishamba, miti <strong>ya</strong> matunda, asali, wadudu waliwao,<br />
vyote hivyo vimeongeza uhakika wa maisha wakati wa majira <strong>ya</strong><br />
ukame. Upanuzi wa matumizi wa ngitili huenda ulisaidia kuongeza<br />
mvuto wake na kiwango cha kukubalika pia kiliongezeka.Wakati<br />
jitihada za ku<strong>hifadhi</strong> ziliongezeka kidogokidogo siku za mwanzoni,<br />
jitihada hizo za u<strong>hifadhi</strong> zilipanuka kwa kasi kwenye mkoa mzima<br />
kwenye miaka <strong>ya</strong> 1990.<br />
6
Upandaji miti uliojikita katika uwezo wa wanavijiji na<br />
taasisi<br />
Kusambaa kwa mafanikio <strong>ya</strong> mkabala wa HASHI kuliletwa na<br />
kiwango chake kikubwa cha kuwawezesha wananchi katika ngazi za<br />
vijiji, tofauti na <strong>programu</strong> nyingine za maendeleo <strong>ya</strong> vijiji <strong>ya</strong> miaka <strong>ya</strong><br />
1980. Matumizi <strong>ya</strong> ngitili kama nyenzo <strong>ya</strong> ku<strong>hifadhi</strong>, na kushirikisha<br />
taasisi za kijadi za wasukuma na serikali za vijiji kusimamia u<strong>hifadhi</strong><br />
vilichangia sana mafanikio ha<strong>ya</strong>. Serikali za vijiji zilizochaguliwa<br />
zilisimamia ngitili za kijumui<strong>ya</strong>, na kuwa kama mpatanishi wa<br />
mwisho wa migogoro <strong>ya</strong> umiliki wa ngitili binafsi, wakati kiutendaji,<br />
taasisi za kijadi zilikuwa na majukumu sawa katika vijiji vilivyo vingi.<br />
Mathalani, kila kijiji kiliweka sheria zake za u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili na<br />
usimamizi wake, vijiji vingi vilitumia pia askari wa kijadi <strong>ya</strong>ani<br />
sungusungu na mikutano <strong>ya</strong> pamoja inayofahamika kama Dagashida<br />
kwaajili <strong>ya</strong> kutekeleza maamuzi <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong>. Dagashida huongozwa<br />
wazee wa kimila wa kisukuma, na huamua ni adhabu zipi zitolewe<br />
kwa yeyote anayekiuka taratibu za u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili, kwa mfano<br />
kulisha mifugo kwenye eneo lililotengwa kwa ajili kuotesha.<br />
Kanuni zinazosimamia u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili ni pamoja kutoza faini<br />
(mchen<strong>ya</strong>). Katika kijiji kimoja, wachungaji wanaokamatwa<br />
kuchunga kimakosa katika ngitili wanatozwa shilingi za kitanzania<br />
20,000 (kama dola 14 za kimarekani). Kila adhabu inayofanana na<br />
hiyo kwa wanaokata miti kwenye ngitili. Kwa makosa makubwa,<br />
kama vile kuchoma moto uoto wa maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa, wafugaji<br />
hutozwa ng’ombe mzima aliye hai, ambaye baadaye huchinjwa.<br />
Kama migogoro haitaweza kuamuliwa na Dagashida, basi hupelekwa<br />
katika mahakama za chini na za wila<strong>ya</strong> kwa ajili <strong>ya</strong> maamuzi.<br />
Ingawa uanzishwaji wa ngitili haukuwa wa kidemokrasia kwa kila<br />
kijiji, mwelekeo wa jumla ulikuwa kuongezeka kwa uwajibikaji wa<br />
taasisi hizo za kijadi. Maofisa misitu wa HASHI walijitahidi kuzipa<br />
nguvu serikali na taasisi za kijadi kwa kutumia sheria <strong>ya</strong> Ardhi <strong>ya</strong> Vijiji<br />
<strong>ya</strong> mwaka 1999 iliyoruhusu serikali za vijiji kupitisha sheria ndogo<br />
zilizosaidia ku<strong>hifadhi</strong> ngitili. Sheria hizo ndogo, zikishapitishwa<br />
katika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong>, zilitambulika na serikali <strong>ya</strong> kitaifa.<br />
7
Matokeo<br />
MATOKEO YA KIMAZINGIRA<br />
Kuongezeka kwa bayoanuwai halikuwa lengo kuu la <strong>programu</strong> <strong>ya</strong><br />
U<strong>hifadhi</strong> wa Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga, bali msisitizo ulikuwa kuongezeka<br />
kwa tija <strong>ya</strong> kilimo katika mkoa mzima. Hata hivyo, urejeshaji wa<br />
bidhaa na huduma zitokanazo na maeneo yenye miti hufanywa kwa<br />
njia <strong>ya</strong> kuruhusu mimea kukua na kupanda miti <strong>ya</strong> kienyeji imesaidia<br />
kurejea kwa aina mbalimbali za miti, majani na mitishamba. Baadhi<br />
