12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.


BARUA YA MHARIRI

Hello!

Mpendwa msomaji, natumai ni mzima wa

afya na mwingi wa furaha kuwasiliana na

wewe tena katika toleo hili la pili. Nashukuru

kwa kuendelea kuwa sehemu ya wasomaji

wetu tangu tulipotoa toleo la awali, bila wewe

jarida hili halina maana yoyote.

Maoni yaliyotolewa katika jarida lililopita

yametusaidia sana kuboresha toleo hili,

kuanzia usanifu, agenda na idadi ya kurasa.

Tutaendelea kupokea maoni na kuyafanyia

kazi kwa kadri tutakavyoweza. Lengo ni

kuwapa vitu bomba; vyenye kuelimisha,

kuburudisha na kukupa hamasa ya kuwa

sehemu ya mabadiliko katika jamii.

Toleo la pili limejikita katika mambo ya

kidijitali. Kama tunavyofahamu, siku hizi kila

kitu ni kidijitali. Tanzania ni moja ya nchi

ambazo matumizi ya intaneti na simu za

mkononi yanakua kwa kasi kubwa.

Watumiaji wakubwa ni vijana kuanzia miaka

18 mpaka 35. Licha ya fursa lukuki zilizopo

katika ulimwengu wa teknolojia ya kidijitali, ni

vijana wachache wanaochangamkia na

kuzifikia fursa zilizopo. Walau kwa vijana wa

kiume, kwa wakike bado wapo nyuma zaidi.

Toleo hili ni mahsusi kukufungulia njia kijana

mwenzetu kusanuka na kuzibaini fursa

zilizopo ili kukabiliana na tatizo la ajira

ambalo vijana ni wahanga wakubwa.

Nakukaribisha katika ulimwengu wa fursa.

Hassan Kiyungi

2 | MEMA MAGAZINE AUG 2021


YALIYOMO

05 STORY ZA MTEMBEZI | KUNANI MUHEZA?

07 CHIMBO | FURSA ZA KIDIJITALI

09 MMOJA KWA MMOJA

| FURSA NDANI YA UDAKU

14

10 JIBEBE | IMANI NSAMILA: SAFARI YA BWANA LENS

12 TUBONGE | MASWALI NA MAJIBU KUHUSU DIJITALI

13 KOLEZO

| URAIBU WA KIDJITALI, TUNATOBOAJE?

14 GENGE | G.NAKO: MWEUSI MWENYE LADHA ADIMU

16 SOCIAL HIT

| HABA NA HABA HUJAZA KIBABA

19

17 KIZAZI KIPYA | MWAISA MTU MBAD NA STORY ZA MAWIFI

19 WAKILISHA

| TWENZETU MIKOCHENI

MSAFIRI MWENYE VIPAJI LUKUKI | VIPAJIKA

WANAWAKE NA DIJITALI | SAUTI YA MTAA

NDOTO YA MWANDISHI KWA DAKTARI R!SE

|

SMART CLASS, BUKUA KIDIJITALI | UBUNIFU

21

23

24

27

24 10

16 27

7

3 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE


LAMEMANS

TUFUATE

Mema Magazine ni jarida linalotoka kila

baada ya miezi minne kwa lugha ya

kiingereza na kiswahili. Ni jarida

linalopatikana kwa njia ya mtandaoni na

nakala ngumu. Tufuatilie katika mitandao ya

kijamii ili kuwa wa kwanza kujipatia nakala

yako.

PAKUA JARIDA

www.memayouth.org/magazine

www.issuu.com/memamagazine

www.issuu.com/memamagazine

MAWASILIANO

S.L.P 36397, Dar Es Salaam

Whatsapp: +255743 813972

Simu/SMS: +255783 765953

mematanzania@outlook.com

MKURUGENZI MTENDAJI

HASSAN KIYUNGI

MHARIRI MKUU

NANCY MBOGORO

MHARIRI MSAIDIZI

ELIAS MAEDA

MHASIBU

ADIOS O. KAKILA

WAPIGA PICHA

MOHAMMED KAYUNGI

IMANI NSAMILA

DIONIZY SHOTS

WACHANGIAJI

ZENA MCHOME

ABBASI ISMAIL

GILLSANT MLASEKO

SECILIA BASILIO

MEDIA CRAFTERS

KATUNI

MWENDA ART

USANIFU

KUZA CREATIVE

UCHAPISHAJI

HNP PRINTING

@MemaMagazine

MUHIMU

Yaliyomo humu ndani ni jukumu la

Mema Tanzania ambao ni

wazalishaji na wasambazaji wa

jarida la Mema na hayawakilishi

mitazamo au maoni ya wafadhili au

wadhamini.

4 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

@MemaTanzania

MAGAZINE

Mema Magazine linachapishwa na kusambazwa na

taasis ya Mema Tanzania. Jarida hili haliuzwi, na

linasambazwa bure kwa njia ya mtandoni na nakala

ngumu. Pindi upatapo nakala hii tafadhali shirikisha na

marafiki zako wa karibu ili kupata elimu. Unaruhusiwa

kuchapisha kwa lengo la kutoa elimu tu na si kwa

biashara.

MEMA TANZANIA TOLEO No. 2 AUG, 2021


Waja leo, huondoki leo

ABBASI ISMAIL

Mambo vipi washikaji? Naitwa Abbasi maarufu Abby boy. Ni

mzaliwa na mkazi wa Muheza, mkoani Tanga. Leo

nakutembeza Muheza ujue yale usiyoyajua. Muheza ni wilaya

kongwe nchini ilianzishwa mwaka 1976. Kihistoria kulipiganwa

vita kati ya Wabondei na Wadigo katika pwani ya Tanga.

Wabondei walichakazwa na kukimbilia maeneo ya Muheza na

walipofika hapo walisema “Hanu Mheza” ikimaanisha hapa

mmekwisha. Kweli Wadigo waliufuata moto kwani

walitembezewa kichapo na kurudi pwani ya Tanga na mpaka

leo Wadigo wapo wengi Tanga mjini na Wabondei wakabaki

kama wenyeji hapa Muheza.

Ukipita Muheza utakuta imepambwa na mandhari ya kuvutia

yenye milima, mito na majengo ya kihistoria yaliyoachwa na

wakoloni. Wilaya ya Muheza ina mitaa mingi maarufu ikiwemo

Magila ambapo kuna shule ya kwanza ya msingi kujengwa

hapa nchini wakati wa ukoloni. Mitaa mingine ni Tongwe,

Ngomeni, Pande, Mtimbwane n.k. Wilaya yetu ina ukubwa wa

eneo la kilomita za mraba 1,470.

Mishe za kibiashara zipo kibao, muhimu kuchangamkia fursa.

Kuna mishe za kilimo kama machungwa, katani n.k. Muheza

ina vivutio vingi vya utalii ikiwemo misitu maarufu ya Amani na

Magoroto maarufu Bali of Africa. Huko kuna mambo mengi ya

kupendeza ambayo huwezi kujutia ikiwemo maporomoko ya

maji, bwawa zuri la kuogelea, wanyama kama farasi na ndege

wengi wazuri. Msitu wa hifadhi ya Amani una vipepeo wa

pekee duniani ambao wananchi huwafuga na kuwauza nje ya

nchi.

5 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Hamis Mwinjuma maarufu Mwana FA ni

mbunge na moja ya watu maarufu kutoka

Muheza.




Anasema "Mwanzoni nilikuwa na wateja

wachache na kupelekea kupata hasara mara

kadhaa. Nikaamua kuongeza wateja wapya

na njia rahisi niliona ni mitandao ya kijamii.

Nilifungua akaunti Instagram ndipo kasi ya

wateja ikaongezeka kutoka mikoa ya jirani na

kuniongezea mtaji mpaka wa Tsh milioni 5.”

