19.02.2015 Views

Haki Elimu Report ya PETS swa mail.pdf

Haki Elimu Report ya PETS swa mail.pdf

Haki Elimu Report ya PETS swa mail.pdf

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Je, kuna uwajibikaji sahihi<br />

katika utekelezaji wa MMEM II?<br />

Ripoti <strong>ya</strong> Ufuatiliaji wa Matumizi <strong>ya</strong> Fedha za Umma<br />

(<strong>PETS</strong>)<br />

Februari 2011


Je, kuna uwajibikaji sahihi katika<br />

utekelezaji wa MMEM II?<br />

Ripoti <strong>ya</strong> Ufuatiliaji wa Matumizi <strong>ya</strong> Fedha za Umma<br />

(<strong>PETS</strong>)<br />

Februari 2011<br />

i


Shukrani<br />

Uandaaji wa ufuatiliaji huu, uchambuzi wa takwimu na uandishi wa ripoti hii ulifanywa na Godfrey<br />

Boniventura. Shukrani za pekee ziwaendee Tony Baker ambaye alishiriki katika uandaaji wa dhana za<br />

ufuatiliaji na ukusan<strong>ya</strong>ji wa taarifa.<br />

Uhariri, mrejesho na ushauri ulitolewa na Elizabeth Missokia, Mtemi Zombwe, Fausta Musokwa,<br />

Charles Mtoi, Pius Makomelelo na Robert Mihayo. Pia Tunapenda kuwashukuru David Kagondi, Pius<br />

Makomelelo, Benedicta Mrema, Maisory Chacha ambao walishiriki kukusan<strong>ya</strong> taarifa za ufuatiliaji<br />

huu.<br />

Shukrani nyingi kwa wakurugenzi watendaji na maafisa elimu wa wila<strong>ya</strong> za Bunda, Morogoro, Nzega,<br />

Iramba, Babati na Njombe kwa ushirikiano wao mzuri ambao uliwezesha utafiti huu kufanyika kwa<br />

urahisi. Pia tunawashukuru marafiki wa elimu waliosaidiana na wafan<strong>ya</strong>kazi wa <strong>Haki</strong>elimu kukusan<strong>ya</strong><br />

taarifa ambao ni Peter Kololly, Asia Mtibua, Richard Lucas, Salumu Ally, Bernard Clement, Mary<br />

Talas, Wenseslaus B<strong>ya</strong>bato, Hamis Rashid na Juma Kalwani.<br />

©<strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong>, 2011 ISBN 978-9987-18-00907<br />

<strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong>, SLP 79401, Dar es Salaam<br />

Simu: (255 22) 2151852/3, Faksi: (255 22) 2152449<br />

Barua pepe: info@hakielimu.org<br />

Tovuti: www.hakielimu.org<br />

Sehemu yoyote <strong>ya</strong> kitabu hiki inaweza kutolewa kwa namna yoyote kwa madhumuni <strong>ya</strong> kielimu na<br />

siyo <strong>ya</strong> kibiashara, kwa kuzingatia kuwa chanzo kitatajwa na nakala mbili zitapelekwa <strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong>.<br />

ii


Yaliyomo<br />

Vifupisho<br />

1.0 Utangulizi………………………………………………………………………………………1<br />

1.1 Usuli……………………………………………………………………………….…1<br />

1.2 Malengo <strong>ya</strong> Ufuatiliaji ...............................……………...............................................2<br />

2.0 Mbinu za Ufuatiliaji ...............................………..........................................................3<br />

2.1 Maeneo <strong>ya</strong> Ufuatiliaji ...............................……………...............................................3<br />

2.2 Wadau Waliohusishwa Katika Ukusan<strong>ya</strong>ji wa Taarifa .......................................................3<br />

2.2.1 Afisa <strong>Elimu</strong> ...............................……………............................................... 3<br />

2.2.2 Walimu Wakuu ....................................…………….....................................4<br />

2.2.3 Wazazi ....................................……………...................................................4<br />

3.0 Matokeo ....................................…………….........................................................................5<br />

3.1 Ruzuku <strong>ya</strong> Mwanafunzi Ngazi <strong>ya</strong> Wila<strong>ya</strong> ............................................................5<br />

3.1.1 Ruzuku inayofika Wila<strong>ya</strong>ni ............................................................................5<br />

3.1.2 Ruzuku na idadi <strong>ya</strong> Wanafunzi......................................................................6<br />

3.1.3 Matumizi Maba<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Ruzuku Ngazi <strong>ya</strong> Wila<strong>ya</strong> ...............................................7<br />

3.2 Ruzuku <strong>ya</strong> Mwanafunzi Ngazi <strong>ya</strong> Shule<br />

3.2.1 Ruzuku Inayofika Shuleni ....................................…………….....................8<br />

3.2.2 Uelewa wa Walimu Wakuu Kuhusu Ruzuku <strong>ya</strong> Mwanafunzi ..........................9<br />

3.2.3 Muda wa Ruzuku Kufika Shuleni ........................................................……10<br />

3.2.4 Hali <strong>ya</strong> Matumizi <strong>ya</strong> Ruzuku Shuleni .......................................................10<br />

3.3 Fedha za Maendeleo ....................................................................................……12<br />

3.3.1 Hali <strong>ya</strong> Ujenzi wa Miundo Mbinu ..............................................................12<br />

3.3.2 Matumizi Maba<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Fedha za Maendeleo .................................................13<br />

3.4 Michango <strong>ya</strong> Wazazi ..............................................................................................16<br />

3.4.1 Mwamko wa Wazazi Kuchangia <strong>Elimu</strong> ......................................................16<br />

4.0 Ulinganishi wa MMEM I na MMEM II ...........................................................................17<br />

5.0 Hitimisho na Mapendekezo ...............................................................................................18<br />

5.1 Hitimisho ..................................................................................................................18<br />

5.2 Mapendekezo ..........................................................................................................19<br />

Marejeo ........................................................................................................................................ 21<br />

Viambatisho .................................................................................................................................22<br />

iii


Vifupisho<br />

BEST<br />

GBS<br />

MMEM I<br />

MMEM II<br />

<strong>PETS</strong><br />

REPOA<br />

URT<br />

Basic Education Statistics of Tanzania<br />

General Budget Support<br />

Mpango wa Kwanza wa Maendeleo <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> Msingi<br />

Mpango wa Pili wa Maendeleo <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> Msingi<br />

Public Expenditure Tracking Survey<br />

Research on Poverty Alleviation<br />

United Republic of Tanzania<br />

iv


1.0 UTANGULIZI<br />

1.1 Usuli<br />

Baada <strong>ya</strong> kufanikiwa kuongeza udahili wa wanafunzi kwa shule za msingi toka 88% mwaka 2001 hadi<br />

96% mwaka 2006 kupitia Mpango wa kwanza wa Maendeleo <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> Msingi (MMEM I), Serikali<br />

iliandaa Mpango wa pili wa Maendeleo <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> Msingi (MMEM II) ambapo utekelezaji wake<br />

ulianza mwaka wa fedha 2007/2008 1 . Moja <strong>ya</strong> malengo makuu <strong>ya</strong> MMEM II ilikuwa ni kuboresha<br />

hali <strong>ya</strong> mazingira <strong>ya</strong> kujifunzia kwa kujenga miundombinu kama vile madarasa, nyumba za walimu,<br />

vyoo na madawati. Kiambatisho namba 2 kinaonesha miundombinu ambayo ilibainishwa kujengwa au<br />

kununuliwa katika muda wote wa utekelezaji wa MMEM II. Pia ilidhamiria kuboresha mchakato wa<br />

kujifunza na kufundisha kwa kuongeza vifaa kama vile vitabu v<strong>ya</strong> kiada na ziada kwa ajili <strong>ya</strong> wanafunzi.<br />

Ili kutekeleza adhma hii, MMEM II, ilibainisha kuwa Sh. 10,000 itatolewa kwa kila mwanafunzi wa<br />

shule <strong>ya</strong> msingi kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II. Ruzuku <strong>ya</strong><br />

mwanafunzi inalenga kuboresha mazingira <strong>ya</strong> kujifunzia na kufundishia kwa kuboresha upatikanaji<br />

wa vitabu v<strong>ya</strong> kianda(Asilimia 40), ukarabati mdogo wa miundo mbinu iliyopo shuleni(Asilimia<br />

20), kuboresha upatikanaji wa madaftari, kalamu,penseli, chaki na vifaa vingine v<strong>ya</strong> kufundishia<br />

walimu(Asilimia 20), uwezo wa kuendesha mazoezi na mitihani mbalimbali(Asilimia 10) na uendeshaji<br />

wa shule (Asilimia 10).<br />

Ikiwa miaka mitatu <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II imepita, na huku bajeti <strong>ya</strong> sekta <strong>ya</strong> elimu ikiongezeka<br />

mwaka hadi mwaka, hali halisi <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II bado ina changamoto nyingi. Ndani <strong>ya</strong><br />

miaka mitatu <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II, nyumba za walimu 986 2 tu zimejengwa kati <strong>ya</strong> nyumba<br />

65,808 zilizopangwa kujengwa kati <strong>ya</strong> mwaka 2007 na 2009. Vyombo v<strong>ya</strong> habari hasa magazeti<br />

vimekuwa vikiripoti kuhusu idadi <strong>ya</strong> wanafunzi wengi kukaa chini katika shule mbalimbali hapa<br />

nchini (Picha 1). Uwiano wa mwanafunzi kwa kitabu ni 1:5 3 tofauti na lengo la kuwa na uwiano wa<br />

1:1 kwa mwaka 2010. Tatizo hili limekuwa likiathiri mazingira <strong>ya</strong> kufundishia na kujifunzia kwani<br />

wanafunzi watano wanasoma kitabu kimoja. Changamoto hizi zote zinaibua ma<strong>swa</strong>li! Kama bajeti<br />

<strong>ya</strong> sekta <strong>ya</strong> elimu inaongezeka mwaka hadi mwaka 4 na utekelezaji wa MMEM II si wa kuridhisha,<br />

fedha hizi zinatumikaje? Je, fedha zinazopangwa katika bajeti zinawafikia walengwa? Na mipango yote<br />

inatekelezwa kama inavyopa<strong>swa</strong>? Majibu <strong>ya</strong> ma<strong>swa</strong>li ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>nahitaji ufuatiliaji wa bajeti hasa fedha<br />

zinazotengwa na kutolewa kwa ajili <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II.<br />

MMEM II unabainisha pia umuhimu wa jamii kuchangia michango mbalimbali ili kufanikisha<br />

utekelezaji wa mpango huu na hatimaye kuleta maendeleo <strong>ya</strong> shule za msingi. Jamii inapa<strong>swa</strong> kuchangia<br />

asilimia 20 <strong>ya</strong> gharama za utekelezaji wa MMEM II 5 , na hii inamaanisha kuwa elimu haitolewi bure<br />

kama inavyoelekezwa katika MMEM II. Kutokana na agizo hilo, wazazi wamekuwa wakiombwa na<br />

