19.02.2015 Views

Kurejesha Hadhi ya Mwalimu I - Muhtasari.pdf - HakiElimu

Kurejesha Hadhi ya Mwalimu I - Muhtasari.pdf - HakiElimu

Kurejesha Hadhi ya Mwalimu I - Muhtasari.pdf - HakiElimu

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>HakiElimu</strong><br />

<strong>Muhtasari</strong> Na. 10.3K<br />

<strong>Kurejesha</strong> <strong>Hadhi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Mwalimu</strong>:<br />

Matokeo <strong>ya</strong> Kujifunza, TDMS, na Bajeti <strong>ya</strong> mwaka 2010/11<br />

Ufuatao ni muhtasari wa ripoti iliyoandiliwa na <strong>HakiElimu</strong> inayosisitiza baadhi <strong>ya</strong> programu katika Mkakati wa<br />

Maendeleo na Menejimenti <strong>ya</strong> Ualimu (TDMS) ambazo hazijatekelezwa kutokana na ukosefu wa fedha, na inachangia<br />

mawazo kuhusu namna fedha hizo zinavyoweza kutolewa. Kwa tarifa zaidi, soma ripoti kamili.<br />

Kadiri maendeleo <strong>ya</strong> Tanzania <strong>ya</strong>navyosonga mbele<br />

ndivyo ambavyo jukumu la kila raia katika mchakato<br />

wa maendeleo hayo linavyozidi kuwa muhimu.<br />

Tukiangalia familia, jamii na taifa tunaona namna<br />

tunavyotegemeana kwa ajili <strong>ya</strong> mafanikio makubwa<br />

kwa wote. Kwa kutumia juhudi za pamoja na zenye<br />

mshikamano tunapata mafanikio mengi kuliko<br />

ambavyo tungepata kama mtu mmoja mmoja.<br />

Miongoni mwa zana muhimu ambazo raia wa serikali<br />

<strong>ya</strong> uwakilishi wanaunda kufanikisha malengo <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong><br />

pamoja ni bajeti <strong>ya</strong> taifa. Bajeti ni mwongozo<br />

unaosaidia kugeuza kwa ufanisi zaidi fedha kuwa<br />

maendeleo katika utoaji wa huduma, kama vile maji<br />

salama <strong>ya</strong> kunywa, huduma za af<strong>ya</strong> za kuaminika<br />

zaidi, na barabara bora zaidi.<br />

Kama ambavyo bajeti inavyoweza kuwa na athari<br />

kwa huduma za jamii kama vile maji, af<strong>ya</strong> na<br />

miundombinu, ina athari pia kwenye elimu. Athari<br />

hizi si kwa maendeleo <strong>ya</strong> vitu kama shule<br />

zinazojengwa, vitabu vilivyonunuliwa na mitihani<br />

iliyotolewa tu. Athari hizo zinatafsiriwa katika<br />

matokeo halisi <strong>ya</strong>nayohitajika katika elimu—<br />

matokeo <strong>ya</strong> kujifunza ambayo watoto, wanajamii na<br />

raia wamepata uwezo wa kufikiria kwa makini,<br />

kutanzua matatizo magumu zaidi na kupata<br />

ufumbuzi wa kiubunifu kupeleka mbele maendeleo<br />

<strong>ya</strong> jamii na taifa kwa ujumla.<br />

Ufundi. Madhumni <strong>ya</strong>ke ni “kushughulikia mahitaji<br />

<strong>ya</strong>liyopo <strong>ya</strong> walimu, na pia ukijaribu kushughulikia<br />

changamoto zinazohusiana na ubora ikiwemo<br />

taaluma <strong>ya</strong> ualimu, usimamizi na motisha.” Kwa<br />

pamoja, TDMS ina malengo 13 <strong>ya</strong> kimkakati ikiwemo<br />

“kuajiri na kuwabakiza kazini idadi <strong>ya</strong> kutosha <strong>ya</strong><br />

walimu na wakufunzi wenye ujuzi ili kumudu<br />

ipasavyo ufundishaji wa shule za awali, shule za<br />

msingi, shule za sekondari, elimu <strong>ya</strong> watu wazima na<br />

elimu isiyo rasmi pamoja na Vyuo v<strong>ya</strong> Ualimu.” Yote<br />

<strong>ya</strong>nalenga kuhakikisha kwamba kizazi kijacho cha<br />

Tanzania kina walimu bora na elimu bora ili waweze<br />

kuleta mabadiliko katika jamii zao na nchi <strong>ya</strong>o.<br />

Ingawa mkakati huu unashughulikia masuala mengi<br />

<strong>ya</strong>nayokera taaluma <strong>ya</strong> ualimu na matokeo <strong>ya</strong><br />

