12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Anasema "Mwanzoni nilikuwa na wateja

wachache na kupelekea kupata hasara mara

kadhaa. Nikaamua kuongeza wateja wapya

na njia rahisi niliona ni mitandao ya kijamii.

Nilifungua akaunti Instagram ndipo kasi ya

wateja ikaongezeka kutoka mikoa ya jirani na

kuniongezea mtaji mpaka wa Tsh milioni 5.”

Kuna vijana pia ambao wanatumia ushawishi

walionao katika mitandao ya kijamii

kutangaza biashara za makampuni,

kuendesha kampeni za taasis na baadhi

wameanzisha kurasa zinazochapisha maudhui

tofauti ikiwemo udaku na kujipatia wafuasi

wengi hivyo kuwafungulia dili za matangazo

ya biashara.

Kabla ya kuolewa mwaka 2018 alikuwa

akijihusisha na mauzo ya bidhaa mtandaoni.

"Nilikuwa nikifanya biashara ya kuuza nguo za

watoto na wanawake. kupitia Instagram. Akaunti

yangu ilikuwa imefikisha wafuasi zaidi ya elfu 10.

Ni biashara nilianza tangu nikiwa nasoma chuo

na nilikuwa na wateja wengi sana. Baada ya

kuolewa mme wangu hakuwa anapendezwa

navyo wasiliana na wateja mara kwa mara.

Kuepusha mikwaruzano katika ndoa yangu

nikaamua kuachana na biashara ile na kuajiriwa

katika kampuni ambayo mme wangu alinitafutia.

Changamoto za kifamilia hasa kwa wanawake

waliolewa kiukweli zinatukwamisha kujihusisha

na mambo ya dijitali labda uwe na mwenza

muelewa na mambo haya" anasema Aisha.

Utawala wa kijinsia

Licha ya fursa lukuki za kidijitali bado sio wote

wananufaika nazo. Utofauti upo zaidi katika

upande wa jinsia ambapo wanawake ni wachache

kuliko wanaume. “Kwa mtazamo wangu sababu

kama kutingwa kwa majukumu ya familia, ukosefu

wa ujuzi, hofu ya ukatili wa kijinsia zinachangia

wanawake kuwa wachache” anasema Dkt Julieth

Sebba, moja ya vijana wenye ushawishi katika

mtandao wa Twitter. Mtazamo wake unaungwa

mkono na Mariam, mkazi wa Tanga. ambaye

anaamini uchache wa wasichana na wanawake

katika dunia ya kidijitali inachangiwa na uoga wa

kushambuliwa mitandaoni hali inayowarudisha

nyuma katika kuzifilkia fursa zilizopo katika

mitandao ya kijamii.Aisha mkazi wa Tabata jijini

Dar Es Salaam, ni kijana mwenye umri wa miaka

32 ni mke na mama mwenye mtoto mmoja.

8 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Sheria ya ngoma

Mafanikio hayaji haraka na kwa urahisi hasa

katika kuzifikia fursa za kidijitali. Unahitaji kutia

bidii katika kujifunza ujuzi fulani, hata kama ni

kutangaza biashara yako mtandaoni unapaswa

kufahamu namna gani ya kuandika maudhui,

muda gani, nani unayemlenga n.k.

Jinsi unavyofanyia kazi ujuzi wako ndivyo

unavyozidi kuwa na uelewa wa kutosha na jamii

itatambua ujuzi wako hivyo fursa zitaanza

kukufikia. Jipe muda kujifunza, usikate tamaa.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!