Kuna vijana pia ambao wanatumia ushawishi

walionao katika mitandao ya kijamii

kutangaza biashara za makampuni,

kuendesha kampeni za taasis na baadhi

wameanzisha kurasa zinazochapisha maudhui

tofauti ikiwemo udaku na kujipatia wafuasi

wengi hivyo kuwafungulia dili za matangazo

ya biashara.

Kabla ya kuolewa mwaka 2018 alikuwa

akijihusisha na mauzo ya bidhaa mtandaoni.

"Nilikuwa nikifanya biashara ya kuuza nguo za

watoto na wanawake. kupitia Instagram. Akaunti

yangu ilikuwa imefikisha wafuasi zaidi ya elfu 10.

Ni biashara nilianza tangu nikiwa nasoma chuo

na nilikuwa na wateja wengi sana. Baada ya

kuolewa mme wangu hakuwa anapendezwa

navyo wasiliana na wateja mara kwa mara.

Kuepusha mikwaruzano katika ndoa yangu

nikaamua kuachana na biashara ile na kuajiriwa

katika kampuni ambayo mme wangu alinitafutia.

Changamoto za kifamilia hasa kwa wanawake

waliolewa kiukweli zinatukwamisha kujihusisha

na mambo ya dijitali labda uwe na mwenza

muelewa na mambo haya" anasema Aisha.

Utawala wa kijinsia

Licha ya fursa lukuki za kidijitali bado sio wote

wananufaika nazo. Utofauti upo zaidi katika

upande wa jinsia ambapo wanawake ni wachache

kuliko wanaume. “Kwa mtazamo wangu sababu

kama kutingwa kwa majukumu ya familia, ukosefu

wa ujuzi, hofu ya ukatili wa kijinsia zinachangia

wanawake kuwa wachache” anasema Dkt Julieth

Sebba, moja ya vijana wenye ushawishi katika

mtandao wa Twitter. Mtazamo wake unaungwa

mkono na Mariam, mkazi wa Tanga. ambaye

anaamini uchache wa wasichana na wanawake

katika dunia ya kidijitali inachangiwa na uoga wa

kushambuliwa mitandaoni hali inayowarudisha

nyuma katika kuzifilkia fursa zilizopo katika

mitandao ya kijamii.Aisha mkazi wa Tabata jijini

Dar Es Salaam, ni kijana mwenye umri wa miaka

32 ni mke na mama mwenye mtoto mmoja.

8 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Sheria ya ngoma

Mafanikio hayaji haraka na kwa urahisi hasa

katika kuzifikia fursa za kidijitali. Unahitaji kutia

bidii katika kujifunza ujuzi fulani, hata kama ni

kutangaza biashara yako mtandaoni unapaswa

kufahamu namna gani ya kuandika maudhui,

muda gani, nani unayemlenga n.k.

Jinsi unavyofanyia kazi ujuzi wako ndivyo

unavyozidi kuwa na uelewa wa kutosha na jamii

itatambua ujuzi wako hivyo fursa zitaanza

kukufikia. Jipe muda kujifunza, usikate tamaa.



JIBEBE

IMANI NSAMILA

SAFARI YA BWANA LENS NA

MSIMULIZI WA MAZINGIRA

PETER LAZARO

Mwanzo wa Safari

Naitwa Imani Nsamila, ni mpiga picha na

mwanaharakati wa mabadiliko ya tabia nchi.

Tangu nikiwa mdogo napenda kupiga picha.

Wakati nipo shule ya sekondari baba yangu

alikuwa na kamera ndogo ambayo alikuwa

akiitumia katika ofisi yake.

Nikawa naichukua naenda kuwapiga picha

marafiki zangu ambao walikuwa wana bendi

ya muziki, baadhi ya picha zao mpaka leo

ninazo. Awali nilikuwa nafanya tu kwa

mapenzi, nilipomaliza sekondari nikachagua

kusomea fani ya utengenezaji wa filamu

katika chuo cha Kilimanjaro Film Institute

katika jiji la Arusha. Nikiwa mwaka wa tatu

sikufanikiwa kumaliza chuo, nilipata ajali na

kuvunjika mkono. Ilinilazimu nirudi nyumbani

Dar Es Salaam na madaktari walinishauri

nisibebe vitu vizito, ingekuwa ngumu

kuendelea na mafunzo ya utengenezaji filamu

kutokana na kamera tulizokuwa tunatumia

katika mafunzo zilikuwa ni nzito.

Wakati nipo nyumbani nikawa nahudhuria

katika mtandao wa vijana uliofahamika kama

Youth Climate Activist Network uliokuwa chini

ya Norwegian Church Aid. Walikuwa na

programu ya Climate Change Caravan na

tulikuwa tunazunguka maeneo tofauti nchini

kutoa elimu ya mabadiliko ya tabia

nchi.Kipindi cha ugonjwa na baada ya

ugonjwa niliendelea kuwa najitolea kama

mpiga picha.

Novemba 2014 nilitolewa vyuma mkononi na

kurudi katika maisha yangu ya kawaida.

Nikaendelea na shughuli za kupiga picha,

nikawa nakutana na watu tofauti katika mishe

zangu. Mwaka 2015 nilipata kazi ya kushoot

katika taasisi fulani ambao baada ya

kumaliza walipenda sana kazi yangu.

Nashukuru Mungu nimeendelea kupata fursa

tofauti ambazo nyingi zinatokana na watu

ambao nilifanya nao kazi kunipendekeza

zinapojitokeza fursa.

Mfano mwaka 2017 nilibahatika kushuhudia

uchaguzi wa Liberia kama mpiga picha,

uchaguzi ambao ulimpa ushindi aliyekuwa

mchezaji mpira maarufu George Weah.

10 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE


Tujibebe

Kila mtu ana njia yake katika kufikia mafanikio. Bado

na ndoto ya kutimiza mambo mengi katika kazi

yangu, na hata hapa nilipofika nashukuru Mungu.

Binafsi mambo yafuatayo yamechangia kunipa

mafanikio niliyonayo sasa na pengine hata wewe

kijana mwenzangu yanaweza kuchochea ndoto

yako ya kuwa mpiga picha mashuhuri;

Michongo

Katika picha kuna fursa nyingi. Dunia

imehamia katika teknolojia na huwezi

kutenganisha picha na teknolojia. Upigaji picha

imekuwa inachangia sehemu kubwa katika

kusukuma agenda mbali mbali za kisiasa na

kijamii. Kuna fursa za kifedha lakini pia

inaweza kukupenyeza katika fursa

usiyoitegema. Kwa mfano ukihudhuria

mkutano mkubwa wa kimataifa mbali ya pesa

utakayolipwa lakini yale yatakayokuwa

yanazungumzwa utayasikia na kujifunza pia.

Kamera inakupa elimu mpya kila siku ambayo

inakufungulia fursa kibao.

Sasa hivi pia biashara zinahamia kwenye

mitandao ya kijamii. Nyenzo muhimu

inayohitajika ni picha, hivyo kwa mpiga picha

kuna dili utazipata kwa watu wanaofanya

biashara mtandaoni. Binafsi kuna programu

naifanya inayowezesha vijana wa kike

kujifunza upigaji picha na kufungua fursa kwa

upande wao kwa sababu tasnia ya picha

imetawaliwa na wanaume zaidi. Pia picha

inakusaidia kusafiri maeneo tofauti na

kujifunza mila na tamaduni za watu.

Nimefanikiwa kufika Germany, Netherlands,

France, Belgium, Czech Republic, Zimbabwe,

Italy n.k. na kote nimejifunza mambo mengi.

Kupenda unachokifanya. Hii kazi yetu unahitaji

kuipenda sana ili inapotokea hata kazi nyingi

zimekutinga una enjoy kwa sababu ni kitu

unachokipenda. Imenisaidia sana katika upigaji picha

kwa sababu siku zote ni kazi naifanya kutoka moyoni.