kujifunza, TDMS bado haijapata fedha za kutosha<br />

katika bajeti <strong>ya</strong> taifa kuwezesha hata kiwango kidogo<br />

cha utekelezaji wake.<br />

Bajeti katika Sera <strong>ya</strong> TDMS<br />

Sh. bil<br />

146<br />

Sh. bil<br />

162<br />

2009<br />

2010<br />

Bajeti Halisi <strong>ya</strong> TDMS<br />

Sh. bil<br />

25<br />

Sh. bil<br />

50<br />

Ufuatano ni uchambuzi wa namna <strong>ya</strong> kuboresha<br />

matokeo ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> kujifunza kwa kurekebisha baadhi<br />

<strong>ya</strong> taratibu za bajeti. Ufumbuzi muhimu<br />

uliobainishwa ni:<br />

Sh. bil<br />

172<br />

2011<br />

Sh. bil<br />

28<br />

1) Kuwapa motisha walimu waliopangwa<br />

kufundisha shule za pembezoni.<br />

2) Kuwapandisha daraja walimu wa shule<br />

za sekondari wenye leseni na wale wasio<br />

na taaluma.<br />

3) Kuwahakikishia fursa za kuendelea<br />

kitaaluma kwa njia <strong>ya</strong> mafunzo <strong>ya</strong><br />

kujiendeleza kazini.<br />

TDMS ni Nini?<br />

Kwa bahati nzuri Tanzania ta<strong>ya</strong>ri inao mkakati wa<br />

kushughulikia mambo ha<strong>ya</strong> ambao ni TDMS au<br />

Mkakati wa Maendeleo na Menejimenti <strong>ya</strong> Ualimu.<br />

TDMS ni mpango wa miaka mitano uliopitishwa<br />

mwaka 2008 na Wizara <strong>ya</strong> Elimu na Mafunzo <strong>ya</strong><br />

Kutoa Motisha kwa Maeneo <strong>ya</strong> Pembezoni<br />

Miongoni mwa vipengele v<strong>ya</strong> TDMS ni kutoa motisha<br />

kwa walimu wanaofan<strong>ya</strong> kazi katika maeneo <strong>ya</strong><br />

pembezoni. Pia zinajulikana kama posho za kufan<strong>ya</strong><br />

kazi katika mazingira magumu, motisha hizo<br />

zinaweza kuwa posho za kiwango kimoja au<br />

ongezeko kwa asilimia <strong>ya</strong> mishahara.<br />

Motisha <strong>ya</strong> maeneo <strong>ya</strong> pembezoni ni njia makini <strong>ya</strong><br />

kubakiza walimu katika maeneo <strong>ya</strong> vijijini. Sasa hivi<br />

Tanzania inakabiliana changamoto <strong>ya</strong> walimu wengi<br />

wap<strong>ya</strong> wanaopangiwa maeneo <strong>ya</strong> pembezoni<br />

hawaripoti kazini, wanahamia shule za mijini, au<br />

wanaacha kazi ndani <strong>ya</strong> mwaka mmoja, mwenendo<br />

unaogharimu nchi shilingi milioni 511 kwa mwaka.


<strong>Muhtasari</strong> 10.3K<br />

Hii inasababisha upungufu wa walimu hasa katika<br />

maeneo <strong>ya</strong> vijijini. Ingawa lengo la taifa ni mwalimu<br />

mmoja kwa wanafunzi 40, utafiti wa Wizara wa hivi<br />

karibuni uligundua shule za vijijini kuwa na wastani<br />

wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 59 na shule moja<br />

kuwa na mwalimu mmoja kwa wanafunzi 283!<br />

Katika kushughulika tatizo hili, kila mwaka Wizara<br />

inapanga walimu wap<strong>ya</strong> wengi zaidi wa kwenda<br />

shule za vijijini kuliko shule za mijini. Mwaka 2008,<br />

ingawa Wizara ilipanga walimu wap<strong>ya</strong> tisa kati <strong>ya</strong><br />

