Kurejesha Hadhi ya Mwalimu I - Muhtasari.pdf - HakiElimu
Kurejesha Hadhi ya Mwalimu I - Muhtasari.pdf - HakiElimu
Kurejesha Hadhi ya Mwalimu I - Muhtasari.pdf - HakiElimu
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>HakiElimu</strong><br />
<strong>Muhtasari</strong> Na. 10.3K<br />
<strong>Kurejesha</strong> <strong>Hadhi</strong> <strong>ya</strong> <strong>Mwalimu</strong>:<br />
Matokeo <strong>ya</strong> Kujifunza, TDMS, na Bajeti <strong>ya</strong> mwaka 2010/11<br />
Ufuatao ni muhtasari wa ripoti iliyoandiliwa na <strong>HakiElimu</strong> inayosisitiza baadhi <strong>ya</strong> programu katika Mkakati wa<br />
Maendeleo na Menejimenti <strong>ya</strong> Ualimu (TDMS) ambazo hazijatekelezwa kutokana na ukosefu wa fedha, na inachangia<br />
mawazo kuhusu namna fedha hizo zinavyoweza kutolewa. Kwa tarifa zaidi, soma ripoti kamili.<br />
Kadiri maendeleo <strong>ya</strong> Tanzania <strong>ya</strong>navyosonga mbele<br />
ndivyo ambavyo jukumu la kila raia katika mchakato<br />
wa maendeleo hayo linavyozidi kuwa muhimu.<br />
Tukiangalia familia, jamii na taifa tunaona namna<br />
tunavyotegemeana kwa ajili <strong>ya</strong> mafanikio makubwa<br />
kwa wote. Kwa kutumia juhudi za pamoja na zenye<br />
mshikamano tunapata mafanikio mengi kuliko<br />
ambavyo tungepata kama mtu mmoja mmoja.<br />
Miongoni mwa zana muhimu ambazo raia wa serikali<br />
<strong>ya</strong> uwakilishi wanaunda kufanikisha malengo <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong><br />
pamoja ni bajeti <strong>ya</strong> taifa. Bajeti ni mwongozo<br />
unaosaidia kugeuza kwa ufanisi zaidi fedha kuwa<br />
maendeleo katika utoaji wa huduma, kama vile maji<br />
salama <strong>ya</strong> kunywa, huduma za af<strong>ya</strong> za kuaminika<br />
zaidi, na barabara bora zaidi.<br />
Kama ambavyo bajeti inavyoweza kuwa na athari<br />
kwa huduma za jamii kama vile maji, af<strong>ya</strong> na<br />
miundombinu, ina athari pia kwenye elimu. Athari<br />
hizi si kwa maendeleo <strong>ya</strong> vitu kama shule<br />
zinazojengwa, vitabu vilivyonunuliwa na mitihani<br />
iliyotolewa tu. Athari hizo zinatafsiriwa katika<br />
matokeo halisi <strong>ya</strong>nayohitajika katika elimu—<br />
matokeo <strong>ya</strong> kujifunza ambayo watoto, wanajamii na<br />
raia wamepata uwezo wa kufikiria kwa makini,<br />
kutanzua matatizo magumu zaidi na kupata<br />
ufumbuzi wa kiubunifu kupeleka mbele maendeleo<br />
<strong>ya</strong> jamii na taifa kwa ujumla.<br />
Ufundi. Madhumni <strong>ya</strong>ke ni “kushughulikia mahitaji<br />
<strong>ya</strong>liyopo <strong>ya</strong> walimu, na pia ukijaribu kushughulikia<br />
changamoto zinazohusiana na ubora ikiwemo<br />
taaluma <strong>ya</strong> ualimu, usimamizi na motisha.” Kwa<br />
pamoja, TDMS ina malengo 13 <strong>ya</strong> kimkakati ikiwemo<br />
“kuajiri na kuwabakiza kazini idadi <strong>ya</strong> kutosha <strong>ya</strong><br />