Muda mwingi nafanya kazi, na safiri mara kwa mara

sipumziki. Kwangu sioni tatizo kwa sababu na enjoy.

Kujitahidi kujifunza kupitia watu na kuwekeza kwenye

elimu. Kuna wengine wamepata bahati ya kusoma

chuo na wengine mitandaoni. Lakini kwa namna

yoyote uwe ni mtu wa kuitafuta elimu ya upigaji picha.

Elimu isiwe tu ya upigaji picha, kujifunza mambo

mengine kwa sababu kama mpiga picha lazima

utambulike wewe ni mpiga picha wa namna gani.

Kuna mteja anaweza kuhitaji picha ambazo zitatoa

elimu ya mabadiliko ya tabia nchi na wewe hujui nini

maana ya mabadiliko ya tabia nchi hawezi kukupa

kazi. Ukijifunza mambo tofauti ndivyo wateja tofauti

watakufuata kwa sababu ya uelewa wako wa mambo

tofauti.

Kujenga mahusiano na watu. Hizi kazi watu wanavyo

kuzungumzia wakati haupo ndio zinasaidia ndio

inavyoamua kufunga au kukufungulia fursa.

Mahusiano bora ndio kila kitu katika maisha.

Kuchagua unataka kuwa mpiga picha wa namna gani.

Mwanzoni wakati unaanza unaweza kuwa unapiga tu.

Baadae ukachagua ujikite eneo gani ambalo watu hata

wakitaja jina lako wanajua wewe ni mpiga picha wa

aina gani. Inaweza kuwa michezo, sherehe, sanaa n.k.

11 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE


ULIZA UJIBIWE

NA ELIAS MAEDA

Je, una swali kuhusu

masuala ya kidijitali?

Tucheki kupitia Whatsapp

na tutakupatia majibu

haraka. Namba ipo katika

ukurasa wa 4.

Mambo vipi? Naitwa Hadija, ni mkazi wa Arusha.

Swali langu, nafanya biashara ya vipodozi nawezaje

kuwafikia wateja wengi katika mitandao ya kijamii?

Kabla hujafikiria kuwafikia wateja kwanza hakikisha

kuwa umetengeneza ukurasa wako kwa namna

ambayo watu wataamini huduma au bidhaa unazouza.

Njia ya haraka ya kufikia wateja wengi ndani ya muda

mfupi ni kwa kulipia matangazo au kuwalipa watu

mashuhuri wakutangazie. Kama kipato chako ni kidogo

unaweza kuanza tu wewe mwenyewe na

kujitengenezea wafuasi wako ambao pia ndio wateja

wako.

Mimi naitwa Zainab naishi ilala. Ninauza mitandio

ya wanawake, nifanyaje akaunti yangu iwe na

followers wengi ?

Unapofanya biashara mtandaoni haupaswi

kuhadaika zaidi na followers. Kumbuka kuwa wewe

upo mtandaoni kutafuta wateja na sio followers.

Wateja wako ndio watakuwa followers wako. Weka

nguvu zaidi kuwafikia watu wengi; kidogo kidogo

utapata wateja ambao watakuwa wanafatilia

biashara yako na hao ndio watakuwa followers wako.

Mtandao upi wa kijamii ni mzuri kwa mimi nayeuza

mchele? Rajab Selaman, Tanga

Swali zuri sana. Mitandao yote ni mizuri ila kwa

mfanyabiashara ni lazima kuzingatia wateja wa bidhaa

au huduma zako wapo wapi zaidi. Mitandao mikubwa

zaidi ni Facebook, Twitter na Instagram; hii mitandao

ina aina zote za watu japo kuwa kwa sasa Instagram

na Facebook inatumika na wengi zaidi Tanzania.

Binafsi ningeshauri uwekeze zaidi kwenye mitandao

hiyo mikubwa mitatu ila chagua mmoja wapo wa

Mwaka huu namaliza chuo na napenda sana

mambo ya digital. Ujuzi gani naweza kujifunza na

kuniingiza hela haraka?

kuanza nao. Hongera sana Andronicus. Sijajua ulivyosema

'haraka ni uharaka wa kiasi gani ila binafsi naamini

kiwanda cha digitali kina fursa nyingi na ni vyema

ukazingatia kujifunza na kupata uzoefu wake kabla

ya kuwaza kupata hela haraka. Hata hivyo, hizi ni

baadhi ya fursa na ujuzi ambao yanaweza kukupa

kipata cha haraka ukiwe kufanya kwenye ubora;

graphics designing, content creation, social media

management, masoko ya mtandaoni

Utaratibu wa kodi TRA ukoje kama nikiwa nauza

biashara yangu online tu? Jennifer, Dar

Sina elimu kubwa sana ya kodi, ila binafsi naamini

kuwa kwa biashara yoyote ile halali ambayo inaingiza

kipato ni lazima itambulike kisheria na kuchangia kodi.

Naelewa hili swala ni gumu kidogo haswa kwa

wanaoanza biashara, ila unaweza kujipanga taratibu

na ukaangalia ni namna gani unachangia kodi au

kufika ofisi za TRA kwa ushauri zaidi. Nadhani wao

wanaweza kuwa na

jibu zuri zaidi.

Naona kuna watu huwa wanauza akaunti.

Nikinunua akaunti na biashara yangu nikahamishia

huko ni sawa? Abdul, Chanika

Sio sawa na wala sikushauri kufanya hivyo. Wewe

upo mtandao kutafuta wateja na sio followeres.

Tengeneza ukurasa wako wa biashara na utakua

taratibu, utakuletea wateja na hao ndio watakuwa

followers wako wa kweli. Wewe unauza biashara ya

mayai unaweza ukaenda kununua ukurasa wenye

wafuasi wengi ukiamini kuwa umepata wateja

kumbe hao wafuasi waliufata huo ukirasa sababu

ulikuwa ukisambaza maudhui ambayo hata

hayaendani na biashara yako.

12 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE


Uraibu wa Kidijitali,

tunatoboaje?

MEDIA CRAFTERS

KOLEZO

Tunatoboaje washikaji?

Umewahi kusikia au kukutana

na neno Detox ?! Tukiwauliza

wataalamu wa afya , watasema

ni utoaji au uepukaji wa sumu

mwilini(huweza kuwa na

maelezo zaidi ya haya).

Sasa kuna kitu kinaitwa Digital

detox. Digital Detox ni kuepuka

au kusitisha matumizi ya vifaa

na majukwaa ya mawasiliano

na habari kwa kipindi fulani ili

kuruhusu muingiliano zaidi na

jamii yako au huweza kuwa

sababu nyingine pia.

Wengi wanaofanya digital

detox hudhamiria kupunguza

/kuondoa digital addiction

(uraibu wa kidijitali); ambao

wenyewe huwa ni matumizi

yaliyopitiliza (na kushindwa

kabisa kujizuia) ya vifaa,

teknolojia na majukwaa ya

kidijitali na hasa mitandao ya

kijamii.

Uraibu wa matumizi ya vifaa

vya kidijitali imekuwa na athari

lukuki ikiwemo kuchelewa

kazini, ajali za barabarani,

kupunguza ubunifu na

uzalishaji, msongo wa mawazo

kutokana na kujilinganisha na

yale unayoyaona katika

majukwaa ya kidijitali n.k.

Digital detox huweza kuwa na

faida nyingi ikiwemo, kukupa

nafasi zaidi ya kujichanganya

na jamii yako, kukupa muda

zaidi wa kufanya shughuli zako

za kikazi au mazoezi.

Kuacha au kupunguza matumizi ya vifaa na

majukwaa ya kidijitali sio jambo la siku moja.

Kumbuka huu ni uraibu kama matumizi ya

madawa ya kulevya au sigara, unahitaji muda

kuweza kupona. Unahitaji muda wa kujifanyia

tathmini binafsi na kujua ungependa uishi vipi

na dunia ya kidijitali pasipo kukuacha na uraibu.