kumi kwenda maeneo <strong>ya</strong> vijijini, mwisho wa mwaka,<br />

walimu wap<strong>ya</strong> wengi zaidi waliishia katika shule za<br />

mijini kuliko shule za vijijini. Kushughulikia tatizo la<br />

upungufu wa walimu wakati hali hii <strong>ya</strong> walimu<br />

kuacha kazi inaendelea ni kazi bure, ni sawa na<br />

kujaza maji kwenye ndoo inayovuja kwa kasi: maji<br />

mengi <strong>ya</strong>tapotezwa, kuna mashaka kama ndoo itajaa,<br />

na hata ikijaa kwa muda mfupi, itaanza kumwaga<br />

maji tena.<br />

Motisha za maeneo <strong>ya</strong> pembezoni, zinazosaidia<br />

kutatua tatizo hili, ni sehemu <strong>ya</strong> TDMS lakini<br />

hazijatekelezwa kutokana na upungufu wa bajeti.<br />

Hili siyo suala la upatikanaji wa fedha za umma,<br />

lakini ni la namna ambavyo fedha za umma<br />

zinatumika. Posho za kufan<strong>ya</strong> kazi katika mazingira<br />

magumu hazijatolewa kwa walimu wakati posho kwa<br />

maofisa wengi wa serikali kuu zinaongezeka sana<br />

mwaka hadi mwaka.<br />

Motisha za Maeneo<br />

Pembezoni<br />

KUTOTOLEWA kwa<br />

Walimu Kutokana na<br />

“Ukosefu wa Fedha”<br />

2009 Sh. bil 2<br />

2010 Sh. bil 2.2<br />

2011 Sh. bil 2.4<br />

Jumla <strong>ya</strong><br />

Posho za Serikali<br />

2009 Sh. bil 171<br />

2010 Sh. bil 216<br />

2011 Sh. bil 269<br />

Wakati serikali <strong>ya</strong> Tanzania imeshindwa kutoa hata<br />

asilimia moja <strong>ya</strong> posho zake zote kwa ajili <strong>ya</strong> walimu<br />

wanaofundisha vijijini kama motisha <strong>ya</strong> maeneo <strong>ya</strong><br />

pembezoni, nchi jirani zimefanikiwa kutekeleza<br />

motisha <strong>ya</strong> maeneo <strong>ya</strong> pembezoni. Kwa mfano,<br />

Uganda ilianzisha posho <strong>ya</strong> kufan<strong>ya</strong> kazi katika<br />

mazingira magumu kwa kuongeza asilimia 20 <strong>ya</strong><br />

mshahara mwaka 2001, na imeongezeka hadi kufika<br />

asilimia 30 mwaka huu. Serikali <strong>ya</strong> Tanzania<br />

itaendelea kubaki nyuma kwa muda gani?<br />

Kuwapandisha Daraja Walimu wenye<br />

Leseni na Wale wasio na Taaluma<br />

Kipengele kingine muhimu cha TDMS ni<br />

kuwapandisha daraja walimu wenye leseni wawe na<br />

digrii kwa sababu kutokuwa na sifa kwa walimu pia<br />

imekuwa na athari katika matokeo <strong>ya</strong> kujifunza.<br />

Ingawa serikali <strong>ya</strong> Tanzania imefaulu kwa kuongeza<br />

uandikishaji wa wanafunzi shuleni na kujenga shule<br />

za sekondari, kwa upande mwingine umesababisha<br />

upungufu wa rasilimali watu.<br />

Ili kukabiliana na upungufu huo, shule za sekondari,<br />

hasa shule za kata zilizojengwa hivi karibuni,<br />

zinalazimika kuwaajiri walimu wenye sifa za chini<br />

kabisa. Kwa mujibu wa utafiti wa Wizara, kwa<br />

wastani, nusu <strong>ya</strong> walimu wanaofunisha katika shule<br />

za sekondari za serikali wana diploma na nusu wana<br />

digrii. Lakini katika shule za sekondari za kata,<br />

takribani hakuna walimu wenye digrii, na walimu<br />

watatu kati <strong>ya</strong> kumi wana leseni tu au ni wahitimu<br />

wa Kidato cha VI walioajiriwa na jamii kama walimu<br />

wasio na taaluma. Kiwango duni cha elimu cha<br />

mwalimu alichofikia kinaathiri ubora wa elimu<br />

itolewayo kwa wanafunzi, na inakadiriwa kwamba<br />

shule zote zinalipa shilingi bilioni 59.8 kwa mwaka<br />

kwa walimu hawa wasio na sifa, ingawa michango<br />

<strong>ya</strong>o katika matokeo <strong>ya</strong> kujifunza ni ndogo sana.<br />

