12.01.2015 Views

programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative

programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative

programu ya hifadhi ardhi shinyanga (hashi) - Equator Initiative

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Empowered lives.<br />

Resilient nations.<br />

PROGRAMU YA<br />

HIFADHI ARDHI<br />

SHINYANGA (HASHI)<br />

Tanzania<br />

Miradi <strong>ya</strong> <strong>Equator</strong><br />

Wanafijiji na Maendeleo Himili <strong>ya</strong> Jamii


MIRADI YA UNDP EQUATOR<br />

Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni mbinu zinazonuiwa ku<strong>ya</strong>kidhi mahitaji <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong> kila siku na <strong>ya</strong> kimazingira. Kuna kazi<br />

chache ambazo zimechapishwa za kuelezea kinagaubaga hizo mbinu bunifu na vile zilianzishwa,vile ziliathiri wakaaji wa<br />

sehemu mbali mbali na vile zimekuwa zikibadilika pindi wakati unapotita. Wachache wamejitokeza kuelezea wazi wazi juu<br />

<strong>ya</strong> miradi <strong>ya</strong>o, na hata wale ambao wamefan<strong>ya</strong> hivyo ni wakuu wa vijiji ambao wamefan<strong>ya</strong> kuelezea kufaulu kwao.<br />

Mradi huu wa <strong>Equator</strong> Katika unadhamiria kujaza hili pengo kama njia moja <strong>ya</strong> kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa<br />

kwake. Masimulizi juu <strong>ya</strong> huu mradi ni baadhi tu <strong>ya</strong> mingi ambayo imefaulu na kushinda tuzo za <strong>Equator</strong> baada <strong>ya</strong> kukaguliwa<br />

na kutathiminiwa katika kitengo cha makundi <strong>ya</strong> kijamii <strong>ya</strong>nayo <strong>hifadhi</strong> mazingira na kuinua maisha <strong>ya</strong> wanafijiji. Miradi hii<br />

inakusudiwa kuwa mifano <strong>ya</strong> kuiwa na kuwatia shime kuzungumzia ilivyofaulu ili kuhamasisha ulimwengu juu <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong><br />

wa mazingira.<br />

Bonyeza katika ramani <strong>ya</strong> miradi <strong>ya</strong> <strong>Equator</strong> ili upate kupata habari zaidi<br />

Wahariri<br />

Mhariri Mkuu :<br />

Muhariri Meneja :<br />

Wahariri Waliochangia :<br />

Joseph Corcoran<br />

Oliver Hughes<br />

Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Erin Lewis, Whitney Wilding<br />

Wahandishi Waliochangia<br />

Eda<strong>ya</strong>tu Abieodun Lamptey, Erin Atwell, Toni Blackman, Jonathan Clay, Joseph Corcoran, Larissa Currado, Sarah Gordon, Oliver Hughes,<br />

Wen-Juan Jiang, Sonal Kanabar, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Rachael Lader, Patrick Lee, Erin Lewis, Jona Liebl, Mengning Ma,<br />

Mary McGraw, Gabriele Orlandi, Juliana Quaresma, Peter Schecter, Martin Sommerschuh, Whitney Wilding, Luna Wu<br />

Uchoraji<br />

Oliver Hughes, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Amy Korngiebel, Kimberly Koserowski, Erin Lewis, John Mulqueen, Lorena de la Parra,<br />

Brandon Payne, Mariajosé Satizábal G.<br />

Shukrani<br />

<strong>Equator</strong> ingependa kuwashukuru wanachama wa Programu <strong>ya</strong> Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga (HASHI). Picha zote ni za HASHI na Charlie Pye-<br />

Smith, World Agroforestry Centre. Ramani ni za CIA World Factbook na Wikipedia. Masimulizi juu <strong>ya</strong> mradi huu <strong>ya</strong>litafsiriwa kwa Kiswahili<br />

na Dr. Ken Ramani.<br />

Nukuu ziada<br />

United Nations Development Programme. 2012. Shin<strong>ya</strong>nga Soil Conservation Programme (HASHI), Tanzania. <strong>Equator</strong> <strong>Initiative</strong> Case Study<br />

Series. New York, NY.


PROGRAMU YA HIFADHI ARDHI<br />

SHINYANGA (HASHI)<br />

Tanzania<br />

MAELEZO KUHUSU MRADI HUU<br />

Programu <strong>ya</strong> Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga inafahamika<br />

zaidi kwa Kiswahili kwa kifupi cha HASHI (Hifadhi Ardhi<br />

Shin<strong>ya</strong>nga) iliyodumu kutoka mwaka 1986 hadi 2004 ikiwa<br />

na lengo la kurejesha rutuba <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> iliyoharibika <strong>ya</strong> mkoa<br />

wa Shin<strong>ya</strong>nga ulioko kaskazini magharibi mwa Tanzania;<br />

mkoa ambao ulipewa jina la “Jangwa la Tanzania” na Rais<br />

wa wakati huo Julius Nyerere katikati <strong>ya</strong> miaka <strong>ya</strong> 1980.<br />

Mkoa huu ambao ni ukanda wa miombo umeharibiwa kwa<br />

miongo kadhaa kwa kukata na kuchoma misitu (kwa ajili<br />

<strong>ya</strong> kutokomeza mbung’o) na kulazimishwa makazi map<strong>ya</strong><br />

chini <strong>ya</strong> mpango wa taifa wa kuanzisha vijiji Tanzania.<br />

Jitihada hizi zilifanywa kwa ushirikiano wa pamoja kati<br />

<strong>ya</strong> serikali na washirika wa kimataifa, lakini hata hivyo ni<br />

muhimu kutambua kuwa upandaji miti katika eneo hilo<br />

lazima ushirikishe wanajamii ili wawe mstari wa mbele<br />

katika juhudi hizi. Mfumo wa jadi wa kuishi pamoja kwenye<br />

eneo moja, au ngitili ulianzishwa, na wasukuma ambao<br />

ni wakulima na wafugaji walipewa jukumu la ku<strong>hifadhi</strong><br />

maeneo <strong>ya</strong> misitu. Matokeo ni kwamba hadi mwaka 2004,<br />

angalau hekta 350,000 za ngitili zilikuwa zimerejeshwa au<br />

kuanzishwa katika vijiji 833 kwa mkoa mzima.<br />

MUHTASARI<br />

ULISHINDA TUZO YA EQUATOR: Mwaka 2002<br />

ULIANZISHWA: Mwaka 1986<br />

ENEO: Shin<strong>ya</strong>nga kaskazini magharibi mwa Tanzania<br />

WANAOFAIDIKA: 833 villages<br />

MAZINGIRA: 145 bird species, 152 tree and shrub species<br />

YALIYOMO<br />

Historia na Mandhari 4<br />

Majukumu Makuu na Ubunifu 6<br />

Matokeo <strong>ya</strong> Kimazingira 8<br />

Matokeo <strong>ya</strong> Kijamii 8<br />

Matokeo <strong>ya</strong> Kisera 10<br />

Jinsi <strong>ya</strong> Kudumisha Mradi Huu 12<br />

Wahisani 13<br />

3


Historia na Mandhari<br />

Ukiwa unapatikana upande wa kusini mwa ziwa Victoria, mkoa wa<br />

Shin<strong>ya</strong>nga upo kaskazini magharibi mwa Tanzania na eneo lake<br />

kubwa ni la mazingira <strong>ya</strong> ukame ukiwa na wakazi karibu milioni<br />

tatu, kwa wastani wa watu 42 kwa kila kilometa <strong>ya</strong> mraba. Shin<strong>ya</strong>nga<br />

ni moja <strong>ya</strong> mikoa <strong>ya</strong> Tanzania maskini zaidi, wenye vilima v<strong>ya</strong> kimo<br />

cha chini na tambarare zenye kipindi kirefu cha kiangazi ukiwa<br />

na wastani wa milimeta 700 za mvua kwa mwaka. Kabila kubwa<br />

la mkoa huu ni Wasukuma ambao hujishughulisha na ufugaji na<br />

kilimo; mazao makubwa wanayozalisha ni mahindi, mtama, uwele,<br />

mihogo, pamba, na mchele. Zaidi <strong>ya</strong> asilimia 80 <strong>ya</strong> wakazi wa mkoa<br />

huu wanamiliki na kuendeleza mifugo kwenye malisho <strong>ya</strong> jamii zao.<br />