walimu na wakufunzi wenye ujuzi ili kumudu<br />
ipasavyo ufundishaji wa shule za awali, shule za<br />
msingi, shule za sekondari, elimu <strong>ya</strong> watu wazima na<br />
elimu isiyo rasmi pamoja na Vyuo v<strong>ya</strong> Ualimu.” Yote<br />
<strong>ya</strong>nalenga kuhakikisha kwamba kizazi kijacho cha<br />
Tanzania kina walimu bora na elimu bora ili waweze<br />
kuleta mabadiliko katika jamii zao na nchi <strong>ya</strong>o.<br />
Ingawa mkakati huu unashughulikia masuala mengi<br />
<strong>ya</strong>nayokera taaluma <strong>ya</strong> ualimu na matokeo <strong>ya</strong><br />
kujifunza, TDMS bado haijapata fedha za kutosha<br />
katika bajeti <strong>ya</strong> taifa kuwezesha hata kiwango kidogo<br />
cha utekelezaji wake.<br />
Bajeti katika Sera <strong>ya</strong> TDMS<br />
Sh. bil<br />
146<br />
Sh. bil<br />
162<br />
2009<br />
2010<br />
Bajeti Halisi <strong>ya</strong> TDMS<br />
Sh. bil<br />
25<br />
Sh. bil<br />
50<br />
Ufuatano ni uchambuzi wa namna <strong>ya</strong> kuboresha<br />
matokeo ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> kujifunza kwa kurekebisha baadhi<br />
<strong>ya</strong> taratibu za bajeti. Ufumbuzi muhimu<br />
uliobainishwa ni:<br />
Sh. bil<br />
172<br />
2011<br />
Sh. bil<br />
28<br />
1) Kuwapa motisha walimu waliopangwa<br />
kufundisha shule za pembezoni.<br />
2) Kuwapandisha daraja walimu wa shule<br />
za sekondari wenye leseni na wale wasio<br />
na taaluma.<br />
3) Kuwahakikishia fursa za kuendelea<br />
kitaaluma kwa njia <strong>ya</strong> mafunzo <strong>ya</strong><br />
kujiendeleza kazini.<br />
TDMS ni Nini?<br />
Kwa bahati nzuri Tanzania ta<strong>ya</strong>ri inao mkakati wa<br />
kushughulikia mambo ha<strong>ya</strong> ambao ni TDMS au<br />
Mkakati wa Maendeleo na Menejimenti <strong>ya</strong> Ualimu.<br />
TDMS ni mpango wa miaka mitano uliopitishwa<br />
mwaka 2008 na Wizara <strong>ya</strong> Elimu na Mafunzo <strong>ya</strong><br />
Kutoa Motisha kwa Maeneo <strong>ya</strong> Pembezoni<br />
Miongoni mwa vipengele v<strong>ya</strong> TDMS ni kutoa motisha<br />
kwa walimu wanaofan<strong>ya</strong> kazi katika maeneo <strong>ya</strong><br />
pembezoni. Pia zinajulikana kama posho za kufan<strong>ya</strong><br />
kazi katika mazingira magumu, motisha hizo<br />
zinaweza kuwa posho za kiwango kimoja au<br />
ongezeko kwa asilimia <strong>ya</strong> mishahara.<br />
Motisha <strong>ya</strong> maeneo <strong>ya</strong> pembezoni ni njia makini <strong>ya</strong><br />
kubakiza walimu katika maeneo <strong>ya</strong> vijijini. Sasa hivi<br />
Tanzania inakabiliana changamoto <strong>ya</strong> walimu wengi<br />
wap<strong>ya</strong> wanaopangiwa maeneo <strong>ya</strong> pembezoni<br />
hawaripoti kazini, wanahamia shule za mijini, au<br />
wanaacha kazi ndani <strong>ya</strong> mwaka mmoja, mwenendo<br />
unaogharimu nchi shilingi milioni 511 kwa mwaka.