<strong>ya</strong> aina za wan<strong>ya</strong>ma zimeanza kurejea katika eneo husika.<br />
Kiwango cha urejeshaji miti kwenye maeneo tengefu<br />
Kwa mwaka 1986, kiasi cha hekta 600 za ngitili zilijulikana kuwepo<br />
mkoani Shin<strong>ya</strong>nga. Utafiti kwa vijiji 172 kama sampuli ndani <strong>ya</strong><br />
kipindi cha miaka <strong>ya</strong> 1990 ulionyesha kulikuwepo na ngitili 18,607<br />
(284 za jumui<strong>ya</strong>, na zilizobaki zikimilikiwa na ka<strong>ya</strong>) zikichukua eneo<br />
la hekta 78,122. Kwa kuzingatia sampuli hii, mameneja wa mradi<br />
wa HASHI walikadiria kuwa zaidi <strong>ya</strong> hekta 350,000 zilitumika kama<br />
ngitili, na wakazi tisa kati <strong>ya</strong> kumi kwa kila kijiji kwa jumla <strong>ya</strong> vijiji 833<br />
v<strong>ya</strong> mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga wanafurahia bidha na huduma zitokanazo<br />
na u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili<br />
Historia <strong>ya</strong> hivi karibuni kuhusu mradi uliosimamiwa na kituo cha<br />
kimataifa cha kilimo cha misitu inadai kuwa kiwango cha ngitili<br />
kimepunguzwa kwenye taarifa rasmi, inawezekana kuwa kuna zaidi<br />
<strong>ya</strong> hekta 500,000 za <strong>ardhi</strong> zilizotengwa.<br />
Karibu asilimia 60 za ngitili zinamilikiwa na watu binafsi, na zilizobaki<br />
zikimilikiwa na serikali za vijiji au taasisi kama vile shule, asasi<br />
za kijamii, makanisa, na misikiti. Inakadiriwa kuwa asilimia 90 <strong>ya</strong><br />
wafugaji, na asilimia 50 <strong>ya</strong> wakulima wanamiliki ngitili zao wenyewe.<br />
Zinatofautiana kwa viwango v<strong>ya</strong> ukubwa na umri.<br />
Kwa upande wa mashariki wa mkoa, eneo lenye mvua kidogo,<br />
ngitili za hekta 500 ni kawaida kuwepo, lakini hupatikana kwa wingi<br />
maeneo <strong>ya</strong> kati <strong>ya</strong> mkoa na maeneo <strong>ya</strong> magharibi ambako kuna<br />
mvua <strong>ya</strong> kutosha, zinaweza kuwa za ukubwa wa chekta chache. Kwa<br />
mwaka 2003, maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa kwaajili <strong>ya</strong> jumui<strong>ya</strong> ni <strong>ya</strong> wastani<br />
wa hekta 164, wakati maeneo binafsi <strong>ya</strong>na wastani wa hekta 2.3.<br />
Kuimarika kwa mimea na wan<strong>ya</strong>ma<br />
Mradi umesaidia kuwepo kwa jumla <strong>ya</strong> aina 152 za miti na vichaka,<br />
hasa kwa njia <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong> wa miti michanga kwenye ngitili ambazo<br />
hapo awali <strong>ya</strong>likuwa maeneo ambayo <strong>ya</strong>likuwa ha<strong>ya</strong>na miti. Zaidi<br />
<strong>ya</strong> aina 60 za miti zimetumika na wenyeji kwa malengo tofauti,<br />
kama vile dawa za mitishamba, matunda na mbogamboga, nishati,<br />
mbao, ususi, malisho, uzio, na kuezeka. Aina kumi na tatu za n<strong>ya</strong>si na<br />
ishirini na tano za mitishamba zinapatikana kwenye maeneo <strong>ya</strong> uoto<br />
<strong>ya</strong>liyo<strong>hifadhi</strong>wa. Ngitili za jumui<strong>ya</strong> zinasaidia ku<strong>hifadhi</strong> maeneo <strong>ya</strong><br />
vilima na pembezoni mwa mito, kuzuia mmomonyoko wa udongo,<br />
na ku<strong>hifadhi</strong> v<strong>ya</strong>nzo v<strong>ya</strong> maji.<br />
Wan<strong>ya</strong>ma,kwa hali fulani, wamerejea katika baadhi <strong>ya</strong> maeneo,<br />
hususani ndege kufuatia kuimarika kwa miombo na migunga.<br />
Jumla <strong>ya</strong> spishi 145 za ndege zinapatikana Shin<strong>ya</strong>nga ambazo<br />
hapo awali zilitoweka au ilikuwa nadra kuwepo, zikiwemo aina saba<br />
ambazo hupatikana katika maeneo maalumu. Fisi na wan<strong>ya</strong>ma<br />
wengine kama vile nguruwe pori, sungura, nk. sasa wanapatikana<br />
kama kawaida kiasi kwamba kumekuwepo na migogoro kati <strong>ya</strong><br />
wan<strong>ya</strong>ma na binadamu. Kwa ujumla, mbali na uharibifu unaoletwa<br />
na wan<strong>ya</strong>ma unaokadiriwa kuwa ni hasara <strong>ya</strong> dola 63 za kimarekani<br />
kwa kila familia, kwa mwaka kwa kipindi cha 2004, faida za kiuchumi<br />
