12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

SMART CLASS

BUKUA KIDIJITALI, FURSA KWA WALIMU

MEMA TEAM

Ulishawahi kufikiria itafikia kipindi watu watachagua

kubaki nyumbani na kusoma kupitia mifumo ya

kimtandao badala ya kwenda shuleni? Janga la

COVID19 lilitupa funzo juu ya uwezekano wa jambo

hili.Wakati wa COVID19, mwezi March 2020 shule

zilifungwa na tulishuhudia vituo kadhaa vya Tv na

majukwaa ya kidijitali yakitoa elimu kwa wanafunzi.

Moja ya majukwaa hayo ni Smart Class ambao

wanatoa huduma ya mafunzo kwa wanafunzi wa shule

za msingi na sekondari kwa njia ya mtandao na nje ya

mtandao. Adam Duma, ni moja ya waanzilishi wenza

wa Smart Class na hapa anatuelezea kuhusu ubunifu

huu.

Mlipata wapi mtaji?

UBUNIFU

Unapoanzisha wazo lazima uangalie nani anaweza

kuwekeza pesa zake. Hili wazo lilikuja mimi bado

nipo chuo mwaka wa pili, kuna mwalimu wa Chuo

Kikuu cha Dar Es Salaam nilimshirikisha na akawa

tayari kuwekeza baadhi ya pesa kutoka kwenye

mshahara wake kama mtaji. Mimi niliomba msaada

wa kifedha kutoka nyumbani na pia yule mwalimu

alikuwa na rafiki yake anafanya kazi Nokia na yeye

aliungana nasi na hatimaye tukaanzisha kampuni.

Siku zilivyozidi kusonga tukaanza kupokea pesa

kutoka kwa wafadhili tofauti.

Smart Class ni nini?

Ni jukwaa la mtandaoni linalokutanisha walimu, wazazi

na wanafunzi na inapatikana nchini Tanzania na

Kenya kwa njia ya tovuti kutoa mafunzo ya ziada

maarufu ‘tuition’. Makundi yote haya matatu yanajisajili

bure na kisha kuanza kutumia huduma hii. Smart Class

inamuunganisha mwanafunzi au mzazi ambao ndio

wasimamizi wa taaluma kwa watoto wao na kisha

anachagua aidha asome ‘online’ au mwalimu amfuate

nyumbani. Mafunzo yanapokamilika, mwanafunzi

anatupatia ripoti ya huduma aliyopewa na malipo

yanafanyika Smart Class kisha mwalimu hupokea 85%

na 15% hubakia kwetu. Gharama za mafunzo

zinatofautiana kulingana na muda na mfumo wa

utolewaji wake, kwa ‘online’ ni nafuu kuliko kufuatwa

nyumbani ‘offline’.

Wazo liliibuka vipi?

Wazo tulianza nalo mwaka 2018 pamoja na wenzangu

wawili wakati huo tulikuwa Chuo Kikuu

cha Dar Es Salaam. Tulifanya utafiti kwa takribani

mwaka mmoja ili kubaini ni namna gani tutaweza

kutatua tatizo la ajira kwa walimu wakati wakisubiri ajira

za kudumu kutoka serikalini na kuondoa pengo la elimu

bora. Baada ya kufanya utafiti tulishiriki katika

maonyesho ya Research Innovation Week 2019

yanayoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na

mapokeo tuliyoyapata ndio yalitushawishi njia pekee ya

kutatua changamoto hii ni teknolojia na wazo la Smart

Class tukaanza kulifanyia kazi na kuizindua rasmi

mwaka huo huo.

Mapokeo kwa waTanzania yakoje?

Mapokeo ni mazuri kwa maana ya idadi ya

watumiaji tulio nao ambao kwa Tanzania wanafika

12,000 (walimu, wazazi na wanafunzi). Shule

zilipofungwa kipindi cha COVID19 naweza kusema

kwetu ilikuwa ni neema kwa sababu kulikuwa na

ongezeko kubwa la watumiaji wa jukwaa letu.

Changomoto iliyopo kwa Tanzania kunapoibuka

teknolojia mpya watu wengi huwa wanakuwa

wagumu kuipokea kwa haraka. Ila taratibu watu

wanazidi kuelea huduma tunayotoa.

Mliwezaje kufika Kenya?

Kwanza tulifikiria kujitanua Kenya kutokana na

uelewa mkubwa uliopo kule katika masuala ya

teknolojia. Kuna watumiaji wengi wa intaneti,

kwenda kule ilikuwa ni kulifikia kwa urahisi soko

ambalo tayari lipo. Kuna jamaa yetu anaitwa

Kimathi aliacha kazi na kusimamia mchakato

mzima wa kuanzisha Smart Class Kenya na ndio

msimamizi pamoja na watu wengine watatu.

Kenya tunawatumiaji zaidi ya 5,000 wa Smart

Class.

Mnajionaje miaka 5 ijayo?

Kuwa jukwaa kubwa la elimu Afrika. Kwa

mwalimu, mzazi au mwanafunzi anaweza kuipata

Smart Class kwa kutembelea

www.smartclasstz.com na kuanza kutumia

huduma zetu.

27 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!