1<br />

URT (2009), Ripoti <strong>ya</strong> utekelezaji wa Mpango wa pili wa Maendeleo <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> Msingi (MMEM II)<br />

2<br />

URT (2009), Ripoti <strong>ya</strong> utekelezaji wa Mpango wa pili wa Maendeleo <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> Msingi(MMEM II) na URT (2010), Ripoti <strong>ya</strong><br />

utekelezaji wa sekta <strong>ya</strong> elimu kwa mwaka 2009<br />

3<br />

URT (2010), Ripoti <strong>ya</strong> utekelezaji wa sekta <strong>ya</strong> elimu kwa mwaka 2009<br />

4<br />

Hotuba za bajeti za Tanzania tangu mwaka 2007 hadi 2010.<br />

5<br />

Ukurasa wa 38 katika MMEM II umebainisha kuwa michango <strong>ya</strong> jamii kwa ajili <strong>ya</strong> utekelezaji wa miundo mbinu ni asilimia 20<br />

6<br />

Ripoti <strong>ya</strong> utafiti <strong>ya</strong> <strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> mwaka 2010, Je, jamii inawezaje kuboresha elimu <strong>ya</strong> watoto wao?<br />

1


wakati mwingine kushinikizwa 6 kutoa michango mbalimbali kama vile, michango <strong>ya</strong> mitihani na<br />

mahitaji mengine <strong>ya</strong> shule. Ripoti <strong>ya</strong> ufuatiliaji wa matumizi <strong>ya</strong> fedha za umma <strong>ya</strong> Wizara <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong><br />

na Mafunzo <strong>ya</strong> Ufundi <strong>ya</strong> mwaka 2009, imebainisha kutolewa kwa michango hiyo na wazazi. Mwaka<br />

wa fedha 2007/2008, jumla <strong>ya</strong> fedha za michango <strong>ya</strong> wazazi zilizokusanywa na walimu wakuu ilikuwa<br />

asilimia 7.7 <strong>ya</strong> fedha iliyotumika kwenye shule 7 . Moja <strong>ya</strong> mapungufu <strong>ya</strong> ripoti hii ni kwamba ilitumia<br />

takwimu za walimu wakuu pekee na haikuhoji wazazi ili kufahamu kiwango wanachotoa kwa mwaka<br />

na kama wanatoa michango je, kuna matumizi sahihi <strong>ya</strong> fedha hizo? Hitaji la majibu <strong>ya</strong> ma<strong>swa</strong>li ha<strong>ya</strong><br />

<strong>ya</strong> ufuatiliaji wa fedha za utekelezaji wa MMEM II ndio lililotoa msukumo kwa Shirika la <strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong>,<br />

kufan<strong>ya</strong> ufuatiliaji wa fedha za umma toka serikalini hadi shuleni ukihusisha utekelezaji wa MMEM II<br />

kwa kipindi cha miaka mitatu 8 .<br />

Picha 1: Makala za vyombo v<strong>ya</strong> habari kuhusu matatizo <strong>ya</strong> elimu hapa nchini.<br />

1.2 Malengo <strong>ya</strong> Ufuatiliaji<br />

1. Kufahamu kiasi cha fedha za ruzuku <strong>ya</strong> mwanafunzi na fedha za maendeleo zinazofika shuleni.<br />

2. Kufahamu hali <strong>ya</strong> matumizi <strong>ya</strong> fedha za ruzuku na maendeleo, na kubaini mafanikio na<br />

mapungufu <strong>ya</strong>ke.<br />

3. Kubainisha kiasi cha fedha wanachochanga wazazi.<br />

4. Kulinganisha hali <strong>ya</strong> uwajibikaji wa serikali kati <strong>ya</strong> MMEM I na MMEM II.<br />

7<br />

Fedha hii haihusishi fedha za mishahara <strong>ya</strong> walimu<br />

8<br />

Kuanzia mwaka wa fedha 2007/2008 hadi 2009/2010<br />

2


2.0 MBINU ZA UFUATILIAJI<br />

Kabla <strong>ya</strong> kuanza ufuatiliaji, shirika la <strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong> lilituma barua kwa Wakurugenzi wa wila<strong>ya</strong><br />

zilizochaguliwa kuomba kupatiwa kibali cha kufan<strong>ya</strong> ufuatiliaji na baada <strong>ya</strong> kupata ruhusa, wafan<strong>ya</strong>kazi<br />

wa shirika la <strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong> walifika katika ofisi <strong>ya</strong> Mkurugenzi wa wila<strong>ya</strong> husika, kujitambulisha<br />

na kuonana na Afisa <strong>Elimu</strong> kwa ajili <strong>ya</strong> mahojiano. Katika kila wila<strong>ya</strong>, Afisa Takwimu wa elimu<br />

alishirikiana na watafiti wasaidizi wakati wa kufan<strong>ya</strong> mahojiano na wakuu wa shule na pia kuhakiki<br />

takwimu zinazotolewa na walimu wakuu. Kwa kuwa ufuatiliaji huu ulidhamiria kufahamu hali <strong>ya</strong><br />

matumizi <strong>ya</strong> fedha katika utekelezaji wa MMEM II, miaka mitatu <strong>ya</strong> fedha kuanzia 2007/2008 hadi<br />

2009/2010 ilihusishwa kwa kuzingatia kuwa mwaka wa fedha 2007/2008 ndio ulikuwa mwaka wa<br />

kwanza wa utekelezaji wa MMEM II. Pia ukusan<strong>ya</strong>ji wa taarifa ulifanyika mwezi Oktoba 2010 katika<br />

mwaka wa fedha 2010/2011 ambapo ta<strong>ya</strong>ri mwaka wa fedha 2009/2010 ulikuwa umemalizika tangu<br />

mwezi Juni 2010.<br />

2.1 Maeneo <strong>ya</strong> Ufuatiliaji<br />

Ufuatiliaji wa fedha za umma ulihusisha wila<strong>ya</strong> sita toka mikoa sita ambayo ilichaguliwa kwa kutumia<br />

uchaguzi nasibu toka kanda <strong>ya</strong> Ziwa (Mara), Magharibi (Tabora), Mashariki (Morogoro), N<strong>ya</strong>nda za<br />

juu kusini (Njoluma), Kati (Singida) na Kaskazini (Man<strong>ya</strong>ra). Baada <strong>ya</strong> kuchagua mikoa, uchaguzi<br />

nasibu ulitumika kupata wila<strong>ya</strong> moja toka kila mkoa, wila<strong>ya</strong> hizo ni Manispaa <strong>ya</strong> Morogoro, Nzega,<br />

Iramba, Bunda, Njombe na Babati (Kiambatisho namba 1). Jumla <strong>ya</strong> shule 24 zilihusishwa katika<br />

ufuatiliaji huu, ambapo shule nne zilichaguliwa toka kila wila<strong>ya</strong> kwa kutumia uchaguzi nasibu. Katika<br />

shule nne za kila wila<strong>ya</strong>, shule mbili zilikuwa za mjini na shule mbili za vijijini. Kabla <strong>ya</strong> kuchagua<br />

shule, Mtafiti Msaidizi aliomba kupatiwa orodha <strong>ya</strong> shule za mjini na vijijini toka kwa Afisa <strong>Elimu</strong> na<br />

ndipo shule mbili zilichaguliwa toka kila kundi.<br />

2.2 Wadau Waliohusishwa katika Ukusan<strong>ya</strong>ji wa Taarifa<br />

2.2.1 Afisa <strong>Elimu</strong><br />

Afisa <strong>Elimu</strong> wa shule za msingi ni msimamizi mkuu wa michakato na mikakati yote <strong>ya</strong> utoaji elimu <strong>ya</strong><br />

msingi katika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong>. Na pia ndiye anayepokea fedha toka kwa Mtunza Hazina wa wila<strong>ya</strong> na<br />

kuzipeleka shuleni. Katika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong>, Afisa <strong>Elimu</strong> wa wila<strong>ya</strong> wa shule za msingi na Afisa Takwimu<br />

wa shule za msingi walihojiwa ili kuelezea kiasi cha fedha za ruzuku na maendeleo walizopokea<br />

toka hazina katika kipindi cha mwaka 2007/2008 hadi 2009/2010; na pia kueleza kiasi cha fedha<br />

kilichopelekwa kwenye shule nne zilizochaguliwa kwa ufuatiliaji katika wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>ke. Pia Afisa <strong>Elimu</strong><br />

alipatiwa dodoso ili kujaza takwimu mbalimbali za idadi <strong>ya</strong> shule, idadi <strong>ya</strong> wanafunzi na pia kutoa<br />

maoni kuhusu fedha za ruzuku na fedha za maendeleo kwa shule za msingi.<br />

3


2.2.2 Walimu Wakuu<br />

Walimu wakuu ni wataalamu waendeshaji wa shule ambao ndio wanapokea fedha toka kwa Afisa <strong>Elimu</strong><br />

wa shule za msingi na kuzitumia kutekeleza mipango mbalimbali <strong>ya</strong> shule. Walimu wakuu walihojiwa<br />

ili kueleza kiasi cha fedha za ruzuku na fedha za maendeleo walichopata katika miaka mitatu <strong>ya</strong> fedha<br />

(2007/2008 hadi 2009/2010), na jinsi walivyozitumia. Pia walihojiwa kiasi cha michango <strong>ya</strong> wazazi<br />

walichokusan<strong>ya</strong> katika mwaka wa fedha 2009/2010 9 ili kuweza kubaini kiasi cha fedha wanachochanga<br />

wazazi na jinsi zilivyotumika katika mwaka husika. Ili kuboresha ufuatiliaji huu, kila Mwalimu Mkuu<br />

alitakiwa kugonga mhuri wa shule juu <strong>ya</strong> dodoso mara baada <strong>ya</strong> kumaliza kujaza takwimu mbalimbali<br />

zilizohitajika.<br />

2.2.3 Wazazi<br />

Wazazi walihojiwa ili kujua kiasi wanachochanga kwa mwaka, na pia kuelezea jinsi fedha zinavyotumika<br />

kama ni sahihi au si sahihi, na jinsi wanavyoshirikishwa katika taarifa za mapato na matumizi <strong>ya</strong><br />

shule. Pia waliulizwa kutoa maoni kuhusu fedha za ruzuku <strong>ya</strong> mwanafunzi na maendeleo na kama<br />

wanapatiwa risiti mara wanapotoa michango <strong>ya</strong>o. Wazazi kumi walihojiwa katika kila shule, na hivyo<br />

kufan<strong>ya</strong> jumla <strong>ya</strong> wazazi waliohojiwa kuwa 240. Kigezo kikubwa kilichotumika kuchagua wazazi ni<br />

kwamba mzazi alipa<strong>swa</strong> kuwa na mtoto anayesoma katika shule iliyochaguliwa kwa ufuatiliaji. Ili<br />

kuwapata wazazi, wanafunzi wawili kwa kila darasa kuanzia darasa la tatu hadi la saba walichaguliwa<br />

kwa kutumia uchaguzi nasibu, na hao wanafunzi 10 ndio walitakiwa kwenda kuwaita wazazi wao kwa<br />

ajili <strong>ya</strong> mahojiano.<br />

9<br />

Wakati wa majaribio <strong>ya</strong> dhana za ufuatiliaji wazazi wengi walionekana kutokuwa na kumbukumbu za michango <strong>ya</strong><br />

miaka <strong>ya</strong> nyuma, hivyo ufuatiliaji ulitumia mwaka 2009/2010 ili kuepuka tatizo la wazazi kutokumbuka michago <strong>ya</strong>o<br />