za kuwepo kwa ngitili katika vijiji vingi zinazidi hasara hiyo.<br />
MATOKEO YA KIJAMII<br />
i. Faida za kukadiriwa: Faida za kiuchumi na kijamii za <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong><br />
uoto wa ngitili zilikadiriwa mwaka 2004 na kikosi kazi cha watu kumi<br />
kilichowekwa na serikali <strong>ya</strong> Tanzania na Shirika la Kimataifa la Hifadhi<br />
<strong>ya</strong> Mazingira, kilichokusan<strong>ya</strong> taarifa za utafiti za kisoko kwa ka<strong>ya</strong> 240<br />
kwa vijiji 12 na uchambuzi mwingine wa data kwa ajili <strong>ya</strong> kupima<br />
athari chan<strong>ya</strong> za HASHI. Utafiti huu ulikadiria thamani <strong>ya</strong> pesa<br />
kutokana na ngitili kuwa ni dola za kimarekani 14 kwa mwezi kwa<br />
kila mtu. Hiki ni kiwango kikubwa kwa mtanzania ukizingatia kuwa<br />
kipato cha chini kwa mtanzania wa kijijini ni dola za kimarekani 8.50<br />
kwa mtu mmoja kwa mwezi kwa mwaka 2004.<br />
8
Wastani wa thamani <strong>ya</strong> rasilimali muhimu 16 zilizovunwa<br />
kutokana na ngitili kwa wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Bukombe (Monela na<br />
wenzake, IUCN, 2004)<br />
Kwa ka<strong>ya</strong> Dola 1,190<br />
Kwa kijiji Dola 700,000<br />
Kwa wila<strong>ya</strong> Dola milioni 89.6<br />
Punguzo la muda wa kutafuta rasilimali (Monela na<br />
wenzake, IUCN, 2004)<br />
Kuni<br />
Nguzo<br />
Ezeko<br />
Maji<br />
Malisho<br />
Asilimia za ka<strong>ya</strong> kwa wila<strong>ya</strong> saba za mkoa wa Sin<strong>ya</strong>nga<br />
zinazotumia bidhaa za ngitili (Monela na wenzake, IUCN,<br />
2004)<br />
Kubadili lishe 22%<br />
Kutoa malisho kwa wan<strong>ya</strong>ma 21%<br />
Upatikanaji wa mitishamba 14%<br />
Upatikanaji wa kuni 61%<br />
Kulipia elimu <strong>ya</strong> watoto 36%<br />
Chanzo: Monela et al, IUCN, 2004.<br />
Saa 2-6 kwa siku<br />
Saa 1-5 kwa uvunaji<br />
Saa 1-6 kwa uvunaji<br />
Saa 1-2 kwa siku<br />
Saa 3-6 kwa uvunaji<br />
Thamani hizi za kipesa zimetokana na matumizi mbalimbali <strong>ya</strong><br />
bidhaa zilizovunwa na kila ka<strong>ya</strong> kutoka kwenye ngitili. Kati <strong>ya</strong> bidhaa<br />
16 za maliasili zinazotokana na ngitili; kuni, mbao na mitishamba<br />
ndizo zilizoonekana kuwa na umuhimu mkubwa kiuchumi kwa<br />
ka<strong>ya</strong>. Mazao mengine yenye umuhimu ni kama vile malisho, n<strong>ya</strong>si za<br />
kuezekea, n<strong>ya</strong>ma pori, matunda, mboga na asali.<br />
ii. Sifa za kuelezeka – kuimarika kwa maisha: Kwa vijiji vilivyofanyiwa<br />
utafiti, zaidi <strong>ya</strong> asilimia 64 <strong>ya</strong> ka<strong>ya</strong> zote zilisema kuwa zilikuwa na<br />
hali nzuri kutokana na faida za ngitili. Kikosi kazi kilichoongozwa na<br />
Profesa Monela wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Tanzania,<br />
kilihitimisha kwamba u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili ulidhirisha umuhimu wa<br />
rasilimali miti kwa uchumi wa wananchi wa kawaida na kuwa chanzo<br />
muhimu cha kiuchumi kama nyongeza kwa kilimo kwa maisha <strong>ya</strong><br />
wananchi wa Shin<strong>ya</strong>nga.Utafiti ulionyesha pia faida zinazohusiana<br />
na uongezaji wa kipato. Kuendeleza ngitili kumewawezesha<br />
wanakijiji kulipa karo za shule, kununua zana mp<strong>ya</strong> za kilimo, na<br />
kuajiri vibarua kwenye shughuli za kilimo, hasa kutoka na mauzo <strong>ya</strong><br />
mbao na bidhaa nyingine za miti. Kipato kilichotokana na ngitili za<br />
jumui<strong>ya</strong> kimetumika kujenga madarasa, ofisi za kijiji, na vituo v<strong>ya</strong><br />
af<strong>ya</strong>.<br />
Ngitili binafsi zimechangia pia kuongeza thamani <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong><br />
mkulima. Mwelekeo wa kuongezeka kwa maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa<br />
kunaweza kuashiria mabadiliko kutoka kwenye umiliki wa kijumui<strong>ya</strong><br />
had umiliki binafsi ndani <strong>ya</strong> mkoa wa Sin<strong>ya</strong>nga.<br />
Upatikanaji wa matunda, mboga na wadudu waliwao umeweza<br />