Kati <strong>ya</strong> mwaka 1986 na 2004, mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulianzisha Mpango<br />

wa Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga uliofahamika kwa kifupi kama HASHI<br />

(Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga). HASHI ilianzishwa na Rais Julius Nyerere<br />

baada <strong>ya</strong> kutembelea mkoa huo mwaka 1984 na akashtushwa na<br />

kiwango kikubwa cha ukataji miti. Kwa miaka <strong>ya</strong> 1980, Shin<strong>ya</strong>nga<br />

ilikuwa inajulikana kama ‘Jangwa la Tanzania ‘. Miongo kadhaa <strong>ya</strong><br />

usimamizi mbovu wa <strong>ardhi</strong> ilichangia kuendelea kuharibika kwa<br />

mazingira katika mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga, lakini mwanzo mkuu wa<br />

uharibifu huu ni mpango wa kukata misitu kipindi cha kabla <strong>ya</strong> vita v<strong>ya</strong><br />

pili v<strong>ya</strong> dunia. Hapo awali, mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulikuwa umefunikwa<br />

na uoto wa miombo na mshita, ambayo ilitoa lishe kwa mifugo na<br />

mafuta kwaajili <strong>ya</strong> kilimo na ufugaji kwa wasukuma. Hata hivyo<br />

misitu hii ilikuwa pia <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong> mbun’go, na magonjwa <strong>ya</strong> vimelea,<br />

na malale ambayo <strong>ya</strong>liwashambulia binadamu na wan<strong>ya</strong>ma. Katika<br />

miaka <strong>ya</strong> 1920, mamlaka <strong>ya</strong> kikoloni ilibuni mpango wa kuwalipa<br />

wenyeji kwa kukata miti kwenye maeneo makubwa <strong>ya</strong> miombo. Hii<br />

kwa kiasi kikubwa ilisaidia mafanikio katika kutokomeza Mbun’go,<br />

na pia kuanzisha maeneo map<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> malisho kwa ajili <strong>ya</strong> wasukuma,<br />

lakini kwa upande mwingine ikaathiri uzuri wa mazingira <strong>ya</strong> mkoa.<br />

Kadiri idadi <strong>ya</strong> mifugo na binadamu ilivyoongezeka katika nusu <strong>ya</strong><br />

mwisho <strong>ya</strong> karne <strong>ya</strong> ishirini, mahitaji kwa ajili <strong>ya</strong> kuni na kilimo pia<br />

<strong>ya</strong>liongezeka. Hii ilisababisha ufugaji uliokithiri kwenye malisho na<br />

mapori, wakati maeneo makubwa <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong>likuwa kwa ajili kilimo<br />

cha mazao <strong>ya</strong> biashara kama vile pamba na tumbaku, na kuacha<br />

<strong>ardhi</strong> kidogo kwa ajili <strong>ya</strong> kupanda mazao <strong>ya</strong> chakula. Zaidi <strong>ya</strong> hayo,<br />

mpango wa uanzishwaji wa vijiji wa Rais Nyerere wa miaka 1970<br />

ulilazimisha familia nyingi ku<strong>ya</strong>acha makazi <strong>ya</strong>o kuhamia maeneo<br />

map<strong>ya</strong>.<br />

Kupotea kwa mfumo wa kijadi wa usimamizi wa rasilimali<br />

Hali hizi zilisababisha mmomonyoko wa mfumo wa kijadi wa<br />

usimamizi wa <strong>ardhi</strong> ambao wasukuma walitumia ku<strong>hifadhi</strong><br />

chakula cha mifugokwaajili <strong>ya</strong> msimu wa kiangazi. Mfumo huu<br />

unaofahamika kama ngitili ulijumuisha utengaji wa maeneo<br />

maalumu <strong>ya</strong> ku<strong>hifadhi</strong> n<strong>ya</strong>si za mifugo kwa ajili <strong>ya</strong> matumizi <strong>ya</strong><br />

kifamilia au <strong>ya</strong> jamii kwa ku<strong>ya</strong>acha maeneo <strong>ya</strong>kiwa na n<strong>ya</strong>si mpaka<br />

msimu wa mvua unapoanza. Ngitili hugawanywa katika sehemu<br />

kadhaa: kila sehemu <strong>ya</strong> ngitili lazima itumike yote kwa malisho kabla<br />

<strong>ya</strong> kuhamia sehemu nyingine. Hifadhi za kifamilia au za mtu mmoja<br />

4


mmoja huanzishwa kwenye <strong>ardhi</strong> binafsi; maeneo <strong>ya</strong> <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong> jamii<br />

nzima hutengwa kutoka kwenye maeneo <strong>ya</strong>nayofaa kwa malisho<br />

<strong>ya</strong> wakati wa kiangazi.Ngitili kwaajili <strong>ya</strong> jamii nzima mara nyingi<br />

hupatikana kandokando <strong>ya</strong> mito na kwenye vilima. Chini <strong>ya</strong> mfumo<br />

wa usimamizi wa kijadi wa umiliki <strong>ardhi</strong>, umiliki wa ngitili na <strong>ardhi</strong><br />

katika mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulisimamiwa na sheria ndogo za serikali<br />

za mitaa. Uanzishwaji wa vijiji na sheria <strong>ya</strong> vijiji v<strong>ya</strong> ujamaa <strong>ya</strong> mwaka<br />

1975 ilimaanisha kuwa mali zote za kifamilia kama vile nyumba,<br />

mashamba na ngitili viliachwa na wanaka<strong>ya</strong> kuhamia kwenye makazi<br />

<strong>ya</strong> pamoja. Mfumo mp<strong>ya</strong> wa vijiji, ingawa ulikuwa na manufaa<br />

kiutawala, ulisababisha ugumu wa kuendeleza utaratibu wa kijadi<br />

wa ku<strong>hifadhi</strong> mazingira.Hali hizi ziliendelea kuathirika kwa sababu<br />

<strong>ya</strong> kuongezeka kwa idadi <strong>ya</strong> watu na upanuzi wa maeneo <strong>ya</strong> kilimo.<br />

Matokeo <strong>ya</strong>ke ni kwamba mambo ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>lisababisha kujitokeza<br />

kwa changamoto mbili: uharibifu wa haraka wa <strong>ardhi</strong>, na ukosefu wa<br />

kuni kwaajili <strong>ya</strong> nishati. Ka<strong>ya</strong> nyingi zililazimika kusafiri umbali mrefu<br />

zaidi <strong>ya</strong> kilometa kumi kwaajili kukusan<strong>ya</strong> kuni, jukumu linalofanywa<br />

na wanawake.<br />

HASHI: urithi wa kudumu Shin<strong>ya</strong>nga<br />

Kwa miaka <strong>ya</strong> 1980 hekta 600 za ngitili zilikuwa zime<strong>hifadhi</strong>wa. Kuanzia<br />

1986, Hifadhi Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga ikahuisha mfumo huu kwa lengo<br />

la kuendeleza u<strong>hifadhi</strong> wa uoto wa maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa. Mpaka<br />

mwaka 2004, inakadiriwa kuwa hekta 350,000 za ngitili, zikiwemo<br />

<strong>hifadhi</strong> binafsi za miti, zilikuwa zime<strong>hifadhi</strong>wa au kuanzishwa katika<br />

vijiji 833 yenye idadi <strong>ya</strong> watu milioni 2.8.Programu iliendeshwa na<br />

kufadhiliwa na serikali <strong>ya</strong> Tanzania, na kwa muda mrefu ikisaidiwa<br />

na Mfuko wa Ushirikiano Maendeleo wa Norway (NORAD) na Kituo<br />

cha Kimataifa cha Kilimo cha Misitu (ICRAF). Mafanikio makubwa <strong>ya</strong><br />