<strong>ya</strong> miaka <strong>ya</strong> nyuma.<br />

4


3.0 MATOKEO YA UFUATILIAJI<br />

3.1 RUZUKU YA MWANAFUNZI NGAZI YA WILAYA<br />

3.1.1 Ruzuku Inayofika Wila<strong>ya</strong>ni<br />

Jumla <strong>ya</strong> fedha <strong>ya</strong> ruzuku iliyopokelewa katika wila<strong>ya</strong> sita ni Sh. bilioni 2.1 kwa mwaka wa fedha<br />

2007/2008, Sh. bilioni 2.6 kwa mwaka 2008/2009 na Sh. bilioni 1.9 kwa mwaka 2009/2010. Kwa<br />

kuwa jumla <strong>ya</strong> wanafunzi katika wila<strong>ya</strong> hizi sita ni 442,334, na 447,614 na 440,541 katika miaka<br />

<strong>ya</strong> 2008, 2009 na 2010, wila<strong>ya</strong> hizi zingepa<strong>swa</strong> kupokea takribani Sh. bilioni 4.4, Sh. bilioni 4.5<br />

na Sh. bilioni 4.4 katika miaka mitatu iliyopita kwa mujibu wa MMEM II. Ukilinganisha fedha<br />

halisi zilizofika kwa miaka mitatu na idadi <strong>ya</strong> wanafunzi unapata picha kuwa fedha halisi za ruzuku<br />

zilizofika katika wila<strong>ya</strong> sita ilikuwa Sh 4,909(mwaka 2007/2008,) Sh 5,811(mwaka 2008/2009) na Sh.<br />

4,297(mwaka 2009/2010). Na wastani kwa miaka mitatu ilikuwa Sh 5,005 badala <strong>ya</strong> Sh. 10,000 kama<br />

ilivyoainishwa katika MMEM II.<br />

Jedwali 1: Tofauti kati <strong>ya</strong> ruzuku halisi iliyofika wila<strong>ya</strong>ni na iliyopa<strong>swa</strong> kufika wila<strong>ya</strong>ni kwa mujibu<br />

wa MMEM II<br />

Mwaka<br />

2007/08<br />

2008/09<br />

2009/10<br />

Idadi <strong>ya</strong><br />

wanafunzi<br />

442,334<br />

447,614<br />

440,541<br />

Chanzo: Takwimu za ufuatiliaji<br />

Ruzuku iliyofika<br />

wila<strong>ya</strong>ni<br />

2.2 bilioni<br />

2.6 bilioni<br />

1.9 bilioni<br />

Ruzuku iliyopa<strong>swa</strong><br />

kufika wila<strong>ya</strong>ni<br />

4.4 bilioni<br />

4.5 bilioni<br />

4.4 bilioni<br />

Upungufu<br />

2.2 bilioni<br />

1.9 bilioni<br />

2.5 bilioni<br />

Asilimia<br />

pungufu<br />

50%<br />

42%<br />

57%<br />

Chati 1:<br />

Tofauti kati <strong>ya</strong> ruzuku halisi iliyofika wila<strong>ya</strong>ni na iliyopa<strong>swa</strong> kufika wila<strong>ya</strong>ni kwa mujibu<br />

wa MMEM II.<br />

Ruzuku<br />

(Sh. bilioni)<br />

5<br />

4.5<br />

4<br />

3.5<br />

3<br />

2.5<br />

2<br />

1.5<br />

1<br />

0.5<br />

0<br />

4.4 4.5 4.4<br />

2.6<br />

2.2<br />

1.9<br />

2007/08 2008/09 2009/10<br />

Ruzuku iliyopa<strong>swa</strong> kufika wila<strong>ya</strong>ni<br />

Ruzuku iliyofika wila<strong>ya</strong>ni<br />

Chanzo:Takwimu za ufuatiliaji<br />

5


Chati 2:<br />

Mwenendo wa ruzuku kwa kila mwanafunzi iliyofika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> kwa miaka<br />

mitatu(2007/08-2009/10)<br />

3.1.2 Ruzuku na Idadi <strong>ya</strong> Wanafunzi<br />

MMEM II umeainisha kuwa fedha za ruzuku zinapa<strong>swa</strong> kutolewa kulingana na idadi <strong>ya</strong> wanafunzi<br />

waliopo wila<strong>ya</strong>ni katika mwaka husika. Taarifa za wila<strong>ya</strong> sita zinaonesha kuwa upelekaji wa ruzuku<br />

wila<strong>ya</strong>ni toka serikali kuu hauzingatii idadi <strong>ya</strong> wanafunzi. Wila<strong>ya</strong> nyingine zilipokea fedha nyingi zaidi<br />

ilihali zina wanafunzi wachache, wakati wila<strong>ya</strong> nyingine zilipata fedha kidogo na zina wanafunzi wengi.<br />

Jedwali namba 2 linaonesha kuwa katika mwaka wa fedha 2009/2010, wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Nzega iliyokuwa na<br />

wanafunzi 90,529 ambao ni wengi zaidi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> nyingine, ilipata Sh. milioni 316.8 na hivyo wastani<br />

wa ruzuku kwa mwanafunzi ilikuwa Sh. 3,307 ilihali wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Bunda yenye wanafunzi 81,283 ilipata<br />

Sh. milioni 503.8 ambapo wastani wa ruzuku ni Sh. 6,199. Ugawaji wa fedha za ruzuku bila kuzingatia<br />

idadi <strong>ya</strong> wanafunzi, umefan<strong>ya</strong> kuwe na tofauti kubwa <strong>ya</strong> kiwango cha ruzuku kwa mwanafunzi<br />

zinazofika wila<strong>ya</strong>ni kati <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> na wila<strong>ya</strong>. Utafiti huu unaonesha kuwa, kiwango cha chini ni Sh.<br />

1,705 kwa wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Njombe na kiwango cha juu ni Sh. 6,199 kwa wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Bunda (Jedwali namba 2).<br />

Jedwali 2: Ulinganifu kati <strong>ya</strong> fedha zilizofika wila<strong>ya</strong>ni na idadi <strong>ya</strong> wanafunzi<br />

Wila<strong>ya</strong><br />

Bunda<br />

Iramba<br />

Babati<br />

Nzega<br />

Morogoro<br />

Njombe<br />

Jumla <strong>ya</strong> Fedha za ruzuku<br />

zilizofika wila<strong>ya</strong>ni (Sh)<br />

503,830,500<br />

514,263,750<br />

303,770,000<br />

316,827,000<br />

112,825,824<br />

130,553,600<br />

2009/2010<br />

Idadi <strong>ya</strong><br />

wanafunzi<br />

81,283<br />

85,406<br />

61,254<br />

90,529<br />

45,703<br />

76,366<br />

Ruzuku kwa kila<br />

mwanafunzi (Sh)<br />

6,199<br />

6,021<br />

4,959<br />

3,500<br />

2,469<br />

1,705<br />

6


Chati 3:<br />

Ulinganifu wa ruzuku <strong>ya</strong> mwanafunzi iliyofika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> kwa mwaka wa fedha<br />

2009/2010<br />

Ruzuku(Sh)<br />

7,000<br />

6,000<br />

5,000<br />

4,000<br />

3,000<br />

2,000<br />

1,000<br />

0<br />

6,199 6,021<br />

4,959<br />

2.6<br />

1.9<br />

3,500<br />

2,469<br />

1,705<br />

Bunda Iramba Babati Nzega Morogoro Njombe<br />

Ruzuku kwa kila mwanafunzi<br />

3.1.3 Matumizi Maba<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Ruzuku Ngazi <strong>ya</strong> Wila<strong>ya</strong><br />

Katika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> kulikuwa na matumizi maba<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> ruzuku kwa miaka miwili <strong>ya</strong> fedha iliyopita.<br />

Matumizi ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>nabainishwa kwa kulinganisha wastani wa ruzuku iliyopokelewa ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> na<br />

wastani wa ruzuku iliyofika shuleni. Katika mwaka wa fedha 2008/2009 tofauti ilikuwa Sh. milioni<br />

208.1 ambayo ni asilimia 8 kati <strong>ya</strong> fedha iliyofika shuleni na iliyoripotiwa kupelekwa shuleni toka<br />

wila<strong>ya</strong>ni (Kisanduku namba 1). Katika mwaka wa fedha 2009/2010 tofauti ilikuwa Sh. milioni<br />

293.4 ambayo ni asilimia 16 kati <strong>ya</strong> fedha iliyofika shuleni na iliyoripotiwa kupelekwa shuleni toka<br />

wila<strong>ya</strong>ni(Kisanduku namba 1). Hii inamaanisha kuwa fedha za ruzuku hazifika kwa walengwa ambao<br />

ni wanafunzi ambao ndio wanahitaji fedha hizi kwa ajili <strong>ya</strong> kuboresha mazingira <strong>ya</strong> kujifunzia na<br />

kufundishia.<br />

Kisanduku 1. Ukokotoaji wa tofauti kati <strong>ya</strong> fedha zilizofika shuleni na fedha zilizoripotiwa<br />

kupelekwa shuleni toka wila<strong>ya</strong>ni.<br />

• Kwa mwaka wa fedha 2008/2009, taarifa za wila<strong>ya</strong> sita zinaonesha kuwa, wastani wa ruzuku iliyofika<br />

wila<strong>ya</strong>ni toka hazina kuu ni Sh. 5,811 kwa kila mwanafunzi na taarifa za wakuu wa shule 24 zinaonesha<br />

kuwa wastani wa fedha za ruzuku zilizofika shuleni ni Sh. 5,346. Hivyo Sh. 465 kwa kila mwanafunzi<br />

zilikomea ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> ambapo hazikwenda mashuleni. Tukizidisha Sh. 465 na idadi <strong>ya</strong> wanafunzi<br />

wa wila<strong>ya</strong> sita ambao ni 447,614 kwa mwaka 2009 tunapata tofauti <strong>ya</strong> Sh. milioni 208.1 ambayo ni<br />

asilimia 8 kati <strong>ya</strong> fedha iliyofika shuleni na iliyoripotiwa kupelekwa shuleni toka wila<strong>ya</strong>ni. Utofauti huu<br />

ungekuwa wastani kwa wila<strong>ya</strong> zote 133 za Tanzania, ungekuwa sawa na Sh bilioni 4.6<br />