kuchangia kuimarika kwa af<strong>ya</strong> za watu, huku upatikanaji wa n<strong>ya</strong>si<br />
za kuezekea ukisaidia kuboresha makazi. Kupanda kwa tabaka la<br />
maji kulikotokana na u<strong>hifadhi</strong> wa maeneo kumesaidia upatikanaji<br />
wa maji. Uuzwaji wa dawa za kienyeji umesaidia pia kuimarika kwa<br />
uhakika wa maisha. Wanasa<strong>ya</strong>nsi kutoka Chuo Kikuu cha Heidelberg,<br />
Ujerumani walifan<strong>ya</strong> kazi na watafiti wa HASHI na kugundua<br />
matumizi ishirini <strong>ya</strong> dawa za mitishamba. Waganga wa kienyeji<br />
wa Shin<strong>ya</strong>nga wanawakilisha mfumo wa tiba asilia katika vijiji v<strong>ya</strong><br />
Tanzania, lakini hata hivyo uvunaji wa mitishamba umechangia<br />
uharibifu wa <strong>hifadhi</strong> za miti. Umoja wa waganga wa jadi 32 umesifu<br />
mradi wa HASHI kwa kutunza mazingira ambayo huweza kuwapatia<br />
miti <strong>ya</strong> dawa.<br />
Wanakiji, hasa wanawake, wana uwezo wa kuokoa muda kwa<br />
kutotembea umbali mrefu kutafuta kuni, malisho na majani <strong>ya</strong><br />
kuezekea. Hii inawapa nafasi wanaume na wanawake kutumia muda<br />
mwingi kufan<strong>ya</strong> shughuli za kiuchumi, na wakati huohuo kuweza<br />
kulea watoto.<br />
Ngitili zimesaidia kupunguza kero <strong>ya</strong> kusafiri umbali mrefu kwa<br />
wafugaji na wakulima kwa ajili <strong>ya</strong> kutafuta malisho wakati wa<br />
kiangazi. Hii imesadia kupunguza wizi wa mifugo na magonjwa.<br />
Maeneo binafsi <strong>ya</strong>liyotengwa <strong>ya</strong>nasaidia pia kupunguza athari<br />
za vipindi v<strong>ya</strong> ukame, na hivyo kurudi katika hali <strong>ya</strong> kawaida kwa<br />
haraka.<br />
Mafanikio endelevu <strong>ya</strong> majaribio <strong>ya</strong> HASHI <strong>ya</strong>mesaidia kupandisha<br />
hadhi na umuhimu wa serikali za vijiji na mamlaka <strong>ya</strong> kijadi kwa<br />
wasukuma. Ushushaji wa madaraka kwa ngazi za chini za vijiji<br />
9
Thamani <strong>ya</strong> bidhaa za ngitili zilizotumika na ka<strong>ya</strong> za wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Bukombe 2004 (Monela na wenzake, IUCN, 2004)<br />
Bidhaa za ngitili<br />
% <strong>ya</strong> ka<strong>ya</strong> zinazotumia bidhaa hizi<br />
kwa vijiji v<strong>ya</strong> utafiti<br />
wastani wa kipato cha ka<strong>ya</strong> kwa dola za<br />
kimarekani<br />
Mbao 59 71.74<br />
Kuni 64 13.09<br />
Nguzo 29 2.87<br />
miti <strong>ya</strong> <strong>hifadhi</strong> za maji 36 8.97<br />
Maji 21 34.04<br />
Asali 14 2.39<br />
N<strong>ya</strong>ma pori 7 0.72<br />
Wadudu waliawao 36 0.48<br />
Uyoga 36 2.87<br />
Mitishamba 7 10.76<br />
N<strong>ya</strong>si za kuezekea 36 2.15<br />
Malisho 7 1.15<br />
Mboga 29 2.15<br />
Matunda 43 2.87<br />
Useramala 14 1,021.60<br />
Ufin<strong>ya</strong>nzi 7 12.91<br />
Jumla <strong>ya</strong> thamani <strong>ya</strong> kiuchumi kwa kila ka<strong>ya</strong> kwa<br />
mwaka<br />
Dola za Kimarekani 1,190.77<br />
Chanzo: Monela et al, IUCN, 2004.<br />
umekuwa moja <strong>ya</strong> sababu muhimu za mafanikio <strong>ya</strong> HASHI. Kwa<br />
muda mrefu, hii imesaidia kutambuliwa kwa umuhimu wa taasisi za<br />
kijadi na madaraka <strong>ya</strong> vijiji katika usimamizi endelevu wa maliasili.<br />
Kijiji cha Wigelekeko :utafiti<br />
Kijiji cha Wigeleko kilichopo wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Maswa mkoani Shin<strong>ya</strong>nga ni<br />
mfano wa mafanikio <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili. Miaka <strong>ya</strong> kati <strong>ya</strong> 1980,<br />
ulishaji wa malisho na usafishaji wa mashamba kwa ajili <strong>ya</strong> pamba<br />
vilisababisha ukame na ukosefu wa bidhaa zitokanazo na miti,<br />
majani na maji kwa ka<strong>ya</strong> 408.<br />
Kwa mwongozo wa HASHI, vijiji mwanzoni vilitenga jumla <strong>ya</strong> hekta<br />
157 za <strong>ardhi</strong> iliyoharibika <strong>ya</strong> ngitili za jumui<strong>ya</strong> na binafsi. Ulishaji<br />
mifugo na ukataji miti vilipigwa marufuku kwa miaka mitano, na<br />
