12.08.2021 Views

Mema Magzine Edition 2 #FursaKidijitali

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

ULIZA UJIBIWE

NA ELIAS MAEDA

Je, una swali kuhusu

masuala ya kidijitali?

Tucheki kupitia Whatsapp

na tutakupatia majibu

haraka. Namba ipo katika

ukurasa wa 4.

Mambo vipi? Naitwa Hadija, ni mkazi wa Arusha.

Swali langu, nafanya biashara ya vipodozi nawezaje

kuwafikia wateja wengi katika mitandao ya kijamii?

Kabla hujafikiria kuwafikia wateja kwanza hakikisha

kuwa umetengeneza ukurasa wako kwa namna

ambayo watu wataamini huduma au bidhaa unazouza.

Njia ya haraka ya kufikia wateja wengi ndani ya muda

mfupi ni kwa kulipia matangazo au kuwalipa watu

mashuhuri wakutangazie. Kama kipato chako ni kidogo

unaweza kuanza tu wewe mwenyewe na

kujitengenezea wafuasi wako ambao pia ndio wateja

wako.

Mimi naitwa Zainab naishi ilala. Ninauza mitandio

ya wanawake, nifanyaje akaunti yangu iwe na

followers wengi ?

Unapofanya biashara mtandaoni haupaswi

kuhadaika zaidi na followers. Kumbuka kuwa wewe

upo mtandaoni kutafuta wateja na sio followers.

Wateja wako ndio watakuwa followers wako. Weka

nguvu zaidi kuwafikia watu wengi; kidogo kidogo

utapata wateja ambao watakuwa wanafatilia

biashara yako na hao ndio watakuwa followers wako.

Mtandao upi wa kijamii ni mzuri kwa mimi nayeuza

mchele? Rajab Selaman, Tanga

Swali zuri sana. Mitandao yote ni mizuri ila kwa

mfanyabiashara ni lazima kuzingatia wateja wa bidhaa

au huduma zako wapo wapi zaidi. Mitandao mikubwa

zaidi ni Facebook, Twitter na Instagram; hii mitandao

ina aina zote za watu japo kuwa kwa sasa Instagram

na Facebook inatumika na wengi zaidi Tanzania.

Binafsi ningeshauri uwekeze zaidi kwenye mitandao

hiyo mikubwa mitatu ila chagua mmoja wapo wa

Mwaka huu namaliza chuo na napenda sana

mambo ya digital. Ujuzi gani naweza kujifunza na

kuniingiza hela haraka?

kuanza nao. Hongera sana Andronicus. Sijajua ulivyosema

'haraka ni uharaka wa kiasi gani ila binafsi naamini

kiwanda cha digitali kina fursa nyingi na ni vyema

ukazingatia kujifunza na kupata uzoefu wake kabla

ya kuwaza kupata hela haraka. Hata hivyo, hizi ni

baadhi ya fursa na ujuzi ambao yanaweza kukupa

kipata cha haraka ukiwe kufanya kwenye ubora;

graphics designing, content creation, social media

management, masoko ya mtandaoni

Utaratibu wa kodi TRA ukoje kama nikiwa nauza

biashara yangu online tu? Jennifer, Dar

Sina elimu kubwa sana ya kodi, ila binafsi naamini

kuwa kwa biashara yoyote ile halali ambayo inaingiza

kipato ni lazima itambulike kisheria na kuchangia kodi.

Naelewa hili swala ni gumu kidogo haswa kwa

wanaoanza biashara, ila unaweza kujipanga taratibu

na ukaangalia ni namna gani unachangia kodi au

kufika ofisi za TRA kwa ushauri zaidi. Nadhani wao

wanaweza kuwa na

jibu zuri zaidi.

Naona kuna watu huwa wanauza akaunti.

Nikinunua akaunti na biashara yangu nikahamishia

huko ni sawa? Abdul, Chanika

Sio sawa na wala sikushauri kufanya hivyo. Wewe

upo mtandao kutafuta wateja na sio followeres.

Tengeneza ukurasa wako wa biashara na utakua

taratibu, utakuletea wateja na hao ndio watakuwa

followers wako wa kweli. Wewe unauza biashara ya

mayai unaweza ukaenda kununua ukurasa wenye

wafuasi wengi ukiamini kuwa umepata wateja

kumbe hao wafuasi waliufata huo ukirasa sababu

ulikuwa ukisambaza maudhui ambayo hata

hayaendani na biashara yako.

12 | AUG 2021 MEMA MAGAZINE

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!