<strong>programu</strong> <strong>ya</strong>litokana na uelewa mzuri kuhusu maswala <strong>ya</strong> mazingira<br />

wa jamii <strong>ya</strong> watu wa mkoa huu, wasukuma, ambao ni wafugaji na<br />

wakulima.<br />

Kwa mwaka 2004, <strong>programu</strong> hii ilirithiwa na Kituo cha Usimamizi<br />

wa Rasilimali za Misitu <strong>ya</strong> Asili na Kilimo cha Misitu (NAFRAC), lakini<br />

mfumo wa ngitili bado unaendelea. Kwa sasa ngitili zinakadiriwa<br />

kuchukua eneo la ukubwa wa hekta 500,000<br />

Faida za u<strong>hifadhi</strong> wa mfumo wa ekolojia zilizotokana na mradi<br />

wa HASHI ni pamoja na ongezeko la kipato cha ka<strong>ya</strong> kitokanacho<br />

na kilimo na ufugaji, lishe bora, na uhakika wa maisha kwenye<br />

familia ndani <strong>ya</strong> mkoa. Pia bayoanuai imenufaika na mradi huu<br />

kwa kuongezeka idadi <strong>ya</strong> miti, vichaka, n<strong>ya</strong>si, na aina mbalimbali za<br />

mitishamba, pamoja na ndege na spishi kadhaa za wan<strong>ya</strong>ma. Aina<br />

mbalimbali za mitishamba zimevunwa na kuuzwa kwa wenyeji kwa<br />

ajili <strong>ya</strong> kutengeneza dawa. Wakulima wamenufaika pia na kilimo cha<br />

misitu kwa njia mbalimbali kama vile upandaji wa mimea <strong>ya</strong> mfumo<br />

wa kinaitrojeni iliyosaidia kuongezaa tija katika kilimo. Mradi wa<br />

HASHI na washirika wake wa kimataifa wameweza kutoa mafunzo<br />

kwa walimu zaidi <strong>ya</strong> 150 kwaajili <strong>ya</strong> kusambaza uelewa kuhusu<br />

maswala <strong>ya</strong> mazingira kwenye shule za ndani <strong>ya</strong> mkoa.<br />

5


Majukumu Makuu na Ubunifu<br />

Kabla <strong>ya</strong> kuanzishwa kwa HASHI, jitihada za kupanda miti<br />

zilizoanzishwa na serikali <strong>ya</strong> Tanzania na mashirika <strong>ya</strong> kimaendeleo<br />

kama vile Benki <strong>ya</strong> Dunia zilishindwa kwa kiasi kikubwa kuzuia<br />

upotevu wa uoto wa misitu katika mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga. Mkabala wa<br />

mradi wa HASHI ulitofautiana na jitihada zilizotangulia kwa kufan<strong>ya</strong><br />

kazi karibu zaidi na wenyeji, kwanza kwa kubainisha maeneo<br />

<strong>ya</strong>liyohitaji kupewa umuhimu zaidi wa u<strong>hifadhi</strong>, na ku<strong>ya</strong><strong>hifadhi</strong> kwa<br />

kutumia mbinu za kijadi. Maofisa misitu walioajiriwa na Idara <strong>ya</strong><br />

Misitu na Nyuki ndani <strong>ya</strong> Wizara <strong>ya</strong> Maliasili na Utalii walifan<strong>ya</strong> kazi<br />

kwa ukaribu sana na wafan<strong>ya</strong>kazi wa wila<strong>ya</strong> na wa serikali za vijiji<br />

Kuunganisha maarifa <strong>ya</strong> jadi na msaada wa kimataifa<br />

Mafanikio <strong>ya</strong> awali <strong>ya</strong> mradi <strong>ya</strong>lichangiwa sana na msaada wa kifedha<br />

na kiufundi kutoka nje. Hadi mwaka 1987 HASHI ilikuwa inafan<strong>ya</strong><br />

kazi kikamilifu, na mwaka 1989 iliweza kuvutia ufadhili wa Shirika la<br />

Ushirikiano wa Maendeleo la Norway (NORAD).<br />

Mwongozo wa kiufundi na mawasiliano ulitolewa Kituo cha Utafiti<br />

wa Kilimo cha Misitu (ICRAF) kilichopo Nairobi, ambacho tangu<br />

mwaka 2002 kinajulikana kama Kituo cha Kimataifa cha Kilimo cha<br />

Misitu. Tafiti za ICRAF zinaonyesha mbinu sahihi za usimamizi wa<br />

uoto na malisho, na kuonyesha mchango wa maarifa <strong>ya</strong> kijadi na<br />

njia za kienyeji kama vile ngitili katika usimamizi wa <strong>ardhi</strong> wenye<br />

mafanikio.<br />

Malengo <strong>ya</strong> awali <strong>ya</strong> mradi<br />

Katika hatua za awali, mradi ulihusisha shughuli za upandaji miti<br />

na uhamasishaji kuhusu uelewa wa maswala <strong>ya</strong> mazingira. Katika<br />

vijiji vingi, maofisa misitu wa HASHI walitumia mbegu za miti <strong>ya</strong><br />

asili na vipingili v<strong>ya</strong> mizizi kwa ku<strong>hifadhi</strong> maeneo kwa ajili <strong>ya</strong> ngitili.<br />

Mahali pengine, upandaji wa miti mip<strong>ya</strong> (miti <strong>ya</strong> kigeni, na aina za<br />

miti <strong>ya</strong> asili inayopendelewa na wenyeji) ulifanyika, hasa kuzunguka<br />

maeneo <strong>ya</strong> karibu na nyumba.<br />

Baadhi <strong>ya</strong> ngitili zilikuwepo hata kabla <strong>ya</strong> mpango wa uanzishwaji wa<br />

vijiji, wakati ngitili nyingine zilianzishwa na wakulima na wanakijiji.<br />

Mbali na ku<strong>hifadhi</strong> ngitili, wanakijiji walihamasishwa kupanda<br />

mti kuzunguka nyumba zao (hasa miti <strong>ya</strong> matunda na kivuli), miti<br />

kwaajili <strong>ya</strong> kuonyesha mipaka <strong>ya</strong> maeneo na mashamba. Hii ilisaidia<br />

kuongeza rutuba na kutoa kuni, na ilisaidia pia kuonyesha mipaka<br />

<strong>ya</strong> wakulima na kuhalalisha umiliki wa <strong>ardhi</strong> ndani <strong>ya</strong> kijiji.<br />

Uelewa kuhusu mazingira uliongezeka na wanakijiji waliwezeshwa<br />

kwa njia mbalimbali. Njia hizi ni pamoja na video, uigizaji, n<strong>ya</strong>raka,<br />

na makongamano kwa ajili <strong>ya</strong> kuonyesha uhusiano baina <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong><br />

wa <strong>ardhi</strong>, u<strong>hifadhi</strong> wa misitu, na uhakika wa maisha.<br />

Mbinu shirikishi <strong>ya</strong> tathmini vijijini ilisaidia wanavijiji kubainisha<br />

matatizo kuhusiana na maliasili zao na kukubaliana kuhusu mbinu za<br />

utatuzi. Wakulima na wanavijiji walipata mafunzo juu <strong>ya</strong> namna bora<br />

<strong>ya</strong> kusimamia ngitili zao. Mathalani, wataalamu wa HASHI na ICRAF<br />

walitoa ushauri kuhusu aina za miti <strong>ya</strong> kienyeji zilizofaa kuboresha<br />

<strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong> wakulima au mimea inayofaa kwa mipaka imara.<br />

Ukuaji wa Biashara na mipango<br />

Jamii za vijijini zikiwa zimejitosheleza kimaarifa na kushiriki v<strong>ya</strong><br />

kutosha katika kuhuisha maarifa <strong>ya</strong> jadi, wanavijiji katika mkoa<br />

mzima wa Shin<strong>ya</strong>nga walipanua uwigo wa matumizi <strong>ya</strong> ngitili kutoka<br />

kwenye u<strong>hifadhi</strong> wa <strong>ardhi</strong> na n<strong>ya</strong>si za mifugo hadi kuwa <strong>hifadhi</strong><br />

<strong>ya</strong> maeneo <strong>ya</strong> miti kwa ajili <strong>ya</strong> bidhaa mbalimbali za miti, n<strong>ya</strong>si za<br />

mifugo, kuni, mitishamba, miti <strong>ya</strong> matunda, asali, wadudu waliwao,<br />

vyote hivyo vimeongeza uhakika wa maisha wakati wa majira <strong>ya</strong><br />

ukame. Upanuzi wa matumizi wa ngitili huenda ulisaidia kuongeza<br />

mvuto wake na kiwango cha kukubalika pia kiliongezeka.Wakati<br />

jitihada za ku<strong>hifadhi</strong> ziliongezeka kidogokidogo siku za mwanzoni,<br />

jitihada hizo za u<strong>hifadhi</strong> zilipanuka kwa kasi kwenye mkoa mzima<br />

kwenye miaka <strong>ya</strong> 1990.<br />

6


Upandaji miti uliojikita katika uwezo wa wanavijiji na<br />

taasisi<br />

Kusambaa kwa mafanikio <strong>ya</strong> mkabala wa HASHI kuliletwa na<br />

kiwango chake kikubwa cha kuwawezesha wananchi katika ngazi za<br />

vijiji, tofauti na <strong>programu</strong> nyingine za maendeleo <strong>ya</strong> vijiji <strong>ya</strong> miaka <strong>ya</strong><br />