<strong>Muhtasari</strong> 10.3K<br />
Hii inasababisha upungufu wa walimu hasa katika<br />
maeneo <strong>ya</strong> vijijini. Ingawa lengo la taifa ni mwalimu<br />
mmoja kwa wanafunzi 40, utafiti wa Wizara wa hivi<br />
karibuni uligundua shule za vijijini kuwa na wastani<br />
wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 59 na shule moja<br />
kuwa na mwalimu mmoja kwa wanafunzi 283!<br />
Katika kushughulika tatizo hili, kila mwaka Wizara<br />
inapanga walimu wap<strong>ya</strong> wengi zaidi wa kwenda<br />
shule za vijijini kuliko shule za mijini. Mwaka 2008,<br />
ingawa Wizara ilipanga walimu wap<strong>ya</strong> tisa kati <strong>ya</strong><br />
kumi kwenda maeneo <strong>ya</strong> vijijini, mwisho wa mwaka,<br />
walimu wap<strong>ya</strong> wengi zaidi waliishia katika shule za<br />
mijini kuliko shule za vijijini. Kushughulikia tatizo la<br />
upungufu wa walimu wakati hali hii <strong>ya</strong> walimu<br />
kuacha kazi inaendelea ni kazi bure, ni sawa na<br />
kujaza maji kwenye ndoo inayovuja kwa kasi: maji<br />
mengi <strong>ya</strong>tapotezwa, kuna mashaka kama ndoo itajaa,<br />
na hata ikijaa kwa muda mfupi, itaanza kumwaga<br />
maji tena.<br />
Motisha za maeneo <strong>ya</strong> pembezoni, zinazosaidia<br />
kutatua tatizo hili, ni sehemu <strong>ya</strong> TDMS lakini<br />
hazijatekelezwa kutokana na upungufu wa bajeti.<br />
Hili siyo suala la upatikanaji wa fedha za umma,<br />
lakini ni la namna ambavyo fedha za umma<br />
zinatumika. Posho za kufan<strong>ya</strong> kazi katika mazingira<br />
magumu hazijatolewa kwa walimu wakati posho kwa<br />
maofisa wengi wa serikali kuu zinaongezeka sana<br />
mwaka hadi mwaka.<br />
Motisha za Maeneo<br />
Pembezoni<br />
KUTOTOLEWA kwa<br />
Walimu Kutokana na<br />
“Ukosefu wa Fedha”<br />
2009 Sh. bil 2<br />
2010 Sh. bil 2.2<br />
2011 Sh. bil 2.4<br />
Jumla <strong>ya</strong><br />
Posho za Serikali<br />
2009 Sh. bil 171<br />
2010 Sh. bil 216<br />
2011 Sh. bil 269<br />
Wakati serikali <strong>ya</strong> Tanzania imeshindwa kutoa hata<br />
asilimia moja <strong>ya</strong> posho zake zote kwa ajili <strong>ya</strong> walimu<br />
wanaofundisha vijijini kama motisha <strong>ya</strong> maeneo <strong>ya</strong><br />
pembezoni, nchi jirani zimefanikiwa kutekeleza<br />
motisha <strong>ya</strong> maeneo <strong>ya</strong> pembezoni. Kwa mfano,<br />
Uganda ilianzisha posho <strong>ya</strong> kufan<strong>ya</strong> kazi katika<br />
mazingira magumu kwa kuongeza asilimia 20 <strong>ya</strong><br />
mshahara mwaka 2001, na imeongezeka hadi kufika<br />
asilimia 30 mwaka huu. Serikali <strong>ya</strong> Tanzania<br />
itaendelea kubaki nyuma kwa muda gani?<br />
Kuwapandisha Daraja Walimu wenye<br />
Leseni na Wale wasio na Taaluma<br />
Kipengele kingine muhimu cha TDMS ni<br />
kuwapandisha daraja walimu wenye leseni wawe na<br />
digrii kwa sababu kutokuwa na sifa kwa walimu pia<br />
imekuwa na athari katika matokeo <strong>ya</strong> kujifunza.<br />
Ingawa serikali <strong>ya</strong> Tanzania imefaulu kwa kuongeza<br />
uandikishaji wa wanafunzi shuleni na kujenga shule<br />
za sekondari, kwa upande mwingine umesababisha<br />
upungufu wa rasilimali watu.<br />
Ili kukabiliana na upungufu huo, shule za sekondari,<br />