wanakijiji walilisha mifugo <strong>ya</strong>o kwenye ngitili binafsi.<br />
Marufuku ilipoisha, maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa <strong>ya</strong> jumui<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>liongezeka<br />
kuwa na miti na vichaka. Serikali <strong>ya</strong> kijiji na maofisa misitu wa HASHI<br />
walibuni mfumo rahisi wa usimamizi uliodhibiti utafutaji kuni kwa<br />
kupunguza matawi na kudhibiti ulishaji mifugo kipindi cha kiangazi.<br />
Wakulima waliruhusiwa kulima mazao katika maeneo madogo<br />
madogo, lakini kukiwa na uzingatiaji wa kanuni za ku<strong>hifadhi</strong> <strong>ardhi</strong>.<br />
Ulinzi wa ngitili za jumui<strong>ya</strong> ulifanywa na askari wa jadi maarufu kama<br />
sungusungu na kwa kuzingatia sheria ndogo za vijiji.<br />
Mwaka 1997, wanavijiji waliamua kupanua maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa<br />
kwa kuongeza hekta 20 kwa ajili <strong>ya</strong> kujenga mabwawa madogo <strong>ya</strong><br />
ku<strong>hifadhi</strong>a maji kwa matumizi <strong>ya</strong> nyumbani na kunyweshea mifugo.<br />
Kila ka<strong>ya</strong> ilichangia dola nne kwa ajili <strong>ya</strong> kujenga bwawa ambalo<br />
lilikamilika mwaka 1998. Mwaka mmoja baadaye, <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong> maji<br />
ilikuwa na maji muda wote na ilikadiriwa kuwa thamani <strong>ya</strong>ke ilifikia<br />
dola za Kimarekani 26,500 kwa mwaka. Maji kwa ajili <strong>ya</strong> mifugo<br />
<strong>ya</strong>lichangia zaidi pato ambalo lilikadiriwa kufikia dola 92,000 kwa<br />
mwaka kwa kuhudumia mifugo 1900. Mwaka 2000 uvuvi ulianzishwa<br />
kwenye bwawa na hivyo kuchangia zaidi uhakika wa maisha. Kuna<br />
umoja wa watumiaji maji wa kijiji cha Wigelekeko ambao husimamia<br />
bwawa kwa idhini <strong>ya</strong> mkutano mkuu wa kijiji, na huuza maji kwa<br />
watu wa nje.<br />
Mwaka 2001, dola 250 zilizopatikana kutokana na mauzo zilitolewa<br />
kwa ajili <strong>ya</strong> maendeleo <strong>ya</strong> kijamii. Ili kupunguza mahitaji makubwa<br />
<strong>ya</strong> ngitili za jumui<strong>ya</strong>, theluthi mbili <strong>ya</strong> wanakijiji wamepanda miti<br />
kwenye mashamba <strong>ya</strong>o, kwa wastani wa miche 100 kwa hekta moja.<br />
MATOKEO YA KISERA<br />
Ukiwa ni mradi wa serikali <strong>ya</strong> Tanzania, majaribio <strong>ya</strong> HASHI<br />
<strong>ya</strong>lisaidia kujua kwa kina kuhusu dhima <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong> wa bayoanuwai<br />
kama jambo la msingi katika kuhakikisha maisha <strong>ya</strong>ko salama na<br />
kupunguza umaskini, na hiyo ndiyo jitihada <strong>ya</strong> msingi <strong>ya</strong> serikali <strong>ya</strong><br />
Tanzania katika kuleta maendeleo.<br />
HASHI imekuwa ni kitu cha msingi kabla <strong>ya</strong> mabadiliko <strong>ya</strong> sera<br />
nchini Tanzania ambayo imesaidia sana jamii ziweze kusimamia<br />
maliasili. Mwaka 1998, Tanzania ilifan<strong>ya</strong> mapitio <strong>ya</strong> sera <strong>ya</strong> misitu na<br />
kuidhinisha, na sera imetilia mkazo zaidi katika usimamizi shirikishi<br />
na ughatuzi.<br />
10
Hii ilizingatia mipango <strong>ya</strong> usimamizi wa bayoanuwai kwa misitu<br />
yenye matumizi mengi. Jamii pia zilihimizwa kushiriki katika<br />
usimamizi wa misitu, kutenga maeneo <strong>ya</strong>liyoharibiwa ili <strong>ya</strong>weze<br />
kusimamiwa. Hii ilikamilishwa kwa sheria <strong>ya</strong> Misitu <strong>ya</strong> mwaka 2002.<br />
Umiliki wa <strong>ardhi</strong>: suala nyeti<br />
Jambo lililokwamisha kupanuka kwa mfumo wa ngitili ni utata<br />
kwenye sheria <strong>ya</strong> Tanzania kuhusu umiliki wa <strong>ardhi</strong>. Kukosekana<br />
kwa uhakika wa miliki, au hisia kuwa hakuna uhakika na umiliki,<br />
vilichangia kwa miaka <strong>ya</strong> 1990 kuwazuia watu binafsi kuendelea<br />
kuwa na maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa, na hali imeendelea kupunguza fursa<br />
za miradi <strong>ya</strong> HASHI kupanuka katika mikoa mingine nchini. Ingawa<br />