1980. Matumizi <strong>ya</strong> ngitili kama nyenzo <strong>ya</strong> ku<strong>hifadhi</strong>, na kushirikisha<br />

taasisi za kijadi za wasukuma na serikali za vijiji kusimamia u<strong>hifadhi</strong><br />

vilichangia sana mafanikio ha<strong>ya</strong>. Serikali za vijiji zilizochaguliwa<br />

zilisimamia ngitili za kijumui<strong>ya</strong>, na kuwa kama mpatanishi wa<br />

mwisho wa migogoro <strong>ya</strong> umiliki wa ngitili binafsi, wakati kiutendaji,<br />

taasisi za kijadi zilikuwa na majukumu sawa katika vijiji vilivyo vingi.<br />

Mathalani, kila kijiji kiliweka sheria zake za u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili na<br />

usimamizi wake, vijiji vingi vilitumia pia askari wa kijadi <strong>ya</strong>ani<br />

sungusungu na mikutano <strong>ya</strong> pamoja inayofahamika kama Dagashida<br />

kwaajili <strong>ya</strong> kutekeleza maamuzi <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong>. Dagashida huongozwa<br />

wazee wa kimila wa kisukuma, na huamua ni adhabu zipi zitolewe<br />

kwa yeyote anayekiuka taratibu za u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili, kwa mfano<br />

kulisha mifugo kwenye eneo lililotengwa kwa ajili kuotesha.<br />

Kanuni zinazosimamia u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili ni pamoja kutoza faini<br />

(mchen<strong>ya</strong>). Katika kijiji kimoja, wachungaji wanaokamatwa<br />

kuchunga kimakosa katika ngitili wanatozwa shilingi za kitanzania<br />

20,000 (kama dola 14 za kimarekani). Kila adhabu inayofanana na<br />

hiyo kwa wanaokata miti kwenye ngitili. Kwa makosa makubwa,<br />

kama vile kuchoma moto uoto wa maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa, wafugaji<br />

hutozwa ng’ombe mzima aliye hai, ambaye baadaye huchinjwa.<br />

Kama migogoro haitaweza kuamuliwa na Dagashida, basi hupelekwa<br />

katika mahakama za chini na za wila<strong>ya</strong> kwa ajili <strong>ya</strong> maamuzi.<br />

Ingawa uanzishwaji wa ngitili haukuwa wa kidemokrasia kwa kila<br />

kijiji, mwelekeo wa jumla ulikuwa kuongezeka kwa uwajibikaji wa<br />

taasisi hizo za kijadi. Maofisa misitu wa HASHI walijitahidi kuzipa<br />

nguvu serikali na taasisi za kijadi kwa kutumia sheria <strong>ya</strong> Ardhi <strong>ya</strong> Vijiji<br />

<strong>ya</strong> mwaka 1999 iliyoruhusu serikali za vijiji kupitisha sheria ndogo<br />

zilizosaidia ku<strong>hifadhi</strong> ngitili. Sheria hizo ndogo, zikishapitishwa<br />

katika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong>, zilitambulika na serikali <strong>ya</strong> kitaifa.<br />

7


Matokeo<br />

MATOKEO YA KIMAZINGIRA<br />

Kuongezeka kwa bayoanuwai halikuwa lengo kuu la <strong>programu</strong> <strong>ya</strong><br />

U<strong>hifadhi</strong> wa Ardhi Shin<strong>ya</strong>nga, bali msisitizo ulikuwa kuongezeka<br />

kwa tija <strong>ya</strong> kilimo katika mkoa mzima. Hata hivyo, urejeshaji wa<br />

bidhaa na huduma zitokanazo na maeneo yenye miti hufanywa kwa<br />

njia <strong>ya</strong> kuruhusu mimea kukua na kupanda miti <strong>ya</strong> kienyeji imesaidia<br />

kurejea kwa aina mbalimbali za miti, majani na mitishamba. Baadhi<br />

<strong>ya</strong> aina za wan<strong>ya</strong>ma zimeanza kurejea katika eneo husika.<br />

Kiwango cha urejeshaji miti kwenye maeneo tengefu<br />

Kwa mwaka 1986, kiasi cha hekta 600 za ngitili zilijulikana kuwepo<br />

mkoani Shin<strong>ya</strong>nga. Utafiti kwa vijiji 172 kama sampuli ndani <strong>ya</strong><br />

kipindi cha miaka <strong>ya</strong> 1990 ulionyesha kulikuwepo na ngitili 18,607<br />

(284 za jumui<strong>ya</strong>, na zilizobaki zikimilikiwa na ka<strong>ya</strong>) zikichukua eneo<br />

la hekta 78,122. Kwa kuzingatia sampuli hii, mameneja wa mradi<br />

wa HASHI walikadiria kuwa zaidi <strong>ya</strong> hekta 350,000 zilitumika kama<br />

ngitili, na wakazi tisa kati <strong>ya</strong> kumi kwa kila kijiji kwa jumla <strong>ya</strong> vijiji 833<br />

v<strong>ya</strong> mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga wanafurahia bidha na huduma zitokanazo<br />

na u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili<br />

Historia <strong>ya</strong> hivi karibuni kuhusu mradi uliosimamiwa na kituo cha<br />

kimataifa cha kilimo cha misitu inadai kuwa kiwango cha ngitili<br />

kimepunguzwa kwenye taarifa rasmi, inawezekana kuwa kuna zaidi<br />

<strong>ya</strong> hekta 500,000 za <strong>ardhi</strong> zilizotengwa.<br />

Karibu asilimia 60 za ngitili zinamilikiwa na watu binafsi, na zilizobaki<br />

zikimilikiwa na serikali za vijiji au taasisi kama vile shule, asasi<br />

za kijamii, makanisa, na misikiti. Inakadiriwa kuwa asilimia 90 <strong>ya</strong><br />

wafugaji, na asilimia 50 <strong>ya</strong> wakulima wanamiliki ngitili zao wenyewe.<br />

Zinatofautiana kwa viwango v<strong>ya</strong> ukubwa na umri.<br />

Kwa upande wa mashariki wa mkoa, eneo lenye mvua kidogo,<br />

ngitili za hekta 500 ni kawaida kuwepo, lakini hupatikana kwa wingi<br />

maeneo <strong>ya</strong> kati <strong>ya</strong> mkoa na maeneo <strong>ya</strong> magharibi ambako kuna<br />

mvua <strong>ya</strong> kutosha, zinaweza kuwa za ukubwa wa chekta chache. Kwa<br />

mwaka 2003, maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa kwaajili <strong>ya</strong> jumui<strong>ya</strong> ni <strong>ya</strong> wastani<br />

wa hekta 164, wakati maeneo binafsi <strong>ya</strong>na wastani wa hekta 2.3.<br />

Kuimarika kwa mimea na wan<strong>ya</strong>ma<br />

Mradi umesaidia kuwepo kwa jumla <strong>ya</strong> aina 152 za miti na vichaka,<br />

hasa kwa njia <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong> wa miti michanga kwenye ngitili ambazo<br />

hapo awali <strong>ya</strong>likuwa maeneo ambayo <strong>ya</strong>likuwa ha<strong>ya</strong>na miti. Zaidi<br />

<strong>ya</strong> aina 60 za miti zimetumika na wenyeji kwa malengo tofauti,<br />

kama vile dawa za mitishamba, matunda na mbogamboga, nishati,<br />

mbao, ususi, malisho, uzio, na kuezeka. Aina kumi na tatu za n<strong>ya</strong>si na<br />

ishirini na tano za mitishamba zinapatikana kwenye maeneo <strong>ya</strong> uoto<br />