hasa shule za kata zilizojengwa hivi karibuni,<br />
zinalazimika kuwaajiri walimu wenye sifa za chini<br />
kabisa. Kwa mujibu wa utafiti wa Wizara, kwa<br />
wastani, nusu <strong>ya</strong> walimu wanaofunisha katika shule<br />
za sekondari za serikali wana diploma na nusu wana<br />
digrii. Lakini katika shule za sekondari za kata,<br />
takribani hakuna walimu wenye digrii, na walimu<br />
watatu kati <strong>ya</strong> kumi wana leseni tu au ni wahitimu<br />
wa Kidato cha VI walioajiriwa na jamii kama walimu<br />
wasio na taaluma. Kiwango duni cha elimu cha<br />
mwalimu alichofikia kinaathiri ubora wa elimu<br />
itolewayo kwa wanafunzi, na inakadiriwa kwamba<br />
shule zote zinalipa shilingi bilioni 59.8 kwa mwaka<br />
kwa walimu hawa wasio na sifa, ingawa michango<br />
<strong>ya</strong>o katika matokeo <strong>ya</strong> kujifunza ni ndogo sana.<br />
Kama juhudi za TDMS, kuwapandisha daraja walimu<br />
wasio na sifa wawe wataalamu wenye sifa kama<br />
inavyohitajika, zingefanikiwa zingegharimu shilingi<br />
bilioni 7.5 kwa mwaka 2011, lakini inaonekana<br />
kwamba Wizara haijapanga bajeti kutekeleza<br />
shughuli hii. Si lazima iwe hivyo; inaonekana<br />
kwamba kuna fedha nyingi sehemu nyingine.<br />
Kwa mfano, kuangalia elimu <strong>ya</strong> juu, wakati nchi<br />
nyingine za Afrika kama vile Ken<strong>ya</strong> zinatenga<br />
kiwango sahihi cha asilimia 20 (au moja kati <strong>ya</strong> kila<br />
shilingi tano) <strong>ya</strong> fedha zao za elimu kuenda kwa<br />
elimu <strong>ya</strong> juu, Tanzania imekuwa inaipa elimu <strong>ya</strong> juu<br />
wastani wa asilimia 26 <strong>ya</strong> fedha zote za elimu na<br />
kuongeza kipande chake mwaka 2011 kiwe asilimia<br />
36 (au moja kati <strong>ya</strong> kila shilingi tatu)!<br />
Licha <strong>ya</strong> kuchukua theluthi <strong>ya</strong> bajeti <strong>ya</strong> elimu, elimu<br />
<strong>ya</strong> juu inatumia asilimia 1.5 <strong>ya</strong> aina zote za<br />
wanafunzi wanaoandikishwa katika ngazi yoyote <strong>ya</strong><br />
elimu Tanzania. Kwa mfano, kulinganisha wanafunzi<br />
wa vyuo vikuu na shule za sekondari, kuna
<strong>Muhtasari</strong> 10.3K<br />
wanafunzi 118,911 wa vyuo vikuu wakati kuna<br />
1,388,347 (mara 12 <strong>ya</strong> idadi hiyo) walioandikishwa<br />
katika shule za sekondari za serikali.<br />
Bajeti kubwa na uandikishaji mdogo katika elimu <strong>ya</strong><br />
juu inamaanisha kwamba, hata ukiondoa mikopo <strong>ya</strong><br />
wanafunzi, bado Wizara inatumia fedha nyingi zaidi<br />
kwa kila mwanafunzi wa chuo kikuu kuliko<br />
mwanafunzi wa shule <strong>ya</strong> sekondari:<br />
<strong>ya</strong>nasaidia kushughulikia shida kubwa katika mfumo<br />
wa elimu Tanzania, <strong>ya</strong>ani, utoro wa walimu. Utafiti<br />
kutoka Wizarani unaonesha kwamba wastani wa<br />
zaidi <strong>ya</strong> asilimia 13 <strong>ya</strong> walimu wa shule za msingi na<br />
za sekondari hawako kazini kwa miezi au hata<br />
miaka :<br />
Idadi <strong>ya</strong> wanafunzi katika shule za sekondari za<br />
serikali ni mara 12 zaidi <strong>ya</strong> wale walio katika<br />
vyuo vikuu na vyuo vingine v<strong>ya</strong> serikali.<br />