ngitili zilikuwa zimekubalika na kusajiliwa chini <strong>ya</strong> mradi wa HASHI,<br />
umiliki wake bado hauko wazi katika sheria <strong>ya</strong> sasa <strong>ya</strong> Tanzania.<br />
Vijiji kwa pamoja vina hati miliki kwa kupitia mipaka <strong>ya</strong>ke halali,<br />
wakati ka<strong>ya</strong> zikipata hati kwa maeneo <strong>ya</strong>o wanayolima na umiliki<br />
huo huridhiwa na mkutano wa kijiji. Sehemu <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong> kijiji iliyobaki<br />
baada <strong>ya</strong> kuwagawia wakulima hubaki kama eneo la kijiji kwa ajili <strong>ya</strong><br />
matumizi <strong>ya</strong> kijumui<strong>ya</strong> chini <strong>ya</strong> usimamizi wa serikali <strong>ya</strong> kijiji.<br />
Hii <strong>ardhi</strong> ambayo imetengwa kwa matumizi <strong>ya</strong> jumui<strong>ya</strong> inaweza<br />
kutumika kama ngitili, lakini bado kigezo cha uchaguzi wa<br />
matumizi <strong>ya</strong> hayo maeneo kuwa ngitili hakiko wazi kwenye sheria,<br />
na kwahiyo ni haki ipi <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> inayohusika. Jambo lililochangia<br />
kukwamisha jitihada za u<strong>hifadhi</strong> ni kwa kusisitiza kuhusu maeneo<br />
<strong>ya</strong>liyotengwa: serikali za vijiji na mikutano <strong>ya</strong> wanakijiji wanaogopa<br />
kutangaza ngitili kama maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa kwa kuogopa serikali<br />
kuu ku<strong>ya</strong>chukua na kubadili matumizi <strong>ya</strong>ke kwa ku<strong>ya</strong>weka chini <strong>ya</strong><br />
wila<strong>ya</strong> au kwa shughuli za kitaifa.<br />
Maswala <strong>ya</strong> umiliki <strong>ya</strong>naweza kuingilia kati uanzishwaji wa ngitili<br />
kwenye maeneo binafsi. Wamiliki binafsi wa <strong>ardhi</strong> wasio na hati<br />
miliki za maeneo <strong>ya</strong>o wamekuwa wakisita kuanzisha au kupanua<br />
ngitili kwa kuhofia migogoro ndani <strong>ya</strong> jamii.<br />
Kwa wakati mwingine, upimaji wa mipaka umesaidia kuwa na hati<br />
miliki za jumui<strong>ya</strong> na watu binafsi zisizo na mashaka yoyote. Mbali na<br />
hilo, kupanuka kwa mahitaji <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> kutokana na kuongezeka kwa<br />
watu na wan<strong>ya</strong>ma kumesababisha kuzuka kwa migogoro <strong>ya</strong> umiliki<br />
<strong>ardhi</strong> na ugomvi kuhusu maeneo <strong>ya</strong> kulishia mifugo.<br />
Sera <strong>ya</strong> Ardhi <strong>ya</strong> mwaka 1997 na Sheria <strong>ya</strong> Ardhi <strong>ya</strong> Kijiji <strong>ya</strong> Mwaka<br />
1999 vimetoa mwelekeo utakaovisaidia vijiji kupata hati miliki za<br />
vijiji, na watu binafsi kupata hati zao ndani <strong>ya</strong> eneo la kijiji, na hivyo<br />
kusaidia uanzishwaji rasmi wa ngitili<br />
Mabadiliko ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> kisera <strong>ya</strong>liwezesha serikali za vijiji kupitisha sheria<br />
ndogo kuzilinda ngitili zao kwa kutumia sheria za kijadi na walinzi<br />
wa vijiji. Kuweka sheria maalumu <strong>ya</strong> kusimamia umiliki na haki <strong>ya</strong><br />
kutumia <strong>ardhi</strong> iliyotengwa kama ngitili za jumui<strong>ya</strong> na kuepusha<br />
matatizo <strong>ya</strong> umiliki. Kuzitambua rasmi ngitili za kifamilia na binafsi<br />
chini <strong>ya</strong> sheria <strong>ya</strong> Tanzania kama kundi maalumu la usimamizi wa<br />
<strong>ardhi</strong> ambapo itakuwa rasmi kusambaza mfumo wa ngitili.<br />
11
Jinsi <strong>ya</strong> Kudumisha Mradi Huu<br />
JINSI YA KUDUMISHA MRADI HUU<br />
Mradi wa HASHI uliisha mwaka 2004 na ukarithiwa na Kituo cha<br />
Usimamizi wa Kilimo cha Misitu (NAFRAC), kilichopo Shin<strong>ya</strong>nga.<br />
Shughuli zake zimeendelezwa, ila kwa kuonyesha kiwango kikubwa<br />
cha uendelevu, umiliki wa wenyeji, na uwezo uliojengwa kwa miaka<br />
kumi na nane tangu mradi uanzishwe.<br />
Wakati wa uhai wa mradi, jitihada kadhaa zilifanyika kupanua<br />
shughuli zilizoanzishwa na wafan<strong>ya</strong>kazi wa HASHI na watafiti kutoka<br />