<strong>ya</strong>liyo<strong>hifadhi</strong>wa. Ngitili za jumui<strong>ya</strong> zinasaidia ku<strong>hifadhi</strong> maeneo <strong>ya</strong><br />

vilima na pembezoni mwa mito, kuzuia mmomonyoko wa udongo,<br />

na ku<strong>hifadhi</strong> v<strong>ya</strong>nzo v<strong>ya</strong> maji.<br />

Wan<strong>ya</strong>ma,kwa hali fulani, wamerejea katika baadhi <strong>ya</strong> maeneo,<br />

hususani ndege kufuatia kuimarika kwa miombo na migunga.<br />

Jumla <strong>ya</strong> spishi 145 za ndege zinapatikana Shin<strong>ya</strong>nga ambazo<br />

hapo awali zilitoweka au ilikuwa nadra kuwepo, zikiwemo aina saba<br />

ambazo hupatikana katika maeneo maalumu. Fisi na wan<strong>ya</strong>ma<br />

wengine kama vile nguruwe pori, sungura, nk. sasa wanapatikana<br />

kama kawaida kiasi kwamba kumekuwepo na migogoro kati <strong>ya</strong><br />

wan<strong>ya</strong>ma na binadamu. Kwa ujumla, mbali na uharibifu unaoletwa<br />

na wan<strong>ya</strong>ma unaokadiriwa kuwa ni hasara <strong>ya</strong> dola 63 za kimarekani<br />

kwa kila familia, kwa mwaka kwa kipindi cha 2004, faida za kiuchumi<br />

za kuwepo kwa ngitili katika vijiji vingi zinazidi hasara hiyo.<br />

MATOKEO YA KIJAMII<br />

i. Faida za kukadiriwa: Faida za kiuchumi na kijamii za <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong><br />

uoto wa ngitili zilikadiriwa mwaka 2004 na kikosi kazi cha watu kumi<br />

kilichowekwa na serikali <strong>ya</strong> Tanzania na Shirika la Kimataifa la Hifadhi<br />

<strong>ya</strong> Mazingira, kilichokusan<strong>ya</strong> taarifa za utafiti za kisoko kwa ka<strong>ya</strong> 240<br />

kwa vijiji 12 na uchambuzi mwingine wa data kwa ajili <strong>ya</strong> kupima<br />

athari chan<strong>ya</strong> za HASHI. Utafiti huu ulikadiria thamani <strong>ya</strong> pesa<br />

kutokana na ngitili kuwa ni dola za kimarekani 14 kwa mwezi kwa<br />

kila mtu. Hiki ni kiwango kikubwa kwa mtanzania ukizingatia kuwa<br />

kipato cha chini kwa mtanzania wa kijijini ni dola za kimarekani 8.50<br />

kwa mtu mmoja kwa mwezi kwa mwaka 2004.<br />

8


Wastani wa thamani <strong>ya</strong> rasilimali muhimu 16 zilizovunwa<br />

kutokana na ngitili kwa wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Bukombe (Monela na<br />

wenzake, IUCN, 2004)<br />

Kwa ka<strong>ya</strong> Dola 1,190<br />

Kwa kijiji Dola 700,000<br />

Kwa wila<strong>ya</strong> Dola milioni 89.6<br />

Punguzo la muda wa kutafuta rasilimali (Monela na<br />

wenzake, IUCN, 2004)<br />

Kuni<br />

Nguzo<br />

Ezeko<br />

Maji<br />

Malisho<br />

Asilimia za ka<strong>ya</strong> kwa wila<strong>ya</strong> saba za mkoa wa Sin<strong>ya</strong>nga<br />

zinazotumia bidhaa za ngitili (Monela na wenzake, IUCN,<br />

2004)<br />

Kubadili lishe 22%<br />

Kutoa malisho kwa wan<strong>ya</strong>ma 21%<br />

Upatikanaji wa mitishamba 14%<br />

Upatikanaji wa kuni 61%<br />

Kulipia elimu <strong>ya</strong> watoto 36%<br />

Chanzo: Monela et al, IUCN, 2004.<br />

Saa 2-6 kwa siku<br />

Saa 1-5 kwa uvunaji<br />

Saa 1-6 kwa uvunaji<br />

Saa 1-2 kwa siku<br />

Saa 3-6 kwa uvunaji<br />

Thamani hizi za kipesa zimetokana na matumizi mbalimbali <strong>ya</strong><br />

bidhaa zilizovunwa na kila ka<strong>ya</strong> kutoka kwenye ngitili. Kati <strong>ya</strong> bidhaa<br />

16 za maliasili zinazotokana na ngitili; kuni, mbao na mitishamba<br />

ndizo zilizoonekana kuwa na umuhimu mkubwa kiuchumi kwa<br />

ka<strong>ya</strong>. Mazao mengine yenye umuhimu ni kama vile malisho, n<strong>ya</strong>si za<br />

kuezekea, n<strong>ya</strong>ma pori, matunda, mboga na asali.<br />

ii. Sifa za kuelezeka – kuimarika kwa maisha: Kwa vijiji vilivyofanyiwa<br />

utafiti, zaidi <strong>ya</strong> asilimia 64 <strong>ya</strong> ka<strong>ya</strong> zote zilisema kuwa zilikuwa na<br />

hali nzuri kutokana na faida za ngitili. Kikosi kazi kilichoongozwa na<br />

Profesa Monela wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Tanzania,<br />

kilihitimisha kwamba u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili ulidhirisha umuhimu wa<br />

rasilimali miti kwa uchumi wa wananchi wa kawaida na kuwa chanzo<br />

muhimu cha kiuchumi kama nyongeza kwa kilimo kwa maisha <strong>ya</strong><br />

wananchi wa Shin<strong>ya</strong>nga.Utafiti ulionyesha pia faida zinazohusiana<br />

na uongezaji wa kipato. Kuendeleza ngitili kumewawezesha<br />

wanakijiji kulipa karo za shule, kununua zana mp<strong>ya</strong> za kilimo, na<br />

kuajiri vibarua kwenye shughuli za kilimo, hasa kutoka na mauzo <strong>ya</strong><br />

mbao na bidhaa nyingine za miti. Kipato kilichotokana na ngitili za<br />

jumui<strong>ya</strong> kimetumika kujenga madarasa, ofisi za kijiji, na vituo v<strong>ya</strong><br />

af<strong>ya</strong>.<br />

Ngitili binafsi zimechangia pia kuongeza thamani <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong><br />

mkulima. Mwelekeo wa kuongezeka kwa maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa<br />

kunaweza kuashiria mabadiliko kutoka kwenye umiliki wa kijumui<strong>ya</strong><br />

had umiliki binafsi ndani <strong>ya</strong> mkoa wa Sin<strong>ya</strong>nga.<br />

Upatikanaji wa matunda, mboga na wadudu waliwao umeweza<br />

kuchangia kuimarika kwa af<strong>ya</strong> za watu, huku upatikanaji wa n<strong>ya</strong>si<br />

za kuezekea ukisaidia kuboresha makazi. Kupanda kwa tabaka la<br />

maji kulikotokana na u<strong>hifadhi</strong> wa maeneo kumesaidia upatikanaji<br />

wa maji. Uuzwaji wa dawa za kienyeji umesaidia pia kuimarika kwa<br />

uhakika wa maisha. Wanasa<strong>ya</strong>nsi kutoka Chuo Kikuu cha Heidelberg,<br />

Ujerumani walifan<strong>ya</strong> kazi na watafiti wa HASHI na kugundua<br />

matumizi ishirini <strong>ya</strong> dawa za mitishamba. Waganga wa kienyeji<br />

wa Shin<strong>ya</strong>nga wanawakilisha mfumo wa tiba asilia katika vijiji v<strong>ya</strong><br />