Unaweza kutumia mbinu zifuatazo kama

mwongozo wa kuacha au kupunguza tatizo

uraibu wa majukwaa na vifaa vya kidijitali hasa

simu;

Zima 'notifications'

Hizi ni taarifa ambazo unazipokea kutoka katika akaunti za

majukwaa ya kidijitali ambayo unayafuatilia kama Facebook,

Instagram, Youtube n.k. Unapozima ‘notifications’ inakusaidia

kupunguza shauku ya kujua yale yanayoendelea katika majukwaa

ya kidijitali na kuwekeza muda wako katika mambo mengine.

Jichanganye na watu

Vifaa vya kidijitali hasa simu vimetusogeza karibu kiasi kwamba hatuoni

umuhimu wa kutembeleana na kukaa pamoja kwa sababu

tunawasiliana katika whatsapp groups, Facebook n.k. Muda ambao

huna kazi ya kufanya tembelea marafiki, ndugu au majirani. Itakusaidia

kuboresha mahusiano na watu na kuepuka tatizo husika.

Usilale na simu

Kwa mujibu wa mtandao wa Time To Log Off, zaidi ya asilimia 45%

ya watu hutumia simu badala ya kulala wanapokuwa kitandani. Hii

inachangia kukosa muda wa kutosha wa kulala na kuathiri mwili na

akili. Unapoweka simu mbali kwa mfano chumba tofauti itakupa

ugumu kuweza kuifuata mpaka ukiwa na matumizi nayo muhimu tu.

Kuwa na ratiba maalum

Nafahamu inaweza kuwa ni rahisi kwa kusema lakini si kwa kufanya.

Moja ya dalili kubwa ya uraibu wa mitandao ya kijamii ni kufikiria sana

uchapishe maudhui gani au kufuatilia muda wote nani kachapisha nini,

unakosa hadi raha simu ikizima chaji au ikiishiwa bando. Hii

inakusababishia msongo wa mawazo. Usianze na pupa. Unaweza

kuweka ratiba wiki ya kwanza kila siku utatumia mitandao ya kijamii

masaa 6 tu au utatumia kuanzia saa 8 mchana mpaka saa 2 usiku.

Kila wiki ukipunguza saa 1 taratibu utaondoa uraibu na kuzoea kabisa.

13 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Leo tumeamua kukoleza na hizi mbinu chache tu. Kumbuka hizi mbinu sio sheria, unaweza

kubuni mbinu zako kulingana na mazingira au majukumu uliyonayo. Kikubwa sote tuweze

kushinda tatizo hili. Mbinu gani unadhani kwako zinafaa kuweza kupambana na uraibu wa

matumizi ya vifaa na majukwaa ya kidijitali? Tutumie ujumbe kwa njia ya Whatsapp au SMS

kupitia namba zilizopo katika ukurasa wa mawasiliano tupeane madini zaidi. Amini mtu

wangu..!




SOCIAL HIT

‘Mwaka jana (2020) nilipanga kununua friji lakini

kila nikipata hela inakwenda kufanya matumizi

mengine. Siwezi kununua vyakula vingi sababu

vitaharibika hivyo inanilazimu kununua mahitaji

kidogo kidogo ambayo ni gharama kuliko kununua

kwa jumla’ anasema Prisca, kijana mwenye miaka

28 na mkazi wa Kinondoni jijini Dar Es salaam.

Licha ya kufanya kazi na kupata mshahara mzuri,

Prisca ameshindwa kutimiza lengo lake la kununua

friji zaidi ya mwaka mmoja sasa. Hata wewe

pengine una lengo fulani lakini kila ukipata mtonyo

unaishia kwenye matumizi mengine ikiwemo kulipa

madeni.

Tunzaa App!

Aplikesheni inayodhamiria

kuboresha tabia chanya

ya kutunza fedha.

Kutatua changamoto hii Tunzaa Fintech ambayo

ni kampuni changa inayomilikiwa na vijana

wazawa wa kitanzania wamezindua App

inayolenga kuimarisha tabia ya kutunza fedha

kwa watanzania. “Mwaka 2019 tulitembelea Tanga

na Dar kuzungumza na wanawake pamoja na

wanaume ili kuelewa wanapopata pesa

wanazitunza vipi na wanazitumia namna gani. Kati

ya watu tuliozungumza nao vipato vyao kwa

mwezi vilikuwa ni kati ya laki 3 mpaka milioni 6.

Lakini pia moja ya maswali ambayo tulikuwa nayo

ni watu hawatunzi pesa kwa sababu ya matumizi

mabaya, hawana njia nzuri na rahisi za kutunza

fedha na watu wengi hawarudishi kabisa pesa

wanazokopa au hawarudishi kwa wakati”

anasema Ngw’inula Kingamkono ambaye ni

mtaalamu wa teknolojia na mkurugenzi mtendaji

wa Tunzaa Fintech. Wazo la kuja na app ya

Tunzaa lilitokana na changamoto za watanzania

wengi kutokuwa na tabia ya kutunza pesa na

kuziba mwanya wa ukosefu wa njia rahisi, salama

na ya haraka ya kuhifadhi pesa pindi mtu

anapotaka kununua bidhaa kwa malipo ya kidogo

kidogo.

“Sisi hatukutunzii pesa yako. Unapojisajili katika

app ya Tunzaa unachagua aidha Tunzaa au

Nunua Sasa. Ukichagua Tunzaa maana yake

bidhaa au huduma uliyoichagua unahitaji

kuinunua kwa kutunza pesa kidogo kidogo

kulingana na wewe ulivyochagua iwe malipo kwa

siku, wiki au mwezi. Pesa unayolipa inakwenda

moja kwa moja kwa muuzaji husika. Unaponunua

bidhaa unapata point ambazo unaweza kuzitumia

kununua bidhaa au huduma sehemu fulani.”

anaongezea Ngw’inula Kingamkono. Ili mtu aweze

kuwa muuzaji wa bidhaa au huduma, Tunzaa

Fintech hupitia taarifa zote muhimu na pindi

wanapojiridhisha muuzaji ana uwezo wa

kupandisha bidhaa au huduma yake. Malipo

yanafanyika kwa njia ya simu kwa mitandao iliyo

kwenye orodha ya Tunzaa App. Ili kuweza

kuituimia Tunzaa App inabidi kupakua app kisha

kufuata hatua rahisi za kujisajili.

16 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Kwa sasa Tunzaa App inapatikana katika Google

Playstore (kwa simu zenye mfumo wa Android) na

iStore kwa simu za iPhone.“Sisi bado ni kampuni

changa hatuwezi kuanza mikoa yote kwa mara

moja. Tulichagua kuanza na Dar kwanza kwa

sababu ya watumiaji wengi wa simu janja na

uelewa wa masoko ya mtandaoni ni mkubwa.

Lakini pia kutupa urahisi wa kuthibitisha taarifa za

wauzaji” anamalizia Ngw’inula Kingamkono

maarufu pia kama Unu. Watoto wa mjini Tunzaa

app tunaita ni kibubu cha kidijitali. Pakua kisha

furahia maisha.


KIZAZI KIPYA

Afisa Misitu mvunja mbavu

MEMA TEAM

Binafsi sipendi sana kujulikana kwa sababu ya

kazi na napenda kuwa na maisha binafsi.