• Katika mwaka wa fedha 2009/2010, wastani wa ruzuku iliyofika wila<strong>ya</strong>ni toka hazina kuu ni Sh.<br />

4,297 kwa kila mwanafunzi na taarifa za wakuu wa shule 24 zinaonesha kuwa wastani wa fedha za<br />

ruzuku zilizofika shuleni ni Sh. 3,631. Hivyo Sh. 666 kwa kila mwanafunzi zilikomea ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong><br />

ambapo hazikwenda mashuleni. Tukizidisha Sh. 666 na idadi <strong>ya</strong> wanafunzi wa wila<strong>ya</strong> sita ambao ni<br />

440,541 kwa mwaka 2010 tunapata tofauti <strong>ya</strong> Sh. milioni 293.4 ambayo ni asilimia 16 kati <strong>ya</strong> fedha<br />

iliyofika shuleni na iliyoripotiwa kupelekwa shuleni toka wila<strong>ya</strong>ni. Utofauti huu ungekuwa wastani kwa<br />

wila<strong>ya</strong> zote 133 za Tanzania, ungekuwa sawa na Sh bilioni 6.5.<br />

7


Jedwali 3: Hali <strong>ya</strong> matumizi <strong>ya</strong> ruzuku kwa mwanafunzi ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong>(2008/09-2009/2010)<br />

Mwaka Ruzuku iliyofika Ruzuku iliyofika<br />

wila<strong>ya</strong>ni(A) shuleni(B)<br />

2008/09<br />

2009/10<br />

5,811<br />

4,297<br />

Chanzo: Takwinu za uchunguzi<br />

5,346<br />

3,631<br />

Ruzuku ambayo<br />

haikufika<br />

shuleni(C)<br />

C=A-B<br />

465<br />

666<br />

Idadi <strong>ya</strong><br />

wanafunzi<br />

katika wila<strong>ya</strong> 6<br />

(D)<br />

447,614<br />

440,541<br />

Jumla <strong>ya</strong><br />

Ufujaji ngazi<br />

<strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong>(E)<br />

E=C x D<br />

208.1 milioni<br />

293.4 milioni<br />

3.2 RUZUKU YA MWANAFUNZI NGAZI YA SHULE<br />

3.2.1 Ruzuku Inayofika Shuleni<br />

Katika shule 24 zilizofanyiwa ufuatiliaji wa ruzuku, wastani wa kiwango cha ruzuku kilichofika shuleni<br />

kwa miaka mitatu iliyopita kuanzia mwaka wa fedha 2007/2008 hadi 2009/2010 ni Sh. 4899 kwa<br />

mwaka 2007/2008, Sh. 5,346 kwa mwaka 2008/2009 na Sh. 3,631 kwa mwaka 2009/2010 kwa kila<br />

mwanafunzi. Katika mwaka wa fedha 2009/2010, ruzuku <strong>ya</strong> mwanafunzi inayofika shuleni imepungua<br />

zaidi kwa Sh. 1,715 tofauti na mwaka 2008/2009. Wastani wa ruzuku iliyofika shuleni kwa miaka<br />

mitatu ni Sh. 4,736. Pia wastani wa ruzuku <strong>ya</strong> mwanafunzi iliyofika shuleni kwa miaka mitatu <strong>ya</strong><br />

utekelezaji wa MMEM II ni ndogo zaidi <strong>ya</strong> fedha ambazo zilifika wila<strong>ya</strong>ni 10 kwa miaka hiyo.<br />

Kuna tofauti kubwa <strong>ya</strong> kiwango cha ruzuku kilichofika shuleni kati <strong>ya</strong> shule na shule. Katika mwaka<br />

2007/2008 kiwango kidogo cha ruzuku kilikuwa Sh. 1,823 ilihali kiwango cha juu kilikuwa Sh.<br />

6,797. Kwa mwaka 2008/2009 kiwango cha chini kilikuwa Sh. 2,222 na kiwango cha juu Sh. 7,849.<br />

Kiwango cha chini kilipungua zaidi mwaka 2009/2010 ambacho kilikuwa Sh. 726 kwa shule <strong>ya</strong><br />

msingi Kingorwila (Manispaa <strong>ya</strong> Morogoro) wakati kiwango cha juu kilikuwa Sh. 8,543 kwa shule<br />

<strong>ya</strong> msingi Mazoezi (Bunda, Mara). Tofauti hii ndiyo inasababisha baadhi <strong>ya</strong> shule kuwa na vifaa vingi<br />

v<strong>ya</strong> kujifunzia na kufundishia na shule zingine zinakuwa na vifaa vichache. Hii inafan<strong>ya</strong> pia hata shule<br />

zinazopata ruzuku kidogo kushindwa kufaulisha wanafunzi wengi na hivyo kufan<strong>ya</strong> wanafunzi wengi<br />

kushindwa kuendelea na elimu <strong>ya</strong> sekondari.<br />

Pia kuna tofauti <strong>ya</strong> ruzuku inayofika shuleni kati <strong>ya</strong> shule za vijijini na shule za mjini. Jedwali namba<br />

4 linaonesha kuwa katika miaka mitatu iliyopita shule za mjini zimekuwa zikipata ruzuku kati <strong>ya</strong> Sh.<br />

5,741, Sh. 5,678 na Sh. 3,712 wakati shule za vijijini zimekuwa zikipata ruzuku kati <strong>ya</strong> Sh. 4,440, Sh.<br />

4,785 na Sh. 3,550. Matokeo ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>nafanana sana na ufuatiliaji kama huu uliofanywa na Wizara <strong>ya</strong><br />

<strong>Elimu</strong> na Mafunzo <strong>ya</strong> Ufundi mwaka 2009 ambapo ilibainika pia kuwa shule za mjini zinapata ruzuku<br />

kubwa zaidi <strong>ya</strong> shule za vijijini. Kama ilivyokuwa kwenye ripoti ufuatiliaji wa fedha za umma (<strong>PETS</strong>)<strong>ya</strong><br />

Wizara <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> na Mafunzo <strong>ya</strong> Ufundi, ufuatiliaji huu haukuweza pia kubainisha sababu za utofauti<br />

wa fedha za ruzuku kati <strong>ya</strong> shule za mjini na vijijini.<br />

10<br />

Wastani wa Ruzuku kwa kila mwanafunzi iliyofika wila<strong>ya</strong>ni ni Sh.5005<br />

8


Jedwali 4: Ugawaji wa ruzuku kwa shule za mjini na vijijini<br />

Mwaka wa fedha<br />

2007/2008<br />

2008/2009<br />

2009/2010<br />

Chanzo: Takwinu za uchunguzi<br />

Ruzuku kwa shule za mjini(A)<br />

5,741<br />

5,678<br />

3,712<br />

Ruzuku kwa shule za vijijini(B)<br />

4,440<br />

4,785<br />

3,550<br />

Tofauti(A-B)<br />

1,301<br />

893<br />

162<br />

Chati 4: Ulinganifu wa ruzuku kati <strong>ya</strong> shule za mjini na vijijini<br />

Ruzuku(Sh)<br />

7,000<br />

6,000<br />

5,000<br />

4,000<br />

3,000<br />

2,000<br />

1,000<br />

0<br />

5,741 5,678<br />

4,785<br />

4,440<br />

3,712 3,550<br />

2007/2008 2008/2009 2009/2010<br />

Ruzuku kwa shule za mjini<br />

Ruzuku kwa shule za vijijini<br />

3.2.2 Uelewa wa Walimu Wakuu kuhusu Ruzuku <strong>ya</strong> Mwanafunzi<br />

Walimu wakuu waliulizwa wataje kiasi cha ruzuku ambacho kila mwanafunzi anapa<strong>swa</strong> kupata. Licha<br />

<strong>ya</strong> kuwa katika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> uelewa wa ruzuku ni mkubwa, hali ni tofauti katika ngazi <strong>ya</strong> shule.<br />

Kati <strong>ya</strong> walimu wakuu 24 waliohojiwa kuhusu uelewa wa ruzuku na kiasi cha ruzuku ambacho kila<br />

mwanafunzi anapa<strong>swa</strong> kupata kwa mujibu wa MMEM II, walimu 11 kati <strong>ya</strong> 24(sawa na asilimia<br />

46) hawajui kiasi ambacho kila mwanafunzi anapa<strong>swa</strong> kupata. Hii inafan<strong>ya</strong> walimu wengi washindwe<br />

kufahamu hata jumla <strong>ya</strong> fedha wanayopa<strong>swa</strong> kupata kwa mwaka mzima. Maana jumla <strong>ya</strong> fedha<br />

inategemea na idadi <strong>ya</strong> wanafunzi. Sababu kubwa za kutofahamu ni pamoja na walimu kutokuwa<br />

na Kitabu cha MMEM II. Walimu wote 24 waliohusishwa katika uchunguzi huu walibainisha kuwa<br />

hawajawahi kuwa na nakala <strong>ya</strong> kitabu au waraka wa MMEM II tangu utekelezaji wake uanze. Kama<br />

walimu wakuu ambao ndio watendaji na wadau wakuu katika utekelezaji wa MMEM II ngazi <strong>ya</strong> shule<br />

hawana nakala <strong>ya</strong> MMEM II ni dhahiri kuwa hawataweza kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake<br />

kama vile kuhoji endapo watapata fedha pungufu toka wila<strong>ya</strong>ni au kutengeneza mpango mkakati wa<br />

shule unaozingatia malengo na viashiria v<strong>ya</strong> MMEM II.<br />

9


Kisanduku 2<br />

“Mimi sijawahi kupata nakala <strong>ya</strong> MMEM II na wala sijui huu mpango una maanisha nini. Sijui hata mambo<br />

ambayo sisi walimu wakuu tunapa<strong>swa</strong> kufan<strong>ya</strong> ili kuboresha mpango”. (Mwalimu Mkuu, Njombe)<br />