Kama juhudi za TDMS, kuwapandisha daraja walimu<br />

wasio na sifa wawe wataalamu wenye sifa kama<br />

inavyohitajika, zingefanikiwa zingegharimu shilingi<br />

bilioni 7.5 kwa mwaka 2011, lakini inaonekana<br />

kwamba Wizara haijapanga bajeti kutekeleza<br />

shughuli hii. Si lazima iwe hivyo; inaonekana<br />

kwamba kuna fedha nyingi sehemu nyingine.<br />

Kwa mfano, kuangalia elimu <strong>ya</strong> juu, wakati nchi<br />

nyingine za Afrika kama vile Ken<strong>ya</strong> zinatenga<br />

kiwango sahihi cha asilimia 20 (au moja kati <strong>ya</strong> kila<br />

shilingi tano) <strong>ya</strong> fedha zao za elimu kuenda kwa<br />

elimu <strong>ya</strong> juu, Tanzania imekuwa inaipa elimu <strong>ya</strong> juu<br />

wastani wa asilimia 26 <strong>ya</strong> fedha zote za elimu na<br />

kuongeza kipande chake mwaka 2011 kiwe asilimia<br />

36 (au moja kati <strong>ya</strong> kila shilingi tatu)!<br />

Licha <strong>ya</strong> kuchukua theluthi <strong>ya</strong> bajeti <strong>ya</strong> elimu, elimu<br />

<strong>ya</strong> juu inatumia asilimia 1.5 <strong>ya</strong> aina zote za<br />

wanafunzi wanaoandikishwa katika ngazi yoyote <strong>ya</strong><br />

elimu Tanzania. Kwa mfano, kulinganisha wanafunzi<br />

wa vyuo vikuu na shule za sekondari, kuna


<strong>Muhtasari</strong> 10.3K<br />

wanafunzi 118,911 wa vyuo vikuu wakati kuna<br />

1,388,347 (mara 12 <strong>ya</strong> idadi hiyo) walioandikishwa<br />

katika shule za sekondari za serikali.<br />

Bajeti kubwa na uandikishaji mdogo katika elimu <strong>ya</strong><br />

juu inamaanisha kwamba, hata ukiondoa mikopo <strong>ya</strong><br />

wanafunzi, bado Wizara inatumia fedha nyingi zaidi<br />

kwa kila mwanafunzi wa chuo kikuu kuliko<br />

mwanafunzi wa shule <strong>ya</strong> sekondari:<br />

<strong>ya</strong>nasaidia kushughulikia shida kubwa katika mfumo<br />

wa elimu Tanzania, <strong>ya</strong>ani, utoro wa walimu. Utafiti<br />

kutoka Wizarani unaonesha kwamba wastani wa<br />

zaidi <strong>ya</strong> asilimia 13 <strong>ya</strong> walimu wa shule za msingi na<br />

za sekondari hawako kazini kwa miezi au hata<br />

miaka :<br />

Idadi <strong>ya</strong> wanafunzi katika shule za sekondari za<br />

serikali ni mara 12 zaidi <strong>ya</strong> wale walio katika<br />

vyuo vikuu na vyuo vingine v<strong>ya</strong> serikali.<br />

Hata ukiondoa mikopo <strong>ya</strong> wanafunzi,<br />

serikali inatumia wastani wa fedha<br />

mara 19 zaidi kwa kila mwanafunzi wa<br />

chuo kikuu kuliko kwa kila mwanafunzi<br />

wa shule <strong>ya</strong> sekondari.<br />

Kati <strong>ya</strong> kila walimu 15 wanaolipwa kufundisha,<br />

wawili hawapatikani shuleni.<br />

Zaidi <strong>ya</strong> upotevu wa maarifa kwa watoto na viongozi<br />

wa baadaye wa Tanzania, utoro huu wa walimu<br />

unakadiriwa kusababisha hasara yenye jumla <strong>ya</strong><br />

shilingi bilioni 58.7 kwa mwaka.<br />

Ndiyo, nyenzo za elimu <strong>ya</strong> juu ni ghali sana na ni<br />

vigumu kutetea bajeti kupunguzwa katika sekta moja<br />

<strong>ya</strong> elimu kuleta maboresho katika nyingine; lakini, je,<br />

hakuna namna tofauti hii kubwa kati <strong>ya</strong> elimu <strong>ya</strong> juu<br />