Hakika Nyonyoma

Babe Mama aibua mgodi

Naitwa Hakika Nyonyoma Mwapongo, wengi mnanifahamu kama Mwaisa Mtu Mbad. Safari ya kuanza

kutambulika kama mchekeshaji ilianza mwaka 2018-2019. Nilianza kuchekesha kwa kutumia wanyama

tangu muda mrefu lakini sikuwa na post kwa sababu ya ofisini, si unajua ofisi za umma ingeonekana

sipo serious na kazi. Mara nyingi nilikuwa nafanya vinaishia for fun. Nilikuwa nikizitengeneza nampatia

baby mama wangu, si unajua Mwaisa mambo ya Mtu Mbad kumchekesha mama watoto. Yeye alikuwa

akizi share katika mitandao ya kijamii kama Whatsapp Status na Instagram. Marafiki zake walikuwa

wakiziona wanazipenda, eeh shemeji shemeji kwanini usipost kwenye page yako. Eeeh Mwaisa

sokapohapa, mimi nafanya for fun tu. Baada ya baby mama kuni shawishi sana ndiyo nikaanza kuzipost

kwenye page yangu ya Instagram. Baada ya miezi kama mitatu Nyonyoma Mtu Mbad nikaanza

kusambaa kwenye mitandao.

Mawifi wa kinyakyusa si mchezo

Nakumbuka kuna video nilitumia ya samaki aina ya Penguin wakionyesha tabia

ya mawifi wa Kinyakyusa. Nyonyoma alimpeleka mchumba wake Mbeya

kwenda kumtambulisha nyumbani kwao. Basi wakawa wanamdhihaki, “we

Nyonyoma yaani unaleta kibonge na ujanja wote huo” ile video ika-trend

kinoma. Kuanzia hapo watu wakaanza kufuatilia kwa wingi page yangu na

video watu wakawa wanazi share katika mitandao tofauti.

Wanyama na sauti

Kitaaluma mimi ni Afisa Misitu, wanyama nakutana nao katika kazi

zangu mara kwa mara. Kwangu haikuwa ngumu kuchagua mtindo wa

kuwatumia wanyama na kuingiza sauti kwa sababu wanyama

nawafahamu vizuri. Lakini pia tangu utotoni nilikuwa ni mtu wa utani,

tunaweza kuwa tumekaa nje na kina mama ghafla kuku akipita naanza

kumuigiiza kama mtu anaongea, basi watu watacheka. Sanaa yangu

inawasilisha maisha ya watu tofauti. Wanafunzi wa chuo ni mashabiki

wangu wakubwa kwa sababu huwa nazungumzia changamoto zao

nyingi, si unajua mtu anadaiwa ada, boom limechelewa au kazinguana

na mwalimu wake. Video zangu huwa zinagusa maisha yao halisi.

17 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE


Ndoto iliyotimia haraka

Wakati naanza ku-share vichekesho vyangu sikutegemea ningepata umaarufu haraka hivi, nilijua

itachukua muda mrefu na nilikuwa na imani ipo siku. Nashukuru Mungu watu wamepokea kazi zangu

vizuri. Umaarufu umenisaidia kunifungulia fursa nyingine nyingi kama kupata connection na watu tofauti,

kupokea dili za matangazo na kusambaa kwa brand yangu ya mavazi ya Mwaisa. Watu mpaka wilayani

ndani huko wanaijua.

Kuficha utambulisho

Binafsi sipendi sana kujulikana kwa sababu ya kazi na pia napenda kuwa na maisha binafsi. Napofanyia

kazi asilimia kubwa mwanzoni walikuwa hawajui kama Nyonyoma Mtu Mbad ndiyo mimi. Kuna muda

nilikuwa nawakuta wanacheki video zangu tunacheka bila kujua ndiyo mimi. Baada ya kuanza kufanya

mahojiano na vyombo tofauti vya habari ndiyo wakaanza kunifuatilia.

Mahojiano yangu nilikuwa naficha sura kwa kitambaa, sasa waki-zoom wanajiuliza mbona huyu jamaa

anafanana jina na sura na mshikaji tunayefanya nae kazi? Nikawa nakwepa kwepa baadae wakajua

ndiyo mimi. Ila maeneo mengine watu hawanifahamu kwa sura.

Watu wanacheka lakini maisha yanabadilika

Sikutegemea wakati naanza kama vichekesho vyangu vitabadili maisha ya watu. Kwa mfano

kuna mtu alinipigia simu kutoka Dodoma alikiri ndoa yake ilikuwa inayumba.

Ilifikia mahali mke wake alirudi mpaka nyumbani. Jamaa akawa anamtumia video

zangu na kumkumbushia kipindi walivyokuwa wakifurahi pamoja wakati wakizitazama.

Kweli mwanamke akatuliza hasira na mpaka sasa wanaishi pamoja. Kuna mtu pia

alishawahi nitafuta baada ya kutazama video clip nikimulezea nyani anampiga kofi

mwenzake kwa kula mtaji badala ya faida. Yule dada aliniambia ile video ilimsaidia yeye

na mme wake, biashara yao ilisimama kwa sababu ya kula mtaji wa biashara.

Majina yanakua haraka kuliko mafanikio

Tasnia yetu ina chgangamoto nyingi, majina yetu yanakua haraka kuliko mafanikio

tunayopata. Kikubwa kutokuta tamaa, mbele kuna faida nyingi japo itachukua muda.

Lakini pia sanaa yetu inachelewa kukua ukilinganisha na nchi nyingine mfano chukulia

Kenya. Wenzetu vichekesho vya majukwaani (stand up comedy) walianza muda kwetu

tulichelewa kidogo. Vipaji vipo vya kutosha. Kwa sasa mambo yanaanza kubadilika,

tasnia ya vichekesho watu wameanza kuingalia kwa umakini.

Aminia kipaji chako

Mitandao ya kijamii bahati nzuri watu wengi wapo huko. Vijana

wengi wanaitumia kupandisha video zinazoonyesha vipaji vyao

na wanatoka. Cha msingi upende unachokifanya na usikate

tamaa. Halafu matarajio vijana tusiwe nayo makubwa sana

hasa tunapoanza, tuna expect too much tukikwama tunakata

tamaa.

18 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE


ni Kama Njia Maisha

baba, dada, kaka, Maisha tunapitia,

Mama,

kwamba ni karaha, bali ni kuvumilia,

Sio

Shule ya sekondari Mikocheni ni moja ya shule ya kwanza kuwa na Mema

Club nchini tangu zilipoanza rasmi Oktoba 2018. Kuna vijana kibao

ambao walianza kuwa wanachama tangu wakiwa kidato cha kwanza na

mwaka huu wanamaliza kidato cha nne. Ni kama mtoto ambaye tangu

amezaliwa hajawahi kuhama mji, na sasa yupo tayari kukusimulia hadithi

ya tangu utotoni. Pia, Sia na Subira walitema vina na mashairi moto moto.

Naitwa Hassana Ali. Wakati najiunga na club sikuwa

najiamini. Nikiwa kidato cha pili nilichaguliwa kuwa

makamu wa rais wa Mema Club.

Hapo nilionyesha uwezo wangu wa uongozi,

kuliniongezea ufaulu na kuchaguliwa kuwa kiranja wa

elimu. Mema Club siku zote itaendelea kuwa familia

yangu.

Nakumbuka wakati najiunga na klabu tulikuwa

tunafundishwa elimu ya hedhi. Sio siri nilikuwa najihisi

aibu, unawaza washikaji watanichukuliaje kujifunza

mambo yanayohusu wanawake. Taratibu aibu

iliniisha hata washikaji zangu nikawa napiga na

ostory za afya ya uzazi ile fresh tu.

Kuwa sehemu ya klabu kumenibadili sana mtazamo

na kunianda kuwa kijana muwajibikaji.

Naitwa Beatrice Ulindula. Kuchaguliwa kuwa kiongozi

wa Mema Club kulinipa hamasa ya kutambua

nafasi yangu katika jamii ni ipi. Unapokuwa kiongozi

inabidi uwe mstari wa mbele kwa kuonyesha

uwajibikaji kwa watu wengine.

Kuwa kiongozi katika klabu ni mwanzo wa kutimiza

ndoto yangu ya kuwa kiongozi siku za usoni. Safari

yangu inaanzia katika klabu.