“Sina nakala ila niliona kwenye kalenda inazungumzia MMEM II, inasema eti Wizara imeboresha madarasa<br />

na imetoa picha yenye madarasa mazuri. Sasa sijui ha<strong>ya</strong> madarasa <strong>ya</strong>ko wapi maana ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>ngu ni mabovu na<br />

watoto wanakaa chini kama ulivyoona kwenye lile darasa la kwanza na la pili zaidi <strong>ya</strong> watoto 40 wanakaa chini<br />

kwa kila Darasa”. (Mwalimu mkuu, Morogoro)<br />

3.2.3 Muda wa Ruzuku Kufika Shuleni<br />

Ufuatiliaji huu umebainisha kuwa ruzuku <strong>ya</strong> mwanafunzi inachelewa kufika shuleni licha <strong>ya</strong> kwamba<br />

inafika wila<strong>ya</strong>ni katika muda muafaka. Kati <strong>ya</strong> shule 24, ni shule 9(asilimia 37 ndizo zilipata fedha<br />

za ruzuku kwa muda muafaka katika mwaka wa fedha 2009/2010. Kwa shule zinazochelewa kupata<br />

ruzuku, zinapata ruzuku miezi miwili hadi mitatu baada <strong>ya</strong> kuanza kwa robo <strong>ya</strong> kila mwaka. Fedha za<br />

robo <strong>ya</strong> kwanza zinafika kati <strong>ya</strong> mwezi wa Septemba na Oktoba badala <strong>ya</strong> mwezi Julai. Na fedha za robo<br />

<strong>ya</strong> mwisho zinafika mwezi wa Juni badala <strong>ya</strong> mwezi Aprili. Katika maoni <strong>ya</strong>o walimu wakuu wamekiri<br />

kuwa ucheleweshaji wa ruzuku unaathiri kwa kiwango kikubwa ununuzi wa mahitaji <strong>ya</strong> kufundishia na<br />

kujifunzia kama vile vitabu na vifaa v<strong>ya</strong> kufundishia. Na hivyo, kurudisha nyuma maendeleo <strong>ya</strong> elimu<br />

hapa nchini.<br />

Kisanduku 3<br />

“Fedha za ruzuku zinachelewa sana kufika shuleni na ndio maana mmekuta fedha nyingi karibu Tsh milioni<br />

4 hazijatumika katika mwaka husika. Sisi tumepata ruzuku <strong>ya</strong> robo <strong>ya</strong> tatu ikiwa pamoja na robo <strong>ya</strong> nne<br />

mwanzoni mwa mwezi Juni mwaka huu” (Mwalimu Mkuu, Nzega.)<br />

“Hii ruzuku inachelewa sana kufika hapa shuleni na kuathiri mipango yetu <strong>ya</strong> hapa shuleni na mi nashauri<br />

Serikali itoe hizi fedha mapema hata ikibidi mwezi Januari zitoke zote na pia watoe Sh 10,000 kwa kila<br />

mwanafunzi ili tupunguze utegemezi wa wazazi”. (Mwalimu Mkuu, Njombe).<br />

3.2.4 Hali <strong>ya</strong> Matumizi <strong>ya</strong> Ruzuku Shuleni<br />

Hali <strong>ya</strong> matumizi <strong>ya</strong> fedha za ruzuku katika ngazi <strong>ya</strong> shule si <strong>ya</strong> kuridhisha. Kati <strong>ya</strong> shule 24, shule 14<br />

(asilimia 58) zilishindwa kutumia fedha zote katika mwaka wa fedha 2009/2010. Mwaka wa fedha<br />

2009/2010, asilimia 25 <strong>ya</strong> fedha za ruzuku zilizofika katika shule 24 hazikutumika. Jumla <strong>ya</strong> Tsh<br />

milioni 64.2 zilifika katika shule hizo lakini fedha halisi zilizotumika zilikuwa Tsh milioni 48.3. Hii<br />

inamaanisha kuwa kuna baadhi <strong>ya</strong> mahitaji kama vile vitabu havikununuliwa katika shule hizo na<br />

hivyo kuathiri maendeleo <strong>ya</strong> elimu katika shule.<br />

10


Picha 2: Ripoti <strong>ya</strong> mwalimu mkuu inayoonesha jinsi fedha za ruzuku zilivyotumika<br />

Ili kubainisha kama fedha za ruzuku zimetumika ipasavyo, walimu wakuu walitakiwa kuonesha risiti za<br />

matumizi mbalimbali <strong>ya</strong> ruzuku <strong>ya</strong> wanafunzi kwa mwaka 2009/2010. Ukaguzi wa risiti za manunuzi<br />

<strong>ya</strong> vitabu ulitumika na kubaini kuwa ulinganifu wa bei zilizopo kwenye risiti 11 na idadi <strong>ya</strong> vitabu<br />

vilivyonunuliwa si sawa. Risiti zinaonesha kuwa vitabu vilinunuliwa kwa bei kati <strong>ya</strong> Sh. 4,000 na Sh.<br />

6,000 ambayo ni wastani wa Sh. 5,000. Lakini tukihusisha jumla <strong>ya</strong> vitabu vilivyonunuliwa katika<br />

shule 24 na bei <strong>ya</strong> wastani iliyopo kwenye risiti tunapata picha kuwa hakukuwa na matumizi sahihi <strong>ya</strong><br />

fedha za ruzuku zilizotumika kununua vitabu. Katika mwaka wa fedha 2009/2010 jumla <strong>ya</strong> Sh. milioni<br />

25.7 12 zilitumika kununua vitabu katika shule 24 na vitabu vilivyonunuliwa ni 2,673. Ukigawan<strong>ya</strong> Sh.<br />

milioni 25.7 na idadi <strong>ya</strong> vitabu utaona kuwa kila kitabu kiligharimu Sh. 9,610, bei hii ni tofauti na<br />

wastani wa bei iliyopo kwenye risiti za manunuzi <strong>ya</strong> vitabu. Hivyo basi, kwa kila kitabu kuna tofauti<br />

<strong>ya</strong> Sh. 4,610, na ukizidisha tofauti <strong>ya</strong> bei (Sh. 4,610) kwa idadi <strong>ya</strong> vitabu 2,673 tunapata takribani Sh.<br />

milioni 12.3 (asilimia 47.9) zilitumika viba<strong>ya</strong> katika shule 24 katika ngazi <strong>ya</strong> shule. Hii inamaanisha<br />

kuwa katika kila Sh. 100 <strong>ya</strong> ununuzi wa vitabu inayofika shuleni, takribani Sh. 48 13 zinatumika viba<strong>ya</strong>.<br />

Matumizi maba<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> fedha za ununuzi wa vitabu <strong>ya</strong>naashiria kuwa kuna changamoto kubwa kuboresha<br />

mazingira <strong>ya</strong> kujifunzia na kufundishia hasa katika kuwezesha upatikanaji wa vitabu shuleni ili kufikia<br />

lengo la kuwa na uwiano wa kitabu kimoja kwa kila mwanafunzi kwani hivi sasa uwiano bado ni kitabu<br />

kimoja kwa wanafunzi watano.<br />

11<br />

Hizi ni risiti za shule 5 ambazo ziliweza kupatikana katika shule 5 kati <strong>ya</strong> 24 za wila<strong>ya</strong> nne tofauti, hivyo zimetumika kama<br />

sampuli kuwakilisha bei <strong>ya</strong> wastani kwa shule zote. Risiti 5 ni asilimia 20.8 <strong>ya</strong> risiti zote ambazo zilitakiwa kuoneshwa na<br />

wakuu wa shule 24<br />

12<br />

Jumla hii imepatikana kwa kujumlisha fedha zote ambazo ziliripotiwa kutumika kununua vitabu na wakuu wa shule<br />

katika mwaka wa fedha 2009/2010.<br />

13<br />

Hii ni asilimia <strong>ya</strong> fedha zilizofujwa kwenye ununuzi wa vitabu=(12.3/25.7) x100 %= 47.9%<br />

11


Jedwali 5: Ulinganifu wa idadi <strong>ya</strong> vitabu vilivyonunuliwa na bei halisi<br />

2009/10<br />

Vitabu vilivyo<br />

nunuliwa<br />

katika shule<br />

24(A)<br />

2673<br />

Jumla <strong>ya</strong> fedha<br />

iliyotumika<br />

kununua vitabu<br />

katika shule<br />

24 (B)<br />

Sh milioni 25.7<br />

Wastani wa Bei<br />

iliyotumika<br />

(C)<br />

(B gawan<strong>ya</strong> A)<br />

Sh 9610<br />

Bei<br />

wastani<br />

iliyopo<br />

kwenye<br />

risiti (D)<br />

Sh 5000<br />

Tofauti <strong>ya</strong><br />

Bei<br />

E=(C-D)<br />

Sh 4610<br />

Ufujaji(D)<br />

(E x A)<br />

Sh milioni 12.3<br />

Picha namba 3: Kuonyesha risiti na bei halisi <strong>ya</strong> vitabu<br />

3.3 FEDHA ZA MAENDELEO<br />

3.3.1 Hali <strong>ya</strong> Ujenzi wa Miundo Mbinu<br />

Huku hali <strong>ya</strong> miundo mbinu ikiwa si <strong>ya</strong> kuridhisha katika shule za msingi, hali <strong>ya</strong> utekelezaji wa<br />

ujenzi wa miundo mbinu iliyobainishwa katika MMEM II si <strong>ya</strong> kuridhisha. Katika miaka mitatu <strong>ya</strong><br />

utekelezaji wa MMEM II, kati <strong>ya</strong> shule 24, ni shule 1 tu ilipata fedha za ujenzi wa madarasa. Pia shule<br />

1 ilipata fedha za ujenzi wa nyumba za walimu na shule 2 zilipata fedha za ujenzi wa vyoo na kupokea<br />

madawati kutoka wila<strong>ya</strong>ni. Katika matumizi <strong>ya</strong> fedha hizi, nyumba 1 tu <strong>ya</strong> walimu imejengwa, darasa<br />

1 limejengwa, vyoo 2 vimejengwa na madawati 24 <strong>ya</strong>menunuliwa. Hii inaonesha kuwa utekelezaji<br />

wa MMEM II kwa miaka mitatu sio mzuri. Ufuatiliaji wa fedha za maendeleo umebainisha kuwa ni<br />

kiwango kidogo sana cha fedha zinafika shuleni. Kwa mujibu wa takwimu za wakuu wa shule zote 24,<br />

jumla <strong>ya</strong> Sh. milioni 15.9 tu ndizo zilipokelewa kati <strong>ya</strong> mwaka wa fedha 2007/2008-2009/2010. Kati<br />