na <strong>ya</strong> sekondari inaweza kutatuliwa? Pamoja na<br />

bajeti <strong>ya</strong> elimu <strong>ya</strong> juu kuongezeka kuwa shilingi<br />

bilioni 698 mwaka 2011, je, haiwezekani kwa hata<br />

asilimia moja <strong>ya</strong> hii kuenda kwenye kipengele cha<br />

TDMS kwa kuwapandisha daraja walimu ili<br />

kuboresha elimu <strong>ya</strong> sekondari? Pamoja na ongezeko<br />

la uandikishaji wa wanafunzi katika shule za<br />

sekondari, bajeti lazima irekebishwe kuhakikisha<br />

kwamba wananchi wengi wanapewa elimu bora, sio<br />

tabaka la wachache tu, ili kujenga taifa bora la<br />

baadaye.<br />

Kuhakikisha Fursa za Kujiendeleza<br />

Kitaaluma<br />

Pia TDMS ina hatua nyingi za kuhakikisha fursa za<br />

kujiendeleza kitaaluma kwa walimu, hasa mafunzo<br />

kazini. Umuhimu wa mafunzo <strong>ya</strong> walimu kazini si<br />

kufundisha walimu up<strong>ya</strong> ili kuwawezesha<br />

kuwafundisha wanafunzi wao bora zaidi bali pia<br />

Utafiti unapendekeza kwamba njia nzuri <strong>ya</strong><br />

kupambana na utoro wa walimu ni kutoa fursa za<br />

kujiendeleza kitaaluma kama vile mafunzo kazini<br />

ambayo <strong>ya</strong>tawafan<strong>ya</strong> walimu wapende kazi <strong>ya</strong>o.<br />

TDMS <strong>ya</strong> Tanzania ina lengo kuu la “kuhakikisha<br />

mafunzo <strong>ya</strong> kujiendeleza kazini <strong>ya</strong> mara kwa mara na<br />

ukuaji wa kitaaluma,” linalolenga ufufuo wa Vituo<br />

v<strong>ya</strong> Walimu (TRC), mahali ambapo walimu<br />

wanaweza kupata mafunzo <strong>ya</strong> ziada na rasilimali <strong>ya</strong><br />

kufundishia. Ingawa kuna vituo v<strong>ya</strong> TRC 600 nchini<br />

kote, vimetelekezwa kwa miaka mingi, vinatoa<br />

huduma chache, na havina rasilimali za kutosha.<br />

Ndiyo sehemu kubwa <strong>ya</strong> bajeti <strong>ya</strong> mafunzo kazini<br />

katika TDMS inaelekezwa kuimarisha TRC.<br />

Gharama za sehemu hii <strong>ya</strong> TDMS kwa mwaka<br />

2010/11 ni shilingi bilioni 22.9, lakini fedha hizi<br />

hazijatolewa kutokana na TDMS kutopewa<br />

kipaumbele cha juu. Vipaumbele hivi lazima<br />

vizingatiwe up<strong>ya</strong>. Ni usimamizi mba<strong>ya</strong> wa fedha<br />

kuruhusu utoro wa walimu unaogharimu nchi<br />

shilingi bilioni 58.7 kwa mwaka ingeweza<br />

kudhibitiwa na mkakati unaogharimu chini <strong>ya</strong> nusu<br />

<strong>ya</strong> kiasi hicho.