Jina langu ni Sarafina Thobias. Kuwa katika klabu

kumenipa nafasi ya kuonyesha kipaji changu cha

kuigiza ambacho watu hawakuwa wanakifahamu.

Maigizo tofauti tumekuwa tukianda shuleni

yenye kuelimisha na kuburudisha. Huu ni mwanzo

wa kutimiza ndoto.

19 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Ushairi

ya Mwanamke Tohara

kale hadi sasa, tohara imesambaa,

Tangu

na bara, wanawake walalama,

Visiwani

na vijana, wote wanalalamika,

Watoto

kwa mwanamke, si sawa nakwambia.

Tohara

wamejaa, ngariba wasio na maana,

Vijijini

vijana, kupata hiyo tohara,

Wanalazimisha

wakiambizana, ushupavu utapata,

Eti

kwa mwanamke, si sawa nina kwambia.

Tohara

nimeshafikia, naanza kuwausia,

Mwisho

kwa nia, kuanza kutokomeza,

Watanzania

kwa rabana, janga hili litaisha,

Naapa

kwa mwanamke, si sawa nina kwambia.

Tohara

Shairi hili limetungwa na Subira Hassna

ni kujipanga, hata kama ni fukara,

Maisha

ni kama njia,kila mtu anapitia.

Maisha

yetu ni ndefu, yapasa kupambania,

Safari

tufue dafu, mbali sana kufikia,

Vijana

ni wafu, na ilhali tuna afiya,

Tusijifanye

ni kama njia,kila mtu anapitia.

Maisha

Shairi hili limetungwa na Sia Kalula

WAKILISHA


Naitwa Rigeye Ally, ni mwanafunzi wa kidato

cha nne shule ya sekondari Mikocheni. Nilikuwa

pia rais wa Mema Club kuanzia mwaka 2019

mpaka 2021. Mimi ni kiongozi na nina jiamini

katika kuongoza. Ndoto yangu ni kuwa daktari

wa binadamu na kiongozi. Wanafunzi

wenzangu huniita Mema, kwa sababu nilikuwa

rais wa Mema Club tangu nikiwa kidato cha pili

mpaka cha nne. Awali sikuwa najua kama nina

karama ya uongozi.

Mara nyingi nilikuwa mstari wa mbele kutuliza

kelele katika klabu na kujitolea kufundisha

wengine masuala ya hedhi. Wanafunzi

wenzangu walianza kuvutiwa na mimi na kisha

wakanichagua kuwa kiongozi wao. Kujitolea

katika kufundisha wenzangu, kunyamazisha

kelele na kuhudhuria siku za klabu kulisaidia

kuaminiwa na kuchaguliwa kuwa kiongozi wa

klabu. Umaarufu wa uongozi wangu ulichochea

pia kuchaguliwa kuwa kiongozi wa mazingira

na afya shuleni.

Kujitolea katika kufundisha

wenzangu,kunyamazisha kelele

na kuhudhuria siku za klabu

kulisaidia kuaminiwa na

kuchaguliwa kuwa kiongozi wa

klabu.

Changamoto niliyopitia kubwa ni

wakati wa COVID19. Wasimamizi

wetu hawakuwa wanakuja kwa

tahadhari ya mikusanyiko na

mwalimu mlezi alienda

masomoni. Klabu ikawa haiendi

sawa. Baadhi ya viongozi

walihama klabu. Ila nilisimama

sana imara wakati huo.

Niliendelea kusimamia na

kufundisha kupitia vitabu vya

afya ya uzazi Mema Tanzania

walivyotuachia.Ilinisaidia sana

kunijenga kujiamini na kuwa

kiongozi bora zaidi.

Klabu yetu imekuwa inatupa

motisha kufanya vyema katika

mitihani. Kuwa kiongozi wa

Mema Club kumenipa motisha

ya kuamini naweza kuwa

kiongozi.

Rigeye Ally

Ndoto yangu ni udaktari

20 | AUG 2021MEMA MAGAZINE


VIPAJIKA

NIKIZA JR

MSAFIRI MWENYE VIPAJI

Karibu katika kisima cha vipaji. Ninaweza

kuigiza, kukuvunja mbavu na utangazaji pia.

Yote haya nafanya na bado nakomaa na

kitabu katika chuo cha NIT, shahada ya

Computer Science.. Kwa majina naitwa

Justine Nikiza, jukwaani nafahamika kama

Nikiza Jr.

Nilianza kuigiza tangu nikiwa darasa la 4

shule ya msingi Nkololo B, Simiyu. Nilikuwa

nafanya maigizo kwenye mahafali mbali

mbali shuleni kwetu na kwenye matamasha

mengine yaliyokuwa yakihusisha shule

tofauti. Baada ya kumaliza shule ya msingi,

kipaji kilinoga nilipojiunga shule ya sekondari

Nyegezi iliyopo Mwanza. Tofauti na Simiyu,

Mwanza ni jiji. Kama una kipaji rahisi watu

kukiona na kupata shavu la kushiriki

mashindano na matamasha mbali mbali.

Kwa upande wa elimu nilichagua kusoma

Computer Science kwa sababu napenda

kompyuta. Nahitaji kufahamu mifumo mbali

mbali ya kompyuta inavyofanya kazi

Nisingeweza kusomea sanaa sababu tayari

vipaji ninavyo vya kuzaliwa. Siamini kipaji mtu

anaweza kufundishwa ila ni karama mtu

anazaliwa nayo na kuendeleza kwa

kuitendea kazi na kukinoa kwa kujifunza kwa

watu wengine walioendelea.

21 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE


Nilipofika chuo, nilianza kufanya comedy

kwa kuji-record video fupi kisha naziweka

katika akaunti yangu ya Instagram. Baadae

kazi zangu zilianza kufuatiliwa sana na

nikaona nahitaji kukua zaidi. Nikaanza

kushiriki katika vichekesho vya jukwaani

(stand-up comedy). Awali nilifanya kama

msanii wa kujitegema baadae nikapata

bahati ya kuwa sehemu ya familia ya Watu

Baki, japo bado sijawa mwaanachama rasmi.

Watu Baki imekuwa ni familia, najifunza

mambo mengi kutoka kwao. Ni kundi lenye

vipaji lukuki na wengine tayari wameshakuwa

na majina makubwa.

Watu Baki nafanya nao mazoezi na kushiriki

katika tamasha linalofanyika The Base Club

kila alhamis. Mwaka huu kuna rafiki yangu ni

mchekeshaji pia alikuja na wazo la kuanzisha

kundi letu litakalo husisha wanachuo wenye

vipaji vya uchekeshaji, ndipo Unicomedy

ilipoanza. Tumekuwa tukiandaa matamasha

yetu wenyewe yanayofanyika chuoni na nje

ya chuo. Kazi yangu imenipa heshima kwa

mwaka huu kupewa tuzo ya mchekeshaji

bora chuoni kwetu.

Mwaka huu Unicomedy tumefanikiwa

kuandaa matamasha mawili na yote

yalifanya vizuri. Mwanzoni tulifanyia London

Lounge, Ubungo. Watu walihudhuria wengi na

baadhi kukosa viti. La pili tukahamia ukumbi

mwingine.

Kati ya vitu ambavyo haviwezi kuepukika ni

mitandao ya kijamii. Mitandao ya kijamii

inasaidia sana kusukuma kazi zangu kufika

mbali. Japo changamoto ukishakuwa

maarufu watu wanaanza kutumia jina lako

hali inayowapa ugumu watu wanaponitafuta.

Mitandao imesaidia sana kujenga brand

yangu na kuonyesha uwezo wangu kwa

watu. Napgia simu na kupata mialiko kuperform

katika sherehe tofauti.

Mitandao pia imenikutanisha na ma-star

wakubwa, wengine ni role model wangu.