<strong>ya</strong> fedha hizo, ujenzi wa madarasa ni Sh. milioni 3.1, ujenzi wa nyumba za walimu ni Sh. milioni 10.6<br />

ujenzi wa vyoo ni Sh. milioni 1.6 na Sh. 635,000 kwa ajili <strong>ya</strong> madawati. Utekelezaji hafifu wa ujenzi<br />

wa miundo mbinu katika shule za msingi umeendelea kuathiri mazingira <strong>ya</strong> shule na hivyo kuathiri<br />

kiwango cha ufaulu. Hivi sasa uwiano wa choo kwa wanafunzi ni 1:57 kwa wasichana badala <strong>ya</strong> 1:20,<br />

na kwa wavulana ni 1:55 badala <strong>ya</strong> 1:20. Pia uwiano wa darasa kwa wanafunzi ni 1:73 badala <strong>ya</strong> 1:40<br />

(BEST 2010); hii inamanisha kila mwalimu anapoingia darasani anafundisha wanafunzi 73.<br />

12


Picha namba 4: Moja <strong>ya</strong> madarasa <strong>ya</strong>nayotumika katika shule <strong>ya</strong> msingi Sofia, wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Iramba<br />

3.3.2 Matumizi Maba<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Fedha za Maendeleo<br />

Ili kupata kiasi cha fedha za maendeleo ambazo zimetumika viba<strong>ya</strong> kwa shule 24, ulinganifu wa<br />

fedha zilizopelekwa katika shule 14 na fedha walizopokea walimu wakuu ulihusishwa. Maofisa elimu<br />

wa kila wila<strong>ya</strong> walitakiwa kutaja fedha za maendeleo zilizotumwa kwa kila shule katika shule nne<br />

zilizochaguliwa, na walimu wakuu nao pia walitakiwa kujaza fedha za maendeleo ambazo walipokea<br />

toka wila<strong>ya</strong>ni kuanzia mwaka wa fedha 2007/2008 hadi 2009/2010. Mwaka 2007/2008 taarifa za<br />

wila<strong>ya</strong> sita zilionesha kuwa, jumla <strong>ya</strong> Sh. milioni 8.1 zilipelekwa katika shule 24. Lakini taarifa za<br />

walimu wakuu zilionesha kuwa jumla <strong>ya</strong> Sh. milioni 7.7 zilifika shuleni kwa mwaka 2007/2008. Hivyo,<br />

kwa mwaka 2007/2008 jumla <strong>ya</strong> Sh. 400,000 hazikufika shuleni licha <strong>ya</strong> kuwa zimeripotiwa na wila<strong>ya</strong><br />

kuwa zilipelekwa shuleni. Pia mwaka 2008/2009 fedha zilizopelekwa shuleni ni Sh. milioni 8 na fedha<br />

zilizofika shuleni ni Sh. milioni 6.6, hivyo kiasi cha Sh. milioni 1.4 hakikufika shuleni.<br />

Mwaka wa fedha 2009/2010, Sh. milioni 25.3 zilipelekwa shuleni lakini kiasi cha Sh. milioni 1.6 tu<br />

ndizo zilifika shuleni. Hivyo, kiasi cha Sh. milioni 23.7 hakikufika. Hii inamaanisha kuwa katika miaka<br />

mitatu, hali <strong>ya</strong> matumizi maba<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> fedha za maendeleo imekuwa ukiongezeka kila mwaka na kwa<br />

mwaka 2009/2010 iliongezeka maradufu (asilimia 361) tofauti na mwaka 2008/2009. Jedwali namba<br />

8 linaonyesha kuwa wila<strong>ya</strong> za Iramba, Bunda na Njombe zilitumia fedha viba<strong>ya</strong> ambapo kwa wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong><br />

Iramba milioni Sh. 16.2 hazikufika shuleni, wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Bunda ni Sh.milioni 8.9 na wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Njombe<br />

Sh. Milioni 2.7.<br />

14<br />

Kwa mujibu wa ripoti <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> kuhusu fedha zilizopelekwa shuleni.<br />

13


Jedwali 6.<br />

Mwaka wa<br />

fedha<br />

2007/2008<br />

2008/2009<br />

2009/2010<br />

Jumla<br />

Tofauti kati <strong>ya</strong> fedha za maendeleo zilizopelekwa shuleni na fedha halisi zilizopokelewa<br />

na walimu wakuu.<br />

Chanzo: Takwinu za Ufuatiliaji<br />

Fedha za Maendeleo<br />

zilizopelekwa katika shule 24 (A)<br />

8.1milioni<br />

8 milioni<br />

25.3 milioni<br />

41.5 milioni<br />

Fedha za Maendeleo zilizofika<br />

katika shule 24 (B)<br />

7.7 milioni<br />

6.6 milioni<br />

1.6 milioni<br />

15.9 milioni<br />

Tofauti<br />

(A-B)<br />

400,000<br />

1.4 milioni<br />

23.7 milioni<br />

25.5 milioni<br />

Chati namba 5. Tofauti kati <strong>ya</strong> fedha za maendeleo zilizopelekwa shuleni na fedha halisi zilizopokelewa<br />

na walimu wakuu.<br />

Fedha Maendeleo<br />

(Sh. Milioni)<br />

30<br />

25<br />

20<br />

15<br />

10<br />

5<br />

0<br />

25.4<br />

8.1 7.7<br />

8<br />

6.6<br />

1.6<br />

2007/2008 2008/2009 2009/2010<br />

Fedha za Maendeleo zilizopelekwa shuleni<br />

Fedha za Maendeleo zilizofika shuleni<br />

14


Jedwali 7: Tofauti kati <strong>ya</strong> fedha za maendeleo zilizopelekwa shuleni toka wila<strong>ya</strong>ni na fedha halisi<br />

zilizopokelewa na walimu wakuu.<br />

Mwaka 2007/2008 hadi Mwaka 2009/2010<br />

WILAYA SHULE Fedha iliyopelekwa<br />

shule toka wila<strong>ya</strong>ni(A)<br />

Fedha iliyofika<br />

shule(B)<br />

Tofauti(A- -B)<br />

MOROGORO KAMBARAGE 3,000,000 3,300,000 (300,000)<br />

MSAVU A 0 0 0<br />

KINGOLWIRA 0 0 0<br />

MCHIKICHINI B 0 0 0<br />

Jumla 3,000,000 3,300,000 (300,000)<br />

NZEGA ISESE Hakuna taarifa 1,598,166 0<br />

NYASA Hakuna taarifa 260,000 0<br />

IMELI Hakuna taarifa 0 0<br />

MWAMALA Hakuna taarifa 0 0<br />

Jumla Hakuna 1,858,166 0<br />

NJOMBE LUSISI 429,382 0<br />

IGIMA 1,218,038 0<br />

SOVI 473,038 0<br />

LUNGUYA 553,038 0<br />

Jumla 2,673,496 0<br />

429,382<br />

1,218,038<br />

473,038<br />

553,038<br />

2,673,496<br />

BABATI KWARAA 0 0 0<br />

GALAPO 0 0 0<br />

LUXMANDA 0 0 0<br />

GIDGWAR 0 0 0<br />

Jumla 0 0 0<br />

IRAMBA SOFIA 3,166,000 0 3,166,000<br />

KYENGEGE 13,375 ,000 375,000 13,000,000<br />

SALALA 0 0 0<br />

KIOMBOI 0 0 0<br />

Jumla 16,541,000 375,000 16,166,000<br />

BUNDA MAZOEZI 5,267,743 3,600,000 1,667,743<br />

BALILI A 6,661,429 0 6,661,429<br />

KASUNGUTI 3,693,177 3,123,000 570,177<br />

KIBARA 3,671,971 3,671,000 0<br />

Jumla 19,294,320 10,394,000 8,899,349<br />

JUMLA KUU 41,408,816 15,927,166 25,481,655<br />

Chanzo: Takwimu za Ufuatiliaji<br />

15


3.4 MICHANGO YA WAZAZI<br />

3.4.1 Mwamko wa Wazazi Kuchangia <strong>Elimu</strong><br />

Kwa mujibu wa takwimu za walimu wakuu wa shule 24, Jedwali namba 8 linaonesha kwamba wastani<br />

wa jumla <strong>ya</strong> Sh. milioni 13 zilikusanywa toka kwa wazazi mwaka wa fedha 2007/2008 hadi 2009/2010.<br />

Hivyo, fedha za michango <strong>ya</strong> wazazi katika miaka mitatu ilikuwa ni asilimia 16.4 <strong>ya</strong> jumla <strong>ya</strong> wastani<br />

wa fedha ruzuku <strong>ya</strong> wanafunzi zilizopokelewa katika shule 24. Ili kuhakiki kiwango hiki cha michango,<br />

walimu wakuu waliulizwa kama wanatoa risiti kwa wazazi wanaochangia. Walimu wakuu 13 tu kati <strong>ya</strong><br />

24 ndio wanatoa risiti. Moja <strong>ya</strong> sababu iliyobainishwa na walimu wakuu ni kwamba ununuzi wa vitabu<br />

v<strong>ya</strong> risiti na mihuri <strong>ya</strong> shule ni gharama. Hivyo, ni afadhali watumie daftari kuorodhesha michango<br />

hiyo. Wastani wa fedha wanayochangia wazazi ni kati <strong>ya</strong> Sh. 2000 hadi 9000 kwa mwaka kwa kila<br />

mwanafunzi. Gharama za uchangiaji zinakuwa kubwa sana kama mzazi ana watoto wengi shuleni au<br />

wanaojiandaa kufan<strong>ya</strong> mitihani <strong>ya</strong> darasa la saba kwa sababu kuna mitihani mingi sana <strong>ya</strong> maandalizi,<br />

na hivyo wazazi hulazimika kuchanga fedha nyingi zaidi pindi watoto wao wanapokuwa darasa la saba.<br />

Kisanduku 4<br />

“Michango hii inatuumiza sana kama mimi nina watoto watatu na wawili wako darasa la saba hivyo kwa<br />

mwaka huu wa 2010 nimechangia kama Tsh 9,000 kwa kila mtoto, na huyu wa darasa la pili nimechangia Tsh<br />

4,000.” (Mzazi, Nzega)<br />

“Nimekuwa ninachangia kila mwaka, wakati mwingine nachangia Tsh 3,000 au Tsh 7,000 inategemea mtoto<br />

kama ana mitihani mingi na majaribio mengi. Pia ninachangia kwa mchango wa mlinzi na maji.” (Mzazi,<br />