Tanzania, lakini hata hivyo uvunaji wa mitishamba umechangia<br />

uharibifu wa <strong>hifadhi</strong> za miti. Umoja wa waganga wa jadi 32 umesifu<br />

mradi wa HASHI kwa kutunza mazingira ambayo huweza kuwapatia<br />

miti <strong>ya</strong> dawa.<br />

Wanakiji, hasa wanawake, wana uwezo wa kuokoa muda kwa<br />

kutotembea umbali mrefu kutafuta kuni, malisho na majani <strong>ya</strong><br />

kuezekea. Hii inawapa nafasi wanaume na wanawake kutumia muda<br />

mwingi kufan<strong>ya</strong> shughuli za kiuchumi, na wakati huohuo kuweza<br />

kulea watoto.<br />

Ngitili zimesaidia kupunguza kero <strong>ya</strong> kusafiri umbali mrefu kwa<br />

wafugaji na wakulima kwa ajili <strong>ya</strong> kutafuta malisho wakati wa<br />

kiangazi. Hii imesadia kupunguza wizi wa mifugo na magonjwa.<br />

Maeneo binafsi <strong>ya</strong>liyotengwa <strong>ya</strong>nasaidia pia kupunguza athari<br />

za vipindi v<strong>ya</strong> ukame, na hivyo kurudi katika hali <strong>ya</strong> kawaida kwa<br />

haraka.<br />

Mafanikio endelevu <strong>ya</strong> majaribio <strong>ya</strong> HASHI <strong>ya</strong>mesaidia kupandisha<br />

hadhi na umuhimu wa serikali za vijiji na mamlaka <strong>ya</strong> kijadi kwa<br />

wasukuma. Ushushaji wa madaraka kwa ngazi za chini za vijiji<br />

9


Thamani <strong>ya</strong> bidhaa za ngitili zilizotumika na ka<strong>ya</strong> za wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Bukombe 2004 (Monela na wenzake, IUCN, 2004)<br />

Bidhaa za ngitili<br />

% <strong>ya</strong> ka<strong>ya</strong> zinazotumia bidhaa hizi<br />

kwa vijiji v<strong>ya</strong> utafiti<br />

wastani wa kipato cha ka<strong>ya</strong> kwa dola za<br />

kimarekani<br />

Mbao 59 71.74<br />

Kuni 64 13.09<br />

Nguzo 29 2.87<br />

miti <strong>ya</strong> <strong>hifadhi</strong> za maji 36 8.97<br />

Maji 21 34.04<br />

Asali 14 2.39<br />

N<strong>ya</strong>ma pori 7 0.72<br />

Wadudu waliawao 36 0.48<br />

Uyoga 36 2.87<br />

Mitishamba 7 10.76<br />

N<strong>ya</strong>si za kuezekea 36 2.15<br />

Malisho 7 1.15<br />

Mboga 29 2.15<br />

Matunda 43 2.87<br />

Useramala 14 1,021.60<br />

Ufin<strong>ya</strong>nzi 7 12.91<br />

Jumla <strong>ya</strong> thamani <strong>ya</strong> kiuchumi kwa kila ka<strong>ya</strong> kwa<br />

mwaka<br />

Dola za Kimarekani 1,190.77<br />

Chanzo: Monela et al, IUCN, 2004.<br />

umekuwa moja <strong>ya</strong> sababu muhimu za mafanikio <strong>ya</strong> HASHI. Kwa<br />

muda mrefu, hii imesaidia kutambuliwa kwa umuhimu wa taasisi za<br />

kijadi na madaraka <strong>ya</strong> vijiji katika usimamizi endelevu wa maliasili.<br />

Kijiji cha Wigelekeko :utafiti<br />

Kijiji cha Wigeleko kilichopo wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Maswa mkoani Shin<strong>ya</strong>nga ni<br />

mfano wa mafanikio <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong> wa ngitili. Miaka <strong>ya</strong> kati <strong>ya</strong> 1980,<br />

ulishaji wa malisho na usafishaji wa mashamba kwa ajili <strong>ya</strong> pamba<br />

vilisababisha ukame na ukosefu wa bidhaa zitokanazo na miti,<br />

majani na maji kwa ka<strong>ya</strong> 408.<br />

Kwa mwongozo wa HASHI, vijiji mwanzoni vilitenga jumla <strong>ya</strong> hekta<br />

157 za <strong>ardhi</strong> iliyoharibika <strong>ya</strong> ngitili za jumui<strong>ya</strong> na binafsi. Ulishaji<br />

mifugo na ukataji miti vilipigwa marufuku kwa miaka mitano, na<br />

wanakijiji walilisha mifugo <strong>ya</strong>o kwenye ngitili binafsi.<br />

Marufuku ilipoisha, maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa <strong>ya</strong> jumui<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>liongezeka<br />

kuwa na miti na vichaka. Serikali <strong>ya</strong> kijiji na maofisa misitu wa HASHI<br />

walibuni mfumo rahisi wa usimamizi uliodhibiti utafutaji kuni kwa<br />

kupunguza matawi na kudhibiti ulishaji mifugo kipindi cha kiangazi.<br />

Wakulima waliruhusiwa kulima mazao katika maeneo madogo<br />

madogo, lakini kukiwa na uzingatiaji wa kanuni za ku<strong>hifadhi</strong> <strong>ardhi</strong>.<br />

Ulinzi wa ngitili za jumui<strong>ya</strong> ulifanywa na askari wa jadi maarufu kama<br />

sungusungu na kwa kuzingatia sheria ndogo za vijiji.<br />

Mwaka 1997, wanavijiji waliamua kupanua maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa<br />

kwa kuongeza hekta 20 kwa ajili <strong>ya</strong> kujenga mabwawa madogo <strong>ya</strong><br />

ku<strong>hifadhi</strong>a maji kwa matumizi <strong>ya</strong> nyumbani na kunyweshea mifugo.<br />

Kila ka<strong>ya</strong> ilichangia dola nne kwa ajili <strong>ya</strong> kujenga bwawa ambalo<br />

lilikamilika mwaka 1998. Mwaka mmoja baadaye, <strong>hifadhi</strong> <strong>ya</strong> maji<br />

ilikuwa na maji muda wote na ilikadiriwa kuwa thamani <strong>ya</strong>ke ilifikia<br />

dola za Kimarekani 26,500 kwa mwaka. Maji kwa ajili <strong>ya</strong> mifugo<br />

<strong>ya</strong>lichangia zaidi pato ambalo lilikadiriwa kufikia dola 92,000 kwa<br />

mwaka kwa kuhudumia mifugo 1900. Mwaka 2000 uvuvi ulianzishwa<br />

kwenye bwawa na hivyo kuchangia zaidi uhakika wa maisha. Kuna<br />

umoja wa watumiaji maji wa kijiji cha Wigelekeko ambao husimamia<br />

bwawa kwa idhini <strong>ya</strong> mkutano mkuu wa kijiji, na huuza maji kwa<br />

watu wa nje.<br />

Mwaka 2001, dola 250 zilizopatikana kutokana na mauzo zilitolewa<br />

kwa ajili <strong>ya</strong> maendeleo <strong>ya</strong> kijamii. Ili kupunguza mahitaji makubwa<br />

<strong>ya</strong> ngitili za jumui<strong>ya</strong>, theluthi mbili <strong>ya</strong> wanakijiji wamepanda miti<br />

kwenye mashamba <strong>ya</strong>o, kwa wastani wa miche 100 kwa hekta moja.<br />

MATOKEO YA KISERA<br />

Ukiwa ni mradi wa serikali <strong>ya</strong> Tanzania, majaribio <strong>ya</strong> HASHI<br />

<strong>ya</strong>lisaidia kujua kwa kina kuhusu dhima <strong>ya</strong> u<strong>hifadhi</strong> wa bayoanuwai<br />

kama jambo la msingi katika kuhakikisha maisha <strong>ya</strong>ko salama na<br />

kupunguza umaskini, na hiyo ndiyo jitihada <strong>ya</strong> msingi <strong>ya</strong> serikali <strong>ya</strong><br />

Tanzania katika kuleta maendeleo.<br />

HASHI imekuwa ni kitu cha msingi kabla <strong>ya</strong> mabadiliko <strong>ya</strong> sera<br />

nchini Tanzania ambayo imesaidia sana jamii ziweze kusimamia<br />

maliasili. Mwaka 1998, Tanzania ilifan<strong>ya</strong> mapitio <strong>ya</strong> sera <strong>ya</strong> misitu na<br />

kuidhinisha, na sera imetilia mkazo zaidi katika usimamizi shirikishi<br />

na ughatuzi.<br />

10


Hii ilizingatia mipango <strong>ya</strong> usimamizi wa bayoanuwai kwa misitu<br />

yenye matumizi mengi. Jamii pia zilihimizwa kushiriki katika<br />

usimamizi wa misitu, kutenga maeneo <strong>ya</strong>liyoharibiwa ili <strong>ya</strong>weze<br />

kusimamiwa. Hii ilikamilishwa kwa sheria <strong>ya</strong> Misitu <strong>ya</strong> mwaka 2002.<br />