Hata ukiondoa mikopo <strong>ya</strong> wanafunzi,<br />
serikali inatumia wastani wa fedha<br />
mara 19 zaidi kwa kila mwanafunzi wa<br />
chuo kikuu kuliko kwa kila mwanafunzi<br />
wa shule <strong>ya</strong> sekondari.<br />
Kati <strong>ya</strong> kila walimu 15 wanaolipwa kufundisha,<br />
wawili hawapatikani shuleni.<br />
Zaidi <strong>ya</strong> upotevu wa maarifa kwa watoto na viongozi<br />
wa baadaye wa Tanzania, utoro huu wa walimu<br />
unakadiriwa kusababisha hasara yenye jumla <strong>ya</strong><br />
shilingi bilioni 58.7 kwa mwaka.<br />
Ndiyo, nyenzo za elimu <strong>ya</strong> juu ni ghali sana na ni<br />
vigumu kutetea bajeti kupunguzwa katika sekta moja<br />
<strong>ya</strong> elimu kuleta maboresho katika nyingine; lakini, je,<br />
hakuna namna tofauti hii kubwa kati <strong>ya</strong> elimu <strong>ya</strong> juu<br />
na <strong>ya</strong> sekondari inaweza kutatuliwa? Pamoja na<br />
bajeti <strong>ya</strong> elimu <strong>ya</strong> juu kuongezeka kuwa shilingi<br />
bilioni 698 mwaka 2011, je, haiwezekani kwa hata<br />
asilimia moja <strong>ya</strong> hii kuenda kwenye kipengele cha<br />
TDMS kwa kuwapandisha daraja walimu ili<br />
kuboresha elimu <strong>ya</strong> sekondari? Pamoja na ongezeko<br />
la uandikishaji wa wanafunzi katika shule za<br />
sekondari, bajeti lazima irekebishwe kuhakikisha<br />
kwamba wananchi wengi wanapewa elimu bora, sio<br />
tabaka la wachache tu, ili kujenga taifa bora la<br />
baadaye.<br />
Kuhakikisha Fursa za Kujiendeleza<br />
Kitaaluma<br />
Pia TDMS ina hatua nyingi za kuhakikisha fursa za<br />
kujiendeleza kitaaluma kwa walimu, hasa mafunzo<br />
kazini. Umuhimu wa mafunzo <strong>ya</strong> walimu kazini si<br />
kufundisha walimu up<strong>ya</strong> ili kuwawezesha<br />
kuwafundisha wanafunzi wao bora zaidi bali pia<br />
Utafiti unapendekeza kwamba njia nzuri <strong>ya</strong><br />
kupambana na utoro wa walimu ni kutoa fursa za<br />
kujiendeleza kitaaluma kama vile mafunzo kazini<br />
ambayo <strong>ya</strong>tawafan<strong>ya</strong> walimu wapende kazi <strong>ya</strong>o.<br />
TDMS <strong>ya</strong> Tanzania ina lengo kuu la “kuhakikisha<br />
mafunzo <strong>ya</strong> kujiendeleza kazini <strong>ya</strong> mara kwa mara na<br />
ukuaji wa kitaaluma,” linalolenga ufufuo wa Vituo<br />
v<strong>ya</strong> Walimu (TRC), mahali ambapo walimu<br />
wanaweza kupata mafunzo <strong>ya</strong> ziada na rasilimali <strong>ya</strong><br />
kufundishia. Ingawa kuna vituo v<strong>ya</strong> TRC 600 nchini<br />
kote, vimetelekezwa kwa miaka mingi, vinatoa<br />
huduma chache, na havina rasilimali za kutosha.<br />
Ndiyo sehemu kubwa <strong>ya</strong> bajeti <strong>ya</strong> mafunzo kazini<br />
katika TDMS inaelekezwa kuimarisha TRC.<br />
Gharama za sehemu hii <strong>ya</strong> TDMS kwa mwaka<br />
2010/11 ni shilingi bilioni 22.9, lakini fedha hizi<br />
hazijatolewa kutokana na TDMS kutopewa<br />
kipaumbele cha juu. Vipaumbele hivi lazima<br />
vizingatiwe up<strong>ya</strong>. Ni usimamizi mba<strong>ya</strong> wa fedha<br />
kuruhusu utoro wa walimu unaogharimu nchi<br />
shilingi bilioni 58.7 kwa mwaka ingeweza<br />
kudhibitiwa na mkakati unaogharimu chini <strong>ya</strong> nusu<br />
<strong>ya</strong> kiasi hicho.