Morogoro)<br />

Jedwali 8. Tofauti kati <strong>ya</strong> fedha za maendeleo zilizopelekwa shuleni na fedha halisi zilizopokelewa<br />

na walimu wakuu.<br />

2007/2008<br />

2008/2009<br />

2009/2010<br />

Wastani<br />

Ruzuku iliyofika<br />

shule<br />

84.2 milioni<br />

88 milioni<br />

64.2 milioni<br />

78.8 milioni<br />

Chanzo: Takwinu za Ufuatiliaji<br />

Michango <strong>ya</strong><br />

wazazi<br />

11.8 milioni<br />

13.6 milioni<br />

14 milioni<br />

13.1 milioni<br />

Uwiano wa michango <strong>ya</strong> wazazi na<br />

ruzuku(katika asilimia)<br />

14%<br />

15.5%<br />

21.8%<br />

16.4%<br />

16


Licha <strong>ya</strong> kwamba MMEM II inataka wazazi wachangie kwa kiwango cha asilimia 20 katika ujenzi wa<br />

miundo mbinu, wazazi wengi bado wana mwamko mdogo wa kutoa michango <strong>ya</strong> ujenzi na ununuzi<br />

wa miudombinu. Na wanaona kuwa ujenzi wa miundombinu bado ni jukumu la serikali. Kati <strong>ya</strong><br />

wazazi waliohojiwa, asilimia 65 walibainisha kuwa ujenzi wa miundo mbinu ni jukumu la serikali.<br />

Kati <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> sita, wazazi wa wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Babati, Bunda na Nzega wana mwamko mdogo sana wa kutoa<br />

michango ambapo kati <strong>ya</strong> wazazi waliohojiwa, asilimia 52 <strong>ya</strong> wazazi ndio walitoa michango kwa mwaka<br />

2009/2010. Mwamko ni mkubwa sana katika wila<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Njombe, na Iramba ambapo karibu asilimia<br />

98 <strong>ya</strong> wazazi waliohojiwa walitoa michango kwa mwaka 2009/2010. Uchunguzi umebainisha kuwa<br />

wila<strong>ya</strong> zinazotekeleza mpango wa chakula shuleni ndizo ambazo wazazi wana mwamko mkubwa na<br />

hivyo kinachowasukuma wazazi kuchanga ni kwa ajili <strong>ya</strong> gharama za uandaaji wa chakula cha mchana<br />

kwa wanafunzi ili kuepuka usumbufu wa kuwaandalia watoto chakula cha mchana na pia wanaona ni<br />

sehemu <strong>ya</strong> majukumu <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong> kila siku.<br />

Kisanduku 5.<br />

“Mpango huu wa chakula umeondoa usumbufu kwa wanafunzi kurudi nyumbani mchana kwa ajili <strong>ya</strong> chakula<br />

na kurejea tena shuleni, ikizingatiwa kuwa wanafunzi wengi hasa kwa shule za vijijini wanakaa mbali na shule<br />

wanazosoma. Pia mpango huu umesaidia sana kuongezeka kwa idadi <strong>ya</strong> wanafunzi wanaohudhuria darasani<br />

sambamba na kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu kwa shule zinazotekeleza mpango huu”. (Mwalimu Mkuu,<br />

Njombe).<br />

4.0 ULINGANISHI WA MMEM I NA MMEM II<br />

Ili kulinganisha MMEM I na MMEM II, ripoti hii inatumia ufuatiliaji wa fedha za utekelezaji wa<br />

MMEM I uliofanywa na REPOA 16 . Zifuatazo ni baadhi <strong>ya</strong> tofauti kuu za utekelezaji wa MMEM I na<br />

MMEM II.<br />

Katika utekelezaji wa MMEM I, fedha za ruzuku kutoka serikali kuu kwenda ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> zilitolewa<br />

kama zilivyoainishwa katika mpango. Wastani wa ruzuku iliyopelekwa wila<strong>ya</strong>ni kwa kila mwanafunzi<br />

kwa miaka yote ilikuwa Sh. 8,700. Hali ni tofauti kwa MMEM II ambapo wastani wa fedha za ruzuku<br />

zilizopelekwa wila<strong>ya</strong>ni ni Sh. 5,005 kwa kipindi cha miaka mitatu <strong>ya</strong> utekelezaji.<br />

Upelekaji wa fedha za maendeleo shuleni ulikuwa mzuri zaidi katika MMEM I tofauti na MMEM II.<br />

Katika MMEM I, karibu asilimia 85 <strong>ya</strong> fedha za maendeleo zilizopangwa zilifika mashuleni. Lakini<br />

katika utekelezaji wa MMEM II kuna shule ambazo hazijawahi kupokea fedha zozote katika kipindi<br />

cha miaka mitatu <strong>ya</strong> utekelezaji wake.<br />

16<br />

REPOA (2004), Public Expenditure Tracking Survey.<br />

17


Kati <strong>ya</strong> shule 24 zilizohusishwa katika ufuatiliaji, ni shule 5 tu ndizo zilipata fedha za maendeleo.<br />

Hivyo, shule 19 hazijawahi kupokea fedha za maendeleo. Kwa kuwa MMEM I ilitekelezwa kwa<br />

kutengewa fedha maalumu zilizotoka kwa wahisani wa maendeleo na MMEM II unatekelezwa kwa<br />

kutengewa fedha za mfuko wa pamoja wa bajeti (GBS). Ni dhahiri kuwa hii inaweza kuwa ni moja<br />

<strong>ya</strong> sababu inayoathiri utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu kwa serikali kutenga fedha kidogo za<br />

utekelezaji wa MMEM II tofauti na mpango ulivyobainisha. Katika utekelezaji wa MMEM I, fedha za<br />

wahisani zilielekezwa moja kwa moja kwenye utekelezaji wa mpango, lakini kwa MMEM II, wahisani<br />

wanapa<strong>swa</strong> kuchangia fedha kwenye mfuko wa pamoja wa bajeti na serikali ndio inaamua kutenga<br />

fedha kwa ajili <strong>ya</strong> utekelezaji wa miradi mbalimbali.<br />

5.0 HITIMISHO NA MAPENDEKEZO<br />

5.1 Hitimisho<br />

Ruzuku inayotolewa haiendani na maelekezo <strong>ya</strong> MMEM II. Katika miaka mitatu <strong>ya</strong> utekelezaji wa<br />

MMEM II, wastani wa ruzuku inayofika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> toka serikali kuu ni Sh. 5,005, hivyo serikali<br />

imekuwa inatoa asilimia 50 <strong>ya</strong> fedha za ruzuku kwa kila mwanafunzi iliyoanishwa katika MMEM II<br />

ambayo ni Sh. 10,000. Fedha za ruzuku kwa mwanafunzi hupungua kadri inavyoelekezwa shuleni<br />

toka ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong>. Tofauti hii inajitokeza ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong> ambapo mwaka 2008/2009 asilimia 8 <strong>ya</strong><br />

fedha haikufika shuleni na mwaka 2009/2010 ni asilimia 16. Kama fedha hii ilipangwa kutolewa kwa<br />

ajili <strong>ya</strong> kuboresha elimu <strong>ya</strong> msingi kwa kuboresha mazingira <strong>ya</strong> kujifunzia na kufundishia ni dhahiri<br />

kuwa utekelezaji wa MMEM II hautafikia malengo <strong>ya</strong>ke kama vile kupunguza uwiano wa kitabu<br />

kwa mwanafunzi toka 1:5 hadi 1:1. Kuendelea kuwa na mazingira duni <strong>ya</strong> kufundishia na kujifunzia<br />

kutaendelea kuathiri upatikanaji wa elimu bora na pia viwango v<strong>ya</strong> ufaulu, na hivyo kufan<strong>ya</strong> wanafunzi<br />

wengi washindwe kuendelea katika ngazi <strong>ya</strong> sekondari.<br />

Licha <strong>ya</strong> kwamba MEMM II umebainisha kutumia fedha nyingi kwa ajili <strong>ya</strong> kuboresha miundo mbinu,<br />

hadithi imekuwa kinyume. Serikali inatoa kiwango kidogo cha fedha za maendeleo kwa ajili <strong>ya</strong> ujenzi<br />

wa miundombinu <strong>ya</strong> shule. Ufuatiliaji wa fedha za maendeleo umebainisha kuwa kiwango kidogo sana<br />

cha fedha za maendeleo zinafika shuleni. Kwa mujibu wa takwimu za wakuu wa shule zote 24, jumla<br />

<strong>ya</strong> Sh. milioni 15.9 tu ndizo zilizopokelewa kati <strong>ya</strong> mwaka wa fedha 2007/2008-2009/2010. Kama<br />

serikali inatoa fedha kidogo kwa ajili <strong>ya</strong> uboreshaji wa miundo mbinu, je tutaweza kutekeleza MMEM<br />

II kwa kuzingatia viashiria v<strong>ya</strong> kupima utekelezaji wa MMEM II katika kuboresha miundo mbinu<br />

kwa kujenga nyumba za walimu 87,744, madarasa 60,896, vyoo 107,224 na madawati 821,877?<br />

Kushindwa kuboresha miundombinu hii shuleni kutaendelea kuathiri hali <strong>ya</strong> ufundishaji kwa walimu,<br />

na pia watoto wataendelea kusoma katika mazingira magumu. Hali hii itaendelea kuathiri upatikanaji<br />

wa elimu bora hapa nchini.<br />

Kwa kuwa wazazi wanachangia michango mbalimbali, elimu <strong>ya</strong> msingi si bure hapa nchini. Wazazi<br />

wengi bado wanasumbuliwa kutoa michango mbalimbali kwa ajili <strong>ya</strong> uendeshaji wa shule kama vile<br />

kuchangia gharama za mitihani. Mzazi anapokuwa na mtoto aliye darasa la saba anakuwa na mzigo<br />

