12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Ndoto iliyotimia haraka

Wakati naanza ku-share vichekesho vyangu sikutegemea ningepata umaarufu haraka hivi, nilijua

itachukua muda mrefu na nilikuwa na imani ipo siku. Nashukuru Mungu watu wamepokea kazi zangu

vizuri. Umaarufu umenisaidia kunifungulia fursa nyingine nyingi kama kupata connection na watu tofauti,

kupokea dili za matangazo na kusambaa kwa brand yangu ya mavazi ya Mwaisa. Watu mpaka wilayani

ndani huko wanaijua.

Kuficha utambulisho

Binafsi sipendi sana kujulikana kwa sababu ya kazi na pia napenda kuwa na maisha binafsi. Napofanyia

kazi asilimia kubwa mwanzoni walikuwa hawajui kama Nyonyoma Mtu Mbad ndiyo mimi. Kuna muda

nilikuwa nawakuta wanacheki video zangu tunacheka bila kujua ndiyo mimi. Baada ya kuanza kufanya

mahojiano na vyombo tofauti vya habari ndiyo wakaanza kunifuatilia.

Mahojiano yangu nilikuwa naficha sura kwa kitambaa, sasa waki-zoom wanajiuliza mbona huyu jamaa

anafanana jina na sura na mshikaji tunayefanya nae kazi? Nikawa nakwepa kwepa baadae wakajua

ndiyo mimi. Ila maeneo mengine watu hawanifahamu kwa sura.

Watu wanacheka lakini maisha yanabadilika

Sikutegemea wakati naanza kama vichekesho vyangu vitabadili maisha ya watu. Kwa mfano

kuna mtu alinipigia simu kutoka Dodoma alikiri ndoa yake ilikuwa inayumba.

Ilifikia mahali mke wake alirudi mpaka nyumbani. Jamaa akawa anamtumia video

zangu na kumkumbushia kipindi walivyokuwa wakifurahi pamoja wakati wakizitazama.

Kweli mwanamke akatuliza hasira na mpaka sasa wanaishi pamoja. Kuna mtu pia

alishawahi nitafuta baada ya kutazama video clip nikimulezea nyani anampiga kofi

mwenzake kwa kula mtaji badala ya faida. Yule dada aliniambia ile video ilimsaidia yeye

na mme wake, biashara yao ilisimama kwa sababu ya kula mtaji wa biashara.

Majina yanakua haraka kuliko mafanikio

Tasnia yetu ina chgangamoto nyingi, majina yetu yanakua haraka kuliko mafanikio

tunayopata. Kikubwa kutokuta tamaa, mbele kuna faida nyingi japo itachukua muda.

Lakini pia sanaa yetu inachelewa kukua ukilinganisha na nchi nyingine mfano chukulia

Kenya. Wenzetu vichekesho vya majukwaani (stand up comedy) walianza muda kwetu

tulichelewa kidogo. Vipaji vipo vya kutosha. Kwa sasa mambo yanaanza kubadilika,

tasnia ya vichekesho watu wameanza kuingalia kwa umakini.

Aminia kipaji chako

Mitandao ya kijamii bahati nzuri watu wengi wapo huko. Vijana

wengi wanaitumia kupandisha video zinazoonyesha vipaji vyao

na wanatoka. Cha msingi upende unachokifanya na usikate

tamaa. Halafu matarajio vijana tusiwe nayo makubwa sana

hasa tunapoanza, tuna expect too much tukikwama tunakata

tamaa.

18 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!