19.06.2014 Views

rufiji environment management project - Coastal Forests of Kenya ...

rufiji environment management project - Coastal Forests of Kenya ...

rufiji environment management project - Coastal Forests of Kenya ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

REMP Technical Report 40: Rangeland Resources in Rufjiji<br />

Kwa ujumla matokeo hayo yanahusu upimaji wa nyasi tu, yanaonyesha kwamba Rufiji ina maeneo<br />

machache yanayoweza kulisha mifugo katika usimamizi wa aina ya “extensive” yaani eneo kubwa<br />

linahitajika kwa wanyama wachache. Maeneo mengi yaliyotathminiwa yalionyesha kuwa yana uoto<br />

mzuri wa nyanda za malisho kwa sababu pengine yalikuwa hayajatumika na wanyama kwa muda<br />

mrefu. Mengine yalikuwa na mapungufu/ au matatizo yaliyojitokeza.<br />

Maeneo ya nyanda za malisho yanayoweza kufikiriwa kuwa yanafaa kwa idadi kadhaa ya mifugo<br />

yametajwa. Eneo lo lote lisitumike kama nyanda za malisho kabla ya tathmini kufanyika kwa<br />

wanyama kulisha katika eneo husika kwa muda maalaum. Kabla ya eneo kutangazwa kuwa nyanda za<br />

malisho utafiti wa kina wa kijamii na kiuchumi lazima ufanyike. Miundo mbinu kwa ajili ya mifugo<br />

katika maeneo yote zilikuwa hakuna. Utafiti huu umeorodhesha mahitaji ya kila kijiji ikijumuisha<br />

majosho, maeneo ya maji, uzuiaji wa mbung’o. Minada inayohitajika na mapendekezo ya wapi<br />

kujengwa yametajwa.<br />

Ushauri ufuatao umependekezwa ili kusaidia Halmashauri ya Wilaya kutengeneza mkakati wa<br />

Kusimamia na Kuendeleza Ufugaji Endelevu.<br />

• Halmashauri ya Wilaya itoe tamko la kuzuia uingiaji wa wafugaji wa asili kutoka Mikoa<br />

mingine hadi hapo Halmashauri, ikishirikiana na vijiji vikamilishe Mkakati wa Kusimamia na<br />

Kuendeleza Ufugaji ambao utatoa matumizi bora na endelevu ya Nyanda za Malisho yaliyopo.<br />

Wakati huo huo wafugaji jadi ambao wamekwishaingia inabidi washirikiane pamoja na wenyeji<br />

wa maeneo husika ili kutenga mipaka kwa ajili ya kugawa maeneo kwa matumizi mbali mbali<br />

kama vile maeneo ya kilimo, uvuvi, misitu, malisho, vyanzo vya maji na njia za mifugo.<br />

• Ramani za uoto wa asili zianzishwe ili zisaidie kama mwongozo kwa Halmashuri ya Wilaya<br />

katika kupanga mipango, utekelezaji na uchanganuaji wa matokeo yaliy<strong>of</strong>anywa juu ya Utafiti<br />

wa Nyanda za Malisho. Kwa taarifa hizo Halmashauri ya Wilaya pamoja na vijiji vitaweza<br />

kufanya maamuzi yanay<strong>of</strong>aa hususan usimamizi wa nyanda za malisho yanahitaji kuhusu<br />

mabadiliko ya uoto, msimu hadi msimu. Taarifa za takwimu yazingatiwe mabadiliko<br />

yanayoweza kufuatana na uchomaji moto malisho na wafugaji wa jadi. Hii inaweza kuwa moja<br />

ya njia ya kuelewa matokeo yanayosababishwa na uchomaji moto kwa Wilaya nzima.<br />

• Halmashauri ya Wilaya itenge maeneo ambayo wafugaji wa jadi hawaruhusiwi kuingia na<br />

kukaa, kuruhusiwa kuchungia kwa misimu/majira mbali mbali, kuruhusiwa kwa masharti<br />

yaliyolotolewa na Halmashauri au sheria ndogo za vijiji. Wilaya izingatie kanuni za tahadhari<br />

zinazohusu uzuiaji wa wafugaji wa jadi kuingia katika maeneo ambayo yana wingi wa<br />

bioanuai.<br />

• Pia iwekwe taratibu na kanuni za pekee kuepuka uharibifu wa mazao na upondaji wa miche<br />

katika tambarare ya Mafuriko. Kilimo cha Mlao kitakuwa kigeni kwa wafugaji wa jadi wengi.<br />

• Watumiaji wote wote wa nyanda za malisho wanashauriwa wakae pamoja ili kujadili, kuratibui<br />

na kukisia mabadiliko. Kwa asili mabadiliko mengi ni ya muda mrefu, hivyo mipango ya<br />

kuratibu mbuga inafaa iwe ya muda mrefu. Inafaa watumiaji wa nyanda za malisho wakae<br />

mara kwa mara ilio kujadili na kupima hali ya nyanda kwa vipindi maalum. Halmashauri ya<br />

Wilaya iwe na mpango na bajeti kwa ajili ya kuratibu masuala hayo na inafaa watafutwe<br />

wahisani waweze kusaidia.<br />

• Wafugaji wa jadi, wakazi wa vijiji husika na wataalam wa ugani inafaa wafikirie mahitaji ya<br />

watumiaji wengine wa Nyanda za malisho na ardhi kama vile wachota maji, wavuvi, vimelea<br />

vya mimea na wanyama wadogo, ukadiriaji wa idadi ya mifugo ambao wanaweza kutunzwa<br />

vi

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!