<strong>Muhtasari</strong> 10.3K<br />

Je, Tanzania Inaweza Kumudu<br />

Kutotekeleza TDMS?<br />

Mkakati wa Maendeleo na Menejimenti <strong>ya</strong> Ualimu<br />

(TDMS) una hatua ambazo, zikichukuliwa,<br />

zinaweza kuhakikisha elimu bora kwa watoto na<br />

vijana wa Tanzania itakayowezesha ukuaji<br />

endelevu kwa Tanzania na kwa siku za baadaye.<br />

<strong>Muhtasari</strong> huu umesistiza malengo matatu <strong>ya</strong><br />

TDMS <strong>ya</strong>nayoweza kuwezesha ukuaji huo, <strong>ya</strong>ani:<br />

1) K u w a p a m o t i s h a w a l i m u<br />

waliopangwa kufundisha shule za<br />

pembezoni.<br />

2) Kuwapandisha daraja walimu wa<br />

shule za sekondari wenye leseni na<br />

wale wasio na taaluma.<br />

3) Kuwahakikishia fursa za kuendelea<br />

kitaaluma kwa njia <strong>ya</strong> mafunzo <strong>ya</strong><br />

kujiendeleza kazini.<br />

Hata hivyo, hatua hizi bado hazijatekelezwa<br />

kikamilifu, na TDMS inabaki na fedha kidogo sana<br />

kama kipaumbele cha chini kwenye bajeti.<br />

Katika hali <strong>ya</strong> kusikitisha, kwa kushindwa<br />

kutekeleza mkakati huo taifa hulazimika kulipa<br />

hasara ambazo TDMS ingeweza kuzizuia. Wakati<br />

mwaka 2011 TDMS ingegharimu shilingi bilioni<br />

102, fedha nyingi zaidi huenda zikatumika kwa<br />

vipengele vinavyopunguza ubora wa elimu Tanzania:<br />

Gharama <strong>ya</strong> walimu wap<strong>ya</strong> wasioripoti vituoni<br />

au wanaotelekeza vituo v<strong>ya</strong>o v<strong>ya</strong> kazi: Sh. mil 511<br />

Gharama <strong>ya</strong> walimu wenye leseni na wale wasio na<br />

taaluma ambao hawana mchango mkubwa<br />

katika matokeo <strong>ya</strong> kujifunza: Sh. bil 59.8<br />

Gharama <strong>ya</strong> utoro wa walimu wa shule za msingi: Sh. bil 47<br />

Gharama <strong>ya</strong> utoro wa walimu wa shule za sekondari: Sh. bil 11.7<br />

Sh. bil 119<br />

Hapana shaka, gharama za kutotekeleza TDMS<br />

haziishii hapa. Hasara <strong>ya</strong> rasilimali za taifa<br />

inayotokea kila mwaka kwa wanafunzi wa shule za<br />

msingi na za sekondari wanaomaliza shule bila <strong>ya</strong><br />

kufundishwa vizuri na wenye uwezo mdogo<br />

usiowafaa wao wenyewe wala kulisaidia taifa lao<br />

haipimiki. Wakati huo huo, kutafuta rasilimali<br />

zinazotakiwa katika kutekeleza TDMS inaweza kuwa<br />

rahisi kuliko ilivyofikiriwa mwanzo, na kutekeleza<br />

TDMS inaweza kuwa na gharama nafuu zaidi kuliko<br />

kutoitekeleza.<br />

Hatuna budi kukumbusha kwa nukuu <strong>ya</strong> Darek Bok,<br />

msomi na mwanasheria, ambaye alikaririwa na<br />

Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika hotuba <strong>ya</strong>ke <strong>ya</strong><br />

mwaka 2008: “Kama unadhani elimu ni ghali basi<br />

jaribu ujinga.” Suala la TDMS linaonesha namna<br />

ilivyo ghali kufan<strong>ya</strong> jambo lisilo na busara. Swali<br />

linalobaki ni: Je, Tanzania itaendelea kulipia ujinga<br />

kwa muda gani ?<br />

Utoro wa Walimu<br />

wa Shule za Msingi<br />

Walimu<br />

wasio na<br />

Sifa<br />

Mkakati wa<br />

Maendeleo na<br />

Menejimenti <strong>ya</strong><br />

Ualimu (TDMS)<br />

Walimu Wap<strong>ya</strong><br />

Wanaoacha Kazi<br />

Utoro wa<br />

Walimu wa<br />

Shule za<br />

Sekondari<br />

<strong>HakiElimu</strong> inawezesha wananchi<br />

kuleta mabadaliko katika elimu<br />

na demokrasia.<br />

SLP 79401 ● Dar es Salaam ● Tanzania<br />

Simu (255 22) 2151852/3 ● Faksi (255 22) 2152449<br />

info@hakielimu.org ● www.hakielimu.org

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!