Mfano Kendrick Mulamula kutoka Kenya,

tuliwasiliana kupitia mitandao ya kijamii na

kubadilishana namba. Mpaka leo

tunawasiliana vizuri tu. Mpaka sasa

nimefanikiwa kufanya kazi na wasanii

wakubwa tofauti kama Idris Sultan ambaye ni

role model wangu, Francis Nalimi na wengine

kutoka Watu Baki.

Comedy kwa sasa sio kama zamani ambapo

ili uonekane mchekshaji uvae kiajabu ajabu

na watu kukuona kama kituko. Na ilichangia

sana malipo madogo ukilinagnisha na

wasanii wengine wa bongo movie kwa

sababu tulionekana kama vituko tu.

Mtazamo hasa kwa Dar umebadilika sana.

Changamoto bado mikoani kama kule kwetu

Simiyu bado waigizaji wengi wamekuwa na

mtazamo wa vituko badala ya vichekesho.

Kama mwanafunzi changamoto kubwa

nayopitia ni kupigana vizinga, wanafunzi

wengi wanafikiri nina hela nyingi. Wakiona na

star mkubwa wanajua jamaa

ameshayapatia, ukimnyima hela anahisi

umemkazia. Pia nyumbani wana-support

lakini kwa mashaka. Wazazi wananilipia ada

wanahisi sanaa inaweza kuniharibia masomo.

Ila taratibu wanazidi kuelea hii ni kazi na kwa

upande wa masomo haina athari yoyote ile.

22 | AUG 2021MEMA MAGAZINE


na Instagram 4.37% na jumla ya watu milioni 5.4 wanatumia

46.86%

ya kijamii. Wanawake wanaotumia mitandao ya kijamii ni

mitandao

37% na wanaume 63%. Kwa mtazamo wako, ni sababu zipi

asilimia

ufinyu wa wanawake kuingia katika ulingo wa fursa za

zinachochea

Sema nasi kupitia namba yetu ya Whatsapp iliyopo

kidijitali?

wa mawasiliano.

ukurasa

Sauti ya Mtaa

Kwanini wanawake ni wachache

katika fursa za kidijitali?

Nicholaus Mukasa

-Arusha

Ni ukweli ni wachache sana, kwa mfano ni asilimia 27% tu ya

wanawake ndio wanaotumia intaneti duniani. Kuna sababu

nyingi. Kwa uchache kwanza ni uelewa wa teknolojia. Wadada

wengi bado hawafahamu jinsi ya kutumia kwa usahihi

teknolojia za simu na kompyuta ambapo ndipo fursa zote za

kidijitali zipo. Uwezo wa kifedha pia kwa wanawake wengi sio

mzuri hivyo inakuwa ni ghali kwa wao kununua teknolojia za

kidijitali ambazo ni gharama. Wanawake pia wanafanyiwa

ukatili katika mitandao kama kutukanwa. Kwao wanaona sio

sehemu salama kuweza kushiriki na kujikuta wapo wachache

katika matumizi ya mitandao na fursa zake.

Wanawake wanauelewa mdogo juu ya elimu nzima

ya kidijitali. Wengi wanachojua nikijiunga Instagram

au Facebook ni kutuma picha, kuangalia likes na

comments nilizopata. Kumbe kuna fursa nyingi mbali

ya kushare tu picha na kutoka huyoo. Mimi

napofanya kazi sasa boss wangu nilikutana nae

kupitia mtandao wa Twitter. Usalama mitandaoni ni

mdogo kwa wanawake. Mfano mwanamke anaweza

ku-post picha akiishia kudhalilishwa na kutumiwa

messages za vitisho. Mwisho anaona hii sio sehemu

sahihi kwangu anaacha kutumia na fursa zinampita.

Happie Thomas

-Dar Es Salaam

Wanawake tuna dhana mambo yanayohusu dijitali au teknolojia

ni mambo magumu na jamii ni kama imeshajenga mtazamo vitu

vigumu ni vya wanaume. Hata mimi mwenyewe mambo kama

graphics designing naona ni vyema zaidi kufanywa na wanaume.

Ni kama tumeamua mambo yanayohusu sayansi tumeamua

kuwaachia wanaume. Wanawake mara nyingi tumekuwa wazito

kujifunza zinapotokea fursa za mafunzo tofauti na wanaume

utakuta mara nyingi wanakuwa wepesi kuzichangamkia. Nadhani

inatokana na sababu niliyosema hapo awali, kwamba mambo

haya ni kama tumeshajijengea dhana ni mambo ya wanaume.

Mwajabu Galmos

-Zanzibar

mujibu wa mtandao wa Statista, mpaka Februali 2021,

Kwa

ilikuwa na watumia wa Facebook asilimia 27.41%, Twitter

Tanzania

23 | AUG 2021MEMA MAGAZINE



Namna gani ningeweza kushika

vitu na kufanya majaribio ya kisayansi.

Nashukuru wazazi na walimu hasa wa

Loyola niliposoma O-Level waliniamini na

kunitia moyo na niliweza kuvuka kikwazo.

Mbali ya udaktari, una ujuzi gani

mwingine?

Nina ujuzi katika kufanya utafiti, kuandika na

kusimamia miradi,ufuatiliaji

na tathmini ya miradi, uzalishaji wa maudhui

na ujuzi wa dijitali.

Changamoto zipi unakumbana nazo

katika udaktari?

Upotoshaji wa taarifa za afya

hasa

katika mitandao ya kijamii hali

inayosababisha kuzuka kwa

baadhi ya taarifa potofu.Lakini

nikizungumzia kwa ujumla bado

kuna uhitaji wa

kuboresha mazingira ya kazi za

madaktari na watoa huduma

wa afya kwa ujumla ili kufanya

kazi kwa ufanisi.

Pia tuna changamoto ya

mfumo wetu wa elimu ambao

unatuanda wote kufikiria mstari

mmoja yaani kila mmoja ajiriwe.

Tutengeneze madaktari watakaohitimu na

uwezo wa kufikiri nakuboresha afya za

wagonjwa wao kwanzia kwenye mazingira

wanayotoka na mitindo yao ya maisha.

Wenye uwezo wa kutengeneza solutions za

changamoto za afya.

Tangu umeanza kuwa daktari,

muelimishaji na mtafiti umepata

mafanikio kiasi gani?

Mafanikio makubwa ya kwanza ni

kubadilika kimtazamo kwa kupata ujuzi

tofauti. Kufanya kazi maeneo tofauti

kumenibadilisha kifikra na kuwa na ufahamu

wa mambo mengi yanayohusiana na afya

kwa ujumla. Ujuzi pia kama graphics

designing, digital skills,project management

vimenipa mafanikio makubwa.

Kutoa huduma na watu

wakapona/kujikinga na maradhi

ni mafanikio makubwa sana.

Kwa mafanikio mengine mwaka 2017 nikiwa

chuo mwaka wa nne nilibahatika kupata

tuzo kutoka MILEAD (Maremi Institute of

Leadership and Development) nchini Ghana.

Tangu mwaka wa kwanza nilikuwa na wenzangu

tunafanya shughuli tofauti za kutoa elimu na

huduma za afya. Watu waliona nastahili kushiriki

hayo mashindano, na nilifanikiwa kushinda kati ya

wasichana 27 na mtanzania nilikuwa peke yangu.

Tulienda Ghana na kupewa mafunzo ya uongozi.

Mwaka 2020 pia nilipata heshima ya utambuzi

kutoka taasisi ya Launchpad na ubalozi wa

Sweden kwa kuchaguliwa kuwa miongoni mwa

wanawake 100 waliofanya mabadiliko chanya

katika jamii kwa mwaka huo. Pia nimepata

heshima kwa kufanya kazi na mashirika makubwa

ya kimataifa kama UNICEF na vyombo vya habari

kama Clouds, Redio France International, DW n.k.

kama muelimishaji katika kipindi cha COVID19.