18


mkubwa sana kwani analipia fedha nyingi ili mtoto aweze kufan<strong>ya</strong> mitihani mbalimbali <strong>ya</strong> kujiandaa<br />

na mtihani wa kumaliza elimu <strong>ya</strong> msingi. Kama fedha <strong>ya</strong> ruzuku kwa wanafunzi kiasi cha Sh. 10,000<br />

ingekuwa inafika shuleni na kutumika kama inavyobainishwa na MEMM II, ni dhahili kuwa wazazi<br />

wasingesumbuliwa kutoa michango. Na hapa ndio tungeweza kujidai kwa kusema sasa Tanzania inatoa<br />

elimu bure.<br />

5.2 Mapendekezo<br />

Mapendekezo ha<strong>ya</strong> <strong>ya</strong>natolewa ili kusaidia utekelezaji wa MMEM III 17 ambayo itaanza kutekelezwa<br />

baada <strong>ya</strong> kumalizika kwa MMEM II. Pia itasaidia utekelezaji wa MMES II ambapo utekelezaji wake<br />

umeanza mwaka wa fedha 2010/2011.<br />

a) Serikali haina budi kuwajibika ipasavyo kwa wananchi ili kuhakikisha kuwa utekelezaji wa<br />

mipango mbalimbali <strong>ya</strong> maendeleo <strong>ya</strong> sekta <strong>ya</strong> elimu inafanikiwa. Hili litafanikiwa pale serikali<br />

itakapoamua kuheshimu mipango <strong>ya</strong> maendeleo. MMEM I ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa<br />

sababu serikali ilipeleka fedha za ruzuku na maendeleo shuleni kama ilivyobainishwa katika<br />

mpango.<br />

b) Hivi sasa serikali inaandaa MMEM III ambapo utekelezaji wake utaanza baada <strong>ya</strong> MMEM II<br />

kumalizika 18 na ili kufanikisha utekelezaji wake, wahisani hawana budi kuhimiza fedha zao za<br />

maendeleo zipelekwe moja kwa moja kwenye mpango husika na si kutumia mfuko wa bajeti wa<br />

pamoja. MMEM I ilifanikiwa kiutekelezaji na pia fedha za ruzuku zilizopangwa kwenye mpango<br />

ndizo zilizofika mashuleni kwa sababu ilitumia mtindo wa wahisani wa maendeleo kupeleka<br />

fedha moja kwa moja kwenye mpango au mradi.<br />

c) Kwa kuwa ruzuku inachelewa kutoka wila<strong>ya</strong>ni kwenda shuleni, serikali haina budi kubadilisha<br />

mfumo wa upelekaji wa ruzuku shuleni ili kuondokana na ucheleweshaji wa ruzuku. Hii pia<br />

itapunguza matumizi maba<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> ruzuku katika ngazi <strong>ya</strong> wila<strong>ya</strong>. Hili linawezekana kwa sababu<br />

shule zote zina akaunti za benki, hivyo ruzuku ipelekwe moja kwa moja shuleni toka serikali<br />

kuu. Kama serikali itaridhia kutuma fedha za ruzuku moja kwa moja, kuna haja pia <strong>ya</strong> kuanzisha<br />

mfumo huru wa ufuatiliaji wa ruzuku katika ngazi <strong>ya</strong> serikali kuu na shule utakaokuwa unahakiki<br />

matumizi <strong>ya</strong> ruzuku zinazofika shuleni na jinsi zilivyotumika ili kupunguza matumizi maba<strong>ya</strong><br />

katika ngazi <strong>ya</strong> shule na pia kuhakiki fedha zinazotolewa na serikali kuu kwenda ngazi <strong>ya</strong> shule.<br />

d) Kalenda <strong>ya</strong> shule za msingi huanza mwezi Januari na kuisha mwezi Desemba wakati kalenda <strong>ya</strong><br />

serikali <strong>ya</strong> mwaka wa fedha inaanza Julai 1 hadi Juni 31. Ili kurahisisha upangaji wa mpango wa<br />

shule na utekelezaji wake serikali haina budi kubadilisha mtindo wa utoaji wa fedha za ruzuku<br />

kwa kutoa fedha za ruzuku kwa awamu moja katika mwezi Januari badala <strong>ya</strong> mtindo wa robo<br />

mwaka kwa kufuata kalenda <strong>ya</strong> serikali. Fedha nyingi hazitumiki kwa sababu zinachelewa kufika<br />

na pia kalenda <strong>ya</strong> shule na ile <strong>ya</strong> mwaka wa fedha wa serikali zinapishana.<br />

17<br />

Hotuba <strong>ya</strong> bajeti <strong>ya</strong> Wizara <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> na Mafunzo <strong>ya</strong> Ufundi <strong>ya</strong> mwaka 2010/2011<br />

19


e) Wasimamizi katika utekelezaji wa MMEM II hasa walimu wakuu hawana budi kupewa maelekezo<br />

na miongozo <strong>ya</strong> kutosha juu <strong>ya</strong> MMEM, ili waweze kuufuatilia, kutekeleza na kuusimamia vizuri<br />

katika misingi bora na yenye tija kwa maendeleo <strong>ya</strong> elimu nchini. Baadhi <strong>ya</strong> viongozi ngazi <strong>ya</strong><br />

wila<strong>ya</strong> wanafurahia uelewa mdogo wa watendaji hawa kuhusu MMEM kwa manufaa <strong>ya</strong>o binafsi.<br />

20


Marejeo<br />

REPOA (2004). Ripoti <strong>ya</strong> Ufuatiliaji wa fedha za Umma, Utekelezaji wa MMEM I mwaka 2002<br />

na 2003.<br />

URT (2006). Mpango wa pili wa Maendeleo wa <strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> Msingi (MMEM II).<br />

URT (2009). Ripoti <strong>ya</strong> Utekelezaji wa Mpango wa pili wa Maendeleo wa <strong>Elimu</strong> <strong>ya</strong> Msingi kwa<br />

Mwaka 2007/2008.<br />

URT (2010). Ripoti <strong>ya</strong> Ufuatiliaji wa Fedha za Umma kwa Mwaka wa fedha 2007/2008, Wizara<br />

<strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> na Mafunzo <strong>ya</strong> Ufundi<br />

URT (2009). Ripoti <strong>ya</strong> Utekelezaji katika Sekta <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> mwaka 2008<br />

URT (2010). Ripoti <strong>ya</strong> Utekelezaji katika Sekta <strong>ya</strong> <strong>Elimu</strong> mwaka 2009<br />

URT (2010) Basic Education Statistics of Tanzania for 2010<br />

21


Viambatisho<br />

Kiambatisho 1. Sampuli <strong>ya</strong> Mikoa na wila<strong>ya</strong> zilizohusishwa kwenye ufuatiliaji<br />

Kanda<br />

Sampuli <strong>ya</strong> Mikoa<br />

Sampuli <strong>ya</strong> Wila<strong>ya</strong><br />

Idadi <strong>ya</strong> shule<br />

Ziwa<br />

Mara<br />

Bunda<br />

4<br />

Magharibi<br />

Tabora<br />

Nzega<br />

4<br />

Mashariki<br />

Morogoro<br />

Manispaa <strong>ya</strong> Morogoro<br />

4<br />

N<strong>ya</strong>nda za juu-kusini<br />

Njoluma<br />

Njombe<br />

4<br />

Kati<br />

Singida<br />

Iramba<br />

4<br />

Kaskazini<br />

Man<strong>ya</strong>ra<br />

Babati<br />

4<br />

Jumla <strong>ya</strong> Shule<br />

24<br />

Kiambatisho 2. Malengo <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II<br />

Mwaka<br />

Madarasa<br />

Nyumba<br />

Vyoo<br />

Madawati<br />

2007/08<br />

16,485<br />

21,936<br />

29,328<br />

211,467<br />

2008/09<br />

16,485<br />

21,936<br />

29,328<br />

211,467<br />

2009/10<br />

16,485<br />

21,936<br />

29,328<br />

223,122<br />

2010/11<br />

11,441<br />

21,936<br />

19,240<br />

175,815<br />

Jumla<br />

60,896<br />

87,744<br />

107,224<br />

821,871<br />

22


Moja <strong>ya</strong> malengo makuu <strong>ya</strong> Mpango wa pili wa Maendeleo <strong>ya</strong> Msingi (MMEM II) ilikuwa ni kuboresha<br />

hali <strong>ya</strong> mazingira <strong>ya</strong> kujifunzia na kufundishia kwa kujenga miundombinu kama vile madarasa, nyumba<br />

za walimu, vyoo na madawati. Pia ilidhamiria kuboresha mchakato wa kujifunzia na kufundishia kwa<br />

kuongeza vifaa kama vile vitabu v<strong>ya</strong> kiada na ziada kwa ajili <strong>ya</strong> wanafunzi. Ili kutekeleza adhima hii,<br />

MMEM II, ilibainisha kuwa Sh. 10,000 itatolewa kwa kila mwanafunzi wa shule <strong>ya</strong> msingi kila mwaka<br />

kwa kipindi cha miaka mitano <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II kwa ajili <strong>ya</strong> kununua vitabu, kukidhi gharama<br />

za mitihani, kufanyia ukarabati mdogo na gharama za utawala.<br />

Ikiwa miaka mitatu <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II imepita, hali halisi <strong>ya</strong> utekelezaji wa MMEM II bado<br />

ina changamoto nyingi. Hivi sasa uwiano wa choo kwa wanafunzi ni 1:57 kwa wasichana badala <strong>ya</strong><br />

1:20, na kwa wavulana ni 1:55 badala <strong>ya</strong> 1:20. Pia uwiano wa darasa kwa wanafunzi ni 1:73 badala<br />

<strong>ya</strong> 1:40 na uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi ni 1:5 badala <strong>ya</strong> 1:1. Kama bajeti <strong>ya</strong> sekta <strong>ya</strong> elimu<br />

inaongezeka mwaka hadi mwaka na utekelezaji wa MMEM II si wa kuridhisha, fedha hizi zinatumikaje?<br />

Je, fedha zinazopangwa katika bajeti zinawafikia walengwa? Uhitaji wa majibu <strong>ya</strong> ma<strong>swa</strong>li ha<strong>ya</strong> ndio<br />

<strong>ya</strong>lishawishi <strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong> kufuatilia matumizi <strong>ya</strong> fedha za umma(<strong>PETS</strong>) katika wila<strong>ya</strong> sita ambazo ni<br />

Njombe, Morogoro, Nzega, Bunda, Iramba na Babati.<br />

Matokeo <strong>ya</strong> jumla <strong>ya</strong>naonesha kuwa ni wastani wa Sh. 4,736 ndizo zilifika shuleni kama ruzuku kwa<br />

mwanafunzi badala <strong>ya</strong> Sh.10,000. Pia hali <strong>ya</strong> utekelezaji wa miundo mbinu si <strong>ya</strong> kuridhisha ambapo katika<br />

shule 24 za wila<strong>ya</strong> sita ni nyumba 1 tu <strong>ya</strong> walimu imejengwa, darasa 1 limejengwa, vyoo 2 vimejengwa<br />

na madawati 24 <strong>ya</strong>menunuliwa kati <strong>ya</strong> mwaka 2007/08 hadi 2009/2010. Licha <strong>ya</strong> kwamba fedha kidogo<br />

zinafika shuleni, hali <strong>ya</strong> matumizi si <strong>ya</strong> kuridhisha ambapo kwa kila Sh. 100 inayofika shuleni kwa ajili <strong>ya</strong><br />

ununuzi wa vitabu Sh. 48 inatumika viba<strong>ya</strong>.<br />

Matokeo <strong>ya</strong> ripoti hii <strong>ya</strong>naweza kutumika kama nyenzo muhimu kwa ajili <strong>ya</strong> utekelezaji wa mipango<br />

mingine <strong>ya</strong> maendeleo kama MMEM III na MMES II ili kuboresha sekta <strong>ya</strong> elimu hapa nchini.<br />

<strong>Haki</strong><strong>Elimu</strong> inawezesha wananchi<br />

kuleta mabadiliko katika elimu<br />

na demokrasia<br />

SL P 79401, Dar es Salaam, Tanzania<br />

Simu. (255 22) 2151852/3 • Faksi (255 22) 215244<br />

info@hakielimu.org • www.hakielimu.org

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!