Umiliki wa <strong>ardhi</strong>: suala nyeti<br />

Jambo lililokwamisha kupanuka kwa mfumo wa ngitili ni utata<br />

kwenye sheria <strong>ya</strong> Tanzania kuhusu umiliki wa <strong>ardhi</strong>. Kukosekana<br />

kwa uhakika wa miliki, au hisia kuwa hakuna uhakika na umiliki,<br />

vilichangia kwa miaka <strong>ya</strong> 1990 kuwazuia watu binafsi kuendelea<br />

kuwa na maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa, na hali imeendelea kupunguza fursa<br />

za miradi <strong>ya</strong> HASHI kupanuka katika mikoa mingine nchini. Ingawa<br />

ngitili zilikuwa zimekubalika na kusajiliwa chini <strong>ya</strong> mradi wa HASHI,<br />

umiliki wake bado hauko wazi katika sheria <strong>ya</strong> sasa <strong>ya</strong> Tanzania.<br />

Vijiji kwa pamoja vina hati miliki kwa kupitia mipaka <strong>ya</strong>ke halali,<br />

wakati ka<strong>ya</strong> zikipata hati kwa maeneo <strong>ya</strong>o wanayolima na umiliki<br />

huo huridhiwa na mkutano wa kijiji. Sehemu <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> <strong>ya</strong> kijiji iliyobaki<br />

baada <strong>ya</strong> kuwagawia wakulima hubaki kama eneo la kijiji kwa ajili <strong>ya</strong><br />

matumizi <strong>ya</strong> kijumui<strong>ya</strong> chini <strong>ya</strong> usimamizi wa serikali <strong>ya</strong> kijiji.<br />

Hii <strong>ardhi</strong> ambayo imetengwa kwa matumizi <strong>ya</strong> jumui<strong>ya</strong> inaweza<br />

kutumika kama ngitili, lakini bado kigezo cha uchaguzi wa<br />

matumizi <strong>ya</strong> hayo maeneo kuwa ngitili hakiko wazi kwenye sheria,<br />

na kwahiyo ni haki ipi <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> inayohusika. Jambo lililochangia<br />

kukwamisha jitihada za u<strong>hifadhi</strong> ni kwa kusisitiza kuhusu maeneo<br />

<strong>ya</strong>liyotengwa: serikali za vijiji na mikutano <strong>ya</strong> wanakijiji wanaogopa<br />

kutangaza ngitili kama maeneo <strong>ya</strong>liyotengwa kwa kuogopa serikali<br />

kuu ku<strong>ya</strong>chukua na kubadili matumizi <strong>ya</strong>ke kwa ku<strong>ya</strong>weka chini <strong>ya</strong><br />

wila<strong>ya</strong> au kwa shughuli za kitaifa.<br />

Maswala <strong>ya</strong> umiliki <strong>ya</strong>naweza kuingilia kati uanzishwaji wa ngitili<br />

kwenye maeneo binafsi. Wamiliki binafsi wa <strong>ardhi</strong> wasio na hati<br />

miliki za maeneo <strong>ya</strong>o wamekuwa wakisita kuanzisha au kupanua<br />

ngitili kwa kuhofia migogoro ndani <strong>ya</strong> jamii.<br />

Kwa wakati mwingine, upimaji wa mipaka umesaidia kuwa na hati<br />

miliki za jumui<strong>ya</strong> na watu binafsi zisizo na mashaka yoyote. Mbali na<br />

hilo, kupanuka kwa mahitaji <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> kutokana na kuongezeka kwa<br />

watu na wan<strong>ya</strong>ma kumesababisha kuzuka kwa migogoro <strong>ya</strong> umiliki<br />

<strong>ardhi</strong> na ugomvi kuhusu maeneo <strong>ya</strong> kulishia mifugo.<br />

Sera <strong>ya</strong> Ardhi <strong>ya</strong> mwaka 1997 na Sheria <strong>ya</strong> Ardhi <strong>ya</strong> Kijiji <strong>ya</strong> Mwaka<br />

1999 vimetoa mwelekeo utakaovisaidia vijiji kupata hati miliki za<br />

vijiji, na watu binafsi kupata hati zao ndani <strong>ya</strong> eneo la kijiji, na hivyo<br />

kusaidia uanzishwaji rasmi wa ngitili<br />

Mabadiliko ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> kisera <strong>ya</strong>liwezesha serikali za vijiji kupitisha sheria<br />

ndogo kuzilinda ngitili zao kwa kutumia sheria za kijadi na walinzi<br />

wa vijiji. Kuweka sheria maalumu <strong>ya</strong> kusimamia umiliki na haki <strong>ya</strong><br />

kutumia <strong>ardhi</strong> iliyotengwa kama ngitili za jumui<strong>ya</strong> na kuepusha<br />

matatizo <strong>ya</strong> umiliki. Kuzitambua rasmi ngitili za kifamilia na binafsi<br />

chini <strong>ya</strong> sheria <strong>ya</strong> Tanzania kama kundi maalumu la usimamizi wa<br />

<strong>ardhi</strong> ambapo itakuwa rasmi kusambaza mfumo wa ngitili.<br />

11


Jinsi <strong>ya</strong> Kudumisha Mradi Huu<br />

JINSI YA KUDUMISHA MRADI HUU<br />

Mradi wa HASHI uliisha mwaka 2004 na ukarithiwa na Kituo cha<br />

Usimamizi wa Kilimo cha Misitu (NAFRAC), kilichopo Shin<strong>ya</strong>nga.<br />

Shughuli zake zimeendelezwa, ila kwa kuonyesha kiwango kikubwa<br />

cha uendelevu, umiliki wa wenyeji, na uwezo uliojengwa kwa miaka<br />

kumi na nane tangu mradi uanzishwe.<br />

Wakati wa uhai wa mradi, jitihada kadhaa zilifanyika kupanua<br />

shughuli zilizoanzishwa na wafan<strong>ya</strong>kazi wa HASHI na watafiti kutoka<br />

kituo cha kimataifa cha kilimo cha misitu. Matokeo <strong>ya</strong>ke mradi<br />

uliwanufaisha makumi elfu <strong>ya</strong> familia za wakulima. Tangu mwaka<br />

2004 wafan<strong>ya</strong>kazi wa serikali za vijiji wameendelea kuhamasisha<br />

kilimo cha misitu na usimamizi wa <strong>ardhi</strong> ulio endelevu. Katika wila<strong>ya</strong><br />

<strong>ya</strong> Shin<strong>ya</strong>nga, wakulima wa mfano walibainishwa kwa kila kata na<br />

kupewa ushauri wa kiufundi na vifaa. Tangu mwaka 1998, zaidi <strong>ya</strong><br />

walimu 150 wamepata mafunzo kwa ajili <strong>ya</strong> kuhamasisha maswala<br />

<strong>ya</strong> mazingira kwenye shule, wakipata msaada toka kwa Ofisa Maliasili<br />

wa Wila<strong>ya</strong>. Mikoa mingine miwili, Mwanza na Tabora walianza nao<br />

kutekeleza mradi kama wa HASHI kwaajili <strong>ya</strong> ku<strong>hifadhi</strong> maliasili.<br />

Moja <strong>ya</strong> sababu kuu <strong>ya</strong> kudumu kwa mfumo wa ngitili ni kwamba<br />

unaendelea kutoa matunda <strong>ya</strong> kiuchumi kwa wakulima na wafugaji<br />

ndani <strong>ya</strong> mkoa. Maeneo yenye miti <strong>ya</strong>meonyesha kuwa na faida;<br />

ngitili kwa malisho <strong>ya</strong> mifugo; na uanzishwaji wa teknolojia za kilimo<br />

cha misitu kama vile kupandikiza matunda kumeongeza kipato<br />

kwenye familia.<br />

Nishati, kaboni na uhusiano na kilimo<br />

Miradi mip<strong>ya</strong> imesaidia kuimarisha u<strong>hifadhi</strong> na urejeshaji wa<br />

misitu. Idara za serikali za vijiji zimehamasisha matumizi <strong>ya</strong> majiko<br />