<strong>Muhtasari</strong> 10.3K<br />
Je, Tanzania Inaweza Kumudu<br />
Kutotekeleza TDMS?<br />
Mkakati wa Maendeleo na Menejimenti <strong>ya</strong> Ualimu<br />
(TDMS) una hatua ambazo, zikichukuliwa,<br />
zinaweza kuhakikisha elimu bora kwa watoto na<br />
vijana wa Tanzania itakayowezesha ukuaji<br />
endelevu kwa Tanzania na kwa siku za baadaye.<br />
<strong>Muhtasari</strong> huu umesistiza malengo matatu <strong>ya</strong><br />
TDMS <strong>ya</strong>nayoweza kuwezesha ukuaji huo, <strong>ya</strong>ani:<br />
1) K u w a p a m o t i s h a w a l i m u<br />
waliopangwa kufundisha shule za<br />
pembezoni.<br />
2) Kuwapandisha daraja walimu wa<br />
shule za sekondari wenye leseni na<br />
wale wasio na taaluma.<br />
3) Kuwahakikishia fursa za kuendelea<br />
kitaaluma kwa njia <strong>ya</strong> mafunzo <strong>ya</strong><br />
kujiendeleza kazini.<br />
Hata hivyo, hatua hizi bado hazijatekelezwa<br />
kikamilifu, na TDMS inabaki na fedha kidogo sana<br />
kama kipaumbele cha chini kwenye bajeti.<br />
Katika hali <strong>ya</strong> kusikitisha, kwa kushindwa<br />
kutekeleza mkakati huo taifa hulazimika kulipa<br />
hasara ambazo TDMS ingeweza kuzizuia. Wakati<br />
mwaka 2011 TDMS ingegharimu shilingi bilioni<br />
102, fedha nyingi zaidi huenda zikatumika kwa<br />
vipengele vinavyopunguza ubora wa elimu Tanzania:<br />
Gharama <strong>ya</strong> walimu wap<strong>ya</strong> wasioripoti vituoni<br />
au wanaotelekeza vituo v<strong>ya</strong>o v<strong>ya</strong> kazi: Sh. mil 511<br />
Gharama <strong>ya</strong> walimu wenye leseni na wale wasio na<br />
taaluma ambao hawana mchango mkubwa<br />
katika matokeo <strong>ya</strong> kujifunza: Sh. bil 59.8<br />
Gharama <strong>ya</strong> utoro wa walimu wa shule za msingi: Sh. bil 47<br />
Gharama <strong>ya</strong> utoro wa walimu wa shule za sekondari: Sh. bil 11.7<br />
Sh. bil 119<br />
Hapana shaka, gharama za kutotekeleza TDMS<br />
haziishii hapa. Hasara <strong>ya</strong> rasilimali za taifa<br />
inayotokea kila mwaka kwa wanafunzi wa shule za<br />
msingi na za sekondari wanaomaliza shule bila <strong>ya</strong><br />
kufundishwa vizuri na wenye uwezo mdogo<br />
usiowafaa wao wenyewe wala kulisaidia taifa lao<br />
haipimiki. Wakati huo huo, kutafuta rasilimali<br />
zinazotakiwa katika kutekeleza TDMS inaweza kuwa<br />
rahisi kuliko ilivyofikiriwa mwanzo, na kutekeleza<br />
TDMS inaweza kuwa na gharama nafuu zaidi kuliko<br />
kutoitekeleza.<br />
Hatuna budi kukumbusha kwa nukuu <strong>ya</strong> Darek Bok,<br />
msomi na mwanasheria, ambaye alikaririwa na<br />
Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika hotuba <strong>ya</strong>ke <strong>ya</strong><br />
mwaka 2008: “Kama unadhani elimu ni ghali basi<br />
jaribu ujinga.” Suala la TDMS linaonesha namna<br />
ilivyo ghali kufan<strong>ya</strong> jambo lisilo na busara. Swali<br />
linalobaki ni: Je, Tanzania itaendelea kulipia ujinga<br />
kwa muda gani ?<br />
Utoro wa Walimu<br />
wa Shule za Msingi<br />
Walimu<br />
wasio na<br />
Sifa<br />
Mkakati wa<br />
Maendeleo na<br />
Menejimenti <strong>ya</strong><br />
Ualimu (TDMS)<br />
Walimu Wap<strong>ya</strong><br />
Wanaoacha Kazi<br />
Utoro wa<br />
Walimu wa<br />
Shule za<br />
Sekondari<br />
<strong>HakiElimu</strong> inawezesha wananchi<br />
kuleta mabadaliko katika elimu<br />
na demokrasia.<br />
SLP 79401 ● Dar es Salaam ● Tanzania<br />
Simu (255 22) 2151852/3 ● Faksi (255 22) 2152449<br />
info@hakielimu.org ● www.hakielimu.org