Una wafuasi zaidi ya elfu 14 katika mtandao wa

Twitter, nini siri ya kuwa na wafuasi wengi?

Watu wanatafuta taarifa muhimu hasa za afya.

Tangu nilipojiunga Twitter nimekuwa nikiwasilisha

maudhui na dondoo muhimu hivyo watu kuvutiwa

na ukurasa wangu. Pia ku-engage na watu kama

kujibu comments na jumbe zao ilisaidia kujenga

mahusiano ya kibinadamu. Pia vijana tukumbuke

si kitu kinakuja haraka. Inabidi kujifunza namna ya

kutumia mitandao kwa kusoma na kuhududhuria

mafunzo mbalimbali.

Watu walio katika kada ya afya kuna umuhimu

gani wa kutumia teknolojia ya kidijitali hasa

mitandao ya kijamii?

Ni rahisi kusambaza taarifa kwa haraka hasa za

afya lakini pia kuna fursa ya kufanya utafiti na

kujifunza. Hivyo ni muhimu sana kujua matumizi

sahihi ya mitandao ya kijamii au teknolojia ili

kuboresha maisha na huduma kwa jamii.

Usingekuwa daktari ungekuwa nani?

Ahahaha! Sijui kwa kweli. Ila pengine ningekuwa

mwandishi wa habari sababu tangu mdogo

napenda kudadisi na kufuatilia

mambo.

Una ushauri gani kwa binti na kijana mwenye

ndoto ya kuwa mwanasayansi?

Kuamini unaweza, kuwa na lengo na kuzidi

kumuomba Mungu akuwezeshe kutimiza ndoto

yako. Ukitia juhudi na kufanya kazi kwa bidii ndoto

yako itatimia. Pia kuwa karibu na watu ambao

wameshafikia sehemu ambayo unafikiria kufika.

Julieth tunashukuru kwa kuchonga nasi,

tuna amini kuna mengi tumejifunza toka kwako.

Ahsanteni sana kwa kunipa nafasi hii.

25 | AUG 2021MEMA MAGAZINE


DID YOU KNOW?

We have all it takes to develop and strengthen

your relationship with your audience.

ABOUT US

We are trusted and professional digital, media-tech, and audio-visual experts with a dedicated

team that fulfil and deliver output to its clients at optimum level. We deploy skillful and

innovative human-centered designs in approaching and undertaking each and every task.

We are more than fit to serve you with the best up-to-date technologies in taking your brand

above the top notch.

WHAT WE DO

Public and Media Relation

Content Creation and Dissemination

Digital Marketing

Audio-Visual Production

Web Platforms and Apps Development

REACH US

0655 921 330 welcome@mediacrafters.co.tz

www.mediacrafters.co.tz @MediaCraftersTz


SMART CLASS

BUKUA KIDIJITALI, FURSA KWA WALIMU

MEMA TEAM

Ulishawahi kufikiria itafikia kipindi watu watachagua

kubaki nyumbani na kusoma kupitia mifumo ya

kimtandao badala ya kwenda shuleni? Janga la

COVID19 lilitupa funzo juu ya uwezekano wa jambo

hili.Wakati wa COVID19, mwezi March 2020 shule

zilifungwa na tulishuhudia vituo kadhaa vya Tv na

majukwaa ya kidijitali yakitoa elimu kwa wanafunzi.

Moja ya majukwaa hayo ni Smart Class ambao

wanatoa huduma ya mafunzo kwa wanafunzi wa shule

za msingi na sekondari kwa njia ya mtandao na nje ya

mtandao. Adam Duma, ni moja ya waanzilishi wenza

wa Smart Class na hapa anatuelezea kuhusu ubunifu

huu.

Mlipata wapi mtaji?

UBUNIFU

Unapoanzisha wazo lazima uangalie nani anaweza

kuwekeza pesa zake. Hili wazo lilikuja mimi bado

nipo chuo mwaka wa pili, kuna mwalimu wa Chuo

Kikuu cha Dar Es Salaam nilimshirikisha na akawa

tayari kuwekeza baadhi ya pesa kutoka kwenye

mshahara wake kama mtaji. Mimi niliomba msaada

wa kifedha kutoka nyumbani na pia yule mwalimu

alikuwa na rafiki yake anafanya kazi Nokia na yeye

aliungana nasi na hatimaye tukaanzisha kampuni.

Siku zilivyozidi kusonga tukaanza kupokea pesa

kutoka kwa wafadhili tofauti.

Smart Class ni nini?

Ni jukwaa la mtandaoni linalokutanisha walimu, wazazi

na wanafunzi na inapatikana nchini Tanzania na

Kenya kwa njia ya tovuti kutoa mafunzo ya ziada

maarufu ‘tuition’. Makundi yote haya matatu yanajisajili

bure na kisha kuanza kutumia huduma hii. Smart Class

inamuunganisha mwanafunzi au mzazi ambao ndio

wasimamizi wa taaluma kwa watoto wao na kisha

anachagua aidha asome ‘online’ au mwalimu amfuate

nyumbani. Mafunzo yanapokamilika, mwanafunzi

anatupatia ripoti ya huduma aliyopewa na malipo

yanafanyika Smart Class kisha mwalimu hupokea 85%

na 15% hubakia kwetu. Gharama za mafunzo

zinatofautiana kulingana na muda na mfumo wa

utolewaji wake, kwa ‘online’ ni nafuu kuliko kufuatwa

nyumbani ‘offline’.

Wazo liliibuka vipi?

Wazo tulianza nalo mwaka 2018 pamoja na wenzangu

wawili wakati huo tulikuwa Chuo Kikuu

cha Dar Es Salaam. Tulifanya utafiti kwa takribani

mwaka mmoja ili kubaini ni namna gani tutaweza

kutatua tatizo la ajira kwa walimu wakati wakisubiri ajira

za kudumu kutoka serikalini na kuondoa pengo la elimu

bora. Baada ya kufanya utafiti tulishiriki katika

maonyesho ya Research Innovation Week 2019

yanayoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na

mapokeo tuliyoyapata ndio yalitushawishi njia pekee ya

kutatua changamoto hii ni teknolojia na wazo la Smart

Class tukaanza kulifanyia kazi na kuizindua rasmi

mwaka huo huo.

Mapokeo kwa waTanzania yakoje?

Mapokeo ni mazuri kwa maana ya idadi ya

watumiaji tulio nao ambao kwa Tanzania wanafika

12,000 (walimu, wazazi na wanafunzi). Shule

zilipofungwa kipindi cha COVID19 naweza kusema

kwetu ilikuwa ni neema kwa sababu kulikuwa na

ongezeko kubwa la watumiaji wa jukwaa letu.

Changomoto iliyopo kwa Tanzania kunapoibuka

teknolojia mpya watu wengi huwa wanakuwa

wagumu kuipokea kwa haraka. Ila taratibu watu

wanazidi kuelea huduma tunayotoa.

Mliwezaje kufika Kenya?

Kwanza tulifikiria kujitanua Kenya kutokana na

uelewa mkubwa uliopo kule katika masuala ya

teknolojia. Kuna watumiaji wengi wa intaneti,

kwenda kule ilikuwa ni kulifikia kwa urahisi soko

ambalo tayari lipo. Kuna jamaa yetu anaitwa

Kimathi aliacha kazi na kusimamia mchakato

mzima wa kuanzisha Smart Class Kenya na ndio

msimamizi pamoja na watu wengine watatu.

Kenya tunawatumiaji zaidi ya 5,000 wa Smart

Class.

Mnajionaje miaka 5 ijayo?

Kuwa jukwaa kubwa la elimu Afrika. Kwa

mwalimu, mzazi au mwanafunzi anaweza kuipata

Smart Class kwa kutembelea

www.smartclasstz.com na kuanza kutumia

huduma zetu.

27 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE


Dr. Julieth Sebba

NO TIME TO GIVE UP

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!