kituo cha kimataifa cha kilimo cha misitu. Matokeo <strong>ya</strong>ke mradi<br />
uliwanufaisha makumi elfu <strong>ya</strong> familia za wakulima. Tangu mwaka<br />
2004 wafan<strong>ya</strong>kazi wa serikali za vijiji wameendelea kuhamasisha<br />
kilimo cha misitu na usimamizi wa <strong>ardhi</strong> ulio endelevu. Katika wila<strong>ya</strong><br />
<strong>ya</strong> Shin<strong>ya</strong>nga, wakulima wa mfano walibainishwa kwa kila kata na<br />
kupewa ushauri wa kiufundi na vifaa. Tangu mwaka 1998, zaidi <strong>ya</strong><br />
walimu 150 wamepata mafunzo kwa ajili <strong>ya</strong> kuhamasisha maswala<br />
<strong>ya</strong> mazingira kwenye shule, wakipata msaada toka kwa Ofisa Maliasili<br />
wa Wila<strong>ya</strong>. Mikoa mingine miwili, Mwanza na Tabora walianza nao<br />
kutekeleza mradi kama wa HASHI kwaajili <strong>ya</strong> ku<strong>hifadhi</strong> maliasili.<br />
Moja <strong>ya</strong> sababu kuu <strong>ya</strong> kudumu kwa mfumo wa ngitili ni kwamba<br />
unaendelea kutoa matunda <strong>ya</strong> kiuchumi kwa wakulima na wafugaji<br />
ndani <strong>ya</strong> mkoa. Maeneo yenye miti <strong>ya</strong>meonyesha kuwa na faida;<br />
ngitili kwa malisho <strong>ya</strong> mifugo; na uanzishwaji wa teknolojia za kilimo<br />
cha misitu kama vile kupandikiza matunda kumeongeza kipato<br />
kwenye familia.<br />
Nishati, kaboni na uhusiano na kilimo<br />
Miradi mip<strong>ya</strong> imesaidia kuimarisha u<strong>hifadhi</strong> na urejeshaji wa<br />
misitu. Idara za serikali za vijiji zimehamasisha matumizi <strong>ya</strong> majiko<br />
<strong>ya</strong>nayotumia nishati kidogo. Hii imesaidia kupunguza mzigo wa<br />
kutegemea sana maliasili za misitu, pamoja na kupunguza muda<br />
ambao familia huupoteza kutafuta kuni. Kikundi cha wanawake cha<br />
Upendo ni moja <strong>ya</strong> asasi za kijamii zinazohamasisha matumizi <strong>ya</strong><br />
majiko <strong>ya</strong>siyotumia nishati kubwa, kwa wanachama wake na kwa<br />
wale wa vijiji v<strong>ya</strong> jirani.<br />
Utafiti wa hivi karibuni unaonyesha kuwa kuna uwezekano kwa<br />
<strong>hifadhi</strong> za miti za mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga kuzalisha kaboni, na mradi<br />
wa miaka minne unaosimamiwa na shirika la taifa la maendeleo<br />
<strong>ya</strong> viwanda v<strong>ya</strong> asili na mazingira (TaTEDO), kwa kushirikiana na<br />
kampuni iitwayo Development Associates Ltd (DASS) ambayo hutoa<br />
msaada wa kiufundi; na ambayo kwa sasa inatafiti jinsi ambavyo<br />
jamii za vijijini zinavyoweza kunufaika na pesa zitakazotolewa<br />
kupitia mradi wa kupunguza hewa <strong>ya</strong> ukaa itokanayo na ukataji miti<br />
na uharibifu wa misitu (REDD+).<br />
Pia Tanzania hivi karibuni ilizindua mkakati wake wa kuinua kilimo<br />
nchini ujulikanao kama ‘Kilimo Kwanza’. Mkakati huu umelenga<br />
kutenga pesa zaidi kwa ajili <strong>ya</strong> kilimo, kuhamasisha sekta binafsi<br />
kuwekeza katika kilimo, na kuwa na matumizi <strong>ya</strong> sa<strong>ya</strong>nsi na<br />
teknolojia katika kubadili maeneo makame <strong>ya</strong>weze kufaa kwa kilimo.<br />
Imependekezwa kuwa mradi huu utatumia sana majaribio <strong>ya</strong> HASHI,<br />
kusaidia kuboresha na kusaidia zaidi maeneo makavu <strong>ya</strong>nayotumika<br />
kwa kilimo na ufugaji nchini Tanzania.<br />
Changamoto za mazingira na kijamii<br />
Kuna maswala kadhaa <strong>ya</strong>nayoweza kukwamisha mafanikio <strong>ya</strong>liyopo,<br />
ukuaji, na kupanuka kwa mfumo wa ngitili. Kubwa kati <strong>ya</strong> ha<strong>ya</strong> ni<br />
ongezeko la idadi <strong>ya</strong> watu ambalo linatishia kuondoa mafanikio<br />
<strong>ya</strong>liyofikiwa <strong>ya</strong> mradi wa HASHI.<br />
Mwaka 1988, mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulikuwa na wakazi milioni 1.77.<br />
Mwaka 2002, idadi <strong>ya</strong> wakazi imefikia 2.8. Ongezeko la idadi <strong>ya</strong><br />
watu limekuwa likikua kwa asilimia 2.9 kwa mwaka na kukadiriwa<br />