<strong>ya</strong>nayotumia nishati kidogo. Hii imesaidia kupunguza mzigo wa<br />

kutegemea sana maliasili za misitu, pamoja na kupunguza muda<br />

ambao familia huupoteza kutafuta kuni. Kikundi cha wanawake cha<br />

Upendo ni moja <strong>ya</strong> asasi za kijamii zinazohamasisha matumizi <strong>ya</strong><br />

majiko <strong>ya</strong>siyotumia nishati kubwa, kwa wanachama wake na kwa<br />

wale wa vijiji v<strong>ya</strong> jirani.<br />

Utafiti wa hivi karibuni unaonyesha kuwa kuna uwezekano kwa<br />

<strong>hifadhi</strong> za miti za mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga kuzalisha kaboni, na mradi<br />

wa miaka minne unaosimamiwa na shirika la taifa la maendeleo<br />

<strong>ya</strong> viwanda v<strong>ya</strong> asili na mazingira (TaTEDO), kwa kushirikiana na<br />

kampuni iitwayo Development Associates Ltd (DASS) ambayo hutoa<br />

msaada wa kiufundi; na ambayo kwa sasa inatafiti jinsi ambavyo<br />

jamii za vijijini zinavyoweza kunufaika na pesa zitakazotolewa<br />

kupitia mradi wa kupunguza hewa <strong>ya</strong> ukaa itokanayo na ukataji miti<br />

na uharibifu wa misitu (REDD+).<br />

Pia Tanzania hivi karibuni ilizindua mkakati wake wa kuinua kilimo<br />

nchini ujulikanao kama ‘Kilimo Kwanza’. Mkakati huu umelenga<br />

kutenga pesa zaidi kwa ajili <strong>ya</strong> kilimo, kuhamasisha sekta binafsi<br />

kuwekeza katika kilimo, na kuwa na matumizi <strong>ya</strong> sa<strong>ya</strong>nsi na<br />

teknolojia katika kubadili maeneo makame <strong>ya</strong>weze kufaa kwa kilimo.<br />

Imependekezwa kuwa mradi huu utatumia sana majaribio <strong>ya</strong> HASHI,<br />

kusaidia kuboresha na kusaidia zaidi maeneo makavu <strong>ya</strong>nayotumika<br />

kwa kilimo na ufugaji nchini Tanzania.<br />

Changamoto za mazingira na kijamii<br />

Kuna maswala kadhaa <strong>ya</strong>nayoweza kukwamisha mafanikio <strong>ya</strong>liyopo,<br />

ukuaji, na kupanuka kwa mfumo wa ngitili. Kubwa kati <strong>ya</strong> ha<strong>ya</strong> ni<br />

ongezeko la idadi <strong>ya</strong> watu ambalo linatishia kuondoa mafanikio<br />

<strong>ya</strong>liyofikiwa <strong>ya</strong> mradi wa HASHI.<br />

Mwaka 1988, mkoa wa Shin<strong>ya</strong>nga ulikuwa na wakazi milioni 1.77.<br />

Mwaka 2002, idadi <strong>ya</strong> wakazi imefikia 2.8. Ongezeko la idadi <strong>ya</strong><br />

watu limekuwa likikua kwa asilimia 2.9 kwa mwaka na kukadiriwa<br />

kuwa sasa hivi mkoa unakadiriwa kuwa na wakazi kama milioni 3<br />

au asilimia 70 <strong>ya</strong> wakazi wameongezeka mkoani shin<strong>ya</strong>nga tangu<br />

mradi ulipoanza. Mifugo nayo imeongezeka kwa kiwango kikubwa.<br />

12


Kwa muktadha huu, mafanikio <strong>ya</strong> HASHI <strong>ya</strong>naonekana kuwa <strong>ya</strong><br />

maana, lakini ongezeko la watu vijijini limesababisha matumizi<br />

makubwa na uharibifu wa maeneo mengi <strong>ya</strong> ngitili. Changamoto hii<br />

imefan<strong>ya</strong> kuwa ngumu kwasababu <strong>ya</strong> kuzidi kwa migogoro kati <strong>ya</strong><br />

wan<strong>ya</strong>ma na binadamu, hasa kwa maswala <strong>ya</strong> uharibifu wa mazao.<br />

Moja <strong>ya</strong> athari za ongezeko la idadi <strong>ya</strong> watu na ongezeko la<br />

mahitaji <strong>ya</strong> <strong>ardhi</strong> ni ongezeko la mauzo <strong>ya</strong>siyodhibitiwa <strong>ya</strong> ngitili<br />

zinazomilikiwa na watu binafsi. Kumekuwepo na mashauri kadhaa<br />

ambapo akina baba wanagawiawa vijana wao wa kiume ngitili zao,<br />

na hivyo kupunguza ukubwa na tija itokanayo na ngitili. Wakulima<br />

wila<strong>ya</strong>ni Maswa, kwa mfano, waliripotiwa mwaka 2004 kupunguza<br />

ukubwa wa ngitili zao binafsi na kulazimika kulishia mifugo ile<br />

yenye mahitaji zaidi wakati wa msimu wa ukame. Mabadiliko ha<strong>ya</strong><br />

<strong>ya</strong>naweza kuathiri uwezo wa ka<strong>ya</strong> na jamii kuendana na mabadiliko<br />

<strong>ya</strong> hali <strong>ya</strong> hewa na changamoto nyingine za tabianchi.<br />

WAHISANI<br />

• Serikali <strong>ya</strong> Jamhuri <strong>ya</strong> Muungano wa Tanzania: chini <strong>ya</strong> rais Julius<br />

Nyerere ilianzisha mradi mwaka 1986<br />

• Shirika la Ushirikiano wa Mandeleo la Norway (NORAD): lilitoa<br />

ufadhili wa muda mrefu kwa HASHI<br />

• Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Kilimo cha Misitu (ICRAF):<br />

kilitoa ushauri wa kiufundi na kisa<strong>ya</strong>nsi na kuwasaidia maofisa<br />

misitu wa HASHI<br />

• Mamlaka za serikali za vijiji na wila<strong>ya</strong><br />

13


MAREJELEO YA ZIADA<br />

• Ghazi, P., Barrow, E., Prof. Monela, G. and Mlenge, W. 2005. Regenerating Woodlands: Tanzania’s HASHI Project, in World Resources Report<br />

2005, pp. 131-138. http://pdf.wri.org/wrr05_full_hires.pdf<br />

• Barrow, E. and Mlenge, W. ‘Forest Restoration in Shin<strong>ya</strong>nga, Tanzania’, in Fisher, R.J., Maginnis, S., Jackson, W.J., Barrow, E., and Jeanrenaud,<br />

S. 2005. Poverty and Conservation: Landscapes, People and Power. IUCN, Gland, Switzerland, and Cambridge, UK. pp. 61-71. http://data.<br />

iucn.org/dbtw-wpd/edocs/FR-LL-002.pdf<br />

• Pye-Smith C. 2010. A Rural Revival in Tanzania: How agroforestry is helping farmers to restore the woodlands in Shin<strong>ya</strong>nga Region. ICRAF<br />

Trees for Change no. 7. Nairobi: World Agroforestry Centre. http://www.worldagroforestry.org/downloads/publications/PDFs/B16751.<br />

PDF<br />

• HASHI Soil Conservation Project video (Vimeo) http://vimeo.com/36989655<br />

Masimulizi kuhusu miradi mingine, bonyeza hapa:<br />

<strong>Equator</strong> <strong>Initiative</strong><br />

Environment and Energy Group<br />

United Nations Development Programme (UNDP)<br />

304 East 45th Street, 6th Floor<br />

New York, NY 10017<br />

Tel: +1 646 781-4023<br />

www.equatorinitiative.org<br />

Mradi wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa ndio unaoendesha miradi <strong>ya</strong> maendeleo <strong>ya</strong> Umoja wa Mataifa kote ulimwenguni<br />

kwa kutoa mwito wa mageuzi na kuelekeza mataifa kwa maarifa, na malighafi ili kusaidia watu kujiimarisha kimaisha.<br />

Mradi huu wa <strong>Equator</strong> huleta pamoja Umoja wa Mataifa , serikali, mashirika <strong>ya</strong>siyo <strong>ya</strong> kiserikali, wafanyibiashara na makundi <strong>ya</strong><br />

mashinani ili kutambua na kuimaliza maendeleo himili kwa watu na jamii kwa jumla.<br />

©2012 Haki Zote ni za Mradi wa <strong>Equator</strong>

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!