19.06.2014 Views

rufiji environment management project - Coastal Forests of Kenya ...

rufiji environment management project - Coastal Forests of Kenya ...

rufiji environment management project - Coastal Forests of Kenya ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

REMP Technical Report 40: Rangeland Resources in Rufjiji<br />

Muhtasari Wa Taarifa<br />

MSHAURI BINGWA WA UOTO WA NYANDA ZA MALISHO KUHUSU<br />

TATHMINI YA UOTO WA NYANDA ZA MALISHO KATIKA MAENEO<br />

YALIYOTAJWA KWA LENGO LA KUWA NA MKAKATI WA<br />

KUSIMAMIA NAKUENDE LEZA MIFUGO WILAYA YA RUFIJI<br />

Wilaya ya Rufiji ni miongoni mwa wilaya sita zinazounda Mkoa wa Pwani na ambayo iko kusini zaidi<br />

ya wilaya zingine. Wilaya hii ina ukubwa wa eneo za mraba km² 13,339 na imegawanyika katika<br />

makundi manne(4) ya aina za udongo kama ifuatavyo:-<br />

• Udongo wa kichanga uliokosa mbolea uliogubikwa na miti aina ya Miombo na aina nyingine za<br />

Misitu ya Pwani yenye ukubwa wa eneo km² 4,250 (pamoja na eneo la Selous Game Reserve<br />

lenye ukubwa wa eneo za mraba km² 3,400).<br />

• Udongo mwekundu laini wa kichanga wenye asili ya kugubikwa na Misitu ya Pwani wenye<br />

ukubwa wa eneo la mraba km² 2,700.<br />

• Bonde la Mafuriko la Mto Rufiji lenye udongo tifu tifu uliochanganyika na udongo wa<br />

mfinyanzi wenye ukubwa wa eneo la mraba km² 1,700. Aina hii ya udongo una kiasi kidogo<br />

cha mchanga uliotawaliwa na nyasi ndefu na miti ya hapa na pale.<br />

• Udongo laini wa kifinyanzi wa chumvi chumvi ulioko maeneo ya Delta uliogubikwa na misitu<br />

ya mikoko (kapa) na mbuga za nyasi zenye ukubwa wa km² 1,300.<br />

Wilaya inapata wastani wa mvua kati ya mm 1200 kwa maeneo ya pwani mpaka mm 600 magharibi<br />

mwa maeneo ya mafuriko ya Mto Rufiji. Wilaya huwa inapata mvua za aina mbili yaani mvua kubwa<br />

za Masika zinazoanza katikati ya mwezi wa March na kumalizika mwishoni mwa mwezi Mei; pia kuna<br />

mvua za Vuli zinazoanza katikati ya mwezi wa Novemba na kukatika mwezi Januari.<br />

Ni eneo kiasi tu ya bonde la Mafuriko la Mto Rufiji ndilo lenye udongo wenye rutuba nzuri inay<strong>of</strong>aa<br />

kwa kilimo. Tena ni kwa sababu ya kilimo cha kupumzisha ardhi au kulazimishwa kupumzishwa kwa<br />

sababu ya mafuriko ya mwaka yanapotokea ambayo husababisha maeneo hayo kutokulimwa. Kiasi<br />

cha makisio ya hektari 45,000 ambazo ziko katika ukanda wa Mafuriko zinaz<strong>of</strong>aa kwa Kilimo ni<br />

hektari 15,000 ndizo zinazolimwa kila mwaka. Kiasi cha hektari zipatazo 25,000 zilizo na misitu ya<br />

pwani na ambazo zimetawaliwa na Milima ya Kaskazini yenye udongo mwekundu zimefyekwa kwa<br />

ajili ya kilimo. Kutokana na hali hiyo kuna maeneo machache yaliyobaki ambayo kiendelevu yanafaa<br />

kwa kilimo wilayani.<br />

Kwa asili, wananchi wa wilaya hii huwa wanapata viini lishe vya protini kutokana na uvuvi, uwindaji<br />

na ufugaji wa kuku. Ni wananchi waishio katika Delta tu walio na ng’ombe ,mbuzi na kondoo.<br />

Sababu moja inayowafanya wananchi wa maeneo hayo kutokufuga wanyama wakubwa (mbuzi,<br />

kondoo na ng’ombe) ni uwingi wa mbung’o. Kwa hiyo ni wazi kuwa idadi ya wanyama wakubwa kwa<br />

asili ni kidogo/asilimia chache ya wanyama wakubwa zaidi sana wanamilikiwa na wafanyakazi<br />

wahamiaji wa serikali.<br />

Tangu mwaka 2002 kumekuwa na mabadiliko makubwa kutokana na wafugaji wa jadi na wakulima<br />

wafugaji kuingia wilayani toka mikoa na wilaya zingine kwa ajili ya kutafuta malisho na maji.<br />

Wafugaji hao wameingia na idadi kubwa ya mifugo.<br />

Mpaka sasa wilaya inakadiriwa kuwa na idadi ifuatayo ya mifugo:-<br />

iv

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!