kuwa sasa hivi mkoa unakadiriwa kuwa na wakazi kama milioni 3<br />
au asilimia 70 <strong>ya</strong> wakazi wameongezeka mkoani shin<strong>ya</strong>nga tangu<br />
mradi ulipoanza. Mifugo nayo imeongezeka kwa kiwango kikubwa.<br />
12
Kwa muktadha huu, mafanikio <strong>ya</strong> HASHI <strong>ya</strong>naonekana kuwa <strong>ya</strong><br />
maana, lakini ongezeko la watu vijijini limesababisha matumizi<br />
makubwa na uharibifu wa maeneo mengi <strong>ya</strong> ngitili. Changamoto hii<br />
imefan<strong>ya</strong> kuwa ngumu kwasababu <strong>ya</strong> kuzidi kwa migogoro kati <strong>ya</strong><br />
wan<strong>ya</strong>ma na binadamu, hasa kwa maswala <strong>ya</strong> uharibifu wa mazao.<br />
Moja <strong>ya</strong> athari za ongezeko la idadi <strong>ya</strong> watu na ongezeko la<br />
mahitaji <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> ni ongezeko la mauzo <strong>ya</strong>siyodhibitiwa <strong>ya</strong> ngitili<br />
zinazomilikiwa na watu binafsi. Kumekuwepo na mashauri kadhaa<br />
ambapo akina baba wanagawiawa vijana wao wa kiume ngitili zao,<br />
na hivyo kupunguza ukubwa na tija itokanayo na ngitili. Wakulima<br />
wila<strong>ya</strong>ni Maswa, kwa mfano, waliripotiwa mwaka 2004 kupunguza<br />
ukubwa wa ngitili zao binafsi na kulazimika kulishia mifugo ile<br />
yenye mahitaji zaidi wakati wa msimu wa ukame. Mabadiliko ha<strong>ya</strong><br />
<strong>ya</strong>naweza kuathiri uwezo wa ka<strong>ya</strong> na jamii kuendana na mabadiliko<br />
<strong>ya</strong> hali <strong>ya</strong> hewa na changamoto nyingine za tabianchi.<br />
WAHISANI<br />
• Serikali <strong>ya</strong> Jamhuri <strong>ya</strong> Muungano wa Tanzania: chini <strong>ya</strong> rais Julius<br />
Nyerere ilianzisha mradi mwaka 1986<br />
• Shirika la Ushirikiano wa Mandeleo la Norway (NORAD): lilitoa<br />
ufadhili wa muda mrefu kwa HASHI<br />
• Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Kilimo cha Misitu (ICRAF):<br />
kilitoa ushauri wa kiufundi na kisa<strong>ya</strong>nsi na kuwasaidia maofisa<br />
misitu wa HASHI<br />
• Mamlaka za serikali za vijiji na wila<strong>ya</strong><br />
13
MAREJELEO YA ZIADA<br />
• Ghazi, P., Barrow, E., Prof. Monela, G. and Mlenge, W. 2005. Regenerating Woodlands: Tanzania’s HASHI Project, in World Resources Report<br />
2005, pp. 131-138. http://pdf.wri.org/wrr05_full_hires.pdf<br />
• Barrow, E. and Mlenge, W. ‘Forest Restoration in Shin<strong>ya</strong>nga, Tanzania’, in Fisher, R.J., Maginnis, S., Jackson, W.J., Barrow, E., and Jeanrenaud,<br />
S. 2005. Poverty and Conservation: Landscapes, People and Power. IUCN, Gland, Switzerland, and Cambridge, UK. pp. 61-71. http://data.<br />
iucn.org/dbtw-wpd/edocs/FR-LL-002.pdf<br />
• Pye-Smith C. 2010. A Rural Revival in Tanzania: How agroforestry is helping farmers to restore the woodlands in Shin<strong>ya</strong>nga Region. ICRAF<br />
Trees for Change no. 7. Nairobi: World Agroforestry Centre. http://www.worldagroforestry.org/downloads/publications/PDFs/B16751.<br />
PDF<br />
• HASHI Soil Conservation Project video (Vimeo) http://vimeo.com/36989655<br />
Masimulizi kuhusu miradi mingine, bonyeza hapa:<br />
<strong>Equator</strong> <strong>Initiative</strong><br />
Environment and Energy Group<br />
United Nations Development Programme (UNDP)<br />
304 East 45th Street, 6th Floor<br />
New York, NY 10017<br />
Tel: +1 646 781-4023<br />
www.equatorinitiative.org<br />
Mradi wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa ndio unaoendesha miradi <strong>ya</strong> maendeleo <strong>ya</strong> Umoja wa Mataifa kote ulimwenguni<br />
kwa kutoa mwito wa mageuzi na kuelekeza mataifa kwa maarifa, na malighafi ili kusaidia watu kujiimarisha kimaisha.<br />
Mradi huu wa <strong>Equator</strong> huleta pamoja Umoja wa Mataifa , serikali, mashirika <strong>ya</strong>siyo <strong>ya</strong> kiserikali, wafanyibiashara na makundi <strong>ya</strong><br />
mashinani ili kutambua na kuimaliza maendeleo himili kwa watu na jamii kwa jumla.<br />
©2012 Haki Zote ni za Mradi wa <strong>Equator</strong>