12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

SOCIAL HIT

‘Mwaka jana (2020) nilipanga kununua friji lakini

kila nikipata hela inakwenda kufanya matumizi

mengine. Siwezi kununua vyakula vingi sababu

vitaharibika hivyo inanilazimu kununua mahitaji

kidogo kidogo ambayo ni gharama kuliko kununua

kwa jumla’ anasema Prisca, kijana mwenye miaka

28 na mkazi wa Kinondoni jijini Dar Es salaam.

Licha ya kufanya kazi na kupata mshahara mzuri,

Prisca ameshindwa kutimiza lengo lake la kununua

friji zaidi ya mwaka mmoja sasa. Hata wewe

pengine una lengo fulani lakini kila ukipata mtonyo

unaishia kwenye matumizi mengine ikiwemo kulipa

madeni.

Tunzaa App!

Aplikesheni inayodhamiria

kuboresha tabia chanya

ya kutunza fedha.

Kutatua changamoto hii Tunzaa Fintech ambayo

ni kampuni changa inayomilikiwa na vijana

wazawa wa kitanzania wamezindua App

inayolenga kuimarisha tabia ya kutunza fedha

kwa watanzania. “Mwaka 2019 tulitembelea Tanga

na Dar kuzungumza na wanawake pamoja na

wanaume ili kuelewa wanapopata pesa

wanazitunza vipi na wanazitumia namna gani. Kati

ya watu tuliozungumza nao vipato vyao kwa

mwezi vilikuwa ni kati ya laki 3 mpaka milioni 6.

Lakini pia moja ya maswali ambayo tulikuwa nayo

ni watu hawatunzi pesa kwa sababu ya matumizi

mabaya, hawana njia nzuri na rahisi za kutunza

fedha na watu wengi hawarudishi kabisa pesa

wanazokopa au hawarudishi kwa wakati”

anasema Ngw’inula Kingamkono ambaye ni

mtaalamu wa teknolojia na mkurugenzi mtendaji

wa Tunzaa Fintech. Wazo la kuja na app ya

Tunzaa lilitokana na changamoto za watanzania

wengi kutokuwa na tabia ya kutunza pesa na

kuziba mwanya wa ukosefu wa njia rahisi, salama

na ya haraka ya kuhifadhi pesa pindi mtu

anapotaka kununua bidhaa kwa malipo ya kidogo

kidogo.

“Sisi hatukutunzii pesa yako. Unapojisajili katika

app ya Tunzaa unachagua aidha Tunzaa au

Nunua Sasa. Ukichagua Tunzaa maana yake

bidhaa au huduma uliyoichagua unahitaji

kuinunua kwa kutunza pesa kidogo kidogo

kulingana na wewe ulivyochagua iwe malipo kwa

siku, wiki au mwezi. Pesa unayolipa inakwenda

moja kwa moja kwa muuzaji husika. Unaponunua

bidhaa unapata point ambazo unaweza kuzitumia

kununua bidhaa au huduma sehemu fulani.”

anaongezea Ngw’inula Kingamkono. Ili mtu aweze

kuwa muuzaji wa bidhaa au huduma, Tunzaa

Fintech hupitia taarifa zote muhimu na pindi

wanapojiridhisha muuzaji ana uwezo wa

kupandisha bidhaa au huduma yake. Malipo

yanafanyika kwa njia ya simu kwa mitandao iliyo

kwenye orodha ya Tunzaa App. Ili kuweza

kuituimia Tunzaa App inabidi kupakua app kisha

kufuata hatua rahisi za kujisajili.

16 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Kwa sasa Tunzaa App inapatikana katika Google

Playstore (kwa simu zenye mfumo wa Android) na

iStore kwa simu za iPhone.“Sisi bado ni kampuni

changa hatuwezi kuanza mikoa yote kwa mara

moja. Tulichagua kuanza na Dar kwanza kwa

sababu ya watumiaji wengi wa simu janja na

uelewa wa masoko ya mtandaoni ni mkubwa.

Lakini pia kutupa urahisi wa kuthibitisha taarifa za

wauzaji” anamalizia Ngw’inula Kingamkono

maarufu pia kama Unu. Watoto wa mjini Tunzaa

app tunaita ni kibubu cha kidijitali. Pakua kisha

furahia maisha.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!